SBS Swahili - SBS Swahili

Follow SBS Swahili - SBS Swahili
Share on
Copy link to clipboard

Listen to interviews, features and community stories from the SBS Radio Swahili program, including news from Australia and around the world. - Sikiza mahojiano, makala na hadithi za jumuiya kutoka Idhaa ya Kiswahili ya SBS Radio, ikijumuisha taarifa za habari kutoka Australia na ulimwenguni.

SBS Swahili


    • Jul 28, 2026 LATEST EPISODE
    • daily NEW EPISODES
    • 12m AVG DURATION
    • 2,119 EPISODES


    Search for episodes from SBS Swahili - SBS Swahili with a specific topic:

    Latest episodes from SBS Swahili - SBS Swahili

    Taarifa ya Habari:Kiongozi wa Victoria, ajiuzulu baada ya siku kadhaa za shinikizo dhidi ya uongozi wake

    Play Episode Listen Later Jul 28, 2026 14:42


    Jacinta Allan amejiuzulu kama Kiongozi wa Victoria, akisema ni uamuzi sahihi kwa Wa-Victoria. Tangazo hilo limekuja nusu saa tu baada ya changamoto inayotarajiwa ya uongozi katika mkutano uliopangwa wa chama cha wabunge, kuashiria kurudi kwa bunge la jimbo.

    Australia Yafafanuliwa:Tamasha ya Garma ni nini, na kwa nini ni muhimu?

    Play Episode Listen Later Jul 28, 2026 10:45


    Kila mwaka, maelfu ya watu husafiri kwenda katika jamii ya kijijini kaskazini mashariki mwa Arnhem Land katika Eneo la Kaskazini.

    Makala Leo: Jacinta Allan akataa kujiuzulu, pambano la uongozi wa chama cha Labor cha Victoria likiongezeka kasi

    Play Episode Listen Later Jul 28, 2026 11:00


    Kiongozi wa Jimbo la Victoria, Jacinta Allan, anasema atapambana na changamoto ya uongozi inayokuja baada ya viongozi wa mirengo tafuati ndani ya chama cha Labor, kukutana na kukubaliana kwamba amepoteza uungwaji mkono wa wengi katika mkutano wao.

    Taarifa ya Habari: Kiongozi wa Victoria asisitiza hajiuzulu!

    Play Episode Listen Later Jul 27, 2026 5:00


    Kiongozi wa jimbo la Victoria, Jacinta Allan, anasema hatajiuzulu kutoka wadhifa wake, miezi minne kabla ya uchaguzi wa jimbo hilo.

    Yaliyojiri Afrika:Kenya yapokea tani 4.5 zavifaa vya matibabu vya Ebola kutoka India

    Play Episode Listen Later Jul 24, 2026 7:44


    Kenya imepokea shehena ya kwanza ya tani 4.5 za vifaa vya matibabu kutoka kwa serikali ya India, ili kuimarisha uwezo wa nchi kujiandaa kukabiliana na uwezekano wa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

    Taarifa ya Habari: Hatua ya Marekani kuongeza ushuru kwa mauzo ya nje ya Australia yazua ukosoaji

    Play Episode Listen Later Jul 24, 2026 13:33


    Utawala wa Trump umeongeza ushuru kwa mauzo ya nje ya Australia kutoka asilimia 10 hadi 12.5, huku kiwango kipya kikianza kutumika alasiri ya leo Ijumaa.

    Makala Leo:Nini cha kutarajia kutoka kwa mfumo mpya wa tahadhari ya dharura wa Australia

    Play Episode Listen Later Jul 24, 2026 15:16


    Australia inajiandaa kuanzisha mfumo mpya wa kitaifa wa tahadhari ya dharura, ulioundwa kutoa tahadhari muhimu haraka na kwa uhakika zaidi wakati wa majanga.

    Makala Leo:China yaambia Australia iache kuzungumzia Bahari ya Kusini mwa China wakati mvutano ukiongezeka katika Mkutano wa ASEAN

    Play Episode Listen Later Jul 24, 2026 10:03


    Mkutano wa Kikanda wa ASEAN unakamilika mjini Manila, ambapo Australia imeibua wasiwasi kuhusu hatua za kijeshi za China katika eneo hilo.

    Taarifa ya Habari:Waziri Mkuu ataka chama cha Labor, kijitolee kupunguza shinikizo za gharama ya maisha

    Play Episode Listen Later Jul 23, 2026 6:25


    Waziri Mkuu Anthony Albanese, amesisitiza kujitolea kwa chama chake kupunguza shinikizo la gharama la maisha katika mkutano wa kitaifa wa chama tawala.

    Yaliyojiri Afrika:Kituo chakujitenga cha Ebola nchini Kenya cha wapokea wamarekani 7 kutoka DRC

    Play Episode Listen Later Jul 23, 2026 7:24


    Wahudumu7 wamisaada kutoka wamarekani walikuowa wakisaida kupambana na Ebola DRC, wamewekwa katika kituo cha karantini nchini Kenya.

    SBS Learn Eng Ep 115 Jinsi yakuzungumza kuhusu kufanya kazi ya ziada

    Play Episode Listen Later Jul 21, 2026 11:11


    Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kufanya kazi ya ziada?

    Taarifa ya Habari:Waziri Wong aelekea katika kongamano lamawaziri wa mambo ya nje wa ASEAN kuimarisha uhusiano wa Australia na nchi wanachama

    Play Episode Listen Later Jul 21, 2026 13:03


    Waziri wa Mambo ya Nje Penny Wong anatarajiwa kwenda Ufilipino kuhudhuria Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Asia Mashariki na Jukwaa la Kikanda la ASEAN.Tume ya Dhamana na Uwekezaji ya Australia inasema imepata rekodi ya dola milioni 830 katika amri za adhabu za kiraia wakati wa Mwaka wa Fedha wa 2025-2026. Tume hiyo ilianzisha chunguzi zaidi ya 250, ambazo zilisababisha hatia 25 za jinai na watu 11 kuhukumiwa kifungo cha gerezani.Karibu watu 930 wamefariki dunia kutokana na Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, hii ikiwa ni kulingana na Wizara ya afya nchini humo. Vifo hivyo vimerekodiwa miongoni mwa visa 2,344 vya maambukizi vilivyothibitishwa hadi siku ya Jumamosi imesema wizara hiyo hii leo. Vifo vipya vilirekodiwa katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita, idadi ya juu kabisa kuwahi kurekodiwa kwa siku moja.Meli ya mafuta yenye bendera ya Tanzania imetekwa nyara na maharamia wanaoshukiwa kuwa wa Somalia katika pwani ya Yemen, vimebaini vyanzo vya usalama na maafisa wa eneo hilo kuhusu tukio hilo. Meli hiyo imehamishwa hadi majini katika eneo la Bari kaskazini mashariki mwa Somalia, kulingana na maafisa wa eneo hilo.

    Australia Yafafanuliwa:Kijana wangu anaweza anza kufanya kazi lini nchini Australia?

    Play Episode Listen Later Jul 21, 2026 12:25


    Kuanza kazi ya muda mfupi kunaweza kuwa uzoefu wenye maana kwa kijana, kuongeza kujithamini kwake, kumsaidia kujifunza ujuzi mpya na kupata pesa zake za kwanza.

    Makala Leo:Mazoezi muhimu yakimataifa yajeshi yaanza katika Wilaya ya Kaskazini

    Play Episode Listen Later Jul 21, 2026 7:03


    Zoezi kubwa zaidi la kimataifa la Jeshi la Anga la Australia, linaendelea katika Eneo la Kaskazini na litafanyika kwa wiki tatu zijazo.

    Taarifa ya Habari:Greens wataka makampuni ya mawasiliano nchini kutoa huduma yakuaminika kwa wateja

    Play Episode Listen Later Jul 20, 2026 4:49


    Chama cha Greens kinatoa wito wa mageuzi ambayo kisheria yatahitaji kampuni zama wasiliano kama Telstra, Optus na Vodafone kutoa huduma ya kuaminika kwa wateja.

    Makala Leo: Mitandao ya teknolojia yaambiwa irekebishe pengo za ulaghai wakujamiana

    Play Episode Listen Later Jul 17, 2026 11:22


    Kamishna wa Usalama Mtandaoni wa Australia anatoa tahadhari kuhusu ulaghai wa kingono mtandaoni, baada ya kupokea malalamiko zaidi ya 2,000 katika miezi sita tu.

    Taarifa ya Habari:Watoto wa Australia kuanza kuamua katika shule ya msingi kama watafuata taaluma za sayansi na teknolojia kwa msaada wa wazazi

    Play Episode Listen Later Jul 17, 2026 14:12


    Utafiti mpya unaonyesha kuwa watoto wa Australia wanaweza kuanza kuamua katika shule ya msingi kama watafuata taaluma za sayansi na teknolojia wanapokuwa wakubwa, huku wazazi wakiwa na ushawishi zaidi kuliko walimu katika maamuzi hayo.

    Makala Leo: Argentina na Uhispania zaishi ndoto zakipekee za Kombe la Dunia

    Play Episode Listen Later Jul 17, 2026 5:07


    Argentina na Uhispania wanaishi ndoto ya kipekee ya Kombe la Dunia, baada yakutinga fainali ya kombe hilo. Mjini Buenos Aires na Madrid, mashabiki wanachangia jinsi walivyopitia tamthilia, hisia na sherehe.

    Taarifa ya Habari:Ombi latolewa kuharamisha matamshi ya chuki dhidi yawa Aboriginal na wakaazi wa Torres Strait

    Play Episode Listen Later Jul 16, 2026 5:20


    Kuna wito wa kuharamisha matamshi ya chuki dhidi yawa Aboriginal na watu kutoka Visiwa vya Torres Strait, huku vikao vikiendelea katika uchunguzi wa ubaguzi wa rangi wa Serikali ya Shirikisho huko Darwin.

    Makala Leo:Ufaransa na Uhispania tayari kwa pambano la nusu fainali

    Play Episode Listen Later Jul 14, 2026 5:41


    Nusu fainali za Kombe la Dunia zimewadia, Ufaransa na Uhispania zikijiandaa kufufua moja ya ushindani mkubwa wa soka la kimataifa. Tunaangalia kwa karibu habari za hivi punde za timu hizo na kusikia kutoka kwa kambi zote mbili kabla ya pambano kubwa la kesho.

    Taarifa ya Habari:Vyuo vikuu kukabiliwa na faini kubwa vikishindwa kupambana na ubaguzi wa rangi

    Play Episode Listen Later Jul 14, 2026 13:56


    Serikali ya Shirikisho inasema vyuo vikuu vinaweza kukabiliwa na faini ikiwa vitashindwa kupambana na ubaguzi wa rangi chini ya viwango vipya vilivyoanzishwa Jumatatu 13 Julai 2026.

    Makala Leo:Kusini Australia yatoa mpango wakupiga marufuku wahalifu wa vurugu kutoka programu zakuchumbiana

    Play Episode Listen Later Jul 14, 2026 10:50


    Jimbo la Kusini Australia limefichua mpango wa kwanza wa kupiga marufuku vurugu za majumbani na wahalifu wa kujamiana kutoka kwa programu za kuchumbiana.

    Makala Leo:Mashambulizi mapya yashuhudiwa Iran na Marekani zikibishana kuhusu kufunguliwa kwa Hormuz

    Play Episode Listen Later Jul 14, 2026 10:22


    Marekani na Iran zimebadilishana wimbi jingine la mashambulizi, huku mapigano yakiongezeka kuhusu Mlango-Bahari wa Hormuz yakisukuma makubaliano ya kidiplomasia ya mwezi uliopita karibu kuvunjika.

    Taarifa ya Habari:Daglo na maafisa wengine wa RSF wahukumiwa adhabu ya kifo

    Play Episode Listen Later Jul 13, 2026 5:22


    Mahakama ya Kupambana na Ugaidi na Makosa Dhidi ya Taifa iliyoko mjini Port Sudan nchini Sudan, , imemhukumu kifo kiongozi wa kundi la wanamgambo wa RSF, Mohamed Hamdan Daglo pamoja na maafisa wengine 15 wa RSF.

    Yaliyojiri Afrika: Usalama waimarishwa katika mitaa ya Tanzania

    Play Episode Listen Later Jul 10, 2026 7:47


    Usalama unaendelea kuimarishwa katika miji mikubwa ya Tanzania, maafisa wa Polisi na Jeshi wenye silaha wakifanya doria.

    Mbappé aiweka Ufaransa katika nusu fainali

    Play Episode Listen Later Jul 10, 2026 4:16


    Ufaransa imetinga nusu fainali ya Kombe la Dunia, baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Morocco. Kylian Mbappé amefunga mabao nane sawa na Lionel Messi, wakati Ousmane Dembélé akikamilisha ushindi huo.

    Taarifa ya Habari:Polisi wachunguza kama kifo katika jimbo la Kusini Australia, kina husishwa na kupotea kwa huduma za Telstra Jumatano

    Play Episode Listen Later Jul 10, 2026 14:24


    Polisi wanachunguza kama kifo kinahusishwa na kupotezwa kwa huduma ya Telstra kote nchini Jumatano. Wapelelezi wa Kusini Australia wamethibitisha mtu mmoja alifariki katika hospitali ya kanda Jumatano, lakini polisi hawakuwa wamearifiwa kuhusu kifo hicho.

    Australia Yafafanuliwa: Sensa ya 2026: Unacho stahili jua kuhakikisha una hesabiwa

    Play Episode Listen Later Jul 10, 2026 12:16


    Sensa ya 2026 itafanyika Jumanne tarehe 11 Agosti na kila mtu nchini Australia usiku huu lazima ahesabiwe.

    Makala Leo: Waziri Mkuu Albanese aendeleza msukumo wake wakidiplomasia katika Pasifiki

    Play Episode Listen Later Jul 10, 2026 11:51


    Waziri Mkuu Anthony Albanese ameweka ratiba kabambe ya mkataba mpya kamili na Visiwa vya Solomon, akisema angependa kuuona ukikamilika mwishoni mwa mwaka huu.

    Taarifa ya Habari:Unyanyasaji wa kingono unaendelea kutumiwa kama silaha ya kivita DRC

    Play Episode Listen Later Jul 9, 2026 6:18


    Mamlaka katika jimbo la Kusini Australia, zimethibitisha kisa cha pili cha homa ya ndege aina ya H5 katika jimbo hilo.

    Chiry"wasichana wenzangu njooni tuboreshe afya zetu kupitia mpira"

    Play Episode Listen Later Jul 7, 2026 9:01


    Jamii ya wakenya wanao ishi mjini Sydney, NSW walishuhudia historia ikiandikwa jioni ya Jumapili 28 Juni 2026 timu mpya ya mpira wa miguu ya kina dada ilipo cheza mechi yao ya kwanza katika uwanja wa Rydalmere.

    Uhispania na Ubelgiji za tinga robo fainali wakati Ronaldo aaga Kombe la Dunia

    Play Episode Listen Later Jul 7, 2026 4:51


    Uhispania na Ubelgiji zimefuzu kwa robo fainali, wakati ndoto za Kombe la Dunia za wenyeji Marekani na Ureno ya Cristiano Ronaldo ziki gonga miamba.

    Taarifa ya Habari:Ofisi ya Takwimu ya Australia yazindua kampeni ya tamaduni mbalimbali kabla ya Sensa ya mwezi ujao

    Play Episode Listen Later Jul 7, 2026 14:00


    Ofisi ya Takwimu ya Australia imezindua kampeni ya tamaduni mbalimbali kabla ya Sensa ya mwezi ujao, ikijumuisha matangazo katika lugha 28 tofauti.

    Makala Leo: Wiki ya NAIDOC ni nini, na nini kimejificha nyuma ya kauli mbiu ya mwaka huu?

    Play Episode Listen Later Jul 7, 2026 11:28


    Maadhimisho ya Wiki ya NAIDOC ya Kitaifa yanafanyika kote nchini Australia wiki hii, kwa ajili ya kusherehekea na kutambua historia, utamaduni na mafanikio ya watu wa Asili na wakaazi wa Visiwa vya Torres Strait.

    Makala Leo: Makampuni makubwa ya mtandao wakijamii yatetea sera zao mbele ya Tume ya Kifalme

    Play Episode Listen Later Jul 7, 2026 8:21


    Kampuni kubwa ya mtandao ya kijamii, Meta, ilifika mbele ya Tume ya Kifalme kuhusu Unyanyasaji wa Wayahudi na Uwiano wa Kijamii jana Julai 6, ikitetea rekodi yake ya kukomesha matumizi mabaya mtandaoni.

    Taarifa ya Habari:Tiba ya majaribio ya Ebola yazinduliwa Mashariki mwa DR Congo

    Play Episode Listen Later Jul 6, 2026 6:19


    Raia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamepata matumaini mapya baada ya kuanza kwa majaribio ya dawa mbili zinazolenga kuudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

    SBS Learn Eng Ep 114 Jinsi yakuzungumza kuhusu Sensa na usalama wa data

    Play Episode Listen Later Jul 3, 2026 11:52


    Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu Sensa na usalama wa data?

    Yaliyojiri Afrika:Mvutano wakidiplomasia waiubuka kati ya Ghana, Nigeria na Afrika Kusini

    Play Episode Listen Later Jul 3, 2026 7:24


    Nigeria imesema itaitaka Afrika Kusini ilipe fidia kwa raia wake acha mali na biashara zao baada yaku kimbia nchi hiyo kutoka na maandamano dhidi ya wahamiaji.

    nigeria afrika ghana nigeria
    Mtao "Ukosefu wa utulivu wa kiakili na usimamizi mubovu wa mchezo umezigharimu timu za Afrika"

    Play Episode Listen Later Jul 3, 2026 7:41


    Mashabiki wa timu za Afrika katika Kombe la Dunia la FIFA 2026, walipata pigo kubwa katika siku ya 20 na 21 ya michuano hiyo.

    Taarifa ya Habari:Serikali ya shirikisho yaongeza gharama ya maombi kwa vitengo kadhaa vya visa za Australia kwa asilimia 25

    Play Episode Listen Later Jul 3, 2026 14:08


    Ada ya maombi ya visa ya mwanafunzi imeongezeka tangu Julai 1 kutoka $2,000 hadi $2,500, huku Visa ya Muda ya Uzamili, au visa nambari 485, sasa inagharimu $5,750.

    Ureno yavunja mioyo yawa Kroeshia wakati Uhispania yatinga raundi ya 16

    Play Episode Listen Later Jul 3, 2026 4:20


    Katika Siku ya 22 ya Kombe la Dunia la FIFA, Ureno iliwashinda Kroeshia katika mechi ya mwisho ya Kombe la Dunia ya Luka Modrić, Uhispania ili icharaza Austria, na Uswisi ikaishinda Algeria na kufuzu kwa Raundi ya 16.

    'Elimu kama chombo cha matumaini': Mwanafunzi mkimbizi Alina kuhusu kujenga upya maisha yake nchini Australia

    Play Episode Listen Later Jul 3, 2026 14:55


    Wanafunzi wakimbizi wanajenga upya maisha yao nchini Australia kupitia mpango mpya wa majaribio ya makazi, unaounganisha masomo yao ya chuo kikuu na viwanda ambapo kuna uhaba mkubwa wa wafanyakazi kama vile uuguzi.

    Taarifa ya Habari: Wanafunzi wanane washitakiwa kwa mauaji Kenya

    Play Episode Listen Later Jul 2, 2026 6:45


    Polisi wamewakamata vijana wawili baada ya mvulana wa miaka 15 kuachwa afe nje ya kituo cha matibabu cha jamii mjini Melbourne.

    DR Congo yawapa mamilioni fahari

    Play Episode Listen Later Jul 2, 2026 13:47


    Mwaka huu DR Congo ilimaliza ukame wakuto shiriki katika Kombe la Dunia la FIFA baada ya zaidi ya miaka 50.

    Taarifa ya Habari: Mamilioni ya Waustralia kuamka kesho Julai 1 kwa mishahara ya juu na kodi ya chini ya mapato

    Play Episode Listen Later Jun 30, 2026 13:47


    Bei ya petroli imeshuka hadi viwango ambavyo havijaonekana tangu mwanzo wa 2022. Taasisi ya Petroli ya Australia inasema wastani wa kitaifa wa lita moja ya mafuta yasiyo na risasi ulishuka zaidi ya senti 6 wiki iliyopita - hadi chini kidogo ya dola 1.60.

    Wajerumani na Waholanzi watupwa nje ya Kombe la Dunia 2026

    Play Episode Listen Later Jun 30, 2026 6:04


    Siku ya 19 ya Kombe la Dunia la FIFA ilijumuisha mechi tatu za mchujo zenye ushindani mkali, huku Ujerumani na Uholanzi zikiondolewa baada ya mikwaju ya penati, wakati huo huo Brazil ilinyakua ushindi katika mechi yao muda mfupi kabla ya kipenga cha mwisho.

    Australia Yafafanuliwa: Jinsi yakujiunga na soka jumuishi nchini Australia

    Play Episode Listen Later Jun 30, 2026 14:27


    Sio kutia chumvi tunaposikia kwamba Kombe la Dunia la FIFA lina tarajiwa kuleta dunia pamoja katika mwezi wa Juni. Baada ya yote, mpira wa miguu unajulikana kama mchezo maarufu zaidi duniani.

    Taarifa ya Habari: Mkuu wa jeshi azuia shughuli za Nation Media Group nchini Uganda

    Play Episode Listen Later Jun 29, 2026 4:20


    Shirika kubwa zaidi huru la habari nchini Uganda Nation media group limearifu kuwa limewekwa chini ya ulinzi mkali wa kijeshi mapema Jumapili.

    Baranga"nakaribisha wanaume wote katika kongamano maalum, tujadili maswala muhimu kwetu"

    Play Episode Listen Later Jun 27, 2026 7:28


    Wanaume kutoka jumuiya za Afrika Mashariki wanao ishi jimboni New South Wales, wana jiandaa kwa kongamano maalum Jumamosi 27 Juni 2026.

    Taarifa ya Habari:"Sheria tata za mageuzi ya kodi zitawafaidi watu wengi" asema Mweka Hazina wa Shirikisho

    Play Episode Listen Later Jun 26, 2026 12:37


    Mweka Hazina wa Shirikisho Jim Chalmers anasema wafanyakazi, wanunuzi wa nyumba za kwanza na vizazi vijavyo watafaidika na sheria zenye utata za mageuzi ya kodi ambazo zimepitishwa hivi karibuni bungeni.Polisi warusha mabomu ya kutoa machozi dhidi ya waandamanaji katika maeneo mbalimbali mjini Nairobi huku makundi yanayoongozwa na vijana yakikumbuka miaka miwili tangu maandamano ya Gen Z. Watu kadhaa wametiwa nguvuni kufuatia maandamano hayo. Mawingu mazito ya moshi yalitanda angani huku umati wa watu ukikimbia kujinusuru, wengi wao wakifunika nyuso zao kutokana na harufu kali na madhara ya gesi hiyo.Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.

    Australia yatinga raundi ya 32 baada ya sare yakutofungana dhidi ya Paraguayi

    Play Episode Listen Later Jun 26, 2026 4:39


    Socceroos wamefanikiwa kufika hatua ya mchujo baada ya kupata sare yakutofungana katika Kundi D, wakati Ecuador ikiwaacha wajerumani vinywa wazi katika Kundi E na kufuzu kushiriki katika hatua ya timu bora 32.

    Claim SBS Swahili - SBS Swahili

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel