Listen to interviews, features and community stories from the SBS Radio Swahili program, including news from Australia and around the world. - Sikiza mahojiano, makala na hadithi za jumuiya kutoka Idhaa ya Kiswahili ya SBS Radio, ikijumuisha taarifa za habari kutoka Australia na ulimwenguni.

Je, unajua kwamba zawadi tatu kati ya nne zinazouzwa nchini Australia, kama za asili au zilizotengenezwa kwa mtindo wa Asili zimegundulika kuwa si za kweli?

Salamu za rambirambi zinatolewa kwa Mwanamke aliyekuwa akitoa mwongozo na ushauri katika shirika la habari la SBS kutoka ukoo wa Widjabul Wia-bal, Shangazi Rhoda Roberts, ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 66.

Australia inatafuta kupata uhakikisho wa usambazaji wa nishati kutoka kwa washirika wa biashara wakati kukiwa ongezeko la hofu kuwa nchi zitahifadhi mauzo ya nje ya mafuta kwa ajili ya masoko yao ya ndani.

Marais wa Kenya na Uganda walikutana mjini Kisumu, kuzindua ujenzi uliocheleweshwa wa upanuzi wa reli yenye thamani ya mabilioni ya dola iliyojengwa na China.

Vita katika maeneo ya Mashariki ya Kati, na kufungwa kwa Mlango-Bahari wa Hormuz, kumesababisha kile ambacho wataalamu wanakielezea kama moja ya migogoro mikubwa zaidi ya nishati katika miongo kadhaa.

Serikali ya shirikisho inaagiza Tathmini ya Kitaifa ya Mnyororo wa Ugavi wa Chakula kwa ajili yakulinda sekta ya kilimo ya nchi dhidi ya usumbufu wa kimataifa.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu vyakula vya ajabu?

Waziri Mkuu Anthony Albanese amesema usambazaji wa mafuta nchini Australia uko salama, lakini anataka Australia iwe tayari kupita kiasi linapokuja suala la kudhibiti uhaba wa mafuta nchini humu.

Waziri Mkuu amemteua 'mratibu wa mafuta' kusaidia kushughulikia masuala ya mnyororo wa ugavi yaliyosababishwa na vita katika maeneo ya Mashariki ya Kati.

Waziri Mkuu Anthony Albanese, amteua mratibu wa kitaifa wa mafuta, kushughulikia masuala ya usambazaji.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu mitihani?

Waziri wa Nishati Chris Bowen amehakikishia taifa kwamba usambazaji wa mafuta nchini Australia bado uko salama, huku usafirishaji ukifika kama ilivyopangwa na akiba ya kutosha kuifunika nchi kwa siku 37.

Wanawake kutoka jumuiya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wana jiandaa kwa sherehe maalum ya siku ya wanawake.

Madhara ya vita vya Israel na Marekani dhidi ya Iran, yame anza kushuhudiwa nchini Australia.

Serikali ya Shirikisho imebadilisha hatua nyingine kwa ajili yakushughulikia athari za mgogoro wa usambazaji wa mafuta Australia.

Serikali ya shirikisho ime wasilisha sheria mpya ya kuweka marufuku ya muda, kwa baadhi ya nchi kutumia viza fulani kuja Australia.

Mataifa tajiri zaidi duniani yamekubali kutoa idadi kubwa ya mapipa ya mafuta kutoka akiba ya dharura, kwa ajili ya kupunguza ongezeko kubwa la bei kutokana na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.

Forodha kwa ujumla ndio sehemu ya kwanza ya mawasiliano kwa watu wanaoingia Australia. Maafisa wa Kikosi cha Mpakani cha Australia wako tayari kwenye lango, wakilenga kuweka bidhaa zilizopigwa marufuku nje ya nchi.

Nchini kenya idadi ya waliofariki kutokana na mafuriko yaliosababishwa na mvua kubwa wiki iliopita, imeongezeka kutoka 23 na sasa idadi hiyo imefikia watu 45, kwa mujibu wa taarifa ya polisi nchini humo.

Waziri Mkuu wa Australia amesema serikali itamsaidia yeyote kati ya timu ya soka ya wanawake ya Iran ambaye bado hajaomba hifadhi hapa.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu mitihani?

Wanawake kote duniani walijitokeza mitaani kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, wakitaka kukomeshwa kwa ukosefu wa usawa na ubaguzi.

Mojtaba Khamenei ametangazwa kuwa kiongozi mkuu mpya wa Iran.

Onyo za mafuriko zimewekwa kote jimboni Queensland, wakati hali ya hewa ya kitropiki inatabiriwa kufika pwani mchana wa leo kati ya miji ya Cairns na Townsville.

Kupata mahali pa kuishi pazuri na pa bei nafuu kunazidi kuwa vigumu kwa watu wengi kote Australia.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu mitihani?

Waziri wa Mambo ya Nje wa Australia Penny Wong amesema dunia ina wasiwasi kuhusu jinsi Iran inavyo jibu mashambulizi ya Marekani na Israel yaliyomuua kiongozi wake, Ayatollah Khamenei na kulenga miundombinu ya nyuklia.

Siku kadhaa baada ya Israel na Marekani kuanza mashambulizi yao dhidi ya Iran, wachambuzi wame anza kuelezea madhara ya vita hivyo katika kanda hiyo na duniani kote kwa ujumla.

Waziri wa Ulinzi Richard Marles amethibitisha kwamba Australia haishiriki katika hatua za kijeshi zinazoendelea dhidi ya Iran.

Viongozi kadhaa wa bara la Afrika wameungana na Muungano wa Afrika kulaani vita vinavyo endelezwa na Marekani na Israel dhidi ya Iran.

Wairani-Waaustralia wanaelezea hisia mseto kuhusu mashambulizi ya Marekani na Israel nchini Iran, pamoja na mauaji ya Kiongozi Mkuu Ayatollah Ali Khamenei.

Mchakato unaendelea kuamua ni nani atakaye iongoza Iran, baada ya kuuawa kwa kiongozi mkuu wa nchi hiyo, Ayatollah Ali Khamenei.

Wizara ya afya Tanzania imesema kuwa maambukizi ya wagonjwa wa mafua makali ya Influenza na Uviko-19 yameongezeka na kuwataka wananchi kuchukua hatua stahiki za kujikinga na maambukizi hayo.

Kuondolewa kwa dharura kwa Waziri Mkuu kutoka nyumbani kwake mjini Canberra kwa sababu ya tisho la bomu lililolengwa, kumesababisha maonyo ya kuongezeka kwa mazingira ya usalama, ambapo uadui mtandaoni unazidi kujitokeza kama vitisho vya kimwili vyenye madhara makubwa.

Mvua kubwa imesababisha mafuriko ya ghafla katika sehemu za Sydney usiku kucha wa Alhamisi hadi Ijumaa, wafanyakazi wakujitolea wa S-E-S wakitoa huduma za uokoaji 44 za maji ya haraka.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kuchumbiana mtandaoni?

Kwa wanafunzi wa kimataifa wanaosomea nchini Australia, kupata huduma ya afya mara nyingi huonekana kama swala ghali sana... au la kutatanisha sana kuweza kuipitia.

Polisi wanaamini kuna watu wengi zaidi wanaohusika, katika utekaji nyara na mauaji ya babu mmoja wa Sydney Chris Baghsarian.

Serikali ya Sudan inayoungwa mkono na jeshi imekosoa UIganda kwa kumkaribisha mkuu wa wanamgambo wa RSF Mohamed Hamdan Daglo maarufu kama Hemeti.

Kama ume ishi kwa muda wowote nchini Australia, labda umegundua jinsi maisha yalivyo na utulivu.

Ripoti ya kwanza ya kitaifa kuhusu ubaguzi wa rangi katika vyuo vikuu nchini Australia imegundua kuwa ni tatizo lililo enea na la kimfumo.

Australia's hot, dry climate and unique landscapes make it one of the most bushfire-prone countries in the world. As climate change drives higher temperatures and drier conditions, we can expect more frequent and more intense bushfires in the future. But once the fire is out, how do you return home safely, find support, and look after yourself? - Hali ya mazingira ya joto, ukavu pamoja na mandhari yakipekee, hufanya Australia iwe mojawapo ya nchi zinazo kabiliwa na moto wa vichaka zaidi dunini. Mabadiliko ya tabianchi yanapo sababisha ongezeko ya hali ya joto na mazingira ya ukame, tunaweza tarajia moto ya vichaka mikali zaidi mara kwa mara katika siku za usoni. Ila moto unapo zimwa, unaweza rudi nyumbani salama, pata msaada na kujihudumia?

Sehemu nyingi za Australia ziko katika hali ya juu ya tahadhari, hali mbaya ya hewa na mvua zikiendelea kuathiri jamii na kuharibu njia muhimu za usafiri.

Takriban idadi yawa Kenya 1,000 wameajiriwa kupigania Urusi, kulingana na ripoti ya ujasusi ya Kenya inayoelezea mtandao wa maafisa wahalifu wanaodaiwa kushirikiana na makundi ya biashara haramu ya binadamu.

Serikali ya New South Wales inachunguza mazingira yaliyozunguka kutoroka kwa wagonjwa wawili kutoka hospitali moja, ambao siku chache baadaye walidaiwa kuhusika katika matukio tofauti ambapo watu watatu walifariki.

Mwezi mtukufu wa Ramadan ume anza, Waislamu kote duniani wakisherehekea Iftar katika siku ya pili ya kipindi cha mfungo.

Andrew Mountbatten-Windsor ameachiliwa huru chini ya uchunguzi baada ya polisi wa Uingereza kumhoji kwa saa muda wa masaa 12 kwa tuhuma za utovu wa nidhamu katika ofisi ya umma.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kuchumbiana mtandaoni?

Ripoti mpya ya kiuchumi inaonya Australia ina elekea kupoteza hadhi yake, kama taifa lenye deni la chini, huku mikopo ya serikali ikifikia viwango ambavyo havija onekana tangu vita vya pili vya dunia.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kuchumbiana mtandaoni?

Angus Taylor amechukua uongozi wa chama cha Liberal katika kura ya maamuzi ya chama chake kwa ushindi thabiti wa kura 34 dhidi ya 17 zilizotolewa kwa aliyekuwa kiongozi wake.