SBS Swahili - SBS Swahili

Follow SBS Swahili - SBS Swahili
Share on
Copy link to clipboard

Listen to interviews, features and community stories from the SBS Radio Swahili program, including news from Australia and around the world. - Sikiza mahojiano, makala na hadithi za jumuiya kutoka Idhaa ya Kiswahili ya SBS Radio, ikijumuisha taarifa za habari kutoka Australia na ulimwenguni.

SBS Swahili


    • Aug 17, 2026 LATEST EPISODE
    • daily NEW EPISODES
    • 12m AVG DURATION
    • 2,138 EPISODES


    Search for episodes from SBS Swahili - SBS Swahili with a specific topic:

    Latest episodes from SBS Swahili - SBS Swahili

    Taarifa ya Habari:Wafanyakazi wa kusambaza vyakula kuongezewa mshahara kuanzia leo

    Play Episode Listen Later Aug 17, 2026 5:35


    Takriban idadi yawa Australia 250,000 wanaosafirisha vyakula kutoka hotelini na dukani kwa ajili ya kujikimu, wanatarajiwa kupokea mshahara wa chini kisheria kwa mara ya kwanza.

    Makala Leo:Serikali kuwekeza mamilioni katika nyumba za waathiriwa wa unyanyasaji wa majumbani; lakini je, inatosha?

    Play Episode Listen Later Aug 14, 2026 11:36


    Mgogoro wa makazi ukiendelea, vurugu za kifamilia na majumbani (DFSV) ndio sababu kuu ya wanawake na watoto kuondoka nyumbani kwao na kukosa makazi.

    SBS Learn Eng Ep 117 Jinsi yakuzungumza kuhusu kukopa vitabu

    Play Episode Listen Later Aug 14, 2026 15:27


    Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kukopa vitabu katika maktaba?

    Taarifa ya Habari:Ripoti ya mwisho kuhusu mabadiliko yaliyopendekezwa na Serikali kwa Mpango wa Kitaifa wa Bima ya Ulemavu itawasilishwa Bungeni

    Play Episode Listen Later Aug 14, 2026 15:52


    Ripoti ya mwisho kuhusu mabadiliko yaliyopendekezwa na Serikali kwa Mpango wa Kitaifa wa Bima ya Ulemavu itawasilishwa Bungeni leo. Uchunguzi huo ulizinduliwa katika mwezi Mei ili kuchunguza mapendekezo ya Serikali, ya kuokoa karibu dola bilioni 38 kwa kipindi cha miaka minne.

    Yaliyojiri Afrika: Uganda na Tanzania za zindua ushirikiano wa nishati

    Play Episode Listen Later Aug 14, 2026 6:59


    Bandari ya Tanga itakuwa kitovu muhimu cha nishati katika jumuiya ya Afrika Mashariki, chini ya ushirikiano mpya wa nishati uliozinduliwa kati ya serikali ya Uganda na Tanzania.

    Makala Leo:Sensa imekwisha ila, bado hauja chelewa kama hauja jaza fomu yako

    Play Episode Listen Later Aug 14, 2026 6:49


    Sensa ya 2026 imekwisha na idadi kubwa ya Waaustralia walikamilisha utafiti huo mtandaoni.

    Taarifa ya Habari:Serikali yawahakikishia watu kwamba Sensa itakuwa salama

    Play Episode Listen Later Aug 11, 2026 13:24


    Serikali inawahakikishia watu kwamba Sensa itakuwa salama, kufuatia visa vya hivi karibuni vya roboti za AI kufanya ujambazi na uvunjaji wa data katika mashirika makubwa.

    Yaliyojiri Afrika:Wanariadha wa Uganda watoweka Scotland

    Play Episode Listen Later Aug 11, 2026 7:58


    Mabondia wanne wa timu ya Uganda, wametoweka baada yakufeli kujitokeza kwa safari zao za ndege zakurejea nyumbani, baada ya kushiriki katika michezo ya jumuiya yamadola mjini Glasgow.

    Makala Leo: Watetezi wa ulemavu waomba mlinzi nakuonya kuhusu 'athari kubwa' mageuzi yanapokaribia

    Play Episode Listen Later Aug 11, 2026 9:10


    Watetezi wa ulemavu wanaihimiza serikali kufikiria upya mabadiliko ya Mpango wa Kitaifa wa Bima ya Ulemavu unao julikana kama NDIS, kabla ya kura ya bunge inayokaribia kuhusu mageuzi yaliyopendekezwa.

    Taarifa ya Habari:Wafanya biashara waomba ushirikiano na serikali kabla ifanye mabadiliko katika uhamiaji

    Play Episode Listen Later Aug 10, 2026 6:09


    Vikundi vya wafanyabiashara vinaihimiza serikali ya shirikisho kushirikiana nao, katika mashauriano kabla ya mabadiliko yoyote makubwa kutangazwa kuhusu sera ya uhamiaji.

    Taarifa ya Habari:Ofisi ya takwimu ya Australia yahimiza wanao ishi katika nyumba zenye watu wengi wasiwe na hofu kushiriki katika sensa

    Play Episode Listen Later Aug 7, 2026 12:52


    Usiku wa sensa ukikaribia, maafisa wa Ofisi ya Takwimu ya Australia wanawahimiza watu wanao ishi katika makaazi yenye watu wengi sana, wasiwe na hofu yakushiriki kwa sababu hapatakuwa athari yoyote ya kisheria.

    What are my rights if stopped by police in Australia? - Australia Yafafanuliwa:Haki zangu ni zipi kama nitasimamishwa na polisi nchini Australia?

    Play Episode Listen Later Aug 7, 2026 13:43


    Police officers have a range of operational powers they can exercise under legislation, including to ask questions, give ‘move on' directions and conduct searches. Here's what you need to know about your basic rights and obligations in a police interaction. - Maafisa wa jeshi la polisi wana mamlaka mbalimbali ya kiutendaji ambayo wanaweza kuyatumia chini ya sheria, ikiwa ni pamoja na kuuliza maswali, kutoa maelekezo ya 'kutoka ulipo' na kufanya upekuzi. Haya ndiyo unayohitaji kujua kuhusu haki na wajibu wako wa msingi katika mwingiliano wa polisi.

    SBS Learn Eng Ep 116 Jinsi yakuzungumza kuhusu kumtembelea daktari wa wanyama

    Play Episode Listen Later Aug 7, 2026 15:22


    Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kumtembelea daktari wa wanyama?

    Taarifa ya Habari:Mfanyabiashara afariki mjini Melbourne baada ya tukio linalo shukiwa kutekelezwa na wezi

    Play Episode Listen Later Aug 7, 2026 5:15


    Mfanyabiashara mmoja wa duka mjini Melbourne amefariki baada ya kushambuliwa alipokuwa akijaribu kuzuia kundi la vijana walio kuwa waki iba dukani.

    Yaliyojiri Afrika: DRC yaadhimisha GENOCOST

    Play Episode Listen Later Aug 4, 2026 7:38


    Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Félix Tshisekedi, ameongoza kumbukumbuku ya mauaji ya GENOCOST jijini Kinshasa, inayofanyika kila tarehe 2 mwezi Agosti.

    Taarifa ya Habari:Mamia ya watu wakimbia mapigano Tigray na kuingia Sudan

    Play Episode Listen Later Aug 4, 2026 13:24


    Mamia yawa Ethiopia kutoka eneo la kaskazini mwa Tigray, wamevuka mpaka na kuingia nchi jirani ya Sudan katika siku mbili zilizopita, wakikimbia mapigano karibu na mpaka.

    Makala Leo:Australia inakabiliwa na 'tsunami ya uharibifu' mkubwa kutokana na mlipuko wa virusi vya homa ya ndege H5

    Play Episode Listen Later Aug 4, 2026 11:30


    Jimbo la Kusini Australia huenda linakabiliwa na tukio la kwanza la vifo vingi vya wanyamapori nchini Australia linalohusishwa na homa ya ndege ya H5N1.

    Makala Leo:Benki ya Hifadhi yasema wa Australia wengi hawa elewi jinsi viwango vya riba vinavyofanya kazi

    Play Episode Listen Later Aug 4, 2026 8:05


    Kiwango cha mfumuko wa bei nchini Australia kimepungua, lakini shinikizo la bei la msingi linabaki kuwa juu sana.

    Taarifa ya Habari

    Play Episode Listen Later Aug 3, 2026 5:09


    Mdhibiti wa ushindani [[ACCC]] ameombwa na serikali ya shirikisho kufuatilia vituo vya mafuta kwa matukio yoyote ya kupunguzwa kwa bei - sasa kwa kuwa punguzo la muda la ushuru wa mafuta limeisha.Visa 74 vya aina ya H-5 ya homa ya ndege vimethibitishwa nchini Australia.Hiyo inajumuisha uthibitisho wa tukio la kwanza la vifo vingi humu nchini kutokana na virusi hivyo Kusini mwa Australia.Mji wa Ceuta mwishoni mwa juma haukuonekana tena kama jiji lililokuwa na wasiwasi, lakini wakazi bado walikuwa wameshtushwa na matukio ya wiki. Wengi wa wahamiaji 60,000 walioingia Ceuta wamerudi Morocco.Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.

    Taarifa ya Habari:Kiongozi wa Victoria, ajiuzulu baada ya siku kadhaa za shinikizo dhidi ya uongozi wake

    Play Episode Listen Later Jul 28, 2026 14:42


    Jacinta Allan amejiuzulu kama Kiongozi wa Victoria, akisema ni uamuzi sahihi kwa Wa-Victoria. Tangazo hilo limekuja nusu saa tu baada ya changamoto inayotarajiwa ya uongozi katika mkutano uliopangwa wa chama cha wabunge, kuashiria kurudi kwa bunge la jimbo.

    Australia Yafafanuliwa:Tamasha ya Garma ni nini, na kwa nini ni muhimu?

    Play Episode Listen Later Jul 28, 2026 10:45


    Kila mwaka, maelfu ya watu husafiri kwenda katika jamii ya kijijini kaskazini mashariki mwa Arnhem Land katika Eneo la Kaskazini.

    Makala Leo: Jacinta Allan akataa kujiuzulu, pambano la uongozi wa chama cha Labor cha Victoria likiongezeka kasi

    Play Episode Listen Later Jul 28, 2026 11:00


    Kiongozi wa Jimbo la Victoria, Jacinta Allan, anasema atapambana na changamoto ya uongozi inayokuja baada ya viongozi wa mirengo tafuati ndani ya chama cha Labor, kukutana na kukubaliana kwamba amepoteza uungwaji mkono wa wengi katika mkutano wao.

    Taarifa ya Habari: Kiongozi wa Victoria asisitiza hajiuzulu!

    Play Episode Listen Later Jul 27, 2026 5:00


    Kiongozi wa jimbo la Victoria, Jacinta Allan, anasema hatajiuzulu kutoka wadhifa wake, miezi minne kabla ya uchaguzi wa jimbo hilo.

    Yaliyojiri Afrika:Kenya yapokea tani 4.5 zavifaa vya matibabu vya Ebola kutoka India

    Play Episode Listen Later Jul 24, 2026 7:44


    Kenya imepokea shehena ya kwanza ya tani 4.5 za vifaa vya matibabu kutoka kwa serikali ya India, ili kuimarisha uwezo wa nchi kujiandaa kukabiliana na uwezekano wa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

    Taarifa ya Habari: Hatua ya Marekani kuongeza ushuru kwa mauzo ya nje ya Australia yazua ukosoaji

    Play Episode Listen Later Jul 24, 2026 13:33


    Utawala wa Trump umeongeza ushuru kwa mauzo ya nje ya Australia kutoka asilimia 10 hadi 12.5, huku kiwango kipya kikianza kutumika alasiri ya leo Ijumaa.

    Makala Leo:Nini cha kutarajia kutoka kwa mfumo mpya wa tahadhari ya dharura wa Australia

    Play Episode Listen Later Jul 24, 2026 15:16


    Australia inajiandaa kuanzisha mfumo mpya wa kitaifa wa tahadhari ya dharura, ulioundwa kutoa tahadhari muhimu haraka na kwa uhakika zaidi wakati wa majanga.

    Makala Leo:China yaambia Australia iache kuzungumzia Bahari ya Kusini mwa China wakati mvutano ukiongezeka katika Mkutano wa ASEAN

    Play Episode Listen Later Jul 24, 2026 10:03


    Mkutano wa Kikanda wa ASEAN unakamilika mjini Manila, ambapo Australia imeibua wasiwasi kuhusu hatua za kijeshi za China katika eneo hilo.

    Taarifa ya Habari:Waziri Mkuu ataka chama cha Labor, kijitolee kupunguza shinikizo za gharama ya maisha

    Play Episode Listen Later Jul 23, 2026 6:25


    Waziri Mkuu Anthony Albanese, amesisitiza kujitolea kwa chama chake kupunguza shinikizo la gharama la maisha katika mkutano wa kitaifa wa chama tawala.

    Yaliyojiri Afrika:Kituo chakujitenga cha Ebola nchini Kenya cha wapokea wamarekani 7 kutoka DRC

    Play Episode Listen Later Jul 23, 2026 7:24


    Wahudumu7 wamisaada kutoka wamarekani walikuowa wakisaida kupambana na Ebola DRC, wamewekwa katika kituo cha karantini nchini Kenya.

    SBS Learn Eng Ep 115 Jinsi yakuzungumza kuhusu kufanya kazi ya ziada

    Play Episode Listen Later Jul 21, 2026 11:11


    Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kufanya kazi ya ziada?

    Taarifa ya Habari:Waziri Wong aelekea katika kongamano lamawaziri wa mambo ya nje wa ASEAN kuimarisha uhusiano wa Australia na nchi wanachama

    Play Episode Listen Later Jul 21, 2026 13:03


    Waziri wa Mambo ya Nje Penny Wong anatarajiwa kwenda Ufilipino kuhudhuria Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Asia Mashariki na Jukwaa la Kikanda la ASEAN.Tume ya Dhamana na Uwekezaji ya Australia inasema imepata rekodi ya dola milioni 830 katika amri za adhabu za kiraia wakati wa Mwaka wa Fedha wa 2025-2026. Tume hiyo ilianzisha chunguzi zaidi ya 250, ambazo zilisababisha hatia 25 za jinai na watu 11 kuhukumiwa kifungo cha gerezani.Karibu watu 930 wamefariki dunia kutokana na Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, hii ikiwa ni kulingana na Wizara ya afya nchini humo. Vifo hivyo vimerekodiwa miongoni mwa visa 2,344 vya maambukizi vilivyothibitishwa hadi siku ya Jumamosi imesema wizara hiyo hii leo. Vifo vipya vilirekodiwa katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita, idadi ya juu kabisa kuwahi kurekodiwa kwa siku moja.Meli ya mafuta yenye bendera ya Tanzania imetekwa nyara na maharamia wanaoshukiwa kuwa wa Somalia katika pwani ya Yemen, vimebaini vyanzo vya usalama na maafisa wa eneo hilo kuhusu tukio hilo. Meli hiyo imehamishwa hadi majini katika eneo la Bari kaskazini mashariki mwa Somalia, kulingana na maafisa wa eneo hilo.

    Australia Yafafanuliwa:Kijana wangu anaweza anza kufanya kazi lini nchini Australia?

    Play Episode Listen Later Jul 21, 2026 12:25


    Kuanza kazi ya muda mfupi kunaweza kuwa uzoefu wenye maana kwa kijana, kuongeza kujithamini kwake, kumsaidia kujifunza ujuzi mpya na kupata pesa zake za kwanza.

    Makala Leo:Mazoezi muhimu yakimataifa yajeshi yaanza katika Wilaya ya Kaskazini

    Play Episode Listen Later Jul 21, 2026 7:03


    Zoezi kubwa zaidi la kimataifa la Jeshi la Anga la Australia, linaendelea katika Eneo la Kaskazini na litafanyika kwa wiki tatu zijazo.

    Taarifa ya Habari:Greens wataka makampuni ya mawasiliano nchini kutoa huduma yakuaminika kwa wateja

    Play Episode Listen Later Jul 20, 2026 4:49


    Chama cha Greens kinatoa wito wa mageuzi ambayo kisheria yatahitaji kampuni zama wasiliano kama Telstra, Optus na Vodafone kutoa huduma ya kuaminika kwa wateja.

    Makala Leo: Mitandao ya teknolojia yaambiwa irekebishe pengo za ulaghai wakujamiana

    Play Episode Listen Later Jul 17, 2026 11:22


    Kamishna wa Usalama Mtandaoni wa Australia anatoa tahadhari kuhusu ulaghai wa kingono mtandaoni, baada ya kupokea malalamiko zaidi ya 2,000 katika miezi sita tu.

    Taarifa ya Habari:Watoto wa Australia kuanza kuamua katika shule ya msingi kama watafuata taaluma za sayansi na teknolojia kwa msaada wa wazazi

    Play Episode Listen Later Jul 17, 2026 14:12


    Utafiti mpya unaonyesha kuwa watoto wa Australia wanaweza kuanza kuamua katika shule ya msingi kama watafuata taaluma za sayansi na teknolojia wanapokuwa wakubwa, huku wazazi wakiwa na ushawishi zaidi kuliko walimu katika maamuzi hayo.

    Makala Leo: Argentina na Uhispania zaishi ndoto zakipekee za Kombe la Dunia

    Play Episode Listen Later Jul 17, 2026 5:07


    Argentina na Uhispania wanaishi ndoto ya kipekee ya Kombe la Dunia, baada yakutinga fainali ya kombe hilo. Mjini Buenos Aires na Madrid, mashabiki wanachangia jinsi walivyopitia tamthilia, hisia na sherehe.

    Taarifa ya Habari:Ombi latolewa kuharamisha matamshi ya chuki dhidi yawa Aboriginal na wakaazi wa Torres Strait

    Play Episode Listen Later Jul 16, 2026 5:20


    Kuna wito wa kuharamisha matamshi ya chuki dhidi yawa Aboriginal na watu kutoka Visiwa vya Torres Strait, huku vikao vikiendelea katika uchunguzi wa ubaguzi wa rangi wa Serikali ya Shirikisho huko Darwin.

    Makala Leo:Ufaransa na Uhispania tayari kwa pambano la nusu fainali

    Play Episode Listen Later Jul 14, 2026 5:41


    Nusu fainali za Kombe la Dunia zimewadia, Ufaransa na Uhispania zikijiandaa kufufua moja ya ushindani mkubwa wa soka la kimataifa. Tunaangalia kwa karibu habari za hivi punde za timu hizo na kusikia kutoka kwa kambi zote mbili kabla ya pambano kubwa la kesho.

    Taarifa ya Habari:Vyuo vikuu kukabiliwa na faini kubwa vikishindwa kupambana na ubaguzi wa rangi

    Play Episode Listen Later Jul 14, 2026 13:56


    Serikali ya Shirikisho inasema vyuo vikuu vinaweza kukabiliwa na faini ikiwa vitashindwa kupambana na ubaguzi wa rangi chini ya viwango vipya vilivyoanzishwa Jumatatu 13 Julai 2026.

    Makala Leo:Kusini Australia yatoa mpango wakupiga marufuku wahalifu wa vurugu kutoka programu zakuchumbiana

    Play Episode Listen Later Jul 14, 2026 10:50


    Jimbo la Kusini Australia limefichua mpango wa kwanza wa kupiga marufuku vurugu za majumbani na wahalifu wa kujamiana kutoka kwa programu za kuchumbiana.

    Makala Leo:Mashambulizi mapya yashuhudiwa Iran na Marekani zikibishana kuhusu kufunguliwa kwa Hormuz

    Play Episode Listen Later Jul 14, 2026 10:22


    Marekani na Iran zimebadilishana wimbi jingine la mashambulizi, huku mapigano yakiongezeka kuhusu Mlango-Bahari wa Hormuz yakisukuma makubaliano ya kidiplomasia ya mwezi uliopita karibu kuvunjika.

    Taarifa ya Habari:Daglo na maafisa wengine wa RSF wahukumiwa adhabu ya kifo

    Play Episode Listen Later Jul 13, 2026 5:22


    Mahakama ya Kupambana na Ugaidi na Makosa Dhidi ya Taifa iliyoko mjini Port Sudan nchini Sudan, , imemhukumu kifo kiongozi wa kundi la wanamgambo wa RSF, Mohamed Hamdan Daglo pamoja na maafisa wengine 15 wa RSF.

    Yaliyojiri Afrika: Usalama waimarishwa katika mitaa ya Tanzania

    Play Episode Listen Later Jul 10, 2026 7:47


    Usalama unaendelea kuimarishwa katika miji mikubwa ya Tanzania, maafisa wa Polisi na Jeshi wenye silaha wakifanya doria.

    Mbappé aiweka Ufaransa katika nusu fainali

    Play Episode Listen Later Jul 10, 2026 4:16


    Ufaransa imetinga nusu fainali ya Kombe la Dunia, baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Morocco. Kylian Mbappé amefunga mabao nane sawa na Lionel Messi, wakati Ousmane Dembélé akikamilisha ushindi huo.

    Taarifa ya Habari:Polisi wachunguza kama kifo katika jimbo la Kusini Australia, kina husishwa na kupotea kwa huduma za Telstra Jumatano

    Play Episode Listen Later Jul 10, 2026 14:24


    Polisi wanachunguza kama kifo kinahusishwa na kupotezwa kwa huduma ya Telstra kote nchini Jumatano. Wapelelezi wa Kusini Australia wamethibitisha mtu mmoja alifariki katika hospitali ya kanda Jumatano, lakini polisi hawakuwa wamearifiwa kuhusu kifo hicho.

    Australia Yafafanuliwa: Sensa ya 2026: Unacho stahili jua kuhakikisha una hesabiwa

    Play Episode Listen Later Jul 10, 2026 12:16


    Sensa ya 2026 itafanyika Jumanne tarehe 11 Agosti na kila mtu nchini Australia usiku huu lazima ahesabiwe.

    Makala Leo: Waziri Mkuu Albanese aendeleza msukumo wake wakidiplomasia katika Pasifiki

    Play Episode Listen Later Jul 10, 2026 11:51


    Waziri Mkuu Anthony Albanese ameweka ratiba kabambe ya mkataba mpya kamili na Visiwa vya Solomon, akisema angependa kuuona ukikamilika mwishoni mwa mwaka huu.

    Taarifa ya Habari:Unyanyasaji wa kingono unaendelea kutumiwa kama silaha ya kivita DRC

    Play Episode Listen Later Jul 9, 2026 6:18


    Mamlaka katika jimbo la Kusini Australia, zimethibitisha kisa cha pili cha homa ya ndege aina ya H5 katika jimbo hilo.

    Chiry"wasichana wenzangu njooni tuboreshe afya zetu kupitia mpira"

    Play Episode Listen Later Jul 7, 2026 9:01


    Jamii ya wakenya wanao ishi mjini Sydney, NSW walishuhudia historia ikiandikwa jioni ya Jumapili 28 Juni 2026 timu mpya ya mpira wa miguu ya kina dada ilipo cheza mechi yao ya kwanza katika uwanja wa Rydalmere.

    Uhispania na Ubelgiji za tinga robo fainali wakati Ronaldo aaga Kombe la Dunia

    Play Episode Listen Later Jul 7, 2026 4:51


    Uhispania na Ubelgiji zimefuzu kwa robo fainali, wakati ndoto za Kombe la Dunia za wenyeji Marekani na Ureno ya Cristiano Ronaldo ziki gonga miamba.

    Claim SBS Swahili - SBS Swahili

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel