Listen to interviews, features and community stories from the SBS Radio Swahili program, including news from Australia and around the world. - Sikiza mahojiano, makala na hadithi za jumuiya kutoka Idhaa ya Kiswahili ya SBS Radio, ikijumuisha taarifa za habari kutoka Australia na ulimwenguni.

Jacinta Allan amejiuzulu kama Kiongozi wa Victoria, akisema ni uamuzi sahihi kwa Wa-Victoria. Tangazo hilo limekuja nusu saa tu baada ya changamoto inayotarajiwa ya uongozi katika mkutano uliopangwa wa chama cha wabunge, kuashiria kurudi kwa bunge la jimbo.

Kila mwaka, maelfu ya watu husafiri kwenda katika jamii ya kijijini kaskazini mashariki mwa Arnhem Land katika Eneo la Kaskazini.

Kiongozi wa Jimbo la Victoria, Jacinta Allan, anasema atapambana na changamoto ya uongozi inayokuja baada ya viongozi wa mirengo tafuati ndani ya chama cha Labor, kukutana na kukubaliana kwamba amepoteza uungwaji mkono wa wengi katika mkutano wao.

Kiongozi wa jimbo la Victoria, Jacinta Allan, anasema hatajiuzulu kutoka wadhifa wake, miezi minne kabla ya uchaguzi wa jimbo hilo.

Kenya imepokea shehena ya kwanza ya tani 4.5 za vifaa vya matibabu kutoka kwa serikali ya India, ili kuimarisha uwezo wa nchi kujiandaa kukabiliana na uwezekano wa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

Utawala wa Trump umeongeza ushuru kwa mauzo ya nje ya Australia kutoka asilimia 10 hadi 12.5, huku kiwango kipya kikianza kutumika alasiri ya leo Ijumaa.

Australia inajiandaa kuanzisha mfumo mpya wa kitaifa wa tahadhari ya dharura, ulioundwa kutoa tahadhari muhimu haraka na kwa uhakika zaidi wakati wa majanga.

Mkutano wa Kikanda wa ASEAN unakamilika mjini Manila, ambapo Australia imeibua wasiwasi kuhusu hatua za kijeshi za China katika eneo hilo.

Waziri Mkuu Anthony Albanese, amesisitiza kujitolea kwa chama chake kupunguza shinikizo la gharama la maisha katika mkutano wa kitaifa wa chama tawala.

Wahudumu7 wamisaada kutoka wamarekani walikuowa wakisaida kupambana na Ebola DRC, wamewekwa katika kituo cha karantini nchini Kenya.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kufanya kazi ya ziada?

Waziri wa Mambo ya Nje Penny Wong anatarajiwa kwenda Ufilipino kuhudhuria Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Asia Mashariki na Jukwaa la Kikanda la ASEAN.Tume ya Dhamana na Uwekezaji ya Australia inasema imepata rekodi ya dola milioni 830 katika amri za adhabu za kiraia wakati wa Mwaka wa Fedha wa 2025-2026. Tume hiyo ilianzisha chunguzi zaidi ya 250, ambazo zilisababisha hatia 25 za jinai na watu 11 kuhukumiwa kifungo cha gerezani.Karibu watu 930 wamefariki dunia kutokana na Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, hii ikiwa ni kulingana na Wizara ya afya nchini humo. Vifo hivyo vimerekodiwa miongoni mwa visa 2,344 vya maambukizi vilivyothibitishwa hadi siku ya Jumamosi imesema wizara hiyo hii leo. Vifo vipya vilirekodiwa katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita, idadi ya juu kabisa kuwahi kurekodiwa kwa siku moja.Meli ya mafuta yenye bendera ya Tanzania imetekwa nyara na maharamia wanaoshukiwa kuwa wa Somalia katika pwani ya Yemen, vimebaini vyanzo vya usalama na maafisa wa eneo hilo kuhusu tukio hilo. Meli hiyo imehamishwa hadi majini katika eneo la Bari kaskazini mashariki mwa Somalia, kulingana na maafisa wa eneo hilo.

Kuanza kazi ya muda mfupi kunaweza kuwa uzoefu wenye maana kwa kijana, kuongeza kujithamini kwake, kumsaidia kujifunza ujuzi mpya na kupata pesa zake za kwanza.

Zoezi kubwa zaidi la kimataifa la Jeshi la Anga la Australia, linaendelea katika Eneo la Kaskazini na litafanyika kwa wiki tatu zijazo.

Chama cha Greens kinatoa wito wa mageuzi ambayo kisheria yatahitaji kampuni zama wasiliano kama Telstra, Optus na Vodafone kutoa huduma ya kuaminika kwa wateja.

Kamishna wa Usalama Mtandaoni wa Australia anatoa tahadhari kuhusu ulaghai wa kingono mtandaoni, baada ya kupokea malalamiko zaidi ya 2,000 katika miezi sita tu.

Utafiti mpya unaonyesha kuwa watoto wa Australia wanaweza kuanza kuamua katika shule ya msingi kama watafuata taaluma za sayansi na teknolojia wanapokuwa wakubwa, huku wazazi wakiwa na ushawishi zaidi kuliko walimu katika maamuzi hayo.

Argentina na Uhispania wanaishi ndoto ya kipekee ya Kombe la Dunia, baada yakutinga fainali ya kombe hilo. Mjini Buenos Aires na Madrid, mashabiki wanachangia jinsi walivyopitia tamthilia, hisia na sherehe.

Kuna wito wa kuharamisha matamshi ya chuki dhidi yawa Aboriginal na watu kutoka Visiwa vya Torres Strait, huku vikao vikiendelea katika uchunguzi wa ubaguzi wa rangi wa Serikali ya Shirikisho huko Darwin.

Nusu fainali za Kombe la Dunia zimewadia, Ufaransa na Uhispania zikijiandaa kufufua moja ya ushindani mkubwa wa soka la kimataifa. Tunaangalia kwa karibu habari za hivi punde za timu hizo na kusikia kutoka kwa kambi zote mbili kabla ya pambano kubwa la kesho.

Serikali ya Shirikisho inasema vyuo vikuu vinaweza kukabiliwa na faini ikiwa vitashindwa kupambana na ubaguzi wa rangi chini ya viwango vipya vilivyoanzishwa Jumatatu 13 Julai 2026.

Jimbo la Kusini Australia limefichua mpango wa kwanza wa kupiga marufuku vurugu za majumbani na wahalifu wa kujamiana kutoka kwa programu za kuchumbiana.

Marekani na Iran zimebadilishana wimbi jingine la mashambulizi, huku mapigano yakiongezeka kuhusu Mlango-Bahari wa Hormuz yakisukuma makubaliano ya kidiplomasia ya mwezi uliopita karibu kuvunjika.

Mahakama ya Kupambana na Ugaidi na Makosa Dhidi ya Taifa iliyoko mjini Port Sudan nchini Sudan, , imemhukumu kifo kiongozi wa kundi la wanamgambo wa RSF, Mohamed Hamdan Daglo pamoja na maafisa wengine 15 wa RSF.

Usalama unaendelea kuimarishwa katika miji mikubwa ya Tanzania, maafisa wa Polisi na Jeshi wenye silaha wakifanya doria.

Ufaransa imetinga nusu fainali ya Kombe la Dunia, baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Morocco. Kylian Mbappé amefunga mabao nane sawa na Lionel Messi, wakati Ousmane Dembélé akikamilisha ushindi huo.

Polisi wanachunguza kama kifo kinahusishwa na kupotezwa kwa huduma ya Telstra kote nchini Jumatano. Wapelelezi wa Kusini Australia wamethibitisha mtu mmoja alifariki katika hospitali ya kanda Jumatano, lakini polisi hawakuwa wamearifiwa kuhusu kifo hicho.

Sensa ya 2026 itafanyika Jumanne tarehe 11 Agosti na kila mtu nchini Australia usiku huu lazima ahesabiwe.

Waziri Mkuu Anthony Albanese ameweka ratiba kabambe ya mkataba mpya kamili na Visiwa vya Solomon, akisema angependa kuuona ukikamilika mwishoni mwa mwaka huu.

Mamlaka katika jimbo la Kusini Australia, zimethibitisha kisa cha pili cha homa ya ndege aina ya H5 katika jimbo hilo.

Jamii ya wakenya wanao ishi mjini Sydney, NSW walishuhudia historia ikiandikwa jioni ya Jumapili 28 Juni 2026 timu mpya ya mpira wa miguu ya kina dada ilipo cheza mechi yao ya kwanza katika uwanja wa Rydalmere.

Uhispania na Ubelgiji zimefuzu kwa robo fainali, wakati ndoto za Kombe la Dunia za wenyeji Marekani na Ureno ya Cristiano Ronaldo ziki gonga miamba.

Ofisi ya Takwimu ya Australia imezindua kampeni ya tamaduni mbalimbali kabla ya Sensa ya mwezi ujao, ikijumuisha matangazo katika lugha 28 tofauti.

Maadhimisho ya Wiki ya NAIDOC ya Kitaifa yanafanyika kote nchini Australia wiki hii, kwa ajili ya kusherehekea na kutambua historia, utamaduni na mafanikio ya watu wa Asili na wakaazi wa Visiwa vya Torres Strait.

Kampuni kubwa ya mtandao ya kijamii, Meta, ilifika mbele ya Tume ya Kifalme kuhusu Unyanyasaji wa Wayahudi na Uwiano wa Kijamii jana Julai 6, ikitetea rekodi yake ya kukomesha matumizi mabaya mtandaoni.

Raia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamepata matumaini mapya baada ya kuanza kwa majaribio ya dawa mbili zinazolenga kuudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu Sensa na usalama wa data?

Nigeria imesema itaitaka Afrika Kusini ilipe fidia kwa raia wake acha mali na biashara zao baada yaku kimbia nchi hiyo kutoka na maandamano dhidi ya wahamiaji.

Mashabiki wa timu za Afrika katika Kombe la Dunia la FIFA 2026, walipata pigo kubwa katika siku ya 20 na 21 ya michuano hiyo.

Ada ya maombi ya visa ya mwanafunzi imeongezeka tangu Julai 1 kutoka $2,000 hadi $2,500, huku Visa ya Muda ya Uzamili, au visa nambari 485, sasa inagharimu $5,750.

Katika Siku ya 22 ya Kombe la Dunia la FIFA, Ureno iliwashinda Kroeshia katika mechi ya mwisho ya Kombe la Dunia ya Luka Modrić, Uhispania ili icharaza Austria, na Uswisi ikaishinda Algeria na kufuzu kwa Raundi ya 16.

Wanafunzi wakimbizi wanajenga upya maisha yao nchini Australia kupitia mpango mpya wa majaribio ya makazi, unaounganisha masomo yao ya chuo kikuu na viwanda ambapo kuna uhaba mkubwa wa wafanyakazi kama vile uuguzi.

Polisi wamewakamata vijana wawili baada ya mvulana wa miaka 15 kuachwa afe nje ya kituo cha matibabu cha jamii mjini Melbourne.

Mwaka huu DR Congo ilimaliza ukame wakuto shiriki katika Kombe la Dunia la FIFA baada ya zaidi ya miaka 50.

Bei ya petroli imeshuka hadi viwango ambavyo havijaonekana tangu mwanzo wa 2022. Taasisi ya Petroli ya Australia inasema wastani wa kitaifa wa lita moja ya mafuta yasiyo na risasi ulishuka zaidi ya senti 6 wiki iliyopita - hadi chini kidogo ya dola 1.60.

Siku ya 19 ya Kombe la Dunia la FIFA ilijumuisha mechi tatu za mchujo zenye ushindani mkali, huku Ujerumani na Uholanzi zikiondolewa baada ya mikwaju ya penati, wakati huo huo Brazil ilinyakua ushindi katika mechi yao muda mfupi kabla ya kipenga cha mwisho.

Sio kutia chumvi tunaposikia kwamba Kombe la Dunia la FIFA lina tarajiwa kuleta dunia pamoja katika mwezi wa Juni. Baada ya yote, mpira wa miguu unajulikana kama mchezo maarufu zaidi duniani.

Shirika kubwa zaidi huru la habari nchini Uganda Nation media group limearifu kuwa limewekwa chini ya ulinzi mkali wa kijeshi mapema Jumapili.

Wanaume kutoka jumuiya za Afrika Mashariki wanao ishi jimboni New South Wales, wana jiandaa kwa kongamano maalum Jumamosi 27 Juni 2026.

Mweka Hazina wa Shirikisho Jim Chalmers anasema wafanyakazi, wanunuzi wa nyumba za kwanza na vizazi vijavyo watafaidika na sheria zenye utata za mageuzi ya kodi ambazo zimepitishwa hivi karibuni bungeni.Polisi warusha mabomu ya kutoa machozi dhidi ya waandamanaji katika maeneo mbalimbali mjini Nairobi huku makundi yanayoongozwa na vijana yakikumbuka miaka miwili tangu maandamano ya Gen Z. Watu kadhaa wametiwa nguvuni kufuatia maandamano hayo. Mawingu mazito ya moshi yalitanda angani huku umati wa watu ukikimbia kujinusuru, wengi wao wakifunika nyuso zao kutokana na harufu kali na madhara ya gesi hiyo.Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.

Socceroos wamefanikiwa kufika hatua ya mchujo baada ya kupata sare yakutofungana katika Kundi D, wakati Ecuador ikiwaacha wajerumani vinywa wazi katika Kundi E na kufuzu kushiriki katika hatua ya timu bora 32.