Listen to interviews, features and community stories from the SBS Radio Swahili program, including news from Australia and around the world. - Sikiza mahojiano, makala na hadithi za jumuiya kutoka Idhaa ya Kiswahili ya SBS Radio, ikijumuisha taarifa za habari kutoka Australia na ulimwenguni.

Wizara ya afya Tanzania imesema kuwa maambukizi ya wagonjwa wa mafua makali ya Influenza na Uviko-19 yameongezeka na kuwataka wananchi kuchukua hatua stahiki za kujikinga na maambukizi hayo.

Kuondolewa kwa dharura kwa Waziri Mkuu kutoka nyumbani kwake mjini Canberra kwa sababu ya tisho la bomu lililolengwa, kumesababisha maonyo ya kuongezeka kwa mazingira ya usalama, ambapo uadui mtandaoni unazidi kujitokeza kama vitisho vya kimwili vyenye madhara makubwa.

Mvua kubwa imesababisha mafuriko ya ghafla katika sehemu za Sydney usiku kucha wa Alhamisi hadi Ijumaa, wafanyakazi wakujitolea wa S-E-S wakitoa huduma za uokoaji 44 za maji ya haraka.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kuchumbiana mtandaoni?

Kwa wanafunzi wa kimataifa wanaosomea nchini Australia, kupata huduma ya afya mara nyingi huonekana kama swala ghali sana... au la kutatanisha sana kuweza kuipitia.

Polisi wanaamini kuna watu wengi zaidi wanaohusika, katika utekaji nyara na mauaji ya babu mmoja wa Sydney Chris Baghsarian.

Serikali ya Sudan inayoungwa mkono na jeshi imekosoa UIganda kwa kumkaribisha mkuu wa wanamgambo wa RSF Mohamed Hamdan Daglo maarufu kama Hemeti.

Kama ume ishi kwa muda wowote nchini Australia, labda umegundua jinsi maisha yalivyo na utulivu.

Ripoti ya kwanza ya kitaifa kuhusu ubaguzi wa rangi katika vyuo vikuu nchini Australia imegundua kuwa ni tatizo lililo enea na la kimfumo.

Australia's hot, dry climate and unique landscapes make it one of the most bushfire-prone countries in the world. As climate change drives higher temperatures and drier conditions, we can expect more frequent and more intense bushfires in the future. But once the fire is out, how do you return home safely, find support, and look after yourself? - Hali ya mazingira ya joto, ukavu pamoja na mandhari yakipekee, hufanya Australia iwe mojawapo ya nchi zinazo kabiliwa na moto wa vichaka zaidi dunini. Mabadiliko ya tabianchi yanapo sababisha ongezeko ya hali ya joto na mazingira ya ukame, tunaweza tarajia moto ya vichaka mikali zaidi mara kwa mara katika siku za usoni. Ila moto unapo zimwa, unaweza rudi nyumbani salama, pata msaada na kujihudumia?

Sehemu nyingi za Australia ziko katika hali ya juu ya tahadhari, hali mbaya ya hewa na mvua zikiendelea kuathiri jamii na kuharibu njia muhimu za usafiri.

Takriban idadi yawa Kenya 1,000 wameajiriwa kupigania Urusi, kulingana na ripoti ya ujasusi ya Kenya inayoelezea mtandao wa maafisa wahalifu wanaodaiwa kushirikiana na makundi ya biashara haramu ya binadamu.

Serikali ya New South Wales inachunguza mazingira yaliyozunguka kutoroka kwa wagonjwa wawili kutoka hospitali moja, ambao siku chache baadaye walidaiwa kuhusika katika matukio tofauti ambapo watu watatu walifariki.

Mwezi mtukufu wa Ramadan ume anza, Waislamu kote duniani wakisherehekea Iftar katika siku ya pili ya kipindi cha mfungo.

Andrew Mountbatten-Windsor ameachiliwa huru chini ya uchunguzi baada ya polisi wa Uingereza kumhoji kwa saa muda wa masaa 12 kwa tuhuma za utovu wa nidhamu katika ofisi ya umma.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kuchumbiana mtandaoni?

Ripoti mpya ya kiuchumi inaonya Australia ina elekea kupoteza hadhi yake, kama taifa lenye deni la chini, huku mikopo ya serikali ikifikia viwango ambavyo havija onekana tangu vita vya pili vya dunia.

Je, unajua jinsi yakuzungumza kuhusu kuchumbiana mtandaoni?

Angus Taylor amechukua uongozi wa chama cha Liberal katika kura ya maamuzi ya chama chake kwa ushindi thabiti wa kura 34 dhidi ya 17 zilizotolewa kwa aliyekuwa kiongozi wake.

Mbunge wa chama cha One Nation Barnaby Joyce, amesema ni wazi sera ya uhamiaji ya chama chake, ina ungwa mkono na chama cha Liberal, akihoji madai ya baadhi yama seneta wa chama cha Liberal kuwa hawana taarifa kuhusu mpango huo wa uhamiaji.

Kuteuliwa kwa Burundi kuwa mwenyekiti wa umoja wa Afrika, kunatarajiwa kuleta tija katika juhudi zakutatuwa migogoro inayo zikabili baadhi ya nchi za jumuia hiyo kutokana na Burundi kuwa na uzoefu katika maswala ya kusimamia amani.

Shirika la uangalizi la watumiaji la Australia, lina fungulia mashtaka duka la Coles katika mahakama ya shirikisho.

Mwanaume ambaye ame shtumiwa kwa kushiriki katika shambulizi laki gaidi katika fukwe ya Bondi, amefikishwa mahakamani.

Upinzani dhidi ya mpango waku ruhusu kampuni za Marekani kupata madini muhimu nchini Jamhuri yakidemokrasia ya Congo, una ongezeka baada ya Rais Tshisekedi kurejea nchini kutoka mkutano wa madini ulio fanyika Marekani wiki iliyopita.

Kiongozi wa upinzani wa kwanza wa kike nchini Australia Sussan Ley ametangaza kuwa amestaafu kutoka siasa.

Hali ya mazingira ya joto na ukavu pamoja na mandhari yakipekee, hufanya Australia iwe mojawapo ya nchi zinazo kabiliwa na moto wa vichaka zaidi duniani.

**ZIARA YA RAISI WA ISRAEL AUSTRALIA YAZUA UTATA HUKU WAANDAMANAJI NA POLISI WAKIKABILIANA KATIKA MAANDAMANO DHIDI YA RAIS HUYO ** SERIKALI YAZINDUA MPANGO WA KWANZA WA FAMILIA NA UNYANYASAJI WA WANAWAKE NA WATOTO WA MATAIFA YA KWANZA. **NA CHAMA CHA LIBERAL BADO LIANENDELEA KUWA NA MZOZO WA UONGOZI WA CHAMA BAADA YA KUGAWANYIKA KWA SIKU 17

Kwa habari na melezo zaidi, tembelea tovuti ya sbs.com.au.

January 26 is one of the most debated dates in Australia's history. Often described as the nation's birthday, the day marks neither the formal founding of the colony nor the creation of the Commonwealth. Instead, it reflects a layered history shaped by colonisation, political decisions, and ongoing First Nations resistance. Understanding what actually happened on January 26 reveals why the date is experienced so differently across the country. - Tarehe 26 Januari ni moja ya tarehe zinazojadiliwa sana katika historia ya Australia. Mara nyingi inatajwa kama siku ya kuzaliwa ya taifa, lakini siku hiyo haimaanishi kuundwa rasmi kwa koloni au kuanzishwa kwa Jumuia. Badala yake, inaakisi historia yenye tabaka nyingi inayoundwa na ukoloni, maamuzi ya kisiasa, na upinzani unaoendelea wa Mataifa ya Kwanza. Kuelewa kilichotokea hasa tarehe 26 Januari kinafunua ni kwa nini tarehe hiyo inaathiriwa kwa namna tofauti katika nchi nzima.

Waziri Mkuu Anthony Albanese amepongeza makubaliano mapya ya usalama na Indonesia kama mabadiliko muhimu kuelekea ushirikiano wa karibu wa ulinzi kati ya nchi hizi mbili. Hata hivyo, wachambuzi wanaonya kwamba mkataba huo unaweza kuja na gharama kubwa, ikiwezekana kupuuza masuala ya haki za binadamu yanayoendelea huko Papua Magharibi na wasiwasi kuhusu mwelekeo wa kisiasa wa siku zijazo wa serikali ya Indonesia

Demokrasia na utaratibu wa kimataifa unaozingatia sheria ziko hatarini, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya Shirika la haki za binadamu ama Human Rights Watch. Kuna msisitizo mahususi juu ya Marekani na kile ambacho chombo cha kimataifa kinaelezea kama kudorora kwa haki za binadamu, lakini pia kuna tahadhari juu ya Australia. Sera za uhamiaji na kuwekwa kizuizini kwa vijana za Australia zinaorodheshwa kama 'mapungufu makubwa', zikionyeshwa kuwa ni demokrasia pekee ya Magharibi isiyo na sheria ya kitaifa ya haki za binadamu.

**WAZIRI MKUU ANTHONY ALBANESE YUKO INDONESIA KUSAINI MKATABA WA KIHISTORIA WA USALAMA **MAJESHI YA MAREKANI NA URUSI YATANGAZA KUANZA KUSHIRIKIANA TAARIFA ZA KIJESHI HUKU MAZUNGUMZO YA AMANI NA UKRAINE YAKIENDELEA **WATU ZAIDI YA MIA MOJA HAMSINI WAFARIKI BAADA YA SHAMBULIO NIGERIA

*AL-Islam Gaddafi auwawa Libya *Vikwazo vimewekwa na Marekani dhidi ya watu wanaodaiwa kuchochea vita Sudan

Benki ya Hifadhi ya Australia imehitimisha mapumziko ya miaka miwili kwa kuongeza viwango vya riba hadi asilimia 15, jambo ambalo limeanzisha mjadala mkali wa kisiasa juu ya kama matumizi ya serikali au mahitaji ya watu binafsi ndiyo yanayosababisha mfumuko wa bei kuendelea. Wakati Mweka Hazina anatetea bajeti na kuashiria mashinikizo ya nje, Upinzani na Kijani wanadai kuwa sera za sasa zinawaadhibu Waustralia wa kawaida na zinaacha mbali njia zingine za kiuchumi.

Utafiti mpya unaonyesha kuwa jamii zilizo na mchanganyiko wa rangi tofauti zinafanyiwa upekuzi bila kibali mara tatu na nusu zaidi kuliko jamii katika maeneo yenye watu wengi weupe. Kulingana na uchambuzi wa matumizi ya nguvu za upekuzi zisizo za kawaida na Polisi wa Victoria, hali hii inaonekana hata pale ambapo maeneo ya jamii zenye watu wengi weupe yana viwango vya juu vya uhalifu.

Did you know that IVF is not the first, but in fact the last step in a sequence of fertility treatments? In Vitro Fertilisation is regulated by state and territory laws. It can also be expensive and emotionally challenging. Here's what to expect when aiming to start a pregnancy with IVF in Australia. - Je, mnajua kwamba IVF si hatua ya kwanza, bali ni hatua ya mwisho katika mlolongo wa matibabu ya uzazi? Uliopo wa Mbolea ya Nje ya Mwili unasimamiwa na sheria za mitaa na eneo. Pia inaweza kuwa ghali na pia ngumu kihisia. Hiki ndicho mnachopaswa kutegemea ama kuzingatia mkitaka kuanzisha ujauzito kwa kutumia IVF nchini Australia.

Kwa wengi katika kusini-mashariki mwa Australia, siku baada ya Siku ya Australia ilileta hali ya joto kali na rekodi za viwango vya joto. Katika Mildura, jimboni Victoria, kaskazini-magharibi zaidi, joto lilifikia nyuzi 48.6. Na wakati maeneo ya pwani yalifurahia kupungua kwa joto, maeneo ya bara yalilazimika kukabiliana na joto kali lililodumu kwa wiki moja. Wataalamu wanasema aina hizi za matukio zitaendelea kuongezeka kwa wakati kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi - lakini wakati kumejaa habari nyingi kuhusu jinsi hiyo inaathiri vituo vya mijini, maeneo ya vijijini nchini Australia hayajapata umakini sawa. SBS ilitembelea Mildura kuona jinsi eneo hilo lilivyohisi joto, na wanavyofanya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa katika ngazi ya eneo hilo.

**BENKI YA HIFADHI INATARAJIWA KUONGEZA KIWANGO CHA RIBA **INDIA NA MAREKANI WAMEFIKIA MAKUBALIANO YA KIBIASHARA **KITUO CHA KITAIFA CHA DAWA ZA KULEVYA CHATOA TAHADHARI KUHUSU DAWA HATARI ZA STAREHE ** IRAN INAJIANDAA KWA MAZUNGUMZO NA MAREKANI KUHUSU NYUKLIA

Kwa maelezo ama habari zaidi elekea kwenye tovuti yetu ya sbs.com.au/swahili.

Mkataba wa Muungano wa Falepili kati ya Australia na Tuvalu uliangaziwa kama wa kwanza wa aina yake duniani, ukiwa na kifungu kimoja cha makubaliano kinachoruhusu hadi watu 280 wa Tuvalu kuhamia Australia kila mwaka kama njia ya kukabiliana na viwango vya bahari vinavyoongezeka na kutishia ardhi yao. Kikundi cha kwanza cha wahamiaji chini ya makubaliano haya sasa wamewasili Australia. Hata hivyo, pamoja na kuwepo kwa jamii ndogo ya watu wa Tuvalu huko, wanakabiliwa na changamoto ya kuzoea makazi mapya, huku wakidumisha uhusiano na jamii na utamaduni wao.

Learn practical English phrases for getting organised and managing daily tasks, including planning ahead, meeting deadlines, and staying on top of responsibilities. - Jifunze misemo ya Kiingereza kwa vitendo ili kujipanga na kusimamia majukumu ya kila siku, ikiwemo kupanga mapema, kufikia tarehe za mwisho, na kuwajibikia majukumu yenu.

Learn how to talk about things that make you laugh. Practise phrases that help you share stories, react to jokes, and enjoy conversations more. - Jifunze jinsi ya kuzungumzia mambo yanayowachekesha. Fanyeni mazoezi ya misemo inayowasaidia kushiriki hadithi, kuitikia vichekesho, na kufurahia mazungumzo zaidi.

Like in most countries, public transport in Australia is the cheapest way to get around. It includes trams, buses, trains and ferry services. And each state or territory has its own transport network. However, navigating Australia's public transport system with ease requires knowing the basics around how it works and what to expect. - Kama ilivyo katika nchi nyingi, usafiri wa umma nchini Australia ni njia ya bei nafuu zaidi ya kusafiri. Unajumuisha tramu, mabasi, treni, na huduma za feri. Kila jimbo au eneo la nchi lina mtandao wake wa usafiri. Hata hivyo, kuzunguka kwa urahisi katika mfumo wa usafiri wa umma wa Australia kunahitaji kujua mambo ya msingi kuhusu jinsi unavyofanya kazi na nini cha kutarajia.

**WATU WAWILI WAKAMATWA NA POLISI BAADA YA TUKIO LA UFYATULIAJI RISASI HUKO GEELONG. **KIPITO CHA RAFAH KATI YA EGYPT NA GAZA KUFUNGULIWA BAADA YA MIAKA MIWILI ** TAHADHARI KUHUSU MLIPUKO WA VIRUSI VYA NIPAH HUKO INDIA.

Watanzania bado wanakabiliwa na athari za baada ya uchaguzi wa hivi karibuni, huku wanahabari wakizuiwa kuripoti usimulizi mbele ya tume ya uchunguzi. Makubaliano kati ya Congo na Marekani kuhusu madini yana dosari kubwa.

Ripoti muhimu imefichua kuwa Service Australia ilikwepa kwa makusudi sheria za malezi ya watoto kwa muda wa miaka sita, ikiwa imezuia ndani kwa ndani malipo kwa zaidi ya wazazi 16,000 ambao walitoa chini ya asilimia 35 ya huduma kwa watoto wao. Wakati shirika hilo lilipinga kuwa sheria ilileta "matokeo yasiyotarajiwa" kwa kuulazimisha walezi wakuu kulipa wale wenye majukumu kidogo ya huduma, Ombudsman aliamua kwamba kupuuza sheria si chaguo kwa watumishi wa umma.

Wanafunzi wanaporudi shuleni kwa mwaka mpya, Polisi wa Shirikisho la Australia(Federal Police) wanatoa wito kwa shule kuwa waangalifu kwa ishara za wanafunzi kulazimishwa kuingia kwenye ndoa za kulazimishwa.

Vitisho vya kijeshi vya Donald Trump na vita vya kibiashara vinavyoandika wasiwasi kwa washirika, baadhi ya wataalamu wanatoa wito wa kufikiria upya ushirikiano wa muda mrefu wa Australia na Marekani. Mjadala umeimarishwa na hotuba ya Waziri Mkuu wa Canada, Mark Carney, katika Jukwaa la Kiuchumi Duniani, ambayo iliwashauri nchi zenye nguvu ya kati kupinga kudhoofisha maadili yao kwa maamuzi ya nguvu kubwa za dunia.

Mamilioni ya watu duniani kote huugua kila mwaka kutokana na vyakula visivyo salama au vilivyochafuliwa. Baadhi ni kutokana na udanganyifu wa vyakula, kitendo cha kuuza makusudi bidhaa za chakula bandia, zilizodanganywa au zilizobadilishwa kwa faida ya kifedha. Wanasayansi wa Australia wameunda njia mpya za kukabiliana na tatizo hili la mabilioni ya dola

Siku ya Australia imeadhimishwa kote nchini kwa sherehe za uraia na tuzo za Mwanaustralia wa Mwaka. Siku hiyo pia imeadhimishwa na watu wa Kabila la Aborijini na Visiwa vya Torres Strait ambao wamekusanyika kote nchini kwa matukio ya kila mwaka kuadhimisha Januari 26 - ikiwa ni pamoja na maandamano ya Siku ya Mvamizi.

**MAMLAKA ZA DHARURA ZATOA TAHADHARI KUHUSU HALI YA HEWA LEO PANDE TOFAUTI VICTORIA **CHAMA CHA LIBERALS LIKO CHINI YA SHINIKIZO NA MSUKUMO WA ZIADA **KUNA PENDEKEZO MPYA YA KUFANYA MAFUTA YA KUJIKINGA NA JUA KUWA LAZIMA SHULENI