Listen to interviews, features and community stories from the SBS Radio Swahili program, including news from Australia and around the world. - Sikiza mahojiano, makala na hadithi za jumuiya kutoka Idhaa ya Kiswahili ya SBS Radio, ikijumuisha taarifa za habari kutoka Australia na ulimwenguni.

Serikali ya Victoria imetoa ripoti ya mwisho ya uchunguzi kuhusiana na uzoefu wa wanawake katika suala la maumivu - na ni taarifa inayosumbua kusoma. kutokana na uzoefu wa wanawake na wasichana 13,000, ripoti hiyo imebaini mapengo katika huduma za afya kwa jinsia, upendeleo katika matibabu, ubaguzi wa kijinsia, na hisia za kupuuzwa au kutopingwa na wataalamu wa afya zinazoenea katika mfumo wa afya wa Victoria.

Maandamano ya neo-Nazi mbele ya bunge la New South Wales yamezua mshtuko katika jamii za Kiyahudi na za tamaduni mbalimbali huko Sydney. Serikali ya jimbo hilo imekashifiwa baada ya kufichuliwa kwamba tukio hilo liliendelea na idhini kutoka kwa Polisi wa New South Wales. Je, ni vipi maandamano haya ya neo-Nazi yalipewa kibali cha kufanyika mwanzoni?

Mkutano wa kwanza wa African Youth Summit uliandaliwa na kufanyika mwaka huu, na mratibu wa vijana aliyehudhuria anajiunga nasi kuzungumzia mada ya mkutano huo.

Serikali ya majimbo na maeneo nchini Australia zitachunguzwa kama sehemu ya uchunguzi wa bunge kuhusu matokeo na athari za kifungo kwa vijana. Kati ya maswala ya kuzingatia katika uchunguzi huu ni Kuzidishwa kwa kufungwa kwa watoto wa Mataifa ya Kwanza.

Mtandao wa Reddit na jukwaa la Kick zitaongezwa kwenye majukwaa yanayohitajika kuzuia watumiaji walio na umri chini ya miaka 16, sheria mpya zitakapoanza kutekelezwa mwezi Desemba. Marufuku ya Australia ya mitandao ya kijamii kwa watoto chini ya miaka 16, ambayo inajumuisha majukwaa nane kuu, inategemea tathmini zinazoendelea za eSafety ambazo zinaweza kufafanua kati ya huduma za mitandao ya kijamii, ujumbe, na michezo, kuelezea ni kwanini majukwaa kama Steam na Twitch hayakujumuishwa. Wakati serikali ilihakikishiwa na Roblox kwamba wataanzisha teknolojia za kuthibitisha umri ili kupunguza tabia za uwindaji wa watoto, watetezi wa haki za kidigitali wanatahadharisha kwamba marufuku haya yanaweza kuhamasisha watoto kutumia majukwaa madogo yasiyo na uangalizi ambapo wanaweza kukumbana na madhara makubwa zaidi.

Australia inatarajia kutoa kibali cha kila kudumu ama permanent humanitarian visa , cha milioni moja tangu kumalizika kwa Vita Kuu ya Pili ya Dunia mwisho wa mwaka huu. Hatua hii imewezesha sherehe juu ya mchango mkubwa ambao wakimbizi hufanya katika hadithi ya kitaifa ya Australia. Lakini mashirika ya haki za wakimbizi yanasema ni wakati muafaka kufikiria jinsi Australia inaweza kuboresha jibu lake kwa ukimbizi mkubwa wa dunia nzima.

Mahitaji ya mayai ya uzazi yanaongezeka nchini Australia kadiri watu wanavyokumbwa na changamoto za uzazi. Lakini mahitaji ya mayai ni makubwa mno kuliko upatikanaji wao na sasa, wataalamu wanapendekeza Australia ifikirie kubadilisha kanuni zinazohusu utoaji mayai.

Wahamiaji wengi wanakumbana na matatizo tofauti wanapojaribu kupata msaada wa afya ya akili. Umoja wa Mataifa unasema kwamba upatikanaji wa huduma za afya ya akili ni haki ya msingi kwa kila mtu , ikiwemo wahamiaji na wakimbizi. Umoja wa Mataifa unasisitiza kwamba wahamiaji mara nyingi wanakabiliwa na changamoto nyingi kama vile msongo wa mawazo, huzuni, kiwewe na ata upweke kutokana na mazingira mapya. Mtaalamu wa Afya ya Akili Terry Kiguru anatueleza jinsi ya kupata msaada huo na kwanini.

Jamii ya watu wa Sudan walio nchini Australia wana wasiwasi mkubwa ,wakisubiri habari kutoka kwa familia zao walionaswa katika jiji la Al-Fasher baada ya mlipuko wa ghasia. Jiji hilo lilitekwa na Rapid Support Forces wiki mbili iliyopita, na wataalamu wanaamini kwamba maelfu huenda wameuawa katika mauaji ya kutisha. Kwa kuwa huduma za intaneti na simu zimekatwa, wanaoishi nje ya nchi wanalazimika kukaa na kusubiri ili kujua kama wapendwa wao bado wako hai.

Maelfu ya kaya za Wenyeji kaskazini mwa Australia wanaishi na mfumo wa kulipa kabla wa umeme, ambapo kukatwa kunaweza kutokea wakati wowote. Ripoti mpya sasa imeonya kwamba bila ulinzi wa kutosha, mfumo huu unaweza kuwa hatari katika joto kali.

Timu ya kimataifa ya wanasayansi imeonya kuwa pIngwini wanaweza kuwa katika hatari kutokana na madhara ya hali mbaya ya hewa. Utafiti mpya unapendekeza kwamba si tukio moja kama vile joto kali inayosababisha hatari kubwa zaidi, bali ni athari zake zilizoungana pamoja katika ardhi na baharini.

Miaka kumi baada ya utafiti muhimu kudhibitisha kwamba kuwalisha watoto wachanga bidhaa za karanga inaweza kuendeleza mzio hatari, utafiti mpya umebaini kuwa kuna uwezekano wa kuepuka kuendeleza mizio ya chakula.

Waziri wa Mambo ya Ndani, Tony Burke, anasema kwamba serikali inafanya kazi juu ya uwezekano wa kutambua ujuzi wa nje ya nchi. Anasema hii itasaidia kuokoa muda na pesa kwa wahamiaji wenye ujuzi wanaotafuta kuhamia Australia. Katika hotuba yake kwa Klabu ya Waandishi wa Habari huko Canberra, Bw. Burke pia ametangaza mabadiliko kwenye akaunti za benki zisizotumika ili kukabiliana na utakatishaji wa fedha.

Australia is home to the world's oldest living cultures, yet remains one of the few countries without a national treaty recognising its First Peoples. This means there has never been a broad agreement about sharing the land, resources, or decision-making power - a gap many see as unfinished business. Find out what treaty really means — how it differs from land rights and native title, and why it matters. - Waingereza walipowasili Australia walitangaza ardhi kuwa ‘terra nullius' kumaanisha ardhi isiyomilikiwa na yeyote. Hawakuona haja ya kuzungumza na mataifa ya waaboriginals na kwa hivyo wenyeji wa Australia wanasema kwamba hii ni biashara ambayo haijakamilika.

Waziri wa Mambo ya Nje Penny Wong amesema Australia ina simama kidete juu ya tamaduni nyingi, baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kukosoa uhamiaji katika hotuba yake kwa kikao cha mkutano wa Umoja wa Mataifa.

Waziri Mkuu amesema ombi la utaifa wa Palestina ni fursa ya amani, katika hotuba yake kuhusu soluhu ya nchi mbili, alipo hudhuria kikao cha Umoja wa Mataifa hii leo Jumanne 23 Septemba 2025.

Waziri wa Shirikisho wa Mawasiliano amesema Optus inastahili tarajia adhabu kubwa, kufuatia kupotea kwa huduma ya namba ya dharura ya 000, hali ambayo ime husishwa na vifo kadhaa.

Taratibu zinazolenga kumfuta kazi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Vital Kamerhe zinaendelea huku kukishuhudiwa hali ya mfarakano kati ya rais Félix Tshisekedi na mshirika wake huyo wa zamani.

Kampuni ya pili kwa ukubwa ya madini imetangaza inapunguza ajira. Anglo American Australia imesema ita angaza kupunguza idadi ya wafanyakazi Queensland, na takriban wafanyakazi 200 wata athirika.

Maelfu ya watu wanasherehekea kuwa raia wapya wa Australia, katika sherehe zilizo andaliwa na halamshauri za jiji kote nchini kwa siku ya Uraia wa Australia.

Je, unajua jinsi ya kujigamba kuhusu gari lako?

Naibu Waziri Mkuu Richard Marles amekana madai kuwa uwekezaji wa $12 bilioni iliyo tangazwa juzi ime undwa ili kutuliza maombi ya Marekani kwa Australia kuongeza matumizi yake katika ulinzi.

Je, unajua jinsi ya kuelezea kuhusu anga la usiku?

Popote ulipo nchini Australia, kutoka jiji kuu lenye shughuli nyingi, hadi katika viunga vya mji, katika mji wa kikanda au kijijini, kuna uwezekano unaweza kutana na aina mbali mbali za wanyamapori wazuri wa Australia.

Benki ya ANZ imekiri kujihusisha na mwenendo usiofaa, katika huduma iliyotoa kwa serikali ya Australia, kulingana na Tume ya Uwekezaji na usalama ya Australia (ASIC).

Waziri wa Sheria wa zamani wa DR Congo, Constant Mutamba amehukumiwa na mahakama mjini Kinshana kufanya kazi ngumu kwa miaka mitatu.

Mshukiwa wa mauaji ya kimbari ya Rwanda, Félicien Kabuga anakabiliana na wakati mgumu kupata nchi itakayo mpokea kwa muda kutoka gereza la The Hague, Uholanzi.

Waziri Mkuu amesifu msaada wa wanachama wa kongamano la Visiwa vya Pasifiki, Australia inapo saka uenyeji wa kongamano la mazingira la Umoja wa Mataifa la, COP-31.

Je, unajua jinsi ya kuwapa watu mwaliko rasmi na usio rasmi?

Cervical cancer is preventable, but only if you catch it early. Cultural and personal barriers have often meant that women avoid cervical cancer testing. But now with the help of a world-leading test, Australia is aiming to eliminate cervical cancer by 2035. The test is a safe and culturally sensitive option for women from all backgrounds. Best of all it could save your life—or that of someone close to you. - Saratani ya Kizazi inaweza zuiliwa, kama ina gunduliwa mapema. Vizuizi vya kitamaduni na kibinafsi mara nyingi vime kuwa na maana kwamba, wanawake wanachelewesha kufanya uchunguzi wa saratani ya kizazi. Ila sasa, kwa msaada wa kipimo kinacho ongoza duniani, Australia ina lenga kutokomeza saratani ya kizazi kufikia mwaka wa 2035. Uchunguzi huo ni salama, na kitamaduni ni chaguo nyeti kwa wanawake kutoka mazingira yote. Muhimu zaidi, kipimo hicho kinaweza okoa maisha yako au mtu wa karibu yako.

Saratani ya Kizazi inaweza zuiliwa, kama ina gunduliwa mapema.

Dau Akouny, mmoja wa wavulana wawili walio uawa katika shambulizi la kisu mjini Melbourne wikiendi iliyopita, amekumbukwa na familia yake kama "mtoto mzuri" na alikuwa "sehemu ya mustakabali wa kesho wa jumuiya."

Serikali ya shirikisho imetangaza mpango wenye thamani ya $30 milioni, kupiga jeki idadi ya wakufunzi wa elimu ya ufundi.

Waziri wa mambo ya tamaduni nyingi Anne Aly, amechangia ujumbe wa mshikamano na jumuiya yawa Hindi wa Australia, kufuatia maandamano dhidi ya wahamiaji.

Je, unajua jinsi ya kuzungumza kuhusu autism?

Wanasiasa wame laani ubaguzi wa rangi na chuki dhidi ya wageni iliyo onyeshwa katika maandamano kadhaa dhidi ya uhamiaji wikiendi iliyo pita.

Mbunge wa upinzani Matt Canavan amesema sera za uhamiaji za seriakli, zina wasukumu watu kuwa na maoni yenye misimamo mikali. Amesema serikali ya Labor imefungua anacho ita milango ya mafuriko ya uhamiaji baada ya janga la UVIKO-19, na inawaruhusu watu kuingia nchini kiholela chini ya ya sera zake za sasa.

Shirika la UNHCR limesema viongozi wa Rwanda na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamekubali kuwarejesha wakimbizi walio toroka makwao mashariki mwa DRC.

Wimbi la maandamano ya kitaifa dhidi ya uhamiaji yame shuhudiwa katika miji mikubwa ya Australia.

Waziri Mkuu Anthony Albanese amesema Richard Marles alikuwa na mkutano wenye tija na mshiriki wake kutoka Marekani Pete Hegseth, huku kukiwa mkanganyiko kuhusu kama, kuna mkutano rasmi ulio fanyika kati yao.

You may hear the protest chant, “what do we want? Land rights!” —but what does it really mean? Land is at the heart of Aboriginal and Torres Strait Islander identity, culture, and wellbeing. Known as “Country,” it includes land, waterways, skies, and all living things. In this episode of Australia Explained, we explore Indigenous land rights—what they involve, which land is covered, who can make claims, and the impact on First Nations communities. - Unaweza sikia wito huu katika maandamano, “tuna taka nini? Haki za ardhi!” ila wito huo una maana gani? Ardhi iko katika kiini cha utambulisho, utamaduni na ustawi wa wa Aboriginal na watu kutoka Visiwa vya Torres Strait. Inajulikana kama “nchi” na inajumuisha ardhi, njia za maji, anga na kila kitu kilicho hai. Katika makala haya ya Australia ya Fafanuliwa, tuta chunguza haki za ardhi zawa Australia wa asili, wanacho husisha, ardhi gani ina funikwa, nani anaweza fanya madai na madhara kwa jamii za Mataifa ya Kwanza.

Serikali ya Albanese inatarajiwa kuleta mbele mpango wakupanua mfumo unao ruhusu wanao nunua nyumba ya kwanza, kuweka amana ya hadi asilimia tano. Wakati marudio ya awali ya mpango huo yalikuwa na kikomo cha kila mwaka kwa washiriki, mfuno huo kwa sasa utakuwa wazi wa kila mtu anaye nunua nyumba.

Unaweza sikia wito huu katika maandamano, “tuna taka nini? Haki za ardhi!” ila wito huo una maana gani?

Australia ita tambua Palestina kama taifa katika mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa wa Septemba.

Waziri wa mambo ya nje Penny Wong ame muhamasisha Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, asikize wito wakisitisha vita mara moja Gaza.

Sherehe ya Garma katika Kijiji cha Kaskazini Mashariki Arnhem Land, cha Wilaya ya Kaskazini, ime tamatika kwa mwaka mwingine.

Je, unajua jinsi ya kuzungumza kuhusu nyumba yako?

Serikali ya shirikisho imetangaza msaada kwa Gaza uta ongezwa kwa $20 milioni hii leo Jumatatu 4 Agosti, masaa machache baada yamakumi yama elfu kutembea katika Daraja maarufu la bandari ya Sydney, jana Agosti 3, katika maandamano dhidi ya vita vinavyo endelea Gaza.

Wapenzi wa soka barani Afrika wana elekea Kenya, Uganda na Tanzania kuhudhuria michuano ya Afrika iliyo ahirishwa mwaka jana.

Kenya imepinga sheria mpya za biashara na kodi za Tanzania ikizitaja kuwa za kibaguzi na zinazohatarisha ushirikiano wa kiuchumi Afrika Mashariki.

Waziri Mkuu Anthony Albanese ana enda kuhudhuria tukio kubwa linalo waleta pamoja wa Australia wa Asili katika wilaya ya Kaskazini.