Hoja za Wahariri

Follow Hoja za Wahariri
Share on
Copy link to clipboard

Wahariri wetu wenye tajriba wanatoa hoja na mitazamo mizito kuhusu masuala yanayogonga vichwa vya habari, kila wiki.

The Standard Group PLC


    • Feb 25, 2022 LATEST EPISODE
    • infrequent NEW EPISODES
    • 24m AVG DURATION
    • 11 EPISODES


    Search for episodes from Hoja za Wahariri with a specific topic:

    Latest episodes from Hoja za Wahariri

    Vita vya Urusi na Ukraine; athari kwa dunia

    Play Episode Listen Later Feb 25, 2022 7:51


    Mwanahabari mstaafu wa kimataifa, Abdu Mtullya anasema vita vya Urusi na Ukraine havistahili na huenda vikaathiri zaidi uchumi duniani, ikiwamo Afrika. Vita hivyo vimesababisha kupanda kwa bei ya mafuta, Urusi ikiendelea kurusha makombora katika ngome za Ukraine, hali ambayo haijawahi kushuhudiwa tangu mwaka wa 2014.

    Mzozo wa Urusi na Ukraine; Mohamed Abdul-Rahman anachambua

    Play Episode Listen Later Feb 22, 2022 14:45


    Je, unafahamu chimbuko la mgogoro kati ya Urusi na Ukraine, athari zake na unamaanisha nini kwa Afrika na dunia nzima? Mwanahabari/ Mhariri mstaafu na mchambuzi wa masuala ya kimataifa, Mohamed Abdul-Rahman anasimulia.

    Hoja za Wahariri: Kitendawili cha mili Mto Yala - ndani ya magunia

    Play Episode Listen Later Jan 20, 2022 43:29


    Dunia inazidi kushangazwa na suala la mili zaidi ya 20 kupatikana ndani ya magunia katika Mto Yala. Mili hiyo ina alama na ishara za mateso. Je, waliouliwa ni akina nani na sababu za kuuliwa ni gani? Aidha, twajadili siasa za OKA vilevile usajili wa wapigakura wapya. Ali Manzu anawashirikisha wanahabari, Shisia Wasilwa na Kennedy Wandera katika kudadavua masuala haya.

    Hoja za Wahariri Podcast: Nchi bila umeme; ni njama?

    Play Episode Listen Later Jan 14, 2022 41:22


    Kupotea kwa umeme nchini Kenya kwa takribani siku tatu kumechochea ghadhabu. Baadhi wanahisi kwamba ni njama ya wafanyakazi fulani wa kampuni za umeme kusababisha hali hiyo maksudi. Kwamba huenda wanalalamikia mageuzi ya usimamizi katika Kenya Power, ama ni kero la wasambazaji wa kawi kulalamikia viwango vipya vya ada za umeme ambavyo ni vya chini, na kuishia wao kupata hasara. Aidha, tunajadili kujiuzulu kwa Mshirikishi wa Utawala, Bonde la Ufa, George Natembeya ili kulenga kiti cha kisiasa. Ali Manzu anawashirikisha wahariri, Charles Otieno na Kennedy Wandera katika kuyajadili masuala haya.

    Hoja za Wahariri Podcast: Ahadi za wanasiasa; watatekeleza?

    Play Episode Listen Later Oct 16, 2021 12:08


    Wagombea mbalimbali wa urais nchini Kenya wanazidi kutoa ahadi wanazosema watatekeleza endapo watashinda uchaguzi wa 2022. Katika podcast hii, wahariri Geoffrey Mung'ou, Roselyne Obala na mwanahabari mwandamizi, Mike Nyagwoka wanajadili iwapo ahadi zenyewe zinatekelezeka au la kwa kuweka kwenye mizani ahadi za sasa na za awali.

    Hoja za Wahariri Podcast: Raila ni chaguo la Uhuru, huku siasa zikichacha Mlima Kenya

    Play Episode Listen Later Aug 13, 2021 26:43


    Rais Uhuru Kenyatta amewasihi wanasiasa wa One Kenya Alliance kumuunga mkono Raila Odinga kuelekea uchaguzi mkuu wa 2022, huku pendekezo lake likikataliwa vikali na wanasiasa hao. Aidha, wanasiasa mbalimbali wanazidi kujitokeza kwenye eneo la Mlima Kenya wakishindania udhibiti wa siasa za eneo hilo, Uhuru anapoelekea kustaafu. Je, kati ya William Ruto na Raila Odinga, ni nani atakayenufaika katika siasa za Mlima Kenya na ni nani atakayepoteza? Eneo la Mlima Kenya litaamua siasa za 2022? Wawaniaji wa urais wawateue wagombea wenza kutoka maeneo gani ya nchi? Mhariri, Geoffrey Mung'ou na wanahabari wa Standard - Chris Thairu na Mike Nyagwoka wanayapambanua masuala haya.

    HOJA ZA WAHARIRI PODCAST; Kivumbi kati ya Jubilee na UDA Kiambaa na Muguga

    Play Episode Listen Later Jul 20, 2021 27:12


    Baada ya chama kipya cha UDA kushinda uchaguzi mdogo wa ubunge kwenye eneo la Kiambaa, kisha Jubilee kukishinda kiti cha uwakilishi wadi Muguga, kivumbi kinatifuka; UDA inaelekea mahakamani kutaka kura za Muguga zihesabiwe upya huku nayo Jubilee ikitaka kura za Kiambaa zihesabiwe tena. Aidha, nani ana ufuasi mkubwa Mlima Kenya baina ya Uhuru Kenyatta na William Ruto? Kuelekea 2022, farasi watakuwa wawili au watatu? Wahariri, Geoffrey Mung'ou na Odeo Sirari wanamshirikisha mwanahabari Victor Mulama aliyekuwa mashinani kuangazia chaguzi hizo, katika kujadili kwa kina masuala haya.

    HOJA ZA WAHARIRI PODCAST; Siasa za miungano, kulumbana na kuhamia mirengo

    Play Episode Listen Later Jun 24, 2021 23:51


    Je, muungano baina ya Jubilee na ODM utaafikia malengo ya kubuni serikali 2022? Aidha, kuhama au kuhamia mirengo ya kisiasa kumeshika kasi nchini bila kusahau joto la kisiasa Mlima Kenya; nani atanufaika au kupoteza kisiasa? Geoffrey Mung'ou, Odeo Sirari na Murimi Mwangi wanayazamia masuala haya.

    Hoja za Wahariri Podcast; Maraga na Mutunga wana hoja nzito - Mung'ou, Zubeida na Sirari

    Play Episode Listen Later Jun 10, 2021 26:43


    Uchanganuzi wa wahariri kuhusu hoja nzito za David Maraga na DkT. Willy Mutunga (majaji wakuu wastaafu) dhidi ya hulka ya Rais Kenyatta ya kukiuka sheria. Wanasema taifa linafuata mkondo mbaya na wabunge wanafaa kumtimua Uhuru mamlakani.

    HOJA ZA WAHARIRI PODCAST; Kura ya maamuzi itafanyika? Maendeleo ni ya kibaguzi? Mung'ou, Zubeida na Odeo wanachanganua

    Play Episode Listen Later Jun 3, 2021 20:59


    Wakati wa maadhimisho ya Madaraka jijini Kisumu, Rais Kenyatta aliilaumu Idara ya Mahakama kwa maamuzi aliyotaja kuchelewesha utashi wa mwananchi na kuzidisha gharama, mfano kurudia uchaguzi. Je, anakandamiza uhuru wa mahakama? Suala jingine ni iwapo kura ya maamuzi itafanyika au la kwa kuzingatia kesi za kuipinga. Na je, Uhuru anatekeleza maendeleo kwa ubaguzi? Wahariri, Geoffrey Mung'ou, Zubeida Koome na Odeo Sirari wanachambua masuala haya.

    Hoja za Wahariri Podcast; Mahakama Kuhusu BBI

    Play Episode Listen Later May 15, 2021 27:05


    Suala la majaji watano wa Mahakama Kuu kuharamisha mchakato wa kuifanyia katiba marekebisho limechochea gumzo. Aidha, walisema kwamba Rais Kenyatta alikosea katika kuanzisha mchakato wa kuirekebisha katiba badala ya kuanzishwa na wananchi, vilevile kwamba anaweza kushtakiwa. Je, huo ulikuwa uamuzi wa kisheria au kisiasa? Wahariri wetu, Geoffrey Mung'ou, Zubeida Koome na mwanahabari nguli, Duncan Khaemba wamelizamia suala hili kwa kina.

    Claim Hoja za Wahariri

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel