Podcasts about wakati

  • 64PODCASTS
  • 504EPISODES
  • 15mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • May 30, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about wakati

Latest podcast episodes about wakati

Habari za UN
30 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 30, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya elimu kwa watoto mashariki mwa DRC na Mkutano wa pili wa Baraza Kuu la Makazi la shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani UNHABITAT unaofunga pazia leo jijini Nairobi Kenya. Makala inaturejesha nchini DRC na mashinani inatupeleka katika bonde la Ziwa Victoria, kulikoni?Wakati ghasia zinazoendelea huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC zinaripotiwa kusababisha zaidi ya watoto milioni 1.8 kutokuweko shuleni, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF nchini humo linajitahidi kwa udi na uvumba kuhakikisha watoto wanapata elimu kwani ni haki yao ya msingi.Mkutano wa pili wa siku mbili wa Baraza Kuu la Makazi la shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani UNHABITAT leo unafunga pazia jijini Nairobi Kenya. Baraza hilo linalofanyika kila baada ya miaka minne ni chombo cha juu kabisa duniani cha kufanya maamuzi kuhusu maendeleo ya miji endelevu na limewaleta pamoja wawakilishi kutoka nchi zote 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa pamoja na wadau mbalimbali wa amendeleo ya miji.Makala inakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususan jimboni Kivu Kaskazini katika kitongoji cha Mavivi kuwasikia walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania,kikosi cha 11, TANZBATT11, wanaohudumu katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO wakielezea sio tu majukumu yao, bali pia wanajivunia kile wanachofanya kwa kuzingatia Mei 29 imeadhimishwa siku ya kimataifa ya walinda amani.Na katika fursa ni yake Mhandisi Coletha Ruhamya, Naibu Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria, Mradi unaofanikishwa na Benki ya Dunia ambao unakabiliana na masuala ya usafi wa mazingira katika ziwa hilo. Anaeleza umuhimu wa usimamizi endelevu wa bonde hilo kote nchini Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda na Burundi chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Licha ya ukata UNICEF yajitahidi watoto nchini DRC warejee shuleni

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 30, 2025 2:09


Wakati ghasia zinazoendelea huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC zinaripotiwa kusababisha zaidi ya watoto milioni 1.8 kutokuweko shuleni, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF nchini humo linajitahidi kwa udi na uvumba kuhakikisha watoto wanapata elimu kwani ni haki yao ya msingi. Je ni kwa vipi? Anold Kayanda anasimulia zaidi.

Habari za UN
Mkimbizi wa Haiti aliyepata faraja na matumaini nchini Mexico

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 23, 2025 2:02


Wakati raia wa Haiti Giovanni Rotschild alipowasili Mexico mwaka 2022 baada ya safari ndefu isiyo na uhakika kutoka nchi mwake kulikosheheni ghasia, hakufahamu mtu yeyote wala hakuzungumza kabisa lugha ya kispanyola. Lakini msaada alipata msaada kumwezesha kujenga upya maisha na kupata jamii mpya. Flora Nducha na maelezo zaidi.

Habari za UN
23 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 23, 2025 9:56


Hii leo jaridani tunaangazia haki za kibinadamu za raia nchini Uganda, na simulizi ya mkimbizi nchini Mexico ambaye alikimbia machafuko nchini mwake Haiti. Makala tunakwenda nchini Kenya na mashinani nchini Ethiopia, kulikoni?Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa , Volker Türk, leo Ijumaa mjini Geneva, Uswisi kupitia msemaji wake ameelezea wasiwasi wake kuhusu kupitishwa kwa muswada uliopendekezwa na Bunge la Uganda unaoruhusu raia kuhukumiwa katika mahakama za kijeshi.Wakati raia wa Haiti Giovanni Rotschild alipowasili Mexico mwaka 2022 baada ya safari ndefu isiyo na uhakika kutoka nchi mwake kulikosheheni ghasia, hakufahamu mtu yeyote wala hakuzungumza kabisa lugha ya kispanyola. Lakinialipata msaada kumwezesha kujenga upya maisha na kupata jamii mpya.Makala tukielekea siku ya kandanda, kabumbu au mpira wa miguu duniani itakayoadhimishwa Jumapili wiki hii Mei 25 ikibeba maudhui nguvu ya kdandanda katika kuleta mabadiliko tuabisha hodi Nairobi Kenya ambapo leo Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Global Youth Forum linalounganisha vijana Kenya kwa lengo la kutokomeza umasikini na kuishi maisha bora kupitia michezo mbalimbali ikiwemo kandanda akizungumza na Idhaa hii ya Kiswahili anaeleza umuhimu wa kandanda katika ajenda ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu.Na katika mashinani, fursa ni yake Hola msichana mwenye umri wa miaka 15 kutoka wilaya ya Sire nchini  Ethiopia ambaye  kutokana na mafunzo ya stadi za maisha ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF yanayoungwa mkono na asasi ya kupinga ndoa za utotoni ya GPChild Marriage ameweza kuepuka ndoa za utotoni na sasa anatumia mafunzo hayo kutahadharisha na kulinda wenzake.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Mapambano dhidi ya ndoa za kulazimishwa - Fatou Cissé

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 21, 2025 3:41


Wakati ulimwengu ukiendelea kupaza sauti dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia, tunaelekea nchini Mali, ambako Fatou Cissé, mkurugenzi wa filamu na mwanzilishi wa filamu iitwayo FURU, anatumia sanaa kuangazia suala zito la ndoa za kulazimishwa. Kupitia video maalum iliyoandaliwa na Umoja wa Mataifa, tunapata simulizi hiyo inayohusu wasichana wawili waliokumbwa na changamoto hizi. Fatou anawapa wasichana wa Kiafrika sauti na jukwaa la kuzungumza hadharani kuhusu dhuluma wanazokumbana nazo. Sharon Jebichii anasimulia.

Habari za UN
15 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 15, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha katika mkutano wa CSW68 kumsikia Christina Kamili Ruhinda, Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Mashirika yanayotoa huduma ya msaada wa kisheria nchini Tanzania, TANLAP. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno la wiki.Wakati dunia ikiadhimisha miaka 77 tangu Nakba ambapo zaidi ya wapalestina 700,000 walifurushwa kutoka vijiji na miji yao mwaka 1948, shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa Wakimbizi wa Kipalestina UNRWA limetoa onyo kali kuhusu sura mpya ya mateso na ufurushwaji wa lazima uonaoendele Gaza.Akiwa na wasiwasi kutokana na ripoti za kuaminika kwamba wakimbizi wa Rohingya kutoka Myanmar walilazimishwa kushuka kutoka kwenye meli ya jeshi la wanamaji la India na kutoswa katika bahari ya Andaman wiki iliyopita, Mtaalamu wa UN wa Haki za Binadamu kuhusu wakimbizi wa Myanmar, ameanzisha uchunguzi kuhusu kitendo hicho alichoeleza kuwa ni cha kushangaza na kisichokubalika.Na baada ya muda mrefu kuonekana kama mchangiaji mkubwa wa utoaji wa hewa chafuzi duniani, sekta ya usafirishaji majini sasa iko mstari wa mbele katika kuonesha ushirikiano wa kipekee wa kimataifa wa kupunguza hewa hizo zitolewazo na meli za usafirishaji majini.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "KIANGO".Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
13 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 13, 2025 11:36


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo inamulika lengo namba moja la Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDG1 la kutokomeza umaskini na inatupeleka nchini Tanzania ambako Umoja wa Mataifa umeona bora kusaidia wafugaji kuku kuondokana na umaskini.Katika mkutano wa ngazi ya mawaziri kuhusu mustakabali wa ulinzi wa amani unaofanyika leo mjini  Berlin Ujerumani Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameeleza vipaumbele vitatu vya msingi katika mageuzi ya ulinzi wa amani kwa muktadha wa dunia inayobadilika kwa kasi.Mashariki ya Kati leo shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO limeonya kuhusu vifo vya watoto kutokana na utapiamlo Gaza, sababu kubwa ikiwa ni kuendelea kukosekana kwa msaada wa kibinadamu unaojumuisha lishe maalum kwa watoto.Wakati mahitaji ya kibinadamu yakizidi kuongezeka duniani watu milioni 308 katika nchi 73 wakihitaji msaada wa dharura , Shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women limeonya kuwa wanawake na wasichana ndio wanaoathirika zaidi wa migogoro, wakikumbwa na utapiamlo, vifo vinavyoweza kuzuilika vinavyohusiana na ujauzito, na ukatili wa kingono kwa kiwango cha juu, huku mfumo wa misaada ya kibinadamu ukikumbwa na ukata wa fedha.Na katika mashinani, fursa ni yake Jean Todt, Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu usalama barabarani akieleza ni jambo gani lifanyike kuhakikisha usalama barabarani wakati huu dunia inaadhimisha Wiki ya Usalama Barabarani maudhui yakijikita kwenye kuhakikisha barabara ni salama kwa ajili ya waenda kwa miguu na waendesha baiskeli.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
09 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 9, 2025 12:09


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu katika katika jimbo la Upper Nile nchini Sudan, na haki za binadamu na watu kutoweka kwa wingi nchini Sudan. Makala inatupeleka nchini Kenya na Mashinani tunakwenda Gaza, kulikoni?Nchini Sudan Kusini, familia zilizo kwenye hali duni katika eneo la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo ziko katika hali tete sana huku mapigano yakizidi kuongezeka na njaa ikikaribia kufikia viwango vya juu kabisa, limeonya leo Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP).Wakati hofu ikiendelea kuhusu watu kutoweka kwa wingi nchini Sudan, Mtaalam maalum wa Umoja wa Mataifa aliyeteuliwa na Ofisi ya Haki za Binadamu OHCHR anayehusika na haki za binadamu nchini humo Radhouane Nouicer ametoa wito wa dharura kuhusu hali ya raia waliokwama katika vita kubwa nchini humo.Katika inatupeleka nchini Kenya kufuatilia simulizi ya Shalyne Kaputa, mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 16 kutoka kaunti ya Turkana ambaye tofauti na shangazi yake ambaye hakuweza kuendelea na elimu  yake kutokana na kukosa karo, yeye anasoma elimu ya sekondari sasa ili aweze kutimiza ndoto yake ya kuwa mwandishi wa habari. Yote yanawezekana kutokana na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kwa msaada wa shirika la Norway la Maendeleo NORAD na wadau wengine.Na mashinani fursa ni yake Lama, mtoto mwenye umri wa miaka 10 kutoka Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli ambaye anasimulia maumivu na juhudi za kila siku za kutafuta maji mapigano yakiwa ni mwaka mmoja na nusu sasa. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) linatoa msaada mkubwa kwa familia na watoto wa Gaza kwa kusambaza maji salama.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!  

Habari za UN
Lazima hatua madhubuti zichukuliwe kukomesha mzunguko wa watu kutoweka nchini Sudan - Radhouane Nouicer

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 9, 2025 3:22


Wakati hofu ikiendelea kuhusu watu kutoweka kwa wingi nchini Sudan, Mtaalam maalum wa Umoja wa Mataifa aliyeteuliwa na Ofisi ya Haki za Binadamu OHCHR anayehusika na haki za binadamu nchini humo Radhouane Nouicer ametoa wito wa dharura kuhusu hali ya raia waliokwama katika vita kubwa nchini humo. Flora Nducha na taarifa zaidi.

Radio Maria Tanzania
Je, wafahamu umuhimu wa mafundisho matakatifu wakati wa Kwaresima?

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Apr 8, 2025 54:40


Ungana nami Happiness Mlewa, katika kipindi cha Katekisimu Katoliki Shirikishi, Mwezeshaji ni Padre Dominic Mavula C.PP.S, Mkurugenzi wa Matangazo Radio Maria Tanzania, akituongoza kujifunza Umuhimu wa mafundisho matakatifu wakati wa Kwaresima. L'articolo Je, wafahamu umuhimu wa mafundisho matakatifu wakati wa Kwaresima? proviene da Radio Maria.

SBS Swahili - SBS Swahili
The legal loophole allowing political lies during elections - Mwanya wa kisheria unao ruhusu uongo wakisiasa wakati wa uchaguzi

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 3, 2025 7:46


With an election date set for May 3rd, campaigning has officially begun. But political advertisements have already been circulating for months. Can you trust what they say? - Baada ya tarehe ya uchaguzi kutangazwa kuwa 3 Mei, kampeni zime anza rasmi. Ila matangazo ya kisiasa yame kuwa yaku sambazwa kwa miezi kadhaa. Je, unaweza amani wanavyo sema?

Habari za UN
Zanzibar tumetekeleza kwa vitendo azimio la Beijing: Waziri Riziki Pembe

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 21, 2025 5:39


Wakati mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani CSW69 ukifikia ukingoni mshiriki kutoka Zanzibar Tanzania ameweleza Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili kwamba Zanzibar imepiga hatua kubwa katika usawa wa kijinsia na utekelezaji kwa vitendo matakwa ya Azimio la Beijing la usawa wa kijinsia na hatua. Je wametekeleza vipi na hatua gani walizopiga? Ungana nao katika mahojiano haya.

Radio Maria Tanzania
Ni, vyakula gani vinavyoshauriwa kuliwa wakati wa mfungo?

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Mar 21, 2025 49:23


Karibu katika Kipindi Cha Chakula na Lishe ambapo leo Bi Maria Ngilisho Afisa Lishe Mtafiti mwandamizi kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) anazungumzia juu ya Ulaji sahihi wakati wa Mfungo. L'articolo Ni, vyakula gani vinavyoshauriwa kuliwa wakati wa mfungo? proviene da Radio Maria.

SBS Swahili - SBS Swahili
Matt Gitau "wakati wakuongoza kulingana na katiba na matumaini yawa Kenya umefika"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 14, 2025 12:43


Wakenya wana endelea kukabiliana na uongozi mpya wa mseto kati ya serikali ya Kenya Kwanza na chama kikuu cha upinzani cha Orange Democratic Movement (ODM).

Habari za UN
Jumuiya ya kimataifa ishikeni mkono Sudan Kusini kwa maslahi ya wananchi - Micklina Kenyi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 12, 2025 2:10


Wakati mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake Duniani CSW69 ukiendelea hapa New York Marekani nchini Sudan Kusini wanawake na wasichana wanaendelea kuonja shubiri ya vita, wakibakwa, kuuawa, kukosa elimu na kupitia changamoto nyingine lukuki sababu ya vita. Mmoja wa washiriki wa mkutano wa CSW69 kutoka Sudan Kusini akizungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili amesema sasa imetosha amekuja na ujumbe mmoja tu, anataka jinamizi la vita lazima likome. 

Habari za UN
12 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 12, 2025 11:18


Hii leo jaridani tunaangazia mpango mpya wa UN80, unaolenga kuimarisha kazi na ufanisi wa chombo hicho ambacho mwaka huu kinatimiza miaka 80, na yaliyojiri katika mkutano wa CSW69. Makala na mashinani tunasalia hapa hapa makao makuu, kulikoni?Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amezindua Mpango mpya wa UN80, unaolenga kuimarisha kazi na ufanisi wa chombo hicho ambacho mwaka huu kinatimiza miaka 80 tangu kuanzishwa kwake huku akisisitiza umuhimu wa mshikamano wa kimataifa..Wakati mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake Duniani CSW69 ukiendelea hapa New York Marekani nchini Sudan Kusini wanawake na wasichana wanaendelea kuonja shubiri ya vita, wakibakwa, kuuawa, kukosa elimu na kupitia changamoto nyingine lukuki sababu ya vita. Mmoja wa washiriki wa mkutano wa CSW69 kutoka Sudan Kusini akizungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili amesema sasa imetosha amekuja na ujumbe mmoja tu, anataka jinamizi la vita lazima likome.Makala tukisalia hapa hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York, Marekani ambako Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, (CSW69) umeingia siku ya tatu, nimezungumza na Nuria Mshare ambaye amewakilisha taasisi ya Haki Elimu ya nchini Tanzania.Na Katika mashinani fursa ni yake Janet Zebedayo Mbene kutoka Tanzania aliyehududhuria mkutano huu hapa makao makuu, kama mwenyekiti wa shirika lisilo la kiserikali la mtandao wa uwezeshaji wa wanawake Tanzania na angependa kuwashauri wanawake na wasichana wanaopitia changamoto wajikite katika fursa mbalimbali. Kila kitu kina changamoto. Wajitie moyo na waondoe uoga, na kwa kile kidogo walicho nacho wanaweza kujiinua na kuinua jamii kwa ujumla.Mwenyeji wako ni Assumpta, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Ukraine na Marekani wapendekeza sitisho la mapigano la siku 30 wakati majibu wa Russia yakisuburiwa. - Machi 12, 2025

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 12, 2025 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Wimbi la Siasa
Serikali ya umoja wa kitaifa itasuluhisha mzozo wa DRC ?

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Mar 12, 2025 10:12


Wakati huu serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, inapoendelea kukabiliwa na changamoto ya usalama Mashariki mwa nchi hiyo, baada ya waasi wa M23 kuingia katika miji ya Bukavu na Goma, rais Felix Tshisekedi ametangaza mpango wa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa kwa kuwashirikisha wanasiasa wa upinzani.Tunajadili iwapo hatua hii itasaidia kutatua mzozo wa mashariki mwa DRC.

Siha Njema
Hali halisi ya Malaria barani Afrika wakati huu ufadhili ukiendelea kushuka

Siha Njema

Play Episode Listen Later Mar 10, 2025 10:26


Serikali za Afrika zitalazimika kuchangia ufadhili wa mipango ya kupambana na Malaria kufidia pengo kubwa la ufadhili Muungano wa viongozi wa Afrika wa kupambana na Malaria ,Africa  Leaders Malaria Alliance unasema Afrika inahitaji dola bilioni 5 nukta nane mwaka huu wa kifedha hadi 2026.Hali hii pia imechangiwa na  Marekani kukata ufadhili wa misaada kwa nchi za kigeni

Habari za UN
UN: Sasa ni wakati wa kutimiza ahadi ya usawa wa kijinsia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 7, 2025 3:28


Katika kuelekea siku ya kimataifa ya wanawake ambayo huadhimishwa kila mwaka Machi 8 leo hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kunafanyika hafla maalum ya kuadhimisha siku hiyo ambayo mwaka huu imebeba maudhui “Kwa wanawake na wasichana wote: haki, usawa, uwezeshaji.” Akizungumza kwenye hafla hiyo Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women Sima Bahous amesema ni wakati wa kutekeleza kwa vitendo ndoto ya azimio la Beijing miaka 30 iliyopita la kufanya usawa wa kijinsi kuwa hali halisiKwa upande wake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres pamoja na kupongeza mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kusongesha usawa wa kijinsia duniani amesemaNatts….“Hata hivyo, mafanikio haya yaliyopatikana kwa jitihada kubwa bado ni dhaifu na hayatoshi kabisa.Mateso ya muda mrefu, ukatili, ubaguzi na ukosefu wa usawa wa kiuchumi bado vinaathiri jamii zetu.Kila baada ya dakika kumi, mwanamke huuawa na mwenzi wake au mwanafamilia.”Ameongeza kuwa wanawake na wasichana milioni 612 wanaishi chini ya kivuli cha migogoro ya silaha ambapo haki zao mara nyingi huchukuliwa kama zisizo na thamani.Akitaja takwimu amesema chini ya theluthi mbili ya wanawake duniani wanashiriki katika soko la ajira na wale wanaoshiriki hulipwa mishahara ya chini kuliko wanaume.Hivyo ameonya kwamba“Kwa kasi hii, itachukua miaka 130 kutokomeza umasikini uliokithiri kwa wanawake na wasichana.Amemesema badala ya kuingiza usawa wa haki kama jambo la kawaida, dunia inashuhudia kuenea kwa ubabe na chuki dhidi ya wanawake.Kwa muktadha huo amesistiza kwamba “Hatuwezi kukaa kimya wakati maendeleo yanaporudishwa nyuma. Lazima tupambane.”Akizungumzia sauti za vijana kushiriki katika harakati za usawa na haki za wanawake, kwenye hafla iliyofanyika mjini Geneva Uswisi kuadhimisha siku ya wanawake mwanafunzi kutoka Kenya James Mumo Nyumu amesisitiza kuwa hakuna nchi yoyote iliyotekeleza ahadi yao ya dunia isiyo na ukatili dhidi ya wanawake.Amesema “Maono ya Beijing yalikuwa ramani ya siku zijazo ambazo bado hatujazifikia kikamilifu,” alisema akiongeza kuwa “Nguvu kwa wanawake si tishio ni zawadi kwa jamii.”Hivyo amesisitiza kwamba“Kizazi changu kinadai hatua zaidi,” akitoa wito wa kuchukua hatua zaidi ya Beijing kwani“Kazi yetu haijakamilika.”

VOA Express - Voice of America
Wanawake nchini DRC wanaelezea magumu wanayoyapitia wakati dunia inajiandaa kusheherekea siku ya mwanamke kimataifa. - Machi 07, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 7, 2025 29:59


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Radio Maria Tanzania
Fahamu ulaji sahihi wakati wa mfungo.

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Mar 7, 2025 52:38


Karibu katika Kipindi Cha Chakula na Lishe ambapo leo Bi Maria Ngilisho Afisa Lishe Mtafiti mwandamizi kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) anazungumzia juu ya Ulaji sahihi wakati wa Mfungo. L'articolo Fahamu ulaji sahihi wakati wa mfungo. proviene da Radio Maria.

Radio Maria Tanzania
Ni, kwanini Padre ananawa mikono wakati wa Misa Takatifu?

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Feb 27, 2025 21:51


Karibu katika Kipindi cha Maswali yahusuyo Imani ukiwa nami Frateri Jackob Mkandawile Kutoka Seminari Kuu ya Mtakatifu Augustino Peramiho, Jimbo Kuu la Songea nikijibu swali la Msikilizaji linalosema wakati wa Misa Padre huwa ananawa Mikono yake  wakati mikono yake ni misafi. Je, kwa tendo hilo anatuonesha ishara gani? L'articolo Ni, kwanini Padre ananawa mikono wakati wa Misa Takatifu? proviene da Radio Maria.

SBS Swahili - SBS Swahili
Jinsi yakupata shughuli za baada ya shule za bei nafuu na jumuishi

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Feb 25, 2025 13:30


Shughuli za baada ya shule huwapa watoto na vijana faida nyingi, kuanzia kujifunza ujuzi mpya hadi jinsi yakupata marafiki wapya. Wakati kuna chaguzi nyingi nchini ya vitu vyakufanya nchini Australia, shughuli hizo zina weza kuwa ghali.

Habari za UN
UNICEF na WFP wawezesha watoto nchini Sudan Kusini kwenda shule ili watimize ndoto zao

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 24, 2025 2:03


Mashirika ya Umoja wa Mataifa, lile la Kuhudumia Watoto, UNICEF na la Mpango wa Chakula duniani, WFP kwa kushirikiana na mradi wa pamoja wa kimataifa wa mnepo ,au Joint Resilience Project (JRP) nchini Sudan Kusini ,wanatekeleza msaada wa chakula bora na salama bila malipo kwa watoto shuleni ,kwa zaidi ya wanufaika laki tano alfu Hamsini 550,000 ili kuhakikisha ndoto za watoto hao zinatimia. Ni sauti ya watoto wakitembea kuelekea shuleni huku wakiwa wamevibeba vitabu vyao mikononi.Kupitia video iliyoandaliwa na UNICEF, Tieng Maleng, mnufaika wa mradi wa JRP kutoka kijiji cha Pangapdit anaonekana akiwapa watoto wake kiamsha kinywa huku wakiwa wamekaa nje ya boma lao wakiwa wamevalia sare zao tayari kwenda shule. Kwa furaha anaeleza jinsi mradi huu umekuwa wa manufaa kwa familia yake.“Baada ya kupokea msaada wa kifedha, nilitumia fedha kidogo kulipa ada ya shule ya watoto wangu. Nikachukua sehemu kidogo ya fedha hizo kununua viatu vyao, na dawa. Pia nilitumia sehemu nyingine ya msaada huo katika kilimo.”Katika shule ya msingi ya Pangapdit inayoungwa mkono na mradi huu, watoto wanaonekana wakiwa wamesimama kwenye gwaride la shule wakisikiliza maelekezo kutoka kwa walimu wao. Aluel,Mwanawe Tieng Maleng, ambaye ni mwanafunzi katika shule hiyo anasema, “Tunaenda shule kila asubuhi na ndoto yangu ni kufanya kazi na mashirika yanayosaidia watu. Wakati kengele ya shule inapolia, tunakusanyika kwa ajili ya mkutano na baadaye tunaenda darasani.”Kupitia mradi huu,wanafunzi wamepokea vitabu vya kusoma,wamejengewa madarasa mapya, vyoo bora , na mifereji ya kunawa mikono.UNICEF na WFP wanafanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa watoto wanatimiza ndoto zao.

VOA Express - Voice of America
Vijana nchini Tanzania wanaelezea changamoto wanazoziona wakati wanapotaka kujihusisha na nafasi za uongozi katika siasa. - Februari 20, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 20, 2025 29:52


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Habari za UN
18 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 18, 2025 10:34


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina leo inayotupeleka DRC katika mji wa Goma uliokuwa mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini ambao sasa uko mikoni mwa waasi wa kundi la M23. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ujumbe kutoka mashinani.Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu, OHCHR imesema hali huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC inazorota kwa kasi kubwa, na kusababisha ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu, ukatili kama vile watu kuuawa kiholela, wakiwemo watoto, wakati huu ambapo waasi wa M23 yaripotiwa wametwaa mji wa Bukavu, jimboni Kivu Kusini.Wakati hayo ya kiendelea ndani ya DRC, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limeripoti kuwa katika siku chache zilizopita, wakongo kati ya 10,000 na 15,000 wamevuka mpaka wa DRC na kuingia Burundi wakikimbia mapigano.Na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP limekaribisha mchango wa dola milioni 5 kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kusini. kwa ajili ya kujengea mnepo na kuimarisha upatikanaji wa chakula kwa familia za maeneo kame nchini Kenya.Na mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, fursa ni yake Faraja Kashindi Malumalu kutoka Tanzania ambaye ni mkimbizi katika kambi la Nyarugusi na mfanyakazi wa kituo hicho cha matibabu  ambaye anaonesha furaha kutokana na ujenzi wa kituo kipya cha wagonjwa wa ukimwi ambao umesaidia kuhifadhi faragha(privacy) ya wagonjwa.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Bw Omari "watu wana anza sema wakati wa Kabila ulikuwa afadhali kuliko sasa"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Feb 3, 2025 11:42


Hali ya usalama inavyo zidi kudorora katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ndivyo serikali ya Rais Tshisekedi inavyo zidi kuwa chini ya shinikizo kubwa.

Habari za UN
Umeme wa uhakika wanufaisha wanafunzi na jamii nchini Senegal

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 31, 2025 3:17


Senegal, taifa lenye watu zaidi ya milioni 18.5 liko kwenye mwelekeo wa kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma ya umeme. Benki ya Dunia inasema kiwango cha kupata umeme kwenye taifa hilo sasa ni asilimia 84. Wakati huu ambapo asilimia zaidi ya 30 ya jamii za vijijini hazina huduma hiyo, serikali kwa kushirikiana na wadau kama vile Benki ya Dunia na sekta binafsi imechukua hatua na mabadiliko yameanza kuonekana. Je ni yapi? Assumpta Massoi anaelezea kwenye makala hii.

Habari za UN
Huu ni wakati wa kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na AI-Guterres

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 22, 2025 3:20


Viongozi wa kimataifa wa masuala ya kisiasa na biashara wanaokutana Davos Uswisi kwa ajili ya jukwaa la kiuchumi duniani WEF, leo wamekabiliwa na ukweli mchungu kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, akilaani ukosefu wa ushirikiano wa kimataifa katika dunia inayokosa mwelekeo, ikikabiliwa na hatari mbili kubwa ambazo ni mabadiliko ya tabianchi na akili mnemba au AI isiyodhibitiwa. Flora Nducha na taarifa zaidiAkizungumza katika Jukwaa hilo la kila mwaka la Kiuchumi Duniani Katibu Mkuu amewaonya viongozi wa dunia na wakuu wa biashara kuhusu vitisho viwili vinavyoongezeka kwa ubinadamu mabadiliko ya tabianchi na akili mnemba au AI isiodhibitiwa amesema “Kunapokuja suala la tishio la kimataifa nyuklia sio tishio pekee. Leo hii tunakabiliwa na matishio mawili makubwa ambayo yanahitaji kupewa uziti Mkubwa wa kimataifa na hatua kwa sababu yanatishia kubadili kabisa maisha tunayoyajua, janga la mabadiliko ya tabianchi na upanuzi wa kasi wa wigo wa akili mnemba.”Akikosoa ukosefu wa ushirikiano katika kukabiliana na changamoto hizi kubwa, Guterres ametoa wito wa kuchukua hatua za pamoja haraka ili kushughulikia dunia aliyoiita  dunia inayokosa mwelekeo “Hebu tukabili ukweli , leo hii watu wengi wanapoitazama dunia hawaoni ushirikiano mkubwa wala maarifa ya kutosha . Licha yah atua zilizopigwa uwekezaji katika nishati jadidifu , teknolojia na masuala ya  kiafya ni dunia na matatizo yetu mengi yanazidi kuwa mbaya”Kuhusu mabadiliko ya tabianchi, Guterres amelinganisha uraibu wa dunia kwa nishati ya mafuta na mnyama wa Frankenstein, akisisitiza madhara yake makubwa.Amebainisha kuwa baadhi ya bandari kuu za mafuta duniani ziko hatarini kutokana na viwango vya bahari kuongezeka, jambo linalosababishwa na uchomaji wa makaa ya mawe, mafuta, na gesi asilia.Katibu Mkuu amekemea viwanda na taasisi za kifedha zinazosuasua kwenye ahadi zao za tabianchi, akisema hii ni kukosa maono na usaliti wa sayansi na watumiaji wanaotafuta uendelevu.Akizungumzia hatari na fursa za AI, Guterres ameelezea kama upanga wa makali mawili. Ingawa inatoa matumaini katika kubadilisha sekta za afya, kilimo, na elimu, ameonya kuhusu hatari kubwa ikiwa haitadhibitiwa.Amesema AI isiyodhibitiwa inaweza kuvuruga uchumi, kudhoofisha imani kwa taasisi, na kuongeza ukosefu wa usawa.Guterres amehitimisha kwa kutoa wito wa mshikamano wa kimataifa katika kukabiliana na changamoto hizi muhimu akisema “kubadili mwelekeo wa taasisi kunahitaji kubadili fikra kwa sababu tunakabiliwa na changamoto kubwa zinazoweza kuiangamiza dunia na sishawishiki kwamba viongozi wanalielewa hili.”Amesisitiza umuhimu wa kurekebisha mifumo ya utawala wa kimataifa ili kukabiliana ipasavyo na migogoro ya kisasa, akionya kuwa utashi wa kisiasa ni muhimu lakini bado haupo katika kiwango cha kutosha.Ujumbe wake ni bayana kwamba sasa ni wakati wa kuchukua hatua za pamoja na za haraka.

Siha Njema
Ongezeko la mafua na magonjwa yenye dalili za mafua wakati wa joto

Siha Njema

Play Episode Listen Later Jan 21, 2025 9:27


Kumeendelea kushuhudiwa kwa idadi  kubwa ya watu wanaougua mafua au magonjwa yanayoathiri mfumu wa kupumua mwezi Januari ambao una joto jingi na vumbi.  Hii inajiri wakati China ikiwa imeripoti mlipuko wa ugonjwa wa Human metapneumovirus ,HPMV unaofanana na COVID 19 .Daktari  Juma Maleve kutoka Hospitali ya rufaa ya Mombasa ,Pwani ya Kenya anafafanua.

Alfajiri - Voice of America
Wakati Tanzania ikijiandaa kwa uchaguzi mkuu baadaye mwaka huu, je hali ya kisiasa ikoje? - Januari 16, 2025

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 16, 2025 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
UNICEF: Zama mpya za majanga kwa watoto , wakati vita vikishika kasi na pengo la usawa likiongezeka

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 13, 2025 2:22


Ripoti mpya ya kila mwaka kuhusu mustakabali wa watoto ambayo imetolewa  leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, imeonya kwamba dunia inaingia katika zama mpya za majanga kwa watoto . Taarifa ya Flora Nducha inafafanua zaidi

Habari za UN
Fikra za kikoloni zimeiharibu Afrika ni wakati wa kuziondoa: Padre Toussaint Murhula

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 4, 2024 3:41


Mkutano wa mwaka 2024 wa Taaluma kuhusu Afrika leo katika leo umeingia siku ya pili hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Mkutano huo ulioandaliwa na Ofisi ya mshauri maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Afrika UNOSAA ni wa siku tatu na umebeba maudhui "Nguvu, Haki, na watu” kwa ajili ya mabadiliko ya Afrika.Na moja ya mabadiliko ni kuondoa fikra za kikoloni tangu kufanyika mkutano wa Berlin ulioligawa mapande bara hilo  yapata miaka 140 iliyopita amesema mmoja wa washiriki wa mkutano huo aliezungumza na  Flora Nducha wa idhaa hii kuhusu kile wanachojadiliana na anaanza kwa kujitambulisha

Habari za UN
UNODC yajivunia miaka 20 ya kupambana na UKIMWI magerezani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 2, 2024 2:17


Wakati jana Desemba Mosi Ulimwengu ukiadhimisha Siku ya Kimataifa ya UKIMWI kwa kuhamasisha haki za binadamu ili kufanikisha vita dhidi ya ugonjwa huu hatari, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya ya Kudhibiti Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) inajivunia miaka 25 ya kujiunga na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kukabiliana na UKIMWI (UNAIDS) katika kushughulikia janga la Virusi Vya UKIMWI (VVU) miongoni mwa watu wanaotumia dawa za kulevya na miaka 20 ya kazi ya kupambana na UKIMWI magerezani.  Anold Kayana na taarifa zaidi.

Habari za UN
02 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 2, 2024 10:42


Hii leo jaridani tunaangazia mashauriano huko Busan kuhusu matumizi ya plastiki, na ripoti ya UNODC kuhusu UKIMWI na kudhibiti dawa za kulevya katika magereza. Makala inaturejesha Havana Cuba na mashinani inatupeleka nchini Kenya, kulikoni?Vuta nikuvute kwenye mashauriano huko Busan, Korea Kusini kuhusu mkataba wenye nguvu za kisheria dhidi ya uchafuzi utokanao na matumizi ya plastiki na kulinda mazingira ya baharini imefikia ukingoni kwa mkutano kuahirishwa na wawakilishi wa nchi zilizokuwa zinashiriki kuridhia rasimu mpya yenye ibara 32 itakayojadiliwa mwakani.Wakati jana Desemba Mosi Ulimwengu ukiadhimisha Siku ya Kimataifa ya UKIMWI kwa kuhamasisha haki za binadamu ili kufanikisha vita dhidi ya ugonjwa huu hatari, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya ya Kudhibiti Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) inajivunia miaka 25 ya kujiunga na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kukabiliana na UKIMWI (UNAIDS) katika kushughulikia janga la Virusi Vya UKIMWI (VVU) miongoni mwa watu wanaotumia dawa za kulevya na miaka 20 ya kazi ya kupambana na UKIMWI magerezani.Makala leo inamulika jinsi bidhaa za kitamaduni zinavyotumika kukuza na kuendeleza mila na desturi za Kiswahili mkoani Tanga Kaskazini mwa Tanzania. Je ni bidhaa zipi hizo na zinatumika vipi? Tuungane na Flora Nducha aliyeyabaini hayo hivi karibuni alipokuwa Havana Cuba kwenye kongamano la kimataifa la Kiswahili.Na mashinani tunasikiliza manufaa ya ufadhili wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya kilimo, IFAD kwa wakulima kutoka kwake Sharon Kirui kutoka Kaunti ya Nakuru nchini Kenya ambaye ni mnufaika wa vocha za kielektroniki za ununuzi kutoka kwa IFAD na ameweza kupanua biashara yake ya kilimo.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Kuna mkwamo kwenye mkutano wa COP29 huku mapendekezo mapya yakitaka nchi tajiri kuzilipa masikini dola bilioni 250 kwa mwaka

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 2:07


Majadiliano ya mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP29 yamekumbwa na mkwamo huko Baku Azerbaijana muafaka haujapatikana. Majadiliano hayo yaliyotarajiwa kukunja jamvi leo sasa yanaendelea kwa kuwekwa mezani mapendekezo mapya kuhusu ufadhili wa mabadiliko ya tabianchi hasa kwa matifa yanayoendelea. Hakika vuta nikuvute bado inaendelea hata sasa washiriki wako mezani kwakikuna vichwa na kujadili mapendekezo mapya. Mkwamo huo umetokana na kushindwa kuafikiana katika masuala kadhaa kubwa likiwa ufadhili wa  mabadiliko ya tabianchi na hususasn kuhusu ni kiasi gani cha fedha nchi zinazoendelea zinapaswa kupokea kila mwaka hadi ifikapo mwaka 2030 na wapi fedha hizo za ufadhili zitatoka.Nchi zinazoendelea zinataka kulipwa dola trilioni 1.3 kwa mwaka lakini hilo halijaafikiwa na mapendekezo mapya yaliyowasilishwa na raia wa mkataba huo wa UNFCCC yanaonyesha tofauti kubwa na safari ndefu ya kufikia muafaka.Kwa mujibu wa mapendekezo hayo mapya yaliyowasilishwa leo mezani na Rais wa COP29 Mukhtar Babayev yanataka nchi zinazoendelea kupokea dola bilioni 250 kwa mwaka hadi kufikia mwaka 2035 kwa ajili ya kuchukua hatua didi ya mabadiliko ya tabianchi.Na maesema “Fedha hizi zitatoka katika vyanzo mbalimbali ikiwemo sekta za umma na za binafsi, na kitaifa na kimataiifa ikiwemo vyanzo mbadala”.Wakati pia COP29 ikitoa wito wa kufikia lengo la ufadhili wa dola trilioni 1.3 ifikapo mwaka 2035 pia imezikaribisha nchi zinazoendelea kutoa michango ya ziada.Kiwango kilichopendekezwa cha ufadhili kinatarajiwa kuzusha vuta ni kuvute katika majadiliano hayo kwa siku nzima ya leo huenda hadi kesho ingawa mkutano huo unahisi ahuweni kwamba kuna kiwango kilichowasilishwa na unataka hitimisho la mkutano haraka iwezekanavyo. Je nchi zinazoendelea zitapokea vipi pendekezo hili jawabu bado halijulikani. Wapenzi wa UN News Kiswahili endeleeni kufuatilia kwenye kurasa zetu kufahamu hatma ya mkutano huo.

Habari za UN
Walinda amani wa UNIFIL nchini Lebanon wasimilia kinachowakabili mashambulizi ya Israel yakiendelea

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 28, 2024 2:20


Kikosi cha muda cha Umoja wa Mataifa nchini Lebanon, UNIFIL, ambapo, katikati ya mvutano unaoongezeka kati ya Lebanon na Israel, walinda amani walioko katika makao makuu ya UNIFIL huko Naqoura wamekuwa wakivumilia mazingira magumu. Ushuhuda wa hivi karibuni kutoka kwa walinda amani hao unaonesha ukubwa wa changamoto wanazokabiliana nazo, ikiwemo vitisho vilivyoongezeka kutoka kwa shughuli za kijeshi za Israel zilizo karibu na eneo hilo, vizuizi vya kusafiri, na changamoto za uendeshaji wa shughuli. Kupitia video ya  Kikosi hicho cha muda cha Umoja wa Mataifa nchini Lebanon, UNIFIL, tunaona picha ya makao makuu yake huko Naqoura, Lebanon. Hapa tunaona ofisi za walinda amani hao, karibu na ofisi hii kuna mnara wa ulinzi, sehemu yake ikiwa imeharibiwa na mlipuko. Meja Kalpani Fernando anaelekeza kwenye mnara huo akieleza kilichotokea.“Ghafla, tuliona, na kusikia mlipuko. Kisha tukaona vumbi kubwa likitokea na moshi mweusi. Tulikimbia ndani ya ofisi, na ndani ya sekunde chache, mlipuko wa pili ulitokea. Kisha wanajeshi wawili kati ya kikosi changu walijeruhiwa walipokuwa wakifanya kazi katika Kituo cha Uangalizi cha 6. Walikuwa nje ya Kituo cha Uangalizi wakati huo, na walijeruhiwa kutokana na mlipuko wakati huo. Kisha nikafunga lango, na tukawapeleka hospitalini ndani ya muda wa dakika mbili hadi tatu.”Ingawa mzozo huu umesababisha madhara kwa afya ya walinda amani hawa, huku baadhi yao wakipata upasuaji kutokana na majeraha, bado wanaendelea kuwa na dhamira ya kuhudumu katika ujumbe wa kulinda amani. Mmoja wao ni Koplo Wickramage akisema….‘‘Wakati nilipokuwa kwenye zamu katika Kituo cha Uangalizi cha 6, kulitokea mlipuko na nikajeruhiwa kwenye sehemu ya nyuma ya bega langu. Nilihamishwa haraka kwenye hospitali ya UNIFIL. Nimefanyiwa upasuaji, na ninaendelea na matibabu. Sasa, ninapata nafuu na natumai kuungana na walinda amani wa Sri Lanka hivi karibuni ili kurudi kuhudumu katika UNIFIL.”Mbali na majukumu yao ya kawaida, wafanyakazi wa afya wa UNIFIL wamekuwa wakifanya kazi kwa bidii, wakitoa huduma si tu kwa walinda amani waliojeruhiwa bali pia kwa raia walionaswa katikati mwa mapigano hao kama anayoeleza Luteni Kanali Shilpi Mankotia,“Mbali na huduma za kawaida za matibabu, siku hizi tunatoa msaada na huduma kwa majeruhi na manusura waliolengwa kimakosa, ikiwa ni pamoja na raia na wahudumu wa kibinadamu. Nilikuwa kwenye likizo niliposikia kuhusu mzozo  unaoendelea kwa sasa. Nilirudi kazini mara moja kutoka India. Nilifika Beirut usiku wa manane na baada ya kupambana kwa siku saba, hatimaye niliweza kurudi kwenye kituo changu cha kazi.”

Habari za UN
Grandi: Msaada wa haraka unahitajika DRC wakati wakimbizi wanaendelea kufungasha virago

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 25, 2024 1:38


Wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC wanaendelea kukimbilia Uganda kukwepa machafuko nchini mwao, huku rasilimali zikikaribia kikomo. Ameonya Kamishina mkuu wa  shirika la Umoja wa Mtaifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, Filippo Grandi, akiwa ziarani nchini Uganda hivi karibuni kwenye kambi inayohifadhi wakimbizi wa DRC na kutoa wito kwa jamii ya kimataifa kuongeza msaada.Wakimbizi wanaokimbia mzozo  nchini DRC wanashuhudia matukio ya kutisha ya mauaji na ubakaji amesema Grandi, alipotembelea kambi ya ......aliyetembelea kambi za wakimbizi, Uganda na kusimuliwa hadithi za uchungu mkubwa“Sijawahi kusikia simulizi za machungu na hofu kama hizi za mauaji, ubakaji wa watoto mbele ya mama zao, wanawake wajawazito kukatwa vipande na makundi yenye silaha, na hofu kutawala maeneo yote ya Mashariki mwa Congo.”Kutokana na hali hii, Grandi anasema amani ndiyo inahitajika zaidi kwa sasa ili kumaliza dhuluma zinazowakumba wakimbizi wa Congo.“Ni wakati sasa jamii ya kimataifa ijitolee kwa dhati kusaidia Congo kutoka kwenye hali hii. Nilifanya kazi kama afisa wa eneo zaidi ya miaka 30 iliyopita Mashariki mwa Congo, na hali haijabadilika kimsingi.”Uganda inahifadhi jumla ya wakimbizi...... wengi wakiwa kutoka DRC, Sudan na Sudan Kusini.

Habari za UN
Mohamed hajakata tamaa ya kuwa mwanasoka maarufu - Gaza

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 18, 2024 1:53


Katika ufukwe wa Al- Mawasi, magharibi mwa mji wa Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza huko Mashariki ya Kati, mchezaji mpira wa Klabu ya Soka ya Rafah Services anaendelea na mazoezi yake ili kuendeleza uthabiti wa mwili kama mchezaji wa soka wa kulipwa wa klabu hiyo muhimu wakati huu mashambulizi ya makombora yakiendelea kwenye eneo hilo. Jua linazama hapa kwenye ufukwe wa Al Mawasi, kwenye bahari ya Mediteranea, wengine wakiwa wanaogelea, na kwa mbali mahema ya waliosaka hifadhi baada ya kufurushwa kaskazini mwa Gaza, mmoja anaonesha mbwembwe za dana dana ya mpira, anajitambulisha."Naitwa Mohamed Abu Jalda, mchezaji wa Klabu ya Rafah Services katika daraja la kwanza. Nilikuwa na ari kubwa ya kuwa mchezaji mkubwa wa soka kama wengine walioko nje ya Ukanda wa Gaza, lakini kutokana na vita, tamaa yangu na maisha yangu yalicheleweshwa, sasa nina zaidi ya miaka 20, nikijaribu kuwa mchezaji wa soka, lakini siwezi kwa sababu naishi Gaza ambapo kuna mapigano ya mara kwa mara. Kila siku nahisi kama ninakufa; Mungu atujalie uvumilivu kuhimili maisha haya."Mohamed amekuwa akiwa na ndoto ya kucheza soka ya kulipwa tangu akiwa na umri wa miaka 10 na sasa ana umri wa miaka 20 anaona ndoto inayoyoma, lakini ana matumaini.."Wakati wowote nikipata muda na kutamani kucheza soka,ninakuja ufukweni, kwani ni sehemu pekee naweza kucheza kama mchezaji mwingine. Natumai Mungu atanijalia kufanikiwa kuwa mchezaji wa soka, na najivunia kuwa mpalestina kutoka Gaza. Natamani kucheza soka nje ya Gaza na timu ya taifa ya Palestina, kwa sababu ni haki yangu."

Habari za UN
Guterres: Ni wakati muafaka sisi kuwasikiliza wasichana

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 11, 2024 1:45


Ikiwa le oni Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa kuwapa sikio watoto wa kike akianza ujumbe wake mahususi kwa ajili ya siku hii akisema uwezo wa wasichana zaidi ya bilioni 1.1 duniani hauna kikomo lakini tunapokaribia tarehe mwaka 2030, wa mwisho kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu, ulimwengu unaendelea kuwaangusha wasichana.“Wasichana wanachangia zaidi ya asilimia 70 ya maambukizi mapya ya Virusi Vya Ukimwi, VVU” anasema Guterres na kwamba wana uwezekano mara mbili zaidi wa wavulana kukosa elimu au mafunzo. Na ndoa za utotoni bado zimeenea, huku takriban msichana mmoja kati ya watano duniani akiolewa kabla ya kufikia umri wa miaka 18. Kotekote duniani, mafanikio yaliyopatikana kwa bidii ya usawa wa kijinsia yanafutwa na vita dhidi ya haki za kimsingi za wanawake na wasichana, na kuhatarisha maisha yao. kuzuia uchaguzi wao, na kuweka kikwazo cha mustakabali wa wasichana.Kwa kutumia kaulimbiu ya mwaka huu ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike ambayo ni ‘Dira ya Msichana' kwa Zama Zijazo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anasema, wasichana tayari wana dira ya ulimwengu ambamo wanaweza kustawi. Wanafanya kazi kugeuza maono hayo kuwa vitendo, na kutaka sauti zao zisikike. Ni wakati muafaka sisi kusikiliza. Ni lazima tuwape wasichana nafasi kwenye meza, kupitia elimu, na kwa kuwapa rasilimali wanazohitaji na fursa za kushiriki na kuongoza.Ujasiri, matumaini na uamuzi wa wasichana ni nguvu ya kuzingatia. Ni wakati wa ulimwengu kuchukua hatua na kusaidia kubadilisha maono na matarajio yao kuwa ukweli.

Habari za UN
Mwaka 1 wa vita Mashariki ya Kati: Ni wakati wa amani Gaza, asema Guterres

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 7, 2024 2:14


Leo ni mwaka mmoja tangu vita ianze huko Gaza, Mashariki ya Kati baada ya wanamgambo wa kipalestina, Hamas kushambulia Israeli na kuua waisraeli 1250 pamoja na wageni, kisha Israeli kujibu mashambulizi yaliyoripotiwa kuua hadi sasa zaidi ya wapalestina 41,000 ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa pamoja na wakuu wa mashirika mbali mbali ya chombo hicho wametoa wito kutaka kukoma kwa vita hiyo. Assumpta Massoi na maelezo zaidi. Antonio Guterres huyu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kupitia ujumbe wake kwa njia ya video leo ikiwa in mwaka mmoja, anasema hii ni siku kwa jamii ya kimataifa kurejelea tena kwa sauti kubwa zaidi kulaani kwetu kwa vitendo vya kuchukiza vya Hamas ikiwemo utekaji nyara wa siku ile.Hamas waliteka nyara zaidi ya watu 250. Guterres amesema katika kipindi cha mwaka mmoja amezungumza na familia ambazo ndugu zao wanashikiliwa mateka hadi sasa. Amezungumzia pia machungu yaliyoibuka baada ya vita kuanza. Sasa anasema ni wakati wa kuachilia huru mateka. Wakati wa kunyamazisha bunduki. Wakati wa kukomesha machungu yaliyogubika ukanda huo. Wakati wa amani, sheria ya kimataifa na haki. Umoja wa Matiafa umejizatiti kufanikisha malengo hayo. Pisha nikupishe za manusura, magari ya wagonjwa na viwewe ni hali ya kawaida Gaza kwa mwaka mmoja sasa.Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la afya ulimwenguni, WHO, pamoja na kusaidia waathiriwa wa vita, linashirikiana na mashirika ya kiraia kusaidia wale wanaosaidia manusura, mathalani madereva wa magari ya wagonjwa, wahudumu wa afya ambao waliathiriwa na kile walichokiona wakati wakisafirisha mahututi au kutambua maiti kwenye vifusi.Lile la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina, UNRWA limemnukuu Abu Majdi mpalestina mwenye umri wa miaka 80 akisema baada ya mwaka mmoja wa ukimbizi, joto kali na baridi kali, hadi lini tutaendelea kuhimili ukimbizi huu? Hadi lini tutapata haki na maisha yetu?Naye Kaimu Mkuu wa Ofisi ya UN ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA  Joyce Msuya anasema hakuna takwimu zinazoweza kueleza bayana madhila ya kimwili, kiakili na kijamii ya vita hiyo.

Habari za UN
UN: Lebanon inakabiliwa na zahma kubwa wakati mashambulizi ya Israel yakiendelea

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 4, 2024 2:01


Mashirikika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yameonya kwamba hali ya kibinadamu inazidi kuwa mbaya nchini Lebanon wakati mashambulizi ya anga ya Israel yakiendelea kushika kasi na kuwafungisha virago maelfu ya watu, wengi wakikimbia nchi jirani ya Syria ambako nako si shwari. Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO linasema hali nchini Lebanon ni janga la kibinadamu watu wengi wamejeruhiwa , wengine kupoteza maisha na mfumo wa afya umelemewa.Kupitia ukurasa wake wa  X Mkurugenzi mkuu wa WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema katika jitihada za kuwasaidia waathirika ndege ya kwanza ya msaada wa vifaa vya kitabibu vya upasuaji, dawa na vifaa tiba vingine imewasili mapema leo mjini Beiruti na vifaa hivyo vitatosha kuwatibu maelfu kwa maelfu ya watu na kuokoa maisha yao na ndege nyingine mbili zitawasili baadaye leo.Kwa upande wake Shirika la Umoja wa  Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema maelfu ya watu wanaendelea kukimbia mashambulizi ya makombora ya Israel na wengine wakivuka mpaka kwa miguu kuingia Syria kusaka uslama. Pamoja na kwamba linafanya kila liwezekanalo kuwasidia , limesema msaada zaidi unahitajika kukabiliana na wimbi la watu wanaoendelea kufurushwa.Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa mjini Geneva wao “ Wamelaani vikali mashambulizi yanayotekelezwa kwenda Israel na makundi yenye silaha yasiyo ya kiserikali yaliyopo Lebanon ambayo yamesababisha watu 63,000 kutawanywa nchini Israel. Wamesema wahusika lazima wawajibishwe na watu waliotawanywa wapewe msaada na ulinzi.”Hata hivyo wamesisitiza kwamba“ Israel haiwezi kutumia uhalifu huo kama sababu ya kuhalalisha uhalifu wao nchini Lebanon unaojumuisha vitendo vya machafuko yenye lengo la kuleta hofu miongoni mwa raia wanaowashambulia.”Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, chini ya muda wa mwezi mmoja idadi ya wakimbizi wa ndani nchini Lebanon imeongezeka mara tatu na zaidi ya watu 1,600 wameuawa  na wengine takriban 346,000 kujeruhiwa wakiwemo watoto 127.

Habari za UN
UNESCO: Tunapaswa kuthamini sauti za walimu kote duniani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 4, 2024 2:58


Washiriki wa hafla ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Walimu ililofanyika leo Oktoba 4 katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) jijini Paris, Ufaransa  wamesisitiza wito wa kuthamini mawazo ya walimu katika kuboresha elimu ya ulimwengu. Kama tunavyofahamu, siku yenyewe ya Kimataifa ya Walimu ni kesho Oktoba 5 kama ilivyo ada ya kila mwaka lakini katika makao makuu ya UNESCO hapa Paris Ufaransa, maadhimisho yamefanyika leo kuelekea mkesha wa siku hii muhimu kwa elimu ya ulimwengu.Miongoni mwa waliozungumza ni Mkurugenzi Msaidizi Mkuu wa Elimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi Stefania Giannini, ambaye ameitumia nafasi hii kusisitiza kauli mbiu ya mwaka huu ambayo ni 'Kutambua sauti za walimu.'Anasema, “walimu ni uti wa mgongo wa mifumo ya elimu na mawakala wakuu wa mabadiliko ya kubuni sera za elimu na kufanikisha SDGs. Tunapaswa kuthamini sauti za walimu; hili ndilo lengo kuu la Siku ya Kimataifa ya Walimu mwaka huu.”Kulingana na takwimu zilizotolewa na UNESCO, dunia inahitaji walimu wa ziada milioni 44 ili kufikia elimu ya msingi na sekondari kwa wote ifikapo mwaka 2030. Ingawa mahitaji ya walimu ni makubwa zaidi katika baadhi ya maeneo, uhaba wa walimu ni wa kimataifa.Walimu wanajiondoa kwenye taaluma hii kwa kiwango mara mbili zaidi ya miaka mitano iliyopita, hasa katika elimu ya sekondari. Hii inatokana na hali zao za kazi, zikiwemo mishahara midogo, mzigo mkubwa wa kazi, na ukosefu wa ushiriki katika maamuzi yanayohusu elimu. Akiiangizia changamoto hii, Mkurugenzi wa Kimataifa wa Elimu na Maendeleo ya Vijana katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) Bi. Pia Britto, aliyejiunga katika hafla ya leo kwa njia ya video akiwa Pakistani amesema,"Leo nilikuwa na fursa nzuri ya kuzungumza na walimu wengi, ikiwa ni pamoja na mwalimu Tahseen Bashir hapa Islamabad, ambaye amenieleza baadhi ya changamoto wanazokabiliana nazo ikiwa ni pamoja na kufundisha madarasa mengi, uhaba wa vifaa vya kujifunzia, na changamoto za kutoweza kufundisha namna wanavyodhamiria. Lakini pia amenieleza jinsi alivyofurahi kuona wanafunzi wake wakifaulu. Wakati sauti ya mwalimu inaposikilizwa na wakati sauti za walimu zinapopewa kipaumbele, wanajiona kama wadau katika kuboresha elimu kwa wakati wote, na hatua hizo zinahitajika ili kuleta mabadiliko chanya hasa katika hali ngumu zaidi."Siku hii ya kimataifa ya walimu ni mahususi kwa ajili ya kutambua na kusherehekea mchango muhimu wa walimu ulimwenguni kote katika kutoa elimu bora na kujenga mustakabali wa jamii. Pia, ni fursa ya kuangazia changamoto wanazokabiliana nazo walimu.Kutoka hapa Paris Ufaransa, mimi ni Cecily Kariuki..

SBS Swahili - SBS Swahili
Francis "wakati wakubadilisha shule ni sasa"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 18, 2024 10:35


Idadi ya wanafunzi wakimataifa itapunguzwa mwaka ujao, serikali inapojaribu kupunguza uhamiaji wa ng'ambo.

Habari za UN
Mnara wa kudumu kukumbuka mauaji ya kimbari ya 1994 dhidi ya Watutsi nchini Rwanda umewekwa katika makao makuu ya UN

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 13, 2024 2:13


Mnara wa kudumu wa kumbukumbu ya mauaji ya kimbari ya 1994 dhidi ya Watutsi nchini Rwanda umesimikwa kwenye bustani ya makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York kuhakikisha kilichotokea hakitosahaulika na  asilani kisitokee tena. Hapa katika bustani ya Umoja wa Mataifa mnara huo uliopewa jina “Kumbukumbu ya Mshumaa wa matumaini au Mshumaa wa mautumaini wa Kwibuka” unaonekana bayana hata ukiwa mbali. Na umetengenezwa mithili ya mshumaa Mkubwa uwakao ikiwa ni zawadi maalum kutoka Jamhuri ya Rwanda kwa Umoja wa Mataifa na umesimikwa hapa rasimi jana Alhamisi.Una kitako cha rangi neyusi na maadhindi ya rangi ya dhahabu ukiwa ni mfano wa mshumaa uwkao wa rangi ya kijivu ukiwa umeandikwa maneno  ya kiingereza yakimaanisha “Mauji ya kimbari ya mwaka 1994 dhidi ya Watutsi nchini Rwanda, kumbuka-ungana-upya na Kwibuka mshumaa wa matumaini”Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa mnara huu ni ishara ya mnepo na ujasiri wa watu wa Rwanda tangu mauaji ya kimbari ya 1994 dhidi ya Watutsi na wengine wenye msimamo wa wastani ambapo zaidi ya watu milioni 1 waliuawa kufuatia miaka mingi ya taarifa potofu, za uongo, na kauli za chuki zilizochochea mivutano ya kijamii.Wakati wakisimika mnara huo msaididizi wa Katibu Mkuu wa idara ya mawasiiano ya kimataifa Melissa Flemming alifunguka akisema "Mshumaa wa matumaini wa Kwibuka utawaka milele kama kumbusho kwa jumuiya ya kimataifa  na wageni wote wanaokuja hapa kwenye Umoja wa Mataifa kuhusu haja ya kuzungumza wazi na kusema Hapana kwa chuki.”Mnara huo umesimikwa wakati Umoja wa Mataifa ukijiandaa na mkutano wa zama zijazo utakaoanza mwisho wa wiki ijayo ukifuatiwa na mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kikao cha 79.

Habari za UN
WHO na Zanzibar zashirikiana kutokomeza ugonjwa wa matende

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 4, 2024 1:52


Huko Zanzibar Tanzania, shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO kanda ya AFrika, linashirikiana na serikali kukabili ugonjwa wa matende ambao ni miongoni mwa magonjwa ya kitropiki yaliyopuuzwa au NTDs. Bosco Cosmas na maelezo zaidi.(Taarifa ya Bosco Cosmas)Video ya WHO kanda ya Afrika inatupeleka Zanzibar, Tanzania nyumbani kwa  Hamis Njani akitembea kwa shida, miguu imevimba. Alipata ugonjwa wa matende akiwa na umri wa miaka 18 lakini sasa WHO imempatia matumaini.(Sauti ya Hamis Njani)“Inaweza kukupata homa siku mbili kwa wiki, kwa hiyo nikashindwa kwenda shuleni.  Wakati mwingine nashindwa kuhudhuria shule kwa miezi hata mitatu. Ninapokwenda kule hospitali, ninapata huduma na mafunzo ya jinsi ya kuishi na haya maradhi kama vile kusafisha, kutumia dawa na mengine yote.”Ugonjwa huu huenezwa na mbu. Husababisha miguu au korodani kujaa maji  .Tangu mwaka 2010 Zanzibar imeendesha kampeni 20 za mgao wa dawa na WHO imetoa dawa kutibu watu milioni 1.5 kila mwaka. Asha Makame ni Mgawaji wa dawa kwenye jamii.(Sauti ya Asha Makame)“Mwanzo ulikuwa mgumu kwa sababu watu walikuwa hawaelewi.  Kwa sasa hivi mwitikio ni mzuri kwa sababu kile kitu watu wamekitumia na wanajua faida yake.WHO imefundisha pia madaktari katika kila hospitali ya wilaya kufanya upasuaji wa kisasa wa mabusha kwa wagonjwa 500.  Dkt. Shali Ahmed ni Meneja Mradi wa NTDs, Wizara ya Afya, Zanzibar.(Sauti ya Dkt. Shali Ahmed - Meneja wa mradi)“Ninaamini kufikia mwaka 2030, hata kabla ya hapo tutakuwa tumekomesha ugonjwa wa matende. Kwa hiyo tunawashukuru sana WHO kwa ushirikiano tunaoupata kwa kupata dawa, mara nyingi tunapata dawa kwa wakati na za kutosha kwa ajili ya nchi nzima.”

Alfajiri - Voice of America
Rais Biden asema wakati umefika kukabidhi mwenge kwa kizazi kipya - Julai 25, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jul 25, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

SBS Swahili - SBS Swahili
Wa Australia wa Mataifa ya Kwanza wasema 'Sasa zaidi ya Wakati wowote' upatanisho wa kweli unahitajika

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 28, 2024 9:07


Hii ni wiki ya Upatanisho, ina adhimisha tarehe mbili muhimu katika historia ya Australia kwa haki zawatu wa Mataifa ya Kwanza.

SBS Swahili - SBS Swahili
Afrika Kusini ya adhimisha mwisho wa kumbukumbu ya apartheid wakati wa ongezeko ya kutoridhika nchini humo

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 3, 2024 6:42


Africa Kusini ina adhimisha miaka 30 tangu uchaguzi wakwanza wayo waki demokrasia ambapo kila raia wa Afrika Kusini aliweza piga kura.