Podcasts about katika

Place in Paphos District, Cyprus

  • 128PODCASTS
  • 2,853EPISODES
  • 21mAVG DURATION
  • 1DAILY NEW EPISODE
  • Dec 15, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024

Categories



Best podcasts about katika

Show all podcasts related to katika

Latest podcast episodes about katika

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho
Kituo cha jambo Redio nchini DRC chapokea tuzo kwenye COP30

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho

Play Episode Listen Later Dec 15, 2025 10:00


Nchini jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Kituo cha Jambo redio, kimejitwika jukumu la kuelimisha jamii kuhusu masuala ya mazingira na tabianchi, lakini muhimu sana ni haki zao. Katika mkutano wa tabianchi uliotamatika jijini Belem nchini Brazil, kituo cha Jambo Redio kilipokea tuzo kutoka kwa shirikika linalotetea haki za wanawake Women Engage for a Common Future, WECF. Kituo hiki, kimekuwa kikitoa habari kwa jamii ambazo wakati mwingine hazina uwezo wa kupata habari.

brazil congo belem jambo katika kwenye redio mazingira kidemokrasia
Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali "“MWENDAWAZIMU HAPEWI UPANGA"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 11, 2025 1:39


Katika kujifunza lugha Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya,  kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "“MWENDAWAZIMU HAPEWI UPANGA" 

Habari za UN
11 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 11, 2025 11:30


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Sudan Kusini kufuatilia mradi wa kilimo cha mpunga ulivyoleta ustawi kwa jamii ya katikati mwa Sudan unaofanikishwa kwa msaada wa mafunzo wa walinda amani wa UN kutoka Korea Kusini wanaohudumu katika UNMISS kupitia wanasayansi na wakulima wa eneo la Bor katika. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ufafanuzi wa methali.Mapigano makali mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yamesababisha vifo vya zaidi ya raia 70, kuwafurusha watu zaidi ya 200,000, na kusitisha msaada wa chakula kwa maelfu. Umoja wa Mataifa unasema hali katika Kivu Kusini imezorota kwa kasi, huku msaada wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP ukisimama na shule zaidi ya 30 zikigeuzwa makazi ya dharura. Katika taarifa yake, Naibu Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Farhan Haq, amesema hali imefikia kiwango cha hatari, akionya: “Familia zinazoishi kwa njaa sasa zinagawana chakula chao cha mwisho na watu waliokimbia makazi. Hii ni dharura inayovuka mipaka.” UN inazitaka pande zote kusitisha mapigano mara moja na kuruhusu misaada kufika kwa walio hatarini.Mkutano wa kikao cha 7 wa Baraza La Mazingira la Umoja wa Mataifa UNE-7 unaeelekea ukingoni jijini Nairobi Kenya na miongoni mwa washiriki ni kijana mwanaharakati wa mazingira kutoka asasi ya Umoja wa Mataifa YUNA nchini Tanzania Ally MwamzoraNa leo Umoja wa Mataifa unaadhimisha Siku ya Kimataifa ya Milima, ukisisitiza umuhimu wa milima kama “kitovu cha maji ya dunia.”  Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO, takriban asilimia 70 ya maji safi ya Dunia yamehifadhiwa kama theluji au barafu, yakitoa mito inayosambaza maji ya kunywa, kilimo, viwanda, na umeme wa maji na takriban watu bilioni mbili, ikiwa ni pamoja na jamii nyingi za asili, wanategemea maji ya milima kwa mahitaji yao ya kila siku, maisha, na tamaduni zao. Wataalamu wanasisitiza kuwa kulinda mazingira ya milima ni muhimu ili kuhakikisha upatikanaji wa maji kwa vizazi vijavyo.Katika kujifunza lugha Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya,  kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "“MWENDAWAZIMU HAPEWI UPANGA"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Wataalamu waonya kuwa msimu wa moto umeanza tunapotarajia joto kuongezeka

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 11, 2025 8:03


Katika wiki za hivi karibuni, moto wa nyika umesababisha uharibifu wa nyumba na mali katika maeneo ya pwani ya katikati ya kaskazini ya New South Wales, Geraldton huko Magharibi mwa Australia na mashariki mwa Tasmania. Wataalamu wanaonya kuwa huu ni mwanzo tu wa msimu wa moto na nyinyi ambao mnasafiri kwa ajili ya likizo mnahitaji kuwa na ufahamu na maandalizi mkiwa mbali na nyumbani.

Habari za UN
09 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 9, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea ufafanuzi wa umuhimu wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Haki za binadamu kutoka kwa Seifu Magango Msemaji wa Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa ambaye anaanza kwa kuzungumzia azimio la tamko hilo la haki za binadamu.Utafiti uliofanywa na Tume ya Ulaya kwakushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa linalaoshughulikia masuala ya wanawake UN Women umebaini kuwa wanawake saba kati ya kumi wakiwemo watetezi wa haki za binadamu, wanaharakati na waandishi wa habari wanakumbana na ukatili mtandaoni.Meneja Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masuala ya watoto UNICEF Tess Ingram yupo ziarani Ukanda wa Gaza huko Mashariki ya kati ambapo hii leo amezungumza na waandishi wa habari jijini Geneva Uswisi na kuwaeleza aliyoshuhudia huko ikiwemo wajawazito walio na utapiamlo kujifungua watoto wenye uzito mdogo au kuzaliwa kabla ya wakati, ambao wengine wanakufa katika vyumba vya wagonjwa mahututi      au wengine hupona lakini watoto hao hukabiliwa na utapimlo au matatizo mengine ya kiafya.Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Kutokomeza Ubaguzi wa Rangi CERD, leo imetoa onyo kali kwa Sudan, ikieleza wasiwasi mkubwa kuhusu ongezeko la matumizi ya lugha ya kudhalilisha, kauli za chuki na ukiukaji Mkubwa wa haki za binadamu unaochochewa na misingi ya kikabila. Kamati imesem Mashambulizi haswa dhidi ya jamii za Fur, Masalit na Zaghawa, yanadaiwa kufanywa na Kikosi cha Msaada wa Haraka RSF na makundi washirika katika maeneo ya El Fasher, Darfur Kaskazini.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "PEKUPEKU"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "PEKUPEKU"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 9, 2025 0:46


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "PEKUPEKU." 

Habari za UN
UN: Mchango wa watu wanaojitolea ni muhimili wa mabadiliko

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 5, 2025 3:03


Katika dunia inayohitaji mshikamano ili kufikia maendeleo, mchango wa watu wanaojitolea umeendelea kuwa nguvu muhimu ya kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa. Kila mwaka tarehe 5 mwezi Desemba, dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanaojitolea, mwaka huu ikiwa imebeba maudhui“Kila Mchango Una Umuhimu.”  Maadhimisho ya mwaka huu pia yanazindua rasmi Mwaka wa Kimataifa wa Wanaojitolea kwa Maendeleo Endelevu 2026. Kutoka Dar es Salaam, Tanzania Sabrina Saidi amezungumza na kijana  ambaye anajitolea katika Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa Tanzania YUNA Je kasema nini?.

Habari za UN
Kutoka changamoto hadi mafanikio: Safari ya Kibra kupitia mfuko wa CERF

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 5, 2025 2:18


Katika eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia, jitihada za kuimarisha makuzi na elimu kwa watoto wenye ulemavu zinaendelea kuleta matumaini mapya, kupitia programu inayoungwa mkono na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu na Masuala ya Dharura OCHA,  na Mfuko wa Dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF. Je nini kinafanyika? Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi

Habari za UN
05 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 5, 2025 11:07


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya haki za binadamu na maandamano ya amani nchini Tanzania, siku ya kujitolea tukikuletea ujumbe wa mfanyakazi wa kujitolea, na elimu jumuishi kwa ajili ya watu wenye ulemavu nchini Ethiopia.Wakati Tanzania ikijiandaa kwa maandamano makubwa yaliyopangwa kufanyika tarehe 9 Desemba siku ya maadhimisho ya Uhuru, Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR imetoa tahadhari na wito kwa serikali ya taifa hilo la Afrika Mashariki. Seif Magango ni msemaji wa ofisi ya Haki za binadamu ametufafanulia kuhusu tamko lao.Katika dunia inayohitaji mshikamano ili kufikia maendeleo, mchango wa watu wanaojitolea umeendelea kuwa nguvu muhimu ya kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa. Kila mwaka tarehe 5 mwezi Desemba, dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanaojitolea, mwaka huu ikiwa imebeba maudhui “Kila Mchango Una Umuhimu.”  Maadhimisho ya mwaka huu pia yanazindua rasmi Mwaka wa Kimataifa wa Wanaojitolea kwa Maendeleo Endelevu 2026.Katika eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia, jitihada za kuimarisha makuzi na elimu kwa watoto wenye ulemavu zinaendelea kuleta matumaini mapya, kupitia programu inayoungwa mkono na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu na Masuala ya Dharura OCHA, na Mfuko wa Dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF. Je nini kinafanyika?Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "MADHALI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 4, 2025 0:34


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "MADHALI"

Habari za UN
04 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 4, 2025 12:02


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kwa mwanariadha na mchchemuzi wa masuala ya wanawake, akieleza hatua zinazochukuliwa kutokomeza dhulma wa kijinsia. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze lugha ya Kiswahili.Huku mapigano yakizidi kushika kasi katika eneo la Kordofan nchini Sudan, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ameonya hii leo kuhusu hatari ya mashambulizi mapya dhidi ya raia, baada ya kuripotiwa vifo zaidi ya watu 269 kutokana na mashambulizi ya angani, mabomu na mauaji ya kiholela tangu mwishoni mwa mwezi Oktoba. Ofisi yake imeeleza kupokea taarifa za ulipizaji kisasi, utekaji, ukatili wa kingono na ulazimishaji wa watoto kujiunga na makundi ya kivita, huku miji kama Kadugli, Dilling na El Obeid ikikabiliwa na njaa, kuzingirwa na kukwama kwa misaada ya kibinadamu.Malaria, ugonjwa ambao takriban asilimia 95 ya vifo vinavyoripotiwa duniani ni kutoka nchi za Afrika tena kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka 5. Ulionekana kuweza kudhibitiwa lakini sasa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus, anasema unaelekea kubaya kutokana na kuongezeka kwa usugu wa dawa, hali inayotishia kuyafuta mafanikio yaliyookoa maisha ya watu milioni moja mwaka 2024 kupitia chanjo na vyandarua vipya vyenye dawa ya kukabiliana na mbu waenezao Malaria.Na tuhitimishie nchini Msumbiji ambako Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM Amy Pope amefanya ziara ya siku tatu na kujionea athari zilizoletwa na Mafuriko, vimbunga na kuzorota kwa usalama huko Kaskazini mwa nchi hiyo hali iliyosababisha zaidi ya 100,000 wameyakimbia makazi yao, na zaidi ya 600,000 wakihitaji msaada.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "MADHALI"Mwenyeji wako ni Sabrina Moshi, karibu!

Habari za UN
Guterres: Kunapokuwa na ujumuishwaji wa kweli kila mtu ananufaika katika jamii

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 3, 2025 2:53


Umoja wa Mataifa leo Desemba 3 unaadhimisha Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu kwa ujumbe mzito kutoka kwa Katibu Mkuu António Guterres ujumbe unaotaka jamii ziwe si tu zinazoweza kufikiwa na watuwenye ulemavu, bali pia zenye ujumuishi wa kweli. Flora Nducha na taarifa zaidi

Habari RFI-Ki
EAC : Wanasiasa wanatumia wahuni kujihami

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Dec 3, 2025 10:03


Katika makala haya tujadili hatua ya ongezeko la visa vya wanasiasa wa upande wa serikali na upinzani kutumia makundi ya vijana au wahuni kutisha na kuvuruga mikutano ya mahasimu wao wa kisiasa hili likifanyika hata  kwenye mitandao. Tunakuliza unafikiri kwa nini wanasiasa wanaendelea kutumia makundi ya vijana au wahuni katika siasa. skiza makala haya.

Habari RFI-Ki
EAC : Wanasiasa wanatumia wahuni kujihami

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Dec 3, 2025 10:03


Katika makala haya tujadili hatua ya ongezeko la visa vya wanasiasa wa upande wa serikali na upinzani kutumia makundi ya vijana au wahuni kutisha na kuvuruga mikutano ya mahasimu wao wa kisiasa hili likifanyika hata  kwenye mitandao. Tunakuliza unafikiri kwa nini wanasiasa wanaendelea kutumia makundi ya vijana au wahuni katika siasa. skiza makala haya.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali "KOTI LA BABU HALIKOSI CHAWA"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 2, 2025 1:15


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "KOTI LA BABU HALIKOSI CHAWA".

Habari za UN
UN: Dunia ipo katika kipindi cha maamuzi kuhusu mustakbali wa ukimwi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 2:50


Kama tulivyokujuza le oni Siku ya UKIMWI Duniani na mwaka huu inaadhimishwa kwa onyo kali kuhusu janga hilo pamoja na wito wa kuchukua hatua. Ikibeba kaulimbiu “Kukabili misukosuko, kubadili mwelekeo wa hatua za UKIMWI,” Umoja wa Mataifa unasema dunia ipo katika kipindi cha uamuzi muhimu katika vita dhidi ya VVU. Flora Nducha na taarifa zaidi

Habari za UN
UNICEF na KISE wawapiga jeki watoto wenye ulemavu katika Kaunti ya Wajir nchini Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 3:05


Katika Kaunti ya Wajir Kaskazini Mashariki mwa Kenya, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu Maalum ya Kenya KISE wameanzisha mpango maalum wa kuwasaidia watoto wenye ulemavu kupata tathmini za kitabibu na kielimu. Mpango huu umeleta matumaini mapya kwa familia nyingi ambazo hapo awali zilikuwa na ugumu wa kupata huduma hizi kama anavyofafanua Sheilah Jepngetich  katika taarifa hii

Habari za UN
“VVU si mwisho wa maisha” – Safari ya Pooja Mishra kutoka mshtuko hadi uongozi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 3:19


Pooja aliolewa akiwa na umri wa miaka 15, baadaye akiwa mdogo bado akagundua kuwa ana Virusi Vya Ukimwi, VVU, na leo ni Mratibu wa Kitaifa wa Vijana chini ya Muungano wa Kitaifa wa Watu wanaoishi na VVU nchini India (NCPI+), akifanya kazi moja kwa moja na zaidi ya vijana 1,800 kote India. Katika mahojiano yaliyofanywa na Anshu Sharma wa Idhaa ya Kihindi ya Umoja wa Mataifa, Pooja anasimulia safari yake, nafasi ya jamii na familia, na ujumbe wake kwa watu wanaoishi na VVU. Anaposema ART anazungumzia dawa za kufubaza virusi, sawa na ARV lakini katika mkusanyiko wa dawa nyingi kwa pamoja.

Habari za UN
01 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 11:33


Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa Umoja wa Mataifa katika Siku ya UKIMWI Duniani, simulizi wa mwathirika wa ugonjwa huu amabye aliolewa na umri wa miaka 15, na juhudi za UNICEF Wajir nchini Kenya za kuhakikisha ujumuishwaji wa watoto wenye ulemavu darasani.Leo ni Siku ya UKIMWI Duniani na mwaka huu inaadhimishwa kwa onyo kali kuhusu janga hilo pamoja na wito wa kuchukua hatua. Ikibeba kaulimbiu “Kukabili misukosuko, kubadili mwelekeo wa hatua za UKIMWI,” Umoja wa Mataifa unasema dunia ipo katika kipindi cha uamuzi muhimu katika vita dhidi ya VVU.Pooja aliolewa akiwa na umri wa miaka 15, baadaye akiwa mdogo bado akagundua kuwa ana Virusi Vya Ukimwi, VVU, na leo ni Mratibu wa Kitaifa wa Vijana chini ya Muungano wa Kitaifa wa Watu wanaoishi na VVU nchini India (NCPI+), akifanya kazi moja kwa moja na zaidi ya vijana 1,800 kote India. Katika mahojiano yaliyofanywa na Anshu Sharma wa Idhaa ya Kihindi ya Umoja wa Mataifa, Pooja anasimulia safari yake, nafasi ya jamii na familia, na ujumbe wake kwa watu wanaoishi na VVU. Anaposema ART anazungumzia dawa za kufubaza virusi, sawa na ARV lakini katika mkusanyiko wa dawa nyingi kwa pamoja.Katika Kaunti ya Wajir Kaskazini Mashariki mwa Kenya, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu Maalum ya Kenya KISE wameanzisha mpango maalum wa kuwasaidia watoto wenye ulemavu kupata tathmini za kitabibu na kielimu. Mpango huu umeleta matumaini mapya kwa familia nyingi ambazo hapo awali zilikuwa na ugumu wa kupata huduma hizo.Mwenyeji wako ni Sabrina Moshi, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Australia yafafanuliwa;bei za upangaji zinaendelea kupanda wakati gharama ya maisha inaongezeka.

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 6:12


Licha ya viwango vya riba kutulia, stress ya kodi bado haijabadilika kote Australia. Katika miji mingi mikubwa, kaya bado zinatoa karibu theluthi moja ya mapato yao ili kuweka paa juu ya vichwa vyao. Na mara nyingine tena, Perth inashika nafasi mbaya zaidi. Jiji kuu lisilopatikana kwa urahisi zaidi nchini limeporomoka hata zaidi — likirekodi kushuka kwa asilimia nne zaidi katika uwezo wa kumudu gharama juu ya rekodi ya chini ya mwaka uliopita.

Habari za UN
WFP: Suluhisho bunifu kwa wafugaji wa maeneo yenye ukame nchini Kenya zaleta tija

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 26, 2025 2:40


Katika maeneo yaliyoghubikwa na athari za mabadiliko ya tabianchi kaskazini mwa Kenya, wafugaji wamekuwa wakikumbwa na changamoto kubwa kwani ukame na mafuriko, vinatishia sio tu mali zao bali pia maisha yao. Lakini kupitia mradi wa bima ya mifugo unaoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula  duniani WFP, kwa ushirikiano na asasi ya Zoetis na kampuni ya ZEP-RE, jamii zinaanza kupata ahuweni na matumaini mapya. Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi.

Habari za UN
26 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 26, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia usafirir endelevu, udhalilishaji wa mtandaoni tukikuletea ujumbe kutoka Uganda, na ufugaji endelevu unaowawezesha wafugaji katika maeneo kame ya Isiolo na Garissa nchini Kenya.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameadhimisha Siku ya Kimataifa ya Usafiri Endelevu Duniani kwa kuonya kwamba mifumo ya usafiri duniani ambayo ni muhimu kwa uchumi na maisha ya kila siku inayochochea dunia kuelekea janga la tabianchi na kwa hivyo siku hii inatukumbusha kwamba njia ya kuelekea mustakabali bora inategemea mifumo safi na yenye uendelevu wa usafiri.Siku 16 za uhamasishaji kupinga ukatili dhidi ya wanawake zikiendelea leo tunakupeka mjini Hoima Magharibi mwa Uganda kusiki maoni kutoka kwa wa mji huo kuhusu ukatili mtandaoni yakienda sanjari na kauliimbiu ya kampeni ya ya mwaka huu isemayo “Ukatili wa mtandaoni ni ukatili halisi na hakuna visingizo kwa ukatili mtandaoni”.Katika maeneo yaliyoghubikwa na athari za mabadiliko ya tabianchi kaskazini mwa Kenya, wafugaji wamekuwa wakikumbwa na changamoto kubwa kwani ukame na mafuriko, vinatishia sio tu mali zao bali pia maisha yao. Lakini kupitia mradi wa bima ya mifugo unaoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula  duniani WFP, kwa ushirikiano na asasi ya Zoetis na kampuni ya ZEP-RE, jamii zinaanza kupata ahuweni na matumaini mapya.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "MADUYUNI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 25, 2025 1:02


Katika kujifunza lugha Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "MADUYUNI"

Habari za UN
25 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 25, 2025 12:23


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, na leo zinaanza siku 16 za uanaharakati kuelimisha umma kuhusu janga la ukatili wa kijinsia, tunamsikia  mmoja wa waathirika wa ukatili wa kingono.Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa onyo kali kuhusu ongezeko la ukatili mtandaoni dhidi ya wanawake na wasichana.Ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya wanawake UN Women na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya dawa na uhalifu UNODC inaonya kwamba mwaka 2024, wanawake na wasichana 50,000 waliuawa na wapenzi au jamaa sawa na mwanamke mmoja kila dakika 10.Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo (UNCTAD) inaonya kwamba uchumi wa Eneo la Palestina Linalokaliwa kwa Mabavu na Israel umerudi nyuma miaka 22 kwa muda usiozidi miaka miwili kwani umeingia katika hali mbaya zaidi ya mdororo kuwahi kurekodiwa, huku miongo ya maendeleo ikifutwa na operesheni za kijeshi zilizodumu kwa muda mrefu pamoja na vizuizi vya muda mrefu.Katika kujifunza lugha Kiswahili hii leo,  mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "MADUYUNI"Mwenyeji wako ni Sabrina Said, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Australia yafafanuliwa:Afya ya akili katika ujauzito na baada ya kujifungua

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 24, 2025 9:51


Karibu mmoja kati ya Waustralia wanne hawatafuti msaada wanapopata matatizo ya afya ya akili wakati wa ujauzito au baada ya kujifungua. Wataalamu wanasema kwamba taarifa zilizotolewa na Gidget Foundation zinaonyesha ukosefu wa kuelewa dalili na ishara, pamoja na unyanyapaa unaoendelea kuhusu suala hili.

Habari za UN
21 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 21, 2025 12:02


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, mbinu bunifu za kilimo cha kakao nchini Peru, na mradi wa miundombinu wa kupunguza athari ya mafuriko na kugeuza maji ziada kuwa rasilimali muhimu kwa jamii nchini Rwanda.Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ujulikanao kama MONUSCO, leo umelaani vikali mashambulizi makubwa yaliyofanywa na kundi lenye silaha la Allied Democratic Forces ADF kati ya tarehe 13 na 19 Novemba 2025 katika baadhi ya maeneo ya Lubero, jimboni Kivu Kaskazini na kukatili maisha ya raia wengi.Katika msitu wa Amazon upande wa nchi ya Peru, jamii za watu wa asilizimeonesha namna mbinu bunifu za kilimo zinaweza kuongeza uzalishaji na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Yote haya yanakuja wakati dunia ikiendelea kujadili mustakabali wa hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika mkutano wa Umoja wa Mataifa COP30 unaoendelea huko Belém, Brazil.Mwezi Mei 2023, Rwanda nchi iliyozungukwa na milima ilikumbwa na mafuriko makubwa yaliyosababisha maporomoko ya ardhi na kusababisha maji kutoka katika milima ya volkano, yakiambatana na mawe mazito kuharibu mashamba, makazi na barabara. Baada ya mafuriko hayo ili kupunguza athari za majanga kama hayo, kwa wakati mwingine Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) nchini Rwanda, kwa ufadhili wa Serikali ya Japan, linatekeleza mradi wa Kukabiliana na Majanga Yanayohusiana na Maji katika wilaya za Rutsiro na Burera. Lengo ni kupunguza Athari na kugeuza maji ziada kuwa rasilimali muhimu kwa jamii.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Jamii za asili Peru zaongeza uzalishaji wa kakao kwa mbinu bunifu za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 21, 2025 4:01


Katika msitu wa Amazon upande wa nchi ya Peru, jamii za watu wa asilizimeonesha namna mbinu bunifu za kilimo zinaweza kuongeza uzalishaji na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Yote haya yanakuja wakati dunia ikiendelea kujadili mustakabali wa hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika mkutano wa Umoja wa Mataifa COP30 unaoendelea huko Belém, Brazil.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana na matumizi ya neno "UPUNGUFU"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2025 0:57


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "UPUNGUFU"

Habari za UN
18 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2025 11:32


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Brazil kwenye mkutano wa COP30, ambako Dkt. Richard Muyungi, Mjumbe maalumu kwenye masuala ya mabadiliko ya tabianchi na mazingira kutoka nchini Tanzania anaeleza ni nini bara la Afrika linahitaji.Umoja wa Mataifa umekaribisha kupitishwa kwa Azimio namba 2803 la Baraza la Usalama kuhusu Gaza hapo jana, ukilitaja kuwa hatua muhimu katika kuimarisha usitishaji mapigano. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, anazitaka pande zote kuheshimu kikamilifu makubaliano hayo na kutafsiri kasi ya kidiplomasia kuwa hatua za dharura na za wazi kwa watu walioko katika eneo hilo. Katika taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Guterres, Stéphane Dujarric, amesema Umoja wa Mataifa umejizatiti kuongeza misaada ya kibinadamu na kuunga mkono jitihada zinazoelekezwa katika hatua inayofuata ya usitishaji mapigano.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), hali ya kibinadamu katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kusini bado ni tete. Mkurugenzi wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu, Kanda ya Afrika Patrick Youssef  ambaye amerejea hivi karibuni kutoka DRC amewaleza waandishi wa habari jijini Geneva, Uswisi kwamba raia wa DRC wanaendelea kubeba mzigo mzito wa mapigano, hata wakati shughuli chache za kibiashara zikiendelea kurejea Goma. Ametoa tahadhari kuwa mgogoro huo unakabiliwa na upungufu mkubwa wa ufadhili, ukatili wa kingono unaongezeka, na zaidi ya asilimia 70 ya watu waliojeruhiwa kwa silaha mwaka huu ni raia.Kuanzia leo tarehe 18 inaanza Wiki ya Kimataifa ya Kuelimisha Umma kuhusu Usugu wa Vijiumbemaradhi dhidi ya dawa. Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, linaonya kuwa usugu wa vimelea yaani hali ambapo bakteria, virusi na vijidudu vingine havidhuriki tena kwa dawa tayari unatishia mifumo ya afya, uchumi na uhakika wa chakula. Kwa kaulimbiu “Chukua Hatua Sasa: Linda Leo Yetu, Linda Mustakabali Wetu,” WHO inatoa wito kwa serikali, wahudumu wa afya, wakulima, wadau wa mazingira na umma kuchukua hatua madhubuti kutekeleza ahadi za kisiasa ili kupunguza kuenea kwa maambukizi sugu ya dawa.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "UPUNGUFU"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
13 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 13, 2025 10:40


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia simulizi za waahirika wa Kimbunga Melissaikiwa ni wiki ya pili sasa baada ya kupiga magharibi mwa Jamaica, na kuacha zahma kubwa kwa wakaazi. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze Kiswahili.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akieleza kuwa na wasiwasi mkubwa kutokana na ripoti za ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na mauaji ya halaiki mjini El Fasher, pamoja na kuongezeka kwa mapigano katika maeneo ya Kordofan nchini Sudan. Guterres amesema “Mtiririko wa silaha na wapiganaji kutoka nje lazima ukatwe. Misaada ya kibinadamu lazima iweze kuwafikia haraka raia wanaohitaji, na mapigano lazima yakome,”.Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumatano limemchagua Phoebe Okowa kutoka Kenya kuwa Jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), baada ya duruu nne za upigaji kura. Upigaji kura huo ulifanyika kwa wakati mmoja na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, lakini kwa utaratibu tofauti, kama inavyotakiwa na Katiba ya Mahakama hiyo ya Haki. Bi. Okowa amechaguliwa kwa wingi wa kura ambapo alipata kura 8 katika Baraza la Usalama na kura 106 katika Baraza Kuu.Kumekuwa na ongezeko la uraibu wa nikotini na bidhaa nyingine zinazozalishwa kwa kutumia tumbaku duniani hususani miongoni mwa vijana na tena wengi hivi sasa wanatumia sigara za kielektroniki, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO. Tarehe 17 mpaka 21 Novemba utafanyika mkutano mkubwa kujadili namna serikali, mashirika ya kimataifa na asasi za kiraia zitakavyoweza kusaidia kupambana na janga la tumbaku duniani, linalosababisha vifo zaidi ya milioni saba kila mwaka.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KASIMU"Mwenyeji wako ni Sabrina Said Moshi, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "KASIMU".

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 13, 2025 1:00


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo,  mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KASIMU".

Habari za UN
Ripoti mpya ya FAO/WFP yaonya muda unayoyoma kuzuia mamilioni kuingia kwenye njaa katika maeneo 16 hatarishi.

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 12, 2025 3:39


Ripoti mpya ya pamoja kutoka mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa lile la  Chakula na Kilimo Duniani (FAO) na la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) inaonya kwamba uhaba mkubwa wa chakula unazidi kuongezeka katika maeneo 16 yenye njaa duniani, hali inayoweza kusababisha mamilioni zaidi ya watu kukumbwa na njaa kali au hatari ya kufikia kiwango cha baa la njaa. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali "CHA KIPOFU KI MKONONI MWAKE"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 11, 2025 1:31


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Daktari. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya,  kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "CHA KIPOFU KI MKONONI MWAKE"

Habari za UN
Urejerezaji: Usajili wa warejeshaji wa mazingira Afrika Kusini waleta nuru katika kazi yao

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 10, 2025 2:35


Habari za UN
05 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 5, 2025 11:27


Katika jarida la habari za Umoja wa Mataifa hii leo utasikia kuhusu wito wa mataifa yote kuwekeza kwenye mifumo ya tahadhari za mapema ikiwa leo dunia inaadhimisha Siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu Tsunami. Utasikia pia ziara ya Rais wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa nchini Qatar ambapo amewatembelea wakimbizi wa kipalestina walioko nchini humo. Kutoka nchini Kenya utasikia juhudi za taasisi ya FODDAJ kusaidia jamii nchini Kenya kupambana na ukatili wa kijinsia. 

Habari za UN
Guterres atumia siku ya elimu kuhusu tsunami kukumbusha mkakati wa kujikinga

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 5, 2025 1:51


leo ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu Tsunami Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesisitiza umuhimu wa kuwekeza katika kujiandaa dhidi ya mawimbi hayo makubwa ya bahari yanayotokana na tetemeko chini ya bahari. Anold Kayanda na maelezo zaidi.Asante Assumpta,Katika ujumbe wake, Guterres amesema maandalizi hayo yanahusisha kuweka mifumo ya kutoa maonyo ya mapema au tahadhari kwenye kila ufukwe, jamii na kokote kule.Bwana Guterres amefafanua kuwa tsunami si matokeo ya mara kwa mara lakini pindi yanapotokea madhara yake yanaweza kuwa makubwa na hata kusababisha vifo.“Husababisha vifo vya maelfu na hata mamia ya maelfu ya watu. Lakini kuna mbinu za kuweka watu salama,” anasema Guterres.Ametolea mfano janga la tsunami kwenye bahari ya Hindi mwaka 2004, janga ambalo lilisababisha dunia kuamua kuwekeza katika mifumo ya kutoa maonyo mapema.“Miongo kadhaa baadaye, uamuzi huo umelipa,” amesema Katibu Mkuu akitolea mfano tetemeko kubwa la ardhi lililokumba pwani ya Urusi mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu akisema, “lilisababisha tahadhari kwa mamilioni ya watu kuanzia pwani za Japani hadi visiwa vilivyoko bahari ya Pasifiki hadi California.”Ingawa hivyo amesema madhara ya janga hilo la tsunami yanaendelea kubadilika kutokana na mabadiliko kadhaa ikiwemo yale ya tabianchi.Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa akieleza kuwa kuheshimu baharí ni kutambua nguvu yake anasema,  “kiwango cha maji ya bahari kikiongezeka, na idadi ya watu wanaoishi maeneo ya pwani ya bahari ikiongezeka, mifumo ya kutoa maonyo mapema nayo inahitaji uwekezaji zaidi na kuboreshwa,”Ni kwa mantiki hiyo amesema hilo ndio lengo la mpango wa Umoja wa Mataifa wa Mfumo wa Tahadhari kwa Wote ulioanzishwa kwa lengo la kuhakikisha kila mtu anafikiwa na mpango wa utoaji onyo mapema dhidi ya tsunami ifikapo mwaka 2027.Maadhimisho ya mwaka huu ni ya 10, ambapo Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilianzisha siku hii kupitia azimio namba 70/203 la mwaka 2005.

Habari za UN
Nashukuru FODDAJ imenirejeshea matumaini ya maisha - Mnufaika

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 5, 2025 3:16


Nchini Kenya, shirika la kiraia la FODDAJ  au la Forum for Women Development, Democracy and Justice linatekeleza kivitendo lengo namba 3 la Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs la afya bora na ustawi ambalo pamoja na mambo mengine linataka manusura wa ukatili wa kijinsia wapatiwe huduma sio tu za afya bali pia za kijamii. Je linafanya nini, Sheilah Jepngetich amezungumza na mwakilishi wa shirika hilo.Ni Salome Gatakaa Araka, Mwakilishi wa FODDAJ ambaye katika mazungumzo nami anaanza kwa kuelezea walianzia wapi harakati zao.  Akisema Policy and Advocacy anamaanisha Sera na Uchechemuzi.“FODAJ ilianza na uundaji wa ufahamu yaani policy and advocacy kumaanisha kwamba kuwe  kutengwa kwa fedha za kutengeneza mahali pa waathiriwa kuishi, na pia kusisitiza ufahamu wa kutetea wale ambao wametengwa. Katika kata ya Kajiado, tumesukuma sera za GBV ili kuimarisha juhudi za kuzuia waathiriwa kuumia zaidi.”Pamoja na kukabili ukatili wa kijinsia, nikataka kufahamu iwapo wanawejengea wanawake uwezo wa kujitegemea.“FODDAJ imekuwa mstari wa mbele katika katika kupaza sauti za wanawake na wasichana, na pia kuhimiza akina mama kuweka akiba za vikundi, kushirikiana na kusaidiana ili kujikimu kiuchumi. Tumehimiza akina mama kuweka akiba kwa vikundi vya maendeleo, kushirirki mafunzo ya ujasiriamali na kushirikiana na wengine kwa pamoja. Na pia wanafundishwa mambo tofauti kama vile kutengeneza nywele , kusoma na kuandika na pia na kuhesabu.”Maneno ya Bi. Araka si matupu kwani Geraldine Ndayisenga mkazi wa Kitengela ambaye ni manusura wa ukatili na mnufaika wa miradi ya FODDAJ anafunguka.“Mimi ni mmoja wa wale waliopitia dhuluma. Nilijua kuhusu FODDAJ kupitia rafiki yangu. Nikasaidiwa, nilipata matibabu, nikapata ushauri (counselling) kwa mwezi mmoja. Baada ya hapo nikajiunga na mafunzo ya kutengeneza nywele, makucha na ushonaji. Mafunzo hayo yamenisaidia sana, sasa najisikia niko huru na nina furaha kuwa sehemu ya jamii tena. Fodaj Foundation imenishika mkono na kunionesha namna bora ya kuishi hapa Kitengela. Wamenisaidia kwa mambo mengi, na kwa kweli maisha yangu yamebadilika kwa njia chanya sana.”Nikarejea kwa Bi. Araka, kufahamu iwapo wana ushirikiano na serikali na mashirika ya kiraia. Akisema Post Traumatic anamaanisha kiwewe baada ya dhuluma.“Kwa kushirikiana na serikali na mashirika mengine ya kiraia, waathirika wanapatiwa msaada kwa ajili ya huduma za afya. Mfano wale waliobakwa au kupigwa, hupata matibabu kwa vipimo au dawa. Aidha, waathirika wa kimawazo wanapewa msaada wa kisaikolojia ili iwasaidie kuondokana na madhara ya post trauma ambayo wamepitia.

SBS Swahili - SBS Swahili
Serikali kudhibitisha umuhimu wa wahamiaji kwenye uchumi

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 4, 2025 5:42


Waziri wa Mambo ya Ndani, Tony Burke, anasema kwamba serikali inafanya kazi juu ya uwezekano wa kutambua ujuzi wa nje ya nchi. Anasema hii itasaidia kuokoa muda na pesa kwa wahamiaji wenye ujuzi wanaotafuta kuhamia Australia. Katika hotuba yake kwa Klabu ya Waandishi wa Habari huko Canberra, Bw. Burke pia ametangaza mabadiliko kwenye akaunti za benki zisizotumika ili kukabiliana na utakatishaji wa fedha.

Kiswahili, Lugha Ya Afrika
Ni nini huipa atomi umbo lake?

Kiswahili, Lugha Ya Afrika

Play Episode Listen Later Nov 3, 2025 2:56


Katika video hii fupi na ya kielimu, tunaingia ndani kabisa ya ulimwengu mdogo wa atomi na kuchunguza siri inayofanya muundo wake kuwa imara na thabiti. Tutatumia mifano rahisi, kama vile sumaku, kukusaidia kuelewa sheria za msingi za fizikia zinazotawala ulimwengu wetu.Jifunze sayansi kwa njia rahisi na ya kuvutia!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "SUMIA"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 30, 2025 1:06


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo,  mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "SUMIA."

Habari za UN
30 OKTOBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 30, 2025 11:41


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Bi. Lucy Githinji, mkazi wa jimbo la New Jersey nchini Marekani amezungumza na idhaa hii baada ya matembezi ya hiari kwa ajili ya kuhamasisha jamii kuhusu saratani ya titi, akisema hakika dawa zinafanya kazi.Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Kibinadamu nchini Sudan, Denise Brown amesema ni kweli wamepokea ripoti za mauaji ya baadhi ya wahudumu wa kujitolea huko El Fasher jimboni Darfur wakati huu ambapo mji huo umetwaliwa na wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka, (RSF).Kimbunga Melissa kimepungua nguvu baada ya kutua nchini Jamaica kama kimbunga cha kiwango cha 5, na kuvunja rekodi ya kimbunga chenye nguvu zaidi, kabla ya kuelekea kaskazini mashariki kupita Cuba hadi Bahamas, na kusababisha mafuriko makubwa, uharibifu na kukatika kwa umeme katika maeneo mbalimbali ya Karibea na Amerika ya Kati.Nchini Cameroon, kufuatia mauaji ya raia wakati wa maandamano ya kupinga kutangazwa kwa Paul Biya kuwa mshindi wa kiti cha Urais kwenye uchaguzi uliofanyika Oktoba 12, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu imeeleza wasiwasi wake juu ya ripoti za vifo hivyo.Na katika Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo,  mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "SUMIA."Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Wagonjwa wanaohitaji tiba zaidi Gaza wasafirishwa kupata tiba zaidi Afrika Kusini na kwingineko

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 29, 2025 3:24


Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO, limeongoza uhamishwaji wa wagonjwa kutoka Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, ikiwa ni  mara ya kwanza tangu kuanza kwa awamu mpya ya kusitishwa kwa mapigano kwenye  ukanda huo.Katika muda wa siku mbili, wagonjwa 41 waliokuwa katika hali mbaya pamoja na familia zao 145 wamehamishwa kutoka eneo la mgogoro, kuelekea Afrika Kusini, Uswisi na kwingineko, huku maelfu zaidi wakiendelea kusubiri matibabu ya dharura.Katika hospital iliyojengwa kwa mahema  katika eneo la AL-MAWASI, RAFAH kwenye Ukanda wa Gaza wagonjwa wakihudumiwa kila kona watoto kwa wakubwa Miongoni mwao ni Ibrahim Abu Ashiba, mkurugenzi wa filamu ambaye maisha yake yamebadilika ghafla. Anakumbuka wakati alipojeruhiwa. Anasema, "Nilipigwa risasi mara kadhaa, mara moja kwenye kifua, mara moja kwenye bega, mara mbili mkononi. Risasi hizo mbili zilikata mishipa ya neva ya mkono wangu. Sasa siwezi kushika kamera wala kunyoosha mkono wangu kawaida. Ghafla, maisha yangu yote yalisimama."Safari ya kupona kwa Ibrahim inaanzia Afrika Kusini, ambapo amekubaliwa kwenda kupokea matibabu maalum ambapo anasema "Maisha yangu yote yalikuwa yamesimama baada ya kujeruhiwa hadi waliponipigia simu na kunijulishakwamba nitasafiri kwenda Afrika Kusini kwa matibabu. Ilionekana kama nimezaliwa upya."Mgonjwa mwingine katika hospitali hii ni, Maria Al-Shaer, alijeruhiwa vibaya katika mashambulizi yaliyokuwa yakiendelea Gaza, huku akipoteza ndugu zake. Mama yake, Raghda Ahmed Al Shaer, anaelezea mateso hayo. "Maria amepoteza baba yake na ndugu zake wote. Alijeruhiwa na kuvunjika mguu, mifupa na kupoteza nyama. Anahitaji upasuaji wa kuwekewa viungo bandia. Maisha yake yamegeuka, hawezi kutembea, na hali yake ya kisaikolojia imeathirika sana."Uhamishwaji huu umeratibiwa na Shirikisho la Chama cha Msalaba Mwekundu Palestina, kwa msaada wa WHO. Dkt. Luca Pigozzi, Mratibu wa Timu ya Dharura ya WHO, anafafanua umuhimu wake."Huu ni uhamishaji wa kwanza wa matibabu tangu kusitishwa kwa mapigano Oktoba 10. Tumejizatiti kuongeza uwezo wetu kusaidia na kuratibu uhamishaji kwa ajili ya matibabu, kwa ushirikiano wa karibu na Shirikisho la chama cha Msalaba Mwekundu la Palestina."Raghda anaeleza matumaini kwa ajili ya binti yake wanapohama kwenda Uswisi. "Wametupigia kutuarifu kwamba Maria amekubaliwa kusafiri kwenda Uswisi kwa matibabu. Tumefurahi sana kwamba atatembea tena, na hali yake ya kisaikolojia itaboreka. Atarudi kuwa Maria wa kawaida kama tuliyemjua."WHO inasisitiza kuwa wagonjwa takriban 15,000 bado wanangojea idhini ya kupata matibabu nje ya Gaza na inatoa wito kwa nchi zote kufungua milango yote za dharura kwa ajili ya uokoaji wa wagonjwa.

Habari za UN
29 OKTOBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 29, 2025 9:53


Leo jaridani tunamulika kimbunga Melissa huko Karibea, uhamishaji wagonjwa kutoka Gaza kwenda nchi za nje kupata huduma za kigeni na hali tete kwa watoto nchini Sudan. Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi.Katibu Mkuu wa Umoja wa MataifaAntonio Guterres ameonesha wasiwasi mkubwa wakati Kimbunga Melissa kikiwa miongoni mwa vimbunga vyenye nguvu zaidi kuwahi kurekodiwa katika Bahari ya Atlantiki kinaendelea kusababisha uharibifu mkubwa katika eneo la Karibea.Kupitia taarifa yake iliyotolewa leo mjini New York Marekani na msemaji wake Katibu Mkuu amesema kimbunga hicho kimeacha athari kubwa nchini Jamaica, Cuba na Bahamas  huku mafuriko makubwa yakiripotiwa pia nchini Haiti na Jamhuri ya Dominika.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani, WHO, limeongoza uhamishwaji wa kwanza  wagonjwa kutoka Gaza tangu awamu mpya ya kusitishwa kwa mapigano. Katika muda wa siku mbili, wagonjwa 41 waliokuwa katika hali mbaya pamoja na familia zao 145 wamehamishwa kutoka eneo la mgogoro, huku maelfu zaidi wakiendelea kusubiri matibabu ya dharura. Flora Nducha na taarifa zaidi.Nchini Sudan hususani katika eneo la El Faher kusinimagharibi mwa nchi, hali ya kibinadamu inazidi kuwa mbaya kila siku, huku ghasia, njaa, na vizuizi vya utoaji misaada vikiendelea kuathiri mamilioni ya watu wakiwemo watoto waliokwama katika maeneo ya vita. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

Habari za UN
27 OKTOBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 27, 2025 10:00


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko ya muda mrefu nchini Myanmar, hali ya kibinadamu nchini Sudan kufuatia ripoti za vifo vya raia na wimbi la wakimbizi wa ndani, na masuala ya afya nchini Kenya.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito kwa dunia na mataifa wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kusini-Mashariki mwa Asia, ASEAN kuchukua hatua za haraka kumaliza machafuko ya muda mrefu nchini Myanmar, akisisitiza kuwa mgogoro huo si tishio kwa watu wa Myanmar pekee bali pia kwa amani na usalama wa kanda nzima ya Asia ya Kusini Mashariki.Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) imeelezea wasiwasi mkubwa kufuatia ripoti za vifo vya raia na wimbi la wakimbizi wa ndani, kufuatia kuendelea kwa mapigano makali katika mji wa El Fasher, huko Darfur Kaskazini nchini Sudan. Tupate tarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.Katika kaunti ya Mombasa nchini Kenya, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wa Mastercard Foundation na Serikali ya Kaunti ya Mombasa, imechukua hatua za kukabiliana na mlipuko wa MPOX kwa kutoa huduma muhimu za afya na WASH kwa wagonjwa na waliopona, ikiwa ni pamoja na vifaa vya kujikinga (PPEs), vituo vya kusafisha mikono na ujumbe wa mabadiliko ya tabia za kijamii.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
UNICEF yachukua hatua za kukabiliana na mlipuko wa MPOX nchini Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 27, 2025 3:02


Katika kaunti ya Mombasa nchini Kenya, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wa Mastercard Foundation na Serikali ya Kaunti ya Mombasa, imechukua hatua za kukabiliana na mlipuko wa MPOX kwa kutoa huduma muhimu za afya na WASH kwa wagonjwa na waliopona, ikiwa ni pamoja na vifaa vya kujikinga (PPEs), vituo vya kusafisha mikono na ujumbe wa mabadiliko ya tabia za kijamii. Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi

Habari za UN
24 OKTOBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 24, 2025 9:56


Hii leo jaridani tunaangazia siku ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni miaka 80 tangu kuanzishwa kwake 1945.Leo ni siku ya Umoja wa Mataifa ni miaka 80 tangu kuanzishwa kwake 1945, lakini pia ni kumbukizi ya miaka 80 tangu kuanzishwa kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambalo lilikuwa ni tukio la kihistoria na la kukumbukwa. Akiwahutubia wajumbe wa Baraza hilo kwa njia ya mtandao katika kikao cha kumbukizi hii, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa mageuzi ya dharura na mwamko mpya wa uwajibikaji, akiwakumbusha jukumu lao kuu la kulinda amani ya dunia.Tukiendelea na Siku ya Umoja wa Mataifa, ikitukumbusha kuanzishwa kwake tarehe 24 mwezi Oktoba mwaka 1945. Maudhui ya mwaka huu ni "Miaka 80 ya Umoja wa Mataifa: Kujenga Mustakabali Wetu kwa Pamoja - Ishara ya Matumaini kwa ushirikiano wa Kimataifa." Katika kumulika hili, Sabrina Saidi wa idhaa hii amezungumza na mwakilishi wa vijana pamoja na mmoja wa watumishi wa Umoja wa Mataifa kuhusu maadhimisho ya siku hii, huko jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania.Msikilizaji, bila shaka umeyasikia mengi kuhusu Umoja wa Mataifa, lakini Umoja wa Mataifa ni nini hasa? Japo kwa ufupi, Anold Kayanda anakufahamisha akianza na historia.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Siku ya UN ni ukumbusho wa wajibu wetu kuendelea maono ya shirika hilo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 24, 2025 2:10


Leo ni Siku ya Umoja wa Mataifa, ikitukumbusha kuanzishwa kwake tarehe 24 mwezi Oktoba mwaka 1945. Maudhui ya mwaka huu ni "Miaka 80 ya Umoja wa Mataifa: Kujenga Mustakabali Wetu kwa Pamoja - Ishara ya Matumaini kwa ushirikiano wa Kimataifa." Katika kumulika hili, Sabrina Saidi wa idhaa hii amezungumza na mwakilishi wa vijana pamoja na mmoja wa watumishi wa Umoja wa Mataifa kuhusu maadhimisho ya siku hii, huko jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania. 

Habari za UN
UNMISS yasaidia katika utoaji wa elimu ya uraia nchini Sudan Kusini

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 22, 2025 3:34


Kuanzia furaha ya uhuru hadi maumivu ya kurejea kwa mzozo, safari ya amani ya kudumu Sudan Kusini imekuwa ndefu na bado inaendelea. Licha ya changamoto hizo, matumaini bado ni makubwa miongoni mwa jamii nchini kote kwamba uchaguzi wa amani, huru na wa haki utaleta usalama uliotafutwa kwa muda mrefu pamoja na fursa za maendeleo na ukuaji wa uchumi. Leah Mushi anatuletea taarifa ikiangazia namna Sudan Kusini inavyojiandaa na uchaguzi wake mkuu mwakani 2026. 

katika vijana elimu unmiss uchaguzi sudan kusini
Habari za UN
21 OKTOBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 21, 2025 13:03


Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Leah Mushi anakuletea-Gaza Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula Duniani WFP lasema usitishaji wa mapigano umeleta afueni kwa wakaazi kwani sasa misaada inaendelea kuwafikia wenye uhitaji-Naibu Mratibu wa Misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Joyce Msuya amekuwa ziarani Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR na kujionea hali halisi ya wakimbizi, wakimbizi wa ndani na msaada wa kibinadamu-Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa leo limesema katika tathimini yake kuwa ukataji wa misitu umepungua duniani kote ingawa bado kuna shinikizo na hatua zaidi zahitajika-Katika mada kwa kina tunakupeleka nchini Tanzania ambako Vyuo Vikuu vinachukua hatua ya kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs hususan lile namba 17 la ubia kupitia umataifishaji. -Na kwenye jifunze Kiswahili unapata ufafanuzi wa methali " “NG'OMBE WA MNYONGE HAZAI" 

Habari za UN
WMO na wadau wajadili kuhusu tahadhari za mapema

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 20, 2025 3:29


Shirika la Umoja wa Mataifa ka Utabiri wa Hali ya Hewa Duniani WMO linaongeza kasi ya jitihada za kulinda maisha ya watu dhidi ya madhara ya mabadiliko ya tabianchi. Mkutano wake Maalum uliofunguliwa leo mjini Geneva Uswisi, unalenga kuharakisha mpango wa kimataifa wa Tahadhari za Mapema kwa Wote, sambamba na maadhimisho ya miaka 75 ya WMO. Flora Nducha amefuatilia na anafafanua zaidi (TAAFIFA YA FLORA NDUCHA)Asante Leah, kwa mujibu wa WMO idadi ya nchi zenye mifumo ya tahadhari za mapema kwa ajili ya majanga ya tabianchi imeongezeka maradufu katika kipindi cha miaka kumi iliyopita lakini bado mamilioni ya watu hawana ulinzi dhidi yah atua hiyo muhimu.Ndiyo maana shirika hilo limewakutanisha mawaziri na wataalamu kutoka nchi wanachama 193 kuharakisha mpango wa Tahadhari za Mapema kwa Wote, uliozinduliwa mwaka 2022 na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres unatekelezwa kwa vitendo.Katika mkutano huo Celeste Saulo Katibu Mkuu wa WMO amesema “Miaka 75 iliyopita, Shirika la WMO lilianzishwa kutokana na ukweli kwamba hali ya hewa, maji na tabianchi havina mipaka ya kitaifa. Ushirikiano wa kimataifa katika uchunguzi na utabiri ni wa lazima, kwa sababu hakuna nchi inayoweza kufanya hivyo peke yake.”Ripoti mpya ya WMO, iliyopewa jina Tahadhari za Mapema kwa Wote Mtazamo wa Dunia, inaonesha kuwa licha ya maendeleo makubwa katika ubadilishanaji wa takwimu na utabiri wa kidijitali, bado kuna mapengo makubwa, hasa katika nchi maskini na visiwa vidogo vinavyoendelea.Celeste amesisitiza kuwa“Tahadhari za Mapema kwa Wote sasa siyo mpango tena, bali ni nembo ya mshikamano wa dunia. Pamoja, tunaokoa maisha, tunaunda sera, na kuimarisha mnepo.”Takwimu za shirika hilo zinaonesha uzito wa changamoto. Katika miaka 50 iliyopita, WMO inasema majanga yanayohusiana na hali ya hewa na maji yamesababisha vifo vya zaidi ya watu milioni mbili huku asilimia 90 kati yao ni katika nchi zinazoendelea.Na ingawa mataifa 108 sasa yana mifumo ya tahadhari za majanga mchanganyiko, shirika hilo linasema viwango vya vifo bado ni mara sita zaidi katika maeneo yasiyo na mifumo hiyo.WMO inasema teknolojia mpya ikiwemo akili mnemba na matumizi ya takwimu za setilaiti kwa wakati halisi zinabadilisha uwezo wa utabiri, lakini pengo la kidijitali bado linawaacha wengi wakiwa hatarini.“Mafanikio ya Tahadhari za Mapema kwa Wote hayapimwi kwa ripoti au maazimio, anasema Celesto bali kwa maisha yanayookolewa na riziki zinazolindwa. Tunapoelekea mwaka 2027, hebu tuongeze juhudi kuhakikisha hakuna mtu anayeachwa bila ulinzi.”Mkutano huo Maalum wa WMO utaendelea wiki nzima mjini Geneva, huku Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akitarajiwa kuhutubia siku ya Jumatano.Shirika la WMO wakati likiadhimisha miaka 75 ya kile linachoita Sayansi kwa Vitendo  linataka kuhakikisha sayansi hiyo inawafikia wote, kabla ya majanga kutokea.