Podcasts about katika

Place in Paphos District, Cyprus

  • 128PODCASTS
  • 2,884EPISODES
  • 21mAVG DURATION
  • 1DAILY NEW EPISODE
  • Jan 23, 2026LATEST

POPULARITY

20192020202120222023202420252026

Categories



Best podcasts about katika

Show all podcasts related to katika

Latest podcast episodes about katika

SBS Swahili - SBS Swahili
Makala:Serikali ya Victoria kuendelea na ubomozi wa nyumba za umma licha ya upinzani

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jan 23, 2026 13:05


Katika wakati wa mgogoro wa makazi na gharama za maisha, serikali ya Victoria iko katika mchakato wa kubomoa minara yote 44 ya makazi ya umma ya Melbourne. Licha ya upinzani mkubwa na uchunguzi wa bunge unaotaka kusitishwa kwa haraka kwa kazi hizo, serikali ya Victoria inaendelea na mipango hiyo. Kuhama nyumba huchukuliwa kuwa moja ya matukio yenye msongo mkubwa zaidi katika maisha ya mtu. Kwa hivyo, mwaka 2023, wakati maelfu ya wakaazi wa Victoria walipokea taarifa kwamba nyumba zao zitabomolewa wakati fulani kati ya mwaka huo na 2051, msongo ulikuwa dhahiri. Tembelea tovuti yetu sbs.com.au kwa taarifa ama maelezo zaidi.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya "SIKU ZA MUAMBO" katika muktadha wa uchumi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 22, 2026 0:29


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya "SIKU ZA MUAMBO" katika muktadha wa uchumi.

Habari za UN
Dunia inaingia katika zama za kufilisika kwa maji kote duniani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 21, 2026 3:07


Katika muktadha wa kupungua kwa muda mrefu kwa maji ya chini ya ardhi, matumizi kupita kiasi ya rasilimali za maji, uharibifu wa ardhi na mmomonyoko wa udongo, ukataji miti, pamoja na uchafuzi wa mazingira, Chuo Kikuu cha Umoja wa Mataifa UNU  kimetoa ripoti inayotangaza kuingia katika“zama za kufilisika kwa maji duniani” na kutoa wito kwa viongozi wa dunia kuendana na uhalisia huu mpya kwa kuzingatia ushahidi wa kisayansi.Kulikoni ?  Flora Nducha anaeleza kwa kina ripoti hiyo.

Habari za UN
21 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 21, 2026 10:45


Hii leo jaridani tunaangazia mafuriko makubwa yaliyoikumba Msumbiji, ripoti inayomulika kupungua kwa muda mrefu kwa maji ya chini ya ardhi, na mradi unaolenga kuimarisha sekta ya kilimo katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan kwa ajili ya kuwasaidia wakulima.Kufuatia mafuriko makubwa yaliyoikumba Msumbiji kutokana na mvua zinazoendelea, serikali ya nchi hiyo ya kusinimashariki mwa Afrika imetangaza kuwa hadi kufikia sasa imerekodi vifo vya watu 120 na maelfu ya nyumba zimeharibiwa huku kiwango kikubwa cha fecha kikihitajika.Katika muktadha wa kupungua kwa muda mrefu kwa maji ya chini ya ardhi, matumizi kupita kiasi ya rasilimali za maji, uharibifu wa ardhi na udongo, ukataji miti, pamoja na uchafuzi wa mazingira, Chuo Kikuu cha Umoja wa Mataifa UNU leo kimetoa ripoti ikitangaza kuingia kwa “enzi ya kufilisika kwa maji duniani” na kutoa wito kwa viongozi wa dunia kuendana na uhalisia huu mpya kwa kuzingatia ushahidi wa kisayansi.Kwa muongo mmoja kuanzia mwaka wa 2016 hadi mwaka wa 2025, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) kwa ushirikiano na serikali ya Canada limechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha sekta ya kilimo katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan likilenga kuwasaidia wakulima na vyama vya ushirika kushinda changamoto za muda mrefu za uzalishaji, masoko na mnepo wa maisha.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Msumbiji: Serikali na UN wanaendelea kusaidia waathirika wa mafuriko katika hali ngumu ya kifedha

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 21, 2026 2:17


Kufuatia mafuriko makubwa yaliyoikumba Msumbiji kutokana na mvua zinazoendelea, serikali ya nchi hiyo ya kusinimashariki mwa Afrika imetangaza kuwa hadi kufikia sasa imerekodi vifo vya watu 120 na maelfu ya nyumba zimeharibiwa huku kiwango kikubwa cha fecha kikihitajika. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno “KING'ANI”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 20, 2026 1:13


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mtaalam wetu ONNI SIGALA Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA, anafafanua maana ya neno “KING'ANI”

Habari za UN
Türk aeleza aliyoyashuhudia katika ziara yake Sudan, aitaka dunia ichukue hatua za haraka

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 19, 2026 3:20


Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, baada ya ziara yake ya siku tano nchini Sudan, ametahadharisha kuhusu kuongezeka kwa hali mbaya zaidi ya ukikukwaji wa haki za binadamu na ongezeko la janga la kibinadamu nchini humo.Rashid Malekela na taarifa zaidi.

Habari za UN
Ili maisha yaendelee katika ukanda wa Gaza umeme unahitajika kwa udi na uvumba - UNOPS

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 16, 2026 2:48


Uharibifu Mkubwa uliosalia Gaza baada ya vita baina ya Israel na Hamas kusitishwa uko bayana katika kila kona ya jiji hilo majengo yaliyoporomoka, vyuma vililivyotapakaa kila mahali, na vitongoji vilivyogeuka kuwa vifusi. Hayo ndiyo aliyoshuhudia Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Huduma za Miradi UNOPS, Jorge Moreira da Silva, wakati wa ziara yake katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Nuseirat, katikati ya Gaza, ambako timu za Umoja wa Mataifa za kutegua mabomu ya ardhini zinashughulika kusafisha mabaki ya vita. Flora Nducha amefuatilia ziara hiyo na kutuandalia taarifa hii

Habari za UN
Kupunguzwa kwa misaada ya kibinadamu kwawasukuma mamilioni katika njaa Afrika Magharibi na Kati

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 16, 2026 2:42


Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) leo limeonya kuwa bila rasilimali na hatua za haraka, watu walio katika mazingira magumu zaidi Afrika Magharibi na Kati wanakabiliwa na mwaka mwingine mgumu sana wa njaa. Anold Kayanda na taaarifa zaidi.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "MAHULUCHI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 13, 2026 1:12


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, Mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "MAHULUCHI"

Habari za UN
13 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 13, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika mwaka mpya 2026 kwa wakazi wa Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel ambao wanaendelea kukabiliwa na hali ngumu ya maisha katika kambi za wakimbizi na katika makazi ambayo ni magofu na vifusi vya nyumba zilizoharibiwa wakati wa vita baina ya Jeshi la Israel na Wanamgambo wa Hamas.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linasema licha ya sitisho la mapigano huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, maisha ya watoto bado yako katika hali tete, huku zaidi ya watoto 100 wakiwa wameuawa tangu Oktoba mwaka jana lilipoanza sitisho hilo.Vinywaji vyenye sukari na vileo vinazidi kuwa nafuu kwa bei kutokana na viwango vya kodi kwa muda mrefu kuwa vya chini katika nchi nyingi, jambo linalochochea unene kupita kiasi, ugonjwa wa kisukari, magonjwa ya moyo, saratani na maradhi mengineyo hasa miongoni mwa watoto na vijana balehe, zimesema ripoti mpya mbili zilizotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususan jimboni Ituri, mashariki mwa nchi hiyo ambako ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, MONUSCO umepatia mafunzo ya ujasiriamali wafungwa kwenye gereza kuu lililoko Bunia, ambao ni mji mkuu wa jimbo hilo.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "MAHULUCHI"Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
12 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 12, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia wito wa kuimarishwa kwa mshikamano wa kimataifa na uwekezaji endelevu kwa wakimbizi nchini Kenya, usugu wa Viuaji- Vyasumu au AMR na utekelezaji wa mradi wa kusambaza nishati ya umeme na vifaa vya nishati nchini Chad.Katika ziara yake ya kwanza rasmi iliyofanyika nchini Kenya kama Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi, Barham Salih ametoa wito wa kuimarishwa kwa mshikamano wa kimataifa na uwekezaji endelevu ili kuwasaidia wakimbizi kujenga upya maisha yao, akionya kuwa upungufu mkubwa wa ufadhili unatishia kurudisha nyuma mafanikio yaliyopatikana kwa juhudi kubwa katika ulinzi na kujitegemea kwa wakimbizi.Shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani linaendelea na juhudi za kupambana na changamoto ya usugu wa Viuaji- Vyasumu au AMR na sasa imetoa miongozo na taratibu za kuhakikisha kuna matumizi sahihi ya dawa na wahudumu wa sekta ya afya katika nchi wanachama wanaendelea kuwapatia mafunzo ili kuzitumia kwa usahihi na kwa uwajibikaji.Nchini Chad, utekelezaji wa mradi wa kusambaza nishati ya umeme PAAET umefanikisha vifaa 145,000 vya nishati ya sola kusambazwa kwa gharama nafuu kwa kaya zilizoko majimbo 23 ya taifa hilo na sasa maisha yamekuwa bora.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Mkuu wa UNHCR ahimiza mshikamano na suluhu zaidi kwa wakimbizi Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 12, 2026 3:18


Katika ziara yake ya kwanza rasmi iliyofanyika nchini Kenya kama Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi, Barham Salih ametoa wito wa kuimarishwa kwa mshikamano wa kimataifa na uwekezaji endelevu ili kuwasaidia wakimbizi kujenga upya maisha yao, akionya kuwa upungufu mkubwa wa ufadhili unatishia kurudisha nyuma mafanikio yaliyopatikana kwa juhudi kubwa katika ulinzi na kujitegemea kwa wakimbizi. Flora Nducha na taarifa zaidi  

Habari za UN
UNDP Kenya yaunga mkono wanawake wa jamii ya asili Narok katika uhifadhi wa misitu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 9, 2026 3:33


Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, (UNDP), nchini Kenya, kupitia mradi wa kuhimili tabianchi au Climate Promise Guarantee, limewawezesha wanawake wa jamii ya asili katika Kaunti ya Narok, nchini humo kuongoza juhudi za uhifadhi wa misitu huku wakilinda urithi wao wa kitamaduni na kuboresha maisha ya familia zao. Sheilah jepnge'tich na taarifa zaidi.

Habari za UN
08 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 8, 2026 11:07


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini DRC kufuatilia yaliyojiri kwenye kikao mahsusi cha kuimarisha uhusiano mwema na wakazi wa eneo la Beni-Mavivi jimboni Kivu Kaskazini ili kuimarisha ulinzi wa amani wakati huu ambapo kwasasa hatua za kidiplomasia za kutatua mgogoro unaoikumbuka nchi hiyo zikiendelea.Hatimaye matumaini yamerejea ya kuwa na mlo mezani huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli baada ya shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP kuweza kupatia raia mgao kamili wa chakula, ikiwa ni mara ya kwanza tangu vita vianze Oktoba 7, 2023.Huko nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MINUSCA umesambaza radio zinazotumia nishati ya sola kwa jamii ikiwa ni sehemu ya  usaidizi wake wa kuhakikisha wananchi wanapata taarifa za uhakika na kwa wakati. Katika mkoa wa Nana-Mambéré, MINUSCA imekabidhi radio 600 kwa mamlaka za serikali za mitaa, wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji wa Mkataba wa Amani, viongozi wa kidini, wanawake, vijana, watetezi wa haki za binadamu, vikosi vya ulinzi na usalama, wanahabari, wauza maduka na waendesha bodaboda.Mkuu wa Idara ya Umoja wa Mataifa ya  Operesheni za Ulinzi wa Amani, Jean-Pierre Lacroix akiwa ziarani nchini Lebanon amekuwa na mazungumzo na viongozi wa jeshi la taifa hilo ambapo amewashukuru kwa ushirikiano wao na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa mpito nchini humo, UNIFIL. Wamejadili pia mpango wa unaoendelea wa kupeleka tena vikosi vya UNIFIL kusini mwa Lebanon na jinsi gani ujumbe huo unaweza kuendelea kusaidia jeshi la Lebanon kutekeleza azimio namba 1701 la Baraza la Usalama kuhusu sitisho la uhasama kati ya Israeli na wanamgambo wa Hezbollah.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na ya neno "UMWESO"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana na ya neno "UMWESO"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 8, 2026 0:33


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na ya neno "UMWESO"

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Matumizi ya neno "KUKANIA"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 6, 2026 1:03


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, Mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anatuelimisha namna ya matumizi ya neno "KUKANIA"

Habari za UN
05 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 5, 2026 11:19


Hii leo jaridani tunaangazia hali nchini Venezuela operesheni ya kijeshi ya Marekani, afya ya uzazi Tana River nchini Kenya, na wanawake wakimbizi wa DR Congo wanaopitia ukatili wa kijinsia wakikimbia machafuko. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana leo katika kikao cha dharura baada ya operesheni ya kijeshi ya Marekani nchini Venezuela tarehe 3 Januari mwaka huu, hatua iliyozua hofu ya kuongezeka kwa hali ya kutokuwa na utulivu nchini humo na katika eneo zima.Huko nchini Kenya katika kaunti ya Tana River, hali mbaya ya hewa na migogoro imesababisha takriban watu 140,000 kuyahama makazi yao. Upatikanaji wa huduma za afya nao umekuwa mgumu na kuongeza magumu hususani kwa wanawake na watoto. Katika kukabiliana na hali hiyo Wizara ya Afya nchini humo inashirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO katika kutoa huduma za afya kipaumbele kikielekezwa kwenye masuala ya uzazi salama.Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi (UNFPA), nchini Burundi, linaongeza juhudi zake kukabiliana na mahitaji yanayoongezeka ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) wanaokimbia mapigano yanayoendelea mashariki taifa hilo la Maziwa Makuu ili kulinda afya, usalama na utu wao na wa jamii zinazowapokea.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Kenya: WHO yasaidia huduma za afya katika Kaunti ya Tana River

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 5, 2026 2:43


Huko nchini Kenya katika kaunti ya Tana River, hali mbaya ya hewa na migogoro imesababisha takriban watu 140,000 kuyahama makazi yao. Upatikanaji wa huduma za afya nao umekuwa mgumu na kuongeza magumu hususani kwa wanawake na watoto. Katika kukabiliana na hali hiyo Wizara ya Afya nchini humo inashirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO katika kutoa huduma za afya kipaumbele kikielekezwa kwenye masuala ya uzazi salama. Rashidi Malekela na taaria zaidi

Habari za UN
29 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 29, 2025 9:59


Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea-Katika ujumbe wake wa mwaka mpya 2026 Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres ameitaka dunia kushikamana kwa ajili ya amani, maendeleo, na usalama badala ya kuongeza mateso-Huko Somalia kwa msaada wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na wadau wakaazi wa Laascanood waboreshewa huduma za afya baada ya kuvurugika kwa miaka miwili-Na Mkuu wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO amesema mwaka 2025 ulighubikwa na changamoto lukuki za afya ya umma duniani ikiwemo ukata wa ufadhili, lakini kuna matumaini hasa katika suala la utipwatipwa

Habari za UN
Guterres: Mwaka mpya 2026 tudumishe mshikamano na amani badala ya mateso

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 29, 2025 2:29


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa ujumbe mzito wa Mwaka Mpya kwa ulimwengu akisema ulimwengu uko katika njia panda, ukikabiliwa na machafuko, sintofahamu na migawanyiko mikubwa na hivyo kutoa wito kwa wanadamu kuinuka pamoja kwa ajili ya haki, ubinadamu na amani. Karibu Anold Kayanda kwa maelezo zaidi.(Taarifa ya Anold Kayanda)Katika ujumbe wake wa video uliosambazwa leo asubuhi saa za New York, Marekani, kwa ajili ya mwaka mpya wa 2026, Katibu Mkuu wa Umoja wa Maraifa anauanza ujumbe wake kwa kusema, “tunapoingia mwaka mpya, dunia iko njia panda.”  Amesema dunia inakumbwa na vurugu zinazoendelea, athari kubwa za mabadiliko ya tabianchi pamoja na ukiukwaji wa kimfumo wa sheria za kimataifa  hali ambayo, kwa mujibu wake, inatishia misingi inayounganisha binadamu kama familia moja ya dunia.Guterres amesema watu kote ulimwenguni wanaendelea kujiuliza iwapo viongozi wao wanasikiliza kilio cha wananchi na kama wako tayari kuchukua hatua za dhati kukabiliana na changamoto hizi.Akigeukia takwimu, Katibu Mkuu ameeleza kuwa matumizi ya kijeshi duniani yamefikia dola trilioni 2.7, ongezeko la karibu asilimia kumi kiwango ambacho ni mara kumi na tatu zaidi ya misaada yote ya maendeleo, na kinacholingana na Pato la Bidhaa za ndani la Bara zima la Afrika.Amesema ongezeko hilo linatokea wakati dunia ikishuhudia mizozo mikubwa kwa viwango ambavyo havijawahi kuonekana tangu Vita Vikuu Vya Pili Vya Dunia.Kutokana na hali hiyo, Katibu Mkuu ametoa wito kwa dunia kutumia mwanzo wa mwaka mpya kuweka vipaumbele sahihi, akisisitiza kuwa ulimwengu salama hujengwa kwa kuwekeza zaidi katika kupambana na umaskini badala ya kuwekeza katika vita.Guterres amesisitiza kuwa dunia ina rasilimali za kutosha kuinua maisha ya watu, kuponya sayari na kujenga mustakabali wa amani na haki, endapo tu zitatumika ipasavyo.Kwa mwaka 2026, amewataka viongozi wa dunia kuwa makini zaidi na kufanya uamuzi unaoweka mbele maslahi ya watu na mazingira badala ya kuendeleza mateso.Aidha, amewahimiza raia wote duniani kushiriki kikamilifu katika kujenga dunia bora, akisema mustakabali wa ubinadamu unategemea ujasiri wa pamoja wa kuchukua hatua.Katika kuhitimisha ujumbe wake, Katibu Mkuu ametoa wito wa mshikamano kwa ajili ya haki, ubinadamu na amani duniani.

Habari za UN
UNICEF na washirika wasaidia kuboresha huduma za afya Laascaanood Somalia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 29, 2025 2:43


Huko kaskazini mashariki mwa Somalia, eneo la Laascaanood linaendelea kushuhudia maboresho ya huduma muhimu za afya baada ya miaka miwili ya kuvurugika kwa huduma hizo kutokana na mizozo, maboresho haya yanaleta huduma za afya karibu zaidi na akina mama na watoto shukran kwa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF na washirika wake. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.(Taarifa ya Leah)Kwa mujibu wa UNICEF nchini Somalia, mamilioni ya watoto wanakua katika kivuli au mazingira ya ukimya na dharura zilizosahaulika, takribani watoto milioni 1.8 wanahitaji matibabu ya utapiamlo mwaka huu wa 2025. Kila mwaka watoto wapatao 75,000 walio chini ya umri wa miaka mitano hufariki dunia kutokana na magonjwa yanayozuilika na yanayoweza kutibiwa.Miaka miwili ya migogoro imesababisha kusambaratika kwa huduma muhimu huko Laascaanood. Kurejea kwa hali ya utulivu kumeanza kushuhudia urejeshwaji wa taratibu wa huduma hizi muhimu zinazookoa maisha. UNICEF, kwa msaada wa KSRelief na Saudi Esports Federation, inachangia kwenye kutoa huduma jumuishi za afya ya msingi, huku huduma hizo zote zikitolewa chini ya paa moja.Mpaka sasa maelfu ya watu wamefikiwa huku ukisaidia vituo 13 vya afya kama anavyoeleza Dayid Said Ismail Afisa Lishe (Sauti ya Dayid Said Ismail – Evarist)“Mradi huu unasaidia vituo 13 vya afya na unahudumia zaidi ya watu 150,000. Huduma zake zinajumuisha chanjo za watoto, matibabu ya magonjwa kama nimonia na kuhara, pamoja na huduma za magonjwa mengine ya kawaida ya utotoni.”Katika huduma za matibabu tumsikilize Saida Ali Elmi ambaye ni mhudumu wa Afya(Sauti ya Saida Ali Elmi- Sheilah)“Kama mnavyoona, akina mama wengi wamekuwa kwenye foleni tangu saa moja asubuhi na sasa ni saa 5:30 asubuhi. Kwa hiyo wapo hapa kwa ajili ya chanjo za kinga, ikiwemo chanjo za kifua kikuu, surua, polio, pepopunda, kifaduro, pamoja na chanjo mpya iitwayo PCV ya nimonia.”Juhudi hizi zinazofanywa na mashirika haya, tayari zimeanza kuleta matumaini mapya kwa Ayan Hassan Abdi mama mzazi wa Maryam “Nimemleta Maryam kwa sababu alikuwa na homa. Amepatiwa matibabu na pia chanjo. Alifanyiwa vipimo vya homa na kuharisha, na akatibiwa vizuri, Masha'Allah.”

Habari za UN
Tiba asilia zina nafasi muhimu katika kuimarisha mifumo ya afya duniani - WHO

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 19, 2025 2:44


Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, linasema tiba asilia na tiba jadidifu zina nafasi muhimu katika mifumo ya afya duniani, hasa katika kinga, huduma za usaidizi wa magonjwa na kuongeza upatikanaji wa huduma za afya kwa jamii. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Kitengo cha Tiba Asilia, Jadidifu na Jumuishi cha WHO, Dkt. Sung Chol Kim, katika mahojiano maalum kando ya Mkutano wa Kimataifa wa Tiba Asilia unaoendelea huko New Delhi, India. Sabrina Saidi na taarifa zaidi..

Habari za UN
Ubakaji kama silaha ya vita - Safari ya manusura wa DRC katika kupata uponyaji na heshima

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 17, 2025 3:20


Ubakaji unaotumika kama silaha ya vita huacha majeraha yasiyofutika ya mwili,  akili na ya roho. Katika ushuhuda huu wenye nguvu, manusura mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa anaishi kama mkimbizi nchini Burundi, anasimulia safari yake ya maumivu baada ya kunusurika ukatili wa kingono uliomsababishia majeraha makubwa ya mwili, ikiwemo fistula, pamoja na makovu ya kina ya kihisia.Sheilah  Jepng'etich na taarifa zaidi

Habari za UN
17 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 17, 2025 11:14


Hii leo jaridani tunaangazia tiba asili, machafuko katika jimbo la Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na ubakaji unaotumika kama silaha ya vita nchini humo humo.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO, linaweka mkazo mpya wa kisayansi katika tiba asili au mitishamba, wakati mawaziri, wanasayansi na viongozi wa jamii za asili kutoka zaidi ya nchi 100 wakikutana mjini New Delhi India kuanzia leo kuangazia mchango wa tiba za asili.Kuongezeka kwa machafuko katika jimbo la Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kumesababisha watu wengi kuyahama makazi yao ndani na kumbilia kusaka hofadhi nchi Jirani ya Burundi. Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wakimbizi limeeleza mpaka sasa karibu wakimbizi 64,000 tayari wamewasili Burundi, na idadi ikitarajiwa kuongezeka.Ubakaji unaotumika kama silaha ya vita huacha majeraha yasiyofutika ya mwili,  akili na ya roho. Katika ushuhuda huu wenye nguvu, manusura mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa anaishi kama mkimbizi nchini Burundi, anasimulia safari yake ya maumivu baada ya kunusurika ukatili wa kingono uliomsababishia majeraha makubwa ya mwili, ikiwemo fistula, pamoja na makovu ya kina ya kihisia.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
11 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 11, 2025 11:30


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Sudan Kusini kufuatilia mradi wa kilimo cha mpunga ulivyoleta ustawi kwa jamii ya katikati mwa Sudan unaofanikishwa kwa msaada wa mafunzo wa walinda amani wa UN kutoka Korea Kusini wanaohudumu katika UNMISS kupitia wanasayansi na wakulima wa eneo la Bor katika. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ufafanuzi wa methali.Mapigano makali mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yamesababisha vifo vya zaidi ya raia 70, kuwafurusha watu zaidi ya 200,000, na kusitisha msaada wa chakula kwa maelfu. Umoja wa Mataifa unasema hali katika Kivu Kusini imezorota kwa kasi, huku msaada wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP ukisimama na shule zaidi ya 30 zikigeuzwa makazi ya dharura. Katika taarifa yake, Naibu Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Farhan Haq, amesema hali imefikia kiwango cha hatari, akionya: “Familia zinazoishi kwa njaa sasa zinagawana chakula chao cha mwisho na watu waliokimbia makazi. Hii ni dharura inayovuka mipaka.” UN inazitaka pande zote kusitisha mapigano mara moja na kuruhusu misaada kufika kwa walio hatarini.Mkutano wa kikao cha 7 wa Baraza La Mazingira la Umoja wa Mataifa UNE-7 unaeelekea ukingoni jijini Nairobi Kenya na miongoni mwa washiriki ni kijana mwanaharakati wa mazingira kutoka asasi ya Umoja wa Mataifa YUNA nchini Tanzania Ally MwamzoraNa leo Umoja wa Mataifa unaadhimisha Siku ya Kimataifa ya Milima, ukisisitiza umuhimu wa milima kama “kitovu cha maji ya dunia.”  Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO, takriban asilimia 70 ya maji safi ya Dunia yamehifadhiwa kama theluji au barafu, yakitoa mito inayosambaza maji ya kunywa, kilimo, viwanda, na umeme wa maji na takriban watu bilioni mbili, ikiwa ni pamoja na jamii nyingi za asili, wanategemea maji ya milima kwa mahitaji yao ya kila siku, maisha, na tamaduni zao. Wataalamu wanasisitiza kuwa kulinda mazingira ya milima ni muhimu ili kuhakikisha upatikanaji wa maji kwa vizazi vijavyo.Katika kujifunza lugha Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya,  kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "“MWENDAWAZIMU HAPEWI UPANGA"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali "“MWENDAWAZIMU HAPEWI UPANGA"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 11, 2025 1:39


Katika kujifunza lugha Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya,  kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "“MWENDAWAZIMU HAPEWI UPANGA" 

SBS Swahili - SBS Swahili
Wataalamu waonya kuwa msimu wa moto umeanza tunapotarajia joto kuongezeka

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 11, 2025 8:03


Katika wiki za hivi karibuni, moto wa nyika umesababisha uharibifu wa nyumba na mali katika maeneo ya pwani ya katikati ya kaskazini ya New South Wales, Geraldton huko Magharibi mwa Australia na mashariki mwa Tasmania. Wataalamu wanaonya kuwa huu ni mwanzo tu wa msimu wa moto na nyinyi ambao mnasafiri kwa ajili ya likizo mnahitaji kuwa na ufahamu na maandalizi mkiwa mbali na nyumbani.

Habari za UN
09 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 9, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea ufafanuzi wa umuhimu wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Haki za binadamu kutoka kwa Seifu Magango Msemaji wa Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa ambaye anaanza kwa kuzungumzia azimio la tamko hilo la haki za binadamu.Utafiti uliofanywa na Tume ya Ulaya kwakushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa linalaoshughulikia masuala ya wanawake UN Women umebaini kuwa wanawake saba kati ya kumi wakiwemo watetezi wa haki za binadamu, wanaharakati na waandishi wa habari wanakumbana na ukatili mtandaoni.Meneja Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masuala ya watoto UNICEF Tess Ingram yupo ziarani Ukanda wa Gaza huko Mashariki ya kati ambapo hii leo amezungumza na waandishi wa habari jijini Geneva Uswisi na kuwaeleza aliyoshuhudia huko ikiwemo wajawazito walio na utapiamlo kujifungua watoto wenye uzito mdogo au kuzaliwa kabla ya wakati, ambao wengine wanakufa katika vyumba vya wagonjwa mahututi      au wengine hupona lakini watoto hao hukabiliwa na utapimlo au matatizo mengine ya kiafya.Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Kutokomeza Ubaguzi wa Rangi CERD, leo imetoa onyo kali kwa Sudan, ikieleza wasiwasi mkubwa kuhusu ongezeko la matumizi ya lugha ya kudhalilisha, kauli za chuki na ukiukaji Mkubwa wa haki za binadamu unaochochewa na misingi ya kikabila. Kamati imesem Mashambulizi haswa dhidi ya jamii za Fur, Masalit na Zaghawa, yanadaiwa kufanywa na Kikosi cha Msaada wa Haraka RSF na makundi washirika katika maeneo ya El Fasher, Darfur Kaskazini.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "PEKUPEKU"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "PEKUPEKU"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 9, 2025 0:46


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "PEKUPEKU." 

Habari za UN
05 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 5, 2025 11:07


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya haki za binadamu na maandamano ya amani nchini Tanzania, siku ya kujitolea tukikuletea ujumbe wa mfanyakazi wa kujitolea, na elimu jumuishi kwa ajili ya watu wenye ulemavu nchini Ethiopia.Wakati Tanzania ikijiandaa kwa maandamano makubwa yaliyopangwa kufanyika tarehe 9 Desemba siku ya maadhimisho ya Uhuru, Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR imetoa tahadhari na wito kwa serikali ya taifa hilo la Afrika Mashariki. Seif Magango ni msemaji wa ofisi ya Haki za binadamu ametufafanulia kuhusu tamko lao.Katika dunia inayohitaji mshikamano ili kufikia maendeleo, mchango wa watu wanaojitolea umeendelea kuwa nguvu muhimu ya kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa. Kila mwaka tarehe 5 mwezi Desemba, dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanaojitolea, mwaka huu ikiwa imebeba maudhui “Kila Mchango Una Umuhimu.”  Maadhimisho ya mwaka huu pia yanazindua rasmi Mwaka wa Kimataifa wa Wanaojitolea kwa Maendeleo Endelevu 2026.Katika eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia, jitihada za kuimarisha makuzi na elimu kwa watoto wenye ulemavu zinaendelea kuleta matumaini mapya, kupitia programu inayoungwa mkono na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu na Masuala ya Dharura OCHA, na Mfuko wa Dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF. Je nini kinafanyika?Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Kutoka changamoto hadi mafanikio: Safari ya Kibra kupitia mfuko wa CERF

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 5, 2025 2:18


Katika eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia, jitihada za kuimarisha makuzi na elimu kwa watoto wenye ulemavu zinaendelea kuleta matumaini mapya, kupitia programu inayoungwa mkono na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu na Masuala ya Dharura OCHA,  na Mfuko wa Dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF. Je nini kinafanyika? Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi

Habari za UN
UN: Mchango wa watu wanaojitolea ni muhimili wa mabadiliko

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 5, 2025 3:03


Katika dunia inayohitaji mshikamano ili kufikia maendeleo, mchango wa watu wanaojitolea umeendelea kuwa nguvu muhimu ya kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa. Kila mwaka tarehe 5 mwezi Desemba, dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanaojitolea, mwaka huu ikiwa imebeba maudhui“Kila Mchango Una Umuhimu.”  Maadhimisho ya mwaka huu pia yanazindua rasmi Mwaka wa Kimataifa wa Wanaojitolea kwa Maendeleo Endelevu 2026. Kutoka Dar es Salaam, Tanzania Sabrina Saidi amezungumza na kijana  ambaye anajitolea katika Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa Tanzania YUNA Je kasema nini?.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "MADHALI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 4, 2025 0:34


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "MADHALI"

Habari za UN
04 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 4, 2025 12:02


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kwa mwanariadha na mchchemuzi wa masuala ya wanawake, akieleza hatua zinazochukuliwa kutokomeza dhulma wa kijinsia. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze lugha ya Kiswahili.Huku mapigano yakizidi kushika kasi katika eneo la Kordofan nchini Sudan, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ameonya hii leo kuhusu hatari ya mashambulizi mapya dhidi ya raia, baada ya kuripotiwa vifo zaidi ya watu 269 kutokana na mashambulizi ya angani, mabomu na mauaji ya kiholela tangu mwishoni mwa mwezi Oktoba. Ofisi yake imeeleza kupokea taarifa za ulipizaji kisasi, utekaji, ukatili wa kingono na ulazimishaji wa watoto kujiunga na makundi ya kivita, huku miji kama Kadugli, Dilling na El Obeid ikikabiliwa na njaa, kuzingirwa na kukwama kwa misaada ya kibinadamu.Malaria, ugonjwa ambao takriban asilimia 95 ya vifo vinavyoripotiwa duniani ni kutoka nchi za Afrika tena kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka 5. Ulionekana kuweza kudhibitiwa lakini sasa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus, anasema unaelekea kubaya kutokana na kuongezeka kwa usugu wa dawa, hali inayotishia kuyafuta mafanikio yaliyookoa maisha ya watu milioni moja mwaka 2024 kupitia chanjo na vyandarua vipya vyenye dawa ya kukabiliana na mbu waenezao Malaria.Na tuhitimishie nchini Msumbiji ambako Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM Amy Pope amefanya ziara ya siku tatu na kujionea athari zilizoletwa na Mafuriko, vimbunga na kuzorota kwa usalama huko Kaskazini mwa nchi hiyo hali iliyosababisha zaidi ya 100,000 wameyakimbia makazi yao, na zaidi ya 600,000 wakihitaji msaada.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "MADHALI"Mwenyeji wako ni Sabrina Moshi, karibu!

Habari za UN
Guterres: Kunapokuwa na ujumuishwaji wa kweli kila mtu ananufaika katika jamii

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 3, 2025 2:53


Umoja wa Mataifa leo Desemba 3 unaadhimisha Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu kwa ujumbe mzito kutoka kwa Katibu Mkuu António Guterres ujumbe unaotaka jamii ziwe si tu zinazoweza kufikiwa na watuwenye ulemavu, bali pia zenye ujumuishi wa kweli. Flora Nducha na taarifa zaidi

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali "KOTI LA BABU HALIKOSI CHAWA"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 2, 2025 1:15


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "KOTI LA BABU HALIKOSI CHAWA".

Habari za UN
UNICEF na KISE wawapiga jeki watoto wenye ulemavu katika Kaunti ya Wajir nchini Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 3:05


Katika Kaunti ya Wajir Kaskazini Mashariki mwa Kenya, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu Maalum ya Kenya KISE wameanzisha mpango maalum wa kuwasaidia watoto wenye ulemavu kupata tathmini za kitabibu na kielimu. Mpango huu umeleta matumaini mapya kwa familia nyingi ambazo hapo awali zilikuwa na ugumu wa kupata huduma hizi kama anavyofafanua Sheilah Jepngetich  katika taarifa hii

Habari za UN
“VVU si mwisho wa maisha” – Safari ya Pooja Mishra kutoka mshtuko hadi uongozi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 3:19


Pooja aliolewa akiwa na umri wa miaka 15, baadaye akiwa mdogo bado akagundua kuwa ana Virusi Vya Ukimwi, VVU, na leo ni Mratibu wa Kitaifa wa Vijana chini ya Muungano wa Kitaifa wa Watu wanaoishi na VVU nchini India (NCPI+), akifanya kazi moja kwa moja na zaidi ya vijana 1,800 kote India. Katika mahojiano yaliyofanywa na Anshu Sharma wa Idhaa ya Kihindi ya Umoja wa Mataifa, Pooja anasimulia safari yake, nafasi ya jamii na familia, na ujumbe wake kwa watu wanaoishi na VVU. Anaposema ART anazungumzia dawa za kufubaza virusi, sawa na ARV lakini katika mkusanyiko wa dawa nyingi kwa pamoja.

Habari za UN
01 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 11:33


Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa Umoja wa Mataifa katika Siku ya UKIMWI Duniani, simulizi wa mwathirika wa ugonjwa huu amabye aliolewa na umri wa miaka 15, na juhudi za UNICEF Wajir nchini Kenya za kuhakikisha ujumuishwaji wa watoto wenye ulemavu darasani.Leo ni Siku ya UKIMWI Duniani na mwaka huu inaadhimishwa kwa onyo kali kuhusu janga hilo pamoja na wito wa kuchukua hatua. Ikibeba kaulimbiu “Kukabili misukosuko, kubadili mwelekeo wa hatua za UKIMWI,” Umoja wa Mataifa unasema dunia ipo katika kipindi cha uamuzi muhimu katika vita dhidi ya VVU.Pooja aliolewa akiwa na umri wa miaka 15, baadaye akiwa mdogo bado akagundua kuwa ana Virusi Vya Ukimwi, VVU, na leo ni Mratibu wa Kitaifa wa Vijana chini ya Muungano wa Kitaifa wa Watu wanaoishi na VVU nchini India (NCPI+), akifanya kazi moja kwa moja na zaidi ya vijana 1,800 kote India. Katika mahojiano yaliyofanywa na Anshu Sharma wa Idhaa ya Kihindi ya Umoja wa Mataifa, Pooja anasimulia safari yake, nafasi ya jamii na familia, na ujumbe wake kwa watu wanaoishi na VVU. Anaposema ART anazungumzia dawa za kufubaza virusi, sawa na ARV lakini katika mkusanyiko wa dawa nyingi kwa pamoja.Katika Kaunti ya Wajir Kaskazini Mashariki mwa Kenya, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu Maalum ya Kenya KISE wameanzisha mpango maalum wa kuwasaidia watoto wenye ulemavu kupata tathmini za kitabibu na kielimu. Mpango huu umeleta matumaini mapya kwa familia nyingi ambazo hapo awali zilikuwa na ugumu wa kupata huduma hizo.Mwenyeji wako ni Sabrina Moshi, karibu!

Habari za UN
UN: Dunia ipo katika kipindi cha maamuzi kuhusu mustakbali wa ukimwi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 2:50


Kama tulivyokujuza le oni Siku ya UKIMWI Duniani na mwaka huu inaadhimishwa kwa onyo kali kuhusu janga hilo pamoja na wito wa kuchukua hatua. Ikibeba kaulimbiu “Kukabili misukosuko, kubadili mwelekeo wa hatua za UKIMWI,” Umoja wa Mataifa unasema dunia ipo katika kipindi cha uamuzi muhimu katika vita dhidi ya VVU. Flora Nducha na taarifa zaidi

SBS Swahili - SBS Swahili
Australia yafafanuliwa;bei za upangaji zinaendelea kupanda wakati gharama ya maisha inaongezeka.

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 6:12


Licha ya viwango vya riba kutulia, stress ya kodi bado haijabadilika kote Australia. Katika miji mingi mikubwa, kaya bado zinatoa karibu theluthi moja ya mapato yao ili kuweka paa juu ya vichwa vyao. Na mara nyingine tena, Perth inashika nafasi mbaya zaidi. Jiji kuu lisilopatikana kwa urahisi zaidi nchini limeporomoka hata zaidi — likirekodi kushuka kwa asilimia nne zaidi katika uwezo wa kumudu gharama juu ya rekodi ya chini ya mwaka uliopita.

Habari za UN
26 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 26, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia usafirir endelevu, udhalilishaji wa mtandaoni tukikuletea ujumbe kutoka Uganda, na ufugaji endelevu unaowawezesha wafugaji katika maeneo kame ya Isiolo na Garissa nchini Kenya.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameadhimisha Siku ya Kimataifa ya Usafiri Endelevu Duniani kwa kuonya kwamba mifumo ya usafiri duniani ambayo ni muhimu kwa uchumi na maisha ya kila siku inayochochea dunia kuelekea janga la tabianchi na kwa hivyo siku hii inatukumbusha kwamba njia ya kuelekea mustakabali bora inategemea mifumo safi na yenye uendelevu wa usafiri.Siku 16 za uhamasishaji kupinga ukatili dhidi ya wanawake zikiendelea leo tunakupeka mjini Hoima Magharibi mwa Uganda kusiki maoni kutoka kwa wa mji huo kuhusu ukatili mtandaoni yakienda sanjari na kauliimbiu ya kampeni ya ya mwaka huu isemayo “Ukatili wa mtandaoni ni ukatili halisi na hakuna visingizo kwa ukatili mtandaoni”.Katika maeneo yaliyoghubikwa na athari za mabadiliko ya tabianchi kaskazini mwa Kenya, wafugaji wamekuwa wakikumbwa na changamoto kubwa kwani ukame na mafuriko, vinatishia sio tu mali zao bali pia maisha yao. Lakini kupitia mradi wa bima ya mifugo unaoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula  duniani WFP, kwa ushirikiano na asasi ya Zoetis na kampuni ya ZEP-RE, jamii zinaanza kupata ahuweni na matumaini mapya.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
WFP: Suluhisho bunifu kwa wafugaji wa maeneo yenye ukame nchini Kenya zaleta tija

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 26, 2025 2:40


Katika maeneo yaliyoghubikwa na athari za mabadiliko ya tabianchi kaskazini mwa Kenya, wafugaji wamekuwa wakikumbwa na changamoto kubwa kwani ukame na mafuriko, vinatishia sio tu mali zao bali pia maisha yao. Lakini kupitia mradi wa bima ya mifugo unaoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula  duniani WFP, kwa ushirikiano na asasi ya Zoetis na kampuni ya ZEP-RE, jamii zinaanza kupata ahuweni na matumaini mapya. Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi.

Habari za UN
25 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 25, 2025 12:23


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, na leo zinaanza siku 16 za uanaharakati kuelimisha umma kuhusu janga la ukatili wa kijinsia, tunamsikia  mmoja wa waathirika wa ukatili wa kingono.Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa onyo kali kuhusu ongezeko la ukatili mtandaoni dhidi ya wanawake na wasichana.Ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya wanawake UN Women na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya dawa na uhalifu UNODC inaonya kwamba mwaka 2024, wanawake na wasichana 50,000 waliuawa na wapenzi au jamaa sawa na mwanamke mmoja kila dakika 10.Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo (UNCTAD) inaonya kwamba uchumi wa Eneo la Palestina Linalokaliwa kwa Mabavu na Israel umerudi nyuma miaka 22 kwa muda usiozidi miaka miwili kwani umeingia katika hali mbaya zaidi ya mdororo kuwahi kurekodiwa, huku miongo ya maendeleo ikifutwa na operesheni za kijeshi zilizodumu kwa muda mrefu pamoja na vizuizi vya muda mrefu.Katika kujifunza lugha Kiswahili hii leo,  mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "MADUYUNI"Mwenyeji wako ni Sabrina Said, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "MADUYUNI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 25, 2025 1:02


Katika kujifunza lugha Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "MADUYUNI"

SBS Swahili - SBS Swahili
Australia yafafanuliwa:Afya ya akili katika ujauzito na baada ya kujifungua

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 24, 2025 9:51


Karibu mmoja kati ya Waustralia wanne hawatafuti msaada wanapopata matatizo ya afya ya akili wakati wa ujauzito au baada ya kujifungua. Wataalamu wanasema kwamba taarifa zilizotolewa na Gidget Foundation zinaonyesha ukosefu wa kuelewa dalili na ishara, pamoja na unyanyapaa unaoendelea kuhusu suala hili.

Habari za UN
Jamii za asili Peru zaongeza uzalishaji wa kakao kwa mbinu bunifu za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 21, 2025 4:01


Katika msitu wa Amazon upande wa nchi ya Peru, jamii za watu wa asilizimeonesha namna mbinu bunifu za kilimo zinaweza kuongeza uzalishaji na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Yote haya yanakuja wakati dunia ikiendelea kujadili mustakabali wa hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika mkutano wa Umoja wa Mataifa COP30 unaoendelea huko Belém, Brazil.

Habari za UN
21 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 21, 2025 12:02


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, mbinu bunifu za kilimo cha kakao nchini Peru, na mradi wa miundombinu wa kupunguza athari ya mafuriko na kugeuza maji ziada kuwa rasilimali muhimu kwa jamii nchini Rwanda.Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ujulikanao kama MONUSCO, leo umelaani vikali mashambulizi makubwa yaliyofanywa na kundi lenye silaha la Allied Democratic Forces ADF kati ya tarehe 13 na 19 Novemba 2025 katika baadhi ya maeneo ya Lubero, jimboni Kivu Kaskazini na kukatili maisha ya raia wengi.Katika msitu wa Amazon upande wa nchi ya Peru, jamii za watu wa asilizimeonesha namna mbinu bunifu za kilimo zinaweza kuongeza uzalishaji na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Yote haya yanakuja wakati dunia ikiendelea kujadili mustakabali wa hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika mkutano wa Umoja wa Mataifa COP30 unaoendelea huko Belém, Brazil.Mwezi Mei 2023, Rwanda nchi iliyozungukwa na milima ilikumbwa na mafuriko makubwa yaliyosababisha maporomoko ya ardhi na kusababisha maji kutoka katika milima ya volkano, yakiambatana na mawe mazito kuharibu mashamba, makazi na barabara. Baada ya mafuriko hayo ili kupunguza athari za majanga kama hayo, kwa wakati mwingine Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) nchini Rwanda, kwa ufadhili wa Serikali ya Japan, linatekeleza mradi wa Kukabiliana na Majanga Yanayohusiana na Maji katika wilaya za Rutsiro na Burera. Lengo ni kupunguza Athari na kugeuza maji ziada kuwa rasilimali muhimu kwa jamii.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
18 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2025 11:32


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Brazil kwenye mkutano wa COP30, ambako Dkt. Richard Muyungi, Mjumbe maalumu kwenye masuala ya mabadiliko ya tabianchi na mazingira kutoka nchini Tanzania anaeleza ni nini bara la Afrika linahitaji.Umoja wa Mataifa umekaribisha kupitishwa kwa Azimio namba 2803 la Baraza la Usalama kuhusu Gaza hapo jana, ukilitaja kuwa hatua muhimu katika kuimarisha usitishaji mapigano. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, anazitaka pande zote kuheshimu kikamilifu makubaliano hayo na kutafsiri kasi ya kidiplomasia kuwa hatua za dharura na za wazi kwa watu walioko katika eneo hilo. Katika taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Guterres, Stéphane Dujarric, amesema Umoja wa Mataifa umejizatiti kuongeza misaada ya kibinadamu na kuunga mkono jitihada zinazoelekezwa katika hatua inayofuata ya usitishaji mapigano.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), hali ya kibinadamu katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kusini bado ni tete. Mkurugenzi wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu, Kanda ya Afrika Patrick Youssef  ambaye amerejea hivi karibuni kutoka DRC amewaleza waandishi wa habari jijini Geneva, Uswisi kwamba raia wa DRC wanaendelea kubeba mzigo mzito wa mapigano, hata wakati shughuli chache za kibiashara zikiendelea kurejea Goma. Ametoa tahadhari kuwa mgogoro huo unakabiliwa na upungufu mkubwa wa ufadhili, ukatili wa kingono unaongezeka, na zaidi ya asilimia 70 ya watu waliojeruhiwa kwa silaha mwaka huu ni raia.Kuanzia leo tarehe 18 inaanza Wiki ya Kimataifa ya Kuelimisha Umma kuhusu Usugu wa Vijiumbemaradhi dhidi ya dawa. Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, linaonya kuwa usugu wa vimelea yaani hali ambapo bakteria, virusi na vijidudu vingine havidhuriki tena kwa dawa tayari unatishia mifumo ya afya, uchumi na uhakika wa chakula. Kwa kaulimbiu “Chukua Hatua Sasa: Linda Leo Yetu, Linda Mustakabali Wetu,” WHO inatoa wito kwa serikali, wahudumu wa afya, wakulima, wadau wa mazingira na umma kuchukua hatua madhubuti kutekeleza ahadi za kisiasa ili kupunguza kuenea kwa maambukizi sugu ya dawa.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "UPUNGUFU"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!