Podcasts about katika

Place in Paphos District, Cyprus

  • 128PODCASTS
  • 3,041EPISODES
  • 20mAVG DURATION
  • 1DAILY NEW EPISODE
  • Jun 11, 2026LATEST

POPULARITY

20192020202120222023202420252026

Categories



Best podcasts about katika

Show all podcasts related to katika

Latest podcast episodes about katika

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali “Lililo lujani ni la lusu”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 11, 2026 0:52


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Lililo lujani ni la lusu”.

kenya nairobi kiswahili katika maana dkt jifunze chuo kikuu
Siha Njema
Shinikizo kutaka mataifa kuja na sera endelevu na salama za uchukuzi

Siha Njema

Play Episode Listen Later Jun 11, 2026 9:46


Shinikizo zinazidi kutolewa kwa mataifa ya Afrika kukumbatia sera za uchukuzi zilizo salama na endelevu ili kupunguza idadi ya vifo vinavyotokana na barabara na madhara ya ajali za barabara kwa jamii. Katika  kongamano la kujadili mpango huo wa usalama ulio endelevu ,wadau wamesikitika vifo vya barabarani bado vinaripotiwa miongoni mwa watembea miguu na waendesha pikipiki. Katika makala ya Siha Njema wiki hii tunajadili kwa nini swala hili ni muhimu kwa ustawi wa jamii.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana na matumizi ya neno "MKWARUZO."

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 9, 2026 0:40


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "MKWARUZO."

Habari za UN
09 JUNI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 9, 2026 9:57


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Kesho kutwa Alhamisi ya Juni 11, macho na masikio yanaelekezwa Mexico, Canada na hapa Marekani kwa ajili ya fainali za kombe la dunia kwa mpira wa miguu, au soka al maarufu kabumbu. Ingawa hivyo zama za sasa za mchezo huo maarufu zaidi duniani zinakumbwa na madhara ya  athari za mabadiliko ya tabianchi. Ongezeko la joto kali linavuruga mechi na kuzua wasiwasi kuhusu mustakabali wa mchezo huo. Ni kwa kuzingatia hilo, Sekretarieti ya Mkataba wa Kimataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, UNFCCC inamulika suala hilo na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike kwani hivi sasa madhara ya joto kali kwenye kabumbu ni dhahiri. Feissal Kirwa anamulika hilo kupitia video iliyoandaliwa na UNFCCC.Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze Kiswahili.Takriban watoto milioni 138 duniani kote bado wako katika ajira za watoto, wakiwemo watoto milioni 54 wanaofanya kazi hatarishi. Hayo yamo katika ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa ILO. Katika ujumbe wakwe kwenye ripoti hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa ILO, Gilbert F. Houngbo, ametoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka ili kubadili hali hii.“Habari njema ni kwamba hadi sasa tuna wagonjwa 19 ambao wamepona, hivyo utambuzi wa mapema na matibabu vinaokoa maisha,”  Huyo ni Mkurugenzi wa Operesheni za Tahadhari na Hatua za Dharura za Afya wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani (WHO), Dkt. Abdirahman Mahamud, akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva leo kwa njia ya video kutoka Bunia katika Jimbo la Ituri, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, jimbo ambalo linachangia asilimia 94 ya wagonjwa wote wa Ebola.Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, umeanza leo Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York na utaendelea hadi 11 Juni. Kaulimbiu ya mwaka huu ni “kuadhimisha miaka 20 ya mkataba huo na kuimarisha utekelezaji wake katika dunia inayobadilika.” Washiriki wanajadili namna ya kutokomeza ukandamizaji, ukatili na manyanyaso dhidi ya watu wenye ulemavu, kuimarisha mifumo ya huduma na msaada, pamoja na kuongeza ushiriki na uwakilishi wao katika maisha ya kisiasa na umma.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "MKWARUZO."Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

new york canada mexico fifa tanzania ebola jimbo zanzibar drc ilo kazi unfccc umoja congo drc hayo hii haki kiswahili katika afya ituri baraza habari joto dkt hatua jamhuri mataifa bunia marekani shirika kimataifa mkutano kesho kidemokrasia mkurugenzi alhamisi
SBS Swahili - SBS Swahili
Yaliyojiri Afrika: Swala lakubadilisha katiba lazua mpasuko katika makanisa DR Congo

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 9, 2026 7:02


Kume kuwa mgwanyiko kati ya kambi yamakanisa katika Jamuhuri yakidemokrasia ya Kongo, kutakana na swala lakubadilisha katiba.

Habari za UN
Lazima tujenge uhusiano mpya na bahari- Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 8, 2026 2:50


Bahari duniani zinakabiliwa na changamoto kubwa zinazotishia afya ya mazingira na ustawi wa binadamu, ameonya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres na kutoa wito wa hatua za haraka na za pamoja kukabiliana na hali hiyo. Akizungumza kwa njia ya video katika ujumbe wake wa Siku ya Kimataifa ya Bahari inayoadhimishwa kila mwaka Juni 8, Bwana Guterres amesema bahari ni msingi wa maisha na maendeleo duniani, lakini zimekuwa zikikabiliwa na shinikizo linalozidi uwezo wake wa kustahimili."Bahari inaongoza tabianchi yetu, inalinda mifumo ya ikolojia na uchumi, na inalisha mabilioni ya watu duniani," anasema Guterres na kuongeza kuwa, "bahari ipo kwenye zahma kubwa na tunaishinikiza kupita uwezo wake."Guterres amerejelea Ripoti ya Tatu ya Tathmini ya Bahari Duniani iliyozinduliwa leo, ambayo imebainisha kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabianchi, uvuvi uliokithiri, kupotea kwa bionuwai na uchafuzi wa bahari.Katibu Mkuu Guterres amesisitiza akisema, "hatuwezi kuendelea kuichukulia bahari kama kitu kisicho na ukomo," akihimiza kujengwa kwa uhusiano mpya na bahari unaozingatia sayansi, unaoongozwa na sheria za kimataifa na unaojengwa juu ya wajibu wa pamoja wa mataifa, sekta mbalimbali na vizazi vyote.Ametaja mafanikio ya Mkutano wa Tatu wa Bahari wa Umoja wa Mataifa uliofanyika mwaka jana pamoja na kuanza kutekelezwa kwa Makubaliano ya Baiyonuai ya Bahari katika maeneo yaliyo nje ya mamlaka ya kitaifa mwaka huu kama ushahidi kwamba ushirikiano wa kimataifa unaweza kuleta matokeo.Anasema, "hatua za pamoja za kimataifa zinawezekana na ni za lazima."Katika hitimisho la ujumbe wake wake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewataka viongozi wa dunia, sekta binafsi na wananchi kuchukua hatua kwa haraka ili kulinda bahari kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.Anasema, "katika Siku hii ya Kimataifa ya Bahari, hebu tuchukue hatua kwa nia thabiti na kutatua mahitaji ya wakati huu."Hakika yanayosemwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa yanaendana na aliyoyasema Mwenyekiti aliyechaguliwa wa ya Tume ya Kiserikali ya Bahari ya UNESCO (IOC) kwa Afrika na Nchi za Visiwa vinavyokaribia bara la Afrika (IOCAFRICA) Hellen Gichuhi alipozungumza na Idhaa ya Umoja wa Mataifa.

ant afrika guterres tatu umoja bahari katika siku tume nchi mataifa mkuu kimataifa mkutano ripoti
MAELEZO PODCASTS
Balozi Kombo Aeleza Umuhimu wa Ziara ya Rais Samia katika Kuimarisha Mahusiano ya Tanzania na Urusi

MAELEZO PODCASTS

Play Episode Listen Later Jun 8, 2026 25:29 Transcription Available


Send us Fan MailMkutano na Waandishi wa Habari kuhusu ziara ya Kitaifa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini Urusi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, tarehe 7 Juni, 2026.Support the showIdara ya Habari MAELEZO 

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali “La kiliwacho kisicholiwa ni sumu”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 4, 2026 1:07


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “La kiliwacho kisicholiwa ni sumu”

kenya nairobi kiswahili katika maana dkt jifunze chuo kikuu
Gurudumu la Uchumi
Umuhimu wa bara la Afrika kufanya biashara za ndani

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Jun 3, 2026 10:01


Katika makala ya wiki hii, tunajadili ni kwanini nchi za Afrika zinapaswa kuongeza kasi ya ufanyaji wa biashara za wenyewe kwa wenyewe kukuza utangamano wa kikanda.

kenya afrika bara katika biashara umuhimu
Gurudumu la Uchumi
Umuhimu wa bara la Afrika kufanya biashara za ndani

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Jun 3, 2026 10:01


Katika makala ya wiki hii, tunajadili ni kwanini nchi za Afrika zinapaswa kuongeza kasi ya ufanyaji wa biashara za wenyewe kwa wenyewe kukuza utangamano wa kikanda.

kenya afrika bara katika biashara umuhimu
Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno “CHOTORA”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 2, 2026 0:50


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Mtalaam wetu Onni Sigalla kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania BAKITA anafafanua maana ya neno “CHOTORA”

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Wanafunzi 16 wafa katika moto wa shule ya bweni Kenya, mkuu wa WHO azuru DRC

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later May 30, 2026 20:07


Wanafunzi kadhaa kupoteza maisha na wengine kujeruhiwa katika shule ya Sekondari ya wasichana Nakuru nchini Kenya, ziara ya mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani WHO, Uganda kutangaza kuufunga mpaka wake na DRC, hali nchini Sudan, huku Nigeria, kuelekea uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika mwezi Januari mwaka ujao, na pia ripoti zinasema Marekani na Iran zakubaliana kuongeza usitishwaji wa vita kwa siku zingine 60

Habari za UN
29 MEI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 29, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina maalumu ambapo tunamwangazia mmoja wa maafisa waandamizi wa Umoja wa Mataifa, Joyce Msuya. Mwisho wa wiki hii, Joyce, raia wa Tanzania ambaye pia amewahi kuhudumu katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo, UNEP na pia Benki ya Dunia anahitimisha utumishi wake katika Umoja wa Mataifa akiwa Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya kibinadamu na pia Naibu wa Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu (OCHA). Katika mazungumzo haya na Anold Kayanda wa Idhaa hii, Joyce Msuya anaanza kwa kuitafari miaka minne aliyohudumu katika nafasi hii.Jamhuri ya Kidemokrasia Congo DRC inakumbwa na ugonjwa wa Ebola ambapo Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO, Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amefika huko na anaeleza sababu. ‘Nimefika hapa kuzieleza jamii za Ituri, Kivu Kaskazini na Kivu kusini kuwa hawako pekeyao, na kwamba tupo hapa kuwaunga mkono, na tunaelewa machungu yao, lakini pia tunafahamu wana nguvu na yote yanayohitajika kukomesha hili. Ninatumia fursa hii kuziomba jumuiya za kimataifa kuongeza usaidizi wao ili wahudumu wa afya waweze kupata vifaa tiba na vya kujilinda na maambukizi.'Kupigwa marufuku watoto kutumia mitandao ya kijamii, si suluhisho la mara moja kwa suala mtambuka lenye sura nyingi, ndio maana hii leo Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk ametaka hatua kali zichukuliwe na kila nchi, pamoja na makampuni ya teknolojia, ili kufanya mitandao ya kijamii kuwa salama zaidi kwa watoto, akisisitiza udhibiti, usimamizi na uwajibikaji unaofaa. Kamishna Türk amesema "Kuimarisha ulinzi wa watoto mtandaoni ni kipaumbele cha dharura ambacho tunahitaji kuhakikisha sio tu kwamba kinafanyika, bali pia kinafanyika ipasavyo,".Na ukatili wa kingono kwenye maeneo yenye migogoro ulifurutu ada mwaka 2025, hii inamanisha kuna ongezeko kubwa la ukatili wa kingono huku wanawake na wasichana ndio idadi kubwa ya waliokumbwa na madhila hayo yaliyohusisha pia waathirika hao kuuawa baada ya kubakwa. Haya yamebainika kwenye ripoti ya ukatili wa kijinsia unaohusiana na migogoro iliyotolewa na Umoja wa Mataifa leo ambayo pia imeonya kuwa kuongezeka kwa matumizi ya kijeshi duniani na kupungua kwa bajeti za misaada ya kibinadamu kulidhoofisha uwezo wa serikali na taasisi kuzuia na kuchunguza ukatili huo wa kingono. Ripoti hiyo imetoa wito wa kuchukuliwa hatua madhubuti zaidi za kimataifa pamoja na kuhakikisha upatikanaji endelevu wa fedha ili kulinda raia, na kuwasaidia manusura wa ukatili wa kingono unaohusiana na migogoro.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

tanzania ebola dunia drc haya unep umoja hii haki kivu katika afya ituri dkt naibu jamhuri mataifa maendeleo mkuu shirika ripoti
Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana na matumizi ya neno "PEKEPEKE."

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 22, 2026 0:42


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "PEKEPEKE."

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali “Kware hutetemekea majanini.”

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 21, 2026 1:06


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Kware hutetemekea majanini.”

kenya nairobi kiswahili katika maana dkt jifunze chuo kikuu
SBS Swahili - SBS Swahili
Anne "kina mama wanawezaje sawazisha kuhudumia naku imarisha mali ya familia zao"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 21, 2026 8:40


Kuto simamia mali vizuri, kunaweza weka mahusiano na familia nyingi katika hali mbaya.Anne Mureithi hutoa mafunzo kwa familia na jinsi yaku kuza mali zao. Katika mazungumzo maalum na SBS Swahili, Bi Anne alichangia mbinu ambazo familia zinaweza tumia kuimarisha familia na mali zao.Bonyeza hapo juu kwa mahojiano kamili.

SBS Swahili - SBS Swahili
Labor yatetea mabadiliko ya kodi ya nyumba katika bajeti licha ya ukosoaji katika kura za maoni

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 19, 2026 12:37


Mjadala unaendelea kuhusu mustakabali wa mfumo wa kodi wa Australia, baada yakutolewa kwa bajejeti ya Shirikisho wiki iliyopita.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno “Payapaya.''

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 12, 2026 1:02


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania anafafanua maana ya neno “Payapaya.''

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Ugavi wa nyumba utakuwa muhimu katika bajeti ya shirikisho ya kesho serikali ya sema

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 11, 2026 8:00


Waziri wa Makazi Clare O'Neil, anasema bajeti ya shirikisho itasaidia sana kushughulikia upungufu wa usambazaji wa makazi.

sema katika habari waziri serikali nyumba kesho
Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "MKUNGUNI."

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 7, 2026 0:30


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "MKUNGUNI."

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali “Kwendako mema hurudi mema."

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 5, 2026 1:02


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Kwendako mema hurudi mema."

kenya nairobi kiswahili mema katika maana dkt jifunze chuo kikuu
Habari za UN
05 MEI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 5, 2026 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kumsikia kijana ambaye baada ya kukosa ajira, alichagua kujiajiri kwa kuuza miwa na juisi yake, hatua iliyomwezesha kujipatia kipato na kupambana na umaskini. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze KiswahiliShirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO limesema abiria na wahudumu waliokumbwa na mlipuko wa hantavirus katika meli ya utalii iliyokuwa Bahari ya Atlantiki huenda waliambukizwa virusi hivyo kabla ya kupanda meli hiyo, ingawa maambukizi miongoni mwa watu ndani ya meli hayawezi kuondolewa kabisa licha ya kuwa ni nadra. Watu saba kati ya abiria na wahudumu 147 wameugua huku wengine wakifariki dunia.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO, linaadhimisha Siku ya Kimataifa ya Usafi wa Mikono hii leo 2026 chini ya kauli mbiu “Hatua Zinazookoa Maisha,” kikisisitiza haja ya kuimarisha uzuiaji wa maambukizi katika vituo vya afya. WHO inaonya kuwa maambukizi yanayotokana na huduma za afya bado ni tishio la kila siku katika hospitali na kliniki, yakichangia usugu wa dawa za viua vijasumu au antibiotiki, ongezeko la gharama, pamoja na vifo vinavyoweza kuzuilika.Leo Mei 5 ni Siku ya Kimataifa ya Wakunga, huku Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi, UNFPA, likisema wakunga ni wadau muhimu katika huduma za afya ya uzazi duniani kote. Shirika hilo linasema dunia inahitaji wakunga milioni moja zaidi ili kuboresha huduma za afya na kuokoa maisha ya wanawake na watoto wachanga. Kwa mujibu wa UNFPA, wakunga wanahakikisha ujauzito na kujifungua salama, huku pia wakisaidia kupunguza mimba zisizotarajiwa, maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto na upasuaji usio wa lazima wakati wa kujifungua.”Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Kwendako mema hurudi mema."Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Serikali yakana shutuma kwamba inawalenga wawekezaji wa "mama na baba" katika bajeti mpya

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 5, 2026 15:28


Jim Chalmers amepuuza mapendekezo kwamba mabadiliko yanayowezekana kwa matumizi hasi ya vifaa au kodi ya faida ya mtaji yatakuwa ni kuvunja ahadi na wapiga kura.

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Akiba itazidi matumizi na kodi katika bajeti ijayo Mweka Hazina aeleza taifa

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 4, 2026 4:47


Mweka Hazina Jim Chalmers amesema bajeti ya shirikisho ya wiki ijayo itakuwa na kikomo chake kikubwa zaidi, wakati akiba ikitarajiwa kuzidi mabadiliko ya matumizi na kodi.

Habari za UN
Mkutano wa WHO kuhusu mifumo ya afya katika kanda ya Afrika umekunja jamvi Nairobi Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 29, 2026 2:46


Mkutano wa Kikanda wa Afya Barani Afrika wa mwaka 2026 “World Health Summit 2026” umehitimishwa leo mjini Nairobi nchini Kenya, ukiwaleta pamoja zaidi ya wajumbe elfu moja kutoka takribani nchi 50 kujadili namna ya kuimarisha mifumo ya afya barani Afrika na duniani. Anold Kayanda na taarifa zaidi

Habari za UN
Kenya: Mradi wa majaribio walenga kudhibiti plastiki na kemikali kwenye kilimo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 27, 2026 2:54


FAO nchini Kenya inasema mradi huo wa miaka mitano uitwao FARM, unalenga kuimarisha uwekezaji katika mbinu mbadala na usimamizi endelevu wa kemikali hatari na plastiki kwenye sekta ya kilimo barani Afrika na Amerika ya Kusini. Tweet URLUkifadhiliwa na Fuko la Mazingira Duniani, GEF, mradi unafanya kazi na vikundi vya wataalamu wa kitaifa kutoka taasisi mbalimbali, kuangazia vipaumbele na changamoto za ndani ili kutengeneza mitaala ya mafunzo inayolinda mazingira. Ripoti ya mradi imebainisha kuwa matumizi ya viuatilifu yamekuwa na madhara makubwa kwa viumbe wanaosaidia uchavushaji wa mimea. Aidha, mabaki ya sumu hizi yanaweza kukaa kwenye udongo kwa zaidi ya miaka 30, jambo ambalo ni hatari sio tu kwa mazao ya chakula bali pia kwa afya za wakulima. Madhara ya matumizi kupita kiasiMatumizi yaliyopitiliza yamehusishwa na magonjwa ya saratani na matatizo ya mfumo wa mishipa ya fahamu, huku yakipunguza uwezo wa nchi kuuza mazao yao kwenye masoko ya kimataifa kutokana na viwango vya sumu kuzidi mipaka ya usalama wa chakula.  Afisa wa FAO, Oxana Perminova anasema, "plastiki na kemikali za kilimo ni jambo linalotia wasiwasi duniani kote. Suala hilo limekuwa katika ajenda za nchi nyingi. Kwa upande wa Kenya, tunaamini kuwa ushirikiano huu ambao umeanzishwa hapa na ambao kwa kweli unafanya kazi ya na unawaleta wadau wote pamoja utakuwa na manufaa makubwa kwa kanda hii. Hivyo nchi nyingine jirani zinaweza kuangalia mifano na bidhaa zitakazozalishwa ndani ya ushirikiano huu na kuzitumia mahususi kwa ajili ya kupunguza uchafuzi wa mazingira kutokana na kemikali na plastiki za kilimo na kuwalinda wakulima, hasa katika maeneo haya." Fahamu kuhusu madhara ya plastiki za vifungashioKuhusu plastiki za vifungashio vya pembejeo za kilimo, takwimu zinaonesha kuwa takriban tani 330,000 za plastiki hutumika kila mwaka kama vifungashio vya viuatilifu duniani kote. Inakadiriwa kuwa asilimia 35 ya plastiki hizi hazidhibitiwi ipasavyo, ambapo asilimia 10 huishia baharini na nyingine nyingi kubaki kwenye udongo. Grace Muchemi, ni Meneja Mkuu wa bodi ya kudhibiti bidhaa za viuatilifu, PCPB, nchini Kenya, anaeleza hatua zinazochukuliwa kuwa ni "tunapotazamia njia mbadala salama zaidi, tumekuwa tukipitia upya viuatilifu ili kuhakikisha viuatilifu vyenye hatari ndogo vinatumika ndani ya nchi. Pia, utoaji wa uelewa umefanyika ndani ya kaunti, na tunafanya kazi pamoja na mashirika mengine ya serikali na pia wadau wa maendeleo kutoa uelewa juu ya matumizi salama ya viuatilifu ili kuhakikisha chakula salama na pia kuwezesha biashara na nchi nyingine." Katika hatua muhimu ya kuleta usawa, mradi huu umehakikisha uwiano sawa wa washiriki wanaume na wanawake katika mafunzo yote yatakayotolewa. 

Habari za UN
Balozi Ngoga: Manusura wana mchango mkubwa katika ujenzi wa Rwanda baada ya mauaji ya kimbari

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 27, 2026 2:20


Tweet URLSuala hilo la mchango wa manusura katika kuepusha mauaji kama hayo hayajirudii tena, nililimulika wakati wa mazungumzo yangu ya hivi karibuni na Mwakilishi wa Kudumu wa Rwanda kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Martin Ngoga ambaye bila kumung'unya maneno alinieleza kuwa, “ wanamchango mkubwa sana kwa sababu kwanza wanapambana na hali ambayo katika hali ya kawaida ya ubinadamu ni ngumu. Chukulia mfano wetu sisi Rwanda walionusurika mauaji na waliotekeleza wanaishi pamoja kwa sababu Rwanda hakuna mgawanyiko wa kikabila wa kwamba kuna baadhi wanaishi mkoa fulani. Wanaishi pamoja katika vijiji hivyo, hivyo wanaenda shule hizo hizo wanaenda hospitali pamoja na wanaishi pamoja. Kwa mtu ambaye amepoteza familia yake nzima na anawajua wauaji walioua familia yake na anaendelea kuishi nao kijijini, ni hali ambayo kwa kweli katika akili ya kawaida unaweza usielewe lakini imetokea Rwanda.”Mwaka huu wa 2026 ni miaka 32 tangu kutokea kwa mauaji hayo ya kimbari. Hivyo Balozi Ngoga ambaye aliwahi kuwa Mwakilishi wa Rwanda kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu uliotokea Rwanda (ICTR) akafafanua kwamba, “Baadhi ambao walikuwa ni wadogo wakati huo ambao sasa ni watu wazima, wanaandika hata vitabu kueleza nini kilitokea. Lakini wamekubali kuingia katika mchakato wa maridhiano, kujenga upya taifa la Rwanda."Akaongeza kuwa, "na kama ambavyo aliwahi kusema kiongozi wetu Rais Paul Kagame wakati fulani kwamba wao walionusurika ndio wanacho cha kutoa. Wao ndio wanaombwa watoe zaidi katika kuchangia juhudi za kulijenga upya taifa kwa sababu muuaji unaenda kumuomba nini. Tunashukuru kwamba wamekubaliana na hiyo, hali ambayo katika mazingira ya kawaida ya kibinadamu ni ngumu sana. Lakini kwa miaka yote hii tunakwenda.”

rwanda umoja wana kwa katika wao baada mwaka lakini baadhi kimataifa uhalifu
Habari za UN
Vijana wasomi wa vyuo vikuu katika ukanda wa Gaza walazimika kufanya kazi ndogo ndogo ili kujikimu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 24, 2026 3:21


Hali ngumu ya kiuchumi inayoendelea kuzorota katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel imewafanya vijana waliokuwa wakisoma vyuo vikuu na wahitimu kuhangaika kufanya kazi ndogo ndogo ili kujikimu baada ya ndoto zao za masomo na taaluma kuvurugwa na vita iliyodumu kwa miaka mitatu. Leah Mushi anatuletea simulizi za baadhi ya vijana hao na shuhuli wanazozifanya hivi sasa.

SBS Swahili - SBS Swahili
Makala leo: Watetezi waunga mkono uamuzi wa kuoga bure katika huduma ya utunzaji wa wazee nyumbani

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 24, 2026 12:23


Wiki hii umakini mkubwa umekuwa kwenye Mfumo wa Kitaifa wa Bima ya Watu Wenye Ulemavu (NDIS), serikali ya shirikisho ikitangaza makato ambayo yanakadiriwa yata ondoa makumi ya maelfu ya watu kwenye mfumo huo.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "KUPARAMA."

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 23, 2026 0:43


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KUPARAMA."

Habari za UN
23 APRILI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 23, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo juzi Jumanne na jana Jumatano wagombea wa nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa walipata fursa kunadi serra zao mbele ya nchi wanachama kwenye Baraza Kuu wakiwemo wawakilishi wa asasi za kiraia walioweza kuwauliza maswali. Miongoni mwa wawakilishi hao ni Irene Kitoti, Mwanzilishi na mkurugenzi wa asasi ya kiraia ya Genesis For Children Organization ya nchini Tanzania aliyezungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo.Kutokana na mafanikio ya kihistoria kwa afya ya umma ya eneo la Karibe, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO limeipongeza nchi ya Bahamas kwa kuwa taifa la hivi karibuni zaidi katika ukanda huo wa Karibe kuthibitishwa kuwa limekomesha maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI, VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Daktari Tedros Adhanom Ghebreyesus, kupitia taarifa ya shirika hilo ameipongeza Bahamas kwa mafanikio haya makubwa, yanayoimarisha miaka ya dhamira ya kisiasa na kujitolea kwa wahudumu wa afya.Ikiwa leo imetimia miaka 15 tangu kuanza maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wasichana katika Teknolojia ya Habari na Mawasilino, TEHAMA au ICT, Katibu Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mawasiliano (ITU), Doreen Bogdan-Martin katika ujumbe wake mahususi wa maadhimisho ya mwaka huu amesema, “kwa sasa tunaishi katika kipindi cha mabadiliko makubwa na ya kusisimua zaidi ya kiteknolojia katika historia ya binadamu lakini vilevile kwa sasa fursa zinazohusiana na mabadiliko haya ya kiteknolojia hazimfikii kila mtu kwa usawa”.Mgogoro wa usafirishaji katika Mlango Bahari wa Hormuz uliosababishwa na vita vya Mashariki ya Kati umefichua tishio jipya: upungufu  wa madini ya kimkakati yanayoendesha uchumi duniani kote  na sasa nchi huenda zitaanza kuhaha kuyapata. Katika mkutano na waandishi wa habari leo jijini Geneva Uswisi, Dario Liguti, Mkurugenzi wa Kitengo cha Nishati Endelevu cha Tume ya kiuchumi ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Ulaya, UNICE amesema,  “hatua ya kwanza, mbali na ongezeko la bei bila shaka, itakuwa viwanda kupunguza matumizi yake yake ya madini ya kimkakati na hivyo kupunguza uzalishaji… iwe ni paneli za sola, sumaku, betri na kadhalika, katika siku zijazo.”Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KUPARAMA"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

bahamas tanzania hormuz ict umoja hii kiswahili katika siku afya taifa tume baraza habari tehama mataifa aprili shirika kimataifa mashariki ikiwa teknolojia miongoni mkurugenzi doreen bogdan martin
SBS Swahili - SBS Swahili
The overlooked story: Aboriginal and Torres Strait Islander service on ANZAC Day - Hadithi iliyopuuzwa: Huduma yawa Aboriginal na wana Visiwa wa vya Torres Strait katika siku ya ANZAC

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 23, 2026 9:48


Each year Australians gather on ANZAC Day to remember those who served in wars, conflicts and peacekeeping missions. But whose stories are we remembering? Are there stories we don't always hear? In this episode we explore an important part of Australia's history that has often been overlooked—the service of Aboriginal and Torres Strait Islander peoples. - Kila mwaka Waaustralia hujumuika katika siku ya ANZAC kuwakumbuka waliohudumu katika vita, migogoro na misheni za kulinda amani. Lakini tunakumbuka hadithi za nani? Je, kuna hadithi ambazo hatuzisikii kila wakati? Katika makala haya tunachunguza sehemu muhimu ya historia ya Australia ambayo mara nyingi imekuwa ikipuuzwa—huduma ya watu wa Asili na wakaazi wa Visiwa vya Torres Strait.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana na matumizi ya neno "UNYUMBA"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 21, 2026 0:52


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Mtaalam wetu Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "UNYUMBA" 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari:Australia ya omba matokeo ya mazungumzo katika Mlango-Bahari wa Hormuz

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 21, 2026 13:51


Waziri wa Mambo ya Nje Penny Wong anasema Australia ina omba matokeo ya mazungumzo katika Mlango-Bahari wa Hormuz, baada ya Marekani kushambulia na kukamata meli ya mizigo yenye bendera ya Iran.

Habari za UN
UN yaadhimisha miaka 25 ya Jukwaa linalojikita katika haki za Watu wa Asili mkazo ukiweka zaidi katika changamoto za afya na mabadiliko ya tabianchi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 20, 2026 3:06


Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa kuhusu Masuala ya Watu wa Asili (UNPFII) limefungua kikao chake cha ishirini na tano leo Aprili 20 katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani likiadhimisha miaka 25 tangu kuanzishwa kwake kama jukwaa la kipekee la kimataifa linalowakutanisha wadau kuhusu Watu wa Asili. Kikao hiki kinafanyika katika muktadha wa changamoto zinazoendelea duniani, zikiwemo afya, migogoro na ukosefu wa usawa. Pia kinakuja wakati ambapo mfumo wa ushirikiano wa kimataifa, ndani ya mfumo wa mipango kama Mpango wa Mageuzi ya Umoja wa Mataifa, UN80 unakabiliwa na mahitaji yanayoongezeka ya ujumuishwaji, uhalali na ufanisi. Anold Kayanda amelifuatilia tukio hilo. 

new york zaidi umoja haki katika asili afya watu miaka mataifa aprili marekani jukwaa
SBS Swahili - SBS Swahili
Hadithi iliyopuuzwa: Huduma yawa Aboriginal na wana Visiwa wa vya Torres Strait katika siku ya ANZAC

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 20, 2026 11:11


Siku ya ANZAC ni moja ya siku muhimu zaidi za kitaifa nchini Australia. Kila mwaka, watu hukusanyika kuwakumbuka waliohudumu katika vita, migogoro na misheni za kulinda amani.

Habari za UN
Zaidi ya wanawake elfu thelatini na nane wameauawa katika ukanda wa Gaza - Ripoti mpya ya UN Women

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 17, 2026 3:02


Uchambuzi mpya wa utafiti uliotolewa leo Aprili 17 na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wanawake, UN Women umeweka wazi kuwa zaidi ya wanawake na wasichana 38,000 wameauawa kati ya mwezi Oktoba mwaka 2023 na Desemba 2025 huko Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel ikiwa ni wastani wa takribani wanawake na wasichana 47 wanaouawa kila siku. Anold Kayanda ameufuatilia utafiti huo na kutuandalia taarifa ifuatayo. 

israel gaza palestina un women zaidi umoja nane katika wanawake mataifa aprili oktoba shirika ripoti desemba
Habari za UN
16 APRILI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Uganda ambayo ni moja ya nchi zinazohifadhi wakimbizi wengi zaidi duniani na tutasikia simulizi za wakimbizi kutoka Sudan ambao Uganda iliwapokea na kuwapa makazi katika Makazi ya Wakimbizi ya Kiryandongo yaliyoko magharibi mwa nchi.Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wametaka uchunguzi wa haraka na uwajibikaji wa kimataifa kufuatia madai ya usafirishaji haramu wa wanawake na wasichana yaliyoibuliwa katika “faili za Epstein.” Wamesema madai hayo yanaonyesha mtandao mpana wa unyonyaji wa kingono uliodumu kwa miaka mingi na kuhusisha watu mashuhuri.mashambulizi makali ya anga ya Israel yameendelea kusini mwa Lebanon, yakilenga maeneo karibu na ngome ya Hezbollah ya Bint Jbeil, huku mashambulizi ya roketi kuelekea kaskazini mwa Israel nayo yakiendelea na kuongeza hofu ya kuongezeka kwa mapigano. Katika hatua nyingine, jeshi la Marekani limesema limezuia meli 10 kupita katika Mlango Bahari wa Hormuz, likitekeleza zuio lake lililotangazwa dhidi ya bandari za Iran. Wakati huo huo, mvutano wa kidiplomasia unaongezeka katika Umoja wa Mataifa, ambapo Baraza Kuu linakutana leo kujadili matumizi ya kura ya turufu kufuatia azimio la Baraza la Usalama kuhusu Mashariki ya Kati lililoungwa mkono na wengi lakini kuzuiwa na China na Urusi.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, leo limeeleza wasiwasi mkubwa kufuatia ongezeko la watoto waliouawa au kujeruhiwa nchini Ukraine, ambapo watoto 89 wameathirika mwezi Machi 2026 pekee. Kwa mujibu wa takwimu zilizothibitishwa na ripoti ya uangalizi wa haki za binadamu nchini Ukraine, idadi hiyo imeongezeka kwa asilimia 65 ikilinganishwa na mwezi Februari, hali inayoonesha madhara makubwa ya mashambulizi yanayoendelea kwa familia na jamii. Mashambulizi mabaya ya usiku wa tarehe 15 Aprili yalipiga miji kadhaa mikubwa, ikiwemo Dnipro, Kharkiv, Kyiv na Odesa, yakionesha hatari kubwa inayowakabili watoto.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye Kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “AWALI KUWA HERI SI AJABU” asMwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali “AWALI KUWA HERI SI AJABU”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2026 1:02


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye Kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “AWALI KUWA HERI SI AJABU” 

kenya nairobi heri kiswahili katika kuwa maana dkt jifunze chuo kikuu
Habari za UN
Simulizi za mateso na matumaini ya wakimbizi wa muda mrefu katika makazi ya wakimbizi ya Kiryandongo Uganda

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2026 5:08


Uganda ni moja ya nchi zinazohifadhi wakimbizi wengi zaidi duniani. Kwa Afrika ni ya kwanza ikihifadhi wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Burundi, rwanda, Sudan, Sudan Kusini na hata Kenya. Katika mada kwa kina hii tunaangazia wakimbizi kutoka Sudan ambao Uganda iliwapokea na kuwapa makazi katika Makazi ya Wakimbizi ya Kiryandongo yaliyoko magharibi mwa nchi. Abdelmonem Makki wa Idhaa ya Kiarabu ya Umoja wa Mataifa hivi karibuni ameyatembelea makazi hayo na kuzungumza na wakimbizi hao kutoka Sudan. Na sasa kwa lugha ya Kiswahili, Feissal Kirwa wa Idhaa hii anasimulia.

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Zima moto wakabiliana na moto mkubwa katika kiwanda cha kusafisha mafuta

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 16, 2026 6:15


Kuna ripoti za uharibifu mkubwa kwa moja ya viwanda viwili vya mwisho vya kusafisha mafuta vilivyosalia nchini Australia, kikosi cha zimamoto kikiitikia moto uliozuka katika eneo la kampuni ya Viva Energy Group karibu na Geelong.

SBS Swahili - SBS Swahili
Wiki hii Afrika: Rais Ruto ataka mageuzi katika muundo wa Muungano wa Afrika ili ifikie uwezo wayo kamili

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 16, 2026 7:56


Rais wa Kenya, William Ruto amesema Umoja wa Afrika katika muundo wake wa sasa, hauja andaliwa ipaswavyo ili kulisaidia bara la Afrika kufikia uwezo walo kamili wa maendeleo na ustawi.

Habari za UN
15 APRILI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 15, 2026 11:11


Hii leo jaridani tunaangazia juhudi za Umoja wa Mataifa za kutafuta suluhu ya vita nchini Sudan pamoja na simulizi za wakimbizi ikiwa leo ni miaka mitatu kamili tangu vita vilipoanza nchini humo, na miundombinu na ujenzi wenye mnepo nchini Tanzania.Wakati vita nchini Sudan ikiingia mwaka wa nne tangu kuvuka kwa mapigano baina ya jeshi la Sudan na kikosi vya msaada wa haraka RSF, hii leo huko Berlin nchini Ujerumani unafanyika mkutano wa Kimataifa ukilenga kurejesha mgogoro wa Sudan katika ajenda ya juu ya kidiplomasia duniani.Leo ni miaka mitatu kamili tangu vita vilipoanza nchini Sudan 15 Aprili 2023, mgogoro ambao umegeuka kuwa moja ya majanga makubwa zaidi ya kibinadamu duniani. Mamilioni ya watu wamekwama katikati ya mapigano, kuwa wakimbizi wa ndani na nje, njaa na ukosefu wa makazi, huku mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa yakionya kuwa mateso yanaendelea kuongezeka kila uchao.Katika kuunga mkono lengo namba 9 la Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs kuhusu miundombinu na ujenzi wenye mnepo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP nchini Tanzania, limeingia makubaliano ya kimkakati na Taasisi ya wanawake wasanifu Majenzi, TAWAH, kwa ajili ya kuboresha sekta ya ujenzi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

berlin tanzania sudan sdgs undp rsf umoja hii katika wakati wanawake mataifa aprili maendeleo shirika kimataifa ujerumani
Habari za UN
UNDP yasaini makubaliano kuwezesha wanawake wasanifu majenzi Tanzania

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 15, 2026 3:21


Katika kuunga mkono lengo namba 9 la Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs kuhusu miundombinu na ujenzi wenye mnepo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP nchini Tanzania, limeingia makubaliano ya kimkakati na Taasisi ya wanawake wasanifu Majenzi, TAWAH, kwa ajili ya kuboresha sekta ya ujenzi. Makubaliano hayo yaliyowekwa saini Aprili 8, 2026, yanalenga kutambua madini ya ujenzi na viwandani yaliyosahaulika, kukuza ujenzi usioharibu mazingira na kuwawezesha wanawake kiuchumi. Rashid Malekela na taarifa zaidi.

tanzania sdgs undp umoja katika wanawake mataifa aprili maendeleo shirika
Habari za UN
Jifunze Kishwahili: Maana za neno "KUDA"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 14, 2026 0:59


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KUDA"

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Kenya na Ufaransa zapiga hatua katika mkataba wa ulinzi

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 13, 2026 5:39


Serikali ya Australia inasema haifikirii kutuma meli katika Mlango-Bahari wa Hormuz, baada ya Rais Donald Trump kusema mataifa mengine yatahusika katika kizuizi cha Marekani kwenye njia hiyo ya maji.

australia kenya hormuz katika habari hatua serikali marekani ufaransa
SBS Swahili - SBS Swahili
Makala leo: Maumivu ya madereva katika vituo vya petroli yanaweza endelea kwa muda

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 10, 2026 8:31


Tangazo la kusitisha mapigano Mashariki ya Kati linaonekana kupunguza maumivu ya madereva katika vituo vya petroli, Iran ikikubali kuruhusu meli kupitia Mlango-Bahari wa Hormuz.

iran muda hormuz makala katika mashariki tangazo endelea
Habari za UN
09 APRILI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 9, 2026 9:58


Jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kusikia ujumbe wa Hanna Wendot Cheptumo Waziri wa Jinsia, Utamaduni na Maslahi ya Watoto wa Jamhuri ya Kenya ambaye alikuwa miongoni mwa washiriki wa CSW70 akieleza ni kwa namna gani Kenya inapiga hatua katika Lengo namba 5 la Usawa wa Kijinsia.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani vikali mashambulizi makubwa ya anga yaliyofanywa na Israel dhidi ya Lebanon tarehe 8 Aprili, mashambulizi ambayo yamesababisha mamia ya raia kuuawa na kujeruhiwa, wakiwemo watoto, sambamba na kuharibu kwa kiasi kikubwa miundombinu ya kiraia. Taarifa iliyotolewa New York, Marekani na Msemaji wa Umoja wa Mataifa inamnukuu Guterres akionesha wasiwasi mkubwa kuhusu ongezeko la vifo miongoni mwa raia na kutoa pole kwa watu na Serikali ya Lebanon, akiwatakia nafuu ya haraka wale waliojeruhiwa.Katika tukio jingine hii leo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezindua Mfuko wa Urejeshaji wa Palestina uliopewa jina la Horizon Fund, akisisitiza umuhimu wa kuchukuliwa kwa hatua za haraka kusaidia wananchi wa Palestina kurejesha maisha yao na kujenga mustakabali bora. Akizungumza kupitia ujumbe wa video wakati wa uzinduzi uliofanyika Ramallah, huko Ukingo wa Magharibi eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel, Guterres amesema mfuko huo ni sehemu muhimu ya ushirikiano kati ya Umoja wa Mataifa na Taifa la Palestina.Wakati mgogoro wa Sudan ukikaribia kutimiza miaka mitatu, zaidi ya wakimbizi milioni moja wa Sudan walioko nchini Chad wanakabiliwa na hatari kubwa ya kupunguzwa kwa msaada muhimu wa kibinadamu. Onyo hilo limetolewa leo na mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa ambayo ni lile la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) pamoja na la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) wakitanabaisha kuwa huduma za msingi kama chakula, maji, malazi, ulinzi na huduma za afya zitalazimika kupunguzwa zaidi katika miezi ijayo iwapo pengo la ufadhili la dola milioni 428 halitazibwa haraka.Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Mahojiano: Je makanisa yanastahili watenga viongozi ambao wame sababisha maafa katika nchi zao na duniani?

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 8, 2026 10:46


Waumini wa dini laki Kristo kote duniani, wali jumuika katika sehemu mbali mbali kusherehekea Pasaka.

kristo katika maafa pasaka nchi
Habari za UN
02 APRILI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 2, 2026 11:45


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kupata ujumbe wa Zahra Salehe, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la ICCAO linaloshughulika na masuala ya vijana amabye kwa kuwa mwaka huu 2026 ameshiriki tena katika  mkutano wa CSW70 anatueleza ni kwa kiasi gani wameweza kulitekeleza malengo ya mikutano haya katika nchini humo.Vita Mashariki ya Kati vilivyoanzishwa na Marekani na Israeli dhidi ya Iran vikiingia mwezi wa pili, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo hapa makao makuu ya UN jijini New York, Marekani amezungumza na waandishi wa habari akisisitiza sio tu vita hivyo vikome bali pia anaendeleza diplomasia za kusaka suluhu. Guterres amesema, Ninamtuma Mjumbe wangu Maalum Jean Arnault. Lengo ni kuunga mkono jitihada za kikanda. Lazima tupate njia ya amani ya kutoka katika hali hii. Ujumbe wangu uko wazi. Kwa Marekani na Israeli, ni wakati muafaka kusitisha vita vinavyosababisha mateso makubwa ya kibinadamu na tayari vinaanzisha athari mbaya za kiuchumi. Kwa Iran, isitishe kushambulia majirani zake.. Ripoti mpya ya Kamisheni  ya Umoja wa Mataifa kwa Uchumi wa Afrika, (ECA)  imependekeza umuhimu wa kuimarisha mifumo ya usimamizi wa deni la umma barani Afrika, ikionya kwamba uendelevu hautegemei tu kiwango cha kukopa bali pia ubora wa taasisi, mifumo ya kisheria, na uwazi. Ikitolewa leo huko Addis Ababa, Ethiopia, ripoti hiyo inataja udhaifu kama vile uwezo mdogo wa kufanya uchambuzi wa hatari, na ushawishi wa mashinikizo ya kisiasa katika maamuzi ya kukopa ikisema kuwa kuboresha usimamizi ni jambo muhimu ili kuhakikisha kuwa deni la umma linachangia ukuaji wa uchumi endelevu badala ya kuwa chanzo cha kuyumba kifedha.Wakati dunia hii leo ikiadhimisha Siku ya Uelewa wa Usonji, familia katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli,  zinakabiliwa na changamoto zinazoongezeka katika kuwahudumia watoto usonji katikati ya mzozo unaoendelea na hali mbaya ya kibinadamu. Katika kitongoji cha Sheikh Radwan kaskazini mwa Jiji la Gaza, Layan Abu Qousa mwenye umri wa miaka 16, ambaye ana usonji, anaishi na familia yake katika magofu ya nyumba yao. Familia yake inasema hali ngumu ya maisha imeongeza changamoto zinazohusiana na hali yake, huku ukosefu wa utulivu na mkwamo wa kupata huduma za kitaalamu ukiendelea kudhoofisha ustawi wake.Na katika jifunze Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye Kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “ATANGULIAYE KUFIKA HUCHAGUA PA KUKAA”Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!