Podcasts about katika

Place in Paphos District, Cyprus

  • 120PODCASTS
  • 1,444EPISODES
  • 20mAVG DURATION
  • 1DAILY NEW EPISODE
  • Mar 13, 2023LATEST

POPULARITY

20152016201720182019202020212022

Categories



Best podcasts about katika

Show all podcasts related to katika

Latest podcast episodes about katika

Habari za UN
Mitandao ya intaneti kwenye ngazi ya jamii ndio jawabu la kufikisha teknolojia kwa walio pembezoni- Bi. Lugangira

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 13, 2023 0:04


Mkutano wa 67 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW67 ukiendelea na maudhui makuu yakiwa ni namna ugunduzi na teknolojia ya dijitali inaweza kuchangia kumkwamua mwanamke, Idhaa ya Kiswahili  ya Umoja wa Mataifa nayo inaendelea kuzungumza na washiriki ili kufahamu kule watokako hali iko namna gani na nini kinafanyika ili kuhakikisha teknolojia ya kidijitali inatumika kivitendo badala ya kusalia kwenye makabrasha au kumilikiwa na wachache na hivyo kuzidi kuongeza pengo la kidijitali. Miongoni mwa washirii ambao Idhaa hii imezungumza nao ni Neema Lugangira, mbunge wa Chama Cha Mapinduzi, CCM, nchini Tanzania akiwakilisha mashirika yasiyo ya kiserikali. Katika mahojiano yake na Flora Nducha wa Idhaa  ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa, Bi. Lugangira amezungumzia ni kwa kiwango gani teknolojia ya  kidijitali inatumika Bungeni na zaidi ya yote mikakati yake ya kuona intaneti inafikia wengi walio pembezeno. Lakini kwanza anamulika matumizi ya teknolojia kwa ujumla wake nchini Tanzania. 

bi tanzania ccm umoja katika makala kiswahili kwenye jamii lakini wanawake mataifa mkutano teknolojia miongoni
Habari za UN
UNICEF: Watoto katika nchi 11 za Mashariki na Kusini mwa Afrika wako hatarini sababu ya kipindupindu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 10, 2023 0:02


Nchi 11 Mashariki na Kusini mwa Afrika zinakabiliwa na hali mbaya ya mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambako hadi sasa kumeripotiwa wagonjwa 67,822 na vifo 1, 788 kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.Taarifa ya UNICEF iliyotolewa leo mjini Nairobi, Johannesburg na New york inasema huenda idadi kamili ya wagonjwa na vifo ikawa kubwa zaidi kutokana na changamoto ya mifumo ya ufuatiliaji, utoaji taarifa na unyanyapaa.Nchi mbili ambazo zina mzigo mkubwa zaidi ni Malawi na Msumbuji ambazo shirika hilo linasema “kwa pamoja zaidi ya watu milioni 5.4 wanahitaji msaada wakiwemo watoto zaidi ya milioni 2.8.”Naibu mkurugenzi wa kinanda wa UNICEF Lieke van de Wiel ambaye amehudhuria mkutano wa mawaziri kuhusu kipindupindu mjini Lilongwe Malawi amesema “Tulifikiri ukanda huu hautoshuhudia mlipuko wa kipindupindu wa kiwango hiki cha kusambaa kwa zama hizi. Mifumo duni yam aji na usafi, matukio mabaya ya hali ya hewa, mizozo inayoendelea na mifumo duni ya afya vimezidisha adha na kuweka rehani maisha ya mamilioni ya watoto kote Kusini mwa Afrika.”Msaada wa UNICEF katika ngazi za kitaifa unajumuisha “utoaji wa maji safi na huduma ya usafi, kuweka tembe za kusafisha maji, sabuni za kunawia mikono,dawa za kuongeza maji mwilini, huduma ya kubadili mwenendo wa tabia, na kusambaza ujumbe wa kampeni ya kuishirikisha jamii na zaidi ya hayo UNICEf na washirika wake pia wanatoa msaada wa vifaa vya afya na mahema kwa ajili ya kukabiliana na kiwango kikubwa cha wagonjwa.”Kutokana na kuendelea kuzorota kwa hali hususani katika nchi zilizoathirika zaidi na kipindupindu sasa “UNICEF inaomba dola milioni 150 kwa aajili ya kuzisaidia nchi zote 11 zilizoathirika ikiwemo dola milioni 34.9 kwa ajili ya Malawi, na milioni dola 21.6 kwa ajili ya Msumbiji kuweza kutoa huduma za kuokoa Maisha kwa watu walioathirika na mlipuko huo.”Hadi sasa washirika wa UNICEF wameshachangia dola milioni 2.9 kukabiliana na mlipuko nchini Malawili na dola 550,000 kwa ajili ya Msumbiji.

Habari za UN
09 MACHI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 9, 2023 0:12


Ni Alhamisi tulivu kabisa ya tarehe Tisa ya mwezi Machi mwaka 2023, siku ya mwisho ya mkutano wa 5 hapa Qatar wa nchi zenye maendeleo duni zaidi duniani ambapo leo ni mada kwa kina na tutasalia hapa Doha, Qatar ambako katika mkutano waw a 5 wa nchi zenye maendeleo duni zaidi duniani, LDC5, miongoni mwa washiriki ni vijana ambao walifika hapa kuhakikisha sauti zao zinakuwa sehemu ya maazimio ya mkutano huo. Miongoni mwa vijana hao ni Jadot Nkurunziza ambaye kwa kushirikiana na wenzake wanaunga mkono mkono mradi unaotekelezwa na Rais wa kurejesha misitu nchini Burundi kwa kupanda miti. Pia tunakuletea habari kwa ufupi za kutokoa LDC5 na ripoti ya dawa za kulevya. Katika kujifunza kujifunza Kiswahili , leo tukipata ufafanuszi wa neno "MANYEZI" kutoka kwa mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania , BAKITA.Mkutano wa Tano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Nchi Zenye Maendeleo Duni zaidi duniani, uliokuwa unafanyika mjini Doha Qatar umemalizika jioni ya leo kwa saa za Qatar kwa nchi kuidhinisha hatua madhubuti za kutekeleza Mpango wa Utekelezaji wa Doha (DPoA) - unaolenga kuhuisha na kuimarisha ahadi kati ya nchi zenye maendeleo duni zaidi duniani LDCs na wadau wao wa maendeleo  kuashiria mageuzi kwa nchi zilizo hatarini zaidi duniani.Tukisalia huko huko Doha vijana walikuwa sehemu kubwa ya mkutano huo wa tano wa nchi masikini zaidi duniani LDC ili kuhakikisha sauti zao zinasikika. Humphrey Mrema kutoka taasisi isiyo ya kiserikali ya vijana ijulikanayo kama Youth Survivour Organization ni miongoni mwao na anasema nini ametoka nacho kwenye mkutano huo.Na ripoti mpya ya mwaka 2022 iliyotolewa leo na bodi ya kimataifa ya kudhibiti dawa za kulevya INCB inaonya kwamba kuhalalisha matumizi yasiyo ya kitabibu ya bangi ambayo yanakwenda kinyume na mkataba wa mwaka 1961 wa matumizi ya dawa za kulevya kunaonekana kuongeza kwa kiasi kikubwa matumizi ya dawa hizo na kupunguza uelewa wa hatari zake hususan miongoni mwa vijana.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili ambapo leo nakuleta ufafanuzi wa neno "MANYEZI" kutoka kwa mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania , BAKITA.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

Habari za UN
Jifunze Lugha ya Kiswahili: MANYEZI

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 9, 2023 0:01


Katika kujifunza Kiswahili, leo tukipata ufafanuzi wa neno "MANYEZI" kutoka kwa mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, BAKITA, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Leyla "wanawake wameleta maendeleo na utendaji bora katika uongozi"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 8, 2023 7:33


Wanawake kote duniani wana jumuika katika sherehe za siku yakimataifa ya wanawake.

bora katika wanawake maendeleo
Habari za UN
06 MACHI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 6, 2023 0:12


Jaridani leo tunaangazia mkutano wa CSW67 hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa na amani na usalama nchi i DRC. Makala tutaelekea Doha nchini Qatar na mashinani tunasalia hapa makao makuu, kulikoni?Mkutano wa 67 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW umeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ukileta pamoja wawakilishi kutoka serikali, mashirika ya kiraia yanayotambuliwa na Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC pamoja na vijana.Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC Bintou Keita amesema kwamba mpango wa Umoja wa Mataifa nchini huomo MONUSCO unasisitiza wito wa Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa makundi yenye silaha yanayoendesha operesheni zao DRC kuweka chini silaha zao mara moja pasi na masharti yoyote.Katika makala Anold Kayanda wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa aliyeko Doha Qatar kunakofanyika mkutano wa 5 wa nchi zenye maendeleo duni zaidi duniani, LDCs, yeye amezungumza na vijana Cosmas Msoka na Humphrey Mrema ambao wako kwenye ujumbe wa vijana wanaoshiriki mkutano huo.Na katika mashinani tunasalia hapa hapa Umoja wa Mataifa kukuletea matarajio ya kijana kutoka Tanzania aliyekuja kushiriki mkutano wa hali ya wanawake duniani.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
03 MACHI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 3, 2023 0:15


Jaridani leo  tunaangazia afya na hali ya kiuchumi katika nchi zenye maendeleo duni- LDC5.  Makala tutaelekea nchini Tanzania na mashinani nchini Sudan, kulikoni?Ikiwa leo ni siku ya kusikia duniani , shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO limesema maelfu ya watu duniani wanakabiliwa na changamoto ya kupoteza uwezo wa kusikia katika kiwango cha kuhitaji vipimo na matibabu.Kuanzia siku ya jumapili tarehe 5 mpaka 9 ya mwezi huu wa Machi, huko Doha nchini Qatar viongozi kutoka kila pembe ya dunia watakutana katika mkutano wa tano wa Umoja wa Mataifa wa nchi zenye maendeleo duni- LDC5 ili kukubaliana na kuangalia namna ya kuzisaidia nchi hizo ziweze kustawi wakati huu ambapo dunia inakabiliwa na changamoto lukuki.Katika makala tunakwenda nchini Tanzania kumulika ni kwa vipi mradi wa Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori, WMAs, unaotekelezwa kwa pamoja kati ya Wizara ya Maliasili na Utalii nchini humo na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo duniani, UNDP wa kuzuia ujangili na uhifadhi wa wanyamapori umesaidia jamii kunufaika sio tu na uwepo wa wanyamapori kwenye maeneo yao lakini pia kuishi kwa utangamano na wanyama kwa kuzingatia kuwa leo ni siku ya wanyamapori duniani na ujumbe ni ushirikishaji jamii katika hifadhi ya wanyamapori.Na katika mashinani na tutaelekea nchini Sudan kusikia njia mbadala za kuhakikisha usalama wa chakula na kuondokana na umaskini kwa jamii ambazo zilikuwa zinategemea upatikanaji wa ardhi, maji na malisho ya mifugo wengi.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Matunda ya ubia katika kuhifadhi wanyamapori wazaa matunda pori la Waga Tanzania

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 3, 2023 0:05


Nchini Tanzania kumulika ni kwa vipi mradi wa Jumuiya za Hifadhi za WAnyamapori, WMAs, unaotekelezwa kwa pamoja kati ya Wizara ya Maliasili na Utalii nchini humo na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo duniani, UNDP wa kuzuia ujangili na uhifadhi wa wanyamapori umesaidia jamii kunufaika sio tu na uwepo wa wanyamapori kwenye maeneo yao lakini pia kuishi kwa utangamano na wanyama kwa kuzingatia kuwa leo ni siku ya wanyamapori duniani na ujumbe ni ushirikishaji jamii katika hifadhi ya wanyamapori.Mwenyeji wetu ni Sawiche Wamunza, Mkuu wa Mawasiliano UNDP Tanzania akizungumza na Mwenyekiti na Katibu wa Jumuiya ya eneo la hifadhi ya wanyamapori ya Waga inayojumuisha vijiji vilivyoko mkoa wa Iringa na Mbeya. 

tanzania undp umoja katika makala pori waga mataifa wmas mbeya
Habari za UN
Msemo: Kauka nikuvae sanduku msumari

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 2, 2023 0:01


Katika kujifunza Kiswahili, leo tunafafanuliwa  maana ya msemo "KAUKA NIKUVAE SANDUKU MSUMARI" na mchambuzi wetu ni   Onni Sigalla Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, BAKITA. Karibu!

Habari za UN
Katibu Mkuu Guterres ziarani nchini Iraq

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 1, 2023 0:02


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amefanya ziara nchini Iraq lengo likiwa ni kusisitiza mshikamano na kuunga mkono juhudu za nchi za kuleta amani ,haki za binadamu na maendeleo endelevu.Ziara ya mwisho ya Katibu Mkuu Guterres nchini Iraq ilikuwa miaka sita iliyopita, na alipofika Baghdad alipokelewa na Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya nje Fued Hussein ambapo walifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari.Katika hotuba yake Katibu Mkuu Guterres aliipongeza serikali ya Iraq kwa kuwaruhusu wananchi wa Iraq walio nje ya nchi hiyo kurejea na kusema Umoja wa Mataifa unaunga mkono kikamilifu juhudi zote za kuhakikisha nchi hiyo inakuwa na mustakabali wa amani na ustawi na taasisi zake zinaunganishwa na demokrasia.Katika mkutano huo pia alizungumzumzia changamoto zinazowakabili wananchi wa nchi hiyo ikiwemo uhaba wa maji na athari za mabadiliko ya tabianchi na kusema “Moyo wangu unavunjika nikiona wakulima wanaacha ardhi zao na mazao ambayo wamekuwa wakilima kwa milenia. Uhaba wa maji nchini Iraq umechangiwa na kupungua kwa uingiaji kutoka nje, usimamizi usio endelevu wa maji, na sasa athari za mabadiliko ya tabianchi. Ni tishio linalohitaji umakini wa kimataifa.”Katika kupata suluhu kwenye changamoto hiyo amesema mkutano Umoja wa Mataifa wa Maji utakaofanyika baadae mwezi huu jijini New York, Marekani utajadili mengi kuhusu changamoto ya maji huku akidhibitisha kuelewa ni kwa namna gani suala ya uhakika wa maji ni muhimu kwa nchi hiyo.Katika ziara yake hiyo, Katibu Mkuu atakutana na viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo Waziri Mkuu Mohammed Shia' Al Sudani.Akiwa katika mji mkuu, Katibu Mkuu pia atakutana na kuwasikiliza wawakilishi wa vikundi vya haki za vijana na wanawake na kufanya mkutano na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa.Hapo kesho Katibu Mkuu Guterres atatembelea kambi ya Wakimbizi wa Ndani na Kituo cha Urekebishaji kilichoko kaskazini mwa nchi hiyo na kufanya mazungumzo na wakazi wa kituoni hapo.Kisha ataenda Erbil na kukutana na maafisa wa Serikali ya Mkoa wa Kurdistan.

Habari za UN
24 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 24, 2023 0:13


Hii leo jaridani linaangazia vita vya mwaka mmoja nchini Ukraine na kimbunga Freddy.  Makala na mashinani tunasalia huko huko Ukraine.Vita ya Ukraine ikiwa inaingia mwaka wake wa pili, wawakilishi mbalimbali wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wametoa maoni yao kufuatia uamuzi kwa njia ya kura uliofanywa na Kikao Maalumu cha  dharura cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kupitisha azimio jipya la kutaka amani ya haki na ya kudumu nchini Ukraine na kwamba Urusi bila masharti yoyote iondoe mara moja majeshi yake katika ardhi ya Ukraine.Kimbunga Freddy moja ya vimbunga vilivyodumu kwa muda mrefu na kusababisha athari kubwa sehemu mbalimbali sasa kimeondoka Madagascar na kubisha hodi Msumbiji ambako kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO kinaleta tishio kubwa kwa sababu ya kiwango cha mvua kinachoambatana nacho.Katika makala tunamulika mwaka mmoja wa uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.Na katika mashinani mashinani tutasalia nchini Ukraine katika kituo cha muda cha watoto wakimbizi wa ndani nchini Ukraine kusikia ni jinsi gani wafanyakazi wa kujitolea wanavyowasaidia watoto hao kurejesha afya yao ya kiakili.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Jifunze Lugha ya Kiswahili: MBWANDA

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 23, 2023 0:01


Katika kujifunza Lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa Tanzania, BAKITA anafafanua neno MBWANDA.

Habari za UN
22 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 22, 2023 0:11


Hii leo jaridani tunakuletea habari kuhusu mwelekeo wa matumizi ya maji barani Afrika, na elimu kwa watoto waliotumikishwa jeshini nchini DR Congo.  Makala tutakupeleka nchini Tanzania na mashinani tunarudi tena nchini DR Congo.Ni wakati kufikiria upya jinsi ya kutumia maji kwa njia endelevu na yenye uwiano huku ubunifu katika kilimo ukiwa kitovu cha mipango yote, amesema Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO limesema Qu Dongyu hii leo wakati akizungumza na viongozi na wataalamu wa Afrika kwenye warsha ya kwanza ya kikanda kuhusu mwelekeo wa matumizi ya maji barani Afrika, warsha inayofanyika nchini Zimbabwe.Mradi mpya wa shule nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC uliozinduliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto,  UNICEF na wadau wake kwa ufadhili kutoka mfuko wa Umoja wa Mataifa wa kuchagiza elimu kwenye maeneo ya mizozo, Education Cannot Wait, ECW, au Elimu Haiwezi Kusubiri umewezesha watoto waliokuwa wametumikishwa vitani kuanza kurejea kwenye masomo na hata kutangamana na wenzao kwa amani.Katika makala tunakupeleka Njombe mkoa ulioko kusini mwa Tanzania kusikia harakati za Umoja wa Mataifa na wadau za kusongesha ulaji wa mazao ya jamii ya mikunde ili kuboresha lishe.Na katika mashinani tutaelekea tena Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kumsikia mvulana aliyekuwa ametumikishwa vitani.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
21 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 21, 2023 0:11


Ni Jumanne   ya tarehe 21  mwezi Februari mwaka 2023, Siku ya Kimataifa ya Lugha Mama ambapo leo tutasalia hapa hapa nchini Marekani kuangazia juhudi za mzazi kuwarithisha watoto wake lugha mama licha ya changamoto ya kuwa wanaishi katika mazingira ya lugha tofauti. Pia tutakuletea habari za Umoja wa Mataifa kwa ufupi. Katika mashinani utamsikia ujumbe wa mtoto Nia Gitau kuhusu kwa watoto wenzake kuhusu lugha mama.Elimu itolewayo kwa wanafunzi kupitia lugha mama ikielezwa kuwa ni muhimu sio tu katika kuwezesha mtu kustawi na kuendelea bali pia kuhamisha urithi wa lugha, asilimia 40 ya wanafunzi duniani kote bado hawana fursa ya kufundishwa darasani kwa lugha yao wanaozungumza au wanaoelewa zaidi, amesema Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO, Audrey Azoulay katika ujumbe wake wa siku ya lugha mama duniani hii leo.Kwingineko takriban mwaka mmoja tangu kushika kasi kwa vita nchini Ukraine hapo 24 Februari 2022, kizazi cha watoto kimepitia miezi 12 ya machafuko, hofu, hasara na misiba. Limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na kuongeza kuwa hakuna kipengele hata kimoja cha maisha ya watoto hao ambacho mzozo haujakiathiri, kwani watoto wameuawa, kujeruhiwa, kulazimishwa kukimbia nyumba zao, kukosa elimu muhimu na kunyimwa faida za mazingira huru na salama.Na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi na wadau wengine wa kibinadamu na maendeleo 108 leo wamezindua ombi la dola bilioni 1.3 ili kuwalinda na kuwasaidia wakimbizi wa Sudan Kusini milioni 2.2 kwa mwaka huu wa 2023.Na katika mashinani utamsikia ujumbe wa mtoto Nia Gitau kuhusu kwa watoto wenzake kuhusu lugha mama. Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

ukraine unesco unicef umoja katika siku mataifa elimu kimataifa marekani sudan kusini
Habari za UN
20 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 20, 2023 0:11


Hii leo jaridani linaangazia lugha ya mama tunapoelekea katika siku ya Lugha ya Mama Duniani, na huduma za afya nchini Syria baada ya tetemeko la ardhi.  Makala tutakupeleka nchini Tanzania na mashinani nchini Uganda.Kuelekea siku ya kimataifa ya lugha mama duniani hapo kesho, mtaalamu huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu makabila madogo amesema serikali lazima zichukue hatua zaidi juu ya matumizi ya lugha za makabila hayo madogo kwani zama za kuchagua lugha moja tu kutumiwa na taifa zima huku nyingine zikienguliwa zimepitwa na wakati.Ujumbe wa mashirika ya Umoja wa Mataifa umetembelea hospitali na kliniki zinazoungwa mkono na shirika lisilo la kiserikali la Misaada na Maendeleo la Syria au SRD, Kaskazini Magharibi mwa Syria na kujionea athari za tetemeko la Ardhi lililoikumba nchi hiyo wiki mbili zilizopita pamoja na kujionea usambazaji wa misaada iliyotolewa na Umoja wa Mataifa.Katika makala tunaelekea kaskazini magharibi mwa Tanzania katika eneo la Mugumu, Wilaya ya Serengeti mkoani Mara kuangazia harakati za shirika la Hope For Girls and Women in Tanzania kupigania haki za kijamii.Na katika mashinani tutaelekea wilayani Kaabong nchini Uganda kupata ushauri kutoka msichana muathirika wa mimba za utotoni.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
17 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 17, 2023 0:11


Hii leo jaridani linaangazia utalii endelevu na ujenzi wa amani Sudani Kusini. Makala tunakupeleka nchini Somalia na mashinani nchini Kenya.Leo ni siku ya mnepo katika sekta ya utalii duniani, na Umoja wa Mataifa unahimiza umuhimu wa kujenga mnepo katika sekta hiyo kwa kuwa ni chanzo cha kipato na ajira kwa mamilioni ya watu lakini pia kuweza kuhimili mishtuko na majanga makubwa kama COVID-19.Katika kuhakikisha wanavutia wakimbizi wa ndani kurejea makwao, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini UNMISS, umekarabati na kukabidhi jengo la mahakama pamoja na kujenga jengo jipya la magereza huko jimboni Equatorial Magharibi katika kaunti ya Maridi.Katika makala tunaelekea nchini Somalia kuangazia ziara ya kwanza ya Robert Piper ambaye ni Mshauri Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika kutafuta masuluhisho kwa wakimbizi wa ndani duniani.Na katika mashinani tunaelekea Turkana nchini Kenya ambapo baadhi ya watoto wanaacha shule kutokana na ukame wa muda mrefu unaosababisha ukosefu wa chakula.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Mahakama ya zamani yakarabatiwa na jela mpya kujengwa jimboni Equatorial magharibi: UNMISS

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 17, 2023 0:02


Katika kuhakikisha wanawavutia wakimbizi wa ndani kurejea makwao, ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS, umekarabati na kukabidhi jengo la mahakama pamoja na kujenga jengo jipya la jela huko jimboni Equatorial Magharibi katika kaunti ya Maridi.Nchini Sudan Kusini wananchi waliokuwa wakimbizi wa ndani na sasa wameanza kurejea katika vijiji vyao wanataka kurejea katika mazingira ambayo kuna utawala wa sheria.Sarah Barnet ni kiongozi wa wanawake wa kaunti ya Maridi iliyoko jimboni Equatorial Magharibi, “Tunahitaji kuona haki ikitendeka, hasa kwa wanawake. Kuna kesi nyingi za unyanyasaji wa kijinsia katika jamii yetu, na zinapaswa kushughulikiwa na mahakama. Haki zetu kama wanawake lazima ziheshimiwe.”Kwakutambua hili na kutekeleza jukumu lake la kuhakikisha wanalinda amani na kuimarisha mifumo ya haki nchini Sudan Kusini UNMISS wametekeleza mradi uliogharimu takriban dola 100,000 kwa kukarabati jengo la mahakama ya kaunti ya Maridi na kujenga jengo jipya la jela ili yaweze kutoa huduma ya kuhakikisha sheria zinafuatwa na wale wasiofuata sheria jela mpya iliyojengwa lipo kwa ajili yao.Ibrahim Tahiru ni afisa wa Ulinzi, Mpito na Uunganishaji wa UNMISS na anasema wanachukulia utekelezaji wa miradi hii ya kuleta mabadiliko haraka kuwa ni kichocheo muhimu cha kuwavutia watu wengi zaidi kuweza kurejea makwao kutoka ukimbizini, "Tunaamini kuwa tutaweza kukuza hali ya kudumu ya watu kurejea makwao na kuwaunganisha wakimbizi hawa wa ndani pamoja na waliokimbilia nje ya mipaka ya nchi. Tunataka waweze kujisikia kulindwa na kujua kwamba hawata pokonywa mali zao kiholela. Pia tunataka wajue watalipwa ikiwa, walipokuwa wakikimbia mzozo baadhi ya mali zao zilichukuliwa na watu wengine. Kwa hivyo, taratibu zote hizi kama ujenzi wa mahakama na jela zinategemeana. Tunaamini kuwa mfumo madhubuti wa haki utawasaidia sana watu wanaotafuta haki.”Ujumbe wa Umoja wa Mataifa ya kulinda amani nchini humo, UNMISS haujajitolea tu kuboresha uwezo wa mfumo wa haki nchini Sudan Kusini, bali pia kukuza heshima na kufuata matakwa ya haki za binadamu.Jamii ikiwa imewekewa mazingira bora ya kuwawajibisha wahalifu, ukiukaji wa haki za binadamu unatarajiwa kupungua.

kuna umoja haki kwa equatorial katika zamani jamii mataifa unmiss magharibi sudan kusini
Habari za UN
UN: Kujenga mnepo katika sekta ya utalii ni muhimu ili kuhimili majanga kama COVID-19

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 17, 2023 0:02


Leo ni siku ya mnepo katika sekta ya utalii duniani, na Umoja wa Mataifa unahimiza umuhimu wa kujenga mnepo katika sekta hiyo kwa kuwa ni chanzo cha kipato na ajira kwa mamilioni ya watu lakini pia kuweza kuhimili mishtuko na majanga makubwa kama COVID-19.Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa nchi nyingi zikiwemo zenye maendeleo duni, mataifa ya visiwa vidogo vinavyoendelea, nchi za Afrika na nchi za kipato cha kati “utalii ni chanzo kikuu cha uchumi, pato la nje, kodi na ajira.” Na kwa sababu utalii unaunganisha watu na asili, Umoja wa Mataifa unasema utalii endelevu una uwezo wa kipekee wa kuchagiza jukumu la kulinda na kuhifadhi mazingira.  Umeongeza kuwa “zahma yoyote inapoikumba sekta ya utalii basi inasambaratisha na kupindua maisha ya nchi na ya mamilioni ya watu mathalani lilipozuka janga la COVID-19, sekta ya utalii imekuwa moja ya sekta zilizoathirika vibaya.” Na pigo kubwa zidi Umoja huo unasema limeshuhudiwa katika nchi za visiwa vidogo zinazoendelea ambako utalii unachangia zaidi ya asilimia 20 ya pato la taifa GDP na asilimia zaidi ya 30 ya palo la jumla la nje. Duniani kote “sekta ya utalii inatoa ajira kwa mamilioni ya watu  iwe moja kwa moja na kwa njia isiyo ya moja kwa moja hususani kwa wanawake na vijana na ndio maana mwaka 2020 takriban ajira milioni 120 za moja kwa moja kwenye sekta hiyo  zilikuwa hatarini kutokana na janga la COVID-19.” Hata hivyo kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la utalii duniani UNWTO kuna matumaini kwani “mwaka huu wa 2023 utalii wa kimataifa unatarajiwa kuongezeka na kufikia asilimia 80 hadi 95 ya ilivyokuwa kabla ya janga la COVID-19 ukitegemeana na kiwango cha kudorora kwa uchumi, kujikwamua kwa safari za kimataifa Asia na Pasifiki na mwenendo wa vita ya Urusi dhidi ya Ukraine inayoendelea miongoni mwa sababu zingine.” Takwimu za UNWTO zinaonyesha kuwa “mwaka jana 2022 zaidi ya watalii milioni 900 walisafiri kimataifa idadi ambayo ni mara mbili ya ilivyokuwa mwaka 2021.” Shirika hilo linasisitiza kuwa sekta ya utalii endelevu na wenye mnepo unachangia katika ufikiaji wa malengo ya maendeleo endelevu kupitia ukuzaji wa uchumi, kupunguza umasikini na kuzalisha ajira na kazi zenye staha kwa wote. Pamoja na kujenga mnepo lengo lingine kubwa la siku hii “ni kutoa wito kwa nchi wanachama kuunda mikakati ya kitaifa ya kujikwamua baada ya majanga ikiwemo kupitia ushirikiano na sekta binafsi na kupanua wigo wa shughuli za sekta hiyo na bidhaa zake.” 

Habari za UN
16 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 16, 2023 0:12


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo tunakwenda nchini Kenya kuangazia juhudi zinazofanywa na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kupambana na dawa na uhalifu UNODC katika kuwasaidia askari magereza na wafungwa kukabilia changamoto za msongo wa mawazo na afya ya akili. Katika kujifunze Kiswahili tunapata ufafanuszi wa neno "SAKARANI" na Onni Sigalla.Mkutano wa kuchangisha fedha kwa ajili ya kufanikisha elimu kwa zaidi ya watoto milioni 222 duniain ukianza leo huko Geneva Uswisi ukiandaliwa na mfuko wa Umoja wa Mataifa wa kusongesha elimu kwenye maeneo ya majanga na mizozo ya muda mrefu, Education Cannot Wait au elimu haiwezi kusubiri, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema watoto milioni 78 wa kike na wa kiume duniani kote hawaendi shuleni kwa sababu ya vita, majanga ya tabianchi na ukimbizi wa ndani na mamilioni wengine wanapata elimu isiyo makinifu, hivyo ametoa wito wa fedha zaidi kwa elimu kwa watoto kwenye maeneo ya dharura.Mamia ya wanawake nchini Tanzania wameanza kunufaika na upatikanaji wa huduma bora zaidi za saratani ya shingo ya kizazi baada ya kufungwa kwa mashine za kuimarisha kiwango cha juu cha dozi HDR katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) jijini Dar es Salaam, mashine ambazo zinayoratibiwa na IAEA.Na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani, WFP limeongeza kwa asilimia 43 mgao wa chakula kwa wakimbizi wanaoishi kwenye kambi zote tano nchini humo ili waweze kukidhi mahitaji yao ya msingi, kufuatia ongezeko la bei za vyakula na nishati duniani kote.Na katika kujifunza Kiswahili leo tukipata ufafanuszi wa neno "SAKARANI" na mtaalam wetu ni Onni Sigalla Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania , BAKITA. Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
15 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 15, 2023 0:12


Hii leo jaridani tunaangazia kazi za Umoja wa Mataifa kwa waathirika wa tetemeko la ardhi, na pia kazi za umoja huo nchini Ukraine. Makala tunakupeleka nchini Burundi na mashinani nchini Tanzania, kulikoni?Wakati vita nchini Ukraine ikikaribia kuingia mwaka wa pili, ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR leo kwa pamoja wameomba jumla ya dola bilioni 5.6 ili kupunguza madhila yanayowakabili mamilioni ya watu walioathirika na vita nchini Ukraine.Mkuu wa kanda ya nchi za kiarabu katika shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya watu duniani, na afya ya uzazi, UNFP Leila Baker amesema pamoja na shirika hilo kuhitaji fedha ili kuweza kuwahudumia wanawake na wasichana waliathiriwa na matetemeko nchini Turkiye na Syria lakini kila sehemu anapopita nchini Syria wanawake hutoa ombi moja tu nalo ni kuhitaji amani.Katika makala Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR linaendelea na hatua zake za kuhakikisha wakimbizi waliorejea nyumbani wanaishi maisha ya utu na ustawi, ambapo pamoja na kuwapatia wakimbizi hao huduma bora pia linazidi kuomba wahisani waoneshe ukarimu zaidi.Na katika mashinani tutaelekea nchini Tanzani kusikia njia mbadala na fimbo za kuleta nidhamu shuleni. Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
13 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 13, 2023 0:10


Hii leo jaridani tunaangazia siku radio duniani, na wakimbizi wanaorejea nyumbani Burundi. Makala tunakupeleka nchini DR Congo na mashinani tutamsikia Balozi Mwema wa UNHCR.        Katika siku ya redio duniani Umoja wa Mataifa unamulika nafasi ya chombo hicho kilichobuniwa takribani karne moja iliyopita katika kukuza na kujenga amani  wakati huu ambapo pia ni miaka 75 tangu kuanzishwa kwa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa.Nchini Burundi wakimbizi waliokimbia ghasia, wanaendelea kurejea nyumbani kutokana na hali ya amani kuzidi kuimarika, na hivi karibuni zaidi wakimbizi wamerejea kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC wakiwa na matumaini kutokana na kile wanachoshuhudia.Makala mwandishi wetu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Byobe Malenga anaangazia Redio Ngoma ya Amani, kituo cha redio cha mjini Fizi jimboni Kivu Kusini kinachohamasisha amani hususani katika maeneo ya mashariki mwa DRC.Na katika mashinani tutamsikia Balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR akipasa sauti kwa ajili ya wakimbizi na wote walio hatarini kutojumuishwa katika mijadala ya malengo ya maendeleo endelevu. Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Tunataka kuwafikia waathirika wote wa tetemeko la ardhi licha ukosefu wa usalama katika baadhi ya maeneo: WFP Syria

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 10, 2023 0:02


Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanaendelea kupeleka na kusambaza misaada nchini Uturuki au Türkiye na Syria ili kusaidia walioathiriwa na matetemeko makubwa ya ardhi yaliyotokea Jumatatu wiki hii na kujeruhi, kuua maelfu na kuharibu miundombinu. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) lina lengo la kuwafikia watu nusu milioni katika nchi zote mbili ijapokuwa kuna changamoto za kiusalama katika baadhi ya maeneo.Si Jindires, si Allepo, kote ni milio ya magari ya wagonjwa, majengo yameporoka, ni magofu, vilio, buludoza, harakati za uokozi na juhudi za kusambaza misaada zikiendelea.  WFP inasema kufikia mwishoni mwa wiki hii itakuwa imewapa wadau wake chakula cha kutosha wiki nzima kwa watu 125,000. Hali hii ya matetemeko imeikuta WFP tayari ikiwa na mzigo wa kuwahudumia  watu milioni 1.4 kila mwezi Kaskazini Magharibi mwa Syria pekee. Kenny Crossley, ni Mkurugenzi wa WFP nchini Syria, akiwa katika mji mkuu wa Syria, Damascus anasema,  "Siku chache zilizopita, tetemeko la ardhi la kutisha lilitokea hapa nchini Syria na Uturuki. Mamia pengine maelfu ya waliokufa, maelfu kujeruhiwa, makumi, pengine maelfu ya watu waliokimbia makazi yao, kupoteza makazi yao, watu hawawezi kurejea katika maeneo ambayo huwa wanalala, sasa wanalala mitaani wakijibana kwenye vibanda. Kwa WFP bila shaka, kwetu ni muhimu, kwamba watu lazima wale. Saa chache tu baada ya tetemeko la ardhi, tulikuwa tukifanya kazi na wadau wetu wa eneo hilo watu walikuwa wakila chakula cha moto katika makazi ya muda waliyokuwa wakiishi.” Pamoja na juhudi za WFP, shirika hilo la Umoja wa Mataifa linasema matetemeko ya ardhi yamezidisha ugumu uliopo wa kufika Kaskazini Magharibi mwa Syria kutokana na migogoro na hivyo kusababisha uhitaji zaidi kama anavyofafanua Kenny Crosseley, "Moja ya changamoto zetu kubwa kwa sasa sio usafiri, sio chakula, ni ufikiaji wa maeneo. Baadhi ya watu ambao ni vigumu kuwafikia wako katika maeneo ambayo kuna migogoro inayoendelea. Tunahitaji kuwa na uwezo wa kufikia watu ambao wako katika maeneo haya ambayo kuna migogoro inayoendelea." Mjini Aleppo, WFP kwa haraka kupitia majiko ya wadau wake imetoa chakula cha moto kwa watu 4,000 walioathirika katika makazi ya muda. Usaidizi utaendelea hadi kesho tarehe 11 mwezi huu Februari, kulingana na tathmini zinazoendelea za mahitaji. WFP pia kupitia wadau inasambaza milo iliyo tayari kuliwa inayotosha watu 5,000 walioathirika. 

Habari za UN
Kuwa na wanawanake na wasichana wengi katika nyanja ya sayansi ni faida kwa wote: UN

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 10, 2023 0:02


Uwepo wa idadi kubwa ya wanawake na wasichana katika sekta ya sayansi ni faida kuwa kwa sekta ya sayansi na jamii kwa ujumla amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akihimiza kuchagiza wanawake na wasicha kuingia zaidi katika sekta hiyo.Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi ambayo huadhimishwa kila mwaka Februari 11 amesima siku hii ni ya kutanabaisha hesabu rahisi kabisa kwamba “Wanawake na wasichana zaidi katika sayansi ni sawa na sayansi bora. Wanawake na wasichana huleta utofauti katika utafiti, kupanua wigo wa kundi la wataalamu wa sayansi, na kutoa mitazamo mipya kwa sayansi na teknolojia, ikinufaisha kila mtu.”Ujumbe wake umeendelea kueleza kuwa kuna ushahidi unaoongezeka kwamba upendeleo wa kijinsia katika sayansi unasababisha matokeo mabaya zaidi, kuanzia kwenye majaribio ya dawa za ambayo huchukulia mwili wa mwanamke kama wa hali isiyo ya kawaida, kutafuta kanuni zinazoendeleza upendeleo na ubaguzi. Hata hivyo Guterres ameongeza kuwa katika maeneo mengi sana duniani, upatikanaji wa elimu kwa wanawake na wasichana ni mdogo au unakataliwa kabisa.Wanawake wanapotazamia maendeleo katika taaluma za kisayansi, ukosefu wa usawa na ubaguzi unaendelea kuzuia uwezo wao. Kana kwamba hiyo haitoshi ameongeza kuwa “Wanawake ni chini ya theluthi moja ya wafanyikazi katika sekta ya sayansi, teknolojia, uhandisi, na hesabu na kidogo zaidi katika nyanja za kisasa. Mtaalamu mmoja tu kati ya watano wanaofanya kazi kwenye akili bandia ni mwanamke. Ni lazima na tunaweza kufanya juhudi zaidi kuchagiza wanasayansi wanawake na wasichana kupitia ufadhili, mafunzo kwa vitendo na program za mafunzo ambazo zinatoa jukwaa la kufanikiwa.” Katibu Mkuu amehitimisha ujumbe wake akisema kupitia mfumo maalum, vivutio vya kuwafanya wabaki, na programu za ushauri ambazo huwasaidia wanawake kushinda vikwazo vilivyopo na kujenga taaluma vitasaidia sana. Na muhimu zaidi, ameongeza ni kwa kuzsisitiza haki za wanawake na kuvunja mila potofu, upendeleo, na vizuizi vya kimuundo. Na wito wake ni kwamba “Sote tunaweza kufanya sehemu yetu kuibua talanta kubwa sana ya ulimwengu ambayo haijatumiwa tukianza na kujaza madarasa, maabara na vyumba vya bodi na wanasayansi wanawake.” 

Habari za UN
Msemo: KUFANYA AJIZI

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 9, 2023 0:01


Katika jifunze Kiswahili hii leo mtaalam wetu  Onni Sigalla Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKIZA nchini Tanzania, anatufafanulia maana ya msemo "KUFANYA AJIZI", karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Hoja ya the Voice yamwondoa Seneta Lidia Thorpe katika chama cha Greens

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Feb 9, 2023 8:10


Seneta maarufu wa chama cha Greens amejiuzulu kutoka chama chake, kwa ajili yakufuatilia uhuru wa weusi.

Habari za UN
Hatupati msaada wa kutosha, anasema Mratibu wa Misaada wa UN nchini Syria

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 8, 2023 0:02


Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mratibu wa muda wa Misaada ya Kibinadamu nchini Syria El- Mostafa Benlamlih amesema ingawa mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau wengine wa misaada wanafanya kila juhudi kusaidia wananchi walioathiriwa na matetemeko ya ardhi lakini hali ni mbaya kwani hawapati msaada ya kutosha.Katika mahojiano maalum aliyofanya na Idhaa ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani El- Mostafa akiwa nchini Syria ameeleza mpaka sasa ingawa wanafahamu athari ni kubwa lakini bado hakuna ripoti kamili ya makadirio ya waathiriwa wa matetemeko ya ardhi hata hivyo kuna timu zinazofanya tathmini katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo ikiwemo Halab na Aleppo, “Majengo mengi yameanguka, watu wakiongea wanataja namba kubwa, lakini ni takriban majengo 40 yameanguka na mengine yamepiga nyufa hivyo yanaweza kuanguka muda wowote.  Kwahiyo nadhani hii inaweza kukuonesha athari.”Na je nini mashirika ya Umoja wa Mataifa yanafanya kusaidia wananchi walioathiriwa na matetemeko? “Sawa. Sote tunajaribu kuratibu na kuhakikisha kuwa tunafanya jambo sahihi na ili kuepuka kurudia kile mwingine anafanya. WHO wanaleta ndege mbili za misaada ya matibabu kutoka katika maghala yake yaliyoko Dubai ili kushughulikia mahitaji ya haraka.  WFP wanatoa chakula, tena kile kilicho tayari kuliwa na tena kwakutumia majiko yake wanatoa chakula chamoto kwa maelfu ya watu hasa wale wanaosaka hifadhi katika makazi ya muda na shule, nadhani tuna kama shule 70 au 80 ambazo zinatumika kama makazi ya muda ya watu wenye uhitaji na tunajitahidi kuwapa msaada wowote ule tunaoweza. UNFPA nao wanasaida hapo na kutoa misaada ya utu kwa watoto. UNICEF wanafanya tathmini pamoja na kuleta umakini kwenye mahitaji ya watoto. Pia shirika la kusaidia wakimbizi UNHCR nao wanatoa yale yanayohitajika ikiwemo kuweka makazi na vifaa vinavyohitajikana na watu.”Hata hivyo mratibu huyo wa misaada wa UN amesema changamoto kubwa yanayokabiliana nayo hivi sasa ni mafuta ya petroli ili kuweza kufikisha misaada mahali inapohitajika kwani Syria hivi sasa inakabiliwa na uhaba wa mafuta hata hivyo kwa ushirikiano wa mashirika ya UN wanatumia mafuta waliyonayo hususan ya WFP kusambaza misaada.Mratibu huyo alihitimisha mahojiano yake akieleza kuwa wasiwasi mkubwa hivi sasa ni kupata misaada ya kutosha kuweza kuwasaidia wananchi, “Ujumbe wa mwisho ni kwamba tunahitaji msaada kutoka kwa kila mtu. Hatupati msaada wa kutosha. Tunafanya kila tuwezalo kufika katika maeneo yanayohitaji usaidizi wetu, na tunahitaji usaidizi wa kila mtu. Na hilo ni jambo ambalo ni la haraka sana. Hatuwezi kusubiri hadi iwe tumechelewa sana.”

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية
Faraja katika Muziki, Baraka

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية

Play Episode Listen Later Feb 4, 2023 29:00


Mahojiano na kwaya ya Mwisenge, Baraka yageuka kuwa laana

Habari za UN
ECW: Watoto milioni 222 walio katika maeneo yaliyoathirika na migogoro wanahitaji msaada wa haraka wa elimu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 3, 2023 0:03


Habari za UN
MSEMO - Sikio halilali njaa

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 2, 2023 0:01


Na leo Katika jifunze Kiswahili tuko Baraza la Kiswahili la ZANZIBAR nchini Tanzania ambapo hii leo Dkt. Mwanahija Ally Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, BAKIZA anafafanua msemo “sikio halilali njaa.”  

Habari za UN
02 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 2, 2023 0:12


Hii leo katika Jarida tunakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa Kina na Jifunze lugha ya Kiswahili.Katika Habari kwa Ufupi Leah Mushi anamulika ziara ya Papa Francis nchini DR Congo na wito wake kwa vijana na viongozi wa dini kukataa rushwa. Halikadhalika anamulika maeneo oevu na umuhimu wake bila kusahau nchini Sudan Kusini ambako Umoja wa Mataifa unaendelea kutoa misaada kwa familia zilizokimbia kutoka katika eneo la Pibor.Mada kwa Kina inamulika mmea aina ya Azolla, hili ni gugu maji na ni kwa vipi nchini Tanzania limeanza kuchangamkiwa na vijana katika kujiongezea kipato.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ni msemo ya kwamba sikio halilali njaa.Karibu na mwenyeji wako ni Anold Kayanda.

Habari za UN
Maambukizi ya ukimwi kwa watoto kutokomezwa: Viongozi wa Afrika /UNAIDS

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 1, 2023 0:01


Mawaziri wa afya na wawakilishi kutoka nchi 12 za Afrika na wadau wa kimataifa leo wameahidi na kuweka mipango ya kutokomeza ukimwi miongoni mwa watoto ifikapo mwaka 2030,  limesema shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na kutokomeza VVU na ukimwi UNAIDS.Ahadi hiyo imetolea jijini Dar es salaam Tanzania wakati wa uzinduzi wa “Muungano wa kimataifa kutokomeza ukimwi kwa wtoto Afrika” muungano ambao utafanyakazi kwa miaka 8 hadi mwaka 2030 ukilenga kushughulikia moja ya changamoto kubwa katika vita dhidi ya ukimwi. Taarifa ya UNAIDS inasema wakati robo tatu ya watu wazima wanaoishi na virusi vya ukimwi VVU wako katika matibabu au asilimia 76% , Watoto ni nusu tu sawa na asilimia 52% ndio wanaopata matibabu ya dawa za kurefusha maisha na kupunguza makali ya ukimwi.  Na kwa mujibu wa takwimu za shirika hilo mwaka 2021 jumla ya watoto 160,000 walipata maambukizi mapya ya VVU na watoto ni asilimia 15% ya vifo vyote vitokanavyo na ukimwi licha ya kwamba wao ni asilimia 4% pekee ya watu wote wanaoishi na VVU.  Kwani hivi sasa kote duniani mtoto hufa kila baada ya dakika 5 kutokana na sababu zinazohusiana na ukimwi. Muungano huo mpya “ni wa kutetea na kuhamasisha dhamira ya kisiasa na rasilimali ili kuhakikisha hatua na uwajibikaji kuhusu malengo na ahadi za pamoja.” Katika awamu hii ya kwanza nchi 12 zimejiunga na muungano huo ambazo ni  Angola, Cameroon, Côte d'Ivoire, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Kenya, Msumbiji, Nigeria, Afrika Kusini, Tanzania, Uganda, Zambia,na Zimbabwe.  Tanzania ambayo ni mwenyeji wa mkutano wa uzinduzi wa muungano huo uliofanyika jijini Dar es salaam imekuwa ya kwanza kujisajili.  

Habari za UN
01 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 1, 2023 0:10


Hii leo jaridani tunaangazia mshikamano wa viongozi barani Africa kutokomeza ukimwi, na kazi ya walinda amani nchini CAR. Makala tunakupeleka nchini Sudan Kusini na mashinani nchini Rwanda, kulikoni?      Mawaziri wa afya na wawakilishi kutoka nchi 12 za Afrika na wadau wa kimataifa leo wameahidi na kuweka mipango ya kutokomeza ukimwi miongoni mwa Watoto ifikapo mwaka 2030 limesema shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na kutokomeza VVU na ukimwi UNAIDS.Viongozi wa eneo la utawala la Mambéré-Kadéï nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR wamewashukuru viongozi wa walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MINUSCA katika eneo hilo la Berbérati kwa kutambua kuwa ulinzi wa amani unategemea ushirikiano wa wageni na wenyeji.Makala tunakupeleka nchini Sudan kusini ambapo Mpango wa Amani unaoungwa mkono na  Ujumbe wa Umoja wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo UNMISS umezaa matunda na sasa wakimbizi wa ndani waliokuwa katika eneo la Tambura jimboni Equatoria Magharibi wameanza kurejea katika vijiji vyao kutokana na kuwepo kwa amani na utulivu katika eneo hilo..Katika mashinani tunampisha Floribert, mkimbizi kutoka Burundi aliyeko nchini Rwanda ambaye baada ya kutafuta kazi ya ualimu kwa muda mrefu na kukosa ajira alijiunga katika mafunzo ya upishi yanayowezeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR kwa ushirikiano na kampuni ya Vatel Hospitality and Catering katika mgahawa wa Nyruah mjini Kigali, na leo akiwa na umri wa miaka 38, Floribert hatimaye anahisi ana nafasi ya kufanikiwa. Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
31 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 31, 2023 0:11


Hii leo jaridani tuakuletea mada kwa kina na tunakwenda nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kumulika kampeni ya chanjo iliyomalizika jana Jumanne.  Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za afya, haki za binadamu na wakimbizi. Katika mashinani tutakupeleka Geneva nchini Uswisi kupata ujumbe wa shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na UKIMWI, UNAIDS kuhusu kizazi cha watato ulimwenguni ambao wako hatarini kusahaulika.      Wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa wametaka kufanyika mara moja kwa uchunguzi huru nchini Mali kwa kile walichoeleza kuwa ni kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu pamoja na uwezekano wa uhalifu wa kivita unaosadikiwa kufanywa na vikosi vya serikali kwa kushirikiana na kundi binafsi la wanajeshi la Wagner group.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limezindua Baraza la vijana lililofanyika kwa siku nne jijini Geneva Uswisi na kuwaleta pamoja viongozi vijana kutoka mashirika 22 ya vijana duniani yanayojishughulisha na masuala ya afya na masuala yasiyo ya afya lengo likiwa ni kuwasikiliza vijana, kupata utaalamu na uzoefu wao katika masuala ya afya kwa umma pamoja na kufanya nao kazi katika kutengeneza harakati za vijana katika afya.Na shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM limesema kumekuwa na ongezeko kubwa la wakimbizi wa Rohingya wanaowasili Kusini Mashariki mwa Asia kwa njia ya bahari na njia za barabara. IOM imese mwaka 2022 imerrkodi kuwasili kwa watu 3300 nchini Malaysia, Indonesia na Thailand hili likiwa ni takriban ongezeko la asilimia 290 ikilinganishwa na watu 850 waliowasili mwaka 2021.Katika mashinani tutakupeleka Geneva nchini Uswisi kupata ujumbe wa Charlotte Sector, Msemaji wa Mpango wa Pamoja wa Umoja wa Mataifa kuhusu VVU / UKIMWI (UNAIDS) akisisitiza umuhimu nchi za Afrika kuzindua "Muungano wa kimataifa wa Kutokomeza Ukimwi kwa Watoto" katika kanda huo  ili kuzuia maambukizi mapya ya VVU miongoni mwa watoto wachanga Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu !

Habari za UN
Mada kwa kina: Chanjo dhidi ya Kipindupindu yaendelea Kivu Kaskazini, DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 31, 2023 0:05


Kampeni ya utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu  iliyoanza tarehe 25 mwezi huu huko Kivu Kaskazini nchini jamhuri ya Kidemokraia ya Congo, DRC imekunja jamvi jana Jumanne ya tarehe 30 mwezi hu uwa Januari ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO lilizindua kampeni hiyo ya chanjo kwa wakimbizi wa ndani katika kambi ya wakimbizi hao ya Kanyaruchinya wilayani nyiragongo katika mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini.Mwandishi wetu wa DRC Byobe Malenga ambaye ameshuhudia uzinduzi huo amesema uliongozwa na Gavana wa jimbo la Kivu Kaskazini Jenerali Ndima Constant, na Mwakilishi wa shirika WHO nchini DRC kwa lengo la kuokoa mamia ya familia hususan za wakimbizi wa ndani ambao tayari makumi kwa makumi wameripotiwa kupata ugonjwa huo na wengine wamefariki dunia.Jean Bruno, ni Mkuu wa Ofisi ya WHO Kivu Kaskazini na anasema ameridhishwa na shauku ya siku ya kwanza na zaidi ya yote amesema,« Tumewalenga watu 364,127 ambao ni wakimbizi wa ndani, pamoja na familia zinazowapokea. Tayari tumepokea dozi 364,150 ambazo zipo na zitatumika. chanjo itafanyika kwa awamu ya dozi moja na tutafanya hivyo kupitia kampeni ya nyumba kwa nyumba kwenye maeneo haya . Tumeridhika na ukweli ni kwamba kumekuwa na dhamira muhimu kwa upande wa serikali kwenye ngazi ya taifa na mkoa, lakini pia tumekuwa na hakikisho kutoka kwa jamii ya watu na wakimbizi wa ndani ambayo imekubali chanjo hiyo ambayo itafanyika kwa wakati».Eneo la Nyiragongo lilipokea idadi kubwa ya watu waliokimbia makazi yao kutokana na mashambulizi yanayofanywa na waaasi wa M23 huku watu 233 elfu waliokimbia makazi yao, zaidi ya 95% yao wamelundikana kwenye makanisa, shule, viwanja vya michezo na maeneo yasio salama kwa afya yao.Gavana wa Kivu Kaskazini, Jenerali Ndima Constant, anakiri kwamba janga la kipindupindu linaathiri sana eneo la Nyiragongo akisema kwamba hadi Jumanne ya Januari 24  wagonjwa 3706 wa kipindupindu walisajiliwa huku kukiwa na vifo 16 na ili kupunguza mlolongo wa maambukizi amewasihi raia kupata chanjo akishukuru WHO kwa msaada wao.« Madhumuni ya kampeni hii  ya chanjo ni kulinda idadi ya watu dhidi ya kipindupindu katika jimbo la Kivu Kaskazini na hasa katika maeneo ya watu waliofurushwa ili kupunguza vifo. Mabibi na mabwana, wageni mashuhuri, ili kufunga maoni yangu, ningependa kuwakumbusha kuwa pamoja na chanjo utakayopokea, kufuata hatua za kuzuia maambukizi ni muhimu..”Ametaja njia za kujikunga kuwa ni pamoja na kunawa mikono mara kwa mara kwa maji safi na sabuni au majivu, kunywa maji yaliyotakasishwa tu au yaliyochemshwa. Kupika na kufunika milo yetu, matumizi sahihi ya vyoo huku tukiwa wasafi na kuweka usafi kwenye maeneo yetu ya makazi  kila wakati.Waliokimbia makazi yao wanafahamu tishio hilo kwa sababu janga hilo limeathiri zaidi ya 89% ya waliokimbia makazi katika miezi ya hivi karibuni na chanjo inatekelezwa nyumba kwa nyumba.Watu waliohamishwa wanasubiri dozi zao nyumbani. Damaseni Butera ni miongoni mwa watu wa kwanza kupata dozi moja dhidi ya kipindupindu na anashukuru mpango huu wa WHO na anasema, «chanjo ni muhimu sana katika mapambano dhidi ya magonjwa kama kipindupindu, malaria na mengine.Tumejifunza habari kuhusu chanjo hiyo, tumefurahi sana kwa sababu tutakuwa na kinga, asante sana kwa shirika la WHO ambalo lilitufikiria. Asante sana»Kando na hilo, Mweze Shemba, aliyekimbia kutoka kijiji cha Kiwanja, pia alinufaika na chanjo hii. Licha ya njaa,yeye anapendelea kujilinda pamoja na familia yake dhidi ya janga hili akisema, «kilichonifanya nipate chanjo ya leo hapa katika kambi ya wakimbizi ni kwa sababu tunapatwa na magonjwa ya taabu. kama vile kuharana kutapika hasa tunapokunywa maji machafu. Lakini wakati tunapata hii chanjo tunaona kama vile ni kinga kwetu tunashukuru sana »Katika juhudi za kuepusha msongamano wa wagonjwa wa janga hili , WHO ilijenga vitalu 3 kama kitengo cha matibabu ya wagonjwa wa Kipindupindu (UTC) katika eneo la Bushagara na…

congo kina drc goma asante umoja m23 katika kivu watu nyiragongo tayari lakini mataifa medair mwandishi kampeni
Habari za UN
30 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 30, 2023 0:12


Hii leo jaridani tuakuletea habari njema kuhusu afya na pia kuangazia jamii ya Benet nchini Uganda wakiwa bado hawana utaifa. Makala tunakwenda nchini Kenya na mashinani tunasalia huko huko Kenya, kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO, limesema mataifa mengi zaidi duniani yametokomeza magonywa ya kitropiki yaliyosahaulika, au NTDs huku ikisema bado uwekezaji zaidi unahitajika kusongesha maendeleo hayo dhidi ya magonjwa hayo kama vile ukoma, vikope na kung'atwa na nyoka.Baada ya zaidi ya takriban miongo minane ya kutokuwa na utaifa, jamii ya watu wa asili ya Benet nchini Uganda inahaha kuishi, na kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR bila kuwa na nyaraka rasmi muhimu jamii hiyo haiwezi kupata huduma za msingi kama elimu na afya , na sasa jamii hiyo inaiomba serikali ya Uganda kumaliza zahma hiyo iliyowaghubika kwa miongo.Makala tunakupeleka Kenya ambako huko mwandishi wetu Thelma Mwadzaya anamulika faida ya kuwa na kiwanda cha kutengeneza chakula lishe au tiba lishe kwa ajli ya watoto wenye utapiamlo uliokithiri.Katika mashinani tutasalia huko huko nchini Kenya kusikia ni jinsi gani wakimbizi wa Dadaab na wenyeji wameendelea kusihi pamoja kwa amani.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
27 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 27, 2023 0:11


Hii leo jaridani tuakuletea ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kuhusu makumbusho ya Holocaust, pia tunamulika kazi ya walinda amani nchini DR Congo. Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani tunasalia hapa makao makuu wa Umoja wa Mataifa.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kumbukizi ya waathitrika wa mauaji ya maangamizi makubwa au Holocaust dhidi ya wayahudi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mauaji hayo yalikuwa ni malimbikizo ya miongo ya chuki dhidi ya Wayahudi ndio maana sasa ni wakati wa kuhakikisha chuki za aina yoyote ile zinakomeshwa duniani.Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini.Makala tunakwenda nchini Tanzania kusikia ni kwa vipi Mahakama inachagiza moja ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs na shuhuda wetu ni Hamad Rashid wa Redio washirika MVIWATA FM mkoani Morogoro, Mashariki mwa Tanzania.Katika mashinani leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kukumbuka waathirika na waliokufa kutokana na mauaji ya maangamizi dhidi ya wayahudi yaliyofanywa na manazi nakuletea ujumbe wa nini kifanyike kuepusha hali hiyo na ujumbe unatolewa na Dani Dayan, Mwenyekiti wa jumba la makumbusho ya mauaji ya maangamizi ya wayahudi huko Israel, liitwalo Yad Vashem. Ujumbe huu ameutoa wakati wa uzinduzi wa maonesho ya kitabu chenye majina ya wayahudi waliouawa na manaziMwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Tuepushe mlolongo wa chuki unaoweza kusababisha maangamizi ya binadamu- UN

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 27, 2023 0:02


Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kumbukizi ya waathitrika wa mauaji ya maangamizi makubwa au Holocaust Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema mauaji hayo yalikuwa ni malimbikizo ya miongo ya chuki dhidi ya wayahudi ndio maana sasa ni wakati wa kuhakikisha chuki za aina yoyote ile zinakomeshwa duniani.Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu Antonio Guterres amesema ni siku ya kuwaenzi na kuwakumbuka wayahudi milioni 6 watoto, wanawake na wanaume lakini pia , waroma na wasinti , watu wenye ulemavu na wengine wasio hesabila ambao walipoteza maisha katika ukatili huo. Hivyo ameongeza kuwa, “tunatafakari maisha ya mamilioni ya watu yaliyokatizwa, mamilioni ya mustkbali wa watu ulioibwa. Tunapoomboleza kupotea kwa watu wengi na mambo mengi, tunatambua pia kwamba mauaji ya maangamizi hayakuwa yasiyoyakuepukika kama ilivyokuwa mauaji ya kimbari.Ilikuwa ni kilele cha miongo ya chuki dhidi ya Wayahudi” Ujumbe huo wa Bwana Guterres umeendelea kueleza kwamba manazi waliweza tu kusonga mbele na ukatili huo uliopangwa kutoka na ubaguzi wa wayahudi uliokuwa Ulaya hadi kuangamizwa kwao kwa sababu wachache sana walisimama kupinga na wengi waliangalia tu. “Ilikuwa ni ukimya wa uziwi wa ndani na nje ya nchi  uliowatia moyo amesema kwani kengele za hatari zilikuwa zikilia tangu mwanzo, mmatamshi ya chuki na habari potofu.” Na zaidi ya hayo ameongeza ni “kudharau haki za binadamu na utawala wa sheria. Kushabikia machafuko na hadithi za kutukuza rangi pia kudharau demokrasia na utofauti. Tunapokumbuka mauaji ya Holocaust tunatambua vitisho dhidi ya uhuru, utu na ubinadamu ikiwemo katika wakati wetu.” Amesema katika wakati huu ambao dunia inakabiliwa na changamoto zinazoongezeka za kiuchumi , na kisiasa, kuendelea kutukuza ugaidi wa walio weupe na kuongezeka kwa chuki na ubaguzi wa kidini ni lazima kuwa wawazi zaidi kuliko wakati mwingine wowote. “Hatupaswi kamwe kusahau wala kuruhusu wengine kusahau, kupotosha au kukataa mauaji ya Holocaust. Leo na kila siku, tuazimie kutonyamaza tena wakati wa uovu na kutetea daima utu na haki za wote.” 

holocaust umoja katika chuki mataifa ikiwa
Habari za UN
26 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 26, 2023 0:12


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo leo tunakwenda nchini Kenya kuangazia juhudi za mradi wa Teen Seed Africa unavyorejesha matumaini ya elimu kwa wasichana walioacha shule kutokana na mimba za mapema.  Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo kutoka nchini DR Congo, Ethiopia na Senegal. Katika kujifunza Kiswahili   ambapo utapata ufafanusi wa msemo "TABIA NI NGOZI."Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO umesema wataalamu wake wa kutegua mabomu na wale wa ofisi ya Umoja huo ya kudhibiti mabomu ya kutegwa ardhini, UNMAS wamefika katika mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini hususan kitongoji cha Macampagne ambako jana Jumatano bomu la kutengenezwa lililipuka kwenye soko na kujeruhi watu 17.Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za binadamu, imesema Kamisheni ya Kimatiafa kuhusu haki za binadamu nchini Ethiopia imetambua chapisho la serikali la rasimu ya kwanza ya kisera kuhusu haki kwenya kipindi cha mpito.Na Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani, ILO Gilbert F. Houngbo yuko ziarani nchini Senegal,  ikiwa ni ziara yake ya kwanza kufanywa na kiongozi wa shirika hilo nchini humo na anatumia fursa ya ziara yake hiyo ya siku 4 kujadili na mamlaka na vyama vya wafanyakazi mwelekeo wa ajira katika dunia ya sasa hususan ajira yenye hadhi kwa vijana na wanawake, ulinzi wa wafanyakazi wahamiaji na urasimishaji wa uchumi usio rasmi.Leo katika kujifunza Kiswahili mtaalam wetu  Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, BAKIZA nchini Tanzania anafafanua maana ya msemo "TABIA NI NGOZI."Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
25 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 25, 2023 0:11


Hii Leo jaridani tunaangazia mkutano nchini Niger kuhusu kanda ya Ziwa Chad, na habari njema kwa wakulima wa vitunguu nchini Sierra Leone. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Uganda, kulikoni?Mkutano wa 3 wa Ngazi ya Juu kuhusu Kanda ya Ziwa Chad umehitimishwa leo kwa kuthibitishwa ahadi kutoka kwa nchi za Bonde la Ziwa Chad na wadau kwa mwitikio ulioratibiwa, wa kikanda na ulio endelevu.Vitunguu kuoza na kukosekana kwa kipato ulikuwa ni uhalisia kwa wakulima wa vitunguu kwenye mji wa Kabala nchini Sierra Leone wakati janga la COVID-19 lilipoibuka mapema mwaka 2020. Hali ilikuwa tete lakini kilio cha wakulima hao kilisikika na mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo, IFAD ukaingilia kati. Nini kilifaniyika? Assumpta Massoi anafafanua kwenye ripoti hii iliyoandaliwa na IFAD.Katika makala nakuunganisha na Thelma Mwadzaya mwandishi wetu wa Nairobi Kenya akimulika harakati za Shirika la Umoja wa mataifa la Afya duniani, WHO kwa ushirikiano na serikali ya Kenya za kusambaza chakula tiba cha dharura cha msaada mahsusi kwa watoto walio na utapia mlo sugu.Na katika mashinani tunakwenda nchini Uganda kukutanana msichana muelimishaji rika ambapo anatumia nyimbo kuelezea wajibu wa wazazi na walezi wote kuachana na ndoa za utotoni kwa watoto wao wa kike na badala yake wapatiwe fursa ya masomo.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda karibu!

Habari za UN
Usalama unawezarejeshwa katika sehemu za kanda ya Ziwa Chad - Niamey

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 25, 2023 0:01


Mkutano wa 3 wa Ngazi ya Juu kuhusu Kanda ya Ziwa Chad umehitimishwa leo kwa kuthibitishwa ahadi kutoka kwa nchi za Bonde la Ziwa Chad na wadau kwa mwitikio ulioratibiwa, wa kikanda na ulio endelevu.Mkutano huo uliohitimishwa leo katika mji mkuu wa Niger, Neamey, ulilenga kuhakikisha usaidizi wa kibinadamu na ulinzi na kukuza fursa za ufumbuzi wa kudumu, ikiwa ni pamoja na kurejea, kuunganishwa tena katika jamii na kuwapa makazi wakimbizi wa ndani na wakimbizi kutoka nje kwa kuzingatia uamuzi wa wa hiari, wenye heshima na ufahamu kuhusu uamuzi huo.  Mkutano huo wa siku mbili umeleta pamoja zaidi ya nchi 30, mashirika ya kimataifa na zaidi ya mashirika 100 ya kiraia ambapo wamekubaliana kufanya kazi pamoja kutatua changamoto zilizopo. Washiriki wametambua kuwa usalama unarejeshwa katika sehemu za kanda hiyo ya Ziwa Chad, kutokana na juhudi za nchi hizo nne - Niger, Nigeria, Cameroon na Chad. Hata hivyo mkutano huo umekumbushia hitaji muhimu la kushughulikia mahitaji ya kibinadamu yanayoongezeka, sababu za msingi za chanzo cha mgogoro wa Bonde la Ziwa Chad na kuimarisha mnepo wa mamilioni ya watu walioathirika. Eneo la Bonde la Ziwa Chad linaendelea kukabiliana na mgogoro wa muda mrefu na tata unaotokana na umaskini uliokithiri, mabadiliko ya tabianchi, migogoro ya vurugu na ukosefu wa huduma za kijamii, licha ya mafanikio mengi. Taarifa ya shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA inaeleza kuwa leo, zaidi ya watu milioni 24 katika eneo hilo la Bonde la Ziwa Chad wameathiriwa na mgogoro huo na takriban watu milioni 5.3 wamelazimika kuyahama makazi yao. Mwisho Nchi Wanachama na wafadhili wa kitaasisi wametangaza zaidi ya dola milioni 500 za kimarekani kusaidia hatu za kikanda zilizoratibiwa za kushughulikia mgogoro katika kanda ya Ziwa Chad.  

Habari za UN
24 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 24, 2023 0:13


Ni Jumanne ya tarehe 24 mwezi Januari mwaka 2023 ambapo leo tunakwenda nchini Tanzania kuangalia juhudi zinavyofanyika kuhakikisha wanafunzi hususan wa vijijini wanakuwa na mazingira bora ya kuweza kujisomea  nyakati zote. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikimulika hali ya usalama DR Congo, ujumbe wa Katibu Mkuu ya siku hii ya elimu duniani na ripoti ya usafirishaji haramu wa binadamu. Katika mashinani tunakupeleka nchini Kenya.Hali ya usalama inazidi kuwa mbaya huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususa jimboni Ituri ambako vikundi vilivyojihami vimeendelea kuua rai ana katika wiki sita zilizopita zaidi ya raia 200 wameuawa, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi duniani, UNHCR.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya elimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza kwamba elimu ni haki ya msingi ya binadamu na hivyo kila mtu anastahili kuipata. Kupitia ujumbe wake wa siku hii inayoadhimishwa kila mwaka Januari 24 Antonio Guterres amesema “Ni msingi wa jamii, uchumi, na uwezo wa kila mtu. Lakini bila uwekezaji wa kutosha, uwezo huu utaishia kwenye mzabibu".Na ripoti mpya iliyotolewa leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu UNDOC kuhusu usafirishaji haramu wa binadamu inaelezea hofu kwamba rasilimali za kuwaokoa waathirika wa usafirishaji haramu zimeelekezwa kwenye janga la COVID-19.Na leo katika mashinani tutakwenda Turkana nchini Kenya kumsikia Gabriel Ekaale, ambaye alianza kazi yake kama mwalimu wa shule ya upili nchini Kenya, lakini baada ya muda mfupi aligundua kwamba kazi yake inaweza kuwa na manufaa kwa jamii nzima, na sasa anafanya kazi na jamii zilizoathiriwa na ukame.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

covid-19 kenya congo tanzania drc unhcr antonio guterres umoja katika turkana ituri lakini mataifa jamhuri elimu north kivu mashariki kidemokrasia ikiwa
Habari za UN
WFP na serikali ya Madagascar zaungana mikono kubadilisha jamii za vijijini kusini mwa Madagascar kupitia mradi wa RTT

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 23, 2023 0:02


kupitia mradi wa mabadiliko ya haraka vijijini (RRT) shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP na wadau wake wameanzisha kituo maalum cha paneli za sola ambacho ni chanzo kikuu na endelevu cha maji na teknolojia ya mawasiliano ICT katika maeneo ya vijijini nchini Madagascar, hatua inayoruhusu upatikanaji wa huduma muhimu kama vile nishati, maji na mitandao ya kijamii kwa wakazi wa jamii hizo na kwa njia inayojali mazingira.Katika video ya WFP iliyopigwa na drone kutoka angani katika mkoa wa Anosy Kusini mwa Madagaska mtambo mkubwa wa paneli za sola uliojengwa na WFP na wadau unaonekana mtambo ambao ni muhimu sana kwa wana jamii wa eneo hili kwani unawasaidia kwa huduma mbalimbali ikiwemo kilimo cha umwagiliaji kwenye mashamba kwa ajili ya uzalishaji wa chakula. Pia mtambo huo ni chanzo kikuu cha kusukuma maji ambayo ni huduma ya msingi na ya lazima kwa wakaazi hawa. Ujumbe wa WFP ukiongozwa na naibu mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo Manoj Juneja umefunga safari kutoka Malagasy mji mkuu wa Madagascar hadi Anosy kushuhudia jinsi mradi huo unavyofanyakazi na kuwasaidia wananchi. Juneja anasema, “Paneli hizi za sola za mradi wa mabadiliko ya haraka vijijini zitaruhusu jamii kupata huduma ya msingi ya nishati inayojali mazingira. Na nishati hiyo inaweza kubadilishwa kwa pampu za maji, tunaweza kuchimba maji y ardhini ambayo yanaweza kutumika kunywa na kumwagilia na pia kuna fursa nyingine nyingi zinazoweza kupatikana kama ualishaji wa kilimo kupitia mafunzo, mitambo iliyopo inaweza kuruhusu pia upatikanaji wa elimu, mlo shuleni uliozalishwa hapa na mengine mengi ambayo bado hatujayafikiria”  Mradi huu unaoendeshwa na mamlaka ya mkoa unawaruhusu wadau mbalimbali kuutumia ikiwemo kuweka vituo vya mafunzo kwa ajili ya wanawake na vijana ya uzalishaji wa chakula na stadi za biashara lakini pia madarasa ya kidijitali.Madagascar ni miongoni mwa nchi 10 zilizo katika hatari kubwa ya majanga duniani na ni moja ya nchi zilizohatarini zaidi kwa vimbunga barani Afrika na mradi huu unaisaidia Anosy kujikinga na baadhi ya majanga hayo kwani takriban watu milioni 2.2 Kusini na Kusini Mashariki mwa Madagascar wanakabiliwa na kiwango cha juu cha kutokuwa na uhakika wa chakula. 

Habari za UN
Kampeni ya utoaji chanjo ya homa ya mafua makali yaendelea ukanda wa ulaya: WHO

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 20, 2023 0:02


Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya ulaya tangu kuanza kwa msimu wa baridi kali katikati ya mwezi Novemba mwaka 2022 wamebaini kuongezeka kwa wagonjwa wanaolazwa kutokana na magonjwa ya homa ya mafua makali au flu,  matatizo ya kupumua na COVID-19. Walio hatarini zaidi kupata maambukizi ya magonjwa hayo ni wahudumu wa afya pamoja na wazee, ndio maana wanaendesha kampeni ya kutoa chanjo. Katika msimu wa baridi mwaka uliopita WHO ukanda wa Ulaya ilifanikiwa kutoa chanjo ya homa ya mafua makali kwa asilimia 65 ya kundi la watu walio hatarini ambao wengi ni wazee na wahudumu wa afya na msimu huu wa baridi lengo ni kuwafikia asilimia 75 ya watu hao. Afisa wa kiufundi wa WHO Kyrgyzstan Kasymbekova Kaliya, anasema wanafahamu namna ugonjwa wa guo ulivyo hatari.…. “tunajua kwamba ugonjwa huu wa homa ya mafua makali unaweza kusababisha matatizo makubwa hasa kwa wazee wenye umri zaidi ya miaka 65, wale ambao wana magonjwa sugu ya moyo, mapafu, kisukari, na wenye hali ya uzio”. Chanjo imeanza kutolewa kwa makundi yaliyo hatarini kuathirika zaidi ya homa ya mafua makali kama anavyoeleza Baktygul Mamatova, mtaalamu wa Kinga katika kituo cha afya cha Bishkek, “Sisi, wahudumu wa afya, kama kundi lililo hatarini ndio tumekuwa wa kwanza kupata chanjo. Siwezi sema kwamba siwezi kupata magonjwa, napata, lakini kwa kuwa nimepata chanjo ni rahisi kuhimili.” Wazee wanfahamu umuhimu wa kupata chanjo kama anavyoeleza Kanai Alamanov, aliyefika katika  kituo cha afya cha Bishkek, “Hapo awali, kulikuwa na uhamasishaji wa kupata chanjo dhidi ya virusi vya CORONA nami nilikuja kupata chanjo hiyo ya COVID-19, na sasa ni chanjo ya homa ya mafua makali. Chanjo hii inatupa fursa ya kujikinga na magonjwa, inatupa aina fulani ya hakikisho la maisha yenye afya.” Chanjo hazitolewi kwa wale wanaoenda hospitali pekee, wanaoishi katika nyumba maalum za kutunza wazee nao hufuatwa na kupewa chanjo kama anavyothibitisha Ludmila Kinda Ivanovna, “Mimi ninaugua sana. Mwili wangu haukubali kabisa kutumia aina nyingi ya dawa ikiwemo zile za viua vijasumu, nina pumu , nina matatizo ya moyo, nilishapata mstuko wa moyo mara mbili. Kiufupi mwili wangu ni dhaifi sana hivyo chanjo ina maana kubwa sana kwangu.”  

Habari za UN
Misaada wawasili kwa mara ya kwanza katika eneo la Donetsk Oblast Ukraine: OCHA

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 20, 2023 0:01


Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA limesema kwa mara ya kwanza misaada ya mashirika ya Umoja wa Mataifa imefanikiwa kuwasili katika eno linalodhibitiwa na serikali karibu na Soledar Mashariki mwa Donetsk Oblast nchini Ukraine.Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo mjini Geneva Uswis na OCHA msaada huo wa kibinadamu uliosheheni kwenye malori matatu ni kwa ajili ya kuwasaidia zaidi ya watu 800 ambao walisalia katika jamii zinazozunguka eneo laSoledar. “Msaada huo unaojumuisha chakula, maji, vifaa vya usafi na kujisafi, madawa na vifaa tiba vingine umetolewa na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la afya duniani WHO, la kuhudumia Watoto UNICEF, la uhamiaji IOM na la mpango wa chakula duniani WFP na unaratibiwa na OCHA.” Mashirika hayo yamesema mapigano ya hivi karibuni katika viunga vya Soledar yamesababisha uharibifu mkubwa na kuwaacha mamia ya watu kwenye eneo hilo katika hali mbaya na hivyo kutegemea msaada wa kibinadamu. Hii ni mara ya kwanza msafara huo wa misaada wa mashirika ya kibinadamu unawasili katika eneo hilo na OCHA inasema “ Tumeziarifu mapema pande zote katika mzozo kuhusu msafara wetu kupitia mfumo wa taarifa wa masuala ya kibinadamu.” Mashirika ya kibinadamu nchini Ukraine yakiratibiwa na OCHA yanajitahidi kuongeza idadi ya misafara ya misaada ya pamoja katika eneo hilo lililo mstari wa mbele wa mapambano nchini Ukraine ambako mahitaji ni makubwa.  OCHA inasema misafara zaidi ya misaada inatarajiwa katika siku chache zijazo. 

Habari za UN
19 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 19, 2023 0:11


Hii leo jaridani tuna habari kwa ufupi, mada kwa kina na jifunze lugha ya kiswahili.Katika Habari kwa Ufupi na Leah Mushi:Kuelekea siku ya kimataifa ya elimu tarehe 24 Januari, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO Bi. Audrey Azoulay, amesema ametoa heshima ya siku hiyo kuwa maalum kwa wanawake na wasichana wa Afghanistan ambao mamlaka ya Taliban imewanyima fursa ya kupata elimu.Mahakama nchini Afrika Kusini imewaruhusu wataalamu wa Umoja wa Mataifa kushiriki kwenye kesi iliyofunguliwa na wananchi wa wilaya ya Kambwe nchini Zambia walioathirika na uchimbaji wa madini uliofanywa na Kampuni ya madini ya Anglo Amerika.Na leo ni siku ya mwaka mpya wa Kichina ambapo kwa mujibu wa kalenda ya nchi hiyo ni mwaka wa Sungura. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametuma salamu za mwaka mpya kwa taifa hilo na kulishukuru kwa ushirikiano wake linaoutoa kwa Umoja wa Mataifa na dunia kwa ujumla.Na katika Mada kwa Kina tunakwenda Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako takriban watu 233,000, wamelazimika kuyahama makazi yao katika wilaya ya Nyiragongo jimboni Kivu Kaskazini  kutokana na vita vinavyochochewa na kundi la wapiganaji waasi la M23 na sasa UNHCR imewajengea makazi badala ya kutegemea kuishi tu katika maeneo ya wazi, shuleni au makanisani. Shuhuda ni mwandishi wetu wa DRC, Byobe Malenga.Katika kujifunza lugha ya kiswahili, tunabisha hodi Baraza la Kiswahili la Taifa, Zanzibar, BAKIZA kwake Katibu Mtendaji Dkt. Mwanahija Ali Juma akifafanua methali ACHEKAYE KOVU HAJAONA JERAHA.Karibu na mwenyeji wako ni Anold Kayanda

Habari za UN
Guterres atoa onyo kuwa hatuwezi kutatua zahma zinazotukabili katika dunia iliyogawanyika bila mshikamano

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 18, 2023 0:02


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema dunia haiwezi kutatua changamoto kubwa inazokabiliwa nazo hivi sasa kuanzia mabadiliko ya tabianchi, vita ya Ukraine, mdororo wa uchumi na athari zinazoendelea za janga la COVID-19 katikia hali ya sasa ya mgawanyiko na kutokuwa na mshikamano hivyo wakati wa kufumbia macho changamoto hizi umepita na wanaochangia wawajibishwe.Katibu Mkuu Guterres ameyasema hayo mjini Davos Uswis katika hotuba yake kuhusu hali ya dunia kwenye siku ya pili ya jukwaa la uchumi duniani akibainisha kwamba wakati dunia inahitaji ushirikiano zaidi katika masuala ya mabadiliko ya tabianchi , upunguzaji wa mzigo wa madeni na afya uya kimataifa kuna mgawanyiko na changamoto inaongezeka linapokuja suala ya vita ya Ukraine  akisema "Hasa uvamizi wa Urusi kwa Ukraine sio tu kwa sababu ya mateso yasiyoelezeka kwa watu wa Ukraine, lakini kwa sababu ya athari zake kubwa za kimataifa kwa bei ya chakula na nishati, kwenye minyororo ya biashara na usambazaji na maswala ya usalama wa nyuklia, kwa misingi hiyo hiyo ya sheria za kimataifa”. Akisisitioza kuhusu suala la mabadiliko ya tabianchi amelaani makampuni makubwa ya mafuta kwa kupuuza sayansi kuhusu mabadiliko ya tabianchi, na kushutumu sekta ya mafuta na gesi kwa kutafuta kupanua zaidi wigo wa uzalishaji licha ya kujua kwamba kwamba mtindo wao wa biashara hauendani na maisha ya binadamu.  Amesema"Baadhi ya makampuni makubwa ya mafuta wanadanganya kwa kiasi kikubwa na kama vile ilivyo kwa sekta ya tumbaku, wale wanaohusika kuchochea mabadiliko ya tabianchi lazima wawajibishwe." Pia amezungumzia migawanyiko ikiwemo baina ya Mashariki na Magharibi hasa Marekani na Uchina hususan katika suala la haki za binadamu na usalama wa kikanda na Kaskazini na Kusini ambao amesema hashawishiki kwamba Kaskazini inatambua kiwango cha madhila yanayowakabili watu wa Kusini hasa linapokuja suala la afya kuhusu usawa wa usambazaji wa chanjo. Amehitimisha hotuba yake kwa kutoa wito kwa serikali zote, sekta binafsi na wadau wote kuunda njia za ushirikiano zaidi, ikisisitiza haja ya kuziba pengo la migawanyiko yote kwa kurekebisha na kujenga usawa katika mfumo wa fedha wa kimataifa, Kuchukua hatua za maana dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, Kurekebisha muundo wa biashara na mazoea ili kuendeleza malengo ya maendeleo endelevu, kuongoza njia ya kufikia fursa za kiuchumi kwa wanawake, na kufikia lengo la uhakika wa chakula duniani . Hivyo amesisitiza  kwamba “Sasakuliko wakati mwingine wowote, ni wakati wa kutengeneza njia za ushirikiano katika dunia yetu lililogawanyika kwani dunia haiwezi kusubiri." 

Habari za UN
17 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 17, 2023 0:12


Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina na tunakupeleka nchini Belize, taifa la ukanda wa karibea kuona jinsi mabadiliko ya tabianchi yamesomba si tu nyumba bali pia makaburi. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo kuhusu watoto katika kaya maskini, afya, na hatari zinazokumba wahamiaji. Katika mashinani leo utasikiliza ujumbe kuhusu janga la upatikanaji wa chakula kwa mwaka huu 2023.Watoto kutoka katika kaya maskini zaidi ndio wanaonufaika kidogo zaidi na ufadhili wa kitaifa wa elimu ya umma, imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF huku ikitoa wito wa uwekezaji wa ziada na wa usawa zaidi ili kuwaondoa mamilioni ya watoto kutoka katika changamoto ya kupata elimu.Kongamano la uchumi duniani linaendelea mjini Davos Uswis chini ya mada “ushirikiano katika ulimwengu uliogawanyika” na miongoni mwa mada kuu zinazojadiliwa leo ni kukomesh kifua kikuu tutafikaje huko. Kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO ambalo ndio kiongozi wa mjadala huo mwaka 2021 pekee zaidi ya watu milioni 10 waliougua kifua kikuu au Tb na milioni 1.6 kati yao walipoteza maisha. Na hadi sasa kwa takriban miaka 100 hakuna chanjo mpya dhidi ya ugonjwa huo.Na idadi ya wahamiaji wanaovuka isivyo kawaida na kuingia Panama baada ya kupitia kwenye njia hatari ya Darien Gap ilivunja rekodi mwaka 2022, na kufika karibu mara mbili ya takwimu za mwaka uliopita.Na leo katika mashinani viongozi wa serikali, mashirika pamoja na watu matajiri zaidi duniani walioko Davos wamepewa ujumbe!Mwenyeji wako ni Anold Kayanda karibu!

Habari za UN
13 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 13, 2023 0:12


Jaridani hii leo tutakupeleka Potopoto nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR na huko Lesvos nchini Ugiriki. Makala tunabisha hodi nchini Rwanda, na mashinani tunakwenda huko Walungu jimboni Kivu Kusini, kulikoni?Wananchi wa eneo la Potopoto nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, wameeleza furaha yao baada ya walinda amani wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MINUSCA kutoka kikosi cha 6 cha Tanzania, TANBAT 6 , kutumia wataalamu wake wa afya kutoa matibabu na dawa kwenye zahanati ya Potopoto wilayani Mambéré-Kadéï.Umoja wa Mataifa umeelezea wasiwasi wake kuhusu kesi iliyoanza huko Lesvos nchini Ugiriki dhidi ya watetezi 24 wa haki za binadamu wanaoshtakiwa kwa kutekeleza jukumu la kuokoa wahamiaji ambao walikumbwa na zahma baharini wakati wakikimbilia barani Ulaya kusaka maisha bora.Katika makala leo tunabisha hodi nchini Rwanda kumulika jinsi vijana wawili ndugu wameukumbatia wito wa Umoja wa Mataifa wa kutaka vijana kutofikiria ajira ni ofisini pekee kwani baada ya kuhitimu mafunzo ya Chuo Kikuu na kusaka ajira kwa muda mrefu bila mafanikio, walikata shauri na kuamua kujiajiri katika sekta ya Sanaa ya kuuza bidhaa za kitamaduni. Je safari yao ilikuwaje?Na katika mashinani tunakwenda huko Walungu jimboni Kivu Kusini kumulika suala la lishe. Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili - msemo, "Funga Funganya"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 12, 2023 0:50


Katika kujifunza Kiswahili, leo mtaalam wetu  Onni Sigalla Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, anatufafanulia maana ya msemo "FUNGA FUNGANYA", karibu!

Habari za UN
12 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 12, 2023 0:12


Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina ambapo leo tunakwenda nchini Kenya kumulika harakati za elimu ikiwa ni kuelekea siku ya elimu duniani. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo kutoka IAEA, msaada wa kibinadamu nchini DRC na matokeo ya mkutano wa Baraza la Usalama wa Umoja wa Mataifa. Mashinani tunakwenda nchini Uganda. Katika kujifunza kiswahili tunapata ufafanuzi wa msemo "FUNGA FUNGANYA" Shirika la Umoja wa Mataifa la nishati ya atomiki, IAEA limesema mbegu za mazao zilizopelekwa kituo cha anga za juu mwezi Novemba mwaka jana tayari zimepandwa eneo la ndani na nje ya kituo hicho na hivyo zinapata miali kamilifu ya anga za juu pamoja na viwango vya juu zaidi vya joto kwenye eneo hilo.Mkuu wa masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura wa Umoja wa Mataifa Martin Griffiths, ametangaza kutenga dola milioni 10 kutoka mfuko mkuu wa dharura wa Umoja wa Mataifa (CERF) ili kusaidia shughuli za misaada ya kibinadamu nchini Jamhuri ya kidemokrasia Kongo DRC.Na hii leo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana kujadili utawala wa sheria ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Matifa Antonio Guterres amesema ingawa nchi wanachama, mashirika ya kikanda, ya kiraia na sekta binafsi wana wajibu wa kuchangia katika kujenga na kulinda utawala wa sheria, hali ilivyo hivi sasa ni tofauti na kinachoonekana bado kuna safari ndefu ya kufikia lengo la utawala wa sheria.Na katika kujifunza Kiswahili , leo mtaalam wetu  Onni Sigalla Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania , anatufafanulia maana ya msemo "FUNGA FUNGANYA" Mwenyeji wako ni Anold Kayanda karibu!