Podcasts about katika

Place in Paphos District, Cyprus

  • 128PODCASTS
  • 2,681EPISODES
  • 21mAVG DURATION
  • 1DAILY NEW EPISODE
  • Jul 7, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024

Categories



Best podcasts about katika

Show all podcasts related to katika

Latest podcast episodes about katika

SBS Swahili - SBS Swahili
Rwanda yajipata pabaya katika ripoti ya kamati ya usalama ya Umoja wa Mataifa

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jul 7, 2025 7:07


Ripoti ya siri ya watalaam wa Umoja wa Mataifa imeishtumu Rwanda kwa kutoa maagizo na kudhibiti shughuli za waasi wa M23.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno KUTOHOA

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 3, 2025 1:16


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mchabuzi wetu Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA nchini Tanzania, anachambua neno KUTOHOA.

Habari za UN
02 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 2, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia wahamiaji na njia bunifu ya kuwawezesha kujikimu kimaisha, na malezi bora ya watoto nchini Tanzania. Makala tunasalia huko huko Tanzania kumulika uwekezaji na ufadhili wa miradi ya maendeleo, na mashinani tunakwenda nchini Kenya.Katika Mkutano wa 4 wa Kimataifa wa Ufadhili wa Maendeleo (FFD4) unaoendelea jijini Seville, Hispania, Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limetoa wito wa kuimarisha uwekezaji wa kibunifu katika uhamiaji wa watu ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kusaidia kuziba pengo la kila mwaka la dola trilioni 4 za ufadhili wa maendeleo.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limekuwa likihimiza umuhimu wa malezi na makuzi chanya kwa watoto kama njia mojawapo ya kulinda haki kuu nne za msingi za mtoto ambazo ni kuishi, kuendelezwa, kushirikishwa na kulindwa..Katika makala mkutano wa 4 wa Ufadhili wa Maendeleo (FFD4) ukikunja jamvi leo huko Sevilla Hispania, juhudi za kuhakikisha nchi zinajitegemea kifedha kupitia vyanzo jumuishi na vya ubunifu zimezidi kupewa kipaumbele. Katika hafla ya kufungua mafunzo ya Muongozo wa Upatikanaji wa Fedha kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa, au Intergrated Local Financing Framework (ILFF) yaliyofanyika katika Manispaa ya Morogoro kaskazini-mashariki mwa Tanzania  hivi majuzi , Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la Mpango wa Maendeleo nchini humo, UNDP umetoa mafunzo ya  namna halmashauri zinaweza kuandaa mikakati madhubuti ya kuhimiza maendeleo ya ndani kupitia ushirikiano kati ya sekta binafsi, mashirika ya kiraia, benki na jamii.Na mashinani, vijana na wahudumu wa afya katika kaunti ya Kajiado nchini Kenya, wameshikamana kuhamasisha umma kuhusu hedhi salama. Kupitia video iliyoandaliwa na washirika wetu Radio Domua, mmoja wa vijana anaelezea umuhimmu wa hedhi salama kama njia ya kutokomeza unyanyapaa dhidi ya wanawake na wasichana.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
IOM yasema uwekezaji wa kibunifu katika uhamiaji ni muhimu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 2, 2025 1:59


Katika Mkutano wa nne wa kimataifa wa Ufadhili wa Maendeleo (FFD4) unaoendelea jijini Seville, Hispania, Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limetoa wito wa kuimarisha uwekezaji wa kibunifu katika uhamiaji wa watu ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kusaidia kuziba pengo la kila mwaka la dola trilioni 4 za ufadhili wa maendeleo. Anold Kayanda anaeleza zaidi.

Habari za UN
UNDP Tanzania yahimiza ubunifu wa vyanzo vya mapato ili kuvutia wawekezaji

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 2, 2025 3:45


Mkutano wa 4 wa Ufadhili wa Maendeleo (FFD4) ukiendelea huko Sevilla Hispania, juhudi za kuhakikisha nchi zinajitegemea kifedha kupitia vyanzo jumuishi na vya ubunifu zimezidi kupewa kipaumbele. Katika hafla ya kufungua mafunzo ya Muongozo wa Upatikanaji wa Fedha kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa, au Intergrated Local Financing Framework (ILFF) yaliyofanyika katika Manispaa ya Morogoro kaskazini-mashariki mwa Tanzania  hivi majuzi , Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la Mpango wa Maendeleo nchini humo, UNDP umetoa mafunzo ya  namna halmashauri zinaweza kuandaa mikakati madhubuti ya kuhimiza maendeleo ya ndani kupitia ushirikiano kati ya sekta binafsi, mashirika ya kiraia, benki na jamii. Lengo ni kuendelea kuunga mkono serikali na wadau mbalimbali barani Afrika  katika kutafuta mbinu mbadala za kufadhili maendeleo.Sharon Jebichii na maelezon zaidi.

SBS Swahili - SBS Swahili
Uwakilishi wa Mataifa ya Kwanza katika vyombo vya habari: Nini kinabadilika, kwa nini ni muhimu

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jul 1, 2025 12:00


Uwakilishi wa WaAustralia wa Asili katika vyombo vya habari kihistoria umechangiwa na mila potofu na kutengwa ila, hali hii inabadilika pole pole.

Habari za UN
30 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 30, 2025 11:41


Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa 4 wa ufadhili kwa ajili ya maendeleo FFD4 huko Sevilla Hispania, na siku ya Mabunge tukizungumza na mmoja wao kutoka Tanzania. Makala inatupeleka nchi Kenya na mashinani tunarejea huko huko Tanzania, kulikoni?Mkutano wa 4 wa ufadhili kwa ajili ya maendeleo FFD4 umeng'oa nanga rasmi leo huko Selilla Hispania kwa wito wa kuziba pengo la ufadhili wa maendeleo ili kutimiza ahadi ya kimataifa ya kutomwacha yeyote nyumba. Mkutano huo uliowaleta pamoja washiriki 2,500 kutoka nchi 150 wakiwemo wakuu wa nhi 50 na wadau wengine unasema kuna pengo la dola trilioni 4 katika ufadhili wa maendeleo linalohitaji kuzibwa.Leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya mabunge ikijikita katika harakati za kuwezesha mabunge kufanikisha usawa wa kijinsia wakati huu ambapo Umoja wa Mataifa unaeleza ni kwa vipi Wanawake bado hawawakilishwi kwa kiwango cha kutosha katika mabunge ya kitaifa na ya mitaa duniani kote, jambo ambalo linapunguza haki zao za kisiasa na ushawishi wao juu ya sheria na bajeti..Katika makala tanatupeleka kaunti ya Kajiado, Kenya, katika eneo la EMbulbul, kukutana na vijana wanaotumia maarifa ya kilimo cha kisasa kubadilisha maisha yao na ya jamii, wakisema teknolojia imefungua njia mpya ya kuinua maisha ya wakulima wadogo, hasa kwa kutumia ukulima wa kisasa unaotumia maarifa na Teknolojia.Na mashinani, fursa ni yake Sandra Aloyce, Msichana mwenye umri wa miaka 12 kutoka Tanzania ambaye kupitia Mpango wa Vijana unaofadhiliwa na shirika la UNICEF uitwao “Furaha” unaotoa mafunzo kwa wazazi kuhusu umuhimu wa uwepo wa wazazi wote katika ukuaji wa mtoto ana ujumbe.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
27 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 27, 2025 9:59


Hii leo jaridanitunaangazia msaada wa kibinadamu Gaza, na mauaji yaliyofanyika nchini Rwanda kati ya mwaka 1972 hadi 1973. Makala tunamulika inayochukuliwa nchini Kenya za kutekeleza haki za watu wenye ulemavu wa kutoona, na mashinani tunakwenda DRC, kulikoni?Hatimaye shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO limeweza kufikisha huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, shehena ya kwanza ya vifaa vya matibabu ikiwa ni mara ya kwanza tangu tarehe pili mwezi Machi mwaka huu.Serikali ya Burundi inataka mauaji yaliyofanyika nchini mwake kati ya mwaka 1972 hadi 1973 yatambulike kimattaifa kama ni mauaji ya kimbari dhidi ya Wahutu, je kwa nini wito huo umekuja sasa.Katika makala leo ikiwa ni Siku ya Kimataifa ya viziwi wasioona, tunamulika hatua kubwa inayochukuliwa nchini Kenya katika kuhakikisha watoto wenye ulemavu wa kuona wanapata elimu bora na jumuishi. Mafunzo maalum yaliyofanyika jijini Nairobi yalileta pamoja wataalamu, walimu na mashirika ya maendeleo, kwa lengo la kuchochea elimu hiyo kwa njia ya michezo, kwa msaada wa Shirika la LEGO kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Kenya.Na mashinani, fursa ni yake Tom Fletcher, Mratibu wa Umoja wa mataifa wa Misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura akihitimisha ziara yake Goma Mashariki mwa DRC amezungumza na waandishi wa habari akieleza kuwa raia wameteseka vya kutosha na ukata unawazidishia madhila”Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
UNICEF Kenya - Elimu Jumuishi kupitia michezo: Watoto wenye ulemavu wa kuona wapate nafasi sawa

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 27, 2025 3:09


Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya ulemavu wa uziwi na kutoona, tunamulika hatua kubwa inayochukuliwa nchini Kenya katika kuhakikisha watoto wenye ulemavu wa kuona wanapata elimu bora na jumuishi. Mafunzo maalum yaliyofanyika jijini Nairobi yalileta pamoja wataalamu, walimu na mashirika ya maendeleo, kwa lengo la kuchochea elimu hiyo kwa njia ya michezo, kwa msaada wa Shirika la LEGO kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Kenya. Sharon Jebichii na makala zaidi.

Habari za UN
26 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 26, 2025 10:13


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania, ambako mshikamano na wakimbizi unatekelezwa kwa vitendo na mashirika ya Umoja Mataifa likiwemo lile la Chakula na Kilimo (FAO) na la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kupitia Programu wa Pamoja ya Kigoma (KJP).Katika siku ya kimataifa ya kupambana na dawa za kulevya na usafirishaji haramu, ripoti mpya ya dunia ya Dawa za Kulevya mwaka 2025 iliyotolewa leo imeonya kuwa kutokuwepo kwa utulivu duniani kunachochea ongezeko la matumizi ya dawa za kulevya na uhalifu wa kupangwa. Kwa mujibu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Dawa na Uhalifu UNODC, watu milioni 316 walitumia mihadarati mwaka 2023. Mkurugenzi Mtendaji wa UNODC, Ghada Waly, amesema "Makundi haramu yanatumia migogoro kama fursa tunahitaji ushirikiano na uwekezaji kulinda jamii zetu.”Leo ni kumbukizi ya uzinduzi wa Chata ya Umoja wa Mataifa miaka 80 iliyopita mjini San Francisco, hatua iliyoweka msingi wa kuundwa kwa Umoja wa Mataifa mnamo Oktoba 24, 1945. Katibu Mkuu António Guterres anasema Umoja wa Mataifa bado unaakisi matumaini yaliyozaliwa kutoka kwenye majivu ya vita naye mwanahistoria Stephen Schlesinger akizungumza na UN News ameakumbusha kuwa “Chata hii ilikuwa kilio cha wanadamu wakitafuta amani, suluhu za mazungumzo, na maisha bora duniani.”Asilimia 93 ya kaya Gaza hazina uhakika wa maji safi kutokana na ukosefu wa mafuta unaopelekea mifumo ya maji kukaribia kusambaratika yameonya mashirika ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yakiongeza kuwa familia zinakumbwa na njaa kali, wakila mlo mmoja kwa siku huku watu wazima wakikosa kula ili kuwasaidia watoto na wazee.Na leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya neno "AFRITI KIJITI”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno AFRITI KIJITI

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 26, 2025 0:36


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya neno "AFRITI KIJITI.”

SBS Swahili - SBS Swahili
Shariff "vijana tuongeze bidii katika shughuli zetu, tusitegemee wanasiasa"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 26, 2025 11:29


Neno goons lina sifa mbaya katika jamii, haswa kwa vijana wengi ambao hu husishwa na maswala yanayo enda kinyume na sheria na maadili mazuri.

Habari za UN
UN80: Umoja wa Mataifa wajitathmini kwa ajili ya karne mpya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 25, 2025 3:02


Katika dunia inayokumbwa na migogoro inayoendelea kuongezeka, kupanuka kwa pengo la usawa, na kupungua kwa imani katika taasisi za kimataifa, Umoja wa Mataifa umeanzisha juhudi kabambe za kuboresha namna unavyowahudumia watu kote ulimwenguni. Mpango wa UN80, uliotangazwa mwezi Machi na Katibu Mkuu António Guterres, ni juhudi ya mfumo mzima inayolenga kurahisisha utendaji kazi, kuongeza ufanisi, na kuthibitisha tena umuhimu wa Umoja wa Mataifa katika dunia inayobadilika kwa kasi. Je nini nini kinatarajiwa katika mpango huo wa UN80? Ungana na Flora Nducha katika Makala hii

Radio Maria Tanzania
Fahamu vipaumbele vinavyokusudiwa katika kuufariji Moyo Mtakatifu wa Yesu

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Jun 25, 2025 54:27


Karibu katika kipindi cha Katekisimu Katoliki Shirikishi, Padre Dominic Mavula C.PP.S na Mkurugenzi wa matangazo Radio Maria, anaendelea kutoa mafundisho kuhusu kuufariji Moyo Mtakatifu.  Mimi ni Esther Magai Hangu, ninakualika kwa niaba ya Padre Dominic. L'articolo Fahamu vipaumbele vinavyokusudiwa katika kuufariji Moyo Mtakatifu wa Yesu proviene da Radio Maria.

Habari za UN
TANLAP Tanzania tunahamasisha wanawake wengi kushiriki kwenye uchaguzi ili washiriki kuamua mambo yanayowahusu - Christina Kamili Ruhinda

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 23, 2025 3:13


Katika mahojiano haya, Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Mashirika yanayotoa huduma ya msaada wa kisheria nchini Tanzania, TANLAP, Christina Kamili Ruhinda alipozungumza na Anold Kayanda wa Idhaa hii kandoni mwa Mkutano wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW69 uliofanyika mapema mwaka huu hapa New York, Marekani, anaeleza wanavyotekeleza mpango wao wa kuhakikisha wanawake  wanapata nafasi zaidi kwenye meza za uamuzi nchini Tanzania.

Habari za UN
23 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 23, 2025 10:27


Hii leo jaridani tunaangazia mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Marekani dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran, na juhudi za kurejesha matumaini miongoni mwa jamii zilizotengana kwa migogoro Sudan Kusini.  Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani nchini Kenya.Hali ya taharuki yaendelea kushuhudiwa Mashariki ya Kati kufuatia mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Marekani dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran mwishoni mwa wiki. Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki IAEA, Rafael Grossi, leo ametoa wito wa dharura wa shirika hilo kuruhusiwa kufika kwenye maeneo hayo yaliyoharibiwa, ili kutathmini kiwango halisi cha uharibifu.Katika juhudi za kuimarisha mshikamano na kurejesha matumaini miongoni mwa jamii zilizotengana kwa migogoro, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini, UNMISS, kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, hivi karibuni waliandaa tamasha maalum la muziki katika mji wa Malakal, jimbo la Upper Nile – eneo ambalo kwa miezi ya hivi karibuni limekuwa kitovu cha machafuko.Katika makala Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Mashirika yanayotoa huduma ya msaada wa kisheria nchini Tanzania, TANLAP, Christina Kamili Ruhinda anaeleza wanavyotekeleza mpango wao wa kuhakikisha wanawake  wanapata nafasi zaidi kwenye meza za uamuzi nchini Tanzania.Na mashianani fursa ni yake Priscillah Lesurkukwa, Mwanamke mkulima kutoka kaunti kame ya Samburu nchini Kenya ambaye ni mnufaika wa mradi wa Shrika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP, ambao umewapatia wakulima mafunzo ya kutengeneza makinga maji na kuchimba mashimo yenye umbo la nusu mwezi ili kuvuna na kuhifadhi maji kwenye mashamba yao, na sasa mbinu hizo zimebadilisha mazingira kuwa na malisho ya kijani kibichi na miti inayostawi.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Muziki waunganisha jamii zilizogawanyika Malakal nchini Sudan Kusini

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 23, 2025 2:05


Katika juhudi za kuimarisha mshikamano na kurejesha matumaini miongoni mwa jamii zilizotengana kwa migogoro, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini, UNMISS, kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, hivi karibuni waliandaa tamasha maalum la muziki katika mji wa Malakal, jimbo la Upper Nile – eneo ambalo kwa miezi ya hivi karibuni limekuwa kitovu cha machafuko. Sharon Jebichii anatupasha zaidi

Radio Maria Tanzania
Karibu ujifunze thamani ya Ekarist Takatifu katika maisha yako ya Kikristo.

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Jun 23, 2025 56:42


Leo katika kipindi cha Katekisimu Katoliki Shirikishi Padre Domini Mavula C.PP.S , Mkurugenzi wa Matangazo Radio Maria Tanzania, anatupatia mafundisho juu ya Ekaristi Takatifu. Karibu ujichotee mafundisho ya kina kupitia kipindi hiki nami ni mtangazaji wa Happiness Mlewa. L'articolo Karibu ujifunze thamani ya Ekarist Takatifu katika maisha yako ya Kikristo. proviene da Radio Maria.

Habari za UN
20 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 20, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia siku ya Wakimbizi Duniani, mwaka huu ikibeba maudhui “Mshinamano na wakimbizi”, tukisikia ujumbe wa Umoja wa Mataifa na kazi wanazozifanya kuinua Maisha ya wakimbizi, na pia tunakuletea sauti za wakimbizi kutoka DRC, Burundi, Ethiopia na Sudan Kusini.Leo ni Siku ya Wakimbizi Duniani, mwaka huu ikibeba maudhui “Mshinamano na wakimbizi” na Umoja wa Mataifa umetaka mshikamano huo kwa vitendo wakati idadi ya watu wanaolazimika kufungasha virago na kukimbia makayo yao ikifikia kiwango cha kihistoria.Tukisalia na siku ya wakimbizi duniani tunaelekea  eneo la Mata, karibu na mpaka wa Ethiopia na Sudan Kusini, ambakomaelfu ya wakimbizi kutoka Sudan Kusini wanapokea msaada wa dharura kupitia juhudi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP. unaolenga kuwalinda baada ya kukimbia  mapigano makali nchini mwao. Nyibol Chueny Puok, mama wa watoto 4 ni miongoni mwao.Katika makala Assumpta Massoi kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR anakupeleka Kusini-Magharibi mwa Burundi kwenye kituo cha wakimbizi cha Musenyi kumsikia mkimbizi kutoka DRC ambaye ananufaika na kauli mbiu ya siku ya wakimbizi mwaka huu ya Mshikamano na Wakimbizi.Na mashianani tukisalia na siku ya wakimbizi duniani, tutakwenda nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kumsikia mtoto mkimbizi ambaye alitumikishwa katika vita na waasi wenye silaha.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Wakimbizi kutoka Sudan Kusini wanapatiwa msaada na WFP mpakani mwa Ethiopia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 20, 2025 2:04


Katika eneo la Mata, karibu na mpaka wa Ethiopia na Sudan Kusini, ambakomaelfu ya wakimbizi kutoka Sudan Kusini wanapokea msaada wa dharura kupitia juhudi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP. unaolenga kuwalinda baada ya kukimbia  mapigano makali nchini mwao. Nyibol Chueny Puok, mama wa watoto 4 ni miongoni mwao. Sharon Jebichi anatupasha zaidi...

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno KIHORO

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 19, 2025 0:40


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIHORO!"

Habari za UN
19 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 19, 2025 10:44


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina, ikiwa kesho tarehe 20 mwezi Juni ni siku ya kimataifa ya wakimbizi maudhui yakiwa Mshikamano na Wakimbizi, tunakupeleka kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyoko kaunti ya Turkana, kaskazini-magharibi mwa Kenya.Uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje FDI umeshuka kwa mwaka wa pili mfululizo, ukihatarisha mustakabali wa maendeleo katika nchi zinazoendelea, kwa mujibu wa wa ripoti iliyotolewa leo na kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD. ikionya kuwa pengo la mitaji linaongezeka huku sekta muhimu kama nishati safi na miundombinu zikikosa ufadhili wa muda mrefu.Katika siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono kwenye mizozo, Umoja wa Mataifa umetoa onyo kuwa ukatili wa kingono unazidi kutumika kama silaha ya vita huku wanawake na wasichana wakiathirika zaidi. Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA "Huu si uharibifu wa bahati mbaya  ni uhalifu wa kivita. Na waathirika lazima wawe kiini cha amani, haki, na urejeshwaji wa maisha."Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa  Duniani (WHO) leo limezindua mwongozo wake wa kwanza wa kimataifa wa kudhibiti ugonjwa wa seli mundu (sickle cell) wakati wa ujauzito, ukilenga kupunguza hatari za maisha kwa mama na mtoto. WHO inasema wanawake wenye ugonjwa huu wana hatari hadi mara 11 zaidi ya kufariki dunia wakati wa ujauzito. Hivyo huduma bora za afya zinaweza kuokoa maisha, lakini visa vya seli mundu vinaongezeka duniani, huku Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara ikichangia asilimia 80.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIHORO!.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Mafanikio ya Mradi wa ACP MEAs 3 Rwanda katika kuboresha kilimo endelevu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 18, 2025 3:40


Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO, kwa kushirikiana na Serikali ya Rwanda, linaendelea kujenga uwezo wa kitaifa katika kuhimiza matumizi ya mbinu rafiki kwa mazingira katika kilimo pamoja na usimamizi salama wa viuatilifu. Hili linafanyika kupitia utekelezaji wa awamu ya tatu ya mradi wa ACP MEAs 3 unaofadhiliwa na Muungano wa Ulaya EU. Mpango huu unalenga kuwawezesha wakulima wadogo kuhamia kwenye mifumo ya kilimo endelevu kimazingira na kuwajengea uwezo wa utekelezaji wa mikataba ya kimataifa ya mazingira. Sharon Jebichii anatupeleka nchini humo kumulika mradi huo..

Habari za UN
18 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 18, 2025 10:29


Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa Katibu Mkuu Guterres, wa siku ya kimataifa ya kupambana na kauli za chuki na mradi wa lishe bora kwa watoto huko Kilifi Kenya. Makala tunakwenda nchini Rwanda na mashinani nchini Ghana, kulikoni?Leo Juni 18 ni siku ya kimataifa ya kupambana na kauli za chuki ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametumia ujumbe wake kwa siku hii kutoa onyo kuhusu hatari zinazoongezeka za chuki mtandaoni, hasa zikichochewa na akili mnemba au (AI) na  na majukwaa ya kidijitali.Katika Kaunti ya Kilifi, iliyoko pwani ya Kenya barani Afrika, Mpango wa Kuboresha Lishe kwa kupatia jamii Fedha na Elimu ya Afya (NICHE) unasaidia kuwaelimisha wazazi kuhusu umuhimu wa baba na mama kulea watoto wao kwa pamoja, mradi unaotekelezwa na shirika la Umoja wa MAtaifa la kuhudumia watoto, UNICEF.Katika makala shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO, kwa kushirikiana na Serikali ya Rwanda, linaendelea kujenga uwezo wa kitaifa katika kuhimiza matumizi ya mbinu rafiki kwa mazingira katika kilimo pamoja na usimamizi salama wa viuatilifu. Hili linafanyika kupitia utekelezaji wa awamu ya tatu ya mradi wa ACP MEAs 3 unaofadhiliwa na Muungano wa Ulaya EU. Mpango huu unalenga kuwawezesha wakulima wadogo kuhamia kwenye mifumo ya kilimo endelevu kimazingira na kuwajengea uwezo wa utekelezaji wa mikataba ya kimataifa ya mazingira.Na katika mashinani leo ikiwa ni siku ya kimataifa Sayansi ya Mapishi au Gastronomia,  fursa ni yake Mpishi Mkuu mashuhuri Fatmata Binta kutoka Sierra Leone, ambaye kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, ya kipindi kiitwacho Mazungumzo ya Jikoni , anapazia sauti matumizi ya vyakula vya kiasili kama njia ya kuepuka kusahaulika kwa vyakula vya kiasili ili hatimaye kuweko na lishe endelevu.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
FAO/WFP: Nchi 13 katika ongezeko la njaa, 5 kati ya hizo wanakabiliwa na njaa kali zaidi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 16, 2025 1:56


Ripoti mpya ya pamoja ya Umoja wa Mataifa inaonya kuwa watu katika nchi 5 kati ya nchi 13 zenye njaa kali duniani wako kwenye hatari kubwa ya kukumbwa na njaa kali, vifo na maafa ikiwa msaada wa kibinadamu hautatolewa haraka na juhudi za kimataifa hazitaelekezwa kukomesha migogoro, kupunguza ufurushwaji na kuongeza msaada wa haraka kwa kiwango kikubwa. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

Habari za UN
16 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 16, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia baa la njaa katika nchi 13 duniania amabzo hakuna uhakika wa chakula, na hali ya kibinadamu kwa wakimbizi wa DRC. Makala tunasalia hapa makao makuu na mashinani tunakwenda nchini Nepal, kulikoni?Ripoti mpya ya pamoja ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo jijini Roma, Italia inatahadharisha kuwa watu katika nchi 5 kati ya nchi 13 zenye njaa duniani wako kwenye hatari kubwa ya kukumbwa na njaa kali, vifo na maafa ikiwa msaada wa kibinadamu hautatolewa haraka na juhudi za kimataifa hazitaelekezwa kukomesha migogoro, kupunguza ufurushwaji na kuongeza msaada wa haraka kwa kiwango kikubwa.Huko jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, juhudi za kidiplomasia zinaendelea kumaliza mapigano, huko nalo shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP likitoa wito wa msaada kwa watu waliofurushwa makwao kutokana na mashambulizi ya waasi wa M23, msaada ambao utawasaidia kujenga upya maisha yao na njia zao za kujipatia riziki.  Katika makala leo Flora Nducha wa Idhaa hii amemuuliza Amon Anastaz Mpanju, Naibu Katibu Mkuu wizara ya Maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake na makundi maalum nchini Tanzania aliyeshiriki mkutano wa 18 wa mkataba wa watu wenye ulemavu COSP18 uliokunja jamvi mwishoni mwa wiki nini kikubwa alichotoka nacho kwenye mkutano huo.Na katika mashinani leo ikiwa ni siku ya Kimataifa ya utumaji fedha kwa familia kutoka ughaibuni, fursa ni yake Bibha kutoka Chinnamastrial nchini Nepal, mnufaika wa utumaji fedha kutoka wanafamilia walioko ughaibuni akielezea jinsi ambavyo fedha hizo zinavyosaidia jamii zake kuondokana na umaskini.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Socceroos wafuzu kucheza katika Kombe la Dunia baada ya kuishinda Saudi Arabia

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 13, 2025 7:31


Wiki hii timu ya mpira wa miguu ya taifa Socceroos, ili fuzu kwa Kombe la Dunia tena baada yakupata ushindi dhidi wenyeji wao Saudi Arabia.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya maneno "MBEUZI, MNYWANYWA NA MACHAGU.”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 12, 2025 0:54


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno "MBEUZI, MNYWANYWA NA MACHAGU.”

Kiswahili, Lugha Ya Afrika
Sumaku Ya Dunia - Nguvu Ya Ajabu Inayotulinda Kutoka Kwa Hatari Za Angani!

Kiswahili, Lugha Ya Afrika

Play Episode Listen Later Jun 12, 2025 19:35


Je, umewahi kujiuliza ni nini hasa hutulinda dhidi ya hatari za anga za juu?Katika video hii ya kuvutia, tunazama ndani ya mojawapo ya miujiza mikuu ya sayari yetu, sumaku ya Dunia. Kutoka kwa sumaku za utotoni hadi kwenye chuma cha kiowevu chenye joto kali maili elfu chini ya miguu yetu, utaelewa jinsi Dunia yetu inavyozalisha kinga yake ya asili dhidi ya upepo wa jua na hatari kutoka angani.

Habari za UN
IOM yachukua hatua za dharura baada ya wahamiaji kufa maji katika pwani ya Djibouti

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 11, 2025 1:52


Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, (IOM) kwa ushirikiano wa karibu na mamlaka za Djibouti, linaongeza juhudi zake za kibinadamu kufuatia tukio la kusikitisha lililotokea pwani ya Djibouti ambapo takriban wahamiaji wanane walikufa maji na wengine 22 hawajulikani walipo. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: maana ya neno KIHEREHERE

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 5, 2025 0:45


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno KIHEREHERE.

Habari za UN
Kuelekea Mkutano wa Bahari UNOC3, UNEP yatoa wito wa hatua za kukabili taka za plastiki

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 4, 2025 3:23


Katika kuelekea Mkutano wa Tatu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Bahari UNOC3, utakaofanyika mjini Nice, Ufaransa kuanzia tarehe 9 hadi 13 Juni 2025, Ofisi ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira UNEP nchini Tanzania imetoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua za haraka na madhubuti kukabiliana na changamoto ya uchafuzi wa bahari, hasa wa taka za plastiki. Akizungumza na Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini humo UNIC jijini Dar es Salaam, Clara Makenya, Mkuu wa Ofisi ya UNEP nchini Tanzania na Afisa Mawasiliano wa shirika hilo kwa Namibia, alisisitiza umuhimu wa kushughulikia kwa haraka tatizo la taka za plastiki ambazo nyingi hutokea nchi kavu na kuishia baharini.

Habari za UN
29 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 29, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa ikitupeleka nchini DRC, Sierra Leone na Ghana. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na maana ya neno "MISHEMISHE.”Leo ni Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani ambayo mwaka huu inajikita na maudhui ya “mustakabali wa ulinzi wa amani.”Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema walinda amani wa Umoja wa Matafa wako katika changamoto kubwa “Leo hii, walinda amani wanakabiliwa na hali zinazozidi kuwa ngumu katika dunia inayozidi kuwa na changamoto, ikiwemo uugawanyika na kutofautiana kwa mitazamo duniani kunazidi kuongezeka, operesheni za ulinzi wa amani zinakabiliwa, hatari zaidi kutokana na wingi wa vitisho kama vile ugaidi na walinda amani kulengwa kwa makusudi kupitia taarifa potofu zenye madhara makubwa na changamoto zinazovuka mipaka kuanzia janga la mabadiliko ya tabianchi hadi uhalifu wa kimataifa.Kikosi cha 11 cha Tanzania kinachohudumu chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO kimeungana na walinda amani wengine kuadhimisha Siku ya Walinda Amani Duniani. Maadhimisho hayo yamefanyika Mavivi, yakiongozwa na Brigedia Jenerali Diamond Meshack Madie, Mnadhimu Mkuu wa Vikosi vya MONUSCO.Shirika la Umja wa Mataifa la Mazingira UNEP limezindua mpango mpya wa dola milioni 15 kusaidia uwekezaji endelevu katika Bonde la Kongo – moja ya mifumo muhimu zaidi ya ikolojia duniani. Mpango huu unalenga kufungua fursa za biashara rafiki kwa mazingira kwa wajasiriamali wadogo na wa kati katika sekta za kijani. Msitu wa mvua wa Bonde la Kongo ni moja ya vyanzo vikubwa vya kaboni duniani na ni makazi ya watu zaidi ya milioni 75, wakiwemo jamii za asili.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi  Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "MISHEMISHE.”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "MISHEMISHE.”

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 29, 2025 0:38


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi  Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "MISHEMISHE.”

Habari za UN
28 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 28, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia haki za binadamu nchini Ukraine na upatikanaji wa elimu nchini Kenya. Makala tunakupeleka nchini Sudan Kusini, na amashinani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kulikoni?Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya Uchunguzi kuhusu Ukraine imehitimisha kwamba vikosi vya kijeshi vya Urusi vimetenda uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu, hasa mauaji, kupitia mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (drones) yaliyoelekezwa dhidi ya raia.Mradi wa "operesheni rejea shuleni" unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF kwa ushirikiano na wizara ya elimu ya Kenya, shirika liliso la kiserikali la Hapag Lloyd na wadau wengine kwa kuzipa fedha familia zisizojiweza kuendesha shughuli za kiuchumi, umerejesha mautumaini ya elimu kwa mamia ya watoto katika Kaunti ya Kwale Pwani ya Kenya  ambao waliacha shule sababu ya umasikini.  Katika makala ikielekea siku ya walinda amani kesho Mei 29, tunamulika harakati za walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini SUdan Kusini za kulinda raia na mwenyeji wako katika makala hii iliyoandaliwa kupitia video ya ujumbe wa  Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani Sudan Kusini, UNMISS ni Sharon Jebichii.Na katika mashinani huku machafuko yakiendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, wafanyakazi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR wako mashinani mjini Goma na maeneo mengine yaliyoathirika ili kutoa msaada muhimu, ikiwa ni pamoja na kufanikisha nia ya wakimbizi wanaorejea nchini mwao Rwanda. Raab na Ruusi ni baadhi yao.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Walinda amani wa UN kutoka Mongolia waokoa wakazi wa Abiemnhom nchini Sudan Kusini

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 28, 2025 2:58


Kuelekea siku ya walinda amani Mei 29, tunakwenda nchini Sudan Kusini kumulika walinda amani na ulinzi wa raia. Katika taifa hilo changa zaidi duniani  walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Mongolia wanaohudumu kwenye Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo (UNMISS) walikuwa msaada mkubwa wakati kijiji cha Abiemnhom kaskazini mwa Sudan Kusini kilipovamiwa. Walinda amani hao walifika haraka  kutoka kituo chao cha karibu na kutoa msaada wa kuokoa manusura na miili ya waliouawa. Je nini kilifanyika zaidi Sharon Jebichii anasimulia kwenye makala hii iliyotokana na video ya UNMISS.

SBS Swahili - SBS Swahili
Tafakari, na wito wakuchukua hatua, katika siku ya Kitaifa yakusema Pole

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 27, 2025 9:22


Matukio yame fanyika kote nchini Kuadhimisha Siku ya Kitaifa yakuomba msamaha 26 Mei, hatua ambayo ni kukiri kuondolewa kwa lazima kwa watoto wa Mataifa ya Kwanza kutoka kwa familia na tamaduni zao.

Habari za UN
Raia kuhukumiwa katika mahakama za kijeshi, Türk amsihi Rais kukataa muswada - Uganda

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 23, 2025 1:52


Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa , Volker Türk, leo Ijumaa mjini Geneva, Uswisi kupitia msemaji wake ameelezea wasiwasi wake kuhusu kupitishwa kwa muswada uliopendekezwa na Bunge la Uganda unaoruhusu raia kuhukumiwa katika mahakama za kijeshi. Anold Kayanda ameifuatilia taarifa hiyo.

Habari za UN
Vijana Kenya watumia mpira wa miguu kutokomeza umasikini na kuishi maisha bora - Peter Omondi

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 23, 2025 3:06


Katika kuelekea siku ya kandanda, kabumbu au mpira wa miguu duniani itakayoadhimishwa Jumapili wiki hii Mei 25 ikibeba maudhui nguvu ya kdandanda katika kuleta mabadiliko tuabisha hodi Nairobi Kenya ambapo leo Peter Omondi, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Global Youth Forum linalounganisha vijana Kenya kwa lengo la kutokomeza umasikini na kuishi maisha bora kupitia michezo mbalimbali ikiwemo kandanda akizungumza na Idhaa hii ya Kiswahili anaeleza umuhimu wa kandanda katika ajenda ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu. Anaanza kwa kujitambusha.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "DAHARI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 22, 2025 0:36


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DAHARI."

Habari za UN
21 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 21, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia msaada wa kibinadamu katika ukanda wa Gaza, na mradi wa kutengeneza barabara katika kaunti ya Meru nchini Kenya. Makala tunaangazia simulizi ya mkurugenzi na mwanzilishi wa filamu iitwayo FURU, na mashinani tunakwenda Tanzania.Wafanyakazi wa misaada wa Umoja wa Mataifa leo wamesema kwamba bado wanangoja kibali kutoka kwa Israel ili kusambaza msaada wa kuokoa maisha ulioruhusiwa kuingia Gaza mwanzoni mwa wiki ambapo  malori matano yalifanikiwa kuingia baada ya vikwazo kwa wiki 11.Nchini Kenya, katika kaunti ya Meru hatua rahisi iliyochukuliwa inaleta mabadiliko makubwa na dhahiri kwani maeneo ambako awali barabara zilikuwa hazipitiki na hakuna mawasiliano, ubunifu wa kijapani umerejesha matumaini.Katika makala wakati ulimwengu ukiendelea kupaza sauti dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia, tunaelekea nchini Mali, ambako Fatou Cissé, mkurugenzi wa filamu na mwanzilishi wa filamu iitwayo FURU, anatumia sanaa kuangazia suala zito la ndoa za kulazimishwa.Na mashinani, fursa ni yake Ruth Nkurlu, Mtaalamu wa lishe kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF Tanzania, ambaye anatoa mafunzo ya lishe bora kwa watoto Mkoani Njombe kwa ajili ya kupunguza udumavu wakati wa ukuaji wa mtoto.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
19 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 19, 2025 11:08


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya afya, na wakimbizi wa Syria wanaorejea nchini mwao. Makala tukwenda nchini Kenya kumulika ufukaji wa nyuki, na mashinani tunakuletea ujumbe wa Katibu Mkuu wa IMO kuhusu Siku ya Kimataifa ya wanawake mabaharia.Wajumbe kutoka kote duniani wamekusanyika mjini Geneva, Uswisi, kwa ajili ya Mkutano wa 78 wa Baraza la Afya Duniani (WHA78) unaofanyika kuanzia leo Mei 19 hadi 27 Mei mwaka huu.Tangu kuangushwa kwa utawala wa aliyekuwa Rais wa Syria Bashar al Assad aliyekuwa madarakani kwa zaidi ya muongo mmoja, wananchi wa Syria wamekuwa wakimiminika kurejea nchini mwao ambapo takwimu za sasa zinaonesha zaidi ya Wasyria 500,000 wamerejea kutoka nchi jirani. Mmoja wa waliorejea ni Babu Jassim na Leah Mushi anatuletea simulizi yake.Katika makala tunaelekea Kajiado nchini Kenya, ambako juhudi za utunzaji mazingira kupitia mradi wa ufugaji wa nyuki unaofadhiliwa na shirika la misaada la Marekani USAID kwa kushirikiana na idara ya misitu ya Kenya KFS hazichangii tu katika kukuza uchumi wa jamii, bali pia kulinda mazingira. Kupitia Makala hii iliyoandaliwa na Sharon Jebichii, Bwana Mureithi mmoja wa wanufaika wa mradi huo anaanza kwa kueleza mafanikio yao.Nakatika mashinani, fursa ni yake Arsenio Dominguez, Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usafirishaji Majini, IMO akitoa ujumbe wa ujumuishaji na usawa wa kijinsia wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya wanawake mabaharia ambayo huadhimishwa tarehe 18 mwezi Mei kila mwaka.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Ufugaji nyuki katika Kaunti ya Kajiado umeleta manufaa kwa wenyeji - Bwana Mureithi

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 19, 2025 3:55


Kesho ikiwa ni siku ya nyuki duniani ikimulika umuhimu wa nyuki tunakupeleka nchini Kenya, katika kijiji cha Embulmbul, ambapo mradi wa ufugaji nyuki uliofanikishwa na Shirika la Marekani la Misaada ya maendeleo, USAID, kwa kushirikiana na Idara ya Misitu ya Kenya, KFS na wadau wengine, umeleta tija kwa wenyeji. Mmoja wa wanufaika hao ni mwanamazingira Christopher Mureithi ambaye ni kiongozi wa kikundi cha kufuga nyuki katika msitu wa Ololua ambao wamefanikiwa sio tu kuboresha uzalishaji wa asali, bali pia kuchangia katika uhifadhi wa bioanuwai na misitu. Katika makala hii iliyoandaliwa na Sharon Jebichii Bwana Mureithi anaanza kwa kueleza mafanikio yao.

Habari za UN
16 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 16, 2025 12:25


Hii leo jaridani tunaangazia uhakika wa chakula, na takwimu za afya za janga la COVID-19 kusababisha vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla. Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani nchini DRC, kulikoni?Ukosefu wa uhakika wa kupata chakula na utapiamlo kwa watoto uliongezeka kwa mwaka wa sita mfululizo mwaka 2024, na kuwatumbukiza mamilioni ya watu karibu na baa la njaa, huku wengine wakiepuka kutokana na misaada ya kimkakati. Imesema Ripoti ya Kimataifa kuhusu Janga la Chakula (GRFC) iliyotolewa leo huko Roma, Italia na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO.Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) ya takwimu za afya duniani iliyochapishwa jana Mei 15 ikionesha athari kubwa zaidi za kiafya zilizosababishwa na janga la COVID-19 kuhusu vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla, imeweka wazi kuwa katika kipindi cha miaka miwili pekee, kati ya mwaka 2019 na 2021, matarajio ya kuishi yalipungua kwa mwaka mmoja na miezi nane  ikiwa ni maporomoko makubwa zaidi katika historia ya hivi karibuni hali iliyobatilisha mafanikio ya afya yaliyopatikana kwa muongo mmoja.Katika makala Leah Mushi anatupeleka nchini Tanzania kusikia namna wanawake wenye ulemavu walivyoweza kujikwamua kutoka kwenye changamoto mbalimbali ikiwemo za kiuchumi na kuchangamkia fursa za uongozi.Na katika fursa ni yake Bernadette Kambonesa, mkimbizi wa ndani kutoka kijiji cha Bogoro, jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akizungumzia manufaa yatokanayo na uwepo wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini humo (MONUSCO).Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "KIANGO."

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 15, 2025 0:52


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "KIANGO."

Habari za UN
Akina mama wakimbizi katika ukanda wa Gaza wanataabika bila huduma za afya

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 14, 2025 2:23


Huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli, wanawake na wasichana wakiwemo wanawake wajawazito na wale waliojifungua, wamelazimika kukimbia makazi yao na wanaishi katika mazingira hatarishi bila huduma za msingi za kiafya. Sharon Jebichii anaangazia simulizi ya mama mmoja, mkazi wa kambi ya wakimbizi ya Jabalia, Kaskazini mwa Gaza, ambaye alijifungua akiwa amekimbia vita,na sasa anahangaika kumtunza binti yake mchanga.

Habari za UN
14 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 14, 2025 10:48


Hii leo jaridani tunaangazia haki za wanawake na wasichana nchini Sudan na hali ya kina mama na wanawake wajawazitio katika ukanda wa Gaza. Makala tukwenda nchini Burundi na mashinani nchini Tanzania, kulikoni?Wataalamu huru wa haki za binadamu, leo Mei 14 wamekemea vikali ukiukwaji mkubwa na wa kimfumo dhidi ya wanawake na wasichana nchini Sudan ukiwemo ukatili wa kingono unaohusiana na vita, utekaji nyara, na mauaji, ambayo mengi yameripotiwa kufanywa na kundi la kijeshi la Rapid Support Forces (RSF).Huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli, wanawake na wasichana wakiwemo wanawake wajawazito na wale waliojifungua, wamelazimika kukimbia makazi yao na wanaishi katika mazingira hatarishi bila huduma za msingi za kiafya. Sharon Jebichii anaangazia simulizi ya mama mmoja, mkazi wa kambi ya wakimbizi ya Jabalia, Kaskazini mwa Gaza, ambaye alijifungua akiwa amekimbia vita,na sasa anahangaika kumtunza binti yake mchanga.Katika makala Assumpta Massoi kwa makala hiyo na zaidi ya yote shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi nchini Burundi kwa kuiandaa na kuhakikisha wakimbizi wanapata usaidizi.Na mashinani, fursa ni yake Juliana Sanga, mama kutoka Mkoa wa Njombe nchini Tanzania ambaye ni mnufaika wa mafunzo ya lishe bora kwa ajili ya kupunguza udumavu kwa watoto inayofanikishwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF Tanzania. Yeye anaeleza kile anachoondoka nacho.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
13 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 13, 2025 11:36


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo inamulika lengo namba moja la Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDG1 la kutokomeza umaskini na inatupeleka nchini Tanzania ambako Umoja wa Mataifa umeona bora kusaidia wafugaji kuku kuondokana na umaskini.Katika mkutano wa ngazi ya mawaziri kuhusu mustakabali wa ulinzi wa amani unaofanyika leo mjini  Berlin Ujerumani Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameeleza vipaumbele vitatu vya msingi katika mageuzi ya ulinzi wa amani kwa muktadha wa dunia inayobadilika kwa kasi.Mashariki ya Kati leo shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO limeonya kuhusu vifo vya watoto kutokana na utapiamlo Gaza, sababu kubwa ikiwa ni kuendelea kukosekana kwa msaada wa kibinadamu unaojumuisha lishe maalum kwa watoto.Wakati mahitaji ya kibinadamu yakizidi kuongezeka duniani watu milioni 308 katika nchi 73 wakihitaji msaada wa dharura , Shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women limeonya kuwa wanawake na wasichana ndio wanaoathirika zaidi wa migogoro, wakikumbwa na utapiamlo, vifo vinavyoweza kuzuilika vinavyohusiana na ujauzito, na ukatili wa kingono kwa kiwango cha juu, huku mfumo wa misaada ya kibinadamu ukikumbwa na ukata wa fedha.Na katika mashinani, fursa ni yake Jean Todt, Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu usalama barabarani akieleza ni jambo gani lifanyike kuhakikisha usalama barabarani wakati huu dunia inaadhimisha Wiki ya Usalama Barabarani maudhui yakijikita kwenye kuhakikisha barabara ni salama kwa ajili ya waenda kwa miguu na waendesha baiskeli.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Bi. Joy :Teknolojia inatatua changamoto za kijamii - Wasichana katika TEHAMA

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 12, 2025 3:38


Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO, sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano TEHAMA, au ICT inaendelea kutawala na kuunda fursa mpya, lakini wanawake bado wanakumbana na changamoto kubwa ya upungufu wa uwakilishi. Hata hivyo, wanawake wanavuka mipaka na sasa Bi. Joy, msichana kutoka Nairobi Kenya, ambaye ni mtaalamu katika teknolojia ya kidijitali, amekalia nafasi muhimu katika kubadili mtindo wa maisha kupitia elimu ya ICT. Katika mahojiano na washirika wetu Radio Domus, alizungumzia umuhimu wa kuhamasisha wasichana kujiunga na masomo ya teknolojia ili kutengeneza mustakabali mpya wa kidijitali, na kubadili dunia kwa njia ya kidigitali na usawa. Sharon Jebichii na Makala zaidi

Men. Men. Men. - The Podcast -
Embracing The Legacy, Creating My Own Path

Men. Men. Men. - The Podcast -

Play Episode Listen Later May 6, 2025 101:36


“Walking in the shadow of a giant” si jambo rahisi—na inakuwa ngumu zaidi pale “Giant” huyo akiwa  ni Augustine Mahiga, mwanadiplomasia mashuhuri wa Tanzania, na wewe ni mtoto wake wa kiume, unayejulikana kama Andrew Mahiga.Kwa wengi, jina la mwisho linaweza kufungua milango, lakini je, kila nafasi unayoipata ni kwa sababu ya uwezo wako au kwa sababu unaitwa Mahiga? Hilo ndilo swali ambalo Andrew amekuwa akilazimika kulikabili katika safari yake ya kujitambua.Katika episode hii ya kipekee ya Men Men Men: The Podcast, Andrew anakaa nasi na kufungua moyo wake kuhusu changamoto za kuishi na jina kubwa, shinikizo la kulingana na hadhi ya baba, na hatimaye furaha aliyopata alipogundua kuwa—ndiyo, yeye ni mtoto wa baba yake, lakini si lazima awe kama baba yake.Zaidi ya hayo, Andrew anazungumzia kwa kina umuhimu wa mentorship kwa wanaume—na jinsi kuwepo au kutokuwepo kwa wanasihi kunaweza kumjenga au kumvunjilia mbali mwanaume wa Kitanzania.Baada ya kuisikiliza episode hii, utaelewa kwa nini tumeiita: "Embracing the Legacy, Creating My Own Path."