Podcasts about nchi

  • 50PODCASTS
  • 498EPISODES
  • 14mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • Jun 8, 2026LATEST

POPULARITY

20192020202120222023202420252026


Best podcasts about nchi

Latest podcast episodes about nchi

Habari za UN
Lazima tujenge uhusiano mpya na bahari- Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 8, 2026 2:50


Bahari duniani zinakabiliwa na changamoto kubwa zinazotishia afya ya mazingira na ustawi wa binadamu, ameonya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres na kutoa wito wa hatua za haraka na za pamoja kukabiliana na hali hiyo. Akizungumza kwa njia ya video katika ujumbe wake wa Siku ya Kimataifa ya Bahari inayoadhimishwa kila mwaka Juni 8, Bwana Guterres amesema bahari ni msingi wa maisha na maendeleo duniani, lakini zimekuwa zikikabiliwa na shinikizo linalozidi uwezo wake wa kustahimili."Bahari inaongoza tabianchi yetu, inalinda mifumo ya ikolojia na uchumi, na inalisha mabilioni ya watu duniani," anasema Guterres na kuongeza kuwa, "bahari ipo kwenye zahma kubwa na tunaishinikiza kupita uwezo wake."Guterres amerejelea Ripoti ya Tatu ya Tathmini ya Bahari Duniani iliyozinduliwa leo, ambayo imebainisha kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabianchi, uvuvi uliokithiri, kupotea kwa bionuwai na uchafuzi wa bahari.Katibu Mkuu Guterres amesisitiza akisema, "hatuwezi kuendelea kuichukulia bahari kama kitu kisicho na ukomo," akihimiza kujengwa kwa uhusiano mpya na bahari unaozingatia sayansi, unaoongozwa na sheria za kimataifa na unaojengwa juu ya wajibu wa pamoja wa mataifa, sekta mbalimbali na vizazi vyote.Ametaja mafanikio ya Mkutano wa Tatu wa Bahari wa Umoja wa Mataifa uliofanyika mwaka jana pamoja na kuanza kutekelezwa kwa Makubaliano ya Baiyonuai ya Bahari katika maeneo yaliyo nje ya mamlaka ya kitaifa mwaka huu kama ushahidi kwamba ushirikiano wa kimataifa unaweza kuleta matokeo.Anasema, "hatua za pamoja za kimataifa zinawezekana na ni za lazima."Katika hitimisho la ujumbe wake wake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewataka viongozi wa dunia, sekta binafsi na wananchi kuchukua hatua kwa haraka ili kulinda bahari kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.Anasema, "katika Siku hii ya Kimataifa ya Bahari, hebu tuchukue hatua kwa nia thabiti na kutatua mahitaji ya wakati huu."Hakika yanayosemwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa yanaendana na aliyoyasema Mwenyekiti aliyechaguliwa wa ya Tume ya Kiserikali ya Bahari ya UNESCO (IOC) kwa Afrika na Nchi za Visiwa vinavyokaribia bara la Afrika (IOCAFRICA) Hellen Gichuhi alipozungumza na Idhaa ya Umoja wa Mataifa.

ant afrika guterres tatu umoja bahari katika siku tume nchi mataifa mkuu mkutano kimataifa ripoti
Habari za UN
03 JUNI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 3, 2026 10:33


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania Kaskazini mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, ambako Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro inaendelea kuwa mfano wa jinsi binadamu, wanyamapori na urithi wa kitamaduni vinavyoweza kuishi pamoja huku vikichangia maendeleo ya utalii endelevu na ulinzi wa mazingira. Je nini kinafanyika kuhakikisha uhifadhi, utamaduni, mazingira na utalii vinakutana kwa mustakabali endelevu? Ili kupata majawabu Flora Nducha wa Idhaa hii amezungumza na Kamishna wa Hifadhi ya Ngorongoro, Abdul-Razaq Badru.Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus ameendelea kusisitiza umuhimu wa ugunduzi wa mapema kwani hatua zikichukuliwa haraka wagonjwa wa Ebola wanapona. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Geneva Usiswi baada kurejea kutoka ziarani mashariki mwa DRC amesema, Kufikia sasa, watu sita wamepona nchini DRC na wawili nchini Uganda, jambo linaloonesha kuwa watu wanaweza kupona Ebola iwapo watapata huduma za afya na kwenda vituo vya afya mara tu wanapoanza kuonyesha dalili za ugonjwa huo.Kuelekea kuanza kwa michuano ya Kombe la Dunia la FIFA wiki ijayo hapa Marekani na katika nchi jirani, Canada na Mexico, Shirika la Afya la Nchi za Amerika (PAHO) limetoa wito kwa nchi za bara la Amerika kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa wa surua na Rubella kufuatia  mikusanyiko mikubwa inayotarajiwa na milipuko inayoendelea ya surua na ongezeko la safari za kimataifa vinaweza kuongeza kasi ya kuenea kwa ugonjwa huo. Shirika hilo linazitaka mamlaka za afya kubaini maeneo yaliyo katika hatari kubwa na kuimarisha hatua za kukabiliana haraka ili kuzuia maambukizi zaidi. Na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa asubuhi hii kwa saa za New York, Marekani wanachagua wanachama watano wapya wasio wa kudumu wa Baraza la Usalama kwa muhula kipindi cha miaka miwili kuanzia tarehe 1 Januari 2027 hadi 31 Desemba 2028. Kutoka Barani Afrika mgombea mmoja ni Zimbabwe ambaye hata hivyo anatarajiwa kupita kwani hana mpinzani katika nafasi hiyo. Nchi zitakazochaguliwa zinachukua nafasi za Somalia, Pakistan, Panama, Denmark na Ugiriki, ambazo mihula yao itaisha mwishoni mwa mwaka huu 2026.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
18 MEI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 18, 2026 11:11


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia mlipuko wa Ebola nchini DRC na Uganda na ujumbe wa Profesa Mohamed Yakub Janabi Mkurugenzi wa WHO kanda ya Afrika kuhusu hatua WHO inachukua kudhibiti ugonjwa huo. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo..Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, kupitia ujumbe alioutuma kwa njia ya video kwa washiriki wa Mkutano wa 79 wa Baraza la Afya Duniani ulioanza leo mjini Geneva, Uswisi amesema changamoto za afya duniani hazijawahi kuwa kubwa kiasi hiki na hivyo akawakumbusha wahudhuriaji kwamba mkutano huu ni fursa muhimu kwa Mataifa Wanachama kuoanisha na kuharakisha juhudi za kukabiliana na changamoto za afya duniani..Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, limetoa wito kwa nchi za Afrika kuwajumuisha wakimbizi, watu wasio na uraia, na wale walio katika hatari ya kukosa uraia katika mifumo ya kitaifa ya vitambulisho vya kidijitali. UNHCR imetoa ushauri huo katika mkutano wa ID4Africa uliofanyika mjini Abidjan, Côte d'Ivoire. Nchi za Kenya na Uganda ni miongoni mwa nchi zilizotumika kama mfano mzuri..Na kundi la watoto kutoka nchi mbalimbali lililotumia miezi 15 kuandaa muongozo waliouita ‘Tujumuisheni' wakilenga kushughulikia upungufu katika ushiriki bora wa watoto kwenye uamuzi wa msuala mbalimbali kwa ngazi zote, wametoa wito kwa mashirika yanayofanya kazi na watoto na vijana kuutumia muongo wa viwango hivyo.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Siha Njema
Mashirika ya kiraia Afrika yanataka nchi za Afrika kuwa na taratibu za pamoja kudhibiti magonjwa

Siha Njema

Play Episode Listen Later May 16, 2026 9:37


Taratibu hizo za pamoja yatahakikisha kuwa nchi za Afrika zinaweka bajeti kwenye sera ya uchumi na kuipa kipau mbele ufadhili wa afya

Habari RFI-Ki
Ziara ya Rasi William Ruto nchini Tanzania na makubaliano baina ya nchi hizo

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later May 8, 2026 9:39


Kenya na Tanzania zimekubaliana kuondoa vikwazo vyote visivyo vya kikodi vya kibiashara, ili kuimarisha ushirikiano wa kibiashara. Unaamini yaliyokubaliwa kati ya nchi hizo mbili yatatekelezwa ?

Habari RFI-Ki
Ziara ya Rasi William Ruto nchini Tanzania na makubaliano baina ya nchi hizo

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later May 8, 2026 9:39


Kenya na Tanzania zimekubaliana kuondoa vikwazo vyote visivyo vya kikodi vya kibiashara, ili kuimarisha ushirikiano wa kibiashara. Unaamini yaliyokubaliwa kati ya nchi hizo mbili yatatekelezwa ?

SBS Swahili - SBS Swahili
Wiki Hii Barani Afrika: Nchi za Afrika Mashariki kujenga kiwanda chakusafisha mafuta Tanga, Tanzania

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 28, 2026 7:51


Baadhi ya nchi za Afrika Mashariki zime anza mazungumzo kuhusu, ujenzi wa kiwanda chakusafisha mafuta katika bandari ya Tanga, nchini Tanzania.

tanzania wiki tanga nchi baadhi afrika mashariki
SBS Swahili - SBS Swahili
Wiki Hii barani Afrika:Papa Leo aomba mamlaka ya Angola kumaliza ubaguzi ambao ume endelea kusumbua nchi hiyo

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 21, 2026 6:59


Kiongozi wa kanisa Katoliki Papa Leo XIV, amekemea vitendo vya rushwa na kuzitaka mamlaka za Angola kumaliza ubaguzi ambao ume endelea kusumbua nchi hiyo tangu kumalizika kwa vita vya wenyewe kwa mwenyewe 2002.

papa afrika angola wiki hiyo nchi kiongozi mamlaka endelea
SBS Swahili - SBS Swahili
Mahojiano: Je makanisa yanastahili watenga viongozi ambao wame sababisha maafa katika nchi zao na duniani?

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 8, 2026 10:46


Waumini wa dini laki Kristo kote duniani, wali jumuika katika sehemu mbali mbali kusherehekea Pasaka.

kristo katika maafa pasaka nchi
Habari za UN
Baraza la Haki za Binadamu: Tofauti zozote zilizopo kati ya nchi hazitatatuliwa kwa kuwaua wanafunzi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 27, 2026 3:06


Katika mjadala wa dharura kuhusu “shambulizi la anga dhidi ya Shule ya Wasichana ya Shajareh Tayyebeh huko Minab, nchini Iran, Baraza la Haki za binadamu la Umoja wa Mataifa limejadili tukio hilo kama ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa za kibinadamu na haki za binadamu.”Mjadala huu wa dharura unafanyika kufuatia tukio hilo lililotajwa kuwa la kutisha lililofanyika siku ya kwanza kabisa ya mashambulizi ya Israel na Marekani dhidi ya Iran. Simulizi ya mamaTuanze na simulizi ya Mohaddeseh Fallahat, huyu ni mama wa Iran aliyepoteza watoto wake wawili katika shambulizi hilo ambaye anasema “asubuhi ile ilikuwa kama kawaida.” Aliwafunga wanawe gidamu za viatu na kuwavalisha mabegi mgongoni na hakukuwa na dalili yoyote kwamba hiyo ingekuwa mara ya mwisho, kuonana nao.Anasema “Walipotoka mlangoni, waliniambia, ‘Mama, njoo utuchukue baada ya shule.' Sentensi hiyo rahisi sasa inajirudia akilini mwangu mara elfu moja, na kila mara moyo wangu unaungua kwa maumivu. Hakuna mama anayewahi kufikiria atampeleka mtoto wake shuleni kwa tabasamu, kisha akumbane na ukimya. Hakuna mama aliyejiandaa kusikia maneno haya: ‘Mtoto wako hatarudi tena.'” © Mshiriki Jengo moja katika eneo la mashariki mwa Tehran likionesha dalili za uharibifu uliosababishwa na mabomu.WaokoajiAkizungumza na waandishi wa habari huko Geneva akiwa Tehran kupitia mawasiliano ya satelaiti, Mkuu wa shirika la Msalaba mwekundu na Hilal nyekundu IFRC, Maria Martinez amesema zaidi ya watu 1,900 wameuawa, wakiwemo wanawake na watoto, na takriban watu 20,000 wamejeruhiwa.Martinez amesimulia masahibu yanayowakuta watoa huduma ya kwanza “Moja ya nyakati za kushtusha na kuvunja moyo ni pale mhudumu wa uokoaji na utafutaji alipogundua miili ya wafamilia yake mwenyewe chini ya vifusi vya jengo lililoshambuliwa.Katika mji wa Qom, kusini mwa Tehran, mhudumu mwingine aliokoa mwili wa shangazi yake pamoja na mume wake na mtoto wao mdogo.” Huo ndio uhalisia wanaokumbana nao wahudumu wa kibinadamu, wanaokoa maisha huku wakibeba maumivu makubwa yasiyovumilika ya kupoteza wapendwa wao.UN GenevaMjadala wa Baraza la Haki za Binadamu ukifanyika Geneva UswisiKauli ya UNTofauti zozote zilizopo kati ya nchi na nchi, sote tunaweza kukubaliana kuwa hazitatatuliwa kwa kuwaua wanafunzi.Akizungumza katika mjadala huo wa dharura, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk ametoa wito kwa mamlaka za kijeshi za Marekani kuchapisha haraka iwezekanavyo matokeo ya uchunguzi wao kuhusu shambulizi hilo. Türk amesema “Mashambulizi ya mabomu katika Shule ya Msingi ya Shajareh Tayyebeh huko Minab yameibua hofu kubwa na maumivu makali. Picha za madarasa yaliyoharibiwa na wazazi waliogubikwa na huzuni zinaonesha wazi ni nani hulipa gharama kubwa zaidi ya vita: raia wasio na uwezo wowote katika maamuzi yaliyopelekea mzozo. Katika tukio hili, inaripotiwa kuwa wanafunzi, walimu, wafanyakazi wa shule, na wapendwa wao 168 wameathirika.Maafisa waandamizi wa Marekani wamesema shambulizi hilo linafanyiwa uchunguzi. Natoa wito mchakato huo ukamilike haraka iwezekanavyo, na matokeo yake yawekwe wazi kwa umma. Lazima kuwe na haki kwa madhara makubwa yaliyosababishwa.”

Habari za UN
Azimio lapitishwa kutambua biashara ya utumwa kupitia bahari ya Atlantiki ni uhalifu mkubwa dhidi ya binadamu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 25, 2026 3:23


Umoja wa Mataifa leo umekuwa na tukio la kumbukizi ya siku ya kimataifa ya kukumbuka waathiriwa wa biashara ya  utumwa kupitia bahari ya Atlanitiki ambapo nchi 123 wanachama wa Umoja huo wamepitisha azimio lililoandaliwa na mataifa 58 kutambua usafirishaji wa watu wa kiafrika na utumwa kwa misingi ya rangi ya waafrika kuwa uhalifu mkubwa dhidi ya binadamu. Nchi hizo 123 ni pamoja na zile wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ilhali nchi 3 zilizopinga azimio ni Marekani, Israeli na Argentina. Nchi 52 hazikuonesha msimamo wowote. Mwakilishi wa Marekani akizungumza baada ya kupiga kura ya kupinga azimio hilo amesema, "tunalaani makosa yoyote yaliyofanyika kuhusiana na utumwa kuvuka bahari ya Atlantiki, jangwa la Sahara na kwingineko, lakini tumepinga azimio kwa sababu hatuoni msingi wa kulipatia kiwango cha juu hivyo cha hadhi tukio hilo. Na zaidi ya yote kama ni fidia, fidia hiyo atalipwa nani,?" amehoji.Rais wa Ghana aliwasilisha rasimu ya azimio mbele ya Baraza KuuUN/Manuel EliasRais John Mahama wa Ghana akihutubia Baraza Kuu wakati wa siku ya Kimataifa ya Kumbukizi ya Waathirika wa Utumwa na Biashara ya Watumwa kupitia bahari ya Atlantiki.Rasimu ya azimio hilo iliwasilishwa na Rais wa Ghana John Mahama ambaye ni Balozi wa Muungano wa Afrika wa Kuendeleza Hali ya Haki na Fidia. Azimio hilo namba A/80/L.48 limepatiwa jina kutambua usafirishaji wa watu waliokuwa watumwa kutoka Afrika na utumwa kwa msingi wa rangi ya watu wa kiafrika kama mojawapo ya uhalifu mkubwa zaidi dhidi ya binadamu.  Azimio hilo lililoandaliwa na mataifa 58 yakiwemo mataifa ya Afrika Mashariki, lina vipengele 16 vya utekelezaji ikiwemo kutambua usafirishaji huo wa watumwa kutoka Afrika kuwa uhalifu mkubwa zaidi dhidi ya binadamu, kurejeshwa kwa mali za kitamaduni kutoka Afrika na zaidi ya yote kulipwa fidia.Kauli ya Rais wa Baraza KuuTukio la kumbukizi lilianza kwa Annalena Baerbock Rais wa Baraza Kuu kuitisha kikao na kisha kuelekea kwenye mimbari kutoa hotuba yake akirejelea simulizi ya mtumwa Oladuk Ekwano kutoka Nigeria ya sasa akielezea machungu ya safari ndani ya meli iliyowabeba.UN/Manuel EliasRais wa Baraza Kuu la UN Annalena Baerbock akitoa hotuba katika tukio la siku ya Kimataifa ya Kumbukizi ya Waathirika wa Utumwa na Biashara ya Watumwa kupitia bahari ya Atlantiki.Anasema Makumi ya mamilioni ya wengine kama Egvano walinyang'anywa kutoka kwa familia zao, nchi zao na tamaduni zao, wakafanywa watumwa na kupelekwa kufanya kazi katika nchi za kigeni—kwenye mashamba ya pamba hapa Marekani, na kwenye mashamba ya miwa na kahawa katika makoloni yaliyodhibitiwa na Ulaya. Katika maeneo ambayo leo yanajulikana kama Brazili, Barbados, Jamaica, na maeneo mengine mengi. Wote wakiwa mbali na nyumbani, mbali na familia, mbali na maisha yao.Tunatambua nchi zinazoomba radhi lakini hatua zaidi zahitajikaKwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amerejelea mateso waliyopata mamilioni ya waafrika waliotekwa nyara na kusafirishwa katika hali dhalili na kugeuzwa watumwa barani Amerika. Amesema kumbukumbu pekee haitoshi.Amebainisha kuwa mfumo huo haukuwa tu ukatili wa zamani bali pia ulikuwa msingi wa miundo ya uchumi wa dunia ambayo madhara yake yanaendelea hadi leo katika mfumo wa ubaguzi wa rangi wa kimfumo na ukosefu wa usawa.UN/Manuel EliasKatibu Mkuu António Guterres akitoa hotuba katika tukio la siku ya Kimataifa ya Kumbukizi ya Waathirika wa Utumwa na Biashara ya Watumwa kupitia bahari ya Atlantiki.Hotuba hiyo imesisitiza kuwa kumbukumbu pekee haitoshi. Badala yake, nchi lazima zikabiliane na dhuluma za muda mrefu zinazoendelea kuwaathiri watu wenye asili ya Kiafrika. “Kiini cha juhudi hizo, alisema, ni kutafuta ukweli, haki, na marekebisho, ikiwa ni pamoja na mijadala yenye maana na hatua kuhusu fidia,” amesema Katibu Mkuu. Guterres anasema, “Ndiyo maana Muongo wa Pili wa Kimataifa kwa Watu wenye Asili ya Kiafrika na Muongo wa Fidia wa Muungano wa…

argentina nigeria israelis jamaica ghana amerika afrika sahara barbados guterres pili rais brazili umoja haki bahari katika asili watu kauli nchi wote biashara mataifa marekani kimataifa afrika mashariki fidia azimio uhalifu kiini
Habari za UN
Fahamu jinsi serikali ya Kenya inasambaza visima vya maji kwa wananchi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 23, 2026 3:00


Katika mazungumzo yafuatayo kati ya Anold Kayanda wa Idhaa hii na Hanna Wendot Cheptumo Waziri wa Jinsia, Utamaduni na Maslahi ya Watoto wa Kenya, Nchi hiyo ya Afrika Mashariki inajivunia kupiga hatua katika kuitatua changamoto hiyo.  Waziri Hanna Wendot Cheptumo anaeleza kwamba Kenya kupitiua mfuko ilioupa jina NGAAF yaani National Government Affirmative Action Fund, mfuko wa fecha mahususi kusaidia makundi maalumu katika jamii hususani wanawake kupitia wawakilishi wa wanawake. Pesa hizo wanazopewa wanawake si mkopo hivyo hawarudishi lakini wanatakiwa kuzitumia kijiendeleza “na hizo nidizo wanatumia kununua matanki ya maji” anasema Bi. Cheptumo. Visima vya jumuiya Pia kupitia miradi ambayo iko vijijini, Serikali ya Kenya inachimba visima vya maji vya jumuiya na wanaweka sola au mashine za kuvuta maji kwa njia ya nishati ya jua kwa hiyo hakuna mzigo au gharama ya umeme kwa wanawake hao. Waziri Hanna Wendot Cheptumo anakumbuka akisema, “hata mimi nikiwa mdogo nilikuwa ninaenda kilomita saba kwenda kutafuta maji lakini saa hizo ukienda kijijini unapata maji yako hapo na haulipishwi. Unaenda unachota maji yako na unaenda.” Mabwawa Aidha, kwa mujibu wa Bi. Cheptumo, Serikali ya Kenya imechimba mabwawa ya kusambaza maji katika vijiji na ni kazi ambayo inaendelea, “tunataka kusema hata kama maji hayajafikia kila mahali, lakini serikali iko na mikakati ambayo imewekwa ya kuhakikisha kila mtu anapata maji.Hupiti hata kilomita moja. Lakini sanasana weni sasa wana maji nyumbani.” Anahitimisha. 

kenya bi pesa maji katika watoto lakini jinsi nchi serikali fahamu afrika mashariki wananchi
Habari RFI-Ki
Bobi Wine ameweka hadharani alikimbia nchi yake baada ya kuhangaishwa

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 20, 2026 10:12


Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Uganda Bobi Wine baada ya kuwa mafichoni kwa miezi miwili alifunguka na kusema kafanikiwa kukimbia baada ya kuwindwa na vikosi vya usalama

Habari RFI-Ki
Urusi imehakikishia Kenya haitawasajili raia wake kupigana vita vya Ukraine

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 20, 2026 9:30


Nchi zaidi za Afrika zimejitokeza kusema raia wake walihadhaiwa na kusajiliwa kwenda kupigana na vikosi vya Urusi nchini Ukraine

Habari RFI-Ki
Bobi Wine ameweka hadharani alikimbia nchi yake baada ya kuhangaishwa

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 20, 2026 10:12


Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Uganda Bobi Wine baada ya kuwa mafichoni kwa miezi miwili alifunguka na kusema kafanikiwa kukimbia baada ya kuwindwa na vikosi vya usalama

Habari RFI-Ki
Urusi imehakikishia Kenya haitawasajili raia wake kupigana vita vya Ukraine

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 20, 2026 9:30


Nchi zaidi za Afrika zimejitokeza kusema raia wake walihadhaiwa na kusajiliwa kwenda kupigana na vikosi vya Urusi nchini Ukraine

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Iran yaonya nchi dhidi yakujiunga katika vita vya Marekani na Israel dhidi yao

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 16, 2026 5:42


Waziri wa Nishati Chris Bowen amehakikishia taifa kwamba usambazaji wa mafuta nchini Australia bado uko salama, huku usafirishaji ukifika kama ilivyopangwa na akiba ya kutosha kuifunika nchi kwa siku 37.

Habari RFI-Ki
EAC : Mafuriko yatatiza jiji la Nairobi

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 10, 2026 10:02


Katika makala haya  tunajadili kinachoendelea jijini Nairobi nchini Kenya ambapo jiji hilo limeendelea kushuhudia mvua kubwa ambazo zimesababisha maafa ya zaidi ya watu 40. Nchi nyingine za Afrika Mashariki pia zinaendelea kushuhudia mvua kubwa. Skiza makala haya.

kenya nairobi eac jiji katika nchi afrika mashariki
Habari RFI-Ki
EAC : Mafuriko yatatiza jiji la Nairobi

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 10, 2026 10:02


Katika makala haya  tunajadili kinachoendelea jijini Nairobi nchini Kenya ambapo jiji hilo limeendelea kushuhudia mvua kubwa ambazo zimesababisha maafa ya zaidi ya watu 40. Nchi nyingine za Afrika Mashariki pia zinaendelea kushuhudia mvua kubwa. Skiza makala haya.

kenya nairobi eac jiji katika nchi afrika mashariki
Habari RFI-Ki
Kikao cha dharura cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Feb 18, 2026 9:35


Rais wa Kenya William Ruto, ameitisha kikao cha dharura cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika mashariki  mwezi ujao kujadili changamoto ya kifedha ambayo imetatiza shughuli za taasisi za jumuiya hiyo, tatizo kubwa likiwa baadhi ya nchi kuchelewesha kutoa michango kwa wakati. Mkutano huo utajadili mfumo mpya wa uchangishaji fedha na namna ya kupunguza matumizi ya jumuiya hiyo.

afrika rais eac nchi mkutano afrika mashariki kenya william ruto
Habari RFI-Ki
Kikao cha dharura cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Feb 18, 2026 9:35


Rais wa Kenya William Ruto, ameitisha kikao cha dharura cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika mashariki  mwezi ujao kujadili changamoto ya kifedha ambayo imetatiza shughuli za taasisi za jumuiya hiyo, tatizo kubwa likiwa baadhi ya nchi kuchelewesha kutoa michango kwa wakati. Mkutano huo utajadili mfumo mpya wa uchangishaji fedha na namna ya kupunguza matumizi ya jumuiya hiyo.

afrika rais eac nchi mkutano afrika mashariki kenya william ruto
Habari za UN
Mkutano wa AI waanza New Delhi Mjumbe wa UN asisitiza ujumuishi wa nchi zote

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 16, 2026 2:41


Mkutano wa kimataifa unaofahamika kama AI Impact 2026 umeanza leo mjini New Delhi, India ukiwakutanisha viongozi kutoka sehemu mbalimbali za dunia ili kujadili namna akili mnemba (AI) inavyoweza kuendelezwa na kutumika kwa uwajibikaji kuchangia maendeleo endelevu. Amandeep Singh Gill, Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia teknolojia za kidijitali na zinazoibuka, amesisitiza ushiriki mpana wa kimataifa kwani ni muhimu ili kuhakikisha AI inanufaisha nchi zote. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

ai new delhi sdgs ai impact umoja nchi zote mataifa mkutano
Habari RFI-Ki
Matumizi ya mitandao ya kijamii kwa watoto chini ya miaka 15

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Jan 30, 2026 9:56


Nchi za magahribi kupitisha sheria za kupiga marufuku mitandao ya kijamii kwa watoto walio chini ya miaka 15.

australia afrika chini watoto nchi miaka ufaransa matumizi
Habari RFI-Ki
Matumizi ya mitandao ya kijamii kwa watoto chini ya miaka 15

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Jan 30, 2026 9:56


Nchi za magahribi kupitisha sheria za kupiga marufuku mitandao ya kijamii kwa watoto walio chini ya miaka 15.

australia afrika chini watoto nchi miaka ufaransa matumizi
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya habari:Nchi za Ulaya zajiandaa kutetea eneo la Denmark

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jan 20, 2026 12:13


**Papa waendelea kuwashambulia watu huko Sydney ** Rais Donald Trump aendelea na mchakato wake wa kuchukua Greenland **Soko la Samaki la Sydney sasa limefunguliwa

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho
Jinsi jamii ya wamasaai wanavyohamia kwenye ufugaji wa samaki baada ya mabadiliko ya tabia nchi

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho

Play Episode Listen Later Jan 18, 2026 9:53


Jamii ya wamaasai ambayo Kwa miaka mingi inategemea mifugo imekuwa ikipata changamoto haswa wakati wa kiangazi.  Kiangazi uathiri mifugo kwani ukosefu wa lishe unasababisha wanyama kufa. Hata hivyo Jamii hiyo imebuni mbinu mbadala ya kisasa ya ufugaji samaki. Lakini kutokana na joto jingi linaloshuhudia katika eneo la kajiado, tatizo la kuwakuza samaki hao katika vidimbwi inaonekana wazi wazi kwani wakulima hawana vifaa vya kisasa vya kupima nyuzi joto katika vidimbwi vya samaki. 

hata kwa tabia baada kwenye jamii lakini jinsi nchi samaki mazingira ufugaji
Habari za UN
Udadavuzi: Fahamu taratibu za matumizi ya nguvu za kijeshi dhidi ya nchi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 6, 2026 6:36


Miaka 80 iliyopita baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia, mataifa 50 yalikutana huko San Francisco hapa nchini Marekani na kupitisha Chata iliyoanzisha Umoja wa Mataifa. Miongoni mwa malengo ni kuzuia vita na kujenga uhusiano mwema baina ya mataifa. Mathalani kuepusha nchi moja kuvamia nchi nyingine na kulinda haki za binadamu. Leo hii Chata hiyo imeendelea kusiginwa na kilichoibua mjadala zaidi ni tukio la Januari 3 la Vikosi Maalum vya Marekani kuingia Venezuela na kumtwaa Rais wa nchi hiyo Nicolas Maduro pamoja na mkewe kwa madai ya kwamba wanatakiwa wajibu tuhuma nchini MArekani za uhalifu mkubwa ikiwemo usafirishaji wa dawa za kulevya. Je Chata hiyo inasema nini? Assumpta Massoi na Rashid Malekela wanapitia baadhi ya vifungu pamoja na yaliyojiri baada ya hatua ya Marekani.

san francisco venezuela dunia nicolas maduro pili rais chata umoja makala nchi miaka nguvu mataifa fahamu marekani matumizi miongoni
SBS Swahili - SBS Swahili
Yaliyojiri Afrika:Burundi kuanza kusafirisha madini nje ya nchi ili kuimarisha uchumi

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jan 5, 2026 8:44


Kwa taarifa zaidi elekea katika mitandao yetu ya kijamii au pia tovuti yetu sbs.com.au/swahili.

Siha Njema
Mabadiliko ya tabia nchi yanayovyochochea magonjwa ya milipuko

Siha Njema

Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 10:08


Tafiti zimeonesha kuwa magonjwa mengi ya milipuko haswa barani Afrika yanachochewa na mabadiliko ya tabia nchi Mafuriko ,ukame au kupanda joto yanaweza kusababisha kusambaa kwa haraka kwa vimelea vinavyosababisha magonjwa au kuzaana kwa haraka.

Habari za UN
27 OKTOBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 27, 2025 10:00


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko ya muda mrefu nchini Myanmar, hali ya kibinadamu nchini Sudan kufuatia ripoti za vifo vya raia na wimbi la wakimbizi wa ndani, na masuala ya afya nchini Kenya.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito kwa dunia na mataifa wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kusini-Mashariki mwa Asia, ASEAN kuchukua hatua za haraka kumaliza machafuko ya muda mrefu nchini Myanmar, akisisitiza kuwa mgogoro huo si tishio kwa watu wa Myanmar pekee bali pia kwa amani na usalama wa kanda nzima ya Asia ya Kusini Mashariki.Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) imeelezea wasiwasi mkubwa kufuatia ripoti za vifo vya raia na wimbi la wakimbizi wa ndani, kufuatia kuendelea kwa mapigano makali katika mji wa El Fasher, huko Darfur Kaskazini nchini Sudan. Tupate tarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.Katika kaunti ya Mombasa nchini Kenya, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wa Mastercard Foundation na Serikali ya Kaunti ya Mombasa, imechukua hatua za kukabiliana na mlipuko wa MPOX kwa kutoa huduma muhimu za afya na WASH kwa wagonjwa na waliopona, ikiwa ni pamoja na vifaa vya kujikinga (PPEs), vituo vya kusafisha mikono na ujumbe wa mabadiliko ya tabia za kijamii.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
Guterres: ASEAN chukueni hatua kukomesha ukatili Myanmar

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 27, 2025 2:47


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito kwa dunia na mataifa wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kusini-Mashariki mwa Asia, ASEAN kuchukua hatua za haraka kumaliza machafuko ya muda mrefu nchini Myanmar, akisisitiza kuwa mgogoro huo si tishio kwa watu wa Myanmar pekee bali pia kwa amani na usalama wa kanda nzima ya Asia ya Kusini Mashariki.  Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

Habari za UN
02 OKTOBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 2, 2025 11:08


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika ujumbe wa Omon Ukpoma-Olaiya, Kiongozi wa Uwekezaji wa UNCDF kwa Kanda ya Afrika Mashariki, Kusini na Nchi za Kiarabu. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi neno la wiki.Haiti, hali ya kibinadamu imefika kiwango cha hatari, amesema Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk. Akihutubia Baraza la Haki za Binadamu mjini Geneva, Türk amesema Haiti imefika kiwango cha kulipuka kutokana na ukatili na ukiukwaji Mkubwa wa haki za binadamu. Amesisitiza kuwa  “Tunaweza na lazima kubadili hali hii kwa ajili ya watu wa Haiti,” akiongeza kuwa “bila hatua za haraka hali mbaya zaidi huenda ikaja kwa Haiti na eneo zima.”Tukielekea Mashariki ya Kati huko Gaza, janga la kibinadamiu linaongezeka ambapo mashambulizi yanayoendelea yameathiri vibaya upatikanaji wa chakula na maji. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA, limeripoti kuwa usambazaji wa chakula kilichopikwa kaskazini mwa Gaza umepungua kwa asilimia 70, huku vituo vinne pekee ndivyo vinavyofanya kazi. Takriban watu milioni moja wanapata maji chini ya lita sita kwa siku, kiwango kilicho chini ya hali ya dharura.Nchini Sudan Kamishina Mkuu wa Haki za Binadamu Volker Türk ameonya kuhusu hali katika mji wa El Fasher, Darfur Kaskazin , akisema mji huo “uko kwenye ukingo wa janga kubwa zaidi ikiwa hatua za haraka hazitachukuliwa kulegeza mzingiro wa kijeshi na kuwalinda raia,” huku Kikosi cha Usaidizi wa Haraka (RSF) kikiongeza juhudi za kutwaa mji huo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "USHINZI NA USHENZI"Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

gaza haiti tanzania sudan umoja kanda ocha hii haki kiswahili nchi mataifa oktoba kiongozi shirika afrika mashariki
Habari za UN
Mshikamano wa nchi zinazoendelea kuchagiza SDGs

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 12, 2025 2:46


Leo ni siku ya kimataifa ya ushirikiano baina ya nchi zinazoendelea zikijulikana pia kama nchi za kusini ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa tamko lenye msukumo mkubwa likitambua ustahimilivu, ubunifu, na ushawishi unaoongezeka wa nchi zinazoendelea katika kuleta maendeleo ya kimataifa. Assumpta Massoi anatoa maelezo zaidi.(Taarifa ya Assumpta Massoi)Kwanza kabisa ni vema kufahamu kuwa nchi hizi zinaitwa za kusini, kwa maana kwamba bado ziko nyuma kimaendeleo zikilinganishwa na zile za kaskazini, (ingawa si kijiografia) ambazo zinaonekana kuwa zina maendeleo kiuchumi.Maudhui ya siku hii ni – fursa mpya na ubunifu kupitia ushirikiano wa kusini-kusini na ushirikiano wa pembetatu, ikimaanisha ushirikiano kati ya nchi zinazoendelea, na vile vile mashirika ya kimataifa na nchi zilizoendelea.Sasa katika siku hii ya leo iliyopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 22 mwezi Desemba mwaka 2003 kwa lengo la kusongesha ushirikiano wa kiufundi baina ya nchi zinazoendelea Guterres anasema “katika dunia inayozidi kuwa na nguvu nyingi za ushawishi, nchi zinazoendelea zinaonesha ustahimilivu wa kipekee na ubunifu wa hali ya juu. Sio tu katika kukabiliana na migogoro, bali pia katika kusukuma mbele mageuzi.”Mathalani nchi hizo zinabuni na kubadilishana majawabu bunifu katika maeneo muhimu kama vile kilimo kinachozingatia mabadiliko ya tabianchi, teknolojia rafiki kwa mazingira, fedha za kidijitali, na ubunifu katika sekta ya afya.Amesisitiza kuwa mafanikio haya yanajengwa juu ya misingi ya kuheshimu pande zote, kujifunza kwa pamoja, na lengo la pamoja—ambayo ndiyo misingi ya ushirikiano wa Kusini-Kusini na ule wa pembetatu.Hata hivyo amesisitiza kuwa ushirikiano huu si ishara tu ya mshikamano, bali pia ni nguvu kuu ya maendeleo inayohitajika kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).Amepongeza juhudi za nchi za Kusini katika kuendeleza Ajenda ya 2030, licha ya changamoto zinazoendelea kama vile ukosefu wa usawa wa kiuchumi na mabadiliko ya tabianchi.Vilevile, ametoa wito kwa nchi zilizoendelea kutambua na kutekeleza wajibu wao katika kusaidia juhudi za maendeleo duniani.Katibu Mkuu anasema kuwa “tunatambua pia wajibu wa nchi zilizoendelea katika kushughulikia ukosefu wa usawa unaozidi kuongezeka na kuendeleza maendeleo endelevu.”Katika hitimisho la ujumbe wake, Guterres amehimiza jumuiya ya kimataifa kukumbatia ushirikiano wa nchi za kusini kama kichocheo cha kuhuisha ushirikiano wa kimataifa, akisisitiza haja ya kuchukua hatua kwa pamoja kujenga dunia iliyo jumuishi, yenye usawa, na endelevu kwa wote.Akizungumzia siku hii, , Mkurugenzi wa  Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusika na masuala ya ushirikiano wa nchi za kusini, UNOSSC, Dima Khatib, amesisitiza kuwa nchi za Kusini zinamiliki "uwezo mkubwa wa kuendeleza maendeleo," kwani ndiko makazi ya asilimia 80 ya watu wote duniani na ni chanzo cha ustahimilivu, ubunifu, pamoja na rasilimali watu na asili ambazo hazijatumika kikamilifu.Katika mahojiano mahsusi na Idhaa ya  Umoja wa Mataifa, Bi. Khatib amesema kwamba katikati ya hali ya kisiasa ya kimataifa iliyojaa mvutano ambayo dunia inashuhudia leo, ushirikiano kati ya nchi za kusini unaweza kuwa injini ya kufufua na kuimarisha mfumo wa ushirikiano wa kimataifa.Amepigia chepuo ushirikiano kati ya nchi za kusini na zile za kaskazini akisema, “hakuwezi kuweko na mgawanyiok wa nchi kati ya zile za kaskazini zilizoendelea na zile za kusini zinazohaha kuendelea. Badala yake “lazima tujenge madaraja. Umoja wa Mataifa una uwezo wa kubeba jukumu hili kwa kuwa ni mfumo muhimu ambao unahudumia nchi zote kwa usawa.

SBS Swahili - SBS Swahili
Félicien Kabuga apambana kupata nchi itakayo mpokea badala ya Rwanda

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 12, 2025 7:19


Mshukiwa wa mauaji ya kimbari ya Rwanda, Félicien Kabuga anakabiliana na wakati mgumu kupata nchi itakayo mpokea kwa muda kutoka gereza la The Hague, Uholanzi.

Habari za UN
Kwa mara ya kwanza watoto wenye utipwatipwa duniani ni wengi kuliko wenye utapiamlo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 10, 2025 2:59


Kwa mara ya kwanza idadi ya watoto na vijana wa umri wa kwenda shule wenye unene wa kupindukiaau utipwatipwa imezidi idadi ya watoto wenye utapiamlo duniani ikiathiri watoto milioni 188 sawa na mtoto 1 kati ya kila watoto 10 imesema leo ripoti iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. Tuungane na Leah Mushi kusikia zaidi kuhusu ripoti hiyo, karibu LeahRipoti hii mpya ya UNICEF iitwayo “Faida kwenye vyakula: Jinsi Mazingira ya Chakula yanavyowaangusha watoto” imechambua takwimu kutoka nchi zaidi ya 190 na kubaini kwamba kiwango cha watoto wenye utapiamlo kimepungua tangu mwaka 2000, lakini wale wenye unene wa kupindukia kimeongezeka mara tatu.Kwa sasa, utipwatipwa umeenea katika kila eneo la dunia isipokuwa Afrika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara na Asia Kusini. Nchi za visiwa vidogo vya Pasifiki ndizo zinaongoza kwa kuwa na viwango vya juu zaidi, ikiwemo Niue yenye asilimia 38 ya watoto wenye umri wa miaka 5 hadi 19 wakiwa na unene wa kupindukia.Nini kimesababisha?UNICEF inasema mabadiliko ya mifumo ya lishe kutoka vyakula vya asili hadi vyakula vya kutengenezwa kwa haraka na vya bei nafuu lakini vyenye sukari, mafuta na chumvi nyingi ndiyo chanzo kikuu cha ongezeko hili.Pia inatahadharisha kuwa matangazo ya kidijitali ya vinywaji vyenye sukari na vyakula vya viwandani yanawafikia vijana wengi, hata katika nchi zenye migogoro.Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEF, Catherine Russell, amesema utipwatipwa ni changamoto kubwa  ya kiafya kwa watoto kwa sababu huongeza hatari ya kupata kisukari, shinikizo la damu na magonjwa ya moyo katika maisha ya baadaye.Russell amesema “Tunapozungumza kuhusu utapiamlo, hatuzungumzii tu kuhusu watoto wenye uzito mdogo, utipwatipwa ni changamoto kubwa inayoendelea kuongezeka ambayo inaweza kuathiri afya na maendeleo ya watoto. Vyakula vya viwandani vinazidi kuongezeka na kuchukua nafasi ya matunda, mboga mboga na protini katika wakati ambao lishe ina jukumu muhimu katika ukuaji wa watoto, ukuaji wa utambuzi na afya ya akili.”Nini kifanyike?Ili kukabiliana na hali hii, UNICEF inazitaka serikali kuchukua hatua madhubuti ikiwemo kupiga marufuku uuzaji wa vyakula visivyo na lishe shuleni, kudhibiti matangazo ya vyakula vyenye sukari na mafuta, na kuweka sera za kusaidia familia kupata chakula bora na chenye lishe.Kwa mujibu wa UNICEF, bila hatua za haraka, gharama za kiafya na kiuchumi zitakazotokana na tatizo la utipwatipwa wa utotoni zinatarajiwa kupindukia dola trilioni 4 kila mwaka ifikapo mwaka 2035.Zipo juhudi za kupambana na hali hiyo ambazo zimeanza kuchukuliwa na baadhi ya nchi, mfano mzuri ni Mexico ambayo hivi karibuni imepiga marufuku uuzaji wa vyakula vilivyosindikwa na vile vyenye chumvi, sukari na mafuta mengi katika  maeneo ya shule za umma.

Habari za UN
Türk ataka Israeli ishinikizwe iondoke maeneo inayokalia ya wapalestina

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 28, 2025 1:54


Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu Volker Türk ameyahimiza mataifa yote ulimwenguni kuchukua hatua za haraka ili Israel ikomeshe uwepo wake kinyume cha sheria katika ardhi ya Palestina inayoikalia kimabavu, na kuhakikisha suluhu ya mataifa mawili inapatikana. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah MushiKamishna Turk ameyasema hayo katika tarifa yake aliyoitoa kwa njia ya video kabla ya kuanza kwa mkutano wa ngazi ya juu hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani unaolenga kujadili Suluhu ya kudumu kwa mgogoro kati ya Israel na Palestina ambao umedumu kwa miongo kadhaa sasa.Turk amesema: “Ninahimiza hatua za haraka za Israel kukomesha uwepo wake kinyume cha sheria katika ardhi ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu, na kwa pande zote kufanyia kazi maendeleo yanayoonekana kuelekea suluhu ya Serikali mbili.”Akatoa angalizo kwa zile nchi zitakazo shindwa kuweka shinikizo kwa Israel kukomesha mauaji huko katika Ukanda wa Gaza.“Nchi ambazo zinashindwa kutumia nguvu zao zinaweza kuwa na hatia katika uhalifu wa kimataifa. Kila siku tunaona madhila yasiyoelezeka huko Gaza na Ukingo wa Magharibi kwa hofu na kufadhaika. Kila siku, tunaona uharibifu zaidi, mauaji zaidi, na udhalilishaji zaidi wa Wapalestina.”Mkuu huyo wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa amehitimisha video yake ya dakika 4 na sekunda 7 kwa kusema kuwa dunia itaihukumu mikutano ya aina hii kwa kile inachokifanya kwa vitendo, na kuongeza kuwa ofisi yake iko tayari kusaidia taifa la Palestina katika ujenzi wa nchi yenye msingi wa haki za binadamu na utawala wa sheria, pindi utulivu utakapopatikana.

israel gaza israelis palestina turk umoja kila nchi mataifa serikali mkuu magharibi
Habari za UN
FAO/WFP: Nchi 13 katika ongezeko la njaa, 5 kati ya hizo wanakabiliwa na njaa kali zaidi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 16, 2025 1:56


Ripoti mpya ya pamoja ya Umoja wa Mataifa inaonya kuwa watu katika nchi 5 kati ya nchi 13 zenye njaa kali duniani wako kwenye hatari kubwa ya kukumbwa na njaa kali, vifo na maafa ikiwa msaada wa kibinadamu hautatolewa haraka na juhudi za kimataifa hazitaelekezwa kukomesha migogoro, kupunguza ufurushwaji na kuongeza msaada wa haraka kwa kiwango kikubwa. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

hizo zaidi umoja katika nchi mataifa ripoti
Habari za UN
Ripoti kuhusu Mpox yazitaja nchi 11 za Afrika, Ulaya, China na Amerika nao wamo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 30, 2025 2:03


Maambukizi ya ugonjwa wa mpox kutokana na aina ya virusi vya monkeypox clade Ib /ˈmʌŋ.ki.pɑks kleɪd one bee/ (MPXV) yanaendelea kuripotiwa hasa barani Afrika, ambapo mataifa kumi na moja yameripoti maambukizi ya ndani ya jamii katika kipindi cha wiki sita zilizopita. Hiyo kwa mujibu wa ripoti 51 ya Shrika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO kuhusu hali ya mlipuko wa mpox katika nchi mbalimbali duniani. Anold Kayanda amefuatilia ripoti hiyo na anatufafanulia kwa ufupi. 

china amerika afrika ib mpox umoja afya hiyo nchi wamo mataifa ripoti
SBS Swahili - SBS Swahili
Wangeci "katika hii nchi wanathamini sana watu wenye ujuzi wa kazi za mikono"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Feb 28, 2025 7:43


Wangeci Kones alikuja Australia akiwa na matumaini yakutumia shahada yake ya masoko, katika kazi sawia na alivyo kuwa akifanya nchini Kenya.

SBS Swahili - SBS Swahili
Uchomaji wakitamaduni: kutumia moto kulinda dhidi ya moto na kufufua Nchi

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Feb 18, 2025 15:34


Kuishi katika mazingira yenye moto kama Australia, wengi wetu hupata ugumu waku ona moto kama kitu kingine zaidi yakuwa tisho.

australia moto nchi kuishi
Habari za UN
Kenya tumepiga hatua kuhakikisha maendeleo ya ustawi wa jamii: Mary Wambui Munene

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 14, 2025 4:58


Kikao cha 63 cha Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC kuhusu maendeleo ya ujamii kinakunja jamvi hii leo jijini New York Marekani baada ya majadiliano ya juma zima kuhusu maendeleo ya ustawi wa jamii, hatua zinazochukuliwa nan chi katika kufanikisha hilo na kuchagiza mshikamano wa kimataifa kutimiza lengo. Nchi mbalimbali zimetuma wakilishi kuanzia katika ngazi ya serikali, taasisi, mashirika yasiyo ya kiserikali na asasi za kiraia. Flora Nducha wa Idhaa hii amepata fursa kuzungumza na Mary Wambui Munene, mmoja wa washiriki kutokana Kenya. Ungana nao katika Makala hii

kenya umoja makala baraza jamii nchi hatua maendeleo ungana
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 6 Februari 2025

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Feb 6, 2025 7:01


Nchi zaki Arabu, Umoja wa Mataifa na washirika wakaribu wa Marekani wamekosoa pendekezo la Donald Trump kuchukua ukanda wa Gaza, naku tawanya wa Palestina kuwa hatua hiyo ita yumbisha kanda hiyo na kudhoufisha juhudi zakupata suluhu ya nchi mbili.

SBS Swahili - SBS Swahili
Jaguar "Tunaomba nchi jirani zisaidie kutafuta amani na usalama DRC"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jan 28, 2025 10:51


Milipuko ya mizinga imeitikisa Goma Jumatatu, saa chache baada ya wanajeshi wa Rwanda na wapiganaji kundi la waasi la M23 kuingia mjini humo.

Habari za UN
UN yaahidi kusaidia Wasyria kuiboresha nchi yao

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 9, 2024 1:49


Kufuatia jana Wananchi wa Syria kutwaa madaraka kutoka kwa uongozi uliowatawala kwa mabavu kwa zaidi ya miongo mitano, viongozi wa Umoja wa Mataifa wameendelea kutoa wito wa kuhakikisha mabadiliko haya yanakuwa fursa ya mustakabali bora kwa kuzingatia haki za binadamu, uhuru na haki kisheria. Taarifa iliyoandaliwa na Anold Kayanda inaeleza zaidi.

syria umoja nchi mataifa wananchi
Habari za UN
Miaka 15 ya Mkataba wa Kampala kuhusu wakimbizi wa ndani au IDPs, wito watolewa kwa nchi kuidhinisha na kutekeleza

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 6, 2024 2:06


Katika kuadhimisha miaka 15 tangu kupitishwa kwa Mkataba wa Kampala wa Ulinzi na Usaidizi wa Wakimbizi wa Ndani barani Afrika chini Muungano wa Afrika, Kamishna Mkuu Msaidizi wa Ulinzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, Ruven Menikdiwela na Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu za Wakimbizi wa ndani Paula Gaviria Betancur wametoa kauli ya pamoja ya kupongeza Muungano wa Afrika kwa maono haya ya mbali na pia kuzisihi nchi zote barani Afrika kuutekeleza mkataba huo muhimu. Selina Jerobon na maelezo zaidi.

afrika kampala umoja idps katika nchi miaka mataifa shirika
SBS Swahili - SBS Swahili
Mh JP Mwirigi "ili nchi ipate heshima yake, kuna miundombinu lazima ijenge"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 3, 2024 13:23


Maamuzi ya utoaji wa kandarasi ya ukarabati ya baadhi ya miundombinu, yame iweka serikali ya Kenya chini ya shinikizo kubwa hivi karibuni.

kenya kuna yake nchi heshima
So what you're saying is...
BBC Verify Bias + Labour's Authoritarian Crack Down: Respect Orders To Non - Crime Hate Incidents

So what you're saying is...

Play Episode Listen Later Dec 1, 2024 42:07


Labour's Authoritarian Crack Down: Respect Orders to Non-Crime Hate Incidents + BBC Verify Bias On today's #NCFNewspeak, NCF Director Peter Whittle, Senior Fellows Rafe Heydel-Mankoo and Dr. Philip Kiszely and Amy Gallagher of Stand Up To Woke discuss: * BBC Verify bias exposed: Who will verify BBC Verify? * Labour's new Respect Orders: What are they and should we be worried? * The bizarre list of Non-Crime Hate Incidents. 65 people a day have a NCHI recorded against them.

Habari za UN
Kuna mkwamo kwenye mkutano wa COP29 huku mapendekezo mapya yakitaka nchi tajiri kuzilipa masikini dola bilioni 250 kwa mwaka

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 2:07


Majadiliano ya mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP29 yamekumbwa na mkwamo huko Baku Azerbaijana muafaka haujapatikana. Majadiliano hayo yaliyotarajiwa kukunja jamvi leo sasa yanaendelea kwa kuwekwa mezani mapendekezo mapya kuhusu ufadhili wa mabadiliko ya tabianchi hasa kwa matifa yanayoendelea. Hakika vuta nikuvute bado inaendelea hata sasa washiriki wako mezani kwakikuna vichwa na kujadili mapendekezo mapya. Mkwamo huo umetokana na kushindwa kuafikiana katika masuala kadhaa kubwa likiwa ufadhili wa  mabadiliko ya tabianchi na hususasn kuhusu ni kiasi gani cha fedha nchi zinazoendelea zinapaswa kupokea kila mwaka hadi ifikapo mwaka 2030 na wapi fedha hizo za ufadhili zitatoka.Nchi zinazoendelea zinataka kulipwa dola trilioni 1.3 kwa mwaka lakini hilo halijaafikiwa na mapendekezo mapya yaliyowasilishwa na raia wa mkataba huo wa UNFCCC yanaonyesha tofauti kubwa na safari ndefu ya kufikia muafaka.Kwa mujibu wa mapendekezo hayo mapya yaliyowasilishwa leo mezani na Rais wa COP29 Mukhtar Babayev yanataka nchi zinazoendelea kupokea dola bilioni 250 kwa mwaka hadi kufikia mwaka 2035 kwa ajili ya kuchukua hatua didi ya mabadiliko ya tabianchi.Na maesema “Fedha hizi zitatoka katika vyanzo mbalimbali ikiwemo sekta za umma na za binafsi, na kitaifa na kimataiifa ikiwemo vyanzo mbadala”.Wakati pia COP29 ikitoa wito wa kufikia lengo la ufadhili wa dola trilioni 1.3 ifikapo mwaka 2035 pia imezikaribisha nchi zinazoendelea kutoa michango ya ziada.Kiwango kilichopendekezwa cha ufadhili kinatarajiwa kuzusha vuta ni kuvute katika majadiliano hayo kwa siku nzima ya leo huenda hadi kesho ingawa mkutano huo unahisi ahuweni kwamba kuna kiwango kilichowasilishwa na unataka hitimisho la mkutano haraka iwezekanavyo. Je nchi zinazoendelea zitapokea vipi pendekezo hili jawabu bado halijulikani. Wapenzi wa UN News Kiswahili endeleeni kufuatilia kwenye kurasa zetu kufahamu hatma ya mkutano huo.

Coffee House Shots
Making sense of non-crime hate incidents

Coffee House Shots

Play Episode Listen Later Nov 15, 2024 11:51


The government has announced a review into how to properly police non-crime hate incidents (NCHIs). This follows the experience of Allison Pearson who, on Remembrance Day morning, was doorstepped by Essex Police demanding an interview about a long-forgotten tweet. Reports of NCHIs have dramatically increased in the last year, with 13,200 recorded in the 12 months to June (around 36 a day). What qualifies as an NCHI and how can the police be expected to enforce them? Is this police overreach or a necessary measure to tackle the rise in instances of anti-Semitism and Islamophobia? Oscar Edmondson speaks to James Heale and Danny Shaw, former adviser to Yvette Cooper. Produced by Oscar Edmondson. 

Habari za UN
Nchi zote pamoja na mashirika ya kimataifa ikiwemo UN yanawajibika kukomesha ukaliwaji wa Palestina

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 18, 2024 2:03


Tume hiyo huru imeyasema hayo katika taarifa mpya ya msimamo wa kisheriia iliyotolewa mjini Geneva Uswis kuhusu eneo linalokaliwa la Palestina ikiwemo Jerusalem Mashariki ambayo imeweka wazi maoni ya tume kuhusiana na wajibu wa serikali na jinsi Baraza Kuu na Baraza la Usalama linavyoweza kutambua na kutekeleza mbinu na hatua sahihi zinazohitajika kwa kazi hiyo hadi mwisho wa ukaliwaji huo, na kwa haraka iwezekanavyo.Tume ihiyo imebaini kwamba maoni ya ushauri ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki kuhusu matokeo ya Kisheria yanayotokana na sera na desturi za Israel katika eneo linalokaliwa la Palestina ikiwa ni pamoja na Jerusalem Mashariki ni wenye mamlaka na usio na utata kwa kusema kwamba kuendelea kuwepo kwa Israel katika eneo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu ni kinyume cha sheria na sheria ya kimataifa.Taarifa hiyo ikitolewa Geneva Gaza kwenyenyewe hali inaendelea kuwa tete, kwa mujibu wa Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestinna UNRWA Phillipe Lazzarini, kwani shule nyingine ya UNRWA imeshambuliwa leo Jabalia Kaskazini mwa Gaza, watu kadhaa wameripotiwa kuuawa na miongoni mwao Watoto wengi waliokuwa wakipata hifadhi katika jengo hilo.Lazzarini amesema hili ni shambulio la tatu dhidi ya majengo ya UNRWA kwa wiki moja. Na pia wafanyakazi wa shirika hilo wanaendelea kuuawa sasa wameffikia 231 tangu kuanza kwa vita hii Oktoba mwaka jana.Naye msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF James Elder akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva Uswisi hii leo amesema “Gaza ni mfano halisi wa ulimwengu wa kuzimu duniani kwa watoto milioni moja wa eneo hilo. Na hali inazidi kuwa mbaya, siku baada ya siku, tunapoona athari za kutisha za mashambulizi ya anga ya kila siku na operesheni za kijeshi za Israek kwa watoto wa Kipalestina.”Nalo shirika la kuratibu misaada ya kibinadamu OCHA likiangazia Ukingo wa Magharibi limesema “Vikosi vya Israel vimekuwa vikitumia mbinu mbaya za vita katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, na kuibua wasiwasi mkubwa juu ya matumizi ya nguvu kupita kiasi na kuongeza mahitaji ya kibinadamu ya watu.” Ameelezea wasiwasi kuhusu mashambulizi ya walowezi wa Israel dhidi ya Wapalestina na miti yao ya mizeituni wakati huu wa mavuno ya kila mwaka.

israel gaza palestine palestina unrwa umoja ocha nalo haki naye watoto tume lazzarini pamoja baraza nchi zote mataifa oktoba mkuu kimataifa magharibi mashirika