Podcasts about jifunze

  • 21PODCASTS
  • 124EPISODES
  • 17mAVG DURATION
  • 1EPISODE EVERY OTHER WEEK
  • Dec 19, 2024LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about jifunze

Latest podcast episodes about jifunze

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Ufafanuzi wa neno Akraba

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 19, 2024 0:38


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya neno “AKRABA.”  

Radio Maria Tanzania
Jifunze haya juu ya Dominika ya Tatu ya Maajilio katika Kanisa Katoliki.

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Dec 18, 2024 41:59


Ungana nami Mtangazaji wako Judith Mpalanzi katika Kipindi cha Katekisimu  Katoliki Shirikishi, leo tupo na Padre Leonard Maliva, Paroko wa Parokia ya Isimani na Mkurugenzi wa Utume wa Walei Jimbo Katoliki Iringa, anaendelea kutufundisha juu ya Maajilio. L'articolo Jifunze haya juu ya Dominika ya Tatu ya Maajilio katika Kanisa Katoliki. proviene da Radio Maria.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Ufafanuzi maana ya neno MIDABWADA

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 12, 2024 0:28


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno MIDABWADA” 

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya maneno “MBUKU NA MSUNUNU”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 5, 2024 0:48


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno “MBUKU NA MSUNUNU.” 

Habari za UN
COP29 Georgina Magesa: Watoto wana haki ya kuishi katika mazingira salama

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 20, 2024 4:01


Mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29 unaoendelea huko Baku Azerbaijan umeleta pia watoto na vijana wanaharakati wa mazingiria kutoka kote ulimwenguni na kuwapatia fursa kuketi katika meza moja na viongozi ili kuhakikisha mustakabali wao umewekwa katika ajenda ya mkataba huo. Jukumu lao kama wachechemuzi wa mabadiliko chanya na hitaji la mazungumzo na ushirikiano kati ya vizazi lilitambuliwa rasmi katika matokeo ya Mkutano wa Zama Zijazo, SOTF mnamo Septemba 2024.Georgina Magesa, msichana mwenye umri wa miaka tisa na mwanaharakati wa mazingira, ambaye amewakilisha watoto wenzake kutoka Tanzania katika Mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29 huko Baku, Azerbaijan. Anatoa ujumbe mahsusi akianza kwa kusistiza kuwa watoto pia wana mchango katika kutatua changamoto za mabadiliko ya tabianchi.“Watoto wenzangu duniani kote, nyie pia mnaweza kuleta mabadiliko chanya. Anza na hatua ndogo pia muwe na ndoto kubwa. Panda miti. Hifadhi maji. Jifunze kuhusu mazingira yetu. Kwa Pamoja vitendo vyetu vidogo vitageuka mabadiliko makubwa”Katika mwaka huu wa 2024 ambao viwango vya joto duniani vimevunja rekodi duniani, watoto na vijana wanaendelea kupaza sauti zao wakihimiza viongozi wa dunia kuchukua hatua za haraka zinazohitajika ili kushughulikia janga la mabadiliko ya tabianchi. Georgina anasema Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF liko mstari wa mbele, lakini sasa ni wakati wa mshikamano kwa ajili ya mazingira bora kwa watoto wa leo, na wa zama zijazo..“Kwa viongozi wa dunia walioko hapa leo, hii si kazi ya UNICEF pekee. UNICEF inafanya kazi nzuri na sisi watoto, lakini tunahitaji msaada wako ili kujenga ulimwengu wa kesho ambapo hakuna mtoto anayepaswa kuchagua kati ya afya na elimu yake; ambapo hakuna mtoto anayekunywa maji yasiyo salama; hakuna mtoto anayekosa shule kwa sababu ya masuala yanayohusiana na mabadiliko ya tabianchi; na ambapo kila mtoto ana nafasi ya kuwa na afya bora na elimu bora.”Georgina anatamatisha kwa kusisitiza kuwa janga la mabadiliko ya tabianchi limenyima watoto haki zao hivyo kwa kila mtu...“Kumbuka unapolinda mazingira unalinda afya, elimu na ndoto za watoto. Mtoto mwenye afya bora na elimu bora anaweza kubadilisha ulimwengu.”Ama kweli watoto wana haki ya kuishi katika mazingira salama!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili - Ufafanuzi wa maneno “MADHALI, WAMA, FALAU NA HOBE”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 14, 2024 1:05


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno “MADHALI, WAMA, FALAU NA HOBE” 

Habari za UN
Jifunze Kiswahili - Ufafanuzi wa neno HEREREZA na Dkt. Mwanahija Ali Juma

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 31, 2024 0:37


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno HEREREZA! 

Habari za UN
Jifunze Kiswahili - maana ya neno HEKEMUA!

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 24, 2024 0:22


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno HEKEMUA!  

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Ufafanuzi wa methali “Mapenzi ni kikohozi hayawezi kufichika.”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 10, 2024 1:01


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu hii leo ni Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia maana ya methali “Mapenzi ni kikohozi hayawezi kufichika.”

Habari za UN
Jifunze Kiswahili - Maana ya neno “NGEJA”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 3, 2024 1:03


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo fursa ni yake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “NGEJA”

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Ufafanuzi wa methali “Mke ni nguomgomba ni kupalilia”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 19, 2024 1:12


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia maana ya methali “Mke ni nguomgomba ni kupalilia.”

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno “KILIWAZO”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 12, 2024 0:57


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo fursa ni yake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “KILIWAZO”.

SBS Swahili - SBS Swahili
#39 Kuwasilisha marejesho yako ya ushuru | Vidokezo vyakudai gharama (Adv)

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 9, 2024 17:25


Jifunze jinsi yakuzungumza kuhusu marejesho ya ushuru. Pia jua jinsi punguzo ya ushuru inaweza kusaidia kupunguza bili yako ya ushuru.

yako jifunze
Habari za UN
JIFUNZE KISWAHILI: TAFSIRI YA NENO LINK

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 30, 2024 0:58


Maendeleo ya teknolojia hasa kwenye mitandao ya kijamii yamesababisha kushamiri kwa matumizi ya neno la kiingereza link. Baadhi  ya watu wanalitohoa lakini Idhaa ya  Umoja wa Mataifa imemuuliza Mhadhiri Mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa Tanzania, BAKITA ni nini tafsiri sahihi ya neno link kwa lugha ya kiswahili.

SBS Swahili - SBS Swahili
#3 Kuzungumza kuhusu asili zakitamaduni| Jan 26 (Australia Day)

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Aug 27, 2024 12:53


Jifunze jinsi yakuzungumza kuhusu historia ya utamaduni wako. Pia jua kwa nini Australia Day inaendelea kuwa siku ya maandamano kwa wa Australia wa kwanza.

SBS Swahili - SBS Swahili
#66 Maswali yaku uliza unapo tazama nyumba unayo taka kodi

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Aug 21, 2024 17:49


Jifunze jinsi yaku uliza maswali, unapo tazama nyumba unayo tarajia ku kodi.

taka kodi yaku nyumba jifunze maswali
Dr Boaz Mkumbo
Jifunze kupunguza kitambi bila dawa

Dr Boaz Mkumbo

Play Episode Listen Later May 4, 2024 11:14


karibu sana NSAMBO HEALTHCARE kupata huduma za matibabu kwa magonjwa ya lishe  ikiwemo Ugumba, mvurugiko wa Homoni na ukosefu wa hisia za tendo la ndoa, kisukari, shinikizo la damu, kitambi na uzito mkubwa n.k. Huduma zetu NSAMBO HEALTHCARE ni kuazia saa nne asubuhi mpaka saa kumi na moja jioni au weka miasi ya kuonana na daktari kwa kupiga simu namba 0767 030 160 . Karibu kuagiza chakula ambacho kimepikwa kwa kuzingatia muongozo wa sayansi ya mapishi, chakula hiki kinamfaa mtu yoyote mwenye magonjwa ya lishe na yule anayependa kula kiafya. Agiza chakula kwa kupiga simu namba 0787 999 994 . Jiunge na programu ya kupunguza kitambi na uzito mkubwa ya NHC WAEIGHTLOSS BOOT CAMP Fuata Taratibu hizi za Malipo ili kujiunga. TIGO PESA LIPA NO: 7780779 MPESA LIPA NO: 5567920 JINA: HEALTHY EATING COMPANY LIMITED Ukisha Lipia Nitumie SMS, EMAIL na MAJINA YAKO kwenye meseji Moja usajili Uanze Leo na Masomo Utumiwe Leo Leo. Namba ya Whatsapp Ya Kutuma Taarifa zako: 0767 030 160 AU WASILIANA NASI SIMU: +255767 074 124 +225787 999 994     Usisahahu KUSUBCRIBE kwa elimu zaidi kuhusu magonjwa ya lishe kama vile KISUKARI KITAMBI NA UZITO MKUBWA SHINIKIZO LA DAMU (PRESHA) MVURUGIKO WA HOMONI UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME TEZI DUME MAGONJWA YA GOITA   Tufuatilie katika mitandao ya kijamii INSTAGRAM https://www.instagram.com/sayansiyama... https://www.instagram.com/nsambohealt... FACEBOOK https://www.facebook.com/drboazmkumboMD BLOG https://blog.heaprogram.co.tz/ WEBSITE https://heaprogram.co.tz/ http://nsambohealthcare.tilda.ws/

Dr Boaz Mkumbo
Chakula kinawezaje kuleta magonjwa ya lishe? jifunze hapa

Dr Boaz Mkumbo

Play Episode Listen Later Oct 5, 2023 2:03


Katika epsod hii utajifunzza juu ya uhusiano wa chakula unachokula kinavyoweza kukusababishia magonjwa ya lishe   kitabu cha sayansi ya mapishi ni kitabu kinachotoa muongozo wa lishe bora na kukusaidia kubadilisha  jiko lako kuandokana na magonjwa ya lishe. kwa mahitaji ya nakala ya kitabu cha sayansi ya mapishi wasiliana nasi kwa simu namba  Jiunge na programu ya kupunguza kitambi na uzito mkubwa ya NHC WAEIGHTLOSS BOOT CAMP Fuata Taratibu hizi za Malipo ili kujiunga. TIGO PESA LIPA NO: 7780779 MPESA LIPA NO: 5567920 JINA: HEALTHY EATING COMPANY LIMITED Ukisha Lipia Nitumie SMS, EMAIL na MAJINA YAKO kwenye meseji Moja usajili Uanze Leo na Masomo Utumiwe Leo Leo. Namba ya Whatsapp Ya Kutuma Taarifa zako: 0767 030 160 AU WASILIANA NASI SIMU: +255767 074 124 +255787 999 994   Usisahahu KUSUBCRIBE kwa elimu zaidi kuhusu magonjwa ya lishe kama vile KISUKARI KITAMBI NA UZITO MKUBWA SHINIKIZON LA DAMU (PRESHA) MVURUGIKO WA HOMONI UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME TEZI DUME MAGONJWA YA GOITA   Tufuatilie katika mitandao ya kijamii INSTAGRAM https://www.instagram.com/sayansiyama... https://www.instagram.com/nsambohealt... FACEBOOK https://www.facebook.com/drboazmkumboMD BLOG https://blog.heaprogram.co.tz/ WEBSITE https://heaprogram.co.tz/ http://nsambohealthcare.tilda.ws/  

Dr Boaz Mkumbo
Je wajua elimu ya afya ya uzazi? jifunze hapa

Dr Boaz Mkumbo

Play Episode Listen Later Sep 2, 2023 1:58


katika epsod hii, utajifunza elimu ya afya ya uzazi kwa mwanaume na mwanamke  ili kujikinga na magonjwa au changamoto za uzazi kama vile ugumba, ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa, maumivu makali wakati wa hedhi, kukosa hedhi kwa muda mrefu n.k Jiunge na programu ya kupunguza kitambi na uzito mkubwa ya NHC WAEIGHTLOSS BOOT CAMP Fuata Taratibu hizi za Malipo ili kujiunga. TIGO PESA LIPA NO: 7780779 MPESA LIPA NO: 5567920 JINA: HEALTHY EATING COMPANY LIMITED Ukisha Lipia Nitumie SMS, EMAIL na MAJINA YAKO kwenye meseji Moja usajili Uanze Leo na Masomo Utumiwe Leo Leo. Namba ya Whatsapp Ya Kutuma Taarifa zako: 0767 030 160 AU WASILIANA NASI SIMU: +255767 074 124 +225787 999 994     Usisahahu KUSUBCRIBE kwa elimu zaidi kuhusu magonjwa ya lishe kama vile KISUKARI KITAMBI NA UZITO MKUBWA SHINIKIZON LA DAMU (PRESHA) MVURUGIKO WA HOMONI UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME TEZI DUME MAGONJWA YA GOITA   Tufuatilie katika mitandao ya kijamii INSTAGRAM https://www.instagram.com/sayansiyama... https://www.instagram.com/nsambohealt... FACEBOOK https://www.facebook.com/drboazmkumboMD BLOG https://blog.heaprogram.co.tz/ WEBSITE https://heaprogram.co.tz/ http://nsambohealthcare.tilda.ws/  

Dr Boaz Mkumbo
unajua kama kitambi niugonjwa wa homoni? jifunze hapa

Dr Boaz Mkumbo

Play Episode Listen Later Aug 8, 2023 5:13


katika epsodi hii utajifunza juu ya ugonjwa kitambi na njia rahisi ya kupunguza kitambi na uzito mkubwa itakayokupa matokeo mazuri ndani ya muda mfupi. Jiunge na programu ya kupunguza kitambi na uzito mkubwa ya NHC WAEIGHTLOSS BOOT CAMP Fuata Taratibu hizi za Malipo ili kujiunga. TIGO PESA LIPA NO: 7780779 MPESA LIPA NO: 5567920 JINA: HEALTHY EATING COMPANY LIMITED Ukisha Lipia Nitumie SMS, EMAIL na MAJINA YAKO kwenye meseji Moja usajili Uanze Leo na Masomo Utumiwe Leo Leo. Namba ya Whatsapp Ya Kutuma Taarifa zako: 0767 030 160 AU WASILIANA NASI SIMU: +255767 074 124 +225787 999 994     Usisahahu KUSUBCRIBE kwa elimu zaidi kuhusu magonjwa ya lishe kama vile KISUKARI KITAMBI NA UZITO MKUBWA SHINIKIZON LA DAMU (PRESHA) MVURUGIKO WA HOMONI UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME TEZI DUME MAGONJWA YA GOITA   Tufuatilie katika mitandao ya kijamii INSTAGRAM https://www.instagram.com/sayansiyama... https://www.instagram.com/nsambohealt... FACEBOOK https://www.facebook.com/drboazmkumboMD BLOG https://blog.heaprogram.co.tz/ WEBSITE https://heaprogram.co.tz/ http://nsambohealthcare.tilda.ws/      

Habari za UN
Jifunze Lugha ya Kiswahili: Neno "NDEKWA"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 3, 2023 0:24


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ally Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Zanzibar, BAKIZA anatufafanualia maana ya neno “NDEKWA”.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Neno "TATABISI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 22, 2023 0:01


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo tunafafanuliwa maana ya neno "TATABISI" na mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA.

Swahili with Stacey
Greetings || Salamu na Maamkuzi Part II

Swahili with Stacey

Play Episode Listen Later Jun 20, 2023 12:12


Learn new and common ways to greet others in Swahili. | Jifunze jinsi ya kuamkua na kusalimu watu. To follow along go to: https://www.buymeacoffee.com/p/1944143

swahili jifunze
Habari za UN
Jifunze kiswahili: Je, wajua maana ya neno "KUYEYESA"?

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 15, 2023 0:01


Leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili tunafafanuliwa maana ya neno "KUYEYESA" na mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, BAKITA, karibu!

Swahili with Stacey
Greetings || Salamu na Maamkuzi Part I

Swahili with Stacey

Play Episode Listen Later Jun 10, 2023 16:48


Learn how to say hello to different people at different times. || Jifunze kuamkua watu katika nyakati tofauti. To follow along go to: https://www.buymeacoffee.com/p/1819856

jifunze
Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Uchambuzi wa neno, "RUWI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 8, 2023 0:55


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo tunafafanuliwa maana ya neno "RUWI" na mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, BAKITA, Karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: "Mama ni Mama Hata Kama ni Rikwama"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 1, 2023 0:02


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili Dkt. Mwanahija Ally Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili visiwani Zanzibar, BAKIZA anachambua methali: Mama ni Mama Hata Kama ni Rikwama! 

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Ufafanuzi wa neno "KONGO"

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 11, 2023 0:47


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo tunapata ufafanuzi wa neno "KONGO" kutoka kwa mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA.

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية
Muziki safarini, jifunze kutumia vyema ulimi wako

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية

Play Episode Listen Later Apr 29, 2023 29:00


Kumtukuza Mungu kwa muziki mtulivu wa kikristo, usijitamkie na kujitabiria mambo mabaya

wako muziki jifunze
Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "NDUI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 27, 2023 0:57


Katika kujifunza Kiswahili, leo tunapata ufafanuzi wa neno "NDUI" kutoka kwa mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, BAKITA. 

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: "KITENDAWILI NI NINI."

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 20, 2023 0:02


Katika kujifunza Lugha ya Kiswahili leo tunaye Mwenyekiti wa idara za Kiswahili katika vyuo vikuu Afrika Mashariki Aida Mutenyo akiwa Kampala Uganda anatufafanulia "KITENDAWILI NI NINI."

Habari za UN
Jifunze kiswahili - Methali: "Mshale kwenda msituni haukupotea"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 6, 2023 0:01


Katika kujifunza Lugha ya Kiswahili leo mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia methali isemayo “Mshale kwenda msituni haukupotea.” Karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Kongamano za Idhaa za Kiswahili Duniani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 30, 2023 0:57


Katika Jifunze Kiswahili Profesa Aldin Mutembei  Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kigoda cha Kiswahili cha Mwalimu Nyerere hivi karibuni nilipokutana naye visiwani Zanzibar Tanzania ambako kulifanyika Kongamano za Idhaa za Kiswahili Duniani, alinidokeza kuhusu jitihada wanazozifanya ili kuwashawishi viongozi wa Bara la Afrika hususani wa Afrika Mashariki kuanza kutumia lugha ya Kiswahili katika hotuba zao wanapokuwa katika majukwaa makubwa ya kimataifa mathalani Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. 

Habari za UN
Jifunze Lugha ya Kiswahili: HAKIBIZA

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 23, 2023 0:01


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo tunapata ufafanuszi wa neno "HAKIBIZA" kutoka kwa mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, BAKITA.

Habari za UN
Jifunze lugha ya Kiswahili: Tofouti ya maneno Yeyote na Yoyote

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 16, 2023 0:01


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili tuaelekea visiwani Zanzibar nchini Tanzania ambako mchambuzi wetu Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Zanzibar, BAKIZA anafafanua matumizi ya maneno Yeyote na Yoyote, karibu!

Habari za UN
Jifunze Lugha ya Kiswahili: MANYEZI

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 9, 2023 0:01


Katika kujifunza Kiswahili, leo tukipata ufafanuzi wa neno "MANYEZI" kutoka kwa mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, BAKITA, karibu!

Habari za UN
Jifunze Lugha ya Kiswahili: MBWANDA

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 23, 2023 0:01


Katika kujifunza Lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa Tanzania, BAKITA anafafanua neno MBWANDA.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: SAKARANI

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 16, 2023 0:50


Leo katika kujifunza Kiswahili tunapata ufafanuszi wa neno "SAKARANI" na mtaalam wetu ni Onni Sigalla Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, BAKITA.

Habari za UN
02 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 2, 2023 0:12


Hii leo katika Jarida tunakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa Kina na Jifunze lugha ya Kiswahili.Katika Habari kwa Ufupi Leah Mushi anamulika ziara ya Papa Francis nchini DR Congo na wito wake kwa vijana na viongozi wa dini kukataa rushwa. Halikadhalika anamulika maeneo oevu na umuhimu wake bila kusahau nchini Sudan Kusini ambako Umoja wa Mataifa unaendelea kutoa misaada kwa familia zilizokimbia kutoka katika eneo la Pibor.Mada kwa Kina inamulika mmea aina ya Azolla, hili ni gugu maji na ni kwa vipi nchini Tanzania limeanza kuchangamkiwa na vijana katika kujiongezea kipato.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ni msemo ya kwamba sikio halilali njaa.Karibu na mwenyeji wako ni Anold Kayanda.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili - msemo, "Funga Funganya"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 12, 2023 0:50


Katika kujifunza Kiswahili, leo mtaalam wetu  Onni Sigalla Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania, anatufafanulia maana ya msemo "FUNGA FUNGANYA", karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili - Msemo: "FANYA ILHAM"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 5, 2023 0:58


Katika kujifunza Kiswahili mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa  nchini Tanzania , anatufafanulia maana ya msemo "FANYA ILHAM". Karibu! 

Habari za UN
JIFUNZE KISWAHILI: METHALI - "USISHINDANE NA KARI KARI NI MJA WA MUNGU"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 15, 2022 0:01


Katika kujifunza kiswahili tutasikia maana ya methali “USISHINDANE NA KARI, KARI NI MJA WA MUNGU”na mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani. Anaanza kwa kusema kari ni neno linalotokana na neno "karima" au "karama", ambalo linamaanisha zawadi au kipawa maalum kutoka kwa mwenyezi Mungu, ama kweli usishindane na mwenzako, tosheka na kari yako maana yote yatoka kwake mwenyezi Mungu!

Habari za UN
JIFUNZE KISWAHILI: Misemo - 'Ndoa imejibu', 'Andaa meza'

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 1, 2022 0:01


Hii leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi katika Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anaeleza maana ya misemo na anachambua misemo miwili; 'andaa meza' na 'ndoa imejibu." Karibu

Habari za UN
JIFUNZE KISWAHLI: Paka hakubali kulala chali

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 20, 2022 0:41


Hii leo katika kujifunza lugha ya kiswahili tunakwenda Zanzibar nchini Tanzania ambako Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, BAKIZA Dkt. Mwanahija Ali Juma anachambua methali isemayo "Paka hakubali kulala chali." Karibu!

Habari za UN
JIFUNZE KISWAHILI: Buga, Boga, Tama- Ndege asili ya Buga kufugwa hawezekani...

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 29, 2022 0:01


Na sasa ni kujifunza lugha ya Kiswahili mchambuzi wetu Dkt. Mwanahija Ali Juma Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, BAKIZA, anachambua msemo kutoka kwenye wimbo RAHA wake Zuchu kutoka Tanzania usemao Ndege asili ya buga kufugwa hawezekani atenda tafuta boga japo tama li bandani.

Habari za UN
JIFUNZE KISWAHILI : Mzishi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 22, 2022 0:52


Leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi wa Baraza la Kiswahili Taifa Tanzania, BAKITA, anafafanua maana ya neno Mzishi, akisema katika hali ya msiba ndio kuna mzishi. Huyu ni ndugu au jamaa anayeshughulikia mazishi ya mtu. Mzishi anashughulikia mazishi ya mtu na ni mtu ambaye anaweza kuwa karibu na mtu wakati wa shida na raha.

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Fahamu maana ya neno Mustakabali

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 15, 2022 0:47


Je wafahamu maana ya neno Mustakabali na matumizi yake kwenye sentensi? Basi ungana na Josephat Gitonga, Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu Nairobi, Kitivo cha Tafsiri na Ukalimani jijini Nairobi nchini Kenya.

Habari za UN
Jifunze Kiswahil: Methali- Ukipewa shubiri, usichukue pima

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 23, 2022 0:51


Habari za UN
JIFUNZE KISWAHILI-METHALI: Asiye na kitoweo humangiria

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 11, 2022 1:17


Hii leo katika kujifunza lugha ya kiswahili, Josephat Gitonga  Mhadhiri wa Chuo Kikuu Nairobi nchini Kenya katika Kitivo cha Ukalimani anafafanua maana  ya methali, Asiye na kitoweo hurumangia.

Habari za UN
Jifunze kiswahili- Neno: Shake

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 4, 2022 1:04


Hii leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu Onni Sigalla ambaye ni Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA, anafafanua maana ya neno, shake. Anasema shake ni ile hali anayokuwa nayo mtu kama vile furaha au huzuni ya kupitiliza lakini haionekani usoni mwake. Mtu analia kwa kwikwi bila kutoa sauti.