Podcasts about HII

  • 233PODCASTS
  • 2,098EPISODES
  • 14mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • Feb 27, 2026LATEST

POPULARITY

20192020202120222023202420252026

Categories



Best podcasts about HII

Show all podcasts related to hii

Latest podcast episodes about HII

Habari za UN
27 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 27, 2026 10:39


Hii leo jaridani tunaangazia haki za wanawake, na uhuru wa kiraia, ujumbe wa Bi Cindy McCain, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa WFP, na ripoti ya IPC kuhusu njaa nchini Somalia.Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu Volker Türk ameonya kuwa shinikizo linaongezeka duniani kote dhidi ya haki za wanawake, uhuru wa kiraia na taasisi za kimataifa akitoa wito kwa serikali kujitolea upya katika ushirikiano, uwajibikaji na utawala wa sheria.Kiongozi wa shirika kubwa zaidi la msaada wa chakula duniani ametangaza kujiuzulu. Bi. Cindy McCain, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP amesema atajiuzulu wadhifa wake huo  baada ya miezi mitatu ili kuzingatia afya yake, akisema bado hajapona kikamilifu baada ya kupata kiharusi mwaka jana 2025.Fundi wa magari mwanamke kutoka nchini Ethiopia anayehudumu na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini, UNMISS, Meja Tigist Ferede ametunukiwa nishani ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, kwa kusimamia jukumu muhimu la wanawake katika operesheni za kulinda amani nje ya kushika bunduki.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

ethiopia bi somalia ipc wfp umoja hii haki fundi cindy mccain wanawake mataifa unmiss kiongozi shirika ujumbe sudan kusini
Habari za UN
26 FEBRUARY 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 26, 2026 12:06


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania ambako UNHCR inasema ufadhili endelevu na wa uhakika unahitajka ili kuendeleza ulinzi wa wakimbizi na kusaidia urejeaji na ujumuishaji wa raia wanaorudi nchini Burundi. Pia tunakuletea jifunze Kiswahili.Ushirikiano wa kimataifa kupitia mikataba ya kimataifa ya kudhibiti dawa umesaidia watu duniani kote, imesema hii leo Bodi ya Kimataifa ya kudhibiti dawa za kulevya, INCB wakati ikizindua ripoti ya mwaka 2025 kuhusu hali yad awa za kulevya duniani.Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu wamelaani vikali ukatili unaodaiwa kufanywa na kundi la waasi la M23 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, dhidi ya watetezi wa haki za binadamu katika majimbo ya  Kivu Kaskazini na Kivu Kusini mashariki mwa taifa hilo la Maziwa Makuu.Na leo ikiwa ni siku ya tatu ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) huko The Hague Uholanzi kuthibitisha iwapo kuna ushahidi wa kutosha wa kumfikisha mahakamani Rais wa zamani wa Ufilipino Rodrigo Duterte kwa madai ya uhalifu dhidi ya ubinadamu unaohusianana kile kilichoitwa “vita dhidi ya dawa za kulevya” nchini mwake, wakili upande wa utetezi, Nicholas Kaufmann amesema hakuna uhusiano uliothibitishwa kati ya hotuba zake za “kipekee, zenye kauli kali” na mauaji anayotuhumiwa kuyafanya.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “ANUIAYE KUKUTUKANA HAKOSI MATANGO”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!

kenya congo tanzania nairobi burundi drc unhcr rais m23 bodi umoja hii kiswahili dkt jamhuri mataifa kimataifa kidemokrasia chuo kikuu
Luli y Nabi
Dos misterios: La esfera de Buga y el hundimiento del Titanic

Luli y Nabi

Play Episode Listen Later Feb 24, 2026 54:54 Transcription Available


Si nos quieres apoyar a seguir creando este podcast, lo puedes hacer aquí: Get more from Luli y Nabi on Patreon

Defense & Aerospace Report
Defense & Aerospace Daily Podcast [Feb 23, 2026] Look Ahead w/ Byron Callan

Defense & Aerospace Report

Play Episode Listen Later Feb 23, 2026 35:01


On today's Look Ahead program, sponsored by HII, Byron Callan of the independent Washington research firm Capital Alpha Partners joins Defense & Aerospace Report Editor Vago Muradian to discuss defense industrial implications of the Supreme Court's rulings against most of President Trump's tariffs and his reaction to impose an additional 15 percent tariff across the board; prospect the administration will retaliate against European nations that shift rapidly increasing spending away from US weapons in favor of domestic ones; Canada's new defense strategy; consequences of a possible Iran attack and Britain's decision to deny US forces use of bases in UK and Diego Garcia; analysis of Russia's war on Ukraine as the conflict enters its fifth year; a changing competitive US defense industrial landscape; and a look at the week ahead.

Habari za UN
20 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 20, 2026 11:34


Hii leo jaridani tunaangazia athari ya baa la nja nchini Somalia, kampeni ya chanjo la polio nchini Malawi, na juhudi za UNMISS nchini Sudan Kusini za kuwapatia hifadhi na lishe watoto yatima huko Juba.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP limesema hali ya upatikanaji wa chakula nchini Somalia imefikia hatua mbaya ambapo watu milioni 4.4 hivi sasa wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula na kwamba ni mtu 1 tu kati ya 7 ndiye anayepata mgao wa chakula.Takribani watoto milioni 1.3 nchini Malawi wamepatiwa chanjo ya polio katika kampeni maalum ya siku nne, kufuatia kugunduliwa kwa mgonjwa mpya wa polio mwishoni mwa mwezi Januari 2026. Huyu ni mgonjwa wa kwanza kuripotiwa tangu mwaka 2022, wakati virusi vya polio pori vilivyokuwa na uhusiano wa kijenetiki na mlipuko ulioripotiwa nchini Pakistan vilipobainika.Sudan Kusini ambako mizozo inaendelea kuvuruga utoto wa watoto, kituo kidogo cha watoto yatima katika mji Mkuu Juba kinawapa makumi ya watoto walio hatarini si tu makazi, bali pia matumaini, uponyaji, na nafasi ya kujenga upya mustakabali wao. Anold Kayanda na taarifa zaidi.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

pakistan somalia malawi juba umoja hii afya mataifa unmiss shirika sudan kusini
Habari za UN
19 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 19, 2026 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina tukimsikia Barbara Batte Guevara, Mkufunzi anayefundisha lugha ya Kiswahili katika Chuo Kikuu cha Havana nchini Cuba. Kwa kushirikiana na Tanzania chuo hicho ambacho mwezi uliopita kimetimiza miaka 298 tangu kuanzishwa kwake, hivi karibuni kimetoa fursa kwa Wacuba kujifunza lugha ya Kiswahili.Anold Kayanda wa Idhaa hii amemtembelea Profesa Barbara Batte katika jiji la Havana nchini Cuba ili kufahamu zaidi kuhusu hatua hii na mafanikio yaliyofikiwa hadi kufikia sasa. Pia tunakuletea habari kwa ufupi kama zifuatazo.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito wa kuanzishwa kwa Mfuko wa Kimataifa wa Akili Mnemba au AI wenye thamani ya dola bilioni 3, ili kuhakikisha teknolojia hiyo inawanufaisha watu wote duniani, badala ya kuwa mali ya mataifa machache au kampuni chache zenye nguvu. Akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa wa kujadili Athari za AI huko New Delhi nchini India, Guterres amesema mustakabali wa AI unapaswa kujengwa kwa ushirikiano wa kimataifa”.Mashambulizi makali yanayoendelea kufanywa na Israeli dhidi ya maeneo ya Palestina ya Gaza na Ukingo wa Magharibi ambayo inakalia kimabavu yanatia hofu ya uwezekano wa utokomezaji wa kabila, imesema Ripoti mpya ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR), ya kuanzia Novemba 1 2024 hadi Desemba 31 2025. Ripoti inasema mashambulizi ya Israeli yameweka mazingira ambamo kwamo wapalestina kama kundi watashindwa kuendelea kuishi Gaza huku Ajith Sunghay, Mkuu wa Ofisi ya OHCHR Palestina akisema, “ripoti inachambua  mwenendo wa mapigano ya jeshi la Israeli, linaloendelea kuua idadi kubwa ya raia, kusababisha njaa, kuwahamisha takribani wakazi wote wa Gaza, tena zaidi ya mara moja — na kuharibu miundombinu iliyosalia ya kiraia ya Gaza.”wanamgambo wa vikosi vya Rapid Support Forces (RSF) nchini Sudan walitekeleza kampeni iliyoratibiwa ya uharibifu dhidi ya jamii zisizo za kiarabu ndani ya mji wa El-Fasher na viunga vyake, kampeni yenye viashiria vya mauaji ya kimbari, imeeleza ripoti mpya iliyotolewa leo na Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya Kuchunguza Ukweli kuhusu Sudan. Ripoti imetaja vitendo hivyo ni pamoja na kuua wanachama wa kundi la kikabila linalolindwa; kusababisha madhara makubwa ya kimwili na kiakili; ambavyo ni vipengele muhimu vya kosa la mauaji ya kimbari chini ya sheria za kimataifa.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili tunawasikiliza baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Havana wanaojifunza lughaya Kiswahili. Tuanze na Yibran Nunez Batte.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

ai cuba gaza israelis tanzania sudan havana palestina new delhi guterres umoja hii haki kwa kiswahili mataifa mkuu novemba mkutano kimataifa ripoti magharibi desemba chuo kikuu
Habari za UN
18 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 18, 2026 12:01


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya Akili Mnemba na wabunifu wa maudhui duniani kwa lugha, waumini wa dini ya kiislamu wakati huu wa Ramadhani katika ukanda wa Gaza, na matibabu ya kwanza ya ugonjwa wa kichocho huko Mwanza nchini Tanzania.Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, limesema wabunifu wa maudhui duniani kwa lugha ya kiingereza content creators wanakabiliwa na hatari ya kupoteza hadi asilimia 24 ya mapato yao ifikapo mwaka 2028 kutokana na kasi ya maendeleo ya Akili Mnemba, au AI.Waumini wa dini ya kiislamu duniani kote wameanza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, kipindi kinachoambatana na sio tu ibada bali pia mlo kama vile futari na daku. Hata hivyo kwa wakazi wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na kimabavu na Israeli hali si hali kwani mlo na mengine yanayoambatana na kipindi hiki vinasalia kuwa ndoto.Serikali ya Tanzania na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo UNDP kupitia Ushirikiano wa Upatikanaji na Ufikishaji wa Huduma (ADP), inaendesha mpango wa majaribio wa kihistoria katika mikoa ya Simiyu, Mwanza, na Kigoma ili kutoa matibabu ya kwanza ya ugonjwa wa kichocho yaliyoandaliwa mahususi kwa ajili ya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.Mwenyeji wako ni Anold Kyanda, karibu!

Defense & Aerospace Report
Defense & Aerospace Daily Podcast [Feb 17, 2026] Look Ahead w/ Byron Callan

Defense & Aerospace Report

Play Episode Listen Later Feb 17, 2026 31:55


On today's Look Ahead program, sponsored by HII, Byron Callan of the independent Washington research firm Capital Alpha Partners joins Defense & Aerospace Report Editor Vago Muradian to discuss takeaways from the Munich Security Conference; what transatlantic cooperation will look like as Europe works to decouple from its historic dependence on the United States; Canada's new defense industrial strategy from buying 75 percent of its weapons from the United States to directing 70 percent of military purchases to domestic firms with the goal of increasing exports to 50 percent; outlook for reconciliation 2.0 as President Trump abruptly opposes the funding maneuver; what Amentum, Parsons and SAIC say about the future of the services market; Mike Cadenazzi, the assistant secretary of defense for industrial base, addresses the Hudson Institute; and a look at the week ahead.

Habari za UN
17 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 17, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania, ambako Magonjwa ya kimeta, miguu na midomo yanayokumba mifugo kama vile ng'ombe pamoja na mdondo unaoshambulia kuku yameendelea kuwa mwiba duniani na hata nchini Tanzania, ambako mbinu mbali mbali zimekuwa zikitumika kuyadhibiti ili kunusuru afya ya mifugo.Uchambuzi mpya kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) na HRP, ambao ni mpango wa taasisi za Umoja wa Mataifa za utafiti kuhusu uzazi wa binadamu, unaonesha kuwa takribani theluthi mbili ya vifo vya wajawazito duniani hutokea katika nchi zilizoathiriwa vibaya na migogoro au zenye udhaifu wa mifumo, ambapo ujauzito ni hatari mara tano zaidi ikilinganishwa na nchi zilizo thabiti.Vita vya Ukraine vikielekea kuingia katika mwaka wa tano, zaidi ya theluthi moja ya watoto wa Ukraine bado wameyakimbia makazi yao wengi wao sasa wakilazimika kuishi katika majengo yaliyoko chini ya ardhi. Akizungumza na waandishi wa habari kutoka kwenye chumba cha chini ya jengo katika mji wa Kherson, mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) nchini Ukraine, Munir Mammadzade, amesema mji huo “upo chini ya mashambulizi ya mara kwa mara,” huku mashambulizi ya kila siku yakiharibu nyumba na miundombinu muhimu, pamoja na huduma ambazo watoto na familia wanazitegemea.Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wameeleza wasiwasi mkubwa kuhusu madhara yanayoweza kuwapata waathirika waliotajwa katika nyaraka zinazojulikana kama “Epstein Files”, wakisema mchakato wa utoaji wa taarifa hizo haukulinda ipasavyo faragha na usalama wao na pia wametaka hatua stahili za kisheria zichukuliwe kwa wale wote waliotajwa katika nyaraka hizo kwa mujibu wa sheria. Nyaraka hizo zinafichua maovu yaliyotendwa na watu mbalimbali kupitia mmarekani Jeffrey Epstein.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya"KOO" katika mkitadha wa wanyama.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
16 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 16, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa kimataifa unaofahamika kama AI Impact 2026 mjini New Delhi, India, hali ya kibinadamu nchini Cuba, na huduma za Afya, maji safi na salama nchini DR Congo.Mkutano wa kimataifa unaofahamika kama AI Impact 2026 umeanza leo mjini New Delhi, India ukiwakutanisha viongozi kutoka sehemu mbalimbali za dunia ili kujadili namna akili mnemba (AI) inavyoweza kuendelezwa na kutumika kwa uwajibikaji kuchangia maendeleo endelevu. Amandeep Singh Gill, Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia teknolojia za kidijitali na zinazoibuka, amesisitiza ushiriki mpana wa kimataifa kwani ni muhimu ili kuhakikisha AI inanufaisha nchi zote.Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imetoa onyo kali kuhusu kuzorota kwa hali ya kiuchumi nchini Cuba, ikisema uhaba wa mafuta na vikwazo vya muda mrefu vinaathiri vibaya huduma za msingi kote nchini humo.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF wakishirikiana na Shirika la Maendeleo la Korea KOICA wanawasaidia wananchi wa Nyunzu katika jimbo la Tanganyika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC kwa miradi ya kusaidia huduma za afya ya watoto ambapo wamepanua upatikanaji wa huduma muhimu na endelevu.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
13 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 13, 2026 11:49


Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya Redio Duniani likitupeleka nchini Tanzania kusikia jinsi ambavyo redio inavyochochea maendeleo ya kijamii, nchini Uganda kumsikia mkimbizi kutoka DRC, na katika ukanda wa Gaza ambako redio inaunganisha tena jamii ndani ya vifusi.Leo ni siku ya redio duniani ambayo msingi wake unatokana na kuanzishwa kwa redio ya Umoja wa Mataifa tarehe 13 Februari mwaka 1946 jijini New York, Marekani. Kwa mantiki hiyo ikiwa mwaka huu redio hiyo ya Umoja wa Mataifa inatimiza miaka 80 tumeangazia mchango wa vipingi vyake vilivyokuwa vinarushwa na redio zingine ikiwemo iliyokuwa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) nchini Tanzania wakati huo. Assumpta Massoi amemulika suala hilo.Katika maeneo ya migogoro, duniani redio huwa nguzo ya utulivu na wakati mwingine daraja la kuokoa maisha. Na ndivyo ilivyokuwa kwa mkimbizi Bahati Yohane kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kwani kwake, redio haikuwa tu combo cha habari ilikuwa dira ya kuokoa maisha yake.Kabla ya vita vya sasa kuanza katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina lilalokaliwa kimabavu na Israel, Redio ilikuwa chombo muhimu kwa umma na kwa hakika umuhimu wake haujakoma isipokuwa huduma ya matangazo ya redio ndio iliyokuwa imekoma kutokana na vituo vya redio kusambaratishwa kwa makombora, lakini sasa juhudi zinafanyika kuirejesha huduma hiyo muhimu.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
12 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 12, 2026 11:24


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina kesho Ijumaa tarehe 13 Februari ikiwa ni ni siku ya Redio Duniani mwaka huu ikijikita  katika Redio na Akili tunakupeleka mashariki mwa DRC, kwa George Musubao kutoka Televishen na Radio washirika Canal Victoire Du People Kasindi.Leo tarehe 12 Februari ni siku ya Kimataifa ya Kuzuia Itikadi Kali Zinazochochea Ugaidi, ikiwa ni maadhimisho ya nne tangu kuanzishwa kwake na mwaka huu kauli mbiu inasema “Kuzuia ugaidi wa kikatili katika enzi ya teknolojia mpya na zinazoibuka”. Ugaidi na itikadi kali vinaendelea kuwa tishio kubwa kwa amani na usalama wa dunia, huku vikigusa watu wa rika, dini na tamaduni mbalimbali na ndio maana Umoja wa Mataifa unasema ingawa teknolojia kama akili mnemba au AI, mitandao ya kijamii na majukwaa ya kidijitali inaweza kusaidia juhudi za kuzuia misimamo mikali, pia inatumiwa na magaidi kueneza chuki, upotoshaji na kuhamasisha vurugu ndio maana shirika hilo linahimiza ushirikiano wa kimataifa, matumizi ya teknolojia kwa uwajibikaji na suluhisho shirikishi zinazoheshimu haki za binadamu ili kuzuia kuenea kwa itikadi kali.Barani Ulaya ambapo Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ametoa tamko kali akilaani mashambulizi ya mfululizo yanayofanywa na nchi ya Urusi dhidi ya mifumo ya nishati nchini Ukraine. Taarifa iliyotolewa leo kutoka Geneva, Uswisi, imeeleza kuwa mashambulizi hayo yanawanyima raia mahitaji muhimu ikiwemo mifumo ya kupasha joto, maji, na umeme katikati ya msimu wa baridi kali uliopitiliza.Kuelekea kuanza kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani hapo wiki ijayo, katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametuma ujumbe akisema kuwa “Katika zama hizi ngumu na za mgawanyiko, hebu tuitikie wito wa stahmala wa Ramadhani. Kuziba pengo la mgawanyiko. Kufikisha msaada na matumaini kwa wale wanaoumini. Na kulinda haki na utu wa kila mtu…..Hebu Mwezi huu Mtukufu ututie hamasa ya kufanya kazi pamoja ili kujenga dunia yenye amani zaidi, ukarimu na haki kwa watu wote.  Ramadhani njema.”Na Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "UNGUKA"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
11 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 11, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya IPU kuhusu uhasama wa wabunge, siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi, na yalitojiri katika Jukwaa la akili unde au AI lililofanyika kwa siku mbili huko Nairobi, nchini Kenya.Wabunge kote ulimwenguni wanakabiliwa na viwango vinavyoongezeka vya vitisho, unyanyasaji na vurugu kutoka kwa umma imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na Muungano wa Mabunge Duniani (IPU). Rashid Malekela na taarifa zaidi.Leo ni siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi mwaka huu mauadhui yakihimiza “Sayansi kwa Mustakabali Jumuishi kwa Wanawake na Wasichana” Kwamujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , Sayansi na Utamaduni UNESCO leo hii , wanawake wanachangia chini ya theluthi moja ya watafiti duniani, kulingana hivyo kuziba pengo hili la kijinsia si suala la haki pekee ni muhimu kwa ubora, uhalisia na mchango wa sayansi, teknolojia na ubunifu.Jukwaa la akili unde au AI lililofanyika kwa siku mbili huko Nairobi, nchini Kenya limekunja jamvi ambapo mmoja wa washiriki amesema wanaodai kuwa bara la Afrika liko nyuma kwenye teknolojia hiyo, ni dhahiri shairi hawalifahamu vema bara hilo lenye mataifa 54.

ai kenya tanzania afrika nairobi umoja hii ipu wanawake mataifa shirika jukwaa
Habari za UN
10 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 10, 2026 13:04


Hii leo jaridani Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na Wakili Amon Mpanju, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kutoka Tanzania aliyehudhuria Mkutano wa Kamisheni ya Maendeleo ya Kijamii (CSocD64).Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yametoa onyo kali kuhusu hali mbaya ya kibinadamu inayowakumba watoto nchini Sudan. Mashirika hayo lile la kuhudumia watoto UNICEF, la afya WHO na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu wamenasema ghasia zisizoisha, njaa na magonjwa vinawasababisha watoto kupoteza Maisha na kudhoofika, huku mashambulizi dhidi ya vituo vya afya na vikwazo vya upatikanaji wa misaada vikizorotesha juhudi za kuwaokoa. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, msemaji wa UNICEF, Ricardo Pires, amesema “Katika baadhi ya maeneo ya jimbo la Darfur Kaskazini, zaidi ya nusu ya watoto wote wanakabiliwa na utapiamlo mkali, si makadirio, si mfano, imethibitishwa.”.Kikosi cha 12 cha Ulinzi wa Amani kutoka Tanzania TANZBAT 12 kinachohusumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Condo DRC chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO kimeendelea kudumisha uhusiano wa kijamii na wakazi wa mji wa Beni Mashariki mwa DRC, kwa kutoa msaada wa vifaa vya elimu kwa wanafunzi katika shule ya msingi Ngite iliyopo eneo la Mavivi. Mkuu wa shule hiyo Neema Nyamwaka amewashukuru walinada amani hao kutoka Tanzania kwa kujali sekta ya elimu.Leo ni siku ya mikunde duniani Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO likisistiza umuhimu kwa chakula hicho kwa lishe na mazingira. Huko Kigoma Tanzania FAO kupitia mpango wa Pamoja wa KJP imekuwa ikitoa mafunzo kwa wakulima kuhusu umuhimu wa mazao ya jamii ya mikunde huyu ni mmoja wa wanufaika wa mafunzo hayo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Atokeapo mtoto wa fuko mshike japo wawinda fuko.”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!

kenya ethiopia tanzania sudan unicef nairobi drc fao maisha umoja hii haki kiswahili katika monusco pamoja jamii wanawake dkt jamhuri mataifa maendeleo mkuu mkutano shirika kidemokrasia wizara mashirika tigrai chuo kikuu
Defense & Aerospace Report
Defense & Aerospace Daily Podcast [Feb 09, 2026] Look Ahead w/ Byron Callan

Defense & Aerospace Report

Play Episode Listen Later Feb 9, 2026 32:58


On today's program, sponsored by HII, Byron Callan of the independent Washington research firm Capital Alpha Partners joins Defense & Aerospace Report Editor Vago Muradian to discuss the latest headlines and looks at the week ahead.

Habari za UN
09 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 9, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini DRC, mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu mwenye ulemavu wa kutoona nchini Vietnam, na harakati za kutokomeza ukeketaji nchini Kenya.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, (MONUSCO) umetoa taarifa kwamba umefahamishwa na Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa kuwa Afrika Kusini itaondoa vikosi na wanajeshi wake waliobaki ndani ya MONUSCO. Ninamualika Rashid Malekela aliyeifuatilia kwa kina taarifa hiyo ili atueleza zaidi.Nchini Vietnam taifa lililoko kusini-mashariki mwa Asia, mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu mwenye ulemavu wa kutoona anajitahidi kuhakikisha anatimiza ndoto yake ya kuwa mtaalamu wa mawasiliano licha ya vikwazo anavyokumbana navyo kila uchao, na hii ni kwa sababu si kwamba njia ni rahisi bali kwa sababu dhamira yake ni kubwa zaidi.Ukeketaji au FGM ni jinamizi linalowaandama waathirika maisha yao yote likisababisha changamoto sio tu za kimwili lakini pia za kiafya na kuwaacha na makovu yasiyofutika. Katika Kaunti ya Tana River Kusini Mashariki mwa Kenya tunakutana na manusura na shujaa mwanaharakati wa kupambana na mila hiyo potofu ya ukeketaji Saadia Hussein, raia wa Somalia anayeishi Kenya hivi sasa. Mkurugenzi mtendaji na mwanzilishi wa taasisi  isiyo ya kiserikali ya Brighter Society Initiative anatusimulia safari yake ya machungu ya ukeketaji.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

vietnam kenya congo somalia drc fgm umoja hii monusco mataifa jamhuri ujumbe kidemokrasia mkurugenzi chuo kikuu
CAVASShips
CAVASSHIPS Podcast [Feb 06, '26] Ep: 229 HII's Eric Chewning on Focus Areas and Partnerships for the Future Fleet

CAVASShips

Play Episode Listen Later Feb 6, 2026 52:44


Welcome to the CavasShips Podcast with Christopher P. Cavas and Chris Servello…a weekly podcast looking at naval and maritime events and issues of the day – in the US, across the seas and around the world. This week…we are joined by HII's EVP for Maritime Systems and Corporate Strategy, Eric Chewning, where we discuss the integration of crewed and uncrewed systems, as well as the type of technology and partnership[s needed to build the future fleet.  Please send us feedback by DM'ing @CavasShips or @CSSProvision or you can email chriscavas@gmail.com or cservello@defaeroreport.com.

Habari za UN
06 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 6, 2026 10:52


Hii leo jaridani tunaangazia juhudi za kutokomeza ukeketaji, watu waliotoweka katika ukanda wa Gaza kufuatia vita vya Hamas na Israeli, na msaada wa chakula kwa wakimbizi katika mpaka kati ya Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, na Sudan.Zaidi ya wasichana milioni 4.5 duniani kote, wengi wao wakiwa wenye umri wa chini ya miaka mitano, wako hatarini kufanyiwa ukeketaji mwaka huu pekee, wameonya viongozi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa katika ujumbe wao wa siku hii ya kimataifa ya kutokomeza ukeketaji kwa wanawake na watoto wa kike.Huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel, wiki hii, mamlaka za Israel zimewasilisha miili 54 pamoja na mifuko 66 iliyosheheni mabaki ya viungo vya binadamu ya Wapalestina waliopotea wakati wa vita. Na kutokana na kutokuwepo kwa mfumo madhubuti wa kisasa kupima vinasaba kutambua mwili upi ni wa nani inakuwa changamoto kubwa hususani kwa ndugu.Katika mpaka kati ya Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, na Sudan, maelfu ya familia waliokimbia makazi yao kutokana na vurugu wanapokea msaada wa chakula unaookoa maisha kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP uliosafirishwa kwa ndege hadi kwenye moja ya maeneo magumu zaidi kufikika nchini humo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

I - On Defense Podcast
US & Iran to Meet in Oman on Friday + Russia & Ukraine Agree to Prisoner Exchange + US & Russia Reestablish Military Communication + US Navy CCA Program

I - On Defense Podcast

Play Episode Listen Later Feb 6, 2026 29:19


For review:1. US President Donald Trump on Wednesday said Iran's Supreme Leader Ali Khamenei “should be very worried” in the wake of reports that suggested that planned nuclear talks set for the end of the week were unravelling.A White House official confirmed to The Times of Israel that nuclear talks with Iran would be held Friday in Muscat.2. Iran's army spokesperson said Thursday that the military is ready for a conflict, if that is what the US wants, Commenting on the addition of 1,000 drones to the Iranian military, Iranian Brig. Gen. Mohammad Akraminia said Thursday: “We have always announced that we are ready to confront any option and any scenario that the enemy considers, and if the enemy chooses the option of war, we are ready for any option in war conditions.”3. Trilateral talks between American, Ukrainian and Russian negotiators concluded in the United Arab Emirates on Thursday, with Moscow and Kyiv exchanging hundreds of prisoners of war.4. The ‍US and Russia have agreed to reestablish high level military-to-military ​dialogue, following ‍talks in Abu Dhabi, more than ​four years after suspension, according to the US military.5. The Kremlin said Thursday it regretted the expiration of the last remaining nuclear arms pact between Russia and the United States, while U.S. President Donald Trump declared he was against keeping its limits and wants a better deal.New START restricted each side to no more than 1,550 nuclear warheads on no more than 700 missiles and bombers — deployed and ready for use.6. Boeing's MQ-28 Ghost Bat Collaborative Combat Aircraft (CCA) will gain internal weapons bays along with an increased wingspan, the global program director announced during this week's Singapore Airshow.Boeing is currently developing the Ghost Bat in Australia for the Royal Australian Air Force (RAAF), which has ordered seven aircraft for delivery in 2028.7. Two aviation companies under contract to develop armed, unmanned aircraft and control systems for the U.S. Navy teased what they are working on this week during the Singapore Air Show.Anduril's YFQ-44 Fury, under development for the Air Force's CCA program, is in competition with the General Atomics YFQ-42A.The Navy wants its own version of the “uncrewed, modular, interoperable, interchangeable and versatile platforms” that it can field from an aircraft carrier.8. Aircraft carrier John F. Kennedy (CVN-79) is back at HII's Newport News Shipbuilding division after wrapping up builder's trials, the company said Wednesday.John F. Kennedy, the second in the Ford class of aircraft carriers, is slated to deliver to the Navy in March 2027.

Habari za UN
04 JANAUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 4, 2026 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia juhudi za kutokomeza sarati, mashambilizi dhidi ya misafara ya chakula katika kaunti ya Baliet, jimbo la Upper Nile, nchini Sudan Kusini na tunamulika miaka kumi na nne baada ya wakimbizi wa kwanza wa Syria kuvuka mpaka kuingia Jordan.Mabadiliko ya mfumo wa maisha na mazingira yanaweza kuzuia ugonjwa wa saratani kwa wagonjwa wanne katika kila wagonjwa kumi, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, (WHO) na shirika lake tangu la Utafiti kuhusu saratani, IARC.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) leo Februari 4, 2026 limetangaza kusitisha shughuli zake zote katika kaunti ya Baliet, jimbo la Upper Nile, nchini Sudan Kusini kufuatia mfululizo wa mashambulizi dhidi ya msafara wake wa majini mwishoni mwa wiki iliyopita. Anold Kayanda na taarifa zaidi.Miaka kumi na nne baada ya wakimbizi wa kwanza wa Syria kuvuka mpaka kuingia Jordan kusaka usalama, kambi ya wakimbizi ya Zaatari bado ni makazi ya maelfu ya watu wanaosubiri suluhu ya kudumu. Wiki hii, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi, Barham Salih, ametembelea kambi hiyo na kukutana na familia ambazo zimeishi ukimbizini kwa zaidi ya muongo mmoja wengi wao wakiwa bado na matumaini ya kurejea nyumbani, lakini tu pale ambapo itakuwa salama.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

syria wiki umoja hii iarc zaatari miaka mataifa shirika sudan kusini barham salih
Habari za UN
03 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 3, 2026 12:52


Hii leo jaridani kesho ikiwa ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu ugonjwa wa saratani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kumulika hatua ambazo ni uzinduzi wa Mpango wa Utekelezaji wa Kitaifa wa kutokomeza saratani ifikapo mwaka 2030.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa  Duniani, WHO, leo limetoa ombi la dola bilioni moja ili kukabiliana na majanga ya afya mwaka 2026 katika dharura 36 zilizo mbaya zaidi duniani. Ombi hilo linalenga kusaidia huduma za afya zinazookoa maisha katika nchi zilizoathiriwa na migogoro na majanga, zikiwemo Gaza, Sudan, Haiti na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.Mashariki ya Kati, wakati muda ukiendelea kuyoyoma kwa maelfu ya wagonjwa mahututi huko Gaza, kufunguliwa tena kwa kivuko cha Rafah kunaleta mwanga wa matumaini. Kivuko hicho kilifunguliwa Jumatatu baada ya kufungwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, chini ya mpango wa amani unaoungwa mkono na Marekani, na kuruhusu uhamisho wa kwanza wa wagonjwa tangu mwaka 2025.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF leo liimesema linaongeza juhudi zake zamsaada wa msimu wa baridi nchini Ukraine huku watoto na familia wakikabiliwa na kukatika kwa umeme, kukosa vipasha joto na maji kufuatia mashambulizi yanayoendelea dhidi ya miundombinu ya nishati na baridi kali. Tangu Novemba, shirika hilo limesambaza jenereta 106 kote nchini kusaidia huduma za maji na mifumo ya kupasha joto, huku takribani jenereta 150 zaidi zikitarajiwa kuwasili katika wiki zijazo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "KUNVI"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Defense & Aerospace Report
Defense & Aerospace Daily Podcast [Feb 02, 2026] Look Ahead w/ Byron Callan

Defense & Aerospace Report

Play Episode Listen Later Feb 2, 2026 35:48


On today's program, sponsored by HII, Byron Callan of the independent Washington research firm Capital Alpha Partners joins Defense & Aerospace Report Editor Vago Muradian to discuss the latest headlines and looks at the week ahead.

Habari za UN
30 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 30, 2026 9:45


Hii leo jaridani tunaangazia mafuriko nchini Msumbiji yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizoanza kunyesha katikati ya mwezi uliopita, hali ya kibinadamu kwa watoto Sudan na migogoro na uhakika wa chakula Sudan Kusini..Idadi ya watu waliofurushwa makwao nchini Msumbiji kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizoanza kunyesha katikati ya mwezi uliopita wa Desemba inakaribia 400,000 hali inayoongeza hatari kubwa katika fursa ya kuwapatia ulinzi na huduma zinazohitajika. Limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR.Makubaliano ya amani nchini Sudan Kusini yanakabiliwa na vitisho na hivyo wadau lazima husika wautekeleze licha ya changamoto zilizoko, amesema Luteni Jenerali Mohan Subramanian ambaye ni Kamanda Mkuu wa kikosi cha ujumbe wa  Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, UNMISS.Sudan inakabiliana na viwango vya hatari vya njaa, ambapo mamilioni ya watoto kama Noon wako katika hatari kubwa. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) liko shambani, likitoa msaada muhimu wa lishe, maji safi, na ulinzi. Hata hivyo, mahitaji ni makubwa, na msaada zaidi unahitajika haraka ili kuokoa maisha ya watoto hawa.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

sudan unicef unhcr hata umoja hii watoto mataifa unmiss shirika desemba sudan kusini
Habari za UN
29 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 29, 2026 11:03


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Jamhuri Africa ya Kati CAR kusikia mama mkimbizi anayesimulia aliyoyapitia, maisha ya uhamishoni na alivyojipatia nguvu iliyo kuu kuliko silaha yoyote ya vita. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na neno la wiki.Nchini Ethiopia, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO limeeleza kwamba Ethiopia imefanikiwa kutekeleza mizunguko minne ya uchanjaji watoto kwa njia ya matone dhidi ya ugonjwa wa polio. Mwaka jana 2025 Ethiopia kwa kutumia chanjo ya nOPV2 ilitekeleza uchanjaji huo kupitia mzunguko mmoja wa nchi nzima na mitatu kupitia maeneo mbalimbali ya nchi na kufanikiwa kuwafikia watoto milioni 26 katika mikoa yote.Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO), Beth Bechdol, ameeleza umuhimu wa kilimo wakati wa migogoro kulingana na mafanikio aliyoyashuhudia wakati wa ziara yake nchini Haiti na majirani zao Jamhuri ya Dominika.Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, (FAO) kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Asia (ADB) wametangaza kuwa wanatekeleza mpango wa dola milioni 100 ili kuimarisha uhakika wa chakula na lishe pamoja na kurejesha kipato kinachotokana na kilimo kwa zaidi ya watu milioni moja walio katika mazingira magumu kote nchini Afghanistan.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya "SIKU ZA JANGUO."Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
28 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 28, 2026 10:45


Hii leo jaridani tunaangazia….mafunzo ya usalama katika Ziwa Victoria, na harakati za Shirika la kiraia la kusongesha elimu kwa watoto wa kike, CAMFED za kuwawezesha wanafunzi wa kike nchini Tanzania.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukumbuka waathirika pamoja na manusura wa mauaji ya kimbari ya holokosti hususan yale yaliyofanywa na manazi wa kijerumani, hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa katika ukumbi wa Baraza Kuu kumefanyika kumbukizi ikileta pamoja manusura waliotoa shuhuda za waliyopitia wakikimbia maeneo kadhaa ikiwemo Austria baada ya kutwaliwa na wajerumani.Ziwa Viktoria barani Afrika, licha ya kuwa mhimili muhimu wa maisha kwa zaidi ya watu milioni 40 nchini Kenya, Uganda na Tanzania, bado linakabiliwa na vitisho vihusianavyo na biashara haramu za magendo, usafirishaji haramu binadamu na uvuvi haramu. Ili kupatia suluhu changamoto hiyo Ofisi ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na dawa za kulevya na utekelezaji wa sheria (INL) ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani na Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, (IOM), na walinzi wa pwani wa Kenya wamechukua hatua.Nchini Tanzania shirika la kiraia la kuendeleza elimu kwa watoto wa kike, CAMFED limeendelea kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs kwa kuwezesha wanafunzi wa kike kuimarika sio tu kimasomo darasani bali pia stadi za maisha na hatimaye wawajengee uwezo wenzao.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

kenya austria uganda tanzania afrika sdgs mambo inl iom umoja ili hii vijana nje mataifa camfed marekani shirika kimataifa ikiwa wizara
Habari za UN
27 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 27, 2026 12:40


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulika juhudi za vijana katika kuchagiza maisha wayatakayo kuanzia kujiondoa kwenye umasikini, ukosefu wa usawa hadi kwenye upatikanaji mdogo wa elimu bora na kazi zenye staha.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukumbuka waathirika pamoja na manusura wa mauaji ya kimbari ya holokosti hususan yale yaliyofanywa na manazi wa kijerumani, hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa katika ukumbi wa Baraza Kuu kumefanyika kumbukizi ikileta pamoja manusura waliotoa shuhuda za waliyopitia wakikimbia maeneo kadhaa ikiwemo Austria baada ya kutwaliwa na wajerumani.Huko Geneva, Uswisi ambako inaelezwa kuwa kurejesha mfumo wa elimu uliosambaratika huko Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, ni jambo la kuokoa maisha, na kuwarudisha watoto shuleni lazima kiwe kipaumbele cha haraka, amesema James Elder Msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF.Umoja wa Mataifa umezindua Mpango wa Mahitaji na Hatua za Kibinadamu wa dola milioni 852 kwa ajili ya Somalia, huku ukionya kuwa ukosefu mkubwa wa ufadhili utaacha mamilioni ya watu walio katika mazingira magumu bila msaada wa kuokoa maisha, huku hali ya kibinadamu kuendelea kuzorota.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana ya neno "TWINGA"Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Defense & Aerospace Report
Defense & Aerospace Daily Podcast [Jan 26, 2026] Look Ahead w/ Byron Callan

Defense & Aerospace Report

Play Episode Listen Later Jan 26, 2026 32:53


On today's Look Ahead program, sponsored by HII, Byron Callan of the independent Washington research firm Capital Alpha Partners joins Defense & Aerospace Report Editor Vago Muradian to discuss the prospect of another government shutdown in the wake of the second fatal shooting in Minneapolis; analysis of the defense appropriations conference report that added $8.4 billion to the administration's $838 billion Pentagon budget request; the odds that President Trump will get the $1.5 trillion for defense he wants; the long-awaited National Defense Strategy; US Army priorities; a roller coaster week that started with the president vowing up to 25 percent tariffs on Europe unless Washington got control of Greenland that ended with a “framework” agreement to bolster NATO's Arctic security as Trump responded to Canadian Prime Minister Mark Carney's landmark address with a pledge to impose 100 percent tariffs if Ottawa strikes a trade deal with China; bolstering US defense industrial capabilities and how Pentagon leaders need to think about “shareholders” in the space; and a look at the week ahead.

Habari za UN
26 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 26, 2026 11:20


Hii leo jaridani tunaangazia hatua za kuelekea nishati safi, wavuvi nchini Kenya wanaotumia nishati safi kuhifadhi samaki yao kwa ajili ya kuuza, na mradi wa FAO wa masuala ya biashara HASTEN unaosaidia wajasiriamali nchini Rwanda.Katika Siku hii ya Kimataifa ya Nishati Safi mwaka huu iliyobeba maadhui “Nishati safi kwa wote”, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema dunia inaelekea kubadilika lakini ameonya kuwa kasi ya mabadiliko hayo kuelekea nishati safi haitoshi na ni lazima iongezwe.Nchini Kenya, mkakati wa Umoja wa Mataifa wa kuhakikisha uzalishaji wa nishati mbadala unaongezeka mara tatu ifikapo mwaka 2030 unazidi kushika kasi kwani hivi sasa hata wavuvi na wamiliki wa migahawa wameanza kutumia majokofu yanayotumia nishati ya sola kuhifadhi samaki, na hivyo kuwa na sio tu uhakika wa samaki wakati wote bali pia wachuuzi kuepukana na kitoweo hicho kuoza umeme unapokatika. Assumpta Massoi anatupatia simulizi hiyo ya mafanikio kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Nishati endelevu, IRENA.Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na kilimo Duniani FAO, kupitia mradi wake wa masuala ya biashara HASTEN limeendesha warsha maalum ya kuanzisha biashara kwa vijana na wanawake,  mjini Kigali Rwanda, lengo likiwa ni kuwapa miradi 10 mipya ya biashara itakayofanyika kwa msaada maalum kutoka kwa wakufunzi wa kitaifa na kimataifa juu ya mbinu za kupanua biashara, kuongeza ufanisi na kuchangia katika malengo ya maendeleo endelevu SDGs.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

kenya rwanda sdgs fao hasten umoja hii mataifa shirika kimataifa
Habari za UN
23 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 23, 2026 11:40


Hii leo jaridani tunaangazia miaka themanini tangu Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC, AI katika elimu na juhudi za kuhakikisha wananchi wamepata huduma bora za afya kupitia kliniki tembezi nchini Niger.Katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, hii leo historia na dharura vilikutana chini ya paa moja. Ni miaka themanini tangu Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC lifanye kikao chake cha kwanza tarehe 23 Januari 1946 na linaadhimisha hatua hii muhimu wakati ambapo Umoja wa Mataifa unasema ni wa maamuzi kwa mustakabali wa ushirikiano wa kimataifa.Wakati dunia ikijiandaa kusherehekea Siku ya Elimu Duniani hapo kesho tarehe 24 Januari, 2026 embu sasa tuangazie mjadala unaozidi kushika kasi duniani kote kuhusu matumizi ya Akili Mnemba - AI katika elimu, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni – UNESCO linasisitiza kuwa si kila kilicho cha kisasa ni suluhisho la changamoto za elimu duniani.Huko Afrika Magharibi taifa la Niger linaongeza uwezo wa wananchi wake walio maeneo hatarishi na ya pembezoni kufikia huduma bora za afya kupitia kliniki tembezi. Kwa usaidizi kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO, Kanda ya Afrika, kliniki hizo tembezi zinaziba pengo la wale wanaoishi mbali na vituo vya afya, na wakati huo huo kuhakikisha umbali sio tena kikwazo cha mtu kupata huduma.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
22 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 22, 2026 11:26


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumsikia kijana Baraka Ayubu ambaye amekuwa kielelezo cha jinsi teknolojia inavyoweza kuleta mageuzi katika mifumo ya ujifunzaji na ustawi wa wanafunzi.Umoja wa Mataifa umesisitiza kuwa uchunguzi wa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu unaohusishwa na vita kati ya Hamas na Israel huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel utaendelea, licha ya kuanzishwa kwa Bodi ya Amani ya Gaza ambayo imezinduliwa hii leo na Rais wa Marekani Donald Trump.Tuelekee nchini Kenya ambako zaidi ya watu milioni mbili wanakabiliwa na hali mbaya ya ukosefu wa uhakika wa kupata chakula kufuatia msimu wa mvua fupi za mwezi Oktoba hadi Desemba mwaka 2025 kuwa mkavu zaidi kuwahi kurekodiwa. Kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO, uhaba wa maji unalazimu familia kutegemea vyanzo visivyo salama, jambo linaloongeza hatari ya kipindupindu, homa ya matumbo, na magonjwa ya kuhara.Mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa lile la Afya Duniani, WHO, la kuhudumia watoto, UNICEF pamoja na la Makazi, UN-Habitat, kwa pamoja wamezindua mwongozo mpya unaozitaka serikali na viongozi wa miji kuweka kipaumbele kwa watoto katika upangaji wa miji ili kurejesha maeneo ya michezo yanayozidi kutoweka.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya "SIKU ZA MUAMBO" katika muktadha wa uchumi.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
21 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 21, 2026 10:45


Hii leo jaridani tunaangazia mafuriko makubwa yaliyoikumba Msumbiji, ripoti inayomulika kupungua kwa muda mrefu kwa maji ya chini ya ardhi, na mradi unaolenga kuimarisha sekta ya kilimo katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan kwa ajili ya kuwasaidia wakulima.Kufuatia mafuriko makubwa yaliyoikumba Msumbiji kutokana na mvua zinazoendelea, serikali ya nchi hiyo ya kusinimashariki mwa Afrika imetangaza kuwa hadi kufikia sasa imerekodi vifo vya watu 120 na maelfu ya nyumba zimeharibiwa huku kiwango kikubwa cha fecha kikihitajika.Katika muktadha wa kupungua kwa muda mrefu kwa maji ya chini ya ardhi, matumizi kupita kiasi ya rasilimali za maji, uharibifu wa ardhi na udongo, ukataji miti, pamoja na uchafuzi wa mazingira, Chuo Kikuu cha Umoja wa Mataifa UNU leo kimetoa ripoti ikitangaza kuingia kwa “enzi ya kufilisika kwa maji duniani” na kutoa wito kwa viongozi wa dunia kuendana na uhalisia huu mpya kwa kuzingatia ushahidi wa kisayansi.Kwa muongo mmoja kuanzia mwaka wa 2016 hadi mwaka wa 2025, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) kwa ushirikiano na serikali ya Canada limechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha sekta ya kilimo katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan likilenga kuwasaidia wakulima na vyama vya ushirika kushinda changamoto za muda mrefu za uzalishaji, masoko na mnepo wa maisha.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

canada afrika umoja hii maji kwa katika mataifa shirika magharibi chuo kikuu
Defense & Aerospace Report
Defense & Aerospace Daily Podcast [Jan 20, 2026] Look Ahead w/ Byron Callan & Chris Servello

Defense & Aerospace Report

Play Episode Listen Later Jan 20, 2026 40:35


On today's program, sponsored by HII, Byron Callan of the independent Washington research firm Capital Alpha Partners and Chris Servello, a founder of Provision Advisors public relations firm (and Defense and Aerospace team member) join Defense & Aerospace Report Editor Vago Muradian to discuss the latest headlines and looks at the week ahead.

washington defense look ahead aerospace hii capital alpha partners provision advisors
Habari za UN
20 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 20, 2026 11:51


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya ambako wasichana juhudi za kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) zimewezesha vijana wa kike kushiriki masomo ya Teknolojia ya Habari na Maewasiliano, TEHAMA na kujifunza stadi za teknolojia ili waweze kuedeleza biashara ya mtandaoni pamoja na matumizi mengine.Zaidi ya watu nusu milioni wameathiriwa na mafuriko makubwa katika mikoa ya kusini na kati ya Msumbiji, huku mvua kubwa ikiendelea kuvuruga usafiri, huduma za afya na njia za ugavi. Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA nchini humo, Paola Emerson, amewaambia waandishi wa habari huko Geneva, Uswisi kuwa majimbo ya Gaza, Sofala na Maputo ndiyo yaliyoathirika vibaya zaidi.Huko Mashariki ya Kati mapema leo Jumanne, vikosi vya Israel vimebomoa kwa tingatinga makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA, huko Yerusalemu Mashariki eneo linalokaliwa kimabavu na Israel. Mkuu wa UNRWA, Philippe Lazzarini, amelieleza tukio hilo kama “shambulio lisilo na kifani dhidi ya Umoja wa Mataifa,”.Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, leo imesema imeanza kutekeleza mpango wa kurejesha kwa hatua mamlaka ya dola katika mji wa Uvira, mashariki mwa nchi hiyo, kufuatia kuondoka kwa kundi lenye silaha la AFC/M23. Serikali inasema vikosi vya usalama, polisi na huduma nyingine za serikali vinarejea ili kulinda raia, kulinda mali na kuleta utulivu katika eneo hilo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mtaalam wetu ONNI SIGALA Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA, anafafanua maana ya neno “ KING'ANI”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!

israel kenya gaza tanzania drc unrwa zaidi maputo umoja congo drc ocha hii kiswahili taifa philippe lazzarini baraza habari uvira vijana tehama wanawake jamhuri mataifa serikali mkuu shirika teknolojia kidemokrasia sofala
Habari za UN
19 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 19, 2026 11:28


Hii leo jaridani tunaangazia ongezeko kubwa la idadi ya watu walionyongwa duniani mwaka 2025, hali ya kibinadamu nchini Sudan na utafiti wa kutumia nyuklia kuwafanya tasa mbu dume nchini Austria.Tathimini mpya iliyotolewa leo na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imeonya kuhusu ongezeko kubwa la idadi ya watu walionyongwa duniani mwaka 2025, ikisema kuwa idadi ndogo ya nchi ndiyo inachochea mwenendo huu unaotia wasiwasi mkubwa wa haki za binadamu.Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, baada ya ziara yake ya siku tano nchini Sudan, ametahadharisha kuhusu kuongezeka kwa hali mbaya zaidi ya ukikukwaji wa haki za binadamu na ongezeko la janga la kibinadamu nchini humo.Utafiti wa kutumia nyuklia kuwafanya tasa mbu dume ili kudhibiti magonjwa ya dengue, virusi vya zika na chikungunya nchini Austria umeonesha matumaini ya kupunguza mbu mwitu jike aina ya Aedes albopictus anayeeneza vimelea vya magonjwa hayo. Utafiti ulifanyika mwaka jana kwa ushirikiano kati ya mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la nishati ya atomiki, IAEA na la chakula na kilimo, FAO.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
16 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 16, 2026 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia njaa na utapiamlo katika Afrika Magharibi na Kati, miundombinu za umeme katika ukanda wa Gaza, na harakati za UNMISS za kujenga na kuimarisha kingo za kuzuia mafuriko ili kuzuia ufurushwaji watu na kulinda Maisha nchini Sudan Kusini.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) leo limeonya kuwa bila rasilimali na hatua za haraka, watu walio katika mazingira magumu zaidi Afrika Magharibi na Kati wanakabiliwa na mwaka mwingine mgumu sana wa njaa.Uharibifu Mkubwa uliosalia Gaza baada ya vita baina ya Israel na Hamas kusitishwa uko bayana katika kila kona ya jiji hilo majengo yaliyoporomoka, vyuma vililivyotapakaa kila mahali, na vitongoji vilivyogeuka kuwa vifusi. Hayo ndiyo aliyoshuhudia Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Huduma za Miradi UNOPS, Jorge Moreira da Silva, wakati wa ziara yake katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Nuseirat, katikati ya Gaza, ambako timu za Umoja wa Mataifa za kutegua mabomu ya ardhini zinashughulika kusafisha mabaki ya vita.Wakazi wa Bentiu, jimbo la Unity nchini Sudan Kusini, wanaishi katika hofu ya kudumu ya mafuriko yanayosababishwa na mvua kubwa, huku wahandisi kutoka Pakistan wanaohudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) wakiendelea kujenga na kuimarisha kingo za kuzuia mafuriko ili kuzuia ufurushwaji watu na kulinda maisha.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

israel unity gaza pakistan hamas sahel maisha umoja hayo hii mataifa unmiss shirika ujumbe sudan kusini wakazi
CAVASShips
CAVASSHIPS Podcast [Jan 15, '25] SNA Day 3…Talking Coast Guard w/ George Kovatch

CAVASShips

Play Episode Listen Later Jan 15, 2026 40:59


Welcome to the CavasShips Podcast with Christopher P. Cavas and Chris Servello…a weekly podcast looking at naval and maritime events and issues of the day – in the US, across the seas and around the world. On today's special podcast we discuss the U.S. Coast Guard with retired cutterman and experienced senior government executive George Kovatch.  The SNA National Symposium runs Jan 13-16 and is held at the Crystal City Hyatt Regency. Our daily SNA pod coverage is sponsored by Lockheed Martin in conjunction with our weekly pod sponsors HII and GE Aerospace.

Habari za UN
15 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 15, 2026 11:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika Mkataba wa Kimataifa wa kulinda viumbe hai wa baharini kwenye Bahari Kuu na ujumbe wa Mzee Ali Haji, Naibu Katibu Mkuu anayehusika na Katiba na Sheria katika Ofisi ya Rais, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar nchini Tanzania kuhus umuhimu wa mkataba huu.Kesi inaendelea katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ mjini The Hague, kuhusu madai kwamba Myanmar ilitekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Rohingya. Mawakili wa Gambia wameiambia mahakama hiyo kuwa jeshi la Myanmar lilichochea ghasia kupitia kauli za chuki, likiwaita Warohingya “mbwa Waislamu”kabla ya mashambulizi ya mwaka 2017.Baada ya zaidi ya siku 1,000 za mzozo, Sudan inakabiliwa na mgogoro mkubwa zaidi wa njaa na uhamaji wa watu duniani. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP, leo linaonya kuwa operesheni zake za kuokoa maisha ziko hatarini kutokana na uhaba mkubwa wa ufadhili.Mamilioni ya raia wa Uganda leo walipiga kura katika uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na serikali za mitaa huku Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR likisisitiza umuhimu wa wakimbizi zaidi ya milioni moja nchini humo kubaki bila kuegemea upande wowote wa kisiasa. Shirika hilo limeonya kuwa kushiriki katika siasa kunaweza kuwakosesha wakimbizi usalama, kupelekea mateso kutoka nchi zao za asili, au kuathiri ulinzi na hali yao ya hifadhi nchini Uganda.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na ya neno "MLOWIMA"Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!

CAVASShips
CAVASSHIPS Podcast [Jan 14, '25] SNA Day 2…TOTE Service VP of Legal Jeff Vogel

CAVASShips

Play Episode Listen Later Jan 14, 2026 28:59


Welcome to the CavasShips Podcast with Christopher P. Cavas and Chris Servello…a weekly podcast looking at naval and maritime events and issues of the day – in the US, across the seas and around the world. On today's special podcast we talk to Jeff Vogel of Legal at Tote Services. The SNA National Symposium runs Jan 13-16 and is held at the Crystal City Hyatt Regency. Our daily SNA pod coverage is sponsored by Lockheed Martin in conjunction with our weekly pod sponsors HII and GE Aerospace.

Habari za UN
14 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 14, 2026 9:50


Hii leo jaridani tnaangazia uchumi wa dunia unaoendelea kukua ila maendeleo katika kupata kazi zenye ubora na staha yamekwama, pia tunaangazia afya ya uzazi nchini Uganda na homa ya bonde la ufa (RVF) kwa mifugo nchini Tanzania. Licha ya uchumi wa dunia kuendelea kukua, maendeleo katika kupata kazi zenye ubora na staha yamekwama, huku mamilioni ya wafanyakazi wakisalia katika lindi la umaskini na ajira zisizo rasmi. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani (ILO)iliyotolewa hii leo huko Geneva Uswisi.Baada ya kuhitimu shahada ya udaktari nchini mwake Uganda, huko Afrika Mashariki, Daktari mmoja alibaini kuwa hiyo haitoshi, bali alienda mbali zaidi kubuni kifaa kinachosaidia wajawazito hasa wale wanaoishi maeneo ya ndani zaidi kufahamu hali ya afya ya watoto wao tumboni, na hivi sasa kifaa hicho kinaelekea kupata hakibunifu kupitia shirika la Umoja wa Mataifa la Hakibunifu, WIPO.Mfumo wa kubaini mapema homa ya bonde la ufa (RVF) iliyobuniwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO nchini Tanzania imewezesha wizara, wakulima, na madaktari wa mifugo kuchukua hatua za mapema, hivyo kulinda maisha na mali dhidi ya ugonjwa huo unaoshambulia mifugo na binadamu.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

uganda tanzania fao ilo kazi umoja hayo hii wipo afya baada wanawake mataifa ajira afrika mashariki shirika rvf
CAVASShips
CAVASSHIPS Podcast [Jan 13, '25] SNA Day 1…Lockheed Martin's Joe DePietro and Paul Lemmo

CAVASShips

Play Episode Listen Later Jan 13, 2026 33:37


Welcome to the CavasShips Podcast with Christopher P. Cavas and Chris Servello…a weekly podcast looking at naval and maritime events and issues of the day – in the US, across the seas and around the world. On today's special podcast we dive into the naval portfolio of Lockheed Martin with VPs and General Managers Paul Lemmo and Joe DePietro. The SNA National Symposium runs Jan 13-16 and is held at the Crystal City Hyatt Regency. Our daily SNA pod coverage is sponsored by Lockheed Martin in conjunction with our weekly pod sponsors HII and GE Aerospace.

Habari za UN
13 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 13, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika mwaka mpya 2026 kwa wakazi wa Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel ambao wanaendelea kukabiliwa na hali ngumu ya maisha katika kambi za wakimbizi na katika makazi ambayo ni magofu na vifusi vya nyumba zilizoharibiwa wakati wa vita baina ya Jeshi la Israel na Wanamgambo wa Hamas.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linasema licha ya sitisho la mapigano huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, maisha ya watoto bado yako katika hali tete, huku zaidi ya watoto 100 wakiwa wameuawa tangu Oktoba mwaka jana lilipoanza sitisho hilo.Vinywaji vyenye sukari na vileo vinazidi kuwa nafuu kwa bei kutokana na viwango vya kodi kwa muda mrefu kuwa vya chini katika nchi nyingi, jambo linalochochea unene kupita kiasi, ugonjwa wa kisukari, magonjwa ya moyo, saratani na maradhi mengineyo hasa miongoni mwa watoto na vijana balehe, zimesema ripoti mpya mbili zilizotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususan jimboni Ituri, mashariki mwa nchi hiyo ambako ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, MONUSCO umepatia mafunzo ya ujasiriamali wafungwa kwenye gereza kuu lililoko Bunia, ambao ni mji mkuu wa jimbo hilo.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "MAHULUCHI"Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Defense & Aerospace Report
DEFAERO Daily Pod [Jan 12, 26] Week in Review & Byron Callan's Week Ahead

Defense & Aerospace Report

Play Episode Listen Later Jan 12, 2026 42:48


On today's Look Ahead program, sponsored by HII, Byron Callan of the independent Washington research firm Capital Alpha Partners joins Defense & Aerospace Report Editor Vago Muradian to discuss the geopolitical implications of the Trump administration's muscular foreign policy from its Venezuela operation to threats of military force against Iran and Greenland; whether a 50 percent increase in US defense spending to $1.5 trillion is feasible; how the president's executive order on dividends, share buybacks and executive compensation can be enforced; Lockheed Martin's tentative seven-year deal with the Pentagon to invest in capabilities to dramatically increase Patriot air defense missile production; and a look at the week ahead, including the Surface Navy Association's annual symposium. We are an SNA media partner and our coverage of the conference and tradeshow are brought to you in part by Lockheed Martin.

CAVASShips
CAVASSHIPS Podcast [Jan 12, '25] SNA Preview…Interview w/ Executive Director Chris Bushnell

CAVASShips

Play Episode Listen Later Jan 12, 2026 21:19


Welcome to the CavasShips Podcast with Christopher P. Cavas and Chris Servello…a weekly podcast looking at naval and maritime events and issues of the day – in the US, across the seas and around the world. On today's special podcast we preview this week's Surface Navy Association National Symposium with SNA Executive Director Chris Bushnell. The SNA National Symposium runs Jan 13-16 and is held at the Crystal City Hyatt Regency. Our daily SNA pod coverage is sponsored by Lockheed Martin in conjunction with our weekly pod sponsors HII and GE Aerospace.

Habari za UN
12 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 12, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia wito wa kuimarishwa kwa mshikamano wa kimataifa na uwekezaji endelevu kwa wakimbizi nchini Kenya, usugu wa Viuaji- Vyasumu au AMR na utekelezaji wa mradi wa kusambaza nishati ya umeme na vifaa vya nishati nchini Chad.Katika ziara yake ya kwanza rasmi iliyofanyika nchini Kenya kama Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi, Barham Salih ametoa wito wa kuimarishwa kwa mshikamano wa kimataifa na uwekezaji endelevu ili kuwasaidia wakimbizi kujenga upya maisha yao, akionya kuwa upungufu mkubwa wa ufadhili unatishia kurudisha nyuma mafanikio yaliyopatikana kwa juhudi kubwa katika ulinzi na kujitegemea kwa wakimbizi.Shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani linaendelea na juhudi za kupambana na changamoto ya usugu wa Viuaji- Vyasumu au AMR na sasa imetoa miongozo na taratibu za kuhakikisha kuna matumizi sahihi ya dawa na wahudumu wa sekta ya afya katika nchi wanachama wanaendelea kuwapatia mafunzo ili kuzitumia kwa usahihi na kwa uwajibikaji.Nchini Chad, utekelezaji wa mradi wa kusambaza nishati ya umeme PAAET umefanikisha vifaa 145,000 vya nishati ya sola kusambazwa kwa gharama nafuu kwa kaya zilizoko majimbo 23 ya taifa hilo na sasa maisha yamekuwa bora.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
09 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 9, 2026 11:17


Hii leo jaridani tunaangazia uchaguzi mkuu nchini Uganda, elimu kwa watoto nchini Sudan leo ikitimia siku 1000 tangu kuzuka kwa vita nchini humo, na juhudi za wanawake za kuhifadhi misitu huko Narok nchini Kenya.Ikiwa zimebakia siku 6 kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini Uganda, hii leo Umoja wa Mataifa imetoa ripoti inayobainisha kuwa uchaguzi huo utafanyika katika mazingira yaliyogubikwa na ukandamizaji, vitisho dhidi ya wapinzani wa kisiasa, watetezi wa haki za binadamu, na waandishi wa habari.Leo imetimia siku 1000 tangu kuzuka kwa vita nchini Sudan, vita vinavyohusisha Jeshi la Sudan SAF na Kikosi cha Wanamgambo wa Sudan cha Msaada wa Haraka RSF. Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM limesema mtu mmoja kati ya watatu nchini humo ni mkimbizi ndani yanchi yake au amekimbilia nje ya nchi huku Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF likieleza mzozo huo ambao umeendelea kusababisha janga kubwa la kibinadamu unawatesa zaidi wanawake na watoto kwani wanabeba mzigo mkubwa wa madhara ya vita.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, (UNDP), nchini Kenya, kupitia mradi wa kuhimili tabianchi au Climate Promise Guarantee, limewawezesha wanawake wa jamii ya asili katika Kaunti ya Narok, nchini humo kuongoza juhudi za uhifadhi wa misitu huku wakilinda urithi wao wa kitamaduni na kuboresha maisha ya familia zao.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

kenya uganda sudan unicef undp umoja hii jeshi elimu mataifa maendeleo shirika kaunti ikiwa uchaguzi mkuu
Habari za UN
08 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 8, 2026 11:07


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini DRC kufuatilia yaliyojiri kwenye kikao mahsusi cha kuimarisha uhusiano mwema na wakazi wa eneo la Beni-Mavivi jimboni Kivu Kaskazini ili kuimarisha ulinzi wa amani wakati huu ambapo kwasasa hatua za kidiplomasia za kutatua mgogoro unaoikumbuka nchi hiyo zikiendelea.Hatimaye matumaini yamerejea ya kuwa na mlo mezani huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli baada ya shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP kuweza kupatia raia mgao kamili wa chakula, ikiwa ni mara ya kwanza tangu vita vianze Oktoba 7, 2023.Huko nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MINUSCA umesambaza radio zinazotumia nishati ya sola kwa jamii ikiwa ni sehemu ya  usaidizi wake wa kuhakikisha wananchi wanapata taarifa za uhakika na kwa wakati. Katika mkoa wa Nana-Mambéré, MINUSCA imekabidhi radio 600 kwa mamlaka za serikali za mitaa, wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji wa Mkataba wa Amani, viongozi wa kidini, wanawake, vijana, watetezi wa haki za binadamu, vikosi vya ulinzi na usalama, wanahabari, wauza maduka na waendesha bodaboda.Mkuu wa Idara ya Umoja wa Mataifa ya  Operesheni za Ulinzi wa Amani, Jean-Pierre Lacroix akiwa ziarani nchini Lebanon amekuwa na mazungumzo na viongozi wa jeshi la taifa hilo ambapo amewashukuru kwa ushirikiano wao na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa mpito nchini humo, UNIFIL. Wamejadili pia mpango wa unaoendelea wa kupeleka tena vikosi vya UNIFIL kusini mwa Lebanon na jinsi gani ujumbe huo unaweza kuendelea kusaidia jeshi la Lebanon kutekeleza azimio namba 1701 la Baraza la Usalama kuhusu sitisho la uhasama kati ya Israeli na wanamgambo wa Hezbollah.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na ya neno "UMWESO"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
07 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 7, 2026 11:50


Hii leo jaridani tunaangazia ukandamizaji wa haki za binadamu na uchaguzi mkuu nchini Uganda, juhudi za Rwanda za kutokomeza Saratani ya shingo ya kizazi, na mafunzo kwa ya kutengeneza kilelezi cha vifaranga au kinengunengu yaliyoendeshwa Kigoma Tanzania.Wakati nchi ya Uganda ikijiandaa na uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 15 mwezi huu wa Januari, wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa hii leo wametoa taarifa ikionya kwamba hali ya haki za binadamu nchini Uganda si rafiki kwa uchaguzi wa amani.Saratani ya shingo ya kizazi ndiyo saratani inayowapata wanawake wengi zaidi nchini Rwanda kwani takribani kila mwaka kati ya wagonjwa wapya 1230, 830 hufariki dunia. Ili kupunguza mzigo wa ugonjwa huu na kuokoa maisha, mwaka 2020 Rwanda ilianzisha mkakati wa kitaifa unaoendana na lengo la Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) la kuondoa saratani ya shingo ya kizazi ifikapo 2030.Mafunzo kwa vitendo ya kutengeneza kilelezi cha vifaranga au Kinengunengu yaliyoendeshwa mkoani Kigoma kaskazini-magharibi mwa Tanzania na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, nchini huko yameendelea kusambaa na sasa  yamebisha hodi kwenye viunga vya mji mkuu wa kibiashara Dar es salaam kwa lengo la kusaidia wafugaji kujiongezea kipato badala ya kupoteza vifaranga kwa vifo au kuliwa na kunguru.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

dar uganda rwanda tanzania fao umoja ili hii afya wakati mataifa shirika uchaguzi mkuu ufugaji
Habari za UN
06 JANUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 6, 2026 11:44


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika Chata iliyoanzisha Umoja wa Mataifa miaka 80 iliyopita baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia na kukutanisha mataifa 50 San Francisco hapa Marekani na kupitisha Chata hiyo, ikilengaa kuzuia vita na kujenga uhusiano mwema baina ya mataifa. Operesheni ya kijeshi iliyofanywa na Marekani tarehe 3Januari nchini Venezuela ambayo ilimchukua Rais wa nchi hiyo Nicolàs Madura na hapo jana walimfikisha mahakamani jijini New York Marekani. Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya masuala ya haki za binadamu OHCHR kupitia msemaji wake Revina Shamdasani akizungumza na waandishi wa habari jijini Geneva Uswisi amewaeleza kuwa kitendo hicho ni uvunjaji wa sheria za kimataifa na wala kisingizio cha haki za binadamu kisitumike.Tukisalia na Venezuela, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya masuala ya Kiutu OCHA imeeleza inaendelea kuwasaidia wenye uhitaji nchini humo na mwaka jana ili ainisha zaidi ya wahitaji milioni 8. Msemaji wa OCHA Jens Laerke amewaambia waandishi wa habari jijini Geneva kuwa “Kati ya hao watu milioni nane, "900,000 wamewekwa katika makundi ya juu sana ya wenye uhitaji wa sekta mbalimbali ... kama vile chakula, lishe, elimu, na huduma za afya, kimsingi mambo yote ambayo nchi ya Venezuela halijaweza kutoa kwa raia wake kwa miaka mingi”.Msemaji wa Umoja wa Mataifa ameeleza kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anafuatilia akiwa na wasiwasi mkubwa maandamano yanayoendelea nchini Iran. Guterres amesikitishwa na ripoti za vifo na majeruhi kutokana na mapigano kati ya vikosi vya usalama na waandamanaji, akitaka mamlaka zizingatie haki ya kuandamanana na kukusanyika kwa amani.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Defense & Aerospace Report
DEFAERO Daily Pod [Jan 5, 26] Week in Review & Byron Callan's Week Ahead

Defense & Aerospace Report

Play Episode Listen Later Jan 5, 2026 32:54


On today's program, sponsored by HII, Byron Callan of the independent Washington research firm Capital Alpha Partners joins Defense & Aerospace Report Editor Vago Muradian to discuss the latest headlines and looks at the week ahead.

washington defense week ahead hii capital alpha partners
Habari za UN
05 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 5, 2026 11:19


Hii leo jaridani tunaangazia hali nchini Venezuela operesheni ya kijeshi ya Marekani, afya ya uzazi Tana River nchini Kenya, na wanawake wakimbizi wa DR Congo wanaopitia ukatili wa kijinsia wakikimbia machafuko. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana leo katika kikao cha dharura baada ya operesheni ya kijeshi ya Marekani nchini Venezuela tarehe 3 Januari mwaka huu, hatua iliyozua hofu ya kuongezeka kwa hali ya kutokuwa na utulivu nchini humo na katika eneo zima.Huko nchini Kenya katika kaunti ya Tana River, hali mbaya ya hewa na migogoro imesababisha takriban watu 140,000 kuyahama makazi yao. Upatikanaji wa huduma za afya nao umekuwa mgumu na kuongeza magumu hususani kwa wanawake na watoto. Katika kukabiliana na hali hiyo Wizara ya Afya nchini humo inashirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO katika kutoa huduma za afya kipaumbele kikielekezwa kwenye masuala ya uzazi salama.Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi (UNFPA), nchini Burundi, linaongeza juhudi zake kukabiliana na mahitaji yanayoongezeka ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) wanaokimbia mapigano yanayoendelea mashariki taifa hilo la Maziwa Makuu ili kulinda afya, usalama na utu wao na wa jamii zinazowapokea.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

venezuela kenya congo burundi drc umoja hii katika afya watu baraza jamhuri mataifa marekani huko shirika kidemokrasia wizara