Podcasts about kiswahili

Bantu language spoken mainly in East Africa

  • 156PODCASTS
  • 1,145EPISODES
  • 21mAVG DURATION
  • 1DAILY NEW EPISODE
  • Dec 4, 2025LATEST
kiswahili

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about kiswahili

Show all podcasts related to kiswahili

Latest podcast episodes about kiswahili

Habari za UN
04 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 4, 2025 12:02


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kwa mwanariadha na mchchemuzi wa masuala ya wanawake, akieleza hatua zinazochukuliwa kutokomeza dhulma wa kijinsia. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze lugha ya Kiswahili.Huku mapigano yakizidi kushika kasi katika eneo la Kordofan nchini Sudan, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ameonya hii leo kuhusu hatari ya mashambulizi mapya dhidi ya raia, baada ya kuripotiwa vifo zaidi ya watu 269 kutokana na mashambulizi ya angani, mabomu na mauaji ya kiholela tangu mwishoni mwa mwezi Oktoba. Ofisi yake imeeleza kupokea taarifa za ulipizaji kisasi, utekaji, ukatili wa kingono na ulazimishaji wa watoto kujiunga na makundi ya kivita, huku miji kama Kadugli, Dilling na El Obeid ikikabiliwa na njaa, kuzingirwa na kukwama kwa misaada ya kibinadamu.Malaria, ugonjwa ambao takriban asilimia 95 ya vifo vinavyoripotiwa duniani ni kutoka nchi za Afrika tena kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka 5. Ulionekana kuweza kudhibitiwa lakini sasa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus, anasema unaelekea kubaya kutokana na kuongezeka kwa usugu wa dawa, hali inayotishia kuyafuta mafanikio yaliyookoa maisha ya watu milioni moja mwaka 2024 kupitia chanjo na vyandarua vipya vyenye dawa ya kukabiliana na mbu waenezao Malaria.Na tuhitimishie nchini Msumbiji ambako Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM Amy Pope amefanya ziara ya siku tatu na kujionea athari zilizoletwa na Mafuriko, vimbunga na kuzorota kwa usalama huko Kaskazini mwa nchi hiyo hali iliyosababisha zaidi ya 100,000 wameyakimbia makazi yao, na zaidi ya 600,000 wakihitaji msaada.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "MADHALI"Mwenyeji wako ni Sabrina Moshi, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "MADHALI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 4, 2025 0:34


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "MADHALI"

Habari za UN
02 DESEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 2, 2025 12:39


Hii leo jaridani tukiendelea kukupa taarifa mbalimbali kuhusu siku 16 za kuhamasisha umma kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake, leo tunaelekea Mjini Hoima Magharibi mwa Uganda kusikia hisia za wanawake kuhusu ukatili dhidi ya wanawake mtandaoni.Watu takribani 100,000 wamekimbia makazi yao kaskazini mwa Msumbiji ndani ya wiki mbili, huku Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi UNHCR likionya kuwa mashambulizi yanaongezeka na kuyakumba hata maeneo yaliyokuwa salama. Mwakilishi wa UNHCR, Xavier Creach, amesema mgogoro “unazidi kuzorota kwa kasi ya kutisha” huku familia zikikimbia usiku gizani wakati watu wenye silaha wakivamia vijiji vyao. UNHCR inasema linahitaji dola milioni 38.2 kukidhi mahitaji yanayoongezeka.Kaskazini mwa Asia, dhoruba za kitropiki na mvua zisizo za kawaida zimesababisha vifo vya mamia na watu wengi kukimbia makazi yao, imesema WMO. Clare Nullis, msemaji wa shirika hilo, alisema Indonesia, Ufilipino, Sri Lanka, Thailand na Vietnam ndizo zimeathirika zaidi. “Tunahitaji kuzingatia kuwa Asia iko hatarini sana kutokana na mafuriko,” amesema Nullis, akibainisha kuwa dhoruba karibu na Ekweta ni nadra na jamii hazina uzoefu wa kukabiliana nazo. Indonesia pekee, watu 604 wamefariki, 464 hawajulikani walipo, na 2,600 wamejeruhiwa, huku zaidi ya milioni 1.5 wakiathirika na 570,000 wakikimbia makazi yao.Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kukomesha Utumwa leo Desemba      2 Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi Duniani ILO limeonya kuhusu kuongezeka kwa utumwa wa kisasa wa binadamu, likionesha kuwa watu milioni 10 zaidi walikuwa wakiishi katika kazi za kulazimisha au ndoa za shuruti mwaka 2021 ikilinganishwa na mwaka 2016. Makadirio haya mapya yanaweka idadi ya walioathirika duniani kote kuwa watu milioni 50 huku wanawake na watoto wakiendelea kuwa wenye hatari kubwa zaidi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "KOTI LA BABU HALIKOSI CHAWA".Mwenyeji wako ni Sabrina Moshi, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali "KOTI LA BABU HALIKOSI CHAWA"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 2, 2025 1:15


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "KOTI LA BABU HALIKOSI CHAWA".

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(20)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 45:33


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(38)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 52:31


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(27)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 56:45


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(16)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 56:48


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(30)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 47:58


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(29)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 50:01


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(32)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 48:40


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(21)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 51:11


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(25)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 54:17


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(35)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 51:21


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(37)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 48:49


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(51)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 54:11


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(33)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 45:25


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(18)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 47:25


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(28)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 46:58


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(34)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 45:57


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(22)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 52:37


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(19)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 50:33


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(36)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 47:09


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(57)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 53:03


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(41)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 56:25


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(46)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 55:30


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(47)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 45:32


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(53)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 50:34


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(49)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 44:21


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(54)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 58:59


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(43)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 45:18


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(56)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 45:26


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(42)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 41:56


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(50)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 55:48


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(45)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 49:24


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(60)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 53:49


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(44)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 54:56


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(48)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 47:35


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(55)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 58:35


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(58)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 51:43


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

NOOR INTERNATIONAL
Hizb(52)

NOOR INTERNATIONAL

Play Episode Listen Later Nov 27, 2025 45:00


Qurani yenye maana kwa Kiswahili na Hizb

Habari za UN
25 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 25, 2025 12:23


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, na leo zinaanza siku 16 za uanaharakati kuelimisha umma kuhusu janga la ukatili wa kijinsia, tunamsikia  mmoja wa waathirika wa ukatili wa kingono.Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa onyo kali kuhusu ongezeko la ukatili mtandaoni dhidi ya wanawake na wasichana.Ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya wanawake UN Women na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya dawa na uhalifu UNODC inaonya kwamba mwaka 2024, wanawake na wasichana 50,000 waliuawa na wapenzi au jamaa sawa na mwanamke mmoja kila dakika 10.Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo (UNCTAD) inaonya kwamba uchumi wa Eneo la Palestina Linalokaliwa kwa Mabavu na Israel umerudi nyuma miaka 22 kwa muda usiozidi miaka miwili kwani umeingia katika hali mbaya zaidi ya mdororo kuwahi kurekodiwa, huku miongo ya maendeleo ikifutwa na operesheni za kijeshi zilizodumu kwa muda mrefu pamoja na vizuizi vya muda mrefu.Katika kujifunza lugha Kiswahili hii leo,  mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "MADUYUNI"Mwenyeji wako ni Sabrina Said, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "MADUYUNI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 25, 2025 1:02


Katika kujifunza lugha Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "MADUYUNI"

Habari za UN
20 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 20, 2025 10:45


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka katika Kaunti ya Kajiado iliyoko Kusini na Kusini magharibi mwa jiji la Nairobi nchini Kenya kumulika upatikanaji wa huduma za choo na hasa choo safi na salama ambazo bado ni kizungumkuti kote dunianini.Katibu Mkuu wa Umoja wa, António Guterres,akizungumza na waandishi wa habari hii leo ametoa onyo kali COP30 huko Belém, Brazil, akisisitiza dharura ya hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi. Amesema “Jamii zilizo mstari wa mbele zinaangalia zikiesabu nyumba zao zilizozamishwa na mafuriko mavuno yaliyoshindikana, vyanzo vya maisha vilivyopotea na kuuliza kwa kiasi gani zaidi wateseke . Wamesikia visingizio vya kutosha, sasa wanatakahatua”.Leo ni Siku ya mtoto Duniani, mwaka huu ikibeba kaulimbiu “Sikilizeni watoto, simameni kwa ajili ya haki za kila mtoto, kila siku.” Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF iliyotolewa leo ya Hali ya Watoto Duniani 2025 sanjari na maadhimisho haya  inaonya kwamba zaidi ya watoto milioni 417, sawa na mtoto 1 kati ya 5 katika nchi za kipato cha chini na cha kati, wanakabiliwa na ukosefu mkubwa wa mahitaji muhimu angalau katika maeneo mawili ya msingi ya maisha.Mkutano wa wanaharakati vijana wavumbuzi kutoka kila pembe ya dunia umeaanza leo mjini Geneva Uswisi ukibeba mafda kuu “Kutoka Hashtag hadi Hatua”, ukisherehekea vijana wanaobadilisha maisha ya jamii zao kupitia zana za kidijitali na majukwaa ya mtandaoni. Mwaka huu, washindi wa uvumbuzi huo wanatoka nchi mbalimbali, ikiwemo Côte d'Ivoire, India, Lebanon, Japan, na Brazil, wakitambuliwa kwa kazi zao zenye athari kubwa chanya. Waandaaji wa Jukwaa hilo amba oni Umoja wa Mataifa wanasema tukio hili lina lengo la kuhamasisha vijana wengi zaidi kubadilisha ushiriki wao wa mtandaoni kuwa hatua halisi zinazoboresha jamii, kuthibitisha kuwa uanaharakati wa kidijitali unaweza kuleta mabadiliko ya kweli.Na katka kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "MTAWALIA.”Mwenyeji wako ni Sabrina Said, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za maneno MTAWALIA

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 20, 2025 0:42


Katka kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "MTAWALIA.”

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana na matumizi ya neno "UPUNGUFU"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2025 0:57


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "UPUNGUFU"

Habari za UN
18 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2025 11:32


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Brazil kwenye mkutano wa COP30, ambako Dkt. Richard Muyungi, Mjumbe maalumu kwenye masuala ya mabadiliko ya tabianchi na mazingira kutoka nchini Tanzania anaeleza ni nini bara la Afrika linahitaji.Umoja wa Mataifa umekaribisha kupitishwa kwa Azimio namba 2803 la Baraza la Usalama kuhusu Gaza hapo jana, ukilitaja kuwa hatua muhimu katika kuimarisha usitishaji mapigano. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, anazitaka pande zote kuheshimu kikamilifu makubaliano hayo na kutafsiri kasi ya kidiplomasia kuwa hatua za dharura na za wazi kwa watu walioko katika eneo hilo. Katika taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Guterres, Stéphane Dujarric, amesema Umoja wa Mataifa umejizatiti kuongeza misaada ya kibinadamu na kuunga mkono jitihada zinazoelekezwa katika hatua inayofuata ya usitishaji mapigano.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), hali ya kibinadamu katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kusini bado ni tete. Mkurugenzi wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu, Kanda ya Afrika Patrick Youssef  ambaye amerejea hivi karibuni kutoka DRC amewaleza waandishi wa habari jijini Geneva, Uswisi kwamba raia wa DRC wanaendelea kubeba mzigo mzito wa mapigano, hata wakati shughuli chache za kibiashara zikiendelea kurejea Goma. Ametoa tahadhari kuwa mgogoro huo unakabiliwa na upungufu mkubwa wa ufadhili, ukatili wa kingono unaongezeka, na zaidi ya asilimia 70 ya watu waliojeruhiwa kwa silaha mwaka huu ni raia.Kuanzia leo tarehe 18 inaanza Wiki ya Kimataifa ya Kuelimisha Umma kuhusu Usugu wa Vijiumbemaradhi dhidi ya dawa. Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, linaonya kuwa usugu wa vimelea yaani hali ambapo bakteria, virusi na vijidudu vingine havidhuriki tena kwa dawa tayari unatishia mifumo ya afya, uchumi na uhakika wa chakula. Kwa kaulimbiu “Chukua Hatua Sasa: Linda Leo Yetu, Linda Mustakabali Wetu,” WHO inatoa wito kwa serikali, wahudumu wa afya, wakulima, wadau wa mazingira na umma kuchukua hatua madhubuti kutekeleza ahadi za kisiasa ili kupunguza kuenea kwa maambukizi sugu ya dawa.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "UPUNGUFU"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "KASIMU".

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 13, 2025 1:00


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo,  mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KASIMU".

Habari za UN
13 NOVEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 13, 2025 10:40


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia simulizi za waahirika wa Kimbunga Melissaikiwa ni wiki ya pili sasa baada ya kupiga magharibi mwa Jamaica, na kuacha zahma kubwa kwa wakaazi. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze Kiswahili.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akieleza kuwa na wasiwasi mkubwa kutokana na ripoti za ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na mauaji ya halaiki mjini El Fasher, pamoja na kuongezeka kwa mapigano katika maeneo ya Kordofan nchini Sudan. Guterres amesema “Mtiririko wa silaha na wapiganaji kutoka nje lazima ukatwe. Misaada ya kibinadamu lazima iweze kuwafikia haraka raia wanaohitaji, na mapigano lazima yakome,”.Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumatano limemchagua Phoebe Okowa kutoka Kenya kuwa Jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), baada ya duruu nne za upigaji kura. Upigaji kura huo ulifanyika kwa wakati mmoja na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, lakini kwa utaratibu tofauti, kama inavyotakiwa na Katiba ya Mahakama hiyo ya Haki. Bi. Okowa amechaguliwa kwa wingi wa kura ambapo alipata kura 8 katika Baraza la Usalama na kura 106 katika Baraza Kuu.Kumekuwa na ongezeko la uraibu wa nikotini na bidhaa nyingine zinazozalishwa kwa kutumia tumbaku duniani hususani miongoni mwa vijana na tena wengi hivi sasa wanatumia sigara za kielektroniki, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO. Tarehe 17 mpaka 21 Novemba utafanyika mkutano mkubwa kujadili namna serikali, mashirika ya kimataifa na asasi za kiraia zitakavyoweza kusaidia kupambana na janga la tumbaku duniani, linalosababisha vifo zaidi ya milioni saba kila mwaka.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KASIMU"Mwenyeji wako ni Sabrina Said Moshi, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya methali "CHA KIPOFU KI MKONONI MWAKE"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 11, 2025 1:31


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Daktari. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya,  kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "CHA KIPOFU KI MKONONI MWAKE"