Bantu language spoken mainly in East Africa
POPULARITY
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kushuhudia mafunzo ya ukufunzi kwa wanadhimu wa Umoja wa Mataifa. Pia tunakuletea muhtasari wa habari zikiwemo za mkataba wa amani DRC na Rwanda, UKIMWI, na maadhimisho ya Siku ya kimataifa ya Kiswahili, na uchambuzi wa neno.Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wamekaribisha mkataba wa amani kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Rwanda uliotiwa saini tarehe 27 mwezi uliopita wa Juni, huku wakishukuru Marekani, Qatar na Muungano wa Afrika kwa juhudi za usuluhishi.Ukata uliosababishwa na wahisani kukata au kupunguza ghafla na kwa kiasi kikubwa ufadhili kwenye miradi ya kupambana na UKIMWI umekuwa na madhara kwa nchi zilizoathiriwa vibaya na ugonjwa huo, imesema ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na Ukimwi, UNAIDS.Leo kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Nairobi, Kenya kumefanyika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya lugha ya Kiswahili ambapo wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Juu ya Mangu wametuma ujumbe wao wa umuhimu wa lugha hiyo kupitia ngonjera.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno "CHARAKAMU na BARAKALA!Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno "CHARAKAMU na BARAKALA
Kuelekea siku ya Kiswahili duniani hapo Julai 7 mwaka huu ikibeba maudhui “Kiswahili: zama zilizopita, sasa na zijazo” kwa lengo la kutathimini ukuaji na mabadiliko katika ligha hiyo adhimu leo tunakupeka Nairobi Kenya kwenye mpango wa kujitolea wa Umoja wa Mataifa UNV apmbapo mmoja wa wafanyakazi wa mpango huo mghani wa mashairi Jescah Muyia ameamua kuienzi lugha hiyo kwa shairi murua.
Hii leo jaridani tunaangazia mafuriko katika Jimbo la Texas, Marekani, na shairi linaloenzi siku ya Kiswahili Duniani. Makala inamulika haki za watu wenye ulemavu hususani wanawake, na mashinani tunakwenda Osaka nchini Japani kunakofanyika maonesho au EXPO2025, kulikoni?Umoja wa Mataifa umeonesha mshikamano mkubwa na watu wa Jimbo la Texas, Marekani serikali kufuatia mafuriko makubwa yaliyotokea Ijumaa na kusababisha vifo hasa vya watoto na uharibifu mwingine mkubwa.Kuelekea siku ya Kiswahili duniani hapo Julai 7 mwaka huu ikibeba maudhui “Kiswahili: zama zilizopita, sasa na zijazo” kwa lengo la kutathimini ukuaji na mabadiliko katika ligha hiyo adhimu leo tunakupeka Nairobi Kenya kwenye mpango wa kujitolea wa Umoja wa Mataifa UNV apmbapo mmoja wa wafanyakazi wa mpango huo mghani wa mashairi Jescah Muyia ameamua kuienzi lugha hiyo kwa shairi murua.Makala inaturejesha Zanzibar Tanzania katika sehemu ya mwisho ya mahojiano baina Flora Nducha wa Idhaa hii na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Abeida Rashid Abdallah kuhusu ujumuishwaji wa watu wenye ulemavu ungana nao.Na katika mashinani, kuanzia Aprili 13 hadi Oktoba 2025 huko Osaka nchini Japani kunafanyika maonesho au EXPO2025 ikileta nchi na mashirika ya Umoja wa Mataifa maudhui yakiwa Kuumba Jamii za siku zijazo kwa maisha yetu. Banda la Umoja wa Mataifa limedadavua maudhui hayo na kuwa kujikita kwenye Kuungana kwa Mustakabali Bora washiriki wakionesha masuala tofauti tofauti ikiwemo onesho la picha likisimamiwa na mpiga picha kutoka Ufaransa. Mhusika anafafanua.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayokupeleka nchini Uganda katika Mbuga ya Wanyama inayofahamika kwa jina Murchison Falls National Park kuangazia namna washiriki wa Kongamano la kimataifa la lugha ya Kiswahili lililofanyika mapema mwaka huu jijini Kampala walivyofurahia mazigira asili nchini Uganda na namna yanavyounufaisha ulimwengu.Mkutano wa 4 wa ufadhili kwa maendeleo umemalizika leo huko Sevilla, Hispania ambapo mashirika ya kiraia yametaka utekelezaji kwa vitendo kwa yale yaliyomo katika nyaraka iliyopitishwa iliyopatiwa jina Makubaliano ya Sevilla.Mmoja wa wawakilishi wa mashirika ya kiraia, Paula Sevilla amesema kinachohitajika ni uongozi kutoka nchi tajiri ambako ndiko zilizko kampuni kubwa zinazokwepa kodi.Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO kuhusu vijana na mifumo ya uzalishaij chakula na kilimo inaonesha kuwa karibu asilimia 85 ya vijana duniani wanaishi katika nchi za kipato cha chini na cha kati, ambako mifumo hiyo ni muhimu kwa ajira na maisha yao. Ripoti inasema kuwajumuisha vyema vijana katika mifumo hiyo kunaweza kuleta mchango wa hadi trilioni moja ya dola kwa uchumi wa dunia..Na mwezi uliopita wa Juni umeshuhudia ongezeko kubwa la familia za raia wa Afghanistan zikirejeshwa nyumbani kutoka Iran, tofauti na awali ambapo waliokuwa wakirejeshwa walikuwa ni wanaume peke yao.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mchabuzi wetu Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA nchini Tanzania, anachambua neno KUTOHOA.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mchabuzi wetu Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA nchini Tanzania, anachambua neno KUTOHOA.
In today’s edition of Bring It On!, hosts Clarence Boone and Liz Mitchell spend the hour with Dr. Alwiya Saleh Omar and Dr. Ng’uono Okelo to discuss World Kiswahili Language Day. Both Dr. Omar and Dr. Ng'uono are affiliated with the African Studies Program and the National African Language Resource Center at Indiana University’s Hamilton …
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania, ambako mshikamano na wakimbizi unatekelezwa kwa vitendo na mashirika ya Umoja Mataifa likiwemo lile la Chakula na Kilimo (FAO) na la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kupitia Programu wa Pamoja ya Kigoma (KJP).Katika siku ya kimataifa ya kupambana na dawa za kulevya na usafirishaji haramu, ripoti mpya ya dunia ya Dawa za Kulevya mwaka 2025 iliyotolewa leo imeonya kuwa kutokuwepo kwa utulivu duniani kunachochea ongezeko la matumizi ya dawa za kulevya na uhalifu wa kupangwa. Kwa mujibu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Dawa na Uhalifu UNODC, watu milioni 316 walitumia mihadarati mwaka 2023. Mkurugenzi Mtendaji wa UNODC, Ghada Waly, amesema "Makundi haramu yanatumia migogoro kama fursa tunahitaji ushirikiano na uwekezaji kulinda jamii zetu.”Leo ni kumbukizi ya uzinduzi wa Chata ya Umoja wa Mataifa miaka 80 iliyopita mjini San Francisco, hatua iliyoweka msingi wa kuundwa kwa Umoja wa Mataifa mnamo Oktoba 24, 1945. Katibu Mkuu António Guterres anasema Umoja wa Mataifa bado unaakisi matumaini yaliyozaliwa kutoka kwenye majivu ya vita naye mwanahistoria Stephen Schlesinger akizungumza na UN News ameakumbusha kuwa “Chata hii ilikuwa kilio cha wanadamu wakitafuta amani, suluhu za mazungumzo, na maisha bora duniani.”Asilimia 93 ya kaya Gaza hazina uhakika wa maji safi kutokana na ukosefu wa mafuta unaopelekea mifumo ya maji kukaribia kusambaratika yameonya mashirika ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yakiongeza kuwa familia zinakumbwa na njaa kali, wakila mlo mmoja kwa siku huku watu wazima wakikosa kula ili kuwasaidia watoto na wazee.Na leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya neno "AFRITI KIJITI”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya neno "AFRITI KIJITI.”
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIHORO!"
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina, ikiwa kesho tarehe 20 mwezi Juni ni siku ya kimataifa ya wakimbizi maudhui yakiwa Mshikamano na Wakimbizi, tunakupeleka kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyoko kaunti ya Turkana, kaskazini-magharibi mwa Kenya.Uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje FDI umeshuka kwa mwaka wa pili mfululizo, ukihatarisha mustakabali wa maendeleo katika nchi zinazoendelea, kwa mujibu wa wa ripoti iliyotolewa leo na kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD. ikionya kuwa pengo la mitaji linaongezeka huku sekta muhimu kama nishati safi na miundombinu zikikosa ufadhili wa muda mrefu.Katika siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono kwenye mizozo, Umoja wa Mataifa umetoa onyo kuwa ukatili wa kingono unazidi kutumika kama silaha ya vita huku wanawake na wasichana wakiathirika zaidi. Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA "Huu si uharibifu wa bahati mbaya ni uhalifu wa kivita. Na waathirika lazima wawe kiini cha amani, haki, na urejeshwaji wa maisha."Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani (WHO) leo limezindua mwongozo wake wa kwanza wa kimataifa wa kudhibiti ugonjwa wa seli mundu (sickle cell) wakati wa ujauzito, ukilenga kupunguza hatari za maisha kwa mama na mtoto. WHO inasema wanawake wenye ugonjwa huu wana hatari hadi mara 11 zaidi ya kufariki dunia wakati wa ujauzito. Hivyo huduma bora za afya zinaweza kuokoa maisha, lakini visa vya seli mundu vinaongezeka duniani, huku Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara ikichangia asilimia 80.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIHORO!.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno "MBEUZI, MNYWANYWA NA MACHAGU.”
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kupinga utumikishaji wa watoto ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani, ILO, linasema maudhui ni Maendeleo yako dhahiri, lakini bado kuna mengi ya kufanya: Hebu tuongeze kasi. Tunakupeleka nchini Tanzania kumulika harakati za kuwaepusha watoto kutumikishwa.Watu waliolazimika kukimbia makazi yao kutokana na vita, ukatili na mateso duniani kote imefikia kiwango cha juu kisichovumilika, hasa wakati huu ambapo ufadhili wa misaada ya kibinadamu unapungua kwa kasi. Kwa mujibu wa Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi UNHCR iliyotolewa leo kuhusu mwelekeo wa Ulimwengu, kufikia mwisho wa Aprili mwaka huu, kulikuwa na watu milioni 122.1 waliolazimika kuhama kwa nguvu, ikilinganishwa na watu milioni 120 mwaka uliopita katika kipindi kama hicho.Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya kupinga ajira kwa watoto, utafiti uliofanywa na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la kazi duniani, ILO na la kuhudumia Watoto UNICEF unaonesha licha ya hatua zilizopigwa, ajira kwa watoto bado inaathiri watoto milioni 138 duniani kote, kati yao milioni 54 wakifanya kazi hatarishi ambazo zinaweza kuhatarisha afya yao, usalama wao au maendeleo yao kwa ujumla.Nchini Sudan Kusini watu wako katika hatari ya njaa katika miezi ijayo, kutokana na kuongezeka kwa mapigano katika jimbo la Upper Nile. Utafiti mpya kutoka katika Mfumo wa Uainishaji wa Viwango vya Uhakika wa Chakula (IPC) unaonesha kudorora kwa hali ya chakula na lishe katika maeneo ya Sudan Kusini yaliyoathiriwa na mapigano katika miezi ya karibuni.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno "MBEUZI, MNYWANYWA NA MACHAGU.”Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia ajali mbayá ya meli katika pwani ya Djibouti lililokuwa linabeba wahamiaji wengi. Pia tunasalia hapa makao makuu ambapo Kikao cha 18 cha Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu wenye Ulemavu COSP18. Mashinani tutakwenda nchini DRC.Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, (IOM) kwa ushirikiano wa karibu na mamlaka za Djibouti, linaongeza juhudi zake za kibinadamu kufuatia tukio la kusikitisha lililotokea pwani ya Djibouti ambapo takriban wahamiaji wanane walikufa maji na wengine 22 hawajulikani walipo.Katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Kikao cha 18 cha Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu wenye Ulemavu COSP18, kinaendelea na mwaka huu, mada kuu ni kuongeza uelewa wa haki na mchango wa watu wenye ulemavu katika maendeleo ya kijamii. Miongoni mwa washiriki ni ya kijana kutoka Louisiana, hapa Marekani.Makala tutasalia hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani ambapo Kikao cha 18 cha Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu wenye Ulemavu COSP18, kinaendelea na tutamsikiliza mmoja wa washiriki wa mkutano huu Bongani Simphiwe Makama kutoka Ufalme wa Eswatini ambaye amepata nafasi ya kuzungumza na idhaa ya Kiswahili.Na katika mashinani fursa ni yake fursa ni yake Byamungu Rukera, Mwakilishi wa watu waliokimbia makazi yao huko Sake, Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC akipazia sauti wakimbizi wenzake kwa wafanyakazi wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu na misaada ya dharura OCHA ambao wanawagawia chakula licha ya uhaba wa msaada huo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Kikao cha 18 cha Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu – COSP18 – kinaendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ikiangazia juhudi za kimataifa za kuhakikisha usawa na ujumuishaji kwa watu wenye ulemavu. Miongoni mwa washiriki ni Bongani Simphiwe Makama mwakilishi wa watu wenye ulemavu kutoka Ufalme wa Eswatini, ambaye amepata nafasi ya kuzungumza na Idhaa ya Kiswahili kuhusu uzoefu wake, yale aliyojifunza, na changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu nchini kwake. Sharon Jebichii na Makala zaidi.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo leo ikiwa ni siku ya mazingira duniani mwaka ikibeba maudhui “Tokomeza taka za Plastiki,” tunakwenda Tanzania kumsikia Clara Makenya, Mkua wa UNEP nchini humo na afisa mawasiliano wa shirika hilo kwa ajili ya Namibia akizungumza kuhusu changamoto ya taka za plastiki Tanzania na nini kifanyike kuzitokomeza.Naanzia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York, Marekani ambapo leo kumefanyika tukio maalum la kukumbuka na kuenzi watumishi 168 wa Umoja wa Mataifa waliopoteza maisha wakitekeleza majukumu yao ya ulinzi wa amani, haki, na usaidizi, Mishumaa iliwashwa na kisha walitajwa majina yao mmoja baada ya mwingine akiwemo Nats.. mlinda amani wa UN kutoka Tanzania. Wanafamilia walipokea tuzo maalum za kutambua mchango wao.Leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya mazingira, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametaka hatua za dharura kutokomeza janga la uchafuzi utokanao na taka za plastiki, akilitaja kama “janga” linaloikaba dunia na kutishia afya ya binadamu, mifumo ya ikolojia, na hali ya hewa. Guterres amesema, kadri plastiki zinavyovunjika na kuwa vipande vidogo vidogo zinaingia kila mahali: kuanziaubongo wa binadamu hadi maziwa ya mama.Huko nchini Tanzania hii leo kwenye Chuo Kikuu Mzumbe mjini Morogoro, kumefanyika kongamano kumulika uhaba wa maji na sera bora zinazoweza kufanikisha upatikanaji wa huduma hiyo, kongamano lililoandaliwa kwa pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP na Muungano wa Ulaya. Dkt. Saida Fundi Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu Mzumbe anasema.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIHEREHERE!.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno KIHEREHERE.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa ikitupeleka nchini DRC, Sierra Leone na Ghana. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na maana ya neno "MISHEMISHE.”Leo ni Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani ambayo mwaka huu inajikita na maudhui ya “mustakabali wa ulinzi wa amani.”Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema walinda amani wa Umoja wa Matafa wako katika changamoto kubwa “Leo hii, walinda amani wanakabiliwa na hali zinazozidi kuwa ngumu katika dunia inayozidi kuwa na changamoto, ikiwemo uugawanyika na kutofautiana kwa mitazamo duniani kunazidi kuongezeka, operesheni za ulinzi wa amani zinakabiliwa, hatari zaidi kutokana na wingi wa vitisho kama vile ugaidi na walinda amani kulengwa kwa makusudi kupitia taarifa potofu zenye madhara makubwa na changamoto zinazovuka mipaka kuanzia janga la mabadiliko ya tabianchi hadi uhalifu wa kimataifa.Kikosi cha 11 cha Tanzania kinachohudumu chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO kimeungana na walinda amani wengine kuadhimisha Siku ya Walinda Amani Duniani. Maadhimisho hayo yamefanyika Mavivi, yakiongozwa na Brigedia Jenerali Diamond Meshack Madie, Mnadhimu Mkuu wa Vikosi vya MONUSCO.Shirika la Umja wa Mataifa la Mazingira UNEP limezindua mpango mpya wa dola milioni 15 kusaidia uwekezaji endelevu katika Bonde la Kongo – moja ya mifumo muhimu zaidi ya ikolojia duniani. Mpango huu unalenga kufungua fursa za biashara rafiki kwa mazingira kwa wajasiriamali wadogo na wa kati katika sekta za kijani. Msitu wa mvua wa Bonde la Kongo ni moja ya vyanzo vikubwa vya kaboni duniani na ni makazi ya watu zaidi ya milioni 75, wakiwemo jamii za asili.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "MISHEMISHE.”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "MISHEMISHE.”
Katika kuelekea siku ya kandanda, kabumbu au mpira wa miguu duniani itakayoadhimishwa Jumapili wiki hii Mei 25 ikibeba maudhui nguvu ya kdandanda katika kuleta mabadiliko tuabisha hodi Nairobi Kenya ambapo leo Peter Omondi, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Global Youth Forum linalounganisha vijana Kenya kwa lengo la kutokomeza umasikini na kuishi maisha bora kupitia michezo mbalimbali ikiwemo kandanda akizungumza na Idhaa hii ya Kiswahili anaeleza umuhimu wa kandanda katika ajenda ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu. Anaanza kwa kujitambusha.
Hii leo jaridani tunaangazia haki za kibinadamu za raia nchini Uganda, na simulizi ya mkimbizi nchini Mexico ambaye alikimbia machafuko nchini mwake Haiti. Makala tunakwenda nchini Kenya na mashinani nchini Ethiopia, kulikoni?Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa , Volker Türk, leo Ijumaa mjini Geneva, Uswisi kupitia msemaji wake ameelezea wasiwasi wake kuhusu kupitishwa kwa muswada uliopendekezwa na Bunge la Uganda unaoruhusu raia kuhukumiwa katika mahakama za kijeshi.Wakati raia wa Haiti Giovanni Rotschild alipowasili Mexico mwaka 2022 baada ya safari ndefu isiyo na uhakika kutoka nchi mwake kulikosheheni ghasia, hakufahamu mtu yeyote wala hakuzungumza kabisa lugha ya kispanyola. Lakinialipata msaada kumwezesha kujenga upya maisha na kupata jamii mpya.Makala tukielekea siku ya kandanda, kabumbu au mpira wa miguu duniani itakayoadhimishwa Jumapili wiki hii Mei 25 ikibeba maudhui nguvu ya kdandanda katika kuleta mabadiliko tuabisha hodi Nairobi Kenya ambapo leo Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Global Youth Forum linalounganisha vijana Kenya kwa lengo la kutokomeza umasikini na kuishi maisha bora kupitia michezo mbalimbali ikiwemo kandanda akizungumza na Idhaa hii ya Kiswahili anaeleza umuhimu wa kandanda katika ajenda ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu.Na katika mashinani, fursa ni yake Hola msichana mwenye umri wa miaka 15 kutoka wilaya ya Sire nchini Ethiopia ambaye kutokana na mafunzo ya stadi za maisha ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF yanayoungwa mkono na asasi ya kupinga ndoa za utotoni ya GPChild Marriage ameweza kuepuka ndoa za utotoni na sasa anatumia mafunzo hayo kutahadharisha na kulinda wenzake.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini kumsikia mgeni wetu Prof. Wallah Bin Wallah, mwandishi mashuhuri wa vitabu vya Kiswahili kutoka Kenya ambaye anamulika umuhimu wa vitabu katika kukuza lugha ya Kiswahili. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno.Kwa mara ya kwanza tangu mwezi Februari, msaada wa kuokoa maisha umefika Gaza. Baada ya wiki 11 za kizuizi kutoka kwa mamlaka za Israeli, malori 198 yaliyobeba chakula, dawa na unga wa ngano yameingia leo kupitia mpaka wa Kerem Shalom kwa mujibu wa mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa.Mratibu mkuu wa misaada wa Umoja wa Mataifa, Tom Fletcher, ameiitaja hatua hiyo kuwa ya muhimu sana, huku malori 90 yakipakuliwa usiku kwa ajili ya kusambazwa haraka.Mwaka 2024, vita havikuishia kwenye uwanja wa mapambano pekee vilivunja nyumba, masoko na shule. Kuanzia Gaza hadi Ukraine, Sudan hadi Myanmar na zaidi ya raia 36,000 walipoteza maisha yao katika mizozo 14 ya kivita kulimgana na ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kwa Baraza la Usalama hii leo linalojadili ulinzi wa raia katika mizozo ya silaha.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DAHARI”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DAHARI."
Je, unajua kuwa kuna eneo maalum kwenye anga ambapo maisha yanaweza kustawi?
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "KIANGO."
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha katika mkutano wa CSW68 kumsikia Christina Kamili Ruhinda, Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Mashirika yanayotoa huduma ya msaada wa kisheria nchini Tanzania, TANLAP. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno la wiki.Wakati dunia ikiadhimisha miaka 77 tangu Nakba ambapo zaidi ya wapalestina 700,000 walifurushwa kutoka vijiji na miji yao mwaka 1948, shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa Wakimbizi wa Kipalestina UNRWA limetoa onyo kali kuhusu sura mpya ya mateso na ufurushwaji wa lazima uonaoendele Gaza.Akiwa na wasiwasi kutokana na ripoti za kuaminika kwamba wakimbizi wa Rohingya kutoka Myanmar walilazimishwa kushuka kutoka kwenye meli ya jeshi la wanamaji la India na kutoswa katika bahari ya Andaman wiki iliyopita, Mtaalamu wa UN wa Haki za Binadamu kuhusu wakimbizi wa Myanmar, ameanzisha uchunguzi kuhusu kitendo hicho alichoeleza kuwa ni cha kushangaza na kisichokubalika.Na baada ya muda mrefu kuonekana kama mchangiaji mkubwa wa utoaji wa hewa chafuzi duniani, sekta ya usafirishaji majini sasa iko mstari wa mbele katika kuonesha ushirikiano wa kipekee wa kimataifa wa kupunguza hewa hizo zitolewazo na meli za usafirishaji majini.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "KIANGO".Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Safari ya kuchunguza methali za Kiswahili - kutoka maana ya juu hadi hekima ya ndani. Kila kipindi kinatufunulia ukweli uliofichika kwenye maneno ya wahenga, tukielewa matumizi yake katika maisha ya leo. Jiunge nasi tukichambua busara za jadi zinazoendelea kuongoza maisha yetu.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa ambayo Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili alipata fursa ya kuzungumza na kiongozi wa kijamii kutoka Jamii ya wafugaji ya Wamaasai mkoani Morogoro nchini Mashariki mwa Tanzania Adam Kulet Ole Mwarabu.Wiki kumi baada ya kuanza kwa mzingiro kamili wa Israel dhidi ya wakazi wa Gaza, zaidi ya robo tatu ya kaya katika eneo la Palestina kuna uhaba mkubwa wa huduma ya maji, huku hali ya usafi ikizidi kuwa mbaya, yameonya leo mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu athari za "uhaba huo wa maji kwa kuzingatia kuwa msimu wa joto unakaribia.”Ripoti kutoka Sudan zikidai kwamba juzi jumatano kulikuwa na jaribio la mashambulizi mapya ya ndege zisizo na rubani dhidi ya kitovu muhimu cha misaada nchini humo juzi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kupitia tamko alilolitoa jana jioni kwa saa za New York, Marekani, ameongeza nguvu yake katika kutoa wito unaozidi kuwa wa muhimu kuhamasisha kuanzishwa kwa mazungumzo ya amani ya kweli.Kufuatia kuendelea kwa mvutano wa majirani, India na Pakistani, Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Philemon Yang, ametoa wito wa kuzitaka nchi hizo mbili kuchukua tahadhari na kuepuka hatua zinazoweza kuongeza mzozo. Balozi Yang anasisitiza mazungumzo ya amani na kufuata sheria za kimataifa ndiyo njia pekee ya kusuluhisha migogoro.”Na katika jifunze Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DALALI”Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DALALI”
Jukwaa la Umoja wa Mataifa kuhusu watu wa jamii za asili limekunja jamvi mwishoni mwa wiki iliyopita hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa na kandoni mwa jukwaa hilo Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili alipata fursa ya kuzungumza na mmoja wa washiriki kiongozi wa kijamii kutoka Jamii ya wafugaji ya Wamaasai mkoani Morogoro Mashariki mwa Tanzania Adam Kulet Ole Mwarabu, wamejadili mengi lakini Ole Mwarabu anaanza kwa kukumbusha alichokibeba kwenye jukwaa la mwaka jana kinavyotekelezwa nchini mwake.
Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, mkutano wa 24 wa Jukwaa la Kudumu la Watu wa jamii za asili (UNPFII) linaendelea kujadili utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili na kubaini mbinu bora za kushughulikia changamoto zinazowakabili, ukileta pamoja washiriki kutoka maeneo mbalimbali kote duniani. Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa walipata fursa ya kuzungumza na baadhi yao.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika Chata ya Umoja wa Mataifa inayolenga kusongesha amani, maendeleo, urafiki na haki za binadamu. Je, wajumbe wa Umoja wa Mataifa hufanya nini? Assumpta Massoi amezungumza na mmjoa wao Balozi Yabesh Monari wa Kenya, lakini kwanza ni muhtasari wa habari na ufafanuzi wa maneno.Mratibu wa misaada ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa nchini Ukraine, Matthias Schmale, amelaani vikali shambulio jipya la Urusi dhidi Ukraine lililosababisha vifo na majeruhi kwa raia, wakiwemo watoto na mwanamke mjamzito. Bwana Schmale amesema shambulio hilo la usiku wa kuamkia leo katika maeneo ya makazi jijini Kyiv na maeneo ya jirani ni ukiukaji wa kutisha wa sheria za kimataifa za kibinadamu na kwamba matumizi haya ya nguvu yasiyo na maana lazima yakome.Wiki ya Chanjo Duniani ikiwaimeanza leo, mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la afya duniani, WHO, na la kuhudumia Watoto, UNICEF, na Ubia wa chanjo duniani, Gavi wametoa onyo kwamba milipuko ya magonjwa yanayozuilika kwa chanjo inaongezeka kwa kasi. Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus, anasema, “Chanjo zimeokoa maisha ya watu zaidi ya milioni 150 katika kipindi cha miongo mitano iliyopita. Kupunguzwa kwa ufadhili wa afya ya kimataifa kumeweka hatarini mafanikio haya yaliyopatikana kwa juhudi kubwa.”Na ikiwa pia leo Siku ya kimataifa wasichana katika Teknolojia ya mawasiliano, ICT, Mshauri wa masoko ya kidijitali nchini Kenya Maryann Mwangi akizungumza na washirika wetu Redio Domus amehimiza wasichana kujikita kwenye ICT kwani huu ndio mustakabali.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua matumizi ya maneno "MKALIMANI NA MFASIRI"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua matumizi ya maneno "MKALIMANI NA MFASIRI."
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza, na harakati za utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili. Makala tunasalia hapa hapa makao makuu na mashinani tunakwenda nchini Burundi, kulikoni?Hali si hali huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli ambako wakimbizi wa ndani wanakabiliwa na hatari za kiafya ambako panya na wadudu kama vile viroboto na nzi wamesambaa kutokana na mlundikano wa taka na ukosefu wa huduma muhimu kama vile maji safi na salama.Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, mkutano wa 24 wa Jukwaa la Kudumu la Watu wa jamii za asili (UNPFII) linaendelea kujadili utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili na kubaini mbinu bora za kushughulikia changamoto zinazowakabili. Miongoni mwa shiriki wa jukwaa hilo nimwakilishii wa Shirika la Ereto Solidarity Funds ambaye amepata fursa ya kuzungumza na Sharon Jebichii wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa.Makala ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Kitabu na Haki Miliki ambapo kila mwaka tarehe kama ya leo siku hii huadhimishwa ili kutambua nguvu ya vitabu kama daraja kati ya vizazi na vizazi na tamaduni mbalimbali. Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na mwandishi maarufu wa vitabu vya elimu, Uchumi na uhamiaji, Ernest Makulilo mkazi wa Marekani katika jimbo la Missouri.Na mashinani kupitia video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO fursa ni yake Meena Poudel kutoka nchini Nepal, Kusini mwa Asia ambaye ni Katibu wa kikundi cha wanawake watumiaji wa msitu ambacho kinabadilisha takataka za misitu kuwa mbolea rafiki kwa mazingira huku pia wakijipatia kipato."Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Mkutano wa 24 wa Jukwaa la Kudumu la Watu wa jamii za asili (UNPFII) hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa linaendelea kujadili utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili na kubaini mbinu bora za kushughulikia changamoto zinazowakabili. Miongoni mwa shiriki wa jukwaa hilo nimwakilishii wa Shirika la Ereto Solidarity Funds ambaye amepata fursa ya kuzungumza na Sharon Jebichii wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa. Anaanza kwa kujitambulisha
Karibu kusikiliza jarida la Umoja wa Mataifa ambapo hii leo tunamulika Kongamano la Kimataifa la Kiswahili linalofanyika mjini Kampala Uganda likiwaleta pamoja wadau kutoka kila kona ya Afrika na kwingineko kujadili mikakati ya kukuza lugha hiyo adhimu ya Kiswahili. Utasikiliza muhtasari wa habari ukiangazia miaka miwili tangu kuanza kwa vita vya sasa vya Sudan, UNHCR, yatoa wito kwamba mwitiko mkubwa wa kibinadamu ulioratibiwa vema ni muhimu ili kuzuia mateso zaidi na vifo kwa wananchi wa DRC, na Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) limeanza leo tarehe 15 hadi tarehe 17 katika Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "FIFILIZA"
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Idhaa hii inazungumza na Mwenyekiti wa Tanzania Women Ecocomic Empowerment Network (TAWEN), ambaye pia ni mchumi mbobezi Bi. Janet Zebedayo Mbene. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na neno la wiki.Shukran Anold na leo tunaanzia huko Geneva Uswisi ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limetoa muongozo wake wa kwanza duniani wa kutambua, kutoa matibabu kwa haraka na matibabu ya muda mrefu kwa ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.Nchini Chad katika mpaka wake na Sudan ambako Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR Filippo Grandi ametembelea na kuzungumza na wakimbizi wa Sudan pamoja na kujionea hali zao wakati huu ambapo wamepunguza kutoa chakula, malazi , maji na dawa na kauli yake ikawa moja tu, “Ninatoa wito kwa wafadhili, tafadhali msipunguze msaada kwa wathirika wa vita vya Sudan.”.Taarifa ya pamoja ya mashirika ya kibinadamu inayotolewa kila baada ya wiki mbili imeeleza kuhusu hali katika Ukanda wa Gaza inasema kuwa watu wanazidi kuuwawa na kujeruhiwa. Kwa zaidi ya mwezi sasa hakuna misafara ya misaada inayoruhusiwa kuingia Gaza. Watu kulazimishwa kuhama kinguvu kunaendelea, makazi ya wakimbizi yamefikia pomoni, huduma za usafi na kujisafi nazo ni mbaya.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "FIFILIZA"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha kwenye mkutano wa hivi majuzi wa CSW69 kufuatilia harakati za Mfuko wa CRDB za kujengea uwezo na kuinua wanawake nchini Tanzania. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno “MHARUMA.”Mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau wa misaada ya kibinadamu leo wamesema wanaendelea kuwasaidia watu wa Muyanmar na mahitaji ya msingi baada ya tetemeko kubwa la ardhi la Ijuma iliyopita ambapo idadi ya waliopoteza maisha sasa ni zaidi ya 2,800, maelfu wamejerihiwa na mamia bado hawajulikani wako.Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu, Volker Türk, amesema leo kwamba ameshtushwa na ripoti za mauaji ya raia bila kufuata utaratibu wa kisheria yaliyoenea mjini Khartoum baada ya kurejeshwa kwa mji huo chini ya udhibiti wa Jeshi la Sudan (SAF) tarehe 26 Machi.Na majadiliano ya siku mbili ya kila mwaka ya será kuhusu maendeleo endelevu yaliyoandaliwa na Club De Madrid yameanza leo Nairobi Kenya mwaka huu yakijikita na ufadhili wa maendeleo. shududa wetu huko ni Stella Vuzo kutoka kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIS Nairobi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno MHARUMA”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "MHARUMA.”
Hii leo dunia ikiadhimisha siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu usonji, Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imezungumza na Muasisi na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Lukiza Foundation nchini Tanzania inayoelimisha umma kuhusu usonji. Usonji ni hali inayompata mtoto au utofauti au changamoto katika mfumo wake wa ufahamu na ubongo na kusababisha changamoto za kimawasiliano, tabia na kudhibiti hisia mwili. Hoja kubwa ni kwamba hadi sasa sababu ya hali hiyo kumpata mtoto haijajulikana na ndipo taasisi hiyo inachagiza Umoja wa Mataifa na wadau washikamane katika tafiti kujua chanjo kama njia mojawapo ya kudhibiti au kutibu ugonjwa huo. Basi kwa kina kufahamu harakati za taasisi hiyo nchini Tanzania, nampisha Assumpta Massoi wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa.
Karibu kujifunza Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye Kitivo cha Tafsiri na Ukalimani na anafafanua methali Ndoto njema haihadithiwi.
Rekodi ni chache sana ya vitu ambavyo wanawake wamefanya hapa duniani, anasema Dkt. Rose Reuben, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania anapozungumza na Anold Kayanda wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa wakati wa Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake, CSW69, jijini New York, Marekani.Mkutano huu muhimu kuhusu wanawake umefanyika kuanzia tarehe 10 hadi 21Machi 2025 na kuhudhuriwa na maelfu ya wanawake kutoka kote duniani naye Dkt. Rose Reuben akiwa mmoja wao.Kiongozi huyu wa waandishi wa habari nchini Tanzania anaona kwamba kuna hatua nyingi zimepigwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuwekwa kwa Azimio la Beijing ili kumkomboa mwanamke lakini bado kuna kazi kubwa ya kufanya.“Na hii kazi sipendi kujilaumu sana kwamba je, hakuna kitu ambacho kimefanyika?! Mambo yamefanyika mengi lakini masuala ya kijamii hayamaliziki kwa usiku mmoja kwasababu kila unapoamka jamii inabadilika kwa namna nyingine. Kwa hiyo tukitazama kwa mtazamo huo tunaona kwamba kuna kazi imefanyika.” Anasema Mkrugenzi huyo Mtendaji wa TAMWA.Kwake, mwandishi wa habari nguli, anaona moja ya maeneo ambayo ni muhimu yafanyiwe kazi ni kuzipa nafasi taarifa zinazohusu shughuli kubwa zinazofanywa na wanawake katika jamii kote duniani kwani licha ya wanawake kuwa na michango mikubwa katika mustakabali wa ulimwengu, taarifa zao hazipewi kipaumbele cha kutosha.“Mimi kwa mtazamo wangu naona wanawake wamefanya kazi nyingi lakini hazijarekodiwa. Rekodi ni chache sana.” Anasisitiza na kuongeza, “kwa hiyo tunatakiwa kuanza kurekodi vile vitu ambavyo vilifanywa na wanawake wale wa miaka 30 iliyopita lakini hata na hawa wanaokuja kizazi kipya.”Dkt. Rose Reuben anahamasisha pia vyombo vya habari kuangazia masuala mengine ambayo kwa namna moja amba nyingine yanaigusa jamii moja kwa moja na hiyo ni kusema yanamgusa mwanamke moja kwa moja kama vile mabadiliko ya tabianchi, tekonolojia, “na vitu vingine ambavyo vinaweza kuathiri usawa wa kijinsia na hali ya mwanamke duniani.”Aidha kiongozi huyo wa TAMWA anatoa wito kwa wanawake popote walipo kutumia nyenzo zinazopatikana katika jamii yao kuhakikisha wanapata taarifa, wanasambaza taarifa na kujipatia maarifa.
Wakati mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani CSW69 ukifikia ukingoni mshiriki kutoka Zanzibar Tanzania ameweleza Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili kwamba Zanzibar imepiga hatua kubwa katika usawa wa kijinsia na utekelezaji kwa vitendo matakwa ya Azimio la Beijing la usawa wa kijinsia na hatua. Je wametekeleza vipi na hatua gani walizopiga? Ungana nao katika mahojiano haya.
Hii leo jaridani katika mada kwa kina tunajikita katika mkutano CSW69 ambao umebakiza siku moja tu, kesho Machi 21 unakunja jamvi, na tunamsikia Dkt. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Tanzania, Waziri Riziki Pembe kutoka Zanzibar na Profesa Smile Dzisi, Mkugenzi wa Shirika la “I believe Global” kutoka Ghana.Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR Filippo Grandi amesema kukata ufadhili kwa mashirika yanayotoa huduma za kibinadamu kunasababisha janga la uwajibikaji. Kupitia taarifa iliyotolewa leo Geneva, Uswisi na UNHCR, Bwana Grandi amesema kukata ufadhili kunaweka hatarini maisha ya mamilioni ya watu na madhara yake kwa watu wanaokimbia majanga, yatakuwa makubwa zaidi na yataonekana wazi ikiwemo wanawake na watoto wa kike kukosa huduma zitokanazo na kubakwa.Leo ni siku ya furaha duniani maudhui yakimulika umuhimu wa watu kusaidiana na kujaliana katika masuala mbalimbali ikiwemo chakula. Ripoti mpya ya wadau wa UN iliyozinduliwa leo imeonesha kuwa nchi yenye furaha zaidi duniani ni Finland na ya mwisho kabisa ni Afghanistani. Katika 10 bora zenye furaha hakuna hata moja ya Afrika, ilihali kwenye 10 za mwisho nchi za Afrika ni 7 ambazo ni Lesotho, Comoro, Botswana, Zimbabwe, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Malawi na Sierra Leone.Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW69 ukikaribia ukingoni hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa tumemuuliza mshiriki Wakili Rosemary Mwaipopo kutoka Tanzania mkutano umekidhi kiu yake ya kusongesha usawa wa kijinsia?Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno “Ashiraf, Janabi, gayagaya, kiti cha marimba na kiti cha msaji”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno “Ashiraf, Janabi, gayagaya, kiti cha marimba na kiti cha msaji”
Katika makala Flora Nducha wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa anazungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la ICCAO kutoka Tanzania, Zahra Salehe, mshiriki mwingine kutoka Tanzania anayehudhuria mkutano wa 69 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW69 unaoendelea hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, jijini New York Marekani.
Hii leo jaridani tunaangazia madhara ya mabadiliko ya tabianchi yanayosababishwa na binadamu, na yaliyojiri hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa mkutano wa 69 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW69.Madhara ya mabadiliko ya tabianchi yanayosababishwa na binadamu yameongezeka kwa viwango vya kutisha mwaka 2024, na baadhi ya athari hasi zinaweza kuwa zisizoweza kurekebishwa kwa karne nyingi – kama si milenia, imesema ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa, (WMO).Tukirejea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake Duniani CSW69 unaendelea kujadili mafanikio yaliyopatikana na nini kifanyike zaidi kutimiza lengo la miaka 30 iliyopita la azimio la Beijing. Mwanzilishi na mkurugenzi mkuu wa shirika la slums foundation lililoko jijiniNairobi, Kenya naye anashiriki mkutano huu wa CSW69 na ameueleza Sharon Jebichii wa Idhaa hii kilichomleta hapa, matarajio yake na ushauri kwa wasichana na wanawake..Makala Flora Nducha wa Idhaa hii anazungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la ICCAO kutoka Tanzania, Zahra Salehe, mshiriki mwingine kutoka Tanzania anayehudhuria mkutano wa 69 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW69 unaoendelea hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, jijini New York Marekani lakini kwanza ni makala ambapo.Na katika mashinani fursa ni yake Dewa Sitabile kutoka Zimbabwe ambaye amezungumza na idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa mataifa kandoni mwa mkutano wa CSW69 akisema hatua zimepigwa lakini bado kazi yahitajika kuhahikisha wanawake na wasichana wamepata haki zao.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Idhaa hii imezungumza na Lucy Gidamis, Wakili ambaye kwa sasa anafanya kazi na shirika la Msichana Initiative nchini Tanzania akijikita katika kutetea na kutekeleza haki za wanawake. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ufafanuzi wa neno Wakfu.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC hii leo Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO umekabidhi magari sita kwa gavana wa kijeshi wa jimbo la Kivu Kaskazini ili kuwezesha shughuli za polisi katika kuimarisha ulinzi na usalama.Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Afya duniani WHO na la kuhudumia watoto UNICEF yametangaza kuwepo kwa idadi kubwa ya wagonjwa wa surua barani ulaya, jumla ya wagonjwa 127,350 waliripotiwa kati yao watoto wakiwa zaidi ya asilimia 40.Na hii leo ikiwa ni chungu cha 10 cha Ramadhan, ikikamilisha fungu la kwanza kati ya mafungu matatu ambapo ni siku 30 za mwezi Mtukufu wa Ramadhan, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameanza ziara yake ya siku nne nchini Bangladesh ikiwa ni utaratibu wake wa kila mwaka wa kushiriki Ramadhan na jamii za waislamu walio kwenye changamoto mbalimbali.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua neno Wakfu.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Kate Pilcher is the founder of Globetrotting, a travel agency offering horse riding holidays and unique horse cultural experiences all around the world. Kate discovered this remarkable form of travel at age 25, when she ran away from her business, her boyfriend Steven, and her mortgage in pursuit of the magic that comes with exploring new, wild places in the saddle. She worked as a horse riding guide in Kenya and Argentina, and learnt conversational Kiswahili and Spanish. When she finally returned home, Globetrotting was born. Kate considers it her true calling to share the life-changing experience of Globetrotting with as many people as possible. She and Steven - now her husband - live on Australia's Sunshine Coast with their three girls, who often join them on guided Globetrotting rides, and an ever-growing herd of horses.Support the showBecome a Patreon Member today! Get access to podcast bonus segments, ask questions to podcast guests, and even suggest future podcast guests while supporting Warwick: https://www.patreon.com/journeyonpodcastWarwick has over 650 Online Training Videos that are designed to create a relaxed, connected, and skilled equine partner. Start your horse training journey today!https://videos.warwickschiller.com/Check us out on Facebook: https://www.facebook.com/WarwickschillerfanpageWatch hundreds of free Youtube Videos: https://www.youtube.com/warwickschillerFollow us on Instagram: @warwickschiller