Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kutana na Maseka ambaye ni miongoni mwa makumi ya maelfu ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, waliovuka mpaka na kuingia nchi Jirani ya Burundi baada ya ghasia kulazimisha familia yake kukimbia mashariki mwa DRC. Flora Nducha na taarifa zaidi

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limesema ukosefu wa chakula utaendelea kuwa katika viwango vya kutisha katika mwaka ujao wa 2026, huku mamilioni ya watu wakikabiliwa na njaa kali duniani. Leah Mushi na maelezo zaidi.

Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya WFP ya uhakika wa chakula mwaka 2026 duniani, wakimbizi kutoka DRC, waliovuka mpaka na kuingia Burundi, na kilimo cha umwagiliaji kwa jamii za Hirshabelle nchini Somalia. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limesema ukosefu wa chakula utaendelea kuwa katika viwango vya kutisha katika mwaka ujao wa 2026, huku mamilioni ya watu wakikabiliwa na njaa kali duniani.Kutana na Maseka ambaye ni miongoni mwa makumi ya maelfu ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, waliovuka mpaka na kuingia nchi Jirani ya Burundi baada ya ghasia kulazimisha familia yake kukimbia mashariki mwa DRC.Jamii za wakulima katika mkoa wa middle Shabelle, Somalia, zimeathiriwa vibaya na ukame na mafuriko yanayodhoofisha kilimo na uhakika wa chakula. Ili kukabiliana na hili, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO), Somalia kwa ufadhili wa Serikali ya Uswisi imetekeleza mradi wa BRiMS unaolenga kuimarisha mnepo kwa wakulima kupitia ukarabati wa miundombinu ya vijijini, urejeshaji wa mifumo ya umwagiliaji, na kuijengea jamii uwezo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Jamii za wakulima katika mkoa wa middle Shabelle, Somalia, zimeathiriwa vibaya na ukame na mafuriko yanayodhoofisha kilimo na uhakika wa chakula. Ili kukabiliana na hili, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO), Somalia kwa ufadhili wa Serikali ya Uswisi imetekeleza mradi wa BRiMS unaolenga kuimarisha mnepo kwa wakulima kupitia ukarabati wa miundombinu ya vijijini, urejeshaji wa mifumo ya umwagiliaji, na kuijengea jamii uwezo. Sheilah Jepng'etich na taarifa zaidi.

Katika Jarida la Umoja wa Mataifa hii leo Anold Kayanda anakuletea Jarida Maalum linalomulika Maoni ya washirika wetu mbalimbali wa Televisheni na Radio kutoka Afrika Mashariki.Wanazungumzia umuhimu wa ushirika na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa Yale waliyofaidika nayo katika ushirika huu na nini kiboreke mwakaniMapendekezo yao kwa mwaka ujao wa 2026Na salamu zao za mwaka mpya 2026

Mwaka 2025 umeelezwa kuwa mwaka wa kihistoria kwa sekta ya afya duniani. Hayo ni kwa mujibu wa ujumbe uliotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO,Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus, wakati akitoa tathmini yake ya mwisho ya mwaka 2025. Taarifa zaidi na Sabrina Saidi. Karibu Sabrina..(TAARIFA YA SABRINA SAIDI) Asante Flora,Akizungumza kutokea makao makuu ya WHO mjini Geneva, Uswisi, Dkt. Tedros amesema mwaka 2025 umekuwa na mafanikio makubwa pamoja na changamoto nzito kwa afya ya dunia, huku akisisitiza kwamba dunia bado inahitaji uwepo wa WHO. (Clip 1-Sauti ya Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus)“Kweli mwaka 2025 umekuwa mwaka wa mafanikio makubwa na changamoto nyingi kwa afya ya dunia na kwa WHO. Mafanikio makubwa zaidi yalikuwa kupitishwa kwa Mkataba wa WHO wa kukabiliana na milipuko ya magonjwa, ambao ni mfano wa nguvu ya ushirikiano wa kimataifa pale nchi zinapochagua kushirikiana badala ya kugawanyika. Pia, mwaka huu WHO imethibitisha nchi 13 kufanikiwa kutokomeza magonjwa, ikatoa miongozo kuhusu tiba mpya kama Lenacapavir kwa kinga dhidi ya VVU na matibabu ya GLP-1 kwa utipwatipwa,na ikachukua hatua dhidi ya majanga 48 katika nchi na maeneo 79, ikiwemo Gaza, Sudan na Ukraine.”Akizungumzia changamoto, Dkt. Tedros amesema kupunguzwa kwa misaada ya kimataifa na bajeti kumeathiri sekta ya afya duniani, lakini ameeleza kuwa hali hiyo pia inaleta fursa mpya.(Clip 2- Sauti ya Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus)“Lakini ndani ya changamoto hizi pia kuna fursa. Ni fursa kwa nchi kuondokana na utegemezi wa misaada na kujenga mifumo ya afya inayojitegemea, na ni fursa kwa WHO kuwa taasisi imara zaidi na inayojipanga kwa siku zijazo. Dunia bado inahitaji WHO, na WHO itaendelea kushikilia maono yake ya msingi kuhakikisha kiwango cha juu kabisa cha afya kinapatikana kwa wote, si kama upendeleo wa wachache, bali kama haki ya kila mtu.”Dkt. Tedros amehitimisha ujumbe wake kwa kusema kuwa WHO itaendelea kushirikiana na nchi wanachama ili kukabiliana na changamoto za sasa na zijazo za afya duniani.

Huko kaskazini mashariki mwa Somalia, eneo la Laascaanood linaendelea kushuhudia maboresho ya huduma muhimu za afya baada ya miaka miwili ya kuvurugika kwa huduma hizo kutokana na mizozo, maboresho haya yanaleta huduma za afya karibu zaidi na akina mama na watoto shukran kwa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF na washirika wake. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.(Taarifa ya Leah)Kwa mujibu wa UNICEF nchini Somalia, mamilioni ya watoto wanakua katika kivuli au mazingira ya ukimya na dharura zilizosahaulika, takribani watoto milioni 1.8 wanahitaji matibabu ya utapiamlo mwaka huu wa 2025. Kila mwaka watoto wapatao 75,000 walio chini ya umri wa miaka mitano hufariki dunia kutokana na magonjwa yanayozuilika na yanayoweza kutibiwa.Miaka miwili ya migogoro imesababisha kusambaratika kwa huduma muhimu huko Laascaanood. Kurejea kwa hali ya utulivu kumeanza kushuhudia urejeshwaji wa taratibu wa huduma hizi muhimu zinazookoa maisha. UNICEF, kwa msaada wa KSRelief na Saudi Esports Federation, inachangia kwenye kutoa huduma jumuishi za afya ya msingi, huku huduma hizo zote zikitolewa chini ya paa moja.Mpaka sasa maelfu ya watu wamefikiwa huku ukisaidia vituo 13 vya afya kama anavyoeleza Dayid Said Ismail Afisa Lishe (Sauti ya Dayid Said Ismail – Evarist)“Mradi huu unasaidia vituo 13 vya afya na unahudumia zaidi ya watu 150,000. Huduma zake zinajumuisha chanjo za watoto, matibabu ya magonjwa kama nimonia na kuhara, pamoja na huduma za magonjwa mengine ya kawaida ya utotoni.”Katika huduma za matibabu tumsikilize Saida Ali Elmi ambaye ni mhudumu wa Afya(Sauti ya Saida Ali Elmi- Sheilah)“Kama mnavyoona, akina mama wengi wamekuwa kwenye foleni tangu saa moja asubuhi na sasa ni saa 5:30 asubuhi. Kwa hiyo wapo hapa kwa ajili ya chanjo za kinga, ikiwemo chanjo za kifua kikuu, surua, polio, pepopunda, kifaduro, pamoja na chanjo mpya iitwayo PCV ya nimonia.”Juhudi hizi zinazofanywa na mashirika haya, tayari zimeanza kuleta matumaini mapya kwa Ayan Hassan Abdi mama mzazi wa Maryam “Nimemleta Maryam kwa sababu alikuwa na homa. Amepatiwa matibabu na pia chanjo. Alifanyiwa vipimo vya homa na kuharisha, na akatibiwa vizuri, Masha'Allah.”

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa ujumbe mzito wa Mwaka Mpya kwa ulimwengu akisema ulimwengu uko katika njia panda, ukikabiliwa na machafuko, sintofahamu na migawanyiko mikubwa na hivyo kutoa wito kwa wanadamu kuinuka pamoja kwa ajili ya haki, ubinadamu na amani. Karibu Anold Kayanda kwa maelezo zaidi.(Taarifa ya Anold Kayanda)Katika ujumbe wake wa video uliosambazwa leo asubuhi saa za New York, Marekani, kwa ajili ya mwaka mpya wa 2026, Katibu Mkuu wa Umoja wa Maraifa anauanza ujumbe wake kwa kusema, “tunapoingia mwaka mpya, dunia iko njia panda.” Amesema dunia inakumbwa na vurugu zinazoendelea, athari kubwa za mabadiliko ya tabianchi pamoja na ukiukwaji wa kimfumo wa sheria za kimataifa hali ambayo, kwa mujibu wake, inatishia misingi inayounganisha binadamu kama familia moja ya dunia.Guterres amesema watu kote ulimwenguni wanaendelea kujiuliza iwapo viongozi wao wanasikiliza kilio cha wananchi na kama wako tayari kuchukua hatua za dhati kukabiliana na changamoto hizi.Akigeukia takwimu, Katibu Mkuu ameeleza kuwa matumizi ya kijeshi duniani yamefikia dola trilioni 2.7, ongezeko la karibu asilimia kumi kiwango ambacho ni mara kumi na tatu zaidi ya misaada yote ya maendeleo, na kinacholingana na Pato la Bidhaa za ndani la Bara zima la Afrika.Amesema ongezeko hilo linatokea wakati dunia ikishuhudia mizozo mikubwa kwa viwango ambavyo havijawahi kuonekana tangu Vita Vikuu Vya Pili Vya Dunia.Kutokana na hali hiyo, Katibu Mkuu ametoa wito kwa dunia kutumia mwanzo wa mwaka mpya kuweka vipaumbele sahihi, akisisitiza kuwa ulimwengu salama hujengwa kwa kuwekeza zaidi katika kupambana na umaskini badala ya kuwekeza katika vita.Guterres amesisitiza kuwa dunia ina rasilimali za kutosha kuinua maisha ya watu, kuponya sayari na kujenga mustakabali wa amani na haki, endapo tu zitatumika ipasavyo.Kwa mwaka 2026, amewataka viongozi wa dunia kuwa makini zaidi na kufanya uamuzi unaoweka mbele maslahi ya watu na mazingira badala ya kuendeleza mateso.Aidha, amewahimiza raia wote duniani kushiriki kikamilifu katika kujenga dunia bora, akisema mustakabali wa ubinadamu unategemea ujasiri wa pamoja wa kuchukua hatua.Katika kuhitimisha ujumbe wake, Katibu Mkuu ametoa wito wa mshikamano kwa ajili ya haki, ubinadamu na amani duniani.

Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea-Katika ujumbe wake wa mwaka mpya 2026 Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres ameitaka dunia kushikamana kwa ajili ya amani, maendeleo, na usalama badala ya kuongeza mateso-Huko Somalia kwa msaada wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na wadau wakaazi wa Laascanood waboreshewa huduma za afya baada ya kuvurugika kwa miaka miwili-Na Mkuu wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO amesema mwaka 2025 ulighubikwa na changamoto lukuki za afya ya umma duniani ikiwemo ukata wa ufadhili, lakini kuna matumaini hasa katika suala la utipwatipwa

WHO: Pombe yasababisha kifo cha mtu 1 kati ya 3 kutokana na majeraha barani Ulaya.Gaza: Uhaba wa vifaa tiba unawatesa wagonjwa.UNICEF na wadau wafanikisha kampeni ya chanjo ya Mpox katika kaunti ya Mombasa - Kenya.

Hii leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "USIAHI, UKENJA AU UNYENDE"

Karibu kusikiliza jarida la habari za Umoja wa Mataifa ambapo hii leo mada kwa kina inaangazia juhudi za kuwa na nishati safi nchini Tanzania ambapo vijana watazungumzia mradi wao wa kuchakata taka za plastiki na kupata nishati safi ya kupikia. Pia utapata fursa ya kusikiliza muhtasari wa habari ukiangazia wakimbizi wa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Congo DRC, Masuala ya Haki za Binadamu nchini Burundi na Matumaini ya watoto wa Gaza. Mwenyeji wako ni Leah Mushi.


Umoja wa Mataifa unaendelea kuonesha wasiwasi mkubwa kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu katika eneo la Darfur, Sudan, ukionya kuwa mashambulizi yanayolenga makundi maalum ya watu yanaweza kuashiria hatari kubwa zaidi ya mauaji ya kimbari. Flora Nducha na Taarifa zaidi

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, linasema tiba asilia na tiba jadidifu zina nafasi muhimu katika mifumo ya afya duniani, hasa katika kinga, huduma za usaidizi wa magonjwa na kuongeza upatikanaji wa huduma za afya kwa jamii. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Kitengo cha Tiba Asilia, Jadidifu na Jumuishi cha WHO, Dkt. Sung Chol Kim, katika mahojiano maalum kando ya Mkutano wa Kimataifa wa Tiba Asilia unaoendelea huko New Delhi, India. Sabrina Saidi na taarifa zaidi..

Hii leo jaridani tunaangazia uchaguzi wa Barham Ahmed Salih wa kuwa Kamishna Mkuu ajaye wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, Tiba asili, na haki za binadamu nchini Sudan. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amekaribisha hatua ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ya hapo jana kumchagua Rais Mstaafu wa Iraq, Barham Ahmed Salih wa kuwa Kamishna Mkuu ajaye wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, kwa muhula wa miaka mitano ijayo.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, linasema tiba asilia na tiba jadidifu zina nafasi muhimu katika mifumo ya afya duniani, hasa katika kinga, huduma za usaidizi wa magonjwa na kuongeza upatikanaji wa huduma za afya kwa jamii. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Kitengo cha Tiba Asilia, Jadidifu na Jumuishi cha WHO, Dkt. Sung Chol Kim, katika mahojiano maalum kando ya Mkutano wa Kimataifa wa Tiba Asilia unaoendelea huko New Delhi, IndiaUmoja wa Mataifa unaendelea kuonesha wasiwasi mkubwa kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu katika eneo la Darfur, Sudan, ukionya kuwa mashambulizi yanayolenga makundi maalum ya watu yanaweza kuashiria hatari kubwa zaidi ya mauaji ya kimbari.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amekaribisha hatua ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ya hapo jana kumchagua Rais Mstaafu wa Iraq, Barham Ahmed Salih wa kuwa Kamishna Mkuu ajaye wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, kwa muhula wa miaka mitano ijayo. Selina Jerobon na taarifa zaidi.

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ya vijana wanaotafuta fursa za mafunzo kwa vitendo. Umoja wa Mataifa ni moja ya mashirika ya kimataifa yanayotoa fursa hii kwa vijana kutoka duniani kote kuja hapa Makao Makuu jijini New York Marekani au hata katika nchi husika.Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo imefichua mauaji ya kutisha, ubakaji na matumizi ya njaa kama silaha ya vita katika kambi ya Zamzam, Darfur, Sudan. Kwa mujibu wa ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR, raia wasiopungua 1,013 waliuawa katika mashambulizi ya siku tatu ya wanamgambo wa RSF mwezi Aprili, huku zaidi ya watu 400,000 wakilazimika kukimbia makazi yao.Leo, katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wahamiaji, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amemulika mchango mkubwa wa mamilioni ya wahamiaji duniani, wakati uhamiaji ukiendelea kuwa mgumu zaidi kutokana na migogoro, majanga yanayohusiana na tabianchi na shinikizo za kiuchumi. Ameeleza kuwepo kwa viwango vya juu zaidi vya watu waliolazimika kuhama makazi yao na idadi kubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa ya vifo vya wahamiaji wakiwa safarini, huku akisisitiza kuwa uhamiaji salama na unaosimamiwa vyema unaweza kuchochea ukuaji wa uchumi, ubunifu na maendeleo katika nchi za asili na zinazopokea wahamiaji. Guterres amesema, “Uhamiaji unapokuwa salama na unasimamiwa vyema, si janga la kuogopa, bali ni nguvu kubwa ya kuleta mema.”.Na Ama K. Babebrese Balozi mwema wa kitaifa wa shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM mwenye asili ya Ghana ambaye sasa ni muhamiaji nchini Uingereza, katika siku hii ya uhamiaji ametoa ujumbe maalum akisema "Napenda kumtia moyo kila mtu kwamba tunaweza kuwa tofauti, hadithi zetu za uhamiaji ni tofauti tumetoka kwenye mazingira tofauti lakini kitu cha muhimu ni kwamba kama jamii sisi ni kitu kimoja. Uhamiaji ndio hadithi yangu”.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO, linaweka mkazo mpya wa kisayansi katika tiba asili au mitishamba, wakati mawaziri, wanasayansi na viongozi wa jamii za asili kutoka zaidi ya nchi 100 wakikutana mjini New Delhi India kuanzia leo kuangazia mchango wa dawa za asili. Flora Nducha na taarifa zaidi

Kuongezeka kwa machafuko katika jimbo la Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kumesababisha watu wengi kuyahama makazi yao ndani na kumbilia kusaka hifadhi nchi Jirani ya Burundi. Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wakimbizi limeeleza mpaka sasa karibu wakimbizi 64,000 tayari wamewasili Burundi, na idadi ikitarajiwa kuongezeka. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi

Hii leo jaridani tunaangazia tiba asili, machafuko katika jimbo la Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na ubakaji unaotumika kama silaha ya vita nchini humo humo.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO, linaweka mkazo mpya wa kisayansi katika tiba asili au mitishamba, wakati mawaziri, wanasayansi na viongozi wa jamii za asili kutoka zaidi ya nchi 100 wakikutana mjini New Delhi India kuanzia leo kuangazia mchango wa tiba za asili.Kuongezeka kwa machafuko katika jimbo la Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kumesababisha watu wengi kuyahama makazi yao ndani na kumbilia kusaka hofadhi nchi Jirani ya Burundi. Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wakimbizi limeeleza mpaka sasa karibu wakimbizi 64,000 tayari wamewasili Burundi, na idadi ikitarajiwa kuongezeka.Ubakaji unaotumika kama silaha ya vita huacha majeraha yasiyofutika ya mwili, akili na ya roho. Katika ushuhuda huu wenye nguvu, manusura mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa anaishi kama mkimbizi nchini Burundi, anasimulia safari yake ya maumivu baada ya kunusurika ukatili wa kingono uliomsababishia majeraha makubwa ya mwili, ikiwemo fistula, pamoja na makovu ya kina ya kihisia.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Ubakaji unaotumika kama silaha ya vita huacha majeraha yasiyofutika ya mwili, akili na ya roho. Katika ushuhuda huu wenye nguvu, manusura mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa anaishi kama mkimbizi nchini Burundi, anasimulia safari yake ya maumivu baada ya kunusurika ukatili wa kingono uliomsababishia majeraha makubwa ya mwili, ikiwemo fistula, pamoja na makovu ya kina ya kihisia.Sheilah Jepng'etich na taarifa zaidi

Frida Amani, msanii wa muziki wa kizazi kipya wa kwa hip hop au muziki wa kufokafoka almaarufu kama rap kutoka nchini Tanzania, ambaye pia ni mtangazaji na mwanamazingira, amepata heshima kubwa ya kuwa Balozi wa Shirika la Umoja wa Mataifa wa Mazingira UNEP, akiwa na jukumu la kuhamasisha kurejesha ikolojia duniani. Akizungumza katika mahojiano maalum na UN News Kiswahili kandoni mwa mkutano wa 7 wa Baraza la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEA7 uliokunja jamvi mwishoni mwa wiki, Frida amesema “Ni nafasi kubwa sana ambayo nimeipata. Sio kwangu tu, ni kwa ajili ya vijana wenzangu”. Tuungane na Afisa Habari wa Umoja wa Mataifa Stella Vuzo na mchechemuzi huyu katika makala hii.

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kwake Afisa Habari wa UN Stella Vuzo ambaye kandoni mwa mkutano wa UNEA-7 uliokunja jamvi mwishoni mwa wiki, alizungumza na Frida Amani, Mchechemuzi wa UNEP wa masuala ya mazingira.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, linasema aina mpya ya virusi vya mafua inaenea kwa kasi duniani, ikiwa imeripotiwa katika zaidi ya nchi 30. WHO wanasema licha ya aina hiyo kutosababisha ugonjwa mkali zaidi wa mafua, chanjo bado ni kinga bora zaidi dhidi ya madhara makubwa na kulazwa hospitalini na inawahimiza wananchi, hasa makundi yaliyo hatarini, kupata chanjo mapema huku ikionya kuwa msimu huu wa likizo unaweza kuongeza maambukizi ya magonjwa ya njia ya hewa.Tuelekee Bujumbura Burundi ambapo maelfu ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia Congo wamepatiwa hifadhi baada ya kukimbia machafuko nchini mwao. Innocent Chubaka kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR aliyeko katika kambi ya muda ya Mugara katika jimbo la Rumonge nchini Burundi anasema “tumepokea idadi kubwa ya wakimbizi wa Congo ambao wamefika kupitia njia ya ziwa wakiwa na mitumbwi kuu kuu.Na kwa mara nyingine tena Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk amezisihi pande zote katika mzozo nchini Sudan na Mataifa yenye ushawishi kuhakikisha mapigano yanasitishwa mara moja na kuzuia ukatili. Turk amelaani vikali mauaji ya raia zaidi ya watu 104 pia mauaji ya walinda amani sita wa Umoja wa Mataifa katika mashambulizi ya ndege zisizo na rubani kwenye kambi ya Umoja wa Mataifa huko Kaduguli, Kordofan Kusini, mnamo Desemba 13.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO linaendelea na mfululizo wa programu ya kuiunganisha jamii au Social Connection ikiwa na lengo la kusaidia watu kutojitenga na kujihisi wapweke, mmoja kati ya walionufaika wa programu hiyo ni Roz, binti mwenye umri wa miaka 21 raia wa India, aliyehisi upweke mkubwa wakati baba yake alipokuwa akipambana na ulevi. Nini kilitokea na aliwezaje kuishinda hali hiyo??? Tuungane na Leah Mushi katika simulizi hii.

Hii leo jaridani tunaangazia kilichojiri katika Mkutano wa COSP11 kuhusu ufisadi mjini Doha Qatar, haki za kibinadamu na vijana nchini Kenya, afya ya akili ikimulika upweke na jinsi unavyoweza kuepukana nayo.Mkutano mkubwa zaidi duniani wa kupambana na rushwa au ufisadi umeanza leo Desemba 15 mjini Doha nchini Qatar kwa wito wa kutumia teknolojia zinazoibuka katika mapambano dhidi ya rushwa na kushughulikia uhusiano wake na uhalifu wa kupangwa na makosa mengine ya kifedha.Haki ni msingi wa Kila siku, hiyo ndio ilikuwa kaulimbiu ya siku ya Haki za binadamu mwaka huu iliyoadhimishwa wiki iliyopita. Lakini kila uchao haki za binadamu zinaendelea kukiukwa kuanzia nyumbani hadi kwenye mtandao. Kwa kutambua umuhimu wa kushirikisha vijana katika kupambana na ukiukwaji wa haki hasa mtandaoni, Ofisi ya Umoja wa Maataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) jijini Nairobi Kenya umewakusanya vijana kujadiliana nao na kuwapa mafunzo ya kumakinika hasa mtandaoni.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO linaendelea na mfululizo wa programu ya kuiunganisha jamii au Social Connection ikiwa na lengo la kusaidia watu kutojitenga na kujihisi wapweke, mmoja kati ya walionufaika wa programu hiyo ni Roz, binti mwenye umri wa miaka 21 raia wa India, aliyehisi upweke mkubwa wakati baba yake alipokuwa akipambana na ulevi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Mkutano mkubwa zaidi duniani wa kupambana na rushwa au ufisadi umeanza leo Desemba 15 mjini Doha nchini Qatar kwa wito wa kutumia teknolojia zinazoibuka katika mapambano dhidi ya rushwa na kushughulikia uhusiano wake na uhalifu wa kupangwa na makosa mengine ya kifedha. Selina Jerobon na maelezo zaidi.

Haki ni msingi wa Kila siku, hiyo ndio ilikuwa kaulimbiu ya siku ya Haki za binadamu mwaka huu iliyoadhimishwa wiki iliyopita. Lakini kila uchao haki za binadamu zinaendelea kukiukwa kuanzia nyumbani hadi kwenye mtandao. Kwa kutambua umuhimu wa kushirikisha vijana katika kupambana na ukiukwaji wa haki hasa mtandaoni, Ofisi ya Umoja wa Maataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) jijini Nairobi Kenya umewakusanya vijana kujadiliana nao na kuwapa mafunzo ya kumakinika hasa mtandaoni.

Nchini Sudan, barani Afrika, wasiwasi mkubwa unaendelea kuhusu makumi ya maelfu ya watu wanaoaminika kuwa bado wamenaswa mjini El Fasher katika eneo la Darfur, magharibi mwa nchi lakini mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa yanaamini kwamba huenda yakaruhusiwa kufika katika mji huo uliogubikwa na mapigano. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

Leo Dunia inapoadhimisha miaka kumi tangu Mkataba wa Paris wa mabadiliko ya Tabianchi kupitishwa, wataalamu wa masuala ya tabianchi barani Afrika wanasema maadhimisho haya ni wakati wa kupima hatua zilizofikiwa lakini pia kukabili pengo linalopanuka kati ya sera na utekelezaji wa hatua za tabianchi. Flora Nducha na taarifa zaidi

Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini Sudan, mkutano unaomulika hatua za tabianchi barani Afrika UNEA7, na juhudi za vijana nchini Kenya za kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo endelevu.Nchini Sudan, barani Afrika, wasiwasi mkubwa unaendelea kuhusu makumi ya maelfu ya watu wanaoaminika kuwa bado wamenaswa mjini El Fasher katika eneo la Darfur,magharibi mwa nchi lakini mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa yanaamini kwamba huenda yakaruhusiwa kufika katika mji huo uliogubikwa na mapigano.Leo Dunia inapoadhimisha miaka kumi tangu Mkataba wa Paris wa mabadiliko ya Tabianchi kupitishwa, wataalamu wa masuala ya tabianchi barani Afrika wanasema maadhimisho haya ni wakati wa kupima hatua zilizofikiwa lakini pia kukabili pengo linalopanuka kati ya sera na utekelezaji wa hatua za tabianchi.Kutoka mashambani hadi kwenye majukwaa ya kidijitali, vijana wa kaunti ya Kirinyaga nchini Kenya wanaongoza enzi mpya ya kilimo kinachoendana na mabadiliko ya tabianchi. Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Watoto UNICEF limeunga mradi wa vijana uitwao Empowering Kenyan Youth in Agribusiness and Nutrition (EKYAN) kuwawezesha vijana kwa mafunzo ya vitendo na zana muhimu ili kukuza biashara zao za kilimo, kuimarisha mifumo ya chakula ya ndani, na kujenga jamii zinazohimili mabadiliko ya tabianchi.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Kutoka mashambani hadi kwenye majukwaa ya kidijitali, vijana wa kaunti ya Kirinyaga nchini Kenya wanaongoza enzi mpya ya kilimo kinachoendana na mabadiliko ya tabianchi. Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Watoto UNICEF limeunga mradi wa vijana uitwao Empowering Kenyan Youth in Agribusiness and Nutrition (EKYAN) kuwawezesha vijana kwa mafunzo ya vitendo na zana muhimu ili kukuza biashara zao za kilimo, kuimarisha mifumo ya chakula ya ndani, na kujenga jamii zinazohimili mabadiliko ya tabianchi. SheilaH Jepngetich na taarifa zaidi

Katika kujifunza lugha Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "“MWENDAWAZIMU HAPEWI UPANGA"

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Sudan Kusini kufuatilia mradi wa kilimo cha mpunga ulivyoleta ustawi kwa jamii ya katikati mwa Sudan unaofanikishwa kwa msaada wa mafunzo wa walinda amani wa UN kutoka Korea Kusini wanaohudumu katika UNMISS kupitia wanasayansi na wakulima wa eneo la Bor katika. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ufafanuzi wa methali.Mapigano makali mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yamesababisha vifo vya zaidi ya raia 70, kuwafurusha watu zaidi ya 200,000, na kusitisha msaada wa chakula kwa maelfu. Umoja wa Mataifa unasema hali katika Kivu Kusini imezorota kwa kasi, huku msaada wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP ukisimama na shule zaidi ya 30 zikigeuzwa makazi ya dharura. Katika taarifa yake, Naibu Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Farhan Haq, amesema hali imefikia kiwango cha hatari, akionya: “Familia zinazoishi kwa njaa sasa zinagawana chakula chao cha mwisho na watu waliokimbia makazi. Hii ni dharura inayovuka mipaka.” UN inazitaka pande zote kusitisha mapigano mara moja na kuruhusu misaada kufika kwa walio hatarini.Mkutano wa kikao cha 7 wa Baraza La Mazingira la Umoja wa Mataifa UNE-7 unaeelekea ukingoni jijini Nairobi Kenya na miongoni mwa washiriki ni kijana mwanaharakati wa mazingira kutoka asasi ya Umoja wa Mataifa YUNA nchini Tanzania Ally MwamzoraNa leo Umoja wa Mataifa unaadhimisha Siku ya Kimataifa ya Milima, ukisisitiza umuhimu wa milima kama “kitovu cha maji ya dunia.” Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO, takriban asilimia 70 ya maji safi ya Dunia yamehifadhiwa kama theluji au barafu, yakitoa mito inayosambaza maji ya kunywa, kilimo, viwanda, na umeme wa maji na takriban watu bilioni mbili, ikiwa ni pamoja na jamii nyingi za asili, wanategemea maji ya milima kwa mahitaji yao ya kila siku, maisha, na tamaduni zao. Wataalamu wanasisitiza kuwa kulinda mazingira ya milima ni muhimu ili kuhakikisha upatikanaji wa maji kwa vizazi vijavyo.Katika kujifunza lugha Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "“MWENDAWAZIMU HAPEWI UPANGA"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Kwa manusura wengi wa usafirishaji haramu wa binadamu, msaada hukatika mapema mno. Kutokana na rasilimali chache na mifumo isiyotoa huduma za muda mrefu, wengi hutolewa kwenye mfumo bila kupata usaidizi wa kutosha wa kisaikolojia au utambuzi unaozidi simulizi zao. Malaika Oringo, mama, mwanaharakati, na manusura wa usafirishaji haramu wa binadamu ameamua kubadilisha hali hiyo. Kama mwanzilishi wa shirika la Footprint to Freedom, linaloongozwa na manusura na linalolenga kuwawezesha na kuwarejesha katika jamii waathiriwa wa usafirishaji haramu wa binadamu, anatetea kuhakikisha sauti za manusura zinakuwa kiini cha utungaji wa sera na hatua za serikali duniani. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Kikosi cha 4 cha ulinzi wa amani kutoka Tanzania kinachohudumu chini ya mwamvuli wa FIB MONUSCO, kimehitimisha rasmi jukumu lake la ulinzi wa amani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya kongo DRC kwa gwaride maalumu la makabidhiano lililofanywa na Tanzqrf ya 4 pamoja na Tanzqrf ya 5 katika makao makuu ya kikosi hico mjini Beni Mavivi katika jimbo la kivu kaskazini. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Habibu Shaban

Hii leo jaridani tunaangaziz siku ya Haki za Binadamu tukikuletea ujumbe wa Volker Türk, Safari ya manusura wa usafirishaji haramu wa binadamu, na vikosi vya 4 na 5 vya ulinzi wa amani kutoka Tanzania nchini DRC.Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ametumia Siku ya Haki za Binadamu hii leo kutoa onyo kali akisema ulinzi wa haki za binadamu uko mashakani wakati migogoro na ukandamizaji vinaongezeka kwa kasi isiyo na mfano.Kwa manusura wengi wa usafirishaji haramu wa binadamu, msaada hukatika mapema mno. Kutokana na rasilimali chache na mifumo isiyotoa huduma za muda mrefu, wengi hutolewa kwenye mfumo bila kupata usaidizi wa kutosha wa kisaikolojia au utambuzi unaozidi simulizi zao. Malaika Oringo, mama, mwanaharakati, na manusura wa usafirishaji haramu wa binadamu ameamua kubadilisha hali hiyo. Kama mwanzilishi wa shirika la Footprint to Freedom, linaloongozwa na manusura na linalolenga kuwawezesha na kuwarejesha katika jamii waathiriwa wa usafirishaji haramu wa binadamu, anatetea kuhakikisha sauti za manusura zinakuwa kiini cha utungaji wa sera na hatua za serikali duniani.Kikosi cha 4 cha ulinzi wa amani kutoka Tanzania kinachohudumu chini ya mwamvuli wa FIB MONUSCO, kimehitimisha rasmi jukumu lake la ulinzi wa amani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya kongo DRC kwa gwaride maalumu la makabidhiano lililofanywa na Tanzqrf ya 4 pamoja na Tanzqrf ya 5 katika makao makuu ya kikosi hico mjini Beni Mavivi katika jimbo la kivu kaskazini.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ametumia Siku ya Haki za Binadamu hii leo kutoa onyo kali akisema ulinzi wa haki za binadamu uko mashakani wakati migogoro na ukandamizaji vinaongezeka kwa kasi isiyo na mfano. Flora Nducha anaeleza zaidi

Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "PEKUPEKU."

Hii leo jaridani tunakuletea ufafanuzi wa umuhimu wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Haki za binadamu kutoka kwa Seifu Magango Msemaji wa Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa ambaye anaanza kwa kuzungumzia azimio la tamko hilo la haki za binadamu.Utafiti uliofanywa na Tume ya Ulaya kwakushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa linalaoshughulikia masuala ya wanawake UN Women umebaini kuwa wanawake saba kati ya kumi wakiwemo watetezi wa haki za binadamu, wanaharakati na waandishi wa habari wanakumbana na ukatili mtandaoni.Meneja Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masuala ya watoto UNICEF Tess Ingram yupo ziarani Ukanda wa Gaza huko Mashariki ya kati ambapo hii leo amezungumza na waandishi wa habari jijini Geneva Uswisi na kuwaeleza aliyoshuhudia huko ikiwemo wajawazito walio na utapiamlo kujifungua watoto wenye uzito mdogo au kuzaliwa kabla ya wakati, ambao wengine wanakufa katika vyumba vya wagonjwa mahututi au wengine hupona lakini watoto hao hukabiliwa na utapimlo au matatizo mengine ya kiafya.Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Kutokomeza Ubaguzi wa Rangi CERD, leo imetoa onyo kali kwa Sudan, ikieleza wasiwasi mkubwa kuhusu ongezeko la matumizi ya lugha ya kudhalilisha, kauli za chuki na ukiukaji Mkubwa wa haki za binadamu unaochochewa na misingi ya kikabila. Kamati imesem Mashambulizi haswa dhidi ya jamii za Fur, Masalit na Zaghawa, yanadaiwa kufanywa na Kikosi cha Msaada wa Haraka RSF na makundi washirika katika maeneo ya El Fasher, Darfur Kaskazini.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "PEKUPEKU"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Leo katika Jarida la UNMlipuko wa kipindupindu wa mwaka huu nchini DRC ni mbaya zaidi katika kipindi cha miaka 25.Wananchi wanaojitolea wanavyosaidia wananchi wenzao nchini Sudan.Janga la kibinadamu Sudan haliwezi tena kupuuzwa, wakati ni sasa kulishughulikia.

Katika dunia inayohitaji mshikamano ili kufikia maendeleo, mchango wa watu wanaojitolea umeendelea kuwa nguvu muhimu ya kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa. Kila mwaka tarehe 5 mwezi Desemba, dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanaojitolea, mwaka huu ikiwa imebeba maudhui“Kila Mchango Una Umuhimu.” Maadhimisho ya mwaka huu pia yanazindua rasmi Mwaka wa Kimataifa wa Wanaojitolea kwa Maendeleo Endelevu 2026. Kutoka Dar es Salaam, Tanzania Sabrina Saidi amezungumza na kijana ambaye anajitolea katika Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa Tanzania YUNA Je kasema nini?.

Katika eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia, jitihada za kuimarisha makuzi na elimu kwa watoto wenye ulemavu zinaendelea kuleta matumaini mapya, kupitia programu inayoungwa mkono na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu na Masuala ya Dharura OCHA, na Mfuko wa Dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF. Je nini kinafanyika? Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi

Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya haki za binadamu na maandamano ya amani nchini Tanzania, siku ya kujitolea tukikuletea ujumbe wa mfanyakazi wa kujitolea, na elimu jumuishi kwa ajili ya watu wenye ulemavu nchini Ethiopia.Wakati Tanzania ikijiandaa kwa maandamano makubwa yaliyopangwa kufanyika tarehe 9 Desemba siku ya maadhimisho ya Uhuru, Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR imetoa tahadhari na wito kwa serikali ya taifa hilo la Afrika Mashariki. Seif Magango ni msemaji wa ofisi ya Haki za binadamu ametufafanulia kuhusu tamko lao.Katika dunia inayohitaji mshikamano ili kufikia maendeleo, mchango wa watu wanaojitolea umeendelea kuwa nguvu muhimu ya kuleta mabadiliko chanya kwenye jamii kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa. Kila mwaka tarehe 5 mwezi Desemba, dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanaojitolea, mwaka huu ikiwa imebeba maudhui “Kila Mchango Una Umuhimu.” Maadhimisho ya mwaka huu pia yanazindua rasmi Mwaka wa Kimataifa wa Wanaojitolea kwa Maendeleo Endelevu 2026.Katika eneo la Tigray kaskazini mwa Ethiopia, jitihada za kuimarisha makuzi na elimu kwa watoto wenye ulemavu zinaendelea kuleta matumaini mapya, kupitia programu inayoungwa mkono na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu na Masuala ya Dharura OCHA, na Mfuko wa Dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF. Je nini kinafanyika?Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Wakati Tanzania ikijiandaa kwa maandamano makubwa yaliyopangwa kufanyika tarehe 9 Desemba siku ya maadhimisho ya Uhuru, Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR imetoa tahadhari na wito kwa serikali ya taifa hilo la Afrika Mashariki. Seif Magango ni msemaji wa ofisi ya Haki za binadamu ametufafanulia kuhusu tamko lao.