Habari za UN

Follow Habari za UN
Share on
Copy link to clipboard

Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN Global Communications


    • Nov 14, 2025 LATEST EPISODE
    • daily NEW EPISODES
    • 4m AVG DURATION
    • 3,662 EPISODES


    More podcasts from UN Global Communications

    Search for episodes from Habari za UN with a specific topic:

    Latest episodes from Habari za UN

    Je wajua nini kinasababisha ugonjwa wa kisukari na ujikinge vipi?

    Play Episode Listen Later Nov 14, 2025 2:54


    Tarehe 14 Novemba kila mwaka dunia huadhimisha Siku ya Kisukari na mwaka huu kauli mbiu ni “Kisukari katika hatua mbalimbali za maisha.” Je wafahamu ugonjwa huu unampata mtu gani na unawezaje kujikinga usiugue? Leah Mushi anatujuza zaidi.

    COP30 ni jukwaa kwa wakimbizi kupaza sauti juu ya athari za tabianchi kwao - Alfonso Herrera

    Play Episode Listen Later Nov 14, 2025 2:57


    Wiki ya kwanza ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP30, unaofanyika Belém Brazil, ikielekea ukingoni, viongozi wa dunia na wanaharakati wanakutana kujadili jinsi ya kushughulikia moja ya changamoto kubwa za wakati huu, ‘janga la mabadiliko ya tabianchi,” Na athari zake kwa wakimbizi hazikupewa kisogo. Flora Nducha anafafanua zaidi katika taarifa hii

    14 NOVEMBA 2025

    Play Episode Listen Later Nov 14, 2025 11:36


    Hii leo jaridani tunaangazia ugonjwa wa kisukari, chanjo ya polio katika ukanda wa Gaza na janga la mabadiliko ya tabianchi na athari zake kwa wakimbizi.Tarehe 14 Novemba kila mwaka dunia huadhimisha Siku ya Kisukari na mwaka huu kauli mbiu ni “Kisukari katika hatua mbalimbali za maisha.” Je wafahamu ugonjwa huu unampata mtu gani na unawezaje kujikinga usiugue? Leah Mushi anatujuza zaidi.Mashirika ya Umoja wa Mataifa WHO, UNICEF na UNRWA wameanzisha kampeni ya pamoja ya Uchanjaji watoto waliokosa huduma muhimu za kuokoa maisha kutokana na miaka miwili ya machafuko katika Ukanda wa Gaza umeanza kutekelezwa na mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa, lile la afya duniani, la kuhudumia watoto UNICEF na la kusaidia wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA.Wiki ya kwanza ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP30, unaofanyika Belém Brazil, ikielekea ukingoni, viongozi wa dunia na wanaharakati wanakutana kujadili jinsi ya kushughulikia moja ya changamoto kubwa za wakati huu, ‘janga la mabadiliko ya tabianchi,” Na athari zake kwa wakimbizi hazikupewa kisogo. Flora Nducha anafafanua zaidi katika taarifa hii.Mwenyeji wako ni Sabrina Said Moshi, karibu!

    WHO, UNICEF na UNRWA waanza uchanjaji zaidi ya watoto 44,000 Gaza

    Play Episode Listen Later Nov 14, 2025 3:12


    Mashirika ya Umoja wa Mataifa WHO, UNICEF na UNRWA wameanzisha kampeni ya pamoja ya Uchanjaji watoto waliokosa huduma muhimu za kuokoa maisha kutokana na miaka miwili ya machafuko katika Ukanda wa Gaza umeanza kutekelezwa na mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa, lile la afya duniani, la kuhudumia watoto UNICEF na la kusaidia wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA. 

    Jifunze Kiswahili: Maana za neno "KASIMU".

    Play Episode Listen Later Nov 13, 2025 1:00


    Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo,  mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KASIMU".

    13 NOVEMBA 2025

    Play Episode Listen Later Nov 13, 2025 10:40


    Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia simulizi za waahirika wa Kimbunga Melissaikiwa ni wiki ya pili sasa baada ya kupiga magharibi mwa Jamaica, na kuacha zahma kubwa kwa wakaazi. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze Kiswahili.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akieleza kuwa na wasiwasi mkubwa kutokana na ripoti za ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na mauaji ya halaiki mjini El Fasher, pamoja na kuongezeka kwa mapigano katika maeneo ya Kordofan nchini Sudan. Guterres amesema “Mtiririko wa silaha na wapiganaji kutoka nje lazima ukatwe. Misaada ya kibinadamu lazima iweze kuwafikia haraka raia wanaohitaji, na mapigano lazima yakome,”.Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumatano limemchagua Phoebe Okowa kutoka Kenya kuwa Jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), baada ya duruu nne za upigaji kura. Upigaji kura huo ulifanyika kwa wakati mmoja na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, lakini kwa utaratibu tofauti, kama inavyotakiwa na Katiba ya Mahakama hiyo ya Haki. Bi. Okowa amechaguliwa kwa wingi wa kura ambapo alipata kura 8 katika Baraza la Usalama na kura 106 katika Baraza Kuu.Kumekuwa na ongezeko la uraibu wa nikotini na bidhaa nyingine zinazozalishwa kwa kutumia tumbaku duniani hususani miongoni mwa vijana na tena wengi hivi sasa wanatumia sigara za kielektroniki, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO. Tarehe 17 mpaka 21 Novemba utafanyika mkutano mkubwa kujadili namna serikali, mashirika ya kimataifa na asasi za kiraia zitakavyoweza kusaidia kupambana na janga la tumbaku duniani, linalosababisha vifo zaidi ya milioni saba kila mwaka.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KASIMU"Mwenyeji wako ni Sabrina Said Moshi, karibu!

    Ripoti mpya ya FAO/WFP yaonya muda unayoyoma kuzuia mamilioni kuingia kwenye njaa katika maeneo 16 hatarishi.

    Play Episode Listen Later Nov 12, 2025 3:39


    Ripoti mpya ya pamoja kutoka mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa lile la  Chakula na Kilimo Duniani (FAO) na la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) inaonya kwamba uhaba mkubwa wa chakula unazidi kuongezeka katika maeneo 16 yenye njaa duniani, hali inayoweza kusababisha mamilioni zaidi ya watu kukumbwa na njaa kali au hatari ya kufikia kiwango cha baa la njaa. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

    UNDP inavyosaidia jamii za kampala kukabili mafuriko

    Play Episode Listen Later Nov 12, 2025 3:46


    Kituo cha utafiti wa kusaka Suluhu kuhusu mafuriko kinachoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) nchini Uganda kimetumia maarifa ya pamoja kukabiliana na changamoto za mafuriko katika eneo la Makerere Kavule, makazi yasiyo rasmi yaliyo pembezoni mwa mji wa Kampala, mji mkuu wa Uganda. Kituo hicho kimeunganisha juhudi za jamii, maarifa asilia, na teknolojia ya kisasa kubuni mfumo wa mifereji ya maji unaoendana na Mpango Mkuu wa Mifereji ya Maji wa Jiji la Kampala (Kampala Capital City Drainage Master Plan). Mfumo huu unalenga kupunguza mafuriko si tu katika jamii hiyo, bali pia katika eneo la katikati ya jiji. Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi.

    12 NOVEMBA 2025

    Play Episode Listen Later Nov 12, 2025 11:27


    Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya FAO ya uhaba wa chakula, Mwanaharakati kijana kutoka Kenya katika mkutano wa pili wa WSSD Doha, na mradi wa Mifereji ya Maji wa Jiji la Kampala (Kampala Capital City Drainage Master Plan) inayosaidia kupunguza mafuriko Uganda.Ripoti mpya ya pamoja kutoka mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa lile la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) na la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) inaonya kwamba uhaba mkubwa wa chakula unazidi kuongezeka katika maeneo 16 yenye njaa duniani, hali inayoweza kusababisha mamilioni zaidi ya watu kukumbwa na njaa kali au hatari ya kufikia kiwango cha baa la njaa.Mkutano wa Pili wa Dunia wa Maendeleo ya Kijamii umefunga pazia mjini Doha, Qatar, mwishoni mwa wiki hii, ukiwaleta pamoja viongozi wa dunia, mashirika ya kiraia na vijana wakitoka na wito wa pamoja dhidi ya umasikini, ukosefu wa usawa na kutengwa kijamii. Kutoka Kenya, mwanaharakati kijana amesema mkutano huo umekuwa wa kuhamasisha akitoa wito wa hatua za haraka.Kituo cha utafiti wa kusaka Suluhu kuhusu mafuriko kinachoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) nchini Uganda kimetumia maarifa ya pamoja kukabiliana na changamoto za mafuriko katika eneo la Makerere Kavule, makazi yasiyo rasmi yaliyo pembezoni mwa mji wa Kampala, mji mkuu wa Uganda. Kituo hicho kimeunganisha juhudi za jamii, maarifa asilia, na teknolojia ya kisasa kubuni mfumo wa mifereji ya maji unaoendana na Mpango Mkuu wa Mifereji ya Maji wa Jiji la Kampala (Kampala Capital City Drainage Master Plan). Mfumo huu unalenga kupunguza mafuriko si tu katika jamii hiyo, bali pia katika eneo la katikati ya jiji.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

    Hatua ndizo zinazohitajika baada ya mkutano wa dunia wa Maendeleo ya Kijamii - Diana Pasha

    Play Episode Listen Later Nov 12, 2025 2:18


    Mkutano wa Pili wa Dunia wa Maendeleo ya Kijamii umefunga pazia mjini Doha, Qatar, mwishoni mwa wiki hii, ukiwaleta pamoja viongozi wa dunia, mashirika ya kiraia na vijana wakitoka na wito wa pamoja dhidi ya umasikini, ukosefu wa usawa na kutengwa kijamii. Kutoka Kenya, mwanaharakati kijana amesema mkutano huo umekuwa wa kuhamasisha akitoa wito wa hatua za haraka. Flora Nducha na taarifa zaidi

    Jifunze Kiswahili: Maana ya methali "CHA KIPOFU KI MKONONI MWAKE"

    Play Episode Listen Later Nov 11, 2025 1:31


    Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Daktari. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya,  kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "CHA KIPOFU KI MKONONI MWAKE"

    11 NOVEMBA 2025

    Play Episode Listen Later Nov 11, 2025 12:07


    Michezo kwa ajili ya amani: Mpira wa kikapu wabadilisha maisha ya vijana wa Yambio nchini Sudan Kusini

    Play Episode Listen Later Nov 10, 2025 2:13


    maisha vijana michezo sudan kusini
    Urejerezaji: Usajili wa warejeshaji wa mazingira Afrika Kusini waleta nuru katika kazi yao

    Play Episode Listen Later Nov 10, 2025 2:35


    Mkutano wa UN kuhusu mabadiliko ya tabianchi wang'oa nanga Brazil: COP30

    Play Episode Listen Later Nov 10, 2025 3:28


    10 NOVEMBA 2025

    Play Episode Listen Later Nov 10, 2025 10:00


    Tigray: UNICEF yatoa msaada wa mabegi na vifaa vya shule kwa watoto

    Play Episode Listen Later Nov 7, 2025 2:53


    WFP - Janga la njaa DRC linazidi kuwa baya kutokana na mapigano na ukosefu wa ufadhili wa misaada

    Play Episode Listen Later Nov 7, 2025 2:24


    Sudan: Maafisa wa UN na AU kukutana leo kujadili viashiria vya mauaji ya kimbari El Fasher

    Play Episode Listen Later Nov 7, 2025 2:22


    JIFUNZE KISWAHILI- MANENO - Jamala na Bulbul

    Play Episode Listen Later Nov 7, 2025 0:23


    Na sasa ni wakati wa kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "JAMALA na BULBUL"

    07 NOVEMBA 2025

    Play Episode Listen Later Nov 7, 2025 9:55


    Jarida hii leo tunamulika harakati za kuzuia  mauaji ya kimbari El Fasher, Sudan, hakuna dalili za kumalizika kwa janga la njaa mashariki mwa DRC na furaha kwa watoto waliopatiwa mabegi ya kwenda shule huko Tigray, Ethiopia.Unapokabiliana na ukatili na mauaji ya kimbari ni vema kuhakikisha wanaotekeleza wanafahamu kuwa wanafuatiliwa na kutazamwa ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa dhidi yao, amesema Chaloka Beyani Mshauri Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu kuzuia mauaji ya kimbari.Mgogoro katika mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) unaendelea kuwa mbaya huku mapigano yakizidi, na kusababisha makumi ya maelfu ya watu kukimbia makazi yao na kuzidisha njaa kali, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeeleza leo.Nchini Ethiopia, Kaskazini Magharibi mwa jimbo la Tigray watoto wamefurahia kupatiwa vifaa kwa ajili ya kurejea upya shuleni baada ya vita ya muda mrefu, shukrani kwa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.

    Global Youth Forum: Shirika linalotumia kandanda kusongesha SDGs nchini Kenya

    Play Episode Listen Later Nov 6, 2025 5:28


    06 NOVEMBA 2025

    Play Episode Listen Later Nov 6, 2025 9:59


    Akiwa Doha, Rais wa Baraza Kuu aona watoto wa kipalestina walivyo na matumaini licha ya zahma walizopita

    Play Episode Listen Later Nov 5, 2025 4:06


    Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Annalena Baerbock ametembelea wakimbizi wa kipalestina huko Doha nchini Qatar kuwajulia hali na kujionea maisha yao baada ya kuondolewa wakati wa vita kali huko Ukanda wa Gaza eneo la wapalestina linalokaliwa kimabavu na Israel na kuletwa nchini Qatar kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Leah Mushi anatupa taswira ya ziara yake hiyo.Wakati wa michuano ya kombe la dunia mwaka 2022 nchini Qatar nchi hiyo ilitenga eneo maalum na kujenga nyumba nyingi kwa ajili ya makazi kwa wale walioenda kutazama mechi za kombe la Dunia, eneo hilo pia lilikuwa na kiwanja cha mpira, eneo hilo ni Al-Thumama maarufu kama Al-Thumama complex katika mji wa Doha.Mtoto na simulizi kupitia pichaEneo hilo sasa limegeuzwa makazi ya dharura kwa zaidi ya wakimbizi 1,700 wa Kipalestina ambao waliondolewa nchini mwao wakati wa vita Kali kati ya majeshi ya Israel na wanamgambo wa Hamas vita ambayo imesitishwa hivi sasa. Wakimbizi hao wa kipalestina wakiwa katika eneo la Al-Thumama wanapatiwa matibabu ya kawaida, ya viungo na usaidizi wa kijamii.Rais wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Annalena Baerbock amefika katika eneo hilo ili kuwajulia hali.Kwanza alikutana na watoto, video inamuonesha akizungumza na mtoto wa kiume ambaye ameandika kitabu kwa njia ya picha na ndoto yake ni kitafsiriwe kutoka kiarabu kwenda lugha mbalimbali. toto huyo akatia saini nakala ya kitabu chake na kumpa Rais wa Baraza Kuu.Watoto licha ya majeraha bado wana matumainiKisha, Rais Baerbock anaonekana akizungumza na familia nyingine, pembeni mtoto mmoja mwenye umri kama wa miaka mwili hivi mkono wake wa kulia unaonekana umekatwa chini kidogo ya bega. Mtoto huyo anarukaruka kwenye kochi huku wanafamilia yake wakizungumza na mgeni.Anatoka akitembea kwenda eneo jingine lakini ndani ya eneo hilo hilo la Al-Thumama kwenye chuo cha ufundi stadi na kujionea namna wanawake wanavyojishughulisha na kazi za mikono ikiwemo ufumaji kwa kutumia mashine za kisasa za mkono.Akitoka huko akiwa na wanawake kadhaa akawa anaelekea eneo lenye hospitali … njiani akakutana na mwanamke akiwa kwenye kiti mwendo, wakasimama na mwanamke huyo akawapa vitafunywa wakala na kufurahia huku Rais wa Baraza Kuu akisifu kwa utamu wa vitafunio hivyo.Baada ya hapo safari ya kwenda hospitali ikaendelea, na huko akakutana na madaktari na kujionea mashine mbalimbali za kisasa kwa ajili ya kuwahudumia wakimbizi wa kipalestina.Ziara hiyo aliyoianza tangu mchana kweupe alihitimisha giza likiwa limeshatanda nje na akatoa ujumbe kwa dunia kile alichojionea.Amesema, “nimeona yale hawa watoto walipitia, nyuso zao ziliungua kwa moto, wamepoteza mikono, wazazi, familia nzima, lakini bado wanaonesha ujasiri na wanamatumaini na maisha yao ya baadae, wakijaribu kurejea shuleni na hii inaweka mkazo wa jukumu letu ni lipi kama jumuiya ya kimataifa. Tunapaswa kukomesha kabisa mgogoro huu uliodumu kwa muongo mmoja, mzozo wa muda mrefu na kwamba amani ya kudumu haita hakikishwa kwa kupitia vita, ugaidi wala kukalia eneo kimabavu bali kwa makubaliano ya amani ya kuwa na mataifa mawili yanayojitegemea, kupelekea kwa taifa huru la Kipalestina ambapo kizazi kijacho kinaweza kuishi kwa heshima pia.”

    Nashukuru FODDAJ imenirejeshea matumaini ya maisha - Mnufaika

    Play Episode Listen Later Nov 5, 2025 3:16


    Nchini Kenya, shirika la kiraia la FODDAJ  au la Forum for Women Development, Democracy and Justice linatekeleza kivitendo lengo namba 3 la Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs la afya bora na ustawi ambalo pamoja na mambo mengine linataka manusura wa ukatili wa kijinsia wapatiwe huduma sio tu za afya bali pia za kijamii. Je linafanya nini, Sheilah Jepngetich amezungumza na mwakilishi wa shirika hilo.Ni Salome Gatakaa Araka, Mwakilishi wa FODDAJ ambaye katika mazungumzo nami anaanza kwa kuelezea walianzia wapi harakati zao.  Akisema Policy and Advocacy anamaanisha Sera na Uchechemuzi.“FODAJ ilianza na uundaji wa ufahamu yaani policy and advocacy kumaanisha kwamba kuwe  kutengwa kwa fedha za kutengeneza mahali pa waathiriwa kuishi, na pia kusisitiza ufahamu wa kutetea wale ambao wametengwa. Katika kata ya Kajiado, tumesukuma sera za GBV ili kuimarisha juhudi za kuzuia waathiriwa kuumia zaidi.”Pamoja na kukabili ukatili wa kijinsia, nikataka kufahamu iwapo wanawejengea wanawake uwezo wa kujitegemea.“FODDAJ imekuwa mstari wa mbele katika katika kupaza sauti za wanawake na wasichana, na pia kuhimiza akina mama kuweka akiba za vikundi, kushirikiana na kusaidiana ili kujikimu kiuchumi. Tumehimiza akina mama kuweka akiba kwa vikundi vya maendeleo, kushirirki mafunzo ya ujasiriamali na kushirikiana na wengine kwa pamoja. Na pia wanafundishwa mambo tofauti kama vile kutengeneza nywele , kusoma na kuandika na pia na kuhesabu.”Maneno ya Bi. Araka si matupu kwani Geraldine Ndayisenga mkazi wa Kitengela ambaye ni manusura wa ukatili na mnufaika wa miradi ya FODDAJ anafunguka.“Mimi ni mmoja wa wale waliopitia dhuluma. Nilijua kuhusu FODDAJ kupitia rafiki yangu. Nikasaidiwa, nilipata matibabu, nikapata ushauri (counselling) kwa mwezi mmoja. Baada ya hapo nikajiunga na mafunzo ya kutengeneza nywele, makucha na ushonaji. Mafunzo hayo yamenisaidia sana, sasa najisikia niko huru na nina furaha kuwa sehemu ya jamii tena. Fodaj Foundation imenishika mkono na kunionesha namna bora ya kuishi hapa Kitengela. Wamenisaidia kwa mambo mengi, na kwa kweli maisha yangu yamebadilika kwa njia chanya sana.”Nikarejea kwa Bi. Araka, kufahamu iwapo wana ushirikiano na serikali na mashirika ya kiraia. Akisema Post Traumatic anamaanisha kiwewe baada ya dhuluma.“Kwa kushirikiana na serikali na mashirika mengine ya kiraia, waathirika wanapatiwa msaada kwa ajili ya huduma za afya. Mfano wale waliobakwa au kupigwa, hupata matibabu kwa vipimo au dawa. Aidha, waathirika wa kimawazo wanapewa msaada wa kisaikolojia ili iwasaidie kuondokana na madhara ya post trauma ambayo wamepitia.

    Guterres atumia siku ya elimu kuhusu tsunami kukumbusha mkakati wa kujikinga

    Play Episode Listen Later Nov 5, 2025 1:51


    leo ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu Tsunami Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesisitiza umuhimu wa kuwekeza katika kujiandaa dhidi ya mawimbi hayo makubwa ya bahari yanayotokana na tetemeko chini ya bahari. Anold Kayanda na maelezo zaidi.Asante Assumpta,Katika ujumbe wake, Guterres amesema maandalizi hayo yanahusisha kuweka mifumo ya kutoa maonyo ya mapema au tahadhari kwenye kila ufukwe, jamii na kokote kule.Bwana Guterres amefafanua kuwa tsunami si matokeo ya mara kwa mara lakini pindi yanapotokea madhara yake yanaweza kuwa makubwa na hata kusababisha vifo.“Husababisha vifo vya maelfu na hata mamia ya maelfu ya watu. Lakini kuna mbinu za kuweka watu salama,” anasema Guterres.Ametolea mfano janga la tsunami kwenye bahari ya Hindi mwaka 2004, janga ambalo lilisababisha dunia kuamua kuwekeza katika mifumo ya kutoa maonyo mapema.“Miongo kadhaa baadaye, uamuzi huo umelipa,” amesema Katibu Mkuu akitolea mfano tetemeko kubwa la ardhi lililokumba pwani ya Urusi mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu akisema, “lilisababisha tahadhari kwa mamilioni ya watu kuanzia pwani za Japani hadi visiwa vilivyoko bahari ya Pasifiki hadi California.”Ingawa hivyo amesema madhara ya janga hilo la tsunami yanaendelea kubadilika kutokana na mabadiliko kadhaa ikiwemo yale ya tabianchi.Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa akieleza kuwa kuheshimu baharí ni kutambua nguvu yake anasema,  “kiwango cha maji ya bahari kikiongezeka, na idadi ya watu wanaoishi maeneo ya pwani ya bahari ikiongezeka, mifumo ya kutoa maonyo mapema nayo inahitaji uwekezaji zaidi na kuboreshwa,”Ni kwa mantiki hiyo amesema hilo ndio lengo la mpango wa Umoja wa Mataifa wa Mfumo wa Tahadhari kwa Wote ulioanzishwa kwa lengo la kuhakikisha kila mtu anafikiwa na mpango wa utoaji onyo mapema dhidi ya tsunami ifikapo mwaka 2027.Maadhimisho ya mwaka huu ni ya 10, ambapo Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilianzisha siku hii kupitia azimio namba 70/203 la mwaka 2005.

    05 NOVEMBA 2025

    Play Episode Listen Later Nov 5, 2025 11:27


    Katika jarida la habari za Umoja wa Mataifa hii leo utasikia kuhusu wito wa mataifa yote kuwekeza kwenye mifumo ya tahadhari za mapema ikiwa leo dunia inaadhimisha Siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu Tsunami. Utasikia pia ziara ya Rais wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa nchini Qatar ambapo amewatembelea wakimbizi wa kipalestina walioko nchini humo. Kutoka nchini Kenya utasikia juhudi za taasisi ya FODDAJ kusaidia jamii nchini Kenya kupambana na ukatili wa kijinsia. 

    JIFUNZE KISWAHILI - NENO: MHANGA

    Play Episode Listen Later Nov 4, 2025 0:57


    Je wafahamu maana ya neno Mhanga ambalo wingi wake ni Wahanga? Basi ambatana na Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, BAKIZA akikupatia ufafanuzi huo.  

    04 NOVEMBA 2025

    Play Episode Listen Later Nov 4, 2025 11:34


    Hii leo Jaridani, Anold Kayanda anakupeleka nchini Kenya kusikia usaidizi wa FAO kwenye harakati za kuondokana na njaa katika taifa hilo la Afrika Mashariki kupitia uimarishaji wa sekta ya kilimo. Lakini pia kuna Muhtasari kutoka kwa Leah Mushi akimulika:Baa la Njaa kuthibitishwa huko El Fasher na Kadugli nchini SudanAzimio la Doha lenye lengo la kuimarisha maendeleo ya jamii dunianiKauli ya Joyce Msuya, Naibu Mkuu wa OCHA akiwa huko Doha, Qatar kufuatia kupitishwa kwa azimio hilo.Na kipengele cha Jifunze Kiswahili leo kinaelezea matumizi ya neno Mhanga na Wahanga.Karibu!

    Bisha hodi Mbezi Garden Tanzania uone manufaa ya mradi wa We-Fi wa Benki ya Dunia na wadau

    Play Episode Listen Later Nov 3, 2025 2:45


    Mpango wa Ufadhili Wajasiriamali Wanawake, (We-Fi) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia na wadu umewezesha biashara kukwamuka nchini Tanzania baada ya janga la COVID-19, hatua ambayo imeinua pia jamii nzima na si wajasiriamali wanawake peke yao. Simulizi hii ya Assumpta Massoi inamulika mjasiriamali mwanamke Haika Lawere anayemiliki hoteli ya Mbezi Garden jijini Dar Es Salaam ambako ni jiji kuu la biashara la taifa hilo la Afrika.

    Kilimo cha umwagiliaji kinavyobadilisha maisha ya wakulima Nigeria

    Play Episode Listen Later Nov 3, 2025 2:24


    Kilimo ni moja ya sekta muhimu za kiuchumi nchini Nigeria, kikiajiri zaidi ya theluthi moja ya watu wote nchini humo. Lakini hali ya hewa isiyotabirika imefanya kilimo kuwa shughuli yenye mashaka makubwa — ukame, mafuriko na mvua zisizo na mpangilio zimekuwa tishio kubwa kwa wakulima, ambapo kilio chao kimesikiwa na Benki ya Dunia iliyokuja na suluhisho kwa kuanzisha mradi wa kilimo cha umwagiliaji. Selina Jerobon ana taarifa zaidi.

    03 NOVEMBA 2025

    Play Episode Listen Later Nov 3, 2025 9:50


    Hii leo jaridani tunaangazia hali ya haki za binadamu nchini Sudan, Mpango wa Ufadhili Wajasiriamali Wanawake, (We-Fi) nchini Tanzania, na kilimo ni moja ya sekta muhimu za kiuchumi nchini Nigeria.Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) imetoa tamko juu ya wasiwasi mkubwa kufuatia ripoti mpya kutoka El-Fasher, jimboni Darfur Kaskazini, nchini Sudan, zikieleza kuwepo kwa mauaji ya halaiki, ubakaji, na uhalifu mwingine unaodaiwa kufanywa wakati wa mashambulizi ya Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF).Mpango wa Ufadhili Wajasiriamali Wanawake, (We-Fi) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia na wadu umewezesha biashara kukwamuka nchini Tanzania baada ya janga la COVID-19, hatua ambayo imeinua pia jamii nzima na si wajasiriamali wanawake peke yao. Simulizi hii ya Assumpta Massoi inamulika mjasiriamali mwanamke Haika Lawere anayemiliki hoteli ya Mbezi Garden jijini Dar Es Salaam ambako ni jiji kuu la biashara la taifa hilo la Afrika.Kilimo ni moja ya sekta muhimu za kiuchumi nchini Nigeria, kikiajiri zaidi ya theluthi moja ya watu wote nchini humo. Lakini hali ya hewa isiyotabirika imefanya kilimo kuwa shughuli yenye mashaka makubwa — ukame, mafuriko na mvua zisizo na mpangilio zimekuwa tishio kubwa kwa wakulima, ambapo kilio chao kimesikiwa na Benki ya Dunia iliyokuja na suluhisho kwa kuanzisha mradi wa kilimo cha umwagiliaji.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

    Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ICC yaeleza wasiwasi mkubwa kuhusu mauaji na uhalifu El Fasher

    Play Episode Listen Later Nov 3, 2025 2:37


    Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) imetoa tamko juu ya wasiwasi mkubwa kufuatia ripoti mpya kutoka El-Fasher, jimboni Darfur Kaskazini, nchini Sudan, zikieleza kuwepo kwa mauaji ya halaiki, ubakaji, na uhalifu mwingine unaodaiwa kufanywa wakati wa mashambulizi ya Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF). Taarifa zaidi na Sheilah Jepngetich.

    UN: Majiji ya kisasa pamoja na kukumbatia teknolojia izingatie watu

    Play Episode Listen Later Oct 31, 2025 2:45


    Dunia leo ikiadhimisha Siku ya Kimataifa ya Majiji, majiji ya kisasa pamoja na kukumbatia teknolojia yametakiwa kuhakikisha yanazingatia zaidi watu ili wengine wasiachwe nyuma au kutengwa na maendeleo hayo. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

    Chaguo Langu Haki Yangu: Kuwezesha wanawake na wasichana nchini Tanzania - UNFPA

    Play Episode Listen Later Oct 31, 2025 2:54


    Mpango wa “Chaguo Langu, Haki Yangu” nchini Tanzania ni jitihada thabiti zinazolenga kuwawezesha wanawake na wasichana kuishi maisha huru dhidi ya ukatili na vitendo hatarishi. Kwa ufadhili wa Serikali ya Finland, Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la IPS, linafanya mabadiliko halisi katika jamii. Sheilah Jepngetich anafafanua zaidi.

    31 OKTOBA 2025

    Play Episode Listen Later Oct 31, 2025 9:59


    Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya Kimataifa ya Majiji, vifo na majeruhi vilivyotokea katika maandamano yanayohusiana na uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Tanzania na uwezeshaji wa wanawake nchini huko huko Tanzania.Dunia leo ikiadhimisha Siku ya Kimataifa ya Majiji, majiji ya kisasa pamoja na kukumbatia teknolojia yametakiwa kuhakikisha yanazingatia zaidi watu ili wengine wasiachwe nyuma au kutengwa na maendeleo hayo.Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu imeeleza wasiwasi mkubwa kufuatia vifo na majeruhi vilivyotokea katika maandamano yanayohusiana na uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Tanzania tarehe 29 mwezi huu wa Oktoba.Mpango wa “Chaguo Langu, Haki Yangu” nchini Tanzania ni jitihada thabiti zinazolenga kuwawezesha wanawake na wasichana kuishi maisha huru dhidi ya ukatili na vitendo hatarishi. Kwa ufadhili wa Serikali ya Finland, Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la IPS, linafanya mabadiliko halisi katika jamii.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

    Kauli ya ofisi ya UN ya Haki za binadamu kufuatia vurugu Tanzania baada ya uchaguzi mkuu

    Play Episode Listen Later Oct 31, 2025 2:42


    Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu imeeleza wasiwasi mkubwa kufuatia vifo na majeruhi vilivyotokea katika maandamano yanayohusiana na uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Tanzania tarehe 29 mwezi huu wa Oktoba. Selina Jerobon na maelezo zaidi.

    Jifunze Kiswahili: Maana za neno "SUMIA"

    Play Episode Listen Later Oct 30, 2025 1:06


    Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo,  mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "SUMIA."

    30 OKTOBA 2025

    Play Episode Listen Later Oct 30, 2025 11:41


    Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Bi. Lucy Githinji, mkazi wa jimbo la New Jersey nchini Marekani amezungumza na idhaa hii baada ya matembezi ya hiari kwa ajili ya kuhamasisha jamii kuhusu saratani ya titi, akisema hakika dawa zinafanya kazi.Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Kibinadamu nchini Sudan, Denise Brown amesema ni kweli wamepokea ripoti za mauaji ya baadhi ya wahudumu wa kujitolea huko El Fasher jimboni Darfur wakati huu ambapo mji huo umetwaliwa na wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka, (RSF).Kimbunga Melissa kimepungua nguvu baada ya kutua nchini Jamaica kama kimbunga cha kiwango cha 5, na kuvunja rekodi ya kimbunga chenye nguvu zaidi, kabla ya kuelekea kaskazini mashariki kupita Cuba hadi Bahamas, na kusababisha mafuriko makubwa, uharibifu na kukatika kwa umeme katika maeneo mbalimbali ya Karibea na Amerika ya Kati.Nchini Cameroon, kufuatia mauaji ya raia wakati wa maandamano ya kupinga kutangazwa kwa Paul Biya kuwa mshindi wa kiti cha Urais kwenye uchaguzi uliofanyika Oktoba 12, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu imeeleza wasiwasi wake juu ya ripoti za vifo hivyo.Na katika Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo,  mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "SUMIA."Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

    Hali si hali huko El Fasher nchini Sudan, watoto 'walipa gharama' zaidi

    Play Episode Listen Later Oct 29, 2025 2:43


    Ghasia zinazoendelea kwa kasi zinawakwamisha zaidi watoto katikati ya mashambulizi ya mabomu yasiyokoma, mapigano makali, na uhaba mkubwa wa chakula, maji salama na dawa kwa zaidi ya siku 500 sasa.“Hakuna mtoto aliye salama,” anasema Catherine Russell, Mkurugenzi Mtendaji wa Shrika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF kupitia taarifa iliyotolewa na makao makuu ya shirika hilo jijini New York, Marekani leo.Taarifa hiyo pia inamnukuu Catherine Russell akisema, “ingawa athari kamili bado haijulikani kutokana na kukatika kwa mawasiliano kote nchini Sudan, inakadiriwa kuwa watoto wapatao 130,000 huko Al Fasher wako katika hatari kubwa ya kukiukwa haki zao, huku kukiripotiwa visa vya utekaji nyara, mauaji na ukataji viungo vya mwili, pamoja na ukatili wa kingono.”Pia kuna taarifa za wafanyakazi wa mashirika ya kibinadamu kukamatwa au kuuawa.UNICEF inatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano, kuhakikisha upatikanaji salama na usiokatizwa wa misaada ya kibinadamu, ulinzi wa raia hasa watoto, na kupatiwa uhakika wa njia salama kwa familia zinazotafuta hifadhi, kwa mujibu wa sheria za kimataifa za kibinadamu. Wale wanaohusika na ukiukaji lazima wawajibishwe.Wakati huohuo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limethibitisha kwamba Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan imewataarifu kuwa viongozi  wawili wa juu wa WFP nchini  wametangazwa kuwa watu wasiotakiwa nchini Sudan na hivyo wameamriwa kuondoka nchini humo ndani ya saa 72, bila maelezo yoyote.WFP inaeleza kwamba uamuzi huu wa kuwafukuza Mkurugenzi wa WFP nchini Sudan na Mratibu wa Dharura wa WFP nchini humo unakuja katika kipindi muhimu kwani mahitaji ya kibinadamu nchini Sudan hayajawahi kuwa makubwa zaidi kama kipindi hiki, huku zaidi ya watu milioni 24 wakikabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula na jamii zikikumbwa na baa la njaa.Wakati ambapo WFP na washirika wake wanapaswa kupanua wigo wa msaada, uamuzi huu unalazimisha shirika kubadilisha uongozi bila mpango, jambo linalohatarisha shughuli zinazowaunga mkono mamilioni ya Wasudani walio hatarini kukumbwa na njaa kali, utapiamlo, na hata kifo kutokana na njaa.WFP na maafisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa wanaendelea kuzungumza na mamlaka za Sudan kupinga hatua hii na kutaka ufafanuzi wa uamuzi huo.Tags: Sudan, El Fasher, WFP, UNICEF

    Wagonjwa wanaohitaji tiba zaidi Gaza wasafirishwa kupata tiba zaidi Afrika Kusini na kwingineko

    Play Episode Listen Later Oct 29, 2025 3:24


    Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO, limeongoza uhamishwaji wa wagonjwa kutoka Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, ikiwa ni  mara ya kwanza tangu kuanza kwa awamu mpya ya kusitishwa kwa mapigano kwenye  ukanda huo.Katika muda wa siku mbili, wagonjwa 41 waliokuwa katika hali mbaya pamoja na familia zao 145 wamehamishwa kutoka eneo la mgogoro, kuelekea Afrika Kusini, Uswisi na kwingineko, huku maelfu zaidi wakiendelea kusubiri matibabu ya dharura.Katika hospital iliyojengwa kwa mahema  katika eneo la AL-MAWASI, RAFAH kwenye Ukanda wa Gaza wagonjwa wakihudumiwa kila kona watoto kwa wakubwa Miongoni mwao ni Ibrahim Abu Ashiba, mkurugenzi wa filamu ambaye maisha yake yamebadilika ghafla. Anakumbuka wakati alipojeruhiwa. Anasema, "Nilipigwa risasi mara kadhaa, mara moja kwenye kifua, mara moja kwenye bega, mara mbili mkononi. Risasi hizo mbili zilikata mishipa ya neva ya mkono wangu. Sasa siwezi kushika kamera wala kunyoosha mkono wangu kawaida. Ghafla, maisha yangu yote yalisimama."Safari ya kupona kwa Ibrahim inaanzia Afrika Kusini, ambapo amekubaliwa kwenda kupokea matibabu maalum ambapo anasema "Maisha yangu yote yalikuwa yamesimama baada ya kujeruhiwa hadi waliponipigia simu na kunijulishakwamba nitasafiri kwenda Afrika Kusini kwa matibabu. Ilionekana kama nimezaliwa upya."Mgonjwa mwingine katika hospitali hii ni, Maria Al-Shaer, alijeruhiwa vibaya katika mashambulizi yaliyokuwa yakiendelea Gaza, huku akipoteza ndugu zake. Mama yake, Raghda Ahmed Al Shaer, anaelezea mateso hayo. "Maria amepoteza baba yake na ndugu zake wote. Alijeruhiwa na kuvunjika mguu, mifupa na kupoteza nyama. Anahitaji upasuaji wa kuwekewa viungo bandia. Maisha yake yamegeuka, hawezi kutembea, na hali yake ya kisaikolojia imeathirika sana."Uhamishwaji huu umeratibiwa na Shirikisho la Chama cha Msalaba Mwekundu Palestina, kwa msaada wa WHO. Dkt. Luca Pigozzi, Mratibu wa Timu ya Dharura ya WHO, anafafanua umuhimu wake."Huu ni uhamishaji wa kwanza wa matibabu tangu kusitishwa kwa mapigano Oktoba 10. Tumejizatiti kuongeza uwezo wetu kusaidia na kuratibu uhamishaji kwa ajili ya matibabu, kwa ushirikiano wa karibu na Shirikisho la chama cha Msalaba Mwekundu la Palestina."Raghda anaeleza matumaini kwa ajili ya binti yake wanapohama kwenda Uswisi. "Wametupigia kutuarifu kwamba Maria amekubaliwa kusafiri kwenda Uswisi kwa matibabu. Tumefurahi sana kwamba atatembea tena, na hali yake ya kisaikolojia itaboreka. Atarudi kuwa Maria wa kawaida kama tuliyemjua."WHO inasisitiza kuwa wagonjwa takriban 15,000 bado wanangojea idhini ya kupata matibabu nje ya Gaza na inatoa wito kwa nchi zote kufungua milango yote za dharura kwa ajili ya uokoaji wa wagonjwa.

    Kimbunga Jamaica, Katibu Mkuu wa UN azungumza

    Play Episode Listen Later Oct 29, 2025 1:38


    Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameonesha wasiwasi mkubwa wakati huu Kimbunga Melissa kikiwa miongoni mwa vimbunga vyenye nguvu zaidi kuwahi kurekodiwa katika Bahari ya Atlantiki kinaendelea kusababisha uharibifu mkubwa katika eneo la Karibea.Kupitia taarifa yake iliyotolewa leo mjini New York Marekani na msemaji wake, Katibu Mkuu amesema kimbunga hicho kimeacha madhara makubwa nchini Jamaica, Cuba na Bahamas  huku mafuriko makubwa yakiripotiwa pia nchini Haiti na Jamhuri ya Dominika.Taarifa hiyo imemnukuu Katibu  Mkuu wa Umoja wa Mataifa  kwamba “ana wasiwasi mkubwa” na anashikamana na serikali pamoja na wananchi walioathiriwa vibaya na Kimbunga Melissa.”Katibu Mkuu pia “Amewapa pole familia zote za waliopoteza wapendwa wao katika kimbunga hicho na anawatakia majeruhi wote ahueni ya haraka.”Umoja wa Mataifa umeanza kutoa msaada wa dharura, huku timu zake zikiwa tayari mashinani kusaidia kutathmini madhara na kusaidia juhudi za kitaifa. Pia, umetoa dola milioni nne kwa Haiti na vile vile dola milione nne kwa Cuba kutoka Mfuko wake wa Dharura (CERF) ili kusaidia jamii kujiandaa na kupunguza madhara ya kimbunga hicho.Taarifa hiyo imesema Umoja wa Mataifa uko tayari “kutuma wahudumu wa ziada kwa muda mfupi na kuzindua maombi ya misaada ya dharura kukabiliana na mahitaji ya kibinadamu yatakayosababishwa na kimbunga hicho.”Kimbunga Melissa ni miongoni mwa vimbunga vyenye nguvu zaidi kuwahi kuikumba Karibea, na kinatishia maisha ya mamilioni ya watu kutokana na mafuriko, uharibifu na watu kufurushwa katika makazi yao.

    29 OKTOBA 2025

    Play Episode Listen Later Oct 29, 2025 9:53


    Leo jaridani tunamulika kimbunga Melissa huko Karibea, uhamishaji wagonjwa kutoka Gaza kwenda nchi za nje kupata huduma za kigeni na hali tete kwa watoto nchini Sudan. Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi.Katibu Mkuu wa Umoja wa MataifaAntonio Guterres ameonesha wasiwasi mkubwa wakati Kimbunga Melissa kikiwa miongoni mwa vimbunga vyenye nguvu zaidi kuwahi kurekodiwa katika Bahari ya Atlantiki kinaendelea kusababisha uharibifu mkubwa katika eneo la Karibea.Kupitia taarifa yake iliyotolewa leo mjini New York Marekani na msemaji wake Katibu Mkuu amesema kimbunga hicho kimeacha athari kubwa nchini Jamaica, Cuba na Bahamas  huku mafuriko makubwa yakiripotiwa pia nchini Haiti na Jamhuri ya Dominika.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani, WHO, limeongoza uhamishwaji wa kwanza  wagonjwa kutoka Gaza tangu awamu mpya ya kusitishwa kwa mapigano. Katika muda wa siku mbili, wagonjwa 41 waliokuwa katika hali mbaya pamoja na familia zao 145 wamehamishwa kutoka eneo la mgogoro, huku maelfu zaidi wakiendelea kusubiri matibabu ya dharura. Flora Nducha na taarifa zaidi.Nchini Sudan hususani katika eneo la El Faher kusinimagharibi mwa nchi, hali ya kibinadamu inazidi kuwa mbaya kila siku, huku ghasia, njaa, na vizuizi vya utoaji misaada vikiendelea kuathiri mamilioni ya watu wakiwemo watoto waliokwama katika maeneo ya vita. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

    28 OKTOBA 2025

    Play Episode Listen Later Oct 28, 2025 11:02


    Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia mradi wa TANZIE huko Chuo Kikuu Mzumbe, mkoani Morogoro, mashariki mwa Tanzania, unaolenga kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu SDGs. Pia tunakuletea habari kwa ufupi na uchambuzi wa neno la wiki.Mamilioni ya watu nchini Jamaica na katika ukanda wote wa Karibea wanajiandaa kukabiliana na madhara makubwa ya kimbunga Melissa huku Umoja wa Mataifa na washirika wake wakionya kuhusu tishio kubwa na la haraka la kibinadamu.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameelezea wasiwasi wake mkubwa kufuatia kuongezeka kwa mapigano ya kijeshi mjini El Fasher, jimbo la Darfur Kaskazini, nchini Sudan. Kupitia taarifa iliyotolewa na Msemaji wake usiku wa tarehe27 Oktoba 2025 kwa saa za New York marekani, Guterres amesema kwa zaidi ya miezi kumi na minane, wakazi wa El Fasher na maeneo ya jirani wamekuwa wakikabiliwa na mateso makubwa huku makundi ya Wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF) yakizingira mji huo.Na hii leo, Ofisi ya Umoja wa Matiafa ya Haki za Binadamu na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Usaidizi nchini Afghanistan wamechapisha waraka wa taarifa kuhusu madhara makubwa ya kina za haki za binadamu yaliyotokana na kusitishwa kwa huduma za mawasiliano nchini Afghanistan tarehe 29 Septemba hadi tarehe mosi mwezi huu, — hatua ambayo imezidisha changamoto nyingi ambazo tayari zinawakabili wananchi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya neno "KIMBIMBI"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

    Guterres: ASEAN chukueni hatua kukomesha ukatili Myanmar

    Play Episode Listen Later Oct 27, 2025 2:47


    Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito kwa dunia na mataifa wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kusini-Mashariki mwa Asia, ASEAN kuchukua hatua za haraka kumaliza machafuko ya muda mrefu nchini Myanmar, akisisitiza kuwa mgogoro huo si tishio kwa watu wa Myanmar pekee bali pia kwa amani na usalama wa kanda nzima ya Asia ya Kusini Mashariki.  Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

    UNICEF yachukua hatua za kukabiliana na mlipuko wa MPOX nchini Kenya

    Play Episode Listen Later Oct 27, 2025 3:02


    Katika kaunti ya Mombasa nchini Kenya, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wa Mastercard Foundation na Serikali ya Kaunti ya Mombasa, imechukua hatua za kukabiliana na mlipuko wa MPOX kwa kutoa huduma muhimu za afya na WASH kwa wagonjwa na waliopona, ikiwa ni pamoja na vifaa vya kujikinga (PPEs), vituo vya kusafisha mikono na ujumbe wa mabadiliko ya tabia za kijamii. Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi

    27 OKTOBA 2025

    Play Episode Listen Later Oct 27, 2025 10:00


    Hii leo jaridani tunaangazia machafuko ya muda mrefu nchini Myanmar, hali ya kibinadamu nchini Sudan kufuatia ripoti za vifo vya raia na wimbi la wakimbizi wa ndani, na masuala ya afya nchini Kenya.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito kwa dunia na mataifa wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kusini-Mashariki mwa Asia, ASEAN kuchukua hatua za haraka kumaliza machafuko ya muda mrefu nchini Myanmar, akisisitiza kuwa mgogoro huo si tishio kwa watu wa Myanmar pekee bali pia kwa amani na usalama wa kanda nzima ya Asia ya Kusini Mashariki.Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) imeelezea wasiwasi mkubwa kufuatia ripoti za vifo vya raia na wimbi la wakimbizi wa ndani, kufuatia kuendelea kwa mapigano makali katika mji wa El Fasher, huko Darfur Kaskazini nchini Sudan. Tupate tarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.Katika kaunti ya Mombasa nchini Kenya, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wa Mastercard Foundation na Serikali ya Kaunti ya Mombasa, imechukua hatua za kukabiliana na mlipuko wa MPOX kwa kutoa huduma muhimu za afya na WASH kwa wagonjwa na waliopona, ikiwa ni pamoja na vifaa vya kujikinga (PPEs), vituo vya kusafisha mikono na ujumbe wa mabadiliko ya tabia za kijamii.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

    Claim Habari za UN

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel