Habari za UN

Follow Habari za UN
Share on
Copy link to clipboard

Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN Global Communications


    • Feb 25, 2026 LATEST EPISODE
    • daily NEW EPISODES
    • 4m AVG DURATION
    • 3,866 EPISODES


    More podcasts from UN Global Communications

    Search for episodes from Habari za UN with a specific topic:

    Latest episodes from Habari za UN

    JIFUNZE KISWAHILI - NENO: PEMBUA

    Play Episode Listen Later Feb 25, 2026 0:42


    Leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili, Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "PEMBUA" . Kama umezoea kuwa unapembua mchele basi fahamu kuna zaidi ya maana hiyo. Karibu.

    24 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 24, 2026 11:41


    Tuliyokuandalia katika Jarifada la Habari hii leoNi miaka miine tangu uvamizi kamili wa Urusi nchini Ukraine, Umoja wa Mataifa wataka vita vikome mara moja kuwapunguzia madhila raiaHuko Gaza Shirika la UNICEF limezindua mpango wa Gaza we want au Gaza tuitakayo ili kukusanya maoni ya watoto baada ya miaka miwili ya vitaHuko The Hague Uholanzi kikao cha majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, (ICC) cha kuthibitisha iwapo kuna ushahidi wa kutosha wa kumfikisha mahakama aliyekuwa Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte kwa madai ya uhalifu dhidi ya ubinadamu kinaendeleaMada yetu kwa kina inajikita Tanzania kuangazia juhudi za kuhakikisha wasichana na wanawake hawaachwi nyuma katika sayansiNa katika jifunze Kiswahili utasikia maana na neno "PEMBUA"

    Matumaini katikati ya migogoro: Kituo cha watoto yatima cha Juba chawapa watoto fursa ya pili

    Play Episode Listen Later Feb 20, 2026 3:45


    Sudan Kusini ambako mizozo inaendelea kuvuruga utoto wa watoto, kituo kidogo cha watoto yatima katika mji Mkuu Juba kinawapa makumi ya watoto walio hatarini si tu makazi, bali pia matumaini, uponyaji, na nafasi ya kujenga upya mustakabali wao. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

    pili juba watoto sudan kusini
    WHO yaunga mkono kampeni ya dharura ya kutoa chanjo ya polio nchini Malawi baada ya kubainika kwa mgonjwa wa polio

    Play Episode Listen Later Feb 20, 2026 3:22


    Takribani watoto milioni 1.3 nchini Malawi wamepatiwa chanjo ya polio katika kampeni maalum ya siku nne, kufuatia kugunduliwa kwa mgonjwa mpya wa polio mwishoni mwa mwezi Januari 2026. Huyu ni mgonjwa wa kwanza kuripotiwa tangu mwaka 2022, wakati virusi vya polio pori vilivyokuwa na uhusiano wa kijenetiki na mlipuko ulioripotiwa nchini Pakistan vilipobainika. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.

    20 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 20, 2026 11:34


    Hii leo jaridani tunaangazia athari ya baa la nja nchini Somalia, kampeni ya chanjo la polio nchini Malawi, na juhudi za UNMISS nchini Sudan Kusini za kuwapatia hifadhi na lishe watoto yatima huko Juba.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP limesema hali ya upatikanaji wa chakula nchini Somalia imefikia hatua mbaya ambapo watu milioni 4.4 hivi sasa wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula na kwamba ni mtu 1 tu kati ya 7 ndiye anayepata mgao wa chakula.Takribani watoto milioni 1.3 nchini Malawi wamepatiwa chanjo ya polio katika kampeni maalum ya siku nne, kufuatia kugunduliwa kwa mgonjwa mpya wa polio mwishoni mwa mwezi Januari 2026. Huyu ni mgonjwa wa kwanza kuripotiwa tangu mwaka 2022, wakati virusi vya polio pori vilivyokuwa na uhusiano wa kijenetiki na mlipuko ulioripotiwa nchini Pakistan vilipobainika.Sudan Kusini ambako mizozo inaendelea kuvuruga utoto wa watoto, kituo kidogo cha watoto yatima katika mji Mkuu Juba kinawapa makumi ya watoto walio hatarini si tu makazi, bali pia matumaini, uponyaji, na nafasi ya kujenga upya mustakabali wao. Anold Kayanda na taarifa zaidi.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

    Ukata WFP wasababisha mtu 1 tu kati ya 7 apatiwe msaada wa chakula

    Play Episode Listen Later Feb 20, 2026 2:20


    Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP limesema hali ya upatikanaji wa chakula nchini Somalia imefikia hatua mbaya ambapo watu milioni 4.4 hivi sasa wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula na kwamba ni mtu 1 tu kati ya 7 ndiye anayepata mgao wa chakula. Rashid Malekela na taarifa zaidi.

    19 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 19, 2026 9:58


    Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina tukimsikia Barbara Batte Guevara, Mkufunzi anayefundisha lugha ya Kiswahili katika Chuo Kikuu cha Havana nchini Cuba. Kwa kushirikiana na Tanzania chuo hicho ambacho mwezi uliopita kimetimiza miaka 298 tangu kuanzishwa kwake, hivi karibuni kimetoa fursa kwa Wacuba kujifunza lugha ya Kiswahili.Anold Kayanda wa Idhaa hii amemtembelea Profesa Barbara Batte katika jiji la Havana nchini Cuba ili kufahamu zaidi kuhusu hatua hii na mafanikio yaliyofikiwa hadi kufikia sasa. Pia tunakuletea habari kwa ufupi kama zifuatazo.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito wa kuanzishwa kwa Mfuko wa Kimataifa wa Akili Mnemba au AI wenye thamani ya dola bilioni 3, ili kuhakikisha teknolojia hiyo inawanufaisha watu wote duniani, badala ya kuwa mali ya mataifa machache au kampuni chache zenye nguvu. Akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa wa kujadili Athari za AI huko New Delhi nchini India, Guterres amesema mustakabali wa AI unapaswa kujengwa kwa ushirikiano wa kimataifa”.Mashambulizi makali yanayoendelea kufanywa na Israeli dhidi ya maeneo ya Palestina ya Gaza na Ukingo wa Magharibi ambayo inakalia kimabavu yanatia hofu ya uwezekano wa utokomezaji wa kabila, imesema Ripoti mpya ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR), ya kuanzia Novemba 1 2024 hadi Desemba 31 2025. Ripoti inasema mashambulizi ya Israeli yameweka mazingira ambamo kwamo wapalestina kama kundi watashindwa kuendelea kuishi Gaza huku Ajith Sunghay, Mkuu wa Ofisi ya OHCHR Palestina akisema, “ripoti inachambua  mwenendo wa mapigano ya jeshi la Israeli, linaloendelea kuua idadi kubwa ya raia, kusababisha njaa, kuwahamisha takribani wakazi wote wa Gaza, tena zaidi ya mara moja — na kuharibu miundombinu iliyosalia ya kiraia ya Gaza.”wanamgambo wa vikosi vya Rapid Support Forces (RSF) nchini Sudan walitekeleza kampeni iliyoratibiwa ya uharibifu dhidi ya jamii zisizo za kiarabu ndani ya mji wa El-Fasher na viunga vyake, kampeni yenye viashiria vya mauaji ya kimbari, imeeleza ripoti mpya iliyotolewa leo na Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya Kuchunguza Ukweli kuhusu Sudan. Ripoti imetaja vitendo hivyo ni pamoja na kuua wanachama wa kundi la kikabila linalolindwa; kusababisha madhara makubwa ya kimwili na kiakili; ambavyo ni vipengele muhimu vya kosa la mauaji ya kimbari chini ya sheria za kimataifa.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili tunawasikiliza baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Havana wanaojifunza lughaya Kiswahili. Tuanze na Yibran Nunez Batte.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

    Watengeneza maudhui kupoteza mapato kutokana na kasi ya maendeleo ya Akili Mnemba

    Play Episode Listen Later Feb 18, 2026 3:43


    Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, limesema wabunifu wa maudhui duniani kwa lugha ya kiingereza content creators wanakabiliwa na hatari ya kupoteza hadi asilimia 24 ya mapato yao ifikapo mwaka 2028 kutokana na kasi ya maendeleo ya Akili Mnemba, au AI. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.

    18 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 18, 2026 12:01


    Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya Akili Mnemba na wabunifu wa maudhui duniani kwa lugha, waumini wa dini ya kiislamu wakati huu wa Ramadhani katika ukanda wa Gaza, na matibabu ya kwanza ya ugonjwa wa kichocho huko Mwanza nchini Tanzania.Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, limesema wabunifu wa maudhui duniani kwa lugha ya kiingereza content creators wanakabiliwa na hatari ya kupoteza hadi asilimia 24 ya mapato yao ifikapo mwaka 2028 kutokana na kasi ya maendeleo ya Akili Mnemba, au AI.Waumini wa dini ya kiislamu duniani kote wameanza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, kipindi kinachoambatana na sio tu ibada bali pia mlo kama vile futari na daku. Hata hivyo kwa wakazi wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na kimabavu na Israeli hali si hali kwani mlo na mengine yanayoambatana na kipindi hiki vinasalia kuwa ndoto.Serikali ya Tanzania na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo UNDP kupitia Ushirikiano wa Upatikanaji na Ufikishaji wa Huduma (ADP), inaendesha mpango wa majaribio wa kihistoria katika mikoa ya Simiyu, Mwanza, na Kigoma ili kutoa matibabu ya kwanza ya ugonjwa wa kichocho yaliyoandaliwa mahususi kwa ajili ya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.Mwenyeji wako ni Anold Kyanda, karibu!

    Wakazi katika ukanda wa Gaza wahaha kumudu mlo wakati wa mfungo wa Ramadhani

    Play Episode Listen Later Feb 18, 2026 2:54


    Waumini wa dini ya kiislamu duniani kote wameanza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, kipindi kinachoambatana na sio tu ibada bali pia mlo kama vile futari na daku. Hata hivyo kwa wakazi wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na kimabavu na Israeli hali si hali kwani mlo na mengine yanayoambatana na kipindi hiki vinasalia kuwa ndoto. Assumpta Massoi anafafanua zaidi.

    Tanzania yajipanga kutokomeza ugonjwa wa kichocho kwa watoto wadogo

    Play Episode Listen Later Feb 18, 2026 3:30


    Serikali ya Tanzania na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo UNDP kupitia Ushirikiano wa Upatikanaji na Ufikishaji wa Huduma (ADP), inaendesha mpango wa majaribio wa kihistoria katika mikoa ya Simiyu, Mwanza, na Kigoma ili kutoa matibabu ya kwanza ya ugonjwa wa kichocho yaliyoandaliwa mahususi kwa ajili ya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano. Rashid Malekela na taarifa zaidi. 

    Jifunze Kiswahili: Maana ya "KOO" katika muktadha wa wanyama

    Play Episode Listen Later Feb 17, 2026 0:27


    Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya "KOO" katika muktadha wa wanyama

    17 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 17, 2026 9:59


    Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania, ambako Magonjwa ya kimeta, miguu na midomo yanayokumba mifugo kama vile ng'ombe pamoja na mdondo unaoshambulia kuku yameendelea kuwa mwiba duniani na hata nchini Tanzania, ambako mbinu mbali mbali zimekuwa zikitumika kuyadhibiti ili kunusuru afya ya mifugo.Uchambuzi mpya kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) na HRP, ambao ni mpango wa taasisi za Umoja wa Mataifa za utafiti kuhusu uzazi wa binadamu, unaonesha kuwa takribani theluthi mbili ya vifo vya wajawazito duniani hutokea katika nchi zilizoathiriwa vibaya na migogoro au zenye udhaifu wa mifumo, ambapo ujauzito ni hatari mara tano zaidi ikilinganishwa na nchi zilizo thabiti.Vita vya Ukraine vikielekea kuingia katika mwaka wa tano, zaidi ya theluthi moja ya watoto wa Ukraine bado wameyakimbia makazi yao wengi wao sasa wakilazimika kuishi katika majengo yaliyoko chini ya ardhi. Akizungumza na waandishi wa habari kutoka kwenye chumba cha chini ya jengo katika mji wa Kherson, mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) nchini Ukraine, Munir Mammadzade, amesema mji huo “upo chini ya mashambulizi ya mara kwa mara,” huku mashambulizi ya kila siku yakiharibu nyumba na miundombinu muhimu, pamoja na huduma ambazo watoto na familia wanazitegemea.Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wameeleza wasiwasi mkubwa kuhusu madhara yanayoweza kuwapata waathirika waliotajwa katika nyaraka zinazojulikana kama “Epstein Files”, wakisema mchakato wa utoaji wa taarifa hizo haukulinda ipasavyo faragha na usalama wao na pia wametaka hatua stahili za kisheria zichukuliwe kwa wale wote waliotajwa katika nyaraka hizo kwa mujibu wa sheria. Nyaraka hizo zinafichua maovu yaliyotendwa na watu mbalimbali kupitia mmarekani Jeffrey Epstein.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya"KOO" katika mkitadha wa wanyama.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

    DRC: UNICEF na KOICA waboresha huduma za usafi na lishe kwa wakazi wa Tanganyika

    Play Episode Listen Later Feb 16, 2026 2:34


    Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF wakishirikiana na Shirika la Maendeleo la Korea KOICA wanawasaidia wananchi wa Nyunzu katika jimbo la Tanganyika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC kwa miradi ya kusaidia huduma za afya ya watoto ambapo wamepanua upatikanaji wa huduma muhimu na endelevu. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi

    Mkutano wa AI waanza New Delhi Mjumbe wa UN asisitiza ujumuishi wa nchi zote

    Play Episode Listen Later Feb 16, 2026 2:41


    Mkutano wa kimataifa unaofahamika kama AI Impact 2026 umeanza leo mjini New Delhi, India ukiwakutanisha viongozi kutoka sehemu mbalimbali za dunia ili kujadili namna akili mnemba (AI) inavyoweza kuendelezwa na kutumika kwa uwajibikaji kuchangia maendeleo endelevu. Amandeep Singh Gill, Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia teknolojia za kidijitali na zinazoibuka, amesisitiza ushiriki mpana wa kimataifa kwani ni muhimu ili kuhakikisha AI inanufaisha nchi zote. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

    16 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 16, 2026 9:59


    Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa kimataifa unaofahamika kama AI Impact 2026 mjini New Delhi, India, hali ya kibinadamu nchini Cuba, na huduma za Afya, maji safi na salama nchini DR Congo.Mkutano wa kimataifa unaofahamika kama AI Impact 2026 umeanza leo mjini New Delhi, India ukiwakutanisha viongozi kutoka sehemu mbalimbali za dunia ili kujadili namna akili mnemba (AI) inavyoweza kuendelezwa na kutumika kwa uwajibikaji kuchangia maendeleo endelevu. Amandeep Singh Gill, Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia teknolojia za kidijitali na zinazoibuka, amesisitiza ushiriki mpana wa kimataifa kwani ni muhimu ili kuhakikisha AI inanufaisha nchi zote.Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imetoa onyo kali kuhusu kuzorota kwa hali ya kiuchumi nchini Cuba, ikisema uhaba wa mafuta na vikwazo vya muda mrefu vinaathiri vibaya huduma za msingi kote nchini humo.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF wakishirikiana na Shirika la Maendeleo la Korea KOICA wanawasaidia wananchi wa Nyunzu katika jimbo la Tanganyika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC kwa miradi ya kusaidia huduma za afya ya watoto ambapo wamepanua upatikanaji wa huduma muhimu na endelevu.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

    Cuba: Hali ya kibinadamu imefikia pabaya yaonya OHCHR

    Play Episode Listen Later Feb 16, 2026 2:59


    Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imetoa onyo kali kuhusu kuzorota kwa hali ya kiuchumi nchini Cuba, ikisema uhaba wa mafuta na vikwazo vya muda mrefu vinaathiri vibaya huduma za msingi kote nchini humo. Flora Nducha na taarifa zaidi

    Vipindi vya Redio ya Umoja wa Mataifa vilitoa tafsiri sahihi ya wapigania uhuru

    Play Episode Listen Later Feb 13, 2026 3:40


    Leo ni siku ya redio duniani ambayo msingi wake unatokana na kuanzishwa kwa redio ya Umoja wa Mataifa tarehe 13 Februari mwaka 1946 jijini New York, Marekani. Kwa mantiki hiyo ikiwa mwaka huu redio hiyo ya Umoja wa Mataifa inatimiza miaka 80 tumeangazia mchango wa vipingi vyake vilivyokuwa vinarushwa na redio zingine ikiwemo iliyokuwa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD)  nchini Tanzania  wakati huo. Assumpta Massoi amemulika suala hilo.

    Redio Okapi iliokoa maisha yangu: Mkimbizi Bahati Yohane

    Play Episode Listen Later Feb 13, 2026 3:33


    Katika maeneo ya migogoro, redio huwa nguzo ya utulivu. Mathalani Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Radio Okapi ya Umoja wa Mataifa imekuwa sauti ya kuaminika na kuwasaidia wakimbizi kusaka usalama tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002 kama sehemu ya ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO. Mmoja wa wakimbizi kutoka Mashariki mwa DRC ambaye sasa anaishi kambi ya wakimbizi ya Kyangwali nchini Uganda amemweleza John Kibego kutoka Redio washirika wetu Kazi Njema FM ya mjini Hoima jinsi matangazo ya redio Okapi yalivyonusuru maisha yake wakati wa vita

    13 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 13, 2026 11:49


    Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya Redio Duniani likitupeleka nchini Tanzania kusikia jinsi ambavyo redio inavyochochea maendeleo ya kijamii, nchini Uganda kumsikia mkimbizi kutoka DRC, na katika ukanda wa Gaza ambako redio inaunganisha tena jamii ndani ya vifusi.Leo ni siku ya redio duniani ambayo msingi wake unatokana na kuanzishwa kwa redio ya Umoja wa Mataifa tarehe 13 Februari mwaka 1946 jijini New York, Marekani. Kwa mantiki hiyo ikiwa mwaka huu redio hiyo ya Umoja wa Mataifa inatimiza miaka 80 tumeangazia mchango wa vipingi vyake vilivyokuwa vinarushwa na redio zingine ikiwemo iliyokuwa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) nchini Tanzania wakati huo. Assumpta Massoi amemulika suala hilo.Katika maeneo ya migogoro, duniani redio huwa nguzo ya utulivu na wakati mwingine daraja la kuokoa maisha. Na ndivyo ilivyokuwa kwa mkimbizi Bahati Yohane kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kwani kwake, redio haikuwa tu combo cha habari ilikuwa dira ya kuokoa maisha yake.Kabla ya vita vya sasa kuanza katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina lilalokaliwa kimabavu na Israel, Redio ilikuwa chombo muhimu kwa umma na kwa hakika umuhimu wake haujakoma isipokuwa huduma ya matangazo ya redio ndio iliyokuwa imekoma kutokana na vituo vya redio kusambaratishwa kwa makombora, lakini sasa juhudi zinafanyika kuirejesha huduma hiyo muhimu.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

    Kati ya magofu na uhaba, vituo vya redio vinafanya juhudi kuunganisha tena jamii Gaza

    Play Episode Listen Later Feb 13, 2026 2:42


    Kabla ya vita vya sasa kuanza katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina lilalokaliwa kimabavu na Israel, Redio ilikuwa chombo muhimu kwa umma na kwa hakika umuhimu wake haujakoma isipokuwa huduma ya matangazo ya redio ndio iliyokuwa imekoma kutokana na vituo vya redio kusambaratishwa kwa makombora, lakini sasa juhudi zinafanyika kuirejesha huduma hiyo muhimu. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

    Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "UNGUKA"

    Play Episode Listen Later Feb 12, 2026 0:57


    Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "UNGUKA" 

    12 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 12, 2026 11:24


    Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina kesho Ijumaa tarehe 13 Februari ikiwa ni ni siku ya Redio Duniani mwaka huu ikijikita  katika Redio na Akili tunakupeleka mashariki mwa DRC, kwa George Musubao kutoka Televishen na Radio washirika Canal Victoire Du People Kasindi.Leo tarehe 12 Februari ni siku ya Kimataifa ya Kuzuia Itikadi Kali Zinazochochea Ugaidi, ikiwa ni maadhimisho ya nne tangu kuanzishwa kwake na mwaka huu kauli mbiu inasema “Kuzuia ugaidi wa kikatili katika enzi ya teknolojia mpya na zinazoibuka”. Ugaidi na itikadi kali vinaendelea kuwa tishio kubwa kwa amani na usalama wa dunia, huku vikigusa watu wa rika, dini na tamaduni mbalimbali na ndio maana Umoja wa Mataifa unasema ingawa teknolojia kama akili mnemba au AI, mitandao ya kijamii na majukwaa ya kidijitali inaweza kusaidia juhudi za kuzuia misimamo mikali, pia inatumiwa na magaidi kueneza chuki, upotoshaji na kuhamasisha vurugu ndio maana shirika hilo linahimiza ushirikiano wa kimataifa, matumizi ya teknolojia kwa uwajibikaji na suluhisho shirikishi zinazoheshimu haki za binadamu ili kuzuia kuenea kwa itikadi kali.Barani Ulaya ambapo Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ametoa tamko kali akilaani mashambulizi ya mfululizo yanayofanywa na nchi ya Urusi dhidi ya mifumo ya nishati nchini Ukraine. Taarifa iliyotolewa leo kutoka Geneva, Uswisi, imeeleza kuwa mashambulizi hayo yanawanyima raia mahitaji muhimu ikiwemo mifumo ya kupasha joto, maji, na umeme katikati ya msimu wa baridi kali uliopitiliza.Kuelekea kuanza kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani hapo wiki ijayo, katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametuma ujumbe akisema kuwa “Katika zama hizi ngumu na za mgawanyiko, hebu tuitikie wito wa stahmala wa Ramadhani. Kuziba pengo la mgawanyiko. Kufikisha msaada na matumaini kwa wale wanaoumini. Na kulinda haki na utu wa kila mtu…..Hebu Mwezi huu Mtukufu ututie hamasa ya kufanya kazi pamoja ili kujenga dunia yenye amani zaidi, ukarimu na haki kwa watu wote.  Ramadhani njema.”Na Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "UNGUKA"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

    Fungueni minyororo ya kihistoria inayokwamisha Afrika

    Play Episode Listen Later Feb 11, 2026 2:14


    Jukwaa la akili unde au AI lililofanyika kwa siku mbili huko Nairobi, nchini Kenya limekunja jamvi ambapo mmoja wa washiriki amesema wanaodai kuwa bara la Afrika liko nyuma kwenye teknolojia hiyo, ni dhahiri shairi hawalifahamu vema bara hilo lenye mataifa 54. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

    Wanawake sayansi tunaiweza kinachotakiwa ni kujiamini: Dkt. Mugara Mahungururo

    Play Episode Listen Later Feb 11, 2026 2:59


    Leo ni siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi mwaka huu mauadhui yakihimiza “Sayansi kwa Mustakabali Jumuishi kwa Wanawake na Wasichana” Kwamujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , Sayansi na Utamaduni UNESCO leo hii , wanawake wanachangia chini ya theluthi moja ya watafiti duniani, kulingana hivyo kuziba pengo hili la kijinsia si suala la haki pekee ni muhimu kwa ubora, uhalisia na mchango wa sayansi, teknolojia na ubunifu. Flora Nducha na taarifa zaidi 

    11 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 11, 2026 9:59


    Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya IPU kuhusu uhasama wa wabunge, siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi, na yalitojiri katika Jukwaa la akili unde au AI lililofanyika kwa siku mbili huko Nairobi, nchini Kenya.Wabunge kote ulimwenguni wanakabiliwa na viwango vinavyoongezeka vya vitisho, unyanyasaji na vurugu kutoka kwa umma imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na Muungano wa Mabunge Duniani (IPU). Rashid Malekela na taarifa zaidi.Leo ni siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi mwaka huu mauadhui yakihimiza “Sayansi kwa Mustakabali Jumuishi kwa Wanawake na Wasichana” Kwamujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , Sayansi na Utamaduni UNESCO leo hii , wanawake wanachangia chini ya theluthi moja ya watafiti duniani, kulingana hivyo kuziba pengo hili la kijinsia si suala la haki pekee ni muhimu kwa ubora, uhalisia na mchango wa sayansi, teknolojia na ubunifu.Jukwaa la akili unde au AI lililofanyika kwa siku mbili huko Nairobi, nchini Kenya limekunja jamvi ambapo mmoja wa washiriki amesema wanaodai kuwa bara la Afrika liko nyuma kwenye teknolojia hiyo, ni dhahiri shairi hawalifahamu vema bara hilo lenye mataifa 54.

    Ripoti: Uhasama wa umma dhidi ya wabunge waongezeka duniani

    Play Episode Listen Later Feb 11, 2026 3:02


    Wabunge kote ulimwenguni wanakabiliwa na viwango vinavyoongezeka vya vitisho, unyanyasaji na vurugu kutoka kwa umma imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na Muungano wa Mabunge Duniani (IPU). Rashid Malekela na taarifa zaidi.

    umma ripoti
    Jifunze Kiswahili: Maana ya methali “Atokeapo mtoto wa fuko mshike japo wawinda fuko.”

    Play Episode Listen Later Feb 10, 2026 1:42


    Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Atokeapo mtoto wa fuko mshike japo wawinda fuko.”

    10 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 10, 2026 13:04


    Hii leo jaridani Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na Wakili Amon Mpanju, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kutoka Tanzania aliyehudhuria Mkutano wa Kamisheni ya Maendeleo ya Kijamii (CSocD64).Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yametoa onyo kali kuhusu hali mbaya ya kibinadamu inayowakumba watoto nchini Sudan. Mashirika hayo lile la kuhudumia watoto UNICEF, la afya WHO na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu wamenasema ghasia zisizoisha, njaa na magonjwa vinawasababisha watoto kupoteza Maisha na kudhoofika, huku mashambulizi dhidi ya vituo vya afya na vikwazo vya upatikanaji wa misaada vikizorotesha juhudi za kuwaokoa. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, msemaji wa UNICEF, Ricardo Pires, amesema “Katika baadhi ya maeneo ya jimbo la Darfur Kaskazini, zaidi ya nusu ya watoto wote wanakabiliwa na utapiamlo mkali, si makadirio, si mfano, imethibitishwa.”.Kikosi cha 12 cha Ulinzi wa Amani kutoka Tanzania TANZBAT 12 kinachohusumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Condo DRC chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO kimeendelea kudumisha uhusiano wa kijamii na wakazi wa mji wa Beni Mashariki mwa DRC, kwa kutoa msaada wa vifaa vya elimu kwa wanafunzi katika shule ya msingi Ngite iliyopo eneo la Mavivi. Mkuu wa shule hiyo Neema Nyamwaka amewashukuru walinada amani hao kutoka Tanzania kwa kujali sekta ya elimu.Leo ni siku ya mikunde duniani Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO likisistiza umuhimu kwa chakula hicho kwa lishe na mazingira. Huko Kigoma Tanzania FAO kupitia mpango wa Pamoja wa KJP imekuwa ikitoa mafunzo kwa wakulima kuhusu umuhimu wa mazao ya jamii ya mikunde huyu ni mmoja wa wanufaika wa mafunzo hayo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Atokeapo mtoto wa fuko mshike japo wawinda fuko.”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!

    MONUSCO yaishukuru Afrika Kusini baada ya kutangaza uamuzi wake wa kuondoa wanajeshi wake nchini DRC

    Play Episode Listen Later Feb 9, 2026 2:06


    Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, (MONUSCO) umetoa taarifa kwamba umefahamishwa na Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa kuwa Afrika Kusini itaondoa vikosi na wanajeshi wake waliobaki ndani ya MONUSCO. Rashid Malekela ameifuatilia kwa kina taarifa hiyo na anaeleza zaidi.

    Nilirubunika nikadhani ukeketaji ni usafi kumbe ni jinamizi: Manusura Saadia Hussein

    Play Episode Listen Later Feb 9, 2026 3:41


    Ukeketaji au FGM ni jinamizi linalowaandama waathirika maisha yao yote likisababisha changamoto sio tu za kimwili lakini pia za kiafya na kuwaacha na makovu yasiyofutika. Katika Kaunti ya Tana River Kusini Mashariki mwa Kenya tunakutana na manusura na shujaa mwanaharakati wa kupambana na mila hiyo potofu ya ukeketaji Saadia Hussein, raia wa Somalia anayeishi Kenya hivi sasa .Ni Mkurugenzi mtendaji na mwanzilishi wa taasisi  isiyo ya kiserikali ya Brighter Society Initiative. Anatusimulia safari yake ya machungu ya ukeketaji

    09 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 9, 2026 9:59


    Hii leo jaridani tunaangazia walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini DRC, mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu mwenye ulemavu wa kutoona nchini Vietnam, na harakati za kutokomeza ukeketaji nchini Kenya.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, (MONUSCO) umetoa taarifa kwamba umefahamishwa na Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa kuwa Afrika Kusini itaondoa vikosi na wanajeshi wake waliobaki ndani ya MONUSCO. Ninamualika Rashid Malekela aliyeifuatilia kwa kina taarifa hiyo ili atueleza zaidi.Nchini Vietnam taifa lililoko kusini-mashariki mwa Asia, mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu mwenye ulemavu wa kutoona anajitahidi kuhakikisha anatimiza ndoto yake ya kuwa mtaalamu wa mawasiliano licha ya vikwazo anavyokumbana navyo kila uchao, na hii ni kwa sababu si kwamba njia ni rahisi bali kwa sababu dhamira yake ni kubwa zaidi.Ukeketaji au FGM ni jinamizi linalowaandama waathirika maisha yao yote likisababisha changamoto sio tu za kimwili lakini pia za kiafya na kuwaacha na makovu yasiyofutika. Katika Kaunti ya Tana River Kusini Mashariki mwa Kenya tunakutana na manusura na shujaa mwanaharakati wa kupambana na mila hiyo potofu ya ukeketaji Saadia Hussein, raia wa Somalia anayeishi Kenya hivi sasa. Mkurugenzi mtendaji na mwanzilishi wa taasisi  isiyo ya kiserikali ya Brighter Society Initiative anatusimulia safari yake ya machungu ya ukeketaji.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

    “Tuwekeeni mazingira sahihi ili nasi tuoneshe uwezo wetu,” asema Msichana mwenye ulemavu wa kuona.

    Play Episode Listen Later Feb 9, 2026 2:37


    Nchini Vietnam taifa lililoko kusini-mashariki mwa Asia, mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu mwenye ulemavu wa kutoona anajitahidi kuhakikisha anatimiza ndoto yake ya kuwa mtaalamu wa mawasiliano licha ya vikwazo anavyokumbana navyo kila uchao, na hii ni kwa sababu si kwamba njia ni rahisi bali kwa sababu dhamira yake ni kubwa zaidi. Assumpta Massoi anasimulia zaidi kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani, ILO.

    UN: Wasichana zaidi ya milioni 4.5 wapo hatarini kufanyiwa ukeketaji mwaka huu wa 2026

    Play Episode Listen Later Feb 6, 2026 2:33


    Zaidi ya wasichana milioni 4.5 duniani kote, wengi wao wakiwa wenye umri wa chini ya miaka mitano, wako hatarini kufanyiwa ukeketaji mwaka huu pekee, wameonya viongozi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa katika ujumbe wao wa siku hii ya kimataifa ya kutokomeza ukeketaji kwa wanawake na watoto wa kike. Rashid Malekela na maelezo zaidi.

    Njiapanda ya matumaini na machungu, familia katika ukanda wa Gaza zinatafuta wapendwa wao kwa kuangalia picha za miili

    Play Episode Listen Later Feb 6, 2026 3:34


    Huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel, wiki hii, mamlaka za Israel zimewasilisha miili 54 pamoja na mifuko 66 iliyosheni mabaki ya viungo vya binadamu ya Wapalestina waliopotea wakati wa vita. Na kutokana na kutokuwepo kwa mfumo madhubiti wa kisasa kupima vinasaba kutambua mwili upi ni wa nani inakuwa changamoto kubwa hususani kwa ndugu. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

    06 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 6, 2026 10:52


    Hii leo jaridani tunaangazia juhudi za kutokomeza ukeketaji, watu waliotoweka katika ukanda wa Gaza kufuatia vita vya Hamas na Israeli, na msaada wa chakula kwa wakimbizi katika mpaka kati ya Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, na Sudan.Zaidi ya wasichana milioni 4.5 duniani kote, wengi wao wakiwa wenye umri wa chini ya miaka mitano, wako hatarini kufanyiwa ukeketaji mwaka huu pekee, wameonya viongozi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa katika ujumbe wao wa siku hii ya kimataifa ya kutokomeza ukeketaji kwa wanawake na watoto wa kike.Huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel, wiki hii, mamlaka za Israel zimewasilisha miili 54 pamoja na mifuko 66 iliyosheheni mabaki ya viungo vya binadamu ya Wapalestina waliopotea wakati wa vita. Na kutokana na kutokuwepo kwa mfumo madhubuti wa kisasa kupima vinasaba kutambua mwili upi ni wa nani inakuwa changamoto kubwa hususani kwa ndugu.Katika mpaka kati ya Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, na Sudan, maelfu ya familia waliokimbia makazi yao kutokana na vurugu wanapokea msaada wa chakula unaookoa maisha kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP uliosafirishwa kwa ndege hadi kwenye moja ya maeneo magumu zaidi kufikika nchini humo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

    WFP yagawa msaada wa chakula cha kuokoa maisha ya wakimbizi mpakani mwa CAR na Sudan

    Play Episode Listen Later Feb 6, 2026 2:55


    Katika mpaka kati ya Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, na Sudan, maelfu ya familia waliokimbia makazi yao kutokana na vurugu wanapokea msaada wa chakula unaookoa maisha kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP uliosafirishwa kwa ndege hadi kwenye moja ya maeneo magumu zaidi kufikika nchini humo. Flora Nducha na taarifa zaidi

    JIFUNZE KISWAHILI - NENO - KINYONYI

    Play Episode Listen Later Feb 5, 2026 0:57


    Je wajua maana ya neno kinyonyi? Leo hii mtaalamu wetu Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi katika Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua neno hilo ambalo ni kifaa tunachotumia kila siku kwenye kuhamisha kitu kutoka kwenye kompyuta.

    05 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 5, 2026 11:39


    Jaridani hii leo tuna Muhtasari wa Habari ukiangazia hali ya njaa Sudan, mchango wa Marekani dhidi ya VVU/ Ukimwi na kauli ya UNRWA kufuatia taarifa potofu dhidi ya shirika hilo. Halikadhalika mada kwa kina kutoka AfyaAFRIKA.Maeneo mawili zaidi katika jimbo la Darfur Kaskazini ya Um Baru na Kernoi sasa yameingia katika baa la njaa kufuatia utapiamlo wa kupindukia au unyafuzi kuvuka wiwango vya kutokuwa na uhakika wa chakula.Shirika la Umoja wa mataifa linalohusika na vita dhidi ya ukimwi UNAIDS limekaribisha kwa dhati hatua ya Marekani kutia saini kuwa sheria kifurushi cha matumizi ya kimataifa chenye thamani ya dola bilioni 5.88, kwa ajili ya hatua za kimataifa za kukabiliana na virusi vya ukimwi VVU .Kamishina Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA  Phillippe Lazzarini amesema taarifa potofu dhidi ya UNRWA zinaendelea kulenga shirika hilo katikati ya mgogoro Gaza ikiwemo madai ya hivi karibuni kabisa, yaliyoibuliwa na video ya jeshi la Israel ikionesha mifuko mitupu ya unga karibu na mabomu, ambapo amesema ni taarifa za uongo na  hazijadhibitishwa.Katika Mada kwa Kina: Kuelekea siku ya kutokomeza FGM kesho Februari 6, tunazungumza na Catherine Mootian, Muasisi na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la kiraia la AfyAfrika la huko Narok nchini Kenya. Yeye ni manusura wa FGM aliyeamua kuchukua hatua kuepusha wengine. 

    UNHCR SALIH: Asante Jordan kwa kuendelea kukirimmu wakimbizi wa Syria

    Play Episode Listen Later Feb 4, 2026 2:59


    Miaka kumi na nne baada ya wakimbizi wa kwanza wa Syria kuvuka mpaka kuingia Jordan kusaka usalama, kambi ya wakimbizi ya Zaatari bado ni makazi ya maelfu ya watu wanaosubiri suluhu ya kudumu. Wiki hii, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi, Barham Salih, ametembelea kambi hiyo na kukutana na familia ambazo zimeishi ukimbizini kwa zaidi ya muongo mmoja wengi wao wakiwa bado na matumaini ya kurejea nyumbani, lakini tu pale ambapo itakuwa salama. Flora Nducha amefuatilia ziara ya Salih na kutuandalia taarifa hii.

    Je, wajua ukibadili mfumo wa maisha unaweza kujiepusha na saratani?

    Play Episode Listen Later Feb 4, 2026 2:40


    Mabadiliko ya mfumo wa maisha na mazingira yanaweza kuzuia ugonjwa wa saratani kwa wagonjwa wanne katika kila wagonjwa kumi, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, (WHO) na shirika lake tangu la Utafiti kuhusu saratani, IARC kama anavyoripoti Rashid Malekela.

    04 JANAUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 4, 2026 9:58


    Hii leo jaridani tunaangazia juhudi za kutokomeza sarati, mashambilizi dhidi ya misafara ya chakula katika kaunti ya Baliet, jimbo la Upper Nile, nchini Sudan Kusini na tunamulika miaka kumi na nne baada ya wakimbizi wa kwanza wa Syria kuvuka mpaka kuingia Jordan.Mabadiliko ya mfumo wa maisha na mazingira yanaweza kuzuia ugonjwa wa saratani kwa wagonjwa wanne katika kila wagonjwa kumi, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, (WHO) na shirika lake tangu la Utafiti kuhusu saratani, IARC.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) leo Februari 4, 2026 limetangaza kusitisha shughuli zake zote katika kaunti ya Baliet, jimbo la Upper Nile, nchini Sudan Kusini kufuatia mfululizo wa mashambulizi dhidi ya msafara wake wa majini mwishoni mwa wiki iliyopita. Anold Kayanda na taarifa zaidi.Miaka kumi na nne baada ya wakimbizi wa kwanza wa Syria kuvuka mpaka kuingia Jordan kusaka usalama, kambi ya wakimbizi ya Zaatari bado ni makazi ya maelfu ya watu wanaosubiri suluhu ya kudumu. Wiki hii, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi, Barham Salih, ametembelea kambi hiyo na kukutana na familia ambazo zimeishi ukimbizini kwa zaidi ya muongo mmoja wengi wao wakiwa bado na matumaini ya kurejea nyumbani, lakini tu pale ambapo itakuwa salama.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

    WFP yasitisha msaada nchini Sudan Kusini kufuatia mashambulizi dhidi ya misafara ya chakula

    Play Episode Listen Later Feb 4, 2026 2:25


    Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) leo Februari 4, 2026 limetangaza kusitisha shughuli zake zote katika kaunti ya Baliet, jimbo la Upper Nile, nchini Sudan Kusini kufuatia mfululizo wa mashambulizi dhidi ya msafara wake wa majini mwishoni mwa wiki iliyopita. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

    Jifunze Kiswahili: Maana na matumizi ya neno "KUNVI"

    Play Episode Listen Later Feb 3, 2026 0:34


    Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "KUNVI"

    03 JANUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 3, 2026 12:52


    Hii leo jaridani kesho ikiwa ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu ugonjwa wa saratani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kumulika hatua ambazo ni uzinduzi wa Mpango wa Utekelezaji wa Kitaifa wa kutokomeza saratani ifikapo mwaka 2030.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa  Duniani, WHO, leo limetoa ombi la dola bilioni moja ili kukabiliana na majanga ya afya mwaka 2026 katika dharura 36 zilizo mbaya zaidi duniani. Ombi hilo linalenga kusaidia huduma za afya zinazookoa maisha katika nchi zilizoathiriwa na migogoro na majanga, zikiwemo Gaza, Sudan, Haiti na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.Mashariki ya Kati, wakati muda ukiendelea kuyoyoma kwa maelfu ya wagonjwa mahututi huko Gaza, kufunguliwa tena kwa kivuko cha Rafah kunaleta mwanga wa matumaini. Kivuko hicho kilifunguliwa Jumatatu baada ya kufungwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, chini ya mpango wa amani unaoungwa mkono na Marekani, na kuruhusu uhamisho wa kwanza wa wagonjwa tangu mwaka 2025.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF leo liimesema linaongeza juhudi zake zamsaada wa msimu wa baridi nchini Ukraine huku watoto na familia wakikabiliwa na kukatika kwa umeme, kukosa vipasha joto na maji kufuatia mashambulizi yanayoendelea dhidi ya miundombinu ya nishati na baridi kali. Tangu Novemba, shirika hilo limesambaza jenereta 106 kote nchini kusaidia huduma za maji na mifumo ya kupasha joto, huku takribani jenereta 150 zaidi zikitarajiwa kuwasili katika wiki zijazo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "KUNVI"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

    02 FEBRUARI 2026

    Play Episode Listen Later Feb 2, 2026 10:00


    Chukua hatua za kupunguza hatari ya kupata ugonjwa wa saratani.Sudan Kusini iko nijia panda na wananchi wanalitambua hilo: UNMISS.UNCDF: Uwekezaji bunifu wasaidia wakulima Dodoma, Tanzania

    tanzania unmiss sudan kusini
    Hali ya njaa inatishia maisha ya watoto nchini Sudan

    Play Episode Listen Later Jan 30, 2026 2:15


    Sudan inakabiliana na viwango vya hatari vya njaa, ambapo mamilioni ya watoto kama Noon wako katika hatari kubwa. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) liko shambani, likitoa msaada muhimu wa lishe, maji safi, na ulinzi. Hata hivyo, mahitaji ni makubwa, na msaada zaidi unahitajika haraka ili kuokoa maisha ya watoto hawa. Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi

    Claim Habari za UN

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel