Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya Kimataifa ya Majiji, vifo na majeruhi vilivyotokea katika maandamano yanayohusiana na uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Tanzania na uwezeshaji wa wanawake nchini huko huko Tanzania.Dunia leo ikiadhimisha Siku ya Kimataifa ya Majiji, majiji ya kisasa pamoja na kukumbatia teknolojia yametakiwa kuhakikisha yanazingatia zaidi watu ili wengine wasiachwe nyuma au kutengwa na maendeleo hayo.Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu imeeleza wasiwasi mkubwa kufuatia vifo na majeruhi vilivyotokea katika maandamano yanayohusiana na uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Tanzania tarehe 29 mwezi huu wa Oktoba.Mpango wa “Chaguo Langu, Haki Yangu” nchini Tanzania ni jitihada thabiti zinazolenga kuwawezesha wanawake na wasichana kuishi maisha huru dhidi ya ukatili na vitendo hatarishi. Kwa ufadhili wa Serikali ya Finland, Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la IPS, linafanya mabadiliko halisi katika jamii.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu imeeleza wasiwasi mkubwa kufuatia vifo na majeruhi vilivyotokea katika maandamano yanayohusiana na uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Tanzania tarehe 29 mwezi huu wa Oktoba. Selina Jerobon na maelezo zaidi.

Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "SUMIA."

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Bi. Lucy Githinji, mkazi wa jimbo la New Jersey nchini Marekani amezungumza na idhaa hii baada ya matembezi ya hiari kwa ajili ya kuhamasisha jamii kuhusu saratani ya titi, akisema hakika dawa zinafanya kazi.Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Kibinadamu nchini Sudan, Denise Brown amesema ni kweli wamepokea ripoti za mauaji ya baadhi ya wahudumu wa kujitolea huko El Fasher jimboni Darfur wakati huu ambapo mji huo umetwaliwa na wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka, (RSF).Kimbunga Melissa kimepungua nguvu baada ya kutua nchini Jamaica kama kimbunga cha kiwango cha 5, na kuvunja rekodi ya kimbunga chenye nguvu zaidi, kabla ya kuelekea kaskazini mashariki kupita Cuba hadi Bahamas, na kusababisha mafuriko makubwa, uharibifu na kukatika kwa umeme katika maeneo mbalimbali ya Karibea na Amerika ya Kati.Nchini Cameroon, kufuatia mauaji ya raia wakati wa maandamano ya kupinga kutangazwa kwa Paul Biya kuwa mshindi wa kiti cha Urais kwenye uchaguzi uliofanyika Oktoba 12, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu imeeleza wasiwasi wake juu ya ripoti za vifo hivyo.Na katika Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "SUMIA."Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Ghasia zinazoendelea kwa kasi zinawakwamisha zaidi watoto katikati ya mashambulizi ya mabomu yasiyokoma, mapigano makali, na uhaba mkubwa wa chakula, maji salama na dawa kwa zaidi ya siku 500 sasa.“Hakuna mtoto aliye salama,” anasema Catherine Russell, Mkurugenzi Mtendaji wa Shrika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF kupitia taarifa iliyotolewa na makao makuu ya shirika hilo jijini New York, Marekani leo.Taarifa hiyo pia inamnukuu Catherine Russell akisema, “ingawa athari kamili bado haijulikani kutokana na kukatika kwa mawasiliano kote nchini Sudan, inakadiriwa kuwa watoto wapatao 130,000 huko Al Fasher wako katika hatari kubwa ya kukiukwa haki zao, huku kukiripotiwa visa vya utekaji nyara, mauaji na ukataji viungo vya mwili, pamoja na ukatili wa kingono.”Pia kuna taarifa za wafanyakazi wa mashirika ya kibinadamu kukamatwa au kuuawa.UNICEF inatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano, kuhakikisha upatikanaji salama na usiokatizwa wa misaada ya kibinadamu, ulinzi wa raia hasa watoto, na kupatiwa uhakika wa njia salama kwa familia zinazotafuta hifadhi, kwa mujibu wa sheria za kimataifa za kibinadamu. Wale wanaohusika na ukiukaji lazima wawajibishwe.Wakati huohuo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limethibitisha kwamba Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan imewataarifu kuwa viongozi wawili wa juu wa WFP nchini wametangazwa kuwa watu wasiotakiwa nchini Sudan na hivyo wameamriwa kuondoka nchini humo ndani ya saa 72, bila maelezo yoyote.WFP inaeleza kwamba uamuzi huu wa kuwafukuza Mkurugenzi wa WFP nchini Sudan na Mratibu wa Dharura wa WFP nchini humo unakuja katika kipindi muhimu kwani mahitaji ya kibinadamu nchini Sudan hayajawahi kuwa makubwa zaidi kama kipindi hiki, huku zaidi ya watu milioni 24 wakikabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula na jamii zikikumbwa na baa la njaa.Wakati ambapo WFP na washirika wake wanapaswa kupanua wigo wa msaada, uamuzi huu unalazimisha shirika kubadilisha uongozi bila mpango, jambo linalohatarisha shughuli zinazowaunga mkono mamilioni ya Wasudani walio hatarini kukumbwa na njaa kali, utapiamlo, na hata kifo kutokana na njaa.WFP na maafisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa wanaendelea kuzungumza na mamlaka za Sudan kupinga hatua hii na kutaka ufafanuzi wa uamuzi huo.Tags: Sudan, El Fasher, WFP, UNICEF

Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO, limeongoza uhamishwaji wa wagonjwa kutoka Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuanza kwa awamu mpya ya kusitishwa kwa mapigano kwenye ukanda huo.Katika muda wa siku mbili, wagonjwa 41 waliokuwa katika hali mbaya pamoja na familia zao 145 wamehamishwa kutoka eneo la mgogoro, kuelekea Afrika Kusini, Uswisi na kwingineko, huku maelfu zaidi wakiendelea kusubiri matibabu ya dharura.Katika hospital iliyojengwa kwa mahema katika eneo la AL-MAWASI, RAFAH kwenye Ukanda wa Gaza wagonjwa wakihudumiwa kila kona watoto kwa wakubwa Miongoni mwao ni Ibrahim Abu Ashiba, mkurugenzi wa filamu ambaye maisha yake yamebadilika ghafla. Anakumbuka wakati alipojeruhiwa. Anasema, "Nilipigwa risasi mara kadhaa, mara moja kwenye kifua, mara moja kwenye bega, mara mbili mkononi. Risasi hizo mbili zilikata mishipa ya neva ya mkono wangu. Sasa siwezi kushika kamera wala kunyoosha mkono wangu kawaida. Ghafla, maisha yangu yote yalisimama."Safari ya kupona kwa Ibrahim inaanzia Afrika Kusini, ambapo amekubaliwa kwenda kupokea matibabu maalum ambapo anasema "Maisha yangu yote yalikuwa yamesimama baada ya kujeruhiwa hadi waliponipigia simu na kunijulishakwamba nitasafiri kwenda Afrika Kusini kwa matibabu. Ilionekana kama nimezaliwa upya."Mgonjwa mwingine katika hospitali hii ni, Maria Al-Shaer, alijeruhiwa vibaya katika mashambulizi yaliyokuwa yakiendelea Gaza, huku akipoteza ndugu zake. Mama yake, Raghda Ahmed Al Shaer, anaelezea mateso hayo. "Maria amepoteza baba yake na ndugu zake wote. Alijeruhiwa na kuvunjika mguu, mifupa na kupoteza nyama. Anahitaji upasuaji wa kuwekewa viungo bandia. Maisha yake yamegeuka, hawezi kutembea, na hali yake ya kisaikolojia imeathirika sana."Uhamishwaji huu umeratibiwa na Shirikisho la Chama cha Msalaba Mwekundu Palestina, kwa msaada wa WHO. Dkt. Luca Pigozzi, Mratibu wa Timu ya Dharura ya WHO, anafafanua umuhimu wake."Huu ni uhamishaji wa kwanza wa matibabu tangu kusitishwa kwa mapigano Oktoba 10. Tumejizatiti kuongeza uwezo wetu kusaidia na kuratibu uhamishaji kwa ajili ya matibabu, kwa ushirikiano wa karibu na Shirikisho la chama cha Msalaba Mwekundu la Palestina."Raghda anaeleza matumaini kwa ajili ya binti yake wanapohama kwenda Uswisi. "Wametupigia kutuarifu kwamba Maria amekubaliwa kusafiri kwenda Uswisi kwa matibabu. Tumefurahi sana kwamba atatembea tena, na hali yake ya kisaikolojia itaboreka. Atarudi kuwa Maria wa kawaida kama tuliyemjua."WHO inasisitiza kuwa wagonjwa takriban 15,000 bado wanangojea idhini ya kupata matibabu nje ya Gaza na inatoa wito kwa nchi zote kufungua milango yote za dharura kwa ajili ya uokoaji wa wagonjwa.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameonesha wasiwasi mkubwa wakati huu Kimbunga Melissa kikiwa miongoni mwa vimbunga vyenye nguvu zaidi kuwahi kurekodiwa katika Bahari ya Atlantiki kinaendelea kusababisha uharibifu mkubwa katika eneo la Karibea.Kupitia taarifa yake iliyotolewa leo mjini New York Marekani na msemaji wake, Katibu Mkuu amesema kimbunga hicho kimeacha madhara makubwa nchini Jamaica, Cuba na Bahamas huku mafuriko makubwa yakiripotiwa pia nchini Haiti na Jamhuri ya Dominika.Taarifa hiyo imemnukuu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwamba “ana wasiwasi mkubwa” na anashikamana na serikali pamoja na wananchi walioathiriwa vibaya na Kimbunga Melissa.”Katibu Mkuu pia “Amewapa pole familia zote za waliopoteza wapendwa wao katika kimbunga hicho na anawatakia majeruhi wote ahueni ya haraka.”Umoja wa Mataifa umeanza kutoa msaada wa dharura, huku timu zake zikiwa tayari mashinani kusaidia kutathmini madhara na kusaidia juhudi za kitaifa. Pia, umetoa dola milioni nne kwa Haiti na vile vile dola milione nne kwa Cuba kutoka Mfuko wake wa Dharura (CERF) ili kusaidia jamii kujiandaa na kupunguza madhara ya kimbunga hicho.Taarifa hiyo imesema Umoja wa Mataifa uko tayari “kutuma wahudumu wa ziada kwa muda mfupi na kuzindua maombi ya misaada ya dharura kukabiliana na mahitaji ya kibinadamu yatakayosababishwa na kimbunga hicho.”Kimbunga Melissa ni miongoni mwa vimbunga vyenye nguvu zaidi kuwahi kuikumba Karibea, na kinatishia maisha ya mamilioni ya watu kutokana na mafuriko, uharibifu na watu kufurushwa katika makazi yao.

Leo jaridani tunamulika kimbunga Melissa huko Karibea, uhamishaji wagonjwa kutoka Gaza kwenda nchi za nje kupata huduma za kigeni na hali tete kwa watoto nchini Sudan. Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi.Katibu Mkuu wa Umoja wa MataifaAntonio Guterres ameonesha wasiwasi mkubwa wakati Kimbunga Melissa kikiwa miongoni mwa vimbunga vyenye nguvu zaidi kuwahi kurekodiwa katika Bahari ya Atlantiki kinaendelea kusababisha uharibifu mkubwa katika eneo la Karibea.Kupitia taarifa yake iliyotolewa leo mjini New York Marekani na msemaji wake Katibu Mkuu amesema kimbunga hicho kimeacha athari kubwa nchini Jamaica, Cuba na Bahamas huku mafuriko makubwa yakiripotiwa pia nchini Haiti na Jamhuri ya Dominika.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani, WHO, limeongoza uhamishwaji wa kwanza wagonjwa kutoka Gaza tangu awamu mpya ya kusitishwa kwa mapigano. Katika muda wa siku mbili, wagonjwa 41 waliokuwa katika hali mbaya pamoja na familia zao 145 wamehamishwa kutoka eneo la mgogoro, huku maelfu zaidi wakiendelea kusubiri matibabu ya dharura. Flora Nducha na taarifa zaidi.Nchini Sudan hususani katika eneo la El Faher kusinimagharibi mwa nchi, hali ya kibinadamu inazidi kuwa mbaya kila siku, huku ghasia, njaa, na vizuizi vya utoaji misaada vikiendelea kuathiri mamilioni ya watu wakiwemo watoto waliokwama katika maeneo ya vita. Anold Kayanda na taarifa zaidi.

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia mradi wa TANZIE huko Chuo Kikuu Mzumbe, mkoani Morogoro, mashariki mwa Tanzania, unaolenga kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu SDGs. Pia tunakuletea habari kwa ufupi na uchambuzi wa neno la wiki.Mamilioni ya watu nchini Jamaica na katika ukanda wote wa Karibea wanajiandaa kukabiliana na madhara makubwa ya kimbunga Melissa huku Umoja wa Mataifa na washirika wake wakionya kuhusu tishio kubwa na la haraka la kibinadamu.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameelezea wasiwasi wake mkubwa kufuatia kuongezeka kwa mapigano ya kijeshi mjini El Fasher, jimbo la Darfur Kaskazini, nchini Sudan. Kupitia taarifa iliyotolewa na Msemaji wake usiku wa tarehe27 Oktoba 2025 kwa saa za New York marekani, Guterres amesema kwa zaidi ya miezi kumi na minane, wakazi wa El Fasher na maeneo ya jirani wamekuwa wakikabiliwa na mateso makubwa huku makundi ya Wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF) yakizingira mji huo.Na hii leo, Ofisi ya Umoja wa Matiafa ya Haki za Binadamu na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Usaidizi nchini Afghanistan wamechapisha waraka wa taarifa kuhusu madhara makubwa ya kina za haki za binadamu yaliyotokana na kusitishwa kwa huduma za mawasiliano nchini Afghanistan tarehe 29 Septemba hadi tarehe mosi mwezi huu, — hatua ambayo imezidisha changamoto nyingi ambazo tayari zinawakabili wananchi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya neno "KIMBIMBI"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito kwa dunia na mataifa wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kusini-Mashariki mwa Asia, ASEAN kuchukua hatua za haraka kumaliza machafuko ya muda mrefu nchini Myanmar, akisisitiza kuwa mgogoro huo si tishio kwa watu wa Myanmar pekee bali pia kwa amani na usalama wa kanda nzima ya Asia ya Kusini Mashariki. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

Katika kaunti ya Mombasa nchini Kenya, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wa Mastercard Foundation na Serikali ya Kaunti ya Mombasa, imechukua hatua za kukabiliana na mlipuko wa MPOX kwa kutoa huduma muhimu za afya na WASH kwa wagonjwa na waliopona, ikiwa ni pamoja na vifaa vya kujikinga (PPEs), vituo vya kusafisha mikono na ujumbe wa mabadiliko ya tabia za kijamii. Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi

Hii leo jaridani tunaangazia machafuko ya muda mrefu nchini Myanmar, hali ya kibinadamu nchini Sudan kufuatia ripoti za vifo vya raia na wimbi la wakimbizi wa ndani, na masuala ya afya nchini Kenya.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa wito kwa dunia na mataifa wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kusini-Mashariki mwa Asia, ASEAN kuchukua hatua za haraka kumaliza machafuko ya muda mrefu nchini Myanmar, akisisitiza kuwa mgogoro huo si tishio kwa watu wa Myanmar pekee bali pia kwa amani na usalama wa kanda nzima ya Asia ya Kusini Mashariki.Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) imeelezea wasiwasi mkubwa kufuatia ripoti za vifo vya raia na wimbi la wakimbizi wa ndani, kufuatia kuendelea kwa mapigano makali katika mji wa El Fasher, huko Darfur Kaskazini nchini Sudan. Tupate tarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.Katika kaunti ya Mombasa nchini Kenya, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wa Mastercard Foundation na Serikali ya Kaunti ya Mombasa, imechukua hatua za kukabiliana na mlipuko wa MPOX kwa kutoa huduma muhimu za afya na WASH kwa wagonjwa na waliopona, ikiwa ni pamoja na vifaa vya kujikinga (PPEs), vituo vya kusafisha mikono na ujumbe wa mabadiliko ya tabia za kijamii.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) imeelezea wasiwasi mkubwa kufuatia ripoti za vifo vya raia na wimbi la wakimbizi wa ndani, kufuatia kuendelea kwa mapigano makali katika mji wa El Fasher, huko Darfur Kaskazini nchini Sudan. Tupate tarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi

Msikilizaji, bila shaka umeyasikia mengi kuhusu Umoja wa Mataifa, lakini Umoja wa Mataifa ni nini hasa? Japo kwa ufupi, Anold Kayanda anakufahamisha akianza na historia.

Leo ni Siku ya Umoja wa Mataifa, ikitukumbusha kuanzishwa kwake tarehe 24 mwezi Oktoba mwaka 1945. Maudhui ya mwaka huu ni "Miaka 80 ya Umoja wa Mataifa: Kujenga Mustakabali Wetu kwa Pamoja - Ishara ya Matumaini kwa ushirikiano wa Kimataifa." Katika kumulika hili, Sabrina Saidi wa idhaa hii amezungumza na mwakilishi wa vijana pamoja na mmoja wa watumishi wa Umoja wa Mataifa kuhusu maadhimisho ya siku hii, huko jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania.

Hii leo jaridani tunaangazia siku ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni miaka 80 tangu kuanzishwa kwake 1945.Leo ni siku ya Umoja wa Mataifa ni miaka 80 tangu kuanzishwa kwake 1945, lakini pia ni kumbukizi ya miaka 80 tangu kuanzishwa kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambalo lilikuwa ni tukio la kihistoria na la kukumbukwa. Akiwahutubia wajumbe wa Baraza hilo kwa njia ya mtandao katika kikao cha kumbukizi hii, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa mageuzi ya dharura na mwamko mpya wa uwajibikaji, akiwakumbusha jukumu lao kuu la kulinda amani ya dunia.Tukiendelea na Siku ya Umoja wa Mataifa, ikitukumbusha kuanzishwa kwake tarehe 24 mwezi Oktoba mwaka 1945. Maudhui ya mwaka huu ni "Miaka 80 ya Umoja wa Mataifa: Kujenga Mustakabali Wetu kwa Pamoja - Ishara ya Matumaini kwa ushirikiano wa Kimataifa." Katika kumulika hili, Sabrina Saidi wa idhaa hii amezungumza na mwakilishi wa vijana pamoja na mmoja wa watumishi wa Umoja wa Mataifa kuhusu maadhimisho ya siku hii, huko jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania.Msikilizaji, bila shaka umeyasikia mengi kuhusu Umoja wa Mataifa, lakini Umoja wa Mataifa ni nini hasa? Japo kwa ufupi, Anold Kayanda anakufahamisha akianza na historia.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Leo ni siku ya Umoja wa Mataifa ni miaka 80 tangu kuanzishwa kwake 1945, lakini pia ni kumbukizi ya miaka 80 tangu kuanzishwa kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambalo lilikuwa ni tukio la kihistoria na la kukumbukwa. Akiwahutubia wajumbe wa Baraza hilo kwa njia ya mtandao katika kikao cha kumbukizi hii, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa mageuzi ya dharura na mwamko mpya wa uwajibikaji, akiwakumbusha jukumu lao kuu la kulinda amani ya dunia. Flora Nducha amefuatilia kikao hicho cha maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Mataifa na kutuandalia tarifa hii.

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia siku ya Umoja wa Mataifa na tutasikia kutoka mashinani wananchi na asasi za kiraia zina yapi ya kusema kuhusu shirika hili kubwa na la kipekee linalounganisha nchi wanachama 193 duniani.Mashirika manne ya Umoja wa Mataifa lile la uhamiaji IOM, la kuhudumia wakimbizi UNHCR, la Kuhudumia watoto UNICEF na la mpango wa chakula duniani WFP leo yametoa wito wa dharura kwa dunia kuchukua hatua mara moja kukabiliana na janga la kibinadamu linaloongezeka nchini Sudan. Zaidi ya watu milioni 30 wanahitaji msaada, nchini humo wakiwemo watoto milioni 15 na wakimbizi karibu milioni moja.Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) jana Oktoba 22 ilisema Israeli lazima itimize majukumu yake kama “anayekalia kimabavu” kwa kuhakikisha kuwa msaada unaweza kupita bila vizuizi na kwa kuheshimu haki za Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kibinadamu yanayofanya kazi katika Ardhi ya Palestina Iliyokaliwa kwa Mabavu. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameelezea maoni hayo ya ICJ kuwa “muhimu sana,” akiongeza kuwa yametolewa wakati ambapo Umoja wa Mataifa unafanya kila juhudi kuongeza kasi ya misaada kuingia Gaza baada ya kusitishwa kwa mapigano.Nchini Kenya, wahudumu wa afya waliokuwa wakisubiri hadi siku 15 kupata malipo sasa wanapokea pesa ndani ya saa 72 pekee, shukrani kwa mfumo mpya wa malipo ya kidijitali uliotolewa na Shirika la Sfya la Umoja wa Mataifa WHO na Wizara ya Afya ya nchi hiyo. Mfumo huu unapeleka fedha moja kwa moja kwenye pochi za simu za wafanyakazi, ukipunguza ucheleweshaji, gharama na kuongeza motisha. Wafanyakazi zaidi ya 120,000 sasa wanafaidika, kuboresha ufanisi wa kampeni za chanjo na juhudi za kudhibiti polio.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema mifumo ya tahadhari za mapema dhidi ya majanga si chaguo tena, bali ni lazima kwa kila mtu duniani, akisisitiza kuwa hatua hizo zinaokoa maisha na mali. Flora Nducha na taarifa zaidi

Kuanzia furaha ya uhuru hadi maumivu ya kurejea kwa mzozo, safari ya amani ya kudumu Sudan Kusini imekuwa ndefu na bado inaendelea. Licha ya changamoto hizo, matumaini bado ni makubwa miongoni mwa jamii nchini kote kwamba uchaguzi wa amani, huru na wa haki utaleta usalama uliotafutwa kwa muda mrefu pamoja na fursa za maendeleo na ukuaji wa uchumi. Leah Mushi anatuletea taarifa ikiangazia namna Sudan Kusini inavyojiandaa na uchaguzi wake mkuu mwakani 2026.

Hii leo jaridani tunaangazia mifumo ya tahadhari za mapema dhidi ya majanga, elimu kuhusu uraia nchini Sudan kusini, na kilimo endelevu na vijana nchini Rwanda.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema mifumo ya tahadhari za mapema dhidi ya majanga si chaguo tena, bali ni lazima kwa kila mtu duniani, akisisitiza kuwa hatua hizo zinaokoa maisha na mali.Kuanzia furaha ya uhuru hadi maumivu ya kurejea kwa mzozo, safari ya amani ya kudumu Sudan Kusini imekuwa ndefu na bado inaendelea. Licha ya changamoto hizo, matumaini bado ni makubwa miongoni mwa jamii nchini kote kwamba uchaguzi wa amani, huru na wa haki utaleta usalama uliotafutwa kwa muda mrefu pamoja na fursa za maendeleo na ukuaji wa uchumi.Wanawake ni nguzo muhimu katika maendeleo ya kilimo na jamii za vijijini. Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo( IFAD) inahakikisha zaidi ya asilimia 50 ya washiriki wa miradi yake ni wanawake, kwa lengo la kuimarisha usawa wa kijinsia na kupunguza umaskini. Kupitia mafunzo, huduma za kifedha, na upatikanaji wa masoko, wanawake wanawezeshwa kiuchumi na kijamii. Tafiti zinaonesha kuwa kufuta pengo la kijinsia katika kilimo kunaweza kuongeza pato la dunia kwa asilimia 1. Nchini Rwanda, miradi kama R-YES imewezesha wanawake vijana kuanzisha biashara za kilimo na kutoa ajira.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Wanawake ni nguzo muhimu katika maendeleo ya kilimo na jamii za vijijini. Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo( IFAD) inahakikisha zaidi ya asilimia 50 ya washiriki wa miradi yake ni wanawake, kwa lengo la kuimarisha usawa wa kijinsia na kupunguza umaskini. Kupitia mafunzo, huduma za kifedha, na upatikanaji wa masoko, wanawake wanawezeshwa kiuchumi na kijamii. Tafiti zinaonesha kuwa kufuta pengo la kijinsia katika kilimo kunaweza kuongeza pato la dunia kwa asilimia 1. Nchini Rwanda, miradi kama R-YES imewezesha wanawake vijana kuanzisha biashara za kilimo na kutoa ajira. Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi.

Leo mchambuzi ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "NG'OMBE WA MNYONGE HAZAI"

Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Leah Mushi anakuletea-Gaza Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula Duniani WFP lasema usitishaji wa mapigano umeleta afueni kwa wakaazi kwani sasa misaada inaendelea kuwafikia wenye uhitaji-Naibu Mratibu wa Misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Joyce Msuya amekuwa ziarani Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR na kujionea hali halisi ya wakimbizi, wakimbizi wa ndani na msaada wa kibinadamu-Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa leo limesema katika tathimini yake kuwa ukataji wa misitu umepungua duniani kote ingawa bado kuna shinikizo na hatua zaidi zahitajika-Katika mada kwa kina tunakupeleka nchini Tanzania ambako Vyuo Vikuu vinachukua hatua ya kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs hususan lile namba 17 la ubia kupitia umataifishaji. -Na kwenye jifunze Kiswahili unapata ufafanuzi wa methali " “NG'OMBE WA MNYONGE HAZAI"

Sudan Kusini yaahidi kutotumikisha tena watoto jeshiniHuko nchini Sudan Kusini barani Afrika, matumaini mapya yamechipua baada ya watoto waliokuwa wametumikishwa kwenye jeshi la nchi hiyo, SSPDF kuachiliwa rasmi katika hafla iliyoungwa mkono na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, UNMISS. Tukio hilo limeelezwa kuwa ishara muhimu ya kumaliza utumikishaji wa watoto katika jeshi na kuwapa nafasi ya kujenga maisha mapya. Sabrina Saidi ana taarifa zaidi...(TAARIFA YA SABRINA SAIDI)Nats..Video ya UNMISS inaanzia kwenye tukio la viongozi wakikabidhi vifaa vya shule kwa watoto walioachiliwa kutoka jeshi la serikali.Nats..Ni siku ya matumaini hapa mjini Yambio, jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini — siku ambayo watoto waliopoteza utoto wao vitani, sasa wanaupokea tena, wakiwa na ndoto mpya za elimu na maisha bora zaidi.Hafla ya makabidhiano iliyofanyika kwa ushirikiano kati ya Jeshi la serikali na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo (UNMISS), imeashiria azma ya serikali ya kuondokana na utumikishaji wa watoto jeshini.Brigedia Akech Maker, Kamanda wa Kikosi cha 16 cha SSPDF, anasema ….Clip- Sauti ya Brigedia Akech Maker“Hatutaruhusu watoto kujiunga na jeshi. Watoto wanaoonesha nia, tutawaelekeza kwenye elimu, na taasisi ziwaunge mkono ili wasirudi kambini.”Afisa wa Ulinzi wa Watoto UNMISS,, Rita Bampo, akatoa ahadi akisema watoto lazima warejee kwenye jamii, na kwamba…Clip- Sauti ya Rita Bampo“Tutahakikisha mchakato huu unafanikiwa na hakuna atakayewarudisha kwenye makundi ya kijeshi. Viongozi wote wahakikishe watoto wanapelekwa kwa mashirika yanayohusika."UNICEF pia imetoa huduma za kisaikolojia na vifaa vya kujifunzia kwa watoto hao, kuwasaidia kuanza upya safari yao ya elimu na matumaini.

Matunda ya warsha zilizokuwa zinaendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, (UNDP) nchini Tanzania katika mikoa ya Tanga na Mtwara iliyoko kando mwa baharí ya Hindi kuhusu uchumi rejeshi yameanza kuonekana na mipango zaidi inafanyika ili matunda hayo yasambae mikoa mingine.Afisa wa UNDP Peter Nyanda ameiambia Idhaa ya Umoja wa Mataifa hivi karibuni kuwa warsha hizo mbili zilizofanyika mwaka huu na kujumuisha vikundi vya kijamii na mamlaka za serikali za mitaa katika mikoa husika zililenga pamoja na mambo mengine kuhakikisha taka hasa taka ngumu hazitupwi bali zinarejeshwa katika mzunguko wa thamani kwa njia za ubunifu na endelevu.Nyanda anataja baadhi ya matokeo;(Sauti ya Peter Nyanda 1)“Ni kuwa na mpango wa utekelezaji katika kila mkoa ambao wadau hawa wanajiwekea ili kubainisha hatua za haraka, fursa na namna gani wanaweza kupata uwekezaji. Lakini pia tumeweza kuwatambua wadau katika uchumi rejeshi na pia tumeangalia wabunifu walioko kwenye maeneo ya viwanda. Kwa mfano tu kwa Mtwara tumefahamishwa hapa kwamba kiwanda cha Dangote tayari kinatumia taka katika kuwasha mitambo yake hasa . Lakini pia tunatarajia majadiliano pamoja na wafadhili na wadau wengine wa kimaendeleo hasa sekta binafsi katika kupata rasilimali za kufanya uwekezaji.”Akazungumzia pia matarajio ya baadaye ya UNDP kupitia warsha hizo akisema,(Sauti ya Peter Nyanda 2)“Ni kuanzisha vituo vya ubunifu na ubora katika ujenzi wa miundombinu, sio UNDP peke yake bali kwa ujumla, kama matarajio ya wadau. Lakini pia kuna wabunifu kama kuanzisha vituo vya kutenganisha taka. Lakini kufanikisha ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi na taasisi za kifedha, ambao ni muundo wa utatu tunaojaribu kufanikisha kwa serikali, wadau na UNDP ikiwemo kuweza kuhakikisha mitaji inapatikana ili kuweza kusaidia kukuza biashara hizo. Kingine ni kupanua juhudi katika mikoa mingine sio tu ile ambayo mikoa mingine ya pwani ya sasa tunajua taka hizi za plastiki zinaathiri zaidi maeneo ya baharini.”Na hatimaye,(Sauti ya Peter Nyanda 3)“Ujumbe wangu wa mwisho ni kwamba uchumi rejeshi ni fursa ya kiuchumi, kiteknolojia na kimazingira. Kwa kuwekeza katika kurejesha thamani ya taka, tunalinda mazingira na wakati huo huo tunafungua ajira za ubunifu mpya kwa vijana na jamii yetu.”

Shirika la Umoja wa Mataifa ka Utabiri wa Hali ya Hewa Duniani WMO linaongeza kasi ya jitihada za kulinda maisha ya watu dhidi ya madhara ya mabadiliko ya tabianchi. Mkutano wake Maalum uliofunguliwa leo mjini Geneva Uswisi, unalenga kuharakisha mpango wa kimataifa wa Tahadhari za Mapema kwa Wote, sambamba na maadhimisho ya miaka 75 ya WMO. Flora Nducha amefuatilia na anafafanua zaidi (TAAFIFA YA FLORA NDUCHA)Asante Leah, kwa mujibu wa WMO idadi ya nchi zenye mifumo ya tahadhari za mapema kwa ajili ya majanga ya tabianchi imeongezeka maradufu katika kipindi cha miaka kumi iliyopita lakini bado mamilioni ya watu hawana ulinzi dhidi yah atua hiyo muhimu.Ndiyo maana shirika hilo limewakutanisha mawaziri na wataalamu kutoka nchi wanachama 193 kuharakisha mpango wa Tahadhari za Mapema kwa Wote, uliozinduliwa mwaka 2022 na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres unatekelezwa kwa vitendo.Katika mkutano huo Celeste Saulo Katibu Mkuu wa WMO amesema “Miaka 75 iliyopita, Shirika la WMO lilianzishwa kutokana na ukweli kwamba hali ya hewa, maji na tabianchi havina mipaka ya kitaifa. Ushirikiano wa kimataifa katika uchunguzi na utabiri ni wa lazima, kwa sababu hakuna nchi inayoweza kufanya hivyo peke yake.”Ripoti mpya ya WMO, iliyopewa jina Tahadhari za Mapema kwa Wote Mtazamo wa Dunia, inaonesha kuwa licha ya maendeleo makubwa katika ubadilishanaji wa takwimu na utabiri wa kidijitali, bado kuna mapengo makubwa, hasa katika nchi maskini na visiwa vidogo vinavyoendelea.Celeste amesisitiza kuwa“Tahadhari za Mapema kwa Wote sasa siyo mpango tena, bali ni nembo ya mshikamano wa dunia. Pamoja, tunaokoa maisha, tunaunda sera, na kuimarisha mnepo.”Takwimu za shirika hilo zinaonesha uzito wa changamoto. Katika miaka 50 iliyopita, WMO inasema majanga yanayohusiana na hali ya hewa na maji yamesababisha vifo vya zaidi ya watu milioni mbili huku asilimia 90 kati yao ni katika nchi zinazoendelea.Na ingawa mataifa 108 sasa yana mifumo ya tahadhari za majanga mchanganyiko, shirika hilo linasema viwango vya vifo bado ni mara sita zaidi katika maeneo yasiyo na mifumo hiyo.WMO inasema teknolojia mpya ikiwemo akili mnemba na matumizi ya takwimu za setilaiti kwa wakati halisi zinabadilisha uwezo wa utabiri, lakini pengo la kidijitali bado linawaacha wengi wakiwa hatarini.“Mafanikio ya Tahadhari za Mapema kwa Wote hayapimwi kwa ripoti au maazimio, anasema Celesto bali kwa maisha yanayookolewa na riziki zinazolindwa. Tunapoelekea mwaka 2027, hebu tuongeze juhudi kuhakikisha hakuna mtu anayeachwa bila ulinzi.”Mkutano huo Maalum wa WMO utaendelea wiki nzima mjini Geneva, huku Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akitarajiwa kuhutubia siku ya Jumatano.Shirika la WMO wakati likiadhimisha miaka 75 ya kile linachoita Sayansi kwa Vitendo linataka kuhakikisha sayansi hiyo inawafikia wote, kabla ya majanga kutokea.

Karibu kusikiliza jarida la habari za Umoja wa Mataifa, leo utasikia mengi ikiwemo mkutano wa kujadili kuhusu tahadhari za mapema unaoenda sambamba na miaka 75 tangu kuanzishwa kwa shirika la Umoja wa Mataifa la hali ya hewa WMO. Pia utasikia juhudi za mashirika ya UN kusaidia wananchi huko mashinani na kuboresha maisha yao. UNDP nchini Tanzania na UNMISS huko jimboni Yambui nchini Sudan Kusini. Mtangazaji wako ni Leah Mushi.

Mradi wa kusaidia jamii kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi nchini Zambia mbali na kusaidia wananchi kwenye kilimo pia umewawezesha kiuchumi na kuwaondoa baadhi yao kwenye mstari wa umasikini. Mmoja wa walio utupa mkono umasikini ni Judith Mabeta aliyetoka kuishi nyumba ya udongo mpaka kuwa na nyumba ya kupangisha na sasa ni mama mwenye nyumba. Leah Mushi anatujuza zaidi.

Kupitia msaada wa fedha kutoka Ufaransa, juhudi za kuboresha hali ya lishe kwa watoto nchini Kenya, hasa kwa jamii zilizo katika mazingira hatarishi zinaendelea ambapo juhudi za hivi karibuni ni kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya ambao kwa pamoja wameimarisha huduma hizo kwa manusura wa mafuriko Magharibi mwa taifa hilo la Afrika Mashariki. Huduma hizi ni sehemu muhimu ya kuhakikisha watoto na familia wanapata vyakula vyenye virutubishi kwa ustawi wa maisha yao. Sheilah Jengetich na taarifa zaidi kupitia video ya UNICEF Kenya.

Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya UNDP ya umaskini, mradi wa kusaidia jamii kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi nchini Zambia na juhudi za kuboresha hali ya lishe kwa watoto nchini Kenya.Takribani watu milioni 887 duniani ambao ni maskini wanaishi kwenye maeneo yanayokumbwa moja kwa moja na madhara manne yasababishwayo na mabadiliko ya tabianchi ambayo ni joto kali, mafuriko, ukame na uchafuzi wa hewa, imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP kwa kushirikiana na wadau. Ripoti inaonesha bayana kuwa hali hiyo inazidi kutwamisha watu hao kwenye hali tete zaidi.Mradi wa kusaidia jamii kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi nchini Zambia mbali na kusaidia wananchi kwenye kilimo pia umewawezesha kiuchumi na kuwaondoa baadhi yao kwenye mstari wa umasikini. Mmoja wa walio utupa mkono umasikini ni Judith Mabeta aliyetoka kuishi nyumba ya udongo mpaka kuwa na nyumba ya kupangisha na sasa ni mama mwenye nyumba.Kupitia msaada wa fedha kutoka Ufaransa, juhudi za kuboresha hali ya lishe kwa watoto nchini Kenya, hasa kwa jamii zilizo katika mazingira hatarishi zinaendelea ambapo juhudi za hivi karibuni ni kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya ambao kwa pamoja wameimarisha huduma hizo kwa manusura wa mafuriko Magharibi mwa taifa hilo la Afrika Mashariki. Huduma hizi ni sehemu muhimu ya kuhakikisha watoto na familia wanapata vyakula vyenye virutubishi kwa ustawi wa maisha yao.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Takribani watu milioni 887 duniani ambao ni maskini wanaishi kwenye maeneo yanayokumbwa moja kwa moja na madhara manne yasababishwayo na mabadiliko ya tabianchi ambayo ni joto kali, mafuriko, ukame na uchafuzi wa hewa, imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP kwa kushirikiana na wadau. Ripoti inaonesha bayana kuwa hali hiyo inazidi kutwamisha watu hao kwenye hali tete zaidi. Assumpta Massoi amepitia ripoti hiyo na kuandaa taarifa hii.

Katika kujifunza Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "KIMWA."

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia siku ya chakula duniani ikienda sambamba na maadhimisho ya miaka 80 ya kuanzishwa shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, na utamsikia Mwakilishi wa FAO nchini Tanzania Bi. Nyabenyi Tito Tipo akieleza.Maadhimisho ya siku ya chakula duniani yamefanyika kimataifa leo huko Roma nchini Italia, yakienda sambamba na sikukuu ya miaka 80 tangu kuanzishwa kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na kilimo, FAO. Katika ujumbe wake alioutoa kwa njia ya video Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema, “Miaka themanini iliyopita, katika dunia iliyosambaratishwa kwa vita, nchi zilikutana kukabiliana na njaa. Miongo kadhaa tangu wakati huo, dunia imepiga hatua kubwa. Lakini bado majanga yanyoonesha kuwa hatuwezi kubweteka iwapo tunataka kuendeleza mafanikio tuliyopata. Tuna mbinu, ufahamu, rasilimali za kutokomeza njaa, na kupatia kila mtu chakula kizuri na chenye afya. Tunachohitaji ni umoja.Huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli, raia wamerejea kufuatia makubaliano ya sitisho la mapigano lakini wanahaha kujenga upya makazi yao huku wakiwa wamezingirwa na vifusi. Miongoni mwao Ayman Awadallah, amesema “hakuna maji, hakuna miundombinu ya majitaka, hakuna maisha hapa, hakuna chochote.”Na kufuatia kifo cha aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga, kilichotokea Jumatano Oktoba 15 nchini India, Umoja wa Mataifa kupitia Katibu Mkuu umetuma salamu za rambirambi na kusema hayati Odinga, alikuwa mtu muhimu katika maendeleo ya kidemokrasia nchini Kenya na pia mtetezi thabiti wa mageuzi ya kikatiba na utawala jumuishi.Na katika kujifunza Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "KIMWA"Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Kuanzia Oktoba 15 mwaka 2008 dunia imekuwa ikiadhimisha siku ya Kimataifa ya Wanawake wa Vijijini kama fursa ya kutambua mchango mkubwa wa wanawake hawa katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi, na kimazingira.. Sheilah Jepngetich amefuatilia mchango wa wanawake wa vijijini nchini Kenya na kutuandalia taarifa hii.

Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani, WMO, inasema kiwango cha gesi ya hewa ukaa, yaani carbon dioxide au CO₂, kimeongezeka kwa kiwango cha kuvunja rekodi mwaka 2024, na kufikia viwango vipya vya juu zaidi kuwahi kurekodiwa. Flora Nducha ameisoma ripoti hiyo na anatupa tathimini

Hii leo jaridani tunaangazia kiwango cha gesi ya hewa ukaa, yaani carbon dioxide au CO₂, siku ya Kimataifa ya Wanawake wa Vijijini inayotupeleka nchini Kenya kumulika juhudi za wanawake za kumudu mahitaji ya familia zao, na uvuvi na uhalifu katika Ziwa Victoria.Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani, WMO, inasema kiwango cha gesi ya hewa ukaa, yaani carbon dioxide au CO₂, kimeongezeka kwa kiwango cha kuvunja rekodi mwaka 2024, na kufikia viwango vipya vya juu zaidi kuwahi kurekodiwa.Kuanzia Oktoba 15 mwaka 2008 dunia imekuwa ikiadhimisha siku ya Kimataifa ya Wanawake wa Vijijini kama fursa ya kutambua mchango mkubwa wa wanawake hawa katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi, na kimazingira.Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM kwa kushirikiana na Ofisi ya Marekani ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na Dawa za Kulevya na Utekelezaji wa Sheria (INL), na mamlaka kutoka Kenya, Tanzania na Uganda wanashirikiana kuimarisha uwezo na kukabiliana na uhalifu wa kimataifa unaotekelezwa katika ziwa victoria ambao ukiachwa unaweza kuleta athari kwa zaidi ya watu milioni 40 wanaotegemea ziwa hilo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM kwa kushirikiana na Ofisi ya Marekani ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na Dawa za Kulevya na Utekelezaji wa Sheria (INL), na mamlaka kutoka Kenya, Tanzania na Uganda wanashirikiana kuimarisha uwezo na kukabiliana na uhalifu wa kimataifa unaotekelezwa katika ziwa victori ambao ukiachwa unaweza kuleta athari kwa zaidi ya watu milioni 40 wanaotegemea ziwa hilo. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi

Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "MKWECHE"!

Hii leo jaridani tnakuletea mada kwa kina inayoangazia siku ya Mwalimu Nyerere na tunakupeleka nchini Tanzania ambako kunaendelea juhudi za kuimarisha matumimizi ya lugha ya Kiswahili na utangamano katika Jumuiya ya Afrika Mashairki, manufaa ya kiuchumi na kijami na kuenzi mchango wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Umoja wa Mataifa leo umeonya kwamba Gaza itahitaji karibu dola bilioni 70 kwa ajili ya ujenzi upya baada ya miaka miwili ya mzozo, huku dola bilioni 20 zikitakiwa katika miaka mitatu ijayo. Makadirio haya yanatokana na, tathmini ya pamoja kati ya Umoja wa Mataifa, Muungano wa Ulaya, na Benki ya Dunia. Mwakilishi Maalum wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo UNDP kwa ajili ya programu za msaada kwa Wapalestina Jaco Cilliers,amesema “Viwango vya uharibifu sasa vimefikia karibu asilimia 84, na katika baadhi ya sehemu za Jiji la Gaza, ni hadi asilimia 92.”Umoja wa Mataifa umeongeza hatua zake za dharura huko Gaza kwa kutoa dola milioni 11 kutoka Mfuko wake wa Dharura (CERF) kukidhi mahitaji ya haraka kabla ya kuanza kwa msimu wa baridi. Mgao huu, uliozinduliwa na Mratibu wa Misaada ya Dharura Tom Fletcher, utaunga mkono utoaji wa chakula, maji, huduma za afya na makazi kwa raia walioathiriwa na mzozo wa miaka miwili. Hatua hii inafuatia mgao wa dola milioni 9 wiki iliyopita kwa ajili ya kuhakikisha upatikanaji wa mafuta kwa hospitali na huduma muhimu, na kufanya jumla ya msaada wa hivi karibuni kufikia dola milioni 20.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO limeonya kuhusu ongezeko la magonjwa ya neva duniani, ambayo sasa yanachangia zaidi ya vifo milioni 11 kila mwaka. Ripoti mpya ya WHO iliyotolewa leo mjini Geneva inaonesha kuwa zaidi ya watu bilioni 3 sawa na zaidi ya asilimia 40 ya watu duniani wanaishi na magonjwa yanayoathiri ubongo, ikiwemo kiharusi, ugonjwa wa kusahau, kifafa, na maumivu ya kichwa ya muda mrefu. Kwa mujibu wa ripoti nchi maskini ndizo zinazoathirika zaidi, zikiwa na upungufu mara 80 wa idadi ya wataalamu wa magonjwa ya neva ikilinganishwa na nchi tajiri. WHO inazitaka serikali kutoa kipaumbele kwa afya ya ubongo, kuongeza fedha na kuboresha upatikanaji wa huduma za tiba."Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "MKWECHE!Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, leo amekaribisha kwa furaha kuachiliwa kwa mateka wote waliokuwa hai kutoka Gaza, huku mashirika ya misaada yakiripoti kwamba usambazaji wa misaada ya kuokoa maisha sasa unafanyika na misaada inaingia kwa kiwango kikubwa katika eneo hilo lililoharibiwa vibaya na vita: Flora Nducha amefuatilia na hii hapa taarifa yake

Tarehe 11 mwezi Oktoba kila mwaka dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike, ikiwa ni siku muhimu ya kutambua mchango na uwezo wa mabinti katika jamii. Huko nchini Tanzania, kumefanyika hafla ya maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Plan International Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Ofisi za Umoja wa Mataifa Tanzania, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), na lile linalojishughulisha na Masuala ya Wanawake (UN Women). Sabrina Moshi na taarifa zaidi

Hii leo jaridani tunaangazia sitisho la mapigano Gaza na kurejeshwa kwa mateka wote, matumizi ya fecha za umma nchini Tanzania, na Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike ambayo uliadhimishwa tarehe 11 mwezi huu.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, leo amekaribisha kwa furaha kuachiliwa kwa mateka wote waliokuwa hai kutoka Gaza, huku mashirika ya misaada yakiripoti kwamba usambazaji wa misaada ya kuokoa maisha sasa unafanyika na misaada inaingia kwa kiwango kikubwa katika eneo hilo lililoharibiwa vibaya na vita.Licha ya mabilioni ya fedha kutumika katika sekta za elimu, afya na miundombinu, mataifa mengi bado yanashindwa kufikia maendeleo ya maana. Swali ni je, suluhisho ni kutumia fedha zaidi, au kuzitumia vyema? Benki ya dunia inatoa jibu kwa swali hilo tuungane na Leah Mushi akitujuza wamesema nini.Tarehe 11 mwezi Oktoba kila mwaka dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike, ikiwa ni siku muhimu ya kutambua mchango na uwezo wa mabinti katika jamii. Huko nchini Tanzania, kumefanyika hafla ya maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Plan International Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Ofisi za Umoja wa Mataifa Tanzania, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), na lile linalojishughulisha na Masuala ya Wanawake (UN Women)."Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Licha ya mabilioni ya fedha kutumika katika sekta za elimu, afya na miundombinu, mataifa mengi bado yanashindwa kufikia maendeleo ya maana. Swali ni je, suluhisho ni kutumia fedha zaidi, au kuzitumia vyema? Benki ya dunia inatoa jibu kwa swali hilo tuungane na Leah Mushi akitujuza wamesema nini.

Mnamo mwaka wa 2021, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) liliongeza kwenye orodha ya turathi za dunia za tamaduni zisizoshikika au kugusika, Pooja Durga ambayo ni sherehe kubwa ya kihindu ya ushindi wa mungu wa kike aitwaye Durga dhidi ya jini Mahishasura, ikiwa ni ishara ya ushindi wa mema dhidi ya maovu. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imekaribisha uamuzi wa Kamati ya Tuzo ya Amani ya Nobel kumtangaza Maria Corina Machado kiongozi wa upinzani nchini Venezuela kuwa mshindi wa mwaka huu wa tuzo ya amani ya Nobel, kwa kutambua kazi yake ya kuendeleza matumaini ya demokrasia ya watu wa Venezuela. Flora Nducha na maelezo zaidi.

Hii leo jaridani tunaangazia mshindi wa mwaka huu wa tuzo ya amani ya Nobel, sauti za wanawake nchini Kenya ambazo zimeanza kusikika kwa uthabiti, zikililia haki, heshima, na usawa, na Puja Durga ambayo ni sherehe kubwa ya kihindu ya ushindi wa mungu wa kike.Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imekaribisha uamuzi wa Kamati ya Tuzo ya Amani ya Nobel kumtangaza Maria Corina Machado kiongozi wa upinzani nchini Venezuela kuwa mshindi wa mwaka huu wa tuzo ya amani ya Nobel, kwa kutambua kazi yake ya kuendeleza matumaini ya demokrasia ya watu wa Venezuela.Katika kila kona ya Kenya, sasa sauti za wanawake zimeanza kusikika kwa uthabiti, zikililia haki, heshima, na usawa. Kupitia msaada wa mashirika ya kimataifa kama shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo, UNDP na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na dawa za Kulevya na Uhalifu(UNODC), mabadiliko yanaanza kushika kasi.Mnamo mwaka wa 2021, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) liliongeza kwenye orodha ya turathi za dunia za tamaduni zisizoshikika au kugusika, Puja Durga ambayo ni sherehe kubwa ya kihindu ya ushindi wa mungu wa kike aitwaye Durga dhidi ya jini Mahishasura, ikiwa ni ishara ya ushindi wa mema dhidi ya maovu"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!