Podcasts about baraza

Kenyan volleyball player

  • 62PODCASTS
  • 438EPISODES
  • 12mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • Jun 19, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about baraza

Latest podcast episodes about baraza

Habari za UN
19 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 19, 2025 10:44


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina, ikiwa kesho tarehe 20 mwezi Juni ni siku ya kimataifa ya wakimbizi maudhui yakiwa Mshikamano na Wakimbizi, tunakupeleka kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyoko kaunti ya Turkana, kaskazini-magharibi mwa Kenya.Uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje FDI umeshuka kwa mwaka wa pili mfululizo, ukihatarisha mustakabali wa maendeleo katika nchi zinazoendelea, kwa mujibu wa wa ripoti iliyotolewa leo na kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD. ikionya kuwa pengo la mitaji linaongezeka huku sekta muhimu kama nishati safi na miundombinu zikikosa ufadhili wa muda mrefu.Katika siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono kwenye mizozo, Umoja wa Mataifa umetoa onyo kuwa ukatili wa kingono unazidi kutumika kama silaha ya vita huku wanawake na wasichana wakiathirika zaidi. Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA "Huu si uharibifu wa bahati mbaya  ni uhalifu wa kivita. Na waathirika lazima wawe kiini cha amani, haki, na urejeshwaji wa maisha."Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa  Duniani (WHO) leo limezindua mwongozo wake wa kwanza wa kimataifa wa kudhibiti ugonjwa wa seli mundu (sickle cell) wakati wa ujauzito, ukilenga kupunguza hatari za maisha kwa mama na mtoto. WHO inasema wanawake wenye ugonjwa huu wana hatari hadi mara 11 zaidi ya kufariki dunia wakati wa ujauzito. Hivyo huduma bora za afya zinaweza kuokoa maisha, lakini visa vya seli mundu vinaongezeka duniani, huku Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara ikichangia asilimia 80.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIHORO!.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno KIHORO

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 19, 2025 0:40


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIHORO!"

Habari za UN
05 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 5, 2025 11:03


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo leo ikiwa ni siku ya mazingira duniani mwaka ikibeba maudhui “Tokomeza taka za Plastiki,” tunakwenda Tanzania kumsikia Clara Makenya, Mkua wa UNEP nchini humo na afisa mawasiliano wa shirika hilo kwa ajili ya Namibia akizungumza kuhusu changamoto ya taka za plastiki Tanzania na nini kifanyike kuzitokomeza.Naanzia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York, Marekani ambapo leo kumefanyika tukio maalum la kukumbuka na kuenzi watumishi 168 wa Umoja wa Mataifa waliopoteza maisha wakitekeleza majukumu yao ya ulinzi wa amani, haki, na usaidizi, Mishumaa iliwashwa na kisha walitajwa majina yao mmoja baada ya mwingine akiwemo Nats.. mlinda amani wa UN kutoka Tanzania. Wanafamilia walipokea tuzo maalum za kutambua mchango wao.Leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya mazingira, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametaka hatua za dharura kutokomeza janga la uchafuzi utokanao na taka za plastiki, akilitaja kama “janga” linaloikaba dunia na kutishia afya ya binadamu, mifumo ya ikolojia, na hali ya hewa. Guterres amesema, kadri plastiki zinavyovunjika na kuwa vipande vidogo vidogo zinaingia kila mahali: kuanziaubongo wa binadamu hadi maziwa ya mama.Huko nchini Tanzania hii leo kwenye Chuo Kikuu Mzumbe mjini Morogoro, kumefanyika kongamano kumulika uhaba wa maji na sera bora zinazoweza kufanikisha upatikanaji wa huduma hiyo, kongamano lililoandaliwa kwa pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP na Muungano wa Ulaya. Dkt. Saida Fundi Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu Mzumbe anasema.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIHEREHERE!.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: maana ya neno KIHEREHERE

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 5, 2025 0:45


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno KIHEREHERE.

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 5 Juni 2025

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 5, 2025 5:45


Marekani imetumia kura yake ya turufu dhidi ya azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, lililo kuwa likiomba kusitishwa kwa vita pamoja na misaada yakibinadam kuruhusiwa kuingia katika ukanda wa Gaza bila vizuizi.

Habari za UN
Malawi inachukua hatua madhubuti kukabiliana na changamoto za makazi - Mercy Bety Dube

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 30, 2025 2:16


Mkutano wa pili wa siku mbili wa Baraza Kuu la Makazi la shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani UNHABITAT leo unafunga pazia jijini Nairobi Kenya. Baraza hilo linalofanyika kila baada ya miaka minne ni chombo cha juu kabisa duniani cha kufanya maamuzi kuhusu maendeleo ya miji endelevu na limewaleta pamoja wawakilishi kutoka nchi zote 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa pamoja na wadau mbalimbali wa amendeleo ya miji. Flora Nducha na taarifa zaidi.

Habari za UN
30 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 30, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya elimu kwa watoto mashariki mwa DRC na Mkutano wa pili wa Baraza Kuu la Makazi la shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani UNHABITAT unaofunga pazia leo jijini Nairobi Kenya. Makala inaturejesha nchini DRC na mashinani inatupeleka katika bonde la Ziwa Victoria, kulikoni?Wakati ghasia zinazoendelea huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC zinaripotiwa kusababisha zaidi ya watoto milioni 1.8 kutokuweko shuleni, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF nchini humo linajitahidi kwa udi na uvumba kuhakikisha watoto wanapata elimu kwani ni haki yao ya msingi.Mkutano wa pili wa siku mbili wa Baraza Kuu la Makazi la shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani UNHABITAT leo unafunga pazia jijini Nairobi Kenya. Baraza hilo linalofanyika kila baada ya miaka minne ni chombo cha juu kabisa duniani cha kufanya maamuzi kuhusu maendeleo ya miji endelevu na limewaleta pamoja wawakilishi kutoka nchi zote 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa pamoja na wadau mbalimbali wa amendeleo ya miji.Makala inakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususan jimboni Kivu Kaskazini katika kitongoji cha Mavivi kuwasikia walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania,kikosi cha 11, TANZBATT11, wanaohudumu katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO wakielezea sio tu majukumu yao, bali pia wanajivunia kile wanachofanya kwa kuzingatia Mei 29 imeadhimishwa siku ya kimataifa ya walinda amani.Na katika fursa ni yake Mhandisi Coletha Ruhamya, Naibu Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria, Mradi unaofanikishwa na Benki ya Dunia ambao unakabiliana na masuala ya usafi wa mazingira katika ziwa hilo. Anaeleza umuhimu wa usimamizi endelevu wa bonde hilo kote nchini Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda na Burundi chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
29 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 29, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa ikitupeleka nchini DRC, Sierra Leone na Ghana. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na maana ya neno "MISHEMISHE.”Leo ni Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani ambayo mwaka huu inajikita na maudhui ya “mustakabali wa ulinzi wa amani.”Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema walinda amani wa Umoja wa Matafa wako katika changamoto kubwa “Leo hii, walinda amani wanakabiliwa na hali zinazozidi kuwa ngumu katika dunia inayozidi kuwa na changamoto, ikiwemo uugawanyika na kutofautiana kwa mitazamo duniani kunazidi kuongezeka, operesheni za ulinzi wa amani zinakabiliwa, hatari zaidi kutokana na wingi wa vitisho kama vile ugaidi na walinda amani kulengwa kwa makusudi kupitia taarifa potofu zenye madhara makubwa na changamoto zinazovuka mipaka kuanzia janga la mabadiliko ya tabianchi hadi uhalifu wa kimataifa.Kikosi cha 11 cha Tanzania kinachohudumu chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO kimeungana na walinda amani wengine kuadhimisha Siku ya Walinda Amani Duniani. Maadhimisho hayo yamefanyika Mavivi, yakiongozwa na Brigedia Jenerali Diamond Meshack Madie, Mnadhimu Mkuu wa Vikosi vya MONUSCO.Shirika la Umja wa Mataifa la Mazingira UNEP limezindua mpango mpya wa dola milioni 15 kusaidia uwekezaji endelevu katika Bonde la Kongo – moja ya mifumo muhimu zaidi ya ikolojia duniani. Mpango huu unalenga kufungua fursa za biashara rafiki kwa mazingira kwa wajasiriamali wadogo na wa kati katika sekta za kijani. Msitu wa mvua wa Bonde la Kongo ni moja ya vyanzo vikubwa vya kaboni duniani na ni makazi ya watu zaidi ya milioni 75, wakiwemo jamii za asili.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi  Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "MISHEMISHE.”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "MISHEMISHE.”

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 29, 2025 0:38


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi  Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "MISHEMISHE.”

Lafiya Jari ce
Sharhi kan ƙiba fiye da ƙima da ke baraza ga matasan Afirka

Lafiya Jari ce

Play Episode Listen Later May 26, 2025 10:12


Shirin 'Lafiya Jari Ce na wannan mako tare da Azima Bashir Aminu ya mayar da hankali kan hasashen da wata ƙungiya ta yi cewar nan da shekarar 2025 raɓin al'ummar Afirka masamman matasa za su fuskanci cutar ƙibar da ta wuce ƙima ko Obesity a turance.

obesity baraza najeriya afirka
PLAZA PÚBLICA
PLAZA PÚBLICA T06C181 Paca Baraza: "El Plan de Ordenación Territorial del Mar Menor debería estar ya aprobado" (23/05/2025)

PLAZA PÚBLICA

Play Episode Listen Later May 23, 2025 28:35


La Comisionada del Ciclo del Agua y Restauración de Ecosistemas en el Ministerio de Transición Ecológica, Paca Baraza, ha mostrado su preocupación por la intensificación de los planes urbanísticos en zonas del campo de Murcia y de Cartagena, que pertenecen a la cuenca vertiente del Mar Menor. Baraza urge al Gobierno regional a aprobar el Plan de Ordenación Territorial contemplada en la Ley de Protección del Mar Menor para poner orden.En una entrevista en el programa Plaza Pública de Onda Regional y preguntada por los planes del ayuntamiento de Murcia para hacer más de 8.000 viviendas de uso turístico residencial en Corvera y Baños y Mendigo, Baraza ha recordado que los resorts construidos en los últimos años en el término municipal han influido en la impermeabilización del suelo generando grandes escorrentías de agua que acaban llegando al Mar Menor. La comisaria cree que el Plan de Ordenación Territorial, dependiente de la Comunidad Autónoma, ya debería estar aprobado.Baraza ha señalado que la laguna salada está padeciendo las consecuencias de lo que se hace en su entorno en materia agrícola, ganadera y urbanística. La comisionada cree que antes de lanzar una urbanización concreta hay que determinar cuántas viviendas son posibles y en qué condiciones.Visitas a los proyectos de recuperación del Mar Menor El Ministerio de Transición Ecológica organiza dos visitas gratuitas los días 10 y 12 de junio para enseñar a los ciudadanos todos los proyectos de recuperación que se están ejecutando en el Mar Menor.Las visitas se llevarán a cabo en autobús y saldrán desde Murcia y Cartagena coincidiendo con el Día Mundial del Medio Ambiente. Aquellos que lo deseen podrán conocer de mano de los técnicos los proyectos contemplados en el Marco de Actuaciones Prioritarias para recuperar el Mar Menor en zonas como la rambla de El Albujón, la Sierra Minera, la Caleta del Estacio o Puerto Mayor. Paca Baraza ha destacado como el Marco de Actuaciones Prioritarias en el Mar Menor, con una inversión prevista de 675 millones de euros, está sirviendo de ejemplo para otros territorios que están en una situación crítica y para el Plan de Restauración de la Naturaleza que prepara el Gobierno.La Comisionada del Ciclo del Agua también se ha referido al Pacto Verde Europeo, rechazado por el PP como pide Vox para llegar a un acuerdo sobre Presupuestos. Se ha referido a esa herramienta como esencial para frenar el calentamiento global y el incremento de temperatura que afecta al mar Menor y al Mediterráneo. Baraza se muestra optimista y cree que el Pacto Verde no va a caer

Habari za UN
22 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 22, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini kumsikia mgeni wetu Prof. Wallah Bin Wallah, mwandishi mashuhuri wa vitabu vya Kiswahili kutoka Kenya ambaye anamulika umuhimu wa vitabu katika kukuza lugha ya Kiswahili. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno.Kwa mara ya kwanza tangu mwezi Februari, msaada wa kuokoa maisha umefika Gaza. Baada ya wiki 11 za kizuizi kutoka kwa mamlaka za Israeli, malori 198 yaliyobeba chakula, dawa na unga wa ngano yameingia leo kupitia mpaka wa Kerem Shalom kwa mujibu wa mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa.Mratibu mkuu wa misaada wa Umoja wa Mataifa, Tom Fletcher, ameiitaja hatua hiyo kuwa ya muhimu sana, huku malori 90 yakipakuliwa usiku kwa ajili ya kusambazwa haraka.Mwaka 2024, vita havikuishia kwenye uwanja wa mapambano pekee      vilivunja nyumba, masoko na shule. Kuanzia Gaza hadi Ukraine, Sudan hadi Myanmar na zaidi ya raia 36,000 walipoteza maisha yao katika mizozo 14 ya kivita kulimgana na ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kwa Baraza la Usalama hii leo linalojadili ulinzi wa raia katika mizozo ya silaha.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DAHARI”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "DAHARI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 22, 2025 0:36


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DAHARI."

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
DRC: Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki wamtaka Rais Felix Tshisekedi kuwaamini viongozi wa dini

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later May 22, 2025 20:00


Makala haya yanaangazia taarifa mbalimbali ikiwemo, Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini DRC wamtaka Rais Felix Tshisekedi kuwaamini viongozi wa dini kusaidia kuleta amani na utulivu Mashariki mwa nchi hiyo na pia serikali ya Uganda yawasilisha mswada tata bungeni kuruhusu kesi za kiraia kupelekwa kwenye Mahakama ya kijeshi. Taarifa zingine ambazo utaziskia ni uongozi wa kijeshi nchini Mali wasitisha sheria kuhusu vyama vya siasa nchini humo na Mazungumzo ya ana kwa ana kati ya wajumbe wa Ukraine na Urusi yamefanyika wiki hii nchini Uturuki kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2022.

Habari za UN
19 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 19, 2025 11:08


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya afya, na wakimbizi wa Syria wanaorejea nchini mwao. Makala tukwenda nchini Kenya kumulika ufukaji wa nyuki, na mashinani tunakuletea ujumbe wa Katibu Mkuu wa IMO kuhusu Siku ya Kimataifa ya wanawake mabaharia.Wajumbe kutoka kote duniani wamekusanyika mjini Geneva, Uswisi, kwa ajili ya Mkutano wa 78 wa Baraza la Afya Duniani (WHA78) unaofanyika kuanzia leo Mei 19 hadi 27 Mei mwaka huu.Tangu kuangushwa kwa utawala wa aliyekuwa Rais wa Syria Bashar al Assad aliyekuwa madarakani kwa zaidi ya muongo mmoja, wananchi wa Syria wamekuwa wakimiminika kurejea nchini mwao ambapo takwimu za sasa zinaonesha zaidi ya Wasyria 500,000 wamerejea kutoka nchi jirani. Mmoja wa waliorejea ni Babu Jassim na Leah Mushi anatuletea simulizi yake.Katika makala tunaelekea Kajiado nchini Kenya, ambako juhudi za utunzaji mazingira kupitia mradi wa ufugaji wa nyuki unaofadhiliwa na shirika la misaada la Marekani USAID kwa kushirikiana na idara ya misitu ya Kenya KFS hazichangii tu katika kukuza uchumi wa jamii, bali pia kulinda mazingira. Kupitia Makala hii iliyoandaliwa na Sharon Jebichii, Bwana Mureithi mmoja wa wanufaika wa mradi huo anaanza kwa kueleza mafanikio yao.Nakatika mashinani, fursa ni yake Arsenio Dominguez, Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usafirishaji Majini, IMO akitoa ujumbe wa ujumuishaji na usawa wa kijinsia wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya wanawake mabaharia ambayo huadhimishwa tarehe 18 mwezi Mei kila mwaka.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
WHO: Mkutano wa 78 wa Baraza la Afaya Duniani umeng'oa nanga Geneva

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 19, 2025 2:18


Wajumbe kutoka kote duniani wamekusanyika mjini Geneva, Uswisi, kwa ajili ya Mkutano wa 78 wa Baraza la Afya Duniani (WHA78) unaofanyika kuanzia leo Mei 19 hadi 27 Mei mwaka huu. Kaulimbiu ya mkutano wa mwaka huu ni “Ulimwengu Mmoja kwa Afya” inaakisi dhamira ya pamoja ya kujenga mfumo wa afya wa kimataifa ulio imara, jumuishi na thabiti. Flora Nducha amefuatilia na hapa anatupasha zaidi

Broadcasts – Christian Working Woman
What is Your Banana Ministry?

Broadcasts – Christian Working Woman

Play Episode Listen Later May 17, 2025 14:28


My friend Judy was a missionary living in Nairobi, Kenya. She traveled a good deal in and around Nairobi, and if you've ever been there, you know it's pretty much a continual traffic jam. And there are always people lined up on the streets selling everything you can imagine—including to my horror, puppies. One day Judy was traveling with her driver, Baraza, and she saw a woman selling bananas, with a baby strapped to her back and two others playing at her feet. Judy told Baraza, “Pull over; I want to buy some bananas.” She gave him the equivalent of about two dollars and told him to buy all her bananas—about 20. “But Sister,” he said, “why are you buying 20 bananas? You can't eat that many.” “Just buy them,” she told him. He was baffled as to why Judy would want so many bananas, since she lives alone, but he did as she insisted. When he paid the lady for all her bananas, her face lit up with a huge, incredulous smile. That probably represented two days of food for her and her family. Baraza said, “Sister, did you see how happy she was. You did a good thing for her.” Then they traveled on, and Judy saw a crippled man with only one leg by the side of the road. She told Baraza to stop and give him some bananas. Once again, Baraza saw how thrilled the man was to get the bananas. This went on for their entire journey until Judy had given away all the bananas. Baraza—who is a wonderful believer—said, “Sister, this was so good. I can do this. I can give away bananas.” And as a result, Baraza began to carry bananas, apples, and other fruit with him to give to people randomly as God led him. So, he had a banana ministry. What do you have in your hands that could easily become gifts of love to the people in your life—strangers, coworkers, family, friends—whoever?  I'm suggesting that every one of us should look for our banana ministry—something we intentionally do to share the love of God. You're probably familiar with the phrase “random acts of kindness.” Actually, it has become a movement, encouraging people to purposely plan and perform kind acts for others. Lots of research has been done that shows the incredible benefits for the person who decides to plan and execute random acts of kindness. According to research from Emory University, when you are kind to another person, your brain's pleasure and reward centers light up, as if you were the recipient of the good deed—not the giver. This phenomenon is called the “helper's high.” Isn't it interesting that when people follow the principles of Scripture, whether they are believers or not, they discover it benefits everyone. The Apostle Paul wrote to Timothy: And the Lord's servant must not be quarrelsome but must be kind to everyone. . . (2 Timothy 2:24). And to the church in Colossae he wrote: Therefore, as God's chosen people, holy and dearly loved, clothe yourselves with compassion, kindness, humility, gentleness and patience (Colossians 3:12). He was preaching “random acts of kindness” long before the term was coined. Certainly, as followers of Jesus Christ, we should share “random acts of kindness” more than any others because we have the Holy Spirit, and we also have the great privilege of showing God's love to a loveless, often cruel world. And then, as the studies show, we discover what Jesus told us—it is truly more blessed to give than to receive. Let me tell you about my friend, Kiyoko, a Japanese woman in my church. She was inspired to use her creativity to share the gospel. So, she made beautiful little bookmarks with a Bible verses, using things people throw away, like candy wrappers. She carried her bookmarks with her and whenever she had an opportunity—with a stranger, a store clerk, someone she sat by on the bus or airplane—she gave them one of her bookmarks. She called them “born-again bookmarks,” and explained how she makes them from scraps of paper that people throw away. This opened the door for her to tell them that her born-again boo...

SBS Swahili - SBS Swahili
Nafasi za baraza la waziri za tangazwa: Nani yuko ndani, nani yuko nje?

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 13, 2025 9:13


Tanya Plibersek ame shushwa cheo nakupewa wizara ya Huduma za Jamii, wakati Anthony Albanese anatangaza baraza lake la mawaziri, atakao fanya kazi nao katika muhula wake wa pili serikalini.

Habari za UN
08 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 8, 2025 11:12


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa ambayo Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili alipata fursa ya kuzungumza na kiongozi wa kijamii kutoka Jamii ya wafugaji ya Wamaasai mkoani Morogoro nchini Mashariki mwa Tanzania Adam Kulet Ole Mwarabu.Wiki kumi baada ya kuanza kwa mzingiro kamili wa Israel dhidi ya wakazi wa Gaza, zaidi ya robo tatu ya kaya katika eneo la Palestina kuna uhaba mkubwa wa huduma ya maji, huku hali ya usafi ikizidi kuwa mbaya, yameonya leo mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu athari za "uhaba huo wa maji kwa kuzingatia kuwa msimu wa joto unakaribia.”Ripoti kutoka Sudan zikidai kwamba juzi jumatano kulikuwa na jaribio la mashambulizi mapya ya ndege zisizo na rubani dhidi ya kitovu muhimu cha misaada nchini humo juzi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kupitia tamko alilolitoa jana jioni kwa saa za New York, Marekani, ameongeza nguvu yake katika kutoa wito unaozidi kuwa wa muhimu kuhamasisha kuanzishwa kwa mazungumzo ya amani ya kweli.Kufuatia kuendelea kwa mvutano wa majirani, India na Pakistani, Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Philemon Yang, ametoa wito wa kuzitaka nchi hizo mbili kuchukua tahadhari na kuepuka hatua zinazoweza kuongeza mzozo. Balozi Yang anasisitiza mazungumzo ya amani na kufuata sheria za kimataifa ndiyo njia pekee ya kusuluhisha migogoro.”Na katika jifunze Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DALALI”Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "DALALI”

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 8, 2025 0:45


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DALALI”

America's Work Force Union Podcast
Al Baraza, IUPAT | Dave Megenhardt, ULA

America's Work Force Union Podcast

Play Episode Listen Later May 7, 2025 53:57


Al Barraza, Director of Organizing for the International Union of Painters and Allied Trades District Council 14, joined America's Work Force Union Podcast to discuss a campaign for worker safety at Sure Built Concrete Forms and Accessories.  Dave Megenhardt, Executive Director of the United Labor Agency (ULA), joined the America's Work Force Union Podcast to discuss the agency's efforts in supporting displaced federal workers in Northeast Ohio and promoting mental health awareness. 

Habari za UN
29 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 29, 2025 11:44


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka katika mkoa wa Mwanza kaskazini magharibi mwa Tanzania ambapo vijana wameshika hatamu kuboresha mustakabali wao. Pia tunakuletea muhtasari wa habari  na mashinani tunasalia hapa makao makuu.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kudumisha Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, MONUSCO, umeikaribisha kusainiwa kwa “Azimio la Kanuni” tarehe 25 Aprili 2025 mjini Washington, D.C chini ya usimamizi wa Wizara ya mambo ya nje ya Marekani, kati ya serikali za DRC na Rwanda kwa lengo la kulinda rai ana kutekeleza azimio la Baraza la Usalama namba 2773 (2025).Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA, Juliette Touma, akizungumza na waandishi wa habri mjini Geneva kwa njia ya video kutoka mji mkuu wa Jordan, Amman, wakati  kuzingirwa kwa Ukanda wa Gaza kukikaribia kuingia mwezi wa pili amesema “Mzingiro wa Gaza ni muuaji wa kimya muuaji wa watoto, wazee, na watu walioko katika mazingira magumu zaidi. Mzingiro huu unamaanisha kwamba familia nzima, watu saba au wanane wanalazimika kushirikiana kopo moja la maharagwe au njegere”.Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO limezitaka nchi za Kaskazini Magharibi mwa Afrika kuongeza ufuatiliaji na kuchukua hatua za mapema kudhibiti makundi ya nzige wa jangwani. Hii ni baada ya nzige wakubwa na makundi madogo kutoka ukanda wa Sahel kuhamia maeneo ya kusini mwa Sahara, hasa katikati ya Algeria, magharibi mwa Libya, na kusini mwa Tunisia tangu Februari hadi Machi mwaka huu.Na katika mashinani fursa ni yake Maruping Onkemetse Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kituo cha Msaada wa Familia, shirika linaloongozwa na wanawake wa asili  katika Wilaya ya Gantsi, kijiji cha Chobokwane nchini Botswana anayeshiriki mkutano unaoendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa wa Jukwaa la Watu wa Asili akizungumzia alichojifunza hadi sasa.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Matumizi ya maneno "MKALIMANI NA MFASIRI"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 24, 2025 1:12


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni  Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi  Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua matumizi ya maneno "MKALIMANI NA MFASIRI."

Habari za UN
24 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 24, 2025 11:35


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika Chata ya Umoja wa Mataifa inayolenga kusongesha amani, maendeleo, urafiki na haki za binadamu. Je, wajumbe wa Umoja wa Mataifa hufanya nini? Assumpta Massoi amezungumza na mmjoa wao Balozi Yabesh Monari wa Kenya, lakini kwanza ni muhtasari wa habari na ufafanuzi wa maneno.Mratibu wa misaada ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa nchini Ukraine, Matthias Schmale, amelaani vikali shambulio jipya la Urusi dhidi Ukraine lililosababisha vifo na majeruhi kwa raia, wakiwemo watoto na mwanamke mjamzito. Bwana Schmale amesema shambulio hilo la usiku wa kuamkia leo katika maeneo ya makazi jijini Kyiv na maeneo ya jirani ni ukiukaji wa kutisha wa sheria za kimataifa za kibinadamu na kwamba matumizi haya ya nguvu yasiyo na maana lazima yakome.Wiki ya Chanjo Duniani ikiwaimeanza leo, mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la afya duniani, WHO, na la kuhudumia Watoto, UNICEF, na Ubia wa chanjo duniani, Gavi wametoa onyo kwamba milipuko ya magonjwa yanayozuilika kwa chanjo inaongezeka kwa kasi. Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus, anasema, “Chanjo zimeokoa maisha ya watu zaidi ya milioni 150 katika kipindi cha miongo mitano iliyopita. Kupunguzwa kwa ufadhili wa afya ya kimataifa kumeweka hatarini mafanikio haya yaliyopatikana kwa juhudi kubwa.”Na ikiwa pia leo Siku ya kimataifa wasichana katika  Teknolojia ya mawasiliano, ICT, Mshauri wa masoko ya kidijitali nchini Kenya Maryann Mwangi akizungumza na washirika wetu Redio Domus amehimiza wasichana kujikita kwenye ICT kwani huu ndio mustakabali.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni      Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi      Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua matumizi ya maneno "MKALIMANI NA MFASIRI"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Jamii inapaswa kusikiliza na kujifunza kutoka kwa vijana

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2025 3:42


Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) linafanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani ambapo limeanza tarehe 15 Aprili na linatarajiwa kukamilika tarehe 17 Aprili 2025. Vijana kutoka nchi mbalimbali pamoja na wadau wengine wa masuala ya maendeleo na Uchumi wanakuja pamoja kujadili changamoto mbalimbali na namna bora ya kupatia ufumbuzi katika kuubadilisha ulimwengu kuwa mahali penye usawa zaidi na endelevu chini ya mwongozo wa Ajenda ya mwaka 2030 na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).  Miongoni mwa wanaohudhuria jukwaa hilo ni Kapwani Kavenuke kutoka nchini Tanzania ambaye amefanyiwa mahojiano na Leah Mushi na hapa anaanza kwa kueleza umuhimu wa mikutano huo.

Habari za UN
16 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2025 9:57


Hii leo jaridani Assumpta Massoi anamulika masuala ya afya hususan harakati za kukabiliana na majanga yajayo ya afya;  wakimbizi huko Zambia ambako sera jumuishi zimewajengea uwezo; Jukwaa la vijana na mchango wa sanaa kwenye usawa na utengamano. Baada ya zaidi ya miaka mitatu ya mazungumzo ya kina, hatimaye leo huko mjini Geneva, Uswisi, nchi wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) zimekamilisha rasimu ya makubaliano ambayo itawasilishwa katika Mkutano wa Afya Duniani mwezi ujao wa Mei. Pendekezo hili linakusudia kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na vitisho vya majanga ya kiafya yajayo. Anold Kayanda amefuatilia anatujulisha zaidi.Zambia inaendelea kuwahifadhi zaidi ya wakimbizi 106,000, wengi wao wakiwa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Burundi, pamoja na wakimbizi wa zamani kutoka Rwanda na Angola. Limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, likiongeza kwamba kwa kuzingatia sera jumuishi ya Zambia, taifa hilo linakuza mshikamano na wakimbizi na kuwawezesha kujitegemea kupitia makazi maalum na ushirikiano na jamii za wenyeji. Flora Nducha na taarifa zaidi.Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) limeanza jana hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa na litamalizika kesho tarehe 17 Aprili. Vijana kutoka nchi mbalimbali wamehudhuria jukwaa hilo akiwemo Kapwani Kavenuke kutoka nchini Tanzania ambaye amehojiwa na Leah Mushi wa Idhaa hii. Kapwani anaanza kwa kueleza  umuhimu wa mikutano hii.Gislain Kalwira, Muandaaji wa tamasha la Musika na Kipaji  nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC linalofanyika kila mwaka kuleta pamoja wasanii wa kike na wa kiume wa fani mbalimbali, kwa kutambua kuwa jana dunia imeadhimisha siku ya sanaa duniani. Kalwira kupitia video iliyochapishwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani  nchini DRC, MONUSCO, anafafanua mantiki ya tamasha hilo na kujenga usawa kijinsia.

Habari za UN
15 Aprili 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 15, 2025 9:59


Karibu kusikiliza jarida la Umoja wa Mataifa ambapo hii leo tunamulika Kongamano la Kimataifa la Kiswahili linalofanyika mjini Kampala Uganda likiwaleta pamoja wadau kutoka kila kona ya Afrika na kwingineko kujadili mikakati ya kukuza lugha hiyo adhimu ya Kiswahili. Utasikiliza muhtasari wa habari ukiangazia miaka miwili tangu kuanza kwa vita vya sasa vya Sudan, UNHCR, yatoa wito kwamba mwitiko mkubwa wa kibinadamu ulioratibiwa vema ni muhimu ili kuzuia mateso zaidi na vifo kwa wananchi wa DRC, na Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) limeanza leo tarehe 15 hadi tarehe 17 katika Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. 

Habari za UN
10 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 10, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Idhaa hii inazungumza na Mwenyekiti wa Tanzania Women Ecocomic Empowerment Network (TAWEN), ambaye pia ni mchumi mbobezi Bi. Janet Zebedayo Mbene. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na neno la wiki.Shukran Anold na leo tunaanzia huko Geneva Uswisi ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limetoa muongozo wake wa kwanza duniani wa kutambua, kutoa matibabu kwa haraka na matibabu ya muda mrefu kwa ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.Nchini Chad katika mpaka wake na Sudan ambako Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR Filippo Grandi ametembelea na kuzungumza na wakimbizi wa Sudan pamoja na kujionea hali zao wakati huu ambapo wamepunguza kutoa chakula, malazi , maji na dawa na kauli yake ikawa moja tu, “Ninatoa wito kwa wafadhili, tafadhali msipunguze msaada kwa wathirika wa vita vya Sudan.”.Taarifa ya pamoja ya mashirika ya kibinadamu inayotolewa kila baada ya wiki mbili imeeleza kuhusu hali katika Ukanda wa Gaza inasema kuwa watu wanazidi kuuwawa na kujeruhiwa. Kwa zaidi ya mwezi sasa hakuna misafara ya misaada inayoruhusiwa kuingia Gaza. Watu kulazimishwa kuhama kinguvu kunaendelea, makazi ya wakimbizi yamefikia pomoni, huduma za usafi na kujisafi nazo ni mbaya.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "FIFILIZA"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "FIFILIZA"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 10, 2025 0:51


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "FIFILIZA"

Habari za UN
03 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 3, 2025 11:45


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha kwenye mkutano wa hivi majuzi wa CSW69 kufuatilia harakati za Mfuko wa CRDB za kujengea uwezo na kuinua wanawake nchini Tanzania. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno “MHARUMA.”Mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau wa misaada ya kibinadamu leo wamesema wanaendelea kuwasaidia watu wa Muyanmar na mahitaji ya msingi baada ya tetemeko kubwa la ardhi la Ijuma iliyopita ambapo idadi ya waliopoteza maisha sasa ni zaidi ya 2,800, maelfu wamejerihiwa na mamia bado hawajulikani wako.Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu, Volker Türk, amesema leo kwamba ameshtushwa na ripoti za mauaji ya raia bila kufuata utaratibu wa kisheria yaliyoenea mjini Khartoum baada ya kurejeshwa kwa mji huo chini ya udhibiti wa Jeshi la Sudan (SAF) tarehe 26 Machi.Na majadiliano ya siku mbili ya kila mwaka ya será kuhusu maendeleo endelevu yaliyoandaliwa na Club De Madrid yameanza leo Nairobi Kenya mwaka huu yakijikita na ufadhili wa maendeleo. shududa wetu huko ni Stella Vuzo kutoka kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIS Nairobi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno MHARUMA”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "MHARUMA.”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 3, 2025 0:31


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "MHARUMA.”

Habari za UN
13 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 13, 2025 11:00


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Idhaa hii imezungumza na Lucy Gidamis, Wakili ambaye kwa sasa anafanya kazi na shirika la Msichana Initiative nchini Tanzania akijikita katika kutetea na kutekeleza haki za wanawake. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ufafanuzi wa neno Wakfu.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC hii leo Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO umekabidhi magari sita kwa gavana wa kijeshi wa jimbo la Kivu Kaskazini ili kuwezesha shughuli za polisi katika kuimarisha ulinzi na usalama.Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Afya duniani WHO na la kuhudumia watoto UNICEF yametangaza kuwepo kwa idadi kubwa ya wagonjwa wa surua barani ulaya, jumla ya wagonjwa 127,350 waliripotiwa kati yao watoto wakiwa zaidi ya asilimia 40.Na hii leo ikiwa ni chungu cha 10 cha Ramadhan, ikikamilisha fungu la kwanza kati ya mafungu matatu ambapo ni siku 30 za mwezi Mtukufu wa Ramadhan, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameanza ziara yake ya siku nne nchini Bangladesh ikiwa ni utaratibu wake wa kila mwaka wa kushiriki Ramadhan na jamii za waislamu walio kwenye changamoto mbalimbali.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua neno Wakfu.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: Maana ya neno Wakfu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 13, 2025 1:01


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mchambuzi wetu Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua neno Wakfu.

Capital FM
From Crisis to Action: Dr Nancy Baraza on GBV & Femicide in Kenya on #DriveInn With Chiko and Fellaris

Capital FM

Play Episode Listen Later Mar 6, 2025 44:43


From Crisis to Action: Dr Nancy Baraza on GBV & Femicide in Kenya on #DriveInn With Chiko and Fellaris by Capital FM

Habari za UN
Miaka 30 baada ya Azimio la Beijing kuhusu haki za wanawake, safari bado ni ndefu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 5, 2025 2:08


Kuelekea siku ya wanawake duniani itakayoadhimishwa mwishoni mwa wiki hii ambayo ni tarehe 8 mwezi Machi, Mkurugenzi Mtendaji wa  shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women, Sima Bahous, amesisitiza kwamba ahadi zilizowekwa kwenye Azimio la Beijing miaka 30 iliyopita kuhusu haki za wanawake hazipaswi tu kukumbukwa bali zinahitaji kutekelezwa kikamilifu. Flora Nducha anafafanua zaidiAkizungumza wiki hii mjini Geneva Uswisi katika majadiliano ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa ya kuadhimisha miaka 30 ya Azimio la Beijing (#Beijing30), Bi. Bahous amebainisha umuhimu wa kuharakisha maendeleo ya usawa wa kijinsia akiwataka viongozi wa dunia kuchukua hatua thabiti ili kuhakikisha haki za wanawake zinapewa kipaumbele wakati wa changamoto zinazoendelea duniani.Amesema “Miaka 30 iliyopita dunia iliweka ahadi ya kusongesha fursa na utu wa wanawake na wasichana wote. Ahadi hiyo haikuwa maneno matupu kwenye karatasi, ilikuwa ramani ya njia na wito wa mshikamano . Na kwa miongo mitatu imechochea hatua, wasichana wengi sasa wako shule, wanawake wengi wako bungeni , kuna sheria nyingi zaidi zinawalinda wanawake dhidi ya ukatili, na mataifa mengi zaidi yanatambua usawa wa kijinsia ni lazima.”Licha ya mafanikio hayo yote Bi, Bahous amesema ndio kwanza mkoko unaalika maua kwani safari bado ni ndefu“Hebu tuwe wakweli hatujafika tunapopaswa kuwa. Haki za wanawake na wasichana zinashambuliwa, fursa za wanawake kupaza sauti zinazidi kupungua na endapo tutaendelea na kasi hii msichana aliyezaliwa leo atakuwa na umri wa miaka 39 kabla wanawake hawaja na viti vingi bungeni kama wanaume, atakuwa na umri wa miaka 68 kabla ndoa za utotoni hazijakomeshwa, na atakuwa na umri wa miaka 137 kabla umasikini uliokithiri kwa wanawake na wasicha haujatokomezwa. Hatuwezi kulikubali hili.”Mkuu huyo wa UN Women ameyahimiza mataifa yote kuchukua hatua sasa ili kuhakikisha ndoto za azimio la Beijing hazisalii kuwa ndoto bali maisha halisi.

Habari za UN
Hali ya usalama ikidorora DRC, hofu sasa ni mustakabali wa watetezi wa haki za binadamu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 5, 2025 1:57


Hali ya kibinadamu ikiendelea kuzorota mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mtaalamu Maalumu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na hali ya watetezi wa haki za binadamu, Mary Lawlor leo ametoa wito wa msaada wa dharura na wa vitendo kwa watetezi wa haki za binadamu katika eneo hilo. Anold Kayanda na taarifa zaidi. (Taarifa ya Anold Kayanda)Mary Lawlor akizungumza leo jijini Geneva-Uswisi amesema, "watetezi wa haki za binadamu mashariki mwa DRC wako hatarini sana kulengwa na kulipiziwa kisasi kwa kazi yao ya kutetea haki za binadamu. Wanahitaji msaada sasa, ikiwa ni pamoja na usaidizi wa kuhamishwa kwa muda pamoja na familia zao.”Kundi la waasi la M23, limeendelea kusonga mbele katika eneo hilo la mashariki mwa DRC tangu lilipoanza mashambulizi yake mapema mwaka huu, na wale waliorekodi na kufichua ukiukwaji wa haki zao wamekuwa wakilengwa moja kwa moja, amesisitiza Bi. Lawlor."Katika wiki za hivi karibuni nimepokea taarifa nyingi za tahadhari zinazohitaji msaada na nimezungumza moja kwa moja na watetezi walioko mashinani," amesema Lawlor na kuongeza kuwa watu hao wanaishi kwa hofu na hatari ni halisi na kwama hivi karibuni, mtetezi mmoja alimpa taarifa kuwa waasi wa M23 wameandaa orodha ya watetezi wa haki za binadamu watakaokamatwa katika maeneo waliyoyadhibiti.Mtaalamu huyo  amesema amepokea ripoti za kuaminika za watetezi wa haki za binadamu kushikiliwa bila mawasiliano, kutoweshwa kwa nguvu, na kuteswa huko Rutshuru na Masisi, Kivu Kaskazini, huku takribani watetezi sita wa haki za binadamu wakiripotiwa kutoweka baada ya kujaribu kutoroka Goma baada ya jiji hilo kuchukuliwa na M23."Baadhi ya watetezi wa haki za binadamu hawakuwa na chaguo jingine ila kukimbia makazi yao. Wale wanaofanikisha kufika katika miji mingine wanakosa rasilimali za kupata malazi au kukidhi mahitaji yao ya kila siku," amesema na kwamba, "wengine wamebaki katika maeneo yanayodhibitiwa na waasi lakini wana hofu kubwa kuhusu usalama wao. Mtetezi mmoja alimuuliza jinsi wanavyoweza kuendelea kujificha huku M23 ikianza kufanya ukaguzi huko Goma.Tangu magereza yalipovunjwa  huko Goma, Kalehe, Bukavu, na Uvira, maelfu ya wafungwa, wakiwemo wahalifu wakatili na viongozi wa makundi yenye silaha waliohukumiwa kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu unaofikia uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu, walitoroka na kuingia mitaani. Baadhi yao wanawatishia watetezi wa haki za binadamu waliotoa msaada wa matibabu, kisaikolojia na msaada wa kisheria kwa waathiriwa na mashahidi waliotoa ushahidi wakati wa kesi hizo. Na wakati huo huo watetezi wa haki za binadamu wakikabiliwa na vitisho na hofu ya kulipiziwa kisasi, waathiriwa hawana wa kuwategemea, ameeleza mtaalamu huyo.Katika mazingira ambayo tayari ni magumu kwa watetezi wa haki za binadamu, Mtaalamu huyo maalumu wa Umoja wa Mataifa anasisitiza hatari kubwa ya ukatili wa kingono inayowakabili watetezi wa haki wa kike."Tunajua kuwa ukatili wa kingono unaohusiana na migogoro mashariki mwa DRC ni wa kiwango cha juu, na kwamba wanawake wanaopinga ukiukwaji wa haki za binadamu katika muktadha huu, na wanaojitokeza kwa kazi yao, mara nyingi ndio wanaoathirika zaidi," Lawlor amesema akiongeza kuwa ni jambo la kusikitisha kufikiria kwamba miaka 25 tangu kupitishwa kwa azimio la kihistoria la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu wanawake, amani na usalama, matukio haya yanatokea mbele ya ulimwengu unaoonekana kutokuwa na msimamo thabiti.Mtaalamu huyo pia ameelekeza umakini kwa hatari wanazokabiliana nazo watetezi wa haki za binadamu katika maeneo ya vijijini na yaliyojitenga, ikiwa ni pamoja na mauaji, kutoweshwa kwa nguvu, na utekaji nyara, na akaangazia athari za kisaikolojia zinazowakumba wale walioko mashinani."Watetezi tayari walikuwa wakikabiliwa na vitisho katika eneo hilo – kutoka kwa serikali na makundi yenye silaha  lakini kama alivyonieleza mtetezi mmoja wa haki za binadamu wa…

Habari za UN
Viongozi wababe, wa kiimla na wenye fedha wanasigina haki za binadamu duniani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 2:57


Kwenye kikao cha 58 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kinachoendellea mjini Geneva Uswisi, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa M ataifa, Volker Türk , amezungumzia hali ya kuzorota na kutoeleweka inayohusu haki za binadamu duniani kote akielezea wasiwasi mkubwa kuhusu kudhoofika kwa makubaliano ya kimataifa kuhusu haki za binadamu,na kuonya kwamba ushawishi wa viongozi wa kiimla, matajiri wakubwa, na viongozi wa kimabavu unatishia kuvuruga maendeleo ya miongo kadhaa. Anold Kakayanda na taarifa kamili.Asante Flora katika taarifa yake Türk  amesisitiza umuhimu wa kuhifadhi haki za binadamu na utawala wa sheria ili kuzuia kurudiwa kwa ukatili wa zamani.Moja ya masuala ya dharura yaliyotiliwa mkazo na Türk  ni mgogoro wa kibinadamu unhaoendelea huko Gaza. Amelaani uharibifu uliosababishwa na hatua za kijeshi za Israeli dhidi ya mashambulizi ya Oktoba 7, 2023 yaliyofanywa na Hamas na makundi mengine ya wapiganaji wa Kipalestina.Türk  amesisitiza haja ya kudumisha usitishaji mapiganona kutoa wito wa mchakato wa amani unaozingatia haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na haki ya kujitawala na uwajibikaji. Ametaka kuachiliwa kwa mateka, kukomeshwa kwa vizuizi vya kiholela, na kuanza tena kwa msaada wa kibinadamu mara moja ndani ya Gaza.Kuhujsu mgogoro unaoendelea nchini Ukraine amersema bado ni suala la kutia wasiwasi, huku raia wakiishi kwa hofu ya mara kwa mara kutokana na mashambulizi yasiyokoma.Türk  amekemea vikali vikwazo vya Shirikisho la Urusi juu ya haki za msingi katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu na kuelezea masikitiko yake kuhusu ripoti za mauaji ya kiholela na mateso ya kimfumo ya wafungwa wa vita wa Kiukraine.Almeihimiza jumuiya ya kimataifa kufanya kazi kuelekea amani endelevu inayoheshimu haki na matarajio ya watu wa Ukraine.Türk  pia ameelekeza mawazo kwenye maeneo mengine yenye migogoro, ikiwa ni pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Myanmar, Haiti, na Sudan.Alielezea jinsi watawala wa kiimla, wanasiasa wahubiri wa chuki, na walanguzi wanavyotumia machafuko kwa faida zao binafsi.Amesema Athari za migogoro huenea zaidi ya mstari wa mbele, zikiathiri minyororo ya usambazaji duniani na nafasi za kidijitali.Ametoa  wito kwa watu binafsi kutambua jukumu lao la pamoja kwa kufanya maamuzi ya kimaadili ya ununuzi, kushiriki kisiasa, na kuunga mkono uwajibikaji kwa ukiukwaji wa haki za binadamu.Hata hivyo amesema demokrasia zilizoimarika haziko salama dhidi ya kudorora kwa haki za binadamu. Türk  ameelezea wasiwasi mkubwa kuhusu mwelekeo nchini Marekani, ambako maendeleo kuhusu usawa wa kijinsia na sera za kupinga ubaguzi yanarudi nyuma.Pia amekosoa Shirikisho la Urusi kwa ukandamizaji wake wa jamii za kiraia na vyombo vya habari huru, ambapo wapinzani wanakabiliwa na unyanyasaji, kukamatwa, au kufurushwa.Kudhoofika kwa haki za binadamu katika mataifa yenye nguvu, Türk  alionya kwamba kunaweka mfano hatari kwa ulimwengu mzima, akisisitiza hitaji la dharura la mshikamano wa kimataifa na uwajibikaji kuhusu haki za binadamu.

Habari za UN
03 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 11:49


Karibu jaridani hii leo na mwenyeji wako ni Flora Nducha akikuletea habari kuhusu haki za binadamu, elimu ya STEM kwa wasichana wakimbizi nchini Kenya; Harakati za kuhamishia wakimbizi wa DRC nchini Burundi kuelekea maeneo salama; mafunzo ya ujasiriamali wa ushoni kwa wanawake na wasichana.Kwenye mkutano wa 58 wa Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu unaoendelea mjini Geneva Uswisi, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu  Volker Türk , amezungumzia hali ya kuzorota na kutoeleweka inayohusu haki za binadamu duniani, akionya kwamba ushawishi wa viongozi wa kiimla, matajiri wakubwa, na viongozi wa kimabavu unatishia kuvuruga maendeleo ya miongo kadhaa. Ripoti yake Anold Kayanda.Nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na wadau wengine wanafanikisha mpango wa kuhamasisha wasichana kuingia katika masomo ya STEM yaani Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati.Ripoti yake Sharon Jebiichi.Makala Assumpta Massoi anakupeleka mpakani mwa Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kusikia harakati za kuhamishia wakimbizi eneo salama zaidi.Mashinani anasalia nchini Jamhuri ya kidemkrasia ya Congo DRC kusikia jinsi ambavyo mafunzo ya ujasiriamali wa ushoni yanavyowawezesha wanawake na wasichana kujimudu kimaisha. Karibu

Habari za UN
Ukraine: Miaka 3 ya kumbukumbu mbaya, juhudi zifanyike mzozo uishe - Guterres

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 24, 2025 2:29


Mkutano wa 58 wa Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu umeanza leo jijini Geneva, Uswisi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumzia kiza kilichotanda duniani hivi sasa kutokana na mapigano  yanayoendelea sehemu mbalimbali kuanzia Ukraine, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC  hadi Ukanda wa Gaza, yakiambatana na ukiukwaji mkubwa wa haki, akitaka kila juhudi zichukuliwe kusaka amani ya kudumu. Selina Jerobon na taarifa kamili..

Habari za UN
24 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 24, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia miaka mitatu ya vita nchini Ukraine, machafuko nchini DRC na elimu Sudan Kusini. Makala inatupeleka katika ukanda wa Gaza kumulika harakati za chanjo ya polio, na mashinani nchini Kenya kusikia ujumbe kuhusu umuhimu wa lugha mama.Mkutano wa 58 wa Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu umeanza leo jijini Geneva, Uswisi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumzia kiza kilichotanda duniani hivi sasa kutokana na mapigano  yanayoendelea sehemu mbalimbali kuanzia Ukraine, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC  hadi Ukanda wa Gaza, yakiambatana na ukiukwaji mkubwa wa haki, akitaka kila juhudi zichukuliwe kusaka amani ya kudumu.Huko Gaza Kaskazini, kwenye eneo la wapalestina linalokaliwa na Israeli, wanafamilia zilizofurushwa makwao kutokana na vita kati ya Israeli na wanamgambo wa Hamas wanavumilia msimu wa baridi kali katika makazi ya muda ya mahema yanayopigwa na upepo na mvua usiku na mchana, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF. Nyumba zao zimeharibika na kuacha watoto kuishi katika mazingira mabaya.Katika makala Anold Kayanda wa Idhaa hii anaangazia chanjo inayoendelea katika Ukanda wa Gaza dhidi ya polio chini ya usimamizi wa Wizara ya Afya ya Palestina kwa kusaidiwa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa.Na mashinani ikiwa hivi majuzi Dunia iliadhimisha siku ya kimataifa ya lugha mama, tunakwenda Kajiado nchini Kenya kusikia ujumbe kuhusu umuhimu wa lugha mamaMwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
19 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 19, 2025 9:55


Hii leo jaridani tunaangazia msaada wa kibinadamu nchini DRC, na simulizi y amkimbizi wa DRC aliyekimbilia nchini Uganda. Makala inatupeleka nchini Tanzania, namashinani nchini Kenya, kulikoni?Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likifanya kikao cha dharura jijini New York, Marekani kujadili hali ya usalama inayozidi kuzorota kila uchao huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya kibinadamu nchini humo, Bruno Lermaquis amesema kupanuka kwa mzozo huo kumezidi kugharimu maisha na mustakabali wa raia.Sina mpango tena wa kurejea nyumbani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ni kauli yake Twagirayesu Gato, mwanafunzi huyu raia wa DRC aliyekimbia  nchini mwake mwaka jana na kuingia Uganda ambako sasa anapata hifadhi. Amesema hayo kwenye video ya shirika la Umoja wa MAtaifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR iliyochapishwa katika ukurasa wa YouTube wa shirika hilo.Makala inatupeleka nchini Tanzania ambako tunamsikiliza Brigedia Jenerali George Mwita Itang'are, Mkuu wa Kituo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani cha Tanzania (TPTC) akitoa wito kwa Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa kuendelea kuunga mkono ulinzi wa amani duniani kwa kuzikabili changamoto wanazokutana nazo walinda amani. Anold Kayanda anasimulia.Na mashinani ikiwa hivi majuzi Dunia iliadhimisha siku ya redio duniani fursa ni yake Irene munyua kutoka Kenya akieleza washirika wetu Radio Domus kuhusu umuhimu wa radio kwa jamii katika maisha ya kila siku.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
OCHA yasihi kufunguliwa kwa viwanja vya ndege Goma na Kavumu - DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 19, 2025 1:55


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likifanya kikao cha dharura jijini New York, Marekani kujadili hali ya usalama inayozidi kuzorota kila uchao huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya kibinadamu nchini humo, Bruno Lermaquis amesema kupanuka kwa mzozo huo kumezidi kugharimu maisha na mustakabali wa raia. Selina Jerobon na maelezo zaidi.

Habari za UN
14 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 14, 2025 11:25


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko na hali ya wakimbizi wa ndani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Makala inaturejesha hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa na mashinani inatupeleka nchini  Jamhuri ya Africa ya Kati (CAR), kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, lina wasiwasi mkubwa kuhusu janga la kibinadamu linalozidi kuwa baya tena kwa kasi kubwa huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kwani kushindwa kufikia wahitaji kumekwamisha ufikishaji misaada ya haraka inahoyitajika..Katika kitongoji cha Komanda jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, doria za pamoja zinazoendeshwa na walinda amani wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO na jeshi la serikali FARDC zimeimarisha usalama kwenye maeneo ya raia.Makala leo inaturejesha hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kwenye mkutano wa 63 wa Baraza la Kiuchumi na Kijamii ECOSOC kuhusu maendeleo ya jamii. Flora Nducha amepata fursa ya kuzungumza na mmoja wa washiriki wa mkutano huo kutoka Kenya.Na mashinani fursa ni yake Albertine Yantijba ,manusurawa ukatili wa kijinsia kutoka Sango CAR , ambaye anatueleza jinsi Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya watu na Afya ya Uzazi (UNFPA) limeletamabadiliko baada ya kuanzishwa kwa maeneo salama ya wasichana kujieleza na kuhudumiwa”Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
Kenya tumepiga hatua kuhakikisha maendeleo ya ustawi wa jamii: Mary Wambui Munene

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 14, 2025 4:58


Kikao cha 63 cha Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC kuhusu maendeleo ya ujamii kinakunja jamvi hii leo jijini New York Marekani baada ya majadiliano ya juma zima kuhusu maendeleo ya ustawi wa jamii, hatua zinazochukuliwa nan chi katika kufanikisha hilo na kuchagiza mshikamano wa kimataifa kutimiza lengo. Nchi mbalimbali zimetuma wakilishi kuanzia katika ngazi ya serikali, taasisi, mashirika yasiyo ya kiserikali na asasi za kiraia. Flora Nducha wa Idhaa hii amepata fursa kuzungumza na Mary Wambui Munene, mmoja wa washiriki kutokana Kenya. Ungana nao katika Makala hii

Habari za UN
13 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 13, 2025 11:05


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulika siku ya redio duniani, maudhui yakiwa Radio na Tabianchi, na ni kwa vipi chombo kinachodaiwa kutwamishwa na maendeleo ya teknolojia kinaendelea kusaidia kuelimisha umma kuhusu madhara ya mabadiliko ya tabianchi, Teonas Aswile wa TBC Taifa nchini Tanzania anaeleza.Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambapo hali inazidi kuwa tete na leo Mkurugenzi Mtendaji wa shirkika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, Catherine Russell, ameelezea wasiwasi mkubwa kuhusu kuongezeka kwa ghasia mashariki mwa mwa  nchi hiyo katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, ambapo watoto na familia wanakabiliwa na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.Naibu mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masiala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA nchini Sudan Edmore Tondhlana akizungumza na UN News amesema hali nchini Sudan inaendelea kuwa janga la kibinadamu wakati vita ikishika kasi na watu wakiendelea kufurushwa makwao. Amesema "Tunashuhudia hali ambapo Sudan ina mahitaji ya kibinadamu yaliyo miongoni mwa makubwa zaidi duniani. Takriban watu milioni 30 wanahitaji msaada wa kibinadamu. Hili ni ongezeko la takriban watu milioni tano zaidi ikilinganishwa na mwaka uliopita, pia, Sudan ina idadi kubwa zaidi ya watu waliopoteza makazi yao.Na leo ni siku ya Redio Duniani mwaka huu ikibeba maudhui Redio na mabadiliko ya tabianchi. Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO lengo la maudhui haya ni kudhihirisha jukumu la redio katika kusambaza ujumbe na kuelimisha kuhusu changamoto za mabadiliko ya tabianchi, kutanabaisha kuhusu hatua endelevu na kuwapa sauti wanaharakati wa mabadiliko ya tabianchi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo fursa ni yake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa      nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno “MSUMBI”.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Jifunze Kiswahili: maana za neno “MSUMBI”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 13, 2025 0:57


Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo fursa ni yake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa      nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno “MSUMBI”

RISE Urban Nation
Fearlessness, Fashion, and the Pursuit of Abundance with Haze Baraza

RISE Urban Nation

Play Episode Listen Later Feb 12, 2025 43:41


• Haze's early passion for fashion and how her Kenyan roots influenced her career• The biggest challenges she faced and how she overcame self-doubt• Her philosophy on fearlessness and abundance—and how you can apply it in your life• The power of representation in the fashion industry and beyond• Practical advice for entrepreneurs, creatives, and those stepping into their purpose 

Habari za UN
Mabaya zaidi nchini DRC yanakuja iwapo hatutauchukua hatua, aonya Mkuu wa Haki za Binadamu wa UN

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 7, 2025 2:18


Kamishna Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, leo akizungumza katika Kikao Maalum cha Baraza la Haki za Binadamu kinachofanyika jijini Geneva, Uswisi, ameonya kuwa ghasia zinazoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) zinaweza kuwa mbaya zaidi ikiwa hazitashughulikiwa. Flora Nducha na taarifa zaidi.

Habari za UN
07 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 7, 2025 10:56


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya haki za binadamu nchini Jamhuri ya kidemokasia ya Congo DRC, Na masuala ya afya nchini Jamhuri ya Congo, au Congo-Brazaville. Makala inatupeleka nchini Tanzania, na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Kamishna Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, leo akizungumza katika Kikao Maalum cha Baraza la Haki za Binadamu kinachofanyika jijini Geneva, Uswisi, ameonya kuwa ghasia zinazoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) zinaweza kuwa mbaya zaidi ikiwa hazitashughulikiwa.Wananchi wa Jamhuri ya Congo, au Congo-Brazaville, ni mashuhuda wa jinsi shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO limewasaidia kukabiliana na ugonjwa wa macho na ngozi unaosababishwa na nzi mweusi wanaozaliana kwenye mito na vijito, ugonjwa ambao uliathiri shughuli zao za kijamii na kiuchumi kutokana na muwasho wa kila mara na upofu.Katika makala Hamad Rashid wa Redio washirika KidsTime FM ya mkoani Morogoro Tanzania anaangazia kuhusu namna Tanzania inaendelea kufanikisha Lengo Namba 16 la Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa linalotilia mkazo upatikanaji wa amani, haki na taasisi imara kwa kupunguza mrundikano wa mashauri au kesi mahakamani, kuwezesha upatikanaji wa haki kwa makundi maalumu katika jamii.Na mashinani fursa ni yake Ahmed kutoka kaunti ya Laikipia nchini Kenya, ambaye kupitia video iliyoandalia na Shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji, IOM anaeleza jinsi ambavyo ukame wa mara kwa mara unavyoathiri mifugo ya.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
04 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 4, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kushuhudia sintofahamu na maombi ya wakazi wa Goma baada ya waasi wa M23 kutwaa mji huo. Mashinani tunakwenda Somalia na pia tunakuletea muhutasari wa habari.Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Bruno Lemarquis, ametoa wito wa kufunguliwa haraka kwa Uwanja wa Ndege wa Goma. Amesema uwanja huu uliofungwa kutokana na mapigano kati ya vikosi vya jeshi la DRC na waasi wa M23 ni muhimu kwa usafirishaji wa misaada ya kibinadamu. Hospitali zimejaa na maelfu ya raia hawana msaada wa dharura.Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la idadi ya watu na afya ya uzazi, (UNFPA), na la misaada ya kibinadamu na dharura (OCHA) leo yamesisitiza kuwa kusitishwa kwa ufadhili wa Marekani kunawaacha mamilioni 'hatarini'. Hayo yakijiri tayari imefahamika kuwa Rais Donald Trump anaiondoa Marekani katika Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu na pia kuacha kulifadhili shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi wa Kipalestina.Na ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Saratani, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) limeeleza kiasi takwimu kuhusu ugonjwa huo kwamba mathalani  kwa mwaka 2020 saratani ilisababisha vifo karibu milioni 10 sawa na kifo kimoja kati ya sita duniani. Aidha WHO imebainisha kuwa saratani zinazojitokeza zaidi ni saratani ya matiti, mapafu na utumbo mpana.Na katika mashinani  fursa ni yake Safiya Jeylaani, mkazi wa Barawe katika Jimbo la Kusini Magharibi mwa Somalia ambye baada ya kuhudhuria hafla ya kujadili umuhimu wa upatikanaji wa huduma za afya kwa Wasomali wote katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu iliyoandaliwa na Umoja wa Mataifa anasema jamii wanapaswa kuelimishwa kuhusu afya kutumia lugha mama.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!