Podcasts about Kwa

  • 197PODCASTS
  • 830EPISODES
  • 19mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • Sep 12, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about Kwa

Show all podcasts related to kwa

Latest podcast episodes about Kwa

Habari za UN
UNICEF yawawezesha vijana kwenye kilimo nchini Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 12, 2025 3:09


Kaunti ya Kirinyaga, iliyoko katikati mwa nchi ya Kenya kaskazini mwa mji mkuu wa nchi hiyo, Nairobi, inashuhudia mageuzi mapya katika sekta ya kilimo kupitia mradi wa kuwahusisha vijana  katika kilimo na lishe unaojulikana kama EKYAN. Mradi huu unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF, na wadau nchini humo.  Karibu Sabrina Saidi utupe taarifa zaidi.....(TAARIFA YA SABRINA SAIDI)Mradi wa EKYAN ni mfano wa ujasiriamali wa kilimo unaoongozwa na vijana, ukiwa na lengo la kutengeneza fursa za ajira, kuwanufaisha na kubadilisha maisha ya vijana walioko vijijini, kupitia mbinu bora za kilimo na lishe, ukitekelezwa kwa ushirikiano kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF, serikali ya kaunti ya Kirinyaga na shirika linalotoa mafunzo, elimu ya biashara ndogo ndogo na uwezeshaji barani Afrika KUZA Biashara.Felista Nyakio Mutungi kijana mkulima wa kaunti ya Kirinyaga, ni mmoja wa wanufaika wa mafunzo kupitia mradi huo. Na hapa anasema....CUT 2- Sauti ya Felista Nyakio Mutungi“Kabla ya kuanza kilimo, nilikuwa nauza barabarani viazi vya kukaanga au chipsi,  na mihogo, pamoja na nafaka. Haikuwa vizuri sana, lakini ndiyo nafasi pekee niliyokuwa nayo wakati huo. Kupitia serikali ya kaunti ya Kirinyaga, tulisajiliwa kama vijana wanaopenda kilimo na tukapata mafunzo kupitia KUZA na UNICEF. Sasa mimi ni mkulima na mjasiriamali.”Felista anasema awali alikuwa akilima robo ekari ya mpunga na kuvuna magunia manne hadi matano pekee. Lakini baada ya mradi wa EKYAN, kwa robo ekari hiyo hiyo sasa anapata hadi magunia saba. Aidha, shamba lake limepanuka hadi ekari nne katika eneo la 'mradi wa umwagiliaji wa Bura.Felista hakutaka kuwa mchoyo wa manufaa aliyopata, hivyo ameamua kueneza ujuzi wa kilimo cha kibiashara kwa kuwafundisha baadhi ya wakulima wengine mbinu na maarifa ya kilimo hiki.CUT- Sauti ya Felista  Nyakio Mutungi“Sasa si tu kwamba nalima, bali pia nawafundisha wakulima wengine kuongeza thamani katika mazao yao. Wanapata ujuzi wa kufanya biashara kupitia kilimo. Na kwa kweli tunawashukuru wahisani na UNICEF kwa kutuwezesha. Bila mpango huu, nisingekuwa hapa nilipo leo.”Kwa upande wake mtaalamu wa ubunifu wa UNICEF nchini Kenya Lilian Njoro, anaeleza kwa nini mradi huo ni muhimu kwa vijana.CUT- Sauti ya Lilian Njoro."Ni asilimia 10 pekee ya vijana wanaojihusisha na sekta ya kilimo. Kwa hivyo, kupitia mradi wa EKYAN, tulitaka kuona jinsi ya kuwahusisha vijana wengi zaidi katika kilimo na kuwavutia ili waweze kuanza kupata maisha yenye utulivu na ajira bora kupitia sekta hii.”Njoro anasisitiza kuwa teknolojia mpya zinafungua njia kwa kilimo cha kisasa tofauti na enzi za wazazi na mababu zao.Namna kilimo kinavyofanyika nyakati hizi ni tofauti na zamani,hii ni kwa sababu ya uwepo wa teknolojia bunifu, majukwaa ya kidijitali, na fursa nyingi.Kwa sasa, mradi wa EKYAN umeendelea kuwajengea vijana ujuzi, kuwapatia nafasi ya ajira, na kubadilisha mtazamo wao kuhusu kilimo, kutoka shughuli ya kizamani hadi kuwa biashara yenye faida.Link: https://youtu.be/hv17nk-2l5kTAGS:UNICEF Kenya/Kilimo/Biashara na ujasiriamali

Habari za UN
10 SEPTEMBA 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 10, 2025 10:18


Leo jaridani Assumpta Massoi anamulika kauli ya OHCHR kufuatia maandamano yanayoendelea Nepal; Utipwatipwa 'wapiku' utapiamlo na harakati za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi huko Karamoja nchini Uganda,Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu ameonesha wasiwasi mkubwa kufuatia ghasia zinazoendelea na kushika kasi nchini Nepal, huko barani Asia, ambako maandamano dhidi ya ufisadi na marufuku ya mitandao ya kijamii yamesababisha vifo vya watu wengi pamoja na majeruhi. Flora Nducha amefuatilia taarifa hiyo na anatupasha zaidi.Kwa mara ya kwanza idadi ya watoto na vijana wa umri wa kwenda shule wenye unene wa kupindukiaau utipwatipwa imezidi idadi ya watoto wenye utapiamlo duniani ikiathiri watoto milioni 188 sawa na mtoto 1 kati ya kila watoto 10 imesema leo ripoti iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. Tuungane na Leah Mushi kusikia zaidi kuhusu ripoti hiyo, karibu LeahKaramoja, eneo la kaskazini mashariki mwa Uganda, linakabiliwa na changamoto kubwa za tabianchi kama vile ukame wa mara kwa mara na milipuko ya magonjwa ya mimea na mifugo, hali inayotishia uhakika wa chakula. Kupitia mradi wa PROACT, mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la  Chakula na Kilimo Duniani (FAO), na Mpango wa chakula Duniani (WFP) pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu wa Uganda kwa ufadhili wa Muungano wa Ulaya, EU, wameshirikiana katika kuimarisha mifumo ya kushughulikia mabadiliko ya kiikolojia na kijamii. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
Türk ataka uwajibikaji wa vikosi vya usalama Nepal na waandamanaji wazingatie kanuni

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 10, 2025 2:49


Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu ameonesha wasiwasi mkubwa kufuatia ghasia zinazoendelea na kushika kasi nchini Nepal, huko barani Asia, ambako maandamano dhidi ya ufisadi na marufuku ya mitandao ya kijamii yamesababisha vifo vya watu wengi pamoja na majeruhi. Flora Nducha amefuatilia taarifa hiyo na anatupasha zaidi.Kamishna wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, akizungumza mjini Geneva amesema“nimeshtushwa na ongezeko la ghasia nchini Nepal ambalo limesababisha vifo kadhaa na kujeruhi mamia ya waandamanaji wengi wao wakiwa vijana, pamoja na uharibifu mkubwa wa mali.”Katika siku za karibuni, maandamano yaliyoanzia katika mji mkuu Kathmandu sasa yamesambaa katika miji na vijiji vya Nepal, yakiacha barabara zikifunikwa na mabaki ya vitu vilivyoteketezwa kwa moto na kulazimisha maduka kufungwa pia kuhofia usalama.Kwa mujibu wa duru za habari maandamano hayo yanayoo nngozwa na vijana wa kati ya umri wa miaka 13 hadi 28 au Gen Z yameshakatili Maisha ya takribani watu 22, kusababisha waziri mkuu wa nchi hiyo KP Sharma Oli kujiuzulu na kuliwasha moto jengo la bunge .Türk ametoa wito kwa vikosi vya usalama kujiepusha na mapambano na waandamanajI akisema, “Naomba vikosi vya usalama waoneshe uvumilivu wa hali ya juu, na kuepusha umwagaji damu na madhara zaidi. Vurugu siyo suluhisho. Mazungumzo ndiyo njia bora na ya pekee ya kushughulikia malalamiko ya watu wa Nepal. Ni muhimu sauti za vijana zisikike.”Waandamanaji wanasema wameshikwa na hasira kutokana na ufisadi na marufuku ya serikali juu ya majukwaa ya mitandao ya kijamii, ingawa kwa sasa huduma za mitandao ya kijamii zimerejea. Türk anasema anatambua haki yao ya kusikika, lakini pia amewasihi wawe na uwajibikaji.“Nawakumbusha waandamanaji kuwa nao pia lazima washikamane na kuzingatia dhamira ya kukusanyika kwa amani na wajiepushe na ghasia.”Türk ametaka uchunguzi wa haraka, wa wazi na huru ufanyike kuhusu madai ya matumizi ya nguvu kupita kiasi ya vikosi vya usalama, huku pia akilaani mashambulizi dhidi ya majengo ya umma, biashara, na hata maafisa waandamizi wa serikali.Amesisitiza kuwa dunia inathamini safari ya Nepal kutoka kwenye migogoro hadi kuwa na demokrasia yenye amani na ametoa mwito kwa wadau wote kulinda mafanikio hayo. Amesema Umoja wa Mataifa uko tayari kusaidia kupitia mazungumzo na hatua za kujenga imani ambazo zinaweza kusaidia kupunguza mvutano na kurejesha hali ya utulivu.

Habari za UN
Kwa mara ya kwanza watoto wenye utipwatipwa duniani ni wengi kuliko wenye utapiamlo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 10, 2025 2:59


Kwa mara ya kwanza idadi ya watoto na vijana wa umri wa kwenda shule wenye unene wa kupindukiaau utipwatipwa imezidi idadi ya watoto wenye utapiamlo duniani ikiathiri watoto milioni 188 sawa na mtoto 1 kati ya kila watoto 10 imesema leo ripoti iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. Tuungane na Leah Mushi kusikia zaidi kuhusu ripoti hiyo, karibu LeahRipoti hii mpya ya UNICEF iitwayo “Faida kwenye vyakula: Jinsi Mazingira ya Chakula yanavyowaangusha watoto” imechambua takwimu kutoka nchi zaidi ya 190 na kubaini kwamba kiwango cha watoto wenye utapiamlo kimepungua tangu mwaka 2000, lakini wale wenye unene wa kupindukia kimeongezeka mara tatu.Kwa sasa, utipwatipwa umeenea katika kila eneo la dunia isipokuwa Afrika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara na Asia Kusini. Nchi za visiwa vidogo vya Pasifiki ndizo zinaongoza kwa kuwa na viwango vya juu zaidi, ikiwemo Niue yenye asilimia 38 ya watoto wenye umri wa miaka 5 hadi 19 wakiwa na unene wa kupindukia.Nini kimesababisha?UNICEF inasema mabadiliko ya mifumo ya lishe kutoka vyakula vya asili hadi vyakula vya kutengenezwa kwa haraka na vya bei nafuu lakini vyenye sukari, mafuta na chumvi nyingi ndiyo chanzo kikuu cha ongezeko hili.Pia inatahadharisha kuwa matangazo ya kidijitali ya vinywaji vyenye sukari na vyakula vya viwandani yanawafikia vijana wengi, hata katika nchi zenye migogoro.Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEF, Catherine Russell, amesema utipwatipwa ni changamoto kubwa  ya kiafya kwa watoto kwa sababu huongeza hatari ya kupata kisukari, shinikizo la damu na magonjwa ya moyo katika maisha ya baadaye.Russell amesema “Tunapozungumza kuhusu utapiamlo, hatuzungumzii tu kuhusu watoto wenye uzito mdogo, utipwatipwa ni changamoto kubwa inayoendelea kuongezeka ambayo inaweza kuathiri afya na maendeleo ya watoto. Vyakula vya viwandani vinazidi kuongezeka na kuchukua nafasi ya matunda, mboga mboga na protini katika wakati ambao lishe ina jukumu muhimu katika ukuaji wa watoto, ukuaji wa utambuzi na afya ya akili.”Nini kifanyike?Ili kukabiliana na hali hii, UNICEF inazitaka serikali kuchukua hatua madhubuti ikiwemo kupiga marufuku uuzaji wa vyakula visivyo na lishe shuleni, kudhibiti matangazo ya vyakula vyenye sukari na mafuta, na kuweka sera za kusaidia familia kupata chakula bora na chenye lishe.Kwa mujibu wa UNICEF, bila hatua za haraka, gharama za kiafya na kiuchumi zitakazotokana na tatizo la utipwatipwa wa utotoni zinatarajiwa kupindukia dola trilioni 4 kila mwaka ifikapo mwaka 2035.Zipo juhudi za kupambana na hali hiyo ambazo zimeanza kuchukuliwa na baadhi ya nchi, mfano mzuri ni Mexico ambayo hivi karibuni imepiga marufuku uuzaji wa vyakula vilivyosindikwa na vile vyenye chumvi, sukari na mafuta mengi katika  maeneo ya shule za umma.

Habari za UN
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya,WHO laongeza orodha ya dawa muhimu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 8, 2025 3:05


Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO limefanya mabadiliko muhimu katika orodha yake ya dawa muhimu duniani au Essential Medicines List – EML na orodha ya dawa muhimu kwa watoto (EMLc) ikijumuisha dawa za kisasa za saratani, kisukari, unene uliopitiliza na magonjwa mengine sugu.Orodha za WHO za dawa muhimu ni nyenzo za mwongozo zinazotumiwa na zaidi ya nchi 150 kupanga ununuzi, bima za afya na upatikanaji wa dawa. Kwa lugha rahisi, dawa zinazoorodheshwa hapa huwa na nafasi kubwa zaidi ya kununuliwa na kutolewa kwa wagonjwa kupitia huduma za umma kwani wanachama wa WHO wanaziweka dawa hizi kama kipaumbele cha kiafya kwa mamilioni ya watu duniani.WHO wakati wakitangaza orodha hiyo mpya waliweka bayana kuwa dawa hizi mpya si za majaribio, bali ni zile ambazo zimethibitishwa kitabibu kuwa zinaokoa maisha, kupunguza madhara ya magonjwa na kuboresha maisha ya wagonjwa.Nini maana yake?Kuongezwa kwa dawa hizi ni hatua ya mbele katika safari ya kuhakikisha afya bora kwa wote. Inamaanisha wagonjwa zaidi wa saratani, kisukari na magonjwa mengine sugu wanaweza kuwa na matumaini ya maisha marefu na bora. Pia ni wito kwa mataifa kuchukua hatua ili kuhakikisha upatikanaji wa dawa unakuwa wa haki na usawa, bila kumwacha mtu yeyote nyuma.Changamoto ya bei na usawa wa kiafyaChangamoto kubwa sasa ni bei kubwa ya dawa hizi mpya, ambazo zinaweza kufanya wagonjwa wengi kushindwa kuzipata.WHO inapendekeza mikakati ya kupunguza gharama na kuhakikisha dawa hizi zinapatikana kwenye ngazi ya huduma za msingi za afya.Deusdedit Mubangizi, Mkurugenzi wa Sera na Viwango vya Dawa WHO, anasema “Sehemu kubwa ya matumizi ya nje ya mfuko wa magonjwa yasiyoambukiza yanaelekezwa kwenye dawa, ikiwa ni pamoja na zile zinazoainishwa kama muhimu na ambazo kimsingi, zinapaswa kupatikana kwabei rahisi kwa kila mtu. Ili kufikia upatikanaji sawa wa dawa muhimu kunahitajika mwitikio madhubuti wa mfumo wa afya unaoungwa mkono na dhamira dhabiti ya kisiasa, ushirikiano wa sekta nyingi na programu zinazozingatia watu ambazo hazimwachi mtu nyuma.”Kwa maneno mengine, dawa hizi haziwezi kuwa za matajiri pekee  lazima mifumo ya afya, serikali na sekta binafsi zishirikiane kuhakikisha kila mtu anayehitaji anapata dawa kwa gharama nafuu.© UNOCHA/Ali Haj SuleimanDaktari akimpatia matibabu mgonjwa wa Saratani huko nchini SyriaSaratani, kisukari na unene uliopitiliza ni changamotoSaratani na kisukari ni miongoni mwa magonjwa yanayosababisha vifo na ulemavu kwa mamilioni ya watu duniani kila mwaka. Kwa mfano, saratani pekee inaua karibu watu milioni 10 kila mwaka.Kuongeza dawa mpya za saratani kama pembrolizumab na atezolizumab, ambazo zinasaidia kinga ya mwili kushambulia chembe chembe za saratani, kunaleta matumaini mapya hasa kwa wagonjwa katika nchi zenye rasilimali chache.Kwa upande mwingine, dawa za kundi la GLP-1 receptor agonists kama semaglutide na tirzepatide zimeingizwa kwenye orodha ili kusaidia wagonjwa wa kisukari cha aina ya pili wanaoishi pia na unene uliopitiliza au matatizo ya moyo na figo. Dawa hizi husaidia kudhibiti sukari, kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo na figo, na pia kusaidia kupunguza uzito. 

Habari za UN
WMO: Ubora wa hewa duniani wazidi kuzorota japo kuna nafuu Asia na Ulaya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 5, 2025 2:59


Wakati mabilioni ya watu wakiendelea kuvuta hewa chafu inayosababisha zaidi ya vifo vya mapema milioni 4.5 kila mwaka, wataalamu wa hali ya hewa wa Umoja wa Mataifa leo Ijumaa (5 Septemba) wamebainisha madhara ya chembe ndogo ndogo za moshi kutoka katika moto wa nyika ambazo husafiri umbali mrefu duniani kote. Philip Mwihava na maelezo zaidi.(Taarifa ya Mwihava)“Ubora wa hewa hauheshimu mipaka,” anasema Lorenzo Labrador, Afisa wa Kisayansi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani (WMO). Anaendelea kueleza kwamba, “moshi na uchafuzi unaotokana na moto wa nyika katika msimu huu wa kihistoria katika Rasi ya Iberia tayari umepatikana Ulaya Magharibi, kwa hiyo athari zake hazibaki tu kwenye Rasi ya Iberia, bali zinaweza kusambaa kote barani Ulaya.”Akiwasilisha taarifa ya WMO kuhusu Hewa Safi na Tabianchi, ambayo inakusanya data kutoka vyanzo mbalimbali vya kimataifa, leo jijini Geneva, Uswisi Bwana Labrador ametangaza mwendelezo wa mwenendo wa kuzorota kwa ubora wa hewa duniani.Ameonyesha ramani ya dunia ya mwaka 2024 iliyoonesha alama za chembechembe ndogo zinazojulikana kama “PM 2.5” kutokana na moto wa nyika, zikionekana kwa alama nyekundu kwenye maeneo ya Chile, Brazil na Ecuador, pamoja na Canada, Afrika ya Kati na Siberia. Takwimu hizo zinathibitisha mwenendo wa kuendelea kwa kuzorota kwa ubora wa hewa duniani kama ilivyoonekana katika miaka iliyopita.Kwa upande wa habari njema, mwanasayansi huyo wa WMO amesisitiza kupungua kwa uzalishaji wa hewa chafuzi katika baadhi ya maeneo ya dunia.(Sauti ya Labrador) - sauti ya kiume“Tunaona mwenendo wa kuzorota kwa ubora wa hewa hasa kwa kuhusiana na PM 2.5, na pia tunaona kupungua kwa uzalishaji wa hewa chafuzi katika maeneo fulani ya dunia, hasa mashariki mwa China na Ulaya, mwaka baada ya mwaka.”Mfano mzuri uliotolewa katika taarifa ya leo mashariki mwa China, katika miji kama Shanghai, ambako kumepigwa hatua katika kuboresha ubora wa hewa kwa kufungua bustani zaidi na kupanda miti mingi. Na ingawa bado kuna msongamano mkubwa wa magari, mengi sasa ni ya umeme.Hata hivyo WMO inasema licha ya mafanikio hayo, miji michache tu duniani ina viwango vya ubora wa hewa chini ya vile vinavyopendekezwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO). Hii inamaanisha kuwa, licha ya maboresho ya karibuni, ubora wa hewa bado ni changamoto kubwa kwa afya ya umma.Umoja wa Mataifa unaongoza juhudi za kupambana na uchafuzi wa hewa majumbani ambao ni mojawapo ya vitisho vikubwa zaidi kwa afya ya umma duniani na hasa ni hatari kwa watoto.

Habari za UN
UNICEF: Mateso kwa watoto wa Gaza ni bayana

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 5, 2025 2:27


Sasa twende Gaza, hii ni hadithi ya maisha, ya watoto wa Gaza wanaokabiliana na baa la njaa, hofu, na kuporomoka kwa kila kitu kinachowaweka hai. Ni hadithi inayoelezwa kupitia macho ya wale wanaoshuhudia mateso kila siku wakiwemo madaktari, akina mama, na wahudumu wa kibinadamu wanaopiga kengele ya tahadhari. Miongoni mwa wahudumu hao ni Tess Ingram afisa mawasiliano wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF ofisi ya Kanda ya Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini. Flora Nducha anasimulia alichokishudia(TAARIFA YA FLORA NDUCHA)Tess aliyefunga safari na kushuhudia hali halisi Gaza akizungumza na waandishi wa habari kutoka mji wa Al Mawasi amesema mwenye macho haambiwi tazama na alichokishuhudia ni cha kutisha kwani jiji hilo sasa linazidi kuzama kwenye lindi la baa la njaa, vituo vya lishe vimefungwa, familia zinalia na kuhaha na watoto wanakufa kila uchao bila msaada.(Tess Ingram- Sheillah)“Jiji la Gaza, kimbilio la mwisho kwa familia za Kaskazini, linakuwa mahali ambapo utoto hauwezi kuishi. Ni jiji la hofu, wakimbizi na mazishi.”Anasema zaidi ya nusu ya vituo vya lishe vya watoto vimefungwa na kina mama wanapofika hospitalini wakiwa wamebeba watoto wao unaoweza kuhesabu mbavu sababu ya kukonda wanaambulia patupu kwani msaada ni haba na kwengine hakuna kabisa.(Tess Ingram 2-Sheilah):“Kilichokuwa hakifikiriki si jambo lijalo ni hali ambayo iko hapa tayari. Kuanguka kwa huduma muhimu na kunawaacha watoto wasiojiweza Gaza wakihaha kusalia uhai.”Tess anasema ukiingia katika vituo vya msaada ndio utatambua wanachokipitia watoto wa Gaza kwani, mateso yanaonekana bayana(Tess Ingram 3-Sheillah)“Saa moja tu ndani ya kliniki ya lishe inatosha kuondoa shaka na shuku yoyote uliyonayo ya endapo Gaza kuna baa la njaa.”UNICEF inasisitiza wito wake kuwa raia walindwe, msaada wa chakula na dawa upelekwe kwa wahitaji bila vizuizi. Kwa sababu watoto wa Gaza bado wako hai na dunia ina uwezo wa kuamua endapo wasalie hai.

Habari za UN
MINUSCA washiriki kutoa elimu ya usalama barabarani CAR

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 5, 2025 2:41


Kila mwaka,Wizara ya Uchukuzi na Usafirishaji wa Anga nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR,  kwa msaada wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MINUSCA,huandaa kampeni za usalama barabarani. Na hivi karibuni katika mji mkuu wa nchi hiyo,Bangui, MINUSCA kwa kushirikiana na Vikosi vya Usalama vya Ndani ISF wameungana kupambana na ajali za barabarani zinazoongezeka kila uchao,doria ya pamoja imefanyika kutoa elimu kwa watumiaji wa barabara. Sabrina Saidi anatujuza zaidi....​(TAARIFA YA SABRINA SAIDI)Natts ....ongeza hii; katikaa mitaa ya Banguimji mji mkuu wa CAR pisha nikupishe ni nyingi. Kufuatia ongezeko la ajali za barabarani,zinazopoteza maisha ya watu kila uchao, kikosi cha polisi cha Ujumbe wa Umoja wa Mataifa MINUSCA kimeendesha doria ya pamoja ya usalama kwa kushirikiana na Vikosi vya Usalama vya nchi hii (ISF) katika mji mkuu BanguiOperesheni hii iliyofanyika tarehe 4 mwezi Septemba,mwaka huu imelenga kutoa elimu kwa waendesha pikipiki za abiria maarufu kama "moto taxi" nchini CAR na watumiaji wengine wa barabara kuhusu umuhimu wa kufuata sheria za barabarani.Kwa mujibu wa MINUSCA Hatua hii ina lengo la kuimarisha usalama na kujenga uhusiano mwema kati ya vikosi vya usalama na raia.​Akizungumza kuhusu umuhimu wa hatua hii, Kamanda wa Mkoa wa Plateaux(PLATIU) na Bas-Oubangui(BA OBANGI), Douflé Avi Chico( DOFLE AVII CHIKO BERNAA) Bernard, amesema,CUT- Sauti ya Douflé Avi Chico Bernard“Kwa kushirikiana na MINUSCA, kupitia brigedi yao ya magari, tunafanya kazi ya kuongeza uelewa kwa watumiaji wa barabara, waendesha pikipiki au teksi, ili kupunguza ajali nyingi ambazo kwa bahati mbaya zinagharimu maisha ya watu. Tutaendelea na kampeni hizi kubwa ili kurekebisha hali hii.”​Kwa upande wa watumiaji wa barabara, dereva wa pikipiki za abiria, Jean Terence Bokassa (JANI TEREE BOKASA), ameomba serikali iimarishe udhibiti wa sekta hiyo.CUT- Sauti ya Jean Terence Bokassa“Tunaomba serikali ihakikishe usalama wa waendesha pikipiki za abiria kwa sababu sisi ni watu kama wengine. Tunatoka nje kutafuta riziki, lakini maisha yetu yako hatarini. Tungependa serikali itusaidie kwa kuwafundisha ndugu zetu ambao hawana leseni ya udereva kanuni za barabarani ili kuhakikisha usalama wao.”Nattss.. Sauti za magari honi nk.​Doria hii ya pamoja inaonesha ushirikiano mzuri kati ya Polisi wa Umoja wa Mataifa na ISF, wote wakiwa wamejitolea kulinda raia na kupunguza ajali za barabarani na MINUSCA inasema wananchi wakipata uelewa wa kutosha basio sio tu barabara zitakuwa salama bali pia idadi ya vifo vitokanavyo na ajali za barabarani vitapungua.

Habari za UN
Wakimbizi Nyarugusu wahamasika kufanya usafi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 3, 2025 2:40


Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR kwa kushirikiana na Baraza la Wakimbizi la Norway NRC wanahakikisha wakimbizi wanaoishi katika kambi za wakimbizi za mkoani Kigoma Magharibi mwa Tanzania ikiwemo kambi ya nyarugusu wanapata huduma muhimu za maji na usafi kupitia ushirikiano wa viongozi wa wakimbizi. Huduma hizo  zimekuwa changamoto kubwa katika kambi za wakimbizi zikichangiwa na ukata wa ufadhili. Flora Nducha na taarifa zaidi (TAARIFA YA FLORA NDUCHA)Vita vya wenyewe kwa wenyewe vilipoibuka Burundi mwaka 2015, na baadaye mapigano kuighubika upya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, maelfu ya  watu walikimbia na kuvuka mpaka kuingia Tanzania. Leo, wengi wao wanaishi katika kambi za wakimbizi mkoani Kigoma kama vile Mtendeli, Nduta, na Nyarugusu.Lakini maisha kambini hayajakuwa rahisi. Kwa ufadhili mdogo, familia zinapata shida kupata huduma za msingi kama maji safi, makazi, na elimu.Hapo ndipo Shirika la UNHCR, na Baraza la Wakimbizi la Norway NRC, wanapoingia. Tangu mwaka 2016, wamekuwa wakitoa huduma muhimu ikiwemo kufunga mifumo ya maji, kujenga vyoo, na kusambaza sabuni na mahitaji mengine ya usafi.Miongoni mwa wanaofanya mabadiliko kupitia msaada huo ni Ahunga Msama, mkimbizi mwenye umri wa miaka 55 kutoka DR Congo, ambaye ni afisa msimamizii wa huduma za maji, usafi, kujisafi na usafi wa mazingiira WASH katika kambi ya Nyarugusu.(AHUNGA CLIP 1)“Ninasaidia jamii yetu ya kambi ya Nyarugusu ili wawe wanapata maji safi na salama”Ahunga anasema jamii yake iliteseka sana iliteseka sana kwa magonjwa yanayosababishwa na maji machafu ndio maana aliamua kuchukua hatua kulinda afya zao. Kila siku ahakikisha watu wanapata maji safi na huduma za usafi salama.Akiwa pamoja na wakimbizi wenzake, Ahunga anapita nyumba kwa nyumba kufundisha familia jinsi ya kuzuia magonjwa kupitia usafi kwani anaamini elimu ni ufunguo(AHUNGA CLIP 2)“Tunasaidia kuelimisha jamii yetu ili wawe wasafi. Wawe na vyoo, wawe na mabafu, wawe na vichanja na wawe na mashimo ya takataka.”Watu wakielewa, wanaweza kujilinda.Anasema watu wakieelewa ni rahisi kujilinda na juhudi zake zinaokoa maisha na kuhamasisha wengine, zikionyesha kwamba hata katika mazingira magumu, wakimbizi wanaweza kuongoza mabadiliko katika jamii zao na anasema hilo ni la muhimu sana kwani(AHUNGA CLIP 3)“Tunasaidia jamii yetu ili wajilinde na magonjwa ya milipuko”Kwa msaada wa UNHCR na Baraza la Wakimbizi la Norway, maelfu ya wakimbizi katika kambi za wakimbizi za Kigoma sasa wana maji salama, usafi wa mazingira ni bora, na wana matumaini mapya ya maisha.

Habari za UN
UN yatumia kila mbinu kuhakikisha inawafikia waathirika wa tetemeko Afghanistan

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 3, 2025 2:22


Juhudi kubwa za msaada kwa waathirika wa tetemeko la ardhi lililoipiga Afghanstan mwishoni mwa wiki, zimeendelea leo huku watoa misaada wakikabiliwa hali ngumu ya kuwafikia wanaohitaji msaada kutokana na Barabara kuzibwa na kukatika kwa mawasiliano. Anold Kayanda na taarifa zaidi.(Taarifa ya Anold Kayanda)Taarifa mpya kutoka kwa timu za tathmini za Umoja wa Mataifa zilizofanikiwa kuwafikia waathirika katika wilaya ya milimani ya Ghazi Abad jana Jumanne kwa njia ya miguu, zimeweka wazi umuhimu wa kuendeleza tena kwa haraka msaada wa kibinadamu.Salam Al-Jabani kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) mjini Kabul anasema, “jambo la dharura ni kuwatoa watu chini ya vifusi na Watu wanasema wanachohitaji kwa haraka ni msaada wa kuwazika waliofariki dunia na kuwatoa waliofunikwa.”UNICEF inasema watoa misaada wake walilazimika kutembea kwa saa mbili ili kuwafikia watu na bado kuna vijiji ambavyo ili kuvifikia unahitaji kutumia saa sita hadi saba na hata helikopta hazijafanikiwa kufika huko.Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP ambao walikuwa wa kwanza kupeleka msaada kwenye eneo la tukio,  Bwana John Aylieff, akiwa mjini Kabul amesema, “WFP inaweza tu kumudu kuwalisha waathirika wa tetemeko la ardhi kwa wiki chache zijazo kabla ya ufadhili kuisha.”Kwa upande wake, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) linapeleka msaada muhimu wa dharura kutoka maghala yake yaliyopo Kabul, ikiwemo mahema, blanketi na taa za sola. Pia maelfu ya wanajamii wa eneo hilo wameelekea eneo lililoathirika kusaidia juhudi za uokoaji, wakiwa na maji na chakula.

Siha Njema
Utengano wa familia unaweza kuleta shinikizo la damu au kisukari

Siha Njema

Play Episode Listen Later Sep 2, 2025 10:04


Wanadamu ni viumbe ambao hukamilika wanapokuwa kwenye jamii ambapo wanaweza kuelezea hisia zao,kujihisi wanathaminiwa na wana mchango kwa wengine. Mambo  hayo yanapokosa,inaweza kuwa chanzo cha matatizo ya kiafya.Na hii ni hali ambao hukuwa nao wakimbizi ambao wametenganishwa na wapendwa wao. Katika kambi ya Kakuma iliyoko kaunti ya Turkana,kaskazini mwa Nchi ya Wakenya,tulizungumza na wakimbizi ambao walilazimika kutengana na wapendwa wao kwa sababu ya migogoro ya kifamilia,ukoo na hata vita. Ingawa wamepata makao katika kambi ya wakimbizi bado maisha yao hayajakamilika . Wengi wameishi kwenye hali ya upweke,huzuni na kiwewe  na kupata matatizo ya kiafya yakiwemo matatizo ya afya ya akili. Aidha kuna wale ambao wamepatwa na maradhi kama shinikizo la damu ,kisukari,ukosefu wa usingizi na chanzo ni matatizo ambayo wamekumbana nao katika kambi,ugumu wa maisha bila watu walio karibu nawe ambao unaweza kuzungumza nao na kuliwazana. Kamati ya kimataifa ya msalaba mwekundu,ICRC pamoja na shirika la msalaba mwekundu nchini ,KRC,katika kujaribu kukabili hali hiyo ,zinatekeleza mpango wa kujaribu kurejesha mawasiliano na uhusiano wa familia za wakimbizi. Kwa kuwatafuta namna ambao wakimbizi hao wanaweza kuwasiliana kupitia ujumbe wa kuandikiwa au  kwa njia ya simu,mashirika hayo wanasema wamefanikiwa kuwarejeshea tabasamu wachache wenye bahati na wanaendelea kuwasaka wanafamilia zaidi kila mwaka. Matunda ya mpango huo yameonekana miongoni mwa wakimbizi wanaozungumza na jamaa zao na pia kwa wahudumu wa kujitolea wanaotangamana karibu kila siku na wakimbizi hao kwenye kambi.

Habari za UN
Mradi wa MONUSCO kwa ushirikiano na PAMI waleta nuru kwa wakazi Nyiragongo, DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 27, 2025 4:04


Kwa zaidi ya muongo mmoja, eneo la Nyiragongo lililoko jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) limekumbwa na hali ya kutokuwepo kwa utulivu wa kudumu kutokana na uwepo wa makundi yenye silaha. Maelfu ya familia wamekimbia makazi yao na watoto wengi kulazimishwa kujiunga na makundi hayo ya kijeshi. Kati ya mwaka 2024 na 2025, kuzuka upya kwa mapigano kunakohusishwa na kuibuka tena kwa waasi wa M23 kumeongeza zaidi hali ya hatari kwa wakazi wa eneo hilo, hasa watoto na vijana. Ili kuleta ahueni kwa wakazi, Umoja wa Mataifa umechukua hatua. Je ni zipi hizo? Ungana basi na Anold Kayanda kwenye makala hii.

L'Heure H
La véritable histoire du pont de la rivière Kwaï

L'Heure H

Play Episode Listen Later Aug 27, 2025 41:40


La véritable histoire du pont de la rivière Kwaï Au printemps 1942, Loet Velmans, jeune soldat néerlandais, est fait prisonnier par les Japonais sur l'île de Java. Il est envoyé, avec des milliers d'autres captifs, travailler à la construction du "Chemin de Fer de la Mort", une ligne reliant la Thaïlande à la Birmanie. Le pont de la rivière Kwaï, rendu célèbre par un roman et un film, n'en est qu'un élément ; la réalité fut bien plus tragique. Loet endure violences, maladies et conditions inhumaines dans le Spring Camp. Blessé, il devient aide-soignant et assiste à l'horreur quotidienne. Le chantier, inutile militairement, a coûté la vie à plus de 250 000 personnes. Après la guerre, Loet retourne sur les lieux en 2000, choqué par leur transformation en site touristique. Il ne retrouvera jamais exactement son ancien camp. Ce récit rappelle l'absurdité et l'horreur d'un projet oublié derrière une fiction romancée. Merci pour votre écoute Vous aimez l'Heure H, mais connaissez-vous La Mini Heure H https://audmns.com/YagLLiK , une version pour toute la famille.Retrouvez l'ensemble des épisodes de l'Heure H sur notre plateforme Auvio.be :https://auvio.rtbf.be/emission/22750 Intéressés par l'histoire ? Vous pourriez également aimer nos autres podcasts : Un jour dans l'Histoire : https://audmns.com/gXJWXoQL'Histoire Continue: https://audmns.com/kSbpELwAinsi que nos séries historiques :Chili, le Pays de mes Histoires : https://audmns.com/XHbnevhD-Day : https://audmns.com/JWRdPYIJoséphine Baker : https://audmns.com/wCfhoEwLa folle histoire de l'aviation : https://audmns.com/xAWjyWCLes Jeux Olympiques, l'étonnant miroir de notre Histoire : https://audmns.com/ZEIihzZMarguerite, la Voix d'une Résistante : https://audmns.com/zFDehnENapoléon, le crépuscule de l'Aigle : https://audmns.com/DcdnIUnUn Jour dans le Sport : https://audmns.com/xXlkHMHSous le sable des Pyramides : https://audmns.com/rXfVppvVous aimez les histoires racontées par Jean-Louis Lahaye ? Connaissez-vous ces podcast?Sous le sable des Pyramides : https://audmns.com/rXfVppv36 Quai des orfèvres : https://audmns.com/eUxNxyFHistoire Criminelle, les enquêtes de Scotland Yard : https://audmns.com/ZuEwXVOUn Crime, une Histoire https://audmns.com/NIhhXpYN'oubliez pas de vous y abonner pour ne rien manquer.Et si vous avez apprécié ce podcast, n'hésitez pas à nous donner des étoiles ou des commentaires, cela nous aide à le faire connaître plus largement. Hébergé par Audiomeans. Visitez audiomeans.fr/politique-de-confidentialite pour plus d'informations.

PULS BIZNESU do słuchania
Akcyza na alko, weto prezydenta, zmiany w CPK i rezygnacja „bulteriera” Solorza. PB BRIEF

PULS BIZNESU do słuchania

Play Episode Listen Later Aug 26, 2025 16:19


Dziś w PB BRIEF najważniejsze tematy polityczne i gospodarcze: spór o podwyżkę akcyzy na wódkę i zapowiadane weto prezydenta, rezygnację Radosława Kwaśnickiego z funkcji prezesa 12 spółek fundacji Zygmunta Solorza, a także decyzje rządu w sprawie CPK i nowego portalu mieszkaniowego. Do tego świeże dane GUS o bezrobociu, decyzja banku centralnego Węgier, amerykańskie wskaźniki i oczekiwane wyniki Nvidii.

Habari za UN
Apoteza mwanae akikimbia machafuko

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 25, 2025 2:25


Machafuko yanayoendelea Kaskazini Mashariki mwa Burkina Faso yamefurusha maelfu ya watu, kukatili maisha na kuwalazimisha wengi kuwa wakimbizi ndani ya nchi yao. Miongoni mwa simulizi za kugusa ni ya Fadima Bandé mama aliyelazimika kufungasha virago kunusuru maisha yake na wanawe wawili lakini akaishia kupoteza mmoja, je ilikuwaje?  kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Flora Nducha anasimulia zaidi.Katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Dori Mashariki mwa Burkina Faso, sasa ni maskani ya Fadima, maisha hapa ni magumu na hana tena njia ya kujipatia kipato. Kila uchao analazimika kupambana kuhakikisha watoto wake wanapata angalau mahitaji ya msingi, anakumbuka safari ya uchugu kutoka Kijiji kwake Sohlan hadi hapaWakati tunakimbia mmoja wa binti zangu mapacha aliugua baada ya kunyeshewa na mvua kubwa na kupata mafua makali, wakati tayari alikuwa anaumwa utapiamlo. Tulimkimbiza hospitai mjini Sebba lakini akafariki dunia.”Baada ya kupata hifadhi kambini Dori Fadima akajaliwa mapacha wengine wawili ambao sasa wana umri wa miezi tisa na kwa bahati mbaya wote wana utapiamlo kutokana na changamoto ya chakula.“Hapa Dori tumebarikiwa watoto mapacha lakini wametukuta hatua makazi, hatuna chochote na tuna njaa na kibaya zaidi sikuwa hata na maziwa ya kutosha kuwanyonyesha”Watoto wa Fadima wamekuwa wakiishi kwa msaada wa kibinadamu unaotolewa na mashirika mbalimbali ikiwemo UNICEF ambayo sasa inasema hali yao inaweza kuwa mbaya zaidi kutokana na kupunguzwa kwa bajeti ya kimataifa misaada wanayoitoa na hivyo kuhatarisha maisha na mustakabali wa watoto wake. Fadima anasema“Unapotawanywa na machafuko huwezi kufanya kazi, unakuwa kama mtu asiye na ajira na hapo ndio madhila yanapokuwa makubwa zaidi, lakini bado hapa ni bora kuliko ningesalia kijijini kwetu.”Kwa mujibu wa UNICEF Burkina Faso ni moja ya migogoro ya kibinadamu iliyopuuzwa zaidi duniani. Ingawa UNICEF iko hapa kusaidia, lakini  inasema msaada zaidi unahitajika haraka.

Habari za UN
Tangu 2017 hadi leo warohingya wanahaha bila kujua mustakabali wao

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 25, 2025 1:46


Leo Agosti 25 ni miaka minane tangu kufurushwa kwa wingi watu wa kabila la Rohingya kutoka katika jimbo la Rakhine nchini Myanmar. Umoja wa Mataifa unatoa wito wa mshikamano wa kimataifa kuwasaidia kwani mateso kwa watu hao yanaendelea kuwa mabaya zaidi kila uchao. Anold Kayanda na taarifa zaidi.Asante AssumptaMyanmar (zamani ikiitwa Burma) ni nchi ya Kusini Mashariki mwa Asia yenye zaidi ya makabila 100, inayopakana na India, Bangladesh, China, Laos na Thailand.Warohingya wanafurushwa na kuteswa kwasababu mbalimbali zikiwemo za kihistoria kwa madai kuwa walitoka Bangladesh ingawa wameishi vizazi na vizazi nchini Myanmar. Pia sababu ya imani yao kwa uislamu miongoni mwa sababu nyingine.Ni miaka minane sasa tangu ufurushwaji mkubwa wa jami hii kutoka jimbo la Rakhine pwani ya Magharibi mwa Myanmar. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres anaonya kuwa Warohingya na raia wengine bado wanakabiliwa na ukiukaji wa haki za binadamu na kufurushwa. Anaeleza wasiwasi wake kuhusu tarifa za kufukuzwa na kupunguzwa kwa nafasi za hifadhi katika ukanda huo, huku wakimbizi walioko Bangladesh wakikabiliana na upungufu mkubwa wa msaada wa chakula, elimu na huduma za afya.Guterres anasisitiza tena wito wake wa kulindwa kwa raia wote kwa mujibu wa sheria za kimataifa na anataka mshikamano mkubwa wa kimataifa. Hata hivyo ana matumaini kuwa Mkutano wa Ngazi ya Juu kuhusu Rohingya utakaofanyika New York mwezi ujao utasaidia kupata suluhu za kudumu.Kwa upande wake, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, anaeleza kuwa jeshi la Myanmar na Jeshi la Rakhine bado wanaendeleza uhalifu mkubwa dhidi ya Rohingya bila kuchukuliwa hatua, kinyume na sheria za kimataifa na maagizo ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki na anatoa wito wa kukomesha matendo hayo ili kuvunja mzunguko wa vurugu.

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho
Mtokeo ya majadiliano ya kimataifa kuhusu mkataba wa kisheria wa kukabili taka za plastiki

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho

Play Episode Listen Later Aug 20, 2025 9:53


Kwa mara nyingine tena, dunia ilipoteza fursa muhimu ya kuwa na mkataba huo, majadilianao yakigonga mwamba kutokana na nchi kutofautiana kwenye baadhi ya maandishi.  

Habari za UN
12 AGOSTI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 12, 2025 9:59


Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Bahrain, wadau kwa kushirikiaa na ofisi ya Uwekezaji na Uendelezaji Teknolojia, ITPO ya shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda, UNIDO wanachukua hatua kuondolea wanawake umaskini kwa kuimarisha talanta walizonazo. Mengine ni kama yafuatayo..Leo ni siku ya Kimataifa ya vijana duniani maadhinisho yanafanyika jijini Nairobi nchini Kenya chini ya ushirikiano na shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani UNHABITAT. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amewatumia vijana ujumbe maalum akisema “Kwa kijana: Sauti yako, mawazo yako na uongozi ni muhimu.”Je, vijana wanasemaje kuhusu siku hii? Kutoka Dar es Salaam nchini Tanzania, Sabrina Saidi wa Idhaa hii amezungumza na baadhi yao.Na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani WFP limepokea zaidi ya dola milioni 2 kutoka Japan kwa ajili ya msaada wa chakula nchini Malawi. Kwa msaada huu WFP inatarajia kusambazana tani 1970 za mahindi katika msimu wa mwambo kwa mwaka 2025/ 2026.Na katika mashinani fursa ni yake Maryam Bukar Hassan al maaruf Alhanislam, mshairi kutoka Nigeria ambaye ni mwanaharakati wa haki za binadamu na Mchechemuzi wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Amani. Hivi karibuni alighani shairi lake kwenye tamasha la majira ya joto hapa      jijini New York, nchini Marekani.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Radio Wnet
"Kronika Paryska" Piotra Witta: Nowy prezydent, stare nadzieje

Radio Wnet

Play Episode Listen Later Aug 7, 2025 5:28


W swoim najnowszym felietonie publicysta komentuje historyczne doświadczenia Polaków z prezydentami III RP i z nadzieją, ale i ostrożnością, odnosi się do objęcia urzędu przez Karola Nawrockiego. Powitaliśmy nowego prezydenta, pożegnaliśmy dawnego– mówi Piotr Witt.Karol Nawrocki, jak zauważa, budzi nadzieje nie tylko w kraju, ale i wśród Polonii. Ale publicysta – doświadczony historią i polityką – nie ulega euforii. Przypomina, że i po poprzednikach oczekiwano wiele:Jaruzelski, Wałęsa, Kwaśniewski, Komorowski – doświadczyliśmy wszystkiego. Generał, elektryk, ekonomista, arystokrata.Piotr Witt przywołuje obraz polskiego wyborcy zmęczonego zawodami, nieufnego wobec lewicowych prezydentów, czasem wręcz sentymentalnie wspominającego... Bieruta.Duda bez protokołuW kontekście przeszłości Piotr Witt wspomina wizytę Andrzeja Dudy w Paryżu 28 października 2015 roku. Wydarzenie miało symboliczną wymowę. Prezydent był witany ciepło przez Polonię, choć – jak zauważa autor – nie było to wydarzenie należycie obsłużone przez oficjalne struktury państwa.Ambasada RP we Francji w tamtym czasie według publicysty nie umieściła żadnej informacji o wizycie na swoich stronach internetowych. Próżno było jej szukać w rubrykach „informacje” i „aktualności”. Brak też było doniesień w mediach francuskich. Witt ironizuje:Ambasada ma ataszat prasowy – od informowania mediów. Ale o wizycie nie wiedział nikt.To – jak podkreśla – rażący kontrast wobec czasów prezydentury Bronisława Komorowskiego, którego wizyty we Francji szeroko relacjonowały wszystkie media.Orędzie Karola NawrockiegoPiotr Witt kończy felieton mocnym akcentem – osobistym wrażeniem z orędzia prezydenta Nawrockiego. Przemówienie na Placu Zamkowym i inauguracyjne wystąpienie w Sejmie ocenia wysoko, wyraźnie oddzielając je od rytuału politycznego.To nie była zwyczajna mowa polityka, ale wypowiedź wybitnego męża stanu. Nie był to zwykły akt objęcia urzędu, ale akt objęcia władzy. Tego po nim oczekiwaliśmy wszyscy- podsumowuje Piotr Witt.

Siha Njema
Ukiwa utatembea hatua elfu saba kila siku unaweka magonjwa hatari mbali

Siha Njema

Play Episode Listen Later Jul 29, 2025 10:06


Utafiti uliofanywa wa shirika la utafiti wa afya Lancet Public Health umebaini hatua elfu 7 kila siku unapunguza hatari ya kupatwa na magonjwa ya Saratani,Kisukari,magonjwa ya moyo, shinikizo la damu,sonona na  kupoteza kumbu kumbu Kwa mujibu wa shirika la afya duniani ,WHO,mazoezi ya kudumu dakika 150 kila wiki au mazoezi makali ya dakika 75 ni mkakati wa kuimarisha afya. Katika makala haya nimejiunga na kundi la Nairobi Walk Movement,tawi la Buru Buru ambalo limejitoa kufanya matembezi ya kuanzia kilomita 10 hadi 20 na wakati mwingine hadi 40 kila Jumamosi asubuhi au Jumapili alasiri kuanzia saa tisa na nusu. Kundi hili pia limejisajili kwenye kundi  la kuhesabu hatua ambazo kila mtu hutembea kila siku ,hatua hizo zikihesabiwa kutumia application maalum ya kuhesabu hatua,lengo likiwa hatua hadi elfu 10 kila siku. Kushindana kwa kuhesabu hatua kila siku umekuwa mchezo ambao huwatia moyo Wanachama hao wameelezea faida nyingi kutokana na kujiunga kwenye kundi hilo na kushiriki matembezi. Wapo waliokuwa na wanatumia dawa za kudhibiti shinikizo la damu na sasa wameachana nazo. Aidha wengine wameeleza matembezi kuwaondolea maumivu ya viungo na pia kupata marafiki wazuri.

Habari za UN
Mauaji ya raia Komanda, Ituri, MONUSCO yalaani waasi wa ADF

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 28, 2025 1:47


 MONUSCO, ambao ni Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, imelaani vikali shambulio lililoanza usiku wa juzi tarehe 26 hadi jana 27 Julai 2025 huko Komanda eneo la Irumu, takribani kilomita 60 kusini-magharibi mwa Bunia mji mkuu wa jimbo la Ituri, mashariki mwa nchi. Anold Kayanda ameifuatilia taarifa hiyo na anatujuza zaidi.Taarifa iliyotolewa na MONUSCO jijini katika mji mkuu wa DRC, Kinshasa imeeleza kwamba kwa mujibu wa taarifa za uhakika, shambulio hilo lililofanywa na wapiganaji wa kundi la waasi wa Allied Democratic Forces (ADF) limesababisha vifo vya raia wasiopungua 43 (wanawake 19, wanaume 15 na watoto 9).Inaripotiwa kuwa waathirika wengi waliuawa kwa kutumia silaha za jadi wakiwa ndani ya nyumba ya ibada. Watu kadhaa walitekwa nyara. Nyumba na maduka pia yalichomwa moto, jambo ambalo limezidisha zaidi hali mbaya ya mazingira ya kibinadamu ambayo tayari ni ya kutisha katika jimbo hilo.Naibu Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa Masuala ya Ulinzi na Operesheni ambaye pia ndiye Kaimu Mkuu wa MONUSCO, Vivian van de Perre, amenukuliwa akisema, “mashambulizi haya ya kulenga raia wasio na hatia, hasa ndani ya nyumba za ibada, ni ya kushtusha na ni kinyume kabisa na viwango vyote vya haki za binadamu na sheria ya kimataifa ya kibinadamu. MONUSCO itaendelea kushirikiana kwa karibu na mamlaka za DRC ili kuwalinda raia kwa mujibu wa mamlaka yake.”Kwa kushirikiana na mamlaka za eneo, MONUSCO imetoa msaada kwa hatua za awali, ikiwemo kuratibu shughuli za maziko na kutoa huduma za matibabu kwa majeruhi. Wakati huohuo, MONUSCO imeongeza juhudi za kiusalama ndani na nje ya eneo la Komanda kwa kuongeza idadi ya doria katika eneo hilo.MONUSCO imeweka wazi kuwa inasalia na dhamira thabiti ya kushirikiana na mamlaka za DRC na jamii za wenyeji kusaidia kuzuia mashambulizi mengine, kuwalinda raia, kupunguza mvutano, na kuchangia katika kuimarisha utulivu katika maeneo yaliyoathiriwa na machafuko ya kivita.Ujumbe huo wa Umoja wa Mataifa umeeleza masikitiko na ghadhabu kubwa juu ya vitendo hivi vya kikatili, ambavyo ni ukiukaji mkubwa wa sheria ya kimataifa ya kibinadamu na haki za binadamu. Ujumbe huu unatoa rambirambi zake za dhati kwa familia na jamii zilizoathirika na unasisitiza mshikamano wake na wakazi wa maeneo hayo. MONUSCO pia inazitaka mamlaka za DRC kufanya uchunguzi wa kina kuhusu mauaji haya na kuwafikisha wahusika mbele ya sheria.Aidha, MONUSCO imeurudia wito wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa makundi yote ya waasi kutoka nchi za nje kuweka silaha chini bila masharti na kurejea katika nchi zao za asili.

Habari za UN
Kujituma na kutokata tamaa ndio siri ya kufanikiwa kwenye mafunzo kwa vitendo UN - Sarah Nshoka

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 16, 2025 3:27


Kutoka Dar es Salaam hadi Geneva, na sasa New York. Ni safari ya kujifunza, kujaribu na kufanikiwa. Kwa vijana wengi barani Afrika, Umoja wa Mataifa huonekana kuwa ndoto isiyowezekana. Lakini kijana huyu kutoka Tanzania anathibitisha kuwa kwa nia thabiti na bidii, ndoto hiyo inaweza kuwa kweli. Kupitia programu ya mafunzo kwa vitendo ya Umoja wa Mataifa, amejifunza mengi kuhusu utawala, maendeleo na kujenga ujasiri wa kushiriki katika kazi za kimataifa. Sarah Nshoka alipata fursa kuzungumza na Shraon Jebichii katika makala hii.

Laïcidade, la voix laïque et sociale
Laïkino #152 : Les films sur la seconde guerre mondiale

Laïcidade, la voix laïque et sociale

Play Episode Listen Later Jul 9, 2025 3:23


Alain Defremont chroniqueur cinématographique de l'UFAL vous présente les films :« Le pont de la rivière KwaÏ », « Le jour le plus long », « La grande vadrouille »Hébergé par Ausha. Visitez ausha.co/politique-de-confidentialite pour plus d'informations.

Habari za UN
Pamoja na mafanikio makubwa bado kuna changamoto kumjumuisha kikamili mwanamke mwenye ulemavu Zanzibar: Ms. Abeida Abdallah

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 7, 2025 3:33


Kisiwa cha Zanzibar nchini Tanzania Mashariki mwa Afrika kimepiga hatua kubwa katika suala la ujumuishaji wa watu wenye ulemavu katika sekta mbalimbali kwa kuzingatia mikataba ya Umoja wa Mataifa ya watu wenye ulemavu na pia usawa wa kijinsia kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma. Lakini licha ya mafanikio waliyoyapata katika masuala kama elimu na haki za watu wenye ulemavu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Abeida Rashid Abdallah akizungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii kandoni mwa kikao cha mwaka huu cha 69 cha kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW69 amesema bado kuna kibarua kikubwa cha kufanya kuhakikisha kila mtu  hususan mwanamke mwenye ulemavu anajumuishwa. Kwa undani zaidi ungana nao katika makala hii.

Habari za UN
Vijana wakumbatia kilimo bunifu kupambana na mabadiliko ya tabianchi Kajiado nchini Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 30, 2025 3:20


Kwa mujibu wa wataalamu wa kilimo, teknolojia imefungua njia mpya ya kuinua maisha ya wakulima wadogo, hasa kwa kutumia ukulima wa kisasa unaotumia maarifa na Teknolojia. Sharon Jebichii anatupeleka kaunti ya Kajiado, Kenya, katika eneo la EMbulbul, kukutana na vijana wanaotumia maarifa ya kilimo cha kisasa kubadilisha maisha yao na ya jamii.

Habari za UN
26 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 26, 2025 10:13


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania, ambako mshikamano na wakimbizi unatekelezwa kwa vitendo na mashirika ya Umoja Mataifa likiwemo lile la Chakula na Kilimo (FAO) na la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kupitia Programu wa Pamoja ya Kigoma (KJP).Katika siku ya kimataifa ya kupambana na dawa za kulevya na usafirishaji haramu, ripoti mpya ya dunia ya Dawa za Kulevya mwaka 2025 iliyotolewa leo imeonya kuwa kutokuwepo kwa utulivu duniani kunachochea ongezeko la matumizi ya dawa za kulevya na uhalifu wa kupangwa. Kwa mujibu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Dawa na Uhalifu UNODC, watu milioni 316 walitumia mihadarati mwaka 2023. Mkurugenzi Mtendaji wa UNODC, Ghada Waly, amesema "Makundi haramu yanatumia migogoro kama fursa tunahitaji ushirikiano na uwekezaji kulinda jamii zetu.”Leo ni kumbukizi ya uzinduzi wa Chata ya Umoja wa Mataifa miaka 80 iliyopita mjini San Francisco, hatua iliyoweka msingi wa kuundwa kwa Umoja wa Mataifa mnamo Oktoba 24, 1945. Katibu Mkuu António Guterres anasema Umoja wa Mataifa bado unaakisi matumaini yaliyozaliwa kutoka kwenye majivu ya vita naye mwanahistoria Stephen Schlesinger akizungumza na UN News ameakumbusha kuwa “Chata hii ilikuwa kilio cha wanadamu wakitafuta amani, suluhu za mazungumzo, na maisha bora duniani.”Asilimia 93 ya kaya Gaza hazina uhakika wa maji safi kutokana na ukosefu wa mafuta unaopelekea mifumo ya maji kukaribia kusambaratika yameonya mashirika ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yakiongeza kuwa familia zinakumbwa na njaa kali, wakila mlo mmoja kwa siku huku watu wazima wakikosa kula ili kuwasaidia watoto na wazee.Na leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya neno "AFRITI KIJITI”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
19 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 19, 2025 10:44


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina, ikiwa kesho tarehe 20 mwezi Juni ni siku ya kimataifa ya wakimbizi maudhui yakiwa Mshikamano na Wakimbizi, tunakupeleka kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyoko kaunti ya Turkana, kaskazini-magharibi mwa Kenya.Uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje FDI umeshuka kwa mwaka wa pili mfululizo, ukihatarisha mustakabali wa maendeleo katika nchi zinazoendelea, kwa mujibu wa wa ripoti iliyotolewa leo na kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD. ikionya kuwa pengo la mitaji linaongezeka huku sekta muhimu kama nishati safi na miundombinu zikikosa ufadhili wa muda mrefu.Katika siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono kwenye mizozo, Umoja wa Mataifa umetoa onyo kuwa ukatili wa kingono unazidi kutumika kama silaha ya vita huku wanawake na wasichana wakiathirika zaidi. Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA "Huu si uharibifu wa bahati mbaya  ni uhalifu wa kivita. Na waathirika lazima wawe kiini cha amani, haki, na urejeshwaji wa maisha."Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa  Duniani (WHO) leo limezindua mwongozo wake wa kwanza wa kimataifa wa kudhibiti ugonjwa wa seli mundu (sickle cell) wakati wa ujauzito, ukilenga kupunguza hatari za maisha kwa mama na mtoto. WHO inasema wanawake wenye ugonjwa huu wana hatari hadi mara 11 zaidi ya kufariki dunia wakati wa ujauzito. Hivyo huduma bora za afya zinaweza kuokoa maisha, lakini visa vya seli mundu vinaongezeka duniani, huku Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara ikichangia asilimia 80.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIHORO!.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Total Trax
David Lean – Chapitre #1

Total Trax

Play Episode Listen Later Jun 17, 2025 85:46


Alors que l'esprit s'amuse d'une brève rencontre avec Madeleine, trouvant enfin chaussure à son pied au détour de vacances à Venise, les amants passionnés franchissent allègrement le mur du son, tandis que ceux qui servent en mer nourrissent les grandes espérances de voir Oliver Twist traverser un jour le pont de la rivière Kwaï. Pendant ce temps, David Lean écoute le tout premier épisode de Total Trax qui lui est consacré.Hébergé par Ausha. Visitez ausha.co/politique-de-confidentialite pour plus d'informations.

Habari za UN
12 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 12, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kupinga utumikishaji wa watoto ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani, ILO, linasema maudhui ni Maendeleo yako dhahiri, lakini bado kuna mengi ya kufanya: Hebu tuongeze kasi. Tunakupeleka nchini Tanzania kumulika harakati za kuwaepusha watoto kutumikishwa.Watu waliolazimika kukimbia makazi yao kutokana na vita, ukatili na mateso duniani kote imefikia kiwango cha juu kisichovumilika, hasa wakati huu ambapo ufadhili wa misaada ya kibinadamu unapungua kwa kasi. Kwa mujibu wa Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi UNHCR iliyotolewa leo kuhusu mwelekeo wa Ulimwengu, kufikia mwisho wa Aprili mwaka huu, kulikuwa na watu milioni 122.1 waliolazimika kuhama kwa nguvu, ikilinganishwa na watu milioni 120 mwaka uliopita katika kipindi kama hicho.Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya kupinga ajira kwa watoto, utafiti uliofanywa na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la kazi duniani, ILO na la kuhudumia Watoto UNICEF unaonesha licha ya hatua zilizopigwa, ajira kwa watoto bado inaathiri watoto milioni 138 duniani kote, kati yao milioni 54 wakifanya kazi hatarishi ambazo zinaweza kuhatarisha afya yao, usalama wao au maendeleo yao kwa ujumla.Nchini Sudan Kusini watu wako katika hatari ya njaa katika miezi ijayo, kutokana na kuongezeka kwa mapigano katika jimbo la Upper Nile. Utafiti mpya kutoka katika Mfumo wa Uainishaji wa Viwango vya Uhakika wa Chakula (IPC) unaonesha kudorora kwa hali ya chakula na lishe katika maeneo ya Sudan Kusini yaliyoathiriwa na mapigano katika miezi ya karibuni.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno "MBEUZI, MNYWANYWA NA MACHAGU.”Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
10 JUNI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 10, 2025 10:50


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka katika ukanda wa Gaza, huko mashariki ya Kati kwenye eneo la Palestina lialokaliwa kimabavu na Israeli ambapo vinazidi kuibua changamoto mpya kila uchao.Changamoto ya uzazi duniani si kuhusu watu kukataa kuwa wazazi ni kuhusu kunyimwa fursa ya kuchagua kuwa mzazi imesema ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA iliyotolewa leo na kuonesha kuwa kuwa matatizo ya kiuchumi, ukosefu wa usawa wa kijinsia, na hofu kuhusu maisha ya baadaye vinawazuia mamilioni ya watu kupata familia wanazotamani.Tishio la baa la njaa linaendelea kuiandama Sudan iliyoharibiwa vibaya na vita, limeonya leo Shirika laUmoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP, likitoa wito wa dharura kwa jamii ya kimataifa kusaidia kukidhi mahitaji yanayoongezeka na kuzuia maafa zaidi ya kibinadamu.Kwa mara ya kwanza dunia inaadhimisha siku ya kimataifa ya Mazungumzo baina ya Ustaarabu tofauti yenye lengo la kuchagiza amani, maelewano na mshikamano katika ulimwengu wa sasa uliogubikwa na chuki na mizozo.Na katika mashinani fursa ni yake Maria “Mãezinha” Sábado de Horta Fidalgo, Rais wa Ushirika wa wavuvi wadogo wa samaki katika kijiji cha Rincão kilichoko kisiwa cha Santiano nchini Cabo Verde barani Afrika anaelezea jinsi wanakabiliana na uhaba wa samaki kwenye eneo lao, na hii ni kutokana na mradi wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs unaotekelezwa na mashirka ya Umoja wa Mataifa.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Poranna rozmowa w RMF FM
Aleksander Kwaśniewski: Jestem zasmucony, ale nie zaskoczony

Poranna rozmowa w RMF FM

Play Episode Listen Later Jun 2, 2025 23:59


"Jestem zasmucony, ale nie zaskoczony" – tak wynik drugiej tury wyborów na prezydenta Polski skomentował były prezydent naszego kraju, Aleksander Kwaśniewski. Był on gościem Tomasza Terlikowskiego w Porannej rozmowie w RMF FM. Kwaśniewski został zapytany o to, jakim – jego zdaniem – prezydentem może być Karol Nawrocki. Jaką głową państwa będzie prezes Instytutu Pamięci Narodowej? "Drogi są dwie" – stwierdził były prezydent Polski.

De Grote Podcastlas
Werelddelen #2: Afrika

De Grote Podcastlas

Play Episode Listen Later May 29, 2025 88:54


Behalve backpackers die hun fotoalbum van een zomertje Thailand, Cambodja en Vietnam steevast “Azië” noemen, is er geen grotere geografische generalisatie dan het concept ‘Afrika'. 54 landen plus een rafelrandje, gereduceerd tot een handzaam pakketje vooroordelen en snel getrokken conclusies, die zó makkelijk toepasbaar zijn op nieuwsberichten en borrelpraat dat ze ons altijd in ons gelijk bevestigen. Nuance is het schrikbeeld in ons denken over Afrika, want nuance kost moeite. En dus is het lopen op linguïstische eieren. Is het Afrika-correspondent of correspondent Afrika? Spreken we simpelweg van ‘Afrika' of van ‘het Afrikaanse continent'? Nuance, nuance, nuance. Veel meer dan wij in deze anderhalf uur kunnen bieden.

Radio Omniglot
Omniglot News (25/05/25)

Radio Omniglot

Play Episode Listen Later May 25, 2025 2:15


Here's the latest news from the world of Omniglot. New language pages: Kebu (Kǝkpǝǝkǝ), a Kwa language spoken in southern Togo and southeastern Ghana. Bangubangu (Kibangubangu), a Bantu language spoken in the east and south the Democratic Republic of the Congo. Cherepon (Kyiripong), a Kwa language spoken in the Eastern Region of Ghana. New numbers […]

Habari za UN
22 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 22, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini kumsikia mgeni wetu Prof. Wallah Bin Wallah, mwandishi mashuhuri wa vitabu vya Kiswahili kutoka Kenya ambaye anamulika umuhimu wa vitabu katika kukuza lugha ya Kiswahili. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno.Kwa mara ya kwanza tangu mwezi Februari, msaada wa kuokoa maisha umefika Gaza. Baada ya wiki 11 za kizuizi kutoka kwa mamlaka za Israeli, malori 198 yaliyobeba chakula, dawa na unga wa ngano yameingia leo kupitia mpaka wa Kerem Shalom kwa mujibu wa mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa.Mratibu mkuu wa misaada wa Umoja wa Mataifa, Tom Fletcher, ameiitaja hatua hiyo kuwa ya muhimu sana, huku malori 90 yakipakuliwa usiku kwa ajili ya kusambazwa haraka.Mwaka 2024, vita havikuishia kwenye uwanja wa mapambano pekee      vilivunja nyumba, masoko na shule. Kuanzia Gaza hadi Ukraine, Sudan hadi Myanmar na zaidi ya raia 36,000 walipoteza maisha yao katika mizozo 14 ya kivita kulimgana na ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kwa Baraza la Usalama hii leo linalojadili ulinzi wa raia katika mizozo ya silaha.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DAHARI”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Bi. Joy :Teknolojia inatatua changamoto za kijamii - Wasichana katika TEHAMA

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 12, 2025 3:38


Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO, sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano TEHAMA, au ICT inaendelea kutawala na kuunda fursa mpya, lakini wanawake bado wanakumbana na changamoto kubwa ya upungufu wa uwakilishi. Hata hivyo, wanawake wanavuka mipaka na sasa Bi. Joy, msichana kutoka Nairobi Kenya, ambaye ni mtaalamu katika teknolojia ya kidijitali, amekalia nafasi muhimu katika kubadili mtindo wa maisha kupitia elimu ya ICT. Katika mahojiano na washirika wetu Radio Domus, alizungumzia umuhimu wa kuhamasisha wasichana kujiunga na masomo ya teknolojia ili kutengeneza mustakabali mpya wa kidijitali, na kubadili dunia kwa njia ya kidigitali na usawa. Sharon Jebichii na Makala zaidi

Habari za UN
Chokoleti itengenezwayo Uganda yavuka mpaka na mabara -UNCTAD

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 9, 2025 3:55


Kutoka kakao ghafi huko Bundibugyo, magharibi mwa Uganda hadi Kampala mji mkuu wa kibiashara wa taifa hilo la Afrika Mashariki ndiko kunapatikana kiwanda cha kutengeneza chokoleti cha Equator kinachomilikiwa na Barbara Gonget na mume wake Gustav. Awali wazo la biashara hii lilionekana kutokuwa na mashiko. Ingawa hivyo baada ya ITC, ambacho ni Kituo cha Kimataifa ha Biashara kilicho chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo, UNCTAD pamoja na wadau wao kuweka usaidizi wao, hali imebadilika na sasa biashara inavuka sio tu mipaka bali mabara. Wawili hao Kwa kuchanganya mbinu za hali ya juu, zinazojali jamii, na ufundi wa kitaalamu, wanabadili taswira ya uzalishaji wa chokoleti nchini humo.Je wamefanya nini? Assumpta Massoi anafafanua zaidi kwenye makala hii iliyofanikishwa na ITC.

Men. Men. Men. - The Podcast -
Embracing The Legacy, Creating My Own Path

Men. Men. Men. - The Podcast -

Play Episode Listen Later May 6, 2025 101:36


“Walking in the shadow of a giant” si jambo rahisi—na inakuwa ngumu zaidi pale “Giant” huyo akiwa  ni Augustine Mahiga, mwanadiplomasia mashuhuri wa Tanzania, na wewe ni mtoto wake wa kiume, unayejulikana kama Andrew Mahiga.Kwa wengi, jina la mwisho linaweza kufungua milango, lakini je, kila nafasi unayoipata ni kwa sababu ya uwezo wako au kwa sababu unaitwa Mahiga? Hilo ndilo swali ambalo Andrew amekuwa akilazimika kulikabili katika safari yake ya kujitambua.Katika episode hii ya kipekee ya Men Men Men: The Podcast, Andrew anakaa nasi na kufungua moyo wake kuhusu changamoto za kuishi na jina kubwa, shinikizo la kulingana na hadhi ya baba, na hatimaye furaha aliyopata alipogundua kuwa—ndiyo, yeye ni mtoto wa baba yake, lakini si lazima awe kama baba yake.Zaidi ya hayo, Andrew anazungumzia kwa kina umuhimu wa mentorship kwa wanaume—na jinsi kuwepo au kutokuwepo kwa wanasihi kunaweza kumjenga au kumvunjilia mbali mwanaume wa Kitanzania.Baada ya kuisikiliza episode hii, utaelewa kwa nini tumeiita: "Embracing the Legacy, Creating My Own Path."

Habari za UN
VoTAN sio tu mtandao wa kidijitali kusaidia manusura wa ugaidi bali pia ni familia - Manusura

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 5, 2025 5:02


Hatimaye kilio cha manusura wa ugaidi duniani cha kuwa na Mtandao wa Mashirika yao ili kuweza kupaza zaidi sauti zao kwa ajili ya sio tu kusaidiwa bali pia kuepusha matukio kama hayo, kimepata jawabu baada ya Mtandao huo au VoTAN kuzinduliwa kwenye Umoja wa Mataifa. Kwa msaada wa kifedha kutoka Hispania, Iraq na nchi nyingine wanachama, mtandao huu ulio chini ya Programu ya kusaidia manusura wa ugaidi kwenye Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabilana na Ugaidi, UNOCT, unatarajiwa kuziba mapengo ya msaada na kuinua ushuhuda wa manusuta kutoka maeneo yaliyopuuzwa duniani. Assumpta Massoi amefuatilia uzinduzi huo na kuandaa makala hii.

Habari za UN
Tume huru ya UN ya kusaka ukweli kuhusu Sudan imelaani vikali mauaji ya watu zaidi ya 100

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 14, 2025 2:02


Vita ya sasa ya Sudan ikielekea kuingia mwaka wa tatu, Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya kusaka ukweli kuhusu Sudan imelaani vikali mauaji ya watu zaidi ya 100 yaliyotokea wikiendi hii katika kambi za wakimbizi wa ndani Darfur, ikionya kwamba hali inaweza kuwa mbaya zaidi. Anold Kayanda na taarifa zaidi.(Taarifa ya Anold Kayanda)Shukrani LeahTangu kuanza kwa vita kati ya Jeshi la Sudan (SAF) na kikosi cha waasi cha RSF mnamo tarehe 15 Aprili mwaka 2023, maelfu ya watu wamepoteza maisha, huku mamilioni wakikumbwa na njaa, ubakaji, na ufurushwaji. Kambi kama ya Zamzam, yenye wakazi zaidi ya laki saba – nusu yao wakiwa watoto – zinaripotiwa kuzingirwa, wakazi wake wakikosa chakula, dawa, na maji, imeeleza Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya kusaka ukweli kuhusu Sudan.Mwenyekiti wa tume hiyo, Mohamed Chande Othman, ananukuliwa akisema, “Dunia imeshuhudia miaka miwili ya mzozo usio na huruma ambao umewanasa mamilioni ya raia katika mazingira ya kutisha, wakiwekwa katika hali ya ukatili bila matumaini ya mwisho.”Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, Catherine Russell kuhusu tukio hili la hivi karibuni ni kwamba watoto takriban 23 na wahudumu 9 wa misaada wameripotiwa kuuawa katika mfululizo wa mashambulizi katika eneo la Darfur Kaskazini, katika kipindi cha siku tatu zilizopita.Jana Jumapili, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesisitiza kuwa mashambulizi yanayolenga raia ni marufuku kabisa chini ya sheria ya kimataifa ya kibinadamu. Wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu na wafanyakazi wa afya wanapaswa kuheshimiwa na kulindwa,anasema.Kesho Jumanne huko London Uingereza, mataifa takriban 20 yanatarajiwa kujadili hali ya kibinadamu nchini Sudan. Umoja wa Mataifa unatoa wito wa hatua za haraka kulinda raia, kusitisha uungwaji mkono kwa pande zinazopigana, na kuhakikisha haki na uwajibikaji kwa uhalifu wa kivita.

Habari za UN
Chonde chonde tusiipe kisogo Sudan: Nkweta-Salami

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 14, 2025 2:07


Sudan Clementine Nkweta-Salami, Mwakilishi Mkazi na Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan akizungumza na UN News amesema hali si hali kama anavyofafanua Flora Nducha.(TAARIFA YA FLORA NDUCHA)Bi Nkweta-Salami amesema ufurushwaji wa watu unaendelea, mahitaji ni makubwa sana, tayari baa la njaa limeshabainika katika baadhi ya maeneo ya nchi, na wanakimbizana na muda kuzuia baa hilo lisienee zaidi.(SAUTI CLEMENTINE 1-SABRINA)"Hali ya kibinadamu ni ya kutisha, bado tunahaha. Hatuna uwezo wa kufikia maeneo yote yenye machafuko. Tunajitahidi kuhakikisha kwamba rasilimali tulizo nazo zinaweza kufikishwa haraka iwezekanavyo kwa kutumia njia zote tulizo nazo. Watu milioni 12 wametawanywa.   Kwa ujumla, bado tunahitaji juhudi kubwa, ado tunahitaji msaada kutoka kwa jumuiya ya kimataifa kwa upande wa rasilimali, na bado tunahitaji msaada zaidi wa kuruhusu utoaji wa misaada kutoka kwa makundi yote yenye silaha yanayohusika katika mzozo huu.”Licha ya kukosena suhuhu ya kisasa hadi sasa amesema wataendelea kusaidia wenye uhitaji(CLEMENTINE 2-SABRINA)“Msaada wa kibinadamu unapaswa kuendelea hata kama hakuna suluhisho la kisiasa kwa mzozo huu, na hata kama hakuna makubaliano ya kusitisha mapigano. Tunaendelea kushirikiana na jumuiya ya kimataifa na nchi wanachama zinazoshiriki kwenye majadiliano na mazungumzo ya kisiasa kujaribu kutumia majadiliano hayo kuwezesha kazi zetu kupitia usitishaji wa muda wa mapigano na kujaribu kuwashawishi makundi yenye silaha kukubaliana na njia ambazo tunaweza kutumia bila kuhatarisha maisha kwa kushambuliwa, kulipuliwa au kupigwa makombora”.Na rai yake ni kwamba(CLEMENTINE 3-SABRINA)Watu wako katika hali ya zahma kubwa, msaada unahitajika na tunatoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kutowasahau watu wa Sudan wanaume, wanawake na watoto wanaojikuta katika hali hii ngumu sana kwa sasa.TAGS: Sudan, Vita, amani na usalama, msaada wa kibinadamu

Habari za UN
10 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 10, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Idhaa hii inazungumza na Mwenyekiti wa Tanzania Women Ecocomic Empowerment Network (TAWEN), ambaye pia ni mchumi mbobezi Bi. Janet Zebedayo Mbene. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na neno la wiki.Shukran Anold na leo tunaanzia huko Geneva Uswisi ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limetoa muongozo wake wa kwanza duniani wa kutambua, kutoa matibabu kwa haraka na matibabu ya muda mrefu kwa ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.Nchini Chad katika mpaka wake na Sudan ambako Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR Filippo Grandi ametembelea na kuzungumza na wakimbizi wa Sudan pamoja na kujionea hali zao wakati huu ambapo wamepunguza kutoa chakula, malazi , maji na dawa na kauli yake ikawa moja tu, “Ninatoa wito kwa wafadhili, tafadhali msipunguze msaada kwa wathirika wa vita vya Sudan.”.Taarifa ya pamoja ya mashirika ya kibinadamu inayotolewa kila baada ya wiki mbili imeeleza kuhusu hali katika Ukanda wa Gaza inasema kuwa watu wanazidi kuuwawa na kujeruhiwa. Kwa zaidi ya mwezi sasa hakuna misafara ya misaada inayoruhusiwa kuingia Gaza. Watu kulazimishwa kuhama kinguvu kunaendelea, makazi ya wakimbizi yamefikia pomoni, huduma za usafi na kujisafi nazo ni mbaya.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "FIFILIZA"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
25 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 25, 2025 11:16


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo tunasalia hapa makao makuu katika mkutano wa CSW69 uliokunja chamvi Ijumaa wiki jana, tunamsikia aliyekuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa 4 wa Umoja wa Mataifa wa Wanawake, Mkutano wa Beijing Bi. Gertrude Mongella.Hapa New York, Umoja wa Mataifa leo umetoa wito wa kuachiliwa kwa wafanyakazi wake wanaoshikiliwa kote ulimwenguni ambao wamejikuta matatani wakati wakiwahudumia watu walio katika hatari, huku wakihatarisha usalama wao binafsi kwa kukabiliwa na vitisho vya kutekwa nyara, vurugu, unyanyasaji, na kifungo katika maeneo yenye migogoro na majanga.Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kuhusu vifo vya watoto imeonya kwamba miongo ya maendeleo katika kupunguza vifo vya watoto na watoto wachanga wakati wa kuzaliwa yako hatarini kutokana na kupunguzwa kwa ufadhili. Idadi ya vifo vya watoto wa chini ya umri wa miaka mitano ilipungua hadi watoto milioni 4.8 mwaka 2023, huku vifo vya wakati wa kuzaliwa vikiendelea kubaki takriban milioni 1.9.Leo ni Siku ya Kimataifa ya Kumbukumbu ya Waathirika wa Utumwa na Biashara ya Watumwa ya Bahari ya Atlantiki, ikiwakumbuka mamilioni ya Waafrika walioteswa, kunyanyaswa, na kunyimwa utu wao. Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema “Kwa zaidi ya karne nne, mamilioni ya Waafrika walitekwa kwa nguvu, kusafirishwa kwa meli hadi mataifa ya kigeni, na kufanyishwa kazi katika hali mbaya za kikatili.”Na katika mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP, Lea mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa amekimbilia Burundi na familia anasilimua hali ilivyokuwa wakati wa kukimbia.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!  

Habari za UN
Wanawake wamefanya mengi lakini hayajarekodiwa - Dkt. Reuben CSW69

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 24, 2025 3:50


Rekodi ni chache sana ya vitu ambavyo wanawake wamefanya hapa duniani, anasema Dkt. Rose Reuben, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania anapozungumza na Anold Kayanda wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa wakati wa Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake, CSW69, jijini New York, Marekani.Mkutano huu muhimu kuhusu wanawake umefanyika kuanzia tarehe 10 hadi 21Machi 2025 na kuhudhuriwa na maelfu ya wanawake kutoka kote duniani naye Dkt. Rose Reuben akiwa mmoja wao.Kiongozi huyu wa waandishi wa habari nchini Tanzania anaona kwamba kuna hatua nyingi zimepigwa  katika kipindi cha miaka 30 tangu kuwekwa kwa Azimio la Beijing ili kumkomboa mwanamke lakini bado kuna kazi kubwa ya kufanya.“Na hii kazi sipendi kujilaumu sana kwamba je, hakuna kitu ambacho kimefanyika?! Mambo yamefanyika mengi lakini masuala ya kijamii hayamaliziki kwa usiku mmoja kwasababu kila unapoamka jamii inabadilika kwa namna nyingine. Kwa hiyo tukitazama kwa mtazamo huo tunaona kwamba kuna kazi imefanyika.” Anasema Mkrugenzi huyo Mtendaji wa TAMWA.Kwake, mwandishi wa habari nguli, anaona moja ya maeneo ambayo ni muhimu yafanyiwe kazi ni kuzipa nafasi taarifa zinazohusu shughuli kubwa zinazofanywa na wanawake katika jamii kote duniani kwani licha ya wanawake kuwa na michango mikubwa katika mustakabali wa ulimwengu, taarifa zao hazipewi kipaumbele cha kutosha.“Mimi kwa mtazamo wangu naona wanawake wamefanya kazi nyingi lakini hazijarekodiwa. Rekodi ni chache sana.” Anasisitiza na kuongeza, “kwa hiyo tunatakiwa kuanza kurekodi vile vitu ambavyo vilifanywa na wanawake wale wa miaka 30 iliyopita lakini hata na hawa wanaokuja kizazi kipya.”Dkt. Rose Reuben anahamasisha pia vyombo vya habari kuangazia masuala mengine ambayo kwa namna moja amba nyingine yanaigusa jamii moja kwa moja na hiyo ni kusema yanamgusa mwanamke moja kwa moja kama vile mabadiliko ya tabianchi, tekonolojia, “na vitu vingine ambavyo vinaweza kuathiri usawa wa kijinsia na hali ya mwanamke duniani.”Aidha kiongozi huyo wa TAMWA anatoa wito kwa wanawake popote walipo kutumia nyenzo zinazopatikana katika jamii yao kuhakikisha wanapata taarifa, wanasambaza taarifa na kujipatia maarifa.

Habari za UN
UN: Sasa ni wakati wa kutimiza ahadi ya usawa wa kijinsia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 7, 2025 3:28


Katika kuelekea siku ya kimataifa ya wanawake ambayo huadhimishwa kila mwaka Machi 8 leo hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kunafanyika hafla maalum ya kuadhimisha siku hiyo ambayo mwaka huu imebeba maudhui “Kwa wanawake na wasichana wote: haki, usawa, uwezeshaji.” Akizungumza kwenye hafla hiyo Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women Sima Bahous amesema ni wakati wa kutekeleza kwa vitendo ndoto ya azimio la Beijing miaka 30 iliyopita la kufanya usawa wa kijinsi kuwa hali halisiKwa upande wake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres pamoja na kupongeza mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kusongesha usawa wa kijinsia duniani amesemaNatts….“Hata hivyo, mafanikio haya yaliyopatikana kwa jitihada kubwa bado ni dhaifu na hayatoshi kabisa.Mateso ya muda mrefu, ukatili, ubaguzi na ukosefu wa usawa wa kiuchumi bado vinaathiri jamii zetu.Kila baada ya dakika kumi, mwanamke huuawa na mwenzi wake au mwanafamilia.”Ameongeza kuwa wanawake na wasichana milioni 612 wanaishi chini ya kivuli cha migogoro ya silaha ambapo haki zao mara nyingi huchukuliwa kama zisizo na thamani.Akitaja takwimu amesema chini ya theluthi mbili ya wanawake duniani wanashiriki katika soko la ajira na wale wanaoshiriki hulipwa mishahara ya chini kuliko wanaume.Hivyo ameonya kwamba“Kwa kasi hii, itachukua miaka 130 kutokomeza umasikini uliokithiri kwa wanawake na wasichana.Amemesema badala ya kuingiza usawa wa haki kama jambo la kawaida, dunia inashuhudia kuenea kwa ubabe na chuki dhidi ya wanawake.Kwa muktadha huo amesistiza kwamba “Hatuwezi kukaa kimya wakati maendeleo yanaporudishwa nyuma. Lazima tupambane.”Akizungumzia sauti za vijana kushiriki katika harakati za usawa na haki za wanawake, kwenye hafla iliyofanyika mjini Geneva Uswisi kuadhimisha siku ya wanawake mwanafunzi kutoka Kenya James Mumo Nyumu amesisitiza kuwa hakuna nchi yoyote iliyotekeleza ahadi yao ya dunia isiyo na ukatili dhidi ya wanawake.Amesema “Maono ya Beijing yalikuwa ramani ya siku zijazo ambazo bado hatujazifikia kikamilifu,” alisema akiongeza kuwa “Nguvu kwa wanawake si tishio ni zawadi kwa jamii.”Hivyo amesisitiza kwamba“Kizazi changu kinadai hatua zaidi,” akitoa wito wa kuchukua hatua zaidi ya Beijing kwani“Kazi yetu haijakamilika.”

Write Now with Scrivener
Episode 48: Write Now with Scrivener, Episode no. 48: Mimi Kwa, Author of a Memoir about Four Generations of a Chinese Family

Write Now with Scrivener

Play Episode Listen Later Mar 5, 2025 32:43


Mimi Kwa is an Australian television personality and descendant of a Chinese family with a rich history. Her book, House of Kwa, tells about four generations of this family. Show notes: Mimi Kwa (https://www.mimitv.com.au) House of Kwa (https://www.mimitv.com.au/books) The Dressmaker, Rosie Ham (https://rosalieham.com/the-dressmaker/) A Radical Awakening, Dr. Shefali (https://www.aradicalawakening.com) Learn more about Scrivener (https://www.literatureandlatte.com/scrivener/overview), and check out the ebook Take Control of Scrivener (https://www.literatureandlatte.com/store). If you like the podcast, please follow it on Apple Podcasts (https://podcasts.apple.com/us/podcast/write-now-with-scrivener/id1568550068) or your favorite podcast app. Leave a rating or review, and tell your friends. And check out past episodes of Write Now with Scrivener (https://podcast.scrivenerapp.com).

Habari za UN
Burundi yahamishia wakimbizi wa DRC eneo salama zaidi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 3:48


Machafuko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) yanaendelea kufurusha watu na wengine wanaamua kukimbilia nchi jirani ikiwemo Burundi. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR nchini Burundi limesema wazi kuwa katika wiki mbili za mwezi Februari kuanzia tarehe 14 walipokea wakimbizi zaidi ya 60,000, wengi wakiwa tayari walishafurushwa awali. Kwa waliowasili katika eneo la Kaburantwa  nchini Burundi, bado wanahofia usalama. Serikali ya Burundi imetenga eneo lingine salama zaidi na sasa wanahamishiwa huko. Je ni wapi? Assumpta Massoi kwa msaada wa video ya UNHCR Burundi anasimulia zaidi. 

Habari za UN
Napenda sana maabara na imenihamasisha kusoma sayansi - Zamzam

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 2:34


Nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na wadau wengine wanafanikisha mpango wa kuhamasisha wasichana kuingia katika masomo ya STEM yaani Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati. Baadhi ya wasichana wakimbizi katika kambi ya Dadaab nchini Kenya ni wanufaika wa mpango huu. Sharon Jebiichi na maelezo zaidi.Zamzam Hussein,aliyekuwa mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Hagadera. Ni mkimbizi mwenye asili ya Somalia na sasa anaishi katika kambi ya wakimbizi ya Daadab nchini Kenya akiwa na ndoto ya kuwa daktari. Kupitia mpango huu ambao ni sehemu ya programu ya PROSPECTS ambao ni ushirikiano wa kimataifa unaojumuisha mashirika kadhaa ya Umoja wa Mataifa ukilenga kuboresha upatikanaji wa elimu, ulinzi wa jamii, na ajira yenye hadhi kwa jamii zinazowakaribisha wakimbizi na watu waliolazimika kuhama makazi yao Zamzam Hussein ameweza kukumbatia sayansi.“Nilikuwa mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Hagadera na nikamaliza elimu yangu mwaka wa 2024. Nilijiunga na shule hiyo Agosti 2021. Nilichopenda zaidi nikiwa shuleni ni maktaba, maabara ya sayansi na maabara ya kompyuta. Napenda kuwashauri wasichana wadogo wanaosoma shuleni  na walio wakimbizi wafanye kazi kwa bidii bila kujali changamoto wanazokabiliana nazo. Watatimiza ndoto zao na waweze kufanikiwa katika siku za usoni. Nataka kuwa daktari kwa sababu nilipokuwa shule ya upili nilijifunza mambo mengi kuhusiana na matibabu. Ningependa kuwashukuru wafadhili wetu kwa sababu bila wao nisingekuwa hapa.”Mpango huu wa STEM umetoa msaada wa rasilimali kama vile kuajiri walimu zaidi wa sayansi, kutoa mafunzo kwa walimu, kutoa vifaa vya sayansi kwa ajili ya maabara ya shule na kuanzisha programu ya maabara ya mtandaoni (virtual lab) ambapo wanafunzi wanaweza kufanya majaribio ya sayansi  kwenye mtandao wa intaneti. Kupitia video iliyorekodiwa na UNICEF, Patrick Njogu, Mwalimu Mkuu wa shule  ya Sekondari ya Hagadera anasema,“Nimemfundisha Zamzam na wasichana wengine ili waweze kutimiza ndoto na malengo yao. Wasichana wamekuwa wakikabiliana na changamoto kama vile ndoa za mapema. UNICEF imekuwa ya manufaa zaidi kwao. Kwa sasa walimu wawili zaidi wa sayansi  wameajiriwa. Mbali na hayo imekuwa ikiendesha mafunzo ya walimu, imetoa vifaa vya sayansi kwa ajili ya maabara ya shule na kuanzisha  programu ya maabara ya mtandaoni (virtual lab). Programu hii ya mtandao (virtual lab) imetengeneza  uhusiano nzuri wa wanafunzi katika masomo ya sayansi.” 

Układ Otwarty. Igor Janke zaprasza
Aleksander Kwaśniewski: Okrągły Stół, wybory i transformacja – polityczna biografia. Michał Sutowski

Układ Otwarty. Igor Janke zaprasza

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 124:49


(00:00) Wstęp(2:37) Czy Aleksander Kwaśniewski jest bohaterem dla lewicowca? Wejście Kwaśniewskiego do polityki(12:12) Wpływ Aleksandra Kwaśniewskiego na polską politykę(30:32) Dom rodzinny Kwaśniewskich i środowisko studenckie(55:09) Przebijanie się do gór – etapy wchodzenia do elity(1:01:30) Okrągły stół i rola Kwaśniewskiego Czy Kwaśniewski rozumiał dobrze polskie interesy?(1:19:33) Magdalenka i znaczenie spotkań(1:34:46) Jak Kwaśniewski zrozumiał kulturę paryską? Spotkanie z Jerzym Giedroyciem(1:48:18) Działalność w polityce międzynarodowej – kwestia Ukrainy i relacje z Rosją(2:00:09) Jaką rolę odegrał Aleksander Kwaśniewski w III RP?Gościem rozmowy jest Michał Sutowski, autor książki pt. „Aleksander Kwaśniewski. Biografia polityczna. Tom I 1954-1995”.Mecenasi programu: Zapoznaj się z trendami rynkowymi na 2025 rok według OANDA TMS Brokers: https://go.tms.pl/UkladOtwarty Casa Playa: https://casaplaya.pl/zakup-nieruchomosci-w-hiszpanii-pdf-instruktaz/ AMSO-oszczędzaj na poleasingowym sprzęcie IT: https://amso.pl/Uklad-otwarty-cinfo-pol-218.htmlMódl się z Hallow: https://hallow.app.link/ukladotwartySzkoła Przywództwa: https://szkolaprzywodztwa.pl/Link do zbiorki: https://zrzutka.pl/en6u9a

Habari za UN
UNICEF na WFP wawezesha watoto nchini Sudan Kusini kwenda shule ili watimize ndoto zao

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 24, 2025 2:03


Mashirika ya Umoja wa Mataifa, lile la Kuhudumia Watoto, UNICEF na la Mpango wa Chakula duniani, WFP kwa kushirikiana na mradi wa pamoja wa kimataifa wa mnepo ,au Joint Resilience Project (JRP) nchini Sudan Kusini ,wanatekeleza msaada wa chakula bora na salama bila malipo kwa watoto shuleni ,kwa zaidi ya wanufaika laki tano alfu Hamsini 550,000 ili kuhakikisha ndoto za watoto hao zinatimia. Ni sauti ya watoto wakitembea kuelekea shuleni huku wakiwa wamevibeba vitabu vyao mikononi.Kupitia video iliyoandaliwa na UNICEF, Tieng Maleng, mnufaika wa mradi wa JRP kutoka kijiji cha Pangapdit anaonekana akiwapa watoto wake kiamsha kinywa huku wakiwa wamekaa nje ya boma lao wakiwa wamevalia sare zao tayari kwenda shule. Kwa furaha anaeleza jinsi mradi huu umekuwa wa manufaa kwa familia yake.“Baada ya kupokea msaada wa kifedha, nilitumia fedha kidogo kulipa ada ya shule ya watoto wangu. Nikachukua sehemu kidogo ya fedha hizo kununua viatu vyao, na dawa. Pia nilitumia sehemu nyingine ya msaada huo katika kilimo.”Katika shule ya msingi ya Pangapdit inayoungwa mkono na mradi huu, watoto wanaonekana wakiwa wamesimama kwenye gwaride la shule wakisikiliza maelekezo kutoka kwa walimu wao. Aluel,Mwanawe Tieng Maleng, ambaye ni mwanafunzi katika shule hiyo anasema, “Tunaenda shule kila asubuhi na ndoto yangu ni kufanya kazi na mashirika yanayosaidia watu. Wakati kengele ya shule inapolia, tunakusanyika kwa ajili ya mkutano na baadaye tunaenda darasani.”Kupitia mradi huu,wanafunzi wamepokea vitabu vya kusoma,wamejengewa madarasa mapya, vyoo bora , na mifereji ya kunawa mikono.UNICEF na WFP wanafanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa watoto wanatimiza ndoto zao.

Habari za UN
13 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 13, 2025 11:05


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulika siku ya redio duniani, maudhui yakiwa Radio na Tabianchi, na ni kwa vipi chombo kinachodaiwa kutwamishwa na maendeleo ya teknolojia kinaendelea kusaidia kuelimisha umma kuhusu madhara ya mabadiliko ya tabianchi, Teonas Aswile wa TBC Taifa nchini Tanzania anaeleza.Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambapo hali inazidi kuwa tete na leo Mkurugenzi Mtendaji wa shirkika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, Catherine Russell, ameelezea wasiwasi mkubwa kuhusu kuongezeka kwa ghasia mashariki mwa mwa  nchi hiyo katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, ambapo watoto na familia wanakabiliwa na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.Naibu mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masiala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA nchini Sudan Edmore Tondhlana akizungumza na UN News amesema hali nchini Sudan inaendelea kuwa janga la kibinadamu wakati vita ikishika kasi na watu wakiendelea kufurushwa makwao. Amesema "Tunashuhudia hali ambapo Sudan ina mahitaji ya kibinadamu yaliyo miongoni mwa makubwa zaidi duniani. Takriban watu milioni 30 wanahitaji msaada wa kibinadamu. Hili ni ongezeko la takriban watu milioni tano zaidi ikilinganishwa na mwaka uliopita, pia, Sudan ina idadi kubwa zaidi ya watu waliopoteza makazi yao.Na leo ni siku ya Redio Duniani mwaka huu ikibeba maudhui Redio na mabadiliko ya tabianchi. Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO lengo la maudhui haya ni kudhihirisha jukumu la redio katika kusambaza ujumbe na kuelimisha kuhusu changamoto za mabadiliko ya tabianchi, kutanabaisha kuhusu hatua endelevu na kuwapa sauti wanaharakati wa mabadiliko ya tabianchi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo fursa ni yake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa      nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno “MSUMBI”.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!