Podcasts about Kwa

  • 190PODCASTS
  • 795EPISODES
  • 19mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • May 25, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about Kwa

Show all podcasts related to kwa

Latest podcast episodes about Kwa

Radio Omniglot
Omniglot News (25/05/25)

Radio Omniglot

Play Episode Listen Later May 25, 2025 2:15


Here's the latest news from the world of Omniglot. New language pages: Kebu (Kǝkpǝǝkǝ), a Kwa language spoken in southern Togo and southeastern Ghana. Bangubangu (Kibangubangu), a Bantu language spoken in the east and south the Democratic Republic of the Congo. Cherepon (Kyiripong), a Kwa language spoken in the Eastern Region of Ghana. New numbers […]

Habari za UN
22 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 22, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini kumsikia mgeni wetu Prof. Wallah Bin Wallah, mwandishi mashuhuri wa vitabu vya Kiswahili kutoka Kenya ambaye anamulika umuhimu wa vitabu katika kukuza lugha ya Kiswahili. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno.Kwa mara ya kwanza tangu mwezi Februari, msaada wa kuokoa maisha umefika Gaza. Baada ya wiki 11 za kizuizi kutoka kwa mamlaka za Israeli, malori 198 yaliyobeba chakula, dawa na unga wa ngano yameingia leo kupitia mpaka wa Kerem Shalom kwa mujibu wa mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa.Mratibu mkuu wa misaada wa Umoja wa Mataifa, Tom Fletcher, ameiitaja hatua hiyo kuwa ya muhimu sana, huku malori 90 yakipakuliwa usiku kwa ajili ya kusambazwa haraka.Mwaka 2024, vita havikuishia kwenye uwanja wa mapambano pekee      vilivunja nyumba, masoko na shule. Kuanzia Gaza hadi Ukraine, Sudan hadi Myanmar na zaidi ya raia 36,000 walipoteza maisha yao katika mizozo 14 ya kivita kulimgana na ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kwa Baraza la Usalama hii leo linalojadili ulinzi wa raia katika mizozo ya silaha.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DAHARI”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Bi. Joy :Teknolojia inatatua changamoto za kijamii - Wasichana katika TEHAMA

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 12, 2025 3:38


Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO, sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano TEHAMA, au ICT inaendelea kutawala na kuunda fursa mpya, lakini wanawake bado wanakumbana na changamoto kubwa ya upungufu wa uwakilishi. Hata hivyo, wanawake wanavuka mipaka na sasa Bi. Joy, msichana kutoka Nairobi Kenya, ambaye ni mtaalamu katika teknolojia ya kidijitali, amekalia nafasi muhimu katika kubadili mtindo wa maisha kupitia elimu ya ICT. Katika mahojiano na washirika wetu Radio Domus, alizungumzia umuhimu wa kuhamasisha wasichana kujiunga na masomo ya teknolojia ili kutengeneza mustakabali mpya wa kidijitali, na kubadili dunia kwa njia ya kidigitali na usawa. Sharon Jebichii na Makala zaidi

Habari za UN
Chokoleti itengenezwayo Uganda yavuka mpaka na mabara -UNCTAD

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 9, 2025 3:55


Kutoka kakao ghafi huko Bundibugyo, magharibi mwa Uganda hadi Kampala mji mkuu wa kibiashara wa taifa hilo la Afrika Mashariki ndiko kunapatikana kiwanda cha kutengeneza chokoleti cha Equator kinachomilikiwa na Barbara Gonget na mume wake Gustav. Awali wazo la biashara hii lilionekana kutokuwa na mashiko. Ingawa hivyo baada ya ITC, ambacho ni Kituo cha Kimataifa ha Biashara kilicho chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo, UNCTAD pamoja na wadau wao kuweka usaidizi wao, hali imebadilika na sasa biashara inavuka sio tu mipaka bali mabara. Wawili hao Kwa kuchanganya mbinu za hali ya juu, zinazojali jamii, na ufundi wa kitaalamu, wanabadili taswira ya uzalishaji wa chokoleti nchini humo.Je wamefanya nini? Assumpta Massoi anafafanua zaidi kwenye makala hii iliyofanikishwa na ITC.

Men. Men. Men. - The Podcast -
Embracing The Legacy, Creating My Own Path

Men. Men. Men. - The Podcast -

Play Episode Listen Later May 6, 2025 101:36


“Walking in the shadow of a giant” si jambo rahisi—na inakuwa ngumu zaidi pale “Giant” huyo akiwa  ni Augustine Mahiga, mwanadiplomasia mashuhuri wa Tanzania, na wewe ni mtoto wake wa kiume, unayejulikana kama Andrew Mahiga.Kwa wengi, jina la mwisho linaweza kufungua milango, lakini je, kila nafasi unayoipata ni kwa sababu ya uwezo wako au kwa sababu unaitwa Mahiga? Hilo ndilo swali ambalo Andrew amekuwa akilazimika kulikabili katika safari yake ya kujitambua.Katika episode hii ya kipekee ya Men Men Men: The Podcast, Andrew anakaa nasi na kufungua moyo wake kuhusu changamoto za kuishi na jina kubwa, shinikizo la kulingana na hadhi ya baba, na hatimaye furaha aliyopata alipogundua kuwa—ndiyo, yeye ni mtoto wa baba yake, lakini si lazima awe kama baba yake.Zaidi ya hayo, Andrew anazungumzia kwa kina umuhimu wa mentorship kwa wanaume—na jinsi kuwepo au kutokuwepo kwa wanasihi kunaweza kumjenga au kumvunjilia mbali mwanaume wa Kitanzania.Baada ya kuisikiliza episode hii, utaelewa kwa nini tumeiita: "Embracing the Legacy, Creating My Own Path."

Habari za UN
VoTAN sio tu mtandao wa kidijitali kusaidia manusura wa ugaidi bali pia ni familia - Manusura

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 5, 2025 5:02


Hatimaye kilio cha manusura wa ugaidi duniani cha kuwa na Mtandao wa Mashirika yao ili kuweza kupaza zaidi sauti zao kwa ajili ya sio tu kusaidiwa bali pia kuepusha matukio kama hayo, kimepata jawabu baada ya Mtandao huo au VoTAN kuzinduliwa kwenye Umoja wa Mataifa. Kwa msaada wa kifedha kutoka Hispania, Iraq na nchi nyingine wanachama, mtandao huu ulio chini ya Programu ya kusaidia manusura wa ugaidi kwenye Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabilana na Ugaidi, UNOCT, unatarajiwa kuziba mapengo ya msaada na kuinua ushuhuda wa manusuta kutoka maeneo yaliyopuuzwa duniani. Assumpta Massoi amefuatilia uzinduzi huo na kuandaa makala hii.

Habari RFI-Ki
Mchakato wa kumchagua kiongozi mpya wa kanisa katoliki duniani

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Apr 28, 2025 10:02


Kwa sasa macho yakiwamulika makadinali 135 watakaochagua papa mpya ndani ya siku chache zijazo, mjadala kuhusu Papa kutoka Afrika ukishamiri.Mchakato wa kumchagua p

Habari RFI-Ki
Mchakato wa kumchagua kiongozi mpya wa kanisa katoliki duniani

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Apr 28, 2025 10:02


Kwa sasa macho yakiwamulika makadinali 135 watakaochagua papa mpya ndani ya siku chache zijazo, mjadala kuhusu Papa kutoka Afrika ukishamiri.Mchakato wa kumchagua p

Habari za UN
Tume huru ya UN ya kusaka ukweli kuhusu Sudan imelaani vikali mauaji ya watu zaidi ya 100

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 14, 2025 2:02


Vita ya sasa ya Sudan ikielekea kuingia mwaka wa tatu, Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya kusaka ukweli kuhusu Sudan imelaani vikali mauaji ya watu zaidi ya 100 yaliyotokea wikiendi hii katika kambi za wakimbizi wa ndani Darfur, ikionya kwamba hali inaweza kuwa mbaya zaidi. Anold Kayanda na taarifa zaidi.(Taarifa ya Anold Kayanda)Shukrani LeahTangu kuanza kwa vita kati ya Jeshi la Sudan (SAF) na kikosi cha waasi cha RSF mnamo tarehe 15 Aprili mwaka 2023, maelfu ya watu wamepoteza maisha, huku mamilioni wakikumbwa na njaa, ubakaji, na ufurushwaji. Kambi kama ya Zamzam, yenye wakazi zaidi ya laki saba – nusu yao wakiwa watoto – zinaripotiwa kuzingirwa, wakazi wake wakikosa chakula, dawa, na maji, imeeleza Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya kusaka ukweli kuhusu Sudan.Mwenyekiti wa tume hiyo, Mohamed Chande Othman, ananukuliwa akisema, “Dunia imeshuhudia miaka miwili ya mzozo usio na huruma ambao umewanasa mamilioni ya raia katika mazingira ya kutisha, wakiwekwa katika hali ya ukatili bila matumaini ya mwisho.”Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, Catherine Russell kuhusu tukio hili la hivi karibuni ni kwamba watoto takriban 23 na wahudumu 9 wa misaada wameripotiwa kuuawa katika mfululizo wa mashambulizi katika eneo la Darfur Kaskazini, katika kipindi cha siku tatu zilizopita.Jana Jumapili, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesisitiza kuwa mashambulizi yanayolenga raia ni marufuku kabisa chini ya sheria ya kimataifa ya kibinadamu. Wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu na wafanyakazi wa afya wanapaswa kuheshimiwa na kulindwa,anasema.Kesho Jumanne huko London Uingereza, mataifa takriban 20 yanatarajiwa kujadili hali ya kibinadamu nchini Sudan. Umoja wa Mataifa unatoa wito wa hatua za haraka kulinda raia, kusitisha uungwaji mkono kwa pande zinazopigana, na kuhakikisha haki na uwajibikaji kwa uhalifu wa kivita.

Habari za UN
Chonde chonde tusiipe kisogo Sudan: Nkweta-Salami

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 14, 2025 2:07


Sudan Clementine Nkweta-Salami, Mwakilishi Mkazi na Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan akizungumza na UN News amesema hali si hali kama anavyofafanua Flora Nducha.(TAARIFA YA FLORA NDUCHA)Bi Nkweta-Salami amesema ufurushwaji wa watu unaendelea, mahitaji ni makubwa sana, tayari baa la njaa limeshabainika katika baadhi ya maeneo ya nchi, na wanakimbizana na muda kuzuia baa hilo lisienee zaidi.(SAUTI CLEMENTINE 1-SABRINA)"Hali ya kibinadamu ni ya kutisha, bado tunahaha. Hatuna uwezo wa kufikia maeneo yote yenye machafuko. Tunajitahidi kuhakikisha kwamba rasilimali tulizo nazo zinaweza kufikishwa haraka iwezekanavyo kwa kutumia njia zote tulizo nazo. Watu milioni 12 wametawanywa.   Kwa ujumla, bado tunahitaji juhudi kubwa, ado tunahitaji msaada kutoka kwa jumuiya ya kimataifa kwa upande wa rasilimali, na bado tunahitaji msaada zaidi wa kuruhusu utoaji wa misaada kutoka kwa makundi yote yenye silaha yanayohusika katika mzozo huu.”Licha ya kukosena suhuhu ya kisasa hadi sasa amesema wataendelea kusaidia wenye uhitaji(CLEMENTINE 2-SABRINA)“Msaada wa kibinadamu unapaswa kuendelea hata kama hakuna suluhisho la kisiasa kwa mzozo huu, na hata kama hakuna makubaliano ya kusitisha mapigano. Tunaendelea kushirikiana na jumuiya ya kimataifa na nchi wanachama zinazoshiriki kwenye majadiliano na mazungumzo ya kisiasa kujaribu kutumia majadiliano hayo kuwezesha kazi zetu kupitia usitishaji wa muda wa mapigano na kujaribu kuwashawishi makundi yenye silaha kukubaliana na njia ambazo tunaweza kutumia bila kuhatarisha maisha kwa kushambuliwa, kulipuliwa au kupigwa makombora”.Na rai yake ni kwamba(CLEMENTINE 3-SABRINA)Watu wako katika hali ya zahma kubwa, msaada unahitajika na tunatoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kutowasahau watu wa Sudan wanaume, wanawake na watoto wanaojikuta katika hali hii ngumu sana kwa sasa.TAGS: Sudan, Vita, amani na usalama, msaada wa kibinadamu

Habari za UN
10 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 10, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Idhaa hii inazungumza na Mwenyekiti wa Tanzania Women Ecocomic Empowerment Network (TAWEN), ambaye pia ni mchumi mbobezi Bi. Janet Zebedayo Mbene. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na neno la wiki.Shukran Anold na leo tunaanzia huko Geneva Uswisi ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limetoa muongozo wake wa kwanza duniani wa kutambua, kutoa matibabu kwa haraka na matibabu ya muda mrefu kwa ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.Nchini Chad katika mpaka wake na Sudan ambako Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR Filippo Grandi ametembelea na kuzungumza na wakimbizi wa Sudan pamoja na kujionea hali zao wakati huu ambapo wamepunguza kutoa chakula, malazi , maji na dawa na kauli yake ikawa moja tu, “Ninatoa wito kwa wafadhili, tafadhali msipunguze msaada kwa wathirika wa vita vya Sudan.”.Taarifa ya pamoja ya mashirika ya kibinadamu inayotolewa kila baada ya wiki mbili imeeleza kuhusu hali katika Ukanda wa Gaza inasema kuwa watu wanazidi kuuwawa na kujeruhiwa. Kwa zaidi ya mwezi sasa hakuna misafara ya misaada inayoruhusiwa kuingia Gaza. Watu kulazimishwa kuhama kinguvu kunaendelea, makazi ya wakimbizi yamefikia pomoni, huduma za usafi na kujisafi nazo ni mbaya.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "FIFILIZA"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Gurudumu la Uchumi
Sehemu I: Madhara ya ushuru wa Trump kwa bara la Afrika na biashara ya dunia

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Apr 9, 2025 10:01


Kwa majuma kadhaa, mijadala mikali duniani kote kufuatia uamuzi wa rais wa Marekani, Donald Trump, kutangaza ushuru zaidi wa bidhaa zinazoingia kwenye taifa hilo, mataifa ya Afrika yakiwa miongoni mwa waathirika, baadhi wakiwekewa ushuru wa hadi asilimia 50. Katika makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunadadavua na wataalamu athari za ushuru wa Trump kwa nchi za Afrika na biashara ya dunia kiujumla. Tutakuwa na Ali Mkimo, mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

Kiswahili, Lugha Ya Afrika
Ukubwa wa Ulimwengu - Mwaka wa Mwangaza (Light Year)

Kiswahili, Lugha Ya Afrika

Play Episode Listen Later Mar 28, 2025 9:43


Je, unajua kwa nini wanasayansi hutumia mwaka wa mwanga badala ya kilomita kupima umbali wa nyota na miili mingine ya anga?

Habari za UN
25 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 25, 2025 11:16


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo tunasalia hapa makao makuu katika mkutano wa CSW69 uliokunja chamvi Ijumaa wiki jana, tunamsikia aliyekuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa 4 wa Umoja wa Mataifa wa Wanawake, Mkutano wa Beijing Bi. Gertrude Mongella.Hapa New York, Umoja wa Mataifa leo umetoa wito wa kuachiliwa kwa wafanyakazi wake wanaoshikiliwa kote ulimwenguni ambao wamejikuta matatani wakati wakiwahudumia watu walio katika hatari, huku wakihatarisha usalama wao binafsi kwa kukabiliwa na vitisho vya kutekwa nyara, vurugu, unyanyasaji, na kifungo katika maeneo yenye migogoro na majanga.Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kuhusu vifo vya watoto imeonya kwamba miongo ya maendeleo katika kupunguza vifo vya watoto na watoto wachanga wakati wa kuzaliwa yako hatarini kutokana na kupunguzwa kwa ufadhili. Idadi ya vifo vya watoto wa chini ya umri wa miaka mitano ilipungua hadi watoto milioni 4.8 mwaka 2023, huku vifo vya wakati wa kuzaliwa vikiendelea kubaki takriban milioni 1.9.Leo ni Siku ya Kimataifa ya Kumbukumbu ya Waathirika wa Utumwa na Biashara ya Watumwa ya Bahari ya Atlantiki, ikiwakumbuka mamilioni ya Waafrika walioteswa, kunyanyaswa, na kunyimwa utu wao. Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema “Kwa zaidi ya karne nne, mamilioni ya Waafrika walitekwa kwa nguvu, kusafirishwa kwa meli hadi mataifa ya kigeni, na kufanyishwa kazi katika hali mbaya za kikatili.”Na katika mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP, Lea mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa amekimbilia Burundi na familia anasilimua hali ilivyokuwa wakati wa kukimbia.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!  

Habari za UN
Wanawake wamefanya mengi lakini hayajarekodiwa - Dkt. Reuben CSW69

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 24, 2025 3:50


Rekodi ni chache sana ya vitu ambavyo wanawake wamefanya hapa duniani, anasema Dkt. Rose Reuben, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania anapozungumza na Anold Kayanda wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa wakati wa Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake, CSW69, jijini New York, Marekani.Mkutano huu muhimu kuhusu wanawake umefanyika kuanzia tarehe 10 hadi 21Machi 2025 na kuhudhuriwa na maelfu ya wanawake kutoka kote duniani naye Dkt. Rose Reuben akiwa mmoja wao.Kiongozi huyu wa waandishi wa habari nchini Tanzania anaona kwamba kuna hatua nyingi zimepigwa  katika kipindi cha miaka 30 tangu kuwekwa kwa Azimio la Beijing ili kumkomboa mwanamke lakini bado kuna kazi kubwa ya kufanya.“Na hii kazi sipendi kujilaumu sana kwamba je, hakuna kitu ambacho kimefanyika?! Mambo yamefanyika mengi lakini masuala ya kijamii hayamaliziki kwa usiku mmoja kwasababu kila unapoamka jamii inabadilika kwa namna nyingine. Kwa hiyo tukitazama kwa mtazamo huo tunaona kwamba kuna kazi imefanyika.” Anasema Mkrugenzi huyo Mtendaji wa TAMWA.Kwake, mwandishi wa habari nguli, anaona moja ya maeneo ambayo ni muhimu yafanyiwe kazi ni kuzipa nafasi taarifa zinazohusu shughuli kubwa zinazofanywa na wanawake katika jamii kote duniani kwani licha ya wanawake kuwa na michango mikubwa katika mustakabali wa ulimwengu, taarifa zao hazipewi kipaumbele cha kutosha.“Mimi kwa mtazamo wangu naona wanawake wamefanya kazi nyingi lakini hazijarekodiwa. Rekodi ni chache sana.” Anasisitiza na kuongeza, “kwa hiyo tunatakiwa kuanza kurekodi vile vitu ambavyo vilifanywa na wanawake wale wa miaka 30 iliyopita lakini hata na hawa wanaokuja kizazi kipya.”Dkt. Rose Reuben anahamasisha pia vyombo vya habari kuangazia masuala mengine ambayo kwa namna moja amba nyingine yanaigusa jamii moja kwa moja na hiyo ni kusema yanamgusa mwanamke moja kwa moja kama vile mabadiliko ya tabianchi, tekonolojia, “na vitu vingine ambavyo vinaweza kuathiri usawa wa kijinsia na hali ya mwanamke duniani.”Aidha kiongozi huyo wa TAMWA anatoa wito kwa wanawake popote walipo kutumia nyenzo zinazopatikana katika jamii yao kuhakikisha wanapata taarifa, wanasambaza taarifa na kujipatia maarifa.

Habari za UN
UN: Sasa ni wakati wa kutimiza ahadi ya usawa wa kijinsia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 7, 2025 3:28


Katika kuelekea siku ya kimataifa ya wanawake ambayo huadhimishwa kila mwaka Machi 8 leo hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kunafanyika hafla maalum ya kuadhimisha siku hiyo ambayo mwaka huu imebeba maudhui “Kwa wanawake na wasichana wote: haki, usawa, uwezeshaji.” Akizungumza kwenye hafla hiyo Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women Sima Bahous amesema ni wakati wa kutekeleza kwa vitendo ndoto ya azimio la Beijing miaka 30 iliyopita la kufanya usawa wa kijinsi kuwa hali halisiKwa upande wake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres pamoja na kupongeza mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kusongesha usawa wa kijinsia duniani amesemaNatts….“Hata hivyo, mafanikio haya yaliyopatikana kwa jitihada kubwa bado ni dhaifu na hayatoshi kabisa.Mateso ya muda mrefu, ukatili, ubaguzi na ukosefu wa usawa wa kiuchumi bado vinaathiri jamii zetu.Kila baada ya dakika kumi, mwanamke huuawa na mwenzi wake au mwanafamilia.”Ameongeza kuwa wanawake na wasichana milioni 612 wanaishi chini ya kivuli cha migogoro ya silaha ambapo haki zao mara nyingi huchukuliwa kama zisizo na thamani.Akitaja takwimu amesema chini ya theluthi mbili ya wanawake duniani wanashiriki katika soko la ajira na wale wanaoshiriki hulipwa mishahara ya chini kuliko wanaume.Hivyo ameonya kwamba“Kwa kasi hii, itachukua miaka 130 kutokomeza umasikini uliokithiri kwa wanawake na wasichana.Amemesema badala ya kuingiza usawa wa haki kama jambo la kawaida, dunia inashuhudia kuenea kwa ubabe na chuki dhidi ya wanawake.Kwa muktadha huo amesistiza kwamba “Hatuwezi kukaa kimya wakati maendeleo yanaporudishwa nyuma. Lazima tupambane.”Akizungumzia sauti za vijana kushiriki katika harakati za usawa na haki za wanawake, kwenye hafla iliyofanyika mjini Geneva Uswisi kuadhimisha siku ya wanawake mwanafunzi kutoka Kenya James Mumo Nyumu amesisitiza kuwa hakuna nchi yoyote iliyotekeleza ahadi yao ya dunia isiyo na ukatili dhidi ya wanawake.Amesema “Maono ya Beijing yalikuwa ramani ya siku zijazo ambazo bado hatujazifikia kikamilifu,” alisema akiongeza kuwa “Nguvu kwa wanawake si tishio ni zawadi kwa jamii.”Hivyo amesisitiza kwamba“Kizazi changu kinadai hatua zaidi,” akitoa wito wa kuchukua hatua zaidi ya Beijing kwani“Kazi yetu haijakamilika.”

Write Now with Scrivener
Episode 48: Write Now with Scrivener, Episode no. 48: Mimi Kwa, Author of a Memoir about Four Generations of a Chinese Family

Write Now with Scrivener

Play Episode Listen Later Mar 5, 2025 32:43


Mimi Kwa is an Australian television personality and descendant of a Chinese family with a rich history. Her book, House of Kwa, tells about four generations of this family. Show notes: Mimi Kwa (https://www.mimitv.com.au) House of Kwa (https://www.mimitv.com.au/books) The Dressmaker, Rosie Ham (https://rosalieham.com/the-dressmaker/) A Radical Awakening, Dr. Shefali (https://www.aradicalawakening.com) Learn more about Scrivener (https://www.literatureandlatte.com/scrivener/overview), and check out the ebook Take Control of Scrivener (https://www.literatureandlatte.com/store). If you like the podcast, please follow it on Apple Podcasts (https://podcasts.apple.com/us/podcast/write-now-with-scrivener/id1568550068) or your favorite podcast app. Leave a rating or review, and tell your friends. And check out past episodes of Write Now with Scrivener (https://podcast.scrivenerapp.com).

Habari za UN
Burundi yahamishia wakimbizi wa DRC eneo salama zaidi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 3:48


Machafuko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) yanaendelea kufurusha watu na wengine wanaamua kukimbilia nchi jirani ikiwemo Burundi. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR nchini Burundi limesema wazi kuwa katika wiki mbili za mwezi Februari kuanzia tarehe 14 walipokea wakimbizi zaidi ya 60,000, wengi wakiwa tayari walishafurushwa awali. Kwa waliowasili katika eneo la Kaburantwa  nchini Burundi, bado wanahofia usalama. Serikali ya Burundi imetenga eneo lingine salama zaidi na sasa wanahamishiwa huko. Je ni wapi? Assumpta Massoi kwa msaada wa video ya UNHCR Burundi anasimulia zaidi. 

Habari za UN
Napenda sana maabara na imenihamasisha kusoma sayansi - Zamzam

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 2:34


Nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na wadau wengine wanafanikisha mpango wa kuhamasisha wasichana kuingia katika masomo ya STEM yaani Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati. Baadhi ya wasichana wakimbizi katika kambi ya Dadaab nchini Kenya ni wanufaika wa mpango huu. Sharon Jebiichi na maelezo zaidi.Zamzam Hussein,aliyekuwa mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Hagadera. Ni mkimbizi mwenye asili ya Somalia na sasa anaishi katika kambi ya wakimbizi ya Daadab nchini Kenya akiwa na ndoto ya kuwa daktari. Kupitia mpango huu ambao ni sehemu ya programu ya PROSPECTS ambao ni ushirikiano wa kimataifa unaojumuisha mashirika kadhaa ya Umoja wa Mataifa ukilenga kuboresha upatikanaji wa elimu, ulinzi wa jamii, na ajira yenye hadhi kwa jamii zinazowakaribisha wakimbizi na watu waliolazimika kuhama makazi yao Zamzam Hussein ameweza kukumbatia sayansi.“Nilikuwa mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Hagadera na nikamaliza elimu yangu mwaka wa 2024. Nilijiunga na shule hiyo Agosti 2021. Nilichopenda zaidi nikiwa shuleni ni maktaba, maabara ya sayansi na maabara ya kompyuta. Napenda kuwashauri wasichana wadogo wanaosoma shuleni  na walio wakimbizi wafanye kazi kwa bidii bila kujali changamoto wanazokabiliana nazo. Watatimiza ndoto zao na waweze kufanikiwa katika siku za usoni. Nataka kuwa daktari kwa sababu nilipokuwa shule ya upili nilijifunza mambo mengi kuhusiana na matibabu. Ningependa kuwashukuru wafadhili wetu kwa sababu bila wao nisingekuwa hapa.”Mpango huu wa STEM umetoa msaada wa rasilimali kama vile kuajiri walimu zaidi wa sayansi, kutoa mafunzo kwa walimu, kutoa vifaa vya sayansi kwa ajili ya maabara ya shule na kuanzisha programu ya maabara ya mtandaoni (virtual lab) ambapo wanafunzi wanaweza kufanya majaribio ya sayansi  kwenye mtandao wa intaneti. Kupitia video iliyorekodiwa na UNICEF, Patrick Njogu, Mwalimu Mkuu wa shule  ya Sekondari ya Hagadera anasema,“Nimemfundisha Zamzam na wasichana wengine ili waweze kutimiza ndoto na malengo yao. Wasichana wamekuwa wakikabiliana na changamoto kama vile ndoa za mapema. UNICEF imekuwa ya manufaa zaidi kwao. Kwa sasa walimu wawili zaidi wa sayansi  wameajiriwa. Mbali na hayo imekuwa ikiendesha mafunzo ya walimu, imetoa vifaa vya sayansi kwa ajili ya maabara ya shule na kuanzisha  programu ya maabara ya mtandaoni (virtual lab). Programu hii ya mtandao (virtual lab) imetengeneza  uhusiano nzuri wa wanafunzi katika masomo ya sayansi.” 

Układ Otwarty. Igor Janke zaprasza
Aleksander Kwaśniewski: Okrągły Stół, wybory i transformacja – polityczna biografia. Michał Sutowski

Układ Otwarty. Igor Janke zaprasza

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 124:49


(00:00) Wstęp(2:37) Czy Aleksander Kwaśniewski jest bohaterem dla lewicowca? Wejście Kwaśniewskiego do polityki(12:12) Wpływ Aleksandra Kwaśniewskiego na polską politykę(30:32) Dom rodzinny Kwaśniewskich i środowisko studenckie(55:09) Przebijanie się do gór – etapy wchodzenia do elity(1:01:30) Okrągły stół i rola Kwaśniewskiego Czy Kwaśniewski rozumiał dobrze polskie interesy?(1:19:33) Magdalenka i znaczenie spotkań(1:34:46) Jak Kwaśniewski zrozumiał kulturę paryską? Spotkanie z Jerzym Giedroyciem(1:48:18) Działalność w polityce międzynarodowej – kwestia Ukrainy i relacje z Rosją(2:00:09) Jaką rolę odegrał Aleksander Kwaśniewski w III RP?Gościem rozmowy jest Michał Sutowski, autor książki pt. „Aleksander Kwaśniewski. Biografia polityczna. Tom I 1954-1995”.Mecenasi programu: Zapoznaj się z trendami rynkowymi na 2025 rok według OANDA TMS Brokers: https://go.tms.pl/UkladOtwarty Casa Playa: https://casaplaya.pl/zakup-nieruchomosci-w-hiszpanii-pdf-instruktaz/ AMSO-oszczędzaj na poleasingowym sprzęcie IT: https://amso.pl/Uklad-otwarty-cinfo-pol-218.htmlMódl się z Hallow: https://hallow.app.link/ukladotwartySzkoła Przywództwa: https://szkolaprzywodztwa.pl/Link do zbiorki: https://zrzutka.pl/en6u9a

Habari za UN
UNICEF na WFP wawezesha watoto nchini Sudan Kusini kwenda shule ili watimize ndoto zao

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 24, 2025 2:03


Mashirika ya Umoja wa Mataifa, lile la Kuhudumia Watoto, UNICEF na la Mpango wa Chakula duniani, WFP kwa kushirikiana na mradi wa pamoja wa kimataifa wa mnepo ,au Joint Resilience Project (JRP) nchini Sudan Kusini ,wanatekeleza msaada wa chakula bora na salama bila malipo kwa watoto shuleni ,kwa zaidi ya wanufaika laki tano alfu Hamsini 550,000 ili kuhakikisha ndoto za watoto hao zinatimia. Ni sauti ya watoto wakitembea kuelekea shuleni huku wakiwa wamevibeba vitabu vyao mikononi.Kupitia video iliyoandaliwa na UNICEF, Tieng Maleng, mnufaika wa mradi wa JRP kutoka kijiji cha Pangapdit anaonekana akiwapa watoto wake kiamsha kinywa huku wakiwa wamekaa nje ya boma lao wakiwa wamevalia sare zao tayari kwenda shule. Kwa furaha anaeleza jinsi mradi huu umekuwa wa manufaa kwa familia yake.“Baada ya kupokea msaada wa kifedha, nilitumia fedha kidogo kulipa ada ya shule ya watoto wangu. Nikachukua sehemu kidogo ya fedha hizo kununua viatu vyao, na dawa. Pia nilitumia sehemu nyingine ya msaada huo katika kilimo.”Katika shule ya msingi ya Pangapdit inayoungwa mkono na mradi huu, watoto wanaonekana wakiwa wamesimama kwenye gwaride la shule wakisikiliza maelekezo kutoka kwa walimu wao. Aluel,Mwanawe Tieng Maleng, ambaye ni mwanafunzi katika shule hiyo anasema, “Tunaenda shule kila asubuhi na ndoto yangu ni kufanya kazi na mashirika yanayosaidia watu. Wakati kengele ya shule inapolia, tunakusanyika kwa ajili ya mkutano na baadaye tunaenda darasani.”Kupitia mradi huu,wanafunzi wamepokea vitabu vya kusoma,wamejengewa madarasa mapya, vyoo bora , na mifereji ya kunawa mikono.UNICEF na WFP wanafanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa watoto wanatimiza ndoto zao.

Habari za UN
13 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 13, 2025 11:05


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulika siku ya redio duniani, maudhui yakiwa Radio na Tabianchi, na ni kwa vipi chombo kinachodaiwa kutwamishwa na maendeleo ya teknolojia kinaendelea kusaidia kuelimisha umma kuhusu madhara ya mabadiliko ya tabianchi, Teonas Aswile wa TBC Taifa nchini Tanzania anaeleza.Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambapo hali inazidi kuwa tete na leo Mkurugenzi Mtendaji wa shirkika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, Catherine Russell, ameelezea wasiwasi mkubwa kuhusu kuongezeka kwa ghasia mashariki mwa mwa  nchi hiyo katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, ambapo watoto na familia wanakabiliwa na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.Naibu mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masiala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA nchini Sudan Edmore Tondhlana akizungumza na UN News amesema hali nchini Sudan inaendelea kuwa janga la kibinadamu wakati vita ikishika kasi na watu wakiendelea kufurushwa makwao. Amesema "Tunashuhudia hali ambapo Sudan ina mahitaji ya kibinadamu yaliyo miongoni mwa makubwa zaidi duniani. Takriban watu milioni 30 wanahitaji msaada wa kibinadamu. Hili ni ongezeko la takriban watu milioni tano zaidi ikilinganishwa na mwaka uliopita, pia, Sudan ina idadi kubwa zaidi ya watu waliopoteza makazi yao.Na leo ni siku ya Redio Duniani mwaka huu ikibeba maudhui Redio na mabadiliko ya tabianchi. Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO lengo la maudhui haya ni kudhihirisha jukumu la redio katika kusambaza ujumbe na kuelimisha kuhusu changamoto za mabadiliko ya tabianchi, kutanabaisha kuhusu hatua endelevu na kuwapa sauti wanaharakati wa mabadiliko ya tabianchi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo fursa ni yake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa      nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno “MSUMBI”.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Akibomoa kibanda chake Goma DRC, mkimbizi asema ana hofu kurejea Saké

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 12, 2025 1:45


Baada ya waasi wa M23 jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kupatia wakimbizi waliokuwa wamesaka hifadhi kambini mjini Goma, wawe wamerejea makwao ndani ya saa 72 kuanzia juzi jumatatu, mamia wameanza kutii amri hiyo.Miongoni mwao ni Kibira Bakulu, baba wa watoto 5, aliyekimbia mapigano eneo la Saké, mwezi Februari mwaka jana, takriban kilomita 10 kutoka Goma.Akiwa katika harakati za kubomoa kibanda chake katika kambi ya nane ya CEPAC Mugunga huko Goma, Bwana Bakulu anasema walishangaa, bila kuwa tayari, kuambiwa warudi walikotoka."Tumepatiwa saa 72 tuwe tumeondoka na kurejea Saké, kwani vita vimeisha. Sisi hatua uhakika kamili kwa sababu tuliondoka Saké kutokana na vita. Kama inabidi kusukumwa tuondoke, hatuna la kuchagua,” amesema Bwana Bakulu.Ana hofu ya kurejea Saké, akisema, “kule tulikuwa tunaishi Sake na tukirejea tutaishi vipi? Tunaomba viongozi wajitahidi watusaidie ili watuhakikishia usalama.Alipoeleza hali halisi amesema, “ hii siku ya leo hapa unaniona, watu wamepita hapa wakifanya vurugu, wananyang'anya kila kitu ulichonacho, iwe simu wanabeba. Sasa tunashindwa kufahamu amani iko katika kiwango gani?”Kwa mujibu wa Bwana Bakulu, walishaamua kuwa hawataweza kurudi na kama ni kufa basi watafia Goma, lakini sasa wamelazimishwa kurejea Saké.

Habari za UN
Hali ni tete mashariki mwa DRC, msaada wa kibinadamu haufikii wahitaji - Mashirika

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 31, 2025 1:52


Mashirika ya Umoja wa Mataifa yameendelea kutoa wito wa kurejeshwa kwa amani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo (DRC) kwani hali inazidi kuwa tete na kuuzidi uwezo wa mashirika hayo kusaidia. Selina Jerobon amefuatilia matamko ya mashirika hayo na kutuandalia taarifa ifuatayo. Janga la haki za binadamu katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) linaendelea kuzidi kuwa baya kutokana na ripoti zinazonyesha kuwa kundi la wapiganaji la M23 limeendelea kusonga kusini kuelekea Bukavu, imeeleza Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa (OHCHR) leo Januari 31 mjini Geneva, Uswisi.Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) katika taarifa iliyotolewa katika mji Mkuu wa DRC, Kinshasa, limesema licha ya juhudi hizo zinazoendelea ili kusaidia watu, kuongezeka kwa ghasia kumelazimisha IOM na mashirika mengine ya kibinadamu kusitisha operesheni katika maeneo yaliyoathirika zaidi, na hivyo kusitisha msaada wa kuokoa maisha kwa maelfu ya watu.Kwa upande wake Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeeleza wasiwasi wake kuhusu ugumu wa ufikiaji wa wanaohitaji msaada mashariki mwa DRC.Msemaji wa WFP DRC, Shelley Thakral leo Januari 31 akiwa jijini Kinshasa DRC anasema, "kwa kweli watu wanakosa chakula, maji safi, vifaa tiba na huo ni wasiwasi mkubwa kwa hivyo mnyororo wa usambazaji umenyongwa kwa sasa ikiwa unafikiria kuhusu ufikiaji kwa njia ya ardhi, anga, wakati kila kitu kimefungwa. Kwa hivyo kipaumbele chetu cha kwanza ni wazi ni usalama wa wafanyakazi. Tunataka kurejea kwenye shughuli zetu mara tu usalama utakapoturuhusu.”

Habari za UN
UNEP: Mradi wa UNREDD umekuwa mkombozi kwa mazingira na kwa wakulima DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 29, 2025 3:41


Karibu nusu ya idadi ya watu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, wanategemea misitu kwa chakula, nishati, afya, riziki na huduma za mfumo wa ikolojia kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP ambao ni takriban watu zaidi ya milioni 40. Kwa kulitambua hilo mradi wa Umoja wa Mataifa wa kulinda bayoanuai huku ukipambana na umasikini UNREDD unaleta nuru kwa raia hususani mashariki mwa nchi hiyo. Ungana na Flora Nducha kwa ufafanuzi zaidi katika makala hii.

Habari za UN
20 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 20, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia juhudi za kukabiliana na mlipuko wa homa ya marburg Tanzania, na elimu kwa wakimbizi katika makazi ya Kakuma nchini Kenya.  Makala inatupeleka nchini Lebanon na mashinani inaturejesha Gaza.Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus amesema wanashirikiana na serikali ya Tanzania kudhibiti mlipuko wa homa ya Marbug iliyoripotiwa mkoani Kagera, kaskazini magharibi mwa taifa hilo la Afrika Mashariki.Migogoro, vita na mabadiliko ya tabianchi mara nyingi vimekuwa vikiwapora watoto fursa ya elimu na hata kusambaratisha mustakbali wao na wengi wanajikuta wakiishia kwenye makambi ya wakimbizi linasema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. Kwa kulitambua hilo shirika hilo linaendesha miradi mbalimbali ya kuhakikisha watoto waliokosa elimu hata kama wana umri mkubwa wanapewa fursa ya pili kusoma kama ilivyokuwa kwa mkimbizi Philip Lon'golea kutoka Sudan aliyekimbilia Uganda kwanza lakini sasa yuko kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya.Katika makala Thelma Mwadzaya anatupeleka Lebanon ambako tarehe 17 mwezi huu wa Januari Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiwa ziarani Lebanon alitembelea walinda amani wa Umoja wanaohudumu chini ya ujumbe wa Mpito wa UN nchini Lebanon, UNIFIL, ambao walikumbwa na zahma wakati jeshi la Israeli liliposhambulia kituo chake kinyume na azimio namba 1701 la mwaka 2006, linalozuia mashambulizi kwenye eneo tenganishi kati ya Israeli na Lebanon.Na mashinani tutaelekea Gaza kusikia kauli kutoka kwa mkimbizi wa ndani baada ya kuanza kutekelezwa usitishaji uhasama na kuachiliwa kwa mateka na wafungwa.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

Habari za UN
Elimu haina umri wala kuchelewa, wala mwisho: Philip Long'olea

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 20, 2025 2:14


Migogoro, vita na mabadiliko ya tabianchi mara nyingi vimekuwa vikiwapora watoto fursa ya elimu na hata kusambaratisha mustakbali wao na wengi wanajikuta wakiishia kwenye makambi ya wakimbizi linasema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. Kwa kulitambua hilo shirika hilo linaendesha miradi mbalimbali ya kuhakikisha watoto waliokosa elimu hata kama wana umri mkubwa wanapewa fursa ya pili kusoma kama ilivyokuwa kwa mkimbizi Philip Lon'golea kutoka Sudan aliyekimbilia Uganda kwanza lakini sasa yuko kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya. Cicely Kariuki anatujuza zaidi

Habari za UN
Antonio Guterres atembelea kikosi cha UNIFIL na kukipongeza kwa kazi nzuri

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 17, 2025 2:26


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amepongeza na kutoa shukrani kubwa kwa uvumilivu na kujitolea kunakofanywa na walinda amani wa Kikosi cha Muda cha Umoja wa Mataifa nchini Lebanon UNIFIL, wakati wa ziara yake hii leo katika makao makuu kikosi hicho mjini Naqoura. Flora Nducha na taarifa zaidi Asante Assumpta Guterres ambaye yuko Lebanon tangu jana kwenye ziara ya mshikamano akizungumza na uongozi wa kikosi hicho cha UNIFIL na wafanyakazi, amewapongeza kwa ujasiri na juhudi zao katika mazingira magumu zaidi ya kazi ya kulinda amani duniani.Amesema “Hampo tu kwenye mstari wa Bluu wa Lebanon, mpo kwenye mstari wa mbele wa amani,”akitambua jukumu lao muhimu katika kudumisha utulivu licha ya mashambulizi na vitisho vya kiusalama.Katibu Mkuu ameelezea kuhusu mchango muhimu wa kikosi hicho katika kuzuia vurugu, kupunguza mvutano, kuruhusu upatikanaji wa misaada ya kibinadamu, na kuwalinda raia amesema “Kazi yenu imekuwa muhimu na ya kipekee katika kurejesha utulivu kusini mwa Lebanon na katika mstari wa Bluu.”Audio fileAmesisitiza umuhimu wa kufuata Azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa namba 1701, akitoa wito kwa pande zote kuheshimu usalama wa maeneo ya Umoja wa Mataifa na kuhakikisha usalama wa walinda amani ikiwemo msitari wa Bluu amba oni eneo tenganishi baina ya Israel na Lebanon.Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa ameonya kwamba “Mashambulizi dhidi ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa  hayakubaliki kabisa, yanakiuka sheria za kimataifa, na yanaweza kuwa uhalifu wa kivita.”Pia alilaani uwepo wa vikundi vyenye silaha na ukiukwaji unaofanywa na vikosi vya ulinzi vya Israeli ndani ya eneo la kazi la UNIFIL.Akiangazia siku zijazo, Guterres ameelezea matumaini ya kipindi endelevu cha utulivu na maendeleo katika kutekeleza Azimio namba 1701, linalolenga kuimarisha amani na utulivu wa kudumu kati ya Lebanon na Israeli.Amehitimisha taarifa yake kwa kusema“Kwa pamoja, tunaweza kufanikisha fursa hii ya kipekee,” na kuahidi kuendelea kuunga mkono kikosi hicho na kushirikiana kwa karibu na nchi zinazochangia wanajeshi wa UNIFIL ili kuboresha uwezo wa kiutendaji na kuhakikisha usalama wa walinda amani.

Habari za UN
Angela Tabiri, mbobevu wa hisabati anayehaha kuona wasichana Afrika wanapenda STEM

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 17, 2025 4:23


 Ikiwa Umoja wa Mataifa unaunga mkono masomo ya Sayansi, Teknolojia na Hisabati, au STEM, Angela Tabiri ni mwanahisabati bora duniani, Mtafiti na Mhadhiri kutoka Chuo cha African Institute for Mathematical Sciences (AIMS) kilichoko Accra nchini Ghana Magharibi mwa bara la Afrika, amekuwa akitoa mchango katika kuhakikisha wasichana nchini humo wanapata elimu ya hisabati kupitia taasisi yake ya FemAfricMaths. Kwa kufanya hivyo anatimiza lengo namba 4 ya Malengo endelevu ya Umoja Mataifa(SDGs) linalohimiza elimu bora kwa wote na lile namba 5 linalozungumzia usawa wa kijinsia. Kutoka mjini Mwanza kaskazini magharibi mwa Tanzania, Sabrina Moshi wa redio washirika Saut Fm amefanya mahojiano na mtaalamu huyo. Angela anaanza kwa kueleza namna alivyokuwa na ndoto hadi kuanzisha FemAfricMaths ili kuwasaidia wasichana barani Afrika.

Habari za UN
Serikali patieni vijana taarifa sahihi na stahiki ili watekeleze wajibu wao

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 10, 2025 3:38


Umoja wa Mataifa unaeleza kwamba duniani kote kuna vijana bilioni 1.2 wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 24. Idadi hii ni saw ana asilimia 16 ya wakazi wote wa dunia. Kama hiyo haitoshi, idadi hiyo ya vijana inatarajiwa kufikia bilioni 1.3 ifikapo mwaka 2030, yaani miaka mitano ijayo. Lakini changamoto ni kwamba bado serikali nyingi hazijaweza kutumia wingi wa idadi hii kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs. Kwa hali hiyo baadhi ya vijana wameamua kutumia fursa na kujiongeza ili vijana wenzao waweze kufahamu wanachopaswa kufanya ili SDGs zifanikiwe ifikapo 2030. Miongoni mwao ni Paul Siniga, kijana kutoka Tanzania ambaye mwezi Oktoba mwaka huu alikuweko kwenye makao makuu ya UN jijini New York, Marekani kushiriki vikao vya ngazi ya juu. Assumpta Massoi alitaka kufahamu kwa kina ni hatua zipi alichukua hadi kufika aliko sasa.

Habari za UN
Gaza: Zaidi ya watoto 70 wameuawa tangu Januari 1 huku gharama za maisha zikizidi kupanda

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 8, 2025 1:55


Hali ya maisha kwa raia wa Gaza inaendelea kuwa mbaya msimu huu wa baridi kali kutokana na vikwazo vya kufikisha misaada, kupanda kwa gharama za maisha na mashambuizi yanayoendelea kukatili maisha ya raia wakiwemo watoto 74 waliouawa tangu Januri Mosi mwaka huu  yamesema mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF ambalo linasema kuuawa kwa watoto hao 74 katika siku saba za kwanza za mwezi huu ni dhihirisho la jinamizi linaloendelea kuighubika Gaza na mashambulizi ya Israel hayaonyeshi dalili yoyote ya kukoma ikiwemo ya jana usiku katika mji wa Gaza, Khan Younis na kwenye makazi ya Pwani ya wakimbizi wa ndani ya Al Mawasi ambayo Israel yenyewe iliyatenga hapo awali kama maeneo salama. Kwa mujibu wa UNICEF jana Jumanne pekee watoto 5 wameripotiwa kuuawa Al Mawasi. Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEFF Catherine Russell amesema "Kwa watoto wa Gaza, mwaka mpya umeleta vifo zaidi na mateso kutokana na mashambulizi, kunyimwa huduma, na kuongezeka kwa hali ya baridi. Usitishaji wa mapigano umechelewa kwa muda mrefu na watoto wengi sana wameuawa au kupoteza wapendwa wao katika mwanzo mbaya wa mwaka mpya.”© UNRWA/Fadi ThabetMwanaume na mwanae wakiwa wameketi wakiota moto Nuseirat katikati mwa GazaGharama za chakula zinaendelea kupanda GazaKwa upande wake shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula Duniani WFP limesema kana kwamba mashambulizi hayatoshi sasa kupanda kwa gharama za chakula ni mtihani mwingine kwa watu wa Gaza kwani kilo 25 za unga zinauzwa hadi dola za Marekani 150 gharama ambayo watu wengi hawawezi kumudu  na watoto ni wahanga wakubwa wakilzimika kulala njaa. Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X limesema linapokuja suala la mashambulizi Gaza “Hakuna tofauti, wahudumu wa kibinadamu, hata wawe ni nani nao wamekuwa wakilengwa mara kwa mara. Kupuuzwa huku kwa wazi kwa sheria za kimataifa za kibinadamu hakuwezi kuachwa kuwa ndio kawaida mpya.” Pia limesema Gaza hospitali zimekuwa mitego ya vifo, familia zimesambaratika, watoto wanakufa kwa baridi na njaa inakatisha maisha  ya watu wengi 

Habari za UN
07 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 7, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini DRC katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Bulengo kushuhudia jinsi Umoja wa Mataifa unavyowasaidia wanawake waathrika wa ukatili wa kingoni kuweza kujitegemea na kumudu mahitaji ya familia zao.Kwa mujibu wa takwimu zilizothibitishwa na Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa, takriban watu 5,601 waliuawa nchini Haiti mwaka 2024 kutokana na ghasia za magenge, likiwa ni ongezeko la zaidi ya mauaji 1,000 ya mwaka 2023. Katika moja ya matukio mabaya zaidi na ya kushtua mwaka jana, takriban watu 207 waliuawa mapema Desemba kwenye mauaji yaliyoratibiwa na kiongozi wa genge lenye nguvu la Wharf Jérémie katika eneo la Cité Soleil huko Port-au-Prince. Wengi wa waliouawa walikuwa wazee walioshutumiwa kusababisha kifo cha mtoto wa kiongozi huyo kwa njia ya uchawi.Leo, Umoja wa Mataifa na Serikali ya Lebanon wametoa ombi la nyongeza ya dola milioni 371.4 za kimarekani, zikilenga kutoa msaada wa kuokoa maisha ya walioathiriwa na mzozo wa hivi karibuni na janga la kibinadamu linaloendelea nchini humo.Na Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk leo ameeleza kusikitishwa sana na ongezeko kubwa la watu walionyongwa nchini Iran mwaka jana. Takriban watu 901 wameripotiwa kunyongwa katika mwaka 2024, arobaini wakiwa wamenyongwa katika wiki moja tu ya mwezi Desemba.Mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi, UNFPA tunamsikia Zubaida AbouBaker, mama mkimbizi wa ndani katika kambi ya Tawila iliyoko Darfur Kaskazini nchini Sudan akisimulia machungu yaliyomkumba kufuatia migogoro inayoendelea nchini humo.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
UN: Vifo vitokanavyo na baridi Gaza vinazuilika, usitishaji mapigano na misaada ndio jawabu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 3, 2025 1:58


Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM leo limeonya juu ya vifo vitokanavyo na msimu wa baridi kali Gaza likisema limesikitishwa sana na athari mbaya za mvua za msimu wa baridi na baridi kali kwa Wapalestina waliokimbia makazi yao na kuishi katika mazingira magumu huko Gaza, kwani hilo ni janga la kibinadamu lisilo na kifani. Kupitia taarifa iliyotolewaleo mjini Geneva Uswisi Mkurugenzi Mkuu wa IOM Amy Pope  amesema "Watu walio katika mazingira magumu, ikiwa ni pamoja na takriban watoto wachanga saba, wamekufa kutokana na baridi kali au hypothermia, na vifo hivi vya kusikitisha vinasisitiza haja ya haraka ya makazi na msaada mwingine wa kibinadamu kuwafikia watu wa Gaza mara moja," Ameongeza kuwa hali hii inachochea janga zaidi la kibinadamu ambalo tayari linawakumba watu waUkanda wa Gaza. Mvua kubwa na mafuriko yameyakumba makazi ya wakimbizi wa ndani yaliyojengwa kwa mahema na kulazimisha familia kuachwa katika maeneo ya wazi kwenye hali mbaya ya baridi, zikijitahidi kutengeneza mahema yaliyoharibika kutokana na matumizi ya miezi kadhaa. © UNRWAChakula kinagawiwa kwa watu waliokimbia makazi yao huko Jabalia, kaskazini mwa Gaza.Vikwazo vya Israel ni changamoto kwa misaadaPia IOM imesema vikwazo vya utaratibu wa kufikia wenye uhitaji, kama ilivyoripotiwa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA, vimezuia kwa kiasi kikubwa utoaji wa misaada, huku watu 285,000 pekee wakipokea msaada wa makazi tangu Septemba 2024. Kwa mujibu wa IOM hadi kufikia Katikati ya Desemba mwaka jana inakadiriwa kuwa watu wapatao 945,000 bado wanahitaji msaada wa haraka wa kukabiliana na msimu wa baridi ikiwemo nguo za kuongeza joto, mablanketi na tepu za kuima mahema dhidi ya mvua na baridi. Tangu Katikati ya Novemba mwaka jana IOM imewasilisha karibu vifaa 180,000 vya makazi ya dharura kwa washirika ndani ya Gaza na ina zaidi ya vifaa milioni 1.5 vya msimu wa baridi ikiwemo mahema, vifaa vya kuziba  na vitanda ambavyo viko tayari kwenye maghala na sehemu zavivuko, lakini vikwazo vikali vya ufikiaji vinawazuia kufikia wenye uhitaji. © UNICEF/Abed ZaqoutWavulana wawili wakibeba chupa za maji katika kambi ya wakimbizi inayofadhiliwa na UNWRA huko Khan Younis kusini mwa Gaza.Usitihsaji mapigano ndio suluhuIOM imesisitiza wito wake wa dharura wa kusitisha mapigano ili kuwezesha utoaji salama na wa haraka wa msaada wa kuokoa maisha kwa wale wanaouhitaji sana. Pia inasisitiza wito wake kwa pande zote kuzingatia sheria za kimataifa za kibinadamu, kuhakikisha ulinzi wa raia, kuachiliwa kwa mateka wote na kuruhusu ufikiaji salama, wa haraka, usiozuiliwa na endelevu wa wenye uhitaji. Watu wa Gaza wanastahili usalama, makazi na utu. IOM iko tayari kuhamasisha misaada na kusaidia jamii zilizofurushwa, lakini fursa ya ufikiaji wa kibinadamu lazima itolewe ili kuwezesha hili amesisitiza mkuu wa IOM. Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA limesema Licha ya hali ngumu, timu za UNRWA zinaendesha makao yote ya Umoja wa Mataifa, na kutoa msaada wa kuokoa maisha kwa watu wanaohitaji. Limeongeza kuwa Vita vilipoanza karibu miezi 15 iliyopita, UNRWA iligeuza shule zake, vituo vya afya, na maghala kuwa makazi na kuna wakati ambapo vita ikiendelea UNRWA ilipokea watu milioni 1 waliokimbia makazi yao 

Habari za UN
FAO Tanzania yatoa mafunzo ya ufugaji wa nyuki kwa wenyeji Tanzania kupitia Mradi wa ACP MEAs 3

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 18, 2024 2:50


Mradi wa ACP MEAs 3 unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO, na kufadhiliwa na Muungano wa Ulaya, EU umetoa mafunzo ya ufugaji nyuki kwa wakulima nchini Tanzania. Mradi huu unawapa wakulima zana na ujuzi muhimu katika ufugaji nyuki endelevu, na hivyo kuboresha maisha yao huku wakikuza bayoanuwai na uhifadhi wa mazingira. Kwa kuunga mkono jamii za wenyeji, Mradi huu unalenga kukuza ukuaji wa uchumi na kuwawezesha wakulima kulinda wachavushaji, ambao ni muhimu kwa uzalishaji katika kilimo na afya ya mfumo ikolojia. Tupate simulizi zaidi katika makala hii iliyoandaliwa na Flora Nducha kupitia video ya FAO Tanzania.

Habari za UN
UNHCR: Chonde chonde jumuiya ya Kimataifa tuishike mkono Uganda kwa faida ya waomba hifadhi na wakimbizi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 16, 2024 2:04


Mwaka 2024 ukielekea ukingoni, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR  nchini Uganda limetoa rai kwa jumuiya ya kimataifa kutolisahau taifa hilo la Afrika Mashariki ambalo ni maskani ya idadi kubwa zaidi ya waomba hifadhi na wakimbizi barani Afrika. Rai hiyo iliyotolewa mwishoni mwa wiki inataka ufadhili wa fedha uongezwe ili liweze kuendelea kukirimu watu hao ambao wengi wanakimbia machafuko. Huyo ni Moulid Hujale afisa wa UNHCR nchini Uganda akitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kushikamana na Uganda akiwa  kwenye makazi makubwa ya wakimbizi ya Kiryandongo Magharibi mwa nchi hiyo. Anasema kuna mambo matatu muhimu ambayo dunia inapaswa kufahamu kuhusu Uganda na wakimbizi.“Mosi Uganda inahifadhi idadi kubwa zaidi ya wakimbizi na waomba hifadhi Afrika ikiwa na zaidi ya watu milioni 1.7 wengi wao wakitoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na Sudan Kusini.”Zaidi ya hapo ukarimu wa Uganda anasema hauna kipimo“Pili, Uganda ina sera ya kufugua mlango kwa wakimbizi na pia kwa miongo mingi imekuwa ikiwakaribisha watu wanaokimbia machafuko bila kujali utaifa wao. Kitu ambacho ni kikubwa na cha kipekee kuhusu nchi hii ni kwamba wakati wakimbizi wanapowasili hapa hupewa ardhi, mahali pa kuishi na hata kulima mazao kwa ajili ya kujikimu. Wana uhuru wa kutembea na haki ya kuajiriwa. Hawajatengwa lakini wanaishi  ndani ya jamii inayowahifadhi. Sera hii ya Uganda inawaruhusu wakimbizi kujumuishwa katika huduma za kitaifa ambapo wanafaidika na elimu na huduma za afya.”Lakini Kutokana na changamoto za fedha Moulid anasema ukarimu huo sasa uko njia panda"Tatu: Ukarimu wa Uganda uko hatarini kwani wakimbizi zaidi wanaingia kutoka nchi jirani. UNHCR, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, liko mashinani kufanya kazi na Serikali ya Uganda kusaidia kutoa msaada wa kuokoa maisha kwa watu hawa. Hata hivyo, rasilimali ni chanche. Tunahitaji msaada wenu ili Uganda iendelee kuwa mfano wa kuigwa kwa dunia nzima.”Kwa nyjibu wa UNHCR licha ya idadi kubwa ya watu na rasilimali kidogo, sera za Uganda zinammanisha kwamba wakimbizi ni sehemu ya maisha ya kijamii na kiuchumi na ongezeko la rasilimali litakidhi haja za waliopo sasa na watakaokuja.

Men. Men. Men. - The Podcast -
Usilalamike, Furahia Mchakato

Men. Men. Men. - The Podcast -

Play Episode Listen Later Dec 3, 2024 103:56


Dr. Lwidiko Mhamilawa ameibuka kwenye studio zetu siyo kwa ajili ya kutuambia jinsi maisha ni magumu (tulishajua hiyo), bali kutufundisha jinsi ya kufurahia safari ya maisha – hata pale unapotaka kutupa lapa na kusema, “Inatosha!” Unajua, kuwa mwanaume ni kama kuwa kocha wa timu isiyoelewa mchezo: kila mtu anakutegemea wewe, lakini hakuna anayekuelewa!

Habari za UN
Namayombo Mgonela: Utamaduni wa Kiswahili umeniinua kiuchumi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 26, 2024 6:16


Lengo namba 5 la Maendeleo ya Maendeleo Endelevu, SDGs, ya Umoja wa Mataifa ni usawa wa kijinsia ambao ni pamoja na kuwawezesha wanawake kiuchumi kwa kuwapatia fursa. Akiwa Havana Cuba hivi karibuni kwenye kongamano la kimataifa la Kiswahili Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili, alikutana na kuzungumza na Namayombo Nyanzala Mgonela, mwanamke mjasiriamali kutoka visiwa vilivyoko Karibea St. Kitts na Nevis ambaye anatumia fursa ya utamaduni wake mchanganyiko wa asili ya Visiwa hivyo na wa Kiswahili kujikwamua kiuchumi kupitia ubunifu wa mitindo na shughuli za mama lishe katika jitihada za kutimiza lengo hilo. Kwa kina zaidi tuungane na Flora Nducha. 

Habari za UN
UN: Mwanamke au msichana mmoja aliuawa kila baada ya dakika 10 na mwenzi au ndugu 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 25, 2024 3:13


Leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake, Je wajua kwamba wanawake na wasichana 140 walifariki dunia kila siku duniani kote mwaka 2023 wakiwa mikononi mwa wapenzi wao au ndugu wa karibu, ikimaanisha kuwa mwanmake mmoja anauawa katika kila dakika 10. Na zaidi ya yote bara la Afrika linaongoza? Maudhui ya siku hii yanasema “Hakuna kisingizio” cha ukatili dhidi ya wanawake lama alioushuhudia Ester manusura kutoka Uganda, ambaye kwa miaka mingi amekuwa akifanyiwa ukatili na mpenzi wake anaema “Nilikuwa na umri wa miaka 15 aliponioa naye alikuwa na miaka 28wakati mwingine alikuwa akinivua nguo zote na kunilazimisha kukaa kwenye varandana nilikuwa nikichelewa kurudi ananitandika nje nyumba kila mtu kushuhudia Nilikuwa katika hali mbaya ya uchungu Mkubwa na kuvuja damu.”maadhimisho ya mwaka huu yanaambatana na ripoti iliyotolewa leo jijini New York, Marekani na mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la masuala ya wanawake, UN Women na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kudhibiti Dawa za kulevya na Uhalifu, (UNODC), inaangazia mwanga wa janga la mauaji ya wanawake na kutoa wito kwa hatua za dharura ili kukabili janga hilo.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres katika ujumbe wake wa siku hii inayoadhimishwa tarehe 25 mwezi Novemba kila mwaka, ikiashiria pia kuanza kwa siku 16 za kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake, zikiwa na kilele chake tarehe 10 mwezi Desemba, siku ya Haki za Binadamu duniani amesema “Janga la ukatili dhidi ya wanawake na wasichana linaaibisha ubindamu, dunia lazima iitikie wito huu. Tunahitaji hatua za dharura kwa ajili ya haki na uwajibikaji, na kusaidia uchechemuzi.”Mkurugenzi mtendaji wa UN Women Sima Bahous amesisitiza kuwa “Ukatili dhidi ya wanawake na wasichana si kwamba hauepukiki, unaweza kuzuilika. Tunahitaji sheria thabiti, ukusanyaji bora wa takwimu, uwajibikaji zaidi wa serikali, utamaduni wa kutovumilia, na kuongezeka kwa ufadhili kwa mashirika ya kupigania haki za wanawake na taasisi. Tunapokaribia kuadhimisha miaka 30 ya Azimio la Beijing na Jukwaa la Utekelezaji mwaka 2025, ni wakati wa viongozi wa dunia kuungana na kuchukua hatua kwa haraka, kujitolea na kuelekeza rasilimali zinazohitajika kumaliza mgogoro huu mara moja na kwa wote”Mauaji ya wanawake yanavuka mipaka, hali ya kiuchumi na kijamii, utamaduni. Hata hivyo kiwango au ukubwa wake unatofautiana.Kwa mujibu wa ripoti hiyo, bara la Afrika lilivunja rekodi ya kuwa na viwango vya juu vya wanawake kuuawa na wapenzi wao au mwanafamilia. Wanawake 21,700 waliuawa Afrika mwaka huo wa 2023, ikifuatiwa na bara la Amerika na kisha Oshenia.Mashirika ya UN Women na…

Habari za UN
Mafunzo ya walinda amani kutoka Tanzania huko Beni yajengea uwezo walimu kusaidiana na watoto

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 2:25


Umoja wa Mataifa unasema kwamba vita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC imefanya taifa hilo kuwa pahala hatari zaidi duniani kwa watoto kuishi, kutokana na mateso ya kimwili na kisaikolojia wanayoyapitia. Kwa kutambua hilo walinda amani wanawake wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye ujumbe wa UN nchini humo, MONUSCO wamechukua hatua kuona watoto wanaishi kama watoto. Video ya MONUSCO ikianza na walinda amani wakijongea kwa jamii, Kapteni Noella Nyaisanga kiongozi wa kikundi hicho cha wanawake cha kikosi cha 11 cha walinda amani wa Tanzania kwenye MONUSCO, TANZBATT-11 anaeleza jinsi kikundi chao kinavyosogea kwa jamii na hasa watoto ili kutatua changamoto zinazowakabili kutokana na mapigano kati ya jeshi la serikali na waasi kwenye eneo hili la Beni, jimboni Kivu Kaskazini, mashariki mwa DRC. Anafafanua zaidi lengo lao.Lengo ni kujenga uaminifu kwa raia ambao tunawalinda. Kwa hiyo tukaamua kuandaa masomo shuleni, ambayo yataweza kuwaimarisha wao, kuwasaidia tatizo la kuwa wameathirika kisaikolojia.Zavadi Mbambu ni miongoni mwa walimu waliopatiwa mafunzo ya kusaidia watoto walioathiriwa na changamoto lukuki ikiwemo mapigano. Akisema stress, anamaanisha msongo.“Unakuwa na wanafunzi wanaokuwa na msongo wa mawazo kutokana na jambo ambalo wanaishi, na hata mauaji. Kuna wale ambao hata wameua wazazi wao , hata familia yao yote.  Na kwa hao wanafunzi wanapoingia shuleni , wanakuwa kama hawako ndani, fikra zao zinakuwa mbali .  Lakini kupitia mafunzo nimewaelewa , na tumejua namna gani ya kuishi nao. Na tayari mabadiliko yameanza kuonekana.”Pacifique Kyakimwa, mmoja wa wanafunzi anasimulia mkasa mmoja.“Kuna mwenzetu  aliyekuwa na tatizo, yaani tukiwa ndani ya shule, alikuwa anacheka, yaani anatusumbua hadi hatumwelewi mwalimu. Lakini tangu wameanza kufundisha hili somo, wameanza kuelewa . Ameanza kuwa na akili inayotumika vizuri. Mafunzo haya yamefika wakati tunahitaji , na imetusaidia sana.”

Habari za UN
22 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia majadiliano huko Baku Azerbaijan kuhusu ufadhili wa mabadiliko ya tabianchi, na kazi za walinda amani kutoka Tanzania TANZBATT-11 huko DRC. Makala inaturejesha kataika mkutano wa COP29 na mashinani inatupeleka Namibia, kulikoni?Majadiliano ya mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP29 yamekumbwa na mkwamo huko Baku Azerbaijana muafaka haujapatikana. Majadiliano hayo yaliyotarajiwa kukunja jamvi leo sasa yanaendelea kwa kuwekwa mezani mapendekezo mapya kuhusu ufadhili wa mabadiliko ya tabianchi hasa kwa matifa yanayoendelea.Umoja wa Mataifa unasema kwamba vita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC imefanya taifa hilo kuwa pahala hatari zaidi duniani kwa watoto kuishi, kutokana na mateso ya kimwili na kisaikolojia wanayoyapitia. Kwa kutambua hilo walinda amani wanawake wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye ujumbe wa UN nchini humo, MONUSCO wamechukua hatua kuona watoto wanaishi kama watoto.Makala inakupeleka Baku nchini Azerbaijan kunakotamatika mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29 kumsikia kijana kutoka Tanzania akizungumzia kilichompeleka, anachoondoka nacho na ujumbe wake kwa  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.Na katika mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP, tunasikia kauli ya Willem Westhuizen, mkulima kutoka Namibia, akielezea changamoto zinazotokana na ukame unaoathiri maisha yao kila siku”.  Mwenyeji wako ni Bosco Cosmas, karibu! 

Habari za UN
Kuna mkwamo kwenye mkutano wa COP29 huku mapendekezo mapya yakitaka nchi tajiri kuzilipa masikini dola bilioni 250 kwa mwaka

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 2:07


Majadiliano ya mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP29 yamekumbwa na mkwamo huko Baku Azerbaijana muafaka haujapatikana. Majadiliano hayo yaliyotarajiwa kukunja jamvi leo sasa yanaendelea kwa kuwekwa mezani mapendekezo mapya kuhusu ufadhili wa mabadiliko ya tabianchi hasa kwa matifa yanayoendelea. Hakika vuta nikuvute bado inaendelea hata sasa washiriki wako mezani kwakikuna vichwa na kujadili mapendekezo mapya. Mkwamo huo umetokana na kushindwa kuafikiana katika masuala kadhaa kubwa likiwa ufadhili wa  mabadiliko ya tabianchi na hususasn kuhusu ni kiasi gani cha fedha nchi zinazoendelea zinapaswa kupokea kila mwaka hadi ifikapo mwaka 2030 na wapi fedha hizo za ufadhili zitatoka.Nchi zinazoendelea zinataka kulipwa dola trilioni 1.3 kwa mwaka lakini hilo halijaafikiwa na mapendekezo mapya yaliyowasilishwa na raia wa mkataba huo wa UNFCCC yanaonyesha tofauti kubwa na safari ndefu ya kufikia muafaka.Kwa mujibu wa mapendekezo hayo mapya yaliyowasilishwa leo mezani na Rais wa COP29 Mukhtar Babayev yanataka nchi zinazoendelea kupokea dola bilioni 250 kwa mwaka hadi kufikia mwaka 2035 kwa ajili ya kuchukua hatua didi ya mabadiliko ya tabianchi.Na maesema “Fedha hizi zitatoka katika vyanzo mbalimbali ikiwemo sekta za umma na za binafsi, na kitaifa na kimataiifa ikiwemo vyanzo mbadala”.Wakati pia COP29 ikitoa wito wa kufikia lengo la ufadhili wa dola trilioni 1.3 ifikapo mwaka 2035 pia imezikaribisha nchi zinazoendelea kutoa michango ya ziada.Kiwango kilichopendekezwa cha ufadhili kinatarajiwa kuzusha vuta ni kuvute katika majadiliano hayo kwa siku nzima ya leo huenda hadi kesho ingawa mkutano huo unahisi ahuweni kwamba kuna kiwango kilichowasilishwa na unataka hitimisho la mkutano haraka iwezekanavyo. Je nchi zinazoendelea zitapokea vipi pendekezo hili jawabu bado halijulikani. Wapenzi wa UN News Kiswahili endeleeni kufuatilia kwenye kurasa zetu kufahamu hatma ya mkutano huo.

Habari za UN
Jinsi usawa wa kijinsia na rika katika umiliki wa ardhi unavyochochea ukulima na uhakika wa chakula Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 21, 2024 5:05


Mpango wa Usimamizi wa Ardhi (Land Governance program) uliopatiwa jina "Kusaidia kufikia Ajenda 2030 kupitia mageuzi chanya ya ugatuzi wa ardhi (land reforms) katika maeneo ya ardhi za jamii nchini Kenya" umeboresha uhakika wa kupatikana kwa chakula na lishe kupitia upatikanaji wa ardhi kwa wote nchini Kenya. Programu hii imezinduliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kilimo na chakula FAO kwa kushirikiana na Muungano wa Ulaya (EU) katika kaunti 9 ikilenga kuimarisha sekta ya kilimo, ufugaji na uvuvi na umeimarisha usimamizi wa ardhi kwa ajili ya maisha bora na maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika kaunti zote zinazotekeleza. Kupitia video iliyoandaliwa na FAO, Cecily Kariuki anaeleza matokeo yake.Mpango wa Usimamizi wa Ardhi (Land Governance program) uuliopatiwa jina "Kusaidia kufikia Ajenda 2030 kupitia mageuzi chanya ya ugatuzi wa ardhi (land reforms) katika maeneo ya ardhi za jamii nchini Kenya" umeboresha uhakika wa kupatikana kwa chakula na lishe kupitia upatikanaji wa ardhi kwa wote nchini Kenya. Programu hii imezinduliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kilimo na chakula FAO kwa kushirikiana na Muungano wa Ulaya (EU) katika kaunti 9 ikilenga kuimarisha sekta ya kilimo, ufugaji na uvuvi na umeimarisha usimamizi wa ardhi kwa ajili ya maisha bora na maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika kaunti zote zinazotekeleza. Kupitia video iliyoandaliwa na FAO, Selina Jerobon anaeleza matokeo yake katika makala hii..…Wazee wa jamii za kijiji cha Maiyanat iliyoko katika kaunti ya Turkana kaskazini-magharibi mwa Kenya wanafanya kikao cha pamoja hapa, wakiwa wamevalia mavazi yao ya kitamaduni, watoto wakiwa pembeni wakifuatilia kinachoendelea. Wanajadili matumizi mazuri ya mashamba ya jamii zao kwa kuzingatia usawa wa kijinsia na marika yote.Je, awali umiliki wa ardhi ulizingatia usawa huu? Ratinui Macharia ni mwenyekiti wa ardhi ya jamii ya Maiyanat, anasema,“Awali, wanawake na vijana hawakuruhusiwa kushiriki au hata kuchaguliwa kwenye kamati ya ardhi lakini sasa imetuleta sote pamoja.”Lois Kimere ni mwanamke mwanachama wa kamati ya ardhi Maiyanat.“Kulingana na jamii za Maiyanat, wanawake hawakuwa wanaonekana kama watu wenye uwezo wa kuchangia maendeleo ya kijamii. Tulihamasisha wanawake kuhusu mambo ya ardhi, uongozi katika vijijini na katika ngazi za kitaifa hususani serikali, na katika bishara.”Kwa msingi wa dharura, awamu ya kwanza na ya majaribio ya mpango huu ilitekelezwa katika kaunti za Laikipia, Nandi, Pokot magharibi, Baringo, Vihiga, Marsabit, Kajiado, Samburu, Tana River na Turkana.Asha Lekudere ni mwanachama wa ardhi ya jamii ya sereolipi, anasema FAO imeimarisha mtazamo wao.“Zamani tulikuwa na shamba la kikundi. Kisha FAO ikatupeleka kwenye mafunzo kadhaa. Niliweza kujifunza maana ya umiliki wa ardhi kwa jamii yetu ya samburu, uwezo wetu na haki za wanawake.”Chini ya ajenda ya ardhi ya jamii, programu iliwezesha mila shirikishi na jumuishi katika usimamizi wa ardhi kwa njia ya usawa wa jinsia na rika zote.Na hatua gani zinaweza kuchukuliwa mizozo inapotokea? Mpango wa usimamizi wa ardhi umekuza mfumo mbadala wa mahakama, wa kupigania haki za kibinadamu unaojulikana kama AJS, njia bora ya kusuluhisha kesi mashinani na kuachilia ardhi itumike kwa ajili ya jamii zote haraka iwezekanavyo.Jonathan Osewu, Msajili wa ardhi  katika kaunti ya Kajiado anasema,“Katika utamaduni wetu wa kimasai tunazo njia nyingi sana za kutatua mizozo. Kwa hivyo AJS ilipoletwa, ilikuwa ni njia bora ya kuimarisha utaratibu wetu wa jadi wa kutatua kesi.”Na isitoshe, njia za teknolojia za kutoa ramani ya ardhi na rasilimali yote kwa muonekano wa anga, GIS ili kusaidia kufanya maamuzi ya kesi haraka, pia imechangia utangamano katika jamii husika. Vituo hivi vimetekelezwa katika sehemu nyingi ikiwemo kaunti ya Vihiga. Wilber Ottichilo, Gavana wa mkoa wa Vihiga anatoa shukrani kwa FAO.“Kama kaunti ya Vihiga,…

Habari za UN
Waraka kutoka kwa watoto: Kwenu watu wazima, kwa nini mnauruhusu mustakbali wetu kuwekwa rehani?

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 20, 2024 2:20


Leo ni siku ya watoto duniani maudhui mwaka huu yakiwa "Kila mtoto, kila haki"na katika kuhakikisha sauti zao zinasikika kuhusu mustakbali wa utakao, shirika la Umoja wa Maataifa la kuhudumia watoto duniani UNICEF limewapa fursa ya kuandika barua kwenda kwa watu wazima kote duniani ili kutoa madukuduku yao na kutanabaisha wanachokitaka kwa ajili ya mustakbali wao. Hao ni baadhi tu ya makumi ya watoto walioandika barua , hawa ni kutoka Gaza, Tanzania na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC ambao walishika kalamu na karatasi kufikisha ujumbe wao kwa watu wazima wa dunia ya sasa iliyoghubikwa na changamoto lukuki zinazoweka rehani mustakbali wao.Kwa mujibu wa ripoti mpya ya UNICEF ya “Hali ya watoto duniani mwaka 2024: Mustakabali wa Utoto katika Ulimwengu Unaobadilika,” iliyotolewa leo sanjari na maadhimisho ya siku hii kuna masuala matatu makubwa ya kimataifa yatakatoathiri maisha ya watoto ifikapo 2050 na kuendelea. Mosi ni mabadiliko katika idadi ya watu, pili janga la mabadiliko ya tabianchi na migogoro na tatu teknolojiaUNICEF inasema yote haya ni changamoto na fursa ambazo watoto wanaweza kukabiliana nazo katika zama zijazo.Rafif mtoto mkimbizi wa ndani ameandika barua kutoka Palestina ambako vita imetamalaki, anasema“Ninatoka mjini Gaza na sasa nimefurushwa hadi Kusini mwa Gaza. kama watoto Ni haki yetu kuishi kwa usalama na kujenga mustakbali bora”Kutoka mashariki ya Kati hadi Afrika Mashariki kwa Steven akimulika afya“Na nianaandika kwenu kutoka Tanzania. Kwenye jamii yangu watoto wanaugua kila wakati , kwa nini? Huu ndio mustakbali wangu je unasikiliza?”Nako Congo DRC mitihani ni mingi, Andrea anasema“Nataka kushuhudia dunia ambayo kila mtoto anapendwa, dunia ambayo amani inashamiri ni raha na faraja. Napenda kuona hasira zinageuka na kuwa mazungumzo”Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiunga mkono suti hizo za watoto katika ujumbe wake amesema Katika Siku ya Watoto Duniani tunasherehekea washiriki wachanga zaidi wa familia yetu ya kibinadamu. Lakini leo pia ni wakati wa kutambua changamoto kubwa zinazowakabili watoto katika ulimwengu wetu uliogawanyika sana, wenye misukosuko na mara nyingi ulioshamiri ukatili.”Ripoti ya UNICEF imetoa wito wa kuwekeza katika elimu, miji endelevu na yenye mnepo kwa watoto, miundombinu inayohimili mabadiliko ya tabianchi, teknolojia, huduma muhimu na mifumo ya msaada wa kijamii na pia teknolojia iliyo salama kwa watoto ili kupambana na mzigo wa changamoto zinazowakabili.

Habari za UN
COP29 Georgina Magesa: Watoto wana haki ya kuishi katika mazingira salama

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 20, 2024 4:01


Mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29 unaoendelea huko Baku Azerbaijan umeleta pia watoto na vijana wanaharakati wa mazingiria kutoka kote ulimwenguni na kuwapatia fursa kuketi katika meza moja na viongozi ili kuhakikisha mustakabali wao umewekwa katika ajenda ya mkataba huo. Jukumu lao kama wachechemuzi wa mabadiliko chanya na hitaji la mazungumzo na ushirikiano kati ya vizazi lilitambuliwa rasmi katika matokeo ya Mkutano wa Zama Zijazo, SOTF mnamo Septemba 2024.Georgina Magesa, msichana mwenye umri wa miaka tisa na mwanaharakati wa mazingira, ambaye amewakilisha watoto wenzake kutoka Tanzania katika Mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29 huko Baku, Azerbaijan. Anatoa ujumbe mahsusi akianza kwa kusistiza kuwa watoto pia wana mchango katika kutatua changamoto za mabadiliko ya tabianchi.“Watoto wenzangu duniani kote, nyie pia mnaweza kuleta mabadiliko chanya. Anza na hatua ndogo pia muwe na ndoto kubwa. Panda miti. Hifadhi maji. Jifunze kuhusu mazingira yetu. Kwa Pamoja vitendo vyetu vidogo vitageuka mabadiliko makubwa”Katika mwaka huu wa 2024 ambao viwango vya joto duniani vimevunja rekodi duniani, watoto na vijana wanaendelea kupaza sauti zao wakihimiza viongozi wa dunia kuchukua hatua za haraka zinazohitajika ili kushughulikia janga la mabadiliko ya tabianchi. Georgina anasema Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF liko mstari wa mbele, lakini sasa ni wakati wa mshikamano kwa ajili ya mazingira bora kwa watoto wa leo, na wa zama zijazo..“Kwa viongozi wa dunia walioko hapa leo, hii si kazi ya UNICEF pekee. UNICEF inafanya kazi nzuri na sisi watoto, lakini tunahitaji msaada wako ili kujenga ulimwengu wa kesho ambapo hakuna mtoto anayepaswa kuchagua kati ya afya na elimu yake; ambapo hakuna mtoto anayekunywa maji yasiyo salama; hakuna mtoto anayekosa shule kwa sababu ya masuala yanayohusiana na mabadiliko ya tabianchi; na ambapo kila mtoto ana nafasi ya kuwa na afya bora na elimu bora.”Georgina anatamatisha kwa kusisitiza kuwa janga la mabadiliko ya tabianchi limenyima watoto haki zao hivyo kwa kila mtu...“Kumbuka unapolinda mazingira unalinda afya, elimu na ndoto za watoto. Mtoto mwenye afya bora na elimu bora anaweza kubadilisha ulimwengu.”Ama kweli watoto wana haki ya kuishi katika mazingira salama!

Habari za UN
Vijana wafurahia stadi za kuondokana na umaskini Sudan Kusini

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2024 1:57


Vijana katika mji wa Tambura ulioko jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini wanageuza mafunzo ya ufundi stadi kuwa nguvu ya amani na ustawi, mafunzo ambayo yalifanikishwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, UNMISS.Shamrashamra zilitawala wakati vijana 61, wakiwemo wasichana 41 na wavulana 20 walipohitimu mafunzo ya ufundi stadi yenye lengo la kuwaondoa katika umaskini na pia kuwaepusha kutumikishwa katika mzozo unaoendelea nchini humo tangu Desemba 2013.Walifundishwa urembo wa nywele, kutengeneza sabuni, halikadhalika ushoni, mafunzo yaliyofadhiliwa na UNMISS na kutolewa na shirika la kiraia Star Trust Organization, linalohusika na kupunguza ghasia kwenye jamii kwa kuwajegena vijana uwezo.Miongoni mwao ni Suzan James, mama wa watoto wawili aliyejifunza urembo wa nywele na akiwa anamhudumia mteja wakati wa mafunzo anasema.“Ninashukuru mno, kwa sababu nimejifunza mambo mengi ambayo awali sikuyafahamu, lakini sasa ninaweza kufanya. Inanisaidia sana, na ninajivunia na nina furaha. Baada ya hili, nitaenda kufungua sehemu yangu mwenyewe ya urembo wa nywele ili kusaidia jamii.”Huyu ni Justin Alex yeye amejifunza ushoni na akiwa kwenye chereheni yake anasema.. “iwapo nitapekela hii cherehani nyumbani, nitaweza kufanya kazi na kusaidia familia yangu. Kama kijana tusikae nyumbani au tusifanye uhalifu mjini na kusababisha vifo kwa jamii zetu kwa sababu si jambo zuri. Kuanzia sasa tunahitajika kushiriki kwenye shughuli za kusaidia jamii, kama kupeleka hii cherehani nyumbani ili nisaidie jamii yangu.”Wahitimu wamepatiwa vifaa vya kuanzia kufanyie kile walichojifunza. Katika hafla ya utoaji wa vyeti UNMISS iliwakilishwa na afisa wake wa masuala ya ulinzi na ujumuishaji kwenye jamii Ibrahim Tahiru ambaye amesema..“Mradi huu unaweza kuleta amani, lakini pia mradi huu huu unahitaji amani ili uweze kuendelea. Bila amani hivi vitu vitakuwa bure. Kwa sababu wahitimu wanahitaji mazingira yenye amani ili waweze kutumia stadi zao kwa ajili ya kuboresha maisha yao na ya jamii zao. Mradi huu ni ishara ya nia yetu ya kuendelea kushirikiana na Sudan Kusini na kusaidia kufikia amani ya kudumu na kuondokana na umaskini.”Mamlaka za Tambura zina Imani kubwa na mradi huu kama asemavyo Kaimu Kamishna wa Tambura Moses Masisere.“Hakika, Tambura tumekuwa tukililia amani. Kwa hiyo kwa msaada huu tunaamini kuwa mafunzo kwa vijana zaidi kutawasaidia washiriki kwenye harakati za kiuchumi na kupunguza mauaji na uhalifu mwingine Tambura.”

Habari za UN
Uganda inaendelea na mapambano ya kutunza wakimbizi licha ya changamoto za kifedha

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2024 5:11


Kwa miongo kadhaa sasa mfumo wa Uganda wa kuwaweka wakimbizi kwenye makazi badala ya kambi, umesaidia kujengea mnepo wakimbizi na hivyo wanaweza kujitegemea. Wakimbizi wanapata huduma za msingi kama vile hata ardhi ya kulima na kufugia mifugo ili kujipatia kipato. Kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, Selina Jerobon amefuatilia hadithi ya mama mkimbizi kutoka Jamhuri ya  Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ambaye baada ya kupitia machungu na kukimbilia nchini Uganda sasa ameanza kuwa na matumaini ingawa ukata unatishia huduma kama alivyojionea mwenyewe Fillipo Grandi, Kamishna Mkuu wa shirika hilo.

Habari za UN
UNHCR Sudan Kusini yachukua hatua kupunguza madhara ya mafuriko katika sekta ya kilimo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 13, 2024 2:12


Huko Maban, jimboni Upper Nile, kaskazini mashariki mwa Sudan Kusini, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi ,UNHCR linajenga vifaa vya kuhifadhi maji pamoja na makinga maji ili kuepusha mashamba dhidi ya mafuriko ya msimu yanayokumba eneo hilo mara kwa mara, eneo ambalo ardhi yake ina rutuba kwa ajili ya kilimo cha mazao ya chakula na biashara. Hapa shambani jimboni Upper Nile nchini Sudan Kusini, wakulima wakiwemo wenyeji na wakimbizi wakiwa shambani wakiimba.  Awad Usman mwenyeji wa hapa anasema kuimba kunatuliza fikra zangu. Nyimbo hazisaidii kupanda mazao, lakini zinaweza kupunguza msongo wa mawazo.Msongo wa mawazo unatokana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi yaletayo mvua kubwa na mafuriko kwenye mashamba yao.Awad anasema nakumbuka mafuriko ya mwaka 2019, yalisomba kila kitu. Ufuta wote ulisombwa. Mtama pekee ulisalia. Tulikaa ndani ya nyumba kwa siku tano, na tulipotoka tulikuta shamba zima limetwama kwenye maji.Alex Noel Kilong, afisa wa UNHCR anasema mafuriko yanaongeza machungu kwa shida ambazo tayari jamii inakumbana nazo. Mafuriko yanazidi kuongezeka na kusoma barabara, mifugo, mashamba na vituo vya afya hivyo anasema..“Tunahitaji kujenga mbinu za kujipatia kipato. Maban ina fursa kubwa sana, udongo una rutuba, tunatakiwa pia kujenga mapipa ya kuhifadhi maji juu ya ardhi, na maji haya yanaweza kutumiwa wakati wa ukame, ili kilimo kiwe shughuli inayoweza kufanyika mwaka mzima. Kwa njia hiyo tutaweza kupunguza njaa. Tutapunguza ukosefu wa uhakika wa chakula miongoni mwa wenyeji na pia kwa wakimbizi.UNHCR pia imepatia wakulima kama Awad mbegu ya ufuta mweupe, ambayo anasema ni bora na hivyo atakavyovuna , kiasi atauza na nyingine atahifadhi kwa matumizi ya kula nyumbani na pia kama mbegu.

Habari za UN
Mradi wa UNICEF wa kuboresha lishe waleta tabasamu kwa wazazi na watoto Afar Ethiopia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 11, 2024 1:46


Mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF wa kuchagiza kaya kulima bustani za mboga za majani pamoja na ufugaji wa kuku huko jimbo la Afar, kaskazini mashariki mwa Ethiopia umesaidia familia za vijijini kukabiliana na utapiamlo miongoni mwa watoto. Video ya UNICEF Ethiopia inaanza ikimuonesha mtoto akitabasamu, na kisha akiwa na mama yake wakielekea kwenye kituo cha afya. Mama huyu anaitwa Fatuma Kebir na mwanae huyu aliyembeba anaitwa Abdu. Fatuma anasema..“Nilihofia kuwa angeendelea kuwa na utapiamlo. Kwa hiyo nilimpeleka kituo cha afya na mhudumu wa afya akanieleza kuwa mwanangu amepoteza uzito, kama ambavyo nilihisi. Akaniambia nimlishe zaidi, hasa uji uliochanganywa na mayai, maziwa, na mboga.”Video ikimuonesha Fatuma akiandaa uji akichanganya na mayai, mtaalam wa lishe wa UNICEF, Yetayesh Maru, anasema,“Kama sehemu ya mtambuka wa hatua na uratibu dhidi ya utapiamlo kwenye jamii, Fatuma ametambuliwa kuwa ni kaya iliyo hatarini, hivyo amenufaika na mradi wa kisekta wa kuboresha lishe kwa watoto.”Sasa Fatuma na mtoto wake Abdu wanapata tabasamu upya.“Nilimlisha kwa mwezi mmoja kama walivyoshauri na kisha nikarudi kituo cha afya. Mtoa huduma alisema kwamba sasa ana afya na amerudia uzito wake. Nilifurahi sana alipoanza kuongezeka uzito.”Tabasamu lao ni dhahiri hata kwa mtoa huduma Yetayesh, akisema “Sasa Abdul anakua vizuri, na nguvu kamilifu, huku akicheka na mama yake.”

Habari za UN
Uganda imechukua hatua kuhakikisha Kiswahili kinazungumzwa shuleni hadi bungeni: Dkt. Tendo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 6, 2024 6:28


Kwa kutambua thamani na mchango Mkubwa wa lugha ya Kiswahili katika Kanda ya Afrika Mashariki na kimataifa,  sasa serikali ya Uganda imeivalia njuga lugha hiyo kwa kuweka mikakati maalum ya kuhakikisha inafundishwa na kuzungumzwa kuanzia shuleni hadi Bungeni. Flora Nduha wa  Idhaa hii aliyeko mjini Havana Cuba kutujuza yanayojiri katika kongamano la kimataifa la Kiswahili amebainni hayo alipozunggumza na mmoja wa washiriki kutoka nchini Uganda.

Habari za UN
UNICEF na wadau Somalia wafanikisha mradi wa maji kwa wakazi wa Galmudug

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 4, 2024 2:09


Nchini Somalia, ni asilimia 52 tu wananchi ndio wanapata huduma ya maji safi na salama. Wengine hulazimika kutembea umbali mrefu kuteka maji ambayo si ya uhakika. Hata hivyo kwa msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini humo pamoja na wadau, hali sasa inaanza kuimarika. Tuko Adale, mji wa ndani zaidi wa jimbo la kati mwa Somalia, Galmudug. Hapa zaidi ya kaya 2,000 sasa zina huduma ya maji safi na salama, kufuatia ukarabati wa kisima cha maji.Salada Mohammed Omar, yeye ni mfugaji na ni shuhuda wa mradi huu uliotekelezwa na serikali ya jimbo la Galmudug kwa ufadhili wa shirika la Marekani la Misaada ya kimaendeleo USAID na UNICEF.“Tulisafiri muda mrefu kuteka maji, lakini sasa kisima kiko karibu na makazi yetu, tunapata kwa urahisi maji ya kupikia, kufulia na kufanyia usafi.”Video ya UNICEF inaonesha raia na ngamia wakiwa kisimani. Mohammed Yusuf Dirshe ambaye ni kiongozi wa kijamii hapa Adale anasema “awali hakukuwa na tanki la maji wala pampu. Kwa hiyo ilikuwa vigumu kupata maji kwa ajili ya mifugo. Lakini sasa unaona hawa ngamia wanatoka umbali wa hadi wa kilometa 35.”Issack Mohammed, kutoka Kituo cha Amani na Demokrasia mdau wa mradi huu anaeleza kilichofanyika.“Ukarabati ulihusisha kujengea juu matanki, kuweka pampu inayotumia nishati ya jua, na kioski cha maji ili wavulana, wasichana na wanawake waweze kuteka maji kwa urahisi.UNICEF inasema mradi huu unarejesha uhai hapa Adale, kwa kuhakikisha watoto wanakua wakiwa na afya njema, jamii zinastawi na mbinu za kujipatia kipato zinakuwa endelevu.