Podcasts about Umoja

  • 262PODCASTS
  • 3,490EPISODES
  • 14mAVG DURATION
  • 2DAILY NEW EPISODES
  • Jul 29, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024

Categories



Best podcasts about Umoja

Show all podcasts related to umoja

Latest podcast episodes about Umoja

Habari za UN
29 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 29, 2025 11:42


Hii leo jaridani utasikia muhtasari wa habari utakaoangazia hali ya uhaba wa chakula Gaza, mkutano wa maspika wa bunge duniani na mkutano wa tabianchi na afya. Katika jarida pia utasikia mada kwa kina inayoangazia siku ya kimataifa ya marafiki duniani ambayo ilipitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2011 ikiadhimishwa kila mwaka tarehe 30 Julai. Vijana kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino nchini Tanzania - SAUT wanajadili umuhimu wa siku hii.

Habari za UN
Mauaji ya raia Komanda, Ituri, MONUSCO yalaani waasi wa ADF

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 28, 2025 1:47


 MONUSCO, ambao ni Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, imelaani vikali shambulio lililoanza usiku wa juzi tarehe 26 hadi jana 27 Julai 2025 huko Komanda eneo la Irumu, takribani kilomita 60 kusini-magharibi mwa Bunia mji mkuu wa jimbo la Ituri, mashariki mwa nchi. Anold Kayanda ameifuatilia taarifa hiyo na anatujuza zaidi.Taarifa iliyotolewa na MONUSCO jijini katika mji mkuu wa DRC, Kinshasa imeeleza kwamba kwa mujibu wa taarifa za uhakika, shambulio hilo lililofanywa na wapiganaji wa kundi la waasi wa Allied Democratic Forces (ADF) limesababisha vifo vya raia wasiopungua 43 (wanawake 19, wanaume 15 na watoto 9).Inaripotiwa kuwa waathirika wengi waliuawa kwa kutumia silaha za jadi wakiwa ndani ya nyumba ya ibada. Watu kadhaa walitekwa nyara. Nyumba na maduka pia yalichomwa moto, jambo ambalo limezidisha zaidi hali mbaya ya mazingira ya kibinadamu ambayo tayari ni ya kutisha katika jimbo hilo.Naibu Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa Masuala ya Ulinzi na Operesheni ambaye pia ndiye Kaimu Mkuu wa MONUSCO, Vivian van de Perre, amenukuliwa akisema, “mashambulizi haya ya kulenga raia wasio na hatia, hasa ndani ya nyumba za ibada, ni ya kushtusha na ni kinyume kabisa na viwango vyote vya haki za binadamu na sheria ya kimataifa ya kibinadamu. MONUSCO itaendelea kushirikiana kwa karibu na mamlaka za DRC ili kuwalinda raia kwa mujibu wa mamlaka yake.”Kwa kushirikiana na mamlaka za eneo, MONUSCO imetoa msaada kwa hatua za awali, ikiwemo kuratibu shughuli za maziko na kutoa huduma za matibabu kwa majeruhi. Wakati huohuo, MONUSCO imeongeza juhudi za kiusalama ndani na nje ya eneo la Komanda kwa kuongeza idadi ya doria katika eneo hilo.MONUSCO imeweka wazi kuwa inasalia na dhamira thabiti ya kushirikiana na mamlaka za DRC na jamii za wenyeji kusaidia kuzuia mashambulizi mengine, kuwalinda raia, kupunguza mvutano, na kuchangia katika kuimarisha utulivu katika maeneo yaliyoathiriwa na machafuko ya kivita.Ujumbe huo wa Umoja wa Mataifa umeeleza masikitiko na ghadhabu kubwa juu ya vitendo hivi vya kikatili, ambavyo ni ukiukaji mkubwa wa sheria ya kimataifa ya kibinadamu na haki za binadamu. Ujumbe huu unatoa rambirambi zake za dhati kwa familia na jamii zilizoathirika na unasisitiza mshikamano wake na wakazi wa maeneo hayo. MONUSCO pia inazitaka mamlaka za DRC kufanya uchunguzi wa kina kuhusu mauaji haya na kuwafikisha wahusika mbele ya sheria.Aidha, MONUSCO imeurudia wito wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa makundi yote ya waasi kutoka nchi za nje kuweka silaha chini bila masharti na kurejea katika nchi zao za asili.

Habari za UN
Türk ataka Israeli ishinikizwe iondoke maeneo inayokalia ya wapalestina

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 28, 2025 1:54


Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu Volker Türk ameyahimiza mataifa yote ulimwenguni kuchukua hatua za haraka ili Israel ikomeshe uwepo wake kinyume cha sheria katika ardhi ya Palestina inayoikalia kimabavu, na kuhakikisha suluhu ya mataifa mawili inapatikana. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah MushiKamishna Turk ameyasema hayo katika tarifa yake aliyoitoa kwa njia ya video kabla ya kuanza kwa mkutano wa ngazi ya juu hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani unaolenga kujadili Suluhu ya kudumu kwa mgogoro kati ya Israel na Palestina ambao umedumu kwa miongo kadhaa sasa.Turk amesema: “Ninahimiza hatua za haraka za Israel kukomesha uwepo wake kinyume cha sheria katika ardhi ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu, na kwa pande zote kufanyia kazi maendeleo yanayoonekana kuelekea suluhu ya Serikali mbili.”Akatoa angalizo kwa zile nchi zitakazo shindwa kuweka shinikizo kwa Israel kukomesha mauaji huko katika Ukanda wa Gaza.“Nchi ambazo zinashindwa kutumia nguvu zao zinaweza kuwa na hatia katika uhalifu wa kimataifa. Kila siku tunaona madhila yasiyoelezeka huko Gaza na Ukingo wa Magharibi kwa hofu na kufadhaika. Kila siku, tunaona uharibifu zaidi, mauaji zaidi, na udhalilishaji zaidi wa Wapalestina.”Mkuu huyo wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa amehitimisha video yake ya dakika 4 na sekunda 7 kwa kusema kuwa dunia itaihukumu mikutano ya aina hii kwa kile inachokifanya kwa vitendo, na kuongeza kuwa ofisi yake iko tayari kusaidia taifa la Palestina katika ujenzi wa nchi yenye msingi wa haki za binadamu na utawala wa sheria, pindi utulivu utakapopatikana.

Habari za UN
28 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 28, 2025 9:58


Hii leo jaridani Assumpta Massoi anamulika mauaji Ituri, DRC; Haki za binadamu hususan suala la Israeli kukalia Palestina kimabavu; Mifumo ya kuzalisha chakula; Mradi wa umwagiliaji kwa kutumia nishati ya sola huko Bidibidi, Uganda. MONUSCO, ambao ni Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, imelaani vikali shambulio lililoanza usiku wa juzi tarehe 26 hadi jana 27 Julai 2025 huko Komanda eneo la Irumu, takribani kilomita 60 kusini-magharibi mwa Bunia mji mkuu wa jimbo la Ituri, mashariki mwa nchi. Anold Kayanda ameifuatilia taarifa hiyo na anatujuza zaidi.Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu Volker Türk ameyahimiza mataifa yote ulimwenguni kuchukua hatua za haraka ili Israel ikomeshe uwepo wake kinyume cha sheria katika ardhi ya Palestina inayoikalia kimabavu, na kuhakikisha suluhu ya mataifa mawili inapatikana. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah MushiKatika makala Sabrina Said anakupeleka Addis Ababa nchini Ethiopia, kumulika mkutano wa Umoja wa Mataifa wa viongozi kuhusu mifumo ya uzalishaji chakula. Mkutano huu ni wa pili na unafanyika kwa siku tatu, leo ikiwa ni siku ya pili. Mashinani:  Mary, Mkimbizi mwenye umri wa miaka 26 kutoka Sudan Kusini anayeishi katika makazi ya wakimbizi ya Bidibidi nchini Uganda. Yeye ni mkulima wa nyanya kutoka kikundi cha wakulima cha Anika ambao ni wanufaika wa mradi wa umwagiliaji wa Sola uliofanikishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula, WFP.

Habari za UN
Kuinuka Pamoja: Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika Wakiongoza kwa Nguvu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 25, 2025 2:22


Leo, tarehe 25 Julai, ni Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika, ikiwa na kaulimbiu ya mwaka huu: “Kuinuka Pamoja: Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika Wakiongoza kwa Nguvu.” Idhaa ya Umoja wa Mataifa  imefanya mahojiano na Patricia Da Silva, Mratibu wa Kimataifa wa Timu ya Hakuna Kumwacha Yeyote Nyuma katika shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA na akafafanua kidogo siku hii inabeba nini hasa.

Habari za UN
25 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 25, 2025 11:03


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu Gaza, na Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika. Makala inatupeleka nchini Tanzania na mashinani tunakwenda nchini Uganda, kulikoni?Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameonya kuwa mateso yanayoendelea katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, ni zaidi ya janga la kibinadamu – ni janga la maadili linalopasua dhamira ya jumuiya ya kimataifa.Leo, tarehe 25 Julai, ni Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika, ikiwa na kaulimbiu ya mwaka huu: “Kuinuka Pamoja: Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika Wakiongoza kwa Nguvu.” Idhaa ya Umoja wa Mataifa  imefanya mahojiano na Patricia Da Silva, Mratibu wa Kimataifa wa Timu ya Hakuna Kumwacha Yeyote Nyuma katika shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA na akafafanua kidogo siku hii inabeba nini hasa. Makala inatupeleka Pemba, visiwani Zanzibar nchini Tanzania, ambapo mpango mpya wa afya ya mama unawasaidia wanawake wajawazito kukabiliana na upungufu wa damu na kujifungua watoto wenye afya. Kupitia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa ushirikiano na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF na kwa msaada wa kifedha kutoka Wakfu wa Gates, zaidi ya wanawake 16,000 sasa wanapata huduma bora kupitia Virutubisho vya Madini Mbalimbali (MMS) na huduma zilizoboreshwa za kliniki za wajawazito. Assumpta Massoi amefuatilia mradi huo kupitia video ya UNICEF TAnzania.Na katika Arinda Angella, kiongozi wa wanafunzi kutoka Mbarara, Uganda akieleza jinsi ushiriki wake katika mafunzo haya ya uongozi ambayo yameendeshwa kwa ushirikiano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo UNDP na Kituo cha Mafunzo cha Julius Nyerere unavyompa mwanga mpya kuhusu nafasi ya vijana na wanawake katika kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Hali ya Gaza ni janga la maadili linalotikisa dhamira ya ulimwengu - Guterres

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 25, 2025 1:58


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameonya kuwa mateso yanayoendelea katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, ni zaidi ya janga la kibinadamu – ni janga la maadili linalopasua dhamira ya jumuiya ya kimataifa. Leah Mushi na maelezo zaidi.

Habari za UN
Ubia wa Serikali, UNICEF na Wakfu wa Gates Pemba, nchini Tanzania warejesha afya ya wajawazito na watoto

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 25, 2025 3:44


Huko Pemba, visiwani Zanzibar nchini Tanzania, Mpango mpya wa afya ya mama unawasaidia wanawake wajawazito kukabiliana na upungufu wa damu na kujifungua watoto wenye afya. Kupitia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa ushirikiano na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF na kwa msaada wa kifedha kutoka Wakfu wa Gates, zaidi ya wanawake 16,000 sasa wanapata huduma bora kupitia Virutubisho vya Madini Mbalimbali (MMS) na huduma zilizoboreshwa za kliniki za wajawazito. Assumpta Massoi amefuatilia mradi huo kupitia video ya UNICEF TAnzania. 

Habari za UN
24 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 24, 2025 12:16


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika utapiamlo kwa watoto na madhila yasiyo fikirika  kwa wananchi wa kawaida huko Mashariki ya Kati, Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli. Pata pia muhtasari wa habari na jifunze Kiswahili.Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa imeweka bayana jinsi mitandao ya kihalifu duniani inavyoingiza kwenye masoko dawa za binadamu zenye viwango vya juu vya kemikali za sumu ambazo zimesababisha vifo na kuathiri afya ya wagonjwa wengi hasa watoto kwenye nchi za kipato cha chini.Tunasalia na afya ambapo hii leo WHO imethibitisha kwamba Timor-Leste imetokomeza ugonjwa wa malaria, hatua ya kipekee kwa nchi ambayo ilipatia kipaumbele malaria na kuanzisha juhudi za kitaifa na zilizoratibiwa mara tu baada ya kupata uhuru wake mwaka 2002. Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu Volker Türk, amesema maoni ya ushauri yaliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kuhusu wajibu wa Mataifa kuhusiana na mabadiliko ya tabianchi ni ushindi mkubwa kwa wote wanaopigania kulinda hali salama ya tabianchi na sayari kwa ajili ya binadamu wote. Halikadhalika ni uthibitisho usio na shaka kuhusu madhara mapana ya mabadiliko ya tabianchi na wajibu mkubwa wa Mataifa, chini ya sheria za haki za binadamu na zaidi ya hapo, kuchukua hatua za haraka ili kuzuia uharibifu.Na katika kujifunza Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia maana ya methali "UKIONA KIVULI CHA MTU MFUPI KIMEANZA KUREFUKA JUA KUMEKUCHA AU NI MACHWEO."Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
WFP Nigeria kusitisha msaada wa chakula kutokana na ukata na ukosefu wa usalama

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 23, 2025 1:47


Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini Nigeria limesema litalazimika kusitisha msaada wake wa dharura wa chakula na lishe kwa watu milioni 1.3 kaskazini-mashariki mwa nchini hiyo ifikapo mwishoni mwa mwezi huu kutokana na ukata. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
Umwagiliaji kwa kutumia nishati ya sola waleta matumaini kwa wakulima wa Sidama nchini Ethiopia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 23, 2025 2:19


Mradi unaoendeshwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Ethiopia, Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), ubalozi wa China wa kutumia nishati jadidifu ya jua kwa umwagiliaji, umeleta matumaini mapya kwa jamii za wakulima katika mkoa wa Sidama, kusini mwa Ethiopia. Sharon Jebichii na taarifa zaidi.

Habari za UN
Malezi ni kama kukunja shuka lakuvisha kwenye godoro, hakuna ajuae jinsi ya kulikunja

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 23, 2025 3:04


Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF kwakushirikiana na wakfu wa LEGO wametengeneza video yenye kuonesha familia nne na jinsi zinavyopambana na malezi ya Watoto wakiwa ni wazazi kwa mara ya kwanza. Leah Mushi ametazama video hiyo ya takriban dakika 30 na hapa anakuleta simulizi ya familia kutoka nchini Afrika Kusini. 

Habari za UN
23 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 23, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia msaada wa kibinadamu nchini Nigeria, na mradi wa nishati ya sola ya kusaidia wakulima nchini Ethiopia. Makala inakupeleka nchini Afrika Kusini na mashinani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini Nigeria limesema litalazimika kusitisha msaada wake wa dharura wa chakula na lishe kwa watu milioni 1.3 kaskazini-mashariki mwa nchini hiyo ifikapo mwishoni mwa mwezi huu kutokana na ukata.Mradi unaoendeshwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Ethiopia, Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), ubalozi wa China wa kutumia nishati jadidifu ya jua kwa umwagiliaji, umeleta matumaini mapya kwa jamii za wakulima katika mkoa wa Sidama, kusini mwa Ethiopia. Katika makalaShirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF kwakushirikiana na wakfu wa LEGO wametengeneza video yenye kuonesha familia nne na jinsi zinavyopambana na malezi ya Watoto wakiwa ni wazazi kwa mara ya kwanza. Leah Mushi ametazama video hiyo ya takriban dakika 30 na hapa anakuleta simulizi ya familia kutoka nchini Afrika Kusini.Na katika mashinani Noella Bagula, Mwanachama wa Alleluyah Safe Space ambaye ni mama mkimbizi wa ndani kutoka Goma nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ambako wanawake na wasichana wanapitia ukatili wa kijinsia katika migogoro. Bi Bagula anasema yeye sasa anajua jinsi ya kujilinda katika hali hatari kufuatia mafunzo yanayoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya uzazi, (UNFPA) katika maeneo salama yaliyotengwa kwa ajili yao.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
22 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 22, 2025 10:53


Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulika SDG17 katika mazungumzo ya Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa na idhaa hii hivi karibuni hapa New York.  Pia tunakuletea mutasari wa habari na mashinani.Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, leo jijini Geneva Uswisi amekemea amri za hivi karibuni za Israel za kuwahamisha watu Gaza, zilizoambatana na mashambulizi makali katika eneo la kusini-magharibi mwa Deir El Balah na kwamba zimeongeza machungu zaidi kwa mateso ya Wapalestina wenye njaa.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, (WFP) limeeleza leo kuwa kutokana na upungufu wa ufadhili, mamilioni ya watu Sudna Kusini wako hatarini kukosa msaada wa chakula. Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa WFP ambaye pia ni Afisa Mkuu wa Uendeshaji, Carl Skau, ambaye hivi karibuni ametembelea Sudan Kusini anasema, "Kote Sudan Kusini, takriban watu milioni 8 wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula, wengi wao wakitegemea msaada kutoka WFP ili kuendelea kuishi.Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Amina J. Mohammed, ametoa wito mzito wa kuchukua hatua za haraka na za kimfumo ili kuongeza kasi ya maendeleo barani Afrika. Ameyasema hayo wakati wa mkutano wa wadau uliofanyika jana Julai 21 katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, New York, Marekani kujadili matokeo na mapendekezo ya ripoti ya hivi karibuni ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu utekelezaji wa ahadi za maendeleo ya Afrika.Na katika mashinani hii leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameweka bayana shuhuda za kuvutia na madhubuti juu ya kwa nini mapinduzi ya nishati mbadala hayaepukiki sasa, pamoja na manufaa yatakayotokana na mabadiliko ya haki kutoka nishati ya kisukuku kuelekea nishati salama. Ushahidi huo madhubuti ni pamoja na makao makuu ya Umoja wa Mataifa kutumia nishati ya sola na Guterres amefika kwenye eneo lenye paneli hizo.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Wavuta matoroli, wavaa glovu kutekeleza dakika 67 za kujitolea kwa heshima ya Mandela

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 21, 2025 3:42


Kujitolea kwa jamii ni jambo ambalo Umoja wa Mataifa na wadau wanalipatia kipaumbele kama njia ya kusaidia kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs. Ijumaa iliyopita, ofisi ya Masuala ya Kimataifa ya Meya wa jiji la New York, nchini Marekani kwa kushirikiana na Idara ya Mawasiliano ya Kimataifa ya Umoja wa Mataifa pamoja na Ubalozi wa kudumu wa Afrika Kusini kwenye Umoja wa Mataifa, Wakfu wa Kisiwa cha Gavana, Wakfu wa Nelson Mandela na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa walitekeleza mradi wa kujitolea kwenye kisiwa hicho kama sehemu ya maadhimisho ya siku ya Mandela duniani tarehe 18 Julai mwaka huu wa 2025. Mradi ulilenga kulinda mazingira, je ni kwa vipi? Assumpta Massoi alikuwa shuhuda wetu.

Habari za UN
21 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 21, 2025 9:35


Jaridani leo tunaangazia msaada wa kibinadamu katika ukanda wa Gaza, na uhakika wa chakula  nchini Uganda. Makala tunaangazia mradi wa kulinda mazingira na kazi za kujitolea. Mashinani inamulika utayari wa nchi ya Nigeia kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP, kupitia Apu yake ya kidigitali Gawa Chakula au ShareTheMeal, limeingia ushirikiano na Apu maarufu huko Mashariki ya Kati iitwayo Careem na kuzindua kampeni ya kuchangisha msaada wa dharura kwa watu wanaokumbwa na njaa katika eneo la Gaza na Ukingo wa Magharibi maeneo yanayokaliwa kimabavu na Israeli.Licha ya changamoto za ufadhili, Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini Uganda linasisitiza umuhimu wa usafirishaji katika kutoa msaada wa chakula. Sahir Aslam, Mkuu wa Idara ya Ugavi ya WFP Uganda, akizungumza kutokea huko huko Uganda katika maghala ya shirika hilo anafafanua kila kilomita moja ambayo msaada wa chakula wa WFP unasafiri.Katika makala Assumpta Massoi anatupitisha kwenye kazi ya kujitolea iliyofanyika kuadhimisha siku ya Nelson Mandela Julai 18 hapa Marekani.Na katika mashinani fursa ni yake Esse Oduwan, msichana mwenye umri wa miaka 14 kutoka Nigeria, akihoji utayari wa nchi kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs baada ya nchi tatu ikiwemo Eswatini na Bangladesh kuwasilisha tathmini za utekelezaji wa Malengo hayo yanayofikia ukomo 2030.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Toa msaada kupitia Careem App ili WFP izidi kuwasaidia Wapalestina Gaza

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 21, 2025 1:35


Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP, kupitia Apu yake ya kidigitali Gawa Chakula au ShareTheMeal, limeingia ushirikiano na Apu maarufu huko Mashariki ya Kati iitwayo Careem na kuzindua kampeni ya kuchangisha msaada wa dharura kwa watu wanaokumbwa na njaa katika eneo la Gaza na Ukingo wa Magharibi maeneo yanayokaliwa kimabavu na Israeli. Leah Mushi na taarifa zaidi

Habari za UN
Madaraka ni kwa ajili ya kuinua watu si kuwakandamizi – Guterres

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 18, 2025 1:51


Umoja wa Mataifa leo katika makao yake makuu jijini New York, Marekani, umeadhimisha Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela kwa heshima ya maisha na urithi wa shujaa wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi, nchini Afrika Kusini, Nelson Rolihlahla Mandela, al maarufu Madiba. Assumpta Massoi amefuatilia na kutuandalia taarifa ifuatayo.

Habari za UN
Viongozi wa Afrika watambue wao ni watumishi wa wananchi - Kennedy Odede

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 18, 2025 1:29


Mapema kabla ya kushiriki hafla hii ya utoaji wa tuzo katika siku hii ya kimataifa ya Nelson Mandela hapa New York, Kennedy Odede alizungumza na Zipporah Musau wa Umoja wa Mataifa.

Habari za UN
18 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 18, 2025 9:57


Jaridani leo naangazia hafla ya Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela katika makao makuu ya Umoja wa mataifa na ujumbe wa washindi wa Tozo ya Mandela. Makala tunakwenda nchini Angola na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Umoja wa Mataifa leo katika makao yake makuu jijini New York, Marekani, umeadhimisha Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela kwa heshima ya maisha na urithi wa shujaa wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi, nchini Afrika Kusini, Nelson Rolihlahla Mandela, al maarufu Madiba. Assumpta Massoi amefuatilia na kutuandalia taarifa ifuatayo.Mapema kabla ya kushiriki hafla hii ya utoaji wa tuzo katika siku hii ya kimataifa ya Nelson Mandela hapa New York, Kennedy Odede alizungumza na Zipporah Musau wa Umoja wa Mataifa.Katika makala Sabrina Saidi anatupeleka huko Manispaa ya Caluquembe jimboni Hiula, Kusini Magharibi mwa Angola, Shirika la Afya Duniani (WHO), kwa kushirikiana na mamlaka za mitaa, limeongeza juhudi za ushirikishwaji wa jamii na afua za afya ya umma, ili kukabiliana na mlipuko wa kipindupindu unaoendelea nchini humo. Lengo kuu likiwa ni kuongeza uelewa kuhusu kipindupindu kupitia mikutano ya jamii, jumbe za afya ya umma, na ujenzi wa miundombinu muhimu kama vile vyoo na vituo vya kupata maji safi ya kunywa ndani ya manispaa.Na katika mashinani fursa ni yake Purity Christine, mwanzilishi mwenza wa kampuni ya ShopOkoa, jukwaa la kifedha linalowawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati kujiunga na mfumo wa kijamii wa akiba na mikopo nchini Kenya, anasimulia safari yao kupitia Programu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP ya timbuktoo Fintech, ambapo wamejifunza jinsi ya kuboresha jukwaa lao na kuweka malengo makubwa ya kufikia maelfu ya wafanyabiashara barani Afrika.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
17 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 17, 2025 11:05


Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina inayoangazia Afrika Mashariki Fest ya nchini Uganda kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania na Uganda inayotumia  kampeni yake ya “Twende Zetu Butiama” ili kuyatumimiza malengo hayo.Hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO katika eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli limeongoza uhamishaji wa wagonjwa 35, wengi wao watoto kwenda Jordan, kwa ajili ya matibabu zaidi kutokana na huduma za afya kuvurugwa Gaza. WHO inasema zaidi ya watu 10,000 Gaza wanahitaji kuhamishiwa nchi nyingine kwa ajili ya matibabu.Harakati za kusaka amani ya kudumua nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC zinazidi kushamiri ambapo hatua za hivi karibuni ni kutoka Muungano wa Afrika, (AU) zikiongozwa na marais wa zamani, Sahle Work Zewde wa Ethiopia, na Catherine Samba-Panza wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, (CAR).kuelekea mkutano wa 30 wa nchi wanachama wa Mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP30 huko Brazil baadaye mwaka huu, huko Nairobi, nchini Kenya bara la Afrika linajipanga kuhakikisha mkutano huo unakuwa na tija. Dkt. Richard Muyungi, Mwenyekiti wa Kamati ya Wataalamu na mabalozi wanaoshughulikia masuala ya tabianchi barani Afrika, anasema wanachokitaka.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIKWANYUKWANYU!.Mwenyeji wako ni Leah Moshi, karibu!

Habari za UN
Kujituma na kutokata tamaa ndio siri ya kufanikiwa kwenye mafunzo kwa vitendo UN - Sarah Nshoka

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 16, 2025 3:27


Kutoka Dar es Salaam hadi Geneva, na sasa New York. Ni safari ya kujifunza, kujaribu na kufanikiwa. Kwa vijana wengi barani Afrika, Umoja wa Mataifa huonekana kuwa ndoto isiyowezekana. Lakini kijana huyu kutoka Tanzania anathibitisha kuwa kwa nia thabiti na bidii, ndoto hiyo inaweza kuwa kweli. Kupitia programu ya mafunzo kwa vitendo ya Umoja wa Mataifa, amejifunza mengi kuhusu utawala, maendeleo na kujenga ujasiri wa kushiriki katika kazi za kimataifa. Sarah Nshoka alipata fursa kuzungumza na Shraon Jebichii katika makala hii.

Habari za UN
16 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 16, 2025 10:59


Hii leo jaridani tunaangazia wakazi wa Gaza walioko eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli; na ujumbe wa Uganda wa hatua zake katika kulitekeleza lengo namba 5 la Usawa wa Kijinsia. Makala tunasalia hapa makao makuu na mashinani tunakwenda Tanzania, kulinkoni?Amri mpya za kuhama zinazotolewa na jeshi la Israeli kwa wakazi wa Gaza walioko eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli zinazidi kuhatarisha maisha ya makumi ya maelfu ya watu ambao wameshahama mara kadhaa, wakiwemo wagonjwa wanaotakiwa kupata huduma za kusafisha damu mwilini kila wiki.Jukwaa la Kisiasa la Ngazi ya Juu la Umoja wa Mataifa kuhusu Maendeleo Endelevu, HLPF, la mwaka huu wa 2025 linaendelea hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Wadau mbalimbali zikiwemo nchi zinazohudhuria zinabadilishana uzoefu, changamoto na mafaniko katika kutekeleza Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Mendeleo Endelevu, SDGs. Uganda imeeleza hatua zake katika kulitekeleza lengo namba 5 la Usawa wa Kijinsia.Makala tunasalia hapa New York, Marekani, ambako Sharon Jebichii wa idhaa hii ya Kiswahili amezungumza na kijana kutoka Tanzania anayeshiriki mafunzo kwa vitendo kwenye Idara ya hapa Umoja wa Mataifa ya Masuala ya Kiuchumi na Kijamii, UNDESA. Anasimulia safari yake ya mafunzo kwa vitendo, changamoto, mafanikio na ushauri kwa vijana wengine wanaotamani kufuata nyayo zake.Na katika mashinani Edtrudith Lukanga Mkurugenzi wa Mradi wa Usimamizi wa Mazingira na Maendeleo kwenye Ziwa Victoria, EMEDO. Akishiriki kwenye mkutano hapa New York, MArekani wa kusongesha majawabu bunifu yenye ushahidi ili kuzuia watu kuzama majini, ametaja moja ya majawabu hayo ambayo ni Programu ya Shule ya Usalama kwenye maji huko Tanzania.Mwenyeji wako ni Leah Moshi, karibu!

Habari za UN
Uganda yaeleza inavyotekeleza lengo namba 5 la Malengo ya Maendeleo Endelevu - HLPF 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 16, 2025 2:12


Jukwaa la Kisiasa la Ngazi ya Juu la Umoja wa Mataifa kuhusu Maendeleo Endelevu, HLPF, la mwaka huu wa 2025 linaendelea hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Wadau mbalimbali zikiwemo nchi zinazohudhuria zinabadilishana uzoefu, changamoto na mafaniko katika kutekeleza Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Mendeleo Endelevu, SDGs. Uganda imeeleza hatua zake katika kulitekeleza lengo namba 5 la Usawa wa Kijinsia. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
15 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 15, 2025 10:57


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulika juhudi za kinamama wajawazito na wanao kuambatana wakihudhuria kliniki kwa ajili ya mimbasalama. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani.Takribani wapalestina 900 wameuawa katika wiki za hivi karibuni huko Ukanda wa Gaza, eneo linalokaliwa kimabavu na Israeli. wakihaha kupokea chakula. Msemaji wa Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa Thameen Al-Kheetan amewaeleza waandishi wa habari Geneva, Uswisi kuwa watu 674 kati yao waliuawa wakiwa kwenye maeneo ya Mfuko wa Kiutu wa Gaza, (GHF) unaoendeshwa na Israeli na Marekani.Wakati huo huo Bwana Al-Kheetan amezungumzia mauaji yanayoendelea Ukingo wa Magharibi ikiwemo Yerusalemu Mashariki akisema, “muathirika mdogo zaidi ni Laila Khatib mwenye umri wa miaka miwili. Alipigwa risasi ya kichwa na jeshi la Israeli akiwa nyumbani kwao kijijini Ash-Shuhada.”Na leo ikiwa siku ya kimataifa ya stadi kwa vijana Sangheon Lee, Mkurugenzi wa Ajira na Sera katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Ajira amesema …lazima tuhakikishe kuwa vijana wanapata ujuzi ambao ni wa maana, unaoweza kutumika katika mazingira mbalimbali, na unaotambuliwa na waajiri.Na kaika mashinani tunakupeleka jijini Nairobi, Kenya, ambako kupitia video iliyoandaliwa na washirika wetu Radio Domus, tunamsikia Dennis Mabuku, Mkuu wa Idara ya Usalama, Afya, Mazingira na Ubora katika kampuni ya BOC Kenya. Dennis anaeleza jinsi wanavyoichakata hewa ya kawaida na kuisafisha ili kupata  hewa safi ya oksijeni kwa ajili ya matumizi ya hospitali na mabaki mengine kwa ajili ya matumizi mengine ya viwandani.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
14 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 14, 2025 9:51


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya malengo ya maendeleo endelevu, na mradi wa uvuvi unaosaidia kupunguza migogoro Ituri DRC. Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Jukwaa la Kisiasa la Ngazi ya Juu la Maendeleo Endelevu, HLPF la mwaka huu wa 2025 limeanza leo hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ambapo wadau kutoka katika nyanja mbalimbali duniani wanakutana kujadili namna ya kuharakisha utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs.Kutoka msituni kupigana upande wa waasi hadi kuingia ziwani na kuwa mtaalamu wa ufugaji wa samaki, ndio simulizi tunayopata kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, simulizi ya matumaini kwa mustakabali wa jamii iliyogubikwa na vita kila uchao.Katika makala tunakupeleka mkoani Mwanza, kaskazini-magharibi mwa Tanzania ambako kuelekea siku ya kimataifa ya vijana na stadi hapo kesho Julai 15, Sabrina Said anazungumza na mmoja wa vijana  anayetumia majukwaa ya kidijitali kutoa elimu ya      uelimishaji rika.Na kaika mashinani leo fursa ni yake Imam Ustaadhi Matano Bin Salim kutoka Kaunti ya Mombasa nchini Kenya, ambaye amewezesha shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kufika kwenye kituo cha mafunzo ya dini kupatia watoto chanjo. Akisema typhoid ni homa ya tumbo, na measles ni ugonjwa wa surua.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
HLPF 2025: Jukwaa la UN kuangazia afya, usawa wa kijinsia na bahari katika juhudi za kufanikisha SDGs

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 14, 2025 1:57


Jukwaa la Kisiasa la Ngazi ya Juu la Maendeleo Endelevu, HLPF la mwaka huu wa 2025 limeanza leo hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ambapo wadau kutoka katika nyanja mbalimbali duniani wanakutana kujadili namna ya kuharakisha utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
Teknolojia na ushirikiano vinavyotatua changamoto za tabianchi - wakulima wa maeneo kame Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 11, 2025 3:57


Katika maeneo kame ya Kenya, mvua moja ikikosa kunyesha, inaweza kuleta njaa, umaskini na kukosa matumaini. Lakini badala ya kukata tamaa, jamii za wakulima katika kaunti za Tana River sasa zinatoa simulizi kwa ujasiri na mabadiliko. Kupitia msaada kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kitaifa ya Kusimamia Ukame (NDMA) na Serikali za Kaunti, wakulima wanatumia teknolojia rafiki kama umwagiliaji wa maji kwa nishati ya jua, kilimo cha kisasa na ushirika wa kijamii kuinua maisha yao. Sharon Jebichii na maelezo zaidi.

Habari za UN
Trakoma au Vikope si tatizo tena la kiafya la umma nchini Burundi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 11, 2025 1:54


Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) leo Julai 11 limetangaza kwamba limeidhinisha Burundi kuwa imefanikiwa kuondoa ugonjwa wa macho unaofahamika kama trakoma au vikope kama tatizo la kiafya la umma, na kuifanya kuwa nchi ya nane katika Kanda ya Afrika ya WHO kufikia mafanikio haya muhimu. Anold Kayanda anafafanua zaidi kuhusu taarifa hii.

Habari za UN
Wanawake wapatanishi warejesha maelewano baina ya jamii Ituri nchini DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 11, 2025 1:51


Huko Djugu, jimboni Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wanawake wapatanishi waliopatiwa mafunzo na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO, wamewezesha kurejea kwa mazungumzo baina ya jamii za Ezekere na Mandro ambazo kwa miaka kadhaa zilikuwa zinazozana. Sabrina Saidi na maelezo zaidi.

Habari za UN
11 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 11, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya afya nchini Burundi, na elimu ya upatanishi kwa jamii Ituri nchini DRC. Makala tunakupeleka nchini Kenya kumulika kilimo kichopatia riziki jamii na mashinani tunasalia hapa makao makuu kusikia ujumbe kuhusu haki za wasichana.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) leo Julai 11 limetangaza kwamba limeidhinisha Burundi kuwa imefanikiwa kuoandoa ugonjwa wa macho unaofahamika kama trakoma au vikope kama tatizo la kiafya la umma, na kuifanya kuwa nchi ya nane katika Kanda ya Afrika ya WHO kufikia mafanikio haya muhimu.Huko Djugu, jimboni Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wanawake wapatanishi waliopatiwa mafunzo na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO, wamewezesha kurejea kwa mazungumzo baina ya jamii za Ezekere na Mandro ambazo kwa miaka kadhaa zilikuwa zinazozana.Katika makala Sharon Jebichii anatupeleka  Kaunti ya Tana River huko Kenya kumulika juhudi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kitaifa ya Kusimamia Ukame (NDMA) na Serikali za Kaunti katika kilimo, ambayo imeleta mabadiliko na matumaini kwa jamii za wakulima.Na kaika mashinani leo ikiwa siku ya idadi ya watu duniani, nampisha Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na AFya ya Uzazi, Dkt. Natalia Kanem akizungumzia umuhimu wa takwimu katika kuboresha maisha ya wakazi wa dunia!Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

WNHH Community Radio
MarceyLynn, Once Again: Sons of Mystro brothers Malcolm and Umoja McNeish

WNHH Community Radio

Play Episode Listen Later Jul 10, 2025 53:46


MarceyLynn, Once Again: Sons of Mystro brothers Malcolm and Umoja McNeish by WNHH Community Radio

brothers sons umoja mystro wnhh community radio
Habari za UN
10 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 10, 2025 10:36


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kushuhudia mafunzo ya ukufunzi kwa wanadhimu wa Umoja wa Mataifa. Pia tunakuletea muhtasari wa habari zikiwemo za mkataba wa amani DRC na Rwanda, UKIMWI, na maadhimisho ya Siku ya kimataifa ya Kiswahili, na uchambuzi wa neno.Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wamekaribisha mkataba wa amani kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Rwanda uliotiwa saini tarehe 27 mwezi uliopita wa Juni, huku wakishukuru Marekani, Qatar na Muungano wa Afrika kwa juhudi za usuluhishi.Ukata uliosababishwa na wahisani kukata au kupunguza ghafla na kwa kiasi kikubwa ufadhili kwenye miradi ya kupambana na UKIMWI umekuwa na madhara kwa nchi zilizoathiriwa vibaya na ugonjwa huo, imesema ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na Ukimwi, UNAIDS.Leo kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Nairobi, Kenya kumefanyika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya lugha ya Kiswahili ambapo wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Juu ya Mangu wametuma ujumbe wao wa umuhimu wa lugha hiyo kupitia ngonjera.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno "CHARAKAMU na BARAKALA!Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Mradi wa UNFPA wa michezo na elimu warejesha matumaini kwa vijana wakimbizi wa DRC nchini Burundi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 9, 2025 3:11


Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA), kwa kushirikiana na serikali ya Burundi, limekuwa mstari wa mbele katika kuwasaidia vijana wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), walioko kwenye kambi ya Musenyi, mkoani Rutana huko Burundi. Kupitia michezo, tamaduni, na shughuli za elimu ya afya ya uzazi, vijana hawa wamepata matumaini mapya na fursa ya kujenga maisha yao upya. Mradi huu unaangazia umuhimu wa kuwekeza kwa vijana walioko katika mazingira magumu ili kuwasaidia kufikia ndoto zao.

Habari za UN
Angalau kila mtu awe na anwani ya barua pepe - Mshiriki WSIS

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 9, 2025 2:01


Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Viongozi kuhusu Upashanaji wa Taarifa duniani, (WSIS) ukiingia siku ya 3 hii leo huko Geneva, Uswisi, washiriki wanapazia sauti umuhimu wa kila mtu kokote pale aliko afikiwe na teknolojia inayomwezesha kupokea taarifa kwa urahisi, usahihi na kwa haraka.

Habari za UN
09 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 9, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia ziara ya Katibu Mkuu wa UN Amina J. Mohammed akiwa barani Afrika; na Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Viongozi kuhusu Upashanaji wa Taarifa duniani. Makala tunakwenda nchini Burundi na mashinanitunasalia hapa makao makuu, kulikoni?Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed akiwa ziarani barani Afrika ambapo juzi tarehe 7 aliingia nchini Gambia, kwa njia ya mtandao wa X ameonesha namna ziara yake ilivyokuwa ya mafanikio kwa kukutana na viongozi na wadau mbalimbali nchini humo katika harakati za kufanikisha Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu.Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Viongozi kuhusu Upashanaji wa Taarifa duniani, (WSIS) ukiingia siku ya 3 hii leo huko Geneva, Uswisi, washiriki wanapazia sauti umuhimu wa kila mtu kokote pale aliko afikiwe na teknolojia inayomwezesha kupokea taarifa kwa urahisi, usahihi na kwa haraka.Katika makala shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA), kwa kushirikiana na serikali ya Burundi, limekuwa mstari wa mbele katika kuwasaidia vijana wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), walioko kwenye kambi ya Musenyi, mkoani Rutana huko Burundi. Kupitia michezo, tamaduni, na shughuli za elimu ya afya ya uzazi, vijana hawa wamepata matumaini mapya na fursa ya kujenga maisha yao upya. Mradi huu unaangazia umuhimu wa kuwekeza kwa vijana walioko katika mazingira magumu ili kuwasaidia kufikia ndoto zao.Na katika mashinani fursa ni yake Dkt. Natalia Kanem, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA ambaye katika mahojiano maalum na Idhaa ya Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa kila msichana anahitaji huduma muhimu za afya uzazi ili waweze kuendelea na elimu, akitaja mfano wa kazi zao nchini Kenya.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Ziara ya Naibu Katibu Mkuu UN yaangazia usongeshaji SDGs Gambia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 9, 2025 2:04


Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed akiwa ziarani barani Afrika ambapo juzi tarehe 7 aliingia nchini Gambia, kwa njia ya mtandao wa X ameonesha namna ziara yake ilivyokuwa ya mafanikio kwa kukutana na viongozi na wadau mbalimbali nchini humo  katika harakati za kufanikisha Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
08 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 8, 2025 10:03


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha katika mkutano wa 69 wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW69 kumsikia Mkurugenzi wa TEN/MET Nasra Kibukila kuhusu jitihada zao za kuhakikisha watoto wote wa Kitanzania wanapata elimu bora, jumuishi na yenye usawa, kwa kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali wa elimu ndani na nje ya nchi.Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Turk, amesikitishwa sana na mauaji ya jana ya watu wapatao 10, sambamba na uporaji na uharibifu wa mali wakati polisi walipokabiliana na waandamanaji kwenye mji mkuu wa Kenya, Nairobi na katika kaunti nyingine 16.Huko Geneva, Uswisi kumeanza mkutano wa siku 4 kuhusu matumizi ya Akili Mnemba au AI kwa maslahi ya wote ambapo Katibu Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la mawasiliano, ITU, Doreen Bogdan-Martin ameuliza washiriki ni jambo gani wanafanya AI ihudumie ubinadamu.?Na kuelekea kumbukizi yamauaji ya Srebrenica tarehe 11 mwezi huu wa julai, Umoja wa Mataifa unakumbuka mauaji hayo yaliyofanyika wakati wa vita vilivyofuatia baada ya kuvunjika kwa iliyokuwa Yugoslavia. Zaidi ya watu 100,000 huko Bosnia na Herzegovina waliuawa kati ya mwaka 1992 na 1995, wengi wao wakiwa waislamu wa Bosnia. Umoja wa Mataifa unasema mauaji ya Srebrenica ni moja ya vipindi vya kiza zaidi vya vita.Na katika mashinani tunakupeleka katika miji ya mpakani ya Matar na Muon katika eneo la Gambella nchini Ethiopia ambako maelfu ya wakimbizi wamewasili kutoka Jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini wakikimbia vita na njaa, na sasa wanasubiri usajili na usaidizi kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula. Nyandow Wie Deng ni mmoja akisimulia yaliyomkumba.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Kiswahili kitukuzwe shairi - Jescah Muyia UNV

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 7, 2025 1:48


Kuelekea siku ya Kiswahili duniani hapo Julai 7 mwaka huu ikibeba maudhui “Kiswahili: zama zilizopita, sasa na zijazo” kwa lengo la kutathimini ukuaji na mabadiliko katika ligha hiyo adhimu leo tunakupeka Nairobi Kenya kwenye mpango wa kujitolea wa Umoja wa Mataifa UNV apmbapo mmoja wa wafanyakazi wa mpango huo mghani wa mashairi Jescah Muyia ameamua kuienzi lugha hiyo kwa shairi murua.

Habari za UN
Pamoja na mafanikio makubwa bado kuna changamoto kumjumuisha kikamili mwanamke mwenye ulemavu Zanzibar: Ms. Abeida Abdallah

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 7, 2025 3:33


Kisiwa cha Zanzibar nchini Tanzania Mashariki mwa Afrika kimepiga hatua kubwa katika suala la ujumuishaji wa watu wenye ulemavu katika sekta mbalimbali kwa kuzingatia mikataba ya Umoja wa Mataifa ya watu wenye ulemavu na pia usawa wa kijinsia kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma. Lakini licha ya mafanikio waliyoyapata katika masuala kama elimu na haki za watu wenye ulemavu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Abeida Rashid Abdallah akizungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii kandoni mwa kikao cha mwaka huu cha 69 cha kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW69 amesema bado kuna kibarua kikubwa cha kufanya kuhakikisha kila mtu  hususan mwanamke mwenye ulemavu anajumuishwa. Kwa undani zaidi ungana nao katika makala hii.

Habari za UN
07 JULY 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 7, 2025 10:00


Hii leo jaridani tunaangazia mafuriko katika Jimbo la Texas, Marekani, na shairi linaloenzi siku ya Kiswahili Duniani. Makala inamulika haki za watu wenye ulemavu hususani wanawake, na mashinani tunakwenda Osaka nchini Japani kunakofanyika maonesho au EXPO2025, kulikoni?Umoja wa Mataifa umeonesha mshikamano mkubwa na watu wa Jimbo la Texas, Marekani serikali kufuatia mafuriko makubwa yaliyotokea Ijumaa na kusababisha vifo hasa vya watoto na uharibifu mwingine mkubwa.Kuelekea siku ya Kiswahili duniani hapo Julai 7 mwaka huu ikibeba maudhui “Kiswahili: zama zilizopita, sasa na zijazo” kwa lengo la kutathimini ukuaji na mabadiliko katika ligha hiyo adhimu leo tunakupeka Nairobi Kenya kwenye mpango wa kujitolea wa Umoja wa Mataifa UNV apmbapo mmoja wa wafanyakazi wa mpango huo mghani wa mashairi Jescah Muyia ameamua kuienzi lugha hiyo kwa shairi murua.Makala inaturejesha Zanzibar Tanzania katika sehemu ya mwisho ya mahojiano baina Flora Nducha wa Idhaa hii na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Abeida Rashid Abdallah kuhusu ujumuishwaji wa watu wenye ulemavu ungana nao.Na katika mashinani, kuanzia Aprili 13 hadi Oktoba 2025 huko Osaka nchini Japani kunafanyika maonesho au EXPO2025 ikileta nchi na mashirika ya Umoja wa Mataifa maudhui yakiwa Kuumba Jamii za siku zijazo kwa maisha yetu. Banda la Umoja wa Mataifa limedadavua maudhui hayo na kuwa kujikita kwenye Kuungana kwa Mustakabali Bora washiriki wakionesha masuala tofauti tofauti ikiwemo onesho la picha likisimamiwa na mpiga picha kutoka Ufaransa. Mhusika anafafanua.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Mafuriko Texas - Umoja wa Mataifa waonesha mshikamano

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 7, 2025 1:37


Umoja wa Mataifa umeonesha mshikamano mkubwa na watu wa Jimbo la Texas, Marekani serikali kufuatia mafuriko makubwa yaliyotokea Ijumaa na kusababisha vifo hasa vya watoto na uharibifu mwingine mkubwa. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

SBS Swahili - SBS Swahili
Rwanda yajipata pabaya katika ripoti ya kamati ya usalama ya Umoja wa Mataifa

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jul 7, 2025 7:07


Ripoti ya siri ya watalaam wa Umoja wa Mataifa imeishtumu Rwanda kwa kutoa maagizo na kudhibiti shughuli za waasi wa M23.

Habari za UN
03 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 3, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayokupeleka nchini Uganda katika Mbuga ya Wanyama inayofahamika kwa jina Murchison Falls National Park kuangazia namna washiriki wa Kongamano la kimataifa la lugha ya Kiswahili lililofanyika mapema mwaka huu jijini Kampala walivyofurahia mazigira asili nchini Uganda na namna yanavyounufaisha ulimwengu.Mkutano wa 4 wa ufadhili kwa maendeleo umemalizika leo huko Sevilla, Hispania ambapo mashirika ya kiraia yametaka utekelezaji kwa vitendo kwa yale yaliyomo katika nyaraka iliyopitishwa iliyopatiwa jina Makubaliano ya Sevilla.Mmoja wa wawakilishi wa mashirika ya kiraia, Paula Sevilla amesema kinachohitajika ni uongozi kutoka nchi tajiri ambako ndiko zilizko kampuni kubwa zinazokwepa kodi.Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO kuhusu vijana na mifumo ya uzalishaij chakula na kilimo inaonesha kuwa karibu asilimia 85 ya vijana duniani wanaishi katika nchi za kipato cha chini na cha kati, ambako mifumo hiyo ni muhimu kwa ajira na maisha yao. Ripoti inasema kuwajumuisha vyema vijana katika mifumo hiyo kunaweza kuleta mchango wa hadi trilioni moja ya dola kwa uchumi wa dunia..Na mwezi uliopita wa Juni umeshuhudia ongezeko kubwa la familia za raia wa Afghanistan zikirejeshwa nyumbani kutoka Iran, tofauti na awali ambapo waliokuwa wakirejeshwa walikuwa ni wanaume peke yao.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mchabuzi wetu Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA nchini Tanzania, anachambua neno KUTOHOA.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
UNICEF Tanzania: Nidhamu chanya huchagiza makuzi bora kwa mtoto

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 2, 2025 1:45


Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limekuwa likihimiza umuhimu wa malezi na makuzi chanya kwa watoto kama njia mojawapo ya kulinda haki kuu nne za msingi za mtoto ambazo ni kuishi, kuendelezwa, kushirikishwa na kulindwa.

Habari za UN
02 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 2, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia wahamiaji na njia bunifu ya kuwawezesha kujikimu kimaisha, na malezi bora ya watoto nchini Tanzania. Makala tunasalia huko huko Tanzania kumulika uwekezaji na ufadhili wa miradi ya maendeleo, na mashinani tunakwenda nchini Kenya.Katika Mkutano wa 4 wa Kimataifa wa Ufadhili wa Maendeleo (FFD4) unaoendelea jijini Seville, Hispania, Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limetoa wito wa kuimarisha uwekezaji wa kibunifu katika uhamiaji wa watu ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kusaidia kuziba pengo la kila mwaka la dola trilioni 4 za ufadhili wa maendeleo.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limekuwa likihimiza umuhimu wa malezi na makuzi chanya kwa watoto kama njia mojawapo ya kulinda haki kuu nne za msingi za mtoto ambazo ni kuishi, kuendelezwa, kushirikishwa na kulindwa..Katika makala mkutano wa 4 wa Ufadhili wa Maendeleo (FFD4) ukikunja jamvi leo huko Sevilla Hispania, juhudi za kuhakikisha nchi zinajitegemea kifedha kupitia vyanzo jumuishi na vya ubunifu zimezidi kupewa kipaumbele. Katika hafla ya kufungua mafunzo ya Muongozo wa Upatikanaji wa Fedha kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa, au Intergrated Local Financing Framework (ILFF) yaliyofanyika katika Manispaa ya Morogoro kaskazini-mashariki mwa Tanzania  hivi majuzi , Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la Mpango wa Maendeleo nchini humo, UNDP umetoa mafunzo ya  namna halmashauri zinaweza kuandaa mikakati madhubuti ya kuhimiza maendeleo ya ndani kupitia ushirikiano kati ya sekta binafsi, mashirika ya kiraia, benki na jamii.Na mashinani, vijana na wahudumu wa afya katika kaunti ya Kajiado nchini Kenya, wameshikamana kuhamasisha umma kuhusu hedhi salama. Kupitia video iliyoandaliwa na washirika wetu Radio Domua, mmoja wa vijana anaelezea umuhimmu wa hedhi salama kama njia ya kutokomeza unyanyapaa dhidi ya wanawake na wasichana.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
IOM yasema uwekezaji wa kibunifu katika uhamiaji ni muhimu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 2, 2025 1:59


Katika Mkutano wa nne wa kimataifa wa Ufadhili wa Maendeleo (FFD4) unaoendelea jijini Seville, Hispania, Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limetoa wito wa kuimarisha uwekezaji wa kibunifu katika uhamiaji wa watu ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kusaidia kuziba pengo la kila mwaka la dola trilioni 4 za ufadhili wa maendeleo. Anold Kayanda anaeleza zaidi.

Habari za UN
UNDP Tanzania yahimiza ubunifu wa vyanzo vya mapato ili kuvutia wawekezaji

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 2, 2025 3:45


Mkutano wa 4 wa Ufadhili wa Maendeleo (FFD4) ukiendelea huko Sevilla Hispania, juhudi za kuhakikisha nchi zinajitegemea kifedha kupitia vyanzo jumuishi na vya ubunifu zimezidi kupewa kipaumbele. Katika hafla ya kufungua mafunzo ya Muongozo wa Upatikanaji wa Fedha kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa, au Intergrated Local Financing Framework (ILFF) yaliyofanyika katika Manispaa ya Morogoro kaskazini-mashariki mwa Tanzania  hivi majuzi , Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la Mpango wa Maendeleo nchini humo, UNDP umetoa mafunzo ya  namna halmashauri zinaweza kuandaa mikakati madhubuti ya kuhimiza maendeleo ya ndani kupitia ushirikiano kati ya sekta binafsi, mashirika ya kiraia, benki na jamii. Lengo ni kuendelea kuunga mkono serikali na wadau mbalimbali barani Afrika  katika kutafuta mbinu mbadala za kufadhili maendeleo.Sharon Jebichii na maelezon zaidi.

Habari za UN
01 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 1, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulika ukame na uhakika wa upatikanaji wa maji na kusikia jinsi taifa la Chile, linatumia sera kushawishi mabadiliko yanayoweza kukabiliana na tatizo hilo. Pia tunakuletea muhtasari na mashinani.Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Iran, Stefan Priesner amesema wanachofanya hivi sasa ni kupanga upya programu za Umoja wa Mataifa nchini humo wakimulika vipaumbele vipya kufuatia mashambulizi yaliyoanza tarehe 13 mwezi Juni mwaka huu na kubadili mwelekeo wa kazi zao. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi kutokea Tehran mji mkuu wa Iran, Bwana Priesner amesema sasa tuko kwenye mazugumzo ya serikali kuona ni vipi tutapanga upya programu zetu kukidhi mahitaji mapya yanayoanza kuwa dhahiri, ikiwa ni siku chache tu tangu mashambulizi yakome baada ya sitisho la mapigano kuridhiwa.Huko huko Geneva, Uswisi lakini akizungumza kutoka Nairobi Kenya, Shaun Hughes, ambaye ni Mratibu wa Dharura kwa mzozo wa Sudan katika shirika la Umoja wa MAtaifa la Mpango wa Chakula, WFP amewaambia waandishi wa habari kuwa hali ni tete kwa mamilioni ya raia wa Sudan waliokimbilia nchi jirani kuepuka mapigano nchini mwao.Shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake, UN Women linapotimiza miaka 15 tangu kuanzishwa kwake, limesema dunia imeshuhudia maendeleo muhimu katika usawa wa kijinsia ambayo yamebadilisha maisha ya wanawake na wasichana kote duniani. Licha ya ya kusherehekea, juhudi za kusukuma usawa wa kijinsia zinaonekana kurudi nyuma.Na mashinani, Mkutano wa 4 wa Ufadhili wa Maendeleo (FFD4) ukiendelea huko Sevilla Hispania, Natalia Toschi, Mkuu wa kitengo cha uwekezaji wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD annasema ni wakati wa kufikiria upya jinsi maendeleo yanavyofadhiliwa kwa kuzingatia mifumo ya kilimo cha mazao ya chakula ili kukuza ukuaji wa kiuchumi vijijini.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
30 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 30, 2025 11:41


Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa 4 wa ufadhili kwa ajili ya maendeleo FFD4 huko Sevilla Hispania, na siku ya Mabunge tukizungumza na mmoja wao kutoka Tanzania. Makala inatupeleka nchi Kenya na mashinani tunarejea huko huko Tanzania, kulikoni?Mkutano wa 4 wa ufadhili kwa ajili ya maendeleo FFD4 umeng'oa nanga rasmi leo huko Selilla Hispania kwa wito wa kuziba pengo la ufadhili wa maendeleo ili kutimiza ahadi ya kimataifa ya kutomwacha yeyote nyumba. Mkutano huo uliowaleta pamoja washiriki 2,500 kutoka nchi 150 wakiwemo wakuu wa nhi 50 na wadau wengine unasema kuna pengo la dola trilioni 4 katika ufadhili wa maendeleo linalohitaji kuzibwa.Leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya mabunge ikijikita katika harakati za kuwezesha mabunge kufanikisha usawa wa kijinsia wakati huu ambapo Umoja wa Mataifa unaeleza ni kwa vipi Wanawake bado hawawakilishwi kwa kiwango cha kutosha katika mabunge ya kitaifa na ya mitaa duniani kote, jambo ambalo linapunguza haki zao za kisiasa na ushawishi wao juu ya sheria na bajeti..Katika makala tanatupeleka kaunti ya Kajiado, Kenya, katika eneo la EMbulbul, kukutana na vijana wanaotumia maarifa ya kilimo cha kisasa kubadilisha maisha yao na ya jamii, wakisema teknolojia imefungua njia mpya ya kuinua maisha ya wakulima wadogo, hasa kwa kutumia ukulima wa kisasa unaotumia maarifa na Teknolojia.Na mashinani, fursa ni yake Sandra Aloyce, Msichana mwenye umri wa miaka 12 kutoka Tanzania ambaye kupitia Mpango wa Vijana unaofadhiliwa na shirika la UNICEF uitwao “Furaha” unaotoa mafunzo kwa wazazi kuhusu umuhimu wa uwepo wa wazazi wote katika ukuaji wa mtoto ana ujumbe.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!