POPULARITY
A mix beamed in from the future by singeli's young star. If singeli has a new era, DJ Travella is its leading light. At just 23 years old, the Tanzanian producer is pushing the genre into fast, frenetic and unmistakably futuristic territory. And while there aren't too many entries in the RA Podcast's 20-year history where you can say, "this has no parallel whatsoever," RA.984 shatters that assumption in style. Singeli emerged from Dar es Salaam's underground in the early '00s, forged from limited resources and unlimited creativity. Producers looped and sped up taarab instrumentals using basic software like Virtual DJ, creating a sound that was chaotic, witty and lightning fast. With support from local studios like Sisso and Pamoja, singeli took root as the breakneck pulse of Tanzanian youth culture. Travella—real name Hamadi Hassani—came up outside that infrastructure. He began producing music aged ten, self-taught and internet-savvy. By 2022, he was touring Europe with Kampala-based collective Nyege Nyege and gaining global attention for a distinct style he's dubbed "cyber-singeli." Like gabber, hardcore and jungle before it, singeli is unapologetically go hard or go home. It's unique and utterly infectious. After all, what could possibly connect pop provocateur Arca to the late president of Tanzania? Not much—except singeli. Travella's RA Podcast is a white-knuckle ride through this blistering sonic universe. It's wild and joyful yet controlled—a window into one of the most exciting young minds in global club music. @user-643479850 Find the interview and tracklist at ra.co/podcast/984.
Hii leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani unaanza mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW69, kusanyiko kubwa zaidi la kila mwaka la Umoja wa Mataifa linalomulika usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake mwaka huu washiriki wakiwa zaidi ya 25,000. Selina Jeroboni na taarifa zaidi.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Umoja wa Mataifa kupitia miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa Pamoja wa Kigoma, KJP nchini Tanzania, unaolenga kuhakikisha wanawake na wasichana wanajumuishwa kwenye mipango ya kuhimili na kukabili mabadiliko ya tabianchi, kwa kuwajengea uwezo.Kuelekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake Machi 8, tathmini mpya ya Umoja wa Mataifa iliyowekwa wazi leo ikiangazia haki za wanawake miaka 30 baada ya Azimio la Beijing inaonesha uwepo wa maendeleo katika usawa wa kijinsia, kama vile sheria dhidi ya ubaguzi na sera jumuishi za kijinsia. Hata hivyo, ripoti hiyo inaeleza uwepo bado wa ubaguzi wa kijinsia uliojikita katika jamii, ukiendelea kuwazuia wanawake na wasichana kupata fursa.Ripoti nyingine ya Umoja wa Mataifa iliyochapishwa leo ikiangazia Sudan imefichua vitendo vya watu kukamatwa kiholela, mateso, na unyanyasaji huko Khartoum vinavyotekelezwa na Vikosi vya wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF) na pia Jeshi la Serikali ya Sudan (SAF). Ripoti hiyo imearifu pia kuwa makumi ya maelfu ya watu wamewekwa katika mazingira duni tangu Aprili 2023.Kutokana na kupungua kwa ufadhili wa misaada ya kibinadamu duniani, Umoja wa Mataifa leo jijini Geneva, Uswisi kutenga dola milioni 110 ili kusaidia majanga yaliyopuuzwa katika nchi 10 barani Afrika, Asia, na Amerika Kusini, zikiwemo Niger, Somalia, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Zambia.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia maana ya methali “MCHAWI AKIFICHUA MIRIMO YA WACHAWI HU UAWA”.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Katika kitongoji cha Komanda jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, doria za pamoja zinazoendeshwa na walinda amani wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO na jeshi la serikali FARDC zimeimarisha usalama kwenye maeneo ya raia. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Kwa sehemu kubwa makala ya mtazamo wako imeangazia kuhusu hali ya mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na mkutano wa pamoja kati ya jumuia ya Afrika mashariki EAC na jumuia ya Nchi za kusini mwa Afrika SADC kutafuta suluhu ya kudumu ya mzozo wa mashariki mwa DRC, huko Gabon upinzani umemtaka kiongozi wa mpito kuweka wazi msimamo wake kuhusu ushiriki wake katika uchaguzi mkuu, na hatua ya rais wa Marekani Donald Trump kukata ufadhili kwa shirika la misaada USAID pia Marekani kudhibiti eneo la Gaza
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Makala ya Changu Chako ,chako Changu hii leo yanaangazia historia na tamaduni za kabila la Wakalenjin kutokea Kenya.Kisha kwenye kipengele cha Leorparle Francophone tutangaazia maonyesho kuhusu mabadiliko yaliyofanyika kwenye muziki kuanzia miaka ya 1960 alafu kwenye kipengele chetu ya mwisho cha Muziki tutamuangazia mwanamuziki Yemi Alade.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Ikiwa Jumamosi ya mwisho ya mwaka 2024, tunakuuliza ni tukio gani au mashindano gani ya kispoti yalikufurahisha zaidi mwaka huu? Pamoja na hayo; tumeangazia kifo cha mchezaji nguli wa voliboli nchini Kenya Janet Wanja, Uganda yaibuka mabingwa wa CECAFA michuano ya kufuzu AFCON U17, raundi ya mwisho ya kufuzu michuano ya CHAN 2024, uchambuzi wa raundi ya 18 ya mechi za Ligi Kuu ya Soka nchini Uingereza.
Viongozi wa Jumuiya yawa Kalenjin wanao ishi New South Wales wanajiandaa kuwasilisha vyeti vya usajili wa Jumuiya kwa wanachama wao jioni ya Ijumaa 20 Disemba 2024.
Makala haya yataangazia Historia ya nchi ya Kenya na jinsi ilivyopata Uhuru,kwenye kipengele cha pili utaskia safari ya vijana wanaofanya sanaa ya Uchoraji kutoka shirika lisilo la kiserikali la Uweza Art Gallery na mwisho kabisa kwenye kipengele cha historia ya mwanamuziki utaskia historia yake Juma Jux kutokea Tanzania.
Kupitia mradi wa Pamoja wa Kigoma, KJP, awamu ya Pili, Shule ya Msingi Buhigwe, iliyoko wilayani Buhigwe, mkoa wa Kigoma, ilipatiwa mafunzo kupitia Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), likishirikiana na asasi isiyo ya kiserikali RECODA. Mafunzo haya yalilenga mbinu bora za kilimo ambapo wanafunzi waliweza kuanzisha bustani za mboga kupitia somo la Elimu ya Kujitegemea. Mradi umeanza kutekelezwa na matunda yanaanza kuonekana kama asimuliavyo Assumpta Massoi kwenye makala hii.
Katika makala haya, tutazungumza na watu muhimu kama vile mgonjwa wa UKIMWI, daktari, na mkunga anayeelimisha kuhusu jinsi ya kuzuia watoto kuambukizwa virusi vya UKIMWI wakati wanapozaliwa. Pamoja, tutafahamu changamoto, mafanikio na hatua zinazochukuliwa katika vita hivi.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Umaarufu wa wasanii wa injili Ben & Chance, una endelea kuongezeka kila uchao nchini Rwanda na kimataifa.
Tume hiyo huru imeyasema hayo katika taarifa mpya ya msimamo wa kisheriia iliyotolewa mjini Geneva Uswis kuhusu eneo linalokaliwa la Palestina ikiwemo Jerusalem Mashariki ambayo imeweka wazi maoni ya tume kuhusiana na wajibu wa serikali na jinsi Baraza Kuu na Baraza la Usalama linavyoweza kutambua na kutekeleza mbinu na hatua sahihi zinazohitajika kwa kazi hiyo hadi mwisho wa ukaliwaji huo, na kwa haraka iwezekanavyo.Tume ihiyo imebaini kwamba maoni ya ushauri ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki kuhusu matokeo ya Kisheria yanayotokana na sera na desturi za Israel katika eneo linalokaliwa la Palestina ikiwa ni pamoja na Jerusalem Mashariki ni wenye mamlaka na usio na utata kwa kusema kwamba kuendelea kuwepo kwa Israel katika eneo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu ni kinyume cha sheria na sheria ya kimataifa.Taarifa hiyo ikitolewa Geneva Gaza kwenyenyewe hali inaendelea kuwa tete, kwa mujibu wa Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestinna UNRWA Phillipe Lazzarini, kwani shule nyingine ya UNRWA imeshambuliwa leo Jabalia Kaskazini mwa Gaza, watu kadhaa wameripotiwa kuuawa na miongoni mwao Watoto wengi waliokuwa wakipata hifadhi katika jengo hilo.Lazzarini amesema hili ni shambulio la tatu dhidi ya majengo ya UNRWA kwa wiki moja. Na pia wafanyakazi wa shirika hilo wanaendelea kuuawa sasa wameffikia 231 tangu kuanza kwa vita hii Oktoba mwaka jana.Naye msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF James Elder akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva Uswisi hii leo amesema “Gaza ni mfano halisi wa ulimwengu wa kuzimu duniani kwa watoto milioni moja wa eneo hilo. Na hali inazidi kuwa mbaya, siku baada ya siku, tunapoona athari za kutisha za mashambulizi ya anga ya kila siku na operesheni za kijeshi za Israek kwa watoto wa Kipalestina.”Nalo shirika la kuratibu misaada ya kibinadamu OCHA likiangazia Ukingo wa Magharibi limesema “Vikosi vya Israel vimekuwa vikitumia mbinu mbaya za vita katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, na kuibua wasiwasi mkubwa juu ya matumizi ya nguvu kupita kiasi na kuongeza mahitaji ya kibinadamu ya watu.” Ameelezea wasiwasi kuhusu mashambulizi ya walowezi wa Israel dhidi ya Wapalestina na miti yao ya mizeituni wakati huu wa mavuno ya kila mwaka.
VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
Nchini Ethiopia hususan katika jimbo la Somali, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limechukua hatua kusaidia manusura wa ukatili wa kijinsia kuweza kujenga upya maisha yao wakati huu ambapo takwimu za shirika hilo zinaonesha kuwa zaidi ya wanawake na wasichana milioni 370 duniani kote wamekumbwa na ukatili wa kingono wakati wa utoto wao, yaani kabla ya kutimiza umri wa miaka 15. Sauti hiyo ya Nasteyo Sahane Layle, Meneja wa kushughulikia visa vya ukatili wa kijinsia dhidi ya akina mama, watoto na wanawake hapa Gode, jimboni Somali mashariki mwa Ethiopia akisema kuwa kazi kubwa tunayoifanya ni visa vinavyohusu ukatili wa kingono.Ni katika video ya UNICEF iliyochapishwa kuonesha kiza kinachokumba watoto wa kike hususan leo ambayo ni siku ya kimataifa ya mtoto wa kike.Hapa Gode, UNICEF imeanzisha kituo hicho cha kutoa huduma zote na sasa kimekuwa ni kama eneo salama kwa manusura wa ukatili wa kingono.Anaonekana mmoja wa wasaka huduma kituoni hapa akifika tayari kupatiwa huduma, sura yake imefichwa ili kuficha utambulisho wako.Anapatiwa huduma ikiwemo kupimwa mapigo ya moyo na vipimo vingine na kisha kupatiwa dawa.Nasteyo anasema,“kinachotusikitisha zaidi ni watoto wenye umri wa chini ya miaka 18 ambao walibakwa, na sasa mustakabali wao umeharibiwa.”Pamoja na Nasteyo, wahudumu wengine katika kituo hiki ni Nimo, Faduo, Ifrah na Hamdi, wote wanawake.Ni kutokana na huduma zao, manusura wanajiona wako salama kwani wanapatiwa huduma za kisaikolojia na nyingine muhimu wanazohitaji.Na kisha kupata tena uwezo wa kujiamini na kujenga upya maisha yao. TAGS: AfyaAdditional: AfyaNews: Ukatili wa Kingono, EthiopiaRegion: AfrikaUN/Partner: UNICEF
Mashirikika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yameonya kwamba hali ya kibinadamu inazidi kuwa mbaya nchini Lebanon wakati mashambulizi ya anga ya Israel yakiendelea kushika kasi na kuwafungisha virago maelfu ya watu, wengi wakikimbia nchi jirani ya Syria ambako nako si shwari. Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO linasema hali nchini Lebanon ni janga la kibinadamu watu wengi wamejeruhiwa , wengine kupoteza maisha na mfumo wa afya umelemewa.Kupitia ukurasa wake wa X Mkurugenzi mkuu wa WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema katika jitihada za kuwasaidia waathirika ndege ya kwanza ya msaada wa vifaa vya kitabibu vya upasuaji, dawa na vifaa tiba vingine imewasili mapema leo mjini Beiruti na vifaa hivyo vitatosha kuwatibu maelfu kwa maelfu ya watu na kuokoa maisha yao na ndege nyingine mbili zitawasili baadaye leo.Kwa upande wake Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema maelfu ya watu wanaendelea kukimbia mashambulizi ya makombora ya Israel na wengine wakivuka mpaka kwa miguu kuingia Syria kusaka uslama. Pamoja na kwamba linafanya kila liwezekanalo kuwasidia , limesema msaada zaidi unahitajika kukabiliana na wimbi la watu wanaoendelea kufurushwa.Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa mjini Geneva wao “ Wamelaani vikali mashambulizi yanayotekelezwa kwenda Israel na makundi yenye silaha yasiyo ya kiserikali yaliyopo Lebanon ambayo yamesababisha watu 63,000 kutawanywa nchini Israel. Wamesema wahusika lazima wawajibishwe na watu waliotawanywa wapewe msaada na ulinzi.”Hata hivyo wamesisitiza kwamba“ Israel haiwezi kutumia uhalifu huo kama sababu ya kuhalalisha uhalifu wao nchini Lebanon unaojumuisha vitendo vya machafuko yenye lengo la kuleta hofu miongoni mwa raia wanaowashambulia.”Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, chini ya muda wa mwezi mmoja idadi ya wakimbizi wa ndani nchini Lebanon imeongezeka mara tatu na zaidi ya watu 1,600 wameuawa na wengine takriban 346,000 kujeruhiwa wakiwemo watoto 127.
Leo hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kando ya mjadala mkuu wa UNGA79, viongozi wanakutana kwenye Mkutano wa Ngazi ya Juu ukimulika usugu wa viuavijiumbe maradhi, Antimicrobial Resistance, kwa kiswahili ikiitwa pia UVIDA, au Usugu wa Vimelea dhidi ya Dawa. Katika taarifa ya Pamoja iluyotolewa kwenye mkutno huo na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la afya duniani WHO, la mazingira UNEP, la chakula na kilimo FAO na shirika la afya ya Wanyama duniani WOAH, usugu wa viua vijiumbe maradhi unahusika moja kwa moja na vifo milioni 1.3 na kuchangia vingine milioni 5 kila mwaka.Unaweza kujiuliza ni nini na kwa nini ni muhimu wakutane? Bosco Cosmas, wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa amezungumza na Profesa Mshiriki wa Vimelea Vya Magonjwa katika Chuo Kikuu cha Sayans iza Afya Bugando, mkoani Mwanza, Kaskazini Magharibi mwa Tanzania.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka katika hospitali ya kanda Bugando, mkoani Mwanza, kaskazini-magharibi mwa Tanzania kumulika chanzo na madhara ya usugu wa vimelea dhidi ya dawa au UVIDA. Pia tunakuletea habari kwa ufupi na katika kujifunza Kiswahili tunabisha hodi nchini Zimbabwe, kulikoni?Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa leo kandoni mwa mjadala mkuu ulioingia siku ya tatu moja ya mada zinazopewa uzito ni usugu wa vijiuavijiumbe maradhi au Anti-Microbial Resistance (AMR). Katika taarifa ya Pamoja iluyotolewa kwenye mkutno huo na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la afya duniani WHO, la mazingira UNEP, la chakula na kilimo FAO na shirika la afya ya Wanyama duniani WOAH, usugu wa viua vijiumbe maradhi unahusika moja kwa moja na vifo milioni 1.3 na kuchangia vingine milioni 5 kila mwaka.Pia katika katika Mjadala Mkuu wa baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA79 miongoni mwa waliopanda katika mimbari leo kuhutubia ni Rais wa Jamhuri ya Kenya William Samoei Ruto ambaye amesema “Dunia iko katika wakati wa changamoto kubwa za kiusalama, ahati ya chata ya Umoja wa Mataifa kuokoa viizazi kutokana na vita iiko katika hatihati.” Aesema nadhariaya wao dhidi yetu ni chachu ya changamoto kubwa ikiwemo vita. Kuanzia Gaza, Darfur, Ukraine, Yemen, Mashariki mwa DRC , Sudan, Sahel na uhalifunchini Haiti,migogoro inasambaratisha maisha na uwezi wa watukuishi katika kiwangocha kihistoria.”Naye Rais wa Malawi Lazarus McCarthy Chakwera, amesema kila nchi mwanachama wa Umoja wa Mataifa inahusiana na nchi nyingine katika mambo matatu, ushirikiano migogoro na ushindani ulio na usawa, hivyo jinsi ya kushughulikia masuala hayo ndio itaamua mustakbali wa vizazi vvya kesho hasa ushirikiano unaofaidisha wote, ushindani ulio na usawa na utatuzi wa migogoro. Amesisitiza kuwa ushirikiano ni kitu cha muhimu sana na mfano mzuri ni nchi yake Malawi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili fursa ni yake Mary Chigumira kutoka Zimbabwe, mmoja wa waafrika aliyefika kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa hapa Jijini New York kwa ajili ya Mkutano wa Zama Zijazo uliokamilika hivi majuzi akieleza anavyotamani kujifunza zaidi lugha ya Kiswahili.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Mjadala mkuu wa wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kikao cha 79 umeingia siku ya pili hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa nasi tunaendelea kuzungumza na washhiriki mbalimbali wakiwemo kutoka asasi za kiraia kusikia maoni yao kuhusu mkutano huu. Flora Nducha amebahatika kuongea na mwanaharakati mmoja wao kutoka nchini Zimbabwe.Bi. Chigumira ni mwanaharakati anayepiganiia haki za wanawake na wasichana nchini Zimbabwe kupitia shirikika lale la kiraia la “Unlimited hope alliance” au Muungano wa matumaini yasiokwisha ambao unawasaidia wasichana wenye changamto katika masuala ya elimu, huduma za maji , usafi na usafi wa mazingira au WASH na kuwawezesha kiuchumi.Bi. Chigumira amekuwa hapa Umoja wa Mataifa kuhudhuria mkutano uliomalizika wiki hii wa Zama Zijazo na kabla hajarejea nyumbani ana ujumbe kwa viongozi wa dunia wanaokutana katika mjadala mkuu wa UNGA79 kuhusu mchango wao katika hataraki za kusaidia wanasichana na wanawake vijijini, “Kwa viongozi tunawaomba wawe sehemu yetu, hatutaki kuwa katika safari hii peke yetu, tunataka kuambatana nao. Endapo tutaambatana Pamoja nao tufafanikisha lengo letu.”Bi. Chigumira amesema hilo litawatia moyo hata wanawake na wasichana wanaopitia machungu na kukata tamaa, anawashauri akisema, “Kwa wanawake na wasichana ambao mnanisikiliza , asilani hamjachelewa, hata kama maisha yako yaliharibiwa, ulipata mtoto ukiwa na umri wa miaka 14, huo sio mwisho wa safari.”Mkuu huyo wa shirika hilo la kiraia la Unlimited hope Alliance ametoa mfano hai katika shirika lake, “Tulikuwa na wasichana ambao walipata mimba wakiwa na umri wa miaka 14, lakini sasa wamerejea shuleni , hivyo hamjachelewa hata wale walio katika biashara ya ngono, mnaweza kubadili maisha yenu yaliyoharibika. Njooni kwetu mpate mafunzi ili muweze hata kuanzisha biashara zenu.”Bi.Chigumira anasema anaamini wakijengewa uwezo basi shirika lao litaweza kusaidia wasichana wengi zaidi.
Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO nchini Sudan Kusini limesema licha ya uchaguzi mkuu kuahirishwa nchini humo hadi 22 Desemba 2026 kitu kikubwa kwa taifa hilo changa zaidi barani Afrika ni amani. Akizungumza na Flora Nducha wa Idhaa ya Kiswahili katika Makala hii Meshack Malo mwakilishi wa FAO Sudan Kusini amesema kuahirisha uchaguzi huo ambao awali ilikuwa ufanyike 22 Desemba mwaka huu 2024 ni uwamuzi wa Wasudan na wana sababu za msingi, hivyo jumuiya ya kimataifa itaendelea kushirikiana nao na kuliombea amani taifa hilo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa Katibu Mkuu wa UN wa Tabaka la Ozoni, na mssada wa kibinadamu kwa wenyeji wa kisiwa kidogo cha Carriacou, Grenada waliokumbwa na kimbunga Beryl. Makal tunakupeleka nchini Nigeria na mashinani nchini Sudan.Pamoja na chapisho lililotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la hali ya hewa (WMO) kuangazia ushahidi unaoongezeka kwamba tabaka la ozoni kwa hakika liko mbioni kurejea katika hali nzuri, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake maalumu kwa ajili ya siku ya leo ya Kimataifa ya Uhifadhi wa Tabaka la Ozoni amesisitiza mataifa yote ulimwenguni kuidhinisha na kutekeleza maazimio ya maboresho ya Itifaki ya Montreal yaliyozaa Marekebisho ya Kigali kwa lengo la kupunguza gesi chafuzi zenye nguvu zinazoongeza joto duniani.Kimbunga Beryl, kilichopiga tarehe 1 Julai 2024, kimewaacha wakazi wa kisiwa kidogo cha Carriacou, Grenada, na athari kubwa . Kufuatia changamoto zinazowakabili wasamaria kutoka maeneo mbalimbali likiwemo Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) wamewasaidia kurejesha matumaini kama anavyosimulia Anthony St. Hilaire manusura wa kimbunga hicho.Makala inatupeleka Maiduguri Nigeria ambako mafuriko yanayoshuhudiwa baada ya bwawa la Alau kupasua kingo zake kutokana na mvua kubwa hayajawahi kuonekana katika miaka ya karibuni. Shirika la Umoja wa Matifa la mpango wa chakula duniani WFP ni mdau Mkubwa katika kufikisha misaada kwa waathirika na mkuu wa ofisi yake ya Maiduguri Emmanuel Bigenimana anaeleza alichokishuhudia.Na katika mashinani Aziza, mama wa watoto wanne kutoka Sudan ambaye alikuwa mhudumu wa kibinadamu na sasa amejikuta mkimbizi nchini Uganda baada ya kukimbia nyumbani kwao Sudan kufuatia mapigano yaliyoanza Aprili 2023. Nyumba yao iliporwa kila kitu na sasa akiwa ukimbizi anasimulia maisha yalivyo tangu ahamishwe na kuwa mkimbizi huku akinufaika na msaada kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Kimbunga Beryl, kilichopiga tarehe 1 Julai 2024, kimewaacha wakazi wa kisiwa kidogo cha Carriacou, Grenada, na athari kubwa . Kufuatia changamoto zinazowakabili wasamaria kutoka maeneo mbalimbali likiwemo Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) wamewasaidia kurejesha matumaini kama anavyosimulia Anthony St. Hilaire manusura wa kimbunga hicho. Anthony aliyekumbwa na hofu kubwa wakati mawimbi makali ya bahari na upepo wa kimbunga Beryl vilipoanza kusambaratisha nyumba yake anasema hakika hali ilikuwa si hali, kwani akijua fika kulikuwa na hatari ya kupoteza maisha ."Awali, upepo ulianza kuvuma kwa nguvu, tukafunga kila kitu. Kisha kina cha bahari kilianza kupandana mawimbi kugonga madirisha na mlango. Ilibidi tufungue mlango ili kupunguza kasi ya upepo na maji."Anthony anaendelea kueleza jinsi alivyorejea nyumbani baada ya kimbunga, na akakuta kila kitu kimekwenda na maji"Haikuwa rahisi. Rafiki yangu mmoja alinipigia simu na kuniambia kuwa kila kitu kimesafishwa. Nilipofika, karibu nilie. Akaniambia usijali, haya ni mambo ya kidunia. Tumebakiwa na jambo kubwa zaidi ambalo ni uhai."Pamoja na maafa hayo na athari zake IOM ikishirikiana na wadau wengine wamekuwa mstari wa mbele kuhakikisha familia zenye uhitaji mkubwa hazikati tamaa , zinakuwa na matumaini na kuapata misaada haraka iwezekanavyo.
Pamoja na chapisho lililotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la hali ya hewa (WMO) kuangazia ushahidi unaoongezeka kwamba tabaka la ozoni kwa hakika liko mbioni kurejea katika hali nzuri, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake maalumu kwa ajili ya siku ya leo ya Kimataifa ya Uhifadhi wa Tabaka la Ozoni amesisitiza mataifa yote ulimwenguni kuidhinisha na kutekeleza maazimio ya maboresho ya Itifaki ya Montreal yaliyozaa Marekebisho ya Kigali kwa lengo la kupunguza gesi chafuzi zenye nguvu zinazoongeza joto duniani. Katika ujumbe huo, Bwana Guterres ameeleza kwamba Marekebisho ya Kigali ya Itifaki ya Montreal ambayo yanalenga katika kupunguza hydrofluorocarbons (HFCs) ambazo ni gesi zinazoongeza joto duniani yanaweza kuchangia katika kuendeleza juhudi za kukabiliana na tabianchi, kulinda watu na sayari. “Na hilo linahitajika zaidi kuliko wakati mwingine wowote kwani rekodi za joto zinaendelea kuongezeka.” Akasisitiza.Itifaki ya Montreal ilikubaliwa mnamo mwaka 1987 huko nchini Canada na kuanza kutumika mwaka 1989. Maboresho yake yalifanyika mwaka 2016 mjini Kigali Rwanda na marekebisho hayo ya Kigali yakawa sehemu ya Itifaki ya Montreal kuanzia mwaka 2017. Hadi kufikia Aprili mwaka huu 2024 ni nchi 158 pekee zimeidhinisha marekebisho hayo.Guterres anaendelea kueleza kwamba, “iwapo yataidhinishwa kikamilifu na kutekelezwa, Marekebisho ya Kigali ya Itifaki ya Montreal yanaweza kusaidia kuepuka ongezeko la hadi nyuzi joto 0.5 za Selsiasi duniani kufikia mwisho wa karne hii.”Anasema “wakati ambapo ushirikiano kimataifa uko chini ya shinikizo kubwa, Itifaki ya Montreal ya kusaidia kulinda tabaka la ozoni inajitokeza kama ishara yenye nguvu ya matumaini. Ni ukumbusho kwamba nchi zinapoonesha azimio la kisiasa kwa manufaa ya wote, mabadiliko yanawezekana.”Ushahidi wa mafaniko ya Itifaki ya Montreal pia uko katika ujumbe wa Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP), Inger Andersen alioutoa leo kwa njia ya video akisema,“hatua zilizochukuliwa chini ya Itifaki hii ya Montreal ziliondoa gesi zilizokuwa zinatumika viwandani, gesi ambazo zilikuwa zilizoharibu tabaka la ozoni na ziliongeza joto duniani.”
Katika wiki hii Mwalimu anaendelea kutufundisha sura ya 5 ya Kitabu cha Wagalatia. Katika sura hii, Mtume Paulo anazungumzia uhuru wetu katika Kristo na umuhimu wa kuishi kwa kuenenda katika roho. Anaelezea namna sheria inavyopaswa kutumika katika maisha yetu, na jinsi matunda ya Roho yanavyoleta mabadiliko katika mienendo yetu ya maisha. Pamoja na namna ya kushinda changamoto mbalimbali kwa kutumia imani.
Katika wiki hii Mwalimu anaendelea kutufundisha sura ya 5 ya Kitabu cha Wagalatia. Katika sura hii, Mtume Paulo anazungumzia uhuru wetu katika Kristo na umuhimu wa kuishi kwa kuenenda katika roho. Anaelezea namna sheria inavyopaswa kutumika katika maisha yetu, na jinsi matunda ya Roho yanavyoleta mabadiliko katika mienendo yetu ya maisha. Pamoja na namna ya kushinda changamoto mbalimbali kwa kutumia imani.
Katika wiki hii Mwalimu anaendelea kutufundisha sura ya 5 ya Kitabu cha Wagalatia. Katika sura hii, Mtume Paulo anazungumzia uhuru wetu katika Kristo na umuhimu wa kuishi kwa kuenenda katika roho. Anaelezea namna sheria inavyopaswa kutumika katika maisha yetu, na jinsi matunda ya Roho yanavyoleta mabadiliko katika mienendo yetu ya maisha. Pamoja na namna ya kushinda changamoto mbalimbali kwa kutumia imani.
Katika wiki hii Mwalimu anaendelea kutufundisha sura ya 5 ya Kitabu cha Wagalatia. Katika sura hii, Mtume Paulo anazungumzia uhuru wetu katika Kristo na umuhimu wa kuishi kwa kuenenda katika roho. Anaelezea namna sheria inavyopaswa kutumika katika maisha yetu, na jinsi matunda ya Roho yanavyoleta mabadiliko katika mienendo yetu ya maisha. Pamoja na namna ya kushinda changamoto mbalimbali kwa kutumia imani.
Katika wiki hii Mwalimu anaendelea kutufundisha sura ya 5 ya Kitabu cha Wagalatia. Katika sura hii, Mtume Paulo anazungumzia uhuru wetu katika Kristo na umuhimu wa kuishi kwa kuenenda katika roho. Anaelezea namna sheria inavyopaswa kutumika katika maisha yetu, na jinsi matunda ya Roho yanavyoleta mabadiliko katika mienendo yetu ya maisha. Pamoja na namna ya kushinda changamoto mbalimbali kwa kutumia imani.
Mradi wa Vijana Kilimo Biashara (VKB) unaotekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani (WFP) nchini Tanzania unawapatia vijana wakulima wadogo ujuzi na rasilimali zinazohitajika ili kuboresha uzalishaji wa chakula na kujenga uchumi endelevu wakati huu ambao madhara ya El niño [EL NINYO] yanayosabisha ukame na mafuriko yamekuwa dhahiri. Bosco Cosmas na maelezo zaidi.Hali ya El Nino huwa changamoto kwa wakulima kwani hawana uhakika wa mavuno ya kile walichopanda. Hali ni tofauti kwa mkulima kijana Coletha Kiwenge anayeendesha kilimo biashara kupitia mradi huo wa WFP wa Vijana Kilimo Biashara (VKB) nchini Tanzania. Yeye amefanikiwa kuvuna mazao mwaka mzima, licha ya changamoto za hali ya hewa zinazotokana na El Niño.“Pamoja na mradi huu wa Vijana Kilimo Biashara, unaofadhiliwa na Shirika la mpango wa chakula duniani na mtekelezaji ‘Farm Afrika', tumejifunza yafuatayo: - Moja, matumizi ya mbegu bora, na kwa msimu huu tumetumia mbegu bora au mbegu chotara za alizeti Pamoja na mtama Pamoja na kufadhiliwa hizo mbegu ambazo zina mazao mengi.”Kutokana na madhara ya hali ya hewa na tabianchi, WFP imeelekeza nguvu katika kilimo cha umwagiliaji kwa wakulima hao.“Lakini pia tumechimbiwa kisima na Shirika la Mpango wa chakula duniani WFP, kisima hiko ni lengo na madhumuni kwaajili ya kilimo cha bustani, na kwasasa kwenye bustani yetu tumeanza na nyanya na ziko shambani. Lakini kwenye kikundi cha KAPATA, tunaendelea na upando mbalimbali.”
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Kama wewe ni mzazi mtarajiwa au mzazi mpya, huenda umesikia neno hili la kiingereza 'baby blues'. Maana yake ni hisia za uzoefu wa changamoto zaki hisia ambazo wanawake wanne kati ya watano hupata baada ya kujifungua.
Hata kama Australia ina fahari yakuwa na moja ya viwango vya juu zaidi vya matumizi ya vizuizi vya watoto ndani ya gari, watoto wengi bado wana safiri ndani ya magari katika hali isiyo salama kutosha.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Il est surtout connu pour ses exportations de thé, de café ou encore de fleurs coupées, mais le Kenya est aussi un important exportateur de noix de macadamia. Nairobi a d'ailleurs levé l'année dernière l'interdiction de l'exportation des noix de macadamia non décortiquées, qui était en place depuis 2015. Après des années difficiles, le secteur repart. Le groupe Pamoja l'a compris et vient de lever 8,5 millions de dollars pour accélérer la production de ces noix en Tanzanie et au Kenya, notamment à travers sa filiale kényane, TenSenses, qui a une usine de transformation en bordure de la capitale. De notre correspondante à Nairobi,Dans l'usine de TenSenses, les employés s'affairent autour de grandes tables où sont étalées les noix de macadamia. Après les avoir achetées auprès des agriculteurs, l'entreprise doit les sécher, les décortiquer puis les trier. « Là, ce sont les noix qui viennent d'être décortiquées, décrit Hillary Rotich, en charge du contrôle qualité. Il faut maintenant séparer les bonnes des mauvaises. Celles-là, ce sont les bonnes, on les a séparées de celles-ci, qui ont été abîmées par des insectes, de celles-ci qui sont moisies ou encore de celles qui ne sont pas mûres. »Les noix de macadamia de TenSenses partent majoritairement vers les États-Unis ou l'Europe. L'entreprise exporte environ 500 tonnes de noix transformées par an. Des noix qui proviennent d'un réseau de 5 000 fermiers kényans, des petites productions, la plupart en agriculture biologique. « Le Kenya est très différent parce que ce sont 200 000 petits fermiers qui ont des noix de macadamia sur leurs terres, mais avec des productions très petites et en polyculture, comme on le fait souvent au Kenya », explique Guillaume Maillard, directeur général de Pamoja.À lire aussiL'Afrique du Sud veut tenir son rang de premier exportateur mondial de noix de macadamiaUne place de choix sur le marché mondial« Sur le même lopin de terre, ils font des noix de macadamia, mais ils peuvent faire aussi du maïs, des tomates, des mangues, différentes choses. Sur nos 5 000 fermiers, ils ont en moyenne 26 arbres chacun. Sachant qu'en culture commerciale, sur un hectare, on a plus de 300 arbres », précise-t-il encore.Un modèle plus résilient qui permet tout de même au pays d'avoir une place de taille sur le marché mondial. « Quand on regarde le marché mondial de la noix de macadamia, il y a quatre sources principales. Le Kenya, qui devrait avoir une production de 40 000 tonnes cette année, derrière la Chine, l'Australie et enfin l'Afrique du Sud, qui est de loin le plus grand producteur et devrait produire cette année entre 90 000 et 95 000 tonnes. Le Kenya, dans tout ça, détient une part du marché équivalente à, disons, 15 à 20% », analyse Kees Blokland, de l'agence de négoce, Global Trading & Agency.Le secteur sort de deux années difficiles. La macadamia, considérée comme noix de luxe, a fait les frais de pandémie de Covid-19 et d'une hausse de l'inflation mondiale. Depuis, ses prix commencent à remonter. L'offre et la demande aussi, souligne Guillaume Maillard. Pamoja en a fait le pari. Avec sa nouvelle levée de fonds, le groupe compte, entre autres, développer sa capacité de transformation au Kenya.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Kutana Babuu wa Kitaa, Super Star, mkali kutoka King'oko, mwana hiphop, na mtangazaji kutoka moja kati ya vyombo vikubwa sana vya habari hapa nchini Tanzania. Kwa macho ya nje, Babuu ni kijana anayeishi ndoto za watu wengi sana. Kijana, maarufu, ana kazi nzuri, ana familią changa. Nadhani hii ni ndoto ya kila mwanaume. Lakini, kitu ambacho wengi tulikuwa hatukitambui, ni kwamba Babuu anapambana na vita kali sana ndani ya mwili wake na kwenye maisha yake binafsi. Maisha ya Babuu wa kitaa yalibadilika mara baada ya kugundulika kwamba ana saratanı ya ngozi, lakini pia mmoja kati ya watoto zake watatu anasumbuliwa na “Down syndrome” Pamoja na yote hayo, Babuu hajakubali changamoto hizi zimrudishe nyuma na kumfanya kuishi kinyonge. Ameendelea kuwa Babuu yule yule ambae wengi tunamfahamu, na kwa sasa anasisitiza kuwa kubali changamoto zako, na njia pekee ya kupambana nazo ni kwa kuangalia na kusonga mbele na juu . “ONLY WAY UP” Anaketi na Michael pamoja na Nadia, kwa pamoja wanazungumzia vita ya Babuu dhidi ya saratani aliyokutwa nayo, maisha yake kama baba anaelea mtoto ambae yupo tofauti na watoto wengine, na ni vipi ameweza kubaki kuwa Babuu yule yule ambae wote tunamfahamu kati kati ya changamoto zote hizi anazopitia? Na kwanini anaamini sana katika slogan yake ya “ONLY WAY UP”? Subscribe kwenye channel yetu ya YouTube, utazame na kusikiliza mazungumzo haya ya kusisimua na yenye mafunzo mengi sana kuhusu maisha.
Hatimaye Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametimiza ahadi yake ya kuunda Bodi ya Umoja wa Mataifa ya Ushauri wa Kisayansi wakati huu ambapo teknolojia ya Akili Mnemba au ‘Artificial Intelligence' imeshaanza kugonganisha vichwa vya watu kuhusu nafasi yake katika maendeleo duniani. Kwa mujibu wa Katibu Mkuu Guterres Bodi hii mpya aliyoiunda ni kwa ajili ya kuwashauri viongozi wa Umoja wa Mataifa kuhusu mafanikio katika sayansi na teknolojia na jinsi ya kutumia manufaa ya maendeleo haya na kupunguza hatari zinazoweza kutokea. Bwana Guterres anaamini maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia yanaweza kuunga mkono juhudi za kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu lakini pia yanaleta wasiwasi wa kimaadili, kisheria na kisiasa, wasiwasi ambao unahitaji ufumbuzi wa kimataifa. Bodi ya Umoja wa Mataifa ya Ushauri wa Kisayansi ambayo Bwana Guterres anaamini pia kuwa itaimarisha jukumu la Umoja wa Mataifa kama chanzo cha kuaminika cha data na ushahidi wa kisayansi itajumuisha kundi la Maprofesa wanasayansi saba mashuhuri duniani. Maprofesa hao ni Profesa Yoshua Bengio, Profesa Sandra Díaz, Profesa Saleemul Huq, Profesa Fei-Fei Li, Profesa Alan Lightman, Profesa Thuli Madonsela, na Profesa Thomas C. Südhof. Pia kundi jingine ni Wanasayansi Wakuu wa mashirika tofauti ya Umoja wa Mataifa, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Umoja wa Mataifa, na Mjumbe wa Katibu Mkuu kuhusu Teknolojia. Mmoja wa wanaounda Bodi hiyo, Profesa Yoshua Bengio, Mkurugenzi wa Kisayansi wa Taasisi ya Mila - Quebec AI ambaye pia ni Mkufunzi katika Chuo Kikuu cha Montréal anatoa ahadi akisema, “Uamuzi wa Katibu Mkuu wa kuanzisha Bodi ya Ushauri wa Kisayansi unasisitiza kujitolea bila kuyumba kwa viongozi wa Umoja wa Mataifa kwa kanuni za mbinu za kisayansi. Ninatazamia kumuunga mkono Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika kupaza sauti kwa ajili ya sera zinazotegemea sayansi na kufanya uamuzi.” Kupitia juhudi zao za ushirikiano, Bodi na Mtandao wake utawaunga mkono viongozi wa Umoja wa Mataifa katika kutazamia, kuzoea, na kutumia maendeleo ya hivi karibuni ya kisayansi katika kazi yao kwa watu, sayari na ustawi. Bodi itafanya kazi kama kitovu cha mtandao wa mitandao ya kisayansi. Lengo ni kuwa na muunganiko bora kati ya jumuiya ya kisayansi na kufanya uamuzi katika Umoja wa Mataifa. Kwa upande wake Bi. Ismahane Elouafi, Mwanasayansi Mkuu katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo anasema, "Kwa kuhakikisha kwamba sera na programu za Umoja wa Mataifa zimeanzishwa kwa msingi wa ushahidi na utaalamu bora wa kisayansi uliopo, Bodi itachukua jukumu muhimu katika kutatua matatizo changamano ya kimaadili, kijamii na kisiasa yanayowasilishwa na maendeleo ya haraka ya kisayansi na kiteknolojia." Ikumbukwe mwezi Julai mwaka huu, kwa mara ya kwanza Baraza la Usalama lilikuwa na mjadala mahususi kuhusu Akili Mnemba na mstakabali wake katika amani na usalama duniani na kabla yake, Katibu Mkuu Antonio Guterres kupitia moja ya matamko yake ya kisera ya Ajenda Yetu ya Pamoja, alitoa ahadi ambayo imetimia kwa kuunda Bodi hii ya kumshauri katika masuala ya kisayansi.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu lijulikanalo kama HLPF linafikia tamati hii leo hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York-Marekani. Wawakilishi wa nchi na serikali, wanasayansi, wanazuoni, mashirika ya umoja wa Mataifa, asasi mbalimbali na vijana wamekutana kuanzia tarehe 10 Julai kujadili hatua za kuchukua ili kuhakikisha malengo hayo muhimu ya maendeleo yanatimizwa ifikapo mwaka 2030. Leah Mushi ameketi chini na Gavana wa Kauti ya Kakamega Fernandes Baraza pamoja na Mbunge wa Likuyani Innocent Mugabe wote kutoka nchini Kenya kuzungumza nini wanaondoka nacho baada ya Siku 10 za mkutano huu. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo ajenda ya Katibu Mkuu, ubaguzi nchini Libya, Mafuta katika meli nchini Yemen. Katika kujifunza lugha ya Kiswahili nakupeleka kwake Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Zanzibar, BAKIZA upate uchambuzi wa neno NAZAA. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kupitia mfululizo wa mapendekezo yake yanayojulikana kama “Ajenda Yetu ya Pamoja” ambayo yanaonesha maono yake kwa miongo ijayo, hii leo akiwa amejikita na Ajenda Mpya ya Amani, ametoa mapendekezo kadhaa na hatua miongoni mwake ikiwa ni kuondoa silaha za nyuklia; kuboresha mbinu ya shughuli za amani na kushughulikia uhusiano kati ya tabianchi, amani na usalama.Wataalamu wa Umoja wa Mataifa leo wameelezea wasiwasi wao kuhusu sera ya kibaguzi iliyotangazwa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya (GNU) mwezi Aprili mwaka huu 2023 ambayo inazuia haki za wanawake na wasichana kusafiri nje ya nchi bila msimamizi wa kiume au Mahram. Wataalamu hao wamesema, "Siyo tu sera hii ni ya kibaguzi, lakini pia inazuia uhuru wa kutembea ikiwa ni pamoja na wanafunzi wanaoondoka nchini kwenda kusoma nje ya nchi," na kwamba wanawake na wasichana wanaokataa kujaza au kuwasilisha fomu wanazuiwa kuondoka nchini Libya.Na Shirika la Umoja wa Mataifa la UNDP limetangaza kwamba tayari Meli inayofahamika kwa jina Nautica au Yemen, tayari imeifikia meli nyingine ya FSO Safer katika katika ufukwe wa Yemen tayari kuanza kupakua mapipa milioni 1.14 ya mafuta ghafi ambayo kutokana na hali mbaya ya usalama katika ukanda huo yamekwama katika FSO Safer na yanatishia usalama kwani yanaweza kuvuja au kulipuka.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili Dkt. Mwanahija Ally Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Zanzibar, BAKIZA anatufafanualia maana ya neno “NAZAA.”Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 6 kutoka Tanzania (TANBAT 6) na wenzao kutoka kikosi cha polisi kinachotoka Senegal wote wakihudumu chini ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamuhuri wa Afrika ya Kati (MINUSCA), kwa wiki nzima wamefanya mazoezi ya pamoja ya ulinzi wa amani na kutuliza ghasia hususani wakati nchi hiyo ikijiandaa na uchaguzi wa ngazi mbalimbali ikiwemo kura ya maoni kuhusu katiba.Wakiwa wamevalia mavazi maalumu na vifaa vingine vya kujikinga, walinda amani wako katika uwanja wa wazi wanajikumbusha nini kinatakiwa kufanyika pale ambapo watu wenye nia ovu wanapowafanyia vurugu wananchi kwa kuziba barabara na hivyo kukwamisha shughuli za kijamii. Kiongozi wa zoezi hilo Kapteni Boniface Issack ambaye ni Afisa wa mafunzo wa TANBAT 06 anaeleza lengo la zoezi hilo, Naye Mkuu wa uangalizi kwa wanajeshi walioko chini ya MINUSCA Kanali Mussa Abdalla anafafanua zaidi akisema, "Zoezi hili linaonesha kunapokuwa na tatizo wakati wa uchaguzi waandamanaji wanapokuja kwa lengo la kuharibu, kuzuia mchakato wa uchaguzi na kama wana nguvu sana, kikosi cha kuchua hatua za haraka cha Tanzania na Senegal wanaitwa kufanya kazi na kuwaondosha waandamanaji kwenye eneo na uchaguzi kufanyika sawasawa.” Nikiripoti kutoka Beriberati, Mambere Kadei nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, mimi ni Kapteni Mwijage Inyoma, TANBAT 6. TAGS: TANZABAT 06, Jamhuri ya Afrika ya Kati
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono katika mizozo ya vita Umoja wa Mataifa umesenma jinamizi hilo ni janga lililokita mizizi katika kukosekana kwa usawa na kanuni na tamaduni kali za masuala ya kijinsia. Tupate maelezo Zaidi kutoka kwa Flora Nducha(TAARIFA YA FLORA NDICHA)Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa leo mjini Brussells na New York na mwakilishi wa pamoja wa Umoja wa Mataifa kuhusu ukatili wa kingono katika mizozo Pramila Patten na mwakilishi wa Muungano wa Ulaya kwa ajili ya mambo yan je na sera za usalama Josep Borrell wametoa wito wa hatua madhubuti zaidi za kuzuia na kukomesha unyanyasaji wa kingono, na kuendeleza usawa wa kijinsia kama kipaumbele cha kisiasa. Wamesema “Tunasikitishwa na kuongezeka kwa matumizi ya unyanyasaji wa kingono kama mbinu ya kikatili ya vita, mateso, ugaidi na ukandamizaji wa kisiasa, na tishio kwa usalama wa pamoja. Hatari ya kuwa mlengwa wa unyanyasaji wa kingono leo inazidishwa na ukweli kwamba uhalifu huu unaweza pia kuwezeshwa na kukuzwa mtandaoni, kwa kutumia chaneli za kidijitali.”Badala ya kutumika vibaya wamekumbusha kuwa “Wakati huo huo, majukwaa ya kidijitali yanaweza kuwa na jukumu muhimu na kuwa chombo chenye nguvu cha kuboresha usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake na wasichana, na kuchangia katika kujenga uwezo wao wa kustahimili nyakati za shida. Wanaweza pia kusaidia katika kuzuia unyanyasaji wa kingono na kijinsia, na hatua zinazohitajika, kupitia tahadhari za mapema na kuunganisha waathiriwa na njia za kuwatambulisha kwenye huduma, na kuwezesha kuripoti..”Viongozi hao wameonya kwamba badala ya kuwa msaada kwa waathirika leo hii “Mitandao hiyo inatumika vibaya kusambala kauli za chuki na kuchochea ukatili wa kijinsia na ubaguzi, kwani kauli za chuki za kijinsia zinaendelea kuongezeka kutumika kuwanyamazisha watetezi wa haki za binadamu, na wanaharakati wa kisiasa kwa kuchagiza utekelezaji wa ukatili wa kingono. Katika mazingira yaliyoathiriwa na migogoro, majukwaa ya kidijitali yanatumiwa kusafirisha kiharamu wanawake na wasichana kwa madhumuni ya unyanyasaji wa kingono. Walanguzi wa ngono wanatumia mtandao kama zana ya kuajiri wanawake na haswa Watoto na kutangaza huduma za kinyonyaji.”Wameongeza kuwa na katika mazingira mabaya zaidi wanawake na wasichana wanauzwa mtandaoni kama ilivypoainishwa kwenye maenmeo yanayodhibitiwa na kundi la kigaidi la ISILZaidi ya hayo wamesema “ upotoshaji wa habari kwa makusudi na udhibiti kupitia kampeni za kutoa taarifa potofu unaathiri uwezo wa mataifa kulinda raia na kushughulikia unyanyasaji wa kingono. Matumizi ya intaneti kama silaha katika maeneo yenye migogoro pia huzuia waathiriwa wa unyanyasaji wa kingono unaohusiana na migogoro kupata taarifa kuhusu huduma za kuokoa maisha na kupata usaidizi wa mtandaoni kama vile usaidizi wa kisaikolojia.”Kwa mantiki hiyo wametoa wito wa kuwa na “Majukwaa salama ya kidijitali yanayotii sheria za kimataifa, ili waathirika wa unyanyasaji wa kingono unaohusiana na migogoro na wale wanaowaunga mkono watumie mifumo hii kupambana na ukwepaji wa sheria na kudai uwajibikaji ulioboreshwa. Ni muhimu kukuza mazingira ya ulinzi mtandaoni na nje ya mtandao, ambayo yanazuia unyanyasaji wa kijinsia na vile vile kuwezesha kuripoti kwa usalama na makuchukuliwa hatua zinazofaa.”Pia wameitaka Jumuiya ipambane kwa Pamoja dhidi ya tishio linaloongezeka kila mara linaloletwa na teknolojia ya kidijitali na kuziba pengo la mgawanyiko wa kidijitali wa kijinsia ili kuruhusu waathiriwa kupata rasilimali na kupambana na ukwepaji wa sheria kwa kuzingatia kujenga usawa wa kijinsia kwa kuzuia na kupambana na unyanyasaji wa kingono katika migogoro.Wamehitimisha ujumbe wao kwa kusema kuwa “Kwa kushughulikia mgawanyiko wa kidijitali wa kijinsia, tunaweza kuunda ulimwengu ambapo wanawake na watoto wanaweza kuishi bila woga na vurugu.”Siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono katika mizozo…