Nyumba ya Sanaa

Follow Nyumba ya Sanaa
Share on
Copy link to clipboard

Nyumba ya Sanaa ni Makala ya  Utamaduni ambayo inatoa fursa  kwa wasanii  na wadau wa sanaa kuwasilisha maoni yao kwa ajili ya maendeleo ya kweli ya Afrika na dunia kwa ujumla, tukiwa na lengo la kudumisha na kuendeleza tamaduni nzuri katika mwingiliano wa tamaduni uliopo, tukizingatia maisha ya kis…

Rfi - RFI


    • May 24, 2025 LATEST EPISODE
    • every other week NEW EPISODES
    • 20m AVG DURATION
    • 150 EPISODES


    More podcasts from Rfi - RFI

    Search for episodes from Nyumba ya Sanaa with a specific topic:

    Latest episodes from Nyumba ya Sanaa

    Muziki wa dansi na ule wa kizazi kipya nchini Tanzania

    Play Episode Listen Later May 24, 2025 20:03


    Mwandishi Steven Mumbi anaangazia muziki wa dansi na ule wa kizazi kipya nchini Tanzania.

    Msanii sweet Brown wa Beni DRC na mziki wa jamii

    Play Episode Listen Later May 10, 2025 20:08


    Sanaa ya muziki ni dawa inayofariji na kusaidia kutuma ujumbe wa amani kwa jamii amesema msanii wa miondoko mchanganyiko Gloire Tsongo almaarufu sweet Brown fresh Leader mjini Beni katika mkowa wa Kivu kaskazini mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, katika mazungumzo maalum na mwandishi wa habari wa RFI Kiswahili Ruben Lukumbuka alipotembelea eneo hilo mwezi february mwaka huu

    Sanaa ya Ufumaji inayotumia uzi kufuma Mavazi ya aina mbalimbali

    Play Episode Listen Later May 3, 2025 20:16


    Sanaa ya Ufumaji ni sanaa ya Mikono inayotumia uzi kufuma Mavazi ya aina mbalimbali, kutana na Farida na Esther wasanii wanaofanya saa hizo walipozungumza na Steven mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.

    Tanzania: Tunamuangazia Samir Kassim Rashid maarufu Samir Kinyulinyuli

    Play Episode Listen Later Apr 26, 2025 20:17


    Samir Kassim Rashid maarufu Samir Kinyulinyuli ni Msanii wa Sanaa ya Muziki aliyelazimika kukimbilia Dar es salaam akitokea Morogoro  ili kufanikiwa  kisanaa, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa ya Jumahili.

    Utengenezaji wa filamu katika eneo la mashariki mwa DRC

    Play Episode Listen Later Apr 12, 2025 20:19


    Makala ya nyumba ya sanaa inaangazia utengenezaji wa filamu, mabadiliko ya ubunifu wa filamu unaoendana na teknolojia ya kisasa. Mbali na utovu wa usalama eneo la Beni mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, vijana pia wamekuwa wakijitahidi katika kufanikisha namna ya kuwapa burudani ya filamu

    Mchango wa wasanii wa Beni DRC katika juhudi za kuimarisha usalama

    Play Episode Listen Later Apr 5, 2025 20:02


    Nyumba ya sanaa juma hili imekutana na wasanii wa mjini Beni mkoani Kivu kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ambao wamekuwa wakihimiza amani katika nyimbo zao, sanaa ya muziki ikikaribishwa kwa kiasi kikubwa na watu kutoka rika zote nchini na nje ya nchi. Mwenzangu Ruben Lukumbuka hivi karibuni alikutana na msanii wa Beni mashariki mwa DRC Mukombozi Mabenze almaarufu Tata Charles akielezea historia yake na sanaa ya muziki na hali ya eneo hilo 

    Tunazungumza na msani B2K kutoka Njombe kusini mwa Tanzania

    Play Episode Listen Later Mar 29, 2025 20:03


    Sanaa ya Muziki Nyanda za Juu kusini mwa Tanzania, ni sanaa inayokua kwa kasi vijana wanawekeza kulifikia soko la Muziki Afrika Mashariki, B2K ni Msanii anayekonga Nyoyo za Wasichana zaidi kutokana na Tungo zake, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na B2K kutoka Njombe.

    tanzania sanaa b2k makala nyumba juu ungana steven mumbi
    Ajira itokanayo na sanaa ya uchoraji visiwani Zanzibar

    Play Episode Listen Later Mar 22, 2025 20:10


    Uchoraji ni Ajira ,Wasanii wa sanaa hii Zanzibar wananeemeka na kazi zao, Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Obedience na Muki kutoka Zanzibar.

    Muziki wa kizazi kipya Zanzibar

    Play Episode Listen Later Mar 15, 2025 20:10


    Muziki wa kizazi kipya Zanzibar umedorora ukilinganisha na hali ilivyo Tanzania Bara

    Sanaa ya uchoraji katika Visiwa vya Zanzibar

    Play Episode Listen Later Mar 8, 2025 20:16


    Wachoraji visiwani Zanzibar walia na gharama za kupata maeneo ya kunadi kazi zao za Sanaa hiyo, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Mchoraji maarufu visiwani humo Jamal.

    Muziki wa Taarab na Zanzibar Hertage Ensemble

    Play Episode Listen Later Mar 1, 2025 20:13


    Taarab Asilia ni Miongoni mwa Miziki ya kale zaidi katika Mwambao mwa Bahari ya Hindi, Zanzibar Taarab Hertage Ensemble ni miongoni mwa Makundi ya Muziki huo kutoka Visiwani Zanzibar, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.

    Tamasha la Sauti za Busara linalofanyika kila mwezi Februari Zanzibar

    Play Episode Listen Later Feb 1, 2025 20:13


    Wasanii wa Muziki Afrika na Duniani kote wanakutana visiwani Zanzibar kufurahia uzuri na Upekee wa Muziki, wageni mbalimbali hukusanyika kushuhudia Tamasha la Sauti za Busara kila ifikao mwezi Februari. 

    Mfahamu Leo Mkanyia Mwanamuziki wa Muziki wa Asili kutoka Tanzania

    Play Episode Listen Later Jan 25, 2025 20:10


    Wanamuziki wa Muziki wa asili wamebadili vionjo vya asili wakijumuisha na vionjo vya Kisasa ili kuupaisha Muziki Kimataifa, Steven Mumbi amezungumza na Leo Mkanyia Mwanamuziki wa Muziki wa Asili kutoka Tanzania

    Tanzania: Utunzi wa vitabu na Sikudhani Mohamed Jalala

    Play Episode Listen Later Jan 18, 2025 20:00


    Changamoto za wanamuziki wa kizazi kipya wanaochipukia nchini Tanzania

    Play Episode Listen Later Dec 7, 2024 20:04


    Wasanii wa Muziki wa kizazi kipya wanaochipukia nchini Tanzania walalama kutakwa Kimapenzi wa Watayarishaji wa Muziki, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akiwa na Zainisha Nokolage maarufu Zainisha.

    Muziki wa asili kutoka nchini Tanzania

    Play Episode Listen Later Nov 23, 2024 20:12


    Sanaa ya Muziki wa asili ni miongoni mwa sanaa zinazokua kwa kasi nchini Tanzania, Kutana na kundi la Sanaa lililowika katika majukwaa ya kimataifa wakiwa na bendi ya kipekee katika makala ya Nyumba ya Sanaa.

    Sanaa ya Uchongaji Vinyago nchini Tanzania

    Play Episode Listen Later Nov 16, 2024 20:09


    Steven Mumbi amezungumza na Lyala Sebastian Mchongaji wa Sanaa za Vinyago.

    tanzania sanaa steven mumbi
    Sanaa ya uchoraji wa vinyago na fursa wa biashara inazoleta

    Play Episode Listen Later Nov 9, 2024 20:13


    Wabunifu wa Sanaa ya Uchongaji Vinyago wamewekeza katika kung'amua fursa ya biashara kwa Mataifa ya Afrika Mashariki ili kujikwamua na vipato Duni, Steven Mumbi amezungumza na Mintanga Ramadhani Msanii wa Sanaa za Uchongaji Vinyago kutoka nchini Tanzania.

    Muziki wa HIP HOP nchini Tanzania

    Play Episode Listen Later Oct 26, 2024 20:06


     Muziki wa HIP HOP nchini Tanzania umefifia kutokana na ugumu wa kufanya Muziki huo,Msanii PMawenge anasimulia hatua za kuchukua kuurejesha sokoni katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.

    Tanzania: Sanaa ya ushairi na msanii Michael James maarufu Michael

    Play Episode Listen Later Sep 28, 2024 20:10


    Sanaa ya ushairi inawavutia zaidi watu wanaotamani kujua utamu na upekee wa lugha adhimu ya Kiswahili, Chuo kikuu cha Dar es salaam kimewatambua na kuwapa fursa vijana waliosomea fani ya sanaa, kubobea katika kughani Mashairi. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Msanii Michael James maarufu Michael. 

    Tanzania: Muziki wa kizazi kipya kwa vijana

    Play Episode Listen Later Sep 21, 2024 20:10


    Tanzania: Tunazungumza na kundi la wasani la viongozi generation

    Play Episode Listen Later Sep 14, 2024 20:08


    Mwandishi wetu Steven Mumbi amezungumza na kundi la wasani la viongozi generation.

    Tanzania: Muziki wa kizazi kipya na Hussein Mussa Shundi Maarufu Rucky

    Play Episode Listen Later Sep 7, 2024 20:13


    Muziki wa kizazi kipya umewawezesha vijana nchini Tanzania kujikwamua kimaisha kwa kujipatia kipato kupitia Sanaa hiyo,Katika Makala haya Steven Mumbi anazungumza na Hussein Mussa Shundi Maarufu Rucky.

    tanzania hussein sanaa mussa muziki katika makala steven mumbi
    Mwanza: Msanii wa Bongo Fleva, Baraka the Prince ndiye mgeni wetu wiki hii

    Play Episode Listen Later Aug 31, 2024 20:07


    Msanii wa Bongo Fleva, Baraka the Prince anauona muziki ni maisha, jambo linalomfanya afikirie zaidi namna mashabiki wake wataishi na kazi zake, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Msanii huyo.

    Tanzania: Wiki hii tunaliangazia kundi la Muziki la The Mafiki

    Play Episode Listen Later Aug 24, 2024 20:12


    The Mafiki  ni kundi la Muziki lililovuma kwa vionjo vya Muziki wa sasa, sasa wamekuja upya mara baada ya kusambaratika, Ungana na Steven Mumbi akizungumza na wasanii wa kundi hilo.

    Muziki wa Taarab nchini Tanzania naye Jike la Chui

    Play Episode Listen Later Aug 17, 2024 20:18


    Mapinduzi ya Muziki wa Taarab yanajidhihirisha katika tenzi za wasanii wa Muziki huu kutoka tungo za Majigambo na sasa tungo za kuburudisha, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Jike la Chui.

    Zumbukuku nyimbo za taarab zinazokumbukwa hata sasa

    Play Episode Listen Later Aug 3, 2024 20:13


    Zumbukuku ni miongoni mwa nyimbo zilizofanya vizuri katika muziki wa taarab, hii inashehenezwa na sauti ya kipekee ya kiume inayosikika katika muziki huo, Ally Star ndie aliyeimba wimbo huo; Ungana na Steven Mumbi katika makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Ally Star kuhusu namna nyimbo hizo zilivyotia fora.

    Mwanamuziki Ogisha Matale atoa wito wa amani mashariki mwa DRC

    Play Episode Listen Later Jul 27, 2024 20:08


    Makala ya nyumba ya sanaa wiki hii imepiga kambi mjini Goma huko mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ambako mwanzoni mwa mwezi mei mwandishi wetu Ruben Lukumbuka alikutana na msanii Ogisha Matale ambapo katika shughuli zake zake amekuwa akijaribu kuhimiza amani nchini, hususan eneo lake lenye kushuhudia mapigano ya mara kwa mara.

    Mwanamziki Nyota Tiger mwalikwa wa makala Nyumba ya sanaa

    Play Episode Listen Later Jul 20, 2024 20:07


    Nyota Tiger ni mzaliwa wa jijini Mwanza nchini Tanzania alilazimika kusafiri mpaka maeneo ya kusini mwa Afrika kukwepa adha za wazazi kumnyima fursa ya kufanya muziki. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.

    Mchango wa sanaa ya muziki wa asili katika usuluhishi wa mizozo DRC

    Play Episode Listen Later Jul 13, 2024 20:10


    Katika makala ya nyumba ya sanaa wiki hii mwandishi wetu Ruben Lukumbuka ambaye hivi karibuni alitembelea mashariki mwa DRC ambako alikutana na Olivier wabahavu, msanii maarufu sana kufuatia nyimbo zake anazoimba katika lugha ya kihavu na kishi huko Kivu kusini na kaskazini, amezungumzia mchango wa sanaa ya muziki wa kiasili katika usuluhishi wa migogoro ya kivita mashariki mwa DR Congo. 

    Tanzania: Muziki wa Singeli na Man Fongo

    Play Episode Listen Later Jul 6, 2024 20:04


    Muziki wa Singeli ni Miongoni mwa Muziki unaokua kwa kasi nchini Tanzania na nchi za Afrika,Wasanii wa Muziki huo wanapambana kuukuza Kimataifa, Man Fongo ni Miongoni mwa Wasanii Pendwa wa Muziki huo,Ungana na Steven Mumbi anazungumza na Msanii huyo.

    tanzania afrika sanaa muziki kimataifa ungana miongoni fongo steven mumbi
    Tanzania: Muziki wa asili na Jilema Ng'wana Shija

    Play Episode Listen Later Jun 29, 2024 20:05


    Katika Makala ya Wiki hii, Steven Mumbi amezungumza naye Jilema Ng'wana Shija msani wa muziki wa asili kutoka nchini Tanzania.

    tanzania wiki eac asili muziki katika makala steven mumbi
    Nyumba ya sanaa na msanii Tourna Boy kuhusu muziki wa kizazi kipya

    Play Episode Listen Later Jun 22, 2024 20:10


    Karibu katika makala ya Nyumba ya sanaa nami Steven Mumbi, hii leo Msanii Tourna Boy wa kizazi kipya kutoka mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo akielezea kuhusu juhudi za vijana wasanii kuchangia katika juhudi za kurejesha amani ya mashariki mwa nchi hiyo, katika mazungumzo na mwenzangu Ruben Lukumbuka alipotembelea eneo la Goma mwanzoni mwa mwezi mei mwaka huu 2024

    Muziki wa Singeli na Torino Abdul Sykes kutoka Mbagala Tanzania

    Play Episode Listen Later Jun 8, 2024 20:09


    Kwenye Makala ya wiki hii Stephen Mumbi anazungumza na msani Abdul Sykes kutoka Mbagala Tanzania.

    Wasanii wa mashariki ya DRC wachangia juhudi za upatikanaji wa amani

    Play Episode Listen Later Jun 1, 2024 20:10


    Makala ya Nyumba ya sanaa wiki hii inamuangazia msanii wa muziki wa regae Mack El Sambo ambaye kwa zaidi ya miaka ishirini amekuwa akihimiza amani katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, hususan kwenye mji wa Goma katika mkowa wa Kivu Kaskazini. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka ambaye hivi karibuni alitembelea mji wa Goma na kukutana na mwanamziki huyu..

    DRC: Ubunifu wa viatu vya ngozi mjini Goma na Christian Bazika

    Play Episode Listen Later May 25, 2024 20:04


    Katika Nyumba ya sanaa wiki hii Steaven Mumbi akishirikiana na Ruben Lukumbuka ambaye wiki iliyopita alitembelea mji wa Goma ulioko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambako alikutana na mbunifu wa sanaa mbalimbali ikiwemo ubunifu wa kutengeneza viatu bwana Christian Bazika anayetengeneza bidhaa za ngozi mashariki mwa nchi hiyo.

    Muziki wa dansi na prince Muumin mwijuma kutoka nchini Tanzania

    Play Episode Listen Later May 18, 2024 20:05


    Tanzania: Sanaa ya uigizaji, tunamuangazia Asha Jumbe maarufu White Maria

    Play Episode Listen Later May 11, 2024 20:12


     Asha Jumbe maarufu White Maria ni Muigizaji aliyejizolea umaarufu akiwa na umri wa Miaka nane tu, sasa ni mtu Mzima aja kivingine kufanya sanaa ya Fimalu za kiswahili,Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumzia safari yake ya Uigizaji.

    Wiki hii makala haya yanamuangazia Steven Ibrahim maarufu Eddy Music

    Play Episode Listen Later May 4, 2024 20:03


    Sanaa ya Muziki imenihitaji kuliko nilivyo ihitaji, ni kauli yake Steven Ibrahim maarufu Eddy Music alipozungumza na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.  

    Muziki wa injili na Obby Alpha ambaye ametunga vibao kama bora kushukuru

    Play Episode Listen Later Apr 27, 2024 20:02


    Msani huyo amesema kuwa alitunga vibao kama bora kushukuru kutokana na changamoto za kimaisha alizokuwa anakabiliwa nazo kipindi fulani katika maisha yake.

    Zanzibar: Fahamu zaidi kuhusu Muziki wa Baibuda katika makala haya

    Play Episode Listen Later Apr 13, 2024 20:09


    Mwandishi wetu Steven Mumbi amezungumza na msani wa muziki huu wa Baibuda 

    Afrobongo na Bruce Africa

    Play Episode Listen Later Apr 6, 2024 20:03


    Makala haya hukuletea historia ya sanaa na wasani barani Afrika.

    Claim Nyumba ya Sanaa

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel