Podcasts about miongoni

  • 19PODCASTS
  • 230EPISODES
  • 12mAVG DURATION
  • 1WEEKLY EPISODE
  • May 7, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about miongoni

Latest podcast episodes about miongoni

Habari za UN
Wazazi pelekeni watoto wenu kupata chanjo dhidi ya maradhi - Bi. Halfani

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 7, 2025 3:36


Katika Wiki ya Chanjo duniani, iliyotamatishwa tarehe 30 wiki iliyopita, mtaa wa Butiama, ulioko Mtoni Kijichi katika wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania ulishuhudia wazazi na walezi wakijitokeza kuwapatia watoto wao chanjo muhimu za kuwalinda dhidi ya maradhi hatari. Miongoni mwao ni  Hija Halfani ambaye alimpeleka mtoto wake mwenye umri wa siku 42 kupata chanjo yake ya kwanza. Je, ni mafanikio gani yamepatikana na kwa nini chanjo hizi ni muhimu? Ungana na Sharon Jebichii kwa makala hii iliyoandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini  Tanzania.

Habari za UN
07 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 7, 2025 10:54


Hii leo jaridani tunaangazia mvutano unaoendelea barani Asia kati ya majirani wawili India na Pakistani, na msaada wa mguu bandia uliowezesha mtototo nchini Kenya kwenda shule. Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani tunakwenda katika ukanda wa Gaza.Huko barani Asia majirani wawili India na Pakistani wameendelea kuoneshana mvutano kati yao kwenye eneo la Jammu na Kashmiri tangu tarehe 22 mwezi uliopita wa Aprili baada ya shambulizi huko Pahalgam. Katibu Mkuu ametoa wito kwa mara nyingine tena.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na wadau wameleta neema kwa watoto wanaoishi na ulemavu katika Kaunti ya Kisumu Magharibi mwa Kenya baada ya kuwapa msaada wa vifaa ikiwemo viti mwendo na viungo bandia kupitia mradi wa ubunifu kwa ajili ya watoto wenye ulemavu, msaada uliobadili maisha yao.Makala katika wiki ya chanjo duniani, iliyotamatishwa tarehe 30 wiki iliyopita, mtaa wa Butiama, ulioko Mtoni Kijichi katika wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania ulishuhudia wazazi na walezi wakijitokeza kuwapatia watoto wao chanjo muhimu za kuwalinda dhidi ya maradhi hatari. Miongoni mwao ni Hija Halfani ambaye alimpeleka mtoto wake mwenye umri wa siku 42 kupata chanjo yake ya kwanza.”Na mashinani mashinani, kama sehemu ya juhudi za kutoa nafasi ya kujieleza kisanii na kuwaunga mkono Wapalestina kihisia (emotional support), UNRWA imeandaa maonesho ya sanaa katika Shule ya Al-Rimal, ambayo sasa ni makazi ya wakimbizi wa ndani katika ukanda wa Gaza, na watoto walipata fursa ya kuonesha kazi za sanaa zinazoakisi(reflect) madhila wanayopitia wakati wa vita kati ya Israeli na Hamas ambavyo bado vinaendelea. Malak Fayad, msichana mkimbizi kutoka Beit Hanoun ni mmoja wao akionesha sanaa yake.….Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
23 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 11:15


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza, na harakati za utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili. Makala tunasalia hapa hapa makao makuu na mashinani tunakwenda nchini Burundi, kulikoni?Hali si hali huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli ambako wakimbizi wa ndani wanakabiliwa na hatari za kiafya ambako panya na wadudu kama vile viroboto na  nzi wamesambaa kutokana na mlundikano wa taka na  ukosefu wa huduma muhimu kama vile maji safi na salama.Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, mkutano wa 24 wa Jukwaa la Kudumu la Watu wa jamii za asili (UNPFII) linaendelea kujadili utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili  na kubaini mbinu bora za kushughulikia changamoto zinazowakabili. Miongoni mwa shiriki wa jukwaa hilo nimwakilishii wa Shirika la Ereto Solidarity Funds ambaye  amepata fursa ya kuzungumza na Sharon Jebichii wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa.Makala ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Kitabu na Haki Miliki ambapo kila mwaka tarehe kama ya leo siku hii huadhimishwa ili kutambua nguvu ya vitabu kama daraja kati ya vizazi na vizazi na tamaduni mbalimbali. Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na mwandishi maarufu wa vitabu vya elimu, Uchumi na uhamiaji, Ernest Makulilo mkazi wa Marekani katika jimbo la Missouri.Na mashinani kupitia video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO fursa ni yake Meena Poudel kutoka nchini Nepal, Kusini mwa Asia ambaye ni Katibu wa kikundi cha wanawake watumiaji wa msitu ambacho kinabadilisha takataka za misitu kuwa mbolea rafiki kwa mazingira huku pia wakijipatia kipato."Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!  

Habari za UN
Anna Ndiko: Mfuko wa ERETO tunawezesha mashirika ya watu wa asili Afrika Mashariki kutetea haki za ardhi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 2:28


Mkutano wa 24 wa Jukwaa la Kudumu la Watu wa jamii za asili (UNPFII) hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa linaendelea kujadili utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili  na kubaini mbinu bora za kushughulikia changamoto zinazowakabili. Miongoni mwa shiriki wa jukwaa hilo nimwakilishii wa Shirika la Ereto Solidarity Funds ambaye  amepata fursa ya kuzungumza na Sharon Jebichii wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa. Anaanza kwa kujitambulisha 

Habari za UN
Jamii inapaswa kusikiliza na kujifunza kutoka kwa vijana

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2025 3:42


Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) linafanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani ambapo limeanza tarehe 15 Aprili na linatarajiwa kukamilika tarehe 17 Aprili 2025. Vijana kutoka nchi mbalimbali pamoja na wadau wengine wa masuala ya maendeleo na Uchumi wanakuja pamoja kujadili changamoto mbalimbali na namna bora ya kupatia ufumbuzi katika kuubadilisha ulimwengu kuwa mahali penye usawa zaidi na endelevu chini ya mwongozo wa Ajenda ya mwaka 2030 na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).  Miongoni mwa wanaohudhuria jukwaa hilo ni Kapwani Kavenuke kutoka nchini Tanzania ambaye amefanyiwa mahojiano na Leah Mushi na hapa anaanza kwa kueleza umuhimu wa mikutano huo.

Habari za UN
Vita Sudan yamsababishia Walaa tatizo la afya ya akili

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 14, 2025 3:46


Tarehe 15 mwezi April imwaka 2023 wananchi wa Sudan hususan mji mkuu Khartoum waliamshwa na mapigano kati ya jeshi la serikali SAF na wanamgambo wa kikosi cha msaada wa haraka RSF. Hadi leo hii mapigano hayo yanazidi kushika kasi na raia wanafurushwa makwao. Miongoni mwao ni watoto ambao zahma wanayokutana nayo sio tu kufurushwa bali pia changamoto ya afya ya akili. Tayari shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limeona shida hiyo na limeanza kuchukua hatua kama anavyosimulia Assumpta Massoi kwenye makala hii. 

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Ziara ya rais wa Uganda nchini Sudan kusini, waasi wa M23 wajiondoa Walikale

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Apr 5, 2025 20:12


Miongoni mwa matukio makubwa ya juma hili ni pamoja na ziara ya rais wa Uganda Yoweri Museveni, iliyotangulizwa na ziara ya wajumbe wa Umoja wa Afrika, nchini Sudan Kusini baada ya makamu wa rais wa nchini hiyo kukamatwa na kuzuiwa nyumbani kwake, kule DRC waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda waripotiwa kujiondoa katika mji wa Walikale mokowani Kivu kaskazini mashariki mwa DRC, tunaangazia Kenya, Uganda, nchi za Afrika mashariki na magharibi pia kwengineko duniani 

Jukwaa la Michezo
Kenya: Nani atatamba kwenye "Debi ya Mashemeji" AFC Leopards vs Gor Mahia?

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Mar 29, 2025 23:54


Miongoni tuliyokuandalia ni pamoja na matokeo ya raga mkondo wa HongKong 7s, sakata la upangaji mchezaji dhidi ya golikipa wa Kenya Patrick Matasi, maandalizi ya debi ya Mashemeji, Misri yapewa haki za kuandaa AFCON U20 huku CAF ikiifungulia uwanja wa Benjamin Mkapa, tuzo nono kwa washindi wa Kombe la Dunia la vilabu, kocha wa Brazil atimuliwa naye Djokovic akikaribia kushinda taji lake la 100.

Habari za UN
Haki Elimu - Ujumbe wetu mkuu kwenye CSW69 ni elimu kwa mtoto wa kike

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 12, 2025 3:40


Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, (CSW69) umeingia siku ya tatu hii leo Machi 12 katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijinoi New York, Marekani. Mkutano huu wa mwaka huu unafanyika katika hali ya kihistoria kwa kuzingatia kuwa ni miaka 30 tangu Mkutano wa wanawake ulipofanyika jijini Beijing - China  mwaka 1995 na kuweka maazimio muhimu kuhusu masuala mazito ya kumkomboa mwanamke dhidi ya ukandamizaji kote duniani. Maelfu ya wanawake na wadau wengine wanakutana kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York. Miongoni mwao ni Nuria Mshare ambaye amewakilisha taasisi ya Haki Elimu ya nchini Tanzania.

Nyumba ya Sanaa
Muziki wa Taarab na Zanzibar Hertage Ensemble

Nyumba ya Sanaa

Play Episode Listen Later Mar 1, 2025 20:13


Taarab Asilia ni Miongoni mwa Miziki ya kale zaidi katika Mwambao mwa Bahari ya Hindi, Zanzibar Taarab Hertage Ensemble ni miongoni mwa Makundi ya Muziki huo kutoka Visiwani Zanzibar, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.

Habari za UN
Mradi wa ufugaji bora wa mbuzi umenikwamua – Mfugaji Kigoma

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 17, 2025 4:06


Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO nchini Tanzania linaendelea kutekeleza Programu ya pamoja kwa mkoa wa Kigoma KJP iliyoanza kutekelezwa nchini humo mwaka 2017 na mashirika ya Umoja wa Mataifa kwa lengo la kusaidia kutatua changamoto za kipekee za mkoa huo ikiwemo zitokanazo na kuhifadhi wakimbizi kutoka nchi jirani.Miongoni mwa miradi inayotekeleza ni ule wa kupatia wananchi mafunzo ya ufugaji bora wa mbuzi ili waweze kuinua kipato chao na vile kuimarisha lishe kwenye familia.Kupitia video ya FAO, utamsikia mnufaika wa mafunzo hayo kama anavyosimulia Assumpta Massoi kwenye makala hii.

Habari za UN
Wakimbizi Goma waanza kufungasha virago huku wakiwa na hofu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 12, 2025 1:45


Baada ya waasi wa M23 jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kupatia wakimbizi waliokuwa wamesaka hifadhi kambini mjini Goma, wawe wamerejea makwao ndani ya saa 72 kuanzia juzi jumatatu, mamia wameanza kutii amri hiyo licha ya hofu inayowakabili ya kule wanakotakiwa kurejea. Miongoni mwao ni Kibira Bakulu, baba wa watoto 5, aliyekimbia mapigano eneo la Saké, mwezi Februari mwaka jana, takriban kilomita 10 kutoka Goma.

Habari za UN
Akibomoa kibanda chake Goma DRC, mkimbizi asema ana hofu kurejea Saké

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 12, 2025 1:45


Baada ya waasi wa M23 jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kupatia wakimbizi waliokuwa wamesaka hifadhi kambini mjini Goma, wawe wamerejea makwao ndani ya saa 72 kuanzia juzi jumatatu, mamia wameanza kutii amri hiyo.Miongoni mwao ni Kibira Bakulu, baba wa watoto 5, aliyekimbia mapigano eneo la Saké, mwezi Februari mwaka jana, takriban kilomita 10 kutoka Goma.Akiwa katika harakati za kubomoa kibanda chake katika kambi ya nane ya CEPAC Mugunga huko Goma, Bwana Bakulu anasema walishangaa, bila kuwa tayari, kuambiwa warudi walikotoka."Tumepatiwa saa 72 tuwe tumeondoka na kurejea Saké, kwani vita vimeisha. Sisi hatua uhakika kamili kwa sababu tuliondoka Saké kutokana na vita. Kama inabidi kusukumwa tuondoke, hatuna la kuchagua,” amesema Bwana Bakulu.Ana hofu ya kurejea Saké, akisema, “kule tulikuwa tunaishi Sake na tukirejea tutaishi vipi? Tunaomba viongozi wajitahidi watusaidie ili watuhakikishia usalama.Alipoeleza hali halisi amesema, “ hii siku ya leo hapa unaniona, watu wamepita hapa wakifanya vurugu, wananyang'anya kila kitu ulichonacho, iwe simu wanabeba. Sasa tunashindwa kufahamu amani iko katika kiwango gani?”Kwa mujibu wa Bwana Bakulu, walishaamua kuwa hawataweza kurudi na kama ni kufa basi watafia Goma, lakini sasa wamelazimishwa kurejea Saké.

Wimbi la Siasa
Je, maazimio ya jumuiya za EAC na SADC kuhusu DRC yatatekelezwa ?

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Feb 12, 2025 10:08


Makala ya Wimbi la Siasa wiki hii tunaangazia maazimio ya wakuu wa serikali na nchi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki na SADC waliokutana Februari jijini Dar es Salaam, kuthathmini hali ya usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.Miongoni mwa maazimio hayo ni usitishwaji wa vita bila masharti kati ya waasi wa M23 na wanajeshi wa DRC na kutoa wito wa mazungumzo.Wachambuzi wetu ni Chube Ngorombi akiwa Goma, na Francois Alwende akiwa jijini Nairobi.

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Israeli na wapiganaji wa Hamas wakubaliana kusitisha vita huko Gaza

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Jan 18, 2025 20:12


Miongoni mwa yale tumekuandalia wiki hii ni pamoja na kuapishwa kwa Rais Mteule wa Marekani Donald Trump, mapigano yanyoendelea kuripotiwa mashariki ya DRC, makubaliano ya kusitishwa kwa vita kati ya Hamas na Israeli.

Habari za UN
Vyombo vya habari vyawezasongesha agenda 2030 na kukuza haki za binadamu ni muhimu - Faraja Kihongole

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 15, 2025 3:59


Kundi la waandishi wa habari 15 wanawake kutoka nchi za Afrika, ikiwemo Tanzania mwaka jana wa 2024 walitumia siku tano jijini Geneva, Uswisi kushiriki programu ya kushirikisha waandishi wa habari ili wapate uelewa wa kazi za Baraza la Umoja wa Mataifa la haki za Binadamu. Ufadhili wao ulikuwa kupitia mashirika mawili ya kiraia, Universal Rights Group (URG) na Friedrich Naumann Foundation. Wakiwa Geneva, walipata fursa ya kuzungumza mabalozi wanaowakilisha nchi zao kwenye Baraza hilo, wataalamu wa haki za binadamu, mashirika ya kiraia na waandishi wa habari ambao kituo chao cha kazi ni Baraza la Haki za Binadamu. Miongoni mwao ni Faraja Kihongole kutoka Africa Media Group Tanzania Limited. Alihojiwa na Pascal Sim, Afisa wa Mawasiliano katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu jijini Geneva kuhusu masuala kadhaa ikiwemo alichojifunza na anachoondoka nacho. Matokeo ya mahojiano hayo ndio makala ya leo inayoletwa kwako na Assumpta Massoi.

Habari za UN
Serikali patieni vijana taarifa sahihi na stahiki ili watekeleze wajibu wao

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 10, 2025 3:38


Umoja wa Mataifa unaeleza kwamba duniani kote kuna vijana bilioni 1.2 wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 24. Idadi hii ni saw ana asilimia 16 ya wakazi wote wa dunia. Kama hiyo haitoshi, idadi hiyo ya vijana inatarajiwa kufikia bilioni 1.3 ifikapo mwaka 2030, yaani miaka mitano ijayo. Lakini changamoto ni kwamba bado serikali nyingi hazijaweza kutumia wingi wa idadi hii kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs. Kwa hali hiyo baadhi ya vijana wameamua kutumia fursa na kujiongeza ili vijana wenzao waweze kufahamu wanachopaswa kufanya ili SDGs zifanikiwe ifikapo 2030. Miongoni mwao ni Paul Siniga, kijana kutoka Tanzania ambaye mwezi Oktoba mwaka huu alikuweko kwenye makao makuu ya UN jijini New York, Marekani kushiriki vikao vya ngazi ya juu. Assumpta Massoi alitaka kufahamu kwa kina ni hatua zipi alichukua hadi kufika aliko sasa.

Habari za UN
Nilikuwa miongoni mwa Wacuba wa kwanza kujifunza Kiswahili: Profesa Jacomino

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 27, 2024 5:03


Ujumuishwasji wa lugha mbalimbali katika dunia iliyoshikamana katika Nyanja mbalimbali ni moja ya malengu ya Umoja wa Mataifa kuanzia katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa hadi kwenye nchi wanachama unalichagiza hilo. Hamasa hiyo imezichagiza nchi nyingi kuanza kukumbatia lugha ambazo kwa asili hazizungumzwi kama alivyobaini Flora Nducha wa Idhaa hii ambaye hivi karibuni alikuwa Cuba kwenye Kongamano la Kimataifa la Kiswahili na kukutana na Profesa Juan Jacomino ambaye ni mhadhiri katika chuo kikuu cha Havana na ni miongoni mwa watu wa mwanzo waliokwenda Tanzania kujifunza Kiswahili na sasa anakifundisha nchini mwake Cuba. Anafafanua kuhusu safari yake ya kujua Kiswahili katika makala hii..

Habari za UN
Mradi wa kilimo cha umwagiliaji warejesha matumaini kwa wakulima wa Masvingo, Zimbabwe

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 23, 2024 3:09


Hivi karibuni mkutano wa Umoja wa Mataifa wa kuzuia kuenea kwa jangwa, ulikunja jamvi huko Riyadh, Saudi Arabia ambapo Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD ulitumia fursa hiyo kuelezea harakati zake za kusaidia wakulima barani Afrika walioathiriwa vibaya na kuenea kwa jangwa. Miongoni mwa mataifa hayo ni Zimbabwe ambako IFAD imeshaanza kuchukua hatua na kuleta nuru kwa wakulima kama anavyosimulia Assumpta Massoi kwenye makala hii.

Habari za UN
10 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 10, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na tunaelekea nchini Kenya kuangazia moja ya ukiukwaji Mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya wanawake, jinamizi la ukeketaji na jitihada zinazochukuliwa na UNFPA na wadau mbalimbali. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani inayotupeleka nchini Namibia.Baada ya serikali ya Bashar Al-Assad kupinduliwa na kuibuka kwa taarifa za baadhi ya nchi duniani kuanza kusitisha mchakato wa kushughulikia maombi ya Wasyria waliokuwa wameomba hifadhi kuokoa usalama wa maisha yao pindi hali ilipokuwa tete nchini mwao, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) linaendelea kutoa wito kwa mataifa yote kufungua milango, kuwapa hifadhi na ulinzi raia wa Syria wanaotafuta usalama. UNHCR imeahidi pia mara tu hali ya Syria itakapokuwa wazi zaidi, itatoa mwongozo kuhusu mahitaji ya ulinzi kwa Wasyria walioko hatarini.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limekaribisha mchango wa dola za Marekani milioni 22 kutoka shirika la Korea Kusini la Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa (KOICA) ili kuimarisha mnepo kwa tabianchi na uhakika wa chakula kwa wakulima wadogo, wafugaji na makundi yaliyoko pembezoni nchini Kenya, Somalia na Sudan Kusini. Vituo vya utabiri wa hali ya hewa vinatabiri hali ya La Niña mashariki mwa Pembe ya Afrika na uwezekano wa kupunguza mvua katika kipindi hikiNa walinda amani wa kikosi cha 11 cha Tanzania -TANZBATT-11 kinachohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO jimboni Kivu Kaskazini wametunukiwa nishani ya umoja wa mataifa ikiwa ni alama ya kufanya kazi  kwa utii,uhodari na uaminifu. Miongoni mwao ni Private Selina Kisemvule.Katika mashinani ikiwa ni siku ya mwisho ya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, fursa ni yake Rais Nangolo Mbumba wa Namibia ambaye kupitia ukurasa wa X wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA anawahimiza wananchi na dunia nzima kwa jumla kusimama kidete ili  kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

VOA Express - Voice of America
Usawa wa kijinsia, Akili Mnemba na usalama ni miongoni mwa masuala yaliyojadiliwa katika kongamano la wanawake katika Media nchini Senegal. - Desemba 10, 2024

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 10, 2024 29:59


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
DRC:Rais Felix Tchisekedi awataka raia wa nchi yake kuunga mkono mabadiliko ya katiba

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Nov 30, 2024 19:58


Miongoni mwa yale utakayoyasikia kwenye habari ni pamoja na Rais wa DRC, Felix Tschisekedi, kuwataka raia wa nchi yake  kuunga mkono mabadiliko ya katiba, , Chama tawala cha CCM  nchini Tanzania chaongoza kwa asilimia 99 ya kura.Zaidi ya watu 100 hawajulikani walipo baada ya ajali ya maporomoko ya Udongo nchini Uganda,pia Tutaangazia ziara yake  Rais wa Nigeria, Bola Tinubu, nchini Ufaransa,  Raia wa Namibia wapiga kura,     kisha kimataifa tutaangazia mkutano wa  Mawaziri wa mambo ya nje kutoka muungano wa G7,uliofanyika mjini Roma Italia.

Habari za UN
Jukwaa la UN la Muungano wa Ustaarabu limetufungua macho - Dativa Mahanyu na Mariam Mintanga

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 27, 2024 3:37


Jukwaa la 10 la Umoja wa Mataifa la Ustaarabu limekunja jamvi leo huko Cascais, Ureno ambako sambamba na jukwaa hilo, pia vijana kutoka makundi 150 duniani walikusanyika katika Jukwaa lao. Katika vijana hao walikuwemo watengeneza filamu chipukizi ambao kupitia filamu wanaeleza mambo kadha ya ulimwengu kama uhamiaji, ujumuishaji, kupambana na ubaguzi na mengine mengi. Miongoni mwa vijana hao waliohudhuria ni Dativa Mahanyu na Mariam Mintanga kutoka Tanzania. Kwanza tumsikilize Mariam Mintanga akieleza alivyojisikia kuhudhuria mkutano huu kisha tutamsikia Dativa Mahanyu akieleza kuhusu filamu ya Fid ya ambayo kupitia taasisi ya Tai Tanzania imepata tuzo ya PLURAL+

Habari za UN
27 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 27, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya afya na lishe katika nchi zinazokumbana na ukame. Makala tunakwenda Ureno na mashinani nchini Sudan, kulikoni?Mkurugenzi mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO, amesema amestushwa na kusikitishwa na kifo cha aliyetarajiwa kushika wadhifa wa mkurugenzi mkuu wa WHO Kanda ya Afrika Dkt. Faustine Engelbert Ndungulile kutoka nchini Tanzania.Awamu ya pili ya mradi wa kuboresha lishe, SUN II nchini Zambia umewezesha wakulima kupanda mazao yanayohimili ukame na vile vile kukabiliana na viwavi jeshi kwa kutumia mbinu za asili, mradi uliotekelezwa na shirika la Umoja la kuhudumia watoto, UNICEF ili wakulima wasikumbwe na njaa wakati huu ambapo ukame umetikisa nchi za kusini mwa Afrika.Jukwaa la 10 la Umoja wa Mataifa la Ustaarabu limekunja jamvi leo huko Cascais, Ureno ambako sambamba na jukwaa hilo, pia vijana kutoka makundi 150 duniani walikusanyika katika jukwaa lao wakiwemo watengeneza filamu chipukizi ambao kupitia filamu wanaeleza mambo kadha ya ulimwengu kama uhamiaji, ujumuishaji, kupambana na ubaguzi na mengine mengi. Miongoni mwa vijana hao ni Dativa Mahanyu na Mariam Mintanga kutoka Tanzania. Kwanza tumsikilize Mariam Mintanga akieleza alivyojisikia kuhudhuria mkutano huu kisha tutamsikia Dativa Mahanyu akieleza kuhusu filamu ya Fid ya ambayo kupitia taasisi ya Tai Tanzania imepata tuzo ya PLURAL+.Na mashinani fursa ni yake Shaza Ahmed, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la wanawake Nada El Azha linalotoa msaada kwa waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia nchini Sudana akitoa wito kwa viongozi wa kimataifa wa kutokomeza ukatili wa kijinsia.Mwenyeji wako ni Bosco Cosmas, karibu!  

Habari za UN
21 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 21, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kushuhudia jinsi mpango wa Usimamizi wa Ardhi uliopatiwa wa "kusaidia jamii kufikia Ajenda 2030” ambao FAO imetekeleza kwa kaunti kadhaa. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno.Hague kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa ICC ambayo leo imetoa kibali cha kukamatwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, Waziri wa zamani wa ulinzi Yoav Galant  na kiongozi wa kundi la kipalestina la Hamas Mohamed Diab Ibrahim al-Masri alimaarufu kama  kwa makosa ya uhalifu dhidi ya ubinadamu na uhaifu wa vita ulitendeka wakati wa vita inayoendelea baina ya Israel na Hamas.Mjini  Baku nchini Azerbaijan mkutano wa 29 wa mkataba wa nchi wanachanama wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabainchi COP29 unaelekea ukingoni  na leo ukijikita na masuala ya kijinsia na mabadiliko ya tabianchi. Miongoni mwa waliozungumzia changamoto ya tabianchi kwa wanawake ni  Jemimah Njuki, mkuu wa kitengo cha uwezeshaji wa kiuchumi katika shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women.“Raia  wanaoshtakiwa katika mahakama za kijeshi nchini Uganda hukosa dhamana sawa ya mchakato wa kisheria kama wale wanaoshtakiwa katika mahakama za kiraia,” amesema Volker Türk, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu hii leo kufuatia tukio la kutekwa kwa mwanasiasa wa upinzani nchini Uganda Kiiza Besigye akiwa nchini Kenya.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno MHARABU”.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Habari za UN
19 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 19, 2024 11:07


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Baku nchini Azerbaijan kwenye mkutano wa COP29. Miongoni mwa mambo yanayopigiwa chepuo ni madini ya kimkakati yanayoelezwa kuwa ni jawabu la nishati chafuzi kwa mazingira na tunapata ufafanuzi kutoka kwa Adam Anthony, Mkurugenzi Mtendaji wa HakiRasilimali nchini Tanzania.Katibu  Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amewasihi viongozi wa kundi la nchi 20 zenye uchumi mkubwa zaidi duniani, G20 wanaokutana huko Rio De Janeiro, Brazil kuwaagiza mawaziri na washawishi wao huko COP29 wahakikishe wanakubaliana juu ya lengo jipya na kubwa la mwaka huu la ufadhili kwa tabianchi nchi. Guterres amesema sambamba na hilo ni vema kukabiliana na taarifa potofu kuhusu tabianchi.Huko Kusini mwa Lebanon, walinda amani wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha Mpito nchini humo, UNIFIL, wameshuhudia uharibifu mkubwa wa kutisha kwenye vijiji vilivyoko sambamba na eneo      la kati ya Israeli na Lebanon lisilopaswa kuwa na mapigano, huku hali ya watoto nchini humo ikizidi kuwa mbaya.Hii leo ni siku ya choo duniani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema licha ya choo kuwa ni msingi wa kusongesha afya ya binadamu na kusaidia watoto wa kike na wanawake kuishi maisha ya utu, bado wakazi wengi wa dunia hususan kwenye mizozo na majanga wanaishi bila huduma hiyo ya msingi.Mashinani tunasalia huko huko Baku, kwenye COP29 ambapo nampisha msichana mwanaharakati wa mazingira kutoka Tanzania, akieleza ni nini anafanya na nini atakachoondoka nacho kwenye mkutano huo.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

Habari za UN
Vijana wafurahia stadi za kuondokana na umaskini Sudan Kusini

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2024 1:57


Vijana katika mji wa Tambura ulioko jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini wanageuza mafunzo ya ufundi stadi kuwa nguvu ya amani na ustawi, mafunzo ambayo yalifanikishwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, UNMISS.Shamrashamra zilitawala wakati vijana 61, wakiwemo wasichana 41 na wavulana 20 walipohitimu mafunzo ya ufundi stadi yenye lengo la kuwaondoa katika umaskini na pia kuwaepusha kutumikishwa katika mzozo unaoendelea nchini humo tangu Desemba 2013.Walifundishwa urembo wa nywele, kutengeneza sabuni, halikadhalika ushoni, mafunzo yaliyofadhiliwa na UNMISS na kutolewa na shirika la kiraia Star Trust Organization, linalohusika na kupunguza ghasia kwenye jamii kwa kuwajegena vijana uwezo.Miongoni mwao ni Suzan James, mama wa watoto wawili aliyejifunza urembo wa nywele na akiwa anamhudumia mteja wakati wa mafunzo anasema.“Ninashukuru mno, kwa sababu nimejifunza mambo mengi ambayo awali sikuyafahamu, lakini sasa ninaweza kufanya. Inanisaidia sana, na ninajivunia na nina furaha. Baada ya hili, nitaenda kufungua sehemu yangu mwenyewe ya urembo wa nywele ili kusaidia jamii.”Huyu ni Justin Alex yeye amejifunza ushoni na akiwa kwenye chereheni yake anasema.. “iwapo nitapekela hii cherehani nyumbani, nitaweza kufanya kazi na kusaidia familia yangu. Kama kijana tusikae nyumbani au tusifanye uhalifu mjini na kusababisha vifo kwa jamii zetu kwa sababu si jambo zuri. Kuanzia sasa tunahitajika kushiriki kwenye shughuli za kusaidia jamii, kama kupeleka hii cherehani nyumbani ili nisaidie jamii yangu.”Wahitimu wamepatiwa vifaa vya kuanzia kufanyie kile walichojifunza. Katika hafla ya utoaji wa vyeti UNMISS iliwakilishwa na afisa wake wa masuala ya ulinzi na ujumuishaji kwenye jamii Ibrahim Tahiru ambaye amesema..“Mradi huu unaweza kuleta amani, lakini pia mradi huu huu unahitaji amani ili uweze kuendelea. Bila amani hivi vitu vitakuwa bure. Kwa sababu wahitimu wanahitaji mazingira yenye amani ili waweze kutumia stadi zao kwa ajili ya kuboresha maisha yao na ya jamii zao. Mradi huu ni ishara ya nia yetu ya kuendelea kushirikiana na Sudan Kusini na kusaidia kufikia amani ya kudumu na kuondokana na umaskini.”Mamlaka za Tambura zina Imani kubwa na mradi huu kama asemavyo Kaimu Kamishna wa Tambura Moses Masisere.“Hakika, Tambura tumekuwa tukililia amani. Kwa hiyo kwa msaada huu tunaamini kuwa mafunzo kwa vijana zaidi kutawasaidia washiriki kwenye harakati za kiuchumi na kupunguza mauaji na uhalifu mwingine Tambura.”

Habari za UN
08 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 8, 2024 9:57


Hii leo jaridani tunakuletea kipindi maalum kinachotupeleka jijini Havana Cubaambapo kongamano la kimataifa la Kiswahili limeng'oa nanga likiwaleta pamoja takribani washiriki 400 kutoka Afrika, Asia, Amerika na Ulaya ili kujadili ajenda mbalimbali za kupanua wigo wa luugha hiyo na kuitumia kuleta tija ikiwemo kusongesha malengo ya Umoja wa Mataifa kama amani na maendeleo endelevu.Miongoni mwa habari kubwa Umoja wa Mataifa hii leo ni uwajibikaji unasakwa kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya  wapalestina na waisraeli, na pia shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO limeweka bayana gharama za kiuchumi na hata kiafya zilizofichika zitokanazo na mifumo ya uzalishaji, usafirishaji na ulaji wa chakula. Lakini kubwa zaidi nakupeleka Havana, Cuba kupata kwa mahtasari mazungumzo ya Flora Nducha na mmoja wa washiriki.Mashinani tunasalia huko huko Havana Cuba na fursa ni yake Profesa Juan (Huani) Jacomino (Hakumino) raia wa Cuba ambaye ni Mwalimu wa Kiswahii katia  chuo kikuu cha Havana Cuba anayeshiriki Kongamano la Kiswahili lililofunguliwa leo akitoa wito kwa raia wa Cuba na wa nchi zingine kuhusu umuhimu wa kukumbatia  Kiswahili. Mwenyeji wako ni Bosco Cosmas, karibu! 

Habari za UN
Fahamu kuhusu faida za kidiplomasia na kiuchumi zilizoletwa na lugha ya Kiswahii kisiwani Zanzibar

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 7, 2024 6:41


Huko Havana Cuba mambo yanaendelea kuiva kwenye Kongamano la kimataifa la Kiswahili huku wageni wakitoka katika kila pembe ya dunia kushiriki. Miongoni mwao ni Waziri Tabia Maulid Mwita kutoka Zanzibar ambaye amezungumza na shuhuda wetu katika kongamano hilo Flora Nducha kuhusu faida za kiplomasia na kiuchumi zilizoletwa na lugha ya Kiswahii Kisiwani Zanzibar.

Habari za UN
Wiki mbili za kusaka usalama DRC, mkimbizi asimulia madhila na atakacho.

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 7, 2024 2:23


Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, imesalia katika mgogoro kwa miaka mingi, hali ambayo imewasababishia raia mateso ya hali ya juu zaidi yakiwemo mauaji, utekaji nyara, na kuteketezwa kwa nyumbaa zao. Mapigano hayo pia yamewafungisha viragozaidi ya watu milioni 6.4 nchini humo, na kulazimisha familia kutafuta usalama katika makazi ya muda yaliyojaa pomoni. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limeonya kuwa mgogoro huu uliodumu kwa muda mrefu na ukiukwaji wa haki za binadamu ni mwiba kwa wakimbizi hawa wa ndani.  Cicey Kariuki na taarifa zaidiRusayo ni eneo lililo na makazi ya muda ya wakimbizi   mjini Goma katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Miongoni mwa  wakimibizi wa ndani wanaishi kwenye makazi haya ni Sebororo, mwanamke mwenye  miaka 38 akitembea na watoto wake.Sebororo pamoja na wananawe watano wanaishi kwenye makazi ya pamoja na familia nyingine 90 huku wakisubiri kutengewa nyumba katika eneo hilo. Mama huyu anaeleza jinsi alivyojikuta katika makazi ya wakimbizi. Anasema,“tulianza kukimbia kuktoka kule tarehe tano mwezi wa kumi, awali walikuwa wanakuja lakini hawakuua watu, lakini leo hii wanaua watoto,wanaume na wanawake, sisi yalitushinda maanake wengine walikuwa pia wanatekweteza mimea.”Sebororo na watoto wake watano walitembea kwa wiki mbili kutafuta usalama, baada ya wapiganaji kuvamia kijiji chao cha Kiseguru katika Mkoa wa Kivu Kaskazini. Katika nusu ya kwanza ya mwaka wa 2024 pekee, zaidi ya watu 940,000 walilazimika kukimbia kutokana na ukatili, uliofanywa na makundi mengi yenye silaha yasiyo ya kiserikali huku familia nyingi zikifurushwa mara kadhaa. Kwa sasa anachokitamani zaidi Sebroro ni amani. “Haja yetu sisi ni watusaidie kwa kusimamisha vita ili turejee kwetu kwa sababu watu wanaisha.”Anasema.Kufurika kwa watu katika makazi haya ya muda kumezua  wasiwasi mkubwa miongoni mwa wahudumu wa kibinadamu kufuatia hatari ya kuenea kwa magonjwa, ikiwa ni pamoja na virusi vya homa ya nyani au mpox.Ruven Menikdiwela, Kamishna Msaidizi wa Operesheni wa UNHCR ambaye alitembelea eneo hilo na kukutana na familia mbalimbali za wakimbizi na kusikiliza wasiwasi wao, anasema, “leo asubuhi, nilizungumza na mwanamke huyu ambaye ana watoto wadogo watano. Alitembea kwa wiki mbili kufika katika eneo hili, bado anasubiri huduma, bado anasubiri watoto wake watibiwe, na bado anasubiri chakula. Ninatambua kwamba hii ni hali ya kawaida kwa watu wote wanaoishi katika eneo hili. Kila mmoja ana majanga yake binafsi, kwa hivyo hizi siyo tu takwimu, bali kuna hadithi za kibinafsi nyuma ya kila moja ya hizi takwimu na majanga ya kibinafsi na majanga yanayoendelea pia, kwa sababu hatuoni suluhisho lolote kwenye mustakabali.”Katika ziara yake kwenye makazi haya, Ruven Menikdiwela, pia alifanya vikao na wadau kadhaa akiwemo Waziri mkuu, mamlaka za mkoa na mashirika ya umoja wa Mataifa. Ujumbe wake ulikuwa wazi kwamba amani ndiyo suluhisho endelevu na dhabiti zaidi, na inahitajika kwa dharura. “Pande zote zinapaswa kukutana na kujadiliana kutoa fursa kwa amani, ili watu hawa wote, mamilioni ya watu waliolazimika kuhama, waweze kurudi nyumbani au kuunganishwa na jamii mahali walipo, na waweze kuishi kwa amani pamoja kama jamii moja.”

Habari za UN
UNESCO: Tunapaswa kuthamini sauti za walimu kote duniani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 4, 2024 2:58


Washiriki wa hafla ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Walimu ililofanyika leo Oktoba 4 katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) jijini Paris, Ufaransa  wamesisitiza wito wa kuthamini mawazo ya walimu katika kuboresha elimu ya ulimwengu. Kama tunavyofahamu, siku yenyewe ya Kimataifa ya Walimu ni kesho Oktoba 5 kama ilivyo ada ya kila mwaka lakini katika makao makuu ya UNESCO hapa Paris Ufaransa, maadhimisho yamefanyika leo kuelekea mkesha wa siku hii muhimu kwa elimu ya ulimwengu.Miongoni mwa waliozungumza ni Mkurugenzi Msaidizi Mkuu wa Elimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi Stefania Giannini, ambaye ameitumia nafasi hii kusisitiza kauli mbiu ya mwaka huu ambayo ni 'Kutambua sauti za walimu.'Anasema, “walimu ni uti wa mgongo wa mifumo ya elimu na mawakala wakuu wa mabadiliko ya kubuni sera za elimu na kufanikisha SDGs. Tunapaswa kuthamini sauti za walimu; hili ndilo lengo kuu la Siku ya Kimataifa ya Walimu mwaka huu.”Kulingana na takwimu zilizotolewa na UNESCO, dunia inahitaji walimu wa ziada milioni 44 ili kufikia elimu ya msingi na sekondari kwa wote ifikapo mwaka 2030. Ingawa mahitaji ya walimu ni makubwa zaidi katika baadhi ya maeneo, uhaba wa walimu ni wa kimataifa.Walimu wanajiondoa kwenye taaluma hii kwa kiwango mara mbili zaidi ya miaka mitano iliyopita, hasa katika elimu ya sekondari. Hii inatokana na hali zao za kazi, zikiwemo mishahara midogo, mzigo mkubwa wa kazi, na ukosefu wa ushiriki katika maamuzi yanayohusu elimu. Akiiangizia changamoto hii, Mkurugenzi wa Kimataifa wa Elimu na Maendeleo ya Vijana katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) Bi. Pia Britto, aliyejiunga katika hafla ya leo kwa njia ya video akiwa Pakistani amesema,"Leo nilikuwa na fursa nzuri ya kuzungumza na walimu wengi, ikiwa ni pamoja na mwalimu Tahseen Bashir hapa Islamabad, ambaye amenieleza baadhi ya changamoto wanazokabiliana nazo ikiwa ni pamoja na kufundisha madarasa mengi, uhaba wa vifaa vya kujifunzia, na changamoto za kutoweza kufundisha namna wanavyodhamiria. Lakini pia amenieleza jinsi alivyofurahi kuona wanafunzi wake wakifaulu. Wakati sauti ya mwalimu inaposikilizwa na wakati sauti za walimu zinapopewa kipaumbele, wanajiona kama wadau katika kuboresha elimu kwa wakati wote, na hatua hizo zinahitajika ili kuleta mabadiliko chanya hasa katika hali ngumu zaidi."Siku hii ya kimataifa ya walimu ni mahususi kwa ajili ya kutambua na kusherehekea mchango muhimu wa walimu ulimwenguni kote katika kutoa elimu bora na kujenga mustakabali wa jamii. Pia, ni fursa ya kuangazia changamoto wanazokabiliana nazo walimu.Kutoka hapa Paris Ufaransa, mimi ni Cecily Kariuki..

Habari za UN
20 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 20, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia uondoaji wa taka katika ukanda wa Gaza, na ujumbe wa vijana ambao watashiriki mijadala mikuu hapa makaomakuu ya Umoja wa Mataifa. Makala tunasalia hapa hapa makao makuu na mashinani tunakupeleka nchini Sudan Kusini, kulikoni?Hali inazidi kuwa si hali huko Ukanda wa Gaza kwani sasa raia wanakwepa sio tu mashambulizi na magonjwa bali pia nyoka, panya na wadudu ambao wanasambaa kutokana na mazingira machafu. Watu wanajihifadhi kwenye maeneo ya wazi bila mifumo ya majitaka au ya kuondoa maji ya mvua. Timu ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina imefika kupuliza dawa ili kulinda wananchi hao.Leo hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani vijana kutoka kila kona ya dunia wanakutana kuanza kujadili kuhusu mstakabali wao katika zama zijazo. Miongoni mwao ni Jerop Limo kutoka Kenya anayetumia uzoefu wake wa kuishi na Virusi Vya Ukimwi kwa miaka 24 ya umri wake kuhakikisha ulimwengu unakuwa mahali bora kwa watu ambao tayari wanaishi na virusi hivyo.Makala inaturejesha hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani ambako mkutano wa Zama Zijazo umen'goa nanga leo kwa siku mbili za kuchua hatua kabla ya kikao cha ngazi ya juu siku ya Jumapili na Jumatatu. Leo Vijana wanapata fursa ya kupaza sauti zao kuhusu dunia na mustakbali wautakao.Na katika mashinani Balozi Mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, Tendai Mtawarira, mwanamichezo nguli mstaafu wa mpira wa raga mzaliwa wa Zimbabwe lakini alichezea Afrika Kusini, akizungumzia alichokishuhudia katika safari yake ya kwanza nchini Sudan Kusini.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Habari za UN
Mataifa yahakikishe ulimwengu unakuwa mahali bora kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi - Jerop

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 20, 2024 2:15


Leo hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani vijana kutoka kila kona ya dunia wanakutana kuanza kujadili kuhusu mstakabali wao katika zama zijazo. Miongoni mwao ni Jerop Limo kutoka Kenya anayetumia uzoefu wake wa kuishi na Virusi Vya Ukimwi kwa miaka 24 ya umri wake kuhakikisha ulimwengu unakuwa mahali bora kwa watu ambao tayari wanaishi na virusi hivyo. Anold Kayanda amezungumza naye na hapa Jerop Limo anaanza kwa kueleza yale ambayo atawaeleza viongozi wa ulimwengu.

Habari za UN
UNICEF Burundi yachukua hatua mpox isivuruge muhula wa masomo kwa watoto

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 18, 2024 1:53


Nchini Burundi shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linashirikiana na serikali kuhakikisha mlipuko wa ugonjwa wa homa ya nyani au mpox nchini humo hauthiri watoto kurejea shuleni wakati huu ambapo asilimia 33 ya wagonjwa wakiripotiwa kuwa na umri wa kati ya miaka 5 hadi 19. Cecily Kariuki anatupa maelezo zaidi kupitia  video hii ya UNICEF inayotupeleka hospitali ya Prince Louis Rwagasore iliyoko mji mkuu wa taifa hilo la Maziwa Makuu, Afrika, Bujumbura..Video ya UNICEF inaanzia kwenye uwanja wenye mahema yenye nembo ya shirika hilo. Moja kwa moja tunaingia ndani, daktari akitoa maelekezo kwa akina mama walioko na watoto wao wanaougua mpox. Miongoni mwao ni Primitive Nibitanga, mama watoto wawili. Primitive anasema tumelazwa kwa zaidi ya wiki mbili sasa. Nilienda kituo cha afya lakini hawakuweza kumtibu mtoto wangu. Majirani walinishauri nije hapa kliniki. Nilifika na kulazwa. Mtoto wangu alikuwa mahututi, lakini wauguzi walijitahidi kwa kadri ya uwezo wao na haikuchukua muda alipona. Bahati mbayá siku tatu baadaye dada yake alipata dalili zile zile na tukarejea tena hapa.”Daktari Fidel Cishahayoanahusika na usimamizi wa matibabu ya mpox katika hospitali hii ya Prince Rwegasore. Anasema “hatua ya kwanza ilikuwa kutenga hili eneo kwa sababu tulikuwa tunapokea wagonjwa wa mpox na wanaoshukiwa kuwa na maambukizi. Kwa hiyo tuliandaa ili kuwa na eneo la wagonjwa na washukiwa. Tuliandaa pia timu ya wahudumu, wakiwemo madaktari na wauguzi kutoka idara nyingine kwa ajili ya mpox. Wanaopona wanaruhusiwa na kushauriwa kujitenga kwa angalau wiki tatu.” UNICEF tayari imeomba dola milioni 58.8 kusaidia kupambana na mlipuko wa mpox barani Afrika ikiwemo nchini Burundi. Mwakilishi wa UNICEF nchini Burundi France Bégin amesema fedha hizo pamoja na mambo mengine zitasaidia kuwalinda watoto ili warejee shuleni licha ya mlipuko. Vile vile kuepusha kuvurugwa zaidi kwa fursa za wanafunzi kusoma kwani mwaka mpya wa masomo umeanza tarehe 16 mwezi huu wa Septemba.

Habari RFI-Ki
Africa : Ukosefu wa ajira wachangia uhalifu miongoni mwa vijana

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Sep 18, 2024 9:35


 Katika makala haya tunajadili kinachoendelea katika mataifa mengi ya  Afrika kuendelea kushuhudia ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana, hii likichangia kwa kiasi kikubwa uhalifu. Je Wewe unafanya nini ili kupata riziki ya kila siku ?Ndilo swali tumekuulizaHaya hapa baadhi ya maoni yako.

Habari RFI-Ki
Africa : Ukosefu wa ajira wachangia uhalifu miongoni mwa vijana

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Sep 18, 2024 9:35


 Katika makala haya tunajadili kinachoendelea katika mataifa mengi ya  Afrika kuendelea kushuhudia ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana, hii likichangia kwa kiasi kikubwa uhalifu. Je Wewe unafanya nini ili kupata riziki ya kila siku ?Ndilo swali tumekuulizaHaya hapa baadhi ya maoni yako.

Habari za UN
UNHCR yatoa ombi la dharura la dola milioni 21.4 kukabili mpox miongoni mwa wakimbizi barani Afrika

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 11, 2024 2:07


Ugonjwa wa homa ya nyani au mpox ukisalia kuwa dharura ya afya ya umma duniani, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR linasaka zaidi ya dola milioni 21 zitakazotumika hadi mwishoni mwa mwaka huu kuongeza harakati dhidi ya ugonjwa huo miongoni mwa wakimbizi katika nchi zilizokumbwa na dharura ya ugonjwa huo, hususan Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Assumpta Massoi anafafanua zaidi.UNHCR imetangaza ombi hilo leo la dola milioni 21.4, fedha zinazolenga kusaidia watu milioni 9.9 waliolazimika kukimbia makwao kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo vita. Watu hao wako kwenye nchi 35 barani Afrika.Hatua hii ya UNHCR inakuja baada ya wagonjwa 88 wa mpox kuwa ni wakimbizi na kati yao hao 68 wako DR Congo, taifa ambalo limeripoti idadi kubwa zaidi ya wagonjwa wa mpox duniani. Wagonjwa pia wameripotiwa Jamhuri ya Congo au Congo-Brazaville na vile vile Rwanda.Taarifa ya UNHCR kutoka Geneva, USwisi inasema, ingawa mpox ni ugonjwa wa muda mrefu barani Afrika, ongezeko la wagojwa hasa wenye mnyumbuliko mpya wa mpox yaani Clade 1b umefanya shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO kutangaza tarehe 14 mwezi Agosti kuwa mpox ni dharura ya afya ya umma duniani. Na tangu wakati huo watu 20,000 barani Afrika wameshukiwa kuwa na ugonjwa huo.Allen Maina, Mkuu wa Afya ya Umma UNHCR anasema kwa mazingira ya sasa walio hatarini kuambukizwa zaidi ni wakimbizi wanaoishi kwenye mazingira magumu bila maji, wala sabuni na lishe bora.Sasa wanahitaji kusaidia serikali na wadau katika hatua dhidi ya mpox kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma. Hivyo fedha zitaimarisha mifumo ya afya, maji na huduma za kujisafi na kuhakikisha wakimbizi wanajengewa mnepo sasa na siku za usoni.UNHCR inatoa wito kwa wahisani kuonesha ukarimu wao kwa kuwa fedha hizo zitawezesha ujumuishaji wa wakimbizi kwenye mipango ya serikali katika nchi husika ya kujiandaa na kujikinga dhidi ya mpox kwa mujibu wa Mpango wa Afrika dhidi ya mpox ulioandaliwa na kituo cha Afrika cha kudhibiti na kuzuia magonjwa, CDC na WHO.

Habari za UN
Monusco yafadhili ujenzi wa zahanati katika gereza kuu la Beni,DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 28, 2024 1:56


Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,  DRC, MONUSCO, umeboresha huduma za afya kwenye Gereza Kuu la Beni, jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa taifa hilo la Maziwa Makuu barani Afrika kwa kujenga zahanati iliyoboresha sit u mazingira ya kazi kwa wahudumu wa afya bali pia huduma za matibabu kwa wafungwa. Cecily Kariuki anasimulia zaidi(Taarifa ya Cecily Kariuki)Video ya MONUSCO iliyochapishwa kwenye mtandao wa X, zamani Twitter inaonesha jengo la zahanati hiyo likiwa la rangi nyeupe na buluu, wahudumu wa afya wakiwa na makoti meupe, masafi kabisa, halikadhalika mazingira ya kituo hiki.Miongoni mwao ni Dkt. Michel Muhindo ambaye hawezi kuficha furaha yake.(Dkt Michel Muhindo)- Bosco“Msaada huu wa zahanati ni ahueni kubwa kwetu sisi tunaofanya kazi hapa, na hata kwa wafungwa, kwa sababu wanapatiwa huduma nzuri ya uchunguzi, na tunafanikiwa kutoa majibu mazuri na tunawatibu ipasavyo. Tunakadiria kwamba kweli ilikuwa inahitajika.”Je, hali ilikuwa vipi kabla ya maboresho haya?(Dkt Michel Muhindo)- Bosco“Kabla ya kupata huduma hii ya matibabu, yaani zahanati hii, kulikuwa tu na vyumba ambavyo tulikuwa tunawaweka wagonjwa kwa ajili ya uchunguzi. Lakini hakukuwa na maabara, wala ofisi nzuri za ushauri. Tulikuwa na wakati mgumu sana, kulikuwa na kelele. Ilibidi kuwa makini sana ili kuweza kusikiliza wafungwa wagonjwa.”Sasa wafungwa wanapata huduma kwa nafasi kabisa..(Dkt Michel Muhindo)- Bosco“Hii inapunguza muda wa huduma kwa wafungwa katika zahanati hii. Sasa kuna maeneo maalumu yaliobainishwa vizuri. Tunaweza kusema: hiyo ni maabara, hicho ni chumba cha uchunguzi wa wagonjwa, hicho ni chumba cha daktari, kwa wauguzi, pamoja na mapokezi ambapo tunaweza kuwakaribisha wafungwa wanaokuja kwa ushauri wa matibabu.”

Habari za UN
26 AGOSTI 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 26, 2024 9:43


Hii leo jaridani tunamulika kupelekwa kwa chanjo dhidi ya polio huko Gaza; mkimbizi wa Burundi aliyerejea nyumbani kutoka Tanzania ainuliwa kiuchumi; makala ni mkimbizi wa Sudan aliyeko ugenini naye awezeshwa kijasiriamali na mashinani tunabisha hodi nchini Rwanda kumulika usawa wa kijinsia kwenye michezo.Hatimaye shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linapeleka Gaza huko Mashairki ya Kati dozi milioni 1.2 za chanjo dhidi ya ugonjwa wa polio aina ya 2, wakati huu ambapo ugonjwa huo hatari umethibitishwa kuweko eneo hilo. Anold Kayanda na maelezo zaidi.Kwa wakimbizi, kurejea nyumbani ni jambo moja na kuanza upya ni jambo lingine. Wengi wao hawana chaguo lingine isipokuwa kuanza maisha yao upya. Mkoani Makamba, nchini Burundi, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) kwa kushirikiana na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) wanawawezesha waliorejea nyumbani kujijenga upya na kwa tija. Miongoni mwao ni Emelyne Kabura kama anavyosimulia Bosco CosmasKatika makala Evarist Mapesa anatuletea simulizi ya mkimbizi wa Sudan ambaye sasa anaishi Sudan Kusini. Baada ya kupitia madhila lukuki amewezeshwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa na sasa anajishughulisha na ujasiriamali.Na sasa ni mashinani  Christelle Umuhoza, Mkurugenzi wa Programu wa Rwanda katika shirika la Shooting Touch, kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO nchini humo, anaeleza umuhimu wa michezo katika kuondoa vikwazo vya kijinsia.

Habari za UN
Vijana wanaweza kutumia elimu yao kusongesha SDGs iwapo watapata ufadhili wa miradi yao - Gibson

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 19, 2023 0:02


Hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York, Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa la Umoja wa Mataifa  kuhusu malengo ya maendeleo endelevu  kwa kifupi HLPF linakaribia kufikia ukingoni na leo Mjumbe Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu vijana aliitisha kikao cha kando kuzungumza na vijana kuhusu tathmini yao ya utekelezaji wa Mkakati wa Umoja wa Mataifa kuhusu vijana katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Miongoni mwa walioshiriki ni Gibson Kawago, mmoja wa viongozi vijana wa kusongesha SDGs. Nimezungumza naye kufahamu mambo kadhaa ikiwemo alichowasilisha kwenye mkutano huu.

Habari za UN
Ukatili dhidi ya wanawake na wasicha Mashariki mwa DRC umeongezeka - UNHCR

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 14, 2023 0:02


Hali ya kusikitisha inajitokeza Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ambapo ghasia zilizozuka upya kati ya makundi yasiyo ya kiserikali yenye silaha na vikosi vya serikali zimerejea katika majimbo ya Kivu Kaskazini, Kivu Kusini na Ituri zikiambatana na ukatili mkubwa dhidi ya wanawake na wasichana na kutawanya maelfu ya watu , limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR. Katika taarifa yalke iliyotolewa leo mjini Geneva Uswis kamishina msaidizi wa masuala ya ulinzi wa UNHCR Gillian Triggs amesema kutokana na hali hiyo, watu milioni 2.8 wamekimbia makazi yao katika majimbo hayo tangu mwezi Machi 2022. Miongoni mwa orodha ya sheria za kibinadamu na ukiukaji wa haki za binadamu, unaoendelea ni raia kuuawa na kuteswa, huku kukamatwa kiholela, uporaji wa vituo vya afya, nyumba za raia, na uharibifu za shule pia vimeripotiwa.Triggd ameongeza kuwa “Pia tunasikitishwa sana na kuongezeka kwa ripoti za ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na wasichana waliolazimika kukimbia makwao, ikiwa ni pamoja na vitendo vya ubakaji na unyanyasaji wa kijinsia.Cha kusikitisha, zaidi takwimu za hivi karibuni zinaonyesha kwamba kati ya zaidi ya watu 10,000 waliopata huduma za unyanyasaji wa kijinsia (GBV) huko Kivu Kaskazini katika robo ya kwanza ya mwaka, asilimia 66 ya kesi hizi zilikuwa za ubakaji.”Ameendelea kusema kwamba visa vingi vya ukiukaji huu mbaya wa GBV vimeripotiwa kufanywa na watu wenye silaha. Hata hiuvyo amesema anaamini takwimu hizo ni sehemu ndogo tu ya kile kinachoendelea kwani nmanusura wengi wa GBV hawaripoti ukatili huo au kufuata msaada wa huduma kutokana na hofu ya unyanyapaa kwenye jamii lakini pia fursa ya kuwafikia waathirika bado ni finyu kutokana nna hali ya usalama na masuala ya kiufundi.Kwa mujibu wa afisa huyo wa UNHCR hali ngumu ya maisha imewasukuma wanawake na wasichana wengi kugeukia mbinu za hatari kama biashara ya ngono hasa Goma Kivu Kaskazini ili kujikimu kimaisha na familia zao hasa wakati huu ambapo changamoto ya kutokuwa na uhakika wa chakula inaongezeka.Lakini pia amesema wanawake na wasichana wengi wanabakwa wakati wakienda kusenya kuni na kuteka maji.Amehitimisha taarifa yake kwa kusema “Tunatoa wito kwa serikali na mamlaka za mitaa kuchukua hatua za haraka kukabiliana na janga hili la kutisha la GBV. Wale waliohusika na ukiukaji huu mbaya wa haki za binadamu na sheria za kibinadamu lazima wawajibishwe.”

Habari za UN
Vijana tusipoteze matumaini bado tuna fursa ya kukabili changamoto ya tabianchi: Omesa Mukaya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 12, 2023 0:06


Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu HLPF linaendelea hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambapo wawakilishi wa nchi na serikali, wanasayansi, wanazuoni, mashirika ya umoja wa Mataifa asasi mbalimbali na vijana wanashiriki kukuna vichwa kujadili nini cha kufanyua kuhakikisha malengo hayo muhimu ya maendeleo yanatimizwa ifikpo mwaka 2030 na nini kifanyike kuzisaidia nchi zinazosuasua. Miongoni mwa washiriki ni kijana Omesa Mukaya kutoka Kenya ambaye mwezi Mei mwaka huu amehitimu shahada ya kwanza ya masuala ya sayansi ya mazingira na será katika chuo kikuu cha Clark Jimboni Massachussets hapa Marekani, amemweleza Flora Nducha wa Idhaa hii kilichomleta katika jukwaa hili.

Habari za UN
UN: Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa HLPF kuhusu SDG's limengoa nanga leo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 10, 2023 0:02


Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu ,malengo ya maendeleo endelevu lijulikanalo kama HLPF limeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa hapa New York Marekani chini ya mwamvuli wa baraza la kiuchumi na kijamii ECOSOC.Jukwaa hilo ambalo litakunja jamvi 20 Julai mwaka huu limebeba maudhui "Kuharakisha kujikwamua kutokana na janga la ugonjwa wa  virusi vya corona au COVID-19 na utekelezaji kamili wa ajenda ya 2030 ya maendeleo endelevu katika ngazi zote".Mbali ya viongozi wa ngazi ya juu katikia jukwaa hilo kutakuwa na siku tatu za majadiliano katika ngazi ya mawaziri.Kwa mujibu wa ECOSOC jukwaa hilo “litajumuisha mapitio ya mada ya malengo ya maendeleo endelevu namba 6 kuhusu maji safi na usafi wa mazingira, namba 7 kuhusu nishati nafuu na safi, namba 9 linalohusu viwanda, uvumbuzi na miundombinu, namba 11 linalohusu miji na jamii endelevu, na namba 17 linalohusu ubia kwa ajili ya malengo.”Pia jukwaa hili ltashughulikia changamoto maalum zinazokabili nchi zilizo katika hali maalum. Zaidi ya hapo litathimini vipimo vya kikanda na vya ndani ya nchi kuhusu kujikwamua kutoka kwaenye janga la COVID-19 na hali kuhusu malengo ya maendeleo endelevu SDGs. Na kisha litaunga mkono mapitio ya muda wa kati wa malengo ya SDGs na maandalizi ya mkutano wa mwa ka huu 2023 wa SDG mutaotarajiwa kufanyika Septemba.Leo katika siku ya kwanza ya jukwaa hilo mada kuu zitakazopewa kipaumbele ni “kushinda majanga, kuleta mabadiliko kwa aajili ya SDGs, na kutomwacha mtu yeyote nyuma, Kufadhili hatua zetu za kukabiliana na majanga na kuwekeza katika SDGs.”Nchi 39 zikiwemo Tanzania, Rwanda na Zambia zitafanya mapitio ya kitaifa ya hiari (VNRs) ya utekelezaji wao wa ajenda ya 2030 ya malengo ya maendeleo endelevu katika katika jukwaa hilo la HLPF 2023.Miongoni mwa wazungumzaji  wa leo katika jukwaa hilo ni wasaidizi wa Katibu Mkuu Li Junhua, Qu Dongyu ambaye ni mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO, Guy Ryder ambaye ni msaidizi wa Katibu Mkuu kuhusu masuala ya sera, Mami Mizutori msaidizi wa Katibu Mkuu na mkuu wa ofisi ya Umoja wa Msataifa ya upunguzaji wa hatari ya majanga UNDDR,  na Filippo Grandi ambaye ni Kamisha mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.

Habari za UN
UNFPA inasaidia kuhakikisha uzazi salama kwa wanawake na wasichana wanaokimbia ghasia Khartoum

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 30, 2023 0:02


Wanawake na wasichana wanaokimbia machafuko yanayoendelea mjini Kharthoum nchini Sudan wanakabiliwa na changamoto lukuki hususan kwa wajawazito wanaohitaji msaada wa kujifungua, kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA ambalo sasa limechukua jukumu la kuhakikisha uzazi salama kwa wanawake hao. Miongoni mwa wanawake hao ni Omnia hili si jina lake halisi amepewa ili kulinda usalama wake, akiwa na ujauzito wa miezi tisa,  alilazimika kuacha nyumba yake na kila kitu alichojua ili kuepuka vita kali iliyoukumba mji mkuu wa Sudan, Khartoum kuokoa maisha yake.Kwa uchumngu mkubwa anasema "Nimepoteza kila kitu katika vita hii. Lakini sikutaka kumpoteza mtoto wangu ambaye bado hajazaliwa.”Ingawa kusafiri katika hali yake ilikuwa hatari, alihisi hakuwa na chaguo, ukosefu wa usalama, risasi zinazorindima, uporaji na uharibifu wa vituo vya afya ulimaanisha kuwa hakuweza kumuona daktari kwa wiki kadhaa, ilikuwa safari ngumu ya siku tano, hatimaye mapema Juni alifanikiwa kufika Port Sudan, kwenye ufuo wa jimbo la bahari ya Sham.Omnia alikuwa akilia njia nzima kutoka Khartoum na aliogopa kwamba angepata uchungu na kujifungulia njiani kuelekea Port Sudan.Kwa mujibu wa UNFPA Omnia ni kisa kimoja tu lakini maelfu ya wanawake na wasichana wanapitia changamoto hiyo hivi sasa Sudan. Alikuwa na bahati kwani aliwasili katika hospitali ya mafunzo ya Port Sudan ambako alianza kuumwa uchungu na kusaidiwa kujifungua salama mtoto wa kike kwa njia ya upasuaji. Hata hivyo UNFPA inasema “hiyo ni hospital pekee ya serikali inayotoa huduma za uzazi kwa watu milioni 1.6 na sasa shirika hilo la idadi ya watu na wadau wa bahari ya Sham wanaisaidia hospitali hio kwa vifaa, dawa na mafunzo kwa wahudumu ili kuhakikisha wakina mama wajawazito kama Omnia waliotawanywa na vita na kuwasili Port Sudan kutoka nchi nzima wanajifungua salama.”Mkurugenzi mkuu wa hospitali hiyo Dkt. Randa Osman anasema “Timu yetu imejitolea kikamilifu kusaidia wanawake na wasichana wanaowasili kutoka Khartoum, lakini tunahitaji vifaa zaidi vya dharura, ikiwa ni pamoja na mafuta na vifaa vya kuokoa maisha na dawa. “Kwa mujibu wa UNFPA takriban vituo 46 vya afya nchini Sudan vimeshambuliwa, na karibu theluthi mbili havifanyi kazi tena.Mpango wa hivi karibuni wa msaada wa kibinadamu Sudan unalenga kuwasaidia waty milioni 24.7 ambapo milioni 11 kati yao wanahitaji msaada wa dharura wa huduma za afya na wanawake na wasicha milioni 2.6 miongoni mwao wako katika umri wa kuzaa.

Habari za UN
Mariam: Dawa za kulevya zilinifanya kupoteza mtoto na mume

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 26, 2023 0:04


Tatizo la dawa za kulevya duniani ni suala tata ambalo linaathiri mamilioni ya watu duniani kote. Watu wengi wanaotumia dawa za kulevya hukumbana na unyanyapaa na ubaguzi, jambo ambalo linaweza kudhuru zaidi afya yao ya kimwili na kiakili na kuwazuia kupata usaidizi wanaohitaji.Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na Dawa za Kulevya na Uhalifu UNODC inatambua umuhimu wa kuchukua mtazamo unaozingatia watu kuhusu sera za dawa za kulevya, kwa kuzingatia haki za binadamu, huruma na mazoea yanayotegemea ushahidi. Miongoni mwa shuhuda nzuri katika jamii ni kuwa wale waliotumia dawa za kulevya wanaweza kurejea kwenye afya zao na maisha yao ya awali iwapo wataacha na kukaaa kwenye vituo vya matibabu ya uraibu na matibabu. Mariam, sio jina lake halisi alikubali na kukaa kituoni na hii ni simulizi yake iliyoandaliwa na UNODC na inasomwa kwako na Evarist Mapesa wa redio washirika SAUTFM iliyoko Mwanza nchini Tanzania.  

Habari za UN
UNICEF: Idadi ya watoto waliotawanywa duniani imevunja rekodi na kufikia milioni 43.3

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 14, 2023 0:03


Katika kuelekea siku ya wakimbizi duniani itakayoadhimishwa wiki ijayo, ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF imeonya kwamba idadi inayoongezeka ya watoto kutawanywa duniani, inadhihirisha jinsi gani dunia ilivyoshindwa kushughulikia mizizi ya watu kutawanywa na kutoa suluhu ya muda mrefu hususan kwa watoto wanaolazimika kukimbia makwao.Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa leo mjini New York hadi kufikia mwisho wa mwaka jana 2022 makadirio ya UNICEF yanaonyesha kwamba watoto milioni 43.3 walilazimika kuishi maisha ya kutawanywa na wengi wao katika utoto wao wote.Ripoti inasema idadi ya watoto waliofurushwa kwa lazima kutoka makwao iliongezeka maradufu katika muongo uliopita, na hivyo kupita juhudi za kuweza kuwajumuisha na kuwalinda wakimbizi na watoto ambao ni wakimbizi wa ndani. Na vita nchini Ukraine imechochea hali kuwa mbaya zaidi ikiwalazimu zaidi ya watoto milioni 2 wa Ukraine kuikimbia nchi hiyo na kkuwafanya wengine zaidi ya milioni 1 kuwa wakimbizi ndani.Akizungumzia jinamizi hili mkurugenzi mtendaji wa UNICEF Catherine Russell amesema."Kwa zaidi ya muongo mmoja, idadi ya watoto wanaolazimika kuhama makwao imeongezeka kwa kasi ya kutisha, na uwezo wetu wa kimataifa wa kukabiliana na hali hiyo bado uko katika shinikizo kubwa. Ongezeko hilo linakwenda sambamba na mashambulizi ya mara kwa mara ya migogoro, changamoto na majanga ya tabianchi duniani kote. Lakini pia inadhihirisha hali duni za serikali katika kuhakikisha kila mkimbizi na mtoto aliyetawanywa ndani ya nchi anaweza kuendelea kusoma, kuwa na afya njema na kuendelea ili kufikia uwezo wake kamili.”Miongoni mwa watoto hai milioni 43.3 waliolazimika kutawanywa takribani asilimia 60 sawa na watoto milioni 25.8 walikuwa ni wakimbizi wa ndani waliotokana na mizozo na machafuko.Na idadi ya watoto wakimbizi na wasaka hifadhi ilifikia kiwango cha juu cha watoto milioni 17.5 bila kujumuisha watoto waliotawanywa mwaka huu wa 2023.Kwa mantiki hiyo UNICEF imetoa wito kwa serikali zote kutomwacha mtoto yeyote nyuma kwa kutambua watoto wakimbizi, wahamiaji na waliotawanywa cha kwanza ni watoto na wana haki ya kulindwa, kujumuishwa na kushirikishwa. Pili imezitaka serikali kutoa njia salama na za kisheria kwa watoto kuweza kuhama, kuomba hifadhi na kujumuishwa na familia zao.Tatu kuhakikisha hakuna mtoto anayeshikiliwa kwa sababu ya hali yake ya uhamiaji au kurejeshwa bila mazingira salama isipokuwa tu pale ambapo imebainika kuwa ni kwa maslahi ya mtoto.Nne imezitaka serikali kuimarisha mifumo ya kitaifa ya elimu, afya, ulinzi kwa watoto na mifumo ya hifadhi ya jamii ili kujumuisha watoto waliotawanywa bila ubaguzi.Tano kuwekeza katika mifumo ya ulinzi kwa watoto ili kuweza kuwalinda vyema watoto walio safarini dhidi ya hatari za kunyanyaswa na ukatili hususan watoto wanaokimbia peke yao bila walezi au wazazi.Na mwisho imezitaka serikali kusikiliza na kuwahusisha watoto katika kusaka suluhu ambazo ni endelevu na jumuishi na ambazo zinaweza kuwasaidia watoto hao kufikia uwezo wao.

Habari za UN
Sitisha uhasama miongoni mwa wakimbizi wa ndani Sudan Kusini: UNMISS 

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 9, 2023 0:02


Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umetoa wito wa kusitishwa mara moja kwa uhasama miongoni mwa wakimbizi wa ndani katika Kambi ya Umoja wa Mataifa ya Ulinzi wa Raia nchini humo kufuatia tukio la jana Alhamis ambapo watu kadhaa waliripotiwa kujeruhiwa na wengine kuuawa.Video iliyorekodiwa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS) inaonesha gari la wagonjwa la Umoja wa Mataifa likisindikizwa na walinda amani likipita katika barabara ya vumbi katikati ya umati wa wakimbizi wa ndani katika eneo la Malakal nchini Sudan Kusini.  Kila mmoja aliyefanikiwa kusalia na chochote katika anavyovimiliki, amekibebeba kichwani, mgongoni au mkononi.  Jana muda wa mchana ghasia zilizuka kati ya jamii mbili za wakimbizi wa ndani ambazo zimehifadhiwa katika Kambi ya Umoja wa Mataifa ya Ulinzi wa Raia. UNMISS inasema vurugu hizo zilichochewa na tukio la kuchomana visu huku ripoti za awali zikitaja raia watatu kuuawa na wengine 20 kujeruhiwa hadi kufikia jana Alhamisi mchana. Kabla ya hapo, hiyo-hiyo jana Alhamis asubuhi, milio ya risasi ilitanda alfajiri katika mji mkuu wa jimbo la Upper Nile, Malakal, karibu na makazi ya UNMISS.Walinda amani wa UNMISS waliingia kazini haraka kwa kuwa hali ya wasiwasi imekuwa ikiendelea hapa tangu mwisho wa wiki iliyopita, wakati mzozo katika kituo cha maji uliongezeka haraka na kuwa mzozo kamili ambapo mtu mmoja mwenye umri wa miaka 32 aliuawa. Kwa kuwa kambi ya walinda amani iko karibu na kambi ya Umoja wa Mataifa ya ulinzi kwa raia, mara zote walinda amani wako chonjo kuchukua hatua ya haraka pindi tu wanapopokea taarifa ya vurugu. Wakati wa mapigano ya mwezi uliopita, wanajeshi na polisi walinda amani walitumwa mara moja ili kutuliza hali hiyo. Polisi na walinda amani wa kijeshi kwa sasa wanashika doria ndani ya eneo hilo na kuzunguka eneo la nje, kwa ushirikiano na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Sudan Kusini ili kuondoa hofu miongoni mwa jamii iliyokimbia makazi yao. Zaidi ya hayo, walinda amani matabibu katika hospitali ya UNMISS wanatoa huduma ya dharura kwa baadhi ya waliojeruhiwa.  Kwa mujibu wa usajili wa kibayometriki wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM), kufikia Desemba mwaka jana 2022, baadhi ya watu 37,032 waliokimbia makazi yao wanajihifadhi katika Eneo la Ulinzi la Umoja wa Mataifa la Malakal. 

video zaidi umoja polisi raia kila kwa wakati kambi jeshi mataifa kabla unmiss shirika ujumbe wananchi miongoni desemba malakal sudan kusini alhamis alhamisi
Habari za UN
IOM yaeleza ilivyo hatari kuvuka eneo la msitu wa Darién

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 19, 2023 0:03


Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) linaongeza juhudi za msaada wa kibinadamu kwenye mipaka ya Colombia, Costa Rica na Panama ili kusaidia wahamiaji wanaovuka kuelekea eneo la kaskazini mwa Amerika hasa kupitia msitu hatari wa Darien unaounganisha Amerika kusini na kaskazini.  Kwa miaka mingi, jimbo la Darien nchini Panama limekuwa kituo cha kawaida cha kupita kwa wahamiaji wanaotoka kusini mwa Amerika kuelekea kaskazini. Takwimu za hivi karibuni za mwaka huu 2023 zinazidi kwa kiasi kikubwa idadi ya juu ya mwaka 2022, wakati watu 258,000 walivuka mwaka mzima. Kwa mujibu wa Mradi wa Wahamiaji Wasiofahamika waliko, wahamiaji wengi hawana vifaa vya kutosha vinavyofaa kwa safari ya siku mbili hadi kumi na karibu wahamiaji 137 walifariki dunia au kutoweka mwaka jana 2022. Luz Santo ni Afisa Mratibu wa IOM akiwa tu punde amewapokea wahamiaji waliovuka mto Chucunaque anasema, “Katika kituo hiki, tunapokea takriban watu 700 hadi 1,000 kila siku, na tunawapa taarifa za msingi kuhusu huduma zinazopatikana kwa ajili yao katika kituo cha mapokezi cha uhamiaji cha Lajas Blancas, na pia taarifa kuhusu njia." Wakati wa safari ndefu msituni, watoto na familia hukabiliwa na aina nyingi za unyanyasaji, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kijinsia, unyonyaji, pamoja na ukosefu wa maji salama na chakula, mashambulizi ya wanyama mwitu, na mito inayofurika. Robo tatu ya watu wamejeruhiwa wakiwa safarini, na theluthi moja wamekumbana na aina fulani ya kutendewa vibaya au unyanyasaji, hasa wakati wa kuvuka msitu huo wa Darien, IOM inaeleza. © UNICEF/Eduard SerraMiongoni mwa wahamiaji wapya waliowasili ni Luisa Maria Laya, mama raia wa Venezuela anayesafiri na watoto wake wawili na mumewe. Waliuza kila kitu walichokuwa nacho ili kumudu chakula na sehemu ya njia yako kutoka Venezuela walikuwa wanatumia usafiri wa kuomba msaada njiani. Matumaini yao ni kujiunga na familia ambayo tayari inaishi Marekani, “Tulipoanza safari yetu msituni, ilikuwa ngumu kwa sababu mimi, mume wangu na watoto wangu hatukuwa tumeizoea. Ilikuwa ngumu, kali, na hatari kwa maisha yetu. Namshukuru Mungu tumefika salama. Muhimu ni kwamba tulifika hai kwa sababu watu wengi huko wanadhani ni mchezo. Si mchezo, kinachoendelea si mchezo kujitosa kwenye msitu huo. Ni kitu hatari, hatari. Unahatarisha maisha ya watoto wako na yako mwenyewe.” Wahamiaji wa zaidi ya mataifa 40 wamevuka eneo la Darién mwaka huu. IOM inaeleza kwamba watu hao wanatoka katika mataifa ya Amerika, Asia na Afrika, kama vile Venezuela, Haiti, Ecuador, China, India, Afghanistan, Cameroon, na Somalia. Wengi wao wanatoka Venezuela lakini pia kumekuwa na ongezeko la idadi ya wahamiaji wa Haiti, Ecuador, na Wachina.  

Habari za UN
Nchini Chad WFP na wadau wahaha kusaidia wakimbizi wa Sudan

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 1, 2023 0:03


Chad inashuhudia wimbi jipya la wakimbizi wanaouvuka mpaka kutoka Sudan kuingia nchini humo kufuatia mapigano yaliyoanza tarehe 15 mwezi huu kwenye mji mkuu wa Sudan, Khartoum, hali inayofanya mahitaji ya kibinadamu kuongezeka kwa kuzingatia Chad tayari inahifadhi wakimbizi ilhali rasilimali za kuwapatia ni chache.Msafiri kafiri, walinena wahenga! Na katika video hii ya shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, wasafiri hawa, wakitembea kuingia Chad, hawakuwa wamepanga safari, bali imewalazimu kutokana na mapigano nchini mwao Sudan. Kila mmoja na kirago chake kichwani, wakitembea kwa miguu, punda nao wakitumika kubebea mizigo. WFP inasema wakimbizi 20,00 wameingia Chad na kati yao takribani asilimia 70 ni wanawake na watoto wenye  umri wa chini ya miaka mitano, wengi wao wakisaka hifadhi chini ya miti au vibanda chakavu. Miongoni mwao ni  Beské Abdoulaye, mama huyu akiwa kwenye moja ya vibanda chakavu kwenye kijiji hiki cha Koufroun, mpakani na Sudan anasimulia, “Vita imetufurusha majumbani mwetu. Tulikuwa na watoto wetu pindi watu wenye silaha walipofika na hivyo ilibidi tukimbilie kichakani. Hii yawezekana vipi?” Maisha yasiyo na staha yakiendelea katika eneo hili walikofikia wakimbizi, WFP inasema wakimbizi wengine wapya wanawasili karibu na Farchana, mashariki mwa Chad na maeneo mengine ya mpakani. Tathmini ya pamoja ya WFP na wadau imebaini mahitaji ya kipaumbele huku Mkurugenzi Mkazi wa shirika hilo nchini Chad Pierre Honnorat akiwa kwenye bohari wakipakia shehena za misaada anasema, “Sasa tunapakia shehena kwenye malori kwa sababu kw a mujibu wa takwimu za UNHCR na serikali tayrai watu kati ya 10,000 na 20,000 wameingia kutoka Sudan. Ni muhimu sana kwani kabla ya janga hili tayari tulikuwa na wakimbizi 400,000 kutoka Sudan tuliokuwa tunawapatia msaada. Ni muhimu sana kusambaza sasa kwani katika wiki 6 au 8 zijazo hatutaweza kufikia maeneo kutokana na mvua”Msafara wa malori 10  ukiwa na tani za ujazo 340 unaondoka na hatimaye kufika eneo la Adré mashariki mwa Chad, ambako wakimbizi wanapokea mgao wao wa chakula kama vile maharage. WFP inasema ili kuweza kuendelea kusaidia wakimbizi wapya wanaoingia, jamii zinazowahifadhi na wakimbizi 470,000 walioko tayari Chad, na jamii zilizo hatarini, inahitaji dola milioni 162.4. Iwapo haitopata fedha zaidi, usaidizi kwa makundi hayo utakoma ifikapo mwezi ujao wa Mei. 

Habari za UN
Mashirika yashirikiana kusambaza chakula Sudan

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 28, 2023 0:02


Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR nchini Sudan limesema linaendelea kufanya kazi kwa karibu na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, WFP ili kuona ni kwa vipi chakula kilichomo nchini humo kinawza kusambazwa kwa wahitaji na wakati huo huo misaada mingine inaweza kutolewa kwa ushirikiano na wadau wengine wakati huu ambapo uhasama unashamiri na kuathiri raia wakiwemo wakimbizi, wakimbizi wa ndani na raia nchini kote.Sauti hiyo ya Axel Bisshop, Mwakilishi wa UNHCR nchini Sudan akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi kwa njia ya video kutoka mji wa Port Sudan nchini Sudan akisema changamoto kubwa sasa ni kuhakikisha ni vipi mgao wa chakula utaendelea. Anasema wamewasiliana na WFP na leo asubuhi wamekuwa na  mazungumzo na WFP ambao wamewahakikishia kuwa watasalia na UNHCR ili kuendelea kugawa chakula maeneo ambayo bado yanafikika. Miongoni mwa changamoto wanazokumbana nazo ni kwamba wanashindwa kupata taarifa au kupatia taarifa jamii za wakimbizi katika baadhi ya maeneo. Hata hivyo amesema ofisi za UNHCR zimeendelea kuwa na mawasiliano na viongozi wa jamii za wakimbizi na wajumbe wa kamati za wakimbizi na kwamba wanawapatia ushauri nasaha na usaidizi kwa kadri inavyowezekana. Bwana Bisshop amesema wamepokea ripoti ya kwamba takribani wakimbizi 33,000 wamekimbia mji mkuu Khartoum kusaka hifadhi kwenye kambi za wakimbizi kwenye majimbo ya White Nile, ilhali wakimbizi 2,000 kambi zilizoko Gedaref na wengine 5,000 wamesaka hifadhi huko Kassala tangu mapigano yaanze tarehe 15 mwezi huu wa Aprili. Mwakilishi huyo wa UNHCR Sudan anasema “tuna hofu pia ya kwamba kasi ya mapigano inaweza kuongezeka na tunaweza kuwa na hali ambayo itarudia mazingira ambayo tulikuwa nayo miaka iliyopita.” Hata hivyo amesisitiza kuwa UNHCR itasalia nchini Sudan kulinda wakimbizi kutoka nje ya nchi hiyo, wakimbizi wa ndani na raia wanaohifadhi wakimbizi huku akitoa wito kwa pande kwenye mapigano kusitisha  uhasama ili huduma za usaidizi wa kibinadamu ziweze kufikia wahitaji.