POPULARITY
Categories
Learn a new phrase and make your English sound more natural and interesting. Words We Use is a bilingual series that helps you understand idioms like 'Keep your eye on the ball'. - Jifunze msemo mpya na fanya Kiingereza chako kisikike cha asili na cha kuvutia zaidi. Words we Use ni makala ya lugha mbili, yatakayo kusaidia kuelewa nahau kama vile 'Keep your eye on the ball' (Kuwa makini).
Je, umewahi ona bendera ya rangi nyekundu, nyeusi na njano ikiwa pamoja na bendera ya Australia? Hii ni bendera yawa Aboriginal.
Nairobi ni mwenyeji wa msitu mkubwa wa mvua ulio salama ndani ya mipaka yake: Hifadhi ya Karura yenye ukubwa wa hekari 1,000 ni mapafu muhimu ya mji mkuu wa Kenya, katika kuchuja uchafuzi wa mazingira kwa mamilioni. Ilikuwa ishara ya ukosefu wa usalama, sasa ni mfano mkuu wa kimataifa wa uhifadhi unaoongozwa na jamii haswa shirika la marafiki wa Karura maarufu Friends of Karura. Hata hivyo, msitu wa Karura unakabiliwa na changamoto za kina za kiikolojia. Miti ya kigeni inayokua haraka, uchafuzi wa mazingira wa mijini, magugu vamizi, na kuingiliwa kwa minajili ya upanuzi wa barabara na ujenzi wa miundombinu. Ili kukabiliana na hili, juhudi kubwa za urejesho zinaendelea. Mpango wa utaratibu wa asilimia 60 unaendelea ili kubadilisha miti isiyo ya asili na spishi za urithi katika kurejesha udongo na bioanuwai. Urejeshaji huu unaoendelea hutumika kama mwongozo wa jinsi miji ya kisasa inaweza kurekebisha urithi wao wa asili.
Taratibu hizo za pamoja yatahakikisha kuwa nchi za Afrika zinaweka bajeti kwenye sera ya uchumi na kuipa kipau mbele ufadhili wa afya
Waziri wa Fedha Jim Chalmers ame ongeza mashambulizi ya chama cha Labor dhidi ya hotuba ya majibu ya bajeti ya Angus Taylor, akimshtumu kiongozi huyo wa Upinzani kwa kutoa pendekezo lenye madeni, upungufu wa kifedha, na utengano.
Je Akili mnemba AI inaweza kuchukua ajira yako? Ingawa kila uchwao AI inaandika upya sheria za kazi, ubunifu na kubadili vile tunavyoishi lakini kuna kazi moja ambayo bado watu wanasema hiyo ni ya watu maalum sana na kwamba AI haiwezi kuichukua. Hapo jana jumapili tarehe 10 Mei dunia iliadhimisha siku ya wakina mama duniani, shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya Uzazi UNFPA lilitembelea viunga vya New York Marekani na kuzungumza na wanawake. Tuungane na Leah Mushi kusikia wamesema nini kuhusu AI.
Karibu usikilize Kipindi cha Maswali ya Husuyo Imani. Mwezeshaji ni Frateri Samson Tibianus, kutoka Seminari Kuu ya Mtakatifu Augustino Peramiho, Jimbo Kuu Katoliki Songea. Mada ni JE! NI KWELI KUWA SALA YA BABA YETU TUNAYOSALI WAKATOLIKI IPO KATIKA BIBLIA TAKATIFU? Tarehe 26 Februari 2026 L'articolo JE! NI KWELI KUWA SALA YA BABA YETU TUNAYOSALI WAKATOLIKI IPO KATIKA BIBLIA TAKATIFU? proviene da Radio Maria.
Imethibitishwa kuwa abiria mwingine aliyekuwa kwenye meli ya kitalii iliyohusishwa na mlipuko wa ugonjwa wa virusi vya Hanta au Hantavirus ameambukizwa ugonjwa huo, ugonjwa ambao tayari umeua watu watatu waliokuwa ndani ya meli na kusababisha tahadhari ya kimataifa iliyoratibiwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) la Umoja wa Mataifa. Assumpta Massoi na taarifa zaidi.
Each year Australians gather on ANZAC Day to remember those who served in wars, conflicts and peacekeeping missions. But whose stories are we remembering? Are there stories we don't always hear? In this episode we explore an important part of Australia's history that has often been overlooked—the service of Aboriginal and Torres Strait Islander peoples. - Maalinta la yiraahdo, ANZAC Day waa mid ka mid ah maalmaha qaranka ee ugu muhiimsan Australia. Sannad kasta, dadku waxay isugu soo baxaan inay xusuustaan kuwii u soo adeegay dalkan, xilliyadii dagaallada iyo hawlgallada nabad-ilaalinta.
Karibu usikilize Kipindi cha Elimu Jamii kuhusu “Kampeni ya Fursa Sana” inayoratibiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ili uizfahamu fursa zinazopatikana kwenye mitandao ya kijamii. Wawezeshaji wa Kipindi hiki ni Afisa Mawasiliano Mwandamizi kutoka TCRA Bi. Herieth Shija pamoja na Mhandisi Mohamed Bokko pia kutoka TCRA. Mtangazaji ni Agatha Kisimba. L'articolo UNAJUA KUWA MITANDAO YA KIJAMII NI FURSA YA AJIRA..? proviene da Radio Maria.
Uchaguzi Mkuu nchini Kenya ni mwezi Agosti mwaka 2027, lakini wanasiasa mbalimbali wameanza kuonesha nia ya kugombea kiti cha urais. Miongoni mwao ni Ruben Kigame, mwanasiasa, mwanaharakati, mhadhiri, mwandishi wa Habari na mwanamuziki maarufu wa nyimbo za Injili. Yeye ni mlemavu wa Macho, ameamua kujitosa uwanjani, kutafuta uongozi wa nchi ya Kenya. Nini kimemsukuma ? Wiki hii anazungumza na mwenzangu, Benson Wakoli.
Elimu imeanza kung'aa tena kwa watoto katika kijiji cha Twabagondozi, ambapo njaa iliyokuwa kikwazo kikubwa cha masomo sasa inapungua kupitia mpango wa lishe na malezi bora unaoungwa mkono na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF Tanzania kwa ufadhili wa Serikali ya Japan. Kupitia juhudi hizi, watoto kama Magdalena A. Prosper wamepata nafasi ya kurejea darasani, kujifunza na hata kuwa viongozi shuleni. Feissal kirwa anasimulia.
Ni dhahiri hivi sasa watu wengi zaidi wanatumia mitandao ya kijamii katika shughuli mbalimbali na pia kupata taarifa, na kwakuzingatia ukweli huo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, likishirikiana na Umoja wa wamiliki vya vyombo vya habari vya mtandaoni (Wanablogu) nchini Kenya, BAKE (inatamkwa ‘BEKI'), limeandaa mafunzo maalum jijini Nairobi yaliyopewa jina la "Social Media 4 Peace" yaani mitandao ya kijamii kwa amani. Rashid Malekela anaeleza zaidi.
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye Kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “AWALI KUWA HERI SI AJABU”
Kwa mara ya kwanza katika historia ya Australia, mwanamke ameteuliwa kuwa mkuu wa jeshi la Australia. Waziri Mkuu alitangaza uteuzi wa Luteni Jenerali Susan Coyle mjini Canberra.
Wakati hii leo dunia ikiadhimisha siku ya Kimataifa ya kutozalisha taka, Umoja wa Mataifa umetoa wito kwa kila mtu kujifunza upya yamna ya kufanya manunuzi ya vitu na mapishi ambayo hayatasababisha umwagaji wa chakula ili kunusuru mifumo ya ikolojia na afya ya binadamu. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.
Vita vya Mashariki ya Kati vimeingia mwezi wa pili huku ghasia zikiongezeka katika maeneo kadhaa, ikiwemo Lebanon, Iran na Ghuba. Mlinzi wa amani wa Kikosi cha Mpito cha Umoja wa Mataifa nchini Lebanon UNIFIL ameuawa baada ya kombora kulipuka katika kituo cha Umoja wa Mataifa karibu na Adchit Al Qusayr, huku mwingine akiwa mahtuti hospitali. Flora Nducha na Taarifa zaidi
Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) linaonya kuwa kuongezeka kwa mgogoro katika Ghuba ya Uajemi au Mashariki ya Kati kunahatarisha mifumo ya chakula duniani, likitaja kupanda kwa gharama za nishati, mbolea na uzalishaji wa chakula kama athari kuu. Flora Nducha anafafanua zaidi katika taarifa hii
Madhara ya vita vya Israel na Marekani dhidi ya Iran, yame anza kushuhudiwa nchini Australia.
Sannadkii 2025, gobolka New South Wales oo qura waxaa laga diiwaangeliyey tiradii ugu badnayd ee ah, haween loo dilay sababo la xiriira tacaddiyada qoyska. Maxaa laga qaban karaa?
Ripoti ya kwanza ya kitaifa kuhusu ubaguzi wa rangi katika vyuo vikuu nchini Australia imegundua kuwa ni tatizo lililo enea na la kimfumo.
Demokrasia na utaratibu wa kimataifa unaozingatia sheria ziko hatarini, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya Shirika la haki za binadamu ama Human Rights Watch. Kuna msisitizo mahususi juu ya Marekani na kile ambacho chombo cha kimataifa kinaelezea kama kudorora kwa haki za binadamu, lakini pia kuna tahadhari juu ya Australia. Sera za uhamiaji na kuwekwa kizuizini kwa vijana za Australia zinaorodheshwa kama 'mapungufu makubwa', zikionyeshwa kuwa ni demokrasia pekee ya Magharibi isiyo na sheria ya kitaifa ya haki za binadamu.
Wakati nchi ya Uganda ikijiandaa na uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 15 mwezi huu wa Januari, wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa hii leo wametoa taarifa ikionya kwamba hali ya haki za binadamu nchini Uganda si rafiki kwa uchaguzi wa amani. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.
Katika wiki za hivi karibuni, moto wa nyika umesababisha uharibifu wa nyumba na mali katika maeneo ya pwani ya katikati ya kaskazini ya New South Wales, Geraldton huko Magharibi mwa Australia na mashariki mwa Tasmania. Wataalamu wanaonya kuwa huu ni mwanzo tu wa msimu wa moto na nyinyi ambao mnasafiri kwa ajili ya likizo mnahitaji kuwa na ufahamu na maandalizi mkiwa mbali na nyumbani.
Nchini Australia, karibu tani milioni 7.6 za chakula zinapotezwa kila mwaka. Mwanzilishi mmoja wa kike ameunda suluhisho ndani ya sanduku.Linapokuja suala la usafi wa taka za chakula hatahivo, mwanzilishi wa kampuni ya kuanzisha Olympia Yarger [[Yar-gah]] ana fahari ya kuwa ametengeneza mfumo wa kiteknolojia unaoweza kubadilisha taka kuwa bidhaa zinazoweza kutumika – kwa kutumia wadudu.
Jamii ya watu wa Sudan walio nchini Australia wana wasiwasi mkubwa ,wakisubiri habari kutoka kwa familia zao walionaswa katika jiji la Al-Fasher baada ya mlipuko wa ghasia. Jiji hilo lilitekwa na Rapid Support Forces wiki mbili iliyopita, na wataalamu wanaamini kwamba maelfu huenda wameuawa katika mauaji ya kutisha. Kwa kuwa huduma za intaneti na simu zimekatwa, wanaoishi nje ya nchi wanalazimika kukaa na kusubiri ili kujua kama wapendwa wao bado wako hai.
Ikinamico Urunana. Buri Wa kabiri n'uwakane.
Amakuru y'imonota 30 mutegurirwa na BBC Gahuzamiryango.
Amakuru y'imonota 30 mutegurirwa na BBC Gahuzamiryango.
Ikinamico Urunana. Buri Wa kabiri n'uwakane.
Amakuru y'imonota 30 mutegurirwa na BBC Gahuzamiryango.
Amakuru y'imonota 30 mutegurirwa na BBC Gahuzamiryango.
Umoja wa Mataifa umeonya kuwa hali ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza imefikia hatua ya kutisha, huku hospitali zikigeuzwa kuwa uwanja wa mapambano, kukizidiwa na wagonjwa na misaada kukwama. Maafisa wa Umoja wa Mataifa wameaambia waandishi wa habari leo mjini Geneva kuwa kuwa watoto wanakosa hewa ya oksijeni, wagonjwa wanakufa kwenye meza za upasuaji, na risasi zinavurumishwa moja kwa moja ndani ya hospitali. Flora Nducha amefuatilia na hii hapa taarifa yake
Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukiwa umeingia katika siku yake ya nne hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani leo Ijumaa, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amekuwa wa kwanza kuzungumza akitumia muda wake mwingi kushambulia wanamgambowa kipalestina, Hamas na kutetea kila uamuzi wa Israel. Anold Kayanda ameifuatilia hotuba hiyo kwa kina. Ilikuwa majira ya saa tatu na dakika chache hivi asubuhi ya leo saa za New York nchini Marekani ambapo Waziri Mkuu wa Isreal Benjamin Netanyahu amepewa fursa ya kuhutubia na ndipo ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukakosa utulivu. Wajumbe kwa makundi walinyanyuka katika viti vyao na kuondoka huku wakiwaacha maafisa wa Israel wakimpigia makofi kiongozi wao na pia nchi zinazoiunga mkono Israel zikasalia katika viti vyao ikiwemo Marekani.Baadhi ya wajumbe watoka njeKatika eneo la walipotakiwa kukaa wawakilishi wa Palestina kulikuwa wazi, huku katika eneo la Iran ikibakia picha iliyokusanya sura za baadhi ya watu wao waliouawa na mashambulizi ya Israel. Bwana Netanyahu kwa mara nyingine tena ameingia na ubao wenye picha ya ramani ya eneo la Mashariki ya Kati akiutumia kuishambulia Iran na kwa kutumia kalamu akiweka alama ya vema kuonesha namna ambavyo Israel imefanikiwa kupambana na ngome za Irani katika ukanda huo. Katika suti yake, kifuani upande wa kulia, Bwana Netanyahu pia ameweka kibandiko chenye QR Code na akawaambia watu kuwa Israel bado inakumbuka tukio walilofanyiwa na Hamas mwezi Oktoba mwaka juzi na kwamba ikiwa watu wamesahau hilo basi waelekeze simu zao kwenye QR Code hiyo kwenye nguo yake ili iwaoneshe madhara yaliyofanywa na Hamas.Majina ya mateka yakasomwaWaziri Mkuu huyo wa Israel ameyasoma majina ya mateka ambao bado wako mikononi mwa Hamas katika eneo la Ukanda wa Gaza na pia akaueleza mkutano kuwa amesambaza vipaza sauti au spika katika eneo lote la Gaza ili anapoongea leo, azungumze moja kwa moja na mateka huko walikofichwa. Na hapo akabadilisha lugha na kuongea kwa kihebrania akiwaahidi kuwa atawakomboa. Vilevile amedokeza kuwa kwa namna ya kiintelijensia Israel imefanya simu leo ziweze kusambaza hotuba katika ukanda wa Gaza na hivyo akautumia muda huo kupeleka ujumbe mkali kwa Hamas kuwa ataendelea kuwadhibiti. Bwana Netanyahu pia ameingia ukumbini na vibao viwili vyenye maswali na majibu ya kuchagua japokuwa jibu sahihi kwa mujibu wake na waliojibu kuwa ni All the Above, yaani majibu yote ni sahihi. Maswali yote yalikuwa yakiwatuhumu Iran, Hamas, Al Caeda, Hezbollah na Houthi kuwa pia wanaitakia kifo Marekani na wameua watu wengi Ulaya. Huenda hotuba hii ya Netanyahu ikaingia katika orodha ya hotuba tano ndefu zaidi baada ya ile ya Rais wa Marekani Donald Trump wa Marekani, Ya Mahmoud Abbass wa Palestina na Félix-Antoine Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambao wote hao walitumia zaidi ya dakika arobaini licha ya muda wa hotuba uliopangwa kuwa angalau dakika 15.
Amakuru y'imonota 30 mutegurirwa na BBC Gahuzamiryango.
Amakuru y'imonota 30 mutegurirwa na BBC Gahuzamiryango.
Amakuru yo kuwa mbere 25/8/2025
Kuwa mzazi si rahisi kila wakati, lakini usaidizi unaofaa unaweza kuleta mabadiliko ndio maana Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF limekuwa likiendesha mafunzo kwa wazazi juu ya namna bora za kulea watoto. Alinune Nsemwa ambaye ni mtaalamu wa masuala ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kutoka UNICEF nchini Tanzania ameeleza vidokezo vitatu muhimu vya kuwalea watoto ambavyo vinaweza kuleta utofauti mkubwa.
Jaridani leo tunaangazia mkataba wa Kimataifa wenye nguvu kisheria kuhusu uchafuzi wa plastiki, na vidokezo vya malezi salama ya watoto. Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani nchini Chad, kulikoni?Siku 10 za mkutano wa Kamati ya Kimataifa ya Majadiliano (INC) ya kuandaa Mkataba wa Kimataifa wenye nguvu kisheria kuhusu uchafuzi wa plastiki, ikiwemo katika mazingira ya bahari, zimemalizika huko Geneva, Uswisi bila muafaka kwenye nyaraka tarajiwa, ambapo mkutano umeahirishwa hadi tarehe itakayotangazwa baadaye.Kuwa mzazi si rahisi kila wakati, lakini usaidizi unaofaa unaweza kuleta mabadiliko ndio maana Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF limekuwa likiendesha mafunzo kwa wazazi juu ya namna bora za kulea watoto. Alinune Nsemwa ambaye ni mtaalamu wa masuala ya malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kutoka UNICEF nchini Tanzania ameeleza vidokezo vitatu muhimu vya kuwalea watoto ambavyo vinaweza kuleta utofauti mkubwa.Makala ninakukutanisha na Sawiche Wamunza Mtaalamu wa Mawasiliano ya Kimkakati wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP nchini Tanzania ambaye baada ya mafunzo ya siku tatu ya uchumi rejeleshi katika mkoa wa Mtwara, Kusini-Mashariki mwa Tanzania alizungumza na Godlove Makunge Muasisi na Mkurugenzi wa kampuni ya kuzoa taka na usafi wa mazingira, iitwayo Shikamana Investment. Bwana Makunge anaanza kwa kuelezea mtazamo wa jamii kwake baada ya kuamua kuanza kuzoa taka.Na katika Radwa Ahmed, Mkimbizi kutoka Sudan ambaye alianza kwa kuoka mikate kwa ajili ya familia yake, na kwa ufadhili wa shirika la Umoja wakimbizi Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, ameweza kuigeuza talanta yake kuwa biashara ya kuuza mikate na kuajiri wakimbizi wenzake.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Wakati dunia ikiendelea kugubikwa na changamoto mbalimbali ikiwemo athari za mabadiliko ya tabianchi na hali mbaya za kiuchumi, vijana wamepaza sauti kueleza wasiwasi wao wa kuwa na Watoto siku za usoni. Tuungane na Leah Mushi katika Makala hii aliyotuandalia kutoka kwenye video ya shirika la Umoja wa Mataifa la afya ya uzazi na idadi ya watu UNFPA ambayo iliwahoji vijana kutaka kufahamu iwapo wangependa kuwa na Watoto kwa siku za usoni.
Amakuru y'imonota 30 mutegurirwa na BBC Gahuzamiryango.
Ikinamico Urunana. Buri Wa kabiri n'uwakane.
Amakuru y'imonota 30 mutegurirwa na BBC Gahuzamiryango.
Amakuru y'imonota 30 mutegurirwa na BBC Gahuzamiryango.
Ikinamico Urunana. Buri Wa kabiri n'uwakane.
Umoja wa Mataifa kwa kutambua nafasi ya urafiki katika kujenga amani, utulivu na kusongesha maendeleo kuanzia ngazi ya mtu mmoja mmoja hadi ngazi ya mataifa, mwaka 2011 kupitia Baraza lake Kuu, ulitenga Julai 30 kuwa siku ya urafiki duniani. Umoja wa Mataifa unasema katika wakati ambapo kelele za mgawanyiko zinazidi kuwa kubwa — zikiendeshwa na vita, migogoro, ukosefu wa usawa, na hofu — urafiki unaonekana kuwa wa kishujaa kutokana na unyenyekevu wake. Urafiki huanza na kitu cha utulivu zaidi: mazungumzo, wakati wa pamoja, utayari wa kuonana si kama wageni bali kama wasafiri wenza katika safari ya utu. Je huko Kenya, mkazi mmoja wa Kaunti ya Kajiado, urafiki kwake ni nini? Kelvin Keitany wa Redio washirika Radio Domus amefunga safari na kutuandalia makala hii.
Ikinamico Urunana. Buri Wa kabiri n'uwakane.
Ikinamico Urunana. Buri Wa kabiri n'uwakane.
Ikinamico Urunana. Buri Wa kabiri n'uwakane.