Podcasts about vijana

  • 49PODCASTS
  • 647EPISODES
  • 20mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • May 23, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about vijana

Latest podcast episodes about vijana

Habari za UN
Vijana Kenya watumia mpira wa miguu kutokomeza umasikini na kuishi maisha bora - Peter Omondi

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 23, 2025 3:06


Katika kuelekea siku ya kandanda, kabumbu au mpira wa miguu duniani itakayoadhimishwa Jumapili wiki hii Mei 25 ikibeba maudhui nguvu ya kdandanda katika kuleta mabadiliko tuabisha hodi Nairobi Kenya ambapo leo Peter Omondi, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Global Youth Forum linalounganisha vijana Kenya kwa lengo la kutokomeza umasikini na kuishi maisha bora kupitia michezo mbalimbali ikiwemo kandanda akizungumza na Idhaa hii ya Kiswahili anaeleza umuhimu wa kandanda katika ajenda ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu. Anaanza kwa kujitambusha.

Jukwaa la Michezo
AFCON U20: Michuano ya vijana ya soka yang'oa nanga nchini Misri

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later May 3, 2025 23:53


Hii leo tumeangazia michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya vijana chini ya miaka 20 kuanza nchini Misri, mkondo wa mtoano katika msururu wa raga duniani, diamond league mkondo wa pili huko Uchina na Ligi ya Basketboli mkondo wa Sahara ukiendelea, Cecafa yapata rais mpya, nembo ya Visit Rwanda yaendelea kupanuka, bondia wa DRC Martin Bakole kupigana leo usiku, PSG, Man Utd, Spurs na Chelsea zavuna matokeo mazuri kwenye nusu fainali ligi za vilabu bingwa ulaya.

Habari za UN
29 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 29, 2025 11:44


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka katika mkoa wa Mwanza kaskazini magharibi mwa Tanzania ambapo vijana wameshika hatamu kuboresha mustakabali wao. Pia tunakuletea muhtasari wa habari  na mashinani tunasalia hapa makao makuu.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kudumisha Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, MONUSCO, umeikaribisha kusainiwa kwa “Azimio la Kanuni” tarehe 25 Aprili 2025 mjini Washington, D.C chini ya usimamizi wa Wizara ya mambo ya nje ya Marekani, kati ya serikali za DRC na Rwanda kwa lengo la kulinda rai ana kutekeleza azimio la Baraza la Usalama namba 2773 (2025).Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA, Juliette Touma, akizungumza na waandishi wa habri mjini Geneva kwa njia ya video kutoka mji mkuu wa Jordan, Amman, wakati  kuzingirwa kwa Ukanda wa Gaza kukikaribia kuingia mwezi wa pili amesema “Mzingiro wa Gaza ni muuaji wa kimya muuaji wa watoto, wazee, na watu walioko katika mazingira magumu zaidi. Mzingiro huu unamaanisha kwamba familia nzima, watu saba au wanane wanalazimika kushirikiana kopo moja la maharagwe au njegere”.Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO limezitaka nchi za Kaskazini Magharibi mwa Afrika kuongeza ufuatiliaji na kuchukua hatua za mapema kudhibiti makundi ya nzige wa jangwani. Hii ni baada ya nzige wakubwa na makundi madogo kutoka ukanda wa Sahel kuhamia maeneo ya kusini mwa Sahara, hasa katikati ya Algeria, magharibi mwa Libya, na kusini mwa Tunisia tangu Februari hadi Machi mwaka huu.Na katika mashinani fursa ni yake Maruping Onkemetse Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kituo cha Msaada wa Familia, shirika linaloongozwa na wanawake wa asili  katika Wilaya ya Gantsi, kijiji cha Chobokwane nchini Botswana anayeshiriki mkutano unaoendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa wa Jukwaa la Watu wa Asili akizungumzia alichojifunza hadi sasa.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Jamii inapaswa kusikiliza na kujifunza kutoka kwa vijana

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2025 3:42


Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) linafanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani ambapo limeanza tarehe 15 Aprili na linatarajiwa kukamilika tarehe 17 Aprili 2025. Vijana kutoka nchi mbalimbali pamoja na wadau wengine wa masuala ya maendeleo na Uchumi wanakuja pamoja kujadili changamoto mbalimbali na namna bora ya kupatia ufumbuzi katika kuubadilisha ulimwengu kuwa mahali penye usawa zaidi na endelevu chini ya mwongozo wa Ajenda ya mwaka 2030 na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).  Miongoni mwa wanaohudhuria jukwaa hilo ni Kapwani Kavenuke kutoka nchini Tanzania ambaye amefanyiwa mahojiano na Leah Mushi na hapa anaanza kwa kueleza umuhimu wa mikutano huo.

Habari za UN
16 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2025 9:57


Hii leo jaridani Assumpta Massoi anamulika masuala ya afya hususan harakati za kukabiliana na majanga yajayo ya afya;  wakimbizi huko Zambia ambako sera jumuishi zimewajengea uwezo; Jukwaa la vijana na mchango wa sanaa kwenye usawa na utengamano. Baada ya zaidi ya miaka mitatu ya mazungumzo ya kina, hatimaye leo huko mjini Geneva, Uswisi, nchi wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) zimekamilisha rasimu ya makubaliano ambayo itawasilishwa katika Mkutano wa Afya Duniani mwezi ujao wa Mei. Pendekezo hili linakusudia kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na vitisho vya majanga ya kiafya yajayo. Anold Kayanda amefuatilia anatujulisha zaidi.Zambia inaendelea kuwahifadhi zaidi ya wakimbizi 106,000, wengi wao wakiwa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Burundi, pamoja na wakimbizi wa zamani kutoka Rwanda na Angola. Limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, likiongeza kwamba kwa kuzingatia sera jumuishi ya Zambia, taifa hilo linakuza mshikamano na wakimbizi na kuwawezesha kujitegemea kupitia makazi maalum na ushirikiano na jamii za wenyeji. Flora Nducha na taarifa zaidi.Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) limeanza jana hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa na litamalizika kesho tarehe 17 Aprili. Vijana kutoka nchi mbalimbali wamehudhuria jukwaa hilo akiwemo Kapwani Kavenuke kutoka nchini Tanzania ambaye amehojiwa na Leah Mushi wa Idhaa hii. Kapwani anaanza kwa kueleza  umuhimu wa mikutano hii.Gislain Kalwira, Muandaaji wa tamasha la Musika na Kipaji  nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC linalofanyika kila mwaka kuleta pamoja wasanii wa kike na wa kiume wa fani mbalimbali, kwa kutambua kuwa jana dunia imeadhimisha siku ya sanaa duniani. Kalwira kupitia video iliyochapishwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani  nchini DRC, MONUSCO, anafafanua mantiki ya tamasha hilo na kujenga usawa kijinsia.

Habari za UN
15 Aprili 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 15, 2025 9:59


Karibu kusikiliza jarida la Umoja wa Mataifa ambapo hii leo tunamulika Kongamano la Kimataifa la Kiswahili linalofanyika mjini Kampala Uganda likiwaleta pamoja wadau kutoka kila kona ya Afrika na kwingineko kujadili mikakati ya kukuza lugha hiyo adhimu ya Kiswahili. Utasikiliza muhtasari wa habari ukiangazia miaka miwili tangu kuanza kwa vita vya sasa vya Sudan, UNHCR, yatoa wito kwamba mwitiko mkubwa wa kibinadamu ulioratibiwa vema ni muhimu ili kuzuia mateso zaidi na vifo kwa wananchi wa DRC, na Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) limeanza leo tarehe 15 hadi tarehe 17 katika Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. 

Habari za UN
11 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 11, 2025 9:57


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya watoto nchini DR Congo, na masuala y awanawake nchini Tanzania. Makala inatupeleka nchini Kenya kuangazia harakati za vijana za kusongesha Ajenda2030, na mashinani tunasalia huko huko kumulika misaada kwa wakimbizi.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF limeripoti kwamba huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kila nusu saa takribani mtoto mmoja anaripotiwa kubakwa huku ghasia zikiendelea katikati ya janga linalozidi kukua la ufadhili finyu wa kifedha.Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake UN WOMEN nchini Tanzania chini ya ufadhili kutoka Muungano wa Ulaya wanashirikiana na jeshi la polisi kuendesha mradi huko visiwani Zanzibar wa kukomesha unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana na tayari manufaa ya mradi huo yameanza kuonekana.Makala leo inatupeleka Nairobi Kenya kwa Stella Vuzo kutoka kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIS Nairobi akizungumza na Winifred Njiru mwanafunzi wa chuo kikuu fani ya uhakiki au quantity surveyor aliyeshiriki majadiliano ya wiki iliyopita kuhusu malengo ya maendeleo endelevu yaliyoandaliwa na Club De Madri, anaeleza nini kama kijana anapaswa kufanya      kuchangia ajenda hiyo ya maendeleo.Na katika mashinani Cindy McCain, Mkurugenzi Mtendaji wa WFP, akizungumza kutoka kituo cha shirika hilo kilichopo Mombasa, Kenya anaeleza juhudi wanazofanya kuwasaidia wakimbizi wa Sudan na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC."Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
Vijana tuna jukumu muhimu katika maendeleo ya jamii zetu tuchangamkie fursa: Winfred Njiru

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 11, 2025 3:26


Umoja wa Mataifa unaendelea kuchagiza vijana kujitokeza na kushiriki katika kusongesha ajenda ya maendeleo endelevu katika jamii zao na ndio maana wiki iliyopita majadiliano ya viongozi wastaafu kuhusu maendeleo endelevu ya Club De Madrid yaliyofanyika Nairobi Kenya yalitoa fursa kwa vijana kupaza sauti zao kuhusu jinsi wataavyochangia kufanikisha malengo hayo.  Winfred Njiru mwanafunzi wa chuo kikuu fani ya uhakiki au quantity surveyor alizungumza na Stella Vuzo kutoka kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIS Nairobi na kumueleza matahali Kenya vijana wanapaswa kufanya nini ili kuchangia katika maendeleo.

SBS Swahili - SBS Swahili
Sean MMG "mitandao yaki jamii imefanya iwe rahisi kwa vijana kama sisi kutokea katika muziki"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 10, 2025 7:38


Wasanii maarufu kutoka Kenya; Sean MMG, Ssaru na Tipsy Gee walitembelea studio yet hivi karibuni wakati wa ziara yao ya Australia.

Habari za UN
Uongozi bora na matumizi bora ya rasilimali vitaikomboa Afrika kimaendeleo: Vijana Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 4, 2025 3:22


Majadiliano ya siku mbili yanayofanyika kila mwaka ya será kuhusu maendeleo endelevu. Majadiliano hayo yanayokunja jamvi leo jijini Nairobi Kenya yameandaliwa na Club De Madrid na mwaka huu yakijikita na ufadhili wa maendeleo na kuwaleta pamoja wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wastaafu w anchi na serikali, wadau wa maendeleo na vijana. Stella Vuzo kutoka kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIS Nairobi amepata fursa ya kuzungumza na baadhi ya vijana wanaoshiriki mkutano huo wa club de Madrid je wanasemaje? Ungana nao katika makala hii

Gurudumu la Uchumi
Sehemu ya Pili: Uchakataji taka za plastiki kwa vijana

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Apr 2, 2025 10:09


Msikilizaji takwimu zinaonesha kuwa, ifikapo mwaka 2050, idadi ya watu barani Afrika itaongezeka kufikia bilioni 2.5, ambapo zaidi ya nusu ya watu hawa watakuwa ni vijana walio na umri wa chini ya 25. Hata hivyo Ujasiriamali wa vijana unaonekana kama suluhisho linalowezekana kwa changamoto hii. Msikilizaji juma hili nimebahatika kuwa na mgeni studioni nae si mwingine bali ni Kenneth Ochien'g, ambaye yeyé anajihusisha na uchakataji upya wa taka za plastiki kwa matumizi mengine.

Gurudumu la Uchumi
Sehemu ya Pili: Uchakataji taka za plastiki kwa vijana

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Apr 2, 2025 10:09


Msikilizaji takwimu zinaonesha kuwa, ifikapo mwaka 2050, idadi ya watu barani Afrika itaongezeka kufikia bilioni 2.5, ambapo zaidi ya nusu ya watu hawa watakuwa ni vijana walio na umri wa chini ya 25. Hata hivyo Ujasiriamali wa vijana unaonekana kama suluhisho linalowezekana kwa changamoto hii. Msikilizaji juma hili nimebahatika kuwa na mgeni studioni nae si mwingine bali ni Kenneth Ochien'g, ambaye yeyé anajihusisha na uchakataji upya wa taka za plastiki kwa matumizi mengine.

Gurudumu la Uchumi
Sehemu ya Kwanza: Uchakataji taka za plastiki kwa vijana

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Mar 26, 2025 10:01


Msikilizaji takwimu zinaonesha kuwa, ifikapo mwaka 2050, idadi ya watu barani Afrika itaongezeka kufikia bilioni 2.5, ambapo zaidi ya nusu ya watu hawa watakuwa ni vijana walio na umri wa chini ya 25. Hata hivyo Ujasiriamali wa vijana unaonekana kama suluhisho linalowezekana kwa changamoto hii. Msikilizaji juma hili nimebahatika kuwa na mgeni studioni nae si mwingine bali ni Kenneth Ochien'g, ambaye yeyé anajihusisha na uchakataji upya wa taka za plastiki kwa matumizi mengine.

Gurudumu la Uchumi
Sehemu ya Kwanza: Uchakataji taka za plastiki kwa vijana

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Mar 26, 2025 10:01


Msikilizaji takwimu zinaonesha kuwa, ifikapo mwaka 2050, idadi ya watu barani Afrika itaongezeka kufikia bilioni 2.5, ambapo zaidi ya nusu ya watu hawa watakuwa ni vijana walio na umri wa chini ya 25. Hata hivyo Ujasiriamali wa vijana unaonekana kama suluhisho linalowezekana kwa changamoto hii. Msikilizaji juma hili nimebahatika kuwa na mgeni studioni nae si mwingine bali ni Kenneth Ochien'g, ambaye yeyé anajihusisha na uchakataji upya wa taka za plastiki kwa matumizi mengine.

Habari za UN
IFAD yawaepusha vijana wa kike 5 na kazi za ndani na kuwajengea stadi za kilimo biashara Senegal

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 21, 2025 2:18


Tukiwa bado ndani ya mwezi wa Machi, unaotambuliwa kuwa ni mwezi wa wanawake tunakwenda nchini Senegal ambako huko wasichana waliokuwa wakifanya kazi za ndani, wamewezeshwa na Umoja wa Mataifa na sasa ni wakulima na wanatumia stadi za upigaji na utengenezaji video za mtandaoni kuelimisha jamii kuhusu kilimo chenye tija. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

Habari RFI-Ki
Kenya: Vijana wapinga michango ya wanasiasa kanisani

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 11, 2025 9:56


 Shaba yetu leoinalenga nchini Kenya ambapo Vijana wameanza kuandamana kupinga kile wanadai wanasiasa kutoa kiasi kikubwa cha pesa kwenye maeneo ya kuabudu ili hali wao hawana ajira. Tumekuuliza hatua hii ni sahihi?Haya hapa baadhi ya maoni yako.

Habari RFI-Ki
Kenya: Vijana wapinga michango ya wanasiasa kanisani

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 11, 2025 9:56


 Shaba yetu leoinalenga nchini Kenya ambapo Vijana wameanza kuandamana kupinga kile wanadai wanasiasa kutoa kiasi kikubwa cha pesa kwenye maeneo ya kuabudu ili hali wao hawana ajira. Tumekuuliza hatua hii ni sahihi?Haya hapa baadhi ya maoni yako.

VOA Express - Voice of America
Vijana katika eneo la Afrika mashariki wanaelezea changamoto za bei ya vyakula katika mfungo wa mwezi wa Ramadhan. - Machi 10, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 10, 2025 29:59


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

VOA Express - Voice of America
Program ya Kazi Majuu Initiative nchini Kenya inaelezea utaratibu mpya kuwasaidia vijana kupata ajira nje ya nchi bila matatizo. - Machi 06, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 6, 2025 29:59


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

VOA Express - Voice of America
Mkurugenzi wa haki za watoto na vijana Afrika mashariki anasema vijana wanapaswa kujifunza elimu ya vitendo na nadharia kujiandaa kimaisha. - Machi 03, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 29:59


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Jukwaa la Michezo
Misri, Morocco,Tunisia zang'ara mashindano ya tenisi ya vijana chini ya miaka 14

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Mar 2, 2025 23:46


Tuliyokuandalia hii leo ni pâmoja na matokeo ya mashindano ya tenisi ya vijana barani Afrika chini ya miaka 14, kocha mpya wa Kenya ni nani, matokeo ya mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kina dada, timu sita kushiriki ligi ya Afrika ya basketboli kwa mara ya kwanza, huku Afrika Kusini ikijiandaa kutuma ombi rasmi la kuandaa mkondo mmoja wa F1 na Jose Mourinho apata afueni baada ya adhabu yake kupunguzwa.

VOA Express - Voice of America
Vijana nchini Uganda inaripotiwa wanapata shida ya afya ya akili kutokana na wazazi au walezi kukosa muda wa kusikiliza mahitaji yao. - Februari 28, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 28, 2025 29:59


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

VOA Express - Voice of America
Vijana Kenya waeleza juu ya utafiti ulioonyesha matamanio ya wengi kusoma nje ya nchi - Februari 24, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 24, 2025 29:56


Vijana Kenya waeleza juu ya utafiti ulioonyesha matamanio ya wengi kusoma nje ya nchi

VOA Express - Voice of America
Vijana nchini Tanzania wanaelezea changamoto wanazoziona wakati wanapotaka kujihusisha na nafasi za uongozi katika siasa. - Februari 20, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 20, 2025 29:52


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Radio Maria Tanzania
Fahamu Elimu maswala mbalimbali ya Makuzi na Malezi kwa Vijana.

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Feb 19, 2025 45:43


  Ungana nami Martin Joseph, katika kipindi cha Malezi na makuzi ya Vijana, Mwezeshaji ni Bwana,  Yohana Machibya  Msaidizi wa Sheria Mkoa wa Maghalibi Nzanzibar, Jimbo Katoliki Zanzibar, akiendelea kutuelimisha juu ya mbinu za kujitambua kama vijan na akijibu maswali mbalimbali .   L'articolo Fahamu Elimu maswala mbalimbali ya Makuzi na Malezi kwa Vijana. proviene da Radio Maria.

VOA Express - Voice of America
Vijana katika mji wa Bukavu nchini DRC wanaelezea changamoto za ghafla wanazopitia baada ya kundi la M23 kuingia kwenye mji huo. - Februari 17, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 17, 2025 29:58


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

SBS Swahili - SBS Swahili
Rais Tshisekedi awarai vijana wajiunge na jeshi kupambana na M23

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jan 31, 2025 6:44


Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo Felix Tshisekedi, amewarai vijana kujiunga kwa wingi na jeshi la taifa kusaidia kupambana na waasi wa M23 wanaojaribu kukamata maeneo makubwa zaidi mashariki mwa nchi hiyo.

Habari za UN
Serikali patieni vijana taarifa sahihi na stahiki ili watekeleze wajibu wao

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 10, 2025 3:38


Umoja wa Mataifa unaeleza kwamba duniani kote kuna vijana bilioni 1.2 wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 24. Idadi hii ni saw ana asilimia 16 ya wakazi wote wa dunia. Kama hiyo haitoshi, idadi hiyo ya vijana inatarajiwa kufikia bilioni 1.3 ifikapo mwaka 2030, yaani miaka mitano ijayo. Lakini changamoto ni kwamba bado serikali nyingi hazijaweza kutumia wingi wa idadi hii kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs. Kwa hali hiyo baadhi ya vijana wameamua kutumia fursa na kujiongeza ili vijana wenzao waweze kufahamu wanachopaswa kufanya ili SDGs zifanikiwe ifikapo 2030. Miongoni mwao ni Paul Siniga, kijana kutoka Tanzania ambaye mwezi Oktoba mwaka huu alikuweko kwenye makao makuu ya UN jijini New York, Marekani kushiriki vikao vya ngazi ya juu. Assumpta Massoi alitaka kufahamu kwa kina ni hatua zipi alichukua hadi kufika aliko sasa.

Habari za UN
Msichana Bangladesh: Sikufahamu ufundi bomba ni nini, sasa ILO imeniwezesha

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 8, 2025 1:40


Nchini Bangladesh, mradi wa kuimarisha stadi na kufungua fursa za kiuchumi, ISEC miongoni mwa wanawake na vijana, umewezesha wasichana kuvunja mwiko na kuingia kwenye tasnia ambazo zimezoeleka kuwa ni za wanaume, mathalani ufundi bomba. Mradi huo unaolenga wanufaika 24,000 wenye umri kati ya miaka 18 na 35 unatekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani, ILO kwa kushirikiana na serikali ya Bangladesh.Video ya ILO hapa Cox's Bazaar inamleta kwako mmoja wa wanufaika hao ambaye hata hivyo jina lake halikutajwa, akiwa ameshikilia vifaa vya ufundi bomba anasema, awali sikufahamu kuhusu hii kozi hadi nilipofahamu kupitia Idara ya Maendeleo ya Vijana. Hii ni mara ya kwanza fursa hii imetufikia katika shule ya sekondari ya juu ya Moheshkhali. Tunajifunza stadi badala ya kupoteza muda nyumbani itanisaidia maisha yangu ya baadaye.Nikihitimu masomo naungana na kaka kwenye duka lakeAnakiri kuwa kabla ya kushiriki mafunzo haya hakuwa anafahamu kabisa ufundi bomba ni kitu gani. Lakini sasa amejifunza kuhusu vifaa mbalimbali ikiwemo msumeno wa mabomba, spana na kadhalika.ILOMradi wa kuimarisha stadi na kufungua fursa za kiuchumi, ISEC miongoni mwa wanawake na vijana, umewezesha wasichana Cox's Bazaar nchini Bangladesh.Na ndoto yake ni kwamba nikihitimu masomo nitakwenda kuungana na kaka yangu kwenye duka lake linalounza vifaa vya ujenzi. Nataka niwe mjasiriamali kama yeye, nijitegemee na nisaidie familia yangu. Siku hizi kwenye nyingi zilizoendelea na hata hapa Bangladesh wasichana wanafanya aina zote za kazi.Wanaweza kufanya kazi ngumu kama wanaume, nami nataka kuwa hivyo.Video ya ILO inamalizika mnufaika huyu amekamilisha kufunga bomba na sasa maji yanatoka, na mkufunzi anatumia maji hayo kunawa mikono.Malengo namba 4, 5, na 8 ya SDGs yanatekelezwaMradi huu ulizinduliwa mwezi Septemba mwaka 2023 ukifadhiliwa na…

Alfajiri - Voice of America
Vijana watano waliokuwa wametoweka kwa wiki kadhaa nchini Kenya wameachiwa huru - Januari 07, 2025

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 7, 2025 29:59


Habari za UN
Hadithi ya Alaa Khattab: Kutoka kuwa mzalishaji mdogo kijijini kwake hadi kuwa msafirishaji wa Kikanda wa achari

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 23, 2024 2:09


Mradi wa pamoja wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO ujulikanao kama Nabta kwa lugha ya Kiarabu ukimaanisha "mche" ambao lengo lake ni kuwasaidia vijana wajasiriamali kubadili mawazo yao kuwa  biashara ya kilimo yenye mafanikio umeleta nuru kwa Alaa Khattab kijana aliyekuwa na ndoto ya kuwa mfanyabiashara wa kilimo nchini Syria. Flora Nducha anatujuza zaidI.

Habari za UN
23 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 23, 2024 10:00


Hii leo jaridani tunaangazia ziara ya Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA, Tom Fletcher mashariki wa kati, na uwezeshaji wa vijana katika sekta ya kilimo nchini humo. Makala inatupeleka nchini Zimbabwe na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA, Tom Fletcher akihitimisha ziara yake ya kwanza katika eneo la Mashariki ya kati tangu hivi karibuni alipochukua wadhifa huo ameeleza kuwa alichokishuhudia katika ukanda huo ni hali tete.Mradi wa pamoja wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO ujulikanao kama Nabta kwa lugha ya Kiarabu ukimaanisha "mche" ambao lengo lake ni kuwasaidia vijana wajasiriamali kubadili mawazo yao kuwa  biashara ya kilimo yenye mafanikio umeleta nuru kwa Alaa Khattab kijana aliyekuwa na ndoto ya kuwa mfanyabiashara wa kilimo nchini Syria.Katika makala Assumpta Massoi anakupeleka Zimbabwe kumulika nuru iliyofikia wakulima baada ya Umoja wa Mataifa kuona jinsi mabadiliko ya tabianchi yalivyoathiri shughuli za kilimo.Mashinani fursa ni yake Rukia, kijana wa kike kutoka Tana River nchini Kenya ambaye kupitia mafunzo na uwezeshaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM, yeye hasiti kutoa tahadhari za mapema na kuwahamasisha jamii kujiepusha na madhara panapotokea majanga ya mabadiliko ya tabianchi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
17 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 17, 2024 10:48


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika mafanikio katika kuzuia maambukizi mapya ya VVU na juhudi za vijana wakimbizi nchini Uganda kuhakikisha hilo. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani inayotupeleka Gaza.Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Syria Geir O. Pedersen bado yuko nchini Syria alikowasili jana Jumapili  ikiwa ni wiki moja baada ya wapiganaji wa Hayʼat Tahrir al-Sham (HTS) walioko kwenye orodha ya vikundi vya kigaidi kutwaa mji mkuu Damascus na kusababisha Rais Bashar Al-Assad kukimbia nchi.Mwaka 2024 ukielekea ukingoni, sirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR nchini Uganda limetoa rai kwa jumiya ya kimataifa kutolisahau taifa hilo la Afrika Mashariki ambalo ni maskani ya idadi kubwa zaidi ya waomba hifadhi na wakimbizi barani Afrika. Rai hiyo iliyotolewamwishoni mwa wiki inataka ufadhili wa fedha uongezwe ili liweze kuendelea kukirimu watu hao ambao wengi wanakimbia machafuko.Katika makala Assumpta Massoi anakupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Ethiopia kumulika mwelekeo wa usajili wa watoto wanapozaliwa na faida zake.  Na mashinani Maram, mama kutoka Deir al-Balah Gaza, ambako familia zinahaha kuokoa mali zao na kukarabati mahema yao yaliyoharibiwa na upepo mkali na maji ya mvua wakati huu wa msimu wa baridi, na kuleta athari kwa watoto wao.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

SBS Swahili - SBS Swahili
Kiongozi wa Queensland atetea mabadiliko ya haki ya vijana yenye misimamo mikali

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 6, 2024 6:38


Kiongozi wa Queensland na Mwanasheria Mkuu wame tetea mageuzi ya haki ya vijana yenye utata ya jimbo hilo, licha ya ukosoaji kutoka wadau na Umoja wa Mataifa.

Habari za UN
Mradi wa IFAD wasaidia vijana Senegal kusalia nchini mwao, kulikoni?

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 29, 2024 4:07


Mradi wa uitwao Agri-Jeunes uliozinduliwa na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya kilimo, IFAD ili kusaidia raia wa Senegal kuondokana na umaskini, na janga la njaa, umewapatia vijana wa kiume na wa kike matumaini ya kusalia nchini mwao badala ya kuhamia ughaibuni. Mradi huu umewasaidia vijana hao kwa mafunzo ya kilimo, ufugaji kuku, uvuvi na stadi za kuendesha biashara ndogondogo.Katika miezi mitano ya kwanza ya mwaka 2024, makumi ya maelfu ya watu waligeukia wasafirishaji haramu wa binadamu kwa njia ya bahari ya Atlantiki kuelekea visiwa vya Kanari, lakini zaidi ya watu 5000 wamekufa wakijaribu kufika huko. Haya yote yakisababishwa na ukosefu wa ajira na kipato duni. Kupitia video iliyoandaliwa na IFAD, Bosco Cosmas amefuatilia Maisha ya vijana hao, na kutuandalia makala hii

Habari za UN
Vijana wajumuishwe kwenye majadiliano ya mkataba wa mabadiliko ya tabianchi - Nasra

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 3:14


Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini Tanzania umewajumuisha watoto kwenye harakati za kukabiliana na kuhimili madhara ya mabadiliko ya tabianchi. Huko Baku nchini Azerbaijan kunakotamatika mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29 tunamsikia Nasra Abdallah, mwanaharakati wa mazingira kutoka Tanzania akizungumzia kilichompeleka, anachoondoka nacho na ujumbe wake kwa  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.

Habari za UN
18 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2024 10:46


Hii leo jaridani tunaangazia wakimbizi wa ndani nchini Haiti, na mafunzo ya stadi za kujikimu kimaishwa kwa vijana Tambura Sudan Kusini. Makala inatupeleka nchini Uganda na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Zaidi ya watu 20,000 wamekimbia makazi yao katika mji mkuu wa Haiti Port-au-Prince katika muda wa siku nne tu, ikiwa ni pamoja na watu wengine zaidi ya 17,000 wanaohifadhiwa katika makazi 15 ya wakimbizi wa ndani, kutokana na kuongezeka kwa ghasia za magenge ya uhalifu ambazo ziumevuruga kabisa minyororo muhimu ya usambazaji wa misaada na kulitenga jiji la Port-au-Prince limesema shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM.Vijana katika mji wa Tambura ulioko jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini wanageuza mafunzo ya ufundi stadi kuwa nguvu ya amani na ustawi, mafunzo ambayo yalifanikishwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, UNMISS.Katika makala Selina Jerobon kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi anakupeleka Uganda kuona harakati za wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kujikwamua kiuchumi baada ya machungu waliyopitia nyumbani kwao.Mashinani tutaelekea nchini Kenya kusikia ni kwa jinsi gani jamii katika maeneo kame wanakabiliana na mabadiliko ya tabianchi.Mwenyeji wako ni Bosco Cosma, karibu! 

Habari za UN
Vijana wafurahia stadi za kuondokana na umaskini Sudan Kusini

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2024 1:57


Vijana katika mji wa Tambura ulioko jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini wanageuza mafunzo ya ufundi stadi kuwa nguvu ya amani na ustawi, mafunzo ambayo yalifanikishwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, UNMISS.Shamrashamra zilitawala wakati vijana 61, wakiwemo wasichana 41 na wavulana 20 walipohitimu mafunzo ya ufundi stadi yenye lengo la kuwaondoa katika umaskini na pia kuwaepusha kutumikishwa katika mzozo unaoendelea nchini humo tangu Desemba 2013.Walifundishwa urembo wa nywele, kutengeneza sabuni, halikadhalika ushoni, mafunzo yaliyofadhiliwa na UNMISS na kutolewa na shirika la kiraia Star Trust Organization, linalohusika na kupunguza ghasia kwenye jamii kwa kuwajegena vijana uwezo.Miongoni mwao ni Suzan James, mama wa watoto wawili aliyejifunza urembo wa nywele na akiwa anamhudumia mteja wakati wa mafunzo anasema.“Ninashukuru mno, kwa sababu nimejifunza mambo mengi ambayo awali sikuyafahamu, lakini sasa ninaweza kufanya. Inanisaidia sana, na ninajivunia na nina furaha. Baada ya hili, nitaenda kufungua sehemu yangu mwenyewe ya urembo wa nywele ili kusaidia jamii.”Huyu ni Justin Alex yeye amejifunza ushoni na akiwa kwenye chereheni yake anasema.. “iwapo nitapekela hii cherehani nyumbani, nitaweza kufanya kazi na kusaidia familia yangu. Kama kijana tusikae nyumbani au tusifanye uhalifu mjini na kusababisha vifo kwa jamii zetu kwa sababu si jambo zuri. Kuanzia sasa tunahitajika kushiriki kwenye shughuli za kusaidia jamii, kama kupeleka hii cherehani nyumbani ili nisaidie jamii yangu.”Wahitimu wamepatiwa vifaa vya kuanzia kufanyie kile walichojifunza. Katika hafla ya utoaji wa vyeti UNMISS iliwakilishwa na afisa wake wa masuala ya ulinzi na ujumuishaji kwenye jamii Ibrahim Tahiru ambaye amesema..“Mradi huu unaweza kuleta amani, lakini pia mradi huu huu unahitaji amani ili uweze kuendelea. Bila amani hivi vitu vitakuwa bure. Kwa sababu wahitimu wanahitaji mazingira yenye amani ili waweze kutumia stadi zao kwa ajili ya kuboresha maisha yao na ya jamii zao. Mradi huu ni ishara ya nia yetu ya kuendelea kushirikiana na Sudan Kusini na kusaidia kufikia amani ya kudumu na kuondokana na umaskini.”Mamlaka za Tambura zina Imani kubwa na mradi huu kama asemavyo Kaimu Kamishna wa Tambura Moses Masisere.“Hakika, Tambura tumekuwa tukililia amani. Kwa hiyo kwa msaada huu tunaamini kuwa mafunzo kwa vijana zaidi kutawasaidia washiriki kwenye harakati za kiuchumi na kupunguza mauaji na uhalifu mwingine Tambura.”

Alfajiri - Voice of America
Zaidi ya vijana 500 kutoka nchi tofauti wakutana Arusha, Tanzania kuzungumzia umuhimu wa kumiliki ardhi. - Novemba 05, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 5, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
29 OKTOBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 29, 2024 10:57


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kuwasikia vijna ambao wanashiriki kongamano la vijana, wakieleza kuhusu mkataba wa zama zijazo na mchango wao katika kuutekeleza mashinani mwao. Pia tunakuletea muhtasari wa habar iza Sudan, Kura ya Knesset kuhusu UNRWA, na Siku ya kimataifa ya huduma, na mashinani.Baada ya Bunge la Israel hapo jana Oktoba 28 kupiga kura ya kuizuia Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) kufanya shughuli zake katika maeneo yote yaliyoko chini ya Israel, viongozi wa Umoja wa Mataifa kuanzia Katibu Mkuu Antonio Guterres wameendelea kupaza sauti kwamba kuizuia UNRWA ni ukiukwaji wa sheria za kimataifa na italeta zahma kwa maisha ya watu katika eneo hilo la Mashariki ya Kati. Katibu Mkuu Guterres amesema analileta suala hili kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, na atahakikisha Baraza hilo muda wote linakuwa na taarifa kwa kadri hali inavyoendelea.Ujumbe Huru wa Kimataifa wa Umoja wa Mataifa  wa kutafuta ukweli nchini Sudan umesema katika ripoti yake mpya ya kina leo kwamba Vikosi vya wanamgambo wa RSF, ambavyo vimekuwa vikipigana na Jeshi la Sudan (SAF) katika mzozo unaoendelea nchini humo, vinahusika na kufanya ukatili wa kingono kwa kiasi kikubwa katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wao, ikiwa ni pamoja na ubakaji wa makundi na kuwateka nyara na kuwaweka kizuizini waathiriwa katika hali ambayo ni sawa na utumwa wa ngono.Na leo ikiwa ni Siku ya Kimataifa ya Usaidizi na Matunzo, makadirio mapya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi (ILO), yaliyotolewa leo yanaonesha takribani wanawake milioni 708 duniani kote wako nje ya nguvu kazi zenye ujira kwa sababu ya majukumu ya kutoa usaidizi au matunzo bila malipo. Utafiti huo umefanywa katika nchi 125.Mashinani leo tutakwenda katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Al Matar huko Kassala, Sudan, kusikiliza ujumbe kutoka kwa Ted Chaiban, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF, aliyefanya ziara kambini humo.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

Habari za UN
UNESCO: Tunapaswa kuthamini sauti za walimu kote duniani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 4, 2024 2:58


Washiriki wa hafla ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Walimu ililofanyika leo Oktoba 4 katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) jijini Paris, Ufaransa  wamesisitiza wito wa kuthamini mawazo ya walimu katika kuboresha elimu ya ulimwengu. Kama tunavyofahamu, siku yenyewe ya Kimataifa ya Walimu ni kesho Oktoba 5 kama ilivyo ada ya kila mwaka lakini katika makao makuu ya UNESCO hapa Paris Ufaransa, maadhimisho yamefanyika leo kuelekea mkesha wa siku hii muhimu kwa elimu ya ulimwengu.Miongoni mwa waliozungumza ni Mkurugenzi Msaidizi Mkuu wa Elimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi Stefania Giannini, ambaye ameitumia nafasi hii kusisitiza kauli mbiu ya mwaka huu ambayo ni 'Kutambua sauti za walimu.'Anasema, “walimu ni uti wa mgongo wa mifumo ya elimu na mawakala wakuu wa mabadiliko ya kubuni sera za elimu na kufanikisha SDGs. Tunapaswa kuthamini sauti za walimu; hili ndilo lengo kuu la Siku ya Kimataifa ya Walimu mwaka huu.”Kulingana na takwimu zilizotolewa na UNESCO, dunia inahitaji walimu wa ziada milioni 44 ili kufikia elimu ya msingi na sekondari kwa wote ifikapo mwaka 2030. Ingawa mahitaji ya walimu ni makubwa zaidi katika baadhi ya maeneo, uhaba wa walimu ni wa kimataifa.Walimu wanajiondoa kwenye taaluma hii kwa kiwango mara mbili zaidi ya miaka mitano iliyopita, hasa katika elimu ya sekondari. Hii inatokana na hali zao za kazi, zikiwemo mishahara midogo, mzigo mkubwa wa kazi, na ukosefu wa ushiriki katika maamuzi yanayohusu elimu. Akiiangizia changamoto hii, Mkurugenzi wa Kimataifa wa Elimu na Maendeleo ya Vijana katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) Bi. Pia Britto, aliyejiunga katika hafla ya leo kwa njia ya video akiwa Pakistani amesema,"Leo nilikuwa na fursa nzuri ya kuzungumza na walimu wengi, ikiwa ni pamoja na mwalimu Tahseen Bashir hapa Islamabad, ambaye amenieleza baadhi ya changamoto wanazokabiliana nazo ikiwa ni pamoja na kufundisha madarasa mengi, uhaba wa vifaa vya kujifunzia, na changamoto za kutoweza kufundisha namna wanavyodhamiria. Lakini pia amenieleza jinsi alivyofurahi kuona wanafunzi wake wakifaulu. Wakati sauti ya mwalimu inaposikilizwa na wakati sauti za walimu zinapopewa kipaumbele, wanajiona kama wadau katika kuboresha elimu kwa wakati wote, na hatua hizo zinahitajika ili kuleta mabadiliko chanya hasa katika hali ngumu zaidi."Siku hii ya kimataifa ya walimu ni mahususi kwa ajili ya kutambua na kusherehekea mchango muhimu wa walimu ulimwenguni kote katika kutoa elimu bora na kujenga mustakabali wa jamii. Pia, ni fursa ya kuangazia changamoto wanazokabiliana nazo walimu.Kutoka hapa Paris Ufaransa, mimi ni Cecily Kariuki..

Habari za UN
Vijana - Tumechoka na maneno ya viongozi sasa tunataka vitendo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 24, 2024 7:27


Jana Jumapili ya Septemba 22 viongozi wa dunia walipitisha Mkataba wa Zama Zijazo. Mkataba huu unalenga kukabili changamoto za karne ya 21 kuanzia mizozo, mabadiliko ya tabianchi, haki za binadamu, hadi taarifa potofu na za uongo. Maeneo Matano makuu ni pamoja na maendeleo endelevu, amani na usalama duniani, sayansi na teknolojia, vijana na vizazi vijavyo na marekebisho ya usimamizi wa dunia, kipengele muhimu wakati huu ambapo taasisi za fedha za kimataifa na Umoja wa Mataifa wenyewe wameshindwa kuja na majawabu ya karne ya 21. Mkataba wa Kimataifa wa Kidijitali unaoelenga pamoja na mambo mengine usimamizi bora wa Akili Mnemba, pamoja na Azimio kwa ajili ya Vizazi Vijavyo linalotaka serikali za sasa kutilia maanani vizazi vijavyo zinapopitisha maamuzi yao ya leo, ni sehemu ya viambatanishi vya Mkataba huu wa Zama Zijazo. Assumpta Massoi ametaka kufahamu maoni ya vijana baada ya hatua hii, na ndio mada yetu kwa kina siku ya leo. 

Habari za UN
20 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 20, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia uondoaji wa taka katika ukanda wa Gaza, na ujumbe wa vijana ambao watashiriki mijadala mikuu hapa makaomakuu ya Umoja wa Mataifa. Makala tunasalia hapa hapa makao makuu na mashinani tunakupeleka nchini Sudan Kusini, kulikoni?Hali inazidi kuwa si hali huko Ukanda wa Gaza kwani sasa raia wanakwepa sio tu mashambulizi na magonjwa bali pia nyoka, panya na wadudu ambao wanasambaa kutokana na mazingira machafu. Watu wanajihifadhi kwenye maeneo ya wazi bila mifumo ya majitaka au ya kuondoa maji ya mvua. Timu ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina imefika kupuliza dawa ili kulinda wananchi hao.Leo hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani vijana kutoka kila kona ya dunia wanakutana kuanza kujadili kuhusu mstakabali wao katika zama zijazo. Miongoni mwao ni Jerop Limo kutoka Kenya anayetumia uzoefu wake wa kuishi na Virusi Vya Ukimwi kwa miaka 24 ya umri wake kuhakikisha ulimwengu unakuwa mahali bora kwa watu ambao tayari wanaishi na virusi hivyo.Makala inaturejesha hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani ambako mkutano wa Zama Zijazo umen'goa nanga leo kwa siku mbili za kuchua hatua kabla ya kikao cha ngazi ya juu siku ya Jumapili na Jumatatu. Leo Vijana wanapata fursa ya kupaza sauti zao kuhusu dunia na mustakbali wautakao.Na katika mashinani Balozi Mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, Tendai Mtawarira, mwanamichezo nguli mstaafu wa mpira wa raga mzaliwa wa Zimbabwe lakini alichezea Afrika Kusini, akizungumzia alichokishuhudia katika safari yake ya kwanza nchini Sudan Kusini.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Habari za UN
Viongozi wa kimataifa washikamane kuhakikisha ulimwengu wenye usawa wa kijinsia - Dorice Mkiva

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 20, 2024 3:00


Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani ambako mkutano wa Zama Zijazo umen'goa nanga leo kwa siku mbili za kuchua hatua kabla ya kikao cha ngazi ya juu siku ya Jumapili na Jumatatu. Leo Vijana wanapata fursa ya kupaza sauti zao kuhusu dunia na mustakbali wautakao. Flora Nducha wa Idhaa hii amezungumza na kijana mwenye ulemavu kutoka Tanzania ambaye ni mmoja wa wazungumzaji  wa mkutao wa leo. Anaanza kwa kujitambulisha.

Habari za UN
Mataifa yahakikishe ulimwengu unakuwa mahali bora kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi - Jerop

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 20, 2024 2:15


Leo hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani vijana kutoka kila kona ya dunia wanakutana kuanza kujadili kuhusu mstakabali wao katika zama zijazo. Miongoni mwao ni Jerop Limo kutoka Kenya anayetumia uzoefu wake wa kuishi na Virusi Vya Ukimwi kwa miaka 24 ya umri wake kuhakikisha ulimwengu unakuwa mahali bora kwa watu ambao tayari wanaishi na virusi hivyo. Anold Kayanda amezungumza naye na hapa Jerop Limo anaanza kwa kueleza yale ambayo atawaeleza viongozi wa ulimwengu.

Habari za UN
Guterres: Vita huharibu miili, akili na fikra za vijana na watoto

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 9, 2024 1:47


Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kulinda elimu isishambuliwe wakati wa mizozo kutokana na umuhimu wake kwa watoto na jamii, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema miaka ya karibuni imeshuhudia ongezeko kubwa la mashambulizi dhidi ya wanafunzi, walimu na shule duniani kote. Hivyo ndivyo alivyoanza ujumbe wake wa siku hii. Katibu Mkuu anasema kuanzia Gaza hadi Sudan, Myanmar, Ukraine, Colombia hadi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na kwingineko, vita inasababisha ukatili kwa binadamu, lakini kwa watoto na vijana waliokutwa katikati ya jinamizi la vita, gharama haiwezi kukokotolewa.Anasema ndio maana siku hii inatukumbusha jinsi vita inaharibu miili, akili na fikra za watoto na vijana. Kuanzia majeraha hadi vifo, kutekwa nyara, kulazimika kukimbia, ukatili wa kingono, kutumikishwa vijana na kupoteza fursa. Hatari ni kubwa sana.Anakumbusha kuwa elimu sio tu haki ya msingi ya binadamu, bali ni muhimu kwa ajili ya kutimiza haki nyingine zote za binadamu.Ni kwa mantiki hiyo anataka nchi ziwekeze kwenye elimu na zifanye juhudi zote kuhakikisha wakati wa mizozo elimu na maeneo ya kujifunza yanalindwa, zilinde wanafunzi na walimu na ziwawajibishe wale wote wanaoshambulia shule.Ametumia pia ujumbe huo kuzitaka nchi ziridhie na zitekeleze Azimio la Shule Salama, ziunge mkono Ubia wa Kimataifa wa Kuepusha Mashambulizi dhidi ya Shule na zishikamane na juhudi zote za kuhakikisha watoto na vijana wanaendelea kujifunza iwe wakati wa majanga au wakati majanga yanapokoma.Ametamatisha akisema hebu na tulishe elimu isishambuliwe, tulinde haki ya msingi ya elimu ambayo ni haki ya kila mtoto, kila mtu kokote kule.

Habari za UN
05 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 5, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha nchini Bahrain kufuatilia harakati za vijana za kufanikisha haki za watoto waliozaliwa na usonji au Down Syndrome. Pia tunakuletea habari kwa ufupi na uchambuzi wa methali “Jawabu la kesho andaa leo.”Awamu ya kwanza ya kampeni ya utoaji chanjo ya polio kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka 10 imehamia hii leo eneo la kusini mwa ukanda huo hususan Khan Younis na itakamilika Jumapili hii. Mama mmoja aliyepeleka mtoto wake leo amesema aliposikia tu chanjo inatolewa dhidi ya polio alikimbilia kituo cha jirani cha tiba ili ampatie chanjo kwani anahofia itasambaa kutokana na mazingira machafu ya majitakama wanamoishi. Awamu hii itamalizika Jumapili. Awamu ya Pili itaanza baada ya wiki nne.Nchini China Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anahudhuria mkutano wa China na nchi za Afrika, leo amehutubia mkutano huo na kueleza masuala kadhaa yakusaidia kusongeza nchi za Afrika ikiwemo haja ya kutatua changamoto ya nchi za Afrika kuwa na madeni makubwa na kushindwa kuwekeza katika miradi ya maendeleo, ushirikiano wa kusini -kusini na hitaji la Afrika kuwa na uwakilishi wakudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.Na leo ni siku ya Kimataifa ya ukarimu duniani, mfano mmoja tu wa ukarimu unaoendelea sasa duniani ni ule shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina UNRWA wanaopokea kutoka kila kona ya dunia kuanzia kwa watu maarufu, asasi za kiraia, mpaka watu binafasi, wote lengo likiwa ni kuwawezesha UNRWA kuhudumia wapalestina milioni mbili walio katikati ya mzozo huko Gaza.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili, Mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anafafanua methali “Jawabu la kesho andaa leo.”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

Habari za UN
Mradi wa WFP wawezesha vijana Tanzania kuvuna mazao mwaka mzima

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 30, 2024 1:50


Mradi wa Vijana Kilimo Biashara (VKB) unaotekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani (WFP) nchini Tanzania unawapatia vijana wakulima wadogo ujuzi na rasilimali zinazohitajika ili kuboresha uzalishaji wa chakula na kujenga uchumi endelevu wakati huu ambao madhara ya El niño [EL NINYO] yanayosabisha ukame na mafuriko yamekuwa dhahiri. Bosco Cosmas na maelezo zaidi.Hali ya El Nino huwa changamoto kwa wakulima kwani hawana uhakika wa mavuno ya kile walichopanda. Hali ni tofauti kwa mkulima kijana Coletha Kiwenge anayeendesha kilimo biashara kupitia mradi huo wa WFP wa Vijana Kilimo Biashara (VKB) nchini Tanzania. Yeye amefanikiwa kuvuna mazao mwaka mzima, licha ya changamoto za hali ya hewa zinazotokana na El Niño.“Pamoja na mradi huu wa Vijana Kilimo Biashara, unaofadhiliwa na Shirika la mpango wa chakula duniani na mtekelezaji ‘Farm Afrika', tumejifunza yafuatayo: - Moja, matumizi ya mbegu bora, na kwa msimu huu tumetumia mbegu bora au mbegu chotara za alizeti Pamoja na mtama Pamoja na kufadhiliwa hizo mbegu ambazo zina mazao mengi.”Kutokana na madhara ya hali ya hewa na tabianchi, WFP imeelekeza nguvu katika kilimo cha umwagiliaji kwa wakulima hao.“Lakini pia tumechimbiwa kisima na Shirika la Mpango wa chakula duniani WFP, kisima hiko ni lengo na madhumuni kwaajili ya kilimo cha bustani, na kwasasa kwenye bustani yetu tumeanza na nyanya na ziko shambani. Lakini kwenye kikundi cha KAPATA, tunaendelea na upando mbalimbali.”

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية

Magonjwa ya wanawake, Vijana na changamoto ya ajira