POPULARITY
Safari ya Muziki wa kizazi kipya inaanzia mbali,sasa vijana wanalazimika kusafiri kutoka Mikoani kuja jijini Dar es salaam ili kufaulu kisanaa, Eddy Music ni msanii wa Muziki anazungumza na Steven Mumbi katika Makala haya.
Mara baada ya kutoka Jela Msanii Real Jofu anasema amejifunza kuwa mvumilivu ili kufikia malengo,Ungana na Steven Mumbi kaktika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Msanii huyo.
Samir Kassim Rashid maarufu Samir Kinyulinyuli ni Msanii wa Sanaa ya Muziki aliyelazimika kukimbilia Dar es salaam akitokea Morogoro ili kufanikiwa kisanaa, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa ya Jumahili.
Sanaa ya Muziki Nyanda za Juu kusini mwa Tanzania, ni sanaa inayokua kwa kasi vijana wanawekeza kulifikia soko la Muziki Afrika Mashariki, B2K ni Msanii anayekonga Nyoyo za Wasichana zaidi kutokana na Tungo zake, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na B2K kutoka Njombe.
Uchoraji ni Ajira ,Wasanii wa sanaa hii Zanzibar wananeemeka na kazi zao, Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Obedience na Muki kutoka Zanzibar.
Wachoraji visiwani Zanzibar walia na gharama za kupata maeneo ya kunadi kazi zao za Sanaa hiyo, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Mchoraji maarufu visiwani humo Jamal.
Taarab Asilia ni Miongoni mwa Miziki ya kale zaidi katika Mwambao mwa Bahari ya Hindi, Zanzibar Taarab Hertage Ensemble ni miongoni mwa Makundi ya Muziki huo kutoka Visiwani Zanzibar, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Wanamuziki wa Muziki wa asili wamebadili vionjo vya asili wakijumuisha na vionjo vya Kisasa ili kuupaisha Muziki Kimataifa, Steven Mumbi amezungumza na Leo Mkanyia Mwanamuziki wa Muziki wa Asili kutoka Tanzania
Wasanii wa Muziki wa kizazi kipya wanaochipukia nchini Tanzania walalama kutakwa Kimapenzi wa Watayarishaji wa Muziki, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akiwa na Zainisha Nokolage maarufu Zainisha.
Steven Mumbi amezungumza na Lyala Sebastian Mchongaji wa Sanaa za Vinyago.
Wabunifu wa Sanaa ya Uchongaji Vinyago wamewekeza katika kung'amua fursa ya biashara kwa Mataifa ya Afrika Mashariki ili kujikwamua na vipato Duni, Steven Mumbi amezungumza na Mintanga Ramadhani Msanii wa Sanaa za Uchongaji Vinyago kutoka nchini Tanzania.
Sanaa ya ushairi inawavutia zaidi watu wanaotamani kujua utamu na upekee wa lugha adhimu ya Kiswahili, Chuo kikuu cha Dar es salaam kimewatambua na kuwapa fursa vijana waliosomea fani ya sanaa, kubobea katika kughani Mashairi. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Msanii Michael James maarufu Michael.
Mwandishi wetu Steven Mumbi amezungumza na kundi la wasani la viongozi generation.
Muziki wa kizazi kipya umewawezesha vijana nchini Tanzania kujikwamua kimaisha kwa kujipatia kipato kupitia Sanaa hiyo,Katika Makala haya Steven Mumbi anazungumza na Hussein Mussa Shundi Maarufu Rucky.
Msanii wa Bongo Fleva, Baraka the Prince anauona muziki ni maisha, jambo linalomfanya afikirie zaidi namna mashabiki wake wataishi na kazi zake, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Msanii huyo.
The Mafiki ni kundi la Muziki lililovuma kwa vionjo vya Muziki wa sasa, sasa wamekuja upya mara baada ya kusambaratika, Ungana na Steven Mumbi akizungumza na wasanii wa kundi hilo.
Mapinduzi ya Muziki wa Taarab yanajidhihirisha katika tenzi za wasanii wa Muziki huu kutoka tungo za Majigambo na sasa tungo za kuburudisha, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Jike la Chui.
Zumbukuku ni miongoni mwa nyimbo zilizofanya vizuri katika muziki wa taarab, hii inashehenezwa na sauti ya kipekee ya kiume inayosikika katika muziki huo, Ally Star ndie aliyeimba wimbo huo; Ungana na Steven Mumbi katika makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Ally Star kuhusu namna nyimbo hizo zilivyotia fora.
Nyota Tiger ni mzaliwa wa jijini Mwanza nchini Tanzania alilazimika kusafiri mpaka maeneo ya kusini mwa Afrika kukwepa adha za wazazi kumnyima fursa ya kufanya muziki. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Muziki wa Singeli ni Miongoni mwa Muziki unaokua kwa kasi nchini Tanzania na nchi za Afrika,Wasanii wa Muziki huo wanapambana kuukuza Kimataifa, Man Fongo ni Miongoni mwa Wasanii Pendwa wa Muziki huo,Ungana na Steven Mumbi anazungumza na Msanii huyo.
Katika Makala ya Wiki hii, Steven Mumbi amezungumza naye Jilema Ng'wana Shija msani wa muziki wa asili kutoka nchini Tanzania.
Karibu katika makala ya Nyumba ya sanaa nami Steven Mumbi, hii leo Msanii Tourna Boy wa kizazi kipya kutoka mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo akielezea kuhusu juhudi za vijana wasanii kuchangia katika juhudi za kurejesha amani ya mashariki mwa nchi hiyo, katika mazungumzo na mwenzangu Ruben Lukumbuka alipotembelea eneo la Goma mwanzoni mwa mwezi mei mwaka huu 2024
Asha Jumbe maarufu White Maria ni Muigizaji aliyejizolea umaarufu akiwa na umri wa Miaka nane tu, sasa ni mtu Mzima aja kivingine kufanya sanaa ya Fimalu za kiswahili,Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumzia safari yake ya Uigizaji.
Sanaa ya Muziki imenihitaji kuliko nilivyo ihitaji, ni kauli yake Steven Ibrahim maarufu Eddy Music alipozungumza na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Mwandishi wetu Steven Mumbi amezungumza na msani wa muziki huu wa Baibuda
Steven Mumbi amefanya mahojiano na Rahama Machupa msanii wa nyimbo za taarab nchini Tanzania.
Muziki wa Reggae ni miongoni mwa Miziki iliyopata mashiko mapema zaidi ukilinganisha na aina nyingine ya Muziki nchini Tanzania, Innocent Galinoma akiishi nchini Marekani ni miongoni mwa wasanii wa Mwanzo wa Muziki huo nchini Tanzania, Steven Mumbi amezungumza naye katika Makala haya.
Ambwene Mwasongwe ni Muimbaji wa Nyimbo za Injili kutoka nchini Tanzania, aliyejizolea umaarufu kutokana na nyimbo zilizojaa simulizi za Maisha na kubadili mitizamo kuhusu Maisha, Ungana na Steven Mumbi anazungumza na Muimbaji huyo.
Miongoni ma wanamuziki wa muziki wa dansi waliofanikiwa kwenda barani Ulaya ni pamoja na Fresh Jumbe, baada ya kufanya sanaa hiyo kwa miaka mingi nchini Japan sasa amerejea Tanzania, Ungana na Steven Mumbi katika makala ya nyumba ya sanaa akizungumza na msanii huyo.
Diamond Platinumz ni miongoni mwa wasanii wa Tanzania walimvutia kufanya sanaa hiyo, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa
Muziki wa Dansi unachukua sura mpya baada ya Vijana waofanya muziki wa aina nyingine kugeukia muziki huu, Steven Mumbi amezungumza naye Fredrick Fulmeradius
Wazazi chanzo cha Wasichana kutofanya Muziki Tanzania, Steven Mumbi anazungumza na Zulfa Mohamed maarufu Xoul
Anasema wizi wa kazi za sanaa unawarudisha nyuma wasanii na hivyo kuathiri kazi zao.Ungana na Steven Mumbi katika makala ya nyumba ya sanaa akizungumza na msanii huyo.
Wasanii wa Muziki wa Singeli wafurahia kupewa Msaada na Serikali ya Ufaransa ili kuinua kazi zao kimataifa, Ungana na Steven Mumbi akiangazia namna fedha hizo zitakavyowasaidia kubadili Sanaa zao.
Tommy Thomas Msanii wa HIP HOP anasema Muziki wake unapenya kutokana na aina ya Mashairi anayotunga, Steven Mumbi amezungumza naye katika Makala haya ya Nyumba ya Sanaa.
Muziki wa Reggae ni Sanaa iliyofifia nchini Tanzania, miongoni mwa sababu zinazotajwa ni pamoja na kudorora kwa matamasha ya muziki huo, Steven Mumbi anazungumza na Paul Mihambo mwanamuziki wa Reggae nchini humo.
Abby love na Addo Six, vijana wanaofanya Sanaa ya Muziki wa Bongo Fleva kutoka Dar es salaam wakizungumza na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Faraja Habakuki Group ni kundi la muziki wa Injili kutoka mkowa wa Kivu Kusini eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambako vijana wadogo wameanza kujitokeza na kufanya sanaa ya muziki wa Injili, kuepukana na umasikini lakini pia hofu ya mapigano ya mara kwa mara katika eneo hilo. Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Kundi hilo.
Lwiza Mbutu ni Muimbaji Pekee wa Muziki wa Dansi nchini Tanzania aliyedumu na Bendi ya African Stars maarufu 'twanga pepeta' Pekee tangu kuasisiwa kwa Bendi hiyo mwaka 1998, nini siri, Steven Mumbi amezungumza na Lwiza Mbutu Makala ya Nyumba ya Sanaa .
Muziki wa Hip Hop kwa wanawake si jambo zoeleka katika sanaa ya muziki nchini Tanzania, kutana na msanii TK NENDEZE akizungumza na mwandishi wetu Steven Mumbi katika makala ya Nyumba ya Sanaa wiki hii.
Steve RNB ni msanii wa muziki wa kizazi kipyamakitamba na kibao Jambo Jambo kipi kilisukuma kufanya sanaa hii ya Muziki, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na msanii huyo.
Pokea Vanillah Music ni miongoni mwa watunzi wa nyimbo na sasa kageukia uimbaji wa muziki wa kizazi kipya, kibao " Unanisitiri " ni miongoni mwa vibao pendwa. Kukipata kibao hiki kwa undani zaidi, ungana na mwandishi wetu Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Vanillah.
Makala ya Nyumba ya Sanaa ya juma hili, inamwangazia msanii Steven Charles almaarufu Samertz ni mtayarishaji wa muziki wa kizazi kipya kutoka nchini Tanzania, sasa amegeukia uimbaji wa muziki huo, Je nini kimetokea kiasi cha kuanza kuimba? ungana na Steven Mumbi akizungumza na Msanii huyo katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Mabadiliko ya Sanaa ya uimbaji yamewafikia waimbaji wa nyimbo za Injili, sasa wanafanya Sanaa hiyo kwa kuendana na hali ya mabadiliko ya kiteknolojia kwenye sanaa ya muziki wa kisasa. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na muimbaji wa nyimbo za Injili Goodluck Gozbert.
Uchoraji ni Sanaa ya Urithi, kutoka Mji Mkongwe visiwani Zanzibar urithi wa sanaa hiyo umetamalaki, Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akiangazia sanaa hiyo.
Muziki ni sanaa inachipuka kwa kasi eneo la mashariki mwa DRC, wasanii wanafanya sanaa inakubalika miongoni mwa jamii inayosikiliza lugha adhimu ya Kiswahili, Ogisha Matale ni msanii wa kizazi kipya kutoka mji wa Goma,mkoani Kivu kaskazini mashariki mwa nchi hiyo akielezea changamoto wanazokabiliana nazo wasanii katika kipindi hiki eneo lao likichukuliwa kuwa kitovu cha usalama mdogo. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Sagna ni miongoni mwa wasanii wachache kutoka kanda ya ziwa wanaofanya sanaa ya Muziki wa kizazi kipya, anapambana kufanikiwa licha ya changamoto. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Naomba Stara ni miongoni mwa nyimbo za taarabu zinazokubalika na mashabiki wa muziki huo, katika eneo la Afrika mashariki na kati ambapo Rahma Machupa ndie muimbaji wa kibao hicho. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza nae huku ukipata vionjo vya muziki wake mtamu.
Makala ya Nyumba ya Sanaa ya juma hili inakuletea muziki wa Bongo Fleva ambao sasa unachagizwa na vionjo vipya, wasanii wachanga wanajiimarisha kwa kubobea na kutoa ladha inayokonga nyoyo za wapenzi waliokata tamaa, kutana na Zack Muziki akizungumza na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Kwenye Makala ya wiki hii Steven Mumbi anazungumza naye Zach Music kuhusu masuala ya sanaa ya Muziki.
Kwenye Makala ya wiki hii ya nyumba ya sanaa, Mwandishi wetu Steven Mumbi anazungumzia kuhusu sanaa ya Muziki wa kizazi kipya.
Kwenye makala ya wiki hii Steven Mumbi amezungumza naye Elizabert Pastory kuhusu Ushairi.
Ala za muziki zilizokuwa zinatumiwa zamani katika mataifa mengi ya Afrika, zimeanza kusahaulika. Huko nchini Kenya, serikali kupitia makavazi ya Bomas of Kenya, inahifadhi ala, muziki ,na tamaduni za kale/zamani kwa lengo la kudumisha , kuhifadhi na kufundisha utamaduni wa nchi hiyo. Mengi zaidi ni katika Makala haya, yanayomshirikisha Mwandishi wetu Steven Mumbi na Victor Abuso.
Wiki hii mwandishi wetu Steven Mumbi anatoa nafasi kwa mwanamuziki Abdulrazack Habibu mwanamuziki kutoka nchini Tanzania.
Sanaa ya muziki ushairi ni sanaa nyingine iliyosheheni tenzi za mafu,bo.zilizobeba ujumbe sambamba na matumizi ya nahau na Methali za lugha adhimu ya kiswahili. Kutana na Mrisho Mpoto almaarufu Mjomba katika makala ya Nyumba ya Sanaa na mwandishi wetu Steven Mumbi.
Makala hii ni mwendelezo wa mazungumzo ya mwandishi wetu Steven Mumbi na msanii wa muziki wa taarabu nchini Tanzania Afue Maganga ambaye ameonesha kuwa Taarab ni nyimbo zilizosheheni majigambo hasa kwa wanawake wakitambiana, wake wenza kuibana wanaume na mambo mengine Ungana na mwandishi wetu Steven Mumbi kupata mengi zaidi.
Mbwene Mwasongwe ni miongoni mwa waimbaji wa nyimbo za injili waliofanikiwa kuivusha Sanaa hiyo kutoka kuwa na wapenzi wa aina moja na kuwa wa aina mbalimbali, sasa Sanaa hiyo imefanikiwa kuwatia moyo na hata kufufua matumaini kwa waliokata Tamaa. Ungana na Steven Mumbi katika makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Ambwene Mwasongwe.
Wiki hii, mwandishi wetu Steven Mumbi anaangazia sanaa ya muziki na uchekeshaji nchini Tanzania
Wasanii chipukizi wa muziki wa kizazi kipya wanalazimika kusafiri kutoka mikoa iliyopembezoni kuja jijini Dar es salaam ili kufanikisha safari yao kimuziki, Ramso High alilazimika kusafiri Kutoka Kigoma kuja jijini ili kufanikiwa kimuziki, swali ni je amefanikiwa? Ungana na mwandishi wetu Steven Mumbi akizungumza na msanii huyo katika Makala ya Nyumba ya Sanaa. ------
Wasanii chipukizi wa muziki wa kizazi kipya wanalazimika kusafiri kutoka mikowa iliyopembezoni kufika jijini Dar es salaam ili kufanikisha safari yao kimuziki. Ramso High alilazimika kusafiri Kutoka Kigoma kuenda jijini ili kufanikiwa kimuziki, swali ni je amefanikiwa? Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Msanii huyu katika makala ya nyumba ya Sanaa
Ni msanii aliyeshirikishwa katika wimbo wa kwanza wa Nasib Abdul maarufu Diamond Platinamuz unaoitwa Nitarejea, alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Diamond wakati akirekodi ngoma hiyo, sasa nini kinafuata? Ungana na Steven Mumbi katika makala haya ya Nyumba ya Sanaa akizungumza nae kuhusu Safari yake ya Muziki akiwa na Kbao Kipya Naelewa.
Wasanii wa sanaa za majukwaani nchini Tanzania walia na ukosefu wa ajira hivyo kutumbukia katika kufanya kazi mbadala licha ya kusomea fani hiyo hadi ngazi ya Shahada, Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Chimwenda Wilsaon msanii wa Sanaa za jukwaani nchini humo.
Utengenezaji wa picha jongefu ni Sanaa nyingine inayoibuka kwa kasi nchini Tanzania, Wachoraji wanatumia vipaji vyao kusanifu Michoro inayosimulia hadithi kwa njia ya video fupi ilitengenezwa kwa kutumia katuni, Je Sanaa hiyo ikoje? Ungana na Steven Mumbi katika Makala haya ya Nyumba ya Sanaa.
Msanii wa Muziki wa Reggae kutoka nchini Rwanda, Jah Bone D, baada ya kuishi Uswizi kwa miaka zaidi ya 20 sasa anataka kurejesha muziki wa Reggae katika nchi za Afrika Mashariki. Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Jah Bone D katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Kutana na msichana wa mwaka wa tatu Chuo kikuu cha Dar es salaam,Nasma Mzee akichukua Shahada ya Kwanza ya Sanaa na Ubunifu aliyechagua kuwa Mchoraji ili kuwasilisha Maudhui ya Sanaa aliyosomea. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Nasma Mzee.
Kutana na Mshairi Zawadi Mengele aliyejikuta akifanya Sanaa ya Ushairi baada ya kumzawadia Mama yake shairi lililo amsha hisia ya Malezi. Ungana na mwandishi wetu Steven Mumbi katika makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na mshairi huyo akianisha namna anavyopokelewa Tanzania.
Ukosefu wa elimu ya mahusiano ni miongoni mwa sababu zinazochangia ndoa nyingi kuvunjika, kutana na Ahmed Hassan mtunzi wa vitabu vya mahusiano ya kimapenzi akizungumza na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa wakizungumzia Sanaa ya Utunzi wa vitabu vya mahusiano.
Ushairi ni Sanaa inayokua kwa kasi, Washairi wameongeza ubunifu wakughani Mashairi sambasamba na matumizi ya Mirindimo ya Miziki inayopigwa na chombo kama Violin Ungana na Steven Mumbi katika makala ya nyumba ya sanaa akizungumza na mshairi Elizabeth Pastory.
Taarab Asilia ni Miongoni mwa Muiziki yenye asili ya Mwambao, Maudhui yanayojikita katika kuelimisha uhusiano kati ya Mume na Mke,Nyimbo zilizosheheni Majigambo ,Je Unamfahamu Afua Suleiman Maganga mtunzi wa Wimbo Utalijua jiji ? Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza nae kuhusu safari yake ya Muziki huo aliyoianza mwaka 1982.
Sanaa ya uandishi na utunzi wa vitabu ni miongoni mwa sanaa zinazofifia hivi sasa kutokana na ukuaji wa utandawaji sambamba na wasomaji wengi kugeukia utumiaji wa mitandao ya kijamii na hivyo kuathiri biashara ya uuzaji wa vitabu. Ungana na Steven Mumbi katika makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Emmanuel Mkama Mtunzi wa vitabu Kutoka nchini Tanzania wakizungumzia sanaa hiyo sambamba na Changamoto zake.
Uchoraji si sanaa tu inayohusisha urembo pia ni sanaa inayotumika kutunza kumbukumbu, wachoraji wanafanya sanaa hii kama sehemu mbadala ya kujipatia kipato. Augosto Ngumba ni mchoraji mwenye shahada ya elimu ya Juu katika masuala ya Jamii,baada ya kukosa Ajira akaamua kutumia kipaji chake cha uchoraji kujijiri. Ungana na Steven Mumbi katika Makala haya ya Nyumba ya Sanaa.
Ucheshi ni Sanaa nyingine inayokua kila kukicha nchini Tanzania. Wasanii wanatumia kila mbinu ili kunasa hadhira inayohitaji kuburudika kupitia sanaa hii. Sasa Wasanii wa uimbaji waanza kuwa wabunifu kwa kubuni sanaa ya Uimbaji kupitia Ucheshi, Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Kundi la MAHONA OLD SCHOOL CREW katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Sanaa ya Uchoraji nchini Tanzania imeendelea kudhihirisha uzuri wa Utamaduni uliopo nchini Tanzania,Wachoraji wanajikita kuhifadhi Historia kupitia picha na wengine kufanya sanaa hiyo kwa kuchora picha halisia. Thobius Minzi ni Mchoraji anayechora picha kwa kutimia kalamu za risasi na baadae hutumia rangi za Cliric. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akiangazia sanaa ya Uchoraji. .
Umuhimu wa Ushairi katika kukuza fasihi,Kutana na Steven Mumbi katika Mkala ya Nyumba ya sanaa.
Bendi ya Muziki inayofanya Sanaa ya Muziki kwa kupiga mtaa kwa Mtaa wazungumzia namna walivyofanikiwa kuifanya sanaa hiyo kutokea mkoani Mbeya Nyanda za juu kusini mwa Tanzania mpaka jijini Dar es salaam kufanya sanaa hii. Ungana na Steven Mumbi katika Makala haya akizungumza na Viongozi wa Bendi hiyo.
Sanaa ya Urembo ni Sanaa nyingine inayokuwa kwa kasi miongoni mwa Vijana, Wasichana wanatumia fursa ya kuwaremba si Maharusi tu hivi sasa hata watu wa kawaida wanapenda kurembwa katika sura zao ili kuonekana warembo na Watanashati katika shughuli zao za Kawaida. Makala haya yameangazia Sanaa hii, Steven Mumbi amezungumza na Hilda Koshuma, Mwalimu na Msanii anayefanya Sanaa hii
Wadatooga (pia huitwa Wataturu au Wamang'ati) ni kabila la watu wa Kiniloti nchini Tanzania wanaoishi hasa katika mikoa ya Manyara, Mara, Arusha na Singida. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na kikundi cha WADACA kutoka Ngorongoro kaskazini mwa Tanzania.
Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Mchoraji wa Vibonzo Muhidini Msamba kuhusu safari yake ya sanaa na Mapokeo ya sanaa hiyo kwa Ujumla.
Kwa Mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) zaidi ya wasichana na wanawake milioni 4 ulimwenguni wanaishi na tatizo la Fistula huku wanawake kati ya 50,000 na 100,000 wakipata tatizo hili kila mwaka. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Siha Njema kuangazia Ugonjwa huo.
Ungana na Steven Mumbi katika Makala haya akizungumza na Wasikilizaji wa Rfi Kiswahili kuhusu kurejea DRC Kwa Makamu wa zamani wa Rais wa nchi hiyo Jean-Pierre Bemba.
Upatikanaji wa Vifaa,Gharama pamoja na Uelewa Duni vinachangia Sanaa ya Uchoraji kushindwa kusonga Mbele. Malkia Queens wazungumza na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Makala ya Nyumba ya Sanaa inaangazia changamoto wanazokabiliana nazo wanawake Waigizaji kiasi cha kuwalazimisha kugeukia kazi nyingine ili kujipatia kipato. Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Wasanii mbalimbali nchini Tanzania.
Nyumba ya Sanaa inaangazia Sanaa ya Ususi ama Ufumaji kutoka Mkoani Morogoro Nchini Tanzania. Mtangazaji wa Makala haya Steven Mumbi anazungumza na Kiongozi wa Kikundi cha Mkonge Sisal.
Kutana na Imelda Munyaga Mwalimu wa Sanaa za aina mbalimbali. Katika Makala haya anazungumza na Steven Mumbi kuhusu Sanaa ya Muziki na Uigizaji.
Allain Nyangasa awataka Waimbaji wa Muziki wa Injili kubadilika kufanya Muziki wa Injili kwa ajili ya kumtumikia Mungu na si Biashara Ungana na Steven Mumbi katika Makala haya akizungumza na Msanii huyo.
Muziki wa Singeli ni Miongoni mwa Muziki unaochipukia nchini Tanzania,vijana wanajaribu kuifikia hadhira kwa kutumia maudhui ya Asili. Katika Makala haya ya Nyumba ya Sanaa,Ungana na Steven Mumbi akizungumzia Muziki huo akiwa na S.Kide pamoja na Kiongozi wa Wakupeti Band.
Ushairi ni Sanaa iliyotumika kukuza Lugha ya Kiswahili katika Nchi za Afrika Mashariki,ikiwemo Tanzania hasa wakati wa kupigania uhuru na hata baada ya Uhuru katika kuhamasisha watu kufanya Maendeleo. Steven Mumbi amezungumza na Mshairi wa siku nyingi nchini Tanzania,Charles Mloka, Ungana nae katika Makala haya ya Nyumba ya Sanaa.
Maida waziri Mwanamke aliyeamua kufanya kazi ya Sanaa na hatimaye kufanikiwa kuwa Mbunifu wa Majengo. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akizungumza na Maidfa Waziri kuhusu safari yake katika Sanaa ya Ubunifu
Filamu za Kiswahili ni Miongoni mwa Filamu zinazopendwa sana katika nchi za Afrika Mashariki si kutokana na kuwa zinatumia lugha adhimu ya Kiswahili tu bali pia ni kutokana na Maudhui na upekee zilionao. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Nyumba ya Sanaa akiangazia Sanaa hii na changamoto zinazowakabili Waigizaji nchini Tanzania
Katika Makala haya Tunaangazia Muziki na Cocodo African Music Band wakifanya sanaa ya Muziki kutoka nchini Tanzania Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Lemi na Nelius wakizungumzia Safari yao ya kimuziki katika Sehemu hii ya kwanza.
Hii ni Sehemu ya Pili ya Makala haya tukiangazia Muziki na Cocodo African Music Band wakifanya sanaa ya Muziki kutoka nchini Tanzania Ungana na Steven Mumbi akizungumza na wasanii Remi na Nelius wakizungumzia safari yao ya kimuziki kwa zaidi ya miaka nane sasa
Teknolojia ina athari gani katika Utunzi wa Vitabu? Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Clement Mubanga Mtunzi wa vitabu katika Makala ya Nyumba ya sanaa.
Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Wasikilizaji kupata mitizamo yao baada ya Tume ya Uchaguzi nchini Nigeria kutangaza matokeo ya awali huku Mgombea wa Upinzani PDP akipinga nako Nchini Senegal Mgombea wa chama Tawala ajitangaza Mshindi.
Utotoni mwake Lucky Phillip Dube alilelewa sana na bibi yake kutokana na mama yake kufanya kazi nje ya mahali ambapo wanaishiili aweze kumudu maisha, Katika maisha yake Lucky Dube hakuwahi kumjua baba yake. Ungana na Steven Mumbi katika Makala ya Muziki Ijumaa,akiangazia Maisha yake ya Kimuziki.
Sanaa ya Ubinufu ndio sanaa mama katika Uchoraji,Uchongaji na hata katika matumizi ya vyuma chakavu katika kuunda Vifaa mbalimbali. Katika Makala ya Nyumba ya Sanaa Ungana na Steven Mumbi akizungumzuza na Mhadhiri wa Chuo kikuu cha Dar es salaam UDSM, Safina Kimbokota wakizungumza Sanaa hiyo na Mapokeo ya wanafunzi kusoma Sanaa katika elimu ya juu.
Sisi Tambala Bendi ni Bendi ya Muziki wa Asili kutoka Tanzania, iliundwa mwaka 1997, tayari imefanya maonesho ya jukwaani katika Nchi Mbalimbali Duniani ikiwa ni pamoja na nchi za Ulaya, Asia na Afrika. Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Kiongozi wa Bendi hiyo Nanjuja Nanjuja pamoja na wasanii wanaounda bendi hiyo katika Makala ya Nyumba ya Sanaa wakizungumzia Mfanikio yao kimuziki.
Sanaa ya Muziki inaendelea kukua kila kukicha nchini DRC, Katika Mji wa Goma sanaa hii inasonga mbele licha ya changamoto zilizopo, anatarajia kushirikiana na wasanii wa nchi za Kenya na Tanzania katika nyimbo zake. Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Belamy Paluku katika Makala ya Nyumba ya Sanaa.
Brenda Nokuzola Fassie , alizaliwa Novemba 3, 1964 huko Langa Cape Town nchini Afrika Kusini, akiwa mtoto wa mwisho wa familia yenye watoto 8,amefanya Muziki kwa kiwango cha juu Barani Afrika na kupata umaarufu Mkubwa Duniani. Ungana na Steven Mumbi katika Mkala ya Muziki Ijumaa kuangazia Safari yake ya Kimuziki.