Podcasts about jamhuri

  • 39PODCASTS
  • 754EPISODES
  • 12mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • Jul 14, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about jamhuri

Latest podcast episodes about jamhuri

Habari za UN
Ituri - Aweka silaha pembeni na kubeba nyavu za samaki

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 14, 2025 1:41


Kutoka msituni kupigana upande wa waasi hadi kuingia ziwani na kuwa mtaalamu wa ufugaji wa samaki, ndio simulizi tunayopata kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, simulizi ya matumaini kwa mustakabali wa jamii iliyogubikwa na vita kila uchao. Mwenyeji wako ni Sharon Jebichii.

Habari za UN
14 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 14, 2025 9:51


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya malengo ya maendeleo endelevu, na mradi wa uvuvi unaosaidia kupunguza migogoro Ituri DRC. Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Jukwaa la Kisiasa la Ngazi ya Juu la Maendeleo Endelevu, HLPF la mwaka huu wa 2025 limeanza leo hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ambapo wadau kutoka katika nyanja mbalimbali duniani wanakutana kujadili namna ya kuharakisha utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs.Kutoka msituni kupigana upande wa waasi hadi kuingia ziwani na kuwa mtaalamu wa ufugaji wa samaki, ndio simulizi tunayopata kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, simulizi ya matumaini kwa mustakabali wa jamii iliyogubikwa na vita kila uchao.Katika makala tunakupeleka mkoani Mwanza, kaskazini-magharibi mwa Tanzania ambako kuelekea siku ya kimataifa ya vijana na stadi hapo kesho Julai 15, Sabrina Said anazungumza na mmoja wa vijana  anayetumia majukwaa ya kidijitali kutoa elimu ya      uelimishaji rika.Na kaika mashinani leo fursa ni yake Imam Ustaadhi Matano Bin Salim kutoka Kaunti ya Mombasa nchini Kenya, ambaye amewezesha shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kufika kwenye kituo cha mafunzo ya dini kupatia watoto chanjo. Akisema typhoid ni homa ya tumbo, na measles ni ugonjwa wa surua.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Wanawake wapatanishi warejesha maelewano baina ya jamii Ituri nchini DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 11, 2025 1:51


Huko Djugu, jimboni Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wanawake wapatanishi waliopatiwa mafunzo na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO, wamewezesha kurejea kwa mazungumzo baina ya jamii za Ezekere na Mandro ambazo kwa miaka kadhaa zilikuwa zinazozana. Sabrina Saidi na maelezo zaidi.

Habari za UN
11 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 11, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya afya nchini Burundi, na elimu ya upatanishi kwa jamii Ituri nchini DRC. Makala tunakupeleka nchini Kenya kumulika kilimo kichopatia riziki jamii na mashinani tunasalia hapa makao makuu kusikia ujumbe kuhusu haki za wasichana.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) leo Julai 11 limetangaza kwamba limeidhinisha Burundi kuwa imefanikiwa kuoandoa ugonjwa wa macho unaofahamika kama trakoma au vikope kama tatizo la kiafya la umma, na kuifanya kuwa nchi ya nane katika Kanda ya Afrika ya WHO kufikia mafanikio haya muhimu.Huko Djugu, jimboni Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wanawake wapatanishi waliopatiwa mafunzo na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO, wamewezesha kurejea kwa mazungumzo baina ya jamii za Ezekere na Mandro ambazo kwa miaka kadhaa zilikuwa zinazozana.Katika makala Sharon Jebichii anatupeleka  Kaunti ya Tana River huko Kenya kumulika juhudi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kitaifa ya Kusimamia Ukame (NDMA) na Serikali za Kaunti katika kilimo, ambayo imeleta mabadiliko na matumaini kwa jamii za wakulima.Na kaika mashinani leo ikiwa siku ya idadi ya watu duniani, nampisha Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na AFya ya Uzazi, Dkt. Natalia Kanem akizungumzia umuhimu wa takwimu katika kuboresha maisha ya wakazi wa dunia!Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
10 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 10, 2025 10:36


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kushuhudia mafunzo ya ukufunzi kwa wanadhimu wa Umoja wa Mataifa. Pia tunakuletea muhtasari wa habari zikiwemo za mkataba wa amani DRC na Rwanda, UKIMWI, na maadhimisho ya Siku ya kimataifa ya Kiswahili, na uchambuzi wa neno.Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wamekaribisha mkataba wa amani kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Rwanda uliotiwa saini tarehe 27 mwezi uliopita wa Juni, huku wakishukuru Marekani, Qatar na Muungano wa Afrika kwa juhudi za usuluhishi.Ukata uliosababishwa na wahisani kukata au kupunguza ghafla na kwa kiasi kikubwa ufadhili kwenye miradi ya kupambana na UKIMWI umekuwa na madhara kwa nchi zilizoathiriwa vibaya na ugonjwa huo, imesema ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na Ukimwi, UNAIDS.Leo kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Nairobi, Kenya kumefanyika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya lugha ya Kiswahili ambapo wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Juu ya Mangu wametuma ujumbe wao wa umuhimu wa lugha hiyo kupitia ngonjera.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno "CHARAKAMU na BARAKALA!Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
09 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 9, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia ziara ya Katibu Mkuu wa UN Amina J. Mohammed akiwa barani Afrika; na Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Viongozi kuhusu Upashanaji wa Taarifa duniani. Makala tunakwenda nchini Burundi na mashinanitunasalia hapa makao makuu, kulikoni?Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed akiwa ziarani barani Afrika ambapo juzi tarehe 7 aliingia nchini Gambia, kwa njia ya mtandao wa X ameonesha namna ziara yake ilivyokuwa ya mafanikio kwa kukutana na viongozi na wadau mbalimbali nchini humo katika harakati za kufanikisha Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu.Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Viongozi kuhusu Upashanaji wa Taarifa duniani, (WSIS) ukiingia siku ya 3 hii leo huko Geneva, Uswisi, washiriki wanapazia sauti umuhimu wa kila mtu kokote pale aliko afikiwe na teknolojia inayomwezesha kupokea taarifa kwa urahisi, usahihi na kwa haraka.Katika makala shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA), kwa kushirikiana na serikali ya Burundi, limekuwa mstari wa mbele katika kuwasaidia vijana wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), walioko kwenye kambi ya Musenyi, mkoani Rutana huko Burundi. Kupitia michezo, tamaduni, na shughuli za elimu ya afya ya uzazi, vijana hawa wamepata matumaini mapya na fursa ya kujenga maisha yao upya. Mradi huu unaangazia umuhimu wa kuwekeza kwa vijana walioko katika mazingira magumu ili kuwasaidia kufikia ndoto zao.Na katika mashinani fursa ni yake Dkt. Natalia Kanem, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA ambaye katika mahojiano maalum na Idhaa ya Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa kila msichana anahitaji huduma muhimu za afya uzazi ili waweze kuendelea na elimu, akitaja mfano wa kazi zao nchini Kenya.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Mradi wa UNFPA wa michezo na elimu warejesha matumaini kwa vijana wakimbizi wa DRC nchini Burundi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 9, 2025 3:11


Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA), kwa kushirikiana na serikali ya Burundi, limekuwa mstari wa mbele katika kuwasaidia vijana wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), walioko kwenye kambi ya Musenyi, mkoani Rutana huko Burundi. Kupitia michezo, tamaduni, na shughuli za elimu ya afya ya uzazi, vijana hawa wamepata matumaini mapya na fursa ya kujenga maisha yao upya. Mradi huu unaangazia umuhimu wa kuwekeza kwa vijana walioko katika mazingira magumu ili kuwasaidia kufikia ndoto zao.

Wimbi la Siasa
Je, mkataba kati ya DRC na Rwanda utaleta amani ya kudumu ?

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Jul 2, 2025 10:19


Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Rwanda, walitia saini mkataba wa amani, chini ya uangalizi wa Marekani, Juni Juni 27 2025, jijini Washington DC, unaolenga kurejesha amani ya kudumu Mashariki mwa DRC. Nchi hizo mbili zimekubaliana kushirikiana kuyaondoa makundi yenye silaha. Mkataba huu umepokelewa vipi nchini DRC ?

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Maandamano mapya yaua 16 Kenya, DRC na Rwanda zasaini makubaliano ya amani

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Jun 28, 2025 20:13


Wiki hii ulimwengu umeshuhudia matukio mengi ya ajabu na hatari sana kwa usalama wa nchi mbali mbali, kwanza nchini Kenya watu 16 waliuawa katika maandamano ya kuadhimisha mwaka mmoja wa mauaji ya vijana Gen Z, Rwanda na DRC zatia saini mkataba wa amani kumaliza vita vya mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, siasa za Chad, Zambia na pia mashambulizi kati ya Israeli na Iran, pamoja na mkutano wa jumuia ya NATO..na mengine mengi

Gurudumu la Uchumi
Utakatishaji Fedha: Kenya yawekwa kwenye orodha ya nchi zilizo na changamoto, Uganda ikiondolewa.

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Jun 26, 2025 10:00


Mwezi Juni mwaka 2025, Tume ya Ulaya iliorodhesha Kenya miongoni mwa nchi zenye changamoto ya utakatishaji wa fedha, huku Uganda ikipata afueni kwa kuondolewa kwenye orodha hiyo. Hatua hii ina maana kuwa mashirika ya kifedha – ikiwemo benki – zinalazimika kuzingatia kwa makini uhusiano wa kibiashara na miamala yoyote inayohusiana na nchi zilizo kwenye orodha hiyo, na kuchukua hatua kali za udhibiti wa fedha. Nchi nyingine katika orodha hiyo ni pamoja na Sudan Kusini, Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Msumbiji, Nigeria, Afrika Kusini, na zingine. Katika Makala haya, Gurudumu la Uchumi, tunachambua hatua hii na athari zake kwa uchumi, lakini pia nini mamlaka katika nchi hizo zinaweza kufanya hili kujiondoa kwenye orodha hiyo.

Gurudumu la Uchumi
Utakatishaji Fedha: Kenya yawekwa kwenye orodha ya nchi zilizo na changamoto, Uganda ikiondolewa.

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Jun 26, 2025 10:00


Mwezi Juni mwaka 2025, Tume ya Ulaya iliorodhesha Kenya miongoni mwa nchi zenye changamoto ya utakatishaji wa fedha, huku Uganda ikipata afueni kwa kuondolewa kwenye orodha hiyo. Hatua hii ina maana kuwa mashirika ya kifedha – ikiwemo benki – zinalazimika kuzingatia kwa makini uhusiano wa kibiashara na miamala yoyote inayohusiana na nchi zilizo kwenye orodha hiyo, na kuchukua hatua kali za udhibiti wa fedha. Nchi nyingine katika orodha hiyo ni pamoja na Sudan Kusini, Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Msumbiji, Nigeria, Afrika Kusini, na zingine. Katika Makala haya, Gurudumu la Uchumi, tunachambua hatua hii na athari zake kwa uchumi, lakini pia nini mamlaka katika nchi hizo zinaweza kufanya hili kujiondoa kwenye orodha hiyo.

Habari za UN
20 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 20, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia siku ya Wakimbizi Duniani, mwaka huu ikibeba maudhui “Mshinamano na wakimbizi”, tukisikia ujumbe wa Umoja wa Mataifa na kazi wanazozifanya kuinua Maisha ya wakimbizi, na pia tunakuletea sauti za wakimbizi kutoka DRC, Burundi, Ethiopia na Sudan Kusini.Leo ni Siku ya Wakimbizi Duniani, mwaka huu ikibeba maudhui “Mshinamano na wakimbizi” na Umoja wa Mataifa umetaka mshikamano huo kwa vitendo wakati idadi ya watu wanaolazimika kufungasha virago na kukimbia makayo yao ikifikia kiwango cha kihistoria.Tukisalia na siku ya wakimbizi duniani tunaelekea  eneo la Mata, karibu na mpaka wa Ethiopia na Sudan Kusini, ambakomaelfu ya wakimbizi kutoka Sudan Kusini wanapokea msaada wa dharura kupitia juhudi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP. unaolenga kuwalinda baada ya kukimbia  mapigano makali nchini mwao. Nyibol Chueny Puok, mama wa watoto 4 ni miongoni mwao.Katika makala Assumpta Massoi kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR anakupeleka Kusini-Magharibi mwa Burundi kwenye kituo cha wakimbizi cha Musenyi kumsikia mkimbizi kutoka DRC ambaye ananufaika na kauli mbiu ya siku ya wakimbizi mwaka huu ya Mshikamano na Wakimbizi.Na mashianani tukisalia na siku ya wakimbizi duniani, tutakwenda nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kumsikia mtoto mkimbizi ambaye alitumikishwa katika vita na waasi wenye silaha.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Burundi yamwezesha mkimbizi fundi seremala kutoka DRC kuendeleza stadi yake na kujipatia kipato

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 20, 2025 3:21


Burundi inaonesha kwa vitendo mshikamano na wakimbizi kwa kuwapa fursa ya kupata elimu, huduma za afya, ajira na huduma nyingine za kitaifa, na hivyo kuwasaidia kuchangia katika jamii wanamoishi. Miongoni mwa wakimbizi hao ni Amani Lukoo Elie kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akiambana na mke wake na watoto 5 wamesaka hifadhi kusini-magharibi baada ya kukimbia mapigano jimboni Kivu Kaskazini. Kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, Assumpta Massoi amefuatilia kile wanachofanya sasa ili kuweza kujikimu.

Habari RFI-Ki
MAONI: DRC na Rwanda zitie saini makubaliano kumaliza mauaji ya raia

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Jun 20, 2025 10:02


Kila siku ya Ijumaa, hapa RFI Kiswahili, tunampa mskilizaji wetu nafasi kuzungumzia habari kuu ambazo tumekuwa nazo wiki hii au kutueleza jambo lolote ambalo limetokea nchini mwake. Wiki hii maoni mseto yameangazia, miongoni mwa taarifa zingine, tangazo kwamba Rwanda itatia saini makubaliano na DRC tarehe 27 Juni, kumaliza mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, lakini pia mashambulio baina ya Israeli na Iran.

Habari RFI-Ki
MAONI: DRC na Rwanda zitie saini makubaliano kumaliza mauaji ya raia

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Jun 20, 2025 10:02


Kila siku ya Ijumaa, hapa RFI Kiswahili, tunampa mskilizaji wetu nafasi kuzungumzia habari kuu ambazo tumekuwa nazo wiki hii au kutueleza jambo lolote ambalo limetokea nchini mwake. Wiki hii maoni mseto yameangazia, miongoni mwa taarifa zingine, tangazo kwamba Rwanda itatia saini makubaliano na DRC tarehe 27 Juni, kumaliza mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, lakini pia mashambulio baina ya Israeli na Iran.

Habari za UN
UNDP yaomba msaada kusaidia wakimbizi wa ndani kujikwamua mashariki mwa DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 16, 2025 1:58


Huko jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, juhudi za kidiplomasia zinaendelea kumaliza mapigano, huko nalo shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP likitoa wito wa msaada kwa watu waliofurushwa makwao kutokana na mashambulizi ya waasi wa M23, msaada ambao utawasaidia kujenga upya maisha yao na njia zao za kujipatia riziki. Sharon Jebichii na taarifa zaidi

Habari za UN
16 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 16, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia baa la njaa katika nchi 13 duniania amabzo hakuna uhakika wa chakula, na hali ya kibinadamu kwa wakimbizi wa DRC. Makala tunasalia hapa makao makuu na mashinani tunakwenda nchini Nepal, kulikoni?Ripoti mpya ya pamoja ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo jijini Roma, Italia inatahadharisha kuwa watu katika nchi 5 kati ya nchi 13 zenye njaa duniani wako kwenye hatari kubwa ya kukumbwa na njaa kali, vifo na maafa ikiwa msaada wa kibinadamu hautatolewa haraka na juhudi za kimataifa hazitaelekezwa kukomesha migogoro, kupunguza ufurushwaji na kuongeza msaada wa haraka kwa kiwango kikubwa.Huko jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, juhudi za kidiplomasia zinaendelea kumaliza mapigano, huko nalo shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP likitoa wito wa msaada kwa watu waliofurushwa makwao kutokana na mashambulizi ya waasi wa M23, msaada ambao utawasaidia kujenga upya maisha yao na njia zao za kujipatia riziki.  Katika makala leo Flora Nducha wa Idhaa hii amemuuliza Amon Anastaz Mpanju, Naibu Katibu Mkuu wizara ya Maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake na makundi maalum nchini Tanzania aliyeshiriki mkutano wa 18 wa mkataba wa watu wenye ulemavu COSP18 uliokunja jamvi mwishoni mwa wiki nini kikubwa alichotoka nacho kwenye mkutano huo.Na katika mashinani leo ikiwa ni siku ya Kimataifa ya utumaji fedha kwa familia kutoka ughaibuni, fursa ni yake Bibha kutoka Chinnamastrial nchini Nepal, mnufaika wa utumaji fedha kutoka wanafamilia walioko ughaibuni akielezea jinsi ambavyo fedha hizo zinavyosaidia jamii zake kuondokana na umaskini.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Mashambulizi ya Israeli dhidi ya Iran, yalaaniwa vikali na UN..

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 13, 2025 2:12


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amelaani mashambulizi ya kijeshi yaliyofanywa na Israel dhidi ya vituo vya nyuklia vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, akionya juu ya hatari ya kuongezeka kwa mvutano katika eneo la Mashariki ya Kati huku mkuu wa wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki (IAEA), Rafael Mariano Grossi amesema wanafanya tathimini athari za mashambulizi hayo katika vinu vya nyuklia Iran. Sharon Jebichi na taarifa kamili

Habari za UN
Pamoja na ulinzi wa raia, walinda amani wa UN Ituri waendesha kampeni ya afya..

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 13, 2025 1:48


Huko jimboni Ituri, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Bangladesh wameendesha kampeni ya afya na kusaidia wakimbizi wa ndani kupata matibabu katika eneo hilo lililogubikwa na mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa waasi. Assumpta Massoi anasimulia zaidi.

Habari za UN
13 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 13, 2025 11:07


Katika Jarida la Umoja wa Mataifa leo Flora Nducha anakuleteaUmoja wa Mataifa walaani vikali mashambulizi ya Israel dhidi ya vinu vya nyuklia Jamhuri ya IranHuko Ituri Mashariki mwa DRC walinda amani wa Mpango wa Umoja wa Mataifa MONUSCO watoa huduma za afya kwa wananchiLeo ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu watu wenye Ualibino katika makala utamsikia mbunge kmwenye ualibino kutoka nchini TanzaniaNa mashinani utasiki ujumbe wa nini kifanyike kuhakikisha ndoto za watu wenye ulemavu zinatimia Afrika

Habari za UN
11 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 11, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia ajali mbayá ya meli katika pwani ya Djibouti lililokuwa linabeba wahamiaji wengi. Pia tunasalia hapa makao makuu ambapo Kikao cha 18 cha Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu wenye Ulemavu COSP18. Mashinani tutakwenda nchini DRC.Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, (IOM) kwa ushirikiano wa karibu na mamlaka za Djibouti, linaongeza juhudi zake za kibinadamu kufuatia tukio la kusikitisha lililotokea pwani ya Djibouti ambapo takriban wahamiaji wanane walikufa maji na wengine 22 hawajulikani walipo.Katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Kikao cha 18 cha Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu wenye Ulemavu COSP18, kinaendelea na mwaka huu, mada kuu ni kuongeza uelewa wa haki na mchango wa watu wenye ulemavu katika maendeleo ya kijamii. Miongoni mwa washiriki ni ya kijana kutoka Louisiana, hapa  Marekani.Makala tutasalia hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani ambapo Kikao cha 18 cha Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu wenye Ulemavu COSP18, kinaendelea na tutamsikiliza mmoja wa washiriki wa mkutano huu Bongani Simphiwe Makama kutoka Ufalme wa Eswatini ambaye amepata nafasi ya kuzungumza na idhaa ya Kiswahili.Na katika mashinani fursa ni yake fursa ni yake Byamungu Rukera, Mwakilishi wa watu waliokimbia makazi yao huko Sake, Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC akipazia sauti wakimbizi wenzake kwa wafanyakazi wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu na misaada ya dharura OCHA ambao wanawagawia chakula licha ya uhaba wa msaada huo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
04 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 4, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia haki za jamii za Ogiek nchini Kenya, na masuala ya baharí na tabianchi. Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kulikoni?Mtaalamu wa UN ataka kusitishwa mara moja kwa uwekaji  mipaka unaotishia haki za Waogiek Kenya. Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa ameitaka Serikali ya Kenya kusitisha mara moja shughuli za uwekaji mipaka katika Msitu wa Mau Mashariki nchini humo, akisema kuwa unakiuka haki za jamii ya asili ya Waogiek na kupuuza maamuzi ya lazima ya Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (AfCHPR).Mkutano wa siku mbili kuhusu Ubia wa Kimataifa kwa ajili ya dunia endelevu umekunja jamvi huko Hamburg nchini Ujerumani ambako Balozi wa Mabadiliok ya Tabianchi wa Vijana wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini Tanzania, Madina Jubilate Kimaro ameshiriki. Akiwa huko Hamburg nimemuuliza Madina ni kipi amejulisha washiriki wenzake kuwa kinapaswa kufanyika ili dunia iwe endelevu?.Makala, katika kuelekea mkutano wa tatu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Bahari (UNOC3) utakaofanyika  mjini Nice, Ufaransa, kuanzia tarehe 9 hadi 13 Juni 2025 ukijikita na maudhui "Kuharakisha hatua na kuhamasisha wadau wote kuhifadhi na kutumia bahari kwa njia endelevu", tunaelekea nchini Tanzania kwa Clara Makenya Mkuu wa ofisi ya Shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP nchini humo na afisa mawasiliano wa shirika hilo kwa ajili ya Namibia, akizungumza na kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini Tanzania UNIC Dar es salaam anaeeleza nini kinapaswa kufanywa na jamii ya kitaifa na kimataifa ili kutekeleza azma ya mkutano huo.Na katika mashinani Debora, mkazi wa Sake jimboni Kivu Kaskazini, mashariki mwa DRC, aliyekimbilia mji wa Goma jimboni humo humo kutokana na machafuko sasa amerejea tena Sake ambako wanapatiwa msaada wa chakula kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP. Akisema PAM anamaanisha WFP.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
03 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 3, 2025 10:46


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kinainayomulika kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi katika kaunti kama Kajiado, Kenya, ambayo jamii hukumbwa na hali ya ukame na mazingira magumu, mabadiliko chanya yanaonekana.Mustakabali wa mzingiro wa Israeli kwenye eneo la Palestina la Gaza inalokalia kimabavu ukiendelea kukumbwa na sintofahamu, wanawake na wasichana wamesimulia adha ya ukosefu taulo za kike wakati wanapokuwa kwenye hedhi huku upatikanaji wa maji ukiwa ni wa taabu.Idadi ya wakazi wa nchi zenye maendeleo duni, LDCs na zile za visiwa vidogo, SIDS  wanaopata huduma zilizoboreshwa au za kisasa za maonyo ya mapema kabla ya majanga imefikia takribani milioni 400 na hii ni kutokana na programu ya CREWS iliyoanzishwa mwaka 2015 na shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa, WMO.Rebecca Kalonji, al maaruf Sista Becky, mwimbaji chipukizi wa mtindo wa kufokafoka kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hii leo ametangazwa kuwa Muungano Mkono wa Ngazi ya Juu wa masuala ya lishe na ulaji wenye afya wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP katika taifa hilo la Maziwa Makuu. Watu milioni 28 wakikabiliwa na njaa kali nchini mwake, Sista Becky amesema atatumia sauti na kazi yake kupatia vijana changamoto ya sio tu kupaza sauti zao bali pia kuchukua hatua kwenye masuala nyeti yanayogusa mustakabali wao ikiwemo kupata lishe bora na fursa bora kwa wanawake na Watoto wa kike.Na katika mashinani fursa ni yake Christiana, mama wa watoto sita ambaye ni mwathirika wa mashambulizi ya hivi majuzi ya waasi wenye silaha katika wilaya za Mirebalais na Saut-d'Eau yaliyosababisha watu wengi kuyahama makazi yao. Anasema ana matumaini kwani Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto, UNICEF limewapelekea huduma za afya kupitia kniki tembezi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Licha ya ukata UNICEF yajitahidi watoto nchini DRC warejee shuleni

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 30, 2025 2:09


Wakati ghasia zinazoendelea huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC zinaripotiwa kusababisha zaidi ya watoto milioni 1.8 kutokuweko shuleni, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF nchini humo linajitahidi kwa udi na uvumba kuhakikisha watoto wanapata elimu kwani ni haki yao ya msingi. Je ni kwa vipi? Anold Kayanda anasimulia zaidi.

Habari za UN
30 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 30, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya elimu kwa watoto mashariki mwa DRC na Mkutano wa pili wa Baraza Kuu la Makazi la shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani UNHABITAT unaofunga pazia leo jijini Nairobi Kenya. Makala inaturejesha nchini DRC na mashinani inatupeleka katika bonde la Ziwa Victoria, kulikoni?Wakati ghasia zinazoendelea huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC zinaripotiwa kusababisha zaidi ya watoto milioni 1.8 kutokuweko shuleni, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF nchini humo linajitahidi kwa udi na uvumba kuhakikisha watoto wanapata elimu kwani ni haki yao ya msingi.Mkutano wa pili wa siku mbili wa Baraza Kuu la Makazi la shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani UNHABITAT leo unafunga pazia jijini Nairobi Kenya. Baraza hilo linalofanyika kila baada ya miaka minne ni chombo cha juu kabisa duniani cha kufanya maamuzi kuhusu maendeleo ya miji endelevu na limewaleta pamoja wawakilishi kutoka nchi zote 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa pamoja na wadau mbalimbali wa amendeleo ya miji.Makala inakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususan jimboni Kivu Kaskazini katika kitongoji cha Mavivi kuwasikia walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania,kikosi cha 11, TANZBATT11, wanaohudumu katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO wakielezea sio tu majukumu yao, bali pia wanajivunia kile wanachofanya kwa kuzingatia Mei 29 imeadhimishwa siku ya kimataifa ya walinda amani.Na katika fursa ni yake Mhandisi Coletha Ruhamya, Naibu Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria, Mradi unaofanikishwa na Benki ya Dunia ambao unakabiliana na masuala ya usafi wa mazingira katika ziwa hilo. Anaeleza umuhimu wa usimamizi endelevu wa bonde hilo kote nchini Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda na Burundi chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
29 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 29, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa ikitupeleka nchini DRC, Sierra Leone na Ghana. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na maana ya neno "MISHEMISHE.”Leo ni Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani ambayo mwaka huu inajikita na maudhui ya “mustakabali wa ulinzi wa amani.”Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema walinda amani wa Umoja wa Matafa wako katika changamoto kubwa “Leo hii, walinda amani wanakabiliwa na hali zinazozidi kuwa ngumu katika dunia inayozidi kuwa na changamoto, ikiwemo uugawanyika na kutofautiana kwa mitazamo duniani kunazidi kuongezeka, operesheni za ulinzi wa amani zinakabiliwa, hatari zaidi kutokana na wingi wa vitisho kama vile ugaidi na walinda amani kulengwa kwa makusudi kupitia taarifa potofu zenye madhara makubwa na changamoto zinazovuka mipaka kuanzia janga la mabadiliko ya tabianchi hadi uhalifu wa kimataifa.Kikosi cha 11 cha Tanzania kinachohudumu chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO kimeungana na walinda amani wengine kuadhimisha Siku ya Walinda Amani Duniani. Maadhimisho hayo yamefanyika Mavivi, yakiongozwa na Brigedia Jenerali Diamond Meshack Madie, Mnadhimu Mkuu wa Vikosi vya MONUSCO.Shirika la Umja wa Mataifa la Mazingira UNEP limezindua mpango mpya wa dola milioni 15 kusaidia uwekezaji endelevu katika Bonde la Kongo – moja ya mifumo muhimu zaidi ya ikolojia duniani. Mpango huu unalenga kufungua fursa za biashara rafiki kwa mazingira kwa wajasiriamali wadogo na wa kati katika sekta za kijani. Msitu wa mvua wa Bonde la Kongo ni moja ya vyanzo vikubwa vya kaboni duniani na ni makazi ya watu zaidi ya milioni 75, wakiwemo jamii za asili.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi  Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "MISHEMISHE.”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
28 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 28, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia haki za binadamu nchini Ukraine na upatikanaji wa elimu nchini Kenya. Makala tunakupeleka nchini Sudan Kusini, na amashinani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kulikoni?Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya Uchunguzi kuhusu Ukraine imehitimisha kwamba vikosi vya kijeshi vya Urusi vimetenda uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu, hasa mauaji, kupitia mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (drones) yaliyoelekezwa dhidi ya raia.Mradi wa "operesheni rejea shuleni" unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF kwa ushirikiano na wizara ya elimu ya Kenya, shirika liliso la kiserikali la Hapag Lloyd na wadau wengine kwa kuzipa fedha familia zisizojiweza kuendesha shughuli za kiuchumi, umerejesha mautumaini ya elimu kwa mamia ya watoto katika Kaunti ya Kwale Pwani ya Kenya  ambao waliacha shule sababu ya umasikini.  Katika makala ikielekea siku ya walinda amani kesho Mei 29, tunamulika harakati za walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini SUdan Kusini za kulinda raia na mwenyeji wako katika makala hii iliyoandaliwa kupitia video ya ujumbe wa  Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani Sudan Kusini, UNMISS ni Sharon Jebichii.Na katika mashinani huku machafuko yakiendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, wafanyakazi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR wako mashinani mjini Goma na maeneo mengine yaliyoathirika ili kutoa msaada muhimu, ikiwa ni pamoja na kufanikisha nia ya wakimbizi wanaorejea nchini mwao Rwanda. Raab na Ruusi ni baadhi yao.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
20 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 20, 2025 12:20


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika wafugaji wa nyuki nchini Tanzania leo ikiwa ni siku ya nyuki duniani iliyopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 20 Desemba mwaka 2017 kupitia azimio namba A/72/211.Baada ya miaka mitatu ya majadiliano, leo katika Mkutano wa Kimataifa wa Afya unaoendelea Geneva, Uswisi, nchi zimepitisha rasmi makubaliano ya kihistoria ya kuzuia, kujiandaa, na kukabiliana vyema na majanga ya magonjwa kwa siku zijazo. Taratibu zote zitakapopitishwa na angalau nchi 60, mkataba utaanza kutumika rasmi mwakani.Kutokana na mamlaka za Israeli kulegeza kwa muda mzingiro uliodumu kwa wiki 11, angalau sasa matumaini kidogo yamerejea Gaza, yameeleza leo mashirika ya Umoja wa Mataifa. Msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya dharura, OCHA, Jens Laerke amesema tayari wamepata ruhusa ya kuyavusha malori matano yaliyokuwa yamezuiliwa jana.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP limetahadharisha  leo kwamba bila ufadhili zaidi, huenda katika muda wa wiki chache zijazo likalazimika kusitisha msaada wa chakula kwa takribani nusu ya watu linaowahudumia kwa sasa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.Na katika mashinani, fursa ni yake Hanan Al-Dayya, Mkimbizi wa ndani katika ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli, akisimulia  madhara ya mashambulizi yanayoendelea kutoka Israeli.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
16 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 16, 2025 12:25


Hii leo jaridani tunaangazia uhakika wa chakula, na takwimu za afya za janga la COVID-19 kusababisha vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla. Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani nchini DRC, kulikoni?Ukosefu wa uhakika wa kupata chakula na utapiamlo kwa watoto uliongezeka kwa mwaka wa sita mfululizo mwaka 2024, na kuwatumbukiza mamilioni ya watu karibu na baa la njaa, huku wengine wakiepuka kutokana na misaada ya kimkakati. Imesema Ripoti ya Kimataifa kuhusu Janga la Chakula (GRFC) iliyotolewa leo huko Roma, Italia na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO.Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) ya takwimu za afya duniani iliyochapishwa jana Mei 15 ikionesha athari kubwa zaidi za kiafya zilizosababishwa na janga la COVID-19 kuhusu vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla, imeweka wazi kuwa katika kipindi cha miaka miwili pekee, kati ya mwaka 2019 na 2021, matarajio ya kuishi yalipungua kwa mwaka mmoja na miezi nane  ikiwa ni maporomoko makubwa zaidi katika historia ya hivi karibuni hali iliyobatilisha mafanikio ya afya yaliyopatikana kwa muongo mmoja.Katika makala Leah Mushi anatupeleka nchini Tanzania kusikia namna wanawake wenye ulemavu walivyoweza kujikwamua kutoka kwenye changamoto mbalimbali ikiwemo za kiuchumi na kuchangamkia fursa za uongozi.Na katika fursa ni yake Bernadette Kambonesa, mkimbizi wa ndani kutoka kijiji cha Bogoro, jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akizungumzia manufaa yatokanayo na uwepo wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini humo (MONUSCO).Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Nyumba yetu ilivamiwa na tulilazimika kukimbia hadi hapa Burundi – Mkimbizi Charles

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 14, 2025 4:43


Mapigano yanayoendelea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, yamesababisha zaidi ya watu 70,000 kukimbia makazi yao na kuvuka mpaka kuingia nchi jirani ya Burundi wakitafuta usalama.

Habari za UN
05 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 5, 2025 10:52


Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya kimataifa ya wakunga na kazi zao muhumi, na mafunzo ya jerahani kwa wakimbizi wa ndani nchini DRC. Makala tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa na mashinani tunakwenda Gaza.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya wakunga, tunakwenda nchini Tanzania kummulika mkunga ambaye alinusuru maisha ya wajawazito wawili wakati wa mafuriko makubwa ya Novemba 2023 wilayani Hanang, mkoani Manyara, kaskazini mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, ikiwa ni ushuhuda wa majukumu mazito yanayokumba wakunga.Wanawake 125 katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Kigonze, karibu na Bunia, mji mkuu wa jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ambako ghasia huripokiwa mara kwa mara, sasa wana matumaini mapya ya kujikwamua kiuchumi baada ya kujiunga na mradi wa mafunzo ya kushona nguo unaofadhiliwa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini humo (MONUSCO).Makala Assumpta Massoi anamulika uzinduzi wa mtandao wa Mashirika ya Manusura wa Ugaidi duniani,  VoTAN      uliofanyika wiki iliyopita hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa.Na mashinani kupitia video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM), fursa ni yake Rawhiyeh, mkimbizi kutoka Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israel ambaye anasimulia kwa uchungu madhila yanayowakumba yeye na familia yake baada ya kupoteza makazi yao kutokana na mashambulizi ya mabomu.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
MONUSCO yapatia wanawake wakimbizi DRC mafunzo ya ushoni

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 5, 2025 2:31


Wanawake 125 katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Kigonze, karibu na Bunia, mji mkuu wa jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ambako ghasia huripokiwa mara kwa mara, sasa wana matumaini mapya ya kujikwamua kiuchumi baada ya kujiunga na mradi wa mafunzo ya kushona nguo unaofadhiliwa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini humo (MONUSCO). Sharon Jebichii na taarifa kamili.

Habari za UN
Walinda amani wa UN kutoka Bangladeshi na Indonesia wapewa medali nchini DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 30, 2025 1:49


Huko Bunia, mji mkuu wa jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, walinda amani kutoka Bangladesh na Indonesia, wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO wamepatiwa medali kwa mchango wao wa ulinzi wa raia, moja ya jukumu kubwa la ujumbe huo. Assumpta Masso amefuatilia hafla hiyo na kuandaa ripoti hii.

Habari za UN
30 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 30, 2025 11:14


Hii leo jaridani tunaangazia ugonjwa wa mpox, na walinda amabini wa Umoja wa Mataifa nchini DR Congo. Makala inamuulika siku siku ya kimataifa ya muziki wa Jazz namashinani tunasalia hapa makao maku kusikia ujumbe wa mwakilishi wa shirika la watu wa jamii za Asili.Maambukizi ya ugonjwa wa mpox kutokana na aina ya virusi vya monkeypox clade Ib /ˈmʌŋ.ki.pɑks kleɪd one bee/ (MPXV) yanaendelea kuripotiwa hasa barani Afrika, ambapo mataifa kumi na moja yameripoti maambukizi ya ndani ya jamii katika kipindi cha wiki sita zilizopita. Hiyo kwa mujibu wa ripoti 51 ya Shrika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO kuhusu hali ya mlipuko wa mpox katika nchi mbalimbali duniani.Huko Bunia, mji mkuu wa jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, walinda amani kutoka Bangladesh na Indonesia, wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO wamepatiwa medali kwa mchango wao wa ulinzi wa raia, moja ya jukumu kubwa la ujumbe huo..Makala ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya muziki wa Jazz Flora Nducha anamulika umuhimu wa jazz maadhimisho ya mwaka ambapo maudhui yanachagiza "Amani, umoja, ubunifu na uhuru miongoni mwa tamaduni."Na katika mashinani leo fursa ni yake mshiriki  jukwaa la watu wa asili hapa Makao makuu Helena Steenkamp Mwakilishi wa Shirika la Watu wa jamii za Asili Kusini mwa Jangwa la Kalahari Afrika Kusini anazungumzia alichokipata hadi sasa kwenye jukwaa hilo.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
29 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 29, 2025 11:44


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka katika mkoa wa Mwanza kaskazini magharibi mwa Tanzania ambapo vijana wameshika hatamu kuboresha mustakabali wao. Pia tunakuletea muhtasari wa habari  na mashinani tunasalia hapa makao makuu.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kudumisha Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, MONUSCO, umeikaribisha kusainiwa kwa “Azimio la Kanuni” tarehe 25 Aprili 2025 mjini Washington, D.C chini ya usimamizi wa Wizara ya mambo ya nje ya Marekani, kati ya serikali za DRC na Rwanda kwa lengo la kulinda rai ana kutekeleza azimio la Baraza la Usalama namba 2773 (2025).Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA, Juliette Touma, akizungumza na waandishi wa habri mjini Geneva kwa njia ya video kutoka mji mkuu wa Jordan, Amman, wakati  kuzingirwa kwa Ukanda wa Gaza kukikaribia kuingia mwezi wa pili amesema “Mzingiro wa Gaza ni muuaji wa kimya muuaji wa watoto, wazee, na watu walioko katika mazingira magumu zaidi. Mzingiro huu unamaanisha kwamba familia nzima, watu saba au wanane wanalazimika kushirikiana kopo moja la maharagwe au njegere”.Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO limezitaka nchi za Kaskazini Magharibi mwa Afrika kuongeza ufuatiliaji na kuchukua hatua za mapema kudhibiti makundi ya nzige wa jangwani. Hii ni baada ya nzige wakubwa na makundi madogo kutoka ukanda wa Sahel kuhamia maeneo ya kusini mwa Sahara, hasa katikati ya Algeria, magharibi mwa Libya, na kusini mwa Tunisia tangu Februari hadi Machi mwaka huu.Na katika mashinani fursa ni yake Maruping Onkemetse Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kituo cha Msaada wa Familia, shirika linaloongozwa na wanawake wa asili  katika Wilaya ya Gantsi, kijiji cha Chobokwane nchini Botswana anayeshiriki mkutano unaoendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa wa Jukwaa la Watu wa Asili akizungumzia alichojifunza hadi sasa.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
‘Nenda rudi' ya wakimbizi wa DR Congo nchini Burundi mazingira ya kuishi yakiendelea kuwa tete

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 25, 2025 2:02


Mazingira ya maisha kwa wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC waliongia Burundi na kupelekwa katika kambi ya wakimbizi ya Musenyi si endelevu huku wengine wakifanya safari za nenda rudi wakivuka mto uliosheheni viboko na mamba. Taarifa zaidi na Selina Jerobon.

Habari za UN
25 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 25, 2025 10:57


Hii leo jaridani tunaangazia wakimbizi wa DRC waliokimbilia Burundi, na ujumbe wa Siku ya Kimataifa ya Hakibunifu. Makala inatupeleka nchini Kenya kuangazia ugonjwa wa malaria na mashinani tunasalia hapa makao makuu katika mkutano wa Jukwaa la watu wa asili.Mazingira ya maisha kwa wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC waliongia Burundi na kupelekwa katika kambi ya wakimbizi ya Musenyi si endelevu na yanatishia mustakabali wao. Msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR Ayaki Ito, amesema hayo leo huko Geneva, Uswisi wakati akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu hali ya wakimbizi hao wanaoendelea kumiminika nchini Burundi.Kesho Aprili 26 ni Siku ya Kimataifa ya Hakibunifu - Siku ambayo ni fursa kwa ulimwengu kukumbushwa umuhimu wa haki kwa watu wanaobuni mambo mbalimbali duniani. Ili kufahamu zaidi kuhusu Hakibunifu tumezungumza na mtaalamu wa Sheria za Sanaa na Hakimiliki, Wakili Joshua Msambila wa nchini Tanzania, kwanza anaeleza kilichomsukuma yeye kujikita katika eneo hili la sheria.”Makala hii leo ikiwa ni siku ya Malaria duniani tunaelekea Kenya kwa mwandishi wetu Thelma Mwadzaya akiangazia juhudi zinazofanyika kupitia chanjo ili kupambana na malaria ugonjwa mbao Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO linasema mwaka 2023 pekee ulikatili maisha ya watu 597,000 na na asilimia 95 ya vifo hivyo vilitokea barani Afrika, na sasa linataka juhudi mara dufu zifanyike ili kuutokomeza.Na katika mashinanin fursa ni yake Kulet Adam Ole Mwarabu kiongozi wa jamii ya kimaasai kutoka Tanzania anayeshiriki katika mkutano wa Jukwaa la watu wa asili kutoka hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa na anatoa wito wa maendelo, amani  na utunzaji wa ardhi na mazingira kwa jamii ya asili na dunia nzima kwa jumla.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
22 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 22, 2025 9:56


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo inatupeleka Msasani nchini Tanzania kusikia namna vijana na serikali wanavyolinda Mama Dunia. Pia tunakuletea muhtasari wa habari ujumbe wa Katibu Mkuu, watoto kulinda mazingira DRC, na kifo cha Papa Francis.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya Mama Dunia, ikilenga kuchagiza hatua ya kuhifadhi sayari dunia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametumia neno ‘homa' kuwa inakumba dunia hivi sasa kutokana na viwango vya joto vinavyoongezeka kila mwaka. Hata hivyo amesema majawabu ya kutibu homa hiyo yapo ikiwemo kutumia nishati rejelezi ambayo ni rahisi, ina afya na salama kuliko nishati kisukuku.Huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kando ya mapigano yanayotikisa eneo la mashariki mwa nchi, watoto wamechukua hatua kulinda sayari dunia kwa kuhifadhi misitu kwenye taifa hilo ambako ukataji miti kiholela umefurutu ada.Kufuatia kifo cha Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis hapo jana Jumatatu, ambaye maziko yake yamepangwa kufanyika Jumamosi wiki hii, mashirika ya Umoja wa Mataifa yameendelea kukumbuka mchango wake wa kutetea walio taabuni. Mathalani shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR limekumbuka wito wake wa kutaka kila mtu kukaribisha, kusindikiza na kujumuisha wale wote wanaobisha hodi kwenye milango yao.Na mashinani  kupitia video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO fursa ni yake Meena Poudel kutoka nchini Nepal, Kusini mwa Asia ambaye ni Katibu wa kikundi cha wanawake watumiaji wa msitu ambacho kinabadilisha takataka za misitu kuwa mbolea rafiki kwa mazingira huku pia wakijipatia kipato."Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
16 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2025 9:57


Hii leo jaridani Assumpta Massoi anamulika masuala ya afya hususan harakati za kukabiliana na majanga yajayo ya afya;  wakimbizi huko Zambia ambako sera jumuishi zimewajengea uwezo; Jukwaa la vijana na mchango wa sanaa kwenye usawa na utengamano. Baada ya zaidi ya miaka mitatu ya mazungumzo ya kina, hatimaye leo huko mjini Geneva, Uswisi, nchi wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) zimekamilisha rasimu ya makubaliano ambayo itawasilishwa katika Mkutano wa Afya Duniani mwezi ujao wa Mei. Pendekezo hili linakusudia kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na vitisho vya majanga ya kiafya yajayo. Anold Kayanda amefuatilia anatujulisha zaidi.Zambia inaendelea kuwahifadhi zaidi ya wakimbizi 106,000, wengi wao wakiwa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Burundi, pamoja na wakimbizi wa zamani kutoka Rwanda na Angola. Limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, likiongeza kwamba kwa kuzingatia sera jumuishi ya Zambia, taifa hilo linakuza mshikamano na wakimbizi na kuwawezesha kujitegemea kupitia makazi maalum na ushirikiano na jamii za wenyeji. Flora Nducha na taarifa zaidi.Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) limeanza jana hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa na litamalizika kesho tarehe 17 Aprili. Vijana kutoka nchi mbalimbali wamehudhuria jukwaa hilo akiwemo Kapwani Kavenuke kutoka nchini Tanzania ambaye amehojiwa na Leah Mushi wa Idhaa hii. Kapwani anaanza kwa kueleza  umuhimu wa mikutano hii.Gislain Kalwira, Muandaaji wa tamasha la Musika na Kipaji  nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC linalofanyika kila mwaka kuleta pamoja wasanii wa kike na wa kiume wa fani mbalimbali, kwa kutambua kuwa jana dunia imeadhimisha siku ya sanaa duniani. Kalwira kupitia video iliyochapishwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani  nchini DRC, MONUSCO, anafafanua mantiki ya tamasha hilo na kujenga usawa kijinsia.

Habari za UN
Uhaba wa fedha watishia ukarimu wa Zambia kwa wakimbizi - UNHCR

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2025 2:05


Zambia inaendelea kuwahifadhi zaidi ya wakimbizi 106,000, wengi wao wakiwa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Burundi, pamoja na wakimbizi wa zamani kutoka Rwanda na Angola, kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, ambalo limesema kwa kuzingatia sera yake jumuishi, nchi hiyo inakuza mshikamano na wakimbizi na kuwawezesha kujitegemea kupitia makazi maalum na ushirikiano na jamii za wenyeji. Flora Nducha na taarifa zaidi  Shirika hilo la wakimbizi limesema katika makazi kama Mayukwayukwa na Maheba ambayo ni moja ya kambi kubwa zaidi ya wakimbizi nchini Zambia familia za wakimbizi zilizolazimika kukimbia makwao zinajumuishwa ili ziweze kujikimu na kuishi kwa utangamano na wenyeji wanaowahifadhi. Moulid Hujale, ni afisa habari msaidizi wa UNHCR anasema “Selikali ya Zambia inajumuisha wakimbizi katika huduma za kitaifa kama vile elimu na hata programu za msaada wa kilimo  ili kuongeza uzalishaji” Amebainisha kuwa kwa kufanya hivyo Zambia imeonesha mshikamano wa dhati kwa jamii hizo za wakimbizi kwa kuhakikisha kuwa wanapata fursa ya kujenga upya maisha yao, kujikwamua kiuchumi na kuishi kwa heshima.Hata hivyo, UNHCR inasema nchi hiyo ya Kusini mwa Afrika pamoja na ukarimu wake bado inakumbwa na athari za ukame mkali uliotishia uhakika wa chakula na kuyumbisha uchumi na katika hatua za kukabiliana na hali hiyo, Moulid ansema  “UNHCR inashirikiana na serikali ya Zambia kuunganisha makazi ya wakimbizi kwenye gridi ya taifa ya umeme. Tunajua muundo huu wa ujumuishwaji na maisha endelevu vinagharimu fedha, Lakini hiki ndicho hasa wakimbizi wanachokihitaji, hivyo tunahitaji msaada wako ili kufanikisha hili”. Licha ya mafanikio yaliyopatikana hadi sasa Zambia katika kuwakirimu wakimbizi,  UNHCR imeonya kuwa uhaba wa fedha inaokabiliwa nao  unatishia kuathiri mafanikio hayo na hasa utoaji wa huduma muhimu kwa familia hizo zilizolazimika kufungasha virago na kusaka usalama Zambia. Sasa limetoa ombi la msaada wa haraka wa kimataifa ili kuendelea kufanikisha huduma za kuokoa maisha zinazohitajika sana na wakimbizi hao.

Habari za UN
11 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 11, 2025 9:57


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya watoto nchini DR Congo, na masuala y awanawake nchini Tanzania. Makala inatupeleka nchini Kenya kuangazia harakati za vijana za kusongesha Ajenda2030, na mashinani tunasalia huko huko kumulika misaada kwa wakimbizi.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF limeripoti kwamba huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kila nusu saa takribani mtoto mmoja anaripotiwa kubakwa huku ghasia zikiendelea katikati ya janga linalozidi kukua la ufadhili finyu wa kifedha.Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake UN WOMEN nchini Tanzania chini ya ufadhili kutoka Muungano wa Ulaya wanashirikiana na jeshi la polisi kuendesha mradi huko visiwani Zanzibar wa kukomesha unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana na tayari manufaa ya mradi huo yameanza kuonekana.Makala leo inatupeleka Nairobi Kenya kwa Stella Vuzo kutoka kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIS Nairobi akizungumza na Winifred Njiru mwanafunzi wa chuo kikuu fani ya uhakiki au quantity surveyor aliyeshiriki majadiliano ya wiki iliyopita kuhusu malengo ya maendeleo endelevu yaliyoandaliwa na Club De Madri, anaeleza nini kama kijana anapaswa kufanya      kuchangia ajenda hiyo ya maendeleo.Na katika mashinani Cindy McCain, Mkurugenzi Mtendaji wa WFP, akizungumza kutoka kituo cha shirika hilo kilichopo Mombasa, Kenya anaeleza juhudi wanazofanya kuwasaidia wakimbizi wa Sudan na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC."Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
Mtoto aliyebakwa na kutiwa ujauzito DRC asema "siko tayari kuwa mama"

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 11, 2025 1:58


Mtoto mmoja alibakwa katika kila nusu saa huko Mashariki mwa Jamhuri ya ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wakati mapigano yaliposhika kasi mwanzoni mwa mwaka huu kati ya jeshi la serikali FARDC na waasi wa M23, katikati ya ufadhili finyu wa kifedha, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
08 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 8, 2025 11:50


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika shughuli za shirika lisilo la kiserikali la KINNAPA Development Programme la huko nchini Tanzania katika kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu likijikita zaidi katika usawa wa kijinsia. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani:Uganda, ambayo tayari ni mwenyeji wa wakimbizi wengi zaidi barani Afrika, inakabiliwa na shinikizo kubwa baada ya wakimbizi zaidi ya 41,000 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kuingia nchini humo tangu Januari mwaka huu, wakikimbia machafuko mapya mashariki mwa nchi yao limesema leo Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR. UNHCR imesema watu walioko katika mazingira hatarishi wanatambuliwa kwa msaada maalum, huku familia zilizotengana zikisaidiwa kuunganishwa tena.Siku kumi baada ya matetemeko ya ardhi ya kutisha yaliyoitikisa Myanmar tarehe 28 Machi, idadi ya vifo inaendelea kuongezeka. Titon Mitra, Mwakilishi wa Kikanda wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo UNDP nchini humo, akiripoti leo akiwa katika jiji liloharibiwa sana la Mandalay, kwa njia ya video ameripoti kwa waandishi wa habari jijini Geneva, Uswisi akisema, “idadi ya vifo ya hivi karibuni imepita watu 3,500 na “inaweza kuendelea kuongezeka.”Kenya, Uganda na Rwanda zitanufaika na mpango wa mlo shuleni baada ya leo Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) kutangaza kuwa linaendeleza ushirikiano wake na Taasisi ya Novo Nordisk, kupitia ushirikiano wa kihistoria kati ya sekta binafsi na ya umma unaojumuisha Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark na Taasisi ya Grundfos, ili kupanua mpango wa mlo shuleni kutokana na chakula kinachozalishwa ndani ya nchi husika. Ushirikiano huu utajenga mfumo wa msaada unaohakikisha uendelevu wa muda mrefu wa mpango huu.Na mashinani mashinani jana tarehe 7 Aprili hapa Umoja wa Mataifa kumefanyika kumbukizi ya miaka 31 ya mauaji ya kimbari nchini Rwanda ambapo mmoja wa wazungumzaji alikuwa Germaine Tuyisenge Müller, manusura wa mauaji hayo na wakati huo alikuwa na umri wa miaka 9 wakiishi mji mkuu Kigali.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
M23 na serikali ya DRC kufanya mazungumzo ya ana kwa ana

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 4, 2025 5:52


Duru za pande hasimu nchini Kongo, zimesema serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na waasi wa M23 wanajiandaa kwa mazungumzo ya ana kwa ana 9 Aprili 2025.

Habari za UN
Stadi za kuoka mikate zaleta furaha kwa mkimbizi Thérèse huko Beni nchini DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 2, 2025 1:52


Jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Thérèse Kavira, mwanamke shupavu aliyelazimika kukimbilia mji wa Beni baada ya waasi kuvamia kijiji chake sasa ameona nusu kwenye maisha yake kufuatia mafunzo ya kuoka mikate yaliyotolewa na ofisi ya Utafiti na Usaidizi kwa Mahusiano ya Kimataifa nchini humo pamoja na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO na sasa anajikimu kimaisha. Sharon jebichii na taarifa zaidi.

Habari za UN
02 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 2, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya Kimataifa ya Kuelimisha Umma kuhusu Usonji, na wakimbizi wa ndani nchini DRC. Makala inatupeleka nchini Tanzania kwa mada hiyo hiyo ya elimu kuhusu usonji, na mashinani tunakwenda Gaza.Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kuelimisha Umma kuhusu Usonji (Autism) mwaka huu wa 2025, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesisitiza umuhimu wa ujumuishaji na usawa kwa watu wenye changamoto hiyo akitambua mafanikio yao pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo duniani kote.Jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Thérèse Kavira, mwanamke shupavu aliyelazimika kukimbilia mji wa Beni baada ya waasi kuvamia kijiji chake sasa ameona nusu kwenye maisha yake kufuatia mafunzo ya kuoka mikate yaliyotolewa na ofisi ya Utafiti na Usaidizi kwa Mahusiano ya Kimataifa nchini humo pamoja na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO na sasa anajikimu kimaisha.Makala leo kama tulivyokujulisha ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu usonji, Assumpta Massoi anamulika jinsi shirika moja la kiraia nchini Tanzania linapigia chepuo harakati hizo.Na katika mashinani fursa ni yake Marah Hajjo, msichana mdogo kutoka Gaza huko Palestina Mashariki ya Kati ambaye anasimulia mabadiliko makubwa ya sikukuu ya Eid El Fitr ambayo mwaka huu ilighubikwa na kiza cha vifusi na mateso kutokana na mashambulizi kutoka Israeli.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!  

Habari za UN
Baada ya kukimbilia Burundi, wakimbizi wa DRC wakubwa na uhaba wa mahitaji muhimu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 26, 2025 2:06


Hali ya kibinadamu ya wakimbizi zaidi ya 100,000 wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, waliokimbilia nchini Burundi kusaka usalama kutokana na mapigano mashariki mwa nchi yao katika katika kipindi cha chini ya miezi mitatu, iliyopita ni ya mashaka, wakati huu ambapo ufadhili unazidi kukumbwa na mkwamo, wakikabiliwa na uhaba wa huduma kama chakula, huku kukiwa na pengo la ufadhili. Je ni madhila yapi?  Sharon Jebichii anafafanua zaidi kupitia video iliyoandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR.

Habari za UN
25 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 25, 2025 11:16


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo tunasalia hapa makao makuu katika mkutano wa CSW69 uliokunja chamvi Ijumaa wiki jana, tunamsikia aliyekuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa 4 wa Umoja wa Mataifa wa Wanawake, Mkutano wa Beijing Bi. Gertrude Mongella.Hapa New York, Umoja wa Mataifa leo umetoa wito wa kuachiliwa kwa wafanyakazi wake wanaoshikiliwa kote ulimwenguni ambao wamejikuta matatani wakati wakiwahudumia watu walio katika hatari, huku wakihatarisha usalama wao binafsi kwa kukabiliwa na vitisho vya kutekwa nyara, vurugu, unyanyasaji, na kifungo katika maeneo yenye migogoro na majanga.Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kuhusu vifo vya watoto imeonya kwamba miongo ya maendeleo katika kupunguza vifo vya watoto na watoto wachanga wakati wa kuzaliwa yako hatarini kutokana na kupunguzwa kwa ufadhili. Idadi ya vifo vya watoto wa chini ya umri wa miaka mitano ilipungua hadi watoto milioni 4.8 mwaka 2023, huku vifo vya wakati wa kuzaliwa vikiendelea kubaki takriban milioni 1.9.Leo ni Siku ya Kimataifa ya Kumbukumbu ya Waathirika wa Utumwa na Biashara ya Watumwa ya Bahari ya Atlantiki, ikiwakumbuka mamilioni ya Waafrika walioteswa, kunyanyaswa, na kunyimwa utu wao. Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema “Kwa zaidi ya karne nne, mamilioni ya Waafrika walitekwa kwa nguvu, kusafirishwa kwa meli hadi mataifa ya kigeni, na kufanyishwa kazi katika hali mbaya za kikatili.”Na katika mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP, Lea mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa amekimbilia Burundi na familia anasilimua hali ilivyokuwa wakati wa kukimbia.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!  

Habari za UN
20 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 20, 2025 12:27


Hii leo jaridani katika mada kwa kina tunajikita katika mkutano CSW69 ambao umebakiza siku moja tu, kesho Machi 21 unakunja jamvi, na tunamsikia Dkt. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Tanzania, Waziri Riziki Pembe kutoka Zanzibar na Profesa Smile Dzisi, Mkugenzi wa Shirika la “I believe Global” kutoka Ghana.Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR Filippo Grandi amesema kukata ufadhili kwa mashirika yanayotoa huduma za kibinadamu kunasababisha janga la uwajibikaji. Kupitia taarifa iliyotolewa leo Geneva, Uswisi na UNHCR, Bwana Grandi amesema kukata ufadhili kunaweka hatarini maisha ya mamilioni ya watu na madhara yake kwa watu wanaokimbia majanga, yatakuwa makubwa zaidi na yataonekana wazi ikiwemo wanawake na watoto wa kike kukosa huduma zitokanazo na kubakwa.Leo ni siku ya furaha duniani maudhui yakimulika umuhimu wa watu kusaidiana na kujaliana katika masuala mbalimbali ikiwemo chakula. Ripoti mpya ya wadau wa UN iliyozinduliwa leo imeonesha kuwa nchi yenye furaha zaidi duniani ni Finland na ya mwisho kabisa ni Afghanistani. Katika 10 bora zenye furaha hakuna hata moja ya Afrika, ilihali kwenye 10 za mwisho nchi za Afrika ni 7 ambazo ni Lesotho, Comoro, Botswana, Zimbabwe, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Malawi na Sierra Leone.Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW69 ukikaribia ukingoni hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa tumemuuliza mshiriki Wakili Rosemary Mwaipopo kutoka Tanzania mkutano umekidhi kiu yake ya kusongesha usawa wa kijinsia?Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno “Ashiraf, Janabi, gayagaya, kiti cha marimba na kiti cha msaji”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
UNHCR: Zaidi ya wakimbizi 63,000 wa DRC wamewasili Burundi wengi wanaishi kwenye uwanja wa Rugombo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 10, 2025 2:07


Zaidi ya watu 63,000 sasa wamewasili Burundi wakikimbia machafuko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na wengi wao wanaishi katika hali ngumu ndani ya uwanja wa michezo wa Rugombo jimboni Cibitoke (CHIBITOKE) huku wakisubiri kuhamishiwa kwenye kambi rasmi za wakimbizi. Flora Nducha amefuatilia safari ya mmoja wa wakimbizi hao, kwako Flora.