Podcasts about DRC

  • 752PODCASTS
  • 1,893EPISODES
  • 30mAVG DURATION
  • 1DAILY NEW EPISODE
  • Mar 13, 2023LATEST

POPULARITY

20152016201720182019202020212022

Categories



Best podcasts about DRC

Show all podcasts related to drc

Latest podcast episodes about DRC

Habari za UN
Wajumbe wa Baraza la Usalama watamatisha ziara DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 13, 2023 0:01


Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wametamatisha ziara yao ya siku tatu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC iliyolenga kujadili kwa kina majukumu ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO halikadhalika kujionea hali halisi ya amani na usalama.Kupitia mtandao wa Twitter, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa  Umoja wa Mataifa nchini DRC, Bintou Keita amesema wajumbe wa Baraza pamoja na kuwa na mazungumzo na viongozi wa ngazi ya juu wa serikali na MONUSCO,  walipata pia fursa ya kutembelea maeneo ya Mashariki wa taifa hilo ambako kumegubikwa na mashambulizi kutoka makundi ya waasi. Mathalani walipata fursa ya kusikiliza shuhuda kutoka kwa wawakilishi wa vikundi vya wanawake jimboni Kivu Kaskazini, vikundi ambavyo vinapambania kuheshimiwa kwa haki za wanawake na wasichana waliokumbwa na ukatili wa kingono. Halikadhalika walitembelea kambi ya wakimbizi ya ndani ya Bushagara – Nyiragongo ambako iko karibu na Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini.Bi. Bintou ambaye pia ni Mkuu wa MONUSCO amesema katika kambi hiyo maelfu ya wakimbizi wa ndani wako hatarini na mazingira yao yanakabiliwa na changamoto lukuki. Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ina takribani wakimbiz iwa ndani milioni 5 na mashambulizi kutoka makundi ya waasi yanazidi kukwamisha maisha yao.

congo bi drc goma umoja monusco baraza bintou mataifa jamhuri mashariki ziara kidemokrasia
Habari za UN
13 MACHI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 13, 2023 0:12


Hii leo jaridani tunaangazia hitimisho la ziara ya Baraza la Usalama DRC na UN Global Compact Tanzania. Makala tutasalia tunakurejesha hap makao makuu katika mkutano wa CSW67 na mashinani tunasalia hapa hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa.Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wametamatisha ziara yao ya siku tatu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC iliyolenga kujadili kwa kina majukumu ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO halikadhalika kujionea hali halisi ya amani na usalama.Nchini Tanzania Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kushirikisha kampuni kuzingatia será na misingi endelevu na inayojali jamii, au kwa kiingereza UN Global Compact Tanzania umeanza kuona mabadiliko katika kushirikisha kampuni kuzingatia misingi 7 ya kumwezesha mwanamke kwenye sekta ya biashara.Makala inaturejesha hapa Makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambako mkutano wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani SCW iumeingia wiki ya pili na Flora Nducha wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa amepata fursa ya kuzungumza na mbunge anayewakilisha asasi za kiraia kutoka Tanzania Neema Lugangira ambaye anashiriki mkutano huo wa kikao cha 67 kuhusu mada kuu ya kikao hicho ubunifu na teknolojia katika kusongesha mbele maendeleo ya wanawake akitaka kufahamu suala hilo linapewa uzito gani Tanzania.Na mashinani tutasikia ujumbe kuhusu unyanyasaji wa kijinsia utokanao na  mfumo dume ambao bado  umesalia kuwa kikwazo cha maendeleo katika nchi nyingi duniani.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Simple English News Daily
Monday 13th March 2023. World News. Today: Israel protests. Iran Saudi relations. Australia floods. Peru storm. DRC homeless. Ukraine update

Simple English News Daily

Play Episode Listen Later Mar 12, 2023 7:59


World News in 7 minutes. Monday 13th March 2023. Support us and read the transcripts at send7.org/transcriptsToday: Israel protests. Iran Saudi relations. Australia floods. Peru cyclone. DRC homeless. Ukraine updates. UK BBC crisis. France pensions. Micronesia China interference. Iran Mahsa Amini reports. Germany sleep science.With Stephen Devincenzi.Please leave a rating on Apple podcasts or Spotify.Contact us at podcast@send7.org or send an audio message at speakpipe.com/send7If you enjoy the podcast please help to support us at send7.org/supportSEND7 (Simple English News Daily in 7 minutes) tells the most important world news stories in intermediate English. Every day, listen to the most important stories from every part of the world in slow, clear English. Whether you are an intermediate learner trying to improve your advanced, technical and business English, or if you are a native speaker who just wants to hear a summary of world news as fast as possible, join Stephen Devincenzi, Namitha Ragunath and Juliet Martin every morning. Transcripts can be found at send7.org/transcripts. Simple English News Daily is the perfect way to start your day, by practising your listening skills and understanding complicated stories in a simple way. It is also highly valuable for IELTS and TOEFL students. Students, teachers, and people with English as a second language, tell us that they listen to SEND7 because they can learn English through hard topics, but simple grammar. We believe that the best way to improve your spoken English is to immerse yourself in real-life content, such as what our podcast provides. SEND7 covers all news including politics, business, natural events and human rights. Whether it is happening in Europe, Africa, Asia, the Americas or Oceania, you will hear it on SEND7, and you will understand it. For more information visit send7.org/contact

Habari za UN
Kuna haja ya kusaka amani kwa njia ya majadiliano, lasema Baraza la usalama la UN wakiwa ziarani nchini DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 10, 2023 0:02


Ujumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa umewasili nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC , ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi ya kutathmini hali ya usalama na utekelezaji wa majukumu ya vikosi vya umoja wa mataifa vya kulinda mamani nchini humo MONUSCO. Mara tu baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Kinshasa, bwana Nicolas de Rivière, Balozi wa kudumu wa Ufaransa kwenye Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa makundi yenye silaha, vyovyote vile yalivyo, lazima yasitishe operesheni zao ili kushiriki katika mchakato wa amani, “Ni wakati muhimu wakuchukua hatua na kwamba vikundi vyote vyenye silaha, kwa hali yao lazima visitishe shughuli zao na washiriki katika mchakato wa kisiasa. Naomba makundi ya kigeni yajiondoe na makundi yanayoungwa mkono na mataifa ya kigeni pia yajiondoe ili hatimaye amani irejee katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo”.Ujumbe huo umekuja nchini DRC wakati kukitarajiwa kuwa na uchaguzi mkuu wa raisi pamoja na wabunge mwezi decembe mwaka huu huku bwana Michel Xavier Biang Balozi wa Gabon kwenye Umoja wa Mataifa akisisitiza lazima uchaguzi huo uwe wa haki, wa uwazi na salama, “ Tuko katika mwaka ambao utakuwa mwaka wa uchaguzi, ujumbe wetu ni wakuhimiza wanasiasa wa pande zote kushiriki katika mchakato wa uchaguzi ambao ni wa uwazi, na wa kuaminika kwa mujibu wa Katiba ya DRC na sheria ya uchaguzi. Tuko hapa kuunga mkono hatua ya MONUSCO na kukumbusha kwamba MONUSCO ni sehemu ya fursa ya suluhu”.Wajumbe hao watakutana na watu kutoka tabaka mbali mbali ikiwemo mashirika ya kiraia na Rais wa DRC Félix Tshisekedi jijini Kinshasa na baadae watakwenda mjini Goma jimboni Kivu Kaskazini, ambako mapigano yamezidi kurindima kwa miezi kadhaa sasa kati ya jeshi la serikali na kundi la wanamkambo wa M23. 

congo drc gabon kinshasa goma kuna haja rais umoja congo drc m23 tshisekedi monusco baraza njia mataifa jamhuri tuko katiba ufaransa kidemokrasia uchaguzi mkuu kusaka
Habari za UN
10 MACHI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 10, 2023 0:12


Hii leo jaridani tunaangazia taarif aya UNICEF kuhusu kipindupindu, na ziara ya Baraza la Usalama DR Congo. Makala tutasalia huko huko DR Congo kushuhudia maadhimisho wa makabidhiano kati ya TANZBATT 9 na TANZBATT 10, na mashinani tukuletea ujumbe kutoka CSW67.Nchi 11 Mashariki na Kusini mwa Afrika zinakabiliwa na hali mbaya ya mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambako hadi sasa kumeripotiwa wagonjwa 67,822 na vifo 1, 788 kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.Ujumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa umewasili nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC , ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi ya kutathmini hali ya usalama na utekelezaji wa majukumu ya vikosi vya umoja wa mataifa vya kulinda mamani nchini humo MONUSCO. Mwandishi wetu wa Kinshasa Byobe Malenga amefuatilia kuhusu ziara hiyo na kutuandalia taarifa ifuatayo.Makala tunakwenda nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako huko kikosi cha 9 cha Tanzania kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO kimetamatisha jukumu lake na sasa kimekabidhi majukumu kwa TANZABATT-10 kama anavyoripoti Afisa habari wa kikosi hicho Kapteni Denisia Lihaya.Na mashinani tukuletea ujumbe wa mbunge kutoka Tanzania ambaye anashiriki mkutano wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW kikao cha 67 hapa makao makuu wa Umoja wa Mataifa.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Walinda amani wa UN kutoka Tanzania huko DRC wakabidhiana lindo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 10, 2023 0:04


Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC walinda amani kutoka Tanzania kikosi cha 9 wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO wanaendelea kushika doria na kulinda raia katika jimbo la Kivu Kaskazini ambapo wiki hii kikosi cha 9, TANZBATT 9 kimemaliza muda wake na kukabidhi majukumu kwa kikosi cha 10, TANZBATT 10. Je nini kimejiri katika makabidhiano hayo ? Kapteni Denisia Lihaya, Afisa habari wa TANZBATT 9 kabla ya kurejea nyumbani ametuandalia ripoti  hii ya makabidhiano. 

congo tanzania lindo drc umoja monusco mataifa north kivu huko kidemokrasia
Simple English News Daily
Friday 10th March 2023. World News. Today: Ukraine Russian missiles. Georgia law drop. Mexico no US. DRC attack. Nigeria elections. Jamaica

Simple English News Daily

Play Episode Listen Later Mar 9, 2023 7:45


World News in 7 minutes. Friday 10th March 2023. Support us and read the transcripts at send7.org/transcriptsToday: Ukraine Russian missiles. Georgia law drop. Mexico no US. DRC attack. Nigeria elections. Jamaica convictions. Honduras pills. Nepal President. Thailand duck jail. Japan two dads.With Stephen Devincenzi.Please leave a rating on Apple podcasts or Spotify.Contact us at podcast@send7.org or send an audio message at speakpipe.com/send7If you enjoy the podcast please help to support us at send7.org/supportSEND7 (Simple English News Daily in 7 minutes) tells the most important world news stories in intermediate English. Every day, listen to the most important stories from every part of the world in slow, clear English. Whether you are an intermediate learner trying to improve your advanced, technical and business English, or if you are a native speaker who just wants to hear a summary of world news as fast as possible, join Stephen Devincenzi, Namitha Ragunath and Juliet Martin every morning. Transcripts can be found at send7.org/transcripts. Simple English News Daily is the perfect way to start your day, by practising your listening skills and understanding complicated stories in a simple way. It is also highly valuable for IELTS and TOEFL students. Students, teachers, and people with English as a second language, tell us that they listen to SEND7 because they can learn English through hard topics, but simple grammar. We believe that the best way to improve your spoken English is to immerse yourself in real-life content, such as what our podcast provides. SEND7 covers all news including politics, business, natural events and human rights. Whether it is happening in Europe, Africa, Asia, the Americas or Oceania, you will hear it on SEND7, and you will understand it. For more information visit send7.org/contact

Cork Taint
DRCequel!!!!

Cork Taint

Play Episode Listen Later Mar 9, 2023 60:00


Alright so we didn't actually drink more DRC... BUT we did drink plenty of other delicious things! Including: Cristal Pol Roger Cuvee Sir Winston Churchill 1999 Turley Hayne Vineyard Zinfandel 1976 Grgich Zinfandel 1983 Tommasi Amarone 1962 Bertani Amarone 2010 Giuseppe Quintarelli Rosso del Bepi AND MORE! Next week's Patreon-only episode is about delicious 80's and 90's napa cab, so if you want that and other BONUS CONTENT, sign up at: patreon.com/corktaint Thanks guys

Africa Today
Will DRC's ceasefire hold?

Africa Today

Play Episode Listen Later Mar 7, 2023 25:35


A ceasefire has come into force in the Democratic Republic of Congo to put an end to fighting between the army and M23 rebels. Aid workers in eastern DRC say that clashes are continuing. South Africa's President Cyril Ramaphosa has announced the appointment the country's first-ever minister of electricity. We meet the creators of a new animation series which tells the story of Ghana's independence movement. And musician, Sodi Cookey, tell us about his new album, 'Love, Live and Protest'.

Habari za UN
Makundi yenye silaha DRC waweweke chini silaha zao: Keita

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 6, 2023 0:02


Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC Bintou Keita amesema kwamba mpango wa Umoja wa Mataifa nchini huomo MONUSCO unasisitiza wito wa Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa makundi yenye silaha yanayoendesha operesheni zao DRC kuweka chini silaha zao mara moja pasi na masharti yoyote.Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC Bintou Keita amesema kwamba mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO unasisitiza wito wa Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa makundi yenye silaha yanayoendesha operesheni zao DRC kuweka chini silaha zao mara moja pasi na masharti yoyote. Mwandishi wetu wa Kinshasa BYOBE MALENGA na tarifa zaidi.Bi Bintou Keita, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu nchini DRC ametoa kauli hio wakati wa mkutano na waandishi wa habari wakati ahitimisha ziara yake mwishoni mwa wiki katika majimbo matatu ya Mashariki mwa nchi amambapo amesema amehuzunishwa sana na hali ya wakimbizi wa ndani,“Nilikuja kuona kwa uhakika athari za kuzorota kwa hali ya usalama katika maisha ya mamia kwa maelfu ya watu walio katika mazingira magumu, wakiwemo wanawake na watoto. Nimetembelea maeneo ya Bushagara na mugwera huko Kivu Kaskazini na KISOGE huko Ituri. Nimekutana na wanawake na wanaume walio katika dhiki lakini ambao bado wana matumaini. Wana nia moja tu ya kurejea kwa amani ili warudi majumbani kwao salama. Haya ni matakwa yetu ya pamoja.” Keita amewataka waasi wa kundi la M23 kuheshimu mkataba wa mwisho wa mkutano mdogo wa kilele uliofanyika mjini Launda nchini Angola ambao unaowataka waasi hao kuondoka na kurejea katika nafasi yao ya awali kwenye Mlima Sabinyo kabla ya Jumanne ya Machi 7 mwaka huu bila masharti kabla ya kutaka mazungumzo yoyote na serikali ya DRC, “Ninakaribisha hatua ya mpatanishi wa Umoja wa Afrika, Rais wa Angola Joao Lourenço, ambayo imefanya Ijumaa kutolewa ahadi ya M23 ya kusitisha mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuanzia Jumanne tarehe 7 Machi saa 12 Jioni. Ninatoa wito kwa vuguvugu hili la waasi wa M23 kuheshimu bila masharti au kusita, masharti ya tamko la Luanda la Novemba 23, ambalo linadai wajiondoe katika maeneo yanayokaliwa, kusitishwa kwa mapigano yote, kuwaondoa wapiganaji wao na kurudi katika eneo lao la awali  kwenye Mlima Sabino “. Wito huo unakuja wakati waasi wa M23 wakiteka vijiji kadhaa katika maeneo ya Masisi, Rutshuru na Nyiragongo, hali iliyosababisha zaidi ya watu 600,000 kuyahama makazi yao.

Habari za UN
06 MACHI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 6, 2023 0:12


Jaridani leo tunaangazia mkutano wa CSW67 hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa na amani na usalama nchi i DRC. Makala tutaelekea Doha nchini Qatar na mashinani tunasalia hapa makao makuu, kulikoni?Mkutano wa 67 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW umeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ukileta pamoja wawakilishi kutoka serikali, mashirika ya kiraia yanayotambuliwa na Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC pamoja na vijana.Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC Bintou Keita amesema kwamba mpango wa Umoja wa Mataifa nchini huomo MONUSCO unasisitiza wito wa Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa makundi yenye silaha yanayoendesha operesheni zao DRC kuweka chini silaha zao mara moja pasi na masharti yoyote.Katika makala Anold Kayanda wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa aliyeko Doha Qatar kunakofanyika mkutano wa 5 wa nchi zenye maendeleo duni zaidi duniani, LDCs, yeye amezungumza na vijana Cosmas Msoka na Humphrey Mrema ambao wako kwenye ujumbe wa vijana wanaoshiriki mkutano huo.Na katika mashinani tunasalia hapa hapa Umoja wa Mataifa kukuletea matarajio ya kijana kutoka Tanzania aliyekuja kushiriki mkutano wa hali ya wanawake duniani.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
Kutoka vitani kuua watu hadi darasani kushika kalamu- Simulizi ya Rachel DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 22, 2023 0:02


Mradi mpya wa shule  nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC uliozinduliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto,  UNICEF na wadau wake kwa ufadhili kutoka mfuko wa Umoja wa Mataifa wa kuchagiza elimu kwenye maeneo ya mizozo, Education Cannot Wait, ECW, au Elimu Haiwezi Kusubiri umewezesha watoto waliokuwa wametumikishwa vitani kuanza kurejea kwenye masomo na hata kutangamana na wenzao kwa amani.  Miongoni mwao ni Rachel mwenye umri wa miaka 17 ambaye katika video ya UNICEF anaonekana nyakati za asubuhi akiwa na mfuko wake wa madafari akielekea shuleni Lubile, kijiji cha Mpungwe, jimboni Tanganyika kusini-mashariki mwa DRC.  Maisha yake ni mapya kabisa kwani awali alitumikishwa vitani na waasi akisema,  “vitu ambavyo tulikuwa tunapitia tulikuwa tunaua watu. Tulikuwa tunakula kwa tabu mpaka twende tuibe. Kule tulikuwa hatuna  huruma ya kuhurumiana. Lakini hii ya hapa najikuta niko kwenye masomo na niko huru. Niko ninacheza na wenzangu na mwenzangu akinikosea na akiniomba msamaha najua jinsi ya kumsamehe.” Rachel amepata msaada wa kuondokana na kiwewe na wa kisaikolojia kupitia mradi unaofadhiliwa na ECW. Michel ni mnasisi wa kisaikolojia shuleni hapa na anasema, “mosi, tunawafundisha upendo na watu wote; ya pili tunawafundisha msamaha ndio tunajitahidi kuwasaidia kimafundisho ili wasahau yale maneno ya zamani. Kuna wengi wamesharejea shuleni. Kiwewe ni tatizo kubwa sana na kila mtoto ana changamoto yake.”  Kupitia mradi wa ECW shule ya Rachel sasa ina madawati mapya, huduma za kujisafi kama vile vyoo pamoja na maji.   Mpango wa muda mrefu ni kuhakikisha watoto wengi zaidi wa kike katika jimbo la Tanganyika wanarejea shuleni.   Yasmin Sherif, Mkurugenzi wa ECW akiwa ndani ya darasa hapa Mpungwe anasema, “Education Cannot Wait hadi sasa imewekeza dola milioni 22 na dola nyingine milioni 44 zinahitajika ili kufikia watoto na vijana wengi zaidi jimboni kote Tanganyika ambao ni wakimbizi wa ndani, au wako pembezoni na kufikia kila mtoto na kuwa na shule kama hii hapa kwenye kijiji kidogo cha Mpungwe. Hii inawezekana.”  

congo unicef ecw drc hadi kuna maisha umoja hii tanganyika watu lakini mataifa jamhuri kidemokrasia miongoni kalamu
Habari za UN
22 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 22, 2023 0:11


Hii leo jaridani tunakuletea habari kuhusu mwelekeo wa matumizi ya maji barani Afrika, na elimu kwa watoto waliotumikishwa jeshini nchini DR Congo.  Makala tutakupeleka nchini Tanzania na mashinani tunarudi tena nchini DR Congo.Ni wakati kufikiria upya jinsi ya kutumia maji kwa njia endelevu na yenye uwiano huku ubunifu katika kilimo ukiwa kitovu cha mipango yote, amesema Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO limesema Qu Dongyu hii leo wakati akizungumza na viongozi na wataalamu wa Afrika kwenye warsha ya kwanza ya kikanda kuhusu mwelekeo wa matumizi ya maji barani Afrika, warsha inayofanyika nchini Zimbabwe.Mradi mpya wa shule nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC uliozinduliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto,  UNICEF na wadau wake kwa ufadhili kutoka mfuko wa Umoja wa Mataifa wa kuchagiza elimu kwenye maeneo ya mizozo, Education Cannot Wait, ECW, au Elimu Haiwezi Kusubiri umewezesha watoto waliokuwa wametumikishwa vitani kuanza kurejea kwenye masomo na hata kutangamana na wenzao kwa amani.Katika makala tunakupeleka Njombe mkoa ulioko kusini mwa Tanzania kusikia harakati za Umoja wa Mataifa na wadau za kusongesha ulaji wa mazao ya jamii ya mikunde ili kuboresha lishe.Na katika mashinani tutaelekea tena Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kumsikia mvulana aliyekuwa ametumikishwa vitani.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Last Week in the Church with John Allen
Pope reconsiders papal resignation?

Last Week in the Church with John Allen

Play Episode Listen Later Feb 21, 2023 30:25


In this episode:Pope changes tune on papal resignation?President of Vatican Bank bullied to sign off on loan?Jesuit Fr. Rupnik: who lifted the excommunication?5 archbishops passed over for Cardinal's hatPope Francis: top 5 tripsSupport the show

KPFA - A Rude Awakening
A Rude Awakening with Devlin Kuyek and Frederic Mousseau

KPFA - A Rude Awakening

Play Episode Listen Later Feb 17, 2023 59:58


On today's show, a new report from the Oakland Institute entitled, “Meet the Investors Behind the PHC Oil Palm Plantations in the DRC” exposes the financiers of the perpetual colonization of the DRC. I'll speak to GRAIN researcher Devlin Kuyek and the Oakland Institutes Policy Director Frederic Mousseau. photo: Juan Fernández Originally aired 2/18/22 The post A Rude Awakening with Devlin Kuyek and Frederic Mousseau appeared first on KPFA.

grain frederic drc rude awakening kpfa oakland institute devlin kuyek
Africa Today
Chaos over currency in Nigeria continues

Africa Today

Play Episode Listen Later Feb 17, 2023 19:51


The state of the Nigerian nation ahead of elections, as tensions over the shortage of new currency continue. Also, the M23 rebel movement rejects a new report accusing it of perpetrating rape in the eastern DRC. And South Africa begins ten days of naval training exercises with Russia and China. Those stories and more in this podcast with Esau Williams

JIB/JAB Podcast
JIB/JAB - Episode 33: Provost on Rebel Courts

JIB/JAB Podcast

Play Episode Listen Later Feb 14, 2023 80:35


A conversation with René Provost, professor of law at McGill University, Faculty of Law, in Montreal, about his recent book "Rebel Courts: The Administration of Justice by Armed Insurgents." We discuss the methodology he employed in researching this deep and rich ethnography of rebel courts in conflicts ranging from Afghanistan, Iraq and Syria, to Sri Lanka, Colombia, and the DRC. We discuss how he assesses the legality of insurgents' administration of justice, how the very idea of rebel courts challenges many conceptions of law and justice, and the ways in which rebel administration of justice actually conforms to many aspects of the rule of law. It is a fascinating discussion that ranges from legal anthropology and legal theory to certain technical aspects of IHL and human rights law.

No Bad Reviews: A Coffee Podcast
Anodyne Coffee + Democratic Republic of the Congo

No Bad Reviews: A Coffee Podcast

Play Episode Listen Later Feb 14, 2023 102:29


Steph went on vacation to Milwaukee and brought back a bag of Anodyne Coffee. First she tells us the story of the marathon running founder that has built an incredibly successful business in Milwaukee over the last 25 years.Then we try a coffee from Anodyne, a single-origin coffee from the Democratic Republic of the Congo, a region that is hard to get coffee from due to the ongoing political instability of the country. In this episode we learn about the history of the DRC and how it has shaped the current situation today. Steph also tells about coffee growing in the DRC and the challenges that farmers face getting their coffee exported. We're not going to lie, this episode is a real bummer. But Steph tells a captivating story and it's important that we bring awareness to the hardships that the coffee farmers face. Shop Anodyne Coffee: https://anodynecoffee.com/collections/single-origins/products/dr-congo-north-kivu-Buy a mystery box of past products that we have tried on the podcast! For $10 you will receive 10 cups worth of coffee. Includes shipping! Limited supplies, buy here: https://www.paypal.com/instantcommerce/checkout/YUHJNDHDX2CTEHelp us buy questionable coffee!https://www.patreon.com/nobadreviewspodhttps://www.buymeacoffee.com/nobadreviewspod

Habari za UN
14 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 14, 2023 0:10


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo leo tunakwenda nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kuangazia changamoto za usalama mashariki mwa nchi hiyo hususan jimboni Ituri. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo WHO, watoto katika maeneo ya migogoro na haki za raia nchini Zimbabwe. Mashinani tutasalia hapa makao maku ya Umoja wa Mataifa, kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO hii leo limeitisha mkutano wa dharura wa muungano wa chanjo ya virusi vya Marburg ili kujadili mlipuko mpya wa ugonjwa huo nchini Equatorial Guinea.Mfuko wa Umoja wa Mataifa unaohusika na kusongesha elimu kwenye maeneo yenye majanga na mizozo ya muda mrefu, Education Cannot Wait, au kwa lugha ya Kiswahili, Elimu Haiwezi Kusubiri umetangaza kutoa ruzuku ya dola milioni 7 nchini Syria kwa ajili ya kukuabiliana na dharura zilizopo lengo likiwa ni kusaidia wasichana na wavulana walioathiriwa na tetemeko ili waweze kuwa na mazingira salama ya kujifunzia na kupata usaidizi muhimu wa kisaikolojia, kijamii na ustawi unaohitajika.Na wataalamu wa Umoja wa Mataifa wamemsihi Rais wa Zimbabwe kukataa kuufanya kuwa sheria, mswada ambao utaweka vikwazo vikali kwa asasi za kiraia na kuzuia haki na uhuru wa watu kujumuika nchini humo.Na katika mashinani tunamsikia Najat Maalla M'jid, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu kuhusu Ukatili dhidi ya Watoto akihutubia Baraza la Ulama kuhusu watoto katika maeneo yenye migogoro.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
13 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 13, 2023 0:10


Hii leo jaridani tunaangazia siku radio duniani, na wakimbizi wanaorejea nyumbani Burundi. Makala tunakupeleka nchini DR Congo na mashinani tutamsikia Balozi Mwema wa UNHCR.        Katika siku ya redio duniani Umoja wa Mataifa unamulika nafasi ya chombo hicho kilichobuniwa takribani karne moja iliyopita katika kukuza na kujenga amani  wakati huu ambapo pia ni miaka 75 tangu kuanzishwa kwa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa.Nchini Burundi wakimbizi waliokimbia ghasia, wanaendelea kurejea nyumbani kutokana na hali ya amani kuzidi kuimarika, na hivi karibuni zaidi wakimbizi wamerejea kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC wakiwa na matumaini kutokana na kile wanachoshuhudia.Makala mwandishi wetu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Byobe Malenga anaangazia Redio Ngoma ya Amani, kituo cha redio cha mjini Fizi jimboni Kivu Kusini kinachohamasisha amani hususani katika maeneo ya mashariki mwa DRC.Na katika mashinani tutamsikia Balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR akipasa sauti kwa ajili ya wakimbizi na wote walio hatarini kutojumuishwa katika mijadala ya malengo ya maendeleo endelevu. Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Sijasikia mlio wowote wa risasi, nyumbani Burundi hali ni shwarili - Aline

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 13, 2023 0:02


Nchini Burundi wakimbizi waliokimbia ghasia, wanaendelea kurejea nyumbani kutokana na hali ya amani kuzidi kuimarika, na hivi karibuni zaidi wakimbizi wamerejea kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC wakiwa na matumaini kutokana na kile wanachoshuhudia.Video ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR ikianza kwa kuonesha msafara wa magari uliobeba wakimbizi wa Burundi ukiingia kwenye lango kuu la mpaka wa taifa hilo, huko Bujumbura, ukitokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Baada ya kuingia mpakani, mmoja baada ya mwingine wakaanza kuteremka wakiwemo wanawake na watoto. Wamevalia barakoa zao, kujikinga na ugonjwa wa COVID-19. Kisha kwenye ukumbi wa eneo la mapokezi wakisubiri kusajiliwa na miongoni mwao ni Aline Niagara, mama huyu akiwa na watoto wake wanne, na anaelezea sababu ya kurejea nyumbani Burundi kutoka ukimbizi DRC, “Sasa ni mwaka mmoja na miezi miwili,  tangu nimeanza kusikia kutoka kwa wale waliorejea hapa nyumbani mapema. Wametuambia kuwa njooni, hakuna tatizo lolote nchini kwetu. Hakuna tatizo na majirani. Mkisaidiwa na UNHCR mje nyumbani, na ndio maana tumeamua kurejea na tayari tuko hapa.” Maafisa wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR wamejipanga hapa ambapo wanajaza nyaraka za waliorejea pamoja na kuchukua alama za vidole. Aline anazidi kufunguka juu ya kile anachokiona nchini mwake, “Moyo wangu uko na amani. Tulipovuka mpaka kupitia pale kwa maafisa wa forodha na kuingia hapa, nimeweza kuona watu wanatembea kwa uhuru. Tangu nimefika hapa, sijasikia mlio wowote wa risasi. Sijaona watu wakikimbia. Naona watu wako na amani.” 

covid-19 video congo burundi drc unhcr kisha sasa moyo umoja hakuna baada bujumbura mataifa jamhuri nyumbani kidemokrasia conco
Habari za UN
Redio Ngoma ya Amani inachangia utunzaji wa amani hapa mashariki mwa DRC - Wasikilizaji

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 13, 2023 0:04


Katika Siku ya Redio Duniani mwaka huu wa 2023, UNESCO inaangazia redio huru kama nguzo ya kujenga amani na kuzuia migogoro. Redio inatazamwa kama chombo muhimu na sehemu muhimu ya kutunza amani. Redio hushughulikia visababishi na vichochezi vya migogoro, kabla hazijaweza kulipuka na kuwa vurugu. Inatoa mbinu mbadala ya kuzuia migogoro, au migongano ya maslahi, kuondoa kutoelewana, na kutambua masuala ya kutoaminiana. Hii inaweza kusaidia kukabiliana na chuki, hamu ya kulipiza kisasi, au nia ya kutumia silaha. Na sasa hii leo dunia ikiadhimisha siku hii ya Redio Duniani, mwandishi wetu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Byobe Malenga anaangazia Redio Ngoma ya Amani, kituo cha redio cha mjini Fizi jimboni Kivu Kusini kinachohamasisha amani hususani katika maeneo ya mashariki mwa DRC. 

unesco drc hii hapa ngoma jamhuri mashariki redio kidemokrasia wasikilizaji
Objection to the Rule
OTR February 5th, 2023: Face-Recognition Tech Used to Attack LGBTQ+ NYers - COVID-19 Public Health Emergency Ending in the US - The Horrors of Cobalt Mining in the Democratic Republic of the Congo - The Fight for Hybrid Work for NYC Gov't Employees

Objection to the Rule

Play Episode Listen Later Feb 11, 2023 59:31


Jasmin, Matthew, and Janet discuss a string of attacks against LGBTQ+ New Yorkers using facial recognition technology, what the end of the COVID-19 public health emergency declaration would mean in the United States, the horrors of cobalt mining in the DRC, and progress in negotiations for hybrid work for NYC government employees.

African Catholic Voices
Was the Visit of Pope Francis to Africa a Success? Nigerian Bishops meet amidst confusion over currency change, fuel scarcity, more killings, and pre-elections tension and anxiety

African Catholic Voices

Play Episode Listen Later Feb 10, 2023 31:40


Fr Stan Chu Ilo reflects  on the  Pope's visit to the DRC and South Sudan and points the way to the future. Based on the opinions of many analysts, there is a serious concern that the Pope's visit will amount to nothing, if the local politicians in these two countries are not committed to transparency and inclusive governments; national reconciliation and peace;  the rule of law, and fighting corruption and abuse of power and the use of violence against their own people.  The second part of the episode is a reflection on the current state of Nigeria, and why next week's meeting of the Catholic bishops of Nigeria is the most decisive in a long time. In the face of the terrible suffering of Nigerians, following the change in Nigeria's currency, fuel scarcity, lack of access to their funds by citizens, lack of access to the basic necessities of life, rising hunger and starvation amidst a rise in violence and more killings in the land less than three weeks to the most consequential national elections in a generation, what hope can the Catholic Church give to Nigerians? 

Improve the News
February 10, 2023: ‘Forever war' authorizations, EU Twitter content moderation and Indian hug-a-cow day

Improve the News

Play Episode Listen Later Feb 10, 2023 29:21


Facts & Spin for February 10, 2023 top stories: US lawmakers try to end 'forever war' authorizations, Zelenskyy addresses an EU summit as fighting rages around Bakhmut, North Korea displays a possible new missile at a military parade, The EU reprimands Twitter for an 'incomplete' content-moderation report, Eight civilians are killed in clashes with UN peacekeepers in the DRC, The Church of England approves same-sex union blessings, Missouri votes not to ban children from carrying guns in public, A survey finds that half of Americans are worse off than they were a year ago, Disney plans to lay off 7,000 workers, and India urges citizens to ‘hug a cow' on Valentine's Day. Sources: https://www.improvethenews.org/   Brief Listener Survey: https://www.improvethenews.org/pod

Habari za UN
Kuwa mkimbizi sio kulemaa: Muokoaji mkate Shebulike

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 9, 2023 0:05


Kama nilivyokudokeza hapo awali nabisha hodi nchini Burundi katika kambi ya wakimbizi ya Nyankanda iliyoko Mashariki mwa nchi hiyo kambi ambayo inahifadhi takriban wakimbizi 12,000 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.  Kambini hapo wakimbizi wanapatiwa msaada unaotolewa kwa ushirikiano wa serikali ya Burundi, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na wahisani wengine wa kibinadamu. Hata hivyo msaada huo hautoshelezi hivyo wakimbizi wanachagizwa kujishughulisha na kazi mbalimbali ili kuweza kukidhi mahitaji mengine ya msingi ya kila siku. Wapo waliokumbatia wito huo akiwemo mkimbizi muoka mikate mashuhuri kutoka DRC ambaye amethibitisha kwamba kuwa mkimbizi sio kubweteka wala kulemaa. 

burundi drc unhcr wapo kama hata umoja congo drc kuwa mataifa jamhuri mashariki kidemokrasia
Let Me Be Frank | Bishop Frank Caggiano's Podcast | Diocese of Bridgeport, CT

Current events are on the docket, including: the pope's trip to the DRC, the Synod on Synodality, the appointment of Archbishop Prevost, Catholic schools, “the One”, and more. Links to download the Veritas app: https://www.veritascatholic.com/listen  

African Catholic Voices
Embrace Nonviolence for the Sake of your People: Mother Jurugo and Father Ezama make a Passionate appeal to Congolese and South Sudanese Leaders

African Catholic Voices

Play Episode Listen Later Feb 7, 2023 29:20


We present to you our guest host, Fr Ruffino Ezama of the Comboni Missionaries. Currently, Ruffino is the Provincial Superior of the North American Province. His conversation partner in this episode is Mother Alice Drajea Jurugo, the Superior General of the Sacred Heart of Jesus Sisters, based in Juba, South Sudan. The Sacred Heart Sisters were founded by the Comboni Missionaries in Sudan in the 1950s. In this episode, Fr Ezama and Mother Jurugo discuss the recent apostolic visit of Pope Francis to the DRC and Sudan. They join their voices to that of the Holy Father in calling on all people especially the political leaders to become serious about bringing peace and abundant life to the people of South Sudan and the Congo. Everyone is called to become committed messengers of peace, hope and faith through a change in worldview, practices of forgiveness and reconciliation, and embracing a lifestyle that promotes peace, harmony and humanity!

Habari za UN
07 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 7, 2023 0:11


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na tunakwenda nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako mapigano yanayoendelea yanatenganisha watoto na familia zao na sasa hatua zinachukuliwa kuunganisha watoto na familia zao. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zinazohusiana na janga la tetemeko la ardhi katika mashariki ya kati na pia hali ya usalama nchini Somalia. Mashinani tutasalia huho huko nchini Somalia.Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa nchini Syria Paulo Pinheiro amesema yeye na makamishina wengine wa Umoja wa Mataifa pamoja na timu za misaada wanatoa pole kwa maswahibu yaliyowakumba wananchi wa nchi hiyo na kutoa ombi maalum la pande zote zinazo zozana nchini Syria kuweka silaha chini ili kuwaruhusu wahudumu wa misaada ya kibinadamu na waokoaji kuweza kuwafikia wenye uhitaji bila ya kuwa na wasiwasi wa kushambuliwa.Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO linalohusika pia na usimamizi wa maeneo ya kuhistoria limesema limeanza uchunguzi wa awali kuangalia maeneo ya kuhistoria yaliyoathiriwa na matetemeko. Na tumalizie habari kwa ufupi kutoka Geneva nchini Uswisi ambapo kufuatia mauaji yaliyotokea baada ya mapigano makali kutokea kuanzia tarehe 5 mwezi huu wa Februari nchini Somalia kati ya vikosi vya usalama na wanajamii wa ukoo wa Laas Canood, Kamishna Mkuu wa Haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Turk ametoa wito kwa mamlaka ya Somalia kuhakikisha uchunguzi huru unafanyika bila upendeleo.Na katika mashinani tutaelekea Doolow nchini Somalia kusikia ujumbe wa Dkt. Natalia Kanem, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani UNFPA.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

syria congo unesco somalia drc umoja hii unfpa haki nalo mataifa jamhuri dkt shirika kidemokrasia
Reasonably Shady
| Ep 78 | Reunited … And It Feels So Cold

Reasonably Shady

Play Episode Listen Later Feb 6, 2023 49:35


Gizelle and Robyn discuss a scary (shady) moment, RHOP reunion memories, Last Chance U, Amy + TJ, Mariah Carey, “Pee” Diddy, Ben Simmons, Lori Harvey, vibranium, Buying Beverly Hills, and more!   -GMA 3 Update: https://youtu.be/y9Riu03Zvjc -Vibranium in the DRC?: https://youtu.be/mE3AyP5JyWE    +Patreon: https://www.patreon.com/ReasonablyShady  +Get in touch with the show: whatsup (at) reasonablyshady (dot) com  || Keep up with us on IG: ReasonablyShady  || Follow Robyn: robyndixon10  || Follow Gizelle: gizellebryant || See omnystudio.com/listener for privacy information.

Catholic News
February 2, 2023

Catholic News

Play Episode Listen Later Feb 2, 2023 2:38


A daily news briefing from Catholic News Agency, powered by artificial intelligence. Ask your smart speaker to play “Catholic News,” or listen every morning wherever you get podcasts. www.catholicnewsagency.com - To bring about peace, “prayer is the most powerful weapon there is,” Pope Francis told thousands of young adults and catechism teachers in the Democratic Republic of Congo on Thursday. The meeting in Martyrs' Stadium in Kinshasa, the capital city of the DRC, took place on February 2, the third day of the pope's visit to the central African country. On February 3, Francis will fly to Juba, South Sudan, for the second leg of his peace pilgrimage. Pope Francis on Thursday interacted with an enthusiastic crowd of around 65,000 young people and adults, some of whom traveled days to be present for the papal visit. During the second half of his speech, the pope was repeatedly drowned out by the energetic audience, which broke out in cheering, singing, and dancing despite the hot weather. The pope invited those present in the stadium to open and close their hands while meditating on whether they wanted to choose peace or violence. https://www.catholicnewsagency.com/news/253529/pope-francis-to-congolese-youth-prayer-is-your-secret-weapon-for-peace President Joe Biden is wrong on taxpayer funding of abortion and wrong on Pope Francis's view of it, the president of the US bishops conference said Wednesday. The president suggested Tuesday that neither the pope nor all Catholic bishops oppose public funding for abortion in the United States. Biden, a Catholic who supports legal and publicly funded abortion, made that assertion in a brief exchange with EWTN's White House correspondent, Owen Jensen, on the White House lawn. On Wednesday, Archbishop Timothy Broglio, the president of the United States Conference of Catholic Bishops (USCCB), released a statement contradicting Biden's comments. “As we are taught by Jesus, human life is sacred. God calls us to defend and nurture life from the moment a new human being is conceived. The Catholic Church has been clear and consistent in this teaching,” Broglio said. “The Catholic bishops of the United States are united in our commitment to life and will continue to work as one body in Christ to make abortion unthinkable.” https://www.catholicnewsagency.com/news/253528/head-of-us-bishops-conference-contradicts-biden-s-claims-about-taxpayer-funded-abortions Today, the Church celebrates the Presentation of the Lord in the Jewish temple. At the beginning of the eighth century, Pope Sergius inaugurated a candlelight procession; at the end of the same century the blessing and distribution of candles which continues to this day became part of the celebration, giving the feast its popular name: Candlemass. https://www.catholicnewsagency.com/saint/presentation-of-the-lord-427

Habari za UN
02 FEBRUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 2, 2023 0:12


Hii leo katika Jarida tunakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa Kina na Jifunze lugha ya Kiswahili.Katika Habari kwa Ufupi Leah Mushi anamulika ziara ya Papa Francis nchini DR Congo na wito wake kwa vijana na viongozi wa dini kukataa rushwa. Halikadhalika anamulika maeneo oevu na umuhimu wake bila kusahau nchini Sudan Kusini ambako Umoja wa Mataifa unaendelea kutoa misaada kwa familia zilizokimbia kutoka katika eneo la Pibor.Mada kwa Kina inamulika mmea aina ya Azolla, hili ni gugu maji na ni kwa vipi nchini Tanzania limeanza kuchangamkiwa na vijana katika kujiongezea kipato.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ni msemo ya kwamba sikio halilali njaa.Karibu na mwenyeji wako ni Anold Kayanda.

Habari za UN
Mada kwa kina: Chanjo dhidi ya Kipindupindu yaendelea Kivu Kaskazini, DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 31, 2023 0:05


Kampeni ya utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu  iliyoanza tarehe 25 mwezi huu huko Kivu Kaskazini nchini jamhuri ya Kidemokraia ya Congo, DRC imekunja jamvi jana Jumanne ya tarehe 30 mwezi hu uwa Januari ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO lilizindua kampeni hiyo ya chanjo kwa wakimbizi wa ndani katika kambi ya wakimbizi hao ya Kanyaruchinya wilayani nyiragongo katika mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini.Mwandishi wetu wa DRC Byobe Malenga ambaye ameshuhudia uzinduzi huo amesema uliongozwa na Gavana wa jimbo la Kivu Kaskazini Jenerali Ndima Constant, na Mwakilishi wa shirika WHO nchini DRC kwa lengo la kuokoa mamia ya familia hususan za wakimbizi wa ndani ambao tayari makumi kwa makumi wameripotiwa kupata ugonjwa huo na wengine wamefariki dunia.Jean Bruno, ni Mkuu wa Ofisi ya WHO Kivu Kaskazini na anasema ameridhishwa na shauku ya siku ya kwanza na zaidi ya yote amesema,« Tumewalenga watu 364,127 ambao ni wakimbizi wa ndani, pamoja na familia zinazowapokea. Tayari tumepokea dozi 364,150 ambazo zipo na zitatumika. chanjo itafanyika kwa awamu ya dozi moja na tutafanya hivyo kupitia kampeni ya nyumba kwa nyumba kwenye maeneo haya . Tumeridhika na ukweli ni kwamba kumekuwa na dhamira muhimu kwa upande wa serikali kwenye ngazi ya taifa na mkoa, lakini pia tumekuwa na hakikisho kutoka kwa jamii ya watu na wakimbizi wa ndani ambayo imekubali chanjo hiyo ambayo itafanyika kwa wakati».Eneo la Nyiragongo lilipokea idadi kubwa ya watu waliokimbia makazi yao kutokana na mashambulizi yanayofanywa na waaasi wa M23 huku watu 233 elfu waliokimbia makazi yao, zaidi ya 95% yao wamelundikana kwenye makanisa, shule, viwanja vya michezo na maeneo yasio salama kwa afya yao.Gavana wa Kivu Kaskazini, Jenerali Ndima Constant, anakiri kwamba janga la kipindupindu linaathiri sana eneo la Nyiragongo akisema kwamba hadi Jumanne ya Januari 24  wagonjwa 3706 wa kipindupindu walisajiliwa huku kukiwa na vifo 16 na ili kupunguza mlolongo wa maambukizi amewasihi raia kupata chanjo akishukuru WHO kwa msaada wao.« Madhumuni ya kampeni hii  ya chanjo ni kulinda idadi ya watu dhidi ya kipindupindu katika jimbo la Kivu Kaskazini na hasa katika maeneo ya watu waliofurushwa ili kupunguza vifo. Mabibi na mabwana, wageni mashuhuri, ili kufunga maoni yangu, ningependa kuwakumbusha kuwa pamoja na chanjo utakayopokea, kufuata hatua za kuzuia maambukizi ni muhimu..”Ametaja njia za kujikunga kuwa ni pamoja na kunawa mikono mara kwa mara kwa maji safi na sabuni au majivu, kunywa maji yaliyotakasishwa tu au yaliyochemshwa. Kupika na kufunika milo yetu, matumizi sahihi ya vyoo huku tukiwa wasafi na kuweka usafi kwenye maeneo yetu ya makazi  kila wakati.Waliokimbia makazi yao wanafahamu tishio hilo kwa sababu janga hilo limeathiri zaidi ya 89% ya waliokimbia makazi katika miezi ya hivi karibuni na chanjo inatekelezwa nyumba kwa nyumba.Watu waliohamishwa wanasubiri dozi zao nyumbani. Damaseni Butera ni miongoni mwa watu wa kwanza kupata dozi moja dhidi ya kipindupindu na anashukuru mpango huu wa WHO na anasema, «chanjo ni muhimu sana katika mapambano dhidi ya magonjwa kama kipindupindu, malaria na mengine.Tumejifunza habari kuhusu chanjo hiyo, tumefurahi sana kwa sababu tutakuwa na kinga, asante sana kwa shirika la WHO ambalo lilitufikiria. Asante sana»Kando na hilo, Mweze Shemba, aliyekimbia kutoka kijiji cha Kiwanja, pia alinufaika na chanjo hii. Licha ya njaa,yeye anapendelea kujilinda pamoja na familia yake dhidi ya janga hili akisema, «kilichonifanya nipate chanjo ya leo hapa katika kambi ya wakimbizi ni kwa sababu tunapatwa na magonjwa ya taabu. kama vile kuharana kutapika hasa tunapokunywa maji machafu. Lakini wakati tunapata hii chanjo tunaona kama vile ni kinga kwetu tunashukuru sana »Katika juhudi za kuepusha msongamano wa wagonjwa wa janga hili , WHO ilijenga vitalu 3 kama kitengo cha matibabu ya wagonjwa wa Kipindupindu (UTC) katika eneo la Bushagara na…

congo kina drc goma asante umoja m23 katika kivu watu nyiragongo tayari lakini mataifa medair mwandishi kampeni
Habari za UN
31 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 31, 2023 0:11


Hii leo jaridani tuakuletea mada kwa kina na tunakwenda nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kumulika kampeni ya chanjo iliyomalizika jana Jumanne.  Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za afya, haki za binadamu na wakimbizi. Katika mashinani tutakupeleka Geneva nchini Uswisi kupata ujumbe wa shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na UKIMWI, UNAIDS kuhusu kizazi cha watato ulimwenguni ambao wako hatarini kusahaulika.      Wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa wametaka kufanyika mara moja kwa uchunguzi huru nchini Mali kwa kile walichoeleza kuwa ni kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu pamoja na uwezekano wa uhalifu wa kivita unaosadikiwa kufanywa na vikosi vya serikali kwa kushirikiana na kundi binafsi la wanajeshi la Wagner group.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limezindua Baraza la vijana lililofanyika kwa siku nne jijini Geneva Uswisi na kuwaleta pamoja viongozi vijana kutoka mashirika 22 ya vijana duniani yanayojishughulisha na masuala ya afya na masuala yasiyo ya afya lengo likiwa ni kuwasikiliza vijana, kupata utaalamu na uzoefu wao katika masuala ya afya kwa umma pamoja na kufanya nao kazi katika kutengeneza harakati za vijana katika afya.Na shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM limesema kumekuwa na ongezeko kubwa la wakimbizi wa Rohingya wanaowasili Kusini Mashariki mwa Asia kwa njia ya bahari na njia za barabara. IOM imese mwaka 2022 imerrkodi kuwasili kwa watu 3300 nchini Malaysia, Indonesia na Thailand hili likiwa ni takriban ongezeko la asilimia 290 ikilinganishwa na watu 850 waliowasili mwaka 2021.Katika mashinani tutakupeleka Geneva nchini Uswisi kupata ujumbe wa Charlotte Sector, Msemaji wa Mpango wa Pamoja wa Umoja wa Mataifa kuhusu VVU / UKIMWI (UNAIDS) akisisitiza umuhimu nchi za Afrika kuzindua "Muungano wa kimataifa wa Kutokomeza Ukimwi kwa Watoto" katika kanda huo  ili kuzuia maambukizi mapya ya VVU miongoni mwa watoto wachanga Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu !

Africa Daily
Should Africa play a bigger role in Catholicism?

Africa Daily

Play Episode Listen Later Jan 30, 2023 15:50


Africa is home to more than a sixth of the world's Catholics, and that share is rising. But Africans are significantly under-represented in the Vatican, and other regions such as Latin America currently have far more sway in Rome. As the Pope travels to the DRC and South Sudan this week, many Africans in the Church are hoping he is sincere when he says their voices need to be heard. And despite concerns from more conservative figures on the continent, Pope Francis seems focused on his progressive agenda. Ahead of the trip he criticised laws criminalising homosexuality, which are common in many parts of Africa. So what will this trip mean for the future of Catholicism in Africa? For Africa Daily, Mpho Lakaje puts this to religious thinkers on the continent…

Simple English News Daily
Monday 30th January 2023. World News. Today: Czech election. Russia child protection. Ukraine update. US protests. Israel Palestine violence

Simple English News Daily

Play Episode Listen Later Jan 29, 2023 7:59


World News in 7 minutes. Monday 30th January 2023.Support us and read the transcripts at send7.org/transcriptsToday: Czech election. Russia child protection. Ukraine updates. US protests. Israel Palestine violence. Iran explosions. Pakistan accidents. DRC loss. Peru protests. Australian Djokovic back.Please leave a rating on Apple podcasts or Spotify.With Stephen Devincenzi.Contact us at podcast@send7.org or send an audio message at speakpipe.com/send7If you enjoy the podcast please help to support us at send7.org/supportSEND7 (Simple English News Daily in 7 minutes) tells the most important world news stories in intermediate English. Every day, listen to the most important stories from every part of the world in slow, clear English. Whether you are an intermediate learner trying to improve your advanced, technical and business English, or if you are a native speaker who just wants to hear a summary of world news as fast as possible, join Stephen Devincenzi, Namitha Ragunath and Juliet Martin every morning. Transcripts can be found at send7.org/transcripts. Simple English News Daily is the perfect way to start your day, by practising your listening skills and understanding complicated stories in a simple way. It is also highly valuable for IELTS and TOEFL students. Students, teachers, and people with English as a second language, tell us that they listen to SEND7 because they can learn English through hard topics, but simple grammar. We believe that the best way to improve your spoken English is to immerse yourself in real-life content, such as what our podcast provides. SEND7 covers all news including politics, business, natural events and human rights. Whether it is happening in Europe, Africa, Asia, the Americas or Oceania, you will hear it on SEND7, and you will understand it. For more information visit send7.org/contact

Habari za UN
27 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 27, 2023 0:11


Hii leo jaridani tuakuletea ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kuhusu makumbusho ya Holocaust, pia tunamulika kazi ya walinda amani nchini DR Congo. Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani tunasalia hapa makao makuu wa Umoja wa Mataifa.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kumbukizi ya waathitrika wa mauaji ya maangamizi makubwa au Holocaust dhidi ya wayahudi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema mauaji hayo yalikuwa ni malimbikizo ya miongo ya chuki dhidi ya Wayahudi ndio maana sasa ni wakati wa kuhakikisha chuki za aina yoyote ile zinakomeshwa duniani.Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini.Makala tunakwenda nchini Tanzania kusikia ni kwa vipi Mahakama inachagiza moja ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs na shuhuda wetu ni Hamad Rashid wa Redio washirika MVIWATA FM mkoani Morogoro, Mashariki mwa Tanzania.Katika mashinani leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kukumbuka waathirika na waliokufa kutokana na mauaji ya maangamizi dhidi ya wayahudi yaliyofanywa na manazi nakuletea ujumbe wa nini kifanyike kuepusha hali hiyo na ujumbe unatolewa na Dani Dayan, Mwenyekiti wa jumba la makumbusho ya mauaji ya maangamizi ya wayahudi huko Israel, liitwalo Yad Vashem. Ujumbe huu ameutoa wakati wa uzinduzi wa maonesho ya kitabu chenye majina ya wayahudi waliouawa na manaziMwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
TANZBATT 9 wafanya doria barabara inayounganisha DRC na Uganda

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 27, 2023 0:01


Kufuatia mashambulizi yanayofanywa na makundi mbalimbali ya waasi kwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususani mashariki mwa nchi hiyo ya pili kwa ukubwa wa eneo barani Afrika, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha 9 kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu katika kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kujibu mashambulizi cha FIB-MONUSCO, wamefanya doria katika barabara ya Mbau-Kamango nje ya mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini. Kapteni Ahmad Waziri Said ambaye ni kamanda wa msafara anaanza kwa kueleza umuhimu wa barabara hiyo akisema ni barabara inayounganisha nchi ya DRC na Uganda "kwa hiyo raia wengi wanaitumia barabara hii kwa shughuli za kibiashara  na kujiongezea kipato." Kuhusu lengo la doria hii, Kapteni Said anasema, "tunafanya hivi kwa lengo la kumnyima adui uhuru wa kufanya mauaji kwa kuwa adui amekuwa akifanya uvamizi dhidi ya raia ikiwemo kuwaua watu, kuchoma moto magari na nyumba zao."Sajenti Fredrick John Mwandri ni mmoja wa walinda amani ambaye ameshiriki doria hii anatoa wito kwa wananchi wa DRC lakini kwanza anaeleza namna ambavyo adui amekuwa akibadilishabadilisha mbinu za mashambulizi, "kuna matukio ya ulipukaji wa mabomu kwa hiyo tunawaomba endapo wataona kuna kiashiria chochote ambacho hawajakizoea watoe taarifa kwenye vyombo ambavyo vinahusika ambavyo ni vyombo vya ulinzi. Ninafikiri itatusaidia haya matukio ambayo adui amebadilika kuyafanya yasiweze kujitokeza. Wito wangu kwa raia ni kwamba waendelee kuwa na amani waendelee kufanya shughuli zao ambazo wamekuwa wakizifanya siku zote. Tunaamini kwa jukumu hili ambalo tumeliandaa la ulinzi wa hii barabara hakutakuwa tena na yale matukio ambayo wamekuwawakiyaona mara kwa mara."

uganda congo tanzania afrika beni drc umoja barabara mataifa jamhuri kidemokrasia
Hold Your Fire!
Great Lakes Tensions Spike After Rwanda Nearly Downs a Congolese Fighter Jet

Hold Your Fire!

Play Episode Listen Later Jan 27, 2023 54:09


On 24 January, Rwanda's defence forces fired a missile at a DR Congo army jet for allegedly violating Rwandan airspace. Congolese officials called the incident an “act of war”. The shooting has ratcheted up already high tensions between Rwandan and Congolese authorities, with the two governments at loggerheads since the resurgence of the M23 rebel group in late 2021. The M23 was defeated in 2013 but has re-emerged in the past year, taking control of significant areas in the eastern DR Congo's North Kivu region. Kinshasa accuses Kigali of supporting the M23. Rwanda denies the allegations, though repeated UN reports offer strong evidence that the rebels are, indeed, supported by Rwanda. The fighting has triggered a humanitarian crisis, with hundreds of thousands displaced, many in the last few months. This week on Hold Your Fire!, Richard Atwood speaks with Richard Moncrieff, Crisis Group's interim Great Lakes project director, about the resurgence of the M23 in the DRC and how the conflict could affect the stability of the wider Great Lakes region. They talk about the origins of the M23, what its leaders want and its ties to Rwanda. They discuss how the conflict has worsened already fragile Rwandan-Congolese relations. They also delve into the efforts of the East African Community to defuse tensions in the DRC, particularly Kenya's military and diplomatic involvement in the region, and examine the risks that the crisis in the DRC could trigger a wider conflagration. For more on the situation, check out Crisis Group's latest Q&A “A Dangerous Escalation in the Great Lakes” and our extensive analysis on our Great Lakes regional page. Hosted on Acast. See acast.com/privacy for more information.

Habari za UN
26 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 26, 2023 0:12


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo leo tunakwenda nchini Kenya kuangazia juhudi za mradi wa Teen Seed Africa unavyorejesha matumaini ya elimu kwa wasichana walioacha shule kutokana na mimba za mapema.  Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo kutoka nchini DR Congo, Ethiopia na Senegal. Katika kujifunza Kiswahili   ambapo utapata ufafanusi wa msemo "TABIA NI NGOZI."Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO umesema wataalamu wake wa kutegua mabomu na wale wa ofisi ya Umoja huo ya kudhibiti mabomu ya kutegwa ardhini, UNMAS wamefika katika mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini hususan kitongoji cha Macampagne ambako jana Jumatano bomu la kutengenezwa lililipuka kwenye soko na kujeruhi watu 17.Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za binadamu, imesema Kamisheni ya Kimatiafa kuhusu haki za binadamu nchini Ethiopia imetambua chapisho la serikali la rasimu ya kwanza ya kisera kuhusu haki kwenya kipindi cha mpito.Na Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani, ILO Gilbert F. Houngbo yuko ziarani nchini Senegal,  ikiwa ni ziara yake ya kwanza kufanywa na kiongozi wa shirika hilo nchini humo na anatumia fursa ya ziara yake hiyo ya siku 4 kujadili na mamlaka na vyama vya wafanyakazi mwelekeo wa ajira katika dunia ya sasa hususan ajira yenye hadhi kwa vijana na wanawake, ulinzi wa wafanyakazi wahamiaji na urasimishaji wa uchumi usio rasmi.Leo katika kujifunza Kiswahili mtaalam wetu  Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, BAKIZA nchini Tanzania anafafanua maana ya msemo "TABIA NI NGOZI."Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

VICE News Reports
Why DRC's Rebel Group M23 is Back

VICE News Reports

Play Episode Listen Later Jan 26, 2023 32:17


The rebel group M23 has resumed fighting in the Eastern part of the Democratic Republic of the Congo after nearly a decade of laying dormant. M23 has overrun army military bases, looted weapons, captured large territories north of the city of Goma while leaving hundreds dead and thousands displaced from their homes. Now, the president is asking everyday civilians to join the fight. VICE News' Evelyn Kahungu travels to the DRC to meet a civilian picking up arms and reports from the frontlines of M23's resurgence.Special thanks to our translator Aquelina Mawadza with Bayville Languages, VICE News Nairobi Bureau Chief Julia Steers, and our production crew Adolphe Basengezi and Srdjan Stojiljkovic.This story was produced by Stephanie Brown and edited by Stephanie Kariuki.VICE News Reports is produced by Sam Eagan, Sophie Kazis, Adreanna Rodriguez and Adriana Tapia. Our senior producers are Jesse Alejandro Cottrell, Janice Llamoca and Julia Nutter. Our supervising producer is Ashley Cleek. Our associate producer is Steph Brown. Sound design and music composition by Steve Bone, Pran Bandi, and Kyle Murdock. Annie Aviles is our Executive Editor and Janet Lee is Senior Production Manager for VICE Audio. Fact Checking by Nicole Pasulka. Our theme music is by Steve Bone. Our host is Arielle Duhaime-Ross. Charles Raggio is the head of VICE Audio. Hosted on Acast. See acast.com/privacy for more information.

Mornings with Carmen
Being courageous as we seek after the truth | Remembering the believers in India

Mornings with Carmen

Play Episode Listen Later Jan 25, 2023 47:15


Front Porch Republic's Jeff Bilbro outlines the need for answering the foundational questions in our society, that often ignores them and how we can access our level of faith in a spiritual reality. Mission Network News' Ruth Kramer talks about the dangers that ministries in the DRC are facing and the noteworthy attitude of Ryan Koher while unjustly behind bars. Click here for today's show notes Faith Radio podcasts are made possible by your support. Give now: Click here

seek believers courageous drc faith radio mission network news ruth kramer
Mammalwatching
Episode 9: Jo Setchell

Mammalwatching

Play Episode Listen Later Jan 25, 2023 50:01


Charles and Jon talk to Professor Jo Setchell from her home in the UK. Dr Setchell, a distinguished primatologist and anthropologist, has studied primates in Cameroon, Gabon, the DRC and Borneo and has particular research interests in sexual selection among Mandrills and primate conservation. Destined for a career in primatology from the age of two, when she was inseparable from her toy monkey, Jo's fascinating research has proved important for science and conservation. And some work - such as discovering that the reddest male Mandrills are a sort of simian Brad Pitt - has cast a whole new light on Mandrill romance.Notes: Jon's trip report from Bioko Island will soon be available at https://www.mammalwatching.com/bioko-island/.  Charles's 2022 Lynx trip is here.  And this is a video of the UK "mole hunter" Jon mentioned. But is it a hoax? And if not, how can we learn this magic?!Here is the YouTube trailer.For more information visit www.mammalwatching.com/podcastCover photo - Jo Setchell.Dr Charles Foley is a mammalwatcher and biologist who, together with his wife Lara, spent 30 years studying elephants in Tanzania. They now run the Tanzania Conservation Research Program at the Lincoln Park Zoo in Chicago.Jon Hall set up mammalwatching.com in 2005. Genetically Welsh, spiritually Australian, currently in New York City. He has looked for mammals in over 100 countries.

Habari za UN
24 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 24, 2023 0:13


Ni Jumanne ya tarehe 24 mwezi Januari mwaka 2023 ambapo leo tunakwenda nchini Tanzania kuangalia juhudi zinavyofanyika kuhakikisha wanafunzi hususan wa vijijini wanakuwa na mazingira bora ya kuweza kujisomea  nyakati zote. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikimulika hali ya usalama DR Congo, ujumbe wa Katibu Mkuu ya siku hii ya elimu duniani na ripoti ya usafirishaji haramu wa binadamu. Katika mashinani tunakupeleka nchini Kenya.Hali ya usalama inazidi kuwa mbaya huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususa jimboni Ituri ambako vikundi vilivyojihami vimeendelea kuua rai ana katika wiki sita zilizopita zaidi ya raia 200 wameuawa, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi duniani, UNHCR.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya elimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza kwamba elimu ni haki ya msingi ya binadamu na hivyo kila mtu anastahili kuipata. Kupitia ujumbe wake wa siku hii inayoadhimishwa kila mwaka Januari 24 Antonio Guterres amesema “Ni msingi wa jamii, uchumi, na uwezo wa kila mtu. Lakini bila uwekezaji wa kutosha, uwezo huu utaishia kwenye mzabibu".Na ripoti mpya iliyotolewa leo na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu UNDOC kuhusu usafirishaji haramu wa binadamu inaelezea hofu kwamba rasilimali za kuwaokoa waathirika wa usafirishaji haramu zimeelekezwa kwenye janga la COVID-19.Na leo katika mashinani tutakwenda Turkana nchini Kenya kumsikia Gabriel Ekaale, ambaye alianza kazi yake kama mwalimu wa shule ya upili nchini Kenya, lakini baada ya muda mfupi aligundua kwamba kazi yake inaweza kuwa na manufaa kwa jamii nzima, na sasa anafanya kazi na jamii zilizoathiriwa na ukame.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

covid-19 kenya congo tanzania drc unhcr antonio guterres umoja katika turkana ituri lakini mataifa jamhuri elimu north kivu mashariki kidemokrasia ikiwa
Simple English News Daily
Wednesday 25th January 2023. World News. Today: Ukraine tanks approved. NZ PM. Uganda oil. US shootings. Nepal earthquake. India syrup. DRC

Simple English News Daily

Play Episode Listen Later Jan 24, 2023 7:55


World News in 7 minutes. Wednesday 25th January 2023.Support us and read the transcripts at send7.org/transcriptsToday: Ukraine tanks approved. NZ PM. Uganda oil. US shootings. Nepal earthquake. India syrup. DRC church voting. UK missing kids. Brazil Pele shirt.Please leave a rating on Apple podcasts or Spotify.With Stephen Devincenzi and Khadija Tahir.Contact us at podcast@send7.org or send an audio message at speakpipe.com/send7If you enjoy the podcast please help to support us at send7.org/supportSEND7 (Simple English News Daily in 7 minutes) tells the most important world news stories in intermediate English. Every day, listen to the most important stories from every part of the world in slow, clear English. Whether you are an intermediate learner trying to improve your advanced, technical and business English, or if you are a native speaker who just wants to hear a summary of world news as fast as possible, join Stephen Devincenzi, Namitha Ragunath and Juliet Martin every morning. Transcripts can be found at send7.org/transcripts. Simple English News Daily is the perfect way to start your day, by practising your listening skills and understanding complicated stories in a simple way. It is also highly valuable for IELTS and TOEFL students. Students, teachers, and people with English as a second language, tell us that they listen to SEND7 because they can learn English through hard topics, but simple grammar. We believe that the best way to improve your spoken English is to immerse yourself in real-life content, such as what our podcast provides. SEND7 covers all news including politics, business, natural events and human rights. Whether it is happening in Europe, Africa, Asia, the Americas or Oceania, you will hear it on SEND7, and you will understand it. For more information visit send7.org/contact

The Hidden Economics of Remarkable Women (HERO)
Developing Male Allies in the Democratic Republic of Congo

The Hidden Economics of Remarkable Women (HERO)

Play Episode Listen Later Jan 24, 2023 30:48


On today's episode of HERO, the last show of the season, we look at how a Women for Women International program in the Democratic Republic of Congo worked with families to try to overcome longstanding cultural barriers to women owning land. We hear from a mother, father, and son who participated in this program. Also, Women for Women International's country director in the DRC, Rachel Boketa, explains how this project attempted to change men's and boy's opinions about female property ownership. Special thanks to Francis Shok Mweze, who acted as our field producer for this segment.   Boketa's program was supported with a grant from the United States Agency for International Development, or USAID. The U.S. currently gives more money to international development than any other country in the world, largely through USAID. In the second part of the episode, host Reena Ninan talks to Isobel Coleman, the deputy administrator of USAID. Coleman explains why the Biden administration is doubling funding towards gender programming and how USAID plans to invest that financing. This conversation first took place at Foreign Policy's Her Power Summit, an annual gathering all about women's leadership.  Finally, we are conducting a listener survey to better understand what you like about the podcast and what else you'd like to hear in future episodes. All participants in the survey who provide their email will be placed in a raffle to win a $25 Amazon gift card. To participate, follow the survey link below. Thank you very much for your time and feedback.  https://www.surveymonkey.com/r/heropodcast

Simple English News Daily
Tuesday 24th January 2023. World News. Today: US shooter dead. Argentina Brazil talks. Germany Poland tanks. Russia and Estonia relati

Simple English News Daily

Play Episode Listen Later Jan 23, 2023 6:44


World News in 7 minutes. Tuesday 24th January 2023. Support us and read the transcripts at send7.org/transcriptsToday: US shooter dead. Argentina Brazil talks. Germany Poland tanks. Russia and Estonia relations. DRC rebel attack. Nigeria port. Japan birth rate. Pakistan power outage. 7-year-old joins MENSA.With Namitha Ragunath.Please leave a rating on Apple podcasts or Spotify.Contact us at podcast@send7.org or send an audio message at speakpipe.com/send7If you enjoy the podcast please help to support us at send7.org/supportSEND7 (Simple English News Daily in 7 minutes) tells the most important world news stories in intermediate English. Every day, listen to the most important stories from every part of the world in slow, clear English. Whether you are an intermediate learner trying to improve your advanced, technical and business English, or if you are a native speaker who just wants to hear a summary of world news as fast as possible, join Stephen Devincenzi, Namitha Ragunath and Juliet Martin every morning. Transcripts can be found at send7.org/transcripts. Simple English News Daily is the perfect way to start your day, by practising your listening skills and understanding complicated stories in a simple way. It is also highly valuable for IELTS and TOEFL students. Students, teachers, and people with English as a second language, tell us that they listen to SEND7 because they can learn English through hard topics, but simple grammar. We believe that the best way to improve your spoken English is to immerse yourself in real-life content, such as what our podcast provides. SEND7 covers all news including politics, business, natural events and human rights. Whether it is happening in Europe, Africa, Asia, the Americas or Oceania, you will hear it on SEND7, and you will understand it.For more information visit send7.org/contact

The Ugandan Boy Talk Show
Uganda Meets Switzerland | Sarah Fluck | Ep115

The Ugandan Boy Talk Show

Play Episode Listen Later Jan 21, 2023 39:50


In this episode I host Sarah Fluck, Sarah is originally from Switzerland, and she is a journalist mainly for a Swiss newspaper covering all of East Africa. Sarah is currently based in Kampala Uganda but her main work is in The Democratic Republic Of Congo. Sarah has her Ph.D. in African politics which she studied in the UK. While on the Podcast we talked about Arsenal F.C. beating Tottenham Hotspur F.C. because Sarah is an arsenal fan just like the host of the podcast. She talks about her experience with football and the lifestyle in Uganda. We also talked about African Politics and a little bit about the ADF war in the DRC. Tune in to listen to our conversation. Connect with Sarah on Instagram @sa_fluck --- Send in a voice message: https://anchor.fm/bonny-kibuuka/message

Daily News Brief by TRT World
January 20, 2023

Daily News Brief by TRT World

Play Episode Listen Later Jan 20, 2023 2:27


*) Zelenskyy expects powerful Western military support President Volodymyr Zelenskyy says that Ukraine is waiting for a "decision from one European capital that will activate the prepared chains of cooperation on tanks." Zelenskyy thanked Estonia for the large package of military assistance and Sweden for its package which included howitzers and ammunition. Zelenskyy also thanked Denmark for the NLAW, Archers and APCs. *) Palestine tells Biden adviser to rein in Israel 'before it's too late' Palestine's President Mahmoud Abbas meets US National Security Adviser Jake Sullivan, appealing to the Biden administration to stop the Israeli government from pressing ahead with escalatory measures against the Palestinians. Abbas urged the United States to intervene before it is too late to stop the unilateral measures by the new Israeli coalition's policies. *) Türkiye expects US to extradite FETO terrorists: Cavusoglu Turkish Foreign Minister Mevlut Cavusoglu says that he hopes Washington will extradite members of the Fetullah Terrorist Organization based in the US. Speaking with members of the Turkish-American community and Ahiska Turks in Houston, Texas, Cavusoglu stressed that FETO members are "intensely" present in the city. Cavusoglu said that FETO's educational institutions were shut down in many countries and their members were handed over to Türkiye. *) At least 145 people feared dead in DRC boat tragedy At least 145 passengers are missing and feared dead after a motorised boat overloaded with goods and animals sank at night on a river in northwestern Democratic Republic of Congo. About 55 people survived the disaster, officials said. The boat was travelling to the neighbouring Republic of Congo when it capsized in the Lulonga River. And finally… *) Kashmir, Chad, Venezuela activists win Martin Ennals Award Campaigners from disputed Kashmir region, Chad and Venezuela win the Martin Ennals Award, one of the world's most prestigious human rights prizes. Khurram Parvez, a prominent rights activist in restive India-administered Kashmir, Delphine Djiraibe, one of Chad's first women lawyers and Feliciano Reyna, a rights activist in Venezuela bagged the award, the jury announced. The award ceremony, managed by Martin Ennals Foundation, will take place in Geneva on February 16, the organisers said.

Habari za UN
20 JANUARI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 20, 2023 0:12


Hii leo jarida linaangazia mapigano Soledar Mashariki mwa Donetsk Oblast nchini Ukraine, na habari kuhusu afya kanda ya ulaya. Makala tunakwenda nchini Somalia na mashinani DR Congo.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA limesema kwa mara ya kwanza misaada ya mashirika ya Umoja wa Mataifa imefanikiwa kuwasili katika eneo linalodhibitiwa na serikali karibu na Soledar Mashariki mwa Donetsk Oblast nchini Ukraine.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya ulaya tangu kuanza kwa msimu wa baridi kali katikati ya mwezi Novemba mwaka 2022 wamebaini kuongezeka kwa wagonjwa wanaolazwa kutokana na magonjwa ya homa ya mafua makali au flu, matatizo ya kupumua na COVID-19. Walio hatarini zaidi kupata maambukizi ya magonjwa hayo ni wahudumu wa afya pamoja na wazee, ndio maana wanaendesha kampeni ya kutoa chanjo..Makala tnaangazia kazi za WHO na mashirika mengine ya Umoja wa Mataifa likiwemo la uhamiaji, IOM na wadau wengine wakishirikiana kuwasaidia watu waliko katika hatari zaidi kwenye maeneo mbalimbali ya somalia wakiwemo waliofurushwa katika maeneo ya viunga vya mji wa Baidoa.Na katika mashinani tunakwenda jimboni Kivu Kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako watoto wanafurahia kuwa wasafi shuleni kutokana na huduma za kujisafi zilizofanikishwa na UNICEF. Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!