POPULARITY
Katika Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunatuama nchini Kenya, na tunaiangazia jamii ya Wanandi, ambapo kama ilivyo kwa mataifa mengi ya kiafrika, wanawake hawapewi nafasi ya kumiliki mali kama ardhi, mifugo – hasa ng'ombe wa maziwa – hali ambayo imesababisha uduni wa maendeleo ya kiuchumi miongoni mwao.Kufahamu kwa undani, ungana na Emmanuel Makundi na Victor Moturi, ambaye alizuru eneo la Nandi na kuandaa makala haya.
Katika Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunatuama nchini Kenya, na tunaiangazia jamii ya Wanandi, ambapo kama ilivyo kwa mataifa mengi ya kiafrika, wanawake hawapewi nafasi ya kumiliki mali kama ardhi, mifugo – hasa ng'ombe wa maziwa – hali ambayo imesababisha uduni wa maendeleo ya kiuchumi miongoni mwao.Kufahamu kwa undani, ungana na Emmanuel Makundi na Victor Moturi, ambaye alizuru eneo la Nandi na kuandaa makala haya.
Katika Makala haya mtangazji wa ko Ali Bilali anakuletea Historia ya siku ya wanawake duniani ambayo husherehekewa kila ifikapo machi 8 ya kila mwaka
Katika Makala haya, mtangazaji wako Ali Bilali anazungumza na Cassypool mwanamitandao na muhamasishaji kutoka nchini Kenya, ambae amejizolea umaharufu kupitia kile alichokiita tasnia ya uchawa, ambapo anaeleza kuwa chawa wa rais wa Kenya William Ruto na sasa ni chawa wa rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Kumbuka pia kutufollow kwa instagram @billy_bilali
Katika Makala haya ya kwanza kabisa ya mwaka 2025, mtangazaji wako asiependa makuu Ali Bilali anakupa fursa ya kuwatakia heri ya mwaka mpya ndugu jamaa na marafiki.
Katika Makala haya, tunajadili hatua ya hivi karibuni ambapo baadhi ya mataifa ya Afrika Mashariki yamendelea kurekodi ongezeko la visa vya utekaji na mauaji, vingi vikitekelezwa na idara za usalama au watu wasiojulikana. Unazungumziaje hali hii ? Haya hapa baadhi ya maoni yako.
Katika Makala haya, tunajadili hatua ya hivi karibuni ambapo baadhi ya mataifa ya Afrika Mashariki yamendelea kurekodi ongezeko la visa vya utekaji na mauaji, vingi vikitekelezwa na idara za usalama au watu wasiojulikana. Unazungumziaje hali hii ? Haya hapa baadhi ya maoni yako.
Katika Makala haya Ali Bilali amejielekeza Alliance Francaise ya Nairobi ambayo imeandaa Onyesho la Kwanza la tamthilia ya ‘Mgonjwa Mwitu', utayarishaji wao wa kila mwaka wa maigizo yaliyotolewa na tamthilia za waandishi mashuhuri wa Ufaransa. Kwa maadhimisho ya miaka 75, chaguo ni 'Le Malade Imaginaire' na Molière. Hii ni comedy ya mwisho kuandikwa na Molière. Ingawa ilionyeshwa kwa mara ya kwanza mnamo 1673, kichekesho hiki cha kejeli, mojawapo ya bora zaidi za Moliere, hakijapoteza mvuto wake wa dhati na wa ulimwengu wote.Kumbuka pia kumfollow mtangazaji wako @billy_bilali kwenye mitandao ya kijamii @billy_bilali
Muziki wa kizazi kipya umewawezesha vijana nchini Tanzania kujikwamua kimaisha kwa kujipatia kipato kupitia Sanaa hiyo,Katika Makala haya Steven Mumbi anazungumza na Hussein Mussa Shundi Maarufu Rucky.
Katika Makala ya Wiki hii, Steven Mumbi amezungumza naye Jilema Ng'wana Shija msani wa muziki wa asili kutoka nchini Tanzania.
Mwandishi wetu Steven Mumbi amezungumza na msani wa muziki huu wa Baibuda
Katika Makala haya Ali Bilali anazungumzia kuhusu siku ya kuwambuka watu waliotoa mchango wao katika harakati za ukombozi ambapo kila januari 4 ni siku ya kuwakumbuka wapambanaji hao waliochangia katika ukombozi wa nchi Usikosi pia kumfollow mwanahabari wako Ali Bilali kwa Instagram @billy_bilali
Katika Makala haya, mwanahabari wako Ali Bilali anarejelea historia ya mwanaharakati mtetezi wa Uhuru wa DRC Emery Patrice Lumumba aliezaliwa Julay 2 1925 alifariki Januari 17 mwaka 1961. Usikosi pia kumfollow mtangazaji wako @billy_bilali
Katika Makala haya,Florence Kiwuwa mtangazaji wa maswala ya Historia na utamaduni kutoka RFI Kiswahili anakuletea historia ya wadigo wa Kenya na Tanzania na kwenye le Parler francophone tutaangazia kuhusu maonyesho yake Dj Click katika ukumbi wa Alliance Francaise ya Arusha nchini Tanzania. Na kwenye Muziki tutamuangazia mwanamuziki Koffi Olomide kutokea DRC.
Karibu mpenzi msikilizaji katika Makala ya leo Changu Chako Chako Changu, ambapo nakukumbusha historia na tamaduni ya watu wa kabila la wataita, na kwenye le parler francophone tutaangazia ratiba ya shughuli za kitamaduni Alliance France Francaise ya Nairobi, Dar es salaam, Arusha, na Institut francais ya Lubumbashi. Na kwenye Muziki nitakuletea mwanamuziki Hiro Le Coq rapa wa Ufaransa mwenye asili ya DRC. Mimi naitwa Ali Bilali bienvenue.
Katika Makala ya Gurudumu la Uchumi juma hili, mtayarishaji wa makala haya amezungumza na Profesa Wetengere Kitojo, mtaalamu wa masuala ya uchumi akiwa Tanzania, ambapo wanaangazia kuhusu tatizo la uhaba wa dola ya Marekani kwenye nchi za Afrika Mashariki.
Katika Makala ya Gurudumu la Uchumi juma hili, mtayarishaji wa makala haya amezungumza na Profesa Wetengere Kitojo, mtaalamu wa masuala ya uchumi akiwa Tanzania, ambapo wanaangazia kuhusu tatizo la uhaba wa dola ya Marekani kwenye nchi za Afrika Mashariki.
Katika Makala haya, Ali Bilali mtangazaji wa maswala ya Historia na utamaduni kutoka RFI Kiswahili anakuletea historia ya waswahili wa Burundi katika mazungumzo na mzee mkongwe mwana Historia kutoka Buyenzi, Mzee Anzuruni Hussein, ikiwa ni sehemu ya kwanza, na kwenye le Parler francophone tutaangazia kuhusu ratiba ya shughuli za kitamaduni Alliance Francaise ya Nairobi na Dar es salaam. Na kwenye Muziki tutamuangazia mwanamuziki Vichou Love kutoka nchini Burundi.
Katika Makala haya Mtangazaji wako Ali Bilali wa idhaa ya Kiswahili ya RFI amezungumza na kina Mama kutoka kundi la Warumba wa Nyakanga, ambao hutoa burudani ya kuimba kwa kutumia ngoma maharufu "Msondo" huku wakitoa pia somo la mafunzo ya kumfunda mwali katika utamaduni wa waswahili wa Buyenzi. Na kwenye Muziki utampata Kijana Khalid msanii wa miondoko ya Taarab kutoka nchini Burundi mwenye lengo la kuinua muziki huo nchini Burundi. Usikosi pia kumfollow mtangazaji wako kwenye mitandao ya kijamii instagram na facebook billy_bilali
Katika Makala haya ya burudani huwa tunakupa nafasi wewe msikilizaji wetu kuchagua wimbo nasi tunakuchezea moja kwa moja kwenye redio kila siku ya Ijumma
Katika Makala haya ya burudani huwa tunakupa nafasi wewe msikilizaji wetu kuchagua wimbo nasi tunakuchezea moja kwa moja kwenye redio kila siku ya Ijumma
Katika Makala haya ya leo Ali Bilali anajadili na wachambuzi kuhusu siku mia moja ya vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan
Kila Ijuma rfi Kiswahili inakupa nafasi ya kipekee kuskiza vibao moto moto ndani ya Makala Muziki ijumaa. Katika Makala haya Utaskia vibao moto kutoka kwa wasanii wakale kama vile Madilu System, hadi wa sasa kama vile Hermonize kutoka Tanzania. Kwa uhondo zaidi skiza makala.
Kila Ijuma rfi Kiswahili inakupa nafasi ya kipekee kuskiza vibao moto moto ndani ya Makala Muziki ijumaa. Katika Makala haya Utaskia vibao moto kutoka kwa wasanii wakale kama vile Madilu System, hadi wa sasa kama vile Hermonize kutoka Tanzania. Kwa uhondo zaidi skiza makala.
Hii leo jaridani tunakuletea habari za WHO nchini Burundi na UNICEF eneo la Sahel. Makala tutamsikia mwanafunzi kutoka Tanzania ambaye ni mshiriki wa mkutano wa 67 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW67 na mashinani tutasalia hapa makao makuu kusikia ujumbe kuhusu haki ya maji.Mamlaka ya afya nchini Burundi leo imetangaza mlipuko na kusambaa kwa virusi vya polio type 2 baada ya wagonjwa wanane kuthibitishwa , ikiwa ni mara ya kwanza kuthibitishwa kwa virusi hivyo baada ya zaidi ya miongo 3 kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO.Watoto milioni 10 nchini Burkina Faso, Mali na Niger wana uhitaji mkubwa wa misaada ya kibinadamu, idadi ambayo ni maradufu ikilinganishwa na mwaka 2020, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto duniani, UNICEF hii leo, chanzo kikiwa ni mizozo inayoshamiri kila uchao na kwamba Watoto wengine million 4 nchi Jirani wako hatarini Zaidi kwani mapigano kati ya makundi yaliyojihami na majeshi ya serikali yanavuka mipaka.Katika Makala mwanafunzi kutoka Tanzania ambaye ni mshiriki wa mkutano wa 67 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW67 unaomalizika leo, amezungumza na Selina Jerobon wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa mataifa kuhusu kilichomleta kwenye mkutano huu na matarajio yake katika ulimwengu huu wa kidijitali.Na katika mashinani ikimulika ujumbe kuhusu haki ya maji ikiwa ni kuelekea mkutano wa Umoja wa Mataifa wa maji utakaofanyika wiki ijayo hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Shirika la afya duniani limeonya kuhusu ongezeko la magonjwa yasiyoambukizwa haswa katika mataifa yanayoendelea Magonjwa yasiyoambukizwa ni changamoto kubwa kwa watu wengi kote ulimwenguni ,magonjwa haya yakichangiwa na maisha ya kisasa ambapo watu wengi hawazingatii vyakula vyenye lishe na mazoezi.Katika Makala haya tunakuletea namna moja ya kupambana na magonjwa haya ,mazoezi ya kutembea ambayo wakaazi wa Mombasa wamekumbatia.
Shirika la afya duniania WHO limesambaza tayari dozi kadhaa za chanjo ya Ebola nchini Uganda. Na katika mataifa kadhaa ya Afrika yakiwemo Nigeria ,Kenya ,utapia mlo unaendelea kushuhudiwa. Katika Makala haya ,tumeangazia shughuli ya kuchoma chanjo ya Ebola nchini Uganda. Vile vile hali ya baa la njaa nchini Nigeria na mataifa ya Pembe ya Afrika ,Afrika Mashariki ambapo hali hiyo imesababisha kuongezeka visa vya utapia mlo. Nchini Nigeria ,majimbo yanayokabiliwa na mashambulio ya makundi ya kijihadi ,yameathirika zaidi.
Katika Makala haya ya leo Changu Chako Chako Changu, muandaaji wa makala haya Ali Bilali amekutana na waalimu wa lugha ya Kifaransa huko Mombasa wakati wakiadhimisha siku kuu ya kimataifa ya waalimu wa lugha ya Kifaransa. Mabatana naye.
Katika Makala haya, mwana Historia wetu hapa RFI Ali Bilali anakuletea taarifa kuhusu filamu ya Vuta N'kuvute ambayo inaeleza kwa ufupi Historia ya Zanzibar na itayoonyeshwa kuanzia Jumatatu Octoba 03 Alliance Francaise ya Nairobi, na baadae huko Mombasa na Lamu nchini Kenya.
Katika Makala haya,tunaangazia juhudi za baadhi ya nchi za Afrika kupigania haki za uzazi .Wabunge wa Morocco wamependekeza mswada wa wanawake kupewa likizo ya siku mbili ya hedhi yenye malipo,wakati Zambia ikiwa tayari imepitisha sheria kama hiyo.
Katika Makala tunazungumzia msambao wa hatari wa Monkey Pox ambao umefanya shirika la afya duniani kutangaza janga la hatari.Pia tunaangazia ugonjwa wa homa ya Mgunda ulioripotiwa kusini mwa nchi ya Tanzania.
Mwaka wa 2019 raisi Uhuru Kenyatta alizindua rasmi zoezi la wasichana walio na umri wa miaka 10 kupewa chanjo ya saratani yaani HPV, lakini zoezi hilo lilipata pingamizi kutoka kwa wadau mbalimbali nchini. Katika Makala haya,mhariri wetu Ruth Keah ameangazia kuhusu habari za urongo ambazo zilifanya wazazi kupuuza chanjo hiyo na wataalamu ambao wamekosoa habari hizo za urongo.
Katika Makala haya mtangazaji wako Ali Bilali amewapikea Studio Gez Gez Kasesa kutoka nchini Burundi na Dokta Gharib Mosepe kuzungumzia utamaduni wa watu kutoka Burundi na Kenya katika maswala mbalimbali. na kwenye Kipengele cha Muziki utapata kumfahamu mwanamuziki hayati Oliver Ngoma. Usikosi pia kumfollow Ali Blali kwa Instagram kwa kubonyeza @billy_bilali
Katika Makala haya Carol Korrir anazungumza na daktari Willis Akhwale mshauri wa muungano wa viongozi wa bara la Afrika kuhusu kupambana na Maleria juu ya mbinu za kisasa kukabiliana na ugonjwa huo ambao bado umeendelea kuwa tisho duniani.
Katika Makala haya tunazungumzia kuhusu sherehe za harusi, le parler francophone na kwenye muziki nakuletea mwanamuziki kutoka Burundi anaitwa Vichou Love. Usikosi kuambatana nasi na unanafasi ya kutoa maoni au mapendekezo.
Katika Makala haya Ali Bilali anakuletea Burudani ya Muziki pamoja na chaguo ulilochaguwa wewe msikilizaji. Ambatane naye hadi tamati usikosi pia kumfollow kwa Instagram @billy_bilali
Katika Makala haya Ali Bilali anakuletea Burudani ya Muziki pamoja na chaguo ulilochaguwa wewe msikilizaji. Ambatane naye hadi tamati usikosi pia kumfollow kwa Instagram @billy_bilali
Jamii nyingi uhusisha ulemavu na laana pamoja na ushirikina,huku wengine wakihusisha ulemavu huo na kasoro zinazotokana kwa mzazi haswa wa kike.Kufuatia madai hayo baadhi ya wanajamii uonekana kuwatenga watoto wanaozaliwa na ulemavu. Ukweli ni kwamba watu wenye ulemavu wako sawa tu kama wengine wasio walemavu.Katika Makala haya “Ulemavu Wangu” leo tunaangazia dada watatu waliozaliwa na ulemavu,licha ya baadhi ya watu katika jamii kuwatenga,wazazi wao walijizatiti katika kuwalea na kuwasomesha na kwa sasa wote watatu ni wanaharakati wa kutetea haki za wanawake wenye ulemavu jijini Mombasa chini ya shirika lao la Tunaweza Women With Disability. Lucy Chesi pamoja na dadazake wawili wote walizaliwa na ulemavu na cha kufurahisha ni kwamba licha ya kupitia unyanyasaji na kukashifiwa kwa sababu ya maumbile yao,walipuuza kashifa hizo na kujitahidi katika maisha. Lucy anasimulia stori yake. By:Trezer Odero
Katika Makala haya utapata kufahamu zaidi kuhusu warsha ya kimataifa ya idhaa za kiswahili iliofanyika mjini Arusha na kujumuisha vituo mbalimbali vya idhaa za kiswahili kutoka ukanda wa Afrika mashariki. Usikosi pia ku follow kwa Instagram https://www.instagram.com/billy_bilali/
Mchezo wa Mpira wa miguu maarufu zaidi kama kandanda au soka, ni mchezo unaopendwa na wengi. Katika Makala haya, mhariri wetu Ruth Keah anamuangazi kijana kwa jina Mohammed Munga aliye na ulemavu wa mguu lakini akapuuza ulemavu huo na kwa sasa anang'aa katika ulingo wa soka kimataifa.
Katika Makala haya ,tunaangazia jinsi ambavyo baa la njaa limeathiri afya za raia wengi wa Afrika Mashariki na Pembe ya Afrika.Shirika la misaada la OXFAM linasema kuna zaidi ya watu millioni 15 katika mataifa hayo ambao hawana chakula kutokana na ukame na athari za janga la Corona kwenye chumi za taifa.
Katika Makala haya ,utafahamu kuhusu ugonjwa wa Menengitis unaosababishwa na bacteria zinazoathiri uti wa mgongo na sehemu ya ubongo wa binadaam. Shirika la afya duniani lmeorodhesha Menengitis kuwa ugonjwa hatari unaoweza kusababisha vifo kwa haraka na unaohitaji huduma za dharura.
Katika Makala haya, Hillary Ingati anakuletea Historia ya mfalme wa Buganda nchini Uganda
Katika Makala haya ,tunaangazia madhara ya kiafya ya unywaji pombe . Madhara ya afya pia ni chanzo cha matatizo kwenye familia na jamii.
Mataifa mengi yanazidi kupambana kuhakikisha raia wao wanachomwa chanjo ya kuzuia Corona ambayo imesababisha vifo vya wengi duniani. Hata hivyo bara la Afrika bado lina idadi ndogo ya watu waliochanjwa kamili. Katika Makala haya tunajadili tatizo la raia kusita kupokea chanjo ya kuzuia Corona.
Katika Makala haya Changu chako juma hili, mtangazaji wako Ali Bilali anakuletea Historia ya ngome ya Fort Jesus ilipo Mombasa nchini Kenya na muendelezo wa tamasha la Blu Economy lililofanyika huko Mombasa.
Katika Makala haya mtangazaji wako Ali Bilali anakuletea Historia ya Uhuru wa Burundi ambao husherehekewa kila ifikapo Julay 01. Ambatana naye kufahamu zaidi harakati zilivyokuwa hadi kuuawa kwa mwanamfalme Louis Rwagasore. Usikosi pia kumfollow kwa Instagram @billy_bilali
Katika Makala haya, mtanzaji wako amuandamizi wa Makala za Historia Ali Bilali anakuletea Historia ya Uhuru wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo. DRCongo ilipata uhuru Juni 30 mwaka 1960 kupitia harakati za kinara wa uhuru huo Emery Patrice Lumumba. Usikosi pia kutofollow kwa Instagram kwa kuandika @billy_bilali https://www.instagram.com/billy_bilali/
Katika Makala haya, Ali Bilali anazungumzia kuhusu Historia ya wanaharakati wa Uhuru nchini Kenya Mau Mau.
Kila ijumaa muskilizaji una nafasi ya kuomba wimbo unaopenda wewe, hapa Caro Korr, anavicheza vibao ulivyochagua wewe.
Kila ijumaa muskilizaji una nafasi ya kuomba wimbo unaopenda wewe, hapa Caro Korr, anavicheza vibao ulivyochagua wewe.
Katika Makala haya ,tunaangazia juhudi za watalaam wa afya na viongozi wa Afrika kupigania bara hili kupata chanjo ya kuzuia Corona baada ya madai ya kutokuwepo kwa usawa kwenye usambazaji wa chanjo. Mataifa mengi ya Afrika kutokana na ubaguzi huo na uhaba wa chanjo yamesalia nyuma katika kampeni ya uchomaji chanjo.
Kila ijumaa muskilizaji una nafasi ya kuomba wimbo unaopenda wewe, skiza maka ya juma hili.
Kila ijumaa muskilizaji una nafasi ya kuomba wimbo unaopenda wewe, skiza maka ya juma hili.
Katika Makala haya mpenzi msikilizaji utapata kusikia matatizo ya kuganda kwa damu. Tatizo hili limeongezeka katika kipindi hiki cha maambukizi ya Corona, ambapo baadhi ya dawa zinazotumika kama chanjo dhidi ya Covid-19 zimehusishwa na tatizo hili. Ambatana naye mtangazaji wako Carol Korrir kufahamu mengi zaidi.
Katika Makala haya muandishi wa maswala ya Historia anakuletea Historia ya wimbo wa hisani uliopiga fora kote duniani miaka zaidi ya 30 iliopita mpaka leo We are the World. Wimbo huu uliwajumuisha wanamuziki zaidi ya 80 wa Marekani kwa ajili ya kuchangisha fedha za misaada kuwasaidia watu waliokumbwa na baa la Njaa katika pembe ya Afrika lakini pia Marekani.
Sehemu ya pili ya Katika Makala kuhusu Historia ya wimbo wa hisani uliopiga fora kote duniani miaka zaidi ya 30 iliopita mpaka leo We are the World. Wimbo huu uliwajumuisha wanamuziki zaidi ya 80 wa Marekani kwa ajili ya kuchangisha fedha za misaada kuwasaidia watu waliokumbwa na baa la Njaa katika pembe ya Afrika lakini pia Marekani.
Wakati dunia ikiadhimisha, siku ya kuhamasisha raia wa nchi tofuati kuhusu namna ya kutokomeza ugonjwa wa Malaria Aprili 25, Kwa mujibu wa takwimu za shirika la afya duniani, WHO ripoti,,iliyongazia mwaka mmoja uliopita,mikakati iliyowekwa kuzuia ,kupima na kutibu Malaria ziliathirika katika thuluthi tatu za mataifa ya ulimwengu , kutokana na janga la Corona. Katika Makala ya Siha Njema tunaangazia juhudi tofuati za kupambana na Malaria barani Afrika ikiwemo majaribio ya chanjo ya Malaria nchini Kenya,Ghana na Malawi.
Katika Makala ya Siha Njema tunaangazia Ripoti ya umoja wa mataifa , ya mwaka 2020 ya huduma za upangaji uzazi,mwaka moja tangu kuzuka janga la Corona .Ripoti hiyo imebaini kushuka kwa huduma hizo na kuonya mataifa mengi huenda ikapunguza uwekezaji wao kwenye huduma za kupanga uzazi kutokana na kuathirika kwa chumi zao .
Katika Makala haya Muziki Ijumaa, Ali Bilali anakuletea mwanamuziki wa Hip Hop aliewahi kutamba sana miaka hiyo kutokana na style yake ya Muziki na mavazi, kabla ya kujikita zaidi katika biashara.
Katika Makala haya utapata kufahamu kuhusu historia ya mkutano wa Kimataifa wa Tokyo juu ya maendeleo ya Afrika TICAD. (Tokyo International Conference on Africa Developpment). kwenye kipengele cha utamaduni utafahamu utamaduni wa Ndoa kwa mila za Warundi. Na kwenye kipengele cha Muziki, utaipata Burudani ya Muziki wa Marehemu DJ Arafat (l'Enfant de Dieu) Usikosi pia kutufollow kwa Instagram kwa kuandika billy_bilali
Katika Makala haya utapata kusikia sehemu ya 3 ya Historia ya wakimbizi Duniani, lakini pia Ali Bilali amezungumza na Somo bi Mariam wa Migomba kuhusu uvaaji wa Shanga kwa wanawake. Utapata pia burudani ya wimbo wa mwanamuziki kutoka Ufaransa Frederic Francois
Katika Makala haya, Ali Bilali amezungumza na balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Frederic Clavier kuhusu siku kuu ya mapinduzi nchini Ufaransa ambayo huadhimishwa kila Julay 14.
Katika Makala haya nakuletea Historia ya nchi tajiri Duniani ama G7, lakini pia utapata kusikia utamaduni wa kumuoza binti wa Kiratoga nchini Tanzania, huku nikikupa burudani ya Muziki wa Werrason ambae anahamasisha wananchi wa Mashariki ya DRCongo kujilinda na Ebola.
Kutana na Imelda Munyaga Mwalimu wa Sanaa za aina mbalimbali. Katika Makala haya anazungumza na Steven Mumbi kuhusu Sanaa ya Muziki na Uigizaji.
Muziki wa Singeli ni Miongoni mwa Muziki unaochipukia nchini Tanzania,vijana wanajaribu kuifikia hadhira kwa kutumia maudhui ya Asili. Katika Makala haya ya Nyumba ya Sanaa,Ungana na Steven Mumbi akizungumzia Muziki huo akiwa na S.Kide pamoja na Kiongozi wa Wakupeti Band.
Katika Makala haya Tunaangazia Muziki na Cocodo African Music Band wakifanya sanaa ya Muziki kutoka nchini Tanzania Ungana na Steven Mumbi akizungumza na Lemi na Nelius wakizungumzia Safari yao ya kimuziki katika Sehemu hii ya kwanza.
Sanaa ya Ubinufu ndio sanaa mama katika Uchoraji,Uchongaji na hata katika matumizi ya vyuma chakavu katika kuunda Vifaa mbalimbali. Katika Makala ya Nyumba ya Sanaa Ungana na Steven Mumbi akizungumzuza na Mhadhiri wa Chuo kikuu cha Dar es salaam UDSM, Safina Kimbokota wakizungumza Sanaa hiyo na Mapokeo ya wanafunzi kusoma Sanaa katika elimu ya juu.
Kila mwaka Dunia huadhimisha siku ya upigaji picha za Habari, Picha zinazoelezea hali wanazokabiliana nazo wananchi katika mataifa Mbalimbali, kutoka barani Afrika ni asilimia 2 tu ya picha hizo huonekana Duniani. Katika Makala ya Nyumba ya Sanaa Steven Mumbi anaangazia umuhimu wa Upigaji Picha za Habari.
Yanafanyika maonyesho ya Kimataifa ya biashara jijini Dar Es Salaam nchini Tanzania maharufu kama Sabasaba, inakuwa ni fursa kwa wafanyabiashara kutoka katika mataifa mbalimbali kushindanisha bidhaa zao. Katika Makala haya utaweza kufahamu zaidi kuhusu maonyesho hayo. usikosi pia kumfollow @billy_bilali
Katika Makala haya, Ali Bilali anazungumza na mwanadada anaejihusisha na mitindo ambae amekuwa akipambana kujikwamua kimaisha, ambapo shughuli zake anaendesha katika majengo ya kituo cha kimataifa cha mikutano cha Nyerere Internationale Conference Center. Ambatana naye kufahamu mengi zaidi