Podcasts about kimataifa

  • 27PODCASTS
  • 338EPISODES
  • 13mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • May 29, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about kimataifa

Latest podcast episodes about kimataifa

Habari za UN
29 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 29, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia Walinda Amani wa Umoja wa Mataifa ikitupeleka nchini DRC, Sierra Leone na Ghana. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na maana ya neno "MISHEMISHE.”Leo ni Siku ya Kimataifa ya Walinda Amani ambayo mwaka huu inajikita na maudhui ya “mustakabali wa ulinzi wa amani.”Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema walinda amani wa Umoja wa Matafa wako katika changamoto kubwa “Leo hii, walinda amani wanakabiliwa na hali zinazozidi kuwa ngumu katika dunia inayozidi kuwa na changamoto, ikiwemo uugawanyika na kutofautiana kwa mitazamo duniani kunazidi kuongezeka, operesheni za ulinzi wa amani zinakabiliwa, hatari zaidi kutokana na wingi wa vitisho kama vile ugaidi na walinda amani kulengwa kwa makusudi kupitia taarifa potofu zenye madhara makubwa na changamoto zinazovuka mipaka kuanzia janga la mabadiliko ya tabianchi hadi uhalifu wa kimataifa.Kikosi cha 11 cha Tanzania kinachohudumu chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO kimeungana na walinda amani wengine kuadhimisha Siku ya Walinda Amani Duniani. Maadhimisho hayo yamefanyika Mavivi, yakiongozwa na Brigedia Jenerali Diamond Meshack Madie, Mnadhimu Mkuu wa Vikosi vya MONUSCO.Shirika la Umja wa Mataifa la Mazingira UNEP limezindua mpango mpya wa dola milioni 15 kusaidia uwekezaji endelevu katika Bonde la Kongo – moja ya mifumo muhimu zaidi ya ikolojia duniani. Mpango huu unalenga kufungua fursa za biashara rafiki kwa mazingira kwa wajasiriamali wadogo na wa kati katika sekta za kijani. Msitu wa mvua wa Bonde la Kongo ni moja ya vyanzo vikubwa vya kaboni duniani na ni makazi ya watu zaidi ya milioni 75, wakiwemo jamii za asili.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu leo ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi  Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno "MISHEMISHE.”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
20 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 20, 2025 12:20


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika wafugaji wa nyuki nchini Tanzania leo ikiwa ni siku ya nyuki duniani iliyopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 20 Desemba mwaka 2017 kupitia azimio namba A/72/211.Baada ya miaka mitatu ya majadiliano, leo katika Mkutano wa Kimataifa wa Afya unaoendelea Geneva, Uswisi, nchi zimepitisha rasmi makubaliano ya kihistoria ya kuzuia, kujiandaa, na kukabiliana vyema na majanga ya magonjwa kwa siku zijazo. Taratibu zote zitakapopitishwa na angalau nchi 60, mkataba utaanza kutumika rasmi mwakani.Kutokana na mamlaka za Israeli kulegeza kwa muda mzingiro uliodumu kwa wiki 11, angalau sasa matumaini kidogo yamerejea Gaza, yameeleza leo mashirika ya Umoja wa Mataifa. Msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya dharura, OCHA, Jens Laerke amesema tayari wamepata ruhusa ya kuyavusha malori matano yaliyokuwa yamezuiliwa jana.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP limetahadharisha  leo kwamba bila ufadhili zaidi, huenda katika muda wa wiki chache zijazo likalazimika kusitisha msaada wa chakula kwa takribani nusu ya watu linaowahudumia kwa sasa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.Na katika mashinani, fursa ni yake Hanan Al-Dayya, Mkimbizi wa ndani katika ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli, akisimulia  madhara ya mashambulizi yanayoendelea kutoka Israeli.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
19 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 19, 2025 11:08


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya afya, na wakimbizi wa Syria wanaorejea nchini mwao. Makala tukwenda nchini Kenya kumulika ufukaji wa nyuki, na mashinani tunakuletea ujumbe wa Katibu Mkuu wa IMO kuhusu Siku ya Kimataifa ya wanawake mabaharia.Wajumbe kutoka kote duniani wamekusanyika mjini Geneva, Uswisi, kwa ajili ya Mkutano wa 78 wa Baraza la Afya Duniani (WHA78) unaofanyika kuanzia leo Mei 19 hadi 27 Mei mwaka huu.Tangu kuangushwa kwa utawala wa aliyekuwa Rais wa Syria Bashar al Assad aliyekuwa madarakani kwa zaidi ya muongo mmoja, wananchi wa Syria wamekuwa wakimiminika kurejea nchini mwao ambapo takwimu za sasa zinaonesha zaidi ya Wasyria 500,000 wamerejea kutoka nchi jirani. Mmoja wa waliorejea ni Babu Jassim na Leah Mushi anatuletea simulizi yake.Katika makala tunaelekea Kajiado nchini Kenya, ambako juhudi za utunzaji mazingira kupitia mradi wa ufugaji wa nyuki unaofadhiliwa na shirika la misaada la Marekani USAID kwa kushirikiana na idara ya misitu ya Kenya KFS hazichangii tu katika kukuza uchumi wa jamii, bali pia kulinda mazingira. Kupitia Makala hii iliyoandaliwa na Sharon Jebichii, Bwana Mureithi mmoja wa wanufaika wa mradi huo anaanza kwa kueleza mafanikio yao.Nakatika mashinani, fursa ni yake Arsenio Dominguez, Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usafirishaji Majini, IMO akitoa ujumbe wa ujumuishaji na usawa wa kijinsia wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya wanawake mabaharia ambayo huadhimishwa tarehe 18 mwezi Mei kila mwaka.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
16 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 16, 2025 12:25


Hii leo jaridani tunaangazia uhakika wa chakula, na takwimu za afya za janga la COVID-19 kusababisha vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla. Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani nchini DRC, kulikoni?Ukosefu wa uhakika wa kupata chakula na utapiamlo kwa watoto uliongezeka kwa mwaka wa sita mfululizo mwaka 2024, na kuwatumbukiza mamilioni ya watu karibu na baa la njaa, huku wengine wakiepuka kutokana na misaada ya kimkakati. Imesema Ripoti ya Kimataifa kuhusu Janga la Chakula (GRFC) iliyotolewa leo huko Roma, Italia na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO.Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) ya takwimu za afya duniani iliyochapishwa jana Mei 15 ikionesha athari kubwa zaidi za kiafya zilizosababishwa na janga la COVID-19 kuhusu vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla, imeweka wazi kuwa katika kipindi cha miaka miwili pekee, kati ya mwaka 2019 na 2021, matarajio ya kuishi yalipungua kwa mwaka mmoja na miezi nane  ikiwa ni maporomoko makubwa zaidi katika historia ya hivi karibuni hali iliyobatilisha mafanikio ya afya yaliyopatikana kwa muongo mmoja.Katika makala Leah Mushi anatupeleka nchini Tanzania kusikia namna wanawake wenye ulemavu walivyoweza kujikwamua kutoka kwenye changamoto mbalimbali ikiwemo za kiuchumi na kuchangamkia fursa za uongozi.Na katika fursa ni yake Bernadette Kambonesa, mkimbizi wa ndani kutoka kijiji cha Bogoro, jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akizungumzia manufaa yatokanayo na uwepo wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini humo (MONUSCO).Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
FAO: Mikakati sahihi ya kilimo imeepusha mamilioni kutumbukia kwenye baa la njaa

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 16, 2025 2:17


Ukosefu wa uhakika wa kupata chakula na utapiamlo kwa watoto uliongezeka kwa mwaka wa sita mfululizo mwaka 2024, na kuwatumbukiza mamilioni ya watu karibu na baa la njaa, huku wengine wakiepuka kutokana na misaada ya kimkakati. Imesema Ripoti ya Kimataifa kuhusu Janga la Chakula (GRFC) iliyotolewa leo huko Roma, Italia na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO. Flora Nducha anakutaarifu kwa muhtasari.

Habari za UN
Chokoleti itengenezwayo Uganda yavuka mpaka na mabara -UNCTAD

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 9, 2025 3:55


Kutoka kakao ghafi huko Bundibugyo, magharibi mwa Uganda hadi Kampala mji mkuu wa kibiashara wa taifa hilo la Afrika Mashariki ndiko kunapatikana kiwanda cha kutengeneza chokoleti cha Equator kinachomilikiwa na Barbara Gonget na mume wake Gustav. Awali wazo la biashara hii lilionekana kutokuwa na mashiko. Ingawa hivyo baada ya ITC, ambacho ni Kituo cha Kimataifa ha Biashara kilicho chini ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo, UNCTAD pamoja na wadau wao kuweka usaidizi wao, hali imebadilika na sasa biashara inavuka sio tu mipaka bali mabara. Wawili hao Kwa kuchanganya mbinu za hali ya juu, zinazojali jamii, na ufundi wa kitaalamu, wanabadili taswira ya uzalishaji wa chokoleti nchini humo.Je wamefanya nini? Assumpta Massoi anafafanua zaidi kwenye makala hii iliyofanikishwa na ITC.

Habari za UN
UNESCO: Jazz ni daraja la kudumisha amani, uhuru na mshikamano

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 30, 2025 4:05


Leo tarehe 30 Aprili dunia nzima inaburudika kwa pamoja kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Jazz, Kuanzia New Orleans hadi Nairobi, Tokyo hadi Tunis, miji inawasha taa majukwaani na mioyoni kusherehekea midundo yenye ladha ya kale, ya kisasa na yenye mvuto wa kipekee. Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO linasema Jazz ni zaidi ya muziki, ni daraja la kuunganisha watu na kuleta utangamano. Flora Nducha anatupasha zaidi katika makala hii

Habari za UN
28 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 28, 2025 10:39


Hii leo jaridani tunaangazia siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya Kazini, na juhudi za Umoja wa Mataifa za kusaidia wakulima Sudan Kusini kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Makala tunasalia na usalama kazini na mashinani tunakwenda nchini Kenya, kulikoni?Leo ni Siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya Kazini mwaka huu ikibeba maudhui “Mapinduzi ya usalama na afya Kazini: Nafasi ya Akili mnemba na teknnolojia ya kidijitali mahala pa kazi” lengo likiwa kudhihirisha nguvu ya AI na teknolojia zinapotumika vyema zinaweza kuleta mabadiliko kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani ILO.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP nchini Sudan Kusini chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Korea KOICA wanaendesha mradi wa kusaidia wananchi katika kilimo ili kujenga ustahimilivu na kupambana na utapiamlo. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Evarist Mapesa.Makala tunabisha hodi nchini Indonesia, taifa hili la Kusini-Mashariki mwa bara la Asia, kubwa hasa ni kumulika ni kwa vipi sekta ya uvuvi nchini humu inatekeleza kivitendo wito wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi, ILO kuhusu usalama na afya Kazini.  Na katika mashinani fursa ni yake Abdikani Haji Hassan kutoka kambi ya wakimbizi ya Daadab iliyoko katika kaunti ya Garissa nchini Kenya ambaye  kupitia Mpango wa Prospects unaoungwa mkono na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF amejikwamua kimaisha na sasa ana ndoto ya kuenda ng'ambo ili kuendeleza ujuzi wake wa kupiga picha.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
AI na teknolojia za kidijitali zaweza kuwa chachu ya kuhakikisha afya na usalama kazini - ILO

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 28, 2025 2:58


Leo ni Siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya Kazini mwaka huu ikibeba maudhui “Mapinduzi ya usalama na afya Kazini: Nafasi ya Akili mnemba na teknnolojia ya kidijitali mahala pa kazi” lengo likiwa kudhihirisha nguvu ya AI na teknolojia zinapotumika vyema zinaweza kuleta mabadiliko kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani ILO. Flora Nducha na taarifa zaidi.

Habari za UN
25 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 25, 2025 10:57


Hii leo jaridani tunaangazia wakimbizi wa DRC waliokimbilia Burundi, na ujumbe wa Siku ya Kimataifa ya Hakibunifu. Makala inatupeleka nchini Kenya kuangazia ugonjwa wa malaria na mashinani tunasalia hapa makao makuu katika mkutano wa Jukwaa la watu wa asili.Mazingira ya maisha kwa wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC waliongia Burundi na kupelekwa katika kambi ya wakimbizi ya Musenyi si endelevu na yanatishia mustakabali wao. Msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR Ayaki Ito, amesema hayo leo huko Geneva, Uswisi wakati akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu hali ya wakimbizi hao wanaoendelea kumiminika nchini Burundi.Kesho Aprili 26 ni Siku ya Kimataifa ya Hakibunifu - Siku ambayo ni fursa kwa ulimwengu kukumbushwa umuhimu wa haki kwa watu wanaobuni mambo mbalimbali duniani. Ili kufahamu zaidi kuhusu Hakibunifu tumezungumza na mtaalamu wa Sheria za Sanaa na Hakimiliki, Wakili Joshua Msambila wa nchini Tanzania, kwanza anaeleza kilichomsukuma yeye kujikita katika eneo hili la sheria.”Makala hii leo ikiwa ni siku ya Malaria duniani tunaelekea Kenya kwa mwandishi wetu Thelma Mwadzaya akiangazia juhudi zinazofanyika kupitia chanjo ili kupambana na malaria ugonjwa mbao Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO linasema mwaka 2023 pekee ulikatili maisha ya watu 597,000 na na asilimia 95 ya vifo hivyo vilitokea barani Afrika, na sasa linataka juhudi mara dufu zifanyike ili kuutokomeza.Na katika mashinanin fursa ni yake Kulet Adam Ole Mwarabu kiongozi wa jamii ya kimaasai kutoka Tanzania anayeshiriki katika mkutano wa Jukwaa la watu wa asili kutoka hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa na anatoa wito wa maendelo, amani  na utunzaji wa ardhi na mazingira kwa jamii ya asili na dunia nzima kwa jumla.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
Uelewa wa Hakibunifu bado ni mdogo lakini ni jambo muhimu sana ulimwenguni – Wakili Joshua Msambila

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 25, 2025 2:26


Kesho Aprili 26 ni Siku ya Kimataifa ya Hakibunifu - Siku ambayo ni fursa kwa ulimwengu kukumbushwa umuhimu wa haki kwa watu wanaobuni mambo mbalimbali duniani. Ili kufahamu zaidi kuhusu Hakibunifu tumezungumza na mtaalamu wa Sheria za Sanaa na Hakimiliki, Wakili Joshua Msambila wa nchini Tanzania, kwanza anaeleza kilichomsukuma yeye kujikita katika eneo hili la sheria.

Habari za UN
23 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 11:15


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza, na harakati za utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili. Makala tunasalia hapa hapa makao makuu na mashinani tunakwenda nchini Burundi, kulikoni?Hali si hali huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli ambako wakimbizi wa ndani wanakabiliwa na hatari za kiafya ambako panya na wadudu kama vile viroboto na  nzi wamesambaa kutokana na mlundikano wa taka na  ukosefu wa huduma muhimu kama vile maji safi na salama.Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, mkutano wa 24 wa Jukwaa la Kudumu la Watu wa jamii za asili (UNPFII) linaendelea kujadili utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili  na kubaini mbinu bora za kushughulikia changamoto zinazowakabili. Miongoni mwa shiriki wa jukwaa hilo nimwakilishii wa Shirika la Ereto Solidarity Funds ambaye  amepata fursa ya kuzungumza na Sharon Jebichii wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa.Makala ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Kitabu na Haki Miliki ambapo kila mwaka tarehe kama ya leo siku hii huadhimishwa ili kutambua nguvu ya vitabu kama daraja kati ya vizazi na vizazi na tamaduni mbalimbali. Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na mwandishi maarufu wa vitabu vya elimu, Uchumi na uhamiaji, Ernest Makulilo mkazi wa Marekani katika jimbo la Missouri.Na mashinani kupitia video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO fursa ni yake Meena Poudel kutoka nchini Nepal, Kusini mwa Asia ambaye ni Katibu wa kikundi cha wanawake watumiaji wa msitu ambacho kinabadilisha takataka za misitu kuwa mbolea rafiki kwa mazingira huku pia wakijipatia kipato."Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!  

Habari za UN
Ujumbe wa Ernest Makulilo kuhusu siku ya Kimataifa ya Kitabu na Haki Miliki

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 3:31


Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Kitabu na Haki Miliki ambapo kila mwaka tarehe kama ya leo siku hii huadhimishwa ili kutambua nguvu ya vitabu kama daraja kati ya vizazi na vizazi na tamaduni mbalimbali. Katika makala hii Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na mwandishi maarufu wa vitabu vya elimu, Uchumi na uhamiaji, Ernest Makulilo mkazi wa Marekani katika jimbo la Missouri, kuhusu siku ya leo iliyoanzishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO mnamo mwaka 1995.

Habari za UN
15 Aprili 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 15, 2025 9:59


Karibu kusikiliza jarida la Umoja wa Mataifa ambapo hii leo tunamulika Kongamano la Kimataifa la Kiswahili linalofanyika mjini Kampala Uganda likiwaleta pamoja wadau kutoka kila kona ya Afrika na kwingineko kujadili mikakati ya kukuza lugha hiyo adhimu ya Kiswahili. Utasikiliza muhtasari wa habari ukiangazia miaka miwili tangu kuanza kwa vita vya sasa vya Sudan, UNHCR, yatoa wito kwamba mwitiko mkubwa wa kibinadamu ulioratibiwa vema ni muhimu ili kuzuia mateso zaidi na vifo kwa wananchi wa DRC, na Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) limeanza leo tarehe 15 hadi tarehe 17 katika Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. 

Habari za UN
Kwibuka2025: Katibu Mkuu UN ahimiza mshikamano wa kimataifa dhidi ya chuki

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 7, 2025 2:12


Dunia inapokumbuka miaka 31 tangu mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi nchini Rwanda mwaka 1994, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametuma ujumbe mzito wa maombolezo na onyo, akitaka mshikamano wa kimataifa kupambana na ongezeko la chuki, mgawanyiko, na misimamo mikali kupitia mifumo ya kidijitali. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
04 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 4, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu mabomu ya kutegwa ardhini. Makala inamulika harakati za kusongesha malengo ya maendeleo endelevu ikitupeleka nchini Kenya na mashinani tunasalia huko huko nchini Kenya, kulikoni?Ikiwa leo ni Siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu mabomu ya kutegwa ardhini na Msaada wa Hatua Dhidi ya Mabomu hayo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akisisitiza nchi kuheshimu mikataba ya kimataifa dhidi ya vilipuzi na silaha nyingine, Umoja wa Mataifa leo umethibitisha tena dhamira yake ya kusaidia Somalia katika mapambano dhidi ya hatari za vilipuzi kwa ajili ya mustakabali salama kwa Wasomali wote.Mwaka huu wa 2025, Siku ya Kimataifa ya Uhamasishaji Kuhusu Mabomu ya Ardhi na Usaidizi kwa Hatua Dhidi ya Mabomu inaadhimishwa chini ya kaulimbiu “Mustakabali Salama Unaanzia Hapa.” Umoja wa Mataifa inasisitiza umuhimu wa kufadhili miradi midogo yenye athari za haraka kusaidia watu wenye ulemavu wa viungo waliathirika katika mizozo. Juhudi hizi zinaimarisha ulinzi wa raia na kupanua teknolojia na uvumbuzi katika nchi zinazoendelea.Makala ambayo inamulika majadiliano ya siku mbili yanayofanyika kila mwaka ya será kuhusu maendeleo endelevu. Majadiliano hayo yanayokunja jamvi leo jijini Nairobi Kenya yameandaliwa na Club De Madrid na mwaka huu yamejikita na ufadhili wa maendeleo, Stella Vuzo kutoka kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIS Nairobi amepata fursa ya kuzungumza na baadhi ya vijana wanaoshiriki mkutano huo wa club de Madrid.Na mashinani leo utamsikia mhadhiri kutoka chuo kikuu cha Bayero jimboni Kano nchini Nigeria anayeshiriki mkutano wa majadiliano ya ufadhili wa maendeleo endelevu unaofanyika Nairobi Kenya.Mwenyeji wako ni Assumpta, karibu!

Habari za UN
Stadi za kuoka mikate zaleta furaha kwa mkimbizi Thérèse huko Beni nchini DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 2, 2025 1:52


Jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Thérèse Kavira, mwanamke shupavu aliyelazimika kukimbilia mji wa Beni baada ya waasi kuvamia kijiji chake sasa ameona nusu kwenye maisha yake kufuatia mafunzo ya kuoka mikate yaliyotolewa na ofisi ya Utafiti na Usaidizi kwa Mahusiano ya Kimataifa nchini humo pamoja na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO na sasa anajikimu kimaisha. Sharon jebichii na taarifa zaidi.

Habari za UN
02 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 2, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya Kimataifa ya Kuelimisha Umma kuhusu Usonji, na wakimbizi wa ndani nchini DRC. Makala inatupeleka nchini Tanzania kwa mada hiyo hiyo ya elimu kuhusu usonji, na mashinani tunakwenda Gaza.Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kuelimisha Umma kuhusu Usonji (Autism) mwaka huu wa 2025, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesisitiza umuhimu wa ujumuishaji na usawa kwa watu wenye changamoto hiyo akitambua mafanikio yao pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo duniani kote.Jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Thérèse Kavira, mwanamke shupavu aliyelazimika kukimbilia mji wa Beni baada ya waasi kuvamia kijiji chake sasa ameona nusu kwenye maisha yake kufuatia mafunzo ya kuoka mikate yaliyotolewa na ofisi ya Utafiti na Usaidizi kwa Mahusiano ya Kimataifa nchini humo pamoja na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO na sasa anajikimu kimaisha.Makala leo kama tulivyokujulisha ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu usonji, Assumpta Massoi anamulika jinsi shirika moja la kiraia nchini Tanzania linapigia chepuo harakati hizo.Na katika mashinani fursa ni yake Marah Hajjo, msichana mdogo kutoka Gaza huko Palestina Mashariki ya Kati ambaye anasimulia mabadiliko makubwa ya sikukuu ya Eid El Fitr ambayo mwaka huu ilighubikwa na kiza cha vifusi na mateso kutokana na mashambulizi kutoka Israeli.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!  

Habari za UN
Ujumbe wa Katibu Mkuu UN Siku ya Kimataifa ya Kuelimisha Umma Kuhusu Usonji

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 2, 2025 1:40


Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kuelimisha Umma kuhusu Usonji (Autism) mwaka huu wa 2025, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesisitiza umuhimu wa ujumuishaji na usawa kwa watu wenye changamoto hiyo akitambua mafanikio yao pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo duniani kote. Anold Kayanda anaeleza zaidi.

Habari za UN
28 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 28, 2025 9:59


Umoja wa Mataifa watuma salamu za rambirambi kufuatia tetemeko barani Asia.UNICEF na Ubalozi wa Uholanzi wamesaidia kupunguza magonjwa Kilolo, Tanzania.Makala ni kuhusu Siku ya Kimataifa ya Kutozalisha Taka.Mashinani tunamulika ubunifu wa Janet Chemitei  wa Tengeneza Cafe katika urejelezaji nguo nchini Kenya.

Habari za UN
25 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 25, 2025 11:16


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo tunasalia hapa makao makuu katika mkutano wa CSW69 uliokunja chamvi Ijumaa wiki jana, tunamsikia aliyekuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa 4 wa Umoja wa Mataifa wa Wanawake, Mkutano wa Beijing Bi. Gertrude Mongella.Hapa New York, Umoja wa Mataifa leo umetoa wito wa kuachiliwa kwa wafanyakazi wake wanaoshikiliwa kote ulimwenguni ambao wamejikuta matatani wakati wakiwahudumia watu walio katika hatari, huku wakihatarisha usalama wao binafsi kwa kukabiliwa na vitisho vya kutekwa nyara, vurugu, unyanyasaji, na kifungo katika maeneo yenye migogoro na majanga.Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kuhusu vifo vya watoto imeonya kwamba miongo ya maendeleo katika kupunguza vifo vya watoto na watoto wachanga wakati wa kuzaliwa yako hatarini kutokana na kupunguzwa kwa ufadhili. Idadi ya vifo vya watoto wa chini ya umri wa miaka mitano ilipungua hadi watoto milioni 4.8 mwaka 2023, huku vifo vya wakati wa kuzaliwa vikiendelea kubaki takriban milioni 1.9.Leo ni Siku ya Kimataifa ya Kumbukumbu ya Waathirika wa Utumwa na Biashara ya Watumwa ya Bahari ya Atlantiki, ikiwakumbuka mamilioni ya Waafrika walioteswa, kunyanyaswa, na kunyimwa utu wao. Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema “Kwa zaidi ya karne nne, mamilioni ya Waafrika walitekwa kwa nguvu, kusafirishwa kwa meli hadi mataifa ya kigeni, na kufanyishwa kazi katika hali mbaya za kikatili.”Na katika mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP, Lea mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa amekimbilia Burundi na familia anasilimua hali ilivyokuwa wakati wa kukimbia.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!  

Habari za UN
Wanaume 'wapenzi wetu' msiwe na hofu na sisi - Bi. Gertrude Mongella

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 21, 2025 1:59


Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, CSW69 unafikia tamati hii leo Machi 21 hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.Bi. Gertrude Mongella, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa 4 wa Kimataifa wa wanawake maarufu kama Mkutano wa Beijing uliofanyika mnamo mwaka 1995, hivi tunavyozungumza, pamoja na umri wake mkubwa ameshirikia karibia vikao vyote vya mkutano huu wa CSW69 ambao pia ulikuwa unaangazia utekelezaji wa maazimio yaliyowekwa miaka 30 iliyopita chini yake mama Mongella.Nilipokutana naye nimemuuliza swali hili la kichokozi.Mazungumzo zaidi kati yangu na Mama Gertrude Mongella yatakujia katika vipindi vyetu vijavyo hivi karibuni.

Habari za UN
21 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 21, 2025 10:43


Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, CSW69 unafikia tamati hii leo Machi 21 hapa katika makao makuu, na wakulima wanawake nchini Senegal. Mashinani inatupeleka nchini Tanzania kumulika mradi wa maji.Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, CSW69 unafikia tamati hii leo Machi 21 hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Bi. Gertrude Mongella, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa 4 wa Kimataifa wa wanawake maarufu kama Mkutano wa Beijing uliofanyika mnamo mwaka 1995, hivi tunavyozungumza, pamoja na umri wake mkubwa ameshirikia karibia vikao vyote vya mkutano huu wa CSW69 ambao pia ulikuwa unaangazia utekelezaji wa maazimio yaliyowekwa miaka 30 iliyopita chini yake mama Mongella.Tukiwa bado ndani ya mwezi wa Machi, unaotambuliwa kuwa ni mwezi wa wanawake tunakwenda nchini Senegal ambako huko wasichana waliokuwa wakifanya kazi za ndani, wamewezeshwa na Umoja wa Mataifa na sasa ni wakulima na wanatumia stadi za upigaji na utengenezaji video za mtandaoni kuelimisha jamii kuhusu kilimo chenye tijaMakala inayoturejesha hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kwenye mkutano wa Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake duniani CSW69 unaokunja jamvi hii leo Flora Nducha amebahatika kuzungumza na mmoja wa washiriki wa mkutano huo kutoka asasi za kiraia nchini Tanzania.Na katika mashinani fursa ni yake Janeth Zakaria kutoka kijiji cha Kaguruka mkoani Kigoma nchini Tanzania ambaye kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF anasema alikuwa anatembea umbali wa kilomita 10 kupata maji safi na salama lakini sasa ni hatua chache tu kutoka nyumbani kwake”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

Habari za UN
17 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 17, 2025 11:28


Hii leo jaridani tunaangazia madeni katika nchi zenye mapato ya chini na ujumbe wa washiriki wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani CSW69 hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa.Mkutano wa 14 wa Kimataifa wa Usimamizi wa madeni umeanza rasmi hii leo huko Geneva Uswisi ambapo kubwa linalojadiliwa ni namna ya kuhakikisha wakati serikali zikipambana kulipa madeni hazidumazi maendeleo.Akijibu swali la kwa nini pamoja na ongezeko na idadi ya wanawake katika ngazi za uamuzi nchini Tanzania lakini bado kuna changamoto zinazoukabili usawa wa kijinsia, Dkt. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu anayehudhuria mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake, CSW69 jijini New York, Marekani kupitia mahojiano maalumu na Anold Kayanda wa Idhaa hii ya Umoja wa Mataifa, anaeleza kuwa      mabadiliko chanya katika jamii hayaji kwa kutumia mabavu.Makala pia inatubakisha hapa Umoja wa Mataifa kwenye mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani CSW69. Ili kufanikisha lengo la usawa wa kijinsia Umoja wa Mataifa unasisitiza ushiriki wa wanaume katika mchakato hasa kwa kuzingatia kuwa mfumo dume miaka nenda miaka rudi umekuwa kikwazo cha kufikia lengo hilo, Flora Nducha amebahatika kuzungumza na mmoja wa wanaume wanaoshiriki mkutano huo kusikia maoni yake.Na katika mashinani baadhi ya washiriki wa mkutano wa CSW69 wakizungumza na idhaa hii kandoni mwa mkutano huo, wametoa wito wa mshikamano na msichana na mwanamke yeyote anayepitia changamoto kote duniani hususani wale wanaorejea shuleni baada ya kusitisha masomo kutokana na ujauzito kabla ya wakati. Mshiriki wa kwanza ni Nasra Kibukila anayewakilisha Mtandao wa Elimu Tanzania, TEN/Met.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!  

Habari za UN
UNCTAD: Wekeni wazi mikataba ya madeni mnayokopa ili kujenga imani kwa wananchi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 17, 2025 1:58


Mkutano wa 14 wa Kimataifa wa Usimamizi wa madeni umeanza rasmi hii leo huko Geneva Uswisi ambapo kubwa linalojadiliwa ni namna ya kuhakikisha wakati serikali zikipambana kulipa madeni hazidumazi maendeleo. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Assumpta Massoi

Habari za UN
Jumuiya ya kimataifa ishikeni mkono Sudan Kusini kwa maslahi ya wananchi - Micklina Kenyi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 12, 2025 2:10


Wakati mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake Duniani CSW69 ukiendelea hapa New York Marekani nchini Sudan Kusini wanawake na wasichana wanaendelea kuonja shubiri ya vita, wakibakwa, kuuawa, kukosa elimu na kupitia changamoto nyingine lukuki sababu ya vita. Mmoja wa washiriki wa mkutano wa CSW69 kutoka Sudan Kusini akizungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili amesema sasa imetosha amekuja na ujumbe mmoja tu, anataka jinamizi la vita lazima likome. 

Habari za UN
Ukraine: Mwakilishi wa UNFPA Ukraine Uller Muller na hali ya wanawake wajawazito nchini humo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 7, 2025 1:49


Zikiwa zimesalia siku mbili ya leo na kesho kufika tarehe 8 Machi Siku ya Kimataifa ya Wanawake, tunaendelea kuangazia hali ya wanawake duniani. Sharon Jebiichi anatupeleka Ukraine kutukutanisha na Mwakilishi wa muda wa Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu UNFPA nchini humo ambaye anaangazia madhila wanayokutana nayo wanawake wajawazito wa Ukraine.Ni Ulla Muller, Mwakilishi wa muda wa Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu UNFPA nchini Ukraine, akieleza kuhusu changamoto zinazowakumba wanawake wajawazito wa Ukraine.Anasema, “ninaweza kukuambia hadithi nyingi ambazo zimebaki nami kwa sababu nakutana na wanawake hawa kila mara, na mapenzi yangu kwao hayana mipaka.”Uller Muller anasimulia kisa cha mwanamke mmoja akisema,"Kuna mwanamke anayeitwa Ira ana umri wa miaka 31, na tayari anamlea mtoto mvulana wa umri wa miaka sita. Hivi karibuni aligundua kuwa ni mjamzito tena na anatarajia mapacha watatu. Ni hali ya kutisha na kuchanganya."Bi. Muller anaendelea kueleza kuwa mwanamke huyo alikuwa njiapanda asijue abaki alee ujauzito katika hali hiyo ya mabomu kila mahali au andoke? Hatimaye aliamua kubaki na kwa usaidizi wa UNFPA akafanikiwa kujifungua lakini kabla ya wakati. Uller Muller, anaitathimini hali hiyo akisema,"Faraja yake ya kuweza kujifungua salama iliakisi uthabiti wa akina mama wengi wa Kiukraine ambao wanaamua kutoondoka. Wanaamua kuwa bado wanapaswa kujenga mustakabali wa maisha yao. Bado wanapaswa kuishi maisha yaliyo karibu na hali ya kawaida kadri wawezavyo. Na hilo linajumuisha kuleta uhai katika hali ya vita."

Habari za UN
07 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 7, 2025 11:50


Hii leo jaridani tunaangazia maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wanawake, na hali ya wanawake wajawaito nchini Ukraine. Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani tunakupeleka nchini Kenya, kulikoni?Kuelekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake Machi 8, tathmini mpya ya Umoja wa Mataifa iliyowekwa wazi leo ikiangazia haki za wanawake miaka 30 baada ya Azimio la Beijing inaonesha uwepo wa maendeleo katika usawa wa kijinsia, kama vile sheria dhidi ya ubaguzi na sera jumuishi za kijinsia. Hata hivyo, ripoti hiyo inaeleza uwepo bado wa ubaguzi wa kijinsia uliojikita katika jamii, ukiendelea kuwazuia wanawake na wasichana kupata fursa.Zikiwa zimesalia siku mbili ya leo na kesho kufika tarehe 8 Machi Siku ya Kimataifa ya Wanawake, tunaendelea kuangazia hali ya wanawake duniani. Sharon Jebiichi anatupeleka Ukraine kutukutanisha na Mwakilishi wa muda wa Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu UNFPA nchini humo ambaye anaangazia madhila wanayokutana nayo wanawake wajawazito wa Ukraine.Katika makala Assumpta Massoi anakupeleka kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake kwenye mkoa mmoja ulioko katikati mwa Tanzania.Na mashinani kesho Dunia ikiadhimisa siku ya kimataifa ya wanawake duniani tunakwenda nchini Kenya kusikia ujumbe wa mwanaharakati wa wanawake kuhusu uswa wa kijinsia.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
06 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 6, 2025 10:36


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Umoja wa Mataifa kupitia miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa Pamoja wa Kigoma, KJP nchini Tanzania, unaolenga kuhakikisha wanawake na wasichana wanajumuishwa kwenye mipango ya kuhimili na kukabili mabadiliko ya tabianchi, kwa kuwajengea uwezo.Kuelekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake Machi 8, tathmini mpya ya Umoja wa Mataifa iliyowekwa wazi leo ikiangazia haki za wanawake miaka 30 baada ya Azimio la Beijing inaonesha uwepo wa maendeleo katika usawa wa kijinsia, kama vile sheria dhidi ya ubaguzi na sera jumuishi za kijinsia. Hata hivyo, ripoti hiyo inaeleza uwepo bado wa ubaguzi wa kijinsia uliojikita katika jamii, ukiendelea kuwazuia wanawake na wasichana kupata fursa.Ripoti nyingine ya Umoja wa Mataifa iliyochapishwa leo ikiangazia Sudan imefichua vitendo vya watu kukamatwa kiholela, mateso, na unyanyasaji huko Khartoum vinavyotekelezwa na Vikosi vya wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF) na pia Jeshi la Serikali ya Sudan (SAF). Ripoti hiyo imearifu pia kuwa makumi ya maelfu ya watu wamewekwa katika mazingira duni tangu Aprili 2023.Kutokana na kupungua kwa ufadhili wa misaada ya kibinadamu duniani, Umoja wa Mataifa leo jijini Geneva, Uswisi kutenga dola milioni 110 ili kusaidia majanga yaliyopuuzwa katika nchi 10 barani Afrika, Asia, na Amerika Kusini, zikiwemo Niger, Somalia, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Zambia.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia maana ya methali “MCHAWI AKIFICHUA MIRIMO YA WACHAWI HU UAWA”.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
12 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 12, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia matokeo ya maandamani nchini Bangladesh, na machafuko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Makala inatupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Tanzania, kulikoni?Ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo mjini Geneva Uswisi na ofisi ya haki za binadamu (OHCHR) imefichua kuwa viongozi wa juu wa serikali ya Bangladesh walihusika moja kwa moja katika ukandamizaji wa maandamano makubwa yaliyoitikisa nchi hiyo mwaka 2024 na kusababisha vifo vingi.Baada ya waasi wa M23 jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kupatia wakimbizi waliokuwa wamesaka hifadhi kambini mjini Goma, wawe wamerejea makwao ndani ya saa 72 kuanzia juzi jumatatu, mamia wameanza kutii amri hiyo licha ya hofu inayowakabili ya kule wanakotakiwa kurejea.Makala inatupeleka jijini Nairobi, Kenya ambako ambako Kevin Keitany wa redio washirika wetu Domus FM kwa kuzingatia kuwa kesho Februari 13 ni Siku ya Kimataifa ya Redio, ametutumia maoni ya vijana wawili wanaozungumzia namna redio imewasaidia kusambaza ujumbe wao kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.Mashinani fursa ni yake Tupokigwe Simon, msichana      mwenye  umri wa miaka 16, ambaye ni mwanaharakati wa  Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na hisabati , STEM, wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, akieleza umuhimu wa  msichana katika sayansi na kuwahimiza wasichana wenzake kusoma  sayansi.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
Redio imetusaidia kufikisha elimu kwa umma kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 12, 2025 3:12


Ikiwa kesho Februari 13 ni Siku ya Kimataifa ya Redio, makala inatupeleka jijini Nairobi, Kenya ambako ambako Kevin Keitany wa redio washirika wetu Domus FM kwa kuzingatia kuwa kesho Februari 13 ni Siku ya Kimataifa ya Redio, ametutumia maoni ya vijana wawili wanaozungumzia namna redio imewasaidia kusambaza ujumbe wao kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.

Habari za UN
Wapalestina wahitaji ufadhili na mshikamano wa kimataifa - Tom Fletcher

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 10, 2025 3:40


Huko Mashariki ya Kati Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA Tom Fletcher alifanya ziara ya siku tatu huko Ukingo wa Magharibi na Gaza ili kujionea hali halisi ya raia. Katika Sharon Jebichii amefuatilia ziara yake na kutuandalia makala hii..

Habari za UN
04 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 4, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kushuhudia sintofahamu na maombi ya wakazi wa Goma baada ya waasi wa M23 kutwaa mji huo. Mashinani tunakwenda Somalia na pia tunakuletea muhutasari wa habari.Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Bruno Lemarquis, ametoa wito wa kufunguliwa haraka kwa Uwanja wa Ndege wa Goma. Amesema uwanja huu uliofungwa kutokana na mapigano kati ya vikosi vya jeshi la DRC na waasi wa M23 ni muhimu kwa usafirishaji wa misaada ya kibinadamu. Hospitali zimejaa na maelfu ya raia hawana msaada wa dharura.Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la idadi ya watu na afya ya uzazi, (UNFPA), na la misaada ya kibinadamu na dharura (OCHA) leo yamesisitiza kuwa kusitishwa kwa ufadhili wa Marekani kunawaacha mamilioni 'hatarini'. Hayo yakijiri tayari imefahamika kuwa Rais Donald Trump anaiondoa Marekani katika Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu na pia kuacha kulifadhili shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi wa Kipalestina.Na ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Saratani, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) limeeleza kiasi takwimu kuhusu ugonjwa huo kwamba mathalani  kwa mwaka 2020 saratani ilisababisha vifo karibu milioni 10 sawa na kifo kimoja kati ya sita duniani. Aidha WHO imebainisha kuwa saratani zinazojitokeza zaidi ni saratani ya matiti, mapafu na utumbo mpana.Na katika mashinani  fursa ni yake Safiya Jeylaani, mkazi wa Barawe katika Jimbo la Kusini Magharibi mwa Somalia ambye baada ya kuhudhuria hafla ya kujadili umuhimu wa upatikanaji wa huduma za afya kwa Wasomali wote katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu iliyoandaliwa na Umoja wa Mataifa anasema jamii wanapaswa kuelimishwa kuhusu afya kutumia lugha mama.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!  

Habari za UN
Tutafute majadiliano badala ya kugawanyika - Guterres

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 3, 2025 1:50


Ikiwa kesho Februari 4 ni Siku ya Kimataifa ya Udugu wa Kibinadamu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres,kupitia ujumbe mahususi kwa ajili ya siku hii ametoa wito wa kuimarisha umoja, usawa, na kuheshimiana katika kipindi hiki cha ongezeko la ubaguzi na kutovumiliana duniani. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
03 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 3, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini Jamhuri ya Kidemocrasia ya Congo DRC, na ujumbe wa Katibu Mkuu wa UN kuhusu Siku ya Kimataifa ya Udugu wa Kibinadamu. Makala inatupeleka nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR na mashinani tunarejea DRC, kulikoni?Ikiwa ni wiki moja sasa tangu waasi wa M23 watangaze kutwaa Goma, jimboni Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, na kisha serikali kutangaza Beni kuwa mji mkuu wa sasa wa jimbo hilo, hii leo Jumatatu Februari 3, maandamano makubwa ya amani yamefanyika mjini Beni, yakiongozwa na mashirika ya kiraia na wananchi.Ikiwa kesho Februari 4 ni Siku ya Kimataifa ya Udugu wa Kibinadamu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres,kupitia ujumbe mahususi kwa ajili ya siku hii ametoa wito wa kuimarisha umoja, usawa, na kuheshimiana katika kipindi hiki cha ongezeko la ubaguzi na kutovumiliana duniani.Makala inatupeleka Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, kwenye kambi ya wakimbizi ya Korsi inayohifadhi zaidi ya wakimbizi 18,000 kutoka Sudan wengi wakiwa ni wanawake na watoto na shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA linawasaidia.Na katika mashinani  Lodja Salizre, Mkimbizi wa ndani katika kambi ya Loda jimboni Ituri kaskazini magharibi mwa Jamhuri ya Kidemocrasia ya Congo DRC akileleza ni kwa jinsi gani vita inayoendelea vimeameathiri yeye na familia yake na jinsi ambavyo uwepo wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo inavyosaidia maisha ya kila siku ya wakazi wake.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
Nilikuwa miongoni mwa Wacuba wa kwanza kujifunza Kiswahili: Profesa Jacomino

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 27, 2024 5:03


Ujumuishwasji wa lugha mbalimbali katika dunia iliyoshikamana katika Nyanja mbalimbali ni moja ya malengu ya Umoja wa Mataifa kuanzia katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa hadi kwenye nchi wanachama unalichagiza hilo. Hamasa hiyo imezichagiza nchi nyingi kuanza kukumbatia lugha ambazo kwa asili hazizungumzwi kama alivyobaini Flora Nducha wa Idhaa hii ambaye hivi karibuni alikuwa Cuba kwenye Kongamano la Kimataifa la Kiswahili na kukutana na Profesa Juan Jacomino ambaye ni mhadhiri katika chuo kikuu cha Havana na ni miongoni mwa watu wa mwanzo waliokwenda Tanzania kujifunza Kiswahili na sasa anakifundisha nchini mwake Cuba. Anafafanua kuhusu safari yake ya kujua Kiswahili katika makala hii..

Habari za UN
Siku ya Kimataifa ya Kujitayarisha dhidi ya magonjwa ya mlipuko, Mkuu wa Umoja wa Mataifa atoa wito

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 27, 2024 1:32


Katika kuandhimisha Siku ya Kimataifa ya Kujitayarisha dhidi ya Magonjwa ya Mlipuko, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito kwa nchi kote ulimwenguni kuzingatia masomo yaliyopatikana katika dharura za kiafya zilizopita ili kusaidia kujiandaa kwa dharura zijayo. Assumpta Massoi anaeleza zaidi.

Habari za UN
27 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 27, 2024 9:57


Hii leo jaridani tunaangazia sherehe za krismasi katika ukanda wa Gaza lich ya migogoro inayoendelea, na magonjwa ya mlipuko. Makala inatupeleka Havana Cuba na mashinani nchini Uganda, kulikoni?Katika kuandhimisha Siku ya Kimataifa ya Kujitayarisha dhidi ya Magonjwa ya Mlipuko, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito kwa nchi kote ulimwenguni kuzingatia masomo yaliyopatikana katika dharura za kiafya zilizopita ili kusaidia kujiandaa kwa dharura zijayo.Tukiwa bado katika msimu wa sikukuu ya krismasi, tunakwenda mji wa Gaza, huko Ukanda wa Gaza, Mashariki ya Kati kusikia jinsi sikukuu hii ilivyoadhimishwa na hisia mchanganyiko kwenye kanisa katoliki la Familia Takatifu kwenye viunga vya zamani kwenye mji huo.Makala inatupeleka Havana Cuba kuangazia umuhimu wa utekelezaji wa moja ya ajenda za Umoja wa Mataifa ya kukumbatia lugha mbalimbali duniani ambapo Flora Nducha wa Idhaa hii akiwa Cuba hivi karibuni kwenye kongamano la Kimataifa la Kiswalihi alikutana na raia wa nchi ambaye ni mwalimu wa Kiswahili.Mashinani fursa ni yake Ange Rukenura, msichana alieyekimbia makazi yake pamoja na ndugu zake sita kufuatia mashambulizi ya waasi waliojihami nchini  Jamhuri ya Kidemocrasi ya Congo, DRC akisema licha ya rasilimali ndogo anashukuru ukarimu wa Uganda na msaada wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kwa kuwapatia matumaini.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
20 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 20, 2024 10:53


Hii leo jaridani tunaangazia jitihada za kuudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Maburg nchini Rwanda, na juhudi za kuchunguza virusi vya VVU nchini Ghana. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini DRC, kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) limeipongeza serikali ya Rwanda kwa kufanikiwa kuudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Maburg. Hii leo Rwanda imetangaza mwisho wa mlipuko wa hivi karibuni wa ugonjwa huo baada ya kutokuwepo maambukizi mapya katika siku 42 na mgonjwa wa mwisho akiwa amepimwa mara mbili bila kukutwa na ugonjwa kama matakwa ya WHO yanavyotaka ili kutangaza kuisha kwa mlipuko wa magonjwa namna hii.Mwaka 2020 Ghana iliripoti kuwa na watu 350,000 wanaioshi na virusi vya Ukimwi na kati yao hao 31,000 walikuwa ni wajawazito. Jambo lililoshtua ni kwamba ni sehemu ndogo mno ya wajawazito hao ndio walipimwa kufahamu iwapo wana VVU au la. Jambo lililofanya serikali kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kuchukua hatua.Makala inatupeleka kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyokoko Kaunti ya Turkana Kaskazini Magharibi mwa Kenya kukukutanisha na mkimbizi kutoka Somalia anayetumia mpira wa kikapu anatumia mpira wa vikapu kuhamasisha jamii yake na kupinga mil ana desturi zisizofaa.Mashinani ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Mpira wa Kikapu, fursa ni yake Danny Batachoka, mwanariadha wa Paralimpiki kutoka Goma nchini Jamhuri ya kidemocrasia ya Congo, DRC ambaye kupitia video ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO, anasema ana ndoto ya kuwa mmoja wa wachezaji wakubwa wa mpira wa vikapu katika kitengo chake.” Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
18 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 18, 2024 9:54


Hii leo jaridani tunaangazia siku ya wahamiaji duniani ikimulika mchango wa wakimbizi na wahamiaji katika ukuaji wa kiuchumi na kukuza jamii zao n aza wenyeji. Tutasikia kutoka mkuu wa IOM, Katibu Mkuu wa UN na wahamiaji Burundi na Chad. Pia tunaangazia ufugaji nyuki Tanzania.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake mahususi kwa ajili ya Siku ya Kimataifa ya Wahamiaji ametoa wito kwa ulimwengu kuitumia siku hii kujikumbusha kwamba pamoja na kwamba tunasherehekea michango ambayo mamilioni ya wahamiaji hutoa kwa jamii leo pia ni siku ya kujikumbusha changamoto ambazo wahamiaji wanaweza kukumbana nazo.Nimefurahi sana kwani binti yangu mwenye ulemavu ambaye tulihamia naye makazi ya muda kufuatia kuongezeka kina cha maji ya Ziwa Tanganyika, hapa Burundi sasa amepatiwa stadi za kumwezesha kujikwamua kiuchumi. Ni kauli ya Odette Niyonkuru, raia mhamiaji wa ndani nchini Burundi akizungumzia mustakabali wa binti yake huyo kwenye video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM.Makala inatupeleka nchini Tanzania kufuatilia Mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO uitwao ACP MEAs 3 ambao umwewapa wakulima zana na ujuzi muhimu katika ufugaji nyuki endelevu kwa lengo la kuboresha maisha yao huku wakikuza bayoanuwai na uhifadhi wa mazingira. Kupitia video iliyoandaliwa na FAO Tanzania Selina Jerobon amefuatilia mafanikio ya mradi huu na kituandalia makala hii.Na mashinani katika siku hii ya kimataifa ya wahamajia Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM linasisitiza umuhimu wa kuwawezesha wanawake na wasichana walio ukimbizini na kuongeza mikakati ya kifedha inayozingatia jinsia. Bi Banti Ahmat ni mmoja wa wakimbizi na anelezea jinsi ambavyo mradi wa IOM wa bustani za jamii unavyoleta matokeo chanya kwa wahamiaji na jamii za wenyeji nchini Chad.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Guterres: Siku ya Kimataifa ya Wahamiaji tujikumbushe changamoto wanazokumbana nazo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 18, 2024 1:42


Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya Uhamiaji, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake mahususi kwa ajili ya Siku ya Kimataifa ya Wahamiaji ametoa wito kwa ulimwengu kuitumia siku hii kujikumbusha kwamba pamoja na kwamba tunasherehekea michango ambayo mamilioni ya wahamiaji hutoa kwa jamii leo pia ni siku ya kujikumbusha changamoto ambazo wahamiaji wanaweza kukumbana nazo. Selina Jerobon na maelezo zaidi.

Habari za UN
UNHCR: Chonde chonde jumuiya ya Kimataifa tuishike mkono Uganda kwa faida ya waomba hifadhi na wakimbizi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 16, 2024 2:04


Mwaka 2024 ukielekea ukingoni, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR  nchini Uganda limetoa rai kwa jumuiya ya kimataifa kutolisahau taifa hilo la Afrika Mashariki ambalo ni maskani ya idadi kubwa zaidi ya waomba hifadhi na wakimbizi barani Afrika. Rai hiyo iliyotolewa mwishoni mwa wiki inataka ufadhili wa fedha uongezwe ili liweze kuendelea kukirimu watu hao ambao wengi wanakimbia machafuko. Huyo ni Moulid Hujale afisa wa UNHCR nchini Uganda akitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kushikamana na Uganda akiwa  kwenye makazi makubwa ya wakimbizi ya Kiryandongo Magharibi mwa nchi hiyo. Anasema kuna mambo matatu muhimu ambayo dunia inapaswa kufahamu kuhusu Uganda na wakimbizi.“Mosi Uganda inahifadhi idadi kubwa zaidi ya wakimbizi na waomba hifadhi Afrika ikiwa na zaidi ya watu milioni 1.7 wengi wao wakitoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na Sudan Kusini.”Zaidi ya hapo ukarimu wa Uganda anasema hauna kipimo“Pili, Uganda ina sera ya kufugua mlango kwa wakimbizi na pia kwa miongo mingi imekuwa ikiwakaribisha watu wanaokimbia machafuko bila kujali utaifa wao. Kitu ambacho ni kikubwa na cha kipekee kuhusu nchi hii ni kwamba wakati wakimbizi wanapowasili hapa hupewa ardhi, mahali pa kuishi na hata kulima mazao kwa ajili ya kujikimu. Wana uhuru wa kutembea na haki ya kuajiriwa. Hawajatengwa lakini wanaishi  ndani ya jamii inayowahifadhi. Sera hii ya Uganda inawaruhusu wakimbizi kujumuishwa katika huduma za kitaifa ambapo wanafaidika na elimu na huduma za afya.”Lakini Kutokana na changamoto za fedha Moulid anasema ukarimu huo sasa uko njia panda"Tatu: Ukarimu wa Uganda uko hatarini kwani wakimbizi zaidi wanaingia kutoka nchi jirani. UNHCR, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, liko mashinani kufanya kazi na Serikali ya Uganda kusaidia kutoa msaada wa kuokoa maisha kwa watu hawa. Hata hivyo, rasilimali ni chanche. Tunahitaji msaada wenu ili Uganda iendelee kuwa mfano wa kuigwa kwa dunia nzima.”Kwa nyjibu wa UNHCR licha ya idadi kubwa ya watu na rasilimali kidogo, sera za Uganda zinammanisha kwamba wakimbizi ni sehemu ya maisha ya kijamii na kiuchumi na ongezeko la rasilimali litakidhi haja za waliopo sasa na watakaokuja.

Habari za UN
Mjumbe wa UN aendelea na ziara ya kukutana na wadau nchini Syria

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 16, 2024 1:31


Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Syria Geir O. Pedersen bado yuko nchini Syria alikowasili jana Jumapili  ikiwa ni wiki moja baada ya wapiganaji wa Hayʼat Tahrir al-Sham (HTS) walioko kwenye orodha ya vikundi vya kigaidi kutwaa mji mkuu Damascus na kusababisha Rais Bashar Al-Assad kukimbia nchi. Ikiwa ni sehemu ya juhudi za Umoja wa Mataifa kuhakikisha mabadiliko ya utawala nchini Syria yanafanyika kwa amani na kuisaidia Syria kutokuingia kwenye mgogoro zaidi, Bwana Pederson aliyewasili jana Damascus  hadi sasa ameshakutana na Kamanda wa Utawala Mpya Ahmed al-Sharaa na Waziri Mkuu wa Serikali ya Muda Mohammed al-Bashir.Taarifa iliyotolewa leo na Ofisi yake inasema Pederson ameeleza muhtasari wa matokeo ya Mkutano wa Kimataifa wa Aqaba kuhusu Syria uliofanyika tarehe 14 ya mwezi huu wa Desemba akisisitiza haja ya kuwepo kwa mpito wa kisiasa unaoaminika na unaoongozwa na kumilikiwa na Wasyria wenyewe kama kanuni za azimio 2254 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (2015) zilivyopendekeza. Aidha Mjumbe huyo maalum amesisitiza azma ya Umoja wa Mataifa ya kutoa usaidizi wa kina kwa watu wa Syria.Taarifa imedokeza kuwa Bwana Pedersen ana shughuli nyingi zilizopangwa siku zijazo katika harakati za kusaka suluhu ya amani nchini Syria.

Habari za UN
05 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 5, 2024 9:59


Hii leo jaridani mada kwa kina inayotupeleka katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali nchini Uganda kumulika hali ya ukatili dhidi ya wanawake kwa watu hao waliokimbia vita jinsi inavyoshughulikiwa. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA leo limezindua ombi lake la kimataifa la mwaka 2025, likitafuta dola bilioni 1.4 ili kutoa huduma za afya ya uzazi zinazookoa maisha na programu muhimu za kuzuia unyanyasaji wa kijinsia kwa zaidi ya wanawake, wasichana na vijana milioni 45 kote duniani katika nchi  57 zilizoathiriwa na majanga.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) leo jijini Geneva, Uswisi limetangaza kutoa idhini ya awali kwa kipimo kinachoitwa Xpert® MTB/RIF Ultra dhidi ya ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB). Kipimo hiki pia kinaweza kupima uwezekano wa kuathiriwa kwa viuavijasumu ambacho kinakidhi viwango vya WHO.Biashara ya kimataifa inatazamiwa kufikia dola trilioni 33 mwaka 2024, kulingana na Taarifa mpya ya Biashara ya Kimataifa iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo (UNCTAD). Ongezeko hili la dola trilioni 1, linaloakisi ukuaji wa mwaka wa asilimia 3.3, linaonesha uthabiti katika biashara ya kimataifa licha ya changamoto zinazoendelea.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno “MBUKU NA MSUNUNU.”Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
Umoja wa Mataifa na wadau wazindua ombi la dola bilioni 47 kwa ajili ya mwaka 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 4, 2024 2:04


Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) ikizindua Ripoti ya Kimataifa ya mahitaji ya Kibinadamu (GHO) kwa mwaka ujao wa 2025 imetangaza ombi la ufadhili kwani takriban watu milioni 305 duniani kote watahitaji msaada wa kibinadamu katika mwaka ujao. Selina Jerobon na maelezo zaidi.

Habari za UN
04 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 4, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia uzinduzi wa ombi la ufadhili wa mahitaji ya Kibinadamu (GHO), na umuhimu wa lugha mama katika kukuza haki za binadamu. Makala tunasalia hapa makao makuu ya umoja wa mataifa na mashinani tunakupeleka nchini Senegal, kulikoni?Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) ikizindua Ripoti ya Kimataifa ya mahitaji ya Kibinadamu (GHO) kwa mwaka ujao wa 2025 imetangaza ombi la ufadhili kwani takriban watu milioni 305 duniani kote watahitaji msaada wa kibinadamu katika mwaka ujao.Haki si haki iwapo inatolewa kwa lugha ambayo haileweki kwa wahusika, wamejulishwa washiriki wa mkutano wa pili wa wanazuoni unaofanyika hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York, Marekani na pia mtandaoni ukimulika Madaraka, Haki na Binadamu: Utawala wa Sheria na mabadiliko Afrika.Makala tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambapo mkutano wa mwaka 2024 wa Taaluma kuhusu Afrika leo katika leo umeingia siku ya pili hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Mkutano huo ulioandaliwa na Ofisi ya mshauri maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Afrika UNOSAA ni wa siku tatu na umebeba maudhui "Nguvu, Haki, na watu” kwa ajili ya mabadiliko ya Afrika.Na mashinani fursa ni yake Antar sarr, Kijana mkulima wa mbogamboga kutoka Senegal ambaye ni mmoja wa wanufaika wa mradi wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya kilimo, IFAD unaowawezesha vijana nchini humo kwa kilimo na biashara ndogondogo ili kuondokana na fikra za kwenda Ulaya kusaka Maisha bora na ajira, akisema mradi huo imempatia matumaini.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
03 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 3, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo inamulika harakati za Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kuhakikisha wafugaji kuku wasiotumia dawa kiholela wananufaika kiuchumi baada ya kupatiwa mafunzo. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani ya Timor-Leste.Leo ni Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe mahususi kwa siku hii, ameueleza ulimwengu kuwa maadhimisho ya mwaka huu yanawakumbusha kwamba ulimwengu unahitaji uongozi wa watu wenye ulemavu zaidi kuliko hapo awali. Guterres ameeleza kuwa Watu wenye ulemavu tayari wanabeba mzigo mkubwa wa majanga yanayoumiza ulimwengu lakini mara nyingi wananyimwa haki yao ya kuchangia katika suluhu za majanga haya.Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya Uchunguzi kuhusu Syria hii leo imezitaka pande zinazopigana nchini Syria zifuate kikamilifu sheria za kimataifa na kuwalinda raia. Hii inatokana na ongezeko kubwa la mapigano tangu tarehe 27 mwezi uliopita ambayo yanatishia kuenea katika maeneo mengine ya nchi.Mkutano wa mwaka 2024 wa Taaluma kuhusu Afrika umeanza leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Mada ya mkutano huo wa siku tatu ni "Nguvu, Haki, na Watu: Haki za Binadamu na Utawala wa Sheria kwa Mabadiliko ya Afrika." Mkutano huo wa kila mwaka unalenga kuongeza uwakilishi wa Waafrika katika ufadhili wa kimaendeleo wa kimataifa, ili kuchagiza mustakabali bora wa Afrika.Na mashinani leo ikiwa ni siku ya watu wenye ulemavu duniani tunakupeleka Timor-Leste, kusini-mashariki mwa Asia kuona jinsi mradi uliofadhiliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira, UNEP umemwezesha Antonio Ornai mwenye ulemavu wa kutoona kushiriki zoezi la kuitikia maonyo ya taarifa za majanga kwenye taifa hilo ambalo hugubikwa na majanga ya asili mara kwa mara kama vimbunga na mafuriko.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!  

Habari za UN
02 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 2, 2024 10:42


Hii leo jaridani tunaangazia mashauriano huko Busan kuhusu matumizi ya plastiki, na ripoti ya UNODC kuhusu UKIMWI na kudhibiti dawa za kulevya katika magereza. Makala inaturejesha Havana Cuba na mashinani inatupeleka nchini Kenya, kulikoni?Vuta nikuvute kwenye mashauriano huko Busan, Korea Kusini kuhusu mkataba wenye nguvu za kisheria dhidi ya uchafuzi utokanao na matumizi ya plastiki na kulinda mazingira ya baharini imefikia ukingoni kwa mkutano kuahirishwa na wawakilishi wa nchi zilizokuwa zinashiriki kuridhia rasimu mpya yenye ibara 32 itakayojadiliwa mwakani.Wakati jana Desemba Mosi Ulimwengu ukiadhimisha Siku ya Kimataifa ya UKIMWI kwa kuhamasisha haki za binadamu ili kufanikisha vita dhidi ya ugonjwa huu hatari, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya ya Kudhibiti Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) inajivunia miaka 25 ya kujiunga na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kukabiliana na UKIMWI (UNAIDS) katika kushughulikia janga la Virusi Vya UKIMWI (VVU) miongoni mwa watu wanaotumia dawa za kulevya na miaka 20 ya kazi ya kupambana na UKIMWI magerezani.Makala leo inamulika jinsi bidhaa za kitamaduni zinavyotumika kukuza na kuendeleza mila na desturi za Kiswahili mkoani Tanga Kaskazini mwa Tanzania. Je ni bidhaa zipi hizo na zinatumika vipi? Tuungane na Flora Nducha aliyeyabaini hayo hivi karibuni alipokuwa Havana Cuba kwenye kongamano la kimataifa la Kiswahili.Na mashinani tunasikiliza manufaa ya ufadhili wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya kilimo, IFAD kwa wakulima kutoka kwake Sharon Kirui kutoka Kaunti ya Nakuru nchini Kenya ambaye ni mnufaika wa vocha za kielektroniki za ununuzi kutoka kwa IFAD na ameweza kupanua biashara yake ya kilimo.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
UNODC yajivunia miaka 20 ya kupambana na UKIMWI magerezani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 2, 2024 2:17


Wakati jana Desemba Mosi Ulimwengu ukiadhimisha Siku ya Kimataifa ya UKIMWI kwa kuhamasisha haki za binadamu ili kufanikisha vita dhidi ya ugonjwa huu hatari, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya ya Kudhibiti Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) inajivunia miaka 25 ya kujiunga na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kukabiliana na UKIMWI (UNAIDS) katika kushughulikia janga la Virusi Vya UKIMWI (VVU) miongoni mwa watu wanaotumia dawa za kulevya na miaka 20 ya kazi ya kupambana na UKIMWI magerezani.  Anold Kayana na taarifa zaidi.

Habari za UN
29 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 29, 2024 9:59


Hii leo jaridani Assumpta Massoi anamulika adha zinazokumba raia kwenye eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli; hakari za kukabili UKIMWI Afrika Kusini; IFAD ilivyonusuru vijana na safari za kwenda Ulaya zinazohatarisha maisha yao; Mkimbizi wa ndani Gaza anayezungumzia harakati za kusaka mkate ili kulisha familia yake.Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa katika ofisi ya eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli, Ajith Sungay amesema miezi 13 ya vita imeufanya Ukanda wa Gaza kuwa kama jehanamu, kwani kuna uharibifu usio na kifani, njaa isiyoelezeka magonjwa na kuendelea kwa mashambulizi ya mabomu yanayotawanya raia kila uchao. Flora Nducha na taarifa zaidi.Kuelekea ya Siku ya Kimataifa ya UKIMWI itakayoadhimishwa Jumapili hii, ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kukabiliana na UKIMWI (UNAIDS) iliyotolewa juzi Jumatano imeeleza kuwa dunia inaweza kufikia lengo lililokubaliwa la kukomesha UKIMWI kama tishio la afya ya umma ifikapo mwaka 2030 lakini kwa sharti kwamba viongozi ni lazima walinde haki za binadamu za kila mtu anayeishi na Virusi Vya UKIMWI, VVU au aliyeko hatarini kuambukizwa. Anold Kayanda ameangazia mfano mzuri wa Afrika Kusini unaofahamika kama “Takuwani Riime”.Mkala inayokupeleka nchini Senegal kusikia jinsi mradi wa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo IFAD umewezesha vijana kuondokana na mawazo ya kuweka rehani maisha yao wakisaka maisha bora Ulaya. Mwenyeji wako ni Bosco Cosmas.Mashinani fursa ni yake nampisha Abu Muhammad, mkimbizi wa ndani huko Deir Al Balah, Ukanda wa Gaza akielezea umuhimu wa mgao wa mikate kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula, WFP, kwa wakimbizi hao wakati huu ambapo vita inaendelea eneo hilo.