Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.
RFI - Radio France Internationale

Na Hannah Nalianya Kila Ijumaa rfi Kiswahili inakupa nafasi kuchangia mada yoyote kuhusiana na matangazo yetu. Skiza maoni ya Juma hili

Fainali ya kombe la dunia katika mchezo wa soka, itawakutanisha mabingwa watetezi Argentina na Hispania waliowahi kushinda taji hili mwaka 2010. Mechi hiyo itapigwa siku ya Jumapili nchini Marekani. Unatarajia nani ataibuka mshindi katika mechi hiyo na kwanini. Skiza ya mskilizaji

Na Hannah Naliaka Safari ya Ufaransa kutinga fainali za kombe la dunia imefikia tamati baada ya kushindwa mabao 2-0 na Uhispania katika nusu fainali ya kwanza. Unazungumziaje mechi hiyo ? Skiza maoni ya mskilizaji.

Umoja wa Ulaya unatathmini kuweka marufuku ya matumizi ya mitandao ya kijamii kwa watoto kutokana na athari za mitandao hiyo kwa watoto. Unazungumziaje pendekezo hili? Skiza maoni ya mskilizaji.

Fainali za kombe la dunia zimefikia hatua ya nusu fainali, huku timu nne zikisalia kwenye mbio za kutwaa ubingwa. Uhispania itacheza na Ufaransa, wakati Uingereza itapambana na mabingwa watetezi Argentina. Unatathmini vipi hatua iliyofikia? Skiza maoni ya mskilizaji.

Tangazo hilo limetolewa licha ya kushiriki kwenye mazungumzo ya kisiasa na rais wa Burundi Évariste Ndayishimiye, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika.

Dunia hivi leo inaadhimisha siku ya Kiswahili Duniani, kutambua mchango wa lugha ya Kiswahili katika kuunganisha watu, tamaduni na mataifa mbalimbali, kauli mbiu ikiwa Kiswahili Lugha ya kimataifa ya amani, mshikamano na diplomasia ya kiuchumi.” Siku hii inafanyika wakati pia RFI Kiswahili tunatimiza miaka 16 tangu tulipoanza kurusha matangazo yetu, una ujumbe gani kwetu?

Wiki iliyopita, maelfu ya raia wa mataifa mbalimbali ya Afrika waliondoka Afrika Kusini kutokana na hofu ya usalama baada ya maandamano yaliyolenga wageni. Baadhi ya nchi zimeikosoa serikali ya Afrika Kusini kwa kushindwa kudhibiti hali hiyo.


Tunaangazia serikali ya Uganda kumfurusha wakili na mwanaharakati wa Kenya, Martha Karua nchini humo, ikiwa ni mwendelezo wa matukio ambayo yamekuwa yakishuhudiwa hapa Afrika Mashariki. Skiza maoni ya waskilizaji.

Kila Ijumaa unapata nafasi kuchangia chochote kile, pengine ulikiskia kwenye matangazo yetu au kile kinafanyika hapo uliopo. Skiza maoni ya mskilizaji

Shaba yetu leo inalenga nchini Kenya mbapo raia nchini humo wameadimisha miaka miwili tangu kutokea kwa maandamano ya mwaka 2024 ya vijana waliokuwa wapigigania mageuzi nchini humo. Skiza maoni ya mskilizaji.

Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer ametangaza kujiuzulu baada ya shinikizo kutoka ndani ya chama chake na kupungua kwa uungwaji mkono wa raia. Je, viongozi wanapaswa kujiuzulu wanapopoteza uungwaji mkono wa wananchi? Skiza makala ya maoni ya waskilizaji.

Ulimwengu umeadhimisha wiki ya afya ya akili kwa wanaume, wataalamu wanaonya kuwa msongo wa mawazo na matumizi ya dawa za kulevya vinachangia matatizo ya afya ya akili miongoni mwa wanaume. Unafikiri kwa nini wanaume wengi huumia kimya bila kutafuta msaada? Skiza maoni ya mskilizaji.

Rais Donald Trump anasema Mlango Bahari wa Hormuz pia utafunguliwa tena hivi karibuni.Mkataba wa amani, unatarajiwa kutiwa saini siku ya Ijumaa, wiki hii nchini Uswizi

Licha ya jitihada mbalimbali, bado watu wenye ualbino wanabaguliwa kwenye baadhi ya jamii na hata kuuawa kwa imani za kishirikina.

Kipute cha kombe la dunia kinaanza leo, huku Afrika Kusini ikipambana dhidi ya Mexico mwenyeji. Je, unazungumziaje timu za Afrika zinazoshiriki mashindano ya huu? Skiza makala haya.

Mwamuzi kutoka nchini Somalia Omar Abdulkadir, amezuiwa kuingia nchini Marekani, alikokuwa ameteuliwa na Shirikisho la soka duniani, FIFA kuchezesha mechi za kombe la dunia, kutokana na kile utawala wa rais Trump umemhusisha na maswala ya ugaidi Skiza makala haya kufahamu maoni ya mskilizaji wetu.

Jopo la majaji watatu nchini Kenya limeidhinisha hatua ya bunge la kumuondoa afisini aliyekuwa naibu rais, Rigathi Gachagua kwa kile walichosema, katiba ilifuatwa. Je, unaunga mkono uamuzi wa mahakama kuhusu Rigathi Gachagua na kwa nini? Skiza maoni ya baadhi ya waskilizaji wetu.

Leo dunia inaadhimisha siku ya kimataifa ya Bahari, siku inayolenga kuhamasisha umuhimu wa bahari katika maisha ya binadamu na mazingira. Hata hivyo, bahari zinakabiliwa na changamoto kubwa ikiwemo uchafuzi wa plastiki, mabadiliko ya tabianchi na uvuvi haramu, katika siku hii tunakuuliza. Unadhani hatua gani zinazopaswa kuchukuliwa ili kupunguza uchafuzi wa bahari? Skiza makala haya kufahamu maoni ya waskilizaji wetu.

Karibu kwenye kipindi cha habari Rafiki ,mada ikiwa kuhusu maadhimisho ya siku ya mazingira duniani ambayo yatafanyika Ijumaa,huku kauli mbiu ikiwa kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa. Tumekuuliza, serikali ya nchi yako inafanya vya kutosha kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa ? Na je , sekta binafsi na wananchi wanapaswa kufanya nini sasa,ili kuimarisha mazingira,,karibu tuandamane pamoja .

Kila Ijumaa ndani rfi Kiswahili unapata nafasi kuchangia mada yoyote. skiza makala

Nchini Kenya, msimamo ya kisiasa ya baadhi ya raia kisiasa yazidi kuibua uhasama. Skiza makala

Katika makala ya Habari Rafiki leo tunaangazia hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania, kuunda tume maalumu ya jinai itakayochunguza matukio ya vurugu zilizotokea wakati na baada ya uchaguzi wa Oktoba 29 mwaka uliopita, ili kubaini vitendo vilivyofanywa na kuwataja waliohusika ili waajibishwe kisheria

Siku ya Jumatatu uchukuzi ulitatizwa nchini Kenya kufuatia mgomo wa wahudumu wa magari ya uchukuzi wa umma kupinga ongezeko la bei ya mafuta. Hii ni baada ya serikali kupandisha Lita moja ya Petroli kufikia Shilingi za nchi hiyo 214 huku ile ya Dizeli ikifikia Shilingi 242. Tumemuuliza mskilizaji wetu anzungumziaaje kilichotokea nchini Kenya na nchini mwake hali iko je kuhusu bei ya mafuta.

Shirika la afya duniani limetangaza hali ya dharura ya kiafya duniani kutokana na mlipuko wa virusi vya Ebola mashariki mwa DRC, ikizitaka nchi kuchukua tahadhari kufuatia hofu ya ugonjwa huo kusambaa zaidi. Tumemuuliza mskilizaji wa RFI Kiswahili akiwa DRC na kwenye ukanda wa Afrika Mashariki anachukua hatua gani kujikinga.


Mkutano wa Afrika forward unaoongozwa na Ufaransa umeanza leo jijini Nairobi ambapo karibia marais 30 ,kutoka barani Afrika wanatarajiwa kuudhuria ili kujadili ushirikiano katika sekta ya uchumi wa buluu, mazingira ,afya na kilimo. Mkutano huu umetoa kipaumbele ka ajenda zinazowahusu vijana, na hasa matumizi ya teknolojia, akili unde au AI na namna vijana wanaweza kukumbatia fursa katika sekta hizo.

Sheria kama hiyo pia inatumika na Urusi, inakosolewa na wanaharakati wa haki za kibinadamu huku wapinzani wakisema inawalenga, kwa sababu ya kukosoa utawala wa rais Ypweri Museveni. Unazungumziaje sheria hii mpya nchini Uganda ?

Rais Samia Suluhu Hassan, anataka Kenya na nchi yake ya Tanzania kushirikiana ili kukabili uanaharakati wa 'kuvuka mipaka' kutoka kwa vijana wa Gen Z ambao ameelezea unatishia amani na usalama wa nchi nchi za Afrika Mashariki. Unazungumziaje kauli hii ya rais Samia? Unadhani ni sahihi kwa vijana kuadhibiwa kwa kushinikiza mabadiliko kwenye nchi zao?

Kenya na Tanzania zimekubaliana kuondoa vikwazo vyote visivyo vya kikodi vya kibiashara, ili kuimarisha ushirikiano wa kibiashara. Unaamini yaliyokubaliwa kati ya nchi hizo mbili yatatekelezwa ?

Msikilizaji mei 3 2026 dunia iliadhimisha siku ya kimataifa ya Uhuru wa wanahabari, ripoti zikionesha ongezeko kubwa la vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya waandishi wa habari.

