Habari RFI-Ki

Follow Habari RFI-Ki
Share on
Copy link to clipboard

Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.

RFI - Radio France Internationale


    • May 13, 2025 LATEST EPISODE
    • weekdays NEW EPISODES
    • 9m AVG DURATION
    • 429 EPISODES


    More podcasts from RFI - Radio France Internationale

    Search for episodes from Habari RFI-Ki with a specific topic:

    Latest episodes from Habari RFI-Ki

    Hali ya mafuriko katika mataifa ya Afrika Mashariki na pembeya Afrika

    Play Episode Listen Later May 13, 2025 9:56


    Maoni ya waskilizaji kuhusu vipindi vyetu juma hili

    Play Episode Listen Later May 9, 2025 9:58


    Juma hili waskilizaji wetu walikuwa na maoni haya kuhusu taarifa zetu

    Je kuna hofu ya kutokea kwa vita vya tatu vya dunia

    Play Episode Listen Later May 8, 2025 10:00


    Katika makala haya  tunajadili athari ya vita vya ukraine na Urusi na sasa tishio la vita nyingine kati ya India na Pakistan. Je ni shara ya kutokea kwa vita vya pili vya dunia ? ndilo swali tumekuuliza. Skiza baadhi ya maoni ya waskilizaji.

    News Zealand kudhibiti mitandao ya kijamii kwa watoto

    Play Episode Listen Later May 7, 2025 9:55


     Shaba ya makala haya inalenga news Zealand ambapo serikali inapendekeza marufuku ya matumizi ya mitandao kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka 16, lengo likiwa kuwakinga dhidi ya athari za mitandao. Njia gani wazazi wa kiafrika wanaweza kuwalinda watoto na mitandao ya kijamii? Ndilo swali tumeuuliza na haya hapa baadhi ya maoni yako, skiza makala haya.

    Dunia uhuru wa vyombo vya habari na wanahabari

    Play Episode Listen Later May 5, 2025 9:36


    Leo mada yetu inajikita kwa siku ya kimataifa ya uhuru wa vyombo vya habari, ambapo  Umoja wa Mataifa umesema licha ya baadhi ya nchi kupiga hatua katika ulinzi wa wanahabari, hofu ya uhuru wa habari kuendelea kuminywa inaendelea kutanda. Mwaka jana jumla ya wanahabari 82 walipoteza maisha wakitekeleza majukumu yao. Tuambie nchini mwako vyombo vya habari viko huru? Haya hapa baadhi ya maoni yako, skiza makala.

    Makala habari rafiki Ijumaa Mada huru

    Play Episode Listen Later May 2, 2025 9:48


    Rasimu ya makubaliano kati ya DRC na Rwanda ya kutafuta suluhu ya mzozo

    Play Episode Listen Later Apr 29, 2025 9:40


    Mchakato wa kumchagua kiongozi mpya wa kanisa katoliki duniani

    Play Episode Listen Later Apr 28, 2025 10:02


    Kwa sasa macho yakiwamulika makadinali 135 watakaochagua papa mpya ndani ya siku chache zijazo, mjadala kuhusu Papa kutoka Afrika ukishamiri.Mchakato wa kumchagua p

    Joseph Kabila adaiwa kurejea DRC kupitia Goma

    Play Episode Listen Later Apr 21, 2025 9:53


    Juma lililopita ripoti ambazo hazijathibitishwa rasmi zilieleza kuwa rais wa zamani wa DRC, Joseph Kabila alirejea nchini Mwake kupitia mji wa Goma unaokaliwa na waasi wa M23 wanaosaidiwa na Rwanda. Hata hivyo hatua yake imeifanya serikali ya Kinshasa, kusimamisha shughuli zote za chama chake cha PPRD, ikikituhumu kushurikiana na waasi hao.Unazungumziaje kurejea kwa rais Kabila?Ndilo swali tumekuuliza katika makala haya.Skiza maoni ya mskilizaji.

    DRC: Kujerea kwa Joseph Kabila kwaibua hisia mseto

    Play Episode Listen Later Apr 10, 2025 10:05


    Katika makala haya shaba yetu inalenga nchini DRC, ambapo Rais mustaafu wa DRC, Joseph Kabila, ametangaza kurejea nchini humo, kutoka nchini Afrika Kusini ambako amekuwa akiishi kwa zaidi ya mwaka moja , ili kuchangia kutafuta suluhu kwa mzozo wa usalama mashariki mwa nchi yake. Unazungumziaje hatua hii ya Kabila? Ndilo swali tulikuuliza, skiza makala haya kuskia maoni ya waskilizaji wetu.

    Marekani : Rais Donamd Trump atangaza ushuru zaidi kwa bidhaa za kigeni

    Play Episode Listen Later Apr 9, 2025 10:00


    Kwenye makala haya tunajadili,  hatua ya rais wa Marekani, Donald Trump kutangaza kuongeza ushuru kwa bidhaa zote zanazoingizwa Marekani, kutoka mataifa ya Kigeni, hatua inayoonekana kutikisa uchumi wa Dunia.  Je unahisi hatua ya rais Trump ni sahihi?Ndilo swali tumeuuliza.Skiza makala haya kujua maoni ya waskilizaji.

    Kenya: Yawarejesha nyumbani raia wake waliotapeliwa kuenda Mynamar

    Play Episode Listen Later Apr 8, 2025 9:34


    Shaba yetu kwenye makala haya inalenga hatua ya Serikali ya Kenya, kueeendelea kuwarejesha mamia ya raia wake waliotapeliwa na kusafirishwa hadi nchini Myanmar kwa ahadi ya kupewa ajira.  Nchini mwako visa kama hivi vinaripotiwa?Ndilo swali letu, skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji.

    Africa Mashariki : Viongozi watathimini kudhibiti mitandao ya kijamii

    Play Episode Listen Later Apr 8, 2025 9:56


    Katika makala haya tunajadili haja ya kuwepo sheria za kudhibiti mitandao ya kijamii kwa baadhi ya mataifa ya Africa Mashariki. Skiza makala haya kuskia mano ya waskilizaji wetu.

    africa katika mashariki
    Maoni ya waskilizaji kuhusu wizi unaofanywa kwenye mizani na wafanyabiashara

    Play Episode Listen Later Apr 5, 2025 10:02


    Makala haya ni maoni ya waskilizaji kuhusu ripoti maalum ya namna wananchi wanavyopigwa na wafanyabiashara kwenye mizani wanapopimiwa nafaka mbalimbali za chakula, huku gesi ya kupikia pia ikitajwa.

    Maoni yako kwenye makala ya Habari Rafiki Mada Huru Ijumaa

    Play Episode Listen Later Mar 28, 2025 10:01


    DRC: Majadiliano ya kitaifa kuhusu kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa kitaifa

    Play Episode Listen Later Mar 25, 2025 10:01


    Qatar : Yakutanisha Kagame na Tshisekedi

    Play Episode Listen Later Mar 20, 2025 9:59


    Shaba yetu  leo kwenye makala haya inalenga taifa la Qatar ambapo taifa hilo juma hili lilifanikiwa kuwaleta pamoja marais Felix Tshiesekedi wa DRC na mwenzake wa Rwanda Paul Kagme, katika juhudi za kutafuta suluhu kwa mzozo wa mashariki ya DRC. Unafikiri Qatar itafanikiwa kuzima mzozo wa mashariki mwa DRC. Skiza makala haya kujua baadhi ya maoni ya waskilizaji.

    Kenya : Kanisa katoliki latangaza marufuku kwa wanasiasa

    Play Episode Listen Later Mar 19, 2025 10:00


    Tunajadili  hatua ya Kanisa la Anglikana nchini Kenya, kwa mara nyingine limesisitiza marufuku ya kuwazuia wanasiasa kuzungumza kanisani katika juhudi za kuzuia wanasiasa kufanya siasa kanisani. Je unazungumziaje hatua hii ya kanisa Anglikana nchini Kenya? Skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji wetu.

    Rwanda yasitisha uhusiano na Ubelgiji

    Play Episode Listen Later Mar 18, 2025 9:58


    Katika makala haya tunajadili hatua ya serikali ya Rwanda, kutangaza kusitisha uhusiano wa Kidiplomasia na taifa la Ubelgiji kutokana na kile Rwanda imesema Ubelgiji kuendeleza propaganda kuihusu kutokana na mzozo wa mashariki mwa DRC. Unazungumziaje hatua ya Rwanda Skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji.

    Watu zaidi ya milioni 6 duniani watakosa mahali pakuishi

    Play Episode Listen Later Mar 17, 2025 10:01


    Tunajadili hatua ya bazara la wakikimbizi la Denmark, kuchachapisha ripoti inayoonesha kuwa, watu zaidi ya milioni 6 duniani watakosa mahali pakuishi ifikapo mwishoni mwa mwaka ujao, kutokana na mizozo, mabadiliko ya tabia nchi na kusitishwa kwa misaada toka Marekani. Unazungumziaje hatua hii? ndilo swali tumeuliza, skiza makala haya kufahamu mengi.

    Maoni yako kutokana na habari zetu juma hili

    Play Episode Listen Later Mar 14, 2025 10:07


    Kila Ijumaa rfi Kiswahili inatoa nafasi kwa mskilizaji kuchaniua mada mbalimbali kuhusu taarifa zetu. Juma hili hizi ni haya ni baadhi ya maoni ya waskilizaji wetu

    DRC : Angola kufanikisha mkutano kati ya rais Tshisekedi na waasi wa M23

    Play Episode Listen Later Mar 13, 2025 9:54


    Shaba yetu inalenga nchini DRC, ambapo taifa la Angola limesema linajaribu kufanikisha mazungumzo ya moja kwa moja kati ya rais wa DRC, Felix Tshisekedi na waasi wa M23, ili kutafuta suluhu la mzozo wa mashariki mwa DRC. Je unafiriki Angola itafanikiwa katika hili?Haya hapa baadhi ya maoni yako.

    Sudan Kusini :Wanajeshi wa Uganda wawasili Sudan Kusini

    Play Episode Listen Later Mar 13, 2025 9:46


    Mkuu wa majeshi nchini Uganda, ambaye pia ni mwana wa rais Yoweri Museveni, Muhoozi Kainerugaba, amedai wanjeshi wa taifa lake wamewasili Sudan Kusini ili kusaidia jeshi la taifa hilo kutatua mzozo ndani ya serikali ya umoja wa kitaifa  Tunakuuliza je mzozo wa Sudan Kusini unastahili kutatuliwa kijeshi?Skiza makala haya kuskiza baadhi ya maoni yenu.

    Kenya: Vijana wapinga michango ya wanasiasa kanisani

    Play Episode Listen Later Mar 11, 2025 9:56


     Shaba yetu leoinalenga nchini Kenya ambapo Vijana wameanza kuandamana kupinga kile wanadai wanasiasa kutoa kiasi kikubwa cha pesa kwenye maeneo ya kuabudu ili hali wao hawana ajira. Tumekuuliza hatua hii ni sahihi?Haya hapa baadhi ya maoni yako.

    Kenya : Rais Ruto na mpinzani Raila Odinga kushirikiana

    Play Episode Listen Later Mar 11, 2025 9:58


    Mwishoni mwa juma  lililopita rais wa Kenya William Ruto na kiongozi wa upinzani Raila Odinga walitiliana saini mkataba wa ushirikiano wa kisiasa, wanaosema utasaidia kutatua changamoto  zinazowakabili raia wa taifa hilo.  Unaamini makubaliano ya viongozi hawa ni sahihi?Ndilo swali tumekuuliza na haya hapa maoni yako.

    Hatua ya rais Donald Trump kusitisha msaada wakijeshi kwa nchi ya Ukraine

    Play Episode Listen Later Mar 6, 2025 10:10


    Maoni kuhusu vingozi wa kijeshi wa nchi za Afrika Magharibi kutaka kugombea urais

    Play Episode Listen Later Mar 5, 2025 10:08


    Nchini Gabon, kiongozi wa kijeshi jenerali Brice Oligui Nguema ametangaza kuwa atagombea urais katika uchaguzi wa mwezi ujao, baada ya kutwaa madaraka kupitia mapinduzi ya kijeshi ya 2023.Hili linajiri wakati huu viongozi wengine wa kijeshi kwenye nchi za Burkina Faso, Mali na Niger wakielekea kuchukua mkondo huo.

    Vyama vya upinzani nchini Uganda kufunga kuwaombea wafungwa wa kisiasa

    Play Episode Listen Later Mar 4, 2025 9:37


    Kila Ijumaa ni mada huru ambapo unatoa maoni kuhusu ulichokiona wiki hii

    Play Episode Listen Later Feb 28, 2025 10:02


    Leo ni Ijumaa ,,siku ya mada huru kwenye habari rafiki  ambapo Tunakupa nafasi ya kuzungumzia suala lolote ambalo limetokea nchini mwako wiki hii au kile ambacho umekisikia kwenye matangazo yetu ya juma hili

    Rais wa Uganda Yoweri Museveni asikitishwa na hali ya umaskini nchini mwake

    Play Episode Listen Later Feb 27, 2025 10:06


    Mada  ni kuhusu..kauli ya Rais wa Uganda Yoweri Museveni Akiwa katika ziara ya kawaida kuzungumza na raia wake , ameeleza kuguswa na kusikitishwa na hali ya umasikini anayoshuhudia kwenye nchi yake,,,wakati huu tatizo la umasikini linashuhudiwa pia kwenye mataifa mengine ya ukanda.Tulimuuliza mskilizaji  anazungumziaje kauli ya Rais Museveni na je viongozi wa ukanda wamefanya vyakutosha kupambana na umasikini?

    Rais wa DRC, Felix Tschsekedi, atangaza kuunda Serikali ya umoja wa kitaifa

    Play Episode Listen Later Feb 24, 2025 10:00


    Karibu  kwenye kipindi cha leo ambapo tunaangazia tangazo la  Rais wa DRC, Felix Tschsekedi, kuwa  ataunda Serikali ya umoja wa kitaifa, hatua inayokuja wakati huu akiwa katika shinikizo kutoka ndani na nje ya nchi yake, kuhusu namna alivyoshughulikia mzozo wa mashariki mwa nchi yake, wakati huu waasi wa M23 wakichukua miji zaidi.

    Mada Huru: Maoni kuhusu habari kuu wiki hii na matukio katika maeneo mbalimbali

    Play Episode Listen Later Feb 21, 2025 9:57


    Ikiwa ni siku ya Ijumaa, ni wakati wa mada huru, yaani tunampatia mskilizaji nafasi kuchangia habari kuu ambazo tumekuwa nazo wiki hii hapa RFI Kiswahili au kutueleza jambo ambalo limetokea nchini mwake juma hili. Leo pia msikilizaji ni siku ya lugha mama, ningependa sana nikusalimie kwa lugha yako mama lakini ningependa kusikia kutoka kwako kwanza. Jambo! 

    Maoni: Marekani yaanza mazungumzo na Urusi ya kusitisha vita nchini Ukraine.

    Play Episode Listen Later Feb 21, 2025 9:58


    Haya ni makala ya Habari Rafiki tukiangazia maoni ya waskilizaji wa RFI Kiswahili kuhusu mada kwamba, Marekani imeanza mazungumzo na Urusi, lengo likiwa kupata mkataba wa kusitisha vita nchini Ukraine. Ukraine ambayo haijashirikishwa kwenye mchakato huo inasema haitakubali mkataba wowote bila kuhusishwa.Tumemuuliza msikilizaji je, Marekani inaweza kumaliza vita vya Ukraine? Na anafikiri ni kwanini Marekani haijaishirikisha Ukraine na mataifa ya Ulaya kwenye harakati hizi?

    Wanamgambo wa RSF waandaa mkutano wa kuunda serikali mbadala Nairobi

    Play Episode Listen Later Feb 19, 2025 10:01


    Wanamgambo wa RSF wanaopigana na jeshi nchini Sudan na washirika wake wakiwemo wanasiasa wapo jijini Nairobi nchini Kenya, wanakojadiliana kuhusu uundwaji wa serikali mbadala wakati huu inapoendelea na vita.Unazungumzia vipi harakati hizi za RSF ?Unafikiri ni kwanini Kenya imewaruhusu wanamgambo hao kukutana katika nchi yake ?

    Kikao cha usalama wa DRC na Sudan chakamilika Ethiopia bila suluhu

    Play Episode Listen Later Feb 17, 2025 10:00


    Makala ya leo yanaangazia Kikao cha viongozi wa Afrika, kilichotamatika rasmi mwishoni mwa juma lililopita nchini Ethiopia, mzozo wa DRC na Sudan ukigubika mijadala yao.Hata hivyo vikao hivyo  vimekamilika  bila suluhu ya mizozo ya nchi zote mbili, ambapo vyongozi  waliishia kwa kutoa wito wa kusitisha mapigano. tulimuuliza msikilizaji iwapo anaridhika na matokeo ya kikao hicho na  anadhani nini cha zaidi viongozi hawa wangefanya kukomesha mizozo barani Afrika

    Mkutano wa kila mwaka wa Umoja wa Afrika kuzingatia usalama wa DRC

    Play Episode Listen Later Feb 13, 2025 10:00


    Mkutano wa kila mwaka wa viongozi wa Afrika umeanza rasmi jijini Addis Ababa, #Ethiopia ambapo maswala muhimu ikiwemo usalama mashariki mwa #DRC, mapinduzi ya kijeshi na vita dhidi ya makundi ya kijihadi yakitarajiwa kugubika mkutano huu.Tulimuuliza mskilizaji natarajia nini kipya kutoka kwa viongozi wa AU? na iwapo anafikiri viongozi wameshindwa kumaliza changamoto za bara hili..

    Kauli ya rais Donald Trump kuhamisha wapalestina yapingwa vikali

    Play Episode Listen Later Feb 12, 2025 10:00


    Kwenye kipindi cha leo tunaangazia kauli  tata ya Rais Donald #trump, kuhusu mzozo wa #Gaza, safari hii akitishia kuvunjika kwa mkataba wa usitishaji mapigano, ikiwa Hamas haitawaachia mateka wote ifikapo Jumamosi ya wiki hii.Juma lililopita alidai kuwa nchi yake itachukua udhibiti wa Gaza na kuwahamisha Wapalestina.Tulimuuliza mskilizaji anazungumziaje kauli hiyo ya Trump and je huenda zikachochea mzozo zaidi kati ya #Israel na Hamas?

    Hatua ya Kenya kuondoa mahojiano kwa waomba vitambulisho yaibua hisia mseto

    Play Episode Listen Later Feb 11, 2025 9:57


    Makala haya yanaangazia hatua ya Serikali ya kenya  kusema  hakutakuwa na haja ya mahojiano kwa waomba vitambulisho toka katika maeneo ya mpakani, uamuzi ambao umeibua mjadala kuhusu masuala ya usalama.Tulimuuliza msikilizaji anazungumziaje hatua hiyo ya Kenya  vile vile nchini mwake hali ikoje

    Kauli ya mkutano wa SADC na EAC kuhusu amani nchini DRC waibua maoni mseto

    Play Episode Listen Later Feb 10, 2025 9:58


     kwenye makala ya leo tunaangazia  hatua ya  wakuu wa nchi za #SADC na EAC kutaka kusitishwa mapigano maramoja ,na kutaka  kuondoka kwa vikosi vya kigeni mashariki mwa #DRC, pamoja na Serikali ya Kinshasa kuzungumza moja kwa moja na waasi wa #M23 ambapo  wito huo  umepokelewa kwa hisia mseto na raia wa ukanda.

    Kila siku ya Ijumaa huwa tunaangazia mada huru kwenye makala habari rafiki

    Play Episode Listen Later Jan 31, 2025 10:03


    Kila siku ya  ijumaa ni mada huru  ambapo Tunampa nafasi  msikilizaji kujadili suala lolote ambalo limetokea nchini mwake wiki hii au kile ambacho amekisikiliza kwenye habari zetu juma hili.

    Changamoto za upatikanaji wa Nishati ya Uhakika barani Afrika

    Play Episode Listen Later Jan 30, 2025 9:58


    Wakuu wa nchi za Afrika walikutana juma hili nchini Tanzania ambapo walijadiliana kuhusu changamoto za upatikanaji wa Nishati ya Uhakika katika mataifa hayo.Licha ya rasilimali za bara la Afrika bado hakuna nishati ya uhakika na endelevu? Bonyeza uskilize maoni mbalimbali.

    Athari za Donald Trump kusitisha misaada kwa Afrika na njia mbadala kujitegemea

    Play Episode Listen Later Jan 30, 2025 10:01


    Uamuzi wa Rais wa Marekani #DonaldTrump, kuagiza kusitishwa kwa muda utowaji wa misaada yote ya kigeni umeibua mjadala na sintofahamu hasa kwa nchi za Afrika, ambazo sekta muhimu ikiwemo afya zinategemea msaada wa Marekani.Tulimuuliwa msikilizaji anazungumziaje hatua hii ya Marekani na Nchi za Afrika zifanye nini kuacha kutegemea misaada ya nchi za Kigeni?

    Swali: Je viongozi wa Afrika wanaweza kutatua migogoro inayokumba bara hilo

    Play Episode Listen Later Jan 29, 2025 9:51


    Mizozo inayosibu ukanda wa Afrika ya Mashariki inaendelea kuongezeka, ikiwemo Sudan Kusini na sasa DRC. Viongozi wa Afrika wanasisitiza matatizo ya Afrika sharti kutatuliwa kwa suluhu kutoka Afrika. Je hili linawezekana?

    Wito wa mataifa ya Afrika kutafuta suluhu kwa matatizo ya Afrika

    Play Episode Listen Later Jan 29, 2025 6:54


    Ukanda wa Afrika unazidi kushuhudia ongezeko la migogoro huku viongozi wakisisitiza Afrika ina majibu ya mizozo hiyo

    Nani wa kulaumiwa kuhusu vita vinavyoendelea mashariki mwa DRC

    Play Episode Listen Later Jan 23, 2025 10:01


    Mapigano kati ya waasi wa  M23 na wanajeshi wa serikali ya  DRC yanayoendelea na sasa yamefika jimboni Kivu Kusini,Tume ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia masuala ya kibinadamu OCHA ikisema maelfu ya watu wameendelea kukimbia makaazi yao.Kwenye makala haya tumemuuliza msikilizaji  nani wa kulaumiwa kuhusu vita hivi vinavyoendelea? na anafikiri ni kwanini imekuwa vigumu kupata suluhu?

    Claim Habari RFI-Ki

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel