Habari RFI-Ki

Follow Habari RFI-Ki
Share on
Copy link to clipboard

Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.

RFI - Radio France Internationale


    • Apr 10, 2026 LATEST EPISODE
    • weekdays NEW EPISODES
    • 9m AVG DURATION
    • 569 EPISODES


    More podcasts from RFI - Radio France Internationale

    Search for episodes from Habari RFI-Ki with a specific topic:

    Latest episodes from Habari RFI-Ki

    Makubaliano ya kusitisha vita kwa wiki mbili kati ya Marekani na Iran

    Play Episode Listen Later Apr 10, 2026 9:38


    Rais wa Cameroon Paul Biya amteua mwanaye   Franck Emmanuel Makamu wa rais

    Play Episode Listen Later Apr 10, 2026 9:42


    Uhaba na bei za juu za mafuta zashuhudia kashfa ya maofisa wa serikali kuhodhi

    Play Episode Listen Later Apr 8, 2026 10:03


    DRC kuanza kuwapokea wakimbizi haramu kutoka Marekani katika mkataba maalum

    Play Episode Listen Later Apr 7, 2026 10:06


    Africa : Mila za Africa je zinapotea ?

    Play Episode Listen Later Apr 4, 2026 9:49


    Katika makala haya tunajadili iwapo mila za kiafrica zimeanza kuweka na namna gani zinaweza kudumishwa. Skiza makalaa

    Maoni ya waskilizaji kuhusu matangazo yatu juma hili

    Play Episode Listen Later Apr 3, 2026 9:49


    Kila Ijumaa rfi Kiswahili inakuapa fursa kuchangia mada yoyote ile. Skiza maoni ya juma hili.

    DRC : Yafunzu kucheza Kombe la Dunia 2026

    Play Episode Listen Later Apr 1, 2026 9:59


     DRC imejikatia tiketi ya kucheza kwenye kupute cha kuwania kombe la dunia  Haya hapa maoni ya waskilizaji.

    Kombe la Dunia : Hofu ya dhuluma za wakati wa kombe la dunia

    Play Episode Listen Later Mar 31, 2026 10:00


    Ripoti ya shirika la Amnesty Interenational imeonya kuwa Kombe la Dunia la mwaka huu linaweza kuchangia ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu dunaini kutokana mpango wa mataifa wenyeji kuweka mikakati kali za uhamiaji na ufuatiliaji wa karibu wa mashabiki wa kigeni   Je, unahisi mashabiki kutoka Afrika Mashariki watakuwa salama kushabikia timu zao kule Merekani,Mexico na Canada? Skiza maoni ya waskilizaji.

    Uganda : Kuondoa magari mabovu jijini Kampla

    Play Episode Listen Later Mar 30, 2026 9:39


    Katika makala haya tunajadili hatua ya jiji la Kampala nchini Uganda kutatangaza makataa ya siku 20 kwa wamiliki wa magari ya usafiri wa uma kuondoa magari yaliyochakaa barabarani, mamlaka zikisema lengo ni kupunguza ajali na uchafuzi wa hali ya hewa mjini.   Tunakuuliza, nchi nyingine za Afrika mashariki zinapaswa kuiga mpango huu? Skiza maoni ya waskilizaji hapa.

    Kila Ijumaa RFI kiswahili inakupa nafasi kuchangia mada yoyote ile

    Play Episode Listen Later Mar 27, 2026 10:02


    Mashabiki wa rfi Kiswahili kila Ijumaa hupata nafasi ya kuchangia mada yoyote ile kupitia makala haya. Skiza maoni ya baadhi ya waskilizaji.

    Kufungwa kwa makanisa nchini Rwanda ni kwa lengo la uwajibikaji

    Play Episode Listen Later Mar 26, 2026 9:51


    Rais wa Rwanda Paul Kagame amekanusha madai kuwa serikali yake imekuwa ikiminya uhuru wa kuabudu, akisisitiza kwamba hatua ya serikali kufuatilia taasisi za kidini ni kwa lengo la kuhakikisha uwajibikaji, na kuwalinda raia dhidi ya ulaghai,

    Jez ni sahihi kwa wanasiasa kutusiana kwenye mikutano ya hadhara?

    Play Episode Listen Later Mar 24, 2026 10:01


    Nchini Kenya, rais William Ruto na aliyekuwa naibu wake Rigathi Gachagua, wamekuwa wakirushiana maneno makali, kwenye mikutano ya hadhara na hata kwenda mbali na kutoa matusi na kushambuliana kuhusu maumbile yao, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka ujao. Nini mtazamo wako kuhusu kauli za viongozi hawa ? Katika nchi yako wanasiasa, wanatupiana maneno hivi ?

    CAF iliivua Senegal ubingwa na kuipa Morocco baada ya miezi miwili

    Play Episode Listen Later Mar 20, 2026 9:55


    Katika uamuzi wa kushangaza , Shirikisho la soka barani Afrika CAF, limefuta ushindi wa Senegal kama mabingwa wa taji la AFCON na kulipa taji hilo Morocco ambao walikuwa wenyeji wa michuano hiyo.

    Mahakama ya kikatiba ya Uganda yafuta vipengee vilivyominya uhuru wa kusema

    Play Episode Listen Later Mar 20, 2026 9:55


    Urusi imehakikishia Kenya haitawasajili raia wake kupigana vita vya Ukraine

    Play Episode Listen Later Mar 20, 2026 9:30


    Nchi zaidi za Afrika zimejitokeza kusema raia wake walihadhaiwa na kusajiliwa kwenda kupigana na vikosi vya Urusi nchini Ukraine

    Bobi Wine ameweka hadharani alikimbia nchi yake baada ya kuhangaishwa

    Play Episode Listen Later Mar 20, 2026 10:12


    Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Uganda Bobi Wine baada ya kuwa mafichoni kwa miezi miwili alifunguka na kusema kafanikiwa kukimbia baada ya kuwindwa na vikosi vya usalama

    DRC : Mapendekezo ya kurekebisha katiba yaibua hisia mseto

    Play Episode Listen Later Mar 12, 2026 10:02


    Tunajadili kinachoendelea nchini DRC, ambapo  mjadala kuhusu mapendekezo ya kufanyia katiba marekebisho, ikiwemo muhula wa urais, unazidi kuibua hisia mseto, baadhi ya raia wakionekana kuunga mkono na baadhi kupinga.   Unazungumziaje mjadala huu nchini DRC? Skiza maoni ya mskilizaji.

    drc katiba tunajadili
    EAC : Kenya na Rwanda yakumbatia camera za siri barabarani

    Play Episode Listen Later Mar 11, 2026 9:45


    Tunajadili hatua ya Mataifa ya Kenya na Rwanda, kuanza kukumbatia matumizi ya kamera za siri barabarani ili kunasa madereva wanaokiuka sheria za barabarani, hatua inayolenga kupunguza ajali za mara kwa mara ambazo zimekuwa zikisababisha vifo maelfu ya raia. Je, unafikiri kamera za siri barabarani zitasaidia kupunguza ajali za barabarani? Ndilo swali tumekuuliza. Skiza maoni ya baadhi ya waskizaji.

    EAC : Mafuriko yatatiza jiji la Nairobi

    Play Episode Listen Later Mar 10, 2026 10:02


    Katika makala haya  tunajadili kinachoendelea jijini Nairobi nchini Kenya ambapo jiji hilo limeendelea kushuhudia mvua kubwa ambazo zimesababisha maafa ya zaidi ya watu 40. Nchi nyingine za Afrika Mashariki pia zinaendelea kushuhudia mvua kubwa. Skiza makala haya.

    EAC : Mabadiliko nani ya Jumuiya

    Play Episode Listen Later Mar 9, 2026 10:05


    Katika makala haya tunajdili Juma lililopita wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kumteua rais wa Uganda, Yoweri Museveni kuwa mwenyekiti mpya wa Jumuiya hiyo, huku wakitangaza mabadiliko kadhaa muhimu waliyosema yanalenga kuifanya jumuiya kutosambaratika. Miongoni mwa mabadiliko ni pamoja na nchi wanachama kuwalipa mshahara wabunge wao na namna nchi zinazodaiwa zitalipa madeni yake. Unafikiri mabadiliko haya yatasaidia Jumuiya Kukua? Skiza maoni ya mskilizaji.

    Maoni kuhusu taarifa za Ulimwengu ikiwemo mzozo wa Mashariki ya Kati

    Play Episode Listen Later Mar 8, 2026 10:01


    Leo ni siku ya mada huru. Tunampa msikilizaji wetu nafasi kuzungumzia suala lolote ambalo limetokea nchini mwake wiki hii, lakini pia kujadili kile ambacho amekisikia katika habari zetu wiki hii.

    Somaliland yatangaza kuruhusu Marekani kuchimba madini na kuweka kambi za jeshi

    Play Episode Listen Later Feb 24, 2026 9:46


    Kikao cha dharura cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki

    Play Episode Listen Later Feb 18, 2026 9:35


    Rais wa Kenya William Ruto, ameitisha kikao cha dharura cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika mashariki  mwezi ujao kujadili changamoto ya kifedha ambayo imetatiza shughuli za taasisi za jumuiya hiyo, tatizo kubwa likiwa baadhi ya nchi kuchelewesha kutoa michango kwa wakati. Mkutano huo utajadili mfumo mpya wa uchangishaji fedha na namna ya kupunguza matumizi ya jumuiya hiyo.

    Raia wa Afrika kuendelea kusajiliwa kupigana vita nchini Ukraine

    Play Episode Listen Later Feb 17, 2026 9:57


    Mkutano wa 39 wa umoja wa Afrika jijini Addis Ababa

    Play Episode Listen Later Feb 17, 2026 9:50


    Mwishoni mwa juma mkutano wa 39 wa Umoja wa Afrika (AU) umefanyika jijjini Adis Ababa nchini Ethiopia   Huku viongozi walioudhuria wakilipea kipau mbele swala la usalama  na uchumi wakati huu matafia mengi ya Afrika yakishuhudia migogoro na kudorora kwa uchumi.

    Kamanda wa polisi pwani ya Kenya atoa agizo kuwapiga wahalifu risasi

    Play Episode Listen Later Feb 10, 2026 10:00


    Mwishoni mwa juma Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani nchini Kenya Ali Nuno alitoa agizo kwa polisi kuwapiga risasi washukiwa wa uhalifu baada ya eneo hilo kushuhudia ongezeko la magenge yaliyojihami kwa mapanga. Hata hivyo hatua hiyo imepingwa vikali na mashirika ya kutetea haki za binadamu .Tumekuuliza unazungumziaje agizo hilo,Unadhani ni hatua sahihi kumaliza uhalifu na Nchini mwako hali ikoje

    Marekani yakutana na viongozi wa Afrika kuhusu swala la madini

    Play Episode Listen Later Feb 10, 2026 10:05


    Afrika Kusini yatangaza kuwaondoa wanajeshi wake kutoka kwa monusco nchini DRC

    Play Episode Listen Later Feb 9, 2026 10:00


    Mwishoni mwa juma Afrika Kusini ilitangaza kuondoa wanajeshi wake kutoka kwa tume ya Umoja wa Mataifa ya kulinda amani nchini DRC (MONUSCO) baada ya kikosi hicho kuhudumu kwa miaka 27.Pretoria inasema hatua hiyo ni kutokana na mipango yake ya kurekebisha na kuimarisha raslimali ya jeshi lake.Tumemuuliza msikilizaji anazungumziaje hatua hii ya Afrika kusini,Hatua hii ni kumaanisha Monusco imepoteza nguvu DRC na Nini kifanyike kuleta usalama wa kudumu nchini DRC?

    Maoni yako Ijumaa hii kwenya mada huru

    Play Episode Listen Later Jan 30, 2026 10:00


    Matumizi ya mitandao ya kijamii kwa watoto chini ya miaka 15

    Play Episode Listen Later Jan 30, 2026 9:56


    Nchi za magahribi kupitisha sheria za kupiga marufuku mitandao ya kijamii kwa watoto walio chini ya miaka 15.

    Mwaka mmoja tangu mji mkubwa mashariki mwa DRC kuanguka mikononi mwa M23

    Play Episode Listen Later Jan 30, 2026 10:02


    Marekani kujiondoa rasmi kwenye WHO, hatua hatari kwa sekta ya afya dunaini

    Play Episode Listen Later Jan 27, 2026 9:53


    Wiki iliopita, ilijiondoa kwenye shirika la afya duniani licha ya onyo kuwa hatua hiyo itaathiri ufadhili kwenye sekta ya afya duniani. Wiki chache zilizopita, rais Donald Trump alitangaza pia kuwa Marekani itajiondoa kwenye mashirika 66 ya kimataifa, yakiwemo yaliyo chini ya Umoja wa Mataifa

    Siku ya kimataifa ya nishati safi: Wewe unatumia nishati gani?

    Play Episode Listen Later Jan 27, 2026 9:21


    Januari 26 2026, dunia  inaadhimisha Siku ya Kimataifa ya Nishati Safi, lengo likiwa ni kuhamasisha umuhimu wa matumizi ya nishati safi katika maisha ya kila siku, na mchango wake kwa mazingira na maendeleo endelevu.

    Serikali ya Uganda yafunga mitandao kuelekea uchaguzi mkuu wa siku ya Alhamisi

    Play Episode Listen Later Jan 15, 2026 10:01


    Hii leo tunazungumzia hatua ya serikali ya Uganda kuagiza mitandao kufungwa, ikisema hatua hiyo inalenga kudhibiti habari za kupotosha na kulinda usalama wa taifa, kueleka uchaguzi mkuu unaofanyika Alhamisi hii.

    Maoni: Hatua ya Marekani kutangaza kujiondoa katika mashirika 66 yakiwemo yale ya Umoja wa Mataifa

    Play Episode Listen Later Jan 15, 2026 10:01


    Agizo la kiutendaji lililosainiwa na rais wa Marekani linaagiza Marekani kujiondoa kutoka kwa jumla ya mashirika 66, karibu nusu yake ambayo yana uhusiano na Umoja wa Mataifa, Ikulu ya White House ilisema wiki iliyopita. Miongoni mwa hayo ni Mkataba wa Mfumo wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa (UNFCCC), mkataba wa msingi wa mikataba mingine yote ya kimataifa ya hali ya hewa, uliohitimishwa mwaka wa 1992 katika Mkutano wa Rio Earth.

    Wawakilishi wa Afrika mashariki wayaaga michuano ya AFCON 2025

    Play Episode Listen Later Jan 8, 2026 9:49


    Timu ya DRC "Leorpard" siku ya Jumanne ilikuwa mwakilishi wa mwisho wa Afrika Mashariki kuondolewa kwenye michuano ya kombe la mataifa ya Afrika, baada ya kupoteza mechi yao ya hatua ya 16 bora dhidi ya Algeria. Uganda ilikuwa ya kwanza kuondolewa katika hatua ya makundi ikifuatiwa na Tanzania iliyotolewa kwenye hatua ya mtoano.

    Matukio ya wanahabari kushambuliwa wakati wa kampeni za uchaguzi

    Play Episode Listen Later Jan 7, 2026 9:58


    Nchini Uganda, kuelekea uchaguzi mkuu, kumeripotiwa matukio ya wanahabari kushambuliwa na vyombo vya usalama wakati wakiripoti kampeni za uchaguzi na hasa za upinzani. Matukio kama haya yameshuhudiwa pia katika nchi nyingine za Afrika.

    uganda afrika wakati uchaguzi kampeni
    Marekani kufanya oparesheni ya kijeshi na kumkamata rais Nicolas Maduro

    Play Episode Listen Later Jan 6, 2026 9:52


    Mwishoni mwa juma lililopita, Marekani iliivamia Venezuela na kumkamata rais Nicolas Maduro, na sasa inatarajiwa kumshtaki kwenye mahakama zake kwa tuhuma za ulanguzi wa dawa za kulevya. Unafikiri kilichofanywa na Marekani ni sahihi?

    Mada huru ya mwisho wa mwaka 2025

    Play Episode Listen Later Dec 26, 2025 10:15


    Makala hii ya habari rafiki rafiki ijumaa ya desemba 26 2025 ni siku ya mada huru; tunakupa fursa kuchangia suala lolote ambalo limejiri nchini mwako wiki hii. Unaweza pia kuzungumzia kile ambacho umekisikia kwenye matangazo yetu ya redio juma hili. Nahodha wa Habari Rafiki Ruben Lukumbuka, moja kwa moja kutoka Studio maridai namba2.

    Ulimwengu washerehekea sikukuu ya Krismasi

    Play Episode Listen Later Dec 25, 2025 10:02


    Wakristo wanaadhimisha sikukuu ya Krismasi, wakati baadhi ya nchi kama Sudan, Ukraine na Mashariki mwa DRC yakikabiliwa na changamoto za usalama.-Unaadhimsisha sikuu ya Krismasi ukiwa wapi ? Sikukuu ya mwaka huu ikoje ?

    Maandalizi ya timu za mataifa ya Afrika mashariki na kati katika AFCON 2025

    Play Episode Listen Later Dec 23, 2025 10:01


    Msikilizaji Mashindano makubwa zaidi ya soka barani Afrika, Kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 yanaingia katika siku yake ya tatu leo jumanne ambapo jumla ya timu 24 za mataifa ya Afrika zikiwania taji hilo. Leo DRC wanamenyana na Benin, Tanzania wanakutana na Nigeria. Unazungumziaje maandalizi ya nchi za Afrika Mashariki na kati ?Nini matarajio yako kwenye mashindano haya ?

    Tume ya umoja wa mataifa nchini DRC, MONUSCO yaongezewa mwaka mmoja zaidi

    Play Episode Listen Later Dec 22, 2025 10:00


    Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeongeza muda wa mwaka mmoja kwa ujumbe wa kulinda amani nchini DRC, wakati mapigano yakiongezeka mashariki mwa nchi hiyo kufuatia mashambulizi mapya ya waasi wa M23. Uamuzi huu unakuja wakati mjadala ukiendelea kuhusu ufanisi wa MONUSCO nchini humo. Je, unaamini hatua hii itasaidia au ujumbe huo umepoteza uaminifu na uwezo wa kuleta mabadiliko ya kweli? Je, umoja wa Mataifa unapaswa kufikiria upya mkakati wake wa kulinda amani nchini DRC?

    Marekani yapiga marufuku kwa raia kutoka mataifa kadhaa kuingia ardhi yake

    Play Episode Listen Later Dec 18, 2025 10:01


    Makala hii imeangazia hatua ya hivi karibuni ya rais wa marekani Donald Trump ya kuongeza orodha mpya ya mataifa zaidi yakiwemo ya Afrika ikiwemo Tanzania,  ambayo raia wake wanazuiwa kuingia Marekani, tumekuuliza Je? hatua hii ni ya kibaguzi ama inalenga kuulinda usalama wa Marekani? Na kwa mtazamo wako Hatua hii Ina maana gani? Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kupata maoni ya wasikilizaji

    Waasi wa AFC/M23 watangaza kujiondoa katika mji wa Uvira DRC

    Play Episode Listen Later Dec 17, 2025 10:00


    Kumekuwa na hisia mseto tangu waasi wa AFC/M23 wanaoungwa mkono na Rwanda watangaze kuwa watawaondoa wapiganaji wao katika mji wa Uvira mkoani Kivu Kusini mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.Je? shinikizo la Marekani litazaa matunda? sikiliza maoni ya wasikilizaji wetu katika makala hii ya Habari rafiki 

    Ukoloni mamboleo na maendeleo ya bara la Afrika

    Play Episode Listen Later Dec 15, 2025 9:59


    Tarehe 14/12 dunia iliadhimisha miaka 60 ya azimio la kupinga ukoloni. Hata hivyo ukoloni katika sura zake za zamani na mpya bado unaathiri jamii zetu leo hii, baadhi wanaita ukoloni mamboleo.Je, ukoloni uliisha kweli Afrika au umebadilika tu? Je unaathiri vipi maendeleo ya Afrika? Nini kifanyike kuukomesha?Kupata mengi ungana na mwanahabari wetu Ruben Lukumbuka

    Claim Habari RFI-Ki

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel