POPULARITY
Categories
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania, ambako Magonjwa ya kimeta, miguu na midomo yanayokumba mifugo kama vile ng'ombe pamoja na mdondo unaoshambulia kuku yameendelea kuwa mwiba duniani na hata nchini Tanzania, ambako mbinu mbali mbali zimekuwa zikitumika kuyadhibiti ili kunusuru afya ya mifugo.Uchambuzi mpya kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) na HRP, ambao ni mpango wa taasisi za Umoja wa Mataifa za utafiti kuhusu uzazi wa binadamu, unaonesha kuwa takribani theluthi mbili ya vifo vya wajawazito duniani hutokea katika nchi zilizoathiriwa vibaya na migogoro au zenye udhaifu wa mifumo, ambapo ujauzito ni hatari mara tano zaidi ikilinganishwa na nchi zilizo thabiti.Vita vya Ukraine vikielekea kuingia katika mwaka wa tano, zaidi ya theluthi moja ya watoto wa Ukraine bado wameyakimbia makazi yao wengi wao sasa wakilazimika kuishi katika majengo yaliyoko chini ya ardhi. Akizungumza na waandishi wa habari kutoka kwenye chumba cha chini ya jengo katika mji wa Kherson, mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) nchini Ukraine, Munir Mammadzade, amesema mji huo “upo chini ya mashambulizi ya mara kwa mara,” huku mashambulizi ya kila siku yakiharibu nyumba na miundombinu muhimu, pamoja na huduma ambazo watoto na familia wanazitegemea.Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wameeleza wasiwasi mkubwa kuhusu madhara yanayoweza kuwapata waathirika waliotajwa katika nyaraka zinazojulikana kama “Epstein Files”, wakisema mchakato wa utoaji wa taarifa hizo haukulinda ipasavyo faragha na usalama wao na pia wametaka hatua stahili za kisheria zichukuliwe kwa wale wote waliotajwa katika nyaraka hizo kwa mujibu wa sheria. Nyaraka hizo zinafichua maovu yaliyotendwa na watu mbalimbali kupitia mmarekani Jeffrey Epstein.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya"KOO" katika mkitadha wa wanyama.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imetoa onyo kali kuhusu kuzorota kwa hali ya kiuchumi nchini Cuba, ikisema uhaba wa mafuta na vikwazo vya muda mrefu vinaathiri vibaya huduma za msingi kote nchini humo. Flora Nducha na taarifa zaidi
Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa kimataifa unaofahamika kama AI Impact 2026 mjini New Delhi, India, hali ya kibinadamu nchini Cuba, na huduma za Afya, maji safi na salama nchini DR Congo.Mkutano wa kimataifa unaofahamika kama AI Impact 2026 umeanza leo mjini New Delhi, India ukiwakutanisha viongozi kutoka sehemu mbalimbali za dunia ili kujadili namna akili mnemba (AI) inavyoweza kuendelezwa na kutumika kwa uwajibikaji kuchangia maendeleo endelevu. Amandeep Singh Gill, Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia teknolojia za kidijitali na zinazoibuka, amesisitiza ushiriki mpana wa kimataifa kwani ni muhimu ili kuhakikisha AI inanufaisha nchi zote.Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imetoa onyo kali kuhusu kuzorota kwa hali ya kiuchumi nchini Cuba, ikisema uhaba wa mafuta na vikwazo vya muda mrefu vinaathiri vibaya huduma za msingi kote nchini humo.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF wakishirikiana na Shirika la Maendeleo la Korea KOICA wanawasaidia wananchi wa Nyunzu katika jimbo la Tanganyika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC kwa miradi ya kusaidia huduma za afya ya watoto ambapo wamepanua upatikanaji wa huduma muhimu na endelevu.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Mkutano wa kimataifa unaofahamika kama AI Impact 2026 umeanza leo mjini New Delhi, India ukiwakutanisha viongozi kutoka sehemu mbalimbali za dunia ili kujadili namna akili mnemba (AI) inavyoweza kuendelezwa na kutumika kwa uwajibikaji kuchangia maendeleo endelevu. Amandeep Singh Gill, Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia teknolojia za kidijitali na zinazoibuka, amesisitiza ushiriki mpana wa kimataifa kwani ni muhimu ili kuhakikisha AI inanufaisha nchi zote. Anold Kayanda na taarifa zaidi.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF wakishirikiana na Shirika la Maendeleo la Korea KOICA wanawasaidia wananchi wa Nyunzu katika jimbo la Tanganyika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo DRC kwa miradi ya kusaidia huduma za afya ya watoto ambapo wamepanua upatikanaji wa huduma muhimu na endelevu. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi
Leo tumeangazia CAF kudhibitisha kuwa AFCON 2027 itaandaliwa Afrika Mashariki licha ya tetesi za kuahirishwa au kuhamishwa, uchambuzi wa raundi ya mwisho ya hatua ya makundi mechi za klabu bingwa, mechi za kufuzu kombe la dunia la wasichana U20, siku ya kwanza ya michuano ya raga ya wachezaji saba kila upande divisheni ya pili ya HSBC, mfumo mpya wa mashindano ya Tour du Rwanda, kiungo wa Ghana Thomas Partey akumbwa na shtaka jipya lakini pia michezo ya Olimpiki msimu wa baridi.
Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya Redio Duniani likitupeleka nchini Tanzania kusikia jinsi ambavyo redio inavyochochea maendeleo ya kijamii, nchini Uganda kumsikia mkimbizi kutoka DRC, na katika ukanda wa Gaza ambako redio inaunganisha tena jamii ndani ya vifusi.Leo ni siku ya redio duniani ambayo msingi wake unatokana na kuanzishwa kwa redio ya Umoja wa Mataifa tarehe 13 Februari mwaka 1946 jijini New York, Marekani. Kwa mantiki hiyo ikiwa mwaka huu redio hiyo ya Umoja wa Mataifa inatimiza miaka 80 tumeangazia mchango wa vipingi vyake vilivyokuwa vinarushwa na redio zingine ikiwemo iliyokuwa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) nchini Tanzania wakati huo. Assumpta Massoi amemulika suala hilo.Katika maeneo ya migogoro, duniani redio huwa nguzo ya utulivu na wakati mwingine daraja la kuokoa maisha. Na ndivyo ilivyokuwa kwa mkimbizi Bahati Yohane kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kwani kwake, redio haikuwa tu combo cha habari ilikuwa dira ya kuokoa maisha yake.Kabla ya vita vya sasa kuanza katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina lilalokaliwa kimabavu na Israel, Redio ilikuwa chombo muhimu kwa umma na kwa hakika umuhimu wake haujakoma isipokuwa huduma ya matangazo ya redio ndio iliyokuwa imekoma kutokana na vituo vya redio kusambaratishwa kwa makombora, lakini sasa juhudi zinafanyika kuirejesha huduma hiyo muhimu.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Katika maeneo ya migogoro, redio huwa nguzo ya utulivu. Mathalani Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Radio Okapi ya Umoja wa Mataifa imekuwa sauti ya kuaminika na kuwasaidia wakimbizi kusaka usalama tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002 kama sehemu ya ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO. Mmoja wa wakimbizi kutoka Mashariki mwa DRC ambaye sasa anaishi kambi ya wakimbizi ya Kyangwali nchini Uganda amemweleza John Kibego kutoka Redio washirika wetu Kazi Njema FM ya mjini Hoima jinsi matangazo ya redio Okapi yalivyonusuru maisha yake wakati wa vita
Leo ni siku ya redio duniani ambayo msingi wake unatokana na kuanzishwa kwa redio ya Umoja wa Mataifa tarehe 13 Februari mwaka 1946 jijini New York, Marekani. Kwa mantiki hiyo ikiwa mwaka huu redio hiyo ya Umoja wa Mataifa inatimiza miaka 80 tumeangazia mchango wa vipingi vyake vilivyokuwa vinarushwa na redio zingine ikiwemo iliyokuwa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) nchini Tanzania wakati huo. Assumpta Massoi amemulika suala hilo.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina kesho Ijumaa tarehe 13 Februari ikiwa ni ni siku ya Redio Duniani mwaka huu ikijikita katika Redio na Akili tunakupeleka mashariki mwa DRC, kwa George Musubao kutoka Televishen na Radio washirika Canal Victoire Du People Kasindi.Leo tarehe 12 Februari ni siku ya Kimataifa ya Kuzuia Itikadi Kali Zinazochochea Ugaidi, ikiwa ni maadhimisho ya nne tangu kuanzishwa kwake na mwaka huu kauli mbiu inasema “Kuzuia ugaidi wa kikatili katika enzi ya teknolojia mpya na zinazoibuka”. Ugaidi na itikadi kali vinaendelea kuwa tishio kubwa kwa amani na usalama wa dunia, huku vikigusa watu wa rika, dini na tamaduni mbalimbali na ndio maana Umoja wa Mataifa unasema ingawa teknolojia kama akili mnemba au AI, mitandao ya kijamii na majukwaa ya kidijitali inaweza kusaidia juhudi za kuzuia misimamo mikali, pia inatumiwa na magaidi kueneza chuki, upotoshaji na kuhamasisha vurugu ndio maana shirika hilo linahimiza ushirikiano wa kimataifa, matumizi ya teknolojia kwa uwajibikaji na suluhisho shirikishi zinazoheshimu haki za binadamu ili kuzuia kuenea kwa itikadi kali.Barani Ulaya ambapo Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ametoa tamko kali akilaani mashambulizi ya mfululizo yanayofanywa na nchi ya Urusi dhidi ya mifumo ya nishati nchini Ukraine. Taarifa iliyotolewa leo kutoka Geneva, Uswisi, imeeleza kuwa mashambulizi hayo yanawanyima raia mahitaji muhimu ikiwemo mifumo ya kupasha joto, maji, na umeme katikati ya msimu wa baridi kali uliopitiliza.Kuelekea kuanza kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani hapo wiki ijayo, katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametuma ujumbe akisema kuwa “Katika zama hizi ngumu na za mgawanyiko, hebu tuitikie wito wa stahmala wa Ramadhani. Kuziba pengo la mgawanyiko. Kufikisha msaada na matumaini kwa wale wanaoumini. Na kulinda haki na utu wa kila mtu…..Hebu Mwezi huu Mtukufu ututie hamasa ya kufanya kazi pamoja ili kujenga dunia yenye amani zaidi, ukarimu na haki kwa watu wote. Ramadhani njema.”Na Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "UNGUKA"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Leo ni siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi mwaka huu mauadhui yakihimiza “Sayansi kwa Mustakabali Jumuishi kwa Wanawake na Wasichana” Kwamujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , Sayansi na Utamaduni UNESCO leo hii , wanawake wanachangia chini ya theluthi moja ya watafiti duniani, kulingana hivyo kuziba pengo hili la kijinsia si suala la haki pekee ni muhimu kwa ubora, uhalisia na mchango wa sayansi, teknolojia na ubunifu. Flora Nducha na taarifa zaidi
Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya IPU kuhusu uhasama wa wabunge, siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi, na yalitojiri katika Jukwaa la akili unde au AI lililofanyika kwa siku mbili huko Nairobi, nchini Kenya.Wabunge kote ulimwenguni wanakabiliwa na viwango vinavyoongezeka vya vitisho, unyanyasaji na vurugu kutoka kwa umma imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na Muungano wa Mabunge Duniani (IPU). Rashid Malekela na taarifa zaidi.Leo ni siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi mwaka huu mauadhui yakihimiza “Sayansi kwa Mustakabali Jumuishi kwa Wanawake na Wasichana” Kwamujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , Sayansi na Utamaduni UNESCO leo hii , wanawake wanachangia chini ya theluthi moja ya watafiti duniani, kulingana hivyo kuziba pengo hili la kijinsia si suala la haki pekee ni muhimu kwa ubora, uhalisia na mchango wa sayansi, teknolojia na ubunifu.Jukwaa la akili unde au AI lililofanyika kwa siku mbili huko Nairobi, nchini Kenya limekunja jamvi ambapo mmoja wa washiriki amesema wanaodai kuwa bara la Afrika liko nyuma kwenye teknolojia hiyo, ni dhahiri shairi hawalifahamu vema bara hilo lenye mataifa 54.
Hii leo jaridani Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na Wakili Amon Mpanju, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kutoka Tanzania aliyehudhuria Mkutano wa Kamisheni ya Maendeleo ya Kijamii (CSocD64).Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yametoa onyo kali kuhusu hali mbaya ya kibinadamu inayowakumba watoto nchini Sudan. Mashirika hayo lile la kuhudumia watoto UNICEF, la afya WHO na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu wamenasema ghasia zisizoisha, njaa na magonjwa vinawasababisha watoto kupoteza Maisha na kudhoofika, huku mashambulizi dhidi ya vituo vya afya na vikwazo vya upatikanaji wa misaada vikizorotesha juhudi za kuwaokoa. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, msemaji wa UNICEF, Ricardo Pires, amesema “Katika baadhi ya maeneo ya jimbo la Darfur Kaskazini, zaidi ya nusu ya watoto wote wanakabiliwa na utapiamlo mkali, si makadirio, si mfano, imethibitishwa.”.Kikosi cha 12 cha Ulinzi wa Amani kutoka Tanzania TANZBAT 12 kinachohusumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Condo DRC chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO kimeendelea kudumisha uhusiano wa kijamii na wakazi wa mji wa Beni Mashariki mwa DRC, kwa kutoa msaada wa vifaa vya elimu kwa wanafunzi katika shule ya msingi Ngite iliyopo eneo la Mavivi. Mkuu wa shule hiyo Neema Nyamwaka amewashukuru walinada amani hao kutoka Tanzania kwa kujali sekta ya elimu.Leo ni siku ya mikunde duniani Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO likisistiza umuhimu kwa chakula hicho kwa lishe na mazingira. Huko Kigoma Tanzania FAO kupitia mpango wa Pamoja wa KJP imekuwa ikitoa mafunzo kwa wakulima kuhusu umuhimu wa mazao ya jamii ya mikunde huyu ni mmoja wa wanufaika wa mafunzo hayo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Atokeapo mtoto wa fuko mshike japo wawinda fuko.”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
January 26 is one of the most debated dates in Australia's history. Often described as the nation's birthday, the day marks neither the formal founding of the colony nor the creation of the Commonwealth. Instead, it reflects a layered history shaped by colonisation, political decisions, and ongoing First Nations resistance. Understanding what actually happened on January 26 reveals why the date is experienced so differently across the country. - Tarehe 26 Januari ni moja ya tarehe zinazojadiliwa sana katika historia ya Australia. Mara nyingi inatajwa kama siku ya kuzaliwa ya taifa, lakini siku hiyo haimaanishi kuundwa rasmi kwa koloni au kuanzishwa kwa Jumuia. Badala yake, inaakisi historia yenye tabaka nyingi inayoundwa na ukoloni, maamuzi ya kisiasa, na upinzani unaoendelea wa Mataifa ya Kwanza. Kuelewa kilichotokea hasa tarehe 26 Januari kinafunua ni kwa nini tarehe hiyo inaathiriwa kwa namna tofauti katika nchi nzima.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, (MONUSCO) umetoa taarifa kwamba umefahamishwa na Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa kuwa Afrika Kusini itaondoa vikosi na wanajeshi wake waliobaki ndani ya MONUSCO. Rashid Malekela ameifuatilia kwa kina taarifa hiyo na anaeleza zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini DRC, mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu mwenye ulemavu wa kutoona nchini Vietnam, na harakati za kutokomeza ukeketaji nchini Kenya.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, (MONUSCO) umetoa taarifa kwamba umefahamishwa na Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa kuwa Afrika Kusini itaondoa vikosi na wanajeshi wake waliobaki ndani ya MONUSCO. Ninamualika Rashid Malekela aliyeifuatilia kwa kina taarifa hiyo ili atueleza zaidi.Nchini Vietnam taifa lililoko kusini-mashariki mwa Asia, mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu mwenye ulemavu wa kutoona anajitahidi kuhakikisha anatimiza ndoto yake ya kuwa mtaalamu wa mawasiliano licha ya vikwazo anavyokumbana navyo kila uchao, na hii ni kwa sababu si kwamba njia ni rahisi bali kwa sababu dhamira yake ni kubwa zaidi.Ukeketaji au FGM ni jinamizi linalowaandama waathirika maisha yao yote likisababisha changamoto sio tu za kimwili lakini pia za kiafya na kuwaacha na makovu yasiyofutika. Katika Kaunti ya Tana River Kusini Mashariki mwa Kenya tunakutana na manusura na shujaa mwanaharakati wa kupambana na mila hiyo potofu ya ukeketaji Saadia Hussein, raia wa Somalia anayeishi Kenya hivi sasa. Mkurugenzi mtendaji na mwanzilishi wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Brighter Society Initiative anatusimulia safari yake ya machungu ya ukeketaji.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Nchini Vietnam taifa lililoko kusini-mashariki mwa Asia, mwanafunzi mmoja wa Chuo Kikuu mwenye ulemavu wa kutoona anajitahidi kuhakikisha anatimiza ndoto yake ya kuwa mtaalamu wa mawasiliano licha ya vikwazo anavyokumbana navyo kila uchao, na hii ni kwa sababu si kwamba njia ni rahisi bali kwa sababu dhamira yake ni kubwa zaidi. Assumpta Massoi anasimulia zaidi kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani, ILO.
Katika mpaka kati ya Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, na Sudan, maelfu ya familia waliokimbia makazi yao kutokana na vurugu wanapokea msaada wa chakula unaookoa maisha kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP uliosafirishwa kwa ndege hadi kwenye moja ya maeneo magumu zaidi kufikika nchini humo. Flora Nducha na taarifa zaidi
Hii leo jaridani tunaangazia juhudi za kutokomeza ukeketaji, watu waliotoweka katika ukanda wa Gaza kufuatia vita vya Hamas na Israeli, na msaada wa chakula kwa wakimbizi katika mpaka kati ya Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, na Sudan.Zaidi ya wasichana milioni 4.5 duniani kote, wengi wao wakiwa wenye umri wa chini ya miaka mitano, wako hatarini kufanyiwa ukeketaji mwaka huu pekee, wameonya viongozi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa katika ujumbe wao wa siku hii ya kimataifa ya kutokomeza ukeketaji kwa wanawake na watoto wa kike.Huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel, wiki hii, mamlaka za Israel zimewasilisha miili 54 pamoja na mifuko 66 iliyosheheni mabaki ya viungo vya binadamu ya Wapalestina waliopotea wakati wa vita. Na kutokana na kutokuwepo kwa mfumo madhubuti wa kisasa kupima vinasaba kutambua mwili upi ni wa nani inakuwa changamoto kubwa hususani kwa ndugu.Katika mpaka kati ya Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, na Sudan, maelfu ya familia waliokimbia makazi yao kutokana na vurugu wanapokea msaada wa chakula unaookoa maisha kutoka kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP uliosafirishwa kwa ndege hadi kwenye moja ya maeneo magumu zaidi kufikika nchini humo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Zaidi ya wasichana milioni 4.5 duniani kote, wengi wao wakiwa wenye umri wa chini ya miaka mitano, wako hatarini kufanyiwa ukeketaji mwaka huu pekee, wameonya viongozi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa katika ujumbe wao wa siku hii ya kimataifa ya kutokomeza ukeketaji kwa wanawake na watoto wa kike. Rashid Malekela na maelezo zaidi.
Jaridani hii leo tuna Muhtasari wa Habari ukiangazia hali ya njaa Sudan, mchango wa Marekani dhidi ya VVU/ Ukimwi na kauli ya UNRWA kufuatia taarifa potofu dhidi ya shirika hilo. Halikadhalika mada kwa kina kutoka AfyaAFRIKA.Maeneo mawili zaidi katika jimbo la Darfur Kaskazini ya Um Baru na Kernoi sasa yameingia katika baa la njaa kufuatia utapiamlo wa kupindukia au unyafuzi kuvuka wiwango vya kutokuwa na uhakika wa chakula.Shirika la Umoja wa mataifa linalohusika na vita dhidi ya ukimwi UNAIDS limekaribisha kwa dhati hatua ya Marekani kutia saini kuwa sheria kifurushi cha matumizi ya kimataifa chenye thamani ya dola bilioni 5.88, kwa ajili ya hatua za kimataifa za kukabiliana na virusi vya ukimwi VVU .Kamishina Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA Phillippe Lazzarini amesema taarifa potofu dhidi ya UNRWA zinaendelea kulenga shirika hilo katikati ya mgogoro Gaza ikiwemo madai ya hivi karibuni kabisa, yaliyoibuliwa na video ya jeshi la Israel ikionesha mifuko mitupu ya unga karibu na mabomu, ambapo amesema ni taarifa za uongo na hazijadhibitishwa.Katika Mada kwa Kina: Kuelekea siku ya kutokomeza FGM kesho Februari 6, tunazungumza na Catherine Mootian, Muasisi na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la kiraia la AfyAfrika la huko Narok nchini Kenya. Yeye ni manusura wa FGM aliyeamua kuchukua hatua kuepusha wengine.
Mabadiliko ya mfumo wa maisha na mazingira yanaweza kuzuia ugonjwa wa saratani kwa wagonjwa wanne katika kila wagonjwa kumi, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, (WHO) na shirika lake tangu la Utafiti kuhusu saratani, IARC kama anavyoripoti Rashid Malekela.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) leo Februari 4, 2026 limetangaza kusitisha shughuli zake zote katika kaunti ya Baliet, jimbo la Upper Nile, nchini Sudan Kusini kufuatia mfululizo wa mashambulizi dhidi ya msafara wake wa majini mwishoni mwa wiki iliyopita. Anold Kayanda na taarifa zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia juhudi za kutokomeza sarati, mashambilizi dhidi ya misafara ya chakula katika kaunti ya Baliet, jimbo la Upper Nile, nchini Sudan Kusini na tunamulika miaka kumi na nne baada ya wakimbizi wa kwanza wa Syria kuvuka mpaka kuingia Jordan.Mabadiliko ya mfumo wa maisha na mazingira yanaweza kuzuia ugonjwa wa saratani kwa wagonjwa wanne katika kila wagonjwa kumi, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, (WHO) na shirika lake tangu la Utafiti kuhusu saratani, IARC.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) leo Februari 4, 2026 limetangaza kusitisha shughuli zake zote katika kaunti ya Baliet, jimbo la Upper Nile, nchini Sudan Kusini kufuatia mfululizo wa mashambulizi dhidi ya msafara wake wa majini mwishoni mwa wiki iliyopita. Anold Kayanda na taarifa zaidi.Miaka kumi na nne baada ya wakimbizi wa kwanza wa Syria kuvuka mpaka kuingia Jordan kusaka usalama, kambi ya wakimbizi ya Zaatari bado ni makazi ya maelfu ya watu wanaosubiri suluhu ya kudumu. Wiki hii, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi, Barham Salih, ametembelea kambi hiyo na kukutana na familia ambazo zimeishi ukimbizini kwa zaidi ya muongo mmoja wengi wao wakiwa bado na matumaini ya kurejea nyumbani, lakini tu pale ambapo itakuwa salama.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Miaka kumi na nne baada ya wakimbizi wa kwanza wa Syria kuvuka mpaka kuingia Jordan kusaka usalama, kambi ya wakimbizi ya Zaatari bado ni makazi ya maelfu ya watu wanaosubiri suluhu ya kudumu. Wiki hii, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi, Barham Salih, ametembelea kambi hiyo na kukutana na familia ambazo zimeishi ukimbizini kwa zaidi ya muongo mmoja wengi wao wakiwa bado na matumaini ya kurejea nyumbani, lakini tu pale ambapo itakuwa salama. Flora Nducha amefuatilia ziara ya Salih na kutuandalia taarifa hii.
Hii leo jaridani kesho ikiwa ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu ugonjwa wa saratani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kumulika hatua ambazo ni uzinduzi wa Mpango wa Utekelezaji wa Kitaifa wa kutokomeza saratani ifikapo mwaka 2030.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani, WHO, leo limetoa ombi la dola bilioni moja ili kukabiliana na majanga ya afya mwaka 2026 katika dharura 36 zilizo mbaya zaidi duniani. Ombi hilo linalenga kusaidia huduma za afya zinazookoa maisha katika nchi zilizoathiriwa na migogoro na majanga, zikiwemo Gaza, Sudan, Haiti na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.Mashariki ya Kati, wakati muda ukiendelea kuyoyoma kwa maelfu ya wagonjwa mahututi huko Gaza, kufunguliwa tena kwa kivuko cha Rafah kunaleta mwanga wa matumaini. Kivuko hicho kilifunguliwa Jumatatu baada ya kufungwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, chini ya mpango wa amani unaoungwa mkono na Marekani, na kuruhusu uhamisho wa kwanza wa wagonjwa tangu mwaka 2025.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF leo liimesema linaongeza juhudi zake zamsaada wa msimu wa baridi nchini Ukraine huku watoto na familia wakikabiliwa na kukatika kwa umeme, kukosa vipasha joto na maji kufuatia mashambulizi yanayoendelea dhidi ya miundombinu ya nishati na baridi kali. Tangu Novemba, shirika hilo limesambaza jenereta 106 kote nchini kusaidia huduma za maji na mifumo ya kupasha joto, huku takribani jenereta 150 zaidi zikitarajiwa kuwasili katika wiki zijazo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "KUNVI"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Sudan inakabiliana na viwango vya hatari vya njaa, ambapo mamilioni ya watoto kama Noon wako katika hatari kubwa. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) liko shambani, likitoa msaada muhimu wa lishe, maji safi, na ulinzi. Hata hivyo, mahitaji ni makubwa, na msaada zaidi unahitajika haraka ili kuokoa maisha ya watoto hawa. Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi
Idadi ya watu waliofurushwa makwao nchini Msumbiji kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizoanza kunyesha katikati ya mwezi uliopita wa Desemba inakaribia 400,000 hali inayoongeza hatari kubwa katika fursa ya kuwapatia ulinzi na huduma zinazohitajika. Limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR kama anavyosimulia Flora Nducha.
Hii leo jaridani tunaangazia mafuriko nchini Msumbiji yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizoanza kunyesha katikati ya mwezi uliopita, hali ya kibinadamu kwa watoto Sudan na migogoro na uhakika wa chakula Sudan Kusini..Idadi ya watu waliofurushwa makwao nchini Msumbiji kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizoanza kunyesha katikati ya mwezi uliopita wa Desemba inakaribia 400,000 hali inayoongeza hatari kubwa katika fursa ya kuwapatia ulinzi na huduma zinazohitajika. Limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR.Makubaliano ya amani nchini Sudan Kusini yanakabiliwa na vitisho na hivyo wadau lazima husika wautekeleze licha ya changamoto zilizoko, amesema Luteni Jenerali Mohan Subramanian ambaye ni Kamanda Mkuu wa kikosi cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, UNMISS.Sudan inakabiliana na viwango vya hatari vya njaa, ambapo mamilioni ya watoto kama Noon wako katika hatari kubwa. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) liko shambani, likitoa msaada muhimu wa lishe, maji safi, na ulinzi. Hata hivyo, mahitaji ni makubwa, na msaada zaidi unahitajika haraka ili kuokoa maisha ya watoto hawa.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Makubaliano ya amani nchini Sudan Kusini yanakabiliwa na vitisho na hivyo wadau lazima husika wautekeleze licha ya changamoto zilizoko, amesema Luteni Jenerali Mohan Subramanian ambaye ni Kamanda Mkuu wa kikosi cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, UNMISS. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Jamhuri Africa ya Kati CAR kusikia mama mkimbizi anayesimulia aliyoyapitia, maisha ya uhamishoni na alivyojipatia nguvu iliyo kuu kuliko silaha yoyote ya vita. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na neno la wiki.Nchini Ethiopia, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO limeeleza kwamba Ethiopia imefanikiwa kutekeleza mizunguko minne ya uchanjaji watoto kwa njia ya matone dhidi ya ugonjwa wa polio. Mwaka jana 2025 Ethiopia kwa kutumia chanjo ya nOPV2 ilitekeleza uchanjaji huo kupitia mzunguko mmoja wa nchi nzima na mitatu kupitia maeneo mbalimbali ya nchi na kufanikiwa kuwafikia watoto milioni 26 katika mikoa yote.Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO), Beth Bechdol, ameeleza umuhimu wa kilimo wakati wa migogoro kulingana na mafanikio aliyoyashuhudia wakati wa ziara yake nchini Haiti na majirani zao Jamhuri ya Dominika.Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, (FAO) kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Asia (ADB) wametangaza kuwa wanatekeleza mpango wa dola milioni 100 ili kuimarisha uhakika wa chakula na lishe pamoja na kurejesha kipato kinachotokana na kilimo kwa zaidi ya watu milioni moja walio katika mazingira magumu kote nchini Afghanistan.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya "SIKU ZA JANGUO."Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Kutokana na ufinyu wa ufadhili unaolazimisha Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada ya kibinadamu, OCHA kupunguza idadi ya wanaopatiwa misaada nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, serikali ya DRC kwa kushirikiana na OCHA wamezindua ombi la dola za kimarekani bilioni 1.4 ili kuokoa hali. Flora Nducha na taarifa kwa kina.
Ziwa Viktoria barani Afrika, licha ya kuwa mhimili muhimu wa maisha kwa zaidi ya watu milioni 40 nchini Kenya, Uganda na Tanzania, bado linakabiliwa na vitisho vihusianavyo na biashara haramu za magendo, usafirishaji haramu binadamu na uvuvi haramu. Ili kupatia suluhu changamoto hiyo Ofisi ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na dawa za kulevya na utekelezaji wa sheria (INL) ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani na Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, (IOM), na walinzi wa pwani wa Kenya wamechukua hatua. Je ni hatua zipi? Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia….mafunzo ya usalama katika Ziwa Victoria, na harakati za Shirika la kiraia la kusongesha elimu kwa watoto wa kike, CAMFED za kuwawezesha wanafunzi wa kike nchini Tanzania.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukumbuka waathirika pamoja na manusura wa mauaji ya kimbari ya holokosti hususan yale yaliyofanywa na manazi wa kijerumani, hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa katika ukumbi wa Baraza Kuu kumefanyika kumbukizi ikileta pamoja manusura waliotoa shuhuda za waliyopitia wakikimbia maeneo kadhaa ikiwemo Austria baada ya kutwaliwa na wajerumani.Ziwa Viktoria barani Afrika, licha ya kuwa mhimili muhimu wa maisha kwa zaidi ya watu milioni 40 nchini Kenya, Uganda na Tanzania, bado linakabiliwa na vitisho vihusianavyo na biashara haramu za magendo, usafirishaji haramu binadamu na uvuvi haramu. Ili kupatia suluhu changamoto hiyo Ofisi ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na dawa za kulevya na utekelezaji wa sheria (INL) ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani na Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, (IOM), na walinzi wa pwani wa Kenya wamechukua hatua.Nchini Tanzania shirika la kiraia la kuendeleza elimu kwa watoto wa kike, CAMFED limeendelea kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs kwa kuwezesha wanafunzi wa kike kuimarika sio tu kimasomo darasani bali pia stadi za maisha na hatimaye wawajengee uwezo wenzao.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulika juhudi za vijana katika kuchagiza maisha wayatakayo kuanzia kujiondoa kwenye umasikini, ukosefu wa usawa hadi kwenye upatikanaji mdogo wa elimu bora na kazi zenye staha.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukumbuka waathirika pamoja na manusura wa mauaji ya kimbari ya holokosti hususan yale yaliyofanywa na manazi wa kijerumani, hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa katika ukumbi wa Baraza Kuu kumefanyika kumbukizi ikileta pamoja manusura waliotoa shuhuda za waliyopitia wakikimbia maeneo kadhaa ikiwemo Austria baada ya kutwaliwa na wajerumani.Huko Geneva, Uswisi ambako inaelezwa kuwa kurejesha mfumo wa elimu uliosambaratika huko Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, ni jambo la kuokoa maisha, na kuwarudisha watoto shuleni lazima kiwe kipaumbele cha haraka, amesema James Elder Msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF.Umoja wa Mataifa umezindua Mpango wa Mahitaji na Hatua za Kibinadamu wa dola milioni 852 kwa ajili ya Somalia, huku ukionya kuwa ukosefu mkubwa wa ufadhili utaacha mamilioni ya watu walio katika mazingira magumu bila msaada wa kuokoa maisha, huku hali ya kibinadamu kuendelea kuzorota.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana ya neno "TWINGA"Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia hatua za kuelekea nishati safi, wavuvi nchini Kenya wanaotumia nishati safi kuhifadhi samaki yao kwa ajili ya kuuza, na mradi wa FAO wa masuala ya biashara HASTEN unaosaidia wajasiriamali nchini Rwanda.Katika Siku hii ya Kimataifa ya Nishati Safi mwaka huu iliyobeba maadhui “Nishati safi kwa wote”, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema dunia inaelekea kubadilika lakini ameonya kuwa kasi ya mabadiliko hayo kuelekea nishati safi haitoshi na ni lazima iongezwe.Nchini Kenya, mkakati wa Umoja wa Mataifa wa kuhakikisha uzalishaji wa nishati mbadala unaongezeka mara tatu ifikapo mwaka 2030 unazidi kushika kasi kwani hivi sasa hata wavuvi na wamiliki wa migahawa wameanza kutumia majokofu yanayotumia nishati ya sola kuhifadhi samaki, na hivyo kuwa na sio tu uhakika wa samaki wakati wote bali pia wachuuzi kuepukana na kitoweo hicho kuoza umeme unapokatika. Assumpta Massoi anatupatia simulizi hiyo ya mafanikio kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Nishati endelevu, IRENA.Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na kilimo Duniani FAO, kupitia mradi wake wa masuala ya biashara HASTEN limeendesha warsha maalum ya kuanzisha biashara kwa vijana na wanawake, mjini Kigali Rwanda, lengo likiwa ni kuwapa miradi 10 mipya ya biashara itakayofanyika kwa msaada maalum kutoka kwa wakufunzi wa kitaifa na kimataifa juu ya mbinu za kupanua biashara, kuongeza ufanisi na kuchangia katika malengo ya maendeleo endelevu SDGs.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na kilimo Duniani FAO, kupitia mradi wake wa masuala ya biashara HASTEN limeendesha warsha maalum ya kuanzisha biashara kwa vijana na wanawake, mjini Kigali Rwanda, lengo likiwa ni kuwapa miradi 10 mipya ya biashara itakayofanyika kwa msaada maalum kutoka kwa wakufunzi wa kitaifa na kimataifa juu ya mbinu za kupanua biashara, kuongeza ufanisi na kuchangia katika malengo ya maendeleo endelevu SDGs. Sheilah Jepng'etich na taarifa zaidi.
Nchini Kenya, mkakati wa Umoja wa Mataifa wa kuhakikisha uzalishaji wa nishati mbadala unaongezeka mara tatu ifikapo mwaka 2030 unazidi kushika kasi kwani hivi sasa hata wavuvi na wamiliki wa migahawa wameanza kutumia majokofu yanayotumia nishati ya sola kuhifadhi samaki, na hivyo kuwa na sio tu uhakika wa samaki wakati wote bali pia wachuuzi kuepukana na kitoweo hicho kuoza umeme unapokatika. Assumpta Massoi anatupatia simulizi hiyo ya mafanikio kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Nishati endelevu, IRENA.
Katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, hii leo historia na dharura vilikutana chini ya paa moja. Ni miaka themanini tangu Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC lifanye kikao chake cha kwanza tarehe 23 Januari 1946 na linaadhimisha hatua hii muhimu wakati ambapo Umoja wa Mataifa unasema ni wa maamuzi kwa mustakabali wa ushirikiano wa kimataifa. Flora Nducha amefuatilia maadhimisho hayo na hii hapa taarifa yake
Huko Afrika Magharibi taifa la Niger linaongeza uwezo wa wananchi wake walio maeneo hatarishi na ya pembezoni kufikia huduma bora za afya kupitia kliniki tembezi. Kwa usaidizi kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO, Kanda ya Afrika, kliniki hizo tembezi zinaziba pengo la wale wanaoishi mbali na vituo vya afya, na wakati huo huo kuhakikisha umbali sio tena kikwazo cha mtu kupata huduma. Assumpta Massoi anafafanua zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia miaka themanini tangu Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC, AI katika elimu na juhudi za kuhakikisha wananchi wamepata huduma bora za afya kupitia kliniki tembezi nchini Niger.Katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, hii leo historia na dharura vilikutana chini ya paa moja. Ni miaka themanini tangu Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC lifanye kikao chake cha kwanza tarehe 23 Januari 1946 na linaadhimisha hatua hii muhimu wakati ambapo Umoja wa Mataifa unasema ni wa maamuzi kwa mustakabali wa ushirikiano wa kimataifa.Wakati dunia ikijiandaa kusherehekea Siku ya Elimu Duniani hapo kesho tarehe 24 Januari, 2026 embu sasa tuangazie mjadala unaozidi kushika kasi duniani kote kuhusu matumizi ya Akili Mnemba - AI katika elimu, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni – UNESCO linasisitiza kuwa si kila kilicho cha kisasa ni suluhisho la changamoto za elimu duniani.Huko Afrika Magharibi taifa la Niger linaongeza uwezo wa wananchi wake walio maeneo hatarishi na ya pembezoni kufikia huduma bora za afya kupitia kliniki tembezi. Kwa usaidizi kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO, Kanda ya Afrika, kliniki hizo tembezi zinaziba pengo la wale wanaoishi mbali na vituo vya afya, na wakati huo huo kuhakikisha umbali sio tena kikwazo cha mtu kupata huduma.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Wakati dunia ikijiandaa kusherehekea Siku ya Elimu Duniani hapo kesho tarehe 24 Januari, 2026 embu sasa tuangazie mjadala unaozidi kushika kasi duniani kote kuhusu matumizi ya Akili Mnemba - AI katika elimu, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni – UNESCO linasisitiza kuwa si kila kilicho cha kisasa ni suluhisho la changamoto za elimu duniani.Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumsikia kijana Baraka Ayubu ambaye amekuwa kielelezo cha jinsi teknolojia inavyoweza kuleta mageuzi katika mifumo ya ujifunzaji na ustawi wa wanafunzi.Umoja wa Mataifa umesisitiza kuwa uchunguzi wa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu unaohusishwa na vita kati ya Hamas na Israel huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel utaendelea, licha ya kuanzishwa kwa Bodi ya Amani ya Gaza ambayo imezinduliwa hii leo na Rais wa Marekani Donald Trump.Tuelekee nchini Kenya ambako zaidi ya watu milioni mbili wanakabiliwa na hali mbaya ya ukosefu wa uhakika wa kupata chakula kufuatia msimu wa mvua fupi za mwezi Oktoba hadi Desemba mwaka 2025 kuwa mkavu zaidi kuwahi kurekodiwa. Kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO, uhaba wa maji unalazimu familia kutegemea vyanzo visivyo salama, jambo linaloongeza hatari ya kipindupindu, homa ya matumbo, na magonjwa ya kuhara.Mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa lile la Afya Duniani, WHO, la kuhudumia watoto, UNICEF pamoja na la Makazi, UN-Habitat, kwa pamoja wamezindua mwongozo mpya unaozitaka serikali na viongozi wa miji kuweka kipaumbele kwa watoto katika upangaji wa miji ili kurejesha maeneo ya michezo yanayozidi kutoweka.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya "SIKU ZA MUAMBO" katika muktadha wa uchumi.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia mafuriko makubwa yaliyoikumba Msumbiji, ripoti inayomulika kupungua kwa muda mrefu kwa maji ya chini ya ardhi, na mradi unaolenga kuimarisha sekta ya kilimo katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan kwa ajili ya kuwasaidia wakulima.Kufuatia mafuriko makubwa yaliyoikumba Msumbiji kutokana na mvua zinazoendelea, serikali ya nchi hiyo ya kusinimashariki mwa Afrika imetangaza kuwa hadi kufikia sasa imerekodi vifo vya watu 120 na maelfu ya nyumba zimeharibiwa huku kiwango kikubwa cha fecha kikihitajika.Katika muktadha wa kupungua kwa muda mrefu kwa maji ya chini ya ardhi, matumizi kupita kiasi ya rasilimali za maji, uharibifu wa ardhi na udongo, ukataji miti, pamoja na uchafuzi wa mazingira, Chuo Kikuu cha Umoja wa Mataifa UNU leo kimetoa ripoti ikitangaza kuingia kwa “enzi ya kufilisika kwa maji duniani” na kutoa wito kwa viongozi wa dunia kuendana na uhalisia huu mpya kwa kuzingatia ushahidi wa kisayansi.Kwa muongo mmoja kuanzia mwaka wa 2016 hadi mwaka wa 2025, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) kwa ushirikiano na serikali ya Canada limechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha sekta ya kilimo katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan likilenga kuwasaidia wakulima na vyama vya ushirika kushinda changamoto za muda mrefu za uzalishaji, masoko na mnepo wa maisha.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Kwa muongo mmoja kuanzia mwaka wa 2016 hadi mwaka wa 2025, Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) kwa ushirikiano na serikali ya Canada limechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha sekta ya kilimo katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan likilenga kuwasaidia wakulima na vyama vya ushirika kushinda changamoto za muda mrefu za uzalishaji, masoko na mnepo wa maisha. Sheilah Jepngetich na taaarifa zaidi.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya ambako wasichana juhudi za kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) zimewezesha vijana wa kike kushiriki masomo ya Teknolojia ya Habari na Maewasiliano, TEHAMA na kujifunza stadi za teknolojia ili waweze kuedeleza biashara ya mtandaoni pamoja na matumizi mengine.Zaidi ya watu nusu milioni wameathiriwa na mafuriko makubwa katika mikoa ya kusini na kati ya Msumbiji, huku mvua kubwa ikiendelea kuvuruga usafiri, huduma za afya na njia za ugavi. Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA nchini humo, Paola Emerson, amewaambia waandishi wa habari huko Geneva, Uswisi kuwa majimbo ya Gaza, Sofala na Maputo ndiyo yaliyoathirika vibaya zaidi.Huko Mashariki ya Kati mapema leo Jumanne, vikosi vya Israel vimebomoa kwa tingatinga makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA, huko Yerusalemu Mashariki eneo linalokaliwa kimabavu na Israel. Mkuu wa UNRWA, Philippe Lazzarini, amelieleza tukio hilo kama “shambulio lisilo na kifani dhidi ya Umoja wa Mataifa,”.Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, leo imesema imeanza kutekeleza mpango wa kurejesha kwa hatua mamlaka ya dola katika mji wa Uvira, mashariki mwa nchi hiyo, kufuatia kuondoka kwa kundi lenye silaha la AFC/M23. Serikali inasema vikosi vya usalama, polisi na huduma nyingine za serikali vinarejea ili kulinda raia, kulinda mali na kuleta utulivu katika eneo hilo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mtaalam wetu ONNI SIGALA Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA, anafafanua maana ya neno “ KING'ANI”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
Utafiti wa kutumia nyuklia kuwafanya tasa mbu dume ili kudhibiti magonjwa ya dengue, virusi vya zika na chikungunya nchini Austria umeonesha matumaini ya kupunguza mbu mwitu jike aina ya Aedes albopictus anayeeneza vimelea vya magonjwa hayo. Utafiti ulifanyika mwaka jana kwa ushirikiano kati ya mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la nishati ya atomiki, IAEA na la chakula na kilimo, FAO. Assumpta Massoi anaelezea zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia ongezeko kubwa la idadi ya watu walionyongwa duniani mwaka 2025, hali ya kibinadamu nchini Sudan na utafiti wa kutumia nyuklia kuwafanya tasa mbu dume nchini Austria.Tathimini mpya iliyotolewa leo na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imeonya kuhusu ongezeko kubwa la idadi ya watu walionyongwa duniani mwaka 2025, ikisema kuwa idadi ndogo ya nchi ndiyo inachochea mwenendo huu unaotia wasiwasi mkubwa wa haki za binadamu.Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, baada ya ziara yake ya siku tano nchini Sudan, ametahadharisha kuhusu kuongezeka kwa hali mbaya zaidi ya ukikukwaji wa haki za binadamu na ongezeko la janga la kibinadamu nchini humo.Utafiti wa kutumia nyuklia kuwafanya tasa mbu dume ili kudhibiti magonjwa ya dengue, virusi vya zika na chikungunya nchini Austria umeonesha matumaini ya kupunguza mbu mwitu jike aina ya Aedes albopictus anayeeneza vimelea vya magonjwa hayo. Utafiti ulifanyika mwaka jana kwa ushirikiano kati ya mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la nishati ya atomiki, IAEA na la chakula na kilimo, FAO.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Tathimini mpya iliyotolewa leo na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imeonya kuhusu ongezeko kubwa la idadi ya watu walionyongwa duniani mwaka 2025, ikisema kuwa idadi ndogo ya nchi ndiyo inachochea mwenendo huu unaotia wasiwasi kubwa wa haki za binadamu. Flora Nducha ameisoma tathimini hiyo na hapa anafafanua zaidi
Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, baada ya ziara yake ya siku tano nchini Sudan, ametahadharisha kuhusu kuongezeka kwa hali mbaya zaidi ya ukikukwaji wa haki za binadamu na ongezeko la janga la kibinadamu nchini humo.Rashid Malekela na taarifa zaidi.