POPULARITY
Categories
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia siku ya chakula duniani ikienda sambamba na maadhimisho ya miaka 80 ya kuanzishwa shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, na utamsikia Mwakilishi wa FAO nchini Tanzania Bi. Nyabenyi Tito Tipo akieleza.Maadhimisho ya siku ya chakula duniani yamefanyika kimataifa leo huko Roma nchini Italia, yakienda sambamba na sikukuu ya miaka 80 tangu kuanzishwa kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na kilimo, FAO. Katika ujumbe wake alioutoa kwa njia ya video Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema, “Miaka themanini iliyopita, katika dunia iliyosambaratishwa kwa vita, nchi zilikutana kukabiliana na njaa. Miongo kadhaa tangu wakati huo, dunia imepiga hatua kubwa. Lakini bado majanga yanyoonesha kuwa hatuwezi kubweteka iwapo tunataka kuendeleza mafanikio tuliyopata. Tuna mbinu, ufahamu, rasilimali za kutokomeza njaa, na kupatia kila mtu chakula kizuri na chenye afya. Tunachohitaji ni umoja.Huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli, raia wamerejea kufuatia makubaliano ya sitisho la mapigano lakini wanahaha kujenga upya makazi yao huku wakiwa wamezingirwa na vifusi. Miongoni mwao Ayman Awadallah, amesema “hakuna maji, hakuna miundombinu ya majitaka, hakuna maisha hapa, hakuna chochote.”Na kufuatia kifo cha aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga, kilichotokea Jumatano Oktoba 15 nchini India, Umoja wa Mataifa kupitia Katibu Mkuu umetuma salamu za rambirambi na kusema hayati Odinga, alikuwa mtu muhimu katika maendeleo ya kidemokrasia nchini Kenya na pia mtetezi thabiti wa mageuzi ya kikatiba na utawala jumuishi.Na katika kujifunza Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "KIMWA"Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia kiwango cha gesi ya hewa ukaa, yaani carbon dioxide au CO₂, siku ya Kimataifa ya Wanawake wa Vijijini inayotupeleka nchini Kenya kumulika juhudi za wanawake za kumudu mahitaji ya familia zao, na uvuvi na uhalifu katika Ziwa Victoria.Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani, WMO, inasema kiwango cha gesi ya hewa ukaa, yaani carbon dioxide au CO₂, kimeongezeka kwa kiwango cha kuvunja rekodi mwaka 2024, na kufikia viwango vipya vya juu zaidi kuwahi kurekodiwa.Kuanzia Oktoba 15 mwaka 2008 dunia imekuwa ikiadhimisha siku ya Kimataifa ya Wanawake wa Vijijini kama fursa ya kutambua mchango mkubwa wa wanawake hawa katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi, na kimazingira.Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM kwa kushirikiana na Ofisi ya Marekani ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na Dawa za Kulevya na Utekelezaji wa Sheria (INL), na mamlaka kutoka Kenya, Tanzania na Uganda wanashirikiana kuimarisha uwezo na kukabiliana na uhalifu wa kimataifa unaotekelezwa katika ziwa victoria ambao ukiachwa unaweza kuleta athari kwa zaidi ya watu milioni 40 wanaotegemea ziwa hilo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM kwa kushirikiana na Ofisi ya Marekani ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na Dawa za Kulevya na Utekelezaji wa Sheria (INL), na mamlaka kutoka Kenya, Tanzania na Uganda wanashirikiana kuimarisha uwezo na kukabiliana na uhalifu wa kimataifa unaotekelezwa katika ziwa victori ambao ukiachwa unaweza kuleta athari kwa zaidi ya watu milioni 40 wanaotegemea ziwa hilo. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi
Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani, WMO, inasema kiwango cha gesi ya hewa ukaa, yaani carbon dioxide au CO₂, kimeongezeka kwa kiwango cha kuvunja rekodi mwaka 2024, na kufikia viwango vipya vya juu zaidi kuwahi kurekodiwa. Flora Nducha ameisoma ripoti hiyo na anatupa tathimini
Hii leo jaridani tnakuletea mada kwa kina inayoangazia siku ya Mwalimu Nyerere na tunakupeleka nchini Tanzania ambako kunaendelea juhudi za kuimarisha matumimizi ya lugha ya Kiswahili na utangamano katika Jumuiya ya Afrika Mashairki, manufaa ya kiuchumi na kijami na kuenzi mchango wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Umoja wa Mataifa leo umeonya kwamba Gaza itahitaji karibu dola bilioni 70 kwa ajili ya ujenzi upya baada ya miaka miwili ya mzozo, huku dola bilioni 20 zikitakiwa katika miaka mitatu ijayo. Makadirio haya yanatokana na, tathmini ya pamoja kati ya Umoja wa Mataifa, Muungano wa Ulaya, na Benki ya Dunia. Mwakilishi Maalum wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo UNDP kwa ajili ya programu za msaada kwa Wapalestina Jaco Cilliers,amesema “Viwango vya uharibifu sasa vimefikia karibu asilimia 84, na katika baadhi ya sehemu za Jiji la Gaza, ni hadi asilimia 92.”Umoja wa Mataifa umeongeza hatua zake za dharura huko Gaza kwa kutoa dola milioni 11 kutoka Mfuko wake wa Dharura (CERF) kukidhi mahitaji ya haraka kabla ya kuanza kwa msimu wa baridi. Mgao huu, uliozinduliwa na Mratibu wa Misaada ya Dharura Tom Fletcher, utaunga mkono utoaji wa chakula, maji, huduma za afya na makazi kwa raia walioathiriwa na mzozo wa miaka miwili. Hatua hii inafuatia mgao wa dola milioni 9 wiki iliyopita kwa ajili ya kuhakikisha upatikanaji wa mafuta kwa hospitali na huduma muhimu, na kufanya jumla ya msaada wa hivi karibuni kufikia dola milioni 20.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO limeonya kuhusu ongezeko la magonjwa ya neva duniani, ambayo sasa yanachangia zaidi ya vifo milioni 11 kila mwaka. Ripoti mpya ya WHO iliyotolewa leo mjini Geneva inaonesha kuwa zaidi ya watu bilioni 3 sawa na zaidi ya asilimia 40 ya watu duniani wanaishi na magonjwa yanayoathiri ubongo, ikiwemo kiharusi, ugonjwa wa kusahau, kifafa, na maumivu ya kichwa ya muda mrefu. Kwa mujibu wa ripoti nchi maskini ndizo zinazoathirika zaidi, zikiwa na upungufu mara 80 wa idadi ya wataalamu wa magonjwa ya neva ikilinganishwa na nchi tajiri. WHO inazitaka serikali kutoa kipaumbele kwa afya ya ubongo, kuongeza fedha na kuboresha upatikanaji wa huduma za tiba."Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "MKWECHE!Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia sitisho la mapigano Gaza na kurejeshwa kwa mateka wote, matumizi ya fecha za umma nchini Tanzania, na Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike ambayo uliadhimishwa tarehe 11 mwezi huu.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, leo amekaribisha kwa furaha kuachiliwa kwa mateka wote waliokuwa hai kutoka Gaza, huku mashirika ya misaada yakiripoti kwamba usambazaji wa misaada ya kuokoa maisha sasa unafanyika na misaada inaingia kwa kiwango kikubwa katika eneo hilo lililoharibiwa vibaya na vita.Licha ya mabilioni ya fedha kutumika katika sekta za elimu, afya na miundombinu, mataifa mengi bado yanashindwa kufikia maendeleo ya maana. Swali ni je, suluhisho ni kutumia fedha zaidi, au kuzitumia vyema? Benki ya dunia inatoa jibu kwa swali hilo tuungane na Leah Mushi akitujuza wamesema nini.Tarehe 11 mwezi Oktoba kila mwaka dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike, ikiwa ni siku muhimu ya kutambua mchango na uwezo wa mabinti katika jamii. Huko nchini Tanzania, kumefanyika hafla ya maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Plan International Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Ofisi za Umoja wa Mataifa Tanzania, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), na lile linalojishughulisha na Masuala ya Wanawake (UN Women)."Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Tarehe 11 mwezi Oktoba kila mwaka dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike, ikiwa ni siku muhimu ya kutambua mchango na uwezo wa mabinti katika jamii. Huko nchini Tanzania, kumefanyika hafla ya maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Plan International Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Ofisi za Umoja wa Mataifa Tanzania, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), na lile linalojishughulisha na Masuala ya Wanawake (UN Women). Sabrina Moshi na taarifa zaidi
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, leo amekaribisha kwa furaha kuachiliwa kwa mateka wote waliokuwa hai kutoka Gaza, huku mashirika ya misaada yakiripoti kwamba usambazaji wa misaada ya kuokoa maisha sasa unafanyika na misaada inaingia kwa kiwango kikubwa katika eneo hilo lililoharibiwa vibaya na vita: Flora Nducha amefuatilia na hii hapa taarifa yake
Mnamo mwaka wa 2021, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) liliongeza kwenye orodha ya turathi za dunia za tamaduni zisizoshikika au kugusika, Pooja Durga ambayo ni sherehe kubwa ya kihindu ya ushindi wa mungu wa kike aitwaye Durga dhidi ya jini Mahishasura, ikiwa ni ishara ya ushindi wa mema dhidi ya maovu. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imekaribisha uamuzi wa Kamati ya Tuzo ya Amani ya Nobel kumtangaza Maria Corina Machado kiongozi wa upinzani nchini Venezuela kuwa mshindi wa mwaka huu wa tuzo ya amani ya Nobel, kwa kutambua kazi yake ya kuendeleza matumaini ya demokrasia ya watu wa Venezuela. Flora Nducha na maelezo zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia mshindi wa mwaka huu wa tuzo ya amani ya Nobel, sauti za wanawake nchini Kenya ambazo zimeanza kusikika kwa uthabiti, zikililia haki, heshima, na usawa, na Puja Durga ambayo ni sherehe kubwa ya kihindu ya ushindi wa mungu wa kike.Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu (OHCHR) imekaribisha uamuzi wa Kamati ya Tuzo ya Amani ya Nobel kumtangaza Maria Corina Machado kiongozi wa upinzani nchini Venezuela kuwa mshindi wa mwaka huu wa tuzo ya amani ya Nobel, kwa kutambua kazi yake ya kuendeleza matumaini ya demokrasia ya watu wa Venezuela.Katika kila kona ya Kenya, sasa sauti za wanawake zimeanza kusikika kwa uthabiti, zikililia haki, heshima, na usawa. Kupitia msaada wa mashirika ya kimataifa kama shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo, UNDP na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na dawa za Kulevya na Uhalifu(UNODC), mabadiliko yanaanza kushika kasi.Mnamo mwaka wa 2021, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) liliongeza kwenye orodha ya turathi za dunia za tamaduni zisizoshikika au kugusika, Puja Durga ambayo ni sherehe kubwa ya kihindu ya ushindi wa mungu wa kike aitwaye Durga dhidi ya jini Mahishasura, ikiwa ni ishara ya ushindi wa mema dhidi ya maovu"Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Katika kila kona ya Kenya, sasa sauti za wanawake zimeanza kusikika kwa uthabiti, zikililia haki, heshima, na usawa. Kupitia msaada wa mashirika ya kimataifa kama shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo, UNDP na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na dawa za Kulevya na Uhalifu(UNODC), mabadiliko yanaanza kushika kasi. Katika jamii ambazo kwa muda mrefu mifumo ya jadi na taasisi za kisheria zimewabagua au kuwapuuza wanawake Taarifa ya SHEILAH Jepngetich inafafanua zaidi
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia siku ya posta Duniani na tunakupeleka nchini Tanzania ambako huko Sabrina Said wa idhaa hii amefuatilia harakati za huduma hiyo kwenye shirika la Posta Tanzania lililoanzishwa kwa sheria ya Bunge ya mwaka 1993 na kuanza kutoa huduma Januari 1994.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, leo amekaribisha tangazo la makubaliano ya kusitisha mapigano na kuachiliwa kwa mateka wote huko Gaza lililotolewa na Rais wa Marekani , akiyaita makubaliano hayo ni mafanikio yaliyohitajika sana baada ya miaka ya mzozo..Licha ya mzozo unaoendelea na changamoto za miundombinu nchini Sudan, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF leo limesema limefanikiwa kutoa chanjo kwa zaidi ya watoto 740,000 walio chini ya umri wa miaka mitano kati ya Januari na Juni 2025, na kutoa dozi zaidi ya milioni 16.Katika Siku ya Posta Duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amewashukuru wafanyakazi milioni 4.6 wa posta wanaounganisha jamii kote duniani.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "FUNDI HANA CHOMBO"Mwenyeji wako ni Assumpta, karibu!
Katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuna maonesho ya picha 32 zinazoonesha harakati za wanawake kwenye maeneo yenye mizozo kusongesha amani na usalama, kwa mujibu wa azimio namba 1325 lililopitishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa miaka 25 iliyopita. Maonesho ya picha hizi zilizopigwa na wanawake yamepatiwa jina Kupitia Lensi Yake na yameandaliwa na Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na wadau ili kudhihirisha ujasiri wa wanawake katikati ya mazingira hatarishi, wakihaha kuleta amani kwenye maeneo yao. Assumpta Massoi ametembelea onesho hilo.
Mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa na serikali ya Kenya wanatekeleza mradi unaowashirikisha wananchi wa Kauti ya Samburu katika kuhakika kuna upatikanaji wa chakula kwani eneo hilo linahali ya ukame ikiwa ni hatua mojawapo ya kutafsiri na kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa SDGs huko mashinani. Tuungane na Sheilah Jepngetich anayetuletea tarifa hii iliyoandaliwa na UNICEF Kenya.
Mwaka huu, Tunzo ya Umoja wa Mataifa ya “Muonesha njia” au kwa kiingereza Trailblazer imekwenda kwa Olukemi Ibikunle, afisa wa magereza kutoka Nigeria anayehudumu katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO. Tunzo hii inatambua mchango wake mkubwa katika kazi za haki na magereza kwenye operesheni za kulinda amani, pamoja na ujasiri wake wa kuvunja vizingiti vya kijinsia katika maeneo yanayoongozwa na wanaume. Flora Nducha na taarifa zaidi
Hii leo jaridani tunaangazia tunzo ya Umoja wa Mataifa ya “Muonesha njia” au kwa kiingereza Trailblazer, juhudi za wapiga picha wanawake kwenye maeneo yenye mizozo katika kusongesha amani na usalama, na wafugaji Samburu nchini Kenya.Mwaka huu, Tuzo ya Umoja wa Mataifa ya “Muonesha njia” au kwa kiingereza Trailblazer imekwenda kwa Olukemi Ibikunle, afisa wa magereza kutoka Nigeria anayehudumu katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO. Tunzo hii inatambua mchango wake mkubwa katika kazi za haki na magereza kwenye operesheni za kulinda amani, pamoja na ujasiri wake wa kuvunja vizingiti vya kijinsia katika maeneo yanayoongozwa na wanaume.Katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuna maonesho ya picha 32 zinazoonesha harakati za wanawake kwenye maeneo yenye mizozo kusongesha amani na usalama, kwa mujibu wa azimio namba 1325 lililopitishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa miaka 25 iliyopita. Maonesho ya picha hizi zilizopigwa na wanawake yamepatiwa jina Kupitia Lensi Yake na yameandaliwa na Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na wadau ili kudhihirisha ujasiri wa wanawake katikati ya mazingira hatarishi, wakihaha kuleta amani kwenye maeneo yao.Mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa na serikali ya Kenya wanatekeleza mradi unaowashirikisha wananchi wa Kauti ya Samburu katika kuhakika kuna upatikanaji wa chakula kwani eneo hilo linahali ya ukame ikiwa ni hatua mojawapo ya kutafsiri na kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa SDGs huko mashinani. Tuungane na Sheilah Jepngetich anayetuletea tarifa hii iliyoandaliwa na UNICEF Kenya.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika miaka miwili tangu kuzuka kwa vita kati ya Israel na wanamgambo wa kipalestina wa Hamas, vita ambavyo vimeacha maelfu ya watu wakiwa wamepoteza maisha na mamilioni wakikosa makazi, chakula na huduma za msingi.Leo ikiwa ni miaka miwili kamili tangu kufanyika mashambulizi ya Hamas Oktoba 7 mwaka 2023 Kusini mwa Israel na kuzusha vita vinavyoendelea sasa Gaza, mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa yametoa wito kutisishwa mapigano na mateka wote kuachiliwa. Mratibu mkuu wa misaada wa Umoja wa Mataifa Tom Fletcher amesema maumivu yanayosababishwa na mzozo huo hayaelezeki,”huku Kamishina Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA Philippe Lazzarini akielezea vita inayoendelea Gaza kama jinamizi kwa watu wa Gaza.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) limeelezea wasiwasi wake mkubwa kuhusu ongezeko kubwa la idadi ya watu waliolazimika kuyahama makazi yao kaskazini mwa Msumbiji. Hali hiyo inatokana na kuongezeka kwa machafuko ya mzozo unaoingia mwaka wa nane, hali iliyowalazimu karibu idadi ya watu 22,000 kukimbia makazi yao katika kipindi cha wiki moja tu mwishoni mwa mwezi Septemba. Tangu mzozo huo uanze mwaka 2017, zaidi ya watu milioni 1.3 wamelazimika kuyahama makazi yao.leo ni Siku ya Pamba Duniani na katika kuadhimisha siku hii mbunifu maarufu wa mitindo kutoka Niger, Alphadi, ameendesha darasa la kitaalamu kwa wanafunzi katika Chuo cha Mitindo cha Roma kusherehekea pamba na mitindo ya Kiafrika, kama sehemu ya matukio yaliyopangwa na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) kusherehekea siku hii ambayo huadhimishwa kila mwaka Oktoba 7. Alphadi amesema “Kwangu mimi, hii ni njia ya kuonesha yote ambayo Afrika inaweza kufanya. Na naamini, kwangu mimi, hii ni njia inayofaa ya kuadhimisha bara letu, na pia kuthamini kazi na kuonesha nguvu ya Afrika. Pamba ya Kiafrika ni bidhaa ubora, na inaweza kutumika na watu wa Sahel, pamoja na Wazungu wa Ulaya, Wamarekani ulimwengu wote.”Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, Mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "TITIMA"Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Leo ni Siku ya Makazi Duniani, na Umoja wa Mataifa unatoa wito wa kuchukua hatua za haraka kujenga miji jumuishi, imara na salama hasa kwa mamilioni ya watu waliolazimika kukimbia makazi yao. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres na Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi UNHCR Filippo Grandi wanasema miji sasa ndiyo inabeba mzigo mkubwa wa migogoro duniani lakini pia ndiyo kitovu cha suluhisho. Flora Nducha na taarifa zaidi
Hii leo jaridani tunaangazia siku ya makazi duniani, kazi za walimu katika kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu na afya ya uzazi hasa wakati wa kujifungua na kuepusha vifo kupiti uvujaji damu.Leo ni Siku ya Makazi Duniani, na Umoja wa Mataifa unatoa wito wa kuchukua hatua za haraka kujenga miji jumuishi, imara na salama hasa kwa mamilioni ya watu waliolazimika kukimbia makazi yao. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres na Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi UNHCR Filippo Grandi wanasema miji sasa ndiyo inabeba mzigo mkubwa wa migogoro duniani lakini pia ndiyo kitovu cha suluhisho.Uongozi wa kugawana majukumu na mashauriano ya kina na walimu ni mambo muhimu katika kuboresha ustawi wa waelimishaji na matokeo ya kujifunza ya wanafunzi, amesema Carlos Vargas, Mkuu wa Kitengo na Mkuu wa Sekretarieti ya Kikosi Kazi cha Kimataifa cha Walimu kwa Elimu 2030 katika UNESCO.Mashirika ya afya duniani yametoa miongozo mipya yenye lengo la kuokoa maisha ya maelfu ya wanawake wanaopoteza maisha kutokana na kutokwa damu nyingi baada ya kujifungua hali inayojulikana kama postpartum haemorrhage au PPH.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Umoja wa Mataifa umeonya kuwa hali ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza imefikia hatua ya kutisha, huku hospitali zikigeuzwa kuwa uwanja wa mapambano, kukizidiwa na wagonjwa na misaada kukwama. Maafisa wa Umoja wa Mataifa wameaambia waandishi wa habari leo mjini Geneva kuwa kuwa watoto wanakosa hewa ya oksijeni, wagonjwa wanakufa kwenye meza za upasuaji, na risasi zinavurumishwa moja kwa moja ndani ya hospitali. Flora Nducha amefuatilia na hii hapa taarifa yake
Hii leo jaridani tunaangazia huduma za afya katika hospital Gaza, mradi wa PLEAD nchini Kenya na mafanikio yako katika kesi za mashinani, na kifo cha Jane Goodall mwanamazingira, mtaalamu wa sokwe na nyani, halikadhalika mjumbe wa amani.Umoja wa Mataifa umeonya kuwa hali ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza imefikia hatua ya kutisha, huku hospitali zikigeuzwa kuwa uwanja wa mapambano, kukizidiwa na wagonjwa na misaada kukwama. Maafisa wa Umoja wa Mataifa wameaambia waandishi wa habari leo mjini Geneva kuwa kuwa watoto wanakosa hewa ya oksijeni, wagonjwa wanakufa kwenye meza za upasuaji, na risasi zinavurumishwa moja kwa moja ndani ya hospitali.Mashirika ya Umoja wa Mataifa, lile la Mpango wa Maendeleo, (UNDP) na la Kupambana na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) kwa ushirikiano na viongozi wa sheria nchini Kenya hadi mashinani wamezindua mpando wa PLEAD unaolenga kuboresha mfumo wa haki katika kaunti 12 nchini humo. Lengo lao ni kuimarisha haki jumuishi kwa kutoa majawabu mbadala badala ya kifungo, kupunguza msongamano wa magereza kwa asilimia 30, na kuondoa mkwamo wa maisha. Sheilah Jepngetich anaeleza zaidi kupitia video iliyochapishwa kwenye chaneli ya Youtube ya UNDP.Kufuatia kifo cha Jane Goodall mwanamazingira, mtaalamu wa sokwe na nyani, halikadhalika mjumbe wa amani kilichotokea Jumatano Oktoba 1 leo tunakurejesha mwaka 2002 alipoteuliwa kuwa mjumbe wa amani, halikadhalika salamu za rambirambi kufuatia kifo chake. Assumpta Massoi anakuletea taarifa zaidi kuhusu mwanamazingira huyo aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 91.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Mashirika ya Umoja wa Mataifa, lile la Mpango wa Maendeleo, (UNDP) na la Kupambana na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) kwa ushirikiano na viongozi wa sheria nchini Kenya hadi mashinani wamezindua mpando wa PLEAD unaolenga kuboresha mfumo wa haki katika kaunti 12 nchini humo. Lengo lao ni kuimarisha haki jumuishi kwa kutoa majawabu mbadala badala ya kifungo, kupunguza msongamano wa magereza kwa asilimia 30, na kuondoa mkwamo wa maisha. Sheilah Jepngetich anaeleza zaidi kupitia video iliyochapishwa kwenye chaneli ya Youtube ya UNDP
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika ujumbe wa Omon Ukpoma-Olaiya, Kiongozi wa Uwekezaji wa UNCDF kwa Kanda ya Afrika Mashariki, Kusini na Nchi za Kiarabu. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi neno la wiki.Haiti, hali ya kibinadamu imefika kiwango cha hatari, amesema Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk. Akihutubia Baraza la Haki za Binadamu mjini Geneva, Türk amesema Haiti imefika kiwango cha kulipuka kutokana na ukatili na ukiukwaji Mkubwa wa haki za binadamu. Amesisitiza kuwa “Tunaweza na lazima kubadili hali hii kwa ajili ya watu wa Haiti,” akiongeza kuwa “bila hatua za haraka hali mbaya zaidi huenda ikaja kwa Haiti na eneo zima.”Tukielekea Mashariki ya Kati huko Gaza, janga la kibinadamiu linaongezeka ambapo mashambulizi yanayoendelea yameathiri vibaya upatikanaji wa chakula na maji. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA, limeripoti kuwa usambazaji wa chakula kilichopikwa kaskazini mwa Gaza umepungua kwa asilimia 70, huku vituo vinne pekee ndivyo vinavyofanya kazi. Takriban watu milioni moja wanapata maji chini ya lita sita kwa siku, kiwango kilicho chini ya hali ya dharura.Nchini Sudan Kamishina Mkuu wa Haki za Binadamu Volker Türk ameonya kuhusu hali katika mji wa El Fasher, Darfur Kaskazin , akisema mji huo “uko kwenye ukingo wa janga kubwa zaidi ikiwa hatua za haraka hazitachukuliwa kulegeza mzingiro wa kijeshi na kuwalinda raia,” huku Kikosi cha Usaidizi wa Haraka (RSF) kikiongeza juhudi za kutwaa mji huo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "USHINZI NA USHENZI"Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF linatoa wito kwa viongozi wa Afrika kufanya uwekezaji wa kifedha wa busara utakaowezesha watoto kupata ujuzi wa msingi wa kujifunza na mustakabali wenye nguvu kwa bara la Afrika. Balozi Mwema wa UNICEF, Angelique Kidjo, katika kuunga mkono wito huo anasimulia safari yake kutoka kujifunza alfabeti hadi kuimba kwa ulimwengu mzima. Anold Kayanda anaeleza zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya Kimataifa ya Wazee duniani na mchango wao kwa jamii, hali ya afya katika ukanda wa Gaza, na simulizi ya Balozi Mwema wa UNICEF, Angelique Kidjo.Hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambako kumefanyika tukio maalum la kuadhimisha siku ya wazee duniani leo Oktoba Mosi, kaulimbiu ikiwa Wazee Wanaendesha Hatua za Kijamii na Kimaisha: Matamanio Yetu, Ustawi Wetu na Haki Zetu. Anayekupeleka ukumbini ni Flora Nducha.Huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel wanawake katika eneo la Deir al- Balah wanalazimika kutumia majiko ambayo wanachochea taka za plastiki na makaratasi ili kupota moto wa kuweza kupikia chakula. Hali hiyo imesababisha kuenea kwa magonjwa ya kupumua kama vile numonia na pumu.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF linatoa wito kwa viongozi wa Afrika kufanya uwekezaji wa kifedha wa busara utakaowezesha watoto kupata ujuzi wa msingi wa kujifunza na mustakabali wenye nguvu kwa bara la Afrika. Balozi Mwema wa UNICEF, Angelique Kidjo, katika kuunga mkono wito huo anasimulia safari yake kutoka kujifunza alfabeti hadi kuimba kwa ulimwengu mzima.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Tuanzie hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambako kumefanyika tukio maalum la kuadhimisha siku ya wazee duniani leo Oktoba Mosi, kaulimbiu ikiwa Wazee Wanaendesha Hatua za Kijamii na Kimaisha: Matamanio Yetu, Ustawi Wetu na Haki Zetu. Anayekupeleka ukumbini ni Flora Nducha.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika ujumbe wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, Veronica Nduva ambaye alizungumza na Flora Nducha kandoni mwa UNGA80. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo.Ikiwa ni zaidi ya miaka minane tangu zaidi ya wakimbizi 750,000 waislamu wa kabila la warohingya wakimbie Myanmar kuelekea kwenye kambi kubwa nchini Bangladesh, mgogoro huo bado haujapatiwa suluhisho na leo hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa viongozi wamekutana kusaka suluhu ya kudumu kwa warohingya na makabila mengine madogo nchini Myanmar. Katibu Mkuu Antonio Guterres kupitia Afisa Mtawala Mkuu wa UN Courtenay Rattray amesema, “mgogoro huu, ambao umezidi kuongezeka tangu mapinduzi ya kijeshi Myanmar ya mwaka 2021, unasigina haki za binadamu, utu na usalama wa mamilioni ya watu na unatishia uthabiti wa kikanda. Haitoshi tu kutathmini hali ilivyo. Tunapaswa pia kuendeleza mshikamano na kubuni suluhisho.”Amani nchini DRC imesalia bado ahadi, ni kauli ya Bintou Keita, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC aliyotoa wakati akihutubia Baraza la Usalama lililokutana leo kujadili hali Mashariki mwa DRC. Anasema hali inazidi kuwa tete. “Ghasia zinaendelea kushamiri jimboni Kivu Kaskazini hususan eneo la Rutshuru tangu waasi wa M23 watwae eneo hilo. Kuanzia mwezi Juni na kuendelea ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, MONUSCO umepokea maombi lukuki ya watu wakitaka ulinzi kwenye maeneo yanayodhibitiwa na M23.”.Na mashirika ya Umoja wa Mataifa leo yamesisitiza wito wa kupatikana kwa sitisho la mapigano huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel, ili kupunguza machungu wakati huu ambapo Mpango wa Marekani wa Vipengele 20 unaibua matumaini ya kukomeshwa kwa mapigano. Ricardo Pires, msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto, UNICEF amesema, “ni muhimu tupate sitisho la mapigano na misaada iweze sio tu kuingia na kuepusha baa la njaa, bali pia kuelekezwa maeneo ya kusini. Lakini vile vile kuhakikisha watoto na familia zao wanapata malazi bora wakati huu majira ya baridi kali yanakaribia. La sivyo italeta zahma ya afya kwa watoto na familia zao.”.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Kama unavyofahamu Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 umekunja jamvi rasmi jana Jumatatu. Na tumepata fursa ya kuzungumza na washiriki mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, Veronica Nduva ambaye alizungumza na Flora Nducha kandoni mwa mjadala huo kuangazia mchango wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kutekeleza ajenda ya Umoja wa Mataifa ikiwemo masuala ya Amani na usalama, maendeleo na ushirikiano wa kikanda. Ungana nao.
Leo Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 hotuba za viongozi ukifunga pazia, Afrika imeweka bayana kauli moja ya mshikamano, kwamba lazima iwe na viti na sauti kwenye Baraza la Usalama na kuahidi kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha dhamira hiyo inatimia. Mchakato ulishaanza na unaendelea kuelekea lengo hilo kama ambavyo Balozi Ekitela Lokaale mwakilishi wa kudumu wa Kenya kwenye Umoja wa Mataifa alivyomfahamisha
Hii leo jaridani tunaangazia leo Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 tukimulika hotuba za viongozi na mikutano mingine ya pepmbezoni kuhusu malengo ya maendeleo enedelevu, SDGs.Viongozi wa mataifa ya nchi wanachama 16 waliopanda kwenye mimbari ya ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hii leo Jumatatu ya tarehe 29 Septemba 2025 ambayo ndio ukomo wa Mjadala Mkuu wa mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, (UNGA80) wamepaza sauti zao kuhusu masuala mbalimbali yanayokumba dunia hivi sasa ikiwemo vita Gaza, na hali ya kiuchumi Afrika.Leo Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 hotuba za viongozi ukifunga pazia, Afrika imeweka bayana kauli moja ya mshikamano, kwamba lazima iwe na viti na sauti kwenye Baraza la Usalama na kuahidi kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha dhamira hiyo inatimia. Mchakato ulishaanza na unaendelea kuelekea lengo hilo kama ambavyo Balozi Ekitela Lokaale mwakilishi wa kudumu wa Kenya kwenye Umoja wa Mataifa alivyomfahamisha.Tukisalia hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kandoni mwa Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA80, inafanyika mikutano mingine ya pembezoni kujadili masula mengine ya kusongesha maendeleo ya ulimwengu. Wiki iliyopita tulizungumza na Dkt. Ntuli Kapologwe Mkurugenzi Mkuu wa Jumuiya ya Afya ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika, ECSA wakati alipokuwa akisubiri kushiriki mkutano wa nchi wanachama wa jumuiya hiyo kujadili jinsi ya kusongesha diplomasia ya kisayansi ili kuhakikisha bara la Afrika haliachwi nyuma kwenye kukabiliana na changamoto za kiafya.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kandoni mwa Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA80, inafanyika mikutano mingine ya pembezoni kujadili masuala mengine ya kusongesha maendeleo ya ulimwengu. Wiki iliyopita tulizungumza na Dkt. Ntuli Kapologwe Mkurugenzi Mkuu wa Jumuiya ya Afya ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika, ECSA wakati alipokuwa akisubiri kushiriki mkutano wa nchi wanachama wa jumuiya hiyo kujadili jinsi ya kusongesha diplomasia ya kisayansi ili kuhakikisha bara la Afrika haliachwi nyuma kwenye kukabiliana na changamoto za kiafya. Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza tena na Dkt. Kapologwe mara tu baada ya mkutano huo
Viongozi wa mataifa ya nchi wanachama 16 waliopanda kwenye mimbari ya ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hii leo Jumatatu ya tarehe 29 Septemba 2025 ambayo ndio ukomo wa Mjadala Mkuu wa mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, (UNGA80) wamepaza sauti zao kuhusu masuala mbalimbali yanayokumba dunia hivi sasa ikiwemo vita Gaza, na hali ya kiuchumi Afrika.
Katika Mkutano wa Vijana wa Umoja wa Mataifa unaofanyika kandoni mwa mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 unaoendelea hapa New York, viongozi vijana kutoka duniani kote wanataka uwakilishi mkubwa katika maamuzi ya kimataifa.Miongoni mwao ni daktari wa tiba na mwanaharakati wa kijamii wa vijana wa Uingereza na Ghana, Dkt. Khadija Owusu ambaye amezungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili.Owusu, ambaye pia ni mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Akaya inayowakilisha wasichana wa zama hizi, anasema vijana hawapaswi kuzungumziwa tu, bali wajumuishwe moja kwa moja katika kuandaa Suluhu za changamoto zinazoihusu dunia wakiwemo na wao "Mara nyingi tunazungumza kuwa tunataka ushiriki zaidi wa vijana wakati umefika wa kuacha kuzungumza tu kuhusu kuhitaji vijana wengi, bali tuwe na vijana wengi."Niko hapa kuwakilisha maelfu ya wasichanaAnasema ushiriki wake katika mkutano huu wa ngazi ya juu wa vijana si wa kibinafsi tu, bali unaakisi sauti za wasichana na vijana wengi wanaosaidiwa na taasisi yake ya Akaya."Niko hapa kuwakilisha si mimi peke yangu, si Uingereza tu, na si Ghana tu, bali Taasisi ya Akaya, na wasichana na vijana wengi tunaowahudumia nchini kote."Owusu anaamini vijana wa Kiafrika, hususan wasichana, wanapaswa kupata nafasi kubwa zaidi katika jmaukwaa ya kimataifa kama Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa ili kupaza sauti zao."Bado tunahitaji kuona vijana zaidi kama sisi kwenye vyumba vya mikutano, Waafrika zaidi, vijana zaidi wa Kiafrika na wasichana wa Kiafrika kwenye vyumba vya mijadala, wakishiriki majadiliano kwa sababu tunaleta mabadiliko halisi."Owusu anasema ujumbe wake kwa vijana barani Afrika ni kubeba vipaji vyao, wajiamini, na kuendeleza ndoto zao kwani kila kitu kinawezekana.
Makubaliano yaliyosimamiwa na mashirika ya kimataifa, likiwemo UNITAID ambalo ni shirika tanzu la shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO, halikadhalika Mpango wa afya wa Clinton (CHAI), Wits RHI na Maabara ya Dkt. Reddy, yanalenga kuhakikisha upatikanaji wa Lenacapavir kwa gharama nafuu.Dawa hii, inayodungwa mara mbili pekee kwa mwaka, imeonesha ufanisi mkubwa katika kuzuia maambukizi mapya ya VVU, jambo muhimu hasa kwa wale wanaopata changamoto kutumia dawa za kila siku.Video ya UNITAID inaonesha maabara yenye teknolojia ya hali ya juu, ambamo wanasayansi wanaandaa dawa hiyo inayotarajiwa kuleta mabadiliko makubwa kwa mamilioni ya watu walio katika hatari ya kuambukizwa virusi hivyo.Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa UNITAID, Tenu Avafia, anasema hatua hii ni ushindi mkubwa kwa jamii zinazohitaji kinga ya muda mrefu dhidi ya VVU."Tumeitikia wito kutoka kwa jamii na nchi tunazohudumia kwa kuhakikisha dawa hii inapatikana kwa gharama nafuu. Tunatarajia usambazaji wa toleo la bei nafuu la dawa hii kuanza kufikia mwaka 2027, chini ya miaka miwili tu tangu idhini kutolewa katika nchi za kipato cha juu — kasi ambayo haijawahi kushuhudiwa."Akizungumza kuhusu hatua hii muhimu, Carmen Pérez Casas, Mkuu wa Mikakati Mwandamizi wa UNITAID, anasema:"Kwa kushirikiana na watengenezaji wa dawa mbadala, tumefanikisha bei nafuu mapema zaidi. Lakini bado tunahitaji kusaidia nchi na jamii kwa kuongeza upatikanaji."UNITAID inasema kwa msaada wa mashirika kama PEPFAR ambao ni mfuko wa Rais wa MArekani wa usaidizi wa dharura dhidi ya UKIMWI, pamoja na mfuko wa kimataifa na wakfu wa Gates, hatua hii inaleta matumaini ya kupunguza maambukizi mapya ya VVU duniani.
Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukiwa umeingia katika siku yake ya nne hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani leo Ijumaa, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amekuwa wa kwanza kuzungumza akitumia muda wake mwingi kushambulia wanamgambowa kipalestina, Hamas na kutetea kila uamuzi wa Israel. Anold Kayanda ameifuatilia hotuba hiyo kwa kina. Ilikuwa majira ya saa tatu na dakika chache hivi asubuhi ya leo saa za New York nchini Marekani ambapo Waziri Mkuu wa Isreal Benjamin Netanyahu amepewa fursa ya kuhutubia na ndipo ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukakosa utulivu. Wajumbe kwa makundi walinyanyuka katika viti vyao na kuondoka huku wakiwaacha maafisa wa Israel wakimpigia makofi kiongozi wao na pia nchi zinazoiunga mkono Israel zikasalia katika viti vyao ikiwemo Marekani.Baadhi ya wajumbe watoka njeKatika eneo la walipotakiwa kukaa wawakilishi wa Palestina kulikuwa wazi, huku katika eneo la Iran ikibakia picha iliyokusanya sura za baadhi ya watu wao waliouawa na mashambulizi ya Israel. Bwana Netanyahu kwa mara nyingine tena ameingia na ubao wenye picha ya ramani ya eneo la Mashariki ya Kati akiutumia kuishambulia Iran na kwa kutumia kalamu akiweka alama ya vema kuonesha namna ambavyo Israel imefanikiwa kupambana na ngome za Irani katika ukanda huo. Katika suti yake, kifuani upande wa kulia, Bwana Netanyahu pia ameweka kibandiko chenye QR Code na akawaambia watu kuwa Israel bado inakumbuka tukio walilofanyiwa na Hamas mwezi Oktoba mwaka juzi na kwamba ikiwa watu wamesahau hilo basi waelekeze simu zao kwenye QR Code hiyo kwenye nguo yake ili iwaoneshe madhara yaliyofanywa na Hamas.Majina ya mateka yakasomwaWaziri Mkuu huyo wa Israel ameyasoma majina ya mateka ambao bado wako mikononi mwa Hamas katika eneo la Ukanda wa Gaza na pia akaueleza mkutano kuwa amesambaza vipaza sauti au spika katika eneo lote la Gaza ili anapoongea leo, azungumze moja kwa moja na mateka huko walikofichwa. Na hapo akabadilisha lugha na kuongea kwa kihebrania akiwaahidi kuwa atawakomboa. Vilevile amedokeza kuwa kwa namna ya kiintelijensia Israel imefanya simu leo ziweze kusambaza hotuba katika ukanda wa Gaza na hivyo akautumia muda huo kupeleka ujumbe mkali kwa Hamas kuwa ataendelea kuwadhibiti. Bwana Netanyahu pia ameingia ukumbini na vibao viwili vyenye maswali na majibu ya kuchagua japokuwa jibu sahihi kwa mujibu wake na waliojibu kuwa ni All the Above, yaani majibu yote ni sahihi. Maswali yote yalikuwa yakiwatuhumu Iran, Hamas, Al Caeda, Hezbollah na Houthi kuwa pia wanaitakia kifo Marekani na wameua watu wengi Ulaya. Huenda hotuba hii ya Netanyahu ikaingia katika orodha ya hotuba tano ndefu zaidi baada ya ile ya Rais wa Marekani Donald Trump wa Marekani, Ya Mahmoud Abbass wa Palestina na Félix-Antoine Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambao wote hao walitumia zaidi ya dakika arobaini licha ya muda wa hotuba uliopangwa kuwa angalau dakika 15.
Hii leo ni hotuba ya Israeli kwenye mjadala mkuu wa baraza kuu, nini kilitokea? Kijana daktari mwanaharakati kutoka Ghana aishiye Uingereza akiwa UNGA80 na matumaini mapya ya kinga dhidi ya maambukizi ya VVU.Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukiwa umeingia katika siku yake ya nne hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani leo Ijumaa, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amekuwa wa kwanza kuzungumza akitumia muda wake mwingi kushambulia wanamgambowa kipalestina, Hamas na kutetea kila uamuzi wa Israel. Anold Kayanda ameifuatilia hotuba hiyo kwa kina. Karibu Anold utupe japo kwa muhtasari.Tukisalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa, moja ya mikutano ya ngazi ya juu iliyofanyika kando ya mjadala mkuu wa Baraza Kuu, ni ule wa kuadhimisha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa program ya Umoja wa Mataifa kuhusu vijana, mkutano ukileta vijana kutoka kona mbali mbali za dunia. Miongoni mwao ni daktari wa tiba na mwanaharakati wa kijamii wa vijana kutoka Uingereza mwenye asili ya Ghana, Dkt. Khadija Owusu. Amezungumza na Flora Nducha anayetujulisha zaidi katika taarifa hiiKatika hatua kubwa ya kihistoria kwenye mapambano dhidi ya Virusi Vya UKIMWI (VVU) dawa mpya ya kudungwa inayoitwa Lenacapavir inatarajiwa kupatikana kwa gharama nafuu katika nchi 120 zenye kipato cha chini na kati kuanzia mwaka 2027. Dawa hiyo itauzwa kwa kiasi cha dola 40 pekee ikiwa ni gharama ya vidonge vya kila siku vya kujikinga na VVU ambavyo mhusika atatumia kwa mwaka mzima. Sabrina Saidi ana taarifa zaidi.
Waziri wa Mambo ya Nje Penny Wong amesema Australia ina simama kidete juu ya tamaduni nyingi, baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kukosoa uhamiaji katika hotuba yake kwa kikao cha mkutano wa Umoja wa Mataifa.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina maalum inayomulika mkutano wa ngazi ya juu kuhusu magonjwa yasiyo ya kuambukiza NDCs unaoendelea kandoni mwa UNGA80, na tumezungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa WHO Kanda ya Afrika Dkt. Mohamed Yakub Janabi.Wakati viongozi wa nchi na serikali wanahutubia wakiwa ndani ya jengo la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, Kiongozi wa Palestina, Mahmoud Abbas ujumbe wake kwa UNGA80 ameutoa kwa njia ya video iliyorekodiwa kutokana na kutopata kibali cha kuingia Marekani. Katika hotuba hiyo amesisitiza kuwa, Ukanda wa Gaza utaendelea kuwa sehemu ya Taifa la Palestina na tuko tayari kuwajibika kikamilifu kwenye uongozi na usalama wa eneo hilo. Hamas hawatokuwa na jukumu lolote kwennye utawala.”.Mapema kabla ya Palestina, Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud, alihutubia wajumbe akitaka nchi wanachama kujitolea upya kwa misingi ya usawa, mshikamano na ushirikiano wa kimataifa. Amesema hilo ni muhimu kwa kuwa “wakati ambapo hapo awali tulijitahidi kujiuliza ‘Nini ni sahihi' chini ya sheria ya kimataifa, leo tunashuhudia kwa wazi kuibuka kwa matumizi ya NGUVU ya kitaifa katika kusuluhisha migogoro. Hii ni njia ya giza na ya hatari sana inayotishia utawala wa sheria wa kimataifa tuliokubaliana kwa pamoja kama nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa.”Kando ya hotuba za viongozi, kunafanyika maadhimisho ya miaka 30 tangu kupitishwa kwa Programu ya Dunia kwa ajili ya vijana. Je vijana kutoka Malawi wana ujumbe gani? Mwakilishi wao kwenye mkutano huu Rachel Mganga Wanangwa anasema, “Ujumbe kutoka vijana wa Malawi ni wekezeni kwetu, tusaidieni, shirikianeni nasi, na wanashiriki kwenye meza za mazungumzo ili kuhakikisha kuwa sauti zao zinawakilishiwa.”.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia hotuba ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy katika siku ya pili ya mjadala mkuu wa UNG80, na ujumbe wa washiriki wa mkutano huu kutoka Nigeria na Tanzania.Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy amesema taasisi za kimataifa zimekuwa dhaifu wanachoweza kufanya ni kutoa matamko makali pekee na kwamba kwa sasa duniani sheria pekee za Kimataifa haziwezi kusaidia nchi kujilinda bila ya kuwa na silaha pamoja na marafiki wenye nguvu wa kukusaidia.Katika siku ya pili ya Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA, kando ya hotuba, viongozi wa nchi 9 wanachama wa Jumuiya ya Afya ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika, ECSA watakuwa na mkutano wa kusongesha diplomasia ya kisayansi ili kuhakikisha bara la Afrika haliachwi nyuma kwenye kukabiliana na changamoto za kiafya, baada ya kujifunza kutokana na COVID-19 au UVIKO19.Tukisalia hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Mjadala Mkuu wa UNGA80 mbali ya kusikiza hotuba za viongozi unaambatana na mamia ya matukio na mikutano ya kando. Leo, sauti kutoka pande zote za dunia zinaitaka haki ya kijamii katika moja ya mikutano ya kando na miongoni mwa sauti hizo ni ya mwanaharakati na mhamasishaji wa masuaa ya wasichana kutoka Nigeria ambaye anasema wasichana vigori hawapaswi kusahaulika.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Katika siku ya pili ya Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA, kando ya hotuba, viongozi wa nchi 9 wanachama wa Jumuiya ya Afya ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika, ECSA watakuwa na mkutano wa kusongesha diplomasia ya kisayansi ili kuhakikisha bara la Afrika haliachwi nyuma kwenye kukabiliana na changamoto za kiafya, baada ya kujifunza kutokana na COVID-19 au UVIKO19. Mkurugenzi Mkuu wa ECSA Dkt. Ntuli Kapologwe akihojiwa na Assumpta Massoi wa Idhaa hii ametaja wanachotarajia kwenye mkutano huo..
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina maalum na mada yetu inamulika maoni kuhusu miaka 80 ya Umoja wa Mataifa. Pia tunakuetea muhtasari wa habari unaofuatilia ujumbe wa viongozi katika mjadala mkuu wa UNG80.viongozi wa dunia wamekutana leo hapa kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ikiwa ni siku ya kwanza ya Mjadala Mkuu wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ukiambatana na vikao vya kando vya ngazi ya juu. Katika hotuba yake ya UNGA 80 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa dunia kufanya maamuzi “ni aina gani ya dunia tunataka kujenga pamoja.”Kuanza kwa UNGA maana yake idadi kubwa ya wageni, Msaidizi wa Katibu Mkuu wa UN anayeshughulikia habari na teknolojia, Bernardo Mariano, amesema wamejipanga kutoa huduma ya internet (Wi Fi) kwa watu 40,000 huku wakihakikisha hotuba za viongozi zinapeperushwa bila hitilafu za kiufundi wala kuvurugwa na mashambulizi ya mtandaoni.Na Hapo kesho Jumatano viongozi wa jumuiya ya Afya ya nchi za Afrika Mashariki, Kati na Kusini, ESCA watakutana kumulika Diplomasia ya kisayansi na afya ili kusongesha Mkataba wa Zama Zijazo. Mkurugenzi Mkuu wa ECSA Dkt. Ntuli Kapologwe ameeleza kulikoni?.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Waziri Mkuu amesema ombi la utaifa wa Palestina ni fursa ya amani, katika hotuba yake kuhusu soluhu ya nchi mbili, alipo hudhuria kikao cha Umoja wa Mataifa hii leo Jumanne 23 Septemba 2025.
Kando ya maadhimisho ya siku ya miaka 80 ya Umoja wa Mataifa, hapa makao makuu kumefanyika mashauriano ya faragha yenye lengo la kusaka majawabu ya madhara ya mabadiliko ya tabianchi. Mashauriano ya leo ni sehemu ya mashauriano 10 yatakayofanyika kuelekea mkutano wa tabianchi wa wakuu wa nchi na serikali utakaofanyika keshokutwa Jumatano hapa Umoja wa Mataifa. Assumpta Massoi amezungumza na mmoja wa watoa mada kwenye mashauriano hayo ambayo matokeo yake yatawasilishwa kwenye mkutano wa viongozi. Kwako Assumpta.(Taarifa ya Assumpta Massoi)Nats..Katika uwanda wa wageni nje ya jengo la mikutano nakutana na Emily Mohohlo, Mratibu wa shirika la kiraia la Slum Dwellers International kutoka Afrika Kusini linalojikita katika kuhakikisha maeneo ya mabanda mijini yanakuwa jumuishi, yana mnepo na maisha yao yanaboreshwa.Nikamuuliza umuhimu wa mkutano na kusema..(Sauti ya Emily Mohohlo)“Mkutano huu ni muhimu kwangu kwa sababu katika maisha halisia kuna joto kupindukia na linasababisha vifo kwa wanawake na pia kutoweka kwa mbinu zao za kujipatia kipato. Hivyo kwangu naona kama tunaweza kujumuika pamoja katika ngazi ya kijamii na kupata takwimu sahihi na kisha watafiti watusaidie. Tunahitaji wabia kwani tayari tumeshachukua hatua.”Kwa hiyo ujumbe wake kwa washiriki wa mkutano?(Sauti ya Emily Mohohlo)“Njooni mshirikiane nasi, kwa sababu tuna takwimu kutoka mashinani lakini hatuna uwezo wa kifedha. Tukipata fedha kutoka kwa watafiti itakuwa vema. Tunajua wana takwimu lakini si kutoka mashinani.”Nilipomuuliza umuhimu wa Umoja wa Mataifa wakati huu unatimiza miaka 80 akafunguka..(Sauti ya Emily Mohohlo)“Ndio sasa una miaka 80, lakini bado hatuoni vya kutosha mafanikio yake mashinani. Huwezi kusaidia mtu mmoja mmoja. Waje kwenye vikundi na itakuwa vema kwa sababu kuna idadi kubwa ya watu.”Akatamatisha na ujumbe kwa Umoja wa Mataifa.(Sauti ya Emily Mohohlo)“Tumefika hapa, tafadhali tusikilizeni. Hakuna chetu bila kutushirikisha. Asante,”TAGS: Tabianchi/Afrika/Slum Dweller International/UNGA80
Umoja wa Mataifa hii leo umeadhimisha miaka 80 tangu kusainiwa kwa Mkataba wake tarehe 26 Juni 1945, tukio lililotoa matumaini mapya kwa dunia iliyokuwa imechoka kutokana na vita kuu mbili za dunia, mauaji ya halaiki na ukoloni. Katika maadhimisho hayo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema kumbukizi ya kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa ni fursa ya kukumbuka ujasiri wa waanzilishi wa taasisi hiyo na kuimarisha mshikamano wa kimataifa katika kukabili changamoto zinazokabili dunia hivi sasa. Tuungane na Leah Mushi aliyefuatilia maadhimisho hayo atupatie taarifa zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa washirirki ya mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, hasa maadhimisho ya miaka 80 ya umoja huo. Pia tunamulika mashauriano ya faragha yenye lengo la kusaka majawabu ya madhara ya mabadiliko ya tabianchi.Umoja wa Mataifa hii leo umeadhimisha miaka 80 tangu kusainiwa kwa Mkataba wake tarehe 26 Juni 1945, tukio lililotoa matumaini mapya kwa dunia iliyokuwa imechoka kutokana na vita viwili vya dunia, mauaji ya halaiki na ukoloni. Katika maadhimisho hayo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema kumbukizi ya kuanzishwa kwa UN ni fursa ya kukumbuka ujasiri wa waanzilishi wa taasisi hiyo na kuimarisha mshikamano wa kimataifa katika kukabili changamoto zinazokabili dunia hivi sasa.Tukisalia na maadhimisho ya miaka 80 ya Umoja wa Mataifa , moja ya mchango mkubwa unaotoa kwa dunia tangu ulipoanzishwa mwaka 1945 ni kusaidia mamilioni ya watu wanaolazimika kufungasha virago kukimbia makwao na kuwa wakimbizi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vita. Uganda ni moja ya nchi zinazohifadhi maelfu ya wakimbizi wengi kutoka Sudan, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC wakisaidiwa chini ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na mengine. John Kibego kutoka Radio washirika Kazi-Njema FM iliyoko mjini Hoima Uganda amepata fursa ya kuzungumza na mmoja wa wakimbizi hao akielezea mchango mkubwa wa Umoja wa Mataifa kwake.Kando ya maadhimisho ya siku ya miaka 80 ya Umoja wa Mataifa, hapa makao makuu kumefanyika mashauriano ya faragha yenye lengo la kusaka majawabu ya madhara ya mabadiliko ya tabianchi. Mashauriano ya leo ni sehemu ya mashauriano 10 yatakayofanyika kuelekea mkutano wa tabianchi wa wakuu wa nchi na serikali utakaofanyika keshokutwa Jumatano hapa Umoja wa Mataifa. Assumpta Massoi amezungumza na mmoja wa watoa mada kwenye mashauriano hayo ambayo matokeo yake yatawasilishwa kwenye mkutano wa viongozi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Wakati dunia ikiadhimisha miaka 80 ya Umoja wa Mataifa, moja ya mchango mkubwa unaotoa kwa dunia tangu ulipoanzishwa mwaka 1945 ni kusaidia mamilioni ya watu wanaolazimika kufungasha virago kukimbia makwao na kuwa wakimbizi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo vita. Uganda ni moja ya nchi zinazohifadhi maelfu ya wakimbizi wengi kutoka Sudan, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC wakisaidiwa chini ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na mengine. John Kibego kutoka Radio washirika Kazi-Njema FM iliyoko mjini Hoima Uganda amepata fursa ya kuzungumza na mmoja wa wakimbizi hao akielezea mchango mkubwa wa Umoja wa Mataifa kwake. Kwako Kibego.
Hii leo jaridani tunaangazia wakimbizi wa ndani wa Palestina Gaza, na ujumbe wa mwakilishi wa kudumu wa Kenya kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Ekitela Lokaale kuhusu mchango wa Afrika katika kazi za Umoja wa Mataifa. Pia tunakwenda Tanzania kumulika amani.Baada ya amri iliyotolewa na jeshi la Israel la kuwataka Wapalestina walioko katika eneo la mji wa Gaza huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel kuondoka eneo hilo kwani linataka kufanya mashambulizi, hali imekuwa mbaya kwa wananchi hususan wazee ambao sasa wanafunga safari kilometa nyingi kuondoka eneo hilo.Ilikuwa miezi, wiki na sasa imesalia siku tatu tu kabla ya mjada mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 kun'goa nanga hapa kwenye Makao Makuu jijini New York Marekani ambapo viongozi wa Dunia na wakilishi mbalimbali watashiriki kwenye mkutano wa 80 wa Baraza Kuu. Mada mbalimbali zitajadiliwa ikiwemo maadhimisho ya miaka 80 ya Umoja wa Mataifa.Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Amani, hapo Jumapili tarehe 21 mwezi Septemba 2025, Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kwa kushirikiana na baadhi ya wadau nchini humo, umeendesha warsha ya siku moja ya kutoa elimu kwa wanafunzi wa shule ya msingi Hazina jijini Dar es Salaam kuhusu ya umuhimu wa kuishi kwa amani na kuchukua hatua sasa katika kuidumisha. Warsha hiyo imeongozwa na kauli mbiu “Chukua hatua Sasa, kwa ajili ya Dunia yenye Amani.”Mwenyeji wako ni Assumpta, karibu!
Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Amani, hapo Jumapili tarehe 21 mwezi Septemba 2025, Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kwa kushirikiana na baadhi ya wadau nchini humo, umeendesha warsha ya siku moja ya kutoa elimu kwa wanafunzi wa shule ya msingi Hazina jijini Dar es Salaam kuhusu ya umuhimu wa kuishi kwa amani na kuchukua hatua sasa katika kuidumisha. Warsha hiyo imeongozwa na kauli mbiu “Chukua hatua Sasa, kwa ajili ya Dunia yenye Amani.” Katika warsha hiyo, baadhi ya wanafunzi wameeleza walichojifunza na namna elimu hiyo inavyoweza kuwanufaisha katika maisha yao ya kila siku. Shuhuda wetu katika mafunzo ni Sabrina Saidi anatupasha ilivyokuwa
Ilikuwa miezi, wiki na sasa imesalia siku tatu tu kabla ya mjada mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 kun'goa nanga hapa kwenye Makao Makuu jijini New York Marekani ambapo viongozi wa Dunia na wakilishi mbalimbali watashiriki kwenye mkutano wa 80 wa Baraza Kuu. Mada mbalimbali zitajadiliwa ikiwemo maadhimisho ya miaka 80 ya Umoja wa Mataifa. Flora Nducha ameketi na mwakilishi wa kudumu wa Kenya kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Ekitela Lokaale kuzungumzia Afrika na Umoja wa Mataifa katika miaka na umuhimu wa Umoja huo duniani, hiki ni kionjo tu cha maohojiano hayo akianza na mchango wa Afrika Umoja wa Mataifa