Podcasts about serikali

  • 35PODCASTS
  • 685EPISODES
  • 15mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • Jul 16, 2026LATEST

POPULARITY

20192020202120222023202420252026


Best podcasts about serikali

Latest podcast episodes about serikali

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari:Ombi latolewa kuharamisha matamshi ya chuki dhidi yawa Aboriginal na wakaazi wa Torres Strait

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jul 16, 2026 5:20


Kuna wito wa kuharamisha matamshi ya chuki dhidi yawa Aboriginal na watu kutoka Visiwa vya Torres Strait, huku vikao vikiendelea katika uchunguzi wa ubaguzi wa rangi wa Serikali ya Shirikisho huko Darwin.

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari:Vyuo vikuu kukabiliwa na faini kubwa vikishindwa kupambana na ubaguzi wa rangi

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jul 14, 2026 13:56


Serikali ya Shirikisho inasema vyuo vikuu vinaweza kukabiliwa na faini ikiwa vitashindwa kupambana na ubaguzi wa rangi chini ya viwango vipya vilivyoanzishwa Jumatatu 13 Julai 2026.

Wimbi la Siasa
Rais Ndayishimiye ataweza kuleta maridhiano kati ya upinzani na serikali nchini DRC ?

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Jul 8, 2026 9:41


Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, wiki hii amekutana  na kufanya mazungumzo na viongozi wa upinzani kutoka muungano wa C64 na viongozi wa Kanisa Katoliki na Kiprotestanti nchini DRC, wanaopinga mchakato wa marekebisho ya katiba unaoungwa mkono na rais Felix Tshisekedi. Je, rais Ndayishimiye, atafanikiwa kuleta maridhiano ?

Habari RFI-Ki
Je, serikali ya Afrika Kusini ilichukua hatua za kutosha kulinda usalama wa raia wa kigeni?

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Jul 6, 2026 9:58


Wiki iliyopita, maelfu ya raia wa mataifa mbalimbali ya Afrika waliondoka Afrika Kusini kutokana na hofu ya usalama baada ya maandamano yaliyolenga wageni. Baadhi ya nchi zimeikosoa serikali ya Afrika Kusini kwa kushindwa kudhibiti hali hiyo.

afrika wiki raia hatua baadhi serikali
Habari RFI-Ki
Je, serikali ya Afrika Kusini ilichukua hatua za kutosha kulinda usalama wa raia wa kigeni?

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Jul 6, 2026 9:58


Wiki iliyopita, maelfu ya raia wa mataifa mbalimbali ya Afrika waliondoka Afrika Kusini kutokana na hofu ya usalama baada ya maandamano yaliyolenga wageni. Baadhi ya nchi zimeikosoa serikali ya Afrika Kusini kwa kushindwa kudhibiti hali hiyo.

afrika wiki raia hatua baadhi serikali
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari:Serikali ya shirikisho yaongeza gharama ya maombi kwa vitengo kadhaa vya visa za Australia kwa asilimia 25

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jul 3, 2026 14:08


Ada ya maombi ya visa ya mwanafunzi imeongezeka tangu Julai 1 kutoka $2,000 hadi $2,500, huku Visa ya Muda ya Uzamili, au visa nambari 485, sasa inagharimu $5,750.

Wimbi la Siasa
Serikali nchini Uganda inatumia Mahakama kuwanyanyasa wapinzani ?

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Jun 24, 2026 9:53


Nchini Uganda, mwanasiasa wa upinzani na Meya wa zamani wa jiji la Kampala Erias Lukwago anakabiliwa na mashtaka ya uhaini. Alikamatwa nyumbani kwake na wanajeshi kwa agizo la Mkuu wa Majeshi Jenerali Muhoozi Kainerugaba na kuzuiwa kabla ya kufikishwa Mahakamani. Wiki hii, mwanasiasa mashuhuri na wakili wa Besigye Martha Karua kutoka nchini Kenya, alizuiwa kuingia nchini Uganda na kufukuzwa nchini humo, na sasa serikali ya Uganda imempiga marufuku kurejea nchini humo. Tunachambua.

Habari za UN
23 JUNI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 23, 2026


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambapo Leah Mushi ameketi chini na Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nassriya Nassir Ali akieleza safari yake ya uongozi wa nafasi za umma kupitia mkalimani wake wa lugha ya alama Tusajigwa Ernest. Pia tunakuletea Muhtasariw a habari na jifunze Kiswahili.Janga la tabianchi linakaribia kwa kasi zaidi kuliko inavyodhaniwa ameonya leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, huku akitoa wito wa hatua saba za haraka kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi na kuachana na matumizi ya mafuta ya kisukuku. Akizungumza mjini London kwenye mkutano wa hatua dhidi ya tabianchi, ametaja hatua hizo kuwa ni pamoja na Serikali zichukue hatua madhubuti za tabianchi, dunia iongeze matumizi ya nishati safi, ilinde jamii zilizo hatarini, ihakikishe ufadhili wa haki kwa nchi zinazoendelea, isimamie kwa uwajibikaji matumizi ya teknolojia ya akili mnemba na kupambana na upotoshaji wa taarifa kuhusu tabianchi. Guterres amesema hatua hizo ni muhimu ili kudhibiti ongezeko la joto duniani na kuzuia madhara makubwa zaidi kwa binadamu na mazingira.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, limekaribisha makubaliano mapya kati ya DRC na Rwanda ya kusaidia wakimbizi kurejea nyumbani kwa hiari, usalama na heshima. Katika mkutano uliofanyika Addis Ababa Ethiopia, serikali za nchi hizo mbili zimeahidi kuimarisha ushirikiano kwa msaada wa UNHCR ili kuwezesha urejeaji salama wa wakimbizi.Zaidi ya wagonjwa 1,000 vya Ebola wamethibitishwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, huku watu 254 wakifariki dunia kwa mujibu wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO likiongeza kuwa wagonjwa 100 wamepona, jambo linaloonesha kuwa huduma ya afya ya haraka inaweza kuokoa maisha.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "TANUWINI"Mwenyeji wako ni Feissal Kirwa, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari:Mpango wa serikali wa kurekebisha NDIS waiweka pabaya bungeni

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 23, 2026 14:45


Chama cha Greens kimeita mpango wa serikali wa kurekebisha Mpango wa Kitaifa wa Bima ya Watu Wenye Ulemavu kuwa sheria 'isiyo ya kibinadamu'.

SBS Swahili - SBS Swahili
Yaliyojiri Afrika:Kasi yakuenea kwa ugonjwa wa Ebola kwa lazimisha serikali ya Congo kutoa tahadhari

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 23, 2026 6:07


Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, imetahadharisha umma kuhusu kuenea kwa kasi kwa ugonjwa wa Ebola.

congo afrika ebola kongo kasi jamhuri serikali ugonjwa kidemokrasia
Habari za UN
UN Women na EU waleta matumaini kwa wanawake waathirika wa ukatili viziwani Zanzibar

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 19, 2026 2:43


Je, maisha yangekuwaje kama kila manusura wa ukatili wa kijinsia angejua mahali pa kupata msaada kwa wakati? Kisiwani Zanzibar nchini Tanzania Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wanawake (UN Women), kwa ufadhili wa Muungano wa Ulaya (EU) na kwa ushirikiano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, linaimarisha upatikanaji wa haki na huduma za msaada kwa manusura wa ukatili wa kijinsia, hususan katika maeneo ya pembezoni. Kupitia mradi wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Wasichana Zanzibar na Kuimarisha Uongozi wa Wanawake, manusura wanapata habari muhimu, ushauri nasaha na msaada wa kisheria wakati wowote. Feissal Kirwa na taarifa zaidi.

european union tanzania zanzibar un women gbv umoja wanawake na eu mataifa serikali shirika
Habari za UN
19 JUNI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 19, 2026 9:57


Hii leo jaridani tunaangazia wito wa UN wa kulinda mamilioni wa wakimbizi kote duniani, masuala ya kijinsia Zanzibar nchini Tanzania, na ripoti mpya ya Katibu Mkuu wa UN kuhusu watoto katika maeneo ya machafuko imeonesha hali ya kutisha duniani.Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wakimbizi kesho Juni 20, viongozi wa Umoja wa Mataifa wametoa wito wa kuimarishwa kwa mshikamano na hatua za kimataifa za kuwalinda mamilioni ya watu waliolazimika kuyakimbia makazi yao kote duniani kutokana na vita, vurugu na mateso.Ripoti mpya ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto katika maeneo ya machafuko imeonesha hali ya kutisha duniani. Takribani watoto 24,174 waliuawa, kujeruhiwa, kulazimishwa kujiunga na makundi yenye silaha, kubakwa au kuathiriwa kwa namna nyingine na ukiukwaji mkubwa wa haki katika maeneo yenye mizozo mwaka 2025.Je, maisha yangekuwaje kama kila manusura wa ukatili wa kijinsia angejua mahali pa kupata msaada kwa wakati? Kisiwani Zanzibar nchini Tanzania Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wanawake (UN Women), kwa ufadhili wa Muungano wa Ulaya (EU) na kwa ushirikiano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, linaimarisha upatikanaji wa haki na huduma za msaada kwa manusura wa ukatili wa kijinsia, hususan katika maeneo ya pembezoni. Kupitia mradi wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Wasichana Zanzibar na Kuimarisha Uongozi wa Wanawake, manusura wanapata habari muhimu, ushauri nasaha na msaada wa kisheria wakati wowote.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

tanzania zanzibar gbv umoja hii siku wanawake mataifa serikali kimataifa ripoti
MAELEZO PODCASTS
Kuelekea Kongamano la Pili la Kiswahili la Kimataifa, Paris - Ufaransa

MAELEZO PODCASTS

Play Episode Listen Later Jun 18, 2026 34:12 Transcription Available


Send us Fan MailSerikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inatarajia kufanya Kongamano la pili la kimataifa la Kiswahili kati ya Julai 4 - 7, 2026, jijini Paris, Ufaransa.Tumezungumza na Bw. Tito Lulandala, Afisa Utamaduni Mwandamizi, kutoka Idara ya Maendeleo ya Utamaduni, na Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Maandalizi ya Kongamano la Pili la Kiswahili la Kimataifa kuhusu maendeleo ya Kiswahili, fursa zilizopo, ajenda muhimu kuelekea kongamano la pili la kimataifa la Kiswahili nchini Ufaransa, pamoja na mafanikio ya kongamano la kwanza lililofanyika Havanna, nchini Kuba, mwaka 2024.Support the showMsemaji Mkuu wa Serikali

tanzania kuba bw pili umoja havanna kiswahili julai elimu mataifa jamhuri serikali maendeleo shirika ufaransa kimataifa
Wimbi la Siasa
Kenya kuwalipa fidia waathiriwa wa maandamano ya kisiasa

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Jun 17, 2026 9:59


Serikali ya Kenya, itaanza kuwalipa fidia watu karibu Elfu Mbili, walioathiriwa na visa vya ukiukwaji wa haki za binadamu, ikiwemo kuuawa, kubakwa, kutoweka na kujeruhiwa wakati wa maandamano ya kisiasa yaliyotokea nchini humo kati ya mwaka 2017 hadi 2025. Tume ya taifa ya haki za binadamu nchini Kenya, katika ripoti yake, inasema imewatambua waathiriwa wote wanaopaswa kupokea fidia hiyo, ambayo itaigharimu serikali nchini humo, Dola za Marekani Milioni 15. Tunachambua.

kenya dola tume serikali fidia
Habari za UN
12 JUNI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 12, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, umehitimishwa jana katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Watu wenye ulemavu na wadau mbalimbali wa Serikali na Mashirika yasiyo ya Serikali walikusanyika kutoka kila pembe ya dunia kujadili hatua zilizopigwa katika kipindi cha miaka 20 ya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Watu Wenye Ulemavu, CRPD. Mmoja wa waliohudhuria ni Bwana Kibaya Laibuta ambaye licha ya kupoteza uwezo wa kuona akiwa na umri wa miaka 24 alipokuwa mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Nairobi bado alifanikiwa kusonga mbele akamaliza masomo yake ya sheria na masomo mengine ya ngazi za juu na sasa miaka mingi baadaye ni Jaji katika Mahakama ya Rufaa ya Kenya. Siri yake ya mafaniko ndio hasa anaihamasisha kote duniani na anaiweka wazi katika mazungumzo yafuatayo na Anold Kayanda wa Idhaa hii ya Umoja wa Mataifa ili watu wengine wenye ulemavu wafanikiwe kama yeye. Pia tunakuletea muhtasari wa habari zikiwemo za hatua za kupambana na UKIMWI, maambukizi ya ugonjwa wa Ebola hasa kwa watoto DRC, na ujumbe katika siku ya kimataifa ya kupinga utumikishaji wa watoto.Mwenyeji wako ni Rashid Malekela.

new york kenya siri ebola nairobi drc umoja hii haki afya watoto watu crpd mataifa serikali marekani kimataifa mkutano mashirika chuo kikuu
MAELEZO PODCASTS
Fursa, Ushirikiano kati ya Algeria na Tanzania: Balozi Matinyi

MAELEZO PODCASTS

Play Episode Listen Later Jun 12, 2026 7:19 Transcription Available


Send us Fan MailMheshimiwa Balozi Mobhare Matinyi akizungumza mara baada ya kukabidhi hati zake za utambulisho wa kibalozi kwa Mheshimiwa Abdelmadjid Tebboune, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, katika hafla iliyofanyika kwenye Ikulu ya Algiers tarehe 10 Juni, 2026. Balozi Mobhare Matinyi anayeiwakilisha Tanzania nchini Algeria, ametoa wito kwa Watanzania kutumia fursa za ushirikiano mzuri baina ya nchi hizi kufaidika katika nyanja mbalimbali.Support the showMsemaji Mkuu wa Serikali

tanzania algeria algiers rais watu jamhuri serikali kidemokrasia
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Upinzani wa mseto wapanga njama yakuzuia kupitishwa kwa sheria ya kodi ya serikali ndani ya Seneti

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 5, 2026 13:22


Mabadiliko ya kodi ya serikali ya shirikisho yamepitishwa ndani ya nyumba la Wawakilishi - ila, upinzani wa mseto hauja tupilia mbali uwezekano wa muungano na chama cha Greens kuzuia mabadiliko hayo kupitishwa ndani ya Seneti na kuwa sheria.

SBS Swahili - SBS Swahili
Yaliyojiri Afrika: Duale "serikali haita shauriana na raia kuhusu karantini ya Ebola"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 5, 2026 7:37


Rais wa Kenya, William Ruto, amesema serikali yake inafanya jambo sahihi kwa kuruhusu Marekani kujenga kituo cha karantini ya Ebola nchini humo.

kenya afrika ebola rais raia duale serikali marekani
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari:Chama cha Nationals chataka uchaguzi uitishwe kuhusu hatma ya mageuzi ya kodi ya serikali

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 29, 2026 12:41


Chama cha Nationals kimemtaka Waziri Mkuu Anthony Albanese kuitisha uchaguzi mkuu, kuhusu mabadiliko hasi ya kodi ya vifaa na faida ya mtaji yaliyoainishwa katika bajeti ya shirikisho.

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari:Serikali ya Shirikisho ya tetea jibu lake kwa mlipuko wa Diphtheria

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 22, 2026 5:14


Waziri wa Afya Mark Butler ametetea utoaji wa kifurushi cha dola milioni 7 kutoka kwa serikali kusaidia kujibu mlipuko wa ugonjwa wa diphtheria ambayo ni maambukizi makubwa ya bakteria yanayoambukiza sana na huathiri njia zakupumua na inaweza sababisha vidonda kwenye mwili pia.Kiwango cha ukosefu wa ajira nchini Australia kimepanda hadi asilimia 4.5, huku kazi 19,000 zikiaondoka katika uchumi mnamo Aprili. Ofisi ya Takwimu ya Australia inasema ongezeko la ukosefu wa ajira imechangiwa na kupungua kwa ajira ya wanawake, kushuka kwa kwanza katika kitengo hicho tangu Agosti 2025.Shirika la Afya Duniani WHO limesema mlipuko wa Ebola ambao tayari umesababisha vifo vya watu 130 nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo huenda ulianza miezi miwili iliyopita.Bonyeza hapo juu kwa taarifa zaidi.

australia lake ebola kongo diphtheria agosti habari waziri jamhuri aprili serikali shirika
SBS Swahili - SBS Swahili
SBS Examines:Nini inaweza fanywa kusimamisha kupandisha bei ya mafuta kwa njia ya unyonyaji?

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 21, 2026 12:47


Serikali ya Australia imeanzisha hatua kadhaa za kusaidia kupunguza shinikizo la usambazaji wa mafuta linalo endelea.Hatua hizo zinajumuisha kupunguzwa kwa muda kwa ushuru wa mafuta, na mamlaka zaidi kwa ACCC kupambana na kupandisha bei kwa njia ya unyonyaji.Bonyeza hapo juu kwa taarifa zaidi

australia nini accc njia hatua serikali
SBS Swahili - SBS Swahili
Yaliyojiri Afrika: Seriklai ya DRC kufungua vituo vitatu vya matibabu ya virusi vya Ebola

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 19, 2026 7:20


Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesema Jumatatu itafungua vituo vitatu vya matibabu, kwa ajili ya watu walioambukizwa virusi vya Ebola katika jimbo la Ituri.

afrika ebola kongo ituri jamhuri serikali virusi kidemokrasia
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Ghana kuwaondoa raia wake 300 wanaoishi Afrika Kusini

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 14, 2026 6:06


Serikali ya Ghana imetangaza kuwa itawarudisha raia wake 300-wanaoishi nchini Afrika Kusini, kufuatia ongezeko la visa vya wageni kushambuliwa.

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Ugavi wa nyumba utakuwa muhimu katika bajeti ya shirikisho ya kesho serikali ya sema

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 11, 2026 8:00


Waziri wa Makazi Clare O'Neil, anasema bajeti ya shirikisho itasaidia sana kushughulikia upungufu wa usambazaji wa makazi.

sema katika habari waziri serikali nyumba kesho
Habari za UN
Serikali ya Tanzania inajali usawa na haki kwa watu wote kupata huduma kwa usawa - Profesa Malebo

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 6, 2026 2:34


Siku tano zilizopita Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa kuhusu Masuala ya Watu wa Asili (UNPFII) limefunga pazia hapa katika makao ya Umoja wa Mataifa  jijini New York, Marekani  baada ya majadiliano ya takribani wiki mbili ya wadau kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu sera, mafanikio na kukabiliana na changamoto mbalimbali katika kuhudumia wananchi wao ikiwemo jamii za watu wa asili. Kwa upande wa Tanzania, mmoja wa walioshiriki ni Katibu Mtendaji wa Tume ya shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO ya Taifa la Tanzania, Profesa Hamisi Masanja Malebo.Feisal Kirwa wa idhaa hii alifanya mahojiano naye kwanza akitaka kufahamu Tanzania ina mikakati gani ya kuhakikisha watu wa asili wanajumuishwa katika huduma za afya kwa wote?

new york tanzania unesco umoja kwa haki siku watu taifa tume wote elimu mataifa serikali marekani jukwaa
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Serikali yakana shutuma kwamba inawalenga wawekezaji wa "mama na baba" katika bajeti mpya

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 5, 2026 15:28


Jim Chalmers amepuuza mapendekezo kwamba mabadiliko yanayowezekana kwa matumizi hasi ya vifaa au kodi ya faida ya mtaji yatakuwa ni kuvunja ahadi na wapiga kura.

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Upinzani waikosoa Serikali ya Madola kwa kuto fanya yakutosha kuimarisha usalama wa taifa

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 1, 2026 13:19


Mbunge wa Upinzani Jonathon Duniam amesema Serikali ya shirikisho lazima iende mbali zaidi ili kuimarisha usalama wa taifa, kufuatia kutolewa kwa ripoti ya muda iliyotolewa na Tume ya Kifalme inayochunguza maswala ya chuki dhidi ya wayahudi na Uwiano wa Kijamii.

Habari za UN
30 APRILI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 30, 2026 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo tunamsikia Dkt. Tulia Ackson, Rais wa Muungano wa Mabungeni duniani, (IPU) ambaye hivi karibuni akiwa makao makuu ya UN, Marekani aliongoza kikao kilichokuwa sehemu ya Mkutano wa CSW70. Mara baada ya kikao hicho Assumpta Massoi wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa alizungumza naye masuala kadhaa ikiwemo yale waliyopatia kipaumbele ili kusongesha usawa wa kijinsia duniani.Karibu Dkt. Tulia.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo saa 3 asubuhi kwa saa za New York Marekani ameeleza kuwa na wasiwasi mkubwa kuhusu suala la kufungwa kwa mlango bahari wa Hormuz wakati mzozo huko mashariki ya kati ukiingia mwezi wa tatu licha ya kuwepo kwa usitishaji mapigano aliouita kuwa ni dhaifu. Katibu Mkuu ameonya kuwa kadri hali inavyoendelea, ndivyo gharama kwa ubinadamu zinavyoongezeka, akisisitiza kuwa nchi zinazoendelea zitaathirika zaidi kutokana na madeni makubwa na kupotea kwa ajira na kuwataka wahusika wote kurejesha mara moja uhuru wa usafiri kama ilivyoainishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupitia Azimio namba  2817.Ripoti mpya ya pamoja iliyotolewa leo na mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayohusika na chakula, kilimo na uchumi yakishirikiana na Tume ya Muungano wa Afrika imeonesha kuna pengo kubwa kati ya ufadhili wa sasa wa umma na binafsi wa kilimo na kiwango cha ufadhili kinachohitajika ili kubadilisha mifumo ya kilimo barani Afrika. Ripoti hiyo pia inathibitisha ongezeko linaloendelea la njaa na ukosefu wa uhakika wa chakula kote barani Afrika, ikisisitiza uharaka wa ufadhili mkubwa na endelevu ili kubadilisha mifumo ya kilimo.Na leo ni siku ya kuadhimisha muziki wa jazz duniani, siku inayotukumbusha nafasi ya muziki wa jazz kama daraja la kuleta amani, umoja na mazungumzo kati ya watu wa tamaduni tofauti. Kupitia midundo yake ya kipekee, jazz imeendelea kuwa chombo muhimu cha elimu na ushirikiano, ikiunganisha jamii duniani kote. Serikali, taasisi za elimu, mashirika ya kiraia na watu binafsi huungana kusherehekea mchango wa jazz katika kujenga jamii jumuishi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

ethiopia afrika hormuz rais umoja hii kiswahili tume tulia ipu baraza dkt mataifa aprili serikali marekani mkutano ripoti azimio
Habari za UN
22 APRILI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 22, 2026 9:50


Hii leo jaridani tunaangazia sitisho la mapigano katika Mashariki ya kati, kilimo endelevu kinachowakwamua wakimbizi na wenyeji Kakuma nchini Kenya, na mafunzo ya UNDP ya uchimbaji salama wa madini ya ujenzi nchini Tanzania.Umoja wa Mataifa umekaribisha tangazo la Rais wa Marekani Donald Trump la kuongeza muda wa sitisho la mapigano kati ya Marekani na Iran, ukisema hiyo ni hatua muhimu kuelekea kupunguza mvutano kati ya mataifa hayo mawili.Maisha ya wakimbizi katika eneo la Kakuma, kaskazini mwa Kenya, yanaanza kubadilika kwa kasi kupitia miradi ya kilimo na lishe inayowezeshwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la Mpango wa Chakula Duniani  (WFP) na la Chakula na Kilimo (FAO). Kwa ushirikiano na Serikali ya Kaunti ya Turkana chini ya ufadhili wa  Muungano wa Ulaya (EU) sasa wakimbizi wana uwezo wa kuzalisha chakula chao wenyewe, kuboresha lishe, na kujenga maisha ya kujitegemea.Shirika la Umoja wa Mataifa  la Mpango wa Maendeleo (UNDP), kwa kushirikiana na Tume ya Madini nchini  Tanzania katikati mwa wiki iliyopita yaani Aprili 16 na 17 wamefanya warsha ya mafunzo mkoani Singida katikati mwa nchi. Mafunzo hayo yamelenga kuimarisha ujuzi wa uchimbaji salama, unaozingatia sheria, na wenye faida kwa wanawake na vijana wanaojihusisha na uchimbaji mdogo wa madini ya ujenzi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

iran kenya tanzania undp rais wfp umoja maisha hii kwa turkana kakuma tume mataifa aprili serikali marekani shirika mashariki kaunti singida
Habari za UN
Kilimo endelevu charejesha matumaini ya kujitegemea Kakuma, Neema aibuka kutoka utegemezi hadi uzalishaji

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 22, 2026 3:00


Maisha ya wakimbizi katika eneo la Kakuma, kaskazini mwa Kenya, yanaanza kubadilika kwa kasi kupitia miradi ya kilimo na lishe inayowezeshwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la Mpango wa Chakula Duniani  (WFP) na la Chakula na Kilimo (FAO). Kwa ushirikiano na Serikali ya Kaunti ya Turkana chini ya ufadhili wa  Muungano wa Ulaya (EU) sasa wakimbizi wana uwezo wa kuzalisha chakula chao wenyewe, kuboresha lishe, na kujenga maisha ya kujitegemea. Feissal Kirwa anasimulia.

Habari za UN
20 APRILI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 20, 2026 10:44


Hii leo jaridani tunaangazia yaliyojiri katika Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa kuhusu Watu wa Asili hapa Makao Makuu, mafunzo Kenya ya "Social Media 4 Peace" yaani ya kuondoa habari potofu na deepfakes mtandaoni, na mlo shuleni shuleni nchini Tanzania.Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa kuhusu Watu wa Asili (UNPFII) limefungua pazia leo Aprili 20 ikiwa ni kikao cha ishirini na tano hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani likiadhimisha miaka 25 tangu kuanzishwa kwake kama jukwaa la kipekee la kimataifa linalowakutanisha wadau kuhusu Watu wa Asili.  Maudhim aka huu yakimulika kuhakikisha afya ya watu wa jamii za asili ikiwemo kwenye mizozo.Ni dhahiri hivi sasa watu wengi zaidi wanatumia mitandao ya kijamii katika shughuli mbalimbali na pia kupata taarifa, na kwakuzingatia ukweli huo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, likishirikiana na Umoja wa wamiliki vya vyombo vya habari vya mtandaoni (Wanablogu) nchini Kenya, BAKE (inatamkwa ‘BEKI'), limeandaa mafunzo maalum jijini Nairobi yaliyopewa jina la "Social Media 4 Peace" yaani mitandao ya kijamii kwa amani. Karibu Rashid Malekela utujuze zaidi.Elimu imeanza kung'aa tena kwa watoto katika kijiji cha Twabagondozi, ambapo njaa iliyokuwa kikwazo kikubwa cha masomo sasa inapungua kupitia mpango wa lishe na malezi bora unaoungwa mkono na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF Tanzania kwa ufadhili wa Serikali ya Japan. Kupitia juhudi hizi, watoto kama Magdalena A. Prosper wamepata nafasi ya kurejea darasani, kujifunza na hata kuwa viongozi shuleni.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
Lishe yarejesha matumaini ya elimu Kigoma, Magdalena arejea shuleni na kuwa chanzo cha mabadiliko

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 20, 2026 3:02


Elimu imeanza kung'aa tena kwa watoto katika kijiji cha Twabagondozi, ambapo njaa iliyokuwa kikwazo kikubwa cha masomo sasa inapungua kupitia mpango wa lishe na malezi bora unaoungwa mkono na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF Tanzania kwa ufadhili wa Serikali ya Japan. Kupitia juhudi hizi, watoto kama Magdalena A. Prosper wamepata nafasi ya kurejea darasani, kujifunza na hata kuwa viongozi shuleni. Feissal kirwa anasimulia.

japan tanzania umoja kuwa elimu mataifa serikali
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Kenya na Ufaransa zapiga hatua katika mkataba wa ulinzi

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 13, 2026 5:39


Serikali ya Australia inasema haifikirii kutuma meli katika Mlango-Bahari wa Hormuz, baada ya Rais Donald Trump kusema mataifa mengine yatahusika katika kizuizi cha Marekani kwenye njia hiyo ya maji.

australia kenya hormuz katika habari hatua serikali marekani ufaransa
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Serikali ya Australia na Singapore kutia saini makubaliano mapya ya usambazaji wa mafuta

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 10, 2026 13:11


Waziri Mkuu Anthony Albanese anasema uhusiano kati ya Australia na Singapore ni muhimu zaidi kuliko hapo awali, nchi hizo mbili zikijiandaa kusaini makubaliano mapya ya mafuta.

Habari za UN
09 APRILI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 9, 2026 9:58


Jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kusikia ujumbe wa Hanna Wendot Cheptumo Waziri wa Jinsia, Utamaduni na Maslahi ya Watoto wa Jamhuri ya Kenya ambaye alikuwa miongoni mwa washiriki wa CSW70 akieleza ni kwa namna gani Kenya inapiga hatua katika Lengo namba 5 la Usawa wa Kijinsia.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani vikali mashambulizi makubwa ya anga yaliyofanywa na Israel dhidi ya Lebanon tarehe 8 Aprili, mashambulizi ambayo yamesababisha mamia ya raia kuuawa na kujeruhiwa, wakiwemo watoto, sambamba na kuharibu kwa kiasi kikubwa miundombinu ya kiraia. Taarifa iliyotolewa New York, Marekani na Msemaji wa Umoja wa Mataifa inamnukuu Guterres akionesha wasiwasi mkubwa kuhusu ongezeko la vifo miongoni mwa raia na kutoa pole kwa watu na Serikali ya Lebanon, akiwatakia nafuu ya haraka wale waliojeruhiwa.Katika tukio jingine hii leo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezindua Mfuko wa Urejeshaji wa Palestina uliopewa jina la Horizon Fund, akisisitiza umuhimu wa kuchukuliwa kwa hatua za haraka kusaidia wananchi wa Palestina kurejesha maisha yao na kujenga mustakabali bora. Akizungumza kupitia ujumbe wa video wakati wa uzinduzi uliofanyika Ramallah, huko Ukingo wa Magharibi eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel, Guterres amesema mfuko huo ni sehemu muhimu ya ushirikiano kati ya Umoja wa Mataifa na Taifa la Palestina.Wakati mgogoro wa Sudan ukikaribia kutimiza miaka mitatu, zaidi ya wakimbizi milioni moja wa Sudan walioko nchini Chad wanakabiliwa na hatari kubwa ya kupunguzwa kwa msaada muhimu wa kibinadamu. Onyo hilo limetolewa leo na mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa ambayo ni lile la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) pamoja na la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) wakitanabaisha kuwa huduma za msingi kama chakula, maji, malazi, ulinzi na huduma za afya zitalazimika kupunguzwa zaidi katika miezi ijayo iwapo pengo la ufadhili la dola milioni 428 halitazibwa haraka.Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Hatari ya barabarani wakati wa Pasaka ya zua wito wa kuteuliwa kwa waziri wa usalama

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 7, 2026 12:35


Serikali inasema mahitaji ya mafuta yaliongezeka kwa theluthi moja wakati wa mapumziko ya Pasaka.

hatari habari wakati pasaka waziri serikali
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Australia yapata usambazaji wa mafuta wa mwezi mwingine

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 6, 2026 4:36


Serikali ya shirikisho imesema ugavi wa akiba ya mafuta ya Australia sasa umeongezwa hadi Mei, kuanzia katikati ya Aprili.

australia habari mwezi aprili serikali
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Serikali yachukua hatua yakupunguza bei ya mafuta nchini baada ya siku kadhaa za shinikizo

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 31, 2026 13:35


Waziri Mkuu amesema serikali yake imechukua hatua ya kupunguza bei ya mafuta kote nchini, kwa sababu hata kama vita vitaisha mara moja, madhara ya kiuchumi yataendelea.

siku baada habari hatua serikali waziri mkuu
SBS Swahili - SBS Swahili
Makala leo: Afueni kwa madereva wanaokabiliwa na matatizo baada ya serikali kupunguza ushuru wa mafuta

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 31, 2026 10:34


Baada ya wiki kadhaa za shinikizo kuhusu kupanda kwa bei ya petroli, serikali ya shirikisho imepunguza kodi ya mafuta kwa nusu.

makala baada serikali
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Ongezeko ya bei ya mafuta yalazimisha serikali izingatie hatua zakufanyia kazi nyumbani

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 30, 2026 6:35


Hatua za kufanyia kazi nyumbani zinaweza wasilishwa lakini mgao wa mafuta hauzingatiwi, na viongozi wanaohudhuria mkutano wa kitaifa wa baraza la mawaziri leo kuhusu mgogoro wa mafuta.

kazi habari hatua nyumbani serikali
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Serikali za Australia na Ujerumani za imarisha uhusiano wa usalama

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 26, 2026 5:26


Waziri wa ulinzi wa Ujerumani amekutana na mwenzake wa Australia Richard Marles, katika ziara ya kwanza ya mtu aliyehudumu katika nafasi hiyo katika kipindi cha miaka 8.

australia habari waziri serikali ujerumani
Habari za UN
Fahamu jinsi serikali ya Kenya inasambaza visima vya maji kwa wananchi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 23, 2026 3:00


Katika mazungumzo yafuatayo kati ya Anold Kayanda wa Idhaa hii na Hanna Wendot Cheptumo Waziri wa Jinsia, Utamaduni na Maslahi ya Watoto wa Kenya, Nchi hiyo ya Afrika Mashariki inajivunia kupiga hatua katika kuitatua changamoto hiyo.  Waziri Hanna Wendot Cheptumo anaeleza kwamba Kenya kupitiua mfuko ilioupa jina NGAAF yaani National Government Affirmative Action Fund, mfuko wa fecha mahususi kusaidia makundi maalumu katika jamii hususani wanawake kupitia wawakilishi wa wanawake. Pesa hizo wanazopewa wanawake si mkopo hivyo hawarudishi lakini wanatakiwa kuzitumia kijiendeleza “na hizo nidizo wanatumia kununua matanki ya maji” anasema Bi. Cheptumo. Visima vya jumuiya Pia kupitia miradi ambayo iko vijijini, Serikali ya Kenya inachimba visima vya maji vya jumuiya na wanaweka sola au mashine za kuvuta maji kwa njia ya nishati ya jua kwa hiyo hakuna mzigo au gharama ya umeme kwa wanawake hao. Waziri Hanna Wendot Cheptumo anakumbuka akisema, “hata mimi nikiwa mdogo nilikuwa ninaenda kilomita saba kwenda kutafuta maji lakini saa hizo ukienda kijijini unapata maji yako hapo na haulipishwi. Unaenda unachota maji yako na unaenda.” Mabwawa Aidha, kwa mujibu wa Bi. Cheptumo, Serikali ya Kenya imechimba mabwawa ya kusambaza maji katika vijiji na ni kazi ambayo inaendelea, “tunataka kusema hata kama maji hayajafikia kila mahali, lakini serikali iko na mikakati ambayo imewekwa ya kuhakikisha kila mtu anapata maji.Hupiti hata kilomita moja. Lakini sanasana weni sasa wana maji nyumbani.” Anahitimisha. 

kenya bi pesa maji katika watoto lakini jinsi nchi serikali fahamu afrika mashariki wananchi
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 23 Machi 2026

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 23, 2026 5:46


Serikali ya shirikisho inaagiza Tathmini ya Kitaifa ya Mnyororo wa Ugavi wa Chakula kwa ajili yakulinda sekta ya kilimo ya nchi dhidi ya usumbufu wa kimataifa.

machi habari serikali
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari:Wakazi wa Kusini Australia wa elekea debeni, je kutakuwa mabadiliko ya serikali?

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 20, 2026 12:58


Waziri Mkuu Anthony Albanese amesema usambazaji wa mafuta nchini Australia uko salama, lakini anataka Australia iwe tayari kupita kiasi linapokuja suala la kudhibiti uhaba wa mafuta nchini humu.

australia habari serikali wakazi
SBS Swahili - SBS Swahili
Makala leo: Sheria mpya za Australia kupiga marufuku kwa muda baadhi ya watu kuingia nchini za kosolewa

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 13, 2026 14:01


Serikali ya shirikisho ime wasilisha sheria mpya ya kuweka marufuku ya muda, kwa baadhi ya nchi kutumia viza fulani kuja Australia.

australia muda makala watu sheria baadhi serikali kupiga
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Serikali ya shirikisho yaongeza hatua za usambazaji wa mafuta Australia

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 13, 2026 12:36


Serikali ya Shirikisho imebadilisha hatua nyingine kwa ajili yakushughulikia athari za mgogoro wa usambazaji wa mafuta Australia.

australia habari hatua serikali
SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: Serikali yaamuru familia za wafanyakazi wa ubalozi nchini Israel na Lebanon kuondoka

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Feb 26, 2026 7:17


Polisi wanaamini kuna watu wengi zaidi wanaohusika, katika utekaji nyara na mauaji ya babu mmoja wa Sydney Chris Baghsarian.

SBS Swahili - SBS Swahili
Yaliyo jiri Afrika: Sudan yaikosoa Uganda kwa kumkaribisha mkuu wa RSF Daglo

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Feb 25, 2026 9:24


Serikali ya Sudan inayoungwa mkono na jeshi imekosoa UIganda kwa kumkaribisha mkuu wa wanamgambo wa RSF Mohamed Hamdan Daglo maarufu kama Hemeti.

Habari za UN
Tanzania yajipanga kutokomeza ugonjwa wa kichocho kwa watoto wadogo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 18, 2026 3:30


Serikali ya Tanzania na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo UNDP kupitia Ushirikiano wa Upatikanaji na Ufikishaji wa Huduma (ADP), inaendesha mpango wa majaribio wa kihistoria katika mikoa ya Simiyu, Mwanza, na Kigoma ili kutoa matibabu ya kwanza ya ugonjwa wa kichocho yaliyoandaliwa mahususi kwa ajili ya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano. Rashid Malekela na taarifa zaidi. 

tanzania adp umoja afya mwanza watoto mataifa serikali shirika ugonjwa
Habari za UN
18 FEBRUARI 2026

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 18, 2026 12:01


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya Akili Mnemba na wabunifu wa maudhui duniani kwa lugha, waumini wa dini ya kiislamu wakati huu wa Ramadhani katika ukanda wa Gaza, na matibabu ya kwanza ya ugonjwa wa kichocho huko Mwanza nchini Tanzania.Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, limesema wabunifu wa maudhui duniani kwa lugha ya kiingereza content creators wanakabiliwa na hatari ya kupoteza hadi asilimia 24 ya mapato yao ifikapo mwaka 2028 kutokana na kasi ya maendeleo ya Akili Mnemba, au AI.Waumini wa dini ya kiislamu duniani kote wameanza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, kipindi kinachoambatana na sio tu ibada bali pia mlo kama vile futari na daku. Hata hivyo kwa wakazi wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na kimabavu na Israeli hali si hali kwani mlo na mengine yanayoambatana na kipindi hiki vinasalia kuwa ndoto.Serikali ya Tanzania na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo UNDP kupitia Ushirikiano wa Upatikanaji na Ufikishaji wa Huduma (ADP), inaendesha mpango wa majaribio wa kihistoria katika mikoa ya Simiyu, Mwanza, na Kigoma ili kutoa matibabu ya kwanza ya ugonjwa wa kichocho yaliyoandaliwa mahususi kwa ajili ya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.Mwenyeji wako ni Anold Kyanda, karibu!