POPULARITY
Rais wa zamani wa DRC, Joseph Kabila, Aprili 18, aliripotiwa kurejea nchini na kufikia jijini Goma, linalodhibitiwa na waasi wa M 23. Hata hivyo, taarifa hizi hazijathibitishwa rasmi. Serikali jijini Kinshasa, nayo imesitisha shughuli zote za kisiasa za chama chake cha PPRD. Kabila anashtumiwa na serikali kwa kuunga vitendo vya waasi hao.
Serikali ya Albanese imesema uwekezaji wa serikali wa $1 bilioni moja inatambua pengo muhimu la wafanyakazi katika huduma ya afya ya akili inayo stahili fanyiwa kazi.
Shaba yetu kwenye makala haya inalenga hatua ya Serikali ya Kenya, kueeendelea kuwarejesha mamia ya raia wake waliotapeliwa na kusafirishwa hadi nchini Myanmar kwa ahadi ya kupewa ajira. Nchini mwako visa kama hivi vinaripotiwa?Ndilo swali letu, skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji.
Shaba yetu kwenye makala haya inalenga hatua ya Serikali ya Kenya, kueeendelea kuwarejesha mamia ya raia wake waliotapeliwa na kusafirishwa hadi nchini Myanmar kwa ahadi ya kupewa ajira. Nchini mwako visa kama hivi vinaripotiwa?Ndilo swali letu, skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji.
Duru za pande hasimu nchini Kongo, zimesema serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na waasi wa M23 wanajiandaa kwa mazungumzo ya ana kwa ana 9 Aprili 2025.
Waziri wa Ajira na mahusiano ya kazini, Murray Watt, ame kosoa ahadi ya upinzani yaku futa baadhi ya mageuzi ya mahusiano ya viwanda ya Serikali ya Labor.
Wa Australia wenye asili ya DR Congo, walijumuika mbele ya bunge la taifa mjini Canberra kuandamana dhidi ya vita vinavyo endelea mashariki mwa DR Congo.
Serikali ya Labor na Upinzani wana sifu sera zao za Uchumi, kabla ya kutangazwa kwa bajeti ya shirikisho kesho Jumanne 25 Machi.
Wakati huu serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, inapoendelea kukabiliwa na changamoto ya usalama Mashariki mwa nchi hiyo, baada ya waasi wa M23 kuingia katika miji ya Bukavu na Goma, rais Felix Tshisekedi ametangaza mpango wa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa kwa kuwashirikisha wanasiasa wa upinzani.Tunajadili iwapo hatua hii itasaidia kutatua mzozo wa mashariki mwa DRC.
Serikali za Afrika zitalazimika kuchangia ufadhili wa mipango ya kupambana na Malaria kufidia pengo kubwa la ufadhili Muungano wa viongozi wa Afrika wa kupambana na Malaria ,Africa Leaders Malaria Alliance unasema Afrika inahitaji dola bilioni 5 nukta nane mwaka huu wa kifedha hadi 2026.Hali hii pia imechangiwa na Marekani kukata ufadhili wa misaada kwa nchi za kigeni
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Umoja wa Mataifa kupitia miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa Pamoja wa Kigoma, KJP nchini Tanzania, unaolenga kuhakikisha wanawake na wasichana wanajumuishwa kwenye mipango ya kuhimili na kukabili mabadiliko ya tabianchi, kwa kuwajengea uwezo.Kuelekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake Machi 8, tathmini mpya ya Umoja wa Mataifa iliyowekwa wazi leo ikiangazia haki za wanawake miaka 30 baada ya Azimio la Beijing inaonesha uwepo wa maendeleo katika usawa wa kijinsia, kama vile sheria dhidi ya ubaguzi na sera jumuishi za kijinsia. Hata hivyo, ripoti hiyo inaeleza uwepo bado wa ubaguzi wa kijinsia uliojikita katika jamii, ukiendelea kuwazuia wanawake na wasichana kupata fursa.Ripoti nyingine ya Umoja wa Mataifa iliyochapishwa leo ikiangazia Sudan imefichua vitendo vya watu kukamatwa kiholela, mateso, na unyanyasaji huko Khartoum vinavyotekelezwa na Vikosi vya wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF) na pia Jeshi la Serikali ya Sudan (SAF). Ripoti hiyo imearifu pia kuwa makumi ya maelfu ya watu wamewekwa katika mazingira duni tangu Aprili 2023.Kutokana na kupungua kwa ufadhili wa misaada ya kibinadamu duniani, Umoja wa Mataifa leo jijini Geneva, Uswisi kutenga dola milioni 110 ili kusaidia majanga yaliyopuuzwa katika nchi 10 barani Afrika, Asia, na Amerika Kusini, zikiwemo Niger, Somalia, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Zambia.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia maana ya methali “MCHAWI AKIFICHUA MIRIMO YA WACHAWI HU UAWA”.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Mtumishi wa serikali Tanzania aeleza juhudi za wanawake na wanaume kuendeleza uboreshaji wa usawa wa kijinsia kwa wote
Machafuko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) yanaendelea kufurusha watu na wengine wanaamua kukimbilia nchi jirani ikiwemo Burundi. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR nchini Burundi limesema wazi kuwa katika wiki mbili za mwezi Februari kuanzia tarehe 14 walipokea wakimbizi zaidi ya 60,000, wengi wakiwa tayari walishafurushwa awali. Kwa waliowasili katika eneo la Kaburantwa nchini Burundi, bado wanahofia usalama. Serikali ya Burundi imetenga eneo lingine salama zaidi na sasa wanahamishiwa huko. Je ni wapi? Assumpta Massoi kwa msaada wa video ya UNHCR Burundi anasimulia zaidi.
Kama mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Celestin Mbaruku hakuwa na fursa ya ajira rasmi hadi alipothibitishwa ujuzi wake kupitia mpango wa Serikali ya Kenya wa Utambuzi wa Ujuzi wa Awali, uliotengenezwa kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani, ILO.Kupitia ILO Celestin Mbaruku ni mnufaika wa ufadhili wa PROSPECTS, ushirikiano wa kimataifa unaojumuisha mashirika kadhaa ya Umoja wa Mataifa ukilenga kuboresha upatikanaji wa elimu, ulinzi wa jamii, na ajira yenye hadhi kwa jamii zinazowakaribisha wakimbizi na watu waliolazimika kuhama makazi yao.Kimakosa, Celestin Mbaruku akiwa nchini mwake DRC alidhaniwa kuwa muasi, akafungwa lakini akamudu kutoroka hadi Kenya.Kabla ya masaibu haya, huko DRC alikuwa Mwalimu anayesimamia nidhamu katika shule alikokuwa anafanya kazi ya lakini kwa kuwa vyeti vyake vilipotea, hata alipovuka kuingia Kenya, hakuwa na uthibitisho wa kiwango cha elimu yake licha ya kuwa ana diploma ya mbinu za ufundishaji.Na hapo ndipo ikabidi achomoe kibindoni ujuzi wake mwingine. Ujuzi binafsi, ufundi wa kushona nguo.Celestin sasa anafundisha wanawake wadogo shughuli za kushona nguo.Hatimaye mwaka jana, 2024, kupitia mpango wa Serikali ya Kenya wa Utambuzi wa Ujuzi wa Awali (RPL), uliotengenezwa kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani, ILO utaalamu wake wa kushona nguo ambao haukuwa na cheti, ukathibitishwa rasmi na akapata cheti, hali ambayo imemfungulia milango ya kuomba ajira rasmi.
Wajumbe wa kisiasa kutoka kundi la RSF linaloongozwa na Jenerali Mohamed Hamdan Dagalo linalopigana na wanajeshi wa Sudan, walikutana jijini Nairobi na kutia saini mkataba wa uundwaji wa serikali mbadala kwenye maeneo wanayodhibiti. Nini hatima ya mzozo wa Sudan ?
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Karibu kwenye kipindi cha leo ambapo tunaangazia tangazo la Rais wa DRC, Felix Tschsekedi, kuwa ataunda Serikali ya umoja wa kitaifa, hatua inayokuja wakati huu akiwa katika shinikizo kutoka ndani na nje ya nchi yake, kuhusu namna alivyoshughulikia mzozo wa mashariki mwa nchi yake, wakati huu waasi wa M23 wakichukua miji zaidi.
Karibu kwenye kipindi cha leo ambapo tunaangazia tangazo la Rais wa DRC, Felix Tschsekedi, kuwa ataunda Serikali ya umoja wa kitaifa, hatua inayokuja wakati huu akiwa katika shinikizo kutoka ndani na nje ya nchi yake, kuhusu namna alivyoshughulikia mzozo wa mashariki mwa nchi yake, wakati huu waasi wa M23 wakichukua miji zaidi.
Wanamgambo wa RSF wanaopigana na jeshi nchini Sudan na washirika wake wakiwemo wanasiasa wapo jijini Nairobi nchini Kenya, wanakojadiliana kuhusu uundwaji wa serikali mbadala wakati huu inapoendelea na vita.Unazungumzia vipi harakati hizi za RSF ?Unafikiri ni kwanini Kenya imewaruhusu wanamgambo hao kukutana katika nchi yake ?
Wanamgambo wa RSF wanaopigana na jeshi nchini Sudan na washirika wake wakiwemo wanasiasa wapo jijini Nairobi nchini Kenya, wanakojadiliana kuhusu uundwaji wa serikali mbadala wakati huu inapoendelea na vita.Unazungumzia vipi harakati hizi za RSF ?Unafikiri ni kwanini Kenya imewaruhusu wanamgambo hao kukutana katika nchi yake ?
Makala haya yanaangazia hatua ya Serikali ya kenya kusema hakutakuwa na haja ya mahojiano kwa waomba vitambulisho toka katika maeneo ya mpakani, uamuzi ambao umeibua mjadala kuhusu masuala ya usalama.Tulimuuliza msikilizaji anazungumziaje hatua hiyo ya Kenya vile vile nchini mwake hali ikoje
Makala haya yanaangazia hatua ya Serikali ya kenya kusema hakutakuwa na haja ya mahojiano kwa waomba vitambulisho toka katika maeneo ya mpakani, uamuzi ambao umeibua mjadala kuhusu masuala ya usalama.Tulimuuliza msikilizaji anazungumziaje hatua hiyo ya Kenya vile vile nchini mwake hali ikoje
kwenye makala ya leo tunaangazia hatua ya wakuu wa nchi za #SADC na EAC kutaka kusitishwa mapigano maramoja ,na kutaka kuondoka kwa vikosi vya kigeni mashariki mwa #DRC, pamoja na Serikali ya Kinshasa kuzungumza moja kwa moja na waasi wa #M23 ambapo wito huo umepokelewa kwa hisia mseto na raia wa ukanda.
Serikali ya Wilaya ya Kaskazini ime fikia makubaliano ya thamani yama milioni ya dola na mashirika yawa Australia wa kwanza, kutoa huduma kwa maeneo ya vijijini.
Katika makala haya, tunachunguza nguvu na udhaifu wa aina za serikali tofauti duniani. Kutoka kwa demokrasia hadi utawala wa kioligarki, tunafunua jinsi mifumo hii inavyoathiri maisha ya raia. Pitia mifano halisi na tathmini za kitaalamu, na ujifunze kuhusu changamoto na faida zinazoambatana na kila mfumo wa utawala. Jiunge nasi katika kubaini njia bora za uongozi katika jamii zetu!
Serikali ya shirikisho na Victoria zime tia saini mkataba wa uwekezaji wenye thamani ya dola bilioni $2.5 kwa elimu, ambayo serikali hizo zime sema uwekezaji huo utawasaidia wanafunzi, wafanyakazi pamoja na familia.
Hii leo jaridani tuanaangazia masuala ya ufadhili wa huduma za afya, na kilimo cha cacao nchini Liberia. Makala inatupeleka nchini DRC na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Baada ya Serikali ya Marekani kutoa tangazo jipya sasa kwamba itaendelea kufadhili huduma zinazolenga vita dhidi ya Virusi vya Ukimwi (VVU), shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na VVU na Ukimwi (UNAIDS) limeeleza kuupokea uamuzi huo kwa furaha na kuuita wa kuokoa maisha.Kilimo bora cha kakao huko Liberia kimemwondolea uchovu na kukosa kulala, mkazi wa kaunti ya Nimba, kaskazini mashariki mwa Liberia, baada ya mradi wa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD nchini humo kumwezesha sio tu kugeukia kilimo, bali pia kuajiri vijana wengine na hivyo kufanikisha lengo la Umoja wa Mataifa la kuondokana na umaskini.Makala inatupeleka kwenye msitu wa bonde la mto Congo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC wa pili kwa ukubwa duniani unaofyonza kiasi kikubwa cha hewa ukaa, ambako mradi wa Umoja wa Mataifa wa kulinda bayoanuwai na kupambana na umasikini UNREDD unaleta nuru kwa jamii na mazingira.Na mashinani fursa ni yake fursa ni yake Esther Wangoi Mbugua, Mama mfugaji nyuki kutoka Kaunti ya Kajiado nchini Kenya ambaye alizungumza na washirika wetu Redio Domus akieleza kuwa ameweza kujipatia kipato na kumudu mahitaji ya familia yake kupitia mradi wa ufugajji nyuki.Mwenyeji wako niAnold Kayanda karibu!
Baada ya Serikali ya Marekani kutoa tangazo jipya sasa kwamba itaendelea kufadhili huduma zinazolenga vita dhidi ya Virusi vya Ukimwi (VVU), shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na VVU na Ukimwi (UNAIDS) limeeleza kuupokea uamuzi huo kwa furaha na kuuita wa kuokoa maisha. Selina Jerobon na maelezo zaidi.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Umoja wa Mataifa unaeleza kwamba duniani kote kuna vijana bilioni 1.2 wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 24. Idadi hii ni saw ana asilimia 16 ya wakazi wote wa dunia. Kama hiyo haitoshi, idadi hiyo ya vijana inatarajiwa kufikia bilioni 1.3 ifikapo mwaka 2030, yaani miaka mitano ijayo. Lakini changamoto ni kwamba bado serikali nyingi hazijaweza kutumia wingi wa idadi hii kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs. Kwa hali hiyo baadhi ya vijana wameamua kutumia fursa na kujiongeza ili vijana wenzao waweze kufahamu wanachopaswa kufanya ili SDGs zifanikiwe ifikapo 2030. Miongoni mwao ni Paul Siniga, kijana kutoka Tanzania ambaye mwezi Oktoba mwaka huu alikuweko kwenye makao makuu ya UN jijini New York, Marekani kushiriki vikao vya ngazi ya juu. Assumpta Massoi alitaka kufahamu kwa kina ni hatua zipi alichukua hadi kufika aliko sasa.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini DRC katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Bulengo kushuhudia jinsi Umoja wa Mataifa unavyowasaidia wanawake waathrika wa ukatili wa kingoni kuweza kujitegemea na kumudu mahitaji ya familia zao.Kwa mujibu wa takwimu zilizothibitishwa na Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa, takriban watu 5,601 waliuawa nchini Haiti mwaka 2024 kutokana na ghasia za magenge, likiwa ni ongezeko la zaidi ya mauaji 1,000 ya mwaka 2023. Katika moja ya matukio mabaya zaidi na ya kushtua mwaka jana, takriban watu 207 waliuawa mapema Desemba kwenye mauaji yaliyoratibiwa na kiongozi wa genge lenye nguvu la Wharf Jérémie katika eneo la Cité Soleil huko Port-au-Prince. Wengi wa waliouawa walikuwa wazee walioshutumiwa kusababisha kifo cha mtoto wa kiongozi huyo kwa njia ya uchawi.Leo, Umoja wa Mataifa na Serikali ya Lebanon wametoa ombi la nyongeza ya dola milioni 371.4 za kimarekani, zikilenga kutoa msaada wa kuokoa maisha ya walioathiriwa na mzozo wa hivi karibuni na janga la kibinadamu linaloendelea nchini humo.Na Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk leo ameeleza kusikitishwa sana na ongezeko kubwa la watu walionyongwa nchini Iran mwaka jana. Takriban watu 901 wameripotiwa kunyongwa katika mwaka 2024, arobaini wakiwa wamenyongwa katika wiki moja tu ya mwezi Desemba.Mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi, UNFPA tunamsikia Zubaida AbouBaker, mama mkimbizi wa ndani katika kambi ya Tawila iliyoko Darfur Kaskazini nchini Sudan akisimulia machungu yaliyomkumba kufuatia migogoro inayoendelea nchini humo.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Jeshi la polisi Kenya limekanusha kuhusika na visa vya karibuni vya utekaji unaowalenga wakosoaji wa serikali. Watu 74 walitekwa tangu maandamano ya kuipinga serikali, huku 26 wakiwa bado hawajulikani waliko.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Serikali ya Sudan inaitaka Uganda iombe rasmi msamaha, kutokana na kile imekitaja kuwa ujumbe wa kuchukiza na hatari ulioandikwa na mkuu wa jeshi la Uganda Jenerali Muhoozi Kainerugaba, aliyetishia kuivamia Khartoum kijeshi.
Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Syria Geir O. Pedersen bado yuko nchini Syria alikowasili jana Jumapili ikiwa ni wiki moja baada ya wapiganaji wa Hayʼat Tahrir al-Sham (HTS) walioko kwenye orodha ya vikundi vya kigaidi kutwaa mji mkuu Damascus na kusababisha Rais Bashar Al-Assad kukimbia nchi. Ikiwa ni sehemu ya juhudi za Umoja wa Mataifa kuhakikisha mabadiliko ya utawala nchini Syria yanafanyika kwa amani na kuisaidia Syria kutokuingia kwenye mgogoro zaidi, Bwana Pederson aliyewasili jana Damascus hadi sasa ameshakutana na Kamanda wa Utawala Mpya Ahmed al-Sharaa na Waziri Mkuu wa Serikali ya Muda Mohammed al-Bashir.Taarifa iliyotolewa leo na Ofisi yake inasema Pederson ameeleza muhtasari wa matokeo ya Mkutano wa Kimataifa wa Aqaba kuhusu Syria uliofanyika tarehe 14 ya mwezi huu wa Desemba akisisitiza haja ya kuwepo kwa mpito wa kisiasa unaoaminika na unaoongozwa na kumilikiwa na Wasyria wenyewe kama kanuni za azimio 2254 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (2015) zilivyopendekeza. Aidha Mjumbe huyo maalum amesisitiza azma ya Umoja wa Mataifa ya kutoa usaidizi wa kina kwa watu wa Syria.Taarifa imedokeza kuwa Bwana Pedersen ana shughuli nyingi zilizopangwa siku zijazo katika harakati za kusaka suluhu ya amani nchini Syria.
Mwaka 2024 ukielekea ukingoni, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR nchini Uganda limetoa rai kwa jumuiya ya kimataifa kutolisahau taifa hilo la Afrika Mashariki ambalo ni maskani ya idadi kubwa zaidi ya waomba hifadhi na wakimbizi barani Afrika. Rai hiyo iliyotolewa mwishoni mwa wiki inataka ufadhili wa fedha uongezwe ili liweze kuendelea kukirimu watu hao ambao wengi wanakimbia machafuko. Huyo ni Moulid Hujale afisa wa UNHCR nchini Uganda akitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kushikamana na Uganda akiwa kwenye makazi makubwa ya wakimbizi ya Kiryandongo Magharibi mwa nchi hiyo. Anasema kuna mambo matatu muhimu ambayo dunia inapaswa kufahamu kuhusu Uganda na wakimbizi.“Mosi Uganda inahifadhi idadi kubwa zaidi ya wakimbizi na waomba hifadhi Afrika ikiwa na zaidi ya watu milioni 1.7 wengi wao wakitoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na Sudan Kusini.”Zaidi ya hapo ukarimu wa Uganda anasema hauna kipimo“Pili, Uganda ina sera ya kufugua mlango kwa wakimbizi na pia kwa miongo mingi imekuwa ikiwakaribisha watu wanaokimbia machafuko bila kujali utaifa wao. Kitu ambacho ni kikubwa na cha kipekee kuhusu nchi hii ni kwamba wakati wakimbizi wanapowasili hapa hupewa ardhi, mahali pa kuishi na hata kulima mazao kwa ajili ya kujikimu. Wana uhuru wa kutembea na haki ya kuajiriwa. Hawajatengwa lakini wanaishi ndani ya jamii inayowahifadhi. Sera hii ya Uganda inawaruhusu wakimbizi kujumuishwa katika huduma za kitaifa ambapo wanafaidika na elimu na huduma za afya.”Lakini Kutokana na changamoto za fedha Moulid anasema ukarimu huo sasa uko njia panda"Tatu: Ukarimu wa Uganda uko hatarini kwani wakimbizi zaidi wanaingia kutoka nchi jirani. UNHCR, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, liko mashinani kufanya kazi na Serikali ya Uganda kusaidia kutoa msaada wa kuokoa maisha kwa watu hawa. Hata hivyo, rasilimali ni chanche. Tunahitaji msaada wenu ili Uganda iendelee kuwa mfano wa kuigwa kwa dunia nzima.”Kwa nyjibu wa UNHCR licha ya idadi kubwa ya watu na rasilimali kidogo, sera za Uganda zinammanisha kwamba wakimbizi ni sehemu ya maisha ya kijamii na kiuchumi na ongezeko la rasilimali litakidhi haja za waliopo sasa na watakaokuja.
Serikali ya Albanese imetangaza mfumo mpya waku lazimisha mitandao yakidigitali yakufidia vyombo vya utangazaji vya Australia kwa matumizi ya habari zao.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Mazungumzo ya kuunda serikali ya mseto Sudan Kusini, yame kwama baada ya pande husika kuto afikiana kuhusu jinsi wata wagawa mamlaka.
Mkutano wa 29 wa mkataba wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi COP29 unaofanyika Baku Aberbaijana leo umejikita na ongezeko la gesi ya methane ambayo kwa kiasi kikubwa inachangiwa na shughuli za binadamu na nini kifanyike kuidhibiti. FKulingana na ripoti iliyozinduliwa leo na shirika la Umoja wa Mataifa wa mazingira UNEP katika mkutano huo, mfumo wa teknolojia ya hali ya juu ambao unatambua uvujaji mkubwa wa gesi ya methane umewasilisha tarifa 1,200 kwa serikali na makampuni katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, lakini ni asilimia moja tu ya taarifa hizo ndizo zilizofanyiwa kazi.Ripoti hiyo mpya iliyopewa jina “Jicho kwenye methane: Haionekani lakini inashuhudiwa” inasema licha ya ahadi zilizotolewa chini ya makubaliano ya ahadi za kimataifa za kupunguza uzalishaji wa gesi ya methane kwa asilimia 30 ifikapo 2030 hatua zinazochukuliwa hazitoshelezi kupunguza gesi hiyo.Ripoti imeangazia tahadhari za methane kutoka kwenye Mfumo wa Tahadhari na hatua dhidi ya Methane MARS, ambayo ni sehemu ya UNEP ya uangalizi wa kimataifa wa uzalishaji wa methane IMEO ambayo unawakilisha fursa ambazo haijatumiwa kwa hatua za haraka dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.Akizindua ripoti hiyo Inger Andersen, Mkurugenzi Mtendaji wa UNEP, amesema ili kuwa na nafasi yoyote ya kudhibiti ongezeko la joto duniani, uzalishaji wa methane lazima ushuke, na ushuke haraka."Tunapozingatia kuwa ni asilimia 1 tu ya taarifa 1200 ambazo tulitoa ndizo zilisababisha hatua kuchukuliwa, basi hauitaji kuwa mtaalamu wa hesabu ili kuhesabu ushindi mkubwa unaowezekana hapa. Tuna mifumo iliyothibitishwa ya kutambua uvujaji Mkubwa wa gesi ya methane ili uweze kukomeshwa haraka, mara nyingi kwa ukarabati rahisi na wakati mwingine tunazungumza juu ya kukaza mipira au kubadilisha vichungi.”Ameongeza, kuwa "Serikali na makampuni ya mafuta na gesi ambayo sehemu kubwa ya uchumi wa dunia bado inawategemea lazima waache kupiga domo kwa changamoto hii wakati majawabu yanawatazama usoni. Badala yake, wanapaswa kutambua fursa muhimu ambayo mfumo huu unatoa na kuanza kuchukua hatua kutokana na taarifa kwa kuziba uvujaji ambao unamwaga gesi ya methane ya joto kwenye angahewa.”Amehitimisha kwa kusema, "Serikali na sekta binafsi lazima zizuie uzalishaji wa methane, na lazima zifanye hivyo sasa."Gesi ya Methane kwenye angahewa ni kichocheo cha pili kikubwa cha ongezeko la joto duniani baada ya hewa ya ukaa au CO2 na ina nguvu zaidi ya mara 80 kuliko hewa ya ukaa katika kusambaa kwa muda mfupi.UNEP imesisitiza kuwa utoaji wa gesi ya methane duniani lazima upunguzwe kwa asilimia 40 hadi 45 ifikapo 2030 ili kufikia njia za gharama nafuu zinazopunguza ongezeko la joto duniani hadi kufikia nyuzi joto 1.5°C.Bado taarifa za sayansi za hivi karibuni zinaonyesha viwango vya angahewa vya methane vimepanda kwa kasi iliyovunja rekodi katika kipindi cha miaka 5 iliyopita.
Hii leo jaridani tunaangazia machafuko katika ukanda wa Gaza na masuala ya afya nchini Kenya. Makala inatupeleka nchini DRC kumsikia mkimbizi mjasiriamali na mnufaika wa pesa taslimu kutoka WFP, na mashinani tunakupeleka nchini Lebanonon kwa waathirika wa vita.Kadri siku zinavyozidi kusonga mbele, hali ya usalama na kibinadamu huko Ukanda wa Gaza inazidi kuzorota huku raia na hata wafanyakazi wa kutoa misaada wakisalia wamepigwa butwaa kwani mashambulizi kutoka Israeli yanaendelea kila uchao.Serikali ya Kaunti ya Lamu katika pwani ya kaskazini ya Kenya, kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), wanaendesha shughuli ya kuwafikia wanajamii ili kubadilishana taarifa kuhusu jinsi watu wanaweza kuwalinda watoto na familia zao dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu na kutoa huduma za maji, vifaa vya kujisafi na usafi kwa jamii zilizoathirika. Kutoka katika video iliyoandaliwa na UNICEF.Makala George Musubao, mwandishi wetu wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC anazungumza na mkimbizi Esther Josephine aliyeko kambi ya Bulengo nje kidogo ya mji wa Goma, jimboni Kivu Kaskazini ambaye amenufaika na msaada kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP.Mashinani tutakuwa Lebanon, kumsikia mama aliyenusurika kifo na wanawe kutokana na makombora ya Israel.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Serikali ya Kaunti ya Lamu katika pwani ya kaskazini ya Kenya, kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), wanaendesha shughuli ya kuwafikia wanajamii ili kubadilishana taarifa kuhusu jinsi watu wanaweza kuwalinda watoto na familia zao dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu na kutoa huduma za maji, vifaa vya kujisafi na usafi kwa jamii zilizoathirika. Kutoka katika video iliyoandaliwa na UNICEF.Wamekaa chini ya mti, wanawake kwa wanaume. Nyuma ni nyumba ya makuti na matumbawe, Lamu, Pwani ya Kenya. Muelimishaji wa masuala ya afya anawaeleza namna ya kuweka mazingira safi ili kupambana na kipindupindu. Mwanajuma Kahidi yamewahi kumkuta. Anaposema Cholera anamaanisha hiyo hiyo kipindupindu iliyokuwa imetishia Uhai wake na familia yake.“Nilipopata maambukizi ya Kipindupindu nilihisi siko sawa kwa sababu nilikosa nguvu na nikakosa raha na nikapoteza nuru ya macho ndio nikakimbilia hospitali. Huo ugonjwa ulipitia kwenye maji na chakula. Mimi na watoto wangu tulipatwa na kipindupindu. Mimi nilichukua siku tatu. Watoto wangu wote mmoja baada ya mwingine walichukua siku nane nane. Madaktari wanajibidiisha sana juu yetu. Baada ya siku kadhaa wanajitokeza na kutuuliza, je mnafanya juhudi tulizowaambia?”Leila Abrar ni Mshauri katika UNICEF anayehusika na mabadiliko ya tabia katika jamii anasema, "kiwango cha ufahamu ni cha juu zaidi kuliko tulipokuwa tunaanza uelimishaji. Na pia tunaambiwa kuwa kiwango cha unawaji mikono kimeongezeka. Mabadiliko ya kijamii na tabia kwa kweli yanahusu kushirikisha jamii, kuwezesha jamii.
Serikali imethibitisha kuwa inashikilia mafao ya Medicare ambayo hayaja daiwa yenye thamani yama milioni ya dola, kwa sababu wagonjwa hawajatoa taarifa zao za benki ili wapokee hela hizo.
Serikali ya Shirikisho ya tetea takwimu zake za utoaji wa ajira milioni moja, wakati upinzani una sisitiza kuwa asilimia kubwa ya ajira hizo zime fadhiliwa na serikali ya shirikisho.
KiTiKi yaani Kilimo Tija Kigoma ni mradi wa kuimarisha mnyororo wa thamani ya kilimo cha wakulima wadogo, usawa wa jinsia na amani katika mkoa wa Kioma unaohifadhi wakimbizi zaidi kutoka Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Serikali na watu wa Jamhuri ya Korea wamechangia Dola za Marekani milioni 6 kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) ili kuimarisha kilimo cha wakulima wadogo na kuimarisha uhakikika wa chakula na lishe miongoni mwa wakimbizi na jamii zinazowahifadhi mjini Kigoma kwa miaka minne tangu mwishoni mwa mwaka juzi 2022. Anold Kayanda kupitia video ya WFP Tanzania anatupeleka mkoani Kigoma kaskazini magharibi mwa Tanzania kusikia manufaa ya mradi wa Kilimo.