POPULARITY
Rais wa Burundi Évariste Ndayishimiye achaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika (AU) mwaka 2026, ziara ya ujumbe wa Umoja wa Ulaya huko DRC, vijana wa Afrika wahadaiwa kupewa kazi nzuri Urusi, na kulazimishwa kupigana vita Ukraine, raia 18 wa Senegal na mmoja kutoka Ufaransa wahukumiwa kwa kuzua fujo wakati wa mechi ya fainali AFCON jijini Rabat. Mkutano wa kimataifa kati ya India na Ufaransa kuhusu akili mnemba, pia tishio la Trump kuishambulia Iran
Aliporejea madarakani Januari 20 2025, kwa mara ya pili Trump aliiondoa Marekani katika mkataba wa tabianchi wa Paris wa 2015. Mwaka wa 2025, Washington haikuwatuma maafisa wake wa juu katika mkutano wa tabianchi wa COP30, uliofanyika Belem, Brazil. Na sasa wiki chache zilizopita, utawala wa Trump ulitangaza kuiondoa Marekani katika mashirika 66 ya kimataifa, ikiwemo ile ya UNFCCC.
Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya Redio Duniani likitupeleka nchini Tanzania kusikia jinsi ambavyo redio inavyochochea maendeleo ya kijamii, nchini Uganda kumsikia mkimbizi kutoka DRC, na katika ukanda wa Gaza ambako redio inaunganisha tena jamii ndani ya vifusi.Leo ni siku ya redio duniani ambayo msingi wake unatokana na kuanzishwa kwa redio ya Umoja wa Mataifa tarehe 13 Februari mwaka 1946 jijini New York, Marekani. Kwa mantiki hiyo ikiwa mwaka huu redio hiyo ya Umoja wa Mataifa inatimiza miaka 80 tumeangazia mchango wa vipingi vyake vilivyokuwa vinarushwa na redio zingine ikiwemo iliyokuwa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) nchini Tanzania wakati huo. Assumpta Massoi amemulika suala hilo.Katika maeneo ya migogoro, duniani redio huwa nguzo ya utulivu na wakati mwingine daraja la kuokoa maisha. Na ndivyo ilivyokuwa kwa mkimbizi Bahati Yohane kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kwani kwake, redio haikuwa tu combo cha habari ilikuwa dira ya kuokoa maisha yake.Kabla ya vita vya sasa kuanza katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina lilalokaliwa kimabavu na Israel, Redio ilikuwa chombo muhimu kwa umma na kwa hakika umuhimu wake haujakoma isipokuwa huduma ya matangazo ya redio ndio iliyokuwa imekoma kutokana na vituo vya redio kusambaratishwa kwa makombora, lakini sasa juhudi zinafanyika kuirejesha huduma hiyo muhimu.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Leo ni siku ya redio duniani ambayo msingi wake unatokana na kuanzishwa kwa redio ya Umoja wa Mataifa tarehe 13 Februari mwaka 1946 jijini New York, Marekani. Kwa mantiki hiyo ikiwa mwaka huu redio hiyo ya Umoja wa Mataifa inatimiza miaka 80 tumeangazia mchango wa vipingi vyake vilivyokuwa vinarushwa na redio zingine ikiwemo iliyokuwa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) nchini Tanzania wakati huo. Assumpta Massoi amemulika suala hilo.
Upinzani dhidi ya mpango waku ruhusu kampuni za Marekani kupata madini muhimu nchini Jamhuri yakidemokrasia ya Congo, una ongezeka baada ya Rais Tshisekedi kurejea nchini kutoka mkutano wa madini ulio fanyika Marekani wiki iliyopita.
Kwa habari na melezo zaidi, tembelea tovuti ya sbs.com.au.
Demokrasia na utaratibu wa kimataifa unaozingatia sheria ziko hatarini, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya Shirika la haki za binadamu ama Human Rights Watch. Kuna msisitizo mahususi juu ya Marekani na kile ambacho chombo cha kimataifa kinaelezea kama kudorora kwa haki za binadamu, lakini pia kuna tahadhari juu ya Australia. Sera za uhamiaji na kuwekwa kizuizini kwa vijana za Australia zinaorodheshwa kama 'mapungufu makubwa', zikionyeshwa kuwa ni demokrasia pekee ya Magharibi isiyo na sheria ya kitaifa ya haki za binadamu.
Rais wa Rwanda Paul Kagame asema nchi yake haitatizwi na vitisho vya kuwekewa vikwazo na Jumuiya ya Kimataifa, mkutano unaolenga kuimarisha ushirikiano wa kibishara hasa kwenye sekta ya madini kati ya Marekani na nchi za Afrika wafanyika Washington, tumeangazia siasa za Uganda, yaliyojiri nchini Kenya, hali ya kibinadamu yaendelea kuwa mbaya nchini Sudan, rais wa Nigeria Bola Tinubu aagiza wanajeshi kupelekwa katika jimbo la Kwara kulinda amani, mkutano wa Oman kati ya Marekani na Iran.
*AL-Islam Gaddafi auwawa Libya *Vikwazo vimewekwa na Marekani dhidi ya watu wanaodaiwa kuchochea vita Sudan
Jaridani hii leo tuna Muhtasari wa Habari ukiangazia hali ya njaa Sudan, mchango wa Marekani dhidi ya VVU/ Ukimwi na kauli ya UNRWA kufuatia taarifa potofu dhidi ya shirika hilo. Halikadhalika mada kwa kina kutoka AfyaAFRIKA.Maeneo mawili zaidi katika jimbo la Darfur Kaskazini ya Um Baru na Kernoi sasa yameingia katika baa la njaa kufuatia utapiamlo wa kupindukia au unyafuzi kuvuka wiwango vya kutokuwa na uhakika wa chakula.Shirika la Umoja wa mataifa linalohusika na vita dhidi ya ukimwi UNAIDS limekaribisha kwa dhati hatua ya Marekani kutia saini kuwa sheria kifurushi cha matumizi ya kimataifa chenye thamani ya dola bilioni 5.88, kwa ajili ya hatua za kimataifa za kukabiliana na virusi vya ukimwi VVU .Kamishina Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA Phillippe Lazzarini amesema taarifa potofu dhidi ya UNRWA zinaendelea kulenga shirika hilo katikati ya mgogoro Gaza ikiwemo madai ya hivi karibuni kabisa, yaliyoibuliwa na video ya jeshi la Israel ikionesha mifuko mitupu ya unga karibu na mabomu, ambapo amesema ni taarifa za uongo na hazijadhibitishwa.Katika Mada kwa Kina: Kuelekea siku ya kutokomeza FGM kesho Februari 6, tunazungumza na Catherine Mootian, Muasisi na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la kiraia la AfyAfrika la huko Narok nchini Kenya. Yeye ni manusura wa FGM aliyeamua kuchukua hatua kuepusha wengine.
Hii leo jaridani kesho ikiwa ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu ugonjwa wa saratani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kumulika hatua ambazo ni uzinduzi wa Mpango wa Utekelezaji wa Kitaifa wa kutokomeza saratani ifikapo mwaka 2030.Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani, WHO, leo limetoa ombi la dola bilioni moja ili kukabiliana na majanga ya afya mwaka 2026 katika dharura 36 zilizo mbaya zaidi duniani. Ombi hilo linalenga kusaidia huduma za afya zinazookoa maisha katika nchi zilizoathiriwa na migogoro na majanga, zikiwemo Gaza, Sudan, Haiti na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.Mashariki ya Kati, wakati muda ukiendelea kuyoyoma kwa maelfu ya wagonjwa mahututi huko Gaza, kufunguliwa tena kwa kivuko cha Rafah kunaleta mwanga wa matumaini. Kivuko hicho kilifunguliwa Jumatatu baada ya kufungwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, chini ya mpango wa amani unaoungwa mkono na Marekani, na kuruhusu uhamisho wa kwanza wa wagonjwa tangu mwaka 2025.Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF leo liimesema linaongeza juhudi zake zamsaada wa msimu wa baridi nchini Ukraine huku watoto na familia wakikabiliwa na kukatika kwa umeme, kukosa vipasha joto na maji kufuatia mashambulizi yanayoendelea dhidi ya miundombinu ya nishati na baridi kali. Tangu Novemba, shirika hilo limesambaza jenereta 106 kote nchini kusaidia huduma za maji na mifumo ya kupasha joto, huku takribani jenereta 150 zaidi zikitarajiwa kuwasili katika wiki zijazo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "KUNVI"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Kwa maelezo ama habari zaidi elekea kwenye tovuti yetu ya sbs.com.au/swahili.
Makala hii imeangazia kutomia kwa mwaka mmoja tangu waasi wa AFC/M23 waudhibiti mji wa Goma, Rwanda yaishitaki Uingereza kuhusu mkataba unaohusu wakimbizi, mapigano yashuhudiwa huko Sudan, na katika ukanda wa Afrika magharibi tumeangazia shambulio la watu wenye silaha katika uwanja wa ndege wa Niamey, ECOWAS yaiondolea vikwazo nchi ya Guinea, na tishio la Marekani kuishambulia Iran na mengine zaidi.
Watanzania bado wanakabiliwa na athari za baada ya uchaguzi wa hivi karibuni, huku wanahabari wakizuiwa kuripoti usimulizi mbele ya tume ya uchunguzi. Makubaliano kati ya Congo na Marekani kuhusu madini yana dosari kubwa.
Vitisho vya kijeshi vya Donald Trump na vita vya kibiashara vinavyoandika wasiwasi kwa washirika, baadhi ya wataalamu wanatoa wito wa kufikiria upya ushirikiano wa muda mrefu wa Australia na Marekani. Mjadala umeimarishwa na hotuba ya Waziri Mkuu wa Canada, Mark Carney, katika Jukwaa la Kiuchumi Duniani, ambayo iliwashauri nchi zenye nguvu ya kati kupinga kudhoofisha maadili yao kwa maamuzi ya nguvu kubwa za dunia.
Hii leo jaridani tunaangazia….mafunzo ya usalama katika Ziwa Victoria, na harakati za Shirika la kiraia la kusongesha elimu kwa watoto wa kike, CAMFED za kuwawezesha wanafunzi wa kike nchini Tanzania.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukumbuka waathirika pamoja na manusura wa mauaji ya kimbari ya holokosti hususan yale yaliyofanywa na manazi wa kijerumani, hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa katika ukumbi wa Baraza Kuu kumefanyika kumbukizi ikileta pamoja manusura waliotoa shuhuda za waliyopitia wakikimbia maeneo kadhaa ikiwemo Austria baada ya kutwaliwa na wajerumani.Ziwa Viktoria barani Afrika, licha ya kuwa mhimili muhimu wa maisha kwa zaidi ya watu milioni 40 nchini Kenya, Uganda na Tanzania, bado linakabiliwa na vitisho vihusianavyo na biashara haramu za magendo, usafirishaji haramu binadamu na uvuvi haramu. Ili kupatia suluhu changamoto hiyo Ofisi ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na dawa za kulevya na utekelezaji wa sheria (INL) ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani na Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, (IOM), na walinzi wa pwani wa Kenya wamechukua hatua.Nchini Tanzania shirika la kiraia la kuendeleza elimu kwa watoto wa kike, CAMFED limeendelea kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs kwa kuwezesha wanafunzi wa kike kuimarika sio tu kimasomo darasani bali pia stadi za maisha na hatimaye wawajengee uwezo wenzao.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Ziwa Viktoria barani Afrika, licha ya kuwa mhimili muhimu wa maisha kwa zaidi ya watu milioni 40 nchini Kenya, Uganda na Tanzania, bado linakabiliwa na vitisho vihusianavyo na biashara haramu za magendo, usafirishaji haramu binadamu na uvuvi haramu. Ili kupatia suluhu changamoto hiyo Ofisi ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na dawa za kulevya na utekelezaji wa sheria (INL) ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani na Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, (IOM), na walinzi wa pwani wa Kenya wamechukua hatua. Je ni hatua zipi? Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi.
Wiki iliopita, ilijiondoa kwenye shirika la afya duniani licha ya onyo kuwa hatua hiyo itaathiri ufadhili kwenye sekta ya afya duniani. Wiki chache zilizopita, rais Donald Trump alitangaza pia kuwa Marekani itajiondoa kwenye mashirika 66 ya kimataifa, yakiwemo yaliyo chini ya Umoja wa Mataifa
Wiki iliopita, ilijiondoa kwenye shirika la afya duniani licha ya onyo kuwa hatua hiyo itaathiri ufadhili kwenye sekta ya afya duniani. Wiki chache zilizopita, rais Donald Trump alitangaza pia kuwa Marekani itajiondoa kwenye mashirika 66 ya kimataifa, yakiwemo yaliyo chini ya Umoja wa Mataifa
Katika makala utasikia polisi wa Uganda waendelea kuwakamata washirika wa karibu wa mwanasiasa wa upinzani Robert Kyagulanyi Ssentamu baada ya uchaguzi wa wiki iliopita, waasi wa AFC/M23 Kujiondoa kwenye mji wa Uvira mashariki mwa DRCongo, nini kinaendelea? Siasa za Kenya, Tanzania na hali ya sasa nchini Sudan; wanajihadi kuwateka waumini zaidi ya mia moja na sitini wakiwa kanisani kule Nigeria, na kutamatika kwa jukwaa la Uchumi duniani huko Davos
Msikilizaji mataifa makubwa kama Marekani, China, Urusi na Ulaya yanaendelea kushindana kiuchumi, kuanzia kwenye biashara, teknolojia, nishati na rasilimali. Lakini je, ushindani wao unaathiri vipi uchumi wa dunia? Leo kwenye Makala ya Gurudumu la Uchumi tunajadili, “Athari za Kiuchumi kwa Dunia Zitokanazo na Ushindani wa Maslahi ya Kiuchumi kati ya Mataifa Makubwa.”
Msikilizaji mataifa makubwa kama Marekani, China, Urusi na Ulaya yanaendelea kushindana kiuchumi, kuanzia kwenye biashara, teknolojia, nishati na rasilimali. Lakini je, ushindani wao unaathiri vipi uchumi wa dunia? Leo kwenye Makala ya Gurudumu la Uchumi tunajadili, “Athari za Kiuchumi kwa Dunia Zitokanazo na Ushindani wa Maslahi ya Kiuchumi kati ya Mataifa Makubwa.”
Makala hii imeangazia uchaguzi wa nchini Uganda matokeo yakisubiriwa kutolewa leo, mkutano wa Lome nchini Togo kuhusu mustakabali wa amani ya mashariki mwa DR Congo, hali ya nchini Sudan, Somalia, na ugunduzi wa kaburi la pamoja lenye miili ya wahamiaji 21 huko Libya, hotuba ya rais Macron mbele ya maafisa wa jeshi la nchi yake na kauli ya Marekani kuhusu waandamanaji wa Iran
Agizo la kiutendaji lililosainiwa na rais wa Marekani linaagiza Marekani kujiondoa kutoka kwa jumla ya mashirika 66, karibu nusu yake ambayo yana uhusiano na Umoja wa Mataifa, Ikulu ya White House ilisema wiki iliyopita. Miongoni mwa hayo ni Mkataba wa Mfumo wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa (UNFCCC), mkataba wa msingi wa mikataba mingine yote ya kimataifa ya hali ya hewa, uliohitimishwa mwaka wa 1992 katika Mkutano wa Rio Earth.
Agizo la kiutendaji lililosainiwa na rais wa Marekani linaagiza Marekani kujiondoa kutoka kwa jumla ya mashirika 66, karibu nusu yake ambayo yana uhusiano na Umoja wa Mataifa, Ikulu ya White House ilisema wiki iliyopita. Miongoni mwa hayo ni Mkataba wa Mfumo wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa (UNFCCC), mkataba wa msingi wa mikataba mingine yote ya kimataifa ya hali ya hewa, uliohitimishwa mwaka wa 1992 katika Mkutano wa Rio Earth.
**Kevin Rudd ajiuzulu kama balozi wa Marekani... **Mlipo wa bomu waua maafisa wa polisi kaskazini mwa Pakistan... **Meta yazua shauku kuhusu Australia kuongeza umri wa kutumia mitandao ya kijamii. Kwa habari ama maelezo zaidi tembelea tovuti yetu sbs.com.au/swahili.
Miongoni mwa matukio makubwa ni pamoja na kukamatwa kwa aliyekuwa rais wa Venezuela Nicolas Maduro, kubanduliwa kwa timu ya taifa ya DRCongo kwenye michuano ya AFCON 2025, vifo vya wakimbizi wa Congo Kinshasa katika kambi huko Burundi, siasa za Tanzania, Kenya na Uganda kuelekea uchaguzi wa January 15 hali ya nchini Sudan kusini, Rais Faustin Archange Touadera kutangazwa mshindi wa Uchaguzi wa urais hivi karibuni na kauli ya Urusi kuhusu washirika wa Ukraine, Ulaya
Karibu katika muziki Ijumaa, makala maalumu ya RFI Kiswahili inayokuletea vibao vya kukumbukwa vilivyoacha alama kubwa katika historia ya muziki wa dunia.Wiki hii tunasafiri kimuziki kutoka Marekani, kupitia Karibiani, hadi Afrika Mashariki na Afrika ya Kati, tukifurahia nyimbo zenye ujumbe wa furaha, mapenzi, imani na utu. Safari yetu inaanza nchini Marekani kwa kibao “Celebration” cha kundi la Kool & The Gang wimbo uliogeuka kuwa nembo ya sherehe duniani kote, ukiwahamasisha watu kusahau huzuni na kusherehekea maisha. Kutoka hapo tunatua Karibiani kupitia “Jamaica Farewell” wa Don Williams, wimbo wenye ladha ya country na mguso wa kisiwa, unaoelezea mapenzi, kumbukumbu na uchungu wa kuaga ardhi unayoipenda. Safari inaendelea nyumbani Afrika Mashariki kwa kibao cha Kiswahili “Mulofa wangu” cha marehemu Daudi Kabaka kutoka Kenya, wimbo wa mapenzi uliojaa hisia nzito na lugha tamu, unaothibitisha ubora wa muziki wa zamani wa Afrika Mashariki. Tunafunga safari yetu Afrika ya Kati kwa “Le Bon Samaritain” wa gwiji wa rumba Papa Noël kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), wimbo unaochanganya ala za gitaa za kipekee na ujumbe wa utu, huruma na kusaidiana katika jamii.
Karibu katika muziki Ijumaa, makala maalumu ya RFI Kiswahili inayokuletea vibao vya kukumbukwa vilivyoacha alama kubwa katika historia ya muziki wa dunia.Wiki hii tunasafiri kimuziki kutoka Marekani, kupitia Karibiani, hadi Afrika Mashariki na Afrika ya Kati, tukifurahia nyimbo zenye ujumbe wa furaha, mapenzi, imani na utu. Safari yetu inaanza nchini Marekani kwa kibao “Celebration” cha kundi la Kool & The Gang wimbo uliogeuka kuwa nembo ya sherehe duniani kote, ukiwahamasisha watu kusahau huzuni na kusherehekea maisha. Kutoka hapo tunatua Karibiani kupitia “Jamaica Farewell” wa Don Williams, wimbo wenye ladha ya country na mguso wa kisiwa, unaoelezea mapenzi, kumbukumbu na uchungu wa kuaga ardhi unayoipenda. Safari inaendelea nyumbani Afrika Mashariki kwa kibao cha Kiswahili “Mulofa wangu” cha marehemu Daudi Kabaka kutoka Kenya, wimbo wa mapenzi uliojaa hisia nzito na lugha tamu, unaothibitisha ubora wa muziki wa zamani wa Afrika Mashariki. Tunafunga safari yetu Afrika ya Kati kwa “Le Bon Samaritain” wa gwiji wa rumba Papa Noël kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), wimbo unaochanganya ala za gitaa za kipekee na ujumbe wa utu, huruma na kusaidiana katika jamii.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika Chata iliyoanzisha Umoja wa Mataifa miaka 80 iliyopita baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia na kukutanisha mataifa 50 San Francisco hapa Marekani na kupitisha Chata hiyo, ikilengaa kuzuia vita na kujenga uhusiano mwema baina ya mataifa. Operesheni ya kijeshi iliyofanywa na Marekani tarehe 3Januari nchini Venezuela ambayo ilimchukua Rais wa nchi hiyo Nicolàs Madura na hapo jana walimfikisha mahakamani jijini New York Marekani. Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya masuala ya haki za binadamu OHCHR kupitia msemaji wake Revina Shamdasani akizungumza na waandishi wa habari jijini Geneva Uswisi amewaeleza kuwa kitendo hicho ni uvunjaji wa sheria za kimataifa na wala kisingizio cha haki za binadamu kisitumike.Tukisalia na Venezuela, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya masuala ya Kiutu OCHA imeeleza inaendelea kuwasaidia wenye uhitaji nchini humo na mwaka jana ili ainisha zaidi ya wahitaji milioni 8. Msemaji wa OCHA Jens Laerke amewaambia waandishi wa habari jijini Geneva kuwa “Kati ya hao watu milioni nane, "900,000 wamewekwa katika makundi ya juu sana ya wenye uhitaji wa sekta mbalimbali ... kama vile chakula, lishe, elimu, na huduma za afya, kimsingi mambo yote ambayo nchi ya Venezuela halijaweza kutoa kwa raia wake kwa miaka mingi”.Msemaji wa Umoja wa Mataifa ameeleza kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anafuatilia akiwa na wasiwasi mkubwa maandamano yanayoendelea nchini Iran. Guterres amesikitishwa na ripoti za vifo na majeruhi kutokana na mapigano kati ya vikosi vya usalama na waandamanaji, akitaka mamlaka zizingatie haki ya kuandamanana na kukusanyika kwa amani.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Miaka 80 iliyopita baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia, mataifa 50 yalikutana huko San Francisco hapa nchini Marekani na kupitisha Chata iliyoanzisha Umoja wa Mataifa. Miongoni mwa malengo ni kuzuia vita na kujenga uhusiano mwema baina ya mataifa. Mathalani kuepusha nchi moja kuvamia nchi nyingine na kulinda haki za binadamu. Leo hii Chata hiyo imeendelea kusiginwa na kilichoibua mjadala zaidi ni tukio la Januari 3 la Vikosi Maalum vya Marekani kuingia Venezuela na kumtwaa Rais wa nchi hiyo Nicolas Maduro pamoja na mkewe kwa madai ya kwamba wanatakiwa wajibu tuhuma nchini MArekani za uhalifu mkubwa ikiwemo usafirishaji wa dawa za kulevya. Je Chata hiyo inasema nini? Assumpta Massoi na Rashid Malekela wanapitia baadhi ya vifungu pamoja na yaliyojiri baada ya hatua ya Marekani.
** Rais wa Venezuela Nicolas Maduro na mkewe walikana hatia katika mahakama ya Marekani. ** Mtu anayedaiwa kuwa mfyatuliwa wa risasi Bondi amehamishwa kwenda gereza la Goulbourn supermax. **Na Denmark yaendelea kuikashaifu Marekani kuhusu manoni yao ya Greenland.
Hii leo jaridani tunaangazia hali nchini Venezuela operesheni ya kijeshi ya Marekani, afya ya uzazi Tana River nchini Kenya, na wanawake wakimbizi wa DR Congo wanaopitia ukatili wa kijinsia wakikimbia machafuko. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana leo katika kikao cha dharura baada ya operesheni ya kijeshi ya Marekani nchini Venezuela tarehe 3 Januari mwaka huu, hatua iliyozua hofu ya kuongezeka kwa hali ya kutokuwa na utulivu nchini humo na katika eneo zima.Huko nchini Kenya katika kaunti ya Tana River, hali mbaya ya hewa na migogoro imesababisha takriban watu 140,000 kuyahama makazi yao. Upatikanaji wa huduma za afya nao umekuwa mgumu na kuongeza magumu hususani kwa wanawake na watoto. Katika kukabiliana na hali hiyo Wizara ya Afya nchini humo inashirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO katika kutoa huduma za afya kipaumbele kikielekezwa kwenye masuala ya uzazi salama.Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi (UNFPA), nchini Burundi, linaongeza juhudi zake kukabiliana na mahitaji yanayoongezeka ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) wanaokimbia mapigano yanayoendelea mashariki taifa hilo la Maziwa Makuu ili kulinda afya, usalama na utu wao na wa jamii zinazowapokea.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekutana leo katika kikao cha dharura baada ya operesheni ya kijeshi ya Marekani nchini Venezuela tarehe 3 Januari mwaka huu, hatua iliyozua hofu ya kuongezeka kwa hali ya kutokuwa na utulivu nchini humo na katika eneo zima. Leah Mushi anatufahamisha zaidi.
Rais wa Marekani Donald Trump ameamuru shambulio kubwa dhidi ya Venezuela kuwakamata Rais wa Venezuela Nicolás Maduro na mke wake. Wametuhumiwa na makosa ya dawa za kulevya na silaha huko New York. Hatua hiyo imepongezwa na washirika wa Bw. Trump, lakini imelaaniwa sana na mataifa mengi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ametoa ujumbe mzito wa Mwaka Mpya kwa ulimwengu akisema ulimwengu uko katika njia panda, ukikabiliwa na machafuko, sintofahamu na migawanyiko mikubwa na hivyo kutoa wito kwa wanadamu kuinuka pamoja kwa ajili ya haki, ubinadamu na amani. Karibu Anold Kayanda kwa maelezo zaidi.(Taarifa ya Anold Kayanda)Katika ujumbe wake wa video uliosambazwa leo asubuhi saa za New York, Marekani, kwa ajili ya mwaka mpya wa 2026, Katibu Mkuu wa Umoja wa Maraifa anauanza ujumbe wake kwa kusema, “tunapoingia mwaka mpya, dunia iko njia panda.” Amesema dunia inakumbwa na vurugu zinazoendelea, athari kubwa za mabadiliko ya tabianchi pamoja na ukiukwaji wa kimfumo wa sheria za kimataifa hali ambayo, kwa mujibu wake, inatishia misingi inayounganisha binadamu kama familia moja ya dunia.Guterres amesema watu kote ulimwenguni wanaendelea kujiuliza iwapo viongozi wao wanasikiliza kilio cha wananchi na kama wako tayari kuchukua hatua za dhati kukabiliana na changamoto hizi.Akigeukia takwimu, Katibu Mkuu ameeleza kuwa matumizi ya kijeshi duniani yamefikia dola trilioni 2.7, ongezeko la karibu asilimia kumi kiwango ambacho ni mara kumi na tatu zaidi ya misaada yote ya maendeleo, na kinacholingana na Pato la Bidhaa za ndani la Bara zima la Afrika.Amesema ongezeko hilo linatokea wakati dunia ikishuhudia mizozo mikubwa kwa viwango ambavyo havijawahi kuonekana tangu Vita Vikuu Vya Pili Vya Dunia.Kutokana na hali hiyo, Katibu Mkuu ametoa wito kwa dunia kutumia mwanzo wa mwaka mpya kuweka vipaumbele sahihi, akisisitiza kuwa ulimwengu salama hujengwa kwa kuwekeza zaidi katika kupambana na umaskini badala ya kuwekeza katika vita.Guterres amesisitiza kuwa dunia ina rasilimali za kutosha kuinua maisha ya watu, kuponya sayari na kujenga mustakabali wa amani na haki, endapo tu zitatumika ipasavyo.Kwa mwaka 2026, amewataka viongozi wa dunia kuwa makini zaidi na kufanya uamuzi unaoweka mbele maslahi ya watu na mazingira badala ya kuendeleza mateso.Aidha, amewahimiza raia wote duniani kushiriki kikamilifu katika kujenga dunia bora, akisema mustakabali wa ubinadamu unategemea ujasiri wa pamoja wa kuchukua hatua.Katika kuhitimisha ujumbe wake, Katibu Mkuu ametoa wito wa mshikamano kwa ajili ya haki, ubinadamu na amani duniani.
Viongozi wa dunia wamesifu mkutano wa kwanza wa G20 kufanyika Afrika kama ushindi kwa ushirikiano wa kimataifa, hata walipokuwa wakizungumzia changamoto za mabadiliko ya tabianchi, ukosefu wa usawa na vita, dhidi ya muktadha wa ushindani unaobadilika wa kidiplomasia. Kutokuwepo kwa Rais Donald Trump kumewafanya watu kujiuliza maswali kuhusu nafasi ya Marekani katika mpangilio wa dunia unaobadilika.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Bi. Lucy Githinji, mkazi wa jimbo la New Jersey nchini Marekani amezungumza na idhaa hii baada ya matembezi ya hiari kwa ajili ya kuhamasisha jamii kuhusu saratani ya titi, akisema hakika dawa zinafanya kazi.Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Kibinadamu nchini Sudan, Denise Brown amesema ni kweli wamepokea ripoti za mauaji ya baadhi ya wahudumu wa kujitolea huko El Fasher jimboni Darfur wakati huu ambapo mji huo umetwaliwa na wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka, (RSF).Kimbunga Melissa kimepungua nguvu baada ya kutua nchini Jamaica kama kimbunga cha kiwango cha 5, na kuvunja rekodi ya kimbunga chenye nguvu zaidi, kabla ya kuelekea kaskazini mashariki kupita Cuba hadi Bahamas, na kusababisha mafuriko makubwa, uharibifu na kukatika kwa umeme katika maeneo mbalimbali ya Karibea na Amerika ya Kati.Nchini Cameroon, kufuatia mauaji ya raia wakati wa maandamano ya kupinga kutangazwa kwa Paul Biya kuwa mshindi wa kiti cha Urais kwenye uchaguzi uliofanyika Oktoba 12, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu imeeleza wasiwasi wake juu ya ripoti za vifo hivyo.Na katika Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "SUMIA."Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Ghasia zinazoendelea kwa kasi zinawakwamisha zaidi watoto katikati ya mashambulizi ya mabomu yasiyokoma, mapigano makali, na uhaba mkubwa wa chakula, maji salama na dawa kwa zaidi ya siku 500 sasa.“Hakuna mtoto aliye salama,” anasema Catherine Russell, Mkurugenzi Mtendaji wa Shrika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF kupitia taarifa iliyotolewa na makao makuu ya shirika hilo jijini New York, Marekani leo.Taarifa hiyo pia inamnukuu Catherine Russell akisema, “ingawa athari kamili bado haijulikani kutokana na kukatika kwa mawasiliano kote nchini Sudan, inakadiriwa kuwa watoto wapatao 130,000 huko Al Fasher wako katika hatari kubwa ya kukiukwa haki zao, huku kukiripotiwa visa vya utekaji nyara, mauaji na ukataji viungo vya mwili, pamoja na ukatili wa kingono.”Pia kuna taarifa za wafanyakazi wa mashirika ya kibinadamu kukamatwa au kuuawa.UNICEF inatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano, kuhakikisha upatikanaji salama na usiokatizwa wa misaada ya kibinadamu, ulinzi wa raia hasa watoto, na kupatiwa uhakika wa njia salama kwa familia zinazotafuta hifadhi, kwa mujibu wa sheria za kimataifa za kibinadamu. Wale wanaohusika na ukiukaji lazima wawajibishwe.Wakati huohuo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limethibitisha kwamba Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan imewataarifu kuwa viongozi wawili wa juu wa WFP nchini wametangazwa kuwa watu wasiotakiwa nchini Sudan na hivyo wameamriwa kuondoka nchini humo ndani ya saa 72, bila maelezo yoyote.WFP inaeleza kwamba uamuzi huu wa kuwafukuza Mkurugenzi wa WFP nchini Sudan na Mratibu wa Dharura wa WFP nchini humo unakuja katika kipindi muhimu kwani mahitaji ya kibinadamu nchini Sudan hayajawahi kuwa makubwa zaidi kama kipindi hiki, huku zaidi ya watu milioni 24 wakikabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula na jamii zikikumbwa na baa la njaa.Wakati ambapo WFP na washirika wake wanapaswa kupanua wigo wa msaada, uamuzi huu unalazimisha shirika kubadilisha uongozi bila mpango, jambo linalohatarisha shughuli zinazowaunga mkono mamilioni ya Wasudani walio hatarini kukumbwa na njaa kali, utapiamlo, na hata kifo kutokana na njaa.WFP na maafisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa wanaendelea kuzungumza na mamlaka za Sudan kupinga hatua hii na kutaka ufafanuzi wa uamuzi huo.Tags: Sudan, El Fasher, WFP, UNICEF
Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM kwa kushirikiana na Ofisi ya Marekani ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na Dawa za Kulevya na Utekelezaji wa Sheria (INL), na mamlaka kutoka Kenya, Tanzania na Uganda wanashirikiana kuimarisha uwezo na kukabiliana na uhalifu wa kimataifa unaotekelezwa katika ziwa victori ambao ukiachwa unaweza kuleta athari kwa zaidi ya watu milioni 40 wanaotegemea ziwa hilo. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi
Hii leo jaridani tunaangazia kiwango cha gesi ya hewa ukaa, yaani carbon dioxide au CO₂, siku ya Kimataifa ya Wanawake wa Vijijini inayotupeleka nchini Kenya kumulika juhudi za wanawake za kumudu mahitaji ya familia zao, na uvuvi na uhalifu katika Ziwa Victoria.Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani, WMO, inasema kiwango cha gesi ya hewa ukaa, yaani carbon dioxide au CO₂, kimeongezeka kwa kiwango cha kuvunja rekodi mwaka 2024, na kufikia viwango vipya vya juu zaidi kuwahi kurekodiwa.Kuanzia Oktoba 15 mwaka 2008 dunia imekuwa ikiadhimisha siku ya Kimataifa ya Wanawake wa Vijijini kama fursa ya kutambua mchango mkubwa wa wanawake hawa katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi, na kimazingira.Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM kwa kushirikiana na Ofisi ya Marekani ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na Dawa za Kulevya na Utekelezaji wa Sheria (INL), na mamlaka kutoka Kenya, Tanzania na Uganda wanashirikiana kuimarisha uwezo na kukabiliana na uhalifu wa kimataifa unaotekelezwa katika ziwa victoria ambao ukiachwa unaweza kuleta athari kwa zaidi ya watu milioni 40 wanaotegemea ziwa hilo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia siku ya posta Duniani na tunakupeleka nchini Tanzania ambako huko Sabrina Said wa idhaa hii amefuatilia harakati za huduma hiyo kwenye shirika la Posta Tanzania lililoanzishwa kwa sheria ya Bunge ya mwaka 1993 na kuanza kutoa huduma Januari 1994.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, leo amekaribisha tangazo la makubaliano ya kusitisha mapigano na kuachiliwa kwa mateka wote huko Gaza lililotolewa na Rais wa Marekani , akiyaita makubaliano hayo ni mafanikio yaliyohitajika sana baada ya miaka ya mzozo..Licha ya mzozo unaoendelea na changamoto za miundombinu nchini Sudan, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF leo limesema limefanikiwa kutoa chanjo kwa zaidi ya watoto 740,000 walio chini ya umri wa miaka mitano kati ya Januari na Juni 2025, na kutoa dozi zaidi ya milioni 16.Katika Siku ya Posta Duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amewashukuru wafanyakazi milioni 4.6 wa posta wanaounganisha jamii kote duniani.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "FUNDI HANA CHOMBO"Mwenyeji wako ni Assumpta, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika ujumbe wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, Veronica Nduva ambaye alizungumza na Flora Nducha kandoni mwa UNGA80. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo.Ikiwa ni zaidi ya miaka minane tangu zaidi ya wakimbizi 750,000 waislamu wa kabila la warohingya wakimbie Myanmar kuelekea kwenye kambi kubwa nchini Bangladesh, mgogoro huo bado haujapatiwa suluhisho na leo hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa viongozi wamekutana kusaka suluhu ya kudumu kwa warohingya na makabila mengine madogo nchini Myanmar. Katibu Mkuu Antonio Guterres kupitia Afisa Mtawala Mkuu wa UN Courtenay Rattray amesema, “mgogoro huu, ambao umezidi kuongezeka tangu mapinduzi ya kijeshi Myanmar ya mwaka 2021, unasigina haki za binadamu, utu na usalama wa mamilioni ya watu na unatishia uthabiti wa kikanda. Haitoshi tu kutathmini hali ilivyo. Tunapaswa pia kuendeleza mshikamano na kubuni suluhisho.”Amani nchini DRC imesalia bado ahadi, ni kauli ya Bintou Keita, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC aliyotoa wakati akihutubia Baraza la Usalama lililokutana leo kujadili hali Mashariki mwa DRC. Anasema hali inazidi kuwa tete. “Ghasia zinaendelea kushamiri jimboni Kivu Kaskazini hususan eneo la Rutshuru tangu waasi wa M23 watwae eneo hilo. Kuanzia mwezi Juni na kuendelea ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, MONUSCO umepokea maombi lukuki ya watu wakitaka ulinzi kwenye maeneo yanayodhibitiwa na M23.”.Na mashirika ya Umoja wa Mataifa leo yamesisitiza wito wa kupatikana kwa sitisho la mapigano huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel, ili kupunguza machungu wakati huu ambapo Mpango wa Marekani wa Vipengele 20 unaibua matumaini ya kukomeshwa kwa mapigano. Ricardo Pires, msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto, UNICEF amesema, “ni muhimu tupate sitisho la mapigano na misaada iweze sio tu kuingia na kuepusha baa la njaa, bali pia kuelekezwa maeneo ya kusini. Lakini vile vile kuhakikisha watoto na familia zao wanapata malazi bora wakati huu majira ya baridi kali yanakaribia. La sivyo italeta zahma ya afya kwa watoto na familia zao.”.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukiwa umeingia katika siku yake ya nne hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani leo Ijumaa, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amekuwa wa kwanza kuzungumza akitumia muda wake mwingi kushambulia wanamgambowa kipalestina, Hamas na kutetea kila uamuzi wa Israel. Anold Kayanda ameifuatilia hotuba hiyo kwa kina. Ilikuwa majira ya saa tatu na dakika chache hivi asubuhi ya leo saa za New York nchini Marekani ambapo Waziri Mkuu wa Isreal Benjamin Netanyahu amepewa fursa ya kuhutubia na ndipo ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukakosa utulivu. Wajumbe kwa makundi walinyanyuka katika viti vyao na kuondoka huku wakiwaacha maafisa wa Israel wakimpigia makofi kiongozi wao na pia nchi zinazoiunga mkono Israel zikasalia katika viti vyao ikiwemo Marekani.Baadhi ya wajumbe watoka njeKatika eneo la walipotakiwa kukaa wawakilishi wa Palestina kulikuwa wazi, huku katika eneo la Iran ikibakia picha iliyokusanya sura za baadhi ya watu wao waliouawa na mashambulizi ya Israel. Bwana Netanyahu kwa mara nyingine tena ameingia na ubao wenye picha ya ramani ya eneo la Mashariki ya Kati akiutumia kuishambulia Iran na kwa kutumia kalamu akiweka alama ya vema kuonesha namna ambavyo Israel imefanikiwa kupambana na ngome za Irani katika ukanda huo. Katika suti yake, kifuani upande wa kulia, Bwana Netanyahu pia ameweka kibandiko chenye QR Code na akawaambia watu kuwa Israel bado inakumbuka tukio walilofanyiwa na Hamas mwezi Oktoba mwaka juzi na kwamba ikiwa watu wamesahau hilo basi waelekeze simu zao kwenye QR Code hiyo kwenye nguo yake ili iwaoneshe madhara yaliyofanywa na Hamas.Majina ya mateka yakasomwaWaziri Mkuu huyo wa Israel ameyasoma majina ya mateka ambao bado wako mikononi mwa Hamas katika eneo la Ukanda wa Gaza na pia akaueleza mkutano kuwa amesambaza vipaza sauti au spika katika eneo lote la Gaza ili anapoongea leo, azungumze moja kwa moja na mateka huko walikofichwa. Na hapo akabadilisha lugha na kuongea kwa kihebrania akiwaahidi kuwa atawakomboa. Vilevile amedokeza kuwa kwa namna ya kiintelijensia Israel imefanya simu leo ziweze kusambaza hotuba katika ukanda wa Gaza na hivyo akautumia muda huo kupeleka ujumbe mkali kwa Hamas kuwa ataendelea kuwadhibiti. Bwana Netanyahu pia ameingia ukumbini na vibao viwili vyenye maswali na majibu ya kuchagua japokuwa jibu sahihi kwa mujibu wake na waliojibu kuwa ni All the Above, yaani majibu yote ni sahihi. Maswali yote yalikuwa yakiwatuhumu Iran, Hamas, Al Caeda, Hezbollah na Houthi kuwa pia wanaitakia kifo Marekani na wameua watu wengi Ulaya. Huenda hotuba hii ya Netanyahu ikaingia katika orodha ya hotuba tano ndefu zaidi baada ya ile ya Rais wa Marekani Donald Trump wa Marekani, Ya Mahmoud Abbass wa Palestina na Félix-Antoine Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambao wote hao walitumia zaidi ya dakika arobaini licha ya muda wa hotuba uliopangwa kuwa angalau dakika 15.
Hii leo ni hotuba ya Israeli kwenye mjadala mkuu wa baraza kuu, nini kilitokea? Kijana daktari mwanaharakati kutoka Ghana aishiye Uingereza akiwa UNGA80 na matumaini mapya ya kinga dhidi ya maambukizi ya VVU.Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukiwa umeingia katika siku yake ya nne hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani leo Ijumaa, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amekuwa wa kwanza kuzungumza akitumia muda wake mwingi kushambulia wanamgambowa kipalestina, Hamas na kutetea kila uamuzi wa Israel. Anold Kayanda ameifuatilia hotuba hiyo kwa kina. Karibu Anold utupe japo kwa muhtasari.Tukisalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa, moja ya mikutano ya ngazi ya juu iliyofanyika kando ya mjadala mkuu wa Baraza Kuu, ni ule wa kuadhimisha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa program ya Umoja wa Mataifa kuhusu vijana, mkutano ukileta vijana kutoka kona mbali mbali za dunia. Miongoni mwao ni daktari wa tiba na mwanaharakati wa kijamii wa vijana kutoka Uingereza mwenye asili ya Ghana, Dkt. Khadija Owusu. Amezungumza na Flora Nducha anayetujulisha zaidi katika taarifa hiiKatika hatua kubwa ya kihistoria kwenye mapambano dhidi ya Virusi Vya UKIMWI (VVU) dawa mpya ya kudungwa inayoitwa Lenacapavir inatarajiwa kupatikana kwa gharama nafuu katika nchi 120 zenye kipato cha chini na kati kuanzia mwaka 2027. Dawa hiyo itauzwa kwa kiasi cha dola 40 pekee ikiwa ni gharama ya vidonge vya kila siku vya kujikinga na VVU ambavyo mhusika atatumia kwa mwaka mzima. Sabrina Saidi ana taarifa zaidi.
Makubaliano yaliyosimamiwa na mashirika ya kimataifa, likiwemo UNITAID ambalo ni shirika tanzu la shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO, halikadhalika Mpango wa afya wa Clinton (CHAI), Wits RHI na Maabara ya Dkt. Reddy, yanalenga kuhakikisha upatikanaji wa Lenacapavir kwa gharama nafuu.Dawa hii, inayodungwa mara mbili pekee kwa mwaka, imeonesha ufanisi mkubwa katika kuzuia maambukizi mapya ya VVU, jambo muhimu hasa kwa wale wanaopata changamoto kutumia dawa za kila siku.Video ya UNITAID inaonesha maabara yenye teknolojia ya hali ya juu, ambamo wanasayansi wanaandaa dawa hiyo inayotarajiwa kuleta mabadiliko makubwa kwa mamilioni ya watu walio katika hatari ya kuambukizwa virusi hivyo.Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa UNITAID, Tenu Avafia, anasema hatua hii ni ushindi mkubwa kwa jamii zinazohitaji kinga ya muda mrefu dhidi ya VVU."Tumeitikia wito kutoka kwa jamii na nchi tunazohudumia kwa kuhakikisha dawa hii inapatikana kwa gharama nafuu. Tunatarajia usambazaji wa toleo la bei nafuu la dawa hii kuanza kufikia mwaka 2027, chini ya miaka miwili tu tangu idhini kutolewa katika nchi za kipato cha juu — kasi ambayo haijawahi kushuhudiwa."Akizungumza kuhusu hatua hii muhimu, Carmen Pérez Casas, Mkuu wa Mikakati Mwandamizi wa UNITAID, anasema:"Kwa kushirikiana na watengenezaji wa dawa mbadala, tumefanikisha bei nafuu mapema zaidi. Lakini bado tunahitaji kusaidia nchi na jamii kwa kuongeza upatikanaji."UNITAID inasema kwa msaada wa mashirika kama PEPFAR ambao ni mfuko wa Rais wa MArekani wa usaidizi wa dharura dhidi ya UKIMWI, pamoja na mfuko wa kimataifa na wakfu wa Gates, hatua hii inaleta matumaini ya kupunguza maambukizi mapya ya VVU duniani.