POPULARITY
Kesho ikiwa ni siku ya nyuki duniani ikimulika umuhimu wa nyuki tunakupeleka nchini Kenya, katika kijiji cha Embulmbul, ambapo mradi wa ufugaji nyuki uliofanikishwa na Shirika la Marekani la Misaada ya maendeleo, USAID, kwa kushirikiana na Idara ya Misitu ya Kenya, KFS na wadau wengine, umeleta tija kwa wenyeji. Mmoja wa wanufaika hao ni mwanamazingira Christopher Mureithi ambaye ni kiongozi wa kikundi cha kufuga nyuki katika msitu wa Ololua ambao wamefanikiwa sio tu kuboresha uzalishaji wa asali, bali pia kuchangia katika uhifadhi wa bioanuwai na misitu. Katika makala hii iliyoandaliwa na Sharon Jebichii Bwana Mureithi anaanza kwa kueleza mafanikio yao.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa ambayo Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili alipata fursa ya kuzungumza na kiongozi wa kijamii kutoka Jamii ya wafugaji ya Wamaasai mkoani Morogoro nchini Mashariki mwa Tanzania Adam Kulet Ole Mwarabu.Wiki kumi baada ya kuanza kwa mzingiro kamili wa Israel dhidi ya wakazi wa Gaza, zaidi ya robo tatu ya kaya katika eneo la Palestina kuna uhaba mkubwa wa huduma ya maji, huku hali ya usafi ikizidi kuwa mbaya, yameonya leo mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu athari za "uhaba huo wa maji kwa kuzingatia kuwa msimu wa joto unakaribia.”Ripoti kutoka Sudan zikidai kwamba juzi jumatano kulikuwa na jaribio la mashambulizi mapya ya ndege zisizo na rubani dhidi ya kitovu muhimu cha misaada nchini humo juzi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kupitia tamko alilolitoa jana jioni kwa saa za New York, Marekani, ameongeza nguvu yake katika kutoa wito unaozidi kuwa wa muhimu kuhamasisha kuanzishwa kwa mazungumzo ya amani ya kweli.Kufuatia kuendelea kwa mvutano wa majirani, India na Pakistani, Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Philemon Yang, ametoa wito wa kuzitaka nchi hizo mbili kuchukua tahadhari na kuepuka hatua zinazoweza kuongeza mzozo. Balozi Yang anasisitiza mazungumzo ya amani na kufuata sheria za kimataifa ndiyo njia pekee ya kusuluhisha migogoro.”Na katika jifunze Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DALALI”Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, zimewasilisha mapendekezo ya rasimu ya mkataba wa amani kwa Marekani, kujaribu kutafuta mzozo wa Mashariki mwa DRC. Nchi hizo mbili zinatarajiwa kutia saini mkataba wa kudumu mwezi Juni, jijini Washington. Harakati hizi, zitazaa matunda ?
Makala hii imeamgazia kuuawa kwa mbunge wa Kasipul Charles Ong'ondo Were, kwa kupigwa risasi na watu waliokuwa kwa pikipiki katika barabara ya Ngong Jijini Nairobi, jumatano, kukamatwa kwa mlinzi wake kiongozi wa chama cha upinzani cha NUP nchini Uganda, nao wawakilishi wa DRC na Rwanda wanaokutana Washington Marekani kusaini mkataba kuelekea makubaliano ya amani ya mashariki mwa DRC, siasa za Tanzania na kushambuliwa kwa kasisi wa kikatoliki na matukio kadhaa ya juma hili kutokea duniani
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka katika mkoa wa Mwanza kaskazini magharibi mwa Tanzania ambapo vijana wameshika hatamu kuboresha mustakabali wao. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani tunasalia hapa makao makuu.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kudumisha Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, MONUSCO, umeikaribisha kusainiwa kwa “Azimio la Kanuni” tarehe 25 Aprili 2025 mjini Washington, D.C chini ya usimamizi wa Wizara ya mambo ya nje ya Marekani, kati ya serikali za DRC na Rwanda kwa lengo la kulinda rai ana kutekeleza azimio la Baraza la Usalama namba 2773 (2025).Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA, Juliette Touma, akizungumza na waandishi wa habri mjini Geneva kwa njia ya video kutoka mji mkuu wa Jordan, Amman, wakati kuzingirwa kwa Ukanda wa Gaza kukikaribia kuingia mwezi wa pili amesema “Mzingiro wa Gaza ni muuaji wa kimya muuaji wa watoto, wazee, na watu walioko katika mazingira magumu zaidi. Mzingiro huu unamaanisha kwamba familia nzima, watu saba au wanane wanalazimika kushirikiana kopo moja la maharagwe au njegere”.Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO limezitaka nchi za Kaskazini Magharibi mwa Afrika kuongeza ufuatiliaji na kuchukua hatua za mapema kudhibiti makundi ya nzige wa jangwani. Hii ni baada ya nzige wakubwa na makundi madogo kutoka ukanda wa Sahel kuhamia maeneo ya kusini mwa Sahara, hasa katikati ya Algeria, magharibi mwa Libya, na kusini mwa Tunisia tangu Februari hadi Machi mwaka huu.Na katika mashinani fursa ni yake Maruping Onkemetse Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kituo cha Msaada wa Familia, shirika linaloongozwa na wanawake wa asili katika Wilaya ya Gantsi, kijiji cha Chobokwane nchini Botswana anayeshiriki mkutano unaoendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa wa Jukwaa la Watu wa Asili akizungumzia alichojifunza hadi sasa.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Makala ya yaliyojiri wiki hii imeangazia mazishi ya kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis, DRC na Rwanda zatia saini makubaliano kuhusu njia ya kupatikana amani ya mashariki mwa Congo, siasa za Tanzania kuelekea uchaguzi wa oktoba, ziara ya rais wa Kenya William Ruto huko China, hali ya vita ya Sudan, vita ya Ukraine na huko Gaza Israeli, ni miongoni mwa Habari kuu za dunia zilizojiri kwa juma hili.
Tarehe 25 mwezi Aprili kila mwaka ni siku ya kimataifa ya wajumbe wanaowakilisha nchi zao kwenye Umoja wa Mataifa. Tarehe hiyo mwaka 1945 ndio ulianza mkutano huko San Francisco, Marekani wa wajumbe 850 kutoka nchi 50 waliopitisha Chata ya Umoja wa Mataifa ikilenga kusongesha amani, maendeleo, urafiki na haki za binadamu. Kama unavyofahamu Umoja wa Mataifa sasa umekua na idadi ya wanachama ni 193 na kila moja hupeleka wawakilishi kufanikisha utekelezaij wa malengo ya Umoja huo. Lengo la siku ni kuwatambua kwani wao ndio wamepewa jukumu la kufanikisha chata hiyo. Je wajumbe hao hufanya nini? Assumpta Massoi amezungumza na Balozi Yabesh Monari wa Kenya kwenye mada hii kwa kina.
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza, na harakati za utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili. Makala tunasalia hapa hapa makao makuu na mashinani tunakwenda nchini Burundi, kulikoni?Hali si hali huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli ambako wakimbizi wa ndani wanakabiliwa na hatari za kiafya ambako panya na wadudu kama vile viroboto na nzi wamesambaa kutokana na mlundikano wa taka na ukosefu wa huduma muhimu kama vile maji safi na salama.Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, mkutano wa 24 wa Jukwaa la Kudumu la Watu wa jamii za asili (UNPFII) linaendelea kujadili utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili na kubaini mbinu bora za kushughulikia changamoto zinazowakabili. Miongoni mwa shiriki wa jukwaa hilo nimwakilishii wa Shirika la Ereto Solidarity Funds ambaye amepata fursa ya kuzungumza na Sharon Jebichii wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa.Makala ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Kitabu na Haki Miliki ambapo kila mwaka tarehe kama ya leo siku hii huadhimishwa ili kutambua nguvu ya vitabu kama daraja kati ya vizazi na vizazi na tamaduni mbalimbali. Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na mwandishi maarufu wa vitabu vya elimu, Uchumi na uhamiaji, Ernest Makulilo mkazi wa Marekani katika jimbo la Missouri.Na mashinani kupitia video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO fursa ni yake Meena Poudel kutoka nchini Nepal, Kusini mwa Asia ambaye ni Katibu wa kikundi cha wanawake watumiaji wa msitu ambacho kinabadilisha takataka za misitu kuwa mbolea rafiki kwa mazingira huku pia wakijipatia kipato."Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Kitabu na Haki Miliki ambapo kila mwaka tarehe kama ya leo siku hii huadhimishwa ili kutambua nguvu ya vitabu kama daraja kati ya vizazi na vizazi na tamaduni mbalimbali. Katika makala hii Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na mwandishi maarufu wa vitabu vya elimu, Uchumi na uhamiaji, Ernest Makulilo mkazi wa Marekani katika jimbo la Missouri, kuhusu siku ya leo iliyoanzishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO mnamo mwaka 1995.
Vita ya sudan Kuingia katika mwaka wa tatu wiki hii, Kenya yatangaza marufuku ya biashara ya figo baada ya ufichuzi, rais wa zamani wa DRC arejea nchini aliwasili mjini Goma huku Marekani ikiitaka nchi ya Rwanda kuondoa wanajeshi wake mashariki mwa nchi hiyo, tumeangazia siasa za Tanzania kuelekea uchaguzi wa Oktoba, kule Sahel na wito wa rais wa Ghana wiki hii akiwataka viongozi wa nchi hizo kuungana pamoja na pia mkutano wa Paris kuhusu hatima ya vita ya Ukraine
Msikilizaji kwa majuma kadhaa sasa, kumekuwa na mjadala duniani kote kufuatia uamuzi wa rais wa Marekani, Donald Trump, kutangaza ushuru wa bidhaa zinazoingia kwenye taifa hilo, mataifa ya Afrika yakiwa miongoni mwa waathirika, baadhi wakiwekewa ushuru wa hadi asilimia 50. Hata hivyo juma lililopita, rais Trump alitangaza kusitisha kwa muda wa siku 90 utekelezwaji wa ushuru kwa baadhi ya mataifa isipokuwa Uchina, ambayo imewekewa ushuru wa zaidi ya asilimia 125.Katika sehemu hii ya pili ya makala ya wiki hii, tumezungumza na Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara.
Msikilizaji kwa majuma kadhaa sasa, kumekuwa na mjadala duniani kote kufuatia uamuzi wa rais wa Marekani, Donald Trump, kutangaza ushuru wa bidhaa zinazoingia kwenye taifa hilo, mataifa ya Afrika yakiwa miongoni mwa waathirika, baadhi wakiwekewa ushuru wa hadi asilimia 50. Hata hivyo juma lililopita, rais Trump alitangaza kusitisha kwa muda wa siku 90 utekelezwaji wa ushuru kwa baadhi ya mataifa isipokuwa Uchina, ambayo imewekewa ushuru wa zaidi ya asilimia 125.Katika sehemu hii ya pili ya makala ya wiki hii, tumezungumza na Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara.
Karibu kusikiliza jarida la Umoja wa Mataifa ambapo hii leo tunamulika Kongamano la Kimataifa la Kiswahili linalofanyika mjini Kampala Uganda likiwaleta pamoja wadau kutoka kila kona ya Afrika na kwingineko kujadili mikakati ya kukuza lugha hiyo adhimu ya Kiswahili. Utasikiliza muhtasari wa habari ukiangazia miaka miwili tangu kuanza kwa vita vya sasa vya Sudan, UNHCR, yatoa wito kwamba mwitiko mkubwa wa kibinadamu ulioratibiwa vema ni muhimu ili kuzuia mateso zaidi na vifo kwa wananchi wa DRC, na Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) limeanza leo tarehe 15 hadi tarehe 17 katika Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.
Matukio ya wiki: kukamatwa kwa mwenyekiti wa chama cha upinzani cha Chadema nchini Tanzania, Tundu Lisu, maadhimisho ya miaka 31 ya mauaji ya kimbari ya nchini Rwanda mwaka 1994, mafuriko jijini Kinshasa huko DRC, hali ya sudan Kusini kutokana na kukamatwa na kuzuiwa nyumbani kwa makamu wa kwanza wa rais Riek Machar, uchaguzi wa Gabon, na pia mzozo wa kibiashara kati ya Marekani na mataifa mengine ulimwenguni ni miongoni mwa Habari kuu za dunia zilizojiri kwa juma hili.
Waziri Mkuu amekabiliana na maswali kuhusu uwezekano wa mkataba wa manowari ya Australia na Marekani pamoja na Uingereza, kufuatia utoaji wa ushuru wa Marekani ambao ume tikisa dunia nzima.
Kwenye makala haya tunajadili, hatua ya rais wa Marekani, Donald Trump kutangaza kuongeza ushuru kwa bidhaa zote zanazoingizwa Marekani, kutoka mataifa ya Kigeni, hatua inayoonekana kutikisa uchumi wa Dunia. Je unahisi hatua ya rais Trump ni sahihi?Ndilo swali tumeuuliza.Skiza makala haya kujua maoni ya waskilizaji.
Kwa majuma kadhaa, mijadala mikali duniani kote kufuatia uamuzi wa rais wa Marekani, Donald Trump, kutangaza ushuru zaidi wa bidhaa zinazoingia kwenye taifa hilo, mataifa ya Afrika yakiwa miongoni mwa waathirika, baadhi wakiwekewa ushuru wa hadi asilimia 50. Katika makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunadadavua na wataalamu athari za ushuru wa Trump kwa nchi za Afrika na biashara ya dunia kiujumla. Tutakuwa na Ali Mkimo, mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.
Waziri Mkuu Anthony Albanese amesema serikali ita toa dola milioni 50, kwa sekta zitakazo athiriwa kwa tangazo jipya la ushuru kutoka Marekani.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Rekodi ni chache sana ya vitu ambavyo wanawake wamefanya hapa duniani, anasema Dkt. Rose Reuben, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania anapozungumza na Anold Kayanda wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa wakati wa Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake, CSW69, jijini New York, Marekani.Mkutano huu muhimu kuhusu wanawake umefanyika kuanzia tarehe 10 hadi 21Machi 2025 na kuhudhuriwa na maelfu ya wanawake kutoka kote duniani naye Dkt. Rose Reuben akiwa mmoja wao.Kiongozi huyu wa waandishi wa habari nchini Tanzania anaona kwamba kuna hatua nyingi zimepigwa katika kipindi cha miaka 30 tangu kuwekwa kwa Azimio la Beijing ili kumkomboa mwanamke lakini bado kuna kazi kubwa ya kufanya.“Na hii kazi sipendi kujilaumu sana kwamba je, hakuna kitu ambacho kimefanyika?! Mambo yamefanyika mengi lakini masuala ya kijamii hayamaliziki kwa usiku mmoja kwasababu kila unapoamka jamii inabadilika kwa namna nyingine. Kwa hiyo tukitazama kwa mtazamo huo tunaona kwamba kuna kazi imefanyika.” Anasema Mkrugenzi huyo Mtendaji wa TAMWA.Kwake, mwandishi wa habari nguli, anaona moja ya maeneo ambayo ni muhimu yafanyiwe kazi ni kuzipa nafasi taarifa zinazohusu shughuli kubwa zinazofanywa na wanawake katika jamii kote duniani kwani licha ya wanawake kuwa na michango mikubwa katika mustakabali wa ulimwengu, taarifa zao hazipewi kipaumbele cha kutosha.“Mimi kwa mtazamo wangu naona wanawake wamefanya kazi nyingi lakini hazijarekodiwa. Rekodi ni chache sana.” Anasisitiza na kuongeza, “kwa hiyo tunatakiwa kuanza kurekodi vile vitu ambavyo vilifanywa na wanawake wale wa miaka 30 iliyopita lakini hata na hawa wanaokuja kizazi kipya.”Dkt. Rose Reuben anahamasisha pia vyombo vya habari kuangazia masuala mengine ambayo kwa namna moja amba nyingine yanaigusa jamii moja kwa moja na hiyo ni kusema yanamgusa mwanamke moja kwa moja kama vile mabadiliko ya tabianchi, tekonolojia, “na vitu vingine ambavyo vinaweza kuathiri usawa wa kijinsia na hali ya mwanamke duniani.”Aidha kiongozi huyo wa TAMWA anatoa wito kwa wanawake popote walipo kutumia nyenzo zinazopatikana katika jamii yao kuhakikisha wanapata taarifa, wanasambaza taarifa na kujipatia maarifa.
Hii leo jaridani tunaangazia hatari za usitishwaji wa misaada kutoka marekani kwa waathirika wa viruzi vya Ukimwi, na ujumbe wa washiriki wa Mkutano wa CSW69 uliokunja chamvi Ijumaa wiki jana. Mashinani tunakupeleka nchini Tanzania, kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na ukimwi UNAIDS leo limeonya kwamba kusitishwa kwa ufadhili wa Marekani sio tu janga kwa vita dhidi ya gonjwa hilo bali ni chachu ya vifo na ongezeko la maambukizi mapya. Flora Nducha amefuatilia onyo hilo lililotolewa leo mjini Geneva Uswisi na Mkurugenzi mtendaji wa UNAIDS Winnie Byanyima alipozungumza na waandishi wa habari.Wakati Mkutano wa Kamisheni ya Hali ya wanawake Duniani ulioleta pamoja wawakilishi wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa na mashirika ya Umoja wa Mataifa pamoja na mashirka yasiyo ya kiserikali(NGOs) ulikunja jamvi ijumaa tarehe 21 Machi wiki jana tulipata kuzungumza na wawakilishi wa Shirika lisilo la kiserikali la Forum for Women Democracy Development and Justice, FODAJ ambalo linasaidia wasichana na wanawake waathirika wa ukatili wa kijinsia katika kaunti ya Kajiado nchini Kenya.Makala Anold Kayanda wa Idhaa hii baada ya kukamilika kwa Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake CSW69 uliofikia tamati mwishoni mwa wiki amezungumza na Dkt. Rose Reuben, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanawake wa Vyombo vya Habari Tanzania (TAMWA) kuhusu tathimini yake ya hatua zilizopigwa katika miaka 30 tangu kuwekwa kwa Azimio la Beijing ili kumkomboa mwanamke.Na katika mashinani fursa ni yake Imani Ramadhani kutoka wilaya ya Kilolo, Iringa nchini Tanzania akieleza jinsi ambavyo maisha ya familia yake ilivyobadilika kupitia mradi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watotot UNICEF, uliofadhiliwa kwa ushirikiano na wadau wake unaolenga kuleta usafi enedelevu wa mazingira, ikiwa ni pamoja na vyoo safi na salama ili kupunguza hatari za kila mara za magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na ukimwi UNAIDS leo limeonya kwamba kusitishwa kwa ufadhili wa Marekani sio tu janga kwa vita dhidi ya gonjwa hilo bali ni chachu ya vifo na ongezeko la maambukizi mapya. Flora Nducha amefuatilia onyo hilo lililotolewa leo mjini Geneva Uswisi na Mkurugenzi mtendaji wa UNAUDS Winnie Byanyima alipozungumza na waandishi wa habari.
Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, CSW69 unafikia tamati hii leo Machi 21 hapa katika makao makuu, na wakulima wanawake nchini Senegal. Mashinani inatupeleka nchini Tanzania kumulika mradi wa maji.Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, CSW69 unafikia tamati hii leo Machi 21 hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Bi. Gertrude Mongella, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa 4 wa Kimataifa wa wanawake maarufu kama Mkutano wa Beijing uliofanyika mnamo mwaka 1995, hivi tunavyozungumza, pamoja na umri wake mkubwa ameshirikia karibia vikao vyote vya mkutano huu wa CSW69 ambao pia ulikuwa unaangazia utekelezaji wa maazimio yaliyowekwa miaka 30 iliyopita chini yake mama Mongella.Tukiwa bado ndani ya mwezi wa Machi, unaotambuliwa kuwa ni mwezi wa wanawake tunakwenda nchini Senegal ambako huko wasichana waliokuwa wakifanya kazi za ndani, wamewezeshwa na Umoja wa Mataifa na sasa ni wakulima na wanatumia stadi za upigaji na utengenezaji video za mtandaoni kuelimisha jamii kuhusu kilimo chenye tijaMakala inayoturejesha hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kwenye mkutano wa Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake duniani CSW69 unaokunja jamvi hii leo Flora Nducha amebahatika kuzungumza na mmoja wa washiriki wa mkutano huo kutoka asasi za kiraia nchini Tanzania.Na katika mashinani fursa ni yake Janeth Zakaria kutoka kijiji cha Kaguruka mkoani Kigoma nchini Tanzania ambaye kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF anasema alikuwa anatembea umbali wa kilomita 10 kupata maji safi na salama lakini sasa ni hatua chache tu kutoka nyumbani kwake”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, CSW69 unafikia tamati hii leo Machi 21 hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.Bi. Gertrude Mongella, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa 4 wa Kimataifa wa wanawake maarufu kama Mkutano wa Beijing uliofanyika mnamo mwaka 1995, hivi tunavyozungumza, pamoja na umri wake mkubwa ameshirikia karibia vikao vyote vya mkutano huu wa CSW69 ambao pia ulikuwa unaangazia utekelezaji wa maazimio yaliyowekwa miaka 30 iliyopita chini yake mama Mongella.Nilipokutana naye nimemuuliza swali hili la kichokozi.Mazungumzo zaidi kati yangu na Mama Gertrude Mongella yatakujia katika vipindi vyetu vijavyo hivi karibuni.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu Waziri, Dkt. Dorothy Gwajima, ni mmoja wa wanaohudhuria mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake, CSW69 hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Anold Kayanda wa Idhaa hii amekutana naye na miongoni mwa mambo mengi amemuuliza ni kwa nini pamoja na ongezeko na idadi ya wanawake katika ngazi za uamuzi nchini Tanzania lakini bado kuna changamoto nyingi zinazoukabili usawa wa kijinsia nchini humo?
Hii leo jaridani tunaangazia madeni katika nchi zenye mapato ya chini na ujumbe wa washiriki wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani CSW69 hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa.Mkutano wa 14 wa Kimataifa wa Usimamizi wa madeni umeanza rasmi hii leo huko Geneva Uswisi ambapo kubwa linalojadiliwa ni namna ya kuhakikisha wakati serikali zikipambana kulipa madeni hazidumazi maendeleo.Akijibu swali la kwa nini pamoja na ongezeko na idadi ya wanawake katika ngazi za uamuzi nchini Tanzania lakini bado kuna changamoto zinazoukabili usawa wa kijinsia, Dkt. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu anayehudhuria mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake, CSW69 jijini New York, Marekani kupitia mahojiano maalumu na Anold Kayanda wa Idhaa hii ya Umoja wa Mataifa, anaeleza kuwa mabadiliko chanya katika jamii hayaji kwa kutumia mabavu.Makala pia inatubakisha hapa Umoja wa Mataifa kwenye mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani CSW69. Ili kufanikisha lengo la usawa wa kijinsia Umoja wa Mataifa unasisitiza ushiriki wa wanaume katika mchakato hasa kwa kuzingatia kuwa mfumo dume miaka nenda miaka rudi umekuwa kikwazo cha kufikia lengo hilo, Flora Nducha amebahatika kuzungumza na mmoja wa wanaume wanaoshiriki mkutano huo kusikia maoni yake.Na katika mashinani baadhi ya washiriki wa mkutano wa CSW69 wakizungumza na idhaa hii kandoni mwa mkutano huo, wametoa wito wa mshikamano na msichana na mwanamke yeyote anayepitia changamoto kote duniani hususani wale wanaorejea shuleni baada ya kusitisha masomo kutokana na ujauzito kabla ya wakati. Mshiriki wa kwanza ni Nasra Kibukila anayewakilisha Mtandao wa Elimu Tanzania, TEN/Met.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia mpango mpya wa UN80, unaolenga kuimarisha kazi na ufanisi wa chombo hicho ambacho mwaka huu kinatimiza miaka 80, na yaliyojiri katika mkutano wa CSW69. Makala na mashinani tunasalia hapa hapa makao makuu, kulikoni?Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amezindua Mpango mpya wa UN80, unaolenga kuimarisha kazi na ufanisi wa chombo hicho ambacho mwaka huu kinatimiza miaka 80 tangu kuanzishwa kwake huku akisisitiza umuhimu wa mshikamano wa kimataifa..Wakati mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake Duniani CSW69 ukiendelea hapa New York Marekani nchini Sudan Kusini wanawake na wasichana wanaendelea kuonja shubiri ya vita, wakibakwa, kuuawa, kukosa elimu na kupitia changamoto nyingine lukuki sababu ya vita. Mmoja wa washiriki wa mkutano wa CSW69 kutoka Sudan Kusini akizungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili amesema sasa imetosha amekuja na ujumbe mmoja tu, anataka jinamizi la vita lazima likome.Makala tukisalia hapa hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York, Marekani ambako Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, (CSW69) umeingia siku ya tatu, nimezungumza na Nuria Mshare ambaye amewakilisha taasisi ya Haki Elimu ya nchini Tanzania.Na Katika mashinani fursa ni yake Janet Zebedayo Mbene kutoka Tanzania aliyehududhuria mkutano huu hapa makao makuu, kama mwenyekiti wa shirika lisilo la kiserikali la mtandao wa uwezeshaji wa wanawake Tanzania na angependa kuwashauri wanawake na wasichana wanaopitia changamoto wajikite katika fursa mbalimbali. Kila kitu kina changamoto. Wajitie moyo na waondoe uoga, na kwa kile kidogo walicho nacho wanaweza kujiinua na kuinua jamii kwa ujumla.Mwenyeji wako ni Assumpta, karibu!
Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, (CSW69) umeingia siku ya tatu hii leo Machi 12 katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijinoi New York, Marekani. Mkutano huu wa mwaka huu unafanyika katika hali ya kihistoria kwa kuzingatia kuwa ni miaka 30 tangu Mkutano wa wanawake ulipofanyika jijini Beijing - China mwaka 1995 na kuweka maazimio muhimu kuhusu masuala mazito ya kumkomboa mwanamke dhidi ya ukandamizaji kote duniani. Maelfu ya wanawake na wadau wengine wanakutana kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York. Miongoni mwao ni Nuria Mshare ambaye amewakilisha taasisi ya Haki Elimu ya nchini Tanzania.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Hii leo jaridani tunakuletea Mada kwa kina inayomulika mkutano wa CSW69 ulioanza Jana Jumatatu hapa New York, Marekani, ikiwa ni miaka 30 tangu mkutano wa nne wa kimataifa wa wanawake uliofanyika Beijing mwaka 1995, ukiweka msingi wa mabadiliko yanayoshuhudiwa sasa ya usawa wa kijinsia. Pia tunakuletea muhtasari na sauti za vijana kutoka mashinani.Katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa asubuhi hii kwa saa za New York, Marekani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amekutana na wawakilishi wa Asasi za Kiraia wanaoshiriki Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake CSW69. Bwana Guterres amezitaka Asasi za Kiraia kuendelea kuzisukuma nchi kuweka mazingira bora kwa ajili ya usawa wa wanawake na wasichana na pia akakumbushia kuwa Umoja wa Mataifa utaendelea kuwaunga mkono katika kulitimiza lengo hilo.Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk kupitia Msemaji wake, ameripoti ukatili unaoendelea katika pwani ya Syria tangu Machi 6, ambapo anasema takriban raia 111 wameuawa, wengi wao kwa misingi ya kiimani. Hospitali pia zimeshambuliwa na Umoja wa Mataifa unatoa wito wa uchunguzi huru na uwajibikaji kwa wahusika.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini Malawi limeongeza wigo wa mpango wake wa Mlo Shuleni unaopatikana kwa kununua vyakula vinavyolimwa na wananchi wa karibu katika maeneo hayo. Mradi huo unaotekelezwa wilayani Nkhotakota, unanufaisha wanafunzi 10,000 na kusaidia wakulima wadogo 1,200, hivyo kuimarisha upatikanaji wa chakula na uchumi wa ndani.Na Katika mashinani huku mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW69 ukiendelea hapa makao makuu, tutakwenda Kajiado nchini Kenya kusikia ujumbe wa vijana kuhusu usawa wa kijinsia.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW69 na wakimbizi wanaokimbia machafuko nchini DRC kwenda Burundi. Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani tunakupeleka nchini Lebanon, kulikoni?Hii leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani unaanza mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW69, kusanyiko kubwa zaidi la kila mwaka la Umoja wa Mataifa linalomulika usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake mwaka huu washiriki wakiwa zaidi ya 25,000.Zaidi ya watu 63,000 sasa wamewasili Burundi wakikimbia machafuko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na wengi wao wanaishi katika hali ngumu ndani ya uwanja wa michezo wa Rugombo jimboni Cibitoke (CHIBITOKE) huku wakisubiri kuhamishiwa kwenye kambi rasmi za wakimbizi.Makala leo tunamwangazia Fatuma Mfumia, dereva pekee wa kike katika shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhuduia Watoto, UNICEF Tanzania.Na mashinani mashinani fursa ni yake Ghada Dawiche's ambaye licha ya machungu yaliyomkumba baada ya kupoteza bintiye aliyekuwa mfanyakazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR nchini Lebanon, pamoja na mjukuu wake wa kiume wakati kombora la Israeli lilipopiga nyumba yao nchini Lebanon, anasema Umoja, nguvu na tumaini ndio ujumbe mkuu anaowapa wanawake wote waliopoteza wapendwa wao vitani na katika kupigania haki za wanawake.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Hii leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani unaanza mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW69, kusanyiko kubwa zaidi la kila mwaka la Umoja wa Mataifa linalomulika usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake mwaka huu washiriki wakiwa zaidi ya 25,000. Selina Jeroboni na taarifa zaidi.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Kwenye kikao cha 58 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kinachoendellea mjini Geneva Uswisi, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa M ataifa, Volker Türk , amezungumzia hali ya kuzorota na kutoeleweka inayohusu haki za binadamu duniani kote akielezea wasiwasi mkubwa kuhusu kudhoofika kwa makubaliano ya kimataifa kuhusu haki za binadamu,na kuonya kwamba ushawishi wa viongozi wa kiimla, matajiri wakubwa, na viongozi wa kimabavu unatishia kuvuruga maendeleo ya miongo kadhaa. Anold Kakayanda na taarifa kamili.Asante Flora katika taarifa yake Türk amesisitiza umuhimu wa kuhifadhi haki za binadamu na utawala wa sheria ili kuzuia kurudiwa kwa ukatili wa zamani.Moja ya masuala ya dharura yaliyotiliwa mkazo na Türk ni mgogoro wa kibinadamu unhaoendelea huko Gaza. Amelaani uharibifu uliosababishwa na hatua za kijeshi za Israeli dhidi ya mashambulizi ya Oktoba 7, 2023 yaliyofanywa na Hamas na makundi mengine ya wapiganaji wa Kipalestina.Türk amesisitiza haja ya kudumisha usitishaji mapiganona kutoa wito wa mchakato wa amani unaozingatia haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na haki ya kujitawala na uwajibikaji. Ametaka kuachiliwa kwa mateka, kukomeshwa kwa vizuizi vya kiholela, na kuanza tena kwa msaada wa kibinadamu mara moja ndani ya Gaza.Kuhujsu mgogoro unaoendelea nchini Ukraine amersema bado ni suala la kutia wasiwasi, huku raia wakiishi kwa hofu ya mara kwa mara kutokana na mashambulizi yasiyokoma.Türk amekemea vikali vikwazo vya Shirikisho la Urusi juu ya haki za msingi katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu na kuelezea masikitiko yake kuhusu ripoti za mauaji ya kiholela na mateso ya kimfumo ya wafungwa wa vita wa Kiukraine.Almeihimiza jumuiya ya kimataifa kufanya kazi kuelekea amani endelevu inayoheshimu haki na matarajio ya watu wa Ukraine.Türk pia ameelekeza mawazo kwenye maeneo mengine yenye migogoro, ikiwa ni pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Myanmar, Haiti, na Sudan.Alielezea jinsi watawala wa kiimla, wanasiasa wahubiri wa chuki, na walanguzi wanavyotumia machafuko kwa faida zao binafsi.Amesema Athari za migogoro huenea zaidi ya mstari wa mbele, zikiathiri minyororo ya usambazaji duniani na nafasi za kidijitali.Ametoa wito kwa watu binafsi kutambua jukumu lao la pamoja kwa kufanya maamuzi ya kimaadili ya ununuzi, kushiriki kisiasa, na kuunga mkono uwajibikaji kwa ukiukwaji wa haki za binadamu.Hata hivyo amesema demokrasia zilizoimarika haziko salama dhidi ya kudorora kwa haki za binadamu. Türk ameelezea wasiwasi mkubwa kuhusu mwelekeo nchini Marekani, ambako maendeleo kuhusu usawa wa kijinsia na sera za kupinga ubaguzi yanarudi nyuma.Pia amekosoa Shirikisho la Urusi kwa ukandamizaji wake wa jamii za kiraia na vyombo vya habari huru, ambapo wapinzani wanakabiliwa na unyanyasaji, kukamatwa, au kufurushwa.Kudhoofika kwa haki za binadamu katika mataifa yenye nguvu, Türk alionya kwamba kunaweka mfano hatari kwa ulimwengu mzima, akisisitiza hitaji la dharura la mshikamano wa kimataifa na uwajibikaji kuhusu haki za binadamu.
Wanasiasa wakuu wa Australia wamesema hatma ya mkataba wenye thamana yama bilioni ya dola na Marekani ume hakikishwa, baada ya Rais Donald Trump kuonekana nikama amesahau jina la mkataba huo wa nchi tatu zinazo jumuisha Uingereza.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Hii leo jaridani tunaangazia msaada wa kibinadamu nchini DRC, na simulizi y amkimbizi wa DRC aliyekimbilia nchini Uganda. Makala inatupeleka nchini Tanzania, namashinani nchini Kenya, kulikoni?Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likifanya kikao cha dharura jijini New York, Marekani kujadili hali ya usalama inayozidi kuzorota kila uchao huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya kibinadamu nchini humo, Bruno Lermaquis amesema kupanuka kwa mzozo huo kumezidi kugharimu maisha na mustakabali wa raia.Sina mpango tena wa kurejea nyumbani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ni kauli yake Twagirayesu Gato, mwanafunzi huyu raia wa DRC aliyekimbia nchini mwake mwaka jana na kuingia Uganda ambako sasa anapata hifadhi. Amesema hayo kwenye video ya shirika la Umoja wa MAtaifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR iliyochapishwa katika ukurasa wa YouTube wa shirika hilo.Makala inatupeleka nchini Tanzania ambako tunamsikiliza Brigedia Jenerali George Mwita Itang'are, Mkuu wa Kituo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani cha Tanzania (TPTC) akitoa wito kwa Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa kuendelea kuunga mkono ulinzi wa amani duniani kwa kuzikabili changamoto wanazokutana nazo walinda amani. Anold Kayanda anasimulia.Na mashinani ikiwa hivi majuzi Dunia iliadhimisha siku ya redio duniani fursa ni yake Irene munyua kutoka Kenya akieleza washirika wetu Radio Domus kuhusu umuhimu wa radio kwa jamii katika maisha ya kila siku.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likifanya kikao cha dharura jijini New York, Marekani kujadili hali ya usalama inayozidi kuzorota kila uchao huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya kibinadamu nchini humo, Bruno Lermaquis amesema kupanuka kwa mzozo huo kumezidi kugharimu maisha na mustakabali wa raia. Selina Jerobon na maelezo zaidi.
Nchi zaki Arabu, Umoja wa Mataifa na washirika wakaribu wa Marekani wamekosoa pendekezo la Donald Trump kuchukua ukanda wa Gaza, naku tawanya wa Palestina kuwa hatua hiyo ita yumbisha kanda hiyo na kudhoufisha juhudi zakupata suluhu ya nchi mbili.
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya usalama Goma DRC, na masuala ya haki za binadamu. Makala na mashinani inaturejesha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kufuatilia simulizi za wakimbizi wa ndani.Maisha yanarejea katika hali ya kawaida huko Goma baada ya siku kadhaa za mapigano kati ya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (FARDC) na waasi wa M23 mashariki mwa. Mwandishi wetu wa habari jimboni Kivu Kaskazini amesema kwamba shughuli zinaanza tena katika mji wa ziwa la Kivu, Goma, wakati M23 imechukua wilaya nyingi za mji mkuu wa Jimbo hili.Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa (OHCHR) imesisitiza haja ya kusonga mbele kuelekea awamu inayofuata ya usitishaji mapigano huko Gaza, kuachiliwa kwa mateka na wafungwa wote waliokamatwa kiholela, kukomesha vita na kujenga upya Gaza, kwa kuheshimu kikamilifu sheria ya kimataifa ya kibinadamu na sheria za kimataifa za haki za binadamu.Makala leo inakukutanisha na Mwamini Sebororo mmoja wa mamilioni ya raia wa Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo DRC waliopoteza makazi yao na kila kitu katika jimbo la Kivu Kaskazini mashariki ya taifa hilo huku mgogoro ukiendelea kufurusha watu zaidi, akiwa kambini Bushagara anasimulia kilichomsibuNa katika mashinani tutarejea nchini Jamhuri wa Kidemokrasia ya Congo DRC kusikia ujumbe wa mkimbizi wa ndani ambaye ni mwathirika wa vita Goma.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa,(OHCHR) imesisitiza haja ya kusonga mbele kuelekea awamu inayofuata ya usitishaji mapigano huko Gaza, kuachiliwa kwa mateka na wafungwa wote waliokamatwa kiholela, kukomesha vita na kujenga upya Gaza, kwa kuheshimu kikamilifu sheria ya kimataifa ya kibinadamu na sheria za kimataifa za haki za binadamu.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kushuhudia sintofahamu na maombi ya wakazi wa Goma baada ya waasi wa M23 kutwaa mji huo. Mashinani tunakwenda Somalia na pia tunakuletea muhutasari wa habari.Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Bruno Lemarquis, ametoa wito wa kufunguliwa haraka kwa Uwanja wa Ndege wa Goma. Amesema uwanja huu uliofungwa kutokana na mapigano kati ya vikosi vya jeshi la DRC na waasi wa M23 ni muhimu kwa usafirishaji wa misaada ya kibinadamu. Hospitali zimejaa na maelfu ya raia hawana msaada wa dharura.Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la idadi ya watu na afya ya uzazi, (UNFPA), na la misaada ya kibinadamu na dharura (OCHA) leo yamesisitiza kuwa kusitishwa kwa ufadhili wa Marekani kunawaacha mamilioni 'hatarini'. Hayo yakijiri tayari imefahamika kuwa Rais Donald Trump anaiondoa Marekani katika Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu na pia kuacha kulifadhili shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi wa Kipalestina.Na ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Saratani, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) limeeleza kiasi takwimu kuhusu ugonjwa huo kwamba mathalani kwa mwaka 2020 saratani ilisababisha vifo karibu milioni 10 sawa na kifo kimoja kati ya sita duniani. Aidha WHO imebainisha kuwa saratani zinazojitokeza zaidi ni saratani ya matiti, mapafu na utumbo mpana.Na katika mashinani fursa ni yake Safiya Jeylaani, mkazi wa Barawe katika Jimbo la Kusini Magharibi mwa Somalia ambye baada ya kuhudhuria hafla ya kujadili umuhimu wa upatikanaji wa huduma za afya kwa Wasomali wote katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu iliyoandaliwa na Umoja wa Mataifa anasema jamii wanapaswa kuelimishwa kuhusu afya kutumia lugha mama.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya usalama nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na tutakuletea simulizi ya wakimbizi wa ndani nchini humo. Makala inatupeleka nchini Senegal na mashinani nchini Afghanistan, kulikoni?Mashirika ya Umoja wa Mataifa yameendelea kutoa wito wa kurejeshwa kwa amani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo (DRC) kwani hali inazidi kuwa tete na kuuzidi uwezo wa mashirika hayo kusaidia..Kutana na mkimbizi Masimango Mango kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ambaye kwa sasa anaishi kwenye makazi ya wakimbizi wa ndani ya Lushagara Goma jimboni Kivu Kaskazini Mashariki mwa DRC, anasema kwa hakika vita imemchosha na anacholilia ni amani ili arejee nyumbani na familiia yake.Makala tunakwenda Senegal, magharibi mwa AFrika ambako nishati ya umeme imeleta mabadiliko makubwa kwenye kijiji ambacho awali kiligubikwa na kiza nyakati za usiku.Na katika Zulaikha kutoka Afghanistan ambaye ana matumaini katika msimu huu wa baridi kutokana na msaada wa fedha kutoka Shirika la Marekani la Misaada ya kimaendeleo USAID na lile la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda karibu!
Baada ya Serikali ya Marekani kutoa tangazo jipya sasa kwamba itaendelea kufadhili huduma zinazolenga vita dhidi ya Virusi vya Ukimwi (VVU), shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na VVU na Ukimwi (UNAIDS) limeeleza kuupokea uamuzi huo kwa furaha na kuuita wa kuokoa maisha. Selina Jerobon na maelezo zaidi.
Hii leo jaridani tuanaangazia masuala ya ufadhili wa huduma za afya, na kilimo cha cacao nchini Liberia. Makala inatupeleka nchini DRC na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Baada ya Serikali ya Marekani kutoa tangazo jipya sasa kwamba itaendelea kufadhili huduma zinazolenga vita dhidi ya Virusi vya Ukimwi (VVU), shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na VVU na Ukimwi (UNAIDS) limeeleza kuupokea uamuzi huo kwa furaha na kuuita wa kuokoa maisha.Kilimo bora cha kakao huko Liberia kimemwondolea uchovu na kukosa kulala, mkazi wa kaunti ya Nimba, kaskazini mashariki mwa Liberia, baada ya mradi wa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD nchini humo kumwezesha sio tu kugeukia kilimo, bali pia kuajiri vijana wengine na hivyo kufanikisha lengo la Umoja wa Mataifa la kuondokana na umaskini.Makala inatupeleka kwenye msitu wa bonde la mto Congo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC wa pili kwa ukubwa duniani unaofyonza kiasi kikubwa cha hewa ukaa, ambako mradi wa Umoja wa Mataifa wa kulinda bayoanuwai na kupambana na umasikini UNREDD unaleta nuru kwa jamii na mazingira.Na mashinani fursa ni yake fursa ni yake Esther Wangoi Mbugua, Mama mfugaji nyuki kutoka Kaunti ya Kajiado nchini Kenya ambaye alizungumza na washirika wetu Redio Domus akieleza kuwa ameweza kujipatia kipato na kumudu mahitaji ya familia yake kupitia mradi wa ufugajji nyuki.Mwenyeji wako niAnold Kayanda karibu!
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea -Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres asikitishwa na hatua ya serikali ya Marekani kutangaza kujitoa kwenye mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi wa Paris na kuitaka kufikiria upya uamuzi huo-Rais Donald Trump wa Marekani ametia saini amri ya kiutendaji ya kuondoa uanachama wa Marekani kwenye shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO-Gaza kwa mujibu wa mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa malori ya misaada yanaendelea kuingia Gaza baada ya kuanza utekelezaji wa usitishaji uhasama-Mada kwa kina leo inatupeleka Bahrain Asia Magharibi kumulika uzamiaji na uvunaji wa kito cha thamani cha lulu-Na mashinani tunabisha hodi Kajiado Kenya kuangazia juhudu endelevu za utunzaji wa misitu