POPULARITY
Karibui miaka mitatu tangu Ahmad Ahmad kuchaguliwa kuwa rais wa shirikisho la kandanda barani Afrika, CAF, shirikisho hilo linakabiliwa na mshororo wa tuhuma za rushwa na matumizi mabaya ya fedha. Tunajadili katika makala ya Jukwaa la Michezo. Ungana na Fredrick Nwaka akiwa na wachambuzi wa soka Juma Mudimi na Bonface Osano
Nchi za Rwanda na Uganda zimekubaliana kubadilishana wafungwa huku viongozi wa mataifa hayo wakitarajia kukutana katika mpaka wa Gatuna, ikiwa na hatua ya karibuni zaidi ya kutafuta suluhu ya mzozo wa kidiplomasia baina ya mataifa hayo. Fredrick Nwaka amekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu.
Rais wa shirikisho la kandanda duniani Fifa Gian Infantino amependekeza fainali za mataifa ya Afrika kuchezw akila baada ya miaka minne badala ya miaka miwili ya sasa. Tunajadili kwa kina katika jukwaa la michezo. Ungana na Fredrick Nwaka akiwa na wachambuzi wa soka Mustapha Mtupa, Samwel John na Bonface Osano
Michuano ya klabu bingwa barani Afrika hatua ya makundi imeendelea kurindima ambapo klabu za TP Mazembe, Mamelody Sundowns, Zamalek ni miongoni mwa klabu zilizofuzu hatua ya robo fainali. Je msisimko wa michuano hiyo umepungua msimu huu? Fredrick Nwaka ameungana na wachambuzi wa soka Mohammed Simbaulanga na Aloyce Mchunga kutathimini kwa kina.
Serikali ya Uganda imetangaza kuwaachilia huru raia tisa wa Rwanda waliokuwa wakishikiliwa katika kambi za kijeshi nchini humo. Je hatua hii inaweza kupunguza joto la mvutano uliopo baina ya Kampala na Kigali. Ungana na Fredrick Nwaka aliyekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji.
Mwaka 2019 unafikia ukingoni leo Disemba 31 na tunakupa fursa msikilizaji kutoa maoni yako kuhusu matukio muhimu yaliyotokea katika jamii yako. Ungana na Fredrick Nwaka aliyekuandalia makala haya.
Umoja wa mataifa umelaani vikali hatua ya serikali ya rais Salva Kiir kuajiri wapiganaji katika vyombo vya usalama huku pia ukinyooshea kidole Kenya na Uganda kwa kushindwa kusaidia mchakato wa amani nchini Sudani Kusini. Fredrick Nwaka amezungumza na wasikilizaji ili kupata maoni yao.
Jumuiya ya Afrika mashariki imetimiza miaka 20 tangu ilipoasisiwa kwa mara ya pili mwaka 1999. Fredrick Nwaka amekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji ikiwa jumuiya hiyo imetimiza malengo yake au imesalia kuwa jumuiya ya viongozi.
Shirika la Under The Same Sun lenye makao yake makuu nchini Canada linasema Tanzania imepiga hatua katika kukabiliana na madhila yanayowapata watu wenye ulemavu wa ngozi huku likisema mataifa jirani na Tanzania bado watu wenye ulemavu wa ngozi wanakabiliwa visa ikiwemo mauaji. Fredrick Nwaka ameandaa makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji. Ungana naye.
Daktari Dennis Mukwege ametoa wito kwa Ufaransa na umoja wa Ulaya kuingilia kijeshi nchini DRC ili kupambana na magaidi wa ADF wanaoendesha mauajio ya raia wilayani Beni na mashariki mwa nchi hiyo. Fredrick Nwaka amezungumza na wasikilizaji wetu ili kupata maoni yao.
Rais Paul Kagame wa Rwanda ametoa onyo kali kwa taifa lolote litakalochezea amani na usalam wa Rwanda, onyo linalokuja baada ya kuahirishwa kwa mazungumza baina ya Kigali na Kampala yanayolenga kumaliza mvutano uliopo baina ya mataifa hayo mawili. Fredrick Nwaka amekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji.
Ulimwengu unaadhimisha siku ya kisukari duniani huku idadi ya watu wanaougua maradhi hayo ikiongezeka kutoka milioni 108 mwaka 1980 hadi milioni 420 mwaka 2014. Mtindo wa maisha unatajwa kuwa mojawapo ya sababu. Je kubadili mtindo wa maisha kunaweza kusaidia kukabiliana na maradhi haya? Ungana na Fredrick Nwaka aliyekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji.
Tume ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Burundi imebaini katika ripoti yake kwamba "hali ya hofu" inatawala katika nchi hiyo, ikiwa imesalia miezi minane kabla ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2020. Katika ripoti yake, Tume ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Burundi, iliyoundwa na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mnamo mwaka 2016, inaelezea jinsi mamlaka nchini humo na vijana wa chama tawala, Imbonerakure, wanaendelea kuwafanyia vitisho raia kwa kuwalazimisha kujiunga, kuunga mkono au kuchangia chama tawala, CNDD-FDD. Fredrick Nwaka amekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu
Machache kati ya tuliyoyafumbata katika makala ya mtazamo wako kwa yaliyojiri wiki hii ni pamoja DRC yapata serikali mpya miezi saba baada ya kuapishwa kwa rais Felix Tshisekedi na katika uga wa kimataifa mkutano wa pamoja baina ya viongozi wa Afrika na Japan watia nanga huko Yakohama. Ungana na Fredrick Nwaka aliyekuandalia makala haya.
Dunia inaadhimisha wiki ya unyonyeshaji huku shirika la umoja wa mataifa la watoto UNICEF likitoa wito kwa familia, jamii na serikali duniani kote kuandaa mazingira wezeshi kwa akina mama kunyonyesha watoto katika mazingira ya kazi. Fredrick Nwaka amekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu
Siku ya kimataifa ya kupinga biashara haramu usafirishaji wa binadamu ambayo huadhimishwa duniani kote ifikapo julai 3o kila mwaka. Fredrick Nwaka amekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu ili kupata maoni yao.
Donald Trump, rais wa Marekani ametoa kauli kali ya kuwataka wabunge wanne wa Democrats kurudi waliokotoka, matamshi ambayo yamezua hofu huku wabunge hao wakimshutumu Trump kwa matamshi ya ubaguzi na kumtaka aombe radhi. Fredrick Nwaka amekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji ili kupata maoni yao
Ugonjwa wa ebola umeripotiwa kuingia nchini Uganda katika wilaya ya Kasese, Je mataifa ya Afrika mashariki yanachukua hatua zipi? Fredrick Nwaka amekuandalia makala ya habari rafiki kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu
Waandamanaji nchini Sudan wameingia siku ya pili ya maandamano ya kutotii sheria ili kushinikiza jeshi kukabidhi madaraka kwa raia. Je hatua hiyo itafanikiwa? Ungana na Fredrick Nwaka aliyekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu.
Mwanasiasa wa upinzani nchini DRC, Moise Katumbi ametangaza kufanya ziara katika majimbo yote nchini humo kwa kile anasema ni kuunganisha vyama vya upinzani. Je atafanikiwa? Fredrick Nwaka amekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu
Ungana na Fredrick Nwaka wiki hii akikuletea makala ya Mtazamo wako kwa yaliyojiri wiki hii na baadhi ya habari muhimu ni Rais wa DRC kumteua Sylivester Ilunga Ilukamba kuwa waziri mkuu wa taifa hilo, Cyril Ramaphosa aapishwa kuwa rais wa Afrika Kusini na Narendra Modi achaguliwa tena kuwa waziri mkuu wa India
Ulimwengu leo unaadhimisha siku ya wafanyakazi huku wafanyakazi wakikabiliwa na changamoto mbalimbali. Je serikali za Afrika zinatia juhudi katika kutafuta majawabu ya changamoto zinazowakabili wafanyakazi. Fredrick Nwaka amekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu.
Machi 8 kila mwaka ulimwngu unaadhimisha siku ya wanawake. Je kuna mchango wa kundi hili katika kuibadili jamii? Fredrick Nwaka amezungumza na wasikilizaji wetu ili kupata maoni yao.
Mgogoro wa kidilpomasia baina ya Rwanda na Uganda umechukua sura mpya baada ya wafanyabiashara na wananchi wa Uganda kulalama kuzuiwa na maofisa wa Uganda kutumia mpaka wa Gatuna kwa shughuli za usafirishaji. Fredrick Nwaka amezungumza na wasikilizaji ili kupata maoni yao
Raia zaidi ya elfu kumi wa Sudan Kusini wamekimbilia nchini DRC kwa kile wanasema ukosefu wa usalama na kuapa kutorejea nchini mwao. Haya yanajiri katika wakati ambao kunaripotiwa kuimarika kwa hali ya usalama na amani. Fredrick Nwaka amekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu
Makala haya ya Gurudumu la Uchumi inaangazia changamoto za raia kushindwa kupanga bajeti hususani mwishoni mwa mwaka na kujikuta wakiwa na changamoto za kiuchumi mwanzoni mwa mwaka. Ungana na Fredrick Nwaka, aliyekuandalia makala haya.