POPULARITY
Hii leo jaridani tunaangazia vita nchini Iran, sauti za vijana katika wiki ya pili ya mkutano wa CSW70, na mafunzo ya vitendo kwa vijana nchini Uganda kuhusu mbinu za kisasa za ufugaji nyuki.Katika siku ya 16 ya vita nchini Iran iliyoanza baada ya Marekani na Israeli kushambulia taifa hilo la Mashariki ya Kati na kisha lenyewe kujibu mashambulizi yanayosambaa hadi ukanda mzima wa eneo hilo, hii leo suala hilo limepatiwa kipaumbele kwenye Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu huko Geneva, Uswisi ambapo mtaalamu huru wa Umoja wa Mataifa, Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi na Mwakilishi wa Iran wametoa maoni yao kuhusu kinachoendelea na nini kifanyike.Sauti za vijana zinaendelea kusikika kwa nguvu katika wiki ya pili ya kikao cha 70 cha Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani kinachofanyika hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani ambapo wanaharakati, watunga sera na wadau kutoka sehemu mbalimbali za dunia wamekusanyika kujadili namna ya kuendeleza haki , haki za kisheria na fursa kwa wanawake na wasichana.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) na wadau wake chini ya mpango Kilimo na Msaada wa Masoko (AMS), vijana nchini Uganda wamepata mafunzo ya vitendo kuhusu mbinu za kisasa za ufugaji nyuki. Mafunzo hayo yamewasaidia kukimu mahitaji yao kupitia uzalishaji wa asali.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Sauti za vijana zinaendelea kusikika kwa nguvu katika wiki ya pili ya kikao cha 70 cha Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani kinachofanyika hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani ambapo wanaharakati, watunga sera na wadau kutoka sehemu mbalimbali za dunia wamekusanyika kujadili namna ya kuendeleza haki , haki za kisheria na fursa kwa wanawake na wasichana. Flora Nducha amepata fursa ya kuzungumza na mmoja wa vijana washiriki kutoka Ghana na kutuandalia taarifa hii
Wanawake kutoka jumuiya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wana jiandaa kwa sherehe maalum ya siku ya wanawake.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia yaliyojiri katika mkutano wa CSW70, ambapo kandoni mwa mkutano huo Assumpta Massoi wa Idhaa hii alipata fursa ya kuzungumza na Lucy Kabyemera, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Makazi nchini Tanzania aliyeongoza kikao hicho na kumpatia ufafanuzi wa mambo kadhaa ikiwemo mabadiliko ya sera.Idadi ya watu waliokimbia makazi yao nchini Iran imeongezeka kwa kasi na kufikia takriban watu milioni 3.2 kutokana na mashambulizi makali yanayozidi kushika kasi nchini humo kutoka jeshi la Marekani na Israeli huku nayo Iran ikijibu mashambulizi. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, kupitia taarifa yake iliyotolewa leo jijini Geneva, Uswisi, limebainisha kuwa kaya kati ya 600,000 na milioni 1 zimepoteza makazi yao, huku wengi wakikimbia miji mikubwa kama Tehran kuelekea maeneo ya vijijini na mikoa ya kaskazini kutafuta usalama. “Hali hii imeleta hofu kubwa ya kuongezeka kwa mahitaji ya kibinadamu kadiri uhasama unavyozidi kusambaa katika maeneo mbalimbali,” imesema taarifa hiyo.Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus ameelezea kuhusu matumizi makubwa ya fedha kwenye silaha za kivita wakati huu ambapo dunia ina uhitaji mkubwa wa msaada wa chakula na maeneo kadhaa kuwa na hali mbaya ya chakula huku mgao wa chakula ukitolewa mara moja au mbili badala ya mara tatu sababu ya ufinyu wa ufadhili. Dkt Tedros amesema matumizi ya kijeshi duniani yamefikia $ trilioni 2.7 - katika mwaka mmoja. Na kulingana na makadirio ya Umoja wa Mataifa, kukomesha njaa duniani ifikapo mwaka wa 2030 kutahitaji $ bilioni 93 kila mwaka. “Hiyo ina maana kwamba tunatumia karibu mara 30 zaidi kila mwaka kuuana kuliko kuhakikisha kila mtu anakula.”Leo ni Siku ya Mlo shuleni. Mamilioni ya watoto duniani kote huenda shuleni kila siku bila kutia chochote tumboni. Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani WFP, zaidi ya watoto milioni 100 katika nchi zenye kipato cha chini na cha kati hukabiliwa na njaa kila siku. Hali hii huathiri uwezo wao wa kuzingatia masomo, kujifunza na kufaulu darasani. Ili kukabiliana na changamoto hiyo, WFP inaunga mkono serikali mbalimbali kuhakikisha watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanapata milo shuleni ili wawe na afya njema na wawe tayari kujifunza.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Oluwaseun Ayodeji Osowobi, mwanaharakati wa haki za wanawake nchini Nigeria amezungumzia umuhimu wa kushirikisha wanaume katika harakati za kupigania haki za wanawake duniani wasichana. Rashid Malekela na maelezo zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia habari ya kusikitisha ya kifo cha mfanyakazi wa UNICEF nchini DRC, na ujumbe wa washiriki wa mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake Duniani CSW70 leo unaendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York.Shirika la UNICEF limesema limesikitishwa na kushtushwa na kifo cha mfanyakazi wake Karine Buisset kilichotokea katika shambulio linaloripotiwa kufanywa na droni katika mji wa Goma mashariki mwa Jamhriy a Kidemokrasia ya Congo DRC, eneo ambalo kwa muda mrefu limekumbwa na mapigano na hali mbaya ya kibinadamu. Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEF, Catherine Russell kupitia mtandao wake wa kijamii wa X, amesema shirika hilo pamoja na wafanyakazi wake duniani wameumizwa sana na tukio hilo.Oluwaseun Ayodeji Osowobi, mwanaharakati wa haki za wanawake nchini Nigeria amezungumzia umuhimu wa kushirikisha wanaume katika harakati za kupigania haki za wanawake duniani wasichana.Mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake Duniani CSW70 leo unaendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York ukiwa umeingia siku ya 3. Na vijana hawakusahaulika wamepewa nafasi ya kutoa maoni yao na mapendekezo yao kuhusu maudhui ya mwaka huu ambayo yanasisitiza umuhimu wa kuchukuliwa kwa hatua madhubuti kuhusu haki za wanawake, usawa wa kisheria na ushiriki wa vijana.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake Duniani CSW70 leo unaendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York ukiwa umeingia siku ya 3. Na vijana hawakusahaulika wamepewa nafasi ya kutoa maoni yao na mapendekezo yao kuhusu maudhui ya mwaka huu ambayo yanasisitiza umuhimu wa kuchukuliwa kwa hatua madhubuti kuhusu haki za wanawake, usawa wa kisheria na ushiriki wa vijana. Flora Nducha amekutana na baadhi yao kusikia maoni yao
Wanawake kote duniani walijitokeza mitaani kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, wakitaka kukomeshwa kwa ukosefu wa usawa na ubaguzi.
Waziri Mkuu wa Australia amesema serikali itamsaidia yeyote kati ya timu ya soka ya wanawake ya Iran ambaye bado hajaomba hifadhi hapa.
Alya Abu Shawish, mwanamke aliyeko mstari wa mbele kuondoa hatari ya mabomu Gaza (OVERNIGHT)Hii leo pia hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, imefanyika hafla ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake ambayo duniani kote iliadhimishwa jana Jumapili. Katika muktadha huo huo ninamualika Anold Kayanda atupeleke Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel kumwangazia Alya Abu Shawish, Mwanamke anayefanya kazi katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kutoa huduma ya kutegua mabomu, UNMASakisaidia kuwaweka salama wenzake katika mojawapo ya mazingira hatari zaidi duniani. Karibu Anold.(Taarifa ya Anold)Asante Flora,Hakika Gaza ni moja ya mazingira hatari duniani kwa sasa. Alya Abu Shawish anaposhuka kwenye gari kabla ya kuingia ofis iza UNMAS zilizoko Deir al-Balah katikatimwa Gaza, anavaa jaketi la kujikinga na risasi.Ndani ya ofisi amesimama mbele ya ramani ya kidijitali, akifuatilia mienendo ya timu za wafanyakazi walioko mitaani zilizosambazwa kote katika ukanda huo wa Gaza ili kufanya kazi za kuondoa mabaki ya vilipuzi vya vita katika eneo hilo.Baada ya mipango yote kukamilika ofisini, sasa Alya Abu anaendesha gari akiwa na wenzake kuelekea kazini nje ya ofisi. Anaeleza akisema,(Sauti ya Alya Abu Shawish) – Sharon“Kazi yangu kama mwanamke katika eneo hili inaonyesha kwamba wanawake wanaweza kuwa na nafasi muhimu katika kuhakikisha usalama na kuleta mabadiliko yanayoonekana, hata katika mazingira hatari na yenye changamoto kubwa zaidi katika Ukanda wa Gaza.”Alya Abu Shawish anaonekana na wenzake mitaani wakifanya kazi. Watoto wanafuata, kwa vyovyote wakitambua kazi muhimu inayofanywa na UNMAS kufanya mazingira yawe salama dhidi ya vilipuzi.Hata hivyo, nyuma ya dhamira hii ya kitaaluma kuna hadithi binafsi inaloakisi hali halisi ya maelfu ya wanawake huko Gaza.(Sauti ya Alya Abu Shawish) – Sharon“Kama mwanamke na mama, nimepitia changamoto nyingi ambazo wanawake wa Kipalestina huko Gaza hukabiliana nazo wakati wa vita hofu, kuhama makazi, uhaba wa mahitaji muhimu, na hali ya kutokuwa na uhakika kila wakati. Kama wanawake wengi hapa, nimelazimika kuilinda familia yangu huku nikikabiliana na hali hizi ngumu.”Licha ya changamoto hizi, Alya Abu Shawish anasema uzoefu wake umeimarisha azma yake ya kuwasaidia wengine na kumhamasisha kufanya kazi katika uwanja ambao mara nyingi huonekana kutawaliwa na wanaume.(Sauti ya Alya Abu Shawish) – Sharon“Uzoefu huu haukunidhoofisha; uliimarisha azma yangu ya kuwasaidia wengine. Ulinitia moyo kufanya kazi katika masuala ya kuondoa mabomu na usalama na UNMAS uwanja ambao mara nyingi huonekana kuwa wa wanaume. Katika jukumu hili, ninachangia kupunguza hatari zinazosababishwa na mabaki ya vilipuzi vya vita na kusaidia jamii kuishi kwa usalama zaidi.”Wanawake wengine katika timu za UNMAS pia hushiriki katika shughuli za kuhamasisha jamii kuhusu hatari za mabaki ya vilipuzi, ambayo sasa yamekuwa moja ya changamoto kubwa zaidi za kibinadamu huko Gaza kadri uharibifu unavyoendelea kuenea. Kwa Abu Shawish, juhudi hizi hubeba ujumbe unaokwenda mbali zaidi ya kazi kwani inaonesha uimara na mnepo.
CSW70 yang'oa nanga ikisistiza haki, haki ya kisheria na hatua kwa wanawake na wasichanaKikao cha 70 cha Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani CSW70 kimefungu pazia hii leo jijini New York Marekani, mwaka huu kikibeba maudhui “Haki, haki ya kisheria na Hatua kwa wanawake na wasichana wote”. Zaidi ya washiriki 9000 wakiwemo wawakilishi wa serikali, asasi za kiraia, Umoja wa Mataifa na mashirika yake na wadau wengine wanatarajiwa kushiriki jukwaa hili litakalokunja jamvi 19 Machi likijumuisha mikutano ya kando 750. Leah Mushi amefuatilia ufunguzi huo na hii hapa taarifa yake.(TAARIFA YA LEAH MUSHI)Natts……Katika ukumbi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani …. huu ni ufunguzi wa Mkutano wa 70 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW70 Mgeni rasmi ni Katibu Mkuu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ambaye ameeleza…. Nats.. (SG cut 1 play under 00:06 I am so pleased to be in a…. )furaha yake kuwa katika ukumbi uliojaa viongozi waliokataa kukubali ukosefu wa usawa kama jambo lisiloepukikaKatika hotuba yake Guterres amesema dunia bado inaongozwa zaidi na mfumo dume unaowapa wanaume nafasi kubwa ya mamlaka. (SG Cut 1 – Fiesal )“Tunaishi katika ulimwengu unaotawaliwa na wanaume, na utamaduni unaotawaliwa na wanaume. Usawa wa kijinsia ni suala la mamlaka. Hakuna hatua hata moja mbele kwa haki za wanawake ambayo imewahi kutolewa. Bali imeshinda. Wameshinda vizazi vya wanawake na wasichana, watetezi na wanaharakati, viongozi wa jamii na watafuta haki. Umeshinda wewe na kabla ya kitu chochote napenda kusema Asante.”Amesema hali hiyo imekuwa changamoto kubwa katika jitihada za kufikia usawa wa kijinsia katika taasisi nyingi duniani. Hata hivyo, ndani ya UN kumekuwa na maendeleo muhimu katika kuongeza uwakilishi wa wanawake katika nafasi za juu za uongozi.Kwa mujibu wa Katibu Mkuu huyo, wakati alipoanza uongozi wake, alijiwekea lengo la kuhakikisha kunakuwa na uwiano sawa kati ya wanawake na wanaume katika ngazi za juu za uongozi wa Umoja wa Mataifa. Leo, amesema lengo hilo limefikiwa.(SG cut2 – Fiesal )“Kwa mara ya kwanza katika historia ya Umoja wa Mataifa, wanawake sasa wanaunda nusu kamili ya nguvu kazi ya Umoja wa Mataifa katika vitengo vya kitaaluma na vya juu zaidi. Na kwa mara ya kwanza, tulifikia usawa katika uongozi mkuu. Tumefanya hivyo ikiwa ni miaka miwili kabla ya ratiba - lakini pia natambua imekuwa ni miaka 80 imechelewa.”Katika hotuba yake, Katibu Mkuu wa António Guterres amesisitiza kuwa kufikia usawa wa kijinsia si suala la haki kwa wanawake pekee, bali ni hatua muhimu kwa maendeleo ya dunia nzima. Amesema jamii ambazo wanawake wanapata haki na fursa sawa huwa na maendeleo ya haraka zaidi, uchumi imara na taasisi zenye uwajibikaji zaidi, akisisitiza kuwa kuimarisha usawa wa kijinsia ni msingi muhimu wa kufikia maendeleo endelevu duniani.Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa amesema bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili kuhakikisha wanawake wanapata haki na fursa sawa katika jamii duniani.Ametaja maeneo matano muhimu ya kuharakisha haki na usawa kwa wanawake ambayo ni kuhakikisha haki sawa za kiuchumi kwa wanawake, kuimarisha uwakilishi wao katika maamuzi ya kisiasa, kupanua upatikanaji wa elimu na fursa za kazi, kuondoa ukatili dhidi ya wanawake na wasichana, pamoja na kulinda haki za wanawake katika dunia ya kidijitali.Kwa upande wake mwenyekiti wa Kikao hicho cha 70 cha Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani CSW70 Maritza Chan Valverde amezungumzia maudhui ya mwaka huu ambayo ni “Haki, haki ya kisheria na Hatua kwa wanawake na wasichana wote nakusema kila mtu anajukumu la kufanya (Maritza cut )“Ondo vikwazo na uhakikishe kwamba haki inakuwa ukweli halisi kwa…
Katika Jarida la Habari Hii leo Kutoka Umoja wa Mataifa Assumpta Massoi anakuletea-Mashirika ya UN yatahadharisha kuongezeka kwa vurugu Mashariki ya Kati.-Mafunzo ya haki ya kumiliki ardhi yanayotolewa na Kituo cha Msaada wa Kisehria kwa Wanawake WLAC yamebadilisha maisha ya familia ikiwemo ya Jovita Provius: WLAC-Mpango wa Jamii Rafiki kwa Mtoto wazinduliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF katika Kaunti ya Samburu
Hii leo jaridani tunaangazia hatari inayoongezeka kwa usalama wa nyuklia huku vita vikiendelea kushika kasi nchini Iran, masuala ya afya ya wanawake na watoto nchini Burundi, na maisha ya baadaye ya watoto katika ukanda wa Gaza.Mwelekeo mpya wa mzozo katika eneo la Mashariki ya Kati ukiwa umeingia siku yake ya tatu leo Jumatatu ukichochewa na mashambulizi ya mabomu dhidi ya Iran yaliyofanywa na Israel na Marekani, mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la nishati ya atomiki, IAEA, Rafael Grossi amehimiza kurejea kwa diplomasia, akitaja “hatari inayoongezeka kwa usalama wa nyuklia” katika eneo hilo.Uhaba wa vifaa na maji safi na salama katika kambi ya muda ya wakimbizi ya Busuma iliyoko mashariki mwa Burundi umekuwa changamoto kubwa kwa wanawake wajawazito wanaojifungua kambini hapo, wakati huu ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi, (UNFPA) nchini Burundi linasema katika kipindi cha mwezi mmoja takribani watoto 200 wamezaliwa.Hakuna maisha ya baadaye! Siyaoni maisha ya baadaye kwani sioni wanaoshikamana nasi! Hayo ni sehemu tu ya maoni ya watoto walioko Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli wakati huu ambapo makombora yanaendelea kurindima, mustakabali wao uko mashakani, na wanachohitaji kama inawezekana ni amani na ujenzi mpya wa makazi ili waweze kurejea katika maisha ya kawaida ndani ya nyumba zao na kuacha kuishi kama wakimbizi katika ardhi yao wenyewe.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Uhaba wa vifaa na maji safi na salama katika kambi ya muda ya wakimbizi ya Busuma iliyoko mashariki mwa Burundi umekuwa changamoto kubwa kwa wanawake wajawazito wanaojifungua kambini hapo, wakati huu ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi, (UNFPA) nchini Burundi linasema katika kipindi cha mwezi mmoja takribani watoto 200 wamezaliwa. Assumpta Massoi na taarifa zaidi.
Fundi wa magari mwanamke kutoka nchini Ethiopia anayehudumu na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini, UNMISS, Meja Tigist Ferede ametunukiwa nishani ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, kwa kusimamia jukumu muhimu la wanawake katika operesheni za kulinda amani nje ya kushika bunduki. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Rashid Malekela.
Hii leo jaridani tunaangazia haki za wanawake, na uhuru wa kiraia, ujumbe wa Bi Cindy McCain, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa WFP, na ripoti ya IPC kuhusu njaa nchini Somalia.Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu Volker Türk ameonya kuwa shinikizo linaongezeka duniani kote dhidi ya haki za wanawake, uhuru wa kiraia na taasisi za kimataifa akitoa wito kwa serikali kujitolea upya katika ushirikiano, uwajibikaji na utawala wa sheria.Kiongozi wa shirika kubwa zaidi la msaada wa chakula duniani ametangaza kujiuzulu. Bi. Cindy McCain, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP amesema atajiuzulu wadhifa wake huo baada ya miezi mitatu ili kuzingatia afya yake, akisema bado hajapona kikamilifu baada ya kupata kiharusi mwaka jana 2025.Fundi wa magari mwanamke kutoka nchini Ethiopia anayehudumu na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini, UNMISS, Meja Tigist Ferede ametunukiwa nishani ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, kwa kusimamia jukumu muhimu la wanawake katika operesheni za kulinda amani nje ya kushika bunduki.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu Volker Türk ameonya kuwa shinikizo linaongezeka duniani kote dhidi ya haki za wanawake, uhuru wa kiraia na taasisi za kimataifa akitoa wito kwa serikali kujitolea upya katika ushirikiano, uwajibikaji na utawala wa sheria. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Benki ya Dunia inasema hata katika nchi zenye sheria za kisasa kuhusu usawa kazini, nchi hizo zimeshindwa kuzitekeleza, hadi sasa hakuna nchi iliyofikia kiwango cha juu cha usawa kazini, n ani asilimia kidogo tu ya wanawake wanaishi kwenye nchi zenye angalau sheria bora, huku mataifa 70 ikiwemo Misri, Madagascra na Somalia zikipiga hatua katika kuboresha mazingira ya usawa kati yam waka 2023 na 2025.
Benki ya Dunia inasema hata katika nchi zenye sheria za kisasa kuhusu usawa kazini, nchi hizo zimeshindwa kuzitekeleza, hadi sasa hakuna nchi iliyofikia kiwango cha juu cha usawa kazini, n ani asilimia kidogo tu ya wanawake wanaishi kwenye nchi zenye angalau sheria bora, huku mataifa 70 ikiwemo Misri, Madagascra na Somalia zikipiga hatua katika kuboresha mazingira ya usawa kati yam waka 2023 na 2025.
Leo ni siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi mwaka huu mauadhui yakihimiza “Sayansi kwa Mustakabali Jumuishi kwa Wanawake na Wasichana” Kwamujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , Sayansi na Utamaduni UNESCO leo hii , wanawake wanachangia chini ya theluthi moja ya watafiti duniani, kulingana hivyo kuziba pengo hili la kijinsia si suala la haki pekee ni muhimu kwa ubora, uhalisia na mchango wa sayansi, teknolojia na ubunifu. Flora Nducha na taarifa zaidi
Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya IPU kuhusu uhasama wa wabunge, siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi, na yalitojiri katika Jukwaa la akili unde au AI lililofanyika kwa siku mbili huko Nairobi, nchini Kenya.Wabunge kote ulimwenguni wanakabiliwa na viwango vinavyoongezeka vya vitisho, unyanyasaji na vurugu kutoka kwa umma imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na Muungano wa Mabunge Duniani (IPU). Rashid Malekela na taarifa zaidi.Leo ni siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi mwaka huu mauadhui yakihimiza “Sayansi kwa Mustakabali Jumuishi kwa Wanawake na Wasichana” Kwamujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , Sayansi na Utamaduni UNESCO leo hii , wanawake wanachangia chini ya theluthi moja ya watafiti duniani, kulingana hivyo kuziba pengo hili la kijinsia si suala la haki pekee ni muhimu kwa ubora, uhalisia na mchango wa sayansi, teknolojia na ubunifu.Jukwaa la akili unde au AI lililofanyika kwa siku mbili huko Nairobi, nchini Kenya limekunja jamvi ambapo mmoja wa washiriki amesema wanaodai kuwa bara la Afrika liko nyuma kwenye teknolojia hiyo, ni dhahiri shairi hawalifahamu vema bara hilo lenye mataifa 54.
Hii leo jaridani Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na Wakili Amon Mpanju, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kutoka Tanzania aliyehudhuria Mkutano wa Kamisheni ya Maendeleo ya Kijamii (CSocD64).Mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yametoa onyo kali kuhusu hali mbaya ya kibinadamu inayowakumba watoto nchini Sudan. Mashirika hayo lile la kuhudumia watoto UNICEF, la afya WHO na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu wamenasema ghasia zisizoisha, njaa na magonjwa vinawasababisha watoto kupoteza Maisha na kudhoofika, huku mashambulizi dhidi ya vituo vya afya na vikwazo vya upatikanaji wa misaada vikizorotesha juhudi za kuwaokoa. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, msemaji wa UNICEF, Ricardo Pires, amesema “Katika baadhi ya maeneo ya jimbo la Darfur Kaskazini, zaidi ya nusu ya watoto wote wanakabiliwa na utapiamlo mkali, si makadirio, si mfano, imethibitishwa.”.Kikosi cha 12 cha Ulinzi wa Amani kutoka Tanzania TANZBAT 12 kinachohusumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Condo DRC chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO kimeendelea kudumisha uhusiano wa kijamii na wakazi wa mji wa Beni Mashariki mwa DRC, kwa kutoa msaada wa vifaa vya elimu kwa wanafunzi katika shule ya msingi Ngite iliyopo eneo la Mavivi. Mkuu wa shule hiyo Neema Nyamwaka amewashukuru walinada amani hao kutoka Tanzania kwa kujali sekta ya elimu.Leo ni siku ya mikunde duniani Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO likisistiza umuhimu kwa chakula hicho kwa lishe na mazingira. Huko Kigoma Tanzania FAO kupitia mpango wa Pamoja wa KJP imekuwa ikitoa mafunzo kwa wakulima kuhusu umuhimu wa mazao ya jamii ya mikunde huyu ni mmoja wa wanufaika wa mafunzo hayo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Atokeapo mtoto wa fuko mshike japo wawinda fuko.”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
Ukeketaji au FGM ni jinamizi linalowaandama waathirika maisha yao yote likisababisha changamoto sio tu za kimwili lakini pia za kiafya na kuwaacha na makovu yasiyofutika. Katika Kaunti ya Tana River Kusini Mashariki mwa Kenya tunakutana na manusura na shujaa mwanaharakati wa kupambana na mila hiyo potofu ya ukeketaji Saadia Hussein, raia wa Somalia anayeishi Kenya hivi sasa .Ni Mkurugenzi mtendaji na mwanzilishi wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Brighter Society Initiative. Anatusimulia safari yake ya machungu ya ukeketaji
Zaidi ya wasichana milioni 4.5 duniani kote, wengi wao wakiwa wenye umri wa chini ya miaka mitano, wako hatarini kufanyiwa ukeketaji mwaka huu pekee, wameonya viongozi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa katika ujumbe wao wa siku hii ya kimataifa ya kutokomeza ukeketaji kwa wanawake na watoto wa kike. Rashid Malekela na maelezo zaidi.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Jamhuri Africa ya Kati CAR kusikia mama mkimbizi anayesimulia aliyoyapitia, maisha ya uhamishoni na alivyojipatia nguvu iliyo kuu kuliko silaha yoyote ya vita. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na neno la wiki.Nchini Ethiopia, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO limeeleza kwamba Ethiopia imefanikiwa kutekeleza mizunguko minne ya uchanjaji watoto kwa njia ya matone dhidi ya ugonjwa wa polio. Mwaka jana 2025 Ethiopia kwa kutumia chanjo ya nOPV2 ilitekeleza uchanjaji huo kupitia mzunguko mmoja wa nchi nzima na mitatu kupitia maeneo mbalimbali ya nchi na kufanikiwa kuwafikia watoto milioni 26 katika mikoa yote.Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO), Beth Bechdol, ameeleza umuhimu wa kilimo wakati wa migogoro kulingana na mafanikio aliyoyashuhudia wakati wa ziara yake nchini Haiti na majirani zao Jamhuri ya Dominika.Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, (FAO) kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Asia (ADB) wametangaza kuwa wanatekeleza mpango wa dola milioni 100 ili kuimarisha uhakika wa chakula na lishe pamoja na kurejesha kipato kinachotokana na kilimo kwa zaidi ya watu milioni moja walio katika mazingira magumu kote nchini Afghanistan.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya "SIKU ZA JANGUO."Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na kilimo Duniani FAO, kupitia mradi wake wa masuala ya biashara HASTEN limeendesha warsha maalum ya kuanzisha biashara kwa vijana na wanawake, mjini Kigali Rwanda, lengo likiwa ni kuwapa miradi 10 mipya ya biashara itakayofanyika kwa msaada maalum kutoka kwa wakufunzi wa kitaifa na kimataifa juu ya mbinu za kupanua biashara, kuongeza ufanisi na kuchangia katika malengo ya maendeleo endelevu SDGs. Sheilah Jepng'etich na taarifa zaidi.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya ambako wasichana juhudi za kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) zimewezesha vijana wa kike kushiriki masomo ya Teknolojia ya Habari na Maewasiliano, TEHAMA na kujifunza stadi za teknolojia ili waweze kuedeleza biashara ya mtandaoni pamoja na matumizi mengine.Zaidi ya watu nusu milioni wameathiriwa na mafuriko makubwa katika mikoa ya kusini na kati ya Msumbiji, huku mvua kubwa ikiendelea kuvuruga usafiri, huduma za afya na njia za ugavi. Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA nchini humo, Paola Emerson, amewaambia waandishi wa habari huko Geneva, Uswisi kuwa majimbo ya Gaza, Sofala na Maputo ndiyo yaliyoathirika vibaya zaidi.Huko Mashariki ya Kati mapema leo Jumanne, vikosi vya Israel vimebomoa kwa tingatinga makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA, huko Yerusalemu Mashariki eneo linalokaliwa kimabavu na Israel. Mkuu wa UNRWA, Philippe Lazzarini, amelieleza tukio hilo kama “shambulio lisilo na kifani dhidi ya Umoja wa Mataifa,”.Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, leo imesema imeanza kutekeleza mpango wa kurejesha kwa hatua mamlaka ya dola katika mji wa Uvira, mashariki mwa nchi hiyo, kufuatia kuondoka kwa kundi lenye silaha la AFC/M23. Serikali inasema vikosi vya usalama, polisi na huduma nyingine za serikali vinarejea ili kulinda raia, kulinda mali na kuleta utulivu katika eneo hilo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mtaalam wetu ONNI SIGALA Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA, anafafanua maana ya neno “ KING'ANI”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
Hii leo jaridani tnaangazia uchumi wa dunia unaoendelea kukua ila maendeleo katika kupata kazi zenye ubora na staha yamekwama, pia tunaangazia afya ya uzazi nchini Uganda na homa ya bonde la ufa (RVF) kwa mifugo nchini Tanzania. Licha ya uchumi wa dunia kuendelea kukua, maendeleo katika kupata kazi zenye ubora na staha yamekwama, huku mamilioni ya wafanyakazi wakisalia katika lindi la umaskini na ajira zisizo rasmi. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani (ILO)iliyotolewa hii leo huko Geneva Uswisi.Baada ya kuhitimu shahada ya udaktari nchini mwake Uganda, huko Afrika Mashariki, Daktari mmoja alibaini kuwa hiyo haitoshi, bali alienda mbali zaidi kubuni kifaa kinachosaidia wajawazito hasa wale wanaoishi maeneo ya ndani zaidi kufahamu hali ya afya ya watoto wao tumboni, na hivi sasa kifaa hicho kinaelekea kupata hakibunifu kupitia shirika la Umoja wa Mataifa la Hakibunifu, WIPO.Mfumo wa kubaini mapema homa ya bonde la ufa (RVF) iliyobuniwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO nchini Tanzania imewezesha wizara, wakulima, na madaktari wa mifugo kuchukua hatua za mapema, hivyo kulinda maisha na mali dhidi ya ugonjwa huo unaoshambulia mifugo na binadamu.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Baada ya kuhitimu shahada ya udaktari nchini mwake Uganda, huko Afrika Mashariki, Daktari mmoja alibaini kuwa hiyo haitoshi, bali alienda mbali zaidi kubuni kifaa kinachosaidia wajawazito hasa wale wanaoishi maeneo ya ndani zaidi kufahamu hali ya afya ya watoto wao tumboni, na hivi sasa kifaa hicho kinaelekea kupata hakibunifu kupitia shirika la Umoja wa Mataifa la Hakibunifu, WIPO. Assumpta Massoi anasimulia zaidi.
Licha ya uchumi wa dunia kuendelea kukua, maendeleo katika kupata kazi zenye ubora na staha yamekwama, huku mamilioni ya wafanyakazi wakisalia katika lindi la umaskini na ajira zisizo rasmi. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani (ILO)iliyotolewa hii leo huko Geneva Uswisi. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, (UNDP), nchini Kenya, kupitia mradi wa kuhimili tabianchi au Climate Promise Guarantee, limewawezesha wanawake wa jamii ya asili katika Kaunti ya Narok, nchini humo kuongoza juhudi za uhifadhi wa misitu huku wakilinda urithi wao wa kitamaduni na kuboresha maisha ya familia zao. Sheilah jepnge'tich na taarifa zaidi.
Saratani ya shingo ya kizazi ndiyo saratani inayowapata wanawake wengi zaidi nchini Rwanda kwani takribani kila mwaka kati ya wagonjwa wapya 1230, 830 hufariki dunia. Ili kupunguza mzigo wa ugonjwa huu na kuokoa maisha, mwaka 2020 Rwanda ilianzisha mkakati wa kitaifa unaoendana na lengo la Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) la kuondoa saratani ya shingo ya kizazi ifikapo 2030. Selina Jerobon anafafanua zaidi.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi (UNFPA), nchini Burundi, linaongeza juhudi zake kukabiliana na mahitaji yanayoongezeka ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) wanaokimbia mapigano yanayoendelea mashariki taifa hilo la Maziwa Makuu ili kulinda afya, usalama na utu wao na wa jamii zinazowapokea. Sheilah Jepng'etich na taarifa zaidi
Kukusanya fedha ili kupunguza makazi duni miongoni mwa wanawake ndiyo lengo la hoteli moja mjini Sydney, moja kati ya biashara elfu kumi na mbili ya kijamii nchini Australia zinazochanganya faida na lengo. Likizo za kiangazi ni wakati wenye mafanikio kwa maeneo mengi ya utalii. Lakini hoteli ya Song mjini Sydney inazingatia zaidi ya kutengeneza pesa. Inasaidia miradi ya makazi ya YWCA kwa wanawake wanaohitaji msaada. Meneja Mkuu Jon Ackary anaeleza.
Ubakaji unaotumika kama silaha ya vita huacha majeraha yasiyofutika ya mwili, akili na ya roho. Katika ushuhuda huu wenye nguvu, manusura mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa anaishi kama mkimbizi nchini Burundi, anasimulia safari yake ya maumivu baada ya kunusurika ukatili wa kingono uliomsababishia majeraha makubwa ya mwili, ikiwemo fistula, pamoja na makovu ya kina ya kihisia.Sheilah Jepng'etich na taarifa zaidi
Hii leo jaridani tunakuletea ufafanuzi wa umuhimu wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Haki za binadamu kutoka kwa Seifu Magango Msemaji wa Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa ambaye anaanza kwa kuzungumzia azimio la tamko hilo la haki za binadamu.Utafiti uliofanywa na Tume ya Ulaya kwakushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa linalaoshughulikia masuala ya wanawake UN Women umebaini kuwa wanawake saba kati ya kumi wakiwemo watetezi wa haki za binadamu, wanaharakati na waandishi wa habari wanakumbana na ukatili mtandaoni.Meneja Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masuala ya watoto UNICEF Tess Ingram yupo ziarani Ukanda wa Gaza huko Mashariki ya kati ambapo hii leo amezungumza na waandishi wa habari jijini Geneva Uswisi na kuwaeleza aliyoshuhudia huko ikiwemo wajawazito walio na utapiamlo kujifungua watoto wenye uzito mdogo au kuzaliwa kabla ya wakati, ambao wengine wanakufa katika vyumba vya wagonjwa mahututi au wengine hupona lakini watoto hao hukabiliwa na utapimlo au matatizo mengine ya kiafya.Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Kutokomeza Ubaguzi wa Rangi CERD, leo imetoa onyo kali kwa Sudan, ikieleza wasiwasi mkubwa kuhusu ongezeko la matumizi ya lugha ya kudhalilisha, kauli za chuki na ukiukaji Mkubwa wa haki za binadamu unaochochewa na misingi ya kikabila. Kamati imesem Mashambulizi haswa dhidi ya jamii za Fur, Masalit na Zaghawa, yanadaiwa kufanywa na Kikosi cha Msaada wa Haraka RSF na makundi washirika katika maeneo ya El Fasher, Darfur Kaskazini.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "PEKUPEKU"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kwa mwanariadha na mchchemuzi wa masuala ya wanawake, akieleza hatua zinazochukuliwa kutokomeza dhulma wa kijinsia. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze lugha ya Kiswahili.Huku mapigano yakizidi kushika kasi katika eneo la Kordofan nchini Sudan, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ameonya hii leo kuhusu hatari ya mashambulizi mapya dhidi ya raia, baada ya kuripotiwa vifo zaidi ya watu 269 kutokana na mashambulizi ya angani, mabomu na mauaji ya kiholela tangu mwishoni mwa mwezi Oktoba. Ofisi yake imeeleza kupokea taarifa za ulipizaji kisasi, utekaji, ukatili wa kingono na ulazimishaji wa watoto kujiunga na makundi ya kivita, huku miji kama Kadugli, Dilling na El Obeid ikikabiliwa na njaa, kuzingirwa na kukwama kwa misaada ya kibinadamu.Malaria, ugonjwa ambao takriban asilimia 95 ya vifo vinavyoripotiwa duniani ni kutoka nchi za Afrika tena kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka 5. Ulionekana kuweza kudhibitiwa lakini sasa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus, anasema unaelekea kubaya kutokana na kuongezeka kwa usugu wa dawa, hali inayotishia kuyafuta mafanikio yaliyookoa maisha ya watu milioni moja mwaka 2024 kupitia chanjo na vyandarua vipya vyenye dawa ya kukabiliana na mbu waenezao Malaria.Na tuhitimishie nchini Msumbiji ambako Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM Amy Pope amefanya ziara ya siku tatu na kujionea athari zilizoletwa na Mafuriko, vimbunga na kuzorota kwa usalama huko Kaskazini mwa nchi hiyo hali iliyosababisha zaidi ya 100,000 wameyakimbia makazi yao, na zaidi ya 600,000 wakihitaji msaada.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo ukumbi ni wake mlumbi wa lugha ya Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana za maneno "MADHALI"Mwenyeji wako ni Sabrina Moshi, karibu!
Hii leo jaridani tukiendelea kukupa taarifa mbalimbali kuhusu siku 16 za kuhamasisha umma kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake, leo tunaelekea Mjini Hoima Magharibi mwa Uganda kusikia hisia za wanawake kuhusu ukatili dhidi ya wanawake mtandaoni.Watu takribani 100,000 wamekimbia makazi yao kaskazini mwa Msumbiji ndani ya wiki mbili, huku Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi UNHCR likionya kuwa mashambulizi yanaongezeka na kuyakumba hata maeneo yaliyokuwa salama. Mwakilishi wa UNHCR, Xavier Creach, amesema mgogoro “unazidi kuzorota kwa kasi ya kutisha” huku familia zikikimbia usiku gizani wakati watu wenye silaha wakivamia vijiji vyao. UNHCR inasema linahitaji dola milioni 38.2 kukidhi mahitaji yanayoongezeka.Kaskazini mwa Asia, dhoruba za kitropiki na mvua zisizo za kawaida zimesababisha vifo vya mamia na watu wengi kukimbia makazi yao, imesema WMO. Clare Nullis, msemaji wa shirika hilo, alisema Indonesia, Ufilipino, Sri Lanka, Thailand na Vietnam ndizo zimeathirika zaidi. “Tunahitaji kuzingatia kuwa Asia iko hatarini sana kutokana na mafuriko,” amesema Nullis, akibainisha kuwa dhoruba karibu na Ekweta ni nadra na jamii hazina uzoefu wa kukabiliana nazo. Indonesia pekee, watu 604 wamefariki, 464 hawajulikani walipo, na 2,600 wamejeruhiwa, huku zaidi ya milioni 1.5 wakiathirika na 570,000 wakikimbia makazi yao.Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kukomesha Utumwa leo Desemba 2 Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi Duniani ILO limeonya kuhusu kuongezeka kwa utumwa wa kisasa wa binadamu, likionesha kuwa watu milioni 10 zaidi walikuwa wakiishi katika kazi za kulazimisha au ndoa za shuruti mwaka 2021 ikilinganishwa na mwaka 2016. Makadirio haya mapya yanaweka idadi ya walioathirika duniani kote kuwa watu milioni 50 huku wanawake na watoto wakiendelea kuwa wenye hatari kubwa zaidi.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu ni Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali "KOTI LA BABU HALIKOSI CHAWA".Mwenyeji wako ni Sabrina Moshi, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, na leo zinaanza siku 16 za uanaharakati kuelimisha umma kuhusu janga la ukatili wa kijinsia, tunamsikia mmoja wa waathirika wa ukatili wa kingono.Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa onyo kali kuhusu ongezeko la ukatili mtandaoni dhidi ya wanawake na wasichana.Ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya wanawake UN Women na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya dawa na uhalifu UNODC inaonya kwamba mwaka 2024, wanawake na wasichana 50,000 waliuawa na wapenzi au jamaa sawa na mwanamke mmoja kila dakika 10.Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo (UNCTAD) inaonya kwamba uchumi wa Eneo la Palestina Linalokaliwa kwa Mabavu na Israel umerudi nyuma miaka 22 kwa muda usiozidi miaka miwili kwani umeingia katika hali mbaya zaidi ya mdororo kuwahi kurekodiwa, huku miongo ya maendeleo ikifutwa na operesheni za kijeshi zilizodumu kwa muda mrefu pamoja na vizuizi vya muda mrefu.Katika kujifunza lugha Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "MADUYUNI"Mwenyeji wako ni Sabrina Said, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe katika siku ya Choo Duniani, simulizi za wakinamama wakimbizi wa ndani nchini Sudan, na usugu dhidi ya Viua-Vijasumu (AMR).Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO leo linaadhimisha Siku ya Choo Duniani kwa onyo kali kwamba janga la usafi wa mazingira duniani linagharimu maisha kila siku, na mabadiliko ya tabianchi yanaliweka katika hatari kubwa zaidi huku mamilioni ya watu wakiishi bila huduma muhimu ya choo.Wakinamama wakimbizi wa ndani nchini Sudan wameziomba jumuiya za kimataifa kuwasaidia kuhakikisha vita inaisha nchini mwao ili waweze kuishi kwa amani kwani madhila waliyopitia ni mengi na yanahuzunisha.Usugu dhidi ya Viua-Vijasumu (AMR)unaelezwa kama janga la kimyakimya linalotishia kurudisha nyuma mafanikio ya miongo kadhaa katika tiba na afya. Tunapoadhimisha Wiki ya Kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu usugu dhidi ya Viua-Vijasumu au antibiotics, Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO Kanda ya Afrika, Profesa Mohamed Janabi, ametahadharisha akisema dawa ambazo hapo awali ziliokoa maisha sasa hazifanyi kazi kama ilivyokuwa na hivyo inabidi kuchukua hatua za pamoja na haraka.Mwenyeji wako ni Sabrina Moshi, karibu!
Wakinamama wakimbizi wa ndani nchini Sudan wameziomba jumuiya za kimataifa kuwasaidia kuhakikisha vita inaisha nchini mwao ili waweze kuishi kwa amani kwani madhila waliyopitia ni mengi na yanahuzunisha. Tuungane na Leah Mushi kupata tarifa zaidi.
Serikali ya Victoria imetoa ripoti ya mwisho ya uchunguzi kuhusiana na uzoefu wa wanawake katika suala la maumivu - na ni taarifa inayosumbua kusoma. kutokana na uzoefu wa wanawake na wasichana 13,000, ripoti hiyo imebaini mapengo katika huduma za afya kwa jinsia, upendeleo katika matibabu, ubaguzi wa kijinsia, na hisia za kupuuzwa au kutopingwa na wataalamu wa afya zinazoenea katika mfumo wa afya wa Victoria.
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya haki za binadamu nchini Sudan, Mpango wa Ufadhili Wajasiriamali Wanawake, (We-Fi) nchini Tanzania, na kilimo ni moja ya sekta muhimu za kiuchumi nchini Nigeria.Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) imetoa tamko juu ya wasiwasi mkubwa kufuatia ripoti mpya kutoka El-Fasher, jimboni Darfur Kaskazini, nchini Sudan, zikieleza kuwepo kwa mauaji ya halaiki, ubakaji, na uhalifu mwingine unaodaiwa kufanywa wakati wa mashambulizi ya Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF).Mpango wa Ufadhili Wajasiriamali Wanawake, (We-Fi) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia na wadu umewezesha biashara kukwamuka nchini Tanzania baada ya janga la COVID-19, hatua ambayo imeinua pia jamii nzima na si wajasiriamali wanawake peke yao. Simulizi hii ya Assumpta Massoi inamulika mjasiriamali mwanamke Haika Lawere anayemiliki hoteli ya Mbezi Garden jijini Dar Es Salaam ambako ni jiji kuu la biashara la taifa hilo la Afrika.Kilimo ni moja ya sekta muhimu za kiuchumi nchini Nigeria, kikiajiri zaidi ya theluthi moja ya watu wote nchini humo. Lakini hali ya hewa isiyotabirika imefanya kilimo kuwa shughuli yenye mashaka makubwa — ukame, mafuriko na mvua zisizo na mpangilio zimekuwa tishio kubwa kwa wakulima, ambapo kilio chao kimesikiwa na Benki ya Dunia iliyokuja na suluhisho kwa kuanzisha mradi wa kilimo cha umwagiliaji.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Mpango wa Ufadhili Wajasiriamali Wanawake, (We-Fi) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia na wadu umewezesha biashara kukwamuka nchini Tanzania baada ya janga la COVID-19, hatua ambayo imeinua pia jamii nzima na si wajasiriamali wanawake peke yao. Simulizi hii ya Assumpta Massoi inamulika mjasiriamali mwanamke Haika Lawere anayemiliki hoteli ya Mbezi Garden jijini Dar Es Salaam ambako ni jiji kuu la biashara la taifa hilo la Afrika.
Mpango wa “Chaguo Langu, Haki Yangu” nchini Tanzania ni jitihada thabiti zinazolenga kuwawezesha wanawake na wasichana kuishi maisha huru dhidi ya ukatili na vitendo hatarishi. Kwa ufadhili wa Serikali ya Finland, Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la IPS, linafanya mabadiliko halisi katika jamii. Sheilah Jepngetich anafafanua zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya Kimataifa ya Majiji, vifo na majeruhi vilivyotokea katika maandamano yanayohusiana na uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Tanzania na uwezeshaji wa wanawake nchini huko huko Tanzania.Dunia leo ikiadhimisha Siku ya Kimataifa ya Majiji, majiji ya kisasa pamoja na kukumbatia teknolojia yametakiwa kuhakikisha yanazingatia zaidi watu ili wengine wasiachwe nyuma au kutengwa na maendeleo hayo.Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu imeeleza wasiwasi mkubwa kufuatia vifo na majeruhi vilivyotokea katika maandamano yanayohusiana na uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Tanzania tarehe 29 mwezi huu wa Oktoba.Mpango wa “Chaguo Langu, Haki Yangu” nchini Tanzania ni jitihada thabiti zinazolenga kuwawezesha wanawake na wasichana kuishi maisha huru dhidi ya ukatili na vitendo hatarishi. Kwa ufadhili wa Serikali ya Finland, Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la IPS, linafanya mabadiliko halisi katika jamii.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Bi. Lucy Githinji, mkazi wa jimbo la New Jersey nchini Marekani amezungumza na idhaa hii baada ya matembezi ya hiari kwa ajili ya kuhamasisha jamii kuhusu saratani ya titi, akisema hakika dawa zinafanya kazi.Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Kibinadamu nchini Sudan, Denise Brown amesema ni kweli wamepokea ripoti za mauaji ya baadhi ya wahudumu wa kujitolea huko El Fasher jimboni Darfur wakati huu ambapo mji huo umetwaliwa na wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka, (RSF).Kimbunga Melissa kimepungua nguvu baada ya kutua nchini Jamaica kama kimbunga cha kiwango cha 5, na kuvunja rekodi ya kimbunga chenye nguvu zaidi, kabla ya kuelekea kaskazini mashariki kupita Cuba hadi Bahamas, na kusababisha mafuriko makubwa, uharibifu na kukatika kwa umeme katika maeneo mbalimbali ya Karibea na Amerika ya Kati.Nchini Cameroon, kufuatia mauaji ya raia wakati wa maandamano ya kupinga kutangazwa kwa Paul Biya kuwa mshindi wa kiti cha Urais kwenye uchaguzi uliofanyika Oktoba 12, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu imeeleza wasiwasi wake juu ya ripoti za vifo hivyo.Na katika Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "SUMIA."Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia mifumo ya tahadhari za mapema dhidi ya majanga, elimu kuhusu uraia nchini Sudan kusini, na kilimo endelevu na vijana nchini Rwanda.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema mifumo ya tahadhari za mapema dhidi ya majanga si chaguo tena, bali ni lazima kwa kila mtu duniani, akisisitiza kuwa hatua hizo zinaokoa maisha na mali.Kuanzia furaha ya uhuru hadi maumivu ya kurejea kwa mzozo, safari ya amani ya kudumu Sudan Kusini imekuwa ndefu na bado inaendelea. Licha ya changamoto hizo, matumaini bado ni makubwa miongoni mwa jamii nchini kote kwamba uchaguzi wa amani, huru na wa haki utaleta usalama uliotafutwa kwa muda mrefu pamoja na fursa za maendeleo na ukuaji wa uchumi.Wanawake ni nguzo muhimu katika maendeleo ya kilimo na jamii za vijijini. Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo( IFAD) inahakikisha zaidi ya asilimia 50 ya washiriki wa miradi yake ni wanawake, kwa lengo la kuimarisha usawa wa kijinsia na kupunguza umaskini. Kupitia mafunzo, huduma za kifedha, na upatikanaji wa masoko, wanawake wanawezeshwa kiuchumi na kijamii. Tafiti zinaonesha kuwa kufuta pengo la kijinsia katika kilimo kunaweza kuongeza pato la dunia kwa asilimia 1. Nchini Rwanda, miradi kama R-YES imewezesha wanawake vijana kuanzisha biashara za kilimo na kutoa ajira.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Wanawake ni nguzo muhimu katika maendeleo ya kilimo na jamii za vijijini. Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo( IFAD) inahakikisha zaidi ya asilimia 50 ya washiriki wa miradi yake ni wanawake, kwa lengo la kuimarisha usawa wa kijinsia na kupunguza umaskini. Kupitia mafunzo, huduma za kifedha, na upatikanaji wa masoko, wanawake wanawezeshwa kiuchumi na kijamii. Tafiti zinaonesha kuwa kufuta pengo la kijinsia katika kilimo kunaweza kuongeza pato la dunia kwa asilimia 1. Nchini Rwanda, miradi kama R-YES imewezesha wanawake vijana kuanzisha biashara za kilimo na kutoa ajira. Sheilah Jepngetich na taarifa zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia kiwango cha gesi ya hewa ukaa, yaani carbon dioxide au CO₂, siku ya Kimataifa ya Wanawake wa Vijijini inayotupeleka nchini Kenya kumulika juhudi za wanawake za kumudu mahitaji ya familia zao, na uvuvi na uhalifu katika Ziwa Victoria.Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani, WMO, inasema kiwango cha gesi ya hewa ukaa, yaani carbon dioxide au CO₂, kimeongezeka kwa kiwango cha kuvunja rekodi mwaka 2024, na kufikia viwango vipya vya juu zaidi kuwahi kurekodiwa.Kuanzia Oktoba 15 mwaka 2008 dunia imekuwa ikiadhimisha siku ya Kimataifa ya Wanawake wa Vijijini kama fursa ya kutambua mchango mkubwa wa wanawake hawa katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi, na kimazingira.Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM kwa kushirikiana na Ofisi ya Marekani ya Masuala ya Kimataifa ya kupambana na Dawa za Kulevya na Utekelezaji wa Sheria (INL), na mamlaka kutoka Kenya, Tanzania na Uganda wanashirikiana kuimarisha uwezo na kukabiliana na uhalifu wa kimataifa unaotekelezwa katika ziwa victoria ambao ukiachwa unaweza kuleta athari kwa zaidi ya watu milioni 40 wanaotegemea ziwa hilo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!