Podcasts about watu

  • 88PODCASTS
  • 654EPISODES
  • 19mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • May 27, 2025LATEST
watu

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about watu

Show all podcasts related to watu

Latest podcast episodes about watu

Habari za UN
27 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 27, 2025 9:56


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kuangazia siku ya familia iliyokutanisha wadau wakimulika pamoja na mambo mengine nafasi ya vyombo vya habari katika kuimarisha malezi na makuzi ya mtoto.Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura OCHA hii leo imesema wakati mpango tata wa Israeli wa kugawa misaada kwenye eneo la Palestina la Gaza linalokaliwa kimabavu na Israeli ukiendelea, Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine tena umesihi mamlaka za Israeli kuruhusu ongezeko la kiwango cha misaada ya kufikia walengwa kwenye eneo hilo lililozingirwa ili kuepusha uhaba wa chakula..Kadiri nchi zinavyokumbwa zaidi na majanga ya asili, gharama halisi za majanga ni mara 10 zaidi ya ilivyodhaniwa hapo awali, zikiwa na athari mbaya zaidi katika sekta za afya, makazi, elimu na ajira, imesema Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kupunguza hatari za majanga katika ripoti iliyochapishwa Jumanne.Nchini Namibia, makazi yaliyojengwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi, UNFPA kwa ajili ya wajawazito wanaoishi maeneo ya mbali kusubiria ili kujifungua kwa usalama, yamesaidia kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga.Na katika mashinani, kupitia video iliyoandaliwa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani Sudan Kusini UNMISS, tunakutana na Mary Aban Akon, mkazi wa kijiji cha Hai Matar huko Sudan Kusini. Yeye ni miongoni mwa wakimbizi waliorejea nyumbani baada ya kupatiwa makazi mapya yaliyojengwa kwa msaada wa mashirika ya kibinadamu chini ya mradi uliofadhiliwa na Umoja wa Mataifa na wadau wake.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Watu wakujitolea wana jukumu kubwa nchini Australia, ila idadi yao inapungua

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 20, 2025 10:42


Wiki ya kitaifa yakujitolea ime anza, ita kuwa kuanzia 19 Mei hadi 25 Mei 2025.

Habari za UN
Kutimiza azimio la watu wa jamii za asili ni jukumu la mataifa yote duniani - Adam Ole Mwarabu

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 8, 2025 6:48


Jukwaa la Umoja wa Mataifa kuhusu watu wa jamii za asili limekunja jamvi mwishoni mwa wiki iliyopita hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa na kandoni mwa jukwaa hilo Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili alipata fursa ya kuzungumza na mmoja wa washiriki kiongozi wa kijamii kutoka Jamii ya wafugaji ya Wamaasai mkoani Morogoro Mashariki mwa Tanzania Adam Kulet Ole Mwarabu, wamejadili mengi lakini Ole Mwarabu anaanza kwa kukumbusha alichokibeba kwenye jukwaa la mwaka jana kinavyotekelezwa nchini mwake.

Habari za UN
Bila mafunzo watu tutakuwa watumiaji tu wa AI na sio wanaufaika: Hassan Mhelela

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 2, 2025 5:12


Katika kuelekea siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani itakayoadhimishwa Jumamosi Mei 3 ambayo mwaka huu imebeba maudhui yanayoangazia athari za Akili Mnemba au AI katika uhuru wa habari na vyombo vya habari tunazungumza na mmoja wa wanahabari wa siku nyingi ili kufahamu AI inavyoleta mabadiliko katika tasnia ya habari na vyombo vya habari hususan Afrika Mashariki ambako pia pengo la kidijitali ni kubwa. Ungana na Flora Nducha  kwa undani zaidi katika makala hii.

Habari za UN
30 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 30, 2025 11:14


Hii leo jaridani tunaangazia ugonjwa wa mpox, na walinda amabini wa Umoja wa Mataifa nchini DR Congo. Makala inamuulika siku siku ya kimataifa ya muziki wa Jazz namashinani tunasalia hapa makao maku kusikia ujumbe wa mwakilishi wa shirika la watu wa jamii za Asili.Maambukizi ya ugonjwa wa mpox kutokana na aina ya virusi vya monkeypox clade Ib /ˈmʌŋ.ki.pɑks kleɪd one bee/ (MPXV) yanaendelea kuripotiwa hasa barani Afrika, ambapo mataifa kumi na moja yameripoti maambukizi ya ndani ya jamii katika kipindi cha wiki sita zilizopita. Hiyo kwa mujibu wa ripoti 51 ya Shrika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO kuhusu hali ya mlipuko wa mpox katika nchi mbalimbali duniani.Huko Bunia, mji mkuu wa jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, walinda amani kutoka Bangladesh na Indonesia, wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO wamepatiwa medali kwa mchango wao wa ulinzi wa raia, moja ya jukumu kubwa la ujumbe huo..Makala ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya muziki wa Jazz Flora Nducha anamulika umuhimu wa jazz maadhimisho ya mwaka ambapo maudhui yanachagiza "Amani, umoja, ubunifu na uhuru miongoni mwa tamaduni."Na katika mashinani leo fursa ni yake mshiriki  jukwaa la watu wa asili hapa Makao makuu Helena Steenkamp Mwakilishi wa Shirika la Watu wa jamii za Asili Kusini mwa Jangwa la Kalahari Afrika Kusini anazungumzia alichokipata hadi sasa kwenye jukwaa hilo.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Maoni kutoka washiriki kutoka maeneo mbalimbali waliohudhuria mkutano wa jamii za asili UNPFII

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 30, 2025 3:24


Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, mkutano wa 24 wa Jukwaa la Kudumu la Watu wa jamii za asili (UNPFII) linaendelea kujadili utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili na kubaini mbinu bora za kushughulikia changamoto zinazowakabili, ukileta pamoja washiriki kutoka maeneo mbalimbali kote duniani. Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa walipata fursa ya kuzungumza na baadhi yao.

Habari za UN
29 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 29, 2025 11:44


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka katika mkoa wa Mwanza kaskazini magharibi mwa Tanzania ambapo vijana wameshika hatamu kuboresha mustakabali wao. Pia tunakuletea muhtasari wa habari  na mashinani tunasalia hapa makao makuu.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kudumisha Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, MONUSCO, umeikaribisha kusainiwa kwa “Azimio la Kanuni” tarehe 25 Aprili 2025 mjini Washington, D.C chini ya usimamizi wa Wizara ya mambo ya nje ya Marekani, kati ya serikali za DRC na Rwanda kwa lengo la kulinda rai ana kutekeleza azimio la Baraza la Usalama namba 2773 (2025).Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA, Juliette Touma, akizungumza na waandishi wa habri mjini Geneva kwa njia ya video kutoka mji mkuu wa Jordan, Amman, wakati  kuzingirwa kwa Ukanda wa Gaza kukikaribia kuingia mwezi wa pili amesema “Mzingiro wa Gaza ni muuaji wa kimya muuaji wa watoto, wazee, na watu walioko katika mazingira magumu zaidi. Mzingiro huu unamaanisha kwamba familia nzima, watu saba au wanane wanalazimika kushirikiana kopo moja la maharagwe au njegere”.Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO limezitaka nchi za Kaskazini Magharibi mwa Afrika kuongeza ufuatiliaji na kuchukua hatua za mapema kudhibiti makundi ya nzige wa jangwani. Hii ni baada ya nzige wakubwa na makundi madogo kutoka ukanda wa Sahel kuhamia maeneo ya kusini mwa Sahara, hasa katikati ya Algeria, magharibi mwa Libya, na kusini mwa Tunisia tangu Februari hadi Machi mwaka huu.Na katika mashinani fursa ni yake Maruping Onkemetse Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kituo cha Msaada wa Familia, shirika linaloongozwa na wanawake wa asili  katika Wilaya ya Gantsi, kijiji cha Chobokwane nchini Botswana anayeshiriki mkutano unaoendelea hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa wa Jukwaa la Watu wa Asili akizungumzia alichojifunza hadi sasa.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Radio Maria Tanzania
Fahamu aina za watu na tabia zao.

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Apr 24, 2025 51:20


Karibu uungane nami Happiness Mlewa katika kipindi cha Uraibu, Mwezeshaji ni Padre Richard Matanda Tesha Kutoka Jimbo Katoliki Moshi, akiendelea kutufundisha juu ya aina za watu na tabia zao. L'articolo Fahamu aina za watu na tabia zao. proviene da Radio Maria.

Habari za UN
23 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 11:15


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza, na harakati za utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili. Makala tunasalia hapa hapa makao makuu na mashinani tunakwenda nchini Burundi, kulikoni?Hali si hali huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli ambako wakimbizi wa ndani wanakabiliwa na hatari za kiafya ambako panya na wadudu kama vile viroboto na  nzi wamesambaa kutokana na mlundikano wa taka na  ukosefu wa huduma muhimu kama vile maji safi na salama.Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, mkutano wa 24 wa Jukwaa la Kudumu la Watu wa jamii za asili (UNPFII) linaendelea kujadili utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili  na kubaini mbinu bora za kushughulikia changamoto zinazowakabili. Miongoni mwa shiriki wa jukwaa hilo nimwakilishii wa Shirika la Ereto Solidarity Funds ambaye  amepata fursa ya kuzungumza na Sharon Jebichii wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa.Makala ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Kitabu na Haki Miliki ambapo kila mwaka tarehe kama ya leo siku hii huadhimishwa ili kutambua nguvu ya vitabu kama daraja kati ya vizazi na vizazi na tamaduni mbalimbali. Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na mwandishi maarufu wa vitabu vya elimu, Uchumi na uhamiaji, Ernest Makulilo mkazi wa Marekani katika jimbo la Missouri.Na mashinani kupitia video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO fursa ni yake Meena Poudel kutoka nchini Nepal, Kusini mwa Asia ambaye ni Katibu wa kikundi cha wanawake watumiaji wa msitu ambacho kinabadilisha takataka za misitu kuwa mbolea rafiki kwa mazingira huku pia wakijipatia kipato."Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!  

Habari za UN
Anna Ndiko: Mfuko wa ERETO tunawezesha mashirika ya watu wa asili Afrika Mashariki kutetea haki za ardhi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 2:28


Mkutano wa 24 wa Jukwaa la Kudumu la Watu wa jamii za asili (UNPFII) hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa linaendelea kujadili utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa asili  na kubaini mbinu bora za kushughulikia changamoto zinazowakabili. Miongoni mwa shiriki wa jukwaa hilo nimwakilishii wa Shirika la Ereto Solidarity Funds ambaye  amepata fursa ya kuzungumza na Sharon Jebichii wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa. Anaanza kwa kujitambulisha 

Radio Maria Tanzania
Zifahamu aina za watu na tabia zao.

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 55:47


Karibu uungane nami Happiness Mlewa katika kipindi cha Uraibu, Mwezeshaji ni Padre Richard Matanda Tesha kutoka Jimbo Katoliki Moshi, akiendelea kutufundisha juu ya kwanini upo hivyo ulivyo akijikita katika aina za watu? L'articolo Zifahamu aina za watu na tabia zao. proviene da Radio Maria.

Habari za UN
Tume huru ya UN ya kusaka ukweli kuhusu Sudan imelaani vikali mauaji ya watu zaidi ya 100

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 14, 2025 2:02


Vita ya sasa ya Sudan ikielekea kuingia mwaka wa tatu, Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya kusaka ukweli kuhusu Sudan imelaani vikali mauaji ya watu zaidi ya 100 yaliyotokea wikiendi hii katika kambi za wakimbizi wa ndani Darfur, ikionya kwamba hali inaweza kuwa mbaya zaidi. Anold Kayanda na taarifa zaidi.(Taarifa ya Anold Kayanda)Shukrani LeahTangu kuanza kwa vita kati ya Jeshi la Sudan (SAF) na kikosi cha waasi cha RSF mnamo tarehe 15 Aprili mwaka 2023, maelfu ya watu wamepoteza maisha, huku mamilioni wakikumbwa na njaa, ubakaji, na ufurushwaji. Kambi kama ya Zamzam, yenye wakazi zaidi ya laki saba – nusu yao wakiwa watoto – zinaripotiwa kuzingirwa, wakazi wake wakikosa chakula, dawa, na maji, imeeleza Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya kusaka ukweli kuhusu Sudan.Mwenyekiti wa tume hiyo, Mohamed Chande Othman, ananukuliwa akisema, “Dunia imeshuhudia miaka miwili ya mzozo usio na huruma ambao umewanasa mamilioni ya raia katika mazingira ya kutisha, wakiwekwa katika hali ya ukatili bila matumaini ya mwisho.”Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, Catherine Russell kuhusu tukio hili la hivi karibuni ni kwamba watoto takriban 23 na wahudumu 9 wa misaada wameripotiwa kuuawa katika mfululizo wa mashambulizi katika eneo la Darfur Kaskazini, katika kipindi cha siku tatu zilizopita.Jana Jumapili, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesisitiza kuwa mashambulizi yanayolenga raia ni marufuku kabisa chini ya sheria ya kimataifa ya kibinadamu. Wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu na wafanyakazi wa afya wanapaswa kuheshimiwa na kulindwa,anasema.Kesho Jumanne huko London Uingereza, mataifa takriban 20 yanatarajiwa kujadili hali ya kibinadamu nchini Sudan. Umoja wa Mataifa unatoa wito wa hatua za haraka kulinda raia, kusitisha uungwaji mkono kwa pande zinazopigana, na kuhakikisha haki na uwajibikaji kwa uhalifu wa kivita.

Habari za UN
Chonde chonde tusiipe kisogo Sudan: Nkweta-Salami

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 14, 2025 2:07


Sudan Clementine Nkweta-Salami, Mwakilishi Mkazi na Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan akizungumza na UN News amesema hali si hali kama anavyofafanua Flora Nducha.(TAARIFA YA FLORA NDUCHA)Bi Nkweta-Salami amesema ufurushwaji wa watu unaendelea, mahitaji ni makubwa sana, tayari baa la njaa limeshabainika katika baadhi ya maeneo ya nchi, na wanakimbizana na muda kuzuia baa hilo lisienee zaidi.(SAUTI CLEMENTINE 1-SABRINA)"Hali ya kibinadamu ni ya kutisha, bado tunahaha. Hatuna uwezo wa kufikia maeneo yote yenye machafuko. Tunajitahidi kuhakikisha kwamba rasilimali tulizo nazo zinaweza kufikishwa haraka iwezekanavyo kwa kutumia njia zote tulizo nazo. Watu milioni 12 wametawanywa.   Kwa ujumla, bado tunahitaji juhudi kubwa, ado tunahitaji msaada kutoka kwa jumuiya ya kimataifa kwa upande wa rasilimali, na bado tunahitaji msaada zaidi wa kuruhusu utoaji wa misaada kutoka kwa makundi yote yenye silaha yanayohusika katika mzozo huu.”Licha ya kukosena suhuhu ya kisasa hadi sasa amesema wataendelea kusaidia wenye uhitaji(CLEMENTINE 2-SABRINA)“Msaada wa kibinadamu unapaswa kuendelea hata kama hakuna suluhisho la kisiasa kwa mzozo huu, na hata kama hakuna makubaliano ya kusitisha mapigano. Tunaendelea kushirikiana na jumuiya ya kimataifa na nchi wanachama zinazoshiriki kwenye majadiliano na mazungumzo ya kisiasa kujaribu kutumia majadiliano hayo kuwezesha kazi zetu kupitia usitishaji wa muda wa mapigano na kujaribu kuwashawishi makundi yenye silaha kukubaliana na njia ambazo tunaweza kutumia bila kuhatarisha maisha kwa kushambuliwa, kulipuliwa au kupigwa makombora”.Na rai yake ni kwamba(CLEMENTINE 3-SABRINA)Watu wako katika hali ya zahma kubwa, msaada unahitajika na tunatoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kutowasahau watu wa Sudan wanaume, wanawake na watoto wanaojikuta katika hali hii ngumu sana kwa sasa.TAGS: Sudan, Vita, amani na usalama, msaada wa kibinadamu

Habari za UN
10 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 10, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Idhaa hii inazungumza na Mwenyekiti wa Tanzania Women Ecocomic Empowerment Network (TAWEN), ambaye pia ni mchumi mbobezi Bi. Janet Zebedayo Mbene. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na neno la wiki.Shukran Anold na leo tunaanzia huko Geneva Uswisi ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limetoa muongozo wake wa kwanza duniani wa kutambua, kutoa matibabu kwa haraka na matibabu ya muda mrefu kwa ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.Nchini Chad katika mpaka wake na Sudan ambako Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR Filippo Grandi ametembelea na kuzungumza na wakimbizi wa Sudan pamoja na kujionea hali zao wakati huu ambapo wamepunguza kutoa chakula, malazi , maji na dawa na kauli yake ikawa moja tu, “Ninatoa wito kwa wafadhili, tafadhali msipunguze msaada kwa wathirika wa vita vya Sudan.”.Taarifa ya pamoja ya mashirika ya kibinadamu inayotolewa kila baada ya wiki mbili imeeleza kuhusu hali katika Ukanda wa Gaza inasema kuwa watu wanazidi kuuwawa na kujeruhiwa. Kwa zaidi ya mwezi sasa hakuna misafara ya misaada inayoruhusiwa kuingia Gaza. Watu kulazimishwa kuhama kinguvu kunaendelea, makazi ya wakimbizi yamefikia pomoni, huduma za usafi na kujisafi nazo ni mbaya.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "FIFILIZA"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Lazima hatua madhubuti zichukuliwe kukomesha mzunguko wa watu kutoweka nchini Sudan - Radhouane Nouicer

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 9, 2025 3:22


Wakati hofu ikiendelea kuhusu watu kutoweka kwa wingi nchini Sudan, Mtaalam maalum wa Umoja wa Mataifa aliyeteuliwa na Ofisi ya Haki za Binadamu OHCHR anayehusika na haki za binadamu nchini humo Radhouane Nouicer ametoa wito wa dharura kuhusu hali ya raia waliokwama katika vita kubwa nchini humo. Flora Nducha na taarifa zaidi.

Radio Maria Tanzania
Ni kwa namna gani maneno ya Yesu yanavyotufundisha kwamba maadui wa mtu wanaweza kuwa watu

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Apr 3, 2025 57:21


Karibu uungane nami Judith Mpalanzi katika  kipindi cha Ujumbe wa Biblia, leo nipo na Padre Titus Amigu  kutoka  Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino SAUT Jimbo Kuu Katoliki Mwanza, akitufundisha Maadui wa mtu. L'articolo Ni kwa namna gani maneno ya Yesu yanavyotufundisha kwamba maadui wa mtu wanaweza kuwa watu proviene da Radio Maria.

Habari za UN
UN: Hali inazidi kuwa tete Gaza huku watu zaidi ya milioni wakiwa hatarini kukosa mlo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 26, 2025 2:39


Watu zaidi ya milioni 1 wako katika hatari ya kukosa chakula endapo misaada haitoruhusiwa kuingia Gaza wakati huu mashambulizi makali ya Israel yakizidisha janga la kibinadamu yameonya leo mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa. Flora Nducha na taarifa zaidi.

Radio Maria Tanzania
Kwa nini watu wanashindwa kuishi kwa tabia njema?

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Mar 20, 2025 40:23


Karibu Ungane na Mtangazaji wako Judith Mpalanzi, katika kipindi cha Uraibu na Padri Richard Matanda Tesha kutoka Jimbo Katoliki Moshi, leo tunaangazia  Uraibu wa tabia kwa nini watu hawaishi tabia njema L'articolo Kwa nini watu wanashindwa kuishi kwa tabia njema? proviene da Radio Maria.

Habari RFI-Ki
Watu zaidi ya milioni 6 duniani watakosa mahali pakuishi

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 17, 2025 10:01


Tunajadili hatua ya bazara la wakikimbizi la Denmark, kuchachapisha ripoti inayoonesha kuwa, watu zaidi ya milioni 6 duniani watakosa mahali pakuishi ifikapo mwishoni mwa mwaka ujao, kutokana na mizozo, mabadiliko ya tabia nchi na kusitishwa kwa misaada toka Marekani. Unazungumziaje hatua hii? ndilo swali tumeuliza, skiza makala haya kufahamu mengi.

Habari RFI-Ki
Watu zaidi ya milioni 6 duniani watakosa mahali pakuishi

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 17, 2025 10:01


Tunajadili hatua ya bazara la wakikimbizi la Denmark, kuchachapisha ripoti inayoonesha kuwa, watu zaidi ya milioni 6 duniani watakosa mahali pakuishi ifikapo mwishoni mwa mwaka ujao, kutokana na mizozo, mabadiliko ya tabia nchi na kusitishwa kwa misaada toka Marekani. Unazungumziaje hatua hii? ndilo swali tumeuliza, skiza makala haya kufahamu mengi.

Jioni - Voice of America
Maafisa wa Russia wamesema mashambulizi ya Ukraine yaliyohusisha Drone 90 yamesababisha vifo vya watu wawili na kuwajeruhi wengine 18. - Machi 11, 2025

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 11, 2025 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

SBS Swahili - SBS Swahili
Wangeci "katika hii nchi wanathamini sana watu wenye ujuzi wa kazi za mikono"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Feb 28, 2025 7:43


Wangeci Kones alikuja Australia akiwa na matumaini yakutumia shahada yake ya masoko, katika kazi sawia na alivyo kuwa akifanya nchini Kenya.

Jioni - Voice of America
Watu 11 wamefariki na wengine zaidi ya 70 wamejeruhiwa kufuatia milipuko miwili katika eneo la Bukavu huko mashariki mwa DRC. - Februari 27, 2025

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 27, 2025 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Habari za UN
26 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 26, 2025 11:13


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu nchini Somalia na huduma zaa faya kwa wakimbizi wajawazito nchini Chad. Makala inatupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Uganda, kulikoni?Watu milioni 4.4 nchini Somalia wako hatarini kukumbwa na njaa ifikapo mwezi Aprili mwaka huu wa 2025, kutokana na ukame mkali, mizozo na ongezeko kubwa la bei za vyakula.Nchini Chad, taifa lililoko kaskazini-kati mwa Afrika mkunga mmoja amehamia kwa muda katika kambi ya wakimbizi ili kuhakikisha wajawazito wanapata huduma bora kabla na baada ya kujifungua kama njia mojawapo ya kuepusha vifo vya wajawazito na watoto wachanga.Makala inatupeleka nchini Kenya kumulika mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO, wa kulinda lishe ya wasiojiweza unavyoleta mabadiliko katika  jamii kuanzia kaunti ya Turkana hadi kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma.Katika mashinani fursa ni yake Dkt Annett Alenyo Ngabirano kutoka Uganda akisema juhudi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO na Wizara ya Afya ya Uganda zimeweza kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Ebola nchini humo, WHO ikitoa msaada wa vifaa vya matumizi, dawa ya hospitali, msaada wa kiufundi na kuratibu wadau katika idara hiyo.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Hatari ya watu milioni 4.4 nchini Somalia kukumbwa na njaa mwezi Aprili mwaka huu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 26, 2025 2:05


Watu milioni 4.4 nchini Somalia wako hatarini kukumbwa na njaa ifikapo mwezi Aprili mwaka huu wa 2025, kutokana na ukame mkali, mizozo na ongezeko kubwa la bei za vyakula. Selina Jerobon na taarifa zaidi..

Jioni - Voice of America
MSF imesitisha operesheni zake katika kambi ya wakimbizi yenye takribani watu 500,000 nchini Sudan kutokana na ukosefu wa usalama . - Februari 25, 2025

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 25, 2025 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Alfajiri - Voice of America
WFP lajitahidi kufikisha misaada ya chakula kwa watu wote wa Sudan waliyotatizika kutokana na vita. - Februari 14, 2025

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 14, 2025 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
10 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 10, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya wahamiaji na wakimbizi nchini Libya, na wakimbizi wajasiriamali katika makazi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya. Makala inatupeleka Jerusalemu Mashariki, na mashinani nchini Chad, kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM, limeeleza mshtuko mkubwa na wasiwasi wake kufuatia kugunduliwa kwa makaburi mawili nchini Libya walimozikwa wahamiaji kadhaa, baadhi yao wakiwa na majeraha ya risasi.Katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma, kutokana na ufadhili wa shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), kundi la vijana wanajishughulisha na ufugaji wa wadudu nyenje (Crickets) ili kukabiliana na changamoto ya utapiamlo miongoni mwa watoto wachanga.Katika makala Sharon Jebichii anakupeleka Mashariki ya Kati kumulika ziara aliyofanya Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA huko Ukingo wa Magharibi na Gaza ili kujionea hali halisi ya raia.Na mashinani kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu, UNFPA, nampisha  Daralssalam, kutoka Sudan ambaye alikuwa Mhadhiri Chuo Kikuu lakini sasa mkimbizi nchini  Chad akieleza changamoto alizopitia na kuomba jamii ya kimataifa isaidie wanawake wa Sudan.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
Uhamishaji watu kwa lazima kutoka kutoka ardhi inayokaliwa sio sahihi - OHCHR

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 5, 2025 1:23


Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa,(OHCHR) imesisitiza haja ya kusonga mbele kuelekea awamu inayofuata ya usitishaji mapigano huko Gaza, kuachiliwa kwa mateka na wafungwa wote waliokamatwa kiholela, kukomesha vita na kujenga upya Gaza, kwa kuheshimu kikamilifu sheria ya kimataifa ya kibinadamu na sheria za kimataifa za haki za binadamu. 

SBS Swahili - SBS Swahili
Bw Omari "watu wana anza sema wakati wa Kabila ulikuwa afadhali kuliko sasa"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Feb 3, 2025 11:42


Hali ya usalama inavyo zidi kudorora katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ndivyo serikali ya Rais Tshisekedi inavyo zidi kuwa chini ya shinikizo kubwa.

Habari za UN
Asante IFAD kwa kutuwezesha watu wenye ulemavu Liberia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 22, 2025 1:57


Nchini Liberia, mradi unaotekelezwa na Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD umejengea uwezo watu wenye ulemavu wa kuona na kuwawezesha kuongeza vipato na vile vile uhakika wa kupata chakula. Simulizi ya Sabrina Moshi wa redio washirika SAUT FM mkoani Mwanza nchini Tanzania, inaelezea zaidi.Tuko kaunti ya Lofa, kaskazini kabisa mwa Liberia, magharibi mwa Afrika, tunakutana na Hawa Kamara, yeye ni mlemavu wa kutoona. Yeye pamoja na wenzake wa chama cha watu wenye ulemavu wa kutoona hapa Lofa, wanathibitisha kuwa unapoamua kufanya kitu, hakuna kinachokuzuia.Kupitia mradi wa Mabadiliko ya kilimo kwa wakulima wadogo na uchechemuzi wa kilimo biashara au STAR-P, mavuno ya mpunga kwenye shamba la kikundi hicho, yameongezeka kwa asilimia 300.Hawa anasema, “Mwanzoni hatukuwa na kitu kabisa. Tulihangaika sana kulima mpunga. Lakini baada ya IFAD kutufikia katika maisha yetu na kutusaidia, mambo yalianza kubadilika. Walitupatia pembejeo na mbegu za ubora wa juu kuanzisha mashamba. Tulitumia mbegu hizo kupanda kwenye mashamba yetu Bakadu.”Awali walilima ekari 1.2 tu, lakini baada ya kupatiwa vifaa vya kisasa vya kilimo wameweza kulima hadi ekari 4.3.Mavuno ya mpunga yameongezeka. Wanasagisha mashine, kiasi cham chele wanauza na ziada ni kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.Hawa akiwa kwenye shamba lake la mpunga anasema,“Kabla ya STAR-P nilijihisi nimepotea na mpweke. Lakini sasa ninaweza kulima mwenyewe shambani, na ninaweza kujihudumia mimi na pia familia yangu. Zamani niliacha shule. Lakini baada ya kuanza mradi huu, nimerejea shuleni na ninataka kuwa mhasibu mkubwa duniani.”

Jioni - Voice of America
Watu zaidi ya 27 wamefariki na wengine wametekwa na watu wanaodhaniwa kutoka kundi la ADF huko mashariki mwa DRC. - Januari 16, 2025

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 16, 2025 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Habari za UN
Mlipuko wa homa ya Marburg washukiwa nchini Tanzania; watu 8 wafariki dunia

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 15, 2025 2:01


Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO, linachunguza sampuli za watu wawili kati ya wanane waliofariki dunia mkoani Kagera nchini Tanzania kubaini iwapo wamekufa kwa ugonjwa wa homa ya Marburg ambayo inashukiwa kulipuka kwenye wilaya mbili za mkoa huo ulioko kaskazini-magharibi mwa Tanzania. Selina Jerobon na maelezo zaidi.

Alfajiri - Voice of America
Moto mkali wa msituni waua watu watano na kuteketeza nyumba nyingi huko Los Angeles California - Januari 09, 2025

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 9, 2025 29:59


Alfajiri - Voice of America
Zaidi ya watu 100,000 wamehama makazi yao katika mapigano ya hivi karibuni kati ya M23 na jeshi la Congo - Januari 08, 2025

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 8, 2025 30:00


Habari za UN
UN: Vifo vitokanavyo na baridi Gaza vinazuilika, usitishaji mapigano na misaada ndio jawabu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 3, 2025 1:58


Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM leo limeonya juu ya vifo vitokanavyo na msimu wa baridi kali Gaza likisema limesikitishwa sana na athari mbaya za mvua za msimu wa baridi na baridi kali kwa Wapalestina waliokimbia makazi yao na kuishi katika mazingira magumu huko Gaza, kwani hilo ni janga la kibinadamu lisilo na kifani. Kupitia taarifa iliyotolewaleo mjini Geneva Uswisi Mkurugenzi Mkuu wa IOM Amy Pope  amesema "Watu walio katika mazingira magumu, ikiwa ni pamoja na takriban watoto wachanga saba, wamekufa kutokana na baridi kali au hypothermia, na vifo hivi vya kusikitisha vinasisitiza haja ya haraka ya makazi na msaada mwingine wa kibinadamu kuwafikia watu wa Gaza mara moja," Ameongeza kuwa hali hii inachochea janga zaidi la kibinadamu ambalo tayari linawakumba watu waUkanda wa Gaza. Mvua kubwa na mafuriko yameyakumba makazi ya wakimbizi wa ndani yaliyojengwa kwa mahema na kulazimisha familia kuachwa katika maeneo ya wazi kwenye hali mbaya ya baridi, zikijitahidi kutengeneza mahema yaliyoharibika kutokana na matumizi ya miezi kadhaa. © UNRWAChakula kinagawiwa kwa watu waliokimbia makazi yao huko Jabalia, kaskazini mwa Gaza.Vikwazo vya Israel ni changamoto kwa misaadaPia IOM imesema vikwazo vya utaratibu wa kufikia wenye uhitaji, kama ilivyoripotiwa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA, vimezuia kwa kiasi kikubwa utoaji wa misaada, huku watu 285,000 pekee wakipokea msaada wa makazi tangu Septemba 2024. Kwa mujibu wa IOM hadi kufikia Katikati ya Desemba mwaka jana inakadiriwa kuwa watu wapatao 945,000 bado wanahitaji msaada wa haraka wa kukabiliana na msimu wa baridi ikiwemo nguo za kuongeza joto, mablanketi na tepu za kuima mahema dhidi ya mvua na baridi. Tangu Katikati ya Novemba mwaka jana IOM imewasilisha karibu vifaa 180,000 vya makazi ya dharura kwa washirika ndani ya Gaza na ina zaidi ya vifaa milioni 1.5 vya msimu wa baridi ikiwemo mahema, vifaa vya kuziba  na vitanda ambavyo viko tayari kwenye maghala na sehemu zavivuko, lakini vikwazo vikali vya ufikiaji vinawazuia kufikia wenye uhitaji. © UNICEF/Abed ZaqoutWavulana wawili wakibeba chupa za maji katika kambi ya wakimbizi inayofadhiliwa na UNWRA huko Khan Younis kusini mwa Gaza.Usitihsaji mapigano ndio suluhuIOM imesisitiza wito wake wa dharura wa kusitisha mapigano ili kuwezesha utoaji salama na wa haraka wa msaada wa kuokoa maisha kwa wale wanaouhitaji sana. Pia inasisitiza wito wake kwa pande zote kuzingatia sheria za kimataifa za kibinadamu, kuhakikisha ulinzi wa raia, kuachiliwa kwa mateka wote na kuruhusu ufikiaji salama, wa haraka, usiozuiliwa na endelevu wa wenye uhitaji. Watu wa Gaza wanastahili usalama, makazi na utu. IOM iko tayari kuhamasisha misaada na kusaidia jamii zilizofurushwa, lakini fursa ya ufikiaji wa kibinadamu lazima itolewe ili kuwezesha hili amesisitiza mkuu wa IOM. Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA limesema Licha ya hali ngumu, timu za UNRWA zinaendesha makao yote ya Umoja wa Mataifa, na kutoa msaada wa kuokoa maisha kwa watu wanaohitaji. Limeongeza kuwa Vita vilipoanza karibu miezi 15 iliyopita, UNRWA iligeuza shule zake, vituo vya afya, na maghala kuwa makazi na kuna wakati ambapo vita ikiendelea UNRWA ilipokea watu milioni 1 waliokimbia makazi yao 

Habari za UN
Papua New Guinea: Tuhuma za uchawi dhidi ya wanawake zapatiwa  ‘muarobaini'

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 3, 2025 2:08


Kila mwaka, mamia ya wanawake nchini Papua New Guinea, taifa la visiwani katika bahari ya Pasifiki, hushutumiwa kimakosa kuwa ni wachawi. Matokeo yake hukumbwa na ukatili miongoni mwa wanajamii. Hata hivyo Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la Mpango wa Maendeleo duniani, UNDP nchini humo, limechukua hatua.Kiongozi mkubwa wa Kijiji chetu alifariki dunia, na tulipoenda kwenye maziko, ambapo kila mtu alisema sisi ni wachawi na tulikula moyo wake. Ni kauli ya Annabele, jina lake halisi limehifadhiwa kwa ajili ya usalama wake akielezea tuhuma zilizowakabili kwenye jamii yao ya jimbo la Enga nchini Papua New Guinea, hadi kushambuliwa kwa nondo za moto na nyumba zao kuteketezwa kwa moto. Video ya UNDP inamnukuu akisema kuwa walikuwa 9, ambapo wanne walifariki dunia na watano akiwemo Annabele, walinusurika, “kesho yake asubuhi Askofu na wenzake walifika, halikadhalika jeshi na polisi, na ndio walituokoa.” Askofu huyo Justine Soongie Dayosisi ya Wabag jimboni Enga anasema walipowachukua waliambiwa wahakikishe hawarudi kijijini, “sababu kubwa ya mtu kutuhumiwa ni jamii kukosa uelewa kuhusu chanzo cha kifo. Watu wengi hawafahamu kuwa mtu anaweza kufa kutokana na kiharusi. Watu wetu wa Enga watauliza ni nani amesababisha?” Annabelle baada ya kuokolewa alipelekwa hospitali na kupatiwa matibabu ambayo hata hivyo bado ana kovu na maumivu. Kisha walipelekwa nyumba salama zinazoendeshwa na Kanisa Katoliki kwa ufadhili wa UNDP, ambako waliishi kwa miezi takribani mitano wakipatiwa mavazi, malazi na chakula. Askofu Justine Soongie anasema,“baada ya miezi kadhaa hospitalini, tunarudi kwa familia na jamii na kuzungumza nao mara kadhaa. Tunawaelimisha kuwa ni kosa kumtuhumu mtu uchawi, kuna sheria, na hana pahala pengine pa kwenda, hivyo atarudi.” Jamii ilieleweshwa na Annabelle kwenye video anaonekana tayari yuko kijijini na sasa analima shamba na hata anasema hata mazao anayolima akivuna, anapika na wanajamii wanakula pamoja naye. 

SBS Swahili - SBS Swahili
Jeshi la polisi la Kenya lakanusha kuhusika na utekaji wa wakosoaji wa serikali

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 27, 2024 8:33


Jeshi la polisi Kenya limekanusha kuhusika na visa vya karibuni vya utekaji unaowalenga wakosoaji wa serikali. Watu 74 walitekwa tangu maandamano ya kuipinga serikali, huku 26 wakiwa bado hawajulikani waliko.

Alfajiri - Voice of America
Watu kadhaa washukiwa kufa kutokana na ghasia za matokeo ya uchaguzi wa Msumbiji. - Desemba 25, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 25, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

watu kufa uchaguzi desemba
Alfajiri - Voice of America
Ugonjwa mpya unaofanana na homo DRC wazua wasi wasi baada ya kuuwa darzeni ya watu. - Desemba 20, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 20, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

homo wasi watu baada ugonjwa desemba
Habari za UN
10 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 10, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na tunaelekea nchini Kenya kuangazia moja ya ukiukwaji Mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya wanawake, jinamizi la ukeketaji na jitihada zinazochukuliwa na UNFPA na wadau mbalimbali. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani inayotupeleka nchini Namibia.Baada ya serikali ya Bashar Al-Assad kupinduliwa na kuibuka kwa taarifa za baadhi ya nchi duniani kuanza kusitisha mchakato wa kushughulikia maombi ya Wasyria waliokuwa wameomba hifadhi kuokoa usalama wa maisha yao pindi hali ilipokuwa tete nchini mwao, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) linaendelea kutoa wito kwa mataifa yote kufungua milango, kuwapa hifadhi na ulinzi raia wa Syria wanaotafuta usalama. UNHCR imeahidi pia mara tu hali ya Syria itakapokuwa wazi zaidi, itatoa mwongozo kuhusu mahitaji ya ulinzi kwa Wasyria walioko hatarini.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limekaribisha mchango wa dola za Marekani milioni 22 kutoka shirika la Korea Kusini la Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa (KOICA) ili kuimarisha mnepo kwa tabianchi na uhakika wa chakula kwa wakulima wadogo, wafugaji na makundi yaliyoko pembezoni nchini Kenya, Somalia na Sudan Kusini. Vituo vya utabiri wa hali ya hewa vinatabiri hali ya La Niña mashariki mwa Pembe ya Afrika na uwezekano wa kupunguza mvua katika kipindi hikiNa walinda amani wa kikosi cha 11 cha Tanzania -TANZBATT-11 kinachohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO jimboni Kivu Kaskazini wametunukiwa nishani ya umoja wa mataifa ikiwa ni alama ya kufanya kazi  kwa utii,uhodari na uaminifu. Miongoni mwao ni Private Selina Kisemvule.Katika mashinani ikiwa ni siku ya mwisho ya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, fursa ni yake Rais Nangolo Mbumba wa Namibia ambaye kupitia ukurasa wa X wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA anawahimiza wananchi na dunia nzima kwa jumla kusimama kidete ili  kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Alfajiri - Voice of America
Zaidi ya watu darzeni moja wahofiwa kufa kwenye ajali ya boti Misri - Desemba 10, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 10, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
06 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 6, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia Mkataba wa Kampala wa Ulinzi na Usaidizi wa Wakimbizi wa Ndani barani Afrika, na siku ya kimataifa ya kujitolea inayotupeleka nchini DRC. Makala tunakwenda nchini Kenya na mashinani nchini Zambia, kulikoni?Katika kuadhimisha miaka 15 tangu kupitishwa kwa Mkataba wa Kampala wa Ulinzi na Usaidizi wa Wakimbizi wa Ndani barani Afrika chini Muungano wa Afrika, Kamishna Mkuu Msaidizi wa Ulinzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, Ruven Menikdiwela NA Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu za Wakimbizi wa ndani Paula Gaviria Betancur wametoa kauli ya pamoja ya kupongeza Muungano wa Afrika kwa maono haya ya mbali na pia kuzisihi nchi zote barani Afrika kuutekeleza mkataba huo muhimu.Dunia ikiwa imeadhimisha siku ya kimataifa ya kujitolea kwa ajili ya amani na maendeleo, tunakupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako mmoja wa wafanyakazi wa kujiolea wa Umoja wa Mataifa anaelezea uzoefu wake na ni kwa nini anajivunia kufanya kazi hiyo.Makala leo inatupeleka Kakamega Magharibi mwa Kenya kwa mkulima mdogo wa mahindi Catherine Wanjala aiyeathirika vibaya na magugu yajulikanayo kama Kichawi au Witchweed, na hata kuilamisha familia yake kulaa njaa wakati mwingine kwa kukosa mavuno, lakini ahuweni ilimwijiia pale mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP wa kusambaza dawa za kupambana na magugu hayo ulipomfikia.Katika mashinani wakati huu ambao Dunia inaadhimisha siku 16 ya kupinga ukatili wa kijinsia, fursa ni yake Mheshimiwa Rais Hakainde Hichilema wa Zambia, ambaye kupitia mtandao wa X wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA anasisitiza mchango wa wanaume kwa kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
05 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 5, 2024 9:59


Hii leo jaridani mada kwa kina inayotupeleka katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali nchini Uganda kumulika hali ya ukatili dhidi ya wanawake kwa watu hao waliokimbia vita jinsi inavyoshughulikiwa. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA leo limezindua ombi lake la kimataifa la mwaka 2025, likitafuta dola bilioni 1.4 ili kutoa huduma za afya ya uzazi zinazookoa maisha na programu muhimu za kuzuia unyanyasaji wa kijinsia kwa zaidi ya wanawake, wasichana na vijana milioni 45 kote duniani katika nchi  57 zilizoathiriwa na majanga.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) leo jijini Geneva, Uswisi limetangaza kutoa idhini ya awali kwa kipimo kinachoitwa Xpert® MTB/RIF Ultra dhidi ya ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB). Kipimo hiki pia kinaweza kupima uwezekano wa kuathiriwa kwa viuavijasumu ambacho kinakidhi viwango vya WHO.Biashara ya kimataifa inatazamiwa kufikia dola trilioni 33 mwaka 2024, kulingana na Taarifa mpya ya Biashara ya Kimataifa iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo (UNCTAD). Ongezeko hili la dola trilioni 1, linaloakisi ukuaji wa mwaka wa asilimia 3.3, linaonesha uthabiti katika biashara ya kimataifa licha ya changamoto zinazoendelea.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno “MBUKU NA MSUNUNU.”Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
03 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 3, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo inamulika harakati za Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kuhakikisha wafugaji kuku wasiotumia dawa kiholela wananufaika kiuchumi baada ya kupatiwa mafunzo. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani ya Timor-Leste.Leo ni Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe mahususi kwa siku hii, ameueleza ulimwengu kuwa maadhimisho ya mwaka huu yanawakumbusha kwamba ulimwengu unahitaji uongozi wa watu wenye ulemavu zaidi kuliko hapo awali. Guterres ameeleza kuwa Watu wenye ulemavu tayari wanabeba mzigo mkubwa wa majanga yanayoumiza ulimwengu lakini mara nyingi wananyimwa haki yao ya kuchangia katika suluhu za majanga haya.Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya Uchunguzi kuhusu Syria hii leo imezitaka pande zinazopigana nchini Syria zifuate kikamilifu sheria za kimataifa na kuwalinda raia. Hii inatokana na ongezeko kubwa la mapigano tangu tarehe 27 mwezi uliopita ambayo yanatishia kuenea katika maeneo mengine ya nchi.Mkutano wa mwaka 2024 wa Taaluma kuhusu Afrika umeanza leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Mada ya mkutano huo wa siku tatu ni "Nguvu, Haki, na Watu: Haki za Binadamu na Utawala wa Sheria kwa Mabadiliko ya Afrika." Mkutano huo wa kila mwaka unalenga kuongeza uwakilishi wa Waafrika katika ufadhili wa kimaendeleo wa kimataifa, ili kuchagiza mustakabali bora wa Afrika.Na mashinani leo ikiwa ni siku ya watu wenye ulemavu duniani tunakupeleka Timor-Leste, kusini-mashariki mwa Asia kuona jinsi mradi uliofadhiliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira, UNEP umemwezesha Antonio Ornai mwenye ulemavu wa kutoona kushiriki zoezi la kuitikia maonyo ya taarifa za majanga kwenye taifa hilo ambalo hugubikwa na majanga ya asili mara kwa mara kama vimbunga na mafuriko.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!  

Habari za UN
Waraka kutoka kwa watoto: Kwenu watu wazima, kwa nini mnauruhusu mustakbali wetu kuwekwa rehani?

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 20, 2024 2:20


Leo ni siku ya watoto duniani maudhui mwaka huu yakiwa "Kila mtoto, kila haki"na katika kuhakikisha sauti zao zinasikika kuhusu mustakbali wa utakao, shirika la Umoja wa Maataifa la kuhudumia watoto duniani UNICEF limewapa fursa ya kuandika barua kwenda kwa watu wazima kote duniani ili kutoa madukuduku yao na kutanabaisha wanachokitaka kwa ajili ya mustakbali wao. Hao ni baadhi tu ya makumi ya watoto walioandika barua , hawa ni kutoka Gaza, Tanzania na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC ambao walishika kalamu na karatasi kufikisha ujumbe wao kwa watu wazima wa dunia ya sasa iliyoghubikwa na changamoto lukuki zinazoweka rehani mustakbali wao.Kwa mujibu wa ripoti mpya ya UNICEF ya “Hali ya watoto duniani mwaka 2024: Mustakabali wa Utoto katika Ulimwengu Unaobadilika,” iliyotolewa leo sanjari na maadhimisho ya siku hii kuna masuala matatu makubwa ya kimataifa yatakatoathiri maisha ya watoto ifikapo 2050 na kuendelea. Mosi ni mabadiliko katika idadi ya watu, pili janga la mabadiliko ya tabianchi na migogoro na tatu teknolojiaUNICEF inasema yote haya ni changamoto na fursa ambazo watoto wanaweza kukabiliana nazo katika zama zijazo.Rafif mtoto mkimbizi wa ndani ameandika barua kutoka Palestina ambako vita imetamalaki, anasema“Ninatoka mjini Gaza na sasa nimefurushwa hadi Kusini mwa Gaza. kama watoto Ni haki yetu kuishi kwa usalama na kujenga mustakbali bora”Kutoka mashariki ya Kati hadi Afrika Mashariki kwa Steven akimulika afya“Na nianaandika kwenu kutoka Tanzania. Kwenye jamii yangu watoto wanaugua kila wakati , kwa nini? Huu ndio mustakbali wangu je unasikiliza?”Nako Congo DRC mitihani ni mingi, Andrea anasema“Nataka kushuhudia dunia ambayo kila mtoto anapendwa, dunia ambayo amani inashamiri ni raha na faraja. Napenda kuona hasira zinageuka na kuwa mazungumzo”Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiunga mkono suti hizo za watoto katika ujumbe wake amesema Katika Siku ya Watoto Duniani tunasherehekea washiriki wachanga zaidi wa familia yetu ya kibinadamu. Lakini leo pia ni wakati wa kutambua changamoto kubwa zinazowakabili watoto katika ulimwengu wetu uliogawanyika sana, wenye misukosuko na mara nyingi ulioshamiri ukatili.”Ripoti ya UNICEF imetoa wito wa kuwekeza katika elimu, miji endelevu na yenye mnepo kwa watoto, miundombinu inayohimili mabadiliko ya tabianchi, teknolojia, huduma muhimu na mifumo ya msaada wa kijamii na pia teknolojia iliyo salama kwa watoto ili kupambana na mzigo wa changamoto zinazowakabili.

Habari za UN
IOM: Zaidi ya watu 20,000 wamefuriushwa ndani ya siku 4 Haiti kutokana na machafuko ya magenge ya uhalifu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2024 2:06


Zaidi ya watu 20,000 wamekimbia makazi yao katika mji mkuu wa Haiti Port-au-Prince katika muda wa siku nne tu, ikiwa ni pamoja na watu wengine zaidi ya 17,000 wanaohifadhiwa katika makazi 15 ya wakimbizi wa ndani, kutokana na kuongezeka kwa ghasia za magenge ya uhalifu ambazo ziumevuruga kabisa minyororo muhimu ya usambazaji wa misaada na kulitenga jiji la Port-au-Prince (POTOPRINSI) limesema shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM. Kupitia taarifa iliyotolewa leo na IOM nmini Port-au-Prince asilimia kubwa ya watu hawa waliofurushwa makwao wametawanywa zaidi ya mara moja wakilazimika kukimbia na kuacha kila kitu walichokuwa nacho na shirikika hilo linasema kiwango hiki cha watu kutawanywa hakijashuhudiwa Haiti tangu Agost 2023.Shirika hilo linasema kufungwa kwa usafiri wa anga kufuatia shambulizi lililolenga ndege tatu za kibiashara mjini Port-au-Prince, kuzuia ufikiaji wa bandari kuu ya nchi hiyo, na barabara zisizo salama zinazodhibitiwa na makundi yenye silaha kumeliacha eneo la Katikati ya mji mkuu taabani na kutengwa bila msaada na hivyo kuzidisha mateso kwa watu ambao tayari wako hatarini.Mkuu wa IOM nchini Haiti Grégoire Goodstein ameonya kwamba "Kutengwa kwa Port-au-Prince kunaongeza janga la ibinadamu. Uwezo wetu wa kutoa misaada umewekwa njiapanda na bila msaada wa haraka wa kimataifa, mateso yataongezeka sana kwa raia wa Haiti huku kukiwa na asilimia 20 pekee ya mji wa Port-au-Prince inayofikika, wakati wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu wanakabiliwa na changamoto kubwa katika kufikia watu walioathirika.”Kulingana na Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR, vikundi vya uhalifu katika mji mkuu wa Hati vinaendelea kupanuka wigo vikichukua udhibiti wa vitongoji vya ziada na kutenganisha zaidi jamii.Hadi sasa ofisi hiyo inasema ghasia zinazohusiana na magenge zimesababisha karibu vifo 4,000 mwaka 2024, unyanyasaji wa kijinsia, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kingono unaotumiwa kama silaha ya ugaidi, umefikia viwango vya kutisha.Pia imesema wanawake na watoto wameathiriwa kupita kiasi, huku asilimia 94 ya wanawake na wasichana waliokimbia makazi yao wakiwa katika hatari kubwa ya kudhulumiwa kingono.Licha ya changamoto hizi, IOM na washirika wake wameahidi kuendelea kutoa msaada wa kuokoa maisha.IOM pia inatoa wito wa kuongeza haraka ufadhili kwa shughuli za kibinadamu Haiti kwani hadi kufikia mwezi huu wa Novemba, ombi la dola milioni 674 la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Haiti limefadhiliwa kwa asilimia 42 pekee, na kuwaacha mamilioni ya watu bila msaada wanaohitaji.

Habari za UN
Ushindi wa tuzo ya mtu bora wa mwaka wa UN ni ushindi kwa watu wa Kajiado wanaonufaika na mradi wetu - Kipeto

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 28, 2024 3:02


Kampuni ya Craftskills Wind Energy International Limited wamiliki wa mradi wa nishati ya umeme itokanayo na upepo ya Kipeto Energy iliyoko Kaunti ya Kajiado nchini Kenya wamejitwalia tuzo ya “Mtu Bora wa Mwaka wa Umoja wa Mataifa. 2024”Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo anasema ushindi huo ni kwa watu wa Kaunti ya Kajiado nchini Kenya ambao ni wanaufaika wakubwa wa mradi kwani sio tu umewaletea umeme, bali pia umewainua kiuchumi na kijamii kwa miradi mingine mbalimbali kama inabobainisha makala hii iliyoandaliwa na Flora Nducha..

Habari za UN
16 OKTOBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 16, 2024 9:54


Hii leo jaridani tunaangazi siku ya chakula duniani ikitupeleka jijini Roma Italia kufuatilia maadhimisho yake. Pia tunakupeleka nchini Kenya kusikia ni kwa jinsi gani mashirika wanhaha kusaidia uoni kwa watu wenye changamoto. Makala tunakwengda nchini DRC na mashinani Sierra Leone, kulikoni?Washiriki wa Sherehe za kimataifa za mwaka huu wa 2024 za kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Chakula zilizofanyika leo katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) jijini Roma Italia wamesisitiza haja ya upatikanaji wa vyakula mbalimbali vya kutosha, vyenye lishe, bei nafuu na salama.Nchini Kenya, Idara ya Taifa ya Ulinzi wa Jamii kwa kushirikiana na Baraza la Kitaifa la Watu wenye ulemavu na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, wameendesha kambi ya kusaidia uoni kwa watu wenye changamoto ikiwemo Candy mwenye umri wa miaka 7 ambaye ana ualbino. Baba yake alifika kwenye kambi hiyo na anatusimulia kupitia video ya UNICEF Kenya.Makala inatupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kusikia harakati za shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP la kusaidia wanawake wakimbizi kuondokana na ujinga wa kutokujua kusoma na kuandika.Mashinani tunamsikia Mpishi Mkuu Fatmata Binta kutoka kabila la wafugaji wanaohamahama la fulani nchini Sierra Leone anaeleza jinsi ushirikiano wake na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, kuhusu ni kwa jinsi gani FAO umemwezesha kusambaza manufaa ya fonio, nafaka asili ya Afrika , inayoweza kuwa suluhisho la changamoto za ukosefu wa chakula na tabianchi.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Ancient Warfare Podcast
AWA321 - When was the first wargame?

Ancient Warfare Podcast

Play Episode Listen Later Sep 6, 2024 11:10


Thanks to Jamie for sending this in: "What was the first wargame? Did it really start at WATU, or are there examples of ancient generals playing games to practice for war, an ancient equivalent of a modern wargame?" Join us on Patron patreon.com/ancientwarfarepodcast