POPULARITY
Categories
Waziri Mkuu amesifu msaada wa wanachama wa kongamano la Visiwa vya Pasifiki, Australia inapo saka uenyeji wa kongamano la mazingira la Umoja wa Mataifa la, COP-31.
Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa leo Flora Nducha anakuletea-Utapiamlo kwa watoto katika Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel umefikia kiwango cha kutisha, huku takwimu mpya zikionesha ongezeko kubwa mwezi Agosti kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa-Umoja wa Mataifa umeanzisha mradi mpya wa miaka mitatu wenye lengo la kusaidia nchi za Afrika Mashariki kukabiliana na matumizi ya kigaidi ya vilipuzi. Kupitia mradi huu, Kenya, Somalia na Uganda zitasaidiwa-Hali nchini Haiti inaendelea kuzorota, sehemu kubwa ya nchi inadhibitiwa na magenge yenye silaha, nusu ya idadi ya watu wanakabiliwa na upungufu wa chakula, na idadi ya watu waliofurushwa imefikia kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa amesema Tom Fletshe mkuu wa OCHA-Mada kwa kina inatupeleka Uganda watumiaji wa Ziwa Albert wafunguka kuhusu changamoto za uvuvi haramu na faida za ziwa hilo-Na katika jifunze KIswahili leo mtaalam wetu Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "UKWASI!
-Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea UNGA79yafikia tamati hii leo na kupisha UNGA80 chini ya uongozi wa Rais mpya Annalena Baerbock-Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyozinduliwa leo imesema matumizi ya kijeshi duniani yalifikia dola trilioni 2.7 mwaka 2024, yakiwa yameongezeka kwa zaidi ya asilimia 9 kutoka mwaka 2023-Mratibu wa Misaada ya Dharura wa Umoja wa Mataifa Tom Fletcher ametangaza leo dola milioni 1 za kimarekani kutoka Mfuko wa Dharura wa Umoja wa Mataifa CERF ili kudhibiti mlipuko wa kipindupindu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. -Mada kwa kina inatupeka Pemba Kaskazini kisiwani Zanzibar nchini Tanzania kuangazia mradi wa FAo wa ZJP unavobadili maisha ya wakulima wa ndiziNa katika jifunze Kiswahili utamsikia mlumbi Jorum Nkumbi kutoka Tanzania akifafanua maana ya neno LISANI
Dau Akouny, mmoja wa wavulana wawili walio uawa katika shambulizi la kisu mjini Melbourne wikiendi iliyopita, amekumbukwa na familia yake kama "mtoto mzuri" na alikuwa "sehemu ya mustakabali wa kesho wa jumuiya."
In this episode of the Habari Live Podcast, Damon and Iesha break down the escalating chaos in American politics and public health:
Karibu kusikiliza jarida la Habari za Umoja wa Mataifa ambapo leo tunakuletea taarifa kuhusu hali ya hewa na athari za moto wa nyika, tutaelekea Gaza kusikia kutoka kwa mashuhuda wa madhila wayapatayo watoto na wananchi wa Gaza na kisha tutaelekea Jamhuri ya Afrika ya Kati ambako wanaendesha mafunzo ya usalama barabarani.
Waziri wa mambo ya tamaduni nyingi Anne Aly, amechangia ujumbe wa mshikamano na jumuiya yawa Hindi wa Australia, kufuatia maandamano dhidi ya wahamiaji.
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa leo Flora Nducha anakuletea-Shirika la Umoja wa Mataifa la makazi duniani UN-HABITAT lataka wakusanyaji na wachakataji wa taka watambuliwe kwani ni uti wa mgongo wa kuhakikisha mazingira safi na salama mijini-Katibu MKuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameipongeza Papua New Guinea kwa kuwa kisima cha kuvuna hewa ukaa na kuzitaka nchi za G-20 kuwajibika katika kudhibiti mabadiliko ya tabianchi-Nchini Mali, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, ameonya juu ya kuzorota zaidi kwa hali ya haki za binadamu. -Na leo katika jifunze Kiswahili Je wafahamu maana ya methali "MASIKINI HANA MIIKO"? basi msikilize mtaalam wetu Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani
Mbunge wa upinzani Matt Canavan amesema sera za uhamiaji za seriakli, zina wasukumu watu kuwa na maoni yenye misimamo mikali. Amesema serikali ya Labor imefungua anacho ita milango ya mafuriko ya uhamiaji baada ya janga la UVIKO-19, na inawaruhusu watu kuingia nchini kiholela chini ya ya sera zake za sasa.
Here's a strong title and description for your YouTube upload of this episode:Unmasking Crime: The 13/50 Myth, White Male Violence & Political Deflections | Habari LiveIn this episode of Habari Live, Damon and Iesha cut through the lies and expose how crime statistics are weaponized to distort reality. From the infamous “13/50” myth to overlooked white male violence, we bring the truth others try to hide.
Waziri Mkuu Anthony Albanese amesema Richard Marles alikuwa na mkutano wenye tija na mshiriki wake kutoka Marekani Pete Hegseth, huku kukiwa mkanganyiko kuhusu kama, kuna mkutano rasmi ulio fanyika kati yao.
Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina, wiki ya Maji ikifikia tamati leo Agosti 28 na maudhui yakiwa Maji kwa ajili ya Hatua kwa Tabianchi, tunabisha hodi kaunti ya Kajiado nchini Kenya kumsikia mtendaji kwenye mradi wa maji wa Kerarapon Water Association ambalo ni shirika la kijamii linalohusika na maji na mazingira huko kaunti ya Kajiado nchini Kenya. Mengine ni kama yafuatayo.Ukraine ambapo leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameungama na mashirika mengine ya Umoja wa Mataifa kulaani vikali mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani droni yaliyofanywa na Urusi usiku kucha kuamkila dhidi ya miji ya Ukraine na kusababisha vifo na majeruhi kwa raia, wakiwemo watoto, na pia kuharibu majengo ya kidiplomasia jijini Kyiv. Amesisitiza kuwa mashambulizi dhidi ya raia na miundombinu yao yanakiuka sheria za kimataifa za kibinadamu, akitaka yakome mara moja na kurudia wito wake wa kusitisha mapigano ili kuelekea amani ya kudumu itakayoheshimu uhuru wa watu, uhuru wa kitaifa na mipaka ya Ukraine kama inavyotambuliwa kimataifa.Kuhusu Mashariki ya Kati Katibu Mkuu António Guterres akizungumza na waandishi wa Habari hii leo kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa ameonya kuwa operesheni za kijeshi mjini Gaza zitakuwa na zahma kubwa na amesisitiza “hili lazima likome.” Amesema njaa si tishio tena bali janga la sasa, huku raia, wahudumu wa afya na waandishi wa habari wakiuawa wakati “macho ya dunia yakitazama.” Guterres ameikumbusha Israel wajibu wake wa kisheria kulinda raia na kuruhusu msaada wa kibinadamu bila vikwazo akisema “Hakuna visingizio tena. Hakuna vizuizi tena. Hakuna uongo tena,” akitoa wito wa usitishaji mapigano haraka na kuachiliwa kwa mateka wote.Kikosi cha 11 cha Tanzania TANZBATT 11 kinachohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani MONUSCO kimetoa msaada wa magodoro kwa raia walioathirika na machafuko ya karibuni katika kijiji Oicha jimboni Kivu Kaskazini. Miongoni mwao ni Bi Masika Jistine na Mzee Bahati Paluku ambao hawakusita kuonesha furaha yao.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "MKWIJI!.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakulatea-Ripoti mpya kwa jina Maendeleo katika Maji ya Kunywa na Kujisafi Majumbani iliyozinduliwa leo na mashirika ya Umoja wa Mataifa imeonesha kwamba, licha ya hatua kupigwa, mtu 1 kati ya 4 duniani bado hana upatikanaji wa maji salama ya kunywa. -Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa, OHCHR imetoa wito kwa mamlaka za Misri kukomesha mfumo wa “mzunguko” unaofanya wakosoaji wa Serikali kuzuiliwa kiholela na kwa muda mrefu, hata baada ya kumaliza vifungo vyao. - Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi,UNHCR leo limepongeza Serikali ya Kifalme ya Thailand kwa kupitisha azimio litakalowapa wakimbizi wa muda mrefu kutoka Myanmar haki ya kufanya kazi nchini Thailand.-Katika mada kwa kina tunamulika uzinduzi wa shule ya kwanza ya Akili Mnemba iliyoanzishwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women huko ukanda wa Asia na Pasifiki-Na mashinani utamsikia Ibrahim Al-Najjar mkimbizi huko Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli akielezea hali tete ya ajira hivi sasa tangu vita ianze Oktoba 7, 2023.
Serikali ya Albanese inatarajiwa kuleta mbele mpango wakupanua mfumo unao ruhusu wanao nunua nyumba ya kwanza, kuweka amana ya hadi asilimia tano. Wakati marudio ya awali ya mpango huo yalikuwa na kikomo cha kila mwaka kwa washiriki, mfuno huo kwa sasa utakuwa wazi wa kila mtu anaye nunua nyumba.
Here's a strong YouTube episode description for this Habari Live episode—optimized for engagement and search:In this episode of Habari Live, Damon and Iesha break down the week's biggest political battles:
Kufuatia kuuawa kwa waandishi sita wa habari huko Gaza, viongozi wa mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa wamekosoa vikali shambulio hilo lililotekelezwa na majeshi ya Israel usiku wa kuamkia leo. Sabrina Said na taarifa zaidi.
Waziri wa mambo ya nje Penny Wong ame muhamasisha Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, asikize wito wakisitisha vita mara moja Gaza.
Serikali ya shirikisho imetangaza msaada kwa Gaza uta ongezwa kwa $20 milioni hii leo Jumatatu 4 Agosti, masaa machache baada yamakumi yama elfu kutembea katika Daraja maarufu la bandari ya Sydney, jana Agosti 3, katika maandamano dhidi ya vita vinavyo endelea Gaza.
In this explosive episode of *Habari Live*, Damon and Iesha pull no punches as they uncover the devastating impact of Donald Trump's war on public education. From Arizona's broken voucher experiment to GOP resistance against stock trading bans, we expose how billionaires and politicians are dismantling public trust—one school and one policy at a time.We break down:
Wanafunzi milioni tatu nchini Australia wata punguziwa deni zao za elimu, hii ni baada ya muswada wa Labor ulio tazamiwa sana kupitishwa bungeni hii leo.
Waziri Mkuu Anthony Albanese ana enda kuhudhuria tukio kubwa linalo waleta pamoja wa Australia wa Asili katika wilaya ya Kaskazini.
Waziri Mkuu Anthony Albanese amesema anaendeleza juhudi zakupunguza shinikizo za gharama ya maisha, akimulika mpango wakupunguza bei za madawa.
Australia imefanya makubaliano makubwa na Marekani katika jaribio lakupewa msamaha wa ushuru, kwa kuondoa Marufuku kwa nyama ya Marekani. Hadi sasa, marufuku hiyo ilitumiwa kwa nyama ya ng'ombe walio toka katika nchi za tatu, au ambao asili yao haijulikani.
Australia imefanya makubaliano makubwa na Marekani katika jaribio lakupewa msamaha wa ushuru, kwa kuondoa Marufuku kwa nyama ya Marekani. Hadi sasa, marufuku hiyo ilitumiwa kwa nyama ya ng'ombe walio toka katika nchi za tatu, au ambao asili yao haijulikani.