POPULARITY
Categories
Tuliyokuandalia katika Jarifada la Habari hii leoNi miaka miine tangu uvamizi kamili wa Urusi nchini Ukraine, Umoja wa Mataifa wataka vita vikome mara moja kuwapunguzia madhila raiaHuko Gaza Shirika la UNICEF limezindua mpango wa Gaza we want au Gaza tuitakayo ili kukusanya maoni ya watoto baada ya miaka miwili ya vitaHuko The Hague Uholanzi kikao cha majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, (ICC) cha kuthibitisha iwapo kuna ushahidi wa kutosha wa kumfikisha mahakama aliyekuwa Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte kwa madai ya uhalifu dhidi ya ubinadamu kinaendeleaMada yetu kwa kina inajikita Tanzania kuangazia juhudi za kuhakikisha wasichana na wanawake hawaachwi nyuma katika sayansiNa katika jifunze Kiswahili utasikia maana na neno "PEMBUA"
Sehemu nyingi za Australia ziko katika hali ya juu ya tahadhari, hali mbaya ya hewa na mvua zikiendelea kuathiri jamii na kuharibu njia muhimu za usafiri.
Andrew Mountbatten-Windsor ameachiliwa huru chini ya uchunguzi baada ya polisi wa Uingereza kumhoji kwa saa muda wa masaa 12 kwa tuhuma za utovu wa nidhamu katika ofisi ya umma.
Ripoti mpya ya kiuchumi inaonya Australia ina elekea kupoteza hadhi yake, kama taifa lenye deni la chini, huku mikopo ya serikali ikifikia viwango ambavyo havija onekana tangu vita vya pili vya dunia.
Mbunge wa chama cha One Nation Barnaby Joyce, amesema ni wazi sera ya uhamiaji ya chama chake, ina ungwa mkono na chama cha Liberal, akihoji madai ya baadhi yama seneta wa chama cha Liberal kuwa hawana taarifa kuhusu mpango huo wa uhamiaji.
Mwanaume ambaye ame shtumiwa kwa kushiriki katika shambulizi laki gaidi katika fukwe ya Bondi, amefikishwa mahakamani.
Sintonía: "Hotel Incidental Music" - Usha Khanna (del film "Hotel" de 1981) 1.- "Giraffe Trapping Music" - Sapan & Jagmohan (del film "Habari" de 1978) 2.- "Orchestral Music" - Raghunath Seth (del film "Ek Baar Phir" de 1979) 3.- "Contessa" - Chic Chocolate (del film "Aakhri Khat" de 1966) 4.- "Dance Music" - S.D. Burman (del film "The Jewel Thief" de 1967) 5.- "Mahbooba Mehbooba" - Van Shipley (del film "Sholay" de 1976) 6.- "Bairaag Dance Music" - Kalyanji - Anandji (del film "Bairaag" de 1973) 7.- "Title Music" - O.P. Nayyar (del film "Kismat" de 1968) 8.- "Dance Music" - Govind-Naresh (del film "Ghamandee" de 1981) 9.- "Chhedo na dekho na" - Hazara Singh (del film "Jigri Dost" de 1969)10.- "Awara sadiyoh se" - Babla & His Orchestra (del film "Bandh Honth" de 1983)11.- "Soul of Bobby" - Laxmikant - Pyarelal (del film "Bobby" de 1973)Todas las músicas extraídas de la compilación (1xLP) "Bollywood Nuggets Vol. II - A Collection of Mind Blowing Instrumental Songs From Hindi Films" (Akenaton Records, 2025)Lo mejor de la compilación (1xLP) "Bollywood Nuggets Vol. I" (2024) + "Nippon Girls Vol. 2" (2014) se emitió el 10/06/2024. Puedes "repescarlo" de los podcasts de Radio 3Escuchar audio
Kiongozi wa upinzani wa kwanza wa kike nchini Australia Sussan Ley ametangaza kuwa amestaafu kutoka siasa.
**ZIARA YA RAISI WA ISRAEL AUSTRALIA YAZUA UTATA HUKU WAANDAMANAJI NA POLISI WAKIKABILIANA KATIKA MAANDAMANO DHIDI YA RAIS HUYO ** SERIKALI YAZINDUA MPANGO WA KWANZA WA FAMILIA NA UNYANYASAJI WA WANAWAKE NA WATOTO WA MATAIFA YA KWANZA. **NA CHAMA CHA LIBERAL BADO LIANENDELEA KUWA NA MZOZO WA UONGOZI WA CHAMA BAADA YA KUGAWANYIKA KWA SIKU 17
**WAZIRI MKUU ANTHONY ALBANESE YUKO INDONESIA KUSAINI MKATABA WA KIHISTORIA WA USALAMA **MAJESHI YA MAREKANI NA URUSI YATANGAZA KUANZA KUSHIRIKIANA TAARIFA ZA KIJESHI HUKU MAZUNGUMZO YA AMANI NA UKRAINE YAKIENDELEA **WATU ZAIDI YA MIA MOJA HAMSINI WAFARIKI BAADA YA SHAMBULIO NIGERIA
Jaridani hii leo tuna Muhtasari wa Habari ukiangazia hali ya njaa Sudan, mchango wa Marekani dhidi ya VVU/ Ukimwi na kauli ya UNRWA kufuatia taarifa potofu dhidi ya shirika hilo. Halikadhalika mada kwa kina kutoka AfyaAFRIKA.Maeneo mawili zaidi katika jimbo la Darfur Kaskazini ya Um Baru na Kernoi sasa yameingia katika baa la njaa kufuatia utapiamlo wa kupindukia au unyafuzi kuvuka wiwango vya kutokuwa na uhakika wa chakula.Shirika la Umoja wa mataifa linalohusika na vita dhidi ya ukimwi UNAIDS limekaribisha kwa dhati hatua ya Marekani kutia saini kuwa sheria kifurushi cha matumizi ya kimataifa chenye thamani ya dola bilioni 5.88, kwa ajili ya hatua za kimataifa za kukabiliana na virusi vya ukimwi VVU .Kamishina Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA Phillippe Lazzarini amesema taarifa potofu dhidi ya UNRWA zinaendelea kulenga shirika hilo katikati ya mgogoro Gaza ikiwemo madai ya hivi karibuni kabisa, yaliyoibuliwa na video ya jeshi la Israel ikionesha mifuko mitupu ya unga karibu na mabomu, ambapo amesema ni taarifa za uongo na hazijadhibitishwa.Katika Mada kwa Kina: Kuelekea siku ya kutokomeza FGM kesho Februari 6, tunazungumza na Catherine Mootian, Muasisi na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la kiraia la AfyAfrika la huko Narok nchini Kenya. Yeye ni manusura wa FGM aliyeamua kuchukua hatua kuepusha wengine.
**BENKI YA HIFADHI INATARAJIWA KUONGEZA KIWANGO CHA RIBA **INDIA NA MAREKANI WAMEFIKIA MAKUBALIANO YA KIBIASHARA **KITUO CHA KITAIFA CHA DAWA ZA KULEVYA CHATOA TAHADHARI KUHUSU DAWA HATARI ZA STAREHE ** IRAN INAJIANDAA KWA MAZUNGUMZO NA MAREKANI KUHUSU NYUKLIA
**WATU WAWILI WAKAMATWA NA POLISI BAADA YA TUKIO LA UFYATULIAJI RISASI HUKO GEELONG. **KIPITO CHA RAFAH KATI YA EGYPT NA GAZA KUFUNGULIWA BAADA YA MIAKA MIWILI ** TAHADHARI KUHUSU MLIPUKO WA VIRUSI VYA NIPAH HUKO INDIA.
**MAMLAKA ZA DHARURA ZATOA TAHADHARI KUHUSU HALI YA HEWA LEO PANDE TOFAUTI VICTORIA **CHAMA CHA LIBERALS LIKO CHINI YA SHINIKIZO NA MSUKUMO WA ZIADA **KUNA PENDEKEZO MPYA YA KUFANYA MAFUTA YA KUJIKINGA NA JUA KUWA LAZIMA SHULENI
**Polisi wamsaka mtuhumiwa wa mauaji New South Wales ** Waustralia hamsini na tatu wataiwakilisha taifa kwenye Michezo ya Olimpiki **Na tamasha ya muziki ya Tamworth yaanza kesho.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya ambako wasichana juhudi za kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) zimewezesha vijana wa kike kushiriki masomo ya Teknolojia ya Habari na Maewasiliano, TEHAMA na kujifunza stadi za teknolojia ili waweze kuedeleza biashara ya mtandaoni pamoja na matumizi mengine.Zaidi ya watu nusu milioni wameathiriwa na mafuriko makubwa katika mikoa ya kusini na kati ya Msumbiji, huku mvua kubwa ikiendelea kuvuruga usafiri, huduma za afya na njia za ugavi. Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA nchini humo, Paola Emerson, amewaambia waandishi wa habari huko Geneva, Uswisi kuwa majimbo ya Gaza, Sofala na Maputo ndiyo yaliyoathirika vibaya zaidi.Huko Mashariki ya Kati mapema leo Jumanne, vikosi vya Israel vimebomoa kwa tingatinga makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA, huko Yerusalemu Mashariki eneo linalokaliwa kimabavu na Israel. Mkuu wa UNRWA, Philippe Lazzarini, amelieleza tukio hilo kama “shambulio lisilo na kifani dhidi ya Umoja wa Mataifa,”.Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, leo imesema imeanza kutekeleza mpango wa kurejesha kwa hatua mamlaka ya dola katika mji wa Uvira, mashariki mwa nchi hiyo, kufuatia kuondoka kwa kundi lenye silaha la AFC/M23. Serikali inasema vikosi vya usalama, polisi na huduma nyingine za serikali vinarejea ili kulinda raia, kulinda mali na kuleta utulivu katika eneo hilo.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mtaalam wetu ONNI SIGALA Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA, anafafanua maana ya neno “ KING'ANI”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
**Papa waendelea kuwashambulia watu huko Sydney ** Rais Donald Trump aendelea na mchakato wake wa kuchukua Greenland **Soko la Samaki la Sydney sasa limefunguliwa
** Kikundi cha Kiyahudi kinatoa wito wa mabadiliko na ucheleweshaji wa marekebisho ya hotuba za chuki za serikali... ** Angalau watu watano wameuawa katika mashambulio ya anga ya Israeli katika Ukanda wa Gaza ** Donald Trump ametishia kutuma wanajeshi kwenda Minneapolis ili kutuliza maandamano yanayoendelea juu ya matendo ya maafisa wa uhamiaji wa shirikisho katika Minnesota.
**Kevin Rudd ajiuzulu kama balozi wa Marekani... **Mlipo wa bomu waua maafisa wa polisi kaskazini mwa Pakistan... **Meta yazua shauku kuhusu Australia kuongeza umri wa kutumia mitandao ya kijamii. Kwa habari ama maelezo zaidi tembelea tovuti yetu sbs.com.au/swahili.