POPULARITY
Categories
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs) yanatambua kuwa kuwawezesha vijana, kulinda mazingira na kuimarisha uhakika wa kupata chakula ni miongoni mwa nguzo muhimu za kujenga jamii zenye ustahimilivu na maendeleo endelevu. Kupitia malengo kama vile la Kutokomeza umaskini, kutokomeza njaa na hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi , jamii zinahimizwa kuwekeza katika suluhisho zinazowawezesha wananchi kujitegemea huku zikihifadhi mazingira kwa vizazi vya sasa na vijavyo. Hatua hizo zinatekelezwa katika enoe la Kajiado Kaskazini, katika kaunti ya Kajiado, kusini mwa Kenya kama anavyosimulia Kelvin Keitany wa radio washirika, Domus Radio.Hii leo Umoja wa Mataifa umekuwa na matukio mbalimbali ya kuadhimisha siku ya Mandela, Rais wa kwanza mweusi wa taifa la Afrika Kusini kwa mchango wake wa utetezi wa haki. Miongoni mwa kulikofanyika maadhimisho hayo ni Nairobi, Kenya ambako Stella Vuzo wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa alikuwa shuhuda wetu. Licha ya idadi ya magari duniani kuongezeka kwa zaidi ya bilioni moja, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO limesema vifo vinavyotokana na ajali za barabarani vimepungua kwa asilimia 21 kati ya mwaka 2011 na 2025. Hata hivyo, ajali hizo bado zilisababisha vifo vya zaidi ya watu milioni 1 mwaka jana na zinaendelea kuwa chanzo kikuu cha vifo kwa watoto na vijana wenye umri wa miaka 5 hadi 29Na, Je, msikilizaji wangu, uliwahi kujiuliza kwa nini binadamu bado wanarudi kuchunguza Mwezi ulioko anga za juu , zaidi ya miaka 50 baada ya kutua huko kwa mara ya kwanza? Leo Julai 20, dunia inaadhimisha Siku ya Kimataifa ya mwezi. Umoja wa Mataifa uliitenga siku hii kuenzi tukio la kihistoria la mwaka 1969, wakati wanaanga wa safari ya Apollo 11 walipoweka nyayo za kwanza za binadamu mwezini. Lakini maadhimisho haya hayaishii kwenye historia tu bali yanasisitiza pia umuhimu wa ushirikiano wa kimataifa katika utafiti wa anga za juu na kuhakikisha uchunguzi wa mwezi unafanyika kwa amani na kwa manufaa ya watu wote duniani.".Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Chama cha Greens kinatoa wito wa mageuzi ambayo kisheria yatahitaji kampuni zama wasiliano kama Telstra, Optus na Vodafone kutoa huduma ya kuaminika kwa wateja.
Utafiti mpya unaonyesha kuwa watoto wa Australia wanaweza kuanza kuamua katika shule ya msingi kama watafuata taaluma za sayansi na teknolojia wanapokuwa wakubwa, huku wazazi wakiwa na ushawishi zaidi kuliko walimu katika maamuzi hayo.
Kuna wito wa kuharamisha matamshi ya chuki dhidi yawa Aboriginal na watu kutoka Visiwa vya Torres Strait, huku vikao vikiendelea katika uchunguzi wa ubaguzi wa rangi wa Serikali ya Shirikisho huko Darwin.
Serikali ya Shirikisho inasema vyuo vikuu vinaweza kukabiliwa na faini ikiwa vitashindwa kupambana na ubaguzi wa rangi chini ya viwango vipya vilivyoanzishwa Jumatatu 13 Julai 2026.
Mahakama ya Kupambana na Ugaidi na Makosa Dhidi ya Taifa iliyoko mjini Port Sudan nchini Sudan, , imemhukumu kifo kiongozi wa kundi la wanamgambo wa RSF, Mohamed Hamdan Daglo pamoja na maafisa wengine 15 wa RSF.
Polisi wanachunguza kama kifo kinahusishwa na kupotezwa kwa huduma ya Telstra kote nchini Jumatano. Wapelelezi wa Kusini Australia wamethibitisha mtu mmoja alifariki katika hospitali ya kanda Jumatano, lakini polisi hawakuwa wamearifiwa kuhusu kifo hicho.
Mamlaka katika jimbo la Kusini Australia, zimethibitisha kisa cha pili cha homa ya ndege aina ya H5 katika jimbo hilo.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Kesho, Julai 9, ni miaka 15 tangu Sudan Kusini ipate uhuru wake kutoka Sudan. Hata hivyo, matumaini ya amani yalitikiswa miaka miwili baadaye, mwezi Desemba 2013, baada ya kuzuka kwa mapigano kati ya serikali na makundi pinzani, hali iliyoendelea kuwaathiri mamilioni ya wananchi hadi leo. Katika juhudi za kurejesha amani, Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo, UNMISS, kwa ushirikiano na serikali ya jimbo la Equatoria Magharibi, umezindua kampeni mpya iitwayo "Tusikilizeni, Chukueni Hatua Sasa" (Hear Us, Act Now), inayolenga kuimarisha maridhiano, mshikamano wa kijamii na kuwahamasisha vijana kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa amani. Feissal Kirwa, kupitia video ya UNMISS, amefuatilia uzinduzi wa kampeni hiyo na sasa anatuletea mada hii kwa kina.Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze Kiswahili..Ripoti mpya ya hali ya saratani duniani kwa mwaka huu wa 2026 iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani (WHO) na shirika lake tanzu la utafiti wa saratani, IARC ikionya kuwa unyanyapaa ni moja ya vikwazo vya kutokomeza saratani wakati huu idadi ya wagonjwa ikikadiriwa kuongezeka maradufu ifikapo 2050, manusura wa saratani ya titi Abigael Hartz mkazi wa Ireland lakini anatokea Nigeria anasimulia alichoshuhudia alipotembelea hospitali moja ya kupima saratani Nigeria.Wiki mbili tangu matetemeko makubwa ya ardhi yapige mji mkuu wa Venezuela, Caracas na viunga vyake, idadi ya waliokufa imeripotiwa kufikia 3,685, majeruhi 16,740 na waliookolewa 6,462, Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Msaada wa Dharura, OCHA, Tom Fletcher yuko nchini humo na anasema.. “Hapa ni La Guaira, ambalo kwa hakika ndilo eneo lililokumbwa zaidi na janga hili. Nimekutana na mama mmoja aliyepoteza watoto wake watano waliokuwa kwenye jengo lililo kule. Bado anasubiri kwa matumaini, ingawa matumaini hayo yanazidi kufifia, kwamba huenda watoto wake bado wakapatikana wakiwa hai. Kwa hiyo, tupo hapa katikati ya vifusi na harufu ya miili ya waliopoteza maisha, tukijitahidi kuwafikishia manusura chakula, maji na huduma za matibabu, huku tukiwasaidia kuanza kufikiria namna ya kujenga upya maisha yao. Lakini safari ya kurejea katika hali ya kawaida bado ni ndefu sana.”wakati huu ambapo ripoti za vyombo vya Habari zinaeleza kuwa jeshi la Marekani usiku wa kuamkia leo limekamilisha awamu mpya ya mashambulizi dhidi ya Iran, yakilenga zaidi ya maeneo 80 zikiwemo meli tatu za kibiashara zilizokuwa zinapita Mlango wa Bahari wa Hormuz huko Ghuba ya Uajemi, Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Bahari, IMO Arsenio Dominguez amelaani mashambulizi hayo mapya akionya kuwa kwa mara nyingine maisha ya mabaharia wasio na hatia yanawekwa hatarini.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana za neno "KICHAKATA MATINI".Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Ofisi ya Takwimu ya Australia imezindua kampeni ya tamaduni mbalimbali kabla ya Sensa ya mwezi ujao, ikijumuisha matangazo katika lugha 28 tofauti.
Raia nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamepata matumaini mapya baada ya kuanza kwa majaribio ya dawa mbili zinazolenga kuudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.
Welcome to Habari Live!Is the Democratic Party undergoing a major ideological shift? This week, Damon Ellison and Iesha Rowan take a deep dive into the history of socialism, democratic socialism, and the rise of progressive candidates across the United States.We break down the recent primary victories of Democratic Socialists of America (DSA)-backed candidates, discuss what Zohran Mamdani's rise means for the future of progressive politics, and examine how leaders like Bernie Sanders and Alexandria Ocasio-Cortez have helped reshape the national conversation. We also explore the differences between socialism, democratic socialism, social democracy, capitalism, and communism, separating historical facts from modern political rhetoric.In our first segment, we examine the latest crime data showing that violent crime continues to decline across much of the United States. We compare national trends with Phoenix, Arizona, discuss why many Americans still feel less safe despite improving statistics, and explore the relationship between poverty, economic opportunity, and public safety. We also look at changes in federal law enforcement spending, including Department of Justice budget reductions and expanded funding for Immigration and Customs Enforcement (ICE).Finally, in our "Clips of the Week" segment, we discuss:* Wisconsin dairy farmers and rising production costs* Justice Clarence Thomas at the U.S. Capitol* Zohran Mamdani's comments on Israel* Dr. Elisabeth Potter's fight with UnitedHealthcare* Anti-foreigner protests in South Africa* Vice President JD Vance on birthright citizenship* Donald Trump's comments on the USMCA, immigration enforcement, and insider knowledge* Illinois Governor J.B. Pritzker's criticism of President Trump* Pete Hegseth's remarks about protestersJoin the conversation in the comments:Is the Democratic Party becoming more progressive? What role should the government play in healthcare, housing, and the economy? And what do you think is driving the decline in violent crime across America?If you enjoy thoughtful, fact-based discussions that go beyond the headlines, like this video, subscribe and share it with your friends.Habari Entertainment — We Do the News Our Way.
Ada ya maombi ya visa ya mwanafunzi imeongezeka tangu Julai 1 kutoka $2,000 hadi $2,500, huku Visa ya Muda ya Uzamili, au visa nambari 485, sasa inagharimu $5,750.
Polisi wamewakamata vijana wawili baada ya mvulana wa miaka 15 kuachwa afe nje ya kituo cha matibabu cha jamii mjini Melbourne.
Bei ya petroli imeshuka hadi viwango ambavyo havijaonekana tangu mwanzo wa 2022. Taasisi ya Petroli ya Australia inasema wastani wa kitaifa wa lita moja ya mafuta yasiyo na risasi ulishuka zaidi ya senti 6 wiki iliyopita - hadi chini kidogo ya dola 1.60.
Shirika kubwa zaidi huru la habari nchini Uganda Nation media group limearifu kuwa limewekwa chini ya ulinzi mkali wa kijeshi mapema Jumapili.
Mweka Hazina wa Shirikisho Jim Chalmers anasema wafanyakazi, wanunuzi wa nyumba za kwanza na vizazi vijavyo watafaidika na sheria zenye utata za mageuzi ya kodi ambazo zimepitishwa hivi karibuni bungeni.Polisi warusha mabomu ya kutoa machozi dhidi ya waandamanaji katika maeneo mbalimbali mjini Nairobi huku makundi yanayoongozwa na vijana yakikumbuka miaka miwili tangu maandamano ya Gen Z. Watu kadhaa wametiwa nguvuni kufuatia maandamano hayo. Mawingu mazito ya moshi yalitanda angani huku umati wa watu ukikimbia kujinusuru, wengi wao wakifunika nyuso zao kutokana na harufu kali na madhara ya gesi hiyo.Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.
Hali ya dharura ime anza kutumika nchini Venezuela baada ya matetemeko mawili makubwa ya ardhi, yaliyotokea magharibi mwa mji mkuu wa Caracas, na kuua watu wasiopungua 32 pamoja nakuwajeruhi mamia.
Chama cha Greens kimeita mpango wa serikali wa kurekebisha Mpango wa Kitaifa wa Bima ya Watu Wenye Ulemavu kuwa sheria 'isiyo ya kibinadamu'.
Polisi wamekamata tani 2.7 za kokeni katika kile kinachoelezwa kuwa unyakuaji mkubwa zaidi wa kokeni kuwahi kutokea nchini Australia.
Rais wa Marekani Donald Trump alisaini makubaliano na Iran jana Jumatano ambayo yanaitaka Jamhuri hiyo ya Kiislamu kupunguza kiwango cha akiba yake ya madini ya urani iliyorutubishwa.
Polisi wanachunguza ajali iliyotokea kusini-magharibi mwa Sydney usiku wakuamkia, ambayo imesababisha vifo vya watoto wawili wenye umri wa mwaka moja na miaka mitano.
Mabadiliko katika kodi ya faida ya mtaji yatapunguza uzalishaji na kuifanya Australia isiwe na ushindani mkubwa, makundi ya biashara yanasema, huku hatua za bajeti zenye utata zikichunguzwa kwa darubini. Uchunguzi wa Seneti kuhusu mabadiliko ya kodi unafanya vikao vyake vya kwanza leo.
Iran imethibitisha kwamba vita kati ya Marekani na Israeli katika nyanja mbalimbali Mashariki ya Kati vita isha usiku wa leo.
Is justice truly blind, or does America apply self-defense differently depending on who is involved?This week on Habari Live, Damon Ellison and Iesha Rowan take a deep dive into one of the most controversial questions facing the American justice system: Who gets self-defense?Using decades of research, FBI data, and legal studies, we examine racial disparities in self-defense rulings, Stand Your Ground laws, youth sentencing, and the role implicit bias may play in determining who receives the benefit of the doubt in court.We also investigate the growing influence of white nationalist movements in the United States and abroad. From record levels of extremist propaganda and organized hate groups to the spread of political rhetoric across social media, we explore how these movements are shaping conversations in America, Ireland, South Africa, and beyond.Plus, in our Clips of the Week segment, we break down:
Waziri Mkuu Anthony Albanese haja tupilia mbali uwezekano wa kuongeza muda wa kupunguzwa kwa ushuru wa mafuta kutokana na kufufuliwa upya kwa mapigano Mashariki ya Kati.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Kesho kutwa Alhamisi ya Juni 11, macho na masikio yanaelekezwa Mexico, Canada na hapa Marekani kwa ajili ya fainali za kombe la dunia kwa mpira wa miguu, au soka al maarufu kabumbu. Ingawa hivyo zama za sasa za mchezo huo maarufu zaidi duniani zinakumbwa na madhara ya athari za mabadiliko ya tabianchi. Ongezeko la joto kali linavuruga mechi na kuzua wasiwasi kuhusu mustakabali wa mchezo huo. Ni kwa kuzingatia hilo, Sekretarieti ya Mkataba wa Kimataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, UNFCCC inamulika suala hilo na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike kwani hivi sasa madhara ya joto kali kwenye kabumbu ni dhahiri. Feissal Kirwa anamulika hilo kupitia video iliyoandaliwa na UNFCCC.Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze Kiswahili.Takriban watoto milioni 138 duniani kote bado wako katika ajira za watoto, wakiwemo watoto milioni 54 wanaofanya kazi hatarishi. Hayo yamo katika ripoti mpya iliyotolewa leo na Shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa ILO. Katika ujumbe wakwe kwenye ripoti hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa ILO, Gilbert F. Houngbo, ametoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka ili kubadili hali hii.“Habari njema ni kwamba hadi sasa tuna wagonjwa 19 ambao wamepona, hivyo utambuzi wa mapema na matibabu vinaokoa maisha,” Huyo ni Mkurugenzi wa Operesheni za Tahadhari na Hatua za Dharura za Afya wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani (WHO), Dkt. Abdirahman Mahamud, akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva leo kwa njia ya video kutoka Bunia katika Jimbo la Ituri, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, jimbo ambalo linachangia asilimia 94 ya wagonjwa wote wa Ebola.Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, umeanza leo Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York na utaendelea hadi 11 Juni. Kaulimbiu ya mwaka huu ni “kuadhimisha miaka 20 ya mkataba huo na kuimarisha utekelezaji wake katika dunia inayobadilika.” Washiriki wanajadili namna ya kutokomeza ukandamizaji, ukatili na manyanyaso dhidi ya watu wenye ulemavu, kuimarisha mifumo ya huduma na msaada, pamoja na kuongeza ushiriki na uwakilishi wao katika maisha ya kisiasa na umma.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "MKWARUZO."Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Waziri Mkuu Anthony Albanese anasema serikali lazima zishughulikie mfadhaiko katika uchumi unaoongezeka, baada ya kura mpya ya maoni kuonyesha ongezeko la uungwaji mkono kwa chama cha One Nation.
Wanafamilia na Waziri Mkuu Anthony Albanese wamemkumbuka Richard Scolyer, mshindi wa zamani wa tuzo yamu Australia bora wa mwaka.
Send us Fan MailMkutano na Waandishi wa Habari kuhusu ziara ya Kitaifa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini Urusi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, tarehe 7 Juni, 2026.Support the showIdara ya Habari MAELEZO
Mabadiliko ya kodi ya serikali ya shirikisho yamepitishwa ndani ya nyumba la Wawakilishi - ila, upinzani wa mseto hauja tupilia mbali uwezekano wa muungano na chama cha Greens kuzuia mabadiliko hayo kupitishwa ndani ya Seneti na kuwa sheria.
Mahakama Kuu ya Kenya Jumanne ilisimamisha kwa wiki tatu zaidi mpango wa kujenga kituo cha karantini ya Ebola, kilichopendekezwa na Marekani.
Upinzani wa Mseto unakosoa muswada wa mageuzi ya kodi wa serikali ya Labour, kwa kumpa mweka hazina mamlaka ya kuamua ni mali gani zinaweza wekewa punguzo la kodi ya faida ya mtaji.
Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) lilisema kwenye taarifa yake ya Jumapili (Mei 31) kwamba, wagonjwa wengine zaidi wa Ebola wanatazamiwa kupona, hasa pale ugunduzi na matibabu yanapoanza mapema, wakati juhudi za kukabiliana na ugonjwa huo hatari zikiongezeka.
Republicans Redrawing America?! Black Districts Targeted Across The South | Habari LiveTonight on Habari Live, Damon and Iesha break down the growing redistricting battle sweeping across the South as Alabama lawmakers push for new congressional primaries while courts fight over voting maps and Black representation. Tennessee, South Carolina, Louisiana, and Virginia are now all at the center of a political war over district lines, voting rights, and control of the U.S. House.The discussion explores how recent court rulings and weakened Voting Rights Act protections are reshaping elections, why Black lawmakers and civil rights activists are sounding the alarm, and whether mid-decade redistricting is being used to dilute Black political power. From protests outside the Alabama Statehouse to lawsuits in Tennessee, Habari Live examines the national implications of these moves and what they could mean for democracy heading into the next election cycle.Are these maps about fairness — or political power?Is Black voting strength being intentionally weakened?And what happens when voters feel like politicians are choosing their districts instead of districts choosing their politicians?
Chama cha Nationals kimemtaka Waziri Mkuu Anthony Albanese kuitisha uchaguzi mkuu, kuhusu mabadiliko hasi ya kodi ya vifaa na faida ya mtaji yaliyoainishwa katika bajeti ya shirikisho.
Jeshi la Polisi la Shirikisho la Australia limemkamata mwanamke mmoja, kama sehemu ya uchunguzi unaoendelea chini ya Operesheni Kurrajong.
Waziri Mkuu Anthony Albanese anasema upunguzaji wa kodi ya faida ya mtaji, hautajumuishwa katika sehemu ya kwanza ya sheria inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni katika siku zijazo.