Makala haya yanaangazia maendeleo ya michezo mbalimbali Ulimwenguni na pia huwa haiwaweki kando wanamichezo waliobobea na vilevile kufanya uchanganuzi wa kina wa michezo wakati wa mashindano mbalimbali.
Hii leo tumeangazia michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya vijana chini ya miaka 20 kuanza nchini Misri, mkondo wa mtoano katika msururu wa raga duniani, diamond league mkondo wa pili huko Uchina na Ligi ya Basketboli mkondo wa Sahara ukiendelea, Cecafa yapata rais mpya, nembo ya Visit Rwanda yaendelea kupanuka, bondia wa DRC Martin Bakole kupigana leo usiku, PSG, Man Utd, Spurs na Chelsea zavuna matokeo mazuri kwenye nusu fainali ligi za vilabu bingwa ulaya.
Leo tumeangazia michuano ya klabu bingwa kufuzu fainali, riadha za Diamond League, Boston na London Marathon, Cameroon yafuzu Kombe la Dunia la U17, uchaguzi wa kamati ya Olimpiki nchini Kenya watibuka, Gor Mahia yanuia kujenga uwanja wao, uchambuzi wa debi ya El Clasico huku Carlos Alcaraz akijiondoa kwenye mashindano ya Madrid Open.
Jumamosi hii tunaangazia nusu fainali ya michuano ya klabu bingwa Afrika, waamuzi kutoka Kenya na DRC miongoni mwa waamuzi kusimamia michuano ya Kombe la Dunia la Vilabu Marekani mwaka huu, fainali wa Afcon U17, kwenye riadha Chepngetich na Jepchirchir wajiondoa kwenye London Marathon, mechi za kufuzu Kombe la Dunia la wasichana chini ya umri wa miaka 17 pamoja uchambuzi wa robo fainali tatanishi kwenye ligi za mabingwa ulaya wiki hii.
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa matokeo ya robo fainali mechi za klabu bingwa Afrika, Uganda yalenda kufuzu Kombe la Dunia wasiozidi miaka 17, timu ya taifa ya raga ya kina dada ya Kenya yalenga kurejea katika msururu wa dunia, michuano ya vilabu ya Afrika mchezo wa voliboli, Rwanda yaadhimisha miaka 31 michezoni tangu mauaji ya kimbari, Maluki atangaza nia ya kuwania urais wa Nock, Salah asaini kandarasi mpya Liverpool, Real Madrid itageuza meza dhidi ya Arsenal?
Leo kwenye kipindi tumeangazia mkondo wa kwanza robo fainali ya michuano ya klabu bingwa barani Afrika, matokeo ya Uganda na Tanzania kwenye michuano ya AFCON U17 huk Morocco, nafasi ya Shujaa 7s ya Kenya kusalia kwenye msururu wa raga duniani, mnyarwanda Celestine Nsanzuwera ashinda michuano ya gofu ya Sunshine Tour Afrika Mashariki, wachezaji watano wa ufaransa wa tenisi wapokea adhabu kwa makosa ya upangaji matokeo, Muller na De Bruyne kuondoka vilabuni mwao mwishoni mwa msimu huu.
Miongoni tuliyokuandalia ni pamoja na matokeo ya raga mkondo wa HongKong 7s, sakata la upangaji mchezaji dhidi ya golikipa wa Kenya Patrick Matasi, maandalizi ya debi ya Mashemeji, Misri yapewa haki za kuandaa AFCON U20 huku CAF ikiifungulia uwanja wa Benjamin Mkapa, tuzo nono kwa washindi wa Kombe la Dunia la vilabu, kocha wa Brazil atimuliwa naye Djokovic akikaribia kushinda taji lake la 100.
Mashindano ya dunia ya kukimbiza magari, Safari Rally yanaendelea nchini Kenya. Madereva mbalimbali kutoka duniani, wanakutana mjini Naivasha kwa ajili ya kutafuta ubingwa wa mwaka 2025.
Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na uchaguzi wa CAF, uwanja wa Mkapa wafungiwa kwa muda, michuano ya kufuzu dimba la dunia kwa kina dada chini ya umri wa miaka 17, maandalizi ya mashindano ya kuendesha magari ya WRC Safari Rally, uchambuzi wa mechi za klabu bingwa Ulaya hatua ya kumi na sita bora naye Neymar alazimika kuaga kikosi cha Brazil kufuatia jeraha
Tuliyokuandalia hii leo ni pâmoja na matokeo ya mashindano ya tenisi ya vijana barani Afrika chini ya miaka 14, kocha mpya wa Kenya ni nani, matokeo ya mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kina dada, timu sita kushiriki ligi ya Afrika ya basketboli kwa mara ya kwanza, huku Afrika Kusini ikijiandaa kutuma ombi rasmi la kuandaa mkondo mmoja wa F1 na Jose Mourinho apata afueni baada ya adhabu yake kupunguzwa.
Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na matokeo kwenye mashindano ya kimataifa ya gofu ya Magical Kenya Open, bondia wa DRC kupambana na muingereza huko Saudi Arabia, maandalizi ya Tour du Rwanda, Droo ya robo fainali michuano ya klabu bingwa Afrika, mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kina dada 2026 na basketboli ya 2025, halikadhalika Droo ya 16 bora mechi za klabu bingwa Ulaya na michuano ya raga ya Vancouver 7s.
Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na taarifa kuelekea mashindano ya gofu duniani ya Magical Kenya Open 2025, bodi ya Ligi ya soka nchini Tanzania yashusha rungu kwa Pamba Jiji na Ally Kamwe, timu 18 zimehakikisha kushiriki mashindano ya voliboli ya ukanda wa tano nchini Uganda, droo ya michuano ya Afcon U17 na U20, mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya kina dada 2026, Jannik Sinner akubali kufungiwa miezi mitatu, raundi ya mtoano mechi za klabu bingwa Ulaya.
Hii leo tumeangazia yaliyozungumziwa kwenye mkutano mkuu wa jinsia wa Afrika Mashariki jijini Nairobi, shirikisho la kimataifa la mchezo wa baiskeli yapinga madai kuwa Rwanda itapokonywa haki za kuandaa mashindano ya chipukizi ya dunia mwezi Septemba kufuatia mzozo unaoendelea DRC, uchambuzi wa droo ya AFCON 2025, maandalizi ya CHAN 2024 tarehe mpya zatajwa na uchaguzi wa CAF mwaka huu. Pia tumechabua hatua ya mchujo mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya na tetesi za uhamisho ulaya.
Jioni hii kwenye makala ya Jukwaa la Michezo tumeangazia Congo kufutiliwa kushiriki mashindano ya CHAN 2024, kufutwa kazi kwa kocha wa Rwanda Torsten Spittler, uwanja mpya wa Talanta jijini Nairobi unaendelea kupiga hatua kwenye ujenzi huku ligi ya Tanzania ikitajwa nafasi ya nne katika orodha ya ligi bora Afrika, Kenya yang'ara mashindano ya chipukizi ya tenisi, msururu wa raga ya dunia mkondo wa tatu, fainali za Australian Open na tetesi za uhamisho ulaya na Afrika.
Kipindi cha leo kimeangazia pakubwa droo ya mashindano ya CHAN 2024; adhari ya kuahirishwa kwa kipute na uchambuzi wa makundi. Pia tumetupia jicho raundi ya sita hatua ya makundi mechi za klabu bingwa Afrika, fainali ya mashindano mapya ya wasichana U17, Shujaa yataja kikosi chake cha mkondo wa Perth 7s, Kipchoge akilenga taji la tano la London Marathon, Tyson Fury astaafu ndondi kwa mara ya pili pamoja na mashindano ya tenisi ya Australian Open yakiingia hatua ya robo fainali. Kulingana na droo iliyofanyika Jumatano usiku katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Kenyatta (KICC) jijini Nairobi nchini Kenya, Harambee Stars imepangwa katika 'kundi la kifo' ambapo itamenyana na mabingwa mara mbili Morocco (2018 na 2020) na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (2009 na 2016)."Tuko kwenye kundi la kifo," Mariga alikiri, akibainisha uimara wa wapinzani wao."Hizo ni timu kubwa na inamaanisha lazima tuweke juhudi zaidi katika maandalizi."“Wapinzani wetu ni wagumu, tutashiriki mashindano haya kwa mara ya kwanza lakini haijalishi. Tuna wachezaji wazuri ambao wanaweza kutoa changamoto,” alijibu Kenneth Muguna, mmoja wa wachezaji muhimu katika kikosi cha sasa cha Harambee Stars.Pia katika Kundi A kuna Zambia na Angola. Kenya itakuwa mwenyeji wa mashindano haya yanayofanyika kila baada ya miaka miwili kwa wachezaji wa nyumbani pamoja na Tanzania na Uganda.Wenyeji wenza Tanzania wako katika Kundi B ambapo watamenyana na Madagascar, Mauritania, Burkina Faso na Jamhuri ya Afrika ya Kati.“Tusichukulie kundi hili kama jepesi, sisi kama wenyeji lazima tujitayarishe vyema ili tupite awamu ya makundi na hata kushinda kombe, “ alisema rais wa shirikisho la soka nchini Tanzania (TFF) Wallace Karia.Uganda wataongoza Kundi C ambapo watamenyana na Niger na nchi mbili ambazo zitatinga hatua ya mwisho ya mchujo. Mabingwa watetezi Senegal wataanzisha tena uhasama na Nigeria katika kundi D, ambayo pia ina Sudan na Kongo.“Tumecheza dhidi ya Guinea na Niger mara kadhaa, tunajua wanavyocheza. Tumefuzu mara ya nane mashindano haya, na hatujawahi kuaga mashindano kwenye makundi,” alieleza kwa msisimko Moses Magogo, rais wa shirikisho la soka (FUFA) nchini Uganda. Michuano hiyo yenye timu 19 ambayo awali ilipangwa kufanyika Februari 1 hadi 28, iliahirishwa hadi Agosti mwaka huu. Wasaidizi wa droo hiyo walikuwa wachezaji wa zamani - McDonald Mariga wa Kenya, Mrisho Ngasa wa Tanzania na Hassan Wasswa wa Uganda huku mkurugenzi wa mashindano wa CAF, Samson Adamu akisimamia mchakato wa droo.Katika ujumbe wake wa video kabla ya droo hiyo, rais wa CAF Patrice Motsepe alitoa shukrani zake kwa marais William Ruto (Kenya), Samia Suluhu Hassan (Tanzania) na Yoweri Museveni (Uganda) kwa ushirikiano wao kuhakikisha mashindano hayo yanafanyika kwa mafanikio."Ukarabati wa viwanja, viwanja vya kufanyia mazoezi, miundombinu, hoteli na hospitali katika nchi hizo tatu unaonyesha maendeleo makubwa na motisha, iliyodhihirika wakati wa ziara yangu," ujumbe wake Motsepe ulibainisha."Lengo lilikuwa kuunganisha mataifa matatu ya Afrika Mashariki, pamoja na mengine kutoka sehemu mbalimbali za Afrika."Waziri wa Michezo nchini Kenya Salim Mvurya alipamba hafla hiyo pamoja na wenzake kutoka Uganda na Tanzania, Peter Ogwang na profesa Palamagamba John Aidan Mwaluko.Droo KamiliKundi A: Kenya, Morocco, Angola, DR Kongo, ZambiaKundi B: Tanzania, Madagascar, Mauritania, Burkina Faso, Jamhuri ya Afrika ya KatiKundi C: Uganda, Niger, Guinea, Q2, Q1Kundi D: Senegal, Kongo, Sudan, Nigeria
Tuliyokuandalia jioni hii ni pamoja na uchambuzi wa mashindano ya Mapinduzi, tetesi za uhamisho Afrika Mashariki, raundi ya tano ya mechi za klabu bingwa Afrika, maandalizi ya CHAN 2024, uhamisho wa wachezaji ulaya na mashindano ya tenisi ya Australian Open.
Popote pale ulipo nikukaribishe katika Makala ya jukwaa la michezo ndani ya FRI Kiswahili.Leo tumekuandalia Makala spesheli ambayo inaangazia kushuka pakubwa kwa viwango vya mchezo wa masumbwi nchini Kenya, Makala ambayo tunayapeperusha wiki kadhaa tu baada ya kukamilika kwa michezo ya Olimpiki Jijini Paris nchini Ufaransa. Kwa mara ya kwanza katika, historia ya kenya, hakuna bondia hata mmoja aliyewakilisha taifa katika michezo ya olimpiki jijini Paris. Hatua hii ilizua ngumzo kwa wadau wa mchezo huo.Lakini, Iweje mchezo uliokuwa ukisifika na kuiletea Kenya hadhi katika miaka ya nyuma imedidimia kiasi hiki? Je, ni usimamizi mbaya ama ni ukosefu wa ligi dhabiti au ni kukosa wadhamini wa kuwekeza katika mchezo hili kuiletea fahari inayostahili. Je, Kuna uhasama kati ya wadau ama wasimamizi wameingiwa na kiburi na kujisahau na kuwasahau mabondia?Mwenzangu George Ajowi amezungumza na Mabondia wa zamani, marefa, makocha, mapromota, wanahabari na vile vile wadau wengeni katika sekta hii na kuzungumza nao kuhusiana na matatizo ya ndondi na suhulu ya kufufua mchezo huu katika siku za usoni.
Leo kwenye makala ya kwanza kabisa ya Jukwaa la Michezo mwaka 2025, tumeangazia raundi ya nne hatua ya makundi mechi za Ligi ya vilabu bingwa Afrika. Mwanariadha mkenya Beatrice Chebet avunja rekodi yake ya dunia huku raia wa Eritrea mwendesha baiskeli Biniam Girmay akishinda tuzo la Afrika wakati uo huo mashindano ya magari ya Dakar Rally na Kombe la Mapinduzi yaking'oa nanga. Lakini pia tutatupia jicho tetesi za uhamisho ulaya na michuano ya tenisi ya Brisbane Open inayoendelea.
Ikiwa Jumamosi ya mwisho ya mwaka 2024, tunakuuliza ni tukio gani au mashindano gani ya kispoti yalikufurahisha zaidi mwaka huu? Pamoja na hayo; tumeangazia kifo cha mchezaji nguli wa voliboli nchini Kenya Janet Wanja, Uganda yaibuka mabingwa wa CECAFA michuano ya kufuzu AFCON U17, raundi ya mwisho ya kufuzu michuano ya CHAN 2024, uchambuzi wa raundi ya 18 ya mechi za Ligi Kuu ya Soka nchini Uingereza.
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa ziara ya rais wa CAF Patrice Motsepe Afrika Mashariki kuukagua maandalizi ya CHAN 2024, tuzo za wanasoka bora Afrika na FIFA mwaka huu, pigano la ndondi kati ya Tyson Fury dhidi ya Oleksandr Usyk huku nduguye Paul Pogba, Mathias Pogba akipokea kifungo cha miaka mitatu jela kwa kujaribu kumlaghai Paul Pogba pesa.
Tulikuandalia ni pamoja na yaliyozungumziwa kwenye mkutano mkuu wa shirikisho la mchezo wa kuendesha magari duniani, FIA nchini Rwanda, uchambuzi wa raundi ya tatu ya mechi za ligi ya mabingwa Afrika, Pape Thiaw ateuliwa kuwa kocha mpya wa Senegal, Afrika Kusini yashinda Kombe la Afrika mchezo wa pete, uchambuzi wa mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya, Saudi Arabia ikithibitishwa kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia mwaka 2034
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchaguzi wa shirikisho la soka nchini Kenya FKF, raundi ya pili ya klabu bingwa Afrika na raga ya wachezaji saba kila upande duniani, fainali za kombe la mataifa ya Afrika mchezo wa handboli kwa kina dada, debi la Rwanda, mechi za kufuzu ligi ya Afrika basketboli mwaka ujao, droo ya makundi michuano ya klabu bingwa duniani mwaka ujao nchini Marekani mwaka 2026.
Tuliyokuandalia ni pamoja na mahojiano ya moja kwa moja na washikadau wa mchezo wa Tong IL Moo Do ambao walitutembelea studioni. Mchezo huu unazidi kukua Afrika. Je, unachezwaje, nini umuhimu wake, umepiga hatua kiasi gani, maandalizi ya makala ya Mombasa Open ya mwaka huu yakoje? Pia tumeangazia Ligi ya Klabu bingwa Afrika, msimu mpya wa raga ya HSBC duniani na Kombe la Mataifa ya Afrika ya kina dada mchezo wa handboli ambayo ilianza wiki hii pamoja na uchambuzi wa mechi za klabu bingwa Ulaya
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa droo ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kina dada 2024, fainali ya klabu bingwa Afrika kwa kina dada, nini maana ya Tanzania na Uganda kuwakilisha CECAFA kwenye AFCON 2024, mechi za kufuzu ligi ya Afrika ya Basketboli na michuano ya kufuzu Mashindano ya Afrika ya Basketboli, ligi za ukanda na ulaya Pep Guardiola atia saini mkataba mpya klabuni Man City.
Tuliyoyazungumzia ni pamoja na upekee wa klabu ya voliboli nchini Kenya ya Trailblazers, uchaguzi wa FKF nchini Kenya umeanza, mabadiliko ya makocha klabuni Yanga, timu ya taifa ya Kenya ya walemavu ya soka yamaliza nafasi ya nne Kombe la Dunia, uchambuzi wa michuano ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2025 na pigano la Jake Paul dhidi ya Mike Tyson
Tumeangazia klabu ya Chaux Sport kutoka DRC kubanduliwa kwenye mechi za kufuzu Ligi ya Basketboli Afrika 2024, masaibu ya Yanga SC nchini Tanzania, uchaguzi wa FKF nchini Kenya, mashindano ya kuendesha baiskeli Afrika kwa kina dada nchini Burundi, kifo cha rais wa soka nchini Algeria, matokeo na uchambuzi wa mechi za klabu bingwa Ulaya na fainali ya tenisi kwenye mashindano ya WTA
Tuliyokuandalia ni pamoja na bodi mpya ya uchaguzi wa shirikisho la soka nchini DRC, waziri wa michezo nchini Tanzania Damas Ndumbaro abainisha viwanja 20 kwa ajili ya AFCON 2027, timu ya REG nchini Rwanda yafuzu Ligi ya Basketboli Afrika 2024 kwa kina dada, mechi za kufuzu CHAN 2025, hatma ya kocha wa Rwanda Torsten Spittler, Senegal kuandaa michezo ya Olimpiki ya kwanza barani Afrika ya chipukizi mwaka 2026, kocha mpya wa Man Utd, mashindano ya Paris Masters na Brazilian GP
Tuliyokuandalia ni pamoja na taarifa ya Rais wa CAF Patrice Motsepe kuwania tena urais muhula wa pili, hukumu ya CAF katika mechi ya Nigeria dhidi ya Libya, yaliyotukia kwenye ziara ya rais wa Olimpiki ya kimataifa nchini Kenya na Kongamano la tatu la kibiashara la soka Afrika, uchambuzi wa michuano ya Kombe la Dunia la kina dada U17, Senegal ikihifadhi ubingwa wa Afrika soka ya ufukweni, michuano ya ndondi Afrika jijini Kinshasa, PSG kumlipa Mbappe €55M na uchambuzi wa El Clasico leo usiku.
Tuliyokuandalia ni pamoja na michuano ya kufuzu AFCON U20 mwaka ujao, namna timu za Afrika zilicheza kwenye wiki ya kwanza ya Kombe la Dunia la kina dada wasiozidi miaka 17, timu ambazo tayari zimefuzu AFCON ya 2025 nchini Morocco na nafasi ya timu za Afrika Mashariki na Kati, AFCON ya ufukweni yaanza leo nchini Misri, droo ya klabu bingwa Afrika kwa kina dada, mashindano ya magari ya Rwanda Mountain Gorilla Rally, kutimuliwa kwa kocha Kavazovich klabuni Vipers na Ligi za ukanda na Ulaya
Tuliyokuandalia ni pamoja na faniali za kufuzu mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wasiozidi miaka 20, uchambuzi wa vikosi vilivyotajwa na wakufunzi kuelekea raundi ya tatu ya kufuzu AFCON 2025, masaibu ya Samuel Eto'o na kocha wa Senegal Aliou Cisse kutemwa, kifo cha nyota wa basketboli Dikembe Mutombo pamoja na matokeo ya mechi za ligi ya mabingwa ulaya.
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa mechi ya Kombe la Super Cup Afrika, Kenya kuwa mwenyeji wa mashindano ya baiskeli Afrika kwa mara ya kwanza, matokeo ya riadha jijini New York, sura mpya za wanariadha watakaoshiriki Berlin Marathon hapo kesho, Ligi za ukanda kwenye soka, voliboli na basketboli lakini pia matokeo ya Kombe la Europa League raundi ya kwanza.
Tuliyokuandalia ni pamoja na taarifa ya ziara ya rais wa CAF Patrice Motsepe nchini Kenya, awamu ya pili kufuzu hatua ya makundi mechi za klabu bingwa Afrika, timu za Kenya za soka na mchezo wa Kabaddi tayari kushiriki Kombe la Dunia, timu za taifa Afrika Mashariki zimepanda kwenye msimamo wa dunia wa FIFA, uchambuzi wa raundi ya kwanza mechi za UEFA na mchezo wa ndondi kati ya Anthony Joshua na Daniel Dubois leo usiku.
Tuliyokuandalia hii leo ni mkusanyiko wa uchambuzi na matokeo ya mechi za kufuzu AFCON 2025, mechi za klabu bingwa Afrika kufuzu awamu ya makundi, washindi wa riadha za Diamond League, matokeo ya lLigi ya basketboli ya Afrika U18, droo ya AFCON U20 ukanda wa CECAFA, ligi za ukanda na ulaya pamoja na uchambuzi wa mechi za klabu bingwa Ulaya msimu mpya utakaoanza wiki ijayo
Tuliyokuandalia ni pamoja na matokeo na uchambuzi wa mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika 2025, kifo cha mwanariadha wa Uganda nchini Kenya, matokeo ya Zurich Diamond League, matokeo ya U18 Afrobasket na Congo Cup, uchambuzi wa matokeo ya mataifa ya Afrika kwenye Olimpiki ya walemavu jijini Paris, mechi za Ligi ya Mataifa ya Ulaya na tuzo za Ballon D'Or mwaka 2024
Tuliyokuandalia ni pamoja na michuano ya kufuzu klabu bingwa kwa kina dada, uchambuzi wa vikosi vya timu za Afrika Mashariki na kati kuelekea mechi za kufuzu AFCON 2025, matokeo ya riadha ya Rome Diamond League na riadha za dunia U20, mashindano ya Tong IL Moo Do Mombasa Open kufutiliwa mbali, matokeo ya Olimpiki ya walemavu na uhamisho wa wachezaji ulaya.
Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na uchambuzi wa mechi za kufuzu klabu bingwa Afrika, riadha za Diamond League, FIBA Afrobasket kwa kina dada, hatma ya mashindano ya Mombasa Open Tong IL Moo Do mwaka huu, unachostahili kujua kuhusu Olimpiki ya walemavu inayoanza wiki ijayo jijini Paris huku kiungo Ilkay Gundogan akirejea klabuni Man City.
Jumamosi hii tumezungumzia namna wanariadha wa Afrika walivyopokelewa na mataifa yao kutoka Olimpiki ya Paris, michuano ya klabu bingwa Afrika imeanza kusaka tiketi ya hatua ya makundi, uhamisho tata wa wachezaji wa soka nchini Kenya huku ligi za Afrika Mashariki na Ulaya zikianza kurejea, Mbappe ashinda taji la kwanza Real Madrid, Pochettino kuwa kocha wa Marekani
Tuliyokuandalia Jumamosi hii kutoka taasisi ya Alliance Francaise, ni pamoja na uchambuzi wa matokeo ya marathon, riadha na mashindano mengine ya Olimpiki ya Paris yaliyotukia wiki hii. Pia tunaangazia fainali kubwa zinazosubiriwa jioni ya leo na kesho asubuhi kwenye marathon ya kina dada lakini pia kifo cha aliyekuwa rais wa tano wa shirikisho la soka Afrika CAF, Issa Hayattou.
Tuliyokuandalia ni pamoja na matokeo ya Olimpiki hapo jana raia wa St Lucia Julien Alfred akishindia taifa lake medali ya kwanza ya Olimpiki, Sudan Kusini yaaga mashindano ya basketboli kibingwa, uchambuzi wa wanariadha wa Afrika Mashariki wanaotarajiwa kushiriki nusu fainali na fainali kadhaa leo usiku na kesho, uchambuzi wa mechi za nusu fainali ya soka lakini pia kwenye mjadala tunazungumzia kashfa ya jinsia ya mabondia Angela Carini na Imane Khelif
Joshua Cheptegei ashinda medali ya dhahabu kwenye mbio za mita 10,000 huku Malkia Strikers ikibanduliwa mashindanoni. Morocco na Misri zafuzu nusu fainali huku waafrika kwenye uogeleaji wakifanya vibaya. Pia tutakufahamisha matokeo ya judo, basketboli, kuendesha basikeli na jedwali la medali ambapo Uchina inazidi kuongoza jedwali hilo
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa matokeo ya Olimpiki na mjadala kuhusu wanariadha wanaotarajiwa kung'ara kwenye Olimpiki wiki ijayo riadha zitakapoanza pamoja na matokeo ya Toyota Cup Yanga ikiilaza Kaizer Chiefs huku George Russel akishinda mkondo wa Belgian GP kwenye mashindano ya langalanga.
Tuliyokuandalia ni pamoja na mambo muhimu unahitaji kujua kuhusu Olimpiki ya mwaka huu kabla ya kuanza, uchambuzi wa fainali ya CECAFA Kagame Cup kati ya APR ya Rwanda na Red Arrows ya Zambia, tetesi za uhamisho Afrika Mashariki n aUlaya pamoja na matokeo ya Tour de France ikielekea ukingoni huku kocha wa Uingereza Gareth Southgate akijiuzulu kuifunza timu ya taifa ya wanaume.
Tuliyokuandalia ni pamoja na droo ya hatua ya awali kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika msimu ujao, matokeo ya Monaco Diamond League, Team Kenya yaanza kuwasili Ufaransa tayari kwa Olimpiki, matokeo ya CECAFA Kagame Cup na tetes iza uhamisho pamoja na uchambuzi wa fainali ya EURO, Copa America na fainali za tenisi kwenye Wimbledon.
Miongoni mwa yale tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa droo ya mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya mwaka 2025, fainali ya Cosafa Cup, mipango ya Team Kenya kuelekea Olimpiki ya mwaka huu, uchambuzi wa mechi za robo fainali michuano ya Euro na Copa America, raia wa Eritrea Girmay Hailu Biniam ashinda hatua ya nane ya Tour de France wakati kocha wa Manchester United Erik ten Hag aongeza mkataba wake.
Tumekuandalia mengi ikiwemo matokeo na uchambuzi wa mashindano ya COSAFA Cup inayoendelea nchini Afrika Kusini, Leopards voliboli ya ufukweni yafuzu Kombe la Dunia wakati Kinshasa yajiandaa kuandaa mechi za kufuzu kombe la mataifa ya Afrika mchezo wa basketboli ya kutumia viti vya magurudumu, Kenya yateua kikosi kitakachoshiriki riadha za dunia U20 nchini Peru, tetesi za uhamisho katika vilabu vya Afrika Mashariki, Kenya Police yafuzu kombe la shirikisho barani Afrika msimu ujao. Tour de France yaanza leo nchini Italia kabla ya kurejea Ufaransa huku michuano ya EURO na Copa America ikiingia hatua za mtoano.
Tuliyokuandalia ni pamoja na matokeo ya riadha za Afrika nchini Cameroon, matokeo ya tenisi ya Davis Cup nchini Angola, bondia wa DRC Christophe Mputu ashinda medali ya 70, watu 13 wapigwa marufuku nchini Uganda kwa visa vya upangaji mechi, Ons Jabeur na Aryna Sabalenka kukosa Olimpiki kuzingatia afya yao.
Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na mchujo wa kitaifa wa Kenya kuteua timu itakayowakilisha kwenye Olimpiki ya Paris mwaka huu, Kenya yakosa kupandishwa daraja kwenye tenisi mashindano ya Billie Jean King Cup, uwanja wa Amahoro nchini Rwanda umeidhinishwa na FIFA kuandaa mechi za kimataifa, Junior Starlets ipo guu moja kufuzu Kombe la Dunia, droo ya kufuzu AFCON 2025 kuandaliwa Julai na michuano ya EURO kuanza Ujerumani.
Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na uchambuzi wa mechi za kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2026 (Afrika), Kenya kuandaa mashindano ya mchujo kutafuta timu itakayowakilisha katika Olimpîki ya Paris mwezi Julai huku wanamichezo 33 wakipigwa na marufuku kwa kutumia dawa za kusisimua misuli, matokeo ya Congo Cup, kocha Gamondi arefusha mkataba wake klabuni Yanga huku zikiwa zimesalia siku sita kabla ya mashindano ya EURO nchini Ujerumani, Iga Swiatek ashinda ubingwa wake wa nne wa French Open
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa fainali ya Ligi ya Basketboli Afrika mwaka huu, matokeo ya Diamond League mkondo wa Oslo na mchujo wa raga duniani, uchambuzi wa vikosi vya Afrika Mashariki na Kati kuelekea mechi za kufuzu Kombe la Dunia la mwaka 2026, uchambuzi wa Fainali ya Klabu bingwa Ulaya (Dortmund dhidi ya Real Madrid) na matokeo ya French Open huku Ronaldo akitokwa na machozi baada ya kupoteza fainali ya Saudi Kings Cup
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa fainali ya Klabu bingwa Afrika, Tanzania waibuka na kombe la shule za upili afrika mchezo wa soka, fainali za ligi ya basketboli kuanza nchini Rwanda wakati makocha wa Kenya na Uganda wataja vikosi vyao kufuzu Kombe la Dunia na matokeo ya Ligi za ulaya.
Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa fainali ya Klabu Bingwa Afrika mwaka 2024, Zanzibar kuandaa fainali za mashindano ya shule za upili barani Afrika, Mkusanyiko wa michezo kwenye ukanda wa Afrika Mashariki, Maniema yarejea kwenye mashindano ya vilabu barani Afrika, uchambuzi wa mbio za kuwania taji la Uingereza kati ya Man City na Arsenal, Ngolo Kante arejea kikosini mwa Ufaransa, Brazil yateuliwa kuandaa Kombe la Dunia la kina dada la mwaka 2027.
Tuliyokuandalia hii leo ni pamoja na matokeo ya riadha kwenye Doha Diamond League, AFCON UAE kuanza hapo kesho huko Dubai, michuano ya Congo Cup, uchambuzi wa mechi za Ligi ya Basketboli ya Afrika, Guinea yafuzu fainali za Olimpiki kwenye soka, mechi za kufuzu Kombe la Dunia la U17 kwa kina dada, Mbappe atangaza rasmi kuondoka PSG na uchambuzi wa fainali za mwaka huu za michuano ya bara Ulaya.