Podcasts about huko

  • 29PODCASTS
  • 152EPISODES
  • 20mAVG DURATION
  • 1EPISODE EVERY OTHER WEEK
  • May 7, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about huko

Latest podcast episodes about huko

Habari za UN
07 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 7, 2025 10:54


Hii leo jaridani tunaangazia mvutano unaoendelea barani Asia kati ya majirani wawili India na Pakistani, na msaada wa mguu bandia uliowezesha mtototo nchini Kenya kwenda shule. Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani tunakwenda katika ukanda wa Gaza.Huko barani Asia majirani wawili India na Pakistani wameendelea kuoneshana mvutano kati yao kwenye eneo la Jammu na Kashmiri tangu tarehe 22 mwezi uliopita wa Aprili baada ya shambulizi huko Pahalgam. Katibu Mkuu ametoa wito kwa mara nyingine tena.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na wadau wameleta neema kwa watoto wanaoishi na ulemavu katika Kaunti ya Kisumu Magharibi mwa Kenya baada ya kuwapa msaada wa vifaa ikiwemo viti mwendo na viungo bandia kupitia mradi wa ubunifu kwa ajili ya watoto wenye ulemavu, msaada uliobadili maisha yao.Makala katika wiki ya chanjo duniani, iliyotamatishwa tarehe 30 wiki iliyopita, mtaa wa Butiama, ulioko Mtoni Kijichi katika wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam, nchini Tanzania ulishuhudia wazazi na walezi wakijitokeza kuwapatia watoto wao chanjo muhimu za kuwalinda dhidi ya maradhi hatari. Miongoni mwao ni Hija Halfani ambaye alimpeleka mtoto wake mwenye umri wa siku 42 kupata chanjo yake ya kwanza.”Na mashinani mashinani, kama sehemu ya juhudi za kutoa nafasi ya kujieleza kisanii na kuwaunga mkono Wapalestina kihisia (emotional support), UNRWA imeandaa maonesho ya sanaa katika Shule ya Al-Rimal, ambayo sasa ni makazi ya wakimbizi wa ndani katika ukanda wa Gaza, na watoto walipata fursa ya kuonesha kazi za sanaa zinazoakisi(reflect) madhila wanayopitia wakati wa vita kati ya Israeli na Hamas ambavyo bado vinaendelea. Malak Fayad, msichana mkimbizi kutoka Beit Hanoun ni mmoja wao akionesha sanaa yake.….Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Operesheni za kijeshi Jammu na Kashmir hazina tija – Guterres

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 7, 2025 2:07


Huko barani Asia majirani wawili India na Pakistani wameendelea kuoneshana mvutano kati yao kwenye eneo la Jammu na Kashmiri tangu tarehe 22 mwezi uliopita wa Aprili baada ya shambulizi huko Pahalgam. Katibu Mkuu  wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito kama anavyoelezea Assumpta Massoi.

Habari za UN
Kampuni Indonesia zachukua hatua kuimarisha usalama na afya pahala pa kazi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 28, 2025 3:32


Huko mashariki mwa Indonesia, kampuni za usindikaji samaki za PT Chen Woo Fisheries na PT Harta Samudra zimeongeza motisha wa kazi miongoni mwa wafanyakazi wake baada ya kuchukua hatua za kuimarisha usalama na afya pahala pa kazi. Hatua hizo ambazo zimeweka mazingira ya staha pahala pa kazi zinafuatia mradi wa pamoja wa shirika la Umoja wa Mataifa la kazi, ILO na Umoja wa Kampuni za Uvuvi na Usindikaji Samaki nchini Indonesia, AP2H1. Je nini kilifanyika na hali sasa iko vipi? Assumpta Massoi anafafanua zaidi katika makala hii inayoletwa leo hii ikiwa ni siku ya kimataifa ya usalama na afya pahala pa kazi.

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Mazishi ya papa Francis huko vatican, DRC na Rwanda zakubaliana kuelekea amani

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Apr 26, 2025 20:16


Makala ya yaliyojiri wiki hii imeangazia mazishi ya kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis, DRC na Rwanda zatia saini makubaliano kuhusu njia ya kupatikana amani ya mashariki mwa Congo, siasa za Tanzania kuelekea uchaguzi wa oktoba, ziara ya rais wa Kenya William Ruto huko China, hali ya vita ya Sudan, vita ya Ukraine na huko Gaza Israeli, ni miongoni mwa Habari kuu za dunia zilizojiri kwa juma hili.

Habari za UN
22 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 22, 2025 9:56


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo inatupeleka Msasani nchini Tanzania kusikia namna vijana na serikali wanavyolinda Mama Dunia. Pia tunakuletea muhtasari wa habari ujumbe wa Katibu Mkuu, watoto kulinda mazingira DRC, na kifo cha Papa Francis.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya Mama Dunia, ikilenga kuchagiza hatua ya kuhifadhi sayari dunia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametumia neno ‘homa' kuwa inakumba dunia hivi sasa kutokana na viwango vya joto vinavyoongezeka kila mwaka. Hata hivyo amesema majawabu ya kutibu homa hiyo yapo ikiwemo kutumia nishati rejelezi ambayo ni rahisi, ina afya na salama kuliko nishati kisukuku.Huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kando ya mapigano yanayotikisa eneo la mashariki mwa nchi, watoto wamechukua hatua kulinda sayari dunia kwa kuhifadhi misitu kwenye taifa hilo ambako ukataji miti kiholela umefurutu ada.Kufuatia kifo cha Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis hapo jana Jumatatu, ambaye maziko yake yamepangwa kufanyika Jumamosi wiki hii, mashirika ya Umoja wa Mataifa yameendelea kukumbuka mchango wake wa kutetea walio taabuni. Mathalani shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR limekumbuka wito wake wa kutaka kila mtu kukaribisha, kusindikiza na kujumuisha wale wote wanaobisha hodi kwenye milango yao.Na mashinani  kupitia video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO fursa ni yake Meena Poudel kutoka nchini Nepal, Kusini mwa Asia ambaye ni Katibu wa kikundi cha wanawake watumiaji wa msitu ambacho kinabadilisha takataka za misitu kuwa mbolea rafiki kwa mazingira huku pia wakijipatia kipato."Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Stadi za kuoka mikate zaleta furaha kwa mkimbizi Thérèse huko Beni nchini DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 2, 2025 1:52


Jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Thérèse Kavira, mwanamke shupavu aliyelazimika kukimbilia mji wa Beni baada ya waasi kuvamia kijiji chake sasa ameona nusu kwenye maisha yake kufuatia mafunzo ya kuoka mikate yaliyotolewa na ofisi ya Utafiti na Usaidizi kwa Mahusiano ya Kimataifa nchini humo pamoja na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO na sasa anajikimu kimaisha. Sharon jebichii na taarifa zaidi.

Jioni - Voice of America
Watu 11 wamefariki na wengine zaidi ya 70 wamejeruhiwa kufuatia milipuko miwili katika eneo la Bukavu huko mashariki mwa DRC. - Februari 27, 2025

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 27, 2025 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
Afisa wa polisi nchini Kenya aliyepelekwa Haiti kama sehemu ya kikosi cha usalama chini ya Umoja wa Mataifa ameuawa akiwa kazini huko Haiti - Februari 24, 2025

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 24, 2025 29:58


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Habari za UN
Doria za pamoja za MONUSCO na FARDC huko Ituri DRC zaimarisha usalama

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 14, 2025 1:58


Katika kitongoji cha Komanda jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, doria za pamoja zinazoendeshwa na walinda amani wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO na jeshi la serikali FARDC zimeimarisha usalama kwenye maeneo ya raia. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

VOA Express - Voice of America
Super Bowl ya 59 Marekani itachezwa Februari tisa na mafahari wawili wa timu ya Kansas City Chiefs na Philadelphia Eagles huko New Orleans. - Februari 07, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 7, 2025 29:59


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Habari za UN
Maandamano huko Goma DRC, wakimbizi waomba UN iwafikishie misaada

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 3, 2025 3:44


Ikiwa ni wiki moja sasa tangu waasi wa M23 watangaze kutwaa Goma, jimboni Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, na kisha serikali kutangaza Beni kuwa mji mkuu wa sasa wa jimbo hilo, hii leo Jumatatu Februari 3, maandamano makubwa ya amani yamefanyika mjini Beni, yakiongozwa na mashirika ya kiraia na wananchi. Taarifa zaidi na Assumpta Massoi

Jioni - Voice of America
Milio ya risasi inaendelea kurindima katika mji wa Goma huko mashariki mwa DRC kufuatia mapigano ya waasi wa M23 na wanajeshi wa serikali. - Januari 28, 2025

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 28, 2025 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

VOA Express - Voice of America
Vijana huko mashariki mwa DRC wanaelezea hali ya mapigano katika eneo na namna inavyoathiri shughuli zao za kila siku za kuleta maendeleo. - Januari 28, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 28, 2025 29:58


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Jioni - Voice of America
Jeshi la Sudan na wanamgambo wa RSF wanashutumiana kila mmoja kwa kushambulia kiwanda cha kusafisha mafuta Khartoum huko Al-Jaili. - Januari 23, 2025

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 23, 2025 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Israeli na wapiganaji wa Hamas wakubaliana kusitisha vita huko Gaza

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Jan 18, 2025 20:12


Miongoni mwa yale tumekuandalia wiki hii ni pamoja na kuapishwa kwa Rais Mteule wa Marekani Donald Trump, mapigano yanyoendelea kuripotiwa mashariki ya DRC, makubaliano ya kusitishwa kwa vita kati ya Hamas na Israeli.

Jioni - Voice of America
Watu zaidi ya 27 wamefariki na wengine wametekwa na watu wanaodhaniwa kutoka kundi la ADF huko mashariki mwa DRC. - Januari 16, 2025

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 16, 2025 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
Zaidi ya watu laki moja wamekimbia katika siku tano za mapigano huko mashariki mwa DRC, kati ya vikosi vya serikali na waasi wa M23. - Januari 10, 2025

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 10, 2025 59:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Alfajiri - Voice of America
Moto mkali wa msituni waua watu watano na kuteketeza nyumba nyingi huko Los Angeles California - Januari 09, 2025

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 9, 2025 29:59


Jukwaa la Michezo
Mashindano ya magari ya Dakar Rally 2025 yang'oa nanga huko Saudi Arabia

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Jan 4, 2025 23:57


Leo kwenye makala ya kwanza kabisa ya Jukwaa la Michezo mwaka 2025, tumeangazia raundi ya nne hatua ya makundi mechi za Ligi ya vilabu bingwa Afrika. Mwanariadha mkenya Beatrice Chebet avunja rekodi yake ya dunia huku raia wa Eritrea mwendesha baiskeli Biniam Girmay akishinda tuzo la Afrika wakati uo huo mashindano ya magari ya Dakar Rally na Kombe la Mapinduzi yaking'oa nanga. Lakini pia tutatupia jicho tetesi za uhamisho ulaya na michuano ya tenisi ya Brisbane Open inayoendelea.

VOA Express - Voice of America
Mmoja wa wazazi huko Tanzania anatoa maoni yake kufuatia tabia ya baadhi ya wazazi kuwaacha watoto peke yao majumbani au maeneo ya michezo. - Desemba 26, 2024

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 26, 2024 29:59


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Jioni - Voice of America
Kimbunga Chido kimesababisha vifo vya watu 73 nchini Msumbiji, imesema Taasisi ya Kitaifa ya Usimamizi wa Hatari na Maafa huko Msumbiji - Desemba 19, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 19, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Ziara ya rais Joe Biden huko Angola, watano wahukumiwa kifo huko DRC

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Dec 7, 2024 20:18


Habari kuu wiki hii ni pamoja na mkutano kati ya rais wa Marekani anayejiandaa kuondoka madarakani Joe Biden na viongozi wa Afrika huko Lobito Angola, mazungumzo ya amani ya Sudan Kusini kuanza tena baada ya miezi minne, maafisa 20 wa Kenya waliopelekwa Haiti wajiuzulu, rais wa DRC Felix Tshisekedi kukutana na rais wa Rwanda Paul Kagame desemba 15, yaliyojiri Sudan uchaguzi nchini Ghana, na wabunge wa Ufaransa walivyoiangusha serikali ya Michel Barnier lakini pia kanisa kubwa la Notre Dame lafunguliwa jijini Paris Ufaransa, Israel yaendeleza mashambulizi Gaza 

Jioni - Voice of America
Mapigano makali yaendelea kati ya waasi wa M23 na jeshi la Congo huko Lubero - Desemba 04, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 4, 2024 30:00


Habari za UN
Mafunzo ya walinda amani kutoka Tanzania huko Beni yajengea uwezo walimu kusaidiana na watoto

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 2:25


Umoja wa Mataifa unasema kwamba vita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC imefanya taifa hilo kuwa pahala hatari zaidi duniani kwa watoto kuishi, kutokana na mateso ya kimwili na kisaikolojia wanayoyapitia. Kwa kutambua hilo walinda amani wanawake wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye ujumbe wa UN nchini humo, MONUSCO wamechukua hatua kuona watoto wanaishi kama watoto. Video ya MONUSCO ikianza na walinda amani wakijongea kwa jamii, Kapteni Noella Nyaisanga kiongozi wa kikundi hicho cha wanawake cha kikosi cha 11 cha walinda amani wa Tanzania kwenye MONUSCO, TANZBATT-11 anaeleza jinsi kikundi chao kinavyosogea kwa jamii na hasa watoto ili kutatua changamoto zinazowakabili kutokana na mapigano kati ya jeshi la serikali na waasi kwenye eneo hili la Beni, jimboni Kivu Kaskazini, mashariki mwa DRC. Anafafanua zaidi lengo lao.Lengo ni kujenga uaminifu kwa raia ambao tunawalinda. Kwa hiyo tukaamua kuandaa masomo shuleni, ambayo yataweza kuwaimarisha wao, kuwasaidia tatizo la kuwa wameathirika kisaikolojia.Zavadi Mbambu ni miongoni mwa walimu waliopatiwa mafunzo ya kusaidia watoto walioathiriwa na changamoto lukuki ikiwemo mapigano. Akisema stress, anamaanisha msongo.“Unakuwa na wanafunzi wanaokuwa na msongo wa mawazo kutokana na jambo ambalo wanaishi, na hata mauaji. Kuna wale ambao hata wameua wazazi wao , hata familia yao yote.  Na kwa hao wanafunzi wanapoingia shuleni , wanakuwa kama hawako ndani, fikra zao zinakuwa mbali .  Lakini kupitia mafunzo nimewaelewa , na tumejua namna gani ya kuishi nao. Na tayari mabadiliko yameanza kuonekana.”Pacifique Kyakimwa, mmoja wa wanafunzi anasimulia mkasa mmoja.“Kuna mwenzetu  aliyekuwa na tatizo, yaani tukiwa ndani ya shule, alikuwa anacheka, yaani anatusumbua hadi hatumwelewi mwalimu. Lakini tangu wameanza kufundisha hili somo, wameanza kuelewa . Ameanza kuwa na akili inayotumika vizuri. Mafunzo haya yamefika wakati tunahitaji , na imetusaidia sana.”

Kwa Undani - Voice of America
Meza ya waandishi inamulika kuanguka kwa jengo huko Kariakoo nchini Tanzania, na kukamatwa Kizza Besigye kiongozi wa upinzani huko Uganda. - Novemba 22, 2024

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 29:59


Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.

VOA Express - Voice of America
Vijana na mashabiki wa muziki wanaelezea walivyoguswa na kifo cha King Kiki, gwiji wa muziki wa Rumba huko Tanzania na Afrika Mashariki. - Novemba 15, 2024

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 15, 2024 29:59


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Habari za UN
Simulizi ya Ombeni baada ya kutoroka waasi na kurejea uraiani huko DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 6, 2024 2:04


Harakati za ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC za kunasua watoto na vijana wanaotumikishwa vitani zinaendelea na tukio la hivi karibuni zaidi ni la kijana.Katika video ya MONUSCO iliyochapishwa kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, Ombeni anasimulia jinsi waasi wa FDLR mashariki mwa DRC walivyowakamata msituni."Tulikuwa vijana watanoFDLR walitukamata na kutupeleka msituni. Maisha ilikuwa ngumu sana na hatukuweza kutoroka"Kazi wanatumikishwa bila mshahara na zaidi ya yote."Kila saa ni mateso, kazi mingi bila malipo."Alitumikishwa msituni kwa miaka minane, akionesha makovu ya vipigo alivyopatiwa."Tuliteseka sana, tulitumikishwa kwa muda wa miaka minane, tukachapwa viboko, tuliumizwa sana na kubaki na majeraha"Lakini siku moj aliweza kutoroka. Akiwa Kibirizi akamweleza mkubwa wake ya kwamba.." Siku moja nikamwambia mkubwa wangu naenda kusalamia rafiki yangu, wakati huo tukapata nafasi ya kutoroka."Katika harakati hizo akakutana na MONUSCO. Anasema kwamba, "Njiani nikakutana na wanajeshi wa MONUSCO, nikainua bunduki juu na kujisalimisha, nikisindikizwa na mkubwa wao nikaeleza kile tulichopitia"Sasa Ombeni anashiriki programu za kumjumuisha tena kwenye jamii, DDR-S inayondeshwa na MONUSCO huko Beni, jimboni Kivu Kaskazini.

Habari za UN
Walinda amani wa UN kutoka Tanzania wasaidia watoto yatima huko Beni, DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 4, 2024 3:16


Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mapigano kati ya jeshi la serikali, FARDC na vikundi vilivyojihami, yamesababisha vifo na hata watu kufurushwa makwao. Watoto wamesalia yatima na hawana walezi. Vituo vya kulea watoto yatima vimebeba jukumu la kuwatunza, lakini navyo viko taabani. Walinda amani wa Umoja wa Mataifa, kutoka Tanzania, TANZBATT-11 wanaohudumu katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO waliguswa na kuamua kujiongeza na kuwasilisha msaada kwa watoto hao. Afisa Habari wa TANZBATT-11 Kapteni Fadhillah Nayopa anasimulia kile walichofanya.

Alfajiri - Voice of America
Israel inawataka wanajeshi wa Umoja wa Mataifa kuondoka katika maeneo ya vita huko Lebanon - Oktoba 14, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Oct 14, 2024 29:58


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Wimbi la Siasa
Maadhimisho ya mwaka mmoja wa shambulio la Hamas huko Gaza Oktoba 7 2024

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Oct 9, 2024 10:16


Makala wimbi la siasa inaangazia maadhimisho ya kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kundi la Hamas, litekeleze shambulio baya zaidi kuwahi kutekelezwa huko Israeli, tukio ambalo lilianzisha vita ambayo imesababisha vifo kwa maelfu ya raia wa Kipalestina na maandamano duniani kote kupinga vita hiyo, wakati huu mzozo huo ukihofiwa kuenea katika mashariki ya kati. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka na waalikwa wake

Radio Maria Tanzania
Je, Kanisa linawatambuaje watoto waliouwawa na Herode huko Bethlehem?

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Oct 8, 2024 25:50


Karibu katika kipindi cha Maswali yahusuyo Imani ukiwa nami Frateri  Daudi Fungameza,  kutoka Seminari kuu ya Mtakatifu Augustino Peramiho  Jimbo  Kuu la Songea  nikijibu swali la Msikilizaji linalosema, Naomba kueleweshwa juu ya watoto waliouwawa na Herode huko Bethrehemu badala ya Yesu Je, Kanisa linawatambuaje watoto hao? L'articolo Je, Kanisa linawatambuaje watoto waliouwawa na Herode huko Bethlehem? proviene da Radio Maria.

Jioni - Voice of America
Israel imesema imepata miili ya mateka sita huko Gaza akiwemo raia mmoja wa Marekani mwenye asili ya Israel. - Septemba 01, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Sep 1, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Habari za UN
MONUSCO yachukua hatua kudhibiti waasi wa CODECO huko Ituri, DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 30, 2024 1:47


Afya ya mlinda amani wa Umoja wa Mataifa aliyejeruhiwa katika shambulizi lilitekelezwa na kundi la waasi, CODECO juzi Agosti 28 huko Bali, kaskazini mashariki mwa Djugu jimboni Ituri, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) inaendelea vizuri. Anold Kayanda na maelezo zaidi. Stéphane Dujarric, Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, amewaeleza waandishi wa habari jana Agosti 29 katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani kuhusu tukio hilo la kushambuliwa kwa walinda amani wa Umoja wa Mataifa wakiwa katika shughuli zao za kuwahakikishia usalama raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.“Walinda amani walizuia shambulio hilo, na kuwalazimisha wanamgambo kuondoka. Hata hivyo, tunasikitika kuripoti kwamba mlinda amani mmoja alijeruhiwa.” Anaeleza Dujarric lakini akiwaondolea wasiwasi waandishi waliokuwa wakimsikiliza kwamba mlinda amani huyo aliyejeruhiwa sasa yuko katika hali nzuri.Licha ya kushambuliwa, walinda amani wanaohudumu nchini DRC katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO wameendelea na shughuli za ulinzi si tu kaskazini mashariki mwa Djugu, bali pia kusini mashariki mwa eneo hilo jimboni Ituri ambako CODECO wameweka kambi katika maeneo mawili. Msemaji wa Katibu Mkuu anaeleza kwamba walinda amani walifanikiwa kusaidia raia wa kawaida kuweza kutoka eneo moja kwenda jingine.Mashambulizi haya yanatokea ikiwa imesalia miezi michache kufika Desemba 31 mwaka huu ambayo ni tarehe iliyoridhiwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwamba uwe mwisho wa MONUSCO kutokana na ombi la serikali ya DRC lilioomba MONUSCO iondoke katika nchi hiyo iliyogubikwa na vita kwa miaka mingi.  

Alfajiri - Voice of America
Blinken ziarani nchini Israel kushinikiza sitisho la mapigano huko Gaza - Agosti 19, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Aug 19, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Jioni - Voice of America
Wapatanishi wa kimataifa wanafanya mazungumzo huko Qatar yenye lengo la makubaliano ya kusitisha mapigano Gaza - Agosti 15, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Aug 15, 2024 30:00


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
Taliban nchini Afghanistan wanaukaribisha mwaliko wa Umoja wa Mataifa katika mkutano wa kimataifa huko Qatar baadaye mwezi huu. - Juni 24, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Jun 24, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Alfajiri - Voice of America
Rais Biden amekutana White House na Rais Ruto wa Kenya kwa ziara ya kitaifa wakati Kenya ikijiandaa kupeleka askari wake 1,000 huko Haiti. - Mei 23, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later May 23, 2024 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Alfajiri - Voice of America
Rais Biden ametoa amri ya kuzuia kampuni ya madini ya Cryptocurrenvy inayoungwa mkono na China kumiliki ardhi huko Wyoming. - Mei 14, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later May 14, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Jioni - Voice of America
Qatar inawasihi Israel na Hamas kuonyesha kujitolea na umakini mkubwa katika mashauriano ya kusitisha mapigano huko Gaza. - Aprili 28, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Apr 28, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
Watu zaidi ya milioni 8.4 huko Sudan wakiwemo watoto milioni mbili walio chini ya miaka mitano wako ukingoni mwa baa la njaa; inasema MSF. - Aprili 14, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Apr 14, 2024 30:00


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
Mashirika ya misaada ya UN yanaiomba jumuiya ya kimataifa kukumbuka madhila ya mamilioni ya watu ambao wanaendelea kuteseka huko Syria - Machi 16, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 16, 2024 30:00


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Alfajiri - Voice of America
Mafuriko huko katikati mwa Congo yamesababisha vifo vya watu 22 wakiwemo watu 10 kutoka familia moja. - Desemba 27, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 27, 2023 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Alfajiri - Voice of America
Mvua kubwa imesababisha maporomoko ya ardhi huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na kupelekea vifo na uharibifu wa mali - Desemba 26, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 26, 2023 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

congo mali jamhuri huko mashariki desemba
Alfajiri - Voice of America
Jeshi la Israel linasema wanajeshi wake 10 waliuawa katika mapigano huko Ukanda wa Gaza wakati wa kampeni ya kuwaondoa wanamgambo wa Hamas - Desemba 14, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 14, 2023 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Alfajiri - Voice of America
Mamlaka nchini Nigeria inasema shambulizi la anga la kijeshi lililowalenga magaidi huko Kaduna limepiga na kuwauwa raia - Desemba 05, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 5, 2023 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Alfajiri - Voice of America
Afisa mmoja katika chama cha upinzani nchini DRC ameuawa wakati wa mapigano kati ya makundi hasimu ya kisiasa huko mashariki mwa Congo - Novemba 29, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 29, 2023 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Alfajiri - Voice of America
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameshinikiza siku ya Jumatatu juu ya usitishaji kamili wa mapigano huko Gaza - Novemba 28, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 28, 2023 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Alfajiri - Voice of America
Wanamgambo wa Hamas wamewaachilia mateka wengine 17 waliokuwa wakishikiliwa huko Gaza akiwemo binti wa miaka minne - Novemba 27, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 27, 2023 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Feelin Good Podcast
Episode 275 Huko Clothing Mini Talk - Drip Fest Flint Mi

Feelin Good Podcast

Play Episode Listen Later Sep 16, 2023 2:28


Feelin Good Podcast
Episode 186 Huko Clothing Mini Talk at Tri City Vintage FLUM Market

Feelin Good Podcast

Play Episode Listen Later Jun 14, 2023 2:09


A legend I have been vending at Aton of events and Huko has been at damn near every one of em. He's a true legend in the community, and having em attend multiple tri city vintage flea market events it's been a pleasure working and having em out.