Gurudumu la Uchumi

Follow Gurudumu la Uchumi
Share on
Copy link to clipboard

Fahamu masuala kadha wa kadha kuhusu uchumi kama vile, namna ya kupambana na umaskini, mfumuko wa bei, kushamiri kwa matumizi ya dola na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia kwa nchi za Afrika. Mada hizi zinafanyiwa utafiti wa kina na zinazungumzwa kwa lugha rahisi inayoeleweka ili kukufanya uelew…

RFI


    • May 28, 2025 LATEST EPISODE
    • weekly NEW EPISODES
    • 9m AVG DURATION
    • 134 EPISODES


    More podcasts from RFI

    Search for episodes from Gurudumu la Uchumi with a specific topic:

    Latest episodes from Gurudumu la Uchumi

    Sehemu ya II: Sehemu ya I: Je, Teknolojia Inaweza Kupunguza changamoto za Biashara barani Afrika?

    Play Episode Listen Later May 28, 2025 9:54


    Msikilizaji wiki iliyopita katika makala ya Gurudumu la Uchumi, tulianza na sehemu ya kwanza ya mada kuhusu namna teknolojia inavyoweza kuhusihwa kwenye biashara kutatua changamoto zinazolikabili bara la Afrika, ikiwemo biashara ya kidijitali kuchochea utangamano, kuongeza ufanisi na kuleta maendeleo.Leo nakuletea sehemu ya pili ya mazungumzo yangu na Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

    Sehemu ya I: Je, Teknolojia Inaweza Kupunguza changamoto za Biashara barani Afrika?

    Play Episode Listen Later May 21, 2025 9:51


    Leo Katika makala ya gurudumu la uchumi tunakuletea sehemu ya kwanza ya mada kuhusu namna teknolojia inavyoweza kuhusihwa kwenye biashara kutatua changamoto zinazolikabili bara la Afrika, ikiwemo biashara ya kidijitali kuchochea utangamano, kuongeza ufanisi na kuleta maendeleo.Leo nakuletea sehemu ya kwanza ya mazungumzo yangu na Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

    Kenya: Wanawake Nandi waruka vikwazo kujikwamua kiuchumi

    Play Episode Listen Later May 14, 2025 10:06


    Katika Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunatuama nchini Kenya, na tunaiangazia jamii ya Wanandi, ambapo kama ilivyo kwa mataifa mengi ya kiafrika, wanawake hawapewi nafasi ya kumiliki mali kama ardhi, mifugo – hasa ng'ombe wa maziwa – hali ambayo imesababisha uduni wa maendeleo ya kiuchumi miongoni mwao.Kufahamu kwa undani, ungana na Emmanuel Makundi na Victor Moturi, ambaye alizuru eneo la Nandi na kuandaa makala haya.

    kenya nandi wanawake katika makala
    Kodi ya lipa Kadiri unavyopata (PAYE): Athari kwa wafanyakazi na waajiri

    Play Episode Listen Later May 7, 2025 10:06


    Msikilizaji wakati dunia ilipoazimisha siku ya kimataifa ya wafanyakazi, viongozi barani Afrika na hasa kwenye ukanda wa Afrika Mashariki walitangaza nyongeza ya mshahara huku wengine wakitoa ahueni ya ushuru wa mapato. Kwenye makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunaangazia kodi ya lipa kadiri unavyopata (PAYE) kwa wafanyakazi na waajiri. Kuzungumzia hili msikilizaji kwenye line ya simu nimemualika Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

    Vita ya Biashara: Athari kwa Biashara na Uwekezaji kwa nchi za ukanda

    Play Episode Listen Later Apr 30, 2025 10:06


    Mizozo ya kibiashara kati ya nchi wanachama wa jumuiya za kikanda kama zile zilizoko SADC na EAC, ina athari endelevu kwa uchumi, biashara na jamii kiujumla.Mfano hivi karibuni Tanzania iliingia katika mvutano na nchi za Malawi na Afrika Kusini, zote zikiwa ni wanachama wa SADC, aidha wakati fulani Tanzania, Kenya na Uganda zilishawahi kuvutana.Ali Mkimo mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara anadadavua hili kwa kina kwenye makala ya wiki hii.

    Kilimo na teknolojia ya Akili Mnemba Afrika

    Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 10:02


    Katika juhudi za kuimarisha ubunifu na ushindani wa kilimo biashara barani Afrika, Kenya kwa kushirikiana na Ufaransa zimeanzisha mpango wa mafunzo ya matumizi ya teknolojia kwa wakulima wanawake, yakiangazia Akili Mnemba (AI) kuongeza thamani ya mazao, mpango umefikia zaidi ya vikundi na mashirika 1200 ya wanawake wakulima na kuwawezesha kutumia teknolojia za kisasa kuongeza ubora, usindikaji na masoko.

    Sehemu II: Madhara ya ushuru wa Trump kwa bara la Afrika na biashara ya dunia

    Play Episode Listen Later Apr 16, 2025 9:46


    Msikilizaji kwa majuma kadhaa sasa, kumekuwa na mjadala duniani kote kufuatia uamuzi wa rais wa Marekani, Donald Trump, kutangaza ushuru wa bidhaa zinazoingia kwenye taifa hilo, mataifa ya Afrika yakiwa miongoni mwa waathirika, baadhi wakiwekewa ushuru wa hadi asilimia 50. Hata hivyo juma lililopita, rais Trump alitangaza kusitisha kwa muda wa siku 90 utekelezwaji wa ushuru kwa baadhi ya mataifa isipokuwa Uchina, ambayo imewekewa ushuru wa zaidi ya asilimia 125.Katika sehemu hii ya pili ya makala ya wiki hii, tumezungumza na Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara.

    Sehemu I: Madhara ya ushuru wa Trump kwa bara la Afrika na biashara ya dunia

    Play Episode Listen Later Apr 9, 2025 10:01


    Kwa majuma kadhaa, mijadala mikali duniani kote kufuatia uamuzi wa rais wa Marekani, Donald Trump, kutangaza ushuru zaidi wa bidhaa zinazoingia kwenye taifa hilo, mataifa ya Afrika yakiwa miongoni mwa waathirika, baadhi wakiwekewa ushuru wa hadi asilimia 50. Katika makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunadadavua na wataalamu athari za ushuru wa Trump kwa nchi za Afrika na biashara ya dunia kiujumla. Tutakuwa na Ali Mkimo, mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

    Sehemu ya Pili: Uchakataji taka za plastiki kwa vijana

    Play Episode Listen Later Apr 2, 2025 10:09


    Msikilizaji takwimu zinaonesha kuwa, ifikapo mwaka 2050, idadi ya watu barani Afrika itaongezeka kufikia bilioni 2.5, ambapo zaidi ya nusu ya watu hawa watakuwa ni vijana walio na umri wa chini ya 25. Hata hivyo Ujasiriamali wa vijana unaonekana kama suluhisho linalowezekana kwa changamoto hii. Msikilizaji juma hili nimebahatika kuwa na mgeni studioni nae si mwingine bali ni Kenneth Ochien'g, ambaye yeyé anajihusisha na uchakataji upya wa taka za plastiki kwa matumizi mengine.

    Sehemu ya Kwanza: Uchakataji taka za plastiki kwa vijana

    Play Episode Listen Later Mar 26, 2025 10:01


    Msikilizaji takwimu zinaonesha kuwa, ifikapo mwaka 2050, idadi ya watu barani Afrika itaongezeka kufikia bilioni 2.5, ambapo zaidi ya nusu ya watu hawa watakuwa ni vijana walio na umri wa chini ya 25. Hata hivyo Ujasiriamali wa vijana unaonekana kama suluhisho linalowezekana kwa changamoto hii. Msikilizaji juma hili nimebahatika kuwa na mgeni studioni nae si mwingine bali ni Kenneth Ochien'g, ambaye yeyé anajihusisha na uchakataji upya wa taka za plastiki kwa matumizi mengine.

    Ushirikiano wa kibiashara kati ya Kenya na Ufaransa

    Play Episode Listen Later Mar 19, 2025 10:01


    Msikilizaji juma moja lililopita, mtandao wa wafanyabishara na makampuni ya Ufaransa hapa nchini Kenya, walikutana na wenzao wa Kenya kuangalia namna bora zaidi ya kushirikiana hasa katika masuala ya teknolojia. Kwa mujibu wa takwimu zilizoko hali ya biashara za mtandaoni kikanda inaendelea kuimarika, huku matarajio ya matumizi ya akili mnemba yakionekana kuleta mageuzi makubwa katika sekta hiyo. Victor Moturi alizungumza na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia wa Kenya, William Kabogo.

    Miundombinu; changamoto ya upatikanaji wa nishati (umeme) Afrika

    Play Episode Listen Later Mar 12, 2025 10:02


    Wiki hii katika makala ya Gurudumu la Uchumi, tunajadili changamoto za upatikanaji wa nishati ya uhakika barani Afrika, ambapo pamoja na baadhi ya mataifa kuwa na rasilimali za kutosha kuzalisha nishati ya ziada, suala la miundombinu limeendelea kusalia kikwazo, ambapo baadhi ya mataifa yanalazimika kununua nishati toka mataifa jirani.Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya Uchumi atakuwa nasi kudadavua hili kwa kina.

    Athari kwa uchumi wa dunia kutokana na vikwazo vya kibiashara vilivyotangazwa na Marekani

    Play Episode Listen Later Mar 5, 2025 9:52


    Katika makala ya Gurudumu la Uchumi juma tunajadili athari za kibiashara kimataifa kutokana na hatua ya hivi karibuni ya Marekani kutangaza vikwazo vya kikodi kwa mataifa ya Canada, Mexico, India na Uchina ambao ni washirika wake wakubwa kibiashara.Kujadili hili, kwenye line ya simu tunaungana na Profesa Wetengere Kitojo, mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

    Sehemu ya Pili: Afrika na harakati za kudai mabadiliko kwenye taasisi za kifedha za kimataifa

    Play Episode Listen Later Feb 26, 2025 9:52


    Msikilizaji juma lililopita tulianza kwa kujadili yaliyotokana na mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika, na suala kuu lilikuwa ni je, nchi za Afrika zitafanikiwa kushinikiza mabadiliko katika taasisi za kifedha za kimataifa na kuondokana na mikopo na madeni yasiyostahimilika ?Leo katika makala ya Gurudumu la Uchumi, nakuletea sehemu ya pili ya mjadala huu, nimemualika Ali Mkimo, mtaalamu namchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa nchini Tanzania.

    Je, Afrika itafanikiwa kushinikiza mabadiliko katika mifumo ya kimataifa ya kifedha

    Play Episode Listen Later Feb 19, 2025 10:01


    Msikilizaji mwishoni mwa wiki iliyopita, viongozi wa Afrika waliokutana mjini Addis Ababa, Ethiopia, walikubaliana kuongeza kasi ya kudai mabadiliko kwa mifmo ya kifedha ya kimataifa, ili kuziwesha kuwa na nafasi katika maamuzi. Afrika inalalamika kutokuwepo usawa, na hivyo kuyaweka mataifa ya Afrika katika hali ya kutegemea mikopo yenye masharti magumu.Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunajadili ikiwa azma hii ya viongozi wa Afrika itafanikiwa.

    Migogoro inavyotatiza ukuaji wa uchumi, maendeleo na utawala bora Afrika

    Play Episode Listen Later Feb 12, 2025 9:43


    Hujambo msikilizaji wa RFI Kiswahili popote pale unapotegea sikio matangazo yetu, makala ni Gurudumu la Uchumi na leo hii tunazungumzia kuhusu athari za kiuchumi kutokana na mizozo kwenye nchi za Afrika.Tutazungumza na Hamduni Marcel, mchambuzi wa siasa za kimataifa akiwa Tanzania na Ali Mkimo, mchambuzi wa masuala ya uchumi akiwa Tanzania.

    Afrika inajifunza nini baada ya Marekani kusitisha kwa muda misaada ya nje.

    Play Episode Listen Later Feb 5, 2025 9:48


    Juma hili katika makala ya Gurudumu la Uchumi, tunajadili kuhusu athari za hatua ya Marekani kusitisha kwa muda utoaji wa misaada ya nje. Uamuzi huu tayari umeonekana kutishia baadhi ya sekta zilizokuwa zinasaidiwa kupitia USAID kama vile Afya na Elimu.Tumezungumza na Ali Mkimo, mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

    Changamoto ya upatikanaji wa nishati ya uhakika barani Afrika

    Play Episode Listen Later Jan 29, 2025 9:55


    Juma hili viongozi wa nchi za Afrika walikutana Tanzania, kujadili namna bora ya kuhakikisha raia wake wanaunganishwa na nishati ya uhakika, endelevu na nafuu ifikapo mwaka 2030.Takwimu zinaonesha raia zaidi ya milioni 600 hawana umeme, bilioni 1 hawatumii nishati safi na salama.Makala ya Gurudumu la Uchumi juma hili imezungumza na Walter Nguma, mchambuzi wa masuala ya uchumi akiwa Tanzania, kuangazia changamoto zinazokwamisha upatikanaji wa nishati, fursa zilizopo.

    Wataalamu waonya kuhusu pengo la walionacho na wasionacho

    Play Episode Listen Later Jan 22, 2025 9:49


    Msikilizaji ripoti mpya ya shirika la kupambana na umasikini Oxfam, inaonesha kuwa utajiri wa mabilionea uliongezeka mara tatu zaidi katika mwaka uliopita, ikiwa ni zaidi ya ilivyokuwa mwaka 2023.Katika makala ya Gurudumu la Uchumi, tumezungumza Ali Mkimo, mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara, kuangazia kwa kina ripoti hii na athari ya kuendelea kushuhudiwa kwa pengo la matajiri na masikini.

    Nchini Kenya Vijana wa mitaa duni wakumbatia Teknolojia ya biashara ndogo ndogo

    Play Episode Listen Later Jan 15, 2025 9:55


    Teknolojia bunifu ya biashara ndogo ndogo  imekuwa ikijulikana kuwa ya watu waliojiweza katika jamiii kutokana na gharama yake ,hali ambayo inawafungia nje watu hasa vijana kutoka maeneo duni na vijijini hivyo kukosa kuimarika kibiashara na kiuchumi kupitia teknolojia hizo .Lakini hata hivyo vijana pamoja na mashirika mbalimbali mtaa wakibera jijini Nairobi Kenya  wapata fursa ya mafunzo na kuimarika kibiashara

    Sehemu ya II: Umuhimu wa kuwa na nidhamu ya kuweka akiba ya fedha

    Play Episode Listen Later Jan 8, 2025 10:05


    Hivi leo ni sehemu ya pili ya makala ya Gurudumu la Uchumi, hasa tunapouanza mwaka 2025 tunaenda kujadili kuhusu nidhamu ya kuweka akiba ya fedha, ufanye nini kuongeza kipato, unatumiaje fedha ulizonazo kuwekeza ? Haya ni baadhi ya mambo ambayo tutaenda kuyatazama kwenye makala ya juma hili. Tutakuwa na Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

    Sehemu ya I: Kwanini ni muhimu kuwa na nidhamu ya kuweka akiba ya fedha

    Play Episode Listen Later Jan 1, 2025 9:44


    Heri ya mwaka mpya 2025 msikilizaji wa RFI Kiswahili popote pale unapotegea sikio matangazo yetu na hasa makala ya Gurudumu la Uchumi, ni imani yetu kuwa nyote mbuheri wa afya. Makala ya Gurudumu la Uchumi, tutajadili kuhusu nidhamu ya kuweka akiba ya fedha. Kuzungumzia hili msikilizaji kwenye line ya simu nimemualika Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

    Nidhamu ya matumizi ya fedha

    Play Episode Listen Later Dec 25, 2024 10:03


    Katika makala ya hivi leo, tunajadili kuhusu umuhimu wa kuwa na nidhamu ya fedha, kwanini ipo haja ya kuwa na nidhamu ya matumizi binafsi, vipi unaweza kujipanga kwa mwaka ujao? Haya ni miongoni mwa maswali ambayo mtaalamu wetu wa uchumi na biashara Ali Mkimo anaenda kuyajibu.

    Akina mama jimbo la Migori nchini Kenya wanzisha kiwanda cha kuchakata samaki

    Play Episode Listen Later Dec 19, 2024 9:50


     Makala haya yanazungumzia hatua za  wanawake na wasichana katika eneo la Opapo, Kaunti ya Migori nchini Kenya, kwa msaada wa mashirika yasiyo ya kiserikali  na serikali ya kaunti, wameanzisha kiwanda  cha kuchakata samaki, kuboresha biashara ya samaki, na kuongeza thamani kwa kutengeneza bidhaa kama soseji na baga,hivyo kuinua uchumi

    Manufaa na changamoto za mkataba wa biashara huria barani Afrika, AfCFTA

    Play Episode Listen Later Dec 4, 2024 10:02


    Msikiliza mataifa 54 ya Afrika yametia saini mkataba wa biashara huria barani Afrika, mataifa 48 yakitia saini itifaki kuanza kuutekeleza. Huu ni moja ya mikataba mikubwa ya kibiashara duniani, ukitarajiwa kuwaondoa raia milioni 30 kutoka kwenye umasikini na kuongeza mapato ya bara hil hadi kufikia dola bilioni 450 ifikapo mwaka 2030.Kuangazia kwa kina mkataba huu pamoja na hali ya madeni ya nchi za Afrika, tumezungumza na Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi akiwa Tanzania.

    Vijana pwani ya Kenya waachana na dawa za kulevya na kugeukia shughuli za kiuchumi

    Play Episode Listen Later Nov 13, 2024 10:00


    Msikilizaji kwa muda sasa, eneo la pwani ya Kenya limekuwa likikabiliwa na kiwango kikubwa cha matumizi ya dawa za kulevya miongoni mwa vijana, Hali hii ikichangia vitendo vya utovu wa nidhamu, kuongezeka kwa magonjwa ya zinaa na ndoa za mapema. Hata hivyo, kutokana na juhudi za mashirika mbalimbali ya kijamii na yasiyo ya kiserikali, vijana wengi walioacha kutumia dawa za kulevya sasa wanajihusisha na miradi ya kibiashara ili kujikimu.Makala ua Gurudumu la Uchumi juma hili, inawaangazia vijana wa eneo la Pwani ambao wameamua kuachana na matumizi ya dawa za kulevya.

    Sehemu ya pili: Je kuongeza kodi ni suluhu kwa matatizo ya Afrika

    Play Episode Listen Later Nov 7, 2024 10:02


    Msikilizaji kwa muda sasa mataifa ya Afrika yameendelea kupitia changamoto za kifedha, kuanzia katika kukusanya mapato na matumizi kwa ajili ya maendeleo yake, hali ambayo imesababisha nchi nyingi kujikuta pabaya kutokana na kulazimika kukopa fedha toka kwa taasisi za kimataifa au nchi zilizoendelea huku ziklipa riba kubwa katika urejeshaji.Lakini je, kuongza kodi ndio suluhu? Mchambuzi wa masuala ya uchumi kutoka Tanzania, Ali Mkimo anafafanua.

    Je, nyongeza ya kodi ni suluhu kwa nchi zinazoendelea kujikwamua kiuchumi

    Play Episode Listen Later Oct 30, 2024 10:03


    Mataifa ya Afrika yameendelea kupitia changamoto za kifedha, katika kukusanya mapato kwa ajili ya maendeleo, hali ambayo imesababisha nchi nyingi kujikuta pabaya kutokana na kulazimika kukopa fedha toka kwa taasisi za kimataifa au nchi zilizoendelea huku ziklipa riba kubwa katika ureje shaji.Lakini je, kuongeza wigo wa kodi kwa mataifa yanayoendelea ndio njia pekee kuwezesha mataifa haya kujikwamua kiuchumi? Tumezungumza na Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya uchumi akiwa Tananzania

    Athari za Kiuchumi kutokana na ongezeko la watu barani Afrika: Changamoto na fursa

    Play Episode Listen Later Oct 9, 2024 10:03


    Msikilizaji dunia inashuhudia ongezeko kubwa la idadi ya watu katika miongo 6 iliyopita, ambapo mwaka 1960 idadi ilikuwa bilioni 3 lakini katika miongo miwili tu hadi mwaka 1982 ilikuwa imevuka watu bilioni 5 na November mwaka 2022 kulikuwa na watu bilioni 8 duniani.Makala ya Gurudumu la Uchumi juma hili, tunajadili Athari za Kiuchumi kutokana na ongezeko la watu barani Afrika: Changamoto na fursa.Tumezungumza na Walter Nguma, mchambuzi wa masuala ya uchumi akiwa Tanzania

    Athari za utoroshaji na utakatishaji fedha barani Afrika

    Play Episode Listen Later Oct 2, 2024 9:58


    Tatizo la fedha haramu barani Afrika linaligharibu bara hili kiasi cha dola za Marekani bilioni 50 na bilioni 80 kila mwaka, Asilimia 44 ya utajiri wa kifedha wa Afrika inadhaniwa kuwa nje ya nchi. Kwa mujibu wa Ripoti ya Maendeleo ya Uwazi wa Ushuru barani Afrika ya 2023, nchi za Afrika zimeokoa dola bilioni 2 kwa mwaka kutokana na watu kuweka wazi mapato yao, ubora wa kubadilishana taarifa na uchunguzi wa nje ya nchi.Tumezungumza na Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

    Fursa na changamoto ya huduma jumuishi za mifumo ya kifedha kidijitali barani Afrika

    Play Episode Listen Later Sep 18, 2024 9:58


    Msikilizaji kwa mujibu wa benki ya dunia, ni asilimia 49 tu ya watu wazima wanamiliki akaunti benki, takwimu za hivi karibuni zikionesha ongezeko la asilimia 55 mwaka 2021 kutoka asilimia 43 mwaka 2017, hata hivyo kiwango hiki kikiwa kidogo ukilinganisha na wastani wa kidunia wa asilimia 76. Makala ya Gurudumu la Uchumi, juma hili tunajadili kuhusu huduma jumuishi za mifumo ya kifedha barani Afrika. Machambuzi wa masuala ya uchumi ALI MKIMO anajibu maswali kadhaa kuhusu sekta hii.

    Afrika na usalama wa chakula

    Play Episode Listen Later Sep 11, 2024 9:36


    Msikilizaji juma lililopita Rwanda ilikuwa mwenyeji wa kongamano la mfumo wa chakula barani Afrika, ambapo wadau zaidi ya elfu 4 kutoka kila pembe ya mataifa ya Afrika walishiriki.Mkutano uliangazia kuhusu mifumo ya chakula, mbinu bora na teknolojia  ambazo zinaweza kubadilisha mifumo ya kilimo na chakula barani Afrika na wakati huohuo kutengeneza nafasi za kazi na fursa kwa wanawake.Msikilizaji wiki hii nimeshirikiana na mwanahabari wetu wa Kigali, Christopher Karenzi;

    Ndio au hapana, mkutano kati ya Uchina na Afrika

    Play Episode Listen Later Sep 4, 2024 9:56


    Uchina wiki hii imekuwa mwenyeji wa mkutano kati yake na viongozi wa Afrika, kwa mujibu wa takwimu zilizoko, China ni taifa la pili duniani kufanya biashara nyingi zaidi na bara la Afrika, biashara inayokadiriwa kufikia dola za Marekani bilioni 167 kwa mwaka. Kuangazia mkutano huu na wasiwasi ulioko kuhusu uwekezaji wa China barani Afrika, tumezungumza na Ali Mkimo, mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

    Athari za kutokuwa na usawa wa kijinsia kwa soko la ajira Afrika

    Play Episode Listen Later Aug 28, 2024 9:42


    Kwa wastani, wanawake hufanya angalau mara mbili na nusu zaidi ya kazi za nyumbani zisizo na malipo kuliko wanaume. Zaidi ya hayo, wanawake hutumia saa 4 na dakika 30 kwa siku kwa kazi ya matunzo bila malipo, ikilinganishwa na saa 1 dakika 20 kwa wanaume katika nchi zinazoendelea.Makala ya Gurudumu la uchumi wiki hii tunajikita kule mashariki mwa nchi ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambako baadhi ya wanawake kwenye mji wa Goma, sasa wanalazimika kuponda mawe kujikimu na familia zao.

    Tatizo la ajira na changamoto nyingine kwa vijana wa Afrika Mashariki

    Play Episode Listen Later Aug 21, 2024 10:07


    Msikilizaji asilimia 70 ya watu katika mataifa ya Afrika yaliyoko Kusini mwa Jangwa la Sahara wana umri wa chini ya miaka 30, hata hivyo ni hatari ikiwa mataifa yatashindwa kuhakikisha vijana wana nafasi nzuri za maisha, kwakuwa Vijana wana haki sio tu ya afya bora, lishe bora na elimu, lakini fursa za uhuru na kazi nzuri.Kuzungumzia mada hii hivi leo, kwa njia ya simu nimemualika Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa nchini Tanzania.

    Ugunduzi wa tekonolojia ya akili mnemba teknolojia nyingine na mchango wake kwa ukuaji wa uchumi

    Play Episode Listen Later Jun 26, 2024 9:54


    Msikilizaji kwa mujibu wa Jukwaa la dunia la uchumi, World Economic Forum, ujio wa teknolojia mpya kama akili mnemba (Artuificial inteligency), ikiwa zitatumika vizuri, zitasaidia kujenga uchumi wenye ushindani, unaostahimili changamoto na endelevu.Katika makala ya gurudumu la uchumi juma hili, tunajadili Kuibuka au ugunduzi wa teknolojia na ushawishi wake katika kukuza uchumi.

    Athari za uchumi na biashara kwenye mji wa Kalemie nchini DRC

    Play Episode Listen Later Jun 12, 2024 9:53


    Msikilizaji juma hili katika makala ya Gurudumu la uchumi nakuletea mseto wa taarifa za uchumi na biashara toka kwenye kanda ya Afrika Mashariki, katika Makala ya leo mwenzangu victor Abuso, alizungumza na Christian Yoka, mkurugenzi wa shirika la maendeleo la Ufaransa, AFD kanda ya Afrika, lakini pia mwandishi wetu wa Lubumbashi, Denise Mayoo, alizuru mji wa Kalemie nchini DRC ulioathirika pakubwa na mafuriko, ambako shughuli za biashara na uchimi zimeathiriwa pakubwa.

    Afrika iwe makini inaposhirikiana au kusaidiwa na nchi zilizoendelea

    Play Episode Listen Later Jun 5, 2024 9:59


    Msikilizaji katika miaka ya hivi karibuni, mataifa ya Ulaya, Amerika, Asia na sasa Uarabuni, yameongeza kasi ya uwekezaji, utoaji wa mikopo na misaada kwa nchi za Afrika, mataifa haya yamewekeza mabilioni ya dola za marekani kwa bara hilo kwa kubadilishana na rasilimali zake, hatua ambayo mbali na kuonekana kama ni urafiki lakini inaibua maswali kuhusu nia hasa ya nchi hizo kwa bara la Afrika. Ni juma hili tu, Korea Kusini kwa mara ya kwanza imefanya kongamano na viongozi wa Afrika, ambapo imetangaza msaada wad ola za marekani bilioni 10 kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na biashara kati yake na nchi hizo. Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, tunaangazia kasi hii mpya ya nchi za magharibi kwa bara la Afrika, tukijiuliza maswali kadhaa, je nia yao ni safi? Na vipi Afrika inaweza kutumia fursa hii kujikwamua kiuchumi?

    Hofu kwa wafanyabiashara kuhusu muswada wa fedha 2024 nchini Kenya

    Play Episode Listen Later May 29, 2024 10:05


    Msikilizaji kwa wiki kadhaa sasa nchini Kenya, kumekuwa na mjadala mkali baada ya kutolewa kwa mapendekezo ya serikali kuhusu muswada wa fedha wa mwaka 2024 unaolenga kuongeza kodi katika baadhi ya sekta na bidhaa nchini humo.Wazalishaji na wawekezaji wakitarajiwa kuwa waathiriwa wakbwa ikiwa muswada huu utapitishwa kama ulivyo, ambapo baadhi ya vinavyolalamikiwa na wazalishaji ni nyongeza ya ushuru wa thamani katika malighafi kutoka nje pamoja na tozo za mazingira maarufu kama Eco Levy. Sekta ya uzalishaji wa viwanda inatarajiwa kuchangia asililia 20 katika pato ghafi la taifa hadi kufikia mwaka 2030. Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, imezungumza na mwenyekiti wa shirikisho la wazalishaji nchini Kenya, Antony Mwangi, kuangazia changamoto na faida za muswada huu. Jina langu ni Emmanuel Makundi, karibu. Msikilizaji nilianza kwa kumuuliza Antony, wao wanautazamaje muswada huu? Insert /// Msikilizaji kama umeungana nasi Makala ni Gurudumu la uchumi na leo tunaujadili muswada wa fedha nchini Kenya unaoelnga kuongeza ushuru wa bidhaa na wazalishaji, na tunazungumza na Antony Mwangi, mwenyekiti wa shirikisho la wazalishaji nchini Kenya. Insert /// Kufikia hapa ndio tunatia nanga ya Makala ya Gurudumu la uchumi kwa juma hili, shukrani kwa Antony Mwangi, mwenyekiti wa shirikishi la wazalishaji nchini Kenya, usikose kuungana nami katika makala nyingine wiki ijayo, ulikuwa nami Emmanuel Makundi, kwaheri.

    Afrika na jitihada za kutaka kuwa katika meza ya majadiliano ya kidunia na sio mualikwa

    Play Episode Listen Later May 22, 2024 10:02


    Msikilizaji wakati wa kongamano la kimataifa la wakurugenzi wakuu wa kampuni mbalimbali duniani waliokutana nchini Rwanda, maswali kadhaa yaliibuliwa, kubwa lilikuwa ni je bara la Afrika linapaswa kuwa katika meza ya maamuzi au kwenye orodha, na ikiwa huu ni muda muafaka wa kutoa mustakabali wake. Ni maswali magumu ambayo hata hivyo viongozi wa Afrika walioshiriki, wanakubaliana kuwa bara hili lina rasilimali zakutosha kubadili uelekeo wake na maendeleo kwa raia, lakini pia halipaswi kuwa linaomba kwa viongozi wa magharibi kuwa katika meza ya majadiliano kuhusu mustakabali wa uchumi na maendeleo ya dunia. Suala la mabadiliko ya tabia nchi na utekelezaji wa mkataba wa biashara huria wa bara hili, maarufu kama AfCFTA, liliibuka, ambapo licha ya utiwaji saini itifaki yake, bado kuna vikwazo vya kufanya biashara baina ya nchi za Afrika.

    Changamoto na fursa kwa vijana wajasiriamali na ajira kwenye nchi za Afrika Mashariki

    Play Episode Listen Later May 15, 2024 9:58


    Hujambo msikilizaji wa rfikiswahili popote pale unapotegea sikio matangazo yetu nikukaribishe katika makala ya Gurudumu la Uchumi, na hivi leo tunaangazia ukanda wa Afrika Mashariki, eneo lililojaa nguvu kazi ya vijana pamoja na ari ya ujasiriamali, lakini bado linakabiliwa na tatizo la ukosefu wa ajira. Takwimu za hivi karibuni za benki ya dunia zinaonesha uhalisia wa tatizo, takwimu zikitofautiana baina ya nchi na nchi, lakini kiujumla ni kuanzia kati ya asilimia 4 hadi 19 ya vijana hawana ajira, huku wanawake walioko vijijini wakiwa waathirika wakubwa. Katika makala haya hivi leo, tutaangazia kwa kina namna gani bora ya kukabiliana na tatizo la ajira na kuongeza wajasiriamali wengi zaidi kwenye ukanda. Kwenye line ya simu nimewaalika, Ali Mkimo, yeye ni mchambuzi wa masuala ya Uchumi pamoja na Emmanuel Cosmas, kijana mbunifu wa masuala teknolojia na nibalozi wa UNICEF, wote hawa wakiwa nchini Tanzania.

    Mchango wa biashara ndogondogo na kati kwa uchumi wa nchi za Afrika Mashariki

    Play Episode Listen Later May 10, 2024 8:14


    Makala ya Gurudumu la Uchumi juma hili, inaangazia mchango na changamoto ya biashara ndogondogo na zile za kati kwenye nchi za Afrika Mashariki.Matayarishaji amezungumza na wafanyabiashara wadogowadogo na kati nchini Kenya, lakini mchambuzi wa masuala ya uchumi Ally Mkimo.

    Claim Gurudumu la Uchumi

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel