Podcasts about desemba

  • 19PODCASTS
  • 561EPISODES
  • 22mAVG DURATION
  • ?INFREQUENT EPISODES
  • May 20, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about desemba

Latest podcast episodes about desemba

Habari za UN
20 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 20, 2025 12:20


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika wafugaji wa nyuki nchini Tanzania leo ikiwa ni siku ya nyuki duniani iliyopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 20 Desemba mwaka 2017 kupitia azimio namba A/72/211.Baada ya miaka mitatu ya majadiliano, leo katika Mkutano wa Kimataifa wa Afya unaoendelea Geneva, Uswisi, nchi zimepitisha rasmi makubaliano ya kihistoria ya kuzuia, kujiandaa, na kukabiliana vyema na majanga ya magonjwa kwa siku zijazo. Taratibu zote zitakapopitishwa na angalau nchi 60, mkataba utaanza kutumika rasmi mwakani.Kutokana na mamlaka za Israeli kulegeza kwa muda mzingiro uliodumu kwa wiki 11, angalau sasa matumaini kidogo yamerejea Gaza, yameeleza leo mashirika ya Umoja wa Mataifa. Msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya dharura, OCHA, Jens Laerke amesema tayari wamepata ruhusa ya kuyavusha malori matano yaliyokuwa yamezuiliwa jana.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP limetahadharisha  leo kwamba bila ufadhili zaidi, huenda katika muda wa wiki chache zijazo likalazimika kusitisha msaada wa chakula kwa takribani nusu ya watu linaowahudumia kwa sasa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.Na katika mashinani, fursa ni yake Hanan Al-Dayya, Mkimbizi wa ndani katika ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli, akisimulia  madhara ya mashambulizi yanayoendelea kutoka Israeli.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
Waathirika wa kimbunga Chido: Asante UNHCR kwa kutotusahu lakini mahitaji ni makubwa

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 10, 2025 2:19


Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR linaendelea kusambaza msaada wa kibinadamu ili kurejesha matumaini ya waathirika wa kimbunga Chido kilichotokea tarehe 15 Desemba mwaka jana nchini Msumbiji na kuziacha taabani jamii za majimbo ya Cabo Delgado, Nampula na Niassa. Flora Nducha na taarifa zaidi.

Habari za UN
10 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 10, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia moto wa nyika mjini California Marekani, na waathirika wa kimbunga Chido nchini Msumbiji. Makala tunasikia kijana Paul Siniga kutoka Tanzania na mashinani tunakupeleka nchini Kenya, kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la hali ya hewa duniani (WMO) leo hii likiwa limeutangaza mwaka jana 2024 kuwa mwaka uliokuwa na joto zaidi kuwahi kurekodiwa, leo pia WMO imeendelea kusisitiza umuhimu wa tahadhari za mapema kuhusu majanga ya tabianchi ili kuokoa maisha ya watu. WMO imeeleza kwamba tahadhari za mapema zilizotolewa na Idara ya Hali ya Hewa ya Taifa la Marekani  zimesaidia kwa kiasi fulani kuokoa maisha ya watu katika moto wa nyika uliosambaa na kuteketeza maeneo makubwa mji wa Los Angels katika jimbo la California.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR linaendelea kusambaza msaada wa kibinadamu ili kurejesha matumaini ya waathirika wa kimbunga Chido kilichotokea tarehe 15 Desemba mwaka jana nchini Msumbiji na kuziacha taabani jamii za majimbo ya Cabo Delgado, Nampula na Niassa.Katika makala Assumpta Massoi wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa anazungumza na kijana Paul Siniga kutoka Tanzania ili kufahamu safari yake hadi kuweza kufika makao makuu ya Umoja wa MAtaifa, New York, Marekani.Na mashinani Nur Bashir kutoka jamii ya wfugaji katika kaunti ya Turkana nchini Kenya ambaye kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji anaeleza jinsi jamii zake zinavyoathiriwa na mabadiliko ya tabianchi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
09 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 9, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea Mada kwa Kina inayotupeleka Kenya ambapo Shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limefanikiwa kumnyanyua msichana Nosizi Dube na kutimiza ndoto yake ya kuepuka ndoa ya utotoni na kupata shahada ya kwanza ya chuo kikuu. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchaambizi wa neno KWEGO.Mwezi mmoja tangu kuanguka kwa utawala wa Bashar Al-Assad, zaidi ya wakimbizi 125,000 wamerejea Syria "wakiwa na matumaini baada ya miaka mingi ya kuishi uhamishoni", lakini wamejikuta wakikabiliwa na hali mbaya nchini mwao, wameeleza leo wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa. Likiwa linaongoza wito kwa jumuiya ya kimataifa "kutoka kwenye maneno hadi vitendo" ili kuwasaidia watu walio waliorejea ambao sasa wako katika mazingira magumu, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, limesema familia nyingi zina uhaba wa makazi na njia kidogo za kiuchumi.Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limeongeza ombi lake la fedha kufikia dola milioni 73.2 kwa ajili ya kusaidia zaidi ya watu milioni 1.1 kote nchini Syria katika kipindi cha miezi sita ijayo, wakati nchi hiyo ikiingia katika kipindi cha mpito kufuatia kuanguka kwa serikali ya Bashar Al-Assad. Ombi hili ni nyongeza katika ombi la awali la dola milioni 30 lililotolewa mwezi Desemba mwaka jana 2024 likilenga mahitaji yanayoongezeka ya majira ya baridi Kaskazini Magharibi mwa Syria.Miezi 15 baada ya vita huko Gaza, mamia kwa maelfu wanaendelea kuishi katika shule za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina (UNRWA) zenye msongamano ambazo zimegeuzwa kuwa makazi. UNRWA imeeleza kuwa hata viwanja vya michezo kwa watoto sasa ni nyumba kwa waliofurushwa. Shirika hilo limesisitiza kuwa misaada zaidi ya kibinadamu lazima iingie Gaza na kusitishwa kwa mapigano ni muhimu zaidi kuliko hapo awali.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo fursa ni yake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “KWEGO”.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

Habari za UN
07 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 7, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini DRC katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Bulengo kushuhudia jinsi Umoja wa Mataifa unavyowasaidia wanawake waathrika wa ukatili wa kingoni kuweza kujitegemea na kumudu mahitaji ya familia zao.Kwa mujibu wa takwimu zilizothibitishwa na Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa, takriban watu 5,601 waliuawa nchini Haiti mwaka 2024 kutokana na ghasia za magenge, likiwa ni ongezeko la zaidi ya mauaji 1,000 ya mwaka 2023. Katika moja ya matukio mabaya zaidi na ya kushtua mwaka jana, takriban watu 207 waliuawa mapema Desemba kwenye mauaji yaliyoratibiwa na kiongozi wa genge lenye nguvu la Wharf Jérémie katika eneo la Cité Soleil huko Port-au-Prince. Wengi wa waliouawa walikuwa wazee walioshutumiwa kusababisha kifo cha mtoto wa kiongozi huyo kwa njia ya uchawi.Leo, Umoja wa Mataifa na Serikali ya Lebanon wametoa ombi la nyongeza ya dola milioni 371.4 za kimarekani, zikilenga kutoa msaada wa kuokoa maisha ya walioathiriwa na mzozo wa hivi karibuni na janga la kibinadamu linaloendelea nchini humo.Na Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk leo ameeleza kusikitishwa sana na ongezeko kubwa la watu walionyongwa nchini Iran mwaka jana. Takriban watu 901 wameripotiwa kunyongwa katika mwaka 2024, arobaini wakiwa wamenyongwa katika wiki moja tu ya mwezi Desemba.Mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi, UNFPA tunamsikia Zubaida AbouBaker, mama mkimbizi wa ndani katika kambi ya Tawila iliyoko Darfur Kaskazini nchini Sudan akisimulia machungu yaliyomkumba kufuatia migogoro inayoendelea nchini humo.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
UN: Vifo vitokanavyo na baridi Gaza vinazuilika, usitishaji mapigano na misaada ndio jawabu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 3, 2025 1:58


Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM leo limeonya juu ya vifo vitokanavyo na msimu wa baridi kali Gaza likisema limesikitishwa sana na athari mbaya za mvua za msimu wa baridi na baridi kali kwa Wapalestina waliokimbia makazi yao na kuishi katika mazingira magumu huko Gaza, kwani hilo ni janga la kibinadamu lisilo na kifani. Kupitia taarifa iliyotolewaleo mjini Geneva Uswisi Mkurugenzi Mkuu wa IOM Amy Pope  amesema "Watu walio katika mazingira magumu, ikiwa ni pamoja na takriban watoto wachanga saba, wamekufa kutokana na baridi kali au hypothermia, na vifo hivi vya kusikitisha vinasisitiza haja ya haraka ya makazi na msaada mwingine wa kibinadamu kuwafikia watu wa Gaza mara moja," Ameongeza kuwa hali hii inachochea janga zaidi la kibinadamu ambalo tayari linawakumba watu waUkanda wa Gaza. Mvua kubwa na mafuriko yameyakumba makazi ya wakimbizi wa ndani yaliyojengwa kwa mahema na kulazimisha familia kuachwa katika maeneo ya wazi kwenye hali mbaya ya baridi, zikijitahidi kutengeneza mahema yaliyoharibika kutokana na matumizi ya miezi kadhaa. © UNRWAChakula kinagawiwa kwa watu waliokimbia makazi yao huko Jabalia, kaskazini mwa Gaza.Vikwazo vya Israel ni changamoto kwa misaadaPia IOM imesema vikwazo vya utaratibu wa kufikia wenye uhitaji, kama ilivyoripotiwa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA, vimezuia kwa kiasi kikubwa utoaji wa misaada, huku watu 285,000 pekee wakipokea msaada wa makazi tangu Septemba 2024. Kwa mujibu wa IOM hadi kufikia Katikati ya Desemba mwaka jana inakadiriwa kuwa watu wapatao 945,000 bado wanahitaji msaada wa haraka wa kukabiliana na msimu wa baridi ikiwemo nguo za kuongeza joto, mablanketi na tepu za kuima mahema dhidi ya mvua na baridi. Tangu Katikati ya Novemba mwaka jana IOM imewasilisha karibu vifaa 180,000 vya makazi ya dharura kwa washirika ndani ya Gaza na ina zaidi ya vifaa milioni 1.5 vya msimu wa baridi ikiwemo mahema, vifaa vya kuziba  na vitanda ambavyo viko tayari kwenye maghala na sehemu zavivuko, lakini vikwazo vikali vya ufikiaji vinawazuia kufikia wenye uhitaji. © UNICEF/Abed ZaqoutWavulana wawili wakibeba chupa za maji katika kambi ya wakimbizi inayofadhiliwa na UNWRA huko Khan Younis kusini mwa Gaza.Usitihsaji mapigano ndio suluhuIOM imesisitiza wito wake wa dharura wa kusitisha mapigano ili kuwezesha utoaji salama na wa haraka wa msaada wa kuokoa maisha kwa wale wanaouhitaji sana. Pia inasisitiza wito wake kwa pande zote kuzingatia sheria za kimataifa za kibinadamu, kuhakikisha ulinzi wa raia, kuachiliwa kwa mateka wote na kuruhusu ufikiaji salama, wa haraka, usiozuiliwa na endelevu wa wenye uhitaji. Watu wa Gaza wanastahili usalama, makazi na utu. IOM iko tayari kuhamasisha misaada na kusaidia jamii zilizofurushwa, lakini fursa ya ufikiaji wa kibinadamu lazima itolewe ili kuwezesha hili amesisitiza mkuu wa IOM. Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA limesema Licha ya hali ngumu, timu za UNRWA zinaendesha makao yote ya Umoja wa Mataifa, na kutoa msaada wa kuokoa maisha kwa watu wanaohitaji. Limeongeza kuwa Vita vilipoanza karibu miezi 15 iliyopita, UNRWA iligeuza shule zake, vituo vya afya, na maghala kuwa makazi na kuna wakati ambapo vita ikiendelea UNRWA ilipokea watu milioni 1 waliokimbia makazi yao 

Habari za UN
31 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 31, 2024 12:00


Kipindi maalumu wakimbizi, wakimbizi wa ndani na wenyeji wao wanaeleza namna walivyonufaika na misaada ya Umoja wa Mataifa na mashirika yake na pia wanaeleza matumaini yao kwa mwaka ujao wa 2025. 

Alfajiri - Voice of America
Waasi wa M23 waendelea kuchukua udhibiti wa miji mashariki mwa Congo. - Desemba 31, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 31, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

congo miji mashariki desemba
Habari za UN
30 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 30, 2024 10:44


Leo jaridani: Mwaka 2024 ulighubikwa na machungu lakini kuna matumaini 2025 asema Guterres.UNMAS yaondolea hofu wakulima Beni, DRC kwa kutegua masalia ya mabomu.Makala inatupeleka Uganda kusikiliza msichana mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Ashiimwe Baganiza mwenye ndoto ya kuwa wakili ili kuwatetea wanawake.Mashinani ni mradi wa Siku 1000 wa UNICEF Zambia. 

Alfajiri - Voice of America
Rais wa zamani wa Marekani Jimmy Carter afariki dunia Jumapili akiwa na umri wa miaka 100. - Desemba 30, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 30, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
27 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 27, 2024 9:57


Hii leo jaridani tunaangazia sherehe za krismasi katika ukanda wa Gaza lich ya migogoro inayoendelea, na magonjwa ya mlipuko. Makala inatupeleka Havana Cuba na mashinani nchini Uganda, kulikoni?Katika kuandhimisha Siku ya Kimataifa ya Kujitayarisha dhidi ya Magonjwa ya Mlipuko, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito kwa nchi kote ulimwenguni kuzingatia masomo yaliyopatikana katika dharura za kiafya zilizopita ili kusaidia kujiandaa kwa dharura zijayo.Tukiwa bado katika msimu wa sikukuu ya krismasi, tunakwenda mji wa Gaza, huko Ukanda wa Gaza, Mashariki ya Kati kusikia jinsi sikukuu hii ilivyoadhimishwa na hisia mchanganyiko kwenye kanisa katoliki la Familia Takatifu kwenye viunga vya zamani kwenye mji huo.Makala inatupeleka Havana Cuba kuangazia umuhimu wa utekelezaji wa moja ya ajenda za Umoja wa Mataifa ya kukumbatia lugha mbalimbali duniani ambapo Flora Nducha wa Idhaa hii akiwa Cuba hivi karibuni kwenye kongamano la Kimataifa la Kiswalihi alikutana na raia wa nchi ambaye ni mwalimu wa Kiswahili.Mashinani fursa ni yake Ange Rukenura, msichana alieyekimbia makazi yake pamoja na ndugu zake sita kufuatia mashambulizi ya waasi waliojihami nchini  Jamhuri ya Kidemocrasi ya Congo, DRC akisema licha ya rasilimali ndogo anashukuru ukarimu wa Uganda na msaada wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kwa kuwapatia matumaini.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Kiongozi wa Al-Shabab auwawa na kundi hilo ladhibitisha - Desemba 27, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 27, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Alfajiri - Voice of America
Alfajiri - Desemba 26, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 26, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

desemba
Alfajiri - Voice of America
Watu kadhaa washukiwa kufa kutokana na ghasia za matokeo ya uchaguzi wa Msumbiji. - Desemba 25, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 25, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

watu kufa uchaguzi desemba
Habari za UN
24 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 24, 2024 12:51


Hii leo jaridani tunakuletea mad akwa kina inayotupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kumulika harakati za kusaidia manusura wa ukatili wa kingono na kijinsia kwenye mizozo. Pia tunakuletea muhtasari wa había za Sudan, Uganda na Tanzania, Mashinani tunarejea Sudan.Ripoti ya Kamati ya Tathmini ya Viwango vya Njaa (IPC) iliyotolewa leo inaeleza kwamba imegundua kuwa kuna maeneo matano zaidi nchini Sudan ambayo yanakabiliwa na baa la njaa kati ya mwezi huu wa Desemba na Mei mwaka ujao wa 2025. Ripoti hiyo imeyataja maeneo hayo kuwa ni ya Darfur Kaskazini yaani Um Kadadah, Melit, El Fasher, Twawisha, na Al Lait.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limekaribisha mchango wa EURO milioni 1 kutoka serikali ya Ujerumani ili kusaidia shughuli za lishe na ustawi kwa zaidi ya wakimbizi na wasaka hifadhi 254,000 nchini Uganda ambayo inawahifadhi wakimbizi milioni 1.7.Na Kikosi cha 7 cha Walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, TANBAT 7 kilichokuwa kinahudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kuleta Utulivu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR (MINUSCA) kimerejea nyumbani Tanzania kikijivunia kuwa kikosi cha kwanza cha nchi hiyo kupokea barua ya pongezi kutoka Umoja wa Mataifa.Mashinani fursa ni yake Najwa Mohamed, mama mjamzito kutoka Jabal Moya nchini Sudan ambaye amepoteza makazi yake kufuatia vurugu zinazoendelea nchini humo na kulieleza Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi,  UNFPA kwamba hali ni ngumu hasa kwa wanawake wajawazito.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!   

Alfajiri - Voice of America
Katika siku ya haki za binadamu, wanawake na wasichana waomba kukomeshwa kwa mauaji dhidi yao Kenya. - Desemba 24, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 24, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
23 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 23, 2024 10:00


Hii leo jaridani tunaangazia ziara ya Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA, Tom Fletcher mashariki wa kati, na uwezeshaji wa vijana katika sekta ya kilimo nchini humo. Makala inatupeleka nchini Zimbabwe na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Misaada ya Dharura, OCHA, Tom Fletcher akihitimisha ziara yake ya kwanza katika eneo la Mashariki ya kati tangu hivi karibuni alipochukua wadhifa huo ameeleza kuwa alichokishuhudia katika ukanda huo ni hali tete.Mradi wa pamoja wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO ujulikanao kama Nabta kwa lugha ya Kiarabu ukimaanisha "mche" ambao lengo lake ni kuwasaidia vijana wajasiriamali kubadili mawazo yao kuwa  biashara ya kilimo yenye mafanikio umeleta nuru kwa Alaa Khattab kijana aliyekuwa na ndoto ya kuwa mfanyabiashara wa kilimo nchini Syria.Katika makala Assumpta Massoi anakupeleka Zimbabwe kumulika nuru iliyofikia wakulima baada ya Umoja wa Mataifa kuona jinsi mabadiliko ya tabianchi yalivyoathiri shughuli za kilimo.Mashinani fursa ni yake Rukia, kijana wa kike kutoka Tana River nchini Kenya ambaye kupitia mafunzo na uwezeshaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM, yeye hasiti kutoa tahadhari za mapema na kuwahamasisha jamii kujiepusha na madhara panapotokea majanga ya mabadiliko ya tabianchi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Alfajiri - Voice of America
Haki ya kikatiba ya uraia wa kuzaliwa Marekani, inaleta mjadala wa kati Trump akikaribia kuingia madarakani - Desemba 23, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 23, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
20 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 20, 2024 10:53


Hii leo jaridani tunaangazia jitihada za kuudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Maburg nchini Rwanda, na juhudi za kuchunguza virusi vya VVU nchini Ghana. Makala tunakupeleka nchini Kenya na mashinani nchini DRC, kulikoni?Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) limeipongeza serikali ya Rwanda kwa kufanikiwa kuudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Maburg. Hii leo Rwanda imetangaza mwisho wa mlipuko wa hivi karibuni wa ugonjwa huo baada ya kutokuwepo maambukizi mapya katika siku 42 na mgonjwa wa mwisho akiwa amepimwa mara mbili bila kukutwa na ugonjwa kama matakwa ya WHO yanavyotaka ili kutangaza kuisha kwa mlipuko wa magonjwa namna hii.Mwaka 2020 Ghana iliripoti kuwa na watu 350,000 wanaioshi na virusi vya Ukimwi na kati yao hao 31,000 walikuwa ni wajawazito. Jambo lililoshtua ni kwamba ni sehemu ndogo mno ya wajawazito hao ndio walipimwa kufahamu iwapo wana VVU au la. Jambo lililofanya serikali kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kuchukua hatua.Makala inatupeleka kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyokoko Kaunti ya Turkana Kaskazini Magharibi mwa Kenya kukukutanisha na mkimbizi kutoka Somalia anayetumia mpira wa kikapu anatumia mpira wa vikapu kuhamasisha jamii yake na kupinga mil ana desturi zisizofaa.Mashinani ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Mpira wa Kikapu, fursa ni yake Danny Batachoka, mwanariadha wa Paralimpiki kutoka Goma nchini Jamhuri ya kidemocrasia ya Congo, DRC ambaye kupitia video ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO, anasema ana ndoto ya kuwa mmoja wa wachezaji wakubwa wa mpira wa vikapu katika kitengo chake.” Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Alfajiri - Voice of America
Ugonjwa mpya unaofanana na homo DRC wazua wasi wasi baada ya kuuwa darzeni ya watu. - Desemba 20, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 20, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

homo wasi watu baada ugonjwa desemba
Habari za UN
19 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 19, 2024 9:43


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Syria, ambako viongozi wa ngazi mbalimbali za Umoja wa Mataifa wamendelea kusisitiza hitaji la kutanguliza ulinzi wa manusura na uhifadhi wa ushahidi wa uhalifu. Pia tunapata ufafanuzi wa neno na muhtasari wa habari.Karla Quintana kutoka Mexico ameteuliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo kuongoza Taasisi Huru ya kuchunguza watu waliotoweshwa nchini Syria, taasisi ambayo imeundwa na Baraza la Kuu la Umoja wa Mataifa mwezi Juni mwaka jana 2023. Guterres amewaambia waandishi wa habari hii leo kwamba yeye na timu yake lazima waruhusiwe kutekeleza kwa kina jukumu lao, na vile vile mifumo yote ya kimataifa ya kusongesha ulinzi wa haki za binadamu nchini Syria na uwajibikaji wa uhalifu uliotendwa lazima wawe na wanachohitaji ili kutekeleza majukumu yao muhimu.Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekuwa na kikao cha ngazi ya mawaziri kuhusu Akili Mnemba, au AI ambapo Katibu Mkuu António Guterres amesema pamoja faida kubwa ya teknolojia hiyo bado kuna changamoto iwapo haitasimamiwa vema na binadamu. Hivyo amependekeza kuundwa mwa mfumo wa kimataifa wa kuendeleza Akili Mnemba kwa uwiano na usawa, ukijikita kusaidia nchi zinazoendelea kuzuia kuibuka kwa pengo la teknolojia hiyo kati ya walio nayo na wasio nayo.Na huko Bunia, jimboni Ituri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemorkrasia ya Congo, DRC vijana 24 wakiwemo wanawake 6 wamenufaika na mafunzo ya siku tano ya mbinu za kisasa za kilimo kutoka walinda amani wa Bangladeshi wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO. Lengo ni kuwezesha kilimo kuwa chanzo cha kipato kwa wakazi na kuimarisha uchumi wa eneo hilo.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya neno “AKRABA.” Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Mazungumzo ya amani ya Sudan Kusini kuanza tena mjini Nairobi. - Desemba 19, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 19, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

nairobi tena desemba sudan kusini
Habari za UN
18 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 18, 2024 9:54


Hii leo jaridani tunaangazia siku ya wahamiaji duniani ikimulika mchango wa wakimbizi na wahamiaji katika ukuaji wa kiuchumi na kukuza jamii zao n aza wenyeji. Tutasikia kutoka mkuu wa IOM, Katibu Mkuu wa UN na wahamiaji Burundi na Chad. Pia tunaangazia ufugaji nyuki Tanzania.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake mahususi kwa ajili ya Siku ya Kimataifa ya Wahamiaji ametoa wito kwa ulimwengu kuitumia siku hii kujikumbusha kwamba pamoja na kwamba tunasherehekea michango ambayo mamilioni ya wahamiaji hutoa kwa jamii leo pia ni siku ya kujikumbusha changamoto ambazo wahamiaji wanaweza kukumbana nazo.Nimefurahi sana kwani binti yangu mwenye ulemavu ambaye tulihamia naye makazi ya muda kufuatia kuongezeka kina cha maji ya Ziwa Tanganyika, hapa Burundi sasa amepatiwa stadi za kumwezesha kujikwamua kiuchumi. Ni kauli ya Odette Niyonkuru, raia mhamiaji wa ndani nchini Burundi akizungumzia mustakabali wa binti yake huyo kwenye video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM.Makala inatupeleka nchini Tanzania kufuatilia Mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO uitwao ACP MEAs 3 ambao umwewapa wakulima zana na ujuzi muhimu katika ufugaji nyuki endelevu kwa lengo la kuboresha maisha yao huku wakikuza bayoanuwai na uhifadhi wa mazingira. Kupitia video iliyoandaliwa na FAO Tanzania Selina Jerobon amefuatilia mafanikio ya mradi huu na kituandalia makala hii.Na mashinani katika siku hii ya kimataifa ya wahamajia Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM linasisitiza umuhimu wa kuwawezesha wanawake na wasichana walio ukimbizini na kuongeza mikakati ya kifedha inayozingatia jinsia. Bi Banti Ahmat ni mmoja wa wakimbizi na anelezea jinsi ambavyo mradi wa IOM wa bustani za jamii unavyoleta matokeo chanya kwa wahamiaji na jamii za wenyeji nchini Chad.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Rais wa Uturuki Reccep Tayip Erdogan asema kwamba yupo tayari kuongoza mazungumzo ya amani ya Sudan - Desemba 18, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 18, 2024 29:58


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
17 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 17, 2024 10:48


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika mafanikio katika kuzuia maambukizi mapya ya VVU na juhudi za vijana wakimbizi nchini Uganda kuhakikisha hilo. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani inayotupeleka Gaza.Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Syria Geir O. Pedersen bado yuko nchini Syria alikowasili jana Jumapili  ikiwa ni wiki moja baada ya wapiganaji wa Hayʼat Tahrir al-Sham (HTS) walioko kwenye orodha ya vikundi vya kigaidi kutwaa mji mkuu Damascus na kusababisha Rais Bashar Al-Assad kukimbia nchi.Mwaka 2024 ukielekea ukingoni, sirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR nchini Uganda limetoa rai kwa jumiya ya kimataifa kutolisahau taifa hilo la Afrika Mashariki ambalo ni maskani ya idadi kubwa zaidi ya waomba hifadhi na wakimbizi barani Afrika. Rai hiyo iliyotolewamwishoni mwa wiki inataka ufadhili wa fedha uongezwe ili liweze kuendelea kukirimu watu hao ambao wengi wanakimbia machafuko.Katika makala Assumpta Massoi anakupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Ethiopia kumulika mwelekeo wa usajili wa watoto wanapozaliwa na faida zake.  Na mashinani Maram, mama kutoka Deir al-Balah Gaza, ambako familia zinahaha kuokoa mali zao na kukarabati mahema yao yaliyoharibiwa na upepo mkali na maji ya mvua wakati huu wa msimu wa baridi, na kuleta athari kwa watoto wao.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Rais wa Chad Mahamat Idriss Deby atetea hatua yake ya kuvunja uhusiano wa kijeshi na Ufaransa. - Desemba 17, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 17, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

rais yake hatua ufaransa desemba mahamat idriss deby
Habari za UN
16 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 16, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia serikali ya mpito nchini Syria na wakimbizi na wahamiaji wanaosaka hifadhi nchini Uganda. Makala tunakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na mashinani nchini Tanzania, kulikoni?Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Syria Geir O. Pedersen bado yuko nchini Syria alikowasili jana Jumapili  ikiwa ni wiki moja baada ya wapiganaji wa Hayʼat Tahrir al-Sham (HTS) walioko kwenye orodha ya vikundi vya kigaidi kutwaa mji mkuu Damascus na kusababisha Rais Bashar Al-Assad kukimbia nchi.Mwaka 2024 ukielekea ukingoni, sirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR nchini Uganda limetoa rai kwa jumiya ya kimataifa kutolisahau taifa hilo la Afrika Mashariki ambalo ni maskani ya idadi kubwa zaidi ya waomba hifadhi na wakimbizi barani Afrika. Rai hiyo iliyotolewamwishoni mwa wiki inataka ufadhili wa fedha uongezwe ili liweze kuendelea kukirimu watu hao ambao wengi wanakimbia machafuko.Katika makala Assumpta Massoi anakupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Ethiopia kumulika mwelekeo wa usajili wa watoto wanapozaliwa na faida zake.  Na mashinani fursa ni yake Mkombola Melio, mhudumu wa afya ambaye pia ni mnufaika wa mradi wa maji na usafi uitwao RUWASA au Rural Water and Sanitation project inaofadhiliwa na Benki ya Dunia Afrika nchini Tanzania akisema mradi huo umezisaidia jamii kuondokana na maambukizi yanayosababisha magonjwa.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Mjumbe wa UN aendelea na ziara ya kukutana na wadau nchini Syria

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 16, 2024 1:31


Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Syria Geir O. Pedersen bado yuko nchini Syria alikowasili jana Jumapili  ikiwa ni wiki moja baada ya wapiganaji wa Hayʼat Tahrir al-Sham (HTS) walioko kwenye orodha ya vikundi vya kigaidi kutwaa mji mkuu Damascus na kusababisha Rais Bashar Al-Assad kukimbia nchi. Ikiwa ni sehemu ya juhudi za Umoja wa Mataifa kuhakikisha mabadiliko ya utawala nchini Syria yanafanyika kwa amani na kuisaidia Syria kutokuingia kwenye mgogoro zaidi, Bwana Pederson aliyewasili jana Damascus  hadi sasa ameshakutana na Kamanda wa Utawala Mpya Ahmed al-Sharaa na Waziri Mkuu wa Serikali ya Muda Mohammed al-Bashir.Taarifa iliyotolewa leo na Ofisi yake inasema Pederson ameeleza muhtasari wa matokeo ya Mkutano wa Kimataifa wa Aqaba kuhusu Syria uliofanyika tarehe 14 ya mwezi huu wa Desemba akisisitiza haja ya kuwepo kwa mpito wa kisiasa unaoaminika na unaoongozwa na kumilikiwa na Wasyria wenyewe kama kanuni za azimio 2254 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (2015) zilivyopendekeza. Aidha Mjumbe huyo maalum amesisitiza azma ya Umoja wa Mataifa ya kutoa usaidizi wa kina kwa watu wa Syria.Taarifa imedokeza kuwa Bwana Pedersen ana shughuli nyingi zilizopangwa siku zijazo katika harakati za kusaka suluhu ya amani nchini Syria.

Habari za UN
Harakati za wazazi kuona watoto wao wanasajiliwa nchini mwao baada ya kuzaliwa

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 16, 2024 4:24


Tarehe 11 mwezi huu wa Desemba, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF lilitoa ripoti yake kuhusu usajili wa vizazi duniani ikionesha maendeleo makubwa katika idadi ya watoto wanaosajiliwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa. Maeneo mengine kama nchi za Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara ongezeko ni dogo ikilinganishwa na kwingineko. Ingawa hivyo licha ya changamoto zilizoko kwa nchi za Afrika zilizo Kusini mwa jangwa la Sahara katika kutoa huduma hiyo, mafanikio yanaanza kuonekana kama inavyosimulia makala hii iliyoandaliwa na Assumpta Massoi kupitia video ya UNICEF.

Alfajiri - Voice of America
Mazungumzo ya amani kati ya Rwanda na DRC yakiongozwa na Angola yakwama tena. - Desemba 16, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 16, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
13 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 13, 2024 9:46


Hii leo jaridani tunaangazia hali nchini Syria, na msaada wa kibinadamu kw awakimbizi nchini Chad. Makala inatupeleka nchini Tanzania na mashinani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC, kulikoni?Ofisi ya mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Syria (OSE) imesema wakati huu ikifuatilia kwa karibu hali na maendeleo nchini Syria ni muhimu kuhakikisha kwamba Wasyria wanashika usukani wa mustakbali wao na kwamba kuna ujumbe wa pamoja na mshikamono kuhusu hilo kutoka kwenye jumuiya ya kimataifa.Kutokana na idadi kubwa ya wakimbizi wanaoingia Chad wakitoka Sudan kuwa ni wanawake na watoto, Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi,  UNFPA limeimarisha huduma za afya ya wanawake na watoto.Katika makala Assumpta Massoi anakupeleka Tanzania kusikia jinsi wanafunzi wananufaika na mradi wa Umoja wa Mataifa shuleni na majumbani.Na mashinani fursa ni yake Aline kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC ambaye ni mnufaika wa mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP wa kuwezesha wanawake na wasichana kusoma na kuandika ili waweze kujimudu kimaisha na kuondokana na unyanyasaji wa kijinsia, akisema JHARDEE anamaanisha bustani, na LEGYUME ni maharage.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Rais Paul Kagame akemea wanaoleta chuki za mauaji ya kimbari nchini mwake. - Desemba 13, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 13, 2024 29:57


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
12 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 12, 2024 10:00


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa ikiangazia wanawake na wasichana mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ambapo ukatili wa kingono ni jinamizi linalowakumba kila uchao kutokana na mapigano yanayoendelea kwenye eneo hilo. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno MIDABWADA.Leo si siku ya kimataifa ya huduma za afya kwa wote mwaka huu ikibeba mudhui “Huduma za afya kwa wote ni jukumu la serikali” yakisisitiza kwamba Uwekezaji katika huduma za afya kwa wote UHC, unaimarisha usawa na uwiano wa kijamii na pia unanufaisha uchumi wa taifa kwa kuboresha afya na ustawi, kuongeza ushiriki wa wafanyikazi na tija, na kujenga mnepo kwa watu, familia na jamii.Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Syri Geir O. Pedersen leo amesema “Picha kutoka kwenye magereza ya Sednaya na vituo vingine vya kizuizini nchini Syria vinadhihirisha unyama na ukatili usiofikirika ambao Wasyria wamevumilia na umekuwa ukiripotiwa kwa miaka mingi.”Na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres yuko ziarani Lesotho ambako akihutubia Bunge la nchi hiyo amesema bara la Afrika lina utajiri mkubwa wa vyanzo vya nishati endelevu kuanzia sola, upepo hadi maji lakini bado haijatumika ipasavyo kwani waafrika milioni 600 hawana umeme.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno MIDABWADA”Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Romania yachunguza iwapo uchaguzi wa Rais wa Jumapili uliingiliwa kimitandao. - Desemba 12, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 12, 2024 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

romania rais uchaguzi desemba jumapili
Habari za UN
11 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 11, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya WHO inayohusu malaria, na juhudi za UNICEF na wadau wake nchini Rwanda za kusaidia watoto waliozaliwa na ulemavu kuweza kutembea. Makala tunakupeleka nchini Yemen na mashinani nchini Tanzania, kulikoni?Takwimu mpya zilizotolewa leo na ripoti ya shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO, zinaonyesha kuwa ingawa takriban wagonjwa bilioni 2.2 wa malaria na vifo milioni 12.7 vya ugonjwa huo vimeepukwa tangu mwaka 2000 bado ugonjwa huo unaendelea kuwa tishio kubwa la kimataifa la afya hususan katika Kanda ya Afrika ya WHO na hivyo juhudi zaidi zahitajika kuutokomeza.Nchini Rwanda Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF kwa msaada wa UNICEF Uswisi na Liechtenstein wamesaidia tiba kwa njia ya mazoezi kuponya watoto wenye ulemavu wa viungo. Selina Jerobon anasimulia akiangazia mtoto mmoja, Joshua.Katika makala Assumpta Massoi anakupeleka Yemen kusikia yaliyojiri baada ya ndoto za vijana kuelekea Saudi Arabia kuishia Yemen.Na mashinani mashinani hivi majuzi dunia iliadhimisha siku ya watu wenye ulemavu duniani ikiangazia uthabiti, ujumuishaji na fursa sawa kwa wote. Kutana na Dorice Mkiva, Mtaalamu wa usimamizi wa maarifa wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Tanzania ambaye alipoteza uwezo wake wa kutembea akiwa na umri mdogo na sasa anatumia sauti yake kutetea haki za watoto.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Marekani haitaki kuona ISIS wanajikita Syria - Desemba 11, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 11, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
10 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 10, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na tunaelekea nchini Kenya kuangazia moja ya ukiukwaji Mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya wanawake, jinamizi la ukeketaji na jitihada zinazochukuliwa na UNFPA na wadau mbalimbali. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani inayotupeleka nchini Namibia.Baada ya serikali ya Bashar Al-Assad kupinduliwa na kuibuka kwa taarifa za baadhi ya nchi duniani kuanza kusitisha mchakato wa kushughulikia maombi ya Wasyria waliokuwa wameomba hifadhi kuokoa usalama wa maisha yao pindi hali ilipokuwa tete nchini mwao, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) linaendelea kutoa wito kwa mataifa yote kufungua milango, kuwapa hifadhi na ulinzi raia wa Syria wanaotafuta usalama. UNHCR imeahidi pia mara tu hali ya Syria itakapokuwa wazi zaidi, itatoa mwongozo kuhusu mahitaji ya ulinzi kwa Wasyria walioko hatarini.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limekaribisha mchango wa dola za Marekani milioni 22 kutoka shirika la Korea Kusini la Ushirikiano wa Maendeleo ya Kimataifa (KOICA) ili kuimarisha mnepo kwa tabianchi na uhakika wa chakula kwa wakulima wadogo, wafugaji na makundi yaliyoko pembezoni nchini Kenya, Somalia na Sudan Kusini. Vituo vya utabiri wa hali ya hewa vinatabiri hali ya La Niña mashariki mwa Pembe ya Afrika na uwezekano wa kupunguza mvua katika kipindi hikiNa walinda amani wa kikosi cha 11 cha Tanzania -TANZBATT-11 kinachohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO jimboni Kivu Kaskazini wametunukiwa nishani ya umoja wa mataifa ikiwa ni alama ya kufanya kazi  kwa utii,uhodari na uaminifu. Miongoni mwao ni Private Selina Kisemvule.Katika mashinani ikiwa ni siku ya mwisho ya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, fursa ni yake Rais Nangolo Mbumba wa Namibia ambaye kupitia ukurasa wa X wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA anawahimiza wananchi na dunia nzima kwa jumla kusimama kidete ili  kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Alfajiri - Voice of America
Zaidi ya watu darzeni moja wahofiwa kufa kwenye ajali ya boti Misri - Desemba 10, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 10, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
09 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 9, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini Syria, na kampeni ya chanjo ya polio huko Pokot nchini Kenya. Makala tunasalia huko huko DRC na mashinani tnakwenda nchini Msumbiji, kulikoni?Kufuatia jana Wananchi wa Syria kutwaa madaraka kutoka kwa uongozi uliowatawala kwa mabavu kwa zaidi ya miongo mitano, viongozi wa Umoja wa Mataifa wameendelea kutoa wito wa kuhakikisha mabadiliko haya yanakuwa fursa ya mustakabali bora kwa kuzingatia haki za binadamu, uhuru na haki kisheria.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa ushirikiano na serikali ya kenya na wadau wengine wa afya  hivi karibuni wamezindua kampeni ya  chanjo ya polio katika jamii ya wafugaji na wakulima ya kaunti ya West Pokot Mashariki mwa Kenya ambako mara nyingi ni vigumu kufikiwa.Makala tunakwenda Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kusikiliza mama ambaye alipatiwa ujauzito na mlinda amani wa Umoja wa Mataifa na kisha kujifungua mtoto ambaye anasimulia kadhia ya kutomfahamu baba na wito wake kwa mama yake mzazi. Msimulizi wako ni George Musubao mwandishi wa Idhaa ya Umoja wa MAtaifa nchini DRC.Katika mashinani wakati huu ambapo Dunia inaendelea kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, fursa ni yake Benilde Nhalivilo. Mkurugenzi mtendaji wa jukwaa la kitaifa la haki za watoto nchini Msumbiji ambaye kupitia video ya Benki ya dunia barani Africa anasisitiza utekelezaji wa sheria kuhakikisha mustakabali usio na ukatili wa kijinsia katika elimu.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Rais wa Syria, Bashar al-Assad adaiwa kukimbilia Russia - Desemba 09, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 9, 2024 29:57


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
06 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 6, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia Mkataba wa Kampala wa Ulinzi na Usaidizi wa Wakimbizi wa Ndani barani Afrika, na siku ya kimataifa ya kujitolea inayotupeleka nchini DRC. Makala tunakwenda nchini Kenya na mashinani nchini Zambia, kulikoni?Katika kuadhimisha miaka 15 tangu kupitishwa kwa Mkataba wa Kampala wa Ulinzi na Usaidizi wa Wakimbizi wa Ndani barani Afrika chini Muungano wa Afrika, Kamishna Mkuu Msaidizi wa Ulinzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, Ruven Menikdiwela NA Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu za Wakimbizi wa ndani Paula Gaviria Betancur wametoa kauli ya pamoja ya kupongeza Muungano wa Afrika kwa maono haya ya mbali na pia kuzisihi nchi zote barani Afrika kuutekeleza mkataba huo muhimu.Dunia ikiwa imeadhimisha siku ya kimataifa ya kujitolea kwa ajili ya amani na maendeleo, tunakupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako mmoja wa wafanyakazi wa kujiolea wa Umoja wa Mataifa anaelezea uzoefu wake na ni kwa nini anajivunia kufanya kazi hiyo.Makala leo inatupeleka Kakamega Magharibi mwa Kenya kwa mkulima mdogo wa mahindi Catherine Wanjala aiyeathirika vibaya na magugu yajulikanayo kama Kichawi au Witchweed, na hata kuilamisha familia yake kulaa njaa wakati mwingine kwa kukosa mavuno, lakini ahuweni ilimwijiia pale mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP wa kusambaza dawa za kupambana na magugu hayo ulipomfikia.Katika mashinani wakati huu ambao Dunia inaadhimisha siku 16 ya kupinga ukatili wa kijinsia, fursa ni yake Mheshimiwa Rais Hakainde Hichilema wa Zambia, ambaye kupitia mtandao wa X wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA anasisitiza mchango wa wanaume kwa kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Wakimbizi wa Malawi waanza kulipwa ridhaa kutokana na hasara waliopata kutokana na El Nino. - Desemba 06, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 6, 2024 29:57


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
05 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 5, 2024 9:59


Hii leo jaridani mada kwa kina inayotupeleka katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali nchini Uganda kumulika hali ya ukatili dhidi ya wanawake kwa watu hao waliokimbia vita jinsi inavyoshughulikiwa. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA leo limezindua ombi lake la kimataifa la mwaka 2025, likitafuta dola bilioni 1.4 ili kutoa huduma za afya ya uzazi zinazookoa maisha na programu muhimu za kuzuia unyanyasaji wa kijinsia kwa zaidi ya wanawake, wasichana na vijana milioni 45 kote duniani katika nchi  57 zilizoathiriwa na majanga.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) leo jijini Geneva, Uswisi limetangaza kutoa idhini ya awali kwa kipimo kinachoitwa Xpert® MTB/RIF Ultra dhidi ya ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB). Kipimo hiki pia kinaweza kupima uwezekano wa kuathiriwa kwa viuavijasumu ambacho kinakidhi viwango vya WHO.Biashara ya kimataifa inatazamiwa kufikia dola trilioni 33 mwaka 2024, kulingana na Taarifa mpya ya Biashara ya Kimataifa iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo (UNCTAD). Ongezeko hili la dola trilioni 1, linaloakisi ukuaji wa mwaka wa asilimia 3.3, linaonesha uthabiti katika biashara ya kimataifa licha ya changamoto zinazoendelea.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno “MBUKU NA MSUNUNU.”Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Waziri Mkuu wa Mali asimamishwa kazi baada ya kukosoa serikali kwa kuchelewesha uchaguzi wa kidemokrasia. - Desemba 05, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 5, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

mali kazi baada serikali uchaguzi desemba kidemokrasia waziri mkuu
Habari za UN
04 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 4, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia uzinduzi wa ombi la ufadhili wa mahitaji ya Kibinadamu (GHO), na umuhimu wa lugha mama katika kukuza haki za binadamu. Makala tunasalia hapa makao makuu ya umoja wa mataifa na mashinani tunakupeleka nchini Senegal, kulikoni?Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) ikizindua Ripoti ya Kimataifa ya mahitaji ya Kibinadamu (GHO) kwa mwaka ujao wa 2025 imetangaza ombi la ufadhili kwani takriban watu milioni 305 duniani kote watahitaji msaada wa kibinadamu katika mwaka ujao.Haki si haki iwapo inatolewa kwa lugha ambayo haileweki kwa wahusika, wamejulishwa washiriki wa mkutano wa pili wa wanazuoni unaofanyika hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York, Marekani na pia mtandaoni ukimulika Madaraka, Haki na Binadamu: Utawala wa Sheria na mabadiliko Afrika.Makala tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambapo mkutano wa mwaka 2024 wa Taaluma kuhusu Afrika leo katika leo umeingia siku ya pili hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Mkutano huo ulioandaliwa na Ofisi ya mshauri maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Afrika UNOSAA ni wa siku tatu na umebeba maudhui "Nguvu, Haki, na watu” kwa ajili ya mabadiliko ya Afrika.Na mashinani fursa ni yake Antar sarr, Kijana mkulima wa mbogamboga kutoka Senegal ambaye ni mmoja wa wanufaika wa mradi wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya kilimo, IFAD unaowawezesha vijana nchini humo kwa kilimo na biashara ndogondogo ili kuondokana na fikra za kwenda Ulaya kusaka Maisha bora na ajira, akisema mradi huo imempatia matumaini.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Kenya kutafuta washirika wengine wa kukarabati uwanjwa wa ndege wa Jomo Kenyatta baada ya mkataba wa Adani kufutwa. - Desemba 04, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 4, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
03 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 3, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo inamulika harakati za Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kuhakikisha wafugaji kuku wasiotumia dawa kiholela wananufaika kiuchumi baada ya kupatiwa mafunzo. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani ya Timor-Leste.Leo ni Siku ya Kimataifa ya Watu wenye Ulemavu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe mahususi kwa siku hii, ameueleza ulimwengu kuwa maadhimisho ya mwaka huu yanawakumbusha kwamba ulimwengu unahitaji uongozi wa watu wenye ulemavu zaidi kuliko hapo awali. Guterres ameeleza kuwa Watu wenye ulemavu tayari wanabeba mzigo mkubwa wa majanga yanayoumiza ulimwengu lakini mara nyingi wananyimwa haki yao ya kuchangia katika suluhu za majanga haya.Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya Uchunguzi kuhusu Syria hii leo imezitaka pande zinazopigana nchini Syria zifuate kikamilifu sheria za kimataifa na kuwalinda raia. Hii inatokana na ongezeko kubwa la mapigano tangu tarehe 27 mwezi uliopita ambayo yanatishia kuenea katika maeneo mengine ya nchi.Mkutano wa mwaka 2024 wa Taaluma kuhusu Afrika umeanza leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Mada ya mkutano huo wa siku tatu ni "Nguvu, Haki, na Watu: Haki za Binadamu na Utawala wa Sheria kwa Mabadiliko ya Afrika." Mkutano huo wa kila mwaka unalenga kuongeza uwakilishi wa Waafrika katika ufadhili wa kimaendeleo wa kimataifa, ili kuchagiza mustakabali bora wa Afrika.Na mashinani leo ikiwa ni siku ya watu wenye ulemavu duniani tunakupeleka Timor-Leste, kusini-mashariki mwa Asia kuona jinsi mradi uliofadhiliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira, UNEP umemwezesha Antonio Ornai mwenye ulemavu wa kutoona kushiriki zoezi la kuitikia maonyo ya taarifa za majanga kwenye taifa hilo ambalo hugubikwa na majanga ya asili mara kwa mara kama vimbunga na mafuriko.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!  

Habari za UN
02 DESEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 2, 2024 10:42


Hii leo jaridani tunaangazia mashauriano huko Busan kuhusu matumizi ya plastiki, na ripoti ya UNODC kuhusu UKIMWI na kudhibiti dawa za kulevya katika magereza. Makala inaturejesha Havana Cuba na mashinani inatupeleka nchini Kenya, kulikoni?Vuta nikuvute kwenye mashauriano huko Busan, Korea Kusini kuhusu mkataba wenye nguvu za kisheria dhidi ya uchafuzi utokanao na matumizi ya plastiki na kulinda mazingira ya baharini imefikia ukingoni kwa mkutano kuahirishwa na wawakilishi wa nchi zilizokuwa zinashiriki kuridhia rasimu mpya yenye ibara 32 itakayojadiliwa mwakani.Wakati jana Desemba Mosi Ulimwengu ukiadhimisha Siku ya Kimataifa ya UKIMWI kwa kuhamasisha haki za binadamu ili kufanikisha vita dhidi ya ugonjwa huu hatari, Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya ya Kudhibiti Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) inajivunia miaka 25 ya kujiunga na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kukabiliana na UKIMWI (UNAIDS) katika kushughulikia janga la Virusi Vya UKIMWI (VVU) miongoni mwa watu wanaotumia dawa za kulevya na miaka 20 ya kazi ya kupambana na UKIMWI magerezani.Makala leo inamulika jinsi bidhaa za kitamaduni zinavyotumika kukuza na kuendeleza mila na desturi za Kiswahili mkoani Tanga Kaskazini mwa Tanzania. Je ni bidhaa zipi hizo na zinatumika vipi? Tuungane na Flora Nducha aliyeyabaini hayo hivi karibuni alipokuwa Havana Cuba kwenye kongamano la kimataifa la Kiswahili.Na mashinani tunasikiliza manufaa ya ufadhili wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya kilimo, IFAD kwa wakulima kutoka kwake Sharon Kirui kutoka Kaunti ya Nakuru nchini Kenya ambaye ni mnufaika wa vocha za kielektroniki za ununuzi kutoka kwa IFAD na ameweza kupanua biashara yake ya kilimo.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
UN: Mwanamke au msichana mmoja aliuawa kila baada ya dakika 10 na mwenzi au ndugu 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 25, 2024 3:13


Leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake, Je wajua kwamba wanawake na wasichana 140 walifariki dunia kila siku duniani kote mwaka 2023 wakiwa mikononi mwa wapenzi wao au ndugu wa karibu, ikimaanisha kuwa mwanmake mmoja anauawa katika kila dakika 10. Na zaidi ya yote bara la Afrika linaongoza? Maudhui ya siku hii yanasema “Hakuna kisingizio” cha ukatili dhidi ya wanawake lama alioushuhudia Ester manusura kutoka Uganda, ambaye kwa miaka mingi amekuwa akifanyiwa ukatili na mpenzi wake anaema “Nilikuwa na umri wa miaka 15 aliponioa naye alikuwa na miaka 28wakati mwingine alikuwa akinivua nguo zote na kunilazimisha kukaa kwenye varandana nilikuwa nikichelewa kurudi ananitandika nje nyumba kila mtu kushuhudia Nilikuwa katika hali mbaya ya uchungu Mkubwa na kuvuja damu.”maadhimisho ya mwaka huu yanaambatana na ripoti iliyotolewa leo jijini New York, Marekani na mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la masuala ya wanawake, UN Women na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kudhibiti Dawa za kulevya na Uhalifu, (UNODC), inaangazia mwanga wa janga la mauaji ya wanawake na kutoa wito kwa hatua za dharura ili kukabili janga hilo.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres katika ujumbe wake wa siku hii inayoadhimishwa tarehe 25 mwezi Novemba kila mwaka, ikiashiria pia kuanza kwa siku 16 za kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake, zikiwa na kilele chake tarehe 10 mwezi Desemba, siku ya Haki za Binadamu duniani amesema “Janga la ukatili dhidi ya wanawake na wasichana linaaibisha ubindamu, dunia lazima iitikie wito huu. Tunahitaji hatua za dharura kwa ajili ya haki na uwajibikaji, na kusaidia uchechemuzi.”Mkurugenzi mtendaji wa UN Women Sima Bahous amesisitiza kuwa “Ukatili dhidi ya wanawake na wasichana si kwamba hauepukiki, unaweza kuzuilika. Tunahitaji sheria thabiti, ukusanyaji bora wa takwimu, uwajibikaji zaidi wa serikali, utamaduni wa kutovumilia, na kuongezeka kwa ufadhili kwa mashirika ya kupigania haki za wanawake na taasisi. Tunapokaribia kuadhimisha miaka 30 ya Azimio la Beijing na Jukwaa la Utekelezaji mwaka 2025, ni wakati wa viongozi wa dunia kuungana na kuchukua hatua kwa haraka, kujitolea na kuelekeza rasilimali zinazohitajika kumaliza mgogoro huu mara moja na kwa wote”Mauaji ya wanawake yanavuka mipaka, hali ya kiuchumi na kijamii, utamaduni. Hata hivyo kiwango au ukubwa wake unatofautiana.Kwa mujibu wa ripoti hiyo, bara la Afrika lilivunja rekodi ya kuwa na viwango vya juu vya wanawake kuuawa na wapenzi wao au mwanafamilia. Wanawake 21,700 waliuawa Afrika mwaka huo wa 2023, ikifuatiwa na bara la Amerika na kisha Oshenia.Mashirika ya UN Women na…

Habari za UN
Vijana wafurahia stadi za kuondokana na umaskini Sudan Kusini

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2024 1:57


Vijana katika mji wa Tambura ulioko jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini wanageuza mafunzo ya ufundi stadi kuwa nguvu ya amani na ustawi, mafunzo ambayo yalifanikishwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, UNMISS.Shamrashamra zilitawala wakati vijana 61, wakiwemo wasichana 41 na wavulana 20 walipohitimu mafunzo ya ufundi stadi yenye lengo la kuwaondoa katika umaskini na pia kuwaepusha kutumikishwa katika mzozo unaoendelea nchini humo tangu Desemba 2013.Walifundishwa urembo wa nywele, kutengeneza sabuni, halikadhalika ushoni, mafunzo yaliyofadhiliwa na UNMISS na kutolewa na shirika la kiraia Star Trust Organization, linalohusika na kupunguza ghasia kwenye jamii kwa kuwajegena vijana uwezo.Miongoni mwao ni Suzan James, mama wa watoto wawili aliyejifunza urembo wa nywele na akiwa anamhudumia mteja wakati wa mafunzo anasema.“Ninashukuru mno, kwa sababu nimejifunza mambo mengi ambayo awali sikuyafahamu, lakini sasa ninaweza kufanya. Inanisaidia sana, na ninajivunia na nina furaha. Baada ya hili, nitaenda kufungua sehemu yangu mwenyewe ya urembo wa nywele ili kusaidia jamii.”Huyu ni Justin Alex yeye amejifunza ushoni na akiwa kwenye chereheni yake anasema.. “iwapo nitapekela hii cherehani nyumbani, nitaweza kufanya kazi na kusaidia familia yangu. Kama kijana tusikae nyumbani au tusifanye uhalifu mjini na kusababisha vifo kwa jamii zetu kwa sababu si jambo zuri. Kuanzia sasa tunahitajika kushiriki kwenye shughuli za kusaidia jamii, kama kupeleka hii cherehani nyumbani ili nisaidie jamii yangu.”Wahitimu wamepatiwa vifaa vya kuanzia kufanyie kile walichojifunza. Katika hafla ya utoaji wa vyeti UNMISS iliwakilishwa na afisa wake wa masuala ya ulinzi na ujumuishaji kwenye jamii Ibrahim Tahiru ambaye amesema..“Mradi huu unaweza kuleta amani, lakini pia mradi huu huu unahitaji amani ili uweze kuendelea. Bila amani hivi vitu vitakuwa bure. Kwa sababu wahitimu wanahitaji mazingira yenye amani ili waweze kutumia stadi zao kwa ajili ya kuboresha maisha yao na ya jamii zao. Mradi huu ni ishara ya nia yetu ya kuendelea kushirikiana na Sudan Kusini na kusaidia kufikia amani ya kudumu na kuondokana na umaskini.”Mamlaka za Tambura zina Imani kubwa na mradi huu kama asemavyo Kaimu Kamishna wa Tambura Moses Masisere.“Hakika, Tambura tumekuwa tukililia amani. Kwa hiyo kwa msaada huu tunaamini kuwa mafunzo kwa vijana zaidi kutawasaidia washiriki kwenye harakati za kiuchumi na kupunguza mauaji na uhalifu mwingine Tambura.”