Podcasts about afya

  • 103PODCASTS
  • 1,107EPISODES
  • 21mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • Aug 5, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about afya

Show all podcasts related to afya

Latest podcast episodes about afya

Siha Njema
Watalaam waonya ongezeko la visa vya H pylori katika maeneo ya mijini

Siha Njema

Play Episode Listen Later Aug 5, 2025 10:03


H pylori isipotibiwa inaweza kugeuka kuwa saratani ya tumbo ,watalaam wameonya Katika makala haya,tunaangazia  sababu ambazo zinaweza kuchangia mtu kupata maambukizo ya H pylori na matibabu yake. Matibabu yake kwa mujibu wa daktari Alex Mungala anayehudumu jijini Nairobi yanaweza kukabiliwa na usugu wa vimelea ,ni ghali na si rahisi kupatikana katika vituo vya afya vya daraja la kwanza.

Siha Njema
Ukiwa utatembea hatua elfu saba kila siku unaweka magonjwa hatari mbali

Siha Njema

Play Episode Listen Later Jul 29, 2025 10:06


Utafiti uliofanywa wa shirika la utafiti wa afya Lancet Public Health umebaini hatua elfu 7 kila siku unapunguza hatari ya kupatwa na magonjwa ya Saratani,Kisukari,magonjwa ya moyo, shinikizo la damu,sonona na  kupoteza kumbu kumbu Kwa mujibu wa shirika la afya duniani ,WHO,mazoezi ya kudumu dakika 150 kila wiki au mazoezi makali ya dakika 75 ni mkakati wa kuimarisha afya. Katika makala haya nimejiunga na kundi la Nairobi Walk Movement,tawi la Buru Buru ambalo limejitoa kufanya matembezi ya kuanzia kilomita 10 hadi 20 na wakati mwingine hadi 40 kila Jumamosi asubuhi au Jumapili alasiri kuanzia saa tisa na nusu. Kundi hili pia limejisajili kwenye kundi  la kuhesabu hatua ambazo kila mtu hutembea kila siku ,hatua hizo zikihesabiwa kutumia application maalum ya kuhesabu hatua,lengo likiwa hatua hadi elfu 10 kila siku. Kushindana kwa kuhesabu hatua kila siku umekuwa mchezo ambao huwatia moyo Wanachama hao wameelezea faida nyingi kutokana na kujiunga kwenye kundi hilo na kushiriki matembezi. Wapo waliokuwa na wanatumia dawa za kudhibiti shinikizo la damu na sasa wameachana nazo. Aidha wengine wameeleza matembezi kuwaondolea maumivu ya viungo na pia kupata marafiki wazuri.

Habari za UN
Kuinuka Pamoja: Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika Wakiongoza kwa Nguvu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 25, 2025 2:22


Leo, tarehe 25 Julai, ni Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika, ikiwa na kaulimbiu ya mwaka huu: “Kuinuka Pamoja: Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika Wakiongoza kwa Nguvu.” Idhaa ya Umoja wa Mataifa  imefanya mahojiano na Patricia Da Silva, Mratibu wa Kimataifa wa Timu ya Hakuna Kumwacha Yeyote Nyuma katika shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA na akafafanua kidogo siku hii inabeba nini hasa.

Habari za UN
25 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 25, 2025 11:03


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu Gaza, na Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika. Makala inatupeleka nchini Tanzania na mashinani tunakwenda nchini Uganda, kulikoni?Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameonya kuwa mateso yanayoendelea katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, ni zaidi ya janga la kibinadamu – ni janga la maadili linalopasua dhamira ya jumuiya ya kimataifa.Leo, tarehe 25 Julai, ni Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika, ikiwa na kaulimbiu ya mwaka huu: “Kuinuka Pamoja: Wanawake na Wasichana wa Asili ya Afrika Wakiongoza kwa Nguvu.” Idhaa ya Umoja wa Mataifa  imefanya mahojiano na Patricia Da Silva, Mratibu wa Kimataifa wa Timu ya Hakuna Kumwacha Yeyote Nyuma katika shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu, UNFPA na akafafanua kidogo siku hii inabeba nini hasa. Makala inatupeleka Pemba, visiwani Zanzibar nchini Tanzania, ambapo mpango mpya wa afya ya mama unawasaidia wanawake wajawazito kukabiliana na upungufu wa damu na kujifungua watoto wenye afya. Kupitia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa ushirikiano na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF na kwa msaada wa kifedha kutoka Wakfu wa Gates, zaidi ya wanawake 16,000 sasa wanapata huduma bora kupitia Virutubisho vya Madini Mbalimbali (MMS) na huduma zilizoboreshwa za kliniki za wajawazito. Assumpta Massoi amefuatilia mradi huo kupitia video ya UNICEF TAnzania.Na katika Arinda Angella, kiongozi wa wanafunzi kutoka Mbarara, Uganda akieleza jinsi ushiriki wake katika mafunzo haya ya uongozi ambayo yameendeshwa kwa ushirikiano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo UNDP na Kituo cha Mafunzo cha Julius Nyerere unavyompa mwanga mpya kuhusu nafasi ya vijana na wanawake katika kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Ubia wa Serikali, UNICEF na Wakfu wa Gates Pemba, nchini Tanzania warejesha afya ya wajawazito na watoto

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 25, 2025 3:44


Huko Pemba, visiwani Zanzibar nchini Tanzania, Mpango mpya wa afya ya mama unawasaidia wanawake wajawazito kukabiliana na upungufu wa damu na kujifungua watoto wenye afya. Kupitia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa ushirikiano na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF na kwa msaada wa kifedha kutoka Wakfu wa Gates, zaidi ya wanawake 16,000 sasa wanapata huduma bora kupitia Virutubisho vya Madini Mbalimbali (MMS) na huduma zilizoboreshwa za kliniki za wajawazito. Assumpta Massoi amefuatilia mradi huo kupitia video ya UNICEF TAnzania. 

Habari za UN
23 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 23, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia msaada wa kibinadamu nchini Nigeria, na mradi wa nishati ya sola ya kusaidia wakulima nchini Ethiopia. Makala inakupeleka nchini Afrika Kusini na mashinani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini Nigeria limesema litalazimika kusitisha msaada wake wa dharura wa chakula na lishe kwa watu milioni 1.3 kaskazini-mashariki mwa nchini hiyo ifikapo mwishoni mwa mwezi huu kutokana na ukata.Mradi unaoendeshwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Ethiopia, Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), ubalozi wa China wa kutumia nishati jadidifu ya jua kwa umwagiliaji, umeleta matumaini mapya kwa jamii za wakulima katika mkoa wa Sidama, kusini mwa Ethiopia. Katika makalaShirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF kwakushirikiana na wakfu wa LEGO wametengeneza video yenye kuonesha familia nne na jinsi zinavyopambana na malezi ya Watoto wakiwa ni wazazi kwa mara ya kwanza. Leah Mushi ametazama video hiyo ya takriban dakika 30 na hapa anakuleta simulizi ya familia kutoka nchini Afrika Kusini.Na katika mashinani Noella Bagula, Mwanachama wa Alleluyah Safe Space ambaye ni mama mkimbizi wa ndani kutoka Goma nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ambako wanawake na wasichana wanapitia ukatili wa kijinsia katika migogoro. Bi Bagula anasema yeye sasa anajua jinsi ya kujilinda katika hali hatari kufuatia mafunzo yanayoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya uzazi, (UNFPA) katika maeneo salama yaliyotengwa kwa ajili yao.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Siha Njema
Watalaam waonya kukaa muda mwingi kunaweza kukusababishia kifo cha mapema

Siha Njema

Play Episode Listen Later Jul 23, 2025 10:09


Kukaa kwa zaidi ya saa sita mfululizi kila siku inaweza kukuweka kwenye hatari ya kupata magonjwa ya uti wa mgongo,kisukari,shinikizo la damu na kifo cha mapema

Habari za UN
WHO na mamlaka za mitaa waungana kupambana na Kipindupindu Caluquembe nchini Angola

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 18, 2025 3:12


Huko Manispaa ya Caluquembe jimboni Hiula, Kusini Magharibi mwa Angola, Shirika la Afya Duniani (WHO), kwa kushirikiana na mamlaka za mitaa, limeongeza juhudi za ushirikishwaji wa jamii na afua za afya ya umma, ili kukabiliana na mlipuko wa kipindupindu unaoendelea nchini humo. Lengo kuu likiwa ni kuongeza uelewa kuhusu kipindupindu kupitia mikutano ya jamii, jumbe za afya ya umma, na ujenzi wa miundombinu muhimu kama vile vyoo na vituo vya kupata maji safi ya kunywa ndani ya manispaa. Sabrina Saidi amefuatilia na kueleza zaidi katika makala hii.

Habari za UN
18 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 18, 2025 9:57


Jaridani leo naangazia hafla ya Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela katika makao makuu ya Umoja wa mataifa na ujumbe wa washindi wa Tozo ya Mandela. Makala tunakwenda nchini Angola na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Umoja wa Mataifa leo katika makao yake makuu jijini New York, Marekani, umeadhimisha Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela kwa heshima ya maisha na urithi wa shujaa wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi, nchini Afrika Kusini, Nelson Rolihlahla Mandela, al maarufu Madiba. Assumpta Massoi amefuatilia na kutuandalia taarifa ifuatayo.Mapema kabla ya kushiriki hafla hii ya utoaji wa tuzo katika siku hii ya kimataifa ya Nelson Mandela hapa New York, Kennedy Odede alizungumza na Zipporah Musau wa Umoja wa Mataifa.Katika makala Sabrina Saidi anatupeleka huko Manispaa ya Caluquembe jimboni Hiula, Kusini Magharibi mwa Angola, Shirika la Afya Duniani (WHO), kwa kushirikiana na mamlaka za mitaa, limeongeza juhudi za ushirikishwaji wa jamii na afua za afya ya umma, ili kukabiliana na mlipuko wa kipindupindu unaoendelea nchini humo. Lengo kuu likiwa ni kuongeza uelewa kuhusu kipindupindu kupitia mikutano ya jamii, jumbe za afya ya umma, na ujenzi wa miundombinu muhimu kama vile vyoo na vituo vya kupata maji safi ya kunywa ndani ya manispaa.Na katika mashinani fursa ni yake Purity Christine, mwanzilishi mwenza wa kampuni ya ShopOkoa, jukwaa la kifedha linalowawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati kujiunga na mfumo wa kijamii wa akiba na mikopo nchini Kenya, anasimulia safari yao kupitia Programu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP ya timbuktoo Fintech, ambapo wamejifunza jinsi ya kuboresha jukwaa lao na kuweka malengo makubwa ya kufikia maelfu ya wafanyabiashara barani Afrika.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
17 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 17, 2025 11:05


Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina inayoangazia Afrika Mashariki Fest ya nchini Uganda kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania na Uganda inayotumia  kampeni yake ya “Twende Zetu Butiama” ili kuyatumimiza malengo hayo.Hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO katika eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli limeongoza uhamishaji wa wagonjwa 35, wengi wao watoto kwenda Jordan, kwa ajili ya matibabu zaidi kutokana na huduma za afya kuvurugwa Gaza. WHO inasema zaidi ya watu 10,000 Gaza wanahitaji kuhamishiwa nchi nyingine kwa ajili ya matibabu.Harakati za kusaka amani ya kudumua nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC zinazidi kushamiri ambapo hatua za hivi karibuni ni kutoka Muungano wa Afrika, (AU) zikiongozwa na marais wa zamani, Sahle Work Zewde wa Ethiopia, na Catherine Samba-Panza wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, (CAR).kuelekea mkutano wa 30 wa nchi wanachama wa Mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP30 huko Brazil baadaye mwaka huu, huko Nairobi, nchini Kenya bara la Afrika linajipanga kuhakikisha mkutano huo unakuwa na tija. Dkt. Richard Muyungi, Mwenyekiti wa Kamati ya Wataalamu na mabalozi wanaoshughulikia masuala ya tabianchi barani Afrika, anasema wanachokitaka.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIKWANYUKWANYU!.Mwenyeji wako ni Leah Moshi, karibu!

Habari za UN
Wanaosaka huduma za kusafisha damu katika ukanda wa Gaza matatani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 16, 2025 1:56


Amri mpya za kuhama zinazotolewa na jeshi la Israeli kwa wakazi wa Gaza walioko eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli zinazidi kuhatarisha maisha ya makumi ya maelfu ya watu ambao wameshahama mara kadhaa, wakiwemo wagonjwa wanaotakiwa kupata huduma za kusafisha damu mwilini kila wiki. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.

Habari za UN
15 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 15, 2025 10:57


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulika juhudi za kinamama wajawazito na wanao kuambatana wakihudhuria kliniki kwa ajili ya mimbasalama. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani.Takribani wapalestina 900 wameuawa katika wiki za hivi karibuni huko Ukanda wa Gaza, eneo linalokaliwa kimabavu na Israeli. wakihaha kupokea chakula. Msemaji wa Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa Thameen Al-Kheetan amewaeleza waandishi wa habari Geneva, Uswisi kuwa watu 674 kati yao waliuawa wakiwa kwenye maeneo ya Mfuko wa Kiutu wa Gaza, (GHF) unaoendeshwa na Israeli na Marekani.Wakati huo huo Bwana Al-Kheetan amezungumzia mauaji yanayoendelea Ukingo wa Magharibi ikiwemo Yerusalemu Mashariki akisema, “muathirika mdogo zaidi ni Laila Khatib mwenye umri wa miaka miwili. Alipigwa risasi ya kichwa na jeshi la Israeli akiwa nyumbani kwao kijijini Ash-Shuhada.”Na leo ikiwa siku ya kimataifa ya stadi kwa vijana Sangheon Lee, Mkurugenzi wa Ajira na Sera katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Ajira amesema …lazima tuhakikishe kuwa vijana wanapata ujuzi ambao ni wa maana, unaoweza kutumika katika mazingira mbalimbali, na unaotambuliwa na waajiri.Na kaika mashinani tunakupeleka jijini Nairobi, Kenya, ambako kupitia video iliyoandaliwa na washirika wetu Radio Domus, tunamsikia Dennis Mabuku, Mkuu wa Idara ya Usalama, Afya, Mazingira na Ubora katika kampuni ya BOC Kenya. Dennis anaeleza jinsi wanavyoichakata hewa ya kawaida na kuisafisha ili kupata  hewa safi ya oksijeni kwa ajili ya matumizi ya hospitali na mabaki mengine kwa ajili ya matumizi mengine ya viwandani.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Siha Njema
Baadhi ya hospitali nchini Kenya zinazalisha chakula kuwalisha wagonjwa

Siha Njema

Play Episode Listen Later Jul 15, 2025 10:17


Katika mkakati wa kuboresha lishe,hospitali zinatumia vipande vya ardhi zao kukuza chakula kuwalisha wagonjwa wao

Habari za UN
HLPF 2025: Jukwaa la UN kuangazia afya, usawa wa kijinsia na bahari katika juhudi za kufanikisha SDGs

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 14, 2025 1:57


Jukwaa la Kisiasa la Ngazi ya Juu la Maendeleo Endelevu, HLPF la mwaka huu wa 2025 limeanza leo hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ambapo wadau kutoka katika nyanja mbalimbali duniani wanakutana kujadili namna ya kuharakisha utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Notícia no Seu Tempo
#18 - Rumo a COP-30 entrevista Virgílio Gibbon, CEO da Afya

Notícia no Seu Tempo

Play Episode Listen Later Jul 14, 2025 37:44


“O Brasil tem um problema sério de distribuição de médicos, não de quantidade”, diz CEO da Afya. Era do Clima: Rumo à COP-30 é patrocinado por Ypê e apresentado por Ambipar, BNDES, Governo Federal, Governo do Pará, Hydro e JBS.See omnystudio.com/listener for privacy information.

Habari za UN
Trakoma au Vikope si tatizo tena la kiafya la umma nchini Burundi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 11, 2025 1:54


Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) leo Julai 11 limetangaza kwamba limeidhinisha Burundi kuwa imefanikiwa kuondoa ugonjwa wa macho unaofahamika kama trakoma au vikope kama tatizo la kiafya la umma, na kuifanya kuwa nchi ya nane katika Kanda ya Afrika ya WHO kufikia mafanikio haya muhimu. Anold Kayanda anafafanua zaidi kuhusu taarifa hii.

Habari za UN
11 JULAI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 11, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya afya nchini Burundi, na elimu ya upatanishi kwa jamii Ituri nchini DRC. Makala tunakupeleka nchini Kenya kumulika kilimo kichopatia riziki jamii na mashinani tunasalia hapa makao makuu kusikia ujumbe kuhusu haki za wasichana.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) leo Julai 11 limetangaza kwamba limeidhinisha Burundi kuwa imefanikiwa kuoandoa ugonjwa wa macho unaofahamika kama trakoma au vikope kama tatizo la kiafya la umma, na kuifanya kuwa nchi ya nane katika Kanda ya Afrika ya WHO kufikia mafanikio haya muhimu.Huko Djugu, jimboni Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wanawake wapatanishi waliopatiwa mafunzo na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO, wamewezesha kurejea kwa mazungumzo baina ya jamii za Ezekere na Mandro ambazo kwa miaka kadhaa zilikuwa zinazozana.Katika makala Sharon Jebichii anatupeleka  Kaunti ya Tana River huko Kenya kumulika juhudi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kitaifa ya Kusimamia Ukame (NDMA) na Serikali za Kaunti katika kilimo, ambayo imeleta mabadiliko na matumaini kwa jamii za wakulima.Na kaika mashinani leo ikiwa siku ya idadi ya watu duniani, nampisha Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na AFya ya Uzazi, Dkt. Natalia Kanem akizungumzia umuhimu wa takwimu katika kuboresha maisha ya wakazi wa dunia!Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

The Trauma Therapist | Podcast with Guy Macpherson, PhD | Inspiring interviews with thought-leaders in the field of trauma.

Veronique Mead, MD, MA is a former Dartmouth-affiliated assistant professor of family medicine and obstetrics. She retrained with a Master's degree in somatic psychotherapy from Naropa University and specialty training in pre and perinatal and other forms of trauma. For the past 25 years she has explored the scientific literature on how effects of trauma from the prenatal and other periods in a person's life can influence risk for autoimmune and other chronic illnesses. She shares the research on her blog Chronic Illness Trauma Studies.Euphrasia (Efu) Nyaki was born and raised in Tanzania where she earned a Bachelor of Science degree, trained as a science teacher, and later was trained as a healer using holistic methods. Efu is a Faculty Member of Somatic Experiencing®, a method founded by Dr Peter Levine, and a Professor of Family Constellation System Therapy by Hellinger Institute. In the last 31 years Efu has been living in Brazil facilitating trainings and Holistic therapy for trauma healing using Somatic Experiencing® and Family Constellation System Therapy. While living in Brazil, Efu has also been traveling in different countries such as India, Egypt, South Korea, China, Bolivia, Peru, Spain, Uruguay, Tanzania, Philippines, Sweden, Portugal, Spain  and Hong Kong facilitating trainings and workshops. After the pandemic situation, Efu has been giving international trainings, workshops, summits, webinars, podcasts, conferences, and individual therapy sessions and case consults through online. Efu is a co- founder of AFYA: Holistic Healing Center located in the northeast of Brazil. Afya supports many people from the local community as well as national and international individuals that approaches the center to receive support and healing.  Efu is a writer of the book titled: Trauma healing using Family Constellation System Therapy and Somatic Experiencing®.In This EpisodeVeronique:https://chronicillnesstraumastudies.com/https://lnk.bio/veroniquemeadFACEBOOK - https://www.facebook.com/chronicillnesstraumastudies/LINKED IN - https://www.linkedin.com/in/veroniquemeadillnessblog/YOUTUBE - https://www.youtube.com/channel/UCh-ng96Ji8rJSIJdXjCpCqA/videosPINTEREST - https://www.pinterest.com/chrillog/_created/INSTAGRAM - https://www.instagram.com/veroniquemead/Euphrasia:https://www.amazon.com/-/e/B0BYXYGQ1Vhttps://linktr.ee/efunyaki?utm_source=linktree_profile_share<sid=8eaad01c-d2dd-4e12-a35e-3b250748f25fYou can learn more about what I do here:The Trauma Therapist Newsletter: celebrates the people and voices in the mental health profession. And it's free! Check it out here: https://bit.ly/4jGBeSaThe Trauma Therapist Podcast:  I interview thought-leaders in the fields of trauma, mindfulness, addiction and yoga such as Peter Levine, Pat Ogden, Bessel van der Kolk and Bruce Perry. https://bit.ly/3VRNy8zBecome a supporter of this podcast: https://www.spreaker.com/podcast/the-trauma-therapist--5739761/support.

Siha Njema
Serikali ya Kenya yazingatia afya ya akili miongoni wa vikosi vya usalama

Siha Njema

Play Episode Listen Later Jul 10, 2025 9:36


Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen amesema polisi wenye changamoto za afya ya akili hawatafukuzwa kazi bali watapewa matibabu stahiki Kumeshuhudiwa hivi karibuni visa vya polisi kutumia silaha zao visivyo na utendakazi wao kukosolewa na raia pamoja na wanaharakati wa haki

Siha Njema
Je ni muda wa nchi za Afrika kujadili huduma ya kusaidiwa kufa ?

Siha Njema

Play Episode Listen Later Jul 2, 2025 10:12


Hivi majuzi bunge la Uingereza limepitisha mswada wa kuhalalisha huduma ya kusaidiwa mtu kufa Huduma hii itatekelezwa katika hospitali chini ya usimamizi wa wahudumu wa afya ,kwa watu wazima wanaougua magonjwa yasiyopona . Watalaam wa afya wanasisitiza kuwa hatua hiyo sharti mgonjwa kuridhia bila  kushinikizwa .

Habari za UN
WHO yasema vifaa vya matibabu vimeingia Gaza lakini bado havitoshi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 27, 2025 2:01


Hatimaye shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO limeweza kufikisha huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, shehena ya kwanza ya vifaa vya matibabu ikiwa ni mara ya kwanza tangu tarehe pili mwezi Machi mwaka huu. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
27 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 27, 2025 9:59


Hii leo jaridanitunaangazia msaada wa kibinadamu Gaza, na mauaji yaliyofanyika nchini Rwanda kati ya mwaka 1972 hadi 1973. Makala tunamulika inayochukuliwa nchini Kenya za kutekeleza haki za watu wenye ulemavu wa kutoona, na mashinani tunakwenda DRC, kulikoni?Hatimaye shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO limeweza kufikisha huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli, shehena ya kwanza ya vifaa vya matibabu ikiwa ni mara ya kwanza tangu tarehe pili mwezi Machi mwaka huu.Serikali ya Burundi inataka mauaji yaliyofanyika nchini mwake kati ya mwaka 1972 hadi 1973 yatambulike kimattaifa kama ni mauaji ya kimbari dhidi ya Wahutu, je kwa nini wito huo umekuja sasa.Katika makala leo ikiwa ni Siku ya Kimataifa ya viziwi wasioona, tunamulika hatua kubwa inayochukuliwa nchini Kenya katika kuhakikisha watoto wenye ulemavu wa kuona wanapata elimu bora na jumuishi. Mafunzo maalum yaliyofanyika jijini Nairobi yalileta pamoja wataalamu, walimu na mashirika ya maendeleo, kwa lengo la kuchochea elimu hiyo kwa njia ya michezo, kwa msaada wa Shirika la LEGO kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Kenya.Na mashinani, fursa ni yake Tom Fletcher, Mratibu wa Umoja wa mataifa wa Misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura akihitimisha ziara yake Goma Mashariki mwa DRC amezungumza na waandishi wa habari akieleza kuwa raia wameteseka vya kutosha na ukata unawazidishia madhila”Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari RFI-Ki
Hatua ya bunge la Uingereza kuruhusu huduma ya kusaidiwa kufa

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Jun 26, 2025 9:38


Bunge la Uingereza hivi majuzi liliidhinisha mswada wa huduma ya kusaidiwa kufa

Habari RFI-Ki
Hatua ya bunge la Uingereza kuruhusu huduma ya kusaidiwa kufa

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Jun 26, 2025 9:38


Bunge la Uingereza hivi majuzi liliidhinisha mswada wa huduma ya kusaidiwa kufa

Habari za UN
19 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 19, 2025 10:44


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina, ikiwa kesho tarehe 20 mwezi Juni ni siku ya kimataifa ya wakimbizi maudhui yakiwa Mshikamano na Wakimbizi, tunakupeleka kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyoko kaunti ya Turkana, kaskazini-magharibi mwa Kenya.Uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje FDI umeshuka kwa mwaka wa pili mfululizo, ukihatarisha mustakabali wa maendeleo katika nchi zinazoendelea, kwa mujibu wa wa ripoti iliyotolewa leo na kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD. ikionya kuwa pengo la mitaji linaongezeka huku sekta muhimu kama nishati safi na miundombinu zikikosa ufadhili wa muda mrefu.Katika siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono kwenye mizozo, Umoja wa Mataifa umetoa onyo kuwa ukatili wa kingono unazidi kutumika kama silaha ya vita huku wanawake na wasichana wakiathirika zaidi. Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA "Huu si uharibifu wa bahati mbaya  ni uhalifu wa kivita. Na waathirika lazima wawe kiini cha amani, haki, na urejeshwaji wa maisha."Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa  Duniani (WHO) leo limezindua mwongozo wake wa kwanza wa kimataifa wa kudhibiti ugonjwa wa seli mundu (sickle cell) wakati wa ujauzito, ukilenga kupunguza hatari za maisha kwa mama na mtoto. WHO inasema wanawake wenye ugonjwa huu wana hatari hadi mara 11 zaidi ya kufariki dunia wakati wa ujauzito. Hivyo huduma bora za afya zinaweza kuokoa maisha, lakini visa vya seli mundu vinaongezeka duniani, huku Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara ikichangia asilimia 80.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "KIHORO!.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Ujumuishaji wazazi wa kiume kwenye malezi ya watoto waleta manufaa kwa jamii

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 18, 2025 2:12


Katika Kaunti ya Kilifi, iliyoko pwani ya Kenya barani Afrika,  Mpango wa Kuboresha Lishe kwa kupatia jamii Fedha na Elimu ya Afya (NICHE) unasaidia kuwaelimisha wazazi kuhusu umuhimu wa baba na mama kulea watoto wao kwa pamoja, mradi unaotekelezwa na shirika la Umoja wa MAtaifa la kuhudumia watoto, UNICEF. Assumpta Massoi anamulika moja ya familia zilizonufaika.

Habari za UN
17 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 17, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika juhuddi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuwajumuisha watu wenye ulemavu kwenye masuala mbalimbali katika jamii, tukipata ujumbe wa Abeida Rashid Abdallah Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya jamii, jinsia wazee na watoto ya kisiwani humo amabye hivi karibuni alihudhuria mkutano wa CSW69.Watu wa Ukraine hawapaswi kulazimika kujificha kusaka hifadhi kila jua lizamapo, amesema Matthias Schmale, Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Misaada ya Kibinadamu nchini humo, kufuatia mashambulizi ya usiku wa kuamkia leo yaliyofanywa na jeshi la Urusi huko Kyiv, Odesa na miji mingine na kuua raia 12 na kujeruhi wengine zaidi ya 50.Mfumo wa afya wa huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israeli unazidi kudarimika, ukizidiwa uwezo kutokana na idadi kubwa ya watu waliouawa au kujeruhiwa karibu na maeneo ya usambazaji wa misaada, amesema Afisa wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya, WHO Dkt. Thanon Gargavanis. Akizungumza na waandishi wa habari Geneva, Uswisi kutokea Gaza, Dkt Gargavanis amesema “tuko katika hali mbaya kila siku ya uwezo wetu wa kutoa huduma kikamilifu au kukumbwa na janga kamili.Leo ni Siku ya Kimataifa ya Kupambana na kuenea kwa Jangwa na ukame na mwaka huu 2025 inasisitiza hatua za dharura kurejesha ubora wa ardhi na kusongesha maendeleo endelevu. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres katika ujumbe wake ametaka hatua zichukuliwe huku akionya kuwa uharibifu wa ardhi unazidi kuongezeka duniani kote na kugharimu uchumi wa dunia kwa takriban dola bilioni 880 kila mwaka, kiasi kikubwa kuliko uwekezaji unaohitajika kurekebisha hali hiyo.Na katika mashinani leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kupambana na jangwa na ukame inayobeba maudhui Rejesha ardhi, fungua fursa Meja Katja Dorner kutoka Boni kupitia video iyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa wa Kupambana na Kuenea kwa Jangwa UNCCD anatoa ujumbe kuhusu matumizi endelevu ya ardhi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Pamoja na ulinzi wa raia, walinda amani wa UN Ituri waendesha kampeni ya afya..

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 13, 2025 1:48


Huko jimboni Ituri, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Bangladesh wameendesha kampeni ya afya na kusaidia wakimbizi wa ndani kupata matibabu katika eneo hilo lililogubikwa na mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa waasi. Assumpta Massoi anasimulia zaidi.

Habari za UN
13 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 13, 2025 11:07


Katika Jarida la Umoja wa Mataifa leo Flora Nducha anakuleteaUmoja wa Mataifa walaani vikali mashambulizi ya Israel dhidi ya vinu vya nyuklia Jamhuri ya IranHuko Ituri Mashariki mwa DRC walinda amani wa Mpango wa Umoja wa Mataifa MONUSCO watoa huduma za afya kwa wananchiLeo ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu watu wenye Ualibino katika makala utamsikia mbunge kmwenye ualibino kutoka nchini TanzaniaNa mashinani utasiki ujumbe wa nini kifanyike kuhakikisha ndoto za watu wenye ulemavu zinatimia Afrika

Habari za UN
27 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 27, 2025 9:56


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kuangazia siku ya familia iliyokutanisha wadau wakimulika pamoja na mambo mengine nafasi ya vyombo vya habari katika kuimarisha malezi na makuzi ya mtoto.Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura OCHA hii leo imesema wakati mpango tata wa Israeli wa kugawa misaada kwenye eneo la Palestina la Gaza linalokaliwa kimabavu na Israeli ukiendelea, Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine tena umesihi mamlaka za Israeli kuruhusu ongezeko la kiwango cha misaada ya kufikia walengwa kwenye eneo hilo lililozingirwa ili kuepusha uhaba wa chakula..Kadiri nchi zinavyokumbwa zaidi na majanga ya asili, gharama halisi za majanga ni mara 10 zaidi ya ilivyodhaniwa hapo awali, zikiwa na athari mbaya zaidi katika sekta za afya, makazi, elimu na ajira, imesema Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kupunguza hatari za majanga katika ripoti iliyochapishwa Jumanne.Nchini Namibia, makazi yaliyojengwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu na Afya ya Uzazi, UNFPA kwa ajili ya wajawazito wanaoishi maeneo ya mbali kusubiria ili kujifungua kwa usalama, yamesaidia kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga.Na katika mashinani, kupitia video iliyoandaliwa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani Sudan Kusini UNMISS, tunakutana na Mary Aban Akon, mkazi wa kijiji cha Hai Matar huko Sudan Kusini. Yeye ni miongoni mwa wakimbizi waliorejea nyumbani baada ya kupatiwa makazi mapya yaliyojengwa kwa msaada wa mashirika ya kibinadamu chini ya mradi uliofadhiliwa na Umoja wa Mataifa na wadau wake.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
20 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 20, 2025 12:20


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika wafugaji wa nyuki nchini Tanzania leo ikiwa ni siku ya nyuki duniani iliyopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 20 Desemba mwaka 2017 kupitia azimio namba A/72/211.Baada ya miaka mitatu ya majadiliano, leo katika Mkutano wa Kimataifa wa Afya unaoendelea Geneva, Uswisi, nchi zimepitisha rasmi makubaliano ya kihistoria ya kuzuia, kujiandaa, na kukabiliana vyema na majanga ya magonjwa kwa siku zijazo. Taratibu zote zitakapopitishwa na angalau nchi 60, mkataba utaanza kutumika rasmi mwakani.Kutokana na mamlaka za Israeli kulegeza kwa muda mzingiro uliodumu kwa wiki 11, angalau sasa matumaini kidogo yamerejea Gaza, yameeleza leo mashirika ya Umoja wa Mataifa. Msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya dharura, OCHA, Jens Laerke amesema tayari wamepata ruhusa ya kuyavusha malori matano yaliyokuwa yamezuiliwa jana.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP limetahadharisha  leo kwamba bila ufadhili zaidi, huenda katika muda wa wiki chache zijazo likalazimika kusitisha msaada wa chakula kwa takribani nusu ya watu linaowahudumia kwa sasa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.Na katika mashinani, fursa ni yake Hanan Al-Dayya, Mkimbizi wa ndani katika ukanda wa Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli, akisimulia  madhara ya mashambulizi yanayoendelea kutoka Israeli.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
WHO: Mkutano wa 78 wa Baraza la Afaya Duniani umeng'oa nanga Geneva

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 19, 2025 2:18


Wajumbe kutoka kote duniani wamekusanyika mjini Geneva, Uswisi, kwa ajili ya Mkutano wa 78 wa Baraza la Afya Duniani (WHA78) unaofanyika kuanzia leo Mei 19 hadi 27 Mei mwaka huu. Kaulimbiu ya mkutano wa mwaka huu ni “Ulimwengu Mmoja kwa Afya” inaakisi dhamira ya pamoja ya kujenga mfumo wa afya wa kimataifa ulio imara, jumuishi na thabiti. Flora Nducha amefuatilia na hapa anatupasha zaidi

Habari za UN
19 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 19, 2025 11:08


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya afya, na wakimbizi wa Syria wanaorejea nchini mwao. Makala tukwenda nchini Kenya kumulika ufukaji wa nyuki, na mashinani tunakuletea ujumbe wa Katibu Mkuu wa IMO kuhusu Siku ya Kimataifa ya wanawake mabaharia.Wajumbe kutoka kote duniani wamekusanyika mjini Geneva, Uswisi, kwa ajili ya Mkutano wa 78 wa Baraza la Afya Duniani (WHA78) unaofanyika kuanzia leo Mei 19 hadi 27 Mei mwaka huu.Tangu kuangushwa kwa utawala wa aliyekuwa Rais wa Syria Bashar al Assad aliyekuwa madarakani kwa zaidi ya muongo mmoja, wananchi wa Syria wamekuwa wakimiminika kurejea nchini mwao ambapo takwimu za sasa zinaonesha zaidi ya Wasyria 500,000 wamerejea kutoka nchi jirani. Mmoja wa waliorejea ni Babu Jassim na Leah Mushi anatuletea simulizi yake.Katika makala tunaelekea Kajiado nchini Kenya, ambako juhudi za utunzaji mazingira kupitia mradi wa ufugaji wa nyuki unaofadhiliwa na shirika la misaada la Marekani USAID kwa kushirikiana na idara ya misitu ya Kenya KFS hazichangii tu katika kukuza uchumi wa jamii, bali pia kulinda mazingira. Kupitia Makala hii iliyoandaliwa na Sharon Jebichii, Bwana Mureithi mmoja wa wanufaika wa mradi huo anaanza kwa kueleza mafanikio yao.Nakatika mashinani, fursa ni yake Arsenio Dominguez, Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Usafirishaji Majini, IMO akitoa ujumbe wa ujumuishaji na usawa wa kijinsia wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya wanawake mabaharia ambayo huadhimishwa tarehe 18 mwezi Mei kila mwaka.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
WHO: Magonjwa yasiyo ya kuambukiza yanachangia nusu ya vifo chini ya umri wa miaka 70

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 16, 2025 2:14


Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) ya takwimu za afya duniani iliyochapishwa jana Mei 15 ikionesha athari kubwa zaidi za kiafya zilizosababishwa na janga la COVID-19 kuhusu vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla, imeweka wazi kuwa katika kipindi cha miaka miwili pekee, kati ya mwaka 2019 na 2021, matarajio ya kuishi yalipungua kwa mwaka mmoja na miezi nane  ikiwa ni maporomoko makubwa zaidi katika historia ya hivi karibuni hali iliyobatilisha mafanikio ya afya yaliyopatikana kwa muongo mmoja.

Habari za UN
16 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 16, 2025 12:25


Hii leo jaridani tunaangazia uhakika wa chakula, na takwimu za afya za janga la COVID-19 kusababisha vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla. Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani nchini DRC, kulikoni?Ukosefu wa uhakika wa kupata chakula na utapiamlo kwa watoto uliongezeka kwa mwaka wa sita mfululizo mwaka 2024, na kuwatumbukiza mamilioni ya watu karibu na baa la njaa, huku wengine wakiepuka kutokana na misaada ya kimkakati. Imesema Ripoti ya Kimataifa kuhusu Janga la Chakula (GRFC) iliyotolewa leo huko Roma, Italia na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO.Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) ya takwimu za afya duniani iliyochapishwa jana Mei 15 ikionesha athari kubwa zaidi za kiafya zilizosababishwa na janga la COVID-19 kuhusu vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla, imeweka wazi kuwa katika kipindi cha miaka miwili pekee, kati ya mwaka 2019 na 2021, matarajio ya kuishi yalipungua kwa mwaka mmoja na miezi nane  ikiwa ni maporomoko makubwa zaidi katika historia ya hivi karibuni hali iliyobatilisha mafanikio ya afya yaliyopatikana kwa muongo mmoja.Katika makala Leah Mushi anatupeleka nchini Tanzania kusikia namna wanawake wenye ulemavu walivyoweza kujikwamua kutoka kwenye changamoto mbalimbali ikiwemo za kiuchumi na kuchangamkia fursa za uongozi.Na katika fursa ni yake Bernadette Kambonesa, mkimbizi wa ndani kutoka kijiji cha Bogoro, jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akizungumzia manufaa yatokanayo na uwepo wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini humo (MONUSCO).Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Akina mama wakimbizi katika ukanda wa Gaza wanataabika bila huduma za afya

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 14, 2025 2:23


Huko Gaza, eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli, wanawake na wasichana wakiwemo wanawake wajawazito na wale waliojifungua, wamelazimika kukimbia makazi yao na wanaishi katika mazingira hatarishi bila huduma za msingi za kiafya. Sharon Jebichii anaangazia simulizi ya mama mmoja, mkazi wa kambi ya wakimbizi ya Jabalia, Kaskazini mwa Gaza, ambaye alijifungua akiwa amekimbia vita,na sasa anahangaika kumtunza binti yake mchanga.

Habari za UN
12 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 12, 2025 11:43


Hali mbaya ya hewa na mabadiliko ya tabianchi vyaliacha hoi bara la Afrika yaonya WMO.WHO yahaha kukabiliana na kipindupindu Angola.Makala Sharon Jebichii anatupeleka nchini Kenya, kumulika masuala ya wasichana katika ICT.Mashinani leo inaangazia ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa wiki ya usalama barababarni.

Habari za UN
WHO na vita dhidi ya kipundupindu Angola.

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 12, 2025 2:15


Tangu Januari mwaka huu 2025 nchini Angola, ugonjwa wa kipindupindu umesambaa katika majimbo 17 kati ya 21 ya nchi hiyo. Mlipuko huu tayari umesababisha karibu vifo 600 linaeleza Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO. António Catunda, ni Msimamizi wa Uhamasishaji wa Afya katika kituo cha afya cha Sambizanga jimboni Luanda unakopatikana mji Mkuu wa Angola. Kupitia video iliyoandaliwa na WHO, anaielezea hali ilivyo.

Habari za UN
06 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 6, 2025 12:03


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha hapa makao makuu ambako Idhaa hii Dokta Willis Ochieng kutoka Kenya aliyehudhuria ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na masuala ya kilimo na maendeleo. Pia tunakuletea muhtasari wa habari, na mashinani tunakwenda Ghana.Ukuaji wa maendeleo ya binadamu – yanayopimwa kwa uhuru na ustawi wa watu – umeendelea kuwa wa kasi ndogo tangu mshtuko mkubwa wa janga la COVID-19 lakini kuna matumaini makubwa kwamba Akili Mnemba au AI, ikiwa itatumika kwa njia sahihi, inaweza kuwa chombo chenye nguvu cha kuboresha maisha ya mamilioni ya watu. Hii ni kwa mujibu wa Ripoti ya kila mwaka ya Maendeleo ya Binadamu iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo duniani, UNDP.Kulengwa kwa hospitali ya Médecins Sans Frontières nchini Sudan Kusini kunaweza kuwa uhalifu wa kivita imeeleza leo Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu Sudan Kusini kufuatia mashambulizi ya angani yaliyotekelezwa dhidi ya hospitali ya Médecins Sans Frontières (MSF) huko Old Fangak, Jimbo la Jonglei mapema majuzi asubuhi ya Jumamosi na kusababisha vifo vya takribani raia saba na kujeruhi wengine. Shambulio hilo lilifanyika baada ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Sudan Kusini (SSPDF) kutoa onyo la kufanya shambulizi iwapo dai lao la kuachiliwa meli zao zilizotekwa halitatekelezwa.Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, iliyotolewa leo imeonesha jinsi mahali mtu anakozaliwa kulivyo na mchango katika maisha yake. Ripoti inasema, “mahali mtu anakozaliwa huweza kuamua kama ataishi zaidi ya miongo mitatu kuliko mtu mwingine aliyezaliwa katika nchi yenye hali duni za makazi, elimu na fursa za ajira.”Na mashinani leo nampa fursa Dorcas Awortwe, Naibu Mkurugenzi wa Tume ya Maendeleo ya Kanda ya Kati kutoka Ghana, aliyeshiriki kwenye mkutano wa jukwaa la watu wa asili hapa Makao Makuu wiki iliyopita anazungumzia changamoto zinazowakabili watu wa asili katika jamii yake na ombi lake kwa Umoja wa Mataifa.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Mkunga nchini Tanzania atoa wito wa uwekezaji kwenye fani hiyo

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 5, 2025 2:07


Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya wakunga, tunakwenda nchini Tanzania kummulika mkunga ambaye alinusuru maisha ya wajawazito wawili wakati wa mafuriko makubwa ya Novemba 2023 wilayani Hanang, mkoani Manyara, kaskazini mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, ikiwa ni ushuhuda wa majukumu mazito yanayokumba wakunga. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
Ripoti kuhusu Mpox yazitaja nchi 11 za Afrika, Ulaya, China na Amerika nao wamo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 30, 2025 2:03


Maambukizi ya ugonjwa wa mpox kutokana na aina ya virusi vya monkeypox clade Ib /ˈmʌŋ.ki.pɑks kleɪd one bee/ (MPXV) yanaendelea kuripotiwa hasa barani Afrika, ambapo mataifa kumi na moja yameripoti maambukizi ya ndani ya jamii katika kipindi cha wiki sita zilizopita. Hiyo kwa mujibu wa ripoti 51 ya Shrika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO kuhusu hali ya mlipuko wa mpox katika nchi mbalimbali duniani. Anold Kayanda amefuatilia ripoti hiyo na anatufafanulia kwa ufupi. 

Habari za UN
Kampuni Indonesia zachukua hatua kuimarisha usalama na afya pahala pa kazi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 28, 2025 3:32


Huko mashariki mwa Indonesia, kampuni za usindikaji samaki za PT Chen Woo Fisheries na PT Harta Samudra zimeongeza motisha wa kazi miongoni mwa wafanyakazi wake baada ya kuchukua hatua za kuimarisha usalama na afya pahala pa kazi. Hatua hizo ambazo zimeweka mazingira ya staha pahala pa kazi zinafuatia mradi wa pamoja wa shirika la Umoja wa Mataifa la kazi, ILO na Umoja wa Kampuni za Uvuvi na Usindikaji Samaki nchini Indonesia, AP2H1. Je nini kilifanyika na hali sasa iko vipi? Assumpta Massoi anafafanua zaidi katika makala hii inayoletwa leo hii ikiwa ni siku ya kimataifa ya usalama na afya pahala pa kazi.

Habari za UN
AI na teknolojia za kidijitali zaweza kuwa chachu ya kuhakikisha afya na usalama kazini - ILO

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 28, 2025 2:58


Leo ni Siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya Kazini mwaka huu ikibeba maudhui “Mapinduzi ya usalama na afya Kazini: Nafasi ya Akili mnemba na teknnolojia ya kidijitali mahala pa kazi” lengo likiwa kudhihirisha nguvu ya AI na teknolojia zinapotumika vyema zinaweza kuleta mabadiliko kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kazi duniani ILO. Flora Nducha na taarifa zaidi.

Habari za UN
Nzi, panya watapakaa Gaza, UNRWA yahaha kuchukua hatua

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 1:42


Hali si hali huko Ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli ambako wakimbizi wa ndani wanakabiliwa na hatari za kiafya ambako panya na wadudu kama vile viroboto na  nzi wamesambaa kutokana na mlundikano wa taka na  ukosefu wa huduma muhimu kama vile maji safi na salama. Assumpta Massoi anaelezea zaidi.

Habari za UN
Wanachama wa WHO wachukua hatua za kujenga uwezo dhidi ya majanga yajayo ya afya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2025 1:50


Baada ya zaidi ya miaka mitatu ya mazungumzo ya kina, hatimaye leo Geneva, Uswisi, Nchi Wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) zimekamilisha rasimu ya makubaliano ambayo itawasilishwa katika Mkutano wa Afya Duniani mwezi Mei mwaka huu wa 2025. Pendekezo hili linakusudia kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na vitisho vya majanga ya kiafya yajayo. Anold Kayanda amefuatilia anatujulisha zaidi.  "Leo mataifa ya dunia yameandika historia mjini Geneva," amesema Dkt. Tedros Ghebreyesus, Mkurugenzi Mkuu wa WHO na kuongeza kwamba, "kwa kufikia makubaliano kuhusu Mkataba wa Majanga ya kiafya, siyo tu wameweka msingi wa makubaliano ya kizazi hiki yanayolenga kuifanya dunia kuwa salama zaidi, bali pia wameonesha kuwa ushirikiano wa kimataifa bado uko hai, na kwamba hata katika dunia iliyogawanyika, mataifa bado yanaweza kushirikiana kutafuta mwafaka na mwitikio wa pamoja dhidi ya vitisho vya pamoja.” Mwezi Desemba mwaka 2021, wakati janga la COVID-19 likiwa limepamba moto, Nchi Wanachama wa WHO ziliunda Mamlaka ya Majadiliano ya Kiserikali ili kuandaa na kujadiliana kuhusu mkataba, makubaliano au nyenzo nyingine ya kimataifa, chini ya Katiba ya WHO, kwa ajili ya kuimarisha uzuiaji, maandalizi na hatua dhidi ya majanga ya kiafya. Mapendekezo katika rasimu iliyotayarishwa ni pamoja na: kuchukua hatua madhubuti za kuzuia majanga ya kiafya kwa kutumia mbinu ya Afya Moja; kujenga uwezo wa utafiti na maendeleo katika maeneo mbalimbali duniani; kuwezesha uhamishaji wa teknolojia na maarifa, ujuzi na utaalamu unaohusiana na uzalishaji wa bidhaa za afya zinazohusiana na majanga ya kiafya; kuchukua hatua madhubuti za kuimarisha maandalizi, utayari na uimara wa mifumo ya afya; na kuanzisha mtandao wa kimataifa wa mnyororo wa usambazaji na vifaa. Pendekezo hilo linathibitisha mamlaka ya nchi kushughulikia masuala ya afya ya umma ndani ya mipaka yao bila kuingiliwa.

Habari za UN
16 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2025 9:57


Hii leo jaridani Assumpta Massoi anamulika masuala ya afya hususan harakati za kukabiliana na majanga yajayo ya afya;  wakimbizi huko Zambia ambako sera jumuishi zimewajengea uwezo; Jukwaa la vijana na mchango wa sanaa kwenye usawa na utengamano. Baada ya zaidi ya miaka mitatu ya mazungumzo ya kina, hatimaye leo huko mjini Geneva, Uswisi, nchi wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) zimekamilisha rasimu ya makubaliano ambayo itawasilishwa katika Mkutano wa Afya Duniani mwezi ujao wa Mei. Pendekezo hili linakusudia kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kuzuia, kujiandaa na kukabiliana na vitisho vya majanga ya kiafya yajayo. Anold Kayanda amefuatilia anatujulisha zaidi.Zambia inaendelea kuwahifadhi zaidi ya wakimbizi 106,000, wengi wao wakiwa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Burundi, pamoja na wakimbizi wa zamani kutoka Rwanda na Angola. Limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, likiongeza kwamba kwa kuzingatia sera jumuishi ya Zambia, taifa hilo linakuza mshikamano na wakimbizi na kuwawezesha kujitegemea kupitia makazi maalum na ushirikiano na jamii za wenyeji. Flora Nducha na taarifa zaidi.Jukwaa la Vijana la Baraza la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ECOSOC) limeanza jana hapa katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa na litamalizika kesho tarehe 17 Aprili. Vijana kutoka nchi mbalimbali wamehudhuria jukwaa hilo akiwemo Kapwani Kavenuke kutoka nchini Tanzania ambaye amehojiwa na Leah Mushi wa Idhaa hii. Kapwani anaanza kwa kueleza  umuhimu wa mikutano hii.Gislain Kalwira, Muandaaji wa tamasha la Musika na Kipaji  nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC linalofanyika kila mwaka kuleta pamoja wasanii wa kike na wa kiume wa fani mbalimbali, kwa kutambua kuwa jana dunia imeadhimisha siku ya sanaa duniani. Kalwira kupitia video iliyochapishwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani  nchini DRC, MONUSCO, anafafanua mantiki ya tamasha hilo na kujenga usawa kijinsia.

Habari za UN
Vita Sudan yamsababishia Walaa tatizo la afya ya akili

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 14, 2025 3:46


Tarehe 15 mwezi April imwaka 2023 wananchi wa Sudan hususan mji mkuu Khartoum waliamshwa na mapigano kati ya jeshi la serikali SAF na wanamgambo wa kikosi cha msaada wa haraka RSF. Hadi leo hii mapigano hayo yanazidi kushika kasi na raia wanafurushwa makwao. Miongoni mwao ni watoto ambao zahma wanayokutana nayo sio tu kufurushwa bali pia changamoto ya afya ya akili. Tayari shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limeona shida hiyo na limeanza kuchukua hatua kama anavyosimulia Assumpta Massoi kwenye makala hii. 

Habari za UN
10 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 10, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo Idhaa hii inazungumza na Mwenyekiti wa Tanzania Women Ecocomic Empowerment Network (TAWEN), ambaye pia ni mchumi mbobezi Bi. Janet Zebedayo Mbene. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na neno la wiki.Shukran Anold na leo tunaanzia huko Geneva Uswisi ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limetoa muongozo wake wa kwanza duniani wa kutambua, kutoa matibabu kwa haraka na matibabu ya muda mrefu kwa ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo.Nchini Chad katika mpaka wake na Sudan ambako Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR Filippo Grandi ametembelea na kuzungumza na wakimbizi wa Sudan pamoja na kujionea hali zao wakati huu ambapo wamepunguza kutoa chakula, malazi , maji na dawa na kauli yake ikawa moja tu, “Ninatoa wito kwa wafadhili, tafadhali msipunguze msaada kwa wathirika wa vita vya Sudan.”.Taarifa ya pamoja ya mashirika ya kibinadamu inayotolewa kila baada ya wiki mbili imeeleza kuhusu hali katika Ukanda wa Gaza inasema kuwa watu wanazidi kuuwawa na kujeruhiwa. Kwa zaidi ya mwezi sasa hakuna misafara ya misaada inayoruhusiwa kuingia Gaza. Watu kulazimishwa kuhama kinguvu kunaendelea, makazi ya wakimbizi yamefikia pomoni, huduma za usafi na kujisafi nazo ni mbaya.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "FIFILIZA"Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Hatua za haraka zinahitajika sasa kuzuia vifo na kulinda afya ya wanawake na wasichana: UN

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 7, 2025 2:40


Leo ni Siku ya Afya Duniani ambayo mwaka huu inangazia suala muhimu kwa afya ya dunia, changamoto maalum wanazokumbana nazo wanawake na wasichana lakini pia vifo vya watoto wachanga, na ili kuhakikisha changamoto hizo zinashughulikiwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO limezindua  kampeni ya mwaka mzima ya “Mwanzo wenye afya ni mustakbali wenye matumaini”. Flora Nducha anafafanua zaidi.

Habari za UN
07 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 7, 2025 11:47


Hii leo jaridani tunaangazia makumbusho ya mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi nchini Rwanda mwaka 1994, na Siku ya Afya Duniani. Makala inamulika nafasi ya michezo katika kusongesha amani na maendeleo, na mashinani tunakwenda nchini Kenya, kulikoni?Dunia inapokumbuka miaka 31 tangu mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi nchini Rwanda mwaka 1994, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametuma ujumbe mzito wa maombolezo na onyo, akitaka mshikamano wa kimataifa kupambana na ongezeko la chuki, mgawanyiko, na misimamo mikali kupitia mifumo ya kidijitali.Leo ni Siku ya Afya Duniani ambayo mwaka huu inangazia suala muhimu kwa afya ya dunia, changamoto maalum wanazokumbana nazo wanawake na wasichana lakini pia vifo vya watoto wachanga, na ili kuhakikisha changamoto hizo zinashughulikiwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO limezindua  kampeni ya mwaka mzima ya “Mwanzo wenye afya ni mustakbali wenye matumaini”..Makala inamulika nafasi ya michezo katika kusongesha amani na maendeleo, ambapo Assumpta Massoi amezungumza na Rosemary Mwaipopo, Muasisi na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la kiraia la DaySpring Foundation nchini Tanzania. Yeye alikuwa ni miongoni mwa washiriki wa Mkutano wa 69 wa Hali ya Wanawake duniani, CSW69 uliofanyika hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa mwezi uliopita wa Machi.Na mashinanileo ikiwa leo ni siku ya afya duniani, kupitia mahojiano yaliyofanikishwa na washirika wetu Radio Domus, fursa ni yake Padri Thaddeus Mukaya wa kanisa la katoliki la Parokia ya Embulbul ambalo pamoja na wadau wengine waliandaa huduma za bure za matibabu kwa wenyeji wa eneo hilo ili kusaidia jamii ambazo haziwezi kujimudu kimaisha.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!