Podcasts about elimu

  • 39PODCASTS
  • 462EPISODES
  • 20mAVG DURATION
  • 1WEEKLY EPISODE
  • May 30, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about elimu

Latest podcast episodes about elimu

Habari za UN
30 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 30, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya elimu kwa watoto mashariki mwa DRC na Mkutano wa pili wa Baraza Kuu la Makazi la shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani UNHABITAT unaofunga pazia leo jijini Nairobi Kenya. Makala inaturejesha nchini DRC na mashinani inatupeleka katika bonde la Ziwa Victoria, kulikoni?Wakati ghasia zinazoendelea huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC zinaripotiwa kusababisha zaidi ya watoto milioni 1.8 kutokuweko shuleni, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF nchini humo linajitahidi kwa udi na uvumba kuhakikisha watoto wanapata elimu kwani ni haki yao ya msingi.Mkutano wa pili wa siku mbili wa Baraza Kuu la Makazi la shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi Duniani UNHABITAT leo unafunga pazia jijini Nairobi Kenya. Baraza hilo linalofanyika kila baada ya miaka minne ni chombo cha juu kabisa duniani cha kufanya maamuzi kuhusu maendeleo ya miji endelevu na limewaleta pamoja wawakilishi kutoka nchi zote 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa pamoja na wadau mbalimbali wa amendeleo ya miji.Makala inakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC hususan jimboni Kivu Kaskazini katika kitongoji cha Mavivi kuwasikia walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania,kikosi cha 11, TANZBATT11, wanaohudumu katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO wakielezea sio tu majukumu yao, bali pia wanajivunia kile wanachofanya kwa kuzingatia Mei 29 imeadhimishwa siku ya kimataifa ya walinda amani.Na katika fursa ni yake Mhandisi Coletha Ruhamya, Naibu Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria, Mradi unaofanikishwa na Benki ya Dunia ambao unakabiliana na masuala ya usafi wa mazingira katika ziwa hilo. Anaeleza umuhimu wa usimamizi endelevu wa bonde hilo kote nchini Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda na Burundi chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Alice Kamau: Asante UNICEF na wadau ndoto ya mwanangu ya elimu imerejea

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 28, 2025 2:48


Mradi wa "operesheni rejea shuleni" unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF kwa ushirikiano na wizara ya elimu ya Kenya, shirika liliso la kiserikali la Hapag Lloyd na wadau wengine kwa kuzipa fedha familia zisizojiweza kuendesha shughuli za kiuchumi, umerejesha mautumaini ya elimu kwa mamia ya watoto katika Kaunti ya Kwale Pwani ya Kenya  ambao waliacha shule sababu ya umasikini. Flora Nducha na maelezo zaidi.

Habari za UN
28 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 28, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia haki za binadamu nchini Ukraine na upatikanaji wa elimu nchini Kenya. Makala tunakupeleka nchini Sudan Kusini, na amashinani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kulikoni?Tume Huru ya Umoja wa Mataifa ya Uchunguzi kuhusu Ukraine imehitimisha kwamba vikosi vya kijeshi vya Urusi vimetenda uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu, hasa mauaji, kupitia mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (drones) yaliyoelekezwa dhidi ya raia.Mradi wa "operesheni rejea shuleni" unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto UNICEF kwa ushirikiano na wizara ya elimu ya Kenya, shirika liliso la kiserikali la Hapag Lloyd na wadau wengine kwa kuzipa fedha familia zisizojiweza kuendesha shughuli za kiuchumi, umerejesha mautumaini ya elimu kwa mamia ya watoto katika Kaunti ya Kwale Pwani ya Kenya  ambao waliacha shule sababu ya umasikini.  Katika makala ikielekea siku ya walinda amani kesho Mei 29, tunamulika harakati za walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini SUdan Kusini za kulinda raia na mwenyeji wako katika makala hii iliyoandaliwa kupitia video ya ujumbe wa  Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani Sudan Kusini, UNMISS ni Sharon Jebichii.Na katika mashinani huku machafuko yakiendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, wafanyakazi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR wako mashinani mjini Goma na maeneo mengine yaliyoathirika ili kutoa msaada muhimu, ikiwa ni pamoja na kufanikisha nia ya wakimbizi wanaorejea nchini mwao Rwanda. Raab na Ruusi ni baadhi yao.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Ujumbe wa Ernest Makulilo kuhusu siku ya Kimataifa ya Kitabu na Haki Miliki

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 3:31


Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Kitabu na Haki Miliki ambapo kila mwaka tarehe kama ya leo siku hii huadhimishwa ili kutambua nguvu ya vitabu kama daraja kati ya vizazi na vizazi na tamaduni mbalimbali. Katika makala hii Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza na mwandishi maarufu wa vitabu vya elimu, Uchumi na uhamiaji, Ernest Makulilo mkazi wa Marekani katika jimbo la Missouri, kuhusu siku ya leo iliyoanzishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO mnamo mwaka 1995.

Habari za UN
09 APRILI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 9, 2025 12:09


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu katika katika jimbo la Upper Nile nchini Sudan, na haki za binadamu na watu kutoweka kwa wingi nchini Sudan. Makala inatupeleka nchini Kenya na Mashinani tunakwenda Gaza, kulikoni?Nchini Sudan Kusini, familia zilizo kwenye hali duni katika eneo la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo ziko katika hali tete sana huku mapigano yakizidi kuongezeka na njaa ikikaribia kufikia viwango vya juu kabisa, limeonya leo Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP).Wakati hofu ikiendelea kuhusu watu kutoweka kwa wingi nchini Sudan, Mtaalam maalum wa Umoja wa Mataifa aliyeteuliwa na Ofisi ya Haki za Binadamu OHCHR anayehusika na haki za binadamu nchini humo Radhouane Nouicer ametoa wito wa dharura kuhusu hali ya raia waliokwama katika vita kubwa nchini humo.Katika inatupeleka nchini Kenya kufuatilia simulizi ya Shalyne Kaputa, mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 16 kutoka kaunti ya Turkana ambaye tofauti na shangazi yake ambaye hakuweza kuendelea na elimu  yake kutokana na kukosa karo, yeye anasoma elimu ya sekondari sasa ili aweze kutimiza ndoto yake ya kuwa mwandishi wa habari. Yote yanawezekana kutokana na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kwa msaada wa shirika la Norway la Maendeleo NORAD na wadau wengine.Na mashinani fursa ni yake Lama, mtoto mwenye umri wa miaka 10 kutoka Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli ambaye anasimulia maumivu na juhudi za kila siku za kutafuta maji mapigano yakiwa ni mwaka mmoja na nusu sasa. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) linatoa msaada mkubwa kwa familia na watoto wa Gaza kwa kusambaza maji salama.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!  

Habari za UN
UNICEF na wadau Kenya waelekea kufanikisha ndoto ya Sharlyne kuwa mwandishi wa habari

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 9, 2025 4:24


Kutana na Shalyne Kaputa, mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 16 kutoka kaunti ya Turkana, Kaskazini-Magharibi mwa Kenya. Tofauti na shangazi yake, ambaye hakuweza kuendelea na elimu  yake kutokana na kukosa karo, yeye anasoma elimu ya sekondari sasa ili aweze kutimiza ndoto yake ya kuwa mwandishi wa habari. Yote yanawezekana kutokana na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kwa msaada wa shirika la Norway la Maendeleo NORAD na wadau wengine. Je ni usaidizi gani wanapatiwa? Ungana na Assumpta Massoi.

Habari za UN
Chad: Wanakikundi watumia faida ya biashara yao kuanzisha shule

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 26, 2025 3:33


Nchini Chad, wanawake wanakikundi cha kutengeneza sabuni na mafuta ya kupata mwilini wameamua kuchukua hatua ili umamuma wa kutokujua kusoma na kuandika ambao umewakumba wao, usiwakumbe pia watoto wao wa kike. Wanakikundi hao wa APROFiCA wanaopata ufadhili kutoka Benki ya Dunia wameona ni vema kuchukua hatua hiyo ili kufanikisha lengo namba 4 la Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs la Umoja wa Mataifa kuhusu elimu, kwani elimu ni mkombozi kwa binadamu. Je wamefanya nini? Assumpta Massoi anafafanua kupitia video ya Benki ya Dunia.

Habari za UN
18 MACHI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 18, 2025 11:24


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kumulika elimu ya mtoto wa kike kama moja ya nguzo muhimu katika jamii ukizingatia malengo endelevu ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa.Pia tunakuletea muhtasari wa habari na sauti za mashinani.Viongozi wa Umoja wa Mataifa leo wamelaani vikali mashambulizi ya anga ya Israel huko Ukanda wa Gaza na kutoa wito kwa kusitisha uhasama mara moja. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameonesha mshtuko na wasiwasi mkubwa kuhusu mashambulizi hayo akitoa wito kwa pande zote kuheshimu usitishaji mapigano, kurejesha misaada ya kibinadamu bila vikwazo, na kuhakikisha kuachiliwa mara moja na bila masharti kwa mateka waliobaki.Ghasia zinazoendelea katika kaunti za Nasir, Ulang, na Baliet, Jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini zimeathiri vibaya jamii za eneo hilo na shughuli za kibinadamu, na kusababisha watu takriban 50,000 kukimbia makazi yao tangu mwishoni mwa mwezi Februari amesema Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, Bi. Anita Kiki Gbeho, na kuonesha wasiwasi mkubwa kuhusu hali hiyo, akiwataka wahusika wote kuheshimu raia, wahudumu wa misaada, na miundombinu muhimu.Siku ya 7 ya mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, Tanzania ina tukio la kando kuonesha harakati za kumwinua mwanamke kiuchumi na miongoni mwa wazungumzaji ni Tully Esther Mwambapa, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Benki ya CRDB nchini Tanzania ambaye ameieleza Idhaa ya Umoja wa Mataifa ujumbe wake kwenye tukio hilo kuhusu walivyosaidia wanawake kuondokana na kikwazo cha kukosa dhamana wanapotaka kujikwamua kiuchumi.Na katika mashinani tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa katika mkutano unaoendelea wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani CSW69, kusikia ujumbe wa mshiriki wa kuwaunga mkono wasichana na wanawake na kutokomeza ndoa za utotoni.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

VOA Express - Voice of America
Wizara ya elimu Kenya imeondoa somo la Hesabu na sayansi kwa wanafunzi wa shule za sekondari kwamba sio lazima kucukua masomo hayo. - Machi 14, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 14, 2025 29:59


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Habari za UN
Haki Elimu - Ujumbe wetu mkuu kwenye CSW69 ni elimu kwa mtoto wa kike

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 12, 2025 3:40


Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, (CSW69) umeingia siku ya tatu hii leo Machi 12 katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijinoi New York, Marekani. Mkutano huu wa mwaka huu unafanyika katika hali ya kihistoria kwa kuzingatia kuwa ni miaka 30 tangu Mkutano wa wanawake ulipofanyika jijini Beijing - China  mwaka 1995 na kuweka maazimio muhimu kuhusu masuala mazito ya kumkomboa mwanamke dhidi ya ukandamizaji kote duniani. Maelfu ya wanawake na wadau wengine wanakutana kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York. Miongoni mwao ni Nuria Mshare ambaye amewakilisha taasisi ya Haki Elimu ya nchini Tanzania.

VOA Express - Voice of America
Mkurugenzi wa haki za watoto na vijana Afrika mashariki anasema vijana wanapaswa kujifunza elimu ya vitendo na nadharia kujiandaa kimaisha. - Machi 03, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 29:59


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Habari za UN
27 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 27, 2025 11:04


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayokupeleka nchini DRC ambako leo tunamulika mmoja wa raia aliyerejea makazi yake huko Sake, nje kidogo ya mji wa Goma, jimboni Kivu Kaskazini baada ya waasi wa M23 kutangaza kuwa wakimbizi wote wa ndani lazima warejee vijijini kwao. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa methali.Ikiwa ni mwezi mmoja sasa tangu waasi wa M23 watwae mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na kuendelea kutwaa miji mingine huku mamia ya maelfu ya watu wakifurushwa makwao, hii leo mashirika ya Kibinadamu nchini humo yametoa ombi la dola bilioni 2.54 ili kusaidia watu milioni 11 walioathiriwa vibaya na mzozo unaoendelea.Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO Dkt. Tedros Ghebreysus ametangaza kuwa ugonjwa wa mpox bado ni tishio la afya ya umma duniani na hivyo nchi lazima ziendelee kuwa makini katika ufuatiliaji, uchunguzi, kinga na matibabu.Na kuelekea Mkutano wa viongozi kuhusu Mifumo ya uzalishaji chakula mwezi Julai mwaka huu huko Addis Ababa, Ethiopia, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed amezungumza hivi karibuni akiwa Nairobi, Kenya kwenye kikao cha maandalizi ambako alitembelea jiko la Giga, mpango wa Chakula kwa ajili ya Elimu, unaoendeshwa na Wawira Njiru, mshindi wa tuzo ya Mtu Maarufu Kenya mwaka 2021.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia maana ya methali “FAHARI ISIYO PARI HAINA HERI.”.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
UNICEF na WFP wawezesha watoto nchini Sudan Kusini kwenda shule ili watimize ndoto zao

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 24, 2025 2:03


Mashirika ya Umoja wa Mataifa, lile la Kuhudumia Watoto, UNICEF na la Mpango wa Chakula duniani, WFP kwa kushirikiana na mradi wa pamoja wa kimataifa wa mnepo ,au Joint Resilience Project (JRP) nchini Sudan Kusini ,wanatekeleza msaada wa chakula bora na salama bila malipo kwa watoto shuleni ,kwa zaidi ya wanufaika laki tano alfu Hamsini 550,000 ili kuhakikisha ndoto za watoto hao zinatimia. Ni sauti ya watoto wakitembea kuelekea shuleni huku wakiwa wamevibeba vitabu vyao mikononi.Kupitia video iliyoandaliwa na UNICEF, Tieng Maleng, mnufaika wa mradi wa JRP kutoka kijiji cha Pangapdit anaonekana akiwapa watoto wake kiamsha kinywa huku wakiwa wamekaa nje ya boma lao wakiwa wamevalia sare zao tayari kwenda shule. Kwa furaha anaeleza jinsi mradi huu umekuwa wa manufaa kwa familia yake.“Baada ya kupokea msaada wa kifedha, nilitumia fedha kidogo kulipa ada ya shule ya watoto wangu. Nikachukua sehemu kidogo ya fedha hizo kununua viatu vyao, na dawa. Pia nilitumia sehemu nyingine ya msaada huo katika kilimo.”Katika shule ya msingi ya Pangapdit inayoungwa mkono na mradi huu, watoto wanaonekana wakiwa wamesimama kwenye gwaride la shule wakisikiliza maelekezo kutoka kwa walimu wao. Aluel,Mwanawe Tieng Maleng, ambaye ni mwanafunzi katika shule hiyo anasema, “Tunaenda shule kila asubuhi na ndoto yangu ni kufanya kazi na mashirika yanayosaidia watu. Wakati kengele ya shule inapolia, tunakusanyika kwa ajili ya mkutano na baadaye tunaenda darasani.”Kupitia mradi huu,wanafunzi wamepokea vitabu vya kusoma,wamejengewa madarasa mapya, vyoo bora , na mifereji ya kunawa mikono.UNICEF na WFP wanafanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa watoto wanatimiza ndoto zao.

Habari za UN
Redio imetusaidia kufikisha elimu kwa umma kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 12, 2025 3:12


Ikiwa kesho Februari 13 ni Siku ya Kimataifa ya Redio, makala inatupeleka jijini Nairobi, Kenya ambako ambako Kevin Keitany wa redio washirika wetu Domus FM kwa kuzingatia kuwa kesho Februari 13 ni Siku ya Kimataifa ya Redio, ametutumia maoni ya vijana wawili wanaozungumzia namna redio imewasaidia kusambaza ujumbe wao kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.

Habari za UN
28 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 28, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kushuhudia matumizi ya nishati safi na ya gharama nafuu kupika mlo shuleni jijini Nairobi linaloofanikishwa na Shirika la Food4Education. Pia tunakuletea habari kwa ufupi na mashinani inatupeleka Ethiopia.Mashirika ya Umoja wa Mataifa yamesema hali ya usalama mjini Goma, jimboni Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC inazidi kuwa mbayá kutokana na mapigano kati ya jeshi la serikali, FARDC na waasi wa M23. Saa 24 zilizopita zimekuwa ni mbayá.Naye Dkt. Adelheid Marschang, Mratibu wa masuala ya dharura wa shirika la Umoja wa MAtaifa la afya duniani, WHO nchini DRC amesema tumesikia ripoti za wahudumu wa afya kupigwa risasi huku wagonjwa pamoja na watoto wakinaswa kwenye mapigano. “WHO inakumbusha kila mtu kuwa mashambulizi dhidi ya huduma za afya ni kinyume na kanuni za vita. Vituo vya afya lazima vilindwe wakati wote.”Mkutano wa viongozi wa Afrika kuhusu nishati ukipatiwa jina Mission 300 umekunja jamvi jijini Dar es Salaam nchini Tanzania kwa kuzindua Mikataba ya Nishati ya Kitaifa kutoka nchi 12 za barani Afrika, ikiwemo Tanzania, hatua ambayo ni msingi wa uwekezaji mkubwa na mageuzi ya será za nishati. Akizungumza kwenye mkutano huo, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed amesema, “kwa kusongesha mipango ya muda mrefu ya kupata nishati na kuisimamia, tunaweza kuimarisha amani, na kuunda ajira zisizoharibu mazingira, na kujenga mnepo wa mbinu za kujipatia kipato, na hivyo kufungua njia ya utulivu na ustawi wa bara letu.”.Na mashinani fursa ni yake mwalimu Beray kutoka eneo la Tigray nchini Ethiopia ambaye amezungumza na maafisa wa msaada wa mfuko wa kimatifa wa elimu haiwezi kusubiri (ECW) akieleza matumaini yake kwa wanafunzi wake iwapo watawezeshwa.Mwenyeji wako niAnold Kayanda karibu!  

Habari za UN
27 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 27, 2025 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini DRC yanosababishwa na kundi la waasi la M23 mjini Goma. Makala tunakupeleka nchini Tanzania na mashinani ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukumbuka waathiriwa wa mauaji ya halaiki tutasikia ujumbe wa Umoja wa Mataifa.Hali ya usalama kwenye mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini, Goma, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ikiendelea kuwa tete, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, nchini humo, MONUSCO pamoja na SAMIDRC ambao ni ujumbe wa kulinda amani kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika, SADC wanadhibiti uwanja wa ndege wa Goma.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, MONUSCO kwa kushirikiana na polisi wa kitaifa wa nchi hiyo  PNC wameongeza doria katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Bushagara jimboni Kivu Kaskazini kufuatia ongezeko la vitisho na mashambulizi ya kundi la wapiganaji wa M23.Katika makala Anold Kayanda anatupeleka nchini Tanzania ambako katika kuhamasisha elimu iliyo salama inayolenga kumlea na kumfundisha mtoto kwa njia chanya zisizoumiza, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, (UNICEF) linamuangazia Mwalimu Magesa Stanslaus ambaye ambaye amebadilika kutoka katika matumizi ya viboko na sasa anatumia motisha tofauti kuwarekebisha wanafunzi wake.Na mashinani fursa ni yake Miguel Ángel Moratinos, Mwakilishi wa Ngazi ya Juu wa Muungano wa Ustaarabu Umoja wa Mataifa UNAOC akitoa ujumbe kuhusu mauaji ya halaiki na sheria za kimataifa za haki za binadamu.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!  

Habari za UN
Sio lazima kiboko, kampeni ya UNICEF Tanzania inayoonesha mafanikio katika elimu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 27, 2025 2:33


Katika makala ya leo Anold Kayanda anatupeleka nchini Tanzania ambako katika kuhamasisha elimu iliyo salama inayolenga kumlea na kumfundisha mtoto kwa njia chanya zisizoumiza, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, (UNICEF) linamuangazia Mwalimu Magesa Stanslaus ambaye amebadilika kutoka katika matumizi ya viboko na sasa anatumia motisha tofauti kuwarekebisha wanafunzi wake. 

Habari za UN
24 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 24, 2025 11:18


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini DRC, na katika elimu tunamsikia msichana wa Afghanistan ambaye ni mnufaika wa ufadhili wa Umoja wa Mataifa. Makala inatupeleka nchini Oaris kumulika matumizi ya AI katika elimu na mashinani tunakwenda nchini Sudan.Mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo yameonya kwamba kuongezeka kwa uhasama kwenye viunga vya mji wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kunakohusisha kundi lisilo la kiserikali linalojihami kwa silaha, M23 kumesababisha watu wengi zaidi kuhama katika eneo hilo lenye utajiri wa madini, huku kukiwa na hofu kwamba mji mkuu wa eneo hilo Goma unaweza kuangukia mikononi mwa wapiganaji hao.Tukiwa bado katika siku ya Elimu duniani kutana na Suhaila msichana mkimbizi kutoka Afghanistan ambaye kupitia mpango wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR wa kuwahamishia wakimbizi katika nchi ya tatu aliwasili Jamhuri ya Kyrgyzstan ambako sio tu alipata maskani ya kudumu na wazazi wake bali pia matumaini na elimu iliyompa ari ya kurejesha matunda yake nyumbani alikotoka.Makala leo ikiwa ni siku ya elimu duniani Assumpta Massoi anakukutanisha na walimu wawili huko Paris nchini Ufaransa wakijadili mustakabali wa Akili Mnemba au AI kwenye ufundishaji darasani. Mahojiano hayo yameandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na UTamaduni, UNESCO.Na katika mashinani Nour Abdallah, Mkimbizi wa ndani katika eneo la Zamzam nchini Sudan kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula Duniani WFP, anasema janga la njaa limelazimisha jamii kula chakula cha mifugo huku wakiwa na matumaini kwani chakula cha msaada kinaendelea kuwasilishwa kwenye maeneo yaliyoathiriwa na vita.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Safari yangu Kyrgyzstan ilikuwa ya matumaini na elimu: Suhaila

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 24, 2025 2:13


Katika siku ya Elimu duniani kutana na Suhaila msichana mkimbizi kutoka Afghanistan ambaye kupitia mpango wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi  UNHCR wa kuwahamishia wakimbizi katika nchi ya tatu aliwasili Jamhuri ya Kyrgyzstan ambako sio tu alipata maskani ya kudumu na wazazi wake bali pia matumaini na elimu iliyompa ari ya kurejesha matunda yake nyumbani alikotoka. Flora Nducha na taarifa zaidi.

Habari za UN
Akili Mnemba haikwepeki, tuiwezeshe ili ituwezeshe kwa manufaa ya walimu na wanafunzi - Walimu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 24, 2025 3:22


Akili Mnemba au AI inakuja kwa kasi kubwa sana na kubadilisha mwenendo wa walimu na wanafunzi darasani. Inaleta fursa za kipekee kama kufundisha kwa njia ya kibinafsi na upangaji wa masomo wenye ufanisi zaidi. Lakini pamoja na zana hizi, changamoto zimeibuka: kutegemea sana teknolojia hii, masuala ya kimaadili, na kupungua kwa ujuzi wa kusoma kwa kina. Walimu wanajifunza jinsi ya kuendesha mabadiliko haya, wakiwaonesha wanafunzi jinsi ya kutumia AI kama mshirika wa kufikiri badala ya njia ya mkato ya kuuliza na kunakili. Ubunifu na kufikiri kwa kina vinabaki kuwa ujuzi muhimu zaidi, ambao hakuna teknolojia inayoweza kuchukua nafasi yake. Je, walimu wana mawazo gani? Assumpta Massoi anakupeleka Paris, Ufaransa kusikia mazungumzo ya walimu wawili wakijadili mustakabali wa Akili Mnemba kwenye ufundishaji. 

Habari za UN
23 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 23, 2025 10:00


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini DRC kumulika mausala ya AI kwenye elimu tukielekea siku ya kimataifa ya elimu inayoangazia matumizi ya AI na changamoto zake. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ufafanuzi wa methali.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO, umethibitisha kuwa waasi wa M23 wametwaa baadhi ya maeneo jimboni Kivu Kusini, miongoni mwao ikiwa mji wa Minova, ukisema hali hiyo inatia wasiwasi mkubwa.Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema watoto na familia zao wanaorejea kaskazini mwa Gaza baada ya kuanza utekelezaji wa usitishaji mapigano wanakutana na uharibifu mkubwa na kuporomoka kwa miundombinu.Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP leo limesema limefanikiwa kuhamisha msaada wa kwanza wa chakula kuingia Sudan kwa ajili ya kulisha watu 80,000 kwa mwezi mmoja kupitia mto Nile.Na katikakujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya msemo “HIVI KWELI KISAUNI KUTOTA MVINDE?”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!  

Habari za UN
Elimu haina umri wala kuchelewa, wala mwisho: Philip Long'olea

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 20, 2025 2:14


Migogoro, vita na mabadiliko ya tabianchi mara nyingi vimekuwa vikiwapora watoto fursa ya elimu na hata kusambaratisha mustakbali wao na wengi wanajikuta wakiishia kwenye makambi ya wakimbizi linasema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF. Kwa kulitambua hilo shirika hilo linaendesha miradi mbalimbali ya kuhakikisha watoto waliokosa elimu hata kama wana umri mkubwa wanapewa fursa ya pili kusoma kama ilivyokuwa kwa mkimbizi Philip Lon'golea kutoka Sudan aliyekimbilia Uganda kwanza lakini sasa yuko kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya. Cicely Kariuki anatujuza zaidi

Habari za UN
UNICEF: Zama mpya za majanga kwa watoto , wakati vita vikishika kasi na pengo la usawa likiongezeka

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 13, 2025 2:22


Ripoti mpya ya kila mwaka kuhusu mustakabali wa watoto ambayo imetolewa  leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, imeonya kwamba dunia inaingia katika zama mpya za majanga kwa watoto . Taarifa ya Flora Nducha inafafanua zaidi

Habari za UN
09 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 9, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea Mada kwa Kina inayotupeleka Kenya ambapo Shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limefanikiwa kumnyanyua msichana Nosizi Dube na kutimiza ndoto yake ya kuepuka ndoa ya utotoni na kupata shahada ya kwanza ya chuo kikuu. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchaambizi wa neno KWEGO.Mwezi mmoja tangu kuanguka kwa utawala wa Bashar Al-Assad, zaidi ya wakimbizi 125,000 wamerejea Syria "wakiwa na matumaini baada ya miaka mingi ya kuishi uhamishoni", lakini wamejikuta wakikabiliwa na hali mbaya nchini mwao, wameeleza leo wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa. Likiwa linaongoza wito kwa jumuiya ya kimataifa "kutoka kwenye maneno hadi vitendo" ili kuwasaidia watu walio waliorejea ambao sasa wako katika mazingira magumu, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, limesema familia nyingi zina uhaba wa makazi na njia kidogo za kiuchumi.Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) limeongeza ombi lake la fedha kufikia dola milioni 73.2 kwa ajili ya kusaidia zaidi ya watu milioni 1.1 kote nchini Syria katika kipindi cha miezi sita ijayo, wakati nchi hiyo ikiingia katika kipindi cha mpito kufuatia kuanguka kwa serikali ya Bashar Al-Assad. Ombi hili ni nyongeza katika ombi la awali la dola milioni 30 lililotolewa mwezi Desemba mwaka jana 2024 likilenga mahitaji yanayoongezeka ya majira ya baridi Kaskazini Magharibi mwa Syria.Miezi 15 baada ya vita huko Gaza, mamia kwa maelfu wanaendelea kuishi katika shule za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina (UNRWA) zenye msongamano ambazo zimegeuzwa kuwa makazi. UNRWA imeeleza kuwa hata viwanja vya michezo kwa watoto sasa ni nyumba kwa waliofurushwa. Shirika hilo limesisitiza kuwa misaada zaidi ya kibinadamu lazima iingie Gaza na kusitishwa kwa mapigano ni muhimu zaidi kuliko hapo awali.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo fursa ni yake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “KWEGO”.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

Habari za UN
Nosizi Ndube: Kukosa utaifa haikukwamisha ndoto yangu ya elimu, asante UNHCR na wadau mbalimbali

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 9, 2025 5:17


Shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limefanikiwa kumnyanyua msichana Nosizi Dube na kutimiza ndoto yake ya kuepuka ndoa ya utotoni na kupata shahada ya kwanza ya chuo kikuu. Msichana huyo mwenye umri wa miaka 24 ni wa kwanza katika jamii ya Washona wanaoishi mjini Nairobi Kenya kupata elimu katika ngazi hiyo. Mpango wa UNHCR wa kupambana na kutokuwa na utaifa kwa ushirikiano na serikali ya Kenya umekuwa chachu ya mafanikio ya msichana huyo. Mwandishi wetu wa Nairobi Thelma Mwadzaya alimtembelea Nosizi nyumbani kwake ili kupata undani wa safari yake..

Les têtes d'affiches de Denise Epoté
Ermann Zannou pour «Green Ker» et Juni Bulabula pour «Kahuzi VR+Elimu»

Les têtes d'affiches de Denise Epoté

Play Episode Listen Later Dec 15, 2024 3:33


Les têtes d'affiches de Denise Epoté de TV5 Monde, comme chaque dimanche sur RFI, aujourd'hui avec Artur Ponchelet. Notre première tête d'affiche est un entrepreneur franco-béninois. Diplômé de l'institut polytechnique de Rennes, Ermann Zannou a fondé Green Ker, une start-up qui produit des foyers améliorés pour réduire la pollution domestique. Notre seconde tête d'affiche est originaire de la RDC. Diplômé en informatique de gestion de l'université catholique de Bukavu, Juni Bulabula a également obtenu un diplôme d'ingénieur système à l'université de Middlesex de Grande-Bretagne sur le campus de Nairobi et une maîtrise en sciences des systèmes de gestion de l'information à l'université de Salford au Royaume-Uni. Grâce à la technologie immersive, il a lancé Kahuzi VR et Elimu, des innovations utilisées dans le tourisme et les EdTech.

Habari za UN
Sasa tunalima mboga shuleni na nyumbani - Wanafunzi Buhigwe Tanzania

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 13, 2024 3:42


Kupitia mradi wa Pamoja wa Kigoma, KJP,  awamu ya Pili, Shule ya Msingi Buhigwe, iliyoko wilayani Buhigwe, mkoa wa Kigoma, ilipatiwa mafunzo kupitia Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), likishirikiana na asasi isiyo ya kiserikali RECODA. Mafunzo haya yalilenga mbinu bora za kilimo ambapo wanafunzi waliweza kuanzisha bustani za mboga kupitia somo la Elimu ya Kujitegemea. Mradi umeanza kutekelezwa na matunda yanaanza kuonekana kama asimuliavyo Assumpta Massoi kwenye makala hii.

Habari za UN
UNFPA: Elimu ndio ufunguo wa kutokomeza FGM Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 10, 2024 5:31


Leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya haki za binadamu tunaelekea Kenya kuangazia moja ya ukiukwaji Mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya wanawake, jinamizi la ukeketaji na jitihada zinazochukuliwa na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa  ya idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA kutokomeza janga hilo. Mwandishi wetu wa Nairobi Thelma Mwadzaya amefuatilia kuhusu suala hilo na kwa undani zaidi ungana naye ..

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية

Elimu ya kujitambua kwa watoto

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية

Elimu kwa watoto

Habari za UN
UNESCO: Tunapaswa kuthamini sauti za walimu kote duniani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 4, 2024 2:58


Washiriki wa hafla ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Walimu ililofanyika leo Oktoba 4 katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) jijini Paris, Ufaransa  wamesisitiza wito wa kuthamini mawazo ya walimu katika kuboresha elimu ya ulimwengu. Kama tunavyofahamu, siku yenyewe ya Kimataifa ya Walimu ni kesho Oktoba 5 kama ilivyo ada ya kila mwaka lakini katika makao makuu ya UNESCO hapa Paris Ufaransa, maadhimisho yamefanyika leo kuelekea mkesha wa siku hii muhimu kwa elimu ya ulimwengu.Miongoni mwa waliozungumza ni Mkurugenzi Msaidizi Mkuu wa Elimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi Stefania Giannini, ambaye ameitumia nafasi hii kusisitiza kauli mbiu ya mwaka huu ambayo ni 'Kutambua sauti za walimu.'Anasema, “walimu ni uti wa mgongo wa mifumo ya elimu na mawakala wakuu wa mabadiliko ya kubuni sera za elimu na kufanikisha SDGs. Tunapaswa kuthamini sauti za walimu; hili ndilo lengo kuu la Siku ya Kimataifa ya Walimu mwaka huu.”Kulingana na takwimu zilizotolewa na UNESCO, dunia inahitaji walimu wa ziada milioni 44 ili kufikia elimu ya msingi na sekondari kwa wote ifikapo mwaka 2030. Ingawa mahitaji ya walimu ni makubwa zaidi katika baadhi ya maeneo, uhaba wa walimu ni wa kimataifa.Walimu wanajiondoa kwenye taaluma hii kwa kiwango mara mbili zaidi ya miaka mitano iliyopita, hasa katika elimu ya sekondari. Hii inatokana na hali zao za kazi, zikiwemo mishahara midogo, mzigo mkubwa wa kazi, na ukosefu wa ushiriki katika maamuzi yanayohusu elimu. Akiiangizia changamoto hii, Mkurugenzi wa Kimataifa wa Elimu na Maendeleo ya Vijana katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) Bi. Pia Britto, aliyejiunga katika hafla ya leo kwa njia ya video akiwa Pakistani amesema,"Leo nilikuwa na fursa nzuri ya kuzungumza na walimu wengi, ikiwa ni pamoja na mwalimu Tahseen Bashir hapa Islamabad, ambaye amenieleza baadhi ya changamoto wanazokabiliana nazo ikiwa ni pamoja na kufundisha madarasa mengi, uhaba wa vifaa vya kujifunzia, na changamoto za kutoweza kufundisha namna wanavyodhamiria. Lakini pia amenieleza jinsi alivyofurahi kuona wanafunzi wake wakifaulu. Wakati sauti ya mwalimu inaposikilizwa na wakati sauti za walimu zinapopewa kipaumbele, wanajiona kama wadau katika kuboresha elimu kwa wakati wote, na hatua hizo zinahitajika ili kuleta mabadiliko chanya hasa katika hali ngumu zaidi."Siku hii ya kimataifa ya walimu ni mahususi kwa ajili ya kutambua na kusherehekea mchango muhimu wa walimu ulimwenguni kote katika kutoa elimu bora na kujenga mustakabali wa jamii. Pia, ni fursa ya kuangazia changamoto wanazokabiliana nazo walimu.Kutoka hapa Paris Ufaransa, mimi ni Cecily Kariuki..

Habari za UN
04 OKTOBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 4, 2024 11:18


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini Lebanon, na kesho ikiwa ni Siku ya walimu Dunia tunakupeleka Paris, Ufaranza kutsikia toka UNESCO. Makala tunafuatili ajali ya boti iliyozama katika ziwa Kivu nchini DRC na mashinani tunakupeleka Burundi, kulikoni? Mashirikika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa leo yameonya kwamba hali ya kibinadamu inazidi kuwa mbaya nchini Lebanon wakati mashambulizi ya anga ya Israel yakiendelea kushika kasi na kuwafungisha virago maelfu ya watu, wengi wakikimbia nchi jirani ya Syria ambako nako si shwari.Washiriki wa hafla ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Walimu ililofanyika leo Oktoba 4 katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) jijini Paris, Ufaransa  wamesisitiza wito wa kuthamini mawazo ya walimu katika kuboresha elimu ya ulimwengu.Makala inakupeleka huko Goma, jimboni Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako janga la kuzama kwa boti ya abiria na mizigo liligubika eneo hilo Alhamisi asubuhi za huko.Na mashinani kupitia video ya WHO Afrika, tunamsikia Dkt. Dieudonné Niyongere akizungumza kuhusu msaada muhimu wa washirika katika kuimarisha juhudi za kukabiliana na mlipuko wa Mpox nchini Burundi.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Francis "Openmaps Global Study imeziba pengo katika utoaji wa elimu ya juu Australia"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Oct 1, 2024 9:43


Sekta ya elimu ya juu nchini Australia, ina thamani yama bilioni ya dola.

Habari za UN
UNESCO na wadau wanajitahidi kuboresha elimu licha ya mashambulizi dhidi ya elimu katika migogoro.

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 30, 2024 4:27


Kama unavyojua, migogoro ya vita, majanga ya tabia nchi, dharura za afya ya umma, na mishtuko ya kiuchumi inaongezeka duniani kote kwa kasi, ugumu, na ukubwa. Mara nyingi dharura hizi hutokea kwa wakati mmoja, kwa mfano, wakati vita vinapoanza katika maeneo ambayo tayari yameathiriwa na majanga ya mabadiliko ya tabianchi. Hali hii inasababisha migogoro tata, iliyo changamana na ya muda mrefu, na athari zake kwenye elimu ni za kutisha. Nafikiri utakubaliana nami kuwa elimu ni mkombozi wa maisha na muhimu kwa kuendeleza maisha wakati wa dharura. Je UNESCO inatatua vipi changamoto hii? Cecili kariuki amezungumza na wataalamu wa elimu nchini Paris, Ufaranza.

Habari za UN
David Tumaini - Umasikini uliniachisha shule lakini asante mradi wa UNICEF sasa naendelea na ndoto yangu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 30, 2024 2:34


Maelfu ya watoto katika Kaunti ya Kilifi Pwani ya Kenya kwa miaka mitatu iliyopita wamelazimika kuacha shule kutokana na umasikini na ukame na mafuriko yaliyochangiwa na mabadiliko ya tabianchi. Lakini sasa wizara ya elimu ya Kenya kwa kushirikiana na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, wakfu wa Education Above all na wadau wengine juhudi zinafanyika kuwarejesha watoto shuleni. “Niliacha shule darasa la nne  ilikuwa mwaka 2022, kwasababu shuleni walikuwa wananirejesha nyumbani nikalete ada. Sasa nikifika nyumbani wazazi wanasema hawana”Huyo ni David Tumaini kijana mwenye umri wa miaka hivi sasa 16 mmoja wa wanafunzi  waliolazimiika kukatiza masomo  miaka miwili iliyopita katika shule ya msingi ya Soyosoyo kutokana na umasikini. Kwa miezi kadhaa alihaha kusaka njia ya kuendelea na masomo."Nilikaa nyumbani kwa muda wa miezi mitano, wakati wenzangu wanakwenda shule na ni siku za masomo na wewe uko nyumbani. Hii inakufanya ujihisi kama wewe si mtu muhimu.”Hisia kama hizo na mustakbali wa watoto hao ndio kilicholisukuma shirika la UNICEF kuanzisha mradi wa “Elimisha mtoto” likishirikisha wizara ya elimu ya kenya na wadau wengine ili kuhakikisha watoto kama David wanarejea shuleni. Elizabeth Waitha ni afisa elimu wa  UNICEF.“Tuliweza kubaini Kaunti 16 ambazo zilikuwa na watoto zaidi ya 10,000 ambao wanaendi shuleni, na hii ilikuwa ni kwa shule za msingi tu. Na tukaangalia ni jinsi gani ya kuhakikisha mazingira bora ya kusoma kwa watoto waliosajiliwa kwenye mradi. Na tumeweza kuwasaidia zaidi ya wanafunzi milioni kwa vifaa vya shule na pia kwa waalimu vifaa vya kuandikia kama chaki, kalamu na vingine.”Na ndipo David akasikia kuhusu mradi huo,“Nilipata taarifa kutoka kwa walimu ya kwamba kuna mradi ambao unawasaidia watoto walioacha shule ili warehjee shuleni kuendelea na masomo. Sasa nilipokuja shuleni nikaambiwa wewe tutakusajili katika huu mradi wa msaada , ndipo nikaweza kurejea masomoni, hadi sasa nipo shuleni kwa sababu ya msaada huu. Vitu ambavyo nilipewa ni pamoja na mkoba wa madaftari, vitabu, kalamu na vifutio.”Hii imemrejeshea David matumaini ya ndoto yake“Mimi nikimaliza kusoma nataka kuwa Daktari ili kusaidia wagonjwa. Na katika kusaidia wagonjwa mshahara nitakaolipwa ntajisaidia mwenyewe na pia kusaidia familia yangu”Kupitia mradi huu mbali ya vifaa umewezesha zaidi ya watoto 256,000 kurejea shuleni na bado wanaendelea na masomo.

Habari za UN
30 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 30, 2024 12:16


Hii leo jaridani tunaangazia amani na usalama nchini DRC, na suala la elimu katika malengo ya maendeleo endelevu tukimulika wanafunzi Kilifi nchini Kenya. Makala tunasalia na mada hiyo hiyo ya elimu na mashiani inamulika sheria za kibnadamu.Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo wameelezwa jinsi ushindani wa uchimbaji kupita kiasi na biashara ya maliasili huko Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC unavyozidi kuchochea mapigano kwenye eneo hilo, madini kama vile dhahabu na Koltani.Maelfu ya watoto katika Kaunti ya Kilifi Pwani ya Kenya kwa miaka mitatu iliyopita wamelazimika kuacha shule kutokana na umasikini na ukame na mafuriko yaliyochangiwa na mabadiliko ya tabianchi. Lakini sasa wizara ya elimu ya Kenya kwa kushirikiana na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, wakfu wa Education Above all na wadau wengine juhudi zinafanyika kuwarejesha watoto shuleni.Makala leo inatupeleka Paris Ufaransa katika makao makuu ya shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO kuzungmzia juhudi za shirika hili katika kuhakikisha kwamba wanafunzi walio katika maeneo ya migogoro wanaendelea na masomo yao na wenzao waliohamishwa wanapata ufikiaji wa elimu juu katika nchi zilizowapokea.Katika mashinani fursa ni yake Mirjana Spoljaric Egger, Rais wa Kamati ya Kimataifa ya chama cha Msalaba Mwekundu ICRC akitoa wito wa kutafakari machungu yanayowakumba waathirika wa mizozo wakati wa mazungumzo yake na waandishi wa habari kandoni mwa mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA79.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu! 

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية

Visa mbali mbali kwa ajili ya watoto kutoka katika Biblia

Inside Syracuse Basketball
Inside Syracuse Basketball: Catching up with walk on fan favorite Elimu Nelson

Inside Syracuse Basketball

Play Episode Listen Later Sep 23, 2024 36:40


Mike Waters welcomes Elimu Nelson to the podcast to relive walking onto the Orange, finally getting a scholarship senior year, and his acting career after Syracuse. Learn more about your ad choices. Visit megaphone.fm/adchoices

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية

Visa mbali mbali kwa ajili ya Watoto

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية

Visa mbali mbali vyenye mafundisho kwa Watoto

Habari za UN
ECW yarejesha matumaini kwa msichana Fatima wa Nigeria

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 9, 2024 3:12


Alipokuwa na umri wa miaka 10 mnamo mwaka 2015, Fatima na familia yake walilazimika kutoroka nyumbani kwao Konduga, ili kuepuka mashambulizi kutoka kwa makundi yenye silaha. Konduga iko kilomita 25 kusini mashariki mwa mji wa Maiduguri, kaskazini mashariki mwa Nigeria.Familia ya Fatima haikuwa na namna ya kumuandikisha katika shule yoyote rasmi. Alitumia muda wake mwingi kuuza chakula.Shukrani kwa usaidizi wa mfuko wa kimatifa wa elimu haiwezi kusubiri yaani Education Cannot Wait (ECW) na wadau wake wa kimkakati, Fatima sasa amesajiliwa katika mpango mesto unaolenga kuwapa elimu wasichana walio nje ya shule.Msichana huyu ni mmoja wa walengwa 250 wa programu ya miezi mitano ya kusoma, kuandika na kuhesabu, ambayo imemwezesha kusoma kwa lugha ya Kihausa na hata kuandika jina lake kama anavyoeleza."Niliingia katika shule ya ufundi baada ya kusikia kuihusu wakati nilipokuwa nimeenda kuuza chakua. Mara moja nilihifadhi kile nilichoenda kuuza kisha nikajiandikisha jina langu. Wale ambao tulikuwa hatuendi shule tulitambuliwa na kuchaguliwa. Tulifundishwa jinsi ya kusoma na kuandika. Kabla hapo nilikuwa siwezi hata kuandika jina langu.”Sehemu ya pili ya programu hii mseto ilihusisha kipengele cha ufundi ambapo wasichana wanaoishi katika mazingira hatarishi hupata mafunzo ya ufundi kwa muda wa miezi mitatu. Mpango unaotekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, Norwegian Refugee Council (NRC) na Save the Children."Pia, sasa ninajua namba, na ninaweza kupima watu  ninaposhona." Anasema Fatima ambaye katika kipengengele cha ufundi yeye amechagua ushoni wa nguo.Mpango huu tayari umewanufaisha wasichana balehe 600 tangu kuanzishwa kwake, na kuwapa vifaa vya kuanzia na ujuzi wa kujitegemea. Fatima naye ana matumaini.“Nataka kujifunza stadi hii ili niwahishimishe wazazi wangu na wawe na furaha. Nikimaliza kujifunza nataka kuwa mtu wa kuwashonea ndugu zangu nguo.”Kama ambavyo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anatoa wito kwa nchi zote kuwekeza katika elimu na kufanya juhudi za kila namna kulinda elimu na maeneo ya kusomea, kulinda wanafunzi na walimu,  Mkurugenzi Mtendaji wa Education Cannot Wait (ECW) Yasmine Sherif, anaeleza namna ambavyo mfuko wa kimatifa wa elimu haiwezi kusubiri umejizatiti kuendelea kuiunga mkono elimu kote duniani wakati huo akitoa wito kwa kila anayeweza kuwaongezea nguvu afanye hivyo."Kuna ustahimilivu na watoto hawa wamepitia kiwewe na mambo mengi. Ni lazima tuwepo kwa ajili yao, na tunaweza kuona matokeo. Tunatazamia kuufanya tena mpango huu mwaka katika mwaka huu, tunatarajia kufanya hivyo kwa takribani dola milioni 15, kama sio zaidi. Ikiwa nyinyi nyote mtakuja na kutusaidia kuongeza."

Habari za UN
09 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 9, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia suala la elimu katika maeneo ya migogoro, na msaada wa kibinadamu huko Upper Nile nchini Sudan Kusini. Makala tunakupeleka nchini Nigeria na mashinani nchini Afghanistan, kulikoni??Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kulinda elimu isishambuliwe wakati wa mizozo kutokana na umuhimu wake kwa watoto na jamii, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema miaka ya karibuni imeshuhudia ongezeko kubwa la mashambulizi dhidi ya wanafunzi, walimu na shule duniani kote. Hivyo ndivyo alivyoanza ujumbe wake wa siku hii.Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini (UNMISS) umewaeleza wananchi wa Kaunti ya Nasir au Keich Kon iliyoko jimboni Upper Nile nchini Sudan Kusini kuwa ili waweze kurejeshewa huduma za misaada ya kibinadamu ni vyema wakafikia makubaliano ya kusitisha mapigano.Makala inatupeleka Maiduguri nchini Nigeria kusikia namna mfuko wa kimatifa wa elimu haiwezi kusubiri yaani Education Cannot Wait (ECW) kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia watoto (UNICEF) na wadau wengine wanarejesha matumaini kwa waliokosa elimu rasmi hasa kutokana na hali mbayá ya usalama katika maeneo yao.Na katika mashinani, fursa ni yake Faeza, mfanyakazi wa kiwanda cha kutengeneza biskuti nchini Afghanistan, mradi unaowezeshwa na shirika la WFP akitueleza manufaa ya mradi huo kwa jamii iliyoathirika na vita hasa wanawake na watoto.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Habari za UN
Guterres: Vita huharibu miili, akili na fikra za vijana na watoto

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 9, 2024 1:47


Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kulinda elimu isishambuliwe wakati wa mizozo kutokana na umuhimu wake kwa watoto na jamii, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema miaka ya karibuni imeshuhudia ongezeko kubwa la mashambulizi dhidi ya wanafunzi, walimu na shule duniani kote. Hivyo ndivyo alivyoanza ujumbe wake wa siku hii. Katibu Mkuu anasema kuanzia Gaza hadi Sudan, Myanmar, Ukraine, Colombia hadi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na kwingineko, vita inasababisha ukatili kwa binadamu, lakini kwa watoto na vijana waliokutwa katikati ya jinamizi la vita, gharama haiwezi kukokotolewa.Anasema ndio maana siku hii inatukumbusha jinsi vita inaharibu miili, akili na fikra za watoto na vijana. Kuanzia majeraha hadi vifo, kutekwa nyara, kulazimika kukimbia, ukatili wa kingono, kutumikishwa vijana na kupoteza fursa. Hatari ni kubwa sana.Anakumbusha kuwa elimu sio tu haki ya msingi ya binadamu, bali ni muhimu kwa ajili ya kutimiza haki nyingine zote za binadamu.Ni kwa mantiki hiyo anataka nchi ziwekeze kwenye elimu na zifanye juhudi zote kuhakikisha wakati wa mizozo elimu na maeneo ya kujifunza yanalindwa, zilinde wanafunzi na walimu na ziwawajibishe wale wote wanaoshambulia shule.Ametumia pia ujumbe huo kuzitaka nchi ziridhie na zitekeleze Azimio la Shule Salama, ziunge mkono Ubia wa Kimataifa wa Kuepusha Mashambulizi dhidi ya Shule na zishikamane na juhudi zote za kuhakikisha watoto na vijana wanaendelea kujifunza iwe wakati wa majanga au wakati majanga yanapokoma.Ametamatisha akisema hebu na tulishe elimu isishambuliwe, tulinde haki ya msingi ya elimu ambayo ni haki ya kila mtoto, kila mtu kokote kule.

Habari za UN
06 SEPTEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 6, 2024 10:00


Hii leo jaridani tunaangazia mashambulizi ya kutisha ya kingono nchini Sudan, na mafunzo ya kidijitali. Makala na mashinani tunakupeleka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kulikoni?Ujumbe Huru wa Kimataifa wa Umoja wa Mataifa  wa kutafuta ukweli nchini Sudan, leo Septemba 6 jijini Geneva, Uswisi, wametoa wito wa kuwekwa vikwazo vya silaha kote nchini Sudan kutokana na kukithiri kwa vitendo vya kikatili kama vile mashambulizi ya kutisha ya kingono.Uhusiano kati ya teknolojia, elimu, na mabadiliko ya tabianchi ni upi? Hili ndilo limekuwa swala kuu katika mkutano wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) uliopewa jina la Wiki ya Kujifunza kwa Kidijitali au Digital Learning Week uliokamilika jana Alhamisi huko Paris Ufaransa. Mkutano huu uliangazia maswala nyeti ya mchango wa teknolojia katika elimu inayolenga maendeleo.Makala tunaelekea DRC ambako George Musubao, Mwandishi wetu wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akizungumza na Mkuu wa kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC-MONUSCO anayemaliza muda wake mwezi huu baada ya kuhudumu kwa mwaka mmoja Brigedia Jenerali Alfred Matambo. Brigedia Jenerali Matambo anaanza kwa kuzungumzia matokeo ya moja ya operesheni  kubwa za kijeshi 15 walizotekeleza dhidi ya makundi yenye silaha likiwemo la CODECO.Na katika mashinani, Daktari Erick Mashimango aliyeko nchini DRC anatueleza kuwa kuenea kwa ugonjwa wa mpox kwa kasi nchini humo ambako kumegharimu maisha ya ziadi ya watu 600 kumewafanya wananchi kuwa tayari kupokea chanjo.Mwenyeji wako ni Assumpta, karibu! 

Habari za UN
UNESCO: Je AI ina nafasi gani katika kudhibiti habari potofu na za uongo?

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 6, 2024 2:09


Huko Paris, Ufaransa kumekamilika mkutano wa wiki moja ulioandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ukipatiwa jina Wiki ya Kujifunza Masuala ya Kidijitali au Digital Learning Week ambapo hoja ya Akili Mnemba kudhibiti habari potofu na za uongo imepatiwa kipaumbele.Mkutano huo ulimulika mchango wa teknolojia ya kidijitali katika elimu inayolenga maendeleo badala ya kuyadumaza. Mathalani ni kwa jinsi gani mifumo ya kidijitali inaweza kukabiliana na taarifa potofu kuhusu mabadiliko ya tabianchi.Simon Wanda, Afisa Programu kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni amefafanua nafasi ya teknolojia kwenye kukabili taarifa hizo.“Mifumo hii inaweza kuchambua na kutathmini yale yanayowekwa kwenye matandao na kutambua taarifa za uongo au za kupotosha.”Mmoja wa washiriki wa mkutano huo ni Doris Mwikali, Mwanasheria na mtetezi wa elimu kutoka Kenya. Tukamuuliza maoni yake kuhusu nafasi ya teknolojia za kidijitali kwa vijana."Ninafahamu kwamba kuna mazungumzo yanaendelea kuhusu jinsi kampuni za mitandao ya kijamii zinavyopambana  na habari potofu na za uongo. Lakini nadhani kuna zana mpya za akili mnemba zinazotumika na baadhi ya kampuni, kuhakiki  taarifa kwenye mitandao ya kijamii. Ingawa haitakuwa na mchango mkubwa ikilinganishwa na  kampuni za mitandao ya kijamii kuchukua jukumu la kudhibiti habari potofu kwenye majukwaa yao, Bado kuna jukumu kubwa kwa akili mnemba katika uhakiki wa taarifa kwenye mitandao ya kijamii, na hiyo imefanywa na mashirika mengi yasiyo ya kiserikali."Nikarejea kwa Bwana Wanda na kumuuliza maoni yake kuhusu maendeleo ya akili mnemba au AI na ujumuishaji wa sauti kutoka pande zote wakati wa  kusongesha AI.“Zipo jamii nyingi zetu za kiafrika kama wamaasai wa Kenya na Tanzania, ambao kwa muda mrefu wamekuwa na elimu ya asili kuhusu kuhifadhi mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, ambayo ni elimu inayofaa kutopuuzwa katika makuzi haya ya teknolojia. Hivyo, hili ni suala la kuhoji sana hasa tunapozingatia kwamba maendeleo katika teknolojia yasiegemee eneo moja la elimu tu, ambayo ni elimu ya magharibi, na kupuuza elimu ya kiasili, ambayo ni tunu.”

SBS Swahili - SBS Swahili
Sekta ya elimu ya juu yasema wanafunzi wakimataifa wamekuwa 'lishe ya mzinga' katika mjadala wa uhamiaji

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 3, 2024 10:28


Idadi ya wanafunzi wakimataifa itawekewa vikomo mwaka ujao, serikali inapojaribu kupunguza uhamiaji wa ng'ambo.

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية

Visa mbali mbali vya watoto

Habari za UN
Kila mmoja achukue hatua kuondokana na vikwazo vya ujumuishaji watu wenye ulemavu - Guterres

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 28, 2024 1:33


Kila mmoja achukue hatua kuondokana na vikwazo vya ujumuishaji watu wenye ulemavu - GuterresUmoja wa Mataifa uko tayari kufanya kazi na Kamati ya Kimataifa ya Michezo ya Olimpiki ya Watu wenye Ulemavu (Paralympic) ili kufikia maono ya jamii shirikishi, jumuishi na endelevu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito michuano ya Paralympic iking'oa leo jijini Paris, Ufaransa. Anold Kayanda na maelezo zaidi.(Taarifa ya Anold Kayanda)Bwana Guterres aliyeko ziarani nchini Timor Leste, barani Asia, ametuma ujumbe kwa Mkutano wa Kimataifa wa Ujumuishaji watu wenye Ulemavu unaofanyika katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) jijini Paris Ufaransa ambako michezo ya Olimpiki ya watu wenye ulemavu, Paralimpiki 2024 imeanza kutimua vumbi leo.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anaamini Michezo ya Olimpiki ya Watu wenye Ulemavu inahimiza kila mtu, kuanzia kwa serikali, mamlaka za mitaa na watoa uamuzi kila mahali, kuchukua hatua ili kuondokana na vikwazo vya ushirikishwaji kamili na wa maana wa watu wenye ulemavu na Umoja wa Mataifa unaahidi kushiriki kikamilifu kutimiza lengo hilo.Aidha katika mkutano huu wa ngazi za juu, UNESCO imeitumia nafasi hiyo kuzindua Kijitabu na mfululizo wa video za mafunzo  kuhusu Usawa wa Ulemavu katika Vyombo vya Habari. Kitabu hicho cha mwongozo kina masomo yanayolenga kuwapa wataalamu wa vyombo vya habari maarifa na zana wanazohitaji ili kuhakikisha mashirika yao yanakuwa jumuishi kwa kuwazingatia watu wenye ulemavu.Moja ya vivutio vikubwa katika paralimpiki za mwaka huu zitakazofanyika hadi tarehe 8 ya mwezi ujao Septemba ni timu ya wakimbizi wanane waliopelekwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR.

Habari za UN
26 AGOSTI 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 26, 2024 9:43


Hii leo jaridani tunamulika kupelekwa kwa chanjo dhidi ya polio huko Gaza; mkimbizi wa Burundi aliyerejea nyumbani kutoka Tanzania ainuliwa kiuchumi; makala ni mkimbizi wa Sudan aliyeko ugenini naye awezeshwa kijasiriamali na mashinani tunabisha hodi nchini Rwanda kumulika usawa wa kijinsia kwenye michezo.Hatimaye shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linapeleka Gaza huko Mashairki ya Kati dozi milioni 1.2 za chanjo dhidi ya ugonjwa wa polio aina ya 2, wakati huu ambapo ugonjwa huo hatari umethibitishwa kuweko eneo hilo. Anold Kayanda na maelezo zaidi.Kwa wakimbizi, kurejea nyumbani ni jambo moja na kuanza upya ni jambo lingine. Wengi wao hawana chaguo lingine isipokuwa kuanza maisha yao upya. Mkoani Makamba, nchini Burundi, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) kwa kushirikiana na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) wanawawezesha waliorejea nyumbani kujijenga upya na kwa tija. Miongoni mwao ni Emelyne Kabura kama anavyosimulia Bosco CosmasKatika makala Evarist Mapesa anatuletea simulizi ya mkimbizi wa Sudan ambaye sasa anaishi Sudan Kusini. Baada ya kupitia madhila lukuki amewezeshwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa na sasa anajishughulisha na ujasiriamali.Na sasa ni mashinani  Christelle Umuhoza, Mkurugenzi wa Programu wa Rwanda katika shirika la Shooting Touch, kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO nchini humo, anaeleza umuhimu wa michezo katika kuondoa vikwazo vya kijinsia.

AWR Swahili / Kiswahili / لغة سواحلية

Visa mbali mbali vya watoto