POPULARITY
Ungana nami Mtangazaji wako Steven Christian Lihizia katika kipindi cha Ijue Liturujia ya Kanisa Katoliki, Studio niko na Padre Clement Kihiyo kutoka Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), akielezea maana ya liturujia katika mtazamo wa kitaaluma. L'articolo Nini maana ya liturujia katika mtazamo wa kitaaluma? proviene da Radio Maria.
Saratani ya shingo ya kizazi, Mtazamo hasi mahali pakazi
Saratani ya shingo ya kizazi, Mtazamo hasi mahali pakazi
Saratani ya shingo ya kizazi, Mtazamo hasi mahali pa kazi
Saratani ya shingo ya kizazi, Mtazamo hasi mahali pa kazi
Saratani ya Shingo ya kizazi, Mtazamo hasi kazini
Saratani ya Shingo ya kizazi, Mtazamo hasi kazini
Msongo wa mawazo, Mtazamo hasi mahali pa kazi
Msongo wa mawazo, Mtazamo hasi mahali pa kazi
Msongo wa Mawazo, Mtazamo hasi mahali pa kazi
Msongo wa Mawazo, Mtazamo hasi mahali pa kazi
VOA Express ni matangazo mapya yenye mwendo wa kasi yakiangalia habari mpya za mchana na maelezo ya maswala yanayohusu vijana na wanawake.
Leo, Joyce anafundisha jinsi tunavyoweza kukabiliana na yale mambo ambayo yanahitaji kushughulikiwa huku tukidumisha mtazamo wa huruma
Tunapokumbuka jinsi Mungu ametupa rehema, inakuwa rahisi zaidi kuwaonyesha wengine rehema.
Episode hii inafichua sababu zinazowapelekea wasichana kudhani sio wazuri, fikira hii imepelekea wengine kufanya maamuzi yalioathiri maisha yao. Wengine wameishinda fikira hii inayotawala katika jamii ya Kiafrika. Wamewezaje? Najma anamhoji Emmy Rose Rugumamu kuhusu kampeni yake ya kusaida wanawake wenye mauombo makubwa. Emmy Rose ni Communication Professional ,anafanya kazi UWC East Africa, Pia ni kiongozi wa TEDxMajengo , Emmy Anapenda kutengeneza maudhui na kujieleza (storytelling ) pia ni mwandaaji wa open mic nights huko Arusha. Kuna sauti za wanawake wengine na experience zao katika kushinda mtazamo wa jamii juu ya umbo au uzuri wao. Subscribe uweze kupata notification kila tunapopublish episode mpya.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina tukiangazia juhudi za kuwajengea watoto tabia ya kupenda kusoma vitabu na pia habari kwa ufupi zikiwemo ripoti ya UNAIDS na WHO, na usaidizi kwa wakimbizi na jamii za wenyeji nchini Chad. Mashinani tutakwenda nchini Cameroon, kulikoni?Msichana Marynsia Mangu kwa kutambua umuhimu na maarifa yanayopatikana kwenye vitabu lakini jitihada zake za kuwashawishi marafiki zake kusoma vitabu kushindwa kuzaa matunda akaamua kufuata usemi wa Kiswahili Samaki mkunje angali mbichi na kuanzisha shirika la success Hands au kwa lugha ya Kiswahili Mikono yenye Mafanikio ambalo jukumu lake ni kuwajengea watoto tabia yakupenda kusoma vitabu tangu wangali tumboni mwa mama zao.Ripoti mpya ya tathimini iliyofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masiuala ya ukimwi UNAIDS kuelekea siku ya ukimwi duniani ambayo kila mwaka huadhimishwa Desemba Mosi inaonyesha kuwa pengo la usawa ni kikwazo kikubwa katikia juhudi za kutokomeza janga la ukiwmi duniani. Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO leo limesema majeraha na machafiuko vinasababisha vifo vya watu 12,000 kila siku kote duniani ambavyo ni sawa na kifo 1 kati ya vifo 12. Kupitia ripoti yake mpya “Mtazamo wa kuzuia majeraha na machafuko” iliyotolewa leo mjini Geneva Uswis WHO inasema sababu kuu tatu kati ya tano zinazosababisha vifo vywa watu wa umri wa kati ya miaka 5 hadi 29 ni majeraha, athari za ajari za barabarani , mauaji na kujiua.Na mashirika ya Umoja wa Mataifa ile la Mpango wa chakula duniani WFP na linaloshughulika na wakimbizi UNHCR wametoa ombi la dola milioni 161 ili wasikatishe huduma ya chakula cha msaada kwa ajili ya kuwasaidia wakimbizi na jamii za wenyeji nchini Chad.Na leo mashinani tutaelekee barani Afrika nchini Cameroon kumsikiliza Cecile Ndjebet ambaye anaeleza uhusiano uliopo kati ya haki ya umiliki wa ardhi hasa kwa wanawake na uhifadhi wa mazingira.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Na Padre Dominic Mavula C.PP.S Mkurugenzi wa Matangazo Radio Maria Tz
Haijalishi nini kinaendelea katika maisha yako, jifunze jinsi tabia ya kuaminiana inavyoachilia furaha huku subira hukuruhusu kufurahiya wakati huo.
Jifunze leo kujiamini wewe ni nani katika Kristo na kuacha kuishi kwa kujilinganisha na wengine.
Je! Unatambua kuwa mtazamo wako unatuma ujumbe kwa adui? Je! Yako inamwambia anashinda au anashindwa?
Marekebisho kidogo kwa mtazamo wako yanaweza kuleta mabadiliko makubwa maishani mwako.
Kuhisi kukwama kwenye hali ya huzuni? Leo, Joyce atakukumbusha kuwa nguvu ya Mungu iliyo ndani yako inaweza kukukamata kutoka kwa hali iliyokukwamiza na kukuelekeza katika hatima yako!
Mtazamo ulio nao wakati wa shida ni muhimu kwa mafanikio yako ya mwisho. Jifunze jinsi kufanya mema kwa wengine kunaweza kuinua roho yako na kukuinua kutoka shimoni.
Je! Yosefu alitokaje kutoka kwenye shimo hadi ikulu? Hakukata tamaa wakati mambo yalikuwa magumu katikati ya safari.
Usijaribu kuwa vile watu wengine walivyo. Gundua kile neema ya Mungu imekujalia kufanya.
Tarehe 10 mwezi Machi mwaka 2022, kumefanyika maadhimisho ya kwanza ya siku ya majaji wanawake duniani. Siku hii imeadhimishwa na maudhui yakiwa "Haki katika Mtazamo wa Kijinsia." Lengo ni kuona ni kwa vipi majaji wanawake wanaweza kuwa chachu katika utoaji wa haki kwenye mahakama kwa kuzingatia kuwa tasnia hiyo imegubikwa na mfumo dume. Katika kufahamu ukweli wa hoja hiyo Assumpta Massoi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa amezungumza na Jaji Hannah Okwengu wa Mahakama ya Rufaa nchini Kenya ambaye anaanza kwa kuelezea anajisikiaje kuwa Jaji kwenye tasnia iliyozoeleka kuwa ya wanaume wengi zaidi.
Kujifunza kungojea kwa subira kwa baraka za Mungu ni sehemu muhimu ya kudumisha furaha yetu.
Sio hali zetu ambazo huamua furaha yetu. Ni mtazamo wetu wakati wa hali zetu ndio huleta tofauti.
Hivi karibuni nchini Kenya na Tanzania, kumekuwa na mjadala kuhusu hatua za serikali ya nchi hizo kuendelea kukopa kiwango kikubwa cha pesa, hali ambayo inaelezwa imeongeza mzigo kwa raia ambao wanalipa kodi kiwango kikubwa. Mtazamo wako ni upi kuhusu hatua ya serikali kuendelea kukopa ? Unahisi fedha zinazochukuliwa na serikali zimetumika ipasavyo ?
Umoja wa Mataifa uliutangaza mwaka huu wa 2021 unaoelekea ukingoni kuwa mwaka wa mbogamboga na matunda lengo likiwa ni kuelimisha watu kuhusu umuhimu na faida za mbogambona na matunda mwilini. Miriam Nabakwe wa nchini Kenya anasema tatizo hilo la watu kutokula mbogamboga lipo na mbaya zaidi ni kuwa hata vyakula ambavyo watu sasa wanavithamini si vile vya asili na hivyo kuongeza tatizo juu ya tatizo kwani anaamini vyakula vya asili vilivyosalia katika maeneo mbalimbali duniani ndivyo vyenye virutubisho asilia. Kwa msingi huo ameamua kufanya juhudi binafsi kuwahamasisha watu wa nchini mwake Kenya angalau kwa kuanzia katika mji mkuu, Nairobi ili watu warejee katika ulaji wa vyakula vya asili. Anafanyaje? Tuungane na mwandishi wetu wa Kenya Jason Nyakundi ambaye amezungumza naye.
Makala hii imeangazia vurugu zinazoshuhudiwa nchini Sudan baada ya kufanyika mapinduzi ya kijeshi na baadaye kuachiwa huru kwa waziri mkuu Abdallah Hamdok ambapo Umoja wa mataifa, Umoja wa Afrika, zimelaani hali hiyo ambapo maandamano yameendelea nchini humo. Huko DRC tumeangazia kuhusu kuapishwa kwa mwenyekiti mpya wa CENI Denis Kadima anayepingwa na dhehebu la kikatoliki na lile la kiprotestanti pamoja na mambo mengine yaliyojiri duniani.
Makala hii imeangazia hatua ya rais wa DRC Felix Tshisekedi kumwidhinisha Denis Kadima kuwa mwenyekiti mpya wa tume ya uchaguzi CENI pamoja na wajumbe 12 ikitarajiwa kwamba upinzani utatoa majina ya wajumbe watatu ili kukamilisha orodha ya wajumbe 15. Kenya na Malawi zilitiliana saini makubaliano kadhaa ikiwemo ya kibiashara na usalama pamoja na mambo mengine mengi..Karibu kuungana na mwandishi wetu Reuben Lukumbuka kusikiliza zaidi
Makala hii imeangazia ziara ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta nchini Marekani na ahadi za mwenyeji wake rais Joe Biden, hali ya wasiwasi inayosababishwa na waasi wa ADF huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika maeneo ya Mutwanga jeshi la congo FARDC lashirikiana na askari walinzi wa mbuga ya wanyamapori ya Virunga katika kukabiliana na kundi la ADF, hali ya kisiasa nchini Rwanda na mataifa ya magharibi pia mambo mengine mengi. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kusikiliza zaidi
Makala hii imeangazia kufukuzwa kwa wafanyakazi wa umoja wa mataifa nchini Ethiopia, mvutano kati ya viongozi wa madhehebu ya kikatoliki kiprotestanti na makanisa ya uamsho huko DRC washindwa kuafikiana kuhusu uteuzi wa mwenyekiti mpya wa tume ya uchaguzi, CENI. Huko Burundi wafanyakazi wa serikali waaswa kuhalalisha ndoa zao; la sivyo wafukuzwe kazi...pamoja na mengine mengi duniani kwa wiki hii. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kusikiliza zaidi.
Miongoni mwa taarifa kuu za dunia tulilozipa uzito wiki hii ni pamoja na Ethiopia kuwafukuza viongozi wa Umoja wa Mataifa nchini mwake, hali ya usalama kuendelea kuzorota Mashariki mwa DRC na Majenerali wa Marekani wasema walimshauri rais Joe Biden kutowandoa wanajeshi wote nchini Afganistan.
Makala hii imeangazia kuzorota kwa mahusiano ya kidiplomasia kati ya Rwanda na Ubelgiji kufuatia kesi ya Paul Rusesabagina, na huko DRC kukamatwa kwa mwandishi wa habari Sosthene Kambidi kupisha uchunguzi kuhusu mauaji ya wataalamu wawili wa Umoja wa mataifa Zaida Catalan na Michael Sharp mwaka 2017, pamoja na mengine mengi yaliyojiri kwenye Mataifa kadhaa.
Makala hii imeangazia ripoti ya tume ya umoja wa mataifa kuhusu haki za binadamu nchini Burundi ambayo imeonesha kuzorota kwa haki za binadamu, katika kipindi cha miezi 15 iliyopita, nchini DR Congo polisi jijini Kinshasa walitumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa muungano wa upinzani wa Lamuka walipoandamana kupinga kuingiliwa kisiasa kwa CENI, Septemba 14 aliuawa mwanachama maarufu wa wakimbizi wa Rwanda nchini Msumbiji Revocat Karemangingo, afisa wa zamani wa jeshi la Rwanda lililopinduliwa na mwenye cheo cha luteni pamoja na mambo mengine mengi kutoka kila kona ya dunia.
Makala hii imeangazia wito wa mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel raia wa DRC, Daktari Denis Mukwege, wa kuundwa kwa mahakama maalumu ya kimataifa itakayoshughulikia kesi za makosa ya uhalifu wa kivita pamoja na makosa mengine katika majimbo ambayo yanashuhudia hali tete ya usalama kwa karibu robo karne..pamoja na mambo mengine mengi kutoka ulimwenguni
Wiki hii, miongoni mwa Habari Kuu za dunia, tulilozipa nafasi kubwa kwenye chumba chetu cha Habari ni hatua ya wanajeshi wa Marekani kuondoka nchini Afghanistan baada ya miaka Ishirini.
Maelfu ya watu wameendelea kuondolewa nchini Afghanistan, baada ya Taliban kuchukua udhubiti wa nchi hiyo, ni miongoni mwa matukio ya dunia tu nayokuletea.
Makala hii imeangazia hali ya wasiwasi ilivyoshuhudiwa nchini Afghanistan baada ya Taliban kuudhibiti mji mkuu wa Kaboul, kule nchini DRC watu 18 wauawa mashariki mwa nchi hiyo, na nchini Kenya mahakama ya rufaa ilitupilia mbali kesi inayohusu mchakato wa mabadiliko ya katiba maarufu kama BBI, na mengine mengi. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kusikiliza zaidi.
Katika makala hii tumeangazia uchaguzi mkuu wa nchini Zambia, na pia watumishi wa umma kutakiwa kuchanja dhidi ya Covid 19 wakati huko DRC mauaji yaliendelea kushuhudiwa huko wilayani Beni, Burundi na mambo mengine mengi...
Makala hii imeangazia mchakato wa upatikanaji wa mwenyekiti mpya wa tume ya uchaguzi nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo CENI, unavyogubikwa na siasa, kuchomwa makanisa, na mauaji,lakini pia ziara ya rais wa Tanzania Samia Suluhu nchini Rwanda, miongoni mwa mengine mengi......
Miongoni mwa yale tuliyokuandalia ni pamoja na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kutaka mipaka ya nchi yake kuheshimu mipaka ya nchi yake, Tanzania kuanza kupokea chanjo na sakata la Pegasus.
Miongoni mwa yale tuliyokuletea wiki hii ni pamoja na ziara ya rais za Burundi Evariste Ndayishimiye nchini DRC, miongoni mwa mengine mengi.....
Makala hii imeangazia mpango wa Umoja wa Ulaya kuiondolea vikwazo nchi ya Burundi, Waziri wa mambo ya nje wa Burundi Albert Shingiro na balozi wa Claude Bochu waliendelea na mazungumzo ya kisiasa jijini Bujumbura, pia mkutano kati ya rais wa DRC Felix Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame, katika eneo la mpakani, lakini siasa za Uganda, pamoja na mwanasiasa wa upinzani wa Tanzania Tundu Lisu alizindua kitabu chake akiwa jijini Nairobi, na mambo mengine yaliyojiri duniani. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kusikiliza zaidi.
Makala ya wiki hii imeangazia ziara ya rais Felix Tshisekedi wa DRC katika eneo la mashariki ya nchi yake, lakini pia huko Zambia maombolezo ya kitaifa kufuatia kifo cha rais wa zamani wa nchi hiyo Kenneth Kaunda, kuachiwa huru kwa wafuasi wa chama cha upinzani nchini Uganda cha NUP, pamoja na matukio mengine barani Afrika na pia mkutano wa rais wa Marekani Joe Biden na rais wa Urusi Vladmir Putin, na siasa za Israeli
Mawaziri wa fedha kutoka mataifa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, alhamisi ya juma hili baadhi waliwasilisha bajeti kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kwenye mabunge yao.Huko DRC wakaazi waliorejea mjini Goma walalamikia ukosefu wa makazi na hali duni, katika eneo la Afrika magharibi rais wa Ufaransa Emmanuel Macron asimamisha operesheni za kijeshi Barkhane nchini Mali, lakini pia mkutano wa viongozi wa G7 Uingereza. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kupata mengi zaidi.
Makala ya wiki hii imeangazia kuhusu hatua ya serikali ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo kutangaza kutokea kwa wimbi la tatu la maambukizi ya virusi vya Corona katika taifa hilo, kufunguliza kwa mpaka wa Gatumba kati ya DRC na Burundi, na pia kukamatwa ka mwanablogu mwengine nchini Rwanda, pamoja na habari mseto za kimataifa. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kusikiliza zaidi..
Makala ya wiki hii imezungumzia kuhusu ziara ya rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, nchini Rwanda, ziara inayolenga kufufua na kuboresha mahusiano ya kidiplomasia kati ya nchi hizi mbili. Huko DRC wakaazi wa mjini Goma mashariki mwa taifa hilo walilazimika kuhamishwa baada ya gavana wa jeshi jenerali Constant Ndima kusema kuwa wataalamu wamemwambia kuna uwezekano wa kuwepo mlipuko wa pili, wakati Huko Burundi milipuko ya guruneti na watu wasiojulikana, pia makala hii imegusia habari zilizojiri kwengineko duniani.
Makala ya juma hili imeangazia kuapishwa kwa jaji Mkuu mpya wa Kenya Martha Koome ambaye ameweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kushikilia wadhifa huo nchini humo, ziara ya rais wa Uganda Yoweri Museveni nchini Tanzania ambako pamoja na mwenyeji wake Bi Suluhu alisaini mkataba kuhusu bomba la mafuta, kule DRC matamshi ya rais wa Rwanda Paul Kagame kwamba hakuna mauaji yaliyofanyika mashariki yakihusisha majeshi ya nchi yake, kwingineko duniani machafuko ya eneo la Gaza huko Israeli
Makala hii imeangazia kuapishwa kwa rais wa Uganda Yowezi Museveni, nchini Kenya mchakato wa kuifanyia katiba mabadiliko wakwamishwa na mahakama kuu, kule Burundi tumemlikia hali ya usalama baada ya kutokea mashambulizi katika eneo la Muranvya, wakati nchini DRC magavana wa kijeshi wiki hii walianza kazi kwenye majimbo yaliyo chini ya hali ya dharura, utasikia mengi kutoka sehemu nyingine za dunia. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka B.S.
Makala hii imeangazia hatua ya viongozi wa Kenya na Tanzania ya kuwahakikishia wafanyibiashara wa nchi hizo mbili kuimarisha mazingira ya kufanya biashara kati ya mataifa hayo jirani, wakati huko DRC rais Felix Tshisekedi aliwateua magavana wa Kijeshi kuongoza mikoa ya Kivu ya kaskazini na Ituri kama hatua ya kumaliza mauaji ya raia wa kawaida mashariki mwa Nchi hiyo, lakini pia siasa za Burundi, na ukanda wa Afrika na rubaa za kimataifa. Ungana na mwandishi wetu Reuben Lukumbuka kupata mengi zaidi.
Miongoni mwa habari kuu za dunia tulizokukusanyia katika makala hii kwa juma hili utasikia kauli ya rais wa DRC Felix Tshisekedi akiomba msaada wa Ufaransa kupambana dhidi ya waasi wa ADF mashariki mwa nchi yake, lakini pia afisa wa polisi Eric Saddam akishuhudia kuhusika na mauaji ya dereva wa mwanaharakati Floribert Chebeya, Kenya kufunga kambi 2 za wakimbizi: Dadaab na Kakuma mwaka ujao, machafuko ya nchini Chad, na kasi ya maambukizi ya Corona huko India.
Kenya na DRC zilitiliana sahini makubaliano ya kidiplomasia, kiusalama na kibiashara, Uganda yajibu madai ya DRC mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki ya ICJ huko Hague, Rais Samia amehutubia bunge na kutoa dira ya serikali yake, Mazishi ya rais wa Chad Idriss Déby Itno mbele ya viongozi kadhaa wa dunia, Urusi yaanza kuondoa vikosi vyake kutoka mipaka ya Ukraine, lakini pia siasa za Marekani Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kupata mengi zaidi
Nchini DRC wiki hii kuliripotiwa makabiliano makali kati ya jeshi la polisi na wakaazi wa eneo la Buhene jimboni Kivu kaskazini, nyumba kuteketezwa na mauaji mengine ya ajabu,wakati huko Barani afrika wiki hii waziri mkuu Hamdock alitangaza nia ya kumaliza mzozo wa mto Nile kati ya mataifa ya Misri na Ethiopia, kimataifa imeangaziwa hatua ya rais wa Marekani Joe Biden ya kuondoa wanajeshi wa nchi yake huko Afghanistan pamoja na waisilamu kote duniani kuanza funga ya mwezi wa ramadhani.
Niger ina rais mpya Mohamed Bazoum, Philip Mpango ateuliwa kuwa Makamu wa rais wa Tanzania huku mazungumzo ya jamii zinazoishi Mashariki mwa DRC yakianza jijini Kinshasa. Tumekuandalia haya na mengine mengi.
Makala hii imeangazia kuzikwa kwa aliyekuwa rais wa awamu ya tano wa Tanzania John Magufuli katika makaburi ya familia huko mjini Chato, mkoani Geita, Kaskazini Magharibi mwa Tanzania, na Huko Kenya kaunti tano, likiwemo jiji kuu Nairobi, Kajiado, Kiambu, Machakos na Nakuru, yalifungwa kuanzia Ijumaa ya marchi 26 kwa lengo la kupambana na ongezeko la maambukizi ya COVID-19 nchini humo, huku muda wa watu kutotembea katika kaunti hizo ni kati ya saa mbili usiku mpaka wa saa 10 Alfajiri.Hali nchini DRC, Uchaguzi wa Congo Brazzaville na kwingineko duniani yaliangaziwa katika makala haya
Ni wiki ambayo raia watanzania, wanaomboleza kifo cha rais wao Joseph Magufuli ambaye alikuwa hajaonekana hadharani kwa zaidi ya wiki mbili baada ya kusambaa kwa uvumi kuwa alikuwa anaumwa maradhi ya moyo kwa mujibu wa tangazo la serikali, nchi za Jumuia ya afrika mashariki zaomboleza pamoja na Tanzania, huko Uganda kiongozi wa upinzani alikamatwa wakati tume ya Monusco huko DRC juma hili iliahidi kuimarisha usalama mashariki mwa nchi hiyo, kimataifa tumeangazia makataa ya Nchini Ufaransa kwa muda wa wiki 4
Makala ya wiki hii imeangazia wito wa upinzani nchini Uganda kuandamana kupinga matokeo ya uchaguzi wa january mwaka huu, nchi ya Kenya imetangaza makataa ya siku 60 zaidi kukabiliana na maambukizi ya virusi vya Corona, huku aliyekuwa waziri mkuu wa nchi hiyo Raila Odinga akutwa na virusi vya Corona.Kule DRC watu waendelea kuuawa wakati ni juma ambalo Marekani ililitaja kundi la ADF kuwa ni la kigaidi, kimataifa tumeangazia maandamano ya nchini Ufaransa kwa juma hili.
Makala ya juma hili imeangazia hatua ya kanisa katoliki nchini Kenya kuunga mkono jitihada za serikali katika kutoa chanjo ya Covid 19 kwa raia wake, kauli inayopingana na msimamo wa madaktari wa kanisa hilo waliowataka waumini wao kutochoma chanjo hiyo kauli inayopingana na msimamo wa madaktari wa kanisa hilo waliowataka waumini wao kutochoma chanjo hiyo, pia mapigano kati ya majeshi ya Rwanda na Burundi, pamoja na mauaji ya watu 14 huko Mambelenge DRC na mengine mengi.
Kipindi hiki nilikibuni makusudi kutusaidia sisi binadamu kujua maana ya mtazamo na amani na kisha kuziunganisha kwa manufaa ya Ulimwengu na walimwengu wake☺️ --- Send in a voice message: https://anchor.fm/unityradio254/message
Yaliyojiri wiki Hii katika baadhi ya mataifa ya afrika kwanza ni Uchaguzi nchini Uganda ambako wananchi walimchagua rais na wabunge wao, mauaji kuendelea kushuhudiwa huko DRC, 40 wauawa Irumu kwenye jimbo la Ituri, Umoja wa mataifa walalamikia utovu wa usalama huko Jamhuri ya Afrika ya kati baada ya Uchaguzi, Wabunge nchini Marekani wakutana kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais Donald Trump.
Ni makala ya kwanza ya mwaka mpya wa 2021 kuuawa kwa watu zaidi ya 20 katika kijiji cha Mwenda mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, wanafunzi warejelea shule nchini Kenya, mgombea wa urais nchini Uganda Bobi Wine ahamisha familia yake nje ya nchi kabla ya kufanyika kwa uchaguzi nchini humo, rais Nana akufo ado wa Ghana kuwania kiti cha urais kwa muhula wa pili, na kimataifa wafuasi wakerais wa Marekani Donald Trump waandamana kupinga ushindi wake Joe Biden na kulivamia bunge la Capital Hill jijini Washington.
Many developing countries still fighting COVID - 19 pandemic. Economically, a lot of them will suffer, but the question is, how will they bounce back to normal? - Nchi zinazoendelea bado pia ziko kwenye mapambano ya janga hili la COVID - 19.Mataifa mengi yatayumba kiuchumi, swali ni je yatajiinua vipi kurudi kwenye hali yake ya kawaida?
Maombolezo ya kitaifa yaliendelea nchini Kenya baada ya kifo cha rais wa zamani wa nchi hiyo Arap Moi. Nchini Malawi, mahakama ya katiba ilibatilisha matokeo ya uchaguzi mkuu uliompa ushindi rais Peter Mutharika na huko DRC sakata la mchungaji na mwimbaji wa nyimbo za injili, Moise Mbiye lazua sintofahamu jijini Kinshasa kufuatia tuhuma za ubakaji, tume ya uchaguzi Burundi yatangaza idadi ya wapigakura, nchini Marekani baraza la seneta lamuondolea makosa rais wa Marekani, Donald Trump
Viongozi mbalimbali wa Afrika mashariki na kwingineko duniani walijiunga na Maelfu ya wakenya kushiriki mazishi ya aliyekuwa rais wa zamani wa nchi hiyo Daniel Arap Moi, katika eneo la Kabarak katika kaunti ya Nakuru, na huko jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, wasiwasi kuongezeka kuhusu maambukizi ya virusi hatari vya ebola, kutokana na maelfu ya wakaazi wa Mangina kutoroka makwao, mawaziri wa nchi za nje kutoka Uganda na Rwanda walikutana jijini Kigali, na kimataifa virusi vya Corona kusababisha maelfu ya watu kupoteza maisha nchini China.
Katika makala hii, tumeangazia maambukizi ya virusi vya Corona nchini China kuendelea kuzua hofu kubwa huku ulimwengu ukihamasika katika kupambana navyo, huko DR Congo mauaji yaliendelea huku maafisa wa serikali wakiahidi kuimarisha usalama kuzuia mauaji yanayotekelezwa na waasi wa ADF. Kimataifa, Uingereza yajivua uanachama wake rasmi katika umoja wa ulaya, pia mchakato wa kumwondoa rais wa Marekani Donald Trump kushika kasi.
Katika makala hii tumeangazia mwaka mmoja wa rais wa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi madarakani lakini pia kauli yake ya kulivunja bunge la kitaifa, nchini Burundi wabunge waidhinisha muswada wa sheria unaopanga marupurupu ya rais atakayestaafu lakini pia faida zingine, suala la ulanguzi wa binadamu nchini Kenya, waziri wa mambo ya ndani wa Tanzania ajiuzulu na mengine mengi katika uga wa kimataifa.
Jeshi la jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, juma hili lilifahamisha kuwa limedhibiti ngome muhimu ya Madina baada ya kuwatimua waasi wa ADF, huko Kenya waalimu watishia kuondoka katika eneo la Garissa kwa sababu za kiusalama, viongozi wa mataifa ya Sahel walikubaliana kuhusu kuimarisha mapambano dhidi ya magaidi, na huko Marekani mchakato wa kumuondoa madarakani rais Donald Trump washika kasi
Katika makala ya wiki hii tumeangazia kuhusu shambulio lililotekelezwa na wanamgambo wa al-Shabaab dhidi ya kambi ya simba huko Lamu pwani ya Kenya, wiki hii serikali ya DR Congo kukifunga chuo kikuu cha Kinshasa kufwatia vurugu zilizojitokeza ambapo askari polisi mmoja aliuawa na mahusiano kati ya Rwanda na Uganda yaanza kuboreka, kimataifa mvutano kati ya Iran na Marekani washika kasi mpya
Makala hii imeangazia namna ambavyo mamia kwa maelfu ya watu kote duniani walivyou karibisha mwaka mpya wa 2020, hali ya usalama kuendelea kuzorota wilayani Beni mashariki mwa DR Congo, wakati Kenya imeimarisha usalama huko Lamu, na kiongozi wa upinzani ashinda uchaguzi wa hivi karibuni, kimataifa kuuawa kwa mkuu wa majeshi ya mapinduzi Irani, na mgomo wa wafanyakazi waendelea Ufaransa
Makala ya wiki hii imeangazia ulimwengu wa wakristo ulivyoikaribisha sikukuu ya krismas mwaka 2019, mwendelezo wa mauaji katika baadhi ya vijiji wilayani Beni mashariki mwa DRC, mazungumzo kuhusu upatikanaji wa serikali ya umoja wa kitaifa nchini Sudan kusini, kurejelewa mwezi february mwakani, pia kuendelea kwa mgomo wa kitaifa nchini Ufaransa kufwatia mpango wa marekebisho ya mfumo wa pensheni
There have been many questions about the growth of the Tanzanian economy. SBS Swahili had the opportunity to speak with some international businessmen about the whole economic trend. And this is the second part of that conversation. - Kumekuwa na maswali mengi juu ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania. SBS Swahili ilipata wasaa wa kuzungumza na baadhi ya wafanyabiashara wa kimataifa kuhusiana na mwenendo huo mzima wa uchumi. Na hii hapa ni sehemu ya pili ya mazungumzo hayo.
Katika makala hii tumeangazia mchakato wa bunge la Marekani kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais Donald Trump, wakati barani afrika kuendelea kwa mauaji ya raia wasio na hatia huko mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo pamoja na siasa za Kenya, Sudan, Niger, na pia hatua ya uibgereza ya kujiondoa kwenye umoja wa ulaya, lakini pia mgomo wa wafanyakazi wa sekta mbali mbali nchini Ufaransa. Ungana na mwandishi wetu Reuben Lukumbuka
There have been many questions about the growth of the Tanzanian economy. SBS Swahili had the opportunity to speak with some international businessmen about the whole economic trend. - Kumekuwa na maswali mengi juu ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania. SBS Swahili ilipata wasaa wa kuzungumza na baadhi ya wafanyabiashara wa kimataifa kuhusiana na mwenendo huo mzima wa uchumi.
Makala ya juma hili imeangazia kukamatwa kwa gavana wa kaunti ya Nairobi Mike Mbuvi Sonko, na baadaye kuachiwa huru kwa makosa ya ufisadi, nchini DRCongo rais Felix Tshisekedi alilihutubia taifa kupitia bunge la nchi hiyo, naye waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed aliipokea tuzo ya amani huko Oslo,huko Niger rais wa Ufaransa Emmanuel Macron aliahirisha mkutano wa viongozi wa G5 Sahel hadi january mwakani. Kimataifa tumeangazia uchaguzi wa Uingereza uliompa ushindi Boris Johnson
Ni juma ambalo limeshuhudia kusitishwa kwa shughuli za maisha pia maandamano ya kupinga uwepo wa Monusco nchini DRC, huku waandamanaji wakiituhumu kwa kushindwa kuwalinda raia wakati huu mauaji yakiendelea wilayani Beni, nchini Kenya gavana wa jimbo la Nairobi Mike Sonko,akamatwa kwa tuhuma za ufisadi. Rais wa Uganda Yoweri Museveni ahimiza matembezi ya kupinga ufisadi nchini mwake. Ufaransa, maandamano ya kupinga mageuzi ya mfumo mpya wa mafao ya pensheni yaliendelea. Ungana na mwandishi wetu Reuben K.Lukumbuka
Katika yaliyojiri huko DRC wiki hii wananchi waomboleza vifo vya watu zaidi ya ishirini katika ajali ya ndege ya shirika la Busy Bee mjini Goma, pia maandamano makubwa yaliripotiwa ambapo wananchi wameishutumu Monusco kwa kushindwa kuuthabitisha usalama katika mji wa Beni. Rais Uhuru Kenyatta akabidhiwa ripoti ya BBI, Nchini Kenya.Mchakato wa kumwondoa madarakani rais Donald Trump washika kasi.
Katika makala ya juma hili tumeangazia mauaji mengine mapya huko Beni mashariki mwa DR Congo ambapo watu wengine saba waliripotiwa kuuawa mwanzoni mwa juma lililopita, vijana waliohamaki waliweka vizuizi vya barabarani, awamu mpya wa mazungumzo ya amani nchini Sudan Kusini, na katika uga wa kimataifa siasa za Marekani na mchakato wa kumng'oa madarakani rais Donald Trump, pamoja na mengine mengi. Ungana na mwandishi wetu Reuben Lukumbuka kusikiliza zaidi.
Rais wa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi Tshilombo alikutana na mwenyeji wake rais wa uganda Museveni na kwa pamoja wamekubaliana kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia kati ya mataifa yao mawili, baada ya kuzuru Uganda rais Tshisekedi alielekea Ufaransa, kabla ya kuenda Ujerumani, mkutano kuhusu idadi ya na maendeleo ya dunia wamalizika wakati kimatifa rais wa Bolivia juma hili alitangaza kujiuzulu kwake.
Makala ya juma hili imeangazia mkutano kati ya rais wa Sudan kusini Salva Kiir na kiongozi wa waasi Riek Machar jijini Kampala chini ya usimamizi wa rais yoweri Museveni. Nchini DRCongo watu wasiopungua 10 waliuawa katika mji wa Kokola, wilayani Beni katika shambulizi linalodaiwa kuwa lilitekelezwa na waasi wa ADF, wakati kimataifa tumeangazia ziara ya rais wa Ufaransa Emmanuel Macron nchini China.
Wakati tarehe ya uundwaji wa serikali ya mpito nchini Sudan kusini, november 12 inapokaribia, kiongozi wa waasi nchini humo Riek Machar asema hayupo tayari kurejea Juba, makala ya mtazamo wako kwa yaliyojiri wiki hii pia imeangazia ziara ya mwanasiasa wa upinzani nchini DRC Moise Katumbi mashariki mwa nchi hiyo, wakati kimataifa tumemulika mvutano wa wabunge nchini Marekani kutaka kumuondoa madarakani rais Donald Trump
Katika makala hii tumeangazia matukio kadhaa huko jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ambako juma hili, mashirika ya kiraia yalipinga mpango uliopo wa kuundwa kwa kikosi cha pamoja cha majeshi kutoka nchi za maziwa makuu kukabiliana na wapiganaji maimai pia makundi mengine ya wapiganaji wa kigeni yanayoendelea kuyumbisha usalama na kutekeleza mauaji nchini DRC, lakini pia Ripoti inayotarajiwa kutoa suluhu ya changamoto zilizojitokeza wakati na baada ya uchaguzi mkuu nchini Kenya, BBI; wakati kimataifa tumeangazia Brexit.
Machache kati ya tuliyoyafumbata katika makala ya mtazamo wako kwa yaliyojiri wiki hii ni pamoja DRC yapata serikali mpya miezi saba baada ya kuapishwa kwa rais Felix Tshisekedi na katika uga wa kimataifa mkutano wa pamoja baina ya viongozi wa Afrika na Japan watia nanga huko Yakohama. Ungana na Fredrick Nwaka aliyekuandalia makala haya.
Makala hii imeangazia makubaliano yaliyofikiwa kati ya viongozi wa waandamanaji na wakuu wa kijeshi kuhusu muundo wa serikali ya mpito nchini Sudan, huko DRCongo rais Felix Tshisekedi alitembelea kambi ya wakimbizi huko Djugu katika jimbo la Ituri, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo, ziara ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta nchini Tanzania, wakati kimataifa mvutano kati ya Marekani na Iran kuhusu suala la Nuklia
Juma hili lilishuhudia kufariki dunia kwa aliyekuwa rais wa Misri, Mohammed Morsi kiongozi aliyechaguliwa kidemokrasia akiwa mahakamani akiisikiliza kesi yake, huko DRC naibu mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Norbert Basengezi alitangaza kujiuzulu, rais wa Marekani Donald Trump aituhumu Iran kwa kudungua ndege yake isiyo na rubani katika anga ya mashariki ya kati.
Katika makala ya juma hili tumeangazia hatua ya Marekani kumtuma mjumbe wake huko Sudan kupatanisha kamati ya kijeshi na waandamanaji, ziara ya rais wa DRC Felix Tshisekedi nchini Tanzania, lakini pia kusomwa kwa badjeti ya mwaka 2019/2020 katika mataifa ya jumuia ya Afrika mashariki, kadhalika mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola nchini Uganda.
Ni juma ambalo limeshuhudia hatua ya umoja wa Afrika kutangaza kusimamisha uanachama nchi ya Sudan na kutaka kuwekwa kwa utawala wa kiraia ili kumaliza mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini humo, na huko DRC waasi 23 wa ADF wameuawa maeneo ya Beni mashariki mwa nchi hiyo, kimataifa ziara ya rais wa Marekani Donald Trump nchini Uingereza.
Katika makala hii tumeangazia mazishi ya aliyekuwa kinara wa upinzani nchini jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, Etienne Tshisekedi, upigaji marufuku wa mifuko ya plastiki nchini Tanzania, kuapishwa kwa rais wa Malawi Peter Mutharika, pia rais wa Nigeria Muhammadou Buhari, na katika uga wa kimataifa kurudiwa kwa uchaguzi wa Israeli baada ya waziri mkuu Benjamin Netanyahu kushindwa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa
A new report has found young Australians are confused about consent and control in relationships.The National Community Attitudes towards Violence Against Women Survey found a disturbing number of young people blame women for being sexually assaulted and having their nude images shared without consent. - Utafiti mpya umebaini, Waustralia wadogo hawaelewi kuhusu swala zima la idhini na mfumo dume (mwanaume pekee kuwa na sauti au udhibiti) kwenye mahusiano.Mtazamo wa Kitaifa wa Jamii kuhusu utafiti wa Unyanyasaji dhidi ya Wanawake umegundua, baadhi ya vijana wadogo wanawalaumu wanawake kwa kudhalilishwa na picha zao za utupu kutumika bila ridhaa zao.
Ungana na Fredrick Nwaka wiki hii akikuletea makala ya Mtazamo wako kwa yaliyojiri wiki hii na baadhi ya habari muhimu ni Rais wa DRC kumteua Sylivester Ilunga Ilukamba kuwa waziri mkuu wa taifa hilo, Cyril Ramaphosa aapishwa kuwa rais wa Afrika Kusini na Narendra Modi achaguliwa tena kuwa waziri mkuu wa India
Makala ya Afrika ya Mashariki inaangazia juu yauapatikanaji katiba mpya nchini Tanzania. Hii ni kuwa wakati huu ndiomuda wa Bunge maalumu la Katiba kurejea Bungeni na kujadili kwa upyarasmu ya pili ya katiba. Kundi la UKAWA wako nje ya Bunge na Kundilingine wako ndani ya Bunge. Je, ni nini Mtazamo wa walioko bungeni nawalioko nje ya Bunge? Kupata mengi ungana na Julian Rubavu.
Swahili: Initiating Spiritual Growth in the Church: Audios, Videos and Articles
Initiating Spiritual Growth in the Church. Translated from English into Swahili - An overview helping believers not only understand his own Christian life but how to help others grow. Mtiririko, Mtazamo wakijumla 1 yohana 2:12-14
Swahili: Initiating Spiritual Growth in the Church: Audios, Videos and Articles
This Video on The Flow: Level #2 shows how young Christians grow and mature. They face specific battles and must learn to master God's Word and trust God to grow. The young believer is likened to the youth in the analogy of the family and largely learns how to overcome temptations. The Flow Level #2 (1 John 2:12-14): helps young believers mature and overcome - Mtiririko, Hatua ya pili, Vijana. Increase the faith of the believers in your church!