Habari RFI-Ki

Follow Habari RFI-Ki
Share on
Copy link to clipboard

Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.

RFI Kiswahili


    • Feb 24, 2026 LATEST EPISODE
    • weekdays NEW EPISODES
    • 9m AVG DURATION
    • 429 EPISODES


    Search for episodes from Habari RFI-Ki with a specific topic:

    Latest episodes from Habari RFI-Ki

    Somaliland yatangaza kuruhusu Marekani kuchimba madini na kuweka kambi za jeshi

    Play Episode Listen Later Feb 24, 2026 9:46


    Kikao cha dharura cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki

    Play Episode Listen Later Feb 18, 2026 9:35


    Rais wa Kenya William Ruto, ameitisha kikao cha dharura cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika mashariki  mwezi ujao kujadili changamoto ya kifedha ambayo imetatiza shughuli za taasisi za jumuiya hiyo, tatizo kubwa likiwa baadhi ya nchi kuchelewesha kutoa michango kwa wakati. Mkutano huo utajadili mfumo mpya wa uchangishaji fedha na namna ya kupunguza matumizi ya jumuiya hiyo.

    Raia wa Afrika kuendelea kusajiliwa kupigana vita nchini Ukraine

    Play Episode Listen Later Feb 17, 2026 9:57


    Mkutano wa 39 wa umoja wa Afrika jijini Addis Ababa

    Play Episode Listen Later Feb 17, 2026 9:50


    Mwishoni mwa juma mkutano wa 39 wa Umoja wa Afrika (AU) umefanyika jijjini Adis Ababa nchini Ethiopia   Huku viongozi walioudhuria wakilipea kipau mbele swala la usalama  na uchumi wakati huu matafia mengi ya Afrika yakishuhudia migogoro na kudorora kwa uchumi.

    Kamanda wa polisi pwani ya Kenya atoa agizo kuwapiga wahalifu risasi

    Play Episode Listen Later Feb 10, 2026 10:00


    Mwishoni mwa juma Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani nchini Kenya Ali Nuno alitoa agizo kwa polisi kuwapiga risasi washukiwa wa uhalifu baada ya eneo hilo kushuhudia ongezeko la magenge yaliyojihami kwa mapanga. Hata hivyo hatua hiyo imepingwa vikali na mashirika ya kutetea haki za binadamu .Tumekuuliza unazungumziaje agizo hilo,Unadhani ni hatua sahihi kumaliza uhalifu na Nchini mwako hali ikoje

    Marekani yakutana na viongozi wa Afrika kuhusu swala la madini

    Play Episode Listen Later Feb 10, 2026 10:05


    Afrika Kusini yatangaza kuwaondoa wanajeshi wake kutoka kwa monusco nchini DRC

    Play Episode Listen Later Feb 9, 2026 10:00


    Mwishoni mwa juma Afrika Kusini ilitangaza kuondoa wanajeshi wake kutoka kwa tume ya Umoja wa Mataifa ya kulinda amani nchini DRC (MONUSCO) baada ya kikosi hicho kuhudumu kwa miaka 27.Pretoria inasema hatua hiyo ni kutokana na mipango yake ya kurekebisha na kuimarisha raslimali ya jeshi lake.Tumemuuliza msikilizaji anazungumziaje hatua hii ya Afrika kusini,Hatua hii ni kumaanisha Monusco imepoteza nguvu DRC na Nini kifanyike kuleta usalama wa kudumu nchini DRC?

    Maoni yako Ijumaa hii kwenya mada huru

    Play Episode Listen Later Jan 30, 2026 10:00


    Matumizi ya mitandao ya kijamii kwa watoto chini ya miaka 15

    Play Episode Listen Later Jan 30, 2026 9:56


    Nchi za magahribi kupitisha sheria za kupiga marufuku mitandao ya kijamii kwa watoto walio chini ya miaka 15.

    Mwaka mmoja tangu mji mkubwa mashariki mwa DRC kuanguka mikononi mwa M23

    Play Episode Listen Later Jan 30, 2026 10:02


    Marekani kujiondoa rasmi kwenye WHO, hatua hatari kwa sekta ya afya dunaini

    Play Episode Listen Later Jan 27, 2026 9:53


    Wiki iliopita, ilijiondoa kwenye shirika la afya duniani licha ya onyo kuwa hatua hiyo itaathiri ufadhili kwenye sekta ya afya duniani. Wiki chache zilizopita, rais Donald Trump alitangaza pia kuwa Marekani itajiondoa kwenye mashirika 66 ya kimataifa, yakiwemo yaliyo chini ya Umoja wa Mataifa

    Siku ya kimataifa ya nishati safi: Wewe unatumia nishati gani?

    Play Episode Listen Later Jan 27, 2026 9:21


    Januari 26 2026, dunia  inaadhimisha Siku ya Kimataifa ya Nishati Safi, lengo likiwa ni kuhamasisha umuhimu wa matumizi ya nishati safi katika maisha ya kila siku, na mchango wake kwa mazingira na maendeleo endelevu.

    Serikali ya Uganda yafunga mitandao kuelekea uchaguzi mkuu wa siku ya Alhamisi

    Play Episode Listen Later Jan 15, 2026 10:01


    Hii leo tunazungumzia hatua ya serikali ya Uganda kuagiza mitandao kufungwa, ikisema hatua hiyo inalenga kudhibiti habari za kupotosha na kulinda usalama wa taifa, kueleka uchaguzi mkuu unaofanyika Alhamisi hii.

    Maoni: Hatua ya Marekani kutangaza kujiondoa katika mashirika 66 yakiwemo yale ya Umoja wa Mataifa

    Play Episode Listen Later Jan 15, 2026 10:01


    Agizo la kiutendaji lililosainiwa na rais wa Marekani linaagiza Marekani kujiondoa kutoka kwa jumla ya mashirika 66, karibu nusu yake ambayo yana uhusiano na Umoja wa Mataifa, Ikulu ya White House ilisema wiki iliyopita. Miongoni mwa hayo ni Mkataba wa Mfumo wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa (UNFCCC), mkataba wa msingi wa mikataba mingine yote ya kimataifa ya hali ya hewa, uliohitimishwa mwaka wa 1992 katika Mkutano wa Rio Earth.

    Wawakilishi wa Afrika mashariki wayaaga michuano ya AFCON 2025

    Play Episode Listen Later Jan 8, 2026 9:49


    Timu ya DRC "Leorpard" siku ya Jumanne ilikuwa mwakilishi wa mwisho wa Afrika Mashariki kuondolewa kwenye michuano ya kombe la mataifa ya Afrika, baada ya kupoteza mechi yao ya hatua ya 16 bora dhidi ya Algeria. Uganda ilikuwa ya kwanza kuondolewa katika hatua ya makundi ikifuatiwa na Tanzania iliyotolewa kwenye hatua ya mtoano.

    Matukio ya wanahabari kushambuliwa wakati wa kampeni za uchaguzi

    Play Episode Listen Later Jan 7, 2026 9:58


    Nchini Uganda, kuelekea uchaguzi mkuu, kumeripotiwa matukio ya wanahabari kushambuliwa na vyombo vya usalama wakati wakiripoti kampeni za uchaguzi na hasa za upinzani. Matukio kama haya yameshuhudiwa pia katika nchi nyingine za Afrika.

    uganda afrika wakati uchaguzi kampeni
    Marekani kufanya oparesheni ya kijeshi na kumkamata rais Nicolas Maduro

    Play Episode Listen Later Jan 6, 2026 9:52


    Mwishoni mwa juma lililopita, Marekani iliivamia Venezuela na kumkamata rais Nicolas Maduro, na sasa inatarajiwa kumshtaki kwenye mahakama zake kwa tuhuma za ulanguzi wa dawa za kulevya. Unafikiri kilichofanywa na Marekani ni sahihi?

    Mada huru ya mwisho wa mwaka 2025

    Play Episode Listen Later Dec 26, 2025 10:15


    Makala hii ya habari rafiki rafiki ijumaa ya desemba 26 2025 ni siku ya mada huru; tunakupa fursa kuchangia suala lolote ambalo limejiri nchini mwako wiki hii. Unaweza pia kuzungumzia kile ambacho umekisikia kwenye matangazo yetu ya redio juma hili. Nahodha wa Habari Rafiki Ruben Lukumbuka, moja kwa moja kutoka Studio maridai namba2.

    Ulimwengu washerehekea sikukuu ya Krismasi

    Play Episode Listen Later Dec 25, 2025 10:02


    Wakristo wanaadhimisha sikukuu ya Krismasi, wakati baadhi ya nchi kama Sudan, Ukraine na Mashariki mwa DRC yakikabiliwa na changamoto za usalama.-Unaadhimsisha sikuu ya Krismasi ukiwa wapi ? Sikukuu ya mwaka huu ikoje ?

    Maandalizi ya timu za mataifa ya Afrika mashariki na kati katika AFCON 2025

    Play Episode Listen Later Dec 23, 2025 10:01


    Msikilizaji Mashindano makubwa zaidi ya soka barani Afrika, Kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 yanaingia katika siku yake ya tatu leo jumanne ambapo jumla ya timu 24 za mataifa ya Afrika zikiwania taji hilo. Leo DRC wanamenyana na Benin, Tanzania wanakutana na Nigeria. Unazungumziaje maandalizi ya nchi za Afrika Mashariki na kati ?Nini matarajio yako kwenye mashindano haya ?

    Tume ya umoja wa mataifa nchini DRC, MONUSCO yaongezewa mwaka mmoja zaidi

    Play Episode Listen Later Dec 22, 2025 10:00


    Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeongeza muda wa mwaka mmoja kwa ujumbe wa kulinda amani nchini DRC, wakati mapigano yakiongezeka mashariki mwa nchi hiyo kufuatia mashambulizi mapya ya waasi wa M23. Uamuzi huu unakuja wakati mjadala ukiendelea kuhusu ufanisi wa MONUSCO nchini humo. Je, unaamini hatua hii itasaidia au ujumbe huo umepoteza uaminifu na uwezo wa kuleta mabadiliko ya kweli? Je, umoja wa Mataifa unapaswa kufikiria upya mkakati wake wa kulinda amani nchini DRC?

    Marekani yapiga marufuku kwa raia kutoka mataifa kadhaa kuingia ardhi yake

    Play Episode Listen Later Dec 18, 2025 10:01


    Makala hii imeangazia hatua ya hivi karibuni ya rais wa marekani Donald Trump ya kuongeza orodha mpya ya mataifa zaidi yakiwemo ya Afrika ikiwemo Tanzania,  ambayo raia wake wanazuiwa kuingia Marekani, tumekuuliza Je? hatua hii ni ya kibaguzi ama inalenga kuulinda usalama wa Marekani? Na kwa mtazamo wako Hatua hii Ina maana gani? Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kupata maoni ya wasikilizaji

    Waasi wa AFC/M23 watangaza kujiondoa katika mji wa Uvira DRC

    Play Episode Listen Later Dec 17, 2025 10:00


    Kumekuwa na hisia mseto tangu waasi wa AFC/M23 wanaoungwa mkono na Rwanda watangaze kuwa watawaondoa wapiganaji wao katika mji wa Uvira mkoani Kivu Kusini mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.Je? shinikizo la Marekani litazaa matunda? sikiliza maoni ya wasikilizaji wetu katika makala hii ya Habari rafiki 

    Ukoloni mamboleo na maendeleo ya bara la Afrika

    Play Episode Listen Later Dec 15, 2025 9:59


    Tarehe 14/12 dunia iliadhimisha miaka 60 ya azimio la kupinga ukoloni. Hata hivyo ukoloni katika sura zake za zamani na mpya bado unaathiri jamii zetu leo hii, baadhi wanaita ukoloni mamboleo.Je, ukoloni uliisha kweli Afrika au umebadilika tu? Je unaathiri vipi maendeleo ya Afrika? Nini kifanyike kuukomesha?Kupata mengi ungana na mwanahabari wetu Ruben Lukumbuka

    Maoni ya Wasikilizaji kuhusu habari zetu juma hili ikiwemo hali mashariki mwa DRC

    Play Episode Listen Later Dec 12, 2025 10:00


    Ilivyo desturi ya kila siku ya Ijumaa, ni mada huru. Tunampa msikilizaji wetu nafasi ya kuzungumzia taarifa ambazo tumeziangazia katika habari zetu juma hili, lakini pia matukio mbalimbali nchini mwake.

    Waasi wa AFC/M23 wanaosaidiwa na Rwanda waudhibiti mji wa Uvira nchini DRC

    Play Episode Listen Later Dec 11, 2025 9:59


    Waasi wa AFC/M23 wanaosaidiwa na Rwanda, ni rasmi sasa wanaudhibiti mji wa kimkakati wa Uvira jimboni Kivu Kusini, hatua inayokuja licha ya wiki iliyopita DRC na Rwanda kutia saini mkataba wa amani.Tunamuuliza msikilizaji anazungumziaje kilichofanywa na waasi wa M23,,Nini kifanyike? na Je, msikilizaji yuko Uvira au amekimbia kutoka Uvira

    Leo ni siku ya kuadhimisha haki za binadamu duniani lakini ukiukaji waripotiwa

    Play Episode Listen Later Dec 10, 2025 9:58


    Leo ni siku ya kimataifa ya haki za binadamu, hata hivyo dunia inaadhimisha siku hii huku vitendo vya ukiukaji wa haki za binadamu vikiendelea kuongezeka kwenye maeneo mbalimbali duniani, maeneo yenye mizozo vitendo hivi vikiwa vya kuogopesha.Tumekuuliza unafikiri kwanini vitendo hivi vinaongezeka licha ya sheria za kimataifa kuwepo?Hali ya haki za binadamu ikoje nchini mwako na Nini kifanyike kuimarisha haki za binadamu ulimwenguni?

    Upinzani barani Afrika waendelea kunyanyaswa na polisi wakati wa kampeni

    Play Episode Listen Later Dec 9, 2025 10:01


    Mada ya leo ni kuhusu kinara wa upinzani  nchini Uganda Bob Wine pamoja na baadhi ya wagombea wengine wa upinzani wameendelea kunyanyaswa na vyombo vya usalama wanapoendelea na kampeni zao, tume ya uchaguzi ikilaani vitendo hivyo.Yanayofanyika Uganda yanashuhudiwa pia kwenye mataifa kadhaa ya Afrika .Tumemuuliza msikilizaji  Hatua hii ya vyombo vya usalama inaathiri vipi demokrasia na nini kifanyike kujenga mazingira sawa ..Karibu

    Vita vyashuhudiwa DRC licha ya makubaliano ya kustisha vita kufanyika

    Play Episode Listen Later Dec 8, 2025 9:59


    Licha ya viongozi wa DRC na Rwanda kutia saini mkataba wa amani juma lililopita, mapigano yameripotiwa mashariki mwa Congo kati ya waasi wa M23 na jeshi la Serikali FARDC.Tulimuuliza mskilizaji Je hii ni ishara kuwa mkataba waliotia saini haujazaa matunda ,nani wakuwajibishwa kwa kinachotokea na  Nini kifanywe kuleta utulivu mashariki mwa Congo,,

    Maoni ya waskilizaji kuhsu taarifa zetu juma hili.

    Play Episode Listen Later Dec 5, 2025 10:03


    Kila ijumaa rfi inakupa nafasi kuchangia mada yoyote kupitia makala ya Habari Rafiki. Skiza kilichopewa kipao mbele kwenye makala ya juma hili.

    DRC/ Rwanda : Marais wasaini awamu ya mwisho ya mkataba

    Play Episode Listen Later Dec 5, 2025 10:01


    Shaba ya makala haya inalenga nchini DRC, viongozi wa DRC    marais Paul Kagame na  mwenzake Felix Tshisekedi wamesaini, awamu ya mwisho ya mkataba wa amani. Tumekuuliza Je, unadhani wananchi wa mashariki mwa DRC watanufaika moja kwa moja na makubaliano ya worshington?

    EAC : Wanasiasa wanatumia wahuni kujihami

    Play Episode Listen Later Dec 3, 2025 10:03


    Katika makala haya tujadili hatua ya ongezeko la visa vya wanasiasa wa upande wa serikali na upinzani kutumia makundi ya vijana au wahuni kutisha na kuvuruga mikutano ya mahasimu wao wa kisiasa hili likifanyika hata  kwenye mitandao. Tunakuliza unafikiri kwa nini wanasiasa wanaendelea kutumia makundi ya vijana au wahuni katika siasa. skiza makala haya.

    Uganda: Je midahalo ina manufaa kuelekea uchaguzi

    Play Episode Listen Later Dec 2, 2025 9:22


    Nchini Uganda, wawaniaji wa urais wameshiriki mdahalo kuelekea uchaguzi wa mwezi ujao, huku rais Museveni akisusia mdahalo huo. Je, unafikiri midahalo huwa na mchango wowote kwa wapiga kura kuelekea siku ya uchaguzi? Skiza baadhi ya maoni ya waskilizaji.

    Siku ya kimataifa ya kupambana na virusi vya ukimwi

    Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 9:59


    Siku ya kimataifa ya mapambano dhidi ya UKIMWI, Umoja wa Mataifa unasema kupungua kwa misaada kunatishia dunia kufikia lengo la kudhibiti ugonjwa huu ifikapo mwaka 2030, huduma za kinga zimevurugika hasa kwenye nchi masikini.  unazungumziaje siku hii, je dunia tumepiga hatua kukabiliana na ugonjwa huu? Skiza maoni ya baadhi ya waskilizaji.

    Viongozi wa umoja wa ulaya na umoja wa Afrika wakutana Luanda Angola

    Play Episode Listen Later Nov 26, 2025 10:08


    Viongozi wa Afrika na wale wa umoja wa Ulaya wamekutana nchini Angola, lengo likiwa ni kuimarisha ushirikiano wa usalama na kiuchumi, rasilimali za bara hilo zikimulikwa na mataifa yenye nguvu ambayo yameongeza kasi ya uwekezaji kwenye bara hilo. Tumekuuliza unaamini ushirikiano uliopo unanufaisha pande zote ? Ushirikiano wa aina gani Afrika inapaswa kuwa nao na nchi za magharibi?

    Vitendo vya utekaji kuongezeka Nigeria na baadhi ya nchi za Afrika ya kati

    Play Episode Listen Later Nov 24, 2025 10:01


    Msikilizaji juma lililopita watu wenye silaha waliwateka wanafunzi zaidi ya 300 pamoja na waalimu katika shule moja kwenye jimbo la Niger nchini Nigeria, tukio linalojiri siku chache tangu kutekwa kwa wanafunzi wengine 25 katika shule ya wasichana kwenye jimbo la Kebbi pia huko Nigeria. Vitendo vya utekaji wa watoto vinazidi kuongezeka katika nchi za Afrika magharibi na kati. Nini kifanyike kukomesha vitendo hivyo Afrika?Je taifa lako linashuhudia utekaji wa watoto? Ungana na Ruben Lukumbuka

    Maoni ya mskilizaji kuhusu matangazo yetu

    Play Episode Listen Later Nov 23, 2025 10:05


    Kila Ijumaa rfi Kiswahili inakupa nafasi ya kuchangi mada yoyote kuhusu taarifa na vipindi vyetu au kile kinafanyika hapo ulipo. Skiza maoni ya waskilizaji juma hili.

    Tanzania : Rais Samia amuteua mwanawe kuwa naibu waziri

    Play Episode Listen Later Nov 20, 2025 9:59


    Tunajadili   hatua ya viongozi kadhaa wa Afrika akiwemo rais wa Uganda, Yoweri Museveni, na rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, wamewateua watu wa familia zao katika nafasi za serikali, hali hii ikionekana kwenda kinyume na maadili ya kazi. Tunakuuliza Je, uteuzi wa ndugu serikalini ni sahihi au si sahihi? skiza Makala haya

    Kenya : Vyama vya kisiasa vina umuhimu kujenga demokrasia

    Play Episode Listen Later Nov 20, 2025 9:56


    Katika makala haya  tunaangazia nchi ya Kenya ambapo chama cha ODM kilichokuwa cha waziri mkuu wa zamani hayati Raila Odinga, kimeadhimisha miaka 20 tangu kuasisiwa kwake. Tunauliza je vya  kisiasa vina mchango gani katika kuimarisha demokrasia hapa Afrika? Skiza makala haya.

    Tanzania : Chakera kuwa mpatanishi

    Play Episode Listen Later Nov 19, 2025 9:53


     Aliyekuwa rais wa Malawi , Lazarus Chakwera kuteuliwa na Jumuiya ya madola kuwa mpatanishi wa mzozo wa kisiasa nchini Tanzania, hasa baada machafuko ya kipindi cha uchaguzi. Tunakuuliza , unafikiri rais Chakwera atafanikiwa kusuluhisha mzozo wa kisiasa nchini Tanzania.

    Ajali za barabarani zazidi kuwaua raia Africa

    Play Episode Listen Later Nov 17, 2025 9:59


    Ulimwengu umeadhimisha siku ya kumbukumbu kwa waathiriwa wa ajali za barabarani. Takwimu za umoja wa mataifa zinaonyesha kuwa, duniani kote, watu zaidi ya milioni moja hufariki dunia kila mwaka kutokana na ajali za barabarani, na millioni hamsini kujeruhiwa. Nini kifanyike kupunguza ajali za barabarani. Skiza makala kufahamau maoni ya mskilizaji zetu.

    Trump atishia kutumia jeshi la Marekani kupambana na wanajihadi wanaowauwa Wakiristo nchini Nigeria

    Play Episode Listen Later Nov 7, 2025 9:59


    Katika makala ya Habari Rafiki hii leo tunazungumzia hatua ya Rais wa Marekani Donald Trump kutishia kutumia jeshi la nchi yake kupambana na wanajihadi wanaowauwa Wakiristo nchini Nigeria. Kauli hii imewakasirisha viongozi wa Nigeria, ambao wanasema serikali nchini humo, haiungi mkono unyanyasaji wa kidini. Tumemuuliza msikilizaji anazungumzia vipi mpango wa huu wa Trump na ni nini kinaweza kufanyika kumaliza mauaji ya kidini nchini Nigeria.

    Tanzania : Maoni ya waskilizaji kuhusu uchaguzi wa Tanzania

    Play Episode Listen Later Nov 1, 2025 9:55


    Nini kilikukera kuhusu uchaguzi wa Tanzania ? Skiza maoni ya waskilizaji wetu.

    Maoni ya waskilizaji kuhusu matukio ya juma hili

    Play Episode Listen Later Oct 31, 2025 10:00


    Kila Ijumaa rfi Kiswahili inakupa nafasi kuchangia mada yoyote kuhusu matukio ya dunia. Skiza maoni ya waskilizaji juma hili.

    Kenya : Mitandao ya kijamii inasababisha matatizo

    Play Episode Listen Later Oct 29, 2025 10:04


    Gazeti la The Star nchini Kenya limewahi chapisha ripoti inayoonesha namna mitandao ya kijamii inavyoathiri watu kwa kusababisha wasiwasi, matatizo ya afya ya akili na athari nyinginezo. Tunakuuliza Je, maisha ya mitandao yanatusaidia kama jamii au yanatuumiza? skiza maoni ya waskilizaji wetu.

    Tanzania : Raia wajitokeza kumchagua rais na wabunge

    Play Episode Listen Later Oct 29, 2025 10:01


    Shaba yetu katika makala haya inalenga nchi ya Tanzania ambapo raia wameshiriki uchaguzi kumchagua rais na wabunge. Je, unauzungumziaje uchaguzi wa Tanzania? Haya hapa maoni ya waskilizaji.

    Djibouti : Laondoa ukomo wa kuwania urais

    Play Episode Listen Later Oct 27, 2025 9:59


        Djibouti  limekuwa taifa la  hivi punde  kuondoa rasmi kikomo cha umri wa rais , hatua inayotoa fursa kwa rais  Ismail Omar Guelleh kugombea muhula wa sita katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Aprili mwaka ujao. Awali Katiba ya nchi hiyo ilikuwa inamzuia rais kugombea tena baada ya kufikisha miaka 75.  Hali hii pia imeonekana kwenye mataifa kadhaa ya Afrika Mashariki kama vile Uganda. Skiza mahakala haya kuskia maoni ya waskilizaji.

    KILA SIKU YA IJUMAA KWENYE KPINDI CHA HABARI RAFIKI NI MADA HURU

    Play Episode Listen Later Oct 24, 2025 10:00


    Leo ni siku ya mada huru. Tunakupa nafasi kuzungumzia suala lolote ambalo limetokea nchini mwako wiki hii Unaweza pia kujadili kile ambacho umekisikia katika matangazo yetu ya wiki hii kwenye redio.

    WANASAYANSI VIONGOZI WAKUTANA AFRIKA KUSINI KUJADILI AFYA BILA UFADHILI WA NJE

    Play Episode Listen Later Oct 23, 2025 10:00


    Viongozi wa dunia, wataalam wa Afya na wanasayansi wanakutana Afrika Kusini siku chache kabla kikao cha G20, ili kuanganzia  kuhusu njia za kufadhili afya bila kutegemea ufadhili wa kigeni.Tumemuuliza msikilizaji maoni yake kuhusu uwezo wa mataifa ya Afrika kufadhili miradi ya afya?

    Mateka wa Israeli waliokuwa wanashikiliwa na Hamas waachiwa huru huko Gaza

    Play Episode Listen Later Oct 13, 2025 10:04


    Hivi leo viongozi wa dunia akiwemo rais wa Marekani, Donald Trump, wanakutana Misri kujadili mustakabali wa eneo la Gaza, baada ya makubaliano ya kihistoria ya wiki iliyopita. Makubaliano haya yameshuhudia kuachiwa kwa mateka, wafungwa na kusitishwa kwa vita vya Gaza. Tunakuuliza, unaamini makubaliano kati ya Hamas na Israel safari hii yatadumu?Nini cha zaidi kifanyike?Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka

    Tuzo ya nobeli kutolewa ijumaa wiki hii

    Play Episode Listen Later Oct 9, 2025 9:58


    Msikilizaji kesho Ijumaa oktoba 10 kamati inayotoa tuzo za kimataifa za Nobel itamtangaza mshindi, wakati huu watu wengi wakiwa wamempendekeza rais wa Marekani Donald Trump kutokana na mchango wake wa kutafuta amani mashariki ya kati, hata hivyo wadadisi wanasema kiongozi huyo hawezi kupewa tuzo hiyo. Unafikiri ni Kiongozi gani anastahili kupewa tuzo hii mwaka huu na kwanini? Ungana nami Ruben Lukumbuka, mubashara kutoka studio namba mbili hapa karibu tuandamane hadi tamati.-

    Claim Habari RFI-Ki

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel