Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.

Katika makala ya Habari Rafiki leo tunaangazia hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania, kuunda tume maalumu ya jinai itakayochunguza matukio ya vurugu zilizotokea wakati na baada ya uchaguzi wa Oktoba 29 mwaka uliopita, ili kubaini vitendo vilivyofanywa na kuwataja waliohusika ili waajibishwe kisheria

Siku ya Jumatatu uchukuzi ulitatizwa nchini Kenya kufuatia mgomo wa wahudumu wa magari ya uchukuzi wa umma kupinga ongezeko la bei ya mafuta. Hii ni baada ya serikali kupandisha Lita moja ya Petroli kufikia Shilingi za nchi hiyo 214 huku ile ya Dizeli ikifikia Shilingi 242. Tumemuuliza mskilizaji wetu anzungumziaaje kilichotokea nchini Kenya na nchini mwake hali iko je kuhusu bei ya mafuta.

Shirika la afya duniani limetangaza hali ya dharura ya kiafya duniani kutokana na mlipuko wa virusi vya Ebola mashariki mwa DRC, ikizitaka nchi kuchukua tahadhari kufuatia hofu ya ugonjwa huo kusambaa zaidi. Tumemuuliza mskilizaji wa RFI Kiswahili akiwa DRC na kwenye ukanda wa Afrika Mashariki anachukua hatua gani kujikinga.


Mkutano wa Afrika forward unaoongozwa na Ufaransa umeanza leo jijini Nairobi ambapo karibia marais 30 ,kutoka barani Afrika wanatarajiwa kuudhuria ili kujadili ushirikiano katika sekta ya uchumi wa buluu, mazingira ,afya na kilimo. Mkutano huu umetoa kipaumbele ka ajenda zinazowahusu vijana, na hasa matumizi ya teknolojia, akili unde au AI na namna vijana wanaweza kukumbatia fursa katika sekta hizo.

Sheria kama hiyo pia inatumika na Urusi, inakosolewa na wanaharakati wa haki za kibinadamu huku wapinzani wakisema inawalenga, kwa sababu ya kukosoa utawala wa rais Ypweri Museveni. Unazungumziaje sheria hii mpya nchini Uganda ?

Rais Samia Suluhu Hassan, anataka Kenya na nchi yake ya Tanzania kushirikiana ili kukabili uanaharakati wa 'kuvuka mipaka' kutoka kwa vijana wa Gen Z ambao ameelezea unatishia amani na usalama wa nchi nchi za Afrika Mashariki. Unazungumziaje kauli hii ya rais Samia? Unadhani ni sahihi kwa vijana kuadhibiwa kwa kushinikiza mabadiliko kwenye nchi zao?

Kenya na Tanzania zimekubaliana kuondoa vikwazo vyote visivyo vya kikodi vya kibiashara, ili kuimarisha ushirikiano wa kibiashara. Unaamini yaliyokubaliwa kati ya nchi hizo mbili yatatekelezwa ?

Msikilizaji mei 3 2026 dunia iliadhimisha siku ya kimataifa ya Uhuru wa wanahabari, ripoti zikionesha ongezeko kubwa la vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya waandishi wa habari.





Serikali ya DRC na waasi wa M23, mwishoni mwa juma wamekubaliana kuruhusu misaada ya kibinadamu kufika kwenye maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo pamoja na kubadilishana wafungwa katika muda wa siku 10 zijazo, haya yakifuatia mazungumzo ya Uswis yalitoratibiwa



Katika makala haya tunajadili iwapo mila za kiafrica zimeanza kuweka na namna gani zinaweza kudumishwa. Skiza makalaa

Kila Ijumaa rfi Kiswahili inakuapa fursa kuchangia mada yoyote ile. Skiza maoni ya juma hili.

DRC imejikatia tiketi ya kucheza kwenye kupute cha kuwania kombe la dunia Haya hapa maoni ya waskilizaji.

Ripoti ya shirika la Amnesty Interenational imeonya kuwa Kombe la Dunia la mwaka huu linaweza kuchangia ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu dunaini kutokana mpango wa mataifa wenyeji kuweka mikakati kali za uhamiaji na ufuatiliaji wa karibu wa mashabiki wa kigeni Je, unahisi mashabiki kutoka Afrika Mashariki watakuwa salama kushabikia timu zao kule Merekani,Mexico na Canada? Skiza maoni ya waskilizaji.

Katika makala haya tunajadili hatua ya jiji la Kampala nchini Uganda kutatangaza makataa ya siku 20 kwa wamiliki wa magari ya usafiri wa uma kuondoa magari yaliyochakaa barabarani, mamlaka zikisema lengo ni kupunguza ajali na uchafuzi wa hali ya hewa mjini. Tunakuuliza, nchi nyingine za Afrika mashariki zinapaswa kuiga mpango huu? Skiza maoni ya waskilizaji hapa.

Mashabiki wa rfi Kiswahili kila Ijumaa hupata nafasi ya kuchangia mada yoyote ile kupitia makala haya. Skiza maoni ya baadhi ya waskilizaji.

Rais wa Rwanda Paul Kagame amekanusha madai kuwa serikali yake imekuwa ikiminya uhuru wa kuabudu, akisisitiza kwamba hatua ya serikali kufuatilia taasisi za kidini ni kwa lengo la kuhakikisha uwajibikaji, na kuwalinda raia dhidi ya ulaghai,

Nchini Kenya, rais William Ruto na aliyekuwa naibu wake Rigathi Gachagua, wamekuwa wakirushiana maneno makali, kwenye mikutano ya hadhara na hata kwenda mbali na kutoa matusi na kushambuliana kuhusu maumbile yao, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka ujao. Nini mtazamo wako kuhusu kauli za viongozi hawa ? Katika nchi yako wanasiasa, wanatupiana maneno hivi ?

Katika uamuzi wa kushangaza , Shirikisho la soka barani Afrika CAF, limefuta ushindi wa Senegal kama mabingwa wa taji la AFCON na kulipa taji hilo Morocco ambao walikuwa wenyeji wa michuano hiyo.


Nchi zaidi za Afrika zimejitokeza kusema raia wake walihadhaiwa na kusajiliwa kwenda kupigana na vikosi vya Urusi nchini Ukraine

Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Uganda Bobi Wine baada ya kuwa mafichoni kwa miezi miwili alifunguka na kusema kafanikiwa kukimbia baada ya kuwindwa na vikosi vya usalama

Tunajadili kinachoendelea nchini DRC, ambapo mjadala kuhusu mapendekezo ya kufanyia katiba marekebisho, ikiwemo muhula wa urais, unazidi kuibua hisia mseto, baadhi ya raia wakionekana kuunga mkono na baadhi kupinga. Unazungumziaje mjadala huu nchini DRC? Skiza maoni ya mskilizaji.

Tunajadili hatua ya Mataifa ya Kenya na Rwanda, kuanza kukumbatia matumizi ya kamera za siri barabarani ili kunasa madereva wanaokiuka sheria za barabarani, hatua inayolenga kupunguza ajali za mara kwa mara ambazo zimekuwa zikisababisha vifo maelfu ya raia. Je, unafikiri kamera za siri barabarani zitasaidia kupunguza ajali za barabarani? Ndilo swali tumekuuliza. Skiza maoni ya baadhi ya waskizaji.

Katika makala haya tunajadili kinachoendelea jijini Nairobi nchini Kenya ambapo jiji hilo limeendelea kushuhudia mvua kubwa ambazo zimesababisha maafa ya zaidi ya watu 40. Nchi nyingine za Afrika Mashariki pia zinaendelea kushuhudia mvua kubwa. Skiza makala haya.

Katika makala haya tunajdili Juma lililopita wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kumteua rais wa Uganda, Yoweri Museveni kuwa mwenyekiti mpya wa Jumuiya hiyo, huku wakitangaza mabadiliko kadhaa muhimu waliyosema yanalenga kuifanya jumuiya kutosambaratika. Miongoni mwa mabadiliko ni pamoja na nchi wanachama kuwalipa mshahara wabunge wao na namna nchi zinazodaiwa zitalipa madeni yake. Unafikiri mabadiliko haya yatasaidia Jumuiya Kukua? Skiza maoni ya mskilizaji.

Leo ni siku ya mada huru. Tunampa msikilizaji wetu nafasi kuzungumzia suala lolote ambalo limetokea nchini mwake wiki hii, lakini pia kujadili kile ambacho amekisikia katika habari zetu wiki hii.


Rais wa Kenya William Ruto, ameitisha kikao cha dharura cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika mashariki mwezi ujao kujadili changamoto ya kifedha ambayo imetatiza shughuli za taasisi za jumuiya hiyo, tatizo kubwa likiwa baadhi ya nchi kuchelewesha kutoa michango kwa wakati. Mkutano huo utajadili mfumo mpya wa uchangishaji fedha na namna ya kupunguza matumizi ya jumuiya hiyo.

Mwishoni mwa juma mkutano wa 39 wa Umoja wa Afrika (AU) umefanyika jijjini Adis Ababa nchini Ethiopia Huku viongozi walioudhuria wakilipea kipau mbele swala la usalama na uchumi wakati huu matafia mengi ya Afrika yakishuhudia migogoro na kudorora kwa uchumi.

Mwishoni mwa juma Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani nchini Kenya Ali Nuno alitoa agizo kwa polisi kuwapiga risasi washukiwa wa uhalifu baada ya eneo hilo kushuhudia ongezeko la magenge yaliyojihami kwa mapanga. Hata hivyo hatua hiyo imepingwa vikali na mashirika ya kutetea haki za binadamu .Tumekuuliza unazungumziaje agizo hilo,Unadhani ni hatua sahihi kumaliza uhalifu na Nchini mwako hali ikoje

Mwishoni mwa juma Afrika Kusini ilitangaza kuondoa wanajeshi wake kutoka kwa tume ya Umoja wa Mataifa ya kulinda amani nchini DRC (MONUSCO) baada ya kikosi hicho kuhudumu kwa miaka 27.Pretoria inasema hatua hiyo ni kutokana na mipango yake ya kurekebisha na kuimarisha raslimali ya jeshi lake.Tumemuuliza msikilizaji anazungumziaje hatua hii ya Afrika kusini,Hatua hii ni kumaanisha Monusco imepoteza nguvu DRC na Nini kifanyike kuleta usalama wa kudumu nchini DRC?

Nchi za magahribi kupitisha sheria za kupiga marufuku mitandao ya kijamii kwa watoto walio chini ya miaka 15.