Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.

Makala hii ya habari rafiki rafiki ijumaa ya desemba 26 2025 ni siku ya mada huru; tunakupa fursa kuchangia suala lolote ambalo limejiri nchini mwako wiki hii. Unaweza pia kuzungumzia kile ambacho umekisikia kwenye matangazo yetu ya redio juma hili. Nahodha wa Habari Rafiki Ruben Lukumbuka, moja kwa moja kutoka Studio maridai namba2.

Wakristo wanaadhimisha sikukuu ya Krismasi, wakati baadhi ya nchi kama Sudan, Ukraine na Mashariki mwa DRC yakikabiliwa na changamoto za usalama.-Unaadhimsisha sikuu ya Krismasi ukiwa wapi ? Sikukuu ya mwaka huu ikoje ?

Msikilizaji Mashindano makubwa zaidi ya soka barani Afrika, Kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 yanaingia katika siku yake ya tatu leo jumanne ambapo jumla ya timu 24 za mataifa ya Afrika zikiwania taji hilo. Leo DRC wanamenyana na Benin, Tanzania wanakutana na Nigeria. Unazungumziaje maandalizi ya nchi za Afrika Mashariki na kati ?Nini matarajio yako kwenye mashindano haya ?

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeongeza muda wa mwaka mmoja kwa ujumbe wa kulinda amani nchini DRC, wakati mapigano yakiongezeka mashariki mwa nchi hiyo kufuatia mashambulizi mapya ya waasi wa M23. Uamuzi huu unakuja wakati mjadala ukiendelea kuhusu ufanisi wa MONUSCO nchini humo. Je, unaamini hatua hii itasaidia au ujumbe huo umepoteza uaminifu na uwezo wa kuleta mabadiliko ya kweli? Je, umoja wa Mataifa unapaswa kufikiria upya mkakati wake wa kulinda amani nchini DRC?

Makala hii imeangazia hatua ya hivi karibuni ya rais wa marekani Donald Trump ya kuongeza orodha mpya ya mataifa zaidi yakiwemo ya Afrika ikiwemo Tanzania, ambayo raia wake wanazuiwa kuingia Marekani, tumekuuliza Je? hatua hii ni ya kibaguzi ama inalenga kuulinda usalama wa Marekani? Na kwa mtazamo wako Hatua hii Ina maana gani? Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kupata maoni ya wasikilizaji

Kumekuwa na hisia mseto tangu waasi wa AFC/M23 wanaoungwa mkono na Rwanda watangaze kuwa watawaondoa wapiganaji wao katika mji wa Uvira mkoani Kivu Kusini mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.Je? shinikizo la Marekani litazaa matunda? sikiliza maoni ya wasikilizaji wetu katika makala hii ya Habari rafiki

Tarehe 14/12 dunia iliadhimisha miaka 60 ya azimio la kupinga ukoloni. Hata hivyo ukoloni katika sura zake za zamani na mpya bado unaathiri jamii zetu leo hii, baadhi wanaita ukoloni mamboleo.Je, ukoloni uliisha kweli Afrika au umebadilika tu? Je unaathiri vipi maendeleo ya Afrika? Nini kifanyike kuukomesha?Kupata mengi ungana na mwanahabari wetu Ruben Lukumbuka

Ilivyo desturi ya kila siku ya Ijumaa, ni mada huru. Tunampa msikilizaji wetu nafasi ya kuzungumzia taarifa ambazo tumeziangazia katika habari zetu juma hili, lakini pia matukio mbalimbali nchini mwake.

Waasi wa AFC/M23 wanaosaidiwa na Rwanda, ni rasmi sasa wanaudhibiti mji wa kimkakati wa Uvira jimboni Kivu Kusini, hatua inayokuja licha ya wiki iliyopita DRC na Rwanda kutia saini mkataba wa amani.Tunamuuliza msikilizaji anazungumziaje kilichofanywa na waasi wa M23,,Nini kifanyike? na Je, msikilizaji yuko Uvira au amekimbia kutoka Uvira

Leo ni siku ya kimataifa ya haki za binadamu, hata hivyo dunia inaadhimisha siku hii huku vitendo vya ukiukaji wa haki za binadamu vikiendelea kuongezeka kwenye maeneo mbalimbali duniani, maeneo yenye mizozo vitendo hivi vikiwa vya kuogopesha.Tumekuuliza unafikiri kwanini vitendo hivi vinaongezeka licha ya sheria za kimataifa kuwepo?Hali ya haki za binadamu ikoje nchini mwako na Nini kifanyike kuimarisha haki za binadamu ulimwenguni?

Mada ya leo ni kuhusu kinara wa upinzani nchini Uganda Bob Wine pamoja na baadhi ya wagombea wengine wa upinzani wameendelea kunyanyaswa na vyombo vya usalama wanapoendelea na kampeni zao, tume ya uchaguzi ikilaani vitendo hivyo.Yanayofanyika Uganda yanashuhudiwa pia kwenye mataifa kadhaa ya Afrika .Tumemuuliza msikilizaji Hatua hii ya vyombo vya usalama inaathiri vipi demokrasia na nini kifanyike kujenga mazingira sawa ..Karibu

Licha ya viongozi wa DRC na Rwanda kutia saini mkataba wa amani juma lililopita, mapigano yameripotiwa mashariki mwa Congo kati ya waasi wa M23 na jeshi la Serikali FARDC.Tulimuuliza mskilizaji Je hii ni ishara kuwa mkataba waliotia saini haujazaa matunda ,nani wakuwajibishwa kwa kinachotokea na Nini kifanywe kuleta utulivu mashariki mwa Congo,,

Kila ijumaa rfi inakupa nafasi kuchangia mada yoyote kupitia makala ya Habari Rafiki. Skiza kilichopewa kipao mbele kwenye makala ya juma hili.

Shaba ya makala haya inalenga nchini DRC, viongozi wa DRC marais Paul Kagame na mwenzake Felix Tshisekedi wamesaini, awamu ya mwisho ya mkataba wa amani. Tumekuuliza Je, unadhani wananchi wa mashariki mwa DRC watanufaika moja kwa moja na makubaliano ya worshington?

Katika makala haya tujadili hatua ya ongezeko la visa vya wanasiasa wa upande wa serikali na upinzani kutumia makundi ya vijana au wahuni kutisha na kuvuruga mikutano ya mahasimu wao wa kisiasa hili likifanyika hata kwenye mitandao. Tunakuliza unafikiri kwa nini wanasiasa wanaendelea kutumia makundi ya vijana au wahuni katika siasa. skiza makala haya.

Nchini Uganda, wawaniaji wa urais wameshiriki mdahalo kuelekea uchaguzi wa mwezi ujao, huku rais Museveni akisusia mdahalo huo. Je, unafikiri midahalo huwa na mchango wowote kwa wapiga kura kuelekea siku ya uchaguzi? Skiza baadhi ya maoni ya waskilizaji.

Siku ya kimataifa ya mapambano dhidi ya UKIMWI, Umoja wa Mataifa unasema kupungua kwa misaada kunatishia dunia kufikia lengo la kudhibiti ugonjwa huu ifikapo mwaka 2030, huduma za kinga zimevurugika hasa kwenye nchi masikini. unazungumziaje siku hii, je dunia tumepiga hatua kukabiliana na ugonjwa huu? Skiza maoni ya baadhi ya waskilizaji.

Viongozi wa Afrika na wale wa umoja wa Ulaya wamekutana nchini Angola, lengo likiwa ni kuimarisha ushirikiano wa usalama na kiuchumi, rasilimali za bara hilo zikimulikwa na mataifa yenye nguvu ambayo yameongeza kasi ya uwekezaji kwenye bara hilo. Tumekuuliza unaamini ushirikiano uliopo unanufaisha pande zote ? Ushirikiano wa aina gani Afrika inapaswa kuwa nao na nchi za magharibi?

Msikilizaji juma lililopita watu wenye silaha waliwateka wanafunzi zaidi ya 300 pamoja na waalimu katika shule moja kwenye jimbo la Niger nchini Nigeria, tukio linalojiri siku chache tangu kutekwa kwa wanafunzi wengine 25 katika shule ya wasichana kwenye jimbo la Kebbi pia huko Nigeria. Vitendo vya utekaji wa watoto vinazidi kuongezeka katika nchi za Afrika magharibi na kati. Nini kifanyike kukomesha vitendo hivyo Afrika?Je taifa lako linashuhudia utekaji wa watoto? Ungana na Ruben Lukumbuka

Kila Ijumaa rfi Kiswahili inakupa nafasi ya kuchangi mada yoyote kuhusu taarifa na vipindi vyetu au kile kinafanyika hapo ulipo. Skiza maoni ya waskilizaji juma hili.

Tunajadili hatua ya viongozi kadhaa wa Afrika akiwemo rais wa Uganda, Yoweri Museveni, na rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, wamewateua watu wa familia zao katika nafasi za serikali, hali hii ikionekana kwenda kinyume na maadili ya kazi. Tunakuuliza Je, uteuzi wa ndugu serikalini ni sahihi au si sahihi? skiza Makala haya

Katika makala haya tunaangazia nchi ya Kenya ambapo chama cha ODM kilichokuwa cha waziri mkuu wa zamani hayati Raila Odinga, kimeadhimisha miaka 20 tangu kuasisiwa kwake. Tunauliza je vya kisiasa vina mchango gani katika kuimarisha demokrasia hapa Afrika? Skiza makala haya.

Aliyekuwa rais wa Malawi , Lazarus Chakwera kuteuliwa na Jumuiya ya madola kuwa mpatanishi wa mzozo wa kisiasa nchini Tanzania, hasa baada machafuko ya kipindi cha uchaguzi. Tunakuuliza , unafikiri rais Chakwera atafanikiwa kusuluhisha mzozo wa kisiasa nchini Tanzania.

Ulimwengu umeadhimisha siku ya kumbukumbu kwa waathiriwa wa ajali za barabarani. Takwimu za umoja wa mataifa zinaonyesha kuwa, duniani kote, watu zaidi ya milioni moja hufariki dunia kila mwaka kutokana na ajali za barabarani, na millioni hamsini kujeruhiwa. Nini kifanyike kupunguza ajali za barabarani. Skiza makala kufahamau maoni ya mskilizaji zetu.

Katika makala ya Habari Rafiki hii leo tunazungumzia hatua ya Rais wa Marekani Donald Trump kutishia kutumia jeshi la nchi yake kupambana na wanajihadi wanaowauwa Wakiristo nchini Nigeria. Kauli hii imewakasirisha viongozi wa Nigeria, ambao wanasema serikali nchini humo, haiungi mkono unyanyasaji wa kidini. Tumemuuliza msikilizaji anazungumzia vipi mpango wa huu wa Trump na ni nini kinaweza kufanyika kumaliza mauaji ya kidini nchini Nigeria.

Nini kilikukera kuhusu uchaguzi wa Tanzania ? Skiza maoni ya waskilizaji wetu.

Kila Ijumaa rfi Kiswahili inakupa nafasi kuchangia mada yoyote kuhusu matukio ya dunia. Skiza maoni ya waskilizaji juma hili.

Gazeti la The Star nchini Kenya limewahi chapisha ripoti inayoonesha namna mitandao ya kijamii inavyoathiri watu kwa kusababisha wasiwasi, matatizo ya afya ya akili na athari nyinginezo. Tunakuuliza Je, maisha ya mitandao yanatusaidia kama jamii au yanatuumiza? skiza maoni ya waskilizaji wetu.

Shaba yetu katika makala haya inalenga nchi ya Tanzania ambapo raia wameshiriki uchaguzi kumchagua rais na wabunge. Je, unauzungumziaje uchaguzi wa Tanzania? Haya hapa maoni ya waskilizaji.

Djibouti limekuwa taifa la hivi punde kuondoa rasmi kikomo cha umri wa rais , hatua inayotoa fursa kwa rais Ismail Omar Guelleh kugombea muhula wa sita katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Aprili mwaka ujao. Awali Katiba ya nchi hiyo ilikuwa inamzuia rais kugombea tena baada ya kufikisha miaka 75. Hali hii pia imeonekana kwenye mataifa kadhaa ya Afrika Mashariki kama vile Uganda. Skiza mahakala haya kuskia maoni ya waskilizaji.

Leo ni siku ya mada huru. Tunakupa nafasi kuzungumzia suala lolote ambalo limetokea nchini mwako wiki hii Unaweza pia kujadili kile ambacho umekisikia katika matangazo yetu ya wiki hii kwenye redio.

Viongozi wa dunia, wataalam wa Afya na wanasayansi wanakutana Afrika Kusini siku chache kabla kikao cha G20, ili kuanganzia kuhusu njia za kufadhili afya bila kutegemea ufadhili wa kigeni.Tumemuuliza msikilizaji maoni yake kuhusu uwezo wa mataifa ya Afrika kufadhili miradi ya afya?

Hivi leo viongozi wa dunia akiwemo rais wa Marekani, Donald Trump, wanakutana Misri kujadili mustakabali wa eneo la Gaza, baada ya makubaliano ya kihistoria ya wiki iliyopita. Makubaliano haya yameshuhudia kuachiwa kwa mateka, wafungwa na kusitishwa kwa vita vya Gaza. Tunakuuliza, unaamini makubaliano kati ya Hamas na Israel safari hii yatadumu?Nini cha zaidi kifanyike?Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka

Msikilizaji kesho Ijumaa oktoba 10 kamati inayotoa tuzo za kimataifa za Nobel itamtangaza mshindi, wakati huu watu wengi wakiwa wamempendekeza rais wa Marekani Donald Trump kutokana na mchango wake wa kutafuta amani mashariki ya kati, hata hivyo wadadisi wanasema kiongozi huyo hawezi kupewa tuzo hiyo. Unafikiri ni Kiongozi gani anastahili kupewa tuzo hii mwaka huu na kwanini? Ungana nami Ruben Lukumbuka, mubashara kutoka studio namba mbili hapa karibu tuandamane hadi tamati.-

Habari rafiki ya jumatano octoba 08 imeangazia vitendo vya utekaji nyara ambavyo vimeongezeka katika nchi za ukanda wa Afrika mashariki, hivi karibuni nchini Uganda wanaharakati wawili kutoka nchini Kenya walikamatwa baada ya kuhudhuria mkutano wa kisiasa wakati nchini Tanzania, aliyekuwa balozi wa nchi hiyo huko Cuba Humphrey Polepole alitekwa na watu wasiojulikana na mpaka sasa hajulikane alipo. Sikiliza makala hii kupata mengi zaidi

Waasi huko mashariki mwa jamhuri ya kidemokrasia ya Congo wameendelea kujiimarisha kiutawala, kisiasa na kimiundo mbinu katika kujenga barabara, kutangaza orodha ya mawakili, hatua inayodhihirisha kuwa waasi hao wanaendea kutengeneza serikali mbadala na ile ya Kinshasa. Makala ya habari rafiki inaangazia hatua hiyo

Mahakama ya kijeshi nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC imemhukumu rais mstaafu wa nchi hiyo Joseph Kabila Kabange adhabu ya kifo bila ya yeye mwenyewe kuwepo mahakamani, ikimtia hatiani kwa usaliti na uhalifu dhidi ya binadamu. Chama chake PPRD kimesema kesi hiyo ni ya kisiasa dhidi ya mpinzani mkubwa wa serikali. Mwandishi wetu Ruben Lukumbuka anaungana na wasikilizaji wa Idhaa kupata maoni yao kuhusu kesi hii, makinika kwa kusikiliza makala hii.-

Serikali ya DRC kupitia wizara ya sheria imesitisha utoaji wa leseni za Makanisa, katika kupambana na Rushwa! kwa maoni yako unaamini kusitisha utoaji wa leseni kutasaidia kupambana na rushwa? Hali ya rushwa ikoje katika taasisi za umma nchini mwako? Mwandishi wetu Ruben Lukumbuka pamoja na wasikilizaji wetu wanajaribu kupata jibu kwa maswali hayo

Makala ya habari rafiki ya jumatatu septemba 29 2025 imeangazia hatua ya tume ya uchaguzi nchini Kenya IEBC kuzindua zoezi la kuwaandika wapiga kura ambalo limeonekana kuwavutia vijana wengi, maarufu kama Gen Z.Tumekuuliza msikilizaji je? unaona vijana wote wako tayari kujiandikisha na katika nchi yako vijana wanahamasishwa vipi. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka, kwa kutuma maoni ya sauti kupitia nambari yetu ya whatsApp: +254110000420 ama pia kupitia Facebook : RFI Kiswahili

Kila Ijumaa rfi kiswahili inakupa nafasi ya kuchangia mada yoyote, iwe kila kinaendelea hapo ulipo au yale umeskia kwenye matangazo yetu. Skiza maoni ya juma hili

Je mataifa ya Africa yanatumia raslimali zake kujinufaisha? Skiza maoni ya wakilizaji

Shaba yetu inalenga Nchini Kenya, ambapo madai ya kupora kwa pesa za bima ya afya ya serikali yanaendelea kutatiza utowaji wa huduma ya afya hili likiwaathiri raia wa kawaida. Mskilizaji nchini mwako huduma za afya ni nafuu na bora, au bado wananchi wa kawaida wanahangaika kupata matibabu. Skiza maoni ya waskilizaji wetu

Je umoja wa mataifa umesalia kimya ukiukaji wa haki ukiendelea? Skiza makala haya kuskia hisia za waskilizaji wetu.

Kila mwaka tarehe 8 Septemba ulimwengu husherehekea maendeleo katika ujuzi wa kusoma na kuandika katika ngazi ya kimataifa, kikanda na kitaifa. Mwaka huu imekuwa ni fursa ya kutafakari kwa kina kuhusu maana ya kusoma na kuandika katika enzi hii ya kidijitali.

Tunazungumzia hatua ya Kenya na Uganda kukubaliana rasmi kuondoa vizuizi vyote vya kibiashara, vikiwemo vizuizi vya ushuru na visivyo vya ushuru, ili kuwezesha mtiririko huru wa bidhaa, huduma, na watu kati ya mataifa hayo mawili

Kampeni za uchaguzi mkuu wa Tanzania utakaofanyika tarehe 29 Oktoba zimeanza. Chama kikuu cha upinzani Chadema hakipo kwenye kampeni hizi, kufuatia msimamo wake wa kutaka mageuzi kwenye mfumo wa uchaguzi. Wasikilizaji wetu wanazungumzia aje kampeni hii na raia wa Tanzania wanatarajia sera gani kutoka kwa viongozi mbalimbali?

Michuano ya CHAN imemalizika rasmi mwishoni mwa juma, nchini Kenya, Morocco wakitawazwa mabingwa na Madagascar wakimaliza wa pili. Kuisha kwa michuano hii ni mwanzo wa maandalizi ya michuano ya AFCON itakayofanyika tena kwenye nchi za Kenya, Uganda na Tanzania mwaka 2027. Tumemuuliza msikilizaji wetu iwapo amefurahia michuano ya mwaka huu? Timu ipi ilikuwa bora kwake na kipi kifanyike kuelekea mashindano ya AFCON 2027.

