Habari RFI-Ki

Follow Habari RFI-Ki
Share on
Copy link to clipboard

Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.

RFI Kiswahili


    • Jul 9, 2025 LATEST EPISODE
    • weekdays NEW EPISODES
    • 9m AVG DURATION
    • 337 EPISODES


    Search for episodes from Habari RFI-Ki with a specific topic:

    Latest episodes from Habari RFI-Ki

    Kenya: Mahakama ya juu yasema mwana haramu si haramu

    Play Episode Listen Later Jul 9, 2025 9:58


    Katika makala haya tujadili hatua ya mahakama ya juu zaidi nchini Kenya, kuagiza kwamba mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa kwenye dini ya kiislamu ana haki ya kumiliki mali ya babake kama watoto wengine waliozailiwa ndani ya ndoa, hatua inayoenda kinyume kabisa na tamaduni za dini hiyo. Unazungumziaje uamuzi huu wa mahakama nchini Kenya ? Haya hapa baadhi ya maoni yako.

    Côte d'Ivoire : Kurejeshewa ngoma maalum kutoka Ufaransa

    Play Episode Listen Later Jul 8, 2025 9:56


    Kaika makala haya tunajadili  hatua ya bunge nchini Ufaransa kupiga kura na kupitisha mswada wa kurudishwa nchini Ivory Coast ngoma maalum inayozungumza iliyochukuliwa katika nchi hiyo ya Afrika kutoka kabila la Ebrie wakati wa ukoloni mwaka 1916. Je umefika wakati kwa koloni za zamani za Bara la Afrika kurejesha vyombo walivyopora ?   Ndilo swali tumekuuliza . Haya hapa maoni yako.

    Siku ya lugha ya kiswahili duniani makala maalum

    Play Episode Listen Later Jul 7, 2025 10:08


    Siku ya kiswahili duniani, ambayo imekuwa ikiadhimishwa tangu mwaka 2022. Maadhimisho ya mwaka huu imefanyika jijini Kigali nchini Rwanda, ambako mamia ya wataalam na wapenzi wa Kiswahili wamekutana kwa siku mbili kujadiliana kuhusu nafasi na umuhimu wa lugha ya Kiswahili kwa raia wa nchi zote za Jumuiya. Kauli mbiu ni kusherehekea lugha ya Umoja, utambulisho na mchango wake kwa dunia.RFI kiswahili imeshirikiana na taasisi ya mafunzo ya biashara na ufundi stadi, NIBS ya jijini Nairobi, kuandaa makala maalum ya Habari RAFIKI na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka ameongoza makala hii

    Maoni yako kwenye mada huru Ijumaa hii

    Play Episode Listen Later Jul 4, 2025 9:53


    Watu karibu 500 wakamatwa nchini Kenya kufuatia maandamano ya Juni 25 2025

    Play Episode Listen Later Jul 2, 2025 10:05


    Wanatuhumiwa kwa mauaji, ugaidi, ubakaji na makosa mengine. Wanaharakati wa haki za binadamu, wanasema, wanawake 14 walibakwa wakati wa maandamano hayo.

    Maoni yako kuhusu azma ya rais wa Uganda Museveni kuwania tena urais

    Play Episode Listen Later Jul 1, 2025 9:55


    Mkataba kati ya DRC na Rwanda ya kuleta amani yakudumu mashariki mwa DRC

    Play Episode Listen Later Jun 30, 2025 9:58


    Umoja wa Afrika umekaribisha makubaliano yaliyotiwa saini mwishoni mwa juma lililopita kati ya Rwanda na DRC, hatua ambayo itashuhudia unyang'anyaji wa silaha na kuondolewa kwa mamluki wa kigeni mashariki mwa Congo.

    Matukio ya wiki likiwemo kuelekea kusainiwa mkataba wa amani nchini DRC

    Play Episode Listen Later Jun 27, 2025 10:15


    Hatua ya bunge la Uingereza kuruhusu huduma ya kusaidiwa kufa

    Play Episode Listen Later Jun 26, 2025 9:38


    Bunge la Uingereza hivi majuzi liliidhinisha mswada wa huduma ya kusaidiwa kufa

    Maandamano ya kumbukizi ya kuwauwa kwa vijana zaidi ya 60 mwaka jana

    Play Episode Listen Later Jun 25, 2025 10:09


    Waandamanaji wakabiliana na polisi siku nzima wakati ya maandamano ya kuwakumbuka watu waliopoteza maisha wakati wa maandamano ya mwaka jana ya Gen Z

    Zambia :Rais Hakainde Hichilema asisitiza serikali kufanya mazizi ya Edgar Lungu

    Play Episode Listen Later Jun 24, 2025 10:05


    Rais wa Zambia Hakainde Hichilema ameendelea kusisitiza kufanya mazishi ya kitaifa kwa mtagulizi wake Edgar Lungu Licha ya mzozo uliopo baina yake na familia juu ya utekelezwaji ya matakwa ya marehemu ya kukataa kufanyiwa mazishi ya kitaifa.Tunakuuliza maoni yako kuhusu mzozo huo.

    MAONI: DRC na Rwanda zitie saini makubaliano kumaliza mauaji ya raia

    Play Episode Listen Later Jun 20, 2025 10:02


    Kila siku ya Ijumaa, hapa RFI Kiswahili, tunampa mskilizaji wetu nafasi kuzungumzia habari kuu ambazo tumekuwa nazo wiki hii au kutueleza jambo lolote ambalo limetokea nchini mwake. Wiki hii maoni mseto yameangazia, miongoni mwa taarifa zingine, tangazo kwamba Rwanda itatia saini makubaliano na DRC tarehe 27 Juni, kumaliza mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, lakini pia mashambulio baina ya Israeli na Iran.

    Burundi : Rais Ndayishimiye ataka mazungumzo na upinzani

    Play Episode Listen Later Jun 16, 2025 10:01


    Rais wa Burundi Evariste #Ndayishimiye ametoa wito kwa upinzani kushiriki katika mazungumzo na chama chake CNDD-FDD baada ya uchaguzi wa wiki iliyopita ambao ulikumbwa na upinzani mkubwa kwa ukosefu wa uwazi.   Hata hivyo upinzani haujaonyesha nia ya kushiriki mazungumzo hayo. Tunakuuliza, ni sahihi upinzani kujiunga na serikali ? skiza makala haya kuskia maoni ya mskilizaji.

    Utumwa wa watoto waendelea kuripotiwa licha ya juhudi mbalimbali zinazowekwa

    Play Episode Listen Later Jun 13, 2025 9:57


    Juni 12, ni Siku ya Kimataifa ya Kupinga Ajira kwa Watoto. Inakadriwa, takriban watoto milioni 200 kote duniani wanatumikishwa badala ya kuwa shuleni.   Tunakuuliza, serikali yako inafanya vya kutosha kukomesha utumwa wa watoto? Unamfahamu mtoto anayefanyishwa kazi?

    Kwa nini wanaume wanashindwa kutafuta ushauri wa afya ya akili

    Play Episode Listen Later Jun 13, 2025 10:00


    Makala haya yanaangazia afya ya akili, ikizingatiwa kuwa Juni ni Mwezi wa Uhamasishaji wa Afya ya Akili ya Wanaume.   Unafikiri ni kwanini wanaume wanashindwa kutafuta ushauri wa afya ya akili? Unadhani afya ya akili ya mwanaume inasahaulika? Skiliza makala ya leo usikie maoni kutoka kwa waskilizaji wetu.

    Rwanda yajiondoa ndani ya muungano wa mataifa ya Africa ya Kati

    Play Episode Listen Later Jun 9, 2025 9:54


    Leo shaba yetu inalenga nchi ya Rwanda ambapo nchi hiyo imetangaza kujiondoa kwenye Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika ya Kati, na kuituhumu jirani wake DRC, kwa kutumia baadhi ya wanachama kuendeleza ajenda zake zinazokandamiza Rwanda. Skiza makala hay kuskia maoni ya mskilizaji wetu.

    Maoni ya waskilizaji wetu Juma hili

    Play Episode Listen Later May 31, 2025 9:54


    Kila Ijumaa rfi Kiswahili inakupa nafasi ya kuchangia mada yoyote iwe kila uliskia kwenye habari zetu au kile kinachoendelea hapo ulipo. Skiza maoni ya mskilizaji.

    Uganda : Ombi la Msamaha wa rais Museveni ni la kweli

    Play Episode Listen Later May 29, 2025 9:56


    Leo shaba yetu inalenga taifa la Uganda ambapo rais Yoweri #Museveni pamoja na mkewe wameomba raia wa nchi hiyo msamaha kwa mabaya yote ambayo serikali yao imetekeleza kwa miaka 39. Je, unafikiri kauli ya Rais Museveni na Mama Janet kuomba msamaha ni ya kweli au ni ya kisiasa?Skiza maoni ya mskilizaji wetu.

    EAC : Je wanachama wana cha kujivunia

    Play Episode Listen Later May 28, 2025 9:52


    Katika makala haya shaba yetu inalenga jumuia ya Africa mashariki, tumekuuliza mskilizaji je unahisi una chochote cha kujivunia kuwa mwanachama wa jumuiya ya Africa Mashariki. Skiza maoni ya mskilizaji wetu.

    Africa: Ina lolote cha kujivunia

    Play Episode Listen Later May 27, 2025 9:50


    Umoja wa Afrika imesherekea siku ya kiafrika, kuadimisha kuundwa kwa Umoja wa Afrika, kipindi hiki nchi ya Uganda nayo ikisitisha ushirikiano wake wa kijeshi na taifa la Ujerumani. Kuna chochote bara la Afrika linaweza kujivunia?Ndilo swali tumekuuliza, skiza makala haya kuskia maoni ya waskilizaji.

    DRC: Kabila kuondolewa kinga je ni sahihi

    Play Episode Listen Later May 26, 2025 9:45


    Kwenye makala haya tunajadili kilichotokea nchini DRC ambapo bunge la seneti lilimuondolea kinga ya kutoshtakiwa rais wa zamani, Joseph Kabila, hatua ambayo sasa inatoa nafasi kwa mahakama ya kijeshi kumshtaki kiongozi huyo kwa tuhuma za uhaini. Unazungumziaje hatua hii ya seneti, unadhani ilikuwa sahihi?Ndio swali tumekuuliza?skiza maoni ya baadhi ya waskilizaji.

    Maoni ya waskilizaji kuhusu habari zetu juma hili

    Play Episode Listen Later May 23, 2025 9:56


    Ilivyo ada  kila siku ya ijumaa rfi Kiswahili hukiupa nafasi kuchangia chochote kile, maana yake nini? unachangia chochote kile, ulichoskia kwenye habari zetu au kile kinachoendelea hapo ulipo. Skiza makala haya kuelewa zaidi.

    Mazungumzo ya Kigali na Washington kuhusu Rwanda kuwapokea wahamiaji kutoka Marekani

    Play Episode Listen Later May 22, 2025 10:01


    Leo hii tunaangazia Mazungumzo kati ya nchi ya Rwanda na Marekani kuhusu Kigali kuwapokea wahamiaji haramu watakaofukuzwa kutoka Washington. Unazungumziaje mazungumzo haya sawia na kauli ya mashirika ya Kimataifa ya kutetea haki za binadamu yakiongozwa na Amnesty International, yanayosema mpango huo utakiuka haki za wakimbizi?Skiliza kauli mbalimbali katika makala ya leo.

    Uganda yapitisha mswada kuruhusu raia kushtakiwa kwenye mahakama ya kijeshi

    Play Episode Listen Later May 21, 2025 9:50


    Wabunge wa upinzani hata hivyo walisusia kikao kilichopitisha mswada huo kwa haraka. Wanasiasa wa upinzani wanadai  mswada huo  unawalenga wakosoaji wa rais Yoweri Museveni 

    Kauli ya rais wa Tanzania Samia Suluhu kuwazuia wanaharakati wa nchi zingine

    Play Episode Listen Later May 20, 2025 9:27


    Leo tunaangazia ,hatua ya  Tanzania kuwazuia  Mawakili, wanaharakati wa haki za binadamu kutoka nchini Kenya, akiwemo Jaji Mkuu mstaafu Willy Mutunga  waliokwenda kusikiliza kesi ya uhaini inayomkabili kiongozi mkuu wa upinzani Tundu Lissu. Rais Samia Suluhu Hassan, amesema serikali yake haitaruhusu wanaharakati wa kigeni kuingia nchini Tanzania na kuingilia masuala ya ndani ya nchi yake.

    Nini kifanyike kumaliza vita vinavyoendelea Sudan,Ukraine na Gaza

    Play Episode Listen Later May 19, 2025 10:02


    Viongozi wa dunia, wameendelea kutoa wito wa amani kwenye nchi  za Sudan Ukraine na Gaza hizo, ambako vita vimesababisha vifo vya maelfu ya raia na wengine kuwa wakimbizi. Hata hivyo licha ya wito huu, mapigano yameendelea kuripotiwa.

    Uteuzi wa Papa Leo XIV kama kiongozi mpya wa kanisa katoliki duniani

    Play Episode Listen Later May 15, 2025 9:46


    Hali ya mafuriko katika mataifa ya Afrika Mashariki na pembeya Afrika

    Play Episode Listen Later May 13, 2025 9:56


    Maoni ya waskilizaji kuhusu vipindi vyetu juma hili

    Play Episode Listen Later May 9, 2025 9:58


    Juma hili waskilizaji wetu walikuwa na maoni haya kuhusu taarifa zetu

    Je kuna hofu ya kutokea kwa vita vya tatu vya dunia

    Play Episode Listen Later May 8, 2025 10:00


    Katika makala haya  tunajadili athari ya vita vya ukraine na Urusi na sasa tishio la vita nyingine kati ya India na Pakistan. Je ni shara ya kutokea kwa vita vya pili vya dunia ? ndilo swali tumekuuliza. Skiza baadhi ya maoni ya waskilizaji.

    News Zealand kudhibiti mitandao ya kijamii kwa watoto

    Play Episode Listen Later May 7, 2025 9:55


     Shaba ya makala haya inalenga news Zealand ambapo serikali inapendekeza marufuku ya matumizi ya mitandao kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka 16, lengo likiwa kuwakinga dhidi ya athari za mitandao. Njia gani wazazi wa kiafrika wanaweza kuwalinda watoto na mitandao ya kijamii? Ndilo swali tumeuuliza na haya hapa baadhi ya maoni yako, skiza makala haya.

    Dunia uhuru wa vyombo vya habari na wanahabari

    Play Episode Listen Later May 5, 2025 9:36


    Leo mada yetu inajikita kwa siku ya kimataifa ya uhuru wa vyombo vya habari, ambapo  Umoja wa Mataifa umesema licha ya baadhi ya nchi kupiga hatua katika ulinzi wa wanahabari, hofu ya uhuru wa habari kuendelea kuminywa inaendelea kutanda. Mwaka jana jumla ya wanahabari 82 walipoteza maisha wakitekeleza majukumu yao. Tuambie nchini mwako vyombo vya habari viko huru? Haya hapa baadhi ya maoni yako, skiza makala.

    Makala habari rafiki Ijumaa Mada huru

    Play Episode Listen Later May 2, 2025 9:48


    Rasimu ya makubaliano kati ya DRC na Rwanda ya kutafuta suluhu ya mzozo

    Play Episode Listen Later Apr 29, 2025 9:40


    Mchakato wa kumchagua kiongozi mpya wa kanisa katoliki duniani

    Play Episode Listen Later Apr 28, 2025 10:02


    Kwa sasa macho yakiwamulika makadinali 135 watakaochagua papa mpya ndani ya siku chache zijazo, mjadala kuhusu Papa kutoka Afrika ukishamiri.Mchakato wa kumchagua p

    Joseph Kabila adaiwa kurejea DRC kupitia Goma

    Play Episode Listen Later Apr 21, 2025 9:53


    Juma lililopita ripoti ambazo hazijathibitishwa rasmi zilieleza kuwa rais wa zamani wa DRC, Joseph Kabila alirejea nchini Mwake kupitia mji wa Goma unaokaliwa na waasi wa M23 wanaosaidiwa na Rwanda. Hata hivyo hatua yake imeifanya serikali ya Kinshasa, kusimamisha shughuli zote za chama chake cha PPRD, ikikituhumu kushurikiana na waasi hao.Unazungumziaje kurejea kwa rais Kabila?Ndilo swali tumekuuliza katika makala haya.Skiza maoni ya mskilizaji.

    DRC: Kujerea kwa Joseph Kabila kwaibua hisia mseto

    Play Episode Listen Later Apr 10, 2025 10:05


    Katika makala haya shaba yetu inalenga nchini DRC, ambapo Rais mustaafu wa DRC, Joseph Kabila, ametangaza kurejea nchini humo, kutoka nchini Afrika Kusini ambako amekuwa akiishi kwa zaidi ya mwaka moja , ili kuchangia kutafuta suluhu kwa mzozo wa usalama mashariki mwa nchi yake. Unazungumziaje hatua hii ya Kabila? Ndilo swali tulikuuliza, skiza makala haya kuskia maoni ya waskilizaji wetu.

    Marekani : Rais Donamd Trump atangaza ushuru zaidi kwa bidhaa za kigeni

    Play Episode Listen Later Apr 9, 2025 10:00


    Kwenye makala haya tunajadili,  hatua ya rais wa Marekani, Donald Trump kutangaza kuongeza ushuru kwa bidhaa zote zanazoingizwa Marekani, kutoka mataifa ya Kigeni, hatua inayoonekana kutikisa uchumi wa Dunia.  Je unahisi hatua ya rais Trump ni sahihi?Ndilo swali tumeuuliza.Skiza makala haya kujua maoni ya waskilizaji.

    Kenya: Yawarejesha nyumbani raia wake waliotapeliwa kuenda Mynamar

    Play Episode Listen Later Apr 8, 2025 9:34


    Shaba yetu kwenye makala haya inalenga hatua ya Serikali ya Kenya, kueeendelea kuwarejesha mamia ya raia wake waliotapeliwa na kusafirishwa hadi nchini Myanmar kwa ahadi ya kupewa ajira.  Nchini mwako visa kama hivi vinaripotiwa?Ndilo swali letu, skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji.

    Africa Mashariki : Viongozi watathimini kudhibiti mitandao ya kijamii

    Play Episode Listen Later Apr 8, 2025 9:56


    Katika makala haya tunajadili haja ya kuwepo sheria za kudhibiti mitandao ya kijamii kwa baadhi ya mataifa ya Africa Mashariki. Skiza makala haya kuskia mano ya waskilizaji wetu.

    Maoni ya waskilizaji kuhusu wizi unaofanywa kwenye mizani na wafanyabiashara

    Play Episode Listen Later Apr 5, 2025 10:02


    Makala haya ni maoni ya waskilizaji kuhusu ripoti maalum ya namna wananchi wanavyopigwa na wafanyabiashara kwenye mizani wanapopimiwa nafaka mbalimbali za chakula, huku gesi ya kupikia pia ikitajwa.

    Maoni yako kwenye makala ya Habari Rafiki Mada Huru Ijumaa

    Play Episode Listen Later Mar 28, 2025 10:01


    DRC: Majadiliano ya kitaifa kuhusu kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa kitaifa

    Play Episode Listen Later Mar 25, 2025 10:01


    Qatar : Yakutanisha Kagame na Tshisekedi

    Play Episode Listen Later Mar 20, 2025 9:59


    Shaba yetu  leo kwenye makala haya inalenga taifa la Qatar ambapo taifa hilo juma hili lilifanikiwa kuwaleta pamoja marais Felix Tshiesekedi wa DRC na mwenzake wa Rwanda Paul Kagme, katika juhudi za kutafuta suluhu kwa mzozo wa mashariki ya DRC. Unafikiri Qatar itafanikiwa kuzima mzozo wa mashariki mwa DRC. Skiza makala haya kujua baadhi ya maoni ya waskilizaji.

    Kenya : Kanisa katoliki latangaza marufuku kwa wanasiasa

    Play Episode Listen Later Mar 19, 2025 10:00


    Tunajadili  hatua ya Kanisa la Anglikana nchini Kenya, kwa mara nyingine limesisitiza marufuku ya kuwazuia wanasiasa kuzungumza kanisani katika juhudi za kuzuia wanasiasa kufanya siasa kanisani. Je unazungumziaje hatua hii ya kanisa Anglikana nchini Kenya? Skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji wetu.

    Rwanda yasitisha uhusiano na Ubelgiji

    Play Episode Listen Later Mar 18, 2025 9:58


    Katika makala haya tunajadili hatua ya serikali ya Rwanda, kutangaza kusitisha uhusiano wa Kidiplomasia na taifa la Ubelgiji kutokana na kile Rwanda imesema Ubelgiji kuendeleza propaganda kuihusu kutokana na mzozo wa mashariki mwa DRC. Unazungumziaje hatua ya Rwanda Skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji.

    Watu zaidi ya milioni 6 duniani watakosa mahali pakuishi

    Play Episode Listen Later Mar 17, 2025 10:01


    Tunajadili hatua ya bazara la wakikimbizi la Denmark, kuchachapisha ripoti inayoonesha kuwa, watu zaidi ya milioni 6 duniani watakosa mahali pakuishi ifikapo mwishoni mwa mwaka ujao, kutokana na mizozo, mabadiliko ya tabia nchi na kusitishwa kwa misaada toka Marekani. Unazungumziaje hatua hii? ndilo swali tumeuliza, skiza makala haya kufahamu mengi.

    Maoni yako kutokana na habari zetu juma hili

    Play Episode Listen Later Mar 14, 2025 10:07


    Kila Ijumaa rfi Kiswahili inatoa nafasi kwa mskilizaji kuchaniua mada mbalimbali kuhusu taarifa zetu. Juma hili hizi ni haya ni baadhi ya maoni ya waskilizaji wetu

    DRC : Angola kufanikisha mkutano kati ya rais Tshisekedi na waasi wa M23

    Play Episode Listen Later Mar 13, 2025 9:54


    Shaba yetu inalenga nchini DRC, ambapo taifa la Angola limesema linajaribu kufanikisha mazungumzo ya moja kwa moja kati ya rais wa DRC, Felix Tshisekedi na waasi wa M23, ili kutafuta suluhu la mzozo wa mashariki mwa DRC. Je unafiriki Angola itafanikiwa katika hili?Haya hapa baadhi ya maoni yako.

    Sudan Kusini :Wanajeshi wa Uganda wawasili Sudan Kusini

    Play Episode Listen Later Mar 13, 2025 9:46


    Mkuu wa majeshi nchini Uganda, ambaye pia ni mwana wa rais Yoweri Museveni, Muhoozi Kainerugaba, amedai wanjeshi wa taifa lake wamewasili Sudan Kusini ili kusaidia jeshi la taifa hilo kutatua mzozo ndani ya serikali ya umoja wa kitaifa  Tunakuuliza je mzozo wa Sudan Kusini unastahili kutatuliwa kijeshi?Skiza makala haya kuskiza baadhi ya maoni yenu.

    Kenya: Vijana wapinga michango ya wanasiasa kanisani

    Play Episode Listen Later Mar 11, 2025 9:56


     Shaba yetu leoinalenga nchini Kenya ambapo Vijana wameanza kuandamana kupinga kile wanadai wanasiasa kutoa kiasi kikubwa cha pesa kwenye maeneo ya kuabudu ili hali wao hawana ajira. Tumekuuliza hatua hii ni sahihi?Haya hapa baadhi ya maoni yako.

    Claim Habari RFI-Ki

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel