Podcasts about kwenye

  • 68PODCASTS
  • 633EPISODES
  • 19mAVG DURATION
  • 5WEEKLY NEW EPISODES
  • Jun 12, 2026LATEST

POPULARITY

20192020202120222023202420252026


Best podcasts about kwenye

Show all podcasts related to kwenye

Latest podcast episodes about kwenye

Kiswahili, Lugha Ya Afrika
Newton Alikosea? Jinsi Einstein Alivyobadilisha Maana ya Gravity Mwaka 1915

Kiswahili, Lugha Ya Afrika

Play Episode Listen Later Jun 12, 2026 4:31


Kwa zaidi ya karne mbili, maelezo ya Newton ndiyo yaliyotawala sayansi. Kisha mwaka 1915, Albert Einstein akaja na wazo lililobadilisha kila kitu: gravity si nguvu ya kuvutana — ni kupinda kwa nafasi na wakati (space-time).

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari: HRW: Rwanda na M23 zinawaajiri watu kwa lazima kwenye vikosi vyao

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 11, 2026 5:46


Waziri Mkuu Anthony Albanese haja tupilia mbali uwezekano wa kuongeza muda wa kupunguzwa kwa ushuru wa mafuta kutokana na kufufuliwa upya kwa mapigano Mashariki ya Kati.

Kiswahili, Lugha Ya Afrika
Kwa Nini Kila Kitu Huanguka CHINI? Siri ya Gravity Iliyowashinda Wanasayansi

Kiswahili, Lugha Ya Afrika

Play Episode Listen Later Jun 11, 2026 4:22


Ukitupa jiwe juu, kwa nini LAZIMA lirudi chini?

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho
Kuna haja ya serikali za Afrika kukumbatia mfumo endelevu ya kukabili taka ngumu kwenye mazingira.

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho

Play Episode Listen Later Jun 1, 2026 10:06


Tatizo la uchafuzi wa mazingira kutokana na taka  ngumu, bado ni changamoto katika miji mingi barani Afrika. Hata hivyo, hivi karibuni, kumekuwa na jitihada kwenye baadhi ya mataifa ambapo sasa nchi zimeanza kuwa na sheria na kanuni za kuhakkisha usimamizi endelevu wa taka, kwa kuwahusisha wazalishaji na waagizaji wa bidhaa.

SBS Swahili - SBS Swahili
Yaliyojiri Afrika: Wanafunzi 16 waangamia kwenye mkasa wa moto shuleni Kenya

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 29, 2026 6:26


Wanafunzi 16 wamekufa katika mkasa wa moto, uliotokea katika mabweni ya shule moja ya wasichana katika Kaunti ya Nakuru nchini Kenya.

MAELEZO PODCASTS
Hotuba ya Rais, Dkt. Samia Kwenye Kongamano la Biashara Baina ya Tanzania na Kenya, Mei 4, 2026

MAELEZO PODCASTS

Play Episode Listen Later May 22, 2026 22:11 Transcription Available


Send us Fan MailRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akihutubia Kongamano la Biashara baina ya Tanzania na Kenya (Tanzania & Kenya Business Forum 2026), tarehe 04 Mei, 2026, JNICC, jijini Dar es Salaam ambapo kongamano hili lilihudhuriwa pia na Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Dkt. William Samoei Ruto.Support the showIdara ya Habari MAELEZO 

Siha Njema
Kwenye kapu la sekta ya afya kufuatia kongamano la Africa Forward

Siha Njema

Play Episode Listen Later May 22, 2026 10:08


Baadhi ya makubaliano yalitotangazwa na Ufaransa baada ya siku mbili ya kongamano la  Africa Forward ni ufadhili kwa uzalishaji wa dawa na chanjo hapa barani Afrika. Shirika la Unitaid  pia lenye ushirikiano na Ufaransa lilitangaza kuratibu mchakato wa kuzalishwa dawa mpya ya kuzuia virusi vya HIV ,Lenacapavir kuzalishwa Afrika Kusini. Na kwenye viungo vingine vilivyosheheni majadiliano ya kuimarisha mifumo ya afya Afrika ni kilimo endelevu .

Jukwaa la Michezo
Michezo kwenye mkutano wa Africa Forward Summit, Ghana yakosolewa mpangilio duni

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later May 16, 2026 23:55


Leo tunaangazia baadhi ya matukio ya michezo yaliyozungumziwa kwenye mkutano wa Africa Forward Summit uliokamilika hiki hii, uchambuzi wa Ghana kukosolewa kuandaa mashindano duni ya Afrika ya riadha, Al Hilal ya Sudan yatwaa ubingwa wa soka Rwanda, Motsengo Omba akizindua nguzo zake tano za uongozi wa Fecofa, fainali ya Kombe la Shirikisho, Afcon U17 yaanza huko Morocco, mataifa yaanza kuzindua vikosi vyao kuelekea Kombe la Dunia, PSG yashinda wa 14 huku Carrick akikaribia kusaini mkataba.

Wimbi la Siasa
Kwanini suala la siasa na usalama, halikupewa nafasi kubwa kwenye mkutano wa Afrika na Ufaransa ?

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later May 14, 2026 10:09


Mkutano wa siku mbili kati ya Ufaransa na mataifa ya Afrika, uliofanyika jijini Nairobi nchini Kenya kati ya Mei 11 hadi 12, haukutoa kipaumbele suala la siasa na usalama katika mataifa ya Afrika, wakati huu nchi kama DRC, Sudan na yale ya ukanda wa Sahel kama Mali, Niger na Burkina Faso yakishuhudia changamoto kubwa ya kiusalama. Tunachambua kwa kina.

Kiswahili, Lugha Ya Afrika
Acha Niseme - (ep2) - Ujio wa Dini kwenye Ukanda wa Afrika Mashariki

Kiswahili, Lugha Ya Afrika

Play Episode Listen Later May 10, 2026 20:55


Dini hizi ambazo zimechukua sehemu kubwa ya maisha yetu, zilitoka wapi? Video hii inagusia ujio wa dini ya kiislamu na kikristo kwenye ukanda wa East Africa. Tazama kisha ushiriki mawazo yako. Asante

Radio Maria Tanzania
Je ni sahihi mtu akiwa kwenye mfungo wowote ule kupokea Ekaristi Takatifu?

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later May 7, 2026 27:42


Karibu usikilize Kipindi cha Maswali yahusuyo Imani. Mwezeshaji ni Frateri Erasto Mwanasindele, kutoka Seminari Kuu ya Mtakatifu Augustino Peramiho, Jimbo Kuu Katoliki Songea. Swali ni Je! ni sahihi mtu kupokea Ekaristi Takatifu akiwa kwenye mfungo wa kwaresma huku akiwa amefunga chakula, pamoja na matendo mengine yahusuyo kipindi hicho cha kwaresma? Tarehe 27 Machi 2026 L'articolo Je ni sahihi mtu akiwa kwenye mfungo wowote ule kupokea Ekaristi Takatifu? proviene da Radio Maria.

machi radio maria karibu kwenye kipindi maswali ekaristi
Habari za UN
Kenya: Mradi wa majaribio walenga kudhibiti plastiki na kemikali kwenye kilimo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 27, 2026 2:54


FAO nchini Kenya inasema mradi huo wa miaka mitano uitwao FARM, unalenga kuimarisha uwekezaji katika mbinu mbadala na usimamizi endelevu wa kemikali hatari na plastiki kwenye sekta ya kilimo barani Afrika na Amerika ya Kusini. Tweet URLUkifadhiliwa na Fuko la Mazingira Duniani, GEF, mradi unafanya kazi na vikundi vya wataalamu wa kitaifa kutoka taasisi mbalimbali, kuangazia vipaumbele na changamoto za ndani ili kutengeneza mitaala ya mafunzo inayolinda mazingira. Ripoti ya mradi imebainisha kuwa matumizi ya viuatilifu yamekuwa na madhara makubwa kwa viumbe wanaosaidia uchavushaji wa mimea. Aidha, mabaki ya sumu hizi yanaweza kukaa kwenye udongo kwa zaidi ya miaka 30, jambo ambalo ni hatari sio tu kwa mazao ya chakula bali pia kwa afya za wakulima. Madhara ya matumizi kupita kiasiMatumizi yaliyopitiliza yamehusishwa na magonjwa ya saratani na matatizo ya mfumo wa mishipa ya fahamu, huku yakipunguza uwezo wa nchi kuuza mazao yao kwenye masoko ya kimataifa kutokana na viwango vya sumu kuzidi mipaka ya usalama wa chakula.  Afisa wa FAO, Oxana Perminova anasema, "plastiki na kemikali za kilimo ni jambo linalotia wasiwasi duniani kote. Suala hilo limekuwa katika ajenda za nchi nyingi. Kwa upande wa Kenya, tunaamini kuwa ushirikiano huu ambao umeanzishwa hapa na ambao kwa kweli unafanya kazi ya na unawaleta wadau wote pamoja utakuwa na manufaa makubwa kwa kanda hii. Hivyo nchi nyingine jirani zinaweza kuangalia mifano na bidhaa zitakazozalishwa ndani ya ushirikiano huu na kuzitumia mahususi kwa ajili ya kupunguza uchafuzi wa mazingira kutokana na kemikali na plastiki za kilimo na kuwalinda wakulima, hasa katika maeneo haya." Fahamu kuhusu madhara ya plastiki za vifungashioKuhusu plastiki za vifungashio vya pembejeo za kilimo, takwimu zinaonesha kuwa takriban tani 330,000 za plastiki hutumika kila mwaka kama vifungashio vya viuatilifu duniani kote. Inakadiriwa kuwa asilimia 35 ya plastiki hizi hazidhibitiwi ipasavyo, ambapo asilimia 10 huishia baharini na nyingine nyingi kubaki kwenye udongo. Grace Muchemi, ni Meneja Mkuu wa bodi ya kudhibiti bidhaa za viuatilifu, PCPB, nchini Kenya, anaeleza hatua zinazochukuliwa kuwa ni "tunapotazamia njia mbadala salama zaidi, tumekuwa tukipitia upya viuatilifu ili kuhakikisha viuatilifu vyenye hatari ndogo vinatumika ndani ya nchi. Pia, utoaji wa uelewa umefanyika ndani ya kaunti, na tunafanya kazi pamoja na mashirika mengine ya serikali na pia wadau wa maendeleo kutoa uelewa juu ya matumizi salama ya viuatilifu ili kuhakikisha chakula salama na pia kuwezesha biashara na nchi nyingine." Katika hatua muhimu ya kuleta usawa, mradi huu umehakikisha uwiano sawa wa washiriki wanaume na wanawake katika mafunzo yote yatakayotolewa. 

Habari RFI-Ki
Maoni yako kwenye makala ya habari rafiki Mada Huru

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Apr 24, 2026 9:57


Habari RFI-Ki
Maoni yako kwenye makala ya habari rafiki Mada Huru

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Apr 24, 2026 9:57


Siha Njema
Miaka mitatu tangu Sudan kuingia kwenye mzozo huduma za afya zimedorora

Siha Njema

Play Episode Listen Later Apr 16, 2026 9:19


Asilimia 37 ya vituo vya afya nchini Sudan vimeharibiwa wakati wa mapigano na haviwezi kutoa huduma za afya Shirika la madaktari wasio na mipaka,MSF limekuwa likiwahudumia wagonjwa wenye majeraha ,waathiriwa wa magonjwa ya milipuko na waathiriwa wa ubakaji. Hali ya usalama imeilazimu  MSF kusitisha huduma katika maeneo kadhaa baada ya kushuhudiwa mashambulizi ya moja kwa moja kwenye vituo vya afya ,vituo hivyo kuporwa na uhaba wa bidhaa za kimatibabu unaohusishwa na vikwazo vya usafiri.

Habari RFI-Ki
Jez ni sahihi kwa wanasiasa kutusiana kwenye mikutano ya hadhara?

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 24, 2026 10:01


Nchini Kenya, rais William Ruto na aliyekuwa naibu wake Rigathi Gachagua, wamekuwa wakirushiana maneno makali, kwenye mikutano ya hadhara na hata kwenda mbali na kutoa matusi na kushambuliana kuhusu maumbile yao, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka ujao. Nini mtazamo wako kuhusu kauli za viongozi hawa ? Katika nchi yako wanasiasa, wanatupiana maneno hivi ?

Habari RFI-Ki
Jez ni sahihi kwa wanasiasa kutusiana kwenye mikutano ya hadhara?

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Mar 24, 2026 10:01


Nchini Kenya, rais William Ruto na aliyekuwa naibu wake Rigathi Gachagua, wamekuwa wakirushiana maneno makali, kwenye mikutano ya hadhara na hata kwenda mbali na kutoa matusi na kushambuliana kuhusu maumbile yao, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka ujao. Nini mtazamo wako kuhusu kauli za viongozi hawa ? Katika nchi yako wanasiasa, wanatupiana maneno hivi ?

Changu Chako, Chako Changu
Changu Chako Chako Changu: Utamaduni wa matumizi ya viungo kwenye chakula march 22 2026

Changu Chako, Chako Changu

Play Episode Listen Later Mar 21, 2026 20:00


Ni jumapili nyingine tunakutana katika makala Changu chako chako changu, makala ambayo hukuletea historia ya mambo mbalimbali, utamaduni le parler francophone na Muziki, ambapo leo nakupelekea visiwani Zanzibar kuangazia utamtuni wa matumizi ya viungo kwenye chakula, kwenye le parler francophone tutaangazia kuhusu sherehe za siku ya kimataifa ya nchi zinazo zungumza lugha ya Kifaransa,  mimi ni Ali Bilali Bienvenue, ama Karibu.  kumbuka pia kutufollow kwenye mitandao ya kijamii @billy_bilali

Jukwaa la Michezo
Senegal yavuliwa ubingwa wa Afrika, Kenya na Ufaransa zashirikiana kwenye tenisi

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Mar 21, 2026 24:02


Leo kwenye kipindi tunaangazia hisia za baada ya Caf kuivua Senegal ubingwa wa Afrika, kwenye tenisi Kenya na Ufaransa zimeingia kwenye ushirikiano, hatma ya Kenya kaundaa Afcon 2027, FIFA yaweka vikwazo kwa Nigeria na DRC, robo fainali ligi ya klabu bingwa Afrika kuanza leo, DRC yashindwa ubingwa wa dunia kwenye basketboli ya vitimagu, ushirikiano wa FIFA na YouTube, Ronaldo kukosa mechi za kirafiki, robo fainali ya ligi ya mabingwa ulaya lakini pia matokeo ya raga divisheni ya pili ya HSBC.

Habari za UN
Wanaume wasiachwe nyuma kwenye harakati za utetezi wa  haki za wanawake na wasicha - Osowobi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 11, 2026 2:43


Oluwaseun Ayodeji Osowobi, mwanaharakati wa haki za wanawake nchini Nigeria amezungumzia umuhimu wa kushirikisha wanaume katika harakati za kupigania haki za wanawake duniani wasichana.  Rashid Malekela na maelezo zaidi.

Gurudumu la Uchumi
Uwazi kwenye ubinafsishaji wa mashirika ya uma ni muhimu kwa maendeleo

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Mar 11, 2026 10:03


Msikilizaji Katika miaka ya hivi karibuni, nchi nyingi za Afrika Mashariki zimekuwa zikifanya mageuzi makubwa ya kiuchumi. Mojawapo ya mageuzi hayo ni ubinafsishaji wa mashirika ya umma. Leo tunajiuliza, Je, ubinafsishaji ni kweli unasaidia uchumi kukua, au serikali inapaswa kubaki na umiliki wa mashirika muhimu?

kenya tanzania eac kwenye maendeleo afrika mashariki mashirika
Gurudumu la Uchumi
Uwazi kwenye ubinafsishaji wa mashirika ya uma ni muhimu kwa maendeleo

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Mar 11, 2026 10:03


Msikilizaji Katika miaka ya hivi karibuni, nchi nyingi za Afrika Mashariki zimekuwa zikifanya mageuzi makubwa ya kiuchumi. Mojawapo ya mageuzi hayo ni ubinafsishaji wa mashirika ya umma. Leo tunajiuliza, Je, ubinafsishaji ni kweli unasaidia uchumi kukua, au serikali inapaswa kubaki na umiliki wa mashirika muhimu?

kenya tanzania eac kwenye maendeleo afrika mashariki mashirika
Jukwaa la Michezo
Regragui aondoka Morocco huku CAF ikiahirisha AFCON ya kina dada

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Mar 7, 2026 24:07


Kwenye kipindi cha leo tumeangazia kuondoka kwa kocha mkuu wa Morocco Walid Regragui, Burkina Fason yapata kocha mpya, athari ya kuahirishwa kwa michuano ya WAFCON, vikwazo vya CAF dhidi ya Al Ahly, Faith Kipyegon aorodheshwa kwa mara ya tatu kuwania tuzo ya dunia ya Laureus. FIFA yatangaza sheria mpya za soka kuelekea Kombe la Dunia. Fred Kerley apigwa marufuku ya miaka miwili. Je, ni suala la muda tu Arsenal kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Uingereza au la?

Changu Chako, Chako Changu
Changu Chako Chako Changu vijana wa Mombasa na fursa kwenye tasnia ya filamu Feb 1 2026

Changu Chako, Chako Changu

Play Episode Listen Later Mar 2, 2026 20:01


Katika safari yangu huko Mombasa, nimekutana na vijana kwenye tasnia ya Filamu na kufanya nao mazungumzo kuhusu tasnia hii namna inavyopiga hatuwa pamoja na chamgamoto zake. Kumbuka kutufualia @billy bilali

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho
Hatau ya Marekani kujiondo kwenye mikataba ya mazingir na tabianchi na athari zake

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho

Play Episode Listen Later Feb 15, 2026 10:00


Aliporejea madarakani Januari 20 2025, kwa mara ya pili Trump aliiondoa Marekani katika mkataba wa tabianchi wa Paris wa 2015. Mwaka wa 2025, Washington haikuwatuma maafisa wake wa juu katika mkutano wa tabianchi wa COP30, uliofanyika Belem, Brazil. Na sasa wiki chache zilizopita, utawala wa Trump ulitangaza kuiondoa Marekani katika mashirika 66 ya kimataifa, ikiwemo ile ya UNFCCC.

Jukwaa la Michezo
Uamuzi wa CAF kwenye fainali ya Afcon 2025: Udhibiti wa Haki au Uharibifu?

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Jan 31, 2026 23:48


Leo tumeangazia kwa undani hukumu na uamuzi wa Caf kufuatia matukio yaliyoibuka kwenye fainali ya AFCON 2025, Simba inajandaa kwa mechi ya kufa kupona kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, raundi ya kwanza ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika mechi za Futsal yakamilika, msimu wa sita wa Ligi ya Afrika ya basketboli kumalizia nchini Rwanda, Faith Kipyegon ajenga hospitali huko Kenya, TP Mazembe yapata kocha mpya, fainali ya Australian Open, Ligi ya Mabingwa Ulaya yaingia raundi ya mtoano.

Habari RFI-Ki
Marekani kujiondoa rasmi kwenye WHO, hatua hatari kwa sekta ya afya dunaini

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Jan 27, 2026 9:53


Wiki iliopita, ilijiondoa kwenye shirika la afya duniani licha ya onyo kuwa hatua hiyo itaathiri ufadhili kwenye sekta ya afya duniani. Wiki chache zilizopita, rais Donald Trump alitangaza pia kuwa Marekani itajiondoa kwenye mashirika 66 ya kimataifa, yakiwemo yaliyo chini ya Umoja wa Mataifa

Habari RFI-Ki
Marekani kujiondoa rasmi kwenye WHO, hatua hatari kwa sekta ya afya dunaini

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Jan 27, 2026 9:53


Wiki iliopita, ilijiondoa kwenye shirika la afya duniani licha ya onyo kuwa hatua hiyo itaathiri ufadhili kwenye sekta ya afya duniani. Wiki chache zilizopita, rais Donald Trump alitangaza pia kuwa Marekani itajiondoa kwenye mashirika 66 ya kimataifa, yakiwemo yaliyo chini ya Umoja wa Mataifa

Siha Njema
Kufunga saum inafaidi afya yako vile vile nafsi yako ikiwa utafanya mara kwa mara

Siha Njema

Play Episode Listen Later Jan 26, 2026 10:19


Kuna ushahidi unaoonesha kwamba kufunga kunaweza kusaidia kurekebisha miili yetu ,wakati mwingine kuongeza maisha yetu, pia  njia bora ya kupunguza uzito,   Kitendo cha kukumbatia  Saum huchochea usafi wa moyo, nafsi na kusafisha mwili wako kwa kuondoa chakula ambacho mara nyingine hugeuka kuma sumu mwilini na chanzo cha magonjwa yasiyoambukiza.     Wataalam wa afya  pamoja na watetezi wa kufunga wanasema kuna uhusiano mkubwa kati ya afya ya kimwili na afya ya kiroho.   Kwenye makala hayo ya Siha Njema  tunakupa ufafanuzi huu tukisaidiwa na daktari  Julius Maleve na pia kiongozi wa kidini  Mtume Julius Suubi ,ambaye ameandika kitabu kuhusu faida za kufunga na ambaye amekuwa akifunga kwa kati ya siku 40 hadi 90 kila mwaka kwa zaidi ya mwaka 20 sasa.

Habari za UN
Kuweka picha za udhalilishaji kwenye mtandao wa intaneti si jambo zuri - Musisa Onya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 26, 2025 2:13


Siku 16 za uhamasishaji kupinga ukatili dhidi ya wanawake zikiendelea leo tunakupeka mjini Hoima Magharibi mwa Uganda kusikia maoni kutoka kwa wa mji huo kuhusu ukatili mtandaoni yakienda sanjari na kauliimbiu ya kampeni ya ya mwaka huu isemayo “Ukatili wa mtandaoni ni ukatili halisi na hakuna visingizo kwa ukatili mtandaoni”

Habari za UN
Dunia inabadilika kwa kiwango cha kutisha - Guterres Katibu aonya kwenye mkutano wa AU–EU

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 24, 2025 3:01


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo ametoa ujumbe mzito kwenye Mkutano wa Muungano wa Afrika AU na Muungano wa Ulaya EU, unaofanyika mjini Luanda, Angola akionya kuwa dunia “inabadilika kwa kiwango cha kutisha,” huku janga la tabianchi, ukosefu wa usawa na mvutano wa kimataifa vikichochea misukosuko mipya duniani . Flora Nducha na taarifa zaidi

SBS Swahili - SBS Swahili
Watu wa asili kwenye hatihati ya kutoweka Brazil

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 18, 2025 8:18


Shirika lisilo la faida linasema karibu nusu ya jamii za Wenyeji wanaoishi mbali na ulimwengu wanakabiliwa na kutoweka ndani ya muongo kutokana na ukataji miti, uchimbaji wa madini na utalii. Survival International wanasema wanataka ulimwengu - hususan serikali na viwanda - kutambua na kushughulikia tatizo hili kama dharura ya kimataifa.

brazil asili survival international watu kwenye shirika
Habari za UN
Ripoti mpya ya FAO/WFP yaonya muda unayoyoma kuzuia mamilioni kuingia kwenye njaa katika maeneo 16 hatarishi.

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 12, 2025 3:39


Ripoti mpya ya pamoja kutoka mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa lile la  Chakula na Kilimo Duniani (FAO) na la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) inaonya kwamba uhaba mkubwa wa chakula unazidi kuongezeka katika maeneo 16 yenye njaa duniani, hali inayoweza kusababisha mamilioni zaidi ya watu kukumbwa na njaa kali au hatari ya kufikia kiwango cha baa la njaa. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

SBS Swahili - SBS Swahili
Serikali kudhibitisha umuhimu wa wahamiaji kwenye uchumi

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 4, 2025 5:42


Waziri wa Mambo ya Ndani, Tony Burke, anasema kwamba serikali inafanya kazi juu ya uwezekano wa kutambua ujuzi wa nje ya nchi. Anasema hii itasaidia kuokoa muda na pesa kwa wahamiaji wenye ujuzi wanaotafuta kuhamia Australia. Katika hotuba yake kwa Klabu ya Waandishi wa Habari huko Canberra, Bw. Burke pia ametangaza mabadiliko kwenye akaunti za benki zisizotumika ili kukabiliana na utakatishaji wa fedha.

Habari za UN
Ili Afrika ‘iimarike kiafya' inabidi isiwe tegemezi kwenye masuala ya kifedha: Dkt. Ntuli Kapologwe

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 29, 2025 3:29


Hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kandoni mwa Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA80, inafanyika mikutano mingine ya pembezoni kujadili masuala mengine ya kusongesha maendeleo ya ulimwengu. Wiki iliyopita tulizungumza na Dkt. Ntuli Kapologwe Mkurugenzi Mkuu wa Jumuiya ya Afya ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika, ECSA wakati alipokuwa akisubiri kushiriki mkutano  wa nchi wanachama wa jumuiya hiyo kujadili jinsi ya kusongesha diplomasia ya kisayansi ili kuhakikisha bara la Afrika haliachwi nyuma kwenye kukabiliana na changamoto za kiafya. Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza tena na Dkt. Kapologwe mara tu baada ya mkutano huo

Habari za UN
Agizo jipya la kuhamisha watu katika ukanda wa Gaza ni ‘msumari wa moto kwenye kidonda'

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 17, 2025 3:57


Wakati Israeli ikiwa imetoa amri mpya ya watu kuhama kutoka jiji la Gaza katika eneo inalokalia kimabavu la Palestina, na kuelekea eneo ililotenga na kuliita ukanda wa kibinadamu kusini mwa Ukanda wa Gaza, shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO limesikitishwa na agizo hilo jipya ikisema eneo halina ukubwa wala huduma za kutosha kusaidia wale walioko tayari huko, sembuse wale watakaowasili. Huduma za afya ni tete kama anavyosimulia Flora Nducha kwa taarifa hii. 

SBS Swahili - SBS Swahili
Kitu chakufanya unapo kutana na wanyamapori kwenye mali yako

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 15, 2025 12:27


Popote ulipo nchini Australia, kutoka jiji kuu lenye shughuli nyingi, hadi katika viunga vya mji, katika mji wa kikanda au kijijini, kuna uwezekano unaweza kutana na aina mbali mbali za wanyamapori wazuri wa Australia.

Habari za UN
UNICEF yawawezesha vijana kwenye kilimo nchini Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 12, 2025 3:09


Kaunti ya Kirinyaga, iliyoko katikati mwa nchi ya Kenya kaskazini mwa mji mkuu wa nchi hiyo, Nairobi, inashuhudia mageuzi mapya katika sekta ya kilimo kupitia mradi wa kuwahusisha vijana  katika kilimo na lishe unaojulikana kama EKYAN. Mradi huu unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF, na wadau nchini humo.  Karibu Sabrina Saidi utupe taarifa zaidi.....(TAARIFA YA SABRINA SAIDI)Mradi wa EKYAN ni mfano wa ujasiriamali wa kilimo unaoongozwa na vijana, ukiwa na lengo la kutengeneza fursa za ajira, kuwanufaisha na kubadilisha maisha ya vijana walioko vijijini, kupitia mbinu bora za kilimo na lishe, ukitekelezwa kwa ushirikiano kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF, serikali ya kaunti ya Kirinyaga na shirika linalotoa mafunzo, elimu ya biashara ndogo ndogo na uwezeshaji barani Afrika KUZA Biashara.Felista Nyakio Mutungi kijana mkulima wa kaunti ya Kirinyaga, ni mmoja wa wanufaika wa mafunzo kupitia mradi huo. Na hapa anasema....CUT 2- Sauti ya Felista Nyakio Mutungi“Kabla ya kuanza kilimo, nilikuwa nauza barabarani viazi vya kukaanga au chipsi,  na mihogo, pamoja na nafaka. Haikuwa vizuri sana, lakini ndiyo nafasi pekee niliyokuwa nayo wakati huo. Kupitia serikali ya kaunti ya Kirinyaga, tulisajiliwa kama vijana wanaopenda kilimo na tukapata mafunzo kupitia KUZA na UNICEF. Sasa mimi ni mkulima na mjasiriamali.”Felista anasema awali alikuwa akilima robo ekari ya mpunga na kuvuna magunia manne hadi matano pekee. Lakini baada ya mradi wa EKYAN, kwa robo ekari hiyo hiyo sasa anapata hadi magunia saba. Aidha, shamba lake limepanuka hadi ekari nne katika eneo la 'mradi wa umwagiliaji wa Bura.Felista hakutaka kuwa mchoyo wa manufaa aliyopata, hivyo ameamua kueneza ujuzi wa kilimo cha kibiashara kwa kuwafundisha baadhi ya wakulima wengine mbinu na maarifa ya kilimo hiki.CUT- Sauti ya Felista  Nyakio Mutungi“Sasa si tu kwamba nalima, bali pia nawafundisha wakulima wengine kuongeza thamani katika mazao yao. Wanapata ujuzi wa kufanya biashara kupitia kilimo. Na kwa kweli tunawashukuru wahisani na UNICEF kwa kutuwezesha. Bila mpango huu, nisingekuwa hapa nilipo leo.”Kwa upande wake mtaalamu wa ubunifu wa UNICEF nchini Kenya Lilian Njoro, anaeleza kwa nini mradi huo ni muhimu kwa vijana.CUT- Sauti ya Lilian Njoro."Ni asilimia 10 pekee ya vijana wanaojihusisha na sekta ya kilimo. Kwa hivyo, kupitia mradi wa EKYAN, tulitaka kuona jinsi ya kuwahusisha vijana wengi zaidi katika kilimo na kuwavutia ili waweze kuanza kupata maisha yenye utulivu na ajira bora kupitia sekta hii.”Njoro anasisitiza kuwa teknolojia mpya zinafungua njia kwa kilimo cha kisasa tofauti na enzi za wazazi na mababu zao.Namna kilimo kinavyofanyika nyakati hizi ni tofauti na zamani,hii ni kwa sababu ya uwepo wa teknolojia bunifu, majukwaa ya kidijitali, na fursa nyingi.Kwa sasa, mradi wa EKYAN umeendelea kuwajengea vijana ujuzi, kuwapatia nafasi ya ajira, na kubadilisha mtazamo wao kuhusu kilimo, kutoka shughuli ya kizamani hadi kuwa biashara yenye faida.Link: https://youtu.be/hv17nk-2l5kTAGS:UNICEF Kenya/Kilimo/Biashara na ujasiriamali

Habari za UN
Wanavyosema wadau kuhusu Siku ya kujua kusoma na kuandika katika zama za kidijitali

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 8, 2025 2:31


Ikiwa leo tarehe 8 Septemba ni siku ya Kimataifa ya kujua kusoma na kuandika ambapo Umoja wa Mataifa ulianzisha siku hii ili kuwakumbusha watunga sera, walimu, wadau wa elimu, na jamii juu ya umuhimu wa ujuzi wa kusoma na kuandika katika kujenga jamii yenye elimu, haki, amani na endelevu,  Sabrina Saidi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa anaiangazia kauli mbiu ya mwaka huu  "Kukuza ujuzi wa kusoma na kuandika katika zama za kidijitali" akiwashirikisha baadhi ya wadau wa elimu nchini Tanzania.Amezungumza na baadhi ya wadau kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino, SAUT kilichoko jijini Mwanza, kaskazini-magharibi mwa Tanzania.Dismas Nziku ni mwalimu wa masomo ya Biashara na Ujasiriamali  anazungumza kuhusu ni kwa jinsi gani ufundishaji wa zama hizi za kidijitali unavyochochea na kukuza ujuzi wa kusoma na kuandika. "Kwenye dunia ya sasa ujuzi wa kusoma na kuandika kidijitali ni msingi mkubwa kwa mwanafunzi, na miongoni mwa juzi hizi muhimu ni kama vile kujua kutumia vifaa vya kidijitali kama kompyuta, simu janja kwa ajili ya kujisomea na kutafuta maarifa, lakini pia kama mwalimu ninawafundisha wanafunzi kwa njia ya vitendo,kuandaa maswali ya utafiti kwa kutumia internet,kufanya kazi na kufanya kazi ya kikundi mitandaoni."Kuhusu umuhimu wa siku hii kwake na inachangia vipi katika kukuza uelewa wa umuhimu wa kusoma na kuandika shuleni na katika jamii Mwalimu Nziku amesema, "Siku ya Kimataifa ya kujua kusoma na kuandika ni kumbusho muhimu kwamba elimu ni haki ya msingi, na ni msingi wa maendeleo kwa kila mmoja kujua kusoma na kuandika hasa hasa kidijitali, inanipa hamasa kama mwalimu kuendelea kuwajengea wanafunzi ujuzi wa kusoma na kuandika si kwa ajili ya mitihani tu, bali kwa maisha yao ya kila siku."Didas Karoli ni mwanafunzi katika chuo hicho cha SAUT akisoma shahada ya kwanza ya Mawasiliano kwa Umma, ameeleza kuhusu siku hii na jinsi maendeleo ya kidijitali yanavyochagiza katika kujifunza kwake akisema "Zana za kidijitali zimebadilisha sana upeo wangu katika suala la kujifunza,kutokana na zamani nilikuwa nategemea vitabu lakini hivi sasa natumia tu smartphone au kompyuta na kutengeneza notisi zangu mwenyewe za kujifunzia.Siku ya hii ya kujua kusoma na kuandika ni siku ambayo ni muhimu inafanya watu waweze kujua umuhimu wa kusoma na kuandika."

tanzania saut zama zana umoja umma kiswahili katika siku mwanza kwenye biashara mataifa kimataifa ikiwa septemba kujua chuo kikuu
Habari za UN
Afisa wa UN ajionea jinsi Tanzania 'inafunda' waendao kwenye operesheni za ulinzi wa amani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 27, 2025 2:15


Mratibu Maalum wa Kuboresha Hatua za Umoja wa Mataifa dhidi ya Unyanyasaji wa kingono (SEA) Christian Saunders amefanya ziara nchini Tanzania kuona maandalizi ya vikosi vya operesheni za ulinzi wa amani katika maeneo mbalimbali duniani. Kutoka Dar es Salaam, Tanzania, Kapteni Mwijage Inyoma Afisa Habari wa Chuo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani cha Tanzania (TPTC) ametuandalia taarifa hii.Ni bendi ya jeshi la Wananchi wa Tanzania, JWTZ ikiongoza askari wengine kumkaribisha Bwana Christian Saunders hapa katika Chuo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani cha Tanzania (TPTC) Kunduchi, Dar es Salaam.Miongoni mwa askari hawa tayari wameandaliwa kwenda katika nchi mbalimbali katika ukanda wa Afrika Mashariki na kati na hata nje ili kuusaidia Umoja wa Mataifa kutekeleza moja ya majukumu yake kwa ulimwengu, kuleta na kuitunza amani.Bwana Saunders anasema, “wacha nianze kwa kusema asante. Kusema asante ni jambo muhimu sana, kwa sababu mko tayari kuanza jukumu la kutumwa, iwe mnaenda Lebanon au Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo au kwingineko. Mkiwa mbali na familia zenu, mbali na nchi yenu, katika mazingira yenye changamoto, na wakati mwingine katika hali hatarishi.”Anawapa moyo zaidi askari lakini akiwakumbusha kuwa wao ni kioo cha ulimwengu wazingatie maadili“Na tunathamini sana kujitolea kwenu. Tunathamini sana kwamba mnaenda kuwasaidia ndugu zenu katika nchi nyingine, iwe ni nchi jirani au sehemu iliyo mbali. Mnapokwenda, mnaliwakilisha dunia. Mnawakilisha watu wa dunia.”Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani cha Tanzania (TPTC), Brigedia Jenerali George Itang'are akamthibitishia mgeni kwamba askari hawa wameiva na hakuna kisingizio chochote cha kutozingatia maadili huko wameandako, kisha akawahoji, Nao wanajibu, “twende pamoja, turudi pamoja.” 

dar lebanon congo tanzania salaam nao umoja kwenye chuo jinsi jamhuri mataifa mkuu afrika mashariki kidemokrasia wananchi miongoni
Habari za UN
Mradi wa IFAD na ILO wadhihirisha nguvu ya vijana kwenye kilimo vijijini

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 18, 2025 1:53


Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa, lile la ajira, ILO na mfuko wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD yanatekeleza mradi wa ProAgro YOUTH  unaolenga kuongeza ajira kwa vijana katika sekta ya biashara ya kilimo vijijini.

ilo umoja kwenye ifad vijana nguvu mataifa maendeleo mashirika
Habari za UN
Malezi ni kama kukunja shuka lakuvisha kwenye godoro, hakuna ajuae jinsi ya kulikunja

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 23, 2025 3:04


Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF kwakushirikiana na wakfu wa LEGO wametengeneza video yenye kuonesha familia nne na jinsi zinavyopambana na malezi ya Watoto wakiwa ni wazazi kwa mara ya kwanza. Leah Mushi ametazama video hiyo ya takriban dakika 30 na hapa anakuleta simulizi ya familia kutoka nchini Afrika Kusini. 

Habari za UN
Kujituma na kutokata tamaa ndio siri ya kufanikiwa kwenye mafunzo kwa vitendo UN - Sarah Nshoka

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 16, 2025 3:27


Kutoka Dar es Salaam hadi Geneva, na sasa New York. Ni safari ya kujifunza, kujaribu na kufanikiwa. Kwa vijana wengi barani Afrika, Umoja wa Mataifa huonekana kuwa ndoto isiyowezekana. Lakini kijana huyu kutoka Tanzania anathibitisha kuwa kwa nia thabiti na bidii, ndoto hiyo inaweza kuwa kweli. Kupitia programu ya mafunzo kwa vitendo ya Umoja wa Mataifa, amejifunza mengi kuhusu utawala, maendeleo na kujenga ujasiri wa kushiriki katika kazi za kimataifa. Sarah Nshoka alipata fursa kuzungumza na Shraon Jebichii katika makala hii.

Habari za UN
TANLAP Tanzania tunahamasisha wanawake wengi kushiriki kwenye uchaguzi ili washiriki kuamua mambo yanayowahusu - Christina Kamili Ruhinda

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 23, 2025 3:13


Katika mahojiano haya, Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Mashirika yanayotoa huduma ya msaada wa kisheria nchini Tanzania, TANLAP, Christina Kamili Ruhinda alipozungumza na Anold Kayanda wa Idhaa hii kandoni mwa Mkutano wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW69 uliofanyika mapema mwaka huu hapa New York, Marekani, anaeleza wanavyotekeleza mpango wao wa kuhakikisha wanawake  wanapata nafasi zaidi kwenye meza za uamuzi nchini Tanzania.

new york tanzania mambo katika kamili kwenye wanawake wengi marekani mkutano uchaguzi mashirika
Habari za UN
Ujumuishaji wazazi wa kiume kwenye malezi ya watoto waleta manufaa kwa jamii

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 18, 2025 2:12


Katika Kaunti ya Kilifi, iliyoko pwani ya Kenya barani Afrika,  Mpango wa Kuboresha Lishe kwa kupatia jamii Fedha na Elimu ya Afya (NICHE) unasaidia kuwaelimisha wazazi kuhusu umuhimu wa baba na mama kulea watoto wao kwa pamoja, mradi unaotekelezwa na shirika la Umoja wa MAtaifa la kuhudumia watoto, UNICEF. Assumpta Massoi anamulika moja ya familia zilizonufaika.

Habari za UN
Guterres: Tuepushe kauli za chuki kwenye ujumbe chanya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 18, 2025 1:53


Leo Juni 18 ni siku ya kimataifa ya kupambana na kauli za chuki ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametumia ujumbe wake kwa siku hii kutoa onyo kuhusu hatari zinazoongezeka za chuki mtandaoni, hasa zikichochewa na akili mnemba au (AI) na  na majukwaa ya kidijitali. Flora Nducha na taarifa zaidi.

Habari za UN
Shirika la kiraia lawezesha vijana wa kike kujiajiri badala ya kutumbukia kwenye umaskini

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 2, 2025 3:36


Nchini Tanzania ugumu wa maisha na kukabiliwa na vishawishi, umewapa fikra mpya vijana wa kike mkoani Morogoro, mashariki mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, ambao sasa wanajimudu kiuchumi,  kwa kuanzisha biashara na shughuli za ujasiriamali. Wanasongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs hususan namba 8 la ajira zenye staha, nan amba 1 la kutokomeza umaskini. Hamad Rashid wa Redio washirika Tanzania Kids Time FM amewatembelea vijana hao na kuandaa makala hii.

tanzania sdgs kwenye vijana shirika afrika mashariki redio
Habari za UN
FAO: Mikakati sahihi ya kilimo imeepusha mamilioni kutumbukia kwenye baa la njaa

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 16, 2025 2:17


Ukosefu wa uhakika wa kupata chakula na utapiamlo kwa watoto uliongezeka kwa mwaka wa sita mfululizo mwaka 2024, na kuwatumbukiza mamilioni ya watu karibu na baa la njaa, huku wengine wakiepuka kutokana na misaada ya kimkakati. Imesema Ripoti ya Kimataifa kuhusu Janga la Chakula (GRFC) iliyotolewa leo huko Roma, Italia na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO. Flora Nducha anakutaarifu kwa muhtasari.

roma italia sdgs fao umoja kwenye janga mataifa kimataifa
Habari za UN
Mkunga nchini Tanzania atoa wito wa uwekezaji kwenye fani hiyo

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 5, 2025 2:07


Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya wakunga, tunakwenda nchini Tanzania kummulika mkunga ambaye alinusuru maisha ya wajawazito wawili wakati wa mafuriko makubwa ya Novemba 2023 wilayani Hanang, mkoani Manyara, kaskazini mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, ikiwa ni ushuhuda wa majukumu mazito yanayokumba wakunga. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

tanzania fani afya hiyo kwenye novemba afrika mashariki ikiwa
Habari za UN
Haki Elimu - Ujumbe wetu mkuu kwenye CSW69 ni elimu kwa mtoto wa kike

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 12, 2025 3:40


Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake Duniani, (CSW69) umeingia siku ya tatu hii leo Machi 12 katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijinoi New York, Marekani. Mkutano huu wa mwaka huu unafanyika katika hali ya kihistoria kwa kuzingatia kuwa ni miaka 30 tangu Mkutano wa wanawake ulipofanyika jijini Beijing - China  mwaka 1995 na kuweka maazimio muhimu kuhusu masuala mazito ya kumkomboa mwanamke dhidi ya ukandamizaji kote duniani. Maelfu ya wanawake na wadau wengine wanakutana kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York. Miongoni mwao ni Nuria Mshare ambaye amewakilisha taasisi ya Haki Elimu ya nchini Tanzania.

new york tanzania machi umoja haki beijing china kwenye elimu mataifa mkuu marekani mkutano ujumbe miongoni