Podcasts about novemba

  • 28PODCASTS
  • 632EPISODES
  • 22mAVG DURATION
  • 1MONTHLY NEW EPISODE
  • May 5, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about novemba

Latest podcast episodes about novemba

Habari za UN
Mkunga nchini Tanzania atoa wito wa uwekezaji kwenye fani hiyo

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 5, 2025 2:07


Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya wakunga, tunakwenda nchini Tanzania kummulika mkunga ambaye alinusuru maisha ya wajawazito wawili wakati wa mafuriko makubwa ya Novemba 2023 wilayani Hanang, mkoani Manyara, kaskazini mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, ikiwa ni ushuhuda wa majukumu mazito yanayokumba wakunga. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Habari za UN
05 MEI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 5, 2025 10:52


Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya kimataifa ya wakunga na kazi zao muhumi, na mafunzo ya jerahani kwa wakimbizi wa ndani nchini DRC. Makala tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa na mashinani tunakwenda Gaza.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya wakunga, tunakwenda nchini Tanzania kummulika mkunga ambaye alinusuru maisha ya wajawazito wawili wakati wa mafuriko makubwa ya Novemba 2023 wilayani Hanang, mkoani Manyara, kaskazini mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, ikiwa ni ushuhuda wa majukumu mazito yanayokumba wakunga.Wanawake 125 katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Kigonze, karibu na Bunia, mji mkuu wa jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ambako ghasia huripokiwa mara kwa mara, sasa wana matumaini mapya ya kujikwamua kiuchumi baada ya kujiunga na mradi wa mafunzo ya kushona nguo unaofadhiliwa na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini humo (MONUSCO).Makala Assumpta Massoi anamulika uzinduzi wa mtandao wa Mashirika ya Manusura wa Ugaidi duniani,  VoTAN      uliofanyika wiki iliyopita hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa.Na mashinani kupitia video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM), fursa ni yake Rawhiyeh, mkimbizi kutoka Gaza eneo la Palestina linalokaliwa na Israel ambaye anasimulia kwa uchungu madhila yanayowakumba yeye na familia yake baada ya kupoteza makazi yao kutokana na mashambulizi ya mabomu.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 13 Machi 2025

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 13, 2025 5:47


Ripoti mpya ya Chuo cha Monash imeonesha matukio ya unyanyasaji dhidi yawa Islamu wa Australia, yali ongezeka zaidi ya mara mbili kati ya Januari 2023 na Novemba 2024.

Habari za UN
UN: Vifo vitokanavyo na baridi Gaza vinazuilika, usitishaji mapigano na misaada ndio jawabu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 3, 2025 1:58


Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM leo limeonya juu ya vifo vitokanavyo na msimu wa baridi kali Gaza likisema limesikitishwa sana na athari mbaya za mvua za msimu wa baridi na baridi kali kwa Wapalestina waliokimbia makazi yao na kuishi katika mazingira magumu huko Gaza, kwani hilo ni janga la kibinadamu lisilo na kifani. Kupitia taarifa iliyotolewaleo mjini Geneva Uswisi Mkurugenzi Mkuu wa IOM Amy Pope  amesema "Watu walio katika mazingira magumu, ikiwa ni pamoja na takriban watoto wachanga saba, wamekufa kutokana na baridi kali au hypothermia, na vifo hivi vya kusikitisha vinasisitiza haja ya haraka ya makazi na msaada mwingine wa kibinadamu kuwafikia watu wa Gaza mara moja," Ameongeza kuwa hali hii inachochea janga zaidi la kibinadamu ambalo tayari linawakumba watu waUkanda wa Gaza. Mvua kubwa na mafuriko yameyakumba makazi ya wakimbizi wa ndani yaliyojengwa kwa mahema na kulazimisha familia kuachwa katika maeneo ya wazi kwenye hali mbaya ya baridi, zikijitahidi kutengeneza mahema yaliyoharibika kutokana na matumizi ya miezi kadhaa. © UNRWAChakula kinagawiwa kwa watu waliokimbia makazi yao huko Jabalia, kaskazini mwa Gaza.Vikwazo vya Israel ni changamoto kwa misaadaPia IOM imesema vikwazo vya utaratibu wa kufikia wenye uhitaji, kama ilivyoripotiwa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA, vimezuia kwa kiasi kikubwa utoaji wa misaada, huku watu 285,000 pekee wakipokea msaada wa makazi tangu Septemba 2024. Kwa mujibu wa IOM hadi kufikia Katikati ya Desemba mwaka jana inakadiriwa kuwa watu wapatao 945,000 bado wanahitaji msaada wa haraka wa kukabiliana na msimu wa baridi ikiwemo nguo za kuongeza joto, mablanketi na tepu za kuima mahema dhidi ya mvua na baridi. Tangu Katikati ya Novemba mwaka jana IOM imewasilisha karibu vifaa 180,000 vya makazi ya dharura kwa washirika ndani ya Gaza na ina zaidi ya vifaa milioni 1.5 vya msimu wa baridi ikiwemo mahema, vifaa vya kuziba  na vitanda ambavyo viko tayari kwenye maghala na sehemu zavivuko, lakini vikwazo vikali vya ufikiaji vinawazuia kufikia wenye uhitaji. © UNICEF/Abed ZaqoutWavulana wawili wakibeba chupa za maji katika kambi ya wakimbizi inayofadhiliwa na UNWRA huko Khan Younis kusini mwa Gaza.Usitihsaji mapigano ndio suluhuIOM imesisitiza wito wake wa dharura wa kusitisha mapigano ili kuwezesha utoaji salama na wa haraka wa msaada wa kuokoa maisha kwa wale wanaouhitaji sana. Pia inasisitiza wito wake kwa pande zote kuzingatia sheria za kimataifa za kibinadamu, kuhakikisha ulinzi wa raia, kuachiliwa kwa mateka wote na kuruhusu ufikiaji salama, wa haraka, usiozuiliwa na endelevu wa wenye uhitaji. Watu wa Gaza wanastahili usalama, makazi na utu. IOM iko tayari kuhamasisha misaada na kusaidia jamii zilizofurushwa, lakini fursa ya ufikiaji wa kibinadamu lazima itolewe ili kuwezesha hili amesisitiza mkuu wa IOM. Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA limesema Licha ya hali ngumu, timu za UNRWA zinaendesha makao yote ya Umoja wa Mataifa, na kutoa msaada wa kuokoa maisha kwa watu wanaohitaji. Limeongeza kuwa Vita vilipoanza karibu miezi 15 iliyopita, UNRWA iligeuza shule zake, vituo vya afya, na maghala kuwa makazi na kuna wakati ambapo vita ikiendelea UNRWA ilipokea watu milioni 1 waliokimbia makazi yao 

Habari za UN
29 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 29, 2024 9:59


Hii leo jaridani Assumpta Massoi anamulika adha zinazokumba raia kwenye eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli; hakari za kukabili UKIMWI Afrika Kusini; IFAD ilivyonusuru vijana na safari za kwenda Ulaya zinazohatarisha maisha yao; Mkimbizi wa ndani Gaza anayezungumzia harakati za kusaka mkate ili kulisha familia yake.Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa katika ofisi ya eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli, Ajith Sungay amesema miezi 13 ya vita imeufanya Ukanda wa Gaza kuwa kama jehanamu, kwani kuna uharibifu usio na kifani, njaa isiyoelezeka magonjwa na kuendelea kwa mashambulizi ya mabomu yanayotawanya raia kila uchao. Flora Nducha na taarifa zaidi.Kuelekea ya Siku ya Kimataifa ya UKIMWI itakayoadhimishwa Jumapili hii, ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kukabiliana na UKIMWI (UNAIDS) iliyotolewa juzi Jumatano imeeleza kuwa dunia inaweza kufikia lengo lililokubaliwa la kukomesha UKIMWI kama tishio la afya ya umma ifikapo mwaka 2030 lakini kwa sharti kwamba viongozi ni lazima walinde haki za binadamu za kila mtu anayeishi na Virusi Vya UKIMWI, VVU au aliyeko hatarini kuambukizwa. Anold Kayanda ameangazia mfano mzuri wa Afrika Kusini unaofahamika kama “Takuwani Riime”.Mkala inayokupeleka nchini Senegal kusikia jinsi mradi wa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo IFAD umewezesha vijana kuondokana na mawazo ya kuweka rehani maisha yao wakisaka maisha bora Ulaya. Mwenyeji wako ni Bosco Cosmas.Mashinani fursa ni yake nampisha Abu Muhammad, mkimbizi wa ndani huko Deir Al Balah, Ukanda wa Gaza akielezea umuhimu wa mgao wa mikate kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula, WFP, kwa wakimbizi hao wakati huu ambapo vita inaendelea eneo hilo.

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 29 Novemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 29, 2024 18:08


Waziri Mkuu amekataa kuweka wazi jinsi mamlaka yaku wafurusha watu katika nchi ya tatu yata tumiwa.

habari novemba waziri mkuu
Alfajiri - Voice of America
Alfajiri - Novemba 29, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 29, 2024 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Alfajiri - Voice of America
Umoja wa Mataifa wakaribisha kuongezwa muda wa kupelekwa misaada ya kibinadamu Sudan - Novemba 28, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 28, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
27 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 27, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia masuala ya afya na lishe katika nchi zinazokumbana na ukame. Makala tunakwenda Ureno na mashinani nchini Sudan, kulikoni?Mkurugenzi mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO, amesema amestushwa na kusikitishwa na kifo cha aliyetarajiwa kushika wadhifa wa mkurugenzi mkuu wa WHO Kanda ya Afrika Dkt. Faustine Engelbert Ndungulile kutoka nchini Tanzania.Awamu ya pili ya mradi wa kuboresha lishe, SUN II nchini Zambia umewezesha wakulima kupanda mazao yanayohimili ukame na vile vile kukabiliana na viwavi jeshi kwa kutumia mbinu za asili, mradi uliotekelezwa na shirika la Umoja la kuhudumia watoto, UNICEF ili wakulima wasikumbwe na njaa wakati huu ambapo ukame umetikisa nchi za kusini mwa Afrika.Jukwaa la 10 la Umoja wa Mataifa la Ustaarabu limekunja jamvi leo huko Cascais, Ureno ambako sambamba na jukwaa hilo, pia vijana kutoka makundi 150 duniani walikusanyika katika jukwaa lao wakiwemo watengeneza filamu chipukizi ambao kupitia filamu wanaeleza mambo kadha ya ulimwengu kama uhamiaji, ujumuishaji, kupambana na ubaguzi na mengine mengi. Miongoni mwa vijana hao ni Dativa Mahanyu na Mariam Mintanga kutoka Tanzania. Kwanza tumsikilize Mariam Mintanga akieleza alivyojisikia kuhudhuria mkutano huu kisha tutamsikia Dativa Mahanyu akieleza kuhusu filamu ya Fid ya ambayo kupitia taasisi ya Tai Tanzania imepata tuzo ya PLURAL+.Na mashinani fursa ni yake Shaza Ahmed, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la wanawake Nada El Azha linalotoa msaada kwa waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia nchini Sudana akitoa wito kwa viongozi wa kimataifa wa kutokomeza ukatili wa kijinsia.Mwenyeji wako ni Bosco Cosmas, karibu!  

Alfajiri - Voice of America
Zaidi ya washukiwa 1,000 wakamatwa na Interpol kutokana na wizi wa kimitandao barani Afrika. - Novemba 27, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 27, 2024 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
26 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 26, 2024 11:25


Hii leo jaridani tunakletea mada kwa kina ambayo tunamskia mwanamke mjasiriamali kutoka visiwa vya Karibea St. Kitts na Neves akitumia fursa ya utamaduni wake mchanganyiko wa asili ya Visiwa hivyo na wa Kiswahili kujikwamua kiuchumi kupitia ubunifu wa mitindo na shughuli za mama lishe. Pia tunakuletea muhtasari wa habari zikiwemo za mgogoro Lebanon, Afya ya kinywa, na Ujumbe wa Katibu Mkuu kutoka Portugal akihutubia Jukwaa la 10 la Umoja wa Mataifa la Muungano wa Ustaarabu, (UNAOC). Mashinani tunakupeleka katika ukanda wa Gaza kumsikia muathirika wa vita ya Israel.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 26 Novemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 26, 2024 15:15


Mchumi mmoja amesema mpango wa usawa wa pamoja waku saidia kununua nyumba wa serikali, hauta leta tofauti kubwa katika soko la nyumba la Australia.

Alfajiri - Voice of America
Somaliland kufanya uchaguzi Jumatano - Novemba 26, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 26, 2024 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
UN: Mwanamke au msichana mmoja aliuawa kila baada ya dakika 10 na mwenzi au ndugu 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 25, 2024 3:13


Leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake, Je wajua kwamba wanawake na wasichana 140 walifariki dunia kila siku duniani kote mwaka 2023 wakiwa mikononi mwa wapenzi wao au ndugu wa karibu, ikimaanisha kuwa mwanmake mmoja anauawa katika kila dakika 10. Na zaidi ya yote bara la Afrika linaongoza? Maudhui ya siku hii yanasema “Hakuna kisingizio” cha ukatili dhidi ya wanawake lama alioushuhudia Ester manusura kutoka Uganda, ambaye kwa miaka mingi amekuwa akifanyiwa ukatili na mpenzi wake anaema “Nilikuwa na umri wa miaka 15 aliponioa naye alikuwa na miaka 28wakati mwingine alikuwa akinivua nguo zote na kunilazimisha kukaa kwenye varandana nilikuwa nikichelewa kurudi ananitandika nje nyumba kila mtu kushuhudia Nilikuwa katika hali mbaya ya uchungu Mkubwa na kuvuja damu.”maadhimisho ya mwaka huu yanaambatana na ripoti iliyotolewa leo jijini New York, Marekani na mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la masuala ya wanawake, UN Women na Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kudhibiti Dawa za kulevya na Uhalifu, (UNODC), inaangazia mwanga wa janga la mauaji ya wanawake na kutoa wito kwa hatua za dharura ili kukabili janga hilo.Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres katika ujumbe wake wa siku hii inayoadhimishwa tarehe 25 mwezi Novemba kila mwaka, ikiashiria pia kuanza kwa siku 16 za kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake, zikiwa na kilele chake tarehe 10 mwezi Desemba, siku ya Haki za Binadamu duniani amesema “Janga la ukatili dhidi ya wanawake na wasichana linaaibisha ubindamu, dunia lazima iitikie wito huu. Tunahitaji hatua za dharura kwa ajili ya haki na uwajibikaji, na kusaidia uchechemuzi.”Mkurugenzi mtendaji wa UN Women Sima Bahous amesisitiza kuwa “Ukatili dhidi ya wanawake na wasichana si kwamba hauepukiki, unaweza kuzuilika. Tunahitaji sheria thabiti, ukusanyaji bora wa takwimu, uwajibikaji zaidi wa serikali, utamaduni wa kutovumilia, na kuongezeka kwa ufadhili kwa mashirika ya kupigania haki za wanawake na taasisi. Tunapokaribia kuadhimisha miaka 30 ya Azimio la Beijing na Jukwaa la Utekelezaji mwaka 2025, ni wakati wa viongozi wa dunia kuungana na kuchukua hatua kwa haraka, kujitolea na kuelekeza rasilimali zinazohitajika kumaliza mgogoro huu mara moja na kwa wote”Mauaji ya wanawake yanavuka mipaka, hali ya kiuchumi na kijamii, utamaduni. Hata hivyo kiwango au ukubwa wake unatofautiana.Kwa mujibu wa ripoti hiyo, bara la Afrika lilivunja rekodi ya kuwa na viwango vya juu vya wanawake kuuawa na wapenzi wao au mwanafamilia. Wanawake 21,700 waliuawa Afrika mwaka huo wa 2023, ikifuatiwa na bara la Amerika na kisha Oshenia.Mashirika ya UN Women na…

Habari za UN
Tanzania: FAO yawezesha ufugaji kuku bila kutumia dawa ili kuepusha UVIDA

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 25, 2024 3:55


Nchini Tanzania wanufaika wa  mradi wa kudhibiti usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa, (AMR) au kwa lugha ya Kiswahili, (UVIDA) unaotekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, (FAO) nchini Tanzania, kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi wamezungumzia manufaa ya ufugaji wa kuku bila kutumia dawa. Unaweza kujiuliza wanafuga vipi kuku bila kutumia dawa. Na je ni kwa nini wanafanya hivi. Je hawatumii dawa kabisa au wanafanya nini?Katika makala hii, mwandishi wa habari wa Redio washirika wetu Tanzania Kids Time ya mkoani Morogoro,mashariki mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, Hamad Rashid, amezungumza na wanufaika hao  ambao pia walipata nafasi ya kuonesha shamba darasa la ufugaji kuku bila ya kutumia dawa kupitia hafla iliyoratibiwa na FAO katika shule ya sekondari Kihonda, Manispaa ya Morogoro, ikienda sambamba na Wiki ya utoaji elimu kuhusu UVIDA  ambayo hufanyika duniani kote kila ifikapo tarehe 18 hadi 24 mwezi Novemba. Kwako Hamad.

Habari za UN
25 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 25, 2024 9:47


Hii leo jaridani tunaangazia siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake, na Meya wa mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC la kukarabati daraja linalounganisha barabara muhimu. Makala tunakwenda nchini Tanznaia na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake, Je wajua kwamba wanawake na wasichana 140 walifariki dunia kila siku duniani kote mwaka 2023 wakiwa mikononi mwa wapenzi wao au ndugu wa karibu, ikimaanisha kuwa mwanmake mmoja anauawa katika kila dakika 10. Na zaidi ya yote bara la Afrika linaongoza?Kiu cha Meya wa mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC, cha kuona daraja linalounganisha barabara muhimu linakarabatiwa kilipata jawabu baada ya ombi lake kwa Ujumbe wa Umoja wa MAtaifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO kuchukua hatua ambayo pia inawezesha doria za ulinzi wa raia mjini humo.Makala inatupeleka Tanzania kwake Hamad Rashid wa redio washirika Kidstime FM ya mkoani Morogoro, mashariki mwa taifa hilo akizungumza na wanufaia wa mafunzo ya shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO la ufugaji kuku bila kutumia dawa.Na mashinani tunakwenda Kenya kusikia harakati za viongozi wa dini ya kiislamu kukabiliana na ukatili wa kijinsia.Mwenyeji wako ni Bosco Cosmas, karibu! 

Alfajiri - Voice of America
Serekali ya DRC yatakiwa kuondoa utawala wa kijeshi - Novemba 25, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 25, 2024 29:57


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
22 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunaangazia majadiliano huko Baku Azerbaijan kuhusu ufadhili wa mabadiliko ya tabianchi, na kazi za walinda amani kutoka Tanzania TANZBATT-11 huko DRC. Makala inaturejesha kataika mkutano wa COP29 na mashinani inatupeleka Namibia, kulikoni?Majadiliano ya mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP29 yamekumbwa na mkwamo huko Baku Azerbaijana muafaka haujapatikana. Majadiliano hayo yaliyotarajiwa kukunja jamvi leo sasa yanaendelea kwa kuwekwa mezani mapendekezo mapya kuhusu ufadhili wa mabadiliko ya tabianchi hasa kwa matifa yanayoendelea.Umoja wa Mataifa unasema kwamba vita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC imefanya taifa hilo kuwa pahala hatari zaidi duniani kwa watoto kuishi, kutokana na mateso ya kimwili na kisaikolojia wanayoyapitia. Kwa kutambua hilo walinda amani wanawake wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye ujumbe wa UN nchini humo, MONUSCO wamechukua hatua kuona watoto wanaishi kama watoto.Makala inakupeleka Baku nchini Azerbaijan kunakotamatika mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29 kumsikia kijana kutoka Tanzania akizungumzia kilichompeleka, anachoondoka nacho na ujumbe wake kwa  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.Na katika mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP, tunasikia kauli ya Willem Westhuizen, mkulima kutoka Namibia, akielezea changamoto zinazotokana na ukame unaoathiri maisha yao kila siku”.  Mwenyeji wako ni Bosco Cosmas, karibu! 

Alfajiri - Voice of America
Kundi jipya la wanamgambo kwa jina Lakurawas, laibuka kaskazini magharibi mwa Nigeria - Novemba 22, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
21 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 21, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Kenya kushuhudia jinsi mpango wa Usimamizi wa Ardhi uliopatiwa wa "kusaidia jamii kufikia Ajenda 2030” ambao FAO imetekeleza kwa kaunti kadhaa. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa neno.Hague kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa ICC ambayo leo imetoa kibali cha kukamatwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, Waziri wa zamani wa ulinzi Yoav Galant  na kiongozi wa kundi la kipalestina la Hamas Mohamed Diab Ibrahim al-Masri alimaarufu kama  kwa makosa ya uhalifu dhidi ya ubinadamu na uhaifu wa vita ulitendeka wakati wa vita inayoendelea baina ya Israel na Hamas.Mjini  Baku nchini Azerbaijan mkutano wa 29 wa mkataba wa nchi wanachanama wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabainchi COP29 unaelekea ukingoni  na leo ukijikita na masuala ya kijinsia na mabadiliko ya tabianchi. Miongoni mwa waliozungumzia changamoto ya tabianchi kwa wanawake ni  Jemimah Njuki, mkuu wa kitengo cha uwezeshaji wa kiuchumi katika shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women.“Raia  wanaoshtakiwa katika mahakama za kijeshi nchini Uganda hukosa dhamana sawa ya mchakato wa kisheria kama wale wanaoshtakiwa katika mahakama za kiraia,” amesema Volker Türk, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu hii leo kufuatia tukio la kutekwa kwa mwanasiasa wa upinzani nchini Uganda Kiiza Besigye akiwa nchini Kenya.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno MHARABU”.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Alfajiri - Voice of America
Viongozi wa mataifa ya kiarabu wampongeza Trump, wakiwa na imani kwamba atasaidia kurejesha amani Mashariki ya Kati - Novemba 21, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 21, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
UNICEF - Maadhimisho ya kimataifa ya siku ya mtoto duniani yafanyika Denmark

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 20, 2024 1:50


Leo ikiwa ni siku ya watoto duniani ikirejelea tarehe 20 Novemba mwaka 1954 kwa mara ya kwanza kabisa ilipoanzishwa na Umoja wa Mataifa ili kusongesha umoja na kujitambua miongoni mwa watoto duniani. Kisha siku hii ikaongezwa nguvu na Azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu Watoto duniani mwaka 1959 na hatimaye mwaka 1989 Baraza hilo lililopitisha Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto, CRC. Mkataba unatambua haki kuu nne za msingi za mtoto: Kuishi, Kuendelezwa, Kulindwa na Kushirikishwa. Hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limefanya maadhimisho ya kimataifa huko Copenhagen Denmark, na Madina Jubilate, Mchechemu wa UNICEF Tanzania kwa Tabianchi anaelezea alivyoshiriki.

Habari za UN
20 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 20, 2024 9:57


Hii leo jaridani tunaangazia ripoti siku ya watoto duniani, na kwa kutambua siku hii tunamulika mikutano yote yanayoendelea kwa ajili ya haki za watoto na vijana, ambao wametoa ujumbe wao kutoka Baku nchini Azerbaijan na Denmark wakiwakilisha nchi zao.Leo ni siku ya watoto duniani maudhui mwaka huu yakiwa "Kila mtoto, kila haki"na katika kuhakikisha sauti zao zinasikika kuhusu mustakbali wa utakao, shirika la Umoja wa Maataifa la kuhudumia watoto duniani UNICEF limewapa fursa ya kuandika barua kwenda kwa watu wazima kote duniani ili kutoa madukuduku yao na kutanabaisha wanachokitaka kwa ajili ya mustakbali wao.Kama ulivyosikia katika taarifa yetu ya kwanza leo ni siku ya watoto duniani ikirejelea tarehe 20 Novemba mwaka 1954 kwa mara ya kwanza kabisa ilipoanzishwa na Umoja wa Mataifa kusongesha umoja na kujitambua miongoni mwa watoto duniani..Makala ikiwa leo ni siku ya watoto duniani, tunakupeleka Baku Azerbaijan katika mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP29,  ambako Selina Jerobon amefuatilia mkutano wa watoto na vijana inayomulika mchango wao katika kuhakikisha mazingira bora.Mashinani katika kuadhimisha siku ya watoto duniani tunabisha hodi msitu wa Amazoni nchini Peru kwa mtoto Susan akitoa wito kwa dunia kuchukua hatua dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi kulinda msitu huo kunusuru kizazi cha watoto wa sasa na wa vizazi vijavyo katika taifa hilo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Alfajiri - Voice of America
Alfajiri - Novemba 20, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 20, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
19 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 19, 2024 11:07


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Baku nchini Azerbaijan kwenye mkutano wa COP29. Miongoni mwa mambo yanayopigiwa chepuo ni madini ya kimkakati yanayoelezwa kuwa ni jawabu la nishati chafuzi kwa mazingira na tunapata ufafanuzi kutoka kwa Adam Anthony, Mkurugenzi Mtendaji wa HakiRasilimali nchini Tanzania.Katibu  Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amewasihi viongozi wa kundi la nchi 20 zenye uchumi mkubwa zaidi duniani, G20 wanaokutana huko Rio De Janeiro, Brazil kuwaagiza mawaziri na washawishi wao huko COP29 wahakikishe wanakubaliana juu ya lengo jipya na kubwa la mwaka huu la ufadhili kwa tabianchi nchi. Guterres amesema sambamba na hilo ni vema kukabiliana na taarifa potofu kuhusu tabianchi.Huko Kusini mwa Lebanon, walinda amani wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kikosi cha Mpito nchini humo, UNIFIL, wameshuhudia uharibifu mkubwa wa kutisha kwenye vijiji vilivyoko sambamba na eneo      la kati ya Israeli na Lebanon lisilopaswa kuwa na mapigano, huku hali ya watoto nchini humo ikizidi kuwa mbaya.Hii leo ni siku ya choo duniani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema licha ya choo kuwa ni msingi wa kusongesha afya ya binadamu na kusaidia watoto wa kike na wanawake kuishi maisha ya utu, bado wakazi wengi wa dunia hususan kwenye mizozo na majanga wanaishi bila huduma hiyo ya msingi.Mashinani tunasalia huko huko Baku, kwenye COP29 ambapo nampisha msichana mwanaharakati wa mazingira kutoka Tanzania, akieleza ni nini anafanya na nini atakachoondoka nacho kwenye mkutano huo.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 19 Novemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 19, 2024 18:42


Ripoti kuhusu mshikamano wakijamii imepata, kuna mitazamo michache chanya, kwa dini kote jimboni katika makundi yote makubwa ya imani.

Alfajiri - Voice of America
Chama cha Rais mpya wa Senegal Bassirou Diomaye Faye chaelekea kupata wingi wa viti vya wabunge baada ya uchaguzi wa Jumapili. - Novemba 19, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 19, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
18 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2024 10:46


Hii leo jaridani tunaangazia wakimbizi wa ndani nchini Haiti, na mafunzo ya stadi za kujikimu kimaishwa kwa vijana Tambura Sudan Kusini. Makala inatupeleka nchini Uganda na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Zaidi ya watu 20,000 wamekimbia makazi yao katika mji mkuu wa Haiti Port-au-Prince katika muda wa siku nne tu, ikiwa ni pamoja na watu wengine zaidi ya 17,000 wanaohifadhiwa katika makazi 15 ya wakimbizi wa ndani, kutokana na kuongezeka kwa ghasia za magenge ya uhalifu ambazo ziumevuruga kabisa minyororo muhimu ya usambazaji wa misaada na kulitenga jiji la Port-au-Prince limesema shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM.Vijana katika mji wa Tambura ulioko jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini wanageuza mafunzo ya ufundi stadi kuwa nguvu ya amani na ustawi, mafunzo ambayo yalifanikishwa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, UNMISS.Katika makala Selina Jerobon kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi anakupeleka Uganda kuona harakati za wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kujikwamua kiuchumi baada ya machungu waliyopitia nyumbani kwao.Mashinani tutaelekea nchini Kenya kusikia ni kwa jinsi gani jamii katika maeneo kame wanakabiliana na mabadiliko ya tabianchi.Mwenyeji wako ni Bosco Cosma, karibu! 

Habari za UN
IOM: Zaidi ya watu 20,000 wamefuriushwa ndani ya siku 4 Haiti kutokana na machafuko ya magenge ya uhalifu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 18, 2024 2:06


Zaidi ya watu 20,000 wamekimbia makazi yao katika mji mkuu wa Haiti Port-au-Prince katika muda wa siku nne tu, ikiwa ni pamoja na watu wengine zaidi ya 17,000 wanaohifadhiwa katika makazi 15 ya wakimbizi wa ndani, kutokana na kuongezeka kwa ghasia za magenge ya uhalifu ambazo ziumevuruga kabisa minyororo muhimu ya usambazaji wa misaada na kulitenga jiji la Port-au-Prince (POTOPRINSI) limesema shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM. Kupitia taarifa iliyotolewa leo na IOM nmini Port-au-Prince asilimia kubwa ya watu hawa waliofurushwa makwao wametawanywa zaidi ya mara moja wakilazimika kukimbia na kuacha kila kitu walichokuwa nacho na shirikika hilo linasema kiwango hiki cha watu kutawanywa hakijashuhudiwa Haiti tangu Agost 2023.Shirika hilo linasema kufungwa kwa usafiri wa anga kufuatia shambulizi lililolenga ndege tatu za kibiashara mjini Port-au-Prince, kuzuia ufikiaji wa bandari kuu ya nchi hiyo, na barabara zisizo salama zinazodhibitiwa na makundi yenye silaha kumeliacha eneo la Katikati ya mji mkuu taabani na kutengwa bila msaada na hivyo kuzidisha mateso kwa watu ambao tayari wako hatarini.Mkuu wa IOM nchini Haiti Grégoire Goodstein ameonya kwamba "Kutengwa kwa Port-au-Prince kunaongeza janga la ibinadamu. Uwezo wetu wa kutoa misaada umewekwa njiapanda na bila msaada wa haraka wa kimataifa, mateso yataongezeka sana kwa raia wa Haiti huku kukiwa na asilimia 20 pekee ya mji wa Port-au-Prince inayofikika, wakati wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu wanakabiliwa na changamoto kubwa katika kufikia watu walioathirika.”Kulingana na Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR, vikundi vya uhalifu katika mji mkuu wa Hati vinaendelea kupanuka wigo vikichukua udhibiti wa vitongoji vya ziada na kutenganisha zaidi jamii.Hadi sasa ofisi hiyo inasema ghasia zinazohusiana na magenge zimesababisha karibu vifo 4,000 mwaka 2024, unyanyasaji wa kijinsia, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kingono unaotumiwa kama silaha ya ugaidi, umefikia viwango vya kutisha.Pia imesema wanawake na watoto wameathiriwa kupita kiasi, huku asilimia 94 ya wanawake na wasichana waliokimbia makazi yao wakiwa katika hatari kubwa ya kudhulumiwa kingono.Licha ya changamoto hizi, IOM na washirika wake wameahidi kuendelea kutoa msaada wa kuokoa maisha.IOM pia inatoa wito wa kuongeza haraka ufadhili kwa shughuli za kibinadamu Haiti kwani hadi kufikia mwezi huu wa Novemba, ombi la dola milioni 674 la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Haiti limefadhiliwa kwa asilimia 42 pekee, na kuwaacha mamilioni ya watu bila msaada wanaohitaji.

Alfajiri - Voice of America
Waziri Mkuu wa India Narendra Modi afanya ziara ya kwanza nchini Nigeria. - Novemba 18, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 18, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
15 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 15, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia suala muhimu wa mabadiliko ya tabianchi tukijikita kataika mkutano wa COP29 huko Baku Azerbaijan kuwasikia wanaharakati wa mazingira kutoka nchi mbalimbali.Mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29 u unaofanyika Baku Azerbaijan, leo umejikita na ongezeko la gesi chafuzi ya methane ambayo kwa kiasi kikubwa inatokana na shughuli za binadamu ikiwemo ufugaji wa ng'ombe, na sasa nini kifanyike ili kuidhibiti.Tunasalia huko huko Baku, Azerbaijan. Wito umetolewa kwa wanawake ambao ni waathirika wakubwa wa janga la mabadiliko ya tabianchi wasipewe kisogo katika harakati za kuhimili na kukabili madhara ya janga hilo.Katika makala Bosco Cosmas anatupeleka Amerika ya Kusini kusikia harakati za mwanamke wa jamii ya asili za kulinda eneo lao.Mashinani leo Fathimath, kijana kutoka Maldives anatoa kauli kwa ajili ya hatua za dharura kupambana na mabadiliko ya tabianchi katika mkutano wa COP29.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 15 Novemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 15, 2024 19:29


Australia ime unga mkono azimio la Umoja wa Mataifa, lakutambua mamlaka yakudumu ya watu wa Palestina kwa mara ya kwanza katika miongo mbili.

Alfajiri - Voice of America
Raia wa kigeni walio nusurika na mapigano waomba msaada kurejea makwao - Novemba 15, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 15, 2024 29:57


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
14 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 14, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Baku kwa mkutan wa COP29, amabyo washiriki wanasaka mbinu za kujumuisha makundi yote katika harakati za kukabili na kuhimili madhara ya mabadiliko ya tabianchi yanayochochewa na ongezeko la hewa chafuzi. Idhaa ya Kiswahili imezungumza na Naomi mmjoja wao kutoka Tanzania. Pata pia muhtasari wa habari na ujifunze Kiswahili.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu ugonjwa wa kisukari, shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO leo limesema idadi ya watu wazima wanaoishi na Kkisukari duniani ni zaidi ya milioni 8000 ikiwa ni ongezeko la zaidi ya mara 4 tangu mwaka 1990.Baku Azerbaijan ambako mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP29 leo umejikita na na lengo la kutozalisha kabisa hewa ya ukaa ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antinio Guterres ameainisha jukumu muhimu ambalo miji, mikoa, biashara na taasisi za kifedha lazima zitekeleze katika kuendesha juhudi za dunia nzima kufikia lengo la kutozalisha kabisa hewa ya ukaa katikati ya karne hii.Nchini Sudan shirika la Umojja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharida OCHA limesema ghasia za kutumia silaha na mashambulizi katika Jimbo la Aj Jazirah zinadhihirisha ukatili wa karibu miezi 19 ya vita nchini Sudan,huku kukiwa na ripoti za ubakaji, mauaji ya halaiki na uporaji mkubwa. Katika chini ya wiki mbili, OCHA inasema uhasama huko Aj Jazirah umefurusha zaidi ya watu 135,000 kutoka makwao, wengi wao walikimbilia majimbo jirani ya Gedaref na Kassala.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno “MADHALI, WAMA, FALAU NA HOBE”Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

Habari za UN
13 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 13, 2024 10:00


Hii leo jaridani tunaangazi ufadhili kwa wakulima huku mkutano wa COP29 ukiendelea Baku, na madhara ya mafuriko kwa wakulima nchini Sudana Kusini tukimulika jinsi Umoja wa Mataifa wanavyohaha kuwasaidia. Makala inatupeleka nchini DRC na mashinani tunasalia huko huko Sudan Kusini, kulikoni?Kuongeza kiwango cha fedha kwenye ufadhili wa miradi ya kukabili na kuhimili tabianchi nchi ikiwa ni moja ya masuala muhimu yanayojadiliwa katika mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP29 huko Baku, Azerbaijan, leo ikiwa ni siku ya pili ya mkutano huo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema bila kupunguza kwa kiasi kikubwa hewa chafuzi, na kuimarisha miradi ya kuhimili na kukabili mabadiliko ya tabianchi, kila uchumi duniani utakumbwa na madhara makubwa.Huko Maban, jimboni Upper Nile, kaskazini mashariki mwa Sudan Kusini, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR linajenga vifaa vya kuhifadhi maji pamoja na makinga maji ili kuepusha mashamba dhidi ya mafuriko ya msimu yanayokumba eneo hilo mara kwa mara, eneo ambalo ardhi yake ina rutuba kwa ajili ya kilimo cha mazao ya chakula na biashara.Katika Makala George Musubao, mwandishi wetu huko Jimboni Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akimulika mkutano ulioandaliwa na watendaji wa Umoja wa Mataifa ya eneo hilo kuangalia jinsi ya kukabiliana na  habari potofu na za uongo.Na mashinani tutakuwa Sudan Kusini, ambako shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP linasaidia jamii zilizoathiriwa na mafuriko kupata suluhisho la kudumu.Mwenyeji wako ni Bosco Cosmas, karibu! 

Habari za UN
12 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 12, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Havana Cuba amabpo Flora Nducha amaezungumza na mshiriki kutoka maitaifa mbalimbali na leo ni Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani inayotupeleka Zimbabwe.Kuongeza kiwango cha fedha kwenye ufadhili wa miradi ya kukabili na kuhimili tabianchi nchi ikiwa ni moja ya masuala muhimu yanayojadiliwa katika mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP29 huko Baku, Azerbaijan, leo ikiwa ni siku ya pili ya mkutano huo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema bila kupunguza kwa kiasi kikubwa hewa chafuzi, na kuimarisha miradi ya kuhimili na kukabili mabadiliko ya tabianchi, kila uchumi duniani utakumbwa na madhara makubwa.Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR iliyotolewa leo huko COP29 inaonesha ni kwa jinsi gani watu wanaokimbia vita, ghasia na mateso wanazidi kujikuta kwenye mazingira yaliyokumbwa na janga la tabianchi, janga ambalo linawaweka kwenye mchanganyiko wa vitisho, lakini bila fedha wala msaada wa kukabiliana navyo.Na mamia ya wakimbizi wanaotaka kujiunga na elimu ya juu sasa watafanya bure mitihani ya kuonesha umahiri wao wa lugha ya kiingereza, au IELTS. Hii inafuatia makubaliano ya ushirikiano kati ya UNHCR na mfumo wa kimataifa wa lugha ya kiingereza, IELTS.Na mashinani COP29 ukiendelea huko Baku Azerbaijan, tunabisha hodi  nchini Zimbabwe ambako Umoja wa Mataifa unawasaidia wakulima kakabiliana na mabadiliko ya tabianchi.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 12 Novemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 12, 2024 16:19


Waziri Mkuu Anthony Albanese ametoa pongezi kwa mkongwe wa vita vya Vietnam Richard Norden, ambaye amepewa tuzo baada ya kufa ya ngazi ya juu zaidi ya jeshi la Australia ya Victoria Cross.

Habari za UN
Stiell: Lazima tuweke malengo ya juu ya ufadhili ili kukabili mabadiliko ya tabianchi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 11, 2024 2:16


Kufuatia mwaka mwingine wa viwango vya juu vya joto kali na matukio ya kupitiliza ya hali ya hewa, Mkuu wa Sekretarieti ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Tabianchi Simon Stiell amewaeleza washiriki wa mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29 , kwamba malengo mapya ya ufadhili kwa tabianchi ni muhimu kwa ajili ya ustawi wa mataifa, yakiwemo yale tajiri na yenye uthabiti. Katika hotuba yake mbele ya washiriki wa mkutano huo ulioanza leo huko Baku, mji mkuu wa Azerbaijan hadi tarehe 22 mwezi huu wa Novemba, Bwana Stiell amesema kwa kadri madhara ya mabadiliko ya tabianchi yalivyo dhahiri ni lazima kukubaliana mwelekeo mpya wa ufadhili kwa miradi ya kukabili na kuhimili.Amehoji, mnataka bei za vyakula na nishati iongezeke zaidi? Je mnataka nchi zenu ziendele kushindwa kushindana kiuchumi? Je mnataka dunia yetu iendelee kukosa utulivu na kugharimu maisha adhimu?Amekumbusha kuwa janga la tabianchi linaathiri kila mkazi wa dunia kwa njia moja au nyingine.Bwana Stiell amesema nimekanganyikiwa kama mtu mwigine yeyote kwamba mkutano mmoja wa COP hauwezi kuleta marekebisho abayo kila taifa linahitaki. Lakini iwapo majibu yenu kwenye maswali hayo ni HAPANA, basi ni hapa pande zote zinahitaji kukubaliana jinsi ya kuondokana na zahma hii.Hivyo amesema, “katika nyakati ngumu, kukiwa na majukumu mazito, sitegemei matumaini na ndoto. Kinachonihamasisha ni stadi na azma ya binadamu. Uwezo wetu wa kuanguka na kuinuka tena na tena, hadi tunapotimiza malengo yetu.”Amekumbusha kuwa mkataba wa tabianchi ndio mchakato pekee ambapo wanaweza kupatia majawabu janga la tabianchi na kuwajibishana kwa wale wanaokwenda kinyume.Ametaka washirika kuonesha stadi zao kwenye COP29 na pande zote zishinikize makubaliano ya ufadhili kwa tabianchi la sivyo kila nchi itagharimika.

Habari za UN
11 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 11, 2024 9:59


Hii leo jaridani tunaangaziamkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29, na mradi wa lishe bora kwa watotot Afar nchini Ethiopia. Makala inatupeleka Havana Cuba na mashinani tunasalia huko huko Havana Cuba, kulikoni?Kufuatia mwaka mwingine wa viwango vya juu vya joto kali na matukio ya kupitiliza ya hali ya hewa, Mkuu wa Sekretarieti ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Tabianchi Simon Stiell amewaeleza washiriki wa mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi, COP29, kwamba malengo mapya ya ufadhili kwa tabianchi ni muhimu kwa ajili ya ustawi wa mataifa, yakiwemo yale tajiri na yenye uthabiti.Mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF wa kuchagiza kaya kulima bustani za mboga za majani pamoja na ufugaji wa kuku huko jimbo la Afar, kaskazini mashariki mwa Ethiopia umesaidia familia za vijijini kukabiliana na utapiamlo miongoni mwa watoto.Makala inatupeleka Havana Cuba ambako kongamano la kimataifa ka Kiswahilii limekunja jamvi mwishoni mwa wiki na shuhuda wetu huo Flora Nducha amezungumza na watu mbalimbali akiwemo mchechemuzi wa Kiswahili hususan kwenye mitandaao ya kijamii Nick Reynold ali maarufu Bongo Zozo, ambaye ni raia wa Uingereza.Na mashinani fursa ni yake Profesa msaidizi Xiaoxi Zhang raia wa China ambaye ni mshirika wa kimataifa au (Global Fellow) na mhadhiri wa masuala ya fasihi linganishi katika chuo kikuu cha Habib kilichopo Sindhi Karachi nchini Pakistan mmoja wa waliohudhuria kongamano la Kiswahili lililomalizika mwishoni mwa wiki akitoa ujumbe kuhusu changamoto ya kujifunza  Kiswhili.Mwenyeji wako ni Bosco Cosmas, karibu! 

Habari za UN
08 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 8, 2024 9:57


Hii leo jaridani tunakuletea kipindi maalum kinachotupeleka jijini Havana Cubaambapo kongamano la kimataifa la Kiswahili limeng'oa nanga likiwaleta pamoja takribani washiriki 400 kutoka Afrika, Asia, Amerika na Ulaya ili kujadili ajenda mbalimbali za kupanua wigo wa luugha hiyo na kuitumia kuleta tija ikiwemo kusongesha malengo ya Umoja wa Mataifa kama amani na maendeleo endelevu.Miongoni mwa habari kubwa Umoja wa Mataifa hii leo ni uwajibikaji unasakwa kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu dhidi ya  wapalestina na waisraeli, na pia shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO limeweka bayana gharama za kiuchumi na hata kiafya zilizofichika zitokanazo na mifumo ya uzalishaji, usafirishaji na ulaji wa chakula. Lakini kubwa zaidi nakupeleka Havana, Cuba kupata kwa mahtasari mazungumzo ya Flora Nducha na mmoja wa washiriki.Mashinani tunasalia huko huko Havana Cuba na fursa ni yake Profesa Juan (Huani) Jacomino (Hakumino) raia wa Cuba ambaye ni Mwalimu wa Kiswahii katia  chuo kikuu cha Havana Cuba anayeshiriki Kongamano la Kiswahili lililofunguliwa leo akitoa wito kwa raia wa Cuba na wa nchi zingine kuhusu umuhimu wa kukumbatia  Kiswahili. Mwenyeji wako ni Bosco Cosmas, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 8 Novemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 8, 2024 19:50


Waziri Mkuu Anthony Albanese ame sisitiza umuhimu wakutetea demokrasia katika hotuba yake, kwenye kongamano la wabunge wa jumuiya yamadola.

Habari za UN
07 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 7, 2024 11:21


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka huko Havana Cuba kwenye Kongamano la kimataifa la Kiswahili kusikia kutoka kwa waziziri Zanzibar kuhusu faida za kiplomasia na kiuchumi. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ujumbe kuhusu Kiswahili.Fedha kwa ajili ya mipango ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, ni jambo lililopatiwa kipaumbele katika ripoti mpya ya leo ya shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira, UNEP wakati huu ambapo kiwango cha joto kinazidi kuongezeka kila uchao na kuleta zahma duniani kote.Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO linasema hii leo watoto 6 wa kipalestina, wamesafirishwa kutoka Gaza kwenye Romania kwa matibabu mahsusi ; watatu wakiwa wanaugua saratani, wawili magonjwa ya  damu na mmoja majeraha. Wameambatana na jumla ya waangalizi 15.Na huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO umezindua mfumo wa uthibitishaji, kama sehemu ya mchakato wa Luanda wenye lengo la kufuatilia makubaliano ya sitisho la mapigano kati ya Rwanda na DRC yaliyoanza kutekelezwa tarehe 4 mwezi Agosti mwaka huu mashariki mwa taifa hilo la Maziwa Makuu.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili tunasalia huko huko Havana Cuba, kwenye kongamano la Kiswahili la Kimataifa ambako Dkt. Kisembo Ronex Tendo mshiriki kutoka taasisi ya vijana ya Afrika Mashriki Fest Uganda anaeleza cha kufanya kusongesha Kiswahili nchini Uganda.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Habari za UN
06 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 6, 2024 10:22


Hii leo jaridani tunaangazia uchaguzi mkuu nchini Marekani, na watoto wanaotumikishwa jeshini na waasi nchini DRC. Makala tunakupeleka Havana nchini Cuba, na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Kufuatia Donald J. Trump kutangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa Rais wa Marekani uliofanyika Jumanne Novemba 5, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa salamu za pongezi.Harakati za ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC za kunasua watoto na vijana wanaotumikishwa vitani zinaendelea na tukio la hivi karibuni zaidi ni la kijana..Makala leo inatupeleka Havana Cuba ikiwa imesalia siku moja tu kabla ya kuanza kwa kongamano la kimataifa la Kiswahili lililobeba maudhui “Kiswahii  na teknolojia, na Kiswahili kama nyenzo ya kudumisha  amani na maendeleo”.Mashinani tutaelekea nchini Kenya kwa mwanamke mwandishi wa habari akitueleza jinsi wanavyochochea haki za binadamu.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Habari za UN
05 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 5, 2024 11:39


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoangazia uvuvi katika mji wa Kalokol karibu na fuo za Ziwa Turkana Kaskazini mwa Kenya. Pia tunakuletea muhtasari wa habari zikiwemo za mkutano wa WUF12 Cairo Misri, chanjo ya malaria Sudan, siku ya Tsunami, na mashinani.Mkutano wa 12 wa Jukwaa la Miji Duniani, WUF12 umeingia siku ya pili hii leo huko Cairo, Misri, ambako Ming Zing ambaye ni Mkurugenzi wa Miji, Mnepo na Ardhi kutoka Benki ya Dunia amezungumzia umuhimu wa kujumuisha wanawake na vijana katika mipango miji.Sudan imekuwa nchi ya 16 barani Afrika na ya kwanza katika Ukanda wa WHO wa Mashariki na Mediterania kuanzisha chanjo dhidi ya Malaria kwa watoto wasiozidi umri wa miezi 12. Chanjo imeanza kutolewa jana katika majimbo ya Gedaref na Blue Nile ambapo WHO na wadau wamesema mwaka 2025 na 2026 chanjo itapelekwa katika maeneo 129 nchini kote Sudan.Na leo ni siku ya kimataifa ya kuhamasisha umma kuhusu tsunami, ambayo ni mawimbi makubwa ya maji yatokanayo na tetemeko chini ya bahari. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake anasema pamoja na kukumbuka waliopoteza maisha kwa tsunami miaka 20 iliyopita,  tunaahidi tena kulinda zaidi ya watu milioni 700 duniani kote walio hatarini kukumbwa na Tsunami.Mashinani tutaelekea Sudan kusini kuangazia  harakati za Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini humo, UNMISS za kuimarisha ulinzi wa wanawake katika migogoro na majanga.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 5 Novemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 5, 2024 19:35


Wanaharakati wa Mataifa ya Kwanza wana muhamasisha Kiongozi wa Queensland David Crisafulli, abatilishe uamuzi wake wakufuta uchunguzi wakusema ukweli na uponyaji.

Habari za UN
04 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 4, 2024 9:49


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko nchini Sudan unaosababisha janga la njaa, na mradi wa maji Galmudug Somalia kwa ajili ya maji safi na salama pamoja na mifugo. Makala tunakupeleka nchini DR Congo na mashinani nchini Kenya, kulikoni?Nchini Sudan ambako vita na janga la njaa vinaendelea kuwa mwiba kwa raia      sasa wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wanaonya juu ya tishio lingine kubwa  la milipuko ya magonja ya kipindupindu na homa ya kidingapopo huku mfumo mzima wa afya ukiwa taabani.Nchini Somalia, ni asilimia 52 tu wananchi ndio wanapata huduma ya maji safi na salama. Wengine hulazimika kutembea umbali mrefu kuteka maji ambayo si ya uhakika. Hata hivyo kwa msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini humo pamoja na wadau, hali sasa inaanza kuimarika.Makala inakupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako Kapteni Fadhillah Nayopa, Afisa habari wa kikosi cha 11 cha walinda amani wa Tanzania, TANZBATT-11 katika ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO anazungumzia usaidizi waliopatia watoto yatima.Mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula, tunakutana na Geoffrey Nawet, Mwanafunzi katika shule ya Kakuma nchini Kenya akitueleza jinsi ambavyo programu ya Mlo shuleni ya lishe bora umewawezesha wanafunzi kumakinika shuleni na kupata motisha ya kuendelea na masomo.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya habari 4 Novemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 4, 2024 7:55


Chama cha Greens kina omba serikali ya shirikisho ilete mipango yake mbele yaku kata deni la wanafunzi kwa asilimia 20 kwa idadi yawa Australia milioni tatu, hatua ambayo itafuta zaidi ya deni ya wanafunzi yenye thamani ya dola bilioni 16.

Habari za UN
01 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 1, 2024 9:58


Hii leo jaridani tunaangazia machafuko katika ukanda wa Gaza na masuala ya afya nchini Kenya. Makala inatupeleka nchini DRC kumsikia mkimbizi mjasiriamali na mnufaika wa pesa taslimu kutoka WFP, na mashinani tunakupeleka nchini Lebanonon kwa waathirika wa vita.Kadri siku zinavyozidi kusonga mbele, hali ya usalama na kibinadamu huko Ukanda wa Gaza inazidi kuzorota huku raia na hata wafanyakazi wa kutoa misaada wakisalia wamepigwa butwaa kwani mashambulizi kutoka Israeli yanaendelea kila uchao.Serikali ya Kaunti ya Lamu katika pwani ya kaskazini ya Kenya, kwa ushirikiano na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), wanaendesha shughuli ya kuwafikia wanajamii ili kubadilishana taarifa kuhusu jinsi watu wanaweza kuwalinda watoto na familia zao dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu na kutoa huduma za maji, vifaa vya kujisafi na usafi kwa jamii zilizoathirika. Kutoka katika video iliyoandaliwa na UNICEF.Makala George Musubao, mwandishi wetu wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC anazungumza na mkimbizi Esther Josephine aliyeko kambi ya Bulengo nje kidogo ya mji wa Goma, jimboni Kivu Kaskazini ambaye amenufaika na msaada kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP.Mashinani tutakuwa Lebanon, kumsikia mama aliyenusurika kifo na wanawe kutokana na makombora ya Israel.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu! 

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 1 Novemba 2024

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 1, 2024 17:15


Serikali imethibitisha kuwa inashikilia mafao ya Medicare ambayo hayaja daiwa yenye thamani yama milioni ya dola, kwa sababu wagonjwa hawajatoa taarifa zao za benki ili wapokee hela hizo.

O'Connor & Company
KT McFarland, Ben Stiller for Kamala, John Ondrasik, AOC on Walz the ‘Uniter'

O'Connor & Company

Play Episode Listen Later Aug 8, 2024 28:53


In the 8 AM Hour: Larry O'Connor and Patrice Onwuka discussed: WMAL GUEST: 8:05 AM -  INTERVIEW - KT MCFARLAND - Former Deputy National Security Advisor to President Trump and author of “REVOLUTION" SOCIAL MEDIA: https://twitter.com/realKTMcFarland Walz's long history with China draws attacks and praise Taylor Swift concerts canceled after ISIS plot narrowly foiled by police BEN STILLER says he "wishes he was black" while urging people to vote for Kamala Harris during a "Comics For Kamala" fundraising call."It's gonna be the first woman president and that's incredibly exciting. And you know, she's Indian, she's black, she's everything." "You know, I'm Jewish and Irish. I wish I was black. Every white Jewish guy wishes he was black." Kamala Harris developed a new accent again when she landed in Detroit: “The courts are gonna handle dat. We gon' beat him in Novemba. We gon' beat him in Novemba” Kamala Harris SNAPS on Pro-Palestine protesters accusing her of supporting Genocide in Gaza: “You know what, if you want Donald Trump to win then say that. Otherwise, I'm speaking” WMAL GUEST: 8:35 AM - INTERVIEW - JOHN ONDRASIK - lead singer of Five for Fighting HIS UPCOMING SHOW: Tuesday, August 13 @ Lincoln Theatre in Washington, DC WEBSITE: https://fiveforfighting.com/ SOCIAL MEDIA: https://x.com/johnondrasik AOC calls Kamala Harris running mate ‘a uniter' with ‘many assets' Where to find more about WMAL's morning show:  Follow the Show Podcasts on Apple podcasts, Audible and Spotify. Follow WMAL's "O'Connor and Company" on X: @WMALDC, @LarryOConnor,  @Jgunlock, @patricepinkfile, and @heatherhunterdc.  Facebook: WMALDC and Larry O'Connor Instagram: WMALDC Show Website: https://www.wmal.com/oconnor-company/ How to listen live weekdays from 5 to 9 AM: https://www.wmal.com/listenlive/ Episode: Thursday, August 8, 2024 / 8 AM Hour  O'Connor and Company is proudly presented by Veritas Academy See omnystudio.com/listener for privacy information.