Ni Makala yanayoangazia kwa jicho la tatu mazingira halisi ya dunia yalivyo bila kusahau kile ambacho kinachangia kuyaharibu. Utapata kufahamu namna ambavyo mazingira na rasilimali zinavyoharibiwa huku pia teknolojia ikijumuishwa. Hakika mazingira mazuri ya leo ni dunia yako kesho.
Rfi - Sabina Chrispine Nabigambo
Ripoti ya umoja wa mataifa inaonesha dunia ipo nyuma sana katika kudhibiti ongezeko la joto chini ya nyuzi joto 1.5.
Baadhi ya wakulima nchini Kenya wameanza kugeukia matumizi ya mbolea asilia inayonyunyiziwa ardhini ili kunusuru mashamba yao.
Kutokana na mabadiliko ya tabianchi, kwa mujibu wa shirika la hali ya hewa duniani WMO, barafu inayopatikana kwenye milima inayeyuka kwa kasi zaidi na ndio sababu ya umoja wamataifa kutenga Machi 21 kama siku ya kimataifa ya kutoa hamasisho kuhusu kuyeyuka kwa barafu hii.
Wakulima wadogo wanachangia kwa zaidi ya asilimia 70 uzalishaji wa chakula barani Afrika, hii ni kwa mujibu wa Benki ya Maendeleo barani, Afdb, wakati uo huo, lengo nambari mbili ya maendeleo endelevu ikinuia kumaliza njaa na kuihakikishia dunia usalama wa chakula kufikia mwaka wa 2030
Binadamu hutegemea rasilimali za wanyamapori na bayoanuwai ili kukidhi mahitaji yao. Tunahitaji chakula, mafuta, makazi, na hata mavazi. Hivyo ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha kwamba mifumo ikolojia inaweza kustawi na mimea na wanyama wanaweza kuwepo kwa ajili ya vizazi vijavyo. Machi 3 mwaka huu, ilikuwa ni fursa ya kutoa uhamasisho wa umuhimu wa wanyama na mimea pori, ili kuongeza ufahamu wa faida zao, na haja ya kuongeza mapambano ya uhalifu dhidi ya wanyamapori na kusababisha athari kubwa za kiuchumi, mazingira na kijamii.Skiliza ufahamu mengi zaidi.
Taka za kieletroniki zinajumuisha vitu vingi ambavyo ni hatari kwa afya ya binadamu na mazingira na utupaji ovyo ni chanzo kikuu cha madhara, dutu hizi hatari zikiwa na uwezo wa kuchafua udongo, maji, hewa na vyanzo vya chakula. Shirika la E-Waste Initiative Kenya linatoa suluhu ya taka za kieletroniki. Bonyeza hapa kufahamu zaidi.
Mkaa wa Briketi hutengenezwa kutoka kwa vumbi la mkaa wa kawaida, taka za kilimo au mabaki ya mbao, na hutumiwa kimsingi kwa mapishi nyumbani, shuleni na hata katika makampuni. Mkaa huu una faida kwa kuwa unapunguza uchafuzi wa mazingira, kupunguza ukataji wa miti lakini pia huwaka kwa muda mrefu na kwa usawa zaidi kuliko mkaa wa kawaida, na kuufanya kuwa chaguo maarufu kwa kupikia.
Makala haya yanazungumzia jinsi Wakulima wengi nchini Kenya wanakumbatia mbinu mpya za kudhibiti wadudu waharibifu wa mimea kwa kutumia madawa ya kiasili badala ya kemikali za viwandani. Kutokana na madhara yanayotokana na matumizi ya dawa za kemikali,wakulima hawa sasa wanageukia madawa hayo asilia kuimarisha mazao na mazingira , Mimea kama vile ,pareto,kitunguu saumu,pilipili na hata mtunguja pori yaani sodom apple sasa inatumika kutengeneza madawa hayo.
Utunzaji wa bustani ya nyumbani, ni mbinu mpya ya kilimo inayolenga kutimiza malengo matatu kwa wakati mmoja: kuongeza mapato ya kilimo, kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa na kuimarisha ustahimilivu, halkadhalika kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi. Bustani ya Nyumbani, kwa kawaida huwa karibu na jikoni au pia kwenye roshani. Bustani hii ambayo mara nyingi hutumia mbolea asilia husaidia kupambana na mabadiliko ya tabianchi kwa kupunguza uzalishaji wa gesi chafu na pia kutunza udongo.Bustani hii hutumika kwa kilimo cha mboga, viungo vya upishi kama vitunguu, matunda, au mimea ya kitiba kwa matumizi.
Rais Donald Trump kwa mara nyingine alitangaza Marekani kujiondoa kwenye Mkataba wa Paris kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, hatua ambayo imeibua mjadala wa kimataifa. Tangazo hilo lilikuja huku ulimwengu ukishuhudia viwango vya joto vinavyovunja rekodi na majanga yanayozidi kuwa makali yanayohusiana na hali ya hewa.Lakini wadadisi wa mambo na viongozi wengine wa ulimwengu wanatazamaje hatua yake Trump? Bonyeza usikilize zaidi.
Sekta ya mitumba inauwezo wa kuchangia mabilioni ya fedha katika mapato ya taifa, pamoja na kutoa maelfu ya ajira katika mataifa ya bara Afrika na ulaya. Kulinga na utafiti wa Oxford Econimics mwaka uliopita; 2024, sekta ya mitumba pekee ina dhamani ya dola bilioni 8 na imetoa ajiri ya idadi ya zaidi laki moja na elfu 60 kwa vijana nchini Msumbiji, Ghana na Kenya.Lakini hata hivyo wanaharakati wa mazingira wanasema baadhi ya nguo hizo za mitumba zinazoletwa Afrika zinachangia katika uchafuzi wa mazingira.Hili kufahamu Zaidi mwandishi wetu George Ajowi alizuru soko la Gikomba na kutuandalia makala yafuatayo .
Matumizi ya kuni yanaweza kuwa na athari chanya na hasi kwa mazingira, kulingana na jinsi zinavyovunwa, kutumiwa na kusimamiwa. Leo mwandishi Christopher Karenzi kutoka Kigali, Rwanda ameangazia hatua ya kuondokana na matumizi yake lakini changamoto pia raia wanazokumbana nazo.
Mashirika kadhaa ya kilimo pamoja na serikali ya Kenya yaliwakutanisha wadau wa kilimo—wakulima, wataalamu wa mabadiliko ya tabianchi, na watunga sera—jijini Nairobi mwezi Novemba mwaka uliopita. Mkutano huo ukilenga kuweka bayana mwelekeo wa kutumia kilimo kinachokabili mabadiliko ya tabianchi yaani climate smart agriculture ili kuongeza uzalishaji wa chakula.Hii leo katika makala mazingira leo dunia yako Kesho ,tunaangania kilimo hicho
Tunaangazia ikiwa tunaweza kuwa na mazingira tulivu bila kelele chafuzi katika maeneo tunayoishi lakini pia sehemu tunazofanya kazi. Tunaangazia ikiwa tunaweza kuwa na mazingira tulivu bila kelele chafuzi katika maeneo tunayoishi lakini pia sehemu tunazofanya kazi.
Makala haya yanazungumzia jinsi dampo la Taka la Nkumba nchini Uganda limekuwa tishio la kimazingira kwa ziwa victoria ambalo ndilo chanzo kuu cha mto Nile.Baada ya dampo la Kiteezi jijini Uganda kuporomoka Agosti 9 mwaka wa 2024 na kuwauwa watu kadhaa,serikali nchini humo ilitoa amri taka zote kutoka Kampala ielekezwe Nkumba karibu na ziwa ,hatua hiyo ikiongeza uchafuzi zaidi wa mazingira .
Katika miji ya pwani ya Kenya, vita dhidi ya uraibu vimepata mwelekeo mpya wa kusisimua. Kupitia miradi ya kimazingira, vijana kutoka vituo vya kuwarekebisha tabia hawajizuia tu na mihadarati, bali wanabadili jamii zao pia kupitia miradi hiyo. Mwanahabari wetu Victor Moturi alitembelea Mtopanga, Kaunti ya Mombasa, ambako vijana wamepata matumaini kutokana na utunzaji wa mazingira huku wakipata riziki.
Mkutano wa kukabiliana na uchafuzi wa plastiki ulikamilika mwanzoni mwa Disemba 2024 bila mwafaka kufikiwa, wataalam wa mazingira wakisema pendekezo la kuchakata plastiki wakati nchi nyingine zikiendelea kuzalisha sio suluhu la tatizo hilo. Kwenye makala hii leo tunaangazia athari za plastiki kwa afya na mazingira, suluhu zinazopendekezwa lakini pia kupata ufafanuzi zaidi kilichokwamisha kupatikana kwa mkataba wa kumaliza tatizo linalosababishwa na uchafuzi wa plastiki.
Mkutano wa hali ya hewa COP29 ukiendelea nchini Azerbaijan, masuala yanayoibua changamoto ni ufadhili, mchakato wa kuondokana na mafuta kisukuku, athari ambazo zimekumba bara la Afrika kutokana na mabadiliko ya tabia nchi, kuongezeka kwa viwango vya joto lakini pia suluhu zinazopendekezwa na wataalam wa mazingira. Kauli mbiu ya mwaka huu kwenye mkutano wa COP29 ni uwajibikaji wa ufadhili haswa kutoka mataifa tajiri ambao wanachangia kwa viwango vikubwa uchafuzi wa mazingira wakati athari zake zinaathiri nchi zisizojiweza na shirika la mazingira la Greenpeace Africa linapendekeza mustakabali wa nishati mbadala na haki ya hali ya hewa kwa Afrika.Kwa mengi zaidi bonyeza ili kusikiliza makala.
Katika dunia ya sasa ambapo ukuaji wa teknolojia ni wa kasi ya juu, wabunifu katika jamii za pwani nchini Kenya, wamekumbatia matumizi ya teknolojia katika kupiga jeki juhudi za kupunguza taka kwenye mazingira wanayoishi.
Wanasayansi na wahifadhi wameibua hofu ya kutokomea kabisa kwa tembo aina ya "Super Tusker" ambaye pembe yake moja ina kilo takriban 45, ikiwa hatua hazitachukuliwa ili kuzuia uwindaji wao.Katika mbuga ya Amboseli inayopakana na Kenya na Tanzania, ndovu hawa wamebaki kumi pekee.
Katika maadhimisho ya wiki ya maji duniani 2024, makala haya yameangazia mradi wa WASH unaofanywa na shirika la SHOFCO mtaani Kibera, kusambaza maji safi ya matumizi kwa wakaazi wa kitongoji hicho chenye changamoto za upatikanaji wa maji safi.
Kundi la vijana la Vision Bearers la mtaani Mathare, jijini Nairobi linavyotumia taka za chupa za plastiki kuendeleza kilimo bila mchanga(Hydroponic farming)
Kwa miaka mingi taka inayotoka kwa samaki na viumbe vingine kwenye ziwa, imekuwa ikichafua mazingira na kusababisha samaki wengi kukosa hewa ya oxigeni hivyo kufariki na kusababisha hasara kubwa.Hata hivyo wenyeji sasa wengi wao vijana wameanza kutumia taka hizo kutengeza bayogesi na bidhaa zingine kama vile viatu,nguo,begi mifuko na kadhalika hivyo kubuni ajira na kuinua uchumi. Katika fuo za Dunga kando na ziwa Victoria kaunti ya kisumu nchini Kenya,wafanyabiashara hapa wanatumia bayogesi kukaanga samaki na kuwauzia wateja wanaotalii êneo hili.Bayogesi hii inayotengenezwa kutokana na mabaki ya samaki ,imewafaidi wenyeji wa hapa kupunguza gharama ya matumizi vile vile kutunza mazingira. Caroline Achieng ni mfanyabiashara wa samaki.“Tunadumisha usafi kwa sababu wageni wanakuja hapa lazima tudumishe usafi ndio mazingira yetu yasiharibike,mradi huo umesaidia sana kwa sababu wametusaidia kuchukuwa hizi takataka za samaki kama matumbo,wanatengeneza nayo bayogasi hivyo kupunguza uchafu”alisema Caroline Achieng mfanyabiashara wa samaki.Kwa mujibu wa Achieng, uwepo wa mradi huu umeimarisha biashara yake ukilinganisha wakati alipokuwa akitumia kuni kukaanga samaki.“Changamoto tuko nayo ni kama samaki haiko kwa sababu mazingira yameharibika,tudumishe usafi tutengeneze mazingira ili samaki ipate kuzalishana baharini.”AlisisitizaAchieng.Mita chache kutoka kwenye wafanyabiashara hawa wanaokaanga samaki,Mary Dede ni mwenye furaha,Kwa sasa anatumia kawi inayotokana na bayogesi vile vile kawi mbadala,kukausha samaki aina ya dagaa kwa minajili ya kuwahifadhi kwa mauzo ya baadaye.“Hapo tunaweka Omena kama tunataka kuikausha na inaweza chukuwa hata masaa tatu kukauka.”Alisema Mary Dede.Kwa miaka mingi taka inayotoka kwa samaki na viumbe vingine kwenye ziwa, imekuwa ikichafua mazingira na kusababisha samaki wengi kukosa hewa ya oxigeni hivyo kufariki na kusababisha hasara kubwa.Mradi huu wa kutengeneza gesi kutokana na taka hizi umeimarisha mazingira na biashara ya hapa. Charles Ochieng ni mtaalam wa kutengeneza bayogesi kwenye shirika flexy biogás, shirika ambalo linaendesha mradi huu wa gesi êneo hili.“Huwa tunachukuwa mabaki ya samaki ikifika jioni tunachukuwa tunaichunga maji yake tunamwaga kwa mtungi huu wa bayogesi, hiyo ndio inatengeneza bayogesi,uchafu mwingine tunatengeneza chakula ya kuku na nguruwe.” AlielezaCharles Ochieng ni mtaalam wa kutengeneza bayogesi.Kwa siku kilo 300 za mabaki ya samaki hukusanywa hapa na kisha kuchakatwa kwa kimombo recycle kisha kuzalisha gesi ambayo kwa mujibu wa Ochieng huuzwa kwenye soko hili na mikahawa karibu.“Bayogasi hii ,akina mama wanakuja hapa hapa wanapika githeri,omena na samaki na vyakula vingine ,wanalipa na inalingana na kiwacho cha chakula wanapika,ada ya juu zaidi ni shilingi 100 ,ada ya chini ni shilingi 50,tumsaidia eneo hili kutunza mazingira kwa vile uchafu huu sasa haurudishwi baharini.” AlisemaCharles Ochieng.Takwimu kutoka taasisi ya Utafiti wa Baharini na Uvuvi nchini Kenya zinaonyesha kuwa tani 150,000 za taka za samaki huzalishwa kila mwaka, ambapo asilimia 80 ya taka hizo hutupwa na kuharibu mazingira .Samuel Okoth ni mtaalam wa mazingira jimbo hili la Kisumu.“Ngozi hii na taka zingine zamani zilikuwa zinatupwa baharini na kuchafua mazingira,ndio tukagundua inaweza tengeneza bayogasi na bidhaa zingine kama viatu ,begi na vile vile kuunda uzi za kushona watu wakati wa upasuaji.”Alisimulia Samuel Okoth ni mtaalam wa mazingira jimbo hili la Kisumu.Okoth anasema kuwa Ufumbuzi wa teknojia umesaidia sana kutengeneza bidhaa mbalimbali kutokana na taka hizi, hivyo kuajiri vijana wengi eneo hili.“Bidhaa hizi kama begi hatuuzi hivi hivi tu tunauza katika masoko ya kimataifa kwa sababu dhamani yake ni ya juu mno,kwa sababu huo mchakato wa kuziunda ni ghali mno kama vile kulainisha hiyo ngozi ya samaki na kuifanya kuwa kubwa.”Kilomita 6 kutoka ufuo huu wa dunga ni ,kijiji cha kajulu kaskazini mwa mji wa Kisumu,,namkuta Sarah Adero akitumia ngozi na magamba ya samaki kutengeza bidhaa kama vile nguo,viatu.magamba haya na ngozi ya samaki hukusanywa kutoka vituo mbalimbali jijini Kisumu .“Ngozi hizi tunazitoa maeneo kama vile ubunga,tunazileta hapa na kuzilainisha na kuzitumia kutengeneza bidhaa tofautitofauti,ngozi hii ikiachwa tu hivyo itachafua mazingira hata kule baharini kisha samaki wengine wataweza kufariki.”Mipango kama hii hata hivyo imeonekana kuchangia uchumi endelevu yaani circular economy hasa katika miji mbalimbali nchini Kenya, huku mashirika ya kaboni yakisema kuwa, fumbuzi hizi zitachangia Zaidi ya ajira millioni nane barani Afrika.“Inaleta mapato sana na nawaambia wenzangu,kila kitu ina kazi,kama hii ngozi ya samaki mtu hawezi jua eti inaweza kutengeneza bidhaa mbalimbali,ingetupwa ingechafua mazingira na pia hatungepata mapato.”Uwepo wa hatua kama hizi za kutumia taka kutengeneza bidhaa mbalimbali ni moja wapo ya mataifa kama vile Kenya ,kuafikia malengo ya ruwaza ya maendeleo endelevu ya mwaka wa 2030 ,ambapo mataifa yanafaa kutumia uvumbuzi na teknolojia ili kutatua changamoto za mazingira,hivyo kubuni nafasi za kazi na kuimarisha mazingira.Victor Moturi,Kisumu RFI Kiswahili.
Juma hili katika makala ya mazingira leo dunia yako kesho, mwandishi wetu wa Goma Benjamin kasemabe, ametuandalia ripoti ya namna mjasiriamali Irene maroy anavyogeuza taka za plastiki kuwa matofali maalum maarufu kama Cabro inayotumika kutengeneza barabara.
Kulingana na jumuiya ya IGAD, zaidi ya vifo 190 vimeriotiwa katika eneo la pembe ya Afrika, huku watu wengine laki 7 wakiyahama makazi yao.
Sote tunataka familia zetu ziwe na chakula cha kutosha ili kula kile ambacho ni salama na chenye lishe. Na lengo la 2 la maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa ni ulimwengu usio na njaa ifikapo 2030. Lakini licha ya juhudi zinazowekwa, suala la njaa na uhaba wa chakula limeonyesha ongezeko la kutisha tangu 2015, hali hii ikichochewa na mseto wa mambo ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa na upungufu wa uzalishaji wa chakula.Kisiwani Pate jimboni Lamu, hapa akina mama wana zaidi ya mashamba matatu ya pweza katika bahari hindi, kwa manufaa ya chakula na mapato.
Wiki chache zilizopita, tulikuletea makala kuhusu pikipiki za umeme, na kupitia ukurasa wetu wa Facebook RFI KIswahili, tukawa na maswali mengi kuhusu pikipiki hizi. Katika makala haya tumemwalika, Raymond Kitunga, kutoka kampuni nyingine inayotengeneza pikipiki za umeme, Spiro Kenya, na hapa atakuwa anayajibu baadhi ya maswali kuhusu pikipiki hizi za umeme.
Nchini Kenya, wakulima wameanza kukumbatia ukulima wa wadudu na hasa nzi aina ya black Soldier Fly, kama njia mbadala ya chakula cha mifugo wao.Kulingana na wanasayansi, nzi hawa wana proteni ya kiwanngo cha juu, na hivyo wanatoa nafasi bora kwa wakulima kuboresha vyakula vya mifugo yao.
Makala ya leo yaliandaliwa Florence Kiwuwa, yanaangazia juhudi za jamii katika mji wa Arusha nchini Tanzania, na kile wanachokifanya kupiga jeki harakati za kukabilianana taka za plastiki.
Mkutano wa COP28 uliafikia mataifa mbalimbali kuanza polepole kuachana na matumizi ya mafuta ya kisukuku, mataifa ya Afrika yakitoa wito wa mataifa yenye nguvu na yanayozalisha nishati hii kwa wingi kuwa mfano katika utekelezwaji wa hilo. Mwenyekiti wa shirika la vijana la Youth Survival Organization, YSO, linalojihusisha pia na mzingira, Humphrey Mrema kutoka nchini Tanzania, anaangazia jinsi mkutano wa COP28 ulivyokuwa na mambo yanayoweza kutekelezwa na nchi kufikia mwaka 2030 lakini pia mwaka 2050.
Suluhu za kiasili zinashirikisha hatua mbalimbali za kulinda na kurejesha mandhari ya bahari, maeneo ya maji na maeneo ya mijini ili viumbe hai waweze kukabiliana na changamoto kama vile usalama wa chakula na maji, mabadiliko ya hali ya hewa, hatari za maafa na afya ya binadamu. Suluhu hizi zinasaidia urejesho wa misitu, ardhioevu na pia kuabdili mbinu za kilimo zinazosaidia udongo wenye afya.Kuangazia suluhu hizi za kiasili katika mabadiliko ya hali ya hewa, tunaungana naye Fredrick Kihara, Mkurugenzi wa hazina ya maji Afrika katika shirika la The Nature Conservancy, TNC, nchini Kenya.