Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho

Follow Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho
Share on
Copy link to clipboard

Ni Makala yanayoangazia kwa jicho la tatu mazingira halisi ya dunia yalivyo bila kusahau kile ambacho kinachangia kuyaharibu. Utapata kufahamu namna ambavyo mazingira na rasilimali zinavyoharibiwa huku pia teknolojia ikijumuishwa. Hakika mazingira mazuri ya leo ni dunia yako kesho.

Rfi - Sabina Chrispine Nabigambo


    • Feb 24, 2026 LATEST EPISODE
    • weekly NEW EPISODES
    • 10m AVG DURATION
    • 218 EPISODES


    Search for episodes from Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho with a specific topic:

    Latest episodes from Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho

    Matumizi ya mitego ya wadudu inayotumia sola yaboresha parachichi na mazingira

    Play Episode Listen Later Feb 24, 2026 10:05


    Wakulima wa Meru kaskazini mashariki mwa Kenya wanakumbatia matumizi ya mitego ya wadudu inayotumia nishati ya jua ili kukabiliana na false codling moth (FCM), mdudu anayeharibu mazao ya parachichi. Eneo la kaskazi mashariki huzalisha kiwango kikubwa cha parachichi zinazouzwa ulaya na Asia Kupitia teknolojia hii, wakulima  sasa wameanza kupata nafasi katika masoko ya nje....vile vile wamepunguza utegemezi wao kwa viuatilifu vya kemikali,hivyo  kuongeza kipato cha wakulima.

    Jukumu la redio katika kuelimisha kuhusu mazingira na tabianchi

    Play Episode Listen Later Feb 17, 2026 10:11


    Dunia inapokabiliwa na mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi  na changamoto zingine za kimazingira, je redio imekuwa na mchango gani katika kuhakikisha jamii zinapata taarifa na habari wanazohitaji kufanya maamuzi muhimu kuhusu mazingira yao.

    afrika dunia katika redio mazingira
    Hatau ya Marekani kujiondo kwenye mikataba ya mazingir na tabianchi na athari zake

    Play Episode Listen Later Feb 15, 2026 10:00


    Aliporejea madarakani Januari 20 2025, kwa mara ya pili Trump aliiondoa Marekani katika mkataba wa tabianchi wa Paris wa 2015. Mwaka wa 2025, Washington haikuwatuma maafisa wake wa juu katika mkutano wa tabianchi wa COP30, uliofanyika Belem, Brazil. Na sasa wiki chache zilizopita, utawala wa Trump ulitangaza kuiondoa Marekani katika mashirika 66 ya kimataifa, ikiwemo ile ya UNFCCC.

    Awamu ya pili Siku ya Kimataifa ya nishati safi 26 01 2026: Biogesi kama moja ya suluhisho

    Play Episode Listen Later Feb 7, 2026 10:00


        Upatikanaji wa nishati safi ya kupikia katika jamii kwenye vitongoji duni. Tumetembelea mtaa wa Kawangware, jijini Nairobi, kufahamu juhudi ambazo shirika la Umande Trust linafanya katika suala zima la upatikanaji wa nishati safi kwa kuzingatia usafi wa mazingira. 

    Siku ya Kimataifa ya nishati safi 26 01 2026: Biogesi kama moja ya suluhisho

    Play Episode Listen Later Jan 27, 2026 10:02


    Upatikanaji wa nishati safi ya kupikia katika jamii kwenye vitongoji duni. Tumetembelea mtaa wa Kawangware, jijini Nairobi, kufahamu juhudi ambazo shirika la Umande Trust linafanya katika suala zima la upatikanaji wa nishati safi kwa kuzingatia usafi wa mazingira. 

    Mfumo wa sola tembezi wanufaisha wakulima maeneo kame nchini Kenya

    Play Episode Listen Later Jan 22, 2026 10:01


    Katika maeneo mengi ya kusini mashariki mwa Kenya, ukame na mvua zisizotabirika zimekuwa changamoto kubwa kwa wakulima. Hata hivyo, katika kijiji cha Gachuriri, Mbeere, teknolojia rahisi ya umwagiliaji  mimea maji kwa kutumia sola tembezi inayotumia nishati ya jua inaanza kubadili kilimo na kurejesha matumaini kwa wakulima wadogo.

    Jinsi jamii ya wamasaai wanavyohamia kwenye ufugaji wa samaki baada ya mabadiliko ya tabia nchi

    Play Episode Listen Later Jan 18, 2026 9:53


    Jamii ya wamaasai ambayo Kwa miaka mingi inategemea mifugo imekuwa ikipata changamoto haswa wakati wa kiangazi.  Kiangazi uathiri mifugo kwani ukosefu wa lishe unasababisha wanyama kufa. Hata hivyo Jamii hiyo imebuni mbinu mbadala ya kisasa ya ufugaji samaki. Lakini kutokana na joto jingi linaloshuhudia katika eneo la kajiado, tatizo la kuwakuza samaki hao katika vidimbwi inaonekana wazi wazi kwani wakulima hawana vifaa vya kisasa vya kupima nyuzi joto katika vidimbwi vya samaki. 

    Awamu ya pili: Matukio muhimu ya mazingira na tabianchi mwaka wa 2025

    Play Episode Listen Later Jan 5, 2026 9:57


    Katika awamu ya kwanza tuliangazia miaka kumi ya mkataba wa tabianchi wa Paris na ahadi mpya za kitaifa NDCs. Awamu  ya pili na mwisho tunaendelea kuangazia mkutano wa tabianchi COP30 uliofanyika jijini Belem, Brazil, pamoja na mkutano wa saba wa kimataifa wa mazingira UNEA-7 uliofanyika jijini Nairobi kati ya Disemba 8 na 12 ùwaka wa 2025.

    Awamu ya kwanza:Matukio muhimu ya mazingira na tabianchi 2025

    Play Episode Listen Later Dec 30, 2025 9:53


    kwanza mazingira
    Wanaharakati wataka uhifadhi wa msitu wa mvua wa Kongo kupewa kipaumbele

    Play Episode Listen Later Dec 26, 2025 9:08


    Misitu ya mvua barani Afrika kimsingi imejikita katika Bonde kubwa la Kongo, msitu wa pili kwa ukubwa duniani wa kitropiki, unaohifadhi wanyamapori wa kipekee kama sokwe, na tembo wa msituni, pamoja na maeneo mengine muhimu kama vile Misitu ya Guinea ya Afrika Magharibi, misitu ya Afromontane Mashariki, na misitu ya pwani kutoka Kenya hadi Msumbiji yenye misitu ya kipekee ya kisiwa cha Madagaska. Mifumo hii muhimu ya ikolojia inakabiliwa na vitisho kutoka kwa ukataji miti, kilimo, na kuathiri bioanuwai yao tajiri. Kutokana na vitisho hivi wanaharakati wamepaza sauti za kulindwa kwa misitu ya mvua.

    Lugha ya kiswahili katika kuimarisha uelewa, uhamasishaji na hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi

    Play Episode Listen Later Dec 19, 2025 10:03


    Wakati viongozi wa dunia, wanasayansi na watunga sera wanapokutana katika miji mikuu ya Dunia kujenga hoja kuhusu hatima ya sayari kupitia mikutano ya tabianchi ya Umoja wa Mataifa,  Wataalamu wa lugha,,  walimu pamoja na  wanafunzi waaendeleza  mijadala. Kaulimbiu ukiwa ni namna lugha adimu ya kiswahili inavyotumika katika kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

    Kituo cha jambo Redio nchini DRC chapokea tuzo kwenye COP30

    Play Episode Listen Later Dec 15, 2025 10:00


    Nchini jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Kituo cha Jambo redio, kimejitwika jukumu la kuelimisha jamii kuhusu masuala ya mazingira na tabianchi, lakini muhimu sana ni haki zao. Katika mkutano wa tabianchi uliotamatika jijini Belem nchini Brazil, kituo cha Jambo Redio kilipokea tuzo kutoka kwa shirikika linalotetea haki za wanawake Women Engage for a Common Future, WECF. Kituo hiki, kimekuwa kikitoa habari kwa jamii ambazo wakati mwingine hazina uwezo wa kupata habari.

    brazil congo belem jambo katika kwenye redio mazingira kidemokrasia
    COP30 uliotamatika jijini Belem, Brazil,, suala la ufadhili wa tabianchi, nishati safi ni miongoni mwa ajenda

    Play Episode Listen Later Dec 5, 2025 9:59


      Miongoni mwa mambo yalioamuliwa ni kuhamasisha kiasi cha fedha trilioni 1.3 kila mwaka kufikia 2035 wa ajili ya hatua za tabianchi, kuimarisha fedha uhimilivu mara tatu kufikia 2035. Msikilizaji, suala la kuharakisha ufadhili wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi inasalia kuwa kipaumbele  cha dharura hasa kwa nchi zinazoendelea ambazo zina athirika pakubwa na janga hilo.

    Shirika la Weather Mtaani labuni teknolojia ya kuepuka majanga ya hali ya hewa Kibera

    Play Episode Listen Later Nov 18, 2025 9:57


    Mvua huja kwa sauti ya baraka lakini katika kitongoji, sauti hiyo hubeba hofu. Maji yanapoteremka kutoka angani, katika sekunde chache, barabara hugeuka mito. Vyumba vya kulala vinageuka mabwawa. Katika kitongoji cha Kibera jijini Nairobi nchini Kenya, hali hiyo ya hofu imebadilishwa kupitia kundi la vijana linalojiita Weather Mtaani. Shirika la Weather Mtaani linatumia teknolojia ya simu kutafsiri jumbe za utabiri wa hali ya hewa kutoka kwa mamlaka ya utabiri wa hali ya hewa ya Kenya, kwa lugha inayoeleweka. 

    Mkutano wa mabadiliko ya tabianchi COP30 jijini Belem, Brazil

    Play Episode Listen Later Nov 12, 2025 9:57


    Mkutano huu unakwenda kufanyika wakati ripoti mpya ya shirika la mazingira la umoja wa mataifa UNEP, ikionesha kuwa bado dunia iko nyuma katika kuafikia malengo ya mkataba wa Paris wa kudhibiti wastani wa jotoridi duniani kufikia nyuzijoto 1.5.

    Ripoti: Matajiri wachache wanateka nyara dunia kwa kuchangia pakubwa utoaji wa hewa ukaa

    Play Episode Listen Later Nov 6, 2025 9:58


    Dunia inapojiandaa kwa mkutano wa kimataifa wa Mazingira COP30 utakaofanyika Belém, Brazil, ripoti mpya imeibua mjadala mkali—si tu kuhusu uzalishaji wa hewa ukaa, bali pia kuhusu ukosefu wa usawa. Utafiti mpya wa shirika la Oxfam, unaonesha kuwa mataifa tajiri na watu wachache wenye utajiri mkubwa wanachangia kwa kiasi kikubwa katika mabadiliko ya tabianchi. Inaitwa “ukosefu wa haki wa hali ya hewa.” Mtaalam wetu leo kulichambua hili ni David Abudho, anayeshughulika na mabadiliko ya tabia nchi barani Afrika kutoka shirika la Oxfam.

    Siku ya Chakula duniani: Mapendo Banque Alimentaire yapambana na ukosefu wa usalama wa chakula

    Play Episode Listen Later Oct 24, 2025 10:01


    maadhimisho ya siku ya kimataifa ya upunguzaji wa hatari ya majanga

    Play Episode Listen Later Oct 18, 2025 9:50


    Ripoti ya 2025 ya tathmini ya kidunia juu ya kupunguza hatari za majanga inakadiria kuwa gharama kamili ya kukabili majanga ni karibu dola trilioni2.3, na licha ya uwekezaji huu, bajeti za kitaifa bado ni za kiwango cha chini mno.

    hatari siku kimataifa ripoti mazingira maadhimisho
    Vijana walioasi uhalifu na kujitosa katika kutunza mazingira ya kijiji chao

    Play Episode Listen Later Oct 7, 2025 10:00


    Fahamu kundi la vijana kutoka mtaa wa korogocho jijini Nairobi, walioasi uhalifu na kuamua kutunza mazingira ya jamii yao. Vijana hawa wananuia kuwa mfano kwa kizazi kijacho kufahamu kuwa hata juhudi ndogo zinaweza kuleta mabadiliko katika jamii inayowazunguka.

    Siku ya kimataifa ya hamasisho kuhusu upotevu na uharibifu wa chakula

    Play Episode Listen Later Sep 29, 2025 9:59


    Wakati mamilioni ya watu wanalala njaa kila siku, chakula kizuri hutupwa mashambani, katika maduka makubwa, mikahawa - na ndiyo, hata katika nyumba zetu wenyewe. Uharibifu wa chakula sio tu kuhusu kile kilicho kwenye sahani zetu. Pia inahusu rasilimali zinazotumiwa kuzalisha chakula hicho: maji, ardhi, nishati, na raslimali watu, zote hupotea wakati chakula kinaharibika.

    ACS2: Addis Ababa: Vijana wasisitiza uwekezaji kwenye ajira za kijani

    Play Episode Listen Later Sep 29, 2025 10:00


    Uchumi wa kijani ni miongoni mwa mada kuu zilizojadiliwa kwenye mkutano wa pili wa mazingira wa bara la Afrika uliofanyika hivi majuzi jijini Addis ababa, ambapo wajumbe walijadili mikakati ya kufadhili maendeleo ya kijani barani Afrika kupitia masuluhisho yanayotegemea asili, teknolojia safi. Mjadala umeibuka kuhusu nafasi ya vijana katika mipango ya serikali za Afrika kuelekea uchumi wa kijani, kupitia ajira za kijani.

    Oxfam: Nchi tajiri zimevunja ahadi zao za ufadhili wa hali ya hewa kwa Afrika

    Play Episode Listen Later Sep 10, 2025 9:55


    Ripoti mpya ya shirika la kimataifa ya Oxfam inasema kuwa nchi tajiri zimetoa tu asilimia 4 pekee ya fedha zinazohitajika Afrika Mashariki kushughulikia mabadiliko ya hali ya hewa. Nchi za Afrika Mashariki ni miongoni mwa nchi zilizoathirika zaidi na mzozo wa hali ya hewa, licha ya kuchangia asilimia 0.09 ya uzalishaji wa hewa ukaa duniani.

    Wiki ya maji duniani na mabadiliko ya tabianchi: Changamoto ya upatikanaji wa maji katika maeneo kame

    Play Episode Listen Later Sep 1, 2025 9:55


    Matumizi ya teknolojia katika utabiriwa hali ya hewa jijini Dar

    Play Episode Listen Later Aug 26, 2025 9:54


    Mtokeo ya majadiliano ya kimataifa kuhusu mkataba wa kisheria wa kukabili taka za plastiki

    Play Episode Listen Later Aug 20, 2025 9:53


    Kwa mara nyingine tena, dunia ilipoteza fursa muhimu ya kuwa na mkataba huo, majadilianao yakigonga mwamba kutokana na nchi kutofautiana kwenye baadhi ya maandishi.  

    UN: Ni asilimia 35 pekee ya malengo ya maendeleo endelevu ndio yako katika njia sahihi kufikiwa

    Play Episode Listen Later Aug 11, 2025 9:49


    Ripoti ya malengo ya maendeleo endelevu mwaka 2025, ikiwa ni miaka kumi tangu mataifa kuanza kufanyia kazi malengo hayo. Katika ripoti hiyo, UN inasema dunia bado iko nyuma katika kuhakikisha malengo hayo 17 yanaafikiwa kikamilifu kufikia mwaka wa 2030.

    Mkataba wa plastiki: Mgawanyiko kuhusu jinsi ya kukabiliana na hatari ya kiafya na kiikolojia.

    Play Episode Listen Later Aug 5, 2025 9:56


    Mataifa mbalimbali ulimwenguni yameombwa kuchukua hatua na kutatua mzozo wa kimataifa wa plastiki, mwenyekiti wa kamati ya majadiliano ya kiserikali, mwanadiplomasia wa Ecuador, Luis Vayas Valdivieso akiwaomba wadau waliokusanyika Geneva, Uswizi kwa siku 10 kuunda mkataba wa kihistoria wa kuzuia uchafuzi wa plastiki. "Uchafuzi wa plastiki unaharibu mazingira, unachafua bahari na mito yetu, unatishia viumbe hai, na unadhuru afya ya binadamu," alisema Valdivieso. Wataalam pia katika ripoti iliyochapishwa kwenye Jarida la matibabu la Lancet, wameonya kuwa uchafuzi wa plastiki ni "hatari kubwa, inayokua na isiyotambulika" kwa afya ambayo inagharimu dunia angalau dola trilioni 1.5 kwa mwaka. Bonyeza hapo juu kusikiliza wito wa watetezi wa mazingira kuhusu umuhimu wa kupatikana kwa mkataba wa plastiki.

    Matokeo ya mkutano wa AMCEN katika jitihada za bara la Afrika kukabili mabadiliko ya tabinanchi

    Play Episode Listen Later Jul 28, 2025 9:50


    Kenya ilikuwa mweneyeji wa mkutano wa 20 wa mawaziri wa mazingira kutoka mataifa ya Afrika, AMCEN, mkutano muhimu kuelekea mikutano ya kimataifa kuhusu mazingira kama vile COP30, INC5.2 na UNEA-7.

    Mafanikio ya miaka 50 ya utekelezaji wa CITES, kulinda wanyamapori na mimea

    Play Episode Listen Later Jul 21, 2025 10:13


    Mkataba wa kimataifa wa CITES ulianza kutekelezwa mnamo Julai mosi 1975. Toka wakati huo mkataba huu umeendelea kusaidia dunia kuzuia kupotea kwa kasi kwa spishi mbalimbali za wanyamapori na mimea zilizokuwa katika hatari ya kutoweka.

    Mradi wa EACOP umekamilika asilimia 62, wanaharakati wakiendelea kuupinga

    Play Episode Listen Later Jul 14, 2025 9:56


    Ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Uganda kwenda Tanzania maarufu EACOP umefikia asilimia 62, hivi majuzi raia 26 wa Uganda ambao ni waathriwa wa miradi ya mafuta ya Total ya Tilenga na EACOP wamewasilisha keshi mpya dhidi ya kamuni ya TotalEnergies nchini Ufaransa,

    Ziwa Viktoria: Nishati ya sola na biogesi yatoa suluhu ya kukabili taka za mabaki ya samaki na dagaa

    Play Episode Listen Later Jul 7, 2025 10:07


    Waachuuzi wa samaki na dagaa walilazimika kutumia mbinu za jadi kama vile kuni na makaa kukausha aina hii ya samaki wadogo, dagaa, hali iliyowasababishia hasara na kuchangia uharibifu wa mazingira kwa kutupa taka za samaki ndani ya Ziwa Victoria.

    Matumizi ya viuatilifu au viuadudu na madhara kwa mazingira

    Play Episode Listen Later Jul 1, 2025 10:12


    Hatua ya serikali ya Kenya kuoiga marufuku matumizi ya takriban viuatilifu au dawa za kuua wadudu takriban 77 kutokana na hofu ya usalama wa dawa hizo kwa mazingira na afya ya binadamu. Baadhi ya viuatilifu vimepigwa marufuku katika soko la kimataifa, kuanzia baranai ulaya, Australia, marekani na Canada, laini viipo kwenye masoko ya nchi za ukanda.

    Vitabu: Kampeni ya kuwafikia watoto milioni moja kuhusu uhifadhi

    Play Episode Listen Later Jun 23, 2025 10:00


    Watoto wana jukumu muhimu katika uhifadhi wa mazingira na wanyamapori kwa kushiriki kikamilifu katika mipango kama vile kupanda miti, udhibiti wa taka, na kuongeza uelewa kuhusu masuala ya mazingira na wanyamapori. Kuwashirikisha watoto katika shughuli hizi kunakuza hisia ya uwakili, kuwaunganisha na mazingira wanayoishi, na kukuza mazoea endelevu kwa siku zijazo.

    moja milioni watoto mazingira kampeni
    Mgogoro wa Bahari: Afrika yataka kushirikishwa kikamilifu katika ulinzi wa bahari

    Play Episode Listen Later Jun 19, 2025 10:00


    Mkutano wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa wa kusaidia kutekeleza lengo nambari 14 la Maendeleo Endelevu, ulifanyika kule Nice, Ufaransa, kujadili mbinu mwafaka za kuhifadhi na kutumia kwa njia endelevu bahari na rasilimali zake, washikadau wakiunda uhusiano mpya kati ya wanadamu na mazingira ya baharini. Mkutano wa kilele ulikamilika Ijumaa tarehe 13 Juni, 2025 wakati huu mataifa yakitarajiwa kukutana mwezi ujao kujadili sheria za uchimbaji madini kwenye kina kirefu cha maji baharini.

    Mkutano wa kimataifa kuhusu ulinzi wa bahari wang'oananga jijini Nice, Ufaransa

    Play Episode Listen Later Jun 9, 2025 10:00


    Mataifa yametakiwa kuchukua misimamo mikali kuhusu uvuvi wa kupindukia, uchafuzi wa mazingira na ulinzi wa mifumo ikolojia ya baharini.

    Maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Mazingira, taka za plastiki suala kuu

    Play Episode Listen Later Jun 2, 2025 10:03


    Uchafuzi wa taka za plastiki umekuwa kero kwa dunia, na kuhatarisha sayari yetu, vyanzo vya maji lakini pia afya ya binadamu na wanyama. Mataifa kukutana mwezi Agosti katika muendelezo wa majadiliano ya kutafuta mkataba wa kisheria wa kimataifa kukabili tatizo hili.

    Je dunia iko katika njia sahihi kutimiza lengo la kumaliza njaa kufikia 2030?

    Play Episode Listen Later May 26, 2025 9:39


    Jumatano ya Mei 28 2025, dunia itaadhimisha siku ya njaa ulimwenguni, siku hii ikilenga kutoa hamasa na kuchochea hatua kuchukuliwa ili kumaliza njaa duniani. Kulingana na ripoti ya kimtaifa ya 2025 kuhusu migogoro ya Chakula, zaidi ya watu milioni 295.3 katika nchi 53 wanakabiliwa na hali mbaya ya ukosefu wa usalama wa chakula.

    Uchakataji wa plastiki katika kuhifadhi mazingira ya bahari na kupata mapato

    Play Episode Listen Later May 15, 2025 9:49


    Jamii za Pwani ya Kenya, zimekumbatia uchakataji wa plastiki kukabili tatizo la uchafuzi utokanao na taka za plastiki ambapo  mujibu wa shirika la mazingira la UNEP, kila siku, kiasi sawa cha malori 2,000 ya kuzoa taka yaliyojaa plastiki hutupwa katika bahari, mito, na maziwa ya ulimwengu.

    Mabadiliko ya tabianchi: Hali ya mifumo ya sheria katika suhughulikia ukatili wa kijinsia.

    Play Episode Listen Later May 5, 2025 10:03


    katika sheria mazingira
    Mabadiliko ya tabianchi yachochea ongezeko la ukatili wa kijinsia

    Play Episode Listen Later Apr 28, 2025 10:06


    Ripoti hiyo mpya ya UN Spotlight initiative, imebaini kuwa mabadiliko yatabianchi yameendelea kuzidisha mogogoro ya kijamii na kiuchumi ambayo inachochea kuongezeka kwa viwango vya unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana.

    afrika ripoti
    Cha kutarajiwa katika ahadi mpya za nchi za kukabili mabadiliko ya tabianchi

    Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 10:10


    Ripoti ya umoja wa mataifa inaonesha dunia ipo nyuma sana katika kudhibiti ongezeko la joto chini ya nyuzi joto 1.5.

    Mbolea asilia: Suluhisho kwa uharibifu wa udongo na changamoto za kilimo Kenya

    Play Episode Listen Later Apr 14, 2025 10:00


    Baadhi ya wakulima nchini Kenya wameanza kugeukia matumizi ya mbolea asilia inayonyunyiziwa ardhini ili kunusuru mashamba yao.

    Mabadiliko ya tabianchi yahatarisha barafu ya milimani, barafu hii ikiyeyuka kwa kasi

    Play Episode Listen Later Mar 31, 2025 10:07


    Kutokana na mabadiliko ya tabianchi, kwa mujibu wa shirika la hali ya hewa duniani WMO, barafu inayopatikana kwenye milima inayeyuka kwa kasi zaidi na ndio sababu ya umoja wamataifa kutenga Machi 21 kama siku ya kimataifa ya kutoa hamasisho kuhusu kuyeyuka kwa barafu hii.

    Juhudi zinazofanywa na wadau kufadhili wakulima wadogo barani Afrika

    Play Episode Listen Later Mar 28, 2025 10:12


    Wakulima wadogo wanachangia kwa zaidi ya asilimia 70 uzalishaji wa chakula barani Afrika, hii ni kwa mujibu wa Benki ya Maendeleo barani, Afdb, wakati uo huo, lengo nambari mbili  ya maendeleo endelevu ikinuia kumaliza njaa na kuihakikishia dunia usalama wa chakula kufikia mwaka wa 2030

    Raundi ya tatu ya mataifa kuwasilisha ahadi zao za kitaifa, NDCs za kukabili mabadiliko ya tabianchi

    Play Episode Listen Later Mar 17, 2025 10:10


    Siku ya wanayampori: Jinsi binadamu hutegemea rasilimali za wanyamapori na bayoanuwai.

    Play Episode Listen Later Mar 11, 2025 10:01


    Binadamu hutegemea rasilimali za wanyamapori na bayoanuwai ili kukidhi mahitaji yao. Tunahitaji chakula, mafuta, makazi, na hata mavazi. Hivyo ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha kwamba mifumo ikolojia inaweza kustawi na mimea na wanyama wanaweza kuwepo kwa ajili ya vizazi vijavyo. Machi 3 mwaka huu, ilikuwa ni fursa ya kutoa uhamasisho wa umuhimu wa  wanyama na mimea pori, ili kuongeza ufahamu wa faida zao, na haja ya  kuongeza mapambano ya uhalifu dhidi ya wanyamapori na kusababisha athari kubwa za kiuchumi, mazingira na kijamii.Skiliza ufahamu mengi zaidi.

    Utupaji salama wa taka za kieletroniki, mashirika yachangamkia fursa kuokoa mazingira

    Play Episode Listen Later Mar 4, 2025 9:57


    Taka za kieletroniki zinajumuisha vitu vingi ambavyo ni hatari kwa afya ya binadamu na mazingira na utupaji ovyo ni chanzo kikuu cha madhara, dutu hizi hatari zikiwa na uwezo wa kuchafua udongo, maji, hewa na vyanzo vya chakula.  Shirika la E-Waste Initiative Kenya linatoa suluhu ya taka za kieletroniki. Bonyeza hapa kufahamu zaidi.

    kenya taka salama shirika mazingira mashirika
    Mwali wa mwisho: Mkaa wa Briketi kama suluhu ya nishati jadidifu

    Play Episode Listen Later Feb 20, 2025 9:59


    Mkaa wa Briketi hutengenezwa kutoka kwa vumbi la mkaa wa kawaida, taka za kilimo au mabaki ya mbao, na hutumiwa kimsingi kwa mapishi nyumbani, shuleni na hata katika makampuni. Mkaa huu una faida kwa kuwa unapunguza uchafuzi wa mazingira, kupunguza ukataji wa miti lakini pia huwaka kwa muda mrefu na kwa usawa zaidi kuliko mkaa wa kawaida, na kuufanya kuwa chaguo maarufu kwa kupikia.

    kenya kama mazingira
    Umuhimu wa matumizi ya madawa ya kiasili kunyunyuzia mimea shambani

    Play Episode Listen Later Feb 10, 2025 10:01


    Makala haya yanazungumzia  jinsi Wakulima wengi nchini Kenya wanakumbatia mbinu mpya za kudhibiti wadudu waharibifu wa mimea kwa kutumia madawa ya kiasili badala ya kemikali za viwandani. Kutokana na madhara yanayotokana na matumizi ya dawa za kemikali,wakulima hawa sasa wanageukia madawa hayo asilia kuimarisha mazao na mazingira , Mimea kama vile ,pareto,kitunguu saumu,pilipili na hata mtunguja pori yaani sodom apple sasa inatumika kutengeneza madawa hayo.

    Wakaaji wa mijini wanavyotumia Bustani ya Nyumbani kukabili mabadiliko ya tabia nchi

    Play Episode Listen Later Feb 3, 2025 9:57


    Utunzaji wa bustani ya nyumbani, ni mbinu mpya ya kilimo inayolenga kutimiza malengo matatu kwa wakati mmoja: kuongeza mapato ya kilimo, kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa na kuimarisha ustahimilivu, halkadhalika kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi. Bustani ya Nyumbani, kwa kawaida huwa karibu na jikoni au pia kwenye roshani. Bustani hii ambayo mara nyingi hutumia mbolea asilia husaidia kupambana na mabadiliko ya tabianchi kwa kupunguza uzalishaji wa gesi chafu na pia kutunza udongo.Bustani hii hutumika kwa kilimo cha mboga, viungo vya upishi kama vitunguu, matunda, au mimea ya kitiba kwa matumizi.

    Hatua ya Marekani kujiondoa kwa mkataba wa Paris kuathiri nchi maskini

    Play Episode Listen Later Jan 28, 2025 9:58


    Rais Donald Trump kwa mara nyingine alitangaza Marekani kujiondoa kwenye Mkataba wa Paris kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, hatua ambayo imeibua mjadala wa kimataifa.  Tangazo hilo lilikuja huku ulimwengu ukishuhudia viwango vya joto vinavyovunja rekodi na majanga yanayozidi kuwa makali yanayohusiana na hali ya hewa.Lakini wadadisi wa mambo na viongozi wengine wa ulimwengu wanatazamaje hatua yake Trump? Bonyeza usikilize zaidi.

    Claim Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel