POPULARITY
Jua zaidi kuhusu neno "Ukungu", tafsiri yake kwa Kiingereza, maana yake, na jinsi linavyotumika katika sentensi. Huu ni mwongozo rahisi kwa yeyote anayetaka kujifunza au kuboresha Kiswahili chao.
Jua hukusu neno "Mlowezi", tafsiri yake kwa Kiingereza, maana yake, na jinsi linavyotumika katika sentensi. Huu ni mwongozo rahisi kwa yeyote anayetaka kujifunza au kuboresha Kiswahili chao.
Makala haya yanazungumzia jinsi Wakulima wengi nchini Kenya wanakumbatia mbinu mpya za kudhibiti wadudu waharibifu wa mimea kwa kutumia madawa ya kiasili badala ya kemikali za viwandani. Kutokana na madhara yanayotokana na matumizi ya dawa za kemikali,wakulima hawa sasa wanageukia madawa hayo asilia kuimarisha mazao na mazingira , Mimea kama vile ,pareto,kitunguu saumu,pilipili na hata mtunguja pori yaani sodom apple sasa inatumika kutengeneza madawa hayo.
Matumizi ya kuni yanaweza kuwa na athari chanya na hasi kwa mazingira, kulingana na jinsi zinavyovunwa, kutumiwa na kusimamiwa. Leo mwandishi Christopher Karenzi kutoka Kigali, Rwanda ameangazia hatua ya kuondokana na matumizi yake lakini changamoto pia raia wanazokumbana nazo.
Mashirika kadhaa ya kilimo pamoja na serikali ya Kenya yaliwakutanisha wadau wa kilimo—wakulima, wataalamu wa mabadiliko ya tabianchi, na watunga sera—jijini Nairobi mwezi Novemba mwaka uliopita. Mkutano huo ukilenga kuweka bayana mwelekeo wa kutumia kilimo kinachokabili mabadiliko ya tabianchi yaani climate smart agriculture ili kuongeza uzalishaji wa chakula.Hii leo katika makala mazingira leo dunia yako Kesho ,tunaangania kilimo hicho
VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
Nchini Kenya mjadala mkali kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii unaendelea, ambapo baadhi wamekuwa wakiitumia kuikosoa Serikali na rais William Ruto, kwa kiwango ambacho wengine wanasema wakosoaji wamevuka mipaka huku baadhi wakisema watu wako huru kukosoa wanavyotaka.Tulimuuliwa mskilizaji je anaamini iwapo vijana wamevuka mipaka au la.
Nchini Kenya mjadala mkali kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii unaendelea, ambapo baadhi wamekuwa wakiitumia kuikosoa Serikali na rais William Ruto, kwa kiwango ambacho wengine wanasema wakosoaji wamevuka mipaka huku baadhi wakisema watu wako huru kukosoa wanavyotaka.Tulimuuliwa mskilizaji je anaamini iwapo vijana wamevuka mipaka au la.
Katika makala ya hivi leo, tunajadili kuhusu umuhimu wa kuwa na nidhamu ya fedha, kwanini ipo haja ya kuwa na nidhamu ya matumizi binafsi, vipi unaweza kujipanga kwa mwaka ujao? Haya ni miongoni mwa maswali ambayo mtaalamu wetu wa uchumi na biashara Ali Mkimo anaenda kuyajibu.
Katika makala ya hivi leo, tunajadili kuhusu umuhimu wa kuwa na nidhamu ya fedha, kwanini ipo haja ya kuwa na nidhamu ya matumizi binafsi, vipi unaweza kujipanga kwa mwaka ujao? Haya ni miongoni mwa maswali ambayo mtaalamu wetu wa uchumi na biashara Ali Mkimo anaenda kuyajibu.
Idadi ya vijana wanaotumia dawa za kulevya katika umri mdogo imeongezeka
Ungana nami Esther Magai Hangu katika Kipindi cha Ijue Afya yako, Kutoka Studio za Radio Maria Tanzania Mwezeshaji ni Mtekinolojia dawa, Ndugu Gibson Sanga kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Fransisko, Jimbo Katoliki Ifakara anazungumzia juu ya Matumizi sahihi ya dawa kwa uzazi salama. L'articolo Je, wafahamu matumizi ya dawa kwa Uzazi Salama? proviene da Radio Maria.
Karibu katika kipindi cha Jinsia na maendeleo katika kipindi hiki tutasikiliza shuhuda za wananchi juu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia pamoja na madhara ya kutumia nishati chafu. L'articolo Sikiliza shuhuda za matumizi ya Nishati safi ya kupikia. proviene da Radio Maria.
L'articolo Fahamu umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia? proviene da Radio Maria.
Karibu uungane nami Martin Joseph katika kipindi cha Ijue Afya yako, Mwezeshaji ni Jimson Sanga Mwanateknolojia Madawa kutoka Hospital ya Rufaa ya Mtakatifu Fransisco wa Asizi Ifakara Afisa , leo anatuelimisha juu Afya ya Moyo wa Binadamu na matumizi sahihi ya Shindikizo la Damu. L'articolo Fahamu matumizi sahihi za kutibu shindikizo la Damu. proviene da Radio Maria.
Matumizi ya madawa ya kulevya kwa kijana
Matumizi ya madawa ya kulevya kwa kijana
Kundi la vijana la Vision Bearers la mtaani Mathare, jijini Nairobi linavyotumia taka za chupa za plastiki kuendeleza kilimo bila mchanga(Hydroponic farming)
Kuongeza matumizi ya ICT yatajwa yatapelekea kuinua uchumi Uganda
Kiswahili kinazungumzwa na zaidi ya watu milioni 200 afrika mashariki na kwenye makala haya ya changu chako,chako changu ,Florence Kiwuwa amefanya majadiliano na wanafunzi katika chuo kikuu cha Multmedia ili kujua kuhusu mchango wa lugha hii katika kuendeleza utamaduni na utengamano na vilevile katika kipengele cha muziki amemuangazia mwanamuziki wa Tanzania Harmonize.
VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
Karibu ungane nami Agatha Kisimba ,katika kipindi cha Ijue Afya yako ambapo leo tupo na Mtaalamu Mwandamizi wa Maabara kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Francisco wa Asizi Ifakara, Bwana Steve Ngatunga akifafanua kuhusu madhara ya kutumia dawa bila kufanya vipimo. L'articolo Je, unafahamu madhara yatokanayo na matumizi ya dawa bila vipimo? proviene da Radio Maria.
karibu sana NSAMBO HEALTHCARE kupata huduma za matibabu kwa magonjwa ya lishe ikiwemo Ugumba, mvurugiko wa Homoni na ukosefu wa hisia za tendo la ndoa, kisukari, shinikizo la damu, kitambi na uzito mkubwa n.k. Huduma zaetu NSAMBO HEALTHCARE ni kuazia saa nne asubuhi mpaka saa kumi na moja jioni au weka miasi ya kuonana na daktari kwa kupiga simu namba 0767 030 160 . Karibu kuagiza chakula ambacho kimepikwa kwa kuzingatia muongozo wa sayansi ya mapishi, chakula hiki kinamfaa mtu yoyote mwenye magonjwa ya lishe na yule anayependa kula kiafya. Agiza chakula kwa kupiga simu namba 0787 999 994 . Jiunge na programu ya kupunguza kitambi na uzito mkubwa ya NHC WAEIGHTLOSS BOOT CAMP Fuata Taratibu hizi za Malipo ili kujiunga. TIGO PESA LIPA NO: 7780779 MPESA LIPA NO: 5567920 JINA: HEALTHY EATING COMPANY LIMITED Ukisha Lipia Nitumie SMS, EMAIL na MAJINA YAKO kwenye meseji Moja usajili Uanze Leo na Masomo Utumiwe Leo Leo. Namba ya Whatsapp Ya Kutuma Taarifa zako: 0767 030 160 AU WASILIANA NASI SIMU: +255767 074 124 +225787 999 994 Usisahahu KUSUBCRIBE kwa elimu zaidi kuhusu magonjwa ya lishe kama vile KISUKARI KITAMBI NA UZITO MKUBWA SHINIKIZO LA DAMU (PRESHA) MVURUGIKO WA HOMONI UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME TEZI DUME MAGONJWA YA GOITA Tufuatilie katika mitandao ya kijamii INSTAGRAM https://www.instagram.com/sayansiyama... https://www.instagram.com/nsambohealt... FACEBOOK https://www.facebook.com/drboazmkumboMD BLOG https://blog.heaprogram.co.tz/ WEBSITE https://heaprogram.co.tz/ http://nsambohealthcare.tilda.ws/
Karibu katika uungane na Happiness Mlewa katika kipindi cha Uraibu, mwezeshaji ni Padre Richard Matanda Tesha, kutoka Jimbo Katoliki Moshi, leo anatuongoza katika mada ya Uraibu wa madawa, akijikita zaidi katika madhara ya matumizi haramu ya madawa ya kulevya kwa vijana katika jamii. L'articolo Fahamu madhara ya matumizi haramu ya madawa ya kulevya kwa Vijana. proviene da Radio Maria.
VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
Ungana na Mtangazaji Happiness Mlewa Katika Kipindi cha Usalama wa Barabarani, mada inayozungumziwa matumizi Sahihi ya Watembea kwa Miguu, Wawezeshaji ni kikosi cha Polisi cha Usalama wa Barabarani, Mkaguzi wa Polisi Dumu Mwalugenge, Staff Sajenti Olele Chuwa koplo Abdaah Ismail. L'articolo Zifahamu mbinu za matumizi Sahihi ya Watembea kwa Miguu wawepo Barabarani. proviene da Radio Maria.
Juma hili kumefanyika Kongamano la Kutathmini Viwango vya Mishahara na Marupurupu wanayopata wafanyakazi wa serikali. Rais amekariri kuwa serikali yake inajizatiti kupunguza mianya ya ufujaji serikalini. Sepetuko inasema kuwa kongamano hili na juhudi hizi ni kazi bure ikiwa serikali bado inaendelea kupanua viwango vya mishahara kwa kuwaajiri Mawaziri Wasaidizi CAS.
Sauti zote ziimbe Utukufu kwa Mungu, Jinsi ya kutumia muda vizuri
Sauti zote ziimbe Utukufu kwa Mungu, Jinsi ya kutumia muda vizuri
Karibu katika kipindi cha Ijue Afya yako kupitia Radio Maria Tanzania ambapo leo tunaangazia madhara ya matumizi holela ya dawa. L'articolo Yafahamu madhara ya matumizi holela ya dawa. proviene da Radio Maria.
Wiki chache zilizopita, tulikuletea makala kuhusu pikipiki za umeme, na kupitia ukurasa wetu wa Facebook RFI KIswahili, tukawa na maswali mengi kuhusu pikipiki hizi. Katika makala haya tumemwalika, Raymond Kitunga, kutoka kampuni nyingine inayotengeneza pikipiki za umeme, Spiro Kenya, na hapa atakuwa anayajibu baadhi ya maswali kuhusu pikipiki hizi za umeme.
Ulimwengu umeanza kukumbatia matumizi ya akili mnemba au AI kuboresha huduma muhimu licha ya kuwa bado kukamilika mchakato wa kudhibiti matumizi ya teknolojia hiyo. Katika sekta ya afya mfumo wa AI umeanza kutumika kwenye ubainishaji wa magonjwa na ufuatiliaji wa matibabu.
Mataifa mengi kama Tanzania, Burundi na DRC yamekabiliwa na athari za matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii kuanzia kwa taarifa za uongo hadi jumbe za chuki hasa nyakati za uchaguzi.Na leo kwenye makala yetu tulitaka kujua iwapo unadhani mitandao ya kijamii inatumika kueneza propaganda? na nini kifanyike ili kuzuia matukio kama haya?Sikiliza
Mataifa mengi kama Tanzania, Burundi na DRC yamekabiliwa na athari za matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii kuanzia kwa taarifa za uongo hadi jumbe za chuki hasa nyakati za uchaguzi.Na leo kwenye makala yetu tulitaka kujua iwapo unadhani mitandao ya kijamii inatumika kueneza propaganda? na nini kifanyike ili kuzuia matukio kama haya?Sikiliza
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Mwezi Septemba dunia inapojiunga kuleta hamasa kuhusu afya ya akili,idadi ya vijana wanaojiua bado iko juu. Na watalaam vile vile wanaonya kuhusu sukari mbadala au artificial sweeteners ambazo japo zinadhaniwa kuwa salama ,zina madhara katika viungo vya mwili na utendakazi wa mwili
Kenya iko mbioni kuimairisha sekta ya usafiri wa uma, na kampuni ya kutengeneza magari ya Roam ni miongoni mwa zinazolenga kutumia fursa hiyo kuchangia katika kupunguza uchafuzi wa hewa unaotokanana sekta ya usafiri.
Matumizi ya mkaa mbadala
Matumizi ya mkaa mbadala
Balozi mwema wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto UNICEF Vanessa Nakate amefanya ziara nchini Rwanda kujionea namna mradi wa pampu ya kuvutia maji inayotumia nishati ya umeme wa jua au Sola ilivyoleta manufaa kwa wanawake na wasichana barubaru 11,000 waliokuwa wakitembea umbali mrefu kusaka hmaji. Ni Vanessa Nakate Balozi mwema wa UNICEF, raia wa Uganda ambaye pia ni mwanaharakati wa mabadiliko ya tabianchi akiwa Nyagashankara nchini Rwanda alikokwenda kutembelea mradi wa maji ambao hapo awali ulikuwa ukitumia mafuta ya diseli lakini saa unatumia nishati safi ya Sola. Akiwa kijijini hapo Vanessa alikutana na mabinti wawili Adele na Graciela ambao kabla ya mradi huu walikuwa wakitembea umbali mrefu kusaka maji …… na anaeleza kuwa, “Ilikuwa hatari kwao, tunajua kuwa kwa uwiano, wasichana na wanawake wanaathirika pakubwa na majanga ya tabianchi, kwa hiyo ni muhimu sana kuelewa kuwa tunavyopamba kupata haki kutokana na athari za mabadilko ya tabianchi ni kuwa pia tunapambana kwa haki ya kijinsia.”Vanessa anaikumbusha jamii kuwa wasichana hawana changamoto moja tu ndani ya jamii, utakuja binti ambaye anaathirika na mabadiliko ya tabianchi, huyo huyo anaweza kuacha shule au kukosa masomo hivyo kuleta majawabu mtambuka kunasaidia kutatua changamoto nyingi ndani ya jamii. “Kuwa na mashine ya kuvuta maji inayotumia umeme wa Sola ambao unawarahisishia kupata maji sio tu unasaidia kuhakikisha wasichana wanasalia shuleni lakini pia inawasaidia kuwa na maono ya dunia bora zaidi. “Vanessa anahitimisha kwa kueleza kuwa ili kuhakikisha wanajamii wengi zaidi wananufaika na miradi kama hii ya maji lazima kuwepo na miradi mingi kama hii na hilo litawezekana iwapo watapata uwezeshaji wa kifedha na rasilimani nyingine nah apo wasichana wengi watakuwa wamehakikishiwa kuendelea kusalia shuleni.
Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO kuhusu ufuatiliaji wa teknolojia katika elimu GEM 2023 imetaka mifumo ya elimu kote duniani siku zote kuhakikisha kwamba matakwa ya wanaojifunza yanakuwa katika kitovu cha teknolojia na kwamba teknolojia zitumike kusaidia elimu inayotokana na mwingiliano wa binadamu badala ya kulenga kuwa mbadala wake. Ripoti hiyo mwaka 2023 ya GEM inashughulikia matumizi ya teknolojia katika elimu duniani kote kupitia muktadha wa umuhimu, usawa, uthabiti na uendelevu.UNESCO inasema teknolojia inabadilika haraka kuliko inavyowezekana kutathminiwa na bidhaa za teknolojia ya elimu hubadilika kila baada ya miezi 36, kwa wastani huku ushahidi mkubwa ukitoka katika nchi tajiri zaidi.Mathalani ripoti inasema “Nchini Uingereza, asilimia 7 ya makampuni ya teknolojia ya elimu yalikuwa yamefanya majaribio yaliyodhibitiwa bila mpangilio, na asilimia 12 yalikuwa yametumia uthibitishaji wa watu wengine. Pia utafiti uliofanywa kwa walimu na wasimamizi katika majimbo 17 ya Marekani ulmeonyesha kuwa ni asilimia 11 tu waliomba tathimini ya ushahidi kabla ya kupitishwa.Katika miaka 20 iliyopita, wanafunzi, waelimishaji na taasisi wamepitisha na kukumbatia kwa kiasi kikubwa zana za teknolojia ya kidijitali.Audrey Azoulay, mkurugenzi mkuu wa UNESCO anaonya kwamba "Mapinduzi ya kidijitali yana uwezo usiopimika lakini, kama vile onyo ambavyo limekuwa likitolewa kuhusu jinsi yanavyopaswa kudhibitiwa katika jamii, tahadhari sawa lazima izingatiwe jinsi mapinduzi hayo yanavyotumiwa katika elimu. Matumizi yake lazima yawe kwa ajili ya uzoefu ulioimarishwa wa kujifunza na kwa ajili ya ustawi wa wanafunzi na walimu, si kwa madhara kwao. Matakwa ya mwanafunzi yawe kipaumbele cha kwanza na yawasaidie walimu. Kuunganishwa mtandaoni sio mbadala wa mwingiliano wa wanadamu.”Azoulay amesisitiza kuwa “Kutumia teknolojia kunaweza kuboresha baadhi ya aina za kujifunza katika baadhi ya miktadha. Ripoti hiyo inataja ushahidi unaoonyesha kuwa manufaa ya kujifunza hutoweka ikiwa teknolojia itatumiwa kupita kiasi au kutokuwepo kwa mwalimu aliyehitimu. Kwa mfano, kusambaza kompyuta kwa wanafunzi hakuboreshi hali ya kujifunza ikiwa walimu hawatahusika katika tajriba ya ufundishaji. Simu za rununu shuleni pia zimeonekana kuwa kero katika kujifunza, lakini ni chini ya robo ya nchi tu ndizo zimepiga marufuku matumizi ya simu hizo shuleni.”Duniani kote ripoti imesema idadi ya watu wanaotumia mtandao wa intaneti imeongezeka kutoka asilimia 16 mwaka 2005 hadi asilimia 66 mwaka 2022.
Ungana na Martin Joseph katika Kipindi cha Maswali ya Imani, na swali linalojibiwa linahoji juu ya maana ya skapulali, Mwezeshaji Frateri Erasto Mwamboka Kutoka Parokia ya Moyo Mtakatifu wa Yesu Ilambo- Jimbo kuu la Mbeya.
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono katika mizozo ya vita Umoja wa Mataifa umesenma jinamizi hilo ni janga lililokita mizizi katika kukosekana kwa usawa na kanuni na tamaduni kali za masuala ya kijinsia. Tupate maelezo Zaidi kutoka kwa Flora Nducha(TAARIFA YA FLORA NDICHA)Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa leo mjini Brussells na New York na mwakilishi wa pamoja wa Umoja wa Mataifa kuhusu ukatili wa kingono katika mizozo Pramila Patten na mwakilishi wa Muungano wa Ulaya kwa ajili ya mambo yan je na sera za usalama Josep Borrell wametoa wito wa hatua madhubuti zaidi za kuzuia na kukomesha unyanyasaji wa kingono, na kuendeleza usawa wa kijinsia kama kipaumbele cha kisiasa. Wamesema “Tunasikitishwa na kuongezeka kwa matumizi ya unyanyasaji wa kingono kama mbinu ya kikatili ya vita, mateso, ugaidi na ukandamizaji wa kisiasa, na tishio kwa usalama wa pamoja. Hatari ya kuwa mlengwa wa unyanyasaji wa kingono leo inazidishwa na ukweli kwamba uhalifu huu unaweza pia kuwezeshwa na kukuzwa mtandaoni, kwa kutumia chaneli za kidijitali.”Badala ya kutumika vibaya wamekumbusha kuwa “Wakati huo huo, majukwaa ya kidijitali yanaweza kuwa na jukumu muhimu na kuwa chombo chenye nguvu cha kuboresha usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake na wasichana, na kuchangia katika kujenga uwezo wao wa kustahimili nyakati za shida. Wanaweza pia kusaidia katika kuzuia unyanyasaji wa kingono na kijinsia, na hatua zinazohitajika, kupitia tahadhari za mapema na kuunganisha waathiriwa na njia za kuwatambulisha kwenye huduma, na kuwezesha kuripoti..”Viongozi hao wameonya kwamba badala ya kuwa msaada kwa waathirika leo hii “Mitandao hiyo inatumika vibaya kusambala kauli za chuki na kuchochea ukatili wa kijinsia na ubaguzi, kwani kauli za chuki za kijinsia zinaendelea kuongezeka kutumika kuwanyamazisha watetezi wa haki za binadamu, na wanaharakati wa kisiasa kwa kuchagiza utekelezaji wa ukatili wa kingono. Katika mazingira yaliyoathiriwa na migogoro, majukwaa ya kidijitali yanatumiwa kusafirisha kiharamu wanawake na wasichana kwa madhumuni ya unyanyasaji wa kingono. Walanguzi wa ngono wanatumia mtandao kama zana ya kuajiri wanawake na haswa Watoto na kutangaza huduma za kinyonyaji.”Wameongeza kuwa na katika mazingira mabaya zaidi wanawake na wasichana wanauzwa mtandaoni kama ilivypoainishwa kwenye maenmeo yanayodhibitiwa na kundi la kigaidi la ISILZaidi ya hayo wamesema “ upotoshaji wa habari kwa makusudi na udhibiti kupitia kampeni za kutoa taarifa potofu unaathiri uwezo wa mataifa kulinda raia na kushughulikia unyanyasaji wa kingono. Matumizi ya intaneti kama silaha katika maeneo yenye migogoro pia huzuia waathiriwa wa unyanyasaji wa kingono unaohusiana na migogoro kupata taarifa kuhusu huduma za kuokoa maisha na kupata usaidizi wa mtandaoni kama vile usaidizi wa kisaikolojia.”Kwa mantiki hiyo wametoa wito wa kuwa na “Majukwaa salama ya kidijitali yanayotii sheria za kimataifa, ili waathirika wa unyanyasaji wa kingono unaohusiana na migogoro na wale wanaowaunga mkono watumie mifumo hii kupambana na ukwepaji wa sheria na kudai uwajibikaji ulioboreshwa. Ni muhimu kukuza mazingira ya ulinzi mtandaoni na nje ya mtandao, ambayo yanazuia unyanyasaji wa kijinsia na vile vile kuwezesha kuripoti kwa usalama na makuchukuliwa hatua zinazofaa.”Pia wameitaka Jumuiya ipambane kwa Pamoja dhidi ya tishio linaloongezeka kila mara linaloletwa na teknolojia ya kidijitali na kuziba pengo la mgawanyiko wa kidijitali wa kijinsia ili kuruhusu waathiriwa kupata rasilimali na kupambana na ukwepaji wa sheria kwa kuzingatia kujenga usawa wa kijinsia kwa kuzuia na kupambana na unyanyasaji wa kingono katika migogoro.Wamehitimisha ujumbe wao kwa kusema kuwa “Kwa kushughulikia mgawanyiko wa kidijitali wa kijinsia, tunaweza kuunda ulimwengu ambapo wanawake na watoto wanaweza kuishi bila woga na vurugu.”Siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili wa kingono katika mizozo…
Watu walioacha kutumia dawa za kulevya nchini Sudan wanasaidia juhudi za kupambana na dawa za kulevya
Usalama wa chakula ni suala muhimu kwa afya ya umma na usalama wa chakula duniani, hata hivyo walaji hawawezi kugundua kwa kuona, kuonja au kunusa chakula kisicho salama, na ndio maaana maabara za usalama wa chakula zinazotumia sayansi ya nyuklia kuhakikisha wananchi wanalindwa.Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO linakadiria watu milioni 600 kila mwaka wanapata madhara kutokana na kula chakula kisicho salama, idadi hii ni sawa na mtu mmoja kati ya kila watu 10 au mara mbili ya idadi yote ya wananchi wa Marekani.Usalama wa chakula ina maanisha chakula kinacholiwa linatakiwa kisilete madhara kwa mlaji na pale chakula kinapobainika kuwa si salama basi wataalamu hukataza wananchi kula chakula hicho.Maendeleo ya sayansi yamewezesha nyuklia kutumika katika ukuaji wa chakula na mbogamboga na pia nyuklia hutumika kupima kiasi cha virutubisho vinavyofyonzwa. Swali ni je nyuklia inawezaje kuhakikisha chakula tunachokula ni salama?Na anayejibu ni Carl Blackburn, mtaalamu kutoka kituo cha pamoja cha Mbinu za Nyuklia katika Chakula na Kilimo kinachosimamiwa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Chakula na Kilimo FAO na la nguzu za Atomiki IAEA.“Kisayansi tuna viwango vya kimataifa vya chakula ambapo tunatoa kikomo kwa vyakula vinavyochafua.Zimewekwa kanuni nzuri za kuanzia uchakataji wa chakula, usindikaji, mpaka uhifadhi wa chakula. Mamlaka ya udhibiti wa chakula kwa kila nchi zinaweka viwango na sheria zinazosaidia usambazaji wa chakula kukidhi viwango vya kimataifa na ni muhimu kwa nchi zote kukidhi viwango hivyo kwa usawa kwani hatutaki viwe kizuizi kwa watu kufanya biashara ya chakula duniani kote.”Zaidi ya nchi 200 zinahusika katika utungaji wa sheria hizo zinazosimamia kuhakikisha chakula kinakuwa salama na IAEA ndio muangalizi wa sheria hizo. Moja ya maabara zinazopima usalama wa chakula kwakutumia nyuklia zipo nchini Botswana, nchi inayofahamika zaidi kwa usambazaji wa nyama duniani kote, Sandy Mookantsa, ni afisa katika maabara ya Kitaifa ya Mifugo ya Botswana na anasema mbali na kupima nyama lakini pia wanasaidia kutoa mafunzo kwa nchi jirani.“Maabara yetu ni ya usalama wa chakula, ilianzishwa mwaka 1989, tunashirikiana na IAEA katika kutujengea uwezo, rasilimali na kiufundi. Kwakupitia IAEA tumeweza kutengeneza mtandao ambapo tumekuwa tukitoa mafunzo kwa wanasayansi kutoka nchini Nigeria, Lesoth, Burundi na Uganda kwakutaja nchi chache tu."
Mataifa ya ulimwengu yanapoadhimisha siku ya Tumbaku Mei 31,kuna hofu juhudi za kupunguza matumizi ya tumbaku zinaonekana kurudishwa nyuma na ukiukaji wa sheria za kupambana na matumizi ya tumbaku Sheria kuhusu ushuru unaotozwa kwenye bidhaa za tumbaku bado haifuatwi kikamilifu .Wafanyibiashara wanaouza sigara chini ya pakiti moja wanatuhumiwa vile vile kurudisha mapambano ya kupunguza matumizi ya tumbaku.Isitoshe kampuni zinazotengeneza bidhaa hizo zimekuja na bidhaa mpya ambazo zinawavutia watumizi wa umri mdogo na pia wanawake .Aidha kwenye makala haya tunakufahamisha kuhusu juhudi za sekta binafsi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kuchangia kupunguza idadi ya raia wanaoumwa kwa kuwatuza na kuwasaidia kuepukana na magonjwa haswa yasiyoambukizwa.
Kwa mujibu wa umoja wa Mataifa, malipo ya kidijiti au ya kimtandao yanachangia pakubwa katika kujenga msingi imara wa kufikia maendeleo endelevu, kwanini? Ni kwasababu malipo haya yanapokuwa rahisi, salama, ya wazi na binafsi, yatawezesha ukuaji wa fursa kama nishati, maji na mikopo.Katika kipindi hiki utamsikia, Lucy Nshuti Mbabazi, kutoka taasisi ya umoja wa Mataifa ya muungano wa Better than Cash, Lacina Kone, mkurugenzi wa Smartafrica pamoja na Kwizela Aristide Basebya, mtafiti wa Teknolojia za Mawasiliano ya Umma na Matumizi yake serikalini, akiwa Beijing, China.
Kwa mujibu wa umoja wa Mataifa, malipo ya kidijiti au ya kimtandao yanachangia pakubwa katika kujenga msingi imara wa kufikia maendeleo endelevu, kwanini? Ni kwasababu malipo haya yanapokuwa rahisi, salama, ya wazi na binafsi, yatawezesha ukuaji wa fursa kama nishati, maji na mikopo.Katika kipindi hiki utamsikia, Lucy Nshuti Mbabazi, kutoka taasisi ya umoja wa Mataifa ya muungano wa Better than Cash, Lacina Kone, mkurugenzi wa Smartafrica pamoja na Kwizela Aristide Basebya, mtafiti wa Teknolojia za Mawasiliano ya Umma na Matumizi yake serikalini, akiwa Beijing, China.
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO, hii leo limetoa mwongozo unaoshauri watu wasitumie vikoleza utamu visivyo sukari halisia (NSS) kwa lengo la kupunguza uzito na kuepusha magonjwa yasiyo ya kuambukiza, NCDs.Taarifa ya WHO iliyotolewa leo Geneva, Uswisi inasema mwongozo huo unafuatia mapitio ya ushahidi unaodokeza kwamba kutumia sukari isiyo halisia kwa ajili ya kupunguza uzito hauna manufaa ya muda mrefu katika kupunguza mafuta mwilini miongoni mwa watoto na watu wazima. Sukari hizo zisizo halisia na ambazo zinatumika ni pamoja na aspartame, advantame, cyclamates, neotame, saccharin, sucralose na stevia. Kitu kibaya zaidi ambacho mapitio hayo yamebaini ni kwamba sukari hizo zisizo halisia zinaongeza hatari ya kupata uognjwa wa kisukari aina ya 2, magonjwa ya moyo na vifo miongoni mwa watu wazima. Mkurugenzi wa WHO Idara ya Lishe na Usalama wa Chakula Dkt. Francesco Branca amesema kuacha kutumia sukari ya kawaida na badala yake kutumia sukari zisizo halisia kwa muda mrefu hakusaidii kupunguza uzito. Amesema “watu wanapaswa kufikiria njia mbadala za kupunguza matumizi ya sukari kwa kula vyakula vyenye sukari ya asili kama vile matunda au vinywaji na vyakula visivyo na sukari.” Amesema “vikoleza utamu visivyo na sukari havina lishe yoyote. Watu wapunguze vyakula vitamu kwenye mlo wao tangu utotoni ili kuimarisha afya zao.” WHO inasema pendekezo hilo linahusu watu wote isipokuwa wale wanaougua kisukari.
Mswada wa matumizi ya fedha Kenya ambao, kati ya mengine, unapendekeza wafanyakazi wa serikali kutozwa kodi ya 3% ya mishahara yao ili kugharamia mradi wa ujenzi wa nyuma umeibua utata huku baadhi ya wafanyakazi wakitishia kugoma.
Matumizi salama ya mtandao kwa maendeleo, ni moja ya ajenda iliyojadiliwa kwa kina katika mkutano wa juma lililopita nchini Zimbabwe, kuhusu namna bara la Afrika linaweza kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano, TEHAMA, kubadili uchumi wake na kurahisisha upatikanaji wa huduma za msingi kwa wananchi wa bara hilo kama vile afya na kilimo. Mtangazaji amezungumza na mbunge wa viti maalumu nchini Tanzania, Neema Lugangira, alipokuwa nchini Zimbabwe.
Matumizi salama ya mtandao kwa maendeleo, ni moja ya ajenda iliyojadiliwa kwa kina katika mkutano wa juma lililopita nchini Zimbabwe, kuhusu namna bara la Afrika linaweza kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano, TEHAMA, kubadili uchumi wake na kurahisisha upatikanaji wa huduma za msingi kwa wananchi wa bara hilo kama vile afya na kilimo. Mtangazaji amezungumza na mbunge wa viti maalumu nchini Tanzania, Neema Lugangira, alipokuwa nchini Zimbabwe.
Msikilizaji mataifa mengi ya Afrika, sasa hivi yanafanya juhudi kuhakikisha raia wake wanaunganishwa na huduma ya internet, kama moja ya harakati za kuchochea maendeleo kupitia teknolojia.Lakini kwa wananchi kuunganishwa na huduma hiyo ni jambo moja, changamoto iliyoko sasa hivi kwa nchi nyingi za Afrika ni kukosekana kwa miundombinu sahihi kuwezesha hilo. Mtangazaji Emmanuel Makundi, akifanya mahojiano na David Karunda, kutoka taasisi ya Digital Impact Alliance, alipokuwa nchini Zimbabwe kuhudhuria mkutano wa Smart Africa
Msikilizaji mataifa mengi ya Afrika, sasa hivi yanafanya juhudi kuhakikisha raia wake wanaunganishwa na huduma ya internet, kama moja ya harakati za kuchochea maendeleo kupitia teknolojia.Lakini kwa wananchi kuunganishwa na huduma hiyo ni jambo moja, changamoto iliyoko sasa hivi kwa nchi nyingi za Afrika ni kukosekana kwa miundombinu sahihi kuwezesha hilo. Mtangazaji Emmanuel Makundi, akifanya mahojiano na David Karunda, kutoka taasisi ya Digital Impact Alliance, alipokuwa nchini Zimbabwe kuhudhuria mkutano wa Smart Africa
Ni wakati kufikiria upya jinsi ya kutumia maji kwa njia endelevu na yenye uwiano huku ubunifu katika kilimo ukiwa kitovu cha mipango yote, amesema Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO limesema Qu Dongyu hii leo wakati akizungumza na viongozi na wataalamu wa Afrika kwenye warsha ya kwanza ya kikanda kuhusu mwelekeo wa matumizi ya maji barani Afrika, warsha inayofanyika nchini Zimbabwe.Mkutano huo ni wa siku tatu na leo ikiwa ni ufunguzi ulioleta viongozi wa ngazi ya juu, Bwana Qu amesema Mikakati ya Kitaifa kuhusu mwelekeo wa matumizi yam aji itasaidia kuimarisha mbinu za usimamizi wa maji ambazo ni muhimu katika kutatua changamoto nyingi zinazozingira kwenye matumizi ya maji, na hivyo kusaidia kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2030. Amesema maji ni moja ya rasilimali adhimu duniani na ni kitovu cha mafanikio ya ajenda 2030 kwa sababu “maij ni chakula, chakula ni maji, chakula ni uhai. Zaidi ya asilimia 95 ya chakula tunachokula kinazalishwa kutoka ardhini, kutoka kwenye udongo na maji. Lakini bado tunakabiliwa na changamoto kubwa za maji: ukame na uhaba wa maji, mafuriko na uchafuzi wa vyanzo vya maji.” Ametanabaisha kuwa ni dhahiri janga la tabianchi linaongeza ukali wa ukame na mafuriko ambavyo vyote vina madhara kwenye uzalishaji wa chakula. Mkurugenzi Mkuu huyo amesema kilimo kikitumia asilimia 70 ya maji duniani ni lazima sasa kutumia ubunifu kusaka mbinu za matumizi ya maji kwa tija kwa kuwa uzalishaji zaidi unahitaij maji zaidi. Majawabu kama vile usimamizi endelevu wa matumizi ya udongo, kuzuia mvurugano wa matumizi ya maji na pia kuhifadhi tabianchi.
VOA Express ni matangazo mapya yenye mwendo wa kasi yakiangalia habari mpya za mchana na maelezo ya maswala yanayohusu vijana na wanawake.
Waziri wa kilimo Hussein Bashe amesema wataendelea kujifunza kutoka nchi ambazo zimeanza kutumia teknoljia hiyo ya GMO kwa sababu serikali ya Tanzania haiwezi kuingia kwenye mjadala wa kutumia au kutokutumia teknolojia hiyo bila kufahamu undani wake
Matumizi ya dawa , mjasiliamali wa upambaji
Matumizi ya dawa , mjasiliamali wa upambaji
Wakati dunia inapoendelea kukusanya mikakati ya kupambana na mabadiliko ya Tabia nchi, sekta ya utalii nchini Tanzania imeboresha mfumo wa Usafirishaji wa watalii kwa kutumia Puto zenye injini isiyotumia Mafuta kutoa moshi. Mwenzangu Ruben Lukumbuka amezungumza NA jOHN CORSE ni mkurugenzi wa Ballon Serengeti Safaris kuangazia mbinu zao.
Mada yetu kwenye habari rafiki tunazungumzia kuhusu hatuwa ya Serikali za mataifa ya Afrika Mashariki zinahimiza wananchi wake kutumia Internet, wakati huo huo tozo za matumizi zikiongezeka.Unaizungumziaje hali hii?Hali ipoje nchini mwako?Je unamudu gharama ya internet katika nchi yako?
Mada yetu kwenye habari rafiki tunazungumzia kuhusu hatuwa ya Serikali za mataifa ya Afrika Mashariki zinahimiza wananchi wake kutumia Internet, wakati huo huo tozo za matumizi zikiongezeka.Unaizungumziaje hali hii?Hali ipoje nchini mwako?Je unamudu gharama ya internet katika nchi yako?
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Kijana Gibson Kawago kutoka Tanzania ambaye ni miongoni mwa vijana 17 walioteuliwa na Umoja wa Mataifa kuwa viongozi vijana wa kusongesha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs amesema atatumia kipindi cha miaka miwili cha nafasi hiyo kusongesha hatua kwa tabianchi ikiwemo kutumia ugunduzi wake kuchakata betri chakavu za kompyuta kutengeneza betri za kuzalisha umeme katika kulinda na kuhifadhi mazingira. Nina furaha sana kuteuliwa na nitakuwa balozi mwema Akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa akiwa Dar es salaam nchini Tanzania, Gibson amesema amepokea kwa furaha kubwa uteuzi huu akisema, “nina furaha kubwa sana kuweza kuteuliwa na Umoja wa Mataifa kwa kutambua mchango wangu kwenye kutatua matatizo katika jamii hii ninayotoka. Kijana huyu mwenye umri wa miaka 27 ambaye sasa anamiliki kampuni ya WAGA inayotengeneza betri hizo amesema anaamini kilichomfanya ateuliwe ni kazi yake ya kulinda mazingira na kubuni mbinu za nishati salama. “Sisi tunajihusisha kuchakata betri za kompyuta mpakato, sasa hivi watu wakibadilisha betri kwenye kompyuta zao wanazitupa na zinachafua mazingira, na mara nyingi zikiingia kwenye udongo huleta madhara kwa afya ya binadamu,” amesema Gibson. Betri hizo zikiisha umeme huchajiwa kwa sola Wanachofanya WAGA ni kuchakata hizo betri na kutengeneza kasha la betri ambalo hutumiwa na wananchi wa vijijini kutumia kupata nishati mbadala na wanachaji kwa sola. Betri hiyo hutumika katika kuwasha taa na hata kuwasha televisheni. Kifuatacho ni nini? Gibson amesema kipindi cha miaka miwili cha nafasi hiyo ya kijana kiongozi wa kusongesha SDGS, atajitahidi kuwa balozi mzuri kuhakikisha vijana wenzake wanafahamu jinsi gani ya kutunza mazingira na wanajua ni jinsi gani watatafuta fursa tofauti kutatua matatizo katika jamii zao na kuhakikisha wanatunza mazingira yao. Kifo cha bibi yangu kilinichochea kutafuta jawabu la nishati Gibson anasema chanzo cha yeye kujikuta kwenye ubunifu huo ni kifo cha bibi yake. “Kuna siku nikiwa kijijini nilikuwa natumia simu yangu kumuonesha bibi picha za harusi. Katikati betri ikaisha na hatukuwa na umeme. Kesho yake nikasafiri umbali mrefu hadi mjini kupata betri.” Anasema hata hivyo aliporejea nyumbani alikuta bibi yake amefariki dunia kwa kuwa hali yake ya kiafya haikuwa nzuri. “Kwa hiyo wakati napata maumivu yale na kuwaza ni watu wangapi wanapata matatizo hayo nje nilipofika Dar es salaam wakati nasoma Chuo Kikuu cha Teknolojia ya Ufundi, DIT nikaanza kutafiti ni kwa vipi naweza kutengeneza betri inayohifadhi umeme,” amesema Gibson. Amesema alisaka mafunzo kwenye mtandao na hatimaye akaweza kutambua jinsi ya kuchakata betri chakavu za kompyuta mpakato ili kuzalisha umeme. Sasa betri zinawasha televisheni na taa vijijini Kwa mujibu wa Gibson, anatengeneza makasha ya betri kutokana na betri chakavu za Lithium na Ion, na betri. “Nimeweza kutengeneza betri kubwa ambazo inawezesha mtu wa kijijini kuweza kuwasha televisheni, kuwasha taa zake na kuweza kutumia na ikiisha anaweza kuchaji kwa nishati ya jua au sola.
Kuna surprise kibao kwenye Ligi Kuu Tanzania bara ambazo tumeziona baada ya Game week mbili. Matumizi ya washambuliaji wawili Timu kuhamia back-four Mawinga wenye speed Singida Big Star Aziz Ki vs Chama Sikiliza episode hii kuyajua yote hayo kisha tupe maoni yako
Na Afisa Lishe Mtafiti Fatma Mwasora kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC)
Serikali ya Albanese ili ahidi kabla ya uchaguzi mkuu kuwa, ita futa matumizi ya malipo ya kadi ya benki yenye utata.
Tume ya Haki za Kibinadamu ya Kenya na mashirika mengine sita ya kiraia yanaeleza uamuzi wa IEBC unatishia kuwafungia nje wapigakura wengi waliohitimu zoezi hilo iwapo mitambo ya kielektroniki ya kutambua wapigakura itashindwa kufanya kazi siku ya uchaguzi Agosti 9
Je! unafahamu matumizi ya namba 116? katika kuhakikisha tunawalinda watoto wetu katika jamii yetu.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kwa ushirikiano na kituo cha kimarekani cha kudhibiti magonjwa, CDC wamesaidia ujenzi wa tenki za maji kwa ajili ya wakazi wa Kiziba mjini Goma, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na hivyo kusaidia kuepusha maambukizi ya magonjwa yatokanayo na matumizi ya maji machafu.
Mchanga na changarawe ni bidhaa muhimu sana na zinazoshika nafasi ya pili zinazotumika zaidi duniani kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP, na hivyo matumizi yake yanapaswa kufikiriwa upya na kwa kina.
Malaria ni ugonjwa unaozuilika na unaotibika. Hata hivyo kila mwaka malaria huwakumba zaidi ya watu milioni 200 na kuua zaidi ya 600,000. Vifo vingi kati ya hivi karibu nusu milioni miongoni mwao ni watoto wadogo katika bara la Afrika
Nchi wanachama 193 wa baraza la umoja wa mataifa zimepitisha azimio lanalohimiza matumizi ya baiskeli katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. UN inatoa wito kwa mataifa kujumuisha baiskeli katika mfumo wa usafiri wa uma katika maeneoya mijini na vijijini katika mataifa yanaoendelea na yalioendelea.
Tunaangazia sababu za kuwepo mwitiko mdogo wa matumizi ya kondomu nchini Kenye licha ya kupendekezwa kuwa mpango ambao unamlinda mtu kutokana na hatari ya kupata virusi vya HIV na magonjwa ya zinaa.
Tunaangazia ufahamu ya matumizi ya kondomu, aina mbali mbali za kondomu na namna zinatumika na watu wa mbali mbali.
Tarehe 23 mwezi uliopita wa Novemba mwaka huu wa 2021, Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO liliridhia tarehe 7 mwezi Julai kila mwaka kuwa siku ya kimataifa ya Kiswahili. Hatua hii imezingatia misingi mbalimbali ikiwemo nafasi ya lugha hiyo katika kuleta utangamano katika jamii, kuwa chanzo cha kipato na hata kusongesha amani na usalama. Uamuzi huo umepitishwa huku nchi mbalimbali za Afrika zikichukua hatua kuimarisha matumizi ya lugha hiyo ikiwemo nchini Uganda ambako serikali ya Uganda imeimarisha utafiti kote nchini ili kubaini kwa nini lugha ya Kiswahili haikui kama inavyotarajiwa katika nchi hiyo mwanachama mkongwe wa Jumuiya ya Afrka Mashariki. Utafiti huo unaotekelezwa kupitia Idara ya lugha ya Chuo Kikuu cha Makerere unalenga pia kuhamasisha wananchi kuhusu manufaa ya lugha ya Kiswahili na kubaini mikati ya kukuza lugha hiyo adhimu huku walengwa zaidi wakiwa ni vijana. Kwa kina kuhusu kinachofanyika ungana na mwandishi wetu wa Uganda John Kibego akizungumza na Dokta Caroline Asiimwe Mhadhiri kwenye Chuo Kikuu cha Makerere, alipokutana naye akifanya utafiti kuhusu lugha hiyo katika jiji la Hoima magharibi mwa Uganda.
Matumizi ya dawa, Mafanikio ya mtinko sekondary
Matumizi ya dawa, Mafanikio ya mtinko sekondary
Makala ya gurudumu la uchumi juma hili inaangazia mjadala kuhusu matumizi sahihi ya fedha za uma kwa maendeleo.
Makala ya gurudumu la uchumi juma hili inaangazia mjadala kuhusu matumizi sahihi ya fedha za uma kwa maendeleo.
Matumizi ya tehama katika kufundishia wanafunzi wa shule ya msingi nchini Kenya yaliyofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF yameongeza ufaulu wa watoto na kupunguza utoro. (Taarifa ya Leah Mushi( Pause) Ni James Lokeny, mwanafunzi ya darasa la 8 katika shule ya msingi ya Namoruputh iliyoko kaunti ya Nakuru nchini Kenya akieleza kuwa hapo awali kabla ya UNICEF kuwafungia intaneti katika shule yao mawasiliano yalikuwa mabovu lakini sasa ni mazuri na wanaweza kusoma kwakupitia kompyuta ndogo au tablet. Anasema akijifunza kupitia kompyuta masomo yanakuwa rahisi kwakuwa ana uwezo wa kuona vitu vingi ikilinganishwa na kujifunza darasani pekee kwakutumia kitabu na anafuraha maana tayari matokeo yake yanaonesha ufaulu umeongezeka. Mwalimu Justus Kingoo anasema zaidi ya kufaulu sasa hakuna utoro kwa wanafunzi ."Sasa, wengi wao kwa kuwa wanaweza wakajifunza wenyewe, na wakagundua vitu wenyewe, mtazamo wao umebadilika sana. Wakiwa na hizi komptuta ndogo kujifunza kwao kunavutia, kwasababu kuna njia mbalimbali za kuipata taarifa moja. Unapata kuona hamu ya wanafunzi wengi. Mathalani, ukiwaambia kesho somo hili tutasoma kidijitali, hakuna hata mtu mmoja atakaye kosa shule." Naye Andrew Brown, mkuu wa mawasiliano,uhamasishaji na uhusiano wa UNICEF nchini Kenya anaeleza sababu za kuwekeza kwa wanafunzi hawa wa vijijini. “Duniani kote, kupitia program yetu ya kujifunza ya kufikiria upya, tunajaribu kufanya kusoma kwa kupitia mtandao kuwa miongoni mwa haki zao za msingi za kusoma kama masomo mengine, kwa wanafunzi wote. Na hii itasaidia kuondoa utofauti mkubwa uliopo baina ya wanafunzi ambao wanauwezo wa kupata masomo kijiditali, na wale ambao hawana uwezo huo. Na utofauti huu mkubwa, ulionekana zaidi wakati wa janga la COVID-19 ambapo wanafunzi wenye uwezo wa kupata mitandao walikuwa wakiendelea na masomo, wakati wale wengine wakishindwa kuendelea na masomo.” Malengo ya maendeleo endelevu SDGs yanahamasisha kuondoa utofauti baina ya matabaka katika jamii, kuleta usawa pamoja na kuhakikisha watu wote wanapata elimu bila kumuacha mtu yeyote nyuma.
Historia kidogoZaidi huduma nyingi kwenye mtandao ilikuwa unalipia mara moja tuuHii ilikuwa ngumu lakini ukiweza lipia unakuwa umemaliza hiyo kitu kwa miaka michacheSasa huduma zimebadilika utasikia manen mengi Software as a Service Hardware as a Service Na hizo subscriptionLengo ni kupunguza gharama za mwanzo na kufanya gharama kuwa nafuu lakini utalipa kila mwezi which posses a riskUtajikuta sasa kila mwisho wa mwezi una lundo la mambo ya kulipia, bado hujalipa bill za maji na umeme.Kama hutokuwa mwangalifu unaweza kujikuta umekatwa pesa kwa subscription zisizo za msingi.
Tatizo la nguvu za kiume ni tatizo gani? Linaathiri wanaume wangapi duniani? Chanzo cha hili tatizo ni nini? Matumizi ya dawa za asili kama “Vumbi la Congo” na “Al Kasusi” ni kweli yanasaidia kutatua tatizo hili? Ni tatizo linalotibika? Kuna madaktari wanaoweza kusaidia kwenye hili tatizo? Linahusiana vipi na afya ya akili? Mbona mara nyingine hili tatizo kama linapotea na mara nyingine kama linarudi? Kuna suluhisho la kudumu? Haya ni baadhi ya maswali ambayo wanaume wengi sana hujiuliza kuhusiana na “Nguvu za Kiume”. Katika nia ya kujenga na kuboresha afya ya akili kwa wanaume, episode hii imeamua kuzungumzia hili tatizo kwa undani tukiwa na matumaini kwamba kwa yeyote atakayesikiliza basi ataweza kupata taarifa za kina na taarifa sahihi. Michael pamoja na Nadia wamefanya mazungumzo ya kina na “Urologist” kutoka Tanzania, Dr Boio Nyamwihura ili kupata ukweli na taarifa zaidi kutusu mwanaume na “nguvu za kiume”
Mvutano wa matumizi ya maji ya mto Nile, bado ni kizungumkuti kati ya Ethiopia, Sudan na Misri na rais wa DRC Felix Thisekedi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, anazuru nchi hizo kujaribu kupata suluhu. Unadhani rais Thisekedi atapata suluhu ? Haya hapa baadhi ya maoni yenu msikilizaji.
Mataifa kadhaa ya Afrika yameharibu chanjo vya covid 19 kutokana na muda wake wa matumizi kupitwa na wakati, hivi punde DRC, ikitajiwa kupeana baadhi ya chanjo yake, ili kuzuia chanjo hiyo kuharibika. Katika makala haya wasikilizaji wanatoa maoni yao kuhusiana na chanjo hiyo ya corona kuharibika kwa kipindi kifupi.
Matumizi ya mkaa mbadala
Matumizi ya mkaa mbadala
Kiswahili ni Lugha ya Taifa na Matumizi ya Kiswahili yanazidi kukua kadri siku zinavyozidi kwenda, pamoja na kukua kwa lugha hii, Kiswahili kimekuwa hakitumiki katika mfumo mzima wa utoaji haki, kwa maana ya kwamba sheria zote za nchi yetu bado zipo kwa lugha ya Kiingereza na hata Mahakama zetu kuanzia ngazi ya Mahakama ya wilaya mpaka Mahakama ya rufani, lugha inayotumika ni Kiingereza. Kitu ambacho kimekuwa ni changamoto kwenye shughuli mbali mbali za utoaji haki. Lugha ya Kiswahili nchini imekuwa ikitumika kwenye mabaraza yote na Mahakama zote za Mwanzo tangu mwaka 1985 kwenye kuendesha mashauri na kutunza kumbukumbu zote, lakini kwenye mahakama za wilaya mpaka mahakama ya rufani, lugha ya kiswahili imekuwa ikutumika kuendesha mashauri laikini kumbukumbu zote za mahakama zimekuwa zikiandikwa kwa Kiingereza. Serikali kupitia Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania, wamepetisha mswada wa mabadiliko ya sheria (Written Laws (Miscellaneous Amendments) Bill of 2021 (Muswada), kupendekeza sheria zote za Tanzania Bara kuwa kwa Lugha ya Kiswahili; Hivyo basi katika kipindi hiki tunajadili kiundani ni nini dhumuni kuu la Serikali katika kuleta mapendekezo haya na ni nini zitakuwa changamoto za mabadiliko hayo, kama wanasheria na maafisa wa mahakama ni nini kingine cha ziada kinaweza kufanyika katika kuhakikisha lugha hii yetu adhimu inakuwa na kuendelea kutumika. --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/sheriapoa/message
1. Uhuru wa kifedha. Uhuru wa kifedha ni zaidi ya kuwa na fedha, uhuru wa kifedha ni kuwa mtu ambaye unatakiwa kuwa maishani na kuweza kufanya au kupata kile unachokihitaji maishani. Hata hivyo pesa ni muhimu sana kwenye suala la uhuru wa kifedha,ingawa pesa hizi zinatakiwa ziambatane na fikra sahihi. Kwa njia ya kujiwekea akiba utaweza kujijengea msingi mzuri wa kifedha ambao ukiambatanishwa na fikra sahihi utakuletea uhuru wa kifedha. 2. Matumizi mazuri ya pesa. Kama nilivyoeleza hapo mwanzo kuwa kuweka akiba sio kuwa na pesa nyingi bali ni maamuzi na mipango stahiki pekee. Hivyo kuweka akiba kutakufaidisha kwa kukuwezesha kutumia pesa vyema.ikiwa unapata elfu 10 kwa siku,itakubidi uitumie vizuri ili uweze kutenga pesa ya akiba. Kama huweki akiba huna haja ya kutumia pesa vyema kwani hakuna sehemu ya akiba inayotakiwa kutengwa. 3. Kujiandaa kwa dharura Watu wengi huingia kwenye madeni au kupata uhitaji mkubwa wa pesa mara wapatwapo na dharura. Hivyo kwa kuweka akiba utapata faida ya kukuepushia mahangaiko wakati wa dharura kama vile magonjwa, misiba majanga n.k 4. Kuweza kufanya manunuzi au miradi ya gharama kubwa Kuna manunuzi au miradi inahitaji pesa nyingi ili kuitekeleza. Maswala kama vile ujenzi wa nyumba, ununuzi wa viwanja kununua gari n.k, ni baadhi ya mambo yanayohitaji fedha nyingi. Hivyo,kwa kuwa na akiba utaweza kutekeleza mambo haya kwa urahisi kuliko ungeyafanya bila akiba. 5. Kuweza kumudu wanaokutegemea Ikiwa kuna watu wanaokutegemea kama vile wazazi, ndugu au watoto ni vyema kuweka akiba ili uwe na fedha ya kukidhi mahitaji yao mara wapatwapo na uhitaji. Kutokuweka akiba kutakufanya uhangaike huku na huko ili kutafuta pesa ya kukidhi mahitaji ya wategemezi wako kama vile chakula, matibabu au hata ada za shule. 6. Utulivu wa akili Unapokuwa huna akiba yoyote huwezi kuwa na utulivu wa akili, Kila wakati unahofu na wasiwasi juu ya maisha yako, unajiuliza likitokea tatizo itakuwaje? au hitaji fulani linalokuja hivi karibuni itakuwaje?n.k Unapokuwa na fungu fulani la akiba huna haja ya kuwa na wasiwasi kwa unajua hata ukikosa pesa akiba yako itakusaidia. 7. Hukuwezesha kuandaa kesho vyema Maandalizi ya kesho yanafanywa leo.kuweka akiba maana yake unajiandaa na mahitaji ya kifedha ya baadaye yaani kesho.mtu asiye kuwa na akiba mara nyingi hafikirii Kuhusu kesho wala hamna malengo kwa ajili ya baadaye yake. Ili kujenga baadae au kesho njema,ni muhimu pia kuimarisha msingi wako wa kiuchumi kwa njia ya kuweka akiba. 8. Hukuwezesha kuwahi fursa Ni mara ngapi umekuwa ukisema au ukisikia kauli kama vile" ningekuwa na pesa ningenunua hiki kitu",au "ningekuwa na pesa ningejiunga kwenye hii huduma" au "ningekuwa na pesa ningejiunga kwenye huu mradi".n.k Hili kinadhihirisha watu hukosa fursa mbalimbali kutokana na kukosa akiba ya pesa,unapokuwa na akiba ya pesa ni rahisi kuwahi fursa mpya au bidhaa zenye manufaa mara zinapopatikana. Hitimisho Fedha ni jambo linalohitaji nidhamu na busara ya hali ya juu, vivyo hivyo kuweka akiba ni swala linalohitaji kufanya maamuzi sahihi ili uweze kulitekeleza.
Matumizi mabaya ya vyombo vya habari