POPULARITY
Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) ya takwimu za afya duniani iliyochapishwa jana Mei 15 ikionesha athari kubwa zaidi za kiafya zilizosababishwa na janga la COVID-19 kuhusu vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla, imeweka wazi kuwa katika kipindi cha miaka miwili pekee, kati ya mwaka 2019 na 2021, matarajio ya kuishi yalipungua kwa mwaka mmoja na miezi nane ikiwa ni maporomoko makubwa zaidi katika historia ya hivi karibuni hali iliyobatilisha mafanikio ya afya yaliyopatikana kwa muongo mmoja.
Hii leo jaridani tunaangazia uhakika wa chakula, na takwimu za afya za janga la COVID-19 kusababisha vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla. Makala tunakwenda nchini Tanzania na mashinani nchini DRC, kulikoni?Ukosefu wa uhakika wa kupata chakula na utapiamlo kwa watoto uliongezeka kwa mwaka wa sita mfululizo mwaka 2024, na kuwatumbukiza mamilioni ya watu karibu na baa la njaa, huku wengine wakiepuka kutokana na misaada ya kimkakati. Imesema Ripoti ya Kimataifa kuhusu Janga la Chakula (GRFC) iliyotolewa leo huko Roma, Italia na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO.Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) ya takwimu za afya duniani iliyochapishwa jana Mei 15 ikionesha athari kubwa zaidi za kiafya zilizosababishwa na janga la COVID-19 kuhusu vifo, muda wa kuishi na hali ya afya na ustawi kwa ujumla, imeweka wazi kuwa katika kipindi cha miaka miwili pekee, kati ya mwaka 2019 na 2021, matarajio ya kuishi yalipungua kwa mwaka mmoja na miezi nane ikiwa ni maporomoko makubwa zaidi katika historia ya hivi karibuni hali iliyobatilisha mafanikio ya afya yaliyopatikana kwa muongo mmoja.Katika makala Leah Mushi anatupeleka nchini Tanzania kusikia namna wanawake wenye ulemavu walivyoweza kujikwamua kutoka kwenye changamoto mbalimbali ikiwemo za kiuchumi na kuchangamkia fursa za uongozi.Na katika fursa ni yake Bernadette Kambonesa, mkimbizi wa ndani kutoka kijiji cha Bogoro, jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akizungumzia manufaa yatokanayo na uwepo wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini humo (MONUSCO).Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Ripoti mpya kuhusu “Hali ya Hewa Afrika 2024” iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Utabiri wa Hali ya Hewa Duniani WMO imeonya kwamba muongo wa joto zaidi kuwahi kushuhudiwa Afrika umeleta madhara makubwa kwa bara hilo. Evarist Mapesa na taarifa zaidi
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa ambayo Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili alipata fursa ya kuzungumza na kiongozi wa kijamii kutoka Jamii ya wafugaji ya Wamaasai mkoani Morogoro nchini Mashariki mwa Tanzania Adam Kulet Ole Mwarabu.Wiki kumi baada ya kuanza kwa mzingiro kamili wa Israel dhidi ya wakazi wa Gaza, zaidi ya robo tatu ya kaya katika eneo la Palestina kuna uhaba mkubwa wa huduma ya maji, huku hali ya usafi ikizidi kuwa mbaya, yameonya leo mashirika ya misaada ya Umoja wa Mataifa huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu athari za "uhaba huo wa maji kwa kuzingatia kuwa msimu wa joto unakaribia.”Ripoti kutoka Sudan zikidai kwamba juzi jumatano kulikuwa na jaribio la mashambulizi mapya ya ndege zisizo na rubani dhidi ya kitovu muhimu cha misaada nchini humo juzi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kupitia tamko alilolitoa jana jioni kwa saa za New York, Marekani, ameongeza nguvu yake katika kutoa wito unaozidi kuwa wa muhimu kuhamasisha kuanzishwa kwa mazungumzo ya amani ya kweli.Kufuatia kuendelea kwa mvutano wa majirani, India na Pakistani, Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Philemon Yang, ametoa wito wa kuzitaka nchi hizo mbili kuchukua tahadhari na kuepuka hatua zinazoweza kuongeza mzozo. Balozi Yang anasisitiza mazungumzo ya amani na kufuata sheria za kimataifa ndiyo njia pekee ya kusuluhisha migogoro.”Na katika jifunze Kiswahili leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno "DALALI”Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha hapa makao makuu ambako Idhaa hii Dokta Willis Ochieng kutoka Kenya aliyehudhuria ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na masuala ya kilimo na maendeleo. Pia tunakuletea muhtasari wa habari, na mashinani tunakwenda Ghana.Ukuaji wa maendeleo ya binadamu – yanayopimwa kwa uhuru na ustawi wa watu – umeendelea kuwa wa kasi ndogo tangu mshtuko mkubwa wa janga la COVID-19 lakini kuna matumaini makubwa kwamba Akili Mnemba au AI, ikiwa itatumika kwa njia sahihi, inaweza kuwa chombo chenye nguvu cha kuboresha maisha ya mamilioni ya watu. Hii ni kwa mujibu wa Ripoti ya kila mwaka ya Maendeleo ya Binadamu iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo duniani, UNDP.Kulengwa kwa hospitali ya Médecins Sans Frontières nchini Sudan Kusini kunaweza kuwa uhalifu wa kivita imeeleza leo Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu Sudan Kusini kufuatia mashambulizi ya angani yaliyotekelezwa dhidi ya hospitali ya Médecins Sans Frontières (MSF) huko Old Fangak, Jimbo la Jonglei mapema majuzi asubuhi ya Jumamosi na kusababisha vifo vya takribani raia saba na kujeruhi wengine. Shambulio hilo lilifanyika baada ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Sudan Kusini (SSPDF) kutoa onyo la kufanya shambulizi iwapo dai lao la kuachiliwa meli zao zilizotekwa halitatekelezwa.Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, iliyotolewa leo imeonesha jinsi mahali mtu anakozaliwa kulivyo na mchango katika maisha yake. Ripoti inasema, “mahali mtu anakozaliwa huweza kuamua kama ataishi zaidi ya miongo mitatu kuliko mtu mwingine aliyezaliwa katika nchi yenye hali duni za makazi, elimu na fursa za ajira.”Na mashinani leo nampa fursa Dorcas Awortwe, Naibu Mkurugenzi wa Tume ya Maendeleo ya Kanda ya Kati kutoka Ghana, aliyeshiriki kwenye mkutano wa jukwaa la watu wa asili hapa Makao Makuu wiki iliyopita anazungumzia changamoto zinazowakabili watu wa asili katika jamii yake na ombi lake kwa Umoja wa Mataifa.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Maambukizi ya ugonjwa wa mpox kutokana na aina ya virusi vya monkeypox clade Ib /ˈmʌŋ.ki.pɑks kleɪd one bee/ (MPXV) yanaendelea kuripotiwa hasa barani Afrika, ambapo mataifa kumi na moja yameripoti maambukizi ya ndani ya jamii katika kipindi cha wiki sita zilizopita. Hiyo kwa mujibu wa ripoti 51 ya Shrika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO kuhusu hali ya mlipuko wa mpox katika nchi mbalimbali duniani. Anold Kayanda amefuatilia ripoti hiyo na anatufafanulia kwa ufupi.
Ripoti hiyo mpya ya UN Spotlight initiative, imebaini kuwa mabadiliko yatabianchi yameendelea kuzidisha mogogoro ya kijamii na kiuchumi ambayo inachochea kuongezeka kwa viwango vya unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana.
Ripoti ya umoja wa mataifa inaonesha dunia ipo nyuma sana katika kudhibiti ongezeko la joto chini ya nyuzi joto 1.5.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambayo tunasalia hapa makao makuu katika mkutano wa CSW69 uliokunja chamvi Ijumaa wiki jana, tunamsikia aliyekuwa Katibu Mkuu wa Mkutano wa 4 wa Umoja wa Mataifa wa Wanawake, Mkutano wa Beijing Bi. Gertrude Mongella.Hapa New York, Umoja wa Mataifa leo umetoa wito wa kuachiliwa kwa wafanyakazi wake wanaoshikiliwa kote ulimwenguni ambao wamejikuta matatani wakati wakiwahudumia watu walio katika hatari, huku wakihatarisha usalama wao binafsi kwa kukabiliwa na vitisho vya kutekwa nyara, vurugu, unyanyasaji, na kifungo katika maeneo yenye migogoro na majanga.Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kuhusu vifo vya watoto imeonya kwamba miongo ya maendeleo katika kupunguza vifo vya watoto na watoto wachanga wakati wa kuzaliwa yako hatarini kutokana na kupunguzwa kwa ufadhili. Idadi ya vifo vya watoto wa chini ya umri wa miaka mitano ilipungua hadi watoto milioni 4.8 mwaka 2023, huku vifo vya wakati wa kuzaliwa vikiendelea kubaki takriban milioni 1.9.Leo ni Siku ya Kimataifa ya Kumbukumbu ya Waathirika wa Utumwa na Biashara ya Watumwa ya Bahari ya Atlantiki, ikiwakumbuka mamilioni ya Waafrika walioteswa, kunyanyaswa, na kunyimwa utu wao. Katika ujumbe wake wa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema “Kwa zaidi ya karne nne, mamilioni ya Waafrika walitekwa kwa nguvu, kusafirishwa kwa meli hadi mataifa ya kigeni, na kufanyishwa kazi katika hali mbaya za kikatili.”Na katika mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP, Lea mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye sasa amekimbilia Burundi na familia anasilimua hali ilivyokuwa wakati wa kukimbia.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Hii leo jaridani katika mada kwa kina tunajikita katika mkutano CSW69 ambao umebakiza siku moja tu, kesho Machi 21 unakunja jamvi, na tunamsikia Dkt. Dorothy Gwajima, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Tanzania, Waziri Riziki Pembe kutoka Zanzibar na Profesa Smile Dzisi, Mkugenzi wa Shirika la “I believe Global” kutoka Ghana.Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR Filippo Grandi amesema kukata ufadhili kwa mashirika yanayotoa huduma za kibinadamu kunasababisha janga la uwajibikaji. Kupitia taarifa iliyotolewa leo Geneva, Uswisi na UNHCR, Bwana Grandi amesema kukata ufadhili kunaweka hatarini maisha ya mamilioni ya watu na madhara yake kwa watu wanaokimbia majanga, yatakuwa makubwa zaidi na yataonekana wazi ikiwemo wanawake na watoto wa kike kukosa huduma zitokanazo na kubakwa.Leo ni siku ya furaha duniani maudhui yakimulika umuhimu wa watu kusaidiana na kujaliana katika masuala mbalimbali ikiwemo chakula. Ripoti mpya ya wadau wa UN iliyozinduliwa leo imeonesha kuwa nchi yenye furaha zaidi duniani ni Finland na ya mwisho kabisa ni Afghanistani. Katika 10 bora zenye furaha hakuna hata moja ya Afrika, ilihali kwenye 10 za mwisho nchi za Afrika ni 7 ambazo ni Lesotho, Comoro, Botswana, Zimbabwe, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Malawi na Sierra Leone.Mkutano wa 69 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW69 ukikaribia ukingoni hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa tumemuuliza mshiriki Wakili Rosemary Mwaipopo kutoka Tanzania mkutano umekidhi kiu yake ya kusongesha usawa wa kijinsia?Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya maneno “Ashiraf, Janabi, gayagaya, kiti cha marimba na kiti cha msaji”Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Ripoti mpya ya Chuo cha Monash imeonesha matukio ya unyanyasaji dhidi yawa Islamu wa Australia, yali ongezeka zaidi ya mara mbili kati ya Januari 2023 na Novemba 2024.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Umoja wa Mataifa kupitia miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa Pamoja wa Kigoma, KJP nchini Tanzania, unaolenga kuhakikisha wanawake na wasichana wanajumuishwa kwenye mipango ya kuhimili na kukabili mabadiliko ya tabianchi, kwa kuwajengea uwezo.Kuelekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake Machi 8, tathmini mpya ya Umoja wa Mataifa iliyowekwa wazi leo ikiangazia haki za wanawake miaka 30 baada ya Azimio la Beijing inaonesha uwepo wa maendeleo katika usawa wa kijinsia, kama vile sheria dhidi ya ubaguzi na sera jumuishi za kijinsia. Hata hivyo, ripoti hiyo inaeleza uwepo bado wa ubaguzi wa kijinsia uliojikita katika jamii, ukiendelea kuwazuia wanawake na wasichana kupata fursa.Ripoti nyingine ya Umoja wa Mataifa iliyochapishwa leo ikiangazia Sudan imefichua vitendo vya watu kukamatwa kiholela, mateso, na unyanyasaji huko Khartoum vinavyotekelezwa na Vikosi vya wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF) na pia Jeshi la Serikali ya Sudan (SAF). Ripoti hiyo imearifu pia kuwa makumi ya maelfu ya watu wamewekwa katika mazingira duni tangu Aprili 2023.Kutokana na kupungua kwa ufadhili wa misaada ya kibinadamu duniani, Umoja wa Mataifa leo jijini Geneva, Uswisi kutenga dola milioni 110 ili kusaidia majanga yaliyopuuzwa katika nchi 10 barani Afrika, Asia, na Amerika Kusini, zikiwemo Niger, Somalia, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Zambia.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia maana ya methali “MCHAWI AKIFICHUA MIRIMO YA WACHAWI HU UAWA”.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Karibu jaridani hii leo na mwenyeji wako ni Flora Nducha akikuletea habari kuhusu haki za binadamu, elimu ya STEM kwa wasichana wakimbizi nchini Kenya; Harakati za kuhamishia wakimbizi wa DRC nchini Burundi kuelekea maeneo salama; mafunzo ya ujasiriamali wa ushoni kwa wanawake na wasichana.Kwenye mkutano wa 58 wa Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu unaoendelea mjini Geneva Uswisi, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu Volker Türk , amezungumzia hali ya kuzorota na kutoeleweka inayohusu haki za binadamu duniani, akionya kwamba ushawishi wa viongozi wa kiimla, matajiri wakubwa, na viongozi wa kimabavu unatishia kuvuruga maendeleo ya miongo kadhaa. Ripoti yake Anold Kayanda.Nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na wadau wengine wanafanikisha mpango wa kuhamasisha wasichana kuingia katika masomo ya STEM yaani Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati.Ripoti yake Sharon Jebiichi.Makala Assumpta Massoi anakupeleka mpakani mwa Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kusikia harakati za kuhamishia wakimbizi eneo salama zaidi.Mashinani anasalia nchini Jamhuri ya kidemkrasia ya Congo DRC kusikia jinsi ambavyo mafunzo ya ujasiriamali wa ushoni yanavyowawezesha wanawake na wasichana kujimudu kimaisha. Karibu
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo mjini Geneva Uswisi na ofisi ya haki za binadamu (OHCHR) imefichua kuwa viongozi wa juu wa serikali ya Bangladesh walihusika moja kwa moja katika ukandamizaji wa maandamano makubwa yaliyoitikisa nchi hiyo mwaka 2024 na kusababisha vifo vingi. Flora Nducha na taarifa zaidi
Hii leo jaridani tunaangazia matokeo ya maandamani nchini Bangladesh, na machafuko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Makala inatupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Tanzania, kulikoni?Ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo mjini Geneva Uswisi na ofisi ya haki za binadamu (OHCHR) imefichua kuwa viongozi wa juu wa serikali ya Bangladesh walihusika moja kwa moja katika ukandamizaji wa maandamano makubwa yaliyoitikisa nchi hiyo mwaka 2024 na kusababisha vifo vingi.Baada ya waasi wa M23 jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kupatia wakimbizi waliokuwa wamesaka hifadhi kambini mjini Goma, wawe wamerejea makwao ndani ya saa 72 kuanzia juzi jumatatu, mamia wameanza kutii amri hiyo licha ya hofu inayowakabili ya kule wanakotakiwa kurejea.Makala inatupeleka jijini Nairobi, Kenya ambako ambako Kevin Keitany wa redio washirika wetu Domus FM kwa kuzingatia kuwa kesho Februari 13 ni Siku ya Kimataifa ya Redio, ametutumia maoni ya vijana wawili wanaozungumzia namna redio imewasaidia kusambaza ujumbe wao kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.Mashinani fursa ni yake Tupokigwe Simon, msichana mwenye umri wa miaka 16, ambaye ni mwanaharakati wa Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na hisabati , STEM, wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, akieleza umuhimu wa msichana katika sayansi na kuwahimiza wasichana wenzake kusoma sayansi.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Hali ya usalama kwenye mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini, Goma, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ikiendelea kuwa tete, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani, nchini humo, MONUSCO pamoja na SAMIDRC ambao ni ujumbe wa kulinda amani kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika, SADC wanadhibiti uwanja wa ndege wa Goma. Ripoti ya Selina Jerobon inafafanua zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia ripoti mpya kuhusu hali ya usalama na afya ya watoto kote duniani, na amnai na usalama nchini Syria. Makala inatupeleka nchini Uganda na mashinani nchini DRC, kulikoni?Ripoti mpya ya kila mwaka kuhusu mustakabali wa watoto ambayo imetolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, imeonya kwamba dunia inaingia katika zama mpya za majanga kwa watoto.Wasyria wana matarajio makubwa kwa nchi yao, na hamu kubwa ya watu kutoka katika kila nyanja ya jamii kuja pamoja na kuunda katiba mpya, ambayo lazima ianze na mazungumzo ya kitaifa yaliyo jumuishi. Hayo ni kwa mujibu wa Najat Rochdi, Naibu Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Syria, ambaye amekuwa Damascus kukutana na wajumbe kadhaa wa mamlaka ya mpito ili kuhakikisha Wasyria wote wana uwezo wa kushiriki katika mustakbali wa nchi hiyo.Makala inatupeleka nchini Uganda ambako shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa muda sasa limekuwa likifanya jukumu muhimu katika kuwezesha usajili wa watoto.Na mashinani fursa ni yake Antoinette Nzale, mkimbizi wa ndani katika kijiji cha Fataki iliyoko Ituri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo, DRC akishuhudia jinsi ambavyo juhudi za pamoja za Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO na wanajeshi wa serikali FARDC zinavyowawezesha wakimbizi wa ndani kuanza kurejea katika mazingira yao ya awali taratibu.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Ripoti mpya ya kila mwaka kuhusu mustakabali wa watoto ambayo imetolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, imeonya kwamba dunia inaingia katika zama mpya za majanga kwa watoto . Taarifa ya Flora Nducha inafafanua zaidi
Hii leo jaridani tunakuletea mad akwa kina inayotupeleka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kumulika harakati za kusaidia manusura wa ukatili wa kingono na kijinsia kwenye mizozo. Pia tunakuletea muhtasari wa había za Sudan, Uganda na Tanzania, Mashinani tunarejea Sudan.Ripoti ya Kamati ya Tathmini ya Viwango vya Njaa (IPC) iliyotolewa leo inaeleza kwamba imegundua kuwa kuna maeneo matano zaidi nchini Sudan ambayo yanakabiliwa na baa la njaa kati ya mwezi huu wa Desemba na Mei mwaka ujao wa 2025. Ripoti hiyo imeyataja maeneo hayo kuwa ni ya Darfur Kaskazini yaani Um Kadadah, Melit, El Fasher, Twawisha, na Al Lait.Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limekaribisha mchango wa EURO milioni 1 kutoka serikali ya Ujerumani ili kusaidia shughuli za lishe na ustawi kwa zaidi ya wakimbizi na wasaka hifadhi 254,000 nchini Uganda ambayo inawahifadhi wakimbizi milioni 1.7.Na Kikosi cha 7 cha Walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, TANBAT 7 kilichokuwa kinahudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kuleta Utulivu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR (MINUSCA) kimerejea nyumbani Tanzania kikijivunia kuwa kikosi cha kwanza cha nchi hiyo kupokea barua ya pongezi kutoka Umoja wa Mataifa.Mashinani fursa ni yake Najwa Mohamed, mama mjamzito kutoka Jabal Moya nchini Sudan ambaye amepoteza makazi yake kufuatia vurugu zinazoendelea nchini humo na kulieleza Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi, UNFPA kwamba hali ni ngumu hasa kwa wanawake wajawazito.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Mwaka 2020 Ghana iliripoti kuwa na watu 350,000 wanaioshi na virusi vya Ukimwi na kati yao hao 31,000 walikuwa ni wajawazito. Jambo lililoshtua ni kwamba ni sehemu ndogo mno ya wajawazito hao ndio walipimwa kufahamu iwapo wana VVU au la. Jambo lililofanya serikali kwa kushirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kuchukua hatua. Ripoti ya Assumpta Massoi inafafanua zaidi.
Hii leo jaridani tunaangazia uzinduzi wa ombi la ufadhili wa mahitaji ya Kibinadamu (GHO), na umuhimu wa lugha mama katika kukuza haki za binadamu. Makala tunasalia hapa makao makuu ya umoja wa mataifa na mashinani tunakupeleka nchini Senegal, kulikoni?Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) ikizindua Ripoti ya Kimataifa ya mahitaji ya Kibinadamu (GHO) kwa mwaka ujao wa 2025 imetangaza ombi la ufadhili kwani takriban watu milioni 305 duniani kote watahitaji msaada wa kibinadamu katika mwaka ujao.Haki si haki iwapo inatolewa kwa lugha ambayo haileweki kwa wahusika, wamejulishwa washiriki wa mkutano wa pili wa wanazuoni unaofanyika hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York, Marekani na pia mtandaoni ukimulika Madaraka, Haki na Binadamu: Utawala wa Sheria na mabadiliko Afrika.Makala tunasalia hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambapo mkutano wa mwaka 2024 wa Taaluma kuhusu Afrika leo katika leo umeingia siku ya pili hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Mkutano huo ulioandaliwa na Ofisi ya mshauri maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Afrika UNOSAA ni wa siku tatu na umebeba maudhui "Nguvu, Haki, na watu” kwa ajili ya mabadiliko ya Afrika.Na mashinani fursa ni yake Antar sarr, Kijana mkulima wa mbogamboga kutoka Senegal ambaye ni mmoja wa wanufaika wa mradi wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya kilimo, IFAD unaowawezesha vijana nchini humo kwa kilimo na biashara ndogondogo ili kuondokana na fikra za kwenda Ulaya kusaka Maisha bora na ajira, akisema mradi huo imempatia matumaini.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) ikizindua Ripoti ya Kimataifa ya mahitaji ya Kibinadamu (GHO) kwa mwaka ujao wa 2025 imetangaza ombi la ufadhili kwani takriban watu milioni 305 duniani kote watahitaji msaada wa kibinadamu katika mwaka ujao. Selina Jerobon na maelezo zaidi.
Leo ni siku ya watoto duniani maudhui mwaka huu yakiwa "Kila mtoto, kila haki"na katika kuhakikisha sauti zao zinasikika kuhusu mustakbali wa utakao, shirika la Umoja wa Maataifa la kuhudumia watoto duniani UNICEF limewapa fursa ya kuandika barua kwenda kwa watu wazima kote duniani ili kutoa madukuduku yao na kutanabaisha wanachokitaka kwa ajili ya mustakbali wao. Hao ni baadhi tu ya makumi ya watoto walioandika barua , hawa ni kutoka Gaza, Tanzania na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC ambao walishika kalamu na karatasi kufikisha ujumbe wao kwa watu wazima wa dunia ya sasa iliyoghubikwa na changamoto lukuki zinazoweka rehani mustakbali wao.Kwa mujibu wa ripoti mpya ya UNICEF ya “Hali ya watoto duniani mwaka 2024: Mustakabali wa Utoto katika Ulimwengu Unaobadilika,” iliyotolewa leo sanjari na maadhimisho ya siku hii kuna masuala matatu makubwa ya kimataifa yatakatoathiri maisha ya watoto ifikapo 2050 na kuendelea. Mosi ni mabadiliko katika idadi ya watu, pili janga la mabadiliko ya tabianchi na migogoro na tatu teknolojiaUNICEF inasema yote haya ni changamoto na fursa ambazo watoto wanaweza kukabiliana nazo katika zama zijazo.Rafif mtoto mkimbizi wa ndani ameandika barua kutoka Palestina ambako vita imetamalaki, anasema“Ninatoka mjini Gaza na sasa nimefurushwa hadi Kusini mwa Gaza. kama watoto Ni haki yetu kuishi kwa usalama na kujenga mustakbali bora”Kutoka mashariki ya Kati hadi Afrika Mashariki kwa Steven akimulika afya“Na nianaandika kwenu kutoka Tanzania. Kwenye jamii yangu watoto wanaugua kila wakati , kwa nini? Huu ndio mustakbali wangu je unasikiliza?”Nako Congo DRC mitihani ni mingi, Andrea anasema“Nataka kushuhudia dunia ambayo kila mtoto anapendwa, dunia ambayo amani inashamiri ni raha na faraja. Napenda kuona hasira zinageuka na kuwa mazungumzo”Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiunga mkono suti hizo za watoto katika ujumbe wake amesema Katika Siku ya Watoto Duniani tunasherehekea washiriki wachanga zaidi wa familia yetu ya kibinadamu. Lakini leo pia ni wakati wa kutambua changamoto kubwa zinazowakabili watoto katika ulimwengu wetu uliogawanyika sana, wenye misukosuko na mara nyingi ulioshamiri ukatili.”Ripoti ya UNICEF imetoa wito wa kuwekeza katika elimu, miji endelevu na yenye mnepo kwa watoto, miundombinu inayohimili mabadiliko ya tabianchi, teknolojia, huduma muhimu na mifumo ya msaada wa kijamii na pia teknolojia iliyo salama kwa watoto ili kupambana na mzigo wa changamoto zinazowakabili.
Ripoti kuhusu mshikamano wakijamii imepata, kuna mitazamo michache chanya, kwa dini kote jimboni katika makundi yote makubwa ya imani.
Mkutano wa 29 wa mkataba wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi COP29 unaofanyika Baku Aberbaijana leo umejikita na ongezeko la gesi ya methane ambayo kwa kiasi kikubwa inachangiwa na shughuli za binadamu na nini kifanyike kuidhibiti. FKulingana na ripoti iliyozinduliwa leo na shirika la Umoja wa Mataifa wa mazingira UNEP katika mkutano huo, mfumo wa teknolojia ya hali ya juu ambao unatambua uvujaji mkubwa wa gesi ya methane umewasilisha tarifa 1,200 kwa serikali na makampuni katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, lakini ni asilimia moja tu ya taarifa hizo ndizo zilizofanyiwa kazi.Ripoti hiyo mpya iliyopewa jina “Jicho kwenye methane: Haionekani lakini inashuhudiwa” inasema licha ya ahadi zilizotolewa chini ya makubaliano ya ahadi za kimataifa za kupunguza uzalishaji wa gesi ya methane kwa asilimia 30 ifikapo 2030 hatua zinazochukuliwa hazitoshelezi kupunguza gesi hiyo.Ripoti imeangazia tahadhari za methane kutoka kwenye Mfumo wa Tahadhari na hatua dhidi ya Methane MARS, ambayo ni sehemu ya UNEP ya uangalizi wa kimataifa wa uzalishaji wa methane IMEO ambayo unawakilisha fursa ambazo haijatumiwa kwa hatua za haraka dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.Akizindua ripoti hiyo Inger Andersen, Mkurugenzi Mtendaji wa UNEP, amesema ili kuwa na nafasi yoyote ya kudhibiti ongezeko la joto duniani, uzalishaji wa methane lazima ushuke, na ushuke haraka."Tunapozingatia kuwa ni asilimia 1 tu ya taarifa 1200 ambazo tulitoa ndizo zilisababisha hatua kuchukuliwa, basi hauitaji kuwa mtaalamu wa hesabu ili kuhesabu ushindi mkubwa unaowezekana hapa. Tuna mifumo iliyothibitishwa ya kutambua uvujaji Mkubwa wa gesi ya methane ili uweze kukomeshwa haraka, mara nyingi kwa ukarabati rahisi na wakati mwingine tunazungumza juu ya kukaza mipira au kubadilisha vichungi.”Ameongeza, kuwa "Serikali na makampuni ya mafuta na gesi ambayo sehemu kubwa ya uchumi wa dunia bado inawategemea lazima waache kupiga domo kwa changamoto hii wakati majawabu yanawatazama usoni. Badala yake, wanapaswa kutambua fursa muhimu ambayo mfumo huu unatoa na kuanza kuchukua hatua kutokana na taarifa kwa kuziba uvujaji ambao unamwaga gesi ya methane ya joto kwenye angahewa.”Amehitimisha kwa kusema, "Serikali na sekta binafsi lazima zizuie uzalishaji wa methane, na lazima zifanye hivyo sasa."Gesi ya Methane kwenye angahewa ni kichocheo cha pili kikubwa cha ongezeko la joto duniani baada ya hewa ya ukaa au CO2 na ina nguvu zaidi ya mara 80 kuliko hewa ya ukaa katika kusambaa kwa muda mfupi.UNEP imesisitiza kuwa utoaji wa gesi ya methane duniani lazima upunguzwe kwa asilimia 40 hadi 45 ifikapo 2030 ili kufikia njia za gharama nafuu zinazopunguza ongezeko la joto duniani hadi kufikia nyuzi joto 1.5°C.Bado taarifa za sayansi za hivi karibuni zinaonyesha viwango vya angahewa vya methane vimepanda kwa kasi iliyovunja rekodi katika kipindi cha miaka 5 iliyopita.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka Havana Cuba amabpo Flora Nducha amaezungumza na mshiriki kutoka maitaifa mbalimbali na leo ni Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani inayotupeleka Zimbabwe.Kuongeza kiwango cha fedha kwenye ufadhili wa miradi ya kukabili na kuhimili tabianchi nchi ikiwa ni moja ya masuala muhimu yanayojadiliwa katika mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP29 huko Baku, Azerbaijan, leo ikiwa ni siku ya pili ya mkutano huo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema bila kupunguza kwa kiasi kikubwa hewa chafuzi, na kuimarisha miradi ya kuhimili na kukabili mabadiliko ya tabianchi, kila uchumi duniani utakumbwa na madhara makubwa.Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR iliyotolewa leo huko COP29 inaonesha ni kwa jinsi gani watu wanaokimbia vita, ghasia na mateso wanazidi kujikuta kwenye mazingira yaliyokumbwa na janga la tabianchi, janga ambalo linawaweka kwenye mchanganyiko wa vitisho, lakini bila fedha wala msaada wa kukabiliana navyo.Na mamia ya wakimbizi wanaotaka kujiunga na elimu ya juu sasa watafanya bure mitihani ya kuonesha umahiri wao wa lugha ya kiingereza, au IELTS. Hii inafuatia makubaliano ya ushirikiano kati ya UNHCR na mfumo wa kimataifa wa lugha ya kiingereza, IELTS.Na mashinani COP29 ukiendelea huko Baku Azerbaijan, tunabisha hodi nchini Zimbabwe ambako Umoja wa Mataifa unawasaidia wakulima kakabiliana na mabadiliko ya tabianchi.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Umaskini umeendelea kukithiri katika baadhi ya maeneo nchini Uganda Ripoti ya shirika moja lisilo la kiserikali nchini #Uganda, inayoonesha kuwa karibu asilimia 68 ya raia nchini humo wanapata ugumu kujikimu kimaisha kutokana umasikini.
Umaskini umeendelea kukithiri katika baadhi ya maeneo nchini Uganda Ripoti ya shirika moja lisilo la kiserikali nchini #Uganda, inayoonesha kuwa karibu asilimia 68 ya raia nchini humo wanapata ugumu kujikimu kimaisha kutokana umasikini.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina mada kwa kina inayotupeleka Zanzibar nchini Tanzania kupata ufafanuzi wa jukumu la “Zanzibar Maisha Bora Foundation” akitueleza Bi. Mariam Mwinyi ambaye pia ni Mke wa Rais wa Zanzibar, wakati wa ziara yake hapa Umoja wa Mataifa hivi karibuni. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ufafanuzi wa neno HEREREZA.Kwa mujibu wa ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo na mashirika yake lile la mpango wa chakula (WFP) na la chakula na kilimo (FAO), uhaba mkubwa wa chakula unatarajiwa kuongezeka kwa ukubwa na ukali katika nchi na maeneo 22 duniani. Ripoti hiyo inaonya kwamba kuenea kwa migogoro, hasa katika Mashariki ya Kati inasukuma mamilioni ya watu ukingoni.Mratibu wa Misaada ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Ukraine, Matthias Schmale, amelaani vikali shambulio la jana usiku lililotekelezwa na Jeshi la Urusi ambapo jengo la makazi la ghorofa nyingi lilipigwa katika mji wa Kharkiv, wa pili kwa ukubwa nchini Ukraine.Na ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya majiji, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amewapigia chepuo vijana akitaka sauti zao na mawazo yao kupewa nafasi kwani kuanzia harakati za chinichini hadi maabara za uvumbuzi, vijana wanasukuma hatua kabambe kukabiliana na tabianchi, wanaunga mkono ujumuishaji wa nishati mbadala, kazi zisizozalisha hewa chafuzi na usafiri safi wa umma, ambayo ni mambo yanayochangia kuunda miji endelevu ambapo kila mtu anaweza kustawi.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana ya neno HEREREZA!Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini DRC kufuatilia kazi za kituo cha Taifa cha Redio na Televisheni, RTNC huko Beni jimboni Kivu Kaskazini za kakabiliana na habari potofu. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na mashinani.Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo mjini Cairo, Misri, imebainisha kwamba athari za vita zimerudisha nyuma maendeleo huko Gaza kwa takriban miaka 69. Ripoti hiyo iliyoratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo UNDP na Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya Kiuchumi na Kijamii kwa Asia Magharibi imeonya kwamba bila kuondoa vikwazo vya kiuchumi na kuwekeza katika maendeleo, uchumi wa Palestina unaweza kushindwa kurejesha viwango vya kabla ya vita na kusonga mbele kwa kutegemea misaada ya kibinadamu pekee.Kiongozi wa timu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) ya kupambana na mlipuko wa ugonjwa wa Marburg Dkt. Janet Diaz ameeleza kwamba uongozi thabiti wa serikali ya Rwanda umewezesha kufanya uamuzi wa haraka na kuchukua hatua kuanzisha mwitikio wa sekta mbalimbali dhidi ya mlipuko wa sasa wa ugonjwa huo wa Marburg nchini humo.Na uongozi wa Kikosi cha Muda cha Umoja wa Mataifa nchini Lebanon (UNIFIL) umeendelea kusisitiza kwamba pamoja na changamoto zilizopo, walinda amani wa UNIFIL wanaendelea kufanya kazi kwa karibu na jamii za kusini mwa Lebanon ili kuwezesha utoaji wa misaada ya kibinadamu kwa wenye uhitaji. Hivi karibuni kumekuwa na mashambulizi dhidi ya walinda amani hao wa Umoja wa Mataifa yanayotekelezwa na majeshi ya Israeli.Mashinani kupitia video ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya Kibinadamu na misaada ya dharura OCHA tunamuangazia mmoja wa watu waliokimbia makazi yao akiwa katika shule ya Al Rimal, akielezea changamoto wanazokutana nazo katika kukabiliana na hali ngumu inayowakabili raia wa Gaza.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Ripoti nyingine mpya ya tathimini ya uchunguzi wa hali na mazingira ya kifo cha aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwaka 1961 Dag Hammarskjöld imetolewa leo ikiwa na vipengele vinne vipya vikiongeza uwezekano kwamba kifo hicho cha ajali ya ndege kilikuwa ni hila. Asante Anold kwanza ikumbukwe kuwa hii sio ripoti ya kwanza na huenda isiwe ya mwisho ya kutathimini hali na mazingira yliyochangia ajali ya ndege iliyokatili maisha ya Dag Hammarskjöld tarehe 17 Septemba 1961 akiwa njia kuelekea Congo ambayo sasa ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Cngo DRC, kujadili usitishwaji wa uhasama ila ni ripoti ya karibuni zaidiRipoti inasema mwenyekiti wa jopo la tathimini ya uchunguzi jaji mkuu wa zamani wa Tanzania Mohamed Chande Othman amepokea taarifa mpya muhimu kutoka kwa nchi wanachama ambazo zinajumuisha maeneo haya Mosi: uingiliaji unaowezekana wa Nchi Wanachama wa mawasiliano husika.Pili: Uwezo wa wanajeshi wa Katanga, au wengine, wa kufanya shambulio linalowezekana kwenye ndege ya SE-BDY,Tatu: kuwepo kwa askari wa kigeni na wafanyakazi wa kijasusi katika eneo hilo la tukioNa nne: Taarifa zaidi mpya zinazohusiana na muktadha na matukio yanayozunguka kifo hicho mwaka 1961.Jaji Othman amemkabidi Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ripoti hii ya tathimini ambaye naye ameiwasilisha kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.Na kufuatiia tathimini hii Guterres amesema anaizingatia ingawa kihistoria kumekuwa na nadharia nyingi zilizotolewa kama sababu inayowezekana ya ajali hiyo, na anazichukulia nadharia hizo nyingi kuwa zisizo na uthibitisho.Hata hivyo mwenyekiti wa jopo la tathimini anasema nadharia nyingine ambayo inabaki na inakubalika ni kwamba shambulio la nje au tishio lilikuwa sababu ya ajali.Pia amesema kuwa dhana mbadala zinazoonekana kuwepo ni kwamba ajali hiyo ilitokana na hujuma, au makosa ya kibinadamu yasiyokusudiwa.Katibu mkuu amekaribisha ushirikiano uliotolewa na baadhi ya nchi wanachama katika tathimini hiyo lakini bado jopo la tathimini linaaminikuna baadhi ya nchi wanachama wana taarifa muhimu ambazo hawajataka kuzitoa.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika malengo ya maendeleo endelevu. Pia tunakuletea muhtasari wa habari zikiwema za Lebanon, afya ya akili na ripoti ya UNICEF kuhusu ukatili wa kingono. Katika kujifunza Kiswahili tunakuletea uchambuzi wa methali.Nchini Lebanon ujumbe wa jeshi la Umoja wa Mataifa la mpito nchini humo, UNIFIL, unasema mapigano kati ya jeshi la Israeli, IDF, na wanamgambo wa Hezbollah kusini mwa Lebanon yamekuwa na madhara kwa ujumbe huo kwani makao yake makuu huko Naqourra na maeneo ya karibu yameshambuliwa mara kwa mara tangu kuanza kwa mapigano kati ya pande hizo mbili.Leo ni siku ya afya ya akili duniani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake amesisitiza udharura wa kupatia kipaumbele afya ya akili pahala pa kazi.Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linasema zaidi ya wasichana na wanawake milioni 370 walioko hai hii leo, walikumbwa na ukatili wa kingono wakati wa utoto wao, yaani kabla ya kutimiza umri wa miaka 18.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu hii leo ni Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia maana ya methali “Mapenzi ni kikohozi hayawezi kufichika.”Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini DRC kumulika ugonjwa wa homa ya nyani au mpox. Pia tunakuletea muhtasari wa habari zikiwemo za machafuko Lebanon, Haiti na Sudan. Katika kujifunza Kiswahili Onni Sigalla anafafanua maana ya neno “NGEJA” Mashariki ya Kati, nchini Lebanon hali inaendelea kuwa tete amesema mratibu maalum wa Umoja wa mataifa nchini humo Jeanine Hennis Plasschaert. Kupiti ukurasa wake wa mtandao wa X amesema umekuwa usiku mwingine wa kutoka kulala mjini Beiruti milipuko ikighubika mji huo bila tahadhari, raia wakikumbwa na taharuki bila kujua mustakbali wao.Mtaalamu mhuru wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu nchini Sudan Radhouane Nouicer, leo ametoa wito kwa jeshi la Sudan (SAF), Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) na wanamgambo wenye silaha kuchukua hatua za haraka kuhakikisha ulinzi wa raia mjini Khartoum, huku kukiwa na ongezeko la uhasama na ripoti za kutatanisha za mauaji ya kiholela.Na zaidi ya watu laki 7, sasa ni wakimbizi wa ndani nchini Haiti huku zaidi ya nusu ya idadi hiyo ni watoto, imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM.Ripoti inasema kuna ongezeko la asilimia 22 la watu waliofurushwa makwao, ambapo machafuko ya magenge ya uhalifu yamewalazimisha watu 110,000 kuzikimbia nyumba zao katika miezi saba iliyopita pkee. IOM imesema ongezeko hilo linasisitiza haja ya msaada zaidi wa kibinadamu kwa ajili ya waathirika.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili leo fursa ni yake mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana ya neno “NGEJA”?Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Umoja wa Mataifa kila uchao unapigia chepuo wadau mbali mbali wakiwemo waandishi wa habari kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs ili sio tu yaweze kufahamika bali pia wale wanaowajibika kuyatekeleza wafanye hivyo ili hatimaye maisha ya wananchi yawe bora na si bora maisha.Hivi karibuni mwandishi wa Radio Washirika KidsTime FM ya mkoani Morogoro nchini Tanzania alikuwa Cairo Misri kwenye mafunzo ya wanahabari ambapo alimuuliza Hanna Dadzie mwandishi wa habari kutoka Shirika la Utangazaji Ghana, GBC ni hatua gani anachukua kusongesha SDGs.“Naamini kama mwana habari wajibu wangu katika kuhamasisha malengo ya maendeleo endelevu, ni kutengeneza uelewa na kusimamia hasa mashirika au taasisi za serikali kuhakikisha kwamba watu wanapata elimu, na tunaposema elimu sio tu elimu ni elimu bora. Kama mwandishi wa habari napaswa kuhakikisha watu hawa wote wanapata elimu bora, kwa sababu sote tumezaliwa kuwa sawa.”Akamulika maeneo ya SDGs ambayo amejikita zaidi.“Naweza kusema nimefanya habari nyingi katika hayo, kuhamasisha SDGs hasa eneo la afya, watu hawana uhakika wa kupata matibabu bora ya afya, naweza kusema kama ukiwa na afya bora una uhai, kama mtu wa habari napaswa kufanya habari zinazohusiana na jamii, kutengeneza uelewa, kuwafanya viongozi wasimame katika nafasi zao, kuhakikisha tunakuwa sawa kwa sababu inatakiwa kuwe na usawa, moja ya lengo la SDGs linazungumzia usawa kwa wote, kwa hivyo, wote tunapaswa kuwa na sawa.”Ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa iliyotolewa hivi karibuni kuhusu utekelezaji wa SDGs inabainisha kuwa malengo hayo 17 yametekelezwa kwa asilimia 17 pekee ikiwa imeasalia 6 kufikia ukomo wake.
Hii leo jaridani tunakuletea kipindi maalum. Leo mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ukiwa umeingia siku ya nne, miongoni mwa wahutubiaji ni Tanzania. Kabla ya kupanda katika mimbari ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili alipata fursa ya kuketi na mwakilishi wa taifa hilo katika mjadala huu, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na kuzungumza naye masuala kadhaa ikiwemo mzigo wa madeni kwa nchi zinazoendelea na pia nafasi ya wanawake katika nyanja ya kimataifa. Lakini kwanza alitaka kufahamu Waziri Mkuu Majaliwa amekuja na ujumbe gani kutoka Tanzania kwenye mjadala huu. Pia tunakuletea muhtasari wa habari.Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu nchini Lebanon, Imran Riza, akizungumza kutoka mji mkuu wa Lebanon, Beirut, kwa njia ya video amewaeleza waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi leo kwamba katika Lebanon kipaumbele kwa sasa ni kuhakikisha usitishaji mapigano wa haraka ili kukomesha mateso zaidi ya raia na uharibifu. Bwana Riza amesisitiza tena wito kwa jamii ya wahudumu wa kibinadamu kwa nchi zote kutumia ushawishi wao kusaidia katika kupunguza machafuko kwa dharura.Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya Wanawake UN Women inaangazia athari kubwa za janga la kibinadamu linaloongezeka kwa wanawake na wasichana wa Sudan, wakiwemo milioni 5.8 ambao ni wakimbizi wa ndani.Ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo mjini Geneva, Uswisi imetoa wito kwa mamlaka ya Haiti na jumuiya ya kimataifa kufanya zaidi kulinda watu na kuzuia mateso zaidi na kwamba hicho ndicho kinapaswa kuwa kipaumbele. Takwimu za hivi karibuni kutoka Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa takribani watu 3,661 wameuawa nchini Haiti tangu Januari mwaka huu.”Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
I le ripoti a le Royal Commission into Defence and Veteran Suicide, na faaalia ai le ta'atele o amioga faamalosi e aofia ai feusua'iga faamalosi na a'afia ai fitafita tama'ita'i i le ADF.
Ua laulauina i le palemene le ripoti a le Komesina o mata'upu i le puipuiga o tina ma fanau i aiga, Micaela Cronin, ma o loo vali mai ai se ata o le tele o le faafitauli i le to'atele o tina o loo sauaina i Ausetalia.
Ripoti mpya kuhusu mauaji nchini Australia, imeonesha kuwa idadi ya wanawake ambao wame uawa na wapenzi wao wa sasa au wazamani, imeongezeka kwa asilimia 28 mwaka huu hadi Juni 2023.
Ripoti ya kila mwaka ya shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu, Amnesty International, inaonyesha hali bado ni mbaya nchini Zimbabwe, DRC na Ethiopia, licha ya kuisifu Zimbabwe kwa kutekeleza sheria kulinda watoto dhidi ya mimba za mapema.
Ua faaalia i se ripoti le se'e i tua o le tulaga maloloina o fanau i Ausetalia ona o le taugata o le tau o le soifuaga ma le le lava o le faamalosi tino.
Ripoti a Galumalemana Autagavaia mai Apia.
O le alii o Henry na le toe mafai ona savali ma ua 'ova i le 10 tausaga o ia fa'aaogaina se nofoa vilivili e fealua'i ai. E ui i lona mana'oga faapitoa, ae na mafai ona ia faavaeina se pisinisi e auala i se fesoasoani mai le malo Ausetalia i le la'eina o 'ie ma isi galuega taulima. Ua mafai ai ona faatu sona fale'oloa i lona nu'u i Savai'i ma fesoasoani ai i le tausiga o lona aiga. (Ripoti na faamaopoopoina ma lipotia e Galumalemana Autagavaia mai Apia).
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na tunakupeleka nchini DRC ambako MONUSCO, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC uko kwenye mchakato wa kuondoka nchini humo na kukabidhi jukumu la ulinzi na usalama kwa serikali. Pia tunakuletea habari kwa ufupi kutoka UNITAMS, FAO na nchini Haiti. Katika kujifunza lugha ya Kiswahili na nitakupeleka kwake Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, BAKIZA nchini Tanzania, salía papo hapo tafadhali! Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kusimamia kipindi cha mpito nchini Sudan, (UNITAMS) umesema una wasiwasi mkubwa kuhusu athari kubwa kwa raia katika eneo la Darfur kutokana na mapigano kati ya Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vinavyoungwa mkono na wanamgambo wa Kiarabu dhidi ya Vikosi vya Wanajeshi wa Sudan (SAF). Ripoti zinaonesha kuwa raia wanazuiwa kuondoka kwenda maeneo salama.Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) limetahadharisha kuhusu kuongezeka kwa janga la chakula nchini Sudan. Kulingana na tathimini ya hivi karibuni ya hali ya uhakika wa chakula (IPC), zaidi ya watu milioni 20.3, wanaowakilisha zaidi ya asilimia 42 ya watu wote nchini humo wanakabiliwa na viwango vya juu vya uhaba wa chakula (IPC ngazi ya 3 au zaidi) kati ya Julai na Septemba mwaka huu 2023.Mtaalamu Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa majaji na wanasheria Margaret Satterthwaite leo ameelezea wasiwasi wake mkubwa kuhusu shambulio la kikatili lililomlenga Jaji wa nchini Haiti Haiti Wilner Morin, ambaye gari lake lilipigwa risasi katika mji mkuu wa Port-au-Prince miezi michache iliyopita. Morin ni jaji wa Mahakama ya Mwanzo ya Port-au-Prince, ambaye anachunguza kesi kadhaa za ufisadi zenye hadhi ya juu.Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili nampisha Dkt. Mwanahija Ally Juma Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Zanzibar, BAKIZA akitufafanualia maana ya neno “NDEKWA”.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Hii leo jaridani tunaangazia ripoti ya UNESCO kuhusu teknolojia na pia afya ya wanawake wajawazito nchini Sudan. Makala tunakupeleka nchini Australia na mashinani Roma nchini Italia, kulikoni? Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO kuhusu ufuatiliaji wa teknolojia katika elimu GEM 2023 imetaka mifumo ya elimu kote duniani siku zote kuhakikisha kwamba matakwa ya wanaojifunza yanakuwa katika kitovu cha teknolojia na kwamba teknolojia zitumike kusaidia elimu inayotokana na mwingiliano wa binadamu badala ya kulenga kuwa mbadala wake.Vita nchini Sudan ambayo sasa imedumu kwa zaidi ya siku 100 imeshuhudia zaidi ya watu milioni 3 wakiyakimbaia makazi yao kwenda kusaka hifadhi katika miji mingine pamoja na nchi Jirani.Makala tunaangazia Timu ya taifa ya mpira wa miguu ya wanawake ambao wako ukimbizini Australia baada ya kuukimbia utawala wa Taliban nchini mwao Afghanistan.Na katika mashinani ikiwa mkutano wa viongozi kuhusu mifumo ya upatikanaji wa chakula unakunja jamvi leo huko Roma nchini Italia tutasikia ujumbe unaotaka jumuiya ya kimataifa kubuni njia mpya za kukabiliana na changamoto za ukosefu wa chakula.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO kuhusu ufuatiliaji wa teknolojia katika elimu GEM 2023 imetaka mifumo ya elimu kote duniani siku zote kuhakikisha kwamba matakwa ya wanaojifunza yanakuwa katika kitovu cha teknolojia na kwamba teknolojia zitumike kusaidia elimu inayotokana na mwingiliano wa binadamu badala ya kulenga kuwa mbadala wake. Ripoti hiyo mwaka 2023 ya GEM inashughulikia matumizi ya teknolojia katika elimu duniani kote kupitia muktadha wa umuhimu, usawa, uthabiti na uendelevu.UNESCO inasema teknolojia inabadilika haraka kuliko inavyowezekana kutathminiwa na bidhaa za teknolojia ya elimu hubadilika kila baada ya miezi 36, kwa wastani huku ushahidi mkubwa ukitoka katika nchi tajiri zaidi.Mathalani ripoti inasema “Nchini Uingereza, asilimia 7 ya makampuni ya teknolojia ya elimu yalikuwa yamefanya majaribio yaliyodhibitiwa bila mpangilio, na asilimia 12 yalikuwa yametumia uthibitishaji wa watu wengine. Pia utafiti uliofanywa kwa walimu na wasimamizi katika majimbo 17 ya Marekani ulmeonyesha kuwa ni asilimia 11 tu waliomba tathimini ya ushahidi kabla ya kupitishwa.Katika miaka 20 iliyopita, wanafunzi, waelimishaji na taasisi wamepitisha na kukumbatia kwa kiasi kikubwa zana za teknolojia ya kidijitali.Audrey Azoulay, mkurugenzi mkuu wa UNESCO anaonya kwamba "Mapinduzi ya kidijitali yana uwezo usiopimika lakini, kama vile onyo ambavyo limekuwa likitolewa kuhusu jinsi yanavyopaswa kudhibitiwa katika jamii, tahadhari sawa lazima izingatiwe jinsi mapinduzi hayo yanavyotumiwa katika elimu. Matumizi yake lazima yawe kwa ajili ya uzoefu ulioimarishwa wa kujifunza na kwa ajili ya ustawi wa wanafunzi na walimu, si kwa madhara kwao. Matakwa ya mwanafunzi yawe kipaumbele cha kwanza na yawasaidie walimu. Kuunganishwa mtandaoni sio mbadala wa mwingiliano wa wanadamu.”Azoulay amesisitiza kuwa “Kutumia teknolojia kunaweza kuboresha baadhi ya aina za kujifunza katika baadhi ya miktadha. Ripoti hiyo inataja ushahidi unaoonyesha kuwa manufaa ya kujifunza hutoweka ikiwa teknolojia itatumiwa kupita kiasi au kutokuwepo kwa mwalimu aliyehitimu. Kwa mfano, kusambaza kompyuta kwa wanafunzi hakuboreshi hali ya kujifunza ikiwa walimu hawatahusika katika tajriba ya ufundishaji. Simu za rununu shuleni pia zimeonekana kuwa kero katika kujifunza, lakini ni chini ya robo ya nchi tu ndizo zimepiga marufuku matumizi ya simu hizo shuleni.”Duniani kote ripoti imesema idadi ya watu wanaotumia mtandao wa intaneti imeongezeka kutoka asilimia 16 mwaka 2005 hadi asilimia 66 mwaka 2022.