Podcasts about kampeni

  • 14PODCASTS
  • 83EPISODES
  • 13mAVG DURATION
  • 1MONTHLY NEW EPISODE
  • May 2, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about kampeni

Latest podcast episodes about kampeni

SBS Swahili - SBS Swahili
Uchaguzi wa Shirikisho 2025- mazuri, mabaya na maswala ya kukera kutoka wiki tano zilizo pita

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 2, 2025 10:39


Kampeni za uchaguzi wa shirikisho wa 2025 zina karibia tamati.

wiki pita tano uchaguzi kampeni
Habari za UN
25 FEBRUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 25, 2025 11:10


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini DRC ambako ghasia za hivi karibuni huko Goma zimeongeza mahitaji ya huduma za afya, WHO imechangia vifaa muhimu vya matibabu ili kukabialiana na hali hiyo. Pata pia muhtasari wa habari na mashinani.Kufuatia ripoti za kuweko kwa ugonjwa usiojulikana huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambao tayari umeambukiza mamia ya watu na kusababisha makumi ya vifo, shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO, limesema bado linaendelea na uchunguzi wa ugonjwa huo uliotangazwa kwa chapisho la kikanda la WHO.Kampeni ya chanjo ya polio inayoendelea ukanda wa Gaza kwa lengo la kudhibiti kusambaa kwa virusi vya polio na kuzuia tishio la ugonjwa huo kusambaa maeneo mengine na nchi jirani, imekuwa na mafanikio makubwa kwani hata eneo la Gaza Kaskazini, mwitikio ulikuwa mkubwa licha ya mvua na baridi kali.Na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP hii leo limetangaza kuwa sitisho la mapigano Gaza limewezesha kufikisha eneo hilo kwa wastani maradufu ya shehena za vyakula kilichokuwa kinapelekwa kabla ya sitisho la mapigano.Katika mashinani, hivi majuzi Shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, UNICEF katika ripoti yake lilibaini kwamba mtoto 1 kati ya watano nchini Ukraine ameripoti kupoteza ndugu au rafiki wa karibu tangu kuzidi kuongezeka kwa vita miaka mitatu sasa. Akitafakari juu ya zama zijazo, Toby Fricker, Afisa Mkuu wa mawasiliano wa Shirika hilo nchini Ukraine anasema UNICEF inaendelea kushikamana nao.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Sio lazima kiboko, kampeni ya UNICEF Tanzania inayoonesha mafanikio katika elimu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 27, 2025 2:33


Katika makala ya leo Anold Kayanda anatupeleka nchini Tanzania ambako katika kuhamasisha elimu iliyo salama inayolenga kumlea na kumfundisha mtoto kwa njia chanya zisizoumiza, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, (UNICEF) linamuangazia Mwalimu Magesa Stanslaus ambaye amebadilika kutoka katika matumizi ya viboko na sasa anatumia motisha tofauti kuwarekebisha wanafunzi wake. 

Radio Maria Tanzania
Fahamu mambo ya kuzingatia kuelekea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Nov 20, 2024 38:15


Ungana nami Mtangazaji wako Judith Mpalanzi katika Kipindi cha Elimu Jamii ambapo leo tupo na Bwana Stephen Motambi kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) akizungumzia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na tunapoelekea kwenye Kampeni za uchaguzi huo. L'articolo Fahamu mambo ya kuzingatia kuelekea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. proviene da Radio Maria.

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Uchaguzi wa Marekani, mapigano DRC, kampeni za Raila kuwania uenyekiti wa tume ya AU

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Nov 9, 2024 20:15


Donald Trump achaguliwa kuwa rais wa 47 wa Marekani, Ziara ya rais wa Kenya William Ruto huko Addis Ababa Ethiopia, na Sudan Kusini, na Raila Odinga kuzindua azma yake ya kuwania uenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika, kuelekea uchaguzi huo utakaofanyika Februari mwaka 2025. Mapigano makali kati ya waasi wa M23 na wazalendo mashariki mwa DRC, Umoja wa Mataifa wasema uamuzi wa kuahirishwa uchaguzi nchini Sudani Kusini haukubaliki, Duma Boko atawazwa rasmi kama rais mpya wa Botswana, Uhusiano wa Urusi na Marekani baada ya Trump kushinda uchaguzi

Habari za UN
UN: Mashambulizi ya anga ya Israel yalazimisha kampeni ya chanjo kusitishwa Gaza Kaskazini

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 23, 2024 2:45


Mashambulizi makali ya anga kutoka kwa jeshi la Israel, idadi kubwa ya watu kutawanywa na ukosefu wa fursa ya kufika Gaza Kaskakzini vimelazimisha kuahirishwa kwa kameni ya chanjo kwa mujibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Afya Duniani WHO, la kuhudumia watoto UNICEF na la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA. Asante Anold, kampeni hiyo iliyoahirishwa ilitakiwa kuanza leo n ani duru ya mwisho ya chango ya kampeni iliyolenga kuwachanja watoto 119,279 kote Gaza Kaskazini kwa dozi ya pili ya chanjo ya polio aina ya nOPV2, lakini hali ya sasa imefanya iwe vigumu kwa familia kupeleka watoto wao kwenye vituo vya chanjo, na kwa wahudumu wa afya kuendesha huduma kwa usalama.Mashambulizi ya makombora yanayoendelea dhidi ya miundombinu ya kiraia yamepunguza maeneo yanayokubaliwa kwa usitishaji wa uhasama kwa mnajili ya masuala ya kibinadamu kuwa kwenye Jiji la Gaza pekee, ikilinganishwa na wakati wa awamu ya kwanza ya chanjo iliyofanyika tarehe 1-12 Septemba 2024.Hali hii inahatarisha kufikiwa kwa lengo la angalau asilimia 90 ya watoto kuchanjwa, jambo ambalo ni muhimu ili kukomesha usambaaji wa virusi vya polio na kulinda afya za watoto.WHO na UNICEF wamesema kuwa kucheleweshwa kwa chanjo ya polio kunaweza kuongeza hatari ya virusi kuenea zaidi Gaza na maeneo Jirani na kuchelewesha utoaji wa dozi ya pili ya chanjo ndani ya wiki sita kunapunguza uwezo wa chanjo hiyo kuimarisha kinga za watoto na kuzuia maambukizi.Tangu  duru ya pili ilipoanza tarehe 14 Oktoba 2024, jumla ya watoto 442,855 wenye umri wa chini ya miaka kumi wamefanikiwa kuchanjwa katika maeneo ya kati na kusini mwa Gaza.UNICEF na WHO wanatoa wito kwa pande zote zinazohusika katika mzozo kutekeleza usitishaji mapigano  wa kibinadamu na kuhakikisha kuwa raia, wahudumu wa afya, na miundombinu ya kiraia kama shule na hospitali inakingwa dhidi ya mashambulizi.Mashirika hayo yamesisitiza umuhimu wa kuanza tena kampeni ya chanjo mara moja ili kuzuia kupooza kwa watoto na kuimarisha kinga dhidi ya polio.Katika juhudi za kuhakikisha huduma bora, takribani watoto 357,802 pia walipatiwa virutubisho vya vitamini A kama sehemu ya juhudi za kuunganisha chanjo ya polio na huduma zingine muhimu za afya.Mashirika ya WHO na UNICEF ymesisitiza kuwa kusitisha vita na kuwezesha chanjo ni hatua muhimu ili kuzuia mlipuko wa polio kuendelea na kulinda afya ya watoto wote Gaza.

Radio Maria Tanzania
Ni, kwa namna gani Familia husaidia kuimarisha Usawa wa Kijinsia katika jamii?

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Oct 21, 2024 27:21


Karibu uungane nami Elizabeth Masanja, katika kipindi cha Jinsia na Maendeleo leo  tupo na Ndugu Anectus Asingizibwe, Mwenyekiti wa Kampeni kupinga ukatili shujaa wa maendeleo na ustawi wa jamii (SMAUJATA) Wilaya ya Kisarawe Mkoa wa  Pwani akituongoza kujifunza mchango wa Mifumo ya Familia katika kuimarisha usawa wa Kijinsia. L'articolo Ni, kwa namna gani Familia husaidia kuimarisha Usawa wa Kijinsia katika jamii? proviene da Radio Maria.

Alfajiri - Voice of America
Swala la vimbunga latawala kwenye kampeni za wagombea urais Marekani. - Oktoba 11, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Oct 11, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Alfajiri - Voice of America
Wizara ya afya nchini DRC yaanzisha kampeni ya kutoa chanjo dhidi ya mpox katika majimbo mbalimbali ya nchi hiyo - Oktoba 01, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Oct 1, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Habari za UN
UN: Watoto zaidi ya 560,000 wamepata chango ya polio katika duru ya kwanza ya kampeni ya chanjo Gaza

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 13, 2024 1:41


Zaidi ya watoto 560,000 wamepokea chanjo dhidi ya virusi vya polio aina ya pili (cVDPV2) kwenye Ukanda wa Gaza katika duru ya kwanza ya kampeni kubwa ya chanjo iliyomalizima jana yamesema mashirika ya Umoja wa Mataifa.Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO, watoto waliopokea chanjo hiyo kupitia kampeni ya dharura ya chanjo Gaza ni wale wenye umri wa chini ya miaka 10.Kupitia ukurasa  wake wa mtandao wa X zamani Twitter Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Adhanon Ghebreyesus amesema “Tunafurahia timu zote za wahudumu wa afya, zilizoendesha operesheni hii ngumu. Tunashukuru sana kwa familia kwa imani na ushirikiano wao. Haya ni mafanikio makubwa huku kukiwa na hali mbaya ya kila siku ya maisha katika Ukanda wa Gaza. Hebu fikiria nini kingeweza kufikiwa endapo kungekuwa na ushitishwaji mapigano.”Awamu ya kwanza ya chango ilianza Septemba Mosi na lengo lilikuwa ni katika kila duru kuchanja  zaidi ya watoto 640 000 wa umri wa chini ya miaka 10.Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA limesema maelfu kwa maelfu ya watoto wmechanjwa na kukamilika kwa awamu hiyo ya kwanza ya chanjo ni mafanikio makubwa kwa shirika hilo na wadau wote walioshiriki kwani wamefikia lengo kwa asilimia 90 ingawa sasa changamoto ni kutoa dozi ya pili ya chanjo hiyo katika awamu ya pili ya kampeni inayotarajiwa katika wiki zijazo.Dozi za chanjo ya polio zaidi ya milioni 1.6 ziliwasili Gaza ili kukamilisha awamu zote mbili za chanjo inayohusisha wahudumu wa afya zaidi ya 2700.

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Kampeni ya Odinga kuwania uenyekiti tume ya AU, DRC yafungua kesi dhidi ya Rwanda

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Aug 31, 2024 20:03


Uzinduzi wa kampeni ya aliyekuwa waziri mkuu wa Kenya Raila Odinga, anayegombea unyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika, kongamano la 74 la WHO mjini Brazzaville, nchini Congo, DRC na Kampeni inayoitwa ICC Haki kwa DRC, hali ya usalama kuendelea kuzorota nchini Sudan, shambulio la kigaidi Burkina Faso laua zaidi ya watu 300, hali nchini Israeli, na mchakato wa uchaguzi wa Marekani mwezi Novemba

Alfajiri - Voice of America
Rwanda kuanza kampeni za uchaguzi wa rais - Juni 21, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jun 21, 2024 29:59


rwanda rais uchaguzi kampeni
Radio Maria Tanzania
Fahamu namna kumlinda Mtoto na kumpatia haki zake za msingi.

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later May 29, 2024


Karibu Ungane na Esther Magai Hangu katika Kipindi cha Elimu Jamii, mwezeshaji Bwana Anetus Asingizibwe Mwenyekiti wa Kampeni ya kupinga ukatili shujaa na Maendeleo Simaujata kutoka Wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani, mada Usalama wa Watoto kwa Maendeleo ya Taifa. L'articolo Fahamu namna kumlinda Mtoto na kumpatia haki zake za msingi. proviene da Radio Maria.

Siha Njema
Wanawake waongoza juhudi za kampeni za Afya bora ,DRC ikizidisha mapambano ya Kipindu Pindu

Siha Njema

Play Episode Listen Later Apr 2, 2024 9:59


Wawawake kutoka ukanda wa Afrika wanajumuika Dar  Es Salaam  mwishoni mwa juma kupiga jeki kampeni za kuboresha afya Nchini DRC mikakati iliyoweka kudhibiti mlipuko wa Kipindu Pindu ulioripotiwa katika mataifa ya Afrika ya Kusini ,inaendelea kulipa na hata kuwa msaada kwa mataifa jirani kama vile Zambia

Jioni - Voice of America
Wanasiasa wa upinzani wa Senegal waanza kampeni zao licha ya kutokuwa na tarehe iliotangazwa ya kufanyika uchaguzi mkuu. - Februari 21, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 21, 2024 30:00


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

senegal afrika mashariki uchaguzi mkuu kampeni
Jioni - Voice of America
Viongozi wa upinzani wa Senegal waendelea na kampeni zao licha ya kuwa hakuna tarehe ya uchaguzi wa rais iliotangazwa. - Februari 20, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 20, 2024 29:57


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Kwa Undani - Voice of America
Kampeni za uchaguzi mkuu Marekani zashika kasi mapema, mchambuzi aeleza kwa nini - Januari 31, 2024

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 31, 2024 29:59


kasi nini mkuu marekani uchaguzi mkuu kampeni
Alfajiri - Voice of America
Gavana wa zamani wa jimbo la New Jersey nchini Marekani Chris Christie ametangaza kusitisha kampeni za urais kupitia chama cha Republican - Januari 11, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 11, 2024 29:58


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Alfajiri - Voice of America
Kampeni za uchaguzi DRC zimemalizika rasmi na sasa raia wanasubiri saa chache kabla ya vituo vya kupiga kura kufunguliwa rasmi nchini humo. - Desemba 19, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 19, 2023 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

humo kura sasa raia kabla uchaguzi desemba kupiga kampeni chache
Kwa Undani - Voice of America
Wagombea DRC wakamilisha kampeni upigaji kura Jumatano - Desemba 19, 2023

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 19, 2023 29:59


Wagombea DRC wakamilisha kampeni upigaji kura Jumatano

kura desemba kampeni
Kwa Undani - Voice of America
DRC: Kampeni za mwisho mwisho kwelekea kwa uchaguzi mkuu Jumatano - Desemba 18, 2023

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 18, 2023 29:59


Kampeni za mwisho mwisho zilifanyika Jumatatu kwelekea kwa uchaguzi mkuu Jumatano huku kukiwa na wasiwasi kama zoezi hilo litakuwa la haki na salama.

mkuu desemba uchaguzi mkuu kampeni
Alfajiri - Voice of America
Jeshi la Israel linasema wanajeshi wake 10 waliuawa katika mapigano huko Ukanda wa Gaza wakati wa kampeni ya kuwaondoa wanamgambo wa Hamas - Desemba 14, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 14, 2023 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Jioni - Voice of America
Kampeni za uchaguzi wa urais nchini Jamhuri ya Kidemokrasni ya Congo zinaendelea kukiwa na wagombea 25 dhidi ya Rais Felix Tshisekedi. - Novemba 24, 2023

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 24, 2023 59:58


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

SBS Swahili - SBS Swahili
Wimbo maarufu wa John Farnham watumiwa katika kampeni ya kura ya Ndio

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 5, 2023 7:01


Kiongozi wa upinzani wa shirikisho Peter Dutton amesema atafanya kura nyingine ya maoni, kama kura yakuweka sauti yawa Australia wa kwanza bungeni ndani ya katiba inafeli.

Wimbi la Siasa
Uchambuzi kuhusu siasa ya Zimbabwe baada ya upinzani kuzuiliwa kufanya kampeni

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Jul 27, 2023 9:59


WImbi la siasa juma hili Ali Bilali na wachambuzi wake wanajadili hali ya kisiasa nchini Zimbabwe kuelekea kwenye uchanguzi mkuu wa rais

SBS Swahili - SBS Swahili
Germain "nataka leta aina mpya ya siasa DRC"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jul 20, 2023 16:44


Kampeni za uchaguzi mkuu zime anza katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

congo aina kidemokrasia kampeni
Wimbi la Siasa
Zimbabwe : Marafuku ya kuanzishwa kwa kampeni za chama cha upinzani

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Jul 15, 2023 9:26


Tunaangazia hatua ya mahakama nchini Zimbabwe kuidhinisha marafuku kuanzishwa kwa kampeni iliyopangwa kufanywa na chama kikuu cha upinzani wakati huu pia kiongozi wake mkuu Nelson Chamisa akikabiliwa na vikwazo.

zimbabwe chama nelson chamisa kampeni tunaangazia
Kwa Undani - Voice of America
Trump anaendelea kupuuza mashtaka dhidi yake na kuendelea kufanya kampeni kuwa rais katika uchaguzi mkuu wa 2024 - Juni 14, 2023

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later Jun 14, 2023 29:59


Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.

Radio Maria Tanzania
Je wafahamu hali ya usalama kwa Watoto katika Jamii.

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Jun 14, 2023 25:26


Ungana na Frank Kashonde katika kipindi cha Jinsia na Maendeleo, mada iliyopo ni hali ya usalama kwa Watoto katika Jamii., Mwezeshaji Bwana Anectus Asingizibwe Mwenyekiti wa Kampeni ya Kitaifa ya Kupinga Ukatili  kwa Wilaya ya Kisarawe, Mkoa wa Pwani, (SMAUJATA)

Habari za UN
Tuhamasishe mawazo chanya duniani – Mchechemuzi wa SDGs, Chioma Ogbonna “Cill”

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 17, 2023 0:04


Mwanamuziki wa Nigeria Chioma Ogbonna akifahamika kwa jina la usanii “Cill” ni mchechemuzi wa Kampeni ya Umoja wa Mataifa ya kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDG Action Campaign ambaye hivi karibuni alihudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa wa nchi zenye maendeleo duni Duniani, LDC5.  Moja ya nyimbo zake maarufu ni Woman alioutoa mwaka 2021 ukiwa mahususi kwa ajili ya Siku ya Mwanamke Duniani. Ni wimbo ambao unaeleza nguvu ya mwanamke licha ya kukatishwa tamaa. Nyimbo zake nyingine maarufu za Cill ni pamoja na Tatarata, Kachifo, Permit me na nyinginezo kadhaa.  Anold Kayanda wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa alipata fursa ya kuzungumza na msanii huyu mjini Doha nchini Qatar. 

Habari za UN
17 APRILI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 17, 2023 0:12


Hii leo jaridani tunasalia hapa makao makuu kukuletea yaliyojiri kwenye Jukwaa la kudumu la watu wa asili, na pia kukupeleka nchini DRC kumulika faida ya mradi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia wa kupanda miti aina ya migunga. Makala tunaangazia SDG 17 na Mashinani tunakupeleka nchini Tanzania, kulikoni?Hii leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani Jukwaa la kudumu la watu wa asili limeanza rasmi ambapo katika ufunguzi wa jukwaa hilo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema pamoja na majukumu muhimu ya jamii za asili hususan katika kulinda mazingira na mbinu nyingine mbadala za maisha, watu hawa wanazidi kuwa masikini na kuzitaka nchi zote duniani zihakikishe zinawasaidia kuondokana na umasikini.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mradi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia wa kupanda miti aina ya migunga imeondoa tishio la ukataji miti holela kwenye msitu wa bonde la mto Congo, ambao ni wa pili kwa ukubwa duniani katika kufyonza hewa ya ukaa na sasa wananchi wananufaika sio tu kwa kupata mkaa bali pia hata watu wa jamii ya asili wanaweza kupata kitoweo porini.Katika makala Mwanamuziki Chioma Ogbonna (tamka Obona) “Cill” au Cillsoul wa Nigeria ambaye ni Mchechemuzi wa Kampeni ya Umoja wa Mataifa ya kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs na anaeleza anavyoutumia kipaji chake kusongesha malengo hayo 17.Na katika mashini tutaelekea nchini Tanzania kusikiliza jinsi ambavyo hakikisho la maji safi na salama limeboresha elimu shuleni.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, Karibu!

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho
Nchini DRC, kundi la MDP laanzisha kampeni ya kukusanya mifuko ya plastiki kutunza mazingira

Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho

Play Episode Listen Later Mar 14, 2023 9:59


The Mutual for Project Development( MDP), ni kikundi kinachohamasisha jamiinamna bora ya kuhifadhi mifuko ya plastiki ili kulinda mazingira.

mutual drc kundi mazingira kampeni
Habari za UN
Mada kwa kina: Chanjo dhidi ya Kipindupindu yaendelea Kivu Kaskazini, DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 31, 2023 0:05


Kampeni ya utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu  iliyoanza tarehe 25 mwezi huu huko Kivu Kaskazini nchini jamhuri ya Kidemokraia ya Congo, DRC imekunja jamvi jana Jumanne ya tarehe 30 mwezi hu uwa Januari ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO lilizindua kampeni hiyo ya chanjo kwa wakimbizi wa ndani katika kambi ya wakimbizi hao ya Kanyaruchinya wilayani nyiragongo katika mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini.Mwandishi wetu wa DRC Byobe Malenga ambaye ameshuhudia uzinduzi huo amesema uliongozwa na Gavana wa jimbo la Kivu Kaskazini Jenerali Ndima Constant, na Mwakilishi wa shirika WHO nchini DRC kwa lengo la kuokoa mamia ya familia hususan za wakimbizi wa ndani ambao tayari makumi kwa makumi wameripotiwa kupata ugonjwa huo na wengine wamefariki dunia.Jean Bruno, ni Mkuu wa Ofisi ya WHO Kivu Kaskazini na anasema ameridhishwa na shauku ya siku ya kwanza na zaidi ya yote amesema,« Tumewalenga watu 364,127 ambao ni wakimbizi wa ndani, pamoja na familia zinazowapokea. Tayari tumepokea dozi 364,150 ambazo zipo na zitatumika. chanjo itafanyika kwa awamu ya dozi moja na tutafanya hivyo kupitia kampeni ya nyumba kwa nyumba kwenye maeneo haya . Tumeridhika na ukweli ni kwamba kumekuwa na dhamira muhimu kwa upande wa serikali kwenye ngazi ya taifa na mkoa, lakini pia tumekuwa na hakikisho kutoka kwa jamii ya watu na wakimbizi wa ndani ambayo imekubali chanjo hiyo ambayo itafanyika kwa wakati».Eneo la Nyiragongo lilipokea idadi kubwa ya watu waliokimbia makazi yao kutokana na mashambulizi yanayofanywa na waaasi wa M23 huku watu 233 elfu waliokimbia makazi yao, zaidi ya 95% yao wamelundikana kwenye makanisa, shule, viwanja vya michezo na maeneo yasio salama kwa afya yao.Gavana wa Kivu Kaskazini, Jenerali Ndima Constant, anakiri kwamba janga la kipindupindu linaathiri sana eneo la Nyiragongo akisema kwamba hadi Jumanne ya Januari 24  wagonjwa 3706 wa kipindupindu walisajiliwa huku kukiwa na vifo 16 na ili kupunguza mlolongo wa maambukizi amewasihi raia kupata chanjo akishukuru WHO kwa msaada wao.« Madhumuni ya kampeni hii  ya chanjo ni kulinda idadi ya watu dhidi ya kipindupindu katika jimbo la Kivu Kaskazini na hasa katika maeneo ya watu waliofurushwa ili kupunguza vifo. Mabibi na mabwana, wageni mashuhuri, ili kufunga maoni yangu, ningependa kuwakumbusha kuwa pamoja na chanjo utakayopokea, kufuata hatua za kuzuia maambukizi ni muhimu..”Ametaja njia za kujikunga kuwa ni pamoja na kunawa mikono mara kwa mara kwa maji safi na sabuni au majivu, kunywa maji yaliyotakasishwa tu au yaliyochemshwa. Kupika na kufunika milo yetu, matumizi sahihi ya vyoo huku tukiwa wasafi na kuweka usafi kwenye maeneo yetu ya makazi  kila wakati.Waliokimbia makazi yao wanafahamu tishio hilo kwa sababu janga hilo limeathiri zaidi ya 89% ya waliokimbia makazi katika miezi ya hivi karibuni na chanjo inatekelezwa nyumba kwa nyumba.Watu waliohamishwa wanasubiri dozi zao nyumbani. Damaseni Butera ni miongoni mwa watu wa kwanza kupata dozi moja dhidi ya kipindupindu na anashukuru mpango huu wa WHO na anasema, «chanjo ni muhimu sana katika mapambano dhidi ya magonjwa kama kipindupindu, malaria na mengine.Tumejifunza habari kuhusu chanjo hiyo, tumefurahi sana kwa sababu tutakuwa na kinga, asante sana kwa shirika la WHO ambalo lilitufikiria. Asante sana»Kando na hilo, Mweze Shemba, aliyekimbia kutoka kijiji cha Kiwanja, pia alinufaika na chanjo hii. Licha ya njaa,yeye anapendelea kujilinda pamoja na familia yake dhidi ya janga hili akisema, «kilichonifanya nipate chanjo ya leo hapa katika kambi ya wakimbizi ni kwa sababu tunapatwa na magonjwa ya taabu. kama vile kuharana kutapika hasa tunapokunywa maji machafu. Lakini wakati tunapata hii chanjo tunaona kama vile ni kinga kwetu tunashukuru sana »Katika juhudi za kuepusha msongamano wa wagonjwa wa janga hili , WHO ilijenga vitalu 3 kama kitengo cha matibabu ya wagonjwa wa Kipindupindu (UTC) katika eneo la Bushagara na…

Habari za UN
Kampeni ya utoaji chanjo ya homa ya mafua makali yaendelea ukanda wa ulaya: WHO

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 20, 2023 0:02


Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya ulaya tangu kuanza kwa msimu wa baridi kali katikati ya mwezi Novemba mwaka 2022 wamebaini kuongezeka kwa wagonjwa wanaolazwa kutokana na magonjwa ya homa ya mafua makali au flu,  matatizo ya kupumua na COVID-19. Walio hatarini zaidi kupata maambukizi ya magonjwa hayo ni wahudumu wa afya pamoja na wazee, ndio maana wanaendesha kampeni ya kutoa chanjo. Katika msimu wa baridi mwaka uliopita WHO ukanda wa Ulaya ilifanikiwa kutoa chanjo ya homa ya mafua makali kwa asilimia 65 ya kundi la watu walio hatarini ambao wengi ni wazee na wahudumu wa afya na msimu huu wa baridi lengo ni kuwafikia asilimia 75 ya watu hao. Afisa wa kiufundi wa WHO Kyrgyzstan Kasymbekova Kaliya, anasema wanafahamu namna ugonjwa wa guo ulivyo hatari.…. “tunajua kwamba ugonjwa huu wa homa ya mafua makali unaweza kusababisha matatizo makubwa hasa kwa wazee wenye umri zaidi ya miaka 65, wale ambao wana magonjwa sugu ya moyo, mapafu, kisukari, na wenye hali ya uzio”. Chanjo imeanza kutolewa kwa makundi yaliyo hatarini kuathirika zaidi ya homa ya mafua makali kama anavyoeleza Baktygul Mamatova, mtaalamu wa Kinga katika kituo cha afya cha Bishkek, “Sisi, wahudumu wa afya, kama kundi lililo hatarini ndio tumekuwa wa kwanza kupata chanjo. Siwezi sema kwamba siwezi kupata magonjwa, napata, lakini kwa kuwa nimepata chanjo ni rahisi kuhimili.” Wazee wanfahamu umuhimu wa kupata chanjo kama anavyoeleza Kanai Alamanov, aliyefika katika  kituo cha afya cha Bishkek, “Hapo awali, kulikuwa na uhamasishaji wa kupata chanjo dhidi ya virusi vya CORONA nami nilikuja kupata chanjo hiyo ya COVID-19, na sasa ni chanjo ya homa ya mafua makali. Chanjo hii inatupa fursa ya kujikinga na magonjwa, inatupa aina fulani ya hakikisho la maisha yenye afya.” Chanjo hazitolewi kwa wale wanaoenda hospitali pekee, wanaoishi katika nyumba maalum za kutunza wazee nao hufuatwa na kupewa chanjo kama anavyothibitisha Ludmila Kinda Ivanovna, “Mimi ninaugua sana. Mwili wangu haukubali kabisa kutumia aina nyingi ya dawa ikiwemo zile za viua vijasumu, nina pumu , nina matatizo ya moyo, nilishapata mstuko wa moyo mara mbili. Kiufupi mwili wangu ni dhaifi sana hivyo chanjo ina maana kubwa sana kwangu.”  

Habari za UN
TANZBATT 9 nchini DRC wahitimisha kampeni ya Amani na Afya kwa kukabidhi jengo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 16, 2023 0:03


Kikosi cha 9 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kupitia Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo - MONUSCO wamehitimisha kampeni yao ya Afya na Amani iliyoanza tarehe 3 mwezi huu wa January ambapo  wamekabidhi jengo kwa ajili ya mahali pa wagonjwa na wahudumu wa afya kula chakula katika Kituo cha Afya cha Mavivi, mjini Beni, Jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa DRC.Akikabidhi jengo hilo Kamanda wa kikosi cha tisa cha Ulinzi wa Amani kutoka Tanzania Luteni Kanali Barakael Mley amesema jengo hilo litabaki kuwa kumbukumbu ya uhusiano mzuri baina ya walinda Amani wa kikundi cha Tisa na wananchi wa maeneo ya Mavivi na maeneo jirani,Akiongea kwa niaba ya Maganga mkuu wa hospital ya Oicha na wananchi wa maeneo ya Mavivi Dr Kasereka Nzala amewapongeza walinda Amani hao wa Tanzania wanaohudumu chini ya mwamvuli wa MONUSCO wamekuwa wakifanya jitihada mbalimbali katika kutatua changamoto za wananchi katika maeneo yao ya uwajibikaji,Kwa upande wake afisa Mahusiano wa kikosi cha tisa cha Ulinzi wa Amani kutoka Tanzania Kepteni Paul Mwesongo amebainisha kuwa hali ya uhusiano baina ya wananchi na walinda Amani hao,Naye bi Kavathama Clarice, mwenyekiti wa kamati ya Afya katika kituo cha afya cha Mavivi amesema,

Habari za UN
TANZBATT 9 waanzisha kampeni kutumia afya kuleta amani DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 5, 2023 0:05


Kikosi cha tisa cha ulinzi wa amani kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu ndani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO, kimeanzisha kampeni iliyopewa jina la “Afya na Amani” ambayo inahusisha utoaji wa dawa za binadamu katika vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali za baadhi ya maeneo ya uwajibikaji ya Kikosi hicho ndani ya mji wa Beni, kaskazini mashariki mwa DRC.Akipokea dawa hizo muuguzi Mkuu wa Kituo cha afya cha Mavivi, Kisu  Kanyambala Janvier, amewashukuru TANZBATT 9 kwa msaada huo na kusema kwamba utawasaidia wananchi wote.“Tunashukuru sana kikundi cha watanzania wa MONUSCO kwa msaada waliotuletea na ni msaada mkubwa wa dawa, tulikuwa na ulazima wa kuipata hii dawa na tulikuwa tunaikosa. Tunashukuru sana msaada huu utasaidia wakina mama, watoto na watu wote.” Anasema Kanyambala.Aidha Kanyambala amebainisha kuwa siyo mara ya kwanza kwa walinda amani wa Tanzania katika eneo hilo kuwasaidia wananchi kwani waliwajengea wodi ya akina mama na watoto na ujenzi wa kantini kwa ajili ya wagonjwa kula chakula ambayo ipo mbioni kukamilika.Kwa upande wake Kamanda Kikosi wa TANZBATT 9  Luteni Kanali Barakael Jackson Mley amesisitiza kuhusu suala la ushirikiano baina ya walinda amani wa MONUSCO na wananchi na kueleza kuwa wananchi wanapokuwa na afya nzuri wataweza kushiriki vyema katika kuleta amani ya maeneo yao, “sisi ujumbe wetu mkubwa ni ushirikiano ili kutatua changamoto za kiusalama tulizo nazo, bila ushirikiano baina ya raia na kikundi chetu cha tisa cha ulinzi wa Amani kutoka Tanzania hatutaweza kufanikisha jukumu hili”. Akisisitiza umuhimu wa kampeni hiyo kwa jamii, Kavumba Dezanji ambaye ni kiongozi wa wanawake katika eneo la Mbau amesema, “nasema afya mbele ya yote, ukiwa na afya njema utafanya kazi yoyote ya maendeleo.” Aidha, Dezanji ameomba usalama uboreshwe katika eneo la Mbau na kuomba mradi kama huo wa Afya na Amani uendelee katika mji huo.Naye Bukuka Makofi Chifu wa kimila wa eneo la Mavivi, amewashukuru walinda amani kutoka Tanzania kwa msaada huo na kusema “ni kitu cha kushukuru sana, inaonesha kama wanaendelea kutuonesha ushirikiano na upendo, mwanzo wa mwaka sisi kama tumebarikiwa kwa sababu tulikuwa na shida ya dawa kutokana na eneo hili kupokea watu wengi kutoka sehemu nyingine, hii itaendelea kutusapoti sana.” Kampeni ya Afya na Amani ni kampeni iliyoanza kuanzia tarehe 03 mwezi huu wa Januari na itadumu hadi tarehe 13 januari 2023.

SBS Swahili - SBS Swahili
Royal Life Saving yazindua kampeni ya usalama wa majira ya joto

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 29, 2022 9:02


Tunapo ingia katika majira ya joto, shirika la Royal Life Saving Australia, limezindua kampeni mpya kukabiliana na ongezeko kubwa kwa idadi ya visa vya vifo vinavyo sababishwa na kuzama majini nchini Australia.

Jioni - Voice of America
Jioni:Boris Johnson ameanza kampeni kuwa waziri mkuu wa Uingereza. Marekani inataka vita vya Ethiopia kumalizika mara moja - Oktoba 22, 2022

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Oct 22, 2022 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Kwa Undani - Voice of America
Marekani: Kampeni za uchaguzi wa katikati ya muhula zashika kasi - Oktoba 19, 2022

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later Oct 19, 2022 29:59


Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.

kasi marekani oktoba uchaguzi kampeni
Alfajiri - Voice of America
Somalia yapata uungwaji mkono katika kampeni ya kutaka kuondolewa vikwazo vya silaha - Oktoba 12, 2022

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Oct 12, 2022 29:59


Somalia inapata uungwaji mkono katika kampeni yake ya kutaka kuondolewa kwa vikwazo vya silaha baada ya Ethiopia kuungana na Uganda kuunga mkono hatua hiyo.

RadioRahma
Wanawake wanaowania viti vya siasa wakumbwa na changamoto za usafri wa kufanyia kampeni

RadioRahma

Play Episode Listen Later Aug 8, 2022 6:10


Licha ya wanawake wenye ulemavu kujitosa kwenye siasa,bado wanakumbwa na changamoto ya usafiri kufuatia maumbile yao,hasa kwa walemavu wenye matatizo ya viungo vya miguu na wale wasioona. Wanasiasa hawa ambao wanawania kama wawaniaji huru jijini Mombasa,hawana gari za kufanyia kampeni mashinani,hatua inayowafanya kulemaza kampeni zao. Mwanahabari wetu Athuman Luchi ametusimulia.

Jioni - Voice of America
Raila, Ruto wahutubia mikutano ya mwisho ya kampeni kabla ya uchaguzi mkuu - Agosti 06, 2022

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Aug 6, 2022 29:59


Odinga anayepeperusha bendera ya muungano wa Azimio la Umoja One Kenya na viongozi wa mrengo huo pamoja na wafuasi wao, walikusanyika katika uwanja wa michezo wa Kasarani huku Ruto, anayewania kwa tiketi ya chama cha UDA chini ya muungano wa Kenya Kwanza akijiunga na wenzake kwenye uwanja wa Nyayo.

uda ruto agosti odinga kabla mkuu azimio uchaguzi mkuu kampeni
VOA Express - Voice of America
UNICEF yazindua kampeni ya kutokomeza ndoa za utotoni Tanzania - Julai 29, 2022

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jul 29, 2022 29:59


Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia watoto, UNICEF, imeeiorodhesha Tanzania kama ya 11 kati ya nchi zenye idadi kubwa zaidi ya ndoto ndoa za utotoni na kuzindua kampeni kabambe iitwayo "Binti."

Habari za UN
Kampeni ya M'mera mpoyamba yasaidia SDG3 Malawi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 18, 2022 2:56


Katika kusongesha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs likiweno lengo namba 3 linalolenga Afya bora na ustawi, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Malawi linaendesha kampeni ya M'mera mpoyamba inayohamasisha wajawazito kufika katika vituo vya afya angalau mara nne kabla ya kujifunga na kuhakikisha wanapata saa moja ya ziada ya kulala ili kujihakikishia ujauzito salama na kujifungua mtoto mwenye afya bora. Kampeni hiyo inaendeshwa kwa njia mbalimbali ikiwemo mchezo wa video ambao Leah Mushi wa Idhaa hiiya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa ameutafsiri kwa lugha ya Kiswahili.

SBS Swahili - SBS Swahili
Alfred aeleza sababu zakujiondoa katika kampeni za ubunge wa Chesumei

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 19, 2022 9:23


Kampeni za uchaguzi mkuu nchini Kenya, zina endelea kupamba moto haswa baada ya vyama kufanya mchujo wa wagombea pamoja nakuwatea vinara na manaibu wao.

Habari za UN
Kampeni ya MINUSCA imezinduliwa kwa lengo la kuimarisha utekelezaji wa majukumu

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 3, 2022 2:33


Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, MINUSCA umezindua kampeni ya ulinzi wa raia ili kusaidia upatikanaji wa amani pamoja na kuwezesha mamlaka za serikali nchini humo kutekeleza majukumu yake.

SBS Swahili - SBS Swahili
Wiki ya tatu ya kampeni ya uchaguzi mkuu yatawaliwa na gharama ya maisha

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 29, 2022 9:07


Wiki ya tatu ya kampeni ya uchaguzi mkuu ili tawaliwa na shinikizo za gharama za maisha, baada ya mfumuko wa bei kuongezeka kwa 5.1%.

wiki tatu maisha mkuu uchaguzi mkuu kampeni
SBS Swahili - SBS Swahili
Kiongozi wa upinzani ana matumaini kuhusu kampeni ya uchaguzi licha yakupatwa na UVIKO-19

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 22, 2022 10:23


Kiongozi wa chama cha Labor Anthony Albanese, amaliza siku yake ya tatu akijitenga baada yakuambukizwa UVIKO-19.

kiongozi uchaguzi kampeni
Habari za UN
Kampeni yasaidia kuondokana na fikra potofu kuhusu chanjo dhidi ya Covid 19 Kisumu, Kenya

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 21, 2022 2:16


Nchini Kenya harakati za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF za kuondoa fikra potofu katika kaunti ya Kisumu kuhusu chanjo dhidi ya Corona au COVID-19 zimezaa matunda na sasa hata wale waliokuwa wamesita kupata chanjo hiyo wameanza kupata. 

Alfajiri - Voice of America
Kenya yazindua kampeni ya kupunguza visa vya Malaria. - Aprili 21, 2022

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Apr 21, 2022 30:00


Wasimamizi wa kampeni hiyo wanasema ni kampeni ya kuongeza uelewa wa athari za Malaria katika jamii na kusukuma mbele lengo la serikali la kutokomeza ugonjwa huo ndani ya jamii.

SBS Swahili - SBS Swahili
Hoja za afya, na usalama wa mipaka zafungua wiki ya pili ya kampeni ya uchaguzi mkuu

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 19, 2022 7:15


Wiki ya pili ya kampeni za uchaguzi mkuu zime tumbukia katika vita vya kampeni zakutisha kati ya vyama viwili vikubwa nchini.

wiki hoja pili afya mkuu uchaguzi mkuu kampeni
SBS Swahili - SBS Swahili
Waziri Mkuu afanya kampeni katika wikendi ya Pasaka

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 16, 2022 9:11


Waziri Mkuu anaendelea kutetea uamuzi wa chagua lake kwa mgombea wa chama cha Liberal, kwa eneo bunge la Warringah ambalo liko mjini Sydney.

Habari RFI-Ki
Kuelekea uchaguzi mkuu wa rais nchini Ufaransa

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Apr 12, 2022 9:59


Raia wa faransa watapiga kura jumapili hii kumchagua rais wao. Jumla kuna  wagombea 12 akiwemo Rais Macron ambaye anawania kuchaguliwa tena. Kampeni za uchaguzi zinatamatika huku matamshi ya kibaguzi yakitolewa na wagombea kadhaa. Una maoni gani kuhusu uchaguzi huo?Je, Ufaransa inaweza kuanguka na kuingia katika hali ya kutovumilia?Unadhani nani atashinda uchaguzi huu?

rais raia mkuu ufaransa uchaguzi mkuu kampeni
Habari za UN
Hakimiliki ya mwili mtandaoni ni muhimu sana kwa wanawake:UNFPA

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 30, 2021 2:03


Kampeni mpya iliyozinduliwa mwezi huu wa DFesemba na shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani linalohusika pia na afya ya uzazi UNFPA ya “Hakimiliki ya miwli wa binadamu” ina lengo la kuwasukuma watunga sera, sekta za teknolojia na mitandao yote ya kijamii kuuchukulia unyanyasaji na ukatili wa miili ya binadamu hususani ya wanawake mtandaoni kuwa ni suala linalohitaji kupewa uzito kama ilivyo ukiukwaji wa hakimiliki zingine. Flora Nducha na taarifa kamili (TAARIFA YA FLORA NDUCHA)  Kupitia video ya UNFPA ya uzinduzi wa kampeni hiyo, mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo Natalia Kanem anahoji endapo dunia inafahamu kwamba asilimia 85 ya wanawake walio na fursa ya intaneti wameripoti kushuhudia ukatili mtandaoni na wengine asilimia 38 wakipitia binafsi ukatili huo.  Amesema wanawake na wasichana, makundi ya walio wachache na watu waliotengwa wana uwezekano mkubwa wa picha zao kutumiwa vibaya mtandaoni, kudhalilishwa na kutumika katika vitendo vya ngono bila ridhaa yao. Hivyo amesisitiza kuwa (SAUTI YA NATALIA KANEM1-MELLISSA) “Ukatili wa mtandaoni unasababisha madhara makubwa, lakini makampuni ya kidijitali na watunga sera wanaonekana kuufumbia macho wakiweka thamani kubwa na ulinzi kwa hatimiliki kuliko wanavyofanya kwa binadamu.”  Hata hivyo amesema (SAUTI YA NATALIA KANEM2-MELLISSA) “Ukweli ni kwamba haumiliki mwili wako mtandaoni. Na hii ndio sababu sisi hapa UNFPA, tumezindua haki ya mwili, hakimiliki ya kwanza kwa ajili ya mwili wa binadamu. Kwa kudai haki yetu ya mwili na kuchukua udhibiti wa miili yetu mtandaoni ndio pekee tutakapoweza kukomesha ukatili wa kijinsia unaoshuhudiwa kila siku kote duniani.”  Bi Kanem ametoa wito kwa kila mtu kuuchukulia ukiukwaji huu wa haki za binadamu kwa uzito mkubwa, na kampeni inawatumia watu mbalimbali wenye ushawishi, mashuhuri, wanaharakati na watumiaji wa mitandao ya kijamii ikiwataka kuongeza herufi (B) kwenye picha zao kuunga mkono ukomeshaji wa ukatili wa kijinsia mtandaoni.   

Habari za UN
UNICEF yawatumia viongozi wa dingi kuhamasisha kampeni ya chanjo ya COVID-19 Garissa

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 30, 2021 2:12


Janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 likiendelea kutikisa dunia huku taarifa potofu kuhusu chanjo zikiendelea kusambaa, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini Kenya limechukua hatua ya kushirikiana na viongozi wa dini ikiwemo wale wa madhehebu ya kiislamu ili kusaidia kuelimisha waumini wao juu ya chanjo na faida zake katika kuepusha kusambaa zaidi kwa virusi vinavyosababisha ugonjwa huo. Taarifa ya John Kibego inafafanua zaidi.(Taarifa ya John Kibego)Nats.. Tuko katika kaunti ya Garissa nchini Kenya waumini wa madhehebu ya kiislamu wakiingia msikitini tayari kwa ibada wakati huu ambapo gonjwa la Corona bado linaendelea kuleta shaka na shuku. Kama mbinu ya kudhibiti kuenea kwa COVID-19 nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF imeshapeleka dozi milioni 21 za chanjo dhidi ya Corona na linasaidiana na Wizara ya afya kuhakikisha watu wanachanjwa. Hata hivyo kuna changamoto ya taarifa potofu kuhusu chanjo na ndipo UNICEF ikashirikisha viongozi wa dini akiwemo Sheikh Omar Dagane, Imán wa msikiti hapa Garissa.(Sauti ya Sheikh Omar Dagane)- Jongo“Kama Imam wa jamii hii niña wajibu wa kushauri jamii kuhusu suala lolote la maslahi yao. Leo nimewaeleza waumini umuhimu wa kujikinga na COVID-19 kwa kupata chanjo. kupata chanjo ili kujikinga na COVID-19. Nimenukuu moja ya kauli za Mtume Muhamad SAW alipoulizwa na mfuasi wake iwapo amfunge kamba ngamia wake ambapo jibu lilikuwa Muamini Mungu lakini funga ngamia wako. Na vivyo hivyo tunapaswa kumuamini Mungu lakini tupate chanjo, vaa barakoa, nawa mikono, ili kujikinga.” Baada ya mahubiri mmoja wa washiriki Isak Abidi akafunguka akisema, “Nimesikiliza mahubiri ya Imam na ujumbe wa afisa wa afya na sasa nimeamua kuwa nakwenda kupata chanjo.” Abdullahi Abagira ni afisa wa UNICEF kaunti ya Garissa na anasema COVID-19 imekuwa na madhara ya aina mbalimbali hususan kwa watoto na hivyo UNICEF imesaidia kwa kusambaza siyo tu chanjo bali pia kufanikisha uwepo wa wahudumu wa afya wa kutoa huduma hizo.  

Habari za UN
Utani baina ya makabila ni moja ya mbinu za kuchagiza amani na maelewano

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 23, 2021 2:39


Tofauti zinapaswa kuimarisha jamii badala ya kuisambaratisha, huo ndio  ujumbe uliotamalaki wakati wa kampeni iliyoendeshwa nchini Mali na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kuweka utulivu nchini humo MINUSMA kwa kushirikiana na chama cha wadau wa Umoja wa Mataifa nchini humo, MANU. Kampeni ilileta pamoja wazee kwa vijana, wanawake kwa wanaume pamoja na Watoto wenye vipaji vya Sanaa na utamaduni. Nini kilifanyika, tujiunge na Jason Nyakundi katika taarifa hii. Utamaduni na sanaa kutoka makundi mbalimbali vilishamiri kwenye tamasha hili la utamduni kwa ajili ya amani kwenye viunga vya mji mkuu wa Mali, Bamako. Ilikuwa ni ngoma, nyingine zikitumia vikaragosi. Chifu wa Kijiji cha Koulouninke Adama Coulibally anasema “ukienda njia mbaya unakuwa hatarini kufika eneo hatarishi. Matamanio yetu ni kwamba katu tusiende njia mbaya. Hicho ndio tumejifunza kutoka kwa wazee wetu. Tunapaswa kupeleka ujumbe huu kwa watoto wetu na marafiki zetu. “ Abdoula Toure, afisa kutoka kitengo cha mawasiliano MINUSMA anasema, “Mali ni nchi kubwa na yenye makabila na tamaduni nyingi tofauti tofauti. Sisi Umoja wa Mataifa tunatambua hilo na ndio  maana tunapatia umuhimu matumizi chanya ya tofauti hizo ili kuleta utangamano.”  Kwa Madani Diabate ambaye ni mhifadhi wa turathi za kiasili anasema “tofauti za kitamaduni na kikabila nchini Mali zinapaswa kutumika kujenga amani. Kupitia huo utofauti ndio tunaleta utani baina ya makabila na kisha ujirani mwema. Hicho ndio kinaweza kuimarisha amani na kujenga utangamano baina yetu.” Wanawake ambao wamekuwa wakitaabika zaidi kutokana na machafuko nchini Mali nao wakapaza sauti kupitia Fatoumata Traore, mshauri wa kijamii mjini Bamako.“Ujumbe ambao naupaza kila wakati ni kwamba wanawake lazima wajumuishwe. Inapaswa wanawake nchini Mali watambue kuwa Mali ni moja na haigawanyiki. Kazi hiyo tunapasa kuifanya na tutaikamilisha.” Na ili kuishi pamoja, wananchi wa Mali wafanye nini? Baba Salah Cisse, mwanamuziki aliyeshiriki kampeni hiyo akatoa ujumbe kupitia wimbo akisema, “Ili kuishi pamoja tunapaswa kukubaliana na kusameheana! Kama huna jinsi, muombe msamaha jirani yako! Kama hatutasameheana, amani haiwezi kupatikana. Na bila amani hakuna maendeleo.”  

SBS Swahili - SBS Swahili
Navazu Ozegbe tayari kutengeza historia katika uchaguzi wama diwani wa Fairfield New South Wales

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 1, 2021 17:23


Kampeni za uchaguzi wa udiwani katika halmashauri ya jiji la Fairfield, NSW zina endelea kwa kina siku chache zikiwa zinasalia kwa wapiga kura kutoa hukumu yao.

SBS Swahili - SBS Swahili
Je! Nani atarithi kazi ya Gladys Berejiklian Jumma Nne?

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Oct 3, 2021 7:51


Kampeni zina endelea ndani ya chama cha Liberal jimboni New South Wales, kwa wadhifa wa kiongozi ambao ume achwa tupu baada yakujiuzulu kwa Gladys Berejiklian.

Habari za UN
Umoja wa Mataifa waadhimisha siku ya wahudumu wa masuala ya kibinadamu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 19, 2021 1:52


Leo ni siku ya wahudumu wa masuala ya kibinadamu duniani ambao wako msitari wa mbele kusaidia kuokoa maisha ya watu walio hatarini zaidi duniani majanga yanapozuka, na kwa kufanya hivyo huweka rehani maisha yao kila uchao amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.  (Taarifa ya Flora Nducha)  Kupitia ujumbe wake kwa ajili ya siku hii Guterres amesema kote duniani wahudumu wa kibinadamu wanakabiliwa na ongezeko la vitisho, Nas katika miaka 20 iliyopita matukio ya kupigwa risasi, kutekwa na mashambulizi mengine dhidi ya mashirika ya kibinadamu yameongezeka mara 10.  Ameongeza kuwa mwaka huu pekee angalau wahudumu wa masuala ya kibinadamu 72 wameuawa katika maeneo ya mizozo, na kwa mantiki hiyo amesisitiza  “Katika siku hii ya wahudumu wa masuala ya kibinadamu tunawaenzi wahudumu hao kila kona ya dunia na kuahidi kufanya kila liwezekanalo kuwalinda wao na kazi yao muhimu.”  Maudhui na kampeni kubwa ya siku ya mwaka huu imejikita katika mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi ambao unatishia kusambaratisha nyumba, uwezo wa watu kuishi na maisha yao miongoni mwa watu masikini kabisa duniani.  Katibu mkuu anamtaka kila mtu kujiunga na kampeni hiyo #TheHumanRace ili kusaidia kufikisha ujumbe kwa viongozi wa dunia kwamba hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi hazitomwacha yeyote nyuma.  Hivyo Guterres ameihimiza dunia kwamba "Dharura ya mabadiliko ya tabianchi ni mbio tunazopoteza. Lakini ni mbio tunazoziweza na lazima tushinde. Hebu tukaze buti zetu zetu za kukimbilia, jiunge na Kampeni ya TheHumanRace, na kwa pamoja, hakikisha kila mtu anakamilisha mbio hizo.” 

Habari za UN
Bhutan imefanikiwaje kutoa chanjo kwa asilimia 90 kwa wananchi wake?

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jul 29, 2021 2:09


Kiwango cha utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona au COVID-19 nchini Bhutan huko barani Asia kimefikia asilimia 90 ya wananchi wote wenye umri wa kupatia chanjo hiyo. Kampeni ya utoaji chanjo imefanywa na serikali ya Bhutan kwa ushirikiano na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.    

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 11 Julai 2021

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jul 11, 2021 12:05


Kampeni mpya ya matangazo inayowahamasisha wa Australia wachukue chanjo za COVID-19, imezinduliwa na serikali ya shirikisho.

Habari za UN
Walinda amani Jamhuri ya Afrika ya kati: Ulinzi tulionao kwa wakati huu ni chanjo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 21, 2021 1:46


Kampeni ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa Covid-19 kwa walinda amani wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR imezinduliwa mwanzoni wa wiki hii kwa kuwa walinda amani ni moja ya makundi ya kipaumbele.  Taarifa ya Anold Kayanda inaeleza zaidi.

Habari za UN
Shehena ya chanjo ya COVID-19 kupitia COVAX yawasili Somalia , kampeni ya anza

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 16, 2021 2:15


Somalia imejiunga na orodha inayozidi kuongezeka ya nchi zinazopokea chanjo za COVID-19, kupitia mpango wa COVAX baada ya kupokea shehena yake ya kwanza ya chanjo hizo tayari kwa usambazaji nchi nzima. Ahmidiwe Olottu na taarifa zaidi (TAARIFA YA AHIMIDIWE OLOTTU)  

SBS Swahili - SBS Swahili
NSW yaregeza vizuizi kampeni mpya ya chanjo ikizinduliwa

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jan 29, 2021 7:06


Kuanzia Ijumaa tarehe 29 Januari, vizuizi vya COVID-19 viliregezwa katika jimbo la New South Wales, baada ya milipuko kadhaa ya virusi hivyo kudhibitiwa.

Habari za UN
WHO/UNICEF wachukua hatua kulinda watoto dhidi ya polio

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 13, 2020 2:26


Kampeni kubwa ya chanjo imezinduliwa leo nchini Sudan Kusini na mashirika ya Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO na la kuhudumia Watoto UNICEF kwa lengo la kuwachanja watoto milioni 1.5 dhidi ya polio baada ya mlipuko mpya kusababisha kupooza kwa watoto 15.

SBS Swahili - SBS Swahili
Douglas: "Usalama wa mitandao ume imarishwa sana kwa uchaguzi wa 2020 wa Marekani"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 13, 2020 13:36


Kampeni za uchaguzi duniani kote zimechukua mifumo tofauti kuwavutia na kuwashawili wapiga kura.

Habari za UN
Kampeni ya kutulia kwanza yaani #PledgetoPause yazinduliwa

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 21, 2020 3:01


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizindiua hatua ya kuzuia usambazaji wa taarifa za uongo mitandaoni, ametoa wito kwa watu kote ulimwenguni kutoa ahadi ya kutulia kwanza kabla ya kusambaza taarifa mitandaoni.

Habari za UN
Kampeni ya chanjo dhidi ya polio na surua Somalia kichocheo cha mustabali bora wa watoto

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 8, 2020 3:06


Malaki ya watoto nchini Somalia wamechanjwa dhidi ya ugonjwa wa surua na polio wakati wa kampeni ya chanjo kudhibiti mlipuko wa magonjwa hayo hatari, imeeleza taarifa ya mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, UNSOM.

SBS Swahili - SBS Swahili
Joto la kampeni ya uchaguzi wa rais laongezeka Tanzania

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Sep 3, 2020 6:37


Kampeni za uchaguzi wa rais zime anza rasmi nchini Tanzania, ambako vyama husika vime anza kuuza sera zao kwa kina.

Habari za UN
Kampeni za nyumba kwa nyumba, eneo kwa eneo zatokomeza Polio Afrika

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 27, 2020 3:58


Polio! Polio! Polio! Ugonjwa uliokuwa ukilemaza watoto 75,000 kila mwaka wakati wa miaka ya 1990 katika nchi za Afrika wanachama wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa kanda ya Afrika. Mataifa hayo ni 47 barani Afrika isipokuwa Somalia, Sudan, Eritrea, Misri, Libya na Tunisia. Gonjwa hilo halina tiba bali lina kinga ambayo ni chanjo, kinga ambayo viongozi kuanzia wa kaya hadi kimataifa walisimamia kidete kuhakikisha inamfikia kila mtoto barani Afrika na tarehe 25 mwezi huu wa Agosti, ukanda huo umetangazwa kuwa hakuna tena Polio! Nini kimefanyika?

Habari za UN
Watoto Haiti na uelewa wa kina jinsi ya kujikinga na COVID-19

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 14, 2020 1:43


Kampeni iliyoendeshwa kwa pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF na Wizara ya Afya ya Umma na Idadi ya watu nchini Haiti kuhusu jinsi ya kujikinga na virusi vya Corona, au COVID-19, imekuwa na mafanikio katika kupunguza maambukizi na hata watoto wana uelewa.

Habari za UN
Malawi, kampeni ya UNICEF yaweka wazi baba wa kipekee

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 29, 2020 1:58


Nchini Malawi, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linapigia chepuo kitendo cha mzazi wa kiume kusaidiana na mzazi mwenzake katika malezi na makuzi ya watoto wao ili hatimaye watoto hao waweze kukua si tu kimwili bali pia kifikra.

Habari za UN
13 Mei 2020

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 13, 2020 12:11


Kampeni ya #Reimagine kuibuka na mpango wa dunia ya watoto baada ya COVID-19. Kitengo cha damu salama katika hospitali ya rufaa mkoa wa Dodoma nchini Tanzania kimewatoa hofu wachangiaji wa damu kuwa uwepo wa ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 usiwatishe kwenda kuchangia damu. Katikati ya COVID-19, WFP yaendelea kunusuru wahitaji.

SBS Swahili - SBS Swahili
Kampeni mpya yalenga vinywaji vyenye sukari

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Feb 24, 2020 6:05


Mashirika kuminatisa nchini Australia, yamejumuika kumulika madhara kwa afya ya vinywaji vyenye sukari.

SBS Swahili - SBS Swahili
Cultural differences cause many migrants to be unaware of alcohol effects - Tofauti za kitamaduni husababisha wahamiaji wengi kutokujua madhara ya pombe

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 16, 2019 4:33


A new educational campaign is aiming to teach multicultural communities about the potential dangers of alcohol consumption. - Kampeni mpya ya uelimishaji inalenga kufundisha jumuiya za kitamaduni kuhusu hatari za matumizi ya pombe.

Habari RFI-Ki
Habari RFI-Ki - Kampeni ya waandamanaji kutotii sheria nchini Sudan italazimisha jeshi kukabidhi mamlaka kwa raia?

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Jun 10, 2019 9:57


Waandamanaji nchini Sudan wameingia siku ya pili ya maandamano ya kutotii sheria ili kushinikiza jeshi kukabidhi madaraka kwa raia. Je hatua hiyo itafanikiwa? Ungana na Fredrick Nwaka aliyekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu.

sudan raia sheria habari ungana kampeni fredrick nwaka
SBS Swahili - SBS Swahili
Jobs and healthcare dominate Sunday election campaigning - Ajira na huduma ya afya, vya tawala kampeni za uchaguzi Jumapili

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 14, 2019 5:22


A day of intense campaigning has seen the Coalition promise to deliver jobs and a strong economy. - Leo jumapili ilikuwa siku nyingine ya kampeni kali, ambako chama cha mseto kili ahadi kutoa ajira pamoja nakuimarisha uchumi.

SBS Swahili - SBS Swahili
A tight finish expected in the race for government in NSW - Kampeni za uchaguzi wa NSW zaingia katika dakika za lala salama

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 22, 2019 9:49


New South Wales residents will go to the polls on Saturday to decide who will lead their state for the next four years. - Wakazi wa NSW wata ingia katika vituo vyakupiga kura jumamosi 23machi2019, kuamua atakaye ongoza jimbo hilo kwa muda wa miaka minne ijayo.

SBS Swahili - SBS Swahili
Vote fraud suspicion increases in DR Congo postponed presidential election - Madai ya wizi wa kura yasambaa katika kampeni za uchaguzi wa urais ujao wa DR Congo

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 23, 2018 28:57


Voters and candidates campaigning for the postponed presidential election in DR Congo, have begun expressing their suspicion about the elections which will now be held on 30 December 2018. - Wapiga kura na wagombea wa uchaguzi wa urais wa DR Congo, wame anza kuelezea wasi wasi wao kuhusu usalama wa kura katika uchaguzi wa urais utakao fanywa tarehe 30 Disemba 2018.

Mjadala wa Wiki
Mjadala wa Wiki - Wananchi wa DRC kupiga kura siku ya Jumapili

Mjadala wa Wiki

Play Episode Listen Later Dec 19, 2018 14:01


Wananchi wa DRC watapiga kura siku ya Jumapili, kumchagua rais mpya. Kampeni zinamalizika wiki hii kuelekea Uchaguzi huo wa kihistoria. Ushindani mkali ni kati ya wagombea watatu, Emmanuel Shadary kutoka chama tawala, Martin Fayulu kutoka muungano wa upinzani wa Lamuka, na Felix Tshisekedi. Tume ya Uchaguzi CENI inasema iko tayari kwa uchaguzi huu licha ya kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiweko kuteketea moto vya baadhi ya vifaa vya kupigia kura.

wiki drc kura siku felix tshisekedi tume martin fayulu uchaguzi wananchi jumapili kupiga kampeni
Wimbi la Siasa
Wimbi la Siasa - Kampeni za DRC zakumbwa na vurugu

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Dec 15, 2018 9:43


Siku 10 kuelekea Uchaguzi Mkuu nchini DRC, mauaji yameripotiwa katika kampeni za siasa hasa katika mikutano ya Martin Fayulu, mgombea vya vyama upinzani lakini pia kuteketea moto kwa jengo la kuhifadhi vifaa vya kupigia kura jijini Kinshasa. Tunajadili hili kwa kina.

drc kinshasa siku martin fayulu uchaguzi mkuu kampeni tunajadili
Wimbi la Siasa
Wimbi la Siasa - Nkurunziza azindua kampeni ya kuibadilisha Katiba

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Dec 15, 2017 10:15


Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza, amezindua kampeni ya kuibadilisha Katiba ya nchi hiyo, lenye lengo la kuongeza muda wa rais kukaaa madarakani kutoka miaka mitano hadi miaka saba. Iwapo mabadiliko hayo yatapitishwa, Nkurunziza ana nafasi ya kuwania tena uongozi wa nchi hiyo mwaka 2020 na kuongoza mihula miwili hadi 2034. Hii ni mbinu ya Nkurunziza kuendelea kukaa madarakani ?

rais hii katiba nkurunziza kampeni
Wimbi la Siasa
Wimbi la Siasa - Kampeni za lala salama zapamba moto nchini Kenya

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Aug 22, 2017 10:19


Kampeni za lala salama nchini Kenya zimepamba moto kuelekea uchaguzi huo Agosti 8 mwaka huu huku wagombea Uhuru Kenyatta wa Chama cha Jubilei na mgombea wa NASA, Raila Odinga wakichuana vikali katika kinyang'anyiro hicho. Je nani atashinda katika uchaguzi huo na kwa nini? Uchambuzi wa kina katika Makala ya Wimbi la Siasa ukiwa naye Victor Robert Wile utakata kiu yako ya kujua mbivu na mbichi kuhusu uchaguzi wa Kenya.