POPULARITY
Kampeni za uchaguzi wa shirikisho wa 2025 zina karibia tamati.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini DRC ambako ghasia za hivi karibuni huko Goma zimeongeza mahitaji ya huduma za afya, WHO imechangia vifaa muhimu vya matibabu ili kukabialiana na hali hiyo. Pata pia muhtasari wa habari na mashinani.Kufuatia ripoti za kuweko kwa ugonjwa usiojulikana huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambao tayari umeambukiza mamia ya watu na kusababisha makumi ya vifo, shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO, limesema bado linaendelea na uchunguzi wa ugonjwa huo uliotangazwa kwa chapisho la kikanda la WHO.Kampeni ya chanjo ya polio inayoendelea ukanda wa Gaza kwa lengo la kudhibiti kusambaa kwa virusi vya polio na kuzuia tishio la ugonjwa huo kusambaa maeneo mengine na nchi jirani, imekuwa na mafanikio makubwa kwani hata eneo la Gaza Kaskazini, mwitikio ulikuwa mkubwa licha ya mvua na baridi kali.Na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula duniani, WFP hii leo limetangaza kuwa sitisho la mapigano Gaza limewezesha kufikisha eneo hilo kwa wastani maradufu ya shehena za vyakula kilichokuwa kinapelekwa kabla ya sitisho la mapigano.Katika mashinani, hivi majuzi Shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, UNICEF katika ripoti yake lilibaini kwamba mtoto 1 kati ya watano nchini Ukraine ameripoti kupoteza ndugu au rafiki wa karibu tangu kuzidi kuongezeka kwa vita miaka mitatu sasa. Akitafakari juu ya zama zijazo, Toby Fricker, Afisa Mkuu wa mawasiliano wa Shirika hilo nchini Ukraine anasema UNICEF inaendelea kushikamana nao.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Katika makala ya leo Anold Kayanda anatupeleka nchini Tanzania ambako katika kuhamasisha elimu iliyo salama inayolenga kumlea na kumfundisha mtoto kwa njia chanya zisizoumiza, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, (UNICEF) linamuangazia Mwalimu Magesa Stanslaus ambaye amebadilika kutoka katika matumizi ya viboko na sasa anatumia motisha tofauti kuwarekebisha wanafunzi wake.
Ungana nami Mtangazaji wako Judith Mpalanzi katika Kipindi cha Elimu Jamii ambapo leo tupo na Bwana Stephen Motambi kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) akizungumzia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na tunapoelekea kwenye Kampeni za uchaguzi huo. L'articolo Fahamu mambo ya kuzingatia kuelekea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. proviene da Radio Maria.
Donald Trump achaguliwa kuwa rais wa 47 wa Marekani, Ziara ya rais wa Kenya William Ruto huko Addis Ababa Ethiopia, na Sudan Kusini, na Raila Odinga kuzindua azma yake ya kuwania uenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika, kuelekea uchaguzi huo utakaofanyika Februari mwaka 2025. Mapigano makali kati ya waasi wa M23 na wazalendo mashariki mwa DRC, Umoja wa Mataifa wasema uamuzi wa kuahirishwa uchaguzi nchini Sudani Kusini haukubaliki, Duma Boko atawazwa rasmi kama rais mpya wa Botswana, Uhusiano wa Urusi na Marekani baada ya Trump kushinda uchaguzi
Mashambulizi makali ya anga kutoka kwa jeshi la Israel, idadi kubwa ya watu kutawanywa na ukosefu wa fursa ya kufika Gaza Kaskakzini vimelazimisha kuahirishwa kwa kameni ya chanjo kwa mujibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la Afya Duniani WHO, la kuhudumia watoto UNICEF na la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA. Asante Anold, kampeni hiyo iliyoahirishwa ilitakiwa kuanza leo n ani duru ya mwisho ya chango ya kampeni iliyolenga kuwachanja watoto 119,279 kote Gaza Kaskazini kwa dozi ya pili ya chanjo ya polio aina ya nOPV2, lakini hali ya sasa imefanya iwe vigumu kwa familia kupeleka watoto wao kwenye vituo vya chanjo, na kwa wahudumu wa afya kuendesha huduma kwa usalama.Mashambulizi ya makombora yanayoendelea dhidi ya miundombinu ya kiraia yamepunguza maeneo yanayokubaliwa kwa usitishaji wa uhasama kwa mnajili ya masuala ya kibinadamu kuwa kwenye Jiji la Gaza pekee, ikilinganishwa na wakati wa awamu ya kwanza ya chanjo iliyofanyika tarehe 1-12 Septemba 2024.Hali hii inahatarisha kufikiwa kwa lengo la angalau asilimia 90 ya watoto kuchanjwa, jambo ambalo ni muhimu ili kukomesha usambaaji wa virusi vya polio na kulinda afya za watoto.WHO na UNICEF wamesema kuwa kucheleweshwa kwa chanjo ya polio kunaweza kuongeza hatari ya virusi kuenea zaidi Gaza na maeneo Jirani na kuchelewesha utoaji wa dozi ya pili ya chanjo ndani ya wiki sita kunapunguza uwezo wa chanjo hiyo kuimarisha kinga za watoto na kuzuia maambukizi.Tangu duru ya pili ilipoanza tarehe 14 Oktoba 2024, jumla ya watoto 442,855 wenye umri wa chini ya miaka kumi wamefanikiwa kuchanjwa katika maeneo ya kati na kusini mwa Gaza.UNICEF na WHO wanatoa wito kwa pande zote zinazohusika katika mzozo kutekeleza usitishaji mapigano wa kibinadamu na kuhakikisha kuwa raia, wahudumu wa afya, na miundombinu ya kiraia kama shule na hospitali inakingwa dhidi ya mashambulizi.Mashirika hayo yamesisitiza umuhimu wa kuanza tena kampeni ya chanjo mara moja ili kuzuia kupooza kwa watoto na kuimarisha kinga dhidi ya polio.Katika juhudi za kuhakikisha huduma bora, takribani watoto 357,802 pia walipatiwa virutubisho vya vitamini A kama sehemu ya juhudi za kuunganisha chanjo ya polio na huduma zingine muhimu za afya.Mashirika ya WHO na UNICEF ymesisitiza kuwa kusitisha vita na kuwezesha chanjo ni hatua muhimu ili kuzuia mlipuko wa polio kuendelea na kulinda afya ya watoto wote Gaza.
Karibu uungane nami Elizabeth Masanja, katika kipindi cha Jinsia na Maendeleo leo tupo na Ndugu Anectus Asingizibwe, Mwenyekiti wa Kampeni kupinga ukatili shujaa wa maendeleo na ustawi wa jamii (SMAUJATA) Wilaya ya Kisarawe Mkoa wa Pwani akituongoza kujifunza mchango wa Mifumo ya Familia katika kuimarisha usawa wa Kijinsia. L'articolo Ni, kwa namna gani Familia husaidia kuimarisha Usawa wa Kijinsia katika jamii? proviene da Radio Maria.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Zaidi ya watoto 560,000 wamepokea chanjo dhidi ya virusi vya polio aina ya pili (cVDPV2) kwenye Ukanda wa Gaza katika duru ya kwanza ya kampeni kubwa ya chanjo iliyomalizima jana yamesema mashirika ya Umoja wa Mataifa.Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO, watoto waliopokea chanjo hiyo kupitia kampeni ya dharura ya chanjo Gaza ni wale wenye umri wa chini ya miaka 10.Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X zamani Twitter Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Adhanon Ghebreyesus amesema “Tunafurahia timu zote za wahudumu wa afya, zilizoendesha operesheni hii ngumu. Tunashukuru sana kwa familia kwa imani na ushirikiano wao. Haya ni mafanikio makubwa huku kukiwa na hali mbaya ya kila siku ya maisha katika Ukanda wa Gaza. Hebu fikiria nini kingeweza kufikiwa endapo kungekuwa na ushitishwaji mapigano.”Awamu ya kwanza ya chango ilianza Septemba Mosi na lengo lilikuwa ni katika kila duru kuchanja zaidi ya watoto 640 000 wa umri wa chini ya miaka 10.Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA limesema maelfu kwa maelfu ya watoto wmechanjwa na kukamilika kwa awamu hiyo ya kwanza ya chanjo ni mafanikio makubwa kwa shirika hilo na wadau wote walioshiriki kwani wamefikia lengo kwa asilimia 90 ingawa sasa changamoto ni kutoa dozi ya pili ya chanjo hiyo katika awamu ya pili ya kampeni inayotarajiwa katika wiki zijazo.Dozi za chanjo ya polio zaidi ya milioni 1.6 ziliwasili Gaza ili kukamilisha awamu zote mbili za chanjo inayohusisha wahudumu wa afya zaidi ya 2700.
Uzinduzi wa kampeni ya aliyekuwa waziri mkuu wa Kenya Raila Odinga, anayegombea unyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika, kongamano la 74 la WHO mjini Brazzaville, nchini Congo, DRC na Kampeni inayoitwa ICC Haki kwa DRC, hali ya usalama kuendelea kuzorota nchini Sudan, shambulio la kigaidi Burkina Faso laua zaidi ya watu 300, hali nchini Israeli, na mchakato wa uchaguzi wa Marekani mwezi Novemba
Karibu Ungane na Esther Magai Hangu katika Kipindi cha Elimu Jamii, mwezeshaji Bwana Anetus Asingizibwe Mwenyekiti wa Kampeni ya kupinga ukatili shujaa na Maendeleo Simaujata kutoka Wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani, mada Usalama wa Watoto kwa Maendeleo ya Taifa. L'articolo Fahamu namna kumlinda Mtoto na kumpatia haki zake za msingi. proviene da Radio Maria.
Wawawake kutoka ukanda wa Afrika wanajumuika Dar Es Salaam mwishoni mwa juma kupiga jeki kampeni za kuboresha afya Nchini DRC mikakati iliyoweka kudhibiti mlipuko wa Kipindu Pindu ulioripotiwa katika mataifa ya Afrika ya Kusini ,inaendelea kulipa na hata kuwa msaada kwa mataifa jirani kama vile Zambia
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Wagombea DRC wakamilisha kampeni upigaji kura Jumatano
Kampeni za mwisho mwisho zilifanyika Jumatatu kwelekea kwa uchaguzi mkuu Jumatano huku kukiwa na wasiwasi kama zoezi hilo litakuwa la haki na salama.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Kiongozi wa upinzani wa shirikisho Peter Dutton amesema atafanya kura nyingine ya maoni, kama kura yakuweka sauti yawa Australia wa kwanza bungeni ndani ya katiba inafeli.
WImbi la siasa juma hili Ali Bilali na wachambuzi wake wanajadili hali ya kisiasa nchini Zimbabwe kuelekea kwenye uchanguzi mkuu wa rais
Kampeni za uchaguzi mkuu zime anza katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Tunaangazia hatua ya mahakama nchini Zimbabwe kuidhinisha marafuku kuanzishwa kwa kampeni iliyopangwa kufanywa na chama kikuu cha upinzani wakati huu pia kiongozi wake mkuu Nelson Chamisa akikabiliwa na vikwazo.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Ungana na Frank Kashonde katika kipindi cha Jinsia na Maendeleo, mada iliyopo ni hali ya usalama kwa Watoto katika Jamii., Mwezeshaji Bwana Anectus Asingizibwe Mwenyekiti wa Kampeni ya Kitaifa ya Kupinga Ukatili kwa Wilaya ya Kisarawe, Mkoa wa Pwani, (SMAUJATA)
Mwanamuziki wa Nigeria Chioma Ogbonna akifahamika kwa jina la usanii “Cill” ni mchechemuzi wa Kampeni ya Umoja wa Mataifa ya kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDG Action Campaign ambaye hivi karibuni alihudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa wa nchi zenye maendeleo duni Duniani, LDC5. Moja ya nyimbo zake maarufu ni Woman alioutoa mwaka 2021 ukiwa mahususi kwa ajili ya Siku ya Mwanamke Duniani. Ni wimbo ambao unaeleza nguvu ya mwanamke licha ya kukatishwa tamaa. Nyimbo zake nyingine maarufu za Cill ni pamoja na Tatarata, Kachifo, Permit me na nyinginezo kadhaa. Anold Kayanda wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa alipata fursa ya kuzungumza na msanii huyu mjini Doha nchini Qatar.
Hii leo jaridani tunasalia hapa makao makuu kukuletea yaliyojiri kwenye Jukwaa la kudumu la watu wa asili, na pia kukupeleka nchini DRC kumulika faida ya mradi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia wa kupanda miti aina ya migunga. Makala tunaangazia SDG 17 na Mashinani tunakupeleka nchini Tanzania, kulikoni?Hii leo katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani Jukwaa la kudumu la watu wa asili limeanza rasmi ambapo katika ufunguzi wa jukwaa hilo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema pamoja na majukumu muhimu ya jamii za asili hususan katika kulinda mazingira na mbinu nyingine mbadala za maisha, watu hawa wanazidi kuwa masikini na kuzitaka nchi zote duniani zihakikishe zinawasaidia kuondokana na umasikini.Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mradi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia wa kupanda miti aina ya migunga imeondoa tishio la ukataji miti holela kwenye msitu wa bonde la mto Congo, ambao ni wa pili kwa ukubwa duniani katika kufyonza hewa ya ukaa na sasa wananchi wananufaika sio tu kwa kupata mkaa bali pia hata watu wa jamii ya asili wanaweza kupata kitoweo porini.Katika makala Mwanamuziki Chioma Ogbonna (tamka Obona) “Cill” au Cillsoul wa Nigeria ambaye ni Mchechemuzi wa Kampeni ya Umoja wa Mataifa ya kusongesha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs na anaeleza anavyoutumia kipaji chake kusongesha malengo hayo 17.Na katika mashini tutaelekea nchini Tanzania kusikiliza jinsi ambavyo hakikisho la maji safi na salama limeboresha elimu shuleni.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, Karibu!
The Mutual for Project Development( MDP), ni kikundi kinachohamasisha jamiinamna bora ya kuhifadhi mifuko ya plastiki ili kulinda mazingira.
Kampeni ya utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu iliyoanza tarehe 25 mwezi huu huko Kivu Kaskazini nchini jamhuri ya Kidemokraia ya Congo, DRC imekunja jamvi jana Jumanne ya tarehe 30 mwezi hu uwa Januari ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO lilizindua kampeni hiyo ya chanjo kwa wakimbizi wa ndani katika kambi ya wakimbizi hao ya Kanyaruchinya wilayani nyiragongo katika mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini.Mwandishi wetu wa DRC Byobe Malenga ambaye ameshuhudia uzinduzi huo amesema uliongozwa na Gavana wa jimbo la Kivu Kaskazini Jenerali Ndima Constant, na Mwakilishi wa shirika WHO nchini DRC kwa lengo la kuokoa mamia ya familia hususan za wakimbizi wa ndani ambao tayari makumi kwa makumi wameripotiwa kupata ugonjwa huo na wengine wamefariki dunia.Jean Bruno, ni Mkuu wa Ofisi ya WHO Kivu Kaskazini na anasema ameridhishwa na shauku ya siku ya kwanza na zaidi ya yote amesema,« Tumewalenga watu 364,127 ambao ni wakimbizi wa ndani, pamoja na familia zinazowapokea. Tayari tumepokea dozi 364,150 ambazo zipo na zitatumika. chanjo itafanyika kwa awamu ya dozi moja na tutafanya hivyo kupitia kampeni ya nyumba kwa nyumba kwenye maeneo haya . Tumeridhika na ukweli ni kwamba kumekuwa na dhamira muhimu kwa upande wa serikali kwenye ngazi ya taifa na mkoa, lakini pia tumekuwa na hakikisho kutoka kwa jamii ya watu na wakimbizi wa ndani ambayo imekubali chanjo hiyo ambayo itafanyika kwa wakati».Eneo la Nyiragongo lilipokea idadi kubwa ya watu waliokimbia makazi yao kutokana na mashambulizi yanayofanywa na waaasi wa M23 huku watu 233 elfu waliokimbia makazi yao, zaidi ya 95% yao wamelundikana kwenye makanisa, shule, viwanja vya michezo na maeneo yasio salama kwa afya yao.Gavana wa Kivu Kaskazini, Jenerali Ndima Constant, anakiri kwamba janga la kipindupindu linaathiri sana eneo la Nyiragongo akisema kwamba hadi Jumanne ya Januari 24 wagonjwa 3706 wa kipindupindu walisajiliwa huku kukiwa na vifo 16 na ili kupunguza mlolongo wa maambukizi amewasihi raia kupata chanjo akishukuru WHO kwa msaada wao.« Madhumuni ya kampeni hii ya chanjo ni kulinda idadi ya watu dhidi ya kipindupindu katika jimbo la Kivu Kaskazini na hasa katika maeneo ya watu waliofurushwa ili kupunguza vifo. Mabibi na mabwana, wageni mashuhuri, ili kufunga maoni yangu, ningependa kuwakumbusha kuwa pamoja na chanjo utakayopokea, kufuata hatua za kuzuia maambukizi ni muhimu..”Ametaja njia za kujikunga kuwa ni pamoja na kunawa mikono mara kwa mara kwa maji safi na sabuni au majivu, kunywa maji yaliyotakasishwa tu au yaliyochemshwa. Kupika na kufunika milo yetu, matumizi sahihi ya vyoo huku tukiwa wasafi na kuweka usafi kwenye maeneo yetu ya makazi kila wakati.Waliokimbia makazi yao wanafahamu tishio hilo kwa sababu janga hilo limeathiri zaidi ya 89% ya waliokimbia makazi katika miezi ya hivi karibuni na chanjo inatekelezwa nyumba kwa nyumba.Watu waliohamishwa wanasubiri dozi zao nyumbani. Damaseni Butera ni miongoni mwa watu wa kwanza kupata dozi moja dhidi ya kipindupindu na anashukuru mpango huu wa WHO na anasema, «chanjo ni muhimu sana katika mapambano dhidi ya magonjwa kama kipindupindu, malaria na mengine.Tumejifunza habari kuhusu chanjo hiyo, tumefurahi sana kwa sababu tutakuwa na kinga, asante sana kwa shirika la WHO ambalo lilitufikiria. Asante sana»Kando na hilo, Mweze Shemba, aliyekimbia kutoka kijiji cha Kiwanja, pia alinufaika na chanjo hii. Licha ya njaa,yeye anapendelea kujilinda pamoja na familia yake dhidi ya janga hili akisema, «kilichonifanya nipate chanjo ya leo hapa katika kambi ya wakimbizi ni kwa sababu tunapatwa na magonjwa ya taabu. kama vile kuharana kutapika hasa tunapokunywa maji machafu. Lakini wakati tunapata hii chanjo tunaona kama vile ni kinga kwetu tunashukuru sana »Katika juhudi za kuepusha msongamano wa wagonjwa wa janga hili , WHO ilijenga vitalu 3 kama kitengo cha matibabu ya wagonjwa wa Kipindupindu (UTC) katika eneo la Bushagara na…
Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya ulaya tangu kuanza kwa msimu wa baridi kali katikati ya mwezi Novemba mwaka 2022 wamebaini kuongezeka kwa wagonjwa wanaolazwa kutokana na magonjwa ya homa ya mafua makali au flu, matatizo ya kupumua na COVID-19. Walio hatarini zaidi kupata maambukizi ya magonjwa hayo ni wahudumu wa afya pamoja na wazee, ndio maana wanaendesha kampeni ya kutoa chanjo. Katika msimu wa baridi mwaka uliopita WHO ukanda wa Ulaya ilifanikiwa kutoa chanjo ya homa ya mafua makali kwa asilimia 65 ya kundi la watu walio hatarini ambao wengi ni wazee na wahudumu wa afya na msimu huu wa baridi lengo ni kuwafikia asilimia 75 ya watu hao. Afisa wa kiufundi wa WHO Kyrgyzstan Kasymbekova Kaliya, anasema wanafahamu namna ugonjwa wa guo ulivyo hatari.…. “tunajua kwamba ugonjwa huu wa homa ya mafua makali unaweza kusababisha matatizo makubwa hasa kwa wazee wenye umri zaidi ya miaka 65, wale ambao wana magonjwa sugu ya moyo, mapafu, kisukari, na wenye hali ya uzio”. Chanjo imeanza kutolewa kwa makundi yaliyo hatarini kuathirika zaidi ya homa ya mafua makali kama anavyoeleza Baktygul Mamatova, mtaalamu wa Kinga katika kituo cha afya cha Bishkek, “Sisi, wahudumu wa afya, kama kundi lililo hatarini ndio tumekuwa wa kwanza kupata chanjo. Siwezi sema kwamba siwezi kupata magonjwa, napata, lakini kwa kuwa nimepata chanjo ni rahisi kuhimili.” Wazee wanfahamu umuhimu wa kupata chanjo kama anavyoeleza Kanai Alamanov, aliyefika katika kituo cha afya cha Bishkek, “Hapo awali, kulikuwa na uhamasishaji wa kupata chanjo dhidi ya virusi vya CORONA nami nilikuja kupata chanjo hiyo ya COVID-19, na sasa ni chanjo ya homa ya mafua makali. Chanjo hii inatupa fursa ya kujikinga na magonjwa, inatupa aina fulani ya hakikisho la maisha yenye afya.” Chanjo hazitolewi kwa wale wanaoenda hospitali pekee, wanaoishi katika nyumba maalum za kutunza wazee nao hufuatwa na kupewa chanjo kama anavyothibitisha Ludmila Kinda Ivanovna, “Mimi ninaugua sana. Mwili wangu haukubali kabisa kutumia aina nyingi ya dawa ikiwemo zile za viua vijasumu, nina pumu , nina matatizo ya moyo, nilishapata mstuko wa moyo mara mbili. Kiufupi mwili wangu ni dhaifi sana hivyo chanjo ina maana kubwa sana kwangu.”
Kikosi cha 9 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kupitia Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo - MONUSCO wamehitimisha kampeni yao ya Afya na Amani iliyoanza tarehe 3 mwezi huu wa January ambapo wamekabidhi jengo kwa ajili ya mahali pa wagonjwa na wahudumu wa afya kula chakula katika Kituo cha Afya cha Mavivi, mjini Beni, Jimboni Kivu Kaskazini mashariki mwa DRC.Akikabidhi jengo hilo Kamanda wa kikosi cha tisa cha Ulinzi wa Amani kutoka Tanzania Luteni Kanali Barakael Mley amesema jengo hilo litabaki kuwa kumbukumbu ya uhusiano mzuri baina ya walinda Amani wa kikundi cha Tisa na wananchi wa maeneo ya Mavivi na maeneo jirani,Akiongea kwa niaba ya Maganga mkuu wa hospital ya Oicha na wananchi wa maeneo ya Mavivi Dr Kasereka Nzala amewapongeza walinda Amani hao wa Tanzania wanaohudumu chini ya mwamvuli wa MONUSCO wamekuwa wakifanya jitihada mbalimbali katika kutatua changamoto za wananchi katika maeneo yao ya uwajibikaji,Kwa upande wake afisa Mahusiano wa kikosi cha tisa cha Ulinzi wa Amani kutoka Tanzania Kepteni Paul Mwesongo amebainisha kuwa hali ya uhusiano baina ya wananchi na walinda Amani hao,Naye bi Kavathama Clarice, mwenyekiti wa kamati ya Afya katika kituo cha afya cha Mavivi amesema,
Kikosi cha tisa cha ulinzi wa amani kutoka Tanzania, TANZBATT 9 kinachohudumu ndani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO, kimeanzisha kampeni iliyopewa jina la “Afya na Amani” ambayo inahusisha utoaji wa dawa za binadamu katika vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali za baadhi ya maeneo ya uwajibikaji ya Kikosi hicho ndani ya mji wa Beni, kaskazini mashariki mwa DRC.Akipokea dawa hizo muuguzi Mkuu wa Kituo cha afya cha Mavivi, Kisu Kanyambala Janvier, amewashukuru TANZBATT 9 kwa msaada huo na kusema kwamba utawasaidia wananchi wote.“Tunashukuru sana kikundi cha watanzania wa MONUSCO kwa msaada waliotuletea na ni msaada mkubwa wa dawa, tulikuwa na ulazima wa kuipata hii dawa na tulikuwa tunaikosa. Tunashukuru sana msaada huu utasaidia wakina mama, watoto na watu wote.” Anasema Kanyambala.Aidha Kanyambala amebainisha kuwa siyo mara ya kwanza kwa walinda amani wa Tanzania katika eneo hilo kuwasaidia wananchi kwani waliwajengea wodi ya akina mama na watoto na ujenzi wa kantini kwa ajili ya wagonjwa kula chakula ambayo ipo mbioni kukamilika.Kwa upande wake Kamanda Kikosi wa TANZBATT 9 Luteni Kanali Barakael Jackson Mley amesisitiza kuhusu suala la ushirikiano baina ya walinda amani wa MONUSCO na wananchi na kueleza kuwa wananchi wanapokuwa na afya nzuri wataweza kushiriki vyema katika kuleta amani ya maeneo yao, “sisi ujumbe wetu mkubwa ni ushirikiano ili kutatua changamoto za kiusalama tulizo nazo, bila ushirikiano baina ya raia na kikundi chetu cha tisa cha ulinzi wa Amani kutoka Tanzania hatutaweza kufanikisha jukumu hili”. Akisisitiza umuhimu wa kampeni hiyo kwa jamii, Kavumba Dezanji ambaye ni kiongozi wa wanawake katika eneo la Mbau amesema, “nasema afya mbele ya yote, ukiwa na afya njema utafanya kazi yoyote ya maendeleo.” Aidha, Dezanji ameomba usalama uboreshwe katika eneo la Mbau na kuomba mradi kama huo wa Afya na Amani uendelee katika mji huo.Naye Bukuka Makofi Chifu wa kimila wa eneo la Mavivi, amewashukuru walinda amani kutoka Tanzania kwa msaada huo na kusema “ni kitu cha kushukuru sana, inaonesha kama wanaendelea kutuonesha ushirikiano na upendo, mwanzo wa mwaka sisi kama tumebarikiwa kwa sababu tulikuwa na shida ya dawa kutokana na eneo hili kupokea watu wengi kutoka sehemu nyingine, hii itaendelea kutusapoti sana.” Kampeni ya Afya na Amani ni kampeni iliyoanza kuanzia tarehe 03 mwezi huu wa Januari na itadumu hadi tarehe 13 januari 2023.
Tunapo ingia katika majira ya joto, shirika la Royal Life Saving Australia, limezindua kampeni mpya kukabiliana na ongezeko kubwa kwa idadi ya visa vya vifo vinavyo sababishwa na kuzama majini nchini Australia.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Somalia inapata uungwaji mkono katika kampeni yake ya kutaka kuondolewa kwa vikwazo vya silaha baada ya Ethiopia kuungana na Uganda kuunga mkono hatua hiyo.
Licha ya wanawake wenye ulemavu kujitosa kwenye siasa,bado wanakumbwa na changamoto ya usafiri kufuatia maumbile yao,hasa kwa walemavu wenye matatizo ya viungo vya miguu na wale wasioona. Wanasiasa hawa ambao wanawania kama wawaniaji huru jijini Mombasa,hawana gari za kufanyia kampeni mashinani,hatua inayowafanya kulemaza kampeni zao. Mwanahabari wetu Athuman Luchi ametusimulia.
Odinga anayepeperusha bendera ya muungano wa Azimio la Umoja One Kenya na viongozi wa mrengo huo pamoja na wafuasi wao, walikusanyika katika uwanja wa michezo wa Kasarani huku Ruto, anayewania kwa tiketi ya chama cha UDA chini ya muungano wa Kenya Kwanza akijiunga na wenzake kwenye uwanja wa Nyayo.
Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia watoto, UNICEF, imeeiorodhesha Tanzania kama ya 11 kati ya nchi zenye idadi kubwa zaidi ya ndoto ndoa za utotoni na kuzindua kampeni kabambe iitwayo "Binti."
Katika kusongesha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs likiweno lengo namba 3 linalolenga Afya bora na ustawi, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Malawi linaendesha kampeni ya M'mera mpoyamba inayohamasisha wajawazito kufika katika vituo vya afya angalau mara nne kabla ya kujifunga na kuhakikisha wanapata saa moja ya ziada ya kulala ili kujihakikishia ujauzito salama na kujifungua mtoto mwenye afya bora. Kampeni hiyo inaendeshwa kwa njia mbalimbali ikiwemo mchezo wa video ambao Leah Mushi wa Idhaa hiiya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa ameutafsiri kwa lugha ya Kiswahili.
Kampeni za uchaguzi mkuu nchini Kenya, zina endelea kupamba moto haswa baada ya vyama kufanya mchujo wa wagombea pamoja nakuwatea vinara na manaibu wao.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, MINUSCA umezindua kampeni ya ulinzi wa raia ili kusaidia upatikanaji wa amani pamoja na kuwezesha mamlaka za serikali nchini humo kutekeleza majukumu yake.
Wiki ya tatu ya kampeni ya uchaguzi mkuu ili tawaliwa na shinikizo za gharama za maisha, baada ya mfumuko wa bei kuongezeka kwa 5.1%.
Kiongozi wa chama cha Labor Anthony Albanese, amaliza siku yake ya tatu akijitenga baada yakuambukizwa UVIKO-19.
Nchini Kenya harakati za shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF za kuondoa fikra potofu katika kaunti ya Kisumu kuhusu chanjo dhidi ya Corona au COVID-19 zimezaa matunda na sasa hata wale waliokuwa wamesita kupata chanjo hiyo wameanza kupata.
Wasimamizi wa kampeni hiyo wanasema ni kampeni ya kuongeza uelewa wa athari za Malaria katika jamii na kusukuma mbele lengo la serikali la kutokomeza ugonjwa huo ndani ya jamii.
Wiki ya pili ya kampeni za uchaguzi mkuu zime tumbukia katika vita vya kampeni zakutisha kati ya vyama viwili vikubwa nchini.
Waziri Mkuu anaendelea kutetea uamuzi wa chagua lake kwa mgombea wa chama cha Liberal, kwa eneo bunge la Warringah ambalo liko mjini Sydney.
Raia wa faransa watapiga kura jumapili hii kumchagua rais wao. Jumla kuna wagombea 12 akiwemo Rais Macron ambaye anawania kuchaguliwa tena. Kampeni za uchaguzi zinatamatika huku matamshi ya kibaguzi yakitolewa na wagombea kadhaa. Una maoni gani kuhusu uchaguzi huo?Je, Ufaransa inaweza kuanguka na kuingia katika hali ya kutovumilia?Unadhani nani atashinda uchaguzi huu?
Kampeni mpya iliyozinduliwa mwezi huu wa DFesemba na shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani linalohusika pia na afya ya uzazi UNFPA ya “Hakimiliki ya miwli wa binadamu” ina lengo la kuwasukuma watunga sera, sekta za teknolojia na mitandao yote ya kijamii kuuchukulia unyanyasaji na ukatili wa miili ya binadamu hususani ya wanawake mtandaoni kuwa ni suala linalohitaji kupewa uzito kama ilivyo ukiukwaji wa hakimiliki zingine. Flora Nducha na taarifa kamili (TAARIFA YA FLORA NDUCHA) Kupitia video ya UNFPA ya uzinduzi wa kampeni hiyo, mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo Natalia Kanem anahoji endapo dunia inafahamu kwamba asilimia 85 ya wanawake walio na fursa ya intaneti wameripoti kushuhudia ukatili mtandaoni na wengine asilimia 38 wakipitia binafsi ukatili huo. Amesema wanawake na wasichana, makundi ya walio wachache na watu waliotengwa wana uwezekano mkubwa wa picha zao kutumiwa vibaya mtandaoni, kudhalilishwa na kutumika katika vitendo vya ngono bila ridhaa yao. Hivyo amesisitiza kuwa (SAUTI YA NATALIA KANEM1-MELLISSA) “Ukatili wa mtandaoni unasababisha madhara makubwa, lakini makampuni ya kidijitali na watunga sera wanaonekana kuufumbia macho wakiweka thamani kubwa na ulinzi kwa hatimiliki kuliko wanavyofanya kwa binadamu.” Hata hivyo amesema (SAUTI YA NATALIA KANEM2-MELLISSA) “Ukweli ni kwamba haumiliki mwili wako mtandaoni. Na hii ndio sababu sisi hapa UNFPA, tumezindua haki ya mwili, hakimiliki ya kwanza kwa ajili ya mwili wa binadamu. Kwa kudai haki yetu ya mwili na kuchukua udhibiti wa miili yetu mtandaoni ndio pekee tutakapoweza kukomesha ukatili wa kijinsia unaoshuhudiwa kila siku kote duniani.” Bi Kanem ametoa wito kwa kila mtu kuuchukulia ukiukwaji huu wa haki za binadamu kwa uzito mkubwa, na kampeni inawatumia watu mbalimbali wenye ushawishi, mashuhuri, wanaharakati na watumiaji wa mitandao ya kijamii ikiwataka kuongeza herufi (B) kwenye picha zao kuunga mkono ukomeshaji wa ukatili wa kijinsia mtandaoni.
Janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 likiendelea kutikisa dunia huku taarifa potofu kuhusu chanjo zikiendelea kusambaa, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini Kenya limechukua hatua ya kushirikiana na viongozi wa dini ikiwemo wale wa madhehebu ya kiislamu ili kusaidia kuelimisha waumini wao juu ya chanjo na faida zake katika kuepusha kusambaa zaidi kwa virusi vinavyosababisha ugonjwa huo. Taarifa ya John Kibego inafafanua zaidi.(Taarifa ya John Kibego)Nats.. Tuko katika kaunti ya Garissa nchini Kenya waumini wa madhehebu ya kiislamu wakiingia msikitini tayari kwa ibada wakati huu ambapo gonjwa la Corona bado linaendelea kuleta shaka na shuku. Kama mbinu ya kudhibiti kuenea kwa COVID-19 nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF imeshapeleka dozi milioni 21 za chanjo dhidi ya Corona na linasaidiana na Wizara ya afya kuhakikisha watu wanachanjwa. Hata hivyo kuna changamoto ya taarifa potofu kuhusu chanjo na ndipo UNICEF ikashirikisha viongozi wa dini akiwemo Sheikh Omar Dagane, Imán wa msikiti hapa Garissa.(Sauti ya Sheikh Omar Dagane)- Jongo“Kama Imam wa jamii hii niña wajibu wa kushauri jamii kuhusu suala lolote la maslahi yao. Leo nimewaeleza waumini umuhimu wa kujikinga na COVID-19 kwa kupata chanjo. kupata chanjo ili kujikinga na COVID-19. Nimenukuu moja ya kauli za Mtume Muhamad SAW alipoulizwa na mfuasi wake iwapo amfunge kamba ngamia wake ambapo jibu lilikuwa Muamini Mungu lakini funga ngamia wako. Na vivyo hivyo tunapaswa kumuamini Mungu lakini tupate chanjo, vaa barakoa, nawa mikono, ili kujikinga.” Baada ya mahubiri mmoja wa washiriki Isak Abidi akafunguka akisema, “Nimesikiliza mahubiri ya Imam na ujumbe wa afisa wa afya na sasa nimeamua kuwa nakwenda kupata chanjo.” Abdullahi Abagira ni afisa wa UNICEF kaunti ya Garissa na anasema COVID-19 imekuwa na madhara ya aina mbalimbali hususan kwa watoto na hivyo UNICEF imesaidia kwa kusambaza siyo tu chanjo bali pia kufanikisha uwepo wa wahudumu wa afya wa kutoa huduma hizo.
Tofauti zinapaswa kuimarisha jamii badala ya kuisambaratisha, huo ndio ujumbe uliotamalaki wakati wa kampeni iliyoendeshwa nchini Mali na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kuweka utulivu nchini humo MINUSMA kwa kushirikiana na chama cha wadau wa Umoja wa Mataifa nchini humo, MANU. Kampeni ilileta pamoja wazee kwa vijana, wanawake kwa wanaume pamoja na Watoto wenye vipaji vya Sanaa na utamaduni. Nini kilifanyika, tujiunge na Jason Nyakundi katika taarifa hii. Utamaduni na sanaa kutoka makundi mbalimbali vilishamiri kwenye tamasha hili la utamduni kwa ajili ya amani kwenye viunga vya mji mkuu wa Mali, Bamako. Ilikuwa ni ngoma, nyingine zikitumia vikaragosi. Chifu wa Kijiji cha Koulouninke Adama Coulibally anasema “ukienda njia mbaya unakuwa hatarini kufika eneo hatarishi. Matamanio yetu ni kwamba katu tusiende njia mbaya. Hicho ndio tumejifunza kutoka kwa wazee wetu. Tunapaswa kupeleka ujumbe huu kwa watoto wetu na marafiki zetu. “ Abdoula Toure, afisa kutoka kitengo cha mawasiliano MINUSMA anasema, “Mali ni nchi kubwa na yenye makabila na tamaduni nyingi tofauti tofauti. Sisi Umoja wa Mataifa tunatambua hilo na ndio maana tunapatia umuhimu matumizi chanya ya tofauti hizo ili kuleta utangamano.” Kwa Madani Diabate ambaye ni mhifadhi wa turathi za kiasili anasema “tofauti za kitamaduni na kikabila nchini Mali zinapaswa kutumika kujenga amani. Kupitia huo utofauti ndio tunaleta utani baina ya makabila na kisha ujirani mwema. Hicho ndio kinaweza kuimarisha amani na kujenga utangamano baina yetu.” Wanawake ambao wamekuwa wakitaabika zaidi kutokana na machafuko nchini Mali nao wakapaza sauti kupitia Fatoumata Traore, mshauri wa kijamii mjini Bamako.“Ujumbe ambao naupaza kila wakati ni kwamba wanawake lazima wajumuishwe. Inapaswa wanawake nchini Mali watambue kuwa Mali ni moja na haigawanyiki. Kazi hiyo tunapasa kuifanya na tutaikamilisha.” Na ili kuishi pamoja, wananchi wa Mali wafanye nini? Baba Salah Cisse, mwanamuziki aliyeshiriki kampeni hiyo akatoa ujumbe kupitia wimbo akisema, “Ili kuishi pamoja tunapaswa kukubaliana na kusameheana! Kama huna jinsi, muombe msamaha jirani yako! Kama hatutasameheana, amani haiwezi kupatikana. Na bila amani hakuna maendeleo.”
Kampeni za uchaguzi wa udiwani katika halmashauri ya jiji la Fairfield, NSW zina endelea kwa kina siku chache zikiwa zinasalia kwa wapiga kura kutoa hukumu yao.
Kampeni zina endelea ndani ya chama cha Liberal jimboni New South Wales, kwa wadhifa wa kiongozi ambao ume achwa tupu baada yakujiuzulu kwa Gladys Berejiklian.
Leo ni siku ya wahudumu wa masuala ya kibinadamu duniani ambao wako msitari wa mbele kusaidia kuokoa maisha ya watu walio hatarini zaidi duniani majanga yanapozuka, na kwa kufanya hivyo huweka rehani maisha yao kila uchao amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres. (Taarifa ya Flora Nducha) Kupitia ujumbe wake kwa ajili ya siku hii Guterres amesema kote duniani wahudumu wa kibinadamu wanakabiliwa na ongezeko la vitisho, Nas katika miaka 20 iliyopita matukio ya kupigwa risasi, kutekwa na mashambulizi mengine dhidi ya mashirika ya kibinadamu yameongezeka mara 10. Ameongeza kuwa mwaka huu pekee angalau wahudumu wa masuala ya kibinadamu 72 wameuawa katika maeneo ya mizozo, na kwa mantiki hiyo amesisitiza “Katika siku hii ya wahudumu wa masuala ya kibinadamu tunawaenzi wahudumu hao kila kona ya dunia na kuahidi kufanya kila liwezekanalo kuwalinda wao na kazi yao muhimu.” Maudhui na kampeni kubwa ya siku ya mwaka huu imejikita katika mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi ambao unatishia kusambaratisha nyumba, uwezo wa watu kuishi na maisha yao miongoni mwa watu masikini kabisa duniani. Katibu mkuu anamtaka kila mtu kujiunga na kampeni hiyo #TheHumanRace ili kusaidia kufikisha ujumbe kwa viongozi wa dunia kwamba hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi hazitomwacha yeyote nyuma. Hivyo Guterres ameihimiza dunia kwamba "Dharura ya mabadiliko ya tabianchi ni mbio tunazopoteza. Lakini ni mbio tunazoziweza na lazima tushinde. Hebu tukaze buti zetu zetu za kukimbilia, jiunge na Kampeni ya TheHumanRace, na kwa pamoja, hakikisha kila mtu anakamilisha mbio hizo.”
Kiwango cha utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona au COVID-19 nchini Bhutan huko barani Asia kimefikia asilimia 90 ya wananchi wote wenye umri wa kupatia chanjo hiyo. Kampeni ya utoaji chanjo imefanywa na serikali ya Bhutan kwa ushirikiano na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.
Kampeni mpya ya matangazo inayowahamasisha wa Australia wachukue chanjo za COVID-19, imezinduliwa na serikali ya shirikisho.
Kampeni ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa Covid-19 kwa walinda amani wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR imezinduliwa mwanzoni wa wiki hii kwa kuwa walinda amani ni moja ya makundi ya kipaumbele. Taarifa ya Anold Kayanda inaeleza zaidi.
Somalia imejiunga na orodha inayozidi kuongezeka ya nchi zinazopokea chanjo za COVID-19, kupitia mpango wa COVAX baada ya kupokea shehena yake ya kwanza ya chanjo hizo tayari kwa usambazaji nchi nzima. Ahmidiwe Olottu na taarifa zaidi (TAARIFA YA AHIMIDIWE OLOTTU)
Kuanzia Ijumaa tarehe 29 Januari, vizuizi vya COVID-19 viliregezwa katika jimbo la New South Wales, baada ya milipuko kadhaa ya virusi hivyo kudhibitiwa.
Kampeni kubwa ya chanjo imezinduliwa leo nchini Sudan Kusini na mashirika ya Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO na la kuhudumia Watoto UNICEF kwa lengo la kuwachanja watoto milioni 1.5 dhidi ya polio baada ya mlipuko mpya kusababisha kupooza kwa watoto 15.
Kampeni za uchaguzi duniani kote zimechukua mifumo tofauti kuwavutia na kuwashawili wapiga kura.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akizindiua hatua ya kuzuia usambazaji wa taarifa za uongo mitandaoni, ametoa wito kwa watu kote ulimwenguni kutoa ahadi ya kutulia kwanza kabla ya kusambaza taarifa mitandaoni.
Malaki ya watoto nchini Somalia wamechanjwa dhidi ya ugonjwa wa surua na polio wakati wa kampeni ya chanjo kudhibiti mlipuko wa magonjwa hayo hatari, imeeleza taarifa ya mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, UNSOM.
Kampeni za uchaguzi wa rais zime anza rasmi nchini Tanzania, ambako vyama husika vime anza kuuza sera zao kwa kina.
Polio! Polio! Polio! Ugonjwa uliokuwa ukilemaza watoto 75,000 kila mwaka wakati wa miaka ya 1990 katika nchi za Afrika wanachama wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa kanda ya Afrika. Mataifa hayo ni 47 barani Afrika isipokuwa Somalia, Sudan, Eritrea, Misri, Libya na Tunisia. Gonjwa hilo halina tiba bali lina kinga ambayo ni chanjo, kinga ambayo viongozi kuanzia wa kaya hadi kimataifa walisimamia kidete kuhakikisha inamfikia kila mtoto barani Afrika na tarehe 25 mwezi huu wa Agosti, ukanda huo umetangazwa kuwa hakuna tena Polio! Nini kimefanyika?
Kampeni iliyoendeshwa kwa pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF na Wizara ya Afya ya Umma na Idadi ya watu nchini Haiti kuhusu jinsi ya kujikinga na virusi vya Corona, au COVID-19, imekuwa na mafanikio katika kupunguza maambukizi na hata watoto wana uelewa.
Nchini Malawi, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linapigia chepuo kitendo cha mzazi wa kiume kusaidiana na mzazi mwenzake katika malezi na makuzi ya watoto wao ili hatimaye watoto hao waweze kukua si tu kimwili bali pia kifikra.
Kampeni ya #Reimagine kuibuka na mpango wa dunia ya watoto baada ya COVID-19. Kitengo cha damu salama katika hospitali ya rufaa mkoa wa Dodoma nchini Tanzania kimewatoa hofu wachangiaji wa damu kuwa uwepo wa ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 usiwatishe kwenda kuchangia damu. Katikati ya COVID-19, WFP yaendelea kunusuru wahitaji.
Mashirika kuminatisa nchini Australia, yamejumuika kumulika madhara kwa afya ya vinywaji vyenye sukari.
A new educational campaign is aiming to teach multicultural communities about the potential dangers of alcohol consumption. - Kampeni mpya ya uelimishaji inalenga kufundisha jumuiya za kitamaduni kuhusu hatari za matumizi ya pombe.
Waandamanaji nchini Sudan wameingia siku ya pili ya maandamano ya kutotii sheria ili kushinikiza jeshi kukabidhi madaraka kwa raia. Je hatua hiyo itafanikiwa? Ungana na Fredrick Nwaka aliyekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu.
A day of intense campaigning has seen the Coalition promise to deliver jobs and a strong economy. - Leo jumapili ilikuwa siku nyingine ya kampeni kali, ambako chama cha mseto kili ahadi kutoa ajira pamoja nakuimarisha uchumi.
New South Wales residents will go to the polls on Saturday to decide who will lead their state for the next four years. - Wakazi wa NSW wata ingia katika vituo vyakupiga kura jumamosi 23machi2019, kuamua atakaye ongoza jimbo hilo kwa muda wa miaka minne ijayo.
Voters and candidates campaigning for the postponed presidential election in DR Congo, have begun expressing their suspicion about the elections which will now be held on 30 December 2018. - Wapiga kura na wagombea wa uchaguzi wa urais wa DR Congo, wame anza kuelezea wasi wasi wao kuhusu usalama wa kura katika uchaguzi wa urais utakao fanywa tarehe 30 Disemba 2018.
Wananchi wa DRC watapiga kura siku ya Jumapili, kumchagua rais mpya. Kampeni zinamalizika wiki hii kuelekea Uchaguzi huo wa kihistoria. Ushindani mkali ni kati ya wagombea watatu, Emmanuel Shadary kutoka chama tawala, Martin Fayulu kutoka muungano wa upinzani wa Lamuka, na Felix Tshisekedi. Tume ya Uchaguzi CENI inasema iko tayari kwa uchaguzi huu licha ya kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiweko kuteketea moto vya baadhi ya vifaa vya kupigia kura.
Siku 10 kuelekea Uchaguzi Mkuu nchini DRC, mauaji yameripotiwa katika kampeni za siasa hasa katika mikutano ya Martin Fayulu, mgombea vya vyama upinzani lakini pia kuteketea moto kwa jengo la kuhifadhi vifaa vya kupigia kura jijini Kinshasa. Tunajadili hili kwa kina.
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza, amezindua kampeni ya kuibadilisha Katiba ya nchi hiyo, lenye lengo la kuongeza muda wa rais kukaaa madarakani kutoka miaka mitano hadi miaka saba. Iwapo mabadiliko hayo yatapitishwa, Nkurunziza ana nafasi ya kuwania tena uongozi wa nchi hiyo mwaka 2020 na kuongoza mihula miwili hadi 2034. Hii ni mbinu ya Nkurunziza kuendelea kukaa madarakani ?
Kampeni za lala salama nchini Kenya zimepamba moto kuelekea uchaguzi huo Agosti 8 mwaka huu huku wagombea Uhuru Kenyatta wa Chama cha Jubilei na mgombea wa NASA, Raila Odinga wakichuana vikali katika kinyang'anyiro hicho. Je nani atashinda katika uchaguzi huo na kwa nini? Uchambuzi wa kina katika Makala ya Wimbi la Siasa ukiwa naye Victor Robert Wile utakata kiu yako ya kujua mbivu na mbichi kuhusu uchaguzi wa Kenya.