POPULARITY
Kufuatia Donald J Trump kutangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa Rais wa Marekani uliofanyika Jumanne Novemba 5, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa salamu za pongezi. Taarifa iliyotolewa Jumatano asubuhi jijini New York, Marekani na msemaji wa Umoja wa Mataifa, imemnukuu Guterres akisema napongeza wananchi wa Marekani kwa ushiriki wao katika mchakato wa demokorasia.Kisha akasema nampongeza Rais Mteule Donald J. Trump na ninarejelea imani yangu kwamba ushirikiano kati ya Marekani na Umoja wa Mataifa ni nguzo muhimu ya uhusiano wa kimataifa.Guterres amesema Umoja wa Mataiifa uko tayari kufanya kazi kwa kina na serikali ijayo ya Marekani il ikutatua changamoto kubwa zinazokabili dunia hivi sasa.Trump ambaye anawakilisha chama cha Repablikani, anakuwa Rais wa 47 wa Marekani.Amemshinda Makamu wa Rais Kamala Harris ambaye alikuwa anagombea kiti cha urais kupitia chama cha Demokrati.Hii ni mara ya pili Trump ataongoza Marekani kwani alikuwa Rais wa 45 wa Marekani kuanzia Januari 20, 2017 hadi Januari 20, 2021 baada ya kushinda uchaguzi wa mwaka 2016.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Chama cha ODM kimeendelea kutoa msimamo kinzani kuhusu hatua ya viongozi wake wakuu kujumuishwa serikalini, na kuibua kumbukumbu ya hatua za kinidhamu zilizochukuliwa dhidi ya Wabunge wake waliotangaza msimamo wao wa kushirikiana na serikali baada ya Uchaguzi Mkuu uliopita. Je, viongozi hawa wakuu wa chama hiki watachukuliwa hatua zozote. Kama sivyo, basi tusihadaiwe zaidi.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Wananchi wa Rwanda wanajiandaa kupiga kura tarehe 15 mwezi Julai kumchagua rais na wabunge.Wiki iiyopita, Tume ya Uchaguzi ilitangaza orodha ya awali ya wagombea urais ambao ni rais Paul Kagame ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1994, Frank Habineza kutoka chama cha Democratic Green na Philippe Mpayimana mgombea binafsi.Mwanasiasa na mpinzani wa Kagame, Diane Rwigara, kutoka chama cha People Salvation Movement, ombi lake lilikataliwa. Tunachambua maandalizi ya uchaguzi nchini Rwanda. Wachambuzi wetu ni Edwin Kegoli akiwa Nairobi na Mali Ali akiwa jijini Paris
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Rais mpya wa Senegal Bassirou Diomaye Faye ameapishwa rasmi kuiongoza nchi hiyo. Faye, mwenye umri wa miaka 44 anakuwa Rais wa tano wa taifa hilo na Rais mchanga zaidi kuongoza taifa hilo la Afrika Magharibi. Ushindi wake katika uchaguzi mkuu uliopita ni wa kihistoria kutokana na kuwa yeye si mtu maarufu mno katika siasa nchini humo, na aliondoka jela siku tisa tu kuelekea Uchaguzi Mkuu. Tunajifunza nini kutokana na hadithi ya ufanisi wa Faye? Kenya inaweza kujifundisha nini?
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.
Wapiga kura katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wanasubiri matokeo ya uchaguzi mkuu, baada ya zoezi hilo kuongezewa muda, wa siku moja, ambao haukutarajiwa, na ambao uliwafanya baadhi ya wagombea wa upinzani kulalamika, wakidai kwamba hiyo ilikuwa ni njama ya kuiba kura.
Kampeni za mwisho mwisho zilifanyika Jumatatu kwelekea kwa uchaguzi mkuu Jumatano huku kukiwa na wasiwasi kama zoezi hilo litakuwa la haki na salama.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), Nicholas Haysom ametahadharisha kwamba muda unazidi kuyoyoma kuelekea Sudan Kusini kufanya uchaguzi mkuu unaotarajiwa mwezi Desemba mwaka ujao wa 2024 lakini bado masuala muhimu ya kuufanya uchaguzi huo uende kama ulivyopangwa bila kuchelewa hayajakamilika."Ikiwa imesalia miezi 17 tu kwenye ratiba ya kuelekea uchaguzi wa mwaka 2024, narudia kile nilichokisema katika mkutano wa awali na waandishi wa habari, kwamba mwaka 2023 ni mwaka wa 'kutengeneza au kuvunja'," amesema Bwana Haysom mapema leo Agosti pili alipozungumza na vyombo vya Habari mjini Juba ambao ni mji mkuu wa nchi hiyo changa zaidi duniani. Ghasia miongoni mwa jamii za Sudan Kusini zinaendelea kuongezeka pamoja na shinikizo la kuongezeka kwa ufinyu wa rasilimali huku maelfu ya watu wakiendelea kuingia nchini humo wakikimbia mapigano katika nchi jirani ya Sudan. Kwa mujibu wa Bwana Haysom, miongoni mwa hatua muhimu ambazo inabidi zichukuliwe ni pamoja na hitaji la kuunda upya vyombo vitatu muhimu, ambavyo ni, Tume ya Kitaifa ya Marekebisho ya Katiba, Tume ya Kitaifa ya Uchaguzi, na Baraza la Vyama vya Kisiasa; kukamilisha mipango ya mpito ya usalama; kuendeleza mchakato wa kudumu wa kutengeneza katiba; na kuunda nafasi za kiraia na kisiasa ambapo kila raia ana uhuru wa kujadili na kujihusisha na uchaguzi wa kisiasa na kikatiba bila woga. "Kufanya uchaguzi tu hakutoshi - uaminifu, uwazi na ushirikishwaji wa mchakato ndio unaoleta uhalali. Hii ni pamoja na kwamba vyama vya siasa lazima viweze kujiandikisha na kufanya kampeni kwa uhuru; asasi ya kiraia kwa ajili ya elimu ya uraia na kuwa waangalizi wa mchakato. Inajumuisha vyombo vya habari vinavyoweza kuripoti kuhusu mchakato huo na kutoa nafasi kwa sauti na maoni mbalimbali kwa wapiga kura kufanya uamuzi sahihi,” amesema Mwakilishi huyo wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini. Aidha Bwana Haysom amesisitiza kuwa UNMISS itaendelea kuiunga mkono Sudan Kusini katika michakato ya uchaguzi na uundaji wa katiba kwa kushirikiana na wadau wa kikanda kama vile Muungano wa Afrika (AU) na mamlaka ya pamoja ya kitaifa kwa ajili ya maendeleo kwenye eneo la Pembe ya Afrika (IGAD).
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya usalama nchini Sudan Kusini na mradi wa maji nchini Rwanda. Makala tunasalia huko huko Sudan Kusini na Mashinani tunakupeleka nchini Zimbabwe, kulikoni? Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), Nicholas Haysom ametahadharisha kwamba muda unazidi kuyoyoma kuelekea Sudan Kusini kufanya uchaguzi mkuu unaotarajiwa mwezi Desemba mwaka ujao wa 2024 lakini bado masuala muhimu ya kuufanya uchaguzi huo uende kama ulivyopangwa bila kuchelewa hayajakamilika.Balozi mwema wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto UNICEF Vanessa Nakate amefanya ziara nchini Rwanda kujionea namna mradi wa pampu ya kuvutia maji inayotumia nishati ya umeme wa jua au Sola ilivyoleta manufaa kwa wanawake na wasichana barubaru 11,000 waliokuwa wakitembea umbali mrefu kusaka hmaji.Katika makala Assumpta Massoi anafuatilia ziara ya wakuu wa mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini.Na tunakupeleka nchini Zimbabwe ambako vijana wameweza sio tu kijikwamua kiuchumi na kuondokana na umaskini bali pia kuhifadhi mazingira na tutasikia kutoka kwa mmoja wao.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Ujumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa umewasili nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC , ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi ya kutathmini hali ya usalama na utekelezaji wa majukumu ya vikosi vya umoja wa mataifa vya kulinda mamani nchini humo MONUSCO. Mara tu baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Kinshasa, bwana Nicolas de Rivière, Balozi wa kudumu wa Ufaransa kwenye Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa makundi yenye silaha, vyovyote vile yalivyo, lazima yasitishe operesheni zao ili kushiriki katika mchakato wa amani, “Ni wakati muhimu wakuchukua hatua na kwamba vikundi vyote vyenye silaha, kwa hali yao lazima visitishe shughuli zao na washiriki katika mchakato wa kisiasa. Naomba makundi ya kigeni yajiondoe na makundi yanayoungwa mkono na mataifa ya kigeni pia yajiondoe ili hatimaye amani irejee katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo”.Ujumbe huo umekuja nchini DRC wakati kukitarajiwa kuwa na uchaguzi mkuu wa raisi pamoja na wabunge mwezi decembe mwaka huu huku bwana Michel Xavier Biang Balozi wa Gabon kwenye Umoja wa Mataifa akisisitiza lazima uchaguzi huo uwe wa haki, wa uwazi na salama, “ Tuko katika mwaka ambao utakuwa mwaka wa uchaguzi, ujumbe wetu ni wakuhimiza wanasiasa wa pande zote kushiriki katika mchakato wa uchaguzi ambao ni wa uwazi, na wa kuaminika kwa mujibu wa Katiba ya DRC na sheria ya uchaguzi. Tuko hapa kuunga mkono hatua ya MONUSCO na kukumbusha kwamba MONUSCO ni sehemu ya fursa ya suluhu”.Wajumbe hao watakutana na watu kutoka tabaka mbali mbali ikiwemo mashirika ya kiraia na Rais wa DRC Félix Tshisekedi jijini Kinshasa na baadae watakwenda mjini Goma jimboni Kivu Kaskazini, ambako mapigano yamezidi kurindima kwa miezi kadhaa sasa kati ya jeshi la serikali na kundi la wanamkambo wa M23.
Rais wa Afrika kusini Cyril Ramaphosa anayekabiliwa na kashfa ya utakatishaji wa fedha amechaguliwa kuwa kiongozi wa chama cha ANC. Je safari yake ya kisiasa itakumbana na vizingiti? Kennes Bwire amaefanya mazungumzo na mchambuzi wa siasa za Afrika kusini Peter Bigenda, akiwa Johannesburg.
Rais wa Afrika kusini Cyril Ramaphosa anayekabiliwa na kashfa ya utakatishaji wa fedha amechaguliwa kuwa kiongozi wa chama cha ANC. Je safari yake ya kisiasa itakumbana na vizingiti? Kennes Bwire amaefanya mazungumzo na mchambuzi wa siasa za Afrika kusini Peter Bigenda, akiwa Johannesburg.
Rais wa Afrika kusini Cyril Ramaphosa anayekabiliwa na kashfa ya utakatishaji wa fedha amechaguliwa kuwa kiongozi wa chama cha ANC. Je safari yake ya kisiasa itakumbana na vizingiti? Kennes Bwire amaefanya mazungumzo na mchambuzi wa siasa za Afrika kusini Peter Bigenda, akiwa Johannesburg.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk ameipongeza serikali ya Kenya kwa kile alichoeleza ni hatua muhimu ya kuelekea uwajibikaji kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Kenya, kufuatia uamuzi wake wa wa kutumia Sheria ya Uhalifu wa Kimataifa kuwafungulia mashitaka maafisa wakuu wa polisi kwa mauaji, ubakaji na utesaji kama uhalifu dhidi ya ubinadamu kufuatia vurugu zilizotokea wakati wa uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo mwaka 2017. Leah Mushi anataarifa zaidi.Taarifa iliyotolewa hii leo huko Geneva, Uswisi na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu imemnukuu Kamishna Mkuu wa Umoja wa Matifa wa Haki za binadamu Volter Turk akipongeza Kenya na kusema hii ni mara ya kwanza kwa Kenya kutumia Sheria ya Kimataifa ya Uhalifu kushtaki uhalifu dhidi ya ubinadamu katika mahakama zake za ndani.Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wakati wa uchaguzi mkuu wa Kenya mwaka 2017, Tume ya Taifa ya Haki za Kibinadamu ilirekodi vifo 94 na matukio 201 yakihusiana na unyanyasaji wa kingono na zaidi ya majeruhi 300 wengi wao wakieleza kufanyiwa vitendo hivyo na vikosi vya usalama.Bwana Turk amesema “Uamuzi uliochukuliwa leo na Kenya ni wa msingi, ni hatua nzuri kuelekea haki na uwajibikaji kwa waathirika na familia za waathirika, wa ghasia za uchaguzi, na inaweza kuimarisha na kuzuia ukiukaji wa haki za binadamu kwa siku zijazo.”Amebainisha kuwa uamuzi huo wa Kenya unatokana na maendeleo ya hivi karibuni ya taasisi za Kenya zinazoungwa mkono na Ofisi yake ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu katika kuimarisha uwajibikaji kwa ukiukaji wa haki za binadamu.Kamishna Mkuu Türk amesema ofisi yake itaendelea kujitolea kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Kenya kuendeleza uwajibikaji kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na kushughulikia mauaji ya kiholela na kulazimisha watu kutoweka.
Chama kikuu cha Upinzani cha Angola, UNITA, kimeliambia shirika la habari la AFP kwamba kitapinga matokeo ya uchaguzi mahakamani baada ya tume ya uchaguzi kutangaza chama cha rais aliye mamlakani kama kilichoshinda uchaguzi wa wiki jana kwa asili mia 51 ya kura.
Mrengo wakisiasa wa Azimio One Kenya unajiandaa kuwasilisha ombi lakubatilisha matokeo ya uchaguzi mkuu nchini humo.
Wagombea urais nchini Angola Jumatatu walihitimisha kampeni za mwezi mzima kabla ya uchaguzi wa Jumatano ambao huenda ukashuhudia ushindani mkali kati ya chama tawala, kilicho madarakani kwa miongo kadhaa, na upinzani unaozidi kuongeza mvuto miongoni mwa vijana.
Kinara wa mrengo wa Azimio One Kenya Raila Odinga, amewania urais mara tano bila mafanikio.
Ni nadra kwa tume ya uchaguzi ya Kenya, kusifiwa kwa jinsi ilivyo simamia uchaguzi mkuu.
Tume huru ya uchaguzi wa Kenya IEBC, kwa mara nyingine inasimamia uchaguzi mkuu miaka mitano baada ya uchaguzi mkuu wa 2017 ulio paka tume hilo tope lakuganda.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Abdushakur Aboud wa VOA ambaye yuko Nairobi aelezea hali ilivyokuwa asubuhi na mapema , wakati wapiga kura wakianza kumininika, pamoja na waangalizi wa kimataifa waliopo nchini humo.
Tunapata ripoti mbalimbali na kuzungumza mubashara na waandishi wetu waliokita kambi maeneo tofauti tofauti ya Kenya kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu wa Jumanne Agosti 9, 2022.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Odinga anayepeperusha bendera ya muungano wa Azimio la Umoja One Kenya na viongozi wa mrengo huo pamoja na wafuasi wao, walikusanyika katika uwanja wa michezo wa Kasarani huku Ruto, anayewania kwa tiketi ya chama cha UDA chini ya muungano wa Kenya Kwanza akijiunga na wenzake kwenye uwanja wa Nyayo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
VOA Express ni matangazo mapya yenye mwendo wa kasi yakiangalia habari mpya za mchana na maelezo ya maswala yanayohusu vijana na wanawake. Matangazo haya yanafuatilia habari zilizojitokeza nyakati za mchana na ripoti za kina za habari ambazo hazisikiki sana katika matangazo mengineyo. VOA Express
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Katika makala hii utasikia kuhusu maandamano makubwa yaliyofanyika nchini DRC kutaka tume ya umoja wa mataifa Monusco iondoke nchini, mijadala kuhusu mdahalo wa kisiasa kwa wagombea wa kiti cha urais nchini Kenya, kuelekea uchaguzi wa agosti 09, ziara ya rais wa Ufaransa Emmanuel Macron nchini Cameroon, Guinea Bissau, na Benin, lakini pia mahusiano kati ya China na Marekani. Kwa hayo na mengine mengi ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Bunge la 12 la kitaifa la Kenya, ambalo linatajwa na wachambuzi kama lililokuwa na vituko chungu nzima, Alhamisi liliahirisha vikao vyake kwelekea kwa uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti.
Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini Kenya IEBC, imesema kwamba haitawazuia watuhumiwa wa kashfa za ufisadi kugombea nafasi mbali mbali katika uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti. IEBC inaeleza kuwa ni lazima mahakama iwakute washukiwa na hatia.
Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.
Tasmania inatoa mvutio mwingi kwa siku ya uchaguzi mkuu, Jumamosi 21 Mei kwa watazamaji wa uchaguzi.
Wiki ya tatu ya kampeni ya uchaguzi mkuu ili tawaliwa na shinikizo za gharama za maisha, baada ya mfumuko wa bei kuongezeka kwa 5.1%.
Wiki ya pili ya kampeni za uchaguzi mkuu zime tumbukia katika vita vya kampeni zakutisha kati ya vyama viwili vikubwa nchini.
Raia wa faransa watapiga kura jumapili hii kumchagua rais wao. Jumla kuna wagombea 12 akiwemo Rais Macron ambaye anawania kuchaguliwa tena. Kampeni za uchaguzi zinatamatika huku matamshi ya kibaguzi yakitolewa na wagombea kadhaa. Una maoni gani kuhusu uchaguzi huo?Je, Ufaransa inaweza kuanguka na kuingia katika hali ya kutovumilia?Unadhani nani atashinda uchaguzi huu?
Wiki hii tunaangazia maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2023 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Mashirika ya kiraia zaidi ya 60 za ndani na nje ya nchi hiyo, yanaonya kuwa, kuna dalilil za uchaguzi huo kucheleweshwa kama ilivyoshuhudiwa mwaka 2011 na 2018. Tunachambua na wanaharakati.
Mseto wa United Democratic Alliance (UDA) ume mtangaza rasmi Naibu Rais wa Kenya, William Samoei Ruto kuwa kinara wake katika uchaguzi mkuu wa 9 Agosti 2022. - Mseto wa United Democratic Alliance (UDA) ume mtangaza rasmi Naibu Rais wa Kenya, William Samoei Ruto kuwa kinara wake katika uchaguzi mkuu wa 9 Agosti 2022.
Rais Uhuru Kenyatta ametangaza kumuunga mkono kiongozi wa upinzani wa muda mrefu Raila Odinga kuwa mrithi wake, kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9. Hatua hii imekuja baada ya Kenyatta, kumtema naibu wake William Ruto ambaye amesema kiongozi huyo wa nchi, amemhadaa kisiasa. Tunachambua.
Joto la siasa nchini Kenya laendelea kuongezeka baada ya mseto wa Azimio kumuidhinisha Raila Odinga kuwa kinara wao katika uchaguzi mkuu 9 Agosti 2022.
Tunaangazia harakati za chama kikuu cha upinzani nchini Kenya Orange Democratic Movement (ODM), kutafuta uongozi wa nchi hiyo ya Afrika Mashariki, baada ya uchaguzi Mkuu mwezi Agosti. Raila Odinga, kiongozi wa chama hicho kilichoundwa mwaka 2005, ameshatangaza nia ya kuwania nafasi hiyo chini ya vuguvugu la kisiasa la Azimio la Umoja. Je, chama hiki kimejiandaa vipi, kuelekea Uchaguzi wa Agosti 9, 2022 ? Mgeni wetu leo, ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Edwin Sifuna.
Tunaangazia joto la kisiasa, linaloendelea kupanda nchini Kenya, kuelekea Uchaguzi Mkuu mwezi Agosti mwaka huu. Wakenya watamchagua rais wao wa tano, baada ya Uhuru Kenyatta ambaye anaondoka madarakani. Kinyanganyiro kinatarajiwa kuwa kati ya kiongozi wa muda mrefu wa upinzani na aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga na naibu rais William Ruto.
Wanasiasa wa upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kutoka muungano wa Lamuka na Ensamble wamekataa uteuzi wa Dennis Kadima kuwa Mwenyekiti mpya wa Tume ya Uchaguzi CENI kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2023. Itakuwaje ? Tunachambua.
Nchini Kenya, wanasiasa wanaendelea kunadi sera zao, kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2022. Miongoni mwa wanasiasa hao ni Raila Odinga na William Ruto. Tunachambua.
Wiki hii tunaangazia hatua ya vyama vya siasa nchini Tanzania kuunda Baraza la pamoja kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2025.
Viongozi wa dini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia wameshindwa kuelewana kuhusu ni nani awe Mwenyekiti mpya wa Tume ya Uchaguzi nchini humo CENI kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2023. Tunajadili
Wimbi la siasa wiki hii, linatupitia jicho siasa za upinzani, kumtafuta mgombea mmoja wa urais kuelekea Uchaguzi Mkuu mwezi Agosti mwaka 2022.
Kenya inajiandaa kuwa na Uchaguzi Mkuu mwaka 2022. Vyama vya siasa vimeanza maandalizi kujiweka tayari kwa uchaguzi huo. Lakini je, vyama hivi vimejiandaa vya kutosha ? Tunajadili.
Uchambuzi Wa Kijasusi Kuhusu Uchaguzi Mkuu Nchini Ufaransa Get full access to Barua Ya Chahali at www.baruayachahali.com/subscribe
Uchambuzi Wa Kijasusi Kuhusu Uchaguzi Mkuu Nchini Ufaransa
Wapiga kura nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, wameanza kuchukua kadi zao za mpiga kura tayari kwa ajili ya uchaguzi mkuu utakaofanyika jumapili hii ya tarehe 27 mwezi Desemba. Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, harakati zikiendelea mitaani huku katika vituo vya kujiandikishia, wananchi waliojiandikisha kupiga kura kwa uchaguzi mkuu jumapili wakichukua vitambulisho vyao. Ari ni kubwa ili kumaliza mgawanyo na ghasia uliogubika taifa hilo tangu mwaka 2013.
Hali inaendelea kuwa tata kwa viongozi wa upinzani nchini Tanzania, wengi wao wakijipata chini ya udhibiti wa vyombo vya usalama nchini humo.
Karibu kwa mara nyingine tena kusikiliza show yako matata una weza ku subscribe ili kuwa wakwanza kupata burudani .
(Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, Tuchague kiongozi anayetambua kuwa, Ikulu ni Mahali Patakatifu, ikulu.)Tanzania is now on her 5th General elections since 1995. We must remember what the Founding Father reminded, which is that in every moment of General Elections, we must choose leaders who are not corrupt, not by words of mouth, or by action! One must be living the national leadership ethics and moral standards as gathered by the public. Be responsible and vote for a man who shall protect our land not mere words promises! (October 25, 2020)
Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa OHCHR, leo imetoa wito kwa wadau wote nchi Tanzania kuhakikisha uchaguzi mkuu unaofanyika kesho Jumatano Oktoba 28, unakuwa wa amani, jumuishi na shirikishi, kwa watu kuweza kupiga kura zao kwa uhuru bila hofu na vitisho.
Shirika la afya la Umoja la Umoja wa Mataifa, WHO, limesema linawasiliana na serikali ya Burundi ili kufahamu sababu ya kufukuzwa kwa mwakilishi wake nchini humo pamoja na wafanyakazi wengine watatu. Serikali ya Burundi ilitangaza jana kumfukuza mwakilishi huyo Dkt. Walter Kazadi Mulombo, ikiwa ni siku chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini humo. Loise Wairimu na taarifa zaidi
Rais wa Tanzania John Magufuli, ametimiza miaka minne madarakani, je ni mafaniko gani na changamoto zipi zilizoshuhudiwa kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2020 ?
Wananchi wa Msumbiji, wanasubiri matokeo ya Uchaguzi Mkuu baada ya kupiga kura siku ya Jumanne. Ni uchaguzi ambao wachambuzi wa siasa wanasema ni kipimo cha demokrasia na utekelezwaji wa mkataba wa amani uliotiwa saini kati ya waasi wa Renamo na serikali, miezi miwili iliyopita. Tunajadili suala hili.
Tume ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Burundi imebaini katika ripoti yake kwamba "hali ya hofu" inatawala katika nchi hiyo, ikiwa imesalia miezi minane kabla ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2020. Katika ripoti yake, Tume ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Burundi, iliyoundwa na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mnamo mwaka 2016, inaelezea jinsi mamlaka nchini humo na vijana wa chama tawala, Imbonerakure, wanaendelea kuwafanyia vitisho raia kwa kuwalazimisha kujiunga, kuunga mkono au kuchangia chama tawala, CNDD-FDD. Fredrick Nwaka amekuandalia makala haya kwa kuzungumza na wasikilizaji wetu
Experts had given the coalition no chance of winning the federal election in favor of the Labor party. - Wataalam wengi, walikuwa hawakupa chama cha mseto matumaini yoyote, yakushinda uchaguzi mkuu wa shirikisho dhidi ya chama cha Labor.
Electorates which are culturally diverse are poised to play a key role in determining the outcome of the election. - Maeneo bunge yenye wakazi kutoka tamaduni tofauti, yatakuwa na jukumu muhimu laku amua matokeo ya uchaguzi mkuu wa shirikisho.
Week three of the federal election campaign began with the opening of the early voting period and the first of three leaders debates. - Wiki ya tatu ya kampeni za uchaguzi mkuu wa shirikisho ilianza kwaku funguliwa kwa vituo vyakupiga kura mapema, pamoja na mjadala wa kwanza kati ya mijadala mitatu ya viongozi kufanywa.
The Nationals take pride in representing the interests of people in regional and rural Australia and have done so for almost 100 years. - Chama cha Nationals huwa na fahari yakuwakilisha watu katika maeneo ya kanda na vijiji vya Australia, na chama hicho kime fanya hivyo kwa takriban miaka miamoja.
Kiongozi wa upinzani nchini DRC Martin Fayulu, anataka maandamano yafanyike nchini humo kumshinikiza rais Felix Thisekedi aondoke madarakani kama ilivyokuwa nchini Sudan na Algeria. Fayulu anasema yeye ndiye aliyeshinda Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2018. Tunachambua hili kwa kina.
The Prime Minister and Opposition Leader will hold the first debate of the election campaign in Perth next week, where as many as six marginal seats are up for grabs. - Waziri Mkuu na kiongozi wa upinzani wata fanya mjadala wa kwanza katika kampeni ya uchaguzi mjini Perth wiki ijayo, ambako chama chochote kinaweza shinda takriban maeneo bunge sita.
Scott Morrison became Australia's 30th prime minister in August last year when the Liberal Party voted him in as leader after a very public and acrimonious leadership spill. - Scott Morrison alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa Australia wa thelathini Agosti mwaka jana, baada ya kura ya uongozi ndani ya chama cha Liberal, ikiwa ni baada ya machafuko ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vya uongozi ndani chama hicho.
This year's federal election finally has a date: May the 18th 2019. - Hatimae tarehe ya uchaguzi wa shirikisho ya mwaka huu imetangazwa, uchaguzi huo utakuwa tarehe 18 Mei 2019.
Facebook will ban foreign political advertising and introduce fact checking during the federal election. - Shirika la Facebook litapiga marufuku matangazo yakisiasa, nakuwasilisha mchakato wakutafuta ukweli wakati wa uchaguzi mkuu wa shirikisho.
Former Deputy Prime Minister and high-profile Liberal M-P Julie Bishop has announced she's retiring from politics. - Naibu waziri mkuu wa zamani na mbunge maarufu wa chama cha Liberal, Julie Bishop ametangaza kuwa anastaafu kutoka siasa.
Mamilioni ya raia wa DRC, pamoja na dunia, inasubiri Tume ya Uchaguzi kumtangaza mshindi wa Uchaguzi wa urais, baada ya wananchi kupiga kura Desemba 30 2018. Nani atashinda Uchaguzi huu na ni kwanini matokeo yamechelewa ? Tunachambua suala hili kwa kina.
Hatimaye, Uchaguzi Mkuu wa DRC utafanyika siku ya Jumapili, lakini Tume ya Uchaguzi imeahirisha zoezi hilo katika maeneo ya Butembo, Beni na Yumbi kwa sababu za kiusalama na maambukizi ya ugonjwa hatari wa Ebola.
Protestors in the Democratic Republic of Congo have attacked a facility used to assess potential ebola cases, angry at what they perceive to be attempts to exclude them from voting in the country's presidential election - Waandamanaji nchini jamuhuri yakidemokrasia ya Congo, wame shambulia kituo kinacho tumiwa kuchunguza kesi za ebola, baada yaku kasirishwa kwa majaribo yaku watenga katika mchakato wakupiga kura katika uchaguzi wa urais nchini humo.
Uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo uliokuwa umepangwa kufanyika tarehe 23 mwezi Desemba, sasa umeahirishwa hadi tarehe 30 baada ya kuteketea kwa ghala la kuhifadhi vifaa vya kupigia kura jijini Kinshasa.
Siku 10 kuelekea Uchaguzi Mkuu nchini DRC, mauaji yameripotiwa katika kampeni za siasa hasa katika mikutano ya Martin Fayulu, mgombea vya vyama upinzani lakini pia kuteketea moto kwa jengo la kuhifadhi vifaa vya kupigia kura jijini Kinshasa. Tunajadili hili kwa kina.
Chama cha Republican cha rais Donald Trump, kimepata ushindi katika bunge la Senate huku kile cha Denocratic, kikirejesha udhibiti wa bunge la wawakilishi, baada ya matokeo ya Uchaguzi wa Wabunge, Maseneta na Magavana, uliofanyika siku ya Jumanne. Matokeo haya yanamaanisha nini kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020. Kujadili hili, ni Abdulkarim Atiki, mchambuzi wa siasa za Kimataifa akiwa mjini Arusha nchini Tanzania na Dokta Brian Wanyama, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kibabii mjini Bungoma nchini Kenya.
Victorians go to the polls on 24 November 2018 - Wakazi wa Victoria, watafanya uchaguzi tarehe 24 mwezi wa kumi na moja mwaka huu wa 2018.
Tume ya Uchaguzi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo CENI, imepata mitambo ya kieletroniki kuwatambua wapiga kura wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi Desemba. Je, mitambo hii itsaidia Uchaguzi huo kuwa huru na haki ? Tunajadili hili na mbunge wa Francois Rubota kutoka muungano unaomuunga mkono rais Joseph Kabila, Majorite Preidentielle, lakini pia Naibu Katibu Mkuu wa chama Kikuu cha upinzani UDPS Reubens Mikindo.
Kenya imeendelea kushuhudia mzozo wa kisiasa, baada ya Uchaguzi Mkuu mwaka uliopita. Kiongozi wa upinzani NASA Raila Odinga, amekataa kumtambua rais Uhuru Kenyatta na amesema ataapishwa kama rais wa watu tarehe 30 mwezi Januari mwaka huu. Je, kuna nafasi ya mazungumzo katika mzozo huu.