Podcasts about uchaguzi mkuu

  • 17PODCASTS
  • 114EPISODES
  • 19mAVG DURATION
  • 1EPISODE EVERY OTHER WEEK
  • Nov 11, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about uchaguzi mkuu

Latest podcast episodes about uchaguzi mkuu

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Uchaguzi mkuu Tanzania: Waangalizi wasema haukuzingatia vigezo vya demokrasia

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Nov 11, 2025 20:02


Katika makala yetu leo tunaangazia pakubwa Uchaguzi Mkuu nchini Tanzania ambapo Rais Samia Suluhu aliapishwa siku ya Jumatatu kuongoza muhula wa pili, hata hivyo ni uchaguzi ambao ulikumbwa na utata huku waangalizi kutoka jumuiya ya Afrika kusini SADC na wale wa umoja wa Afrika AU wakisema haukuzingatia vigezo vya demokrasia. Tunaangazia pia taarifa ya Rais Paul Biya, wa Cameroon kuapishwa Alhamisi iliyopita kuongoza nchi hiyo kwa muhula wa nane, huku upinzani ukiitisha maandamano kupinga matokeo yaliyompa Biya ushindi. Lakini pia tutaangazia kongamano la kimataifa la mazingira, COP30 ambalo linafanyika huko Belem, nchini Brazil, kati ya Novemba 10 na 21.

Wimbi la Siasa
Nini hatima ya Tanzania baada ya uchaguzi mkuu uliokumbwa na vurugu ?

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Nov 5, 2025 10:16


Machafuko yalikumba uchaguzi mkuu wa Tanzania, uliofanyika Oktoba 29, 2025 na rais Samia Suluhu Hassan kutangazwa mshindi kwa kupata asilimia 97.6 ya kura. Chama kikuu cha upinzani CHADEMA, kimesema ushindi wa Samia ni kichekesho cha demokrasia. Anapaswa kufanya nini ili kuirejesha Tanzania katika utulivu wa kisiasa ? Tunachambua.

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Vurugu zaugubika Uchaguzi mkuu nchini Tanzania na hali nchini DRC

Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

Play Episode Listen Later Nov 4, 2025 20:06


Uchaguzi mkuu uliofanyika katika Jamhuri ya muungano wa Tanzania, na ambao uligubikwa na maandamano; mkutano wa Paris nchini Ufaransa kuhusu amani ya mashariki mwa DRC na eneo la maziwa makuu, siasa za nchini Kenya, Uganda lakini pia mauaji yaliyotekelezwa na kundi la RSF nchini Sudan, hali nchini Cameroon na Madagascar, kurejewa kwa mashambulizi nchini Ukraine, na huko Israeli dhidi ya Hamas

Habari za UN
Kauli ya ofisi ya UN ya Haki za binadamu kufuatia vurugu Tanzania baada ya uchaguzi mkuu

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 31, 2025 2:42


Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu imeeleza wasiwasi mkubwa kufuatia vifo na majeruhi vilivyotokea katika maandamano yanayohusiana na uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Tanzania tarehe 29 mwezi huu wa Oktoba. Selina Jerobon na maelezo zaidi.

Habari RFI-Ki
Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Tanzania zimeanza, wagombea wakinadi sera zao.

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Sep 4, 2025 9:46


Kampeni za uchaguzi mkuu wa Tanzania utakaofanyika tarehe 29 Oktoba zimeanza. Chama kikuu cha upinzani Chadema hakipo kwenye kampeni hizi, kufuatia msimamo wake wa kutaka mageuzi kwenye mfumo wa uchaguzi. Wasikilizaji wetu wanazungumzia aje kampeni hii na raia wa Tanzania wanatarajia sera gani kutoka kwa viongozi mbalimbali?

Habari RFI-Ki
Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Tanzania zimeanza, wagombea wakinadi sera zao.

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Sep 4, 2025 9:46


Kampeni za uchaguzi mkuu wa Tanzania utakaofanyika tarehe 29 Oktoba zimeanza. Chama kikuu cha upinzani Chadema hakipo kwenye kampeni hizi, kufuatia msimamo wake wa kutaka mageuzi kwenye mfumo wa uchaguzi. Wasikilizaji wetu wanazungumzia aje kampeni hii na raia wa Tanzania wanatarajia sera gani kutoka kwa viongozi mbalimbali?

Wimbi la Siasa
Tanzania yaingia kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Aug 27, 2025 10:00


Tanzania inaingia kwenye kampeni za uchaguzi Mkuu kuanzia Agosti 28, kuelekea kufanyika kwa uchaguzi uliopangwa kufanyika Oktoba, 29 2025. Rais Samia Suluhu Hassan, kutoka chama tawala CCM, anawania uongozi wa nchi hiyo. Mpinzani wake mkuu Tundu Lissu anaendelea  kuzuiwa jela, kwa tuhma za uchochezi na uhaini.

Radio Maria Tanzania
Je, unafahamu thamani ya ya kura yako katika kipindi cha uchaguzi Mkuu?

Radio Maria Tanzania

Play Episode Listen Later Jul 26, 2025 37:54


Karibu katika kipindi cha Elimu Jamii, Mwezeshaji ni Joseph Kasongwa Mwaiswelo, Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma kutoka Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) ambapo leo tunaangazia juu ya Thamani ya kura wakati wa uchaguzi Mkuu. Studio Kuu Mikocheni mtangazaji wako ni mimi Esther Magai Hangu nikishirikiana na Geofrey Rweyunga kutpka studio ndogo Jijini […] L'articolo Je, unafahamu thamani ya ya kura yako katika kipindi cha uchaguzi Mkuu? proviene da Radio Maria.

Wimbi la Siasa
Tanzania: CHADEMA yashinikiza mabadiliko kabla ya Uchaguzi Mkuu

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Apr 9, 2025 9:54


Mwezi Oktoba 2025, wananchi wa Tanzania, watashiriki kwenye uchaguzi Mkuu, kuwachagua madiwani, wabunge na rais. Hata hivyo, chama kikuu cha upinzani cha CHADEMA, kikiongozwa na Mwenyekiti wake, Tundu Lissu, kinashinikiza mageuzi kwenye sheria za uchaguzi kabla ya kufanyika kwa uchaguzi huo.Je, kitafanikiwa katika harakati zake ?

SBS Swahili - SBS Swahili
Uchaguzi Mkuu 2025: Dutton afuta sera yakumaliza mpangilio wakufanyia kazi nyumbani

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 8, 2025 9:19


Kiongozi wa upinzani wa shirikisho Peter Dutton, ame tupa nje mpango wake waku walazimisha wafanyakazi wa umma kurejea ofisini aki kiri sera hiyo ilikuwa kosa.

VOA Express - Voice of America
Uchaguzi wa viongozi wa CHADEMA, Tanzania wavutia vijana wengi kuelekea uchaguzi mkuu - Januari 21, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 21, 2025 29:59


VOA Express ni matangazo mapya yenye mwendo wa kasi yakiangalia habari mpya za mchana na maelezo ya maswala yanayohusu vijana na wanawake.

Alfajiri - Voice of America
Wakati Tanzania ikijiandaa kwa uchaguzi mkuu baadaye mwaka huu, je hali ya kisiasa ikoje? - Januari 16, 2025

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 16, 2025 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Kwa Undani - Voice of America
Utata unaokumba uchaguzi mkuu Msumbiji - Desemba 23, 2024

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 23, 2024 29:59


Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.

desemba uchaguzi mkuu
Wimbi la Siasa
Uchaguzi mkuu wa Ghana: Chama tawala NPP kushindwa na chama cha upinzani NDC unatoa funzo gani?

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Dec 12, 2024 10:01


Nchini Ghana, rais wa zamani John Dramani Mahama alipata ushindi mkubwa na kumaliza uongozi wa miaka minane wa chama tawala New Patriotic Party (NPP) chake  rais Nana Akufo-Addo, anayeondoka madarakani baada ya kuongoza kwa mihula miwili.

Jioni - Voice of America
LIVE TALK: Wimbi la vyama vya upinzani kushinda uchaguzi mkuu - Novemba 22, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 59:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Habari za UN
Guterres ampongeza Donald J. Trump kwa kuchaguliwa Rais wa Marekani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 6, 2024 1:14


Kufuatia Donald J Trump kutangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa Rais wa Marekani uliofanyika Jumanne Novemba 5,  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa salamu za pongezi. Taarifa iliyotolewa Jumatano asubuhi jijini New York, Marekani na msemaji wa Umoja wa Mataifa, imemnukuu Guterres akisema napongeza wananchi wa Marekani kwa ushiriki wao katika mchakato wa demokorasia.Kisha akasema nampongeza Rais Mteule Donald J. Trump na ninarejelea imani yangu kwamba ushirikiano kati ya Marekani na Umoja wa Mataifa ni nguzo muhimu ya uhusiano wa kimataifa.Guterres amesema Umoja wa Mataiifa uko tayari kufanya kazi kwa kina na serikali ijayo ya Marekani il ikutatua changamoto kubwa zinazokabili dunia hivi sasa.Trump ambaye anawakilisha chama cha Repablikani, anakuwa Rais wa 47 wa Marekani.Amemshinda Makamu wa Rais Kamala Harris ambaye alikuwa anagombea kiti cha urais kupitia chama cha Demokrati.Hii ni mara ya pili Trump ataongoza Marekani kwani alikuwa Rais wa  45 wa Marekani kuanzia Januari 20, 2017 hadi Januari 20, 2021 baada ya kushinda uchaguzi wa mwaka 2016.

Jioni - Voice of America
Yanayoangaziwa mkesha wa uchaguzi mkuu Marekani - Novemba 04, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 4, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

VOA Express - Voice of America
Wakaazi wa jimbo la Maryland nchini Marekani wanatoa maoni yao siku moja kuelekea uchaguzi mkuu wa urais Marekani wenye ushindani mkali. - Novemba 04, 2024

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 4, 2024 30:00


VOA Express pia inafuatilia kwa karibu sana maswala yanayovuma katika mitandao ya kijamii kama sehemu moja muhimu ya upashanaji habari siku hizi.

Jioni - Voice of America
Wa-Afrika waliopo mji wa Washington DC nchini Marekani wanaeleza mtazamo na nafasi zao kuelekea uchaguzi mkuu Marekani hapo Novemba 5. - Oktoba 29, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Oct 29, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Kwa Undani - Voice of America
Utaratibu unaotumika kupata kura 270 ambazo zinahitajika kwa mgombea urais Marekani kuweza kushinda uchaguzi mkuu wa Novemba 5 mwaka huu. - Oktoba 15, 2024

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later Oct 15, 2024 29:59


Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.

Sepetuko
Kumbukumbu ya Hatua za Kinidhamu na Maswali ya Hatima

Sepetuko

Play Episode Listen Later Jul 30, 2024 4:22


Chama cha ODM kimeendelea kutoa msimamo kinzani kuhusu hatua ya viongozi wake wakuu kujumuishwa serikalini, na kuibua kumbukumbu ya hatua za kinidhamu zilizochukuliwa dhidi ya Wabunge wake waliotangaza msimamo wao wa kushirikiana na serikali baada ya Uchaguzi Mkuu uliopita. Je, viongozi hawa wakuu wa chama hiki watachukuliwa hatua zozote. Kama sivyo, basi tusihadaiwe zaidi. 

chama kama odm hatua maswali uchaguzi mkuu
Kwa Undani - Voice of America
Rais Paul Kagame wa Rwanda amefanya mabadiliko ya uongozi katika utawala wake kuelekea uchaguzi mkuu wa Julai 15. - Juni 13, 2024

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later Jun 13, 2024 29:58


Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.

Wimbi la Siasa
Rwanda yaanza maandalizi ya Uchaguzi Mkuu Julai 15 kumchagua rais na wabunge

Wimbi la Siasa

Play Episode Listen Later Jun 12, 2024 10:17


Wananchi wa Rwanda wanajiandaa kupiga kura tarehe 15 mwezi Julai kumchagua rais na wabunge.Wiki iiyopita, Tume ya Uchaguzi ilitangaza orodha ya awali ya wagombea urais ambao ni rais Paul Kagame ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1994, Frank Habineza kutoka chama cha Democratic Green na Philippe Mpayimana mgombea binafsi.Mwanasiasa na mpinzani wa Kagame, Diane Rwigara, kutoka chama cha People Salvation Movement, ombi lake lilikataliwa. Tunachambua maandalizi ya uchaguzi nchini Rwanda. Wachambuzi wetu ni Edwin Kegoli akiwa Nairobi na Mali Ali akiwa jijini Paris

Kwa Undani - Voice of America
Uchaguzi mkuu Afrika kusini - Mei 29, 2024

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later May 29, 2024 29:59


Kwa Undani ni matangazo ya dakika 25 yanayochambua habari kwa undani zaidi na kumpa msikilizaji maelezo ya kina kuliko ilivyo kawaida kuhusu tukio au swala lililojitokeza katika habari.

afrika uchaguzi mkuu
Jioni - Voice of America
Shinkizo la kutaka mabadiliko ya sheria za uchaguzi Tanzania kuelekea uchaguzi mkuu 2025 - Mei 10, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later May 10, 2024 59:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
Mjadala wa Live Talk kuhusu siasa za Marekani kuelelekea kwenye uchaguzi mkuu mwishoni mwa mwaka. - Februari 23, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 23, 2024 59:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
Wanasiasa wa upinzani wa Senegal waanza kampeni zao licha ya kutokuwa na tarehe iliotangazwa ya kufanyika uchaguzi mkuu. - Februari 21, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 21, 2024 30:00


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

senegal afrika mashariki uchaguzi mkuu kampeni
Jioni - Voice of America
Rais wa muda wa Namibia, Nangolo Mbumba anasema hatowania kiti cha urais katika uchaguzi mkuu baadae mwaka huu. - Februari 05, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 5, 2024 30:00


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Alfajiri - Voice of America
Wachambuzi watoa maoni yao kufutia amri ya rais wa Tanzanzia kwamba vyombo vya usalama vijiweke sawa kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao. - Januari 24, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 24, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

rais sawa amri mkuu uchaguzi mkuu
Alfajiri - Voice of America
Kadinali Fridolin Ambongo wa DRC ametumia misa ya Jumapili jioni kuelezea mazingira yaliyokuwepo katika uchaguzi mkuu wa wiki iliyopita. - Desemba 25, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 25, 2023 30:00


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

wiki misa katika fridolin mkuu mazingira jumapili desemba uchaguzi mkuu
Jioni - Voice of America
Wakongomani wasubiri matokeo ya uchaguzi mkuu - Desemba 22, 2023

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 22, 2023 59:58


Wapiga kura katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wanasubiri matokeo ya uchaguzi mkuu, baada ya zoezi hilo kuongezewa muda, wa siku moja, ambao haukutarajiwa, na ambao uliwafanya baadhi ya wagombea wa upinzani kulalamika, wakidai kwamba hiyo ilikuwa ni njama ya kuiba kura.

kongo jamhuri mkuu desemba kidemokrasia uchaguzi mkuu
Jioni - Voice of America
Human Rights Watch inasema Demokrasia katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo imekuwa ikirudi nyuma kuelekea uchaguzi mkuu wa Disemba 20. - Desemba 16, 2023

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 16, 2023 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
LIve Talk: Hali ni ya wasi wasi DRC wiki mbili kabla ya uchaguzi mkuu kutokana na ukosefu wa usalama na upungufu wa vifaa vya uchaguzi - Desemba 08, 2023

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 8, 2023 59:57


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
Maoni ya wachambuzi na wasikilizaji kuhusu uchaguzi mkuu wa Zimbabwe unaofanyika Agosti 23 - Agosti 18, 2023

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Aug 18, 2023 59:59


zimbabwe agosti mkuu uchaguzi mkuu wasikilizaji
Habari za UN
02 AGOSTI 2023

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 2, 2023 0:11


Hii leo jaridani tunaangazia hali ya usalama nchini Sudan Kusini na mradi wa maji nchini Rwanda. Makala tunasalia huko huko Sudan Kusini na Mashinani tunakupeleka nchini Zimbabwe, kulikoni?  Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), Nicholas Haysom ametahadharisha kwamba muda unazidi kuyoyoma kuelekea Sudan Kusini kufanya uchaguzi mkuu unaotarajiwa mwezi Desemba mwaka ujao wa 2024 lakini bado masuala muhimu ya kuufanya uchaguzi huo uende kama ulivyopangwa bila kuchelewa hayajakamilika.Balozi mwema wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto UNICEF Vanessa Nakate amefanya ziara nchini Rwanda kujionea namna mradi wa pampu ya kuvutia maji inayotumia nishati ya umeme wa jua au Sola ilivyoleta manufaa kwa wanawake na wasichana barubaru 11,000 waliokuwa wakitembea umbali mrefu kusaka hmaji.Katika makala Assumpta Massoi anafuatilia ziara ya wakuu wa mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini.Na tunakupeleka nchini Zimbabwe ambako vijana wameweza sio tu kijikwamua kiuchumi na kuondokana na umaskini bali pia kuhifadhi mazingira na tutasikia kutoka kwa mmoja wao.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!

Habari za UN
Nicholas Haysom: Hatua inahitajika sasa kwa ajili ya uchaguzi kwa wakati na wa huru na haki nchini Sudan Kusini

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 2, 2023 0:02


Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini (UNMISS), Nicholas Haysom ametahadharisha kwamba muda unazidi kuyoyoma kuelekea Sudan Kusini kufanya uchaguzi mkuu unaotarajiwa mwezi Desemba mwaka ujao wa 2024 lakini bado masuala muhimu ya kuufanya uchaguzi huo uende kama ulivyopangwa bila kuchelewa hayajakamilika."Ikiwa imesalia miezi 17 tu kwenye ratiba ya kuelekea uchaguzi wa mwaka 2024, narudia kile nilichokisema katika mkutano wa awali na waandishi wa habari, kwamba mwaka 2023 ni mwaka wa 'kutengeneza au kuvunja'," amesema Bwana Haysom mapema leo Agosti pili alipozungumza na vyombo vya Habari mjini Juba ambao ni mji mkuu wa nchi hiyo changa zaidi duniani.    Ghasia miongoni mwa jamii za Sudan Kusini zinaendelea kuongezeka pamoja na shinikizo la kuongezeka kwa ufinyu wa rasilimali huku maelfu ya watu wakiendelea kuingia nchini humo wakikimbia mapigano katika nchi jirani ya Sudan.  Kwa mujibu wa Bwana Haysom, miongoni mwa hatua muhimu ambazo inabidi zichukuliwe ni pamoja na hitaji la kuunda upya vyombo vitatu muhimu, ambavyo ni, Tume ya Kitaifa ya Marekebisho ya Katiba, Tume ya Kitaifa ya Uchaguzi, na Baraza la Vyama vya Kisiasa; kukamilisha mipango ya mpito ya usalama; kuendeleza mchakato wa kudumu wa kutengeneza katiba; na kuunda nafasi za kiraia na kisiasa ambapo kila raia ana uhuru wa kujadili na kujihusisha na uchaguzi wa kisiasa na kikatiba bila woga.  "Kufanya uchaguzi tu hakutoshi - uaminifu, uwazi na ushirikishwaji wa mchakato ndio unaoleta uhalali. Hii ni pamoja na kwamba vyama vya siasa lazima viweze kujiandikisha na kufanya kampeni kwa uhuru; asasi ya kiraia kwa ajili ya elimu ya uraia na kuwa waangalizi wa mchakato. Inajumuisha vyombo vya habari vinavyoweza kuripoti kuhusu mchakato huo na kutoa nafasi kwa sauti na maoni mbalimbali kwa wapiga kura kufanya uamuzi sahihi,” amesema Mwakilishi huyo wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini.  Aidha Bwana Haysom amesisitiza kuwa UNMISS itaendelea kuiunga mkono Sudan Kusini katika michakato ya uchaguzi na uundaji wa katiba kwa kushirikiana na wadau wa kikanda kama vile Muungano wa Afrika (AU) na mamlaka ya pamoja ya kitaifa kwa ajili ya maendeleo kwenye eneo la Pembe ya Afrika (IGAD).  

Habari za UN
Kuna haja ya kusaka amani kwa njia ya majadiliano, lasema Baraza la usalama la UN wakiwa ziarani nchini DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 10, 2023 0:02


Ujumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa umewasili nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC , ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi ya kutathmini hali ya usalama na utekelezaji wa majukumu ya vikosi vya umoja wa mataifa vya kulinda mamani nchini humo MONUSCO. Mara tu baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Kinshasa, bwana Nicolas de Rivière, Balozi wa kudumu wa Ufaransa kwenye Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa makundi yenye silaha, vyovyote vile yalivyo, lazima yasitishe operesheni zao ili kushiriki katika mchakato wa amani, “Ni wakati muhimu wakuchukua hatua na kwamba vikundi vyote vyenye silaha, kwa hali yao lazima visitishe shughuli zao na washiriki katika mchakato wa kisiasa. Naomba makundi ya kigeni yajiondoe na makundi yanayoungwa mkono na mataifa ya kigeni pia yajiondoe ili hatimaye amani irejee katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo”.Ujumbe huo umekuja nchini DRC wakati kukitarajiwa kuwa na uchaguzi mkuu wa raisi pamoja na wabunge mwezi decembe mwaka huu huku bwana Michel Xavier Biang Balozi wa Gabon kwenye Umoja wa Mataifa akisisitiza lazima uchaguzi huo uwe wa haki, wa uwazi na salama, “ Tuko katika mwaka ambao utakuwa mwaka wa uchaguzi, ujumbe wetu ni wakuhimiza wanasiasa wa pande zote kushiriki katika mchakato wa uchaguzi ambao ni wa uwazi, na wa kuaminika kwa mujibu wa Katiba ya DRC na sheria ya uchaguzi. Tuko hapa kuunga mkono hatua ya MONUSCO na kukumbusha kwamba MONUSCO ni sehemu ya fursa ya suluhu”.Wajumbe hao watakutana na watu kutoka tabaka mbali mbali ikiwemo mashirika ya kiraia na Rais wa DRC Félix Tshisekedi jijini Kinshasa na baadae watakwenda mjini Goma jimboni Kivu Kaskazini, ambako mapigano yamezidi kurindima kwa miezi kadhaa sasa kati ya jeshi la serikali na kundi la wanamkambo wa M23. 

Alfajiri - Voice of America
Je, Rais wa Afrika kusini ataepuka mawimbi ya kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu 2024? - Desemba 20, 2022

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Dec 20, 2022 13:47


Rais wa Afrika kusini Cyril Ramaphosa anayekabiliwa na kashfa ya utakatishaji wa fedha amechaguliwa kuwa kiongozi wa chama cha ANC. Je safari yake ya kisiasa itakumbana na vizingiti? Kennes Bwire amaefanya mazungumzo na mchambuzi wa siasa za Afrika kusini Peter Bigenda, akiwa Johannesburg.

Habari za UN
UN yapongeza Kenya kwa kutumia sheria ya kimataifa kushtaki watuhumiwa wa uhalifu baada ya uchaguzi mkuu 2017

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 28, 2022 0:01


Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu Volker Türk ameipongeza serikali ya Kenya kwa kile alichoeleza ni hatua muhimu ya kuelekea uwajibikaji kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Kenya, kufuatia uamuzi wake wa wa kutumia Sheria ya Uhalifu wa Kimataifa kuwafungulia mashitaka maafisa wakuu wa polisi kwa mauaji, ubakaji na utesaji kama uhalifu dhidi ya ubinadamu kufuatia vurugu zilizotokea wakati wa uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo mwaka 2017. Leah Mushi anataarifa zaidi.Taarifa iliyotolewa hii leo huko Geneva, Uswisi na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu imemnukuu Kamishna Mkuu wa Umoja wa Matifa wa Haki za binadamu Volter Turk akipongeza Kenya na kusema hii ni mara ya kwanza kwa Kenya kutumia Sheria ya Kimataifa ya Uhalifu kushtaki uhalifu dhidi ya ubinadamu katika mahakama zake za ndani.Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wakati wa uchaguzi mkuu wa Kenya mwaka 2017, Tume ya Taifa  ya Haki za Kibinadamu ilirekodi vifo 94 na matukio 201 yakihusiana na unyanyasaji wa kingono na zaidi ya majeruhi 300 wengi wao wakieleza kufanyiwa vitendo hivyo na vikosi vya usalama.Bwana Turk amesema “Uamuzi uliochukuliwa leo na Kenya ni wa msingi, ni hatua nzuri kuelekea haki na uwajibikaji kwa waathirika na familia za waathirika, wa ghasia za uchaguzi, na inaweza kuimarisha na kuzuia ukiukaji wa haki za binadamu kwa siku zijazo.”Amebainisha kuwa uamuzi huo wa Kenya unatokana na maendeleo ya hivi karibuni ya taasisi za Kenya  zinazoungwa mkono na Ofisi yake ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu katika kuimarisha uwajibikaji kwa ukiukaji wa haki za binadamu.Kamishna Mkuu Türk amesema ofisi yake itaendelea kujitolea kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Kenya kuendeleza uwajibikaji kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na kushughulikia mauaji ya kiholela na kulazimisha watu kutoweka.

SBS Swahili - SBS Swahili
Je! Azimio One Kenya watafanikiwa kubatilisha matokeo ya uchaguzi mkuu?

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Aug 23, 2022 7:38


Mrengo wakisiasa wa Azimio One Kenya unajiandaa kuwasilisha ombi lakubatilisha matokeo ya uchaguzi mkuu nchini humo.

kenya mkuu azimio uchaguzi mkuu
SBS Swahili - SBS Swahili
Je! nini kitafuata baada ya Raila kushindwa tena katika uchaguzi mkuu?

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Aug 18, 2022 22:51


Kinara wa mrengo wa Azimio One Kenya Raila Odinga, amewania urais mara tano bila mafanikio.

SBS Swahili - SBS Swahili
Wakenya wasifu uwazi wa uchaguzi mkuu

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Aug 15, 2022 10:50


Ni nadra kwa tume ya uchaguzi ya Kenya, kusifiwa kwa jinsi ilivyo simamia uchaguzi mkuu.

kenya mkuu uchaguzi mkuu
SBS Swahili - SBS Swahili
Je! IEBC itakomboa sifa yake baada ya utata ilio zua katika uchaguzi mkuu wa 2017 wa Kenya?

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Aug 11, 2022 11:35


Tume huru ya uchaguzi wa Kenya IEBC, kwa mara nyingine inasimamia uchaguzi mkuu miaka mitano baada ya uchaguzi mkuu wa 2017 ulio paka tume hilo tope lakuganda.

Alfajiri - Voice of America
Wakenya wajitokeza wa wingi ili kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu. - Agosti 09, 2022

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Aug 9, 2022 29:59


Abdushakur Aboud wa VOA ambaye yuko Nairobi aelezea hali ilivyokuwa asubuhi na mapema , wakati wapiga kura wakianza kumininika, pamoja na waangalizi wa kimataifa waliopo nchini humo.

nairobi kura voa agosti mkuu kupiga uchaguzi mkuu
Alfajiri - Voice of America
Kenya: IEBC yasema haitawazuia watuhumiwa wa ufisadi kugombea kwenye uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti - Juni 03, 2022

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jun 3, 2022 29:59


Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini Kenya IEBC, imesema kwamba haitawazuia watuhumiwa wa kashfa za ufisadi kugombea nafasi mbali mbali katika uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti. IEBC inaeleza kuwa ni lazima mahakama iwakute washukiwa na hatia.

SBS Swahili - SBS Swahili
Maeneo bunge ya Tasmania yatoa uvutio mkubwa katika uchaguzi mkuu

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later May 17, 2022 8:13


Tasmania inatoa mvutio mwingi kwa siku ya uchaguzi mkuu, Jumamosi 21 Mei kwa watazamaji wa uchaguzi.

SBS Swahili - SBS Swahili
Wiki ya tatu ya kampeni ya uchaguzi mkuu yatawaliwa na gharama ya maisha

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 29, 2022 9:07


Wiki ya tatu ya kampeni ya uchaguzi mkuu ili tawaliwa na shinikizo za gharama za maisha, baada ya mfumuko wa bei kuongezeka kwa 5.1%.

wiki tatu maisha mkuu uchaguzi mkuu kampeni
SBS Swahili - SBS Swahili
Hoja za afya, na usalama wa mipaka zafungua wiki ya pili ya kampeni ya uchaguzi mkuu

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 19, 2022 7:15


Wiki ya pili ya kampeni za uchaguzi mkuu zime tumbukia katika vita vya kampeni zakutisha kati ya vyama viwili vikubwa nchini.

wiki hoja pili afya mkuu uchaguzi mkuu kampeni
SBS Swahili - SBS Swahili
Dr William S Ruto kupeperusha bendera ya UDA katika uchaguzi mkuu - Mseto wa UDA wamtangaza Dr William S Ruto kuwa kinara wao katika uchaguzi mkuu

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 17, 2022 5:29


Mseto wa United Democratic Alliance (UDA) ume mtangaza rasmi Naibu Rais wa Kenya, William Samoei Ruto kuwa kinara wake katika uchaguzi mkuu wa 9 Agosti 2022. - Mseto wa United Democratic Alliance (UDA) ume mtangaza rasmi Naibu Rais wa Kenya, William Samoei Ruto kuwa kinara wake katika uchaguzi mkuu wa 9 Agosti 2022.

SBS Swahili - SBS Swahili
Uhuru amtangaza Raila kuwa kinara wa mseto wa AZIMIO LA UMOJA katika uchaguzi mkuu

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Mar 14, 2022 7:37


Joto la siasa nchini Kenya laendelea kuongezeka baada ya mseto wa Azimio kumuidhinisha Raila Odinga kuwa kinara wao katika uchaguzi mkuu 9 Agosti 2022.