Siha Njema

Follow Siha Njema
Share on
Copy link to clipboard

Makala inayojadili kwa kina masuala ya afya, tiba na kutambua magonjwa mbalimbali bila ya kusahau namna ya kukabiliana nayo. Watalaam walibobea kwenye sekta ya afya watakujuvya na kukuelimisha juu ya umuhimu wa kuwa na afya bora na si bora afya. Pia utawasikiliza kwa maneno yao watu ambao wameathir…

Rfi - Martha Saranga Amini


    • Apr 16, 2026 LATEST EPISODE
    • every other week NEW EPISODES
    • 9m AVG DURATION
    • 244 EPISODES


    Search for episodes from Siha Njema with a specific topic:

    Latest episodes from Siha Njema

    Miaka mitatu tangu Sudan kuingia kwenye mzozo huduma za afya zimedorora

    Play Episode Listen Later Apr 16, 2026 9:19


    Asilimia 37 ya vituo vya afya nchini Sudan vimeharibiwa wakati wa mapigano na haviwezi kutoa huduma za afya Shirika la madaktari wasio na mipaka,MSF limekuwa likiwahudumia wagonjwa wenye majeraha ,waathiriwa wa magonjwa ya milipuko na waathiriwa wa ubakaji. Hali ya usalama imeilazimu  MSF kusitisha huduma katika maeneo kadhaa baada ya kushuhudiwa mashambulizi ya moja kwa moja kwenye vituo vya afya ,vituo hivyo kuporwa na uhaba wa bidhaa za kimatibabu unaohusishwa na vikwazo vya usafiri.

    Kliniki tembezi za figo zinavyowasaidia wagonjwa wa figo nchini Kenya

    Play Episode Listen Later Apr 7, 2026 10:15


    Idadi ya wagonjwa wa figo imekuwa ikiongezeka kutokana na kuongezeka pia kwa magonjwa yasiyoambukiza kama vile Kisukari.

    Magonjwa ya Autoimune yana uwezo kukusababishia magonjwa mengine zaidi

    Play Episode Listen Later Mar 31, 2026 10:23


    Magonjwa yanayoshambulia kinga yanapompata mtu ,huendelea kusambaa ,kudhuru kingamwili na  kumweka hatarini mgonjwa kiasi cha kuwa mgonjwa anaweza kupatwa na magonjwa zaidi ya moja ya aina hiyo. Elwyn Chebet aligunduliwa na Lupus na baadaye akajikuta anapambana na magonjwa zaidi ya tano aina ya Autoimmune. Mwezi Machi ambapo ulimwengu huelekeza kurunzi kwenye magonjwa ya mfumo wa kinga au Autoimmune,watalaam wanasikitika kuhusu ufahamu mdogo kuhusu magonjwa haya. Wagonjwa wengi huwa na dalili za kukanganya na ubainishaji wa magonjwa haya unaweza kuchukua muda mrefu na kugharimu kiasi kikubwa cha pesa. Na kwa kuwa vyanzo vya magonjwa haya huwa haviko wazi matibabu yake huwa yenye mtihani mkubwa.Watalaam wengi hujaribu kutibu dalili bila kushughulikia chanzo cha ugonjwa wenyewe. Katika makala haya tumezungumza na Elwyn Chebet ambaye ni shujaa na mwanaharakati wa ugonjwa wa Lupus ambao huathiri viungo kadhaa mwilini na hata ngozi. Katika simulizi yake ,anaeleza kuwa kutokana na kinga dhaifu magonjwa tegemezi kama mafua,Malaria na Menegitisi yanaweza kuhatarisha maisha yake hivyo huhitajika kupata chanzo ya mapema dhidi ya magonjwa haya.

    Visa vingi vya TB Afrika bado vinapatikana miongoni mwa vijana hasa wanaume

    Play Episode Listen Later Mar 24, 2026 10:18


    Watalaam wanasema vijana wengi hufikia kwenye maduka ya kuuza dawa kupata huduma za afya baadala ya kufika hospitali kufanyiwa vipimo Unyanyapaa pia inachangia wanaume au vijana kuwa na ari ya kwenda kupata huduma za afya haswa za TB.

    Nini magonjwa yanayoathiri kinga mwili au Autoimmune

    Play Episode Listen Later Mar 24, 2026 10:15


    Unapopata magonjwa ambayo yanaathiri kinga ya mwili wako,ina maana kuwa kinga yako inaweka mifumo yote ya mwili kwenye hatari. Unaweza kujikuta unapata magonjwa kama Lupus,ugonjwa wa Tezi Koo au Mifupo yako kuwa nyepesi kiasi cha kuvunjika kwa urahisi. Ubainishaji wa magonjwa haya unahitaji subira na ufuatialiaji wa karibu ili kuelewa kila dalili anayoonesha mgonjwa .Gharama yake basi inamanisha ni ya juu na huhitaji muda mrefu.

    Kampeni ya kumaliza unyanyapaa wa siku za hedhi kwa kushirikisha wanaume

    Play Episode Listen Later Mar 20, 2026 10:03


    Siku za hedhi huchukuliwa kuwa swala la wanawake na halifai kuzungumzwa hadharani kwa jamii nyingi .Hali hii imesababisha wanawake na wasichana kupitia unyanyapaa ijapokuwa hili ni swala la haki ya uzazi

    Madhara ya afya ya akili yanayotokana na matumizi ya kupitiliza ya simu

    Play Episode Listen Later Mar 3, 2026 10:05


    Ripoti ya afya akili  duniani ,inaonya kuhusu madhara yanayotokana na matumizi ya simu za mkononi miongoni mwa vijana wenye umri wa kati ya miaka 18 na 34 Katika mataifa ya Afrika ambapo matumizi ya simu hizi huanza kwa kuchelewa ,vijana walionekana kuwa afadhali ikilinganishwa na mataifa kama Finland ambapo watoto huanza kutumia simu katika umri mdogo mno.   Katika mataifa yaliyozingatia maswala ya dini na muunganiko wa familia na jamii walionekana pia kuwa na ahueni.

    Fahamu madhara ya mvua kubwa kwa afya yako na namna ya kujikinga

    Play Episode Listen Later Feb 24, 2026 8:59


    Mvua kubwa inaendelea kunyesha katika mataifa mengi ya Afrika ikisababisha mafuriko makubwa ,maafa na uharibifu wa mali Mvua ingawaje ni baraka, kunaponyesha ghafla inaweza kuwa chanzo cha baadhi ya magonjwa kama vile Malaria, Kipindu Pindu na magonjwa ya kusambazwa na minyoo.

    Kupambana na ugonjwa wa mbwa kichaa Nairobi kwa kuzingatia maslahi ya mbwa

    Play Episode Listen Later Feb 10, 2026 10:10


    Mamlaka jijini Nairobi zimefanya operesheni kudhibiti ongezeko la mbwa mtaa katika mkakati wa kupambana na ugonjwa wa mbwa kichaa Mbwa japo anasemekana kuwa rafiki wa karibu na mwaminifu unapomfuga ,matunzo yasiyofaa au kuwatelekeza unaweza kukuweka karibu na ugonjwa wa mbwa kichaa Ukiwa utamfuga mbwa ,sharti kuzingatia usafi na chanjo ya kila mwaka dhidi ya ugonjwa wa mbwa kichaa

    kenya nairobi afya mbwa ugonjwa mamlaka ukiwa
    Kwa nini kuna umuhimu wa kutumia dawa za minyoo baada ya miezi sita

    Play Episode Listen Later Feb 5, 2026 9:42


     Shirika la afya duniani ,WHO hupendekeza matumizi ya dawa za minyoo kwa watoto kati ya mwaka moja hadi 12 ,vijana wenye umri kati ya 13- 19 ,wanawake walio kwenye umri wa kupata watoto na watu wanaoishi katika maeneo yenye minyoo. Hii ni njia mojawapo ya kupambana na utapiamlo, Anamia na matatizo yanayoletwa na minyoo.

    Kufunga saum inafaidi afya yako vile vile nafsi yako ikiwa utafanya mara kwa mara

    Play Episode Listen Later Jan 26, 2026 10:19


    Kuna ushahidi unaoonesha kwamba kufunga kunaweza kusaidia kurekebisha miili yetu ,wakati mwingine kuongeza maisha yetu, pia  njia bora ya kupunguza uzito,   Kitendo cha kukumbatia  Saum huchochea usafi wa moyo, nafsi na kusafisha mwili wako kwa kuondoa chakula ambacho mara nyingine hugeuka kuma sumu mwilini na chanzo cha magonjwa yasiyoambukiza.     Wataalam wa afya  pamoja na watetezi wa kufunga wanasema kuna uhusiano mkubwa kati ya afya ya kimwili na afya ya kiroho.   Kwenye makala hayo ya Siha Njema  tunakupa ufafanuzi huu tukisaidiwa na daktari  Julius Maleve na pia kiongozi wa kidini  Mtume Julius Suubi ,ambaye ameandika kitabu kuhusu faida za kufunga na ambaye amekuwa akifunga kwa kati ya siku 40 hadi 90 kila mwaka kwa zaidi ya mwaka 20 sasa.

    Mpango wa kliniki tembezi unavyowafaidi wakaaji kaskazini mwa Kenya

    Play Episode Listen Later Dec 30, 2025 10:02


    Mpango wa kliniki tembezi yaani mobile clinics  ni pale ambapo wahudumu wa afya wanatembea nyumba kwa nyumba na kuwatibu wenyeji kama vile wazee,akina mama na watoto.Maeneo ya kaskazini mwa Kenya ambapo hospitali  huwa mbali na vijiji ,ndiyo yanayolengwa kwenye mpango huo.

    Juhudi za wazee kukomesha ukeketaji wa wasichana kaskazini mwa Kenya

    Play Episode Listen Later Dec 23, 2025 10:04


    Ukeketaji wa wasichana bado ni changamoto kubwa katika baadhi ya maeneo ya kaskazini mwa Kenya, licha ya marufuku ya kitaifa na juhudi za uhamasishaji zinazoendelea. Takwimu za Kitaifa KNBS na  zile Wizara ya Afya zinaonyesha kuwa asilimia 83 ya wanawake na wasichana wa Marsabit na 66 wa Isiolo tayari wamekeketwa—ikiziweka kaunti hizi miongoni mwa maeneo yenye viwango vya juu zaidi nchini.Sasa wazee maeneo hayo wameanza mchakato kukabiliana na ukeketaji huo

    Je una uhakika wa usalama wa nyama unayoila kila mara nyumbani?

    Play Episode Listen Later Dec 17, 2025 10:09


    Watalaam wa wanyama wanasisitiza wanyama wote wanaochinjwa ni sharti kutimiza viwango vya juu ikiwemo mwonekano ,afya  na usafi. Na kabla kuchinjwa wanyama hao kwa mfano ngombe ,hukaguliwa na kutengwa ili kubainisha nyama yao ni salama. Kwa mlaji unashauriwa kununua nyama iliyo na muhuri ambayo ni alama ya kuonesha nyama hiyo imekaguliwa na kuthibitishwa ni salama. Kwa wale wanaochinjia nyumbani bado unatakiwa kumpata mtalaam wa wanyama kumkagua mnyama wako na kutoa kibali cha kuchinjwa.

    Mzigo wa usugu wa vimelea tishio kubwa kwa mifumo ya afya barani Afrika

    Play Episode Listen Later Dec 13, 2025 9:20


    Matibabu mengi licha ya kupendekezwa au kuorodheshwa sahihi ,yanakabiliwa na usugu wa vimelea tatizo linalofanya dawa hizo kushindwa kutibu inavyotakikana Dawa za kutibu Malaria ,TB na Kipindu Pindu zimetajwa kuathirika sana ,haswa dawa aina ya antibiotics ambazo hutumika kuwa matibabu ya kwanza ya kuua vimelea.

    Kwa nini ni muhimu kuwafikiria akina mama na watoto kwenye kampeni ya magonjwa yaliyosahaulika

    Play Episode Listen Later Dec 2, 2025 9:45


    Ripoti nyingi huonesha kuwa idadi kubwa ya wagonjwa wanaougua magonjwa yaliyotengwa au kusahaulika ni akina mama au watoto  Hii ni kutokana na wao kutangamana moja kwa moja na mazingira ambayo huwa makazi ya vimelea vinavyosababisha magonjwa mbali mbali. Vimelea hao hukaa mchangani,kwenye maji au hupatikana kwenye kinyesi .

    Mabadiliko ya tabia nchi yanayovyochochea magonjwa ya milipuko

    Play Episode Listen Later Dec 1, 2025 10:08


    Tafiti zimeonesha kuwa magonjwa mengi ya milipuko haswa barani Afrika yanachochewa na mabadiliko ya tabia nchi Mafuriko ,ukame au kupanda joto yanaweza kusababisha kusambaa kwa haraka kwa vimelea vinavyosababisha magonjwa au kuzaana kwa haraka.

    Mzigo wa ugonjwa wa Kisukari nchini Sudan Kusini unavyowawaliza wengi

    Play Episode Listen Later Nov 19, 2025 9:52


    Sudan Kusini kando na kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa  wa Kisukari ,upatikanaji wa matibabu bado ni changamoto kubwa Watalaam nchini humo wanahoji mabadiliko ya mtindo wa maisha kama chanzo cha ongezeko la visa hivi.

    afya wengi ugonjwa sudan kusini
    Takwimu sahihi za mapema na maabara wezeshi kupambana na magonjwa ya milipuko

    Play Episode Listen Later Nov 12, 2025 9:01


    WHO inashauri ukanda wa Afrika kuwekeza zaidi katika takwimu zilizo sahihi katika mikakati ya kupambana na magonjwa ya milipuko

    Afueni kwa wanawake wanaokatwa matiti yao kutokana na saratani

    Play Episode Listen Later Nov 2, 2025 9:56


    Kila mwezi wa Oktoba, ulimwengu huadhimisha Mwezi wa Uhamasishaji wa Saratani ya Matiti, lengo kuu likiwa kuhamasisha vipimo vya mapema ili kupunguza hatari ya ugonjwa huu na kutafuta msaada wa kifedha kwa ajili ya utafiti kuhusu saratani ya matiti. Inakadiriwa kuwa, wagonjwa wapya zaidi ya milioni 2.3 wa saratani ya matiti hugunduliwa kila mwaka, kulingana na takwimu za Shirika la Afya Duniani. Wengi wa wanawake waliopatwa na saratani hii walilalzimika kukatawa titi moja au yote mawili ili kuokoa maisha yao,  na hivyo kupoteza kiungo muhimu cha mwili.

    Kabla kuchagua,kununua mafuta ya kupikia ,zingatia mambo hayo

    Play Episode Listen Later Oct 30, 2025 10:19


    Mafuta ya mzeituni, alizeti, mafuta ya nazi,mafuta ya mawese ni baadhi ya mafuta kula ambayo yanapendekezwa kutokana na namna yanavyotengenezwa. Mengi hutengenezwa  kwa kukamuliwa ,bila kuongezwa kemikali bila kutumia joto,hivyo ubora wake ni wa juu.   Mafuta haya hata hivyo ni ya bei juu sana na watalaam wanashauri badala ya kuchagua mafuta ambayo si mazuri na ambayo yanaweza kuongeza mafuta ya Cholesterol mwilini na kusababisha matatizo ya afya ,machaguo mbadala ni mafuta ya uto . Mafuta haya yanaweza kutokana na mimea au mbegu.   Mfano ni mafuta ya Parachichi,Karanga  na hata Canola. Aidha watalaam wanatoa tahadhari kuwa ukitumia mafuta yako kupika ,usipende kuyarudia au kutumia kwa zaidi ya mara moja  na usiyaweke mahali wazi maana yanayoweza kugeuka mabaya bila wewe kufahamu.

    Yafahamu makundi tofauti ya mafuta ya kula,ubora ,madhara na matumizi yake.

    Play Episode Listen Later Oct 15, 2025 9:54


    Kuanzia yale ya nazi hadi mizeituni, mboga hadi kanola, parachichi hadi mafuta ya wanyama maswali yameibuka kuhusu tunajuaje yapi mazuri ya kutumia, na ikiwa tunapaswa kuepuka yoyote yale kabisa Watalaam wa afya wanahoji mafuta ni kiungo muhimu katika mwili wa binadaam kwa  kuwa huchangia madini muhimu na pia husaidia utendakazi wa viungo muhimu mwilini. Hata hivyo wanashauri mafuta kutumika kwa kiasi ili kuzuia mwili kujilimbikizia mafuta  haswa ya Cholestrol ambayo yanaweza kusababisha mishipa ya kupitisha damu kuziba ,kusababisha saratani,shinikizo la damu na magonjwa ya moyo Katika orodha ya mafuta,kuna mafuta yanayotokana na mimea ,wanyama na yale yanayozalisha viwandani maarufu kama Trans Fats Maamuzi ya kutumia mafuta gani ,hata hivyo yanategemea ubora wake ,kazi ya mafuta na mapishi ya mtu Mafuta ya wanyama japo ni asilia yanapaswa kutumika kwa kiasi kidogo mno . Mafuta ya uto haswa ya mimea ni mazuri ila yanaweza kuharibika ikiwa utachanganyika na hewa ya oksijeni  au yanapotumika kwa kurudiwa rudiwa.

    Masaibu ya wakaazi wa kisiwa cha Ndeda nchini Kenya wanaokosa vyoo vya kutosha

    Play Episode Listen Later Oct 9, 2025 9:09


    Mwongozo wa  shirika la afya duniani,WHO kuhusu usafi,unapendekeza choo kimoja kinaweza kutumika na watu 20 ila katika kisiwa cha Ndeda ndani ya Ziwa Victoria ,watu zaidi ya elfu 2 wanachangia vyoo vitano

    Vipimo vya afya kabla ndoa vitakusaidia kuchukua maamuzi sahihi ya afya

    Play Episode Listen Later Oct 3, 2025 9:55


    Kama kuna kipindi watu wengi huwa tumbo joto, ni kusubiri matokeo ya kipimo cha HIV au magonjwa mengi ya zinaa.Au kuambiwa huna uwezo wa kizazi. Hata hivyo unapofanya vipimo hivyo itakuokoa kufanya makosa ambayo yanaweza kuathiri familia yako baadaye. Ikiwa utapima baadhi ya vipimo hivi muhimu utaweza kujipanga kifedha na kuchagua matibabu ambayo yanaweza kutatua changamoto za afya ambazo pengine umekutwa nazo.

    Je unafahamu vipimo vya afya unavyohitaji kupima kabla kufunga ndoa?

    Play Episode Listen Later Sep 24, 2025 10:13


    Watu wengi wanapokaribia kufunga ndoa,hujukumika kufanya vipimo vya virusi vya HIV .Wengi hufanya kipimo hicho si kwa sababu wanajua umuhimu wake bali ni kwa sababu ya ulazima kabla kufunga harusi haswa za Kikristo. Hata hivyo watalaam wa afya wanasema kuna vipimo tele ambavyo ni muhimu pia na vinahitajika kufanywa kabla ndoa. Mwanasaikolojia Naomi Ngugi  anasema kando na kipimo cha HIV,kuna  kipimo cha Rhesus Factor ambayo kama mtu na mwenzake hana ufahamu ,wanaweza kupata shida ya kuharibika mimba. Kuna pia kipimo cha  Genotype  kubaini uwepo wa ugonjwa kama  Selimundu ,Hepatitis B,  Hepatitis C au homa ya ini,vipimo vya  Magonjwa sugu, Magonjwa ya akili na Vipimo vya uzazi kubaini ubora wa mbegu za kiume na matatizo ya  mirija kuziba upande wa wanawake.   Vipimo hivyo vinaweza kugharimu ndoa iwapo wanandoa hawataweka wazi.

    Je unafahamu namna vyakula unavyokula njiani au hotelini vinaandaliwa vipi?

    Play Episode Listen Later Sep 20, 2025 9:21


    Vyakula vinavyoandaliwa nje ya jikoni kwangu huwezi kufahamu viwango gani vya usafi vimezingatiwa Unapoaumua unakula kwa mama nitilie ni vigezo gani unaweza ukaweka ili kuhakikisha unalinda afya yako? Alfred Lobawoi kwenye makala haya ,amewahoji wauza vyakula na walaji kujua mtazamo wao

    kenya afya vyakula
    Nini kifanyike kuwezesha Mipango ya bima ya afya barani Afrika

    Play Episode Listen Later Sep 9, 2025 10:17


    Juhudi za serikali za Afrika kuja na mikakati ya kutoa huduma za afya kwa raia kupitia mipango ya bima ya afya ya kitaifa zimekabiliwa na changamoto za utekelezaji,ufisadi na mifumo isiyo thabiti. Watalaam wa afya sasa wanapendekeza mipango hiyo ya afya iwe kwenye mipango ya kitaifa ya kila mwaka,ikiwa na mwongozi kamili kuhusu huduma gani serikali itatoa kwa raia na kwa kiasi gani. Aidha watalaam wanashauri mipango hiyo iwe inaendana na mahitaji ya kila jamii kwa kuwa serikali nyingi kwa sasa hazina uwezo wa kutoa huduma zote kwa raia Isitoshe,mifumo inyopunguza uvujaji wa raslimali  za umma ni muhimu

    Utengano wa familia unaweza kuleta shinikizo la damu au kisukari

    Play Episode Listen Later Sep 2, 2025 10:04


    Wanadamu ni viumbe ambao hukamilika wanapokuwa kwenye jamii ambapo wanaweza kuelezea hisia zao,kujihisi wanathaminiwa na wana mchango kwa wengine. Mambo  hayo yanapokosa,inaweza kuwa chanzo cha matatizo ya kiafya.Na hii ni hali ambao hukuwa nao wakimbizi ambao wametenganishwa na wapendwa wao. Katika kambi ya Kakuma iliyoko kaunti ya Turkana,kaskazini mwa Nchi ya Wakenya,tulizungumza na wakimbizi ambao walilazimika kutengana na wapendwa wao kwa sababu ya migogoro ya kifamilia,ukoo na hata vita. Ingawa wamepata makao katika kambi ya wakimbizi bado maisha yao hayajakamilika . Wengi wameishi kwenye hali ya upweke,huzuni na kiwewe  na kupata matatizo ya kiafya yakiwemo matatizo ya afya ya akili. Aidha kuna wale ambao wamepatwa na maradhi kama shinikizo la damu ,kisukari,ukosefu wa usingizi na chanzo ni matatizo ambayo wamekumbana nao katika kambi,ugumu wa maisha bila watu walio karibu nawe ambao unaweza kuzungumza nao na kuliwazana. Kamati ya kimataifa ya msalaba mwekundu,ICRC pamoja na shirika la msalaba mwekundu nchini ,KRC,katika kujaribu kukabili hali hiyo ,zinatekeleza mpango wa kujaribu kurejesha mawasiliano na uhusiano wa familia za wakimbizi. Kwa kuwatafuta namna ambao wakimbizi hao wanaweza kuwasiliana kupitia ujumbe wa kuandikiwa au  kwa njia ya simu,mashirika hayo wanasema wamefanikiwa kuwarejeshea tabasamu wachache wenye bahati na wanaendelea kuwasaka wanafamilia zaidi kila mwaka. Matunda ya mpango huo yameonekana miongoni mwa wakimbizi wanaozungumza na jamaa zao na pia kwa wahudumu wa kujitolea wanaotangamana karibu kila siku na wakimbizi hao kwenye kambi.

    Utapiamlo unaweza kukusababishia Diabetes aina ya 5 wameonya watalaam wa afya

    Play Episode Listen Later Aug 26, 2025 10:06


    Hivi karibuni watalaam wa afya pamoja  kwa ushirikiano na  shirikisho la ugonjwa wa kisukari duniani,wamethibitisha uwepo wa Kisukari aina ya tano ambao unahusishwa na utapiamlo Aina hii ya kisukari huathiri watu ambao hawakupata lishe bora wakiwa watoto na kuathiri ukuaji wa kongosho inayozalisha Insulin inayodhibiti sukari mwilini. Aidha kisukari aina ya tano inaweza kuwapata watu ambao wamekumbwa na njaa kwa muda mrefu ,kufanyiwa operesheni ambayo inafanya mtu kupungua mwili kwa kiasi kikubwa.

    Unachohitaji kufahamu kuhusu ugonjwa wa Pneumonia unaoshambulia mapafu yako

    Play Episode Listen Later Aug 21, 2025 9:12


    Watu wengi hudhani kuwa Pneumonia husababishwa na baridi kuingia kwenye kifua lakini watalaam wanasema chanzo cha Pneumonia ni vimelea kushambulia mapafu na mfumo wa kupumulia Watalaam wa afya wanasema ndani ya wiki moja, mtu aliye na Pneumonia hugundulika kwa kuwa anapata ugumu wa kupumua au hata kukosa hewa.

    Kwa nini ni muhimu kuongeza uwekezaji bunifu katika afya ya watoto

    Play Episode Listen Later Aug 12, 2025 10:14


    Hali ya afya ya watoto haswa katika mataifa ya Afrika  imeendelea kuzorota huku kukiwa na ongezeko la visa vya utapiamlo mbaya,ukosefu wa lishe na uhaba wa chanjo muhimu Taasisi zinazojikita kwenye afya ya watoto zinaonya kuwa punguzo kwenye ufadhili kwenye afya ya watoto utaathiri afya ya jamii kwa jumla. Pengo hili limetokana na ongezeko la mizozo na uchumi wa dunia uliotetereka tangu wakati wa janga la Uviko 19,hali hii ikipunguza msaada wa kibinadaam na kushurutisha mataifa kuwekeza kwenye maswala yanayoenekana muhimu zaidi Daktari Ahmed Ogwell afisa mkuu mtendaji wa shirika la VillageReach, anashauri kuwa uwekezaji bunifu katika kitengo hiki cha afya ni muhimu. Dkt Ogwell anapendekeza kuwa wakati huu mataifa yanapokabiliwa na punguzo kwenye ufadhili wa kigeni ni muhimu kwa mataifa kuziba mapengo ya ubadhirifu  wa pesa za umma na kuwekeza kwenye miradi ambayo inakubalika kwenye jamii na isiyo ya gharama ya juu. Hii itahakikisha kuwa mataifa ya Afrika hayawi mataifa tegemezi kwa jamii ya kimataifa ambayo kwa wakati mwingi huwekeza kwenye miradi inayozingatia matakwa yao. Aidha ili kuhakikisha kuwa huduma za afya kama uchomaji chanjo zinawafikia wanajamii wote ni muhimu kwa mataifa ya Afrika kuimarisha huduma za wahudumu wa afya wa jamii ili kuhakikisha kuwa chanjo zinawafikia watoto walengwa baadala ya wazazi kupata ugumu wa kwenda kusaka huduma hizo.

    Watalaam waonya ongezeko la visa vya H pylori katika maeneo ya mijini

    Play Episode Listen Later Aug 5, 2025 10:03


    H pylori isipotibiwa inaweza kugeuka kuwa saratani ya tumbo ,watalaam wameonya Katika makala haya,tunaangazia  sababu ambazo zinaweza kuchangia mtu kupata maambukizo ya H pylori na matibabu yake. Matibabu yake kwa mujibu wa daktari Alex Mungala anayehudumu jijini Nairobi yanaweza kukabiliwa na usugu wa vimelea ,ni ghali na si rahisi kupatikana katika vituo vya afya vya daraja la kwanza.

    Ukiwa utatembea hatua elfu saba kila siku unaweka magonjwa hatari mbali

    Play Episode Listen Later Jul 29, 2025 10:06


    Utafiti uliofanywa wa shirika la utafiti wa afya Lancet Public Health umebaini hatua elfu 7 kila siku unapunguza hatari ya kupatwa na magonjwa ya Saratani,Kisukari,magonjwa ya moyo, shinikizo la damu,sonona na  kupoteza kumbu kumbu Kwa mujibu wa shirika la afya duniani ,WHO,mazoezi ya kudumu dakika 150 kila wiki au mazoezi makali ya dakika 75 ni mkakati wa kuimarisha afya. Katika makala haya nimejiunga na kundi la Nairobi Walk Movement,tawi la Buru Buru ambalo limejitoa kufanya matembezi ya kuanzia kilomita 10 hadi 20 na wakati mwingine hadi 40 kila Jumamosi asubuhi au Jumapili alasiri kuanzia saa tisa na nusu. Kundi hili pia limejisajili kwenye kundi  la kuhesabu hatua ambazo kila mtu hutembea kila siku ,hatua hizo zikihesabiwa kutumia application maalum ya kuhesabu hatua,lengo likiwa hatua hadi elfu 10 kila siku. Kushindana kwa kuhesabu hatua kila siku umekuwa mchezo ambao huwatia moyo Wanachama hao wameelezea faida nyingi kutokana na kujiunga kwenye kundi hilo na kushiriki matembezi. Wapo waliokuwa na wanatumia dawa za kudhibiti shinikizo la damu na sasa wameachana nazo. Aidha wengine wameeleza matembezi kuwaondolea maumivu ya viungo na pia kupata marafiki wazuri.

    Watalaam waonya kukaa muda mwingi kunaweza kukusababishia kifo cha mapema

    Play Episode Listen Later Jul 23, 2025 10:09


    Kukaa kwa zaidi ya saa sita mfululizi kila siku inaweza kukuweka kwenye hatari ya kupata magonjwa ya uti wa mgongo,kisukari,shinikizo la damu na kifo cha mapema

    Baadhi ya hospitali nchini Kenya zinazalisha chakula kuwalisha wagonjwa

    Play Episode Listen Later Jul 15, 2025 10:17


    Katika mkakati wa kuboresha lishe,hospitali zinatumia vipande vya ardhi zao kukuza chakula kuwalisha wagonjwa wao

    Serikali ya Kenya yazingatia afya ya akili miongoni wa vikosi vya usalama

    Play Episode Listen Later Jul 10, 2025 9:36


    Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen amesema polisi wenye changamoto za afya ya akili hawatafukuzwa kazi bali watapewa matibabu stahiki Kumeshuhudiwa hivi karibuni visa vya polisi kutumia silaha zao visivyo na utendakazi wao kukosolewa na raia pamoja na wanaharakati wa haki

    Je ni muda wa nchi za Afrika kujadili huduma ya kusaidiwa kufa ?

    Play Episode Listen Later Jul 2, 2025 10:12


    Hivi majuzi bunge la Uingereza limepitisha mswada wa kuhalalisha huduma ya kusaidiwa mtu kufa Huduma hii itatekelezwa katika hospitali chini ya usimamizi wa wahudumu wa afya ,kwa watu wazima wanaougua magonjwa yasiyopona . Watalaam wa afya wanasisitiza kuwa hatua hiyo sharti mgonjwa kuridhia bila  kushinikizwa .

    Sera ya Kenya kuhakikisha raia wake wanafanya mazoezi kila mara

    Play Episode Listen Later Jun 25, 2025 10:06


    Takwimu zinaonesha watu wengi kupatwa na magonjwa yasiyoambukizwa kutokana na kuishi bila kufanya mazoezi na kula vibaya Sera hii itatoa mwongozo wa  taasisi za serikali na binafsi kuweka mikakati ya kuruhusu mazoezi ya kila mara wakati wa kazi au nje ya kazi

    Mwili wako unavyowasiliana kupitia utendakazi wake na kukupa onyo kukiwa tatizo

    Play Episode Listen Later Jun 20, 2025 10:08


    Kila siku mwili wako hukuzungumzia na ni jukumu lako kusoma mwili wako na kuelewa unasema nini au unakuonya kuhusu nini Baadhi ya matatizo ambayo unaweza kujiepusha nayo ni matatizo ya afya ya akili ,kufeli viungo muhimu au mifumo yako ya afya. Na ili kuhakikisha mwili wako unazungumza na kutoa taarifa iliyo sahihi kuna baadhi ya vitu unaweza kufanya kwa mfano kupata muda wa kutosha kulala,kupata lishe bora  na kufanya mazoezi 

    Uhusiano wa karibu kati ya matatizo ya tezi koo na afya yako ya akili

    Play Episode Listen Later Jun 12, 2025 10:00


    Matatizo ya tezi koo yanaweza kujidhirisha kwa  dalili kama vile msongo wa mawazo,kukosa usingizi,kiwewe na mtu kukosa ari ya chochote maishani Katika makala haya ,tunamtambulisha Daktari Violet Oketch anayesimamia kitengo cha afya ya akili katika hospitali  kuu ya rufaa nchini Kenya ya Kenyatta. Daktari Violet anafafanua ufungumano kati ya matatizo ya tezi koo na matatizo ya afya ya akili. Aidha afisa mkuu mtendaji wa kikundi cha kuhamasisha kuhusu matatizo ya tezi koo,Thyroid  Disease Awareness Kenya Foundation ,TDAK,  Sarah Katulle anaelezea umuhimu wa wagonjwa kuwa kwenye kundi ambapo wanaweza kushirikishana kuhusu mbinu mbadala ya kuishi na matatizo hayo kando na matibabu. Kundi hilo linawasaidia wagonjwa kupata matibabu kwa urahisi kwa kushirikiana na madaktari bingwa ,mahabara maalum na dawa sahihi. Aidha TDAK ili kuwasaidia wagonjwa hao kuishi maisha ya kawaida wakiwa kazini ,inawaandikia barua ambazo zinawasilishwa kwa maajiri kutambua hali halisi ya wagonjwa na mahitaji yao.

    Mzigo wa uvutaji sigara Misri ulivyo pasua kichwa kwa afya ya wengi

    Play Episode Listen Later Jun 3, 2025 9:55


    Misri ipo kwenye njia panda  kuhusu utekelezaji wa sheria zake za kudhibiti matumizi ya tumbaku haswa sigara na Shisha. Kwa njia moja sigara inaleta  mapato makubwa kwa mfuko wa mapato ya  serikali ya Misri ,ni tabia inayoruhusiwa ila kwa upande mwingine inakodolea macho hatari kubwa ya kiafya inayotokana na uvutaji sigara.Unapowasili Cairo jiji kuu la Misri ,ukutana na harufu tamu ya mikate ,keki na bidhaa zingine za ngano za kuokwa,marashi yanayonukia lakini pia kuna harufu ya shisha, aina ya tumbaku ya kisasa zenye ladhaa  za kupendeza lakini pia harufu kali zaidi ya sigara.Zipo sheria zinazokataza uvutaji sigara katika sehemu za umma ,shule ,vituo vya afya ila utekelezaji wake bado ni changamoto kubwa.Kuna mpango pia wa treni mwendo kasi ,maarufu Greenline ambapo uvutaji sigara umeharamishwa.Hata hivyo kibarua bado kipo cha kubadilisha mtazamo wa baadhi ya wananchi wanaoamini uvutaji sigara ni starehe ,kitu cha hadhi  na unaweza kufanya hivyo popote muradi usikamatwe.Misri pia inabidi kuangalia kwa jicho la pili sheria zake za kutoza ushuru bidhaa za tumbaku iwapo lengo ni kuleta mapato kwa serikali ,kuwafaidi wazalishaji au kwa maslahi ya afya ya wengi.Kwa mujibu wa shirika la afya duniani,WHO,  asilimia 20-25% ya watu wazima nchini Misri huvuta sigara.

    Mipango tofauti ya matibabu ya matatizo ya Tezi koo ambayo hutumika Afrika

    Play Episode Listen Later May 28, 2025 10:06


    Kabla mgonjwa yeyote kuanzishwa kwenye  matibabu, awe ana tatizo la tezi koo kuzalisha homoni kupitiliza au kushindwa kuzalisha, ni sharti vipimo maalum kufanyika Kipimo cha kwanzo ni inaangazia homoni tofauti inayozalishwa na tezi koo na hii mtu yeyote anaweza kufanya katika wakati wa kufanya vipimo kujua hali yake ya afya ,hapa mtu si lazima awe ameonesha dalili za tezi koo kuwa na tatizo.Kipimo cha pili ambacho ni muhimu huzingatia zaidi  viwango vya  homoni tatu muhimu zinazozalishwa na tezi koo ambayo ni  (TSH), thyroxine (T4), na  triiodothyronine (T3) .Matokeo yataamua ni mpango gani wa matibabu mgonjwa atapewa  dawa,kudhibiti homoni au kuzalisha homoni mbadala tezi koo inaposhindza kazi yake.Kando na dawa kama mpango wa matibabu ,wagonjwa wenye uvimbe wanaweza kushauriwa kufanya upasuaji kuondoa tezi koo ,sehemu yake au yote.Kuna pia mpango wa kutumia mianzi na madini ya Iodine maarufu kama Radioiodine mpango ambao ni sharti kufanywa kwa ueledi mkubwa na kwenye vituo vya afya vilivyo na vifaa vya viwango vya juu.

    Matatizo ya tezi ya koo ambayo yanaweza kukusababishia matatizo ya akili

    Play Episode Listen Later May 20, 2025 10:09


     Matatizo ya tezi ya koo ,kwa kawaida  yananaletwa na upungufu au wingi wa madini aina ya iodine ambayo huzalishwa na tezi (thyroid gland).  Homoni inapokuwa kidogo hali ambayo inafahamika kama Hypothyroidism, hii inaashiria kwamba tezi inafanya juhudi za hali ya juu kutafuta madini hayo .Mtu aliye na hali hii ,anakuwa hana nguvu ,nywele kudondoka  na hata mzunguko wake wa mwezi wa damu huvurugika.Madini hayo yanapokuwa mengi inamanisha tezi inafanya kazi kupitliza kuzalisha homoni iliyozidi  kwenye mzunguko wa damu na kuchanganyika na vitu vingene ambavyo husababisha kutengeneza kama sumu fulani ambayo huchoma mafuta yaliyo kwenye hifadhi mwilini, mishipa ya fahamu huathirika kiasi kidogo.Mtu ambaye ameathiriwa na aina hii ya pili, huanza kupunga uzito na umbo la mwili taratibu baadaye madhara yanapoongezeka mtu anaanza kupoteza kumbukumbu, anakuwa na hasira, anakula sana, nywele zinanyonyoka mpaka anapata upara, magoti yanakosa nguvu na mtu anashindwa kutembea.Moyo kwenda mbio , macho yanavimba sehemu ya juu kope na jicho lenyewe linatoka nje kama vile linadondoka.Ni vizuri kuwahi hosipitali ili kupata vipimo ambavyo vinaangazia utendakazi wa tezi ,kwa jina la kiingereza ,Thyroid Function ,ili kubaini iwapo una tatizo la kwanzo au la pili.Na si lazima mtu kuwa na uvimbe ili kubainika kuwa ana tatizo la tezi koo. Kuna wale ambao uvimbe unakuwa upande wa ndani ,wale wenye uvimbe unaonokena nje ya koo ya wale ambao hawana uvimbe wowote.

    Mfano wa Misri wa kupambana na Malaria unaweza kutumika na mataifa ya Afrika

    Play Episode Listen Later May 13, 2025 9:50


    Misri imepambana kwa karibu miaka 100 kabla kupata cheti cha WHO cha kufaulu kutokomeza Malaria Oktoba 2024 Katika mkakati ambao umetumia Misri kuangamiza Malaria ni udhibiti wa Mbu,ambapo serikali iliwekeza kwenye kupiga dawa kwenye maeneo yanayoweza kuwa makazi ya mbu .Ufuatiliaji na ubainishaji wa haraka  umechangia pia pakubwa kuushinda ugonjwa wa Malaria ,mkakati ambao pia jamii ilibidi kushirikishwa.Kitengo cha afya ya umma kimekuwa kikifanya hamasisho kwa wanajamii kukumbatia mbinu za kuzuia mbu kwa kutumia vyandarua na pia kupata matibabu ya haraka mtu anapoonesha dalili za Malaria.

    Mchango wa wanaveterinari ulivyo muhimu katika mapambano ya magonjwa ya milipuko

    Play Episode Listen Later May 3, 2025 10:07


    Ongezeko la magonjwa ya milipuko linaibua swala la kwa nini watalaam wa wanyama hawahusishwi kikamilifu katika mifumo ya afya ya binadaam Mpango wa one Health Approach unaonadiwa kwa sasa kwa mataifa ,unahimiza kuipa kipau mbele afya ya wanyama ,ili kuchangia siha njema ,usalama wa chakula na maendeleo endelevu .

    Kwa nini ni muhimu kuyachunguza maziwa unayotumia nyumbani kulinda afya yako

    Play Episode Listen Later May 3, 2025 10:00


    Kumekuwa na malalamishi ya maziwa yaliyo kwenye soko kusababisha madhara ya kiafya Watalaam wa afya ,bodi inayosimamia bidhaa za maziwa nchini Kenya na wanavetirinari wanasema matatizo hayo huenda yanatokana na uzembe wakati wa uchakataji maziwa ,uhifadhi na pia wafanyabiashara wenye pupa.

    Changamoto zinazowakumba watalaam wanaojikita kwenye tiba asilia nchini DRC

    Play Episode Listen Later Apr 8, 2025 10:00


    Baadhi ya changamoto zinazokumba sekta ya tiba asilia ni mwitiko na  ukosefu wa sheria za kuisimamia katika  nchi mbali mbali

    Ufanisi wa Tiba asili nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

    Play Episode Listen Later Apr 7, 2025 10:11


    Waganga wa tiba asilia wana mchango katika ulimwengu wa uzalishaji dawa 

    Ukosefu wa maji salama unavyozidisha hali ya kibinadaam barani Afrika

    Play Episode Listen Later Mar 26, 2025 10:16


    Kuna idadi kubwa ya watu wanaoshindwa kupata maji salama kwa matumizi ya nyumbani ,hospitali na hata mashamba Uhaba wa maji unaorodheshwa kuwa sababu kubwa ya watu kukosa chakula, kujikimu katika nchi zinazoshuhudia migogoro.Katika nchi kama Sudan na DRC kuna ripoti za hospitali ,kambi za wakimbizi kukosa moja hivyo mashirika ya kimsaada yanapata changamoto kuwahudumia wakimbizi

    Mpango wa lishe katika shule za umma nchini Kenya kupambana na utapiamlo

    Play Episode Listen Later Mar 19, 2025 10:07


    Ukosefu wa lishe bora huathiri afya na elimu nchini Kenya Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la linalowahudumia Watoto (UNICEF) imeonesha  kuwa takriban watoto milioni mbili nchini Kenya wanakabiliwa na matatizo yanayotokana na utapiamlo. Mipango ya lishe  bora shuleni  eneo la Nyanza na maghari mwa Kenya umeonekana kuwa suluhu huku wanafunzi wakipata vyakula vilivyo na virutubishi bora vinavyosaidia kuboresha kinga ya mwili,hivyo kuimarisha afya .

    Haja ya huduma muhimu za wanawake waja wazito kupatikana kwa urahisi

    Play Episode Listen Later Mar 11, 2025 10:09


    WHO imetaja ukosefu wa huduma za kuokoa maisha wakati wa kujifungua huchangia vifo vingi vya wanawake waja wazito Huduma hizo za wanawake hata hivyo zina bei kubwa

    Claim Siha Njema

    In order to claim this podcast we'll send an email to with a verification link. Simply click the link and you will be able to edit tags, request a refresh, and other features to take control of your podcast page!

    Claim Cancel