Makala inayojadili kwa kina masuala ya afya, tiba na kutambua magonjwa mbalimbali bila ya kusahau namna ya kukabiliana nayo. Watalaam walibobea kwenye sekta ya afya watakujuvya na kukuelimisha juu ya umuhimu wa kuwa na afya bora na si bora afya. Pia utawasikiliza kwa maneno yao watu ambao wameathir…
Misri ipo kwenye njia panda kuhusu utekelezaji wa sheria zake za kudhibiti matumizi ya tumbaku haswa sigara na Shisha. Kwa njia moja sigara inaleta mapato makubwa kwa mfuko wa mapato ya serikali ya Misri ,ni tabia inayoruhusiwa ila kwa upande mwingine inakodolea macho hatari kubwa ya kiafya inayotokana na uvutaji sigara.Unapowasili Cairo jiji kuu la Misri ,ukutana na harufu tamu ya mikate ,keki na bidhaa zingine za ngano za kuokwa,marashi yanayonukia lakini pia kuna harufu ya shisha, aina ya tumbaku ya kisasa zenye ladhaa za kupendeza lakini pia harufu kali zaidi ya sigara.Zipo sheria zinazokataza uvutaji sigara katika sehemu za umma ,shule ,vituo vya afya ila utekelezaji wake bado ni changamoto kubwa.Kuna mpango pia wa treni mwendo kasi ,maarufu Greenline ambapo uvutaji sigara umeharamishwa.Hata hivyo kibarua bado kipo cha kubadilisha mtazamo wa baadhi ya wananchi wanaoamini uvutaji sigara ni starehe ,kitu cha hadhi na unaweza kufanya hivyo popote muradi usikamatwe.Misri pia inabidi kuangalia kwa jicho la pili sheria zake za kutoza ushuru bidhaa za tumbaku iwapo lengo ni kuleta mapato kwa serikali ,kuwafaidi wazalishaji au kwa maslahi ya afya ya wengi.Kwa mujibu wa shirika la afya duniani,WHO, asilimia 20-25% ya watu wazima nchini Misri huvuta sigara.
Kabla mgonjwa yeyote kuanzishwa kwenye matibabu, awe ana tatizo la tezi koo kuzalisha homoni kupitiliza au kushindwa kuzalisha, ni sharti vipimo maalum kufanyika Kipimo cha kwanzo ni inaangazia homoni tofauti inayozalishwa na tezi koo na hii mtu yeyote anaweza kufanya katika wakati wa kufanya vipimo kujua hali yake ya afya ,hapa mtu si lazima awe ameonesha dalili za tezi koo kuwa na tatizo.Kipimo cha pili ambacho ni muhimu huzingatia zaidi viwango vya homoni tatu muhimu zinazozalishwa na tezi koo ambayo ni (TSH), thyroxine (T4), na triiodothyronine (T3) .Matokeo yataamua ni mpango gani wa matibabu mgonjwa atapewa dawa,kudhibiti homoni au kuzalisha homoni mbadala tezi koo inaposhindza kazi yake.Kando na dawa kama mpango wa matibabu ,wagonjwa wenye uvimbe wanaweza kushauriwa kufanya upasuaji kuondoa tezi koo ,sehemu yake au yote.Kuna pia mpango wa kutumia mianzi na madini ya Iodine maarufu kama Radioiodine mpango ambao ni sharti kufanywa kwa ueledi mkubwa na kwenye vituo vya afya vilivyo na vifaa vya viwango vya juu.
Matatizo ya tezi ya koo ,kwa kawaida yananaletwa na upungufu au wingi wa madini aina ya iodine ambayo huzalishwa na tezi (thyroid gland). Homoni inapokuwa kidogo hali ambayo inafahamika kama Hypothyroidism, hii inaashiria kwamba tezi inafanya juhudi za hali ya juu kutafuta madini hayo .Mtu aliye na hali hii ,anakuwa hana nguvu ,nywele kudondoka na hata mzunguko wake wa mwezi wa damu huvurugika.Madini hayo yanapokuwa mengi inamanisha tezi inafanya kazi kupitliza kuzalisha homoni iliyozidi kwenye mzunguko wa damu na kuchanganyika na vitu vingene ambavyo husababisha kutengeneza kama sumu fulani ambayo huchoma mafuta yaliyo kwenye hifadhi mwilini, mishipa ya fahamu huathirika kiasi kidogo.Mtu ambaye ameathiriwa na aina hii ya pili, huanza kupunga uzito na umbo la mwili taratibu baadaye madhara yanapoongezeka mtu anaanza kupoteza kumbukumbu, anakuwa na hasira, anakula sana, nywele zinanyonyoka mpaka anapata upara, magoti yanakosa nguvu na mtu anashindwa kutembea.Moyo kwenda mbio , macho yanavimba sehemu ya juu kope na jicho lenyewe linatoka nje kama vile linadondoka.Ni vizuri kuwahi hosipitali ili kupata vipimo ambavyo vinaangazia utendakazi wa tezi ,kwa jina la kiingereza ,Thyroid Function ,ili kubaini iwapo una tatizo la kwanzo au la pili.Na si lazima mtu kuwa na uvimbe ili kubainika kuwa ana tatizo la tezi koo. Kuna wale ambao uvimbe unakuwa upande wa ndani ,wale wenye uvimbe unaonokena nje ya koo ya wale ambao hawana uvimbe wowote.
Misri imepambana kwa karibu miaka 100 kabla kupata cheti cha WHO cha kufaulu kutokomeza Malaria Oktoba 2024 Katika mkakati ambao umetumia Misri kuangamiza Malaria ni udhibiti wa Mbu,ambapo serikali iliwekeza kwenye kupiga dawa kwenye maeneo yanayoweza kuwa makazi ya mbu .Ufuatiliaji na ubainishaji wa haraka umechangia pia pakubwa kuushinda ugonjwa wa Malaria ,mkakati ambao pia jamii ilibidi kushirikishwa.Kitengo cha afya ya umma kimekuwa kikifanya hamasisho kwa wanajamii kukumbatia mbinu za kuzuia mbu kwa kutumia vyandarua na pia kupata matibabu ya haraka mtu anapoonesha dalili za Malaria.
Ongezeko la magonjwa ya milipuko linaibua swala la kwa nini watalaam wa wanyama hawahusishwi kikamilifu katika mifumo ya afya ya binadaam Mpango wa one Health Approach unaonadiwa kwa sasa kwa mataifa ,unahimiza kuipa kipau mbele afya ya wanyama ,ili kuchangia siha njema ,usalama wa chakula na maendeleo endelevu .
Kumekuwa na malalamishi ya maziwa yaliyo kwenye soko kusababisha madhara ya kiafya Watalaam wa afya ,bodi inayosimamia bidhaa za maziwa nchini Kenya na wanavetirinari wanasema matatizo hayo huenda yanatokana na uzembe wakati wa uchakataji maziwa ,uhifadhi na pia wafanyabiashara wenye pupa.
Baadhi ya changamoto zinazokumba sekta ya tiba asilia ni mwitiko na ukosefu wa sheria za kuisimamia katika nchi mbali mbali
Waganga wa tiba asilia wana mchango katika ulimwengu wa uzalishaji dawa
Kuna idadi kubwa ya watu wanaoshindwa kupata maji salama kwa matumizi ya nyumbani ,hospitali na hata mashamba Uhaba wa maji unaorodheshwa kuwa sababu kubwa ya watu kukosa chakula, kujikimu katika nchi zinazoshuhudia migogoro.Katika nchi kama Sudan na DRC kuna ripoti za hospitali ,kambi za wakimbizi kukosa moja hivyo mashirika ya kimsaada yanapata changamoto kuwahudumia wakimbizi
Ukosefu wa lishe bora huathiri afya na elimu nchini Kenya Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la linalowahudumia Watoto (UNICEF) imeonesha kuwa takriban watoto milioni mbili nchini Kenya wanakabiliwa na matatizo yanayotokana na utapiamlo. Mipango ya lishe bora shuleni eneo la Nyanza na maghari mwa Kenya umeonekana kuwa suluhu huku wanafunzi wakipata vyakula vilivyo na virutubishi bora vinavyosaidia kuboresha kinga ya mwili,hivyo kuimarisha afya .
WHO imetaja ukosefu wa huduma za kuokoa maisha wakati wa kujifungua huchangia vifo vingi vya wanawake waja wazito Huduma hizo za wanawake hata hivyo zina bei kubwa
Serikali za Afrika zitalazimika kuchangia ufadhili wa mipango ya kupambana na Malaria kufidia pengo kubwa la ufadhili Muungano wa viongozi wa Afrika wa kupambana na Malaria ,Africa Leaders Malaria Alliance unasema Afrika inahitaji dola bilioni 5 nukta nane mwaka huu wa kifedha hadi 2026.Hali hii pia imechangiwa na Marekani kukata ufadhili wa misaada kwa nchi za kigeni
Mamia ya wakaazi wa kaskazini mashariki mwa Kenya maeneo yanayopakana na Somalia na waathiriwa wakubwa wa mzozo wa Somalia hawajakuwa na maji masafi , hali hiyo ikizidisha mgogoro wa kijamii ndani ya jamii hii ya wafugaji wanaotokea upande wa Kenya na upande mwingine wa Somalia. Kukabili hali hii ,kamati ya kimataifa ya msalaba mwekundu , International Committee of the Red cross ,ICRC , shirika la msalaba mwekundu nchini Kenya ,Kenya Red Cross,KRC katika mkakati wa kuleta amani na ustawi imekuwa ikifanya miradi ya kuwapa wakazi maji .Carol Korir amezuru eneo la Masalani ,kaunti ya Garissa kilomita chache na msitu wa Boni ambapo Al shabab wamekuwa wakifanya mashambulizi na kujificha .
Katika siku za hivi punde magonjwa ya milipuko imeripotiwa katika mataifa ya Afrika ,ikiwemo Ebola Marburg na Mpox
Guinea itakuwa ni taifa la nane la Afrika kuthibitishwa kuangamiza ugonjwa wa malale Guinea imekuwa ilishiriki katika majaribio ya matibabu ya ugonjwa wa malale ambayo yalifanyiwa utafiti mara ya kwanza nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya CongoTimu ya madaktari kutoka DRC na Guinea walishirikishwa kwenye majaribio hayo na kwenye makala haya tumezungumza na Dkt Chirac Bulanga kutoka DRC
DRC imeripoti maambukizi ya Ukoma mwisho wa mwaka jana na pia mwaka huu Ukoma ni ugonjwa unaoathiri sana ngozi na unaweza kuharibu baadhi ya viungo kama vile mikono ,miguu na hufanya mtu kutengwa na jamii
Kumeendelea kushuhudiwa kwa idadi kubwa ya watu wanaougua mafua au magonjwa yanayoathiri mfumu wa kupumua mwezi Januari ambao una joto jingi na vumbi. Hii inajiri wakati China ikiwa imeripoti mlipuko wa ugonjwa wa Human metapneumovirus ,HPMV unaofanana na COVID 19 .Daktari Juma Maleve kutoka Hospitali ya rufaa ya Mombasa ,Pwani ya Kenya anafafanua.
Kwa kitaalam mtindio wa ubongo unaitwa Cerebral Palsy kwa kifupi CP..ugonjwa huu unatokana na jereha kwenye ubongo ambao huwa linafanya mtoto kushindwa kudhibiti misuli ya mwili wake hali inayoweza kusababisha viungo vya mtoto kulegea au kukamaa muda wote. Mtoto anaweza kupata majeraha kwenye ubongo akiwa bado yuko tumboni, wakati wa kuzaliwa au baadae maishani.CP husababisha ulemavu wa kudumu katika maisha yote ya mtoto.
Vasectomy ni njia ya kupanga uzazi ambayo inahusisha upasuaji wa mshipa unaopitisha mbegu za kiume, ili mme asiweze kumpachika mke mimba. Ni njia ya upangaji uzazi ya milele.Na pengine unajiuliza hili linafanyiikaje na ina athari gani kwenyen afya ya mwanaume ?Sikiliza makala haya
Kwenye awamu yetu ya Kwanza tuliangazia njia za asilia walizokuwa wanatumia nyanya zetu kabla ya sayansi kuingia.Tukataja njia ya Kalenda,mipira ya kondomu na kumwaga mbegu za kiume nje ya njia ya uzazi almaarufu Withdrawal.Hivyo basi kwenye sehemu hii ya pili tutaangazia njia za homoni na zisizo za homoni na ambazo asilimia kubwa ya wanawake wanatumia.Kama vile vidonge, vipandikizi ,sindano, na IUD.
Makala haya yanaangazia upangaji kupanga uzazi, na jinsi linavyohusiana na afya ya mwanamke. Kupanga uzazi ni sehemu muhimu ya afya, kwani husaidia wanawake kudhibiti idadi ya watoto wanapokuwa nayo, na pia ina athari kubwa katika afya yao ya kimwili na kihisia.
Idadi ya vijana wanaotumia dawa za kulevya katika umri mdogo imeongezeka
Katika makala haya, tutazungumza na watu muhimu kama vile mgonjwa wa UKIMWI, daktari, na mkunga anayeelimisha kuhusu jinsi ya kuzuia watoto kuambukizwa virusi vya UKIMWI wakati wanapozaliwa. Pamoja, tutafahamu changamoto, mafanikio na hatua zinazochukuliwa katika vita hivi.
Umoja wa mataifa umeorodhesha mwaka 2024 kama mwaka hatari zaidi kwa wafanyikazi wa mashirika ya kimsaada Katika takwimu za UN ,wafanyakazi zaidi ya 200 wamewauwa katika mzoz wa Gaza na wengine zaidi ya 20 katika mzozo wa Sudan
Idadi kubwa ya kina dada wameamua kuchagua upasuaji kama njia rahisi ya kujifungua kwa sababu tofauti tofauti.Sehemu ya pili ya makala haya inaangazia ni kwa nini idadi hio inaongezeka kisha hali inakuaje pale kwenye chumba cha kujifungulia.Dakatari Lilian Nkirote kutokea hospitali ya Jacaranda jiji Nairobi anaelezea kwa kina.
Makala ya siha njema wiki hii tunaangazia Afya ya uzazi na kujifungua na sio safari nyepesi.Ni safari yenye changamoto haba na furaha kwa wanawake na familia zao. Ni muhimu kwa kila mama mjamzito kufahamu hatua muhimu za kuhakikisha ustawi wa afya yake na ya mtoto anayemtarajia. Kupitia huduma bora za kiafya na ushauri wa wataalamu, wanawake wanaweza kufurahia safari ya uzazi kwa usalama na utulivu.
Kumekuwa na mikakati maksudi katika nchi za Afrika kuwekeza katika utafiti kuhusu nyoka na matibabu ya simu yake Baadhi ya mikakati hiyo ni utafiti wa kuwa na aina moja ya dawa ambayo inaweza kutumika katika nchi za Afrika Mashariki vile vile kuelimisha jamii kuhusu huduma za kwanza sahihi kuwasaidia wagonjwa na namna ya kuzuia madhara zaidi kutokana na sumu ya nyoka.
Kungatwa na nyoka imeorodheshwa miongoni mwa matatizo ya kiafya yaliyotengwa Takwimu za shirika la afya duniani ,WHO zinasema kila dakika nne ,watu nne duniani, hupoteza maisha kutokana na sumu ya nyoka.Hii ni kutokana na gharama ya juu ya matibabu ,ugumu wa kupatikana na matibabu haya na raia kutofahamu hatua sahihi ya kufuata ukiumwa au kutemewa sumu na nyoka.Nchini Sudan Kusini ,visa vya wagonjwa wanaongatwa imeongezeka maradufu kutokana na mafuriko ya miezi kadhaa kwa mujibu wa shirika la madaktari wasio na mipaka,MSFMSF hata hivyo kudhibiti hali ,inatumia mfumo wa akili mnemba au AI kurahisisha ubainishaji wa ainya ya nyoka na sumu yake vile vile matibabu yake,mradi unaoendeshwa na MSF katika baadhi ya vituo vyake jimbo la Warrap na Abyei.
Kamati ya kimataifa ya msalaba mwekundu,ICRC mara nyingi hubidi kuhudumu katika maeneo yenye mizozo kutoa huduma za dharura ,msaada wa kibinadaam ikiwemo afya Ili kukabiliana na changamoto za kuafikia malengo yake ya kutoa huduma za afya za dharura katika uwanja wa vita ,maeneo yenye majanga ,imebidi kufumbua mbinu ya kuwa na hospitali za muda ambazo zinajengwa kutumia hema na zinaweza kufanya kazi ndani ya saa 96ICRC inaendelea na mafunzo ya kuwaandaa wahudumu wa afya wanaohudumu katika mazingira hatarishi ,ili wapate kuhudumu ipasavyoMafunzo hayo yanatolewa kwenye hospitali halisi ambazo hutumika katika maeneo ya mizozo ,ambapo wahudumu hao hutakiwa kushughulikia mazingira tofauti ya dharuraMafunzo hayo yamefanyika nchini Kenya mara mbili ambapo wahudumu hao kutoka maeneo tofauti wanawekwa kwenye makundi na kutakiwa kutangamana na kushughulikia dharura tofauti kabla kuanza kutumwa kwenye maeneo ya mizozo
Mashirika ya nchini Kenya kwa ushirikiano na serikali za kaunti ,yamezindua mfumo mpya na wa kisasa wa vyoo bunifu visivyotumia maji wala kuunganishwa na mabomba ya maji taka Hatua Ambayo imeonekana kupunguza msambao wa magonjwa kama vile kipindupindu.
Raia wengi bado hawawezi kufurahia haki zao za afya ya uzazi kutokana na ukosefu wa ufahamu Haki hizo ni pamoja na haki ya kuwa mzazi au la,kupata habari kuhusu afya ya uzazi ,kupata huduma bora za uzazi ,kushiriki mapenzi kwa njia stahiki na kuhudumiwa katika vituo vya afya kwa heshima
Ripoti nyingi zinaonesha wanawake pamoja na wanaume wanakabiliwa na changamoto za uzazi Wanandoa nyingi wanalazimika kukaa miaka mingi kabla kupata watoto ,kitu ambacho bado kinazingatiwa na jamii za Afrika kuwa ukamilifu katika kila ndoa au familia.Daktari bingwa wa uzazi dkt Dennis Miskella anaeleza juhudi za kutafuta mtoto zinastahili kuwa ushirikiano kati ya mke na mumeweBaadhi ya sababu zinazohusishwa na hali hii ni kushiriki tendo la ndoa visivyo ,athari za baadhi ya mbinu za kupanga uzazi ,uvutaji sigara na pia unene wa kupitiliza
Mashirika ya kiraia yanayofanya kazi maeneo ya Kisumu nchini Kenya wanawasaidia wanawake kuachana na mpango wa kuuza miili yao ili kupata samaki Tabia hiyo inayofahamika kama ngono samaki kwa wakazi imekuwa ikichangia msambao wa virusi vya HIV
Mikakati ambayo WHO inahimiza nchi za Afrika kukumbatia ni ubadilishanaji wa taarifa kuhusu ugonjwa wa Mpox ,ubainishaji sahihi na kampeni za chanjo Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ,kuna hofu ya msambao hatari wa MPox unaohuishwa na vitendo vya ngonoWatalaam wa afya nchini DRC pia wanahimiza uhamasisho zaidi kuhusu ugonjwa huo ambao umesababisha vifo zaidi ya 500
Shirika la afya duniani ,WHO na taasisi ya kudhibiti magonjwa ya umoja wa Afrika ,CDC zililazimika kuchukua uamuzi mzito wa kutangangaza MPOX dharura ya kiafya Mataifa 16 ya Afrika kati ya 55 yameripoti visa vya MPOX mwaka huu ,CDC ikisema maambukizo yamepanda hadi asilimia 160 mwaka huu ukilinganishwa na mwaka 2023Virusi vya MPOX vimeripotiwa kujibadilisha na kwa sasa msambao hatari wa virusi sugu zaidi unahusishwa na ngono
Kuuza bidhaa za tumbaku za kisasa ,kama bidhaa zisizo na madhara ,kutumia ladhaa tamu na kutumia mitandao ya kijamii kuuza bidhaa hizi ni mbinu ambao kampuni za kutengeneza tumbaku zinatumia kuwavutia vijana na kuwa wateja wao wa kudumu. Kampuni hizi zinafadhili pia utafiti ambao unakinzani na utafiti wa taasisi za afya kuhusu madhara ya Tumbaku.Isitoshe kampuni hizi zinazalisha bidhaa ambazo mtumiaji anaweza kutumia zaidi ya moja .
Kumeshuhudia juhudi makhsusi kutoka sekta ya Tumbaku zinazopinga sheria zinazodhibiti Tumbuka kama vile kupitia ushuri au sheria zenye adhabu kali Sekta hii pia imeonekana kurubuni serikali tofauti kwa kutoa msaada bila wao kufahamu lengo la sekta hiyo. Aidha kuna tafiti za kisayansi zinazofadhiliwa na sekta hii kukabili sayansi zinazorodhesha tumbaku na bidhaa za sigara kuwa zenye madhara makubwa ya kiafya
Ugonjwa wa Endometriosis hudhihirika msichana anapovunja ungo na huja na maumivu makali kabla ,wakati na hata baada ya hedhi Lilian Leley ameishi na maumivu hayo kwa zaidi ya miaka thelathini.Amefanya upasuaji mara mbili na anatazamiwa kwenda kwenye operesheni nyingine hivi karibuni katika kujaribu kutafuta tiba ya ugonjwa wa EndometriosisAnasimulia masaibu yake ,ambapo anasema ndani ya mwezi huenda ni mzimu tu kwa siku 10
Endometriosis hutokea wakati tishu kwenye ukuta wa tumbo la uzazi zinapopatikana katika maeneo mengine ya mwili ikiwemo mapafu ,utumbo na hata ubongo Endemotriosis huwa na dalili zinazofanana magonjwa mengine ya uzazi na unaweza kubainika kupitia kipimo cha Laparoscopy ambapo tishu hizo zinachunguzwa moja kwa moja
Bidhaa za vyakula au vinywaji zikiwa na machapisho ya kuonesha kuwa vina sukari nyingi ,chumvi nyingi au mafuta mengi mnunuzi anakuwa na fursa ya kuchagua vema Watalaam wamesema lishe ni kiungo muhimu katika kupambana na magonjwa yasiyoambukizwa ambayo yanazidi kuongezeka na kuwa mzigo kubwa kwa jamii na mifumo ya afya
Jamii nyingi bado hazielewi kuwa ugonjwa wa Vitiligo hauwezi kuambukizwa kwa kutangamana ,kugusana au hata kushiriki mlo
Vitiligo ni hali ya ngozi ambapo madoa meupe au mabaka yanaonekana. Inaweza kuathiri mtu yeyote, ikiwa ni pamoja na watoto na vijana. Sio hatari, si kama saratani ya ngozi au maambukizi unayoweeza kupata na kwa hiyo huwezi kuipata kutoka kwa mtu mwingine. Watu wengi wenye vitiligo wana afya nzuri. Baada ya muda, mabaka zaidi yanaweza kuonekana kwenye sehemu tofauti za mwili, hata kwenye nywele au ndani ya kinywa na pua. Mara nyingi huanza katika maeneo yaliyopigwa na jua. Takriban 1% ya dunia ina vitiligo
Kumekuwa na mvutano kati ya serikali ,uongozi wa kaunti za Pwani ya Kenya ,kuhusu Muguka kupigwa marufuku kwa sababu za kiafya Wakulima ,wafanyabiashara na wenyeji wa Embu wanaozalisha Muguka kwa kiasi kikubwa hata hivyo wanasema hawajapata madhara yoyoteHata hivyo watalaam wa afya wanaonya uraibu wa Muguka unaweza kudhuru afya
Mataifa ya Afrika bado yanaendelea kushuhudia kasi ya ongezeko la watu ijapokuwa chumi za Afrika hazifanyi vizuri inavyotakikana Watalaam wanaonya iwapo idadi ya watu haitodhibitiwa ,kupangiwa huenda mataifa mengi yakalemewa na idadi ya watu wanaowategemea wengineAidha kuna hatari ya sera za serikali kushindwa kukidhi mahitaji ya raia wake ,idadi inapokuwa kubwa
Mycetoma ni mojawapo ya magonjwa yaliyopuuzwa ingawa unaendelea kuwaathiri wengi haswa watu wanaokaa maeneo kavu na jamii zilizotengwa Mycetoma hujidhihirisha kama donda ambalo haliponi bali linaendelea kukua na kuchimba sehemu athirika katika mwili
Mataifa wanachama wa shirika la afya duniani ,WHO yanayokongamano katika kongamano la afya ya 77 jijini Geneva yanataka kuwepo mwongozo wa afya kukabiliana na hali ya dharura baada ya janga la COVID 19 Mataifa haya yanasisitiza kuwepo usawa kwenye kuzalisha na matumizi ya sampuli za kutengeneza sampuli zinazochangiwa na nchi mbali mbaliAidha usawa kwenye ufadhili ,usambazaji wa chanjo mpya na chanjo zinazotumika wakati wa majanga Kongamano hilo pia linatazamiwa kuja na mwafaka kuhusu marekebisho kwenye sheria za afya za mwaka 2005
Watoto na vijana walioshuhudia dhulma , kupata kiwewe,mara nyingi wanajikuta hawaamini katika uhusiano ,huwa waathiriwa wa dhulma za kimapenzi
Kumekuwa na ongezeko la idadi ya watoto na vijana wanaokabiliwa na changamoto za afya ya akili Kila mwezi Mei dunia huungana kufanya kampeni ya watu kuwa makini na afya zao za akili ili kuzuia changamoto zaidi za akili ambazo wakati mwingi huishia kwenye umauti na matatizo zaidi ya kiafyaWatalaam wa afya wanasema watoto na vijana pia nao hupatwa na changamoto hizi zinazohusishwa na afya ya akili ,matatizo hayo yakiwemo kiwewe na msongo wa mawazo.Daktari bingwa wa afya ya akili katika hospitali ya rufaa ya Kenyatta kitengo cha watoto ,Dkt Josephine Omondi anasema mazingira yanayochochea hali hii ni mizozo ya kifamilia ,matumizi mabaya ya mitandao ,shinikizo kutoka mazingira ya shule na pia matatizo ya kiafya yanayohusishwa na miaka ya awali ya mtotoMshauri Nasaha Naomi Ngugi anasema ni wakati wazazi wakakumbatia ukweli kuwa watoto na vijana huhitaji washauri nasaha na matibabu mengine ya matatizo ya afya ya akili
Idadi kubwa ya wasichana wanaopata mimbo za utotoni wapo katika nchi za Afrika kwa mujibu wa shirika la afya duniani pia UNFPA Sababu zinazochangia mimba za utotoni ni pamoja na umaskini ,dhulma za kimapenzi ,ngono biashara na tamaduni hasi
Kenya imeanza kutumia Methadone kupambana na Ukimwi baada ya Tanzania