Podcasts about fedha

  • 26PODCASTS
  • 183EPISODES
  • 26mAVG DURATION
  • 1WEEKLY EPISODE
  • Jun 18, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about fedha

Latest podcast episodes about fedha

Habari za UN
18 JUNI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 18, 2025 10:29


Hii leo jaridani tunaangazia ujumbe wa Katibu Mkuu Guterres, wa siku ya kimataifa ya kupambana na kauli za chuki na mradi wa lishe bora kwa watoto huko Kilifi Kenya. Makala tunakwenda nchini Rwanda na mashinani nchini Ghana, kulikoni?Leo Juni 18 ni siku ya kimataifa ya kupambana na kauli za chuki ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametumia ujumbe wake kwa siku hii kutoa onyo kuhusu hatari zinazoongezeka za chuki mtandaoni, hasa zikichochewa na akili mnemba au (AI) na  na majukwaa ya kidijitali.Katika Kaunti ya Kilifi, iliyoko pwani ya Kenya barani Afrika, Mpango wa Kuboresha Lishe kwa kupatia jamii Fedha na Elimu ya Afya (NICHE) unasaidia kuwaelimisha wazazi kuhusu umuhimu wa baba na mama kulea watoto wao kwa pamoja, mradi unaotekelezwa na shirika la Umoja wa MAtaifa la kuhudumia watoto, UNICEF.Katika makala shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO, kwa kushirikiana na Serikali ya Rwanda, linaendelea kujenga uwezo wa kitaifa katika kuhimiza matumizi ya mbinu rafiki kwa mazingira katika kilimo pamoja na usimamizi salama wa viuatilifu. Hili linafanyika kupitia utekelezaji wa awamu ya tatu ya mradi wa ACP MEAs 3 unaofadhiliwa na Muungano wa Ulaya EU. Mpango huu unalenga kuwawezesha wakulima wadogo kuhamia kwenye mifumo ya kilimo endelevu kimazingira na kuwajengea uwezo wa utekelezaji wa mikataba ya kimataifa ya mazingira.Na katika mashinani leo ikiwa ni siku ya kimataifa Sayansi ya Mapishi au Gastronomia,  fursa ni yake Mpishi Mkuu mashuhuri Fatmata Binta kutoka Sierra Leone, ambaye kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO, ya kipindi kiitwacho Mazungumzo ya Jikoni , anapazia sauti matumizi ya vyakula vya kiasili kama njia ya kuepuka kusahaulika kwa vyakula vya kiasili ili hatimaye kuweko na lishe endelevu.Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!

Habari za UN
Ujumuishaji wazazi wa kiume kwenye malezi ya watoto waleta manufaa kwa jamii

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 18, 2025 2:12


Katika Kaunti ya Kilifi, iliyoko pwani ya Kenya barani Afrika,  Mpango wa Kuboresha Lishe kwa kupatia jamii Fedha na Elimu ya Afya (NICHE) unasaidia kuwaelimisha wazazi kuhusu umuhimu wa baba na mama kulea watoto wao kwa pamoja, mradi unaotekelezwa na shirika la Umoja wa MAtaifa la kuhudumia watoto, UNICEF. Assumpta Massoi anamulika moja ya familia zilizonufaika.

Mwalimu Huruma Gadi
S1405. Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later May 22, 2025 131:52


S1405. Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu

Mwalimu Huruma Gadi
S1404. Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later May 8, 2025 110:39


S1404. Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu

Mwalimu Huruma Gadi
S1403. Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later May 5, 2025 108:52


Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu

Mwalimu Huruma Gadi
S1402. Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later May 1, 2025 132:09


Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu

Mwalimu Huruma Gadi
S1402B. Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu.mp3

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later May 1, 2025 116:33


Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu

Mwalimu Huruma Gadi
S1401. Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later Apr 23, 2025 111:55


Kanuni 5 Zinazofungua Milango ya Fedha Katika Ufalme wa Mungu.mp3

Habari za UN
Uhaba wa fedha watishia ukarimu wa Zambia kwa wakimbizi - UNHCR

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 16, 2025 2:05


Zambia inaendelea kuwahifadhi zaidi ya wakimbizi 106,000, wengi wao wakiwa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Burundi, pamoja na wakimbizi wa zamani kutoka Rwanda na Angola, kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, ambalo limesema kwa kuzingatia sera yake jumuishi, nchi hiyo inakuza mshikamano na wakimbizi na kuwawezesha kujitegemea kupitia makazi maalum na ushirikiano na jamii za wenyeji. Flora Nducha na taarifa zaidi  Shirika hilo la wakimbizi limesema katika makazi kama Mayukwayukwa na Maheba ambayo ni moja ya kambi kubwa zaidi ya wakimbizi nchini Zambia familia za wakimbizi zilizolazimika kukimbia makwao zinajumuishwa ili ziweze kujikimu na kuishi kwa utangamano na wenyeji wanaowahifadhi. Moulid Hujale, ni afisa habari msaidizi wa UNHCR anasema “Selikali ya Zambia inajumuisha wakimbizi katika huduma za kitaifa kama vile elimu na hata programu za msaada wa kilimo  ili kuongeza uzalishaji” Amebainisha kuwa kwa kufanya hivyo Zambia imeonesha mshikamano wa dhati kwa jamii hizo za wakimbizi kwa kuhakikisha kuwa wanapata fursa ya kujenga upya maisha yao, kujikwamua kiuchumi na kuishi kwa heshima.Hata hivyo, UNHCR inasema nchi hiyo ya Kusini mwa Afrika pamoja na ukarimu wake bado inakumbwa na athari za ukame mkali uliotishia uhakika wa chakula na kuyumbisha uchumi na katika hatua za kukabiliana na hali hiyo, Moulid ansema  “UNHCR inashirikiana na serikali ya Zambia kuunganisha makazi ya wakimbizi kwenye gridi ya taifa ya umeme. Tunajua muundo huu wa ujumuishwaji na maisha endelevu vinagharimu fedha, Lakini hiki ndicho hasa wakimbizi wanachokihitaji, hivyo tunahitaji msaada wako ili kufanikisha hili”. Licha ya mafanikio yaliyopatikana hadi sasa Zambia katika kuwakirimu wakimbizi,  UNHCR imeonya kuwa uhaba wa fedha inaokabiliwa nao  unatishia kuathiri mafanikio hayo na hasa utoaji wa huduma muhimu kwa familia hizo zilizolazimika kufungasha virago na kusaka usalama Zambia. Sasa limetoa ombi la msaada wa haraka wa kimataifa ili kuendelea kufanikisha huduma za kuokoa maisha zinazohitajika sana na wakimbizi hao.

Mwalimu Huruma Gadi
S1306. Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later Apr 15, 2025 176:38


Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi

Mwalimu Huruma Gadi
S1307. Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi.mp3

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later Apr 15, 2025 186:39


S1307. Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi.mp3

Mwalimu Huruma Gadi
S1305. Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later Apr 15, 2025 146:14


Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi

Mwalimu Huruma Gadi
S1304. Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later Apr 15, 2025 152:17


Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi

Mwalimu Huruma Gadi
S1303. Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later Apr 15, 2025 136:58


Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi

Mwalimu Huruma Gadi
S1302. Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later Apr 15, 2025 172:44


Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi

Mwalimu Huruma Gadi
S1301. Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi.mp3

Mwalimu Huruma Gadi

Play Episode Listen Later Apr 15, 2025 147:21


Nguvu ya Agano jipya Katika Fedha na Uchumi

Habari za UN
Viongozi wababe, wa kiimla na wenye fedha wanasigina haki za binadamu duniani

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 3, 2025 2:57


Kwenye kikao cha 58 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kinachoendellea mjini Geneva Uswisi, Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa M ataifa, Volker Türk , amezungumzia hali ya kuzorota na kutoeleweka inayohusu haki za binadamu duniani kote akielezea wasiwasi mkubwa kuhusu kudhoofika kwa makubaliano ya kimataifa kuhusu haki za binadamu,na kuonya kwamba ushawishi wa viongozi wa kiimla, matajiri wakubwa, na viongozi wa kimabavu unatishia kuvuruga maendeleo ya miongo kadhaa. Anold Kakayanda na taarifa kamili.Asante Flora katika taarifa yake Türk  amesisitiza umuhimu wa kuhifadhi haki za binadamu na utawala wa sheria ili kuzuia kurudiwa kwa ukatili wa zamani.Moja ya masuala ya dharura yaliyotiliwa mkazo na Türk  ni mgogoro wa kibinadamu unhaoendelea huko Gaza. Amelaani uharibifu uliosababishwa na hatua za kijeshi za Israeli dhidi ya mashambulizi ya Oktoba 7, 2023 yaliyofanywa na Hamas na makundi mengine ya wapiganaji wa Kipalestina.Türk  amesisitiza haja ya kudumisha usitishaji mapiganona kutoa wito wa mchakato wa amani unaozingatia haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na haki ya kujitawala na uwajibikaji. Ametaka kuachiliwa kwa mateka, kukomeshwa kwa vizuizi vya kiholela, na kuanza tena kwa msaada wa kibinadamu mara moja ndani ya Gaza.Kuhujsu mgogoro unaoendelea nchini Ukraine amersema bado ni suala la kutia wasiwasi, huku raia wakiishi kwa hofu ya mara kwa mara kutokana na mashambulizi yasiyokoma.Türk  amekemea vikali vikwazo vya Shirikisho la Urusi juu ya haki za msingi katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu na kuelezea masikitiko yake kuhusu ripoti za mauaji ya kiholela na mateso ya kimfumo ya wafungwa wa vita wa Kiukraine.Almeihimiza jumuiya ya kimataifa kufanya kazi kuelekea amani endelevu inayoheshimu haki na matarajio ya watu wa Ukraine.Türk  pia ameelekeza mawazo kwenye maeneo mengine yenye migogoro, ikiwa ni pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, Myanmar, Haiti, na Sudan.Alielezea jinsi watawala wa kiimla, wanasiasa wahubiri wa chuki, na walanguzi wanavyotumia machafuko kwa faida zao binafsi.Amesema Athari za migogoro huenea zaidi ya mstari wa mbele, zikiathiri minyororo ya usambazaji duniani na nafasi za kidijitali.Ametoa  wito kwa watu binafsi kutambua jukumu lao la pamoja kwa kufanya maamuzi ya kimaadili ya ununuzi, kushiriki kisiasa, na kuunga mkono uwajibikaji kwa ukiukwaji wa haki za binadamu.Hata hivyo amesema demokrasia zilizoimarika haziko salama dhidi ya kudorora kwa haki za binadamu. Türk  ameelezea wasiwasi mkubwa kuhusu mwelekeo nchini Marekani, ambako maendeleo kuhusu usawa wa kijinsia na sera za kupinga ubaguzi yanarudi nyuma.Pia amekosoa Shirikisho la Urusi kwa ukandamizaji wake wa jamii za kiraia na vyombo vya habari huru, ambapo wapinzani wanakabiliwa na unyanyasaji, kukamatwa, au kufurushwa.Kudhoofika kwa haki za binadamu katika mataifa yenye nguvu, Türk  alionya kwamba kunaweka mfano hatari kwa ulimwengu mzima, akisisitiza hitaji la dharura la mshikamano wa kimataifa na uwajibikaji kuhusu haki za binadamu.

Gurudumu la Uchumi
Sehemu ya II: Umuhimu wa kuwa na nidhamu ya kuweka akiba ya fedha

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Jan 8, 2025 10:05


Hivi leo ni sehemu ya pili ya makala ya Gurudumu la Uchumi, hasa tunapouanza mwaka 2025 tunaenda kujadili kuhusu nidhamu ya kuweka akiba ya fedha, ufanye nini kuongeza kipato, unatumiaje fedha ulizonazo kuwekeza ? Haya ni baadhi ya mambo ambayo tutaenda kuyatazama kwenye makala ya juma hili. Tutakuwa na Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

Gurudumu la Uchumi
Sehemu ya II: Umuhimu wa kuwa na nidhamu ya kuweka akiba ya fedha

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Jan 8, 2025 10:05


Hivi leo ni sehemu ya pili ya makala ya Gurudumu la Uchumi, hasa tunapouanza mwaka 2025 tunaenda kujadili kuhusu nidhamu ya kuweka akiba ya fedha, ufanye nini kuongeza kipato, unatumiaje fedha ulizonazo kuwekeza ? Haya ni baadhi ya mambo ambayo tutaenda kuyatazama kwenye makala ya juma hili. Tutakuwa na Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

Gurudumu la Uchumi
Sehemu ya I: Kwanini ni muhimu kuwa na nidhamu ya kuweka akiba ya fedha

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Jan 1, 2025 9:44


Heri ya mwaka mpya 2025 msikilizaji wa RFI Kiswahili popote pale unapotegea sikio matangazo yetu na hasa makala ya Gurudumu la Uchumi, ni imani yetu kuwa nyote mbuheri wa afya. Makala ya Gurudumu la Uchumi, tutajadili kuhusu nidhamu ya kuweka akiba ya fedha. Kuzungumzia hili msikilizaji kwenye line ya simu nimemualika Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

Gurudumu la Uchumi
Sehemu ya I: Kwanini ni muhimu kuwa na nidhamu ya kuweka akiba ya fedha

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Jan 1, 2025 9:44


Heri ya mwaka mpya 2025 msikilizaji wa RFI Kiswahili popote pale unapotegea sikio matangazo yetu na hasa makala ya Gurudumu la Uchumi, ni imani yetu kuwa nyote mbuheri wa afya. Makala ya Gurudumu la Uchumi, tutajadili kuhusu nidhamu ya kuweka akiba ya fedha. Kuzungumzia hili msikilizaji kwenye line ya simu nimemualika Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

Gurudumu la Uchumi
Nidhamu ya matumizi ya fedha

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Dec 25, 2024 10:03


Katika makala ya hivi leo, tunajadili kuhusu umuhimu wa kuwa na nidhamu ya fedha, kwanini ipo haja ya kuwa na nidhamu ya matumizi binafsi, vipi unaweza kujipanga kwa mwaka ujao? Haya ni miongoni mwa maswali ambayo mtaalamu wetu wa uchumi na biashara Ali Mkimo anaenda kuyajibu.

Gurudumu la Uchumi
Nidhamu ya matumizi ya fedha

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Dec 25, 2024 10:03


Katika makala ya hivi leo, tunajadili kuhusu umuhimu wa kuwa na nidhamu ya fedha, kwanini ipo haja ya kuwa na nidhamu ya matumizi binafsi, vipi unaweza kujipanga kwa mwaka ujao? Haya ni miongoni mwa maswali ambayo mtaalamu wetu wa uchumi na biashara Ali Mkimo anaenda kuyajibu.

Habari za UN
Kuna mkwamo kwenye mkutano wa COP29 huku mapendekezo mapya yakitaka nchi tajiri kuzilipa masikini dola bilioni 250 kwa mwaka

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 22, 2024 2:07


Majadiliano ya mkutano wa 29 wa nchi wanachama wa mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP29 yamekumbwa na mkwamo huko Baku Azerbaijana muafaka haujapatikana. Majadiliano hayo yaliyotarajiwa kukunja jamvi leo sasa yanaendelea kwa kuwekwa mezani mapendekezo mapya kuhusu ufadhili wa mabadiliko ya tabianchi hasa kwa matifa yanayoendelea. Hakika vuta nikuvute bado inaendelea hata sasa washiriki wako mezani kwakikuna vichwa na kujadili mapendekezo mapya. Mkwamo huo umetokana na kushindwa kuafikiana katika masuala kadhaa kubwa likiwa ufadhili wa  mabadiliko ya tabianchi na hususasn kuhusu ni kiasi gani cha fedha nchi zinazoendelea zinapaswa kupokea kila mwaka hadi ifikapo mwaka 2030 na wapi fedha hizo za ufadhili zitatoka.Nchi zinazoendelea zinataka kulipwa dola trilioni 1.3 kwa mwaka lakini hilo halijaafikiwa na mapendekezo mapya yaliyowasilishwa na raia wa mkataba huo wa UNFCCC yanaonyesha tofauti kubwa na safari ndefu ya kufikia muafaka.Kwa mujibu wa mapendekezo hayo mapya yaliyowasilishwa leo mezani na Rais wa COP29 Mukhtar Babayev yanataka nchi zinazoendelea kupokea dola bilioni 250 kwa mwaka hadi kufikia mwaka 2035 kwa ajili ya kuchukua hatua didi ya mabadiliko ya tabianchi.Na maesema “Fedha hizi zitatoka katika vyanzo mbalimbali ikiwemo sekta za umma na za binafsi, na kitaifa na kimataiifa ikiwemo vyanzo mbadala”.Wakati pia COP29 ikitoa wito wa kufikia lengo la ufadhili wa dola trilioni 1.3 ifikapo mwaka 2035 pia imezikaribisha nchi zinazoendelea kutoa michango ya ziada.Kiwango kilichopendekezwa cha ufadhili kinatarajiwa kuzusha vuta ni kuvute katika majadiliano hayo kwa siku nzima ya leo huenda hadi kesho ingawa mkutano huo unahisi ahuweni kwamba kuna kiwango kilichowasilishwa na unataka hitimisho la mkutano haraka iwezekanavyo. Je nchi zinazoendelea zitapokea vipi pendekezo hili jawabu bado halijulikani. Wapenzi wa UN News Kiswahili endeleeni kufuatilia kwenye kurasa zetu kufahamu hatma ya mkutano huo.

Habari za UN
Patricia Kombo COP29: Ufadhili wa fedha utakuwa jawabu mujarabu kudhibiti mabadiliko ya tabianchi Afrika

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 13, 2024 1:51


Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP29 leo ukiingia siku ya nne  mjini Baku Azerbaijan vijana kutoka Afrika wataka ufadhili uongezwe kutoka mataifa makubwa hususan yanayochangia zaidi hewa ukaa ili kudhibiti athari za mabadiliko ya tabianchi kwa mataifa yanayoendelea ambapomiongoni mwa waathirika wakubwa ni vijana.  Asante Bosco na mmoja wa washiriki hao ni Patricial Kombo Mumbua kutoka Kenya  akiwasilisha matakwa ya vijana katika mkutano huo, na akizungumza na UN News  kuhusu ujumbe wake kwa COP29 amesema“Kwangu kama kiongozi wa vijana jambo la kwanza ni kuweza kupata zile fedha au kuzikusanya ili ziweze kusaidia mataifa ambayo yanapambana na kukabiliwa na changamoto ya mabadiliko ya tabianchi . Pili ni kuhakikisha kuwa viongozi kutoka mataifa ambayo yanazalisha zaidi hewa ukaa yanawajibika ili kuyafanya matifa ambayo yanaendelea kuweza kujilinda , kunufaika , kujiinua dhidi ya janga hilo na pia kujenga mnepo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi katika jamii zao.”Na nini anachokitarajia katika mkutano huo wa COP29?“Ni kuweza kuona kuwa hili kongamano litaweza kuhamasisha upatikanaji wa hizo hela kwa mataifa ambayo yanakabiliwa na hizi changamoto za mabadiliko ya tabianchi, Na pia wakati ambapo mataifa yanaendelea kurekebisha michango yao ya kitaifa ya mabadiliko ya tabianchi au NDCs, waweze kuleta michango ambayo inaaambatana na zile changamoto ambazo mataifa yao yanazidi kuathiirika nazo za mabadiliko ya tabianchi.”Mbali ya masuala ya ufadhil mada zingine zinazotamalaki kwenye mijadala ya leo COP29 ni masuala ya nishani safi , mifumo ya tahadhari za mapemba na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa matifa ya visiwa vidogo vinavyoendelea.

Habari za UN
07 NOVEMBA 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 7, 2024 11:21


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka huko Havana Cuba kwenye Kongamano la kimataifa la Kiswahili kusikia kutoka kwa waziziri Zanzibar kuhusu faida za kiplomasia na kiuchumi. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na ujumbe kuhusu Kiswahili.Fedha kwa ajili ya mipango ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, ni jambo lililopatiwa kipaumbele katika ripoti mpya ya leo ya shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira, UNEP wakati huu ambapo kiwango cha joto kinazidi kuongezeka kila uchao na kuleta zahma duniani kote.Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO linasema hii leo watoto 6 wa kipalestina, wamesafirishwa kutoka Gaza kwenye Romania kwa matibabu mahsusi ; watatu wakiwa wanaugua saratani, wawili magonjwa ya  damu na mmoja majeraha. Wameambatana na jumla ya waangalizi 15.Na huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO umezindua mfumo wa uthibitishaji, kama sehemu ya mchakato wa Luanda wenye lengo la kufuatilia makubaliano ya sitisho la mapigano kati ya Rwanda na DRC yaliyoanza kutekelezwa tarehe 4 mwezi Agosti mwaka huu mashariki mwa taifa hilo la Maziwa Makuu.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili tunasalia huko huko Havana Cuba, kwenye kongamano la Kiswahili la Kimataifa ambako Dkt. Kisembo Ronex Tendo mshiriki kutoka taasisi ya vijana ya Afrika Mashriki Fest Uganda anaeleza cha kufanya kusongesha Kiswahili nchini Uganda.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu! 

Jioni - Voice of America
Mawaziri wa fedha kutoka mataifa 200 ya Dunia na wadau wengine wanaanza mkutano mjini Washington huku wakikabiliwa na changamoto za vita. - Oktoba 21, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Oct 21, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Gurudumu la Uchumi
Athari za utoroshaji na utakatishaji fedha barani Afrika

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Oct 2, 2024 9:58


Tatizo la fedha haramu barani Afrika linaligharibu bara hili kiasi cha dola za Marekani bilioni 50 na bilioni 80 kila mwaka, Asilimia 44 ya utajiri wa kifedha wa Afrika inadhaniwa kuwa nje ya nchi. Kwa mujibu wa Ripoti ya Maendeleo ya Uwazi wa Ushuru barani Afrika ya 2023, nchi za Afrika zimeokoa dola bilioni 2 kwa mwaka kutokana na watu kuweka wazi mapato yao, ubora wa kubadilishana taarifa na uchunguzi wa nje ya nchi.Tumezungumza na Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

Gurudumu la Uchumi
Athari za utoroshaji na utakatishaji fedha barani Afrika

Gurudumu la Uchumi

Play Episode Listen Later Oct 2, 2024 9:58


Tatizo la fedha haramu barani Afrika linaligharibu bara hili kiasi cha dola za Marekani bilioni 50 na bilioni 80 kila mwaka, Asilimia 44 ya utajiri wa kifedha wa Afrika inadhaniwa kuwa nje ya nchi. Kwa mujibu wa Ripoti ya Maendeleo ya Uwazi wa Ushuru barani Afrika ya 2023, nchi za Afrika zimeokoa dola bilioni 2 kwa mwaka kutokana na watu kuweka wazi mapato yao, ubora wa kubadilishana taarifa na uchunguzi wa nje ya nchi.Tumezungumza na Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi na biashara akiwa Tanzania.

Habari za UN
Msaada wa fedha kutoka mashirika ya UN wamwezesha mkimbizi wa Sudan kujiwezesha kiuchumi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 26, 2024 3:09


Limiya Daud mwenye umri wa miaka 30 ni mmoja wa wakimbizi wa Sudan aliyekimbilia nchini Sudan Kusini kusaka hifadhi baada ya machafuko kuibuka nchini mwake. Kutokana na wingi wa wakimbizi wanaoingia katika nchi zilizo jirani na Sudan baadhi yao wamekuwa wakihamishwa na kupelekwa katika kambi za wakimbizi ambazo zilishaanzishwa hapo awali ili waweze kupata huduma zote muhimu.Tuungane na Evarist Mapesa akituletea simulizi ya Limiya Daud na watoto wake ambao baada ya kukimbilia nchini Sudan Kusini kusaka hifadhi alihamishiwa katika kambi ya Maban iliyoko huko Renk na msaada wa fedha alioupata kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa umemuwezesha kufungua genge.

sudan renk umoja mataifa fedha mashirika sudan kusini
Jioni - Voice of America
Mahakama ya juu Kenya yasimamisha uamuzi wa mahakama ya chini kuhusu sheria ya fedha ya mwaka 2023 - Agosti 19, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Aug 19, 2024 29:59


Mahakama ya juu Kenya yasimamisha uamuzi wa mahakama ya chini kuhusu sheria ya fedha ya mwaka 2023

Alfajiri - Voice of America
UNHCR yataka fedha zaidi ili kusaidia wakimbizi wa Sudan walio ndani na nje ya nchi. - Julai 03, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jul 3, 2024 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Alfajiri - Voice of America
Wachambuzi wanasema Rais Ruto amechukua uamuzi wa busara kwa kutosaini mswaada wa fedha - Juni 27, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jun 27, 2024 30:00


Jioni - Voice of America
Maandano yaendelea Kenya licha ya Rais Ruto kukataa kutia saini mswada wa fedha wa 2024 ulioibua utata - Juni 27, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Jun 27, 2024 29:59


Maandano yaendelea Kenya licha ya Rais Ruto kukataa kutia saini mswada wa fedha wa 2024

Alfajiri - Voice of America
Wakenya waandamana nje ya Ubalozi wa Kenya jijini Washington kupinga muswada wa fedha wa 2024 - Juni 24, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jun 24, 2024 29:59


SBS Swahili - SBS Swahili
Uhaba wa fedha wakwamisha shughuli za taasisi za Jumuiya ya Afrika Mashariki

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 14, 2024 6:39


Taasisi kadhaa za Jumuiya ya Afrika Mashariki, zimejipata katika hali ngumu baada ya bajeti zao kuathirika sana.

Jioni - Voice of America
Wafanyabiashara nchini Uganda wameandamana kupinga ongezeko la kodi na sera ya kodi isiyo ya haki katika nakala za fedha za kielektronik - Aprili 08, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Apr 8, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Alfajiri - Voice of America
Marekani yasema yawekea vikwazo mtandao mpana wa taasisi, makampuni na watu binafsi, inaosema unafadhili wanamgambo wa al-Shabaab - Machi 12, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 12, 2024 30:00


Afisi ya Wizara ya Fedha ya  Marekani inayohusika na Udhibiti wa Mali za Kigeni (OFAC), Jumatatu imeyawekea vikwazo mashirika 16 na watu binafsi, ambao inasema wanahusika katika mtandao mpana wa biashara unaozunguka Pembe ya Afrika, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Cyprus.

Jioni - Voice of America
Wizara ya fedha Marekani imewawekea vikwazo watu 16 na taasisi katika pembe ya Afrika na Mashariki ya Kati - Machi 12, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 12, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

Jioni - Voice of America
Wabunge nchini Kenya wameongeza mgao wao wa fedha katika bajeti ya mwaka 2024/2025 - Machi 06, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Mar 6, 2024 29:59


Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.

SBS Swahili - SBS Swahili
Taarifa ya Habari 4 Julai 2023

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jul 4, 2023 17:19


Waziri wa Fedha akaribisha uamuzi wa benki ya hifadhi wakuto ongeza kiwango cha riba.

Habari za UN
Huduma za fedha mtandao zamwondolea mwanafunzi adha ya kufuata fedha benki

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 24, 2023 0:03


Misri, taifa lenye watu milioni 100 hivi sasa, lakini ni asilimia 30 tu ya watu hao yani watu milioni 36.8 ndio wenye akaunti za benki. Katika zama hizo za huduma za fedha kimtandao, mashirika ya mawasiliano ya simu yanaingia ubia na benki ili kupanua wigo wa huduma hizo. Ukosefu wa huduma za fedha kimtandao zinakuwa kikwazo kwani wananchi hupoteza muda mwingi benki kusubiria malipo ambayo wangaliweza kuyapokea kupitia simu za kiganjani au rununu. Shuhuda pande zote mbili hizo ni msichana mmoja mkazi wa Cairo nchini Misri kama anavyosimulia Assumpta Massoi kwenye makala hii iliyoandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Mawasiliano duniani, ITU. 

Habari za UN
WFP inasaka fedha kuendelea kuwasaidia waathirika wa Kimbunga Mocha

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 22, 2023 0:01


Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) linasema hadi kufikia mwisho wa mwaka huu 2023 linahitaji dola za Marekani milioni 60 ili kutoa msaada wa chakula cha kuokoa maisha nchini Myanmar kwa watu milioni 2.1 walioathiriwa na majanga mengi na magumu kikiwemo kimbunga Mocha.Kwa mujibu wa WFP, kimbunga Mocha, dhoruba kali zaidi kuwahi kutokea katika Ghuba ya Bengal katika kipindi cha muongo mmoja, kimesababisha maafa kwa mamilioni ya watu walio tayari kwenye wakati mgumu, hasa nchini Myanmar. Kimbunga Mocha kimeacha uharibifu katika Jimbo la Rakhine kaskazini mwa Myanmar ambapo kaya katika vitongoji vingi na maeneo ya watu waliohama katika maeneo ya mabondeni wamepoteza akiba kubwa ya chakula na na vyanzo vingine vya kipato. Miundo muhimu kama hospitali na shule vimeharibiwa hasa katika mji mkuu wa jimbo la Rakhine, Sittwe. Mawasiliano na njia za umeme katika eneo hili la Myanmar zimevurugwa. Stephen Anderson ni Mkurugenzi wa WFP nchini Myanmar anaeleza wanachokifanya, "WFP tayari imeanza usambazaji wa haraka wa chakula kwa watu wenye mahitaji makubwa huko Rakhine na Magwe na iataongeza zaidi katika siku zijazo. Tunatumai kuwafikia angalau watu 800,0000 ambao wanachukuliwa kuwa wenye uhitaji mkubwa zaidi. Timu zetu ziko kwenye eneo kufanya kazi mchana na usiku kufanya lolote wawezalo ili kuongeza msaada ili kuwafikia wale wote wanaohitaji popote walipo.” Wakati wa mchana Mei 14 kimbunga kikali kilipiga Mynmar karibu na mpaka wa Bangladesh kwa upepo unaokadiriwa kuwa na kasi ya karibu kilomita 280 kwa saa na hivyo kukifanya kuwa moja ya vimbunga vikali zaidi kuwahi kutokea katika kipindi cha miaka kumi iliyopita kwenye ukanda huo. 

Habari za UN
UN wachukua hatua kuokoa watoto Malawi hatarini kukumbwa na utapiamlo

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 19, 2023 0:02


Takribani watoto 573,000 wenye umri wa chini ya miaka mitano nchini Malawi wako hatarini kukumbwa na utapiamlo, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto duniani,  UNICEF huku likisema linahitaji dola milioni 87.7 kukidhi mahitaji ya watu milioni 6.5 wakiwemo watoto milioni 3.3 nchini humo, ikiwa ni ombi jipya la fedha lililotolewa leo.Assumpta Massoi na taarifa kwa kina.UNICEF kupitia taarifa yake iliyotolewa jijiini Lilongwe Malawi hii leo, inasema maendeleo yaliyopatikana hivi karibuni ya kukabili utapiamlo yanayoyoma kutokana na uhaba mkubwa wa chakula ukigubikwa na matukio ya mara kwa mara ya madhara ya mabadiliko ya tabianchi, milipuko ya magonjwa yanayozuilika, ukosefu wa utulivu wa kiuchumi na ukosefu mkubwa wa ufadhili kwenye sekta za kijamii.Taarifa hiyo inasema Malawi bado inazingirwa na kiza kinene cha athari mbaya za kimbunga Fredy kilichokumba taifa hilo mwezi Machi na kuacha hadi leo hii watu 659,000 wakimbizi wa ndani wakiwemo watoto.Halikadhalika mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu bado unaendelea na tayari umesababisha vifo vya watu 1,759.UNICEF/Thoko ChikondiDalitso Dines mwenye umri wa miaka 14 in mwanafunzi wa darasa la 8 na manusura wa kimbunga Freddy. Hapa yuko darasani kwenye shule ya msingi ya Chumani huko Mulanje kusini mwa Malawi akijisomea. Hii ni tarehe 23 Machi 2023.Mwakilishi wa UNICEF nchini Malawi Gianfranco Rotigliano anasema watoto nchini Malawi wanakabiliwa na mlolongo wa majanga. Ukosefu wa uhakika wa kupata chakula ukichochewa na janga la mabadiliko ya tabianchi, mlipuko wa magonjwa na kutwama kwa uchumi duniani, vyote vinatishia maisha ya mamilioni ya watoto.Amerejelea ombi la Hatua za Kiutu kwa Watoto, HAC lililozinduliwa leo na UNICEF likionesha ongezeko la matukio ya utapiamlo miongoni mwa watoto katika kipindi cha miaka mitano iliyopita ambapo mwaka 2023 pekee watoto 62,000 wenye umri wa kati ya miezi 6 hadi miaka 5 wako hatarini kukumbwa na unyafuzi au udumavu.Ni kwa mantiki hiyo UNICEF imeongeza ombi lake kwa usaidizi Malawi kutoka zaidi ya dola milioni 52 hadi dola milioni 87 ili kukidhi mahitaji ya watu milioni 6.5 wakiwemo watoto milioni 3.3.Fedha hizo zitatumika kununua mahitaji ya vyakula vilivyo tayari kuliwa ili kutibu unyafuzi, kupata huduma za maji safi na salama, huduma za kujisafi, afya, lishe, elimu, ulinzi dhidi ya watoto na miradi ya fedha taslimu.Bwana Rotigliano amesema bila usaidizi wa kifedha, kaya maskini na za Watoto walio hatarini watasalia bila huduma za msingi na zaidi ya yote amesema pamoja na misaada hiyo ni lazima kujengea mnepo ili kupunguza madhara makubwa ya milipuko na dharura za kiutu.

Habari za UN
Mashirika wafanyia marekebisho ombi la fedha kusaidia Sudan ili kukidhi mahitaji

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 17, 2023 0:02


Mzozo nchini Sudan ukiingia mwezi wa pili, hii leo Umoja wa Mataifa na wadau wake wamefanyia marekebisho ombi la usaidizi kwa nchi hiyo na sasa linafikia dola bilioni 3 kwa ajili ya kusaidia mamilioni ya watu nchini humo na mamia ya maelfu wengine waliokimbilia nchi jirani kusaka usalama.Uzinduzi wa ombi hilo lililorekebishwa umefanywa kwa pamoja hii leo huko Geneva Uswisi na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi duniani, UNHCR. Hivi sasa jumla ya dola bilioni 2.56 zinahitajika kwa mwaka 2023, ikiwa ni nyongeza ya dola milioni 800 kutoka miezi michache iliyopita, ili kusaidia watu milioni 18 hadi mwishoni mwa mwaka huu na hivyo kufanya ombi hili kuwa ombi kubwa zaidi kuwahi kutolewa kwa Sudan. Marekebisho hayo yanazinagatia ongezeko la mahitaji lililochochewa na mapigano yanayoendelea ambapo Mkuu wa ofisi ya OCHA mjini Geneva, Ramesh Rajasingham amewaambia waandishi wa habari kuwa, “mahitaji nchini Sudan ni ya msingi na  yamesambaa kama unavyoweza kufikiria kutokana na majanga: kulindwa dhidi ya mapigano, matibabu, chakula, maji, huduma za kujisafi, malazi na huduma dhidi ya kiwewe. Tunapata pia taarifa za ongezeko la ukatili wa kingono na waathirika hawawezi kupata huduma. Watoto wako hatarini zaidi katika janga hili linalozidi kuibuka.” Akifafanua kuhusu ombi la usaidizi kwa wakimbizi waliosaka hifadhi Jamhuri ya Afrika ya Kati, Chad, Misri, Ethiopia, Sudan Kusini na wakimbizi waliorejea nyumbani kutokana na changamoto Sudan, Kamishna Msaidizi wa UNHCR akihusika na operesheni, Raouf Mazour amesema, “hii leo tunatoa ombi la takribani dola milioni 472 ili kukidhi mahitaji ya zaidi ya watu milioni 1 katika kipindi cha miezi 6 ijayo.” Mapigano yalizuka Sudan tarehe 15 mwezi Aprili mwaka huu na hadi sasa mamia ya watu Sudan wameuawa, zaidi ya 5,000 wamejeruhiwa na mamilioni wamejificha majumbani mwao bila uwezo wa kupata huduma muhimu kama vile matibabu. UNHCR na OCHA wanasema leo hii, watu milioni 25 nchini Sudan, zaidi ya nusu ya idadi ya watu Sudan wanahitaji misaada ya kibinadamu na ulinzi. 

Habari za UN
Mijadala kuhusu utengenezaji wa Katiba ya Kudumu Sudan Kusini - UNMISS

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 17, 2023 0:02


Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini (UNMISS) umefanya warsha za majadiliano katika mji wa Torit na Magwi mashariki mwa mji mkuu Juba jimboni Equatorial Mashariki ili kujadili kuhusu utungaji katiba na michakato ya uchaguzi.Sudan Kusini kwa sasa inatayarisha katiba yake ya kudumu ambayo si tu ni muhimu bali pia ni sharti la kufanya uchaguzi mkuu wa nchi hiyo uliopangwa kufanyika mwakani, 2024. Makundi mbalimbali ya kijamii yaliyoshiriki katika majadiliano haya yaliyoratibiwa na UNMISS ni pamoja na wanawake, vijana, waliorejea kutoka ukimbizini, wakimbizi wa ndani, na viongozi wa kimila. Jessica Kalmas, mkimbizi aliyerejea ambaye sasa ni Msemaji wa Umoja wa Vijana, Equatoria Mashariki anasema, “Kunapaswa kuwa na uzingatiaji wanaorejea. Pia, suala la ukatili wa majumbani na kijinsia likomeshwe. Hili pia lijumuishwe kwenye katiba ya kudumu.”Masuala ambayo washiriki wameyapa uzito katika majadiliano yao ni nafasi sawa kwa wanawake katika maisha ya umma, kuhakikisha wasichana wote wana haki ya kupata elimu, na kukomesha desturi ya ndoa za kulazimishwa au za utotoni. Angel Omex, Mwanafunzi ni Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Sudan Kusini anaeleza, “Nimehudhuria huu mchakato wa kutengeneza katiba, na nina furaha kuwa sehemu yake. Na, kulingana na maoni yangu binafsi nadhani kinachopaswa kujumuishwa katika mchakato wa kutengeneza katiba ya kudumu ni suala la asilimia 35 ya jinsia. Wanawake wanatakiwa kupewa asilimia 35. Haifai kuwa kusema tu bali inapaswa kutekelezwa. Na sio tu kwamba wanaorejea kutoka ukimbizini ni muhimu sana, lakini pia wanapaswa kurejeshwa katika jamii na kusajiliwa.”Kwa pamoja, waliohudhuria walifikia mapendekezo kuhusiana na katiba ya kudumu na uchaguzi unaofuata, ikiwa ni pamoja na ushiriki wenye nguvu Zaidi wa vijana. UNMISS inashirikiana na mamlaka za serikali na Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Fedha na Mipango ili kuandaa warsha kama hizo kote Sudan Kusini.

Ricardo Miranda
Martes 18 de abril: Apple Card ahorros, iOS 17, las novedades de Twitter y Elon Musk. Noticias de tecnología, noticias de Marketing y Noticias de YouTube

Ricardo Miranda

Play Episode Listen Later Apr 18, 2023 12:30


Te comparto los links de las noticias de las que hablo: La cuenta de ahorro de la Apple Card ya está disponible iOS 17 permitirá instalar apps sin pasar por la App Store #hashtag inventor Chris Messina has signed off of Twitter. Canada's CBC is the latest major news org to step away from Twitter. Twitter etiquetará los tweets que promuevan el discurso de odio Elon Musk claims to be working on ‘TruthGPT' — a ‘maximum truth-seeking AI' Who needs a Starship launch when you can pre-order a Starship torch? Esta sería la fecha de lanzamiento del Pixel Fold, el primer móvil plegable de Google McDonald's lanza una campaña protagonizada por el Hamburglar Esta es Fedha, una presentadora de noticias muy popular que, en realidad, no existe Google va a revolucionar su buscador: esto es lo que se avecina impulsado por IA Europa inaugura su herramienta para abrir las cajas negras de los algoritmos en Internet Netflix abre una boutique erótica para promocionar su nueva serie 'Obsession' Noticias de tecnología, noticias de Marketing y Noticias de YouTube Sígueme en @popinteractivo Visita mi página web: ricardomiranda.es

Monde Numérique - Jérôme Colombain
*️⃣ L'HEBDO DU 15/04/23 : ChatGPT est-il conforme à la réglementation européenne ?

Monde Numérique - Jérôme Colombain

Play Episode Listen Later Apr 15, 2023 40:22


Cette semaine, on s'intéresse à OVH qui veut racheter Qwant, aux caméras Tesla trop indiscrètes, au Juice Hacking, à une journaliste virtuelle, à l'automatisation de ChatGPT, à la règlementation de ChatGPT en Europe, au retour de Dailymotion et à la virtualisation des réseaux télécoms. L'ACTU DE LA SEMAINE  - OVH veut racheter Qwant. Le leader français du cloud ambitionne de créer un géant français du numérique. (01:37) - Tesla : des caméras indiscrètes. Des employés de la marque américaine s'échangeaient des vidéos privées provenant des voitures de leurs clients... (03:46) - Gare au Juice Hacking, cette technique de piratage via les bornes de recharge électriques pour téléphones mobiles dans les lieux publics. (06:01) - Fedha, présentatrice virtuelle boostée. Le média Koweït News veut lancer des flash d'actualité réalisés par intelligence artificielle. (08:17) L'INNOVATION DE LA SEMAINE Auto-GPT est une version améliorée de ChatGPT capable de réaliser des projets complexes. (10:23) LES INTERVIEWS DE LA SEMAINE

Daily News Brief by TRT World

*) North Korea leader calls for expansion of war deterrence capabilities North Korean leader Kim Jong-un has called for expanding the country's war deterrence capabilities to counter what it called "frantic" aggression by the United States and South Korea. Kim's call on Tuesday comes as Pyongyang has opened the year with a flurry of weapons tests. These tests included nuclear-capable underwater drones and the launch of two intercontinental ballistic missiles. North Korea last year declared itself an "irreversible" nuclear power, effectively ending the possibility of denuclearisation talks. *) Turkish, Russian, Syrian, Iranian FMs likely to meet in May in Moscow A meeting between foreign ministers of Türkiye, Russia, Iran, and Syria is likely to be held in early May in Moscow. Turkish Foreign Minister Mevlut Cavusoglu said this in an interview on Monday. He said the aim of these talks is to revive the political process, lasting stability and peace, fight against terrorism, and guarantee Syria's border and territorial integrity. *) Five killed, at least 6 injured in Kentucky shooting attack Five people were killed and at least six others hospitalised following a shooting targeting a bank on Monday in downtown Louisville, in the US state of Kentucky. A short while after confirming the attack, police said the shooter was dead, without giving further details. It was unclear whether the death toll of five people included the shooter. The incident triggered a massive police deployment outside the Old National Bank building. *) China completes Taiwan war games aimed at 'sealing off' island China says it has "successfully completed" three days of war games around Taiwan. The three-day show of force saw it simulate targeted strikes and practise a blockade of the self-ruled island. Chinese ally Russia defended the drills, with a Kremlin spokesperson saying Beijing had a "sovereign right" to respond to what Moscow called "provocative acts". Beijing's exercises were a response to Taiwan President Tsai Ing-wen's meeting with US House Speaker Kevin McCarthy last week. *) News anchor generated with AI appears in Kuwait A Kuwaiti media outlet has unveiled a virtual news presenter generated using artificial intelligence with plans for it to read online bulletins. "Fedha" appeared on the Twitter account of the Kuwait News website on Saturday as an image of a woman, her light-coloured hair uncovered, wearing a black jacket and white T-shirt. The site is affiliated with the Kuwait Times, founded in 1961 as the Gulf region's first English-language daily.

Habari za UN
Asante ILO: Kutoka kutumikishwa kitumwa hadi mfanyabiashara ajitegemea

Habari za UN

Play Episode Listen Later Apr 10, 2023 0:02


Nchini Nepal mradi wa BRIDGE unaotekelezwa na shirika la  Umoja wa Mataifa la kazi duniani, ILO umewezesha familia moja ya kimaskini kuondokana na sio tu kutumikishwa kwenye ajira za kitumwa bali pia kuepusha baba wa familia kuondokana na kwenda nchi za nje kusaka vibarua.Tuko wilaya ya Bajura magharibi mwa Nepal barani Asia, tunakutana na Shanti Devi Lohar, mama wa familia mwenye  umri wa miaka 50. Akifungua redio kujiburudisha akiwa anauza mboga mboga na maboga huku akikumbuka maisha yalivyokuwa awali.Shanti anasema mume wangu amekwenda India kusaka kibarua kutokana na hali mbaya ya kifedha ya familia yetu. Peke yangu nyumbani ilikuwa vigumu kupata kazi. Fedha ilikuwa changamoto kwani hatukuwa na ardhi.Punde anapata mteja na anauza boga moja kwa dola tatu. Msingi wa biashara hii ni nini?Shanti anasema “nilibaini kuwa kituo cha rasilimali watu kilikuwa kinaanzisha mafunzo ya kilimo cha mboga mboga nje ya msimu husika wa mazao hayo kwa wafanyakazi waliokuwa wanatumikishwa. Nilijiunga ili nipate mafunzo ya kilimo na niwe mfanyabiashara ninayejitegemea.”Mafunzo yalifanyika na kisha Shanti alimweleza mumewe ambaye alimtumia mtaji wa dola 343 wa kuanzisha kilimo biashara cha mboga mboga. ILO na mdau wake waliwapatia makaratasi ya nailoni ya kuezekea bustani hizo, madumu ya kumwagilia pamoja na mbegu.Faida ni dhahiri na anasema kwa kuuza viazi faida ni kati ya dola 86 hadi 129 kwa mwaka. Mapato kutokana na kuuza nyanya ni kati ya dola 258 hadi 300.”Ingawa watoto wake wa kiume wanasoma bweni na gharama ni dola 429 kwa mwaka, Shanti hana tena hofu kwani anapata fedha hizo kupitia kilimo biashara na binti zake wawili wanasoma shahada ya kwanza. Na zaidi ya yote anachofurahia Shanti ni kwamba mumewe hatokwenda tena nje ya Nepal kusaka kibarua.