Podcasts about wengi

  • 33PODCASTS
  • 93EPISODES
  • 21mAVG DURATION
  • 1MONTHLY NEW EPISODE
  • Jan 7, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about wengi

Latest podcast episodes about wengi

Habari za UN
07 JANUARI 2025

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jan 7, 2025 9:58


Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini DRC katika kambi ya wakimbizi wa ndani ya Bulengo kushuhudia jinsi Umoja wa Mataifa unavyowasaidia wanawake waathrika wa ukatili wa kingoni kuweza kujitegemea na kumudu mahitaji ya familia zao.Kwa mujibu wa takwimu zilizothibitishwa na Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa, takriban watu 5,601 waliuawa nchini Haiti mwaka 2024 kutokana na ghasia za magenge, likiwa ni ongezeko la zaidi ya mauaji 1,000 ya mwaka 2023. Katika moja ya matukio mabaya zaidi na ya kushtua mwaka jana, takriban watu 207 waliuawa mapema Desemba kwenye mauaji yaliyoratibiwa na kiongozi wa genge lenye nguvu la Wharf Jérémie katika eneo la Cité Soleil huko Port-au-Prince. Wengi wa waliouawa walikuwa wazee walioshutumiwa kusababisha kifo cha mtoto wa kiongozi huyo kwa njia ya uchawi.Leo, Umoja wa Mataifa na Serikali ya Lebanon wametoa ombi la nyongeza ya dola milioni 371.4 za kimarekani, zikilenga kutoa msaada wa kuokoa maisha ya walioathiriwa na mzozo wa hivi karibuni na janga la kibinadamu linaloendelea nchini humo.Na Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk leo ameeleza kusikitishwa sana na ongezeko kubwa la watu walionyongwa nchini Iran mwaka jana. Takriban watu 901 wameripotiwa kunyongwa katika mwaka 2024, arobaini wakiwa wamenyongwa katika wiki moja tu ya mwezi Desemba.Mashinani kupitia video ya Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi, UNFPA tunamsikia Zubaida AbouBaker, mama mkimbizi wa ndani katika kambi ya Tawila iliyoko Darfur Kaskazini nchini Sudan akisimulia machungu yaliyomkumba kufuatia migogoro inayoendelea nchini humo.Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!

Habari za UN
Anne Tek: COP29 isiwape kisogo wanawake wanaokabiliiwa na athari za mabadiliko ya tabianchi Afrika

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 15, 2024 1:52


Mkutano wa 29 wa Umoja wa Mataifa wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi COP29 ukianza wiki ya piili mjini Baku Azerbaijan leo, wito umetolewa kwa wanawake amba oni waathirika wakubwa wa janga la mabadiliko ya tabianchi kutopewa kisogo. Anne Cheruto Tek ambaye amebeba bendera ya wanawake waathitika wa mabadiliko ya tabianchi kutoka Afrika ameiambia UN News anachokifanya COP29..“Sana sana kufuatilia haya madhara ya mabadiliko ya tabianchi hasa kwa wanawake na vijana barani Afrika. Sana sana utakuwa wanawake ndio wanaoshughulikia masuala ya maji, masuala ya kuni, masuala ya chakula , lakini mara nyingi kukiwa na janga la mabadiliko ya tabianchi kama ukame, mafuriko, wanawake ndio wanaangamia zaidi, kwa sababu wanawke ndio wanakuwa na jukumu la kuendesha nyumba na hivyo hawana nafasi ya kutafuta fedhha ambaz zinaweza kuwasaidia wakati wa majanga hayo.”Na kutokana na hayo anasema wanawake hukabiliwa na changamoto kubwa“Wengi hupata magonjwa , wengi huathhirika sana wakati wa majanga ikiwemo vifo, ukosefu wa fedha na pia ukatili wa kijinsia wakati wa shida za mabadiliko ya tabianchi.”Na nini ombi lake katika mkutano huo?Kuhakikisha kuwa hizi changamoto zinaangaziwa hasa kwa masuala ya fedha, kuhakikisha kuwa fedha zinawafikia wanawake vijijini , kuhakikisha kuwa wanaweza kuelewa masuala ya mabadiliko ya tabianchi  na pia waweze kuelezea hadithi zao jinsi wanavyoathirika na tunaomba hii COP kuangazia haya majanga hasa kwa wanawake, wasichana na watu wasiojiweza kama wenye ulemavu.”

Siha Njema
Ugonjwa wa Selimundu maarufu Sickle Cell unavyowaathiri wengi

Siha Njema

Play Episode Listen Later Oct 7, 2024 9:45


Habari za UN
26 AGOSTI 2024

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 26, 2024 9:43


Hii leo jaridani tunamulika kupelekwa kwa chanjo dhidi ya polio huko Gaza; mkimbizi wa Burundi aliyerejea nyumbani kutoka Tanzania ainuliwa kiuchumi; makala ni mkimbizi wa Sudan aliyeko ugenini naye awezeshwa kijasiriamali na mashinani tunabisha hodi nchini Rwanda kumulika usawa wa kijinsia kwenye michezo.Hatimaye shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linapeleka Gaza huko Mashairki ya Kati dozi milioni 1.2 za chanjo dhidi ya ugonjwa wa polio aina ya 2, wakati huu ambapo ugonjwa huo hatari umethibitishwa kuweko eneo hilo. Anold Kayanda na maelezo zaidi.Kwa wakimbizi, kurejea nyumbani ni jambo moja na kuanza upya ni jambo lingine. Wengi wao hawana chaguo lingine isipokuwa kuanza maisha yao upya. Mkoani Makamba, nchini Burundi, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) kwa kushirikiana na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) wanawawezesha waliorejea nyumbani kujijenga upya na kwa tija. Miongoni mwao ni Emelyne Kabura kama anavyosimulia Bosco CosmasKatika makala Evarist Mapesa anatuletea simulizi ya mkimbizi wa Sudan ambaye sasa anaishi Sudan Kusini. Baada ya kupitia madhila lukuki amewezeshwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa na sasa anajishughulisha na ujasiriamali.Na sasa ni mashinani  Christelle Umuhoza, Mkurugenzi wa Programu wa Rwanda katika shirika la Shooting Touch, kupitia video ya shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO nchini humo, anaeleza umuhimu wa michezo katika kuondoa vikwazo vya kijinsia.

Habari za UN
UNHCR na KOICA waleta matumaini kwa wakimbizi wanaorejea nyumbani Burundi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Aug 26, 2024 1:56


Kwa wakimbizi, kurudi nyumbani ni jambo moja na kuanza upya ni jambo lingine. Wengi wao hawana chaguo lingine isipokuwa kuanza maisha yao upya. Mkoani Makamba, nchini Burundi, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) kwa kushirikiana na Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) wanawawezesha wakimbizi kujenga upya na kuanza maisha yenye tija. Mmoja wa wakimbizi hao ni KABURA Emelyne, ambaye sasa anamiliki nyumba na ni mfanyabiashara. Bosco Cosmas anatupa habari kamili…Tangu mwaka 2017, takriban wakimbizi 250,000 wa Burundi wamepewa msaada wa kurejea nyumbani kutoka nchi jirani ya Tanzania. Wengi kama Emelyne hawakuwa na chaguo jingine ila kuanza maisha upya. Lakini kwa ufadhili wa  (UNHCR) kwa ushirikiano na  (KOICA) sasa wanaishi kwa tija.Emelyne anasema, “nilifurahi sana kuvuka mpaka wa Manyovu na kurejea nchini mwangu Burundi. Ninapoona  maendeleo mapya na miji inayostawi, najihisi nimeridhika. Nilikimbilia  Tanzania mwaka 2015 na nikarejea mwaka 2021.”Sasa Emelyne ameanza kujishughulisha na kilimo na kuuza mihogo, kutengeneza mafuta ya mawese, na kufuga sungura kwa ajili ya nyama na mbolea. “Najisikia furaha ninapowalisha sungura wangu kwa sababu wananiwezesha kupata mbolea. Nashukuru kwamba kupitia mauzo ya sungura nilikodi kipande cha ardhi kwa ajili ya kulima na nikapata fedha za kuanzisha biashara yangu ya mihogo na mafuta ya mawese.”Msaada kutoka Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) unawawezesha waliorejea kujenga upya na kuanza maisha mapya. Kwa mujibu wa Emelyne, "UNHCR walitukaribisha na kutusaidia. Kwa msaada wa kifedha tuliopewa, tulinunua ardhi hii, tukatengeneza matofali na kujenga kuta za nyumba yetu. Kisha tukapokea mabati, nguzo, madirisha, na milango ili kukamilisha nyumba. Kama ningalikuwa bado kwenye kambi, nisingeweza kupiga hatua kubwa kiasi hiki.”

SBS Swahili - SBS Swahili
Jeff "unaweza dhani ume mdhuru mtu mmoja tu, kumbe ume waathiri wengi zaidi"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Aug 2, 2024 5:21


Hadithi halisi za wahanga wa mauaji ya 1994 nchini Rwanda, zime zinduliwa katika jumba la sanaa mjini.

Alfajiri - Voice of America
Trump aahidi akichaguliwa atarejesha marufuku ya kusafiri kwa baadhi ya nchi zenye waislamu wengi - Mei 03, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later May 3, 2024 30:00


Trump aahidi akichaguliwa atarejesha marufuku ya kusafiri kwa baadhi ya nchi zenye waislamu wengi

SBS Swahili - SBS Swahili
Nicky "kupitia Taunet Nelel vijana wengi wame anza kujijenga kimaisha"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 19, 2024 12:17


Wakenya wanao ishi Australia watajumuika katika jiji la Dandenong jimboni Victoria, kuhudhuria hafla la shirika la Taunet Nelel.

Siha Njema
Watu wengi wanajikuta na magonjwa ya figo na ini,watoto wengi Sudan wakiaga

Siha Njema

Play Episode Listen Later Apr 17, 2024 10:09


Kuna ongezeko la magonjwa ya figo na ini kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO inabashiri kuwa ongezeko hilo litakuwa juu zaidi kufikia mwaka 2030 ,hali hii ikichangiwa na hali ya maisha haswa ya raia katika nchi zinazoendeleaUgonjwa wa ini maarufu Hepatitis pia ni tishio kubwa haswa kwa raia wa Afrika ambayo inachangia asilimia 63 ya visa vya HepatatisNchini Sudan watoto wengi haswa walio chini ya umri wa miaka mitano wanazidi kupoteza maisha kutokana na utapiamlo unaohusishwa na ukosefu msaada  wa kibinadaam wakati huu vita vikiendelea kurindima

Sepetuko
Mgogoro wa Madaktari Unahatarisha Maisha ya Wengi

Sepetuko

Play Episode Listen Later Apr 17, 2024 4:18


Mgomo wa madaktari umetimiza sasa siku 35, naam majuma matano. Hakuna mwafaka wowote wa aina yoyote, na mwananchi anayetegemea huduma za afya katika hospitali za umma ndiye anaumia. Nani atamjali raia huyu?

SBS Swahili - SBS Swahili
Polisi wamtambua mshambuliaji katika mauaji ya watu wengi ambako watu sita walifariki

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Apr 15, 2024 7:58


Jeshi la polisi la New South Wales lime anza uchunguzi kwa shambulizi la kisu, lililo wauwa watu sita ndani ya soko kubwa katika vitongoji vya mashariki ya Sydney.

Meditationsszene Schweiz
Zen und Kommunikation mit Roberta Steuder

Meditationsszene Schweiz

Play Episode Listen Later Mar 1, 2024 80:28


Roberta Steuder ist Zen-Nonne, diplomierte psychologische Beraterin und systematische Aufsteller-Coach. Sie ist Co-Leiterin im Zen-Zentrum Scheunenberg in Wengi bei Büren. Zusammen mit ihrem Mann leitet sie verschiedene Kurse und Ausbildungen, darunter die einjährige Ausbildung «Ganzheitliche Kommunikation». Sie praktiziert Zen seit 1997 und ordinierte 2018 zur Nonne. Im Gespräch erzählt sie, was Religion in der Kindheit für sie bedeutete, wie sie eine Ausbildung machte und eine Familie gründete. Wie sie in einer Treuhandfirma Karriere machte und als Chief Financial Officer, HR-Verantwortliche und Berufsbildnerin tätig war. Ihre Begegnung mit Zen lenkte ihr Leben schliesslich in eine neue Richtung. Roberta blickt aber nicht nur auf ihren Weg zurück, sondern gibt im Gespräch auch ganz praktische Tipps und Hinweise. Sie erläutert, wie man mit Gedanken oder schwierigen Emotionen in der Meditation umgehen kann und wie unterschiedliche Persönlichkeitstypen verschiedene Herangehensweisen brauchen. Anhand des Aufbau des Kurses «Ganzheitliche Kommunikation» gehen wir durch die vier Felder Körper, Emotionen, Geist und Objekte im Geist. Wir sprechen über Projektionen und Projektionsmuster, über das Thema Geld und auch über die Erleuchtung. Wie in der Zen-Tradition üblich, merkt man, wie sehr Roberta im Leben steht und in die Welt wirkt. Mehr zu Roberta findest du auf ihrer Website: www.zencom.ch Inhalt 00:00:00.000 Intro 00:01:48.442 Biografie 00:02:41.642 Religion in der Kindheit 00:07:36.345 Berufswahl und Karriere 00:10:46.955 Warum Zen? 00:14:13.892 Wie funktioniert Zen und in welcher Tradition stehst du? 00:15:53.849 Umgang mit Gedanken in der Meditation 00:22:34.571 Herangehensweisen für verschiedene Persönlichkeitstypen 00:24:18.446 Reaktionen des Umfelds 00:27:00.793 Entscheid, zu ordinieren 00:29:46.104 Bedeutung der Ordination 00:33:25.019 Aufgabe des Treuhandberufs 00:34:56.072 Beschreibung des Zen Zentrums Scheunenberg 00:36:18.883 Kurs «Ganzheitliche Kommunikation» 00:41:13.471 Beschreibung Jahrestraining: Körper 00:47:50.080 Zweite Grundlage der Achtsamkeit: Emotionen 00:54:32.344 Dritter Bereich: Geist 00:56:25.806 Projektionen und Projektionsmuster 01:00:50.815 Objekte des Geistes: Vergänglichkeit, Unzulänglichkeit, Ich-Losigkeit 01:04:25.845 Thema Geld 01:07:23.885 Ziel des Kurses 01:09:25.720 Stellenwert der Erleuchtung 01:12:09.716 Wie sich Robertas Praxis verändert hat 01:14:20.250 Integration ins Leben 01:17:02.491 Umgang mit der Feinfühligkeit 01:19:06.724 Infos zu Robertas Angebot

Jioni - Voice of America
Serikali ya Tanzania yatoa sababu za upungufu wa sukari, umeme na sarafu ya dola, lakini wachambuzi na wananchi wengi hawajaridhishwa. - Februari 22, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 22, 2024 29:59


Serikali ya Tanzania yatoa sababu za upungufu wa sukari, umeme na sarafu ya dola, lakini wachambuzi na wananchi wengi hawajaridhishwa.

The Business of Open Source
Making the Critical Pivot from Closed to Open Source with Federico Wengi

The Business of Open Source

Play Episode Listen Later Jan 31, 2024 32:47


Today I'm joined by Federico Wengi, who is a Partner at SquareOne VC. In this conversation, Federico sheds light on the conversations he's had with many companies who consider making the pivot from a closed-source business strategy to an open-source strategy. Federico explains why it's so uncommon for businesses to make that pivot, and lays out the challenges businesses face when they consider taking on such a change. Federico also gives a great example of a company that did successfully complete the pivot to open source, and the choices they made that led to their success. Federico and I discuss why this is one pivot you can't take back, and also why it won't solve all your problems. Despite all that, Federico shares his optimism for the value of open source and the importance of at least considering this strategy when you need to make a change. Highlights:Intro (00:00)I introduce Federico, who is a Partner at SquareOne (00:59)Federico describes his role at SquareOne and the areas of investment they focus on (01:28)What Federico typically sees when companies move from closed source to open source (04:42)How important conversations come up about business strategy and open source versus closed source (07:40)Why many companies end up not pursuing an open-source strategy (11:17)Federico tells the story of a company he worked with that made the leap from closed source to open source (15:03)The most critical things businesses have to do in order to utilize an open-source strategy (16:23)What decisions led to success in the company Federico helped shift from closed source to open source (18:09)The psychological challenges leaders face when considering making a pivot to open source (23:54)Federico shares the advice he would give to a founder who's considering an open-source strategy (26:40)How you can connect with Federico (31:40)Links:FedericoLinkedIn: https://www.linkedin.com/in/federicowengi/Twitter: https://twitter.com/federicowengiCompany: https://squareone.vc/

VOA Express - Voice of America
Wavulana wengi nchini Uganda waacha shule kabla ya kuhitimu elimu ya msingi kulingana na wadau wa elimu - Januari 26, 2024

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 26, 2024 29:59


VOA Express - Voice of America
Michuano ya AFCON imewashangaza wengi, asema mchambuzi wa soka - Januari 25, 2024

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 25, 2024 30:00


SBS Swahili - SBS Swahili
Hezron "watu wengi wamepata makaazi, ajira na huduma nyingi kupitia Kokwet"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 5, 2023 6:24


Viongozi wa jumuiya ya Kokwet wali wa andalia wanachama wao hafla maalum, ambako walichangia vyakula, walifanya maonesho ya mitindo nakumaliza sherehe kwa miziki ya asili yao.

Alfajiri - Voice of America
Hospitali kuu za Gaza zimesitisha kazi kutokana na ukosefu wa umeme, maafisa wa afya wakihofia watu wengi watafariki kwa ukosefu wa huduma - Novemba 13, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 13, 2023 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Siha Njema
Shirika la madaktari wasio na mpaka lataka wanawake waliodhulumiwa kingono kupata msaada zaidi ya matibabu

Siha Njema

Play Episode Listen Later Oct 10, 2023 9:56


Wanawake wakimbizi jijini Goma waliokimbia vita wameathirika afya ya akili na mwili na wanahitaji msaada hata baada ya kupata matibabu.Wengi wamebakwa zaidi ya mara moja wakienda kutafuta chakula na mahitaji mengine

Habari RFI-Ki
Wanawake wachukuwa majukumu muhimu katika familia

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Oct 4, 2023 9:39


Utafiti wa hivi punde nchini Kenya, umeonesha kuwa idadi kubwa ya wanawake wamechukuwa majukumu ya wanaume nyumbani, hasa katika maeneo ya mijini.  Wengi wakionekana kusimamia majukumu muhimu kwa familia Je unakubaliana na utafiti huu kwamba wanaume wameacha kuteleza majukumu yao kwa jamii?  Haya hapa baadhi ya maoni yako.

Habari RFI-Ki
Wanawake wachukuwa majukumu muhimu katika familia

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Oct 4, 2023 9:39


Utafiti wa hivi punde nchini Kenya, umeonesha kuwa idadi kubwa ya wanawake wamechukuwa majukumu ya wanaume nyumbani, hasa katika maeneo ya mijini.  Wengi wakionekana kusimamia majukumu muhimu kwa familia Je unakubaliana na utafiti huu kwamba wanaume wameacha kuteleza majukumu yao kwa jamii?  Haya hapa baadhi ya maoni yako.

Habari RFI-Ki
Vijana wengi wa Afrika wahatarisha maisha yao kwa kujaribu kwenda Ulaya

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Sep 28, 2023 9:59


Habari RFI-Ki
Vijana wengi wa Afrika wahatarisha maisha yao kwa kujaribu kwenda Ulaya

Habari RFI-Ki

Play Episode Listen Later Sep 28, 2023 9:59


SBS Swahili - SBS Swahili
Justin "Covid ilisaidia watu wengi kujitambulisha katika jamii yawakenya Victoria"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Aug 17, 2023 11:32


Ni kawaida kwa wahamiaji na watu walio wasili Australia kama wakimbizi, kujiunga na vikundi vya jumuiya za asili yao.

SBS Swahili - SBS Swahili
Isaac "Viongozi wengi wa Afrika wanachaguliwa na mataifa ya Magharibi"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jul 6, 2023 11:46


Wanachama wa Jumuiya ya DR Congo wanao ishi mjini Sydney, walijumuika katika hafla maalum yaku adhimisha miaka 63 ya uhuru wa nchi yao pendwa.

Alfajiri - Voice of America
Uamuzi wa Mahakama ya juu Marekani kupuuza mpango wa Rais Biden wa kutoa msamaha kwa wanafunzi wenye mikopo katika vyuo utawaumiza wengi - Julai 03, 2023

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Jul 3, 2023 29:59


Matangazo ya nusu saa kuhusu habari za mapema asubuhi pamoja na habari za michezo.

Siha Njema
Juhudi za kupunguza gharama katika matibabu ya macho

Siha Njema

Play Episode Listen Later Jun 16, 2023 9:57


Raia wengi nchini Kenya wana uhitaji wa miwani kutokana na matatizo ya macho.Wengi wao hata hivyo hawapati miwani kutokana na gharama ya juu Katika makala haya tunaangazia mchango wa kampuni ya Mamy Eye Wear kupunguza gharama ya miwani huku ikizingatia ubora.

Habari za UN
IOM yaeleza ilivyo hatari kuvuka eneo la msitu wa Darién

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 19, 2023 0:03


Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji (IOM) linaongeza juhudi za msaada wa kibinadamu kwenye mipaka ya Colombia, Costa Rica na Panama ili kusaidia wahamiaji wanaovuka kuelekea eneo la kaskazini mwa Amerika hasa kupitia msitu hatari wa Darien unaounganisha Amerika kusini na kaskazini.  Kwa miaka mingi, jimbo la Darien nchini Panama limekuwa kituo cha kawaida cha kupita kwa wahamiaji wanaotoka kusini mwa Amerika kuelekea kaskazini. Takwimu za hivi karibuni za mwaka huu 2023 zinazidi kwa kiasi kikubwa idadi ya juu ya mwaka 2022, wakati watu 258,000 walivuka mwaka mzima. Kwa mujibu wa Mradi wa Wahamiaji Wasiofahamika waliko, wahamiaji wengi hawana vifaa vya kutosha vinavyofaa kwa safari ya siku mbili hadi kumi na karibu wahamiaji 137 walifariki dunia au kutoweka mwaka jana 2022. Luz Santo ni Afisa Mratibu wa IOM akiwa tu punde amewapokea wahamiaji waliovuka mto Chucunaque anasema, “Katika kituo hiki, tunapokea takriban watu 700 hadi 1,000 kila siku, na tunawapa taarifa za msingi kuhusu huduma zinazopatikana kwa ajili yao katika kituo cha mapokezi cha uhamiaji cha Lajas Blancas, na pia taarifa kuhusu njia." Wakati wa safari ndefu msituni, watoto na familia hukabiliwa na aina nyingi za unyanyasaji, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kijinsia, unyonyaji, pamoja na ukosefu wa maji salama na chakula, mashambulizi ya wanyama mwitu, na mito inayofurika. Robo tatu ya watu wamejeruhiwa wakiwa safarini, na theluthi moja wamekumbana na aina fulani ya kutendewa vibaya au unyanyasaji, hasa wakati wa kuvuka msitu huo wa Darien, IOM inaeleza. © UNICEF/Eduard SerraMiongoni mwa wahamiaji wapya waliowasili ni Luisa Maria Laya, mama raia wa Venezuela anayesafiri na watoto wake wawili na mumewe. Waliuza kila kitu walichokuwa nacho ili kumudu chakula na sehemu ya njia yako kutoka Venezuela walikuwa wanatumia usafiri wa kuomba msaada njiani. Matumaini yao ni kujiunga na familia ambayo tayari inaishi Marekani, “Tulipoanza safari yetu msituni, ilikuwa ngumu kwa sababu mimi, mume wangu na watoto wangu hatukuwa tumeizoea. Ilikuwa ngumu, kali, na hatari kwa maisha yetu. Namshukuru Mungu tumefika salama. Muhimu ni kwamba tulifika hai kwa sababu watu wengi huko wanadhani ni mchezo. Si mchezo, kinachoendelea si mchezo kujitosa kwenye msitu huo. Ni kitu hatari, hatari. Unahatarisha maisha ya watoto wako na yako mwenyewe.” Wahamiaji wa zaidi ya mataifa 40 wamevuka eneo la Darién mwaka huu. IOM inaeleza kwamba watu hao wanatoka katika mataifa ya Amerika, Asia na Afrika, kama vile Venezuela, Haiti, Ecuador, China, India, Afghanistan, Cameroon, na Somalia. Wengi wao wanatoka Venezuela lakini pia kumekuwa na ongezeko la idadi ya wahamiaji wa Haiti, Ecuador, na Wachina.  

Habari za UN
Watu wanaoikimbia Sudan kuingia Sudan Kusini waendelea kupata msaada wa kibinadamu: WFP

Habari za UN

Play Episode Listen Later May 5, 2023 0:02


Maelfu ya watu wamevuka na kuingia Sudan Kusini wakikimbia mzozo unaoendelea nchini Sudan. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) liko linawasaidia wanaowasili lakini mzigo huu wa ziada unaweka shinikizo katika shughuli za shirika hilo ambazo tayari ziko katika hali mbaya ya ufadhili.Video iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) inatupeleka katika Kaunti ya Renk iliyoko kaskazinimashariki mwa nchi ya Sudan Kusini inakopakana na Sudan.  Hapa ni kila mtu anajaribu kukumbatia kile alichofanikiwa kutoroka nacho akikwepa mabaya ambayo yangemkumba ikiwa angesalia Sudan ambako tangu tarehe 15 mwezi jana Aprili kunafukuta mapigano makali. Wanaobahatika wanabebwa na magari ya Umoja wa Mataifa, wengine punda na wengine wametembea mwendo mrefu kufika hapa.  Kwa mujibu wa WFP, zaidi ya watu 30,000 hadi sasa wamevuka mpaka kutoka Sudan na kuingia Sudan Kusini. Wengi wao ni waliorejea kwani walikimbia madhila hapa Sudan Kusini lakini nako ugenini Sudan kumechafuka, wamerejea.  Naimat Khamis, ni mmoja wa waliorejea anasema, "Tulilazimika kuja hapa kwa sababu ya mapigano ya Khartoum…tulilazimika kukimbia haraka iwezekanavyo kwa sababu ya vita…ilikuwa safari ngumu…tunataka kubaki na jamaa zetu hapa kwa sababu tumeteseka sana.” Hassan Abdallaziz, kijana mwenye umri wa miaka 17 huyu yeye ni raia wa Sudan kwa hiyo kwa Sudan Kusini yuko ukimbizi anasema, “Hali ya nchi ilinilazimu kuja hapa. Hakuna kitu kizuri kilichobaki nchini, hakuna kazi, ni machafuko. Mtu yeyote anaweza kupora mali yako, ni kama msitu." WFP tayari inawasaidia waliowasili na wanaowasili ikiwa ni pamoja na kuwapa chakula, kuwapima watoto, wajawazito na wanaonyonyesha, lakini mzigo huu wa ziada unaongeza chumvi kwenye kidonda. Mary-Ellen McGroarty ni Mkurugenzi wa WFP nchini Sudan Kusini akiwa mjini Juba anasema,  "Mgogoro huu umekuja katika wakati mbaya zaidi. Unajua nchini Sudan Kusini tunaingia katika msimu wa muambo na msimu wa mvua. Tayari tuna watu milioni 7.4 wanaohitaji msaada wa chakula. Hatuwezi kuwafikia wote kwa sababu ya changamoto za rasilimali. Tumelazimika kupunguza programu zetu kwa sababu ya vikwazo vikali vya ufadhili. Na sasa tena tunalazimika kuweka vipaumbele upya kati ya watu wenye njaa, hawa wapya wanaowasili, ambao wako hatarini sana.”  

Habari za UN
UNICEF: Watoto milioni 10 Sahel ya Kati hatarini, huku ukosefu wa usalama ukitishia janga kusambaa nchi jirani.

Habari za UN

Play Episode Listen Later Mar 17, 2023 0:03


Watoto milioni 10 nchini Burkina Faso, Mali na Niger wana uhitaji mkubwa wa misaada ya kibinadamu, idadi ambayo ni maradufu ikilinganishwa na mwaka 2020, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto duniani, UNICEF hii leo, chanzo kikiwa ni mizozo inayoshamiri kila uchao na kwamba Watoto wengine million 4 nchi Jirani wako hatarini Zaidi kwani mapigano kati ya makundi yaliyojihami na majeshi ya serikali yanavuka mipaka.Tuko Benin na sauti ni ya Abasse, Dahani, mtoto mkimbizi mwenye umri wa miaka 8 kutoka Burkina Faso anasema tulikuja hapa Tanguieta Benin kwa mguu. Tulikimbia nyumbani kwa sababu tulifukuzwa.Abasse anawakilisha mamilioni ya watoto wanaokimbia makwao ukanda wa Sahel kwani Mkurugenzi wa UNICEF  kanda ya Afrika Magharibi na Kati Marie – Pierre Poirier anasema “watoto wanazidi kukumbwa kwenye mapigano kama waathirika wa mapigano au walengwa kutoka vikundi vilivyojihami ambavyo si vya kiserikali.”Afisa huyo anatolea mfano Burkina Faso akisema watoto waliothibitishwa kuuawa katika miezi tisa ya mwanzo yam waka 2022 walikuwa mara tatu zaidi kuliko mwaka 2021.Wengi wa watoto hao walikufa kutokanana majerara ya risasi, vijiji vyao kushambuliwa au kulipuka kwa vilipuzi vya kutengeneza au masalia ya mabomu yatumikayo vitani. Bi. Poirier amesema mwaka 2022 ulikuwa wa kikatili Zaidi kwa Watoto Sahel ya Kati na hivyo pande zote kwenye mzozo lazima zikomeshe mashambulizi kwa Watoto, shule zao, vituo vya afya na makazi yao.UNICEF inasema mapigano yanazidi kuwa ya kikatili ambapo baadhi ya vikundi vilivyojihami vinaendesha operesheni zao katika maeneo ya Mali, Burkina Faso na Niger ambako wanatumia mbinu kama vile kuweka vizuizi mijini na vijijini na hata kuharibu mitandao yam aji.Kama hiyo haitoshi, UNICEF inasema kutokana na mashabulizi hayo zaidi ya watu 20,000 kwenye maeneo ya mpaka baina ya Burkina Faso, Mali na Niger watakuwa na kiwango cha kutisha cha ukosefu wa chakula ifikapo mwezi Juni mwaka huu.Vikundi vilivyojihami ambavyo vinapinga elimu inayotolewa na serikali vinatia moto majengo ya shule na kupora mali, vinaweka vitisho, vinateka nyara au kuua walimu.Zaidi ya shule 8,300 zimefungwa katika shule zote kwa sababu zilishambuliwa moja kwa moja na walimu kukimbia au kwa sababu wazazi walikimbia au wanahofia kupeleka watoto wao shuleni.Sasa Abasse na familia yake wako Benin na akiwa darasani akiandika anasema “kwa kuwa sasa naenda shuleni, nimepata marafiki. Napenda kifaransa, nazungumza kidogo. Na mwalimu wangu ni mzuri.”UNICEF inasema janga la Sahel ya Kati bado halijapata ufadhili wa kutosha kuweza kufanikisha operesheni zake kwani mwaka 2022 ilipokea theluthi moja tu ya dol amilioni 391 na kwamba mwaka huu imeomba dola milioni 473 kufanikisha operesheni za kiutu Sahel ya Kati na nchi Jirani. TAGS: Usaidizi wa kibinadamuAdditional: Usaidizi wa kibinadamuNews: Sahel ya KatiRegion: AfrikaUN/Tags: UNICEF

Habari za UN
Kulima tunalima lakini lishe bado ni changamoto tuchukue hatua- Mkulima Sarah

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 22, 2023 0:04


Jamii ya mikunde! Wengi wanaitambua zaidi kama ni kunde zenyewe, na maharagwe lakini ni zaidi ya hiyo. Kuna choroko, mbaazi, dengu, njegere na kadha wa kadha ambapo kutokana na umuhimu wake katika lishe ya binadamu, kurutubisha udongo na pia kuhimili mabadiliko ya tabianchi, ndio maana Umoja wa Mataifa unapigia chepuo.Mathalani nchini Tanzania, shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo, FAO linafadhili mradi wa AgriConnect ambao pamoja na mambo mengine  unapatia wananchi, wake kwa waume stadi za mapishi sahihi ya jamii ya mikunde.Hivi karibuni wakati wa siku ya mikunde duniani tarehe 10 mwezi huu wa Februari, FAO ilishindanisha washiriki wa mradi huo kufahamu ni nani bingwa zaidi wa mapishi ya mikunde kwa kutambua kuwa Tanzania ni mmoja wa wazalishaji wakubwa wa mikunde lakini ulaji wake bado unachangamoto. Sasa makala hii inamulika harakati za kuchagiza ulaji wa mikunde pamoja na majani yake na mwenyeji wetu ni John Kabambala wa redio washirika Kids Time FM ya Morogoro, Tanzania. Kwako John! 

Habari za UN
Tetemeko la ardhi limevunja si tu majengo ya Syria bali pia matumaini yao - UNFPA

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 15, 2023 0:04


Mkuu wa kanda ya nchi za kiarabu katika shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya watu duniani, na afya ya uzazi, UNFP Leila Baker amesema pamoja na shirika hilo kuhitaji fedha ili kuweza kuwahudumia wanawake na wasichana waliathiriwa na matetemeko nchini Turkiye na Syria lakini kila sehemu anapopita nchini Syria wanawake hutoa ombi moja tu nalo ni kuhitaji amani.Ni Leila Baker huyo, mkuu wa UNFPA katika kanda ya nchi za kiarabu katika mahojiano maalum na Idhaa ya Umoja wa Mataifa akieleza kwa siku nzima amekuwa katika mji wa Aleppo nchini Syria akizunguka kutembelea kliniki zilizoanzishwa na shirika hilo linalohusika na afya ya uzazi na kuzungumza na kila anayehusika katika kukabiliana na dharura iliyoletwa na matetemeko ya ardhi.Bi. Baker anasema ni vigumu sana kwake kueleza kwa sentensi moja au kuchora taswira ya madhila waliyomo wananchi wa Syria kwani madhara si katika miundombinu pekee bali pia kimwili kwani watu hawa kwa takriban muongo mmoja wamekuwa wakihaha kutokana na nchi hiyo kuwa na mizozo na vita.“Kuna majengo ambayo yameanguka, mtaa mzima umebomolewa, lakini kubwa zaidi ni muunganiko wa uchovu mwingi wa watu hawa ambao wamekuwa wakipigania uwepo wao, na sasa wanahisi kwamba wakati huo huo wanaanza kurudi katika matumaini wakiona mwanga mwisho wa handani ukiangaza kuwapa matumaini, janga la asili linatokea. Tetemeko hili kubwa la ardhi limevunja matumaini yao, kama jinsi majengo yalivyobomoka wakati wa tetemeko lenyewe.”Lakini wanawake na wasichana aliokutana nao ni nini hasa wanataka?“Nitakuambia kile hasa nilichowauliza wanawake kila mahali nilipoenda. Nikawaambia, kama ningeweza kuiambia jumuiya ya kimataifa jambo moja, ungeniomba niwaambie nini? Na bila kukosea, katika kila kundi la wanawake, hata awe mtu binafsi au kikundi, ujumbe wao ulikuwa sawa. Imetosha. Tumechoka, na tunachotaka ni upatanisho. Tunataka amani. Na tunatumaini katika wakati huu wa giza nene, itakuwa wakati ambapo mioyo na akili za kila mtu ziko wazi kuwa kuna uwezekano wa amani.”Wengi wa wakimbizi wa ndani nchini Syria ni wanawake na wasichana hivyo hata kabla ya tetemeko la ardhi kulikuwa na mipango kadhaa iliyokuwa ikisimamiwa na UNFPA kwa kushirikiana na wadau wengine ili kusaidia utoaji wa huduma za afya ya uzazi na kukabiliana na unyanyasaji wakijinsia. Na sasa shirika hilo limelazimika kupanua wigo wa huduma zao kwani watu wengi kwa sasa wameweka kuweka makazi ya muda, katika misikiti, shule na bustani ambazo UNFPA imeeleza maeneo hayana vifaa kwa ajili ya wakazi wa kibinadamu kwani wanakosa maji, hawana usafi mzuri wa mazingira, umeme, na nchi hiyo kwas asa ipo katika msimu wa baridi.Nikutokana na hali hiyo ndio maana Bi.Baker amesema UNFPA imetoa ombi la usaidizi ambapo “kwa Uturuki, ni milioni 19.7. Na kwa Syria ni zaidi ya milioni 24.”Mbali na fedha hizo kutumika kwa ajili ya wanawake na wasichana ya nchi hizo mbili lakini pia zitatumika kwa ajili ya wafanyakazi wa UNFPA.“Tutaimarisha watu wetu na uratibu wetu wa kutoa misaada mashinani kwa sababu tuna wajibu wa kuwatunza watoa huduma wetu pia. Naomba usisahau kwamba hawa ni watu ambao, wao wenyewe wamepatwa na kiwewe, na bado wanafanya kazi bila kuchoka usiku kucha. Tuna wafanyakazi ambao wamelala kwenye magari yao kwa siku nane, wakizunguka tu kutoka sehemu moja hadi nyingine baada ya kumaliza kazi na pia kujitolea muda wao. Tunaimani kuwa hiyo itakuwa hatua inayofuata ya kile tunachotowa.”Mkuu huyo wa UNFPA katika kanda ya nchi za kiarabu alihitimisha mahojiano yake kwa kueleza pamoja changamoto lakini pia kuna habari njema na zakutia moyo ikiwemo wakina mama kuweza kuunganishwa na watoto pamoja na wajukuu zao ambao walipoteana baada ya kutokea kwa tetemeko.

Habari za UN
Kuwa na wanawanake na wasichana wengi katika nyanja ya sayansi ni faida kwa wote: UN

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 10, 2023 0:02


Uwepo wa idadi kubwa ya wanawake na wasichana katika sekta ya sayansi ni faida kuwa kwa sekta ya sayansi na jamii kwa ujumla amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akihimiza kuchagiza wanawake na wasicha kuingia zaidi katika sekta hiyo.Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi ambayo huadhimishwa kila mwaka Februari 11 amesima siku hii ni ya kutanabaisha hesabu rahisi kabisa kwamba “Wanawake na wasichana zaidi katika sayansi ni sawa na sayansi bora. Wanawake na wasichana huleta utofauti katika utafiti, kupanua wigo wa kundi la wataalamu wa sayansi, na kutoa mitazamo mipya kwa sayansi na teknolojia, ikinufaisha kila mtu.”Ujumbe wake umeendelea kueleza kuwa kuna ushahidi unaoongezeka kwamba upendeleo wa kijinsia katika sayansi unasababisha matokeo mabaya zaidi, kuanzia kwenye majaribio ya dawa za ambayo huchukulia mwili wa mwanamke kama wa hali isiyo ya kawaida, kutafuta kanuni zinazoendeleza upendeleo na ubaguzi. Hata hivyo Guterres ameongeza kuwa katika maeneo mengi sana duniani, upatikanaji wa elimu kwa wanawake na wasichana ni mdogo au unakataliwa kabisa.Wanawake wanapotazamia maendeleo katika taaluma za kisayansi, ukosefu wa usawa na ubaguzi unaendelea kuzuia uwezo wao. Kana kwamba hiyo haitoshi ameongeza kuwa “Wanawake ni chini ya theluthi moja ya wafanyikazi katika sekta ya sayansi, teknolojia, uhandisi, na hesabu na kidogo zaidi katika nyanja za kisasa. Mtaalamu mmoja tu kati ya watano wanaofanya kazi kwenye akili bandia ni mwanamke. Ni lazima na tunaweza kufanya juhudi zaidi kuchagiza wanasayansi wanawake na wasichana kupitia ufadhili, mafunzo kwa vitendo na program za mafunzo ambazo zinatoa jukwaa la kufanikiwa.” Katibu Mkuu amehitimisha ujumbe wake akisema kupitia mfumo maalum, vivutio vya kuwafanya wabaki, na programu za ushauri ambazo huwasaidia wanawake kushinda vikwazo vilivyopo na kujenga taaluma vitasaidia sana. Na muhimu zaidi, ameongeza ni kwa kuzsisitiza haki za wanawake na kuvunja mila potofu, upendeleo, na vizuizi vya kimuundo. Na wito wake ni kwamba “Sote tunaweza kufanya sehemu yetu kuibua talanta kubwa sana ya ulimwengu ambayo haijatumiwa tukianza na kujaza madarasa, maabara na vyumba vya bodi na wanasayansi wanawake.” 

Yesaya Software Podcast
Andika Ujumbe wa Msaaada Utakaojibiwa na Mtu Mwenye Followers Wengi

Yesaya Software Podcast

Play Episode Listen Later Jan 30, 2023 6:08


Kwenye episode hii nimeeleza kwa kina namna ya kuandika ujumbe wa kuomba msaada kwa mtu mwenye followers wengi. Yawezekana ni programmer au mtu mwenye uzoefu kwenye eneo fulani.

APGCITV Anchor.fm from Lancaster Pennsylvania state in America

News RadioPublic APGCITV-USA --- Support this podcast: https://podcasters.spotify.com/pod/show/apostolicpowerofgod/support

Habari za UN
Hali si shwari Upper Nile, watoto wakimbia bila mwongozo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 23, 2022 0:02


Nchini Sudan Kusini mapigano ya kikabila kwenye jimbo la Upper Nile nchini humo yamesababisha vifo, ukimbizi wa ndani halikadhalika madhila zaidi kwa watoto ambao mustakabali wao unazidi kuwa mashakani huku nao wazee wakishuhudia machungu katika taifa hilo changa zaidi duniani.Nats.. Hospitalini Kodok jimboni Upper Nile nchini Sudan Kusini!  Taswira kutoka video ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa ya kulinda amani nchini humo, UNMISS, ni watoto walio na majeraha! Ya miguu, mgongoni! Wamekata tamaa!! Nyamer Oyac, mwenye umri wa miaka 60 ni mkimbizi wa ndani akiwa na watoto hawa anasema, “tulikimbia kutoka kijiji cha Aburoc na tukaja hapa Kodok. Tulipitia machungu sana kukimbia na kujificha kwenye vichaka, kuvuka mito na mafuriko kwa sababu tulikuwa tunashambuliwa, tunakimbizwa na kupigwa risasi. Tulipovuka mtu, tulikanyaga watoto mamia ya watoto .Kwa bahati mbaya wengi wao walizama na kufa maji. Niliweza kunusuru hawa hapa waliojeruhiwa kwa sababu hakuna mtu anawalea.” Katika hospitali hii ya kiraia ya Kodok, madaktari na wauguzi wanahaha kuhudumia wagonjwa ambao idadi yao inaongezeka kila uchao. Vifaa ikiwamo dawa ni vichache licha ya msaada kutoka mashirika ya Msalaba Mwekundu, na shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO. Wagonjwa mahututi wanapelekwa Malakal na Juba. Dkt Emmanuel William Gordon wa hapa Kodok anafafanua akisema, “idadi ya majeruhi tuliopokea, hasa waliojeruhiwa kwa risasi ni 20. Wengi wao wanajificha kwenye madimbwi ya maji kwa zaidi ya siku 10 wakiwa na majeraha ya kuungua au risasi. Hatuna idadi kamili kwani wagonjwa ni wengi. Kwa mujibu wa tuliowapokea, wengi bado wamejificha na hivyo tunatarajia wagonjwa wengi siku zijazo.” Kwa sasa misaada ya chakula imeanza kuwasili ikiwemo kutoka shirika la World Vision, lakini hofu ya wengi ni usalama na viongozi wao wanatoa wito wa kupatikana kwa amani ili waweze kurejea kwenye makazi yao. 

SBS Swahili - SBS Swahili
Musoni "Mwaka huu GLAPD imebadili maisha ya vijana wengi"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 10, 2022 10:46


Shirika la GLAPD limekuwa likitoa huduma kwa jamii zawatu kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, zinazo ishi nchini AUstralia kwa zaidi ya miaka sita.

Habari za UN
Mapigano Upper Nile yasababisha wakimbizi wengi wahame makwao nchini Sudan Kusini.

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 7, 2022 0:02


Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema limesikitishwa na kuongezeka kwa mapigano katika jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini ambayo umesababisha takriban watu 20,000 kuyahama makazi yao tangu mwezi Agosti, baadhi yao wakilazimika kukimbia hadi mara nne ili kuokoa maisha yao huku mzozo huo ukiendelea. Kwa mujibu wa taarifa ya UNHCR iliyotolewa leo mjini Geneva Uswis na Juba Sudan takriban watu 3,000 tayari wamekimbilia nchi jirani ya Sudan, na hivyo kuzidisha mzozo wa wakimbizi wa Sudan Kusini, ambao ndio mkubwa zaidi barani Afrika. Mapigano yalizuka katika kijiji cha Tonga huko Upper Nile tarehe 15 Agosti 2022. Ghasia zimeenea zaidi katika jimbo la Upper Nile, sehemu za kaskazini za Jonglei na majimbo ya Unity na machafuko yanasambaa sasa katika kaunti ya Fashoda ya Upper Nile na kutishia mji wa Kodok. Mwakilishi wa UNHRC nchini Sudan Kusini Arafat Jamal amesema “Taharuki inaongezeka na watu zaidi wanakimbia wakati machafuko yakishika kasi. Raia wanashambuliwa katika mgogoro huu usio na huruma lazima tuhakikishe ulinzi wao.” Ameongeza kuwa wanawake, watoto na makundi mengine yaliyo katika hatari kubwa ndio idadi kubwa ya waliotawanywa na baadhi ya wazee na watu wenye ulemavu wameshindwa kukimbia na kulazimika kujificha porini na kando yam to Nile wakati wa mashambulizi. Kwa raia wanaokimbia UNHCR inasema ni “Dhahiri wameathirika na wameripoti mauaji, majeruhi, ukatili wa kijinsia, watu kutekwa, uporaji, unyang'anyi na uchopaji wa mali huku wengi wakisema wamepoteza nyumba zao na kutengana na familia zao.” Wakati huohuo jumuioya ya kibinadamu nchini Sudan Kusini imelaani vilaki kuendelea kwa machafuko hayo na kaimu mratibu wa masuala ya kibinadamu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada yad harira OCHA Peter Van der Auweraert akisistiza kwamba "Jumuiya ya kibinadamu nchini Sudan Kusini inasikitishwa na ghasia zinazoendelea ambazo zina athari mbaya kwa uwezo wa watu kuishi na maisha ya wanawake wa kawaida, wanaume na watoto na wale walio hatarini ambao tayari wameathiriwa na hali mbaya ya kibinadamu nchini humo ndio wanaoteseka zaidi.” Hivi sasa UNHCr na wadau wanaongeza juhudi za msaada wa kibinadamu na kuwafikia hata walio maeneo ya vijijini zaidi.  “Watu milioni 6.8 Sudan Kusini wanahitaji haraka msaada wa kuokoa maisha kutokana na changamoto mchanganyiko ikiwemo vita, mafuriko, kutokuwepo uhakika wa chakula na kuyumba kwa uchumi.” Na ombi la UNHCR la usaidiazi kwa taifa hilo mwaka 2022 la dola milioni 214.8 hadi kufikia Novemba mwaka huu lilikuwa limefadhiliwa kwa asilimia 46 pekee. 

Habari za UN
Wagonjwa wengi wa Kisukari barani Afrika hata hawajitambui- WHO

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 14, 2022 0:03


Wakati dunia ikiadhimisha hii leo siku ya kisukari duniani kwa lengo la kuelimisha umma kuhusu ongezeko la mzigo wa ugonjwa huo na mikakati ya kuzuia na kudhibiti tishio lake, bara la Afrika linaonekana kuwa na changamoto kubwa ya ugonjwa huo, kwa mujibu wa takwimu za shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO.   Flora Nducha na taarifa zaidiTakwimu zilizotolewa leo na WHO kanda ya Afrika zinaonyesha kiwango cha changamoto ya ugonjwa wa kisukari Afrika ni kubwa ambapo watu wazima milioni 24 hivi sasa wanaishi na ugonjwa wa kisukari na idadi inatarajiwa kuongezeka kwa asilimia 129 hadi kufikia watu million 55 ifikapo mwaka 2045. Kupitia ujumbe ake wa siku hii Dkt. Matshidiso Moeti mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika amesema “Mwaka janga ugonjwa wa kisukari ulikatili maisha ya watu 416,000 barani Afrika na ugonjwa huo unatarajiwa kuwa miongoni mwa vyanzo vikuu vya vifo Afrika ifikapo mwaka 2030. La msingi zaidi ni kwamba kisukari ndio ugonjwaa pekee usio wa kuambukiza ambao hatari yake ya vifo vya mapema inaongezeka badala ya kupungua.” Mkuu huyo wa WHO Afrika ameendelea kusema kwamba “Sababu kuu hatari zinazochangia ongezeko la ugonjwa huo Afrika ni pamoja na  historia ya familia, ongezeko la umri na sababu zingine maarufu kama uzito wa kupindukia na utipwatipwa, maisha ya kukaa bila mazoezi, lishe isiyofaa, uvutaji wa sigara na unywaji pombe kupita kiasi. Kwa bahati mbaya, sababu hizi za hatari zinazoweza kubadilishwa zinaongezeka katika nchi zote katika Kanda ya Afrika ya WHO.” Dkt. Moeti amesema “Na changamoto kubwa katika juhudi za kukabiliana na ugonjwa huo ni ukweli kwamba zaidi yam to 1 kati ya kila watu wawili barani Afrika anayeishi na kisukari hajawahi kupimwa  na hivyo kuongeza fursa za nyenzo za upimaji na dawa kama insulin,ni moja ya maeneo yanayopaswa kufanyiwa kazi haraka.” WHO imeonya kwamba ukiachwa bila kudhibitiwa, na bila usimamizi na mabadiliko ya mwenendo wa maisha, ugonjwa wa kisukari unaweza kusababisha matatizo mengine mengi.  Matatizo hayo ni pamoja na mshtuko wa moyo, kiharusi, figo kushindwa kufanyakazi, kukatwa kwa viongo vya mwili kama miguu,  ulemavu wa kutoona, upofu, na uharibifu wa mishipa.  Limeendelea kusema shirika hilo kuwa watu walio na ugonjwa wa kisukari pia wako katika hatari kubwa ya kupata dalili kali za COVID-19. Dkt. Moeti amesisitiza kuwa “Leo, tunapoadhimisha siku ya kisukari duniani, ninataka kuchukua fursa hii kutoa wito kwa serikali za nchi wanachama kuweka kipaumbele katika uwekezaji wa bidhaa muhimu, kama vile dawa za insulini, macshine za kuangalia kiwango cha sukaru glucometer na sindano zinazotumika kupimia au strips. Hii ni muhimu ili kuhakikisha fursa sawa kwa kila mtu anayeishi na ugonjwa wa kisukari, bila kujali ni wapi aliko katika bara hili.” Pia amezihimiza serikali za Afrika kupitisha na kubinafsisha malengo ya kimataifa ya ugonjwa wa kisukari, kama sehemu ya mapendekezo ya kuimarisha na kufuatilia hatua za ugonjwa wa kisukari ndani ya programu zao za kitaifa za NCD. Siku ya kisukari duniani huadhimishwa kila mwaka Novemba 14 na maudhui yam waka huu kama yalivyokuwa yam waka jana na yatakavyokuwa mwakani ni “Fursa ya huduma za kisukari” yakisisitiza umuhimu wa kuzuia na juhudi za hatua dhidi ya kisukari. 

SBS Swahili - SBS Swahili
Dor Jok: "Vijana wengi hapa wanaweza cheza katika A-League wakipewa fursa"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Oct 29, 2022 4:09


Lengo la vijana wengi wanao cheza mpira wa miguu nchini Australia, nikuwa wachezaji wakulipwa na hata kushiriki katika michuano yakimataifa.

Uchumi na Biashara
Serikali saidia, biashara zetu zazorota | Uchumi na Biashara Podcast

Uchumi na Biashara

Play Episode Listen Later Oct 29, 2022 14:46


Licha ya serkali kuahidi kushughulikia changamoto za wafanyabiashara wadogo wadogo, bado mahangaiko yanashuhudiwa mwezi mmoja baada ya Kenya Kwanza kuchukua hatamu za uongozi. Wengi wa wafanyabiashara hao wanalalamikia kuongezwa kwa bei ya mafuta, na kusababisha hasara katika sekta ya matatu. Charles Macharia, mhudumu wa teksi na Jimmy Mwangi, mhudumu wa matatu wanatishia kugura biashara hii. Mwanahabari wetu Edwin Mbugua amefanya mazungumzo na baadhi ya wafanyabiashara hao katika Kaunti ya Nyeri.

MalamMalamStories
Misteri Dibalik Lagu Lingsir Wengi

MalamMalamStories

Play Episode Listen Later Oct 27, 2022 4:58


Support Podcast ini via: https://trakteer.id/malammalamstories/tip ----- #224 Credits Host: Mr. I Background Music: Horrorin JY

PHONE CALL
S04EP02 with Lucas Malembo

PHONE CALL

Play Episode Listen Later Oct 21, 2022 84:28


Kila mtu ana story yake kwenye maisha na haijalishi ni wakati mgumu kiasi gani unapitia kwenye maisha yako tambua kila mtu anapitia magumu yake. Lucas Malembo ni mwanzilishi wa "Malembo Farm" inayojishughulisha na maswala yote ya kilimo, Malembo ana amini kua kilimo kinaweza kutengeneza ajira kwa vijana wengi na vile vile kuikuza nchi yetu ki uchumi. Wengi tumemzoea Lucas Malembo akiongelea kilimo mara kwa mara ila kwenye episode hii amegusia mambo aliyopitia kwenye maisha yake kupelekea kuzaliwa kwa "Malembo Farm". Ni matumaini yangu utafurahia mahojiano haya na kujifunza mambo mengi

Meza Huru
Mezani na MIKE TEE #11

Meza Huru

Play Episode Listen Later Oct 14, 2022 118:40


Wengi wanamjua kwa jina la Mnyalu, Mike Tee, The Dangerous Emcee ila jina lake kamili ni Mike Francis Mwakatundu. Mike Tee alianza kuimba mwanzoni mwa miaka ya 90, akiimba kwaya kanisani na taratibu akaanza kujifunza kuandika na kuimba mistari kupitia mashairi ya gazetini baada ya kukutana na Ntwa mmoja wa waanzilishi wa WWA (Wagumu Weusi Asilia). Amefanya kazi na watayarishaji kama P Funk na Master Jay, amefanya hits na wasanii kama Juma Nature, Q Chief, Mad Ice na Komando Jide Unajua kuhusu ugomvi wa Mr. Nice na Dudu Baya? Mike Tee amenyoosha taarifa. Sitaki kumalizia stori yake. Jumuika nasi mezani umsikilize, Karibu #MezaniNaMikeTee #MezaHuru Anchor - https://anchor.fm/meza-huru Google podcast - https://podcasts.google.com/feed/aHR0... Apple Podcast - https://podcasts.apple.com/us/podcast/meza-huru/id1644168683 Spotify - https://open.spotify.com/show/6Ym3U2r... Deezer - https://www.deezer.com/en/show/4499797 Amazon music - https://music.amazon.com/podcasts/bc2... Boomplay - https://www.boomplay.com/podcasts/32087 Castbox - https://castbox.fm/podcasts/meza-huru... YouTube - https://www.youtube.com/channel/UCutp... Facebook - https://www.facebook.com/MEZA-HURU-10... Twitter - https://twitter.com/MezaHuru

RadioRahma
Kukomesha Unyanyapaa na Ubaguzi kwa wanaokabiliwa na tatizo la Afya ya Akili

RadioRahma

Play Episode Listen Later Oct 10, 2022 8:45


Kwa mujibu wa Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu nchini Kenya asilimia 0.3% ya watu wanaugua ulemavu wa akili jijini Mombasa. Wengi wa wenye ulemavu wa akili ukumbwa na unyanyapa,msongo wa mawazo na utengwa katika jamii,hivyo wanajipata wakirandaranda mitaani. Juma Ali ni kijana mwenye umri wa miaka 30, aliyepona matatizo ya akili yaliyomsumbua kwa muda wa miaka 5. Anasema alianza kurukwa na akili baada ya kumpoteza mchumba wake katika ajali ya barabarani.Anataja kifo hicho kilimfanya kukabwa na msongo wa mawazo na kuanza kutembea uchi na kushambulia watu. Mwandishi:Athuman Luchi.

Jioni - Voice of America
Kenya: Mvutano kuhusu nani kiongozi halisi wa walio wengi Bungeni - Oktoba 05, 2022

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Oct 5, 2022 29:58


Mzozo unaozingira swala la ni nani kiongozi halisi wa walio wengi katika bunge la Kenya, umemlazimu Spika wa bunge hilo Moses Wetangula kumteua Naibu Spika Gladys Boss kwa muda mfupi, kusimamia kamati ya kuratibu shughuli za bunge ili kusitisha usambaratishaji wa shughuli za taasisi hiyo.

Alfajiri - Voice of America
Wakimbizi wa Ukraine waomba kupewa ajira Ulaya. - Septemba 26, 2022

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Sep 26, 2022 29:59


Wengi wao hata hivyo wanasema kwamba wanahitaji kuwezeshwa katika kujifunza lugha za wenyeji , pamoja na kusaidiwa kwenye program kama za uangalizi wa watoto, wakati wakitafuta ajira.

Vijana na Mapenzi
Pesa hubadili tabia za mwanamke? | Vijana na Mapenzi Podcast

Vijana na Mapenzi

Play Episode Listen Later Sep 22, 2022 8:32


Katika miaka ya hivi karibuni, jamii imekuwa ikiyafanya kipaumbele maslahi ya mtoto wa kike baada ya kukandamizwa kwa miaka mingi. Wengi sasa wamepata nafasi ya kusoma na hata kuajiriwa. Lakini kuna wanaoamini kwamba mwanamke anapopata kazi na kuwa na cheo katika jamii, mara nyingi hujawa kiburi. Suala hili tunaliangazia kwa kuhusisha kauli za wananchi vilevile kupata ushauri kuhusu masuala ya ndoa.

Salama Na
SE7EP14 - SALAMA NA COACH EVARIST | FIRST QUARTER

Salama Na

Play Episode Listen Later Sep 15, 2022 79:50


Evarist Mapunda ni moja wa makocha wangu wa maisha haya ninayoishi sasa hivi, ananifahamu toka nikiwa na miaka 17 mpaka sasa hivi ingawa hapa katikati baada ya ‘kuwa mkubwa' nilipoteana nae kwenye mahangaiko ya kujitafuta na kutafuta maisha. Ila Mimi na yeye tunajua kila mmoja wetu ni mtu wa aina gani na anamaanisha NINI kwa mwengine. Ukiwauliza watoto na wakubwa wengi wa Upanga watakuambia nini yeye pia anamaanisha kwenye maisha yao, lazima atakua na simulizi kuhusu mwalimu huyu hodari wa basketball na maisha, kama hadithi hiyo itakua haimhusu yeye directly badi itakua inamhusu Ndugu yake au mtoto wake au hata rafiki yake, na kama itakua hana hao wote basi hata ya kusikia atakua nayo. Coach Evarist ni mmoja ya watu ambao wamesaidia kwa kiasi kikubwa mno vijana wa miaka ya 2000 kuwa na HESHIMA ya maisha, Heshima ya kazi na miili yao, kama umepita kwenye mikono yake basi utakua unajua hilo. Na kama ule usemi wa Kiswahili unaosema ‘majuto ni mjukuu' basi ndo faida za yale alotufundisha sisi tunayaona. Tunayaona baada ya kukua maana wakati anatufundisha heshima ya muda na drills ngumu za basketball tulikua tunaona anatuonea sana sana. Binafsi nilikua naona hivyo, nilikua naona kama hanipendi maana kila mara yuko kwenye shingo yangu kuniambia lipi sijafanya vizuri. Sasa hivi nikikaa na kujiuliza kipi hasa kilinifanya nihame Pazi na kwenda kucheza basketball yangu Don Bosco ukiachana na kwamba rafiki zangu wengi walikua kule sasa ndo jibu linakuja kwamba Coach Evarist naye alichangia kwa kiasi kikubwa mimi kuamua hilo. Alikua kijana, mwenye kuujua mchezo na Don Bosco Queens ilikua ni moja ya team BORA zaidi za wasichana kuwahi kutokea miaka hiyo. Wengi wao nilikua aidha nimesoma nao Makongo au nimeenda nao Umiseta mara kadhaa kwahiyo maamuzi yangu hayakua ya kuwaza sana ingawa Pazi ndo ilikua nyumbani kwetu na itaendelea kuwa hivyo. Coach Evarist pia ashawahi kukutana na mitihani kadhaa mikubwa katika maisha yake, ingawa wa yeye kupata ajali mbaya ya gari mwanzoni mwa miaka ya 2000 itaendelea kusimama kuwa mtihani mkubwa zaidi ambao amewahi kukabiliana nao, ukiachana na fainali tele ambazo yeye kama mchezaji au kocha ambazo zilikua dhidi ya timu ngumu na akawahi kushinda, huu ulikua wa aina tofauti sana. Alikua peke yake usiku wa manane wakati anaenda zake nyumbani baada ya kumaliza majukumu yake aliyojiongezea ya basketball ndo mtihani huo ulipomkuta, Coach Evarist anakumbuka idadi ya watu ambao walimzunguka na kumpiga vibaya baada ya ajali hiyo. Mungu pekee ndo anajua alimuokoa okoa vipi katika lile na kwenye operesheni zake zaidi ya kumi na tano ambazo amezifanya mpaka sasa hivi zinamfanya aishi na kwanini haya yote yametokea. Coach Evarist ni muaminifu na mwingi wa imani, mpaka leo hii anaendelea kuishi maisha yake kama hakuna ambalo limemtokea na kubadilisha maisha na muonekano wake kwa maisha yake yote. Yule ambaye anakua na moyo kama ambao Coach Evarist anao pekee ndiye anayeweza kuishi kama ambavyo yeye anaishi. Ndo maana yeye ni wa kipekee sana. Yangu matumaini maongezi yetu juu ya heshima na mustakabali wa mpira wetu wa kikapu na heshima juu ya mambo kadhaa yatakuvutia na kukufunza kitu. Yangu matumaini pia uta enjoy. Love, Salama. --- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support

Habari za UN
Mashambulizi na utekaji vinachochea watoto wengi kutokuwa shuleni Afrika Magharibi:UNESCO

Habari za UN

Play Episode Listen Later Sep 12, 2022 2:30


Siha Njema
Gharama ya juu ya vyakula ilivyo tishio la kiafya kwa wengi.

Siha Njema

Play Episode Listen Later Aug 31, 2022 9:54


  Katika makala haya  tunaangalia namna mfumuko wa bei ya vyakula ,vita vya Ukraine  inasukuma raia wengi kwenye ukingo wa kupata matatizo ya kiafya yakiwemo magonjwa yasiyoambukizwa. Hali ngumu ya maisha imezidi kuwapa wengi mtihani wa kuchagua afya au bora shibe.

Salama Na
SE7EP09 - SALAMA NA DAMIAN SOUL | HARIRI…

Salama Na

Play Episode Listen Later Aug 11, 2022 66:13


Damian Soul ni Superstar na siku ambayo sote tutakubaliana na hiyo statement basi tutaanza kufaidi matunda ya kipaji chake kwa uzuri sana, ila mpaka siku hiyo ifike ni wachache tu ambao wanamuelewa kwa upana huo ndio ambao wataendelea kufaidi kipaji chake kwa nafasi yao. Wale watu wa makampunj mbali mbali kwa mfano CocaCola ambao wanakua na events zao za ndani kwaajili ya watu wao na waalikwa wawili watatu huwa wanamfaidi sana kijana huyu hodari wa ki Tanzania. Na Damian kwa ukali wake akipata nafasi kama hiyo huwa hafanyi makosa hata kidogo, huhakikisha anapeleka mziki wote kwao ili wakati mwengine wanapokua na event basi jina lake liwe la kwanza kwenye list ya waburudishaji wao. Mzaliwa wa Dar es Salaam, mtoto wa Sinza kabisa, Damian amezaliwa kwenye familia ya kishua kabisa, jinsi ambavyo unaona anavaa ki nadhifu vile ukiachana na hereni zake, hivyo ndivyo Marehemu Mzee wake alivyokua ananyuka, nadhifu kabisa. Koti imenyooka na ilivaliwa inakaa hasa mahala pake, kiatu inang'aa vizuri baada ya kuipiga kiwi mwenyewe, Damian anakumbuka unadhifu huo na ki uhakika ameurithi na kuuendeleza. Shule kwake ilikua ni kitu tu ambacho ilibidi akifanye kwasababu pengine kila mtu au mtoto kwa matakwa ya wazazi ilibidi afanye hivyo na ili aweze kutoka pale alipokua ilibidi afunge mabegi yake mpaka Kampala nchini Uganda, kama utakumbuka vizuri kuna miaka ya kati ya 2000 hapo ilikua kama ‘fashion' kwa watoto wa ki Tanzania kwenda kusoma kule, kwa khadithi nyingi nilizo zisikia wengi wao walikua sio waingiaji sana class na badala yake maisha ya ku party na kujitafuta na kujielewa ndo yalikua ki hivyo zaidi. Haikua tofauti pia kwa Damian Soul, Ila yeye sio kwenye ku party ila kwenye kujitafuta na kujua kwamba muziki ndo kitu alitaka kufanya kwa maisha yake yote. Anakumbuka mti ambao alikua anakaa chini yake na ‘kulicharaza' sana gitaa na kila aliyekua anapita pale habari alikua nayo. Upekee wake wa kuanzia sauti mpaka style yake ya mavazi ndo unaomtofautisha yeye na wengine, ukimuona tu utajua kama ni Star maana jinsi ambavyo anajibeba ni tofauti na watu wengine. Hii pia inasababisha watu kujiuliza maswali kuhusu maisha yake na vitu apendavyo kama mtoto wa kiume. Yeye kwa mujibu wa maongezi haya na mengine ambayo mimi na yeye tushawahi kuwa nayo hayamsumbui kabisa. Anajiheshimu na kujielewa na pia anajua mipaka iko wapi. Na pengine kama binadamu tunatakiwa kuwaacha watu wawe wao, especially kwasababu hayo ni maisha yao, na kwa heshima na taadhima wanajua jinsi ya kujibeba kama binadamu na zaidi kama mTanzania. Anakumbuka jinsi ambavyo alikua Sinza hasa baada ya Baba yake kutangulia mbele ya haki, anasema mtaani palikua pa moto sana kwa kugumbikwa na wimbi la vijana kujihusisha na vitendo vya kihuni na wizi na kujikita kwenye matumizi mazito ya madawa ya kulevya. Anasema yeye alifanikiwa kukimbilia kanisani wakati anasubiria mambo yake mengine ya shule yakae sawa. Kanisani ambako alijifunza mambo ya muziki ikiwa pamoja na kujifunza kupiga instruments, ukiachana na sauti yake ya kipekee, Damian pia ni mpiga gitaa mzuri sana na muandishi hodari pia wa ngoma zake. Mimi ni mmoja wa mashabiki wake na binafsi nilichukua nafasi hii ili tukae chini na tuyajenge kama familia na watu wengine pia wapate nafasi ya kumskiliza na kumuelewa vizuri. Wengi wamekua wakimhukumu kwasababu tu ya muonekano wake na kama Dada na rafiki niliona kuna umuhimu wa sisi kupata nafasi ya kukaa chini na kumfahamu kinaga ubaga. Kama binadamu wote tulivyo, kila mmoja wetu ana mitihani yake ambayo anapitia, mengine mpaka leo inaendelea na mengine ilikua tunafaulu na mengine kufeli, ila kupitia huko ndo ambako kumetufanya tuwe bora na wapya na kujifunza ni jinsi gani mmoja anaweza kutengeneza maisha yake na akawa mfano bora kwa familia na jamii ambayo imemzunguka. Kama mtoto kwa Mama yake na kioo cha jamii, Damian yuko humble sana na wala hana papara kwenye kuhakikisha anafika pale ambapo anapaona kuna kitu cha yeye kuweza kukaa. Mpaka sasa hayuko pabaya hata kidogo --- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support

VOA Express - Voice of America
Vijana wengi washutumiwa kutumiwa katika wizi wa mifugo Uganda - Julai 21, 2022

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jul 21, 2022 29:59


Zaidi ya vijana 400 wamematwa katika operesheni ya pamoja ya vyombo vya usalama katika eneo la Karamoja, huku juhudi za serikali za kuhamasisha vijana kuendelea na maosmo zikionekan kutofua dafu.

VOA Express - Voice of America
Wanariadha wengi wa Afrika Mashariki washindwa kuonyesha umahiri wao Oregon - Julai 18, 2022

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jul 18, 2022 29:59


Wanariadha wengi kutoka nchi za Afrika Mashariki kufikia sasa hawajafanya vyema katika mashindano ya kimataifa ya riadha yanayoendelea mjini Eugrne, Oregon, nchini Marekani, Hata hivyo, Uganda iinaonyesha matumaini ya kufanya vyema zaidi.

VOA Express - Voice of America
Kufo cha Waziri Mkuu wa zamani wa Japan chashangaza viongozi wengi - Julai 08, 2022

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jul 8, 2022 29:59


Kufuatia kuuawa kwa waziri mkuu wa zamani wa Japan Shinzo Abe, viongozi mbalmbali duniani wameeleza kushtushwa kwao hususan kwa sababu nchi hiyo haina rekodi mbaya ya uhalifu wa kutumia bunduki.

japan zamani julai wengi mkuu japan shinzo abe waziri mkuu
Ghost Series
Lingsir Wengi Ritual | Bhayanak Indonesian Horror Movie

Ghost Series

Play Episode Listen Later Jun 29, 2022 12:51


Watch full video explanation on YouTube Follow on me Instagram Summary/Synopsis : Mala always deals with Tembang Lingsir, a song taught by her mother from her childhood. After a mysterious fire incident that killed her mother, Mala lost her voice. Then, Mala lives in her uncle's house, Gatot, and his wife Gladys with their two children, Daisy and his younger brother, Ronald. At the house, Mbok Rahma also takes care of their needs. Daisy is disturbed by Mala's presence, while Ronald is happy. Since Mala's arrival, the atmosphere of the house is no longer the same. Many strange events appear. Mbok Rahma accuses Mala of causing all this chaos. Mala feels that there is a big secret in this house that make all the terror appear. Especially when she discovers that she has a twin sister she has never known before. Copyright Disclaimer : Under Section 107 of the Copyright Act 1976, allowance is made for "fair use" for purposes such as criticism, comment, news reporting, teaching, scholarship, and research. Fair use is a use permitted by copyright statute that might otherwise be infringing.

Uchumi na Biashara
Uchumi na Biashara Pocast: Gharama ya maisha; bidhaa bei ghali

Uchumi na Biashara

Play Episode Listen Later Jun 17, 2022 11:16


Wakenya wanaendelea kulalamikia ongezeko la bei za bidhaa ya kimsingi na kupanda kwa gharama ya maisha. Wengi wameamua kupunguza matumizi ya fedha kukiwamo kutembea badala ya kutumia magari au bodaboda na kula chakula mara moja kwa siku. Martin Ndiema amesema na Wakenya mjini Kitale.

Habari za UN
Tunasherehekea watu wenye ualbino leo kwa sababu tumeona ujasiri wenu na bidii-Muluka Anne

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 13, 2022 2:24


Ikiwa leo dunia inaadhimisha siku ya kimataifa ya kuelimisha jamii kuhusu watu wenye ualbino, Umoja wa Mataifa umetoa  rai kwa nchi zote duniani kuwajumuisha watu wenye ualbino katika mijadala na mipango inayoathiri haki zao za kibinadamu, ili kuhakikisha wanafurahia usawa na ulinzi unaotolewa kwao katika sheria na viwango vya kimataifa.  Kauli mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu inasema ”Tuungane pamoja kufanya sauti zetu zisikike” ikihamasisha haja ya kufanya kazi pamoja na kujenga ushirikiano ili kukabiliana na changamoto za haki za binadamu zinazowakabili watu wenye ualbino.    Mtaalam Huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu ualbino Muluka-Anne Miti-Drummond amesema kupitia taarifa yake aliyotoa leo mjini Geneva Uswisi kuwa sehemu za kufanya maamuzi kuanzia ngazi za kimataifa, kitaifa , kijamii na hata katika sekta binafsi kumekosa uwakilishi wa watu wenye ualibino na hivyo wanashindwa kushiriki katika mijadala ya kufanya maamuzi na hali hiyo inaweza kusababisha ukiukwaji wa haki zao za kibinadamu.    Amesema,  “ni ubaguzi wa kimuundo na ukosefu wa usawa wa kihistoria. Hakuwezi kuwa na usawa bila kujumuishwa kwa sauti za walio hatarini zaidi. Ikiwa hatutajumuisha watu wenye ualbino katika majadiliano na maamuzi, tunaendeleza ubaguzi wa kimuundo na ukosefu wa usawa wa kihistoria.”   Hata hivyo ametoa pongezi akisema,  "Tunasherehekea watu wenye ualbino leo kwa sababu tumeona ujasiri wenu na bidii. Tumeona ongezeko la idadi ya watetezi na wapiganaji wa haki za binadamu wenye ualbino, wengi wao ambao wameanzisha mashirika ya kirai wakati waliona haja ya uwepo wa watu wa kuleta mabadiliko. Wengi wenu mmefanya kazi bila kuchoka kukabiliana na mizizi ya unyanyapaa na mauji ya watu wenye ualbino ikiwemo kukabiliana na dhana potofu hatari kupitia kampeni za kuelimisha kwa kuchagiza ufikiaji wa huduma za afya na raslimali na kuhakikisha ujumuishaji katika shule na maeneo ya kazi ili kuongeza nafasi za watu wenye ualbino kupata mbinu za kujipatia kipato endelevu."    Maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kuelimisha jamii kuhusu watu wenye ualbino mwaka huu pia yanasherehekea kazi zilizofanywa na vikundi vya wenye ualbino katika kupaza sauti zao nakuhamasisha kuendeleza mshikamano wakati wakiendelea kupambana kuhakikisha sauti zao zinasikika. 

VOA Express - Voice of America
Wamarekani wengi wasikitishwa na shambulizi lililopelekea vifo vya watu 20, wengi wao watoto - Mei 25, 2022

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later May 25, 2022 29:58


Mjadala mwingine mkali umeibuka tena nchini Marekani kuhusu sheria za kumiliki bunduki kufuatia shambulizi la risasi mjini Uvalde, Texas, ambapo mtu mwenye umri wa miaka 18 amewaua watoto 18 na watu wazima wawili.

Kwa Undani - Voice of America
Hisia bada ya serikali ya Kenya kudai kwamba wanasiasa wengi wanahusika katika utakatishaji fedha - Mei 25, 2022

Kwa Undani - Voice of America

Play Episode Listen Later May 25, 2022 30:00


Tunazungumza na wadau mbalimbali, wakiwemo wachambuzi na wanasiasa, kufuatia tangazo la serikali kwamba visa vya utakatishaji fedha baina ya wanasiasa vimekithiri

SportsCast
Falsafa ya Marcelo Bielsa

SportsCast

Play Episode Listen Later Mar 8, 2022 15:51


Wengi huvutiwa na soka la timu anazofundisha kama Marseille, Lille na Leeds ambayo kwa sasa imemtimua. Kuna mengi ya kujifunza juu ya falsafa ya Marcelo Bielsa na hapo ndipo kunamfanya Clifford Sangai aketi chini na Prosper Bartalomew kujadili kwa kina mbinu na ufundi wa raia huyo wa Argentina. Tumeongelea aina yake ya ukabaji ambayo ni 'MAN TO MAN" tukiangazia kwa kina namna ilivyofaulu na kufeli hasa akiwa na Leeds United. Prosper alienda mbali zaidi kwa kulinganisha mbinu za Bielsa dhidi ya Gian Piero Gasperini ambaye anakinioa kikosi cha Atalanta kinachoshiriki ligi kuu ya nchini Italia maarufu kama Serie A. Sikiliza uchambuzi huu pia share na wengine zaidi.

Uchumi na Biashara
Uchumi na Biashara Podcast: Wauza-bidhaa katika hafla za kisiasa

Uchumi na Biashara

Play Episode Listen Later Feb 17, 2022 14:31


Wanasiasa wakiendeleza mikutano katika kaunti mbalimbali nchini, ni afueni kwa wafanyabiashara ambao biashara zao zilikuwa zimeathirika kutokana na Covid-19. Wengi wa wafanyabiashara hunufaika pakubwa na mikutano ya kisiasa kwa kuuza bidhaa zao katika majukwaa hayo. Katika Kaunti ya Pokot Magharibi, wanasiasa wameendelea kuziinua biashara kwa kuwanunulia wafuasi wao bidhaa mbalimbali. Moses Kiraese amefanya mazungumzo na wafanyabiashara mjini Kapenguria

Habari za UN
Nchi ya Niger yapongezwa kwa ukarimu kwa wasaka hifadhi na wakimbizi

Habari za UN

Play Episode Listen Later Feb 10, 2022 2:52


Viongozi wa mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la kuhudumia wakimbizi UNHCR Filippo Grandi na lile la Uhamiaji IOM Antonio Vittorino wamefanya ziara nchini Niger, huko Agadez ambalo ni eneo la mpito la watu wanaotafuta hifadhi na wahamiaji nchini Niger ambalo limeongezeka kuwa na idadai kubwa ya watu wenye kuhitaji msaada wa usalama na fursa. Taarrifa ya UNHCR inasomwa studioni na Evarist Mapesa wa redio washirika Redio SAUT ya Mwanza, Tanzania. Jamhuri ya Niger, taifa hili lisilo na bahari lililopo Magharibi mwa Afrika limepakana na mataifa saba ya ambayo ni Chad, Benin, Algeria, Nigeria, Mali, Burkina Faso na Libya. Kupakana na mataifa hayo kumeifanya nchi hii kuwa kitovu au njia ya wanaoelekea kaskazini mwa Libya, Algeria, na Bahari ya Mediterania. Kwa sasa nchi hii inashuhudia kuongezeka kwa idadi ya watu wanaokimbia Libya au kufukuzwa kutoka Algeria.  Mmoja wa watu hao ni Safa  Ahmed yeye alikimbia Sudan miaka mitano iliyopita na kukwama nchini Libya. Lakini sasa amefanikiwa kusafiri hadi hapa Agadez nchini Niger. “Kusema ukweli maisha ya hapa, mbali na kwamba sina mama na baba yangu ni mazuri. Asante Mungu. Ninafanya kazi, binti zangu wanasoma tena kwa Kiingereza. Nina biashara ya kuuza nguo na manukato. Naweza kufanya kazi. Sitarajii chochote kutoka kwa mtu yeyote. Nina kila kitu. Kwenye fikra zangu nimeshaachana na Libya.” Kauli yake inaungwa mkono na Mkimbizi huku kutoka Cameroon ambaye anasema,  “Tunamshukuru Mungu kwamba serikali ya Niger ilitupokea na kutupa mahali pa kulala na tunashukuru sana lakini sisi hapa, shida yetu kuu ni maisha yetu ya baadaye.” IOM   Ukarimu wa Niger unamfurahisha Filippo Grandi, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa anahusika na Wakimbizi ambaye anasema lengo kuu la UNHCR ni kuhakikisha wale wanaotafuta ulinzi wanapata usaidizi na wanapata hifadhi.  “Nimefurahi sana, tumekuja hapa kujaribu kuona majukumu yetu ni nini na jinsi ambavyo kwa pamoja, tunaweza kusaidia watu hawa katika harakati zao, wakazi wa eneo hili na mamlaka ya nchi ambayo inabaki kuwa wakarimu sana na iko tayari kukaribisha kila mtu.” Pamoja naye ni Antonio Vittorino, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM ambaye anasema, "UNHCR na shirika letu (IOM) kama sehemu ya Umoja wa Mataifa, kufuatia uamuzi wa Katibu Mkuu, tuna jukumu la kushiriki zaidi kushughulikia mahitaji ya wasaka hifadhi.” Wengi wa wasaka hifadhi wamepokelewa katika Kituo cha misaada ya Kibinadamu, eneo lililopo nje kidogo ya Agadez ambapo wanapata huduma za afya, shughuli za kiuchumi, maji, makazi na chakula yakiwa ni miongoni mwa mahitaji mengine ya kimsingi.

RRI Pro 4 Surabaya
Ludruk - Lingsir Wengi

RRI Pro 4 Surabaya

Play Episode Listen Later Jan 7, 2022 79:47


Ludruk Pro 4 RRI Surabaya

wengi rri surabaya
We Machine Podcasting
Kirusi cha Omricon au ni Mafua ya kawaida & diamond platinumz

We Machine Podcasting

Play Episode Listen Later Dec 20, 2021 1:53


Wengi wamekuwa wakisema tu ni mabadiliko ya hali ya hewa lakini wanasayansi wanasema ni covid, ukweli ni upi. Diamond nae ameachia ngoma yake, amesemwa sana mitamdaoni lakini ngoma inafanya vyema

Habari za UN
Ni lazima wanawake tujiamini – Fundi viatu Jovia Kyomuhendo

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 7, 2021 3:41


Ubunifu ni moja ya mambo yanayotazamwa kuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs. Nchini Uganda, msichana Jovia Kyomuhendo amepata sifa kwa kuwa kijana mbunifu ambaye amefikia hatua ya kujiajiri kwa kuanzisha kiwanda kidogo cha kushona na pia kutengeneza viatu. Safari yake imekuwaje hadi kufikia kutunukiwa tuzo na Muungano wa Viwanda Vidovidogo nchini Uganda USSIA? Tupate taarifa zaidi kutoka kwa mwandishi wetu wa Uganda, John Kibego. Jovia Kyomuhendo akieleza hisia zake baada kushinda tuzo ya kijana mbunifu mwaka jana anasema, “Eee! Mungu wangu, sikuamini kwamba ndio mimi aliyetuzwa kwa sababu tulikuwa na ushindani mkali uliohusisha wavulana na wasichana ambapo kila mmoja alikuwa anafahamu anachofanya.” Tuzo hiyo iliadaliwa kijiimarisha katika utengenezaji wa vyatu ambapo kwa sasa anajiajiri mjini Kinubi, "lakini kwa nguvu za Mwenyezi mungu, nifanikiwa  kuwa wa pili. Nadhani hii ni kwa sababu nilikuwa najiamini sana kuhusu kile ninacchofanya. Na pia ninachofanya kinachangia kwneye uhifadhi wa mazingira kwani natumia magurudumu kutengeneza viatu hivyo na kuyaondoa katika mazingira.” Wengi hushangaa wanapoona mwanamke akijishughulisha na utengenezaji wa viatu, “kila mtu huwa anasema ‘Eee” hiyo kazi ni ya wanaume lakini motisha ulionayo ndio inakusaidia kuchapa kazi. Je, unapenda kazi hiyo? Ikiwa unaipenda bila shaka unaweza kuifanya.” Mazingira ya nyumbani hayakumruhusu Kyomuhendo kuendelea na elimu hadi elimu ya sekondari ya juu na vyuo. Lakini je, anajuta? “sijuti hata kidogo kwa sababu nimefanikiwa. Unakuta kwamba wengi wa walioendelea hadi kwneye vyuo vikuu hawana kazi lakini kwangu ninachapa kazi. Hata wakati wa COVID-19 nilikuwa nikifanya kazi kwani watu walikuwa wakitembea wakitumia viatu nikitengeneza na kuwashonea viatu vipya.” Ujuzi huu umekuwa nuru kwa Kyomuhendo, kijamii na kiuchumi, “nimepata marafiki wengi sana na mawasiliano muhimu sana  duniani. Mfano ni USSIA ambao kupitia kwao nimepata tuzo. Tuzo ya kijana mbunifu” Kwa upande wa kipato, “kiuchumi ninasema kwamba ninajitegemea. Sitegemei yeyote kwa sababu unakuta kwamba wasichana wengi hupenda kutegemea wengine kuwapatia mahitaji wakati wote, wakisema sisi wanawake ni wa kupewa na anakaa nyumbani lakini mimi ninajitegemea” Kyomuhendo anaelezea kwa nini anapenda kazi yake hii, “kwa sababu nina soko kubwa sana kiasi kwamba kila mtu huvaa viatu. Wanawake, watoto wadogo, vijana na wazee hata babu yangu anavaa viatu. Inamaanisha hili ni soko kubwa sana lilopo” Kwa mantiki hiyo, anatoa mawaidha kw awanawake, “ni kwamba sisi wanawake, ni lazima tujiamini. Kuwa mwanamke haimanishi kwamba hauwezi kufanya lolote. Usikubali kupuuzwa kwa sababu unaona sasa hivi mimi aliye mkode namna hivi ndio anayetengeneza viatu hivi” Katika panda shuka ya maisha, Kyomuhendo amewahi kuwa mwalimu katika shule ya msingi na kuanza kuusomea ili awe mtaalamu lakini, aliaacha kwani alipata pesa za kununua machine alizokuwa anaihitaji ili ajiajiri katika utengenezaji wa viatu.

Habari za UN
WFP wachapisha video na picha kuonesha hali mbaya ya chakula nchini Afghanistan

Habari za UN

Play Episode Listen Later Dec 2, 2021 3:35


Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP limetoa video maalum ya zaidi ya dakika 5 na picha kadhaa kuionesha dunia hali mbaya  ya kibinadamu inayoendelea nchini Afghanistan ikiwemo ukosefu wa chakula na kutoa ombi maalum la kusaidia watu wa nchi hiyo bila kujali masuala ya kisiasa ya nchi hiyo kwani wanaoteseka ni wananchi na watoto wenye utapiamlo mkali wakizidi kuongezeka wakati huu ambapo nchi hiyo inaingia kwenye msimu wa baridikali. Leah Mushi anatujulisha yaliyomo kwenye video hiyo. Msimu wa baridi ndio kwanza umeanza nchini Afghanistan, theluji imemwagika na mashambani ukame mtupu, hakuna kitu cha kuweza kuwapa mlo binadamu na wanyama wanaambulia majani makavu ambayo hata kuyang'oa ni taabu. Masokoni hali hii ni ngumu mno, mwanamke huyu anasema kila unayemuona hapa ana watoto yatima watano au sita ambao wameshuhudia vita na kibaya zaidi ni kuwa hakuna chochote chakuwapa kula maisha nyumbani si mazuri. Kauli yake inathibitishwa na Dokta Mustafa katika zahanati moja inayopokea watoto na kupima utapiamlo anasema “Hawana chochote. Wanauza samani zao, wanauza wanyama wao. Wengi wao wameuza mpaka nyumba zao…kwa ajili ya chakula. Lakini sasa hawana chochote chakuwawezesha kununua chakula.” Pengine vijana maeneo mengine duniani wana ndoto kubwa, lakini si Afghanistan, Mahmoud mwenye umri wa miaka 17 na mhitimu wa elimu ya sekondari akitamani kuwa daktari, baba yake amekufa na mama yake haoni, kaka yake amekimbilia Iran sasa amebaki yeye kumlea mama yake na wadogo zake.   (Sauti ya Mahmoud) – Evarist "Labda ni tofauti na nchi zingine. Hapa Afghanistan, kila wakati watu wanafanya kazi tu kwa ajili ya kupata chakula na kuwaletea watoto na wake zao na si kitu kingine. Nina ndoto nyingi na ninataka kufikia ndoto zangu lakini, kwa bahati mbaya hapa hakuna fursa ya kufanya hivyo ... sina nafasi hiyo." Mwakilishi mkaazi wa WFP nchini Afghanistan Mary-Ellen McGroarty anasema sasa jumuiya ya kimataifa inapaswa kuiangalia Afghanstan sio kwa jicho la kisiasa na nani anaongoza nchi hiyo bali kwa jicho la kibinadamu.   ( Sauti ya Mary-Ellen McGroarty) – Devotha ‘Tunahitaji kutenganisha umuhimu wa msaada wa kibinadamu na majadiliano ya kisiasa. Watu wa Afghanistan, watu wasio na hatia wa Afghanistan, watoto wa Afghanistan ambao maisha yao yameharibiwa bila makosa yao wenyewe hawawezi kuhukumiwa kwa njaa juu ya njaa kwa sababu tu ya bahati nasibu ya jiografia iliyowafanya wao kuzaliwa hapa.' WFP imetoa ombi la dola bilioni2.6 kusaidia hali inayoendelea sasa nchini Afghanistan lakini wameeleza mambo mawili makubwa mosi baridi kali inakuja na pili watoto wanaopelekwa zahanati ni wachache na  wanagundulika kuwa na utapiamlo mkali, je wale ambao familia zao haziwapeleki zahanati hali zao zikoje ?

RadioRahma
WAJIPATIA RIZIKI KUPITIA KILIMO CHA MBUYU

RadioRahma

Play Episode Listen Later Nov 29, 2021 12:38


Wengi hufahamu jina mabuyu yaliyozoeleka kuliwa kwa kumumunya utamu wake ambapo hupikwa kwa kuchanganya na sukari, rangi iwe ya kijani nyekundu au hata njano pamoja na viungo vyengine ambapo badae huuzwa katika paketi kati ya shilingi 5-50 Lakini je unapomumunya utamu wake unafahamu pale yanapotokaa?.Yanatoka kwa mti wa m'buyu kwa kimombo baobab tree. Ni mti mkubwa wa ukanda wa tropiki na matunda yake ndio yanaitwa mabuyu na lile gamba la tunda linaitwa kibuyu na ubuyu ndio hupikwa na kisha tunaomumunya utamu wake. Mti wa m'buyu ambao huzalisha mabuyu hustawi sana katika maeneo yenye joto ,yaliyo makavu ya Afrika na una uwezo wa kuhimili makali ya kiangazi. La zaidi ni kwamba wapo wakulima waliozama katika ukulima wa m'buyu kutokana na manufaa mengi yenye kuendeleza uhai. Wakulima hawa wanategemea mibuyu iliyopo mashambani mwao pamoja na ile iliyostawi katika msitu wa Kaya Kauma kaunti ya Kilifi. By: Mwanaharusi Rashid

RadioRahma
Juhudi za kunasua familia kimawazo dhidi ya makovu ya mauaji ya kiholela

RadioRahma

Play Episode Listen Later Nov 26, 2021 11:06


Familia nyingi hupata msongo wa mawazo wanapopoteza wapendwa wao kutokana na mauaji ya kiholela.Katika makala haya Ruth Keah amezungumza na baadhi ya waathiriwa ambao wamepoteza jamaa zao mikononi mwa maafisa wa usalama.Wengi kwa sasa wamejiunga na vikundi vya kubadilishana mawazo ili kupunguza msongo wa mawazo wanaopitia. By:Ruth Keah.

SBS Swahili - SBS Swahili
Wasafiri wengi zaidi na watu wenye viza kutoka ng'ambo wanaweza rejea Australia

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 23, 2021 6:37


Mpango wa serikali ya shirikisho wakufungua nchi, unakaribia ingia katika awamu nyingine.

Habari za UN
Umoja wa Mataifa watoa wito kwa viongozi wa nchi kulinda waandishi wa habari

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 2, 2021


Pamoja na kufanya kazi kubwa ya kuhabarisha umma, waandishi wa habari ulimwenguni kote wanakabiliwa na mashambulio yanayohatarisha usalama wao ambapo mashambulio hayo ni pamoja na kauli za chuki, udhalilishaji kwenye mitandao ya kijamii, vurugu, ubakaji na hata mauaji. Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukomesha uhalifu dhidi ya waandishi wa habari Umoja wa Mataifa unasema muarobaini wa yote hayo ni utashi wa kisiasa. Tuungane na Leah Mushi kwa taarifa kamili.   Tafiti zilizofanywa na shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni,  UNESCO zimebaini kuwa kati ya mwaka 2006 na 2020, zaidi ya waandishi wa habari 1,200 wameuawa kwa kuripoti habari kwa umma. Utafiti huo umeonesha kuwa kati ya vifo 10 ni kisa kimoja tu ndio muhusika au wahusika wanaadhibiwa. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anasema dunia lazima ikomeshe uhalifu huu dhidi ya waandshi wa habari ili kuhakikisha uhuru wa kujieleza na upatikanaji wa habari kwa wananchi wote unakuwepo. "Mwaka jana, kulingana na UNESCO, waandishi wa habari 62 waliuawa kwa kufanya kazi zao tu. Leo tunaadhimisha urithi na mafanikio ya wanahabari waliouawa wakiwa kazini, na tunataka haki itendeke kwa uhalifu unaofanywa dhidi yao. Ninatoa wito kwa Wanachama na jumuiya ya kimataifa kusimama katika mshikamano na waandishi wa habari duniani kote leo na kila siku, na kuonyesha nia ya kisiasa inayohitajika kuchunguza na kushtaki uhalifu dhidi ya waandishi wa habari na wafanyakazi wa vyombo vya habari kwa nguvu zote za sheria. “ Ingawa kwa miaka 5 iliyopita mauaji ya waandishi wa habari yalipungua kwa asilimia 20 lakini takwimu zilizokusanywa mwaka huu wa 2021 zinaonesha uhalifu kwa wanahabari umeongezeka kwa asilimia 87 ikilinganishwa na miaka iliyopita. Wengi wameuawa katika nchi zao. Kati ya waandishi wa habari 400 waliouawa kutoka 2016 hadi 2020, ni waandishi wa habari 22 pekee sawa na asilimia 6 ndio waliuawa nje ya nchi zao. Siku hii kwa mwaka huu inaadhimishwa kwa kufanya mjadala wa ngazi za juu kwa mtindo wa mseto wengine watakuwa mkumbini na wengine mtandaoni kwa pamoja wakiangazia jukumu muhimu la huduma za uendeshaji wa mashtaka katika kuchunguza na kushtaki sio tu mauaji, lakini pia vitisho vya unyanyasaji dhidi ya waandishi wa habari. UNESCO inahusika na masuala ya waandishi wa habari ikiwemo kutoa mafunzo, kufanya tafiti ambazo zinasaidia kutengeneza sera za kuwawezesha waandishi wa habari kuwa wafanisi zaidi na pia kugundua changamoto wanazokabiliana nazo na kuzitafutia ufumbuzi.

Habari za UN
Nimejipa miaka 10 kuhakikisha tuna mabondia wengi wanawake Tanzania kuliko wanaume - Feriche Mashauri

Habari za UN

Play Episode Listen Later Oct 5, 2021 4:04


Umoja wa Mataifa unaamini michezo ni moja ya njia zinazoweza kuchangia kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Kwa upande mmoja michezo huleta furaha na amani, hukutanisha watu na kwa upande mmoja ni chanzo cha mapato katika mnyororo mzima wa watu watoe wanaoshiriki katikati ya uwanja na nje ya uwanja achilia mbali kuwa michezo ni hakikisho la afya bora ya mwili. Kutana na Feriche Mashauri a.k.a ‘Boyka' mwanamke wa kwanza nchini Tanzania kushinda mkanda wa Ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati Mchezo wa ngumi mchezo ambao unahitaji ujasiri wa hali ya juu na mazoezi mengi ambapo jamii inauona mchezo huu ni hatari na ni kwaajili ya wanaume pekee lakini mwanamke huyu ana mawazo tofauti. Feriche anataka kuutumia mchezo huu wa ngumi kupambana na kukosekana kwa usawa wa kijinsia na pia kukuza uchumi. 

Vijana na Mapenzi
Wengi wanaonikatia ni mabwana wa wenyewe. Mbona hivi?

Vijana na Mapenzi

Play Episode Listen Later Oct 1, 2021 22:31


Mara nyingi msichana anapovunja ungo ama tayari kuwa katika mahusiano, hutarajia ampate mtu ambaye hajaoa ili wafunge pingu za maisha. Hata hivyo kuna wale ambao huishia kuchumbiwa zaidi na mabwana wa wenyewe. Je, ni kipi ambacho huchangia zaidi msichana kukumbana na wanaume walio katika ndoa? Ni yeye anayejitangaza kwao ama ni ukosefu wa maadili kwa wanaume walio katika ndoa kutaka kuwa na wapenzi wengi? Vijana na washauri wanatoa hoja zao.

Radio Uhai Broadcast
Dhambi Mbaya Inayotesa Watu Wengi Bila Kujijua (Swahili)

Radio Uhai Broadcast

Play Episode Listen Later Jul 29, 2021 28:00


Radio Uhai Broadcast
Unacheza Step Ili Akuone Lakini Wengi Mnamgombania (Swahili)

Radio Uhai Broadcast

Play Episode Listen Later Jul 29, 2021 21:00


RadioRahma
UBAKAJI WA MATEJA WA KIKE

RadioRahma

Play Episode Listen Later Jul 26, 2021 8:32


Kaunti ya Mombasa ina idadi kubwa ya waraibu wa kike wa mihadharati, ambao wengi wao hujipata wamebakwa wakiwa maskani mwao. Wengi wa waraibu hao hushindwa kutafuta haki baada ya kubakwa,hivyo kuishia kuishi na makovu ya milele. By Athman Luchi

Radio Uhai Broadcast
Watu Wengi Hawajui Kuomba (Swahili)

Radio Uhai Broadcast

Play Episode Listen Later Jul 22, 2021 60:00


Radio Uhai Broadcast
Walio Upande Wetu Ni Wengi (Swahili)

Radio Uhai Broadcast

Play Episode Listen Later Jun 21, 2021 61:00


Radio Uhai Broadcast
Mabinti Wengi Wanalizwa Ma Mahusiano (Swahili)

Radio Uhai Broadcast

Play Episode Listen Later Jun 16, 2021 15:00


Habari za UN
Tulisikia mitetemo na moto kila mahali na tukakimbia- Manusura wa volkano ya Nyiragongo, DRC

Habari za UN

Play Episode Listen Later Jun 2, 2021 2:21


Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR na wadau wengine wanawasaidia watu waliolazimika kuyakimibia makazi yao baada ya mlipuko wa volkano katika Mlima Nyiragongo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC. Wengi walivuka mpaka kwenda nchi jirani ya Rwanda ambako sasa wanapata usaidizi. Taarifa ya Assumpta Massoi inaeleza zaidi.

Radio Uhai Broadcast
Wanaume Wengi Mnashindwa Kufuta Michepuko! (Swahili)

Radio Uhai Broadcast

Play Episode Listen Later May 6, 2021 24:00


Radio Uhai Broadcast
Huyo Ndie Mwanaume Aliye Vunja Record Kuwa Na Wanawake Wengi (Swahili)

Radio Uhai Broadcast

Play Episode Listen Later Apr 28, 2021 30:00


Afrika Ya Mashariki
Afrika Ya Mashariki - Uzalishaji wa chai nchini Tanzania

Afrika Ya Mashariki

Play Episode Listen Later Apr 27, 2021 9:38


Wakulima wa zao la chai katika mkowa wa Kagera, nchini Tanzania, wameshindwa kuzalisha zao hilo kutoka na changamoto nyingi, ikiwemo kukosa kupata pembejeo za zao hilo. Wengi wakiachana na ukulima wa zao hilo. Juliani Rubavu ametuandalia makala kuhusiana na changamoto za wakulima hao.

NMU PODCAST
MY KISARAWE EXPERIENCE (WITH ANTIDIUS MARTINE)

NMU PODCAST

Play Episode Listen Later Apr 14, 2021 21:36


Karibu tena kwenye episode nyingine ya NMU PODCAST, Kutana na mwanzirishi wa NMU PODCAST Mr Antidius martine) Kila Mwanadamu kuna vitu anapenda katika maisha, wapo wanaopenda mziki, Movies , Mpira na mengine mengi, kwa Ujumla yote hayo tunayaweka kwanye kipengere cha lifestyle, Wengi wanasema namna ya kuishi au staili au mtindo wa maisha, jambo ambalo utofautiana kuringana na mtu husika kwenye maisha yake. Kwenye Episode hii kutana na ANTIDIUS MARTINE ambaye kwa upnde wake anapenda sana kuangalia mazingira (adventure), kudurusu vitu vipya na kujifunza , kwenye episide hii ameshare nasi EXPERIENCE YAKE JUU YA SAFARI ALIYOIFANYA KWENDA SEHEMU MOJA WILAYA YA KISARAWE inayoitwa PUGU KAZIMZUMBWI. Kupitia episode hii utaweza kujua mambo mengi ambayo yanapatikana Wlaya ya KISARAWE sehemu ya Ifadhi ya misitu lakini pia sehemu ya UTARII ambayo ata yeye alikuwa suprised saana kuikuta KISARAWE. Miasha yana maajabu sana na katika maajabu hayo, maajabu mengine yanaweza kuliletea faida Nchi Husika, Nini sasa kinachopatikana Kisarawe kama maajabu? ........ Ungana na Mr Antidius Martine kwenye episode hii, MY KISARAWE EXPERIENCE upate kuyajua mengi yapatikanayo KISARAWE PUGU KAZI MZUMBWI NATURE RESERVE.

music movies martine nini karibu wengi ungana miasha steka kutana
Jasusi
Uchambuzi Mfupi Wa Kijasusi Kuhusu Samia Kuapishwa Urais Huku Wengi Wakimlaumu Kwa Kutovaa Barakoa

Jasusi

Play Episode Listen Later Mar 20, 2021 12:07


Uchambuzi Mfupi Wa Kijasusi Kuhusu Samia Kuapishwa Urais Huku Wengi Wakimlaumu Kwa Kutovaa Barakoa.

Jasusi
Uchambuzi Mfupi Wa Kijasusi Kuhusu Samia Kuapishwa Urais Huku Wengi Wakimlaumu Kwa Kutovaa Barakoa

Jasusi

Play Episode Listen Later Mar 20, 2021 12:07


Uchambuzi Mfupi Wa Kijasusi Kuhusu Samia Kuapishwa Urais Huku Wengi Wakimlaumu Kwa Kutovaa Barakoa. Get full access to Barua Ya Chahali at www.baruayachahali.com/subscribe

DAKA CODE
Bruno Mars kushiriki Grammy | Mgunduzi wa Cassette tape Amefariki | Picha iliyotazamwa na watu wengi duniani

DAKA CODE

Play Episode Listen Later Mar 12, 2021 17:24


Usiache kufahamu EP ya Bruno Mars na Anderson .Paak kushiriki katika Grammy. Fahamu story ya Mgunduzi wa Cassette ambaye amefariki wiki hii akiwa na miaka 94. Katika mazungumzo tumegusia kuhusu historia na miaka ya enzi za Cassette duniani. Katika upande wa Photography tumezungumza kuhusu picha ambayo imetazamwa na watu wengi katika historia. Shukran sana kwa wafuatiliaji na msiache ku-follow show hii ili kupata updates daily. Daka Codeee!!!

SportsCast
Namna Mbappé na Haaland wanavyojitengenezea ulimwengu wao wa soka

SportsCast

Play Episode Listen Later Feb 26, 2021 28:10


Wengi wamehusishwa kurithi ufalme wa Lionel Messi na Christiano Ronaldo lakini hawakuweza kufikia kiwango chao. Je, Kylian Mbappé na Erling Braut Haaland wataweza kufikia kiwango cha Messi na Ronaldo? Clifford Sangai anaungana na Prosper Bartalomew kujadili namna makinda hawa wanavyotengeneza ulimwengu wao wa soka. Tunaangazia zaidi takwimu za mchezo na namna wanavyosaidia timu zao kuweza kupata matokeo. Tufuate katika mtandao wa Instagram: https://instagram.com/sportscasttz?igshid=1s7jr9p0pao5 Twitter: https://twitter.com/SportsCastTz?s=09

Salama Na
Ep. 54 - Salama Na VANNY BOY | NDAGHA

Salama Na

Play Episode Listen Later Feb 18, 2021 74:32


Kutoka kwao Mbeya mpaka Dar es Salaam kwaajili ya kutafuta maisha bora na maendeleo kama wengi wetu ndo ilikua nia na madhumuni ya Raymond wa enzi hizo. Ingawa kuna kipindi ilifika alikua hataki kabisa kuskia habari za muziki, ila alipoambia kama kuna pesa ndani yake katika huo mchongo wa mashindano ambayo aliitiwa na akiangalia nyumbani moja haikai na mbili haijulikani ilipo akaona basi sawa, kwani nini? Na huo ndo ulikua mwanzo wa safari nzuri ya ki superstar ambayo anaishi nayo sasa. Najua wengi wenu mlikua mnadhani labda yangezungumziwa madhila alokua nayo sasa ila kwa bahati mbaya (kwako) na nzuri kwetu, sisi tulizungumza naye kabla. So hii ilikua free na natural kama ambayo utaiona au kuiskiliza. Wengi wetu huwa tunapitia madhila na mitihani mingi tu kabla ya kujielewa na kusimama sawa sawa, na kupitia hayo ndo kujifunza na kuwa BORA kunatokea. Kuna msemo mmoja wa Kiswahili unaoenda kama, ‘asipo chafuka, atajifunzaje', something like that. Mimi Ray huyu nilianza kumsikia vizuri zaidi kutoka kwa AY ambaye ali spend naye muda mwingi hapa Bongo wakati wanafanya rekodi remix ya Zigo na nchini Afrika ya Kusini wakati Zee ameenda ku shoot video ya wimbo huo ambao Diamond Platnumz ndo ameshirikishwa, ila Vanny Boy alikuwepo all the way na mpaka kwenye video akatokea. AY aliniambia kuhusu ucheshi wake na uhodari wake, na uhodari huo ameuzungumza humu kwenye maongezi yetu mimi na yeye. Aliniambia jinsi ambavyo alikua akitumia kipaji chake enzi hizo kwa kuwaandikia wenzake wimbo mmoja na pengine mpaka album kwa shilingi ELFU THELATHINI TU. Njia ambazo watu wengi wamepita haiwezi kuwa ndo njia ambayo kila mmoja wetu atapitia pia, ila kunaweza kuwa na mifanano ya hapa na pale, na hii ndo nia na madhumuni ya kipindi hiki. Tunataka wewe usikie na ujifunze ili ujue ‘unatokaje' au watu walipenya vipi mpaka wakafika! Sasa ni mmoja ya wasanii wakubwa tu hapa barani Afrika na duniani anafahamika. Bango la album yake linaning'inia kwenye mitaa ya Times Square huko NY City kwenye mji ambao raia wa nchi mbalimbali duniani wanaishi na kupitia. Sidhani kama wakati anahangaikia kufua nguo zake zilizomwagikiwa mafuta ya mawese wakati akiwa safarini kwenye lori kutoka Mbeya kuja Dar aliwahi kuwaza jambo kama hilo. Mimi na yeye tulizungumzia pia mahusiano yake na wazazi wake, familia ya kufikia ya Baba yake ambaye aliachana na Mama yake na kuhamia na mtu mwengine si mbali na wao walipokua wanakaa. Tumeongelea mapenzi yake na muziki na kipaji chake cha uandishi. Tumeongelea jinsi ambavyo Madee alimpokea na Babu Tale ambavyo alikua na kama kusita hivi kwenye suala la yeye kusajiliwa WCB na mambo mengine mengi ya maisha. Yangu matumaini kama ilivyo ada, hapa utajifunza jambo pia. Tafadhali enjoy. Love, Salama. --- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support

Msasaonline
"COUNTRY BOY" AZUNGUMZIA UMUHIMU WA MSANII KUWA TRENDING YOUTUBE NA VIEWS WENGI KWENYE MUZIKI WAKE.

Msasaonline

Play Episode Listen Later Nov 10, 2020 37:40


"COUNTRY BOY" AZUNGUMZIA UMUHIMU WA MSANII KUWA TRENDING YOUTUBE NA VIEWS WENGI KWENYE MUZIKI WAKE.

It's The Lazycat Pod-Cat Show!
Spooky Talks 01 - The Misidentification of Lingsir Wengi

It's The Lazycat Pod-Cat Show!

Play Episode Listen Later Aug 20, 2020 28:37


(IND) Seekor Kucing lokal berusaha mengungkap kemisteriusan dari lagu "Lingsir Wengi" yang masih dianggap sebagai salah satu lagu terseram di Indo-01001011 01000001 01001101 01001001 00100000 01010011 01000101 01001100 01000001 01001100 01010101 00100000 01000100 01001001 01010011 01001001 01001110 01001001 --- This episode is sponsored by · Anchor: The easiest way to make a podcast. https://anchor.fm/app

Salama Na
Ep. 22 - Salama Na Isaya | KOMAA NAO

Salama Na

Play Episode Listen Later Jun 25, 2020 54:52


Mimi na Isaya mara ya kwanza tumekutana kwenye set wakati tunatengeneza episode hii ya 22 lakini kabla ya hapo ilikua ni kufahamiana tu kule kwa social media na respect kwa kila mmoja wetu kwa kile ambacho mwenzake anakifanya. Kwahiyo mkutano wetu wa kwanza ulikua ndo wa kwanza kabisa na haikua ngumu kuanzisha maongezi kati yetu. Wakati nishamseti ili aje kwenye meza pia niliwauliza wenzangu tunaofanya hii kazi pamoja, kila mmoja apendekeze jina au majina ya watu ambao wangependa waje kwenye kipindi na kila jina liwe na sababu ya kwanini tumpe nafasi huyo mtu. Basi jina lake pia lilikua ni muongoni mwa majina yaliyotajwa. Unaweza ukaelewa mpaka hapo juu ya impact ya shughuli anazozifanya. Kama Isaya asingeelezea khadithi ya maisha yake toka utotoni basi hata kwa miaka 100 nisingeweza kudhania alipita kwenye mitihani na mazingira magumu toka akiwa mtoto. Wengi wetu tuna historia za makuaji yetu ila ya mwenzetu huyu ina ujasiri na masikitiko mengi yatakayokutaka uhakikishe mwanao hatokaa akue kwenye mazingira hayo. Elimu kuipata ilikua kwa mbinde, kuwaona Baba na Mama yake ilikua mtihani, kuishi kwenye ahadi zilikokua hazitimizwi na mpaka kufikia kuwa machinga akiwa mtoto kwenye mitaa ya katikati ya Jiji la Mwanza. Ila ukimuona leo hii alivyopendeza na suti yake pengine ya Mtani Nyamakababi utamjua? Kiatu chake kinanga'aa na tabasamu na kujiamini kunamfanya afunge madili ya mamilioni ya dola kwenye project zake mbali mbali. Huwezi ukaamini ndo yeye aliyekua anaenda kuchota maji mtoni kwa baiskeli siku nzima wakati nduguze wanaenda shuleni! Isaya alipambana, jarida la Forbes Africa lilimtaja kama ni moja kati ya vijana 30 walio chini ya umri wa miaka 30 ambao watakuja kuleta mabadiliko makubwa kwenye upande wa teknolojia na mpaka sasa yuko njia sahihi ya kulitimiza hilo kwa mujibu wa maongezi yetu haya. Isaya ametimiza miaka 30 mwezi wa kumi mwaka jana. Ukiachana na kigugumizi kikubwa ambacho naamini pia kilichangiwa na hasira nyingi alizokua nazo wakati mdogo na kukua nazo, Isaya ni muongeaji na natumai kwenye hilo utapata jambo la kujifunza na ku enjoy pia. Love, Salama. Follow: Twitter: http://twitter.com/YahStoneTown Instagram: http://Instagram.com/YahStoneTown Facebook: http://facebook.com/YahStoneTown --- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support

Salama Na
Ep. 21 - Salama Na Baraka | FAHARI TOKA ITETE

Salama Na

Play Episode Listen Later Jun 18, 2020 89:08


Mimi ni kama wewe tu juu ya ufahamu wa huyu mtu ambaye ameibeba Itete iliyopo kata ya Isuto tarafa ya Isangati, wilaya ya Mbeya vijijini mkoani Mbeya na Tanzania kwa ujumla, jina ni Baraka Adson Mpenja. Wengi humuita sauti ya radi, utamshi wake wa maneno na majina ya wachezaji na viongozi ni wa namna ya kipekee haswa, na bila ya shaka hiyo ndo tofauti kuuubwa kabisa kati yake yeye na watangazaji wengine wa kabumbu ikiwa pamoja na mimi hapa Tanzania. Ni kijana na ni maridadi na pia hajasahau wapi ametoka na ndoto zake ndo hizi ananoziishi sasa kwa mujibu wa maongezi yetu haya. Umaarufu wake si wa kulazimisha wala si wa skendo, kazi yake maridadi aifanyayo kwa ustadi wa hali ya juu ndo imemtambulisha kwetu hapa nyumbani na kanda nyengine za Afrika ambapo king'amuzi cha Azam kinafika. Burudani ambayo anaitoa huku akipeperusha umaarufu wa ligi kuu ya Tanzania bara na mashindano ya kimataifa ni ya mfano wa kuufuata hasa. Yangu hakika katika sajili bora ambazo AzamTV walishawahi kufanya basi ya Baraka Adson Mpenja inaweza ikawa ya kuokota dodo chini ya Mvinje. Basi umaridadi wake huo ndo ulotusukuma haswa sisi kumuita kwenye meza yetu, na akaja bila ya kusita. Tuliongea kuhusu chimbuko lake, ndoto zake jinsi anavyojifunza kila siku kutoka kwa wazoefu walomzunguka, masomo, ndoa, maisha kwa ujumla na mapenzi yake kwa mpira wa miguu. Ilikua matani na ung'amuzi mwingi wakati naongea naye na yangu matumaini uta enjoy. Love, Salama. Follow: Twitter: http://twitter.com/YahStoneTown Instagram: http://Instagram.com/YahStoneTown Facebook: http://facebook.com/YahStoneTown --- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support