POPULARITY
Tarehe 25 mwezi Aprili kila mwaka ni siku ya kimataifa ya wajumbe wanaowakilisha nchi zao kwenye Umoja wa Mataifa. Tarehe hiyo mwaka 1945 ndio ulianza mkutano huko San Francisco, Marekani wa wajumbe 850 kutoka nchi 50 waliopitisha Chata ya Umoja wa Mataifa ikilenga kusongesha amani, maendeleo, urafiki na haki za binadamu. Kama unavyofahamu Umoja wa Mataifa sasa umekua na idadi ya wanachama ni 193 na kila moja hupeleka wawakilishi kufanikisha utekelezaij wa malengo ya Umoja huo. Lengo la siku ni kuwatambua kwani wao ndio wamepewa jukumu la kufanikisha chata hiyo. Je wajumbe hao hufanya nini? Assumpta Massoi amezungumza na Balozi Yabesh Monari wa Kenya kwenye mada hii kwa kina.
Katika makala Flora Nducha wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa anazungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la ICCAO kutoka Tanzania, Zahra Salehe, mshiriki mwingine kutoka Tanzania anayehudhuria mkutano wa 69 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW69 unaoendelea hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, jijini New York Marekani.
Karibu katika Kipindi cha Maswali yahusuyo Imani ukiwa nami Frateri Jackob Venatus Mkandawile, Kutoka Seminari Kuu ya Mtakatifu Augustino Peramiho, nikijibu swali la Msikilizaji linalosema lengo la Jumuiya ndogo ndogo za Kikristo L'articolo Je, wafahamu lengo la Jumuiya ndogo ndogo za Kikristo? proviene da Radio Maria.
Leo katika makala Hamad Rashid wa Redio washirika KidsTime FM ya mkoani Morogoro Tanzania aanaangazia kuhusu namna Tanzania inaendelea kufanikisha Lengo Namba 16 la Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa linatilia mkazo upatikanaji wa amani, haki na taasisi imara kwa kupunguza mrundikano wa mashauri au kesi mahakamani, kuwezesha upatikanaji wa haki kwa makundi maalumu katika jamii.
Kipindi cha leo kimeangazia pakubwa droo ya mashindano ya CHAN 2024; adhari ya kuahirishwa kwa kipute na uchambuzi wa makundi. Pia tumetupia jicho raundi ya sita hatua ya makundi mechi za klabu bingwa Afrika, fainali ya mashindano mapya ya wasichana U17, Shujaa yataja kikosi chake cha mkondo wa Perth 7s, Kipchoge akilenga taji la tano la London Marathon, Tyson Fury astaafu ndondi kwa mara ya pili pamoja na mashindano ya tenisi ya Australian Open yakiingia hatua ya robo fainali. Kulingana na droo iliyofanyika Jumatano usiku katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Kenyatta (KICC) jijini Nairobi nchini Kenya, Harambee Stars imepangwa katika 'kundi la kifo' ambapo itamenyana na mabingwa mara mbili Morocco (2018 na 2020) na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (2009 na 2016)."Tuko kwenye kundi la kifo," Mariga alikiri, akibainisha uimara wa wapinzani wao."Hizo ni timu kubwa na inamaanisha lazima tuweke juhudi zaidi katika maandalizi."“Wapinzani wetu ni wagumu, tutashiriki mashindano haya kwa mara ya kwanza lakini haijalishi. Tuna wachezaji wazuri ambao wanaweza kutoa changamoto,” alijibu Kenneth Muguna, mmoja wa wachezaji muhimu katika kikosi cha sasa cha Harambee Stars.Pia katika Kundi A kuna Zambia na Angola. Kenya itakuwa mwenyeji wa mashindano haya yanayofanyika kila baada ya miaka miwili kwa wachezaji wa nyumbani pamoja na Tanzania na Uganda.Wenyeji wenza Tanzania wako katika Kundi B ambapo watamenyana na Madagascar, Mauritania, Burkina Faso na Jamhuri ya Afrika ya Kati.“Tusichukulie kundi hili kama jepesi, sisi kama wenyeji lazima tujitayarishe vyema ili tupite awamu ya makundi na hata kushinda kombe, “ alisema rais wa shirikisho la soka nchini Tanzania (TFF) Wallace Karia.Uganda wataongoza Kundi C ambapo watamenyana na Niger na nchi mbili ambazo zitatinga hatua ya mwisho ya mchujo. Mabingwa watetezi Senegal wataanzisha tena uhasama na Nigeria katika kundi D, ambayo pia ina Sudan na Kongo.“Tumecheza dhidi ya Guinea na Niger mara kadhaa, tunajua wanavyocheza. Tumefuzu mara ya nane mashindano haya, na hatujawahi kuaga mashindano kwenye makundi,” alieleza kwa msisimko Moses Magogo, rais wa shirikisho la soka (FUFA) nchini Uganda. Michuano hiyo yenye timu 19 ambayo awali ilipangwa kufanyika Februari 1 hadi 28, iliahirishwa hadi Agosti mwaka huu. Wasaidizi wa droo hiyo walikuwa wachezaji wa zamani - McDonald Mariga wa Kenya, Mrisho Ngasa wa Tanzania na Hassan Wasswa wa Uganda huku mkurugenzi wa mashindano wa CAF, Samson Adamu akisimamia mchakato wa droo.Katika ujumbe wake wa video kabla ya droo hiyo, rais wa CAF Patrice Motsepe alitoa shukrani zake kwa marais William Ruto (Kenya), Samia Suluhu Hassan (Tanzania) na Yoweri Museveni (Uganda) kwa ushirikiano wao kuhakikisha mashindano hayo yanafanyika kwa mafanikio."Ukarabati wa viwanja, viwanja vya kufanyia mazoezi, miundombinu, hoteli na hospitali katika nchi hizo tatu unaonyesha maendeleo makubwa na motisha, iliyodhihirika wakati wa ziara yangu," ujumbe wake Motsepe ulibainisha."Lengo lilikuwa kuunganisha mataifa matatu ya Afrika Mashariki, pamoja na mengine kutoka sehemu mbalimbali za Afrika."Waziri wa Michezo nchini Kenya Salim Mvurya alipamba hafla hiyo pamoja na wenzake kutoka Uganda na Tanzania, Peter Ogwang na profesa Palamagamba John Aidan Mwaluko.Droo KamiliKundi A: Kenya, Morocco, Angola, DR Kongo, ZambiaKundi B: Tanzania, Madagascar, Mauritania, Burkina Faso, Jamhuri ya Afrika ya KatiKundi C: Uganda, Niger, Guinea, Q2, Q1Kundi D: Senegal, Kongo, Sudan, Nigeria
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Syria, ambako viongozi wa ngazi mbalimbali za Umoja wa Mataifa wamendelea kusisitiza hitaji la kutanguliza ulinzi wa manusura na uhifadhi wa ushahidi wa uhalifu. Pia tunapata ufafanuzi wa neno na muhtasari wa habari.Karla Quintana kutoka Mexico ameteuliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres hii leo kuongoza Taasisi Huru ya kuchunguza watu waliotoweshwa nchini Syria, taasisi ambayo imeundwa na Baraza la Kuu la Umoja wa Mataifa mwezi Juni mwaka jana 2023. Guterres amewaambia waandishi wa habari hii leo kwamba yeye na timu yake lazima waruhusiwe kutekeleza kwa kina jukumu lao, na vile vile mifumo yote ya kimataifa ya kusongesha ulinzi wa haki za binadamu nchini Syria na uwajibikaji wa uhalifu uliotendwa lazima wawe na wanachohitaji ili kutekeleza majukumu yao muhimu.Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekuwa na kikao cha ngazi ya mawaziri kuhusu Akili Mnemba, au AI ambapo Katibu Mkuu António Guterres amesema pamoja faida kubwa ya teknolojia hiyo bado kuna changamoto iwapo haitasimamiwa vema na binadamu. Hivyo amependekeza kuundwa mwa mfumo wa kimataifa wa kuendeleza Akili Mnemba kwa uwiano na usawa, ukijikita kusaidia nchi zinazoendelea kuzuia kuibuka kwa pengo la teknolojia hiyo kati ya walio nayo na wasio nayo.Na huko Bunia, jimboni Ituri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemorkrasia ya Congo, DRC vijana 24 wakiwemo wanawake 6 wamenufaika na mafunzo ya siku tano ya mbinu za kisasa za kilimo kutoka walinda amani wa Bangladeshi wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo MONUSCO. Lengo ni kuwezesha kilimo kuwa chanzo cha kipato kwa wakazi na kuimarisha uchumi wa eneo hilo.Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mchambuzi wetu mlumbi wa Kiswahili Joramu Nkumbi kutoka nchini Tanzania, anafafanua maana ya neno “AKRABA.” Mwenyeji wako ni Flora Nducha, karibu!
Lengo namba 5 la Maendeleo ya Maendeleo Endelevu, SDGs, ya Umoja wa Mataifa ni usawa wa kijinsia ambao ni pamoja na kuwawezesha wanawake kiuchumi kwa kuwapatia fursa. Akiwa Havana Cuba hivi karibuni kwenye kongamano la kimataifa la Kiswahili Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili, alikutana na kuzungumza na Namayombo Nyanzala Mgonela, mwanamke mjasiriamali kutoka visiwa vilivyoko Karibea St. Kitts na Nevis ambaye anatumia fursa ya utamaduni wake mchanganyiko wa asili ya Visiwa hivyo na wa Kiswahili kujikwamua kiuchumi kupitia ubunifu wa mitindo na shughuli za mama lishe katika jitihada za kutimiza lengo hilo. Kwa kina zaidi tuungane na Flora Nducha.
Umoja wa Mataifa unasema kwamba vita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC imefanya taifa hilo kuwa pahala hatari zaidi duniani kwa watoto kuishi, kutokana na mateso ya kimwili na kisaikolojia wanayoyapitia. Kwa kutambua hilo walinda amani wanawake wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu kwenye ujumbe wa UN nchini humo, MONUSCO wamechukua hatua kuona watoto wanaishi kama watoto. Video ya MONUSCO ikianza na walinda amani wakijongea kwa jamii, Kapteni Noella Nyaisanga kiongozi wa kikundi hicho cha wanawake cha kikosi cha 11 cha walinda amani wa Tanzania kwenye MONUSCO, TANZBATT-11 anaeleza jinsi kikundi chao kinavyosogea kwa jamii na hasa watoto ili kutatua changamoto zinazowakabili kutokana na mapigano kati ya jeshi la serikali na waasi kwenye eneo hili la Beni, jimboni Kivu Kaskazini, mashariki mwa DRC. Anafafanua zaidi lengo lao.Lengo ni kujenga uaminifu kwa raia ambao tunawalinda. Kwa hiyo tukaamua kuandaa masomo shuleni, ambayo yataweza kuwaimarisha wao, kuwasaidia tatizo la kuwa wameathirika kisaikolojia.Zavadi Mbambu ni miongoni mwa walimu waliopatiwa mafunzo ya kusaidia watoto walioathiriwa na changamoto lukuki ikiwemo mapigano. Akisema stress, anamaanisha msongo.“Unakuwa na wanafunzi wanaokuwa na msongo wa mawazo kutokana na jambo ambalo wanaishi, na hata mauaji. Kuna wale ambao hata wameua wazazi wao , hata familia yao yote. Na kwa hao wanafunzi wanapoingia shuleni , wanakuwa kama hawako ndani, fikra zao zinakuwa mbali . Lakini kupitia mafunzo nimewaelewa , na tumejua namna gani ya kuishi nao. Na tayari mabadiliko yameanza kuonekana.”Pacifique Kyakimwa, mmoja wa wanafunzi anasimulia mkasa mmoja.“Kuna mwenzetu aliyekuwa na tatizo, yaani tukiwa ndani ya shule, alikuwa anacheka, yaani anatusumbua hadi hatumwelewi mwalimu. Lakini tangu wameanza kufundisha hili somo, wameanza kuelewa . Ameanza kuwa na akili inayotumika vizuri. Mafunzo haya yamefika wakati tunahitaji , na imetusaidia sana.”
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imeanza chanjo dhidi ya ugonjwa wa homa ya Nyani au MPOX mwishoni mwa wiki iliyopita. Hii ni hatua muhimu ya kuongeza juhudi zinazoendelea za kupambana na mlipuko wa ugonjwa huo ambao DRC inachangia asilimia 90 ya wagonjwa wote zaidi ya 18,000 duniani. Lengo sasa ni kuokoa maisha, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni, WHO, kanda ya Afrika. Shuhuda wetu wakati wa kuanza kazi ya kutoa chanjo alikuwa mwandishi wetu wa Mashariki mwa DRC, George Musubao kutoka Goma, jimboni Kivu Kaskazini.
Tiba Salama Digital Health App shirika la kijamii la lilalolenga kutumia teknolojia kutekeleza Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu, SDGs katika kutoa huduma za afya kwa wanawake wajawazito, wanaolea na watoto.Lengo kuu ni kupunguza na hatimaye kuondoa kabisa vifo vya wajawazito na watoto wadogo kwa kuoresha huduma za afya hususani kwa maeneo ya pembezoni yenye upatikanaji hafifu wa huduma za msingi za afya.Anold Kayanda wa Idhaa hii amezungumza Simon Mashauri, Mkurugenzi na Mwazilishi wa shirika hilo lenye makao yake makuu mkoani Tanga, kaskazini mashariki mwa Tanzania.
Ndoa ni nini pia Lengo la ndoa ni kitu gani
Ndoa ni nini pia Lengo la ndoa ni kitu gani
Yaliyomo kwenye Jarida la Habari za UN hii leo ni pamoja na ziara ya Katibu Mkuu wa UN huko Timor-Leste; maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kupinga majaribio ya nyuklia na kauli ya Mkurugenzi Mteule wa WHO kanda ya Afrika, Dkt. Faustine Ndugulile baada ya kuteuliwa. Mada kwa kina ni Morogoro Tanzania. Na pia kuna kujifunza lugha ya kiswahili. Karibu na mwenyeji wako ni Anold Kayanda.Nchini Tanzania katika mkoa wa Morogoro, ulioko mashariki mwa nchi hiyo, wakulima 50 kutoka skimu za umwagiliaji za Ifakara Dakawa mkoani humo na Mbarali mkoa wa Mbeya, kusini magharibi mwa Tanzania wamepatiwa ujuzi wa kutumia zana bora za kisasa za Kilimo cha mpunga ikiwemo zana za kusawazisha mashamba, kupanda mbegu na kuvuna. Lengo ni kuongeza thamani katika uzalishaji wa zao la mpunga. Mafunzo yaliyotolewa na Taasisis ya Utafiti wa Kilimo TARI kwa usimamizi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, FAO huku zana zikiwezeshwa na shirika la Korea Kusini la ushirikiano wa maendeleo, KOICA. Hamad Rashid wa Redio washirika Tanzania Kids Time FM mkoani Morogoro alifika kwenye skimu hiyo kuzungumza na wakulima walionufaika. Je wajua neno la kiingereza LINK tafsiri yake ni ipi kwa lugha ya Kiswahili? Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania anafafanua.
Lengo la ndoa
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Matangazo ya saa nzima kuhusu habari za kutwa, ikiwa ni pamoja ripoti kutoka kwa waandishi wetu sehemu mbali mbali duniani na kote Afrika Mashariki na Kati, na vile vile vipindi na makala maalum kuhusu afya, wanawake, jamii na maendeleo.
Shirika la Rotary Safe Families hutoa taarifa zaku saidia kuzuia unyanyasaji kupitia miongozo iliyo tafsiriwa pamoja na filamu.
Huu ni utangulizi wa msururu wa vipindi vya kutukuza kiswahili ambavyo vitaangazia kuongezea maarifa ya misamiati kutoka nyaja tofauti tofauti. Lengo kuu ni kukomaaza ufahamu kwa lugha hii tukufu katika miktadha mbali mbali za kimaisha. Karibu sana na kiswahili kitukuzwe!
Hatimaye Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametimiza ahadi yake ya kuunda Bodi ya Umoja wa Mataifa ya Ushauri wa Kisayansi wakati huu ambapo teknolojia ya Akili Mnemba au ‘Artificial Intelligence' imeshaanza kugonganisha vichwa vya watu kuhusu nafasi yake katika maendeleo duniani. Kwa mujibu wa Katibu Mkuu Guterres Bodi hii mpya aliyoiunda ni kwa ajili ya kuwashauri viongozi wa Umoja wa Mataifa kuhusu mafanikio katika sayansi na teknolojia na jinsi ya kutumia manufaa ya maendeleo haya na kupunguza hatari zinazoweza kutokea. Bwana Guterres anaamini maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia yanaweza kuunga mkono juhudi za kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu lakini pia yanaleta wasiwasi wa kimaadili, kisheria na kisiasa, wasiwasi ambao unahitaji ufumbuzi wa kimataifa. Bodi ya Umoja wa Mataifa ya Ushauri wa Kisayansi ambayo Bwana Guterres anaamini pia kuwa itaimarisha jukumu la Umoja wa Mataifa kama chanzo cha kuaminika cha data na ushahidi wa kisayansi itajumuisha kundi la Maprofesa wanasayansi saba mashuhuri duniani. Maprofesa hao ni Profesa Yoshua Bengio, Profesa Sandra Díaz, Profesa Saleemul Huq, Profesa Fei-Fei Li, Profesa Alan Lightman, Profesa Thuli Madonsela, na Profesa Thomas C. Südhof. Pia kundi jingine ni Wanasayansi Wakuu wa mashirika tofauti ya Umoja wa Mataifa, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Umoja wa Mataifa, na Mjumbe wa Katibu Mkuu kuhusu Teknolojia. Mmoja wa wanaounda Bodi hiyo, Profesa Yoshua Bengio, Mkurugenzi wa Kisayansi wa Taasisi ya Mila - Quebec AI ambaye pia ni Mkufunzi katika Chuo Kikuu cha Montréal anatoa ahadi akisema, “Uamuzi wa Katibu Mkuu wa kuanzisha Bodi ya Ushauri wa Kisayansi unasisitiza kujitolea bila kuyumba kwa viongozi wa Umoja wa Mataifa kwa kanuni za mbinu za kisayansi. Ninatazamia kumuunga mkono Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika kupaza sauti kwa ajili ya sera zinazotegemea sayansi na kufanya uamuzi.” Kupitia juhudi zao za ushirikiano, Bodi na Mtandao wake utawaunga mkono viongozi wa Umoja wa Mataifa katika kutazamia, kuzoea, na kutumia maendeleo ya hivi karibuni ya kisayansi katika kazi yao kwa watu, sayari na ustawi. Bodi itafanya kazi kama kitovu cha mtandao wa mitandao ya kisayansi. Lengo ni kuwa na muunganiko bora kati ya jumuiya ya kisayansi na kufanya uamuzi katika Umoja wa Mataifa. Kwa upande wake Bi. Ismahane Elouafi, Mwanasayansi Mkuu katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo anasema, "Kwa kuhakikisha kwamba sera na programu za Umoja wa Mataifa zimeanzishwa kwa msingi wa ushahidi na utaalamu bora wa kisayansi uliopo, Bodi itachukua jukumu muhimu katika kutatua matatizo changamano ya kimaadili, kijamii na kisiasa yanayowasilishwa na maendeleo ya haraka ya kisayansi na kiteknolojia." Ikumbukwe mwezi Julai mwaka huu, kwa mara ya kwanza Baraza la Usalama lilikuwa na mjadala mahususi kuhusu Akili Mnemba na mstakabali wake katika amani na usalama duniani na kabla yake, Katibu Mkuu Antonio Guterres kupitia moja ya matamko yake ya kisera ya Ajenda Yetu ya Pamoja, alitoa ahadi ambayo imetimia kwa kuunda Bodi hii ya kumshauri katika masuala ya kisayansi.
En este episodio charlamos con Lola Rodriguez, Lengo, Brian Sasbon, Fede Sarquis, team de Ethereum Argentina, sobre el evento de Ethereum Argentina. Nota: El evento fue grabado el 18 de julio de 2023, vía Twitter Spaces.
Mkutano wa kimataifa wa Women Deliver 2023 (WD2023) au wanawake wanatekeleza umekunja jamvi mwishoni mwa wiki mjini Kigali nchini Rwanda baada ya kuwaleta pamoja washiriki 6,000 ana kwa ana na wengine zaidi ya 200,000 mtandaoni. Lengo kuu la mkutano huo mkubwa kabisa uliozanza Julai 17 hadi 20 na kubeba kaulimbiu “Nafasi, mshikamano na suluhu” lilijikita katika ujumuishwaji ili kusongesha usawa endelevu wa kijinsia kwa kuhusisha sekta mbalimbali. Wadau wakiwemo wakuu wa nchi na serikali na mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo linalohusika na masuala ya wanawake UN-Women na la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA walikuwa mstari wa mbele katika mkutano huo Martha Wanza alikuwa miongoni mwa washiriki kutoka Kenya , anafanyakazi na shirika lijulikanalo kama Jumuiya ya wanawake vijana Wakristo nchini humo YWCA. Amezungumza na Eugene Uwimana Afisa uratibu msaidizi wa maendeleo, mawasiliano na mipango katika ofisi ya Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Rwanda , maswali yake ynarejewa studio na Flora Nducha na Martha akianza kwa kumfafanulia kuhusu shirika lao
Ikiwa leo ni siku ya kupinga matumizi ya tumbaku duniani shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO, limezitaka nchi kuacha kutoa ruzuku kwa kilimo cha tumbaku na badala yake kuunga mkono na kusaidia kilimo cha mazao endelevu yatakayoweza kulisha mamilioni ya watu wenye uhitaji wa chakula. Kupitia ujumbe wake wa siku hii mkurugenzi mkuu wa WHO Dkt. Tedros Ghebreyesus amesema “Tumbaku inawajibika kwa vifo milioni 8 kila mwaka lakini bado serikali duniani kote zitatumia mamilioni ya dola kuunga mkono mashamba ya tumbaku. Watu duniani kote wanakabiliwa na njaa wakati ekari milioni 300 za dunia yetu zinatumika kulima tumbaku.”Akaenda mbali zaidi na kusistiza kwamba “Ni wakati wa kubadili mwelekeo wa juhudi zetu na kujikita na kilimo ambacho kinastawisha siha yetu na mazingira yetu.”Hivi sasa kwa mujibu wa WHO zaidi ya watu milioni 300 duniani kote wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kutokuwa na uhakika wa chakula wakati ambapo Zaidi ya ekari milioni 300 katika nchi zaidi ya 120 duniani zinatumika kulima tumbaku hata kwenye nchi ambazo watu wana njaa kali.WHOWHO imesema tumbaku inagharimu maisha wa watu milioni 8 kila mwaka.Dkt. Tedros amesema WHO inafanyakazi kwa karibu na mashirika mengi ya Umoja wa Mataifa likiwemo la chakula na kilimo FAO na la mpango wa chakula duniani WFP kuwasaidia wakulima kuhamia kwenye kilimo mbadala wa tumbaku kwani “kwa kuchagua kulima chakula badala ya tumbaku tutatoa kipaumbele kwa afya, kulinda mfumo wa maisha na kuimarisha uhakika wa chakula kwa wote.”Lengo la maadhimisho ya mwaka huu ni kuujulisha umma hatari za matumizi ya tumbaku, mwenendo wa biashara wa makampuni ya tumbaku, nini kinachofanywa na WHO kupambana na janga la tumbaku na nini watu duniani kote wanaweza kufanya ili kudai haki yao ya afya, maisha yenye afya na kuvilinda vizazi vijavyo.Siku ya kupinga matumizi ya tumbaku duniani huadhimishwa kila mwaka Mei 31 na mwaka huu imebeka maudhui “Lima chakula sio tumbaku.”
Nchini Tanzania Shirika la lisilo la kiserikali la Girls Livelihood and Mentorship Initiative (GLAMI) kupitia Mradi wake wa Binti Shupavu, unaowajengea Stadi za Maisha ikiwemo uwezo wa kujitambua, mabinti walioko Shule, unaendelea na juhudi za kufanikisha Lengo la Nne la maendeleo endelevu SDG's linalohusu Elimu, ambapo Jumla ya wasichana 824 wananufaika kutoka katika Shule Tisa zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini, ambapo Mwezi huu wa Tano limekamilisha Programu ya kufanya vikao na wazazi katika Shule hizo ili kuwajengea uwezo wa malezi ya watoto wao. Hamad Rashid wa Redio washirika MVIWATA FM kutoka Morogoro, mashariki mwa Tanzania amehudhuria baadhi ya vikao vya wazazi na GLAMI kisha kutuandalia makala ifuatayo.
On this Episode, I have returning guest, Andrew Lee, back on the podcast!! Andrew and I talk about some of his latest work in media and videography, working with Hmong Artists like Huab Vwj and Win Vang, discuss our hot takes on Hmong Events and more! FOLLOW Andrew Lee at:Facebook - https://www.facebook.com/LengoMedia.AndrewLee/YouTube - https://youtube.com/@lengomediaLIKE, SHARE, RATE, SUBSCRIBE, COMMENT and FOLLOW Spoiler Force Podcast!! You can find more content at:https://linktr.ee/SpoilerForcePodcastYouTube - https://www.youtube.com/spoilerforcepodcastApple Podcasts - https://podcasts.apple.com/us/podcast/spoiler-force-podcast/id1465655015Spotify - https://open.spotify.com/show/3edg2bpJPr85Qwry6kzvOrSoundCloud - https://www.soundcloud.com/spoilerforcepodcastAny kind of guest recommendations, comments, questions, concerns or criticisms can be sent to rickyvang92@gmail.com. I might even respond to your message in a future podcast episode!!Don't Forget to Join the Spoiler Force Discord Community!!Support Spoiler Force Podcast! ALL Tips and Donations will be used for podcasting needs such as Booking Guests, Equipment and Software!https://streamlabs.com/spoilerforcepodcast1/tipIf you want to start your very own Podcast, go tohttps://www.buzzsprout.com/?referrer_id=1059248 and sign up for free!If you want a simpler way to record your Audio or Video Podcast, go to https://streamyard.com/pal/6037820492218368 and sign up to earn a $10 credit!Music from #Uppbeat (free for Creators!):https://uppbeat.io/t/sensho/glow#SpoilerForcePodcast #LengoMedia #Hmong #HmongArtist #HuabVwj #WinVang #Music #Artist #Production #Media #Videography #Photography #PressSupport the show
Ufumbuzi wa ubunifu wa maji unaotumia teknolojia ya nishati ya jua ambao unafanikishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na wadau wake ukiwemo ule wa utekelezaji, Water Mission, na ule wa kutoa msaada wa fedha Grundfos Foundation kutoka nchini Denmark umesaidia serikali ya Tanzania kubuni suluhisho la msingi na la kudumu la maji katika jamii 15 za mkoa wa Kigoma ulioko magharibi mwa taifa hilo la Afrika Mashariki. Lengo lao kubwa ni kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama kwa watu 99,107 mkoani humo ifikapo Machi 2024. Miongoni mwa wanufaika ni jamii, wanafunzi na wahudumu wa afya katika hospitali, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikumbwa na changamoto za ukosefu wa maji na migogoro kati yao inayotokea mara kwa mara wakati kundi kubwa la watu linapokutana katika mto moja ulioko mbali kuteka maji. Hali ilikuwa vipi kabla na baaannoda ya mradi huo? Ungana basi na Selina Jerobon katika makala hii iliyofanikishwa na UNICEF.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na serikali ya Uganda kupitia msaada wa serikali ya Ireland, unawapa fursa ya pili ya kurejea shuleni wasicha waliopata ujauzito na waliojifungua kabla ya kumaliza masono katika jimbo la Karamoja nchini Uganda. Lengo kuu la mradi huo ni kuhakikisha hakuna msichana yeyote anayesalia nyuma kielimu hata kama amekuwa mama katika umri mdogo.Jimbo la Karamoja lililoko Kaskzini Mashariki mwa Uganda linakabiliwa na changamoto kubwa ya wasichana kupata mimba za utotoni na wengi hujikuta wakikatisha ndoto zao za kuendelea na masomo baada ya kujifungua. Lakini sasa mradi wa UNICEF wa “Kutomwacha msichana yeyote nyuma” umewapa nafasi ya pili ya kutimiza ndoto zao kielimu. Joyce Opel ni mwalimu mkuu katika shule ya Napak ambayo ni miongoni mwa shule zinazoshiriki mradi huo wa UNICEF anasema, “Nina kina mama hawa wenye umri mdogo13 , lakini wanapaswa kuwa 17, bado nasubiri wengine kujiunga, baadhi yao walipewa mimba na kutelekezwa bwana zao hawako wamebaki wakilea watoto peke yao, na hicho ndicho kilichonisukuma Kwenda kuongea nao , na nikisha ongea nao na wakaelewa wanarejea shuleni"Ameongeza kuwa pamoja na fursa hiyo kuna changamoto, “Changamoto zinazowakabili kina mama hawa wadogo shuleni ni moja, watoto wao wakiugua basi inabidi wakose masomo, na ndio maana nawachagiza waalimu kuwavumilia ili wakati wanaporejea basi wawasaidie kuanzia pale walipoishia.” Mradi huu umeleta tija Karamoja kwani kufikia mwishoni mwa mwaka 2022 julma ya kina mama watoto 1226 na wasichana wajawazito 296 walisaidiwa kurejea shuleni jimboni humo. kwa mujibu wa Sambey Logira mtaalam wa elimu wa UNICEF “miongoni mwa wasichana hao waliorejea shuleni walifanya mitihani ya kumaliza elimu ya msingi na walifanya vizuri kuliko hata wale waliokuwepo shuleni wakati wote. Na tumaini ni kuhakikisha wanapiga hatua nyingine zaidi katika elimu yao.”. La msingi kwa Solome Aisia ambaye ni mkufunzi katika kituo cha uratibu wa mradi huo Napak ni kutowahukumu wasicha hawa kwa kufanya makosa ya kuzaa utotoni”...anassema ni muhimu sana kutoangalia makosa ya mtu bali suluhu au jinsi gani ya kumsaidia mtu huyo, na daima kuna fursa ya pili. Kama tusingewapa kina mama hawa watoto fursa basi tungekuwa tumewapoteza.” Kwa UNICEF lengo ni kuhakikisha mradi huu unawafikia wasichana wengi zaidi na kurejesha matumaini na ndoto zao za maisha.
Ujumbe wa mashirika ya Umoja wa Mataifa umetembelea hospitali na kliniki zinazoungwa mkono na shirika lisilo la kiserikali la Misaada na Maendeleo la Syria au SRD, Kaskazini Magharibi mwa Syria na kujionea athari za tetemeko la Ardhi lililoikumba nchi hiyo wiki mbili zilizopita pamoja na kujionea usambazaji wa misaada iliyotolewa na Umoja wa Mataifa.Lengo la ziara hiyo iloyohusisha mashirika saba ya Umoja wa Mataifa ni kufanya tathmini ya mahitaji na kusambaza misaada.Mashirika ya UN katika ziara hiyo maalum ni lile la Kuratibu Masuala ya Kibinadamu -OCHA, la Uhamiaji IOM, la Idadi ya watu duniani na Afya ya Uzazi- UNFPA, la Kuhudumia Watoto UNICEF, la Afya duniani -WHO, la Kuhudumia Wakimbizi -UNHCR pamoja na Idara ya Usalama na ulinzi ya Umoja wa Mataifa UNDSS.Wakiwa Kaskazini – Magharibi mwa Syria ujumbe huo ulizungumza na wananchi walionusurika kwenye tetemeko. Akijitambulisha kwa jina moja tu, Muhammed aliwaeleza hali ilivyokuwa."Watoto wangu walikuwa wamelala kwenye ghorofa ya pili. Nilihisi mtikisiko na harufu ya vumbi. Nilikuwa na uhakika kwamba gorofa ya juu ingetuangukia, kisha nikashukuru nilipoona watoto wangu wakikimbia. Jengo lililokuwa mbele yetu liliporomoka. Tulitoka nje na kulikuwa na mvua na radi. Ilikuwa baridi. Umeme ulikatika.”Kisha wakatembelea hospitali na zahanati zinazoungwa mkono shirika lisilo la kiserikali la SRD. Wakiwa katika hospital ya Al-Refah, Daktari Ahmad Jumaa aliwaeleza hali ilivyo.“Tangu mwanzo wa tetemeko la ardhi, tulijaribu kuwapokea watu wote waliojeruhiwa. Ndiyo hospitali pekee inayofanya kazi hapa Jandairis. Tulijaribu kusaidia kila mtu kwa uwezo wetu mdogo na mpaka sasa tunaendelea kujaribu kusaidia majeruhi wote wanakuja hapa wakiwa wamefungwa bandeji na majeraha yaliyoshonwa.”Mbali na kutembelea hospitali nyingine ya Muhammad Wassim Maazi, wajumbe wa ziara hiyo walitembelea bohari inayofanya usambazaji wa misaada iliyotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO, misaada ambayo inajumuisha vifaa vya dharura vya majeraha na upasuaji na dawa mbalimbali za kusaidia waaathirika wa tetemeko.
Somalia! Somalia! Somalia! Kila uchao changamoto zinazidi kukumba wananchi wake kutokana na sio tu ukosefu wa usalama katika baadhi ya maeneo, bali pia madhara ya mabadiliko ya tabianchi. Hivyo ni vichocheo vya mamia ya maelfu ya watu kukimbia makwao na kusalia wakimbizi wa ndani.Sasa hivi karibuni baadhi ya wakimbizi hao wa ndani walipata ugeni kutoka kwa Mshauri Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa kusaka majawabu ya hali ya ukimbizi wa ndani Robert Piper! Lengo ni kujionea hali halisi na kisha kusaka suluhu hizo. Nini amejionea? Na mwelekeo ni upi sasa? Ungana basi na Anold Kayanda katika makala hii.
Lengo namba 16 la malengo ya maendeleo endelevu SDGs yaliyopitishwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa mwaka 2015 linasisitiza amani, haki na taasisi thabiti. Uvunjivu wa amani utokanao na migogoro kwenye jamii ni moja ya maeneo yanayomuikwa ili kuhakikisha amani inakuweko na hivyo kuwezesha kufikia SDGs mwaka 2030.Nchini Tanzania, wiki ya sheria imefungua pazia na Mahakama Kuu inatimiza wajibu wake kusaidia nchi kufanikisha SDGs. Mathalani mkoani Morogoro, Mashariki mwa taifa hilo, Mahakama Kuu imesema sasa itasongesha zaidi elimu ya usuluhishi na haki kwa lengo la sio tu kujenga amani bali pia kuchochea uchumi. Je nini kinafanyika? Hamad Rashid wa Redio washirika MVIWATA FM alikuwa shuhuda wetu na ameandaa makala hii,
Umoja wa Mataifa unatambua kuwa elimu ina uwezo mkubwa wa kumuinua mtu kiuchumi na kijamii, kwa maana ya kwamba ni silaha mujarabu ya kuondokana na umaskini. Kupitai malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, hususan lengo namba 4, Umoja wa Mataifa unataka elimu bora tena isiyomwacha mtu yeyote nyuma, kwa misingi ya rangi, eneo aliko au hali ya mwili wake. Tayari nchi na mashirika ya kimataifa na yasiyo ya kiserikali yanafanikisha lengo hilo, mfano humo nchini Tanzania katika mkoa wa Morogoro ulioko mashariki mwa taifa hilo la Afrika. Shirika moja kutoka Korea Kusini kwa ushirikiano na shirika la SAWA Tanzania wamefanikisha uwekaji wa vifaa kwenye maktaba ya mtandao au eLibray katika shule ya awali na msingi ambayo ni jumuishi na sasa walimu, wazazi na wanafunzi wameona nuru. Nini kimefanyika? Basi shuhuda wetu ni Hamad Rashid wa Radio WAshirika MVIWATA FM kutoka Morogoro nchini Tanzania.
Nchini Kenya shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake, UN Women kwa ushirikiano na wadau wanajengea uwezo wajenzi wa amani mashinani hata kwenye maeneo yenye changamoto kama vile kambi ya wakimbizi ya Daadab kwenye kaunti ya Garissa nchini humo kwa lengo la kuepusha vijana kutumbukizwa kwenye vikundi vyenye msimamo mkali. UN Women inafanya hivyo kupitia warsha inazoendesha kwa ushirikiano na mashirika ya kiraia ya wanawake kama vile WomanKind Kenya ambapo katika moja ya warsha huko kambini Daadab, Nimo Dubat, mwenyekiti wa chama cha wanawake wachuuzi sokoni anaelezea umuhimu wa warsha hizo akisema, “kwa upande wa usalama, wanawake na vijana ndio wanaweza kufuatilia, sisi ndio vijana tumezaa na tunajua ambaye anaanza kuleta shida nyingi. Katika watoto wetu, mama ndiye mzazi, mama ndiye anajua ambaye anaanza tabia mbaya. Mama ndiye anajua nani ameingia kwenye mtaa mgeni, na nani Jirani yake amepokea mgeni, hata tumetengeneza kikundi cha wanawake wa nyumba 10. Hata kuna wasichana wajumbe wa nyumba 10. Sasa tunataka tupatiwe nguvu, tushikamane na polisi kwenye ulinzi. Mama ndiye anabeba mzigo wa shida yote. NasibaAbdi Farah mkazi wa Daadab na mnufaika wa warsha hiyo iliyojumuisha wanaume na vijana wa kike na wa kiume, hakuficha hisia zake akisema kupitia mafunzo waliyopata akisema kuwa "yule kijana ambaye sitamuona nitauliza kwa wenzake ameenda wapi? Ameenda mpakani? Basi nitaenda kwa mama na kumuuliza mtoto wake ameenda kufanya nini mpakani? Akisema sijamuona? Namueleza tafuta kijana wako na umlete.” Warsha hii ilipatia fursa pia viongozi wa eneo la Daadab kushirkiana na mashirika yenye mtazamo sawa kupitisha na kuridhia na kuanza kutekeleza Mpango wa Utekelezaji wa Kaunti ya Garissa wa kuzuia na kukabiliana na misimamo mikali.
Lengo la vijana wengi wanao cheza mpira wa miguu nchini Australia, nikuwa wachezaji wakulipwa na hata kushiriki katika michuano yakimataifa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabili madawa ya kulevya na uhalifu, UNODC, Ghada Waly amesema pamoja na kufanya tafiti za kuelewa vema uhusiano kati ya uhalifu wa kupangwa na ugaidi barani Afrika, ni muhimu pia kuwa na sera na miradi ya kukabili vitendo hivyo haramu. Taarifa ya Ibrahim Rojala wa Televisheni washirika Mamlaka TV kutoka Tanzania inafafanua zaidi. Bi. Waly amesema hayo wakati akihutubia kwa njia ya video mjadala wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu amani na usalama barani Afrika, hususan kuimarisha mapambano dhidi ya usafirishaji haramu wa maliasili ambao hufadhili makundi yaliyojihami na magaidi. Na ndipo Idhaa ya Umoja wa Mataifa ikataka ufafanuzi zaidi kufahamu iwapo UNODC inashirikisha jamii kwenye miradi kama njia ya kukabili usafirishaji haramu wa maliasili ambapo Bi. Waly akataja vijana! “Asilimia 60 ya watu wengi barani Afrika wana umri wa chini ya miaka 25. Vijana ndio mustakabali wa bara hili na pia ndio wako hatarini zaidi. Lakini tunafahamu pia kuwa wakiwezeshwa, vijana hawa hawa ni waleta mabadiliko, wanaweza kujenga mustakabali bora, na kuchechemua kwa niaba yao, na kwa niaba ya jamii yao na pia kulinda maliasili.” Akatolea mfano moja ya mradi wanaotekeleza kwa pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni kupitia mfuko wa ujenzi wa amani , “Tunajengea uwezo vijana kuwa wajenzi wa amani kwenye maeneo ya mipakani ya Gabon, Cameroon na Chad. Lengo la mradi huu ni kujenga mtandao wa vijana 1800 wajenzi wa amani, ili hatimaye wawe watendaji katika kuzuia mizozo, ujenzi wa amani kwenye maeneo ya mpakani, na kuwawezesha kuibua mbinu mbadala za kujipatia kipato kwa jamii za mipakani.” Kwa mujibu wa mkuu huyo wa UNODC, biashara haramu ya pembe za ndovu pekee huzalisha kipato haramu cha dola milioni 400 kila mwaka. Afrika ikiwa na idadi ya watu takribani bilioni 1.3, kati yao milioni 500 mwaka jana waliishi kwenye ufukara na kwamba biashara hiyo haramu inapora Afrika mapato, sambamba na watu wanaotegema maliasili hizo fursa ya kujipatia kipato, na wakati huo huo huchochea mizozo na ukosefu wa utulivu.
Wanaume kote duniani mara nyingi huwa wana lalamikia uhaba wa huduma, namashirika yanayo toa huduma zinazo walenga.
Asasi isiyo ya kiserikali ya TEDI Tanzania, katika kutekeleza Lengo namba 4 la Maendeleo Endelevu linalohusu elimu bora, imeamua kulitekeleza lengo hilo kupitia kampeni yao ya kuishawishi serikali na wadau wengine kuboresha ubora wa elimu nchini Tanzania kuanzia ngazi ya msingi hadi taasisi ya elimu ya juu kwa kuziba pengo kati ya nadharia na vitendo kupitia kuunganisha ujuzi wa vitendo ambao hautolewi katika mtaala wa kawaida wa elimu elimu. Gloria Anderson, Mkurugenzi wa shirika la TEDI Tanzania ambalo linahamasisha elimu inayoendana na hali ya sasa ya sayansi na teknolojia ili kuwaandaa wanafunzi kuanzia ngazi za chini kuweza baadaye kujiajiri na kuajiriwa, akiwa katika safari ya mafunzo na kazi hapa Marekani, kupitia mahojiano haya na Anold Kayanda wa Idhaa hii, anaanza kwa kueleza hatua ambazo wameshazipiga nchini Tanzania.
Katika kutekeleza lengo namba 8 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kuhusu ajira za staha na ukuaji kiuchumi sambamba na namba 5 la usawa wa kijinsia, shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo duniani FAO nchini Tanzania, limezindua tawi la tatu la Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi TAWFA kupitia mradi wake wa kukuza mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi katika ziwa Tanganyika. Devotha Songorwa wa Radio Washirika KIDS Time FM ya Morogoro nchini Tanzania ameshuhudia uzinduzi na kuandaa taarifa hii. Sherehe za uzinduzi huo zimefanyika mkoani Kigoma nchini humo ambapo wanawake wavuvi, viongozi wa serikali na wafanyakazi wa FAO walifungua rasmi tawi hili ikiwa ni la tatu nchini humo baada ya mwengine mawili yaliyozinduliwa huko kanda ya Ziwa Victoria na Ukanda wa Bahari ya Hindi. Uzinduzi huo unafanyika kupitia mradi wa FISH4ACP unaotekelezwa katika mikoa ya Kigoma, Rukwa na Katavi ambapo Mratibu wa Sekta ya Uvuvi Kitaifa kutoka FAO, Oliva Mkumbo akizungumza na Devotha Songorwa wa Redio washirika wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa alimueleza lengo ni kuwawezesha wanawake kiuchumi kupitia uvuvi ili kuinua kipato cha familia na kuondokana na umasikini. “Lengo la kuanzisha jukwaa la wanawake ni kuwawezesha kina mama ili mchango wao utambulike na kuleta athari chanya katika jamii. Tunataka kila mwanamke anayejihusisha na mnyororo wa thamani katika uvuvi anakuwa na sehemu ya kutoa mawazo yake na kubadilishana uzoefu ili kwa pamoja wachangie uboreshaji wa uvuvi,” Anasema Oliva. UN News Oliva Mkumbo Mratibu wa Sekta ya Uvuvi Kitaifa kutoka FAO Mratibu huyo wa FAO amesema hili halitakuwa tawi la mwisho nchini humo. “Jukwaa rasmi kitaifa lilifunguliwa 2017 ili kuwafikia wanawake wengi wakaanzisha Zone Chapters, Chapter ya Kanda ya Ziwa Victoria 2019, baadaye ikaja ya Uvuvi baharini, Kanda ya Ziwa Tanganyika na baadaye huko tutakuwa na linguine linalohusika na wavuvi kutoka katika maziwa madogo madogo,” Ameeleza Mratibu huyo. Beatrice Mmbaga ni Mwenyekiti wa Taifa wa Mtandao wa Wanawake Wanaojihusisha na Shughuli za Uvuvi Tanzania (TAWFA) anasema jukwaa hili ni sehemu ya kutatua changamoto zinazowakabili kina mama walio katika sekta ya uvuvi. “Nia ya kuanzisha chombo hiki ni kumfikia mama popote alipo anayejishusisha na samaki na mazao yake Tanzania nzima ndipo sasa tunashuka ngazi za chini katika Mikoa yetu, Kanda na Wilaya ili tuwe na sauti moja kwa sababu kina mama ndiyo asilimia kubwa wanajihusisha na samaki baada ya mavuvi hasa kwenye kuchakata na masoko lakini wana changamoto nyingi sana,” amebainisha Mwenyekiti huyo. UN News Wanawake wajasiriamali katika sekta ya Uvuvi Tanzania Kwa upande Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia masuala ya Udhibiti Ubora na Mazao ya Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Steven Lukanga amebainisha kwamba wanawake bado wanahitajika kupatiwa elimu ya uvuvi salama na kukidhi mahitaji ya walaji. “Kikubwa ni kuwajengea uwezo wanawake kutambua viwango vinavyopaswa kuzalisha yale mazao yanayowaendea walaji kwa kuzingatia viwango vilivyopo chini ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwahiyo sisi kama wizara tunashirikiana nao kuhakikisha wachakataji wanawake wanakidhi viwango vinavyotakiwa,”Amesema Lukinga.
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kuzuia kuzama majini duniani Shirika la Umoja wa Afya duniani WHO limetoa wito kwa watu wote duniani kuongeza juhudi za kupunguza vifo vitokanavyo na watu kuzama kwenye maji, huku likitoa mapendekezo sita ya kusaidia kupunguza vifo na ajali zinazosababishwa na watu kuzama majini duniani kote. Leah Mushi na maelezo zaidi. “Fanya jambo moja kuzuia kuzama” ndio kauli mbiu ya mwaka huu ya Siku ya Kimataifa ya kuzuia kuzama ikiwa ni moja ya sababu kuu ya vifo ulimwenguni kwa watoto na vijana wenye umri wa kati ya mwaka 1 mpaka miaka 24 na vilevile ni sababu ya tatu ya vifo vinavyohusiana na majeraha kwa ujumla. Taarifa iliyotolewa na WHO kutoka Geneva Uswisi imeeleza kuzama kunasababisha vifo vya zaidi ya watu 236,000 kila mwaka na asilimia 90 ya vifo hivyo vikitokea katika nchi zenye kipato cha chini na cha kati huku watoto walio chini ya umria wa miaka mitano wakiwa katika hatari kubwa zaidi. Sababu za watu kuzama majini Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa WHO Dkt.Tedros Adhanom Ghebreyesus sababu kubwa vya vifo hivi ni watu kwenda kuteka maji kwa ajili ya matumizi ya kawaida nyumbani, watu kwenda kuogelea, watu kusafiri kwa njia ya maji kwakutumia boti na meli pamoja uvuvi bila kusahau athari za hali mbaya ya hewa ikiwa ni pamoja na mafuriko. Dkt Tedros ameeleza kuwa “Vifo hivi vinaweza kuzuilika kupitia kutafuta suluhu za msingi zenye ushahidi n aza gharama ya chini. Leo miji na majiji mengi ulimwenguni yatawasha taa yenye mwanga wa rangi ya bluu kuandishiria wito wa kuchukua hatua za kuzuia na kukomesha watu kuzama.” Ubia na Bloomberg na wadau wengine WHO imesema katika kuzuia vifo vitokanavyo na kuzama wameungana na shirika la Bloomberg pamoja na washirika wengine katika kuhamasisha kutelekeza suluhu zitakazozuia watu kuzama na wametangaza mapendekezo sita ambayo ni kuweka vizuizi vya kudhibiti upatikanaji wa maji, kutoa mafunzo ya kuogelea kwa wanaotazama waogeleaji, kufundisha watoto walio katika shule za msingi kuogelea na usalama wa maji, kutoa huduma ya usimamizi mahala ambapo watoto wanaogelea, kuweka kanuni salama kwenye maboti, meli na feri , kuboresha udhibiti wa hatari za mafuriko. Lengo la Kaulimbiu Kauli mbiu ya mwaka huu ya mwaka huu ni “Fanya jambo moja “ili kuzuia kuzama imelenga kila mwana jamii kwa kuweka katika makundi matatu, lakwanza ni mtu binafsi kujilinda usizame kwa kujifunza kuogelea na kushauri wanafamilia kufanya hivyo, pili kikundi cha watu kufanya kampeni za kutoa elimu ya kujilinda usizame na tatu ni serikali za kila nchi kuweka será za kuzuia kuzama na kuweka ahadi za kusaidia programu za kuzuia kuzama.
Kufuatia mauaji ya raia huko jimboni Tambura nchini Sudan Kusini katika kipindi cha miezi sita iliyopita na zaidi ya wakazi elfu 80 kulazimika kukimbia makazi yao, ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo UNMISS unaendesha doria za mara kwa mara jimboni hapo huku ukitoa ulinzi kwa maelfu ya raia walioyakimbia makazi yao. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi Video ya UNMISS ikionesha watoto wakicheza mtaani kwa furaha, huku wanajamii wengine wakiendelea na shughuli za kila siku kama vile kubeba kuni kwa ajili ya kuuza na kutumia nyumbani. Lakini haya si makazi yao ya kila siku, hapa ni kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Tambura na Margret Mathew mama wa watoto saba anasema hawatamani kukaa kambini hapo lakini hana namna nyingine kwakuwa yeye na watoto wake nyumba yao imeharibiwa. ”Hatutamani kubaki kambini hapa wala kwenye hema hizi. Tunachohitaji ni amani kamili ili tuweze kurejea majumbani kwetu. Haya ndio mambo madogo madogo wanawake wa Tambura tunayolilia. Tulipokimbia kutoka maeneo yetu Umoja wa Mataifa ulitupatia msaada wa kibinadamu. Tunatamani kurudi nyumbani.” Na kuna wale ambao waliamua kukata shauri na kuondoka kambini hapo kurejea kwenye vijiji vyao baada ya UNMISS kuendesha doria na kuimarisha ulinzi wamekuta makazi yao si kama walivyo yaacha, wamekuta mashamba yameharibiwa, mali zimeporwa na nyumba zimeteketezwa kama anavyoeleza Lucia Edward aliyerejea katika kijiji chake cha Nabanga. “Tulikuwa mafichoni, vita ilipotulia tuliamua kurejea nyumbani mwezi Desemba mwaka 2021. Tulipoteza riziki zetu zote wakati huo wa shida, angalau mashirika ya kibinadamu yalituleta dawa katika vituo vya afya lakini tuna uhaba wa maji, zana za kilimo na mbegu. Msimu wa mvua umeanza na tunanyeshewa na mvua kwani hatuna hata karatasi za kufunika nyumba zetu zinazovuja.” Pamoja na kuendeleza doria UNMIS inaamini amani ya kudumu itapatikana katika eneo hilo na watu wote waliokimbia makazi yao wataweza kurejea kwenye jumuiya zao. Akiwa ziarani mjini Tambura Naibu Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya kisiasa nchini Sudan Kusini Guang Cong amesema wana vipaumbele vitatu vya kusaidia kupunguza mzozo wa Tambura. “Hali ya usalama imeendelea kuimarika hapa Tambura. Kwa UNMISS maeneo yakipaumbele kwetu ni matatu kwa miezi michache ijayo. Lakwanza ni kuunga mkono kuimarisha uwezo wa kamati ya amani ya eneo la Tambura. Pili ni kusaidia mchakato wa mazungumzo ya upatanisho kati ya jamii ya Azande na Balanda, na tatu ni kuzindua mpango wa kupunguza unyanyasaji kayika jamii unalolenga zaidi vijana 200 ndani na nje ya Tambura ili waweze kujifunza stadi za ufundi stadi, waweze kujikimu kimaisha na kuboresha Maisha yao.” Wakimbizi hao wa ndani wameiomba serikali yao kuimarisha ulinzi ili waweze kurudi makwao.
Metaphorosis magazine - beautifully written science fiction and fantasy
Lengo's only grandson, Nikolas, committed the unthinkable: murder/suicide. And while she still struggles to come to terms with this tragedy, an old friend of Nikolas appears at her door. What follows at his heel: Truth, revenge, redemption, or even more death? Narrated by host Matt Gomez. Published in Metaphorosis on 13 May 2022. Find the original at magazine.metaphorosis.com.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, MINUSCA umezindua kampeni ya ulinzi wa raia ili kusaidia upatikanaji wa amani pamoja na kuwezesha mamlaka za serikali nchini humo kutekeleza majukumu yake.
Kuelekea kuanza kwa Kikao cha 21 cha Jukwaa la kudumu la Umoja wa Mataifa la watu wa asili ambalo litaanza Jumatatu wiki ijayo kwa kuwakutanisha katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jamii za watu wa asili, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limeutumia mfano wa watu asili wa wa jamii ya Warao wa Venezuela walioko ukimbizini Brazil, kuonesha kuwa watu wa asili ni miongoni mwa makundi yanayoathiriwa zaidi na mizozo inapotokea katika jamii. Evarist Mapesa wa Redio washirika SAUT FM ya Mwanza Tanzania anaisoma taarifa hii. Brazil ni mwenyeji wa zaidi ya wakimbizi na wahamiaji 300,000 kutoka Venezuela, ambao wamekimbia uhaba mkubwa wa chakula na dawa na kuongezeka kwa mfumuko wa bei na ukosefu wa usalama nchini mwao Venezuela. Takriban watu 7,000 kati ya wakimbizi hao 300,000 walioko Brazil ni Warao, watu wa asili ambao wengi wao walifika Brazil wakiwa maskini na wenye utapiamlo. Raia hawa wa Venezuela wanakabiliwa na vikwazo vikali linapokuja suala la kukidhi mahitaji yao ya kimsingi na kuzoea maisha ya Brazili. Katika nchi ya Brazil ambayo inayozungumza Kireno, mara nyingi wanakabiliana na kizuizi cha lugha mbili, kwani wengi, hasa Warao wenye umri mkubwa, wanazungumza tu lugha yao ya asili na hata lugha ya kihispania inayozugumzwa katika nchi yao Venezuela, hawaielewi vizuri. Mmoja wa watu hawa wa asili wa jamii ya watu wa Warao ni Marcelino Moraleda, kiongozi wa Jamii na muhudumu wa afya. Ujuzi na uelewa wa Marcelino unahitajika sana kwa wakimbizi wenzake. “Kazi yangu ni kuwachukua Warao wenzangu na kufuatilia hali yao ya lishe. Lengo ni kupunguza hatari zozote za kiafya za Warao kukaa kwenye makazi hayo.” Marcelino ameiambia UNHCR. Marcelino anasimulia kuwa kabla ya kuhamia hapa katika makazi maalum ya wahamiaji hawa katika eneo la Manaus na kupata usaidizi kutoka kwa Umoja wa Mataifa, walikuwa na hali mbaya hata ya kukosa mlo lakini sasa hali imebadilika, anasema, "hatushughulikii tena matatizo ya utapiamlo. Ninajitahidi kuboresha afya ya Warao mwenzangu. Tuna msemo katika Warao: "Nobarana ja takitane". Yaani Ili kuepuka kuugua." UNHCR inaenda mbali zaidi kiasi imekuwa ikifanya kazi na wadau na vyuo vikuu katika mkakati wa kuwasaidia wakimbizi na wahamiaji wanaoishi nchini humo kuthibitisha viwango vyao vya elimu na vyeti vingine vya kitaaluma. Kiujumla, Marcelino kwa niaba ya wenzake anaishukuru UNHCR akisema, "Wafanyakazi wa UNHCR hutufanya tujisikie salama, pamoja na mashirika mengine ambayo yanatuunga mkono kila wakati, yanatuunga mkono kila wakati."
In this episode, we sat down with Dr. Enoch Kariuki – former CEO at Lengo Therapeutics, CFO at VelosBio, and SVP of Corporate Development at Synthorx. We explore Enoch's upbringing in Kenya and how a family member's battle with HIV inspired his pursuit of a career in healthcare. We also dive into Enoch's journey as a biotech executive at three separate start-ups, all of which were acquired. Enoch is based in San Diego, CA.
Pamoja na uwepo wa lengo namba tano la Umoja wa Mataifa linalosisitiza kupatikana haki sawa kwa jinsia zote, hali bado ni tofauti hasa katika sekta ya ardhi na kilimo. Mfano halisi ukiwa katika maeneo mengi barani Afrika amba wanawake wanaendelea kuwa waathirika wa mfumo dume kandamizi unaowafanya kukosa haki ya kumiliki ardhi. Mtandao unaojulikana kama, Vuguvugu la Wakulima Wadogo Kusini na Mashariki mwa Afrika, La Via Campesina umewakutanisha wanawake wakulima wadogo kutoka mataifa 10 ya Afrika katika mjadala wa kubadilishana ujuzi na uzoefu kwa wakulima wadogo walio kwenye tabaka la chini, wakijadili masuala mbalimbali ikiwemo umiliki wa ardhi, mjadala uliofanyika nchini Tanzania mkoa wa Morogoro katika makao makuu ya Mtandao wa Vikundi vidogo vya Wakulima Tanzania MVIWATA. Hamad Rashid wa Redio washirika Tanzania Kids Time amehudhuria mjadala huo na kuandaa makala ifuatayo.
Tarehe 10 mwezi Machi mwaka 2022, kumefanyika maadhimisho ya kwanza ya siku ya majaji wanawake duniani. Siku hii imeadhimishwa na maudhui yakiwa "Haki katika Mtazamo wa Kijinsia." Lengo ni kuona ni kwa vipi majaji wanawake wanaweza kuwa chachu katika utoaji wa haki kwenye mahakama kwa kuzingatia kuwa tasnia hiyo imegubikwa na mfumo dume. Katika kufahamu ukweli wa hoja hiyo Assumpta Massoi wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa amezungumza na Jaji Hannah Okwengu wa Mahakama ya Rufaa nchini Kenya ambaye anaanza kwa kuelezea anajisikiaje kuwa Jaji kwenye tasnia iliyozoeleka kuwa ya wanaume wengi zaidi.
Makundi ya wahalifu nchini Honduras yalibadili kabisa maisha ya familia ya Daina na kusababisha kuikimbia nchi hiyo kwenda kuomba hifadhi nchini Mexico. Kauli moja ambayo ni maarufu sana mdomoni mwa wakimbizi kutoka kila kona ya dunia ni kuwa hawakutarajia kama wangeweza kuikimbia nchi yao ili kuokoa maisha lakini kufumba na kufumbua walijikuta wakiacha kila kitu na kukimbia kunusuru maisha yao. Na kauli hiyo ndio hasa kilichoikuta familia hii ya Dania ambaye miaka 4 iliyopita yeye na mumewake pamoja na watoto wao wawili wakiwa sebuleni ghafla wakashituka nyumba yao ikimimiwa risasi na genge la wahalifu. Akisimulia anasema walilala chini na kuanza kutambaa sakafuni ili waweze kujificha kuoka maisha yao lakini bahati mbaya risasi moja ilimpata mtoto wakiume wa Dania mguuni. Waliweza kuwatoroka watu hao waliowashambulia nyumbani kwao na kumkimbiza mtoto huyo hospitali. “Mara tu tulipofika hospitalini na mtoto wetu, madaktari walimtoa risasi kwenye mguu wake. Na wakati huo huo, nikaona magari yao yakiwasili. Ilibidi nimkimbize mtoto wangu aliyejeruhiwa nje ya hospitali. Kwa sababu nia ya genge lile ilikuwa ni kuua familia nzima. Sikuwahi kufikiria ningeondoka nyumbani kwangu. Kwa sababu hatukuwa matajiri, lakini tulikuwa na maisha mazuri, tuliishi kwa amani.” Na hapo ndio maisha yao yakabadilika na kuwa wakimbizi. Miaka minne baada ya kutoroka Honduras, familia hiyo iko imara, yenye furaha, na amani nchini Mexico. Watoto wake sasa wanasoma shule. "Tunajenga maisha na mustakabali bora wa baadae wa watoto. Furaha yangu ni kuwaona wakiwa na furaha. Hakuna zawadi kubwa kwa mama kuliko kuwaona watoto wake wakiwa na furaha.” Si watoto pekee walio katika maisha bora kwa sasa, César ambaye ni mume wa Dania naye amepata kazi katika kiwanda cha samani na hapo anajipatia ujira wa kumuwezesha kuihudumia familia yake. "Wakati mtu akiwa na ndoto, hamu, mapenzi ya dhati, na matumaini, ninaamini kuwa hakuna kitu kinachoweza kukuzuia. Naishukuru UNHCR, huwa naitaja, kwa sababu imekuwa msaada muhimu kwa familia yetu.” Uraia wa nchi ya Mexico Afisa programu mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR nchini Mexico Diego Morales anasema furaha na matarajio haya ya wakimbizi kama Dania yamewezekana kutokana na juhudi za miaka kadhaa za kimapinduzi zilizofanywa na shirika hilo kupitia programu maalum inayofuatilia wakimbizi na waomba hifadhi tangu hatua ya mwanzo ya kuomba hifadhi mpaka mwisho kabisa wanapojumuisha kikamilifu katika nchi waliyohifadhiwa. Familia ya Dania na wakimbizi wengine takriban 500 kwasasa wanasubiri kufunguliwa upya kwa mchakato wa kupata uraia kwakuwa sheria za nchi hiyo zinaruhusu wakimbizi waliotambuliwa rasmi na kuishi ndani ya nchi hiyo kwa miaka 2 kupata uraia . Mchakato huo ulisitishwa kutokana na janga la COVID-19 lakini Cesar kifikra yeye na familia yake sasa ni raia wa Mexico wanaosubiri tuu kukabidhiwa rasmi udhibitisho "Timu ya taifa ya mpira wa miguu inapocheza, mimi hushangilia Mexico. Lengo letu ni kupata uraia. Tukiweza kufikia hilo kutatufurahi sana. Iitakuwa jambo nzuri sana kwetu.” Kauli yake inaungwa mkono na mkewake Dania “ Naamini tutakwenda kujivunia wenyewe. Ninajua mwanangu ataniambia: ‘Mama, yaliyotupata huko nyuma yamekwisha. Sasa nina matarajio makubwa ya baadae maishani, naamini siku moja nitamuona mwanangu akiwa na familia yake hapa.” Mexico ni moja kati ya nchi 24 duniani zinazotekeleza mpango wa kuwahudumia vyema wakimbizi na waomba hifadhi unaolenga kutafuta suluhu na ushirikiano chini ya UNHCR.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema linatiwa wasiwasi mkubwa na mazingira dunia wanaoishi wakimbizi na wahamiaji kutoka jamii ya Warao nchini Venezuela ambao kwa sasa wanaishi Guyana. Watu hao wanaishi katika maeneo ambayo ni vigumu kufikika na wanakosa huduma za msingi zikiwemo za afya, malazi, chakula na elimu. Sasa UNHCR na wadau wamelivalia njuga suala lao kwa kuwafikishia misaada. Jason Nyakundi na taarifa kamili. Natss…..Nello Huyo ni Nello kiongozi wa jamii ya watu wa asili ya Warao kutoka Venezuela ambao kwa sasa wanaishi katika ufukara mkubwa kama kama wakimbizi na wahamiaji kwenye maeneo ya vijijini karibu na mpaka baina ya Venezuela na Guyana. Anasema walilazimika kusafiri kuja kusaka hifadhi kwa kitumia ngalawa usiku kucha na mchana kutwa kwa siku mbili ili kuweza kufika hapa kijijini Kaituma Guyana. Nello ni mmoja kati ya Warao 2,500 wanaopata hifadhi hapa wakiwani sehemu ya wakimbizi na wahamiaji 24,000 kutoka Venezuela waliongia Guayana na zaidi ya nusu yao ni watoto , na Nello alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kuwasili katika eneo hilo “Tulikuja kwa kutumia ngalawa kubwa tatu na eneo lote hili lilikuwa pori. Tulikuwa wa kwanza kufika, mimi, baba mkwe wangu, binamu zangu na familia yangu, na kisha familia zingine zikawasili na zingine bado zinaendelea kuja kutoka jamii zingine.” Pamoja na kwamba wamepata hifadhi na wako salama lakini UNHCR inawasiwasi kwani inasema fursa ya kupata huduma za msingi ni finyu hasa kutokana na kwamba wako ndanindani vijijini, hali mbaya ya uchumi, miundombinu duni na na janga la COVID-19. Tathimini ya karibuni ya UNHCR imeonyesha kwamba wakimbizi wengi wa jamii ya Warao wanalazimika kula mlo mmoja tu kwa siku, kwani hawawezi kumudu zaidi ya mlo mmoja na hakuna fursa za ajira, familia nyingi hazina maji safi na salama ya kunywa zinategemea maji ya mto kwa kila kitu na vifaa vya kujikinga na COVID-19 kama barakoa ni mtihani kupata. UNHCR kwa kushirikiana na wadau wengine wa kibinadamu sasa imeanza kuwasambazia msaada muhimu ikiwemo chakula, taa za kandili inazotumia sola, barakoa, vyandarua vya mbu, tembe za kusafisha maji na misaada mingine ya muhimu na tayari watu 400 wa jamii ya Warao wameshapokea msaada. Lengo la UNHCR ni kuendelea kusambaza msaada zaidi ili kuwafikia wakimbizi wote 24,000 walioko Guayana.
Lishe duni kote duniani ni tishio kubwa kwa ustawi wa binadamu kutokana na uhaba wa chakula kwa upande mmoja, na wakati mwingine ukosefu tu wa elimu kuhusu matumizi bora ya vyakula vinavyopatikana katrika jamii. Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu, SDGs, kwa namna tofauti tofauti yanalenga pamoja na mambo mengine, kuliondoa tatizo hili ili kuwaokoa afya za watu hususani watoto duniani kote. Lengo namba moja la Maendeleo endelevu linaongelea kutokomeza umaskini, lengo namba mbili likiongelea kutokomeza njaa na la tatu likitaka kuwahakikishia wanadamu afya na ustawi bora. Ni kupitia msingi huo, mashirika mbalimbali duniani kama Save the Children wanatekeleza miradi yenye lengo la kutokomeza njaa na kustawisha lishe endelevu kama anavyosimulia John Kabambala wa redio washirika wetu, Tanzania KidsTime FM ya Morogoro Tanzania kuhusu mradi wa USAID Lishe Endelevu unaotekelezwa katika mikoa minne ya Tanzania.
En début d'année, Radio Lengo Songo, une des principales stations de Bangui, a radicalement changé sa ligne éditoriale, au point d'être appelée par certains « la radio des Russes ». L'Atelier des médias reçoit Maxime Audinet, chercheur à l'Institut de recherche stratégique de l'École militaire (Irsem), spécialiste des opérations d'influence informationnelle russes, qui publie sur le site La revue des médias, de l'INA, un article sur cette radio centrafricaine. Dans la deuxième partie de l'émission, Sinatou Saka vient présenter la seconde édition du Mooc Connexions citoyennes, proposé par CFI, l'agence française de développement des médias, destiné à la jeunesse africaine. En fin d'émission, Mondoblog audio est consacré aux délestages, ces coupures d'électricité qui compliquent la vie des citoyens dans de nombreux pays sur le continent africain. Boukari Ouédraogo, blogueur burkinabè, se demande pourquoi l'Afrique n'investit pas dans l'énergie solaire – alors que le soleil ne manque pas sur le continent.
Nchini Tanzania vijana wajasiriamali katika mkoa wa Singida wameitikia wito wa Umoja wa Mataifa wa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, TEHAMA kama njia mojawapo ya kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu, SDG hususan kipengele cha teknolojia cha lengo namba 17 la kuimarisha mbinu za utekelezaji wa malengo na kuchochea ubia wa kimataifa. Miongoni mwa vijana hao ni mjasiriamali Simon Sirillo. “Kwa mfano mimi ninazalisha unga wa jasi au gypsum tunachaka jasi kwa maana kwamba tunatengenza chaki na unga wa mikanda ya kupamba au ujenzi wa dari za nyumba. Huu ni ubunifu lakini bila kutumia TEHAMA tunaweza kuishia kuzalisha tu na tusifanikiwe. Kwa hiyo teknolojia inatakiwa katika ubunifu wetu tulio nao, kwa maana tunatumia gharama ndogo za uzalishaji na viwanda vyetu ni vidogo. Ili tuweze kwenda mbali zaidi tunahitaji kutumia teknolojia ili kukuza ubunifu wetu na uvumbuzi wetu kwa ujumla.” Kwa hivyo akatoa wito kwa vijana wenzake. “Tuangalie ni kwa namna gani tunaweza kwenda sambamba na TEHAMA. ili tuweze kufanikiwa katika mambo yetu hatupaswi kuicha mbali Teknolojia kwa sababu inatusaidia kutengeneza mizigo yetu, bidhaa zetu, kuzisambaza na kuziuza ndani ya jamii yetu, ndani ya nchi yetu na hata nje ya nchi kwa ujumla.” Lengo namba 17 la SDGs lina mbinu mbalimbali za kuwezesha kufanikisha malengo yote ya maendeleo endelevu na teknolojia ni miongoni mwa mbinu hizo ambapo Umoja wa Mataifa kupitia wavuti wa SDGs unasema teknolojia rahisi na rafiki kwa mazingira “zinawezesha kuchagiza biashara na hivyo kuchangia katika kutokomeza umaskini."
Wapanda mlima 34 leo wameanza safari ya kupanda mlima mrefu zaidi barani Afrika , mlima Kilimanjaro nchini Tanzania kama sehemu ya juhudi za kimataifa za kuchagiza upatikanaji wa chanjo ya COVID-19 kwa wote. Kundi hilo linalojumuisha watu kutoka katika nyanja za biashara, serikali, wanamichezo mashuhuri na wawakilishi wa vijana linatarajiwa kuwasili kwenye kilele cha mlima huo tarehe 24 Oktoba siku ya Umoja wa Mataifa. (TAARIFA YA FLORA NDUCHA) Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP, wapanda mlima hao kupitia mradi wa Kilimanjaro Initiatibve ,KI wanawakilisha tamaduni, uchumi, mazingira na mabara tofauti wakiwemo vijana 10 waliofadhiliwa kutoka miradi tofauti ya kijamii nchini Tanzania na shule za Tanzania na Kenya na pia wanawake wanariadha nyota wa mbio za milimani, viongozi wa kisiasa, maafisa wa Umoja wa Mataifa, madaktari, wanasayansi na wawakilishi wa vijana. Lengo lao kubwa kupanda mlima Kilimanjaro ni kuelimisha kuhusu haja ya haraka ya kuwa na usawa wa usambazaji wa chanjo dhidi ya COVID-19. Fedha zitakazopatikana wakati wa kupanda mlima zitakwenda kwenye mfuko wa Muungano wa Afrika AU wa kupambana na COVID-19 na kampeni ya Go Give One inayosimamiwa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO. Na huko fedha zitatumika kutoa chanjo za COVID-19, huku kipaumbele kikitolewa kwa wanaozihitaji zaidi katika nchi ambazo haziwezi kumudu chanjo hiyo. Tim Challen, mwanzilishi wa NGO ya Kilimanjaro Innitiative (KI) iliyoandaa upandaji mlima huo au The Big Climb akimkunuu mkurugenzi mkuu wa WHO Dkt. Tedros Ghebreyesus amesema "Kuelimisha kuhusu changamoto ya kutokuwepo haki ya upatikanaji wa chanjo ni muhimu ili kuleta suluhusho lenye usawa. Lazima tushirikiane kama familia ya kimataifa kupambana na COVID-19. The Big Climb inawakilisha mchango wetu katika juhudi hizi za pamoja. " Naye mmoja wa washiriki Dkt. Joseph Msaki wa hospitali ya Kilutheri ya Marangu nchini Tanzania amesema amehamasishwa sana na kiwango cha umakini na msaada wa kimataifa wa kutaka kumaliza janga la COVID-19 Afrika Mashariki . Amesema "Wakati tunaleta angalizo la kimataifa juu ya hitaji la chanjo za COVID-19 duniani, mradi huo pia umeleta vifaa muhimu kama barakoa, vifaa vya upimajia na paneli za sola kwa hospitali ya eneo letu," Madaktari wengine 3 kutoka India, Marekani na kundi la utafiti la ISGlobal wanashiriki katika kampeni hiyo sanjari na mwanariadha Mira Rai kutoka Nepal ambaye ni balozi mwema wa Umoja wa Mataifa wa ushirikiano wa milima na Akinyi Obama-Manners akiwakilisha vijana kutoka wakfu wa Auma Obama Sauti Kuu nchini Kenya. Wadau wengine wakubwa katika kampeni hii ni FAO mountain partnership, mfuko wa Benki ya Umoja wa Mataifa UNFCU, kituo cha Afrika cha kuzuia na kudhibiti magonjwa CDC, Muungano wa chanjo duniani GAVI, AU, mradi wa Women's Brain na Sport and Sustainability International.
Kwa mujibu wa ripoti ufadhili katika nchi za kipato cha chini na cha kati (LMICs) ambazo zinachangia asilimia 98% ya visa vya TB vilivyoripotiwa bado ni changamoto. Kati ya fedha zote zilizopatikana mwaka 2020, asilimia 81% ilitoka kwa vyanzo vya ndani, na nchi za BRICS (Brazil, Shirikisho la Urusi, India, China na Afrika Kusini) ukiwa ni asilimia 65% ya jumla ya ufadhili wa ndani. Mfadhili mkubwa zaidi ni serikali ya Marekani huku mfadhili mkuu wa kimataifa ni mfuko wa kimataifa wa kupambana na UKIMWI, kifua kikuu na malaria. Ripoti hiyo inabainisha kuwa kimataifa matumizi ya huduma za uchunguzi, matibabu na kinga ya kifua Kikuu, yalipungua kutoka dola za Kimarekani bilioni 5.8 hadi dola za Kimarekani bilioni 5.3, ambapo ni chini ya nusu ya lengo la kimataifa la kufadhili kikamilifu hatua za kupambana na kifua kikuu la dola bilioni 13 kila mwaka hadi ifikapo 2022. Wakati huo huo, ingawa kuna maendeleo katika uchunguzi mpya wa kifua kikuu, dawa na chanjo, hii inaathiriwa na kiwango cha jumla cha uwekezaji wa R&D, ambapo kwa dola bilioni 0.9 mwaka 2019 hazifikii lengo la kimataifa la dola bilioni 2 kwa mwaka. Lengo la kutokomeza TB linakwenda mrama Ripoti inasema kubadilika kwa mwelekeo wa hatua zilizopigwa inamaanisha lengo la kimataifa la kutokomeza TB linakwenda mrama na kuonekana kuwa mbali sana kufikiwa ingawa kuna baadhi ya mafanikio yaliyopatikana. Ripoti iansema kimataifa idfadi ya vifo bvya TB kati yam waka 2015-2020 ilikuwa asilimia 9.2 ikilinganishwa na asilimia 35 mwaka 2020. Pia kimataifa idadi ya watu wanaougua TB kila mwaka ilipungua kwa asilimia 11 kutoka mwaka 2015-2020. Ukanda wa WHO wa Ulaya ulizidi malengo yam waka 2020 kwa kupungua kwa asilimia 25, Ukanda wa Afrika nao ulijitahidi karibu ufikie lengo kwa kupungua kwa asilimia 19. "Tumebakiza mwaka mmoja tu kufikia malengo ya kihistoria ya kifua kikuu ya 2022 yaliyofwekwa na wakuu wa nchi katika mkutano wa kwanza wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu kifua kikuu. Ripoti hiyo inatoa habari muhimu na ukumbusho wenye nguvu kwa nchi kuharakisha hatua zao dhidi ya kifua kikuu na kuokoa maisha. Hii itakuwa muhimu wakati maandalizi ya mkutano wa 2 wa kngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu kifua kikuu uliopangwa kufanyika mwaka 2023 ukikaribia."amesema Dkt. Tereza Kasaeva, mkurugenzi wa Programu ya kimataifa ya TB ya WHO. Wito maalum Ripoti hiyo inazitaka nchi kuweka hatua za haraka za kurejesha upatikanaji wa huduma muhimu za kifua kikuu. Inataka uwekezaji maradufu katika utafiti wa TB na uvumbuzi pamoja na hatua za pamoja katika sekta ya afya na zingine kushughulikia viashiria vya athari za kijamii, mazingira na uchumi zitokanazo na TB. Ripoti hiyo mpya ina takwimu za mwenendo wa ugonjwa na hatua zinazochukuliwa kudhibiti janga hilo hilo kutoka nchi na maeneo 197, zikiwemo nchi 182 wanachama wa WHO.
Nchini Sudan Kusini wakati sasa milio ya risasi inaweza kuwa imepungua katika baadhi ya maeneo ya taifa hilo, jinamizi la vita vya wenyewe kwa wenyewe bado linawaandama hasa kwa kuzagaa kwa manbaki ya silaha za vita kama mabomu ya kutegwa ardhini na vifaa vingine vya mlipuko, ambavyo kwa mujibu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa inayochukua hatua dhidi ya mabomu ya kutegwa ardhini UNMAS ni tishio la kila siku kwa maisha ya wanawake, watoto na wanaume kwenye maeneo mbali mbali nchini humo . Flora Nducha anaelezea zaidi. Katika eneo la Ngulere jimboni Equatoria ya Kati Sudan Kusini hali ni Dhahiri kwamba vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea kwa zaidi ya miaka 10 sasa vimeacha alama, na hasa mabaki ya silaha za kivita ikiwemo mabomu ya kutegwa ardhini. Wafanyakazi wa UNMAS wako hapa kwa kampeni maalum ya kukusanya mabadi ya silaha hizo kuanzia mashambani hadi kwenye viwanja vya michezo ili kuwahakikishia usalama watu wa taifa hili changa zaidi duniani. UNMAS imekuwa Sudan Kusini tangu mwaka 2004 likisafisha mabaki ya silaka katika eneo lenye kilometa za mraba milioni 45. Na hapa Ngulere wamekuwa wakisafisha mabaki ya silaha hizo kwenye uwanja wa kandandanda ambao sasa ni salama kwa watoto kucheza kupitia mradi maalum wa viwanja salama ambao unaziunganisha jamii kupitia michezo. Rebecca Bellrose ni afisa wa program wa UNMAS (SAUTI YA REBECCA- MELLISSA) "Mpango wa viwanja salama ni mpango wa miaka mitano ambao ulianza mnamo 2019 na unamalizika mnamo 2023. Lengo kubwa la mpango huu au kwa kampeni hii ni kugeuza viwanja vya mabomu kuwa viwanja vya michezo. Baada ya kusema hayo, tunaona maeneo yaliyochafuliwa na mabomu yako karibu na shule, au viwanja vya michezo au mahali watoto wanapokutana, na tunaondoa uchafu huo. " Kwa wakaazi, eneo hili kuondolewa kwa mabomu hayo yenye historia ya umwagaji damu kutahakikisha biashara inashamiri, watoto wanastawi, na watu wanaweza kuishi bila woga. Na kwa timu ya UNMAS, ni wakati wa kujionea mwenyewe matunda ya kazi yao kwa maisha ya jamii ambazo wako hapo kuzilinda.
Nchini Senegal, mradi wa pamoja wa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo duniani, IFAD na serikali ya taifa hilo la Afrika Magharibi umesaidia kurejeshwa upya kwa maelfu ya hekta za mikoko baharini na hivyo kusaidia jamii za wavuvi kuinua kipato chao na wakati huo huo kuwa na mnepo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi. (Taarifa ya Anold Kayanda) Nyakati za asubuhi Mariane na wanawake wenzake wakiwa kwenye boti kwa matumaini ya kuvua kiasi cha kutosha cha Kamba na chaza kwenye bonde la Saloum lililoko eneo la Fatick nchini Senegal. Miaka 10 iliyopita eneo hili lilikuwa kame baada ya takribani asilimia 40 ya mikoko kutoweka sambamba na eneo la mazalia ya chaza na Kamba kuanzia miaka ya 1970. Mradi wa kurejesha mikoko unaondeshwa na serikali ya Senegal na IFAD umesaidia pia kuepusha eneo la ardhi kumegwa na bahari na hivyo kuleta nuru kama asemavyo Marianne. “Kurejeshwa kwa mikoko ni muhimu sana. Hii leo bahari haijameza kijiji chetu. Tunashukuru mradi kwa kuwa kama hatua isingalichukuliwa, kijiji chetu kingetoweka. Unapohifadhi misitu unaona tope kwenye mikoko, na tope linazuia mawimbi ya bahari na hivyo bahari haiwezi tena kumeza kijiji chetu.” Mikoko ni muhimu katika kuzuia mmomonyoko wa udongo na pia ni mazalia ya viumbe vya baharini. Hata hivyo miaka 25 iliyopita, Afrika imepoteza takribani hekta 500,000 za mikoko kutokana na ukame, ukataji miti hovyo na ujenzi. Yotsna Puri ambaye ni Mkurugenzi wa Mazingira, Tabianchi, Jinsia, Vijana na Lishe IFAD anapatia msisitizo hoja ya uhifadhi wa mikoko.“Ni muhimu sana kuhifadhi maeneo ya misitu ya mikoko inayozingira Senegal kwa sababu inakuwa ndio kingo la mwisho la mnepo kwa nchi kama hii. Ukataji kiholela wa mikoko, ujenzi vimesababisha mmomonyoko wa maeneo kama haya hivyo ikimaanisha kwamba njia za jamii kujipatia kipato zinatoweka na hilo ndio jambo ambalo IFAD inajaribu kurekebisha hivi sasa.” Mradi huu umenufaisha zaidi ya kaya Elfu 50 kwenye eneo la Fatick nchini Senegal kwa kuwapatia mikopo na mafunzo ya jinsi ya kuongeza thamani kwenye mazao yao ikiwemo chaza. Marianne na wenzake wamenufaika na sasa wanakausha chaza na kuwasindika kwenye chupa. “Nilipoanza hii biashara, sikufahamu mambo mengi. Sikufahamu kuwa naweza vuna chaza au hata kuwaweka kwenye kitalu wazaliane. Sasa hivi nachukua chaza, nawachemsha na kuwakausha. Kwa kuwasindika tunapata fedha zaidi. Karai moja la chaza hupati fedha nyingi kama vile ukisindika na kuwaweka kwenye chupa.” Kwa kupata kipato cha ziada, inamaanisha Mariane anawea kulipa karo za shule za watoto wake na kuwanunua mavazi. Lengo la IFAD ni kurejesha zaidi ya hekta nyingine 1,000 katika miaka michache ijayo.
Kwa kutambua ukosefu wa usalama na uhaba wa maji unaowakabili wakimbizi wa ndani walioko Tambura nchini Sudan Kusini, walinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini humo wameanzisha doria maalum ya kuwasindikiza wakimbizi hao kuteka maji maji ili kuwahakikishia usalama katika kusaka rasilimali hiyo adhimu. (Taarifa ya Leah Mushi) Jimboni Equatoria Magharibi nchini Suda Kusini, video ya mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini UNMISS inaonesha mwanajeshi aliyevalia kofia ngumu ya buluu, rangi ya Umoja wa Mataifa akiwa ameshika bunduki akitembea, nyuma yake akifuatiwa na kundi kubwa la watu waliobeba madumu ya maji, na nyuma ya kundi hilo linafuata gari na mwanajeshi mwingine mwenye bunduki. Hii ni doria maalum, si kama zile za kuwasaka wavunjifu wa amani, bali ya kuhakikisha usalama wa raia wanaoenda kuteka maji, na mkimbizi wa ndani Margret Albert anashukuru wanavyosindikizwa. “Tunashukuru kwa kile walinda amani wanafanya kutusindikiza kusaka maji. Tunaogopa kwenda msituni peke yetu. Lakini wanapotusindikiza, tunahisi tumelindwa. Ni jambo zuri ambalo wanafanya. Wanapotusindikiza wakati wa mchana, tunaweza kuteka maji na kukabiliana na uhaba wa rasilimali hii ya thamani”. Hata hivyo idadi kubwa ya wakimbizi hawa wana wasiwasi mkubwa juu ya ukosefu wa maji safi na salama ya kunywa kama anavyoeleza Leticia Mario Sasa. “Maji tunayokunywa ni machafu. Tunahofia kwamba kesho au siku inayofuata sisi sote tutaugua. Watoto wetu na sisi sote tutakuwa wagonjwa na kuanza kufa. Tunaishi katika mazingira yenye msongamano mkubwa, hatupati hewa safi na hatuwezi kuishi mbali kwa sababu tunaogopa. “ Mpaka sasa zaidi ya wakimbizi wa ndani 40,000 wengi wao wakiwa ni wanawake na Watoto wako chini ya uangalizi wa walinda amani wa UNMISS katika maeneo matatu ndani ya eneo la Tambura. Afisa wa masuala ya raia Farai Nyamayaro anasema dhamira yao ni kuwahakikishia usalama wananchi na kuzuia vurugu zaidi. “Lengo la UNMISS [UNMIS] siku zote limekuwa ni kuingilia kati kuokoa maisha. Kile ambacho tumejikita nacho kimsingi ni kujaribu kutuliza vurugu, lakini wakati huo huo kuwapa ulinzi wakimbizi wa ndani. Tunayo maeneo matatu ambayo tunatoa ulinzi, na ndani ya maeneo hayo kumekuwa na mahitaji ambayo tunajaribu kuyashughulikia. Tumefanya doria za kwenda kuteka maji ambapo tunaongozana na wakimbizi wa ndani kuteka maji kutoka vyanzo vya maji vilivyopo karibu. Zaidi ya hayo, tumekuwa pia tukijaribu kuzungumza na viongozi wa serikali wa ngazi za juu pamoja na maafisa wengine wa jeshi ili waweze kufika hapa na kusaidia kumaliza ghasia eneo hili.”
Mashirika ya umoja wa Mataifa yanayotoa misaada ya kibinadamu yameendelea kuwasaidia wananchi wa Afghanistan ambao wengi wanakabiliwa na kutokuwa na uhakika wa chakula kutokana na machafuko nchini humo. Miongoni mwa mashirika hayo ni lile la chakula la Kilimo FAO. (TAARIFA YA LEAH MUSHI) Nats…. “Lengo kubwa la FAO kwa mwaka 2021 ni kuendelea na kazi,tunaendelea na tumedhamiria kuendelea kubaki hapa na kusaidia.“ Ni Rajendra(TAMKA RAHENDRA) Kumar Aryal, mwakilishi wa FAO nchini Afghanistan akieleza dhamira yao ya kuendelea kutoa msaada nchini humo wakati huu ambapo inakadiriwa mtu mmoja kati ya watatu hana uhakika wa chakula kutokana na machafuko yanayoendelea nchini humo, janga la corona na kupanda kwa gharama za chakula. Msaada wa mafunzo na pembejeo unaotolewa na FAO kwa kushirikiana na wadau wake umewanufaisha wakulima kama anavyosema mkulima huyu wa ngano Khialy Gul. “Tumepokea msaada huu wakati tunauhitaji.Tumesaidiwa kilo 50 za ngano, na mbolea ya kupandia na kustawisha” Malek Nemat ni kiongozi wa jamii ya Kuchi anasema msaada uliotolewa kwa wafugaji umewasaidia kuacha kuuza mifugo kiholela ili kupata hela ya chakula. “Hawa watu wamepokea viroba vya chakula cha mifugo yao ili kuweza kuilinda. Watu wanafuraha sana kuhusu hili kwasababu sasa chakula hicho kinaweza kulisha mifugo mpaka miezi miwili au mitatu. Hata kama mtu anasaidiwa kwa miezi 3, hayo ni mafanikio makubwa. “ Msaada wa fedha dola 50 hutolewa kwa wale wasiomiliki ardhi, wanawake na watu wenye ulemavu wakiwa ni kipaumbele. Video ya FAO inamuonesha Nastaran akipokea mgao wake nakusema. “Tupo watu 6 kwenye familia, lakini ni mtu mmoja tuu mjukuu wangu ndio anafanya kazi nchini Iran. Tatizo letu ni kuwa hatuwezi kununua chakula na mahitaji muhimu. Fedha nilizopewa na FAO zitasaidia kununua kiroba cha mchele, mafuta ya kupikia Pamoja na mahitaji ya shule kwa mjukuu wangu.” Licha ya mzozo unaoendelea, FAO imejitolea kuendelea kutoa msaada wa chakula na fedha kwa watu wenye uhutaji sana ili kuepusha kuzorota kwa hali ya uhakika wa chakula.
Mamlaka ya Ukusanyaji Kodi, KRA jijini Mombasa imenadi magari na bidhaa nyingine ambazo hazikulipiwa ushuru na walioziagiza. Aidha, baadhi walishindwa kuwasilisha stakabadhi zinazofaa za uagizaji. Lengo la mnada huo ni kupunguza msongamano katika Bandari ya Mombasa. Shughuli hiyo iliipa KRA kati ya shilingi milioni 150-200. Mwanahabari wetu Robert Menza amezungumza na Wakenya waliofika bandarini humo kununua bidhaa hasa magari.
Nchini Kenya, kijana Karinge Mbugua, kwa namna moja au nyingine anashiriki kulitekeleza lengo namba 8 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linalolenga kazi za staha pamoja na ukuaji wa uchumi. Ni kupitia katika kipaji chake cha uchoraji, amewekeza mud ana ujuzi wake katika kazi hiyo ya staha ambayo inamsaidia kukuza uchumi wake. Mwandishi wetu wa Kenya, Jason Nyakundi amemhoji Karinge na kwanza anaeleza alivyoanza.
Ni kuhusu dhana kuwa mchanganyiko wa tangawizi, maji ya limau na asali ni kinga na vilevile tiba ya corona. Hii ni sehemu ya kwanza ya makala. Lengo ni kusambaza ujumbe kwa wale wanaoamini dhana hii kuwa dawa. ....Baada ya kuzuka kwa virusi vya corona kumekua na habari aina tofauti kuhusu hatua za kuchukua kuepuka kuambukizwa, na habari nyengine kuhusiana na tiba ya corona. Mojawapo ya habari iliyopata umaarufu nchini ni kuhusu utumizi wa tangawizi, limau na asali. Je mchanganyiko wa tangawizi, maji ya limau na asali ni kinga au tiba ya corona. by Mwanaharusi Rashid
Lengo namba 9 kati ya malengo 17 ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu, SDGs linaangazia viwanda, uvumbuzi na miondombinu. Lengo linalenga ujenzi wa miundombinu thabiti, kukuza viwanda endelevu na jumuishi, na kukuza uvumbuzi.
Lengo namba 16 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, yaliyopitishwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa mwaka 2015 linalenga kuimarisha taasisi thabiti na zenye kusimamia haki kwa ajili ya kuwezesha uwepo wa jamii zenye amani na jumuishi. Mashirika ya kiraia katika nchi mbalimbali yamebeba jukumu la kusaidia na serikali kufanikisha lengo hilo na miongoni mwa mashirika hayo ni Restless Development ambalo nchini Tanzania kupitia mradi wa Kijana Wajibika linasaidia taasisi kujumuisha watu wenye ulemavu na wasichana kwenye taasisi hizo.
Lengo namba 5 la Malengo ya Umoja w mataifa ya maendeleo endelevu linaangazia usawa wa kijinsia likilenga kufanya mageuzi ili kuwapa wanawake haki sawa kwa rasilimali za kiuchumi, na pia kupata umiliki na udhibiti wa ardhi na aina nyingine za mali, huduma za kifedha, urithi na maliasili, kwa mujibu wa sheria za kitaifa. Mojawapo ya viashiria vya kufanikiwa kwa lengo hilo ni pale ambapo kutakuwa na uwiano wa nchi ambazo mfumo wa kisheria (pamoja na sheria ya kimila) unahakikishia haki sawa za wanawake kwa umiliki wa ardhi na au udhibiti.
Katika makala ya Ahimidiwe Olotu wa Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam ametuandalia makala ya msichana Modesta Joseph aliyeunda wavuti maalum wa kukusanya taarifa za manyanyaso kwa wanafunzi. Wavuti ambao baadaye umegeuka kuwa shirika.
Ulimwengu uko katika muongo wa kuelekea utimizaji wa malengo 17 ya maendeleo endelevu. Lengo namba 8 linaongelea kazi bora au zenye hadhi pampja na ukuaji wa uchumi. Lengo hilo ni vigumu kulifikia iwapo hakuna maandalizi ya kutosha kwa wale wanaoandaliwa kufanya kazi na hivyo hali hiyo itasababisha sehemu ya pili yaani ukuaji wa uchumi nayo kutokufikiwa. Kwa msingi huo, ndipo asasi ya Umoja wa Mataifa ya vijana, YUNA Tanzania imeamua kuendesha mradi wa kuwapa nafasi vijana waliohitimu masomo na hata walioko masomoni bado ili wapate mafunzo kwa vitendo.
Wasichana 28 nchini Tanzania wamenufaika na mafunzo ya upigaji picha yaliyofanywa na mpiga picha maarufu nchini humo, Imani Nsamila, kwa kushirikiana na shirika la Ladies Joint Forum na Kikoi innovative media. Ni mafunzo yanayolenga kuleta usawa wa kijinsia katika tasnia hiyo inayozidi kukua katika zama hizi za ukuaji wa teknolojia ya dijitali. Kupitia makala hii, baadhi ya wasichana hao wanaeleza namna walivyonufaika na mafunzo hayo na watakavyoyatumia katika maisha yao.
Katika hatua ya pili, lazima uandike tarehe ya kuacha kazi. Lengo bila mipaka ya muda linakosa msukumo. Pia tafuta DIARY ambapo utakuwa unaonyesha mikakati yako ya kila siku.
Lengo namba 5 la Malengo ya maendeleo endelevu SDGs, inahimiza usawa wa kijinsia ili kuwafanya wanaume na wanawake katika jamii kuwa na usawa kwa mstakabali wa jamii nzima.
Lengo namba 9 la maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa, SDGs ifikapo 2030 Iinahimiza juu ya uwepo wa miundombinu bora,viwanda endelevu na uvumbuzi. Katika kuhakikisha lengo hili linatekelezeka,kijana Boris Maximilian Masesa wa nchini Tanzania amevumbua kifaa maalum kinachoweza kunasa mawasiliano ya simu kwa ajili ya kuwasaidia walimu kuwabaini wanafunzi wanaotumia simu bila ruhusa. Ifuatayo ni makala iliyoandaliwa na Nyota Simba na kusimuliwa na Evarist Mapesa kutoka Redio washirika SAUT FM iliyopo jijini Mwanza Tanzania.
Snippets são programas em áudio curtos, apresentando uma informação específica. Padrão ACME apresenta novidades e análises do mundo da animação. Apresentação de Gabriel Cruz. Ajude a Kombo em seu trabalho! No Apoia-se em Reais, no Patreon em dólares! Se você gosta dos trabalhos da Kombo, confira nossas metas da Fase 1 e vamos seguir em frente juntos, […]
Applications are open for the long-awaited new temporary parent visa, designed to provide an alternative to the existing permanent visa options for parents of migrants. - Jumatano tarehe 17 Aprili, huduma ilifunguliwa kupokea maombi, ya viza ya muda mfupi ya wazazi, iliyo subiriwa kwa muda mrefu. Lengo la viza hiyo nikutoa uamuzi mbadala ya viza zakudumu zilizopo kwa wazazi wa wahamiaji.
Sheena began her career with the small, minority, women, and disadvantaged business community in 1999. In her role as Executive Director of both the North Central Texas Regional Certification Agency and the South Central Texas Regional Certification Agency, from May 2006 to June 2013, she developed and improved community awareness programs, built sustainable relationships with local and federal government business partners and participated in a multitude of educational and speaker forums concentrating on business development and certification. Sheena is now the owner of Lengo, a consolatory suite of best business practices which bridge the gaps and facilitates the expansion of unyielding opportunities and results that rest within the potential of a truly focused organizational vision. She also enjoys public and motivational speaking. Some of her speaking topics include the Power in Female Negotiation and the Growth Zone, Finding Potential in Yourself & Others. She enjoys empowering women with her story and transforming their minds to focus on their inner power and ability to exceed their wildest dreams! Sheena was appointed in August 2017 by the City Council, to the Planning & Zoning Commission for the great city of Glenn Heights, TX, and she is currently RUNNING FOR MAYOR! (Election Day is 26 January, 2019) We get into some discussion about her mayoral run later in the program, but our main focus today is to take the pretentiousness out of business talk and strip back techniques to expose just how easy it is to understand the basics of business. Sheena will teach you how to position yourself with strategic plans that support your vision and maximize your company's success and growth! Exclusive Offer Leverage Unleashed is a master class devoted to educating business owners about techniques to maximize their success and develop true strategies aligned with their firm's overall experience. This is a self-paced online program with monthly chat sessions, 1-on-1 coaching, and competitive business development. For any listeners that sign up for the course, there will be a 30% discount offered! Competitive Business Plan Development for all entrepreneurs is now being offered through December 31st for 30% off. Listeners will receive a full competitive business plan, market research included. Secure a free consultation call by December 31st and receive the offer for all plans booked before March 1, 2019! Discount code BP2019 Support Sheena's Run for Mayor of Glenn Heights, TX https://sheenamorgan4glennheights.com sheena4mayor@gmail.com 972-866-4660 Connect With Sheena https://www.lengofocus.com sheena@lengofocus.com https://facebook.com/lengofocus https://twitter.com/lengofocus https://linkedin.com/in/sheenadmorgan https://instagram.com/lengofocus https://www.youtube.com/channel/UCKCpBsNtHweboj3QxaDy5UA
Lengo kama vile mitandao mingine inavyo Fanya
Elsa Laula skirisardas jekh lil thaj o Parno kraj kamlas kodo lil. Akanak si voj te dikhel peske dades thaj peske prales. 3. Pale khetanes Bööresth! Jaj ke mishtoj! Maj dur san amenca ande parne krajesko Saajvoe-rajo. Muro rajo. Fajma kames te djanes sar djal amara amljake a Elsa Laulake? Ande paluno kotor skirisardas e Elsa jekh lungo lil mange. O lil sas pa chavoresko chachipe te avel khetanes peska familjasa, thaj te na aven uni manush shudine kaverendar. Voj musajsas te arakhel jekh kaver vudar kadi data te aresel ande muro rajo thaj kodo kerdas voj kana voj nakhlas perdal jekh mysticno bar, khaj sas lishime khatar e bari kali chirikli. Kana aresena ande paramichia akanak aresena kote kana e Elsa vorta dikhel peske dades. "Aehtjie!" tsipij e Elsa loshasa, thaj lel te nashel karing pesko dat khaj beshel ande jekh tserha ande parne krajesko Saajvoe-rajo. Sar mindik te beshlov kote. Sar te djanglov ke o lil khaj e Elsa skirja avla dosta lashio. Pasha leste tordjiol o Mattias. "Jaj ke mishtoj, ke tume san kate! Chi acharen sar mange sas shusho bi tumaro. Me thaj e tjidtjie, thaj vi e mama!" phenel e Elsa bara loshasa thaj e vorbi huran anda lako muj. Aba chi acharel e dukh ando vast kana kikidel peske dades, voj loshal kade zurales ke soha chi kamel te mukhel peske dades. Pala jekh lungo vrama kikidimasa phenel o Mattias khaj e Elsa ke vov kamel te sikavel lake e parne krajesko Saajvoe-rajo, thaj o tata phenel ke kodo si jekh lashio ghindo. "Zurales shukares si kate", phenel o Mattias thaj sikavel e najesa karing e plaja thaj o len khaj si angla lende. Pe phuv baron parne luludjia thaj e bahovinja pashliov pe bara. Kate birisardov e cherbura te nashen ande slobodia thaj te han pe chale sako djes. Elsa khaj si sikli e cherbonca arakhel sigo e parne krajeske cherbura ande Saajvoe-rajo. "Dikhen sa parnej! Sako jekh cherbo si parno, Mattias!", phenel e Elsa. "E parne krajeske cherbura musaj te aven e maj bahtale cherbura ande ljuma". Elsako dat kerel anda shero thaj harundel peski falka. "Chaches Elsa, but bajura si zurales lashie kate, vi te sam zurales dur keral. O parno kraj phendas ke dela amen unien anda kadal cherbon, feri te inkrov amen pe amari righ thaj te na diljaras les", phenel e Elsako dat. "Me aba dem anav mure cherbos", phenel o Mattias loshasa, thaj e Elsa musaj te serel sostar voj kote avilas. Laki dej thaj lake kaver pral djukaren pe lende khere. "Aehtjie, O parno kraj ande Saajvoe-rajo phendas ke tume aba shaj te aven khere akanak", phenel e Elsa. "Tume trobun amen khere. phares si amenge bi tumaro." Lako dat dikhel brigasa pe late. Mattias, khaj vorta las te nashel karing e cherbura ashavel te nashel, thaj boldel pe lende. Vi vov dikhel pe late jakhenca khaj sikaven ke vov chi pachal ande late. "Elsa, pachas chachimasa ande kodo? O parno kraj anda Saajvoe-rajo si pindjardo ke pharoj thaj chi inkrel mindik peski vorba. Nashtik te aves za brigaki te na mukhela amen te djas khere adjes." Tatasko glaso si khino, thaj e Elsa chi djanel so te phenel leske palpale. "Chak vov si o kraj, jekh kraj musaj te inkrel peski vorba, na?" pushel e Elsa. "No jo" phenel lako dat. "Jekh kraj trobusardov te inkrel peski vorba. Thaj tu djanes kodo , ke univar naj dosta feri te skrij pe jekh lil, thaj te djukarel pe ke o kraj avla thaj zhutija." Tela kodi vrama so o tata vorbijas keradas o Mattias jekh jagh, thaj e Elsa thaj o lengo dat beshen kote pasha leste. "Sar te na avel, katej maj feder, kana si o ivend, ke e cherbura birina te chaljion kate." phenel hirtelen o Mattias. Lengo dat thaj e Elsa dikhen pe leste thaj keren anda shero ke kadej. "Chachimasa si o Saajvoe rajo jekh lashio than e cherbonge thaj kodolenge so len sama pala lende, thaj e maj lashi djela si kodo ke vi te chi birisaras te mukhas kado than bi krajeski permisia, si kado than chachimasa jekh rajo pasha e temlica ande Umeå." Tatasko hango si pharo kana vov vorbij pa Umeå. Na durmut kodolestar dosharnas les kaver Sami ke vov butobi chordas lenge cherbura. Elsa serel mishto kodo djes kana e policia dine andre ande lengo kher thaj line lake dades. Beshlas jekh intrego bersh thaj e familja trajias chorimasa thaj univar chin anas len so te han kodo jivend. "Dostaj, na vorbin pa Umeå!" phenel e Elsa. "Na vorbin pa kodo kana sam khetanes. Chi birij te ghindoj pa kodi vrama". Mattias kerel anda shero thaj von lenas avri o habe anda trasta khaj sas pe Mattiaski trasta. "Akanak trobusaras te has", phenel o Mattias, thaj lel te shingrel anda o shutjardo mas. "Jo, thaj pala kodo tradas amenge khere!" phenel e Elsa loshasa. Kodi rachi beshlas e Elsa, Mattias thaj lengo dat lungo vrama angla jagh thaj vorbin jekh kaveresa, thaj hirtelen nakhlas e vrama 2 pe rachiate. Elsa del pe ghindo ke puznoj thaj ke trobunas aba te djan peske khere, feri zhi pun voj ushpeji te ushjel opre tordjiol kode pasha lende o parno kraj. "Ke mishtoj tumenge kate, si tumen ekcera kava vi mange" phenel o parno kraj, feri ande lesko hango achardjiol pe ke vov kamel variso kaver. "Elsa, chachimasa chalilas man chiro lil" phenel o kraj, "feri me kamav variso maj but tutar, zhi pun birij te mukhav chire prales thaj chire dades tusa khere ". Elsa dikhel chudasa po parno kraj, thaj zhi pun voj ushpeji te putrel pesko muj te phenel variso, vazdel o kraj pesko vast, te na vorbij e Elsa. "Kodo kon pucharel pe ande peske buchia chi agorij butivar intrego buchi", phenel o kraj, "Thaj anda kodo ke tuke gelas kade lokho te skris kado lil, si te dav tut jekh nevi misia te keres. Jekh kasavi phari sar kana phirel pe mashkar duj planeti." "Chak dan chiri vorba!" tsipij e Elsa thaj dikhel holjasa po parno kraj anda Saajvoe-rajo. "hm, me sim o kraj- thaj birij te paruvav muro ghindo kana me kamav thaj akanak kamav te skris mange jekh intrego kevnia, jekh kevnia khaj birij te ushtiavel anda lindri. Djatar thaj si te aves palpale angla dujto kurko ke te na avilan, chi dikhesa soha chire prales thaj chire dades!" Thaj kana o parno kraj anda Saajvoe-rajo phandavel pesko muj lel intrego lesko rajo te boldel pe zurales sigo. Sa e kolorura thaj sa e formi bolden pe khetanes, thaj e Elsa lel te hural opre karing o cheri khaj chachimasa si o jezhoro. Kana e Elsa puterdas peske jakha pashliolas voj korkori pasha o jezhoro, thaj kote usijas e bari kali chiriklori, thaj e Elsa rovel. "Aehtjie, Mattias. Na daran, pa na buteste dikhasam amen", phenel voj rojimasa. "O parno kraj chi njerija manca! dav tumen muri vorba"