POPULARITY
Lionel Messi amekuwa mfungaji bora wa muda wote wa Kombe la Dunia, akifunga mara mbili nakusaidia Argentina kuishinda Austria 2-0 mjini Dallas, na kujihakikishia nafasi ya kwanza katika Kundi J, pamoja na nafasi katika hatua ya mchujo.
Leo tumeangazia kwa undani matukio na matokeo yote ya wiki ya kwanza michuano ya Kombe la Dunia 2026 - Mbappe, Messi waweka historia wakati Cape Verde na DRC zikihangaisha miamba wa soka wa ulaya, Tunisia yamfuta kazi kocha, uchambuzi wa mechi za leo. Aidha ni mwaka mmoja kuelekea Kombe la Mataifa ya Africa 2027, matokeo ya tenisi kombe la Davis Cup, Police fc ya Rwanda yamfuta kazi kocha wake, matokeo ya Cecafa U17 kwa kina dada pamoja na tetesi za uhamisho ulaya.
Ni wiki ambayo imegubikwa na michuano ya kombe la dunia 2026 huko Marekani, wiki hii eneo hili la Afrika mashariki na kati lilichangamka baada ya timu ya DRC Leopards kutoka sare na Ureno, virusi vya ebola na juhudi za kikanda kuudhibiti, kukamatwa kwa wakili Erias Lukwago kule Kampala Uganda, lakini pia mashambulio ya kigaidi kwenye uwanja wa ndege wa mjini Niamey huko Niger, na mkutano wa G7 jijini Paris Ufaransa, na hali kadhalika kusainiwa kwa mkataba kati ya Marekani na Iran
Mafanikio ya awali ya Socceroos katika Kombe la Dunia, yameangazia tena hadithi za mafanikio za Australia yenye tamaduni nyingi.
Mexico ime ingia katika hatua ya mchujo, baada ya kuishinda Jamhuri ya Korea katika siku ambayo iliadhimishwa na jeraha kubwa nchini Canada.
Mashabiki wa soka wana endelea kupata burudani kupitia Kombe la Dunia la FIFA 2026 linalo andaliwa nchini, Canada, Marekani na Mexico.
Mshtuko wa kwanza mkubwa wa Kombe la Dunia la FIFA umeshuhudiwa, baada ya timu ambayo inadhaniwa ina nafasi kubwa yakushinda michuano hiyo, kunyimwa ushindi na Cabo Verde wanao shiriki katika michuano hiyo kwa mara yao ya kwanza.
Ujerumani umeanza vyema kampeni yao ya Kombe la Dunia la 2026, ikiwashinda Curaçao inayo shiriki katika michuano hiyo kwa mara ya kwanza kwa mabao 7-1 katika Kundi E katika Uwanja wa Houston, Marekani.
Tumeangazia Kombe la Dunia 2026 kuanza kwa vikwazo kadhaa, raia wa Afrika waiunga mkono Mexico dhidi ya Afrika Kusini, uchambuzi wa mechi ya leo Brazili dhidi ya Morocco, DRC wakijiandaa kupambana na Ureno wiki ijayo, maandalizi ya mbio za Kigali Marathon zakamilika, klabu ya Gor Mahia nchini Kenya yaamrishwa kufanya uchaguzi upya,
Ni wiki ambayo imegubikwa na maandamano kadhaa nchini huko Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, huko Nanyuki nchini Kenya, na watu kutoka nchi kadhaa za Afrika kuihama Afrika Kusini kutokana na ongezeko la chuki dhidi ya wageni, lakini kubwa kabisa wiki hii lililotikisa ulimwengu ni michuano ya kombe la dunia ya mwaka wa 2026 iliyong'oa nanga huko Marekani, Mexico na Canada, bila kuisahau ziara ya Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Leo wa Kumi na nne huko Uhispania.-Naitwa Ruben Lukumbuka,
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, umetamatishwa leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Idhaa hii imepata fursa ya kuzungumza na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya mkutano huu muhimu, Mtanzania Zuleikha Tambwe. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo..Hatari ya Ebola wakati wa Kombe la Dunia la Soka 2026 ni ndogo na hakuna sababu ya mashabiki kubadili mipango yao ya safari kuelekea Canada, Mexico na Marekani, limesema Shirika la Afya Duniani WHO kombe hilo liking'oa nanga leo. Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Ulaya, Hans Henri P. Kluge, amesema hakuna wagonjwa wa Ebola katika nchi hizo wala Ulaya na amesisitiza, “Safirini kama kawaida na furahieni mashindano hayo.” WHO imefafanua kuwa Ebola haisambai kwa njia ya hewa na visa vingi vipo katika maeneo ya mbali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Annalena Baerbock, amehitimisha ziara ya siku mbili jijini Nairobi nchini Kenya, ambapo amesisitiza nafasi muhimu ya Umoja wa Mataifa katika kuendeleza maendeleo, amani na ushirikiano barani Afrika. "Kila siku Umoja wa Mataifa na washirika wake huokoa maisha. Bila UN, mamilioni ya watoto wasingepata elimu kupitia UNICEF wala chanjo muhimu kupitia WHOna tusingekuwa na ushirikiano kama huu."Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, uliokuwa unafanyika hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani umefikia tamati leo. Kaulimbiu ya mwaka huu ni “kuadhimisha miaka 20 ya mkataba huo na kuimarisha utekelezaji wake katika dunia inayobadilika.” Kibaya Laibuta, Jaji wa Mahakama ya Rufani nchini Kenya, ambaye pia ni mlemavu aliyeoona au kipofu, ameshiriki na anaeleza alivyouona mkutano huu.Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
Kipute cha kombe la dunia kinaanza leo, huku Afrika Kusini ikipambana dhidi ya Mexico mwenyeji. Je, unazungumziaje timu za Afrika zinazoshiriki mashindano ya huu? Skiza makala haya.
Kipute cha kombe la dunia kinaanza leo, huku Afrika Kusini ikipambana dhidi ya Mexico mwenyeji. Je, unazungumziaje timu za Afrika zinazoshiriki mashindano ya huu? Skiza makala haya.
Tuliyokuandalia leo ni mambo muhimu ya kufahamu kuelekea Kombe la Dunia, timu ya Iran na mwamuzi wa Somalia hatimaye wapokea visa zao, namna mataifa ya Afrika yamecheza kwenye mechi za kirafiki kuelekea Kombe la Dunia, Riquelme na Florentino kupambania urais wa Real Madrid, Kenya kuandaa Davis Cup, kocha wa Kenya ajitetea baada ya sare dhidi ya Lesotho, tuzo za Ligi Kuu Kenya, kocha Flaurent Ibenge asalia Azam, Tanzania wavuna shaba kwenye fainali ya Afcon U17, Kenya yafuzu voliboli ya Afrika.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania Kaskazini mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, ambako Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro inaendelea kuwa mfano wa jinsi binadamu, wanyamapori na urithi wa kitamaduni vinavyoweza kuishi pamoja huku vikichangia maendeleo ya utalii endelevu na ulinzi wa mazingira. Je nini kinafanyika kuhakikisha uhifadhi, utamaduni, mazingira na utalii vinakutana kwa mustakabali endelevu? Ili kupata majawabu Flora Nducha wa Idhaa hii amezungumza na Kamishna wa Hifadhi ya Ngorongoro, Abdul-Razaq Badru.Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus ameendelea kusisitiza umuhimu wa ugunduzi wa mapema kwani hatua zikichukuliwa haraka wagonjwa wa Ebola wanapona. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Geneva Usiswi baada kurejea kutoka ziarani mashariki mwa DRC amesema, Kufikia sasa, watu sita wamepona nchini DRC na wawili nchini Uganda, jambo linaloonesha kuwa watu wanaweza kupona Ebola iwapo watapata huduma za afya na kwenda vituo vya afya mara tu wanapoanza kuonyesha dalili za ugonjwa huo.Kuelekea kuanza kwa michuano ya Kombe la Dunia la FIFA wiki ijayo hapa Marekani na katika nchi jirani, Canada na Mexico, Shirika la Afya la Nchi za Amerika (PAHO) limetoa wito kwa nchi za bara la Amerika kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa wa surua na Rubella kufuatia mikusanyiko mikubwa inayotarajiwa na milipuko inayoendelea ya surua na ongezeko la safari za kimataifa vinaweza kuongeza kasi ya kuenea kwa ugonjwa huo. Shirika hilo linazitaka mamlaka za afya kubaini maeneo yaliyo katika hatari kubwa na kuimarisha hatua za kukabiliana haraka ili kuzuia maambukizi zaidi. Na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa asubuhi hii kwa saa za New York, Marekani wanachagua wanachama watano wapya wasio wa kudumu wa Baraza la Usalama kwa muhula kipindi cha miaka miwili kuanzia tarehe 1 Januari 2027 hadi 31 Desemba 2028. Kutoka Barani Afrika mgombea mmoja ni Zimbabwe ambaye hata hivyo anatarajiwa kupita kwani hana mpinzani katika nafasi hiyo. Nchi zitakazochaguliwa zinachukua nafasi za Somalia, Pakistan, Panama, Denmark na Ugiriki, ambazo mihula yao itaisha mwishoni mwa mwaka huu 2026.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Leo asubui Mwalimu wa timu ya taifa ya Australia Tony Popovic ametangaza kikosi chake cha wachezaji 26, cha Socceroos watakao cheza katika Kombe la Dunia la FIFA la 2026.
Leo tumeangazia Arsenal kushinda ubingwa wa Ligi Kuu baada ya miaka 22, kocha wa Uingereza Tuchel azomewa kuwaacha nje wachezaji kadhaa, kocha wa DRC Desabre ataja kikosi cha Kombe la Dunia, Aston Villa yashinda Kombe la Europa, Droo ya kufuzu michuano ya AFCON 2027 yakamilika huku AFCON U17 ikiendelea, fainali za BAL zaanza Kigali, Kipchoge kukimbia marathon ya kwanza Afrika, Motsengo Omba ashinda urais wa Fecofa, raundi ya pili kufuzu Kombe la Dunia la wasichana chini ya miaka 17 yaanza.
Leo tunaangazia baadhi ya matukio ya michezo yaliyozungumziwa kwenye mkutano wa Africa Forward Summit uliokamilika hiki hii, uchambuzi wa Ghana kukosolewa kuandaa mashindano duni ya Afrika ya riadha, Al Hilal ya Sudan yatwaa ubingwa wa soka Rwanda, Motsengo Omba akizindua nguzo zake tano za uongozi wa Fecofa, fainali ya Kombe la Shirikisho, Afcon U17 yaanza huko Morocco, mataifa yaanza kuzindua vikosi vyao kuelekea Kombe la Dunia, PSG yashinda wa 14 huku Carrick akikaribia kusaini mkataba.
Tuliyokuandalia leo ni kufutwa kazi kwa kocha wa Yanga Pedro Goncalves, wawaniaji wengine wawili wajiondoa uchaguzi wa urais DRC, mashindano ya magari ya Africa yangoa nanga nchini Uganda, fainali ya Kombe la Shirikisho mkondo wa kwanza kupigwa leo usiku, mechi za kufuzu Kombe la Dunia la wasichana chini ya miaka 20, FIFA imetoa orodha ya wasanii wa kutumbuiza mechi za ufunguzi Kombe la Dunia, Arsenal imefika fainali ya Uefa baada ya miaka 20 huku IOC ikitoa marufuku ya Belarus.
Leo tumeangazia mashindano ya kwanza kabisa ya kina dada ya FIFA Series inayoandaliwa nchini Kenya, timu tano zimetinga mchujo wa ligi kuu, ziara ya rais wa CAF Motsepe nchini Senegal, ligi ya mabingwa Afrika yaingia hatua ya nusu fainali, kocha Aliou Cisse atua nchini Angola, michuano ya kufuzu Kombe la Dunia la wasichana chini ya miaka 17, droo ya Afcon U17, michuano ya shule za upili za Afrika zakamililka, mageuzi ya mbio za marathon kwenye riadha za dunia, Ndala Ngambo haendi Kombe la Dunia
Leo tumeangazia kufuzu kwa DRC michuano ya kombe la dunia tukiwa na mgeni wetu Felly Mulumba, mchezaji wa soka kutoka DRC, Ghana yamfuta kocha Otto Addo, mageuzi katika kamati andalizi ya AFCON 2027 nchini Kenya, Tigers na Petro de Luanda zafuzu fainali ya BAL, Algeria mabingwa wa basketboli ya vitimagu Afrika, kustaafu kwa Victor Wanyama huku ligi ya Kenya ikilenga kuwa bora Afrika, je De Zerbi ataiokoa Spurs kushushwa daraja?
DRC imejikatia tiketi ya kucheza kwenye kupute cha kuwania kombe la dunia Haya hapa maoni ya waskilizaji.
DRC imejikatia tiketi ya kucheza kwenye kupute cha kuwania kombe la dunia Haya hapa maoni ya waskilizaji.
Ripoti ya shirika la Amnesty Interenational imeonya kuwa Kombe la Dunia la mwaka huu linaweza kuchangia ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu dunaini kutokana mpango wa mataifa wenyeji kuweka mikakati kali za uhamiaji na ufuatiliaji wa karibu wa mashabiki wa kigeni Je, unahisi mashabiki kutoka Afrika Mashariki watakuwa salama kushabikia timu zao kule Merekani,Mexico na Canada? Skiza maoni ya waskilizaji.
Ripoti ya shirika la Amnesty Interenational imeonya kuwa Kombe la Dunia la mwaka huu linaweza kuchangia ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu dunaini kutokana mpango wa mataifa wenyeji kuweka mikakati kali za uhamiaji na ufuatiliaji wa karibu wa mashabiki wa kigeni Je, unahisi mashabiki kutoka Afrika Mashariki watakuwa salama kushabikia timu zao kule Merekani,Mexico na Canada? Skiza maoni ya waskilizaji.
Leo kwenye jukwaa tumeangazia rufaa ya Senegal kwa mahakama kuu ya spoti, ripoti ya CAF yasema Afrika Mashariki haipo tayari kuandaa Afcon 2027, Afrika Kusini na Kenya zafuzu Kombe la Dunia la gofu ya chipukizi, ripoti maalum ya FIFA Series mjini Kigali, mashindano ya KipKeino Classic yapata sura mpya, ni kwa nini Djigui Diarra amepigwa marufuku ya mechi tatu nchini Tanzania?, vikwazo vipya vya Marekani kwa nchi tano za Afrika, DRC kuchuana na Jamaica, IOC dhidi ya huntha, Tiger Woods akamatwa
Kwenye kipindi cha leo tumeangazia kuondoka kwa kocha mkuu wa Morocco Walid Regragui, Burkina Fason yapata kocha mpya, athari ya kuahirishwa kwa michuano ya WAFCON, vikwazo vya CAF dhidi ya Al Ahly, Faith Kipyegon aorodheshwa kwa mara ya tatu kuwania tuzo ya dunia ya Laureus. FIFA yatangaza sheria mpya za soka kuelekea Kombe la Dunia. Fred Kerley apigwa marufuku ya miaka miwili. Je, ni suala la muda tu Arsenal kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Uingereza au la?
Leo tumeangazia CAF kudhibitisha kuwa AFCON 2027 itaandaliwa Afrika Mashariki licha ya tetesi za kuahirishwa au kuhamishwa, uchambuzi wa raundi ya mwisho ya hatua ya makundi mechi za klabu bingwa, mechi za kufuzu kombe la dunia la wasichana U20, siku ya kwanza ya michuano ya raga ya wachezaji saba kila upande divisheni ya pili ya HSBC, mfumo mpya wa mashindano ya Tour du Rwanda, kiungo wa Ghana Thomas Partey akumbwa na shtaka jipya lakini pia michezo ya Olimpiki msimu wa baridi.
Leo tumeangazia kwa undani hukumu na uamuzi wa Caf kufuatia matukio yaliyoibuka kwenye fainali ya AFCON 2025, Simba inajandaa kwa mechi ya kufa kupona kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, raundi ya kwanza ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika mechi za Futsal yakamilika, msimu wa sita wa Ligi ya Afrika ya basketboli kumalizia nchini Rwanda, Faith Kipyegon ajenga hospitali huko Kenya, TP Mazembe yapata kocha mpya, fainali ya Australian Open, Ligi ya Mabingwa Ulaya yaingia raundi ya mtoano.
Leo kwenye kipindi tumeangazia uchambuzi wa mashindano ya AFCON 2025, vilabu vya Afrika Mashariki vinatafuta tiketi ya mchujo mechi za klabu bingwa, Kinshasa kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika ya Voliboli mwaka huu, wachezaji kadhaa wa ligi ya NBA waonesha nia kuiwakilisha Nigeria kwenye Olimpiki ya 2028, mashindano ya Afrika ya handboli inayoendelea Kigali, Uganda yapata kocha mpya wa basketboli, mfumo mpya wa mashabiki kupata visa mapema kuelekea Kombe la Dunia wafunguliwa rasmi
Leo tumeangazia pakubwa uchambuzi wa matukio na matokeo ya mechi za nusu fainali mechi za Kombe la Mataifa ya Afrika 2025 na mechi ya mshindi wa tatu leo usiku, hotuba ya rais wa CAF Patrice Motsepe kabla ya fainali, Droo ya mashindano ya WAFCON ya kina dada ya mwaka huu, Rwanda kuwa mwenyeji wa michuano ya Afrika ya Handboli, Rwanda na Burkina Faso zafuta kazi makocha wao.
Leo tunajadili kwa undani kauli ya kocha wa Afrika Kusini, Hugo Broos kuwa michuano ya mwaka huu haina mvuto na msisimko kama Afcon zilizopita. Uchambuzi wa mechi za jana na leo kwenye hatua ya 16 bora - Tanzania vs Morocco, Afrika Kusini vs Cameroon, DRC vs Algeria. Hatua ya serikali ya Gabon kuvunjilia mbali timu ya Gabon huku marais wa Msumbiji na Benin wakitoa ahadi za pesa kwa timu zao. Morocco kuandaa michuano ya Kombe la Dunia la Vilabu 2029 nayo Ethiopia ikiwania kuandaa Afcon ya 2028.
Leo tumeangazia kwa undani matokeo na matukio ya hatua ya makundi iliyokamilika kwenye michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika inayoendelea Morocco, uchambuzi wa hatua ya 16 bora - nani atafuzu robo fainali?, tathmini ya hatua ya serikali ya Gabon kuvunja kabisa timu ya taifa ya Gabon, ahadi za pesa kutoka kwa marais kadhaa Afrika kwa timu zao kuelekea robo fainali, usajili wa Rayon Sport, kwa nini Maresca aliondoka Chelsea?, dereva wa Anthony Joshua afunguliwa mashtaka baada ya ajali Nigeria.
Tuliyukuandalia leo ni pamoja na timu za Afrika zimepangwa kwenye makundi gani katika Kombe la Dunia la mwaka ujao, nani ataibuka na taji la Formula 1 kesho, Kenya kuandaa mashindano ya dunia ya Taekwondo, michuano ya kufuzu mashindano ya shule za upili barani Afrika, kuanza kwa Ligi ya Afrika ya basketboli ya wanawake, wachezaji wa soka Afrika waanzisha kampeni dhidi ya polio, Onana na Aboubakar watemwa kikosini Cameroon huku nahodha wa Nigeria Troost Ekong akistaafu soka la kimataifa.
Tuliyokuandalia leo ni pamoja na kilio cha washikadau wa mchezo wa fencing Afrika Mashariki kwa serikali za Afrika kusaidia kukuza mchezo, mashindano ya Tong Il Moo Do yarejea tena nchini Kenya baada ya marufuku ya mwaka mmoja, uchambuzi wa mechi za klabu bingwa Afrika, Sudan Kusini yaanza vyema michuano ya kufuzu Kombe la Dunia la Basketboli 2027, mfaransa Sebastian Ogier akaribia kushinda taji la dunia la tisa, uchambuzi wa mechi za ligi ya mabingwa Ulaya.
Leo tumezingatia tuzo za CAF 2025, AS FAR yaibuka washindi wa kombe la Ligi ya Afrika ya kina dada, kuanza kwa michuano ya klabu bingwa Afrika kwa wanaume huku AS FAR ikinyakua taji la kina dada, matokeo ya mechi za kufuzu AFCON U17 ukanda wa Cecafa, Curacao yakuwa taifa dogo zaidi kuwahi kufuzu Kombe la Dunia huku Marekani ikizindua mfumo maalum wa kutoa visa kwa wanunuaji tiketi.
Tuliyokuandalia leo ni pamoja na kuanza kwa michuano ya raga ya Afrika kwa kina dada wachezaji saba kila upande, michuano ya kufuzu Ligi ya Basketboli Afrika kwa kina dada, ligi ya klabu bingwa Afrika kwa kina dada, mechi za kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2026 - Gattuso asema Afrika inafaa kupewa nafasi chache, uchaguzi wa Kamati kuu ya Olimpiki nchini DRC, bingwa wa dunia Beatrice Chebet apokea tuzo ya kitaaluma.
Tuliyokuandalia leo ni pamoja na Sudan kusherehekea kambi ya kwanza kabisa ya ndondi ya wanawake nchini humo, Nairobi itakuwa mwenyeji wa michuano ya kufuzu ligi ya afrika ya basketboli mwezi huu, Kinshasa itaandaa michuano ya kitaifa ya ndondi ya chipukizi, Tanzania na Kenya zimefuzu michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kina dada mwaka 2026, Ethiopia itaandaa michuano ya kufuzu AFCON U17, ratiba ya mechi za mchujo kufuzu Kombe la Dunia, Paris Masters, Pogba apata jeraha jipya.
Tuliyokuandalia leo ni pamoja na waamuzi watatu nchini Rwanda kusimamishwa kwa muda, Kongamano la nne la Kibiashara la Soka lakamilika nchini Kenya, awamu ya mwisho ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kina dada, tuzo za CAF mwaka huu, mechi za kufuzu hatua ya makundi michuano ya Klabu Bingwa Afrika, mkenya Ruth Chepngetich apigwa marufuku ya miaka mitatu, bingwa wa dunia wa MotoGP Marquez kukosa msimu mzima uliosalia na nusu fainali ya tenisi Vienna Open
Tuliyokuandalia leo ni pamoja na tathmini ya timu za Afrika ambazo zimefuzu Kombe la Dunia 2026 na ni nani ambao wana nafasi ya kufuzu kuelekea raundi ya mwisho ya mechi za kufuzu, FIFA yateua wajumbe kutoka CECAFA, Herita Ilunga ndiye mkurugenzi mpya wa FECOFA nchini DRC, kocha wa zamani wa Yanga Nassredine Nabi waachana na Kaizer Chiefs, nyota tajika wa tenisi duniani wabwagwa kwenye mashindano ya Wuhan Open, Rovapera kustaafu mchezo wa kuendesha magari
Tuliyokuandalia leo ni pamoja na Rwanda kuwa taifa la kwanza Afrika kudhamini vilabu vya basketboli Ulaya, nini kinachoendelea klabuni Simba washikadau wanaendelea kuondoka, TP Mazembe yajiondoa katika Chama cha Vilabu vya Soka vya Kongo, Afrika inaandaa kwa mara ya kwanza mashindano ya boti za umeme nchini Nigeria, mwanawe Zidane aitwa kikosini Algeria, FIFA yazindua mpira utakaotumika mwaka ujao kwenye Kombe la Dunia, Hamilton akabiliwa na uchunguzi kuelekea mkondo wa Singapore.
Tuliyokuandalia leo ni pamoja na uchambuzi wa matokeo ya mechi za kufuzu kombe la dunia la mwaka ujao, mechi za kufuzu mashindano ya vilabu bingwa kwa kina dada ukanda wa CECAFA, mashindano ya CECAFA Kagame Cup, wanariadha watatu wa Uganda kukosa Riadha za Dunia mwezi huu nchini Japan, rais wa Marekani Donald Trump kuhudhuria fainali ya wanaume ya US Open, Luis Suarez apewa adhabu ya mechi sita baada ya kumtemea mate mwanachama wa benchi la ufundi ya klabu ya Seattle Sounders.
Leo tumeangazia fainali ya Kombe la Mataifa ya Wanawake kati ya Nigeria na Morocco, maandalizi ya CHAN yapamba moto, kamati ya Olimpiki nchini Kenya yapata viongozi wapya, kurejea kwa soka nchini Sudan licha ya vita, chama cha wachezaji Fifpro kikidai wachezaji wanahofia kulalamikia mrundiko wa mechi kwenye kalenda ya soka, uhamisho wa wachezaji ulaya, Verstappen ashinda mashindano ya mazoezi ya Belgian GP, Tour de France yafikia hatua ya 20 na fainali ya Kombe la EURO kwa wanawake.
Leo tumeangazia raundi ya pili ya makundi mechi za WAFCON, maandalizi ya Kenya kuandaa CHAN, riadha za Monaco Diamond League, michuano ya raga bara Afrika, fainali ya Congo Cup, msimamo wa jedwali wa hivi punde wa FIFA, Rwanda yajiandaa michuano ya bara Afrika basketboli kwa wanawake, uhamisho wa wachezaji kutoka Afrika huko Ulaya, fainali ya Kombe la Dunia la Vilabu, fainali za Wimbledon, hatua ya nane ya Tour du France na mechi za mwisho za makundi Kombe la EURO kwa kina dada.
Wiki hii timu ya mpira wa miguu ya taifa Socceroos, ili fuzu kwa Kombe la Dunia tena baada yakupata ushindi dhidi wenyeji wao Saudi Arabia.
Timu ya Somalia, imekuwa ikishiriki katika michuano ya kombe la Afrika la Kusini Australia bila mafanikio makubwa.
Timu 32 zinashiriki katika michuano ya kombe la dunia, inayo andaliwa na shirika la African Australia Football Association mjini Sydney, NSW.
Wapenzi wa mchezo wa mpira wa miguu kote duniani, walijumuika mbele ya runinga zao kutazama fainali ya Kombe la Dunia la FIFA kutoka mjini Sydney, Australia.