POPULARITY
Tuliyokuandalia leo ni pamoja na kuanza kwa mashindano ya kina dada ya Afcon, Kombe la Cecafa, mashindano ya Jumuiya ya Madola, tetesi za uhamisho Ulaya na Afrika Mashariki, mahakama ya kutatua migogoro duniani kuskiza kesi ya kubaini bingwa wa Afcon 2025 mwezi Oktoba tarehe nane.
Tuliyokuandalia leo ni pamoja uchambuzi wa nusu fainali, mechi ya mshindi wa tatu na taarifa kuu kuhusu Kombe la Dunia kuhusu washindi kutuzwa pete pamoja na medali na kombe huku Ballon d'Or yatangaza mchezaji anayecheza nje ya Ulaya ana uwezo wa kushinda tuzo hiyo. Timu ya taifa ya kina dada ya Kenya na Tanzania zasafiri kwa ajili ya Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Morocco, fainali ya Congo Cup na washindi wa kombe la Afrika la vilabu mchezo wa handboli.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina, leo tunamsikia Pauline Farini Kibuya wa shirika la Congo Notre Avenir yaani Congo Mustakabali Wetu kutoka DRC akizungumza na Idhaa hii kuhusu jinsi wanavyosongesha amani kwa taifa la DRC Congo. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na jifunze Kiswahili.Katibu Mkuu António Guterres aliyeko ziarani nchini China amehutubia mdahalo kuhusu Tahadhari za Mapema kwa Wote katika Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi unaofanyika kwenye jukwaa la kimataifa la Akili Mnemba na Tabianchi jijini Shanghai na kutoa wito wa kuharakisha maendeleo ya mifumo ya tahadhari za mapema inayotumia akili mnemba ili kuzuia majanga yanayosababishwa na mabadiliko ya tabianchi. Hata hivyo amesema "tahadhari lazima zifikie kila mtu aliyeko hatarini kwa lugha wanazoelewa na mifumo ya mawasiliano wanayoweza kuiamini."Kesho Julai 18 ikiwa ni siku ya kimataifa ya Nelson Mandela, Rais wa Kwanza Mweusi wa Afrika Kusini, huko Geneva, Uswisi hii leo mashindano ya 18 ya Nelson Mandela ya Mahakama ya Kimataifa ya Kuigiza yamefikia kilele kwa timu ya Chuo Kikuu cha Midlands State kutoka Zimbabwe kuibuka mshindi ilihali Chuo Kikuu cha Strathmore kutoka Kenya kimeshika nafasi ya pili.Hii leo hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, nchi wanachama na marafiki wa mpira wa miguu au kabumbu, wamezindua kampeni ya mwaka mmoja ya Dunia Moja, Mchezo Mmoja, Lengo Moja kwa lengo la kutumia mpira wa miguu kama kichochea cha kuimarisha afya ya akili kwa vijana, tukio linalofanyika siku mbili kabla ya fainali ya mashindano ya Kombe la Dunia kwa wanaume. Akizungumza mapema kabla ya tukio hilo Sahira Al Nahari, ambaye ni Kiongozi kijana mchechemuzi wa Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs amesema, "kwa hiyo, mpira wa miguu una mengi ya kutufundisha. Tunapokabiliwa na janga la kimataifa, hebu tuzielekeze fikra zetu kwenye viwanja vya mpira wa miguu. Tunapotazama kinachotokea viwanjani, tunajifunza nidhamu, ustahimilivu, na jinsi ya kuinuka tena baada ya kupoteza jambo muhimu sana."Na katika kujifunza lugha ya Kiswahili na hii leo Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili, Zanzibar nchini Tanzania, BAKIZA anafafanua maana na matumizi ya neno "CHOPOCHOPO."Mwenyeji wako ni Anold Kayanda, karibu!
Argentina na Uhispania wanaishi ndoto ya kipekee ya Kombe la Dunia, baada yakutinga fainali ya kombe hilo. Mjini Buenos Aires na Madrid, mashabiki wanachangia jinsi walivyopitia tamthilia, hisia na sherehe.
Na Hannah Naliaka Safari ya Ufaransa kutinga fainali za kombe la dunia imefikia tamati baada ya kushindwa mabao 2-0 na Uhispania katika nusu fainali ya kwanza. Unazungumziaje mechi hiyo ? Skiza maoni ya mskilizaji.
Na Hannah Naliaka Safari ya Ufaransa kutinga fainali za kombe la dunia imefikia tamati baada ya kushindwa mabao 2-0 na Uhispania katika nusu fainali ya kwanza. Unazungumziaje mechi hiyo ? Skiza maoni ya mskilizaji.
Nusu fainali za Kombe la Dunia zimewadia, Ufaransa na Uhispania zikijiandaa kufufua moja ya ushindani mkubwa wa soka la kimataifa. Tunaangalia kwa karibu habari za hivi punde za timu hizo na kusikia kutoka kwa kambi zote mbili kabla ya pambano kubwa la kesho.
Fainali za kombe la dunia zimefikia hatua ya nusu fainali, huku timu nne zikisalia kwenye mbio za kutwaa ubingwa. Uhispania itacheza na Ufaransa, wakati Uingereza itapambana na mabingwa watetezi Argentina. Unatathmini vipi hatua iliyofikia? Skiza maoni ya mskilizaji.
Fainali za kombe la dunia zimefikia hatua ya nusu fainali, huku timu nne zikisalia kwenye mbio za kutwaa ubingwa. Uhispania itacheza na Ufaransa, wakati Uingereza itapambana na mabingwa watetezi Argentina. Unatathmini vipi hatua iliyofikia? Skiza maoni ya mskilizaji.
Tuliyokuandalia leo ni pamoja na uchambuzi wa raundi ya 16 bora na robo fainali michuano ya Kombe la Dunia, Misri na Morocco zikiaga mashindano, Mbappe na Messi wang'ang'ania kiatu cha dhahabu, Yanga yapata kocha mpya Manqoba Mngqithi kutoka Afrika Kusini, Emmanuel Wanyonyi avunja rekodi ya mita 1000m mashindano ya Diamond League, mchezo mpya wa Flag Football waendelea kukua na kupata umaarufu Afrika.
Ufaransa imetinga nusu fainali ya Kombe la Dunia, baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Morocco. Kylian Mbappé amefunga mabao nane sawa na Lionel Messi, wakati Ousmane Dembélé akikamilisha ushindi huo.
Uhispania na Ubelgiji zimefuzu kwa robo fainali, wakati ndoto za Kombe la Dunia za wenyeji Marekani na Ureno ya Cristiano Ronaldo ziki gonga miamba.
Tuliyokuandalia leo ni mkusanyiko wa matukio ya raundi ya 32, je ni wakati timu changa kuanza kutamba? Timu mbili tu za Afrika kati ya tisa zafuzu kumi na sita bora, nini kimeiponza Afrika? uchambuzi wa raundi ya 16 bora inaanza leo, kiatu cha dhahabu na mechi za kufuzu Kombe la Dunia la wasichana chini ya miaka 17. Yanga yashinda ubingwa wa Tanzania kwa mara ya 32 huku DRC ikifuzu raundi ya pili michuano ya kufuzu Kombe la Dunia la basketboli.
Katika Siku ya 22 ya Kombe la Dunia la FIFA, Ureno iliwashinda Kroeshia katika mechi ya mwisho ya Kombe la Dunia ya Luka Modrić, Uhispania ili icharaza Austria, na Uswisi ikaishinda Algeria na kufuzu kwa Raundi ya 16.
Mashabiki wa timu za Afrika katika Kombe la Dunia la FIFA 2026, walipata pigo kubwa katika siku ya 20 na 21 ya michuano hiyo.
Mwaka huu DR Congo ilimaliza ukame wakuto shiriki katika Kombe la Dunia la FIFA baada ya zaidi ya miaka 50.
Siku ya 19 ya Kombe la Dunia la FIFA ilijumuisha mechi tatu za mchujo zenye ushindani mkali, huku Ujerumani na Uholanzi zikiondolewa baada ya mikwaju ya penati, wakati huo huo Brazil ilinyakua ushindi katika mechi yao muda mfupi kabla ya kipenga cha mwisho.
Sio kutia chumvi tunaposikia kwamba Kombe la Dunia la FIFA lina tarajiwa kuleta dunia pamoja katika mwezi wa Juni. Baada ya yote, mpira wa miguu unajulikana kama mchezo maarufu zaidi duniani.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayokupeleka mjini Caracas nchini Venezuela, mshikamano na raia wa nchi hiyo wadhihirika wakati huu wakiwa kwenye majonzi baada ya matetemeko ya ardhi kukumba wananchi. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo.Nchini Venezuela Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanaendelea kutoa msaada kufuatia matetemeko mawili ya ardhi yaliyolikumba taifa hilo wiki iliyopita. Mathalani, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP, limeripoti leo kwamba tayari limetoa zaidi ya tani elfu tatu za chakula, kiasi kinachotosha kusaidia familia zaidi ya elfu kumi kwa kipindi cha miezi miwili.”Huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo DRC, raia wameelezea haki zao zinazokiukwa ikiwemo kuzuiwa kupatiwa misaada ukatili wa kingono na mauaji. Maelezo hayo yamo kwenye ripoti iliyotolewa leo na Tume Huru ya Umoja wa Mataifa inayochunguza hali ya haki za binadamu katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, ikiwa ni ripoti yao ya kwanza mbele ya Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva, Uswisi?”.Na, michuano ya Fainali ya Kombe la Dunia la Mpira wa Miguu inaendelea huku dunia ikishuhudia ongezeko la joto kali. Katika juhudi za kulinda wachezaji, wafanyakazi na mashabiki dhidi ya athari za joto, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani WHO, Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema “WHO tunashirikiana na FIFA na nchi zinazoandaa michuano hiyo katika kampeni iitwayo Beat the Heat inayolenga kuweka mipango ya utekelezaji, kutoa elimu kwa wananchi, kuanzisha mifumo ya tahadhari za mapema, kuboresha upatikanaji wa maji salama ya kunywa, pamoja na kuweka maeneo ya kujipooza.”Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
Hatua ya makundi kwenye Kombe la Dunia inafikia kilele hii leo, ni timu gani zimefuzu hatua ya mtoano? Wiki ya pili ya michuano hii imeshuhudia rekodi zikiwekwa na kuvunjwa huku mataifa ya Afrika yakiendelea kufanya vizuri zaidi, lakini pia tutakupa uchambuzi wa mechi za kesho asubuhi. Aidha tumeangazia michuano ya Afrika Mashariki mchezo wa Baseball, tetesi za uhamisho na mashindano ya Paris Diamond League
Lionel Messi amekuwa mfungaji bora wa muda wote wa Kombe la Dunia, akifunga mara mbili nakusaidia Argentina kuishinda Austria 2-0 mjini Dallas, na kujihakikishia nafasi ya kwanza katika Kundi J, pamoja na nafasi katika hatua ya mchujo.
La RDC s'apprête à passer à la phase de production du lithium, un des minerais stratégiques pour la fabrication des batteries électriques. La société Manono Lithium du groupe chinois Zijin Mining a annoncé la production de 500 000 tonnes de carbonate de lithium d'ici la fin du mois de juin. Avec ce gisement qui est le plus important au monde, Kinshasa pourrait devenir un acteur clé au moment où la demande mondiale en lithium est en forte croissance. De notre correspondante à Lubumbashi, 500 000 tonnes de carbonate de lithium, c'est la quantité de production attendue au mois de juin, avec l'entrée en activité de la société Manono Lithium, du groupe chinois Zijin. Cette production devrait même doubler d'ici la fin de l'année. Eddas Lwaba Kitwa est le directeur des ressources humaines de la société Manono Lithium : « Le projet produira annuellement environ un million de tonnes de concentrés de lithium, dont environ 500 000 tonnes seront transformées en sulfate de lithium. Nous avons une très grande usine et cette transformation se fera localement. » Une transformation locale qui permettra à la société d'exporter ce minerai stratégique par voie lacustre avec une valeur ajoutée. « Les minerais seront exportés par Kalemie. Manono Lithium est aussi en train de construire un port industriel privé, le port de Mutoa », précise Eddas Lwaba Kitwa. À lire aussiRDC: Lubumbashi se rêve en acteur de la batterie automobile grâce au lithium Une production du lithium source de nombreux espoirs Dans cette course au lithium congolais, les Chinois ne sont plus seuls, même s'ils ont une longueur d'avance. Avec un investissement prévu de 50 millions de dollars d'ici 2027, la société américaine KoBold Metals accélère l'exploration dans la région. « Nous avons commencé par collecter les échantillons du sol. Nous avons huit permis de recherche dans la région de Manono et de Malemba Nkulu et nous espérons avoir encore plus de permis dans cette région. Aussi, nous espérons que sur les huit permis, nous aurons au moins un ou deux qui vont aboutir à des découvertes intéressantes de gisements qui pourront ensuite aller vers la production », détaille Benjamin Katabuka, le directeur général de KoBold Metals. La toute première production du lithium dans la province du Tanganyika suscite beaucoup d'espoir en termes de développement local. Forte des expériences passées, Maître Angèle Kombe, membre de la société civile basée à Kalemie, plaide pour que cette richesse profite au maximum aux communautés locales. « De Manono à Kalemie, où passe la route sur laquelle seront transportées des tonnes de lithium, il y a combien d'hôpitaux de qualité, combien d'écoles, combien de marchés ? Pour qu'il y ait développement, il faut d'abord une bonne gouvernance », alerte-t-elle. Avec une capacité de production de 5 millions de tonnes de lithium par an, la RDC se positionne une nouvelle fois comme un acteur clé dans la chaîne d'approvisionnement mondiale des minerais critiques. À lire aussiRDC: à Manono, l'exploitation prochaine du lithium suscite à la fois espoirs et inquiétudes
Ni wiki ambayo imegubikwa na michuano ya kombe la dunia 2026 huko Marekani, wiki hii eneo hili la Afrika mashariki na kati lilichangamka baada ya timu ya DRC Leopards kutoka sare na Ureno, virusi vya ebola na juhudi za kikanda kuudhibiti, kukamatwa kwa wakili Erias Lukwago kule Kampala Uganda, lakini pia mashambulio ya kigaidi kwenye uwanja wa ndege wa mjini Niamey huko Niger, na mkutano wa G7 jijini Paris Ufaransa, na hali kadhalika kusainiwa kwa mkataba kati ya Marekani na Iran
Leo tumeangazia kwa undani matukio na matokeo yote ya wiki ya kwanza michuano ya Kombe la Dunia 2026 - Mbappe, Messi waweka historia wakati Cape Verde na DRC zikihangaisha miamba wa soka wa ulaya, Tunisia yamfuta kazi kocha, uchambuzi wa mechi za leo. Aidha ni mwaka mmoja kuelekea Kombe la Mataifa ya Africa 2027, matokeo ya tenisi kombe la Davis Cup, Police fc ya Rwanda yamfuta kazi kocha wake, matokeo ya Cecafa U17 kwa kina dada pamoja na tetesi za uhamisho ulaya.
Mexico ime ingia katika hatua ya mchujo, baada ya kuishinda Jamhuri ya Korea katika siku ambayo iliadhimishwa na jeraha kubwa nchini Canada.
Mafanikio ya awali ya Socceroos katika Kombe la Dunia, yameangazia tena hadithi za mafanikio za Australia yenye tamaduni nyingi.
Mashabiki wa soka wana endelea kupata burudani kupitia Kombe la Dunia la FIFA 2026 linalo andaliwa nchini, Canada, Marekani na Mexico.
Mshtuko wa kwanza mkubwa wa Kombe la Dunia la FIFA umeshuhudiwa, baada ya timu ambayo inadhaniwa ina nafasi kubwa yakushinda michuano hiyo, kunyimwa ushindi na Cabo Verde wanao shiriki katika michuano hiyo kwa mara yao ya kwanza.
Ujerumani umeanza vyema kampeni yao ya Kombe la Dunia la 2026, ikiwashinda Curaçao inayo shiriki katika michuano hiyo kwa mara ya kwanza kwa mabao 7-1 katika Kundi E katika Uwanja wa Houston, Marekani.
Ni wiki ambayo imegubikwa na maandamano kadhaa nchini huko Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, huko Nanyuki nchini Kenya, na watu kutoka nchi kadhaa za Afrika kuihama Afrika Kusini kutokana na ongezeko la chuki dhidi ya wageni, lakini kubwa kabisa wiki hii lililotikisa ulimwengu ni michuano ya kombe la dunia ya mwaka wa 2026 iliyong'oa nanga huko Marekani, Mexico na Canada, bila kuisahau ziara ya Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Leo wa Kumi na nne huko Uhispania.-Naitwa Ruben Lukumbuka,
Tumeangazia Kombe la Dunia 2026 kuanza kwa vikwazo kadhaa, raia wa Afrika waiunga mkono Mexico dhidi ya Afrika Kusini, uchambuzi wa mechi ya leo Brazili dhidi ya Morocco, DRC wakijiandaa kupambana na Ureno wiki ijayo, maandalizi ya mbio za Kigali Marathon zakamilika, klabu ya Gor Mahia nchini Kenya yaamrishwa kufanya uchaguzi upya,
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, umetamatishwa leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. Idhaa hii imepata fursa ya kuzungumza na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya mkutano huu muhimu, Mtanzania Zuleikha Tambwe. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo..Hatari ya Ebola wakati wa Kombe la Dunia la Soka 2026 ni ndogo na hakuna sababu ya mashabiki kubadili mipango yao ya safari kuelekea Canada, Mexico na Marekani, limesema Shirika la Afya Duniani WHO kombe hilo liking'oa nanga leo. Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Ulaya, Hans Henri P. Kluge, amesema hakuna wagonjwa wa Ebola katika nchi hizo wala Ulaya na amesisitiza, “Safirini kama kawaida na furahieni mashindano hayo.” WHO imefafanua kuwa Ebola haisambai kwa njia ya hewa na visa vingi vipo katika maeneo ya mbali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Annalena Baerbock, amehitimisha ziara ya siku mbili jijini Nairobi nchini Kenya, ambapo amesisitiza nafasi muhimu ya Umoja wa Mataifa katika kuendeleza maendeleo, amani na ushirikiano barani Afrika. "Kila siku Umoja wa Mataifa na washirika wake huokoa maisha. Bila UN, mamilioni ya watoto wasingepata elimu kupitia UNICEF wala chanjo muhimu kupitia WHOna tusingekuwa na ushirikiano kama huu."Mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu CRPD, uliokuwa unafanyika hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani umefikia tamati leo. Kaulimbiu ya mwaka huu ni “kuadhimisha miaka 20 ya mkataba huo na kuimarisha utekelezaji wake katika dunia inayobadilika.” Kibaya Laibuta, Jaji wa Mahakama ya Rufani nchini Kenya, ambaye pia ni mlemavu aliyeoona au kipofu, ameshiriki na anaeleza alivyouona mkutano huu.Mwenyeji wako ni Rashid Malekela, karibu!
Kipute cha kombe la dunia kinaanza leo, huku Afrika Kusini ikipambana dhidi ya Mexico mwenyeji. Je, unazungumziaje timu za Afrika zinazoshiriki mashindano ya huu? Skiza makala haya.
Kipute cha kombe la dunia kinaanza leo, huku Afrika Kusini ikipambana dhidi ya Mexico mwenyeji. Je, unazungumziaje timu za Afrika zinazoshiriki mashindano ya huu? Skiza makala haya.
Tuliyokuandalia leo ni mambo muhimu ya kufahamu kuelekea Kombe la Dunia, timu ya Iran na mwamuzi wa Somalia hatimaye wapokea visa zao, namna mataifa ya Afrika yamecheza kwenye mechi za kirafiki kuelekea Kombe la Dunia, Riquelme na Florentino kupambania urais wa Real Madrid, Kenya kuandaa Davis Cup, kocha wa Kenya ajitetea baada ya sare dhidi ya Lesotho, tuzo za Ligi Kuu Kenya, kocha Flaurent Ibenge asalia Azam, Tanzania wavuna shaba kwenye fainali ya Afcon U17, Kenya yafuzu voliboli ya Afrika.
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania Kaskazini mwa taifa hilo la Afrika Mashariki, ambako Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro inaendelea kuwa mfano wa jinsi binadamu, wanyamapori na urithi wa kitamaduni vinavyoweza kuishi pamoja huku vikichangia maendeleo ya utalii endelevu na ulinzi wa mazingira. Je nini kinafanyika kuhakikisha uhifadhi, utamaduni, mazingira na utalii vinakutana kwa mustakabali endelevu? Ili kupata majawabu Flora Nducha wa Idhaa hii amezungumza na Kamishna wa Hifadhi ya Ngorongoro, Abdul-Razaq Badru.Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus ameendelea kusisitiza umuhimu wa ugunduzi wa mapema kwani hatua zikichukuliwa haraka wagonjwa wa Ebola wanapona. Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Geneva Usiswi baada kurejea kutoka ziarani mashariki mwa DRC amesema, Kufikia sasa, watu sita wamepona nchini DRC na wawili nchini Uganda, jambo linaloonesha kuwa watu wanaweza kupona Ebola iwapo watapata huduma za afya na kwenda vituo vya afya mara tu wanapoanza kuonyesha dalili za ugonjwa huo.Kuelekea kuanza kwa michuano ya Kombe la Dunia la FIFA wiki ijayo hapa Marekani na katika nchi jirani, Canada na Mexico, Shirika la Afya la Nchi za Amerika (PAHO) limetoa wito kwa nchi za bara la Amerika kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa wa surua na Rubella kufuatia mikusanyiko mikubwa inayotarajiwa na milipuko inayoendelea ya surua na ongezeko la safari za kimataifa vinaweza kuongeza kasi ya kuenea kwa ugonjwa huo. Shirika hilo linazitaka mamlaka za afya kubaini maeneo yaliyo katika hatari kubwa na kuimarisha hatua za kukabiliana haraka ili kuzuia maambukizi zaidi. Na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa asubuhi hii kwa saa za New York, Marekani wanachagua wanachama watano wapya wasio wa kudumu wa Baraza la Usalama kwa muhula kipindi cha miaka miwili kuanzia tarehe 1 Januari 2027 hadi 31 Desemba 2028. Kutoka Barani Afrika mgombea mmoja ni Zimbabwe ambaye hata hivyo anatarajiwa kupita kwani hana mpinzani katika nafasi hiyo. Nchi zitakazochaguliwa zinachukua nafasi za Somalia, Pakistan, Panama, Denmark na Ugiriki, ambazo mihula yao itaisha mwishoni mwa mwaka huu 2026.Mwenyeji wako ni Leah Mushi, karibu!
Leo asubui Mwalimu wa timu ya taifa ya Australia Tony Popovic ametangaza kikosi chake cha wachezaji 26, cha Socceroos watakao cheza katika Kombe la Dunia la FIFA la 2026.
Leo tumeangazia Arsenal kushinda ubingwa wa Ligi Kuu baada ya miaka 22, kocha wa Uingereza Tuchel azomewa kuwaacha nje wachezaji kadhaa, kocha wa DRC Desabre ataja kikosi cha Kombe la Dunia, Aston Villa yashinda Kombe la Europa, Droo ya kufuzu michuano ya AFCON 2027 yakamilika huku AFCON U17 ikiendelea, fainali za BAL zaanza Kigali, Kipchoge kukimbia marathon ya kwanza Afrika, Motsengo Omba ashinda urais wa Fecofa, raundi ya pili kufuzu Kombe la Dunia la wasichana chini ya miaka 17 yaanza.
Leo tunaangazia baadhi ya matukio ya michezo yaliyozungumziwa kwenye mkutano wa Africa Forward Summit uliokamilika hiki hii, uchambuzi wa Ghana kukosolewa kuandaa mashindano duni ya Afrika ya riadha, Al Hilal ya Sudan yatwaa ubingwa wa soka Rwanda, Motsengo Omba akizindua nguzo zake tano za uongozi wa Fecofa, fainali ya Kombe la Shirikisho, Afcon U17 yaanza huko Morocco, mataifa yaanza kuzindua vikosi vyao kuelekea Kombe la Dunia, PSG yashinda wa 14 huku Carrick akikaribia kusaini mkataba.
Tuliyokuandalia leo ni kufutwa kazi kwa kocha wa Yanga Pedro Goncalves, wawaniaji wengine wawili wajiondoa uchaguzi wa urais DRC, mashindano ya magari ya Africa yangoa nanga nchini Uganda, fainali ya Kombe la Shirikisho mkondo wa kwanza kupigwa leo usiku, mechi za kufuzu Kombe la Dunia la wasichana chini ya miaka 20, FIFA imetoa orodha ya wasanii wa kutumbuiza mechi za ufunguzi Kombe la Dunia, Arsenal imefika fainali ya Uefa baada ya miaka 20 huku IOC ikitoa marufuku ya Belarus.
Leo tumeangazia mashindano ya kwanza kabisa ya kina dada ya FIFA Series inayoandaliwa nchini Kenya, timu tano zimetinga mchujo wa ligi kuu, ziara ya rais wa CAF Motsepe nchini Senegal, ligi ya mabingwa Afrika yaingia hatua ya nusu fainali, kocha Aliou Cisse atua nchini Angola, michuano ya kufuzu Kombe la Dunia la wasichana chini ya miaka 17, droo ya Afcon U17, michuano ya shule za upili za Afrika zakamililka, mageuzi ya mbio za marathon kwenye riadha za dunia, Ndala Ngambo haendi Kombe la Dunia
Leo tumeangazia kufuzu kwa DRC michuano ya kombe la dunia tukiwa na mgeni wetu Felly Mulumba, mchezaji wa soka kutoka DRC, Ghana yamfuta kocha Otto Addo, mageuzi katika kamati andalizi ya AFCON 2027 nchini Kenya, Tigers na Petro de Luanda zafuzu fainali ya BAL, Algeria mabingwa wa basketboli ya vitimagu Afrika, kustaafu kwa Victor Wanyama huku ligi ya Kenya ikilenga kuwa bora Afrika, je De Zerbi ataiokoa Spurs kushushwa daraja?
DRC imejikatia tiketi ya kucheza kwenye kupute cha kuwania kombe la dunia Haya hapa maoni ya waskilizaji.
DRC imejikatia tiketi ya kucheza kwenye kupute cha kuwania kombe la dunia Haya hapa maoni ya waskilizaji.
Ripoti ya shirika la Amnesty Interenational imeonya kuwa Kombe la Dunia la mwaka huu linaweza kuchangia ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu dunaini kutokana mpango wa mataifa wenyeji kuweka mikakati kali za uhamiaji na ufuatiliaji wa karibu wa mashabiki wa kigeni Je, unahisi mashabiki kutoka Afrika Mashariki watakuwa salama kushabikia timu zao kule Merekani,Mexico na Canada? Skiza maoni ya waskilizaji.
Ripoti ya shirika la Amnesty Interenational imeonya kuwa Kombe la Dunia la mwaka huu linaweza kuchangia ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu dunaini kutokana mpango wa mataifa wenyeji kuweka mikakati kali za uhamiaji na ufuatiliaji wa karibu wa mashabiki wa kigeni Je, unahisi mashabiki kutoka Afrika Mashariki watakuwa salama kushabikia timu zao kule Merekani,Mexico na Canada? Skiza maoni ya waskilizaji.