Podcasts about kombe

  • 24PODCASTS
  • 122EPISODES
  • 22mAVG DURATION
  • 1EPISODE EVERY OTHER WEEK
  • May 3, 2025LATEST

POPULARITY

20172018201920202021202220232024


Best podcasts about kombe

Latest podcast episodes about kombe

Jukwaa la Michezo
AFCON U20: Michuano ya vijana ya soka yang'oa nanga nchini Misri

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later May 3, 2025 23:53


Hii leo tumeangazia michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya vijana chini ya miaka 20 kuanza nchini Misri, mkondo wa mtoano katika msururu wa raga duniani, diamond league mkondo wa pili huko Uchina na Ligi ya Basketboli mkondo wa Sahara ukiendelea, Cecafa yapata rais mpya, nembo ya Visit Rwanda yaendelea kupanuka, bondia wa DRC Martin Bakole kupigana leo usiku, PSG, Man Utd, Spurs na Chelsea zavuna matokeo mazuri kwenye nusu fainali ligi za vilabu bingwa ulaya.

Jukwaa la Michezo
Riadha: Ni nani atashinda mbio za London Marathon mwaka 2025?

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Apr 26, 2025 24:06


Leo tumeangazia michuano ya klabu bingwa kufuzu fainali, riadha za Diamond League, Boston na London Marathon, Cameroon yafuzu Kombe la Dunia la U17, uchaguzi wa kamati ya Olimpiki nchini Kenya watibuka, Gor Mahia yanuia kujenga uwanja wao, uchambuzi wa debi ya El Clasico huku Carlos Alcaraz akijiondoa kwenye mashindano ya Madrid Open.

Jukwaa la Michezo
Jean-Jacques wa DRC kati ya waamuzi waliochaguliwa kwenye Kombe la Dunia la Vilabu

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Apr 19, 2025 23:53


Jumamosi hii tunaangazia nusu fainali ya michuano ya klabu bingwa Afrika, waamuzi kutoka Kenya na DRC miongoni mwa waamuzi kusimamia michuano ya Kombe la Dunia la Vilabu Marekani mwaka huu, fainali wa Afcon U17, kwenye riadha Chepngetich na Jepchirchir wajiondoa kwenye London Marathon, mechi za kufuzu Kombe la Dunia la wasichana chini ya umri wa miaka 17 pamoja uchambuzi wa robo fainali tatanishi kwenye ligi za mabingwa ulaya wiki hii.

Jukwaa la Michezo
CAF: Simba yatinga nusu fainali michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Apr 12, 2025 24:00


Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa matokeo ya robo fainali mechi za klabu bingwa Afrika, Uganda yalenda kufuzu Kombe la Dunia wasiozidi miaka 17, timu ya taifa ya raga ya kina dada ya Kenya yalenga kurejea katika msururu wa dunia, michuano ya vilabu ya Afrika mchezo wa voliboli, Rwanda yaadhimisha miaka 31 michezoni tangu mauaji ya kimbari, Maluki atangaza nia ya kuwania urais wa Nock, Salah asaini kandarasi mpya Liverpool, Real Madrid itageuza meza dhidi ya Arsenal?

Jukwaa la Michezo
Kenya: Nani atatamba kwenye "Debi ya Mashemeji" AFC Leopards vs Gor Mahia?

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Mar 29, 2025 23:54


Miongoni tuliyokuandalia ni pamoja na matokeo ya raga mkondo wa HongKong 7s, sakata la upangaji mchezaji dhidi ya golikipa wa Kenya Patrick Matasi, maandalizi ya debi ya Mashemeji, Misri yapewa haki za kuandaa AFCON U20 huku CAF ikiifungulia uwanja wa Benjamin Mkapa, tuzo nono kwa washindi wa Kombe la Dunia la vilabu, kocha wa Brazil atimuliwa naye Djokovic akikaribia kushinda taji lake la 100.

Jukwaa la Michezo
Misri, Morocco,Tunisia zang'ara mashindano ya tenisi ya vijana chini ya miaka 14

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Mar 2, 2025 23:46


Tuliyokuandalia hii leo ni pâmoja na matokeo ya mashindano ya tenisi ya vijana barani Afrika chini ya miaka 14, kocha mpya wa Kenya ni nani, matokeo ya mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kina dada, timu sita kushiriki ligi ya Afrika ya basketboli kwa mara ya kwanza, huku Afrika Kusini ikijiandaa kutuma ombi rasmi la kuandaa mkondo mmoja wa F1 na Jose Mourinho apata afueni baada ya adhabu yake kupunguzwa.

Jukwaa la Michezo
Simba kukutana na Al Masry kwenye Droo ya robo fainali Kombe la Shirikisho CAF

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Feb 22, 2025 23:49


Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na matokeo kwenye mashindano ya kimataifa ya gofu ya Magical Kenya Open, bondia wa DRC kupambana na muingereza huko Saudi Arabia, maandalizi ya Tour du Rwanda, Droo ya robo fainali michuano ya klabu bingwa Afrika, mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kina dada 2026 na basketboli ya 2025, halikadhalika Droo ya 16 bora mechi za klabu bingwa Ulaya na michuano ya raga ya Vancouver 7s.

Jukwaa la Michezo
Gofu: Wachezaji 150 kutoka mataifa 30 duniani kushiriki Magical Kenya Open 2025

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Feb 15, 2025 23:54


Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na taarifa kuelekea mashindano ya gofu duniani ya Magical Kenya Open 2025, bodi ya Ligi ya soka nchini Tanzania yashusha rungu kwa Pamba Jiji na Ally Kamwe, timu 18 zimehakikisha kushiriki mashindano ya voliboli ya ukanda wa tano nchini Uganda, droo ya michuano ya Afcon U17 na U20, mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya kina dada 2026, Jannik Sinner akubali kufungiwa miezi mitatu, raundi ya mtoano mechi za klabu bingwa Ulaya.

VOA Express - Voice of America
Kenya na Burkinafaso zapewa nafasi kubwa kuchukua kombe la Mapinduzi - Januari 08, 2025

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jan 8, 2025 29:59


Kenya na Burkinafaso zapewa nafasi kubwa kuchukua kombe la Mapinduzi

Jukwaa la Michezo
Mashindano ya magari ya Dakar Rally 2025 yang'oa nanga huko Saudi Arabia

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Jan 4, 2025 23:57


Leo kwenye makala ya kwanza kabisa ya Jukwaa la Michezo mwaka 2025, tumeangazia raundi ya nne hatua ya makundi mechi za Ligi ya vilabu bingwa Afrika. Mwanariadha mkenya Beatrice Chebet avunja rekodi yake ya dunia huku raia wa Eritrea mwendesha baiskeli Biniam Girmay akishinda tuzo la Afrika wakati uo huo mashindano ya magari ya Dakar Rally na Kombe la Mapinduzi yaking'oa nanga. Lakini pia tutatupia jicho tetesi za uhamisho ulaya na michuano ya tenisi ya Brisbane Open inayoendelea.

Jukwaa la Michezo
Kigali: Max Verstappen aongoza katika sherehe za Tuzo za FIA kwenye mkutano mkuu

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Dec 14, 2024 23:54


Tulikuandalia ni pamoja na yaliyozungumziwa kwenye mkutano mkuu wa shirikisho la mchezo wa kuendesha magari duniani, FIA nchini Rwanda, uchambuzi wa raundi ya tatu ya mechi za ligi ya mabingwa Afrika, Pape Thiaw ateuliwa kuwa kocha mpya wa Senegal, Afrika Kusini yashinda Kombe la Afrika mchezo wa pete, uchambuzi wa mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya, Saudi Arabia ikithibitishwa kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia mwaka 2034

Jukwaa la Michezo
Fahamu mchezo wa Tong IL Moo Do kuelekea mashindano ya Mombasa Open 2024

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Nov 30, 2024 23:50


Tuliyokuandalia ni pamoja na mahojiano ya moja kwa moja na washikadau wa mchezo wa Tong IL Moo Do ambao walitutembelea studioni. Mchezo huu unazidi kukua Afrika. Je, unachezwaje, nini umuhimu wake, umepiga hatua kiasi gani, maandalizi ya makala ya Mombasa Open ya mwaka huu yakoje? Pia tumeangazia Ligi ya Klabu bingwa Afrika, msimu mpya wa raga ya HSBC duniani na Kombe la Mataifa ya Afrika ya kina dada mchezo wa handboli ambayo ilianza wiki hii pamoja na uchambuzi wa mechi za klabu bingwa Ulaya

Jukwaa la Michezo
CAF: Droo ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kina dada yakamilika

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Nov 23, 2024 23:52


Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa droo ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kina dada 2024, fainali ya klabu bingwa Afrika kwa kina dada, nini maana ya Tanzania na Uganda kuwakilisha CECAFA kwenye AFCON 2024, mechi za kufuzu ligi ya Afrika ya Basketboli na michuano ya kufuzu Mashindano ya Afrika ya Basketboli, ligi za ukanda na ulaya Pep Guardiola atia saini mkataba mpya klabuni Man City.

Jukwaa la Michezo
AFCON 2025: Uganda yafuzu fainali za mwaka kesho huku Kenya, Ghana zikitupwa nje

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Nov 16, 2024 23:56


Tuliyoyazungumzia ni pamoja na upekee wa klabu ya voliboli nchini Kenya ya Trailblazers, uchaguzi wa FKF nchini Kenya umeanza, mabadiliko ya makocha klabuni Yanga, timu ya taifa ya Kenya ya walemavu ya soka yamaliza nafasi ya nne Kombe la Dunia, uchambuzi wa michuano ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2025 na pigano la Jake Paul dhidi ya Mike Tyson

Jukwaa la Michezo
Nitawania tena urais wa CAF mwaka 2025, amethibitisha Dkt Patrice Motsepe

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Oct 26, 2024 23:47


Tuliyokuandalia ni pamoja na taarifa ya Rais wa CAF Patrice Motsepe kuwania tena urais muhula wa pili, hukumu ya CAF katika mechi ya Nigeria dhidi ya Libya, yaliyotukia kwenye ziara ya rais wa Olimpiki ya kimataifa nchini Kenya na Kongamano la tatu la kibiashara la soka Afrika, uchambuzi wa michuano ya Kombe la Dunia la kina dada U17, Senegal ikihifadhi ubingwa wa Afrika soka ya ufukweni, michuano ya ndondi Afrika jijini Kinshasa, PSG kumlipa Mbappe €55M na uchambuzi wa El Clasico leo usiku.

Jukwaa la Michezo
Tanzania na Kenya zafuzu michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika U20 mwaka ujao

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Oct 19, 2024 24:03


Tuliyokuandalia ni pamoja na michuano ya kufuzu AFCON U20 mwaka ujao, namna timu za Afrika zilicheza kwenye wiki ya kwanza ya Kombe la Dunia la kina dada wasiozidi miaka 17, timu ambazo tayari zimefuzu AFCON ya 2025 nchini Morocco na nafasi ya timu za Afrika Mashariki na Kati, AFCON ya ufukweni yaanza leo nchini Misri, droo ya klabu bingwa Afrika kwa kina dada, mashindano ya magari ya Rwanda Mountain Gorilla Rally, kutimuliwa kwa kocha Kavazovich klabuni Vipers na Ligi za ukanda na Ulaya

Jukwaa la Michezo
AFCON U20: DRC yafuzu Kombe La Mataifa Ya Afrika ya mwaka ujao

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Oct 5, 2024 24:03


Tuliyokuandalia ni pamoja na faniali za kufuzu mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wasiozidi miaka 20, uchambuzi wa vikosi vilivyotajwa na wakufunzi kuelekea raundi ya tatu ya kufuzu AFCON 2025, masaibu ya Samuel Eto'o na kocha wa Senegal Aliou Cisse kutemwa, kifo cha nyota wa basketboli Dikembe Mutombo pamoja na matokeo ya mechi za ligi ya mabingwa ulaya.

Jukwaa la Michezo
Kenya kuwa mwenyeji wa mashindano ya juu zaidi ya baiskeli barani Afrika

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Sep 28, 2024 24:05


Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa mechi ya Kombe la Super Cup Afrika, Kenya kuwa mwenyeji wa mashindano ya baiskeli Afrika kwa mara ya kwanza, matokeo ya riadha jijini New York, sura mpya za wanariadha watakaoshiriki Berlin Marathon hapo kesho, Ligi za ukanda kwenye soka, voliboli na basketboli lakini pia matokeo ya Kombe la Europa League raundi ya kwanza.

Jukwaa la Michezo
CHAN 2024 kuanza Februari 1-28 mwaka 2025 nchini Uganda, Kenya na Tanzania

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Sep 21, 2024 24:04


Tuliyokuandalia ni pamoja na taarifa ya ziara ya rais wa CAF Patrice Motsepe nchini Kenya, awamu ya pili kufuzu hatua ya makundi mechi za klabu bingwa Afrika, timu za Kenya za soka na mchezo wa Kabaddi tayari kushiriki Kombe la Dunia, timu za taifa Afrika Mashariki zimepanda kwenye msimamo wa dunia wa FIFA, uchambuzi wa raundi ya kwanza mechi za UEFA na mchezo wa ndondi kati ya Anthony Joshua na Daniel Dubois leo usiku.

Jukwaa la Michezo
AFCON 2025: Safari ya kuelekea Morocco yaanza kwa mataifa ya Afrika

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Sep 7, 2024 24:02


Tuliyokuandalia ni pamoja na matokeo na uchambuzi wa mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika 2025, kifo cha mwanariadha wa Uganda nchini Kenya, matokeo ya Zurich Diamond League, matokeo ya U18 Afrobasket na Congo Cup, uchambuzi wa matokeo ya  mataifa ya Afrika kwenye Olimpiki ya walemavu jijini Paris, mechi za Ligi ya Mataifa ya Ulaya na tuzo za Ballon D'Or mwaka 2024

VOA Express - Voice of America
Mashabiki wa soka wajindaa kutazama mchuano wa fainali za kombe la Euro-2024 Jumapili - Julai 11, 2024

VOA Express - Voice of America

Play Episode Listen Later Jul 11, 2024 29:59


Mashabiki wa soka wajindaa kutazama mchuano wa fainali za kombe la Euro-2024 Jumapili

euro soka julai kombe jumapili
Jukwaa la Michezo
Shirikisho la soka barani Afrika CAF latangaza droo ya michuano ya kufuzu AFCON 2025

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Jul 6, 2024 23:55


Miongoni mwa yale tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa droo ya mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya mwaka 2025, fainali ya Cosafa Cup, mipango ya Team Kenya kuelekea Olimpiki ya mwaka huu, uchambuzi wa mechi za robo fainali michuano ya Euro na Copa America, raia wa Eritrea Girmay Hailu Biniam ashinda hatua ya nane ya Tour de France wakati kocha wa Manchester  United Erik ten Hag aongeza mkataba wake. 

Jukwaa la Michezo
CAF: Kenya Police FC yafuzu kushiriki Kombe la Shirikisho barani Afrika msimu ujao

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Jun 29, 2024 23:54


Tumekuandalia mengi ikiwemo matokeo na uchambuzi wa mashindano ya COSAFA Cup inayoendelea nchini Afrika Kusini, Leopards voliboli ya ufukweni yafuzu Kombe la Dunia wakati Kinshasa yajiandaa kuandaa mechi za kufuzu kombe la mataifa ya Afrika mchezo wa basketboli ya kutumia viti vya magurudumu, Kenya yateua kikosi kitakachoshiriki riadha za dunia U20 nchini Peru, tetesi za uhamisho katika vilabu vya Afrika Mashariki, Kenya Police yafuzu kombe la shirikisho barani Afrika msimu ujao. Tour de France yaanza leo nchini Italia kabla ya kurejea Ufaransa huku michuano ya EURO na Copa America ikiingia hatua za mtoano.

Sepetuko
Junior Starlets Wafuzu kwa Kombe la Dunia la Wanawake Chini ya Miaka 17

Sepetuko

Play Episode Listen Later Jun 18, 2024 3:41


Heko kwa Junior Starlets kwa kufuzu kushiriki Kombe la Dunia kwa wanawake chipukizi chini ya miaka 17. Historia iliyoje! Junior Starlets inakuwa timu ya kwanza kabisa ya Kenya ya kandanda kufuzu kwa Kombe la Dunia. Maandalizi ya kushiriki kombe hilo yaanze sasa.

Jukwaa la Michezo
Kipyegon, Omanyala wafuzu Olimpiki ya Paris kwenye mchujo wa kitaifa

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Jun 15, 2024 23:43


Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na mchujo wa kitaifa wa Kenya kuteua timu itakayowakilisha kwenye Olimpiki ya Paris mwaka huu, Kenya yakosa kupandishwa daraja kwenye tenisi mashindano ya Billie Jean King Cup, uwanja wa Amahoro nchini Rwanda umeidhinishwa na FIFA kuandaa mechi za kimataifa, Junior Starlets ipo guu moja kufuzu Kombe la Dunia, droo ya kufuzu AFCON 2025 kuandaliwa Julai na michuano ya EURO kuanza Ujerumani. 

Jukwaa la Michezo
French Open: Iga Swiatek ashinda ubingwa wake wa nne wa Roland Garros

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Jun 8, 2024 23:50


Tuliyokuandalia Jumamosi hii ni pamoja na uchambuzi wa mechi za kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2026 (Afrika), Kenya kuandaa mashindano ya mchujo kutafuta timu itakayowakilisha katika Olimpîki ya Paris mwezi Julai huku wanamichezo 33 wakipigwa na marufuku kwa kutumia dawa za kusisimua misuli, matokeo ya Congo Cup, kocha Gamondi arefusha mkataba wake klabuni Yanga huku zikiwa zimesalia siku sita kabla ya mashindano ya EURO nchini Ujerumani, Iga Swiatek ashinda ubingwa wake wa nne wa French Open

Jukwaa la Michezo
BAL2024: Petro de Luanda yaibuka na taji la Ligi ya Basketboli barani Afrika

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later Jun 1, 2024 23:55


Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa fainali ya Ligi ya Basketboli Afrika mwaka huu, matokeo ya Diamond League mkondo wa Oslo na mchujo wa raga duniani, uchambuzi wa vikosi vya Afrika Mashariki na Kati kuelekea mechi za kufuzu Kombe la Dunia la mwaka 2026, uchambuzi wa Fainali ya Klabu bingwa Ulaya (Dortmund dhidi ya Real Madrid) na matokeo ya French Open huku Ronaldo akitokwa na machozi baada ya kupoteza fainali ya Saudi Kings Cup

Jukwaa la Michezo
DRC: Sebastian Desabre arefusha mkataba wake kama kocha wa timu ya taifa

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later May 25, 2024 23:46


Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa fainali ya Klabu bingwa Afrika, Tanzania waibuka na kombe la shule za upili afrika mchezo wa soka, fainali za ligi ya basketboli kuanza nchini Rwanda wakati makocha wa Kenya na Uganda wataja vikosi vyao kufuzu Kombe la Dunia na matokeo ya Ligi za ulaya.

Jukwaa la Michezo
CAF: Nani ataibuka na taji la Klabu bingwa barani Afrika 2024?

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later May 18, 2024 24:42


Tuliyokuandalia ni pamoja na uchambuzi wa fainali ya Klabu Bingwa Afrika mwaka 2024, Zanzibar kuandaa fainali za mashindano ya shule za upili barani Afrika, Mkusanyiko wa michezo kwenye ukanda wa Afrika Mashariki, Maniema yarejea kwenye mashindano ya vilabu barani Afrika, uchambuzi wa mbio za kuwania taji la Uingereza kati ya Man City na Arsenal, Ngolo Kante arejea kikosini mwa Ufaransa, Brazil yateuliwa kuandaa Kombe la Dunia la kina dada la mwaka 2027.

Jukwaa la Michezo
Diamond League: Mary Moraa na Beatrice Chebet waibuka washindi riadha za Doha DL

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later May 11, 2024 23:53


Tuliyokuandalia hii leo ni pamoja na matokeo ya riadha kwenye Doha Diamond League, AFCON UAE kuanza hapo kesho huko Dubai, michuano ya Congo Cup, uchambuzi wa mechi za Ligi ya Basketboli ya Afrika, Guinea yafuzu fainali za Olimpiki kwenye soka, mechi za kufuzu Kombe la Dunia la U17 kwa kina dada, Mbappe atangaza rasmi kuondoka PSG na uchambuzi wa fainali za mwaka huu za michuano ya bara Ulaya.

Jukwaa la Michezo
Uganda : Uwanja wa Namboole kuanza kutumika kwa mechi za kufuzu Kombe la dunia

Jukwaa la Michezo

Play Episode Listen Later May 4, 2024 23:54


Tuliyokuandalia ni pamoja na Uchambuzi wa orodha ya mwisho ya Kikosi cha Marathon cha Team Kenya kuelekea Olimpiki, watu watano nchini Kenya wapigwa marufuku ya muda kwa madai ya upangaji mechi. Nchini Uganda, Rais wa FUFA asema uwanja wa Naambole utakuwa tayari kuandaa mechi wa kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2026 na Ligi ya Basketboli barani Afrika mkondo wa Sahara umeanza leo.

Alfajiri - Voice of America
Shangwe na vigelegele baada ya Ivory Coast kushinda fainali za Afcon - Februari 12, 2024

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 12, 2024 30:00


Sebastien Haller alifunga bao la ushindi dakika tisa kabla ya mchezo kumalizika wenyeji Ivory Coast wakinyakua taji la tatu la Kombe la Mataifa ya Afrika kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Nigeria kwenye mchezo wa fainali Uwanja wa Alassane Ouattara mjini Abidjan Jumapili (Februari 11).

Jioni - Voice of America
Michuano ya Kombe la mataifa ya Afrika ilikuwa ya aina yake - Februari 09, 2024

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Feb 9, 2024 59:59


Michuano ya Kombe la mataifa ya Afrika ilikuwa ya aina yake

SBS Swahili - SBS Swahili
Somalia yatengeza historia katika fainali ya kombe la Afrika Kusini Australia

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 24, 2023 6:58


Timu ya Somalia, imekuwa ikishiriki katika michuano ya kombe la Afrika la Kusini Australia bila mafanikio makubwa.

SBS Swahili - SBS Swahili
Sudan Kusini yapiga hatua ya kwanza kutetea kombe lao

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 2, 2023 4:26


Timu 32 zinashiriki katika michuano ya kombe la dunia, inayo andaliwa na shirika la African Australia Football Association mjini Sydney, NSW.

nsw kwanza timu hatua kombe sudan kusini
SBS Swahili - SBS Swahili
Historia ya tengezwa katika fainali ya kombe la dunia mjini Sydney

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Aug 23, 2023 9:22


Wapenzi wa mchezo wa mpira wa miguu kote duniani, walijumuika mbele ya runinga zao kutazama fainali ya Kombe la Dunia la FIFA kutoka mjini Sydney, Australia.

Jioni - Voice of America
Marekani yaondolewa na Sweden kwenye Kombe la Dunia la Wanawake - Agosti 06, 2023

Jioni - Voice of America

Play Episode Listen Later Aug 6, 2023 29:59


Marekani Jumapili litingwa 5-4 na Sweden kwa mikwaju ya penalti na hivyo kulazimika kuliaga Kombe la Dunia la wanawake.

SBS Swahili - SBS Swahili
Ziara ya kombe la dunia ya anza nchini Australia kabla ya michuano hiyo kuanza

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Jun 11, 2023 7:44


Tiketi milioni moja za kombe la dunia, la soka ya wanawake itakayo andaliwa nchini Australia na New Zealand zime uzwa tayari.

SBS Swahili - SBS Swahili
Morrocco yapeperusha bendera ya Afrika kwa fahari katika kombe la dunia

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 8, 2022 6:21


Michuano ya kombe la dunia ilipoanza, bara zote za dunia zilikuwa na wawakilishi.

SBS Swahili - SBS Swahili
Socceroos waaga kombe la dunia kibabe

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Dec 5, 2022 6:13


Matumaini ya mashabiki wa timu ya taifa ya Australia inayo julikana kwa jina la "Socceroos" kucheza katika robo fainali, yame gonga mlinda lango wa Argentina Emiliano Martinez.

Alfajiri - Voice of America
Senegal yafuzu kuingia raundi ya 16 bora kwenye michuano ya Kombe la Dunia - Novemba 30, 2022

Alfajiri - Voice of America

Play Episode Listen Later Nov 30, 2022 30:00


Timu ya taifa ya Senegal Simba wa Teranga imekuwa ya kwanza ya Afrika kufanikiwa kuingia kwenye raundi ya 16 katika michuano ya mwaka huu baada ya kuifunga Ecuador bao 2-1.

SBS Swahili - SBS Swahili
Socceroos wajipa uhai katika kombe la dunia la FIFA Qatar 2022

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 29, 2022 6:16


Wadau wengi wa soka hawakuipa Australia, nafasi katika orodha ya timu zenye uwezo wakufuzu kutoka kundi lao la D la Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022.

Habari za UN
28 NOVEMBA 2022

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 28, 2022 0:10


Hii leo jarida linakuletea habari za WHO na michuano ya fainali za Kombe la Dunia. Makala inatupeleka kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya kusikia simulizi ya msichana mnufaika wa mradi wa Girl Shine na Mashinani tutaelekea nchini Uganda kwa mkimbizi mwanaharakati wa mazingiraBaada ya mfululizo wa mashauriano na wataalamu wa kimataifa, hatimaye shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO litaanza kutumia jina MPOX badala ya Monkeypox au homa ya Ndui ya Nyani kufuatia mapendekezo ya kubadilishwa kwa jina hilo kwa maelezo ya kwamba lilikuwa linasababisha mambo kadhaa ikiwemo unyanyapaa.Michuano ya fainali za Kombe la Dunia kwa mchezo wa soka kwa wanaume inaendelea nchini Qatar huko Mashariki ya Kati. Mmoja wa watu wanaong'ara katika michuano hii ni Mchechemuzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Rwanda, Salima Mukansanga, ambaye ameweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza mweusi kuwa mwamuzi au refarii katika Kombe la Dunia.Makala inatupeleka kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya kusikia simulizi ya msichana mnufaika wa mradi wa Girl Shine, unaolenga kupatia wasichana barubaru stadi za kiuchumi, uongozi na msaada wa kisaikolojia ili waweze kujikwamua na kujitambua katika mazingira hatarishi waliyomo.Na leo mashinani tutaelekea nchini Uganda kwa mkimbizi mwanaharakati wa mazingiraMwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!

Habari za UN
Kutoka Cyangugu Rwanda hadi kuwa mwamuzi fainali za kombe la dunia, Qatar- Simulizi ya Salima

Habari za UN

Play Episode Listen Later Nov 28, 2022 0:02


Michuano ya Kombe la Dunia inaendelea nchini Qatar huko Mashariki ya Kati. Mmoja wa watu wanaong'ara katika michuano hii ni Mchechemuzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF Rwanda, Salima Mukansanga, ambaye ameweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza mweusi kuwa mwamuzi au refarii katika Kombe la Dunia. Aliingiaje katika tasnia hii ya mpira wa miguu? UNICEF Rwanda ilizungumza naye kabla hajasafiri kwenda Qatar na hapa Anold Kayanda anaeleza kwa lugha ya Kiswahili kilichozungumzwa. “Nilikuwa nyumbani wakati wa likizo nikiwa kidato cha tano nikielekea kidato cha sita katika elimu ya sekondari,” ni Salima Mukansanga, msichana raia wa Rwanda mwenye umri wa miaka 35 mmoja wa waamuzi katika kombe la dunia akieleza kwa kifupi safari yake kwamba alikuwa nyumbani wakati wa likizo wakati huo akiwa kidato cha tano akisubiri kuingia kidato cha sita, aliposikia wakitangaza tangazo kuwa kulikuwa na uandikishaji wa refarii au waamuzi wanawake na wasichana kwa ajili ya mpira wa miguu.  Anasema, “wakati huo  nikafikiria nyakati zote ambapo kwa udadisi wangu nilikuwa najiuliza hawa waamuzi wa mpira huwa wanafanya nini? Haraka nilituma maombi na nikapata bahati nikakubaliwa. Kwenye mafunzo nikafanya vizuri sana. Nilikuwa katika 5 bora na nikawa mwamuzi au refarii.”  Salima ambaye kabla ya kuvunja rekodi ya sasa ya kuwa mwanamke wa kwanza mweusi kuwa mwamuzi katika miaka 92 ya uwepo wa Kombe la dunia, alianza na Kombe la Dunia la Wanawake mwaka 2019 ambapo alikuwa mwanamke wa kwanza kuwa mwamuzi katika michuano hiyo na kabla ya hapo  mwanzoni mwa mwaka huu alivunja rekodi nyingine kwa kuwa Mwamuzi mwanamke wa kwanza katika Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON kwani kabla ya hapo wanawake walikuwa hawajawahi kuwa waamuzi wa kati, ana wito gani kwa wasichana wengine?  Salima anasema, Iii kukifikia kile tunachokitaka, tunahitajika kuwa wavumilivu. Kuwa msichana hakutuzuii katika ulimwengu wa sasa. Hapana, hakuna ambacho huwezi kufanya. Kifanye kikatae, kesho utarudi ujaribu tena na ujifunze kutoka kwenye makosa yako kwa sababu utakuwa umepata uzoefu. Usipojaribu tena, unapoteza njia yako wakati ulikuwa kwenye njia sahihi. Ulichohitaji ni kujaribu zaidi. Kwa hiyo kama mimi Salima kutoka Cyangugu  eneo lisilofahamika sana nje ya mji nimeweza kufanikisha hili katika hatua hii ya maisha yangu, iwe kokote kule unakotokea, hakuna ambako huwezi kufika.”  

SBS Swahili - SBS Swahili
George "Uzuri wa spoti ni kwamba haubagui"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 23, 2022 12:09


Kombe la Dunia la FIFA 2022 nchini Qatar lime ingia katika siku ya tatu, na mashabiki wamepata burudani tele katika kila mechi ambayo wametazama.

fifa qatar dunia uzuri kombe
SBS Swahili - SBS Swahili
Mwalimu na nahodha wake watofautiana kuhusu matarajio kwa kombe la dunia

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 17, 2022 8:42


Kombe la Afrika la Sydney, NSW lina elekea katika robo fainali na tayari timu husika zimejua kinacho wasubiri katika mechi hizo.

SBS Swahili - SBS Swahili
Akram:"Tuko hapa kushinda kombe"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 9, 2022 3:53


Vijana wanao wakilisha Jamhuri ya Congo katika kombe la Afrika la New South Wales, wame jipa fursa yakufuzu kwa robo fainali ya kombe hilo.

SBS Swahili - SBS Swahili
Benin "Benchi la ufundi lita hakikisha tunarekebisha makosa tuliyofanya"

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 4, 2022 5:00


Kombe la Afrika la jamii zinazo ishi mjini Sydney, Australia limefika katika mzunguko wa tatu.

SBS Swahili - SBS Swahili
Nchi za Afrika Mashariki na Kati zinakwama wapi, kufuzu kwa kombe la dunia?

SBS Swahili - SBS Swahili

Play Episode Listen Later Nov 3, 2022 13:24


Nchi ya kwanza naya mwisho kufuzu kwa kombe la dunia la FIFA ilikuwa Zaire (Jamuhuri yakidemokrasia ya Kongo).

Salama Na
SE7EP05 - SALAMA NA OSCAR OSCAR | UALIMU?! SI WITO!!

Salama Na

Play Episode Listen Later Jul 14, 2022 71:15


Mwaka 2018 ndo nilimfahamu Oscar baada ya kukutana nae kwenye kituo changu cha kazi ya kutangaza mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika jijini Johannesburg nchini Afrika ya Kusini. Alikua mmoja ya watu ambao walinikaribisha vizuri sana kwenye team na kwa wakati huo yeye ndo alikua anaishikilia rekodi ya kuwa ndo mtangazaji mdogo zaidi kwenye team ya watangazaji nami nikaja kama Binti PEKEE ambaye ambaye alikua anatangaza mpira wa miguu kwa lugha ya Kiswahili. Combination yetu ilikua nzuri sana na kwa kipindi hiko ambacho kilikua cha mwezi mmoja tulielewana na ku bond vizuri sana. Oscar anapenda raha, anapenda kucheka na kuishi vizuri, anapenda ukweli na kubwa zaidi ni Rafiki mzuri sana. Pengine la zaidi ambalo nna uhakika Mama yake mzazi kule Kaliuwa anajuvunia sana ni la usomi, ni mwanafunzi mzuri ambaye anapenda kujiendeleza, sasa anamalizia Masters yake kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Alishawahi kuwa Mwalimu kipindi cha nyumba kwenye maisha yake na kwa mawazo yangu ya haraka hii ndo ambayo inamfanya awe ni mmoja kati ya wachambuzi makini kabisa ambao nchi hii inayo, nguvu yake ni kuhakikisha pale kwenye ukweli unasemwa hata kama itakua kwa njia ya mas'hara, ila atausema! Aliamua kuwa Baba na hili ni kwa mujibu wake baada ya kunikatalia katakata kwamba mtoto wake wa kwanza alikua ni wa ‘bahati mbaya' kama ambavyo baadhi ya wazazi husema, Oscar anasem alikua anajua nini anafanya na Mama wa mtoto yule so kusema alikuja kwa bahati mbaya ni kama kumkosea mtoto yule ambaye alikuja kipindi ambacho Oscar alikua bado hajajiweka vizuri kwenye maisha yake na zaidi kwenye masuala ya kazi, na pia ananikumbusha jinsi alivyokua anajiona anajua saana na kama vile watu waliokua wanampa nafasi kipindi kile kama vile walikua hawanuelewi kabisa. Anaamini kwenye kujifunza kila kukicha ili kupanua wigo wa uerevu na kwake yeye Elimu ndo ufunguo wa maisha toka siku ya kwanza. Kama Baba wa watoto wawili ambao kwa kiasi kikubwa amekua hapo kwaajili ya vijana wake, Oscar anaamini kwenye kuwa pale kwaajili yao, kuwapa kile ambacho yeye hakukipata kutoka kwa Mzee wake wakati anakua, kuwa pale kwaajili ya watu wa familia yake na zaidi Mama yake ambaye kwa mujibu wa Oscar Mama ndo nguzo yake. Binafsi nayajua mengi ambayo amayafanya Kijijini kwao Kaliuwa kwaajili ya familia yake na hata ambao hawamhusu. Humu mimi na Rafiki YANGU tulijadili mambo mbalimbali ya ki maisha na familia, kazi na muskabali wa biashara ya mpira kwenye NCHI yetu na dunia kwa ujumla, pia tuliongelea umuhimu wa familia na kupata mtoto ukiwa na umri mdogo, suala la ajira na hustle wakati tunakua nalo hatukulicha nyuma. Yangu matumainj nawe uta enjoy pia. Love, Salama. --- Support this podcast: https://anchor.fm/yahstonetown/support